Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[104]

 

 

 

Andiko Kuhusu Matendo ya Sheria - au MMT

(Toleo La 2.0 19950415-19990618))

 

Jarida hili linafafanua kile ambacho Mtume Paulo anachokitaja kama Matendo ya Sheria kwenye nyaraka zake. Somo hili linaloeleweka kimakosa sana limefafanuliwa kwa mtazamo wa ushuhahidi wa watalamu wa uchimbuzi wa mambo ya kale au wanaakaelojia waliotumia kile kinachojulikana kama Gombo zililodunguliwa kwenye Bahari ya Chumvi. Maandiko yaliyotafsiriwa na kina Quimron na Strugnell imaelezewa habari zake pia. Inaonekana kama Matendo ya Sheria ni bodi ya nakala za maandiko yaliyodumu tangu katika karne ya kwanza, yakijulikana kama Miqsat Ma’ase Ha-Torah au MMT, ambayo yamegunduliwa katika siu za hivi karibuni sana. Hii inamfanya Paulo aonekane kuwa ni mtu mahiri sana kwenye Ukristo wa siku hizi.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki © 1995, 1999 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Andiko Kuhusu Matendo ya Sheria – au MMT

 


Jarida hili ni la mwisho kwenye mkururu wa majarida yahusuyo sheria au torati. Linabeba dhima ya dhana ya matendo ya sheria ambayo anaielezea Mtume Paulo. Imekuwa ikishambuliwa au imekuwa ni mashambulizi yaliyofanywa ulimwenguni kote, kwa kipindi kirefu sana, wakijaribu kuondoa au kutangua dhana yoyote inayoonyesha kuwa sheria bado zinahitajika kuzishika, na kwa kutumia ufafanuzi au maelezo ya Paulo kwenye naraka zake kwa Wagalatia na kwa Warumi kama msingi wao. Mijadala yenyewe iliyompelekea kuandika hivyo iko wazi sana kuwa ni uwongo, lakini haieleweki vizuri

Warumi 3:20 kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria; kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria.

 

Mtume Paulo anatumia neno linaloitwa matendo ya sheria. Wakristo wengi wa siku hizi wamedhania tu kwamba anachokiongelea hapa ni torati ya Musa. Wanadhania kwamba anasema kwamba torati imetanguka. Matendo ya sheria sio ni kitu kisicho na maana, na matendo ya sheria sio sehemu imani yao. Kwa hiyo, mtu yeyote anayeandika mawazo kama hayo hurudi nyuma hadi kwenye Agano la Kale kwa ujumla, na anasema kuwa matendo ya sheria hayatuhusu sisi siku hizi. Hoja hizo hazina usahihi kwa sababu ya hoja zilizo kenye jarida la Tofauti ya Sheria (Na. 96). Kwenye jarida hilo ilionyeshwa jinsi sheria za Mungu zilivyo za milele, na zinatokana na tabia yake. Ilionyeshwa pia kuwa sheria ya utoaji dhabihu ndicho kitu kilichogongolelew pale mtini na siyo sheria za Kimaadili zilizo kwene amri zake. Kuna jambo lingine, linaloitwa matendo ya sheria, ambalo linahusiana na sheria hii ya utoaji dhabihu, na linalohusiana na sheria za Mungu tu kwa njia ya moja kwa moja. Dhana ya matendo ya sheria haijaeleweka vyema, na ni siku hizi tu, kwa kupitia ushahidi wa wataalamu wa elimu ya mambo ya kale, ndipo tunaweza kuelewa kwamba kile Paulo alichukuwa anakiongelea hasa. Tunaweza kuonyesha sasa kwamba kwa hakika Paulo alikuwa anaiongelea bodi ya uandishi, ambayo ilikuja kuzuiwa kwenye huduma za madaraja ya kisakwamenti ya Kiyahudi, iliyokuwa na masingi wake kwenye uandishi wa Kumran, na ambayo haikuwa na uhusiano wowote na marabi wa Kiyahudi. Ilitumiwa kwa kuwa ni Muhimu na wengine waliikataa Talmud na utaratibu wa Hekaluni wa makuhani. Vilikuwa ni vikundi vinavyotumia Biblia peke yake vya karne ya kwanza KK/BK. Tutaona kwamba neno hili la Paulo la matendo ya sheria linataja mchanganuo aishishi wa kikundi cha kidini wa utakaso wa kidini ambao hauna uhusiano yoyote wala msingi wa wokovu. Hawazitaji kabisa sheria sheria za Mungu kwa wokovu wa kiroho. Bali wanataja tu moja kwa moja Siku Takatifu. Wanataja ju ya sadaka na utakaso, yaani utakaso wa kidini. Tutaona, kutokana na mlolongo wa mambo ambao ulikuwepo. Kwenye Warumi 3:20 tuna maelezo ya kwanza ya tabia zake. Inasema kwa hiyo kwa matendo ya sheria. Tafsiri ningine zinatafsiri andiko hili kama matendo ya sheria.

Warumi 3:20-27 kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria; kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria. 21 Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii; 22 ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti; 23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; 24 wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 25 ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilzotangulia kufanywa. 26 apate kuonyesha haki yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye Yesu. 27 Ku wapi, basi, kujisifu? Kumefungiwa nje. Kwa sheria ya namna gani? Kwa sheria ya matendo? La! Bali kwa sheria ya imani.

 

Hapa Paulo anasema, kwa hakika, Kwa sheria ya namna gani? Kwa sheria ya matendo? La! Bali kwa sheria ya imani. Hii ni muhimu na jambo kuu na ya muhimu sana kwa wokovu wa mwanadamu. Kisha Paulo anaongelea kuhusu sheria.

Warumi 3:28-31 Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria. 29 Au je! Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Siye Mungu wa Mataifa pia? Naam, ni Mungu wa Mataifa pia; 30 kama kwa kweli Mungu ni mmoja, atakayewahesabia haki wale waliotahiriwa katika imani, nao wale wasiotahiriwa atawahesabia haki kwa njia ya imani iyo hiyo. 31 Basi, je! Twaibatilisha sheria kwa imani hiyo? Hasha! Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria.

 

Hivyo basi, Paulo anasisitizia umuhimu wa sheria kwenye Kanisa la Rumi, kisha anasema kwamba matendo ya sheria hapa hayapo sahihi. Hayasaidii chochote kwenye wokovu. Wokovu unapatikana kwa imani kwa kumwamini Yesu Kristo. Ni kwa nini Paulo anahusishwa na hoja hizi? Wengi, kwa ajili ya mgongano ilioko wazi kuhusu kwenye maneno haya, wanadhania kwamba alikuwa anaelezea kuhusu sheria ya utoaji wa dhabihu dhidi ya wale waliokuwa wanajeribu kuzuia sheria. Hili ni tatizo ambalo maelekezo ya Paulo na kiini au msimamo wa Biblia, kwa kuwa yamekuwa ni mikanganyiko ya wazi kwa kile anachokisema na kukikusudia Paulo. Kwa upande mwingine, anasema mtu anapaswa na ni lazima azishike amri za \mungu, na kwa upande mwingine, anasema kwamba haya matendo ya sheria hayaongezei chochote wala hayafaidishi lolote. Mgongano huu wa wazi wapasa upatiwe ufumbuzi. Jibu la mwisho, nje ya mgongano wa wazi uliopo kati ya sheria ya Kimaadili na za utoaji dhabihu tulizozielezea kwenye jarida letu la Tofauti Iliyopo Kwenye Sheria, linalotuama kwenye bodi ya uandishi, ambayo tulikuwa hatuyajui. Neno alilolitumia hapa ni ergoon nomou, (kwenye Kiyunani chenye mchanganyiko na Kilatini), lenye maana ya matendo ya sheria. Neno hilo linalitafsiri neno la Kiebrania, tulilo kutananalo sasa kutoka kwenye Gombo za Bahari ya Chumvi. Neno lenyewe ni Miqsat Ma’ase Ha-Torah, au MMT, tafsiri ambayo, kwa mujibu wa Strugnell na Qimron, ni Ni Sawa tu na Maagizo ya Torati. Halionekani mahali popote pale kwenye marabi wa Kiyahudi. Haijafanyika kuwa ndiyo mwenendo au tabia tarajiwa na kwa hiyo uelewa ulipotea kabisa. Hata hivyo, neno miqsat halimaanishi kitu hichohicho tu. Linapotumiwa kwenye MMT halionyeshi kuwa ni sheria hizohizo bila kutofautiana. Uelewa wake unaweza kukusanywa kwenye matumizi yake kwenye Talmud. Hivyo, Martin Abegg anaamini na kuchukulia (kwenye kitabu chake cha  Paul, Works of the Law and MMT [Paulo, Matendo ya Sheria na MMT], Biblical Archaeology Review, Nov.-Dec. 1994, pp. 52 ff), kwamba tulipaswa kulitafsiri neno hili kama umuhimu fulani au uvumilivu. Kina Strugnell na Qimron wanakitafsiri kifungu hiki ma’ase ha torah kama ni maagizo ya Torati. Lawrence Schiffman anadhania mamlaka halali ya Torati (kutoka kwaAbegg ibid). Huenda ile ni zaidi ya rafsiri ya kama mahsusi au muhimu kwenye sheria. Lakini matumizi yake kwenye Kiyunani yametafsiriwa kama ergoon nomou. Neno hili lilitumiwa kwenye tafsiri ya Septuagint ili kutafsiri neno hili kama ma’ase ha torah. Neno ergoon nomou ni neno lililotumiwa na Paulo na ndilo lililotafsiriwa kwenye Kiingereza kama matendo ya sheria. Inakujakuwa dhahiri sana kwamba kwa kweli Paulo alikuwa anaongelea mtazamo wa sheria unaong’ang’aniwa na dini ya Kumran, na ambayo ilifanyika kuwepo kwenye dini isiyojumuisha marabi wa Kiyahudi wa karne ya kwanza ya haikuwa sehemu ya mapokeo ya Kitalmud na tafsiri yake. Haikufanyika kuwa sehemu ya kile tunachokijua leo kama dhana au nadharia kuu ya Kiyahudi kwenye karne ya kwanza na haikuchukuliwa kuwa ni sehemu ya mapokeo na tafsiri za Kitalmud. Ndipo, iliondolewa mbali. Ndipo tulisubiria hadi zilipogunduliwa Gombo za Bahari ya Chumvi na kuona nakala ziliwepo na kutafsiriwa. Kutokana na ugunduzi huo ndipo tuliweza kumuelewa Paulo kikamilifu. Tutayaonyesha baadhi ya maandiko hayo, ni halafu tutakwenda kuona Gombo hizi za Bahari ya Chumvi yanasema nini kuhusu utaratibu au kanuni zilivyo. Tutapata hisia ya idadi ya vitu fulani amnavyovikemea Paulo. Tutaona kwamba ni zipi anazozisema kwamba zimeondolewa. Haziongezi wala kupunguza chochote. Havihusiani wala kuongeza chochote kwenye maana yetu kuhusu wokovu, na taratibu za kwenye Agano la Kale, zinazotufunika. Inahusu tu na taratibu za sheria za utakaso wa dhabihu na kidini. Inamfanya mtu atakasike kwa matendo kwa mujibu wa usomaji mpotofu wa andiko hilo.

 

Kuna tukio la kugombea jimbo fulani nchini Marekani lililopelekea kuzuka kwa mapigano kugombea haki ya Matendo ya Sheria au tafsiri za hiki kinachojulikana kama. Elisha Qimron na John Strugnell wameandika habari hiyo. Wanajaribu kudai haki za maandiko ya Qumran. Unaweza kusema “Inatuhusu nini sisi? Inatuhusu vipi hata kama watachimbua majarida na maandiko ya kwenye hiyo Qumran? Na kwani inaweza kutuathiri vipi kiimani?” Jibu ni kwamba inatupa kifaa kingine, silaha au ngao, ya kujikinga dhidi ya wale wanaojaribu kuisambaratisha imani yetu na sheria. Mara tu unapoitangua sheria, unakuwa unatangua pia dhana ya dhambi, na unatangua pia dhana ya maadhimisho ya Siku Takatifu ya Mkate Usiotiwa Chachu. Unakuwa unapingana na misingi muhimu ya mpango wa Mungu wa wokovu. Kupuuzia kwa maana yake kunatufanya iwe vigumu sana kwetu kuelewa kile anachotufanyia Kristo sasa, na jinsi anavyotusogeza mbele.

 

Mjadala wa ni kitu gani alichokisema Paulo kwene nyaraka za Warumi na Wagalatia unaweza kukingiwa kifua na kueleweshwa kwa uelewa unaoongezeka. Maelezo yake ni kwamba alikuwa anaongelea kuhusu Matendo ya Sheria – ambayo ni Miqsat ma’ase ha-torah au MMT, ambayo kwa wazi sana anamaanisha maandiko ya dini za Qumran, ambazo ziliingia kwenye itikadi za kidini ya Kiyahudi katika karne ya kwanza, na ikatoweka kuanzia karne ya pili, ya tatu na ya nne.

 

Baada ya utawanyiko, baada ya kuanguka kwa Yerusalemu, na hasahasa, kuanguka kwa Massada, ndipo MMT ilipotea. Ilisalia kwenye pango la Qumran. Uelewa wa kile alichokuwa anakisema Mtume Paulo ulifungiliwa mbali, ili kwamba watu waliokusudia kupotosha na kuitangua sheria ya Mungu waliyatumia maandiko ya Agano Jipya kuziondoleambali sheria kwa kutumia maneno aliyokuwa anayasema Paulo. Nyaraka za Agano Jipya zilitumika pia kuipinga nia na dhamiri njema ya Paulo, na kisha kwa sababu ya hiyo, Wayahudi wenyewe walijisikia kuwa kwenye shinikizo kwa ajili ya alichokuwa anakisema Paulo. Ilianzisha kile kilichochotokea kuwa mkanganyiko mkubwa kwenye maandiko ya Biblia. Wagalatia 2:13 inatoa hisia ya kile kilichotokea.

Wagalatia 2:13 Na hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa na unafiki wao.

 

Walimwendea Barnaba kwa maneno mengine, kwa hiyo wateule hawakuwa na la kusamehewa kwa sababu hiyo na kwa kujiuliza kwao.

Wagalatia 2:14-16 Walakini, nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kweli ya Injili, nalimwambia Kefa mbele ya wote, Ikiwa wewe uliye Myahudi wafuata desturi za Mataifa, wala si za Wayahudi, kwa nini unawashurutisha Mataifa kufuata desturi za Wayahudi? 15 Sisi tulio Wayahudi kwa asili, wala si wakosaji wa Mataifa, 16 hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki.

 

Sasa nono matendo ya sheria limechukuliwa kwa ujumla kuwa na maana ya maneno mawili kama, kazi ya sheria, lakini kwa kweli lipo kama tunavyoliona, jina lake au wadhifa wake, Matendo ya Sheria, ambalo limetafsiriwa kwa Kiebrania kama Miqsat ma’ase ha-torah. Kutoka sasa na kuendelea mbele, tunaweza kulieleza hili kama ni cheo cha kazi za Kiyahudi kwenye karne ya kwanza, kinachojaribu kuonyesha haki ya namna fulani kupatikana kwa njia ya matendo. Wagalatia 3:1-14 inatoa ufafanuzi wa kina.

Wagalatia 3:1-14 Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa? 2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? 3 Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili? 4 Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli. 5 Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? 6 Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki. 7 Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu. 8 Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa. 9 Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani. 10 Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati, ayafanye. 11 Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye haki ataishi kwa imani. 12 Na torati haikuja kwa imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo. 13 Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; 14 ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.

 

Paulo anamtaja kwa kumlinganisha Ibrahimu kwenye andiko lake kwa Waalatia, kwa kuwa Ibrahimu alihesabiwa kuwa mkamilifu na mwenye haki, kutokana na maandiko yaliyo kwenye kitabu cha Mwanzo. Hali yote ya kuufikia ukamilifu aliyokuwanayo Ibrahimu ilionekana kwenye Mwanzo 22:16 ambapo Ibrahimu alikubali kumtoa sadaka mwanawe Isaka kwa amri ya Mungu. Na Abegg analikuza jambo hili kwenye kipengele chake cha kitabu hichohicho. Anadhania kwamba kuna uwezekano mmoja tu, na ni uwezekano mkubwa sana, vinginevyo Paulo asingetumia rejea ili kuhusianisha na andiko hili. asingeweza kuongelea kuhusu matendo ya sheria, na akautumia mfano wa Ibrahimu, kama mfano ulikuwa unalenga moja kwa moja na matendo na hali ya kuhesabia haki. Ukweli ulikuwa ulikuwa ni kwamba alihesabiwa mwenye haki kwa matendo aliyokuwa anayafanya. Abegg anatoa maelezo mazuri sana, na yanaonekana vizuri na kisahihi kwamba msingi wa matendo ya sheria unawezesha utakatifu huenda ulikuwa umechukuliwa pia kutoka kwenye Zaburi 106:30-31.

Zaburi 106:30-31 Ndipo Finehasi akasimama akafanya hukumu; Tauni ikazuiliwa. 31 Akahesabiwa kuwa ana haki Kizazi baada ya kizazi hata milele.

 

Cha kufafa kilichofanywa na imani ya Kiyahudi na Kanisa, kilichukuliwa dhana hii wakati Finehasi aliposimama, na kwa matendo yake, aliyoyatenda, alihesabiwa kuwa wenye haki kwa kizazi chake chote. Kwa hiyo ndivyo zilivyokuwa dini na imani ya Qumran na MMT, na kwa vikundi vilivyodhania kuwa sheria ingeweza kuwapa haki kwa matendo, wakilichukulia andiko hili na kulitendea kazi kuwa ni kama uhalalisho wa haki iliyotokana na matendo ya mtu binafsi yake. Wana wa Sadoki ndilo lilikuwa jina walilojipa na kulitumia wafuasi wa dini ya Qumran. Hutu Sadoki, Kuhani Mkuu aliyehudumu zama za Daudi na Sulemani, alikuwa ni wa uzao wa moja kwa moja wa Finehasi, ni fikra inayoupa mashiko mtazamo huu. Paulo alisema kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya sheria. Yeye anayehesabiwa haki kwa imani ni mkamilifu na ataishi.

 

Kwa hiyo, haki na utakatifu ni shatri muhimu katika kuzitii sheria kwa njia ya imani. Kuzishika tu sheria pasipo kuamini kwa kiwango cha juu hakuna maana. Hili ndilo wazo linaloshambuliwa. Mtazamo huu wa kimwili haki ulichukuliwa licha ya ukweli kwamba kuna maandiko mengi sana ya biblia kwenye kitabu cha nabii Isaya, hususan Isaya 9:1-6, inayoelezea kuhusu Masihi, na Isaya 53, inayoelezea kuhusu mateso yake na kuichukua kwake dhambi. Maandiko haya yote yalionyesha kwelekea ukomaji wa utoaji dhabihu ya kuondoa dhambi kwa Masihi. Na bado watu hawa walidhania kwamba matendo yangewafikiliza na kuwapatia haki. Ni kama alivyosema Paulo kwamba Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga,? 2 Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?” Kisha ndipo anamwongelea Ibrahimu. Paulo anasema kwamba nafasi yao imetoholewa kutoka kwenye maandiko mawili, ingawa hakumtaja Finehasi. Hata hivyo, inaonekana kwa namna fulani kwamba andiko linalosema kwamba Ibrahimu alihesabiwa haki kwa utii wake na matendo yake aliyoyaonyesha kwa kumtoa sadaka mwanae Isaka, ulikuwa ni msingi wa mawazo. Kwa kweli, kulikuwa na kitu kilichofanyika kwenye maisha yao ya useja wa Kitawa kwa namna fulani. Huenda kwa kuwatoa sadaka watoto, kwa kutokuwa na yeyote, unajiweka kwenye maisha ya useja kwa kutakasika. Kwa hiyo, unahesabiwa kuwa mwenyehaki kwa kitendo cha kuukataa uzao wako tu. Ni kujidanganya tu zaidi ya unavyodhania. Lakini mtu anaweza kudhania kwamba inaweza kuwa ni rahisi. Kuna taratibu nyingine nyingi za utakaso, ambazo zinafanya kuwe na uenezi, kwa kuwa huwezi kutakasika kabisa kwa kufuatisha taratibu hizi wakati wote, chini ya sheria, inayofanya kuyathibiti kikamilifu maisha yote ya mwanadamu. Abegg anaonekana kufaweka hoja nzuri kwa chimbuko la jina hili. Anaonyesha kwamba MMT inatuama kwenye lugha halisi ya kile ambacho Paulo walikuwa anakipinga hoja kwenye waraka wake kwa Wagalatia (Wagalatia 2:16) (Abegg op. cit. p. 55).

 

Ndipo mtu anaweza kuuliza swali: Matendo ya Sheria ni nini? Qimron na Strugnell have wamefanya marekebisho ya maana ya dhana hii ya Matendo ya Sheria kwenye maandiko ya DSS. Yanahusika na sehemu tatu. Nazo ni kwanza kabisa kalenda inayobeba mistari ya idadi inayojiri kwenye tarakimu 1 hadi 21. Cha pili, ni maeneo ya sheria yanayotuama kwenye seti ya pili ya maandiko ya Kiebrania, yaliyopewa tarakimu 1 hadi 82. Tatu, ina kiahitimisha, kinachotuama kwenye seti ya tatu ya maandiko, tangu namba 1 hadi 32.

 

Viambishi vyenye nakala tofauti sita za hii MMT zilikutikana huko Qumran, kwa hiyo hilo sio andiko lililoondolewa au kutendanishwa. Kulikuwa na nakala nyingi sana miongoni mwa hizo. Ziliandikwa kwa kupangiliwa kwa namna mbili, ya kwanza ni kwa tarakimu ya 4Q, ikionyesha kuwa zinatoka kwenye pango la Qumran 4. Nazo ni 4Q394 hadi 4Q399. Pili, zimeonyeshwa kwa herufi kamili ya f. Kwenye pambizo za kushoto chanzo cha maandiko kimeonyeshwa kwa herufi na namba 4Q (kwenye mabano). Hivyo, mistari 18 ya kwanza ya kalenda yanatoka kwenye nakala a, ambayo ni sawasawa na 4Q394. Tarakimu zinazofuatia namba 4Q zinaonyesha nguzo na mistari (mingi imerudiwa kwenye maandiko mengine) (Nyongeza A).

 

Mstari mmoja unasomeka i [(siku) yake ya kumi na sita (yaani ya mwezi wa pili) ni Sabato]. Sasa hizi hazihusiani na nafasi ya kibiblia. Huenda hivi ni vigezo pia kwa kalenda inayotokana na jua kwenye Qumran, ambayo ni potofu. Inaonyesha utaratibu wa kupanga Siku Takatifu nje ya kisima. Hii ndiyo sababu inayopelekea baadhi ya mifumo ya kalenda iliyoathirika iondolewe. Na hii ndiyo iliyopelekea isiruhusiwe kuwepo hadi kufikia karne ya pili.

 

Marekebisho yanasema:

Siku yake ya ishirini na tat uni Sabato. Siku yake ya [thelathini ni Sabato. Siku ya Saba ya (mwezi) wa tat uni Sabato—siku ya kumi na nne yake ni Sabato—siku ya kumi na tato yake ni Idi ya Majuma [ambapo Pentekoste iliangukia siku ya kumi na 14 na 15 ya mwezi wa tatu kwenye hii Qumran: nah ii ni kinyume kabisa na maelekezo ya Mambo ya Walawi 23. Andiko linaendelea]. Siku ya ishirini—na moja) yake ni Sabato. Siku ya ishirini na nane yake ni Sabato. Baada ya siku hii (yaani Sabato) kunafuatiwa na siku za Jumapili na Jumatatu, [Jumanne iliongezwa (kwenye mwezi huu).

 

Haya ni marekebisho (kwenye majina ya siku tunazozitumia, ili kwamba uelewe kwamba siku za juma zipo kwenye maelezo ya siku hizi). Andiko hili linaendelea hivi:

Na majira yanaishia-kwenye siku za thamanini na moja. Siku ya kwanza ya mwezi wa nne ni Siku ya Ukumbusho. Siku ya nne]iii yake [ni Sabato. Siku ya [kumi na moja] yake ni Sabato, siku ya kumi na nane yake ni Sabato. Siku ya ishirini na tano yake ni Sabato. Siku ya pili ya mwezi wa tano ni Sabato. Siku ya tatu yake ni Sikukuu ya Mvinyo (Mpya)...

iv siku ya tisa yake tisa yake ni Sabato]. Siku yake ya kumi na sita ni Sabato. Siku ya ishirini na tatu yake ni Sabato siku ya thelathini [yake ni Sabato. Siku ya saba ya (mwezi) wa sita ni Sabato. Siku ya kumi na tatu yake ni Sabato siku ya kumi na nne yake ni Sabato ...

Andiko linaendelea kwa kuorothesha kisha Sabato zote za mwaka wote ,ona hatimaye kuhitimisha mwaka kwa Sabato zake, kwa kupitia Sikukuu za mafuta mapya na sikukuu za kutoa sadaka za kuni. Hizi sio Siku za sikukuu Takatifu ambazo Biblia imetuamuru sisi kuziadhimisha au tunazohitajika kuziadhimisha kwenye vipindi na majira yote ya Siku Takatifu. Bali kwazo ni mkururu wote tu wa sikukuu zilizo kwenye kalenda zilizopo kwenye mkururu wa majarida ya Matendo ya Sheria, ambayo yamesisitizwa kufanywa na watu bila kukatazwa moja kwa moja na biblia au kwa kiasi kikubwa kwa kutakiwa kuyaendeleza. Yanaonekana kuwa yalimgharimu Barnaba kwa mambo hayo. Hivyo ndivyo yalivyokuwa maandiko yenye madhara kwenye karne ya kwanza.

 

Andiko linaendelea kwamba:

1 Jinsi hizi zilivyo baadhi ya kanuni zetu [...] ambazo [baadhi ya kanuni zinazoambatana nazo ni]

2 [maelekezo] na maagizo ya (Torati) kwa mujibu wa [mapendekezo yetu, na] yote yaliyopo yanayohusiana nayo [...]

Yampasa mtu kukumbuka kwamba haya yamechimbuliwa yapata takriban miaka 2,000 iliyopita ya magombo yajulikanayo kama papyrus, na nakala zake fulani ningine hazionekani. Inaendelea:

3 na utakaso wa [... Na kutokana na vipaji vilivyopandwa au kuwekezwa za] punje za ngano mpya [wamataifa ambao wao...]

4 na hebu na[...] miguso yao na (kunajisi hakuna anayeweza kukila]

5 kila punje ya ngano mpya ya [wamataifa yapasa iletwe kwenye maskani takatifu.

 

Hapa tunapata wao - usiguse - usile - usionje. Maelezo haya ya Paulo yote yanafanya kuwa na mashiko sasa. Anaongelea kuhusu Matendo ya Sheria, jambo ambalo ndilo linalomanishwa kwenye andiko hili. anasema kwamba huwezi kutoholewa na kupelekeshwa vitu hivi. Inasema – usiguse hiki na usionje kile, na usifanye hilo. Hii haileti wala kusaidia chochote kwa wokovu wala kumpa mtu haki. Haki yetu i ndani ya Kristo Yesu. Huu ni ugunduzi mpya wa haraka, na nia andiko muhimu sana la kiutafsiriwa. Hii ni pia moja ya sababu ambayo maandiko Qumran yalijiri hadi miaka 50. Andiko hilo linavunjilia mbali hoja za siku za leo za Waprotestanti. Bali hii inaihalalisha na kupipa mashiko zaidi Sabato tuijuayo na tuliyoizoea na nafasi ya kuziadhimisha Siku Takatifu Kanisani kwa ujumla. Wapinga torati au waanti nomia wa siku hizi wameletwa kwenye msimamo mgumu wa kuyaamini machapisho ya maandiko haya. Hawanaudhuru wowote kabisa wala la kujitetea.

 

Tunaenda moja kwa moja kwenye wazo hili sasa (kwenye mstari wa 5).

Kila punje moja ya ngano ya wa[mataifa], [wala] haifai iletwe kwenye maskani takatifu. [Na kuhusu dhabihu ya utakaso]

6 kile wanachopika kwenye vifaa vya [shaba] [na wana...] ndani yake,

7 nyama aa dhabihu zao, ambazo wana zi [...] kwenye nyua za Hekalu (?)...

 

Na kwa hiyo tunaongelea kuhusu sadaka jinsi walivyokuwa wakizitendea kwenye nyua za Hekalu. Hawakuwa na jinsi ya kulitamalaki Hekalu! Lakini walifanya uelimishaji mdogo walioutaja au kuenekez Hekaluni. Walichokuwa wanakifanya ni kutengeneza kanuni na taratibu kwa kitu ambacho hawakuwa na uthibiti nacho. Lakini kwa kweli, walikuwa wanawaambia Mafarisayo na mamlaka za marabi jinsi utaratibu huo unavyotakiwa uwe. Sasa hili limekujakuwa ni jalada la habari yenye mvuto na ushiwishi mkubwa sana kwenye maeneo yote ya Mashariki ya Kati kipindi cha karne ya kwanza. Ilimpelekea hadi Paulo kuwafanya sehemu ya Warumi na Wagalatia walisome vizuri na kwa uangalifu andiko hili. Hii ndivyo jinsi ilivyoenea ulimwenguni kote ikiwa.

 

Inaelezea kuhusu

8 sadaka au dhabihu zao zote. Na kuhusu sadaka zinazotolewa na wamataifa: [tunashauri kwamba] sdaka

9 yaani [...] ni kama vile ya (mwanamke) aliyezini naye, [Na kuhusu mkururu wa dhabihu] zinazotolewa

 

Kwa maneno mengine, walishambulia moja kwa moja kila kitu walichokifanya Wamataifa kwenye dhabihu zao Hekaluni. Wapinzani wao waliacha mkururu wa dhabihu kutoka siku moja na inayofuatia. Waliasisitiza kwamba zilipaswa kuliwa kabla ya kuchwa cha jua ya siku ile iliyotolewa sadaka.

 

Hata hivyo, mtu anapata wazo likimjia, kama alilokuwanalo Yohana, ambalo linaelezea kuhusu mwanamke, dini potofu ya uwongo, ambayo ni kahaba, kwa kuwa Yuda waliichukulia dini ya uwongo kama ni kahaba ikihusishwa na Mungu na ni kama mwanamke mzinifu.

 

Inasema kuhusu sadaka zao za hiyari, ambazo wapinzani wao wanaziacha juu kutoka siku moja hadi inayofuatia, lakini imeandikwa, kwenye kipengele cha 11, dhabihu zoye zinazotolewa zinapasa ziliwe baada ya shahamu, na nyama zinazotolewa mchana ambazo zinatolewa kabla ya kuzama jua. Kwa watoto wa Makuhani wanawajibika kujitunza na kutilia maanani kuhusiana na jambo hili, ili wasisababishe watu kuadhibiwa. MMT inaonyesha rejea ya sheria takatifu za ng’ombe anayetolewa sadaka, yaani, ng’ombe mwekundu. Yeye anayemchinja ng’mbe huyu na yeye anayemuoka motoni, na yeye anayemkusanya pamoja kwenye majivu, na yeye anayemnyunyizia maji, kwa kumtakasa, ni baada ya kuzama kwa jua ndipo wote watakuwa wasafi.

 

Sasa tunaelewa vyema kuhusu dhabihu hizi za sadaka za mtamba mwekundu (Hesabu 19:2). Waandishi wa MMT wanahusika vyakutosha sana na dhabihu hizi. Wanaziwekea utaratibu dhabihu. Anachokisema Paulo, mara nyingine tena, ni kwamba sadaka hizi zote za utakaso zilikoma. Ni nakala ya msamaha au cheirographon, kama ukipenda ni kusamehewa au kufutiwa deni, iliyogongomelewa mtini kama ilivyoandikwa kwenye Wakolosai. Kitabu au nakala ya msamewa wa madeni, cha kwamba dhambi zote zimekusanywa na kuwekwa ndani mwake, ndicho iliyogongomelewa mtini. Lakini mtu anaweza kuoja jinsi ilivyo hatarishi. Dini ziliyofanya seti ya pili ya kanuni kama za Talmud, ambazo zilifanyika kuwa ni mkururu wa maandiko yaliyowezesha kusaidia maisha yetu ya kila siku, na ilikuja kuwa kama mwendelezo wa marabi wa Kiyahudi, lakini ni kinyume chake. Kwa hiyo, wanashikilia kwa kuosha mikono yao na kwa kuliangalia kile wanachokifanya kula, kile wanachokwenda kukishirikisha au kukiunganishanacho pamoja na dhabihu zao.

 

Sasa ndipo wanaelekeza habari za makuhani. Wanawataja makuhani kama wana wa Haruni. Wanamaelekezo kwa ajili ya maji ya utakaso na kitovu chake cha Mjadala kilichopo kwenye (18 ff.) kwenye maficho ya mifugo ya ng’ombe na kondoo. MMT inaelezea kuhusu kuwaleta kwenye maskani yao takatifu. Pia kwa mfano:

Kuhusu ngozi na mifupa ya wanyama najisi. Imekatazwa kufanya mikono ya vyombo kutoka mifupani mwao na ngozi zao.

Huwezi kumbeba mnama aliyekufa na kutumia mifupa yake na kwato na mikono ya mfupa na kuviweka kwenye vyombo vya kupikia, kwa kuwa itavifanya vifaa vyote vya kupikia vichafuke au vinajisike. Kwa hiyo, hivi vyote ni kanuni unazopaswa kuzifanya kwenye matendo na mwenendo wako wa kila siku. MMT inaichukua Torati na kuienekeza kwenye taratibu hizi za utakaso.

Na kuhusu ngozi ya mizoga ya wanyama najisi, yeye anayebeba mizoga kama hiyo ya wanyama waliosafi, yeye aubebaye mzoga kama huo hataruhusiwa kuingia kwenye chakula safi.

Hivyo basi, hata mizoga safi, na huruhusiwi kula chakula kilicho safi. Kwa mfano, kutokana na hii, kama ulikuwa unafanyakazi kwenye machinjio, hutaweza kushriki kula sadaka ya mkate mtakatifu pamoja na mvyinyo wake. Kwa hiyo, hivi vyote vimeonekana kuwa havina maana wala umhimu na ambavyo Paulo alivipuuzia na kuvielezea kuwa havina mashiko yoyote sawa na dhabihu ya Kristo. Hata hivyo, alikuwa hamaanishi kuwa anazitangua sheria za Agano la Kale. Alikuwa anatangua baadhi ya sheria zilizohusiana na zama za Agano la Kale peke yake. Sheria ya utoaji dhabihu ni wazi sana kabisa kuwa iliondolewa au kukomeshwa na Kristo mwenyewe, kama ilivyofundishwa na mitume, na ni kama nilivyoielezea kwa kina kwenye jarida la Utafauti wa Sheria. Kwa hiyo, una haya mambo matatu. Tunashughulikia mambo haya matatu tofauti ya sheria kwenye Agano Jipya. Paulo mwenyewe anaongelea kuhusu mambo matatu tofauti, na ndiyo maana unapata mkanganyiko wa dhahiri kwenye kile ananachokisema Paulo. Kwa kuwa hatukujua ni nini hasa maana ya Matendo ya Sheria. Lakini Matendo ya Sheria tunayoyajua sasa ni kazi ya uandishi, utunzi na ufafanuzi, kama maandiko ya Talmud, yanayokanganya Agano la Kale. Sasa ulijuapo hilo, ni rahisi. Twaweza kujionea kwa kupitia maandiko ya waantinomia ni kwa kuelewa kwetu tu na kwa kulinganisha kwetu na Biblia kama tufanyavyo. MMT haikutiliwa maanani wakati jarida ya Utofauti wa Sheria lilipokuwa linaandikwa, lakini ilikuwa ni rahisi sana kuzishambulia hoja za waantonomia pasipo hii. Kwa pamoja na maandiko ya MMT, hoja za waantinomia zinaharibika na kukosa maana kabisa. Mtu anaweza kusema na kumwambia mtu yeyote anayesema kwamba sheria imeondolewa au kutaguka, kwamba hawajui kile wanachokisema. Hii ndiyo mana inayokusudiwa na MMT. Tunajua sasa kile kilichokusudiwa na jarida la Matendo ya Sheria.

 

MMT inaendelea kuhusu habari au mambo ya makuhani na kwa yale yanayowahusu watu, ili kuwasababisha watu wahukumiwe.

 

MMT inaweka au kutenga mahali pa kuchinjia wanyaka ndani ya marago – kwa upande wa kaskazini mwa marago. Wanaamini kwamba maskani ni lile hema ya kukutania, na kwamba Yerusalemu ni kambi, na kwamba nje ya marago ni nje ya Yerusalemu.

Haya ndiyo marago ya ukazi wao (29-30). Ni nje ya marago ndiko ambako mtu aliweza [kutoa dhabihu?] sadaka za utakaso, na kuondoa majivu ya madhabahu na kuchoma au kuteketeza sadaka za utakaso, kwa kuwa Yerusalemu ni mahali ambapo amepachagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli.

Inaonekana kuwa wanafikia kutokana na hili kwamba Yerusalemu ni kituo kinachohamishika, kama makazi ya Israeli. Hii ina maana sana kwa shughuli zilizopo kwenye nchi ya utawanyiko.

 

Wanapinga kupitia maandiko haya, kuhusu mahali uchinjaji utafanyika, na ni wapi umwagaji wa majivu utafanyika. Hivyo tunaona kwa wazi sana na kuitazama sheria ya utoaji wa dhabihu, na sadaka za utakaso unaibuka kutoka kwa wanyama na dhabihu, na kutokana na wanyama wanaokufa wenyewe. Maandiko ya MMT yanajiri kuhusu sheria za takaso na usafi kwamba ni jambo kama la ugonjwa ulioenea kwenye jamii ya Kiyahudi kwa wakati ule. Yatupasa kuwahukumu kwa viwango vyao, na kile tunachokifanya.

 

Walikuwa wanajulikana kwa usafi! Wakiwa wanajulikana ubobefu wao kwenye sheria na kanuni! Ilikuwa ni utimilishaji. Paulo alishughulikia na hilo kwa kuwa Kristo alinuia kuweka uelewa wao wa kidini kwa msingi wa kifikra na utimamu mkubwa. Mtazamo huu wa kidini ulikuwa ni kikwazo kwa ulimwengu wote, nab ado ni kikwazo ulimwengu wote. Ni kwa kulisoma kwako tu mambo ya kama majarida ya Matendo ya Sheria, unagundua ukubwa wa tatizo alilokabiliana nalo Paulo.

 

MMT ndipo inaendelea mbele (kutokana 36) kwa namna ya tabia za kula kuhusu wanyama wenye mimba. Huwezi kuwatoa dhabihu mama mtu pamoja na kichanga chake kwa siku moja hiyohiyo. Huwezi kula kichanga kilichokutikana ndani ya tumbo la mnyama aliyekufa; kinaweza kuliwa tu mara tu baada ya kuchinjwa kihalali. Idadi hii yote ya mambo kutokana na kanuni zetu za kawaida za uthibiti, havifanywi na sis kabisa. Lakini hizi ni kanuni na sheria ambazo watu hawakuzitenda hivyo.

 

Nazi zinahusiana na habari au mambo ya ni nani anayeweza kuingia kwenye kutaniko. Waliotajwa ni Waamori, na Wamoabi, na wamamza, na yeyote aliyevunjika mapumbu yaye, na yule ambaye ni mwanaume aliyetoka nje ambaye hajaingia kabisa kwenye mkutano na kujitwalia wanawake na kufanyika kuwa mfupa mmoja, na kuingia kwenye maskani. Hapa MMT inaongelea kuhusu anayeweza kuoa na yule asiyeoa – ambapo sheria na kanuni zake zinavyosema. Na wanaongelea kuhusu unajisi wa wakazi wenza wao na kwa ukweli kwamba hawawezi kuungana na Waisraeli. MMT inaorodhesha mambo yaliyokatazwa kwenye muunganiko au kuoa mataifa mengine. Makatazo ya kuoana makabila au matabaka mbalimbali tofauti pia kuhusiana na ndoa za nje ya makabila. Pia MMT inaongelea kuhusu kuwapofusha watu, hivyo watu walioposhwa wawe makini na wajue kuhusu mchanganyiko, na wasione mchanganyiko unapokuwa unajitokeza. Wanapaswa kuwa na maandalizi ya sadaka. Kwa hiyo, kama wewe ni kipofu, hutaweza kuchanganya kitu chochote kwa kuwa itakupasa kujua kwamba unakula na kuvaa. Ni mzogo gani unaoweza kumtwisha kipofu. Kuna idadi kubwa ya mambo ambayo kwayo yanahusiana na majarida ya Matendo ya Sheria. Sasa unaelewa alichokuwa anakikanusha Paulo. Kwa nini alikuwa akilaumiwa na kushutumiwa sana. Wapingaji wa MMT walidhani kuwa hii inamuwezesha mtu kuwa mtakatifu. Hakuna utakatifu wowote kwenye hiki tunachokisoma kwenye MMT. Sheria za utoaji sadaka zimetanguliwa. Sheria za utoaji sadaka zinachukuliwa kuwa ni somo la kufutiwa madeni au hati ya mashitaka, lakini utakatifu na kuhesabiwa haki kumetokana na Yesu Kristo. Hatupaswi kuchukulia maelezo yoyote ya MMT kuwa ni utakatifu, au lolote kati yake kuwa hata kiini cha imani yetu au kuhusiana na imani yetu.

 

MMT inaendelea kuyapitia swali lote kuhusu vimiminika – mbwa kuingia maragoni – na kuila mifupa ya mahali patakatifu - Yerusalemu kuwa ni kitovu au maskani ya Utakatifu, nk. Vimehusika na hayo kama mahala pake pa kimakao. Waliuona Yerusalemu kama ni makao makuu ya maskani ya Israeli. Walizungumzia kuhusu matunda ya miti iliyopandwa kwa ajili ya chakula kwenye ardhi au nchi ya Israeli. Vilipaswa kushughulikiwa na malimbuko sawasawa na haki ya makuhani. Ni sawa tu pamoja na zaka na mifugo walizopewa

.

Pia, kuhusu wakoma walioponywa, dini za MMT zilikuwa na wazo kwamba hawataweza kuingia mahali popote palipo na chakula kitakatifu, lakini kinapasa kutengwa na kuondolewa, na nje ya kila nyuma (64-70 uk. 59 f.). Kama mtu atahalifu kabisa amri ya marufuku haya, na sababu au ukweli uliomuepusha yeye, basi alilazimika kuleta sadaka ya utakaso. [[Na] kuhusu yeye ambaye anazivunja sheria au kanuni kwa makusudi, imea[ndikwa kwamba anadharau na kukufuru] (70 ibid.).

 

Kwa hiyo ndipo tunakwenda na kuelekea mbele kuhusu dhana ya wakoma na wanyama safi na mchanganyiko na wasio safi, kwa mfano, kupanda mashamba yako kwa mizabibu na kuchanganya na halua au mazao jamii ya viungo. Huruhusiwi kufanya hivyo pia kutokana na maandiko ya biblia. Kisha MMT inaongelea kuhusu ulimaji wa kuwatumia wanyama wasio wa aina moja wakafungiwa nira pamoja. Kuna mkururu wote wa matokeo ya matendo unayopaswa kuyafanya. Sisi, sasa, kwa ajili ya mazoea yetu ya kuishi mijini, tunajifungia nira visvyo sawasawa kwa maana ya watu wa malumbano na mijadala iliyo tofauti. Wao kwanza kabisa waliichukulia hii kwenye dhana au wazo la kimwilia la kuwa hairuhusiwi kufanya hivyo au kuwatumia chini ya sheria, na ndipo walifanya taratibu za zaidi sana (kutokana na maelekezo ya biblia) kuhusiana na kile unachotakiwa kukifanya. Kisha zilikuwepo kanuni na miongozo ya vile unavyopaswa uje navyo nyumbani mwako. Kulikuwapo na dhana ya uzinifu au kuzini na wanawake. Makuhani walikatazwa kuoa wanawake najisi au makahaba au wasio na bikira. Hukuruhusiwa kuchaganya mbegu, kwa hiyo lilikuwa ni suala la kuchanganya mbegu; na halikuwa ni suala au tatizo la kiroho/la kimaadili. Dhana au mawazo haya yote yalikuja onekana kwa mtazamo wa kimwili. Muundo na mfumo mzima wote wa Roho, uelewa wetu wa kile tulichokuwa tunakifanya kiroho, vilidharauliwa kabisa na andiko hili kuhusu Matendo ya Sheria. Ilipunguza kila kitu kwenye kiwango cha kimwili na kisicho na kiroho.

 

Kimsingi, MMT iko pale ili kuwezesha au kutoa baraka na laana. Wanachokisema wandishi ni kwamba, wakati inapochemka, ni kwamba baadhi ya Baraka na laana zimekwisha timilika tayari kama zilivyoandikwa kwene kitabu cha Musa. Baadhi ya Baraka zingine kutoka Sulemani na baadhi ya laana tangu i na baadhi ya laana tangu Yeroboamu (18-19 op. cit. p. 61). Inataja hadi aya ya (21) nyakati za mwisho wakati watakaporudi nchini Israeli (22) milele ... na haitaahirishwa (?) lakini wanyonge na watenda dhambi wanatenda uovu mkubwa. (Kuna matukio ya kupatwa jua kwenye maandiko haya). MMT inaendelea kuanzia aya ya (23 ibid. p. 61)

23 na [...]. Wafikirini wafalme wa Israeli, na yatafakarini matendo yao; kila mmoja wenu

24 walioitii Torati waliokolewa kutoka matesoni, na hawa walikuwa ni watafuta Torati

25 enyi aliosamehewa [maovu yenu. Mtafakarini Daudi ambaye alikuwa mtu mwenye matendo ya haki na

26 yeye ambaye (kwa hiyo) ameokolewa kutoka kwenye mateso mengi na kusamehewa. (Kwa hakika) sisi tumekupeleka wewe

27 miongozo mingine ya Torati kwa mujibu wa maamuzi yetu kwa ajili ya mambo yako na ustawi wa watu wenu. Kwa kuwa tumeliona (hilo)

28 unayo hekima na uelewa wa Torati. Tafakari mambo haya yote, na muombe ili akutie nguvu

29 mapenzi yako, na ondoka kutoka kwako mipango yote miovu na mambo ya Beliali

30 ili uweze kufurahi mwishoni mwa nyakati, ukikuta kwamba baadhi ya matendo yetu yako sahihi.

31 na hii itahesabiwa kama ni matendo makuu yako, kwa kuwa unafanya yanayoelekea na yaliyo mema machoni pake kwa ustawi wako wewe, na

32 kwa ustawi na maslahi ya Israeli.

 

Miongozo ya MMT kuhusu Sheria, au Matendo ya Sheria, ndipo imefanyika muongozo wa kufanikisha kufikia utakatifu. Hii sio kweli. Sasa tunaweza kujua kile alichowa anakipata Paulo a alichokuwa anakisema. Matendo ya Sheria, au MMT au ergon nomou hayamfanyi mtu kuwa mkamilifu wala hayamhesabii haki. Tunaona kwamba alikuwa anapinga na kile alichokuwa anakifananisha na utakatifu au haki ipatikanayo kwa njia ya imani. Tumeandaliwa vizuri na kikamilifu sasa ili kuyapinga masuala ya maana ya nyaraka kwa Warumi na Wagalatia na uadilifu wa maandiko. Kwenye jarida linaloongelea kuhusu MMT na Utofauti wa Shria, tumeandaliwa vizuri kukanusha madai haya ya Waprotestanti wa siku hizi. Kwa sasa unajidhihirisha kwa wazi sana kabisa kwamba wamepotoka na kukosea sana. Siyo Torati inayowezesha kuwa mkamilifu, na kwa kweli siyo sheria hizi za usafi zinazowezesha mtu kuwa mkamilifu. Kile kilichofanywa na hivi ni kiambisho au kurahisisha sheria ya sadaka na ya utakaso kwenye Torati kwa kujaribu na kuifana kuwa ni sehemu ya uwezeshaji wa kuupata utakatifu au haki.

 

Ni sheria ya maadili ya kijamii inayotokana na asili na tabia za Mungu zinazowezesha kuupata utauwa. Unaweza kufikiria kuwa kwenye karne ya kwanza mkiwa kama Wakristo alioketi pamoja na watu wakiwa wanazungumzia hilo. Inakuwa ni gumzo la jumla kwamba tumepewa kufana kitendo hiki au tendo lile. Yatupasa kuwa wasafi. Hatuwezi kuutumia mfupa ule kufanya mikono kwa lengo hilo. Hatuwezi kumtumia mnyama hadi mahala fulani. Huwezi kuifanya kazi hii na isiweze kuifanya ile. Itakuchanganya sana. Tungewasikia watu hawa wakisema kuwa imewezekana kufanyika kwa kuwa imo kwenye Matendo ya Sheria. Matendo ya Sheria yanasema. Ni kama mtu anayesema kwamba kiongozi mmoja wa kidini alisema, au Askofu x alisema. Hii inaonekana kuwa kama ilitokea.

 

Kama ilivyotupasa kuzishughulikia kazi au matendo mapotofu ya uwongo kwa suala la Pasaka inayojaribu kuifanya siku ya 14 Abibu ambayo ni Pasaka kutokana na kifichio cha uwongo, na ndivyo ilivyo pia kwamba ilitupasa kushughulika na suala la hii MMT. Paulo alishughulikia kwayo, kwa kuwa ni wazi sana iliingia na kuathiri Kanisa la Galatia. Haikuwa ni bahati mbaya kwamba hayakuishia Galatia tu bali inasemekana kuwa yalienea na kufika hadi kwa Warumi kwa kuwa jumuia ya Wayahudi wa Roma walikuwa mbali sana kutoka Yerusalemu kuliko ilivyokuwa Galatia. Kadiri ilivyokuwa mbali na matatizo yalipungua, lakini kwa kweli katika Mashariki ya Kati kulikuwa na matatizo mengi na makubwa. Ulikuwa ndiyo kipindi ambacho Hekalu liliwekwa alama ya kuangamizwa. Na ndiyo maana kwamba Hekalu na mazingira yake yote viliangamizwa vyote, kuondolewa mifumo yote iliyowekwa na Wayahudi na ambayo haikuwa ya kibiblia. Kwa hiyo utaratibu wote mzima uliendelea mbele kwenye mfumo wa msafishaji, ili kwamba tuweze kuona kwa maana ya kiroho, badala ya kushikamanishwa kwenye kanuni zote za kidini ya mambo hayo. Hata hivyo, moja wapo ya majeruhi wa uondoaji ulikuwa ni ujuzi ukweli wa uwepo mambo haya. Hatukujua kwamba Matendo ya Sheria kwa kweli lilikuwa ni jarida lililoandikwa. Kilikuwa ni kitabu. Hakikuwa kinatendewa kazi. Tunaweza sasa kuona kwenye maandiko kwa mtazamo wa ukweli kwamba huenda Paulo alichokuwa anakisema kilikuwa, kwa kweli rejea ya MMT. Haijumuiki bado, lakini wasomi wanazuoni sasa wana uhakika – kwamba hivi ndivyo hakika kinachomanishwa. Dalili zake ni za kimabadiliko badiliko. Siyo kwa Kanisa la Mungu, wanaojaribu kutangua. Ni suala mtambuka kwa kwa Waprotestanti wa zama zetu hizi ambao wanapuuzia tofauti kwenye sheria ambayo ilikuwa imeeleweka wazi sana na wao nyakati za Matengenezo hata kama hawakuielewa Pasaka na Siku nyingine Takatifu zilizo kwenye mpango wa wokovu kisahihi. Kanisa limeshuhudiwa kwa kukutwa hivi. Ukristo wa siku hizi ndipo utaweza kuona, kiusahihi zaidi, kwamba Kanisa la Mungu linafanya vizuri na sahihi sana kwa hakika tangu mwanzo.