Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[021L]

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu

cha Malaki

 

(Toleo La 1.0 20141108-20141108 )

 

Jarida hili la ufafnuzi wa Malaki ni andiko la Kanoni ya Agano la Kale. Mtindo wake unaonyesha pia nuru au ashirio la kitabu cha Zekaria.

 

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

 

(Hatimiliki ©  2014 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu cha Malaki

 


Utangulizi

Mathayo 23:35 inasema kuwa Zekaria alikuwa ameuawa katikati ya hekaluni na madhabahuni. Aliuawa kabisa na makuhani, akinuia kuikomesha au kuizima huduma yake. 

 

Mathayo 23:33-36

33 Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum? 34 Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji; 35 hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.

 

Kristo anawaambia makuhani na hii ni hatua ya maana sana. Inaonyesha kuwa Zekaria aliuawa kwa sababu fulani ijulikanayo. Zekaria 1:7 inaonyesha kuwa ni Zekari’a, mwana wa Ido, nabii. (Soma kitabu cha Josephus, cha Wars of the Jews (Vita ya Wyahudi), 4.5.4 ili kupata ufafanuzi, pia na bangokitita za Bullinger.) Hii imeelezwa kama inapoibuka kwenye tatizo lililo kwenye vitabu vya Malaki na Zekaria.

 

Tuna Zekaria mmoja aliyeuawa yapata miaka 800 ya nyuma. Nabii Zekaria aliuawa miaka 400 huko nyuma na kisha miaka 34 baada ya Zekaria wa tatu, mwana wa Baruku ni tatizo kubwa sana. Kumbuka pia kuwa Isaya aliuawa kwa kuchanwa kwa msumeno vipande viwili toka kichwani hadi miguuni na watu hawahawa. Watu hawa hawawaheshimu kabisa manabii a Mungu. “Watu hawa” ni sawa na kama walivyo viongozi wa kidini au ya jamii za kidini za makanisa makongwe ya zamani. Kanisa tunaloliona na tunayoyaheshimu sana siyo kanisa kongwe la zamani sana na haya yanayofuata mrengo wa kipapa yanayosaidiwa na Majesuiti wanaowaua watu kwa malengo yao.

 

Kwenye sura za kitabu cha Zekaria kuna mabadiliko kidogo kwenye mtindo na ule unaochukuliwa kuwa wa Malaki uliofanya kazi na akaanza kuandika na kumaliza sura zote za kitabu cha Zekaria na ambacho ndicho kinachohitimisha utaratibu wa uandishi wa Kanoni. Ilikuwa ni kutokana na Iskanda au Alexander Mkuu ambaye alishinda mwaka 323 KK. Ezra mwandishi alifariki wakati huo huo. Sedum Olam Rabbah kinaonuesha mwongozo kwamba walifariki wakati mmoja huohuo. Kisha walilinganisha na Kanoni ya Agano la Kale tangu wakati wa kufa kwake mwaka 323 KK. Vitabu hivi viliorodheshwa na kuchapishwa na kutumwa mnamo mwaka 321 KK.

 

Malaki ni mmoja vitabu sita visivyopewa tarehe ya wale wanaojulikana kama Manabii kumi na wawili Wadogo. Kitabu chake kinaonyesha kinaonyesha kwamba ibada za Hekaluni pamoja na dhabihu zake zilirejeshwa kabisa bali ilikuwa ni utaratibu au kawaida ya kiibadada na unafiki vilivyokuwa vimeshika kasi katika siku za huduma ya Bwana iliyoonekana kufanyika kikamilifu sana wakati wa Malaki. Siyo kipindi cha karibu sana walizuia ushawishi wa kina Ezra na Nehemia ulioondoka kuliko ulipoanza upotoshaji na vita viliendelea kwa wazi sana kwenye Malaki 1:7-8 na 3:8 nk.

 

Bullinger anakosea hapa. Wakati alipokufa Ezra, halikuwa ni suala la Malaki ambapo ndipo ulionekana mdororo; Ezra alikuwa anakufa ndipo mdororo ulikuwa unaanza na Malaki alikuwa anayapitia kabla Ezra hajafa kwa kuwa Kanoni ilikuwa imefungwa na kitabu cha Malaki. Kama kingekuwa hakijaandikwa kabla ya kufa kwa Ezra, basi kisingekuwa kimejumuishwa na kukubalika kuwa ni kama ni cha mmoja wa Manabii hawa Wadogo Kumi na Mbili. Kilijulikana kama ni unabii wa mwisho kutoka kwa Malaki na Ezra haki kuja kwa Yohana Mbatizaji. Kulikuwa na manabii waliokuwa wakihudumu kanisani lakini hakuna hata mmoja kati yao aliyepokea maelekezo ya moja kwa moja kutoka kwa Bwana yenye kuhusiana na jambo linguine lolote kisawasawa. Kulikuwa na manabii Hekaluni waliojua kuwa Kristo alikuwa anakwenda kuzaliwa na walioijua siku yenyewe aliyokuwa anakwenda kuwekwa wakfu Hekaluni na walikuwa wanamngojea wamuone akiletwa na Yusufu na Mariamu mbele ya Kuhani Mkuu na kwa Makuhani wa Hekalu. Mtu mmoja ambaye maisha yake yalikuwa yamelindwa ili kwamba awepo na amshuhudie Masihi wa Mungu alimpa ruhusa. Kwa hiyo, unabii haukukoma bali shuhuda zilizoandikwa kwenye Biblia ndizo zilikoma.

 

Mtindo wa kiuandishi wa sura chache za mwisho za Zekaria ni sawa tu na ule wa kitabu cha Malaki na unatofautiana na sura za zamani na inadhaniwa kuwa Malaki alimaliza kitabu kwa ajili ya Zekaria, wakati Zekaria alipouawa ndani ya Hekalu na karibu na madhabahuni. Zekaria alikuwa ni nabii mkuu na kitabh chake na kazi yake vinaumuhimu sana, lakini makuhani hawakufikiri chochote walipomuua, na ndivyo pia hawakufikiri lolote walipokuwa wanamuua Isaya. Waliwaogopa kina Samweli na Eliya lakini walimuua kwa kumpiga “katikati ya kichwa, utosini.”

 

Moja ya matatizo tuliyonayo ni kwamba mlolongo wa uzao na wa matukio wa Bullinger unamakosa. Tunauona mwaka 323 KK kama ndio alikufa Ezra na kuzaliwa kwa Masihi kolikuwa mwaka 6 KK, kipindi cha takriban miaka 317. Wanasema kuwa matengenezo ya mwaka wa Artashasta yalifanywa miaka 400 na kwamba siyo sahihi. Mlolongo wa matukio wa Bullinger siyo sahihi na tunahitaji kujihadhari na jambo hilo. Mkururu wa nyakati na utawala wa wafalme vinaeleweka vizuri sana sasa kuliko ilivyokuwa kipindi cha Bullinger alipokuwa anaandika. Katika mwisho wa miaka 130 ya mwisho tumekuwa katika maarifa kwa haraka haraka sana. Kwa mfano, anaweka siku ya mwisho ya Ezra kuwa ni siku ya 1 Nisan 403 KK, wakati Hekalu lilikuwa limejengwa tena mwaka 419 KK na Nehemia alitumwa aende huko katika wiki ya 7 ya miaka ambayo ni miaka 49 baada ya mwaka 419. Ezra alifariki mwaka 323 KK, na siyo mwaka 403. Kwa hiyo siku au tarehe ambazo utakazoziona kwenye tafsiri ya Companion Bible siyo za kweli.

 

Malaki Sura ya 1

1 Ufunuo wa neno la Bwana kwa Israeli kwa mkono wa Malaki 2 Nimewapenda ninyi, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Umetupendaje? Je! Esau siye ndugu yake Yakobo? Asema Bwana; ila nimempenda Yakobo; 3 bali Esau nimemchukia na kuifanya milima yake kuwa ukiwa, na urithi wake nimewapa mbweha wa nyikani. 4 Ijapokuwa Edomu asema, Tumepondwa-pondwa, lakini tutarudi na kupajenga mahali palipoachwa hali ya ukiwa; Bwana wa majeshi asema hivi, Wao watajenga, bali mimi nitaangusha; na watu watawaita, Mpaka wa uovu, na, Watu ambao Bwana anawaghadhabikia milele. 5 Na macho yenu ninyi yataona, nanyi mtasema, Bwana ndiye mkuu kupita mpaka wa Israeli. 6 Mwana humheshimu baba yake, na mtumishi humcha bwana wake; basi, kama mimi ni baba yenu, heshima yangu iko wapi? Na kama mimi ni bwana wenu, kicho changu ki wapi? Bwana wa majeshi awauliza ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau jina langu. Nanyi mwasema, Tumelidharau jina lako kwa jinsi gani? 7 Mnatoa chakula kilichotiwa unajisi juu ya madhabahu yangu Nanyi mwasema, Sisi tumekutia unajisi kwa jinsi gani? Kwa sababu mwasema, Meza ya Bwana ni kitu cha kudharauliwa. 8 Tena mtoapo sadaka aliye kipofu, si vibaya? Na mtoapo sadaka walio vilema na wagonjwa, si vibaya? Haya! Mtolee liwali wako; je! Atakuwa radhi nawe? Au atakukubali nafsi yako? Asema Bwana wa majeshi. 9 Na sasa, nawasihi, ombeni fadhili za Mungu, ili atupe neema; ikiwa jambo hili limetoka katika mikono yenu; je! Atawakubali nafsi zenu? Asema Bwana wa majeshi. 10 Laiti angekuwapo kwenu mtu mmoja wa kuifunga milango; msije mkawasha moto bure madhabahuni pangu! Sina furaha kwenu, asema Bwana wa majeshi, wala sitakubali dhabihu yo yote mikononi mwenu.

 

Hapa ndipo lilipofikia Kanisa la Mungu mwishoni mwa zama za wafuasi wa Armstrong. Hakuna mtu aliyethubutu kufanya kitu bila sababu. Hii ndiyo moja ya sababu inayolifanya kanisa la CCG lisiwe na watumishi wa kulipwa, kwa kuwa andiko hili la Malaki linaonyesha hatima iliyofikia utaratibu huu na pia kwamba Kristo mwenyewe aliukemea na utaratibu ambao ulikuwa umeoza na hakuna aliyefanya kazi kwa minajiri ya kumpenda Mungu. Ilikuwa ni biashara tu. Mungu aliwatawanya kama alivyolitawanya Hekalu. Aliwapelekea Kristo alipofikia umri wa miaka 30. Alikujafanyika kuwa Kuhani mnamo mwaka 27 BK na tangu mwaka 28 BK alianza misheni yake na kanisa lilianzisha. Liliendelea hivyo kwa Yubile 40 na lipo kwenye awamu ya mwisho wa Yubile ya mwisho sasa, Yubile ya 120.

 

Mwaka 1987 Joseph Tkatch alianza safari yake ya kiutalii akiizunguka nchi yote ya Marekani, na ulimwenguni kote kwingine akihubiri kuwa tulikuwa kwenye zma ya Ufunuo sura ya 11, aya za 1 na 2, na kwamba Mungu alikuwa ameanza kulipima Hekalu la Mungu. Mwaka 1987 ulikuwa ni mwanzo wa miaka 40 ya mwisho ya Yubile hii na mwanzo wa parole au hukumu hadi mwaka 2027. Ulikuwa ni mwaka wa tatu wa kalenda takatifu.

 

Sura ya kwanza ya Malaki inaendana na unabii wa kuanzia mwaka 27 BK, hadi kufa kwa Kristo, Pentekoste, miaka 40 hadi kwenye kuangamia kwa Hekalu huko Yerusalemu na tukio la kutawanywa kwao lililotukia mwaka 70 BK. Kanisa lilikubwa na tatizo hilohilo kwenye miaka 40 ya mwisho na hipo kilianza ‘kizazi hiki’, usemi ambao Kristo aliutumia kwenye Injili yake aliposema kuwa ‘kizazi hiki’ hakitapia hadi Masihi atakapokuja na kuyaangamiza mataifa ya duniani na kuyapeleka utumwani kwa vitasa vya hasira ya Mungu. ‘Kizazi hiki’ kinschotajwa hivi na Kristo kilianza mwaka 1987.

 

11 Kwa maana tokea maawio ya jua hata machweo yake jina langu ni kuu katika Mataifa; na katika kila mahali unatolewa uvumba na dhabihu safi kwa jina langu; maana jina langu ni kuu katika Mataifa, asema Bwana wa majeshi. 12 Lakini ninyi mnalitia unajisi, kwa kuwa mwasema, Meza ya Bwana imetiwa unajisi; na matunda yake, yaani, nyama yake, hudharauliwa. 13 Tena mwasema, Tazama, jambo hili linatuchokesha namna gani! Nanyi mmelidharau, asema Bwana wa majeshi; nanyi mmeleta kitu kilichopatikana kwa udhalimu, na kilema, na kilicho kigonjwa; ndivyo mnavyoleta sadaka; je! Niikubali hii mikononi mwenu? Asema Bwana. 14 Lakini na alaaniwe mtu mwenye kudanganya, ambaye katika kundi lake ana mume, akaweka nadhiri, ila amtolea Bwana kitu kilicho na kilema; kwa maana mimi ni Mfalme mkuu, asema Bwana wa majeshi, na jina langu latisha katika Mataifa.

 

Maendeleo yote ya kanisa na kwa Mafarisayo, kuendelea kote kwa Masadukayo kwenye mfumo au huduma za Hekaluni na kuanguka kwake kulitokana na Masihi. Baada ya kuuawa kwa Kristo Masadukayo na huduma za Hekalu vilianza kuongezeka na zikafanyika potofu zaidi na zaidi. Na vivyohivyo kanisa nalo likazidi kupotoka zaidi na zaidi. Kitendo cha kusimamisha au kukataza maadhimisho ya Idi za Pasaka na Mikate Isiyotiwa chachu kwa siku zote saba kamili tangu mwaka 1965 kimeonyeshwa kwenye hii. Hadi kufikia mwaka 1967 ilikuwa hakuna mahali popote ilipoadhimishwa na Kanisa la Mungu. Hili lilikuwa ni sehemu ya tatizo la kuziondoa sadaka na ibada halisi ya Mungu. Inafuatiwa na jinsi ilivyokuwa kwenye wakati wa Kristo na ilivyotokea baada ya kifo cha Ezra hadi wakati wa Kristo wakati ilipofanyika kuwa mbaya zaidi na ndicho cha miaka ya toba iliyowekwa tangu kifo cha Kristo hadi mwaka 70 BK ikiweka kipindi cha hukumu kwa makuhani wote kwenye mwisho wa Kipindi cha huduma za Hekaluni.

 

Kipimo kimewekwa sasa kwa Makanisa ya Mungu na makuhani au makasisi wake wamekuwa wakihukumiwa sasa.

 

Malaki Sura ya 2

1 Na sasa, enyi makuhani, amri hii yawahusu ninyi. 2 Kama hamtaki kusikia, na kama hamtaki kuitia moyoni, ili kulitukuza jina langu, asema Bwana wa majeshi, basi nitawapelekeeni laana, nami nitazilaani baraka zenu; naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamyatii haya moyoni. 3 Angalieni, nitaikemea mbegu kwa ajili yenu, nami nitapaka nyuso zenu mavi, naam, mavi ya sadaka zenu; nanyi mtaondolewa pamoja nayo

 

Andiko hili limeelekezwa kwa makuhani na ukweli wa kwamba sikukuu zao zimekosewa zote. Armstrong na Kanisa la Mungu waliiingiza na kuifuata Kalenda ya Hilleli ambayo ilitungwa au kubuniwa tu na kuchukuliwa kuwa ni kalenda ya Kiyahudi mwaka 358 BK. Haikuwepo huko nyuma hadi ilipobuniwa tu wakati huu, na utaratibu wa maahirisho uliwekwa kwa udanganyifu tangu kuangamizwa kwa Hekalu. Kwa hiyo, siyo tu kwamba ni Yuda tu ndio wanaotabiriwa hapa kwenye Malaki kuwa wamepotosha maadhimisho ya sikukuu na wakazifanya zisishabihiane au zisiendane sawa na zilivyotarajiwa kuwa bali pia Kanisa la Mungu katika nyakati za mwisho chini ya Armstrong liligeuka na kuuuandama ukengeufu wakiitumia kalenda hii hii potofu kama walivyofanya Yuda. Mwisho wa zama ya Wasardi ikiongozwa na Herbert Armstrong ulikuwa ndiyo kipindi cha upotofu zaidi kuziliko zote za watu walioshikilia maongozi ya Kanisa la Mungu. Teolojia ilipotoshwa, uongozi ulikuwa mbovu na mpotofu na wafuasi wake walijikuta wakiwa chini ya mraruo wa kwato.

 

Kumbuka kuwa aya ya 3 kwenye tafsiri ya KJV inasomeka hivi:

3 Angalieni, nitaikemea mbegu kwa ajili yenu, nami nitapaka nyuso zenu mavi, naam, mavi ya sadaka zenu; nanyi mtaondolewa pamoja nayo.

 

Tunaona kuwa moja ya sikukuu itawaowaondoa makuhani hawa. Kenye mfano wa kwanza ulikuwa ni kwenye sikukuu ya Pasaka mwaka 30 BK iliyoiondolea mbali huduma ya kikuhani kwa kifo cha Kristo. Alikuwa amekisha wachagua wale 70 na mamlaka ilikuwa imekwishaondolewa kutoka kwa makuhani na kupewa kanisa. Wakati Roho Mtakatifu alipokuja siku ya Pentekoste ya mwaka 30 BK kwa nguvu na uweza, ndipo utaratibu wote mzima wa makuhani wa Israeli au wa Yuda uliondolewa na kuharibiwa kwa kipindi cha miaka arobaini.

 

4 Nanyi mtajua ya kuwa mimi nimewapelekeeni amri hii, ili agano langu liwe na Lawi, asema Bwana wa majeshi. 5 Agano langu naye lilikuwa agano la uhai na amani; nami nikampa ili aogope, naye akaniogopa, akalicha jina langu. 6 Sheria ya kweli ilikuwa kinywani mwake, wala udhalimu haukuonekana midomoni mwake; alikwenda pamoja nami katika amani na unyofu, na kuwageuza wengi hata wakaacha uovu. 7 Kwa maana yapasa midomo ya kuhani ihifadhi maarifa, tena yawapasa watu kuitafuta sheria kinywani mwake; kwa kuwa yeye ni mjumbe wa Bwana wa majeshi.

 

Ni wajibu wa makuhani na hadi kufikia kufungwa kwa Kanoni ya Agano Jipya Malaki alikuwa anasema kuwa hili ndilo lilikuwa jukumu lao. Maandiko yanatueleza kwamba majukumu haya lilipewa Kanisa na Masihi. Sisi tu wajumbe wa Bwana wa Majeshi. Hawayapati majukumu haya. Tumepewa majukumu katika nyakati za mwisho la kuzibeba siri za Mungu na kufundisha ujio wa Masihi pamoja na mashahidi wake na kushughulikia kuyatatua matatizo hayo. Huduma ya kikuhani kwa pande zote mbili, yaani kwa kanisa na Hekalu, zimeondolewa mbali kabisa.

 

8 Bali ninyi mmegeuka mkaiacha njia; mmewakwaza watu wengi katika sheria; mmeliharibu agano la Lawi, asema Bwana wa majeshi.

 

Hivyo basi, itikadi za kiantinomia ndilo tatizo moja kubwa sana kuliko yote kwenye imani ya dini ya Kikristo kuwahi kutokea katika karne ya 21. Mfumo wote wa imani ya Kikristo ni ya kiantinomiani na wamejikwaa kwa kuipotoa Sheria. Wahayudi wenyewe wameikiuka sharia kwa kuifuata Talmud.

 

9 Kwa sababu hiyo mimi nami nimewafanya ninyi kuwa kitu cha kudharauliwa, na unyonge, mbele ya watu wote, kama vile ninyi msivyozishika njia zangu, bali mmewapendelea watu katika sheria. 10 Je! Sisi sote hatuna Baba mmoja? Mungu aliyetuumba siye mmoja tu? Basi, mbona kila mmoja wetu anamtenda ndugu yake mambo ya hiana, tukilinajisi agano la baba zetu? 11 Yuda ametenda kwa hiana, na chukizo limetendeka katika Israeli, na katika Yerusalemu; maana Yuda ameunajisi utakatifu wa Bwana aupendao, naye amemwoa binti ya mungu mgeni.  

 

Kama hatuamini hilo basi makanisa ya karne ya 21 yameolewa na mungu mgeni na kwa kweli yamekuwa mabinti wa mungu mgeni na tunakuwa hatujafunguliwa tu macho yetu.

 

12 Bwana atamtenga mtu atendaye hayo, yeye aliye macho, na yeye ajibuye, atamtenga na hema za Yakobo, pia atamtenga yeye amtoleaye Bwana wa majeshi dhabihu.  

 

Kwa hiyo yeyote afanyaye hivyo atakatiliwa mbali, hata wale wanaozitoa sadaka Hekaluni.

 

13 Tena mnatenda haya nayo; mnaifunikiza madhabahu ya Bwana kwa machozi, kwa kulia na kwa kuugua, hata asiiangalie tena hiyo dhabihu, wala kuitakabali mikononi mwenu na kuiridhia. 14 Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako. 15 Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. 16 Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa udhalimu namchukia, asema Bwana wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije mkatenda kwa hiana. 17 Mmemchokesha Bwana kwa maneno yenu. Lakini ninyi mwasema, Tumemchokesha kwa maneno gani? Kwa kuwa mwasema, Kila atendaye mabaya ni mwema machoni pa Bwana, naye huwafurahia watu hao, au, Mungu mwenye kuhukumu yuko wapi? Kwa maana yeye ni mfano wa moto wa mtu asafishaye fedha,

 

Kwa maneno mengine ni kwamba kwanini mungu hakushughulikia mambo haya? Sura ya pili inawaambia ,oja kwa ,oja makuhani, makutaniko, matendo au mwenendo wa makuhani na wa watu, nia zao, hali yao ya kuwapendelea watu na kushindwa au makosa ya familia zao. Hali hii inaweza kuonekana kwenye jamii zetu sasa na kwa jinsi mfumo wa kijamii ulivyoweza kuharibika na kupotoka.

 

Malaki Sura ya 3

1 Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema Bwana wa majeshi. 2 Lakini ni nani atakayestahimili siku ya kuja kwake? Au ni nani atakayesimama atakapoonekana yeye?

 

Andiko hili limenukuliwa kwenye Mathayo 11:10, Marko 1:2 na Luka 1:76 na 7:27. Bullinger anadai na kuamini kuwa maneno haya hayakukilenga kizazi chetu; bali yalikilenga kizazi cha wakati wa huduma yake Bwana na katika nyakati zake. Huyu “Mjumbe wangu” anaonekana moja kwa moja kuwa ni Yohana Mbatizaji.

 

Mathayo 11:10

10 Huyo ndiye aliyeandikiwa haya, Tazama, mimi namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako mbele yako.

 

Haya ni maneno anayoyasema Kristo kutoka kwenye aya ya 7:

7 Na hao walipokwenda zao, Yesu alianza kuwaambia makutano habari za Yohana, Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo? 8 Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Tazama, watu wavaao mavazi mororo wamo katika nyumba za wafalme. 9 Lakini kwa nini mlitoka? Ni kuona nabii? Naam, nawaambia, na aliye mkuu zaidi ya nabii.

 

Kwa hiyo Kristo alisema kuwa alikuwa Yohana Mbatizaji ambaye ndiye alikuwa huyu mjumbe aliyetumwa ili aitengeneze njia ya Bwana. Hata hivyo kuna nabii mwingine na sauti iliyotumwa kwa ajili hiyo katika siku za mwisho naye hatokei kwenye Kabila la Lawi bali kutoka kwenye muungano wa masalio ya nyakati za mwisho ya Efraimu na Dani, aliowataja Yeremia (Yeremia 4:15) (soma jarida la Maonyo ya Nyakati za Mwisho (Na. 044)). Kisha tutawaona Mashahidi, mmoja akiwa ni Eliya aliyetabiriwa kuwa atatokea.

 

Kuendelea mbele kutoka kwenye Malaki 3:2:  

2b … ni mfano wa sabuni ya mtu afuaye nguo; 3 naye ataketi kama asafishaye fedha na kuitakasa, naye atawatakasa wana wa Lawi, atawasafisha kama dhahabu na fedha; nao watamtolea Bwana dhabihu katika haki. 4 Wakati ule ndipo dhabihu za Yuda na Yerusalemu zitakapopendeza mbele za Bwana, kama katika siku za kale, na kama katika miaka ya zamani. 5 Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema Bwana wa majeshi. 6 Kwa kuwa mimi, Bwana, sina kigeugeu; ndio maana ninyi hamkuangamizwa, enyi wana wa Yakobo.

 

Kwa hiyo kusudi lote la Bwana linatimia na Yakobo haangamizwi na kumalizwa kabisa kwa kuwa kuna kusudi lililolengwa na Mungu lililomuandaa Yakobo kuwa ni kama uzao nan i kama chimbuko la sharia na unabii. Hii pia imo kwenye rejea za Korani. Kwenye Sura ya: “Wale waliowekwa kwenye matabaka” ambayo inahusiana na unabii wa kufanywa au kuanzishwa kupitia Musa na Haruni hadi kwa Kristo. Mamlaka ya Maandiko Matakatifu yameanzishwa kwa makuhani kupitia kwa Musa na Haruni, Ibrahimu, Isaka na Yakobo hadi kumfikia Kristo na huo ndiyo mlolongo wa kuanzishwa kwa sheria.

 

7 Tokea siku za baba zenu mmegeuka upande, mkayaacha maagizo yangu, wala hamkuyashika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi, asema Bwana wa majeshi. Lakini ninyi mwasema, Turudi kwa namna gani? 8 Je! Mwanadamu atamwibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gani? Mmeniibia zaka na dhabihu. 9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote. 10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la. 11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi. 12 Na mataifa yote watawaiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema Bwana wa majeshi. 13 Maneno yenu yamekuwa magumu juu yangu, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako kwa namna gani? 14 Mmesema, Kumtumikia Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa kwenda kwa huzuni mbele za Bwana wa majeshi? 15 Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao. 16 Ndipo wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. Naye Bwana akasikiliza, akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha Bwana, na kulitafakari jina lake. 17 Nao watakuwa wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye. 18 Ndipo mtakaporudi, nanyi mtapambanua kati ya wenye haki na waovu, na kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.

 

Hii iko wazi kwenye sura ya 3. Watu hawamrudii Mungu. Zaka haitolewi kikamilifu. Utaratibu wa kutoa zaka ni mbovu na umekataliwa. Kanisa la Mungu limeiopotoa na kuitangua sheria mwaka 1995 baada ya kuanzishwa kwa CCG. Joseph Tkatch Snr. alitoa hotuba au mahubiri yaliyotangua sheria ambaye kwaye alizimalizia wiki au majuma 40 kwa kutumia saa moja tu, yaliyoenezwa tangu wakati mbalimbali kutoka wakati aliotoa mahuri haya na alipokufa.

 

Watu engine wamejaribu kupata waumini kwenye makanisa yao kwa kusema kuwa sheria haifai na inakanganya na kuiondoa au kuitangulia mbali. Kuliamuliwa kuitanguliambali hata ile inayofundisha umuhimu wa kutoa zaka, kwa lengo la kuwapata watu wengi lakini hiyo haikufaa.

 

Milolongo hii yote ya kushindwa kuzishika sheria za Mungu inawasababishia watu kuyaacha Makanisa ya Mungu kwa idadi kubwa mno. Watu mara zote hupenda kuwa sehemu ya mwili wa Kristo wakiifanya kazi ya Mungu au wakiwa hawaifanyi. Kama hawaifanyi, basi wanatakiwa waondoke.

 

Mwishoni kutakuwa na watu wawili, Henoko na Eliya, wakifanya kazi Hekaluni. Tutakuwa tunawasaidia kwa kufanya kazi ya kuwabatiza wale watakaotubu katika siku za mwisho. Kwa hiyo kazi hii itakwenda kwa Kristo atakayelijenga kanisa tangu hapo hadi kwenye mataifa yote.

 

Aya ya 17 kwenye tafsiri ya KJV inasema: Nao watakuwa wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe mwenyewe amtumikiaye.

 

Vito hivi vya thamani ni hazina ya kipekee, ni raslimali muhimu, yaani, anayomiliki mtu. Kwa hiyo, matokeo ya mwisho ya kazi ya Mungu litakuwa kanisa la watu ambao watakuwa wa thamani ya kipekee kwa Mungu, na hasa hasa wana wa Mungu.

 

Malaki Sura ya 4

1 Kwa maana, angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuru; na watu wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema Bwana wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi.

 

Hivi ndivyo ilivyonenwa kuhusu nyakati za mwisho. Hii ni wakati mashahidi wawili watakapoletwa kwa maandalio ya Masihi na watasimama mbele ya mungu wa ulimwengu huu wote.

 

2 Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake; nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa mazizini. 3 Nanyi mtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu; katika siku ile niifanyayo, asema Bwana wa majeshi. 4 Ikumbukeni torati ya Musa, mtumishi wangu, niliyomwamuru huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote, naam, amri na hukumu. 5 Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya. 6 Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana.

 

Mlolongo huu upo kwenye sehemu mbili. Sharia zake za Musa aliyopewa huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote ambayo kwayo kwamba sharia au kanuni zote na sharia zote ni lazima zishikwe. Kisha ndipo Eliya atatumwa kuanikiza tena sharia hizo na hukumu mbele ya siku ya Bwana iliyokuu nay a kuogofya.

 

Kutoka na na aya ya 5 Bullinger anaonyesha kuwa: Eliya nabii. Aliita kuwa, hapa tu peke yake, na kwenye 2Nyakati 21:12. Penginepopote, wakati wote “Eliya Mtishbi”, kujionyesha binafsi yake; lakini hapa "Eliya nabii "kwa sababu aliwafanya Israeli wampokee Masihi, Yohana Mbatizaji ndiye anayeweza kudhaniwa kuwa alikuwa Eliya (soma nukuu kwenye Mathayo 17:9-13, Marko 9:11-13): na kwenye chakula chake mahsusi ambacho mvinyo uliwakilisha damu yake ambayo ilichukuliwa (na bado inachukuliwa kuwa) ni “damu ya Agano (Jipya)”, kama ilivyotabiriwa kwenye Yeremia 31:31-34; Waebrania 8:8-13; 10:15-17; 12:24).

 

Siku hii ya Bwana kama tuijuavyo sisi sote ni siku ya mwisho tunayoingojea na siku hiyo ya Bwana kama ilivyoelezewa kwenye Isaya 2:12,17; 13:6f. Bwana abayetajwa kuwa ni Yehova ambaye ni Kristo anayetenda kazi au kuhudumu kama Kuhani Mkuu kwenye Hekalu la Mungu.

 

Malaki ni kazi ya kinabii ambayo inaendelea mbele kwenye ujio wa Masihi na kitabu chake kinatuambia kwa wazi wazi sana jina la nabii ambaye atatumwa aje katika nyakati za mwisho. Kinalimalizia Mkataba au maagizo ya Agano la Kale kikionyesha kile kinachokwenda kutokea na kinaonyesha mambo mawili ya agano ambayo ni: sheria na maagizo na kwamba Eliya atakuja kama mjumbe wa agano na sheria na kwamba kile kitakacho kwenda kuanzishwa katika siku za mwisho.

 

Kinachokwenda kutokea ni kwamba karibu vikundi vyote vya makanisa vitaangamizwa na kutakuwa na kiumbe miongoni mwa Waisraeli na upuuzi wao kenye mwenendo wao vitakomeshwa na kuongolewa kabisa. Ndipo tutakua tumeandaliwa tena na kuingizwa kwenye taifa halisi na kwenye kundi sahihi chini ya wale ambao kwa bahati nzuri sana watakuwepo kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu.

 

Hiki ndicho tunachokitaka na hiki ndicho tunachotarajia kukifikia au kukipata. Tutakwenda kuwa ama kwenye Ufufuo wa Kwanza au wa Pili. Tunafanya kazi kana kwamba tunastahili au tunatimiza vigezo vya kuwa na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza bali iwapo kama tutakuwa kwenye ule wa Pili, ambao huu ndio wa kuhukumiwa na Mungu. Tunapaswa kufanya kile tuwezacho kukifanya.

 

Ishara ya kumrudia Mungu ni utoaji wa zaka na kurudi kwenye mfumo wote mzima; yaani ni kutoa zaka kikamili na kuzishika sheria za Mungu. Wengi hawapendi kulielea Agano la Kale au uhusiano wake na Injili zote zilizopo, ziitwazo “Agano Jipya” la Kristo, ambalo ni mwendelezo tu wa lile agano alilompa nabii Musa pale Sinai. Kristo likuwa ni elohim, Malaika wa Uwepo wake, aliyempa agano Musa na tusilisahau kabisa jambo hili.

q