Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[CB81]
Vita
Kati ya Kristo na Shetani
(Nakala 2.0 20060328-20070320)
Somo hili
linaelezea juu ya historia ya Ahabu na Nabothi
katika 1 Wafalme sura ya 21
likiunganisha vita vya kiroho kati ya
shetani na Kristo.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Haki
milki © 2006, 2007 Russ Hilburn na Diane Flanagan, ed. Wade Cox)
Somo hili linaruhusiwa kunukuliwa, na kusambazwa kwa yeyote mradi tu kama litanukuliwa kikamilifu, bila kubadilishwa au kuondoa namna halisi, Jina la Mchapishaji na anuani yake na tangazo la hati milki lazima vijumlishwe. Hakuna gharama yoyote ipaswayo kuchangiwa na mtumiaji na hairuhusiwi kuuzwa nakala zake kwa msomaji. Nukuu chache zaweza kuchukukuliwa katika makala zinazo tofautiana kimtazamo na kimaoni bila kukiuka maadili ya haki milki.
Somo
hili linapatikana pia katika Tovuti zetu popote Duniani.
http://www.logon.org
na http://www.ccg.org
Vita Kati ya Kristo na Shetani
Kusudi:
Kuangalia historia ya kweli ya Ahabu na Nabothi ikilinganishwa au kufafanuliwa na jinsi vilivyo vita halisi vya kiroho kati ya shetani na Kristo.
Walengwa:
1. Watoto watajifunza ya kwamba kuna masomo ya kiroho ya historia ya kweli ya Biblia.
2. Watoto watambue na kugundua ya kwamba vita kati ya Kristo na shetani ni vita vya kiroho.
3. Watoto watambue na kugundua maana halisi ya dhana katika 1 Wafalme sura ya 21.
Maandiko
yanayohusiana:
Warumi 1:20; 1 Wafalme 21; Mathayo 4:8-10; Walawi 25:23.
Maadili:
Kutokana na matendo ya kimwili tunapata kujifunza matendo ya kiroho (Rum. 1:20).
Vyanzo:
Orodha ya majina na maana yake kitabia:
Nabothi-(SHD 5022 maana yake ni tunda lililopandwa na Mungu )-Kristo Myezreeli (3158: pando la Mungu); Tunda lililopadwa na Mungu.
Ahabu-(256 kutoka 251 na 1: ndugu au rafiki wa baba yake)-Shetani. Shetani na Masihi walikuwa ni ndugu na bado ni ndugu.
Mfalme wa samaria – (8157: mlima wa ulinzi)
utawala wa shetani katika sayari aliopewa na Mungu. Shetani ni mfalme wa nguvu za anga (Efe. 2:2) ni mungu (god) wa sasa wa dunia hii (2 Kor. 4:3-4).
Shamba la Mizabibu katika Yezreeli-
(3157: Pando la Mungu).Utawala wa Kanisa. Mungu/Eloah ndiye Mkulima, na Kristo ndiye Mzabibu (Yn. 15:1-11). Na sisi tumepandikizwa katika Mzabibu (Rum. 11:16-21). Shamba la mizabibu la Bwana ni nyumba yote ya Israeli (Isa. 5:7). Hatuwezi kuuza Urithi wetu (Law. 25:23).
Yezebeli-(348 kutoka 336: ee au sio kama swali, na 2083: mkazi au makazi, kwa hiyo lizebeli siyo makazi yangu (Strong’s inaonyesha ushawishi - Utaratibiu wa uongo au siri ya Babeli Mkuu (Ufu. 17:5). ambaye anafanya vita na watakatifu.(Ufu: 13:7).
Chapa-Mamlaka kama nyota ya mchana aliyopewa shetani: Ni mungu (god) wa dunia hii ya sasa (2 Kor. 4:3-4).
Wana wawili wa Beliali (1100: Uovu au kiburi).Watu waovu wanaoshuhudia uongo na kuleta ushuhuda wa uongo. Hawa wanawakilisha ushuhuda wa uongo dhidi ya Kristo.
Eliya – (452: Mungu wangu ni Yehova au Yehu ndiye Mungu ). Mtishbi (8664:Mgiliadi). Kwa hiyo: Yehu ni Mungu Mhifadhi. Kanisa la kweli linatenda kazi kama nabii akusanyaye.
Utaratibu:
1. Kufungua kwa maombi
2. Tafakari tabia na mienendo ya watu wanaelezewa katika historia na wanacho wakilisha.
3. Soma na kuigiza.
4. Ruhusu majadiliano pamoja na maswali kwa kadri iwezekanavyo.
5. Funga kwa maombi
UTENDAJI:
1. Soma na kuigiza
2. Gawa vikundi
3. Ruhusu watoto watende kwa
kuiga mambo yanayoonekana na kutengeneza mavazi ya bandia katika maonyesho na katika kuigiza.
4. Fanya mazoezi ya kuigiza.
5. Endelea kutafakari kwa kwa kutmia mifano.
6. Kama inawezekana ruhusu watoto watende na kusimulia maigizo, katika maonyesho ya bandia.
Kama unafanya maigizo ya bandia, wasaidie watoto katika hatua za mwanzo za kutengeneza mwili wa bandia. Ruhusu watoto, wavalishe mavazi miili ya bandia,waliyotengeza kwa makaratasi yaliyotengenewza kama nguo, tumia nyuzi zilizosokotwa kama nywele, na tumia rangi kwa kupamba uso. uchaguzi uliyofanikiwa katika nyakati zilizopita ni kuwa na jina la tabia ya mtu bandia liandikwe juu yake kwa sehemu ya mbele na jina lake la mfano chini yake mbele au mgongoni pa mtu bandia. Njia nyingine ni kuandika majina, na maana yake na mifano yake kuelezwa kwa wasikilizaji.
Kung’arisha nakala za sehemu kwa kila usemaji zinasaidia.
Kwa kawaida watoto wanazungumza pole pole, hasa wele ambao bado ni wadogo, kwa hiyo vipaza sauti katika maneno husaidia. Ni maigizo ya bandia na wanakuwa chini ya meza iliyofunikwa shuka juu yake, na sauti zao zikiwa zimebadilishwa. Nakala chache za igizo kwa wasikilizaji zinasaidia kama vipaza sauti havipo.Watoto watafurahi sana ikiwa mtu mwingine anaweza kuwachukua katika video.
Igizo
Kufuata tabia na mwenendo, igizo liendane
na utaratibu wa tabia katika mwonekano:
Msimulizi:
Ahabu – Shetani
Nabothi – Kristo
Yezebeli – Makanisa ya uongo
Wana wawili wa Beliali
Eliya
Sehemu inayofanyiwa maigizo yote ni katika nyumba ya Ahabu akiwa chumbani mwake akichungugulia dirishani akiangalia shamba la mizabibu la Nabothi.
1
Wafalme 21. Ndiyo sehemu ya igizo
Msimulizi:
Mfalme Ahabu alikuwa ni mfalme wa Samaria. alimiliki sehemu ya eneo kubwa mno la ardhi na alikuwa na watu wengi katika ufalme wake. Mfalme kwa kweli hakuridhishwa na mamlaka aliyokuwanayo pamoja na mali yake nyingi aliyomiliki. Hapa tunona ya kwamba shetani ni mungu wa dunia hii (2 Kor. 4:43-4) na ndiye mkuu wa dunia (sayari) hii yote.
Jirani na jumba la kifahari la mfalme Ahabu katika Yezreeli kulikuwa na shamba la mizabibu linalomilikiwa na mtu anaitwa Nabothi, Nabothi katika 1 Wafalme 21 hasa ni Kristo. Kristo ana mamlaka juu ya shamba la mizabibu la Baba yake. Picha hii inaonyesha ya kwamba Kristo ndiye Mwangalizi na Mtawala wa Kanisa. Shamba lote la mizabibu la Bwana ni nyumba yote ya Wana wa Israeli (Isa: 5:7).
Sasa hivi wako wateule wachache tu kati yetu lakini kwa wakati, wote waliyo juu ya nchi watamjua Mungu. Mungu/Eloah ndiye Mkulima, na Kristo ndiye mzabibu (Yn. 15:1-11) na tumepandikizwa kwenye Mzabibu (Rum. 11:16-21) au tunaweza kuwa tawi la Mzabibu kama tukitubu na kubatizwa na kuhifadhi Amri za Mungu. Kristo ndiye Mlezi na Mwangalizi wetu.
Hatukuuza urithi wetu (Law. 25:23). Mfalme alikuwa na ardhi kubwa mno, lakini pia alitaka na kutamani shamba linalolimwa na Nabothi. Ingawaje shetani alikuwa anamiliki na alipewa mamlaka yote ya dunia na sheria za Mungu, alichagua kuasi, kutotii na kutofuata sheria za Mungu. Sasa shetani anatamani na anajaribu kuchukua Kanisa la Mungu kutoka mikononi mwa Yesu kwa hila na kwa njia yoyote inayowezekana.
Ahabu:
Nahitaji shamba lako la mizabibu. Liko karibu na jumba langu la kifahari, na ninataka kutumia ardhi hiyo kwa ajili ya busitani. Nitakupa shamba lingine zuri la mizabibu kwa kufidia au kama utapenda nitalinunua kwa kukulipa pesa nzuri.
Nabothi:
Hapana, Mfalme Ahabu. Nilirithi shamba hili kutoka kwa wazee wa zamani wa baba yangu. BWANA amenikataza nisikuruhusu kuchukua shamba wala nisikuuzie
Msimulizi:
Tunaona ya kwamba mfalme Ahabu (Shetani ) alitaka kubadili shamba la mizabibu la Nabothi kuwa kitu kingine tofauti. Inaonyesha ya kwamba mzabibu ambao unamwonyesha Kristo ungeng’olewa pamoja na mizizi yake na kutupwa nje na kisha kitu kingine tofauti kabisa kingeweza kupandwa mahali pale. Hii inaonyesha ni kumuondoa Kristo na Kanisa lake kutoka katika shamba la Mizabibu la Mungu. Inatuonyesha ya kwamba kama Mungu angemruhusu Mfalme Ahabu (shetani na Jeshi lililoanguka ) la dunia hii kutawala shamba la mizabibu la Mungu, wangeharibu Kanisa la Mungu na sheria za Mungu. Shetani na washirika wake wangegeuka na kuwa kitu kingine tofauti kabisa.
Tunaona sasa katika madhehebu ya duniani, wanasherekea sikukuu ya krismas, easter na kuabudu miungu ya uongo katika siku ambazo hazistahili. Madhehebu ya uongo ya siku hizi hayatufundishi ni nani aliye Mungu Mmoja wa kweli au namna ya kutunza sheria za Mungu.
Katika sentensi hii rahisi. “Hapana, mfalme Ahabu. Nilirithi hili shamba la mizabubu kutoka kwa wazee wa zamani wa baba yangu. BWANA amenikataza ya kwamba nisikupe shamba hili” ! – Tunaona majaribu ya Kristo ambayo Mathayo anatuambia juu yake. Mara tatu shetani ali mjaribu kwa hila Kristo: Kristo alinukuu fungu la Maandiko Matakatifu. Mara ya tatu Kristo alitumia nguvu ya Mungu Mmoja wa kweli ambaye ndiye pekee anayestahili kuabudiwa na akamwambia shetani aondoke.
Mathayo 4:1-11.
Msitari wa 2 unazungumzia jaribu la kutaka kumpa mamlaka ya utawala mapema zaidi katika dunia (sayari) hii.
Mathayo 4:8-9 “Tena” Shetani akamchukua juu katika kilele cha mlima, na kumwonyesha mamlaka yote ya dunia hii,na utukufu wake, na kisha (shetani ) akamwambia, “Haya yote nitakupa kama ukinishujudia mimi (K.J.V).
Shetani ndiye mtawala wa dunia( Sayari) hii kwa sasa. Shetani amejaribu kwa miaka mingi kuw apata watu wa kiroho wamsujudie. Theluthi ya jeshi walimfuata shetani katika maasi yake dhidi ya Mungu Baba (Ufu: 12:4).
Mathayo 4:3 Kisha yesu akasema, “Ondoka, nenda zako shetani ! kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana wako, Umwabudu Yeye peke yake (RSV).
Kisha Ahabu akaenda nyumbani kwake, amehuzunika, na mwenye hasira nyingi kwa majibu ya Nabothi aliyomjibu.
Ahabu akalala katika kitanda chake akiangalia ukutani, na hukula chakula, Hapa tunaona shetani
akiendelea kuasi dhidi ya sheria za Mungu. Shetani anatamani au kutaka kitu ambacho si mali yake na anavunja Amri za Mungu kwa ajili ya tamaa yake. Anachukia anaposhidwa kutimiza azima yake. Mke wake Yezebeli akamwendea.
Yezebeli:
Kwa nini umeuzunika ? kwa nini hukula chakula ?
Ahabu:
kwa sababu ya Nabothi, kwa mambo aliyoniambia. Nilipotaka kununua shamba lake la mizabibu au kama angependelea, nimpe shamba lingine badala ya lile lake, lakini akaniambia ya kwamba siwezi kulipata.
Yezebeli:
Vema, wewe ni mfalme au sio mfalme? Amka toka kitandani, furahi na ule chakula. Nitakupatia shamba la mizabibu la Nabothi !
Msimulizi:
Ingawaje wenye asili ya kiroho hawaowi, katika 1Wafalme 21 Ahabu ( au mke wa shetani ni Yezebeli) anawakilisha makanisa ya uongo ambayo yanaongoza watu mbali kinyume na sheria za Mungu.
Yezebeli aliandika barua kadhaa, akaweka sahihi ya jina la Ahabu juu yake, akazipeleka zile nyaraka kwa wazee, na kwa watu wenye nguvu waliyokuwa katika mji wake, waliyokaa pamoja na Nabothi, Akaandika katika zile nyaraka akasema, mkamweke Nabothi juu mbele ya watu, mkainue watu wawili, watu wasiofaa, ili wamshitaki, na kumshuhudia, kunena, amemtukana Mungu na mfalme Ahabu. Kisha mchukueni nje, mkampige kwa mawe, ili afe. Wale wazee wa mji wake, na walio wenye nguvu waliokaa mjini mwake, wakafanya kama Yezebeli alivyowaagiza, kama ilivyoandikwa katika nyaraka alizowapelekea. Ndipo wakamchukua nje ya mji wakampiga kwa mawe hata akafa. Wakatenda kama wailivyoagizwa. Yezebeli akapokea habari ya kwamba maagizo yake yametimizwa.
Katika wakati wa sasa, Makanisa ya uongo na shetani yanajaribu kwa hila kuwadanganya watu kwa njia zozote yanayoweza kutumia. Wakati mwingine yanajaribu kudanganya watu juu ya sheria za Mungu ya kwamba zimetimizwa na kufutwa au zimebadilishwa.
Kwa wakati fulani makanisa ya uongo kwa kweli walijaribu na kufanikiwa kuwauwa watakatifu wa Mungu. Hatuna lolote la kuogopa, kwa sababu tunamtii Mungu na anatulinda. Hawezi kuruhusu madhara yoyote yatupate na kutuumiza. Yeye ni ngao yetu kila wakati. Mungu aliruhusu Mmoja wa watakatifu wake auwawe kwa sababu mtu huyo alikuwa tayari amehitimu kwa ajili ya ufufuo wa kwanza. Katika warumi. 8:28 inatuambia ya kwamba Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, iwapo tu tunamtii pamoja na kumtumikia.
Katika 1 Wafalme 21 tunamwona Yezebeli, au makanisa ya uongo, yanatumia muhuri wa ahabu au shetani: Mungu alimtupa shetani juu ya nchi ambapo jina lake bado lilikuwa ni Lusifa, lenye maana ya “nyota ya mchana”. 2 Wakorintho 4:3-4 inatuambia ya kwamba shetani ndiye mungu (god) wa dunia hii. Nguvu hii wamepewa makanisa ya uongo. Makananisa haya ya uongo yametumia majina ya uongo au ushahidi wa uongo katika kuingiza nguvu ya Roho mtakatifu kwa ajili ya kuwadanganya na kuharibu watu.
Yezebeli:
Nabothi amekufa. Sasa nenda na uchukue shamba lake la mizabibu na ulimiliki sasa, ambalo alikataa kukuuzia.
Msimulizi:
Kisha BWANA akamwambia Eliya, Nabii, ondoka nenda kwa mfalme Ahabu wa samaria. Utamkuta katika shamba la mizabibu la Nabothi, ndiko alikoshukia ili alitamalaki. Ukamwambie ukisema, BWANA asema hivi, Je umeua ukatamalaki. ? Nawe utamwambia kusema, Bwana asema hivi, Mahali pale mbwa walipoiramba damu ya Nabothi, mbwa watairamba na damu yako, naam, damu yako pia.
Akaenda akamkuta Ahabu katika shamba la mizabibu la Nabothi. Mara kwa mara njia zile watu wanazojaribu kutumia kuwaua wateule wa Mungu, ni kwa njia hizo hizo ambazo wauaji hawa huuwawa. (2 Fal. 1:10-15; 2:23,24). Ni katika njia hizo hizo nao pia ndivyo wanavyouawa.
Ahabu: Je ! umenipata, ewe adui yangu ?
Eliya:
Ndiyo. Nimekupata, kwa sababu umejiuza utende yaliyo mabaya machoni pa BWANA. Kwa hiyo BWANA asema nitaleta mabaya juu yako na juu ya Yezebeli, kwa sababu ya chukizo mlilomchukiza, hata kumghadhabisha Bwana, ukawakosesha Israeli.
Msimulizi:
Hapa tunaendelea kuona Ahabu (shetani) analishitaki Kanisa la Mungu. Tunaona ya kwamba ukweli mwisho unampata na kumkamata shetani. Shetani hataruhusiwa kuendelea kuharibu dunia hii (sayari ) au kuwadanganya na kuwachanganya watu kwa hila za ujanja wa shetani wasimtii Mungu. Shetani atafungwa na kutupwa katika shimo kwa muda wa miaka 1,000. Mungu hatatenda lolote mpaka kwanza awaonye watu wake kwanza (Amos 3:7; Yn. 15:22; Rum. 1:20).
Eliya alipomaliza kusema, Ahabu alirarua mavazi yake, akayavua, na kujivika magunia. Alikataa kula chakula. Alilala akiwa amejivika magunia, na alitembea mwenye majonzi na huzuni kubwa. Katika siku za zamani, hii ndiyo njia iliyoonyesha ya kwamba mtu ametubu dhambi zake.
Bwana akamwambia Nabii Eliya, umeona jinsi Ahabu alivyo nyenyekea mwenyewe na kutubu mbele yangu? Kwa sababu ametenda hivi, sitaleta mabaya juu yake wakati wa maisha yake; itakuwa wakati wa maisha ya watoto wake na nitaleta mabaya katika familia ya Ahabu.
Tunajua kutokana na Mpango wa Mungu wa wokovu ya kwamba Mungu hapendi mtu yeyote apotee (2Pet. 3:9). Katika mwisho wa miaka 7,000 au mwisho wa mileniumu, shetani atafunguliwa kutoka shimoni na ataenda na kuwadanganya mataifa tena. Katika vita hivi vya mwisho shetani atakufa (Isa.14:16). Atanya ng’anywa hali ile ya nguvu za kiroho.
Shetani pia atapata nafasi ya pili kama watu wengine wote waliyoishi tangu zamani ambao hawakujulikana wala kumjua Mungu Mmoja wa kweli na sheria zake. Shetani kama Ahabu katika historia hii, labda atatubu katika hukumu kuu ya Mungu. Kutokana na maasi ya shetani atahukumiwa na kunyag’anywa nafasi yake kama kerubi mkuu na mungu wa dunia hii, lakini kutokana na upendo na rehema za Mungu ambazo hazina ukomo huenda atampa shetani jina jipya baada ya kubadilika na daraja au kazi nyingine katika uumbaji wake.
Kumbuka Daima, “Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu Yeye peke Yake na kumtumikia”.
q