Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[021L]
Ufafanuzi wa Kitabu
cha Malaki
(Toleo La 1.0
20141108-20141108 )
Jarida hili la
ufafnuzi wa Malaki ni andiko la Kanoni ya Agano la Kale. Mtindo wake unaonyesha
pia nuru au ashirio la kitabu cha Zekaria.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 2014 Wade Cox)
(tr. 2016)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu
bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote
atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja
ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia
yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ufafanuzi wa Kitabu cha Malaki
Mathayo 23:35 inasema
kuwa Zekaria alikuwa ameuawa katikati ya hekaluni na madhabahuni. Aliuawa kabisa
na makuhani, akinuia kuikomesha au kuizima huduma yake.
Mathayo 23:33-36
33 Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya
jehanum? 34 Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma
kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na
kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza
mji kwa mji; 35 hivyo ije juu yenu damu yote ya haki
iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya
Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.
Kristo anawaambia
makuhani na hii ni hatua ya maana sana. Inaonyesha kuwa Zekaria aliuawa kwa
sababu fulani ijulikanayo. Zekaria 1:7 inaonyesha kuwa ni Zekari’a, mwana wa Ido,
nabii. (Soma kitabu cha Josephus, cha Wars of the Jews (Vita ya Wyahudi),
4.5.4 ili kupata ufafanuzi, pia na bangokitita za Bullinger.) Hii imeelezwa
kama inapoibuka kwenye tatizo lililo kwenye vitabu vya Malaki na Zekaria.
Tuna Zekaria
mmoja aliyeuawa yapata miaka 800 ya nyuma. Nabii Zekaria aliuawa miaka 400 huko
nyuma na kisha miaka 34 baada ya Zekaria wa tatu, mwana wa Baruku ni tatizo
kubwa sana. Kumbuka pia kuwa Isaya aliuawa kwa kuchanwa kwa msumeno vipande
viwili toka kichwani hadi miguuni na watu hawahawa. Watu hawa hawawaheshimu
kabisa manabii a Mungu. “Watu hawa” ni sawa na kama walivyo viongozi wa kidini
au ya jamii za kidini za makanisa makongwe ya zamani. Kanisa tunaloliona na
tunayoyaheshimu sana siyo kanisa kongwe la zamani sana na haya yanayofuata
mrengo wa kipapa yanayosaidiwa na Majesuiti wanaowaua watu kwa malengo yao.
Kwenye sura za kitabu
cha Zekaria kuna mabadiliko kidogo kwenye mtindo na ule unaochukuliwa kuwa wa
Malaki uliofanya kazi na akaanza kuandika na kumaliza sura zote za kitabu cha Zekaria
na ambacho ndicho kinachohitimisha utaratibu wa uandishi wa Kanoni. Ilikuwa ni
kutokana na Iskanda au Alexander Mkuu ambaye alishinda mwaka 323 KK. Ezra mwandishi
alifariki wakati huo huo. Sedum Olam Rabbah kinaonuesha mwongozo kwamba walifariki
wakati mmoja huohuo. Kisha walilinganisha na Kanoni ya Agano la Kale tangu wakati
wa kufa kwake mwaka 323 KK. Vitabu hivi viliorodheshwa na kuchapishwa na
kutumwa mnamo mwaka 321 KK.
Malaki ni mmoja
vitabu sita visivyopewa tarehe ya wale wanaojulikana kama Manabii kumi na
wawili Wadogo. Kitabu chake kinaonyesha kinaonyesha kwamba ibada za Hekaluni
pamoja na dhabihu zake zilirejeshwa kabisa bali ilikuwa ni utaratibu au kawaida
ya kiibadada na unafiki vilivyokuwa vimeshika kasi katika siku za huduma ya Bwana
iliyoonekana kufanyika kikamilifu sana wakati wa Malaki. Siyo kipindi cha
karibu sana walizuia ushawishi wa kina Ezra na Nehemia ulioondoka kuliko
ulipoanza upotoshaji na vita viliendelea kwa wazi sana kwenye Malaki 1:7-8 na
3:8 nk.
Bullinger anakosea
hapa. Wakati alipokufa Ezra, halikuwa ni suala la Malaki ambapo ndipo ulionekana
mdororo; Ezra alikuwa anakufa ndipo mdororo ulikuwa unaanza na Malaki alikuwa
anayapitia kabla Ezra hajafa kwa kuwa Kanoni ilikuwa imefungwa na kitabu cha
Malaki. Kama kingekuwa hakijaandikwa kabla ya kufa kwa Ezra, basi kisingekuwa
kimejumuishwa na kukubalika kuwa ni kama ni cha mmoja wa Manabii hawa Wadogo
Kumi na Mbili. Kilijulikana kama ni unabii wa mwisho kutoka kwa Malaki na Ezra
haki kuja kwa Yohana Mbatizaji. Kulikuwa na manabii waliokuwa wakihudumu
kanisani lakini hakuna hata mmoja kati yao aliyepokea maelekezo ya moja kwa
moja kutoka kwa Bwana yenye kuhusiana na jambo linguine lolote kisawasawa.
Kulikuwa na manabii Hekaluni waliojua kuwa Kristo alikuwa anakwenda kuzaliwa na
walioijua siku yenyewe aliyokuwa anakwenda kuwekwa wakfu Hekaluni na walikuwa
wanamngojea wamuone akiletwa na Yusufu na Mariamu mbele ya Kuhani Mkuu na kwa
Makuhani wa Hekalu. Mtu mmoja ambaye maisha yake yalikuwa yamelindwa ili kwamba
awepo na amshuhudie Masihi wa Mungu alimpa ruhusa. Kwa hiyo, unabii haukukoma
bali shuhuda zilizoandikwa kwenye Biblia ndizo zilikoma.
Mtindo wa
kiuandishi wa sura chache za mwisho za Zekaria ni sawa tu na ule wa kitabu cha
Malaki na unatofautiana na sura za zamani na inadhaniwa kuwa Malaki alimaliza
kitabu kwa ajili ya Zekaria, wakati Zekaria alipouawa ndani ya Hekalu na karibu
na madhabahuni. Zekaria alikuwa ni nabii mkuu na kitabh chake na kazi yake
vinaumuhimu sana, lakini makuhani hawakufikiri chochote walipomuua, na ndivyo
pia hawakufikiri lolote walipokuwa wanamuua Isaya. Waliwaogopa kina Samweli na
Eliya lakini walimuua kwa kumpiga “katikati ya kichwa, utosini.”
Moja ya matatizo
tuliyonayo ni kwamba mlolongo wa uzao na wa matukio wa Bullinger unamakosa. Tunauona
mwaka 323 KK kama ndio alikufa Ezra na kuzaliwa kwa Masihi kolikuwa mwaka 6 KK,
kipindi cha takriban miaka 317. Wanasema kuwa matengenezo ya mwaka wa
Artashasta yalifanywa miaka 400 na kwamba siyo sahihi. Mlolongo wa matukio wa
Bullinger siyo sahihi na tunahitaji kujihadhari na jambo hilo. Mkururu wa
nyakati na utawala wa wafalme vinaeleweka vizuri sana sasa kuliko ilivyokuwa
kipindi cha Bullinger alipokuwa anaandika. Katika mwisho wa miaka 130 ya mwisho
tumekuwa katika maarifa kwa haraka haraka sana. Kwa mfano, anaweka siku ya mwisho
ya Ezra kuwa ni siku ya 1 Nisan 403 KK, wakati Hekalu lilikuwa limejengwa tena
mwaka 419 KK na Nehemia alitumwa aende huko katika wiki ya 7 ya miaka ambayo ni
miaka 49 baada ya mwaka 419. Ezra alifariki mwaka 323 KK, na siyo mwaka 403. Kwa
hiyo siku au tarehe ambazo utakazoziona kwenye tafsiri ya Companion Bible siyo
za kweli.
1 Ufunuo wa neno la Bwana
kwa Israeli kwa mkono wa Malaki 2 Nimewapenda
ninyi, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Umetupendaje? Je! Esau siye ndugu
yake Yakobo? Asema Bwana; ila nimempenda Yakobo; 3 bali
Esau nimemchukia na kuifanya milima yake kuwa ukiwa, na urithi wake nimewapa
mbweha wa nyikani. 4 Ijapokuwa
Edomu asema, Tumepondwa-pondwa, lakini tutarudi na kupajenga mahali palipoachwa
hali ya ukiwa; Bwana wa majeshi asema hivi, Wao watajenga, bali mimi
nitaangusha; na watu watawaita, Mpaka wa uovu, na, Watu ambao Bwana
anawaghadhabikia milele. 5 Na
macho yenu ninyi yataona, nanyi mtasema, Bwana ndiye mkuu kupita mpaka wa
Israeli. 6 Mwana humheshimu baba
yake, na mtumishi humcha bwana wake; basi, kama mimi ni baba yenu, heshima
yangu iko wapi? Na kama mimi ni bwana wenu, kicho changu ki wapi? Bwana wa
majeshi awauliza ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau jina langu. Nanyi mwasema, Tumelidharau
jina lako kwa jinsi gani? 7 Mnatoa
chakula kilichotiwa unajisi juu ya madhabahu yangu Nanyi mwasema, Sisi
tumekutia unajisi kwa jinsi gani? Kwa sababu mwasema, Meza ya Bwana ni kitu cha
kudharauliwa. 8 Tena mtoapo sadaka aliye
kipofu, si vibaya? Na mtoapo sadaka walio vilema na wagonjwa, si vibaya? Haya!
Mtolee liwali wako; je! Atakuwa radhi nawe? Au atakukubali nafsi yako? Asema
Bwana wa majeshi. 9 Na sasa, nawasihi,
ombeni fadhili za Mungu, ili atupe neema; ikiwa jambo hili limetoka katika mikono
yenu; je! Atawakubali nafsi zenu? Asema Bwana wa majeshi. 10 Laiti angekuwapo kwenu mtu mmoja wa kuifunga
milango; msije mkawasha moto bure madhabahuni pangu! Sina furaha kwenu, asema
Bwana wa majeshi, wala sitakubali dhabihu yo yote mikononi mwenu.
Hapa ndipo
lilipofikia Kanisa la Mungu mwishoni mwa zama za wafuasi wa Armstrong. Hakuna
mtu aliyethubutu kufanya kitu bila sababu. Hii ndiyo moja ya sababu
inayolifanya kanisa la CCG lisiwe na watumishi wa kulipwa, kwa kuwa andiko hili
la Malaki linaonyesha hatima iliyofikia utaratibu huu na pia kwamba Kristo mwenyewe
aliukemea na utaratibu ambao ulikuwa umeoza na hakuna aliyefanya kazi kwa
minajiri ya kumpenda Mungu. Ilikuwa ni biashara tu. Mungu aliwatawanya kama
alivyolitawanya Hekalu. Aliwapelekea Kristo alipofikia umri wa miaka 30. Alikujafanyika
kuwa Kuhani mnamo mwaka 27 BK na tangu mwaka 28 BK alianza misheni yake na
kanisa lilianzisha. Liliendelea hivyo kwa Yubile 40 na lipo kwenye awamu ya
mwisho wa Yubile ya mwisho sasa, Yubile ya 120.
Mwaka 1987 Joseph
Tkatch alianza safari yake ya kiutalii akiizunguka nchi yote ya Marekani, na
ulimwenguni kote kwingine akihubiri kuwa tulikuwa kwenye zma ya Ufunuo sura ya 11,
aya za 1 na 2, na kwamba Mungu alikuwa ameanza kulipima Hekalu la Mungu. Mwaka 1987
ulikuwa ni mwanzo wa miaka 40 ya mwisho ya Yubile hii na mwanzo wa parole au
hukumu hadi mwaka 2027. Ulikuwa ni mwaka wa tatu wa kalenda takatifu.
Sura ya kwanza ya
Malaki inaendana na unabii wa kuanzia mwaka 27 BK, hadi kufa kwa Kristo,
Pentekoste, miaka 40 hadi kwenye kuangamia kwa Hekalu huko Yerusalemu na tukio
la kutawanywa kwao lililotukia mwaka 70 BK. Kanisa lilikubwa na tatizo hilohilo
kwenye miaka 40 ya mwisho na hipo kilianza ‘kizazi hiki’, usemi ambao Kristo aliutumia
kwenye Injili yake aliposema kuwa ‘kizazi hiki’ hakitapia hadi Masihi atakapokuja
na kuyaangamiza mataifa ya duniani na kuyapeleka utumwani kwa vitasa vya hasira
ya Mungu. ‘Kizazi hiki’ kinschotajwa hivi na Kristo kilianza mwaka 1987.
11 Kwa maana tokea maawio
ya jua hata machweo yake jina langu ni kuu katika Mataifa; na katika kila
mahali unatolewa uvumba na dhabihu safi kwa jina langu; maana jina langu ni kuu
katika Mataifa, asema Bwana wa majeshi. 12 Lakini
ninyi mnalitia unajisi, kwa kuwa mwasema, Meza ya Bwana imetiwa unajisi; na
matunda yake, yaani, nyama yake, hudharauliwa. 13 Tena
mwasema, Tazama, jambo hili linatuchokesha namna gani! Nanyi mmelidharau, asema
Bwana wa majeshi; nanyi mmeleta kitu kilichopatikana kwa udhalimu, na kilema,
na kilicho kigonjwa; ndivyo mnavyoleta sadaka; je! Niikubali hii mikononi
mwenu? Asema Bwana. 14 Lakini
na alaaniwe mtu mwenye kudanganya, ambaye katika kundi lake ana mume, akaweka
nadhiri, ila amtolea Bwana kitu kilicho na kilema; kwa maana mimi ni Mfalme
mkuu, asema Bwana wa majeshi, na jina langu latisha katika Mataifa.
Maendeleo yote ya
kanisa na kwa Mafarisayo, kuendelea kote kwa Masadukayo kwenye mfumo au huduma
za Hekaluni na kuanguka kwake kulitokana na Masihi. Baada ya kuuawa kwa Kristo
Masadukayo na huduma za Hekalu vilianza kuongezeka na zikafanyika potofu zaidi
na zaidi. Na vivyohivyo kanisa nalo likazidi kupotoka zaidi na zaidi. Kitendo
cha kusimamisha au kukataza maadhimisho ya Idi za Pasaka na Mikate Isiyotiwa
chachu kwa siku zote saba kamili tangu mwaka 1965 kimeonyeshwa kwenye hii. Hadi
kufikia mwaka 1967 ilikuwa hakuna mahali popote ilipoadhimishwa na Kanisa la
Mungu. Hili lilikuwa ni
sehemu ya tatizo la kuziondoa sadaka na ibada halisi ya Mungu. Inafuatiwa na
jinsi ilivyokuwa kwenye wakati wa Kristo na ilivyotokea baada ya kifo cha Ezra
hadi wakati wa Kristo wakati ilipofanyika kuwa mbaya zaidi na ndicho cha miaka
ya toba iliyowekwa tangu kifo cha Kristo hadi mwaka 70 BK ikiweka kipindi cha
hukumu kwa makuhani wote kwenye mwisho wa Kipindi cha huduma za Hekaluni.
Kipimo kimewekwa
sasa kwa Makanisa ya Mungu na makuhani au makasisi wake wamekuwa wakihukumiwa sasa.
1 Na sasa, enyi makuhani,
amri hii yawahusu ninyi. 2 Kama
hamtaki kusikia, na kama hamtaki kuitia moyoni, ili kulitukuza jina langu,
asema Bwana wa majeshi, basi nitawapelekeeni laana, nami nitazilaani baraka
zenu; naam, nimekwisha kuzilaani, kwa sababu hamyatii haya moyoni. 3 Angalieni, nitaikemea mbegu kwa ajili yenu, nami
nitapaka nyuso zenu mavi, naam, mavi ya sadaka zenu; nanyi mtaondolewa pamoja
nayo
Andiko hili
limeelekezwa kwa makuhani na ukweli wa kwamba sikukuu zao zimekosewa zote. Armstrong
na Kanisa la Mungu waliiingiza na kuifuata Kalenda ya Hilleli ambayo ilitungwa
au kubuniwa tu na kuchukuliwa kuwa ni kalenda ya Kiyahudi mwaka 358 BK. Haikuwepo
huko nyuma hadi ilipobuniwa tu wakati huu, na utaratibu wa maahirisho uliwekwa
kwa udanganyifu tangu kuangamizwa kwa Hekalu. Kwa hiyo, siyo tu kwamba ni Yuda
tu ndio wanaotabiriwa hapa kwenye Malaki kuwa wamepotosha maadhimisho ya
sikukuu na wakazifanya zisishabihiane au zisiendane sawa na zilivyotarajiwa
kuwa bali pia Kanisa la Mungu katika nyakati za mwisho chini ya Armstrong liligeuka
na kuuuandama ukengeufu wakiitumia kalenda hii hii potofu kama walivyofanya
Yuda. Mwisho wa zama ya Wasardi ikiongozwa na Herbert Armstrong ulikuwa ndiyo
kipindi cha upotofu zaidi kuziliko zote za watu walioshikilia maongozi ya
Kanisa la Mungu. Teolojia ilipotoshwa, uongozi ulikuwa mbovu na mpotofu na
wafuasi wake walijikuta wakiwa chini ya mraruo wa kwato.
Kumbuka kuwa aya ya 3 kwenye tafsiri ya KJV inasomeka
hivi:
3 Angalieni, nitaikemea
mbegu kwa ajili yenu, nami nitapaka nyuso zenu mavi, naam, mavi ya sadaka zenu;
nanyi mtaondolewa pamoja nayo.
Tunaona kuwa moja
ya sikukuu itawaowaondoa makuhani hawa. Kenye mfano wa kwanza ulikuwa ni kwenye
sikukuu ya Pasaka mwaka 30 BK iliyoiondolea mbali huduma ya kikuhani kwa kifo
cha Kristo. Alikuwa amekisha wachagua wale 70 na mamlaka ilikuwa imekwishaondolewa
kutoka kwa makuhani na kupewa kanisa. Wakati Roho Mtakatifu alipokuja siku ya
Pentekoste ya mwaka 30 BK kwa nguvu na uweza, ndipo utaratibu wote mzima wa
makuhani wa Israeli au wa Yuda uliondolewa na kuharibiwa kwa kipindi cha miaka
arobaini.
4 Nanyi mtajua ya kuwa
mimi nimewapelekeeni amri hii, ili agano langu liwe na Lawi, asema Bwana wa
majeshi. 5 Agano langu naye
lilikuwa agano la uhai na amani; nami nikampa ili aogope, naye akaniogopa,
akalicha jina langu. 6 Sheria
ya kweli ilikuwa kinywani mwake, wala udhalimu haukuonekana midomoni mwake;
alikwenda pamoja nami katika amani na unyofu, na kuwageuza wengi hata wakaacha
uovu. 7 Kwa maana yapasa midomo
ya kuhani ihifadhi maarifa, tena yawapasa watu kuitafuta sheria kinywani mwake;
kwa kuwa yeye ni mjumbe wa Bwana wa majeshi.
Ni wajibu wa makuhani
na hadi kufikia kufungwa kwa Kanoni ya Agano Jipya Malaki alikuwa anasema kuwa
hili ndilo lilikuwa jukumu lao. Maandiko yanatueleza kwamba majukumu haya
lilipewa Kanisa na Masihi. Sisi tu wajumbe wa Bwana wa Majeshi. Hawayapati
majukumu haya. Tumepewa majukumu katika nyakati za mwisho la kuzibeba siri za
Mungu na kufundisha ujio wa Masihi pamoja na mashahidi wake na kushughulikia
kuyatatua matatizo hayo. Huduma ya kikuhani kwa pande zote mbili, yaani kwa
kanisa na Hekalu, zimeondolewa mbali kabisa.
8 Bali ninyi mmegeuka
mkaiacha njia; mmewakwaza watu wengi katika sheria; mmeliharibu agano la Lawi,
asema Bwana wa majeshi.
Hivyo basi, itikadi
za kiantinomia ndilo tatizo moja kubwa sana kuliko yote kwenye imani ya dini ya
Kikristo kuwahi kutokea katika karne ya 21. Mfumo wote wa imani ya
Kikristo ni ya kiantinomiani na wamejikwaa kwa kuipotoa Sheria. Wahayudi wenyewe
wameikiuka sharia kwa kuifuata Talmud.
9 Kwa sababu hiyo mimi
nami nimewafanya ninyi kuwa kitu cha kudharauliwa, na unyonge, mbele ya watu
wote, kama vile ninyi msivyozishika njia zangu, bali mmewapendelea watu katika
sheria. 10 Je! Sisi sote hatuna
Baba mmoja? Mungu aliyetuumba siye mmoja tu? Basi, mbona kila mmoja wetu
anamtenda ndugu yake mambo ya hiana, tukilinajisi agano la baba zetu? 11 Yuda ametenda kwa hiana, na chukizo limetendeka
katika Israeli, na katika Yerusalemu; maana Yuda ameunajisi utakatifu wa Bwana
aupendao, naye amemwoa binti ya mungu mgeni.
Kama hatuamini
hilo basi makanisa ya karne ya 21 yameolewa na mungu mgeni na kwa
kweli yamekuwa mabinti wa mungu mgeni na tunakuwa hatujafunguliwa tu macho yetu.
12 Bwana atamtenga mtu
atendaye hayo, yeye aliye macho, na yeye ajibuye, atamtenga na hema za Yakobo,
pia atamtenga yeye amtoleaye Bwana wa majeshi dhabihu.
Kwa hiyo yeyote
afanyaye hivyo atakatiliwa mbali, hata wale wanaozitoa sadaka Hekaluni.
13 Tena mnatenda haya nayo;
mnaifunikiza madhabahu ya Bwana kwa machozi, kwa kulia na kwa kuugua, hata
asiiangalie tena hiyo dhabihu, wala kuitakabali mikononi mwenu na kuiridhia. 14 Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa
sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda
mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako. 15 Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa
na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu?
Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake
mambo ya hiana. 16 Maana mimi nakuchukia
kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli; naye aifunikizaye nguo yake kwa
udhalimu namchukia, asema Bwana wa majeshi; basi jihadharini roho zenu, msije
mkatenda kwa hiana. 17 Mmemchokesha
Bwana kwa maneno yenu. Lakini ninyi mwasema, Tumemchokesha kwa maneno gani? Kwa
kuwa mwasema, Kila atendaye mabaya ni mwema machoni pa Bwana, naye huwafurahia
watu hao, au, Mungu mwenye kuhukumu yuko wapi? Kwa maana yeye ni mfano wa moto
wa mtu asafishaye fedha,
Kwa maneno mengine
ni kwamba kwanini mungu hakushughulikia mambo haya? Sura ya pili inawaambia
,oja kwa ,oja makuhani, makutaniko, matendo au mwenendo wa makuhani na wa watu,
nia zao, hali yao ya kuwapendelea watu na kushindwa au makosa ya familia zao.
Hali hii inaweza kuonekana kwenye jamii zetu sasa na kwa jinsi mfumo wa kijamii
ulivyoweza kuharibika na kupotoka.
1 Angalieni, namtuma
mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta
atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia,
angalieni, anakuja, asema Bwana wa majeshi. 2 Lakini
ni nani atakayestahimili siku ya kuja kwake? Au ni nani atakayesimama
atakapoonekana yeye?
Andiko hili
limenukuliwa kwenye Mathayo 11:10, Marko 1:2 na Luka 1:76 na 7:27. Bullinger anadai
na kuamini kuwa maneno haya hayakukilenga kizazi chetu; bali yalikilenga kizazi
cha wakati wa huduma yake Bwana na katika nyakati zake. Huyu “Mjumbe wangu”
anaonekana moja kwa moja kuwa ni Yohana Mbatizaji.
Mathayo 11:10
10 Huyo ndiye aliyeandikiwa haya, Tazama, mimi
namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako mbele yako.
Haya ni maneno
anayoyasema Kristo kutoka kwenye aya ya 7:
7 Na hao walipokwenda zao, Yesu alianza kuwaambia
makutano habari za Yohana, Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi
ukitikiswa na upepo? 8 Lakini mlitoka kwenda kuona
nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Tazama, watu wavaao mavazi mororo wamo
katika nyumba za wafalme. 9 Lakini kwa nini mlitoka?
Ni kuona nabii? Naam, nawaambia, na aliye mkuu zaidi ya nabii.
Kwa hiyo Kristo alisema
kuwa alikuwa Yohana Mbatizaji ambaye ndiye alikuwa huyu mjumbe aliyetumwa ili
aitengeneze njia ya Bwana. Hata hivyo kuna nabii mwingine na sauti iliyotumwa
kwa ajili hiyo katika siku za mwisho naye hatokei kwenye Kabila la Lawi bali kutoka
kwenye muungano wa masalio ya nyakati za mwisho ya Efraimu na Dani, aliowataja
Yeremia (Yeremia 4:15) (soma jarida la Maonyo ya Nyakati za Mwisho (Na. 044)). Kisha tutawaona Mashahidi, mmoja akiwa ni Eliya
aliyetabiriwa kuwa atatokea.
Kuendelea mbele
kutoka kwenye Malaki 3:2:
2b … ni mfano wa sabuni ya mtu afuaye nguo; 3 naye ataketi kama asafishaye fedha na kuitakasa,
naye atawatakasa wana wa Lawi, atawasafisha kama dhahabu na fedha; nao
watamtolea Bwana dhabihu katika haki. 4 Wakati
ule ndipo dhabihu za Yuda na Yerusalemu zitakapopendeza mbele za Bwana, kama katika
siku za kale, na kama katika miaka ya zamani. 5 Nami
nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na
juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye
kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha
mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema Bwana wa majeshi. 6 Kwa kuwa mimi, Bwana, sina kigeugeu; ndio maana
ninyi hamkuangamizwa, enyi wana wa Yakobo.
Kwa hiyo kusudi
lote la Bwana linatimia na Yakobo haangamizwi na kumalizwa kabisa kwa kuwa kuna
kusudi lililolengwa na Mungu lililomuandaa Yakobo kuwa ni kama uzao nan i kama
chimbuko la sharia na unabii. Hii pia imo kwenye rejea za Korani. Kwenye Sura ya:
“Wale waliowekwa kwenye matabaka” ambayo inahusiana na unabii wa kufanywa au
kuanzishwa kupitia Musa na Haruni hadi kwa Kristo. Mamlaka ya Maandiko
Matakatifu yameanzishwa kwa makuhani kupitia kwa Musa na Haruni, Ibrahimu, Isaka
na Yakobo hadi kumfikia Kristo na huo ndiyo mlolongo wa kuanzishwa kwa sheria.
7 Tokea siku za baba zenu
mmegeuka upande, mkayaacha maagizo yangu, wala hamkuyashika. Nirudieni mimi,
nami nitawarudia ninyi, asema Bwana wa majeshi. Lakini ninyi mwasema, Turudi
kwa namna gani? 8 Je! Mwanadamu atamwibia
Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna
gani? Mmeniibia zaka na dhabihu. 9 Ninyi
mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote. 10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula
katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue
kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo
nafasi ya kutosha, au la. 11 Nami
kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala
mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba,
asema Bwana wa majeshi. 12 Na
mataifa yote watawaiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema
Bwana wa majeshi. 13 Maneno yenu yamekuwa
magumu juu yangu, asema Bwana. Lakini ninyi mwasema, Tumesema maneno juu yako
kwa namna gani? 14 Mmesema, Kumtumikia
Mungu hakuna faida; na, Tumepata faida gani kwa kuyashika maagizo yake, na kwa
kwenda kwa huzuni mbele za Bwana wa majeshi? 15 Na
sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao;
naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao. 16 Ndipo
wale waliomcha Bwana waliposemezana wao kwa wao. Naye Bwana akasikiliza,
akasikia; na kitabu cha ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao
waliomcha Bwana, na kulitafakari jina lake. 17 Nao
watakuwa wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam,
watakuwa hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo
mwanawe mwenyewe amtumikiaye. 18 Ndipo
mtakaporudi, nanyi mtapambanua kati ya wenye haki na waovu, na kati ya yeye
amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.
Watu engine
wamejaribu kupata waumini kwenye makanisa yao kwa kusema kuwa sheria haifai na
inakanganya na kuiondoa au kuitangulia mbali. Kuliamuliwa kuitanguliambali hata
ile inayofundisha umuhimu wa kutoa zaka, kwa lengo la kuwapata watu wengi
lakini hiyo haikufaa.
Milolongo hii yote
ya kushindwa kuzishika sheria za Mungu inawasababishia watu kuyaacha Makanisa
ya Mungu kwa idadi kubwa mno. Watu mara zote hupenda kuwa sehemu ya mwili wa
Kristo wakiifanya kazi ya Mungu au wakiwa hawaifanyi. Kama hawaifanyi, basi
wanatakiwa waondoke.
Mwishoni kutakuwa
na watu wawili, Henoko na Eliya, wakifanya kazi Hekaluni. Tutakuwa tunawasaidia
kwa kufanya kazi ya kuwabatiza wale watakaotubu katika siku za mwisho. Kwa hiyo
kazi hii itakwenda kwa Kristo atakayelijenga kanisa tangu hapo hadi kwenye
mataifa yote.
Aya ya 17 kwenye
tafsiri ya KJV inasema: Nao watakuwa
wangu, asema Bwana wa majeshi, katika siku ile niifanyayo; naam, watakuwa
hazina yangu hasa; nami nitawaachilia, kama vile mtu amwachiliavyo mwanawe
mwenyewe amtumikiaye.
Vito hivi vya
thamani ni hazina ya kipekee, ni raslimali muhimu, yaani, anayomiliki mtu. Kwa
hiyo, matokeo ya mwisho ya kazi ya Mungu litakuwa kanisa la watu ambao watakuwa
wa thamani ya kipekee kwa Mungu, na hasa hasa wana wa Mungu.
1 Kwa maana, angalieni,
siku ile inakuja, inawaka kama tanuru; na watu wote wenye kiburi, nao wote
watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema
Bwana wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi.
Hivi ndivyo
ilivyonenwa kuhusu nyakati za mwisho. Hii ni wakati mashahidi wawili watakapoletwa
kwa maandalio ya Masihi na watasimama mbele ya mungu wa ulimwengu huu wote.
2 Lakini kwenu ninyi
mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake;
nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa mazizini. 3 Nanyi mtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu
chini ya nyayo za miguu yenu; katika siku ile niifanyayo, asema Bwana wa
majeshi. 4 Ikumbukeni torati ya
Musa, mtumishi wangu, niliyomwamuru huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote,
naam, amri na hukumu. 5 Angalieni,
nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na
kuogofya. 6 Naye ataigeuza mioyo ya
baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije
nikaipiga dunia kwa laana.
Mlolongo huu upo
kwenye sehemu mbili. Sharia zake za Musa aliyopewa huko Horebu kwa ajili ya
Israeli wote ambayo kwayo kwamba sharia au kanuni zote na sharia zote ni lazima
zishikwe. Kisha ndipo Eliya atatumwa kuanikiza tena sharia hizo na hukumu mbele
ya siku ya Bwana iliyokuu nay a kuogofya.
Kutoka na na aya
ya 5 Bullinger anaonyesha kuwa: Eliya nabii. Aliita kuwa, hapa tu peke yake, na
kwenye 2Nyakati 21:12. Penginepopote, wakati wote “Eliya Mtishbi”, kujionyesha
binafsi yake; lakini hapa "Eliya nabii "kwa sababu aliwafanya Israeli
wampokee Masihi, Yohana Mbatizaji ndiye anayeweza kudhaniwa kuwa alikuwa Eliya (soma
nukuu kwenye Mathayo 17:9-13, Marko 9:11-13): na kwenye chakula chake mahsusi
ambacho mvinyo uliwakilisha damu yake ambayo ilichukuliwa (na bado inachukuliwa
kuwa) ni “damu ya Agano (Jipya)”, kama ilivyotabiriwa kwenye Yeremia 31:31-34;
Waebrania 8:8-13; 10:15-17; 12:24).
Siku hii ya Bwana
kama tuijuavyo sisi sote ni siku ya mwisho tunayoingojea na siku hiyo ya Bwana
kama ilivyoelezewa kwenye Isaya 2:12,17; 13:6f. Bwana abayetajwa kuwa ni Yehova
ambaye ni Kristo anayetenda kazi au kuhudumu kama Kuhani Mkuu kwenye Hekalu la
Mungu.
Malaki ni kazi ya
kinabii ambayo inaendelea mbele kwenye ujio wa Masihi na kitabu chake
kinatuambia kwa wazi wazi sana jina la nabii ambaye atatumwa aje katika nyakati
za mwisho. Kinalimalizia Mkataba au maagizo ya Agano la Kale kikionyesha kile
kinachokwenda kutokea na kinaonyesha mambo mawili ya agano ambayo ni: sheria na
maagizo na kwamba Eliya atakuja kama mjumbe wa agano na sheria na kwamba kile
kitakacho kwenda kuanzishwa katika siku za mwisho.
Kinachokwenda kutokea
ni kwamba karibu vikundi vyote vya makanisa vitaangamizwa na kutakuwa na kiumbe
miongoni mwa Waisraeli na upuuzi wao kenye mwenendo wao vitakomeshwa na
kuongolewa kabisa. Ndipo tutakua tumeandaliwa tena na kuingizwa kwenye taifa
halisi na kwenye kundi sahihi chini ya wale ambao kwa bahati nzuri sana
watakuwepo kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu.
Hiki ndicho
tunachokitaka na hiki ndicho tunachotarajia kukifikia au kukipata. Tutakwenda
kuwa ama kwenye Ufufuo wa Kwanza au wa Pili. Tunafanya kazi kana kwamba
tunastahili au tunatimiza vigezo vya kuwa na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza bali
iwapo kama tutakuwa kwenye ule wa Pili, ambao huu ndio wa kuhukumiwa na Mungu.
Tunapaswa kufanya kile tuwezacho kukifanya.
Ishara ya
kumrudia Mungu ni utoaji wa zaka na kurudi kwenye mfumo wote mzima; yaani ni
kutoa zaka kikamili na kuzishika sheria za Mungu. Wengi hawapendi kulielea
Agano la Kale au uhusiano wake na Injili zote zilizopo, ziitwazo “Agano Jipya”
la Kristo, ambalo ni mwendelezo tu wa lile agano alilompa nabii Musa pale
Sinai. Kristo likuwa ni elohim, Malaika wa Uwepo wake,
aliyempa agano Musa na tusilisahau kabisa jambo hili.
q