Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[076C]

 

 

 

Chimbuko la Uyunitarianism Wenye Itikadi Kali na Ubinitarianism

 

(Toleo La 1.0 20100129-20100129)

 

Wengi wa wale wanajiita kuwa ni Wakristo wanatafuta na kupenda kuifafanua Asili ya Mungu kwa mtazamo wa Uyunitarianism wenye Itikadi Kali au Ubinitariani pasipokujua kuwa mafundisho wanayoshikilia kuyaamini kwa kweli yanatokana na imani ya miungu ya kipagani na yametumika katika kuliharibu Kanisa lililoanzishwa na Yesu Kristo.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hati Miliki © 2010 Wade Cox)

 (Tr. 2013)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


 Chimbuko la Uyunitarianism Wenye Itikadi Kali na Ubinitarianism



Kuna idadi ya watu wengi wanaodai kuwa wanayafuata mafundisho ya kanisa la kwanza na wakati wanapofuatiliwa wanathibitika kuwa wanfuata mafundisho yaliyoanzia kwenye karne ya pili ambayo yalitumika kuingizwa na kuliharibu kanisa la kwanza. Hawajui chanzo asilia cha mafundisho yao na mafundisho ya uzushi yaliyotumika na jinsi yanavyopingana na fundisho la kweli kuhusu Asili ya Mungu.

 

Mafundisho aina mbili yametumika katika kupinga na kuharibu fundisho la kweli kuhusu Asili ya Mungu na kueleweka kwake kwenye imani ya Kiyahudi na hatimaye kwenye kanisa lililokuwepo.

 

Fundisho la kwanza la uwongo lilikuwa ni kuhusu Uyunitarianism wa Imani Kali ambao ulilenga kukataa utendaji-kazi wa Masihi kwenye kipindi cha kabla ya kuzaliwa na kuwepo kwake duniani, na ni fikra iliyokusudia kuiharibu kabisa fikra na imani ya kweli ya Agano la Kale na unabii kuhusu Masihi na kanisa.

 

Fundisho la pili la uwongo lilikuwa ni lile la Ubinitarianism. Lilitokana na ufunuo wa Mungu aliompa nabii Isaya kuhusu kuja kwa Masihi.

 

Mara tu baada ya unabii huu kutumika kwa Israeli, ndipo mara moja mapepo yakaanzisha imani potofu na ya udanganyifu karibu kwenye maeneo yote Syria na Mesopotamia kwa ujumla wake kwa kile kilichojulikana kama dini ya siri. Dini potofu na ya uwongo iliyoenea sana ilikuwa ni ile ya kumuabudu mungu Attis na mungu mke Rhea au Cybele ambaye hatimaye alishirikiana naye.

 

Miungu wengine walikuwa ni kina Adonis aliyekuwa akiabudiwa na Wayunani na Osiris huko Alexandria. Tunaelezea zaidi jinsi mafundisho haya yalivyoshika kasi hapo chini.

 

Kwanza kabisa hebu na tuelezeee maana ya Uyunitariani wa Imani Kali na kisha hebu na tueleze chimbuko lake na mfananisho wa imani hii ya Ubinitarianism na kukielezea kila Kristo alichokisema kuhusu fundisho hili ba tuone jinsi fundisho hili lilivyo kuwa ni la uzushi tu uliofanyizwa unaotokana na kutokuyaelewa Maandiko Matakatifu, yote yote yaani kwenye Agano la Kale na Agano Jipya.

 

Uyunitariani wa Imani Kali 

 

Maana yake: Imani inayosema Kristo hakuwepo wala utendaji wowote wa kazi kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake duniani na mwanamwali Mariamu.

 

Fundisho hili lilishamirishwa na Mafarisayo kwenye imani yao ya Kiyahudi hadi kipindi cha KRisto. Inapuuzia eneo kubwa la Maandiko na ilikataliwa kufanywa kuwa ni mtazamo wa kweli na Kristo mwenyewe aliyenukuu Maandiko ili kuwaonyesha makosa yake. Yamepigiwa upatu na hawa wanaojiita wenyewe leo kuwa ni Wayunitariani Wakristo na pia basalia ya Marabi wa Kiyahudi, ambao kwa siku hizi ni Mafarisayo wanaonukuu vibaya Maandiko Matakatifu ya Agano la Kale, na kudai kwamba Kristo hakuwa anaishi siku za kabla ya kuzaliwa kwake duniani ambao wanakataa pia kuwa hataweza kurudi tena duniani hivi karibuni. Jambo hili limeelezewa kwa kina kwenye jarida la Masihi wa Uwongo (Na. 67B) [The False Messiah (No. 67B)].

 

Ni sawa tu na yalivyo mafundisho ya Watrinitariani yanatuamna kwenye maeneo dhaifu zaidi ya mabishano na wakidai kuwa hicho ni kiwango kikubwa sana cha kuipinga, na kuitumia kuwa kama uthibitisho wa imani yao kwenye maandiko.

 

Kristo aliimaliza kazi ya kutimiliza utendaji kazi wa Amri Kuu Mbili zilizo kwenye Torati ya Mungu kwa Mafarisayo walipomkusanyikia kwa kuwa aliwanyamazisha Masadukayo waliokuwa wanadai na kuamini kuwa hakuna ufufuko wa wafu kwa vile alipowaambia kwa kunukuu Maandiko kuwa: “32 Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai.” (Mathayo 22:32).

 

Mafarisayo walimkutanikia na mwanasheria akamuuliza: “Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?”

 

Kristo akawajibu akasema: “Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.(akinukuu Kumbukumbu la Torati 6:5, 10:12; 30:6). Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii” (Mathayo 22:37-40).

 

Waandishi waliigawa Torati kwenye makundi mawili: amri au maagizo yaliyotakiwa wayafanye na zile za makatazo. Kuna amri za maagizo jumla ya 248 (ambazo zilidaiwa kuwa ni sawa na idadi ya washiriki wa kwenye baraza la bodi yao) na 365 zilikuwa ni za makatazo (moja kati ya kila mojawapo huwakilisha siku moja ya kalenda ya jua ambayo pia inathibitisha imani ya dini ya usiri). Jumla yake ni 613 ambayo inawakilisha idadi ya “nyaraka” za Decalogue au zile ambazo Bullinger anazidai (Kwenye Companion Bible, sawa na Mathayo 22:37).

 

Wakati Kristo alipoweka msingi wa Torati wazi kwenye mgawanyo wake na utendaji kazi wake na alikuwa pamoja na viongozi wa Mafarisayo na alishughulikia tatizo jingine kubwa ambalo lingeigharimu Yuda kwa kipondi cha millennia. Aliwauliza swali alisema: “Mwaonaje katika habari za Kristo Ni mwana wa nani?”

 

Wakamjibu: “mwana wa Daudi.”

 

Kwa kulikanusha hilo alitumia Zaburi 110:1 ambayo ni andiko wanalolipenda sana hawa Wayunitaiani wenye Itikadi Kali leo kwa kupinga uwepo huu wake wa zama kabla ya kuzaliwa kwake.

 

Hili ndilo jibu lake Kristo kwa wote wanaopinga uwepo wake wa siku za nyuma kabla ya kudhihirika kwake duniani: “Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?’

 

Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?”

 

Mafarisayo walinyamaza kimya wakijua kuwa alikuwa ni Yahova wa Majeshi aliyekuwa anamuongelea Masihi kwenye andiko hili.

 

Andiko kwenye Zaburi 110:1 lilikuwa ni “maneno ya Yahova (kama neum Yahova).” Wasopherimu ndipo wakaibadilisha 110:5 kutoka Yahova hadi Adonai badala ya Yahova. Hii ilikuwa moja ya 134 iliyosema kwamba Yahova alibadikishwa na kuwa Adonai kwenye maandiko ya Masoretic Text (MT) ya Sopherim ili kuondoa utambulisho wa kufanya ihusike na tofauti kati ya mambo muhimu nay a kawaida ya Mungu Mwenyezi na Mungu wa Israeli, ambaye alikuwa ni urithi wake (tazama pia uandishi wa Nyongeza 32 wa Companion Bible kwenye nota ya 132 iliyobadilishwa na Nyongeza 98 VI,  i, a, 1A, a, kwa maandiko ya Kiyunani kwenye Mathayo 22:44 ikinukuu Zaburi 110:1 ambapo Yahova anatajwa kama ho kurios pamoja na makala kamilifu kwenye Kiyunani ikiashiria Yahova wa Majeshi maana yake) (pia tazama jarida la Zaburi 110 (Na. 178) [Psalm 110 (No.178)].

 

Maana yake yasingeweza kubadilishwa kwenye baadhi ya maandiko hatahivyo. Andiko moja kati ya hayo ni Zaburi 45:6-7 ambapo Daudi anasema: “Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako”  Waebrania 1:8-9 inaonyesha kwamba hii ilikuwa mahsusi kwa Kristo. Iwapo kama Kristo alikuwa ni Mungu wa pili wa Israeli wakati ule wa Daudi basi iweje badi asiweze kuwa alikuwepo huko nyuma kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake kimwili? (Tazama majarida ya Zaburi 45 (Na. 177) na Uwepo wa Yesu Kristo Kabla ya Kuzaliwa Kimwili (Na. 243) [Psalm 45 (No. 177) and The Pre-existence of Jesus Christ (No. 243)].

 

Nabii Zekaria anaonyesha kuwa Malaika wa Yahova wa kichwani mwa wateule ni elohim kama itakavyokuwa kwa wateule wote na Daudi mwenyewe (Zekaria 12:8) (pia soma jarida la Wateule kama Elohim (Na. 001) [The Elect as Elohim No. 001)]. Zekaria 2:8-9 inaonyesha kwamba Bwana wa Majeshi (Yahova Sabaoth) amemtuma Yahova wa pili kwa mataifa yanayoiharibu na kuikosesha Israeli. Atautikisa mkono wake juu yao na watakuwa mateka kwa watumishi wake nasi hatimaye tutajua kuwa Bwana wa Majeshi amemtuma. Iweje basi kiumbe kama huyu asiwe ni wa aina ya kimalaika au asiye wa kawaida?

 

Wayunitariani hawa wenye Imani Kali wanadai kwamba Mungu Wapekee na wa Kweli alikuwepo kule jangwani na kuwa ndiye aliyempa Musa Torati. Hata hivyo Agano Jipya limeweka wazi likisema kuwa hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu, kote kuwili, yaani kwenye Injili na kwenye Nyaraka za Mitume, na kwamba ni elohim mdogo ndiye aliyekuwa anaongea na Israeli (Yohana 1:18; Yohana 5:37; Yohana 6:46; 1Timotheo 6:16; 1Yohana 5:20). Kristo anasema kwamba alikuja kutoka Mbinguni na kwamba hakuna mtu aliyewahi kwenda Mbinguni mbali ya yeye Kristo aliyeshuka kutoka Mbinguni (Yohana 3:13). Anasema kwamba yeyote anayemuona mwana amemuona Baba pia (Yohana 6:36); hatahivyo, hii haipingi ukweli wa kwamba alisema kwamba hakuna aliyewahi kumuona Baba isipokuwa ni yeye tu aliyeshuka kutoka kwa Mungu, akijisema yeye mwenyewe.

 

Anawatolea mfano wa Roho Mtakatifu kwa kumuelezea kuwa ni uweza tu wa Mungu na kwamba kwa kupitia huyo Roho ndipo alifanyika kuwa ni wa Mungu.

 

Kristo alisema pia kuwa alimuona Shetani akianguka kama umeme kutoka mbinguni (Luka 10:18). Anawezaje basi kuweza kufanya haya yote ikiwa yeye sio kiumbe wa kawaida?

 

Kwenye Yohana 17:5 Kristo anasema kwenye maombi yake: “Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.” Inawezakanaje basi mtu wa kawaida tu aweze kutamka maneno haya ikiwa yeye hajawahi kuishi huko nyuma kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake kibinadamu?  Wabinitariani walikuwa wanadai kwamba Kristo angekuwa wa namna ya umbile sawa na namna sawa ya kuelewa mambo kama alivyo Baba Mungu na lakini asiweze kuwa ni Kristo wa haiba iliyotofauti. Ni madai yenye mtzamo wa kipuuzi tu haya na yasiyo na maana. Wayunitariani hawa wenye Itikadi Kali wanadiriki pia kuyapuuzia maandiko fulani ili kuendekeza mafundisho yao ya kutunga na uzushi kwamba Kristo hakuwepo kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake kimwili, bali alikuwepo tu kuanzia alipotungwa mimba yake tumboni mwa Mariamu. Kwenye Yohana 17:18 anasema tena kwamba Mungu alimtuma humu ulimwenguni (na hii haimaanishi kwa ujio wa mtungo wa mimba).

 

Wafilipi 2:5-7 imetafsiriwa kimakosa na inatumiwa sana na Watrinitariani. Inaelezea juu ya uasi na uaminifu wa Kristo na alivyojitoa kuwa sadaka huko mbinguni. Inasema: “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya (morphe) Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;”

 

Je, ni vigumu sana kulielewa andiko hil?. Mbona limeandikwa kwa lugha ya kawaida na rahisi. Linaelezea kwamba:

1.      Kristo hayuko sawa na Mungu na wala hakutafuta kuwa sawa na Mungu (Isaya sura ya 14 na Ezekieli sura ya 28 zote zinaonyesha kuwa ni Shetani ndiye aliyediriki kufanya hivyo).

2.      Alikuwa kwenye umbo la elohim akiwa ni kiumbe katika ulimwengu wa roho.

3.      Alijijitoa mwenyewe (kwa kukubali kuanhana na mwili wake wa kimbinguni na umbo lake na haiba yake) na akazaliwa kama mwanadamu.

 

Mtu anaweza kutatanishwa na kudai kuwa andiko hili halionyeshi dalili yoyote ya kuwepo kwake siku za nyuma za kabla ya kuzaliwa kwake kimwili. Hata waamini Utatu walikutana na majaribu ya kueuza tafsiri ili kujaribu kumlazimisha aonekane kuwa sawa na Mungu lakini hata walikuwa ni wajinga sana wanapojaribu kukataa uwepo wake wa siku za kabla ya kuzaliwa kwake kimwili. Jambo hili ndilo lililosababisha Watrinitariani wafanikiwe zaidi ya Wayunitariani wenye Imani Kali katika kukubalika kwa mafundisho yao ya uwongo (pamoja na kuyaikataa kwao mafundisho ya Hadithi za Kiislamu).

 

Maneno aliyoyasema Mtume Paulo kwenye 1Timotheo 3:16 yamegeuzwa kwenye tafsiri ya Codex A. Andiko linasema: “Na pasipo utata wowote kwenye ukuu wa siri za Uungu: iliyodhihirika katika mwili, kuhakikishwa katika Roho, ukaonekana na Malaika na Kuhubiriwa kwa Mataifa, ukaaminiwa duniani, na kupokelewa kwa utukufu Bullinger (Mwandishi wa Companion Bible) kwenye maneno fafanuzi yanayoandikwa chini ya ukurasa kuhusu ayah ii ya 16 anaandika kwamba Biblia ya R.V. inasema “Theos (Mungu), jambo linalotupa ushahidi wa kutosha.” Anaendelea kufafanua zaidi kwamba neno lililoandikwa zamani na maandiko asilia la ho (kipi); kwa uandishi wa Kiyunani huandikwa O. Mwaandishhi fulani baadae aliongezea herufi “s” ili kuifanya isomeke “Yeye Ambaye”– akidhania italeta maana zaidi. Na baadae mwingine akaweka alama iliyokatisha kwenye herufi hii ya O na kuifanya iwe Theta. Na kwa hiyo ilionyesha dalili ya kuwa ilikuwa na mkanganyiko kwa jina Theos (Mungu) na ndipo neno Mungu  likaingizwa kwenye maandiko ya Biblia ya KJV. Watrinitarian wanaitumia hii ili kuthibitisha andiko hili na huku wakijua fika kuwa limeingizwa kimakosa na kwa kughushiwa kwenye tarsiri ya Codex A lakini wakituama kwenye hali ya kuwapumbaza wengine. Lakini hakuna mtu aliyejaribu kudai hivyo kwa kumaanisha sana kwamba haihitaji kutafiti ili kupata ukweli kuhusu kuishi kwake kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake kimwili hapa duniani.

 

Paulo anasema kwa wazi na vizuri sana kwamba Kristo alikuwa na Waisraeli jangwani pamoja na Munsa na kwamba wote walikula chakula na kunywa maji ya mwamba ambao ulikuwa pamoja nao, na kwamba mwamba ule ulikuwa ni Kristo (1Wakorintho 10:4). Lakini hawa Wayunitarian wenye Imani kali wanajaribu kupinga andiko hili pia.  

 

Maandiko ya Agano la Kale yenyewe yanasema kuwa hakuna mtu anayeweza kumuona Mungu na akaishi (Mwanzo 32:30). Kwa hiyo, kiumbe huyu ambaye alikuwa ni mdogo ukimlinganisha na Mungu wa Israeli alishindana na Yakobo na akamuita jina lake kuwa Israeli.

 

Wayunitariani wenye Itikadi Kali hadi sasa wanaendelea kupinga na kutafsiri vibaya Maandiko Matakatifu. Moja ya makosa hayo ya utafsiri yapo kwenye Waebrania 1:2. Andiko hili kwenye Waebrania 1:1-2 limasema:

Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.

 

Sasa, Wayunitariani hawa wenye Imani Kali kwa kweli wamelinukuu andiko hili kama ushahidi wao kwenye imani yao na mafundisho kuwa Kristo hakuwa ameishi siku kabla ya kuzaliwa kwake kimwili hapa duniani kwa kuyanyamazisha maneno yasemayo mrithi wav utu vyote. Wao kwa makusudi kabisa na bila woga wanalitumia andiko hili na kushindwa kuendelea kusoma mahali panaposema kwa yeye alifanya au kuweka aeonas, au nyakati (na ambayo imetafsiriwa kama dunia). Zama hizi zipo tatu zinazotokana na uzunguko wa sayari na kuumbwa kwa Adamu hadi kwenye Gharika Kuu, zama za kutoka Nuhu hadi Kristo na zama za mwisho ni kutoka Kristo hadi Siku za Mwisho na za kipindi cha Milenia kitakachokuwa chini ya mamlaka ya Masihi.

Kuyaamini maandiko ni jambo moja na ni susla la imani, lakini kudhania ama kufundisha watu kuwa huyu mwana wa Mungu alikuwa ni mwanadamu au kiumbe aambaye hakuwahi kuishi kipindi cha kabla ya kuzaliwa kimwili ni jambo lisiloingia akilini. Tunajua kwa mujibu wa andiko hili kuwa yeye mi Mwana wa Mungu na tunajua kwa kupitia Maandiko Matakatifu kuwa kulikuwa na wana wengi wa Mungu (Ayubu 1:6, 2:1; 38:4) na pia kwamba walikuwa wanaitwa Yahova au “Aliyesababisha iwe” na tunajua kwamba walikuwepo wanne kwa wakati mmoja walipokuwa wanakwenya kuupatiliza mji wa Sodoma na Gomora (Mwanzo sura ya 18 na 19) (pia tazama jarida la Malaika wa YHVH (Na. 024) [The Angel of YHVH (No. 024)].

 

Tunajua kutokana na gombo maarufu linaloitwa “the Dead Sea Scrolls (DSS)” na tafsiri ya Septuagint (LXX) kwamba andiko la Kumbukumbu la Torati 32:8 liligeuzwa ama kubadilishwa kwenye tafsiri ya MT. Andiko hili kwenye uandishi wake asilia liliandikwa hivi:

 

Yeye Aliye Juu alipowapa mataifa urithi wao, Alipowabagua wanadamu, Aliweka mipaka ya watu Kwa kadiri ya hesabu ya wana wa Mungu (tazama pia kwenye RSV).

 

Tafsiri ya Sopherim ikalibadilisha ili lisomeke sawa na idadi ya wana wa Israeli, ambavyo ni uwongo. Ilifamnywa hivyo makusudi ili kuficha urithi wa Yahova wa Israeli kama inavyoendelea kwenye aya ya 9 moja kwa moja ikielezea kuwa urithi wa Yahova ni watu wake, na Yakobo ana urithi mwingi miongoni mwa wingi wa urithi wake (tazama Kijani, Biblia iitwayo The Interlinear Bible). Andiko hili linasema wazi sana kwmba Yahova wa Israeli alikuwa ni mmoja wa wana wa Mungu na alipewa kuwamiliki Israeli wawe ni urithi wake. Kwa kupitia kwake yeye na urithi wake Mungu alipaswa kuwachukua wanadamu wote wawe wake mwenyewe kama tunavyosoma kwenye Kumbukumbu la Torati 32. Andiko hili lilikuwepo wakati Musa alipowatajia jina la huyu Mungu Mmoja Wapekee na wa Kweli, Eloa kwa mara yake ya kwanza (kwenye mlolongo wa kisasa wa Biblia) na kuiandika mara mbili kwenye aya za 15 na 17. Musa alikuwa ameishalitambulisha tayari jina hili kwenye kitabu cha Ayubu mara kadhaa. Huyu Eloa ndiye mlengwa na kiini cha ibada zetu na anaandikwa kwa lugha ya umoja ikikubali kuwa hakuna namna yoyote ya uwingi kwa namna yoyote ile. Kinyume na neno au jina elohim ambalo ni neno la uwingi lililotafsiriwa kwma miungu kwenye andiko hili, Eloa ni jina la Mungu Mmoja wa Pekee na wa Kweli ambaye ndiye muumbaji na Baba wa wote. Elohim ndivyo vile anavyokuwa kupitia uumbaji wa yote mawili, mbingu na mwanadamu.

 

Kwa hiyo Masihi amepewa urithi wa vitu vyote ili kwamba Mungu afanyike kuwa ni yote katika yote. Kwa hiyo ni lazima mtu wa aina hii awe alikuwepo siku za nyuma kabla ya kuzaliwa kwake, akiwa ni mwana wa Mungu kwenye milki ile na andiko linaonyesha wazi kwamba kwa kweli alishiriki hata kwenye uwekaji au kupangaji wa nyakati ambazo kwazo urithi wake ndizo utaendelezwa. Kwa hiyo Kristo aliwakabili Mafarisayo na kuwataka washughulikia mafundisho ya kizushi ya Wayunitariani wenye Imani Kali wanaopinga uwepo wake siku kabla ya kuja kwake hapa duniani kimwili.

 

Kwa mtazamo wa mandiko hay muhimu ya kibiblia inafuatia kwamba Wayunitariani wa Itikadi Kali hawawezi kuwa ni Wakristo kwa kuwa fundisho lao hili linapingana na kwenana kinyume na maelezo yaliyoko kwenye Biblia na ya Ukristo kibayana. Kuamini uwepo wa Kristo huko nyuma kabla ya kuzaliwa kwake kimwili hapa duniani ni muhimu na ni msingi muhimu kwenye imani ya Kikristo.

 

Inaeleweka bayana sana kwamba Wayahudi wangetafuta nafasi ya kudanganya na kuwaongopea watu ili wathibitishe makosa yao kwa kipindi cha zaidi ya millennia mbili. Lakini ni jambo lisilo na udhuru kwa mtu anayedai kuwa ni Mkristo kufanya hivyo.

 

Hakuna mtu mwenye fikra na akili zake timamu angaliyeweza kutumia nusu ya kwanza ya Waebrania 1:2 ili kupinga kile ambacho nusu nyingine ya pili na aya nyingine ya 3, kinaelezewa kwa wazi sana namna hii, kama tunavyojionea hapo juu.

 

Sasa tutajione Chimbuko la Ubinitarianism na wanavyoyatumia ili kuweka pamoja mafundisho yote mawili ya uzushi.

 

Chimbuko la Ubinitarianism

 

Ubinitarianism sio fundisho la Kikristo. Ulianzia huko Mesopotamia kwenye dini ya waabudu mungu Attis na miungu mingine iliyokuwa inaabudiwa kiuficho au kwa siri. Dini hizi ziliyachukua mafundisho fulanifulani yanayomhusu Masihina  kuyachanganya hasa yale ambayo Mungu alimfunulia nabii Isaya alimweleza jinsi Masihi atakavyokuwa na ili waambie Israeli.

 

Fundisho hili kwa kweli lilikuwa moja ya yaliyotungwa kwa werevu na ujanja mkubwa na likiwa na uvuvio wa kimapepo ili kuwadanganya na kuwapotoa Israeli kutoka kwenye imani ya kweli. Ni moja ya mfano wa jinsi mapepo wanavyojitahidi kufuatilia nabii za Mungu tulizofunuliwa kupitia kwa kanisa na manabii.

 

Isaya mwana wa Amozi alizaliwa kabla ya mwaka 760 KK. Alianza huduma yake mnamo mwaka 742 KK ambao ni kwamba aliofariki mfalme Uzia (Isaya 6:1). Alipata umaarufu kipindi cha kushambuliwa kwake Yuda na majeshi ya  wa Syro-Ephraimitic mwaka 734 KK. Tangu mwaka 734 alitabiri juu ya ujio wa Immanueli na mnamo mwaka 734 alistaafu kutoka kwenye shughuli zilizojulikana na watu wengi za hadhara akimuonya Ahazi dhidi ya uwezekano wa kushambuliwa na majeshi ya muungano ya Wasyria. Ukimya wake uliendelea hadi mwaka 715 KK wakati alipoanza kunena zaidi kwa uhuru kipindi cha mfalme Hezekia. Mwaka 705 kwenye kifo cha mfalme Sargon II kulishuhudiwa maasi ya majenerali dhidi ya dola ya Ashuru na uvamizi wa Senakarebu ulioshuhudia kukataliwa kwa Waashuru na wakafukuzwa na Mungu watoke Yuda na mwisho wa huduma yake mnamo mwaka 701.

 

Dini potofu ya mungu Baali-Ashtorethi ilikuwa inaendelezwa na kujipenyeza katika Israeli na ilikemewa. Dini nyingine potofu ziliyokuwa chini ya majina mengine zilikuwa zinazuka maeneo karibu yote ya Mashariki ya Kati na Ulaya. Dini ya Wahiti au Waceltiki kipindi hiki ilikuwa imejipenyeza pia huko Ulaya mapema zaidi na zimejitwalia na kuzichukua sikukuu na wamekwisha zifanya sehemu ya ibada zao. Walikuwa hawajaiendeleza dini nyingine potofu ya “mungu mfu” kama walivyofanya watu walioishi maeneo ya Mashariki ya Kati, kwa lengo la kuyashinda maandiko ya Kimasihi yakiwa hayajaandikwa bado hadi kipindi cha nabii Isaya yapata kama mwaka 734 KK.

 

Kwenye kipindi cha Yeremia, ambaye huduma yake ilidumu kwenye kipindi cha takriban tangia mwaka 626 hadi 580 KK, tumejionea kuibuka kwa dini potofu ya mungu Attis na kuanzishwa kwa sikukuu dini ya kuliabudu Jua zikifanywa tarehe 24/25 Desemba baada ya majira ya jua kuwatoonekana linapojificha kwenye ncha ya dunia. Mafundisho ya Dini hii ya Siri ya Kuabudu Jua yalikuwa kama ifuatavyo:

1.      Jumapili au siku ya mungu Jua ndiyo ilikuwa siku yao takatifu.

2.      Siku ya kuzaliwa kwa “mungu jua wao” au ya kurudi kutoka mafichoni kipindi hiki cha jua kujificha upande wa pembezoni mwa dunia, ilikuwa pia ndiyo sikukuu yao kuu sana wakati “jua lililokuwa limejificha” linapozaliwa au kuonekana tena (na ilikuwa tarehe za 24/25 Desemba).

3.      Sikukuu ya mungu-mke Ishtar, au Easter ya watu wa mataifa mchanganyiko ya Ulaya maarufu kama Anglo-Saxons, ilianzishwa kwa lengo la kuonysha nguvu za mungu wao mke wa kuingia Kuzimuni na kumfufua “mungu aliyekufa.” Kifo hiki ilidaiwa kilikuwa kinatokea siku ya Ijumaa ya mwezi mkamilifu baada ya majira ambayo usiku na mchana masaa yanalingana na ndipo ufufuko huu ndipo unafanyika katika Siku ya mungu Jua, ambayo ni siku moja na nusu baadae.

 

Mungu anaonekana kuchukizwa kwa wazi na ibada na dini hii za mungu Jua kwenye Yeremia 10:1-10 tunaona Mungu akiikemea sikukuu hii ya majira ya kuonekana kwa jua tena kutoka pande za maficho ya dunia ambayo kwa leo inajulikana kama Christmas.

Mtu yeyote anayeziadhimisha au kufuata sikukuu hizi ni muumini wa kuaminika wa mungu Baali na wa dini hii inayoliabudu jua. Na wala sio Mkristo au Wakristo.

 

Mtu yeyote anayesema kwamba wanapokufa wanakwenda mbinguni, huyo sio Mristo; bali wao ni waumini wa Ugnostiki (tazama kitabu cha Justin Martyr, Dial. LXXX).

 

Ni kwa kipindi cha takriban zaidi ya miaka 110 ulaghai umekuwa ikiendelezwa na ulikuwa kwenye kiwango cha juu sana huko Mashariki ya Kati. Yuda walichukuliwa na kupelekwa utumwani kwa ajili ya kuingia kwao kwenye mtego wa imani hii iliyofananishwa na Marejeo ya Masihi. Kwa hiyo Yuda wakaingia hukumuni. Imani ya dini yao ya kweli iliharibiwa na kupotoshwa na wakapelekwa utumwani kwa kipindi cha miaka elfu mbili.

 

Kuenea kwa Dini hii Potofu ya Kuabudu Mungu Mfu

 

Dini za waabudu jua zilishamiri na kuenea zikitokana na imani nyingine ya mungu Osiris na Isis wa Misri na ambazo zilianzishwa mapema sana zikituama kwenye wazo la kuwepo kwa Mungu Mke Isis ambaye alichorwa kwa picha anayoonekana akiwa amemshika mtoto wake mchanga mkononi mwake ambaye ni mungu jua akiwa kwenye pango siku moja baada ya majira ya jua kutoonekana ya Solistaisi, ambayo kwa mapokeo ni jioni ya tarehe 24 Desemba ambayo ndiyo mwanzo wa tahere 25 Desemba. Dini hii ilienea kwa kasi huko Syria na Mesopotamia kama ilivyopokelewa dini ya kumuabudu Attis na ndipo tokea hapo iliendea na kufika hadi Roma na kufanyika kuwa ni dini kuu.

 

Sikukuu za kuabudu jua hazikuingia kwenye Ukristo hadi mwaka 475 BK kipindi cha kuanguka kwa Dola ya Rumi na mwanzo wa kipindi kinachojulikana kama cha Giza na Baridi au Barafu. Jambo la kufurahisha kabisa ni kwamba ilikuwa ni huko huko Syria ndiko Ukristo uliingia na ukaenea kutoka huko.

 

Hatimaye ukaenda na kuenea hadi Ugiriki na Thrace kutoka Mashariki ya Kati na kuingia kwenye nchi za Balkan kama ilivyoingia dini potofu ya Adonis, na kama ilivyopokelewa pia dini ya mungu Mke na wa urutubisho Demeter na ndipo kipindi hiki imani na mapokeo yote ya dini ya waabudu jua zilipoingia kwenye Ukristo pia (ndipo walipoingiwa kina Madonna mweusi na imani au dini ya mwanamwali na picha zake vilianza kutumiwa kwenye Ukristo).

 

Kuenea kwa dini hizi kumeelezewa kwenye jarida la Chimbuko la Christmas na Easter (Na. 235) [The Origins of Christmas and Easter (No. 235)].

 

Undumilakuwili wa Kiimani wa Wabinitarian kwa Mungu Attis nk.

 

Tukio kuu sana na la udanganyifu kuwahi kutokea kwenye maisha ya wanadamu ni jinsi Ubinitarinai wanavyofanana kiimani na ile ya mungu Attis.

 

Watu wasioyajua mafundisho hujaribu na hukosea kusoma na kuichnganya na Ukristo. Hebu na tuwe wa kweli sana hapa. Ukweli ni kwamba Ubinitarianism sio fundisho la Kikristo kabisa. Na wala hautokani na Maandiko Matakatifu na umetumiwa katika kuliharibu kanisa la kwanza na pia kuyaharibu Makanisa ya Mungu hasa mwishoni mwa karne ya ishirini.

 

Fundisho la imani ya mungu Attis vinasema kuwa yeye alikuwa mungu na alijifanya mwanadamu yeye mwenyewe pasi msaada wa kiumbe mwingine. Kwa hiyo maana yake ni kwamba huyu Attis aliyeuchukua mwili wa kibinadamu alikuwa ni wa cheo cha pili kwenye vyeo vya kimbinguni vya mungu mmoja. Ilikuwa ni kipande kikubwa cha udanganyifu wa shetani akitumia asili za namna mbili za Mungu kwa kuitumia Biblia kiulaghai kuhusiana na umoja wa nafsi ya Eloa aliyejieneza mwenyewe na kuwa Ha Elohim. Kwenye mafundisho ya biblia Eloa amejieneza mwenyewe kupitia Roho wake na wana wote wa Mungu wamekuwa ni elohim au miungu kwenye uumbaji wao kupitia kwenye uenezi wa Roho Mtakatifu akiwa ndiye nguvu ya Mungu iwezeshayo, ili yeye awe ni yote katika yote na ndani ya yote akiwa ni Ha Elohim akienea hadi kwa elohim wote. Huu ulikuwa ni ujumbe mkuu sana na wenye nguvu wa Agano la Kale ambao ulipaswkuhubiriwa na kutafsiriwa na Kristo katika kustahili kueneza uwezo wa mwanadamu kupitia Roho Mtakatifu.

 

Ili kuzima uelewa wa teolojia ya Biblia, ueneaji wa jambo hili ulipaswa usiongelewe kwa mtu mmoja peke yake na kuwa amegawanyika sehemu mbili. Hii ni inapelekea kile kinayodaiwa kuwa ni kuyashinda mabishano ya Wayunani ambayo yalipelekewa kwenye Ukristo na wao yakikusudiwa hasa kuipunguzia nguzu au kuidharau Biblia na kumuweka huyu mungu mwenye vichwa viwili. Walihisi na kuamini kuwa ni kama pekee ndiye anafanya msamaha wa dhambi au anaweza kuwapatanisha wanadamu na Mungu , ma kwa hiyo wanaendelea kuamini kuwa sadaka safi na takatifu isingeweza kumpatanisha mwanadamu na Mungu.

 

Upuuzi unaoonekana wazi akilini wa dhana na fikra hii ulipuuzwa na waumini waaminifu kwa mungu Attis waliojipenyeza na kuingia kwenye Ukristo wakiipiga kumbo na kuiharibu itikadi au fundisho hili.

 

Kudumu kwenye makisio ni upuuzi kwa hili iwapo kama Mungu alisema kwamba angeikubali dhabihu ya Kristo kwa malipo ya dhambi, jambo ambalo alilifanya kupitia kwa nabii Isaya, kisha ikakubalika kuwa ni malipo. Ni kwa namna hiyohiyo kama mtu yeyote alisema kwamba wangekikubali kitu fulani kuwa malipo ya deni chini ya sheria ambayo kwayo ndiyo inaeleza dhambi maana yake nini, na kisha kisheria wangewajibika kufanya hivyo. Kuamini kuwa kitu hiki au malipo yalipaswa yawe na uwezenako wa Mungu wa Pekee na wa Kweli ndiye afanye hivvvyo, vinginevyo haiwezi kuwa ni sadaka kamilifu ni madai ya kijinga nay a uzushi dhidi ya Mungu wa Pekee na wa Kweli. Kitu pekee ambacho Mungu wa Pekee na wa Kweli hawezi kukifanya ni kufa. Ila mmoja kati ya wana wa Mungu ilimpasa afanye hivyo ili kuwapatanisha elohim na wanadamu wengine wote kwa Eloa akiwa ni Ha Elohim au Mungu Mkuu. Na hii ndiyo maana alipaswa awe ni mmoja aliye asilia, kama alivyokuwa kwa Jeshi lote la Malaika. Kwa hiyo alipaswa kuwa ni wa pande zote mbili, yaani elohim na mwanadamu.

 

Fundisho hili ni lazima kuwa lilishindwa na mapepo na kisha wanaushambulia mafundisho ya Wabinitariani na kuyaanzisha kwenye dini za siri au kificho rasmi zikingejea kuja kwa Masihi.

 

Mara tu baada ya kanisa kuanzishwa na mitume wote kufa walianza kuyapenyeza mafundisho haya huko Roma kabisa wakilenga kuchukua madaraka ya kiuongozi na kuthibiti shughuli za kidini huko Roma. Walichokifanya ni kuyahamisha mafundisho kutoka kwenye dini ya Attis kutoka kwenye imani ya mungu Attis hadi kwenye dini mpya inayoibukia ya Kikristo.

 

Kwenye kipindi cha katikati ya karne ya pili mtu aliyejulikana kwa jina la Anicetus, ambaye aliingia kwenye Kanisa la Kikristo, alichaguliwa kuwa Askofu wa Roma. Na mara moja alikuwa na mamlaka ya kutosha kufanya chochote na akaiingiza Easter na kuanza kuiadhimisha kwenye kanisa la mjini Roma. Easter ni neno la Kiingereza lenye maana ya mungu Mke Ishtar wa jua na aliyekuwa akiabudiwa kwenye ibada za siri na za uficho. Kanisa lililokuwa nje ya Roma lilijitahidi kupinga na hatimaye kukapelekea malumbano ya Waquartodeciman (tazama jarida la Mabishano ya Waquartodeciman (Na. 277) [The Quartodeciman Disputes (No. 277)].

 

Mfundisho haya mapotofu nay a uzushi ndiyo yalipelekea kurasmishwa kwa siku ya Jumapili Kanisani huko Roma tangu mwaka 111 BK. Na mara tu walipofanikisha hilo waliingiza sikukuu ya “Mungu Mfu” ya Attis. Sikukuu hii ilikusudiwa iondolee mbali adhimisho la Meza ya Bwana siku ya Pasaka na ifanyike siku nyingine ya Ijumaa iliyowekwa na imani za ibada hizi za opotofu na kwenye “ufufuko” wao ulioratibiwa rasmi uadhimishwe kila mwaka siku ya mungu jua.

Hakuna kitu kwenye imani ya Kikristo kinachojulikana kama maadhimisho ya sikukuu ya Easter kwa namna yoyote ile. Ni imani ya uzushi nay a uwongo. Sisi hatuko miongoni mwa wale waliofarakana na Kanisa hili la Roma mwaka 154 bali tunajaribu kubakia kwa amani sana sambasamba nao.

 

Mara tu baada ya kuiingiza sikukuu hii takriban mwaka 154 BK, walianza kuiyumbisha na kuibadilisha teolojia ya Ukristo na ulipofika mwaka 170 shule ya Alexandrian ilianza kuiingiza imani na mafundisho ya Ubinitarian kwenye Ukristo na kulinganisha muundo wa imani yao moja kwa moja kwa Yesu Kristo. Walifanya hilo kwa mbinu ya kumuinua Kristo juu kuliko elohim wote kwenye Jeshi la Malaika wa Mungu, jambo ambalo halikuwahi kufanyika hadi kwenye karne hii ya pili.

 

Hadi kufikia mwaka 192 walikuwa wameshalichukua kanisa lote la Roma na walikuwa kwenye nafasi nzuri ya kuyaeneza mafundisho yao ya kizushi kwenye Ukristo kwa ujumla. Victor, askofu wa Roma na mafarakano makubwa ambayo kanisa halijawahi kamwe kuyaona, baada ya yeye kuwa askofu mwaka 192 BK alilitangaza Kanisa la Mungu la Quartodeciman kuwa limelaaniuwa. Akaamuru kuwa ili kuwa kwenye ushirikiano na Roma basi ni lazima kukubaliana na maadhimisho ya Sikukuu ya Easter badala ya Pasaka. Matokeo ya tangazo hili ni kwamba Kanisa la Celtic la Uingereza lililipuuzia Kanisa la Roma na wakaendelea kivyaovyao kama walivyokuwa wa Quartodecimans hadi walipolazimishwa hadi kwa upanga ili wakubaliane mafundisho haya ya uwongo ya Roma. Hili lilitokea pia hata mwaka 664 BK kwenye sinodi ya Hilda wa Abbey huko Whitby. Watrinitarian kwa mara nyingine tena waliandika tena upya na kiukweli historia ya kanisa.

 

Ubinitarianism ulitumika ili kuiharibu teolojia ya kweli ya Kanisa tangu mwaka 170 BK. Mwaka 325 huko Nicaea Ubinitarianism ulitangazwa kuwa ni fundisho la Kanisa lote ulimwenguni linalosimamiwa na kimaongozi kutoka Roma. Maaskofu wa Kiyunitariani wa lanisa walifukuzwa na mawazo yao ya kiimani ya Arius kwa amri ya mfalme Constantine.

 

Na ilipofika mwaka 327, ni miaka miwili tu baadae Constantine akagundua kuwa mafundisho ya Kibinitarianism yalikuwa ni ya uwongo na uzushi usio na mashiko yoyote na kuwa ndiyo maana makanisa yaliyokuwa nje ya Roma walikataa kuyapokea na kukubaliana nayo, ndipo alipowaita tena maaskofu wote waliokuwa wamefukuzwa na kuanzisha imani ya Uyunitariani kwenye dola yake, waliobakia, pamoja na wengine waliokuwa kwenye himaya ya Julian muasim au mkengeufu, hadi mwaka 381 BK wakati Gratian alipofanya makosa kwa kumteua Theodosius, mtu aliyezaliwa Uhispania awe ni Liwali wa Constantinople. Alikuwa ni mfuasi wa mafundisho ya Athanasias. Imani ile inawatumia Wacappadocians, waliokuwa wameishaanzisha na kushamirisha fundisho la Mungu wa Utatu na kuipitiliza ile ya Ubinitarianism. Ndipo imani ya Utatu au Utrinitaria ikazaliwa rasmi.

 

Kutoka tangazo la imani la Constantinople wakaandika tena mafundisho ya Nicaea na tangazo potofu la Matamko ya Imani ya Mtaguso wa Nicaea ilizaliwa kwenye kile kilichokuwa Ukristo wa uwongo.

 

Ubinitarianism ni chombo ambacho kilitumika kuudhoofisha Ukristo kwa awamu ya kwanza na hatimaye kwa shuruti ya kijeshi ili kuitokomeza teolojia ya kwanza asilia na kuikomesha kabisa.

 

Waandishi wa uwongo kuhusu historia ya Ukristo na mafundisho yake wanajitahidi kudai kwamba Ubinitarianism ulikuwa ndiyo fundisho asilia la kwanza la Ukristo. Waandishi hao hao katika ulimwengu wa Utrinitareiani mwishoni mwa karne ya ishirini huko Marekani, walifanya bidii kubwa kuhalalisha sababu zao za kuchukua na kuiamini imani ya Utrinitariani, kama vile kwenye makundi kadhaa ya SDA, waliandika vitabu na majarida yaliyotafsiri vibaya teolojia ya kwanza ya kanisa kwenye juhudi zao za kuonyesha kwamba kanisa lilikuwa ni la Ubinitariani huko mwanzoni. Madai yao yanatuama kwenye sababu zinazoonyesha kukosa uelewa tu wa Maandiko Matakatifu na msfundisho ya Kanisa la kwanza na migingano ya kihistoria iliyojitokeza. Madai yao haya ya uwongo yameelezewa kwa kina kwenye jarida la Tafsisri Mbaya ya Wabinitariani na Watrinitariani Kuhusu Teolojia ya Kwanza ya Uungu (Na. 127B) Unitarian and Trinitarian Misrepresentation of the Early Theology of the Godhead (No. 127B)].

 

Mmoja wa hawa “wasomi” wa hizi dini za uwongo zilipoonyesha kuwa hakuwa na sifa za kiteolojia au za kidini, kwa namna ya kisirisiri aligeukia Kujipa Sifa ya Udaktari wa Teolojia na kuwafundisha wengine ili kujifunika na mapungufu haya. Hatahivyo, wakati kiwango chake cha chuki kilipojulikana na akadharauliwa na kuumbuliwa hadharani aliumbuliwa na kujulikana kuwa kumbe aliinunua kwa fedha huko India, ndipo akatoweka na kupotea tena. Hamali alipokuwa anapatumia kama nyingi panatumiwa na kanisa la LCG kwa kuendelea hadaa ili kuwasaidia, dhidi ya kipingamizi cha wao kuwa ni washiriki tu wenye udadisi na mwasho wa masikio.

·         Fundisho la Ubinitarianism lilitumika na mapandikizi na wadanganyifu au wahubiri wa uwongo kwenye Makanisa ya Mungu  mwishoni mwa karne ya ishirini na hata sasa kwenye karne hii ya ishirini na moja ili kuipotosha teolojia ya Makanisa ya Mungu. Ilianza kwa kuingiza Wajesuita kwenye kanisa la SDA huko Marekani. Baada ya Myunitariani aliyekuwa akiifuata Biblia Uriah Smith kufariki mwaka 1931 mapandikizi hawa wakaanza kudai kwamba waamini Ubinitariani na wakaendeleza mchakato huu hadi kukubalika kwa Utrinitariani. Mnamo mwaka 1978 wakatangaza rasmi kuwa wao wapo kwenye kundi la waamini Utatu au Utrinitariani na kwa sasa wengi wao hata hawajui kuwa hii ni kazi iliyofanywa kwa kipindi kifupi cha hivi karibuni tu.

·         Walijiingiza kwenye Kanisa la Worldwide Church of God wakitumia mbinu za aina mbili. Waliitumia imani ya Utrinitarian ili kuliingiza kwenye imani ya Ubiinitarianism ili kuishinda imani iliyoonekana wazi kuwa yakijinga ya Herbert W. Armstrong ya Uditheism (soma jarida la Uditheism (Na. 76B) [Ditheism (No. 76B)].

 

Baadhi ya wanateolojia uchwara kama niliowataja hapo juu wanasema kuwa Herbert Armstrong alifundisha imani ya Ubinitarianism, jambo ambalo ni uwongo wa wazi kabisa. Hata hivyo agenda ilikuwa ni kuliteka Kanisa la Mungu na kulipeleka kwenye Utrinitariani wakitumia Ubinitarianism kama gari lao. Mbinu hii ilifanya kazi na kufanikisha kwenye karne za pili nay a tatu, na ilitumika tena kipindi cha Matengenezo, na kama ilifanikiwa hivyo kwa nini isifanikiwe tena leo? Hata hivyo, hakuna mtu hapa ulimwenguni anayediriki tena kufikiri kwa kina na kwa udadisi, au je, yupo yeyote anayefanya hivyo?

 

Kanisa linaloitwa Church of God (Seventh Day) liliingiliwa pia, na mnamo mwaka 1995 likatangaza kuwa wamekuwa wakati wote wakiamini imani ya Ubinitariani, jambo ambalo ni uwongo mwingine na wa kutisha. Baadhi ya wahubiri wao walishikwa na mshangao. Na baadhi yao waliokuwa nje ya Marekani waliamua kuachana na kanisa hili.. leo hii hakuna hata tawi moja la kanisa hili la COG (SD) barani Afrika, tunalolijua, ambalo lipo na nao linaloendelea kuhubiri ama kufundisha mafundisho haya ya kizushi. Karibu wote wamejiunga nasi kanisa la CCG.

 

Uelewa wa Kiimani wa Watunitariani wa Imani Kali

 

 Mbinu nyingine ya pili iliyotumika ni kuwaingiza waabudu mashetani maarufu kama Freemasons ambao waliingia kwenye Maanisa ya Mungu lakini walikuwa hawajazitubia kwa dhati dhambi zao. Waliingia kwa gea ya kujifanya kuunga mkono Uyunitariani wa Itikadi Kali unaodai kwamba Kristo hakuwahi kuishi wala kutenda lolote zama za nyuma za kabla ya kuzaliwa kwake kimwili hapa duniani. Watu hawa walimudu hata kujihudhurisha kwenye makutaniko ya ibada za kanisa la UCG na kufanya idadi yao kuwa ni zaidi ya 10% ya wanaohudhuria ibada na hata ya watumishi.

 

Shambulio la pamoja liliwashuhudia waunga mkono wa Ubinitariani waliwakilisha kimakosa mafundisho ya Uyunitariani wa Imani Kali. Inawezekana ikatokana na kutoelewa kwa kadiri walivyojionyesha hivyo kila mara. Basi na tuupe muda wakati, utatuambia.

 

Kuna kundi muhimu la Waingereza/Wayunitaria wa Imani kali wamebaki kama masalio ya kwenye kanisa la WCG wanaodhania kuwa wanampendeza Mungu kwa kuendelea kushikilia kuamini uzushi huu. Wanaamini kuwa Mungu na Kristo walikuwa ni mtu mmoja aliyekuwa pale Sinai. Kisha wanashikilia kuamini kwamba huyu Mungu aligawanyika na kuwa viumbe wawili wakati wa kuja kwa mmoja wao azaliwe kimwili hapa duniani. Hawana habari ya kile Kristo na mitume walichokuwa wanakisema. Ni fundisho la Wabinitarinai kabisa la mungu Attis lilalojirudia tena.

 

Kwa hiyo mafundisho yanajirudia kutegemea tu na jinsi asili ya uwili wa Mungu inayoelezewa kwenye kwa wakati wowote.

Kinachotakiwa kieleweke hapa ni kwamba wengi wa watu hawa hawajui wanalosema na hawafananishi na Maandiko Matakatifu na makosa ya kizushi yaliyo kwenye mtazamo wao. Na la muhimu zaidi ni kwamba hawaelewi uharibifu wanaoufanya kuwathiri waumini wapya na wachanga kwenye imani.

Mafundisho ya Sabellianism pia yaliingia kanisani huko Uchina baada ya kipindi cha mwanzo wa miaka ya 1850 na imani ya Kanisa lijulikanalo kama True Jesus Church ilianazshwa baada ya hapo. Walidai na wanaendelea kuamini hivyo hadi leo kwamba Yesu Kristo ndiye Baba pia na kwamba kuna Mungu mmoja tu na Kristo ndiye yeye huyo. Hii ni aina nyingine tu ya Uyunitariani wa Imani Kali ambayo hata Wabinitariani wanaiona haina mashiko yoyote. Mafundisho kama haya yanapaswa yasahihishwe kabla hata hayajatumika kwenye imani na kwa kweli kuyapiga marufuku ili yasilete madhara kwenye imani.

 

Ughosishaji wa mafundisho wa kiteolojia, mbali ya makosa haya makubwa ya huko Uchina, yapo pia nchini Marekani na yalianzishwa na Bi. Ellen G. White na yaliendelea hadi kwenye kanisa la WCG yakipitia kwa Herbert Armstrong na Herman Hoeh na Watrinitarian walimuuliza maswali huko Pasadena, ambao walikusudia kuimaliza kazi. Waliendelea kujipenyeza pia kwenye aina mbalimbali hasa wakijifanya ni washirika wa Church of God (SD) na kwenye kanisa la Seventh Day Baptists likiwa kwa sehemu kubwa na waumini wake wengi nchini Marekani. 

 

Uyunitariani wa Imani Kali ulizidi kushika kasi pia hadi kwenye Baraza Kuu la Maamuzi la Church of God (Seventh Day) na wanachama wake hupuuzia na hukosea kimahubiri Maandiko Matakatifu kwa sababu tulizoziona hapo juu. Viongozi wake wako mbali sana na ukweli, bali watu wake wanajiunga na sisi kwenye nchi mbali mbali kwa jinsi kadri wanavyoenhelea kuyachunguza mafundisho yao kwa karibu na kuwagudnua kuwa hayafuati Maandiko Matakatifu.

 

UCG lina angalau mafundisho manne yahusuyo Asili ya Mungu na yanayorekebishwa wakati wowote. Hata hivyo, kanisa hili la  LCG sio zuri sana.

 

Kuna imani za Watrinitarians, Wabinitarians, Wayunitariani wa Imani Kali, Waditheists na Wayunitariani wachache sana wanaoyafuata Maandiko Matakatifu (wakati mwingine wanaitwa Wasabatariani na wakati mwingine na kimakosa wanaitwa Waarian hasa wanaitwa hivyo na Wattinitarians) wasiochukuliana au kuafikiana na huduma hii, huku wakichukuliana na wengine wote wanaoamini aina zote za uzushi. Hii inaweza kutuambia kila tunachohitaji kukijua wakati watakapoangikwa.

 

Hizi imani za kizushi na potofu za Kibinitarian/Uyunitariani wa Imani Kali sio kwamba hazina madhara na zinapaswa ziumbuliwe kwa jinsi zilivyo na ziondolewe na kuwekwa kando ya Makanisa ya Mungu. Ni zoezi la makusudi na linakomesha uwezo wa Kanisa la Mungu kuenea katika Siku za Mwisho.

 

Mungu ataliwezesha na kusahihisha makosa. Hataweza kuwatumia kama walivyo katika Siku za Mwisho.

 

Kila mmoja na kila mahali alipo anapoaswa aelimishwe vyema jinsi ya kushughulikia mambo haya.

 

Tutajikusanya kiimani sasa ili kushughulika na nguvu za Mnyama anayekuja au za Dola ya Mnyama.

q