Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[075]
Baraka na Laana
(Toleo La 3.0 19941105-19990309-20071220)
Jarida hili linakumbushia yaliyoagizwa kwenye Kumbukumbu la Torati 28 na
jinsi ya kutendea kazi kwenye taifa.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1994, 1999, 2007 Wade Cox)
(tr. 2015)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Baraka na Laana
Wakati Mungu alipoitoa Torati kwa kupitia waombaji na watetezi wao, na kumtumia
Masihi akiwa kama Malaika wa Uwepo wake au muweka Agano na kuwapa Torati
Israeli kupitia kwa nabii Musa, aliweka utaratibu ambao usingeweza kushindwa au
kupungua. Hata hivyo, utaratibu huu ulipunguzwa kwa kuuchanganya na mapokeo au
desturi za Kiyahudi. Baraka na laana zinafanya kazi kwa wote katika Israeli na
sio kwa Yuda peke yao. La muhimu zaidi, vinaonyesha kwamba Mungu hushughulika
na mataifa kibayana na muundo wa Kanisa la mataifa mengi wa kimakosa unataka
kuubadili, kuuondoa muundo maalumu ambao aliuweka ili ashughulike na watu.
La muhimu sana ni kwamba, Israeli watawekwa juu ya mataifa yote ya Dunia
atakapokuja Masihi. Watafanyika kuwa nuru na taifa la kikuhani, kwa hiyo
hatushughuliki na sehemu isiyo na haki ya uweza na lenye ustawi mzuri wa
kiraslimali. Kila taifa linaweza kushirikiana kwa uelewano ustawi wa mali
unaotokana na uti wao katika kuzikubali Amri za Mungu. Na kwa hiyo wanafanyika
kuwa ni sehemu ya Israeli. Hatahivyo, iwapo kama Israei wangeitii Torati kwa
uendelevu bila kuivunja, basi wasingetakiwa iwabidi kusubiria na wangepewa
nafasi ya kipaumbele hapo kabla kwa kupitia Masihi na Malaika.
Kumbukumbu la Torati
28:1-68 Itakuwa utakaposikia
sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote
nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote
ya duniani; 2 na baraka hizi zote
zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako. 3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na
mashambani. 4 Utabarikiwa uzao wa
tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya
ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. 5 Litabarikiwa
kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga. 6 Utabarikiwa
uingiapo, utabarikiwa na utokapo.
Baraka za Bwana zinaenea hadi kufikia mambo yote ya taifa, kwa sehemu zote
mbili yaani mjini na mashambani. Mafanikio ya kimali ni kitu kilichohusishwa na
Torati.
7 Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako
kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa
njia saba.
Hapa maadui wa taifa wanachekwa na kudhihakiwa kwa matendo ya Mungu kwa
kupitia Watakatifu. Mashambulizi ya pamoja ya muungano wa maadui yatashindwa na
kutawanyika.
8 Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala
zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi
akupayo Bwana, Mungu wako.
Tendo la kurudiwarudiwa ahadi ya baraka linategemea kuhusu amri ya Yahoveh
kwenye maeneo yaliyo elezewa na Yahova Elohim. Kwa hiyo Masihi anaziamuru
baraka kwenye makubaliano ya kiutii yaliyowekwa kwenye mataifa ya Mungu.
9 Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama
alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya Bwana, Mungu wako, na kutembea katika
njia zake.
Hapa maelezo yamewekwa kwamba kuanzishwa kwa taifa kama watu watakatifu kwa
Mungu kama dhumuni maalumu na ahadi ya Mungu, na kwamba ni sharti kuhusu
ushikaji wa Amri za Mungu.
10 Na mataifa yote ya duniani watakuona
umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako.
Hapa ahadi inawekwa ya kwamba Bwana atawafanya watu watuogope, kwa kuwa tumeitwa
kwa Jina la Mungu. Maandiko ya kitabu cha fasiri Interlinear yanaonyesha
kwamba maneno yasemayo kwamba jina la
Yahova limetajwa juu yako. Kwa hiyo utambulisho wa wateule unafanyika kwa
kuwaita majina watu na kwa kuijua asili ya Mungu. Kanisa la Wafiladelfia
linajulikana kwa kuwa lina nguvu kidogo, lakini linalishika neno la Mungu na
halilikani jina la Masihi (Ufunuo 3:8).
11 Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri,
katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, na uzao wa nchi
yako, katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako kwamba atakupa. 12 Atakufunulia Bwana hazina yake nzuri,
nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubarikia
kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe.
Kwa hiyo ahadi hizi hapa zinaendana na mambo mawili yakiwa kama alama au
ishara ya baraka za Bwana; kwamba Mungu atainyeshea nchi mvua kwa wakati wake
muafaka, na kwamba taifa litafanyika kuwa la wakopeshaji wakuu na sio wakopaji.
Kwa hiyo ukame ni dalili ya kuwa nje ya mfumo ulio kwenye Kalenda ya Yubile na
sio kwa kutozishika Sheria za Mungu. Matokeo halisi ya kuzishika Sheria za
Mungu ni kwamba taifa kuwa tajiri na halihitaji kukopa. Ukweli wa sababu ya
dunia kwa sasa kutumbukia kwenye masaibu kama haya ni uthibitishisho wa
uhusiano mbaya ya kiroho uliopo kati ya ulimwengu na Mungu.
13 Bwana atakufanya kuwa kichwa, wala si
mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana,
Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya; 14 msipokengeuka
katika maneno niwaamuruyo leo kwa lo lote, kwenda mkono wa kuume wala wa
kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia.
Amri hizi zimeonyeshwa wazi na uthibitisho na usaidizi wake au kukubaliwa
kwake na Mungu. Kushindwa kuzishika Amri kumeelezewa kuwa ni sawa na kuifuata na kuitumikia miungu migeni. Kwa
hiyo, dhana na kuabudu sanamu haimanishi tu na kitendo cha kuabudu mapepo moja
kwa moja au ch kujitoa kuabudu sanamu peke yake. Ukweli ulio wazi wa kwamba mtu
anayefuata mafundisho ya mapepo, anajizinga kwenye umbo lake mwenyewe na tendo
hilo linachukuliwa kuwa mtu anajifanya mwenyewe kuwa ni adui wa Mungu.
Kutozitii Sheria
na Torati ya Mungu ni jambo linalopasa kuadhibiwa, kwa namna zote mbili, yaani
kwa mtu mmoja mmoja au kwa kundi. Mungu hushughulika na taifa sawa na kama anavyoshughulika na familia.
Mataifa hayo pia huhukumiwa kama waliyo Malaika wanaoyatawala mataifa hayo.
(soma jarida la Malaika wa YHVH (Na. 24)).
15 Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata. 16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. 17 Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia. 18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng'ombe wako, na wadogo wa kondoo zako. 19 Utalaaniwa uingiapo, utalaaniwa na utokapo,
Amri za Mungu pamoja na sheria zake zote yapasa zishikwe. Hukumu inatolewa
kwa ajili ya kuziasi na inadhihirika kwa kupitia mazao ya nchi. Taifa
linakaliwa kama watu. Watu watapewa utakaso wa meno; ili wajionee baa la njaa.
Mema ya Nchi yanaendana na jinsi watu wanavyozitenda Sheria za Mungu.
20 Bwana atakuletea laana na mashaka, na
kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea
kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo.
Bwana anashghulika na watu kwa laana na kuwapa bumbuwazi na kuchanganyikiwa.
Bumbuwazi hili linaenea kuanzia juu hadi chini.uongozi au serikali ya taifa
vinapigwa kwa ajili ya ujinga na na ufanyaji wa maamuzi yafanywayo kipuuzi,
yanayotenda kazi kwa kuhusianisha na ustawi wa watu. Maamuzi yanayofanywa kwa
kutofuata Ushuhuda na Torati yanawapelekea watu kuingia gizani. Maangamivu ya
watu yanayotokana na kumuasi Mungu hutokea mara moja na kwa haraka. Fikiria
jinsi taifa la Marekani lilivyodidimia chini. Fikiria jinsi nchi ya Australia
inavyoendelea kudidimia siku hadi siku kwa ajili ya kuufuata mfano wa
Wamarekani. Tazama sasa katika mji wa Sydney na maadhimisho ya sikukuu ziitwazo
Mardi Gras. Taifa hili litapigwa kwa upanga, na kwa haraka sana kuliko hata
jinsi lilivyotarajiwa.
21 Bwana atakuambatanisha na tauni, hata
atakapokwisha kukuondoa katika nchi uingiayo kwa kuimiliki. 22 Bwana
atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto,
na kwa upanga, na kwa ukaufu, na kwa koga; navyo vitakufukuza hata uangamie. 23 Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako
zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma. 24 Bwana
atafanya mvua ya nchi yako iwe vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka
mbinguni hata uangamie.
Tauni itaendelea kuwasumbua watu hadi kuwaangamiza. Tazama kuhusu magonjwa
ambayo yanafanyika kuwa ya kuambukiza kwenye nchi hii. Mwonekano wa mlipuko wa
ugonjwa wa dengue na wa mbu wenye maradhi ya maaria na wanaobeba magonjwa
mengine ni vitu vilivyoshamiri sana na kuonyesha hatari yake. Vimelea vya
wadudu jamii ya kupe na magugu vinaingizwa kwa kupia uzembe wa kimaamuzi ya viongozi.
Paradiso hii imegeuka kuwa jangwa au nyika kwa ajili ya mtazamo wa kizembe na
yaliyochanganyikiwa.
25 Bwana atakufanya upigwe mbele ya adui
zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia mbele yao kwa njia
saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote za duniani. 26 Na mzoga wako utakuwa chakula cha ndege
wote wa angani, na wanyama wote wa duniani, pasiwe na mtu wa kuwafukuza.
Pale ambapo tulipewa haki ya uzaliwa wa kwanza, na kuwachukua kupitia
uingiliaji kati wa Mungu ili kwamba uzao wa wao walio kwenye nchi hizo waweze
kunufaika pia kwa kuwafundisha na kuweka Sheria za haki za Mungu mwenye rehema,
bali badala yake tulizigeuza Sheria hizo na kuwatesa na kuwadhulumu watu hao
wakifanywa marekebisho au kurejeshwa upya. Wamarekani wa jamii ya Wahindi
wekundu na Waaborigines wa Australia walipaswa wawezeshwe wafanyike kuwa
mataifa yenye nguvu kwa uweza wa Mungu; lakini badala yake wamefanwa wajitenge
na kuwa mbali sana na Sheria au Torati kutokana na matendo yetu ya kuipotosha
na kwa kanuni zetu za dini za uwongo. Kamwe Wamarekani hawakulidumisha patano
lao waliloliweka kwa Wahindi wekundu, na hata Waaustralia hawakufanya yaliyo
mazuri yoyote nao pia.
27 Bwana atakupiga kwa majipu ya Misri, na
kwa bawasiri, na kwa pele, na kwa kujikuna, ambayo hupati kupoa. 28 Bwana atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu,
na kwa bumbuazi la moyoni; 29 utakwenda kwa
kupapasa-papasa mchana, kama apapasavyo kipofu gizani, wala hufanikiwi katika
njia zako; nawe sikuzote utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa
kukuokoa.
Aina ya magonjwa yanayoongezeka kila siku inakuwa ni yale ya kutisha sana.
Maambukizo ya UKIMWI yanaonekana kuwa yalitabiriwa kwenye Warumi 1:25-27.
Ongezeko la wendawazimu kwenye jamii za ulimwenguni ni ushahidi wa uvunjifu wa
Sheria za Mungu. Matndo ya ukiukaji wa maadili ndiyo hasa yaliyoleta mateso
kitaifa kwa wale wasioenenda kwa kumfuata Roho Mtakatifu. Inatokana na mateso
au mashutumu ya jamii na mara ningi siyo kwa mwajibiko wa moja kwa moja wa kila
mmoja, yakitokana na vitu vyenye kemikali kwenye mlolongo wa vyakula na
utunzaji wa maji. Rumi ilitumia mabomba yaliyounganishwa kwa kupitia uongozi
usio na upinzani na matokeo yake taifa liliteseka kwa mlipuko wa umajinuni wa
kuambukiza. Mihadarati kwenye jamii hii inaongeza magonjwa ya kisaikolojia na
pia uharibifu wa mfumo bora wa kijenetikali.
Uhusiano wa kifamilia umeporomoka hata kuvunjika na mmomonyoko wa maadili
na uaminifu katika jamii. Wanawake wetu watafanyika kuwa makahaba kwa kutumiwa
majeshini na maongeo yetu watapewa watu wengine.
30 Utaposa mke na mume mwingine atalala naye;
utajenga nyumba usiikae; utapanda mizabibu usitumie matunda yake. 31 Ng'ombe wako atachinjwa mbele ya macho
yako, usile nyama yake; utanyang'anywa punda wako mbele ya uso wako kwa jeuri,
usirudishiwe; kondoo zako watapewa adui zako, usipate mtu wa kukuokoa. 32 Wanao na binti zako litapewa taifa
lingine, na macho yako yataangalia, na kuzimia kwa kuwatamani mchana kutwa;
wala hapatakuwa na kitu katika uwezo wa mkono wako. 33 Matunda
ya nchi yako, na taabu yako yote, vitaliwa na taifa usilolijua; utaonewa tu, na
kupondwa chini daima; 34 hata uwe mwenye
wazimu kwa yaonwayo na macho yako, utakayoyaona. 35 Bwana
atakupiga magoti na miguu kwa jipu lililo zito, usilopata kupozwa, tokea wayo
wa mguu mpaka utosi wa kichwa.
Mlolongo huu wa matukio unatakiwa ili kufanya mambo yaendane kwenye
mchakato wa toba. Pasipo mchakato huu tusingefanyika kuyaona matokeo ya kile
tukifanyacho. Inapasa kuwa ni kwa haraka na sana na vigumu; zaidi ya hapo ni
kuleta nyumbani fundisho la kufananisha mambo.
Hapa tunaon a kwamba Musa alitabiri kuwa ufalme ulipasa uanzishwe.
Kuwatumikia miungu wengine kulienda sambamba na miti na mawe. Uandishi
uliotumika kwenye kamusi ya Interlinear unawatenganisha kwa alama ya
mkato.
36 Bwana atakupeleka wewe, na mfalme wako
utakayemweka juu yako, kwa taifa usilolijua wewe wala baba zako; nawe huko
utatumikia miungu mingine ya miti na mawe
Utumwa huu ni kwa taifa la kigeni ambalo hatulijui. Watatumia lugha ya
kigeni na watapewa moyo wa jiwe watakavyotufanyia. Zaidi sana, njia zetu
zimekengeuka sana kiasi kwamba kile tunachokisema kwenye dini ni tofauti kabisa
na dhana ya kumuabudu Mungu wa Pekee wa Kweli na mafanikio yanayotokana kutoka
kwene Imani ile. Na hadi kufikia hapa sasa, taifa lililindwa na kupewa haki
yake ya uzaliwa wa kwanza kwa sababu ya ahadi alizopewa Yusufu kupitia watoto
wake, Efraimu na Manase.
Mwanzo 48:15-22 Akambariki
Yusufu, akasema, Mungu ambaye baba zangu, Ibrahimu na Isaka, walienenda mbele
zake, yeye Mungu aliyenilisha, maisha yangu yote, hata siku hii ya leo, 16 naye Malaika aliyeniokoa na maovu yote, na awabariki
vijana hawa; jina langu na litajwe juu yao, na jina la baba zangu, Ibrahimu na
Isaka; na wawe wingi wa watu kati ya nchi. 17 Yusufu
alipoona kwamba babaye anaweka mkono wake wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu,
ikawa vibaya machoni pake. Akauinua mkono wa babaye auondoe katika kichwa cha
Efraimu, ili auweke juu ya kichwa cha Manase. 18 Yusufu
akamwambia babaye, Sivyo, babangu, maana huyu ni mzaliwa wa kwanza; weka mkono
wako wa kuume kichwani pake. 19 Babaye akakataa,
akasema, Najua, mwanangu najua, yeye naye atakuwa taifa, yeye naye atakuwa
mkuu; lakini ndugu yake mdogo atakuwa mkubwa kuliko yeye, na uzao wake watakuwa
wingi wa mataifa. 20 Akawabariki siku ile akasema,
Katika ninyi Waisraeli watabariki, wakisema, Mungu na akufanye kama Efraimu na
Manase. Akamweka Efraimu mbele ya Manase. 21 Israeli
akamwambia Yusufu, Angalia, mimi ninakufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi,
naye atawarudisha mpaka nchi ya baba zenu. 22 Nami
nimekupa wewe sehemu moja zaidi kuliko ndugu zako, niliyoitwaa katika mikono ya
Waamori, kwa upanga wangu na upinde wangu.
Malaika aliyewakomboa Israeli alikuwa Masihi akiwa kama Malaika wa YHVH.
Baraka walizopewa Israeli zilikuwa ni kwa kupitia Yusufu, na Efraimu alifanywa
kuwa mlengwa wa baraka hizo. Yuda alichukua fimbo ya kifalme ambayo kwayo
ilimtoa Masihi. Hata hivyo, Yusufu alikuwa na baraka ya uzaliwa wa kwanza na
hazikuwahi kuondolewa kutoka kwake; lakini zinasharti la utii.
Kumbukumbu la Torati 28 inaendelea kusema:
37 Nawe utakuwa ushangao, na mithali, na
dharau, kati ya mataifa yote huko atakakokuongoza Bwana. 38 Mbegu
nyingi utazichukua nje shambani, lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila. 39 Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala
hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu. 40 Utakuwa na mizeituni katika mipaka yako
yote usijipake mafuta yake; kwa kuwa mzeituni wako utapukutika. 41 Utazaa wana na binti, lakini hawatakuwa
wako wewe; kwa sababu watakwenda utumwani. 42 Miti
yako yote, na mazao ya nchi yako, nzige watakuwa nayo. 43 Mgeni
aliye kati yako atazidi kupaa juu yako; nawe utazidi kushuka chini. 44 Yeye atakukopesha, wala wewe usimkopeshe;
yeye atakuwa ni kichwa, wewe utakuwa mkia.
Wana wa mabinti wa taifa watakwenda utumwani. Ataifa halijalindwa dhidi ya matatizo haya.
Walakini, wateule ni sehemu ya taifa hili. Kama tunadhani kuwa tunaweza kubakia
kimya na kwamba bado tunaweza kulindwa wakati laana zinapoikumba au kuiangu
nchi, ndipo tunakosea. Ahadi waliyonayo watakatifu ni kwamba mkate wao na maji
vitakuwa vya hakika; lakini ni hayo tu na sio zaidi. Kama tutanyamaza kimya
wakati uovu huu ukitawala, ndipo Bwana hataweza kutusikia hadi tutakapotubu kwa
kuvaa nguo za magunia na kujitia mavumbi vichwani mwetu.
45 Na laana hizi zote zitakujilia juu yako,
zitakuandama na kukupata, hata uangamizwe, kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana,
Mungu wako, kushika maagizo yake na amri zake alizokuagiza; 46 nazo
zitakuwa juu yako kwa ishara na ajabu, na juu ya uzao wako milele;
Israeli ni watu wa kiroho na Amri na sheria ni ishara kama miujiza kwa
Israeli milele. Zinabakia milele kwa
wale wanaomkiri Yesu Kristo na kasha kuhukumiwa.
47 kwa kuwa hukumtumikia Bwana, Mungu wako,
kwa furaha na moyo wa kushukuru, kwa ajili ya ule wingi wa vitu vyote; 48 kwa hiyo utawatumikia adui zako
atakaowaleta Bwana juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na kwa uhitaji
wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata
atakapokwisha kukuangamiza. 49 Bwana atakuletea
taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa
usiloufahamu ulimi wake; 50 taifa lenye
uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana; 51 naye atakula uzao wa ng'ombe wako wa
mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa; wala hatakuachia
nafaka, wala divai, wala mafuta, wala maongeo ya ng'ombe wako, wala wana-kondoo
wako, hata atakapokwisha kukuangamiza.
Hii inajitokeza sasa, mifugo yetu inauzwa kwa kiasi cha kushangaza sana cha
bei yao kuwa chini. Ukame unawaua watu wetu. Tumeagiza ngano kutoka nje ya nchi
kwa mara ya kwanza katika kumbukumbu zetu za siku tunazoishi. Tumekuwa kwenye
madeni makubwa tukidaiwa na yamesababishwa na wajasiriamali wa kigeni. Wageni
wanakula na kumaliza nguvu zetu na huku tukiwa hatulijui hilo. Mvi zi pamoja
nasi lakini hatulijui hilo nalo. Tunapotoshwa na viongozi vipofu na ukengeufu
wa Manase au, kwa vibaya zaidi, na mataifa ya kigeni, hususan Ulaya.
52 Naye atakuhusuru katika malango yako yote,
hata kuta zako ndefu, zenye maboma, ulizokuwa ukiziamini, zishuke, katika nchi
yako yote kila upande; naye atakuhusuru katika malango yako yote kila upande,
katika nchi yako yote aliyokupa Bwana, Mungu wako.
Ahadi hii inahusu vita ndani ya mipaka ya nchi yetu. Wakati mwingine
tutakuwa tumetawaliwa au kumilikiwa na kushuhudia kuangamia kwa watu wetu.
Tutakuwa bado hatujamaliza kuyakimbia mateso kupitia kwenye miji yote ya
Israeli kaba Mwana wa Adamu hajaja (Mathayo 10:23).
53 Nawe utakula uzao wa tumbo lako mwenyewe,
nyama ya wana wako na binti zako aliokupa Bwana, Mungu wako; katika mazingirwa
na katika mkazo utakaokazwa na adui zako. 54 Mtu
mume kati yenu aliye mwororo na laini sana, jicho lake litakuwa ovu juu ya
nduguye, na juu ya mke wa kifuani mwake, na juu ya masalio ya wanawe waliosalia
naye; 55 hata asitake wao
mmojawapo apewe katika nyama ya wanawe atakaowala, kwa kuwa hana kitu
kilichomsalia kwake; katika mazingirwa na mkazo utakaokazwa na adui yako katika
malango yako yote. 56 Mwanamke kati yenu
aliye mwororo na laini, ambaye hangehatirisha kuweka wayo wa mguu wake nchi kwa
umalidadi na ulaini, jicho lake huyu litakuwa ovu juu ya mume wa kifuani mwake,
na juu ya mwanawe, na juu ya binti yake, 57 na
juu ya mchanga wake atokaye katikati ya miguu yake, na juu ya wanawe
atakaowazaa; kwa kuwa atawala kwa siri, kwa uhitaji wa vitu vyote; katika
mazingirwa na mkazo utakaokazwa na adui yako katika malango yako.
Hili ni fungu la kutisha sana la maandiko na kwa hakika limekwishatokea,
lakini si kwa kiasi kibaya kama itakavyotokea katika siku za mwisho na
maangamizi ya mwisho.
58 Kama hutaki kutunza kufanya maneno yote ya
torati hii yaliyoandikwa katika kitabu hiki, upate kulicha jina hili la fahari
na utisho, Bwana, MUNGU WAKO; 59 ndipo
atakapofanya Bwana mapigo yako yawe ya ajabu, na mapigo ya uzao wako, mapigo
makubwa kwa kweli, ya kudumu sana, na magonjwa mazito ya kudumu sana. 60 Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri
juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe. 61 Tena
kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia
nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa. 62 Nanyi mtasalia wachache kwa hesabu, ninyi mliokuwa mfano wa nyota za
mbinguni kwa wingi; kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako. 63 Tena itakuwa, kama vile alivyokuwa
akifurahi Bwana juu yenu kwa kuwatendea mema na kuwafanya kuwa wengi, ndivyo
atakavyofurahi Bwana juu yenu kwa kuwapoteza na kuwaangamiza; nanyi
mtanyakuliwa katika hiyo nchi mwingiayo kuimiliki. 64 Bwana
atakutawanya katika mataifa yote, tokea ncha hii ya dunia hata ncha hii ya
dunia; nawe huko utatumikia miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako, nayo
ni miti na mawe.
Uzembe huu unajitokeza nchini Australia sasa. Wageni wanaanzisha ibada za
miungu migeni ya sanamu hapa na watu wetu wanaiabudu. Mafundisho ya mapepo
yanashamiri. Imani ya ulaji wa mbogamboga peke yake inafundishwa na kushamiri
kuwa ni ya muhimu na mawazo ya kizembe yanaendelea na kuanzisha mchakato wa
ukengeufu kwa sababu ya vitendo vinavyofanyika waziwazi vya uwehuko na
uwendawazimu au uteja.
Wakati maangamizo ya Siku za Mwisho yatakapolipuka kwenye taifa hili, ni
wateule ndio watakaoteswa. Kwanza kabisa, wapendwa wenzao watakaotafuta jinsi
ya kujiokoa ndio watakaowasaliti, na mwisho kabisa, Mkutano Mkubwa utazifua
nguo zao na kuzifanya kuwa nyeupe kwenye damu ya Mwanakondoo. Kama
hatutaisimamia kweli sasa na kujaribu kuliokoa taifa hili, basi tutawasaliti
kaka zetu na dada zetu wakati utakapowasili. Ndipo magonjwa au tauni ya Siku za
Mwisho itainuka na kumuandama kila mtenda dhambi na aliye dhaifu na kwamba yale
waliyoyaogopa yatakuwa yakitokea na kutendeka.
65 Wala katika mataifa hayo hutapata raha
iwayo yote, wala hutakuwa na kituo cha wayo wa mguu wako; lakini Bwana atakupa
huko moyo wa kutetema, na macho ya kuzimia, na roho ya kudhoofika; 66 na uzima wako utakuwa na wasiwasi mbele
yako; nawe utakuwa na woga usiku na mchana, wala hutaamini kamwe maisha yako; 67 asubuhi utasema, Laiti ingekuwa jioni! Na
jioni utasema, Laiti ingekuwa asubuhi! Kwa kicho cha moyo wako utakavyokucha,
na kuona kwa macho yako utakavyoona. 68 Bwana
atakurudisha tena Misri kwa merikebu, kwa njia ambayo nilikuambia, Hutaiona
tena po pote; nanyi huko mtajiuza nafsi zenu kwa adui zenu kuwa watumwa na
wajakazi, wala hapana atakayewanunua.
Bwana aliahidi kwamba hatutarudi tena
Misri, kwa hiyo kutakuwa na utaratibu utakaowekwa wa imani itakayoshughulikia
kupambana na ukengeufu kwenye taifa. Hakuna atakayeweza kutununua sisi kwakuwa
hataweza kutulisha, na tumeepushwa na magonjwa na hatutasumbuliwa kiasi cha
kutufanya tuwe na sababu ya kuwategemea watu wengine.
Lakini, mafaita yatajaribiwa na sisi. Mungu anatuadhinu ili kushughulika na
sisi, lakini anatutumia sisi pia kwa kuyashughulikia mataifa mengine.
Yeremia 30:11-24
Maana mimi ni pamoja nawe, asema Bwana, nikuokoe; maana nitawakomesha kabisa
mataifa yote huko nilikokutawanya, bali sitakukomesha wewe kabisa; lakini
nitakurudi kwa hukumu, wala sitakuacha bila adhabu. 12 Maana
Bwana asema hivi, Maumivu yako hayaponyekani, na jeraha yako ni kubwa. 13 Hapana mtu wa kukutetea; kwa jeraha yako huna dawa
ziponyazo. 14 Wote wakupendao wamekusahau;
hawakutafuti; maana nimekujeruhi kwa jeraha ya adui, kwa adhabu ya mtu mkatili;
kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zilikuwa zimeongezeka.
15 Mbona unalilia maumivu yako? Hayaponyeki maumivu
yako; kwa sababu ya ukubwa wa uovu wako, kwa sababu dhambi zako zimeongezeka,
nimekutenda haya. 16 Basi, watu wote wakulao wataliwa;
na adui zako wote watakwenda kufungwa; kila mmoja wao; na hao waliokuteka nyara
watatekwa; na wote waliokuwinda nitawafanya kuwa mawindo. 17 Maana
nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu
wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye. 18 Bwana asema hivi, Tazama, nitarudisha tena hema za Yakobo
zilizohamishwa, na kuyahurumia makao yake; nao mji huo utajengwa juu ya magofu
yake wenyewe, nalo jumba litakaliwa, kama ilivyokuwa desturi yake. 19 Tena kwao itasikiwa shukrani, na sauti yao wachangamkao;
nami nitawazidisha, wala hawatakuwa wachache; tena nitawatukuza, wala
hawatakuwa wanyonge. 20 Watoto wao nao watakuwa kama
zamani, na kusanyiko lao litathibitika mbele zangu, nami nitawaadhibu wote
wawaoneao. 21 Na mkuu wao atakuwa mtu wa kwao wenyewe,
naye mwenye kuwatawala atakuwa mtu wa jamaa yao; nami nitamkaribisha, naye
atanikaribia; maana ni nani aliye na moyo wa kuthubutu kunikaribia? Asema
Bwana. 22 Nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa
Mungu wenu. 23 Tazama, tufani ya Bwana, yaani,
ghadhabu yake, imetokea tufani ya kudumu; itawaangukia waovu vichwani. 24 Hasira kali ya Bwana haitarudi, hata atakapokwisha
kutenda, hata atakapokwisha kuyatimiza makusudi ya moyo wake; katika siku za
mwisho mtayafahamu haya.
Kwa hiyo kuna ahadi kwa Israeli kwenye mlolongo huu wote. Somo hili
limetolewa ili tuweze matokeo kamili ya kutisha yatokanayo na uzembe wetu na
kukosa kwetu kuwatendea watu wetu wengine. Kristo amesimama mlangoni mwa Kanisa
la Laodikia; anabisha hodi mlangoni. Atakuja kwa kila mmoja, lakini hayupo ndani
ya Kanisa. Hebu amka na utubu na kisha usaidie kuliita taifa hili kwenye toba
kabla haijawa kuchelewa sana.
q