Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[038A]

 

 

 

Ishara za Mbinguni:

Sehemu ya I

 

(Toleo La 1.5 20080503-20131204)

 

Watu wengi wanadhani kwamba Ishara zinahusiana na Kuja kwa Masihi na Marejesho yaliyonenwa kwenye Biblia ya Waisraeli ni matokeo ya maafa na vita. Wakati vita ikihusiana na wao, baadhi ya ishara hizi kwa kweli zina maana fulani na maalumu ya kivuguvugu ya bodi ya kisayari inayoashiria kipindi cha mlolongo uliosawa na mujibu wa Kalenda ya Zamani ya Hekaluni.

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

 

(Hati Miliki © 2008, 2013 Wade Cox)

(tr. 2014)

 

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ishara za Mbinguni: Sehemu ya I

 


Watu wengi watakuwa makini kujua kwamba tumeweka kipindi cha Siku za Mwisho na ujio wa Masihi kwa miaka zaidi ya 21 ya Yubile 120 ya mwisho, kilichofunika Mizunguko mitatu ya Sabato iliyoanzia katika mwaka wa kumi na tisa, ambao ulikuwa ni mwaka wa kwanza wa Mzunguko wa Tano wa Sabato wa Yubile ya 120. Maandalizi ya mzunguko Utakaso na Marejesho ya Sayari hii ulianzia kwenye vita ile.

 

Tumeshughulika na kuelezea kuhusu Vita vya Mwisho na umuhimu wake kwa Masihi kuwa kwake hapa kuyatiisha mataifa ya Dunia kwa mujibu sawa na ilivyotabiriwa. Kipindi cha mwaka wa Saba cha kuyatiisha mataifa ya dunia ni lazima kiishie mapema kabla ya mwanzo wa Mwaka wa Yubile kuanzia Siku ya Upatanisho ya mwaka 2026 na kuishia mwaka 2027 na kuanza kwa Yubile Mpya ya Yubile zote tangu ile ya Ezra na Nehemia itakayokuwa katika mwakaa 2028 (soma majarida ya Usomaji wa Torati Ulivyofanywa na Ezra na Nehemia (Na. 250) na Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142)).

 

Kwa hiyo ni wazi kabisa kwamba Kristo atakuwa amekwisha kuja hapa, mapema kabisa kabla ya mwaka 2019 na huenda ni mapema kabisa kabla ya mwaka 2018 kwa ajili ya kuhitajika kwa mavuno makuu mnamo mwaka 2025.

 

Tunajua kwa ukweli kwamba Biblia inatuambia kuwa Mashahidi wawili watasimama huko Yerusalemu na kuhudumu kwa kpindi cha siku 1260 na kisha watauawa na kulazwa mitaani kwa siku tatu na hatimaye watafufuliwa (soma jarida la Mashahidi (pamoja na Mashahidi Wawili) (Na. 135)). Hii inamaana kwamba whishoni mwake kabisa hawa Mashahidi watakuwepo hapa duniani wakati wa maadhimisho ya Pasaka mwaka 2015. Tunatarajia pia kushuhudia wongofu wa Yuda na masalia ya Lawi mapema kabla ya Masihi kuanza kuyatiisha mataifa ya dunia.

 

Tunajua kwamba Vita vya Mwisho vimekwishaanza tayari tangu kipindi cha kushambuliwa kwa nchi ya Afghanistan na Iraq, kama tulivyoelezea huko nyuma kabla kwenye jarida la Miaka Thelathini ya Mwisho: Pambano la Mwishp (Na. 219). Kwenye kanda zilizorekodiwa imeelezewa kwa wazi sana kwamba vita hivi vilianza mwaka 2001. Kipindi cha utimilifu wa Mataifa kiliishia mwaka 1996 (soma jarida la Kuanguka kwa Misri (Na. 36)). Miaka Thelathini ya Mwisho ilianzia mwaka 1997. Mchakato huu ulionyeshwa kwa ishara ya tukio la kupatwa kwa mwezi. Kulikuwa na na matukio makuu ya kupatwa kwa mwezi wakati wa Pasaka na Sikukuu ya Vibanda kwenye maadhimisho ya mwaka 1996. Kishea huu mwaka wa 1997 kulikuwa na upatwaji mdogo wa mwezi wakati wa Pasaka na kupatwa kamili kwa mwezi kulitokea wakati wa maadhimisho ya Sikukuu ya Vibanda. Mwaka 1997, kulikuwapo pia upatwaji kamili wa jua katika siku ya 1 ya mwezi wa Abibu au Nisani na upatwaji nusu wa jua ulitokea siku ya 1 ya mwezi Tishri. Matukio haya ya mfululizo ya kupatwa kwa jua na mwezi hayakutokea kwa bahati mbaya. Yanauhusiani pia na Kalenda ya Hekaluni kwa mujibu wa muunganisho wa wala hayaendani na Kalenda ya Hilleli ya Wababeloni (soma pia jarida la Ubadilishaji wa Kalenda ya Mungu katika Yuda (Na. 195B)). Kuna mzunguko kamili wa nyakati kati ya miaka ya 1997 na 2015. Mizunguko iliyo kwenye kipindi hiki yanaonekana au kuoneshwa kwa ishara za matukio haya ya kupatwa mwezi na jua. Kipindi hiki chenye mzunguko na kipindi kingine kilichofuatia kitaonekana namna na umuhimu wake sana kwenye historia ya ulimwengu. Kipindi kinaqchofuatia kwenye miaka kumi na miwili ya kuelekea Yubile ya kurudi kwa mataifa. Hiki ni cha ukamilishaji wa Tukio la Pili la Kutoka lililoandikwa kwenye Isaya sura ya 66.

 

Mapepo wnyewe, na ibada zao za jua, wameuweka mwaka 2012 kuwa ni kama mwaka wa mwisho wa imani yao na mamlaka yao, na Mzunguko Mpya unaanza toka mwaka huu. Tunajua kwamba mfumo wao utapaswa uishe kwa ajili ya ujio wa Mashahidi, wakiwa na shahidi mkuu Eliya, anayeonekana kuwa Atarejesha Mambo Yote ambavyo maana yake pamoja na mabo mengine, kwamba atakuja kurejesha kwa watu umuhimu wa kuzishika sheria zilizo kwenye Torati ambazo Shetani amezivunja na kuzihalifu wakati wa kufungwa kwa Bustani mwanzoni mwa Yubile ya Kwanza, Yubile 120 zilizopita. Mnamo mwaka 3974  KK.

 

Mwaka 2012 ni Mwaka wa Sabato wa mzunguko wa hamsini. Katika mwaka huo Torati ya Mungu itasomwa kwa mara nyingine tena kwa mara ya tatu kabla ya kutolewa kwa hukumu dhidi ya mfumo na utaratibu huu uliopo leo.

 

Vita vimekwishaanza tayari na mfumo wa Munyama unazidi kupata nguvu tena ka tena na huku ukichukua mamlaka ya kiutawala wa Kidola chini ya kile wanachikiita kuwa ni Agizo au Utaratibu Mpya wa Ulimwengu. Mfumo huu unendelea hata sasa chini ya Shetani amoja na wafuasi wake hapa Duniani tangu mwaka 2012 wakati Torati ya Mungu iliposomwa na kutafsiriwa na kuenekezwa kwa Mara ya tatu. Nabii wa Uwongo pamoja na Mpingakristo wataendelea kuendeleza harakati zao tangu sasa hadi atakaporudi Masihi ulimwenguni.

 

Haya ni masomo mawili tofauti kutoka kwenye Maandiko Matakatifu ambayo yamesababisha nadharia fulani ya kukisia na yanaweza kutupatia mwanga kwa masuala ya kama kwenye nyakati.

 

Nabii Yoeli anasema, "Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla haijaja hiyo siku ya Bwana iliyo kuu na itishayo." (Yoeli 2:31)

 

Injili ya Mathayo inamnukuu Kristo akisema, "Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika; ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi." (Mathayo 24:29-30)

 

Kwahiyo tunaweza kudhania na kuamini kwamba kutakuwa na tukio la kiastronomia ambalo litapelekea kutokea maafa au kuharibika kukubwa kwenye mchakato wa mizunguko.

 

Kuna dhana kuhusu vipindi vya mizunguko ambavyo vipindi vine vya mizunguko ya nyakati za kupatwa kwa mwezi, na kuelekea chini hadi kwa kinachoitwa tetradi, kutokea.  Kwa kweli, itatokea mara sita kwenye karne ya ishirini na moja. Kinachomaanisha hapa, kwa vyovyote vile, ni kwamba wakati ule tu ambapo ni kwa bahati mbaya ikatokea wakati wa Siku Takatifu au Sikukuu za Mungu ambapo tunatarajia mlolongo wa mfuatano wa matukio ya kinabii kujitokeza unaomhusu Masihi na nabii hizi za Kibiblia kwenye miaka ya 2014 hadi 2015, na wakati wake muhimu mwaka 2015, kama tutakavyijionea hapo chini. Mnamo mwaka 2034, tarehe 3 Aprili kutakuwa na mkingo wa kipindi cha Pasaka na kupatwa kwa mwezi nusu kutatokea tarehe 28 Septemba 2034. Mwaka huu ni Mwaka wa Kwanza na Usomaji wa kwanza wa Torati kwenye kipindi hiki kinachotarajiwa kuwa ni cha Milenia mpya.

 

Matukio haya ya kupatwa jua na mwezi yataonekana kutokea kwenye Mwandamo wa Mwezi wa Mwaka wa Kwanza na katika Mwandamo wa Mwezi na katika Mwandamo wa tatu wa Mwezi unaofuatiwa na Pentekoste na wakati wa Pasaka mwishoni mwa maadhimisho ya Pasaka katika Siku ya Kwanza ya maadhimisho ya Mikate Isiyo na Chachu kwa kufuata Kalenda ya Hekaluni.

 

Baadhi ya wale walioshiriki na kuamini dhana hizi wamejaribu kuunganisha kwa kuzilinganisha na kalenda ya Hilleli na utaratibu wake ili kuzifanya ziendane na vipindi vya Pasaka kwa mwaka mmoja lakini wakikosa maana muhimu za siku zilizohusishwa. Makala moja kati ya hizo liliandikwa na Joe Kovacs kwenye gazeti latolewalo kila siku maarufu kama World Net Daily la  Aprili 30, 2008.

http://worldnetdaily.com/index.php?fa=PAGE.view&pageId=63076.

 

Usipokuwa unazijua tofauti iliyopo kati ya utaratibu wa Hekalu la Zamani na ile ya Kalenda ya Hilleli ya Wayahudi hatutaweza kufikia kujua maana kamili na kuyana madhanio au fikra kuhusu mambo mengine. Ni kama yalivyo mambo mengine yote ya kiroho hatuyajui hadi pale tunapoyafanya yale tuliyofunuliwa na Mungu. Mche na kumtii Mungu kwanza, na ndipo atayathibitisha mawazo yetu.

 

Kipindi cha mwisho cha mwandamano wa matukio haya ya kupatwa kwa jua na mwezi yaliyotokea kilikuwa na umuhimu na maana sana kwa Wayahudi katika Israeli na kimepelekea vita vya mwaka 1967 na kuiunganisha Yerusalemu kutoka mwaka huo, ikijumuishwa Pasaka ya mwaka 1968. Hii ilikuwa ni miaka 9.5 kabla ya Yubile iliyofuatia kwenye siku ya Upatanisho ya mwaka 1977. Ulikuwa ni mwaka wa sita wa Mzunguko wa miaka ya Sabato, na Yerusalemu ulikuwa mikononi mwa Waisraeli ambao ulikuwa ni mwaka wa Sabato, ambao ni mzunguko mmoja kabla ya Usomwaji wa Torati. Kwa hakika, Yuda hawakuzishika Sabato au Usomaji wa Torati lakini hii haikuenenda sawa na ni kinyume na na Marejesho na watafanya sawasawa na wanavyotakiwa kufanya kwenye kipindi hiki chote cha matukio yote. Upatwaji wa Mwezi mara zote unakuwa mwekundu kwa wale wanaotaka kufanya rangi zaidi.

 

Maana ya tetradi yamekuwa yakionyehwa kama ilivyoripotiwa kwenye makala. Ni tetradi hiyohiyo ya mwezi wa rangi damu iliyotokea baada ya Israeli kufanyika kuwa taifa mwaka 1948 na ilitokea mnamo Siku za Kwanza za mwezi wa Kwanza na wa Saba ya miaka ya 1949 na 1950.

 

Mwaka 2015, upatwaji kamili wa mwezi ulitokea pia katika Mwaka Mpya, mnamo tarehe 20 Machi 2015 na upatwaji kamili wa jua kufanyika tarehe 4 Aprili 2015, ambayo ni siku baada ya Siku Takatifu ya Kwanza ya mwanzo wa Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu.

 

Kuna upatwaji wa sehemu ya jua utakaotokea Siku ya Baragumu ambayo itakuwa ni Jumapili ya tarehe 13 Septemba 2015. Jumapili ya tarehe 27 Septemba, Siku ya Takatifu ya Kwanza ya Sikukuu ya Vibanda, kutakuwa na Upatwaji kamili wa Jua.

 

Inaumuhimu wake sana pia kwamba hakukuwa na tetradi za kiastronomia kwemye miaka ya 1600 hadi karne ya ishirini. Tetradi za miaka ya 1500 hazikutokea wakati wa Sikukuu yeyote ya Kalenda Takatifu. Mungu alitoa ishara kwenye Marejesho.

 

Tofauti iliyopo kati ya Kalenda ya Zamani ya Hekaluni na Kalenda ya Hilleli ina maana na umuhimu wake katika kupambanua mambo haya kwa mtazamo wa kweli. Kalenda haifanyi hivyo. Wale wanaoifuata kalenda ile kwenye Makanisa ya Mungu hawaelewi kabisa.

 

Wakristo wa mrengo wa Utrinitariani wamechanganyika katika kupokea kwao. Hitimisho lake liko wazi. Ishara za Mbinguni zinaendana na kile ambacho Mitume wanachosema, mwandamano wa mfululizo wote wa maukio na matendo. Ni kwa mujibu wa Kalenda ya Zamani ya Hekaluni na hawa Watrinitariani wanaozishika kwa kuziadhimisha Sikukuu za Kipagani watapata mtihani wao wa kwanza wa kutofautisha na kuondoa utaratibu wao mbaya na wa uwongo na imani yao. Tangu hapo na kuendelea kwa kweli inapata joto. Watateseka wakati wa Mashahidi kwa ajili ya uasi wao na hatimaye watawaua, lakini kwa wakati huu kila kitu kitakoma na watalazimika kutii ama vinginevyo watakufa.

 

Ripoti ya Kovacs kuhusu mawazo au dhana ya Blitz yangezewa kusaidia sana iwapo kama yeye na mwenzake Blitz wangekuwa wameelewa maana ya na umuhimu wa Lakenda ya Zamani ya Hekalu na kile kilichotokea kwa kipindi chote hicho. Ukosoaji wao unaweza kuwa una mapungufu kuelezea. Mengineyo mengi kama ya Hal Lindsay aliyafafanua pasipo hata kusoma makala yenyewe.

 

Nukuu kutoka kwenye maneno ya Kristo ilisema: "Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa." (Mathayo 25:13) imetumika kusema kuwa hatuwezi kujua au kuamua ni wakati upi atakaorudi Kristo. Pia anasema, "Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake." (Mathayo 24:36). Mungu yupo kwenye mchakato wa kuwaambia wao sasa.

 

Madai kwamba hizi sikukuu ziliwekwa kwa maana ya kuziadhimisha tu ni ya uwongo. Kipindi cha mpito cha kutoonekana Mwezi kinaamua mwanzo wa miezi na mpangilio wa siku za kuadhimisha sikukuu na vigezo hivi vyenye mashiko na maana vinatuama kwenye nyakati za kutoonekana kwa mwezi vya miezi wa Kwanza na wa Saba. Hukumu ni lazima itawapata wale wote wanaozifuata kalenda za uwongo na potofu na ni pamoja na wale wanaoifuata Kalenda ya Hilleli pia.

 

Imeandikwa kuwa Mungu hafanyi jambo lake lolote mpaka awaonye watu wake kwa kupitia watumishi wake, manabii anaowafunulia kwanza mapema kabla yake.

 

Tumeelezewa kuhusu mchakato na mfuatano wa matukio ya manabii kwa miaka mingi sana na tutaendelea kufanya hivyo.

 

Wanawali wenye busara wanaendelea kujiandaa na Kanisa la Mungu linaaonya Mataifa kwamba Kristo anakuja na wenye kuuzingiraji mji (walinzi wanakuja kutoka nchi ya mbali (Jeremia 4:15)).


Jedwali la ratiba ya kutokea kwa Upatwaji wa jua na mwezi limechorwa hapo chini. Inayofuatia ni Kalenda ya Kale ya Hekaluni kama ilivyoandaliwa na kuchapishwa na Kanisa la CCG na kisha Kalenda ya Hilleli, ambayo inaonyesha matatizo yaliyoko na sababu iliyowapelekea wawe na habari nusu nusu.

 

Ishara za Mbinguni zitalazimika kuonekana zaidi kuliko matukio haya ya kupatwa kwa mwezi na jua na yataamulia na mengine na ni mambo yaliyo na maelezo zaidi nay a kina zaidi.

 



 

Nyongeza ya jarida hili la Ishara za Mbinguni

           

 

Aina ya Kupatwa

Eneo la Kizoni

Tarehe

Nambari za Idadi ya Sarosia

2014

 

 

Jumla ya Upatwaji wa Mwezi

25Li15

2014-4-15

L122

Kupatwa kwa Jua kila Mwaka

8Ta51

2014-4-29

S148

Jumla ya Upatwaji wa Mwezi

15Ar05

2014-10-8

L127

Upatwaji wa Sehemu ya Jua

0Sc24

2014-10-23

S153

2015

Jumla ya Upatwaji

29Pi27

2015-3-20

S120

Jumla ya Upatwaji

14Li24

2015-4-4

L132

Upatwaji wa Sehemu ya Jua

20Vi10

2015-9-13

S125

Jumla ya Upatwaji wa Mwezi

4Ar40

2015-9-27

L137

 

 

CCG

 

Hilleli

Mwandamo wa Mwezi Mpya 2014 Yerusalemu 30/3/14

Uliadhimishwa tarehe 31/3/14

 

 

Mlo wa Meza ya Bwana           

13 Aprili 2014

 

Maadhimisho ya Pasaka           

14 Aprili 14 – 20 Aprili 14

15 Aprili – 21 Aprili

Maadhimisho ya Pentekoste

8 Juni 14         

3/4 Juni                       

Siku ya Baragumu

24 Septemba 14

25/26 Septemba

Iku ya Upatanisho

3 Octoba 14

4 Octoba

Sikukuu ya Vibanda

8 Octoba 14 – 15 Octoba 14  

9-16 Octoba

Mwandamo wa Mwezi Mpya 2015     20 Machi 15

 

 

Mlo wa Meza ya Bwana           

2 Aprili 2015

 

Maadhimisho ya Pasaka           

3 Aprili 15 – 9 Aprili 15         

4 Aprili 15 – 10 Aprili

Maadhimisho ya Pentekoste

24 Mei 15       

24 Mei

Siku ya Baragumu

13 Septemba 15         

14/15 Septemba

Iku ya Upatanisho

22 Septemba 15

23 Septemba

Sikukuu ya Vibanda

27 Septemba 15 – 4 Octoba 15           

28 Septemba – 5 Octoba

 

 


q