Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

 

[CB018]

 

 

 

Naomi na Ruthu

(Toleo La 2.0 20020216-20070202)

 

Kitabu cha Ruthu ni hadithi ya kupendeza sana inayohusika na ujasiri, unyenyekevu, upendo na urafiki katikati ya wanawake wawili. Tutajionea pia kwamba kutoka kwenye hadithi hii kwamba kuna masomo au mafundisho muhimu na maelekezo kwa Wakristo.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki ©  2002, 2007 Christian Churches of God, ed. Wade Cox)

 

 

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Naomi na Ruthu



Tunasoma kwamba Naomi na Ruthu kwenye Kitabu cha Ruthu. Hadithi hii imetokana kipindi ambacho viongozi wa Israeli walikuwa wanaitwa Waamuzi. Kipindi hiki kilikuwa ni kabla ya kile cha wafalme na hakukuwa na wafalme wowote. Naomi alikuwa ni mwanamke wa Kiisraeli wa kabila la Yuda. Ruthi alikuwa ni mwanamke kijana kutoka Moabu. Alikuwa ni Mmataifa (ambaye ni wakutoka taifa linguine) na mgeni miongoni mwa Waisraeli. Habari hii ni muhimu kwenye historia ya Israeli na kwa Mpango wa Mungu.

 

Akiw na mume wake na watoto wake wawili wa kiume, Naomi aliondoka nyumbatni kwake huko Yudea na wakenda kuishi huko Moabu. Familia ilikwenda huko ili kutafuta maisha mazuri kwa kuwa kulikuwa na njaa kali huko Bethelehemu ambalo walikuwa wanaishi hpo kabla (Ruthu 1:1-2). Wakati wana wa Israeli walipokuwa wanamtii Mungu Mmoja Wapekee na wa Kweli walibarikiwa. Lakini wakati walipoiabudu miungu mingine (ya uwongo) waliadhibiwa. Wakati mwingine Mungu aliyaachilia majeshi ya maadui yawashambulie hadi kuwashinda na kuwaibia mazao yao. Wakati mwingine walikosa mvua kabisa ya kuwezesha kukuza mazao wao (Walawi 25). Kwa hiyo, hadithi hii ilikuwa ni wakati ambao watu hawakuwa na hali iliyosawa kwa Mungu.

 

Wamoabu walikuwa ni maadui hapo zamani na Waisraeli na kulikuwa na vita vya mara kwa mara katikati yao. Lakini kwa kipindi hiki Israeli walikuwa katika amani na hawa Wamoabu. Hawa Wamoabu walikuwa ni wa uzao wa Lutu ambaye alikuwa ni mpwa wake Ibrahimu (Mwanzo 19:30-38). Kwa hiyo kulikuwa na uhusiano wa karibu na wa kindugu kati ya watu hawa wawili. Hata hivyo, hawakuwa wanamuabudu Mungu mmoja na wala hwakuwa kwenye imani au dini moja.

 

Mume wa Naomi aliitwa jina lake Elimeleki na watoto wke wakiume walikuwa ni Maloni na Kilioni. Wakati akiwa huko Moabu, mume wake Naomi alifariki na waoto wake wa kiume wakakua na kuwaoa wnawake wa Kimoabu. Majina yao walikuwa ni Orpa na Ruthu (Ruthu 1:3-4). Israeli walifundishwa kuwa wasiwaoane na watu wa makabila ya kipagani ya Wamataifa wanaoishi karibu nao wakiwazunguka wowote, lakini wanawake wa Kimoabi waliruhusiwa kuwaoa (Kumbukumbu la Torati 7:1-3). Hii ilitokana na kwamba wakati Israeli walipojichanganya na makabila mengine, walijikut wanaabudu miungu mingine ya kipagani ya nchi nyingine. Hata hivyo, hakun mwanaume wa Kimoabi aliyeruhusiwa au kujumuishwa kwenye mkutano wa Mungu. Sababu ya hili inaweza kuonekana kwenye Kumbukumbu la Torati 23:3-4.

 

Miaka kumi baada ya kufariki kwa mume wake Naomi alikabiliwa na kipindi cha huzuni kubwa. Wanawe wote wawili kina Maloni na Kilioni walifariki pia (Ruthu 1:5). Kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kuwa kulikuwa na mlipuko wa ugonjwa kwenye familia yake na Mungu aliruhusu wanaume hawa wafariki ili wasiweze kuendeleza maambukizo ya ugonjwa huu kwa vizazi vijavyo. Huko mbeleni kwenye hadithi hii tutajionea kwamba siku za mbeleni watu wawili muhimu kwenye mstari wa kiuzao wa Yuda watazaliwa na Ruthu. Hata hivyo, hakuna mtoto aliyezaliwa na yeyote kati ya watoto hawa wa Naomi kabla ya kufariki kwao.

 

Wakati akiwa huko Moabu, Naomi hakuwa anaabudu miungu migeni ya Wamoabu. Alibakia kuwa mwaminifu kwenye imani yake mwenyewe. Kwa kipindi kirefu na kwa kupitia mfano wake mzuri, Naomi aliweza kuwafundisha wakamwanaze kuhusu imani yake. Kwa kuishika kwake Torati na amri ningine za Mungu na kwa kujiepusha kwake kuiabudu miungu ya kigeni ya nchi za mataifa, Naomi alikuwa ni shuhuda wa Mungu wa Pekee na wa Kweli. Hakujali kuwa wa tofauti na ni kama tulivyo sisi tulio kwenye Kanisa la Mungu leo.

 

Wakati Naomi alipogundua kwamba ile njaa kali iliyoikumba Yudea imekwisha, aliamua kurudi nyumbani. Alitaka kuwa pamoja na watu wake mwenyewe waliokuwa wanaabudu na kumuamini imani sawa kama aliyokuwanayo yeye. Pia kwa kuwa familia yake yote ilikuwa imekufa kwa hiyo hakukuwa na sababu kwa yeye kuendelea kukaa zaidi huko Moabu. Naomi alikuwa bado ana uhusiano wa kifamilia huko nyumbani kwake. Mabinti zake wote wawili ambao walikuwa pia ni wakamwanae waliamua kufuatananaye anaporudi nyumbani kwake ingawaje Naomi alijaribu sana kuongeanao juu ya uamuzi wao huo. Alifanikiwa kumshawishi Orpa lakini Ruthu hakushawishika bado kuendelea kubakia huko Moabu (Ruthu 1:6-15).

 

Ruthu aliweka nadhiri na ahadi ya kwenda pamoja na Naomi na kumkubali Mungu wake na imani yake na jinsi ya kuishi au mtindo wa maisha yake (Ruthu 1:16-18). Hii inamaanisha kwamba alikuwa ameandaliwa kurudi naye nyumbani kwa watu wake na kuachana na miungu yake na imani zao. Hiki siyo kitu rahisi kufanya. Ilimaanisha kwamba angeenda mbali na wazazi wake, kaka zake na dada zake, marafiki zake na mahali alipokulia na kulelewa.

 

Wakristo watuwazima wanatarajiwa kufanya hivi wanapofikia kumjua Mungu Mmoa, Wapekee na Wakweli na Torati yake. Kama watu wazima inatupasa kutubu na kubatizwa katika Mwili wa Kristo, ambao ni Kanisa (Ufalme) wa Mungu. Baada ya kubatizwa haitupasi kurudi nyuma kwa kuyarudia maisha ya dhambi. Inatupasa kujaribu iwezekanavyo kuitii Torati ya Mungu na kuendelea kukua tena na tena katika imani (Warumi 6:1-6; Wakolosai 3:3-10).

 

Ruthu alikuwa ameongoka kikwelikweli. Mungu alimfanya kufikia kuujua na kuuelewa ukweli kupitia Roho wake Mtakatifu kama anavyotufanyia hata sisi leo. Lakini Orpa aliamua kuwa kitendo cha kuondoka na kwenda mbali na nyumbani kwake na kuanza kuishi maisha mapya kingekuwa ni kitendo kigumu kidogo (Ruthu 1:15). Alichagua kuishi pamoja na watu wake mwenyewe na kuendelea kuiabudu miungu ya Wamoabu. Ni sawa tu kama ilivyo kwa Wakristo wanafurahia kumtii Mungu kwa kipindi kifupi, lakini wanapokwazwa na kitu fulani au mtu fulani wanapenda kufanya hivyo, ndipo wanaamua kurudi nyuma na kuzigeukia njia zao za kale za maisha yao ya zamani (soma Luka 9:62). Mungu na Kristo hawawatumii watu wa namna hiyo kuwasaidia kwenye Ufalme.

 

Ndipo Naomi na Ruthu walikwenda Bethlehemu na watu wote walifurahia sana kuwaona. Naomi alikuwa amebadilika sana kiasi kwamba marafiki zake hawakuweza kumtambua kwa mara moja. Alionekana na haiba ya uzee na mwenye huzuni na alikuwa amedhoofika na mwenye mnyong’onyeo mkubwa kwa kuwapoteza watoto wake wakiume na mume wake. Pia alikuwa maskini sana aliyeonekana hohehahe. Lakini marafiki zake wallimtia moyo na wakamwambia kwamba mambo yatakuwa sawa na mazuri tu sasa na kwamba sasa alikuwa nyumbani. Hata kwa mambo haya yote, Naomi alipata mateso na masumbufu wakati alipokuwa huko Moabu hakusimama wala kuacha kumuabudu Mungu wala kuiacha imani yake (Ruthu 1:19-22).

 

Wengi wetu tutapitia mateso ya namna kama haya katika maisha yetu. Wakati mwingine wale tuwapendao wataumwa au kupatwa na magonjwa na kufa na inatufanya tuhuzunike sana. Tunaweza kupatwa na hasira kirahisi na kumchukia Mungu katika vipindi kama hivi na kukata tama kwa kupungukiwa na imani na kurudi nyumbani kama alivyofanya Orpa. Lakini kama tutamtumaini Mungu, ndipo tutapata nguvu zaidi na zaidi kutokana na majaribu yetu. Inatupasa kuishikilia imani na inatupasa kusaidiana kwenye nyati zote ngumu. Kila mtu anahitaji kutiwa moyo kwa wakati na namna fulani.

 

Wote wawili, yaani Naomi na Ruthu walikuwa maskini kwa kuwa walikuwa hawana waume zao wa kuwahudumia. Kwa hiyo iliwapasa kutafuta jinsi ya kujitafutia mahitaji yao wenyewe, hususan chakula cha kutosha kwa ajili ya kukitumia wakati huo huo na kwa siku zilizofuatia mbeleni. Wote wawili walikuwa ni wanawake mahiri na werevu na walikuwa na uwezo wa kujihudumia wao wenyewe. Mara moja tu wakaiona njia ya kufanya hilo.

 

Kuvpura au kuvuna masazo ya mazao au nafaka kilikuwa ni kitu cha kawaida kufanywa na watu maskini katika Israeli. Na haikuwa wizi kufanya hivyo. Kwa mujibu wa Torati, iliagiza kwamba kitu chochote nyua baada ya kuvuna mashambani, kwenye shamba la mizabibu au bustanini kilibakizwa kwa ajili ya kukikusanya na kuvunwa na watu maskini (Walawi 19:9-10). Wajane na wageni waliruhusiwa pia kuvuna. Ni namna ambayo jamii ilikuwa inawahudumia watu maskini. Mungu pia anawatarajia walio matajiri na wenyevingi miongoni mwetu kuwagawia watu maskini.

 

Ruthu alijitoa kwenda kuvuna mavuno kwa minajiri hii kipindi cha majira ya baridi akikusudia apate chakula kwa ajili ya Naomi nay eye mwenyewe. Kwa msaada na neema ya Mungu Ruthu alikwenda kuvuna masalio ya mazao kwenye shamba la Boazi ambaye alikuwa ni ndugu wa marehemu mumewe Naomi. Boazi alikuwa hajaoa na mtu tajiri sana na mwenye kuamini Mungu Mmoja, wa Pekee na wa Kweli. Alinuia kumfanya Ruthu awe salama wakati anapokuwa anavuna masalia ya mazao shambani mwake. Na pia alimpenda na kumzimia sana Ruthu visivyo kawaida (Ruthu 2:1-16).

 

Ruthu alifanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa na akarudisha nyumbani chakula kingi sana. Naomi alipendezwa na akamshauri Ruthu kubakia na kuendelea kuvuna masalia ya mazao ya shambani mwa Boazi na kwamba asiende kwenye shamba lolote linguine. Ruthu akamkubalia na akabakia mle hadi mwishoni mwa mavuno ya shayiri na ngano (Ruthu 2:17-23).

 

Sikukuu za Mungu zinaitwa mavuno pia. Mavuno ya shayiri ni mavuno ya kwanza, yanayovunwa sambamba na majira ya Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu. Mavuno ya ngano yanakuwa wakati wa Pentekoste. Mavuno ya mwisho ni mavuno ya mwisho, yanayofanyika majira ya Sikukuu ya Kukusanya au ya Vibanda. Tutajifunza zaidi kuhusu hilo kwenye jarida la Siku Takatifu za Mungu (Na. CB22).

 

Ni kama vile Ruthu alivyoendelea kuvuna masalio ya mazao hadi mwishoni mwa mavuno, ndivyo pia Wakristo wanapaswa kubakia kwenye Kanisa la Mungu hadi mwishoni mwa mavuno ya Kanisa. Mara tu baada ya kubatizwa kwetu na kuingizwa kwenye Kanisa la Mungu inatupasa kusema hapa na kufanya kazi hadi kazi itakapofikia mwisho na Kristo kurudi. Hatupaswi kuzigeukia njia za dunia za mataifa.

 

Ni jambo linalopendeza kujua kawa ni mmiliki wa mashamba yaliyoandaliwa udongo na kisha kupanda mbegu na kuimwagilia. Lakini wavunaji waliruhusiwa kushiriki kwenye uvunaji mavuno pasipo hata kufanya maandalizi yoyote y kazi. Kazi hizi zote za maandalizi ya udongo, kupanda mbegu na kuvuna mazao kunafanana na kitendo cha kulihubiri Neno la Mungu.

 

Mfano wa mpanzi ulio kwenye Mathayo 13:3-9 unaelezea jambo hili. Hapa Neno la Mungu inaliita “mbegu”. Kristo ndiye anayeuandaa udongo (sisi) kwa hiyo mbegu (Neno la Mungu) liweze kukua maishani mwetu. Hii inajitokeza kwa kipindi kirefu na zaidi sana karibu ianze kipindi ambacho hata hatujaijua. Sio kila mtu anaweza kulielewa Neno la Mungu kwa wakati huu. Mungu amewachagua watu wachache na kumpa Kristo ili wamsaidie kuliandaa Kanisa kwa ajili ya Ufalme wa Mungu. Kristo anafanya kazi kwa maelekezo au mwongozo wa wa Mungu, na sisi tunafanya kazi chini ya maongozi na maelekezo ya Kristo.

 

Kwa hiyo, hebu na tuendelee na hadithi ya Naomi na tujionee kuwa Mungu alikuwa anafanya kazi kwa mujibu sawa na mpango kwenye maisha yake. Pia alijua mengi kuhusu Torati kwa ajili ya kuwalinda wanawake na familia zao. Alimwambia Ruthu amfanye Boazi kujua kwamba alikuwa anataka kuolewa naye. Hii ilihitaji ujasiri mkubwa kwa Ruthu kukifanya kwa kuwa alikuwa ni Mtu wa Mataifa na aliye najisi kwa mujibu wa itikadi ya Waisraeli. Alihesabiwa kuwa duni kuliko hata mtumishi wa Boazi. Lakini ilikuwa ni haki yak echini ya Torati kudai ndoa na ulinzi kutoka kwenye familia ya marehemu mume wake.

 

Ruthu alimpenda na kumheshimu Naomi na alikuwa tayari kumsikiliza mwanamke huyu mtu mzima. Kwa hiyo, kwa maelekezo ya Naomi, chaguo lililokuwa moyoni mwake na aliyemuangukia alikuwa ni Boazi na ndiye ambaye alikwenda kwake kwa kujivuta kimnyato na kulala miguuni mwake. Kisha akaomba kwamba Boazi ndiye atakaye “mfunua vazi lake” na aipeleke juu. Boazi alijua maana ya tendo hilo na alifurahi kuona kuwa Ruthu alimpenda na kumchagua yeye nay eye pia alimpenda. Jambo hili halikuwa dhambi. Jambo hili lingekuwa geni sana kama wanawake wangefanya hivyo leo, lakini ilikuwa ni sesturi ya wakati ule (Ruthu 3:1-10).

 

Inamaanisha tu kwamba Ruthu alikuwa anamuomba Boazi amchukue na kumuweka kwenye himaya yake ya ulinzi ili afanye kazi zake akiwa ni ndugu wa karibu san chini ya Sheria za Kilawi za Kuendeleza ukoo (Ruthu 3:1-18). Alitaka aolewe nay eye ili aendeleze kumzalia mtoto ambaye hatimaye angekuwa ni wa uzao wa marehemu mume wake. Hii ingemuhakikishia pia kwamba yeye pamoja na Naomi wangeweza kuwa na sehemu yao kwenye urithi kwenye kabila la Yuda.

 

Boazi alikuwa na furaha nyingi kuwafanyia hili wanawake hawa. Alikuwa ni ndugu na alikuwa na haki na wajibu wa kisheria kuwasaidia. Alikuwa hajaoa na tajiri sana, lakini alikuwepo ndugu mwingine wa karibu wa Elimeleki ambaye alikuwa na haki ya kwanza ya kudai kumuoa Ruthu kwa mujibu wa Torati. Kwa hiyo jambo hili lilipaswa kushughulikiwa na lipate ufmbuzi wake kwanza (Ruthu 3:11-18).

 

Kwenye jamii zetu leo, mwanamke yuko huru kuolewa tena iwapo kama mume wake atafariki, na ataolewa kwa yeyote ampendaye. Lakini kwenye Israeli ya kale mwanamke aliolewa kwenye kabila la mume wake. Hii inamaana kuwa falimi ya mume wake ilibeba jukumu la kumtunza kwa kipindi chote ambacho atabakia kwenye familia ile. Siku hizo familia ziliishi na kufanya kazi pamoja na kugawana kila walichokuwa nacho. Wanawake hawakwenda mbali nje ya nyumbani kwao ili kutafuta au kufanya kazi huko.

 

Baba alikuwa ni kichwa cha familia. Hii ilikuwa ni pmoja na jukumu la kungalia au kulinda mali pamoja na wanawake walio ndani ya familia. Pia kama mtu yeyote kwenye familia akifa pasipo kuacha mrithi, Torati iliagiza ndugu wa marehemu huyo amuoe mjane aliyefiliwa na huyo mume. Mtoto wa kwanza anyezaliwa kwenye ndoa hiyo ndiye anakuwa mrithi halali wa Yule mwanaume aliyefariki. Hii iliruhusiwa kwa lengo la kuhakikisha kwamba jina lake lisishaulike katika Israeli. Ni jinsi pia ambayo familia zilitumia katika kuwatunza wanawake wajane (Kumbukumbu la Torati 25:5-9).

 

Naomi alikuwa na familia yenye rslimali huko Bethlehemu, ambayo kwayo alitaka kuidai. Kwa hiyo mwanaume ambaye angemuoa Ruthu alipaswa kumkomboa (kumnunua kwa kurudisha kidaiwacho) urithi wa familia ya Naomi. Boazi alisema kuwa angeweza kufanya hivyo, lakini jambo la kwanza alimualika ndugu wa karibu sana ili afanye yampasayo kwanza kwenye familia ya Naomi. Kipindi hiki kil mtu alimjua na kumpenda Ruthu. Waliona jinsi alivyomhudumia mkamwanae na alivyofanya kazi kwa bidii, na kwamba aliamini na kuabudu sawasawa na walivyokuwa wao wote.

 

Boazi akaongea na yule ndugu mwingine kuhusu hali ilivyokuwa na kwamba mtu yule alikuwa amemaanisha kununua ardhi. Boazi akamwambia kuwa kitendo cha kuinunua ardhi kinamaanisha ia kwamba atatakiwa amuoe Ruthu ili amzalie mrithi na atakaye liendeleza jina la Elimeleki, lakini hakuwa tayari kufanya hivyo. Alivua kiatu chake kitendo kilichoashiria kwamba hakupenda kufanya kazi hiyo kwa ajili ya familia ya Elimeleki (Ruthu 4:1-10). Kitendo cha kuvua kiatu kilikuwa ni kama kuweka mkataba ulio kinyume kabisa leo.

 

Ndipo, Boazi na Ruthu waliweza kuoana. Wakazaa mtoto aliyeitwa Obedi. Naomi alimfurahia sana mjukuu wake huyu. Na marafiki zake wakaungana naye kufurahi na wakamwambis kuwa jina lake litakuwa kuu na la kutukuka katika Israeli. Na ndivyo alivyokwa Obedi, kwamba alikuwa ndiye babu yake mfalme Daudi (Ruthu 4:11-22). Pia kuhusu vizazi ishirini na nane baada ya Daudi, Yesu Kristo alizaliwa katika mstari wa uzao wa Yuda (Mathayo 1:7).

 

Yumenena kuhusu mambo yaleyale ambayo Wakristo wanaweza kujifunza kutoka kwenye hadithi hii na kuna mambo mengine mengi tutakayoweza kujifunza baadae huko mbele. Israeli walikuwa ni wateule wake Mungu. Lakini inawezekana kwa kwa Wamataifa (ambao ni wale wanaotokana na taifa linguine lisilo la Israeli) na kufanyika kuwa Israeli wa kiroho. Hii inawezekana tunapogeuka kutokana kwenye ibada za kuiabudu miungu mingine na tunapoanza kumuabudu Mungu wa Pekee na wa Kweli na kuzishika Sheria zake.

 

Tunauona mfano huu kwenye hdithi ya Ruthu, ambaye alikuwa tayari kuziachilia mbali imani zake za kipagani na kuondoka nyumbani kwake, kuwaacha marafiki zake na kuanza kuchukua njia mpya ya uzima pamoja na Naomi. Alijitoa kikamilifu kabisa kumtumikia Mungu wa Pekee na wa Kweli. Sisi sote tunapaswa kuhiyari kufanya hivyo wakati tunapobatizwa na kuitwa kuingia kwenye Kanisa lake Mungu.

 

Kwa kujifunza zaidi na kwa kina kuhusu yaliyjiri kwenye Kitabu cha Ruthu soma jarida la Ruthu (Na. 27).

 

q