Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[102]
Naona Kiu
(Toleo La 1.0 20000416-20000418)
Maneno ya mwisho yaliyonenwa na Kristo alipokuwa anakufa yana maana ya kinabii
na yanahusiana na utaratibu wote wa sheria ya utoaji dhabihu na wa ondoleo la
dhambi au msamaha na upatanisho wa Mungu, kama ulivyotabiriwa kwenye Zaburi na
ushuhuda mwingine.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati
Miliki © 2000 Wade
Cox)
(tr.
2015)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Naona Kiu
Mtume Yohana ananukuu maneno ya mwisho yaliyotamkwa na Masihi, kabla ya
kifo chake pale mtini (au kwenye mti uliosimamishwa wima) alipokuwa
anasulibiwa. Alikuwa ni shuhuda aliyeshuhudia kwa macho yake.
Kulikuwa na maneno saba aliyoyanena pale mtini. Mathayo 27:46 na Marko
15:34 kumenukuliwa na kuandikwa usemi mmoja.
Mathayo 27:46 Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake
kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu
wangu, mbona umeniacha?
Luka ananukuu kwa kuandika maneno mengine matatu kwenye Luka 23: 34, 43,
46.
Luka 23:34 Yesu
akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake,
wakipiga kura.
Luka 23:43 Yesu
akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.
Luka 23:46 Yesu akalia
kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu. Alipokwisha
kusema hayo alikata roho.
Yohana pia ananukuu semi tatu nyingine hapa kwenye sura za 19:26, 27, 28 na
30.
Yohana 19:26-30 Basi
Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu,
alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao. 27 Kisha
akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule
akamchukua nyumbani kwake. 28 Baada ya hayo Yesu, hali
akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona
kiu. 29 Kulikuwako huko chombo kimejaa siki; basi
wakatia sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakampelekea kinywani. 30 Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema,
Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.
Ni wazi sana kutoka kwenye Luka 23:44 kwamba ahadi ya muuaji ilikuwa kabla
ya giza.
Maneno ya kwenye Zaburi 22:1 yalinenwa mwanoni au kabla ya kufika saa tatu
za giza (sawa na tafsiri ya Bullinger, Companion
Bible, angalia Yohana 19:30).
Bullinger anaichukulia hii kuwa ni kwamba Kristo aliitamka au kuiimba
Zaburi yote ya 22 kama ushuhua kwa makuhani wakuu waliokuwepo (Marko 15:31 na Luka
23:35). Kwa kifo chake alifanyika kuwa ushuhuda dhidi ya makuhani hawa na imani
iliyoharibika na kupotoka waliyoiachia kuinuka. Kutoka kwenye hatua hii na
kuendelea walifanyika kuwa Ishara ya Yona na waliwekwa wenye ukomo wa toba au
maangamizo. Ilipofika siku ya 1 Abibu au Nisan, ya mwaka 70 BK, miaka arobaini
kamili ilyofuatia, mwanzoni mwa Mwezi wa Kwanza na Mwaka Mpya, Yerusalemu
ulizingirwa na Majeshi ya Warumi. Utaratibu wa Hekalu pamoja na makuhani wake
walipewa miaka arobaini ya kufanya toba sawa na mlingano wa siku moja kwa mwaka
mmoja walizopewa watu wa Ninawi (soma jarida ya Ishara ya Yona na Historia Ujenzi Tena wa Hekalu (Na. 13)).
Zaburi 22 ni Zaburi ya Mtesekaji, inayomwelezea Mtesekaji na pia utukufu
utakaofuatia.
Zaburi 22:1-31 Mungu
wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno
ya kuugua kwangu? 2 Ee Mungu wangu, nalia mchana
lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha. 3 Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za
Israeli. 4 Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini,
na Wewe ukawaokoa. 5 Walikulilia Wewe wakaokoka,
Walikutumaini wasiaibike. 6 Lakini mimi ni mdudu wala
si mtu, Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu. 7 Wote
wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao; 8
Husema, Umtegemee Bwana; na amponye; Na amwokoe sasa, maana apendezwa
naye. 9 Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni,
Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu. 10 Kwako
nalitupwa tangu tumboni, Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu. 11 Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, Kwa maana hakuna
msaidizi. 12 Mafahali wengi wamenizunguka, Walio
hodari wa Bashani wamenisonga; 13 Wananifumbulia
vinywa vyao, Kama simba apapuraye na kunguruma. 14 Nimemwagika
kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na
kuyeyuka ndani ya mtima wangu. 15 Nguvu zangu
zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika
mavumbi ya mauti 16 Kwa maana mbwa wamenizunguka;
Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu. 17
Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; Wao wananitazama na kunikodolea
macho. 18 Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu
wanalipigia kura. 19 Nawe, Bwana, usiwe mbali, Ee
Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia. 20 Uniponye
nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa. 21 Kinywani
mwa simba uniokoe; Naam, toka pembe za nyati umenijibu. 22 Nitalihubiri
jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu. 23
Ninyi mnaomcha Bwana, msifuni, Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo,
mtukuzeni, Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli. 24 Maana
hakulidharau teso la mteswa, Wala hakuchukizwa nalo; Wala hakumficha uso wake,
Bali alipomlilia akamsikia. 25 Kwako zinatoka sifa
zangu Katika kusanyiko kubwa. Nitaziondoa nadhiri zangu Mbele yao wamchao. 26 Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao Bwana watamsifu;
Mioyo yenu na iishi milele. 27 Miisho yote ya dunia
itakumbuka, Na watu watamrejea Bwana; Jamaa zote za mataifa watamsujudia. 28 Maana ufalme una Bwana, Naye ndiye awatawalaye mataifa. 29 Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu, Humwinamia
wote washukao mavumbini; Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake, 30 Wazao wake watamtumikia. Zitasimuliwa habari za Bwana,
Kwa kizazi kitakachokuja, 31 Nao watawahubiri
watakaozaliwa haki yake, Ya kwamba ndiye aliyeyafanya.
Kwenye maandiko ya Yohana 19:23-24 tunamuona mwingine na unabii wa mwisho
ukitimia. Maaskari waligawana nguo zake kwa kuzipigia kura kwa vazi au kanzu zake
kama ilivyotabiriwa (Zaburi 22:18). Hii ni sehemu ya mwisho ya unabii na huenda
ulitokea baada ya matamshi yake ya Zaburi 22. Lakini Mungu hakumficha uso wake
wala kumsahau kama inavyosema Zaburi (Zaburi 22:24).
Baada ya kumkabidhi mama yake kwenye uangalizi wa mwanafunzi aliyekuwapo na
ambaye alimchukua mara moja kwenye matunzo, ndipo Kristo aliendelea kukamilisha
Maandiko Matakatifu na unabii kwa kusema maneno haya, “Naona Kiu”. Kisha
walihitimisha kwa kumpitishia sponji iliyojazwa siki, ambayo hatimaye waliitia Hisopo
na kumtia kinywani mwake. Wakati Yesu alipoipokea hiyo siki alisema: Imekwisha (teleõ). Hii ilikuwa na maana inayomaanisha kwamba mambo yote
yaliyotakiwa kufanyika yalikuwa yamehitimika, kwa kuwa Maandiko hayatanguki
(Yohana 10:34-35). Kisha aliinamisha kichwa chake chini, ikimaanisha kuwa
kilikuwa bado kinatazama mbele hadi wakati huu na kisha akaitoa roho yake au
kukata pumzi yake (paradidõmi). Mathayo anasema akaitoa roho yake (Mathayo 27:50).
Andiko pekee ambalo lilikuwa halijatimilika bado halikutimilika hadi
alipokuwa tayari na kumtuma roho wake. Hii ilikuwa ni siku ya 14 Nisan ya mwaka
30 BK. Ilianguka siku ya Jumatano. Hakukuwa na mwaka mwingine ambao Kristo
angeweza kuuawa kwa mujibu wa rekodi za Biblia, kwa kuwa siku ya 14 Abibu au
Nisan iliangukia siku ya Ijumaa (soma jarida la Nyakati za Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159)). Fundisho la Kuteswa na Kuuawa siku ya
Ijuma ni sehemu ya imani ya Easter au ibada za Baal-Istar au Easter, imani ya
waabudu mungu-mke aliyekuwa anaabudiwa na makuhani wa Attis katika pande za Magharibi, au ya waabudu Adonis pande
za Mashariki (soma jarida la Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235)). Pia ina uhusiano na imani ya Ndama wa Dhahabu (soma jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222)). Imani hii ilikuwa pia na uhusiano na
Wafilisti na ibada za Derceto na Joka, ambapo alama za samaki na njiwa
zimetokana na ibada hizi (soma majarida ya Daudi na Goliathi (Na. 126) na Piñata (Na. 276)).
Siku ya Alhamisi, katika mwaka 30 BK, ilikuwa Siku Takatifu ikiwa ni Siku
Takatifu ya Kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyo na Chachu. Jioni au usiku ule
ulikuwa ni wa kuila Pasaka (soma jarida la Pasaka (Na. 98)).
Kwa mujibu wa Torati, siku hii haikupasa itiwe unajisi kwa kugusa maiti au
mwili wa mtu aliyekufa. Kwa hiyo, iliwalazimu kuhakikisha kuwa wawe wamekufa
ndani ya wakati ulioruhuiwa. Miguu ya wasulibiwa wawili wa kwanza waliokuwa pamoja
naye ilivunjwa, lakini walipofika kwa Kristo walimkuta amekwisha kufa tayari na
hawakuivunja miguu yake, ila askari mmoja alimchoma mkuki ubavuni mwake na
ikatoka damu na maji na kumwagika chini ardhini.
Hii ilitokea ili kutimiliza Andiko lingine kuhusiana na kifo chake. Kwanza
kabisa, ni kwamba haukupasa mfupa wake uvunjike (sawa na Zaburi 34:20). Andiko
la pili lilisema, “Watamtazama yeye
waliyemchoma”, ambalo linatoka kwenye Zekaria 12:10. Hii inamaana na dalili
kuuhusu mstari wa uzao wa Masihi (soma jarida la Mstari wa Uzao wa Masihi (Na. 119)). Unabii huu una maana yake pia na kumhusu jinsi
alivyokuwa Masihi na pia hatima ya wateule kwa kufanyika kwao elohim (Zekaria
12:8; soma jarida la Mteule Kama Elohim (Na. 1)).
Kisha alichukuliwa na Yusufu wa Arimathaya, ambaye alikuwa ni mwanafunzi wa
riri wa Masihi, na Yusufu akamuoba Pilato ampe mwili wake na alipewa. Na
mwanafunzi mwingine Nikodemo aliyeleta marhamu au marashi yenye uzito wa
takriban paundi au ratili mia, walimchukua wakamzike kwenye kaburi
alilolichonga Yusufu, ambalo lilikuwa jipya. Jambo hili lilikuwa muhimu pia kwa
utakaso wake akiwa kama dhabihu. Kwa kuyajua maandiko na dhabihu ndipo tunaiona
Zaburi na ubii wake. Zaburi 22 inamhusu au kumlenga Kristo akiwa kama Sadaka ya
Dhambi.
Kwenye Zaburi 40 tunamuona Kristo akiwa kama Sadaka Kamili Yote ya Kuteketezwa.
Zaburi 40:1-17 Nalimngoja
Bwana kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu. 2 Akanipandisha
toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu
mwambani, Akaziimarisha hatua zangu. 3 Akatia wimbo
mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao
watamtumaini Bwana 4 Heri aliyemfanya Bwana kuwa
tumaini lake, Wala hakuwaelekea wenye kiburi, Wala hao wanaogeukia uongo. 5 Ee Bwana, Mungu wangu, umefanya kwa wingi Miujiza yako na
mawazo yako kwetu; Hakuna awezaye kufananishwa nawe; Kama ningependa
kuyatangaza na kuyahubiri, Ni mengi sana hayahesabiki. 6 Dhabihu
na matoleo hukupendezwa nazo, Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za
dhambi hukuzitaka. 7 Ndipo niliposema, Tazama
nimekuja, (Katika gombo la chuo nimeandikiwa,) 8 Kuyafanya
mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni
mwangu. 9 Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko
kubwa. Sikuizuia midomo yangu; Ee Bwana, unajua. 10 Sikusitiri
haki yako moyoni mwangu; Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako. Sikuficha
fadhili zako wala kweli yako Katika kusanyiko kubwa. 11 Nawe,
Bwana, usinizuilie rehema zako, Fadhili zako na kweli yako na zinihifadhi
daima. 12 Kwa maana mabaya yasiyohesabika
Yamenizunguka mimi. Maovu yangu yamenipata, Wala siwezi kuona. Yamezidi kuliko
nywele za kichwa changu, Na moyo wangu umeniacha. 13 Ee
Bwana, uwe radhi kuniokoa, Ee Bwana, unisaidie hima. 14 Waaibike,
wafedheheke pamoja, Wanaoitafuta nafsi yangu waiangamize. Warudishwe nyuma,
watahayarishwe, Wapendezwao na shari yangu. 15 Wakae
hali ya ukiwa, na iwe aibu yao, Wanaoniambia, Ewe! Ewe! 16 Washangilie,
wakufurahie, Wote wakutafutao. Waupendao wokovu wako Waseme daima, Atukuzwe
Bwana. 17 Nami ni maskini na mhitaji, Bwana
atanitunza. Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, Ee Mungu wangu, usikawie.
Kwenye Zaburi 69 tunamuon Kristo akiwa kama Sadaka ya Dhambi (huu pia ni mtazam wa Bullingers sawa na ilivyo kwenye
Znye Zaburi 69:1).
Zaburi 69:1-36 Ee
Mungu, uniokoe, Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu. 2 Ninazama
katika matope mengi, Pasipowezekana kusimama. Nimefika penye maji ya vilindi,
Mkondo wa maji unanigharikisha. 3 Nimechoka kwa kulia
kwangu, Koo yangu imekauka. Macho yangu yamedhoofu Kwa kumngoja Mungu wangu. 4 Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa
changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo
kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua. 5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu, Wala hukufichwa dhambi
yangu. 6 Wanaokungoja Wewe wasiaibishwe, Kwa ajili
yangu, Bwana, MUNGU wa majeshi. Wanaokutafuta Wewe wasifedheheshwe, Kwa ajili
yangu, Ee Mungu wa Israeli. 7 Maana kwa ajili yako
nimestahimili laumu, Fedheha imenifunika uso wangu. 8 Nimekuwa
mgeni kwa ndugu zangu, Na msikwao kwa wana wa mama yangu. 9 Maana
wivu wa nyumba yako umenila, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata. 10 Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa
laumu juu yangu.
Zaburi 69:9 inatajwa au kunukuliwa kwenye Yohana 15:25.
Yohana 15:25 Lakini
litimie lile neno lililoandikwa katika torati yao, Walinichukia bure.
Zaburi 69:10 inaendelea
kusema: Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, Nikawa mithali kwao. 12 Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi
hunidhihaki. 13 Nami maombi yangu nakuomba Wewe,
Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika
kweli ya wokovu wako. 14 Uniponye kwa kunitoa
matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika
vilindi vya maji. 15 Mkondo usinigharikishe, wala
vilindi visinimeze, Wala shimo lisifumbe kinywa chake juu yangu. 16 Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema, Kwa
kadiri ya rehema zako unielekee. 17 Wala usinifiche
uso wako, mimi mtumishi wako, Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi. 18 Uikaribie nafsi yangu, uikomboe, Kwa sababu ya adui zangu
unifidie. 19 Wewe umejua kulaumiwa kwangu, Na kuaibika
na kufedheheka kwangu, Mbele zako Wewe wako watesi wangu wote. 20 Laumu imenivunja moyo, Nami ninaugua sana. Nikangoja aje
wa kunihurumia, wala hakuna; Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu. 21 Wakanipa uchungu kuwa chakula changu; Nami nilipokuwa na
kiu wakaninywesha siki. 22 Meza yao mbele
yao na iwe mtego; Naam, wakiwa salama na iwe tanzi. 23 Macho
yao yatiwe giza wasione, Na viuno vyao uvitetemeshe daima. 24
Uimwage ghadhabu yako juu yao, Na ukali wa hasira yako uwapate. 25 Matuo yao na yawe ukiwa, Pasiwe na mtu wa kukaa hemani
mwao. 26 Maana wanamwudhi mtu uliyempiga Wewe,
Wanasimulia maumivu ya hao uliowatia jeraha. 27 Uwaongezee
uovu juu ya uovu, Wala wasiingie katika haki yako. 28 Na
wafutwe katika chuo cha uhai, Wala pamoja na wenye haki wasiandikwe. 29 Nami niliye maskini na mtu wa huzuni, Mungu, wokovu wako
utaniinua. 30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, Nami
nitamtukuza kwa shukrani. 31 Nayo yatampendeza Bwana
kuliko ng'ombe, Au ndama mwenye pembe na kwato. 32 Walioonewa
watakapoona watafurahi; Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe. 33 Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji, Wala hawadharau
wafungwa wake. 34 Mbingu na nchi zimsifu, Bahari na
vyote viendavyo ndani yake. 35 Maana Mungu ataiokoa
Sayuni, na kuijenga miji ya Yuda, Na watu watakaa ndani yake na kuimiliki. 36 Wazao wa watumishi wake watairithi, Nao walipendao jina
lake watakaa humo.
Zaburi 69:14-20 inachukuliwa na Bullinger kuhusiana na Gethsemane inayotajwa
kwenye Mathayo 26:36-45. Inajiri
na matukio ya mateso na kusulibiwa ambapo maadui wa Kristo wakiwa mbele yake.
Mathayo
26:36-45 Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani
iitwayo
Zaburi 69:21 inataja tukio la kusulibiwa (Mathayo 27:34-48; Yohana 19:29). Ni
unabii unaobidi utimilike kabla ya kifo chake kama Masihi, kwa kunywesha siki.
Kitendo hicho na kumnywesha nyongo iliyotolewa mwanzoni kabisa, inaleta hukumu
kwa Yuda. Wamepewa zaidi, kama kabila kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Wanaingia
kwenye madaraja au viwango vya mteule wakiwa kila mmoja peke yake tu.
Hawahitaji kuwa wamefanya hili.
Zaburi 69:25 inamtaja Yuda wa kwenye Matendo 1:20 kama alivyokaririwa hapa.
Hili ni suala sasa kwenye maneno ya mitume kumi na wawili. Tuna mitume kumi na
mbili watakaoyahukumu makabila. Kuna mtume mkuu mmoja na anayeliwakilisha kila
kabila. Kabila la Lawi linauchukua ukuhani, bali kuna makabila kumi na mbili tu
yanayohusika. Yuda aliashiria usaliti ambao Yuda waliomfanyia Masihi aliyetumwa
kao akiwa ni Mjumbe wa Agano aliyewatoa kutoka utumwani kwenye tukio la Kutoka
kwao utumwani. Alikuwa wa kabila la Yuda na wa ukoo uliokuwa katika Bethlehemu ya
Efrata. Kwa hiyo ni zaidi hata ya kumtaja tu Yuda anapokuwa anajumuishwa hapa. Zaburi
69:22-28 Bullinger anaichukulia kuwa inashabihiana na Warumi 11:9,10. Nukuu hii
inafuatia kutoka kwenye Warumi 11:8 inatoshabihiana na andiko lililoandikwa
huko nyuma la Isaya 29:10. Bila shaka hapa unabii huu ulihusiana na kushindwa
kwa Yuda kama taifa kumpokea Roho Mtakatifu kama wakati ule na mapokeo yao
yalifanyika kuwa mitego kamili kwao.
Kila sheria ambayo ilikuwepo kwa ajili ya mambo yao ilifanyika kuwa mtego
kwao. Baada ya kuangushwa au kubomolewa kwa Hekalu, Yuda na Lawi waliiharibu au
kuobadilisha na kuipotosha kalenda kwa kuweka kipengele cha uahirisho na
kuifanya sheria ya ulaji wa vyakula kuwa kitu cha ziada tu hadi leo hii.
Hawakuweza kusikia, wala kuelewa, ili wageuke na kuokoka. Hawakuwa na urithi na
makazi yao yaliangamizwa na kufanywa ukiwa kwa kipindi cha Milenia. Lakini
Mungu atauponya na kuukoa Sayuni na ataijenga miji ya Yuda. Katia siku za
mwisho watafanywa upya na Roho Mtakatifu atamwagwa juu yao kwa kupitia Masihi
waliyemuua atakayerudi kuwaokoa wale wanaomngojea kwa hamu kubwa. Hawa ni wale
wanaozishika amri za Mungu na imani ya Yesu Kristo, au Yoshua Masihi (Ufunuo
12:17: 14:12).
q