Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[A3]

 

                 

 

 

Mwongozo Uliopo wa Kuliendesha Kanisa la CCG

(Toleo La 1.0 20090718-20090718)

 

Ili kuweza kuendana na muundo kamilifu wa Sheria za kibiblia, Mwongozo ufuatao wa Jinsi ya Kuliendesha Kanisa kwa mujibu wa Ktiba ya CCG inatakiwa kutiliwa maanani.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2009 Wade Cox)

(tr. 2014)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Sura ya 1: Shirika




Utangulizi

 

Kanisa la CCG limeweka maongozi yake kwa muundo wa ngazi za kitaifa unaozingatia muundo wa kibiblia kama walivyoelekezwa wana wa Israeli.

 

Kutoka 18:12-27

Yethro mkwewe Musa akamletea Mungu sadaka ya kuteketezwa na dhabihu; na Haruni akaja, na wazee wote wa Israeli, wale chakula pamoja na mkwewe Musa mbele za Mungu. 13 Asubuhi yake Musa akaketi ili awapishie hukumu watu; na hao watu wakasimama kumzunguka Musa tangu asubuhi hata jioni. 14 Mkwewe Musa alipoyaona yote aliyowafanyia watu, akasema, Ni jambo gani hili uwatendealo hao watu? Kwani wewe kuketi hapo peke yako, na watu wote kusimama kwako tangu asubuhi hata jioni? 15 Musa akamwambia mkwewe, Ni kwa sababu watu hunijilia mimi wapate kumwuliza Mungu; 16 wakiwa na neno, hunijilia; nami naamua kati ya mtu na mwenziwe, nami nawajuvisha amri za Mungu, na sheria zake. 17 Mkwewe Musa akamwambia, Jambo hili ufanyalo si jema. 18 Huna budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia; maana jambo hili ni zito mno kwako; huwezi wewe kulitenda peke yako. 19 Sikiza sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe kwa ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao; 20 nawe utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kuifanya. 21 Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi; 22 nao wawaamue watu hawa sikuzote; kisha, kila neno lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno dogo wataliamua wenyewe; basi kwako wewe mwenyewe utapata nafasi zaidi, nao watauchukua huo mzigo pamoja nawe. 23 Kwamba utafanya jambo hili, na Mungu akikuagiza hivyo, basi utaweza kusimama wewe, na watu hawa wote nao watakwenda mahali pao kwa amani. 24 Basi Musa akasikiza neno la mkwewe, akayafanya yote aliyokuwa amemwambia. 25 Musa akawachagua watu wenye uwezo katika Israeli yote, akawaweka wawe vichwa juu ya watu, wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi. 26 Nao wakawaamua watu sikuzote; mashauri magumu wakamletea Musa, lakini kila neno dogo wakaliamua wenyewe. 27 Kisha Musa akaagana na mkwewe; naye akaenda zake, mpaka nchi yake mwenyewe.

 

Tunaona kuchaguliwa kwa viongozi waliotokana na uchaguzi na mapendekezo ya watu, kutoka kwa Musa na maandiko.

 

Kumbukumbu la Torati 1:9-17
Nami wakati ule niliwaambia, nikasema, Siwezi mimi mwenyewe kuwachukua peke yangu. 10 Bwana, Mungu wenu, amewafanya kuwa wengi, nanyi, angalieni, mmekuwa leo mfano wa nyota za mbinguni kwa wingi.11 Bwana, Mungu wa baba zenu, na awafanye kuwa wengi mara elfu kuliko mlivyo, na kuwabarikia, kama alivyowaahidi. 12 Nitachukuaje peke yangu mimi mwenyewe udhia wenu, na mzigo wenu, na mateto yenu? 13 Jitwalieni watu wenye akili na fahamu, watu wanaojulikana, kwa kadiri ya kabila zenu, nami nitawafanya wawe vichwa juu yenu. 14 Nanyi mkanijibu, mkaniambia, Jambo ulilonena ni jema la kufanya. 15 Basi nikatwaa vichwa vya kabila zenu wenye akili, waliojulikana, nikawafanya wawe vichwa juu yenu, maakida ya elfu elfu, na maakida ya mia mia, na maakida ya hamsini hamsini, na maakida ya kumi kumi, na wenye amri, kwa kadiri ya kabila zenu. 16 Nikawaagiza wakati ule waamuzi wenu, nikawaambia, Sikizeni ninyi maneno kati ya ndugu zenu, mkaamue kwa haki kati ya mtu na nduguye, na mgeni aliye pamoja naye. 17 Msitazame nafsi za watu katika hukumu; mwasikize wadogo na wakubwa sawasawa; msiche uso wa mtu awaye yote; kwa kuwa hukumu ni ya Mungu; na lile neno liwashindalo mniletee mimi, nami nitalisikiza.

 

Kwa sababu hii tunawashirikisha wapendwa waumini wetu katika kuwachagua viongozi watakaowaongoza.

 

1.1.

1.1.1. Hii inatokana na mfano wa maandiko matakatifu kwamba kila Halmashauri Kuu ya Taifa kama itaweza kutunga katiba inayoendana na maongozi ya kamati yake ya uongozi, muundo wa kishirika ulio chini ya kiongozi wa maelfu.

 

1.1.2. Kila kundi la hawa elfu linapaswa kuundwa kutokana na muundo wa mgawanyo wa watu mia mia na ulio na vikundi vya hamsinihamsihi na kisha watu kumikumi.

 

1.1.3. Muundo huu wa watu utahusiana na hesabu ya wanaume watu wazima sawasawa na inavyotuambia Biblia kuhusu kuwahesabu wanaume watuwazima wanaozidi umri wa miaka 20.

1.1.4. Wanaume wenye umri wa kati ya miaka 20 hadi 50 wanastahili kuchukua majukumu yote ya kimaongozi kama wataonekana wanafaa kuchukua uongozi na kuhudumu.

 

1.1.5. Wanaume wenye umri wa miaka 50 hadi 70 nanachukuliwa kuwa wanafaa kusaidia kwenye shughuli za kuongoza au kuhudumu kwenye ibada.

 

1.1.6. Hali ya kupatwa na maradhi aua madhara inayothibitishwa na watabibu inaweza kumfanya mtu asihusishwe na mambo ya kihuduma.

 

1.1.7. Wanawake wanajumuishwa pamoja kwa uangalizi wa wanaume kwenye huduma zote zinazowahusu wanawake, na wanaweza kuongezwa kwenye huduma kama wasaidizi tu hasa kwenye huduma za mapishi, masuala yanayohusu usafi na afya za watu, kuangalia nyumba, usafi wa vyakula, mambo yanayohusu wanawake na kuwaelekeza watoto an kuwapa miongozo mbalimbali kama watakavyohitajika na kulingana na jinsi mazingira yatakavyoruhusu.

 

1.2.

1.2.1. Mwenyekiti wa Taifa ni Amirijeshi Mkuu wa kusimamia muundo huu, akisaidiwa na kamati yake.

 

1.2.2. Kila jumla ya watu elfu kama wanavyojulikana na kuitwa ‘eleph au kundi la familia kwa kumaana ya kimaongozi. Neno hili linatokana na neno la Kiebrania linalomaanisha kundi la ng’ome wenye nguvu au maksai au familia na pia ni tarakimu ya 1000. Vikundi hivi kwa kawaida vinaundwa kutoka kwenye wilaya na mijini. Vinapaswa kuitwa kwa majina ya wiiaya ilea ma kata ilea ma na kitu kitakachoweza kutambulisha mahala walipo, mfano kinaweza kuitwa ni Kikundi cha Familia “x”. jedwali linaloonyesha namna ya kupangilia vikundi limeonyshwa hapo chini kwenye ukurasa wa Nyongeza ama Appendix 1. Kwa kweli ni kusanyikon la Maelfu au ni parishi zinazounda mwanzo wa kundi zima lote.

 

1.2.3.1. Kila kikundi kinatakiwa kiwe na mgawanyo wa vikundi vidogovidogo kumi vya vikundi vya familia. Vikundi hivi vitajulikana kama Makanisa ya Mahali Pamoja. Kwa mujibu wa utaratibu huu, kanisa lililo kwenye mgawanyo mdogo litajumuisha wastani wa wanaume wenye uwezo na mwitikio wapatao 100 na familia zao na ni watu wa zamani wa eneo lile. Hili lilijulikana kama la mamia kwa lugha ya kale ya Kianglo-Saxon na hawa Mamia walifanyika kuwa ni chanzo cha kuwepo kwa mfumo Mzima. Hawa “Mia” kimsingi wanamaanisha sawa na parishi na wanachimbuko lake kwa wale mamia walioko kwenye biblia kwenye mwongozo huu

 

1.2.3.2. Wakati kanisa linapokuwa na zaidi ya vikundi vidogovidogo vitatu (kama vile wanaume wenye uwezo zaidi bove 150) kwa kawaida kanisa jipya linatarajiwa lianzishwe kutokana na sehemu ya lile kundi dogo. Kutegemea na eneo, vinginevyo, uwekaji wa kundi hili dogo linaweza kuwa na maeneo la idadi ya wanaume kumi dadi ya kumi ili kuanzisha kanisa jipya. Kundi hlvi dogo la vikundi vitatu linaweza kuundwa kutokana na idadi ya wanaume 100 na 150 na kiongozi anayejulikana kama kamanda wa kundi dogo. Kanisa moja linaweza kujukuisha vikundi hivi vidogovidogo viwili au zaidi kutegemea na umbali wake utakavyokuwa. Kwa sababu hii, Msimamizi au Kamanda wa hawa Mia atamsaidia Kiongozi Mkuu au Kodineta Mkuu. Haipendezi kuona kwamba kundi moja likiwa kubwa sana na linakuwa kivyakevyake au kipekeepekee.

 

1.2.3.3. Kanisa lililo kwenye kundi dogo linakuwa kwenye ukubwa wa wastani unaoweza kuwafanya waandae vizuri sikukuu na kujipikia kama kundi. Kundi la familia la wnaue Elfu Moja ndilo kubwa sana linalojumuisha watu wengine wanaostahili na wenye vifaa vya kupikia waliokusanyika kutoka kwenye vikundi vidogovidogo. Hawa wanaweza kutenganishwa kwenye vikundi vidogovidogo wakati wanaposhiriki mlo kutokana na aina ya vyombo vya kulia vilivyo hata hivyo.

 

1.2.3.4. Mambo yanayohusiana na uadibisho na maongozi yanaweza kushughulikiwa na ngazi hii au yatashughulikiwa kama ni mambo makubwa sana.

 

1.2.3.5. Hawa makamanda ni makodineta wa kanisa pamoja na makamanda wa vikundi wanaojulikana kama makodineta wakubwa.

 

1.2.3.6. Kila kanisa lililo kwenye jumuia ndogo litagawanywa kwa jumuia yenye makundi mawili ya watu hamsini walio chini ya makoodineta wasaidizi.

 

1.2.3.7. Kila jumuia ndogo ya kanisa inatakiwa kuwa na mgawanyo zaidi wa vikundi vidogo vya kumikumi (kwa Kiebrania ehser) wanaume walio chini ya amri ya shemasi kiongozi au ‘acolyte’ shemasi msaidizi aliwa kama mtumishi aliyepitia mafunzo. Msaidizi anaweza kuchaguliwa kama ni msaidizi wa kamanda wa wa jumuia ndogo kutoka kwenye moja ya vikundi hivi. Kundi hili ni kundi la msingi kwa maadhimisho yam lo wa Pasaka katika jioni ya siku ya 15 Abibu, ambao ndio Mwezi wa Kwanza.

 

1.2.3.8. Wanawake walioolewa wanatakiwa kuwatii waume zao kama wanavyomtii Bwana (Waefeso 5:22-24, NIV). Wajane na wanawake wasiiilewa ambao hawaishi na wazazi wao watahudumiwa na mashemasi wa kike wanaotoa ripoti zao kwa viongozi wao au kwenye jumuia ndogondogo na makamanda wa kanisa

 

1.3.1. Maafisa wote wanachaguliwa kwa maelekezo ya Koodineta Mkuu na Kamati ya Halmashauri ya Taifa.

 

1.3.2. Maafisa wote wanatathminiwa tena baada ya kila miaka saba ya kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya Mwaka wa Sabato.

 

1.3.1. Uchaguzi au uteuzi wa wazee wa kanisa na maaskofu unafanywa na Koodineta Mkuu pamoja na jopo la Baraza ya Wazee wa Halmashauri Kuu ya Dunia.

 

Mamlaka ya Juu

1.4.1.1. Kama CCG ilivyo na mataifa yenye jumla wa wafuasi zaidi ya efu ishirini na kwa hiyo inakuwa na zaidi ya migawanyo kumi ya kieneo, itakuwa na ulazima wa kuwaweka pamoja wale walio kwenye maeneo hayo na Makoodineta wa Eneo kwenye kila nchi au jimbo au kwenye eneo husika. Viongozi hawa wasichanganywe na Makoodineta wa Kanda anayeangalia eneo la zaidi ya nchi moja na aliyeteuliwa na Halmashauri Kuu ya Dunia kwa kazi au malengo ya kimisionari.

. 

 

1.4.1.2. Muundo wa kawaida wa baraza kuu umeorodheshwa kwenye maandiko matakatifu.

 

Watu waliokuwa na Daudi wakutegemeka walikuwa elfu sita (1Samweli 23:13).

 

Waliongozwa vizuri na Mashukjaa au Watu wenye Uweza katika Israeli. 

 

Kanisa la CCG lina Halmashauri za Kitaifa zenye watu kumi na wawili. Hawa wanawajibika kwenye maongozi na huduma za kitaifa za makanisa wakiwa chini ya kamanda wao wa taifa.

 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Taifa ana mamlaka ya kiuangalizi na ndiye Kamanda wa hawa Watatu (sawa na isemavyo 2Samweli 23:8-17).

 

Hawa Watatu ni makamanda wa viongozi Watatu wa Kundi la Taifa.

 

Sehemu ya Mia sita ya Komandi Mkuu ya Taifa wapo chini ya mamlaka ya komandi ya Tatu, kwa hiyo ile mia sita inagawanywa kwa makundi Matatu ya Ishiriniishirini (30 x 20 = 600).

 

Kwa hiyo, kila mmoja wa Watatu hawa ni kamanda wa kumi wa Thelathini (1 x 10 x 20 = 200).

 

Watu 600 wanakuwa na uwezo wa kuwa Makapteni wa Mamia na Makapteni wa Maelfu na hatimaye kuwa Makapteni wa Maeneo-jimbo. Kwa hiyo, kila taifa litakalokuwa na uwezo wa kuwa na jeshi kuu la watu 14,400,000 pamoja na makanmanda wao, au linawezakuwa na jumla ya vikundi 100 vikundi vya watu 144,000. Hili ni Jeshi la Mungu litakalokuwepo kwenye marejesho ya ulimwengu mpya chini ya Masihi. Kuna idadi ya migawanyo Maelfu 24 kwenye muundo wa Migawanyo wa Jeshi la Bblia na Migawanyo 200 ya Jeshi la Biblia la migawanyo Mitatu, pamoja na Migawanyo mingine 600 ya Halmashauri iliyo chini ya komandi kwa mazingira mengine yoyote (tazama chati iliyoambatanishwa).

 

Kila mojawapo ya vikundi hivi vitatu vya watu Mia Sita vitakuwa na kiongozi mkuu mmoja aliyechaguliwa kuwa kiongozi wao. Hawa ni wale walio kwenye Kundi la Pili la yale Matatu (2Samweli 23:20-23). Kundi la Tatu la watu 200 liliunda Jeshi la Ulinzi la Daudi. Linaitwa Jeshi la Ulinzi la Mwenyekiti linalotokana na uchaguzi wake hadi Ufufuo wa Kwana wa Wafu.

 

Muundo huu wa hawa Thelathini wameorotheshwa kwenye 2Samweli 23:24-39. Wamwisho kati ya hawa Thelathini alikuwa ni Uria, Mhiti, mume wa Bathsheba, mama wa Sulemani. Ndugu zake wa damu wawatoto wa Bathsheba, wanapatikana kwenye Nyumba ya Daudi hadi hivi leo. Anaweza kuwa wa kundi la nasaba-damu la RxR1 ambalo lilitawanyika baada ya mwaka 900 KK, likiwa na alama za nasaba-damu za R1b na R1a za kundi la kinasaba-damu cha YDNA ni miongoni mwa wa ukoo wa Daudi, na hasa kupitia kwa binti wa Daudi. Wanapatikana kwenye koo za Dayan na Salathiel/Shealtiel hadi leo katika taifa la Israeli. Kwa hiyo ilionekana kuenea kwa kupitia damu za wanawake na uzao uliopitia kwao.

 

2Samweli 23:8-19

Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethia, Mtahkemoni alikuwa ndiye kiongozi wa wale watatu, yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua kwa siku moja. 9Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodaib Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati walipowadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pasi-Daminu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma, 10lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. BWANA akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa. 11Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia. 12Lakini Shama akasimama imara katikati ya shamba. Akatetea na kuwaua Wafilisti, naye BWANA akawapatia ushindi mkubwa. 13Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati ambapo kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi kufika Bonde la Refaimu. 14Wakati huo Daudi alikuwa ndani ya ngome, nao askari walinzi wa ngome wa Wafilisti walikuwa huko Bethlehemu. 15Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti kwamba mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kile kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!’’ 16Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwenye kile kisima kilicho karibu na lango la Bethelemu na kumletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa, badala yake, aliyamimina mbele za BWANA. 17Akasema, “Iwe mbali nami, Ee BWANA , kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao? Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu. 18Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye aliyekuwa kiongozi wa hao watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao watatu. 19Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuwekwa miongoni mwao

 

Tunaona kwamba kulikuwa na kundi la pili la hawa watatu kutoka kwenye aya zinazofuatia za 2Samweli 23:

20Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabzeeli, ambaye alifanya mambo mengi ya ushujaa. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka Shimoni siku kulipokuwa na barafu na kumwuua simba. 21Pia alimwua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumwua kwa mkuki wake mwenyewe. 22Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada, naye pia alikuwa maarufu sawa na wale mashujaa watatu. 23Alipata heshima kubwa zaidi kuliko ye yote wa wale Thelathini, lakini hakuwekwa miongoni mwa wale watatu. Daudi alimweka kuwa kiongozi wa walinzi wake mwenyewe. 24Miongoni mwa wale thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu, Elhana mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu. 25Shama Mharodi, Elika Mharodi, 26Helesi Mpalti, Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, 27Abiezeri kutoka Anathothi, Mebunai Mhushathi, 28Salmoni Mwahohi, Muharai Mnetofathi, 29Heledi mwana wa Baana Mnetofathi, Ithai mwana wa Ribai kutoka Gibea katika Benyamini, 30Benaya Mpirathoni, Hidai kutoka vijito vya Gaashi, 31Abi - Alboni Mwarbathi, Azmawethi Mbarhumi, 32Eliaba Mshaalboni, wana wa Yasheni, Yonathani 33mwana wa Shama Mharari, Ahiamu mwana wa Sharari Mharari, 34Elifeleti mwana wa Ahasbai Mmaakathi, Eliamu mwana wa Ahithofeli Mgiloni, 35Hezro Mkarmeli, Paarai Mwarbi 36Igali mwana wa Nathani kutoka Soba, mwana wa Hagri, 37Seleki Mwaamori, Naharai Mbeerothi, aliyekuwa mchukuzi wa silaha za Yoabu mwana wa Seruya, 38Ira Mwithri, Gerebu Mwithri 39na Uria Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.

 

 

Andiko linaonyesha kwamba 2Samweli 23:20 inawataja ariels wawili au watu wanaofananishwa na samba wa Moabu waliouawa na mmoja wa hawa mashujaa watatu. Hata hivyo, mahala pengine ambapo neno hili limetumika ni kwenye Isaya 29:1,2 ambapo panautaja Mji aliokuwa anaishi Daudi. Jina asilia la mji wa Yerusalemu ni Har-El linalomaanisha milima ya kale ya Wamisri. Neno Ariel linaweza kumaanisha pia kuwa au ni samba wa Mungu kama huenda inavyoonekana hapa au madhabahu ya juu ya Mungu kama ilivyo kwenye Ezekieli 43:15-16.

 

 Muundo huu wa kiuongozi ndio tunaoutarajia kuwa utatumika wakati atakaporudi Masihi na kutawala hapa duniani kwa mamlaka ya Daudi.

 

Miongozo mingine zaidi kuhusu muundo huu ni kama ifuatavyo:

 

1Nyakati27 [1] Hii ni orodha ya watu katika Israeli, vichwa vya nyumba za mababa, makamanda wa maelfu na wa mamia, na wakuu wao waliomtumikia mfalme kwa mambo yote yaliyohusika na vikosi yaliyokuja na kuondoka, mwezi mmoja hadi mwingine kwa mwaka wote, kila kikosi kilikuwa na idadi ya watu elfu ishirini na nne:

 

1Nyakati.28  [1] Daudi aliwakusanya wakuu wote wa Israeli huko Yerusalemu, wakuu wa makabila, wakuu wa vikosi waliomtumikia mfale, makamanda au wakuu wa maelfu, wakuu wa mamia, watumishi walioshughulika na ulinzi wa mali na mifugo ya mfalme na wanawe, pamoja na kasri ya wakuu, watu hodari, na mashujaa wote wa muhula wote.

 

2Nyakati.1 [2] Sulemani akawaambia Israeli wote, kwa wakuu wa maelfu na wa mamia, kwa waamuzi na kwa viongozi wote wa Israeli wote, vichwa vya nyumba za mababa.

 

Kwa hiyo kila kikosi kilipaswa kiundwe na wanaume elfu arobaini na nne.

 

1.4.1.3. Walitakiwa wafundishwe au kuandaliwa kwa kazi na kuhudumu mwezi hadi mwezi, kama vilivyowekwa vikosi kwa mujibu wa biblia.

 

1.4.1.4. Hadi kufikia vikosi ishirini na vinne waliweka makamanda wa maelfu ili wafanye kazi za wakuu wa vikosi pamoja na Maelfu wao. Hawa Elfu hawakuwa na nguvu kamili, bali walipaswa wajengwe na hili kundi la hawa Mamia. Kila mmoja wa hawa Maelfu atatumika kama mtianguvu wa kila komandi ya hivi vikosi. Haawa Maelfu ishirini na nne wanapaswa waundwe kwanza kwenye muundo wa eneo la Kitaifa.

 

Hivi Vikosi kwa ujumla vinaweza kuundwa kwa maana mbili, bali vinaweza kuwa vimeundwa kwa sababu fulani maalumu na Sababu hasa ya kuundwa kwa kila Kikosi ni kwa kutoa huduma za Madawa au Kitabibu na Utoaji Elimu au Uelimishaji.

 

Vyo vikuu vinapaswa pia kuanzishwa vikiwa kama ni kitu tegemezi cha muhimu kwa shughuli za uelimishaji, utabibu na kwa mchakato wa kisayansi ya muundo wa kijamii. Hizi zinaweza pia kuwa na umuhimu wa kuwa ni vyenye kusaidia tu na sio vipaumbele. Wanawake wote wanapaswa kupewa fursa ya elimu. Mafunzo na uelimishaji vinapaswa kuwa ni shughuli endelevu kwa wafanyakazi au wahudumu wa ngazi zote.

 

1.4.1.5. Halmashauri ya Taifa inatakiwa kuwaweka Mahakimu na Mawakili wenye uwezo ili washughulikie masuala ya hukumu na kufanya ufumbuzi wa mabishano na kuanzisha mahakama itakayosikiliza madai au mambo ambayo hayajapatiwa ufumbuzi kwenye Kikundi chao na Eneo lao la Kijimbo. 

 

1.4.1.6. Mahakama Kuu ya Rufaa ni Halmashauri Kuu au Makao Makuu ya Kanisa Ulimwenguni ambayo inajumuisha Wazee waliobobea kuzijua kanuni za kisheria.

 

1.4.1.7. Bodi yote ya Kanisa inapaswa kuuundwa kwa maamuzi ya mchakato wa kimahakama ya Kanisa ambao unapaswa uwe wa mujibu wa sheria za biblia na kanuni zake.

 

1.4.2. Maeneo yanaweza kupangiliwa ndani ya sharika na makoodineta wa majimbo au nchi kama itakavyoonekana inafaa au kwenye muundo wa sehemu nyingine nyingi kadhaa na Makamanda Wasimamizi waliokubalika. Yanweza kuundwa kutoka na eneo lolote la muundo wa Kidivisheni kama mazingira yatakavyolazimika kuwa

 

1.4.3.1. Pale ambapo kuna maeneo matatu ya komandi watatoa ripoti zao moja kwa moja kwa Koodineta wa Taifa. Pale ambapo kuna zaidi ya maeneo matatu ya komandi zinazoundwa kwa divisheni zenye zaidi ya wanaume 24,000. Inatakiwa kuwe na divisheni 24 kwenye eneo maalumu lililogawanywa kwa divisheni mbili maeneo fulani katika nchi. Majimbo yanapaswa kujumuishwa kwa malengo yale. Hawa ni jumla ya watu 576,000 ambao ni wanaume na familia zao kutokana na muudo huu wa jeshi imara na lenye ngivu.

 

1.4.3.2. Kwa hiyo kutaweza sasa kuwa na divisheni mbili iliyokabidhiwa majukumu ya kila wakati na kwenye eneo la masuala ya kidini na kijamii, na watapewa majukumu yote ya kila jambo ambao ni wawili kwa kila mwezi watakaopangiwa sawa miongoni mwa Watatu hadi zitapapoundwa nyingine zaidi ya nane kwenye kila Tatu na kisha zitachukuliwa kama mbili kwa wakati mmoja hadi kufikia kwenye Ishirini ya kila Tatu. Nyingine Maelfu zinaweza kuundwa kama maeneo mengine yatakayoonekana kuna walioongoka baada ya kufikiwa na imani.

 

1.4.4. Pale ambapo kuna zaidi ya divisheni tatu katika lila mgawanyo wa Tatu zinaweza kuundwa na Makamanda wa Kundi na Kundi waliochaguliwa kutoka kwa kila divisheni mbili au zaidi. Mkuu wa hawa Kumi anazisimamia komando zinazoweza kufikia hadi tano hadi Kundi. Kunatalkiwa kuwe na miundombinu ya ziada kusaidia ya wanaume walioko kwenye hawa makamanda wa Makundi ya vikundi vidogovidogo

 

1.4.5. Hawa watatu wanajulikana kama Maafisa wa Huduma-kazi wa Taifa waliopangiwa kusimamia vikundi kadhaa na vitendea kazi vya misaada. Hadi pale shuguli za uongofu itakapokamilika msingi wa muundo wa mataifa utatofautiana kadiri kali ya wongofu inapoendelea na kuwa ni wa dunia nzima.




Mwongozo wa CCG Sura ya 2: Kazi na Huduma

 


Uendeshaji

2.1. Namna za utendaji inatakiwa zifantike sawasawa na zilivyo programu zilizoamuliwa na Halmashauri ya Taifa na kazi za Kimisionari kama zilivyopangwa na kuagizwa na Halmashauri Kuu ya Dunia/ kazi hizo zinaweza kujuisha yafuatayo:

 

2.1.1. Ujenzi wa majengo kwenye maeneo kama ilivyoelekezwa kwa matumizi ya nyumba, shule, hospitali na wanyama wa kufugwa kama ilivyoamuliwa.

 

2.1.2. Ujenzi wa miradi ya mashamba kama ilivyoamuliwa wakiwemo mabwawa ya samaki, miradi ya uvuvi, ufugaji wa kuku, miradi ya kufuga, miradi ya maziwa, matunda na bustani ya mbogamboga.

 

2.1.3. Kununua vifaa au zana za elimu za viwango vyote.

 

2.1.4. Kununua na kutumia vifaa vya utabibu n vya hospitali.

 

2.1.5. Ugawaji na usambazaji wa vifaa vya kupashiana Habari kama ilivyoelekezwa na Halmashauri Kuu ya Dunia na Halmashauri ya Taifa kwa mujibu wa katiba ilivyo. 

 

2.1.6. Kushughulika na kuangalia utendaji kazi wa shughuli za ujenzi na utendaji kazi wa mashine kubwa na vifaa vya kufundishia.

 

2.1.7. Kuendeleza program za ugawaji wa chakula na mavazi.

 

2.1.8. Kushughulika na miradi ya mazao na  uzalishaji wa vifaa vya ujenzi.

 

2.1.9. Kushughulika na usimamizaji wa warsha kwa uzalishaji na utengenezaji wa HIKI kwa mujibu sawa na vifaa vya kuzalishia tena na vya mawasiliano.

 

2.1.10. Kuendesha shughulika za kiusafiri na vifaa vya kila namna.

 

2.1.11. Kuendesha na kutengeneza mashine kubwakubwa na nzitonzito.

 

2.1.12. \kushughulika na kutengeneza mazalia au mimea kwa ajili ya kuzalisha nguvu za umeme, maji na makapi yaliyosazwa na kutokuwa na maana au matumizi au mifereji michafu.

 

Haki

2.2.1. Mnyororo wa kamandi na nidhamu unatakiwa uanzishwe pamoja na mashitaka na ukataji wa rufani kwa kila ngazi.

 

2.2.2. Mahakama ya usuluishi yanatakiwa yafanye kwa kufuata mujibu wa katiba.

 

2.2.3. Ikiwezekana, idara ya sheria inatakiwa iendelezwe na kufundishwa.

 

2.2.4. Pale ambapo kanisa la CCG litakuwa limeshika hatamu kwenye majimbo lote, mahakimu watabidi wawekwe na kama itawezekana na waumini wa CCG.

 

Mahitaji

2.3.1. Kila halmashauri ya kitaifa inawajibika katika kujihudumia kwa mahitaji yake.

 

Ulinzi na Usalama

2.4.1. Kila kikundi kinawajibika katika kuwalinda na kuwapa usalama watu wake na kanisa lao na kanisa linawjibika kuhakikisha kuwa ulinzi imara na usalama unakuwepo kwenye nchi yao.

 

Mafunzo

2.5.1. Kila halmashauri ya taifa ya CCG inapaswa kuwachagua na kuwapa mafunzo watu wake kwa kadri iwezekanavyo.

 

2.5.2. Uwezo wa mkufunzi unapaswa ujaribiwe katika kumudu mafunso ya ufundi yaliyotolewa kama msaada kwenye ngazi ya juu sana iwezekanavyo.

 

2.5.3. Wanawake wanapaswa kuelimishwa kadri iwezekanavyo na wana fursa ya namna moja ya kupata elimu kama waliyonayo wanaume.

 

2.5.4. Maeneo ya Kitaifa ya CCG wanapaswa watumie uwezo wao wa uzalishaji mali katika kujenga taasisi au vyuo vya mafunzo na kununua vifaa vya elimu. Majengo haya yanaweza kutumika kwa matumizi aina mbili yakiwemo ya kuyatumia kama majengo ya makanisa kwa kuwa hayatatumika sikn za Sabaro, Mwandamo wa Mwezi Mpyana siku za Sikukuu zilizoamriwa.

 

2.5.5. Mafunzo yanapaswa kujumuisha mambo yote yanayohusu ufundi wa umeme, umakanika sambamba na ujuzi ama uhandisi wa kujenga, pamoja na useremala na ufundibomba na aina nyingine zote za ufundi wa mikono, pamoja na namna zote za utoaji wa elimu ya juu.

 

 




Mwongozo wa CCG Sura ya 2: Kazi na Huduma

 


Uendeshaji

2.1. Namna za utendaji inatakiwa zifantike sawasawa na zilivyo programu zilizoamuliwa na Halmashauri ya Taifa na kazi za Kimisionari kama zilivyopangwa na kuagizwa na Halmashauri Kuu ya Dunia/ kazi hizo zinaweza kujuisha yafuatayo:

 

2.1.1. Ujenzi wa majengo kwenye maeneo kama ilivyoelekezwa kwa matumizi ya nyumba, shule, hospitali na wanyama wa kufugwa kama ilivyoamuliwa.

 

2.1.2. Ujenzi wa miradi ya mashamba kama ilivyoamuliwa wakiwemo mabwawa ya samaki, miradi ya uvuvi, ufugaji wa kuku, miradi ya kufuga, miradi ya maziwa, matunda na bustani ya mbogamboga.

 

2.1.3. Kununua vifaa au zana za elimu za viwango vyote.

 

2.1.4. Kununua na kutumia vifaa vya utabibu n vya hospitali.

 

2.1.5. Ugawaji na usambazaji wa vifaa vya kupashiana Habari kama ilivyoelekezwa na Halmashauri Kuu ya Dunia na Halmashauri ya Taifa kwa mujibu wa katiba ilivyo. 

 

2.1.6. Kushughulika na kuangalia utendaji kazi wa shughuli za ujenzi na utendaji kazi wa mashine kubwa na vifaa vya kufundishia.

 

2.1.7. Kuendeleza program za ugawaji wa chakula na mavazi.

 

2.1.8. Kushughulika na miradi ya mazao na  uzalishaji wa vifaa vya ujenzi.

 

2.1.9. Kushughulika na usimamizaji wa warsha kwa uzalishaji na utengenezaji wa HIKI kwa mujibu sawa na vifaa vya kuzalishia tena na vya mawasiliano.

 

2.1.10. Kuendesha shughulika za kiusafiri na vifaa vya kila namna.

 

2.1.11. Kuendesha na kutengeneza mashine kubwakubwa na nzitonzito.

 

2.1.12. \kushughulika na kutengeneza mazalia au mimea kwa ajili ya kuzalisha nguvu za umeme, maji na makapi yaliyosazwa na kutokuwa na maana au matumizi au mifereji michafu.

 

Haki

2.2.1. Mnyororo wa kamandi na nidhamu unatakiwa uanzishwe pamoja na mashitaka na ukataji wa rufani kwa kila ngazi.

 

2.2.2. Mahakama ya usuluishi yanatakiwa yafanye kwa kufuata mujibu wa katiba.

 

2.2.3. Ikiwezekana, idara ya sheria inatakiwa iendelezwe na kufundishwa.

 

2.2.4. Pale ambapo kanisa la CCG litakuwa limeshika hatamu kwenye majimbo lote, mahakimu watabidi wawekwe na kama itawezekana na waumini wa CCG.

 

Mahitaji

2.3.1. Kila halmashauri ya kitaifa inawajibika katika kujihudumia kwa mahitaji yake.

 

Ulinzi na Usalama

2.4.1. Kila kikundi kinawajibika katika kuwalinda na kuwapa usalama watu wake na kanisa lao na kanisa linawjibika kuhakikisha kuwa ulinzi imara na usalama unakuwepo kwenye nchi yao.

 

Mafunzo

2.5.1. Kila halmashauri ya taifa ya CCG inapaswa kuwachagua na kuwapa mafunzo watu wake kwa kadri iwezekanavyo.

 

2.5.2. Uwezo wa mkufunzi unapaswa ujaribiwe katika kumudu mafunso ya ufundi yaliyotolewa kama msaada kwenye ngazi ya juu sana iwezekanavyo.

 

2.5.3. Wanawake wanapaswa kuelimishwa kadri iwezekanavyo na wana fursa ya namna moja ya kupata elimu kama waliyonayo wanaume.

 

2.5.4. Maeneo ya Kitaifa ya CCG wanapaswa watumie uwezo wao wa uzalishaji mali katika kujenga taasisi au vyuo vya mafunzo na kununua vifaa vya elimu. Majengo haya yanaweza kutumika kwa matumizi aina mbili yakiwemo ya kuyatumia kama majengo ya makanisa kwa kuwa hayatatumika sikn za Sabaro, Mwandamo wa Mwezi Mpyana siku za Sikukuu zilizoamriwa.

 

2.5.5. Mafunzo yanapaswa kujumuisha mambo yote yanayohusu ufundi wa umeme, umakanika sambamba na ujuzi ama uhandisi wa kujenga, pamoja na useremala na ufundibomba na aina nyingine zote za ufundi wa mikono, pamoja na namna zote za utoaji wa elimu ya juu.