Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[028]

 

 

 

Moto Kutoka Mbinguni

(Toleo La 1.0 20010526-20010526)

 

Mungu ananena kwa kupitia nabii Ezekieli kuwa Siku za Mwisho kuwa atawasha moto kwenye Mashamba ya Kusini na utawaka kuelekea upande wa kaskazini na kuteketeza kila kitu. Hakuna kitakachosalia bila kuguswa na imani au mfumo utakaoanzishwa na kufundishwa utaendelea na kudumu milele. Huu ni mfumo ule utakaofanywa na Masihi. Hii ndiyo maana ya huu Moto unaotoka Mbinguni ambao Mungu ameuahidi kupitia kwa watumishi wake manabii.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2001 Wade Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Moto Kutoka Mbinguni


 


Inatakiwa kwanza Usome majarida yafuatayo:

Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13)

Kuanguka kwa Misri. Unabii wa Mikono Iliovunjika ya Farao (Na. 36)

Maonyo ya Siku za Mwisho (Na. 44)

Samson na Waamuzi (Na. 73) na

Maana ya Maono ya Ezekieli (Na. 108)

 

Utangulizi

Mojawapo ya nabii muhimu sana kwenye Biblia unakutikana kwenye sura ya 20 ya Kitabu cha nabii Ezekieli. Uandishi wake umeelezewa kwenye maandiko mengine yaliyoodheshwa kwenye kitabu hiki cha Ezekieli lakini ni kama ulivyo unabii wote umechukuliwa kwa namna ya kwamba “hapa kidogo na pale kidogo” na ni lazima uwekwe kwenye mlolongo wa wakati ili uweze kueleweka ksahihi na kikamilifu.

 

Kwenye mfuatano huu wa matukio, viongozi wa taifa la Israeli wanakuja kumuuliza Bwana kwa kuwa wanakuja wakiwa chini ya mshitaki au adui wao. Tumeona kutoka kwenye surah ii kuwa Mungu amechukua hatua ya kuwakataa tu na kwamba hatawajibu kitu kwa sababu ya imani yao potofu ya kidini waliyojisimamishia.

 

Imani hii katika Israeli, na ambayo iliendelea pia katika Yudea, inaendelea na kushika kasi katika siku za mwisho. Ni kama ilivyo kwa watu wenye shingo ngumu na waliokengeuka ndivyo ilivyo. Israeli walidhani kuwa ukarimu ungechukua mkondo wake hadi kipindi cha zaidi ya karne tatu za mwisho ya millennia ya pili ya kipindi hiki cha sasa ambacho kwa ajili ya kuishika kwako Biblia kutaamua. Hii ilikuwa ni kwa sehemu pekee nzuri nay a kwali. Israeli walikuwa kwenye uasi na ukengeufu na pia walikuwa wazinzi ambao waliichukua imani ya kuamini mungu wa Utatu au imani ya Kitrinitari na kalenda yake ya uwongo ya mfumo wa kipagani kukiwemo na ibada ya kipagani ya Krisamas na Easter (sawa na yanavyosema majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. 156) na Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235) [God’s Calendar (No. 156) and The Origins of Christmas and Easter (No. 235)].

 

Hata wito wa kuwataka Israeli watubu waliopewa viongozi wa mataifa ya Israeli wa siku hizi ambao ni wa nchi ya Marekani ni wakuwataka wageuke na kuachana na uengeufu wa namna hii hii na wameonywa waachane na ibada za sanamu ambazo ni ibada za Jumapili na ibada za Krismas na kuadhimisha Easter zinazotokana na imani za kipaagani za pande za mashariki na ambazo zilikemewa sana na Mungu kwa kupitia watumishi wake manabii.

 

Yeremia 10:1-25 Enyi nyumba ya Israeli, lisikieni neno awaambialo Bwana; 2 Bwana asema hivi, Msijifunze njia ya mataifa, wala msishangae kwa sababu ya ishara za mbinguni; maana mataifa hushangaa kwa sababu ya ishara hizo. 3 Maana desturi za watu hao ni ubatili, maana mtu mmoja hukata mti mwituni, kazi ya mikono ya fundi na shoka. 4 Huupamba kwa fedha na dhahabu; huukaza kwa misumari na nyundo, usitikisike. 5 Mfano wao ni mfano wa mtende, kazi ya cherehani, hawasemi; hawana budi kuchukuliwa, kwa sababu hawawezi kwenda. Usiwaogope; kwa maana hawawezi kutenda uovu, wala hawana uwezo wa kutenda mema. 

 

Mungu anatuambia kuwa tusijifunze wala kuzifuta njia za mataifa, lakini haichukui muda na uchunguzi mkubwa ili kubaini hili kwa maelezo ya kile kinachojulikana kama maadhimisho ya Krismas ya kuukata mti na kuupamba ukijulikana kama ni mti wa Krismas.

6 Hapana hata mmoja aliye kama wewe, Ee Bwana; wewe ndiwe uliye mkuu, na jina lako ni kuu katika uweza. 7 Ni nani asiyekucha wewe, Ee mfalme wa mataifa? Maana hii ni sifa yako wewe; kwa kuwa miongoni mwa wenye hekima wote wa mataifa, na katika hali yao ya enzi yote pia, hapana hata mmoja kama wewe. 8 Lakini wote pia huwa kama wanyama, ni wapumbavu. Haya ni maelezo ya sanamu, ni shina la mti tu. 9 Iko fedha iliyofuliwa ikawa mabamba, iliyoletwa kutoka Tarshishi, na dhahabu kutoka Ufazi, kazi ya stadi na ya mikono ya mfua dhahabu; mavazi yao ni rangi ya samawi na urujuani; hayo yote ni kazi ya mafundi yao. 10 Bali Bwana ndiye Mungu wa kweli; Ndiye Mungu aliye hai, Mfalme wa milele; Mbele za ghadhabu yake nchi yatetemeka, Wala mataifa hawawezi kustahimili hasira yake. 11 Mtawaambia hivi, Miungu hiyo isiyofanya mbingu na nchi, hiyo itaangamia katika nchi, nayo itatoweka chini ya mbingu. 12 Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu.13 Atoapo sauti yake, pana mshindo wa maji mbinguni, Naye hupandisha mawingu toka ncha za nchi; Huifanyia mvua umeme, Huutoa upepo katika hazina zake. 14 Kila mtu amekuwa kama mnyama, hana maarifa; Kila mfua dhahabu amefedheheshwa na sanamu yake ya kuchonga; Maana sanamu yake ya kuyeyuka ni uongo, Wala hamna pumzi ndani yake. 15 Ni ubatili tu, ni kazi za udanganyifu; Wakati wa kujiliwa kwao watapotea. 16 Yeye, Fungu la Yakobo, siye kama hawa; Maana ndiye aliyeviumba vitu vyote; Na Israeli ni kabila ya urithi wake; Bwana wa majeshi ndilo jina lake. 

Hapa Mungu ameonyesha malundo mblimbali kadiri ya uweza wake, hekima yake, ukuu wake na udhaifu wa mwandamu. Sanamu na vinyago wanavyojifanyia wanadamu ni ubatili mtupu na Mungu anachukia kuwaona watu wakizisujudia badala ya kumsujudia yeye.

 

Yeremia anaendelea mbele kwa kuonyesha kile ambaho Mungu anakichukia zaidi na kile anachokwenda kukifanya kwa ajili ya hilo.

Yeremia 10:17-25 Haya! Kusanya bidhaa yako katika nchi, wewe ukaaye katika mazingiwa. 18 Maana Bwana asema hivi, Tazama, wakati huu nitawatupa wenyeji wa nchi hii kama kwa kombeo, nitawataabisha, wapate kuona taabu. 19 Ole wangu, kwa sababu ya jeraha yangu! Pigo langu laumia; lakini nalisema, Kweli, ni huzuni yangu mimi, nami sina budi kuivumilia. 20 Hema yangu umetekwa nyara, kamba zangu zote zimekatika; watoto wangu wameniacha na kwenda zao, pia hawako. Hapana mtu atakayenitandikia tena hema yangu, na kuyatundika mapazia yangu. 21 Kwa sababu wachungaji wamekuwa kama wanyama, wala hawakuuliza kwa Bwana; basi hawakufanikiwa, na makundi yao yote yametawanyika. 22 Sauti imesikiwa, Tazama, inakuja; mshindo mkuu kutoka nchi ya kaskazini, ili kuifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa, makao ya mbweha. 23 Ee Bwana, najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu. 24 Ee Bwana, unirudi kwa haki; si kwa hasira yako, usije ukaniangamiza. 25 Hasira yako uwamwagie mataifa wasiokujua, na jamaa zao wasioliitia jina lako; kwa maana wamemla Yakobo, naam, wamemla kabisa na kumwangamiza, na kuyafanya makao yake kuwa ukiwa.

 

Mungu aliwapa Israeli haki ya uzaliwa wa kwanza kwa sababu ya ahadi yake aliyompa Ibrahimu na sio kwa matendo mengine yoyote au umuhimu wao Israeli na alikuwa na uelewa mzuri zaidi kuliko hiyo.

 

Hadi leo wanaenda mstuni na kukata miti na kuipamba kwa ajili ya miungu wa uwongo kama walivyokatazwa na kukemewa wasifanye hivyo kupitia manabii kwa kipindi cha zaidi ya karne ishirini na saba zilizopita. Mungu sasa anakwenda kushughulika na imani hii na viongozi wa Israeli walioiingiza imani hii. Israeli wakiwa kama imani mbovu na potofu nao wataangamizwa. Kwenye eneo lake jambo hili litakomeshwa kwenye Biblia ambayo itaichoma na kuiangamiza dunia kwenye jehena la moto na kuacha utaratibu wa kweli na wenye kufanya toba na watu wanyofu.

 

Upanga wa Bwana atatoka nje ya ala yake kwa ajili ya watu wote kutoka kusini hadi kaskazini.

Ezekieli 21:1-7 Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, uelekeze uso wako kuelekea Yerusalemu, ukadondoze neno lako upande wa mahali patakatifu, ukatabiri juu ya nchi ya Israeli; 3 uiambie nchi ya Israeli, Bwana asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, nami nitautoa upanga wangu alani, nami nitamkatilia mbali nawe mtu mwenye haki na mtu mbaya. 4 Basi, kwa kuwa nitamkatilia mbali nawe mtu mwenye haki na mtu mbaya, upanga wangu utatoka alani mwake, uwe juu ya watu wote wenye mwili toka kusini hata kaskazini, 5 na watu wote wenye mwili watajua ya kuwa mimi, Bwana, nimeufuta upanga wangu alani mwake; hautarudi tena. 6 Ugua, basi, Ee mwanadamu; kwa kuvunjika kwake viuno vyako, na kwa uchungu, utaugua mbele ya macho yao. 7 Na itakuwa, wakuambiapo, Mbona unaugua? Ndipo utakaposema, Kwa sababu ya habari hizo, maana linakuja; na kila moyo utayeyuka, na mikono yote itakuwa dhaifu, na kila roho itazimia, na magoti yote yatalegea kama maji; tazama, linakuja, nalo litatendeka, asema Bwana MUNGU.

 

Ni habari ambayo wananamu waliileta kwanza dhidi ya Yerusalemu na kisha italetwa ulimwenguni kwa unabii kwa Israeli wote. Itaanguka katika siku za mwisho kwa watu wote. Ni agizo la sehemu ya Kanisa katika siku za mwisho kuanza kuuhubiri ujumbe huu kuanzia Kusini na itaendelea hadi kaskazini na viongozi wa wazee watahukumiwa sawasawa kwayo na Israeli wote sawasawa na hilo. Mashamba ya kusini mwa Israeli katika siku za mwisho ni mataifa ya Australia na New Zealand na Afrika ya Kusini. Ilikuwa ni kutoka Australia katika mlolongo wa Siku za Mwisho ambazo ujumbe huu unatokea. Ujumbe ule utawasha moto kutoka upande wa kusini hadi kaskazini na utaendelea kutoka taifa moja hadi lingine ukiteketeza watu wote njiani. Ilipaswa ijulikane kutoka Milima ya Efraimu (Yeremia 4:15), inamaanisha kuwa mataifa yaliyopo sasa yaliyotokana na hawa Efraimu. Mataifa haya yanatakiwa kuonywa juu ya kurudi kwake Masihi (sawa inavyosema jarida la Maonyo ya Siku za Mwisho (Na. 44) [The Warning of the Last Days (No. 44)]. Ujumbe huu hautarudi bure na Bwana hatautoa upanda wake bila sababu. Itaanzia kwenye Nyumba ya Mungu na kuchoma hadi watakavyotakasika wote.

Ezekieli 20:1-49 Ikawa katika mwaka wa saba, mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi, baadhi ya wazee wa Israeli walikuja ili kuuliza kwa Bwana, wakaketi mbele yangu. 2 Neno la Bwana likanijia, kusema, 3 Mwanadamu, sema na wazee wa Israeli, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Je! Mmekuja kuniuliza neno? Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sitaulizwa neno na ninyi. 4 Je! Utawahukumu, mwanadamu, utawahukumu? Uwajulishe machukizo ya baba zao; 5 uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Katika siku ile nilipochagua Israeli, na kuwainulia wazao wa nyumba ya Yakobo mkono wangu, na kujidhihirisha kwao katika nchi ya Misri, hapo nilipowainulia mkono wangu, nikisema, Mimi ni Bwana, Mungu wenu; 6 katika siku ile naliwainulia mkono wangu, kuwatoa katika nchi ya Misri, na kuwaingiza katika nchi niliyowapelelezea, ijaayo maziwa na asali, ambayo ni utukufu wa nchi zote; 7 nikawaambia, Kila mtu kwenu na atupilie mbali machukizo ya macho yake, wala msijitie unajisi kwa vinyago vya Misri, Mimi ni Bwana, Mungu wenu. 8 Lakini waliniasi, wala hawakutaka kunisikiliza; hawakutupilia mbali kila mtu machukizo ya macho yake, wala hawakuviacha vinyago vya Misri; ndipo nikasema kwamba nitamwaga ghadhabu yangu juu yao, ili kuitimiza hasira yangu juu yao, katikati ya nchi ya Misri. 9 Lakini nalitenda kwa ajili ya jina langu, ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa, ambao walikaa pamoja nao, ambao machoni pao nalijidhihirisha kwao, kwa kuwatoa katika nchi ya Misri

 

Mungu anatuita tutoke Misri. Alitupa Sabato zake kuwa ni ishara ya kuwa sisi ni watu wake. Tuliziacha Sabato hizo na kuifuata miungu mingine na imani ya mungu jua. Hapa anatukemea kwa kwa kufanya kwetu hivyo. Yuda walionekana kuwa waovu zaidi machoni mwake kwa kuwa walijifanya kuishika kalenda lakini wakaichnganya na kuivuruga kwa kupitia rabi aitwaye Hilleli na kwa kupitia mapkeo ya Mafarisayo, ikawapotoshwa sana waongofu waliowafanya kuwa waovu zaidi ya walivyokuwa hapo kabla na huku Yuda wenyewe wakiwa kwenye.

Ezekieli 20:10-32 Basi nikawatoa katika nchi ya Misri, nikawaleta jangwani. 11 Nikawapa amri zangu, na kuwaonyesha hukumu zangu, ambazo mwanadamu ataishi kwazo, kama akizitenda. 12 Tena naliwapa sabato zangu, ziwe ishara kati ya mimi na wao, wapate kujua ya kuwa mimi, Bwana, ndimi niwatakasaye. 13 Lakini nyumba ya Israeli waliniasi jangwani; hawakuenda katika amri zangu, wakazikataa hukumu zangu, ambazo mwanadamu ataishi kwazo, kama akizitenda; na sabato zangu walizitia unajisi sana; ndipo nikasema, Nitamwaga hasira yangu juu yao jangwani, ili niwaangamize. 14 Lakini nalitenda kwa ajili ya jina langu, lisitiwe unajisi machoni pa mataifa, ambao naliwatoa mbele ya macho yao. 15 Tena naliwainulia mkono wangu jangwani, ya kwamba sitawaingiza katika nchi ile niliyokuwa nimewapa, ijaayo maziwa na asali, ambayo ni utukufu wa nchi zote; 16 kwa sababu walizikataa hukumu zangu, wala hawakuenda katika amri zangu, wakazitia unajisi sabato zangu, kwa maana mioyo yao iliandama vinyago vyao. 17 Walakini jicho langu likawahurumia nisiwaangamize kabisa, wala sikuwakomesha kabisa jangwani. 18 Kisha nikawaambia watoto wao jangwani, Msiende katika amri za baba zenu, wala msizishike hukumu zao, wala msijitie unajisi kwa vinyago vyao.

 

Sababu ya kuwepo kwa kipindi hiki cha miaka arobaini ya wao kuwa jangwani bado hawajajifunza. Watu waliotolewa kutoka Misri hawakuruhusiwa kuingia kwenye Nchi ya Ahadi kwa ajili ya kuasi kwao. Watoto wao waliingia lakini na wao waliangukia kwenye uasi na walilipa fidia kwa kuadhibiwa.

 Mimi ni Bwana, Mungu wenu; endeni katika amri zangu, mkazishike hukumu zangu, na kuzitenda; 20 zitakaseni sabato zangu; zitakuwa ishara kati ya mimi na ninyi, mpate kujua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. 21 Lakini watoto hao waliniasi; hawakuenda katika amri zangu, wala hawakuzishika hukumu zangu kuzitenda, ambazo mwanadamu ataishi kwazo kama akizitenda; walizitia unajisi sabato zangu, ndipo nikasema, kwamba nitamwaga ghadhabu yangu juu yao, ili kuitimiza hasira yangu juu yao jangwani. 22 Lakini naliuzuia mkono wangu, nikatenda kwa ajili ya jina langu, lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa, ambao mbele ya macho yao naliwatoa. 23 Tena naliwainulia mkono wangu jangwani, kwamba nitawatawanya kati ya mataifa, na kuwatapanya katika nchi mbalimbali; 24 kwa sababu hawakuzitekeleza hukumu zangu, bali walizikataa amri zangu, nao walizitia unajisi sabato zangu, na macho yao yaliandama vinyago vya baba zao. 25 Tena naliwapa amri zisizokuwa njema, na hukumu ambazo hawakuweza kuishi kwazo; 26 nami nikawatia unajisi kwa matoleo yao wenyewe, kwa kuwa walipitisha motoni wote waliofungua tumbo; ili kuwafanya kuwa ukiwa, wakapate kujua ya kuwa mimi ndimi Bwana. 27 Basi, mwanadamu, sema na nyumba ya Israeli, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Baba zenu wamenitukana kwa jambo hili, kwa kuwa wamekosa kosa juu yangu. 28 Kwa maana nilipokuwa nimekwisha kuwaingiza katika nchi ile, ambayo naliuinua mkono wangu kuwapa, wakati huo walipoona kila mlima mrefu, na kila mti wenye majani mengi, walitoa matoleo yao huko, na huko walitoa chukizo la sadaka zao, na huko walifanya nukato la kupendeza, na huko walimimina sadaka zao za kunywewa. 29 Ndipo nikawauliza, Nini maana yake mahali palipoinuka mnapopaendea? Basi, jina lake mahali pale ni Bama hata leo. 30 Basi, uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi; Je! Mnajitia unajisi kwa kuzifuata njia za baba zenu? Mnakwenda kufanya uasherati kwa kuyafuata machukizo yao? 31 Tena mtoapo matoleo yenu, na kuwapitisha watoto wenu motoni, je! Mnajitia unajisi kwa vinyago vyenu vyote hata leo? Na mimi je! Niulizwe neno nanyi, Enyi nyumba ya Israeli? Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sitaulizwa neno na ninyi. 32 Na haya yote yaingiayo katika nia zenu hayatakuwa kamwe; ikiwa mmesema, Sisi tutakuwa sawasawa na mataifa, sawasawa na jamaa za nchi nyingine, kutumikia miti na mawe.

 

Ndipo Israeli wakatawanyika lakini Mungu akawaahidi ya kuwakusanya watu wake kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa na kwa hasura yake itakayomwagwa kwetu atawapiga maadui zetu na tutatawala naye. Mungu haendi kutuomba ushauri sisi. Bali atayafanya hayo kwa shuruti na uweza wake kwa Roho wake, ataletwa kwenye agano na kupitishwa chini ya fimbo ya kifalme ya Masihi.

 

Ataangamizwa na waasi wote wataangamizwa kati yetu. Waasi wataondolewa kutoka kwenye nchi watakayokimbilia, hata hivyo, hawataingia kwenye nchi ya Israeli na tena na watajua kuwa Bwana ndiye Mungu.

Ezekieli 20:33-44 Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hakika kwa mkono hodari, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa ghadhabu iliyomwagika, nitakuwa mfalme juu yenu; 34 nami nitawatoa katika mataifa, na kuwakusanya, na kuwatoa katika nchi mlizotawanyika ndani yake, kwa mkono hodari, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa ghadhabu iliyomwagika; 35 nami nitawaingiza katika jangwa la mataifa, na huko ndiko nitakakoteta nanyi uso kwa uso. 36 Kama nilivyoteta na baba zenu katika jangwa la Misri, ndivyo nitakavyoteta nanyi, asema Bwana MUNGU. 37 Nami nitawapitisha chini ya fimbo, nami nitawaingiza katika mafungo ya agano. 38 Nami nitawasafisha kwa kuwatoa waasi, na hao walionikosa; nitawatoa katika nchi wanayokaa ugenini, lakini hawataingia katika nchi ya Israeli; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. 39 Na katika habari zenu, enyi nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi, Enendeni, mkavitumikie vinyago vyenu kila mmoja wenu; na wakati wa baadaye pia, kama hamtaki kunisikiliza; lakini jina langu takatifu hamtalitia unajisi tena, kwa matoleo yenu, na kwa vinyago wenu. 40 Kwa maana katika mlima wangu mtakatifu, katika mlima mrefu sana wa Israeli, asema Bwana MUNGU, ndiko watakakonitumikia nyumba yote ya Israeli, wote pia katika nchi ile; nami nitawatakabali huko, na huko nitataka matoleo yenu, na malimbuko ya dhabihu zenu, pamoja na vitu vyenu vitakatifu vyote 41 Nitawatakabali kama harufu ipendezayo, nitakapowatoa katika mataifa, na kuwakusanya toka nchi zile mlizotawanyika; nami nitatakaswa kwenu machoni pa mataifa.

 

Mchakato huu wa utakaso wa hekalu, Kanisa la Mungu ni mwendelezo ambao unamhusisha Mungu na kuwaita watu binafsi ambao wanasehemu ya kutendea kazi (sawa na lisemavyo jarida la Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. 241) [Sanctification of the Temple of God (No. 241)]. Kama tunavyoona hapo juu hii inajumuisha pia taifa la kimwili lililopo la Israeli na waongofu na kurudi kwenye nchi ya ahadi.

 

42 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapowaingiza katika nchi ya Israeli, katika nchi ile ambayo niliuinua mkono wangu kwamba nitawapa baba zenu. 43 Na huko mtazikumbuka njia zenu, na matendo yenu yote, ambayo mmejitia unajisi kwayo; nanyi mtajichukia katika macho yenu wenyewe, kwa sababu ya maovu yenu yote mliyoyatenda. 44 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapokuwa nimetenda nanyi kwa ajili ya jina langu, si sawasawa na njia zenu mbaya, wala si sawasawa na matendo yenu mabovu, enyi nyumba ya Israeli, asema Bwana MUNGU.

 

Kwa hiyo Mungu anasema kuwa atatenda na atawaweka watu wake kwenye mlima wa Sayuni nchini Israeli na huko watamuabudu yeye, lakini kwa sasa atafanya hilo. Je, awarejeshe hivyo ssa wakiwa wamekengeuka hawa Yuda na wakiwa wanamkataa Masihi? Je, ifanyike hivyo pamoja na kalenda na dini ya uwongo zilizopotoshwa kwa mapokeo ya kinafiki ambayo yaliwasababisha Yuda waende utumwani na utawanyiko mwaka 70 BK na ambako waliongeza kuyaandama maovu yao hata kwa kiwango kilicho zaidi ya ilivyokuwa huko nyuma na wakizidi sana kwenye karne hii. Hapana! Haitaweza kuwa hivyo kwa hatua za Warusi na Waashikenazi. Mungu analiinua hili upande wa kusini mwa Iaraeli katika siku za mwisho kutoka Efraimu/Dani. Kuna mataifa matatu tu ya Israeli upande wa kusini katika siku za mwisho. Neno la Mungu litaendelea kutoka kanisani na kukemea imani za uwongo za kidini iliyochipuka kutoka Babeli kwenye Ukristo na imani za mungu jua na dini za kisirisiri. Chimbuko la jamo hili lilijulikana. Kwa hiyo, ilijulikana kwamba lilikuwa ni mataifa haya ya Israeli kwenye nchi za kusini katika siku za mwisho. Na hii ndiyo sababu unabii wa Wakatoliki Watritarian unaelezea juu ya inayotuama kwenye Torati ya Mungu inayoendelea kutoka mataifa ya kusini hadi mashariki mwa Yerusalemu katikati ya bahari mbili (sawa na linavyosema jarida la Kiti Kimoja Cha Enzi, Wakaliaji Wawili (Na. 26) [One Throne Two Pretenders (No. 26)]. Mapepo wanajua kuhusu haki ya uzaliwa wa kwanza wa Israeli hata kabla hatujapewa sisi. Walifanya propaganda zao za uwongo kwa kipindi cha marne za nyuma za kabla ya tukio na wakadai kuwa ilikuwa ni imani ya Mpingakristo, kwa kuwa iko tofauti kabisa na ile ya Wakatoliki wa Rumi na inaendana kwa mujibu wa Torati ya Mungu.

Ezekieli 20:45-49 Neno la Bwana likanijia, kusema, 46 Mwanadamu, uelekeze uso wako kusini, ukadondoze neno lako upande wa kusini, ukatabiri juu ya msitu wa uwanda wa Negebu, 47 ukauambie msitu wa Negebu, Lisikie neno la Bwana; Bwana MUNGU asema hivi; Tazama nitawasha moto ndani yako, nao utakula kila mti mbichi ndani yako, na kila mti mkavu; miali ya moto ule haitazimika, na nyuso zote toka kusini hata kaskazini zitateketezwa kwa moto huo. 48 Na watu wote wenye mwili wataona ya kuwa mimi, Bwana, nimeuwasha; hautazimika. 49 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, wao hunisema; Je! Mtu huyu si mtu mwenye kupiga mithali?

Kwa hiyo Mungu alisema kwa mifano na fumbo nao walisikia lakini hawakuelewa. Mfano na fumbo lilikuwa fupi lakini hadi kufikia wakati wa mwisho, hadi kipindi muafaka cha wao kuelezwa na cha kuwashwa kwa moto ulao, kama ulivyochomwa na Samsoni wa kabila la Dani kwenye mashamba ya Wafilisti. (kama ilivyoelezwa kwenye jarida la Samsoni na Waamuzi (Na.73) [S amson and the Judges (No. 73)].

 

Nabii Ezekieli alionyeshwa maono ya Makerubi nah ii, kwenye sura ya 1, ilikuwa ni muhimu kujua mfuatano wa huu wa matukio, lakini kwenye sura ya 10 imeonyeshwa tena ili kufafanua kusudio linguine (imefafanuliwa zaidi kwenye jarida la Maana ya Maono ya Ezekieli (Na. 108) [The Meaning of Ezekiel’s Vision (No. 108)]. Jarida hili ni la muhimu kulipitia kabla ya kulisoma hili.

 

Israeli watagawanywa na kuwekewa ukuta nasi tutajua kuwa tumefanya makosa na dhambi. Vita vi kwa ajililyetu na tutajionea hasira ya Mungu kwa ujinga wetu.

Ezekieli 5:1-10 Nawe, mwanadamu, ujipatie upanga mkali, kama wembe wa kinyozi ujipatie, ukaupitishe juu ya kichwa chako na ndevu zako; kisha ujipatie mizani ya kupimia, ukazigawanye nywele hizo. 2 Theluthi ya hizo utaiteketeza katikati ya mji, siku za mazingiwa zitakapotimia; nawe utatwaa theluthi, na kuipiga kwa upanga pande zote; nawe utatawanya theluthi ichukuliwe na upepo, nami nitafuta upanga nyuma yake. 3 Nawe twaa nywele chache katika hizo, na kuzifunga katika upindo wa mavazi yako. 4 Nawe utatwaa tena baadhi ya hizo, na kuzitupa katikati ya moto, na kuziteketeza katika moto huo; kutoka nywele hizo moto utakuja na kuingia katika nyumba yote ya Israeli.

 

Fumbo na mfano huu unahusu mgawanyiko. Nywele zanazotajwa hapa zinaliwakiaisha taifa la Israeli. Nywele hizi zimegawanywa kwenye mafungu matatu. Theluthi moja ya kwanza imeunguzwa kwa moto kwenye mzingiro; na theluthi nyingine imeinizwa kwenye ile vita inayofuatia; na theluthi nyingine iliyobakia nayo inaunguzwa tena. Kwenye ile theluthi moto unaokea kwenye nyumb  yote ya Israeli. Kwa maneno mengine ni kuzema, taifa la Israeli limesafishwa na kutakaswa hadi limetakasika habisa kwa njia ya moto. Miongoni mwao kuna pia waaminifu ambao ni wateule wa Kanisa na ni kutokana na hao moto utawashwa. Uwashughulikie na imeelezwa pia kwamba.

5Bwana MUNGU asema hivi; Huu ndio Yerusalemu; nimeuweka kati ya mataifa, na nchi zauzunguka pande zote. 6 Nao umeasi hukumu zangu, kwa kutenda mabaya kuliko mataifa hayo, nao umeasi sheria kuliko nchi hizo ziuzungukazo; maana wamezikataa hukumu zangu, wala hawakuenda katika sheria zangu. 7 Basi, kwa hiyo Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu ninyi mmefanya ghasia kuliko mataifa wawazungukao ninyi, wala hamkuenda katika sheria zangu, wala hamkuzishika hukumu zangu, wala hamkutenda kama kawaida za mataifa wawazungukao; 8 basi, Bwana MUNGU asema hivi; Angalia, mimi, naam, mimi, ni juu yako; nami nitafanya hukumu kati yako machoni pa mataifa. 9 Nami nitakutenda nisiyoyatenda zamani, wala sitafanya tena mambo kama hayo, kwa sababu ya machukizo yako yote. 10 Kwa sababu hiyo baba za watu watawala wana wao kati yako, nao wana watawala baba zao; nami nitafanya hukumu ndani yako, na hao wote waliosalia kwako nitawatawanya kwa pepo zote.

 

Ahadi lilikuwa jambo kuukuwajia watu wetu kwa kuwa sisi tu wenye shingo ngumu. Iliwapata kwanza Yuda na Yerusalemu mnamo mwaka 70BKyuda walikuwa ni waasi na kufanya ukahaba na walipelekwa utumwani sawasawa na Ishara ya nabii Yona na lakini hawakutubu (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujunzi Mpya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)]. Unabii huu sasa utaendelea katika siku za mwisho hadi tutakapowezeshwa kumrudia Mungu. Imani ya Kisirisiri iliyochukuliwa kutoka kwenye dini za kipagani za Wababeli ndizo imani ile inayoshikilia kuyaondoa mambo ya kaskazini. Imezingirwa na dunia yote (soma jarida la Imani za Sirisiri Toleo la 1 (Na. B7 A) [Mysticism Volume 1 (B7_A)].

 

Ni kwa sababu hiyo ndpo Mungu anaweka wazi na anatuma moto ukaangamize pande za kusini.

Ezekieli 8:1-7 Ikawa katika mwaka wa sita, mwezi wa sita, siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa nikikaa nyumbani mwangu, wazee wa Yuda nao wali wamekaa mbele yangu, mkono wa Bwana MUNGU ukaniangukia huko. 2 Ndipo nikaangalia, na tazama, kana kwamba ni mfano wa moto; tangu mfano wa viuno vyake na chini, moto; na tangu mfano wa viuno vyake na juu, kana kwamba ni mfano wa mwangaza, kama rangi ya kaharabu. 3 Naye akanyosha mfano wa mkono, akanishika kwa kishungi kimoja cha nywele za kichwa changu; nayo roho ikaniinua kati ya dunia na mbingu, ikanileta katika maono ya Mungu mpaka Yerusalemu, mpaka mlango wa kuingilia ua wa ndani uelekeao upande wa kaskazini; mahali palipokuwa pamewekwa sanamu ya wivu, itiayo wivu. 4 Na tazama, huo utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwapo hapo, sawasawa na maono yale niliyoyaona katika uwanda. 5 Ndipo akaniambia, Mwanadamu, inua macho yako sasa, uangalie upande wa kaskazini. Basi nikainua macho yangu, nikaangalia upande wa kaskazini, na tazama, upande wa kaskazini wa mlango, ilikuwako sanamu ile ya wivu, mahali pale pa kuingilia. 6 Akaniambia, Mwanadamu, je! Unayaona wanayoyafanya, yaani, haya machukizo makubwa wanayoyafanya nyumba ya Israeli hapa, hata niende zangu mbali na patakatifu pangu? Lakini utaona tena machukizo makubwa mengine. 7 Akanileta hata mlango wa ua; nami nilipoangalia, tazama, pana tundu katika ukuta.

 

 Sura hii ndipo inaelezea ukengeufu wa kidini katia Israeli uliosababishwa na viongozi wake. Imani hii imeshamiri na kushika dau hata leo na ibada za mungu jua zinaendelea kufanyika katika Mahali pa Juu kwa kiwango kikubwa sana, na sehemu zetu au majengo yetu Matakatifu yametiwa unajisi na mizoga ya wafalme wetu na viongozi kama Mungu alivyotuambia kuwa tusifanye lakini tunaendelea Kumasi bado.

 

Ezekieli 10:1-10 Ndipo nikaangalia, na tazama, katika anga lililokuwa juu ya vichwa vya makerubi, kulionekana juu yao kana kwamba ni yakuti samawi, kuonekana kama mfano wa kiti cha enzi. 2 Naye akamwambia mtu yule aliyevaa bafta, akasema, Ingia kati ya magurudumu yazungukayo, yaani, chini ya kerubi, ukaijaze mikono yako yote miwili makaa ya moto, toka katikati ya makerubi, ukayamwage juu ya mji. Akaingia ndani mbele ya macho yangu. 3 Basi, makerubi walisimama upande wa kuume wa nyumba, hapo alipoingia mtu yule; nalo wingu likaujaza ua wa ndani. 4 Utukufu wa Bwana ukapaa kutoka kwa kerubi yule, ukasimama juu ya kizingiti cha nyumba; nayo nyumba ikajazwa na lile wingu, na ua ulikuwa umejaa mwangaza wa utukufu wa Bwana. 5 Na sauti ya mabawa ya makerubi ikasikiwa, hata katika ua wa nje, kama sauti ya Mungu Mwenyezi, asemapo. 6 Ikawa, hapo alipomwagiza huyo mtu aliyevaa bafta, akisema, Twaa moto kutoka katikati ya magurudumu yazungukayo katikati ya hao makerubi, akaingia, akasimama karibu na gurudumu moja. 7 Na kerubi yule akanyosha mkono wake toka katikati ya makerubi, kwa moto ule uliokuwa katikati ya makerubi, akatwaa baadhi ya moto ule, akautia katika mikono ya mtu yule aliyevaa bafta; naye akautwaa, akatoka. 8 Kukaonekana katika makerubi mfano wa mkono wa mwanadamu chini ya mabawa yao. 9 Nami nikaangalia, na tazama, yalikuwako magurudumu manne karibu na makerubi, gurudumu moja karibu na kerubi mmoja, na gurudumu lingine karibu na kerubi mwingine; na kuonekana kwa magurudumu kulikuwa kana kwamba ni zabarajadi. 10 Na kuonekana kwake, yote manne yalikuwa na mfano mmoja, kana kwamba gurudumu moja lilikuwa ndani ya gurudumu lingine.

 

Moto umechukuliwa kutoka kwa Makerubi na umetolewa kwa uweza wa Roho Mtakatifu ili kufanikisha lengo hili la Mungu kwa Makerubi; kama viumbe wa kiroho wakizukao Kiti cha Enzi cha Mungu waliopewa uelewa huu kwa kupitia Kanisa, na hatimaye inatokea katika Israeli ili kufikiliza au kuhitimisha makusudi ya Mungu.

Ezekieli 15:1-8 Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, mzabibu una sifa gani kuliko mti mwingine, au tawi la mzabibu lililokuwa kati ya miti ya msituni? 3 Je! Mti wake waweza kutwaliwa, ili kufanya kazi yo yote? Watu waweza kufanya chango kwa huo, ili kutundika chombo cho chote? 4 Tazama, watupwa motoni kwa kuni moto umeziteketeza ncha zake zote mbili, nao umeteketea katikati, je! Wafaa kwa kazi yo yote? 5 Tazama, ulipokuwa mzima, haukufaa kwa kazi yo yote; sembuse ukiisha kuliwa na moto, na kuteketea; je! Waweza kufaa kwa kazi yo yote? 6 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kama mzabibu kati ya miti ya msituni, niliyoupa moto uwe kuni, ndivyo nitakavyowatoa wakaao Yerusalemu. 7 Nami nitaukaza uso wangu juu yao; nao watatoka motoni, lakini moto utawateketeza; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoukaza uso wangu juu yao. 8 Nami nitaifanya nchi kuwa ukiwa, kwa sababu wamekosa, asema Bwana MUNGU.

 

Huu mzabibu ni nyumba ya Israeli (Isaya 5:7) iliyoanzia huko Yerusalemu na iliteketezwa lakini itatakaswa hata zaidi yake katika siku za mwisho tutakapozichoma moto mbele ya madhabahu za Moleki na Kemoshi. Tumefanya utoaji wa mimba na kuua watoto wachanga au kuharibu mimba zilizo tumboni na wamefanya hivyo kwa faida zao za kibinafsi zitikanazo na ubinafsi wa wazazi sawa kabisa na ilivyofanyika katika siku za zamani. Huenda Makuhani wa Baali , Kana-Baali au wala nyama za watu wataanza kuila miili ya watoto wachanga waliotolewa kwenye mimba. Bado watu wanaendelea kuabudu ibada za kuitukuwa Krismas na Easter au Ishta na bado watu wanawaua watoto wao na kwa kweli watahukumiwa.

Ezekieli 16:18-25 ukatwaa nguo zako za kazi ya taraza, ukawafunika, ukaweka mafuta yangu na uvumba wangu mbele yao. 19 Mkate wangu niliokupa, unga mzuri, na mafuta, na asali, nilivyokulisha, ukaviweka mbele yao viwe harufu ya kupendeza; na ndivyo vilivyokuwa; asema Bwana MUNGU. 20 Pamoja na hayo uliwatwaa wana wako na binti zako, ulionizalia, ukawatoa sadaka kwao ili waliwe. Je! Mambo yako ya kikahaba ni kitu kidogo tu, 21 hata ukawaua watoto wangu, na kuwatoa kwa kuwapitisha motoni kwa hao? 22 Na katika machukizo yako yote, na mambo yako ya kikahaba, hukuzikumbuka siku za ujana wako, ulipokuwa uchi, huna nguo, ukawa ukigaagaa katika damu yako. 23 Tena, imekuwa baada ya uovu wako wote, (ole wako! ole wako! Asema Bwana MUNGU,) 24 ulijijengea mahali palipoinuka, ukajifanyia mahali palipoinuka katika kila njia kuu. 25 Umejenga mahali pako palipoinuka penye kichwa cha kila njia, ukaufanya uzuri wako kuwa chukizo, ukatanua miguu yako kwa kila mtu aliyepita karibu, ukaongeza mambo yako ya kikahaba.

 

Tunamajengo haya ya kumuabudia mungu jua na miungu inayoabudiwa kimafumbo na kiusiri kwenye kila mahali pa juu katika Israeli. Makuhani wake wakati wote wanavaa majoho meusi na kama wakemishi na hata hatujaweza kutubia kamwe (imefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Ujumbe wa Ufunuo 14 (Na. 270) [The Messages of Revelation 14 (No. 270)].

Ezekieli 19:10-14   Mama yako alikuwa kama mzabibu, katika damu yako, uliopandwa karibu na maji; akazaa sana na kujaa matawi, kwa sababu ya maji mengi. 11 Naye alikuwa na vijiti vya nguvu, kwa fimbo za enzi zao watawalao, na kimo chao kiliinuka kati ya matawi manene, wakaonekana kwa urefu wao, pamoja na wingi wa matawi yao. 12 Lakini aling'olewa kwa ghadhabu, akaangushwa chini, upepo wa mashariki ukakausha matunda yake; vijiti vyake vya nguvu vikavunjika, vikakauka; moto ulivila. 13 Na sasa umepandwa jangwani, katika nchi kavu, ya ukame. 14 Na moto umetoka katika vijiti vya matawi yake, umekula matunda yake, hata hana tena kijiti cha nguvu kifaacho kwa fimbo ya enzi ya kutawala. Na hayo ni maombolezo, nayo yatakuwa maombolezo.

 

Kwa hiyo, moto huu pia ulikwenda kutoka kwenye fimbo matawi yake na atakuwa na fimbo ya nguvu itakayofanyika kuwa ni fimbo ya kifalme ya utawala wakati ule wa wa kipindi cha taabu (soma kwa kina kwene jarida la Kulipima Hekalu (Na. 137) [Measuring the Temple (No. 137)]. Katika siku hizi ufalme utakuwa umeondolewa.

 

Utaratibu na mtindo huu wa ibada ya Waisraeli ambao umechukuliwa pia na Kanisa katika siku hizi za mwisho, unatakiwa uondolewe na kuwekwa kwenye nchi kavu na ukame na kutoka hapo moto utabidi iwashwe ili uiteketeze na kuila dunia yote katika siku za mwisho (Ezekieli 19:10-14). Andiko hili lililo kwenye aya za Ezekieli 19:13 na 14 zinaonyesha unabii wa aina mbili ambao sio tu kuwa unawahusu kina Konia na Sedekia tu, bali pia wa siku za mwisho na kuangamizwa kwao Israeli na Kanisa la Walaodikia.

 

Kupinduliwa kwa ufalme kwa kipindi cha karne nyingi kumeelezewa kwa kina kwnye tovuti ya: www.abrahams-legacy.org

 

Ezekieli 21:25-32 Na wewe, Ewe mtu mwovu, uliyetiwa jeraha kiasi cha kukuua, mkuu wa Israeli, ambaye siku yako imekuja, katika wakati wa uovu wa mwisho; 26 Bwana MUNGU asema hivi; Kiondoe kilemba, ivue taji; haya hayatakuwa tena kama yalivyo; kikweze kilicho chini, kakishushe kilichoinuka. 27 Nitakipindua, nitakipindua, nitakipindua; hiki nacho hakitakuwa tena, hata atakapokuja yeye ambaye ni haki yake; nami nitampa. 28 Nawe, mwanadamu, tabiri useme, Bwana MUNGU asema hivi, katika habari za wana wa Amoni, na katika habari za aibu yao; Nena, Upanga; upanga umefutwa; umesuguliwa, ili kuua, ili kuufanya uue sana, upate kuwa kama umeme; 29 wakati wakuoneapo ubatili, wakati wakufanyiao uganga wa uongo, ili kukuweka juu ya shingo zao waliotiwa jeraha kiasi cha kuwaua, ambao siku yao imekuja, katika wakati wa uovu wa mwisho. 30 Uurudishe alani mwake. Mahali pale ulipoumbwa, katika nchi uliyozaliwa; nitakuhukumu wewe. 31 Nami nitamwaga ghadhabu yangu juu yako; nitakupulizia moto wa hasira yangu; nami nitakutia katika mikono ya watu walio kama hayawani, wajuao sana kuangamiza. 32 Utakuwa kuni za kutiwa motoni; damu yako itakuwa katikati ya nchi; hutakumbukwa tena; maana mimi, Bwana, nimenena neno hili.

Moto utayaangamiza mataifa yote yanayoizunguka Israeli katika siku za mwishona Waamoni watateketea pia pamoja na Israeli na katika siku hizo Waamoni watapatana na kuwa wamoja na Israeli. Wayordani ni watoto wa Lutu na wataingizwa kwenye taifa la Iaraeli kwenye vita inayokuja hivi karibuni na Lutu atakuwa pamoja na Ibrahimu kwa mara nyingi na milele.

 

Israeli wamechukua riba na kuimwaga damu na dhambi hizi zitaondolewa katika Israeli katika kipindi cha miongo michache sana ijayo.

Ezekieli 22:12-25 Ndani yako wamepokea rushwa ili kumwaga damu; umepokea riba na faida; nawe kwa choyo umepata mapato kwa kuwadhulumu jirani zako, nawe umenisahau mimi, asema Bwana MUNGU. 13 Basi, tazama, nimeipigia kofi hiyo faida uliyopata kwa njia isiyo haki, na hiyo damu yako iliyokuwa kati yako. 14 Je! Moyo wako waweza kuvumilia, au mkono wako waweza kuwa hodari, katika siku zile nitakapokutenda mambo? Mimi, Bwana, nimenena neno hili, tena nitalitenda. 15 Nami nitakutawanya kati ya mataifa, na kukutapanya kati ya nchi mbalimbali; nami nitauteketeza uchafu wako, ili ukutoke. 16 Nawe utatiwa unajisi ndani ya nafsi yako, mbele ya macho ya mataifa; nawe utajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. 17 Neno la Bwana likanijia, kusema, 18 Mwanadamu, nyumba ya Israeli imekuwa taka za fedha kwangu; wote wamekuwa shaba, na bati, na chuma, na risasi, kati ya tanuu; wamekuwa taka za fedha. 19 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu ninyi nyote mmekuwa taka za fedha, tazama, nitawakusanya kati ya Yerusalemu. 20 Kama vile watu wakusanyavyo fedha, na shaba, na chuma, na risasi, na bati, kati ya tanuu, ili kuvifukutia moto na kuviyeyusha; ndivyo nitakavyowakusanya ninyi katika hasira yangu, na ghadhabu yangu, nami nitawalaza huko, na kuwayeyusha. 21 Naam, nitawakusanya, na kuwafukutia moto wa ghadhabu yangu, nanyi mtayeyushwa kati yake. 22 Kama fedha iyeyushwavyo kati ya tanuu, ndivyo mtakavyoyeyushwa kati yake; nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, nimemwaga ghadhabu yangu juu yenu. 23 Neno la Bwana likanijia, kusema, 24 Mwanadamu, uiambie nchi, Wewe u nchi isiyosafika, wala kunyeshewa mvua siku ya ghadhabu. 25 Fitina ya manabii wake imo ndani yake, kama simba angurumaye akirarua mawindo; wamekula roho za watu; hutwaa kwa nguvu hazina na vitu vya thamani; wameongeza hesabu ya wajane wake ndani yake.

 

Kwa hiyo Mungu atawahukumu Israeli, na manabii wake na makuhani wake wote watalaumiwa kwa kuwa hawakumuogopa Mungu. Kabla ya kuangamia kwao Israeli tunajua kwamba kondoo watararuliwa au kupokwe kutoka kwenye mikono ya wachungaji. Yukio hili limefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Kulipima Hekalu (Na. 137) [Measuring the Temple (No. 137)].

Ezekieli 34:1-31 Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam, hao wachungaji, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo? 3 Mnawala walionona, mnajivika manyoya, mnawachinja walionona; lakini hamwalishi kondoo. 4 Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala. 5 Nao wakatawanyika, kwa sababu hapakuwa na mchungaji; wakawa chakula cha wanyama- mwitu, wakatawanyika. 6 Kondoo zangu walitanga-tanga katika milima yote, na juu ya kila kilima kirefu; naam, kondoo zangu walitawanyika juu ya uso wote wa dunia; wala hapakuwa na mtu aliyewaulizia, wala kuwatafuta.

 

Mashitaka au lawama za wazi dhidi ya makuhani inaonyeshwa wazi hali ya watu wa Mungu ilivyo leo. Hawalijui neno la Mungu. Wamepotoshwa, kwa kuziendea ibada otofu na za uwongo. Hawamjui Mungu wala Mwanae aliyemtuma na kwa kweli hawazitii amri na sheria zake.

7 Basi, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana; 8 Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, kwa sababu kondoo zangu walikuwa mateka, kondoo zangu wakawa chakula cha wanyama-mwitu wote, kwa sababu hapakuwa na mchungaji, wala wachungaji wangu hawakutafuta kondoo zangu, bali wachungaji walijilisha wenyewe wala hawakuwalisha kondoo zangu; 9 kwa sababu hiyo, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana; 10 Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu ya wachungaji; nami nitawataka kondoo zangu mikononi mwao, nami nitawaachisha hiyo kazi ya kuwalisha kondoo; nao wachungaji hawatajilisha wenyewe tena; nami nitawaokoa kondoo zangu vinywani mwao, wasiwe tena chakula chao. 11 Maana, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi mwenyewe, naam, mimi, nitawatafuta kondoo zangu, na kuwaulizia. 12 Kama vile mchungaji atafutavyo kondoo zake, siku ile anapokuwa kati ya kondoo zake waliotawanyika; ndivyo nitakavyowatafuta kondoo zangu; nami nitawaokoa katika mahali pote walipotawanyika, katika siku ya mawingu na giza. 13 Nami nitawatoa katika watu wa mataifa, na kuwakusanya katika nchi zote, nami nitawarudisha katika nchi yao wenyewe; nami nitawalisha juu ya milima ya Israeli, kando ya mifereji ya maji; na katika mahali pote pa nchi panapokaliwa na watu. 14 Nami nitawalisha malisho mema, pa juu ya milima ya mahali palipoinuka pa Israeli litakuwa zizi lao; huko watalala katika zizi jema; nao watakula malisho mema, juu ya milima ya Israeli. 15 Mimi mwenyewe nitawalisha kondoo zangu, nami nitawalaza, asema Bwana MUNGU. 16 Nami nitawatafuta waliopotea, nitawarudisha waliofukuzwa, nitawafunga waliovunjika, nitawatia nguvu wagonjwa; nao wanono na wenye nguvu nitawaharibu; nitawalisha hukumu.

 

Baada ya kuwapokonya kondoo wachungaji na makuhani, ndipo Mungu atawahukumu kondoo hawa sawasawa na matendo yao na walivyofanyiana kila mmoja na mwenzake. Yangia mwaka 1994 tumejionea na kuyashuhudia matukio yanayoashiria kuwa kondoo wanaondolewa mikononi mwa watumishi walio kwenye Kanisa la Mungu.

17 Na kwa habari zenu, Enyi kundi langu, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nahukumu kati ya mnyama na mnyama, kondoo waume na mbuzi waume pia. 18 Je! Mwaona ya kuwa ni neno dogo ninyi kulishwa malisho mema, hata mkawa hamna budi hukanyaga kwa miguu yenu yaliyosalia? Na kuwa mmekunywa maji yaliyo safi, nanyi hamna budi kuyatibua kwa miguu yaliyobaki? 19 Na kwa habari za kondoo zangu, wao wanakula hayo mliyoyakanyaga kwa miguu yenu, nao wanakunywa maji mliyoyatibua kwa miguu yenu. 20 Kwa sababu hiyo, Bwana MUNGU awaambia hivi; Tazama, mimi, naam, mimi, nitahukumu kati ya wanyama walionona na wanyama waliokonda. 21 Kwa kuwa mmesukuma kwa ubavu, na kwa mabega, na kuwapiga wenye maradhi kwa pembe zenu, hata mkawatawanyia mbali; 22 basi mimi nitaliokoa kundi langu, wala hawatakuwa mateka tena; nami nitahukumu kati ya mnyama na mnyama. 23 Nami nitaweka mchungaji mmoja juu yao, naye atawalisha, naam, mtumishi wangu, Daudi; yeye atawalisha, naye atakuwa mchungaji wao. 24 Na mimi, Bwana, nitakuwa Mungu wao, na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mkuu kati yao; mimi, Bwana, nimesema haya. 25 Nami nitafanya agano la amani nao, nami nitawakomesha wanyama wakali kati yao; nao watakaa salama jangwani, na kulala misituni. 26 Nami nitawafanya wao, na mahali palipo pande zote za mlima wangu, kuwa baraka, nami nitaleta manyunyu kwa wakati wake; yatakuwako manyunyu ya baraka. 27 Na mti wa kondeni utazaa matunda yake, nayo ardhi itatoa mazao yake, nao watakuwa salama katika nchi yao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya kongwa lao, na kuwaokoa katika mikono ya watu wale waliowatumikisha.

 

Andiko hili linaelezea kuhusu Ufufuko wa Kwanza wa wafu na marejesho mapya kwenye kipindi cha millennia. Kutakuwa na mwisho wa mateso ya watu waaminifu wake Mungu.

28 Hawatakuwa mateka ya makafiri tena, wala mnyama wa nchi hatawala; bali watakaa salama salimini, wala hapana mtu atakayewatia hofu. 29 Nami nitawainulia miche iwe sifa njema, wala hawataangamizwa kwa njaa katika nchi yao tena, wala hawatachukua tena aibu ya makafiri. 30 Nao watajua ya kuwa mimi, Bwana, Mungu wao, ni pamoja nao, na ya kuwa wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana MUNGU. 31 Na ninyi, kondoo zangu, kondoo za malisho yangu, ni wanadamu, na mimi ni Mungu wenu, asema Bwana MUNGU.

 

Kwa hiyo, hawa wanaotajwa kuwa walioachwa ni wale walio ni kundi la malisho ya Mungu na waliolishana kila mmoja na mwenzake na kutiana moyo wakiinuana kiimani na hata watakuwa kama wana samba katika siku za mwisho.

 

Na moto utawashwa kwenye mashamba ya upende wa kusini kama tulivyomuona Samsoni.

Waamuzi 15:1-7 Lakini ikawa baadaye, wakati wa mavuno ya ngano Samsoni akaenda kumtazama mkewe, akamchukulia mwana-mbuzi; akasema, Nitaingia chumbani kwa mke wangu. Lakini baba yake mwanamke hakumwacha kuingia. 2 Baba yake akasema, Hakika mimi nalidhani ya kuwa umemchukia kabisa; basi nalimpa rafiki yako. Je! Ndugu yake mdogo mzuri kuliko yeye? Tafadhali, mtwae huyo badala yake. 3 Samsoni akasema, Safari hii nitakuwa sina hatia katika habari za hawa Wafilisti, hapo nitakapowadhuru. 4 Samsoni akaenda akakamata mbweha mia tatu; kisha akatwaa vienge vya moto akawafunga mbweha mkia kwa mkia, akatia kienge kati ya kila mikia miwili. 5 Alipokwisha kuviwasha moto vile vienge, akawaachia mbweha kati ya ngano ya Wafilisti, akayateketeza matita, na ngano, hata na mashamba ya mizeituni. 6 Ndipo Wafilisti wakasema, Ni nani aliyetenda hivi? Wakasema, Ni huyo Samsoni, mkwewe yule Mtimna, kwa sababu alimchukua mkewe akampa mwenzake. Wafilisti wakaenda wakamteketeza yeye na baba yake kwa moto. 7 Samsoni akawaambia, Ikiwa ninyi mnafanya mambo kama hayo, hakika nitajilipiza kisasi juu yenu, na baadaye nitakoma

 

Usemi huu wa kimfano na fumbo unahusiana na wazo la Kanisa kuchukuliwa na kupewa wamataifa. Takriban wanatu 300 (jozi 150), ambako waliwekwa wawili wawili na kuwashwa moto kwenye mashamba ya Wafilisti, inaonyesha ukweli wa kwamba kanisa lilitolewa kwene imani hii ya uwongo na Kristo, kwa kupitia jozi hizi 150, na imani ile inachomwa moto katika siku za mwisho na utawateketeza mfumo wa wamataifa ambao umelipotosha na kulikengeusha kanisa.

 

Moto huo umekwisha washwa tayari. Na ndiyo sababu kumekuwa na mchakato unaoendelea sasa kutoka kusini hadi kaskazini na wote wataangamizwa kipindi hiki kikifika.

 

Kanisa la Mungu lilikuwa lipitia kipindi cha kumwa kwake tangu mwaka 1987. Mwaka huu ulianza zama mpya ya kizazi cha mwisho cha miaka arobaini cha kuifikia Yubile ya mwaka 2027 wakati Masihi atakapokuwa ameuanzisha utawala wake. Mwaka ule ulikuwa ni mwaka wa utoaji wa zaka ya tatu ukiwa ni mwaka wa tatu wa taratibu za mzunguko. Mambo yote yanafanyika kwa kufuata taratibu za miaka saba kutoka mwaka wa utoaji wa zaka ya tatu pamoja na wa Usomaji wa Torati unaofanyika kila Mwaka wa Saba ambao unaitwa kuwa ni Mwaka wa Sabato na hatimaye kufuatiwa na hukumu na marejesho yake katika mwaka wa tatu. Mwaka huu wa Tatu unaanzisha mzunguko mpya wa miaka saba. Mzunguko huu ulianza mnamo mwaka 1987 na kizazi hiki hakitapia kamwe hata yote yatimie. Mwaka wa Sabato wa 1991 ulishuhudia kuanguka kwa huduma kisha watumishi wake wengi waliondolewa na kutawanyika. Mwaka 1994 ulishuhudia muwako wa moto na ujumbe ulihubiriwa kwa kuanzisha upya mfumo ulioendana na maamrisho au maagizo ya Mungu na utateketeza kila kilichopo mbele yake. Kondoo watahukumiwa dhidi ya kondoo na sasa Israeli watahukumiwa tangia mwaka 2001 na Usomaji wa Torati ukafanyika mwaka 2005.

 

Mnamo mwaka 2012 Usomaji wa Pili wa Torati utashuhudia kuhukumiwa kwa mataifa mengi kwa mujibu wa sheria. Baada ya hapo Mashahidi wataweka au kuhubiri Msisitizo wa Umuhimu kwa watu kuyashika maudhuhi ya Torati na kuwaandaa kwa ajili ya Masihi. Mbingu zitafungwa kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu na Moto utashuka moja kwa moja kutoka Mbinguni uje duniani kuangamiza kila aina ya ibada za uwongo na waiiozifanya (sawa na lisemavyo jarida la Mashahidi (pamoja na Wale Mashahidi Wawil) (Na. 135) [The Witnesses (including the Two Witnesses) (No. 135)].

 

Nyuso zote kutoka kusini hadi kaskazini zitateketezwa nao kama tunavyojionea kutoka kwenye Ezekieli 20:47. Umaangamizo yanayotajwa hapo ni yale ya Masihi katika siku za mwisho na yanaendelea hadi hata kwa fimbo ya utawala wa Mungu kama lilivyoahidiwa Kanisa.

Ezekieli 21:1-13 Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, uelekeze uso wako kuelekea Yerusalemu, ukadondoze neno lako upande wa mahali patakatifu, ukatabiri juu ya nchi ya Israeli; 3 uiambie nchi ya Israeli, Bwana asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, nami nitautoa upanga wangu alani, nami nitamkatilia mbali nawe mtu mwenye haki na mtu mbaya. 4 Basi, kwa kuwa nitamkatilia mbali nawe mtu mwenye haki na mtu mbaya, upanga wangu utatoka alani mwake, uwe juu ya watu wote wenye mwili toka kusini hata kaskazini, 5 na watu wote wenye mwili watajua ya kuwa mimi, Bwana, nimeufuta upanga wangu alani mwake; hautarudi tena. 6 Ugua, basi, Ee mwanadamu; kwa kuvunjika kwake viuno vyako, na kwa uchungu, utaugua mbele ya macho yao. 7 Na itakuwa, wakuambiapo, Mbona unaugua? Ndipo utakaposema, Kwa sababu ya habari hizo, maana linakuja; na kila moyo utayeyuka, na mikono yote itakuwa dhaifu, na kila roho itazimia, na magoti yote yatalegea kama maji; tazama, linakuja, nalo litatendeka, asema Bwana MUNGU. 8 Neno la Bwana likanijia, kusema, 9 Mwanadamu, tabiri, useme, Bwana asema hivi; Nena, Upanga, upanga, umenolewa na kusuguliwa, 10 umenolewa ili kufanya machinjo; umesuguliwa ili uwe kama umeme; basi je! Tufanye furaha? Upanga unadharau fimbo ya mwanangu, kama unavyodharau kila mti. 11 Nao umenolewa usuguliwe, upate kushikwa mkononi; upanga umenolewa, naam, umesuguliwa, ili kutiwa katika mkono wake auaye. 12 Piga kelele, utoe sauti ya uchungu, Ee mwanadamu, kwa maana upanga u juu ya watu wangu, u juu ya wakuu wote wa Israeli; wametolewa wauawe na upanga pamoja na watu wangu, basi, jipige pajani. 13 Kwa maana kuna kujaribiwa; itakuwaje, basi, ikiwa upanga unaidharau hiyo fimbo? Haitakuwapo tena; asema Bwana MUNGU.

 

Kwenye aya ya 13 hapo juu, neno lililotafsiriwa kama “dhiki” kwenye kitabu cha fafanuzi cha SHD 974 linamaana ya kujaribiwa au jaribio.

 

Kumbuka kwamba Mungu hapa anaongelea juu ya fimbo ya Mwana wake. Kwa hiyo fimbo hii ya wauaji ni lazima iwe ni dini au kanisa la uwongo ambalo linalipinga na kulipiga vita Kanisa la kweli la Mungu lililo chini ya Kristo. Kanisa hili la uwongo lina fimbo ya kuipigia vita fimbo ya Kristo kwa kuwa limekuwa limeshauweka utawala na nguvu zake hapa duniani. Hii iliwahi kufanyika hivyo hasa kwa kipindi amacho ilijitangazia kuwa ni Dola Takatifu ya Rumi tangu mwaka 590 hadi 1850. Kipindi hiki kilidumu kwa miaka 1260, au ni kipindi cha wakati, nyakati mbili na nusu wakatimbili na nusu wakati za unabii wa Ufunuo ambacho ni cha yule mwanamke ambaye ni kanisa atakachokuwa anafuatiliwa nay le joka na dini ya uwongo na potofu ya ibada (soma jarida la Jukumu la Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu Yanayozitunza Sabato (Na. 170) [The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)].

 

Ezekieli 21:14 inaelezea kuhusu maana yah ii fimbo na ni nani aliyeuawa.

Ezekieli 21:14 Basi, wewe mwanadamu, tabiri, ukapige makofi; upanga huo na uongezwe mara mbili, hata mara tatu; upanga wao waliotiwa jeraha kiasi cha kuwaua; ni upanga wa mkuu aliyetiwa jeraha kiasi cha kumwua; uwazungukao pande zote.

 

Kwa hiyo, watu wakubwa waliyeodhania kuwa watafaidika na imani hii potofu ya mwanamke kahaba basi watauawa kwa upanga kutokana na kile walichotaka kufaidika nacho. Kitaingia kutoka sehemu mbalimbali na katika siku za mwisho na kujiangamiza chenyewe na Mungu aliyehai atawalinda watu wake utakavyokuwa inaangamia.

 

Tumeona kwamba uharibifu huu wa wakuu au watu wenye nguvu uliendelea hadi kwa wafalme wa Israeli na kuondolewa kwake katika siku za kale (Ezekieli 21:27) na hatimaye hii itaondolewa kabisa na hatimaye itatolewa kwa Masihi atakaporudi.

Ezekieli 24:1-27 Tena, katika mwaka wa kenda, mwezi wa kumi, siku ya kumi ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, liandike jina la siku hii, naam, la siku ii hii; mfalme wa Babeli ameukaribia Yerusalemu siku iyo hiyo. 3 Ukawatungie mithali nyumba ya kuasi, ukawaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Teleka sufuria, liteleke; ukatie maji ndani yake; 4 vikusanye vipande vyake ndani yake, naam, kila kipande chema, paja na bega; lijaze mifupa iliyochaguliwa. 5 Uwatwae wateule wa kundi la kondoo, ukafanye chungu ya mifupa chini yake; ukalitokose sana; naam, mifupa yake itokoswe ndani yake. 6 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Ole wake mji wa damu! Hilo sufuria ambalo kutu yake i ndani yake, ambalo kutu yake haikulitoka; litoe kipande kipande; hapana kura iliyoanguka juu yake. 7 Maana damu yake imo ndani yake; aliiweka juu ya jabali lililo wazi; hakuimwaga juu ya nchi, apate kuifunika kwa mavumbi; 8 ili ipandishe ghadhabu ya kulipa kisasi, nimeiweka damu yake juu ya jabali lililo wazi, isipate kufunikwa. 9 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Ole wake mji wa damu! Mimi nami nitaiongeza chungu. 10 Tia kuni nyingi, uchochee moto, itokose nyama sana, fanyiza mchuzi mzito, mifupa ikateketee. 11 Kisha litie juu ya makaa yake, tupu, lipate moto, na shaba yake iteketee, uchafu wake uyeyushwe, na kutu yake iteketee. 12 Amejidhoofisha kwa taabu, lakini kutu yake nyingi haikumtoka; kutu yake haitoki kwa moto. 13 Katika uchafu wako mna uasherati, kwa maana nimekusafisha, ila wewe hukusafika; hutasafishwa tena uchafu wako ukutoke, hata nitakapokuwa nimeituliza hasira yangu kwako. 14 Mimi, Bwana, nimenena neno hili, nalo litakuwa; nami nitalifanya; sitaachilia, wala sitahurumia, wala sitajuta; sawasawa na njia zako, na sawasawa na matendo yako, ndivyo watakavyokuhukumu, asema Bwana MUNGU. 15 Neno la Bwana likanijia tena, kusema, 16 Mwanadamu, tazama, ninakuondolea kwa pigo moja tunu, mteule wa macho yako; walakini hutaomboleza wala kulia, wala yasichuruzike machozi yako. 17 Ugua lakini si kwa sauti ya kusikiwa; usifanye matanga kwa ajili yake yeye aliyekufa; jipige kilemba chako, ukavae viatu vyako, wala usiifunike midomo yako, wala usile chakula cha watu. 18 Basi nalisema na watu asubuhi, na jioni mke wangu akafa; nami nalifanya asubuhi kama nilivyoagizwa. 19 Watu hao wakaniambia, Je! Hutaki kutuambia maana ya mambo haya kwetu, hata umefanya kama vile ufanyavyo. 20 Nikawaambia, Neno la Bwana lilinijia, kusema, 21 Uwaambie nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi; Angalieni, nitapatia unajisi patakatifu pangu, fahari ya uwezo wenu, mahali pa kutamaniwa na macho yenu, ambapo roho zenu zinapahurumia na wana wenu na binti zenu, mliowaacha nyuma, wataanguka kwa upanga. 22 Nanyi mtafanya kama mimi nilivyofanya; hamtaifunika midomo yenu, wala kula chakula cha watu. 23 Na vilemba vyenu vitakuwa juu ya vichwa vyenu, na viatu vyenu miguuni mwenu; hamtaomboleza wala kulia; lakini mtafifia katika maovu yenu, na kuugua kila mtu pamoja na mwenziwe. 24 Basi ndivyo Ezekielii atakavyokuwa ishara kwenu; ninyi mtatenda sawasawa na yote aliyoyatenda yeye; litakapokuja jambo hili, ndipo mtakapojua ya kuwa mimi ndimi Bwana MUNGU. 25 Nawe, mwanadamu, je! Haitakuwa hivi katika siku hiyo nitakapowaondolea nguvu zao, na furaha ya utukufu wao, na kilichotamaniwa na macho yao, ambacho walikiinulia mioyo yao, wana wao na binti zao, 26 kwamba katika siku iyo hiyo yeye atakayeokoka atakuja kwako, akusikize jambo hili kwa masikio yako? 27 Siku hiyo kinywa chako kitafumbuliwa kwake aliyeokoka, nawe utasema; hutakuwa bubu tena; ndivyo utakavyokuwa ishara kwao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.

 

Kwa hiyo neno la nabii Ezekieli, linalohusiana na siku za mwisho, ni unabii wa kuyaelewa mamlaka na uweza wa Mungu. Katika siku hizo Ezekieli ataeleweka vyema. Nabii zake nyingi kwenye sura zilizo kutoka kipengele hiki na kuendelea mbele ni zinazohusiana na mataifa yanayohusiana kwa kipindi kinachodumu kwa miaka 2520 au cha nyakati saba hadi wakati wa mwisho (sawa na jarida la Kuanguka kwa Misri, Unabii wa Mikono Iliyovunjika ya Farao (Na. 36) [The Fall of Egypt The Prophecy of Pharaoh’s Broken Arms (No. 36)].

 

Sehemu hii inamuonyesha au kumtaja mwanadamu na kifo cha mke wake kilivyotokea majira ya jioni. Mateso ya Kanisa yaliendelea bila kukoma na siku za mwisho yatakuwa makubwa kuliko siku zilizopita. Habari za mateso zimeandikwa kwenye tovuti ya : www.holocaustrevealed.org

 

Amepewa Shetani ili awashinde watakatifu wake Aliye Juu Sana katika siku za mwisho. Kitabu cha nabii Danieli kinatuambia hayo.

 

Mkate wa mwanadamu hautaliwa. Mkate wetu na maji vitakuwa vitu vya hakika na tutaendeleakudumu kwa kupitia uweza wa Mungu. Mungu ametupa Roho Mtakatifu akiwa kama Moto Unaoshukua Kutoka Mbinguni na kutokana na sisi ameanzisha moto kwenye mashamba ya watu wa kusini ambao hatimaye utateketeza upande wa kaskazini pia na kuiteketeza dunia yote na kuirudisha kwenye imani na ibada ya kweli katika Mungu Mmoja na wapekee na wa Kweli.

 

q