MAKANISA YA KIKRISTO YA MUNGU
[A2]
Hii ni Katiba halali ambayo imesajiliwa nchini Australia.
MAKANISA YA KIKRISTO YA MUNGU
KATIBA
Ya
HALMASHAURI YA BARAZA KUU LA MAKANISA YA KIKRISTO YA MUNGU ULIMWENGUNI
Sura ya 1 Jina
Shirika hili litajulikana kwa jina la Christian Churches of God (Makanisa ya Kikristo ya Mungu) na baraza lake la uongozi litajulikana kama World Conference of Christian Churches of God, (kwa Kiswahili) “Halmashauri ya Baraza kuu la Makanisa ya Kikristo ya Mungu Ulimwenguni” au kwa ufupisho, Christian Churches of God (World Conference) [kwa Kiswahili ina maana ileile hapo juu] amabayo hatimaye itajulikana kama World Conference (Halamashauri Kuu ya Ulimwengu). Halmashauri hii Kuu Ulimwenguni ndiyo kama mzazi au ni yenye kushikilia maomgozi kwa Halmashauri zote za Kitaifa duniani za Makanisa ya Kikristo ya Mungu popote pale zilipo Ulimwenguni kote. Halamashauri hii ya Baraza Kuu la Ulimwengu, laweza kuwa Mwanachama wa Halmashauri Kuu ya Dunia ya Makanisa ya Mungu kwa njia ya ushirikiano yanapotokea makubaliano fulani na Makanisa mengine yaliyo nje ya ushirika wa Makanisa ya kikristo ya Mungu.
Sura ya 2 Lengo
Lengo kuu la Manisa ya Kikristo ya Mungu ni kuhubiri Injili ya Ufalme wa Mungu kwa mataifa yote kwa njia ya neno na mafano wa kimatendo.
Makanisa mbalimbali yaliyo katika muungano huu yanafungamanishwa pamoja kwa makubaliano ya Ukiri wa Imani kama yalivyoelezewa wazi katika mojawapo ya machapisho yetu lijulikanalo kama Matamko Ya Imani Ya Kikristo (toleo letu la nne) au kwa kadiri itakavyo fanyiwa marekebisho na kuchapishwa ilimradi tu kuwa katika masahihisho yote hayo hayatakusudia kujaribu kufanya aina fulani ya michanganyo au kuchukuliana na mtazamo wa kiimani wa watu wanaoamini juu ya uwepo wa Miungu wawili (Unitarian) au kuingiza mafundisho ya imanai ya waamini wa kinachoitwa Utatu Mtakatifu (Trinitarian) au mafundisho ya Watu wanaoamini juu ya usawa wa Mungu Baba na Yesu kuwa wote ni Miungu na wapo sawasawa katika hali zote (Binitarian) au mafundisho ya wale wanaoamini uwepo wa Miungu miwili mikuu (Ditheist).
Sura ya 3 Mamlaka na Majukumu
(1) Baraza hili la Halmashauri kuu lina Mamlaka isiyo na ukomo. Ndilo linalotoa maamuzi kuhusu mipaka ya kikanda ya uangalizi na kutoa vibali kwa makanisa ya kitaifa kuyakubali kuwa sasa ni wanachama na kuwa sasa ni washirika katika ushirika wa Makanisa ya Kikristo ya Mungu.
(2) Baraza la Halmashauri laweza kupanua usaidizi wake hadi katika Halmashauri nyingine ya Kanisa au hadi kwenye Halmashauri nyingine kadiri itakavyo hitajika usaidizi wake. Usaidizi huu waweza kutolewa kwa njia ya binafsi au kwa ushirikiano na Halmashauri nyinginezo.
(3) Halmashauri ya Baraza kuu la Uangalizi Duniani, ndilo linalo teua Waangalizi wa Kikanda kwa ajili ya kubeba majukumu ya kusimamia Makanisa ya kitaifa ambayo yatawajibika kwa Halmashauri Kuu ya Uangalizi Duniani ili kuhakikishisha kuwa Mafundisho hayakosewi na shughuli za uangalizi wa Kanisa zinaenda sawasawa na Katiba isemavyo na machapisho mbalimbali yanayotolewa kulielezea Kanisa yanavvo sema.
(4) Halmashauri Kuu ya Uangalizi Duniani ndiyo inayohusika na uangalizi wa masuala yote yahusuyo tovuti ya shirika hili Duniani na vyombo vya habari na kila Kanisa halinabudi kudumu katika mafindisho kama yanavyo tolewa.
(5) Halmashauri ya Kanisa kitaifa inaweza kuandaa mikakati ya uanzishaji na uendelezaji wa matumizi ya vyombo vya habari lakini mpango huu unapaswa uendane sawa na mafundisho ya Kanisa yanavyosema na kuwepo na utayari kuruhusu yapitiwe na Uangalizi wa wa Baraza la Halmashauri kuu la Ulimwengu.
Sura ya 4 Muundo wa Halmashauri
Baraza hili litaundwa na Makanisa hayo kukijumlishwa na Kanisa la Halmashauri kama yalivyo au yatapokelewa katika ushirika na Baraza hili.
Ibara ya 1. Maafisa wa Baraza la Halmashauri Kuu ya Ulimwengu
(1) Maafisa wawili wenye kusimamia shughuli za Uongozi wa Halmashauri Kuu ni Mwangalizi Mkuu (Coordinator General) na Makamu Msaidizi wake (Deputy Coordinator General). Wanapaswa kudumu katika uongozi kwa kipindi kinachoanzia Sikukuu ya Vibanda ya mwaka wa saba katika mzunguko hadi kufikia Sikukuu ya Siku iliyo Kuu ya Mwisho ya Sikukuu ya Vibanda ya mzunguko unaofuata. Mwangalizi wa kwanza mbaye kwa sasa pia ni Mwangalizi mkuu wa Halmashauri zilizo katika maeneo ya Australia, New Zealand na Nchi jirani zilizo katika visiwa vya Kusini mwa Bahari ya Pacific (maarufu kama Australasia), pamoja na Makamu wake ambaye pia ni Mwangalizi wa Halmashauri zilizo katika Amerika ya Kaskazini, watadumu katika ofisi kuanzia kipindi ambacho Katiba hii itaanza kushika hatamu hadi katika Mwaka wa Sabato ulio katika mzunguko yaani Mwaka 2005 kwa Kalenda ya Mataifa. Iwapo itatokea kifo cha pengine mmojawapo wa hawa waangalizi, nafasi hiyo itajazwa na mwenye kukaimu ambaye atapatikana kwa njia ya kupigiwa kura na wazee waliosalia kutoka katika Halmashauri za kimajimbo ambao ni waangalizi wa majimbo na wazee wa makanisa ya kitaifa. Ukaimu huu utalazimu kuzingatia makubaliano ya mafundisho ya kiimani na afisa aliyeko ambaye ni ama Mwangalizi Mkuu ua Msaidizi wake. Mzee huyu ajaye itampasa achukue madaraka ya Msaidizi. Ikitokea kuwa wote wawili wamekufa, basi uteuzi wa watakao kaimu utaamuliwa na Halmashauri Kuu. Kama vile ilivyo tolewa katika kifungu cha 1(2) hapo chini, kuanzia mwaka 2005, kuwa katika tukio la kifo cha wote wawili wa hawa, basi Msaidizi wa Mwangalizi Mkuu atakaimu nafasi zao na ukaimu huu utaamuliwa na wazee kutoka Halmashauri Kuu.
(2) Baraza la Halmashauri Kuu litaongezwa katika mwaka wa Sabato wa 2005 na wazee wawili zaidi watateuliwa kwa njia ya kura. Wataridhia kuhudumu kama maafisa wa tatu na wanne katika Halmashauri Kuu ya Ulimwengu na watajulikana kama Msaidizi wa Mwangalizi Mkuu na Msaidizi wa Makamu Mwangalizi Mkuu. Katika kila mwisho wa mwaka wa saba, katika mwaka wa Sabato, waangalizi wakuu hawa wote wanne wakiwemo wale wanaomalizia muda wao ambao ni Mwangalizi Mkuu na Makamu wake watawekwa kwenye orodha ya wagombea wa uongozi ili wapigiwe kura. Iwapo kama huyu Mwangalizi Mkuu aliyeko atateuliwa katika mchujo huu wa wagombea, basi ataendelea kushikilia wadhifa wake kwa kipindi kingine kipya kinachofuata kadiri kilivyowekwa.
(3) Katibu Mkuu ambaye pia ni Mtunza Hazina Mkuu ni mwanachama mshiriki katika Halmashauri Kuu na Baraza la Utendaji. Katibu huyu Mkuu husaidiwa na Wasaidizi wawili Wakuu ambao pia ni wanachama Baraza la Utendaji la Halmashauri Kuu ya Ulimwengu. Umri wa lazima wa kustaafu kwa Katibu Mkuu ni afikiapo miaka sabini.
(4) Baraza la wazee ndilo wasaidizi wa waangalizi wa majimbo na wa waangalizi walioteuliwa wa taifa au waliochaguliwa na Makanisa ya kitaifa.
(5) Wakuu wa makanisa ya kitaifa ya kila jimbo wataunda kila halmashauri za kimajimbo na maafisa wake kadiri walivyopendekezwa na Mwangalizi Mkuu au Makamu wake.
(6) Baraza la Wazee litakutanika lote angalau kila mwaka wa saba au mwaka wa Sabato na kwa wakati mwingine wowote kadiri itakavyoonekana inafaa na Mwangalizi Mkuu na Baraza la Utendaji la Halmashauri kuu ya Ulimwengu. Shughuli zaweza kufanyika na mabaraza madogomadogo katika majimbo kwa ridhaa au ruhusa ya Mwangalizi Mkuu. Mikutano ya Baraza la Wazee yaweza kufanywa kwa njia ya vyombo vya kitaalamu (electronic means) katika Majimbo au kwa Mabaraza, kulingana na maelekezo ya Mwangalizi Mkuu.
(7) Baraza huundwa kwa kuhusisha wakuu wa kila Halmashauri za Taifa na Waangalizi wa Majimbo wa makundi ya Kitaifa na Mwangalizi Mkuu na Msaidizi wa Mwangalizi Mkuu wote wanapaswa kuhusishwa katika kila duru ya maafisa wa baraza la utendaji kuwa ama Mwaangalizi Mkuu na Makamu Mwangalizi Mkuu na /au Msaidizi wa Mwangalizi Mkuu. Aina yoyote ile ya kura hii yapaswa ziendeshwe kwa kufuata taratibu nzuri sahihi na kwa usimamizi mzuri wa kila duru ao kura. Wasimamizi wa uchaguzi wanapaswa kujiepusha na hali yoyote ya upendeleo katika duru hii.
Ibara ya 2: Halmashauri za Makanisa
Makanisa shirikishi, pale yatakapopata kibali, yatakuwa na hiyari ya kuwa ya kitaifa au mchanganyiko wa makundi ya Lugha mbalimbali kadiri inavyowezekana. Hatahivyo makanisa yaweza yakawa Makanisa ya Kimajimbo yakihudumia zaidi ya eneo moja la nchi hadi wakati utakapowadia kwa kanisa la kitaifa litakapopata kibali. Yote yatafanyizwa kupitia ndani ya katiba ya Halmashauri Kuu ya Ulimwengu na kutilia maanani mamlaka yao na uwepo wake kama nakala halali za Makanisa ya Kikristo ya Mungu kutoka na kwa maadili yanayojali ridhaa katika kupokea kibali kutoka kwa Halmashauri Kuu Duniani ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu.
Sura ya 5 Vipindi vya Kushika Madaraka
Ibara ya 1: Vipindi vya Kawaida
Vikao vya Baraza la Halmashauri Kuu Duniani vinafanyika chini ya uenyekiti wa Mwangalizi Mkuu au Makamu Mwangalizi Mkuu kwa wakati wowote au mahala pa uchaguzi wao. Inapotokea vifo vya Katibu Mkuu au Msaidizi wa Katibu Mkuu, afisa yeyote aliyependekezwa kujaza pengo lile, anayo mamlaka ya kuongoza kikao cha halmashauri ambacho kitahusisha waangalizi wakuu waliobakia na waangalizi wa majimbo na wa mataifa kadiri tu Baraza la Wazee pamoja na Makatibu wakuu watatu.
Vikao vya Halmashauri za majimbo zaweza kufanya chini ya uwenyekiti wa waangalizi wa majimbo au na mojawapo wa maafisa wa Halmashauri Kuu ya Dunia ambaye atatoa maamuzi kitadumu kwa muda gani na muundo wa kikao hicho.
Vipindi vya kawaida vya Halmashauri wanachama za kitaifa vitaku ni miaka saba kwa wakati kama ule na kwa mahali ambapo Baraza la Utendaji itakapopachagua na kutangaza Rejea za kikao. Vikao hivi vitafanyika kati ya Siku ya Kwanza ya Mwezi wa Kwanza (uitwao I Abib au Nisan) na mwishoni mwa Sikukuu ya Pasaka na Sikukuu ya Mikate isiyotiwa Chachu sambamba na mwaka wa saba au Mwaka wa Sabato. Kwa vipindi vilivyoko, siku hizi huwa sawa na (I Abib au Nisan 1998) au 1/1/21/40 hadi 1/1/28/40 (yaani I Abib 2005) na baadae katika 2012, 2010, 2026. Mwaka wa Yubile utaongezwa katika mzunguko wa miaka ya Sabato kama mwaka wa nane katika mahesabu ya mihula ya kudumu kwenye wadhifa katika mzunguko ule.
Kila Halmashauri ya Taifa inapaswa kuandaa vikao vya kila mwaka kwa lengo la kutunza taarifa zake na kuandaa taarifa za fedha na kuzituma kwa Halmashauri Kuu Duniani na nakala kwa wahasibu na kwa Serikali chini ya sheria za mataifa kama inavyotakiwa kufanywa.
Ibara ya 2: Vipindi Maalumu au vya Dharura
(1) Vipindi maalumu vya Halmashauri ya Taifa vyaweza kuwa kwa usimamizi wa Halmashauri Kuu ya Ulimwengu au na Baraza la Utendaji la Halmashauri ya Taifa au na mtu yeyote ambaye atapewa ruhusa na Halmashauri kuu Duniani au Halmashauri ya Kitaifa kwa wakati na mahali ambapo msimamizi atakapopendekeza na kuona panafaa. Kikao cha dharura cha Halmashauri hii ya Ulimwengu au Taifa kitafanyika chini ya uwenyekiti kwa njia ya utoaji maombi kimaandishi kutoka kwa viongozi husika ikionyesha kuwa imeridhiwa na waliowengi hapo Kanisani kulingana na sheria iliyopo hapo katika Halmashauri yao.
(2) Shughuli ambazo zitashughulikiwa wakati wa Kipindi hiki Maalumu au cha Dharura na Halmashauri ya Taifa ni:-
(a) Shughuli zilizo mahususi zilizoorotheshwa katika rejea za kikao ili kujadiliwa, na
(b) Dondoo nyingine zaidi ziwe zilizo Maalumu au za Dharura kuwekwa kwenye rejea za kikao ambazo zitajitokeza kutegemea na maazimio yaliyopitishwa na wingi wa wajumbe usiopungua theluthi mbili ya wajumbe waliopiga kura.
(c) Idadi ya wahudhuriaji isiwe chini ya asilimia hamsini ya wajumbe waliotarajiwa au kwa suala la kutaniko la pamoja pia isiwe chini ya idadi ya asilimia hamsini ya wanachama wa kusanyiko hilo.
(3) Usimamizi wa Kikao hiki, kiwe cha Maalumu au cha Dharura waweza kufanywa na kwa kumteua yeyote kati ya maafisa au mtu mwingine au kutoka katika kamati na kupitisha shughuli za kikao na kufanya mambo mengine yote kama kikao cha kawaida chini ya maongozi ya Katiba au Kamati ya Utendaji kipindi hiki cha kikao wanaweza kufanya uteuzi, mabadiliko au kufanya matengenezo.
Ibara ya 3: Tangazo
Tangazo la muda gani au mahala pa kufanyikia kikao litatakiwa kutolewa mapema si chini ya majuma matatu au siku ishirini na moja kabla ya siku ya ufunguzi kwa nia ya kwamba wajumbe wayapitie kwa utulivu ili waweze kutoa maamuzi kulingana na sheria inavyosema.
Ibara ya 4: Upigaji Kura
Kila mjumbe ahudhuriaye kikao atakuwa na haki ya kupiga kura moja tu kati ya maswali yote kuulizwa. Mwenyekiti wa kikao atakuwa na kura ya hiyari ambayo ataitumia pale itakapobainika kuwa na wagombeaji wamefungana matokeo hii ya kwake itatumika kutenganisha ili kumpata mshindi. Maamuzi yahusuyo maongozi yatapitishwa kwa kura zinazotegemea uwingi (simple majority). Masuala yahusuyo Imani ya Kanisa yataamuliwa na makao makuu ya Baraza la Halmashauri Kuu ya Ulimwenguni na yatatangazwa kwenye vyombo vya habari na vy mawasiliano. Wajumbe wale ambao watashiriki kikao wakiwa mbali na kikao kilipo watashiriki kupigia kura kwa njia ya vyombo vya kisasa vya mawasiliano au njia yoyote mbadala kwa kutuma kwa mwenyekiti na makatibu wa kila halmashauri na kwakupitia sera zilivyo elekezwa na Halmashauri Kuu ya Dunia, Makao Makuu. Kadhalika hata kwa mambo mengine, kila mjumbe yeyote wa kawaida ana fursa ya kuwa na kura moja tu kwa ajili yake au katika halmashauri ya nyumbani kwake anakotoka.
Ibara ya 5: Nguvu za Kikao
Usimamizi wa vikao hivi ambavyo hatimaye vitawezeshwa kuwa ni Halmashauri za Taifa, wakati wa vikao vyao watakuwa na mamlaka ya mufanya maamuzi katika mambo yote na mashauri katika utaratibu na mongozi mazuri katika Halmashauri zao na taratibu za mambo yao. Sera hizi au maamuzi ya Halmashauri Kuu ya Dunia ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu wanafungamanishwa na kila Halmashauri ya Taifa. Itokeapo kuwa Makao Makuu ya Halmashauri kuu ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu ikitafuta uanachama na Halmashauri Kuu nyingine za Ulimwengu za Makanisa ya Mungu, lakini hakuna mafungamano yoyote ya kimaamuzi yatayolazimisha kwa halmashauri yoyote isipokuwa idhiani maalumu ya Halmashauri Kuu ya limwengu ya Ushirika wa Makanisa ya Kikriso ya Mungu. Hakuna uwezekano wa kuwa maamuzi yatolewayo hapo yanaweza kuingiliana au kusababisha michanganyo katika muundo wa Ukiri wa Misingi ya Imani kuhusu Uungu na sheria. Hakuna maamuzi yatakayofungamanisha katika Halmashauri za Makanisa ya Kikristo ya Mungu au washirika yenye kupingana na Sheria za Kibiblia au yenye kutilia shaka kuhusu mamlaka na ukuu wa Mungu na mafafanuzi ya Kibiblia kuhusu asili ya Mungu nay a Mwanae Yesu Kristo. Uamuzi huu utafanywa na shauri la kwanza na Halmashauri Kuu ya Ulimwengu ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu.
Sura ya 6 Maamuzi ya Wajumbe Yatokanayo na Vikao vya Halmashauri
Ibara ya 1:
(1) Baraza la Halmashauri Kuu la Dunia litakuwa na maafisa waandamizi watano (hatimaye saba) ambao ndio Baraza la Utendaji la halmashauri na Wanachama wa Bodi ya Halmashauri za Kijimbo ambao pia watashikilia hatamu za uongozi wa kitaifa na waangalizi wa majimbo. Halmashauri zina mamlaka ya kufanya maamuzi katika majimbo na kuweka kamati ndogondogo zitakazokuwa chini ya usimamizi wa viongozi wa kanisa kwa mambo yahusuyo maongozi. Bodi yote nzima yaweza ikahitajika kutoa maoni yahusuyo mambo ya Imani na mambo mengine. Hatahivyo maafisa wawili wa Kanisa kama vile Mwangalizi Mkuu anaweza kutumia mamlaka yake ya Kikatiba kwa kupiga kura ya Turufu kwa ajili ya aina yoyote ya pendekezo au shughuli inayoonakana kuwa imeandaliwa kwa lengo la kushusha kiwango au kubadili misingi ya imani au ubora na uaminifu wa utendaji kazi wa shughuli za Kanisa ambao kwayo yalikuwa ni lengo la uanzishwaji wake.
(2) Wajumbe wa Halmashauri za Taifa watakuwa:
(a) Wajumbe hawa kadiri watakavyoonekana wanafaa na kanisa waliopewa mamlaka kwa wakati ule na Halmashauri Kuu ya Ulimwengu washikilie Halmashauri ya Taifa. Makanisa yaweza kukubalika kupokelewa na Halmashauri pale tu Halmashauri Kuu Duniani itakapotoa mamlaka ya jinsi muundo wa kanisa la mahali pamoja na ushiriki wake katika Halmashauri ya Taifa. Kila kanisa litatambuliwa kwa kutoa mwakilishi mmoja kati ya kila wanachama kumi au baadae itakapojitanua kufikia eneo kubwa.
(b) Wanachama wote wa Baraza la Utendaji la halmashauri.
(c) Wenyeji wanaotokea eneo iliko Halmashauri na kwa wakati ule wanakuwa na sifa zifuatazo, kuweza kupewa leseni na vyeti na halmashauri hii.,
(i) Kitambulisho cha Kukubalika Kihuduma.,
(ii) Kitambuliaho cha Kukubalika Kiumisheni.,
(iii) Kitambulisho cha Kuruhusiwa katika Huduma za Uhariri, Vyombo vya Habari na Muinjilist wa njia ya Maandiko Matakatifu.,
(iv) Kitambulisho cha Kuruhusiwa katika Huduma ya Ualimu au Mwalimu wa Biblia nakadhalika.
(d) Mwanachama wa Halmashuri Kuu ya Dunia huwakilisha au watu wengine kama hao hushikilia taaluma muhimu kadiri itakavyoruhusiwa na Baraza la Utengaji au kamati nyingine yeyote sawa na hiyo iliyowekwa ili kuwakilisha, na kukubalika kwa kupigiwa kura za wajumbe katika kikaoni; idadi ya wawakilishi watakao kaa kikaoni isizidi asilimia ishirini ya wajumbe waliokubalika sawa na makanisa yenye muundo shirikishi.
(3) Wawakilishi hawa walioelezewa hapo juu katika ujumla wao watatumwa kukutana na kanisa pale ambapo uanachama wake bado unaendelea, na watakuwa na haki kamili ya kura na kanisa lile kwa mambo yote yaliyopigiwa kura wakati wa kikao sawa na hicho kilichopita na kikao halali kikatiba.
Sura ya 7 Vitambulisho, Leseni na Vyeti
Ibara ya 1:
(1) Baraza la Halmashauri Kuu ya Dunia kupitia ama Mwangalizi Mkuu au Makamu wake au mjumbe wake wa ama wa kijimbo au kitaifa, wanayo ruhusa na mamlaka ya kusimika au kuiweka wakfu huduma ya kanisa au wazee au mashemasi. Baraza la Utendaji la Halmashauri ya kitaifa kwa mkutano wao wa kwanza unachofuatia kikao litaamua ni kinanani waliohakikishwa kufaa kwa uongozi kwa mujibu wa sheria na kanuni visemavyo, na kuwa wanastahili kupewa nyadhifa zinazostahili, leseni na vyeti kwa watumishi hao na kwa wengine waonekanao kuwa wanastahili kutumika katika masuala ya Halmashauri yao, na kumhakikisha kuwa mtu huyu anastahili kusimikwa kwa mujibu wa vile itakavyotolewa hakikisho la wito wake kumtumikia Mungu na kuwa amepata sifa njema kwa wengi na amemdhaminiwa na Halmashauri yao au Halmashauri ndogo. Hakuna utaratibu wa kusimika wazee kwa marudio kutoka halmashauri ndogondogo za Makanisa ya Kikristo ya Mungu uliyo wa lazima. Hazitakuwepo huduma za mshahara. Watumishi watapaswa wawe na kazi nyingine za kuajiriwa. Posho itatolewa kwa wanachama wa halmashauri. Hakuna mwanachama wa halmashauri ambaye atakuwa pia anapokea posho nyingine kutoka katika hazina ya kanisa.
(2) Hakuna mwanachma wa halmashauri yoyote atakayeshiriki majadiliano ya, au kupiga kura, au shauri lolote ambalo lenyewe au ndugu yake ana manufaa nalo au ana maslahi nalo ya kifedha, uhusiano namna hii utatuama katika daraja la tatu la udugu.
Ibara ya 2:
(1) Vitambulisho, leseni na vyeti hutolewa au huruhusiwa na Kamati ya Utendaji ya Halmashauri ya Taifa, navyo vitadumu kutambulika na kuwa hai hadi kipindi cha pili cha kawaiada kijacho isipokuwa tu kama mtu huyo alisimamishwa huko nyuma na Halmashauri ya Utendaji kwa maana ya ustaafihwaji, mwenendo mmbaya au maazimio ya kusitakiana mahakamani kwa kuhusihwa na Kikao Maalumu cha Halmashauri ya Taifa.
(2) Halmashauri Kuu ya Ulimwengu inayo haki ya kutangua leseni ya kila kanisa au halamashauri ya taifa kuwanya mambo yake kama kanisa lililo katika mwili wa Makanisa ya Kikristo ya Mungu. Kutanguwa kwa leseni kunaweza kusababishwa na kugundulika kwa tofauti za mafundisho ya imani au na sababu nyinginezo. Kanisa lolote lile linaponyang’anywa kitambulisho kwa sababu hizi za kugundulika mafundisho mengine tofauti au aina nyingine ya utovu wa nidhamu, haki zozote za kutumia mali yoyote ya kanisa au kufanya mambo kwa njia yoyote ile kama mwanachama au shirika la Makanisa ya Kikristo ya Mungu au kushikilia raslimali au bidhaa kwa jina la Makanisa ya Kikristo ya Mungu katika hata mojawapo ya halmashauri zake au shirika zake.
(3) Kunyang’anywa kwa kitambulisho cha mtu binafsi au kanisa au halmashauri kutaendeshwa na kufuatana na sheria za kidunia zinazochukuliwa katika kumpa mtu haki yake. Aina yoyote ya utanguaji huu lazima ufanywe kwa njia ya kutaarifiana kwanza na kimaandishi. Utaratibu wa maonyo na kurekebishana, umewekwa wazi katika Sura ya 20.
(4) Hatimiliki za mali zote zitatunzwa Makao Makuu ya Halmashauri Kuu Duniani lakini hakuna kazi itakayoweza kushangaza kuonekana imetumiwa na hakimiliki. Itokeapo kufanya mshangazo namna hiyo, kwa mambo yote ya binafsi ya mtu, au warithi wake na wanaochukua mahala pake, wanaweza kuchapisha kazi zao wenyewe kwa manufaa ya watu wote. Ikionekana kuwa mafundisho hayo yanapingana na mafundisho yetu, basi kazi hiyo haitaruhusiwa kuchapishwa na Halmashauri Kuu ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu. Mwandishi anaweza kuondolewa katika ofisi au uanachama kutokana na unyeti wenyewe kama tendo au kipimo cha kumuadibisha. Ni machapisho yale tu yatolewayo kwa kibali cha Makao Makuu ya Halmashauri Kuu Duniani ndiyo yatatumia jina, chapa za shirika na nembo ya Makanisa ya kikristo ya Mungu. Majina yote, chapa za shirika, nembo na hatimiliki za halmashauri za kitaifa, kwa mfano Christen Gemeenten van God, katika Uholanzi, wanafungamanishwa na Makanisa ya kikristo ya Mungu na wamepewa leseni ya kibali na Halmashauri ya Makao Makuu ya Dunia chini ya katiba hii.
Sura ya 8 Uchaguzi
Ibara ya 1:
(1) Halmashauri za Taifa katika vikao vyake vya kawaiada vitateuwa tafuatao:
(a) Kamati ya Kudumu kwa usawa na kanuni zilizowekwa katika Sera za Halmashauri.
(b) Maafisa wakuu na wasaidizi wao katika Halmashauri zao.
(c) Wanachama wa Kamati ya Utendaji.
(d) Makatibu wa Idara/ waangalizi/ washauri na waangalizi wasaidizi.
(2) (a) Wale wote waliochaguliwa katika kikao hiki hatatakiwa kushikilia nyadhifa zao au kusimikwa hadi kikao kijacho cha pili cha Halmashauri za Kitaifa ispokuwa tu kama nyadhifa zao au kusimikwa kwao kwa hapo mwanzo kulisitishwa. Usitishwaji wa nyadhifa kwaweza kufanywa na Halmashauri ya Taifa katika kikao maalumu au na Kamati ya Utendaji.
(b) Baraza la Halmashauri Kuu Ulimwenguni linayo haki na uweza wa kubatilisha uhalali wa leseni za watu au kanisa kufanya mambo yake kama mwanachama au kanasa ndani ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu kwa njia ya kimafundisho au mambo mengine.
(c) Usimamishaji uteuzi kunafanyika kufuatana na maeneo ya kimafundisho ya imani amabayo inapaswa yaelzewe ki waziwazi kama vile ni jinsi gani mwenendo, imani au mafundisho yanapingana na msingi wa imani wa Makanisa ya Kikristo ya Mungu kama yasemavyo katika Ukiri wa Imani. Hakuna afisa anayeruhusiwa kushikilia wadhifa mahali panapo chukuliana na mafundisho yaliyo nje na imani juu ya Mungu mmoja na tofauti moja tu ikitokea itasababisha kutengwa na ushirikiano wa kanisa.
(d) Usimamishaji uteuzi kwa sababu nyingine lazima kutegemee na ubatizo wa huyu mtu anayehusika katika kusimamishwa kuona kama amewahi kufanya makosa kama hayo huko nyuma yake au baada ya kubatizwa kwake. Hakuna mtu atakayeondolewa kanisani kwa ajili ya makosa yaliyofanywa na mtu kabla ya ubatizo na kusamehewa alipozitubu. Mazingira lazima yaamuliwe kwa mujibu wa sheria. Iwapo mtu atafanya maamuzi yenye kuteta madhara kwa kanisa na anakataa kutii maongozi ya kisheria ya wazee na viongozi wa kanisa wanaweza kumfukuza. Kama bado wanaendelea kufanya matendo ya uhalifu hata baada ya kubatizwa wanapaswa pia kufukuzwa. Maamuzi haya yaweza kufanywa kufuata sheria zilizopo za kidunia zinazoaminika kuweza kumpa mtu haki yake. Maamuzi yaweza kufanywa kufuatana na ngazi za kitaifa na kuidhinishwa na Halmashauri Kuu ya Ulimwengu, au yaweza kufanywa kwa ngazi ya Halmashauri Kuu ya Ulimwengu moja kwa moja au vinginevyo ionekanavyo inafaa.
Ibara ya 2:
Vikao vya Halmashauri Kuu ya Dunia au vya Halmashauri ya Taifa kupitia Kamati zao za Utendaji katikati ya mihula yao wanaweza kuanzisha nyadhifa, na kamati kadiri itakavyo amuliwa na kuonekana kuwa inafaa, ili kusaidia kazi na shughuli za baadae na mtu aliyechaguliwa hapo na kubadilisha au kukomesha aina hii ya wadhifa, cheo na kamati.
Sura ya 9 Maafisa
Ibara ya 1: Baraza la Halmashauri Kuu ya Ulimwengu ni kama ilivyoelezewa hapo juu.
(1) Mwangalizi Mkuu atafanya shughuli za Halmashauri Kuu ya Ulimwengu. Atawateua na kuweka wakfu au kuwasimika maafisa. Yeye pamoja na Makamu Mwangalizi Mkuu watafanya maamuzi ya kiasi cha fedha za kuwalipa wafanyakazi kwa idhini ya mabaraza ya majimbo wakitilia maanani kiwango cha mishahara ilivyo katika kamati za taifa.
(2) Makamu Mwangalizi Mkuu atamsaidia Mwangalizi Mkuu kuhitimisha majukuimu ya kila siku ya kanisa. Wanaweza kushikilia nyadhifa nyingine za kijimbo au za kitaifa kama itaonekena kuwa ni muhimu katika kuimarisha uongozi wa kanisa kwa nyakati mbalimbali. Maafisa wote wawili wanao wajibu wa kulinda mafundisho ya kanisa. Pia wanao wajibu katika maongozi ya kanisa. Majukumu ya maafisa wa kanisa kama vile yalivyoandikwa katika Biblia na hasa katika Agano la Kale (mfano katika Waefeso 4:11) yamekabidhiwa maafisa hawa kwa kuzingatia maadili ya nafasi zao. Wanayo mamlaka ya kumweka mtu katika nafasi hizi kwa nafasi zile zenye kufanya kazi za kanisa.
(3) Mwangalizi mkuu na Makamu Mwangalizi Mkuu watasaidiwa na Msaidizi wa Mwangalizi Mkuu atakayepatikana kwa njia ya kura katika mwaka wa Sabato unaofuatia wa 2005 na ndiye atakaye chukua mahala pa Mwangalizi Mkuu na Makamu Mwangalizi Mkuu katika mwaka wa Sabato wa 2012 katika sikukuu ya Siku ya Mwisho Iliyokuu ya sikukuu ya Mwezi wa Saba, iwapo ikitokea kuwa Mwangalizi Mkuu aliyeko leo hatachaguliwa katika duru ya uchaguzi utakapofanyika.
(4) Katibu Mkuu ambaye pia ni Mtunza Hazina Mkuu wajibu wake ni kuhakiki mahesabu ya zaka za zaka na sadaka nyinginezo na michango na kutunza kumbukumbu za kanisa. Katibu-Mtunza hazina huyu pia atatoa ushauri kwa Mwangalizi Mkuu. Usaidizi kama huu wa kiuongozi kutolewa mahala inapobidi utatolewa na Katibu-Mtunza hazina katika kukamilisha shughuli zake.
(5) Katibu Mkuu atasaidiwa na Makatibu Wakuu Wasaidizi wawili.
(6) Maafisa hawa watapokea posho angalau inaolingana na ya Mwangalizi wa Taifa.
(7) Waangalizi wa Majimbo vilevile wanao wajibu wa kuyaangalia mataifa yaliyo ndani ya majimbo yao nao wanapaswa kulipwa posho kama itakavyo amuliwa na ni siasi karibu sawa na Mwangalizi wa Taifa.
Ibara ya 2: Halmashauri ya Taifa
(1) Maafisa wa Halmashauri za Taifa zitakuwa na rais au mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji, ambaye aweza pia kuwa ni Mwangalizi au mzee kiongozi, katibu na mtunza hazina. (Katibu na mtunza hazina aweza kuwa ni mtu mmoja akajulikana kama Katibu-Mtunza hazina). Mzee kiongozi ni mtumishi mkuu wa kanisa la taifa.
(2) Wanaweza kuweko maafisa wengine zaidi kadiri inavyoonekana inafaa na kuidhinishwa na Baraza la Halmashauri Kuu ya Ulimwengu kupitia vikao vyake na wasaidizi wa maafisa kadiri halmashauri iwapo kikaoni au itakavyo amuliwa na kamati ya utendaji. Iwapo kama mwenyekiti hatakuwepo kamati yaweza kumpendekeza mtu atakayeshika wadhifa wa mwenyekiti.
Ibara ya 3:
(1) Rais atasimamia kazi zote za Halmashauri ya Taifa; kufungua na kushikilia uwenyekiti wa kila vikao vya Halmashauri na vilevile kayika mikutano yote ya Kamati ya Utendaji, lakini aweza kutamani mjumbe yeyote wa Kamati ya Utendaji amsaidie kusimamia kikao cha Halmashauri au mkutano wa Kamati ya Utendaji, atakuwa na mamlaka ya kumuita aje kuchukua kiti.
(2) Kazi za Baraza la Halmashauri Kuu ya Dunia, ziko chini ya Mwangalizi Mkuu na Makamu wake.
Ibara ya 4:
Katibu atatunza taarifa za mambo yote yanayoongelewa katika kikao cha Halmashauri kiwe cha ngazi ya Ulimwengu au Taifa na cha mikutano ya Kamati ya Utendaji na kufanikisha kazi nyingine kama hizi zilizo katika shughuli za kawaida za ofisi yake. Kazi za kikatibu za Kamati ya Kijimbo zaweza kuandaliwa na Katibu wa Taifa au afisa yeyote aliyeteuliwa kufanya kazi hiyo.
Ibara ya 5:
(1) Mtunza hazina atapokea fedha zote zilizo mali ya Halmashauri, kuzitunza katika daftari lake la hesabu, na kuzitia kwa kufuata maelekezo ya Kamati ya Utendaji ili kuweka ripoti kamili baadae kwa wakati woye wa vikao vya Halmashauri na kwa wakati mwingine zaidi kama itakavyo hitajika na Kamati ya Utendaji, na kufanya kazi zilizo za kawaida kwa ofisi hii.
(2) Halmashauri ya Taifa zitafanya malipo ya haraka kwa zaka za zaka na makusanyo mengine kwa Halmashauri Kuu ya Ulimwengu.
Ibara ya 6:
(1) Makatibu wa idara na /au washiriki wao/ au waangalizi wasaidizi watafanya kazi chini ya maelekezo ya Kamati ya Utendaji kupitia rais, na atakaa kwenye wadhifa utakaopendekezwa kimahusiano na kazi.
(2) Kazi za Halmashauri Kuu ya Dunia zitafanywa na ama chini ya kazi za Mwangalizi Mkuu au Makamu wake.
Ibara ya 7:
Maafisa wataweka matoleo kwa makusanyo yanayostahili, na mipangilio ya kitakwimu, taarifa na kuhakiki mahesabu ya kazi zilizo katika himaya ya Halmashauri zao kadiri itakavyoonekana kuna ulazima. Vipindi vya kudumu ofisi kama vilivyo elezewa katika maeneo mbalimbali ya katiba hii na wajibu wa ukomo wake vitatolewa kwa kila Halmashauri kwa njia ya katiba hii.
Ibara ya 8:
(1) Maafisa wa kila Halmashauri ya Taifa watashikilia nyadhifa zao kwa maongozi ya Kamati za Taifa. Maafisa wa Halmashauri Kuu ya Ulimwengu watashikilia nyadhifa zao kwa maongozi ya Mwangalizi Mkuu.
(2) Kuondolewa kwenye wadhifa kokote kule kutafanywa kwa mujibu ulioelezwa ndani ya katiba hii ambao unaweza pengine kuwa ni kutokana na mafundisho au nyanja za kiuongozi kwa manufaa ya kanisa.
Sura ya 10 Uteuzi
(1) Halmashauri ya Taifa iwapo kwenye kikao au Kamati yake ya Utendaji viwapo vikaoni:
(a) Watateuwa wawakilishi wake, watumishi, wamishonari, na watu wengine kadiri inavyoonekana ni mihimu kuchukua majukumu ya Halmashauri ya Taifa, na
(b) Inaweza kukomesha au kubadili maamuzi yoyote yahusuyo uteuzi.
(2) Baraza Kuu la Halmashauri ya Dunia kupitia Mwangalizi Mkuu au akiwa hayupo Makamu wake:
(a) Anaweza kumteua hawa wawakilishi watumishi wamishonari, na watu wengine kadiri itakavyoonekana kuna ulazima katika kuchukua majukumu ya Halmashauri, na
(b) Anaweza kukomesha au kubadili aina maamuzi yoyote ya uteuzi.
Sura ya 11 Kamati ya Utendaji
Ibara ya 1:
Katika kila kikao cha kawaida Halmashauri ya Taifa Kamati ya Utendaji ambayo itajumlishwa na rais na katibu na wajumbe wengine kama itakavyoonekana inapobidi kati ya wale kumi na wakawa kumi na moja idadi yao. Asilimia hamsini ya wajumbe waliochaguliwa wa kila kamati za ngazi zote zitaunda idadi yenye kukubalika kikatiba.
Ibara ya 2:
(1) Katikati ya muhula Kamati ya utendaji itasimamia mambo yote ya Halmashauri ya Taifa na itatumia mamlaka yake kama Halmashauri ya Taifa katika kipindi chao kwa mujibu wa Katiba kama isivyojumlishwa kufanywa na Halmashauri ya Taifa iwapo kwenye muhula wake, kama vile uteuzi wa maafisa wake kwa kipindi cha miaka saba. Kamati ya Utendaji itawajibika kwa Halmashauri ya Taifa na maelekezo yahusuyo sara au vingine-vyovyote na taratibu yoyote iliyotolewa au kufanywa na Halmashauri ya Taifa iwapo madarakani.
(2) Kila Halmashauri ya Taifa na kila afisa anawajibika kwenye afisa anayeshughulikia uangalizi wa sera wa Halmashauri Kuu ya Dunia kwa ujumla wake au anayefanya kazi katika jimbo au katika shughuli za kimisheni.
Ibara ya 3:
Kamati ya Utendaji ya kila Halmashauri ya Taifa iwapo katika muhula wake wanaweza kumbadilisha afisa yeyote katika Halmashauri yao au katika Kamati ya Utendaji mjimbe yeyote aliyeko, iwapo tu kama tendo lile litapata ridhaa ya theluthi mbili ya kura za wajumbe wa Kamati ya Utendaji ikiamliwa na kura za kila mtu au kwa saini ya maazimio yaliyopitishwa kwa maandishi na kupelekwa kwa wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji. Nakala zilizo tenganishwa zihusuzo maamuzi yale yanaweza kutiwa saini kwa madhumuni haya. Rufaa kwa ajili ya kitendo hiki itabidi irudiwe tena na Kikao Maalumu cha Halmashauri ambacho kitaitishwa rasmi kwa ajili hiyo. Madai ya rufaa lazima yawakilishwe kwa rais kimaandishi ambaye hatimaye atachukulia hatua pale inapoonekana ni muhimu kuweka Kikao Maalumu cha Halmashauri.
Ibara ya 4:
Kamati ya Utendaji itakaa angalau kwa maramoja kwa mwaka kikao cha kutathmini na kurekebisha ya watenda-kazi walioko katika Halmashauri zake na kuweka sera za mishahara na posho za Halmashauri ndogondogo kama zilivyowekwa.
Ibara ya 5:
Mikutano ya Ziada ya Kamati ya Utendaji yaweza kuitishwa wakati wowote na mahali popote na rais, au kukiwa na dharura yoyote, na Katibu wa Halmashauri ya Taifa au na wajumbe watatu wa kamati husika. Asilimia hamsini ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji itahitajika kutimiliza idadi inayo hitajika.
Sura ya 12 Wadhamini
Ibara ya 1:
(1) Baraza La Halmashauri Kuu ya Ulimwengu litashikilia rasilimali zilizo katika haki yake na linalo haki ya kumiliki ardhi, kujenga majengo, kumiliki rasilimali za vyombo na kuanzisha taasisi Fulani ionakanapo kuna ulazima na kuwa sawia na malengo ya kuendeleza ufanisi wa kazi. Itashikilia hivi kwa muda wa kudumu.
(2) Halmashauri ya Taifa itamiliki ardhi, na kujenga majengo na kuanzisha taasisi fulani au kununua vifaa Fulani kwa mujibu wa kazi zilizoko na wajibu ulio katika Katiba hii.
(3) Ikibidi, shughuli za Halmashauri Kuu Duniani ikitilia maanani mipaka ya Halmashauri yake na ya Halmashauri ya Taifa lingine. Mahali ambapo utendaji kazi jinsi hii ukitokea raslimali zote zitakuwa chini ya mamalaka ya Halmashauri ya Makao Makuu ya Dunia.
Ibara ya 2:
(1) Mahali am wakfu kwa kufanya kazi mbili. Wanaangalia shughuli za kimwili kanisani ili kuwafanya Wazee wajishughulishe na masuala mengine kwa umakini zaidi au mashemasi waweza kuwekwa wakfu kwa majaribio kuona k bapo Halmashauri ya Taifa imeacha kufanya kazi au imejiondoa katika bodi ya Makanisa Ya Kikristo ya Mungu basi mali zilizobakia na hazina vikabidhiwe kwa uaminifu chini ya uangalizi wa Halmashauri Kuu ya Dunia hadi pale kanisa litakapofanywa upya au washirika waliosalia warejeshwe chini ya usimamizi wa Halmashauri Kuu ya Dunia.
(2) Fedha na rasilimali zitahamishiwa katika Halmashauri ya Makao Makuu ya Dinia kulingana na sheria za nchi husika. Zaka ya za ka ni ya lazima kusafirishwa kulingana na makubaliano yaliyofikiwa ili kupata leseni ya Kanisa.
Sura ya 13 Nyadhifa
(1) Huduma zitaundwa na wale wanaoitwa wazee au mashemasi. Wazee ni wahudumu wa kanisa ambao wamewekwa wakfu ili washirikishe Ibada maalum takatifu na kutunza wakfu wao uliopata baraka za kanisa. Wazee wanaweza kuweka wakfu huduma nyingine kwa mujibu wa miongozo ya kanisa. Mashemasi wanawekwa ama watafaa kwa wakfu wa kudumu kuwa Wazee.
Mashemasi hawawekwi wakfu kwa matakwa yao wenyewe. Wanaweza pia kushirikisha ibada maalum takatifu za kanisa, Kubatiza na Ushirika wa Meza ya Bwana. Wazee (na, kama wanavyoitwa, pia Mashemasi) watahusika na uteuzi wa mambo yafuatayo:
(a) Waangalizi wa Halmashauri Kuu ya Dunia nay a ngazi za Kitaifa
(b) Wainjilist kwa usimamizi wa vyuo na huduma za vyombo vya habari. Kibiblia, mashemasi, kama vile Filipo, vilevile aliteuliwa kushika nafasi hii (Matendo 6:5; 21:8)
(c) Wadhifa wa Rais wa Jimbo wa Halmashauri ndogo ni mchungaji mteuliwa. Anaweza kujulikana kama mwangalizi au mchungaji kama itakavyo pendekezwa. Shemasi anaweza kuteuliwa katika maeneo yaliyo ndani ya Halmashauri ndogondogo za Taifa au halmashaurini kama mwangalizi.
(d) Watenda-kazi waliowekwa wakfu katika kila kanisa lazima wawe wazee. Mahali penye wazee zaidi ya mmoja itapaswa awepo mwangalizi au rais aliyeteuliwa. Baraza la wazee katika kila kanisa halitazidi watu saba. Wazee haitakiwi wachaguliwe kwa kujaza nafasi tu kwa vile zipo wazi. Wazee wote na mashemasi wanayo ruhusa ya kwenda kuhubiri katika Halmshauri moja hadi Nyingine. Lakini ni lazima wapewe ruhusa hiyo upya kila katika kila mwaka wa Sabato. Wazee wanachaguliwa kwa kudumu lakini wanaweza tu kuhubiri kwa niaba ya kanisa kwa ruhusa ya Kisabato.
(e) Mashemasi wanaume na wanawake watateuliwa katika kila moja ya makanisa. Baraza la Mashemasi lisizidi watu saba kwa kila kanisa.
(f) Viongozi wa misheni kwa mataifa mengine au majimbo wanaweza kuteuliwa kwa mujibu wa vile inavyosomeka katika (a) hadi (b) hapo juu.
(2) Halmashauri itaweka mikono juu yao walioshika nyadhifa hizi. Rais wa Halmashauri ya Taifa anaweza kuwaweka wakfu wazee na mashemasi kwa mujibu wa mwongozo wa Halmashauri uwapo kwenye kipindi chake cha uongozi. Mwangalizi-Mkuu wa Halmashauri Kuu ya Dunia au Makamu wake au mteuliwa aweza kumweka wakfu kwa wakati wowote na kwa makudio yoyote.
Sura ya 14 Zaka ya Fungu la Kumi
(1) (a) Zaka kama ilivyotolewa katika kitabu cha Mambo ya Walawi sura ya 27; Kutoka 18; Kumbukumbu la Torati 12&26; yanatakiwa yatolewe kwa kila Halmashauri ya Taifa.
(b) Vitabu vya mahesabu vinatakiwa vitunzwe na vikaguliwe.
(c) Halmashauri Ndogondogo pale zilipofunguliwa zitawajibika kutoa zaka za zaka kwa Halmashauri ya Taifa.
(d) Kila Halmashauri ya Taifa itatoa zaka ya zaka kwa Halmashauri Kuu ya Ulimwengu ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu.
(e) Halmashauri ndogondogo zitaanzishwa tu kwa ruhusa ya Halmashauri Kuu ya Dinia na iwapo idadi ya washirika ikikidhi na kwamba uongozi wa ngazi ya taifa umeona ni vigumu.
(2) (a) Zaka zitabidi kuhesabiwa za aina zote yaani zile za kwanza na zaka ya tatu.
(b) Mahala ambapo mfumo wa usalama uko mzuri ulipaji kwa ajili ya usaidizi mwingine unaweza kuachwa.Halmashauri Kuu ya Dunia itaamua lakufanya kwa aina yoyote ya hitaji linalohitaji msaada wa haraka kama isemavyo Sura ya 15.
(c) Zaka ya tatu inaamuliwa kutokana na zaka ya pili ya mwaka wa tatu wa mzunguko wa mwaka wa saba kufuatana na mfumo wa Yubile kama ulivyo elezewa vizuri katika Matamko ya Imani na mafundisho yahusuyo utoaji Zaka na kuchapishwa katika kalenda ya kanisa.
(3) Sadaka zinatakiwa kukusanywa mara tatu kwa mwaka. Kabla ya asubuhi ya siku ya kwanza ya Siku Takatifu ya Mikate isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Vibanda na siku ya Pentekoste, katika kipindi cha sikukuu hizi tatu.
Sura ya 15 Ustawi na Mambo ya Jamii
Halmashauri inawajibika kuangalia jinsi ya kutoa huduma za kimwili kwa watu wake. Halmashauri yoyote yaweza kutoa msaada kwa maeneo mengine kadiri Kamati ya Utendaji itakavyo amua. Uangalizi wapaswa uwe na Halmashauri Kuu na Waangalizi au Wakurugenzi.
Sura ya 16 Vyombo vya Habari
(1) Utungaji wa mfumo wa tovuti, magazeti na machapisho mbalimbali yatapata uangalizi wa Halmashauri ya Makao Makuu ya Dunia ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu yanayoshikilia na kumiliki machapisho yote. Hakuna chapisho linalopingana katika mafundisho ya Halmashauri Kuu ya Dunia.
(2) Halmashauri ya Taifa au zile ndogondogo waweza kuandaa mikakati ya jinsi ya kutumia vyombo vya habari katika maeneo yao kwa kutumia vingozi wasimikwa. Mpango wa vyombo vya habari kitaifa ni jukumu la Halmashauri ya Taifa. Mikakati kwa mataifa mengine huandaliwa ndani ya maeneo husika kama yatakavyo kubaliwa kati ya Halmashauri Kuu ya Ulimwengu ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu na Halmashauri ya Taifa na Halmashauri ya Jimbo nchi husika kama, zile halmashauri ndogondogo zaweza kutoa usaidizi kama unavyotakiwa chini ya kifungu cha (1) au (2) hapo juu.
(3) Hatimiliki za kila shughuli hutunwa Halmashauri Kuu ya Dunia ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu isipokuwa ikiwa kama inavyosema Sura ya 7 ibara ya 2 (4) hapo juu.
(4) Mikakati ya Vyombo vya Habari Kitaifa na Kwa maeneo enyeji itafanyiwa uhakiki na Halmashauri ya Makao Makuu ya Dunia ili iendane sawa na mafundisho ya msingi na Matamko ya Imani.
(5) Sifa za kielimu au kabrasha zinazofanana na hizo ni lazima zipitiwe na Waangalizi wa Taifa wa Kamati za Utendaji na zitumwe kwa Makao Makuu ya Ulimwengu kwanza ili kupata idhini kupitia machapisho kwa halmashauri yoyote nyingine.
Sura ya 17 Sikukuu na Halmashauri
(1) Halmashauri ya Taifa zitawajibika kuandaa na kuamua na jumuia zao ndogondogo ni mahali gani kati ya Sikukuu hizi wafanyie yaani mahali ambapo watu wa Halmashauri yao watakapokutanika kufanyia Sikukuu ya Pasaka, Pentekoste na Sikukuu ya Vibanda kama inavyotakiwa katika Kumbukumbu la Torati 16:6 na Mambo ya Walawi 23.
(2) Sikukuu na Mahali pa kukutanikia watu walio katika Halmashauri vitakuwa ni wajibu wa wenyeji wa maeneo yale na jumuia zao kadiri zilivyoanzishwa. Zaweza kufanyika kwa pamoja na mkabala na jimbo lingine katika maandalizi mazuri yaliyotarajiwa. Umbali kati ya kambi moja na ya halmashauri nyingine waweza kuwekewa utaratibu na uongozi wa Halmashauri Kuu ya Dunia.
Sura ya 18 Nyakati
(1) Nyakati za kufanya shughuli au Sikukukuu za kila mwaka zitafanyika kwa mujibu wa jinsi kalenda inavyosema kama ilivyokubalika na Halmashauri ya Makao Makuu ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu ikiwa pia ni kwa mujibu wa Sheria za Kibiblia ambazo zimezingawa katika maamuzi yao. Chanzo cha upatikanaji wa hizi Siku Takatifu kimetokana na hesabu ya kalenda ya sayari yaani maadhimisho ya Mwandamo wa Mwezi Mpya katika ujumla wake kama ilivyoelekezwa.
Siku Takatifu kama zinavyo someka katika Kitabu cha Mambo ya Walawi 23 na kutoka maandiko yanayohusisha Miandamo ya Miezi ni:
a) Sabato ni ya milele kwa kila siku ya saba ya juma, ambayo kwa sasa hujulikana kama Jumamosi, kulingana na hesabu zinazoendelea. Inamaana kuanzia siku ya Ijumaa jua linapo zama hadi Jumamosi jua linapozama
b) Sikukuu ijulikanayo kama Pasaka ambayo hudumu kwa siku mbili.
Siku ya kwanza au Ushirika wa Meza ya Bwana hufanyika katika siku ya 14 ya mwezi wa Nisan, siku inayofuatia ya 15 Nisan kunakuwa na mlo wa Pasaka sawa na Kutoka 12, na ni Sikukuu ya Kwanza ya Mikate isiyotiwa Chachu.
c) Pentekoste inaanza kuhesabiwa kuanzia Siku ya sadaka ya Mganda wa Kutikiswa Jumapili inayoangukia wakati wa Sikukuu ya Mikate isiyotiwa Chachu na inapaswa kuwa Jumapili.
d) Sikkukuu ya Baragumu, Upatanisho na Vibanda au Mabua kuadhimisha mwezi wa saba uitwao mwezi wa Tishri, unapatikana kwa kuhesabu kutoka Mwandamo wa Mwezi Mpya wa mwezi wa saba kwa kufuatana na anga za juu.
e) Mwandamo wa Mwezi Mpya huadhimishwa na kila Siku ya Kwanza ya Mwezi wa Kwanza ni siku ya mapumziko na kutaniko takatifu.
Sura ya 19 Ushirikishi Mkuu
(1) Halmashauri hii itautambua uanachama wa Halmashauri Kuu ya Dunia ya Makanisa ya Mungu pale yalipoanzishwa na kule yanakofanya huduma zake kwa mujibu wa sheria za Mungu. Uanachama huu utaendelea kadiri unavyotambuliwa na makanisa yaliyopo hai yanayotaka kuwa na uhusiano shirikishi na Halmashauri.
(2) Makanisa ya Kikristo ya Mungu hutambua uhalali wa ubatizo wa mtu mzima uliofanyika na washirika ambako kama Makanisa hayo ni Makanisa ya Mungu yanayoishika Sabato kwa kufungamana na washirika hao wamebatizwa katika mwili wa Yesu Kristo, kwa jina la Baba na kwa nguvu za Roho Mtakatifu, na sio kutoka katika aina yoyote ya mfumo ujiitao ukristo au dhehebu. Hali hii ya kuumtambua uhalali huu umaanisha pia kuwa mtu hatalazimishwa kubatizwa upya. Miongozo katika makanisa maalumu itaamuliwa na Halmashauri Kuu ya Dunia ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu.
Sura ya 20 Marekebishano
Ibara ya 1:
(1) Kila mshirika wa Kanisa aweza kuwa ni chanzo cha kufikisha hali ya kurekebisha masikitiko. Kila kanisa lapaswa kuweka utaratibu wa mahali pa kusikiliza mashauri au mashitaka itakayo endeshwa na wazee, mashemasi na kutaniko lote au kiasi fulani cha wingi wa watakao fika kusikiliza shauri kwa siku 30 au kama watakavyo kubaliana pande zote.
(2) Rufaa za jumuia ndogondogo kadiri zilivyoanzishwa au za muda Halmashauri ya Taifa iwapo madarakani au kwa vipindi maalumu. Wakati Halmashauri Kuu inapoingilia mwelekeo wa utaratibu mzima utaamuliwa kutoka kwa Halmashauri Kuu ikisaidiwa na Halmashauri ya Taifa ikiwa ni lazima.
Ibara ya 2:
(1) Hakuna mshirika ambaye ataachwa kushirikishwa kwakuwa ameondolewa ushirika wake na kanisa (ambaye amepingwa kwa sababu tu alikiri kuwa hakuipiga kura ushirika wa kanisa) mbali na sababu za Kibiblia ambazo zitawakilishwa kwao kwa njia ya maandishi. Tangazo lake nilazima lichukue muda si chini ya wiki tatu kabla ya siku iliyopangwa na wajumbe wawe na fursa ya kuja kwenye kutaniko kma isemavyo ibara ya 1 hapo juu, ambapo mhusika anaweza kuachilia madai yake. Iwapo mshirika atashitakiwa kwa kosa la kufanya fujo au magomvi au kusababisha migawanyiko au kukosa uaminifu kwa Kanisa lazima ihakikishwe kwanza kama ni kweli kuwa mshirika huyo ni kweli alikuwa anafanya hila za kuligawa Kanisa na kwamba ni kinyume na yasemavyo maandiko katika Biblia (zaidi ya zisemavyo sheria mbalimbali au hii Katiba).
Kila mshirika anatakiwa aheshimu katiba ambayo pia inajumlisha kanuni ndogondogo zinazokubalika katika jamii zetu.
(3) Kuondolewa katika wadhifa kwa ajili ya tofauti ya kimafundisho hakuwezi kumrekebisha mtu katika kifungu hiki. Makanisa ya Kikristo ya Mungu yanayo haki kusimamisha mkataba wa ajira inapohitajika ndani ya kipindi cha mkataba uliowekwa wakati kila upande wa sehemu ya kazi na makumaliano ya kipindi cha majaribio. Iwapo hali kimakubaliano itakuwa mbaya basi kunaweza kutafutwa njia ya kusuluhisha na ikishindikana sheria za kidunia za nchi husika zitatumika.
Sura ya 21 Wahasibu, Fedha na Malipo
Ibara ya 1:
(1) Kila Halmashauri itakuwa na utaratibu wa utunzaji fedha (account) ambayo itakaguliwa kila mwaka.
(2) Taarifa za Fedha za kila mwaka lazima zihakikiwe katika ngazi ya Halmashauri ya Taifa na zitumwe kwenye Halmashauri Kuu ya Makao Makuu ya Ulimwengu
(3) Mwaka wa Fedha unaanzia siku ya 1 ya mwezi wa Nisan hadi siku ya 1 ya Nisan ijayo kwa kufuata kalenda ya Kanisa.
(4) Makabrasha yote yatawasilishwa na maafisa wa kila Halmashauri, wajulikanao kama Wenyeviti na Makatibu.
(5) Akaunti za Bank zitafunguliwa na Katibu na Mtunza Hazina kutoka katika Halmashauri mbalimbali kwa maelekezo ya maafisa wa Halmashauri husika. Kanisa laweza kuwa na Akaunti yake yenyewe. Akaunti nyingine zote ziwe chini ya usimamizi wa Mtunza Hazina kwa kufuata maelekezo ya Kamati ya Utendaji au Mwangalizi Mkuu.
(6) Halmashauri ya Taifa hairuhusiwi kukopa fedha bila idhini ya Halmashauri ya Makao Makuu Duniani.
(7) Waangalizi, Wakurugenzi na Maafisa wa Kanisa lazima walindwe na shughuli zisizo muhimu zifanyikazo katika Halmashuri wanazozitumikia.
(8) kila Halmashauri ijiwekee bima inayoaminika kwa shughuli zake ili kulitambulisha kanisa kwa minajiri ya kulilinda na hasara zitokanazo na mambo ya ajali au kujeruhiwa.
(9) Kiasi kinachotakiwa kwa kuchangishwa kwa washirika itokeapo dharura ya michango Halmashauri zao na zile za shirikishi au matawini na walioko katika ushirika haitakiwi kuzidi kiasi cha Dola za kimarekani (US$) 20.00 au kitu kilicho na thamani sawa na hii.
Ibara ya 2 Muhuri wa Utambulisho
Muhuri unaotumika kulitambulisha Kanisa utatunzwa na Katibu Mkuu kwa niaba ya Mwangalizi-Mkuu ambaye atatoa maelekezo ya jinsi ya kuutumia. Halmashauri ya Taifa yaweza kuruhusiwa kuwa na mihuri ya utambulisho kwa Halmashauri zao za Taifa ambayo itatumika kwa maelekezo ya Kamati za Utendaji kwa mujibu wa mingozo ilivyowekwa na Halmashauri ya Makau Makuu.
Ibara ya 3 Wajibu wa Kuwa Mwanachama
(1) Kila mtu aliye batizwa anaruhusiwa kujiunga na ushirika wetu kwa kupata idhini na Kamati ya Utendaji ya Halmashauri ya Taifa na kama ilivyoelezewa kwenye Katiba hii chini ya usimamizi wa Halmashauri Kuu ya Dunia. Watu waweza kukubaliana kuupigia kura uanachama kwa mwaliko baada ya kipindi cha matatizo.
(2) Wajibu wa mwanachama utarekebishwa kufuatana na ngazi za Halmashauri ya Taifa au ya Ulimwengu. Kuruhusiwa kuwa mshirika hakuna maana ya kuwa ni kurusiwa kupigiwa kura miongoni mwa wanachama wa kanisa. Taarifa za aina hizi zote mbili za ruhusa yabidi zitunzwe na Makatibu wa kila ngazi.
Sura ya 22 Masahihisho
(1)(a) Katiba hii inaweza kufanyiwa masahihisho kwa maamuzi ya Halmashauri Kuu ya Dunia ya Makanisa ya Kikristo ya Mungu iliyo kwenye kipindi chake cha uongozi kwa kupitishwa na uwingi wa wajumbe usiopungua chini ya theluthi mbili za wajumbe waliopiga kura na kukubalika pia na mamlaka ya kura ya turufu za Mwangalizi-Mkuu.
(b) Hakuna masahihisho yatakayofanywa mpaka kwa ruhusa ya Mwangalizi-Mkuu.
Masahihisho ya Katiba ya Taifa yasipingane pia na Katiba hii kuu na itakubalika kwa idhini ya kamati ya utendaji. Tangazo la kufanya hivyo kwa katibu muhutasi si chini ya kipindi cha miezi miwili za kalenda yetu kabla ya siku ya kufanyika kwa Kikao na kwa hali kama hizo tangazo la kukaa kikao lazima libandikwe likielezea nia ya mashahihisho hayo.
(2) Kabla ya masahihisho yaliyokusudiwa ya Shirika ndogondondogo, kwa maana ya Katiba za Halmashauri za Majimbo au Taifa ziwe zimekabidhiwa kwa Halmashauri iliyoko madarakani na itapendekezwa na Kamati ya Utendaji ya Halmashauri Ndogondogo (kama zipo) kwenda kwa Kamati ya Utendaji ya Halmashauri ya Taifa ambayo itafikiria masahihisho yale na kutoa taarifa mbele yake kwa njia ya maandishi kwa Halmashauri Kuu ya Dunia iliyoko madarakani na hatimaye kwenye kikao chenyewe.
MWISHO!