Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[094]

 

 

 

 

Mahali Yalipo Makazi Yetu

(Toleo La 2.0 19950403-20000617)

Jarida hili linaelezea kuhusu anguko la mwanadamu kwenye bustani ya Edeni. Uhusiano wake na Kanisa unaainishwa na msingi wa harakati zetu kupambana na Shetani unaelezwa pia. Mahali akaapo Shetani kwenye Ufunuo 2:12-13 panakanganywa na makazi ya wateule. Mgawanyo wa uumbaji au viumbe uliosababishwa na Malaika waasi unaonekaniaaKanisa la Wamataifa, bali ulikuwa umetokana na kwa kupitia Maandiko Matakatifu.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

 

(Hatimiliki © 2000 1996, 2000 Storm Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Mahali Yalipo Makazi Yetu

 


Jarida hili linatathmini kuhusu dhana sahihi kuhusu mahali tunapoishi kwa kweli, kile tukionacho kuwa ni kama makazi yetu yapasa yawe hivyo hakika.

 

Tutaanza na mwanzo wenyewe hasa kwenye bustani ya Edeni, ambapo kulifanyika kukutana kwa kwanza na adui wetu, ambapo uelewa wetu wa uovu uliingia kwenye nia na mioyo yetu.

 

Nyumbani petu pa kwanza na hatimaye kukataliwa

Mwanzo 2:15-25  Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza. 16 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, 17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.

 

Hii ilikuwa ni amri ya kwanza kuandikwa ambayo Mungu alimwamuru mwanadamu. Amri hii alimpa Adamu kabla hata Hawa hajakuwepo, na hivyo Adamu akafanyika kuwa ni wakuwajibika kwa Mungu kwa dhambi ya mke wake, akiwa ni kama mtu ambaye aliyepewa amri hii.

 

18 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye. 19 Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake. 20 Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye. 21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. 24 Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja. 25 Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.

 

Kwa muda kitambo, Adamu na Hawa waliishi bila dhambi na kwa mtengamano na Mungu na njia zake. Hiki kilikuwa ni kipindi kifupi cha kuishi kwao.

Mwanzo 3:1-19 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani? 2 Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; 3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa. 4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, 5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya. 6 Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala. 7 Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo.

 

Kutoka kwenye hatua hii ndipo mwanadamu akaanza kuijua dhambi. Dhambi ikaingia maishani mwake, kwa vyovyote vile na sheria za mungu au torati haikuwa imeondoka au kutoweka. Mti huu ulikuwa ni wa ujuzi wa mema na mabaya.

8 Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, Bwana Mungu asiwaone. 9 Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi? 10 Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha. 11 Akasema, Ni nani aliyekuambia ya kuwa u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale? 12 Adamu akasema, Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti huo, nikala. 13 Bwana Mungu akamwambia mwanamke, Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala. 14 Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; 15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.

 

Hapa tunaona jinsi Shetani alivyotupwa hapa duniani. Uweza wake una kikomo na Kanisa, ambalo Hawa anafananishwa nalo, liliachwa liteseke na kushambuliwa na Shetani. Kulindwa kwa Kanisa ulikoma na sasa unategemea kabisa na viwango vya matendo yetu kwa Mungu na dhidi ya Shetani. Sisi tu mvuto mizania kwa Shetani kwa jinsi hii. Matendo yetu na kujitoa kwetu kwa Mungu kunaonyesha uwezo au kiwango ambacho kwacho Shetani anaweza kuiendesha na kuitawala sayari hii. Kama tutakuwa wavivu ndipo ndipo nguvu za Shetani zinakuwa kubwa kuliko zetu. Wakati tunapokuwa na nguvu nyingi hapa duniani, kwa kuwa tunafanyakazi kwa ukaribu sana na Mungu, ndipo Shetani anafanyika kuwa dhaifu na idadi kubwa ya watu walioko ulimwenguni inapungua. Hapa kazi ya adui inaendelea. Kanisa limewekwa ili lipambane na uovu na ni wito wetu.

 

16 Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.

 

Hapa tunaona mfano wa kwamba kanisa litapitia mambo magumu. Kristo amepewa kuwa hakimu wetu hapa duniani sasa.

17 Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; 18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; 19 kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi

 

Wakati Adamu na Hawa walipokuwa wanaishi kwenye Bustani ya Edeni walikuwa kwenye nyumba ambayo Mungu alikuwa amewaandalia hapa duniani. Kwa kula kwao tunda lililokatazwa, waliikataa nyumba iliyokuwa waliyokuwa wamejengewa na kuichagua nyumba nyingine ya tofauti. Nyumba hiyo ilikuwa hapa duniani, ambayo ni nyumba au makazi ya Shetani, kwakuwa ni yeye ndiye anayeishi kwenye makazi ya hapa duniani akiwa kama mungu wa dunia hii (2Wakorintho 4:4) na mfalme wa nguvu za anga (Waefeso 2:2).

 

Kwa hiyo, dhambi hii ya kwanza ilikuwa ni uamuzi wa kumkataa Mungu. Mungu hakumuua Adamu kwa ajili ya dhambi zake. Alimpa mapenzi yake ambayo ni uwezo wa kuyajua mema na mabaya na kuwa kinyumba wa Shetani. Ni wazi sana kwamba Mungu anatuacha tuchague na kutufanya kutenda au kuenenda sawasawa na uamuzi huo. Kile ambacho hakukijua Adamu ilikuwa ni mwendelezo wa hali kinyume ya maamuzi ambayo ni kinyume na mapenzi ya Mungu.

 

Kama tunaelewa mahali ambapo Shetani anakaa, tungekuwa na uelewa mzuri wa mahali ambapo hatupaswi kuishi. Haitupasi kutamani kuishi hapo, kama walivyofanya Adamu na Hawa.

 

Ufunuo 2:12-13 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Pergamo andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na huo upanga mkali, wenye makali kuwili. 13 Napajua ukaapo, ndipo penye kiti cha enzi cha Shetani; nawe walishika sana jina langu, wala hukuikana imani yangu, hata katika siku za Antipa shahidi wangu, mwaminifu wangu, aliyeuawa kati yenu, hapo akaapo Shetani.

 

Ni mahali gani basi hapa panapodhaniwa kuwa anaishi Shetani? Kwanza kabisa, tutaona kwa maana makazi ya kidunia kwenye kifungu hiki. Kamusi ya the Strongs inataja tarakimu ya neno hili ni 2730 ambalo inalitafsiri kuwa ni makazi ya kudumu. Je, mahali hapa palikuwa ni wapi? Hebu na tuuchukulie mji wa Pergamo au Pergamoni kama unavyojulikana kwa namna nyingine.

 

Kwenye kitabu cha ufafanuzi kinachoainisha maneno kutoka kwenye tafsiri ya Companion Bible, imeanzia na hilo ikisema:

 

Pergamo. Mji ulioko huko Mysia mashuhuri kwa kumuabudu mungu Esculapius, ambayo jina la kicheo la soter (mwokozi) aliopewa na ambaye alama au nembo yake ilikuwa ni joka kubwa. Anajulikana pia kama Apollo; sawa na ilivyo kwenye Matendo 16.16. Wengine wanawachukulia makuhani wa kipagani wa Kibabeloni kama ni kuondoka na kwenda Pergamo.

Ni watu gani basi hawa ambao hatuwezi kuwataja. Hata hivyo, William Barclay kwenye kitabu hiki cha ufafanuzi kuhusu Ufunuo, anatoa nuru ndogo chumbani ya kupendeza zaidi kwenye somo hili. Hebu na tutathmini kazi hii, kuanzia kwenye ukurasa 88:

 

Pergamo ilijichukuliwa wenyewe kuwa ni mlinzi wa njia ya maisha ya Wayunani na ya ibada za Wayunani. Mnamo mwaka 240 KK, ulipata ushindi mkubwa dhidi ya mashambulizi makubwa ya Galatae au Gauls. Kwa ukumbusho wa ushindi huo, madhabahu kubwa ya mungu Zeus ilijengwa mbele ya hekalu la Athene iliyosimishwa kwa takriban futi 800 kwenda juu kwenye mlima mrefu wa Pergamo. Futi 40 kwenda juu, ulisimamishwa kwa shubaka imullikayo ya mwamba na ikaonekana sawia kabisa kama kiti cha enzi kikubwa upande wa kilima. Siku nzima yote ulinukiwa na moshi wa dhabihu zilizotolewa kwa mungu Zeus. Kwenye kitovu chake kote uliwekwa nembo ya moja ya mafanikio makubwa kwenye ulimwenguni wa makaburi au maziara, michoro iliyoonekana vita vya Giants, ambayo kwamba miungu ya Kiyunani iliwashinda mabarbariani majitu....

 

Hii ni kama tunavyojua, ni ishara au alama ya vita vya Wanefili.

(b) Pergamo kimsingi ulikuwa umeunganishwa na ibada za mungu Asclepios, kwa kiasi kikubwa sana ili iwezeshe kumfanya mungu Asclepios ajulikane kuwa ni kama “mungu wa Pergamo”. Wakati Galen alipoitaja nadhiri za kupendeza, alisema kuwa kwa kawaida watu huapa kwa Artemis wa Efeso, au Apollo wa Delphi, au Asclepios wa Pergamo. Asclepios alikuwa mungu wa uponyaji na mahekalu yake yalikuwa inabarikiana kwa karibu sana na hospitali za ulimwengu wa kale. Kutoka ulimwenguni kote watu walifurika huko Pergamo ili kutafuta ahuani au kutibu magonjwa yao. R. H. Charles ameuita mji wa Pergamo kuwa “Lourdes aliyeishi zama za ulimwengu wa kale.” Kazi ya kuponya ilikuwa ni sehemu ya kazi za makuhani, na sehemu nyingine ikiwa ni ya madaktari waliojulikana kama Galen, wapili kutoka Hippocrates kwenye historia ya ulimwengu wa zama za kati, alizaliwa Pergamo, na kwa sehemu ni kazi ya Asclepios mwenyewe.

 

Barclay anaendelea kufafanua kwamba jina la kicheo la Asclepios lilikuwa ni hili la mwokozi na nembo yake ilikuwa ni hii ya joka kubwa. Hii inamaana bali inagusa tu upeo wa maana ya kweli.

 

....Pergamo ulikuwa ni kitovu cha uongozi cha Asia. Hii ilimaanisha kuwa ulikuwa ni kituo na makao makuu ya dini ya ibada ya kumuabudu Kaisari kwenye jimbo hilo. Bilashaka kabisa kwamba hii ndiyo sababu kwa Pergamo kuwa ni kiti cha enzi cha Shetani; palikuwa ni mahali ambapo watu walitakiwa kuteswa hadi kufa kwa kulichukua jina la Bwana na kumpa Kaisari badala ya Kristo, na kwa Wakristo wahuko hawakuwa na namna nyingine zaidi ya kuwa na ushawishi wa karibu sana wa Kishetani tu.

 

Na hapa kuna maelezo ya mwanzo wa waraka kwa Wapergamo. Kristo aliyekuja aliitwa kuwa yeye aliye na huo upanga mkali, wenye makali kuwili. Maliwali wa Kirumi waligawanyika kwa madaraja mawili—wale waliokuwa na Ius Gladii, haki ya upanga, (Ius maan ayake ni haki na Gladii maana yake ni upanga au silaha ambayo ni upanga wa Haki tunaoujua leo kama Kristo] na wale wasiokuwa nao. Wale waliokuwa na haki ya upanga wao,walikuwa na uweza juu ya uzima na mauti, kwa neno lao, ambapo mtu aliweza kuuawa hapohapo. Usemi wa mwanadamu wa liwali au naibu mwakilishi, aliyekuwa na makao haya makuu ya Wapergamo, alikuwa na Ius Gladdi, haki ya upanga, na kwa wakati wowote aliutumia dhidi ya Mkristo yeyote, bali waraka unawataka Wakristo wasisahau kuwa neno la mwisho bado lina Kristo mfufuka mwenye upanga ukatao kuwili. Uweza wa Kirumi yawezekana ulikuwa wa Kishetani, nguvu za mwanadamu ni Mungu bado ni.

 

Hapa tunaona kuwa Pergamo ulikuwa ni kituo cha nguvu za mnyama na iko huko Asia. Huyu Shetani aliye kwenye kiti chake cha enzi anachukua mamlaka kamili ambayo anayafanya Kristo. Kutokana na hili twaweza kuelewa wazi sana andiko la Mwanzo 3:24.

 

Mwanzo 3:24 Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima.

 

Ni Kristo ndiye anayeilinda Bustani ya Eden na ni kwa kupitia Kristo tu ndipo tutakapoweza kuiingia. Kristo ni mponyaji na ndiye mwenye kuwezesha kuupata utakatifu na haki ya kweli, ambayo ni haki na Kristo ndiye mwenye upanga wa kuume. Anatuhukumu na kututoa kikamilifu kwa Baba, nafasi ambayo Shatani anajaribu kwa wazi sana kufanya taswira ili aweze kuwapata watu wote wamuone yeye kwa namna tunavyomuona Kristo. Yeye ndiye mkombozi na mwokozi wetu.

 

Mtazamo huu hata hivyo, sio mwisho wa kitendawili kilicho kwenye Ufunuo 2:12.

 

Jina Antipas laweza kuwa na maana mbili. Kwenye kamusi ya Strongs linaonyeshwa kumaanisha “kwa sababu ya (au yeye aliye kwa niaba ya) baba” likiwa limetoholewa kwenye 473 na 3962. Kwa hiyo, Antipas mfa shuhuda au shahidi ni moja kwa moja ni mtu anayekufa kwa kuishudia imani ya Baba. Pas linaweza pia kumaanisha wote au kila kitu ambacho kilichofanyika sababu ya vyote. Hata hivyo, jina linguine zaidi la jumla limekataliwa na kamusi ya Strong. Kama tutaangalia nyuma kwenye jarida la Kazi na Wajibu wa Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu Yanayoishika Sabato (Na. 170), tutaona kwamba kilikuwa ni kipindi cha Wapergamo ambacho Wakristo walilazimishwa kuungana na kushirikiana na Waislamu, wakiwapigavita masalia ili wasiteswe na Watrinitariani. Na huku ni kupigana kwa ajili ya Mungu, Baba, ni pigano hilihili tupiganalo sasa (kama lisemavyo pia jarida la Migawanyiko Mikuu ya Makanisa ya Washika Sabato (Na. 122)). Kwa hiyo, ni sahihi kusema kwamba kutajwa huku kwa Antipas ni kwa kinabii na pia ni ujumbe kwetu sisi tulio anaposimama Kristo. Tunajua kwamba hapa tusimamapo kwenye jambo linalotegemea na pale tunaposimama. Kwa kuwa Kristo, yupo kwenye mkono wa kuume wa Baba yake. Yatupasa kuuchukua ujumbe huu kama ni mmoja ya zile kunazozishuhudia kama Antipas, tunapata kibali machoni pa Mungu.

 

Sasa tumepaona mahali anapoishi Shetani. Hebu na tutathimini sasa mahali anapoishi kaka na bwwana wetu.

 

Yohana 1:2-17 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. 3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika. 4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. 5 Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza. 6 Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana. 7 Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye. 8 Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru. 9 Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu. 10 Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua. 11 Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea. 12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; 13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu. 14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.

 

Kama tulivyoona mapema neno akkapo linapotumiwa kumtaja Shetani, likimaanisha kuishi kwa kudumu na moja kwa moja. Hata hivyo, maana hii inakusudi lingiine ls tofauti. Tafsiri hii ya neno skenoo litumikalo kumaanisha kuketi hapa ni mfano pekee kwenye Agano Jipya. Rejea ya kwenye kamusi ya Strongs nambari 4637 na inasomeka;

Kujenga hema au kufanya kambi, kutamalaki (kama mjenzi) au (hususan) kufanya makao (kama Mungu alivyofanya kwenye Maskani ya kale, ishara ya ulinzi na ushirika).

 

Tasfiri yake halisi ya andiko hili inapasa isomeke hivi;

 

Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; ...nk.

 

Kristo alitutembelea sisi ili kufanyika kuwa nuru gizani, kutonyesha tunayotakiwa kuyafanya na kuithibitisha Sheria ya torati kama ilivyotolewa. Kristo alikuwa mgeni aliyetembelea kwa muda hapa ulimwenguni. Makazi yake ya kuishi au nyumbani pake pa kudumu panaonekana kwenye Ufunuo 3:21 ambayo inasema:

 

Ufunuo 3:21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.

 

Kristo anaishi na Mungu. Nasi pia, na yatupasa tutamani hivyo, yaani kuishi na Mungu na sio kuwa mbali na Mungu, kama alivyo na afanyavyo Shetani. Mgawanyiko huu unaashiriwa na mfumo uliopo hapa duniani. Utashi wa kuchagua hata hivyo, kutuwezesha na kutufanya sisi tuchague. Maamuzi yetu yanafanyika kwa namna ambayo tunavyozielewa na kuzishika Sheria za torati; na ndivyo jinsi tulivyoonyeshwa jinsi ya kuabudu na yule tunayemwabudu.

 

Ifuatayo ni hadithi ya msingi sana kwenye tukio la Kutoka na inaonyesha idadi kkadhaa ya vipengele muhimu. Hebu na tusome.

 

Luka 4:1-13  Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani,

Vivyo hivyo pasi ndivyo Israeli walivyoongozwa na Musa chini ya Kristo, akiwa kama Malaika wa Elohim

 

2 akijaribiwa na Ibilisi.

 

Kipindi cha siku arobaini kinahusiana na matujio haya yote mawili kwa miaka arobaini ya kwenye jangwa ka Sinai na la Yubile arobaini za Kanisa la Agano Jipya.

 

Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.

 

Muhu hataki kujidhihirisha tu kwetu sisi kwa namna ya kimwili, bali na pia kwa njia ya uweza wa Roho Mtakatifu ambaye Kristo alijazwa naye alipoingia na kwenye kipindi chake cha kuwa jangwani

3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate. 4 Yesu akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu.

 

Hapa Kristo sanatuambia kwamba uwakilishi wa kimwili wa Mungu hapa duniani haukuwa ni kwa ajili ya kanisa la Wamataifa na wala haukuwa na kanisa hilo, bali zaidi na kimsingi ni wa njia ya Biblia. Kwa hiyo Sheria ilikuwa ni mkate wetu na imani ilikuwa ni maji yetu.

5 Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja. 6 Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo. 7 Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako. 8 Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.

 

Hapa Shetani anaelezea mahali anapopaona kuwa ndipo nyumba na makazi yake, pajulikanapo, hapa duniani. Anampa Kristo kile Mungu alichompa yeye kama sehemu ya wajibu wake mbunguni na anajaribu kuhonga Kristo kwa kitu muhimu cha ufisadi wake (Shetani). Kristo, kwa majibu yake anaonyesha kuamua mahali apendapo kuwa makao yake. Hii ni wazi, kuonekana kuwa mtazamo na nia yake ilikuwa i kwa Mungu Baba na kwenye Mapenzi yake. Ndivyo pia yalivyokuwa mapenzi na nia ya Nuhu na ndivyo alivyokuwa Musa na Ibrahimu, kwa kuwataja wachache tu walioishi maisha ya kumpendeza na kumtii Mungu.

9 Akamwongoza mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini; 10 kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde; 11 na ya kwamba,mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe. 12 Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako. 13 Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake kwa muda.

 

Hapa Shetani anakamilisha majaribu. Kristo, kwa kutuonyesha mfano huu, anatuambia jinsi Shetani anavyotushambulia.

 

1) Anatupa kitu kilekile tunachokitamani baada ya wakati tunapokuwa kwenye hali ya mvurugiko wa kiroho.

 

2) Anatupa nguvu au uweza na mamlaka tunapokuwa kwenye hali dhaifu sana na duni ya uaminifu na kujiamini.

 

3) Anatujaribu kwa vitu vilevile tunavyovishikilia na kuviona kama vitu vyenye nguvu sana na muhimu tuwenavyo, na kuturubuni kwa kuvimiliki ili kutufanya tuwe dhaifu tena na tena. Na hivyo hutufanya tuvunje mawasiliano yetu yote na Mungu.

 

Ulingano wa wakati aliokuwa Kristo akijaribiwa jangwani ni sawa na kipindi wana wa Israeli walipokuwa na Musa. Maana yake ni kwamba sisi tuko jangwani pia, tukitangatanga kwa kuwa hatuna nyumba au makazi. Israeli waliuwa kwa kipindi cha miaka kadhaa ugenini, kabla ya kuachiliwa kwao warudi kwenye jengwa linguine. Ndivyo alivyokuwa pia Kristo kuwa ni mgeni hapa Duniani ambapo alijaribiwa jengwani.

 

Shetani alijatibu kumleta Kristo kwenye hatua ambayo alitimiliza hitaji la kuwa nyumbani mwake na kumfanya aje kuishi kwenye makazi ya Shetani. Shetani anafanya kitu hichohicho na kwetu sisi sote. Kazi ni kujihadhari na maamuzi yetu na mahali ambapo maamuzi hayo yanapotupeleka sisi; ni kwenye nyumba ya Mungu, au, ya Shetani. Nyumba au makazi ya Shetani yako hapa duniani, yakiwa ni ya muda mfupi na hatimaye yatakomeshwa na Mungu. Makazi ya Mungu ni ya kiroho nay a milele au ya kimbinguni. Swali ni kwamba: ‘Je, tunapotangatanga hapa duniani au ni kweli tunajiona kwa hakika kwamba maisha yetu ya hapa ni ya kitambo tu?’ swali hili laweza kuendelea kuulizwa hata sasa.

 

Mwanzo 18:16-19:30 Kisha watu hao wakaondoka huko wakaelekeza nyuso zao Sodoma. Ibrahimu akaenda pamoja nao awasindikize. 17 Bwana akanena, Je! Nimfiche Ibrahimu jambo nilifanyalo, 18 akiwa Ibrahimu atakuwa taifa kuu, hodari, na katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa? 19 Kwa maana nimemjua ya kwamba atawaamuru wanawe, na nyumba yake baada yake waishike njia ya Bwana, wafanye haki na hukumu, ili kwamba Bwana naye akamtimizie Ibrahimu ahadi zake. 20 Bwana akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,

 

Katika wakati huu wa Ibrahimu, tukio la gharika kuu lilikuwa lingali bado ni jambo linakumbukwa kuwa limetokea hivi karibuni. Mungu, hata hivyo, atamuacha mwanadamu ajiangamize mwenyewe na aiangamize dunia tena ili kuonyesha ni nini matokeo ya dhambi na hatimaye kuisafisha dunia. Leo ulimwengu uko kwenye ukengeufu mkubwa wa kiroho zaidi ya ilivyokuwa Sodoma. Hatuwezi kuendelea kumdhihaki Mungu au vinginevyo atatuangamiza na watu wanapaswa kuonywa.

 

21 basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua. 22 Basi wale watu wakatoka huko wakaelekea Sodoma; lakini Ibrahimu alikuwa akali akisimama mbele za Bwana. 23 Ibrahimu akakaribia, akasema, Je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu? 24 Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu, wala hutauacha mji kwa ajili ya hao hamsini wenye haki waliomo? 25 Hasha usifanye hivyo, ukamwue mwenye haki pamoja na mwovu, mwenye haki awe kama mwovu. Hasha; Mhukumu ulimwengu wote asitende haki? 26 Bwana akasema, Nikiona katika Sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha mahali pote kwa ajili yao. 27 Ibrahimu akajibu, akasema, Basi, nimeshika kusema na Bwana, nami ni mavumbi na majivu tu. 28 Huenda wakapunguka watano katika wale hamsini wenye haki, je! Utaharibu mji wote kwa kupungua watano? Akasema, Sitauharibu, nikiona humo arobaini na watano. 29 Akazidi tena kusema naye, akinena, Huenda wakaonekana humo arobaini? Akasema, Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini. 30 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema, Huenda wakaonekana huko thelathini? Akasema, Sitafanya, nikiona humo thelathini. 31 Akasema, Tazama, nimeshika kusema na Bwana, huenda wakaonekana huko ishirini? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao ishirini. 32 Akasema, Bwana asiwe na hasira, nami nitasema mara hii tu, Huenda wakaonekana huko kumi? Akasema, Sitaharibu kwa ajili ya hao kumi. 33 Basi Bwana alipokwisha kuzungumza na Ibrahimu, akaenda zake; Ibrahimu naye akarudi mahali pake.

 

Ibrahamu alikuwa mwenyehaki na mtu mkamilifu na kwa ajili hiyo aliweza kumjongelea Mungu na kuwaombea watu wake kwa ujarisi kama alivyofanya. Hii ndiyo kazi yetu. Nasi pia inatupasa tumwendee Mungu kwa niaba ya watu wetu na kuwaombea rehema. Dhambi isimamayo mlangoni hapa sio moja tu ya uzinzi pekeyake na ushoga tu kama inavyoonekana kuhusishwa na hadithi hii, bali pia na ya unafiki. Kwa Ibrahimu kudhani kuwa kulikuwa na wenye haki zaidi ndani ya mji wa Sodoma, basi ni budi kwamba walikuwepo watu wengi waliojidai kuwa ni wenye haki au watakatifu. Yawezekana kuwa walikuwa wanafanya ibada za wazi na kuzikiri Sheria kwa midomo bali wakizikana kwa wazi mioyoni mwao. Kwa mtazamo wangu, Ibrahimu mwenyewe hakupenda kuuona ule mji ukiangamia. Anaonekana alikuwa na hisia ya kuuhurumia. Lakini wakati Mungu alipomwambia atoke, yeye akiwa kama mtu wa imani, alifanya kama alivyomuamuru Bwana. Imani na utii ni vitu vinavyoenda pamoja.

Mwanzo 19:1-26 Basi, wale malaika wawili wakaja Sodoma jioni; na Lutu alikuwa amekaa mlangoni pa Sodoma. Lutu akawaona akaondoka akaenda kuwalaki, akainama kifudifudi. 2 Akasema, Bwana zangu, karibuni nawasihi mwingie nyumbani mwa mtumwa wenu, mkalale, mkanawe miguu yenu, hata asubuhi mwondoke na mapema mkaende zenu. Wakasema, Sivyo, lakini tutakaa uwanjani usiku kucha. 3 Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa nao wakala. 4 Hata kabla hawajalala, watu wa mji, wenyeji wa Sodoma, wakaizunguka nyumba, vijana kwa wazee, watu wote waliotoka pande zote. 5 Wakamwita Lutu, wakamwambia, Wa wapi wale watu waliokuja kwako usiku huu? Uwatoe kwetu, tupate kuwajua. 6 Lutu akawatokea mlangoni, akafunga mlango nyuma yake. 7 Akasema, Basi, nawasihi, ndugu zangu, msitende vibaya hivi. 8 Tazama, ninao binti wawili ambao hawajajua mtu mume, nawasihi nitawatolea kwenu mkawafanyie vilivyo vyema machoni penu, ila watu hawa msiwatende neno, kwa kuwa wamekuja chini ya dari yangu. 9 Wakasema Ondoka hapa! Kisha wakanena, Mtu huyu mmoja amekuja kwetu kuketi hali ya ugeni; naye kumbe, anataka kuhukumu! Basi tutakutenda wewe vibaya kuliko hawa. Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, wakakaribia wauvunje mlango. 10 Lakini wale watu wakanyosha mikono yao, wakamwingiza Lutu kwao nyumbani, wakaufunga mlango. 11 Kisha wakawapiga hao watu walioko mlangoni kwa upofu, wadogo kwa wakubwa, hata wakachoka kwa kuutafuta mlango. 12 Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa; 13 maana tutapaharibu sisi mahali hapa, kwa kuwa kilio chake kimezidi mbele za Bwana; naye Bwana ametupeleka tupaharibu. 14 Lutu akatoka akasema na wakweze, waliowaposa binti zake, akasema, Ondokeni mtoke katika mahali hapa kwa sababu Bwana atauharibu mji huu. Lakini akawa kama achezaye machoni pa wakweze. 15 Hata alfajiri ndipo malaika wakamhimiza Lutu, wakisema, Ondoka, mtwae mkeo na binti zako wawili waliopo hapa, usipotee katika maovu ya mji huu. 16 Akakawia-kawia; nao wale watu wakamshika mkono, na mkono wa mkewe, na mkono wa binti zake wawili, kwa jinsi Bwana alivyomhurumia, wakamtoa wakamweka nje ya mji. 17 Ikawa walipomtoa nje, mmoja alisema, Jiponye nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea. 18 Lutu akawaambia, Sivyo, bwana wangu! 19 Tazama, mtumwa wako ameona kibali machoni pako, nawe umezidisha rehema zako ulizonifanyia kwa kuponya nafsi yangu, nami siwezi kukimbilia mlimani nisipatwe na yale mabaya, nikafa. 20 Basi mji huu u karibu, niukimbilie, nao ni mdogo, nijiponye sasa huko, sio mdogo huu? Na nafsi yangu itaishi. 21 Akamwambia, Tazama, nimekukubali hata kwa neno hili, kwamba sitauangamiza mji huo uliounena. 22 Hima, ujiponye huko, maana siwezi kufanya neno lo lote, hata uingiapo humo. Kwa hiyo jina la mji ule likaitwa Soari. 23 Jua lilikuwa limechomoza juu ya nchi Lutu alipoingia Soari. 24 Ndipo Bwana akanyesha juu ya Sodoma na juu ya Gomora kiberiti na moto toka mbinguni kwa Bwana. 25 Akaangusha miji hiyo na Bonde lote, na wote waliokaa katika miji hiyo, na yote yaliyomea katika nchi ile. 26 Lakini mkewe Lutu akatazama nyuma yake, akawa nguzo ya chumvi.

 

Sote tunajua kuwa kitendo cha kutazama nyuma kwa mke wa Lutu alichokifanya kiliashiria kuwa hakupenda kuondoka kwenye mji huo. Kwa hatua hii aliona kuwa makazi yake kuwa ni Sodoma na sio na Mungu. Alikosa imani. Nasi tunafanya hivi mara nyingi sana maishani mwetu.

 

Sasa tunajionea maana ya dhana ya makazi ya aina mbili.

 

Aina moja ni ya kubakia duniani na kama hayo ni mapenzi yetu ndipo tutaishi dunaini hadi mwishoni mwa ufufuo wa pili. Kama tutachagua kuishi hapa duniani, ndipo tutajua kuwa hapa sio nyumani kwetu na nyumbani kwetu ni, na yatakuwa, kwenye makao ambayo Kristo ametuandalia.

 

Watu wengi hawachagui kusafiri mwendo mrefu kwenda kuishika Sikukuu na Pasaka. Dhana iliyoko kwa kuazicha nyumba au makazi ya malango ya miji yet uni moja ya taswira ya kuachana na kuondoka Sodoma. Uamuzi wetu wa kubakia nyumbani unaonyesha kuwa tunaziona nyumba na makazi yetu kwenye miji ya ulimwengu. Bali kwa kwenda kwetu ambapo Mungu ameweka kamazi yake na kupafanya kuwa ni mahali pa kukutania kwa sikukuu zake, inaonyesha kuwa tunayaona makazi yetu kama bustani aliyotujenga Mungu sisi.

 

Ifuatayo ni nukuu ya aya ya Korani. Kwenye andiko la Sura ya 66 aya ya 10 inasema:

Mwenyezi Mungu amewapigia mfano walio kufuru: mke wa Nuhu na mke wa Lut'i. Walikuwa chini ya waja wetu wema wawili miongoni mwa waja wetu. Lakini wakawakhuni waume zao, nao wasiwafae kitu. Na ikasemwa: Ingieni Motoni pamoja na wanao ingia!

 

Imani ya Kiislamu inaelezea kinagaubaga kuhusu mke wa Lutu. Hata hivyo, sababu yake ni sahihi. Mke wa Lutu alimsaliti mume wake kwa kubakia na kushikilia njia za kale zilizopita, bila mkutumainia Mungu.

 

Sababu nyingine wanayoinena ni kwamba, uhusiano wa wanawake na wapenzi wao haukuwafunika chochote. kila mmoja wetu ni mdhaifu au anashindwa na anahukumiwa kwa uwezo wetu wenyewe kwenye utii katika kuuingia Ufalme. Uhusiano wetu na mtu mwingine yeyote au kundi, hata hivyo kiwango chochote cha ukamilifu kilichopo, hakiwezi kuwa cha kiwango cha chini ya majukumu au wajibu wetu. Kwa kipindi kirezo sana wawu wamekuwa wakiwasikiliza watumishi au wahubiri wao wakiwaambia mambo wanayotakiwa kuyafanya na wasiyoyapasa kuyafanya pia. Kuzishika sheria ni kitu cha kibinafsi na ni nguvu ya kujitawala na kuamua inayotenda kazi ndani yetu inayoongozwa na viwango vya mawasiliano kwa Mungu kwa njia ya Roho Mtakatifu atendaye kazi pamoja na Mwana.

 

Wakati umefika ambapo sisi binafsi tuziangalie sheria na tepende kibinafsi kuzishika. Kama tutakaa tu kwenye kanisa lisilozishika sheria, basi tujue kuwa tunaifanya hii dunia kuwa ni makao yetu na kuyasahau makazi yetu ya pamoja na Mungu na utashi wetu utatolewa. Tutakuwa hapa duniani hadi kipindi cha mwisho wa kuangamia kwetu au kuangamia kwa duania hii.

 

Kama tutakataa kushiriki kwenye Sabato na watu wa Mungu wanaozishika Sheria, ndipo tunasema kuwa makazi yetu hayapo pamoja na Mungu bali na Shetani. Kama tunapenda kushiriki mlo wetu na Shetani ndipo utashi wetu utaonewa mashaka. Jihadhari sana kwamba kile tukitakacho kama tunaweza kukipata.

 

Watu wenye nia moja, kama sehemu ya mwili wa Kristo, wameamriwa kukusanyika pamoja (Waebrania 10:25).

 

Matendo yetu yanatushuhudia, na sio maneno yetu. Maneno ni kitu tupu. Pale tunaposimama panategemea na tunapoketi. Basi na hakikisha kuwa ni kwenye nyumba na makazi ya Mungu na sio akaapo Shetani.