Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[063B]

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu cha Esta Sehemu ya II:

Purimu Katika Siku za Mwisho

 

(Tolao La 2.0 20090207-20090219)

 

Sehemu ya II inaweka Ufafanuzi wa Kitabu cha Esta katika Siku za Mwisho na inaielezea siku ya Purimu katia Siku za Mwisho na jaribio la kuwaangamiza kwa kuwafutilia mbali Waebrania na matokeo yanayofuatia uamuzi huo.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2009 Wade Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ufafanuzi wa Kitabu cha Esta Sehemu ya II:

Purimu Katika Siku za Mwisho


 


Katika Sehemu ya I ya Ufafanuzi kuhusu kitabu cha Esta tuliona maana halisi ya Kitabu cha Esta na jinsi kinavyolingana kwa Masihi na kwa Kanisa la Mungu likiwa kama bibi arusi wa \kristo. Ilionyesha pia nafasi ya Wayahudi kwenye mchakato huu na maana ya Sikukuu ya Purimu. Sasa tutakwenda kujionea uhusiano wa majaribu au mateso yatakayotokea katika Siku za Mwisho.

 

Katika Sehemu ya I tuliwaona wahusika wa hadithi hii na nyadhifa zao kwa upana zaidi na ikilinganishwa na mambo ya kiroho. Tulimuona Modekai akimuwakilisha Masihi na Esta akiliwakilisha Kanisa.

 

Vashti anaiwakilisha numba ya kifalme ya Yuda ambayo ilikataa wito na ikaachiliwambali lakini haikuuawa ili kwamba mfalme awe anabakia akimkumbuka tu. Esta aliitwa na kuchaguliwa achukue nafasi yake akiwa kama Israeli wa Mungu.

 

Katika Sehemu ya I, Sura ya 7 tuliona kwamba towashi wa mfalme aitwaye Harbona, aliamriwa amtundike Hamani kwenye mti alioutengeneza mwenyewe kwa ajili ya Modekai. Mara tu baada ya Harbona kumtundika Hamani, ndipo hasira za mfalme zilitulia. Ndipo Modekai akainuliwa na kuwekwa kwenye cheo cha uangalizi wa Nyumba ya Hamani na akapewa pete yake ya kiofisi. Hii haiwakilishi tu kuuawa kwa kiongozi wa maadui wa kimwili wa Israeli na Kanisa bali pia inaonyesha mfano wa jinsi Shetani atakapoyavua mamlaka yake na kuyakabithi kwa Kristo katika Siku za Mwisho. Harbona anamuwakilisha Malaika Mkuu kwenye Kiti cha Enzi cha Mungu atakayemariwa kumfanyia hukumu anayostahili Shetani.

 

Ili kutuweka sawa kwa andiko husika mwishoni mwa mchakato huu tunasoma maandiko yafuatayo.

 

Kumbuka kuwa waraka uliotumwa wenye ujumbe wa kuwaangamiza Wayahudi ulitumwa kwenye majimbo yote katika dola nzima uliamuru kuwaua Wayahudi wote kokote waliko kwenye dola yote.

 

Esta 8 inasema:

Siku ile mfalme Ahasuero alimpa malkia Esta nyumba yake Hamani, yule adui ya Wayahudi. Mordekai naye akahudhuria mbele ya mfalme; kwa maana Esta alikuwa amedhihirisha alivyomhusu. 2 Basi mfalme akaivua pete yake, aliyompokonya Hamani, akampa Mordekai. Naye Esta akamweka Mordekai kuwa juu ya mlango wake Hamani.3 Tena Esta akasema na mfalme mara ya pili, akaanguka miguuni pake, akamsihi kwa machozi ayaondoe madhara ya Hamani, Mwagagi, na shauri alilowafanyia Wayahudi. 4 Ndipo mfalme alipomnyoshea Esta fimbo yake ya dhahabu. Basi Esta akaondoka, akasimama mbele ya mfalme. 5 Akasema, Mfalme akiona vema, nami nikiwa nimepata kibali machoni pake, na neno likionekana jema mbele ya mfalme, nami nikimpendeza machoni pake, iandikwe kuzitangua barua za Hamani bin Hamedatha, Mwagagi, alizotunga na kuziandika ili kuwaangamiza Wayahudi walioko katika majimbo yote ya mfalme. 6 Kwa maana niwezeje kuyaona mabaya yatakayowajia watu wangu? Au niwezeje kuyatazama maangamizo ya jamaa zangu? 7 Mfalme Ahasuero akawaambia malkia Esta na Mordekai, Myahudi, kusema, Tazama, nimekwisha kumpa Esta nyumba yake Hamani, naye mwenyewe wamekwisha kumtundika juu ya mti, kwa sababu aliwatia mikono Wayahudi. 8 Basi waandikieni Wayahudi pia vyo vyote mpendavyo, kwa jina la mfalme, mkatie muhuri kwa pete ya mfalme; kwa kuwa andiko lililoandikwa kwa jina la mfalme na kutiwa muhuri kwa pete ya mfalme hakuna awezaye kulitangua. 9 Basi, waandishi wa mfalme wakaitwa pale pale, siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa tatu, ndio mwezi wa Siwani; na kama vile Mordekai alivyoamuru, Wayahudi wakaandikiwa, pamoja na maakida na maliwali, na wakuu wa majimbo toka Bara Hindi mpaka Kushi, majimbo mia na ishirini na saba, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake; na Wayahudi kwa mwandiko wao na kwa lugha yao. 10 Akaandika kwa jina la mfalme Ahasuero, na kutia muhuri kwa pete ya mfalme, akazipeleka barua kwa matarishi, wamepanda farasi, wamepanda wanyama wepesi sana waliotumika kwa huduma ya mfalme, ndio waliozalishwa katika zizi la mfalme. 11 Katika barua hizo mfalme aliwaruhusu Wayahudi wakusanyike katika kila mji na kuzisimamia maisha zao, kuangamiza, na kuua, na kulifisha jeshi lote la watu na la jimbo watakaowaondokea, wao na wadogo wao na wanawake; na kuyachukua mali yao kuwa nyara; 12 siku moja, katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero, yaani, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari. 13 Nakili ya andiko, ya kupigwa mbiu katika kila jimbo, ilitangazwa kwa mataifa yote, na kwa Wayahudi, wawe tayari siku ile ile kujilipiza kisasi juu ya adui zao. 14 Matarishi wakaondoka, wamepanda wanyama wepesi sana waliotumika kwa huduma ya mfalme, huku wakihimizwa na kusukumizwa kwa amri ya mfalme; kukapigwa mbiu huko Shushani ngomeni. 15 Naye Mordekai akatoka usoni pa mfalme, amevaa mavazi ya kifalme, ya rangi ya samawi na nyeupe, mwenye taji kubwa ya dhahabu, na joho ya kitani safi na rangi ya zambarau. Mji wa Shushani wakapaza sauti, wakashangilia. 16 Ikawa nuru na furaha na shangwe na heshima kwa Wayahudi. 17 Na katika kila jimbo, na kila mji, po pote palipowasili amri ya mfalme na mbiu yake, Wayahudi wakapata furaha na shangwe, karamu na sikukuu. Hata wengi wa watu wa nchi wakajifanya Wayahudi, kwa kuwa hofu ya Wayahudi imewaangukia.

 

Mchakato uliopo kwenye sura hii ya 8 ulikuwa ni kuhukumu sawasawa na jinsi ilivyokusudiwa na Shetani na mfumo au taratibu za kidunia kama ulivyokusudiwa na Hamani Mhagagi. Kinachoonyeshwa hapa ni kwamba ulimwengu utahukumiwa sawasawa na kinachotoka kinywani mwake. Na kadri majeshi yalivyojipanga dhidi ya watakatifu na yakikusudia kuwadhuru wateule na ndipo amri ilitokea kuwa wanapaswa kuhukumiwa sawasawa na walivyohukumiwa.

 

Mchakato wa wakati katika Siku za Mwisho ni sehemu ya ujumbe ulioko kwenye kitabu hiki. Maafa haya yalipangwa yatokee katika mwezi wa mwisho wa mwaka. Kwenye maandiko yaliyo kwenye Sehemu ya I tulielezea kwa kulinganisha siku 30 za Maombolezo ya Musa. Kipindi hiki kimeelezewa kwa kina kwenye jarida la Miaka Thelathini ya Mwisho: Mpambano wa Mwisho (Na. 219) [The Last Thirty Years: The Final Struggle (No. 219)].

 

Lakini kumbuka kwamba Waraka wa wokovu kwa Yuda uliandikwa katika mwezi wa Watatu, siku ya ishirini na tatu. Hii ilikuwa ni baada ya kupita idi ya Pentekoste. Mfano wake ni kwamba hii ilikuwa ni baada ya siku ya kutolewa kwa Roho Mtakatifu kwenye Kanisa la Mungu na Kanisa likiwa limefanya maombi na dua kwa Mungu kwa ajili yao Yuda na kwa taifa la Israeli.

 

Wale wajumbe waliotumwa wanafananishwa na manabii wa Mungu na wazee wa Makanisa ya Mungu ambayo yanahudumu kwa njia ya Machapisho na maandiko sambamba na Maandiko Matakatifu vipindi vyote vya Maagano yote mawili. Wajumbe hawa wataendelea bila kukoma hadi katika Siku za Mwisho. Watu hawa na mchakato mzima wa mashahidi wa Injili au Habari Njema ya Ufalme na Sheria au Torati ya Mungu, na habari yake imeelezewa kwa kina kwenye jarida la Mashahidi (pamoja na wale Wawili) (Na. 135) [The Witnesses (including the Two Witnesses (No. 135)].

 

Kiunabii tunapaswa kujua kwamba ni siku 270 kabla ya Purimu au miaka 270 kabla ya Purimu kwa hesabu ya kulinganisha siku moja kwa mwaka. Tutarudi tena kwenye jambo hili baadae. Mwenendo au mchakato wa shahidi unaachwa tangu kipindi hiki kwa ulimwengu wote.

 

Sura ya 9 inaelezea mpambano huu wa mwisho na tutajaribu kuuelezea wakati wake mahsusi kwenye mchakato wa Siku za Mwisho (soma pia jarida la Siku ya Bwana na Siku za Mwisho (Na. 192) [The Day of the Lord and the Last Days (No. 192)].

 

Esta 9 inasema:

Hata ulipofika mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, siku yake ya kumi na tatu, amri ya mfalme na mbiu yake ilipowadia kutekelezwa; ambayo siku ile adui za Wayahudi walitumaini kuwatawala, bali kumebadilika kinyume, hata Wayahudi waliwatawala wale waliowachukia; 2 siku ile ile Wayahudi wakakusanyika mijini mwao katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero ili kuwatia mikono wale watu waliowatakia hasara; wala asiweze mtu kuwazuia, kwa kuwa hofu yao imewaangukia watu wote. 3 Nao maakida wa majimbo, na majumbe, na maliwali, na wale waliofanya shughuli ya mfalme, waliwasaidia Wayahudi; kwa sababu hofu ya Mordekai imewaangukia. 4 Maana Mordekai alikuwa mkuu nyumbani mwa mfalme, na sifa yake imevuma katika majimbo yote, kwa kuwa huyo Mordekai amezidi kukuzwa. 5 Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na machinjo, na maangamizo, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia. 6 Hata huko Shushani ngomeni Wayahudi wakawaua watu mia tano, na kuwaangamiza. 7 Wakawaua na Parshandatha, na Dalfoni, na Aspatha, 8 na Poratha, na Adalia, na Aridatha, 9 na Parmashta, na Arisai, na Aridai, na Waizatha, 10 wana kumi wa Hamani bin Hamedatha, adui ya Wayahudi; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. 11 Siku ile mfalme akaletewa hesabu ya hao waliouawa huko Shushani ngomeni. 12 Mfalme akamwambia malkia Esta, Wayahudi wamewaua watu mia tano hapa Shushani ngomeni na kuwaangamiza, pamoja na wana kumi wa Hamani, je! Wamefanyaje basi katika majimbo ya mfalme yaliyosalia! Basi, una nini uombalo? Nawe utapewa; ama unayo haja gani tena? Nayo itatimizwa. 13 Ndipo Esta aliposema, Mfalme akiona vema, Wayahudi walioko Shushani na wapewe ruhusa kufanya tena kesho sawasawa na mbiu ya leo, na hao wana kumi wa Hamani watundikwe juu ya mti ule. 14 Mfalme akaamuru vifanyike vivyo hivyo, mbiu ikapigwa huko Shushani, wakawatundika wale wana kumi wa Hamani. 15 Basi Wayahudi wa Shushani wakakusanyika tena siku ya kumi na nne pia ya mwezi wa Adari, wakawaua watu mia tatu huko Shushani; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. 16 Nao Wayahudi wengine waliokaa katika majimbo ya mfalme walikusanyika, wakazishindania maisha zao, wakajipatia raha mbele ya adui zao, wakawaua waliowachukia, watu sabini na tano elfu; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. 17 Hii ndiyo siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari; na siku ya kumi na nne ya mwezi huo wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya karamu na furaha. 18 Lakini Wayahudi wa Shushani walikusanyika siku ya kumi na tatu ya mwezi huo, na siku ya kumi na nne pia; na siku ya kumi na tano ya mwezi uo huo wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya karamu na furaha. 19 Kwa sababu hii Wayahudi wa vijijini, wakaao katika miji isiyo na boma, huishika siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, kuwa siku ya furaha na karamu, sikukuu ya kupelekeana zawadi. 20 Basi Mordekai aliyaandika mambo hayo; naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote waliokaa katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero, waliokuwa karibu na waliokuwa mbali, 21 kuwaonya wazishike siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, na siku ya kumi na tano yake, mwaka kwa mwaka, 22 ambazo ni siku Wayahudi walipojipatia raha mbele ya adui zao, na mwezi uliogeuzwa kwao kuwa furaha badala ya huzuni, na kuwa sikukuu badala ya kilio; wazifanye siku hizo ziwe za karamu na furaha, za kupeana zawadi na za kuwapa maskini vipawa. 23 Nao Wayahudi wakakubali kufanya kama walivyoanza, na kama Mordekai alivyowaandikia; 24 kwa sababu Hamani bin Hamedatha, Mwagagi, adui ya Wayahudi wote, alikuwa amefanya shauri juu ya Wayahudi ili kuwaangamiza, akapiga Puri, yaani kura, ili kuwakomesha na kuwaangamiza pia; 25 bali mfalme alipoarifiwa, aliamuru kwa barua ya kwamba hilo shauri baya alilolifanya juu ya Wayahudi limrudie kichwani pake mwenyewe; na ya kwamba yeye na wanawe watundikwe juu ya mti. 26 Hivyo wakaziita siku hizo Purimu, kwa jina la Puri. Basi, kwa ajili ya maneno yote ya barua hiyo, na kwa yale waliyoyaona wenyewe juu ya jambo hilo, na mambo yenyewe yaliyowajia, 27 Wayahudi wakaagiza na kutadariki juu yao wenyewe, na juu ya wazao wao, na juu ya wote watakaojiunga nao, isikome, ya kwamba watazishika siku hizo mbili sawasawa na andiko lile, na kwa majira yake kila mwaka; 28 siku hizo zikumbukwe na kushikwa kwa vizazi vyote na kila jamaa, katika kila jimbo na kila mji; wala siku hizo za Purimu zisikome katikati ya Wayahudi, wala kumbukumbu lake lisiishe kwa wazao wao. 29 Ndipo malkia Esta, binti Abihaili, pamoja na Mordekai Myahudi, alipoandika kwa mamlaka yote kuithibitisha barua hii ya pili ya Purimu. 30 Akapeleka barua kwa Wayahudi wote katika majimbo yote mia na ishirini na saba ya ufalme wake Ahasuero, maneno ya amani na kweli, 31 ili kuzithibitisha siku hizo za Purimu kwa majira yake, kama Mordekai Myahudi na malkia Esta walivyoamuru, na kama walivyojiagizia juu yao wenyewe, na juu ya wazao wao, kwa habari ya kufunga na kilio. 32 Amri yake Esta ikayathibitisha mambo hayo ya Purimu; ikaandikwa katika kitabu.

 

Kumbuka kuwa matukio yaliyo kwenye Sura ya 9 (aya za 7 na 14) yanaonyesha kurudiwa kwa mauaji ya watoto kumi wa Hamani. Mtafaruku huu unaonyesha hali ya mtafaruku wa tukio halisi na tukio kinzanifu la mauaji ya siku ya Purimu na linaonyesha kwenye matukio yatakayotokea katika nyakati za mwisho pamoja na matukio yatakinzana fananisho repeat of the killing of the ten soayotanguli au yatakayotokea kwanza.

 

[aya za 10,15,16] zinarudia maneno haya: “walakini juu ya nyara hawakuweka mikono” (soma jarida la Ndamba wa Dhahabu (Na. 222) [The Golden Calf (No. 222)].

 

Kuingizwa na mahali pa Purimu kwenye Vita vya Mwisho

Tumejua idadi ya Siku za Maombolezo ya Musa kuwa ni kama miaka thelathini ya mwisho kwa hesabu ya siku moja sawa na mwaka kwenye Yubile ya mwisho ya miaka elfu sita ya Utawala wa Shetani. Hiyo ni Yubile ya 120 tangu uumbaji tangu kufukuzwa kwa wanadamu na kufungwa kwa bustani ya Edeni. Kipindi hiki ni cha Nyakati za Mwisho za zama na utimilifu wa Mataifa au Nyakati za utawala wa Mataifa ya dunia. Nyakati hizi ziliishia katikati ya miaka ya 1996-7. Mwaka huu unachukuliwa kuwa ni mwisho wa Miaka Thelathini wa Maombolezo ya Haruni.

 

Mwaka 1967 ulikuwa ni mwaka ambao ulihitimisha mapambano na mataifa yaliyo nje ya Nchi ya Ahadi na kuuteka mji wa Yerusalemu kwa mapambano au Vita ya Siku Sita.

 

Kumbuka kwamba Miriamu alikufa baada ya kuweka matuo yao huko Meriba katika mwaka huu Mwezi wa Kwanza. Waedomu walikataa kuwaruhusu Israeli kupita na wakawatokea kwa vita (Hesabu 20:1).

 

Kipindi hiki kilienda hadi miaka 2520 kutoka Vita ya Karkemishi ya kukomesha mauaji ya kinyama ya Vita Kuu ya I ya Dunia mwaka 1916 na kutekwa kwa miji ya Beersheba na Yerusalem mwaka 1917. 1916 ulianzisha kipindi cha mwisho wa miaka themanini cha utimilifu wa  Mataifa (soma pia jarida la Kuanguka kwa Misri: Unabii wa Mkono Uliovunjika wa Farao (Na. 36) [The Fall of Egypt: The Prophecy of Pharaoh’s Broken Arms (No. 36)].

 

Mnamo mwaka 1967 Yerusalem ulitwaliwa au kukombolewa. Mwaka 1996-7 ulishuhudia ukomo wa Nyakati Saba walizopewa Mataifa tangu kipindi cha Babeli, kama tulivyokiona kwenye Danieli Sura ya 2. Mwendelezo wa Misheni ya Kanisa ulianzia kipindi hiki. Mnamo mwaka 1987 Hekalu liliingia hukumi na lilipimwa au kujaribiwa. Mchakato mzima kuhusu jambo hili umeelezewa kwa kina kwenye jarida la Kupimwa kwa Hekalu (Na. 137) [Measuring the Temple (No. 137)].

 

Kanisa lilijiunda tena kwa awamu ya mwisho ya Makanisa ya Mungu katika mwaka wa Tatu wa Mzunguko wa miaka ya Sabato mnamo mwaka 1994.

 

The end of the Time of the Nations or the Time of the Gentiles was in 1996/7.

 

Mwaka 1997 kilianza kipindi cha Miaka Thelathini ya mwisho kabla ya kuanza kwa kipindi cha utawala wa millennia katika Nchi Takatifu. Kipindi hiki kwa hiyo kinafananishwa na mwezi wa Adari au mwezi wa mwisho wa mwaka cha kabla ya kuanza kwa mamlaka mapya. Katika miaka hii ndipo tunatarajia kuiona Purimu ya mwisho.

 

Mwaka 1998 kulianzishwa Marejesho mapya ya Msisitizo wa Torati yake Mungu na ndio mwaka iliposomwa kwenye mwaka wa Sabato na ilisomwa tena kwa mara ya pili kwenye Mwaka wa Sabato wa mwaka 2005.

 

Purimu tunayoiona hapa ilipasa ianze tangu siku ya 13 ya mwezi na kuendelea hadi siku ya 14 na 15 ya wa Maombolezo ya Musa.

 

Tangu mwaka 1997 wa hwsabu ya mwaka kwa siku tunafikilia hadi kwenye miaka ya 2009, 2010 na 2011.

 

Tungetarajia kuona mwisho wa kipindi hicho, tangu kukoma0kwa vita ya kuangamiza na kutokomeza watu ya mwaka 1967, kipindi cha maandalizi makubwa ya maadui wa Watakatifu wake Aliye Juu. Hii inamaanisha kwanza kabisa Makanisa ya Mungu ambao ni Israeli wa kiroho sambamba na Wayahudi kwa ande zote mbili, yaani Yuda na Israeli.

 

Kipindi hiki kitakuwa na matukio mfululizo nay a kushangaza ya kimikakati ya kuwaangamiza watu na kuzitokomeza kabisa nguvu za Watu Watakatifu sambamba na kuhujumu au kudhoofisha uchumi wao na uwezo wao wa kawaida.

 

Nguvu za majeshi ya Shetani zimekusudiwa kusababisha maangamizi ya kiuchumi kwa watu wa jamii ya Kiebrania na mara tu mkakati huu utakapoanza kutekelezwa, kutazingatiwa kufikwa lengo la kuwaangamiza kabisa kimwili. Jambo hili limeonyeshwa kimfano kwenye mateso yaliyooanndikwa kwenye Kitasa cha Tano kwenye kitabu cha Ufunuo.

 

Tungetarajia jaribio la mwisho kwenye maangamizi haya kutokea na kutekelezwa tangu siku ya 13 hadi 15 Adari au tangu mwaka 2009 hadi 2011 ikiwa ni siku ya 13 hadi 15 za mwezi wa Adari au mwezi wa Maombolezo ya Musa ya Siku za Mwisho. Hatima ya Shetani ni muhimu. Marejesho mapya ya mambo yote ya Eliya na shahidi mwingine yanakuja sambamba na kuanzishwa kwa Yerusalemu. Kufuatia na siku za Mashahidi Wawili tunatarajia kuingia na kupewa nafasi kwa Modekai-Masihi akiwa kama Halifa wa Ufalme wa hii dunia baada ya hukumu ya wale Mashahidi Wawili.

 

Jaribio kubwa la mauaji ya halaiki ya kuwaangamiza Wayahudi na katika Israeli na kwenye Vita Kuu ya II ya Dunia. “Suluhu ya Mwisho” lilipangwa huko Ulaya na kambi zilizokusudiwa na kulengwa kwanza zilikuwa zimejengwa huko Ujerumani katika mji wa Hamburg mwaka 1932 na Watrinitariani au waamini Utatu. Madhehebu haya yote mawili yaani Walutheri na Wakatoliki walihusika na jambo hili lililojulikana kama “Suluhisho la Mwisho.” Mwisho wake watatoa mwito ili kuwapeleka wahalifu wa kivita kwenye nchi za Marekani, Australia na Amerika Kusini. Baadhi ya wazee hawa wanakanusha au kutokea kwa mauaji haya ya kuangamiza wanadamu hata sasa. Mapapa waliwasaidia kwanza kwa kutoa msaada wa dhahiri na wa wazi kabisa na kisha wakafumbia macho na kunyamazia.

 

Ni kama kasisi wa zamani na Mjesuit aitwaye Malachi Martin amebadilika, mauaji ya wengi yalitajwa huko St Peters katika karne ya 20 kwa ajili ya kumtawaza na kumpa Kiti cha enzi Shetani kumfanya kuwa ni mungu. Kasisi huyu aliuawa kabla hajaandika makala ya pili ya kuliweka wazi tukio hili. Yaliyoandikwa kwenye Isaya 14 na Ezekieli 28 yanarudiwa.

 

Kwenye mateso ya Nuremburg kiongozi moja Manazi alisema, wakati alipokuwa anahukumiwa kifo, “Kwa Hakika, Hii ni Purimu”.

 

Kwa kweli majaribio ya kuwaangamiza Wayahudi yalifanywa kwa milolongo endelevu kama kunavyoonekana kuwa kulikuwepo na vita dhidi ya Uingereza na Anglo-Saxons ambao wanafanya sehemu kubwa ya watu hawa. Mnamo mwaka 1739 Waingereza walipigana vita vyao na Uhispania na iliyokuwa Dola Takatifu ya Roma ilishindwa vita kwenye nchi ya Uturuki. Wazungu wa Ulaya, Warusi na Waturuki walitia saini makubaliano katika mwaka huu ili kukomesha uhasama. Pia katika mwaka huu Wayahudi walihusuriwa maisha yao kwa kuhukumiwa vifungo vya maisha huko Lisbon, nchini Ureno. Maaribio ya kuwaangamiza Waisraeli yamekuwa na mtafaruku mkubwa kwa namna endelevu. Mwaka 1739 ulikuwa ni mwaka wa 270 tangia mwaka 2009.

 

Kitabu cha Esta hakikusema kwamba majaribio ya kuwaua Wayahudi yatakoma. Bali kinasema kwamba majatibio haya yatashindwa na wale wanaofanya hila hizi watakufa.

 

Chokocho za Mauaji ya Kimbari

Azimio la Balfour lilitolewa na Waziri Mkuu Balfour baada kuwashindwa Waturuki huko Beersheba na Yerusalem mwaka 1917. Linaanzisha dhana na haki na msaada wa Waingereza kwenye Ardhi ya Wayahudi. Tangu wakati ule na kuendelea mauaji ya kuwaangamiza Wayahudi yamekuwa yakipangwa na kufanyika sehemu zote mbili, yaani huko Ulaya na katika Mashariki ya Kati.

 

Watoto kumi wa kiume wa Hamani ni sawasawa na zile embe Kumi au wafalme wa Dola ya Mnyama na vile vidole Kumi vya chuma na udongo za Dola ya Mwisho ya Roma iliyoonyeshwa kwenye Danieli 2.

 

Kumbuka kwamba Kitabu cha Esta knasema kuwa kwene Mji mkuu huko Shushani mauaji yalifanyika siku ya 14 ya mwezi wa Adar pia. Mauaji kwene miji mingine ya Dola hii yatatokea na yatachukua muda mrefu na yatakuwa mabaya sana kuliko mengine yote yaliyotokea nyuma. Tangu vita vya mwisho yatupasa tutarajie migogoro hii kwisha kwa zaidi ya miaka miwili kuanzia Ulaya hadi Iran.

 

Jaribio lililofanywa huko nyuma kuwaangamiza Waingereza, Waceltiki na wa Anglo-Saxon yamekuwa yalifanywa na Watrinitariani wa Ulaya kwa karne nyingi sasa. Hawajafanikiwa kabisa lakini watafanya jaribio moja linguine tena la mwisho katika miaka michache ijayo.

 

Hujuma na maangamizi ya kiuchumi ya Marekani na Muungano wa Nchi za Jumuia ya Madola inayoongozwa na Uingereza zitachukuliwa na watumishi hawa wa Shetani katika sehemu zote mbili, yaani huko Ulaya na Mashariki ya Kati. Mipango yao na zana au silaha zao za maangamizi zitatumika dhidi yao na watawanyonga kwenye miti wa kuwanyongea wao wenyewe kama alivyoangikwa Hamani na watoto wake kumi walivyoangikwa. Nyayo zilizochangantika chuma na udongo zinawakilisha kukangana malengo na makusudio na watu na imani kwenye dola hii ya mwisho. Kristo ataiangamiza na kukomesha uwepo wake na kuitwaa Mashariki ya Kati na Yerusalemu.

 

Kwa sasa Iran, inasaidiwa na washirika wake ambao ni Wasyrin, Walebanon na Wapalestina, wanatoa mwito wa kuwaangamiza kwa mauaji makubwa Wayahudi. Wanapiga makelele ya “Hamas, Hamas, Wayahudi wachomwe moto wa gesi”. Harakati za Hamas ni matendo yanayofanywa kwa makusudi au ugaidi ambao unaenezwa kwa taarifa za vyombo vya habati kwenye ulimwengu weote wa Kiislamu na nchi za Magharibi na wanajumuisha mambo ya bandia na yakutunga dhidi ya Waisraeli. Mambo yanayofanyia huko Gaza na kwa Wapalestina yamepangwa kwa makusudi ili kuhalalisha mauaji ya kuwaangamiza Israeli. Hakuna taifa hapa duniani linaloweza kuyavumilia makombora yanayopigwa kila mara yakiwashambulia watu wake kama yanayorushwa na Hamas kuishambulia Israeli. Ni sera ya chuki ambayo inafumbiwa macho na Umoja wa Mataifa huku ukijua vema sana kuwa ni uchokozi na uhalifu dhidi ya sheria na sera za Umoja wa Mataifa na Mkataba wa Geneva. Misri inatumiwa kama bomba au njia ya kuyaleta makombora ndani ya Gaza.

 

Kile kinachofanywa na vyombo vya habari ni kufikisha lengo la kuwagawa Israeli machoni pa ulimwengu na kuwafanya israeli wawe chini ya mashambulizi ya kihasama na kwa namna ya kutengwa kiasi cha kwamba sasa itachagua wanasiasa sahihi sana watakaopigana dhidi ya uwepo wa taifa la Israeli.

 

Vyombo vya habari na Umojja wa Mataifa vimehakikisha kwamba falsafa ya uiana dini ya ugaidi wa Kiislamu imejikita na kuwa imara katika nchi za Kiislamu kutoka Afrika hadi Indonesia. Vyombo vya -habari vimewaimarisha wapinga falsafa ya Kisemitiki na kambi za chuki za kidini za Wazungu wa Ulaya.

 

Israeli ndiyo nchi pekee duniani ambayo haikuwa na uchumi kama kigezo chake cha kwanza cha kisiasa katika kipindi cha miezi michache iliyopita kabla ya Pasaka ya mwaka 2009.

 

Waislamu hawasomi Biblia na waamini Utatu au Watrinitariani nao pia hawaisomi Biblia. Hawaisomi kwa kuwa haifaidishi wala kuunga mkono mikaka ti yao. Magaidi wa kidini wanasutwa kwa yale yaliyoandikwa ndani yake.

 

Neno lake Mungu Aliyehai liko wazi sana. Ataruhusu Israeli washughulikiwe nah ii itafanywa au kuhusisha mataifa yaliyotoka kwenye mchanganyiko wa mataifa hayo. Atawaacha watokomezwe na kuuawa kwa upanga pamoja na kusumbuliwa na magonjwa ya tauni na njaa lakini hawataashiwa waangamie kabisa.

 

Kila taifa linaloshirikiana au kujiunga na wahafidhina hawa wenye chuki wanaotoa wito au kujaribu kufanya maangamizi makubwa ya kuwahilikisha Israeli watauawa kwa upanga. Hii itajumuisha viongozi wa imani ile ya kidini.

 

Mashariki ya Kati haitashinda na watajilelea madhara na ungamivu wao wenyewe. Haijalishi ni wapi ilipangwa na haijalishi ni wapi silaha hizo ya vita zimewekwa kwa mkakati wa kuwaangamiza na kuwatokomeza watu wa Mungu, wale wanaopanga mkakati huu watauawa wenyewe kwa kutumia silaha zao wenyewe za mauaji ya kimbari, hata katika nchi za Uingereza na Marekani kwenyewe.

 

Tumeelezea kuhusu kuenea na kuongezeka kwa Israeli kwa mujibu wa unabii, na kuingizwa kwa taifa ndani yake, kwa kiasi fulani kwenye majarida ya Miaka Thelathini ya Mwisho: Mpambano Mkuu (Na. 219) na Vita vya Hamon-Gogu (Na. 294) [The Last Thirty Years: the Final Struggle (No. 219) and War of Hamon-Gog (No. 294)].

 

Majarida haya yamekuwa ni mwongozo na yanaonyesha chanzo cha Vita Vya Mwisho. Vita hivi vimetabiriwa kwenye Maandiko Matakatifu na Kristo alisema kuwa Maandiko hayawezi kutanguka (Yohana 10:35). Mungu amelitoa neno lake kwa kupitia manabii na mambo haya yatatimilika.

 

Swali pekee tulilobakiwanalo sasa ni kwamba kipindi mujarabu kinachongojewa cha ku kumuo Eliya na mashahidi wenyine hapa duniani? (Soma jaridarida la Mashahidi (pamoja na wale Mashidi Wawili (Na. 135) [The Witnesses (including the Two Witnesses (No. 135). Je, mwanzo wa mauaji ya kinyama ya Purimu au ni mwisho? Ratiba hii imetolewa katika mwezi wa mwisho wa Adari kabla ya Zama Mpya ya utawala wa millennia, ambao ni Mwaka Mpya wa 2009 au je, itakuwa katika Mwaka Mpya wa 2012? Muundo wa mchakato wa matukio haya umeelezewa kwa kina kwenye majarida ya Ujio wa Masihi Sehemu ya 1 (Na. 210A) na Yubile ya Dhahabu na Milenia (Na. 300) [The Advent of the Messiah Part I (No. 210A) and The Golden Jubilee and the Millennium (No. 300)].

 

Kuanza huduma kwa Mashahidi Wawili kuna maana na ashirio la moja kwa moja la kujulikana ni lini Masihi atarejea. Ni matukio yanayotegemeana na Maandiko hayawezi kutanguka. Masihi atarudi ili kuja kuwaokoa wale wanaomngojea kwa hamu.

 

Kwa hiyo, kama Mashahidi hawa hayakuanza kazi yao hadi mwaka 2012 au hata pengine baadae, basi hatuwezi kumtarajia Masihi hadi mwaka 2015 au hata bada ya hapo, kutegemea ni lini Mashahidi hawa wataanza kazi yao huko Yerusalemu. Tunajua kuwa Masihi ataingilia kati kwa kukifupisha kipindi hiki cha utawala wa Shetani. Utawale wake utaishia kwenye Yubile ya 120 mnao mwaka 2027 kwa tukio lolote. Kwahiyo, Masihi atarejea na kuanzisha utawala wake utakaodumu kwa millennia huko Yerusalemu kabla ya mwaka 2027. Kutokana na mfano wa kuzingirwa kwa Yeriko kungeweza kutarajia siku saba za misho za mzee wa siku zianze tangu angalau mwaka 2019 au mapema kidogo (soma jarida la Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142) [The Fall of Jericho (No. 142)].

 

Mashahidi hawa kwa hiyo hawakuje mapema kabla ya mwaka 2015. Kristo atawashughulikia na kuweka utaratibu mpya kwenye Nchi Takatifu kwa kutumia matetemeko ya ardhi na kuujenga upya.

 

Kwa hiyo. Kristo atawaleta maadui watakaouchukia utawala na imani ya kidini ya duniani chini huko Har-magedon na kuwaangamiza, kama ilivyoatabiriwa kwenye Maandiko Matakatifu. Hii itatokea hivyo kwa kuwa dunia, hata pamoja na miujiza mingi iliyoshuhudiwa, hawakutubu. Wengi wa hawa wanaodai kuwa ni Wakristo leo watamtangaza Masihi kuwa ni Mpingakristo kwa kuwa, yeye kama walivyo Mashahidi wengine waliotangulia kabla yake, atakuja kuzisisitiza na kuzirejesha Amri au Torati ya Mungu. Mpingakristo wa kweli atakuja kabla yake, na atakuja kwa mwonekano wa kiongozi mwenye kuheshimika na kuaminika kidini, kwa watu hawa hawa. Kristo atamuua na nabii wake wa uwongo wakati atakaporudi. Kwa hiyo, yatubidi kudhania kwamba viongozi hawa mashuhuri wa dini hii potofu nay a uwongo watafanya kazi au huduma zao kipindi kimoja sambamba na Mashahidi hawa wawili. Tunaweza kudhania pia kwamba ni lazima Mpingakristo ataanza kutawala pamoja na huyu nabii wa uwongo wakati wowote tangia mwaka 2012, na kuendelea hadi mwishoni mwa mwaka 2019. Huenda kwa sasa yeye amekwishaanza kwa kuonekana ni mmojawapo kwa kutumia harakati za kuuonga ulimwengu wa kidini – akiwa kama nabii wa uwongo anayeonekana kuwa ni kiongozi wa kidini.

 

Tunweza kuhitimisha kwamba kutokana na utaratibu wa Yubile kama ulivyoonekana kwenye historian a kwenye Biblia na – kukataa utaratibu mpotofu wa marabi wa zama ya baada ya Hekalu ujulikanao kama wa uahirisho wa kila mwaka wa 49 unaotokana na hesabu za Wababeloni walioamua uwepo wa miaka mirefu na mifupi – iliyojumuishwa na hesabu za majira ya Purimu na Mwezi wa Mwisho wa Miaka ya mzunguko wa Yubile na mfano wa Ishara ya Yona na cha Kanisa kuwa jangwani, Mashahidi hawa walipaswa wawe wamekuja tangia wakati wowote kuazia mwaka 2009 hadi 2015, na Masihi afuatie tangu hapo wakati wowote tangu miaka hii ya 2012 hadi 2019.

 

Matukio haya yote ni kutokana na mujibu wa Mpango na Amri ya Mungu (soma majarida ya Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13); Kubadilishwa kwa Kalenda ya Mungu Katika Yudea (Na. 195B) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13); Distortion of God’s Calendar in Judah (No. 195B)].

 

Kitu pekee tunachoweza kuwa na uhakika nacho ni kwamba majeshi ya Shetani yatashindwa na kuangamizwa kote kote, yaani katika Asia na huko Mashariki ya Kati na hata yale ya Waamarekani na kwenye imani yake ya kidini huko Ulaya. Makao yake Makuu yaliyoko huko Ulaya yataharibiwa na kuangamizwa yote. Mkakati huu wa kuwaangamiz na kuwatokomeza Israeli hautaruhusiwa kuufanikisha kwa kuwa Modekai ambaye ni Kristo leo ameimaliza kazi yake na awamu au kipengele cha mwisho kwenye maombi ya Esta nay a wateule kinakamilika hivi sasa.

 

Kristo atatawala kama Kaimu wa Ufalme wa Mungu hapa Duniani. Mungu anaamua kile kinachotakiwa kifanyike kwa Sheria na Torati yake. Zaka za Mungu zinapaswa zikusanywe katika nchi na kwenye maeneo ya pwani pamoja na maongeo yake yote.

 

Esta 10

Basi mfalme Ahasuero alitoza kodi katika nchi na katika visiwa vya bahari. 2 Na matendo yake yote yenye nguvu na ya ushujaa, na habari zote za ukuu wake Mordekai ambao alipewa na mfalme, hazikuandikwa katika kitabu-cha-taarifa cha wafalme wa Umedi na Uajemi? 3 Kwa maana Mordekai Myahudi akawa wa pili wake mfalme Ahasuero, na mkuu wa Wayahudi, amependeza mbele ya jamii ya ndugu zake; ambaye aliwatafuta watu wake wema, na kuiangalia hali njema ya wazao wao wote.

 

Kanisa litatawala na Kristo. Kazi za Kanisa na kuanza kwa kipindi cha utawala wa millennia kutajumuishwa pamoja. Masihi wa uzao wa Yuda na wa Daudi wa Bethelehem ya Efrata atatulisha sisi sote na atakuwa ni Mfalme wa Amani.

 

Ni kwa ufanisi kiasi gani tunavyofanya kazi yetu sasa ndivyo itaamua jinsi tunavyoishi.

 

Na sasa tutaanza kushughulika kuandika majarida ya Vita Kuu ya III ya Dunia: Sehemu ya I Dola ya Mnyama (Na. 299A) na Vita Kuu ya III ya Dunia Sehemu ya II: Mwanamke Kahaba na Mnyama (Na. 299B) [World War III: Part I The Empire of the Beast (No. 299A) and WWIII Part II: The Whore and the Beast (No. 299B]).

 

q