Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[021H]

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu cha Habakuki

 

(Toleo La 1.0 201401107-20141107)

 

Nabii Habakuki aliishi katika kipindi cha zama za uovu na anamlalamikia Bwana kuhusu hali hii na anaambiwa kuwa Yuda watapelekwa utumwani Babeli kwa Wakaldayo ambao watachukua nafasi ya utawala wa dunia ya Waashuru (sawa kama inavyosema Zaburi 73).

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ufafanuzi wa Kitabu cha Habakuki


 


Utangulizi

Habakuki huenda alikuwa ni mtu aliyekuwa akiimba Kwaya Hekaluni na kwa hiyo alikuwa ni wa jamii ya Walawi (sawa na 1:1 na 3:1,19). Neno la karibu sana kwa jina lake la Kiebrania ni neno chabak maana yake kukumbatia na mapokeo ya marabi yanadai kuwa alikuwa ni mtoto wa kiume wa Yule mwnamke Mshunami ambaye nabii Eliya alimponya na akarejesha uhai wake (2Wafalme 4:16). Jina lake linahusiana pia na neno la Kiashuru la hambakuku ambalo ni ua lakini neno chabak ndilo lililokubalika na baraza la marabi. Jina lake linawezekana kabisa kuwa limekubalika au kukumbatiwa kwa kuwa alikuwa ametumiwa kama nabii aliyeshughulikia muungano wa Israeli na Yuda ulioanza katika Nyakati hizi za Mwisho kama tutakavyoona hapo chini.

 

Kwa ujumla inaaminika kuwa alikimbilia Misri kwenye kipindi cha mpitoe kilichofuatiwa mwaka 586 KK akarudi baada ya kuondolewa kwa Wakaldayo. Inasemekana kuwa kaburi lake lipo huko Keila, maili 18 Kusini Mashariki mwa Yerusalemu.

 

Inaonekana kuwa alitabiri mda mfupi baada ya kugunduliwa kwa gombo la Torati Hekaluni wakati wa utawala wa Yosia mnamo mwaka 621 KK. Matengenezo ya urejesho ya Yosia yalidum kipindi kifupi na chini ya Yehoyakimu watu walianza kuabudu na kuzitumikia sanamu tena na ukengeufu ulifanyika kwa kiwango kikubwa sana na kwa kasi kubwa mno. Mfalme aliyageuza matendo yake maovu kwa ukatili mkubwa a vitisho na hatimaye akajikuta akiwa kwenye kongwa la utumwa wa Nebukadneza (sawa na ilivyo kwenye 2Wafalme 14:1).

 

Ufafanuzi wa Seder Olam unafundisha kuwa Yoeli, Nahumu na Habakuki wote walitabiri katika siku za Manase (sawa na usemavyo utangulizi wa kamusi ya Soncino ukurasa wa 211). Kwamba mfalme alikuwa movu sana ikidaiwa kuwa waliacha kuliandika jina lake kwenye vitabu vyao. Uwezekano mkubwa sana ni kwamba huenda mchakato huu ulianza baada ya mwaka 621 na inaanza kwa kuinuka kwa Wakaldayo. Wengine hudhani kuwa huenda ilikuwa ni katikati ya Vita ya Karkemishi ya mwaka 605 KK na kipindi cha kuhusuriwa kwa Hekalu mwaka 586 KK; tuseme ni takriban mwaka 600 KK wakati wa utawala wa Yehoyakimu.

 

Hata hivyo, kuna mambo mengi sana yanayojiri kuyaelezea kuhusu unabii huu kuliko ilivyoelezewa au kufafanuliwa na mamlaka ya marabi. Kikomo au zuio lao la kuiweka Kaekemishi laweza kuwa ni zuio au kikwazo cha kiunabii kama tunavyoona kutokana na uvamizi na utekaji maeneo haya uliofanywa na Nebopolasa, mfalme wa 1 wa kizazi cha Wakaldayo na Wamedi.

 

Mpangilio wa Kitabu ni kama hivi:

  1. Wito na Kilio cha Nabii
  2. Jibu la Yahova
  3. Kilio na Wito wa Nabii
  4. Jibu la Yahova.

 

Kuna aya takriban 56 zilizogawanyika kwenye sura tatu ambayo kinyume chake yanaangukia kwenye migawanyo sita, zaidi kuliko ya mipangilio minne ya kimuundo iliyo hapo juu.

 

Migawanyo yenyewe ilikuwa hivi:

1:2-4 ambapo nabii anamlalamikia Mungu kwa kuwaacha au kuruhusu  watu wasio na hatia wateseke na watu waovu wafanikiwe.

 

1:5-11 ni jibu la Mungu, akisema kuwa ilikuwa ni lazima hasira yake kali imwagwe na kuwafanya hivyo.

 

1:12-17 inaonekana kuwa nabii anaiiuliza na kuionea mashaka hukumu kwa kuwa ni hakika Mungu hawezi kulachia taifa lipatilizwe kwa kuchukuliwa lote na taifa ambalo ni ovu zaidi kuliko wao.

 

Habakuki Sura ya 1

Ufunuo aliouona nabii Habakuki. 2 Ee Bwana, nilie hata lini, wewe usitake kusikia? Nakulilia kwa sababu ya udhalimu, ila hutaki kuokoa. 3 Mbona wanionyesha uovu, na kunitazamisha ukaidi? Maana uharibifu na udhalimu u mbele yangu; kuna ugomvi, na mashindano yatokea. 4 Kwa sababu hiyo sheria imelegea, wala hukumu haipatikani; kwa maana watu wabaya huwazunguka wenye haki; kwa sababu hiyo hukumu ikipatikana imepotoka.

 

Mungu anamjibu Habakuki. Anasema kuwa anawaamsha Wakaldayo, na ndivyo aivyofanya kwa kumtumia Nabpolasa na alisaidiwa na Wamedi wenye harakati zao za kuwaasi Waashuru kwa upande wa Mashariki na Kaskazini.

5 Angalieni, enyi mlio kati ya mataifa, katazameni, kastaajabuni sana; kwa maana mimi natenda tendo siku zenu, ambalo hamtaliamini hata mkiambiwa. 6 Kwa maana, angalieni, nawaondokesha Wakaldayo, taifa lile kali, lenye haraka kupita kiasi; wapitao katikati ya dunia, ili wayamiliki makao yasiyo yao. 7 Hao ni watu wa kutisha sana, wa kuogofya sana; hukumu yao na ukuu wao hutoka katika nafsi zao wenyewe. 8 Farasi zao ni wepesi kuliko chui, ni wakali kuliko mbwa-mwitu wa jioni; na wapanda farasi wao hujitapa naam, wapanda farasi wao watoka mbali sana; huruka kama tai afanyaye haraka ale. 9 Waja wote ili kufanya udhalimu; nyuso zao zimeelekezwa kwa bidii yao kama upepo wa mashariki, nao hukusanya mateka kama mchanga. 10 Naam, huwadhihaki wafalme, na wakuu ni kitu cha kudharauliwa kwake; huidharau kila ngome; kwa maana hufanya chungu ya mavumbi, na kuitwaa. 11 Kisha atapita kwa kasi, kama upepo, atapita na kuwa ana hatia; yeye ambaye nguvu zake ni mungu wake.

 

Habakuki anajua kwamba Mungu amewaamuru au kuwatuma wao kama ni hukumu dhidi ya Yuda. Hata hivyo anamlaumu Mungu kwa kunyamaza kwake kimya wakati wanakabiliwa na watu waovu.

12 Ee Bwana, Mungu wangu, mtakatifu wangu, wewe si wa milele? Hatutakufa. Ee Bwana, umemwandikia hukumu, nawe, Ee Jabali, umemweka imara ili aadhibishwe. 13 Wewe uliye na macho safi hata usiweze kuangalia uovu, wewe usiyeweza kutazama ukaidi, mbona unawaangalia watendao kwa hila; na kunyamaza kimya, hapo mtu mwovu ammezapo mtu aliye mwenye haki kuliko yeye; 14 na kufanya wanadamu kuwa kama samaki wa baharini, kama vitu vitambaavyo, ambavyo havina mtawala? 15 Yeye huwatoa wote kwa ndoana yake, huwakamata katika wavu wake, na kuwakusanya katika juya lake; ndiyo sababu afurahi na kupendezwa. 16 Kwa sababu hiyo huutolea wavu wake sadaka, na kulifukizia uvumba juya lake; kwa sababu kwa vitu vile fungu lake limenona, na chakula chake kimekuwa tele. 17 Je! Atawatoa walio katika wavu wake, asiache kuwaua watu wa mataifa daima?

 

Anajiuliza kuhusu kitendo cha Wakaldayo kuwapora watu na jinsi inavyoonekana kuwa ni kama wana haki zaidi kulikowao na kisha anauliza iwapo kama wataendelea kuwa watu wasio na huruma na wataendelea kuwaua watu kikatili vile kuyatenedea mataifa mengine milele. Na sasa Danieli alidhihirisha kwamba Wakaldayo walikuwa wanakwenda kuanza kuanzisha usimamizi wa mamlaka ya kidola ya kuitawala dunia na ambayo itakwenda kudumu kwa kipindi cha nyakati saba juu ya dola yote ya Wababeloni, Wamedi na Waajemi, Wayunani, iliyojulikana kama Dola Takatifu ya Rumi na dola ya Vidole Kumi yenye mchanganyiko wa Chuma na Udongo ambayo itaishia kwenye Nyakati za Mwisho kwa ujio wa Masihi, ambaye ataiangusha na kuikomesha kwa kuipiga vidoleni na kuikomesha kabsa. Mchakato huu umewekwa kama unabii kwa kuinuka kwa utawala na dola ya Wakaldayo kabla ya Karkemishi mwaka 605 KK  utawala wa Nebukadneza.

Sura ya 2:1-5 inaonyesha nabii akiwa kwenye hali ya pweke kuendelea na jibu la masali yake.

 

Kwenye aya ya 4 Mungu anatoa ujumbe wa maalumu na muhimu wa kimaandiko ambao ni kwamba mwenye haki ataishi kwa imani. Hivyo basi Mungu anaweza kuamua kumuweka mteule wake katikati ya wapagani ili amuendeleze na kumkuza kiimani na kuuondoa uovu katikati yao. Waovu na wakatili hawataweza kuendelea kabisa na hawatawashinda wateule.

 

Kumbuka kuwa ilipasa yaandikwe maono kwa kuwa ilikuwa bado haujafika wakati au majira yaliyokusudiwa ingawaje Wakaldayo walikuwa wanaendelea mble za Wakalkemishi.

Habakuki Sura ya 2

Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwangu. 2 Bwana akanijibu, akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate kuisoma kama maji. 3 Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia. 4 Tazama, roho yake hujivuna, haina unyofu ndani yake; lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake. 5 Naam, pamoja na hayo, divai ni mchumi mdanganyifu, mtu wa kiburi asiyekaa nyumbani mwake; huongeza tamaa yake kama kuzimu, naye huwa kama mauti, hawezi kushibishwa; bali hujikusanyia mataifa yote; hujiwekea kabila zote chungu chungu.

 

Falme au dola hizi zitaundwa na watu wote ulimwenguni na zitadumu kwa kitambo. Kwenye kitabu cha Danieli tunaona kukitajwa Nyakati Saba au miaka 2520.

 

Kwenye 2:6-20 tunawaona waathirika wakiwadhihaki watesi wao kwa mlolongo wa matukio ya ole. Mwisho wa utekaji wao na udhalim wao unatoa fundisho kwa ulimwengu wote kushuhudia. Ni fundisho kuu dhidi ya mfumo na imani ya Wababeloni kwa jinsi ilivyokuwa hadi kuanguka kwake katika Nyakati za Mwisho na sio kuwa ni fundisho au somo tu kwa Nebukadneza aliyeashiriwa kwa Kichwa cha Dhahabu kwenye Danieli sura ya 2 lakini dhidi ya yote yatupasayo kujifunza kwenye Nyakati hizi za Mwisho na ujio wa Masihi.

 

6 Je! Hawa wote hawatapiga mfano juu yake, na mithali ya kusimanga juu yake, wakisema, Ole wake yeye aongezaye kisicho mali yake! Hata lini? Na ole wake yeye ajitwikaye mzigo wa rehani! 7 Je! Hawatainuka ghafula wao watakaokuuma, hawataamka wao watakaokusumbua, nawe utakuwa mateka kwao? 8 Kwa sababu umeteka nyara mataifa mengi, mabaki yote ya kabila watakuteka wewe; kwa sababu ya damu ya watu, na kwa sababu ya udhalimu iliotendwa nchi hii, na mji huu, na watu wote wanaokaa ndani yake. 9 Ole wake yeye aipatiaye nyumba yake mapato mabaya, ili apate kukiweka kioto chake juu, apate kujiepusha na mkono wa uovu! 10 Wewe umeifanyia nyumba yako kusudi la aibu, kwa kukatilia mbali watu wengi, nawe umetenda dhambi juu ya roho yako. 11 Kwa maana jiwe litapiga kelele katika ukuta, nayo boriti katika miti italijibu. 12 Ole wake yeye ajengaye mji kwa damu, awekaye imara mji mkubwa kwa uovu! 13 Angalieni; je! Jambo hili halikutoka kwa Bwana wa majeshi, kwamba watu wajishughulikie moto, na mataifa wajisumbue kwa ajili ya ubatili? 14 Kwa maana dunia itajazwa maarifa ya utukufu wa Bwana, kama maji yaifunikavyo bahari. 15 Ole wake yeye ampaye jirani yake kileo, wewe utiaye sumu yako, na kumlevya pia, ili kuutazama uchi wao! 16 Umejaa aibu badala ya utukufu; unywe nawe, uwe kama mtu asiyetahiriwa; kikombe cha mkono wa kuume wa Bwana kitageuzwa ukipokee, na aibu kuu itakuwa juu ya utukufu wako. 17 Kwa maana udhalimu uliotendwa juu ya Lebanoni utakufunikiza, na kuangamizwa kwao wanyama kutakutia hofu; kwa sababu ya damu ya watu, na kwa sababu ya udhalimu iliotendwa nchi hii, na mji huu, na watu wote wanaokaa ndani yake. 18 Sanamu ya kuchora yafaa nini, hata yeye aliyeifanya ameichora? Sanamu ya kuyeyuka, nayo ni mwalimu wa uongo, yafaa nini, hata yeye aliyeifanya aiwekee tumaini lake, na kufanya sanamu zisizoweza kusema? 19 Ole wake yeye auambiaye mti, Amka; aliambiaye jiwe lisiloweza kusema, Ondoka! Je! Kitu hicho kitafundisha? Tazama, kimefunikwa kwa dhahabu na fedha, wala hamna pumzi ndani yake kabisa. 20 Lakini Bwana yumo ndani ya hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze kimya mbele zake.

 

Imani yote ya mchanganyiko wa dini za Waashuru na Wababeloni ilienea duniani na dini za Siri na Fumbo za waabudu Juan a ibada zao za sanamu za Mungumke; lakini ulimwengu umeonywa kubakia kimya mbele za Mungu na Hekalu lake Takatifu. Waliukata na kuuchonga mwerezi wa Lebanoni na kwa hiyo Mungu anawatia hatiani na watahukumiwa katika siku za mwisho z dini hizi hadi kufikia mwishoni.

 

Kwenye 3:2-19 nabii anaomba na tena anamsihi Mungu aingilie kati kwa niaba ya watu wake. Habakuki analinganisha staili ya maombi yake na ile ya Yeremia na Ezekieli ambaye analaumu na kukemea dhambi za watu watu wake na kuendeleza unabii unaoendelea wa kipindi cha Nyakati za Mwisho za Mataifa na kuanguka kwa Misri kwenye Nyakati za Mwisho. Yeremia anatupeleka kwenye Nyakati za Mwisho na Maonyo ya Manabii wa Mwisho (kwenye Yeremia 4:15). Andiko hili linashughulika na dhambi za dini ya Kibabeloni na ujio wa Mtu wa Dhifa ya Kifalme wa Mungu ili kuuharibu na kuuangamiza mfmo wa kidini za watenda dhambi za ulimwengu.

 

Aya za 16-19 zinaonyesha kujiamini kikamilifu ambayo ni mwenendo wa kimwili wa Waisraeli na sio tu peke yao kuwa ndiyo wataokolewa na kuanzisha tena.

 

Maktaba ya ode kwenye sura hizi za mwisho zinashangaza kwa wataalamu wao wengi wa lugha ya Kiebrania na wengine kama mwanazuoni mashuhuri Driver anavyotilia maanani hilo kuwa ni kama shairi au utenzi mzuri sana wa Kiebrania uliotungwa. Tafsiri ya Soncino inathibitisha pia na kufafanua kwa kumnukuu Driver.

 

Habakuki Sura ya 3

Sala ya nabii Habakuki nabii kwa Mjibu wa Shigionothi.

Shigionothi (sawa na Zaburi 8). Inalinganshwa na ‘shairi au utenzi wa kimtetemo wenye upeo wa vilio vya mtu anayetangatangaji nyikani’ (sawa na alivyoandika Soncino).

 

2 Ee Bwana, nimesikia habari zako, nami naogopa; Ee Bwana, fufua kazi yako katikati ya miaka; Katikati ya miaka tangaza habari yake; Katika ghadhabu kumbuka rehema. 3 Mungu alikuja kutoka Temani, Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani. Utukufu wake ukazifunika mbingu, Nayo dunia ikajaa sifa yake.

 

Teman ni mji ulio Kaskazini Magharibi ya Edomu na Parani ni magharibi mwa Edomu katikati ya Peninsula ya Sinai na na Kadeshi-Barnea. Ni kaskazini mwa bandari ya Aqaba kufuatia upande wa pwani. Huu ni msafara au njia ambayo majeshi ya Jumuia ya Madola aliufuata kwenye mkakati wao wa kuikomboa Israeli na mji wa Yerusalemu mwaka 1917 na kufanikiwa kuuteka tena mji wa Yerusalemu hapo siku ya 25 Kisleu 1917 kwa mujibu wa Kalenda ya Hekaluni, tukio lililohusiana sambamba na kushambuliwa kwa Waaustralia, baada ya kuitwaa Beersheba (soma pia jarida la Maonyo ya Mungu (Na. 184)). Hii ilianzisha mkakati wa kuirejesha na kuifanya upya Israeli katika Nyakati za Mwisho tngu mwaka mtakatifu wa 1916/17 hadi 2027. Kutokana na mchakato huu, ndio Masihi atakuja akitokea Mlima wa Mizeituni tangia kipindi cha mwaka wa 2018/19 ili kuikamilisha kazi.

 

Hii ilikuwa ni mara saba kutoka kwenye Vita vya Karkemishi vya mwaka 605 KK vilivyoishia katika mwaka wa 1916/17; miaka 2520 baada ya vita hivyo na mwanzo wa nyakati za mwisho za kipindi cha miaka arobaini arobaini kilichonenwa kwenye unabii wa Ezekieli, kama ulivyochambuliwa kwenye jarida la Anguko la Misri; Mikono Iliyovunjia ya Farao (Na. 036) kuanza. Hivi vilikuwa ni Vita vya Nyakati za Mwisho kama tunavyoviona kwenye jarida la Anguko la Misri Sehemu ya II: Vita vya Mwisho (Na. 036_2).

 

Muungano wa mataifa ya Anglo-Arabu ulianzishwa katika mwaka mtakatifu wa 1916/17.

 

Mnamo Januari 24, baada ya siku moja ya vita, jeshi la muungano wa Anglo-Arabu liliutwaa mji wa bandari wa Wejh, ambao ulifanyika kuwa kituo muhimu cha usafirishaji na cha kimikakati kwa Waarabu. Na kwa karidi Waarabu walivyokuwa wanakusanyika na kungana, ndipo Jenerali wa Kiingereza aliyejulikana kwa jina la Sir Archibald Murray aligundua kuwa Waarabu walihitajika kumpa msaada kwa ajili ya mkakati wake wa huko Sinai wa kuikomboa Rasi ya Suezi na kuwasukuma wanamgambo wa Ottoman watoke nje ya maeneo ya Gaza. Kazi waliyotakiwa kuifanya Waarabu ilikuwa ni kuyafungia majeshi ya Fakhri na kuhakikisha yasitoke huko Madina na kuitwaa na kuifunga Reli ya Hejaz. Hii ilianzisha kutimia kwa unabii wa Habakuki kwa kuanza kuwakomboa Watoro au Walevanti na kufanya mwisho wa utawala wa Ottoman. Ilianzia kutoka kusini kama Mungu alivyosema kuwa itafanyika, kuanzia huko Parani, ambavyo ni kutoka Sinai hadi Kadeshi Barnea na sambamba na wani ya Aqaba Magharibi ya Edomu na kupitia Temani ambako ni Kaskazini Magharibi ya Edomu kuelekea Yordani na kulikuwa na maji ya kutosha. Ni njiapanda ya barabara muhimu iliyotumiwa kwa misafara ya wafanya biashara kwa zama zote mbili, yaani za kale na za sasa.

 

Hivyo, Waarabu walijikita kwenye mkakati wa “kuishambulia njia ya reli” kwa kipindi chote cha mwaka 1917.

 

Kiongozi wa uasi alibakia kuwa na mtazamo wake mhimu wa kimkakati ulioonekana kuwa muhimu na tishio; akiendelea kusongambele upande wa kaskazini na akijipatia kuungwa mkono na ushirikiano na kuwa na ushawishi na makabila na viongozi wa huko Syria na eneo lote za Mesopotamia. Hali hii, hata hivyo, ililazimu kuwa na bandari nyingine pya inayomudu kazi. Wakati wakiwa ana dalili ya homa ya ugonjwa wa kipindupindu, ndipo T. E. Lawrence alianza hila za kuiteka bandari iliyokuwa kwenye Bahari ya Shamu ya Aqaba, ambayo kwa siku hizi ni sehemu ya Yordani. Aliakataa au kuacha kuishambulia kutoka majini, wakati Aqaba ilikuwa inalindwa kwa bunduki kali na nzito. Zaidi sana, mpango wake wa kijasiri uoliwataka askari kujimega kutoka kwenye Jangwa la Nefudh, ambavyo majeshi ya Ottoman hawakuwa wametarajia. Sehem mhim ya Lawrence na mashujaa 17 wa Agayl waliondoka kutoka Wejh mnamo tarehe 10 Mei, 1917 (kutoka Kipindi cha Pasaka ya Pili). Watu walikuwa na takriban pesa ya Kiingereza, £20,000 iliyotumiwa kuwaingiza jeshini watu wa jamii ya makabila mapya na, walipokuwa wanaendelea kufanya hivyo, idadi yao iliongezeka hadi kufikia idadi ya wapiganaji 700. Kiongozi wa idadi ya Waarabu hawa wa makabila mapya alikuwa ni Auda Abu Tayi chifu wa jami ya Howeitat ambaye alikubali kujiunga na Jenerali Lawrence kwenye mapigano ya mashambulizi.

 

Msafara wa umbali wa urefu wa maili 600 ulipitia mazingira ya magumu na ya ulichukiwa sana kusiko na kuonyeshwa ukarimu wowote kabisa, hata jamii ya Bedouin (Wabedui) waliuita al-Houl (yaani msafara wa Magaidi). Mwandishi wa historian ya matukio na maisha wa Lawrence aliyeitwa Michael Asher aliuita mkakati huu kuwa ni “moja kati ya majaribio magumu na ya hatari sana kuliko ya mashambulizi kuwahi kujaribiwa kwenye midani ya vita.” Waarabu walifanya mashambulizi yao kutoka upande wa kaskazini magharibi, waliyafegiliambali kwa kuyakimbiza na kuyateka majeshi ya Ottoman kwa kuvipoteza vikosi viwili tu vya makabila mnamo tarehe 5 Julai. Siku iliyofuatia, Waarabu ambao sasa walikuwa na jeshi la watu 2,500, waliingia Aqaba bila kutumia kitisho cha milio ya bunduki, ngome au askari walinzi ikiwa imekurupushiliwa mbali. Gaunt, akiwa amechafuka sana, na akiwa amevaa kazu ya utamaduni wa jamii ya Bedouin, Lawrence aliivuka Sinai na kwenda hadi Cairo kumpasha habari kamanda mkuu mpya wa majeshi wa Waingereza, Jenerali Edmund Allenby, kuhusu ushindi wake mkubwa. Na kama zawadi, Waarabu walipokea walipokea malipo mengine ya ziada yenye thamani ya fedha za Kiingereza £16,000, na Lawrence alipandishwa cheo hadi kuwa Meja jeshini.

 

Kwa kipindi hicho tangu kuondoka kwa Lawrence kwenda Allenby huko Cairo na kurudi kwake, Aqaba ulikuwa umejengewa ngome au ukuta au kuzingirwa na majeshi yaliyodumu kama bataliani yenye silaha nzito zilizojlikanna kama Kikosi cha Ngamia cha Mfalme (Imperial Camel Corp), lenye silaha kali na nzitonzito na magari yaliyo na silaha na kinga pamoja na dhahabu. Kundi au Kikosi hiki cha Ngamia na Waarabu walimsaidia kwenye harakati hizi tangu kutwaliwa kwa Aqaba hadi kuendelea kwao kwa kusonga mbele hadi kwenye Bonde la Yordani hadi Damascus ili kuulinda ubavu ya upande wa kulia wa Allenby.

 

Allenby wakaamuru majeshi ya Muungano wa Madola yaende huko Sinai na kile kilichojulikana kama Farasi Mwepesi wa Kiaustralia, [yaani, the Australian Light Horse] ilikamatwa huko Beersheba na kisha Waaustralia waliendelea mbele na kuutwaa mji wa Yerusalemu mnamo tarehe 7 Desemba 1917. Hivyo unabii wa Habakuki wa kurejesha tena himaya ya Levant kutoka Temani na Parani ulitimilika kwa kipindi cha zaidi ya Nyakati Saba au miaka 2520 tangia Vita ya Karkemishi na kukaliwa kwa Wakaldayo kujumlisha na mwaka mmoja kuanzia mwaka 1916 na kuitwaa Yerusalem hapo Desemba 1917. Lawrence aliingia Yerusalemu akiwa na Allenby na kisha Majeshi ya Muungano yaliendelea mbele na kukabiliana na vikosi vya ulinzi vya Ottoman na Wajerumani vilivyokuwa vimeweka kambi zao karibu na Galilaya.

 

Matukio yenye yalikuwa kama ifuatavyo.

 

Vita vya Beersheba

31 Oktoba hadi tarehe 1 Novemba

Tel el Khuweilfe

8 Novemba

Ahueni au ushindi ulipatikana  (Sinai na Palestina 4-8 Novemba)

6-11 Novemba

Tukio Kubwa la Kuwasukuma Maadui lilifanyika

8-15 Novemba

Uwanda wa Bahari ulisafishwa

11-17 Novemba

Mafanikio zaidi ya Yerusalemu

16-24 Novemba

Nahr Auja na El Buij

24 Novemba hadi 1 Desemba

Mashambulizi ya mwisho ya kuutwaa Yerusalemu

7 Desemba

 

Shambulio la mwisho lilifanywa na majeshi ya Muungano tarehe 7 Desemba 1917. Kwa mujibu wa taarifa za kweli za Mwandamo wa Mwezi Mpya, hii ni tarehe kamili na ni siku ya 24 Kiisleu (kalenda ya Hilleli ilianza mwezi mpya siku mbili baadae). Waturuki na Wajerumani walianza harakati za kuondoka haraka na mnamo yarehe 8 Desemba 1917 Yerusalemu ulitwaliwa. Wachanga au wasioelewa vizuri walichinba kiundani na kujikita na ilipotimu tarehe 10 Desemba, Farasi Mwepesi alikimbia au alikimbia kuelekea barabara ya kuelekea Nablus, umbali wa takriban maili nane. Walichukua silaha nzito nzito za Waturuki na za moto. Walizishikilia wakielekea upande wa kusini mwishoni mwa Bonde la Yordani na walikuwa wanajaribu kuyazuia majeshi ya Muungano yasiukatishe mto na kwenda hadi kuifikia reli ya Hejaz na hivyo kuzuia utendaji kazi wa Allenby kwa ubavu wa upande wa kulia.

 

Allenby aliingia rasmi mjini Yerusalemu tarehe 11 Disemba 1917, siku ya 28 ya mwezi Kisleu.

 

Majeshi ya Muungano yalielekea na kuingia Lebanoni na Syria na Feisal aliingia Damascus. Mkataba au makubaliano ya muafaka wa Sikes/Picot kati ya Waingereza na Wafaransa yaliwagawa Levant pamoja na Suez, Palestina na Mesopotamia ambao walipewa Waingereza na Lebanoni na Syria ikatolewa kwa Wafaransa. Hii hata hivyo ilisababisha kuwepo na kile kilichojulikana kama Mkataba au Azimio la Balfour Declaration la mwaka 1917 na Usimamizi au Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1922 wa undwaji au uanzishaji wa Taifa la Israeli kwa kipindi kilichofuatia cha miaka thelathini tangu mwisho wa Vita ya Kwanza ya Dunia hadi mwaka 1948.

 

Unabii ulio kwenye Hagai 2:1-23 unahusiana na unabii hu wa Habakuki.

 

Unabii ulio kwenye Hagai unaithibitisha Kalenda ya Hekaluni inayotokana na Miandamo ya Mwezi Mpya kwa kuanzia kipindi cha mpito wa kuonekana mwezi mpya na sio kama ilivyo kwenye kalenda ya Hilleli.

 

Habakuki na kundi la walioachwa masalia walikimbilia Misri mwaka wa 586 KK na wakarudi baada ya kuondoka kwa Wakaldayo. Huu ni mzungko wa mara moja wa utaratibu wa mizunguko wa  miaka 19 kutoka Karkemishi na kujumlisha mzunguko mmoja kuelekea kwenye mwanzo wa kipindi cha mwisho. Kwa hiyo, Nyakati Saba au miaka 2520 tangu mwanzo wa kipindi cha miaka themanini na mwisho au utimilifu wa mashambulizi ya Cambyses mwaka 525 KK yaliyoishia mwaka 1996/7 kwenye mwisho wa Nyakati au Utilimifu wa Mataifa. Kipindi cha miaka 2520 tangu kuangamia kwa Yerusalemu na kuondoka kwa Wakaldayo, yaani kuanzia mwaka 587/6 KK, ni jumlisha miaka 19. Miaka 2520 tangu mwaka 586 ni mwaka 1937. Mnamo Januari 30 1933 Hitler alichaguliwa kuwa kiongozi mkuu anayejulikana kama chancellor wa Ujerumani. Miaka ya 1933-36 ilifanya mwanzo wa matatizo na migogoro katika Yuda na kuinua kwa utawala na itikazi ya Manazi na kusaidiwa kwa Wapinga-Wasemitiki huko Afrika Kusini tangu wakati ule na kuendelea. Mikakati ya kuwamaliza na kuwaua Wayahudi ilikuwa inaendelea na hususan kwenye kipindi cha miaka ya 1941-1945. Vita dhidi ya Yuda katika Mashariki ya Kati vilisaidiwa na kuungwa mkono tangu kuzuka kwa itikadi ya Manazi na vita vilifuatia mwaka 1948 na ilipelekea kuwepo kwa azimio la kutangazwa taifa la Israeli.

 

Mwaka 1967 kipindi maalum cha nyakati za mwisho kilianza kwa vita ya Siku Sita na madai tena yaliyotolewa ya haki ya kuumiliki Yerusalemu na jamii ya Yuda nchini Israeli.

 

Miaka arobaini baada ya kuibuka kwa itikadi ya Manazi na jarubio la kuwafutilia mbali ulimwenguni kote Wayahudi, mnamo Octoba 1973, vita iliyojulikana kama ya Yom Kippur ilianza na, ingawa amani na Misri iliwekwa na kuhakikishwa, vita na Syria iliendelea na usimamishaji wa mapigano ulikubaliwa tu mnamo Mei 1974. Miaka arobaini baadae katika mwaka 2014, baada ya majira ya Machipuko ya Uarabuni yakiwa yameanza, eneo lote la Mashariki ya Kati lilikubwa na dhahama na kile kilichojlikana kama kutangazwa kwa Dola la Kislamu chini ya Khalifa Mpya wakati wa kikomo na cha matazamio cha miaka arobaini. Vita mbaya na ya kikatili ya kuangamiza watu ilianza baada ya mwisho wa Pasaka ya Pili kuadhimishwa kwenye eneo lote la Syria na Mesopotamia. Mataifa haya sasa yanaletwa kwenye magoti yao kwenye vita vya msuguano na kikatili ambayo haijawahi kuonekana katika Mashariki ya Kati kwa karne kadhaa zilizopita. Vita hivi vinaendelea pia kwenye ncha ya Kaskazini na Mashariki na inaonekana pia kuwa vita vya Baragumu la Tano na la Sita vinachochewa.

 

Kama kuna vipindi viwili vingine vya miaka arobaini kutoka kipindi hiki vilivyowekwa kwa matarajio ya kufanya toba ndipo sisi tunaweza kutarajia Hatua ya kimbinguni tangu mwaka 2015/16 kwa marejesho mapya na kuiunganisha Mashariki ya Kati katika Israeli na hukumu ya Wakaldayo na Waarabu. Hata hivyo, mataifa yanatikisika kwa ujumla kutokana na aya ya 6. Kwa hiyo ndipo tukio linguine la zaidi na la jumla yabidi litarajiwe.

 

Vita vinaendelea mbele kama tunavyoweza kujionea ikitajwa kwenye kitabu cha Ufunuo.


4 Mwangaza wake ulikuwa kama nuru; Alikuwa na mishale ya nuru ubavuni pake; Ndipo ulipofichwa uweza wake. 5 Mbele zake ilikwenda tauni, Na makaa ya moto yakatoka miguuni pake. 6 Akasimama, akaitetemesha dunia; Akatazama, akawasitusha mataifa; Na milima ya zamani ikatawanyika; Vilima vya kale vikainama; Miendo yake ilikuwa kama siku za kale. 7 Naliziona hema za Kushani katika taabu; Mapazia ya nchi ya Midiani yakatetemeka. 8 Je! Bwana aliikasirikia mito? Je! Hasira yako ilikuwa juu ya mito, Au ghadhabu yako juu ya bahari, Hata ukapanda farasi zako, Katika magari yako ya wokovu? 9 Uta wako ukafanywa wazi kabisa; Viapo walivyopewa kabila vilikuwa neno thabiti; Ukaipasua nchi kwa mito. 10 Milima ilikuona, ikaogopa; Gharika ya maji ikapita; Vilindi vikatoa sauti yake, Vikainua juu mikono yake. 11 Jua na mwezi vikasimama makaoni mwao; Mbele ya nuru ya mishale yako ilipotapakaa, Mbele ya mwangaza wa mkuki wako umeremetao. 12 Ulikwenda katikati ya nchi kwa ghadhabu; Ukawapura mataifa kwa hasira. 13 Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa watu wako, Kwa ajili ya wokovu wa masihi wako; Ukakiponda kichwa cha nyumba ya waovu, Ukiuweka wazi msingi hata mwambani. 14 Ukakichoma kichwa cha mashujaa wake kwa fimbo zao wenyewe; Wakaja kama kisulisuli ili kunitawanya; Kama wakifurahi kuwameza maskini kwa siri. 15 Ukaikanyaga bahari kwa farasi zako, Chungu ya maji yenye nguvu. 16 Nikasikia, na tumbo langu likatetemeka, Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile; Ubovu ukaingia mifupani mwangu, Nikatetemeka katika mahali pangu; Ili nipate kuingoja ile siku ya dhiki, Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu. 17 Maana mtini hautachanua maua, Wala mizabibuni hamtakuwa na matunda; Taabu ya mzeituni itakuwa bure, Na mashamba hayatatoa chakula; Zizini hamtakuwa na kundi, Wala vibandani hamtakuwa na kundi la ng'ombe; 18 Walakini nitamfurahia Bwana Nitamshangilia Mungu wa wokovu wangu. 19 YEHOVA, aliye Bwana, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka.

 

Huu ni mwisho wa Nyakati za Mwisho na vita kuu vya mwisho. Ingawaje kuna uharibifu nabii ni kwa ajili ya marejesho mapya ya watu wa Mungu na kuyatiisha au kuyanyenyekeza mataifa ya dunia kwa kupitia Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu atakaporudi Masihi.

 

Kumbuka kuwa mito itatumika kuyaadhibu na kuyatesa mataifa ni kama zitakavyofanya bahari pia. Hii inaonyesha na kuashiria kuwepo kwa vita kubwa vitakavyotokea kwenye kingo za mito ya Tigri na Frati sambamba na vita vya Baragumu la Tano na la Sita ya Ufunuo.

 

Hasira kali na mateso hapa ni dhidi ya watu walio Mashariki ya Kati na Waarabu wa Kushani na Midiani hadi kueleea nchi ya Ugiriki. Kushani inatumika sambamba na Midiani na huenda inaonyesha au kuwataja Wakushi walioko Babeloni zaidi kuliko kwa wale wanaohusiana na wale walioko Sudani na Ethiopia. Mfumo wa Bonde la Ufa uliopo kutoka Lebanoni hadi kwenye Bahari ya Shamu litapasuka kutokana na matetemeko makubwa ya ardhi katika Siku za Mwisho wakati atakapokuja Masihi na kutawanyika kwa Mlima wa Mizeituni. Tukio hili linasababisha kuwepo kwa bonde kubwa upali wa kilometa 66 kutoka Kaskazini hadi Kusini na kupitia Sinai kwa upande wa kusini na kuvunja kingo au midomo ya Bonde la Ufa la Bahari ya Shamu na itafumkilia mbali. Kuna wasiwasi kidogo kuwa watoto wa kiume wa Kiarabu wa Midiani na Wakushi wanamaanisha kwa kiasi kidogo sana. Midiani ilikuwa ni kabila kubwa la kabila la Waarabu upade wa Kusini Mashariki ya Edomu (na ambao pia walikwenda upande wa kaskazini katika nchi ya Iraq); kama walivyo wana wa Ketura kwa ujumla. Ishmaeli ni kabila Lililofanyika kuwa Waarabu lililo kwenye maeneo ya Waarabu na sio Waarabu halisi asili yao ambao walikuwa ni wana wa Ketura.

 

Unabii wa Habakuki bado haujafunuliwa bado na utaendelea hadi kuja kwa Masihi.

 

q