Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[093]
Maandalizi ya Mlo wa Pasaka
Katika Usiku wa Kuangaliwa
Sana
(Toleo:1.0 20020324-20020324)
Mlo huu wa kila mwaka wa Pasaka, ukiandaliwa na kuadhimishwa kwa usahihi sana, unaweza kutoa mazingira bora zaidi ya kuwafundisha watoto na wale ambao hawajaongoka.hii ni fursa nzuri sana kuwawezesha wote wakuze ufahamu wao na uwezo wao katika kushuhudia sababu iliyowapelea kuamini.
Christian Churches of God
E-mail:
secretary@ccg.org
(Copyright © 2002, Diane
Flanagan, ed. Wade Cox)
(Tr. 2005)
Masomo
haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kutufa maneno. Jina la mchapishaji na anuami
yake pamoja na hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya maelezo na kilugha
lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia ynapatikana Ulimwenguni
kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org
au http://www.ccg.org
Maandalizi ya Mlo wa Pasaka
Katika Usiku wa Kuangaliwa
Sana
Utangulizi
Maandalizi yanayofanywa kwa ajili ya
maadhimisho sahihi katika siku ya 15 ya mwezi wa Kwanza (Abibu) yanaanzia na
tendo la kuupambanua mwili wa Kristo au kanisa (1Kor.11:29) na kukusanyika
mahali ambapo Mungu amelikalisha juna
lake (Kum. 16:5-6). Aina yoyote ya masalia ya chachu au amira lazima yatupwe
nje ya makazi yetu ya kudumu mapema kabla ya kuondoka kwenda kwenye Sikukuu
(Kut. 12:15,19; Kum. 16:4)), Wapendwa waliobatizwa kukusanyika na wenzao ili
kushiriki Ushirika wa Meza ya Bwana mara baada ya giza kuingia katika siku ya
14 ya mwezi wa Kwanza yaani wa Abibu.
Sehe mu ya masaa ya wakati wa mchana wa siku ya 14, ibada ta kukumbuka Kifo cha
Mwana Kondoo itaanza majira ya saa 9:00 alasiri, huu ni muda halisi ambao mwana
kondoo alitolewa sadaka (Kut. 12:6; Kum.16:6). Sadaka ya kwanza kati ya zile
tatu za mwaka huchukuliwa mapema wakati wa asubuhi (Kut. 23:18; 34:23; Kum.
16:16). Tunaweza kupata fursa ya kuleta na kuto sadaka zetu za hiyari mbele za
Mungu Baba.
Mkumbu Mkumbushaji wa sehemu ya masaa ya
mchana wa siku ya 14 ya
mwezi wa kwanza atakuwa sasa amefunuliwa kwa kutoa maelezo zaidi.
Majukumu yanayotakiwa yatimizwe
Tunajukusanya katika matuo ta muda na
tunakusanya na kuhakikisha kuwa tumeondoa aina zote za mazalia ya chachu yaani
hamira zisiwepo katika vyumba vyetu tulivyopanga (Kut. 12:15,19; Kum.16:3-4).
Aina yoyote ya nembo inayoashiria kutukuza sanamu na au miungu ya uwongo ni
lazima viondolewe au kufunikwa wakati wote wa Sikukuu inapokuwa inaendelea.
Tukisha ondoka huko nyuma yetu mwenyewe anahiyari ya kuzirudishia tena sehemu
zake au kuzifunua tena lakini hii itatokea tunapokuwa sisi tumesha maliza
maadhimisho na kuondoka.
Wakati wote wa kila kundi linapoamua
kuandaa Pasaka na mlo wa siku ya Sabato
inayofuatia inakuwa ni chaguo la kila mtu
binafsi yake, isipokuwa jambo la kuangalia tu ni kwamba pasiwepo na aina yoyote
ya mazalia ya kitu chenye chachu ndani yake. Chakula ni lazima kipikwe na vitu
visivyo na chachu ndani yake kwa vile tunavyokula vitu visivyotiwa chachu kwa
muda wote wa siku siku saba (Kut.12:15; 13:6-7; 23:15; 34:18; Law. 23:6-8; Hes.
28:17; Kum. 16:3).
Siku ya 15 ya Mwezi wa Kwanza ni Sabato ya
Siku Tukufu ambayo ni Siku ya Kwanza ya Mikate isiyotiwa Chachu. Huu ni usiku
ule ambao Malaika alipita juu ya Misri na kuuwa kila mzaliwa wa kwanza wa binadamu
na wanyama katika Misri. Israeli waliponywa na hukumu hii kutokana na kuua kwao
na kumla mwana-kondoo wakiwa katika malangoni mwao (Kut. 12:7-13).
Kwa hiyo, tunao wajibu mkubwa wa
kuhakikisha kuwa tunanunua na kutayarisha chakula chote kabla ya giza
halijaanza jioni ya siku ya 14 ya mwezi wa Abibu (Law.23:6-8; Hes.28:16-18).
Haturuhusiwi kuuza wala kununua siku ya Sabato (Neh. 10:28-31; Amosi 8:5). Wala
haturuhusiwi kufanya aina yoyote ya kazi ya utumishi siku ya Sabato (Kut.
20:8-11; Kum.5:12-15). Kuna masharti muhimu na maalumu kwa ajili ya ushiriki wa
mlo wa Pasaka katika ule Usiku wa Kuuangalia Sana kama ilivyoelekezwa hapo
chini.
Mnyama kutoka katika kundi lako la mifugo
Mlo huu unatakiwa kujumlisha na mnyama
kutoka katika kundi lako la mifugo, kwa maana nyingine ni kusema kwamba awe
miongoni mwa wanyama wenye kwato zilizopasuka katikati na anayecheua na
atapikwa katika mahali pale ambapo Mungu amelikalisha Jina lake (Kum.
16:2,6-7). Inatakiwa aokwe na asipikwe kwa maji wala kwa kuchemshwa na masalia
ya nyama yake isibakie hadi kufikia asubuhi (Kut. 12:8-11; Hes. 9:11-14; Kum.
16:7).
Kwa jinsi ilivyoanza siku yenyewe ya
kwanza, hakuna nyma au mifupa ya mwana kondoo iliyotolewa dhabihu kule Misri
ilikuwa imesalia hadi asubuhi. Kila kilichosalia kilichomwa kwa moto na
kuteketezwa kabisa; mateketevu makuu katika kila nyumba yalifanyika kwa namna
ya kutisha kabisa. Hii iliweza kuzuia kila mtu aliyetaka kutumia sehemu yoyote
ya sadaka hii ya mwana kondoo asiichukue na kuitoa kama sadaka kwa miungu ya
mingine ya uwongo au katika kuendeleza aina yoyote ya shughuli zozote za ibada
za kipagani kutoka katika masalio ya dhabihu hii. Mara tu baada ya hawa wana
kondoo wakisha tolewa dhabihu kabisa, kama ilivyokuwa kwa dhabihu ya Masihi
ilivyokuwa tayari imeishatolewa (Ebr. 7:27-28; 9:12; 10:10-19; 1Pet. 3:18).
Ilitosheleza mambo yote muhimu yaliyotakiwa na taratibu zote zilizohitajika kwa
ajili ya dhabihu. Aina yoyote ya mnyama aliye safi kutoka kwenye kundi lako la
mifugo kama vile nyama ya ng’ombe, nyama ya kondoo, ya mbuzi, nk, zinakubaliwa
kutumika (Wal. 11:1-8; Kum. 14:4-8).
Tumetengwa kutoka na familia au makundi
madogomadogo ili kuadhimisha na kuula mlo wa Pasaka (Kut. 12:3-4). Kwa hiyo,
inatakiwa kuandaliwe nyama ya kutosha ili kwamba itoshe kuliwa yote na wale
walioko.
Kwa mara ile ya kwanza, damu ilichukuliwa
na kupakwa juu ya miimo ya milango kama alama (Kut. 12:7,23). Tunajua vizuri
sana kwamba damu ya Kristo imetutakasa sisi, na kupitia hiyo watu wote
walionasi katika familia zetu wale ambao hawajaongoka wanatakaswa kupitia
kwetu.
Hakuna mfupa unaotakiwa kuvunjwa
(Kut.12:46; Hes. 9:12; Zab. 34:20; Yoh. 19:33,36) na kwa hakika ni mwana kondoo
asiye na mfupa ndiye anayefaa kuandaliwa.
Pangilia kipimo cha wastani wa wakia 4
(kama gramu 125 hivi) za nyama ya kondoo na umpe kila mtu mzimauwa. Kwa mfano,
kwa watu 12 mmoja anaweza kuhitaji mguu usio na mfupa wa uzito wa wastani wa
paundi 3 (au kg 2.5) iliyookwa kwa kipimo cha pimajoto cha digrii za Falnati
nyuzi 325 (sawa na Setigredi nyuzi 200). Uokaji unahitajika kutumia wastani wa
dakika 40 au 45 kwa mkupuo mmoja au hadi pale kipimo cha joto kifikie na
kuonyesha alama ya Falnati nyuzi 170-180. Kisha iachilie nyama ipoe kwa wastani
wa dakika 10-20 kabla hujaanza kuikatakata vipande.
Kuna maelekezo mbalimbali kuhusiana na
jinsi ya kuandaa nyama ya kondoo. Hapa chini ni baadhi tu tunayoweza kutolea
mfano.
Kondoo wa Kiaustralia
Ijalize wastani wa gramu 150 za jagi la
Marashi Moto ya Kiingereza juu ya kipande chote cha nyama, kisha kichovye chote
kabisa kwa ua la waridi kisha ioke kwa mujibu wa maelekezo yaliyotolewa hapo
juu. Mafuta yatajitenga na nyama kadiri inavyoendelea kupikwa na kila mmoja
atachuja mafuta mwenyewe wakati anajihudumia (Law.3:17). (Jagi zenye Marashi
Moto ya Kiingereza zinapatikana katika mgahawa ujulikanao kwa jina la Queen’s
Pantry huko Leavenworth Kansas na vistoo vinavyofanana na hii huko Marekani).
Nyama ya Kondoo na Viungo
Kwa kutumia aina ya kisu kikali, tengeneza
seleti au visahani vya wazi juu ya kondoo huyu. kisha tia marashi
yaliyotengenezwa kwa karafuu na vituu saumu yaliyotiwa karafuu kwa ndani kabisa
ya nyama. Chagiza nyama kwa mchanganyiko wa unga wa kitunguu saumu, unga wa
kitunguu maji, chumvi na pilipili [tumia wastani wa kipimo cha kijiko 1 cha
chai kwa (mintaarafu ya kipimo cha ujazo wa maji kiitwacho milgram 5) ya kila
kiungo kwa paundi 3 (kilogramu 1 ni sawa na gramu 500) za nyama]. Iliyookwa
kama isemavyo hapo juu.
Mafuta lazima yachujwe mbali na nyama ya
kondoo baada ya kupikwa vinginevyo nyama itakauka kwa ukaufu.
Mboga za Uchungu
Vilevile tumeelekezwa kutumia mboga chungu
katika mlo wetu (kut. 12:8). Hii inahitaji kujumlisha kuwepo na mchunga m’bichi
na sahani ya mboga za majani chungu kama vile mchunga na aina nyingine yoyote
unayoifahamu ya mboga zenye uchungu lakini zinazolika na bila kuleta madhara
zilizoko katika maeneo yako.
Mikate Isiyotiwa Chachu
Kwa mujibu wa neno la Mungu, tumeamriwa
wakati huu kula mikate isiyotiwa chachu tu yaani vitu visivyotiwa amira katika
ule Usiku wa Kuuangalia Sana (Kut. 12:8, 15, 39) na kwa siku nyingine sita
zinazofuatia za Sikukuu (Kut.12:15; 13:6-7; 23:15; 34:18; Law. 23:6-8; Hes.
28:16-18; Kum. 16:3). Katika kitabu cha Kutoka tunaona kuwa ule mkate ulikuwa
hauna chachu kwa sababu waliondoka kwa haraka (Kut.12:34). Katika Kumbukumbu la
Torati inaelezewa kama “Mkate wa mateso” (Kum. 16:3).
Maelekezo kuhusu Mikate isiyotiwa Chachu
Andaa vikombe 4 vyenye unga wenye
kutosheleza mlo mzima.
Tia viini vya mayai 2 ndani yake
Tia jibini vijiko vikubwa 2 ndani yake
Tia kijiko 1/2 vya chai ndani yake
Tia milgramu 220 ya maji au maziwa
Ongezea chumvi kwenye unga,
Mega siagi katika vipande vidogovidogo
kisha ongezea kwenye unga.
Koroga viini vya mayai, mafuta na maziwa au
maji kwa pamoja.
Ongezea kuukoroga ule unga jongeza vizuri
na kisha ukande kande.
Gawanya lile bonge katika vipande vipande
ukubwa sawa na wa mpira wa magongo na kisha uponde kwa mlingano wa kimvuto
mwembamba.
Kisha oka kwa kutumia jokofu lenye moto
mkali kiasi cha nyuzi joto za Setigredi 180 (sawa na Falnati 350) hadi ionekane
kwa rangi ya dhahabu samawati.
(kwa mujibu wa Dale Nelson)
kwa maelekezo mengine zaidi tafadhali soma
jarida la maelekezo kwa ajili ya Mikate isiyotiwa Chachu (Na. R2).
Dhabihu za mikate ya nafaka iliofanywa kwa
ajili ya kumtolea Mungu haikuwa inatiwa aina yoyote ya chachu wala asali (Law.
2:11)
Chumvi
Dhabihu zote zilitakiwa kutiwa chumvi kwa
ajili hiyo basi chmvi ya agano la Mungu wetu haikutakiwa ikosekane (Law. 2:13).
Chumvi hii ya agano ni ya milele (Hes. 18:19). Angalia mistari rejea ya chini
katika Biblia iitwayo “Companion Bible” katika Hesabu 18:19 kuhusiana na chumvi
ya agano. Tunatakiwa sisi sote tukolee munyu (Mk. 9:49-50).
Divai
Sasa tunafahamu kwa vizuri sana kwamba
tumeamriwa kulirudia agano letu la ubatizo kwa Mungu kwa njia ya kushiriki Meza
ya Bwana. Pale tunakunywa divai, ambayo ni ishara ya damu ya Masihi. Mwanzoni
kabisa, sadaka ya vinywaji ilitolewa na dhabihu za aina mbalimbali (Kut. 20:40;
Law.23:12; Hes. 15:5, 7, 10; 28:7, 14). Baadae katika siku za mbele, dhabihu za
asubuhi zita rejeshwa tena kama inavyo onyeshwa katika Ezekieli 46 wakati tendo
au wazo la sadaka ya kinywaji litakapotimilizwa, kwa sababu vitakuwa havipo
kutoka katika aina nyingine ya dhabihu. Hii inaonekana kumuashiria Masihi na
wateule kutimiliza ishara zote za sadaka ya vinywaji.
Tumeambiwa kujihudhurisha kwenye sikukuu na
kula mbele za Mungu zaka ya nafaka zetu, mafuta na divai mpya kwa furaha (Kum.
14:23,26). Pia tunapaswa kuwasaidia wale wote walio yatima na wajane ambao
kutoka na dhati ya mioyo yao wanashindwa kabisa kuhudhuria kwa uwezo wao
wenyewe (Kum. 14:28).
Mahitaji mengine Muhimu
Mlo huu waweza kuhusisha na vitu vingine
kama vile viazi mbatata, na viavi vitamu (vitu visivyo na chachu), lakini
orodha yote ya vitu vilivyoko hapo juu imeamriwa viwepo kwa mujibu wa maandiko
matakatifu. Kama ilivyo kwa mahitaji yoyote katika maisha ya mwanadamu,
maandalizi ya mlo huhusisha mipangilio na maandakizi na mipangilio ili
kukiwezesha kiwe tayari kwa wakati muafaka, ili kwamba wote waweze kushiriki
chakula hicho mara tu giza linapoingia, tena iwe mapema vya kutosha ili kwamba
watoto waweze kuwa na muda mzuri wa kujifunza maana ya Pasaka (Kut. 12:26).
Usiku wa Kuuangalia Sana uliamriwa uadhimishwe na wana wa Israeli milele (Kut.
12:42).
Usiku wa Kuuangalia Sana
Chakula kinachofutia baada ya giza. Hiki
ndicho mlo wa Pasaka (Kut. 12:6-11). Pia unaitwacho ni Usiku wa Kuuadhimisha
sana au ni Usiku wa Kuuangalia (Kut. 12:42; 13:3) (angalia rejea za chini za
Biblia inayoitwa “Companion Bible” kitabu cha Kutoka 12:42; vile vile jarida
lisemalo Usiku wa Kuuadhimisha Sana [101].
Huu ni usiku kwa watoto na wale ambao
hawajaongoka bado kujihudhurisha na kujifunza zaidi kuhusu mpango ya Mungu
Mwenyezi katika kuwakomboa wanadamu wote na wote walioanguka.
Inapokaribia mwisho wa mlo huu watoto (au
yeyote mmojawapo wa wale ambao hawajaongoka wa umri wowote) watauliza “maana
yake ninini kufanya mambo haya yote?” (Kut. 12:26), kadiri inavyoelekea
kuhusiana na matukio ya ule nlo (Kut. 12:8).Maana ya yule mwana kondoo aliyetolewa
dhabihu (Kut. 12:27), maana ya ule mkate usiotiwa Chachu (Kut. 12:39) na maana
ya kuzila zile mboga za uchungu (Kut. 1:14) kisha watafafanuliwa. Kasha wote
watajifunza na kumcha Mungu (Kum. 6:10-16; 14:23; 17:19).
Kila mmoja aliyemo chumbani au ukumbini mle
lazima akae kimya ili kwamba maswali yanayoulizwa yaweze kusikiwa vizuri na pia
kama ikilazimika yaweze kusomwa kutoka katika Biblia na watu binafsi wanaweza
kuombwa washuhudie kuhusu jinsi walivyomgeukia Bwana na kuhusu imani wanayo
amini (Flp. 1:6; 1Pet. 3:15).
Washiriki mbalimbali kutoka kwenye makundi
mbalimbali wapewe nafasi ya kushuhudia au kuelezea mafafanuzi mbalimbali
kuhusiana na kwenye maswali yaliyo ilizwa. Hii inatakiwa hasa ipangiliwe mapema
kabla ya muda kufika, lakini wengine wanaweza kuongezea mahali pale ambapo
pamezungumziwa. Hii huwafanya kila mmoja ajifunze kushiriki na kujifunza
kushuhudia wengine sababu hasa iliyowapelekea wao kudumu katika imani. Hii
ingefaa kufantika kwa njia ya utaratibu maalumu lakini ikiwa inatoka moyoni,ikitolewa
kwa aina inayofaa ili kwamba vijana watiwe akili na iwasisimue kusikia na
kutafakari jinsi ulivyo mzuri mpango wa Mungu.
Mwelekeo unatakiwa ulenge katika kusoma na
kufundisha zaidi kuliko kuiletea bughudha kwenye majadiliano na mazungumzo
haya. Tutatakiwa kuendelea na mazungumzo haya kwa kipindi angalau cha hadi
usiku wa manane muda ambao Mungu Aliye Juu sana kihistoria alionyesha uweza
wake wa kuwakomboa wana wa Israeli (Kut. 11:4-5, 12-29).
Mawazo yanayotakiwa kujadiliwa yanahusika
na lakini hayafungiki na haya:
1 Nini hasa maana ya Ushirika wa Meza ya
Bwana, Pasaka, Mganda wa Kutikiswa na Siku za Mikate isiyotiwa Chachu ambayo ni
ishara za milele (Kut. 13:9-10).
2. Maana ya Ukombozi wa kwanza
kabisa kwa kila mzaliwa wa kwanza (Kut.15:13;
Kum. 21:8, Luka 1:68) na hatimaye ni kwa wote kwa wakati wao wenyewe, maana ya
taratibu hizi, au maelekezo (1Kor. 15:23).
3. Kwa nini tunatoka nje kwa haraka (Kut.
12:11, 33).
4. Maana ya kusema Kumbuka tulikuwa watumwa
katika Misri na mlitoka nje ya mfumo. Tunatakiwa kuelekeza kila wiki kuhusu
kitabu cha Kutoka wakati wa Sabato (Kum. 5:15; 16:3; Zab. 81:10).
5. Maana ya Mkate wa Mateso (Kum.
16:3).
6. Nini maana ya Mkate usiotiwa Chachu ulio
liwa kwa muda wa siku 7 (Kut. 12:15; 13:6-7; 23:15, 34:18; Law. 23:6-8; Hes.
28:16-18; Kum. 16:3)
7. Nini maana ya kula mboga za uchungu
(Kut. 1:14).
8. Nini maana ya Damu ya agano (Kut. 24:8;
Zek.9:11; Mk. 14:24-25; Lk. 22:20; 1Kor. 11:25-29; Efe. 1:7; Kol. 1:14-20; Ebr.
9:14- 22; 10:29; 13:20-21; Ufu.1:5; 5:9; 12:11).
9. Maana ya imeadhimishwa na wote kwa
vizazi vyote (Kut. 12:14, 17, 23-27).
10. fanya marudio ya jinsi ukuu wa ule
msafara wa watu wanaotoka utumwani na hali halisi ambayo Israeli na wale kundi
mchanganyiko walivyo walivyoachwa pamoja. Inaashiria nini kwetu leo? Je,
tunahitaji kusubiria msafara mwingine wa Kutolewa Utumwani? (Isa. 66:18-24).
11. utakaso wetu, unaopatikana kwa njia ya:
. Mungu Baba (Kut. 31:13; 1Pet. 1:2)
. kuhusu Kristo (Efe.5:25-27; Ebr. 10:10; 13:12)
. Kuhusu Roho Mtakatifu (Rum. 15:16; 2The.
2:13)
. Kuhusu Imani (Mdo. 26:15-18)
. Kuhusu Kweli (Yoh. 4:23; Yoh. 17:17, 19)
. Kuhusu kufunga (Yoeli 2:15)
. Kuhusu Maombi (2Nya. 30:18-20)
Usiku wa Kuuangalia Sana unatakiwa
uadhimishwe kiusahihi sana na matokeo yake ni kwamba wote watanufaika.
Ni jambo la baraka sana kwa kweli kufahamu,
kuelewa na kuweza kuwa katika sehemu ya walio kayika mpango wa Mungu wa Pekee
na wa Kweli wa ukombozi katika sayari hii. Hebu basi wote na tujifunze jinsi ya
kumuishia Mungu na kumwabudu kikamilifu na katika usahihi wake.
q