Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[005]
Uchoraji wa Tatuu Mwilini
(Toleo La 1.0 20000513-20000513)
Uchoraji
wa Tatuu au Kujiweka Michoro ya Tatuu mwilini ni jambo la kizamani sana na ina
maana yake maalumu ya kiroho. Kwa sababu njema sana
Biblia imekataza kitendo hiki.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2000 Wade Cox)
(tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Tatuu ni neno
linalotokana na asili ya Kipolynesiani na lilitolewa na Kapteni Cook baada ya
kutembelea kwake kule. Neno hili asili yake linatokana na neno Tatu ambalo
maana yake ni kujigonga chapa au kuweka alama au kujichora picha kwenye ngozi
na limechukuliwa kutoka kwenye neno la Kitahiliani la tatau, ambalo
limefupishwa kutoka kwenye neno ta linalomaanisha kugonga (kwa kujibu
wa kamusi ya Encyclopaedia of Religion and Ethics (ERE), Vol. 12, article ‘Tatuing,’
pp. 208ff).
Kitendo hiki kina
ukale au uzamani kubwa sana ikionekana miongoniwa Waaustralia wa jamii ya
Kiaboriginals ambao wanaichanja na kuipamba miili yao kwa miaka ya zama kati, na
desturi hii inakutikana katikati ya Wapolynesiani na Wajapani, ambayo kwao ni
mtindo mzuri sana wa uchoraji na sanaa kwao.
Kwenye zama za
nyuma za kabla ya mwanzo wa uzao wa kifalme wa Wamisri, tatuu zilionekana
kwenye mumiani iliyobakia, kw mfano ya mwanamke huko Tukh (ERE ibid., p. 208b).
Kwenye dola ya Theban Wamisri walijichora michoro hii ya tatuu kwenye maeneo ya
matiti kwa kujiandika majina, au kujiweka alama au kuandika miungu yao na
kadhalika (ERE ibid.). kwenye kipindi kilichoonekana kama cha kilele cha maisha
kwao tatuu za mapambo zilikuwa adimu kwa Wamisri waliosalia.
Hawa ERE wanafanya
uchunguzi wa sababu iliyopelekea kutakazwa na Biblia kama inavyosema:
Makatazo
yaliyotamkwa kwene Mambo ya Walawi 19:28, ‘Msichanje chale yo yote katika nyama
ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu;’ inaashiria
kuwa Wayahudi walikuwa wameyaonaa matendo haya yakifanywa na wamataifa wasiomcha
Mungu ambao wapo kwenye maeneo iliyoangukia kura yao na huenda hata wao wenyewe
walikuwa wameanza kujifania kwa kuwaiga (ERE, ibid).
Hawa ERE wanaendelea
mbele zaidi kuona migawanyo mikuu ya mambo haya na malengo ya kiuandishi yangepaswa
pia yaashirie chimbuko asilia mawazoni na kusudi ambalo kwalo zilikuwa zinatumiwa
kwayo. Bila shaka kabisa kwamba matendo kama haya yalikuwa yakitumika ili kuonyesha
alama ya kitatuu ya ukoo fulani kwa kuutofautisha na koo nyongine katika
Australia. ERE wanaendelea kusema yafuatayo:
Kuna mwonekno na
dondoo nyingi za uchoraji wa kimadaraja ya tatuu kwa wakazi wa Ulaya. Herodotus
anaandika kuhusu wanawake wa Thracian kuwa walikuwa wanachorwa tatuu zikiwa
kama ni ishara ya ustaarabu au uungwana. Pliny anasema kwamba wanaume wa Dacians
na Sarmatians walichanja miili yao (‘corpora sua inscribunt’). Kwamba tatuu
ilikuwa inajulikana na Wapictones na makabila mengine ya wa Gaul yanaonekana
kwa ushahidi ya machapisho ya kwenye arafu. Mapokeo ya Wachina yanasema kwamba
shujaa mwingine wa Kichina aitwaye Tschaipe alizikuta tatuu miongoni mwa wa
Ainus wa Japan ambao kwa kweli walikuwa wanajichora hadi siku za leo. Huko Uchina
kitendo hiki kilikoma tabgu siku za kale na za nyuma sana kuwa ni mtindo unaopendwa
wa mapambo na kuendelea tu kama kama ni mtindo wa kuchapa au kuchora alama
mbalimbali na zinazotofautiana. A. T. Sinclair anasema kwamba miongoni mwa
hadithi za kale za huko West Indies, Mexico na Amerika ya Kati uchoraji wa
tatuu ulikuwa umeenea kama sio ulimwenguni kote. Ilikuwa inafanywa hivyo na
wakazi wa zmani wa Amerika ya Kusini, kama ilivyoonekana kwenye makabila ya pande
za pwani ya Ecuador na Peru ya kale (ibid).
Tunajua kwamba
ilionyesha mgawanyiko kama huo na ambao ulienea miongoni mwa watu wa maeneo ya
pwani au pengine huenda kwa wao.
G. Elliot Smith analikuta
hilo pamoja na wakazi wa pwani kwa sehemu kubwa ya dunia na ikijumuisha kwenye
desturi na mila mchanganyiko ya ‘kitu kutoka juani (ERE ibid.).
Nukuu hii ina
maana sana. Neno kutoka juani au heliolithic kuhusiana na zama ya kubuni
isiyo rasmi na kwenye jambo hili umri wa jua na safari za waabudu jua za
kihujaji zilichukua kiwango chake cha mgawanyiko au uingiaji. Uhusiano wao na
nchi za pwani unaonyesha kuwa wanahusiana na mjumuiko wa watu wa pwani.
Tunaweza kujipunguza kutoka na hili na ukale wa matukio au matendo
tunayoshughulikanayo kwa vipindi vya wafalme wa kale wa baharini mapema kabla
ya maendeleo ya dola kuu za kimabara ya Wababelonia na ya Wamedi na Waajemi na
ya Wayunani na Warumi.
Darwin kwenye
masomo yake alisema kuwa ilikuwa imeeenea sana ulimwenguni kote kwamba hakuna
nchi moja kuu inayoweza kuitwa ambayo kwamba waaboriginali hawakujichota tatuu
(ERE ibid.).
Tumeona na
kuelewa sasa kwamba ilikuwa inaambukiza miongoni mwa Wamisri wa zamani na
miongoni mwa wa Thracians, wa Picts na wakazi wa Amerika ya Kusini. Katika
Amerika ya Kasakazini inakutikana pia kwa Wahindi hususan kwa wa Iriquois, wa
Pricked Pawnees, wa Delawares na wengineo wengi (ibid.).
Kimsingi, watu
wenye ngozi ya rangi nyeusi walifanya uchanjaji huu wa kimichoro, wakati wale
wenye ngozi nyeupe ama angavu walikuwa wanajichora hizi tatuu.
Uhusiano wa
matendo ya zama kale unaweza kukutikana hata sasa na tunaweza rkuanzisha
utamaduni wa kujichora tatuu uliokatazwa kwenye Biblia kwenye Mambo ya Walawi
19:28.
Flinders Petrie ameguswa
na kuwa makini kwenye ufananishaji kati ya muonekano wa Waalgeria ulioelezewa
na Lucien Jacquot na wale walio kwenye muonekano wa kike waliokutikana huko
Tukh (waliotajwa hapo juu) na kwa Walibya kwenye kaburi la Seti 1. Huyu Farao
Seti 1 alikuwa ni wa Kizazi cha Kifalme cha XIX, takriban mwaka 1300 KK na anahushwa
na wanazuoni na kpindi cha tukio la Kutoka akifuatiwa na kipindi cha utawala wa
Manetho. Kwa hiyo tunaona mlolongo wa matukio ya huko Misri tangu wakati wa
zama ya Mababa hadi siku hizi huko Afrika Kaskazini.
Hata hivyo, tunaweza
kuidhania hii pia kuwa ni chanzo halisi cha dini halisi miongoni mwa imani kuu
yenye mchanganyiko wa Kiashuru na Kibabeloni, ambayo ilikatazwa na Mungu, kwa
kupitia Malaika wa Uwepo wake na Musa. Tumejionea ya kwamba ilikuwa ni ugonjwa
huko Misri ya kale kuiwaklisha miungu, hususan katika kipindi cha wa Theban. Hii
ni muhimu sana kwa aina yake kama mtindo wa ibada ulioenea kutoka Frigia hadi
Misri na hadi huko Ulaya kwenye dini ya Kiseltiki nay a Picts.
Tunajua pia kuna
ushahidi wa hitimisho la jumla la biashara ya kimataifa nay a kimabara na
mawasiliano tangu mwaka 1000 KK kati ya Masharik ya Kati na Amerika ya Kusini.
Ni vizuri na salama sana kudhania kwamba mueneo wa kipwani wa tendo hili ulikwenda
na wachuuzi na imani ya dini ya waabudu jua waliyokuwanayo.
Mitindo
iliojulikana na kupendwa huko Algeria ni
Msalaba na alama
iliyofanana na inzi, ambazo zinadhaniwa kuwa mambo zimetokana na wa swastika – chombo
kilichosambazwa sehemu nyingi barani Afrika na kwingineko, na yenye hali ya
uzamani sana, kama inavyoonyeshwa katika uonekanaji wake kwenye mwonekano
ulioongoza kwenye mji wa pili wa Troy (yapata kama mwaka 2500-2000 KK) na kwa
kulindwa kwake huko Crete ya kale (ERE, ibid, p. 210).
Ni rahisi kuona
kutoka kwenye rejea hizi na tarehe na alama, tunazo shughulika nazo na imani za
zama kale kama zilivyotokea kutoka kwenye mchanganyiko wa Waashuru na
Wababeloni huko Mashariki ya Kati. Ilijumuisha dini siri za kale na dini za jua
zilizoonyeshwa kwa alama kwa msalaba, na kama ilivyotengenezwa kwa mtindo Swastika,
na alama ya Baali-Zeebubu Bwana wa Inzi, mungu wa Ekroni (soma majarida
ya Msalaba: Chimbuko Lake na Maana Yake (Na. 39) na Daudi na
Goliathi (Na. 126).
Tunaiona dini ya Wafilisti,
wenyeji wa maeneo ya pwani ya bahari waliokuja Kanaani na Misri kwa njia ya
visiwa vya Mashariki ya Kati na ambao imani yao ilienea miongoni mwa waumini wote
waabudu Baali na Ashtoreth au Astarte, Ishtar au Easter. Hii ilikuwa ni dini ya
Watrojani. Watu hawa waliondoka Mashariki ya Kati na wakaingia na kuweka makazi
yao huko Ulaya. Tunawaona watoto wao wakiuita mji kwa jina la shujaa wao Paris na
linguine la baada ya ule Troy wa kale. Wao, pamoja na Wahiti, Wahati au
Wakalti, Wakeltoi, ambao wengi wao waliondoka na kwenda Ulaya pamoja na
Waashuru na sehemu kubwa ya Waisraeli wakati wa kuanguka kwa Dola ya Waparthi na
wakajulikana kwenye historia kama Waaryans (soma jarida la Vita vya
Wayunitariani na Watrinitariani (Na. 268)).
Imani hii inaonekana
kwenye maadhimisho ya Easter na Christmas, hususan kwa wafuasi wa kile
kilichoingia kwenye Uktisto kama sikukuu na maadhimisho ya Easter, inayotokana
na ibada ya mungu Attis. Dini ya Siri na ya kuabudu Jua zilikuwa na kanuni na
desturi hizi na tunazikuta kwenye dini potofu na za uwongo za Kiorphik, ya Dionysian,
zile za Attis na pia zile za Adonis.
Makuhani
matowashi wa mungu Attis walijipamba kwa michoro ya tatuu za mti wa mdaha au muivy
ambao ulikuwa ni mtakatifu kwenye imani ya Wadruidiki wote na kwenye imani na
Dini za waabudu Jua kwa ujumla. Neno Attis maana yake ni baba. Kwa hiyo, jina Papa au pope linatokana na dini hizi za kisiri
na kifumbo. Neno au cheo hiki cha baba pia
ni cheo cha daraja imani ya dini ya Mithras na kwa hiyo ujumuisho wa Dini za
Siri na fumbo za waabudu Jua.
James George Frazer anaiweka hii kwenye mtazamo wa kazi hii The Golden Bough (third edition, Macmillan, 1976 print, v. p. 277).
Chimbuko na muonekano wa huyu Attis ni kama
roho ya mti uliojitokeza wazi kwa nje kwa sehemu ambapo mti wa msonobari unaonyesha
umuhimu wake, kanuni yake na sanamu zake. Hadithi inayodai kuwa alikuwa ni mwanadamu
aliyebadilika kuwa mti wa msonobari ni moja pekee kati ya zile zinazojaribu kuweka
wazi katika kuhusianisha na imani za zamani na ambazo zimetukuta sisi mara kwa
mara kwenye mafundisho ya mizimu na mazimwi. Kitendo cha kuuingiza mti wamsonobari
kutoka kwenye mbao zilizotengenezwa kwa mchanganyiko wa makapi na hariri, ni
sawa kama kuuingiza au kuuleta mti wa May au mti wa majira ya Joto kwenye
desturi ya makundi ya kisasa na kinyago au sanamu iliyoambatanishwa kwenye mti
wa msonobari ambao ulikuwa umefanywa kuwa muwakilishi war oho ya mti wa Attis. Baada
ya kuwa umekazwa kwenye mti, ndipo sanamu au kinyago kilitunzwa kwa mwaka mmoja
na kisha ulichomwa moto…. (p.
277)
Imani hii
imefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235). Dhana ya mzimu wa mti na mungu wa Utatu
imeelezwa kwa kina na kuendelezwa kwenye jarida la Fundiho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya I Bustani
ya Edeni (Na. 246).
Kushamiri kwa
imani ya kidini ilikuwa ni kwa kuwa ilikuwa ni imani ile ile ya mwanzoni
asilia. Ilitokana na imani kale za mchanganiko wa Waashuru na Wababwloni
iliyotujia hadi sisi kama Waaryani na dini yao iliyoenea hadi kwenye maeneo ya
mbali ya Wahiti na Waashuru na kwenye Makabila Kumi ya Israeli kutoka Mashariki
ya Karti na katika kingo za kati za Ulaya hadi India.
Frazer alikuwa na
mtazamo kwamba nia ya kwanza ya desturi iliyoelezwa hapo juu na kwa Msonobari kuwa
mti mtakatifu kwa Attis, ilikuwa ni kuendeleza roho ya uoto kwenye maisha kwa
mwaka wote mzima. Hamu hii indelevu ya kuziomba roho ya uzima na imani ya
kutokufa ilijulikana na kuaminika sana miongoni mwa Waaryani ni kama ilivyokuwa
dhana yote nzima isemayo Hutakufa hakika.
Frazer anaongeza
kuwa:
Kwa sababu hizohizo
ndpo huenda Ivy ulikuwa mtakatifu kwa Attis; kwa matukio yote tumesoma kwamba
kulikuwa na makuhani matowashi waliochorwa tatuu zenye alama ya majani ya mti
wa (ibid. p. 278).
ERE inasema:
Daraja zote huamini
kwamba inafaa ya tatuu inafanya mwendelezo zaidi ya maisha yaliyoko leo hadi
yale ya ulimwengu ujao, ambao wanatumika kama ilivyowekwa alama za utambulisho –
kama, Nagas wa Manipur, Kayans wa Borneo, Wahindi wa Amerika Kaskazini, na
wengine wengi, au ni kama mwongozo au ni kama kwa sasa inavyowawezesha wafanikisha
safari yao.
Kwa hiyo, ingekuwa
isemekane tu kwamba sababu ya kuweka tatuu hapo kale ilikuwa ni kama alama ya
utambulisho, inayomfanya mtu aliyechorwa tatuu kwenye dini au imani yake kwa
mungu au kwa mapepo ambayo ilikuwa inaombwa. Hii ilifanywa ili kwamba miungu au
mungu au mapepo wachukue roho ya mwenye kuteseka na magonjwa na kuirejesha upya
roho ile kwenye utaratibu wa maisha baada ya kufariki, iliyo kwenye mfumo au
muundo war oho au ka. Hii ilifanyika ndani ya ufafanuzi kuhusu uzima wa milele
uliotolewa na watu wa zamani kwenye ibada za Mungu wa Utatu, ambaye yeye
mwenyewe anahusiana kama mungu kwene mti. Mungu utatu aliye kwenye mti anaonekana
kutoka na rekodi yetu kwa zamani sana kabla ya kuishi kwa Wahindu waliokuwepo kwenye
kngo za huko Harappa na Mohenjo Daro tangu kipindi cha kale cha majira ya Joto
yapata mwaka 2000 KK. (soma
pia jarida la Fundisho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya I Bustani
ya Edeni (Na. 246)).
Hutu Mungu wa
Utatu alitokea kuwa ni kama imani kuu ya huko Roma kama walivyo wengine kina Jupiter
Juno na Minerva na pia kwa umbo la mungu mke aitwaye Hecate, mungu mwenye sura tatu
kwenye jedwali la chemchabongo.
Kwa hiyp tunaona
kusudi halisi ni kuweka alama au kutambulisha ushikaji wa imani na hasahasa kwa
makuhani matowashi kuwa wamejitoa mhanga kwenye imani, kwa hiyo wametambulika
kwenye maisha baada ya kufa au maisha yajayo.
Ni nyongeza kutoka
kwenye mfumo wa imani wa kimapepo na uliwekwa ili kuendeleza au kutukuza
fundiho la kuwa roho inaendelea kuishi na dhana yake na ni uwongo mkubwa sana
uliotumika pale Edeni kuwa: Hakika hutakufa.
Kwa sababu hii
Mungu amelaani na kukataza jambo hili, kwa kuwa ni ibada ya sanamu.
q