Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[021C]
Ufafanuzi wa Kitabu cha Amosi
(Toleo
La 3.0 20141212-20141225-20150110)
Amosi ni kitabu cha Tatu kwa mujibu wa Kanuni ya Mpangilio wa Manabii Kumi na Mbili wa Agano la Kale, lakini kinachukuliwa kuwa ni kitabu cha Kwanza kati yao kwa wakati ule. Maana yake yameelezewa kwa kina.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2014, 2015 Wade Cox)
(tr. 2015)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu
bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza
kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka
maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Utangulizi
Jina la Amosi linadhaniwa kuwa
linatokana na jina Amazia (7:10) au Amasia (2Nyakati 17:16). Marabi wa baraza
la Talmudi waliamua kuwa anawezekana kuwa alikuwa mzito wa kuongea kama
alivyokuwa Musa (sawa na Soncino Intro., uk. 81). Alikuwa mfugaji
wa mifugo na mkulima na mmwagiliaji wa mikuyu (1:1, 7:14). Wakati alipokuwa
ameajiriwa kuifanya kazi hii ndipo Mungu alipomuita na kumtuma awaendee Israeli
na kuwaarifu kuwa kikombe chao cha uovu kilikuwa kimejaa na kama hawatatubu kwa
haraka na kumrudia Mungu watakumbana na mapatilizo makali na kupelekwa
utumwani. Wito huu wa kumtumikia Mungu ulimlazimu aiache nyumba yake na kuondoka
na kwenda pande za kaskazini mwa Yuda na kuishi huko Samaria na Betheli ili
avishughulikie vituo hivi ambavyo vilikwa ni maeneo ya ibada za sanamu na
vitala na upagani na ibada za sanamu.
Kitabu hiki cha Amosi kinakubalika kwa
ujumla kuwa kiliandikwa katikati ya miaka ya 750 KK wakati wa utawala wa Yeroboamu
II (782-743). Kitabu hiki kileorodheshwa kuwa ni cha tatu kwenye
Kanuni ya mpangilio lakini anakubalika kuwa alikuwa wa kwanza kati ya manabii
na kazi yake ilimtenganisha yeye mwenyewe na manabii wa mwanzoni ambao upotofu
au ukengeufu ulikuwa umeyakumba mafundisho yao kama tunavyoona kutoka kwenye
mandiko yake. Kukataa kwake kuwa yeye hakuwa miongoni mwa manabii haumaanishi
kuwa ni kweli hakuwa miongoni mwao bali ni dhahiri tu kuwa alikuwa analaumu na
kukemea ukenyeufu wao na kuwa yeye hakuwa mmoja wao.
Tetemeko la ardhi analolitaja kwenye
sua ya 1:1 lnaaminika kuwa lilitokea wakati wa Uzia (Zekaria 14:5). Tukio la
kupatwa kwa jua linalotajwa kwenye sura ya 8:9 linahesabiwa kuwa lilitokea
mwaka 763 KK (soma kitabu cha Soncino Intro., p. 81).
Mara tu tunapoona kipindi cha miaka thelathini
au arobaini kinafanyika kwenye toba ya taifa la Israeli (sawa pia na jarida la
Cox la Ufafanuzi wa Kitabu cha Yona (Commentary on Jonah). Maonyo haya
yanaonekana kuwa yalifanyika mwaka 763-2 KK na 733 wakati Waashuru walipoitwaa Damascus
na kuifanya Israeli kuwa ni nchi ya kuitoza kodi. Katika mwaka 723-2 waliondoka
na kwenda Samaria na mwaka 722 KK Waisraeli walichukuliwa utumwani na
wakapelekwa pande za kaskazini, huko Araxes na hawajarudi hadi leo na hadi hapo
kipindi cha Kurudi kwake Masihi Mara ya Pili.
Anajulikana kama ni nabii aliyekuwa anawashambulia
makuhani na manabii wakengeufu kwenye maandiko yake na kwamba aliuawa kwa
kipigo alichopigwa na chuma kizito usoni. Mtazamo wa kwanza ni kwamba inaaminika
kuwa aliuawa kwa kupigwa chuma kizito usoni mwake na Uzia. Dhana ya pili
inaamini kuwa aliuawa kwa kupigwa kitu kizito usoni na Amazia kuhani wa Betheli.
Mitazamo haya yote miwili inakubaliana na jinsi alivyouawa na kwamba ni
watawala tu ndio waliosababisha na kuhusika (soma kitabu cha Soncino,
ibid). Yawezekana kuwa ama aliuawa na mfalme aliyepigwa ukoma wa Yuda au kuhani
mkengeufu wa Israeli. Na jinsi hii ya mauaji ilikuwa ya kawaida kwa manabii wa
Mungu waliuawa waliuawa kwa ajili ya kazi zao walizokuwa wakizifanya.
Ujumbe
Ni muhimu kunukuu mtazamowa marabi
kwenye hilo ingawa wanaelewa na kuija kweli wa ujummbe wanaoukataa na kuupuzia
Yuda nab ado wanalaumiwa kwa sababu ya hilo. Ukristo wa Mimamboleo pia
umelaumiwa sana na Manabii Kumi na Mbili na Amosi kwa ujmla.
“Akiwakama
mwelekezaji wa mambo ya kimaadili na kijamii ya kidini umuhimu wa Amosi
unatangulia. Mungu sio Mungu wa Waisraeli peke yao, bali ni wa ulimwengu wote.
Wala agano lake kwa Israeli halitakoma. Wataadhibiwa kwa ajili ya dhambi zao
tena kwa ukali sana kuliko mataifa mengine, na uovu yanayostahili kuadhibiwa
vikali ni dhuluma kwenye jamii. Maadimiso au uadhimishaji wa uangalifu na
makini kwa taratibu au mapokeo ya kiibada hayataweza kuwaokoa. Amosi anaweka
msisitizo wakati alipokemea udanganyifu kwamba mapokeo au utaratibu kama ulivyo
tu wenyewe yanaweza kumthibitisha au kumpendeza Mungu ambaye anahitaji haki,
utakatifu na rehema. Ni kweli kwamba Israeli walikuwa ni wateule wake, bali ukamilifu
wa umuhimu wa fursa.
Ujumbe huu
wa uingizaji ndani ni ni jamii ile, kama itakuwa inadumu, inapasa iwe kwenye
haki kati ya mtu na mtu, sawasawa na ilivyo kati ya mataifa. Kwa uaminifu wa
Amosi na kuwatendea kwake watu bila upendeleo ilikuwa ni majira muhimu kwa
ustawi wa kitaifa. Kipindi chake cha Kilele ni moja ya nyakati ambazo mawazo ya
wenye hekima na ya urahisi wa maisha wamekuwa wakipatana kiushabihisho.”(Soncino,
ibid).
Hata hivyo, ni Mung ndiye anayetoa unabii
mwishoni mwa wakati ambao Amosi anawaambia Israeli moja kwa moja na mbali na
unabii tulioutaja kutlioutaja kutoka kwenye vitabu vya Torati na kutajwa kwa
manabii wa zamani waliohudumu hapo kale kabla ya nabii Samweli, na kwenye
Wafalme na Mambo ya Nyakati, kama Amosi anavyovijua kuwa ni nabii za zamani
sana zilizodumu hadi sasa.
Kitabu hiki kinajikuta kikiangukia
moja kwa moja kwenye migawanyo mitatu. Sura mbili za kwanza zinachukuliwa kama dibaji
ya uandishi wa nabii au kiusahihi zaidi twaweza kusema kuwa ni maandalizi ya
Mungu kupitia kwa nabii ili kuwashughulikia Israeli.
Israeli wa mataifa yote waliendelea kufanya
ukahaba wa kuabudu sanamu na kama yalivyo mataifa mengine yote hawakujiepusha,
wala kwa Israeli na Mungu yu karibu kuwashughulikia kwanza Israeli kwa
kulitumia taifa ambalo lilikuwa ndivyo lilikuwa limekwisha laumiwa tayari.
Kisha sisi tutakwenda kuyahukumu mataifa yote kama tunavyoona kutoka kwa hawa
Manabii Kumi na Mbili. Hakuna hata moja kati ya dini hizi zinazoendeleza
ukahaba itakayobakia na zote zitaangamizwa na kutokomezwa kabisa.
Sura nne zinazofuatia zinashughulika
na watu waliokuwa wanaoangalia utajiri wao wenyewe kuwa ni kama amala na ishara
ya utakatifu wao. Hali hii inaedelea kuwa ni msingi muhimu wa kimtazamo wa
mataifa ya Israeli ambao wanakuwa bado hara sasa hawajui kuwa walichopewa kuwa
chao ni kwa mujibu wa haki yao ya urithi kutoka kwa Ibrahimu na Mababa zao wa
imani wa zamani na haina uhusiano wowote na thamani yao kama watu na kuwa
majirani zao kuwa ni kama uchafu machoni pa Mungu. Uozo ulioanzia kutoka Ulaya
Magharibi kupitia kwenye Jumuia ya Madola na kwenye mataifa yote na hasa
Marekani. Imani ya kiantinomia ambayp haijali kuzifuata sheria za Mungu ya kile
kinachoitwa Ukristo wa Kisasa inakaribia kuhukumiwa na nabii Amosi anaona
kutoka mbali tangu kwenye utumwa wa Ashuru hadi nyakati za vita ya mwisho na
ujio wa Masihi hakuwezi kuwa na haki na kubakia mtakatifu bila kuwepo Sheria ya
Mungu na Haki. omianism of the so-called Modern Christians is about to be
punished and Amos looks forward from the Assyrian captivity to the final war of
the end and the Messiah. There can be no righteousness without God’s Law and
Justice. Tsedek (au Zedeki) ni neno moja tu kwenye Kiebrania lenye maana na
dhana mbili.
Kumbuka kile andiko linalomtambulisha
yeye kuwa ni mchungaji wa Tekoa. Hii ni sehemu ya mapokeo ya manabii na Kurani
inasema kuwa hakuna nabii ambaye hajawahi kuwa mchungaji.
Amosi Sura ya 1
Maneno ya Amosi,
aliyekuwa mmoja wa wachungaji wa Tekoa; maono aliyoyaona katika habari za
Israeli, siku za Uzia, mfalme wa Yuda, na siku za Yeroboamu, mwana wa Yoashi,
mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la nchi. 2 Naye alisema, Bwana atanguruma toka Sayuni, Atatoa
sauti yake toka Yerusalemu; Na malisho ya wachungaji yataomboleza, Na kilele
cha Karmeli kitanyauka. 3 Haya
ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Dameski, naam, kwa manne, sitaizuia
adhabu yake isimpate; kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya kupuria vya
chuma; 4 lakini nitapeleka moto
uingie katika nyumba ya Hazaeli, nao utayateketeza majumba ya Ben-hadadi. 5 Nami nitalivunja komeo la Dameski, na kuwakatilia
mbali wenyeji wa bondeni mwa Aveni, na yeye aishikaye fimbo ya enzi katika
Beth-Adini; na watu wa Shamu watakwenda hali ya kufungwa hata Kiri, asema
Bwana. 6 Haya ndiyo asemayo
Bwana; Kwa makosa matatu ya Gaza, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate;
kwa sababu waliichukua katika hali ya kufungwa kabila nzima, wawatie katika
mikono ya Edomu; 7 lakini nitapeleka moto
juu ya ukuta wa Gaza, nao utayateketeza majumba yake. 8 Nami nitamkatilia mbali mwenyeji katika Ashdodi;
na yeye aishikaye fimbo ya enzi katika Ashkeloni; nami nitaugeuza mkono wangu
uwe juu ya Ekroni; na mabaki ya Wafilisti wataangamia, asema Bwana MUNGU. 9 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya
Tiro, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameitia
kabila nzima katika mikono ya Edomu, wala hawakulikumbuka agano la udugu; 10 lakini nitapeleka moto juu ya ukuta wa Tiro, nao
utayateketeza majumba yake. 11 Haya
ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Edomu, naam, kwa manne, sitaizuia
adhabu yake isimpate; kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, akatupilia
mbali huruma zake zote; hasira yake ikararua-rarua daima, akaishika ghadhabu
yake milele; 12 lakini nitapeleka moto
juu ya Temani, nao utayateketeza majumba ya Bosra. 13 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya
wana wa Amoni, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu
wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili wapate kuongeza mipaka yao; 14 lakini nitawasha moto katika ukuta wa Raba, nao
utayateketeza majumba yake; pamoja na kupiga kelele siku ya vita, pamoja na
tufani katika siku ya chamchela; 15 na
mfalme wao atakwenda utumwani, yeye na wakuu wake wote pamoja, asema Bwana.
Hitimisho
Kwa hiyo ndipo mataifa ya kaskazini
walichukuliwa utumwani kama onyo kwa Israeli lakini hawakujali maonyo hayo.
Nchi ya Wamoabu wana wa Lutu
iliangamizwa kwa ajili ya kuwatesa kwao Waedomu. Yuda nao walitabiriwa kufikwa
na maafa lakini maangamizo yao yalikuja baadae, baada ya kuangamizwa kwao
Israeli kwa kuondolewa kwao na kupelekwa utumwani mwaka 722 na Yuda hawakuangamia
hadi mwaka 586 KK.
Waashuru na Wafilisti na Waedomu waliangamizwa,
kama ilivyokuwa kwa watu wa Tiro. Adhabu hizi zilirudiwa tena na tena ma
zitaendelea kwenye vipindi vyote hadi mwishoni katika Siku za Mwisho. Miaka 40
ya Toba ya Waashuru ilitolewa kutoka tangu mwishoni mwa vita iliyopiganwa
wakati wa Sikukuu ya Kiyahudi iitwayo Yom Kippur ya mwaka 1974 mwezi Mei na
vita vya kuiangamiza Syria iliendelea tangu Mei 2014. Gaza ilikutatizwa au
kuzongwa kama ilivyofanywa Lebanon. Edom sasa ni sehemu ya itikadi ya Uzayoni
au ya Kiyahudi.
Wamoabu waliokuwa kwenye ukingo wa
mashariki mwa Yordani waliongea kwa lafundhi ya Kiyahudi na walikuwa chini ya mamlaka
ya Israeli hadi kipindi cha utawala wa Ahabu. Masi yaliyofanywa na Mfalme Mesha
dhidi ya mamlaka ya Ahabu kulitajwa kwenye 2Wafalme 3 na pia kwenye jiwe la
Wamoabu.
Amosi Sura
ya 2
Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya
Moabu, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu aliichoma
moto mifupa ya mfalme wa Edomu hata ikawa chokaa; 2 lakini
nitapeleka moto juu ya Moabu, nao utayateketeza majumba ya Keriothi; na Moabu
atakufa pamoja na mshindo, na kelele, na sauti ya tarumbeta; 3
nami nitamkatilia mbali mwamuzi atoke kati yake, nami nitawaua wakuu
wake pamoja naye, asema Bwana. 4 Haya ndiyo asemayo
Bwana; Kwa makosa matatu ya Yuda, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake
isimpate; kwa sababu wameikataa sheria ya Bwana; wala hawakuzishika amri zake;
na maneno yao ya uongo yamewakosesha, ambayo baba zao waliyafuata; 5 lakini nitapeleka moto juu ya Yuda, nao utayateketeza
majumba ya Yerusalemu.
Andiko la
2.1
Aya ya 4: Amosi anaendelea kuitabiri
kuhusu hukumu itakayowakumba Yuda kwa dhambi zao walizozifanywa kwa kuikataa
Torati. Tendo hili linaendelea hadi katika Siku za Mwisho pia. Hadi siku hii ya
leo, wanaigeuza Torati kichwa chini kwa kutumia Talmud na kuibadili na kuitia
unajisi kalenda kwa kutumia mapokeo yao na taratibu za miahirisho za Kibabeloni.
Kwenye Isaya 5:24 na Hosea 4:6 tunaona mabadiliko hayahaya kama yalivyo kwenye kitabu
cha Amosi kuhusu mambo ya kimaadili ya sheria.
Uwongo na upotofu wao vimetajwa kwa
ibada zao za sanamu na miungu wao wa uwongo. Vimeshamiri hadi leo na watu
hawawezi hata kujua chimbuko lao.
Aya ya 5: Moto uliotajwa
kuwateketeza Yuda unamaanisha maangamizo ya Wababeloni yaliyofanywa mwaka 586 KK.
6 Haya ndiyo asemayo Bwana;
Kwa makosa matatu ya Israeli, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate;
kwa sababu wamewauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu; 7 nao hutwetea mavumbi yaliyo juu ya vichwa vya maskini, na
kuipotosha njia ya mwenye upole; na mtu na baba yake humwendea mwanamke mmoja,
hata kulitia unajisi jina langu takatifu; 8 nao
hujilaza karibu na kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani, na katika
nyumba ya Mungu wao hunywa divai ya watu waliotozwa fedha. 9 Lakini
nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa
mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake
toka juu, na mizizi yake toka chini. 10 Pia
naliwapandisha ninyi kutoka nchi ya Misri, nikawaongoza muda wa miaka arobaini
jangwani, ili mpate kuimiliki nchi ya Mwamori. 11 Nami
nikawainua watu miongoni mwa wana wenu wawe manabii, na katika vijana wenu wawe
Wanadhiri; je! Sivyo hivyo, enyi wana wa Israeli? Asema Bwana. 12 Lakini mliwapa Wanadhiri mvinyo wanywe; mkawaamuru
manabii, mkisema, Msifanye unabii. 13 Tazameni,
nitawalemea ninyi, Kama gari lilemeavyo lililojaa miganda. 14
Naye apigaye mbio atapotewa na kimbilio; Wala aliye hodari hataongeza
nguvu zake; Wala shujaa hatajiokoa nafsi yake; 15 Wala
apindaye upinde hatasimama; Wala aliye mwepesi wa miguu hataokoka; Wala
apandaye farasi hatajiokoa nafsi yake; 16 Naye mwenye
moyo mkuu miongoni mwa mashujaa Atakimbia uchi siku ile, asema Bwana.
Hitimisho
Moabu walihukumiwa hapa. Waamoni
walikuwa wamehukumiwa kwenye Sura ya 1. Hukumu ilikuwa kali sana kwa kuwa Israeli
waliagizwa kuwa wasiwashambulie lakini wao waliwashambulia Israeli (Kumbukumbu
la Torati 2:4 nk.). kwa hiyo nchi yote ya Yordani inahukumiwa na kushughulikiwa
vilivyo katika kipindi hiki. Waliambiwa wasiwashambulie Israeli kwenye vita ya
mwaka 1967 lakini waliwashambulia na wakajiepusha baada ya Vita iliyopiganwa
wakati wa Sikuku ya Yom Kippur ya mwaka 1973/4. Kujitoa au kujiepusha katika
Siku za Mwisho kutawatoa nje ya mikono ya nguvu za Mnyama wa kutoka Kaskazini
lakni wataletwa chini ya Taifa la Israeli chini ya Masihi kutokana na jarida la
Vita ya Hamon –Gogu (Na. 294).
Kumbuka kuwa Israeli wamehukumiwa kutokana
na dhambi ya kimwili kama sisi tulivyoutia unajisi Unazarayo wetu wa kidini na
kushindwa kwetu kuenenda sawasawa na unabii wa Mungu na kuwatweza manabii na
kwa kweli kuwaua manabii hawa kama walivyomtendea Amosi mwenyewe. Baba na mwana
wanashirikiana mwanamke mmoja na wanawatesa watakatifu wenye haki na kuwauza
kwa fedha. Wanazichukua nguo au mavazi ya walioweka rehani na kwendanazo kwenye
madhabahu ya Bwana kama watakatifu. Israeli wa leo ni waovu zaidi kuliko
walivyokuwa kipindi kitabu hiki kikiandikwa. Mungu alizivunja nguvu na uweza
wao wa kijeshi waliokuwa wakiutegemea na atafanya hivyo tena katika Siku za
Mwisho.
Kile wanachokitumainia kitapokwa
kutoka kwao na watalazimishwa kumtumaini Mungu peke yake.
Kisha kwenye Sura ya 3 Mungu anaiambia
nyumba yote ya Israeli aliyoitoa kutoka utumwani Misri nah ii inaijumuisha Yuda.
Kwenye Sura hii Mungu anasema kuwa hafanyi chochote ili kuokoa, bali kwanza
kabisa anawaonya kwanza kwa kupitia manabii wake.
Ukweli ni kwamba hakuna laana
inayokuja pasipo kuwa na sababu (Mithali 26:2).
Amosi Sura
ya 3
Lisikieni neno hili alilolisema Bwana juu yenu,
enyi wana wa Israeli, juu ya jamaa yote niliowapandisha kutoka nchi ya Misri,
nikisema, 2 Ni ninyi tu niliowajua katika jamaa zote
zilizo duniani; kwa sababu hiyo nitawapatiliza ninyi maovu yenu yote. 3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa
wamepatana? 4 Je! Simba atanguruma mwituni, asipokuwa
na mawindo? Mwana-simba atalia pangoni mwake, ikiwa hakupata kitu? 5 Je! Ndege ataanguka mtegoni juu ya nchi, mahali
asipotegewa tanzi? Mtego utafyatuka juu ya nchi, bila kunasa
kitu cho chote? 6 Je! Tarumbeta itapigwa mjini, watu
wasiogope? Mji utapatikana na hali mbaya, asiyoileta Bwana? 7
Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lo lote, bila kuwafunulia watumishi
wake manabii siri yake. 8 Simba amekwisha kunguruma,
ni nani asiyeogopa? Bwana MUNGU amenena, ni nani awezaye neno ila kutabiri? 9 Tangazeni habari katika majumba ya Ashdodi, na katika
majumba ya nchi ya Misri, mkaseme, Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria,
katazameni, ni mishindo mikubwa kama nini iliyomo humo, na udhalimu mwingi kama
nini uliomo ndani yake. 10 Kwa maana hawajui kutenda
haki, asema Bwana, hao wawekao akiba ya jeuri na unyang'anyi katika majumba
yao. 11 Basi, haya ndiyo asemayo Bwana MUNGU;
Atakuwako adui, kuizunguka nchi pande zote; naye atazishusha chini nguvu zako
zikutoke; na majumba yako yatatekwa nyara. 12 Haya
ndiyo asemayo Bwana; Kama vile mchungaji apokonyavyo kinywani mwa simba miguu
miwili, au kipande cha sikio; ndivyo watakavyopokonywa wana wa Israeli, wakaao
Samaria katika pembe ya semadari, na juu ya mito ya hariri ya kitanda. 13 Sikieni, mkashuhudu juu ya nyumba ya Yakobo, asema Bwana,
MUNGU wa majeshi. 14 Kwani katika siku ile nitakapompatiliza
Israeli makosa yake, nitazipatiliza pia madhabahu za Betheli, na pembe za
madhabahu zitakatiliwa mbali, na kuanguka chini. 15 Nami
nitaipiga nyumba ya wakati wa baridi pamoja na nyumba ya wakati wa hari; na
hizo nyumba za pembe zitaangamia, nazo nyumba kubwa zitakuwa na mwisho, asema
Bwana.
Hitimisho
Wenyeji wa nchi za Wafilisti na Misri walisihiwa waje na
kushuhudia kuangamia kwa Israeli. Hii ilikuwa inasimama pia kama somo kwao
kwenye Siku za Mwisho. Nchi hizi mbili ziliadhibiwa na kuangamizwa na Israeli
walikumbuka kuangamia kwao na halafu katika Siku za Mwisho nchi yao yote
itachukuliwa hatimaye.
Milima ya Samaria: Walikuwa
wanamudu kuviona vilele vyake wakiwa Samaria kutoka kwenye milima
iliyowazunguka. Nchi ilikuwa imezama kwenye makanganyiko wa machafuko kwa ajili
ya ufisadi na shuruti. Hisia zao za kimaadili zilikuwa zimeharibika kabisa.
Pembe za madhabahu ndizo zilizoshikiliwa na wale waliokuwa
wanatafuta utakatifu wa mahali patakatifu kutoka kwa Mungu. Uwezo wa kutafuta
utakatifu kutoka kwa Mungu utaondolewa. Vyanzo hivyohivyo vya marabi hata vinadai
kwamba misingi ya madhabahu imeondolewa.
Nyumba ya wakati wa baridi imetajwa tena kwenye Yeremia
36:22. Yaonyesha kuwa inautaja utajiri mkubwa wa watu walio kwenye madaraja ya
utawala dhidi ya maskini wasio na kitu. Utajiri wao utaondolewa na hawa walio
kwenye madaraja ya utawala wataachwa watupu.
Makabila yaliadhibiwa kwa ajili ya kuabudu kwao sanamu na
imani yao ya mungue Jua kwa kuwa ndivyo walivyofanya huko Betheli. Katika utumwa
huu, sehemu kubwa ya Walawi walikwenda utumwani pia divisheni au tarafa 24
zilianzishwa tena kutoka kwenye divisheni au tarafa tatu zilizoko bado katika
Yuda ili kwamba huduma za Makuhani zifanyike Hekaluni. Ulikuwa ni mlipuko
mkubwa kwa Walawi nchini kote Israeli. Weote walikwenda utumwani eneo la mbali
zaidi huko Araxes na walichanganyika pamoja na Wahiti au Waseltiki.
Kwenye aya ya 11 na 12 tunaona kwamba unabii ulitimia na
baada ya miaka thelathini Syria ilizingirwa na kutekwa na Waashuru baada ya
kuzingirwa kwa miaka mitatu. Samani zenye thamani kubwa za Samaria ambao lizidharauliwa
na kupuuzwa na Amosi zilivunjiliwa mbali na Waashuru.
Kwenye maandiko yaliyo kwenye Sura ya 4 yanaonyesha kuwa
Mungu yupo kinyume sana na wanawake wa Israeli Ng’ombe wa Bashani ambao
wanawadhulumu maskini. Wanapelekwa utumwani na kuadhibiwa kwa ajili ya kuabudu
kwao sanamu na vinyago huko Betheli zilizoingizwa na Yezebeli kwenye Dini za
waabudu Jua. Upotofu wa Samaria ulikuwa wazi na ulitajwa na Amosi kuwa ni kama
uanzishaji au mwanzo wa choyo kwa wanawake wao na wanafananishwa na ng’ombe wa Bashani.
Ibada hizi za sanam zinaonekana katika Israeli hadi siku
hizi za leo.
Amosi Sura
ya 4
Lisikieni neno hili, enyi ng'ombe wa Bashani, mnaokaa juu ya mlima wa
Samaria, mnaowaonea maskini, na kuwaponda wahitaji; mnaowaambia bwana zao,
Haya! Leteni, tunywe. 2 Bwana MUNGU ameapa kwa utakatifu wake, ya kuwa, tazama, siku zitawajilia,
watakapowaondoa ninyi kwa kulabu, na mabaki yenu kwa ndoana. 3 Nanyi mtatoka kwenye mahali palipobomolewa,
kila mwanamke moja kwa moja mbele yake; nanyi mtajitupa katika Harmoni, asema
Bwana. 4 Njoni
Betheli, mkakose; njoni Gilgali, mkaongeze makosa; kaleteni dhabihu zenu kila
asubuhi, na zaka zenu kila siku ya tatu; 5 mkachome sadaka ya shukrani, ya kitu
kilichotiwa chachu; mkatangaze sadaka mtoazo kwa hiari na kuzihubiri habari
zake; kwa maana ndivyo viwapendezavyo ninyi, enyi wana wa Israeli, asema Bwana
MUNGU. 6 Mimi
nami nimewapa usafi wa meno katika miji yenu yote, na kutindikiwa na mkate mahali
penu pote; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 7 Tena nimeizuia mvua msiipate,
ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja,
nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na
sehemu isiyopata mvua ilikatika. 8 Basi kutoka miji miwili mitatu walitanga-tanga kuendea mji mwingine wapate
kunywa maji, wasipate ya kuwatosha; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 9 Nami nimewapiga kwa ukavu na koga;
wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni
yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 10 Nimewapelekea tauni, kama tauni ya
Misri; vijana wenu nimewaua kwa upanga, na farasi wenu nimewachukulia mbali;
nami nimeupandisha uvundo wa matuo yenu na kuuingiza katika mianzi ya pua zenu;
lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 11 Baadhi yenu nimewaangamiza, kama hapo
Mungu alipoiangamiza Sodoma na Gomora, nanyi mkawa kama kinga kilichonyakuliwa
motoni; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 12 Basi nitakutenda hivi, Ee Israeli, na
kwa sababu nitakutenda hivi, ujiweke tayari kuonana na Mungu wako, Ee Israeli. 13 Kwa maana, angalia, yeye aifanyizaye
milima, na kuuumba upepo, na kumwambia mwanadamu mawazo yake, afanyaye asubuhi
kuwa giza, na kupakanyaga mahali pa dunia palipoinuka; Bwana, Mungu wa majeshi,
ndilo jina lake.
Hitimisho
Kumbuka kuwa Bwana wa Majeshi
anawashughulikia Israeli kwa msingi au muono wa kiuchaguzi na aliwalazimisha
kwa makundi na miji lakini bado hawakutubu na kumrudia.
Andiko lililo kwenye aya za 4-13 linaanza
kwa kusema Njooni Betheli. Mwelekeo huu uko sawa na ule wa Eliya kwenye
Mlima wa Karmeli (1Wafalme sura ya 18). Inakemea ibada zao za kutukuza
sanamu pamoja na sheria zake au mapokeo ya kiibada ambazo kwazo waliziiga na
hazikuwarithisha na zilikataliwa na Mungu ambaye aliwakemea na kuwaadhibu kwa
ukame na moto, tetemeko la ardhi, baa la nyaa, tauni, na kwa vita. Na bado
hawakumzikiliza.
Kwa ujumbe wa kuhusu Gilgali tunaona
andiko kwenye Hosea 4:15.
Dhabihu zilitolewa kwa miungu wa
uwongo na zaka ilitolewa ili kuiwezesha dini ya uwongo ya Baali katika Israeli
nab ado inafanyika hivyo hadi siku hizi. Mzingiro wa matendo ya dhambi zao
ambayo ndiyo yalikuwa makusudio ya watu wa Gilgali yakuwa wamezingiriwa mbali.
Sura ya Tano inaendelea kuuelezea
utaratibu au mfumo jinsi yatakavyotokea maafa. Hakutakuwa
na mtu atakayeliinua na kuifufua Israeli. Taifa zime lote linapasa kuangamizwa.
Aya za kwanza ni wimbo wa maombolezo ya kuwaombolezea Israeli kwa kuwa kwa maombolezo.
Isreali imeanguka. Vebu iliyo iliyo kwenye utimilifu wa kinabii na ndipo
inlionyesha kama nna kamilika au kutimilika. Uwongo wake umekataliwa. Andiko
hili ndipo linaelekea hadi kwene unabii.
Taifa ya kuwaua wajumbe wa kila watu
kumi na kwa hiyo lilikusudiwa lisiwe lenye nguvu tena.
Mungu anatoa maelekezo ya haraka kwa
Israeli akisema kwamba wasiende Gileadi karibu na Yordani kama walivyokuwa
wanakaribia kwenda utumwani kabla ya Samaria. Wala hawakuomba msaada
kutoka kwa waabudu sanamu wenzao wa Betheli wala hawakuruhusiwa kwenda Yuda na
kuishi kwenye nchi za kusini huko Gilagali na Beersheba. Hakuna hata mmoja
aliyewasaidia. Washirika wao hawatawasaidia na Bwana wa Majeshi atawafuata popote
waendapo na kuwatesa.
Kama watamrudia Mungu wataishi lakini
hawatadumu kama hawatafana hivyo. Mungu atawapiga kwa mabaa ya njaa na ukame
katika Israeli yote hadi watakapotubu nah ii itaendelea hadi katika Siku za
Mwisho.
Amosi Sura
ya 5
Lisikieni neno hili
nilitamkalo liwe maombolezo juu yenu, enyi nyumba ya Israeli. 2 Bikira wa Israeli ameanguka; hatainuka tena;
Ameangushwa katika nchi yake; hakuna mtu wa kumwinua. 3 Kwa kuwa Bwana MUNGU asema hivi; Mji uliotoka nje
wenye watu elfu, utasaziwa watu mia, na mji uliotoka wenye watu mia, utasaziwa
watu kumi, kwa nyumba ya Israeli. 4 Maana
Bwana awaambia hivi nyumba ya Israeli, Nitafuteni mimi, nanyi mtaishi; 5 bali msitafute Betheli, wala msiingie Gilgali,
wala msipite kwenda Beer-sheba; kwani Gilgali hakika yake itakwenda utumwani,
na Betheli itakuwa ubatili. 6 Mtafuteni
Bwana, nanyi mtaishi; asije akawaka kama moto katika nyumba ya Yusufu, nao
ukateketeza, asiwepo mtu awezaye kuuzima katika Betheli.,
Endelea na andiko la 5.1
Imani hii ya kidini ambayo imeiharibu na kuipotoa Israeli
kutoka Betheli imeenepokelewa na kukubalika katika Israeli na hawakuitubia na
waliishamirisha imani na itikadi ya uovu na dhuluma nyuani mwao (malangoni
mwao).
Dini za kuliabudu Jua za mungu Baali ambazo hadi leo zinaizunguka
Israeli na wanaabudu siku ya Juan a wanaadhimisha Sikukuu za Krismas na Easter na
kwa ajili hiyo wataadhibiwa (soma jarida la Chanzo cha Krismas na Easter (Na.
235)).
7 Ninyi mnaogeuza hukumu
kuwa uchungu, na kuiangusha haki chini, 8 mtafuteni
yeye afanyaye Kilimia na Orioni, na kukigeuza kivuli cha mauti kuwa asubuhi, na
kuufanya mchana kuwa giza kwa usiku; yeye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga
juu ya uso wa nchi; Bwana, ndilo jina lake; 9 yeye
aletaye uharibifu wa ghafula juu yao walio hodari, hata uharibifu uipate ngome.
Endelea na andiko la 5.2
Itikadi zao za udhalim na dhuluma ziliwagunguka. Ufisadi
ukashamiri kila mahali na wale walio madarakani wakachukia kukemewa. Kweli
ikaondolewa na kufunikwa chini. Mwishoni, Mungu akalazimika kuingilia kati.
Hali hii inaendelea hadi kwenye Siku za Mwisho kama tunavyouona unabii
unaotupeleka kwenye kipindi cha Siku ya Bwana. Tunaambiwa tuwe na busara na kuchukia
uovu na tupende mema na Bwana wa Majeshi atakuwa pamoja nasi. Wadhalimu
walioishi kwenye karne za kabla ya kufanya Makazi yao huko Canada na Marekari na
hukf Australia na New Zealand walikuwa wakimuogopa au kumcha na Mungu aliutumia
udhalilishaji ule ili kuwamilikisha tena maskini nchi nyingine na kuyaokoa
mataifa mengi hadi nyakati za mwisho.
Wamewatesa wenye imani na waliokuwa wanaihubiri na
kuifundisha kweli na waliokuwa wanaishika sheria ya Mungu kwa karne nyingi.
10 Wao
humchukia yeye akemeaye langoni, nao humzira anenaye maneno ya adili. 11 Basi, kwa kuwa mnamkanyaga maskini, na kumtoza
ngano; ninyi mmejenga nyumba za mawe yaliyochongwa, lakini hamtakaa ndani yake;
ninyi mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu, lakini hamtakunywa divai yake. 12 Maana mimi najua jinsi maasi yenu yalivyo mengi,
na jinsi dhambi zenu zilivyo kubwa; ninyi mnaowaonea wenye haki, mnaopokea
rushwa, na kuwageuza wahitaji langoni wasipate haki yao. 13 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya
wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya. 14 Tafuteni
mema, wala si mabaya, mpate kuishi; hivyo Bwana, Mungu wa majeshi, atakuwa
pamoja nanyi, kama msemavyo. 15 Yachukieni
mabaya; yapendeni mema; mkaithibitishe haki langoni; yamkini kwamba Bwana,
Mungu wa majeshi, atawafanyia fadhili mabaki ya Yusufu. 16 Kwa ajili ya hayo, asema Bwana, Mungu wa majeshi,
aliye Bwana; Kutakuwako maombolezo katika njia kuu zote; nao watasema katika
njia zote, Ole! Ole! Nao watamwita mkulima aje kuombolea, na hao walio hodari
wa kulia waje kuomboleza. 17 Tena
katika mashamba yote ya mizabibu kutakuwako kulia; kwa maana mimi nitapita
katikati yako, asema Bwana.
Endelea na andiko la 5.3
Ufisadi upo kila mahali katika Siku hizi za Mwisho na
wenye hekima hawathubutu kusema lolote. Ni watenda haki tu walio nyuani mwa Israeli
ndio watakaookolewa. Na kama inavyozidi kushamiri udhalimu ndivyo
watakavyoadhibiwa.
Ukame uliwafanya wakulima waomboleze na wakulima wa
mizabibu wataomboleza.
Siku ya Bwana sio kitu ambacho watu wanapaswa kukitamani
kwa kuwa itwakuta wakiwa hawajatubu.
18 Ole wenu! Ninyi
mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru.
19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu;
au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma. 20 Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru?
Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga.
Endelea na andiko la 5.4
Mungu anatangaza kwamba anazichukia na kuzidharau sikukuu
zao. Makanisa mengi ya Mungu wameanzisha kalenda ya uwongo na sikuku zao haziangukii
kwenye siku muafaka zilizoamriwa kama walivyofanya kwenye Kalenda ya Hilleli katika
Yuda. Katika Israeli wengi wao wanatangaza makusanyiko yao kama zilivyo sheria
au mapokeo ya ibada za dini za Kipagani za Baali kama walivyokuwa wakiwaabudu
huko Betheli kwenye Dini za Jua na Ibada za Sirisiri na Krismas na Easter ya
mungumke. (Soma majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. 156); Kalenda na Mwezi Mwandamo: Ni Uahirisho au Sikukuu (Na.
195); Ubadilishaji wa Kalenda ya Mungu Katika Yuda (Na. 195B) na Chanzo cha Maadhimisho ya Krismas na Easter (Na. 235).) Mungu
hatawakubalia kitu chochote mahali popote.
21 Mimi nazichukia sikukuu
zenu, nazidharau, nami sitapendezwa na makutano yenu ya dini. 22 Naam, ijapokuwa mnanitolea sadaka zenu za
kuteketezwa na sadaka zenu za unga, sitazikubali; wala sitaziangalia sadaka
zenu za amani, na za wanyama walionona. 23 Niondoleeni
kelele za nyimbo zenu; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu.
Endelea na andiko la 5.5
Ni lazima kuwa haki na maadili mema na mwenendo mwema
vinatokea kwenye kiini au katikati ya Israeli na kwenye imani yake ya kidini na
sio kuwa gamba tupu kama ilivyo sasa.
24 Lakini hukumu na
itelemke kama maji, na haki kama maji makuu. 25 Je!
Mliniletea dhabihu na sadaka jangwani muda wa miaka arobaini, enyi nyumba ya
Israeli? 26 Naam, mtamchukua
Sikuthi, mfalme wenu, na Kiuni, sanamu zenu, nyota ya mungu wenu,
mliojifanyizia wenyewe. 27 Kwa
sababu hiyo nitawahamisha, hali ya kufungwa, mwende mbali kupita Dameski, asema
Bwana, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi
Hitimisho
Utaratibu wa kuabudu katika Israeli ulikengeushwa na
Mungu hatawakubalia.
Sakkuthi na Kaiwani ni miungu ya kipagani
na nyota ya Kiiuni au Kaiwani au Remfani wangali wakitumika
na kuabudiwa bado katia Yuda hadi sasa. Hii ni miungu ya Wababeloni na Waashuru
inayokutikana hadi leo na ingali bado ikiabudiwa kwa pamoja. Walishurutishwa
waibebe miungu yao ya uwongo hadi Ashuru na zaidi ya huko, kaskazini mwa Araxes. Wataadhibiwa
tena katika Siku za Mwisho kwa ajili ya dhambi hizihizi.
Kumbuka kuwa Sura ya Sita inaendelea
hadi kwenye makemeo waliyokemewa Yuda katika Sayuni pamoja na wenyeji wa
Samaria kwa pamoja kwa kuwa ibada hizi zilikuwa zimejiingiza na kukubalika kote
kuwili.
Amosi Sura
ya 6
Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na hao
wanaokaa salama katika mlima wa Samaria, watu mashuhuri wa taifa lililo la
kwanza, ambao nyumba ya Israeli huwaendea. 2 Piteni
hata Kalne, mkaone; tena tokea huko enendeni hata Hamathi iliyo kuu; kisha
shukeni hata Gathi ya Wafilisti; je! Ninyi ni bora kuliko falme hizi? Au mpaka
wao ni mkubwa kuliko mpaka wenu?
Ufafanuzi juu ya Andiko la 6.1
Miji ya Kalne na Hamathi zilianguka mwaka 738 na
720 KK. Kwa hiyo, ni kutokana na hiyo
yalipaswa kukumbwa mapema na maafa anayoyataja nabii Amosi
(soma kitabu cha Soncino fn.). Gathi ni
mku mkuu wa Wafilisti (soma 1:6) na andiko lilipasa lisomwe ili kuashiria swali
lenye mashiko kwa Israeli, yaani; je, mnadhani kuwa ninyi ni bora kuliko ninyi
mtakaoatoroka maafa watakayoyaleta?
3 Ninyi mnaoiweka mbali siku
hiyo mbaya, na kulileta karibu kao la udhalimu; 4 ninyi
mnaolala juu ya vitanda vya pembe, na kujinyosha juu ya masemadari yenu; ninyi
mnaokula wana-kondoo wa kundi, na ndama waliomo zizini; 5 ninyi
mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda
vya namna nyingi, kama vile Daudi; 6 ninyi mnaokunywa
divai katika mabakuli, na kujipaka marhamu iliyo nzuri; lakini hawahuzuniki kwa
sababu ya mateso ya Yusufu. 7 Basi kwa ajili ya hayo
sasa watakwenda utumwani pamoja na wa kwanza watakaokwenda utumwani, na kelele
za machezo za hao waliojinyosha zitakoma. 8 Bwana
MUNGU ameapa kwa nafsi yake, asema Bwana, Mungu wa majeshi; Naizira fahari ya
Yakobo, nachukizwa na majumba yake; kwa sababu hiyo nitautoa huo mji, pamoja na
wote waliomo ndani yake. 9 Hata itakuwa, wakisalia
wanaume kumi katika nyumba moja, watakufa.
Endelea na andiko la 6.2
Kwa hiyo. Mali na nguvu walizokuwanazo matajiri pia matajiri
wa Israeli katika Siku za Mwisho vitakuwa vya kwanza kuangamizwa. Wale
wanaolala kwenye vitanda vya pembe na kujificha kwenye maangamizo watachukuliwa
na kuchomwa moto kama watakavyofanywa kwenye Siku za Mwisho pia.
Watakufa na hakuna hata nyumba moja itakayosalia, na
watategemea ndugu zao kuwachomwa moto kwa sababu ya tauni watakayoteswa kwayo; na
hususan katika Siku za Mwisho mapigo hayo ya magonjwa yatakuwa makubwa sana.
10
Na mjomba wa mtu atakapomwinua, yaani, yeye
amchomaye moto, ili atoe mifupa yake nyumbani, naye atakapomwambia yeye aliye
katika pande za ndani za nyumba, Je! Yuko mtu ye yote pamoja nawe? Naye
atakaposema, La, hapana; ndipo atasema, Nyamaza kimya; maana hatuna ruhusa
kulitaja jina la Bwana. 11 Kwa maana, angalia, Bwana
atoa amri, na nyumba kubwa itapigwa na kuwa na mahali palipobomolewa, na nyumba
ndogo nayo itapigwa iwe na nyufa.
Endelea na andiko la 6.3
Mungu amegeuka na kuwatega mgongo na maombi yao yatageuka
kuwa hukumu.
Kwa mjibu wa Targum Nyumba Kuu inayotajwa inamaanisha
Israeli na hii Nyumba Ndogo ni Yuda. Wote watakatwakatwa vipande. Andiko linataja
upotoshaji wa utoaji wa haki. Ni jambo la hatari sana kupoka au kugeuza haki
kama ilivyo kuwaendesha farasi kwenye miamba na nikazibure kama ilivyo kulima
baharini kwa maksai. Israeli na Yuda wameipotosha Haki na Utakatifu kwa
kuiifisha kwa sumu na kwa kimnyoo. Wao ni sawa tu na Tsedek.
12 Je! Farasi watapiga mbio juu
ya mwamba? Je! Mtu atalima na ng'ombe huko? Hata mmegeuza hukumu kuwa uchungu,
na matunda ya haki kuwa pakanga; 13 ninyi
mnaolifurahia jambo lisilo na maana, msemao, Je! Hatukujipatia pembe kwa nguvu
zetu wenyewe? 14 Maana, angalia, nitaondokesha taifa
juu yenu, enyi nyumba ya Israeli, asema Bwana, Mungu wa majeshi, nao watawatesa
ninyi toka mahali pa kuingilia katika Hamathi hata kijito cha Araba.
Hitimisho
Lo debar ni kitu kisichofaa au kisichokuwepo. (Si
watu wangu, Kumbukumbu la Torati 32:21). Wanahusika na hali ya kutopatilizwa na
ya kipuuzi kwa kile kinachokosesha akiba.
Jina Karnaim maana yake ni pembe na ni neno la fumbo
alilolitumia Amosi ili kuyataja majina ya Israeli. Graetz inadhaniwa
kuwa ni Lo Debar na Karnaim ni mahali palipoitwa Gileadi. Lidbiri na
Lo Dabari imeorodheshwa kwenye Yoshua 13:26; 2Sawueli 9:4f;
17:27. AshtarothKarnaimu umetajwa kwenye Mwanzo 14:5 na unahusiana
na mungumke Ashtarothi au Easter mshirika wa Baali anayeabudiwa katika Israel
hadi leo. Gileadi ulikuwa kwenye mazingira ya vita tangu kipindi cha Yeroboamu
II na Waashuru na Amosi alitabiri kinyume chao kwa kutumia maneno ya fumbo.
Neno “taifa” linamaanisha Syria na kuendelea hadi katika Siku za Mwisho (soma
kitabu cha Soncino fns).
Neno la Hamathi kwenye Kitabu cha Arabah linafananishwa
na Dani hadi Beersheba. Kwa hiyo nchi yote ambayo kwayo Israeli
anatawala itatawaliwa zaidi (sawa na 2Wafalme 14:25). Unabii huu wa maangamizo
inahitimisha sehemu hii ya unabii.
Utangulizi wa Sura ya 7
Kifungu cha andiko kinaanza na Maono ya Kwanza. Tauni na
Nzige.
Kuingilia kati na muhimu kwa Amosi kunawezesha
kusimamisha kwa pigo hili la tauni. Kwa hiyo Mungu anaonyesha kwamba ni kwa
uingiliaji kati tu wa watumishi wake ndipo wataweza kuokoka.
Hii inaendelea tangu hapo hadi mwishoni na ni kwa maombi
tu peke yake ya wateule ndipo wanaweza kuokolewa.
Kuna maono matano.
Tukio la nzige lililotumika hapa linaonyesha kuwa Mungu
alikuwa anawatengeneza ilikuwa ni Gobai pia
iliyotumika kwenye Nahumu 3:17. Kukua kwa baadae (kwa Kiebrania Lekesh, mizizi
inayojitokeza kutoka kwenye malkosh kama “mvua baadae”) inataja na
kuonyesha ukuaji wa mazao ya majira ya Baridi.
“Fagio au Fekeo za Mfalme” ilikuwa ni
kodi au ushuru uliotolewa kwa hiyari na upendo kwa wafalme wa Israeli kwa malisho
au majani ya wanyama kwa kikosi cha magari ya deraya (sawa na 1Wafalme 18:5). Baada
ya kodi hii ikiwa imekwisha lipwa, watu walikata majani kwa ajili ya matumizi
yao lakini nzige walikuja na kuyala (Dereva).
Amosi Sura
ya 7
Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama,
aliumba nzige mwanzo wa kuchipuka kwake mimea wakati wa vuli; na tazama,
ilikuwa mimea ya wakati wa vuli baada ya mavuno ya mfalme. 2 Ikawa,
nzige walipokwisha kula majani ya nchi, ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, samehe,
nakusihi; Yakobo atasimamaje? Kwa maana ni mdogo. 3 Bwana
akaghairi katika jambo hili. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana.
Endelea na andiko la 7.1
Neno la Kiebrania lililotafsiriwa jani hapa linaandikwa
na kutamkwa herb (mboga) kwenye Mwanzo 1:12 na ni neno la jumla kwa
mbogamboga.
Kimsingi Amosi alisema akitumia neno inuka kuwa “Ni
kivipi Israeli watajinasua kutoka kwenye maafa kama haya.” Pia alijua kuwa
hukumu ilikuwa inakuja na kufanywa na Mungu kwa watu wenye dhambi na ndipo
aliwaombea msamaha watu wote. Alidai kwamba licha ya mtazamo wao wa kiutajiri
na mali raslimali zao zilichukuliwa kuwa ni kidogo sana kuweza kufaa kwenye maafa.
Hawa nzige walikuwa ni taswira ya maadui kutoka Kaskazini
kama ilivyotumika kwenye unabii uliofuatia baadae, kama alivyotabiri Nahumu kwa
Waashuru wote na mashambulizi ya Wababeloni.
Kwa hiyo Amosi aliingilia kati kwa niaba ya Israeli. Walisazwa
kutoka kwa Nzige wa Kaskazini lakini Yuda waliruhusiwa kurejea kwenye nchi yao
baada ya maangamizo ya Wababeloni ili wamone na kumshuhudia Masihi kwenye nchi
yao wenyewe.
Kisha Bwana Mungu alimuonyesha Amosi kuwa hawajatubu.
Ndipo Bwana aliwatawanya Yuda ulimwenguni kote na kuuhusuru Yerusalemu kwa
kuuangamiza kwa moto na akalitawanya hata kanisa pia.
4 Haya ndiyo aliyonionyesha
Bwana MUNGU; tazama, Bwana MUNGU aliita ili kushindana kwa moto; nao ukavila
vilindi vikuu, ukataka kuiteketeza nchi kavu. 5 Ndipo
nikasema, Ee Bwana MUNGU, acha, nakusihi; Yakobo atasimamaje? Kwa maana ni
mdogo. 6 Bwana akaghairi katika jambo hili pia. Jambo
hili halitakuwa, asema Bwana MUNGU.
Endelea na andiko la 7.2
Tafsiri ya Soncino inaweka neno hapa kuwa Mungu
wakati wote anawaonya watu kabla ya kumwagwa kwa kamio la Hukumu (mfano ni Isaya
3:13; Yeremia 2:9; Hosea 4:1 Mika 6:1). Neno “Kina kirefu” linadhaniwa kuzitaja
bahari ambayo kwayo dunia imetolewa na wakosoaji wanadhani kuwa ilikuwa
imetuama kwenye kakosa ya kisayansi. Hata hivyo, kina kirefu hatimaye kimekuja
kugundulika na wanasayansi kuwa ni ghala kubwa ya maji iliyoko chini ya maji
huko kwenye bara la Amerika ya Kaskazini. Hii inaweza kuwa ni hukumu kali na ya
kutisha itakayotolewa katika Siku za Mwisho ambayo itaikumba dunia.
Inaweza pia kumaanisha watu wa ulimwengu miongoni mwa
sehemu ambazo Yuda na Israeli.
Maono ya pili yalihusu Timazi. Hii ilikuwa hi
taswira ya hukumu ya Mungu kwa Nyumba ya Isaka na ilikuwa kwamba Israeli walikuwa
wamekwisha hukumiwa kwenda utumwani kwa ajili ya ibada zao za sanam
zilizoongozwa na wafalme wao na makuhani waona watu wake.
Ndipo Amazia Kuhani wa Betheli alijaribu kufanya
hila za kumua Amosi na kutafuta jinsi ya kuzuia wasiende utumwani. Kwa jinsi
hii hii, ndipo makuhani wa uwongo na manabii walijaribu kulinyamazisha neno la
Mungu katika Israeli.
7 Haya ndiyo aliyonionyesha;
na tazama, Bwana alisimama karibu na ukuta uliojengwa kwa timazi, mwenye timazi
mkononi mwake. 8 Bwana akaniambia, Amosii, unaona
nini? Nikasema, Naona timazi. Ndipo Bwana akasema, Tazama, nitaweka timazi kati
ya watu wangu Israeli; sitawapita tena kamwe; 9 na
mahali palipoinuka pa Isaka patakuwa ukiwa, na mahali patakatifu pa Israeli
pataharibika; nami nitaondoka nishindane na nyumba ya Yeroboamu kwa upanga. 10 Ndipo Amazia, kuhani wa Betheli, akapeleka habari kwa
Yeroboamu, mfalme wa Israeli, akisema, Amosii amefanya fitina juu yako kati ya
nyumba ya Israeli; nchi haiwezi kustahimili maneno yake yote. 11 Kwa maana Amosii asema hivi, Yeroboamu atakufa kwa
upanga, na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali, hali ya kufungwa, atoke
katika nchi yake. 12 Tena Amazia akamwambia Amosii,
Ewe mwonaji, nenda zako, ikimbilie nchi ya Yuda, ukale mkate huko, ukatabiri
huko; 13 lakini usitabiri tena huku Betheli; kwa maana
ni mahali patakatifu pa mfalme, nayo ni nyumba ya kifalme. 14
Ndipo Amosii akajibu akamwambia Amazia, Mimi sikuwa nabii, wala sikuwa
mwana wa nabii; bali nalikuwa mchungaji, na mtunza mikuyu; 15
naye Bwana akanitwaa, katika kufuatana na kundi; Bwana akaniambia,
Enenda uwatabirie watu wangu Israeli. 16 Basi, sasa
lisikie neno la Bwana; Wewe unasema, Usitabiri juu ya Israeli, wala usitoe neno
lako juu ya nyumba ya Isaka; 17 kwa hiyo, Bwana asema
hivi, Mke wako atakuwa kahaba mjini, na wana wako na binti zako wataanguka kwa
upanga, na shamba lako litagawanywa kwa kamba; na wewe mwenyewe utakufa katika
nchi iliyo najisi; na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali hali ya kufungwa
kutoka nchi yake.
Hitimisho
Mngu aliitamka hukumu yake kwa Israeli na kwa manabii wa
uwongo wanaomtumikia na kumabudu mungu Jua katika Israeli na hukumu itatolewa
juu yao katika Siku za Mwisho pia.
Wakati kwenye sura inayofuatia Mungu
anawambia Amosi mbali ya utawanyiko utakaofanywa na Waashuru ambako anawafananisha
Israeli na kikapu cha matunda wakati wa hari. Huu ni wakati wa mwisho. Ni Maono
ya Nne.
Amosi Sura
ya 8
Haya ndiyo
aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama, kikapu cha matunda ya wakati wa hari. 2 Akaniambia, Amosii, unaona nini? Nikasema, Naona
kikapu cha matunda ya wakati wa hari. Ndipo Bwana akaniambia, Mwisho wao
umewajilia watu wangu Israeli; sitawapita tena kamwe. 3 Tena nyimbo za hekaluni zitakuwa vilio siku ile,
asema Bwana MUNGU; mizoga itakuwa mingi; kila mahali wataitupa, wakinyamaza
kimya.
Endelea na andiko la 8.1
Sasa Mungu anakataa kuwarehem Israeli. Alikuwa amekwisha
liharibu Hekalu la kimwili lakini Zaburi zilikuwa zinaimbwa bado. Miandamo ya
Mwezi Mpya na Sabato zilikuwa zinaadhimishwa kikamilifu na kwa siku sahihi
zilizoagizwa wakati wote wa maisha ya Kristo na hata baadae kidogo hadi wakati
wa kuangamizwa kwa Hekalu. Hawakuwa wamezigeukia au kurudi kwenye maombolezo na
masikitiko au kudhihirisha hadi kwenye Nyakati za Mwisho wakati
Uprotestanti wa Marekani ulipolifanya ibada za kanisa la Waisraeli kuwa ni
kituko kabisa na kufedhehesha na walilupotosha ulimwengu kwa kudhahirisha
kwao. Kile kinachoitwa kuwa Ukristo hawazishiki Sabato wala Miandamo ya Mwezi
Mpya na waka hawazishiki sikukuu isipokuwa sikukuu za mungu Jua, mungu Baali na
Imani za Kisirisiri (soma jarida la Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235)). Zama
za Wasardi za Makanisa ya Mungu iliondolea mbali maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi
Mpya na Sikuku za Pasaka nay a Mkate Usiotiwa Chachu na waliziadhimisha Siku
Takatifu kwenye siku zisizo sahihi wakiambatana na Hilleli nap engine hata
kwenye miei mingine isivyo sahihi iliyofuata utaratibu uliojlikana kama
uahirisho wa Kibabeloni. Kwa ajili hiyo watakwenda kwenye Ufufuo wa Pili wa
Wafu kama itakavyokuwa kwa waliokuwa kwenye zama za Walaodikia.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Yuda pia ambao waligeuza maadhimisho
ya Miandamo ya Mwezi Mpya kuwa mzaha na Siku Takatifu hazikuadhmishwa tena
kabisa kwa siku zake sahihi isipokuwa pale tu ilipoonekana kutokuwa na chaguo
linguine au kwa nasibu tu.
4 Lisikieni hili, ninyi
mnaopenda kuwameza wahitaji, na kuwakomesha maskini wa nchi, 5 mkisema, Mwezi mpya utaondoka lini, tupate kuuza
nafaka? Na sabato nayo, tupate kuandika ngano? Mkiipunguza efa na kuiongeza
shekeli, mkidanganya watu kwa mizani ya udanganyifu; 6 tupate kuwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji
kwa jozi ya viatu; na kuziuza takataka za ngano.
Endelea na andiko la 8.2
Kumbuka pia kuwa udanganyifu juu ya maadhimisho ya
Miandamo ya Mwezi Mpya na Sabato kunaenda sambamba na matuizi ya mizani ya
uwongo na vipimo vya uwongo na kudanganya kwenye utaratibu wao wa mwisho. Hivi
karibuni kulikuwa na tukio la Marekani kuilipa Ujerumani dhahabu feki baada ya
kusababisha Mgogoro wa Kiuchumi au wa Kifedha Ulimwenguni kwenye shirika
linalojulikana kama Fraudulent Collateralised Debt Obligations
(CDOs).
Mngu hauvumilii mwenendo huu (sawa na Walawi 19:35nk; Kumbukumbu
ka Torati 25:13nk; Mithali 20:10). Hii efa ni kama kipimo cha magaloni
manane.
Ona sasa kwamba Mungu wa Israeli amesema kuhusu kile atakachowafanya
wao. Hii ni katika Siku za Mwisho kwenye siku iliyo karibu sana kabisa. Kama
Israeli hawatatubu watakuwa kwa wingi na Mungu hatawasaza.
7 Bwana ameapa kwa fahari
ya Yakobo, Hakika sitazisahau kamwe kazi zao hata mojawapo. 8 Kwa ajili ya hayo, je! Haitatetemeka nchi, na
kuomboleza kila mtu akaaye ndani yake? Naam, itainuka yote pia kama huo Mto;
nayo itataabika na kupwa tena kama Mto wa Misri. 9 Tena
itakuwa siku hiyo, asema Bwana MUNGU, nitalifanya jua litue wakati wa adhuhuri,
nami nitaitia nchi giza wakati wa nuru ya mchana. 10 Nami nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo, na
nyimbo zenu zote kuwa vilio; nami nitatia nguo za magunia katika viuno vyote,
na upaa katika kila kichwa; nami nitayafanya haya kuwa kama maombolezo kwa
ajili ya mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
Endelea na andiko la 8.3
Jambo hili litafanyika katika nyakati za mwisho wakati
watu hawataweza kuyasikia maneno ya Mungu Aliyehai kutoka kwenye midomo au
vinywa vya watumishi wahudumuo kwenye Makanisa ya Mungu vya manabii watatu wa
mwisho (Yeremia. 4:15-16; Ufunuo 11:3-14) atawashughulikia kama Mungu
anavyoelekeza. Hii ni njaa ya kulikosa Neno la Mungu ambayo imekuweko kwenye
karne iliyopita na makuhani wanapimwa na kuhukumiwa kwa hili. Makasisi wote wa
ibada za Jumapili za Baali wanakaribiwa kupatilizwa na kuangamizwa. Na wale
wanaowafuata nyuma yao watakumbwa na maafa hayohayo.
Kupatwa kwa jua kulikotokea tarehe 15 Juni 763 KK kunadhaniwa
kuwa kulichukuliwa kama taarifa ya ukweli huu (sawa na kitabu cha Soncino n.
to v. 9).
Upara unaotajwa kwenye aya ya 10 ni mfano wa matendo ya
kipagani huko Uarabuni na Ugiriki ya kunyoa usoni mbele na kuziacha nywele
kaburini kama kufanya agano kati ya walihai na waliokufa hapa imekemewa na
Mungu kuwa ni jambo linalostahili hukumu. Kifo cha mtoto wa pekee ni jambo
lenye kutia uchungu sana kwa wenzi waliofiwa walitaabishwa nalo mno katika siku
za kale (sawa na Yeremia 6:26; Zekaria 12:10).
11 Angalia, siku zinakuja,
asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula,
wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana. 12 Nao watatanga-tanga toka bahari hata bahari; na
toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huko
na huko, kulitafuta neno la Bwana, wasilione. 13 Siku
hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kwa kiu. 14 Na hao waapao kwa dhambi ya Samaria, na kusema,
Kama aishivyo Mungu wako, Ee Dani, na, Kama iishivyo njia ya Beer-sheba, hao
nao wataanguka, wasiinuke tena.
Endelea na andiko la 8.4
Dhambi au chukizo (Ashemathi) wa Samaria: Ni neno
lililotumiwa kuelezea dhambi na kuwa ilikuwa ni ugeuzaji au upotoshaji wa
makusudi wa neno Ashima jina la
Mungumke wa Waashuru waliomuiga na kumfanya Mungu Mke wa dini ya waabudu Baali (sawa
na kwenye 2Wafalme 17:30). Ametajwa kwenye gombo la Papyri lililogunduliwa huko
Elephantine na baadhi ya mamlaka ya marabi inaijumuisha hii na Ndaa wa Dhahabu
aliyetengenezwa na kutolewa na Yeroboamu 1. Mungu wako Ee Dani inammaanisha
ndama wa Dhahabu aliyesimamishwa huko (1Wafalme 12:29). Huyu Mngu Mwezi aliyeitwa
pia Sini na wa Dini potofu za Jua bado zinaushawishi kwa Israeli katika Siku za
Mwisho
Andiko linalosema: Kama njia ya Beersheba iishivyo linammana
ya wageni wasafiri au wahujaji wanaokenda kuhiji kwenye hekalu za sanamu
hususan kwenye ibada za Juan a Dini za Sirisiri. Ibada hizi zinafanyika
ulimwenguni kote kwenye zama zote za kudumu kwake dini ya Kiislamu hadi siku
hii ya leo wakiapa na kuweka nadhiri wakiwa
niani kuelekea Maka (G. A. Smith).
Hitimisho
Hakuna hata mmoja kati ya watu hawa atafutaye maarifa
kutoka kwa makuhani na manabii wao wa uwongo watajifunza na kutubu na kuwa hai.
Ni kwa kuwaondoa tu makuhani hawa wa dini za waabudu Jua ndipo tutaishi.
Mungu amesema kuwa hakuna hata mmoja wao atakayeiepuka
hukumu. Mifumo yao itaangamizwa na watu wake watauawa kwa upanga. Hawataweza
kujiepusha.
Tunaelekea mbele kwenye maangamizo ya
wisho kwenye sura inayofuatia. Maono ya Tano ni Hukumu ya Mungu kwa Israeli.
Amosi Sura
ya 9
Nalimwona Bwana akisimama karibu na madhabahu;
akasema, vipigo vichwa vya nguzo, hata vizingiti vitikisike; vivunje vipande
vipande juu ya kichwa cha kila mmoja wao; nami nitamwua mtu wa mwisho wao kwa
upanga; hapana hata mmoja wao atakayekimbia, wala hataokoka hata mmoja wao.
Endelea na
andiko la 9.1
Watachimba mashimo ya kutorokea ya
kujificha ili kujilinda kwenye miamba ardhini lakini hawatajiokoa. Hili ni
fungu la kwenye Ufunuo linaloonyesha kuwa wafalme wa dunia hujificha mapangoni
na kutafuta kujiepusha hasira ya Mungu wakati atakapokuja Masihi, lakini
hawataweza kujiepusha. Hawatakuwa na mahali pa kujificha.
2
Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu
utawatoa huko; nao wajapopanda hata mbinguni, nitawatelemsha toka huko. 3 Nao wajapojificha katika kilele cha Karmeli, nitawatafuta
na kuwatoa toka huko; na wajapositirika katika vilindi vya bahari nisiwaone,
nitamwagiza joka huko, naye atawauma.
Endelea na
andiko la 9.2
Kumbuka kuwa hata kwenye utumwa utakaokuja
kwenye Siku za Mwisho hawatawea kujiepusha. Kuna njia moja tu nayo ni kutubu na
kuliitia jina la Mungu na kuzitii Amri na Sheria zake. Hawatakuwa na namna ya
kujiepusha.
Kila mtu anayetamani kuingia kwenye
utawala wa Milenia watakuwa wametubu na kubatizwa na kuzishika Sabato, Miandamo
ya Mwezi Mpya na Sikukuu zilizoamriwa na Mungu.
Hakuna hata mmoja ajitoaye na kuwa
mshirika wa dini za waabudu Jua atakayebakia hai kama hatatubu.
Kuitaja kwake Karmeli kunaonyesha
ukweli wa kwamba ulikuwa ni mlima mrefu (wa takriban futi 1800) iliyojizinga kwenye
mawe ya chokaa yaliyopindapinda kama joka inayozidi tarakimu 2000 na katika
siku za Strabo ambao waliishi na waporaji au wanyang’anyi au waporaji
waliojificha mapangoni na miituni (soma kitabu cha Soncino).
Kutoroka kwao na kwenda baharini
kutajinea tu mashambulizi zaidi na Mungu ataweka macho yake juu yao kwa hokum
yao na sio kwa faida.
4
Nao wajapokwenda hali ya kufungwa mbele ya adui
zao, nitauagiza upanga huko, nao utawaua; nami nitawaelekezea macho yangu
niwatende mabaya, wala si mema. 5 Kwa maana Bwana,
MUNGU wa majeshi, ndiye aigusaye nchi, nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani
yake wataomboleza; nayo itainuka yote pia kama Mto, nayo itakupwa tena kama Mto
wa Misri. 6 Yeye ndiye avijengaye vyumba vyake
mbinguni, na kuweka misingi ya kuba yake juu ya nchi; yeye ndiye ayaitaye maji
ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; Bwana ndilo jina lake. 7 Je! Ninyi si kama wana wa Wakushi kwangu mimi, enyi wana
wa Israeli, asema Bwana? Je! Mimi sikuwapandisha Israeli toka nchi ya Misri, na
Wafilisti toka Kaftori, na Washami toka Kiri? 8 Angalieni,
macho ya Bwana MUNGU yanauangalia ufalme wenye dhambi, nami nitauangamiza utoke
juu ya uso wa dunia; lakini sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo, asema Bwana.
9 Kwa maana, angalieni, nitatoa amri, nami nitaipepeta
nyumba ya Israeli katika mataifa yote, kama vile ngano ipepetwavyo katika ungo
lakini hata chembe moja iliyo ndogo haitaanguka chini. 10 Wenye
dhambi wote katika watu wangu watakufa kwa upanga, hao wasemao, Mabaya
hayatatupata nyuma wala mbele.
Endelea na
andiko la 9.3
Ufalme wenye dhambi unaonyssha taifa zima la Israeli na
Yuda. Masalia waliobakia hawatakuwa pamoja na Yuda peke yao bali ni kwa
maangamizi ya Yuda (soma pia aya ya 11).
Punje ya nafaka ya mwisho kwa lugh rahisi ni pebble na
utawanyiko wa watu ni sawa punje ya nafaka kupitia kwenye chekecheke. Siku ya
Bwana ni kipindi cha uadibisho na utakaso.
Kwa hiyo Israeli itachekechwa na wote
walio ndani yake wanaotenda dhamb na wasitubu watakufa. Ni wale tu wote ambao watatubu
watakuwa hai. Kisha ulimwengu utafika na kushuhudia Ufufuo wa Kwanza wa wafu kufanywa
upya kwa Hema au Nyumba ya Daudi. Hii inawataja wana wa Mungu kwenye ufufuo wa
Nyumba ya Daudi kulikoelzwa kwenye Zekaria 12:8 ambayo ni kanisa chini ya Yesu
Kristo, Malaika wa Bwana vichwani mwao.
11 Siku hiyo nitaiinua tena
maskani ya Daudi iliyoanguka, na kuziba mahali palipobomoka; nami nitayainua
magofu yake, na kuyajenga kama siku za kale; 12 wapate
kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yaitwayo kwa jina langu, asema
Bwana, afanyaye hayo.
Endelea na
andiko la 9.4
Masalia ya Edomu wanaotajwa ni Waedom
ambao kwa sasa ni sehemu ya masalia ya Yuda walio katikati ya taifa la Kiyahudi
na mataifa yote yanayotajwa kuwa ni wana wa Isaka ambayo kwayo Israeli
inajulikana. Ndipo Mungu ataifanya upya Israeli. Marejesho haya ni yale
yaliyotajwa kwenye Isaya 65 kwa ukamilifu wake kwenye Ufufuo wa Pili wa Wafu na
pia kwenye Zekaria 14:16-19 kipindi cha Milenia.
13
Angalieni, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo huyo
alimaye atamfikilia avunaye, na yeye akanyagaye zabibu atamfikilia apandaye
mbegu; nayo milima itadondoza divai tamu, na vilima vyote vitayeyuka. 14 Nami nitawarejeza tena watu wangu Israeli waliohamishwa,
nao wataijenga miji iliyoachwa maganjo, na kukaa ndani yake; nao watapanda
mizabibu katika mashamba, na kunywa divai yake; nao watafanyiza bustani, na
kula matunda yake. 15 Nami nitawapanda katika nchi
yao, wala hawatang'olewa tena watoke katika nchi yao niliyowapa, asema Bwana,
Mungu wako.
Hitimisho
Kwa hiyo kutoka kurudi kwa Masihi,
Israeli na Yuda watachekechwa kama ngano. Watahukumiwa na kufanywa wapya na
kurkebishwa.
Watakatifu wataunda jamii ya walio
kwenye nyumba ya Daudi kama ilivyokuwa huko Sayuni kabla ya kujengwa kwa Hekalu
la Sulemani wakiwakilisha aswira ya wateule watakaokuwa kwenye Ufufu wa Kwanza
wa Wafu na Hekalu likiwa ni Mji wote wa Mungu.
Wanadamu pamoja na Malaika watakatifu
ndio wataunda misingi ya Mji wa Mungu na ambao utafanyika kuwa Bustani ya Edeni
iakayorurishwa tena kwenye kipindi hiki cha Milenia na Ufufuo wa Kwanza wa Wafu.
Maandiko
kwenye lugha ya Kiebrania kwenye maandiko asilia
Manabii Yeremia na Ezekieli walilitumia
jina la Mungu Yahovih (SHD 3069) ambalo linamaana ya Mungu Mmoja wa
Pekee na wa Kweli, Eloah kama Ha Elohim. Linasomwa na Marabi kama Elohim na
sio Adonai. Kamusi ya Strong inafanya maaana hii muhimu kwenye kamusi yake
ya Exhaustive Concordance kwenye rejea ya 3068 Yahovah na
3069 Yahovih. Kuna viumbe wawili au watatu.
Amosi anaendelea kuliitia jina hili
muhimu wakati kwamba wenzake wengine miongoni mwa hawa manabii kumi na mbili
wanatumia tu 3069 kwenye Mika 1:2; Sefania 1:7 na Zekaria 9:14. Kwenye uandishi
wa nabii Zekaria neno Yahova Sabaiothi linatumka mara 44 kwenye sura za 1-8
na mara tisa kwenye sura za 9-14 ambako ni Yahova Sabaiothi anayenena
na ameonekana kwenye unabii wa Zekaria.
Kwenye Amosi, neno Yahovih kwa
kumtaja Mungu Mmoja wa Kweli limetumika mara 22: kwenye Amosi 1:8; 3:7,8,11,13;
4:2,5; 5:3; 6:8; 7:1,2,4,4,5,6; 8:1,3,9,11; 9:5,8,15. Mifano mingine iliyotumia
neno hili elohim kumtaja Mungu wa Majeshi na kwa elohim kwa
ujmla.
Kutumiwa kwa Yahovih mara 22 ni tarakimu
ya ukamilifu na inamtaja Mungu Mmoja wa Kweli peke yake na ni mhuri wa unabii
unaoanza kushika kas kuelekea kwenye Siku za Mwisho. Jina Elohimu linatumika
mara 11, likiashira mchakato wa kutokamilika kuhusu elohimu na uumbaji wa
Mungu, ambapo unabii umekamilika na kuishia kwenye mchakato kuelekea Siku za
Mwisho. Kwa kulinganisha: matumizi ya neno elohimu mara 11 na lilitafsiriwa
Mungu kwenye kamusi ya SHD 410 linaonekana mara moja tu kwenye kitabu cha Micah
na Yahovih linatumika mra moja tu. Yahova limetumika mara 37 kwenye
uandishi huo na limetafsiriwa Bwana kwenye kamusi ya SHD 136 limetumika mara
mbili na maneno mengine kuwa Bwana wa Hekalu na Bwana wa Mungu kwenye SHD 113 limetumika
mara moja kumuita Bwana wa Dunia Yote.
Jina Yahova kwenye 3068 kwenye
kitabu cha Amosi limetumika mara 60 na limetafsiwa kama Bwana. Hii ni tarakimu
ya mpango wa uumbaji iliyozidishwa kama mlolongo wa matukio.
Kwenye SHD 136 linajitokeza mara 25 na
limeungamishwa pamoja na kusomeka Bwana Mungu au Bwana Mungu wa Majeshi.
Tarakimu hizi za mlolongo wa matukio
ni mihuri ya mamlaka au utawala na zinawatofautisha viumbe na unabii na ni
uthibitisho wa mamlaka ya maandiko.
Inaonyesha pia kwamba watafsiri walijua
kuwa kwenye SHD 3069 Yahovih alikuwa ni Mungu Mmoja wa Kweli na
walilitafsiri hili kwa namna hiyo na kuita Yahova kama ilivyo kwenye viabishi.
Hii inaonyesha kushindwa kuonyesha
busara kwa kumuita hivyo Mungu kwa namna ya kama Yahwe kuwa ni kama jina
lisilokuwepo kwenye lugha ya Kiebrania na halina maana mengine kutoka kwenye
maneno halisia ya maandiko.
Tutafafanua kwa kina mambo mengine
kwenye vitabu vya Hosea na Mika.
************
Maandiko ya Bullinger
kutoka kwenye tafsiri ya the Companion Bible ni kama ifuatavyo:
Amosi 1:1
JINA LA CHEO. Maneno ya
Amosi. Lakini maneno ya Yahova kwa Amosi. Soma 1:3.
Amosi = Mzigo.
herdmen = wachungaji. Kwa Kiebrania nokdim; linaitwa
hivyo kutokana na ufugaji wa kipekee wa kondoo wa fusi (wenye sufi nzuri). Mesha uliitwa nakshi,
ikijlikana kama "bwana wa kondoo" (2Wafalme 3:4). Soma Nyongeza 54. Linatokea
sehemu hizi mbili pekee. Lakini Amosi alikuwa mfugaji, kama inavyoonekana wazi
kwenye 7:14; ambapo neno boker linatokana
na neno bakar, yaani
maksai wa ng’ombe, na kwa hiyo linahusiana na kazi yake ya kulima au kukatua ardhi
(1Wafalme 19:19, 21, nk.) Soma andiko kwenye 7:14.
Tekoa. Sasa unaitwa Khan Telkua, ni
umbali wa maili tano kusini kwa Bethlehemu, na maili kumi kutoka Yerusalemu. Linganisha
na 2Samweli14:2. 2Nyakati 20:20.
ambayo = ambayo [maneno].
aliona = aliona [kwenye maono]. Linganisha na Hesabu
24:4, 16. Isaya 30:10. Ezekieli 12:27.
Israeli. Hili
linatupa sisi kichwa cha somo la kitabu. Katika siku za. Linganisha na Hosea 1:1.
Yeroboamu. Soma 7:10.
Miaka miwili kabla ya tetemeko la
ardhi: yaani kabla ya lile moja linalojulikana sana na kukumbukwa. Linganisha
na Zekaria 14:5.
Tetemeko la ardhi. Kwa lugha ya fumbo
ya Hysteresis.
Nyongeza 6.
Amosi 1:2
BWANA. Kwa Kiebrania Yahova Nyongeza 4. Jina
hili si la mtu wa kawaida kwenye kitabu hiki.
unguruma = unguruma kama samba, au radi.
Ni kilamara, wakati lilipomtabiri Bwana, liliunganisha na utimlifu wa utawala
au zama za Wamataifa. Linganisha na Yeremia 25:30, Yoeli 3:16.
tamka = toa maneno.
makazi = malisho.
wachungani. Si neno moja
na lililo kwenye 1:1, lakini ni neno la kawaida (raah = walishaji).
Kilele cha Mlima Karmeli. Mlima Karmeli
ulio kaskazini, ambao unaitamalaki nchi yote; sasa ni Yebel Kurmuli; sio
Karmeli iliyopo Yuda (kusini mwa Hebroni); sasa ni el Kurmul. Linganisha
na 1Samweli 25:2. Isaya 33:9.
kame = nchi kame.
Amosi 1:3
Asema BWANA. Maneno ya Yahova: sio maneno
ya Amosi. Utaratibu wa kinabii. Tazama sehem ya Nyongeza 82. Soma habari za
hawa kumi na mbili na Yahova, kwenye aya za 3:6, 9, 11, 13; 2:1, 4, 6; 8:12; 5:4; 16;
7:17; na wawili na Adonai Yahova kwenye 3:11; 5:3.
watatu . . . wanne. Usemi wa Kiebrania
kwa kuelezea idadi kadhaa, au wengi (Ayubu 33:29, soma bango kitita) Linganisha
na Mithali 30:15, 18, 21, 29.
Kutenda maovu. Kwa Kiebrania pasha. Nyongeza
44.
geuza = kirudishe nyuma, au kipindishe,
pitisha hukumu ju yao. Hakuna Ellipsis iliyotolewa,
na haitenganishwi kwa ilivyo kwenye neno la Kiebrania la “uso”. Kwa Kiebrania ni lo' ashibennu, Sitasababisha
ligeuke na kurudi: yaani Sitaligeuza.
Pronauni ya “hiki” ni ya kume, ikikubaliana
na kutajwa kwa tukio la tetemeko la ardhi (aya ya 1), na linamaanisha Yahova ambaye lilibakia
lilivyo bila kuligeuka. Kwa hiyo lilionekana kwenye maeneo yote
manane (aya za 3:6, 9, 11, 13; 2:1, 4, 6).
Kupigwa vibaya kwa Gileadi. Linganisha
na Yoeli 8:14. Ni neno hilohilo lililotumika kwenye 2Wafalme 13:7.
Pamoja na = [kama ilivyokuwa] kwenye
Lugha Fumbo ya Hypocatastasis. Nyongeza 6.
Amosi 1:4
Nitauleta moto. Linganisha na 1:7, 10,
12; 2:2, 5. Rejea kwenye Yeremia 17:27; 49:27; 50:32. Hosea 8:14.
Hazaeli. Linganisha na 2Wafalme 8:12; 10:32,
33; 13:3.
Ikulu: au ngome. Kwa Kiebrania 'armon. Limetokea (kwa
uwingi) mara kumi na mbili kwenye kitabu cha Amosi (soma Nyongeza 10): 1:4, 7,
10, 12, 14; 2:2, 5; 3:9, 10, 11; 6:8; mara saba na vebu ya "fakamia"
(Kwa Kiebrania akal).
Ben-hadadi. Ni jina la
cheo la kiofisi la Wafalme wa Ashuru = mwana wa Hadadi, yaani
mngu jua. Ben-hadad
wa kwenye 2Wafalme 13:3; sio wa kwenye 2Wafalme 8:7-15.
Amosi 1:5
Mche. Kumbuka lugha ya Mfano ya Metalepsis (Nyongeza
6), kwa jinsi neno hili "mche" lilivyowekwa kwenye Lugha Fumbo ya Metalepsis, Nyongeza
6, kwa malango, na kisha malango yaliwekwa kwa ulinzi wa mji. Linganisha na
Kumbukumbu la Torati 3:5. 1Wafalme 4:13. Yeremia 51:30. Maombolezo 2:9.
Wakazi: au, mtu aliyeketi, yaani
mtawala, mwenye kushabihiana na andiko la kwenye mstari.
Avon. Sawa na Beth-aveni, mashariki
mwa Beth-eli, unaokaliwa na kabila la Benjamin. Linganisha na Hosea 4:15; 5:8;
10:5, 8.
Nyumba ya Edeni = Beth-edeni.
Kir. Kama ilivyo kwenye 9:7, 2Wafalme 16:9. Isaya
22:6.
Amosi 1:6
Gaza (Ghuzzeh), iko Ufilisti.
Utumwa wote = kuuzwa utumwani.
utumwani = watumwa au mateka. Imewekwa
kwa Lugha ya Kimafumbo ya Metonymy (ya Muunganisho), Nyongeza 6, kwa
kundi lote la watumwa. Soma Yeremia 13:19. Linganisha na Yeremia 47:1. 2Nyakati
21:16, 17; 28:17.
Amosi 1:7
Ukutal. Imewekwa kwa lugha ya Mfanp ya Synecdoche (ya Kundi au
Sehem), nyongeza 6, kwa mji wote.
Amos 1:8
Ashdodi. Baadae uliitwa na Wayunani
jina la, "Azoto".
Sasa unaitwa Escludi, kwenye
uwanda au nchi ya Wafilisti, uko maili thelathini na tano kaskazini mwa Gaza.
Ashkeloni. Sasa unaitwa 'Askalan, upande
wa pwani mwa Ufilisti.
Ekroni. Baadae, Wayunani waliuita "Accaron" (1 Wamakabayo
10.89), kwa sasa unaitwa 'Akiri, uko maili sita magharibi ya Gezeri. Huko
"Gezeri "soma maandiko ya Bullinger kwenye 1Wafalme
9:15-17.
Asema = amesema.
Bwana MUNGU. Kwa Kiebrania Adonai Yehova.
Nyongeza 4. na II. Cheo na Jina hili la Kimungu linatokea mara ishirini na moja
(7 x 3. Soma Nyongeza 10) kwenye kitabu hiki (1:8, 3, 7, 8, 11, 13; 4:2, 5;
5:3; 6:8; 7:1-6; 8:1, 3, 9, 11; 9:5, 8). Kwa hiyo "hivi ndivyo asemavyo Adonai Yehova"
Soma 3:11.
Amosi 1:11
Edomu. Linganisha Isaya 21:11; 34:5. Yeremia
49:8, nk. Ezekieli
25:12-14; Ezekieli
35:2. Yoeli
3:19; Obadia 1:1. Malaki 1:4.
Kwa kuwa, nk. Rejea kwenye Torati (Mwanzo
27:41. Linganisha na Kumbukumbu la Torati 23:7). (sawa na Linganisha tafsiri ya
Companion Bible, Nyingeza 92. Linganisha na Malaki 1:2.
Ndugu yake. Rejea kwenye Torati (Mwanzo
25:24-26).
Tawanya milele: au, tawanya [mawindo
yake] milele. Ginsburg anadhani = aliishikilia kwa
kinyongo chake. Linganisha na 2Nyakati 28:17.
Yeye. Kamusi ya 1611 toleo la A.V. linaruka
neno hili la "yeye".
Amosi 1:12
Temani. Linganisha na Yeremia 49:7.
Obadia 1:9. Habakuki
3:3. Elifazi
alikuwa Mtemani (Ayubu 2:11, nk.)
Bozra; Sasa unaitwa el Buseirah, uko
kusini mashariki mwa Bahari ya Chumvi.
Amosi 1:13
Watoto = wana.
Amoni. Linganisha na 1Saya 11:1.
Raruka au pasuka, nk. Ilitabiriwa
kwenye Hosea 13:16.
2Wafalme 8:12; 15, 16.
Kwamba wasiweze kufanya, nk. Linganisha
na Yeremia 49:1.
14 Rabba. Kwa sasa
unaitwa 'Amman (upo kwenye nyanda
za juu ya Gileadi), "mji wa maji mengi", upo maili ishirini na tano
kaskazini mwa Bahari ya Chumvi linganisha na 2Samweli 11:1, na 2Samweli 12:26,
27. Yeremia 49:2. Rejea kwenye Torati (Kumbukumbu la Torati 3:10, 11). Nyongeza
92.
Piga kelele au mayowe = kilio cha vita
ku.
Siku ya mapigano au ya vita: yaani
siku ya mashambulizi ya makelele na mizomeo ya maadui zao.
Amosi 1:15
Yeye. Ginsburg anadhani hivyo = makuhani
wake, pamoja na kwenye tafsiri ya Septuagint.
(sawa na tafsiri ya Companion
Bible).
Mfalme wao (Malkamu). Ni konsonanti
hizohizo yenye viwango mbalimbali vya vaweli vinavyompa Milcomu mungu wa Waamoni (1Wafalme
11:5). Hii inadaiwa mno kukusudia kuionyesha sera ya watawala wao kwenye uwakilishi
wake lakini inauonyesha mfumo wake wote wa kidini wa watu hawa (sawa na Soncino).
Amosi 2:1
Burnedi ...ndimu. ndimu. Kwa hiyo
inathibitisha mahali ambapo Wamoabi ambao hawakuruhusu au kuwaacha wafu
kupumzika na walihukumiwa hapa kwa kuwa waliichomwa moto mifupa ya Mfalme wa Edom
(adui wa Israeli) kunasa au mnaso. Kwa hiyo hukumu hii hapa kwenye kitabu cha
Amosi inaonyesha tabia ya kutopendelea ya Mungu kwenye mambo yahusuyo hokumu kwa
makabila haya.
Amosi 2:2
Kiriothi: maana yake nyingine ni., miji yake. Sasa
unaitwa el Kureiyat, au
Kiraiathaimu, ulio
katikati ya Diboni na Medeba. (sawa
na Yeremia 48:24) Umetajwa na Mesha kwenye Jiwe la Wamoabu. (Soma
tafsiri ya Companion Bible, Nyongeza 54.) Makao Makuu ya ibada na dini ya
Kemoshi.
Kupiga kelele = kilio au kelele za vita.
Linganisha na 1:14
Tarumbeta au baragumu. Kwa Kiebrania, shofar.
Amosi 2:3
Mwamuzi = mtawala (fimbo ya mfalme-anayeshika
fimbo hiyo; Hesabu 24:17)
Amosi 2:6
Waliuza.
Rejea kwenye Torati. (Walawi 25:39. Kumbukumbu la Torati 15:12). Companion
Bible, Ngoneza 92, Myahudi atajiuza mwenyewe, lakini sio
ndugu yake au sio amdaiwa aliyefilisika au asiye na uwezo wa kulipa (2Wafalme
4:1; Nehemia 5:5),
Mtakatifu
na mwenye haki = mtu wa haki na mtakatifu.
Maskini =
mwenye uhitaji. Kwa Kiebrania ni ebyon. (sawa
pia na Mithali 6:11).
Pea moja ya vitu. Imewekwa kwa lugha
ya Mfanp ya Metonymy (ya
Kiunganishi), soma kwenye Companio Bible, Nyongeza 6, kwa
hatimiliki ya zile zilizoelezewa (linganisha na Ruthu 4:7).
Amosi 2:7
Anguka = vunjiko. Kwa Kiebrania shaaph, Na
hii Homonymyn, maana
yake ni (1) ni mshituko au inayotamani (Ayubu 7:2; 36:20, Zaburi 119:131. Mhubiri 1:5. Yeremia 2:24);
(2) kugonga (kama shuph kwenye Mwanzo 3:15 Ikimaanisha "kumeza
yote" kwenye 8:4. Ayubu 5:5. Zaburi 56:1, 2; 57:3. Ezekieli 36:3. Kwa hiyo
hapa ni = kugonga. Soma kamzi ya Oxford Gesenius, ukurasa
983, vol. 2. Inasema "gonga kichwa cha mtu maskini kwenye mavumbi ya nchi".
Maskini = zenye kusababisha umaskini. Kwa
kiambishi cha Kiebrania (uwingi) Tazama neno “umaskini”, Mithali 6:11. Sio neno moja
na lile la kwenye 2:6.
Geuka na kuacha = geuza njia yao yote.
Mpole = wapole, kwa Kiebrania ni
uwingi wa `ani, Soma
andiko kwenye "ufukara", Mithali 6:11
Mtu mwanaume. Kwa Kiebrania 'ish. Nyongeza
14.
Na baba yake. Hii ilifanyika kenye
ibada za sanamu za Wakanaani, na wanawake waliohudumu mahekaluni, walioitwa Kadeshoth (uke) na Kadeshhim (uume)
kijana = mtu kijana (mwanaume au
mwanamke). Aliitwa hivyo kutokana na nguvu zake au makeke ya kiujana.
Kutia unajisi au kukufuru, nk. Hii
inafanya matokeo, na sio makusudio, na inaonesha machukizo/enormity ya dhambi machoni pa Yahova. Rejea
kwenye Torati, (Walawi 18:21; 20:3). (sawa na Companion Bible, Nyongeza
92). Linganisha na Isaya 48:11. Ezekieli 20:9, 14; 36:20-23, Warumi 2:24. 1Wakorintho
5:1.
Takatifu. Soma andiko la Kutoka 3:5.
Amosi 2:8
Wanajishusha chini wenyewe, nk. Rejea
kwenye Torati (Kutoka 22:26. Kumbukumbu la Torati 24:12), (sawa na Comp. Bible, Nyongeza
92). Kila madhabahu. Dhambi iliyowekwa kwa kweli ilikuwa ni sheria ya madhabahu
moja na ilijlikana kuwa ni kama amri ya zamani pamoja na sheria inayohusiana na
marejesho mapya ya mavazi ya mnadhiri.
Mvinyo, kwa Kibrania Yayin. Linganisha na Comp.
Bible, Nyongeza 27.Mimi
na jarida la Mvinyo Kwenye Biblia (Na. 188).
Wa waliokatazwa: au mvinyo
uliokubalika.
Amosi 2:9
Tena. Baraka za zamani zinatamkwa ili
kuonyesha au kukuza uovu wa uasi wao mara tano. Waamoni Rejea kwenye Torati (Hesabu
21:24. Kumbukumbu la Torati 2:32-34). (sawa na Comp. Bible, Nyongeza
92). Linganisha na Yoshua 24:8. Hawa ni wa uzao wa Wanefili walikusudiwa
kuangamizwa wote, ambao na mataifa meingine ya Wakanaani, waliangamizwa kwa
upanga wa Israeli. (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 23 na Nyongeza 25).
Wao. Maandiko fulani, zenye matoleo
yaliyochapishwa zamani, inasomeka “wewe”.
Urefu. Rejea kwenye Torati (Hesabu
21:24. Kumbukumbu
la Torati 2:32-34). (sawa na Comp. Bible, Nyongeza
92).
Amosi 2:11
Niliikuza, nk. Sio mpaka makuhani
waliposhindwa kwenye huduma yao ya kufundisha torati. Soma Walawi 10:8, 11. Kumbukumbu
la Torati 33:8, 10. Manabii hawakupewa hadhi ya Unazarayo hapo mwanzoni; Rejea kwenye
Torati (Hesabu 6:2). (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 92.
Sivyo . . . ? Neno la Mfano la Erotesis. Nyongeza
6.
Watoto = wana.
Asema Bwana = [ni] mjumbe wa Yahova.
Amosi 2:16
Ujasiri au uhodari = kuwa na ujasiri
moyoni (sawa na Comp.
Bible, Nyongeza 92).
Kuwa uchi: au, kutovaa silaha ya
kujikinga.
(sawa na Bullinger, Companion Bible.)
Amosi 3:1
BWANA. Kwa
Kiebrania Yahova.
Watoto = wana.
Gombo nyingine zenye nakala za maandiko yaliyochapishwa zamani sana, za lugha
za Kiaram, Kiseptuagint zinasomeka “nyumba”. Aitha, usomekaji huu unaonyesha
kuwa sura hizi zinahusiana na taifa la makabila kumi na mbili.
Niliwatoa
na kuwaleta, nk. Rejea kwenye Torati (Kutoka 12:51, nk.)
Ni ninyi tu ninaowajua, nk. Soma Mpangilio wahe hapo juu.
Rejea kwenye Torati (Kumbukumbu la Torati 7:6). (sawa
na Comp.
Bible, Nyongeza 92; sawa na Zaburi 147:19, 20.)
Dunia = ardhi. Kwa Kiebrania addamah.
Kukusukuma = kukutembelea, kama ilivyo
kwenye 3:14. Rejea kwenye Torati (Kutoka 32:34). (linganisha na Comp. Bible, Nyongeza
92)
Maovu au machukizo. Kwa Kiebrania `avah. (sawa na Comp.
Bible, Nyongeza 44).
Amosi 3:3
Yawezekana watu wawili . . . ? Lugha
ya Kimfano ya Erotesis (kwa
kinyume. Kuimarisha au uimarishaji). Nyongeza 6. Huu ni mfano wa kwanza kati ya
mitano. Jibu la kila swali ni ushuhuda unaojishuhudia wenyewe. Kukubaliwa = wamekutanika
pamoja kwa ahadi [ya muda na (mahali].
Amosi 3:6
Itakuwa . . . ? Kwa lugha ya Mfano ya Erotesis. (sawa
na Comp Bible, Ap. 6).
Tarumbeta au baragum. Kwa Kiebrania shofa.
Msiogope = msikimbie pamoja.
Ovu = maafa, kama ilivyo kwenye 5:13. Zaburi
141:5.
Kwa Kiebrania ra'a'. = ovu:
isiyoshika maadili, ovu, lakini uovu unabidi kuadhibiwa, (kama ilivyo kwenye
5:13. Isaya 45:7. Yeremia 18:11. Maombolezo 3:38).
Na BWANA hajatenda hili? Kwa maana ya
kweli ya neno “uovu” Bullinger haoni kuwa hakuna sababu ya kufankwenye lugha ya
Kiebrania ili kuutetea utakatifu au haki ya Yahova ya kushughulika nao.
imefanyika = imeteseka.
Amosi 3:8
Samba ameunguruma. Lugha
ya Mfano ya Hypocatastasis (kama
ilivyo kwenye Comp.
Bible, Nyongeza 6).
Bwana MNGU amesema. Lugha ya Mfano ya Hermeneia (sawa
na ilivyo pia
kwenye Nyongeza 6 ibid). Kuelezea kwa lugha ya Mfano ya Hypocatastasis. Kwenye
mstari uliotangulia kabla yake.
Ni nani awezaye zaidi ya kutoa unabii?
Lugha ya Mfano ya Erotesis. (sawa na
Nyongeza 6 ibid). Wakosoaji wengine wa siku hizi wameibadili maana halisi ya
Kiebrania na kuiandika kuwa “kutishwa”, wasijue kwamba ni kwa nia ya unabii
ndipo Mungu huongea na watu wake (Waebrania 1:1).
Amosi 3:12
Anachukua = anaopoa au kuokoa kutoka
hatarini, kama kitu kipya na kizuri kilichoopolewa kutoka kwenye
muunguzo wa moto.
Kipande kimoja = safari au msafara.
Kwenye kochi au kiti kikubwa cha
kisasa = [kuwa taabani kwa ugonjwa wa] kulala yaani kuwa kwenye raha mstarehe
burudanini. Linganisha na 6:1-4. Ellipsis (ya Marudio). (sawa sawa na Nyongeza
6, ibid).
Amosi 4:3
Ng’ombe, yaani mwanamke.
Kwa hiyo ambayo ni kabla ya yake = kila
mwanamke kwa uvunjaji [kwenye ukuta wa Samaria].
Kabla yake, yaani pasipo kubadilika
kwenye mkono wa kushoto au kume. Linganisha na Yoshua 6:5, 20.
Atammuweka kwenye jumba la kifalme. Jumba
la Kifalme au Ikulu kwa Kiebrania ni harmon (tazama kwenye
andiko la 1:4). Hapa ni kwamba Ha-Harmonah, linalounda
neno la Kimafumbo la Paronomasia (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 6) pamoja
na 'arman (3:11). Kiambishi
hiki yabidi kitafsiriwe kwa 3:11, 12, na 5:27, na kwa hiyo ingepasa lisomeke:
"utatupwa mbele kuelekea Ha-Harmon". Mahali
hapajulikani, ila yaweza kumaanisha "enyi wanawake mliotulia kwenye
majumba yenu ya fahari" (arman, 3:11, 12) mtatolewa na kupelekwa
huko Ha-Harmonah: utumwani.
Andiko hili si lazima “likanganywe” kwa kuwa haitufanyi tujue mahali lilipokusudiwa
jina hilo.
Amosi 4:4
Njooni Beth-eli, nk. Hapa tuna
mwongozo wa Kimungu, kana kwamba inamaanisha “kijazeni kikombe cha uovu wenu".
Linganisha na Mathayo 23:32.
Potosha au tia unajisi . . . upotoshaji
au utiaji unajisi. Kwa Kiebrania pasha'. Nyongeza
44.
Beth-eli . . . Gilgali. Linganisha
na 3:14; 5:5; Hosea 4:15;
9:15; 12:11.
Baada ya miaka mitatu. Mrejesho wake
upo kwenye Torati (Hesabu 28:3. Kumbukumbu la Torati 14:28), (Nyongeza 92
ibid); sio kwenye "siku", au "mahujaji walio kwenye Umma wa Mohammedi".
Amosi 4:7
Mvua kubwa za masika hinyesha kutoka
mwishoni mwa mwezi Oktoba hadi mwishoni mwa mwezi Februari. “Mvua inayofuatia
Baadae” hunyesha mwezi Marchi na Aprili.
Miezi mitatu ya kuendea majira ya
mavuno ndio watati ambao ardhi inaahitaji nvua kwa siasi kikubwa. Kukuza jambo huku
kunafaanyika inapokuwa hakuhitajiki sana na haufanyiki wakati unapohitajika
sana.
Amosi 4:9
Kwa nini wanajenga au kulima bustani
wakati wanataka kuangamia wote.
Neno Hija
au Uhujaji limetajwa pia kwenye Yoeli 1:4.
Amosi 4:10
Njia ya
Misri ni bota zaidi kwa maana au
jinsi ya Misri (sawa na Isaya
10:24,26) na ni
vibaya sana kama ilivyo Misri (sawa na Kutoka 9:3nk).
Amosi 4:12
Andaeni kukutsns nsye, nk, yaani
kwenye hukumu. Sawa na ilivyo kwenye Ezekieli 13:5; 22:30. Aya za 11 na 12 hazipo
“nje ya nafasi” au ni "uondoaji wa maneno", bali wanalazimishwa au
kuamriwa na Maandiko Matakatifu, "M", (Bullinger, ukurasa wa
1236).
Amosi 5:5
Betheli. Gilgali.
Beer-sheba.
Linganisha na Hosea 4:15; 10:8. Haya yalikuwa ni makazi au vituo vya ibada za
Israeli waabudu sanamu.
Usipite = usipite mbali; ambapo ilikuwa
ilikuwa ni mhimu ili kupata kutoka kaskazini hadi Beer-sheba upande wa kusini.
Linganisha na 4:4; 8:14.
Gilgali kwa
hakika itakwenda utumwani. Kumbuka lugha ya Mfano ya Paronomasia (Comp.
Bible, Ap. 6), kwa msisitizo. Kwa Kiebrania Gilgal galoh yigleh = Rola,
inayozinga, litazingilia mbali, yaani kuondolewa kabisa. Hii imesisitizwa kwa lugha
ya Mfano ya Polyptoton (Nyongeza
6).
Amosi 5:15
Chukieni maovu, Linganisha na Zaburi 34:14; 97:10. Warumi
12:9, Hii inajumuisha onyo la mwisho kati ya nasaha tatu.Inaweza kuwa kwa
Kiebrania ‘ulay. Aya yote inajiri na nasaha lakini kwa matamshi ya Kiebrania,
inaiondoa sentensi hii, ikitilia maanani, sio kwa kubahatisha kwa upande wa Yahova, bali kwa magumu ya upande wa Israeli; na utaratibu huu ni kuhamasisha utii
kwa miito. Linganisha na Kutoka 32:30. 2Wafalme 19:4. Yoeli 2:14.
Jina Yusufu. Limewekwa kw lugha ya Mfano ya Synecdoche (kwa
Sehemu), (Nyongeza 6 ibid), kwa sehemu zote za Ufalme wa Kaskazini.
Amosi 5:18
Ole. 0le ya kwanza. Tazama Utaratibu kwa siku ya BWANA (sawa
na jarida la Siku ya Bwana na Nyakati za Mwisho (Na.
192). (Soma maandiko ya Bullinger kuhusu Isaya
2:12; 13:6. Yoeli 2:1.)
Giza, na si nuru. Kumbuka kuwa hii ni lugha ya Mfano ya
aina ya Pleonasm (Nyongeza
6) kwa kukazia. Sawa na Yeremia 30:7. Yoeli 2:2. Sefania 1:15.
Amosi 5:25
Mmetoa sadaka, nk . . . . ? lugha ya Mfano ya Erotesis. Nyongeza
6. Hili ni swali lililo kwenye baadhi ya nakala na matoleo matatu ya machapisho
ya kale, lakini matoleo mengine manne ya nakala zilizochapishwa hapo
zamani, yanasomeka hapa kama usemi imara na thabiti. Kama ni swali, jibu lake
litakuwa ni Hapana. Soma Kumbukumbu la Torati 32:17. Yoshua 5:5-7.
Yeremia 7:22, 23. Ezekieli 20:8, 16, 24.
Kwangu mimi, na Sio “kwa Mashetani". Rejea kwenye
Torati (Walawi 17:7. Kumbukumbu la Torati 32:17). (Nyongeza 92 ibid), (sawa na
Zaburi 106:37. 1Wakorintho 10:7).
Amosi 5:26
Kiuni. Mungu
wa Wamisri na Wayunani sawasawa na alivyokuwa Remphan (kwenye
Septuagint ameandikwa Raiphan; spelingi nyingine imebakizwa kwenye Septuagint
na kwenye Matendo 7:43). Majina halisi yanayotofautiana kila mara kwenye
speling, kwa mfano Ethiopia ni neno la Kiebrania Kushi laweza
kuwa pia na maana ya Kikaldayo; Misri ni Mizraim;
Mesopotamia na Syria ni'Aramu, au 'Aram-naharaim, nk.
Amosi 5:27
Mbele zaidi ya Damascus. Kwenye Matendo 7:43 ng’ambo ya
Babeli, ambalo kulikuwa kwa kweli “ng’ambo ya Damascus", na kulijumuisha
hii, kuoyesha kile lilochokuwa mpando wa Kimngu kwa maneno ya Yahova (aya
ya 27) na Amosi. Zaidi ya yote,, barabara ya kwenda Ashuru ilikuwa inapitia Damascus.
Linganisha na 2Wafalme 15:29; 16:9. Isaya 8:4. 3:12. Mtu mmoja anauliza swali.
Inaweza asiwe Mungu kupitia Roho Mtakatifu aliyenuku na kuiga maneno yake
mwenyewe kama apendavyo?
Amosi 6:1
'Ole. Ole ya pili. Soma kwenye 5:18. Wao, yaani wenye
hekima wa Yuda, kwa kulinganisha na wenye hekima wa Israeli (katika Samaria) kwenye
kifungu kinachofuatia kwenye utulivu na amani = kutojali, linda, au kubali
kirahisi.
Tumainia = tegemea. Kwa Kiebrania ni batah. (sawa
na Nyongeza 69 kinyume cha cha madai).
Hapa Sehemu. = wao waliothibitisha au kuamini.
Ambao wametajwa majina = [wanaume wa] wanaume, sawa na ilivyo
kwenye Hesabu 1:17
Mfalme wa mataifa: yaani Israeli. Rejea kwenye Torati (Kutoka
19:5).(Nyongeza 92 ibid),
Nyumba ya Israeli: yaani Ufalme wa Kaskazini = Watu wa Israeli.
Njooni. Eneza Kimduara
wa umbo la yai: "njooni [kwa ajili ya hukumu na haki]", kama
ilivyoonyeshwa na idadi iliyobakia ya tarakimu hii ("y1").
Amosi 6:10
Mjomba wa mtu = ndugu au jamaa
Yeye, yaani mzoga unaounguzwa motoni. Tazama
ilivyoandikwa kwenye 4:10. Hapa na kwenye 1Samweli 31:12 ni sehem mbili pekee ambapo
uchomaji moto wa maiti umetajwa, nk. Zote mbili ni kesi za aina yake, ila
ilikuwa ni matendo ya kawaida ya Wahiti (Mwanzo 14:6; Kumbukumbu la Torati
2:12, 22) ambako mabaki au masalio yao yanakutikana kwenye kazi ya uchimbuzi wa
mambokale huko Gezeri. Tazama kitabu cha Bullinger na maoni yake kuhusu 1Wafalme
9:15-17.
Mifupa; yaani mtu aliyepunguzwa na kuwa skeleton au
mifupa mitupu. Linganisha na Ayubu 7:15; 19:20.
Yeye aliyeko, nk, aliyeponoka au kupona.
Kwa pande za = katikati ya, au upende unaozuia.
Yeyote, yaani aliyehai au aliyekufa.
Fanya mtajo wa = itia au hiomba dua. Linganisha na Isaya
26:13; 49:1; 62:6.
Amosi 7:9
Mahali pa juu. Palipotumika kwa kujengwa madhabahu za
ibada za sanamu, nk.
Isaka . . . Israeli. Imetumika na Amosi peke yake kwa maana
hii. Imewekwa kwa lugha ya Kimfano ya Metonymy (ya
Kiunganishi), nyongeza ya 6 ibid, kwa taifa la Israeli. Linganisha
na Petro
105:9, 10. Yeremia 33:26, nk.
Nitainuka kinyume, nk. Imetimilika kwenye 2Wafalme 15:10.
Yeroboamu. Sawa na ilivyo kwenye Hosea 1:4.
Amosi 7:10
Kuhani. Kuhani mwongoza ibada za sanamu.
Beth-eli. Linganisha na 3:14; 4:4; 5:5, 6.
Hamasisha = kufanya hila za kuangusha utawala, mapango
yaliyounganishwa na sera ya taifa la Israeli (1Wafalme 12:26-33).
Kwa upande wa katikati, nk: yaani kwa wazi sana.
Linganisha na 7:8.
Vumilia = stahimili.
Amosi 7:11
Yeroboamu atakufa, nk. Mabadiliko haya hayakuwa ya kweli.
Linganisha na Matendo 17:6-7; Matendo 24:5. Zingatia kile alichoacha kukifanyia
toba Amazia.
Amosi 8:3
Hekalu. Toleo la Kamusi ya 1611 la tafsiri ya A.V. inasomeka
mahekalu".
Amosi 8:9
Sababu ya jua. Inaama nyakati za kutimia kwa "mapatilizo"
haya. Soma kwenye Isaya 13:10; 59:9, 10. Yeremia 15:5. Yoeli 2:2; 3:15. Mika
3:6. Yawezekana kuwa hii inamaanisha tetemeko la ardhi la 1:1?
Amosi 9:1
BWANA. Moja ya kamusi hizi za 134 inaliweka jina hili pale
ambapo tafsiri ya Sopherim inasema waligeuza maana ya jina "Yahova" kutoka
kwenye andiko la zama kale na kuandika "Adonai" (Nyongeza
ya 2 ibid). Soma pia kwenye tafsiri ya Comp. Bible, Nyongeza 4. na
II . Hapa inajumuisha na 'eth = Yahova Mwenyewe.
Inategemea upande, au kwayo.
Madhabahu. Huenda ni madhabahu ile ile sawa na ya Beth-ali
ya wakati wa Yeroboamu aliyowahi kjuijenga huko (1Wafalme 13:1). Linganisha na 7:13,
linta = kuu au kubwa. Inasema: "upige mji mku, tingisha misingi yake, ikatilie
mbali [yaani nguzo zake] kwa kichwa, wote miongoni mwao". Na nitawachinja.
Hii ndiyo maana yake tendo hili la mfano.
Neno la mwisho: yaani masalio ya Watu.
Amosi 9:11
Katika siku ile. Kwa kupitia kwenye somo au fundisho la
marejesho mapya yatakaypfanyika siku zijazo na z mwisho (soma jarida la Siku ya Bwana na Nyakati za Mwisho (Na. 192)). Ilinukuu
kutoka kwenye Matendo 15:14-18 kuhusu Daudi. Ilisimamishwa huko Sayuni na Daudi
(2Samweli 6:17. Linganisha na 7:6) kabla halijajengwa Hekalu juu ya Mlima wa
Moria na Sulemani. Mwaka 7:7-9, ulionekana kuwa "nje ya timazi", kwa
hiyo kuwa kwenye nafasi ya kuanguka. Hapa umeanguka chini: kwa hiyo unabii
unabii unatolewa tena hapa. Kwenye Matendo 15 wakati ulikuwa umewasili, na watu
waliuitikia na kuutii wito wa Petro kwenye 3:18-21. Lakini hatimaye ulikataliwa
(Matendo 28:25-28), na unabii huu, kwa hiyo bado unangojea kutimia kwake.
Amosi 9:13
Mtu wa kulima, nk. Hii inaonyesha kuwa utimilifu wa
unabii huu ni bado haukuwa ukitumika, kwa kuwa Baraka hizi za kitambo
ziliahirishwa kwa sababu ya kuukataa kwao wito wa kutubu ulio kwenye Matendo 3:18-26.
Linganisha na Matendo 28:25-58. Kumbuka mrejesho wa Torati (Walawi 26:5). Nyongeza
92 ibid.
Milima, nk. Linganisha na Yoeli 3:18.
Mvinyo mtamu = mvinyo mpya. Kwa Kiebrania asis Soma
jarida la Mvinyo Kwenye Biblia (Na. 188).
Yeyuka, yaani kubobea kwenye unywaji wa mvinyo na
kuyeyushwa kwenye mafuta. Lugha ya Mfano ya Hyperbole (Nyongeza 6), kwa kukazia
au msisitizo.
Amosi 9:15
Nitapanda. Rejea kwenye Torati (Walawi 25:18, 19; 26:5). Nyongeza
92 ibid.
Nchi yao. Rejea kwenye Torati (Mwanzo 13:15, nk.) nyongeza
92 ibid. Linganisha na Isaya 60:21. Yeremia 24:6; 32:41. Ezekieli 34:28; 37:25.
Yoeli 3:20. Mika 4:4.
Hakuna kuvutwa tena. Linganisha na Yeremia 32:41.
Ambayo nimewapa. Hii ni sababu ya Baraka zote. Rejea
kwenye Torati (Hesabu 32:7, 9. Kumbukumbu la Torati 3:18; 26:15; 28:52). Nyongeza
92 ibid. Linganisha na Yoshua 2:6, 15; 18:3; 23:13, 15. Yeremia 25:5. Ile
inayoitwa “Gombo la ‘Makuhani’”, kwa mujibu wa wakosoaji wa siku hizi,
ilitungwa na makuhani huko Babeli, na karibu Torati yote ni ya kipindi cha
“baada ya utumwa” (soma kitabu cha Encyclopaedia. Britania,
eleventh (Cambridge) edition, vol. 3, p. 852, col. I). Tena ilijulikana sana na
Amosi (karne ya 7 KK.) linganisha na 2:4, 7, 8, 12; 4:4, 5; 5:12, 21, 22; 9:4, nk.
Wengine hata wanajaribu kutumia kiunganishi hiki ili kuhalalisha chimbuko
asilia la Amosi.
anasema =
amesema.
q