Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[021J]
Ufafanuzi Kuhusu Haggai
(Toleo la 2.5 20060910-20140905)
Mungu alimuagiza
Haggai kutoa unabii juu ya matengenezo na ujenzi wa Hekalu. Maandiko yanamsifu
Zakaria pamoja kuwa yu kuwili katika tabia ya asili. Huelekeza katika mfumo wa
kipindi cha miaka elfu moja pamoja kuongoka kwa watu wa mataifa.
Christian
Churches of God
Barua pepe: secretary@ccg.org
(Hati miliki © 2006, 2014 Wade Cox)
(tr. 2012)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu yatanukuliwa kikamilifu bila
kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakaotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Utangulishi
Jina Haggai asili
yake inatokana na neno Haghu, karamu au sikukuu. Na kifungu hiki kimetokana na
mwezi mwandamano, ambayo Bulliger kifupi anakili mwandamizi wa Biblia, fn 1)
kuwa kama Sabbato ya mwezi mwandamano. Ni mwezi wa Elul ulikuwa mwaka wa pili
wa atamu ya uongozi wa Dario mfalme wa wajemi ndio wakati agizo la kukamilisha
hekali ulitolewa na Yehova kupitia kwa Haggai.
Andiko hili basi
ni agizo kutoka kwa Yehova kwa Yuda ukiendeleshana na ule unabii uliotolewa
kupitia Zakaria.
Amri hii
ilitolewa katika mwaka wa kwanza wa sikukuu sabini (f10) kwanzia kufungwa kwa
Edeni unakamilishwa na sikukuu ya mwaka wa 424/3 BCE, na hekala sasa linaudwa
upya. Hili ni angizo la pili lililotolewa na Mungu walakini kazi ya ujenzi
ilitamatishwa kwa kipindi Fulani tokea kutolewa kwa amri ya Cyrus kimeendelea
hadi utawala wa Aritaserises wa kwanza ambaye alitamatisha ujenzi na ujenzi huu
ulitamatishwa hadi mwaka wa pili wa utawala wa Dairo mchemi (tazama somo hili Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi mpya wa Hekalu
[013]) [The Sign of Jonah and the History of the
Reconstruction of the Temple (No. 13)].
Kwa ajiri ya
kupuusa kwa Wayuda Mungu amenena dhidi yao. Ujumbe huo umejengwa katika sehemu
nne.
1.
Neno la Yehova. Andiko tulo limeanza na lawama kwao kwa
ajiri ya kuuza maagizo ya Mungu (Hag 1:1-4).
2.
Hapo matamshi ya watu yameshuhudiwa na Yehova.
3. Tena
neno la Yehova limetolewa.
4. Matamshi
ya watu yametolewa na kujibiwa na Yehova.
Mungu kunena kupitia kwa manabii ni msemo
wa waibrenia amabayo ni, “kwa mkon wa”. Hapo hapo hubainisha kusudi lililoko
kwa kutolewa kwa unabii utakaoandikwa kuwa kumbukumbu ya wakati wote mifano
hiyo imo ndani ya maelezo yafuatao kwa Mwandamizi
wa Biblia [Companion Bible].
Neno lilitolewa kwa Zerubabeli, maana kuapishwa katika Babiloni (hiyo ni Babeli). Alikuwa mzao wa fimilia ya kifalme kwa kubaliwa au kuapishwa katika Babiloni, na kwa Yoshua mwana wa Yosedeki, kuhani mukuu.
Jina Yoshua ni sawa na lile Masihi alipewa.
Jina kamili ni Yohoshua au wokovu wa yoho, iliyo jukumu la masihi
kama kuhani mkuu pia kama mfalme wa Israeli. Neno mwana katika andiko
limetumika pia kwa mejukuu (cf. 1 mambo ya nyakati 3:19 na Ezra 2:2 na 3:2).
Tazama pia katika masomo haya Ukoo wa masihi (Nam. 119)[Genealogy of the Messiah (No.
119)].
Yosedeki (Yahosedech) inamaanisha Yahova ni mwenye haki. Kwa ukamilifu jina hilo ni Yahoshua, au Yoshua wa Yosedeki. Maan ukombozi ni kupitia Yahova mtakatifu.
Yoshua ni kuhani mkuu wa kwanza katika Hekalu katika ule ujenzi mpaya. Wote walikuwa wa wakati huu wa masuto. Masihi atakuwa kuhani mkuu wakati wa rejea Yerusalem mara ya mwisho, ambayo hiyo ni mada ya ujumbe ulio katika kitabu cha Zakaria. Maandiko haya yote hivyo yanaungana hadi kipindi cha miaka elfu ambayo ni cha utawala wa Masihi.
Jina Gavana hapa limetokana na neno la wachemi Pechah (kutokana nalo tunapata jina Pasha) kama misimamizi au Liwali.
Shealtiel ina maana kilichoombwa kutoka kwa Mungu. Alikuwa mwana wa Yekonia (Jehoichin) aliyechukuliwa mateka uko Babiloni (2 Wafalme 24:15; 1 Mambo ya nyakati 3:17; cf. Ezra 3:2-8; 5:2; Nehemia 12:1; matayo 1:12, Luka 3:27).
UJUMBE WA KWANZA
Sura ya 1
Haggai: 1-4 Katika mwaka wa pili wa Dario mfalme, mwezi wa sita, siku ya kwanza ya
mwezi, neno la Bwana lilimjia Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda,
na Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, kwa kinywa chake Hagai nabii,
kusema, 2 Bwana wa majeshi asema hivi,
ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa
kujenga nyumba ya Bwana. 3 Ndipo neno la
Bwana lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema, 4 Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao,
iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika? (Biblia Takatifu BT)
Yudah wameulizwa
swali, mbona waliacha nyumba ya Mungu katika mabaki kwa uzuri zaidi ya miaka
mia moja badala wangeijenga karne moja mapema walakini, kulikuwa na Hekalu la
Yerusalem iliyofanay kazi wakati Hekalu la Yerusalem lilikuwa ukiwa na hilo
halipaswi kusahaulika.
Yehova hapo tena
anawakumbusha kuhusu dalili za hali yao.
5 Basi sasa,
Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu. 6 Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa
lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; na
yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka.
7 Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu (Biblia Takatifu
BT)
Hivyo Yehova
uanza na kumalizia kwa maelezo haya “tafakari jinsi umeishi” hawana chochote
sababu hawakumstahiki Mungu.” Neno, tafakari limetumika mara tano katika kitabu
hiki (Haggai 1:5,7; 2:15, 18,23; cf. Job 1:8; 2:3 na Isaya 41: 22).na maana
yake ni weka tayari moyo wako au kuwa mwangalifu. Azimio ni kuhakikisha
pale Yuda waliongozwa na matokeo ya yale wanatenda.
Yehova hapo tena
akatoa amri:
8 Pandeni milimani, mkalete miti,
mkaijenge nyumba; nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana. (Biblia
Takatifu BT)
Neno kuonekana katika utukufu wangu ni
kusema, nitajitwalia hustahiki/sifa.
Jina la Kiebrania ni ekkabda. Hili ni
moja ya maneno ishirini na tisa yasio na herufi HJe pale mwisho (Ginsberg’s Massorah,
vol1, b 281). Herufi he ni sawa na tano. Bullinger (Comp. Biblia fn.to v 8).
Unakili haya kwa
kunena kuwa wasomi wa mafundisho ya wayaudi hufikiria kwamba hili ni kwa sababu
kulikuwa na vipengee vitano ambavyo vimekosea katika Hekalu la pili ambavyo ni:
1.Sanduku la
Agano.
2.Moto uliowekwa
wakfu/ Moto mtakatifu
3.Shekina.
4.Urim na Thummim/vinyago
vitakatifu vilivyowekwa kifuani mwa kuhani enzi zile kwa ajili ya ufunuo wa
penzi la Mungu; na
5. Roho ya
unabii.
Kitu nambari 2 na
3 vinawakilisha Roho mtakatifu na uakilishi wao ndani ya wateule. Kitu na 5, Roho ya unabii, hipo katika kanisa na
ukamilifu wake uko katika Yesu Kristo.
Oroda uhoji
kulinda mwongozo wa neno ulio na herufi He mwisho wake. (mifano hipo katika
kitabu cha kutoka 14:4, 17).
Katika Hekalu la
kipindi cha miaka elfu moja Roho mtakatifu ndani ya wateule kama Hekalu la
Mungu uhamisa upeo huu wote. Hili limekuwa Kanisani Tangu mwanzo wa kanisa pale
haugwani.
Yehova anena kwamba
watatafuta mengi na wakapokea havivu. Waliotunza vilipeperushwa mbali. Hapo
tena alitoa jib: Sababu nyumba hipo katika maangamizi. Hivyo ni kusema
hawajafanya chochote kwa wakati wa karne yote tokea agizo la Cyrus hadi lile la
Dario Hystaspes wakati ambapo wangetenda kazi kujenga, na Mungu aliwaadhibu kwa
hilo. Ilikuwa tu wakati wa utawala wa Artashasta wa 1 ambapo ujenzi ulikatishwa
lakini hawakufanya Juhudi zozote hili kufufua ujenzi baada ya Artashasta
alikomesha vita vya wenyewe kwa wenyewe (taz. masomo Nambari 13 ibid/katika lile
lililotajwa).
9.
Mlitazamia vingi, kumbe vikatokea vichache; tena mlipovileta nyumbani
nikavipeperusha. Ni kwa sababu gani? Asema Bwana wa majeshi. Ni kwa sababu ya
nyumba yangu inayokaa hali ya kuharibika, wakati ambapo ninyi mnakimbilia kila
mtu nyumbani kwake. 10 Basi, kwa ajili
yenu mbingu zimezuiliwa zisitoe umande, nayo nchi imezuiliwa isitoe matunda
yake. 11 Nami nikaita wakati wa joto
uje juu ya nchi, na juu ya milima, na juu ya nafaka, na juu ya divai mpya, na
juu ya mafuta, na juu ya kila kitu itoacho nchi, na juu ya wanadamu, na juu ya
wanyama, na juu ya kazi zote za mikono. (Biblia Takatifu BT)
Mungu aliweka
ardhi chini ya laana na mafuno yalisuhiliwa kwa ajili ya ukaidi wao.
Wakati Mungu
aliwakemea walitubu.
Hapo watu
walikusanyika tayari kutenda kazi. Tena Bwana akanena kupitia Haggai.
13 Ndipo
Hagai mjumbe wa Bwana, katika ujumbe wa Bwana, akawaambia watu, akisema, Mimi
nipo pamoja nanyi, asema Bwana. 14 Bwana
akaiamsha roho ya Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na roho ya
Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, na roho zao mabaki ya watu; wakaenda,
wakafanya kazi katika nyumba ya Bwana wa majeshi, Mungu wao; 15 katika siku ya ishirini na nne ya mwezi,
katika mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa Dario mfalme. (Biblia
Takatifu BT)
Ujumbe na toba
vikafanyika kwa siku ya 24 tangia mwezi mwandamano hadi siku ya ishirini na nne
ya mwezi wa sita.Tazama pia katika masomo haya Daraja
ya Musa [070].
[The
Ascents of Moses (No. 70)]
Unabii wa Haggai ulikaguliwa tena katika masomo haya Vipaumbele Vya Mungu [184] [The Oracles of God (No. 184)] mradi kushulikia hoja nyingi kuhusu kalenda, na kutumika vibaya kwa unabii wa Haggai na Daniel kwa matukio ya nyakati za mwisho. Maoni yaliyo muhimu kwa Haggai yamenakiliwa hapa.
Mafundisho katika sura ya 1 ni kusihi taifa la Yuda ili
kuanza kazi ya Hekalu. Taifa halijabarikiwa kwa sababu wametangulisha matakwa
yao binafsi juu ya yale ya Mungu. Kunayo mambo mengi katika hadithi ambayo ni
sambamba kabisa na ile tabia ya Yuda pamoja na utepetevu wa kazi ya Mungu. Ikiwa unabii huu unauhusu dalili za
siku za mwisho, lazima basi urejelee lile Hekalu la Kiroho, ambalo ni Kanisa.Washirika wenyeji katika unabii huu
ni Zerubbabel, mwana wa Sheltiel msimamizi wa Yuda, na Yoshua, mwana wa Yosedach
kuhani mkuu. Huu wakati ulikuwa mwaka wa pili wa utawala wa Dario II. Jambo
hili limeelezewa kwa kina katika masomo haya Ishara ya Yona na Historia ya
Ujenzi mpya wa Hekalu [013]. Majina hayo ni ya watu binafsi wa
wakati ule wa ukarabati wa Hekalu ya pili (taz. Pia masomo haya Ukoo wa
masihi (Nam. 119).
Ikiwa unabii ni wa siku za baadaye tunaweza tu kutaja juu ya Hekalu ya kiroho, na haina ya Zerubbabel na Yoshua, kama Kuhani Mkuu. Kuhani Mkuu Yoshua, ni Yeshua au ni Masihi kipeo kwa Yesu Kristo upatikana katika Zakaria wakati wa hukumu. Kristo ni kuwili akiwa mfalme na kuhani akitimisha vipeo vyote. Agizo katika sura ya 1 ya kitabu cha Haggai linanena kwamba taifa la Israeli halitanawili hadi pale watakapofanya kazi ya Masihi katika mategenezo kama sehemu ya Hekalu la Mungu. Laana za ardhi zitaongezeka hadi hilo lifanyike (Haggai 1:10-11). Ishara ya kwanza hipo katikasiku ya 24 ya mwezi wa sita. Hili lilitokea katika Hekalu la pili. Itaweza kuwa imepita au kulenga siku sijazo kama asili ya ishara.
Hivyo Haggai anahusika na ujenzi wa Hekalu,
na Baraka za Israeli ni matokeo yanayofuata kitendo hicho. Hivyo ni vigumu kuhusisha matukio katika
sura ya 2 kwa tukio ambalo alifuatani na tukio katika sura ya 1. Hivyo, kazi ya
Nyumba ya Mungu inaheshimiwa katika siku ya 24 ya mwezi wa sita. Sura ya 2 tena
inaanzia siku ya 21 ya mwezi wa saba au siku ya mwisho ya sherehe za vipanda.
Sikukuu ya mwisho ni siku ya nane ya sherehe” (Vipaumbele
Vya Mungu [184].
UJUMBE WA PILI
Ujumbe wa pili
ulitolewa katika siku ya mwisho ya sherehe za vipinda na kabla ya kuanza kwa
siku ya ishirini na mbili ya mwezi wa saba, ambayo ni sikukuu ya mwisho na hua
sherehe katika haki ya kipekee. Ilikuwa Ishara kwamba Mungu, alitoa maelekezo
kutoka mwezi mwandamano wa awali katika mwisho wa kipindi cha majafuko na muozo
na kutawanyisha, na ni baada ya urejesho wao katika Ardhi takatifu.
Tena alinena nao
katika mwezi wa saba na kile kinakisiwa kama uwakilisho wa mfumo wa millennia
na kabla ya kisiwa kuwa kipindi cha ufufuo wa pili wa wafu Walihitajika kutunza
sherehe na ni baada ya sherehe za miaka elfu moja ambapo wangeanzisha ujenzi.
Ujumbe huu na
unabii ulikuwa wa aina mbili kiasili.
Ilikuwa kutazama mbele kuelekea matengenezo ya Yudah katika ardhi takatifu na
kuelekeza kwa kukemewa kwao na toba lao katika kipindi cha mwisho kabla ya
kurejea kwa Masihi.
Tazama katika ujumbe wa Mungu. Ni moja kati
ya zile ambazo utia moyo kuhusu vitendo vyake vya wakati wa kutikishwa kwa
mbingu na ardhi na mataifa. Hili linahusu vita vya mwisho pamoja na siku za
mwisho.Hili halijahusishwa na kuokoka bado bali kuletwa katika kutiishwa na
baadaye tena kuletwa katika toba na kuongoka (taz Masomo
haya siku ya bwana na siku za mwisho (Nam. 192) [The
Day of the Lord and the Last Days (No. 192)] na
Miaka
thelethini ya mwisho: Jitihada za Mwisho
(Nam. 219).
[The
Last Thirty Years: the Final Struggle (No. 219)]
Sura
ya 2
1 Katika mwezi wa saba, siku ya ishirini na moja ya mwezi, neno la
Bwana lilikuja kwa kinywa cha Hagai nabii, kusema, 2 Sema
sasa na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na Yoshua, mwana wa
Yehosadaki, kuhani mkuu, na hayo mabaki ya watu, ukisema, 3 Miongoni
mwenu amebaki nani aliyeiona nyumba hii katika utukufu wake wa kwanza? Nanyi mnaionaje sasa? Je! Mbele ya macho
yenu, siyo kama si kitu? 4 Lakini sasa uwe hodari, Ee
Zerubabeli, asema Bwana; nawe uwe hodari, Ee Yoshua, mwana wa Yehosadaki,
kuhani mkuu, nanyi iweni hodari, enyi watu wote wa nchi hii, asema Bwana;
mkafanye kazi, kwa kuwa mimi ni pamoja nanyi, asema Bwana wa majeshi; 5 kama neno lile nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya
Misri; na roho yangu inakaa kati yenu; msiogope. 6 Kwa
maana Bwana wa majeshi asema hivi, Mara moja tena, ni kitambo kidogo tu, nami
nitazitikisa hizo mbingu, na hii nchi, na bahari, na nchi kavu; 7 nami nitatikisa mataifa yote, na vitu vinavyotamaniwa na
mataifa yote vitakuja; nami nitaijaza nyumba hii utukufu, asema Bwana wa
majeshi. 8 Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali
yangu, asema Bwana wa majeshi. 9 Utukufu wa mwisho wa
nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, asema Bwana wa majeshi;
na katika mahali hapa nitawapa amani, asema Bwana wa majeshi. (Biblia Takatifu
BT)
Siri ya mataifa yote imetolewa katika maandiko ya kale kwa kiyunani
(LXX) Kama wateule wa mataifa yote. Ni
lasima basi kuhihusu Kanisa na uongovu wa watu wa mataifa.
Hekalu la roho
litasengwa kadili ya sikukuu arobaini za sherehe ya jubilee au mwaka elfu mbili
toka 30CE hadi Kristo ataporejea mara ya pili.
Nyumba timilifu
ya mungu itaundua upya bali utakuwa wakati wa mfumo wa kipindi cha miaka elfu
moja ya utawala wa wateule baada ya kurejea kwa masihi mara ya pili na baada ya
kutiishwa kwa mataifa yote. Hii ni hema takakatifu ya miaka elfu moja ya
utawala wa wateule inavyorejelewa na Ezekiel (cf. comp Biblia fn to 2.77
utukufu wa baadaye utakuwa mkuu kuliko ule wa kwanza (ef. Ezekiel 43:2-5)
Nyumba onekanefu haitajengwa kabla ya miaka elfu moja ya utawala wa wateule
bali katika wakati wa elfu moja yenyewe. Sherehe za ukumbuzo wa kwanza wa miaka
elfu moja itakuwa wakati wa ukumbusho wa sherehe za sikukuu ya mwaka wa hamsini
kwa kuwa angizo hili lilikwisha tolewa, Zakaria pia alikabidhiwa mpangilio wa vitendo
(taz Ufafanuzi wa Kitabu cha Zekaria [297] [Commentary on Zechariah (No. 297)] na Yubile
Kuu ya Dhahabu na Milenia [300]) [The Golden Jubilee and the Millennium (No. 300)].
Hekalu la kiroho la
Mungu liliamishwa tangu wakati wa siku za hamsini baada ya pasaka/siku ya roho
mtakatifu (30cc Pentecost) ambao ulikuwa mwaka wa tatu wa andamano baada ya
sikukuu ya Yumbilee ya 27CE tutaweza kuamini kwamba Hekalu onekanefu na miundo
yake vitaasisiwa katika Yerusalemu toka mwaka wa tatu wa ukumbuzo wa sikukuu ya
121 kwa mwandamo wake mfano 2030 wakati huo tutashugulikia utaratibu ulioko
katika masomo yenye mada hii.
Ujumbe ulirejea
tena kupitia Haggai katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa. Ujumbe
ulikuwa juu ya kuwekwa wakfu na ukafiri. Hapa inahusu ukombozi wa watu wa
mataifa na utakaso wao. Maneno mwili
matakatifu katika maandiko ni nyama ya kafara, ambayo uhusiana na wateule
wa Mungu baadaye.Neno lasema kwamba mwili mfu ni nephesh au nafsi na ni moja ya mafungu 13 mahali ambapo neno nephesh linatumika kuashiria nyama mfu. Hapa uleta
mtawinyiko kati ya waliokufa ambao hawakuongoka, na wateule walio hai ambao wamealikwa na
Mungu. Wakati wa kipindi cha miaka elfu moja Yuda na Israel watarejeshwa pia
mataifa yote yatarejeshwa na kuletwa katika utakaso na kuwekwa wakfu katika
msingi wa kuendelea mbele (taz pia masomo Ufafanuzi wa Kitabu cha Zekaria [297] na Utakaso wa Mataifa [077] [Sanctification
of the Nations (No. 77)].
10
Siku ya ishirini na
nne, ya mwezi wa kenda, katika mwaka wa pili wa Dario, neno la Bwana lilikuja
kwa kinywa cha Hagai nabii, kusema, 11 Bwana wa
majeshi asema hivi, Waulizeni sasa makuhani katika habari ya sheria, mkisema,
12 Mtu akichukua nyama takatifu katika upindo wa nguo
yake, naye akagusa kwa upindo wake mkate, au ugali, au divai, au mafuta, au
chakula cho chote, je! Kitu hicho kitakuwa kitakatifu? Makuhani wakajibu,
wakasema, La. 13 Ndipo Hagai akasema, Kama mtu
aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti, akigusa kimojawapo cha vitu hivi, je! Kitakuwa
najisi? Makuhani wakajibu, wakasema, Kitakuwa najisi. 14 Ndipo
Hagai akajibu, akasema, Hivyo ndivyo walivyo watu hawa, na hivyo ndivyo lilivyo
taifa hili mbele zangu, asema Bwana; na hivyo ndivyo ilivyo kila kazi ya mikono
yao; na kitu hicho wakitoacho sadaka huko ni najisi.(Biblia Takatifu BT)
Matabahu
yalijengwa mbele ya Hekalu na kafara zimeainishawa kama najisi. Hata hivyo,
haya yanalenga mbele katika wakati wa jitihada za kafara zitazotekelezwa na
yuda bila toba, uongofu na ubatiso.
15
Na sasa nawaomba,
tafakarini; tangu siku hii na siku zilizopita; kabla halijatiwa bado jiwe juu
ya jiwe katika nyumba ya Bwana; 16 katika
wakati huo wote, mtu alipofikia chungu ya vipimo ishirini, palikuwa na vipimo
kumi tu; na mtu alipofikia shinikizo apate kuteka divai ya vyombo hamsini,
palikuwa na divai ya vyombo ishirini tu. 17 Naliwapiga kwa ukavu, na ukungu, na mvua ya mawe, katika kazi zote za
mikono yenu; lakini hamkunielekea mimi, asema Bwana. (Biblia Takatifu BT)
Maana Mungu
kuwapa mapigo ni mfano tu katika Kumbukumbu la torali 28:22. Hata hivyo, hili
litakuwa badili ya toba.
18 Tafakarini,
nawaomba; tangu siku hii ya leo na siku zijazo; tangu siku ya ishirini na nne
ya mwezi wa kenda, naam, tangu siku hiyo ulipowekwa msingi wa hekalu la Bwana
tafakarini haya. 19 Je! Mbegu ingali ghalani? Naam, huo mzabibu,
wala mtini, wala mkomamanga, wala mzeituni, haikuzaa kitu; tangu siku hii ya
leo nitawabariki. 20 Kisha neno la Bwana likamjia Hagai mara ya
pili, siku ya ishirini na nne ya mwezi, kusema, 21 Sema na
Zerubabeli, liwali wa Yuda, ukisema, Nitazitikisa mbingu na dunia; 22 nami nitakipindua kiti cha enzi cha falme, nami nitaziharibu nguvu za
falme za mataifa; nami nitayapindua magari, na hao wapandao ndani yake; farasi
na hao wawapandao wataanguka chini; kila mtu kwa upanga wa ndugu yake. 23 Katika siku ile, asema Bwana wa majeshi, nitakutwaa wewe, Ee
Zerubabeli, mtumishi wangu, mwana wa Shealtieli, asema Bwana, nami nitakufanya
kuwa kama pete yenye muhuri; kwa kuwa nimekuchagua, asema Bwana wa majeshi. (Biblia
Taakatifu BT)
Mbegu zitapandwa na
Mungu atabariki upanzi huu kabla ya kusanywa na kuletwa ndani na kuzidishwa.
Baraka za Yuda
zitatokea wakati Yuda wataanza kubariki mataifa na Hekalu likiwa limeanzishwa
katika Yerusalemu chini ya Masihi katika siku hiyo. Utajiri/ukuasi wan chi
takatifu utaongezeka mara kumi. Uharibifu wote utaponywa na nchi itarejeshwa.
Unabii huu basi
umeiweka siku ya 24 ya mwezi wa tisa kama asili ya rehema ya Mungu kwa Israel
na baraka zake kwa taifa. Kwa kawaida limekuwa likitazamwa kama neno la wakati unaofaa
kwamba matengenezo yamekamilishwa. Na ndio iliyosababisha jitihada zilizofanywa
kudai taifa la watu wote chini ya Jemedari mkuu Allenbi waliwashinda Yerusalemu
mwaka wa 1917 mwezi wa Chisler siku ya 24. Hata hivyo, kuingia Yerusalemu kwa
Allenby kulikuwa mwezi wa Chislev, lakini ushindi haukuwa siku ya 24 uvamizi
ulianzishwa siku ya 24 mwezi wa chislev kuambatana na mwungano wa mwezi
mwandamo, na si kuambatana takuimu ya Hillel. Yamechunguzwa Kinaganaga katika
masomo haya Vipaumbele
Vya Mungu [184] kusudi maalum ya kimsingi ya masomo hayo
ni kushugulikia hoja ya usia wa Mungu na pale ambapo makaazi ya mamlaka ya
takuimu.
Tutahitajika
kutilia maanani maelezo haya yaliyo elezwa kwa kina ambayo ni hesabu kuhusu
matengenezo ya Israel katika siku za nwisho.
Kunukuu Vipaumbele Vya Mungu [184] tunaona kwamba:
“Ushauri
uliotolewa katika unabii huu ni:
Kutokana na hoja
hizo tunahoji kuwa takuimu ya Hillel basi ni pumsi la Mungu na ni usia wake
Mungu.
Kuambatana na
kuanguka kwa Yerusalemu, kwanza, kamusi ya Biblia ya mpiga kinubi imeandikwa
Wababiloni waliteka mji wa Yerusalemu mwaka wa 598 BCE, na mji huu
ulisawanzishwa katika mwaka 587 BCE. Hakuna kati ya tarehe hizi zote huteta
1917 kwa kujumilisha miandamo mara saba au mwaka 2,520. Tarehe ya kwanza huleta
1923 na tarehe za nyuma zita leta 1933.
Tutakavyona sasa
mchakato huu ni bora ukitafakariwa kimwandamo. Ni bayana kutokana na uchunguzi
wa hadithi ya uhuru wa Yerusalemu ambapo matukio yaliorodheshwa kwa jinsi
yalivyotokukia, ili kutokeza wazo la
Mungu akitekeleza kazi ya utimisho wa unabii sababu watu wa wakati huo waliona
hilo kama utimilifu wa unabii. Tarehe ya 9 Disemba 1917 ikishawekwa itatumika
kuhalalisha takuinu ya Hillel iliyofanya msingi wa uanzilishi wa mara ya
kwanza.
Katika mwaka wa 1917 nchi takatifu ilifunguliwa na wa Australia, New Zealand na Uingereza, na miungano mingine ya kijeshi waliopiga vita Wauturuki pamoja na vikozi vya Ujerumani vilivyoongezea nguvu kulingana na mpangilio rasmi wa vita (H.S. Gullett, The Australian Imperial Force in Sinai and Palestine, Vol. II of the Official History of Australia in the War of 1914-18, Angus and Robertson Ltd, Sydney, 1937), Gaza na Berisheba walikuwa wamechukuliwa kufikia 31st Octoba hadi 1 Novemba 1917. Kuteka kwa Wapalestina hakungesuilika. Mnamo tarehe 2 Novemba 1917 tangazo la Balfour juu ya kuasisiwa kwa Boma ya wayaudi ilitolewa na waziri mkuu Balfour kama tangazo lake la kwaza (tangazo la pili lilihusu jumuia ya madola ya Australia chini ya sheria ya Uingereza). Kutekwa kwa Yerusalemu hakukutelezwa hadi Disemba. Maendeleo ya vikozi ni hifuatayo.
Vita vya Beersheba |
31 Octoba hadi 1 Novemba |
Tel el Khuweilfe |
8 Novemba |
Kukatokea
Ushindi (Sinai na Palestine
4-8 Nov.) |
6-11 Novemba |
The Great Drive was made |
8-15 Novemba |
Pahali Tambalale ba Bahari
yaliondozwa |
11-17 Novemba |
Yerusalemu kuendelzwa Zaidi |
16-24 Novemba |
Nahr Auja na El Buij |
24 Novemba - 1 Disemba |
Mashamblishi ya mwisho kwa kuuteka mji wa Yerusalemu |
7 Disemba |
Mashambulishi ya mwisho yalianzishwa na vikozi vya jumuia ya madola mnamo tarehe7 Disemba 1917. Kuambatana na mwezi mwandamo wa kweli, 24 Chisler ilikuwa tarehe halisi (takuimu ya Hillel ilianza mwezi wake siku mbili baadaye) Waturuki na Wajerumani walianzisha uamisho ghafla, na kufikia 8 Disemba 1917 Yerusalemu ilikuwa huru. Askari wa nchi kavu walikua wamekita misisi kufikia tarehe 10 Disemba askari wafarasi wenye siraha nyepesi walizidi kuingia ndani kupitia barabara ya Nablus takribani umbali wa maili nane. Waliendeleza mizinga mizito ya Uturuki wakiendelea kuteka kusini kuelekea mpaka wa ponde la Yorodani na walijitahidi kudhibiti vinjia vilivyovuka mto kuelekea leli ya Hejaz na hivyo kudhibiti shughuli za Alleby za upande wa kulia.
Hakukuwa na tukio lolote tarehe 9 Disemba 1917 kwa kuwa Yerusalemu tiyare ilikuwa imekombolewa tarehe saba. Wengi wavwanahistoria wa asili ya Kiprotestanti wanaonekana kujaribu kudai kuwa Disemba 9 ilikuwa ndio siku ambayo Allenby aliingia Yerusalemu na kuikomboa.
Ukweli wa mambo ni kuwa Allemby aliingia Yerusalemu rasmi mnamo tarehe 11 Disemba 1917. Allenby alikuwa mwangalifu sana juu ya tamasha za majivuno ya jinsi mfalme wa miliki ya Ujerumani Wilhelm (William) alivyoingia Yerusalemu mwaka wa 1908. Makusudi alifanya kuingia kwake kuwa jambo la hali ya chini sana wakipitia kiingilio chembamba cha mlango wa Jaffa kwa barabara ya Jaffa ili kukabiliana na tukio lolote kama litatokea, hivi vikozi vilijumuhishwa na vikozi vya Uingeresha, Scotland, Ireland, Welsh, Ghurkas, Australians na Waitalia. New Zealanders walisika samu zaidi Jaffa ili utawala uweze kubainishwa. Rangi iliyotambulika tu ni ile ya mtengo ya vokosi vya Ufaransa wakiwa na share za rangi ya samawati na nyeupe. Hii mara ya ishirini na nne ambapo Yerusalemu iliingiwia kwa njia ya uvamishi wa kimabavu (Gullett, ibid., p. 523) lakini haikuwa siku ya 24 Chisler 1917. Kulingana na takuimu ya Hillel ilikuwa 26 Chislev, lakini kutoka mwezi mwandamo halisi ilikuwa mnamo 28 Chislev. Vikozi vyetu kwa kweli waliingia mnamo 24 cheslev, bali kwa njia ya uvamishi. Hayo ni kulingana na muungano halisi na bila kuhairishwa.
Yerusalemu katika wakati wa kutekwa hawa kushwa ushahidi wa kulenga umaskini lakini ilikuwa katika hali ya uchafu isiyoeleweka. Ilikuwa ime chafuliwa na wausaji wa mazao ya kidini na ibada ya kinafiki ambao kawaida walikuwa najisi kwa usaidishi wa desturi za zamani ya askari za uturuki kwa miaka tatu.
Kwamba Kakristo wakumbuka kufika kwao kwa mshangao (ibid, masomo 522) Baada ya shughuli za Yerusalemu mji ulikabiliwa na ukosefu wa cakula na waingelesha walilazimika kusafilisha msaada Yerusalemu kupitia ziwa Meditaranean. Mkopo wetu kutoka kusini ulikuwa unaenda kwa haraka kwamba waturuki hawakuwa na wakati kuwafanya waamiaji wa sehemu za Kusini kuwa bure. Walikuwa wanathibitisha kuwa wao ni wa maana. Agizo la kizionist chini ya Raisi wa muungano wa utawala wa kizionist wa uingereza. Daktari weizmann aliulishwa kwa amri ya serikali la uingereza pamoja na kujenga upya Palestina. Kazi hii iliusisha matengenezo kutokana na uharibifu wa karne ya kumi na nne na nusu (The Times History of the War, Vol. XV, London, 1918, p. 179).
Kusudi hapa inaweza onekana katika mwangaza wa kihistoria ambao hauna uongo wa waprotestant wenye hawakuhusika na ambao ni uvumi wa British Israelite ianayotoka Marekani.
Katika yote haya,
lazima tukumbuke kuwa Yuda haikuwa imebarikiwa katika hatua hii. Ni upotevu
kudhani kuwa Mungu angefanya wakati huu kuwa hitimisho la unabii wa Haggai na
kuwacha unabii mwingine ambao utatimishwa wakati Yuda Angepitia dhiki za maisha
yake kama taifa.
Miandamo saba
halisi kulainishwa kwa Yerusalemu na wababuloni, chama nazi kitwaa utawala
katika Ujerumani na wakaanza utaratibu wa kutesa Wayaudi. Toka 1992 hadi 1945
Ujerumani walitekeleza mauaji yaliyopangwa kwa watu wa ugaidi au tunaweza sema
Nchi yoyote iliyoingia katika kumbukumbu za kihistoria. Kuthibitisha hayo hii ilikuwa
nia ya Mungu kubariki Yuda, katika kukamilisha unabii wa kitabu cha Haggai,
tunaweza sema kwa ufupi kuwa ni njia iliyo patoka mno ikiwa mtu atafikilia kuwa
kitabu cha Haggai kimekamilishwa katika vitendo hivi.
Hairidishi hata hivyo kusema kwamba kitabu cha Haggai kimetimishwa.
Walakini, tunaweza kifupi kuwa tarehe hii
24 Chislev 1917, ilikuwa mwanzo wa kuasisiwa kwa Yerusalemu kama ngome ya
makaazi ya Wayaudi iliyotangazwa na Balfour katika tangazo la tarehe 2 November
1917. Tangazo lingine la Balfour lilikuwa kuhusu
Ikiwa tutazama zoezi hili kama mfano wa
maagizo ili kujenga Hekalu la zamani jinsi ilivyokuwa toka wakati wa amri ya
Cyrus hadi mwanzo wa ujenzi wa Hekalu chini ya Dario Muajemi, hapo tunapata
mlolongo wa nyakati inayotanda kipindi chote cha miaka mia moja na kumi na
sita. Hivyo kutolewa kwa tangazo la Balfour ni mwanzo wa mfururisho wa maagizo tokea
1917. Kuitangaza kulifanyika katika siku ya kumi na nane ya mwezi wa nane wa
mwaka wa arobaini wa sikukuu ya ukumbuzo wa 118 au 2 Novemba 1917. Mwisho wa
kipindi cha miaka 116 kuelekea mfumo wa kipindi cha miaka elfu moja ni katika
mwaka wa 2033, au mwaka wa sita wa mfumo wa Millenia. Tunaweza tarajia mwaka wa tatu hadi wa sita wa
millennia kuhusishwa na Hekalu na ujenzi
wa makaazi ya utawala wa kimellania kuambatana na unabii. Taz. somo Yubile Kuu ya Dhahabu na
Milenia [300] na Ukumbusho wa miaka
hamsini na mileniia sehemu II Israeli na mataifa yanayowazingira( (Nam. 300B).
Kurejelea kwa pete yenye muhuri ni sambamba na Zakaria 4:7-10 na 6:13 (cf mwanzo 41:42 na Esta 3:10) ufananisho huu unaonekana pia katika wimbo uliobora na Yeremia 22:24.
Aliyeteuliwa ni yule mfalme wa kweli na msimamizi wa Isaya 9:6-7 wateule wote wameteuliwa kama Daudi na uzao wake uliteuliwa (Wafalme 8:16, 11:34, cf. pia Zakaria 12:8)
Kuzinduliwa kwa Hekalu ambayo imetajua hapo kunaonekana kuwa Hekalu hili lilikuwa kubwa kuliko lile la Solomon huo ulikuwa mdomo tu.
Kwa kweli unabii katika Daniel 9:25-27 unaonyesha kwamba Hekalu litajengwa zaidi ya majuma sabini ya miaka. Hakuna tashwishi kwamba Hekalu la pili, na ukarabati wa Herodi havingeweza kulinganishwa na Hekalu la Sulemani. Hekalu linalozugumziwa hapa ni unabii unaopambanisha Hekalu la kiroho chini ya masihi na hile Hekalu la kiroho hile Hekalu Onekanevu pamoja na Agano la kale.
Roho wa bwana alikuwa amedumu ndani ya watu na hili lilitokea Kanisani katika miundo msingi thabiti. Haggai 2:6 limeandikwa katika waeberania 12:26-27
26 ambaye sauti yake iliitetemesha nchi wakati ule; lakini sasa ameahidi akisema, Mara moja tena nitatetemesha si nchi tu, bali na mbingu pia. 27 Lakini neno lile, Mara moja tena, ladhihirisha kuhamishwa vile viwezavyo kutetemeshwa, kama vitu vilivyoumbwa, vitu visivyoweza kutetemeshwa vikae. (Biblia Takatifu BT)
Hii ni onyo la moja kwa moja kutoka kwa masihi kunena kwamba unabii huu unahusu tetemesho la mwisho litakalo tetemesha Mbingu na ardhi hivi kwamba kitu ambacho hakitatikishwa kitadumu. Hili tetemeko litaanzia katika Hekalu la Mungu, ambalo amblo ni Kanisa. Wakiwa naos au Mtakatifu wa Watakatifu (1 Wakorintho 3:17) kwa sababu hii hebu tumshukuru Mungu kwa ajili ya kupokea ufalme ambao hautatetemeka (Waeberania 12:28)
Wakati utawadia katika vita vya mwisho na
kurejea kwa Masihi mara ya pili. Vita vya kwanza vya dunia vilitajua kama vita vikuu vya ustaharabu sababu watu
wakizia kwamba mwisho wa dunia umewadia na 1914-1916 katika unabii ilionekana
barabara kama kukamilishwa kwa mara ya saba tokea utawala wa Nebukadresa. Ikianzia
mapigano ya karkemish katika mwaka wa 605 BCE mapigano ya mwisho wa dunia kwa
kweli yalianzia tokea tarehe hii, lakini yangeedelea kwa wakati uliorefushwa na
unabii sanasana uliohusisha matengenezo chini ya Masihi. Tarehe 24 Chisler (mwezi
wa tisa) inahusu swala la utakatifu na unajisi (Haggai 2:10-1). Taifa
linatazamwa kama najisi, na taifa tokea wakati huu limetakaswa kutokana na
unajisi wake. Jambo hili limehusishwa moja kwa moja kwa dhana ile ya kuwekwa
jiwe juu la lingine katika Hekalu. Tokea siku hiyo na kuendelea ni ujenzi wa
Hekalu. Mpangilio huu hauna huusiano na vitu vinavyoonekana bali kubarikiwa kwa
Hekalu kutaendelea. Ndio maana maangamizi ya moto yalitendeka hivyo sababu
taifa lilikuwa alijaongoka na baraka za Bwana hazikuwa zimetolewa. Bado kutakuwa
na vita zaidi na maagamizi zaidi katika Yuda na katika Israeli hadi pale wote
watakapofikia Toba na utakazo kutokana na dhabi zao (Vipaumbele
Vya Mungu [184]).
Hekalu linaendelea Kujengwa kutumia mawe hai na Mungu hataruhusu muundo onekanevu kutenda kazi katika msingi asili unaoendelea hadi wakati ambapo Masihi atarejea na Yuda akiwa ameongoka. Jitihada za kufanya hivyo zimeshindwa hadi leo hii na kusababisha adhabu kali kwa Yuda. Hakuna Myaudi au mtu wa mataifa asiyeongoka ambaye anaruhusiwa kushiriki katika Hekalu.
Wale tu watatubu na kupokea ubatiso ndio wataweza kuwa sehemu ya mchakato huo hili izifanyike najisi. Falme za ulimwengu huu zitaangushwa na kitu kilichoabishwa Babuloni kitafanywa pete yenye muhuri kwa Bwana wa majeshi. Wanajisi watatakaswa na wataitwa watakatifu katika Bwana na watawala kama watakatifu wa Mbiguni, kama wafalme na makuhani ndani na Nche ya Yerusalemu.