Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[090]
Kuulaani
Mtini
(Toleo La 1.0 20020310-20020310)
Tendo la
kuulaani mtini lililofanywa na Yesu Kristo lina maana kubwa sana kwenye imani
na taratibu za Kanisa la Mungu. Kinatuama kwenye mololongo wa Usafishaji na Utakasaji
wa Hekalu la Mungu.
Email: secretary@ccg.org
(Haki Miliki © 2002 Wade Cox)
(tr.
2013)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Kuulaani Mtini
Utangulizi
Kwenye Injili ya Mathayo sura ya 21 tunasoma habari ya kulaaniwa kwa mtini
kwenye mfululizo wa matukio yaliyofuatiwa na kitendo cha kuingia kwake Yesu
kwenye mji wa Yerusalemu, na kulisafisha hekalu.
Matthew 21:1-22 Hata walipokaribia Yerusalemu, na
kufika Bethfage, katika mlima wa Mizeituni, ndipo Yesu alipotuma wanafunzi
wawili akiwaambia, 2 Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na
mara mtaona punda amefungwa, na mwana-punda pamoja naye; wafungueni mniletee. 3 Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka.
4 Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii,
akisema,
Tazama, mfalme wako anakuja kwako,
Mpole, naye amepanda punda,
Na mwana-punda, mtoto wa punda.
6 Wale
wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru, 7 wakamleta
yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake. 8
Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; na wengine
wakakata matawi ya miti, wakayatandaza njiani. 9 Na makutano
waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema,
Hosana, Mwana wa Daudi;
ndiye mbarikiwa, yeye ajaye
kwa jina la Bwana;
Hosana juu mbinguni.
10 Hata alipoingia
Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu? 11 Makutano
wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya.
Yesu Analisafisha
Hekalu
12 Yesu akaingia ndani ya hekalu, akawafukuza wote waliokuwa
wakiuza na kununua hekaluni, akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao
waliokuwa wakiuza njiwa; 13 akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu
itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi. 14
Na vipofu na viwete wakamwendea mle hekaluni, akawaponya. 15 Lakini wakuu wa makuhani na waandishi walipoyaona maajabu aliyoyafanya,
na watoto waliopaza sauti zao hekaluni, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi!
Walikasirika, 16 wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu
akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao
umekamilisha sifa? 17 Akawaacha, akatoka nje ya mji mpaka
Bethania, akalala huko.
Yesu Anaulaani
Mtini
18 Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa. 19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila
majani tu; akauambia, Yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. Mtini
ukanyauka mara. 20 Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema,
Jinsi gani mtini umenyauka mara? 21 Yesu akajibu, akawaambia,
Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini
tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka, ukatupwe baharini, litatendeka. 22
Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.
Tunapojionea
uhusiano wake katika Marko 11 tunaona kwamba mchakato huu unabadilika. Na
kwamba kuna mlolongo wa matendo yanayojitokeza na ambayo yanarudiwa.
Marko 11:1-33
Hata walipokaribia Yerusalemu
karibu na Bethfage na Bethania, kukabili mlima wa Mizeituni, aliwatuma wawili
katika wanafunzi wake, 2 akawaambia, Nendeni mpaka kile kijiji
kinachowakabili; na katika kuingia ndani yake, mara mtaona mwana-punda
amefungwa, asiyepandwa na mtu bado; mfungueni, kamleteni. 3 Na mtu akiwaambia, Mbona mnafanya hivi?
Semeni, Bwana anamhitaji na mara atamrudisha tena hapa. 4 Wakaenda zao, wakamwona mwana-punda
amefungwa penye mlango, nje katika njia kuu, wakamfungua. 5 Baadhi ya watu waliosimama huko wakawaambia,
Mnafanya nini kumfungua mwana-punda? 6 Wakawaambia kama Yesu alivyowaagiza, nao
wakawaruhusu. 7 Wakamletea Yesu yule mwana-punda, wakatandika mavazi yao juu yake; akaketi
juu yake. 8 Watu wengi wakatandaza mavazi yao njiani, na wengine matawi waliyoyakata
mashambani. 9 Nao watu waliotangulia na wale waliofuata wakapaza sauti, Hosana; ndiye
mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana; 10 umebarikiwa na ufalme ujao, wa baba yetu Daudi.
Hosana juu mbinguni. 11 Naye akaingia Yerusalemu hata ndani ya hekalu; na alipokwisha kutazama yote
pande zote, kwa kuwa ni wakati wa jioni, akatoka, akaenda Bethania pamoja na
wale Thenashara.
Yesu Anaulaani Mtini
12 Hata asubuhi yake
walipotoka Bethania aliona njaa. 13 Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili
labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si
wakati wa tini. 14 Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako.
Wanafunzi wake wakasikia.
Yesu Analisafisha Hekalu
15 Wakafika Yerusalemu, naye akaingia ndani ya hekalu, akaanza kuwafukuza wale
waliokuwa wakiuza na kununua ndani ya hekalu, akazipindua meza za wabadili
fedha, na viti vyao wauzao njiwa; 16 wala hakuacha mtu achukue chombo kati ya hekalu. 17 Akafundisha, akasema, Je! Haikuandikwa,
Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa
pango la wanyang'anyi. 18 Wakuu wa makuhani na waandishi wakapata habari
wakatafuta jinsi ya kumwangamiza; maana walimwogopa, kwa sababu mkutano wote
walishangaa kwa mafundisho yake. 19 Na kulipokuwa jioni alitoka mjini.
Fundisho kukutokana na Mtini Ulionyauka
20 Na asubuhi walipokuwa wakipita, waliuona ule mtini umenyauka toka shinani. 21 Petro akakumbuka habari yake, akamwambia,
Rabi, tazama, mtini ulioulaani umenyauka. 22 Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu.
23 Amin,
nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala
asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa
yake. 24 Kwa sababu
hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo
yatakuwa yenu. 25 Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na
Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.
Mamlaka ya Yesu Yanaonewa Mashaka
26 Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe
ninyi makosa yenu.] 27 Wakafika Yerusalemu tena; hata alipokuwa akitembea hekaluni, walimwendea
wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee, 28 wakamwambia, Ni kwa mamlaka gani unatenda
mambo haya? Naye ni nani aliyekupa mamlaka hii uyatende haya? 29 Yesu akawaambia, Nitawauliza neno moja,
nanyi mnijibu, kisha nitawaambia ni kwa mamlaka gani nayatenda haya. 30 Ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni, au kwa
wanadamu? Nijibuni. 31 Wakasemezana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema, Ulitoka mbinguni,
atasema, Mbona, basi, hamkumwamini? 32 Ila tukisema, Ulitoka kwa wanadamu, -- waliogopa
watu; maana watu wote walimwona Yohana kuwa nabii halisi. 33 Wakamjibu Yesu, wakasema, Hatujui. Yesu
akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani nayatenda haya.
Mchakato huu
unaonyesha kwamba aliingia Hekaluni kwa mfuatano maalumu wa siku na
akalisafisha. Aliingia Hekaluni ili kuhakikisha kuwa limesafishika, tangu siku
ya kwanza ya mwezi wa Abibu na
kuendelea kwa mujibu wa maelekezo ya Torati na maeneo tuayoona kuwa imeelezwa na
kuandikwa ni kwenye Ezekieli 45:18-25:
18 Bwana MUNGU
asema hivi; Mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utatwaa ng'ombe mchanga
mume mkamilifu; nawe utapatakasa mahali patakatifu. 19 Na kuhani atatwaa baadhi ya damu ya sadaka ya
dhambi, na kuitia juu ya miimo ya milango ya nyumba, na juu ya pembe nne za
daraja ya madhabahu, na juu ya miimo ya lango la ua wa ndani. 20 Nawe utafanya vivyo hivyo katika mwezi wa
saba, siku ya kwanza ya mwezi kwa ajili ya kila mtu akosaye, na kwa ajili ya
mtu aliye mjinga, ndivyo mtakavyoifanyia nyumba upatanisho. 21 Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya
mwezi, mtakuwa na Pasaka, sikukuu ya siku saba; mkate usiotiwa chachu utaliwa. 22 Na siku hiyo mkuu atatengeneza ng'ombe
kuwa sadaka ya dhambi, kwa ajili ya nafsi yake, na kwa ajili ya watu wote wa
nchi. 23 Tena, katika zile siku saba za sikukuu
atamtengenezea Bwana sadaka ya kuteketezwa, ng'ombe saba na kondoo waume saba
wakamilifu, kila siku kwa muda wa siku saba, na beberu mmoja kila siku kuwa
sadaka ya dhambi. 24 Naye
atatengeneza sadaka ya unga, efa moja kwa ng'ombe, na efa moja kwa kondoo mume,
na hini moja ya mafuta kwa efa moja; 25 katika mwezi wa saba, siku ya kumi na tano ya
mwezi, katika sikukuu atafanya vivyo hivyo kwa muda wa siku saba; sadaka ya
dhambi vivyo hivyo, na sadaka ya kuteketezwa vivyo hivyo, na sadaka ya unga
vivyo hivyo, na mafuta vivyo hivyo.
Nukuu-elekezi ya
karibu iko kwenye vitabu vya Mwanzo 8:13; na Kutoka 12:18; 29:1-14. Kwenye Ezekieli
43:18 tunaona kwamba kitendo cha utakaso na kuweka wakfu kinaanzia madhabahuni,
malali ambako utakaso wa makuhani ulikuwa ni lazima kwa makuhani wanaotokana na
uzao wa Walawi kwa mujibu wa Torati (Walawi 8:1-10). Kwa hiyo, hapa tunashughulika
na makuhani waliokwisha kutakaswa tayari na kufuatiwa na tendo la utoaji wa
dhabihu madhabahuni kwenye utaratibu mpya. Kwa ajili hii, wana wa Sadoki ndio Walawi
pekee walioruhusiwa (Ezekieli 40:46; 44:15; sawa na ilivyoandikwa kwenye Ufunuo
sura ya 7). Huu ni ukuhani wa Melikizedeki. Ukuhani huu uliutangulia ule wa Lawi,
na Lawi alitoa zaka kwake akipitia kwa Ibrahimu. Shemu alikuwa ndiye kuhani
wake mkuu tangu kipindi cha Nuhu. Huduma hii ilikuweko huko Yerusalemu hadi kipindi
ambacho Daudi aliutwaa na kuutamalaki mji huu wa Yerusalemu. Mfalme alipewa cheo
cha Adonai-Sedeki au Melkizedeki kwa cheo cha kudumu kama tunavyojionea kutoka
kwenye Maandiko Matakatifu (sawa na ilivyoandikwa kwenye jarida la Melkizedeki (Na. 128) [Melchisedek (No. 128)].
Mfalme huyu
hakuwa Yesu Kristo kama wanavyodhani na kufundisha wengine, nah ii ni kwa
mujibu wa maandiko kadhaa na mengi yanayoonyesha kuwa huyu asingewezekana kuwa
ni Yesu Kristo, maana asingewezekana kuwa ni mwanadamu aliyekuwa anaishi huko
Yerusalemu na huku anaweza kumtokea Ibrahimu kwa kipindi na wakati huo huo
mmoja akiwa kama Malaika wa Yahiva aliyemtembelea Ibrahimu akiwa na wenzake
wengine wawili wakienda kuuangamiza mji wa Sodoma. Na zaidi sana, akiwa kama
Malaika wa Yahova, alikuwa pamoja na wana wa Israeli pale jangwani, na kwenye
utekaji na kuutamalaki mji wa Yeriko na kwa Kanaani nzima yote. Na angewezaje tena awepo huko Yerusalemu
akiwa kama Adonai-Sedeki? Na kusudi la
kuzaliwa kwake katika mwili kingekuwa na maana gani kama kungekuwa tayari
imekuwa hivyo katika kipindi cha miaka takriban miaka mia tano iliyopita huko
nyuma? (Soma pia jarida la Malaika wa YHVH (Na. 24) (The Angel of YHVH (No. 24).)]
Kwenye maandiko ya
Kutoka 29:36 tunaona kwamba ng’ombe dume alitolewa sadaka katika siku zile saba
muhimu na maalumu. Na hapa kwenye Ezekieli 43 tunaona kuwa natolewa mara moja
tu na kwenye siku nyingine wanatolewa mbuzi wagodo. Hili linaonekana wazi kabisa
kuwa ni Hekalu linguine na ni kwa mlolongo wa shughuli nyingine. Sadaka hizi
kwenye Ezekieli 43:18-27 ni za kitaifa na
za kikuhani ambapo zile za kikuhani zinawakilisha zile za taifa zima.
Bullinger anaona
kwamba hazikuwa za kila mtu binafsi yake, na anadhani kuwa hakutakuweko na Siku
ya Upatanisho na anaamini kutokana na ukweli huu kwamba hazitatolewa chini ya
Sheria. Ingawaje zitatolewa katika kipindi cha millennia na ambacho utekelezaji
wa maagizo ya Torati utakuwa na tofauti aina yak echini na kipindi hiki cha
utawala wa Kristo kwa habari ya masuala haya ya utoaji dhabihu za wanyama,
kwenye sikukuu zote zinazofuatiwa tangia ile ya Psaka hadi Sikukuu ya Vibanda
na ya Upatanisho na ya Baragumu ambazo hazikuandikwa wala kutajwa hapa, (Ezekieli
45:24-25) haimaanishi kuwa hazitaadhimishwa (kama ilivyoandikwa kwenye jarida
la Maswali Yaulizwayo Sana Kuhusu
Ezekieli Sura za 36-48 na Utakaso wa Hekalu (Na. 292) na
Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. 241) [FAQs on Ezekiel Chapters 36-48 and the
Sanctification of the Temple (No. 292) and the Sanctification of the Temple of God (No. 241)]. Inapaswa ijulikane pia kwamba siku za Mwandamo wa Mwezi hazikujumuishwa
kwenye siku za kazi na sheria hii itatumika zaidi kwenye kipindi hiki cha
millennia kama tunavyoona kwenye Ezekieli 45 f, na pia kwenye Isaya 66:23, na
wale ambao hawatazitunza vyema kwa kuziadhimisha watakufa (Isaya 66:24).
Mchakato huu wa kusafisha ndio haatimaye utachukua mahali
pake tangia mwanzoni mwa Mwezi wa Kwanza hadi mwezi wa saba. Kristo alifanya
jambo hili siku ya kumi alipokuwa akiingia mjini Yerusalemu. Alikuwa na njaa pia
alipokuwa akitimiliza utaratibu huu. Hii ingeweza kutafsiriwa pia kwamba
ilikuwa inaonyesha kuwa alikuwa amefunga saumu kwa kipindi hiki.
Ni mchakato wa
ufungaji saumu ulioeleweka na wale wanaofanya mfungo aina hii. Hata njaa ya kawaida tu ya siku kwa siku
ni jambo gumu sana kulivumilia.
Inaeleweka sana
kwamba alikuwa amefunga saumu ya kipndi kirefu na cha siku nyingi, na hata kwa
wao wenyewe. Na ingawaje inaonekana kwamba alikuwa akipita kwenye nyumba kadhaa
za marafiki zake akiwa kwenye hali hii na kipindi kile.
Injili za Mathayo,
Marko na Luka zinatueleza kwamba Kristo alikuwa Hekaluni, akilisafisha na kuhakikisha
kuwa liko safi kwa kuwaondoa wale waliokuwa wanafanya biashara ya kubadilisha
fedha na shughuli nyingine za haramu na za kiharamia.
Kwa hiyo, baada
ya Utakaso kwa ajili ya dhambi zlizozifanywa pasi kukusudia ama kwa Kupotoshwa,
Kristo aliingia Yerusalemu, aliingia kutoka Yeriko siku ya 8 mwezi Abibu, na
akashinda usiku ule nyumbani kwa Zakayo. Uingiaji huu wa kwanza huko Yerusalemu
ulikuwa ni kutokea Bethfegi mnamo siku ya 9 ya Abibu (Ijumaa) na sio kutoka Bethania
(kama ilivyo kwenye Mathayo 21:8-9). Alijitokea pasi kutarajiwa na akaingia na
kulisafisha Hekalu (Mathayo 21:12-16), na kisha aliondoka na kwenda Bethania
(Mathayo 21:17). Mchakato huu umeelezewa kwenye midani za jarida la Kipindi cha Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159) [Timing of the Crucifixion and
the Resurrection (No. 159)].
Ilipofika siku ya
11 mwezi wa Abibu, siku ya nne kabla ya maadhimisho ya Pasaka, aliingia Hekaluni
na kuliangalia na kisha akarejea Bethania (Marko 11:11). Siku ya 12 Abibu, ambayo
ni siku tatu kabla ya Pasaka ya mwaka 30 BK, alijitotokea tena Hekakuni,
akalisafisha tena na kisha akawafundisha watu humo Hekaluni (Marko 11:15-17; Luka
19:45-46). Alikutana na vipingamizi vya wakuu wa Hekalu na watawala (Marko
11:18; Luka 19:47-48) na kisha akaondoka kutoka mjini na huenda alienda tena Bethania
(Marko 11:19; Luka 21:37-38).
Siku ya pili yake
kabla ya Pasaka ambayo ni ya 13 Abibu (Jumanne), Kristo alikuwa tena mjini Yerusalemu
na Hekaluni (Mathayo 21:23-27; Marko 11:27-33; Luka 20:1-8). Unabii wake mkuu
na wa kwanza ndipo ulitolewa humo Hekaluni (Luka 21:5-36).
Maelekezo kuhusu
utaratibu wa Meza ya Bwana yalitolewa kwenye juma hili (Luka 21:37-38).
Kisha unabii
mwingine mkuu ulitolewa kwenye Mlima wa Mizeituni (Mathayo 24:1-51; Marko
13:1-37) na ukaendelea hadi (Mathayo 25:1-46).
Ktisto, kwa mfano
wake ulio wazi kwenye injili hizi, alikuwa analisafisha Hekalu lote kabisa
katika kipindi hiki, tangia siku ya 1 Abibu kama ilivyoagizwa kwenye Torati,
hadi kufikia siku ya 13 Abibu au mwezi wa Nisan, ambayo ilikuwa ni siku ya
mwanzo wa maandalizi ya Psaka. Na mwishoni mwa siku ya 13 Abibu, yeye pamoja na
wanafunzi wake walipumzika kwenye chumba cha ghorofani kwa maadhimisho yake ya
Mwisho au Ushirika wa Meza ya Bwana na ndipo aliposalitiwa, akateswa na
kupelekwa mbele ya wazee wa mabaraza, huyu Masihi, na ndipo aliposulibiwa akiwa
ni Mwanakondoo wa Pasaka majira ya alasiri, siku ya 14 Abibu.
Fundisho
kutokana na Mtini
Fundisho
tunalojifunza kutokana na mchakato wa kulaaniwa kwa mtini lilikuwa ni kwamba,
uliwekwa ndani yake na kuhusianishwa na mchakato mzima wa maandalizi ya
maadhimisho ya Pasaka, na ilikuwa ni sehemu ya mchakato wa utakaso. Maana
yaliyopo sambamba na kutokuwepo kwa matunda ndani yake na kuulani lilikuwa ni
fundisho kwa Makanisa ya Mungu, kwamba kwenye mchakato huu wa utakaso au
kusafisha kile kilishoshindwa kuzaa matunda ni kile kilichoachwa kikinyauka na
kufa.
Fundisho hili
halikuwa na maana sana na muafaka kwenye sehemu ya karne ya ishirini, kipindi
ambacho utakaso ulikuwa haufanyiki kabisa, na maandalizi ya Pasaka yalikuwa
hayaelekezwi kabisa katika utakaso na wokovu wa Israeli na wa mataifa.
Na ni kwa sababu hii ndipo mifano iliyo kwenye Injili za Mathayo na Marko unafuatia, ikielezea juu ya kuwaajiri watenda kazi wengine na wana wengine. Mmoja aliahidi kuwa atakwenda na kufanya na mwingine alikataa kuahidi. Hata hivyo, Yule aliyeahidi kuwa atakwenda hakwenda nayule aliyekataa kuahidi chochote ndiye aliyekwenda na akaifanya ile kazi kama alivyopenda Baba yake iwe. Mfano huu ulielekezwa kwao makabila ya Yuda na Lawi na kwa Israeli wote. Mfsno mwingine wa mwenye shamba aliyesafiri (Marko 12:1-12) ulikuwa ni wa manabii na Kristo mwenyewe, na lile shamba la mizabibu walikuwa ni nyumba yote ya Israeli (Isaya 5:7) (sawa na ilivyofafanuliwa kwenye jarida la. Agano la Mungu (Na. 152) [The Covenant of God (No. 152)].
Shamba la Mzabibu
Mfano wa Mpangaji
Marko 12:1-12 Akaanza kusema nao kwa mifano; Mtu mmoja
alipanda shamba la mizabibu, akazungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo,
akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri. 2 Hata kwa wakati wake akatuma mtumwa kwa wale
wakulima, ili apokee kwa wakulima katika matunda ya mizabibu. 3 Wakamtwaa, wakampiga, wakamtoa nje, hana
kitu. 4 Akatuma tena
kwao mtumwa mwingine, na huyo wakamtia jeraha za kichwa, wakamfanyia jeuri. 5 Akamtuma mwingine, huyo wakamwua; na
wengine wengi, hawa wakiwapiga na hawa wakiwaua. 6 Basi alikuwa na mmoja bado, mwana mpendwa wake;
huyu naye akamtuma kwao mwisho, akisema, Watamstahi mwanangu. 7 Lakini wale wakulima wakasemezana, Huyu ni
mrithi; haya, na tumwue, na urithi utakuwa wetu. 8 Wakamkamata, wakamwua, wakamtupa nje ya shamba la
mizabibu. 9 basi atafanyaje yule bwana wa shamba la mizabibu? Atakuja na kuwaangamiza
wale wakulima, na lile shamba la mizabibu atawapa wengine. 10 Hata andiko hili hamjalisoma,
Jiwe walilolikataa waashi,
Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni.
11 Neno hili limetoka kwa Bwana,
Nalo ni ajabu machoni petu?
12 Nao wakatafuta kumkamata, wakaogopa mkutano; maana walitambua ya kwamba ule
mfano amewanenea wao. Wakamwacha wakaenda zao.
Hapa tuaona
kwamba wapangaji ni nyumba ya Israeli ambao walikuwa ni makuhani na Walawi
waliopewa kuifanya kazi ya Mungu, na pia nyumba ya Yuda ambayo iliangushwa
chini na Waedomu na matendo ya imani ya Waheleni. Ujumbe ulikuwa ni kwa wateule
wa taifa na kisha kwa Kanisa ambao ulipaswa uwafuate.
Kumsheshimu na
Kumpa kodi kwa Kaisari
Mtenganisho kati ya masuala yanayolihusu Kanisa na wale walio kwenye mambo
ya kidunia kwenye kipindi cha maandalizi vilisisitizwa sana kwenye fundisho
lihusulo kumpa Kaisari kwenye Injili ya Marko 12:13-17.
13 Wakatuma kwake baadhi ya Mafarisayo na Maherodi, ili wamnase kwa maneno. 14 Hata walipofika walimwambia, Mwalimu,
twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, wala hujali cheo cha mtu; kwa maana
hutazami sura za watu; lakini katika kweli waifundisha njia ya Mungu. Je! Ni
halali kumpa Kaisari kodi au siyo? 15 Tumpe, tusimpe? Naye, akijua unafiki wao, akawaambia,
Mbona mmenijaribu? Nileteeni dinari niione.
16 Wakaileta.
Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii na anwani hii? Wakamwambia, Ni ya Kaisari. 17 Yesu akajibu, akawaambia, Mpeni Kaisari
yaliyo ya Kaisari, na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu. Wakamstaajabia sana
Mfululizo wa
mifano umetolewa, ili kushirikisha mafundisho kwenye Kanisa.
Kanisa la
Ufufuo
Kristo alishughulika na Masadukayo pia kipindi kile kuhusu Ufufuo wa wafu
katika Marko 12:18-27.
18 Kisha Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea,
wakamwuliza na kusema, 19 Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu
akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie
ndugu yake mzao. 20 Basi kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao. 21 Wa pili naye akamtwaa akafa, wala yeye
hakuacha mzao. Na wa tatu kadhalika; 22 hata na wote saba, wasiache mzao. Mwisho wa wote
yule mwanamke akafa naye. 23 Basi, katika kiyama atakuwa mke wa yupi katika
hao? Maana wote saba walikuwa naye. 24 Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu
hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu? 25 Kwa maana watakapofufuka katika wafu,
hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni. 26 Na kwa habari ya wafu ya kwamba
wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu
alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu
wa Yakobo? 27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana.
Kwenye andiko hili
alizungumzia kuhusu Ufufuo wa wafu (Marko. 12:18-27) na Kanisa kama mzaliwa wa
kwanza aliyefufuka kutoka kwa wafu, kwa kuwa alisema kuwa wakati alipokuwa
anaongea na Musa kwenye kile kichaka kilichokuwa kinawaka kwamba: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa
Isaka, na Mungu wa Yakobo” Yeye ni Mungu wa walio hai na sio wa wafu, na
kwa hiyo Kristo hapa anaeleza juu ya Kanisa—ambalo ni la wale waliolala katika
Bwana.
Ni mchakato wa
maandalio ya Hekalu ambayo yalichukua mahala pake kutoka siku ya 1 Abibu hadi
siku ya Pasaka. Kisha Mkate usiotiwa Chachu ukaliwa kwa siku saba tangu siku ya
15 hadi 21 Abibu, na mwezi wa mfungo wa saumu uliofuatia siku ya saba
iliyokaribia, uliopelekea kwenye mchakato wa kawaida wa kuhesabu siku na majuma
kuelekea Pentekoste na mavuno ya ngano, ambayo ni mavuno ya Kanisa la mzaliwa
wa kwanza.