Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[026]

 

 

 

Kiti cha Enzi Kimoja,

Walaghai Wawili

(Toleo La 1.0 19890125-20010303)

Mfumo uliopo sasa wa Jumuia ya Ulaya una mfumo wa kinidi uliotabiriwa kwenye Kanisa la kale huhusu jumuia hii. Mnyama atakuwa na uwezo mkubwa na wa kustaajabisha kimatokeo kwa watu wengi kwa kipindi cha zaidi ya miongo mitat ijayo. Mmoja wao atashughulika na mambo ya kiutawala au ufalme kwa sehemu zote mbili, yaani kutawala Uingereza na mataifa mengine ya Ulaya.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2001 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Kiti Kimoja cha Enzi, Walaghai Wawili



Mengi yameandikwa ya ujio wa Wazungu wa Ulaya nchini Marekani na kuhusu muungano au umoja wa mataifa ambayo yanalazimisha. Uvunguni mwa mwonekano wa uadilifu wa namna zote mbili, yaani kisiasa na kiuchumi, kuna mashinikizo mengi yanayofanya harakati zake kwa nguvu ili kufanikisha muungano wa kidini na kimfumo, sio wa kisiasa peke yake, bali pia ni kidini, kwenye mistari ya kihistoria.

 

Ulaya inaiona dharura hii kuwa ni kama kutimilika kwa hatima iliyoanzishwa muda mrefu, kuiamsha dola kuu ambayo ilishagakuwepo ya Ulaya. Maono ya Ulaya ni kuwa na dola moja ambayo imejitandaza na kunaenea kutoka kwenye bahari ya Atlantiki hadi Urusi (na kwa wengine wanaamini itajitandaza hadi Urals). Dola hii ya Muungano wa Ulaya inaonekana kama kimsingi imejikusanya au kujiunga karibu na ‘Ulaya ya Kati.’

 

Muunganiko huu kihistoria umeonekana ni kama muungano wa kidini kati ya Kanisa la Katoliki na marejesho ya mfumo au muundo wa kifalme, ambapo ‘Mfalme Mkuu’ au Mtawala Mkuu ataitawala Ulaya yote, akiwa kama upanga wa kiraia unaouwezesha Upanga wa Kikanisa la Roma.

 

Wengi wamewaangalia wa Hapsburgs kuwa ni kama warithi wa kiti hiki cha ufalme wa Ulaya na kwa kweli wanafiki wanaostahili kukirithi kiti hiki cha enzi. Hawa Hapsburgs wamekuwa wakifanya kila liwezekanalo kuelekea kwenye muungano wa Ulaya na inaweza kuwa ni salama kusema kwamba wanajiona wenyewe kuwa ni kama warithi asilia na wanaostahili kukitwaa kiti hiki cha enzi ili kutimiliza unabii uliotolewa hapo kale.

 

Wao hata hivyo sio walaghai pekee kwenye kiti cha enzi na kuna nyumba nyingine inayohitimisha kisawa unabii, (au hata ni zaidi yake) na kwa madhara ya kisiasa, wanaweza kuwazidi hawa Hapsburgs kwenye madai yao ya kukitwa kiti cha enzi cha Ulaya.

 

Mtu anayeweza kuidai heshima hii ni Charles, Mfalme wa Wales; Duke wa Cornwall wa Nyumba ya Windsor. Nyumba ya Windsor kwa kweli ni ya Ufalme bandia ambao ulianzishwa ili kuwondoa wapinga maoni na mawazo ya Kijerumani. Charles Mkuu Mjukuu wa Mfalme George V alichukua jina la Windsor kama lionekane kuwa ni jina la Kiingereza, akitokea kwenye ugunduzi kwamba Edward III alijiita mwenyewe kuwa ni Edward wa Windsor (Robert Lacey, Majesty p. 124, BCA, London 1977).

 

Tangu Mfalme George 1 hadi William IV Wafalme wa Uingereza walikuwa ni watu wanaojulikana kabisa kuwa wanatoka kwenye Nyumba ya Hanover. Wakati Victoria, binamu wa William IV alipoanza kutawala na kuolewa na Mfalme Albert, suala la uhakikisho wa kutoa majina sahihi lilitatanisha sana. Mfalme Albert alikuwa na majina mawili, jina la familia yake ni, Wettin na Jina la Nyumba yake la Saxe-Coburg-Gotha, yote yakiashiria kama ya Kijerumani, na Victoria na aliowazaa Albert walikuwa na majina yake.

 

Kwa hiyo, George V alikuwa ni wa Nyumba za Hanover na Saxe-Coburg-Gotha. Ilimbidi amuoe Mary, Binti Mfalme wa Nyumba ya Teck na alikuwa na uhusiano na wakuu wa Ujerumani. Sebule yake ilijaa mabinamu waliofanyika kuwa ni wa asili kutoka Ujerumani na Denmark, waliokuwa na majina kama ya Gleichen, Schleswig-Holstein na Battenburg.

 

Operesheni kubwa ya kujificha ambayo iliendelea mapema kabla ya mwaka 1939, iliona kuwa Saxe-Coburg-Gotha ilikuwa Nyumba ya Windsor. Na wa Battenbergs ilifanyika kuwa Mountbatten, Tecks ikawa Cambridges na Count Gleichen kwa sababu fulani ikajikuta tu inakuwa Lord Gleichen na kama Lacey anavyosema, 'jamii ya Schleswig-Holsteins walisuluhisha tatizo kwa kuyafisha.' (ibid). hawa walikuwa binti wa kifalme waliozeeka ambao walikujajulikana kama Helena Victoria na Mary Louise ambao hawakuolewa wala kuwa na nyunba hadi kufa kwao.

 

Lacey anasema kuwa Kaiser mara moja alikuwa na neno la mwisho. Wakati ali[poisikia habari hizi za upotoshaji na ndugu zake, alishauri kwamba alikuwa anaangalia mbele kwenye ufanisi wa Wanawake walioolewa Wenye furaha wa Saxe-Coburg-Gotha. (ibid).

 

Lord Louis Mountbatten alikuwa ni mtoto wa kiume wa Mjerumani aliyezaliwa huko Louis Battenburg, mjukuu wa Malkia Victoria, aliyefanyika kuwa mtu wa Kwanza kuwa kwenye wadhifa unaojulikana kama Lord mwenye Mvuto huko Admiralty kwenye kipindi cha mlipuko wa Vita Kuu ya Kwanza vya Dunia. Ingawa Louis Battenburg alishinda cheo chake anachostahili, baada ya miaka arobaini na sita ya huduma zinazotofautiana pamoja na Jeshi la Mfalme la Wanamaji, alilazimishwa kustaafu miezi mitatu baada ya hali ya uadui ilivyoanzishwa na Wajerumani mwaka 1914, kwa sababu ya kilio kikubwa cha hadharani cha watu wale wenye asili ya Ujerumani. Familia ya Kifalme ilikubana na mashambulizi makali zaidi hata. Lord Louis Mountbatten kama alivyokuwa George VI alikuwa ni mmoja wa watukuu wa Malkia Victoria. Mjomba wake Czar Nicholas II (Aliyeitwa Dickie aliyetangazwa na kuheshimiwa kama kumtofautisha na Nicky, (Mjomba Nicky) kwakuwa Nicholas lilikuwa jina lake la mwisho).

 

Elizabeth II, binti wa mfalme George VI ni mrithi halali wa kiti cha Duchess wa Saxe-Coburg-Gotha, pamoja na kuwa mrithi ia wa mstari wa wafalme wa Uingereza. Sio kwamba Charles anarithi milki za mistari na madai yake, bali kutokana na baba yake anarithi mambo mengine moja kwa moja au sio kwa moja kwa moja hata kwenye mstari wa “wablua.”

 

Mwanamfale Phillip wa Ugiriki kiutaalamu hakuwa na damu ya Kigiriki mishipani mwake, bali alikuwa ni kutoka kwenye Nyumba ya Kifalme ya Wadachi wa huko Schleswig-Holstein-Sonderburg-Glucksburg. Familia hii inadhaniwa kuwa ilipita kutokana na wafalme kumi na wa nane wa Denmark na waliotoa mmoja na kuwapa kwa Wanorway, wane kwa Waswiden, sita kwa Wagiriki wafalme wa Warusi na wakati huohuo iliwatoa Masuria wa Malkia kwa wafalme wa Uingereza, Ujerumani na Rumania.

 

Binamu wa Mwana Mfalme Phillip alikuwa ni Malkia Alexandria wa Yugoslavia. Impressive yake ya muda mrefu na ukoo mwingine wa nje kujumuisha alama za umashuhuri kama vile Henry Percy (au Henry Hotspur), Earl wa Northumberland na anajiweka mwenyewe kurudi Charlemagne.

 

Mstari wa kinasaba wa Ufalme wa Uingereza wanadai, tangu Edward III, kipenzi cha wakazi au wananchi wa Ufaransa wakati wa kufa kwake Charles IV mwaka 1328, lakini kwa kupitia mazingira yaliyopoteza hamasa au upendo kwa Phillip wa Valois ambaye alitawazwa kuwa Phillip VI. Mnamo mwaka 1337 Phillip alimtangaza kutaifishwa kwa Gascony na mnamo Oktoba ya mwaka ule, Edward ambaye huko nyuma alidai Kntawazwa kuwa Mfalme wa Ufaransa na kuwagawa majeshi kwa makundi manne pamoja naye, ambayo ilikuwa ni mwanzo wa vita vya 100. Kwa kuwa Ufaransa ilikuwa ndiyo ufalme wa kale zaidi, jamii ya Lilies wajulikanao kama Ufaransa ya Kale, walitawaliwa kijeshi mara ya kwanza na ya nne, na Leopards wa Uingereza mara ya pili nay a tatu (soma maelezo ya Picha ya 1). Gharama za Majeshi huko Ufaransa ilibadilishwa kutoka Ufaransa ya Kale falme tatu za Kifaransa za Fleur de Lys, zilizojulikana kama Ufaransa ya Kisasa na kuongozwa na Charles V mwaka 1376 au mwishoni mwa mwaka 1394. Ilikuwa sio hadi Henry IV alipoinuka na kuchukua ufalme wa Uingereza mwaka 1399 ndipo Majeshi ya Mfalme yalibadilishwa kuimarika. Alama yake ya kwanza ilikuwa ni ile ya mtangulizi wake, bali Mhuti wake Mkuu wa pili ulipungua ilipofikia mwaka 1406, kuonyesha dola za Kisasa za Ufaransa na Uingereza Kwasehemu. (Rodney Dennys, Heraldry and the Heralds, p.100, Cope, London, 1982).

 

Madai ya kuwa Ufaransa ni yao yalitolewa na Edward III ambaye mama yake alikuwa ni Isabella, binti wa Phillip IV (1285-314) na dada wa Wafalme Louis X (1314-16), Phillip V (1316-22) na Charles IV (1322-28).

 

Edward alimuoa Philippa wa Hainault, binti wa William wa Hainault na Jeanne, binti wa Charles wa Valois na mjukuu wa Phillip III wa Ufaransa, alitoa madai mengine zaidi kwa Lilies wa Ufaransa.

 

Alama hii hii ya kale inarudi nyuma hadi kabla ya ustaarabu kwenye kipindi cha mwanzoni, iliyokutwa kwenye Misri ya Kale, ambapo ilikuwa ni alama ya Uzima na Ufufuo. Ilitumiwa na Wafalme wa Byzantine na Warumi na kwa hiyo huko Ulaya, ambako Wafalme wa Carolingian waliitumia kama kitu cha kurembeshea kwenye fimbo za wafalme na sarafuni. Ilikuja kuungana na wafalme wa Wafaransa kwa kutojitokeza kwenye Mihuri Mikuu na muhimu ya Henry I (1031-60) na Louis VII, na zinaonekana, kama Majeshi ya Mfalme wa Ufaransa kwenye Mhuri Mkuu wa Louis VIII mwaka 1223. Kabla ya mwaka 1300 alijulikana kama 'Fleur de Glaieul,' kama ua jeupe au maua yaliyochukuliwa kama ua maalumu na mahsusi la Bikira Maria. Walifanyika kuwa hawajulikan tangu kutoka kipindi zama maarufu cha zama kati, kilichochukiliwa kama Mfalme wa Clovis lipewa Fleur de Lys alipobatizwa na malaika aliyetumwa kwake kutoka kwa Mungu. (ibid., p.98). (Mhuri huu na picha vilijulikana sana na Oriflamme ya Kifaransa, bendera nyekundu ambayo pia inaonyesha nembo hii takatifu). Vita vya Agincourt vilivyopiganwa tarehe 25 Oktoba 1415, lilikuwa ni tukio ambalo hii Oriflamme ilipeperushwa kwenye vita. Kwa hiyo Maua yalifanywa kuwa nembo takatifu ya Warumi nay a Dola Takatifu ya Rumi nay a muhimu, iliyojulikana huko nyumba kwenye unabii unaohusu Himaya au Ufalme wa Siku za Mwisho.

 

Kwa kuucharanga pamoja unabii huu maarufu wa Kanisa Katoliki ambao ulienea kutoka zama kabla ya mwaka 236 AD3 kunaweza kuendeleza taswira ambayo kwayo historia iliyopo inavyosema. (Hitimisho limisho la nabii hizi linakutikana kwenye kitabu kiitwacho Prophecy For Today (Unabii kwa Ajili ya Siku Hizi), sura ya 5, ukurasa wa 31, Fresno 1956. Hippolytus(d.235) aliandika kitabu kiitwacho 'The Great French Monarch [Mfalme Mkuu wa Ufaransa] watakaotamalaki sehemu yote ya Mashariki watokea kipindi kinachokaribia mwisho wa dunia.’

 

Catelados wa Tarentino (yapata mwaka 500) alimtarajia mtu huyu kuwa atakuwa kazini hadi atakapofikia umri wa miaka arobaini na ni Mfalme wa Nyumba ya Lily. Ataishinda Uingereza na dola za visiwa vingine. Ataichukua Ugiriki na kufanywa kuwa ni mfalme wake. Ataiteka na kuitiisha Clochis, Cyprus, Uturuki na Wabarbariani, kuwattisha na kuwafanya watu wote wamwabudu ‘yeye Aliyesulibiwa’. Kwa kiasi kikubwa ataiacha taji yake huko Yerusalemu.

 

Mambo mengi yamenenwa kuhusu mfalme huyu, mengine yakiwa yanaeleweka pasipo shaka kwa asili ya ulimwengu ni kama ilivyonenwa na mengine ni mambo ya kufikirika tu.

 

Hakuna shaaka kwamba Mfalme huyu Mkuu anatarajiwa kumsaidia Papa, kwenye mkakati wake ya kuutiisha ulimwengu mzima alianzia huko Ulaya kwenyewe. Mfalme huyu atakuwa ni chombo muhimu kwene mkakati wa kutenganisha za Kanisa la Rumi. Kwa sasa kuna matawi matatu ya Kanisa Katoliki, ambayo ni Kanisa Katoliki lenyewe, Kanisa la Anglikana na Kanisa la Kiorthodox kongwe ambalo linajulikana kama Katoliki inayoendeleza mafundisho ya Athanasian.

 

Waandishi hawa wanamjumuisha Kaisari wa Arles (469-543), na Mwenyeheri Rabanus Maurus (mwaka 856) amenukuliwa kama 'Madaktari wetu wakuu waliokubali kututangazia kwamba kuelekea nyakati za mwisho mmoja kati ya wazawa wa Wafalme wa Ufaransa atatawala juu ya Dola yote ya Rumi, na kwamba atakuwa ni Mfalme Mku sana kati ya Wafalme wote kuwahi kutawala na kutokea Ufaransa na atahitimisha mbio zake’. Madaktari hawa wa ghafla wanamjua kuwa ataachia madaraka na taji lake la kifalme na fimbo yake ya kifalme huko Yerusalemu pia wakati hii itakapoashiria mwisho Dola iliyochangamana kati ya Rumi na Ukristo.

 

Hii imerudiwa na Monk Adso (mwaka 992), aliyesema kwamba “Huu utakuwa ni mwisho na hatima ya Dola ya Rumi na hatimaye ndipo Mpingakristo atajitokeza mara moja'.

 

Kitabu cha Matukio ya Nyakati ya Magdeburg (karne ya 12?ananukuliwa akisema 'Kwenye utawala wa umwaji damu mkubwa wa Mfalme Charles Mkuu na Mfalme wa Urafansa atainuka kama Mfalme aitwaye Charles atakayetawala kifalme huko Ulaya, ambaye kwa yeye, nchi iliyooza ya Kanisa itaanzishwa na utukufu wa kale wa Dola utarudishwa tena.'

 

Aystinger – Mjerumani (pia kwene karne ya 12) alimuweka mfalme huyu kuwa atatawala katika siku za mwisho, ambaye ataibuka kutoka kwa Mfalme Charles. Ataihuisha nchi ya ahadi, yaani nchi ya ahadi Yerusalemu, na kulifanyia matengenezo kanisa akiwa kama Mfalme wa Ulaya.

 

Abbot 'Merlin' Joachim (mwaka 1202) aliyaelezea utejeshaji huu wa mamlaka na mahali pa kanisa kwa Papa wa siku za mwisho, atakayeihuisha Yerusalemu na kuwanganisha tena mamlaka zilizoondolewa kwa kitambo na kwenye kanisa la pande za Mashariki na Magharibi. Papa huyu anatarajiwa kuwa ataabudiwa kwa kupigiwa magoti na kutoa uwezo hali ya juu sana wanaopinga hila na mafundisho ya kizushi ya kidini. (Kwa maneno mengine, kitendo cha kuanzisha tena Mahakama ya kanisa la Rumi inayoshughulikia Mambo ya Kukufuru au uasi wa mafundisho yao sasa Mkusanyiko Mtakatifu kwa Fundisho la Imani).

 

Papa huyu anatarajiwa kujaza hombwe hilli la Mfalme Repin kwenye kiti cha enzi cha kuda mfupi ambacho kinakuwa tupu (au kuwepo). Hata hivyo, mwandishi ni wazi kabisa kuwa anazitaja harakati au mandendo ya mwanzoni mwa karne hii kutoka kwenye hadithi fupi ya 'Wachungaji Malaika' waliotajwa na Malachi kwenye kitabu chake alichokiandika katika karne ya 12.

 

Kwa mujibu wa Werdin d’Otrante (karne ya 13) Mfalme Mkuu na Papa Mkuu watamtangulia Mpingakristo.

 

Mataifa yatakuwa vitani kwa kipindi cha miaka minne na sehemu kubwa ya dunia itaangamizwa. Dini zote zitakoma (bila shaka zitasaidiwa kwa kiasi ukaribu na kiasi kikubwa na Ofisi Takatifu). Mwandishi huyu anaelezea mfumo wa imani wa Ulaya chini ya Papa na mtawala wa kiraia anayekwenda kuratibu na kusimamia mikakati ya vita vya kumpiga Mpingakristo (ambavyo watashinda). (Hii imewekwa kwenye tarehe za sikukuu zinazofuatia za mwaka 2038 ambazo zinaonekana kukanganya unabii wa biblia na kuonekana kuchelewa sana).

 

Habari hii inendelea mbele kupitia waandishi kama vila Ndugu au Brother John wa huko Cleft Rock (mwaka 1340); na Catherine wa Racconigi (mwaka 1547). Telesphorus wa Cozensa (mwaka 1588) haujui mwisho wa muungano wa Ulaya na bilashaka anakosea.

 

Holzhauser (mwaka 1658) anatoa maelezo ya kina sana ya kile kiachoonekana kama matengenezo ya kimiujiza ya kurejesha kanisa na Taifa, baada ya kinachoonekana kama ni kifo au mauti ya Kanisa Katoliki na falme au tawala umeathirika na viongozi au watawala wao kuuawa.

 

Mfalme huyu ni budi awe Mkatoliki, kutoka uzao wa Louis IX (1214-1270) (tena) wa uzao wa familia ya Ufalme wa kale wa Ujerumani, aliyezaliwa uhamishoni (yaani hakuzaliwa Ujerumani). Ataongoza na kusimamia kikamilifu na kwa umahiri mambo ya kipindi kifupi. Papa atatawala kwa umahiri mkubwa masuala ya kiroho kwa wakati huohuo. Mateso yatakoma na haki itatawala (kwenye Kanisa Katoliki). Dini inaonekana kuelezewa, bali kwa mabadiliko ya falme zote, itaimarishwa zaidi.

 

Ataondoa mafundisho ya uwongo na kuuangamiza utawala wa Kiislamu. Mfalme huyu Mkuu atakuwa na usaidizi usio wa kawaida na wa asilia na atakuwa ni mtu asiyeshindwa. Wakati huu umegawanyika kwa awamu na awamu ya Tano iliyohesabiwa tarehe zake kuanzia Charles V, hadi utawala wa Mfalme Mkuu na awamu ya Sita tangu utawala wa Mfalme Mkuu hadi kipindi cha Mpingakristo. (Cheo au mtu huyu anayeitwa Mpingakristo ni taasiri kubwa na mashuhuri inayojulikana sana na vuguvugu la Wasabato wanaofundisha kinyume na Kanisa Katoliki la Rumi ambaye kwa mtazamo wao wanamuita Mpingaktisro). Kwa kweli, mtu huyu anayatenda yote ambayo Kristo amesema atakuja kuyatenda. Jina la Mpingakristo, yaonekana kuhusiana na taasisi mbili zilizoonyeshwa kwenye unabii wa biblia, Mpingakristo wa Dani (Nabii anayetokea kwenye mchanganyiko wa makabila ya Dani na Efraimu kwenye Yeremia 4:15 sawa na jarida la Maonyo ya Siku za Mwisho (Na. 44) na ni mtawala mahiri wa ulimwengu au Masihi.) Rudolf Gekner (mwaka 1675) anasema kuwa huyu mtu anayetarajiwa ni mfalme mkuu wa Kaskazini. Father Larinsky (mwaka l708) anayaelezea matukio haya kuwa yalikuwepo baada ya kugawanywa kwa nchi ya Ujerumani.

 

Fr. Laurence Ricci SJ (mwaka 1775) alikiweka kipindi hiki kuwa kilikuwa ‘Baada ya utawala wa Napoleon na baada ya kipindi cha vita, baa la njaa, na magonjwa au tauni,’ ambapo 'mtawala au mwana wa mfalme shujaa atainuka kutoka kwenye Nyumba ya Ujerumani ya kale ambayo ilitiishwa na Mfalme wa Ufaransa.' Atarejesha mali na raslimali za kanisa, Uprotestanti utakoma na (Uislamu) au Dola ya Kiislamu ya Uturuki itaanguka na kufikia mwisho.

 

Josepha von Bourg (mwaka l807) anasema kuwa Mungu atamchagua mtu kutoka kizazi cha Constantine, Pepin na Mtakatifu Louis ambaye amekuwa akijaribu kwa kipindi kirefu cha kukatisha tama kuja kutoka uhamishoni ili kuitawala Ulaya, nk..

 

Abbe Souffranid (mwaka 1828) anayaelezea matendo ya miujiza na uzalishaji wa kiasi kingi cha zaidi ya matarajio. Katikati ya vilio kila kitu kinapotea na kila kitu kinaokolewa, kutakuwa na mwadimiko wa kila mwanya au umabli. Marejeo haya ya muujiza wa uponyaji umeshatokea tayari huko Ulaya na kuna mengine mengi bado yanakuja.

 

Brother Louis Rocco (mwaka 184O) anasema kuwa huyu Mfalme Mkuu HATAKUWA Mjerumani. ‘

 

Mheshimiwa Magdalene Parzat (mwaka 1850) alitumia mfano kuelezea kuinuka kwa Mfalme na Papa atakayeitawala dunia, (Ataokoa shingo la dume la ng’ombe), Jamhuri ya Ufaransa (na jamhuri zote nyingine za kimapinduzi inayowazuia?) na kuurudisha ufalme.

 

Kwa mujibu wa Rev. Theophilus Reisenger, OM cap (mwaka 1940) Mfalme huyu Mkuu alikudhaniwa kuwa angekuwa ni Archduke Franz Ferdinand. Anadai kwamba utawala wa Mpingakristo uliahirishwa na hata pia huu wa Mfalme Mkuu. Ni wazi sana kwamba mapokeo haya yamekuwa yakichukuliwa hivyo huko Ulaya kwa kipindi cha takriban miaka 1750, au sambamba na imani ya Waaathanasian wa Kanisa Katoliki inayoendelea hadi sasa.

 

Sababu inayoshinda kabisa ni wa marejesho makuu ya Ufalme na Kanisa kwenye muungano wa Ulaya, chini ya maongozi ya Kanisa moja la Kikatoliki na Papa. Hii itaenda sambamba au kufuatiwa na utokomezaji au kuyakomesha kwa kuyapiga marufuku makanisa yasiyo ya Kikatoliki. Mkakati wa kuyaunganisha dini na makanisa yote ndiyo ajenda iliyopo kwa sasa.

 

Nyumba ya Hapsburg-Lorraine au Hapsburgs, kimapokeo imekuwa ikionekana kuwa ni watawala wanaoitwa kwenye Dola hii ya mwisho ya Ulaya. Wakati kwamba hii yaweza kuwa hivyo si jambo lililo bayana kuwa wao ni washindani wa pekee.

 

Kama ilivyoonyeshwa, Mtawala aliyeko sasa ambaye ni Mfalme wa Wales anakithi vigezo vyote. Jamii ya wa Saxons na Goths walikuwa nje ya mstari wa kiuzawa wa Wajerumani wakiwa ni sehemu ya jamii ya wa Scandinavia, hadi Goths walipohamia huko Ulaya waliwa kama wa Ostrogoths na Visigoths, wakiwa wanaishi huko Gothe au Gotha. Jamii ya wa Saxons hawakuwa kabisa sehemu ya Wajerumani, hadi wakati Charlemagne alipowashinda wao na kuwashirikisha wao kwenye Shirikisho la Ujerumani, kama sehemu ya iliyokuwa Dola Takatifu ya Rumi mnamo mwaka 771-2 na kuwashinda ndugu zao, wa Lombards mwaka 773-4. Kwa hiyo kuna mashaka kuhusu kiwango cha kidaraja cha Wajerumani wa Saxons wa Schleswig-Holstein. Hata hivyo, dunia inawaweka watu hawa kwenye tabaka la Wajerumani ma wa Nyumba ya Hanover na Saxe-Coburg-Gotha wakistahili kwa mambo yaliyonenwa kwenye unabii. Ni kweli kwamba Nyumba ya Ufalme wa Ujerumani na Uingereza zilihusiana na hakuna la kujiuliza kuhusu uhusiano wa Wafaransa na kiti cha ufalme wa Uingereza, huenda ilikuwa ni zaidi sana kuliko ilivyo sasa kwa Wafaransa na jamii ya Austro-Hungary.

 

Tangu kipindi cha kuungana kwa Uingereza na Scotland mwaka 1707, warithi waliochukua ufalme walichukuliwa na kukubalika kuwa ni warithi wa taji za muungano, tangu mara tu baada ya kuzaliwa kwake, akipewa jina la kicheo la Duke wa Rothesay, Earl wa Carrick, Baron Renfrew na Seneschal au Steward wa Scotland, wakichukuliwa kama warithi wa Scotland tangu mwaka 1396.

 

Jina la kicheo la, Mfalme au Prince wa Wales, lilitungwa na Royal Charter tarehe 24 Marchi 1305 na lilichukua mahala pa jina la zama kale la ki Anglo-Saxon la Atheling.  Mfalme huyu wa Wales alipewa kutoka zama za kale, jina la pili la kicheo pia la Duke wa Normandy kutoka kwenye mshikamano wa Normandy na wa tatu kwenye daraja la kicheo kutoka kwenye mwanzoni mwa tarehe 18 Mei 1332 mrithi amapewa jina la kicheo la Earl wa Chester. Duke wa Cornwall ni wa pili kwenye daraja lakini watatu kwenye kipindi cha zamani kutoka kwenye kipindi cha Mwanzoni mwa tarehe 17 Marchi 1336, akiwa mtangulizi wa kwanza wa uundwaji wa cheo hiki cha Duke wa Uiingereza, cheo kilichochokuliwa kutoka kwenye cheo cha zamakale cha Kirumi cha Dux (kutoka neno Duco). Kulikuwa na jumla ya hawa Duces 12 waliokuwa wanasimamia mambo ya kiutawala wa Magharibi ya Dola ya Warumi.

 

Che hiki cha Duchy wa Cornwall, alichopewa Mfalme wa Wales, kilikuwa ni marejesho ya kwanza ya kisasa ya cheo cha lake cha Kirumi cha Duke Mpigana Vita, ambaye lishindwa kicheo na kimatumizi. (Alan wa Britane ambacho kilichukuliwa kama ni cheo cha zamakale zaidi kwa urithi wa Dukedom, mara nyingi sana kiliitwa Kuja au Comes kuliko Dux, kama walivyokuwa waliomfuatia hadi wakati Mfalme wa Ufaransa Phillip mwaka 1277 alipokurejesha cheo cha Duke kwenye familia ile).

 

Charles, akiwa kama mrithi pia wa Ufalme wa Uingereza wa Dola ya Uingereza na Ireland aliyekuwa na haki halali kwenye maeneo mengine zaidi ya Rumi ya Kale nay a Dola Takatifu ya Rumi.

 

Kisiasa, mwenendo wake ulikuwa na dalili zilizokuwa zinaashiria. Taji hii ikiwa ni kama kichwa cha Kanisa la Uingereza lilipaswa kuvaliwa na kwa kuungana harakati na matendo ya Waanglikana wa mrengo wa Kikatoliki na Wakatoliki wa Rumi na muunganoniko kama hizi zitatokea ili kuwezesha mafundisho ya Kiorthodox. Ni rahisi zaidi kwa watu wa Ulaya ambao wana namna ya madai ya viti vya ufalme vya nchi nyingi kama vile Ugiriki na wenye udugu wa karibu kwa wengine kwenye maeneo yote ya Ulaya.

 

Inawezekana kuwa Malkia Elizabeth II atakapofikia kikomo cha utawala au kujiuzulu, kama ilivyokuwa wakati mmoja kukiongezeka msukumo wa yeye kufanya hivyo, zaidi ya ilivyokuwa zikionekana dalili kwamba Charles angeweza kuwa mwenye kulihurumia na kuchukuliana sana na mikakati ya Wakatoliki, kama ilivyoashiria kwenye ziara yake aliyoifanya alipotembelea Roma. Kitendo chake kilichofuatia baadae cha kujitangaza mwenyewe kuwa yeye ni Mtetezi wa Imani, kwa ujumla kimekuwa na maana inayokanganya. Ni Malkia tu ndiye aliyemkataza na kuzuia nia yake ya kushiriki Meza ya Ushirika pamoja na Papa.

 

Swali ni kwamba, huu ulikuwa ni mkakati wa kumtawaza yeye kuwa mfalme wakati ambapo Malkia Elizabeth angali hai bado, na halafu kisha yeye awe mkuu kumliko yeye Malkia naye awe kwenye nafasi chuki. Hali hiyo ingeongeza madhara ya kisiasa. Je, Uingereza ingejitoa, jinsi ya mahala pa kisheria inavyotenda kazi ua pengine wangaliyo kuwa nayo kama Kiti Chake cha Enzi, au hata yeye Mfalme wa Wales, akawa ni Mfalme wa Ulaya?

 

Kimkakati, Dola ya Uingereza ingetakiwa kuchukua Kiti hiki cha Enzi cha Ufalme wa Ulaya yote na hii ingelazimisha Dola kufikia uamuzi wa kujitangaza yenyewe kuwa ni Jamhuri ndogondogo.

 

Mataifa kama vile Australia yangepelekea kwa hiyo kujiengua kwenye umuhimu wa kuhitaji kiapo, kama ilivyotakiwa hata na mstari wa uzawa wa zamakale zaidi ambao Mfalme anatokana kwao na kumuwezesha kuchukua Kiti cha Enzi cha Daudi. Kama katiba ya Australia ilivyo kuwa ni kifaa muhimu kwenye Bunge la Uingereza, ndipo hata uhuru wake unaweza kukosolewa. Mamlaka ya kiutawala ya Canada kimkakati yanaweza pia kwenye nafasi ya uchochezi. Kimkakati, Canada ingefanyika kuwa ni Koloni la Ulaya na kujitangazia kwake kuwa Jamhuri kungechukuliwa kama uasi. Kwa hiyo nchi ya Marekani ingejikuta inazingirwa na jeshi la mataifa ya Wakatoliki.

 

Kwa hakika kitendo cha Mfalme wa Uingereza kuwa kwenye kiti cha ufalme wa Ulaya, kunahalalisha kisheria dhana iliyopo ya mwisho wa taifa la Uingereza kwa kweli. Hii si mara ya kwanza kwamba Muundo wa Jumia ya Ulaya imepokonywa uwezo na kuchezewa na wazo hili. Hitler alijaribu kumuweka Edward VIII kwenye maabusu ya Ulaya na ilibidi nafasi yake ichukuliwe kwa kupitia Wallis Simpson, kisha mapenzi na nia ya kihisia ya watu wa Uingereza iliyotokea kuangamia vibaya kabisa.

 

Malengo ya wazungu wengi wa Ulaya (na wale wa jamii ya Prieure de Sion) hata hivyo, wamekuwa wakijiandaa kuelekea kwenye kuifanya kuwa ni Marekani ya Ulaya, chini ya Hapsburgs na kile kinachoitwa Lstari wa Merovingian wa wafalme, yenye kiini cha Kanisa Katoliki la Rumi.

 

Wakati huuhuu, watu wanataka kumuweka Hapsburg kwenye kiti cha enzi cha ufalme, mazingira ya kisiasa nay a kimuangano yanaweza kutafuta kuyapa nafasi au fursa matumaini ya mnafiki mwingine kwenye kiti cha enzi cha Ulaya, kwa maelekezo ya umakini mkubwa ya Bunge la Ulaya.

 

Tungetarajia kuona shinikizo zaidi la kumtaka Malkia ajiuzulu kwa kadiri muda unavyozidi kwenda, pamoja na uwezekano wa miungano ya makanisa yakiendelea nyuma ya matukio.

 

Kwa Charles, kwa kweli Ulaya ‘ingekuwa inastahili kula Mlo wa Ushirika.' Charles Phillip Arthur George anapewa kazi hili kwa haraka. Wafalme au viongozzi wa Cornwall na Wales walipewa jina la kicheo la Joka, yaani Dragon na alama ya upashaji habari ilikuwa ni joka jekundu. Alimpa jila la maua Phillip, jina maarufu la wafalme walio kwenye Mstari wa Wafaransa. Alitimiliza umaarufu wa kukumbukwa kwa jamii ya Arthurian wa mfalme aliyekuwapo na Yule ajaye akiwa sio kwamba ni Pendragon peke yake (au Mfalme Mkuu) wa Uingereza, bali wa Ulaya chini ya Dola inayoamka tena ya Rumi na kujumuisha wa upande wa Magharibi na Mashariki mwa Ulaya, ni kama George wa mwisho wa Wahellenes.

 

Kuanzishwa tena kwa ufalme huu wa mwisho wa Wafaransa kama Dola Takatifu ya Rumi haikubaliani na hatima ya taifa la Israeli.

 

Hili ni tukio lililowahi kutabiriwa na nabii Ezekieli kwenye sura ya 21:26-27 kuhusu kukomeshwa kwa ufalme wa Israeli, baada ya kupinduliwa kwake mara tatu. Kwa kuwa baada ya kuondolewa Visiwa kulikonenwa na Yeremia na baada ya kupinduliwa tena huko kutoka nchi ya Ireland hadi Scotland na kutoka Scotland hadi England, bado kuna ukomo uliopo, hadi atakapokuja Masihi.

 

Bwana MUNGU asema hivi; Kiondoe kilemba, ivue taji; haya hayatakuwa tena kama yalivyo; kikweze kilicho chini, kakishushe kilichoinuka. 27 Nitakipindua, nitakipindua, nitakipindua; hiki nacho hakitakuwa tena, hata atakapokuja yeye ambaye ni haki yake; nami nitampa.

 

Ukomo wa mwisho wa ufalme wa Waisraeli ulipasa kutarajiwa kwa kutokea tukio la utumwa au uhamisho wa jamii ya watu wanaoongea lugha ya Kiingereza. Uingereza (na Canada) watakwenda wakiwa chini ya mfumo wa Wakatoliki wa Ulaya. Kwa shuruti na ukatili mkubwa, jamii mpya ya Dux Brittanicum watawatumikisha utumwa jamii ya Angles, Saxons, Jutes na Danes.

 

Kutakuwa na uhamisho na mateso makubwa kufanyiwa wale wote ambao hawataukubali Ukatoliki kwenye nchi hizi.. Australia na New Zealand zitakuwa zimeenezwa na hawa wahamiaji wenye asili ya Kiingereza. Wito uliotolewa wa kuwataka watu ukisema ‘tokeni kati yake enyi watu wangu’ una maana mpya. Wazungu wa Ulaya na kama walivyo wahamiaji walipaswa kutarajiwa kujaribu kuiweka Australia chini na Nguvu za Mnyama wa Ulaya. Hii kama ilivyo ingekuwa ni jambo lisilokubalika kwa ‘Wafalme wa Jua Linalokucha’ au ‘Wafalme wa Mashariki’ walioandikwa kwenye Ufunuo 16:12.

 

Inaonekana kuwa Australia ingeshambuliwa na kufikia toba kwa kuvaa nguo za magunia na kujitia majivu na mavumbi vichwani, ila nchi hizi zimefanya kila linaliwezekana kwenye mwandamano wa matukio ya siku za mwishoni.

 

Utabiri wa pili uliofuatia wa Sybilline ulijua jambo hili wakati ulipoandikwa (huenda ni mapema kabla ya mwaka 150 BK). Baada ya kuelezea ongezeko la maafa ya nyakati za mwisho, nabii wa uwongo au kiongozi wa kidini mwenye asili ya kutenda kwake shetani atatenda miujiza na kuleta maafa katika nyakati za mwisho, mambo ambayo yatawachanganya na kuwadanganya watu wendi, kiasi cha kuwachanganya yamkini hata wale waliochaguliwa kuirithi neema au wateule ambao pamoja na Waerania watakuwa wamenyang’anywa. Inasema:

Hasira kali itawajilia wakayi watu wa makabila kumi watakuja kutoka mashariki ili kuwatafuta watu, ambao chipikizi wa Ashuru atakapowaangamiza wenzao Waebrania. Mataifa yataangamia baada ya vitu hivi.

 

Kutokana na Ezekieli sura ya 29-32 ukaliwaji wa mwisho wan chi ya Misri na Wafalme wa Kaskazini utapaswa ufanyike sio kwa kitambo kirefu sana cha siku zijazo, baada ya mgogoro wa Waislamu wa Ulaya kutokea.

 

Wakati Utabii wa Sybilline ulipokuwa unaandikwa, kulikuwa hakuna mataifa yalilojulikana kama ni ya Waisraeli mashariki mwa tunapopaita leo Israeli. Ni makabila kumi pekee au Waisraeli mashariki mwa Yudea ni Waaustralia na wa New Zealand. Kwa kweli, hakuna taifa lolote linguine ambalo hata kwa mtazamo wa kiujima lililotiliwa maanani kuwa limemudu kuuhitimisha au kuutimiliza unabii huu. Uwezekano uliopo hadi sasa ni kwamba nchi ya Marekani inaweza kusaidia kwa kupitia Australia. Unabii huu umechukuliwa kutoka kwenye unabii ulio kwenye biblia unaoelezea kuhusu ujio wa Masihi. Hii inahusisha na unabii mwingine unaohusu kazi za Mungu katika nyakati za mwisho, ambapo kazi ya Mungu itakuwa na nguvu sana upende wa kusini. Jambo hili limeelezewa kwa kina kwenye jarida la Moto Kutoka Mbinguni (Na. 28).

 

Nabii Yeremia anaelezea juu ya maonyo ya kukaribia kwenye sura ya 4:15, ambapo sauti, mateso yanayotangazwa kutoka kwenye milima ya Efraimu, yakionya mataifa kwamba anakuja, naye anauhusiano ia na kabila la Dani.

 

Hii inashabihiana na bashiri za Wakatoliki, zinazomwelezea Mpingakristo wa kabila la Dani, anayejaribu kuzirejesha tena Sheria za Musa anayekuja akitokea nchi ya mashariki iliyo katikati ya bahari mbili.

 

Kwa kweli hii ni kweli kama nabii Isaya alivyowahi kutabiri kwenye sura ya 46:11, ambapo anatangaza mwisho kutoka mwanzo urejesho wa wito wa Milele ‘ndege mtoza ushuru kutoka mashariki, mtu atakayeliondoa shauri langu wa kutoka nchi ya mbali'.

 

Inapasa ikubukwe kwamba ndege tai ni nembo au alama ya kabila la Dani na hii ‘nchi ya mbali’ ni lugha mfano inayoashiria kuwa ni nchi ya Australia, kwa matumizi karibu tangu kuanza kwa makazi yao. Iyaweza kuwa pia inaashiria kuhusu Wafalme wa Mashariki wa unabii unaofuatia. Hii ni mara tu kabla ya kuja kwa Masihi kama ilivyo kwenye aya ya 13 ambako tunapoambiwa 'Tena nitauleta haki yangu, haitakuwa mbali sana, na wokovu wangu hautachelewa; na nitauweka wokovu wangu katika Sayuni kwa ajili ya Israeli utukufu wangu.'

 

Inaweza kuwa huenda kwamba huyu nabii mwenye nasaba mchanganyiko ya Dani na Efraimu ni sauti au kundi litakalotokea mapema kabla ya mashahidi wawili waliotajwa kwenye Ufunuo 11. Wakati wa vita vya mwisho ambavyo vitashuhudiwa kutokea hivi karibuni, mambo ya kiuchumi na kimkakati yatajumuishwa pamoja na kuchukuliwa kwa uzito sawa mambo ya kidini. Dola mpya yenye nguvu kubwa ya Ulaya itakuwa na nguvu z namna zote mbili, yaani za kiraia au kijamii na kidini, na ukubwa wa mataifa yake na uwezo wake wa kivita utawashangaza na kuwahadaa watu wengi. Vita hivi vya mwisho kupiganwa hapa duniani ni vya muhimu sana kiroho na havitapiganwa kwa nguvu za mwili, 'wala si nguvu bali ni kwa Roho wangu, asema Bwana.’ Vita hii na Waislamu inakuja na itatokea hivi punde, na ni ‘vita ya mwisho ya wafalme wa kaskazini na kusini\ iliyotabiriwa na Mungu kwa kupitia nabii Danieli.

 

Kusudi na lengo la jarida hili ni kupembua unabii usio wa kibiblia. Pia limekusudiwa kuonyesha kuwa kuna mlolngo wa uwezekano kwenye mgawanyo ujao wa na uadui. Matendo haya ya siku zijazo yanaweza kufanywa ili kuwavutia au kuwakanganya watumiaji wa lugha ya Kiingereza na kuathiri kwa kuikomesha nguvu za muungano wa Jumuia ya Madola, ambayo pamoja na Marekani, na kuendelea hadi leo, imeuwezesha ulimwengu kujipatia uhuru ambao usingeweza kujipatia kamwe kwenye Ulaya iliyoungana. Utambulisho au alama ya watu wanaotumia lugha ya Kiingereza ni zana muhimu sana katika kuielewa Biblia na matendo au harakati zinazowahusu wao katika nyakati za mwisho.

q


 

 

 

 

 

http://www.ccg.org/s/P026_files/image002.gif

 

 

 

 

http://www.ccg.org/s/P026_files/image004.jpg

 

(kushotot) Sarafu ya Zamakale ya Ufaransa na Uingereza ikiwa na migawanyiko ya roborobo na (kulia) Sarafu ya Kisasa ya Ufaransa na Uingereza roborobo.