Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[021G]

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu cha Nahumu

 

(Toleo La 1.0 20141004-20141004)

 

Nahumu ni nabii wa mwisho kati ya manabii saba waliohudumu kipindi cha kabla ya utumwa Ashuru na akiwa ni wa mwisho kati ya kundi lingine la manabii watatu. Yona alipewa huduma ya kwenda kuwaonya watu wa Ninawi. Sefania aliitwa pia lakini kwa kiwango cha chini kwa namna fulani.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ufafanuzi wa Kitabu cha Nahumu



Utangulizi

Kitabu cha Nahumu ni cha saba kwenye kundi la Manabii Kumi na mbili. Jina lake linamaana ya kumfariji au mwenzi (soma Isaya 57:18). Nabii huyu anatokea huko Elikoshi ambao ni mji ulio Kusini Magharibi ya Yuda ambako ndiko kabila la Simeoni lilikuwa na ambako ni karibu na mipaka ya Wafilisti na Wamisri, katikati ya Beiti Jibrini na Gaza. G. Nestle anauelezea n Kesije, mji mdogo uliokuwa Kusini Magharibi ya Beiti Jibrini, U. Cassuto hata hivyo anauelezea huu na Ummu Lagishi ulioko kati ya Gaza, na hii kwa mujibu wa Epiphanius (soma kamusi ya Interp. Dict. of the Bible,art. ‘Nahum,’ Book Of, Vol. 3, p. 498, col. 1).

 

Wanazuoni wengi wanakubali kwamba makadirio ya tarehe za mwanzoni sana zilizochukuliwa kwenye uandishi ni mwaka 663 KK wakati wa kuanguka kwa mji wa Thebes kwa Waashuru. Tarehe inayokadiriwa hivi karibuni ni ya kuanguka kwa Ninawi mwaka 612 KK. Dola mpya ya Neo-Babylonian ay Babeli ya Kimamboleo ilianzishwa na Nabopolasa mwaka 625 KK na kuyakusaya majeshi ya Wababeloni, akapanda kutoka Frati hadi Kablinu ambako aliyatesa Jeshi la Waashuru kwa ushindi mkubwa na wa kishindo. Wamedi walianza kushambulia kutoka upande wa Mashariki na mwaka 614 waliutwaa na kuuhusuru mji Ashuru. Kisha Nebopolasa akafanya muungano na ushirika nao na wafalme wao. Kwa pamoja Wamedi na Wakaldayo waliendelea kushambulia hadi Ninawi ikaanguka mwaka 612 KK. Mwaka 625 KK ni mwaka unaodhaniwa sana kuwa ndio manabii hawa, Nahumu na Sefania walihudumu kwa mujibu wa ugunduzi wa Gombo la Torati lililosomwa kwenye matengenezo na marejesho mapya ya Yosia katika mwaka wa 18 ya kutawala kwake. Kwa hiyo ulikuwa ni mwanzo wa muungano wa Wababeloni ambao walipaswa walitumike kuiangamiza Ashuru.

 

Bullinger anaamini kuwa maandiko yaliyo kwenye uovu ulioandikwa kwenye aya ya 1:11 ni maandiko halisi ya Rab-shekeh ya 2Wafalme 18:26-28 anayoonekana kuwa Myahudi muasi na aliyekengeuka na ambaye alikuwa ofisa mwenye cheo kikubwa au ofisa mwenye cheo kikubwa na cha juu cha kisiasa wa Senikarebu na ni adui mkubwa sana wa Yahova wa Israeli. Bullinger aliyakadiria maandiko haya kuwa yalifanyika mwaka wa 14 wa Hezekia na kwamba ulikuwa ni mwaka 704/3 KK. Hii yawezekana ilikuwa ni mapema sana lakini ni baada ya kuanguka kwa Israeli.

 

Kama kawaida, wanaowakashifu kwa kashifa hizo za uvuvio wa Kibilia na unabii zilijaribu kuweka tarehe baadhi au kazi zote kwenye tarehe za baada ya kuanguka kwa Ninawi, lakini inawezekana sana kuwa wanazuoni waliweka tarehe za huduma ya Nahumu kuwa ilikuwa ni kabla ya kuanguka kwa Ninawi, lakini ni miaka mingi baada ya unabii wa Yona na kwa wakati mmoja na wakati wa unabii wa Sefania. Wengi wanauona kuwa ni kama kazi ya mtu mwenye uwezo mkubwa wa kimashairi (Interp. Dict., ibid. p. 499).

 

Nahumu anaielezea imani ya Waashuru kwa kuihusisha na Dini potofu wa waabudu Jua na ukaribu wa maadui wa dini za Baali na Mungumke au Mungu Mwanamke ya watesaji wenye dhuluma wa kaskazini na vita vilivyotajwa kwenye imani ya Kibiblia na sikukuu za waabudu sanamu.

 

Baaya ya andiko lililo kwenye 1:1 hapa kuna kutolewa kwa wimbo wenye kifupisho cha kialfabeti unaoelezea teofilia ya mashairi au tenzi hizo kuwa zimepotea kwenye tafsiri. Wimbo unaendelea hadi kufikia beti ya 9 na kila mstari unaanzia kwa herufi tangulizi ya alfabeti za Kiebrania kutoka herufi ya mwanzo ambayo huijulikana kama Aleph hadi ya mwisho iitwayo Nuwn herufi ya 14 iliyosawa au kufanana na n. wanazuoni wengine wamejaribu kuileta au kuiweka kifupisho ili kuifikia herusi ya pili hadi kufikia Nahumu sura za 2:3 au 2:4. Suluhisho jema ni kuifanya ifuate nusu ya kwanza ya Alfabeti za Kiebrania kuanzia Aleph hadi Nuwn na hadi kufikia karibu na Sawmek.

 

Ashuru waliifanya Israeli kuwa ni nchi ya kutoza kodi tangu kutekwa kwake Dameski na hatimaye waliiondoa na kuiangamiza Israeli mnamo mwaka 722 na kuwapeleka upande wa juu wa kaskazini wa Araxes na kuwashawishi Yuda kutoka hapo na kuendelea na walikuwa na mungu wake na imani za kumuabudu Mungumke wa Baali na Ashtorethi au Easter/Ishtar, imani iliyojipenyeza na kushamiri kwa pande mbili zote, za Israel na Yuda kwa kipindi kirefu sana. Kiasi kwamba Yona alituwa kwao na matendo yao yalikatazwa kupitia manabii Isaya na Yeremia na kuendelea hadi kwa nabii Sefania na kwa wengineo zaidi waliofuatia hapo.

 

Kwenye aya za 1:2-13; 2:1,3 kuna ahadi waliyopewa Yuda na kwenye aya za 1:10-11 na huenda hata 14; na 2:2 tunaona mwanzo wa mapatano kwa Ashuru. Hata hivyo, wimbo huu unaonya moja kwa moja kwa viumbe wote na utambulisho wa wale waliookoka kuwa ni wale waliomkimbilia Mungu.

 

Miungu mchanganiko ya Kiashuru na Kibabeloni ya mungu Jua na ya dini za Kisirifumbo itaondolewa. Mataifa ya kaskazini kutoka Bashani na Karmeli na mito yake kutoka Lebanoni itakauka. Dini na imani zao zitahukumiwa.

 

Nahumu Sura ya 1

Ufunuo juu ya Ninawi. Kitabu cha maono aliyoyaona Nahumuu, Mwelkoshi. 2 Bwana ni Mungu mwenye wivu, naye hujilipiza kisasi; Bwana hujilipiza kisasi, naye ni mwingi wa hasira; Bwana hujilipiza kisasi juu ya adui zake, huwawekea adui zake akiba ya hasira. 3 Bwana si mwepesi wa hasira, ana uweza mwingi, wala hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; Bwana ana njia yake katika kisulisuli na tufani, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake. 4 Yeye huikemea bahari na kuikausha, pia huikausha mito yote; Bashani hulegea, na Karmeli; hulegea nalo ua la Lebanoni. 5 Milima hutetema mbele zake, navyo vilima huyeyuka; nayo dunia huinuliwa mbele za uso wake, naam, dunia na wote wakaao ndani yake. 6 Ni nani awezaye kusimama mbele za ghadhabu yake, naye ni nani awezaye kukaa katika ukali wa hasira yake? Hasira yake kali humwagwa kama moto, nayo majabali yapasuliwa na yeye. 7 Bwana ni mwema, ni ngome siku ya taabu; naye huwajua hao wamkimbiliao. 8 Lakini kwa gharika ifurikayo atapakomesha kabisa mahali pake, na kuwafuatia adui zake hata gizani. 9 Mnawaza nini juu ya Bwana? Yeye atakomesha kabisa; mateso hayatainuka mara ya pili. 10 Kwa maana wangawa kama miiba iliyotatana, na kunyweshwa kana kwamba ni katika kunywa kwao, wataliwa kabisa kama mabua makavu. 11 Ametoka mmoja kwako, aniaye mabaya juu ya Bwana, atoaye mashauri yasiyofaa kitu.

 

Kisha Mungu anaendelea na ahadi kwamba kongwa la mfumo wa Kiashuru na dini yenye mchanganyiko wa Waashuru na Wababeloni ya mungu Jua na dini ya Mungumke ya Baali na Ashtorethi au Easter Ishtar vitakomeshwa na kuangamizwa na mahekalu yao yote mengine ambayo yana sanamu hizi na vikorokoro vyake zote zitaondolewa kutoka kwenye mahekalu yao na kuangamizwa.

12 Bwana asema hivi, Ijapokuwa wana nguvu zilizo timilifu, ijapokuwa ni wengi, hata hivyo watakatwa, naye atapita na kwenda zake. Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena. 13 Na sasa nitakuvunjia nira yake, nami nitakupasulia mafungo yako. 14 Tena Bwana ametoa amri katika habari zako, ya kwamba asipandwe tena mtu awaye yote mwenye jina lako; toka nyumba ya miungu yako nitakatilia mbali sanamu ya kuchora, na sanamu ya kuyeyusha; nitakufanyia kaburi lako; kwa maana u mbovu. 15 Tazama, juu ya milima iko miguu yake aletaye habari njema, atangazaye amani. Zishike sikukuu zako, Ee Yuda, uziondoe nadhiri zako; kwa maana yule asiyefaa kitu hatapita kati yako tena kamwe; amekwisha kukatiliwa mbali.

 

Kwa hiyo tunaona hapa kwamba adui hatakuwa jina lake likiendelea kuitiwa tena. Mungu atamwandalia kaburi lake kwa kuwa yeye ni muovu na machukizo. Andiko hili linamhusu Masihi kama tunavyoona kutoka kwenye andiko lifuatalo: Tazama, juu ya milima iko miguu yake aletaye habari njema. Hii ni andiko ka kifumbo kumhusu Masihi inayofuatiw na maandiko ya Isaya na Yeremia.

 

Sura ya 2 ndipo inashughulika na marejesho na kufanywa upya kwa Yakobo kama fahari na utukufu wa Israeli. Sasa Israeli walikwenda utumwani huko Ashuru mwaka 722 KK na kwa hiyo watarejeshwa upya katika Siku za Mwisho ili unabii huu utimie.

 

Nahumu Sura ya 2

Yeye asetaye vipande vipande amepanda juu mbele ya uso wako; zishike silaha, ilinde njia, vitie nguvu viuno vyako, uongeze uwezo wako sana. 2 Kwa maana Bwana anairudisha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli; maana watekao nyara wamewateka, na kuyaharibu matawi ya mizabibu yao. 3 Ngao ya mashujaa wake imefanywa kuwa nyekundu, watu walio hodari wa vita wamevaa nguo nyekundu sana; magari ya vita yametameta kwa chuma cha pua siku ya kujitengeza kwake, na mikuki inatikiswa kwa namna ya kutisha. 4 Magari ya vita yanafanya mshindo njiani, Yanasongana-songana katika njia kuu; Kuonekana kwake ni kama mienge, Yanakwenda upesi kama umeme. 5 Awakumbuka watu wake wenye heshima; Wanajikwaa katika mwendo wao; Wanafanya haraka waende ukutani; Nacho kitu cha kuwafunika kimewekwa tayari. 6 Malango ya mito yamefunguka, na jumba la mfalme limeyeyushwa. 7 Husabu naye amefunuliwa, anachukuliwa, na wajakazi wake wanalia kama kwa sauti ya hua, wakipiga-piga vifua vyao. 8 Lakini Ninawi tokea zamani amekuwa kama ziwa la maji; ila hata sasa wanakimbia; Simameni! Simameni! Lakini hapana hata mmoja atazamaye nyuma. 9 Chukueni nyara za fedha; Chukueni nyara za dhahabu; Kwa maana ni akiba isiyoisha, Fahari ya vyombo vipendezavyo. 10 Amekuwa utupu, na ukiwa, na uharibifu; hata moyo unayeyuka, na magoti yanagongana-gongana; viunoni mwote mna utungu, na nyuso za wote zimekuwa nyeupe kwa hofu. 11 Kao la simba li wapi? Na mahali walishapo wana-simba pa wapi, mahali walipotembea simba mume na simba mke na mwana-simba, wala hapana aliyewatia hofu? 12 Simba alirarua vipande vipande chakula cha kuwatosha watoto wake, aliwasongea wake zake nyama, aliyajaza mapango yake mateka, na makao yake aliyajaza mawindo. 13 Tazama, mimi ni juu yako, asema Bwana wa majeshi, nami nitayateketeza magari yako ya vita katika moshi, na upanga utawala wana-simba wako; nami nitayakatilia mbali mawindo yako katika nchi, na sauti za wajumbe wako hazitasikiwa tena kamwe.

 

Inasihiwa kwamba andiko hili lilieleza na lilitimilika mwaka 612 KK. Hata hivyo Israeli hawakurejeshwa na walikuwa mbali kaskazini ya Araxes na Yuda walikwenda pia utumwani na Hekalu likaharibiwa mwaka 597 KK. Kipindi hiki kiko mbali na siku za mbele na siku nyingi baada ya kuanguka kwa Dola ya Ashuru na mfumo na dini zao na ujio wa Masihi. Kwa sababu hii inakubaliana na Manabii wengine Kumi na Mbilina unahusisha siku za Mwisho.

 

Nahumu Sura ya 3

Ole wake mji wa damu! Umejaa mambo ya uongo na unyang'anyi; mateka hayaondoki. 2 Kelele za mjeledi, kelele za magurudumu yafanyayo kishindo; na farasi wenye kupara-para, na magari ya vita yenye kuruka-ruka; 3 mpanda farasi akipanda, na upanga ukimeta-meta, na mkuki ukimemetuka; na wingi wa waliouawa, na chungu kubwa ya mizoga; mizoga haina mwisho; wanajikwaa juu ya mizoga yao. 4 Kwa sababu ya wingi wa ukahaba wa yule kahaba mzuri, yule bibi wa mambo ya uchawi, auzaye mataifa kwa ukahaba wake, na jamaa za watu kwa uchawi wake. 5 Tazama, mimi ni juu yako, asema Bwana wa majeshi; nami nitafunua marinda yako mbele ya uso wako; nami nitawaonyesha mataifa uchi wako, na falme aibu yako. 6 Nami nitatupa uchafu uchukizao juu yako, kukufanya uwe mchafu, nami nitakufanya kuwa kitu cha kutazamwa kwa dharau. 7 Hata itakuwa, wote wakutazamao watakukimbia, wakisema, Ninawi umeharibika; ni nani atakayeuhurumia? Nikutafutie wapi wafariji? 8 Je! Wewe u mwema kuliko No-amoni, uliowekwa kati ya mito, uliozungukwa na maji; ambao boma lake lilikuwa bahari, na bahari ilikuwa ukuta wake. 9 Kushi na Misri walikuwa nguvu zake, nazo zilikuwa hazina mpaka; Putu na Walibia walikuwa wasaidizi wake. 10 Hata hivyo alichukuliwa mbali, alikwenda utumwani; watoto wake wachanga walisetwa kwenye maachano ya njia kuu zote; watu wake wenye heshima wakapigiwa kura, na wakuu wake wote wakafungwa kwa minyororo. 11 Tena utalewa, utafichwa; tena utatafuta ngome kwa sababu ya adui. 12 Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva kwanza; ikitikisika zaanguka katika kinywa chake alaye. 13 Tazama, watu wako walio ndani yako ni wanawake; malango ya nchi yako yamekuwa wazi kabisa mbele ya adui zako; moto umeteketeza mapingo yako. 14 Teka maji yawe tayari kwa kuzingirwa kwako; Zitie nguvu ngome zako; Ingia katika udongo, yakanyage matope, Itie nguvu tanuru ya kuokea matofali. 15 Huko moto utakuteketeza; Upanga utakukatilia mbali; Utakumeza kama tunutu alavyo; Jifanye kuwa wengi kama tunutu! Jifanye kuwa wengi kama nzige! 16 Umeongeza wafanya biashara wako kuwa wengi kuliko nyota za mbinguni; tunutu huharibu; kisha huruka juu na kwenda zake. 17 Watu wako waliotiwa taji ni kama nzige, na majemadari wako ni kama makundi ya mapanzi, watuao katika vitalu siku ya baridi, lakini jua lipandapo huruka juu na kwenda zao, na mahali pao walipo hapajulikani. 18 Wachungaji wako wanalala usingizi, Ee mfalme wa Ashuru; watu wako wenye heshima wamepumzika; watu wako wametawanyika juu ya milima, wala hapana mtu wa kuwakusanya. 19 Jeraha yako haipunguziki; jeraha yako ni nzito sana; wote wasikiao habari zako wapiga makofi juu yako; kwa maana ni nani ambaye uovu wako haukupita juu yake daima?

 

Mataifa walifurahi kwa kuwa walikuwa wametaabika wote kutoka na maovu yake yasiyokoma na kwamba yangeendelea hata kama walikuwa wameondolewa na kukimbilia milimani. Nguvu zao zilikuwa zimepunguzwa na Wababeloni na wakawa ni sehemu Dola mojawapo ya zile Saba na ya Nane iliyotabiriwa na nabii Danieli sura ya 2 na unabii wa Danieli.

 

                                                            q