Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[076D]
Madhara
Yaliyoyakumba Makanisa ya Mungu Katika Karne ya 20 Kuhusu Fundisho
la Asili ya Mungu
(Toleo La 1.0 20110312-20110312)
Kwenye jarida hili tutaainisha baadhi ya makosa mkubwa kwenye Makanisa ya
Mungu yaliyoingia katika karne ya 20 pamoja na imani ya Kiditheism ya
Herbert Armstrong.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki ©
2011 Wade Cox)
(tr. 2016)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani
yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe Hakuna malipo
atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu
fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila
kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya
pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Madhara
Yaliyoyakumba Makanisa ya Mungu Katika Karne ya 20 Kuhusu Fundisho
la Asili ya Mungu
Tuliyaeleze
makosa ya Herbert Armstrong kwenye jarida la Imani ya Kiditheism (Na. 76B).
Kosa hili la Uditheism limeelezewa kwa kina kwenye kile kinachoonekana
kuwa ni hata kama nj kufuru kubwa sana kwa upande wa mtumishi wa zamani wa
lililokuwa kanisa la WCG na ambaye alikuwa ni muumini mwaminifu wa Herbert
Armstrong, lililoonekana sana kuwa ni sehemu ya ibada ya sanamu. Sambamba na makaribisho
ya maelekezo ya uwongo na sababu za uwongo, mtumishi huyu pia alidai kwa wazi
sana kwamba Herbert Armstrong alivuviwa na Mungu kwenye muono wake na hususan kwenye
suala hili la Asili ya Mungu. Alipinga kwamba kwa kiasi fulani na mabashiri ya
Armstrong inamaana kwamba mtu anamchukia Armstrong. Ni suala la kufikiri tu
kwamba kutokubaliana na nafasi ya kitu chochote hakumaanishi kwamba mtu anamchukia
mtu anayefanya makosa. Ka kweli, huu ni msimamo wa Kibiblia au makatazo kwa wateule
wote na ulitolewa kwa Waberoya walioyatafiti Maandiko Matakatifu kila siku ili
kuona kama kilichosemwa kilikuwa ndivto kilivyo.
aliufuata mtazamo wa kaaida wa Armstrong kwamba Mungu Baba hakua
anajidhihirisha kwenye Agano la Kale kwa mtazamo kwamba Amri ya Kwanza yaimtaji
Mungu Baba bali kwa Yesu Kristo. Kwa hiyo, usemi wa kwamba “Usiwe na miungu
mingine ila Mimi” unamaanisha kwamba usiwe na mingu mingine ila Yesu Kristo.
Hakuna yeyote miongoni mwa maafisa wa CCG aliyelielezea WCG kwamba wamelijadili
jambo hili na alisikia kufuru hii ikitamkwa kwenye kanisa la WCG au kwenye
makanisa yaliyochipuka hapo kabla yake. Baadhi ya fafanuzi zao zimeorodheshwa
hapo chini.
sasa inaweza kuwa kwamba mwamini utatu au Mtrinitarian anaweza kudai kwamba
amri hii inamlenga Baba, Mwana na Roho Mtakatifu wakiwa kama mkusanyiko wa
Utatu. Lakini hatujawahi kusikia kabisa hata Mtrinitarian akidai kufuru kama hiyo.
Hii ngito misingi
ya madai ya mhubiri wa zamani wa WCG. Mtu huyu hana kanisa na hivyo anaweka
sawa na kufundisha msimamo wake pasipo mamlaka yoyote ya kimpangilio. Jambo
hili linahitaji kulielezea kama upanuzi mzuri wa Uditheism wa Armstrong nan i
uzushi mkubwa sana.
Mtunzi: Frank W. Nelte
tarehe: Machi 1994
MUNGU KENYE AGANO LA KALE NA UELEWA WA WAYAHUDI
“Sasa hebu na tutazame kwenye Kutoka sura ya 20.
5) Kumbuka kuwa Kutoka 20 kwa kweli inasema hivi:
Mungu
akanena maneno haya yote akasema, Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika
nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. Usiwe na miungu mingine ila mimi. (Kutoka 20:1-3)
A) Ni MANI aliyekuwa anayanena maneno hayo? Jibu lake ni kwamba YESU KRISTO!
B) Ni kwa namna GANI basi Kristo alijitambisha mwenyewe kwa Waisraeli? Jibu ni
kama kwamba "YHWH Elohim wenu aliyewaleta Israeli mtoke kutoka Misri".
UTAMBULISHO HUU NI WA MUHIMU SANA!
C) KWANINI utambulisho huu imetuama kwenye amri 10 za Mungu? Tutaona zababu ya
jambo hili kwa kipindi kifupi.
D) Ni NINI kwa kweli kinacholengwa au kukusudiwa na andiko la Kutoka 20:3? ...
"Usiwe na miungu mingine ILA MIMI"? ni NANI anayesema maneno haya?
je, ni Yesu Kristo ndite Msemaji wa aya hizi, akisema: ‘usiwe na miungu mingine
ila Mungu Baba’?
HAPANA, hicho sicho alichosema! Kristo aliwaambia israeli ‘mbele YANGU’!
Tunaweza kuishikilia tafsiri ya wazi ya Kutoka 20:3? Israeli hawakujua kwamba
kulikuwa na ‘Mungu Baba’.
Alikuwa hajafunuliwa kwao na Kristo. Yesu Kristo Mwenyewe alikuwa
anashughulika na taifa la Israeli, na aliwaambia wasiwe na miungu mingine ila
yeye, Yesu Kristo.
Aliamua kujidhihirisha kwao kama ‘YHWH, Elohim wako’ aliyewatoa kutoka nchi ya
Misri.
E) Je, Kristo alikuwa anajiweka mwenyewe mbele za Mungu Baba kwa kuwaambia
Israeli wamwabudu yeye, Yesu Kristo?
HAPANA, sivyo kabisa! Mungu Baba na Yesu Kristo waliamua na kukubaliana kwamba
Kristo ndye awe wa kufanya uumbaji wote;- Kristo ndiye angekuwa wa kushughulika
na wanadamu hadi mpango mzima wote wa wokovu utakapokamilika;
- Kristo alijidhihirisha mwenyewe kwa Waisraeli;
- Kristo kwa mapema sana kabla ya ujio wake wa kwanza, angekuwa na uwepo
wa Baba uliofichwa na Baba katika Israeli kwa ujumla;
- Kwenye Agano la Kale, nyakati za Kristo zingedhihirika tu kwa wateule
wale wale tu wachache waliochaguliwa, kwa sababu azijuazo Mungu mwenyewe;
- Ni kwa ujio wake huu tu ndipo Kristo angeudhihirisha uwepo wa Mungu
Baba kwa wanadamu;...”
Madai ya nyingeza yanatuama
kwenye mikururu ya matukio ya uwongo ya sababu za uwongo na madai ya uwongo
kwamba Mungu Baba hakufunuliwa kwenye Agano la Kale. Kumbuka kwamba fafanuzi
zilizotiliwa chumvi ni kwamba kulikuwa na mjadala na Kristo alikubali kufanya
uumbaji wote na kwamba ‘alishughulika na wanadamu hadi pale mpango wote mzima
wa Wokovu ulikamilika.”
Kisha madai ya
uwongo yalifanywa kwamba Kristo alifanya uwepo wa Baba ufichwe na usijulikane
na Waisraeli kwa ujumla. Aliudhihirisha uwepo wa Baba kwa wateule wachache tu. Sasa
ilikuwa ni kwa kutokana na uwongo huu wa teolojia potofu na ya uwongo ya
Armstrong fundisho hili lilijengwa na lilikuwa ni kinyume na yanavyosema
maandiko mengi kadhaa kwenye Agano la Kale na nukuu za Agano jipya zilizotoholewa
kama rejea kutoka kwenye Agano la Kale.
Madai meingine
yanayofuatia ya uwongo ni yale yanayodai kwamba elohim ni wa “uwingi wenye
muunganiko” na neno linalotumika linaonyesha kumhusu Yesu Kristo peke yake.
Ukweli ni kwamba ni neno la uwingi. Hakuna kitu kama hicho kisemwacho kuwa ni
uwingi jumuisho wala neno kama hilo isipokuwa ni kwamba neno elohim linataja
washiriki wa daraja fulani. Wakati linapotumika na kiambishi cha kama Ha
Elohim, kama Elohim Mwenyewe, inaaminika kuwa inamtaja Baba. Kuna idadi kadhaa
ya maneno kwenye Agano la Kale yanayotumika kwa ajili ya Mungu kwamba yanamtaja
Baba peke yake kama Mungu Mmoja wa Kweli na majina yanaonyesha tofauti iliyopo
kati ya Mungu na elohim ambao ni wana wa Mungu.
Baba ndiye
muumbaji na anajulikana kwenye Agano la Kale kwa maeneo mengi sana. Kushindwa
kuyajua majina ya Mungu walikokuwanako kanisa la WCG na tofauti iliyokuwepo
kati ya Baba na wana wa Mungu ambao ni elohim ni kosa au tatizo kubwa sana
kwenye teolojia na upotoshaji wa maelezo yao kuhusu Mpango wa Mungu na
kuyaelewa maagano ya Kale na Jipya. Ilikuwa ni kwa sababu hii ndipo hawakuweza
kumshawishi mtu yeyote kuwaami kutoka jamii ya Kiislamu, au mtu yeyote bali ni msaada
mkubwa kutoka kwa wa SDA na vikundi vingine vya Makanisa ya Mungu na wachache
sana kutoka kwenye dini ya Kiyahudi.
Dalili za makosa haya
ni mafundisho mapotofu na mtazamo huu haukuwa umesikika kamwe kabisa
yakitangazwa kwa wazi sana na kimakosa kabisa kama ilivyokuwa kwenye huduma ya WCG
au makanisa yaliyochipuka kwenye kanisa hilo ya huko Australia au kutangazwa
kutoka Marekani. Waandishi wengine wa jarida la Uditheism (Na 076B) waliulizwa kama waliwahi kusikia
mafundisho haya mapotofu yakifundishwa kwenye kanisa la WCG au kwenye makanisa
haya yaliyochipuka kutoka kwenye kanisa hilo kongwe.
Mmoja wa
Makodineta wa CCG nchini Marekani aliulizwa kuhusu jambo hili. Alizaliwa kwenye
kanisa la WCG, na akahudhuria mafunzo kwenye chuo kilichojulikana kama Ambassador
College, na akakitangaza chuo hicho kwenye jimbo la AC na kukipeleka huko nchini
Jordan. Mtazamo wake ulikuwa ni kama ifuatavyo:
“Baada ya kuyasoma baadhi ya maandiko yake, kwa kweli sikuweza
kushangazwa sana kama kitu kama hicho kinatokea kwa mchungaji wake wa zamani wa
kanisa la WCG wakati teolojia yake ilipotuama kwenye ukweli wa kwamba kitu
chochote anachokisema Herbert Armstrong hakimfanyi yeye kumuona mzee wa kanisa
afananishe na kile kinachosemwa na maandiko matakatifu kuhusu masuala yahusuyo
asili ya Mungu na ya watoto wake wakati Armstrong alipokuwa anasimamia kwenye
msimamo kwamba Mungu alikuwa na mtoto mmoja tu, licha ya maandiko kwenye Ayubu
na penginepo kueleza watoto wengi wa Mungu kuepo kabla ya kuja na kuzaliwa kwa
Kristo ulimwenguni (Mwanzo 6:2,4, Ayubu1:6, 2:1, 38:7) kinyume kabisa na imani
ya Herbert.
Msimamo rahisi na wa pekee kwamba Yesu Kristo ni mwana wa Mungu ungemaanisha
kwamba aliumbwa na a kwamba aliumbwa na Mungu Baba. Na hiki ndicho
wanachokifanya mababa - wanazaa watoto. Vinginevyo utakuwa umejiunga na filosofia
ya waamini Utatu ya uwingi wa miungu na ya kupenda. Ahh, lakini kama Armstrong hakuwahi
kufikiri hivyo, basi ukweli ni lazima uwe umeyumbishwa au kupotoshwa.
kisa hiki cha wachungaji kuwapofusha watu kwa kuwaingiza kwenye ibada za
sanamu, watu wa kada zote za madaraja na kuyatafsiri maandiko kwa kutumia
mitazamo waionayo wao kuwa ina mashiko kwenye tafsiri ya maandiko matakatifu.
Usemi au maelezo haya ya kwamba amri ya kwanza haikusudii kumtaja Mungu Baba na
badala yake inamtaja au kumlenga Yesu Kristo ni wazi sana kwa mara ya kwanza
niliisikia kwenye kanisa la WCG. Hii inanifanya nishangae kwamba ni watumishi
wangapi wa lililokuwa hapo zamani kanisa la WCG huenda walikuwa karibu sana na
imani hii. Hawezi kua ndiye huyu wa pekee na wa kweli.
kwa kweli hii inaonyesha dalili ya kwamba tunapaswa kumwabudu Yesu Kristo, na
tena inakwenda moja kwa moja kinyume na mafundisho ya Kristo ya kwamba tumwabudu
Mungu (Baba) peke yake kwa kuwa ni yeye tu ndiye aliye mwema (Mathayo 19:17, Marko
10:18, Luka 18:19), na maelekezo aliyyotupa Kristo katika kumuomba Mungu Baba.
Hii inanifanya mimi nifikirie kwamba mtu anayeamini hivi anaweza kuwa anamuomba
Yesu Kristo.
mfuasi yeyote wa Herbert Armstrong kwa kweli angedhani na kuona kama ni kufuru
kusema kuwa Kristo alikuwa ni mwana wa Mungu aliyekuwepo tangu hapo nyuma kabla
ya kuzaliwa kwake rasmi duniani aliyekuwepo pamoja na wana wengine wengi wa
Mungu na Kristo akiwa ni kama ndugu yao, au mshirika au ndugu pamoja nao.
Lakini tunajua ni wapi inakoelekea. Ni mkakati wa kuwapofusha tu kunakofanywa
na upotoshaji wa makusudi wa maandiko matakatifu wakati akisema azi kabisa
kwamba Mungu Baba, Mungu wa Yesu Kristo ambaye yu wa chini ya Mungu na ndiye
mwana wa Mungu, alitiwa mafuta na kuinuliwa kuliko ndugu na wenzake wote
(Waebrania 1:9). Kimsingi inasema kwamba kabla ya mtiwa mafuta huyu kutoka kwa
Mungu wake alikuwa ni wa daraja sawa tu na hawa wenzake.
Ni kweli, hii ni sahihi, na siyo teolojia ya Herbert Armstrong ya mfumo wa
imani ya kwamba miungu ya kweli ni wawili, na kama haikubaliki kwenye
mafundisho yasiyo na mashiko na mapotofu ya Herbert Armstrong, teolojia
inayopinga na kwendana kinyume na biblia haitaingia akilini kwao pasi kujalisha
ni maandiko mengi kiasi gani yaliyokosekana kuthibitisha jambo hili la kufuru.”
Mtazamo wa maafisa kuhusu andiko la Waebrania 1:9 unaendana kabisa na wa
Frank Nelte aliyekwenda kulinganisha na Zaburi 45:6-7. Tumesikia pia wengine
wakionyeshwa kwenye Zaburi 45:7 wakidai kuwa andiko hilo linawataka wateule wa
kanisa lililotajwa hapo juu ambamo Kristo alitukuzwa na kuinuliwa juu. Hata
hivyo, andiko la Waebrania linafanya hilo lisiwezekane au iwe vigumu na
inathibitisha pia Baba kuwa alijulikana kwenye Agano la Kale kama ilivyokuwa
imenukuliwa kwenye Waebrania 1:5, hususan ukweli kuhusu Mungu na Mwana wa
Mungu. Uhusiano huu ulithibitishwa pia kwenye Mithali 30:4-5 ambako jina la
Baba lilitambulika kwa wazi sana kama Eloa, Mungu wa Agano la Kale.
Waebrania 1:1-4 inasema:
[1]
Mungu, ambaye alisema
zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana,
aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. 3 Yeye kwa
kuwa ni mng'ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa
amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume
wa Ukuu huko juu; 4 amefanyika bora kupita malaika,
kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao.
(Tafsiri ya RSV inatumia neno kotekote vinginevyo ni kama imenena
kinyume chake.)
Kristo anatajwa hapa kuwa amefanyika kuwa ni bora zaidi ya malaika kwa
maana kwamba hakuwa wakato wote hivyo. Ni kweli kwamba alikuwa ni sehemu ya
Malaika akiwa ni kama Malaika wa Uwepo wake, au Malaika wa Bwana, katika Israeli.
Kumbuka kuwa Mungu anaonekana hapa kama anaongea ka kupitia manabii wa
zamani. Kwa hiyo kitendo cha kudai kwamba manabii hawakujua kuwa Mungu
alikuwepo ni madai ya kipuuzi kutokana na andiko la Agano Jipya lenyewe. Kristo
hapa alifanywa kuwa ni mrithi wa mambo yote. Sisi pia tu warithi pamoja naye.
Maneno yaliyo kwenye tafsiri ya KJV ya “Kwa yeye mwenyewe” na “yetu” yameongezewa
kwenye maandiko ambayo hayakuwepo kwenye maandiko ya zamani na yaliongezewa na
Watrinitarian kwa lengo la kuhalalisha maandiko waliyoyakusudia kuyaanikisha.
Andiko hili kwa Kiebrania yamepotoshwa au kutumiwa vibaya na
Watrinitarian na Waditheis/Wabinitarian wakidai kwamba Kristo kila wakati
alikuwa ni wa tofauti na pia juu ya Jeshi la Malaika wakati Biblia inseam wazi
sana kwamba siyo kweli. Mtazamo wa namna hiyohiyo uliingia kwenye imani ya Kikristo
ukitokea kwa waongofu aliotokea kwenye imani ya mungu Attis wa huko Roma na ikaanza
kuenea mnamo mwaka 170 BK. Habari hii imeelezwa kwa kina kwenye jarida la Imani za Ubinitarian na Utrinitarian (Na.
076) na hasahasa kwenye jarida la Upotoshaji wa Wabinitarian na Watrinitarian
Kuhusu Teolojia ya Zamani ya Uungu (Na. 127B).
Andiko lililoko kwenye Waebrania 1:2 limepotoshwa na kutafsia vibaya
kusema “kwa yeye aliyeiumba dunia pia,” wakati neno lenyewe halisemi dunia bali ni kiambishi cha aion lenye maana ya zama au umri.
Andiko hili hapa linaonyesha kuwa uwepo wa Baba ulijulikana na kutangazwa
kutoka kwenye maandiko mengi ya Agano la Kale lakini mifano hii imepuuziliwambali
na wafuasi wa Armstrong.
Waebrania 1:5 Kwa
maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo
nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?
Aya ya 5 imeinukuu Zaburi 2:7[8] (kwenye tafsiri ya the Septuagint
(LXX), soma tafsiri ya Brenton). Zaburi 2:2 pia inamtaja Bwana Yahova na dhidi ya
mtiwa mafuta wake, ikiwataja viumbe wawili, na aya ya 7 inaonyesha kuwa andiko
hili linawataja Baba na Mwana. Hivyo
kwenye andiko hili tunajionea wazi sana kwamba Baba na Kristo wanatajwa na Yahova
kwenye aya ya 2 ni Baba kama jina au neno la kiuzaa tu. Neno Yahova kwenye aya
ya 4 lilipotoshwa kwa kubadilishwa kuwa Adonai kwenye tafsiri ya the Sopherim kwenye
kipindi cha baada ya kuangamizwa kwa Hekalu ili kupotosha maana halisi
iliyokusudiwa. Andiko lililotafsiriwa mwana
wa pekee lina maana ya moja kwa moja ya aliyekuzaa. Maneno haya yamechukuliwa na Bullinger kuwa ni kwenye
Ufufuo wa Wafu wakati Kristo atakapokuwa “kiongozi wa taifa huru tukufu wa aina
mpya ya viumbe” (kutokana na Matendo 13:33; soma tafsiri ya Companion Bible sawa na Waebrania 1:5). Andiko
hilo liloendelea kwenye aya ya 5 na linasema “Na tena, Mimi nitakuwa
kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana” linatohoa kwenye 2Samweli 7:14 ambalo
linamhusu Mungu na kumtaja Kristo. Mungu anajidhihirisha kwa Nathan kwamba uzao
wa Daudi utamzalia yeye mwana kutoka kwenye aya za 12-16.
Kwa hiyo Daudi aliambiwa na Mungu, kwa kumtumia Roho Mtakatifu kwa
kupitia Nathan kwamba Mungu atamleta Mwanae (Kristo) kutoka kwenye uzao wa Daudi.
Kwa
hiyo madai ya Armstrong ndipo yanathitika tena kuwa ni ya uwongo.
2Samweli 7:12-17 Nawe siku zako
zitakapotimia, ukalala na baba zako, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayetoka
viunoni mwako, nami nitaufanya imara ufalme wake. 13 Yeye
ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu, nacho kiti cha enzi cha ufalme wake
nitakifanya imara milele. 14 Mimi nitakuwa baba yake,
naye atakuwa mwanangu; akitenda maovu nitamwadhibu kwa fimbo ya binadamu na kwa
mapigo ya wanadamu; 15 lakini fadhili zangu
hazitamwondoka, kama vile nilivyomwondolea Sauli, niliyemwondoa mbele yako. 16 Na nyumba yako, na ufalme wako, vitathibitishwa milele
mbele yako. Nacho kiti chako kitafanywa imara milele. 17 Kwa
maneno hayo yote, na kwa maono hayo yote, ndivyo Nathani alivyonena na Daudi.
Andiko la Waebrania 1:6 linalitaja andiko hilo kama prototokos au mzaliwa wa
kwanza ilivyonukuliwa kutoka kwenye Kumbukumbu la Torati 32:43 kwenye tafsiri
ya the LXX (cf. Ps. 97:7).
Waebrania 1:6 Hata tena, amletapo mzaliwa wa kwanza
ulimwenguni, asema, Na wamsujudu malaika wote wa Mungu.
Andiko la kwenye tafsiri ya the LXX linasema kwenye aya hii: “Furahini enyi mbingu pamoja naye na Malaika wote wa Mungu na wamwabudu (proskuneo – msujudie) yeye. Furahini enyi Mataifa pamoja na watu wake na hebu ana wote wa Mungu ajitie nguvu katika yeye.”
Neno la asili lililotumiwa kutaja wana wa Mungu ni pantes uioi theou.
Hili lina maanishwa wazi kuwa ni wana
wote wa Mungu na viumbe hawa siyo Kristo ila ni wana wengine wa Mungu ambao
ni tofauti kabisa na Wamataifa na Waisraeli na hivyo wanakuwa ni viumbe tu wa
kiroho ambao ni Malaika wanaotajwwa tu kwenye Ayubu 1:6, 2:1 na 38:4-7. Andiko hili
pia lilighushiwa kwenye tafsiri ya Maandiko ya Masoretic Text (MT) kama
ilivyokuwa kwenye Kumbukumbu la Torati 32:8 ambalo lilibadilishwa kutoka kwenye
maneno sawasawa na idadi ya wana
wa Mungu kwa maneno yaliyo sawa na idadi ya Wana wa Israeli.
Walilichukua andiko kutokana na aya hii ya 43 ili kubadilisha au kupotosha kutoka
kwenye ukweli ufuatao: Wana wa Mungu walio kwenye aya ya 8 sio kuwa walikuwa na
mataifa waliyopewa na Israeli walitolewa kwa Yahova wa Israeli, lakini,
kutokana na aya ya 43, kwamba wokovu ulifunuliwa na kuwa wazi kwa Wamataifa,
pamoja na Waisraeli na pia kwa wana wa Mungu wakiukubali. Tulikuwa na kweli
kwenye andiko la tafsiri ya LXX kuthibitisha andiko kwenye Waebrania, lakini Watrinitaian
hawakujali hali hii ya kugushi, na liliwapendeza tu. Waamini imani ya Kiditheism
na wafuasi wa Armstrong hawakumudu kujua tu vya kutosha jinsi ya kulifanya
andiko hili. Hata hivyo, hakuna shaka kwa vyovyote vile kwamba andiko hili la
Waebrania linanukuu moja kwa moja andiko liilo kwenye tafsiri ya LXX na andiko kamili
linaloangaza kwenye maana iliyo kwenye Waebrania. Gombo zijulikanazo kama za
Bahari ya Chumvi (The Dead Sea Scrolls (DSS)] linathibitisha pia andiko lililo kwenye
tafsiri ya LXX na inaonyesha kuwa tafsiri hii ya MT ni tafsiri iliyofanywa baadae
kwa kazi ya kughushi ya Wayahudi. Tafsiri ya RSV imesahihisha andiko lililo
kwenye aya ya 8 kwa misingi hiyo.
Waebrania 1:7 imetoholewa kwenye Zaburi 104:4. Rejea hii inathibitisha pia
pasi shaka kabisa kwamba Baba anayetajwa kwenye Zaburi na Kitabu cha Waebrania
vinaonyesha na kuthibitisha ukweli huo kama inavyonekana kwenye Zaburi 104 inayomtaja
Baba kama muumbaji Aliyeiweka misingi ya
dunia (Zaburi 104:5a).
Waebrania 1:7 Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye
malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto.
Zaburi 45 imefanyiwa rejea kwenye aya 8 na inaonyesha kuwa mwana
anayefunuliwa, na hivyo na Baba pia. Kwa hiyo, elohim ambaye ni elohim wa
Kristo anaweza kuwa ni Baba tu, peke yake. Kwa hiyo kwa mara nyingine tena kwa
mifano saba mingine iliyo tofauti kwenye sehemu ya kwanza ya Waebrania sura ya 1,
uthibitisho wa kwamba Baba hakufunuliwa kwenye maandiko ya Agano la Kale
imethibitika kuwa ni uwongo.
Waebrania 1:8-9 [8] Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti
chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo
ya adili. 9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo
Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.
Aya za 10-12 zinafanya rejea kwenye Zaburi 102:25-27. Ni jambo lililo
wazi sana kwamba andiko hili linamtaja Baba kama lilivyotumiwa hapa kwenye
Waebrania kwa kumkanganya na mwana ambaye hatimaye anatajwa tena kwenye aya ya 13
likifanya rejea kwenye Zaburi 110:1 na malaika kwenye aya ya 14.
Waebrania 1:10-14 Na tena, Wewe,Bwana,hapo mwanzo uliitia
misingi ya nchi, Na mbingu ni kazi za mikono yako; 11 Hizo
zitaharibika, bali wewe unadumu; Nazo zote zitachakaa kama nguo, 12 Na kama mavazi utazizinga, nazo zitabadilika; Lakini wewe
u yeye yule, Na miaka yako haitakoma. 13 Je! Yuko
malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata
nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14 Je! Hao
wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?
Ni kwa jinsi gani basi hawa Baba na Mwana hawakujulikana kutoka kwenye mambo
yaliyo kwenye maandiko haya? Kwa nini Baba hajulikani kwenye Zaburi 110 kwenye
Agano la Kale? Swali hili ni la kipuuzi. Andiko lililo kwenye Zaburi 102:27 limetafsiriwa
kutoka kwenye maneno Lakini Wewe U Yeye yule; ili kugeuza
ukweli kwamba tunaongelea kuhusu Mungu wa Pekee wa Kweli na sio mfumo au imani
ya Utatu.
Andiko lenyewe lilikuwa kwa bahati mbaya ni kama lilivyotumika kwenye tadsiri
fulani kadhaa ili kumuinua Kristo juu ya Malaika na kudai kwamba ilikuwa hivyo
kila wakati wakati maandiko yalipoonyesha kuwa yeye alikuwa ni mmoja wao wakiwa
kama wana wa Mungu. Lengo la andiko ni kuonyesha kwamba Kristo, akiwa kama
mmoja wao, alifanywa kuwa wa chini kidogo kuliko malaika, na kisha akainuliwa
juu yao kwa kupitia sadaka yake. Walionyeshwa na kutajwa kwenye tafsiri ya LXX kuwa
ni wana wa Mungu kama sehemu ya kiumbe Malaika akiwa ni tofauti na wanadamu, wa
namna mbili zote, yaani Mwisraeli na Mmataifa. Tutaona tena kwa kuyaelewa
maandiko haya na kisha kwenda mbele kuonyesha kwa kina utambulisho wa Baba kama
Mungu wa Kweli na wa Pekee wa Agano la Kale.
Tukirudi nyuma kwenye suala la Amri ya Kwanza inayomtaja Kristo: mmoja
wa makoodineta wa CCG huko California alilazimika kusema hivi:
“Sijawahi kuskia kabisa jambo hilo kwenye kanisa la Worldwide COG au kwenye
machipukizi yake kwamba Amri ya Kwanza iliyo kwenye Kutoka 20 ilitolewa na
Kristo na siyo na Baba hadi niliposoma hivyo kwenye makala ya Frank Nelte, ya
MPANGO WA MUNGU WA WOKOVU WA MWANADAMU & KURUDI KWA KEISRO. Nimewahi kuwa
na waumini wachache walio kwenye matawi yaliyoibuka kutoka kwenye kanisa la WCG
na sikuweza kusikia kabisa kufuru kama hii.
Lakini hainishangazi mimi kwa kuwa nilisoma kwenye maandiko ya maandalizi ya
mahubiri kutoka kwenye mikururu ya mahubiri ya John Ritenbaugh kuhusu Uhusiano
uliopo wa Baba/Mwana kwamba ni vyema au Sawa tu kumuomba Kristo. Mtazamo huu
ulikuwa haujahuniriwa wala kufundishwa kabisa kwenye kanisa la Worldwide kipindi
cha uhai wa Herbert Armstrong. Ilikuwa ikifundishwa wakati wote na kanisa hili
kumuomba Baba kwa jina la Yesu Kristo ni kama ilivyofundishwa na Kristo mwenyewe.”
kanisa la WCG lilifundisha, kama yalivyofanya Makanisa yote ya Mungu kwa
kipindi cha takriban miaka elfu mbili, kwamba ilikuwa imekatazwa kabisa kumuoba
Kristo. Maombi yote yalilengwa kwa Baba kwa jina la Mwana wake Yesu Kristo.
mara tu unapofanya kosa hili na unapomuinua Kristo na kumfanya kuwa ni sawa na
Mungu wa Pekee wa Kweli ndipo kwamba unaendelea kushamirisha kiwango hili cha
kufuru. Na kwa kadiri watumishi hawa wavyofanya kazi kimakosa na upotoshaji na huku
wakikosa mwongozo wa bodi au naraza la wazee na kujiweka kando au nje ya kinara
cha taa cha Kanisa la Mungu, wanafanya makosa na hivyo haishangazi kile
walichokipata kwenye mwisho huu wa kiumauti. Mtu aliye mlenhwa wa muainisho huu
hata anakana kwamba jina Eloa linamaanisha Mungu Baba kwa maana hii
iliyosababisha kujiuliza maswali. Anapinga pia kwamba kulikuwa na Kalenda ya
Hekaluni na tutauainisha uwongo huu pia.
Koodineta mwingine aliyekuwa na uzoefu na kulijua Kanisa lililoita
Kanisa la Mungu la Kimataifa almaarufu kama Church of God International (CGI) alisema
kuwa hajawahi kusikia kabisa ikisemwa hivyo, wakati alipokuwa kwenye Kanisa la
Mungu la Kimataifa, yaani Church of God, International. Kwenye kanisa hilo
ilifundishwa kwamba Amri ya Kwanza inawataja wote wawili, yaani Baba na Kristo
kwa kuwa Kristo naye alichukuliwa kuwa ni Mungu kutokana na kutolielewa vyema
andiko la Yohana 1. Yohana 1:1 inasema tu kwamba Kristo (Neno) ni theos/elohim,
kama walivyo wana wengine wa Mungu (malaika) kutokana na Ayubu 1:6, 2:1, 38:7 na
Zaburi 82.
Kristo ni anabadilishwa kutoka kuwa Baba, ambaye ndiye Mungu aiye kwenye
Yuhana 1:1 kama Ton Theon/Ha Elohim.
Tatizo ambalo lilikabiliwa kanisa la CGI ni kwamba amri inasema kwamba usiwe na
elohim mwingine ila mimi. Andiko linasema: Mimi ni Yahova Elohim
wako, Usiwe na miungu mingine ila mimi. .
Ni kweli kwamba Yahova ni jina lililotumiwa kwa wana wengi wa Mungu na Manzo 18
na 19 zinawataja Yahovah wanne kwa wakati mmoja. Mmoja aliishi na Ibrahimu na
wawili walikwenda kwa Lutu huko Sodoma na kisha waliuita moto ushuke kutoka kwa
Yahova Mbinguni. Habari hii imeainishwa kwa kina kwenye jarida la Malaika wa YHVH (Na. 024).
Kwa hiyo, lugha ya andiko hili inakubali kuwa ni udogo wa Yahova wa Israeli; hata
hivyo, lama maneno yaliyo kwenye Amri ya Kwanza yalikuwa yanatokana au
kummaanisha Kristo au Yahova mwingine ni dhahiri shahiri kwamba ni ibada ya
sanamu na ni Dhambi ya Shetani.
mtazamo kama huo unatokana na madai ya uwongo na mapotofu kwamba Mungu wa Agano
la Kale alikuwa ni Yesu Kristo, ambavyo ni teolojia ya uwongo na potofu ya
Armstrong inayolenga moja kwa moja kinyume na maandiko ya Agano la Kale. Wakati
madai yakiwa yanafanywa kwamba Yahova hapa inamtaja Kristo na siyo Mungu kama Ha
Elohim ndipo tunakabiliwa na ukweli kwamba andiko hili, likiwa ni umoja,
linamfanya Kristo adai kwamba yeye anastahili kuabudiwa na Waisraeli na siyo
Mungu wa Pekee wa Kweli.
Andiko lenye maana au lugha mbili haliwezi kuwa linavitaja viumbe wawili,
ingawaje madai ya kwamba walikuwa ni viumbe wawili kama mmoja ni hoja ya uwongo
mkubwa ambayo wanatuama kwayo. Uelewa halisi wa Agano la Kale yamegubikwa na
makosa au upotofu wa Armstrong yakiwa yamekuwa akiendelea kwa utetezi huu
uliokubalika kwa kupofushwa sana kuyakubali na kuyajengea juu yake kama
tunavyoona. Hatuna mashaka kwamba Armstrong mwenyewe aliuulaumu au kuuponda mtazamo
huu wa kwamba Amri ya Kwanza inamtaja Kristo.
Ni kama ilivyokuwa imenyooshwa hapa, suala lenyewe lapasa liwe wazi sana
kwa mtu yeyote kama iwapo kama hizo zilikuwa ni amri za Kristo, kwa hiyo
kumwabudu Baba kungekuwa ni makosa kwa kuwa tungekuwa tukimwabudu Baba badala
ya Kristo. Ni dhana ya kipuuzi. Tunaposoma Ezra sura za 4-7 tunaona kwamba Hekalu
lilikuwa la Mungu (SHD #433 Eloahh, Eloah), na sheria zilikuwa ni zile za
Mungu, na kwenye Yohana 17:3 Kristo alimuita Mungu huyu kuwa ni Mungu wa Pekee
wa Keli. Kristo pia alimtaja Mungu huyu kuwa ni Mungu wake kwenye Yohana 20:17 na
kama ni hivyo hii ingemfanya Mungu huyu kuwa ndiye aliye Muumba Kristo na
amemfanya Kristo kuwa ni elohim mdogo saidizi ambaye anatenda kazi kwa niaba ya
Muumba wake. Kwa hiyo sheria hizo zinakuwa ni sheria tu za Mungu Baba na kwamba
Kanisa la Karne ya Kwanza lilimchukulia Kristo kuwa ni Malaika Mkuu wa Agano la
Kale aliyempa Musa Torati, kama inavyosema Biblia.
Mungu wetu ndiye Mungu wa Kristo. Tuna Mungu Mmoja tu wa Pekee na wa
Kweli. Tunamtimikia yeye, kama afanyavyo Kristo.
Uzishi huu mkubwa na usio na haya wa kufundisha kuwa kuna miungu miwili
wa kweli na uwongo wa kwamba Baba hajatajwa kwenye Agano la Kale umekuwa
ukienezwa na watu hawa kwa kiasi cha kwamba tunaona kwamba mtu mmoja au wawili
wa waumini wa Makanisa ya Mungu barani Afrika wamekuwa wakifikiwa kwa njia ya
Internet na mtu mmoja waliokuwa waumini wa lililokuwa kanisa la zamani la WCG, wakionekana
kabisa kuwa huko Afrika Kusini, wanaojaribu kueneza uwezekano wa kwamba Amri ya
Kwanza inamuelezea Kristo. Kwa bahati nzuri sana yamekuwa yakikataliwa na
kuonekana kuwa ni uzushi mkubwa sana na wale tunao wajua.
Biblia imeweka wazi sana kwamba kuna Mungu Mmoja tu wa Kweli na kwamba
Mungu huyo ametajwa kwenye Agano la Kale kuwa ni Baba na muumbaji na jina lake ni
Eloa, na ana mtoto wake mwanadamu. Mithali 30:4 moja kwa moja inamtaka kila
mmoja anayedhania kua anayeyaelewa maandiko alitangaze jina la Baba na jina la
Mwana wake. Hatimaye andiko hili linaendelea kumtaja yeye kwa jina kuwa ni Eloa
ambalo ni jina la umoja na inakubali kuwa hakuna uwingi na inamtaja Baba peke yake.
Kulijua jina hili la Mungu ni kigezo cha uelewa katika Roho Mtakatifu.
Waditheist au Wabinitarian hushindwa mtihani huu. Wanapinga na kufundisha
kimakosa jambo hili.
Eloa ni Mungu wa Hekaluni na tunajua kutokana na Kumbukumbu la Torati 32:15
kwamba yeye ni muumbaji na kwenye Kumbukumbu la Torati 32:17 kwamba yeye ndiye
mlengwa wa sadaka tuzitoazo. Yeye ndiye Mungu wa kwenye Biblia.
Yeye ndiye Mungu Aliye Juu Sana (Eleyon
au Elyon) na kuna Mungu mmoja tu Aliye Juu sana kwa maelezo na mashiko ya
lugha. Aliyagawanya mataifa sawasawa na idadi ya wana wa Mungu (Kumbukumbu la
Torati 32:8 tafsiri za RSV na DSS). Aliwapa mahitaji Waisraeli kutoka kwa Yahova.
Kwa hiyo, Elyon na Yahova, wakiwa kama Mungu na mwana wa Mungu, wanawekwa mahala
pake hapa kwenye Torati ambako Yahova wa Israeli ni mmoja wa wana wa Mungu na
Eloah anafanywa kuwa ni kama muumbaji. Kwa sababu hii tafsiri ya MT ilighushiwa
kwenye andiko hili kwenye kipindi cha baada ya Hekalu na ndiyo sababu tafsiri
ya KJV ni potofu na ya uwongo.
Ayubu anamtaja Eloah sehemu mbalimbali 45. Mkombozi ameorodheshwa kama mmoja wa
Maelfu na siyo Eloah kwenye Ayubu (Ayubu 33:23).
jina hili ni la umoja kwa namna yoyote ile. Maandiko
yana haribu kabisa fumbo aliloliweka Armstrong, lisemalo kwamba Agano la
Kale lilimtaja Kristo peke yake ambaye alikuwa ndiye Mungu wa Agano la Kale na
Baba kakujulikana kwenye Agano la Kale. Huu ni uwongo.
Ezra anamtaja Eloah kuwa ni Mungu wa Hekalu na anaendelea kwenye maandiko
yaliyo kwenye Ezra 4:24 kulionyesha Hekalu kama Nyumba ya Eloah; Mungu (Eloah)
wa Israeli (Ezra 5:1). Manabii wa Nyumba ya Eloah ni manabii wa Eloah (Ezra
5:2). Ni “jicho” la Eloah ambalo linaona na kuamuru harakati na kazi zote
zinazofanyika Hekaluni.
Dario aliombwa asaidie ujenzi wa Nyumba ya Eloah Mkuu huko Yerusalemu (Ezra
5:8).
Wayahudi walijua na walisema kuwa watumishi wa Eloah Mkuu wa Mbinguni na
Duniani (Ezra 5:11). Lakini alikuwa ni mababa wa Yuda ndio waliomkasirisha
Eloah wa Mbinguni na kumtia hasirani (Ezra 5:12). Kuna Eloah mmoja tu wa
Mbingu na Duania na ni Baba. Kudhania vinginevyo ni ibada ya sanamuna kufuru
kubwa.
Wayahudi walitambua kuwa alikuwa ni Koreshi ndiye aliyetoa amri ya kuijenga
Nyumba ya Eloah huko Yerusalemu (Ezra 5:13). Vyombo vya Nyumba ya Eloah
vilirudishwa kwa mfalme wa Yuda (Ezra 5:14) na akaamuru virudishwe kwenye
Nyumba ya Eloah kama ilivyojengwa mahala pake (Ezra 5:15). Ombi lilifanywa kuwa
ni iwapo kama tangazo la Koreshi lilidumu kuhusu Nyumba ya Eloah (Ezra 5:17).
Dario aliamuru kufanyike utafiti na tangazo la Koreshi lilikutwa likiamuru
ujenzi wa Nyumba ya Eloah huko Yerusalemu (Ezra 6:3), pamoja na vyombo vya
dhahabu na vya fedha vilivyochukuliwa na Nebukadneza kutoka kwenye Hekalu la
Eloah vikiwa vimekarabatiwa na kurudishwa kwenye Nyumba ya Eloah (Ezra 6:5). Hivyo,
Hekalu la zamani na hekalu jipya yote mawili yalikuwa ni Nyumba za Eloah.
Ndipo maadui wakaamriwa waache kuijenga Nyumba ya Eloah na ndipo
Wayahudi pekeyao walibakia kuijenga Nyumba hii ya Eloah (Ezra 6:7). Kodi
iliyokuwa inatolewa ng’ambo ya mto iliamriwa itumike kwenye ujenzi wa Nyumba ya
Eloah (Ezra 6:8) na pia kwa kutoa dhabihu za utakaso kwa Eloah wa Mbinguni (Ezra
6:9-10).
Ni Eloah ndiye aliyesababisha jina lake liwekwe humo kwenye Nyumba ya Eloah na
mamia ya mitamba walitolea sadaka kwa maelekezo ya Nyumba ya Eloah (Ezra
6:12,16-17). Makuhani na Walawi waliwekwa kwenye makundi ili wamtumikie Eloah
huyo Yerusalemu (Ezra 6:18).
Artashasta alimjua na kuwamini Ezra kuwa ni mwandishi wa Torati ya Eloah
wa Mbinguni (Ezra 7:12). Ezra alitumwa kuipeleleza Yerusalemu sawasawa na
Torati ya Eloah ambayo ilikuwa mkononi mwake (Ezra 7:14) na mfalme na washauri
wake walitoa sadaka ya vito vya fedha na dhahabu kwa Eloah wa Israeli ambaye
ndiye Eloah wa Mbinguni ambaye makao yake yapo Yerusalemu (Ezra 7:15). Iliwalazimu
kununua wanyama kwa ajili ya sadaka kwa Eloah huko Yerusalemu (Ezra 7:17) na ndio
walipofanya mapumziko sawasawa na Mapenzi ya Eloah (Ezra 7:18). Pia walitoa
vyombo wakampa Eloah mbee ya Nyumba ya Eloah huko Yerusalemu (Ezra 7:19). Chochote
kile kilichokuwa cha muhimu kulileta kwenye Nyumba ya Eloah (Elahh) kilichukuliwa
kutoka kwenye nyumba ya hazina ya mfalme kama alivyoamuru ifanyike na Ezra mwandishi
wa Torati ya Eloah (Ezra 7:20-21). Chochote kilichoamriwa na Eloah wa Mbinguni
kilifanyika kwa umakini mkubwa kwa ajili ya Nyumba ya Eloah wa Mbinguni (Ezra
7:23).
Pia makuhani, Walawi, waimbaji na wahunzi, Wanefini, waliokuwa akihudumu
kwenye Nyumba ya Eloah na haikuruhusiwa kuwatoza ushuru, kodi au riba kwao
(Ezra 7:24). Ezra aliamriwa kutenda mambo sawasawa na busara na hekima ya Eloah
katika kuwachagua maliawali na waamuzi au mahakimu. Yeyote asiyeishika sheria
ya Torati ya Eloah na sheria za mfalme alihukumiwa kifo kwa haraka sana na wao (Ezra
7:25-26). Kiumbe huyu aitwaye Eloah ndiye Mungu wa Pekee wa Kweli.
Jina lake linaonyesha kuwa halina uwingi kwa namna yoyote ile na Torati inatoka
kwake na yeye ndiye mlengwa tunayemtolea sadaka Hekaluni. Kristolitaja Hekalu
kama ni Nyumba ya Baba yake. Makuhani, pamoja na Kristo kama Kuhani Mkuu wa
mfano wa Melkizedeki, humwabudu yeye na kumtumikia yeye. Elohim wanatokana na
yeye wakiwa kama Ha Elohim. Wao ni Elohim, ambalo ni neno la uwingi, nao ni
wana wa Mungu na ni baraza la Elohim wa kwenye Zaburi na ni Baraza la kwenye
Ufunuo sura ya 4 na ya 5.
Ni wazi sana kwamba madai au malumbano ya Herbert Armstrong kwamba Mungu
wa Agano la Kale ndiye Kristo ni uzushi wa wazi kabisa na inaonyesha upungufu
mkubwa wa kulijua maandiko ya Agano la Kale. Kwenye maandiko ya kanisa la WCG kwenye
Mafunzo yake ya Kozi ya Muda Mrefu, kwenye Somo la 8, kanisa la WCG linasema
kwamba neno Eloah lilikuwa ni neno la umoja la Mungu ambalo hapo mwanzoni asili
ya jina Elohim. Somo hili lilibakia bila kubadilishwa kutoka kwenye uasilia
wake kwenye toleo lake la mwisho lililochapishwa chini ya usimamizi wa Tkach
Snr. Herbert Armstrong hakubadilisha kabisa wala kuliondoa. Ilionekana kuwa
hakujua maana ya andiko kama somo lililofuatia lililokuwa kwenye muundo au
mtindo wa Kiditheism. Hata hivyo, washirika wasaidizi wake, kama vile Herman
Hoeh, walijua kuwepo kwake lakini huenda siyo maana zake. Kwa bahati mbaya sana,
hawakuuendeleza kabisa mfumo wa Agano la Kale kama walivyotakiwa kuwa. Kulikuwa
maadiko mengine yanayoelezea kuhusu miungu wawili wa Israeli kama vile Zekaria
2 na wengine wanaoelezea nafasi ya Kristo kama ni Malaika wa Yahova kama ilivyo
kwenye Torati na kwenye Zekaria 12:8.
Tofauti
kati ya Yahova na Yahovi
Tofauti ya Yahovi (SHD 3069) na Yahova (SHD 3068) hawakujulikana na
Armstrong na hata wasaidizi wake.
Upande mmoja
unaoelezea maana ya jambo hili kwenye andiko la Kutoka 4:10 na pia 4:13 ambapo
neno Yahova anafanana na Malaika wa Uwepo anayenena na Musa ambavyo maeneo
mawili kati ya 134 yamelibadilisha jina Adonai na hivyo kuonyesha kwamba
walielewa ukweli wa kwamba alikuwa ni Kristo ndiye aliyenena na Musa na siyo
Mungu wa Pekee wa Kweli ambaye kwa yeye Mungu alimtumia. Vinginevyo maneno haya
yangeweza kuzuiwa na kusomeka elohim. Huu ni mfano tu mwingine wa makosa ya
imani ya uwili ya Armstrong. Kila moja ya maandiko haya 134 linaoneyesha
uhalisia wa tofauti zilizopo kati ya miungu hii.
Yahova wa Majeshi Kama Eloah, na
the Elohim
Inakuwa wazi sana kwamba huduma ya Armstrong na teolojia yake
havikuendana na maana na muundo wa majina ya Mungu na Malaika zake. Ala
hawakuelewa utaratibu wa Hekaluni na kwa hiyo hawakuweza kuendananayo
kisawasawa na muundo wa Waamini Mungu Mmoja, yaani wa Kimonotheist, ambayo ni
wajibu au kazi ambayo inabidi ifanye na Makanisa ya Mungu na Mashahidi katika
Nyakati za Mwisho. Herbert Armstrong alikusudia sana kujitangaza yeye mwenyewe
kuwa ni shahidi mkuu na kuwa yeye ni nabii Eliya ajaye kuliko kuelea au kuijua
kweli na umuhimu wa Mpango wa Mungu. Huo ndio ulikuwa ubatili uliotiwa moyo na
kuungwa mkono na uchanga wake, ambao msimamo wake ulihusiana na makosa au
upotoshaji ambao tumeuona pia uliendelezwa hapa (soma kwenye majarida ya Je, ni Eliya? (Na. 233) na Kweli 18 Zilizorejeshwa za Herbert W.
Armstrong (Na. 233B)).
Kristo mwenyewe analitangaza Hekalu la Yerusalemu kuwa ni Nyumba ya Baba
yake. Ni la Mungu wa Kristo na Baba yake (Yohana 20:17) ambaye ni Mungu wa
taratibu za huduma za Hekalu kwa vipindi vyote viwili, yaani Agano la Kale na
Jipya. Hakuna shaka kwamba Israeli walijua kuwa Hekalu ni Nyumba ya Mungu
mmoja, wa Pekee na wa Kweli na kwamba elohim wa Israeli alikuwa ni msaidizi
wake ambaye ndiye alikuwa mjumbe wa Elyon aliyewapa wao torati mlimani Sinai,
na Kristo na mitume waliunena ukweli huo (linganisha na 1 Wakorintho 10:4).
Kwenye Yohana 2 aya ya 13, Kristo na wanafunzi wake alisafiri kwenda Yerusalemu
kwenda kuishika sikukuu ya Pasaka. Ilikuwa hapa kwamba anatangaza kwamba Hekalu
la Yerusalemu ni Nyumba ya Baba yake, na alilisafisha Hekalu kwa kuwafukuza
waliokuwa wanafanya biashara ya kubadilisha fedha na wanyama (aya za 14-16). Kristo
alikuwa na wivu wa Nyumba ya Baba yake, kama Yohana 2:17 ilivyoinukuu Zaburi
69:9.
Yohana 2:13-17 (tafsiri ya Complete Jewish Bible [Biblia Kamili ya Kiyahudi]). 13 Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; naye Yesu
akakwea mpaka Yerusalemu. 14 Akaona pale hekaluni watu
waliokuwa wakiuza ng'ombe na kondoo na njiwa, na wenye kuvunja fedha wameketi. 15 Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu,
na kondoo na ng'ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza
zao; 16 akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa,
Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara. 17 Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, Wivu wa
nyumba yako utanila.
Ayubu 33:23 inamtaja Mmoja wa maelfu ambao walimkomboa Ayubu. Kiumbe huyu
anaonekana pia kwenye Mwanzo 48:15-16 kama elohim aliyetembea pamoja na Mababu wa
imani na ndiyo waliomlisha Yakobo na ambaye Yakobo alimsema kuwa alikuwa ni
Malaika aliyemkomboa yeye. Hawa elohim ni wana wa Mungu. Elohim wa Yaboko alikuwa
ni mjumbe wa Mungu wa Pekee wa Kweli na Biblia inaonyesha kwamba ili kuwa hivyo
kwenye hatua ya mwazoni sana ya maandiko.
Kwenye Waebrania 1:8-9 tunajua bila shaka kwamba kiumbe huyu anayetajwa kwenye
Zaburi 45:6-7 ni Kristo kama elohim lakini alikuwa elohim aliye juu yake kama
Elohim wake au Mungu wake na kwamba pia ana wenzake hawa au ndugu zake ambao
walikuwa ni sawa na yeye lakini aliye juu yake yeye aliyemtia mafuta. Alikuwa
ni nani basi?
Wao wangali bado ni ndugu zake au washirika wake. Biblia inatuambia ni akina
nani hawa na sio wanadamu kama hawa Waditheists wanavyojaribu kudai. Wafuasi wa
Armstrong walioamini Uditheism, kama vile kina Frank Nelte, (na Wabinitarians) wanajaribu
kulitenganisha neno chabbar iliyotafsiriwa
kuwa Wenzake na Ndugu zake kuwa hayana maana sawa kwenye Kiingereza na kwa kweli
inaibua madai haya ya uwongo ya kwamba wao ni wafuasi wake wa kimwili.
Hata hivyo, neno hili lilikuwa sawa na la Kiyunani kwenye tafsiri za
maagano yote mawili, yaani Agano la Kale na Jipya. Wanazuoni wote wanakubali
kwamba chabbar (SHD 2271) linafanana
kikamilifu sana na Kiingereza ambalo linakubaliana na lile la Kiyunani
lililotumiwa. Ina maana ya washirika, au
marafiki. Linatokana na neno ambishi
la msingi la chabar (SHD 2266). Kiambishi
hiki cha “kuambatana na”, au “kujumuika”, au “kujiunga pamoja, au kwenye
shingano”. Kwenye kila matumizi ya maneno yatokayo kwenye mzizi wa neno humaanisha
wenzake au washirika au marafiki. Hakuna ubahatisho mwingine au matumizi na
mlingano wa Kiingereza unbeba maana yake vizuri sana.
Neno lake la Kiyunani ni metoxous
(SGD 3353). Kiyunani kina maana yake maalumu ya mshiriki ambayo imechukuliwa
kwayo na maana ya mshirikishwaji na kwa kumaanisha mshiriki ambaye ni mwenzake,
mrithi au rafiki. Tafsiri ya kionyesha dalili humini yake bashara e Greek has a
specific meaning of a participant which carried with it the meaning of a sharer
and by implication the LXX inatumia neno hilohilo kwenye tafsiri na Brenton analitafsiri
kama wenzake na tafsiri ya Agano
Jipya inasema kuwa ni marafiki
(Knoch, na Marshall's Interlinear) na ndugu (kwenye tafsiri za KJV, RSV).
Neno hili la Kiyunani linauhusiano halisi kwenye Kiingereza kama ilivyoelezewa
hapa na Kiebrania kina uhusiano kama huo huo kamili. Neno hili la Kiebrania
lina maana yake maalumu kutoka kwenye chanzo maalumu na kudai kwamba halifanani
kwenye Kiingereza ni maezo yenye uwongo mkubwa. Madai ya kwamba halifanani
hayana mashiko kwenye lugha au si ya kweli. Wahubiri watasema wazi kabisa kitu
chochote ili ili kugeuza maandiko matakatifu ili kuyafanya yaendane na
mafundisho ya uwongo ya Armstrong.
Kwa hiyo, kwenye andiko hili, Kristo anaonyeshwa kuwa ana marafiki au
ndugu walio pamoja naye ambao walishiriki nafasi yake na zaidi ya yote ni
kwamba alichaguliwa na kutiwa mafuta. Umuhimu mkubwa wa suala hili kimsingi ni
kwamba haezi kuwa wakati wote juu yao. Alikuwa ni mmoja wao hadi alipotiwa
mafuta kuwa yu juu yao. Kwa hiyo, hawa ni kina nani?
Ni wazi kabisa kuwa wapo kwenye 1Petro 3:21-22 kwamba kutiwa mafuta kwa
Kristo kulifanyika baada ya kufufuliwa kwake na Baba yake, akapaa mbinguni
akiifanya sadaka yake ikubaliwe na baba, na kisha akaketi mkono wa kuume wa
Baba yake. Hili limekubalika na wasomi au wanazuoni wote wa Biblia.
1Petro
3:21-22 Mfano wa mambo hayo ni ubatizo,
unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu
la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo.22 Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda zake
mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.
Kuinuliwa huku
kumefanyika tangu kufufuka kwake Kristo kutoka kwa wafu. Alifufuka na kuinuliwa
juu zaidi ya wana wengine wote wa Mungu, kama tutakavyokwenda kuona hapo chini.
Kutoka kwenye Kumbukumbu la Torati 32:15-17 tunaona kwamba alikuwa ni
Eloah ambaye alikuwa ni Mungu aliyewaumba wao, na ni Mungu ambaye walimtolea
sadaka. Kwenye aya ya 8, Eloah Baba, ni Mungu Aliye Juu Sana aliyeyaweka mataifa
na kwenye aya ya 9 aliwatoa Israeli na kumpa Bwana wetu Yesu Kristo. Kwenye Kutoka
34:5-6 tunauona mfano ambapo Kristo alipaa mawinguni na akasimama pamoja na
Musa, na kisha akapita mbele ya Musa, na akatangaza “Bwana, Bwana Mungu"...
Hakuwa anajitangaza mwenyewe; alikuwa anamtangaza Baba mbele ya Musa, ni
Baba yule yule ambaye Musa alimuita kuwa Eloah kwenye Kumbukumbu la Torati 32. Kwa
hiyo tunaposoma kwenye Kutoka 20:3 tunaona kuwa kwa kweli Israeli walijua
kwamba kulikuwa na Mungu Baba au Mwenyezi ambaye alikuwa ni juu ya Kristo kwa
kuwa Kristo alikuwa amejidhihirisha mwenyewe kwao. Kristo alikuwa ni taswira ya
utukufu wake. Bodi yote mzima ya taifa la Israeli walijua kuwa kiumbe
aliyeongea nao pale Sinai alikuwa ni Malaika wa Bwana ambaye alimdhihirisha au
kumwakilisha Elyon, Mungu wa Israeli kwao. Huu ni mtazamo wa kila wakati wa
Makanisa ya Mungu kwa zaka kadhaa zilizopita.
Kwenye Ezra 7:21 torati inaonekana pia kama ni sheria ya Elahh (SHD 426 Chald.)
ambaye ni Eloah (SHD 433) anayetajwa mahala pengine popote kwenye maandiko na
Ezra. Yeye ni Mungu Mkuu. Kwa hiyo ile amri inayosema: "Usiwe na miungu
mingine ila Mimi" ni amri ya Mungu Baba, Mungu wa Pekee na wa Kweli wa
Mbinguni na Duniani.
kumbukumbu la Torati 32:8 inaonyesha kwamba Elyon alikuwa ni Mungu aliyeyatenga
mataifa na kuwapa wana wa Mungu. Kuna Mungu mmoja tu Aliye Juu sana naye siye Kristo
kwa maana hii. Kristo siyo Eloah wa Mbingu na Dunia. Kiumbe huyu anaweza kuwa
ni Mungu tu ambaye ni Baba. Baba, Elyon, aliwatoa Israeli na kumpa Elohim ambaye
alikuwa ni Kristo. Andiko hili liliteuzwa au kutotoshwa na jopo la Sopherim baada
ya kuanguka kwa Hekalu ili kuvunja moyo fundisho la wokovu wa Wamataifa na
nafasi ya Kristo kama Yahovah wa Israeli. Kwa hiyo walighushi andiko hili ili
lisomeke sawasawa na idadi ya wana wa Israeli
badala ya sawasawa na idadi ya wana wa
Mungu. Hawa walikuwa thenashara zaidi ya kuwa 70[na wawili] wa wana wa
Mungu kama ilivyoonekana pia kwenye baraza la wazee, ambalo linawaashiria wao.
Baraza hilo lilikuwa ni la Sanhedrin lililowekwa Waisraeli huko Sinai ili
kuwakilisha serikali ya Mungu kama Kristo alivyomuonyesha Musa.
Uhusiano kati ya Baba kama Yahova a Majeshi na Kristo kama Yahova wa
Israeli unaonekana kwenye Zekaria sura ya 2:7-12:
7 Haya! Ee
Sayuni, jiponye, wewe ukaaye pamoja na binti Babeli. 8 Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi,
Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye
awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake. 9 Kwa maana, tazama, nitatikisa mkono
wangu juu yao, nao watakuwa mateka ya hao waliowatumikia; nanyi mtajua ya kuwa
Bwana wa majeshi amenituma. 10 Imba, ufurahi, Ee binti Sayuni; maana, tazama, ninakuja, nami nitakaa kati
yako, asema Bwana. 11 Na mataifa mengi watajiunga na Bwana katika siku ile, nao watakuwa watu
wangu; nami nitakaa kati yako, nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma
kwako. 12 Na
Bwana atairithi Yuda, iwe sehemu yake katika nchi takatifu, naye atachagua
Yerusalemu tena.
Kumbuka kuwa kiumbe huyu mdogo hapa ananena kwa niaba ya Yahova wa Majeshi
na alisemekana kuwa Yahova wa Majeshi alimtuma yeye kuwalinda. Kwa hiyo Yahova
wa Majeshi anamtambua yeye na anamtuma kuwashughulikia wale wanaoigusa mboni ya
jicho lake. Kwa kweli Bullinger aliliainisha kwamba andiko hilo kama “mboni ya
jicho langu” kwenye bango kitita la andiko hilo lenyewe. Yahova msaidizi wa
Israeli anaonyekana kuwa ni kama elohim wa Daudi na kuwaongoza ateule waonekane
kama Malaika wa Yahova vichwani mwao kwenye Zekaria 12:8.
Zekaria 12:7-8 [7] Naye
Bwana ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili utukufu wa nyumba ya Daudi, na utukufu
wa wenyeji wa Yerusalemu, usipate kutukuzwa kuliko Yuda. 8 Katika siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa
Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo;
nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana mbele yao.
Huyu elohim ni Malaika wa Bwana akiiongoza nyumba ya Daudi atakayefanyika pia
kuwa elohim.
sasa, wahuriri wa lililokuwa kanisa la WCG hawakulifundisha KABISA andiko hili
au andiko lililoko kwenye sura ya 2. Iliharibu kabisa dhana yao na kwa hiyo
waliachana nalo na kujikita kwenye kile ambacho Agano la Kale lilisema. Pia
walipuuzia ukweli wa kwamba hawa ndugu au marafiki wa Kristo walijulishwa
kwenye Ufunuo sura ya 4 na ya 5. Mzunguko wa ndani wa wale 70 ulikuwa ni
thelathini ambao ulikuwa umeashiriwa au kuonyeshwa kwenye Hekalu la Eloah huko
Yerusalemu. Karibu na kiti cha enzi cha Eloah kulikuwa na Makerubi au viumbe wenye
uhai wanne. Kulikuwa ni makerubi wenye vichwa vya Tai upande wa Kaskazini,
kerubi mwenye kichwa cha Dume la ng’ombe upande wa Magharibi, kerubi mwenye
kichwa cha Simba upande wa Mashariki na kerubi mwenye kichwa cha Mwanadamu upende
wa Kusini. Makerubi hawa wawili wa mwisho waliasi na hukumu yao na kuchukuliwa
kwa nafasi zao kumewekewa taswira kwenye mapambo ya Hekaluni sambamba na Mtende
ambao ulikuwa unamwakilisha Kristo na utambulisho wao unaonyeshwa kwenye andiko
la Kiebrania ya Agano la Kale. Upya au Kerubi aliyezibaji hombwe n kina
Ibwahimu na Musa. Walikuwa ni watumishi tu wa Mungu ambao waliitwa kuwa elohim
kwenye maandiko (soma Mwanzo 23:6 kwenye lugha ya Kiebrania na Kutoka 4:16; 7:1).
wazee ishirini na nne wenye Mataji zilizovikwa na kusimama mbele za Mungu
wamewakilishwa na makuhani wakuu ishirini na wanne wa Hekalu ya Yerusalemu.
Walisimama mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo yuko pale akiwa kama
wa ishirini na tano na Kuhani Mkuu mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Hawa ni
washirika wenzake Kristo ambapo yeye aliinuliwa juu ya wote hawa akiwa kama
Kuhani Mkuu aliye mfano wa Melkizedeki. Hawa wote ni wana wa Mungu. Wanasema
kwamba Kristo ametukomboa sisi, yikiwa ni wanadamu wateule, ili tuwe taifa la
Wafalme na Makuhani na tutatawala hapa duniani.
Hawa ni marafiki washiriki wa Kristo ambao mbele yao Kristo anatukiri kama
tulivyoona kwenye Zaburi 82:1-6 na wote hao ni wana wa Yeye Aliye Juu Sana (Elyon)
kama wana wa Mungu (Kumbukumbu la Torati 32:8; Ayubu 1:6; 2:1; 38:4-7; Luka
12:8). Elohim wa Israeli yu pamoja na elohim (Zaburi 86:8). Andiko hili
liliaminika kuwa linawajata waamuzi wa Israeli na baadhi ya Waamini Utatu, na
wanafunzi waliofundishwa na Armstrong na kuamini imani ya Kiditheist. Hata hivyo,
Kristo hakua na sehemu kabisa kwenye baraza la Sanhedrin au kama hakimu. Baraza
hili ndil lenyewe lililotajwa kwenye Ufunuo 4 na 5. Wanazuoni ndiyo kwa hakika
una ushauri kwamba Baraza la elohim lililo kwenye Zaburi ni lile lililo mbele
ya kiti cha enzi cha Mungu na ni wengi.
Ikitokea kama kuna mashaka yoyote kama kwa jinsi alivyo na hai ya kwamba
ni Malaika wa Yahova awaongozaye Israeli kwenye Zekaria 12:8 mtu anaweza kusoma
tu kwenye andiko linalofuatia ambalo linamtaja Masihi na unabii wake akiwa
amechomwa mkuki na anapoyashughulikia mataifa ambayo yanakuja kuikabili
Yerusalemu. Hakuna shaka kwamba kiumbe huyu ni msaidizi wa Elohim wa Israeli.
Zekaria 12:9-14 9 Hata itakuwa siku hiyo, ya kwamba nitatafuta
kuwaangamiza mataifa yote watakaokuja kupigana na Yerusalemu. 10 Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na
wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye
walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa
pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa
ajili ya mzaliwa wake wa kwanza. 11 Siku
hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya
Hadadrimoni katika bonde la Megido. 12 Nayo
nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na
wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao; 13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke
yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao. 14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na
wake zao peke yao.
Huyu ni Masihi. Yeye ni msaidizi wa Elohim wa Israeli na Malaika wa
Uwepo wake aliyemkomboa Yakobo.
Mwanzo
48:14-16 Israeli akanyosha mkono wake wa kuume akauweka juu
ya kichwa cha Efraimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto akauweka juu
ya kichwa cha Manase, huku akijua atiavyo mikono; maana Manase ndiye
aliyezaliwa kwanza. 15 Akambariki Yusufu, akasema,
Mungu ambaye baba zangu, Ibrahimu na Isaka, walienenda mbele zake, yeye Mungu
aliyenilisha, maisha yangu yote, hata siku hii ya leo, 16 naye
Malaika aliyeniokoa na maovu yote, na awabariki vijana hawa; jina langu na
litajwe juu yao, na jina la baba zangu, Ibrahimu na Isaka; na wawe wingi wa
watu kati ya nchi.
Hakuna siri na hakuna shaka ya yule tunayemsema. Malaika wa Ukombozi
aliye kwenye Ayubu 33:23 na Mwanzo 48:15-16 ni mmojawapo wa ana wa Mungu,
elohim anayetajwa kama Malaika wa Bwana.
Kuna Mungu Mmoja tu kwenye Yohana 17:3, aliyemtuma Yesu Kristo, na mtume
Paulo anatuambia kwamba Mungu huyu ni kiumbe pekee ambaye hawezi kufa wala
kupatwa ma madhara yoyote (1Timotheo 6:16).
Kwa hiyo, kumlinganisha kiumbe mwingine na huyu Mungu ni kukufuru. Kudai
kwamba mwana wa Mungu, ambaye mwenyewe alidai kuwa anamtegemea huyu Mungu wa
Pekee wa Kweli maishani au kwa kuishi kwake (Yohana 6:57), ni sawa tu na kuwa
na yeye ni Mungu wa Kweli, anayetoa uhai kwenye vitu vyote (1Timotheo 6:13) ambavyo
ni kukufuru kabisa.
kudai kwamba mwana wa Mungu naye ni Mungu tunayemwabudu mahali pa Mungu wa
Pekee wa Kweli ni kufuru kubwa sana kwa kuwa Kristo alituambia tumwabudu Baba
ambaye ndiye Mungu wake (Yohana 20:17).
Haya ni maneno yake kwenye Yohana 4:21-24:
21 Yesu
akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima
huu, wala kule Yerusalemu. 22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu
watoka kwa Wayahudi. 23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba
katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. 24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye
imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.
Kristo aliliweka wazi
sana kwamba wamwabuduo wa kweli wamwabudu Baba. Wanamwabudu Baba katika roho na
kweli, na Baba anawatafuta watu kama hao wamwabudu yeye.
Kristo alisema kuwa Wayahudi wamlijua waliyekuwa wakimwabudu na hawakuwa
wanawaabudu wana wa Mungu; na walijua kuwa Hekalu lilikuwa ni Nyumba ya Mungu
Baba. Kristo aliliita Hekalu
kuwa ni Nyumba ya Baba yake kwenye Yohana 2:16.
kwahiyo, kudai kwamba Kristo ni Mungu aliyetolewa sadaka na ni Mungu ambaye
anapaswa kuabudiwa katika roho na kweli ni kufuru kubwa sana.
Ni kitu gani basi
kilichomfanya Kristo atengwe mbali maalumu na wana wengine wa Mungu kwenye Jeshi
la Malaika wa Mbinguni? Jibu lake ni kwamba alikuwa ameinuliwa juu kuliko wana
wengine wa Mungu kwa kufufuliwa kwake kutoka kwa wafu na kuchaguliwa kwake kuwa
Kuhani Mkuu wa Wateule na Malaika wa mfano wa Melkizedeki. Tutakuwa wote elohim (Yohana 10:34-35) na
kufaana na Malaika (SGD 2465 yaani. SGD 2470 + SGD 32 sawasawa au kama malaika)
(Luka 20:36; Mathayo 22:30; Marko 12:25) ambao ni elohim pia kwa hiyo nan i
kama wana wa Mungu na Baraza la elohim aliye kwenye maandiko ya Agano la Kale.
Kristo atatukiri sisi mbele ya malaika hawa wa Mungu (Luka 12:8). Wametajwa
kuwa ni wana wa Mungu kwa maeneo mengi mbalimbali kwenye Agano la Kale na sisi
tulio wana wa Mungu tutakuwa kama elohim kama ilivyoelezwa kwenye maagano yote
mawili, la Kale na Jipya. Wataletwa na Kristo hapa duniani atakaporudi (Mathayo
13:41; 25:31). Kristo anatukiri mbele yao ili kwamba tuweze kukubalika katikati
yao kama elohim.
Tatizo lililopo
kwenye imani za Kiditheism na Kibinitarianism ni kwamba mafundisho ya uwongo
yametafuta kumuinua juu Kristo zaidi ya wana wengine wa Mungu na kuanzisha upotofu
ambao umeingizwa imani ya Kikristo na wafuasi wa mungu Attis wa huko Roma na
ambayo haikuwahi kuwepo kabisa hadi kufikia mwaka 170 BK. Uditheism wa
Armstrong haukuwa KABISA sehemu ya mafundisho ya Kanisa la Mungu kwa kipindi
chake chote cha miaka 1900 kabla hajaanzisha kufundisha uzushi huu. Ubinitariani
ulikuja kutoka kwa waabudu mungu Attis wa huko Roma yapata mwaka 170.
Tunaweza
kuonyesha ukweli huo kwa kuainisha Teolojia ya Kanisa la Kwanza na nyaraka na
rejea za maaskofu waliofundishwa na kanisa huko Smirna kama vile akina Polycarp,
Irenaeus na Hippolytus ambani ni Waamini wahafidhina wa Uyunitarian. Hata
mwanateolojia mashuhuri Mtrinitarian anakubali kabisa kuwa Kanisa la Kwanza
lilikuwa ni la Mrengo wa Kiyunitarian. Kwa kushughulikia maandiko yahusuyo
Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu na kuonyesha kutokuwa na mashaka kwamba Smirna
ilifundisha wanateolojia na kwamba walikuwa ni wa Imani ya Uyunitarian ya
Biblia, Waditheist hawa waliongezea malumbano au hoja ya uhominemu kama vile
hivi ifuatavyo:
· Kwa kuwa wanazuoni na
wasomi mahiri wa Kitrinitaria kama vile kile kina Calvin na Harnack wanatangaza
hadharani kwamba kanisa la kwanza lilikuwa ni la mrengo wa Kibiblia wa
Kiyunitarian wanaweza kupuuzwa kwa kuwa wao ni Watrinitarian. Vivyohivyo Brunner
anayeuonyesha ukweli huo na kukubali naye pia hakuaminika kwa kushambuliwa na
nyongeza ya hominemu. Ukweli wa kwamba Mwanateolojia wa Kittinitarian ni
mwaminifu vya kutosha kiasi cha kukubali kwamba kanisa la kwanza lilikuwa ni la
mrengo wa Kiyunitarian ni kwa heshima yake. Mashambilizi ya hominemu ya
wahubiri hawa waliofundishwa na Armstrong wanalaumiwa kiasi cha kuhuzunisha na
watu kujiuliza kuhusu uadilifu wao wa kiakili.
· Mwonekano wa
Uyunitarian kwa maaskofu waliofundisha huko Smirna kunaelezewa kama hivyo na
mashambulizi ya kihominemu kwa ukweli kwamba walihusika kwenye malumbano ya Kuartodecimen
mnamo mwaka 192 BK (soma kwenye jarida la Hoja za wakuartodecimen (Na. 277)). Irenaeus wa huko Lyon alikuwa Muumini
mzuri sana wa Kiyunitarian kama alivyokuwa Polycarp aliyemfundisha na kama
alivyokuwa Hippolytus, ambaye alifundishwa pia kwenye Shule ya Smirna chini ya
Polycrates. Mmoja wa watu hawa hata alimshambulia Hippolytus kwa sababu ya kwamba
alikuwa ni askofu wa Roma, kwa mujibu wa Wikipedia. Makosa na upotoe huo umeainishwa
muda mrefu uliopita. Hippolytus hakuwa askofu wa Roma KABISA. Alichaguliwa kuwa
askofu wa Ostia Attica, ambao ulikuwa ni mji wa bandari wa Roma umbali wa maili
kadhaa nje. Aliwadharau maaskofu huko Roma na aliwashambulia wazi wazi na mara
kwa mara.
· Ili kuishambulia imani
ya Kiyunitarian na kuutetea Uditheism, Nelte, kwa mfano, alianzisha malumbano
ya mthafidhina na kumshambulia Anthony Buzzard teolojia yake ya Uyunitarian wa
Kihafidhina wa Zama za Baada ya Matengenezo na alijaibu kudai kuwa Uyunitarian
unapinga dhana ya kwamba Kristo alikuwepo hapa duniani hata kipindi cha kabla
ya kuzaliwa kwake rasmi tukujuako wote wakati kuna aina moja tu maalumu ya
Uyunitarian wa zama za Baada ya Matengenezo ambayo imaamini hivyo. Kuna idadi
kadhaa ya Wayunitarian Wahafidhina kwenye imani ya kanisa la WCG na kwenye
vikundi vilivyoibuka baada ya kufa kwa kanisa hili. Uyunitarian halisi wa
Kibibia ulitangaza kwa nguvu zake zote dhana hii ya uwepo wa Kristo kwenye
kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi duniani kama tuonavyo hapo juu (soma
pia kwenye jarida la Uwepo wa Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzalia Kwake
Rasmi Duniani (Na. 243).
Kushindwa kwa
kiakili kwa kanisa la WCG na vikundi vilivyoibuka kutoka kwake ni kizuizi cha
ukuaji wa Makanisa ya Mungu na inaonekana kuwa ni sababu iliyopeleka yaangamie.
Imani yao ya Uditheism ni utani. Ubinitarian wao ni mbinu ya kuvukia kuelekea kwenye
uzushi wa imani ya mungu wa Utatu ambaye amekuja kuibukia kwenye Ubinitarian wa
mungu Attis. Watetezi wa kwenye vikundi hivi vilivyoibuka wanazidi kuendelea
kwa kuyahuisha upya mafundisho potofu ya mungu Attis, Adonis, Osiris na Baali/
Mithra wa dini za waabudu jua na kuyaingiza kwenye Makanisa ya Mungu. Madai ya
kwamba Kristo ameinuliwa juu ya wana wengine wa Mungu kama Jeshi la Malaika ni
hoja inayoendelea ambayo imekuja ikitokea kwenye dini za waabudu jua na ambazo
zilitumiwa na Wakatoliki wafuasi wa Athanasias kwenye Baraza Kuu la Mtaguso wa Nicaea
mwaka 325 BK na ambayo ilikataliwa kwa kuonekana kama ni uzushi na Makanisa ya
Mungu kwa kipindi cha karne kadhaa sasa. Mtazamo huo ulikataliwa na kuchukuliwa
kuwa ni uzushi na ukatupiliwa mbali nje na kanoni zote za baraza la halmashauri
kuu mwaka 327 BK.
Wahubiri hawa wa
machipuko ya kanisa la WCG au watu mmoja mmoja wasiokubaliana walifanya makosa
makubwa sana ya upotoshaji wakidai kuhalalisha kushindwa na makosa ya kanisa la
WCG na imani za makanisa mengine yaliyoibuka kwenye kanisa hilo kwa kushindwa kurejesha
upya maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi Mpya na Yubile na Mizunguko ya Miaka ya
Sabato kwa kufuata Kalenda ya Hekalu. Wengine hata wamejaribu kupinga kwamba kalenda ya Hekalu haikuwepo na
kwamba utaratibu wa kalenda ya Hekaluni haukuwa na maadhimisho ya Miandamo ya
Mwezi kabisa, bali ilikuwa na maadhimisho ya Sabato peke yake. Tutaelezea mambo
hayo mahali pengine. Wengine wamejaribu kudai kwamba utaratibu ulioko kwenye
kalenda ya Hileli ndiyo ulikuepo kwenye huduma na shughuli za Hekaluni na
kwamba ndivyo alivyoshika na kuadhimisha hata Kristo. Madai haya ni ya uwongo nan i ya kujihesabia
hakitu wao wenyewe. Hayana misingi yoyote kwenye ukweli wa kihistoria.
Herbert Armstrong
alithibika kuwa ni nabii wa uwongo nan i kiongozi asiyeelea mambo yalivyo na
ukweli wake (soma pia kwenye majarida ya Unabii wa Uwongo (Na. 269) na lile la Imani ya Kiditheism (Na. 076B)). Hakuwa amewekwa wakfu
kabisa na afisa yeyote wa Kanisa lililojulikana kama Church of God (Seventh
Day). Alibatizwa na mhubiri mwaamini Utatu na akawekwa wakfu kwa kuwekewa
mikono kwenye hema ya kukutania ya mchana kutwa. Kanisa lake la COG (SD) likamkubalia kwa kitambo
kifupi sana baada ya hapo. Mamlaka na nguvu zake zilisababishwa au kuwezeshwa
na waumini waliobatizwa ambao walimwekea mikono, kwa maana ya kwamba Mungu
alikikubali kitendo kile. Hakuwa na sifa za kawaida zainazotambulika. Historia
ya maisha yake ya huko nyuma inathibitisha mambo haya. Teolojia yake ya
Uditheism na madai vinaonyesha ukweli huo, ni kama wanavyofa pia wafuasi wake
kwa namna ya madai wanayoyafanya pia, kama yalivyoonyeshwa hapo juu. Ufafanuzi
uliopo hapo juu hauna nia ya kumpakazia au kumdhalilisha. Bali ni maelezo tu
yenye ukweli. Mamlaka na nguvu za Makanisa yote ya Mungu yanatokana na katiba
iliyothibishwa na kukubaliwa na waumini waliobatizwa wanaounda shirika, chini
ya mamlaka ya Agano Jipya waliyopewa na Kristo ya kufunga na kuachilia au
kusamehe. Makanisa ya Mungu yana historia yake ya mafundisho ambayo
yamekanunishwa na kanisa la WCG pamoja na machipuko yake ni wa imani za
Kiditheisn tu kwenye historia yetu yote.
Madai ya uwongo
ya Wabinitarian na Watrinitarian yanaweza kuonekana kwenye jarida la Makosa ya Kimahubiri ya Wabinitarian na Watrinitarian Kuhusu Teolojia ya
Mwanzo ya Uungu (Na. 127B).
Soma pia jarida
la Biblia (Na. 164) kwa rejea zaidi za maandiko.
q