Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[295]

 

 

 

 

Lea na Raheli

 

(Toleo La 1.0 20060611-20060611)

 

Lea na Raheli wanakuwa ni mfano wa uhusiano wa Kristo na taifa lililoko la Israeli na Israeli ya Kiroho, makundi yote mawili yakiwa ni taifa linaloonekana kimwili na hili la kiroho likiwa ni Kanisa la Mungu.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hakimiliki © 2006 Wade Cox)

(tr. 2012)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Lea na Raheli



Habari ya watu hawa wawili, yaani Lea na Raheli inahusu wanawake wawili ambao hatimaye wote walijikuta wakiwa ni wake wa Yakobo mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu. Hadithi hii ni ya kweli abayo hasa inawahusu wanawake wane yaani, Lea na Raheli, na wajakazi wao wawili, Bilha na Zilpa, ambao pia walikuwa ni mama wa wana wa Yakobo. 

 

Ilimpasa Yakobo abadili jina lake na kuitwa Israeli ambalo maana yake yalikuwa ni “yeye atakayetawala kama El” au kama Mungu. Habari za wanawake hawa na watoto wao waliowazaa ni taswira ya wokovu wa mwanadamu kupitia kwa Masihi. Habari hii imeanzia kwenye sura ya 29 pale Yakobo alipohamia kwenye nchi nyingine, kwa watu wa Mashariki, ili akajitwalie kawa alivyousiwa na wazazi wake.

 

Kila kilichoandikwa na kuonekana kwenye hadithi hii ni mfano unaoashiria kitu fulani kamilifu kutokea baadae. Makundi matatu ya kondoo yannashiria familia kubwa ya Nuhu itakayotokea kwa watoto wake Shemu, Hamu na Yafeti. Dhana ya kondoo na ng’ombe, na usemi unaotumika vinaashiria mambo mawili, anyo ni uhusika na mataifa na wana wa Israeli.

 

Mfano wa jiwe la kisimani unaashiria kwamba maji ya neno la Mungu yalikuwa yaishafungwa, na hufunguliwa lipindi cha jua kuzama tu na kuruhusiwa wayachote manabii peke yao, ambao walikuwa na wajibu wakiwa maka waonaji na watoa habari wa Mungu (pia soma jarida la Waonaji wa Mungu (Na. 184) [The Oracles of God (No. 184)]. Yakobo aawaita kuwa ni ndugu zake asijue kuwa walikuwa ni wa Harani. Tunaona hilo kwenye kitabu cha fasihi cha SHD 2771 charan maanayake ni kuchomwa, yaani ni nchi kame iliyonyauka kwa hasira au mateso. Jina hili la Harani, linahusiana na yule Harani mwana wa Tera, kwa mujibu wa kitabu hiki SHD 2039, ambacho kinatoa maana nyingine ya wapanda milima au wakazi wa milimani (kuna makosa ya kiuchapishaji kwenye kitabu cha fasihi cha Strong’s kwa nambari zake halisi).

 

Kwa hiyo, Yakobo akawauliza kama wanamjua Labani, mwana wa Nahori mjomba wake. Nahori ni jina waliloitwa wote wawili yaani baba yake Tera ambaye ni babu wa Ibrahimu, na pia ni jina la mtoto wa Tera. Kwa mujibu wa kitabu hiki cha (SHD 5152), Nahori maana yake ni mkoromaji kutoka kwenye neno koroma. Labani pia alikuwa ni kaka wa mama yake au mjomba wake (Mwanzo 28:2). Kwa mujibu wa (SHD 3837), Labani maana yake ni mtu mweupe au kitu cheupe (SHD 3837 kutoka kwenye fasiri ya SHD 3835 na 3836).  Harani, mwana wa Tera, na ndugu wa Ibrahimu na Nahori, alikuwa ni baba wa Lutu. Kwa hiyo Yakobo alipelekwa kwenye nchi kaufu ambako ndiko aliwaoa wake zake. Kwa hiyo, wanawake hawa au bibi zake hawa walitokea kwa yeye aliyeanywa mweupe, akiwa kama ni mwana wa mkoromaji. Hoja hapa ni kwamba bibiarusi hawa wanatokea kwa mtu aliyefanywa mweupe, aliyezaliwa kutoka kwa waliolala. Kwa hiyo basi, wokovu ni kwa Wamataifa.

 

Mwanzo 29 inamasema:

Kisha Yakobo akaendelea na safari yake na akafika kwenye nchi za mataifa ya mashariki. 2Huko akaona kisima katika shamba, pamoja na makundi matatu ya kondoo yamelala karibu na kisima hicho kwa sababu walikuwa wanakunywa maji kutoka kwenye kisimani hicho. Jiwe lililokuwa domoni mwa kisima lilikuwa kubwa. 3Wakati kondoo wanapokuwa wamekusanyika hapo, achungaji huvingirisha jiwe hilo kutoka kwenye mdomo wa kisima na kunywesha kondoo. Kisha hulirudisha jiwe mahali pake juu ya mdomo wa kisima. 4Yakobo aliwauliza wachungaji, ‘‘Ndugu zangu, ninyi mmetoka wapi?’’ Wakamjibu, ‘‘Tumetoka Harani.’’5Aliwaambia, ‘‘Je, mnamjua Labani, mjukuu wa Nahori ?’’ Wakamjibu, ‘‘Ndiyo, tunamfahamu.’’ 6Kisha Yakobo akawauliza, ‘‘Je, yeye ni mzima?’’ Wakasema, ‘‘Ndiyo, ni mzima, na hapa yu aja Raheli binti yake akiwa na kondoo.’’ 7Akasema, ‘Tazama, jua bado liko juu, si wakati wa kukusanya kondoo. Nywesheni kondoo na mwarudishe malishoni.’’ 8Walijibu, ‘‘Haiwezekani, mpaka kondoo wote wakusanyike na jiwe liwe limevingirishwa kutoka mdomo wa kisima. Ndipo tutanywesha kondoo.’’

 

Yakoba alirudi kwa Harani ambako ni kwa watu wake mwenyewe na ndiko alikojitwalia mke. Ndivyo ilivyofanyika na Kristo pia kwamba alitumwa kwa watu wake ili amchukue mke. Kisha Yakobo alikwenda kwa Labani ndugu yake. Ndipo Raheli, binti wa Labani alikuja na kundi la mifugo. Kwa mujibu wa (SHD 7354 tangu 7353), Raheli maana yake ni: kufanya safari kama kondoo jike aliye msafiri mwema. Aina hii ya Majike ya kondoo walikuwa maarufu kuwepo kwenye makundi ya kondoo na walimudu safari za mbali malishoni kwa hiyo, kwa mujibu wa SHD 3290; mke waliyechaguliwa na Yakobo ambaye pia ni (mshikilia kisigino au tapeli) ambaye hatimaye alibadilishwa jina lake na kuitwa Israeli (ambaye maana yake ni yeye atakayetawala kama Mungu) alikuwa ni kondoo mke wa kundi lililosafiri kwenda kulishwa neno la Mungu, na familia walioianzisha ingetawala kama Mungu. Israeli anamwakilisha Kristo ambaye alikuja kuchukua mahala pa Shetani aliye Nyota ya Asubuhi.

 

Muda umewekwa kuliko ulivyokuwa hapo kabla jiwe lilipoviringishwa kutoka kwenye mdomo wa kisima. Bila shaka wao wangeweza kufanya hivyo, lakini kwa jinsi ya fumbo inaonekana kuwa tendo hili la kulitoa jiwe kutoka kwenye mlango wa kaburi ndilo lililofanyika wakati wa kufufuka kwa Kristo.

 

Andiko hili linaielezea dhana ya wateule kuwa ni kondoo wa Mungu waliozuiwa na hawawezi kumwagiwa maji hadi walipokusanyika pamoja, na ndipo jiwe lilipoondolewa kutoka modomoni mwa kisima. Kwa kufanya hivyo, Mungu kupitia kwa Kristo, alifanya maji ya Roho Mtakatifu wapewe wateule.

 

 9Alipokuwa akizungumza nao, Raheli akaja pamoja na kondoo wa baba yake, kwa maana alikuwa mchunga kondoo. 10Yakobo alipomwona Raheli binti Labani, ndugu wa mama yake, pamoja na kondoo wa Labani, alikwenda na kulivingirisha jiwe kutoka mdomoni mwa kisima na kuwanywesha kondoo wa mjomba wake. 11Kisha Yakobo akambusu Raheli na akaanza kulia kwa sauti. 12Alikuwa amemwambia Raheli kuwa yeye alikuwa jamaa ya baba yake na kwamba ni mwana wa Rebeka. Basi Raheli alikimbia na kumweleza baba yake. 13Mara Labani aliposikia habari kuhusu Yakobo, mwana wa ndugu yake, aliharakisha kwenda kumlaki. Akamkumbatia na kumbusu halafu akamleta nyumbani kwake, kisha Yakobo akamwambia mambo yote. 14Ndipo Labani akamwambia, ‘‘Wewe ni nyama yangu na damu yangu mwenyewe.’’

 

Andiko hili lililo kwa jinsi ya fumbo linaelezea ukweli wa kwamba Masihi alipaswa kuja na kuanza huduma yake akiwa kwenye (mwezi) wa ke wa thelathini na kwamba huduma yake ile alikuwa anarithi mambo yote mawili yaani Israeli wa kiroho na wa kimwili kuwa bibi arusi wake.

 

Alionyesha uwepo wake kwenye Kanisa la jangwani. Aliwalisha kondoo wachache kabla haujaja wakati wa kuwalisha kondoo wote kutoka kwenye mataifa yote.

 

15Labani akamwambia, ‘‘Kwa vile weweni jamaa yangu, ndiyo unifanyie kazi bila ujira? Niambie ujira wako utakuwa nini.’’ 16Labani alikuwa na binti wawili, binti mkubwa aliitwa Lea na binti mdogo aliitwa Raheli. 17Lea alikuwa na macho dhaifu,[udhaifu wa macho unamaanisha upofu wa kiroho wa Yuda na makabila yasiyoongoka] lakini Raheli alikuwa na umbo la kupendeza na mzuri wa sura. 18Yakobo akampenda Raheli, akamwambia Labani, ‘‘Nitakutimikia kwa miaka saba kwa ajili ya kumpata Raheli binti yako mdogo.’’ 19Labani akasema, ‘‘Ni bora zaidi nikupe Raheli kuliko kumpa mtu mwingine yeyote. Kaa pamoja na mimi hapa.’’

 

Andiko hili linaendelea kwa kutuonyesha kimfano huduma ya Kristo kwa kipindi cha miaka elfo saba ambacho ametumika ili alipate Kanisa la Mungu, na kumkomboa mwanadamu. Hii ndio maana wakilishi ya ile miaka saba. Lengo lake lilikuwa ni hatimaye alipate Kanisa la Mungu la kiroho ambalo litakuwa ni Mji wa Mungu na ndilo lengo la kweli na muhimu kwa watu wote. Ni kipindi hikihiki cha miaka saba ndicho alichotumika ili ampate Lea. Yeye alimpenda Raheli, bali alitakiwa amwoe kwanza Lea ambaye ni mfano wa Israeli wa kimwili. Raheli ni mfano wa Israeli wa kimwili na Uumbaji wa kiroho ulichukua pia miaka elfu saba katika kuumba mambo yote tunayoyaona.

 

20Kwa hiyo Yakobo akatumika miaka saba ili kumpata Raheli, lakini ilionekana kwake kama siku chache tu kwa sababu ya upendo wake kwa Raheli. 21Ndipo Yakobo akamwambia Labani, ‘‘Nipe mke wangu. Muda wangu umekamilika, nami nataka nikutane naye kimwili.’’

 

Hii inashabihiana na Kumbukumbu la Torati 32:8 inapoonyesha kuwa Israeli ni urithi wa Yahova (waeza kuona jambo hili hasa ukisoma tafsiri ya RSV).

 

22Basi Labani akaalika watu wote wa mahali pale na akafanya karamu. 23Lakini ilipofika jioni, akamchukua Lea binti yake akampa Yakobo, naye Yakobo akakutana naye kimwili. 24Naye Labani akamtoa Zilpa mtumishi wake wa kike kuwa mtumishi wa binti yake.

 

Sehemu hii inaelezea udanganyifu wa Yakobo. Ukweli ni kwamba ilimpasa Kristo atumike kwa ajili ya Israeli kwa kipindi cha ziada, na ndipo aipomchukua bibi arusi wake (Kanisa) mara tu baada ya kukomboa Israeli ya kimwili, na kuitengeneza njia ya kuwaokoa mataifa ya wapagani wamataifa. Makundi haya yanawakilishwa na Zilpa na Bilha. Wanawakilisha mchanganyiko wa kundi kubwa la wanaoitwa na kuunganishwa na wote wawili, yaani Israeli wa kimwili na wa kiroho, ambao ni Kanisa.

 

25Kesho yake asubuhi, Yakobo akagundua kuwa amepewa Lea! Basi Yakobo akamwambia Labani, ‘‘Ni jambo gani hili ulilonitendea? Nilikutumikia kwa ajili ya Raheli, Sivyo? Kwa nini umenidanganya?’’ 26Labani akajibu, ‘‘Si desturi yetu kumwoza binti mdogo kabla ya kumwoza binti mkubwa. 27Maliza juma la arusi ya binti huyu, kisha pia nitakupa huyu binti mdogo, kwa kutumika miaka mingine saba.’’ 28Naye Yakobo akafanya hivyo. Akamaliza juma na Lea, kisha Labani akampa Raheli binti yake kuwa mke wake. 29Labani akamtoa Bilha mtumishi wake wa kike kwa Raheli ili kuwa mtumishi wake. 30Pia Yakobo akakutana na Raheli kimwili, naye akampenda Raheli zaidi kuliko Lea. Yakobo akamtumikia Labani kwa miaka mingine saba.

 

Kwenye andiko hili tunaona kwamba dhana ya kwamba Lea alikuwa na matatizo ya matatizo ya macho yake, pia yalikuwa na matatizo pia ya udhaifu wa macho yake. Kwa mtazamo inaweza kumaanisha alikuwa hawezi kuona sawa kama alivykuwa Raheli. Kwa maneno mengine tunaweza kusema kwamba Raheli alikuwa anana vizuri na alikuwa ni mzuri na aliyokuwa amependweza naye, na hiii inamaanishwa kwamba aliweza pia kuona vyema na kusikia na kuelewa. Na aliitwa na Mungu kwa mapenzi yake halisi. Kwa mtazamo huo, tuaweza kusema kwamba mke wa kwanza wa Kristo alikuwa ni taifa la Israeli ambalo linawakilishwa limfano na Lea. Alikuwa hawezi kuona wala kusikia wala kulielewa neno la Mungu kama ilivyoelezwa na manabii. Israeli kama taifa lilikuwa ni bibi arusi, ila aliachika na kutalikiwa kwa ajili ya uzinzi wake alioufanya mara nyingi sana.

 

Israeli ya kiroho, ambayo ni Kanisa, lililetwa na Mungu kwa Kristo kwa kupitia kwa Roho Mtakatifu, na lilitolewa nay eye kama mke wa pili, lakini kwa kweli yeye ndiye aliyekombolewa na Kristo likiwa kama Israeli ya Kiroho tangia mwanzo ulipowekwa msingi wa nchi.

 

Yeye akiwa kama Kanisa, alikuwa ndiye mlengwa wa kweli katika uumbaji kwa mahali pa kwanza. Kanisa lilikuwa ni kitu kilichokusudiwa kiwepo tangu mwanzo hata kabla ya kuwekwa kwa misingi ya hii dunia.

 

Kimsingi, twaweza kusema kwamba Kanisa lilikuwa halina matunda na liliishilia kwa manabii tu ambao ndio walikuwa ni watiwa mafuta wa Mugu. Kwa ajili hiyo lilibakia kuwa tasa.

 

Kwa hiyo, Lea (ambaye alikuwa pia mama wa Yuda) alifanywa kuwa aweze kuzaa wana. Kwa ajili hii Israeli akawa ni taifa lenye kuonekana kimwili, na likazaa taifa na sio Kanisa la Mungu.

 

31BWANA alipoona kwamba Lea hapendwi, akampa watoto, lakini Raheli alikuwa tasa. 32Lea akapata mimba akazaa mwana. Akamwita Reubeni, kwa maana alisema, ‘‘Ni kwa sababuBWANA ameona huzuni yangu. Hakika mume wangu sasa atanipenda.

 

Jina la Rubeni maana yake ni muone mtoto au mtazame mtoto. Inaashiria mwanzo wa Mpango wa Mungu. Mtoto huyu alipata haki yake ya uzaliwa wa kwanza kwa njia ya dhambi. Aliona lakini hakuelewa. Mlolongo wa kusudi la mpango wa Mungu kwanza ni kuona.

 

33Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, ‘‘Kwa sababu BWANA alisikia kwamba sipendwi, amenipa tena huyu mwana.’’ Kwa hiyo akamwita Simeoni

 

Kwa mujibu wa kitabu cha fasiri cha (SHD 8095), neno Simeon maana yake ni kusikia. Limechukuliwa kutoka kwenye neno lililo kwenye kitabu cha SHD 8085 la Shama’ lenye maana ya kusikia kwa umakini na akili sana na utiifu. Walikuwa ni watu katili na walitwanyika kila mahali katika Israeli. Kwa hiyi, mtoto wa kwanza wa Israeli aliona lakini hakuona vema na alisikia lakini hakusikia vema. Jambo la pili ya Mpango wa Mungu ni kusikia na kutii.

 

34Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, ‘‘Sasa afadhali mume wangu ataambatana na mimi, kwa sababu nimemzalia wana watatu.’’ Kwa hiyo akamwita Lawi.

 

Kwa mujibu wa (SHD 3878) jina la Lawi maanayake ni kitu kilichounganishwa au kuambatanishwa. Kwa kuona na kusikia kwetu ndipo tunaungana na Bwana.

 

35Akapata tena mimba, naye alipozaa mwana, akasema, ‘‘Wakati huu nitamsifu BWANA.’’ Kwa hiyo akamwita Yuda. Kisha akaacha kuzaa watoto.

 

Kwahiyo tunaona kwamba mzaliwa wa kwanza Rubeni alikuwa ni mtu mzuri na mwenye akili sana na mtukutu, lakini alikuwa laini kama maji.

 

Mtoto wa pili, Smoni alikuwa ni mkatili. Lawi alikuwa ni mkatili pia lakini aliaminiwa na kupewa kazi ya ukuhani na kazi ya kuua wanyama wa dhabihu waliotolewa wa.

 

Baada ya kumzaa Yuda motto wake wa nne, aliacha kuzaa watoto kwa wakati ule.

 

Jina Yuda maana yake ni sifa. Kwa hiyo, mlolongo huu ilikuwa ni kuona na kutii, na kisha kuunganishwa na Bwana na hatimaye kujitoa ili kumsifu Mungu. Tunafanya hivyo tukiwa kama ni sehemu ya wateule wa Israeli, ambao ni taifa, na Kanisa la Mungu.

 

Kwa hiyo Raheli alijisikia unyonge kwa kuwa alikuwa ni tasa na angekufa kama asingezaa watoto. Lakini ilikuwa ni Mungu ndiye aliyeweka majira ambayo Raheli alichukua mimba na kuzaa watoto, ni sawa kama ilivyokuwa ni yeye Mungu alivyopanga na kuamua ni kipindi gani na siku gani ambacho Kanisa lingeanza tangia ubatizo wa kwanza na kipawa cha Roho Mtakatifu kupitia kwenye utii na kazi aliyoifanya.

 

Mwanzo 30 inasema:

Raheli alipoona hamzalii Yakobo watoto, akamwonea ndugu yake wivu. Hivyo akamwambia Yakobo, ‘‘Nipe watoto, la sivyo nitakufa!’’ 2Yakobo akamkasirikia akamwambia, ‘‘Je, mimi ni badala ya Mungu, ambaye amekuzuia usizae watoto?’’ 3Ndipo Raheli akamwambia, ‘‘Hapa yupo Bilha, mtumishi wangu wa kike. Kutana naye kimwili ili aweze kunizalia watoto na kwa kupitia yeye mimi pia niweze kuwa na uzao.’’ 4Hivyo Raheli akampa Yakobo Bilha awe mke wake. Yakobo akakutana naye kimwili, 5akapata mimba naye akamzalia mwana. 6Ndipo Raheli akasema, “Mungu amenipatia haki yangu, amesikiliza maombi yangu na kunipa mwana.’’ Kwa sababu hiyo akamwita Dani.

 

Mtoto wa kwanza aliyezaliwa na mjakazi wa Raheli aliyeitwa bilha alikuwa Dani, jina ambalo maana yake ni hakimu au mwamuzi, ambaye alizaliwa kuwa ni hakimu au mwamuzi wa Israeli kwa haki yake ya kuzaliwa. Kanisa lilihubiri pia kwa Wamataifa. Dani aliwakilisha hukumu ya kimeili ya taifa kama sehemu ya haki yake ya uzaliwa wa kwanza. Kisha ilipaswa iendelee hadi kwenye hukumu iliyopewa Kanisa kama tutakavyoona hapo chini.

 

Mtoto wa pili aliozaliwa na Bilha alikuwa Naftali, ambaye kwa mujibu wa fasiri ya (SHD 5321) maana yake ni mashindano yangu. Alishinda kwa kuzaliwa kwake huku.

 

7Bilha mtumishi wa kike wa Raheli akapata mimba tena akamzalia Yakobo mwana wa pili. 8Ndipo Raheli akasema, ‘‘Nilikuwa na mashindano makubwa na ndugu yangu, nami nimeshinda.’’ Kwa hiyo akamwita Naftali

 

Lengo lake hapa ni hukumu na kuishindania imani na kuanzisha Kanisa la Mungu.

 

Hatimaye Lea akamruhusu tena Zilpa alale ya Yakobo kwa kuwa alikuwa amesimama kuzaa watoto.

 

9Lea alipoona kuwa amekoma kuzaa watoto, alimchukua mtumishi wake wa kike Zilpa naye akampa Yakobo awe mke wake. 10Mtumishi wa Lea yaani Zilpa, akamzalia Yakobo mwana. 11Ndipo Lea akasema, “Hii ni bahati nzuri iliyoje!’’ Kwa hiyo akamwita Gadi.

 

Kwa mujibu wa kitabu cha fasiri cha (SHD 1410), jina Gadi maanayake ni jeshi au mwanajeshi. Ni neno linalotokana na lile la kwenye kitabu cha fasiri namba 1464 la “goode” ambalo maana yake ni kushambulia au kushinda.

 

Kwahiyo, Zilpa akamzalia Yakobo mtoto mwingine na akamwita jina lake Asheri. Kila mtoto miongoni mwa hawa wote alipewa haki ya uana bila upendeleo au kubaguliwa. Hii ni sawa na tabia za Mungu kuwa yeye hana upendeleo (soma jarida la Kumpendelea Mtu (Na. 221) [Respect of Persons (No. 221)].

 

Kwa mujibu wa kitabu hiki cha (SHD 836), Asheri maana yake ni aliyebarikiwa, na kwenye nambari 833 ya kitabu hiki inamaana kunjooka au kuwasawa, au kuwa mkweli na kwenda moja kwa moja kwenye mafanikio.

 

12Mtumishi wa kike wa Lea akamzalia Yakobo mwana wa pili. 13Ndipo Lea aliposema, “Jinsi gani nilivyo na furaha! Wanawake wataniita furaha.’’ Kwa hiyo akamwita Asheric.

 

Dhana hapa ni kushinda na kufanikiwa. Inapelekea kwenye wongofu wa taifa la Israeli na kuongezeka na kuendelea hadi mwishoni mwa kusudio lililoko kwenye Siku za Mwisho.

 

14Wakati wa kuvuna ngano, Reubeni akaenda shambani akakuta tunguja, ambazo alizileta kwa Lea mama yake. Raheli akamwambia Lea, “Tafadhali nakuomba unipe baadhi ya tunguja za mwanao.” 15Lakini Lea akamwambia, “Haikukutosha kumtwaa mume wangu? Je, utachukua na tunguja za mwanangu pia?’’ Raheli akasema, ‘‘Vema sana.’’ Yakobo atakutana nawe kimwili leo usiku, kwa malipo ya tunguja za mwanao.’’ 16Kwa hiyo Yakobo alipokuja kutoka shambani jioni ile, Lea akaenda kumlaki, akamwambia, ‘‘Lazima ukutane nami kimwili. Nimekukodisha kwa tunguja za mwanangu.’’ Kwa hiyo akakutana naye kimwili usiku ule.

 

Hili ni jambola msingi kwa vile tunavyoona madawa ya kuongeza nguvu yanavyotumiwa kama kifaa cha kuwekea uzani au kufikia tamati. Madai yaliyoko ni kwamba matumizi ya madawa haya ya kuongeza nguvu husababisha uzao mwingi na kuchochea ngono. Kanisa linaangalia na kuona jinsi ya kuwachukua hawa waliopotoshwa na kukengeushwa na walioshindwa kuzaa matunda na kuzaa na kuongezeka, wakati Mungu ndiye anayewezesha watu kuzaa na kuongezeka.

 

17Mungu akamsikiliza Lea, naye akapata mimba akamzalia Yakobo mwana wa tano. 18Ndipo Lea akasema, “Mungu amenizawadia kwa kumpa mume wangu mtumishi wangu wa kike.” Kwa hiyo akamwita Isakari

 

Kwa mujibu wa kitabu cha (SHD 3485), Isakari maana yake ni ataleta zawadi au thawabu.

 

Mlolongo mzima unaendana na tendo la kuona na kusikia na kutii na kuungana na Bwana na kumsifu. Na kwa kupitia vipindi vya hukumu na juhudi na ndipo tunaongezeka na kisha tunashinda kwa kushindana kama mieleka na adui wetu. Tunaanza kwanza kwa kushinda na kisha tunabarikiwa, tukiwa ni wamnifu na tabia za ukweli na uwazi. Na kisha tutapata dhawabu.

 

19Lea akapata mimba tena akamzalia Yakobo mwana wa sita. 20Ndipo Lea aliposema, “Mungu amenizawadia kwa zawadi ya thamani sana. Wakati huu mume wangu ataniheshimu kwa sababu nimemzalia wana sita.’’ Kwa hiyo akamwita Zabuloni

 

Kwa mujibu wa fasiri za (SHD 2074) jina Zabuloni maana yake ni makazi. Mojawapo ya thawabu tutakayopewa ni kuwa na sehemu kwenye Hekalu la Mungu kuwa ni makao yetu. Tangu hapo Kanisa litaendelea na mchakato wa hukumu kama jeshi la kiroho. Kwa mujibu wa fasiri za (SHD 1783), Dina jina la mtoto wa kike linaloweza pia kuandikwa Diyn au Doon na kwa mujibu wa (SHD 1779), ni kama hukumu au dhiki ya wateule, na inawakilisha hukumu inayolipata Kanisa likiwa kama Mwili wa Kristo, ambayo ni.

 

21Baadaye akamzaa mtoto wa kike akamwita Dina.

 

Hali hii inatoa tafsiri ya kubadilisha kwa hali ya Kanisa na kutukuzwa kwake.

 

Kwa hiyo, alikuwa na watoto wanaume sita aliowazaa mwenyewe na watoto wanaume wengine wawili aliomzalia kupitia kwa suria wake. Kwahiyo, alikuwa na jumla ya wana wakiume nane na hawa wanafanya idadi ya theluthi mbili za taifa hili lote.

 

Hii pia ni idadi ya wastani kwa wateule. Theluthi mbili ya watu waliobakia waaminifu na watii kwa Mungu na theluthi moja ni ya wake walioasi ambao wanapaswa kuokolowa.

 

22Ndipo Mungu akamkumbuka Raheli, akasikia maombi yake na akafungua tumbo lake. 23Akapata mimba na akamzaa mwana na kusema, “Mungu ameniondolea aibu yangu.’’ 24Akamwita Yosefug na kusema, “BWANA na anipe mwana mwingine.’’

 

Kisha Raheli akamzaa Yusufu, ambaye kwa mujibu wa (SHD 3130), jina lake lina maana ya mwache aongeze ambayo huenda inaweza kuwa na maana ya kuongeza. Hatua hii inaepelekea kuondoka kwa Yakobo na alipenda amwache Labani na kurudi kwenye nchi yake. Hii inaonyesha mwisho wa kipindi cha utimilifu wa mataifa na ashirio la kuanzishwa kwa ufalme kwenye Nchi Takatifu.

 

Raheli alikuwa ameshamzaa tayari mtoto wake wa kwanza wa kiume ambaye siku moja atawaongoza Israeli. Mtoto wake wa pili wakiume alikuwa Benyamini ambaye kwa mujibu wa fasiri za (SHD 1144), jina lake linamaana ya Mwana wa Mkono wa kuume, na aliangalia mbele akilitazama Kanisa kama lilivyoanzishwa na Kristo kwa utukufu likitawala kutoka Yerusalemu. Lile kabila lililochipuka kutoka kwake liliongezeka kutoka kwa wanawake wa makabila mengine, na kuwa pamoja na wateule walioko huko Israeli walio kama taifa. Kwa kawaida wako kwenye mrengo wa kushoto na jambo hili linaashiria pia wongofu wa Israeli kutoka kwenye hali ya kimwili na kuwa kwenye hali ya kiroho, na kubadilishwa na kuwa wana wa Mungu.

 

Ukweli wa habari hii unaonekana kuelekea kwenye uanzishwaji wa ufalme wa kipindi cha milenia kitakachowajumuisha wale wote walioitwa kwenye ufalme ule pia.

 

25Baada ya Raheli kumzaa Yosefu, Yakobo akamwambia Labani, “Nipe ruhusa nirudi katika nchi yangu. 26Nipe wake zangu na watoto, ambao nimetumika kuwapata, nami niende zangu. Unajua ni kazi kiasi gani ambayo nimekufanyia.’’ 27Lakini Labani akamwambia, ‘‘Ikiwa nimepata kibali machoni pako, tafadhali ukae. Nimegundua kwa njia ya uaguzi kwamba BWANA amenibariki kwa sababu yako.’’

 

Mungu hulibariki taifa kwa ajili yetu, na wale wanaolibariki Kanisa wanabarikiwa pia, kama tunavyoona mfano wa kondoo na mbuzi. Ongezeko la Kanisa linaathiriwa na Mungu katika Siku za Mwisho kwa idadi ya miujiza kama tunavyokwenda kujionea.

 

Andiko hiili la pili linaelezea kuitwa kwa wateule wa Mungu. Mungu hutumia vitu vilivyodhaifu ili kuvishinda vile vyenye nguvu. Shetani ni mshitaki wa wateulle, anatushitakia usiku na mchana. Lakini Mungu anashughulika na wale wote anaowashitakia na kuwafanya weupe wanapokuwa ndani ya Yesu Kristo.

 

Tunaona hapa kwamba Kristo anapewa wale wote waliokuwa wanachukiwa na.kushutumiwa.

 

Kwa ajili hiyo, wateule wanaongezwa na kuongezeka wakiwa kama ni warithi pamoja na Kristo, ambaye ni Mwili wa Kanisa.

 

28Akaongeza kumwambia, ‘‘Taja ujira wako nami nitakulipa.’’ 29Yakobo akamwambia, ‘‘Unajua jinsi ambavyo nimekutumikia na jinsi ambavyo wanyama wako walivyolishwa vizuri chini ya uangalizi wangu. 30Kidogo ulichokuwa nacho kabla sijaja kimeongezeka sana, naye BWANA amekubariki popote nilipokuwa. Lakini sasa, ni lini nitashughulikia mambo ya nyumba yangu mwenyewe?’’

 

Kwa ajili hii, sisi tunashughulika na Nyumba ya Mungu na kuwahudumia wale wote wanaotumika ndani yake. Kristo na Kanisa wameitwa kuwa ni zaka na limbuko la mataifa. Kwa hiyo, wamebarikiwa kwa jinsi wanavyotubariki sisi.

 

31Labani akamwuliza, ‘‘Nikupe nini?’’ 32Niruhusu nipite katika makundi yako yote leo niondoe humo kila kondoo mwenye mabakabaka au madoadoa, kila mwana kondoo mweusi na kila mbuzi mwenye madoadoa au mabakabaka. Hawa watakuwa ujira wangu. 33Uadilifu wangu tanishuhudia siku zijazo, kila utakapochunguza ujira ambao umenilipa mimi. Mbuzi ye yote wangu ambaye hana mabakabaka wala madoadoa, au mwanakondoo ambaye si mweusi, atahesabika ameibwa.’’ 34Labani akasema, “Ninakubali na iwe kama ulivyosema.” 35Siku ile ile Yakobo akawaondoa beberu wote waliokuwa na mistari au madoadoa na mbuzi wake wote waliokuwa na mistari au adoadoa (wote waliokuwa na alama nyeupe juu yao) na wanakondoo weusi wote, akawaweka chini ya uangalizi wa wanawe. 36Kisha Labani akamwacha Yakobo kwa mwendo wa safari ya siku tatu kati yake na akobo, wakati Yakobo akiendelea kuchunga lile kundi la Labani lililobaki. 37Hata hivyo, Yakobo, akachukua fito mbichi zilizokatwa wakati huo huo za miti ya mlubna, mlozi na mwaramoni akazibambua ili mistari myeupe ionekane katika fito hizo. 38Kisha akaweka fito alizozibambua kwenye mabirika yote ya nyweshea mifugo, ili ziwe mbele ya makundi walipokuja kunywa maji. Wanyama walipokuja kunywa maji, hali wakiwa wanahitaji mbegu, 39wakapandwa hizo fito zikiwa mbele yao, wanyama waliopata mimba mbele ya hizo fito, walizaa wanyama wenye mistari, madoadoa na mabakabaka. 40Yakobo kawatenga wadogo wa kundi peke yao, lakini akazielekeza nyuso za hao waliobaki kwenye wale wenye mistari na weusi waliokuwa mali ya Labani. Hivyo akatenga makundi yake mwenyewe na wala kuwachanganya na wanyama wa Labani. 41Kila mara wanyama wenye nguvu walipohitaji mbegu, Yakobo aliweka zile fito kwenye mabirika mbele ya hao wanyama, ili wapandwe karibu na hizo fito, 42lakini ikiwa wanyama walikuwa wadhaifu hakuziweka hizo fito. Hivyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani na wanyama wenye nguvu wakawa wa Yakobo. 43Kwa njia hii Yakobo akastawi sana, tena akawa na makundi makubwa, watumishi wa kike na wa kiume na ngamia na punda.

 

Kwa hiyo, wateule wamechukuliwa kutoka kwenye mataifa na wameimarishwa kwenye ushirika na Israeli, ambao ni mwili wa Kristo.

 

Mwanzo 31 inassema:

Yakobo akawasikia wana wa Labani wakisema, ‘‘Yakobo amechukua kila kitu kilichokuwa cha baba yetu naye amepata utajiri huu wote kutokana na vile vilivyokuwa mali ya baba yetu.’’ 2Yakobo akatambua kwamba moyo wa Labani kwake haukuwa kama ulivyokuwa mwanzo. 3Ndipo BWANA akamwambia Yakobo, ‘‘Rudi katika nchi ya baba zako na kwa watu wako, nami nitakuwa pamoja nawe.’’ 4Hivyo Yakobo akatuma ujumbe kwa Raheli na Lea waje machungani yalikokuwa makundi yake. 5Akawaambia, ‘‘Naona moyo wa baba yenu kwangu sivyo kama ulivyokuwa mwanzoni, lakini Mungu wa baba yangu amekuwa pamoja nami. 6Mnajua kwamba nimemtumikia baba yenu kwa nguvu zangu zote, 7hata hivyo baba yenu amenidanganya kwa kubadilisha ujira wangu mara kumi. Hata hivyo, Mungu hakumruhusu kunidhuru. 8Kama alisema, ‘Wenye madoadoa watakuwa ujira wako,’ basi makundi yote yalizaa wenye madoadoa, kama alisema, ‘Wenye mistari watakuwa ujira wako,’ ‘basi makundi yote yalizaa wenye mistari. 9Hivyo Mungu amechukua mifugo ya baba yenu na amenipa mimi.

 

Mungu anaingilia kati kwa kuanzisha mpango wake wa wokovu. Anampa Kristo wale wato aliowajua tangu mwanzo, anawachagua na kuwaita. Wote hawa amempa Kristo na kisha wamehesabiwa haki na kutukuzwa. Mungu anawajulisha wateule wake kwa.

 

10Wakati fulani majira ya kuzaliana niliota ndoto ambayo niliinua macho na kuona kwamba wale abeberu waliokuwa wakipanda kundi walikuwa wa mistari, madoadoa na mabakabaka. 11Malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, ‘Yakobo.’ nikamjibu, ‘Mimi hapa,’ 12akasema, ‘Inua macho wako uone wale mabeberu wote wanaopanda kundi wana mistari, madoadoa au mabakabaka, kwa maana nimeona yale yote ambayo Labani amekuwa akikutendea. 13Mimi ndiye Mungu wa Betheli, ulikomiminia ile nguzo mafuta na pale mahali uliponiwekea nadhiri. Sasa ondoka katika nchi  hii mara moja urudi katika nchi uliyozaliwa.’’ 14Ndipo Raheli na Lea wakajibu, “Je bado tu tunalo fungu lo lote katika urithi wa nyumba ya baba yetu? 15Je, yeye hatuhesabu sisi kama wageni? Sio kwamba ametuuza tu, bali ametumia hata na vile vilivyolipwa kwa ajili yetu. 16Hakika utajiri wote ambao Mungu ameuchukua kutoka kwa baba yetu ni mali yetu na watoto wetu. Hivyo fanya lo lote lile Mungu alilokuambia.’’

 

Kwa hiyo, urithi wa Kanisa hauhesabiki kwenye mataifa, bali wanahesabiwa kwenye Kanisa la Mungu kama warithi pamoja na Israeli. Kanisa linapaswa kumfuata Kristo. Pia Israeli watarejeshwa na kufanywa upya katika Siku za Mwisho, kwenye uhamisho mkuu uliotabiriwa kwenye Isaya 66:18-20.

 

17Ndipo Yakobo akawapandisha watoto wake na wake zake juu ya ngamia, 18naye akawaswaga wanyama wote mbele yake pamoja na vitu vyote alivyokuwa amechuma huko Padan-Aram kwenda kwa baba yake Isaki katika nchi ya Kanaani. 19Labani alipokuwa amekwenda kukata kondoo wake manyoya, Raheli aliiba miungu ya nyumba ya baba yake. 20Zaidi ya hayo, Yakobo alimdanganya Labani Mwaramu kwa kutokumwambia kwamba anakimbia21Hivyo akakimbia pamoja na vitu vyote alivyokuwa navyo na kuvuka Mto Eufrati akaelekea nchi ya vilima katika Gileadi. 22Siku ya tatu Labani akaambiwa kwamba Yakobo amekimbia. 23Akichukua jamaa zake, akamfuatia Yakobo kwa siku saba na kumkuta kwenye nchi ya vilima katika Gileadi

 

Mungu anakusudia jambo hili litokee kwa wateule na kufanya maamuzi ya maafa yetu. Katika mambo yote Mungu hutenda kazi pamoja na wote wampendao, katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi Lake (Rum. 8:28).

 

24Ndipo Mungu akamjia Labani Mwaramu katika ndoto usiku na kumwambia, “Jihadhari usiseme neno lo lote kwa Yakobo, liwe zuri au baya.’’ 25Yakobo alikuwa amepiga hema lake katika nchi ya vilima katika Gileadi wakati Labani alipomkuta, Labani na jamaa yake wakapiga kambi huko pia. 26Ndipo Labani akamwambia Yakobo, “Umefanya nini? Umenidanganya na umewachukua binti zangu kama mateka katika vita. 27Kwa nini ulikimbia kwa siri na kunidanganya? Kwa nini hukuniambia ili nikuage kwa furaha na nyimbo za matari na vinubi? 28Hata hukuniruhusu niwabusu wajukuu zangu na kuwaaga binti zangu. Umefanya kitu cha kipumbavu. 29Nina uwezo wa kukudhuru, lakini usiku uliopita Mungu wa baba yako alisema nami, ‘Akaniambia, ‘Jihadhari, usiseme neno lolote kwa Yakabo liwe zuri au baya.’ 30Sasa umeondoka kwa sababu umetamani kurudi nyumbani kwa baba yako. Lakini kwa nini umeiba miungu yangu?’’ 31Yakobo akamjibu Labani, “Niliogopa, kwa sababu nilifikiri ungeweza kuninyang'anya binti zako kwa nguvu. 32Lakini kama ukimkuta ye yote aliye na miungu yako, hataishi. Mbele ya jamaa yetu, angalia mwenyewe uone kama kuna cho chote chako hapa nilicho nacho, kama kipo, kichukue.” Basi Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameiba hiyo miungu. 33Kwa hiyo Labani akaingia ndani ya hema la Yakobo na ndani ya hema la Lea na ndani ya hema la watumishi wawili wa kike, lakini hakukuta cho chote. Baadaye alipotoka katika hema la Lea, akaingia hema la Raheli. 34Basi Raheli ndiye aliyekuwa amechukua ile miungu ya nyumbani kwao na kuiweka katika matandiko ya ngamia na kukalia. Labani akatafuta kila mahali kwenye hema lakini hakupata cho chote.

 

Raheli akiwa kama Kanisa, alichukua mali na utajiri wake wote, lakini hakuwa na sehemu kwenye nyumba ya labani. Na ndivyo ilivyo; kwamba ibada za sanamu zinazoliandama Kanisa zimetokana na hali hii ya tamaa na kutoridhika au kupenda kujilimbikizia mali.

 

35Raheli akamwambia baba yake, “Usikasirike, bwana wangu kwa kuwa siwezi kusimama ukiwepo, niko katika hedhi.’’ Labani akatafuta lakini hakuweza kuipata miungu ya nyumbani kwake. 36Yakobo akakasirika na kumshutumu Labani, akisema, “Uhalifu wangu ni nini?’’ Akamwuliza Labani, ‘‘Ni dhambi gani niliyofanya hata unaniwinda? 37Sasa kwa kuwa umepekua vitu vyangu vyote umepata nini kilicho cha nyumbani mwako? Kiweke hapa mbele ya jamaa yako na yangu, nao waamue kati yetu sisi wawili. 38“Mpaka sasa nimekuwa pamoja nawe miaka ishirini. Kondoo wako na mbuzi wako hawajaharibu mimba, wala sijala kondoo waume kutoka katika makundi yako. 39Sikukuletea mfugo aliyeraruliwa na wanyama pori, nilibeba hasara mimi mwenyewe. Tena ulinidai malipo kwa cho chote kilichoibwa mchana au usiku. 40Hii ndiyo iliyokuwa hali yangu: Niliumia kwa joto la mchana na baridi usiku, pia usingizi ulinipaa. 41Ilikuwa hivi kwa miaka ile ishirini niliyokuwa nyumbani kwako. Nilikutumikia miaka ile kumi na minne kwa ajili ya binti zako wawili, miaka sita kwa ajili ya makundi yako, nawe ulibadilisha ujira wangu mara kumi.

 

Mataifa yamekuwa na hali ya kutokuwa waaminifu kila mara kwenye maneno yao na Kanisa limeyumbishwa na neno la Mungu limebadilishwa kila mara pasipo kikomo.

 

42Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Abrahamu na Hofu ya Isaki, hakuwa pamoja nami, hakika ungenifukuza mikono mitupu. Lakini Mungu ameona taabu yangu na kazi ngumu ya mikono yangu, naye usiku uliopita amekukemea.’’ 43Labani akamjibu Yakobo, “Wanawake hawa ni binti zangu, watoto hawa ni watoto wangu na makundi haya ni makundi yangu. Vyote unavyoviona ni vyangu. Lakini hata hivyo ninaweza kufanya nini kuhusu hawa binti zangu, au kuhusu watoto waliowazaa? 44Njoo sasa na tufanye agano, wewe na mimi, na liwe kama shahidi kati yetu.’45Hivyo Yakobo akachukua jiwe akalisimamisha kama nguzo. 46Akawaambia jamaa yake, ‘‘Kusanyeni mawe.’’ Hivyo wakachukua mawe na kuyakusanya yakawa lundo, wakala chakula hapo karibu na hilo lundo. 47Labani akaliita Yegarsahadutha (wana wa kundi la ushuhuda) na Yakobo akaliita Galeedi (shahidi)

 

Maana ni moja na inamaana ya ushahidi.

 

48Labani akasema, ‘‘Lundo hili ni shahidi kati yako na mimi leo.’’ Ndiyo maana likaitwa Galeedi. 49Pia liliitwa Mispa, kwa sababu alisema, “BWANA na aweke ulinzi kati yako na mimi wakati kila mmoja akiwa mbali na mwingine. 50Kama ukiwatenda mabaya binti zangu au ukioa wake wengine zaidi ya binti zangu, hata ingawa hakuna hata mmoja aliye pamoja nasi, kumbuka kwamba Mungu ni shahidi kati yako na mimi.’’ 51Pia Labani akamwambia Yakobo, “Hili ndilo lundo, na hii ndiyo nguzo niliyoisimamisha kati yako na mimi. 52Lundo hili ni shahidi na nguzo hii ni shahidi, kwamba sitavuka lundo hili kuja upande wako kukudhuru, nawe kwamba hutavuka lundo hili na nguzo hii kuja upande wangu kunidhuru. 53Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Nahori, Mungu wa baba zao, aamue kati yetu.’’ Hivyo Yakobo akaapa kwa jina la Hofu ya baba yake Isaki.

 

Mungu Mmoja na Wapekee anajulikana na kukubalika.

 54Yakobo akatoa dhabihu juu ya kilima na akawaalika jamaa zake kula chakula. Baada ya kula, wakalala huko.

 

Dhabihu hii inahusiana na Pasaka na idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu ambayo mataifa yote huila na kuokolewa.

 

55Kesho yake asubuhi na mapema, Labani akawabusu wajukuu zake, binti zake na kuwabariki. Kisha akaondoka akarudi nyumbani.

 

Mgawanyo wa mataifa na wateule kwenye Nchi ya Ahadi utafanyika. Mji wa Yerusalemu utakuwa ni kituo kikuu cha mambo yote ya ibada nay a utawala wa dunia katika siku za mwisho. Mataifa yote yatakuwa na amani. Israeli watabarikiwa na mataifa yote yataibariki Israeli na kuiombea amani.

 

q