Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[175]

 

 

 Uhusiano Kati ya Mwezi Tishri na Ikwinoks

(Toleo La 2.0 19960824-20080404)

Katika kuitetea dhana au mafundisho ya uahirisho uliofanyika kwenye kalenda ya Hilleli, baadhi ya watumishi wenye hamasa wanaohudumu kwenye vuguvugu la Makanisa ya Mungu wamekimbilia kwenye tafsiri za Maandiko Matakatifu wakitafuka kuyapa mashiko madai ya mafundisho yao. Jarida hili linafafanua na kutathmini kwa kina kuhusu madai haya, pamoja na hali isiyo ya kawaida inayojitokeza mfano kama ilivyojitokeza mwaka 1997.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1996, 2008  Wade Cox)

(tr. 2014)

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 


Uhusiano Kati ya Mwezi Tishri na Ikwinoks


 

Baadhi ya watumishi na wahuribi wenye hamasa walio kwenye vuguvugu la Makanisa ya Mungu wamejitahidi sana kutafuta namna ya kuhalalisha mafundisho yanayojulikana kama ya uahirisho yaliyoanzishwa na rabi maarufu anayejulikana kwa jina Hilleli na aliyeanzisha mfumo wa kalenda inayojulikana kwa jina lake hilihili, hali.iayoashiria nia yao ya kuyapotosha Maandiko Matakatifu. Mojawapo ya madai mapotofu waliyonayo kwenye mabishano haya yanatuama kwenye mtazamo kwamba jinsi ya kuweka kigezo cha kuamua siku inayojulikana  Moladi au Siku ya Kwanza ya mwezi huu wa Tishri kwa mujibu wa mafundisho ya Hilleli inauhusiano wa aina fulani au inaendana kwa kutegemeana na mwenendo au mpangilio wa majira ambayo siku moja yake masaa ya usiku na mchana yanalingana ambayo kwa majira ya hari siku hii inaangukia mwezi Septemba na siku hii inaitwa ikwinoksi. Mwandamo wa Mwezi Mwandamo wa Tishri unajulikana vema kuwa ni – Mwandamo wa Mwezi Mpya wa Saba. Neno hili Moladi huenda likawa ni muafaka kulitumia kwa kuwa kwa mujibu wa mafundisho ya kalenda ya Hilleli, ni makosa makubwa kusema kuwa siku ya Kwanza ya mwezi wa Tishri haiangukii kwenye Mwandamo wa Mwezi Mpya.

 

Utetezi unaotumiwa kuhusu fundisho hili la uahirisho na mabadiliko yake yasiyo ya kawaida yaliyojitokeza mara kadhaa, mfano wa jinsi ilivyotokea mwaka 1997, kumejitokeza mabishano makubwa sana yasiyo ya kawaida ambayo bado yanaendelea hadi sasa. Mtu mmoja aliinukuu Kutoka 34:22 kama andiko linalothibitisha Idi ya mwezi wa Saba lazima ifanyike kwenye kipindi ikwinoksi au baada ya mwezi Septemba. Andiko hili linasema wazi sana kwamba: 

Exodus 34:22 Nawe utaitunza sikukuu ya majuma, nayo ni ya malimbuko ya mavuno ya ngano, na sikukuu ya kukusanya vitu mwisho wa mwaka

 

Andiko hili linaweza pia kutafsiriwa kama ni la marudio ya kila mwaka kwa kulitumia kama teqûphâh (SHD 8622) likimanisha mageuzi (ya jua) muafaka (wa muda) marejeo, na kumaanisha mzunguko, kuzunguka au hatima. Hii inaweza kumaanisha mwisho wa majira yanayoendelea au mwisho wa mayukio ya mwaka. Hakuna jinsi inayofikiliza kuwepo kwa uhusiano halisi na siku hii ya ikwinoksi au kama ni lazima ifuatiwe na siku hii ya ikwinksi.

 

Hakuna kanuni yoyote ile kutoka kwa mifumo yote ya kalenda zote za kale zijulikanazo kama za Kiebrania, kiyunani, Kibabeloni, au Kikanaani kwa Kanisa ambayo iliwahi kuahirisha kutangazwa kwa mwezi wa Nisan[u] au Abibu ambao msingi wake unatokana na kutilia maanani kwa kuuhesabia mwezi wa Saba kwamba ndiyo uamue katika kuupata mwezi wa Kwanza wa Kiyahudi na hata wa kwenye mifumo ya kalenda nyingine. Kalenda ya Waseleucidi wa Kimakedonia inaanza mwaka wake kutoka kwenye mwezi unaoshabihiana na na mwezi Tishri na kwa hiyo, inaonekana kuenenda na majira joto ya ikwinoksi ya pande za kaskazini. Kalenda hii ilitumika kama ya nyongeza kwenye mfumo wa Wababelonia katika kuhesabu matukio hayahaya ya Waseleucidi zaidi ya ile ya historia halisi ya Wayahudi wakati ule wa Wamakabayo na wengineo (1Wamakabayo; tazama kitabu cha Schürer, History of the Jewish People in the Age of Jesus Christ [Historia ya Wayahudi katika Siku za Yesu Kristo], Vol. 1, uk. 18-19 na uk. 125-126 kwa mchanganuo wa kina). Hata hivyo, Wamakabayo walianza mwaka wao kwenye majira ya pepo za kaskazi pia (Schürer, ibid.).

 

Mabishano haya yanaonekana kukanganya utendaji kazi wa kalenda hii ya Wamakedonia Waseleucidi  na mfumo wa Waebrania-Wababelonia. Kanuni za uahirisho hazina mashiko wala kuhusiana na majira haya ya kipupwe cha pepo za kaskazini cha ikwinoksi. Kanuni ni kwamba, katika mazingira ya aina yoyote yale ni kwamba lazima Pasaka iangukiwkwenye kipindi cha ikwinoksi ya majira ya hari (Schürer, ibid., uk. 590; imetokana na ruhusa ya, Schürer ambayesema: “wakati jua liliposimama kwa ishara ya Aries”, ibid., uk. 593). Ishara hii ya Aries inaanzia kuonekana kipindi cha takriban tarehe 21 Machi na huishia tarehe 20 Aprili, kwa usemi wa ki Gregorian. Kwa hiyo, Pasaka ya tarehe 21 Aprili imekatazwa kabisa kwa mujibu wa kanuni za zama za kale. (Ikumbukwe pia kwamba elimu ya Nyota na Mambo-anga hazikuweza kutofautishwa na kutenganishwa hadi kipindi cha Wanamatengenezo. Kwa hiyo, hii ilikuwa ni kazi ya elimu ya anga na siyo elimu ya unajimu inavyoonekana) Schürer anamtaja Anatolius, kwa mujibu wa Eusebius (HE, vii 32, 16-19) akisema kwamba huu ni mtazamo usiojulikana kwa wenye mamlaka wote wa Kiyahudi akiwemo Aristobulus, mwana falsafa aliyeishi siku za Ptolemy Philometor, na pia Philo na Josephus (Schürer, op. cit.). Kalenda ya Wamakedonia ilitumika huko Syria tangu mwanzo wa mamlaka ya Waseleucidi hadi ikaingia kwenye mfumo na zama za Waktisto.

 

Ilitumiwa kama ifuatavyo:

(1)   kwendana sambamba na miamdamo halisia ya miezi;

(2)   ili kuipata miezi kumi na miwili ya mwaka unaofuata kalenda ya jua iliyojulikana hapo mwanzo kama kalenda ya Julian, isipokuwa kwamba mwanzo wake ulikuwa ni siku tofauti. Kalenda ya Waseleucidi wa Kimakedonia ilikuwa kutofautina nana kila mara kwa majira mamoja hadi mengine, ambavyo ilionyesha kwamba kanuni haikuhusiana hasa na ile ikwinoksi ya majira ya hari hata hivyo. Huko Tiro, mwaka ulianza tahere 18 Novemba (Schürer, p. 595), baada ya ikwinoksi. Huko Gaza, na kwenyewe, ulianza tarehe 29 Augost (Schürer, ibid.; cf. Bickerman, Chronology, p. 50), ikiwa ni kabla ya ikwinoksi.

(3)   Katika siku zilizofuatia baadae miezi ya kalenda ya Julian ilianza kuitwa kwa majina ya Wamakedonia (Schürer, ibid.). majina ya Kisyria ambayo yalikuwa yakijulikana sana au haya yale yasiyojulikana ya Wayahudi yalitumiwa sambamba nay ale ya Wamakedinia.

 

Kwa hiyo hakuna kanuni inayoonyesha kwamba Tishri ambao ndiyo mwezi wa Saba, unauhusiano na ikwinoksi hii ya majira ya hari. Hii ni hoja ya muhimu katika kuipinga itikadi ya wanaoamini kalenda ya Hilleli, ambayo haina mashiko yoyote. Inatakiwa pia katika jaribio la kutetea udanganyifu mwingine kuhusu kusulibbiwa kwa mwokozi mnamo mwaka 31BK kama ilivyoenezwa na Herman Hoeh kwa kufundishwa na Herbert Armstrong (soma jarida la Majira ya Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159) [The Timing of the Crucifixion and the Resurrection (No. 159)]. Herman Hoeh hata anafikia kuanzisha kanuni ya uahirisho kwa maslahi yake kutokana na nia yake hii (sawa na jarida lisemalo Siku ya |Kusulibiwa Haikuwa Ijumaa).

 

Siku ya maandalio au siku ya 14 Nisan, inaitwa kuwa Siku ya Ushirika wa Meza ya Bwana, na siyo siku ya Pasaka kama inavyofundishwa na yeye. Haya yalikuwa mafundisho ya uwongo yaliyoenezwa na Herbert Armstrong na yalitetewa na baadhi ya watumishi wake, lakini yalikuwa yamekosewa mno (soma jarida la Pasaka (Na. 98) [The Passover (No. 98)].

 

Pasaka ya mwaka 1997 iliadhimishwa kabla ya mwezi mmoja kutokana na kalenda ya Wayahudi kwa kuwa ilikumbwa na mafundisho haya ya uahirisho yaliyofundishwa na kina Hilleli ambayo hayapo kwenye Biblia wala hayana mashiko yoyote kwenye Maandiko Matakatifu, wala kwehye historia ya huko nyuma kabla ya katne ya nne ya zama hizi. Kile wanachokifanya watetea mafundisho haya wanachokifanya kwa bidii zao zote ni kuanzisha kanuni mpya na kusema kwamba kanuni ama sheria ya kuamua ni wakati gani uanze mwezi wa Nisan ni kwamba mwanzo wa mwezi unaanzia pale unapoandama Mwezi Mpya karibu na majira ya ikwinoksi ya majira ya kipupwe cha pepo za kaskazi ambayo kunaadhimishwa Idi za Pasaka na Mikate Isiyo na Chachu kukiwa ni mwezi kamili wa kwanza wa mwaka ikifuatiwa na ikwinoks isipokuwa wakati Sikukuu ya Vibanda inapoangukia ni kabla ya ikwinoks ya pepo za kaskazi (na hata kama Siku ya Mkutano wa Makini ikiangukia kwenye ikwinoks), kwa namna yoyote ile bado Pasaka/Mikate Isiyo na Chachu itakuwa kwenye kipindi cha mwezi mzima unaotuata siku ya ikwinoks ya majira ya baridi. Hakuna mahali kanuni hii inaonekana kuwa ipo na kwa kweli hata ilipoashiria kuwa ilikuwepo, na kama ingekuwepo basi ingeisababishia kalenda ipite kwenye kipindi cha mkanganyiko mkubwa. Maelezo yaliyo kwenye Kutoka 34:22 wanayodhania wafuasi wa Hilleli kuwa yanaunga mkono itikadi yao hayana mashiko yoyote kabisa na hata ya kihistoria hawaungwi mkono. Itikadi yao inatokana na mawazo na mapokeo ya marabi tu yenye kuwapa haki za misingi ya kidunia tu.

 

Sawasawa na hilo, namna ya kuipata Moladi ya Tishri ni kazi nyingine iliyoifanywa na imani ya Hilleli. Hakuna kanuni ya kibiblia ya namna yoyote ile inayotumika kupanga siku hii ya Moladi ya Tishri zaidi ya ile ya Mwandamo wa Mwezi Mpya huu wa Saba peke yake. Kwa hiyo hakuna kitu cha ajabu kinachojitokeza cha kushangaza siku hii, isipokuwa ni umuhimu wake tu wa siku hii kwetu ya mwezi wa Tishri kwa kuwa ndiyo unaoadhimishiwa Siku ya Upatanisho na Sikukuu nyinginezo. Mafundisho yanayosema siku hii ya Moladi iwe katikati ya mwezi huu wa Tishri yanatokana na mapokeo tu ya (kutoka kwa Mafarisayo) kwenye dini ya Kiyahudi, kama ilivyo kwenye siku ya 6 Siwani ni Pentekoste. Mwezi wa Nisani, au Abibu (na siyo Tishri) ndio utakuwa mwanzo wa miezi kwenu (Kutoka 12:2); na wala siyo mwezi wa Kwanza unaanzia tangu mwezi wa Tishri.

 

Kosa linguine lililovumishwa kutoka kwenye malumbano haya ni kwamba siku ya 1 Nisan haiitangulii ikwinoks ya majira ya baridi. Mwandamo wa Mwezi wa Nisan kinaitangulia ikwinoks, kwa mfano, katika miaka ya 1988, 1991, 1994 na 1996. 1997 ilikuwa ni mara tano hii katika kipindi cha miaka kumi ya mwisho kwamba 1 Nisan iliitangulia ikwinoks. Kwa hiyo, inaonekana kuwa ni karibu sawa kuwa hivyo. Ukweli huu pia unafanya mwanzo wa mwezi Tishri uwe mapema kabla ya ikwinoks mara nyingi. Mabishano yale yanayolenga kuweka kanuni ama sheria ya mkaribiano wa Idi ya Vibanda na siku ya ikwinoks ni ya uwongo na yanapingana na ukweli wa kihistoria.

 

Mwaka wa 1994 Sikukuu zote za mwezi wa Tishri ziliangukia kabla ya ikwinoks ya mwezi Septemba isipokuwa siku ya Mkutano wa Makini,  ni kama ilivyojitokeza tena mwaka 1997 na haikupingika pia mwaka 1994, ikichukuliwa pia kwamba kwa kuwa watu waliohudhuria walijisikia vizuri na jambo hilo kama ilivyokuwa pia kwa wale marabi. Hali iliyojitokeza mwaka 1994 kinyume na mwaka 1997 inaonyesha kwamba hakuna kanuni kuhusiana na ikwinoks ya mwezi Septemba.

 

Kuhusu uhusiano au kwa kufananisha na siku za Mwandamo wa Miezi, Mwandamo wa Mwezi kwa kweli ni tukio la kinajimu. Habari yake inapatikana kotekote nchini Uingereza, hadi kwenye shughuli za ulinzi na za kibiashara za nchi, bahari na angani, na idara inayojulikana kama Her Majesty’s Nautical Almanac Office (HMNAO). Hiki SIYO kile kitabu kinachojulikana kama the Queen’s Almanac kama mpendwa wetu mmoja asiye na habari alivyowahi kudhania kuwa huenda ilikuwa ni kazi ya uandishi iliyofanyika hivi karibuni. Taarifa za Miandamo wa Mwezi za hivi karibuni zinaweza kupatikana kwa muda wa masaa yajulikanayo kama Greenwich Mean Time (saa za Kimataifa) na msaada unaweza kutolewa kwa kina kwa kazi ya kuhesabu ya masaa ya Yerusalemu na masaa mengine kutoka kwa vyanzo vyote viwili vya kimuunganiko na kkutoka kwa hawa End Evening Nautical Twilight (EENT) huko Yerusalemu, na pia kwa maeneo ya kinyumbani. Haya masaa ya EENT yanatakiwa katika kuamua au kupangilia siku kwa nia ya kutengeneza kalenda. Tukio la muhimu kulitilia maanani ni Mwandamo wa Mwezi na ndilo linaloweka majira kwa kuunganisha ulimwengu wote. Mwonekano wa mwezi wa kila mahali enyeji hutofautiana.

 

Kwenye baadhi ya kalenda zilizochapishwa, imeonekana kuwa nyakati au masaa hayaonekani, ni kama vile mfano ni kalenda inayotengenezwa na Frank Nelte, haionekani kufanana na muda au majira ya mwezi kutoonrkana kama ilivyofanywa na au kuonyeshwa na vyanzo maalumu kwa namna iliyo wazi sana. Huenda kuna namna ya mkanganyiko kati ya vipindi vya mwonekano au mchomoko wa mwezi na kile cha kutoonekana mwezi kabisa.

 

Hiki ni kipindi chenye fursa njema cha kuondokana na makosa na opotovu mwingine. Mwandamo wa Mezi Mpya haina maana ya Mwezi mchanga. Sheria hii ya uahirisho wa saa za mchana inadai kwamba kipindi cha mpito wa kuandama mwezi kinafanyika mchana na ndipo maamuzi ya kutangaza Mwandamo wa Mwezi kunatangazwa hadi siku inayofuatia.

 

Sheria hii ya majira ya mchana inaweka madai yake kwamba inafanya takriban masaa sita kuwezesha kufanya mwezi mchanga kutoka kwenye sehemu ya giza. Sheria hii yenyewe tu inajishuhudia na kumaanisha kwamba kipindi hiki cha giza chenyewe tu sio mwezi mchanga, bali ni kitu kilichopangwa tu.

 

Inadhaniwa pia kwamba huenda sheria hii ya uahitisho ilianzishwa na Waasia wenye asili ya Kiyahudi waliokuwa wanaishi pande za mashariki ya mbali na ambao Mwandamo wa Mwezi unachelewa kuonekana pengine hata kufikia siku inayofuatia. Kanuni au utaratibu wa kutegemea kuonekana Mwezi mjini Yerusalemu ndiyo inafanya Mwandamo wa Mwezi huko Asia uchelewe kwa masaa hadi manane wakati mwingine, na ndipo inatokea kwamba siku ya kabla yake kwa muonekano huu wa baadae. Kwa hiyo kalenda inaweza kuonyesha tofauti ya siku moja baada ya Mwandamo wa Mwezi kwa upande wa Mashariki hususan katika Australia na New Zealand. Hii ndiyo kanuni pekee ya uahirisho yenye mashiko kwa namna yoyote ya maadhimisho ya kweli. Tatizo lililopo kwenye kalenda ya Hilleli yameainishwa kwenye jarida la  Kalenda ya Mungu (Na. 156) [God’s Calendar (No. 156)].

 

Licha ya haki iliyoko kwenye jambo hili na haifikishi kwenye suluhisho lake kiusahihi na kuondoa tatizo, Makanisa ya Kikristo ya Mungu yameamua kutumia mwonekano wa mwezi wa Yerusalemu Regardless of the merits of this sole position, anna kuhesabu kutoka huko ili kuondokana na matatizo ya kuahirisha na kwa lengo la kutuweka wote kwenye wakati mmoja tu na unaolingana wa kikalenda miongoni mwa Makanisa yote ya Mungu kokote yaliko duniani hadi kufikia kipindi kile cha mkutano mkuu wa Makanisa ya \Mungu ambako tutajadili kwa kina jambo hili.

q