Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[239]

 

 

 

Kwanini Pasaka Ilichelewa Sana Kufanyika Mwaka 1997?

(Toleo La 1.0 19980217-19980217)

 

Makala ilichapishwa kwenye Jarida lililojulikana kama Robo ya Biblia ya kiyahudi [Jewish Bible Quarterly], Toleo la 25, Namba 1, 1997 na lilirudiwa kuchapishwa kwa kuruhusiwa. Chama cha Biblia cha Kiyahudi, yaani The Jewish Bible Association ina tovuti yao ya http://www.jewishbible.org.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hatimiliki ©  1997  Jewish Bible Association)

Published with permission of Executive Secretary, Jewish Bible Association

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org nad  http://www.ccg.org


Toleo la 25, Namba 1, 1997                                                                                                             

JARIDA LIJULIKANALO KAMA “JEWISH BIBLE QUARTERLY”

 

KWANINI PASAKA ILICHELEWA SANA KUFANYIKA MWAKA HUU?

 

SAUL LEEMAN

(Saul Leeman ni Rabi mstaafu aliye kwenye Jimbo la, R.I.)

 


Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie

pasaka Bwana, Mungu wako

 

Unapoisoma aya hii ya Kumbukumbu la Torati 16:1 pamoja na maandiko mengine ya marabi, mtu anaweza kujihisi yuko sahihi kwa kudhania kwamba Torati ilikusudia kwamba sikukuu ilipasa ifanyike, kama inavyofanyika mara nyingi, wakati wa mwezi wa kwanza wa majira ya baridi. Mwaka huu (5757), hata hivyo, haikuweza kuwa hivyo. Ili kuelewa kwa kina uchelewaji wa kuja kwake sikukuu hii ya majira ya baridi, maswali fulani yanapaswa kuulizwa:

Ni kwa nini Pasaka ilichelewa sana mwaka huu?

Pasaka imechelewa sana mwaka huu (Aprili 22) kwakuwa huu ulikuwa ni mwaka mrefu kwenye Kalenda ya Kiyahudi wenye miezi kumi na mitatu ukiwa na mwezi wa nyongeza. Katika kila mzunguko wa mwaka wa 19 kuna miaka 7 mirefu yenye mwezi wa nyongeza: nayo ni mwaka wa 3, wa 6, wa 8, wa 11, wa 14, wa 17, na wa 19.

Ndiyo, najua hilo. Lakini kwenye suala la miaka 10 iliyopita au zaidi, hii imekuwa ni namba ya miaka mirefu, na bado sijaona Pasaka ikichelewa kama mwaka huu,.

Imekuwa hivyo kwa kuwa huu ni mwaka wa 19 wa mzunguko, ni mwaka mrefu unaotokea tu kila baada ya kipindi cha miaka miwili ukifuatiwa na mwaka mrefu uliopita. Vivyohivyo ni kweli (na hata zaidi sana) ilivyo kwenye mwaka wa 8 wa mzunguko. Kwa hiyo, kuna miaka hii miwili katika kila mzunguko ambapo Pasaka inachelewa majira haya ya baridi. Mnamo mwaka 1967 (“mwaka wa 8") Pasala iliangukia tarehe 25 Aprili, uchelewaji mrefu sana kuwahi kutokea.

Unasema “ilichelewa sana.” Je, inaweza kumaanisha kuwa Pasaka inaweza kuchelewa hata ikafanyika baada ya Aprili 25?

Ndiyo, ni kweli – na hili ndilo tatizo kubwa lililo kwenye kalenda ya Kiyahudi; yaani., hii inategemea na uhesabuji wa mwaka wa mfumo wa jua ambao hauko sahihi na unaupotofu wa takriban dakika 6½. Ni hali hii ya mapungufu ndiyo inayopelekea Pasaka kuelekea majira ya joto kwa kiwango cha takriban siku kamili kwenye kila miaka 200, kukijitokeza tofauti ya takriban siku 4½ kwa kila miaka 1,000. Hii ina maana ya kwamba kwenye kipindi cha takriban miaka 1,000, Pasaka itakuwa inaadhimishwa karibia tarehe 1 Mei, na kwenye miaka 8,000 ijayo, itaadhimishwa mnamo hata tarehe 1 Juni.

Je, hali hii inaweza kurekebishwa?

Hali hiyo inaweza kurekebishwa kwa kupitia tu kwenye matengenezo au marekebisho ya kalenda yalituama kwenye hesabu za mfumo wa kalenda.

Unasema kuwa matengenezo au marekebisho ya kalenda hatimaye yatakuwa ya lazima. Kumekisha wahi kufanyika kitu kama hicho kwa siku za hivi karibuni katika historia?

Ndiyo, imewahi kufanyika. Mwaka 1582 kalenda ya Juliani, ambayo ilikuwa ikitumiwa tangu mwaka 46 KK, ilibadilishwa na kuanza kutumika kwa kalenda ya Gregorian. Kalenda ya Julian, iliyoanzishwa na Kaisari Julius, ilituama kwenye mahesabu yaliyotuama kwenye urefu wa mwaka wa mrengo wa jua yenye siku 365 na masaa 6, ambapo kiuhalisia una upungufu wa dakika 11¼.

Tofauti hii ilipelekea kuwa na makosa ya takriban siku 3 katika kila miaka 400 (au siku 7½ kwa kila miaka 1,000). Matokeo yake, mnamo karne ya 16, siku ya ikwinoksi ya majira ya machipuko ilirudishwa nyuma hadi Marchi 11. Ili kuifarekebisha ili iwe na tarehe sahihi, Papa Gregory XIII alitangaza kwamba siku inayofuatia Oktoba 4 haitakuwa au kuitwa Oktoba 5 bali itaitwa Oktoba 15. Kwa tangazo hili, aliirudisha siku ya ikwinoksi ya majira ya baridi iendelee kuwa Marchi 21, tarehe ambayo ilikuwa kwenye mwaka wa 325 BK ambapo Baraza la Mtaguso wa Nicea (likilenga kuiingiza Easter isimame badala ya Pasaka) lilitangaza kwamba utaratibu wa kupangilia tarehe ya kusherehekea Easter ingekuwa “Jumapili ya kwanza baada ya mwezi mkamilifu wa kwanza na zaidi au baada ya ikwinoksi ya majira ya baridi."

Kumbuka kwamba lilikuwa ni jukumu lake kuweka siku maalumu ya kuadhimisha Easter ambayo ilihamasisha marekebisho ya kalenda ya Papa.

Kukiwa kumeondolewa makosa ya kimpangilio ya siku 10, kalenda ya Gregorian ilibidi iwezeshe na kuhakikisha kwamba hakuna kitu kama mwaka wa marejeo ukitokea. Hii ilifanyika kwa kutangaza kwamba miaka ya karne isiwe na mwaka mrefu isipokuwa kama itakuwa inagawanyika kwa tarakimu 400. Matokeo ya uwezesho huu, ndipo miaka ya 1700, 1800, na 1900 – miaka mirefu kwenye kalenda ya Julian – haikuwa miaka mirefu kwenye kalenda ya Gregorian. Rejea kati ya mbili sasa ni siku 13. Ifikapo mwaka 2100, tofauti yake itakuwa siku 14.

Lakini matendo ya kidini ya Kiyahudi hayana uhusiano na kalenda ya jua. Je, maadhimisho yote ya Kiyahudi yanaendana na kalenda inayotokana na mzunguko wa mwezi?

Sio kabisa. Kuna maadhimisho ya aina mbili yanayoendana na kalenda ya mzunguko wa jua. Moja wapo ni ile ya tal umatar, maombi kwa ajili ya umande na mvua. Baraza la Talmud linakusanyika kwa kufanya maombi ya kurudiarudia kwenye maombi haya ili kuanza siku 60 baada ya ikwinoksi ya majira ya mvumo wa upepo na kuendelea hadi Pasaka. Kitabu cha maombi hata hivyo, kinaiweka kwenye orodha hii siku ya tal umatar kwenye Desemba 5 – siku 73 baada ya ikwinoksi (Septemba 23). Tofauti hii ya siku 13 ni tofauti kati ya kalenda za Julian na ya Gregorian, na tofauti hizi zinaendelea kukua kwa kiwango cha siku 7½ kwa kila baada ya miaka 1,000.

Kwa siku hii ya tal umatar kuendelea kwenye mwelekeo wa Pasaka kwa kiwango cha siku 7½ kwenye kila miaka 1,000, wapangaji siku hatimaye watafikia hatimaye kwenye takriban miaka 35,000. Mapema kabla ya hapo, hata hivyo, tarehe ya Pasaka itabidi ifanyiwe marekebisho, na ndipo hili tatizo la tal umatar itapata suluhu.

Katika Israeli kuna kiasi kidogo sana cha "mitambo ya kupiga ashirio" kuhusiana na tatizo hili kwa kuwa kwenye chi Takatifu majira ya hii tal umatar yanaanza kwenye juma la kwanza ya mwezi wa Buli au Heshvan na haiungani au kuhusiana moja kwa moja na kalenda ya mzunguko wa jua kabisa (Soma kitabu cha Bab. Talmud, Taanit 10a).

Ulisema kuwa kulikuwa na “maadhimisho mawili” yanayoendana na kalenda ya mzunguko wa jua. Ni ipi nyingine moja?

Nyingine moja ni Birkat ha-Hammah – Baraka ya Jua, maombi ya dua yanayofanywa kwa kurudiwarudiwa wakati wa ikwinoksi ya majira ya machipuko mara moja kwa kila kipindi cha miaka 28 wakati kwamba, kwa mujibu wa mapokeo na desturi, wanaamini kwamba dunia inarudi mahala pake palepale ikihusiana na jua lililochukua mkondo wakati wa Uumbaji. Ilikuwa ikiombwa kila mara siku ya Jumatano (waliyoamini kuwa ni siku ambayo jua liliumbwa). Maombi yake yaliyofanywa kwa siku za hivi baribuni sana ilikuwa mnamo Aprili 8, 2009. Na haya ni maombi ya kuomba viumbe vilivyo kwenye anga la juu na yasiyo na maana yoyote kabisa, na ambayo kwa hakika yamewekezwa kwetu ndani yetu wakati sherehe hizi za Baraka za Jua zilifanyika mnamo Aprili 8, 1953 wakati tulipokuwa ndipo “tunasherehekea siku ya Ikwinoksi ya majira ya Baridi" – mnamo siku ya 23 ya mwezi wa Abibu au Nisan, siku nane baada ya majilio ya Pasaka!

Wakati marekebisho muhimu ya kalenda yatakapofanyika, ndipo Birkat ha-Hammah itaangukia pia kwenye kipindi cha mwezi wa kwanza cha mwezi kuwa mkubwa na mkamilifu cha majira ya baridi (na sio cha mwezi kamili wa pili kama ilivyo kwenye mwaka huu) na Birkat ha-Hammah itawekwa ili itokee kwenye Jumatano ya kwanza ya majira ya baridi.

Ni lini ambapo kalenda iliyopo sasa ya Kiyahudi ilianzishwa na ni nani aliyeianzisha?

Kalenda ya Kiyahudi kama tuliyonayo leo, ilitungwa na Kiongozi wa Kidini au Rabi aliyeitwa Hilleli II, yapata mwaka 359 BK.

Kwa nini imetuama kwenye mzunguko wa miaka 19?

Kwa kuwa muundo wa msingi wa kalenda ya Kiyahudi unafuatia miaka 19 ya mzunguko wa jua = au sawa na miezi mwandamo 235 (miaka 19 ya kawaida inayofuata mwandamo wa mwezi kujumlisha na miezi 7 ya nyongeza ya mwezi mwandamo). Wayunani walikiita kipindi hiki kuwa ni Mzunguko wa Kimetoniki.

Inamaanisha kwamba kila miaka 19 tarehe za kidunia (ya Gregorian) na “tarehe za Kiyahudi” zinashabihiana?

Ndiyo, kila miaka 19 ama zinashabihiana kabisa au zinapishana kwa takriban siku moja.

Kuna siku ngapi jumla kwenye kalenda ya Kiyahudi?

Inatofautiana. Kwenye mwaka wa kawaida (usio mwaka mrefu) una siku 353 (mara nyingine), siku 354 (mwaka wa kawaida), au siku 355 (ukizidi sana). Sawasawa na ilivyo kwenye mwaka mrefu, kuna siku 383, 384, au siku 385.

Ni nini kinachosababisha hali hii?

Sababu zake ni za kidini. Ya msingi ni [lo 'adu rosh] ni kwamba Rosh Hashanah haipasi kabisa iangukie siku ya Jumapili, Jumatano, au Ijumaa. Iwapo kama Rosh Hashanah itaangukia siku ya Jumatano au Ijumaa, basi Yom Kippur ingetangulia au kufuatia Sabato, ikipelekea au kusababisha mazingira au hali ambayo ingehusisha ugumu kuiadhimisha. Kama Rosh Hashanah ingeangukia siku ya Jumapili, basi Hoshanah Rabbah ingeangukia siku ya Sabato na kungetolewa wito wa kuharibu au kutatiza taratibu fulani za kidini ambazo marabi wa kifarisayo hawakupenda ziondolewe.

Kwa hiyo, kuyaweka mambo sawa kwa kupunguza msimamo kulikuwa lazima ilipojitokeza hivyo, na wakati kwamba, kama Rosh Hashanah zingeangukia siku yoyote kati ya hizi tatu, ingeahirishwa hadi siku inayofuatia.

Hivyo, kwenye mwaka wa kawaida (wa siku 354), urefu wa miezi ni kati ya siku 30 na 29. Kwenye mwaka wa kati (wa siku 353), miezi ya Heshvan na Kisleu kila mmoja una siku 29. Katika mwaka wenye siku nyingi (wa siku 355), miezi ya Heshvani na Kisleu kila mmoja unakuwa na siku 30.

Kulikuwa na utaratibu gani kabla ya Rabi Hillel II hajaanzisha na kuitengeneza kalenda ya sasa ya Kiyahudi?

Kabla ya siku hiyo, tulikuwa na kalenda isiyopangiliwa vizuri “ya kudumu.” Mwezi mpya ulijulikana kwa kuutafuta na kuangalia hapa na pale. Mashahidi waliouona walilazimika kwenda Yerusalemu kushuhudia kuwa wameuona. Iwapo kama baada ya kupeleleza, na Beth Din akakubaliana na taarifa hii ya kuonekana kwake kutokana na ushuhuda huo, ndipo Mwezi Mpya ulikubalika kuwa umeanza na Rosh Hodesh ilitangazwa. Beth Din aliketi kwa utayari ili kupokea taarifa za ushuhuda katika “siku inayokamilisha siku ya 30" ya mwezi unaoishia ili achukue hatua ya kuamjua kama siku hiyo inaweza kutangazwa kuwa “siku ya kwanza” ya mwezi unaoanza. Kama uamuzi kama huo haujafanywa siku hiyo, siku inayofuatia ilitangazwa moja kwa moja (hata kama hakuna anayeshuhudia kuwa ameuona) na kufanyika kuwa ni adhimisho la Mwezi Mpya au Rosh Hodesh, kwa kuwa mwezi una urefu usiopungua siku 29 na hauzidi siku 30. (Soma kitabu cha Mishnah Rosh Hashanah, Sura za 1-2).

Mara tu Mwezi Mpya unapotakaswa au kuadhimishwa, ndipo habari zilitangazwa kwenye Nchi yote Takatifu.

Ilikuwaje basi kuhusu Wayahudi waliokuwa wakiishi nje ya nchi Takatifu? Jumbe uliwafikiaje wao?

Hili ni swali zuri. Mara nyingi kutokana na ugumu wa kimawasiliano, ujumbe haukuwafikia kwa wakati muafaka, nah ii iliwafanya Wayahudi waliokuwa wanaishi nje ya ardhi ya Palestina kwenye matatizo makubwa sana ya kidini. Kwa mfano, wakati ulipofika wakati wa kuadhimisha Pasaka, iliwabidi kubahatisha kuona kama mwezi uliopita ulikuwa na urefu wa siku 29 au 30. Iwapo kama ulikuwa na siku 29, ndipo Pasaka ingeadhimishwa kwa siku fulani; na kama ulikuwa wa siku 30, ndipo Pasaka ingeadhimishwa siku inayofuatia. Ni nini cha kufanya? Ni kuondoa wasiwasi iliyopo, ndipo waliamua “kufanya kitu cha kuwahakikishia usalama” na kuadhimisha Yom Tov kwenye siku zote mbili. Ni sawa tu na ilivyo kweli kwenye Shavuoth na Sukkoth. Kwa hiyo, Wayahudi walioishi Uhamishoni (ukiwaondoa ndugu zetu Wanamatengenezo) walikuwa na maadhimisho zaidi ya matano ya siku za yom tov kwa mwaka kuliko walivyokuwa wanafanya Wayahudi walioishi nchini au ndani ya Israeli.

Vipi kuhusu Rosh Hashanah?

Rosh Hashanah inaadhimishwa kwa muda wa siku mbili hata huko Israel pia.

Kuna mengi sana yahusuyo utaratibu wa kuupangia Mwezi Mpya kipindi cha kabla ya kuanzishwa kwa kalenda. Sasa niambie tafadhali hii miaka mirefu ilipangiliwaje kabla ya kuandikwa kalenda?

Hapa, pia ilikuwa ni hali ya kimaisha ambapo marabi waliamua kabla ya kuutangaza mwezi wa Abibu wakitilia maanani iwapo kama ishara au dalili za majira ya maridi yamefika (kukoma kwa majira ya mvua, kuiva kwa mazao, kutilia maanani kama siku ya ikwinoksi imekuwepo, nk). iwapo kama kutaonekana kuwa majira ya machipuko yamechelewa, ndipo Adari ya Pili iliingizwa ili kufidia mambo haya, na mwaka huu ulifanyika kuwa mrefu (Soma kitabu cha Bab. Talmud Sanhedrin 11 a & b).

Kwa nini ilionekana kuwa ni muhimu kuanzisha kalenda isiyo ya kubahatisha?

Kwa kuwa hata mababu waliosimamia uendeshaji wa dini katika Nchi Takatifu hawakufurahia kabisa hali ile ya kubahatisha na kwa kuwa serikali ya Kirumi ilikataza na kuthibiti uhuru wa kujiamulia wa baraza la Sanhedrin katika kushughulikia mambo haya.

Kalenda ya Kiyahudi haionekani kuwa kama ni ya mrengo wa mzunguko wa jua au mwonekano wa mwezi. Unaiitaje kalenda hii kuwa ni ya mrengo upi?

Ni kalenda ya mrengo wa mwonekano wa mwezi, miezi yake inahesabiwa kutokana na mwonekano wa mwezi na mwaka sambamba na mwonekano wa jua.

Umekwishaonyesha tayari dalili ya kwamba uhesabuji wake wa mwaka unaoenenda kwa mzunguko wa jua unatofautiana kwa upungufu wa takriban dakika 6½ kutoka kwenye mwaka halisi wa mzunguko wa anga. Vipi kuhusu mahesabu ya mwezi wa mzunguko wa mwezi mwandamo?

Hapa ni sahihi sana kama inavyoweza kuwa. Kalenda ya Kiyahudi huhesabiwa mwezi wake kwa siku 29, masaa 12, dakika 44, na sekunde 3.33  -- tofauti yake kutoka kwenye mwezi halisi wa mrengo wa mznguko wa anga sio chini ya sekunde moja tu na nusu.

Kwa kurudi nyuma sasa, ni kwamba umejionea nini kuwa ni kama “tatizo kbwa” lililopo kwenye kalenda ya Kiyahudi  --itachukua muda gani kabla ya kufanyika kwa Pasaka mnmo Juni 21 na tangu hapo inamaana kwamba haitakuja kurejea tena kwenye majira ya machipuko?

Ni kwa kipindi cha miaka 12,500.

Ni kweli hivyo, kwa hiyo ni mapema sana kwa sasa kuogopa kuhusu marekebisho ya kalenda?

Kwa hakika, inaweza kuwa sio mapema sana kufikiria jambo hili.

Marekebisho haya ya kalenda yatapaswa kufanyikaje?

Kuna njia mbili: ya kwanza ni ya kiasili, na nyingine ni ya kimiujiza. Kwa upande mmoja, kunatakiwa kuwe na mkutano wa sinodi ya ulimwengu mzima ya watu watakaowakilisha itikadi zote zinazoamini imani ya Kiyahudi ambayo yatafikia kwenye makubaliano kwamba ni jinsi gani au ni lini watakapoirekebisha kalenda. Kwa upande mwingine, Uliya atakuja na kutusaidia kurekebisha mambo haya kwa faida yetu.

Nimegundua kuwa hujaweka wazi shahiri kuhusu uwezekano upi unaodhania utakuwa wa kiasili na upi wa kimiujiza. Lakini, kwa muono wako, ni upi kati ya hatima hizi mbili unaonekana unaweza kutokea kabisa?

Kwa kweli, ni suala la kungojea na kuona tu.

q