Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[041]

 

 

 

Undumilakuwili wa Vijana

(Toleo La 2.0 19940709-20040504)

 

Mwandishi anahusianisha uzoefu wake na tatizo la vijana na mekebisho. Maana ya maneno ya biblia kwa vijana yameelezwa. Umuhimu wa kuwahudumia watu wa makundi yote mawili yaani vijana na wazee ni ujumbe ambao taifa linapasa kujifunza nao.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hatimiliki ©1994, 2004 Storm Cox)

(tr 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Undumilakuwili wa Vijana

 


Mwandishi alifanya kazi ya uangalizi kwenye programu ya mafunzo kwa vijana wasiokuwa na ajira kwa muda mrefu wenye umri wa miaka kati ya 15 na 20. Hii ilihisisha na kuwahojiana na vijana wengi wenye matatizo ya utumiaji wa mihadarati, ulevi, na migogoro ya nyumbani iliyowapekea kufukuzwa na waliofanya uhalifu wa namna kadhaa mitaani.

 

Wakati mwingine, kijana mmoja mwenye unri wa miaka 20, ambaye alikuwa hawezi kusoma wala kuandika alihojiwa. Alikuwa anavuta bangi ta ngu akiwa na umri wa miaka 12; alikuwa amedhalilishwa kimwili nyumani kwake kwa kipindi cha miaka kadhaa na alikuwa anakunywa kiasi kingi sana cha ulevi kila juma. Mwenendo huu ulikuwa ni kitu kilichoonekana kuaminika. Alionyesha ushahidi wa kudhalilishwa kwa madhara yatokanayo na matumizi ya madawa ya kulevya, yaliyomuonyesha matatizo makubwa sana aliyokuwanayo kwenye kufikiria au kutafakari na kugugumia kwa urefu wowote wa muda.

 

Kwenye mahojiano mengine, kijana wa umri wa miaka 15 aliyekuwa na nywele nyingi zilizosokotwa, alikuwa analipunga bango lake la mihadarati, kwa kujivunia au kuonyesha fahari ya tatizo lake ka ulevi na alikuwa mtu aliye na elimu ya wastani kuliko yule wa kwanza. Alikiri kuwa anawachukia wazazi wake na hakuwa na uhakika sana walikuwa wapi kwa kipindi kile. Alipoulizwa kwamba anataka kuwa nani atakapokuwa mtu mzima alijibu anataka kuwa mpiga ngoma wa bendi za miondoko ya rocki na kupiga ala za shaba au chuma, kama ifanyavyo bendi yake anayoipenda inayosifikana kwa fujo na ghasia zinazofanyika kwa uchokozi wake.

 

Alipokuwa anahojiwa alichora kwa haraka nembo kwenye kipande cha karatasi. Ilikuwa na misalaba mitatu iliyopunduliwa kuelekea chini na akaandika namba 666 juu yake. Kisha aliendelea kujikata chale usoni mwake, kitendo kilichosababisha damu kutoka, kisha akaweka kidolegumba chake kwenye hilo kovu na kisha akaweka sehemu aliyochovya damu ya kidole chake kwenye ile nembo. Alipoulizwa ni kwa nini alijisikia kufanya hivyo, alisema tu kwamba, "Sijui. Utulivu wa Shetani." Pia miongoni mwa vijana hawa kulikuwa na mabinti wa makahaba wenye matatizo makubwa sana na mambo ya kusimulia, na vijana wengine wengi sana waliokuwa wanakabiliwa na kesi mahakamani, kufungwa jela, kuwa watoto wa mitaani, na wengine kukumbwa na vifo kutokana na kuharibu mimba.

 

Alipoikabiliwa na mambo haya yote, mwandishi alilazimika kuketi chini na kuuliza “Kwa nini?” Kwa nini mambo haya yanawakumba vijana wetu? Kwa nini imeruhusiwa mambo haya yatokee? Kwa kulinganisha, mtu anaweza kutafakari kwa kurudisha kumbukumbu zake nyuma hadi kwenye miaka ya 1890 wakati vijana wetu wa hapa nchini, waliokuwa wanafanya kazi za kujitolea kujijenga nchi yetu iliyokuwa na vijana waguvu na wasio na maadili ambao waliweza kuiba, kwa mtonyo wa papo kwa hapo, walibeba mabegi yao, na kupanda farasi zao na kuelekea kwenye Vita vya Walowezi. Mwaka wa 1915, wakati nchi yetu iliposema, “Mtoto, hakuna muda wa kuupoteza ... kuna kazi ya kufanya" walikwenda kwenye mabishano yao. Waliita hii kuwa ni homa ya vita.

 

Watu hawa walifanya kazi kwa ajili ya familia zao, kwa nia ya kutengeneza hatima njema ya siku za mbele tulizonazo leo kwenye jamii zetu, walikufa bila kuonewa mashaka ili kwamba watu wetu wawe salama. Walifanya kazi kwa ajili yao wenyewe kiasi cha kufa ili sisi tuweze kuishi. Watoto wao pia ni kama walivyokuwa wao walikwenda vitani, kukifuatiwa na mchakato mrefu wa mapambano ya ujenzi ili kuruka tena. Mtu haendi vitani kwa ajili ya kujisikia tu kuwa ilikuwa ni utani au kujburudisha. Bali anafanya hivyo ili kuiokoa nchi yake, watu wake na familia yake.

 

Hata hivyo, hali hii ya kujitolea ilipotea baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Lengo letu hapa si kuitukuza au kuisifia vita ila ni kujaribu kuonyesha tabia za unyenyekevu, kujitoa na upendo. Wazee wetu waliotutangulia hawakuogopa kwenda vitani, kwa kuwa walikuwa wanamtumaini Mungu.

 

Kilichofuatiwa na Vita Kuu ya Pili ya Dunia, ni vipindi vya milipuko ya mabomu kila mahali. Miaka ya hamsini kilikuwa ni kipindi muhimu kiuchumi upande wa magharibi, hali iliyokwenda sambamba na Vita Baridi. Watoto waliokuwako miaka hii ya hamsini, waliobeba mabomu huko Marekani walikua kiumri na huku wakirukaruka chini ya meza wakifanya mazoezi kujizoeza ‘iwapo kama kutalipuliwa bomu la nyukilia’. Walifundishwa kuwachukia wakomunisti, mafashisti, watu weusi, Wameksiko, na yeyote asiye Mmarekani halisi.

 

Ili kuondoa majinamizi yasioyo na maana kama hilii,  vijana walipewa uhuru zaidi. Ukuaji wa uchumi na mitindo iliyoimarika ya uzalishaji iliwezesha utengenezwaji au uzalishaji wa magari mengi en masse. Hawa walikuwa ni vijana wengi waliokuwa na hari ya kufanya kazi. Kwa hiyo, kwa vijana, kazi ilikuja kuwa ni uti wa mgongo au mhimili wa kiuchumi kwa mara ya kwanza katia historia. Upatikanaji kirahisi wa magari uliwafanya vijana wapate uvumbuzi mpya wa uhuru au kujiachia. Viwanda vya kutengeneza bidhaa za sinema vilianza kuenea. Sura mpya na zenye kuvutia za kina Dean na Brando, sura zilizojificha nyuma ya mpeperuko wa moshi wa sigara, kwenye pikipiki, kwenye magari yaendayo kasi, na wasichana warembo, na zile zilipelekea uasi mkuu ambayo kizazi hiki kilijikuta vigumu kujizuia au kupingananayo.

 

Vijana wakaanza kuiga matendo ya mashujaa wao. Matendo ya ‘Kujinyonga’ yakaanza kushika kasi. Uhuru wa kuondoka na kuachana na familia zao na matatizo yaliyotokana na hali yao mpya kulipelekea kudai uhuru wa kufanya ngono, ambao kwa namna nyingine zilisisitizwa kwenye miziki mipya iliyopedwa na kuwa maarufu na sinema. Vijana, kaa ajili ya ukweli wa kwamba walikuwa wanajikusanya pamoja kwenye makundi makubwa mbali na majumbani kwao, walifanyika kuwa nguvu ya kisiasa kwa kujiingiza wenyewe pamoja na matabaka ya kiuchumi ya kuwafanya wawe juu zaidi ya maji, kwa hiyo ndivyo kusema.

 

Hali hii ya madaraja ya kiuchumi iliwafanya vijana kudai mazao yaliyoendana na hamasa au ahauku yao isiyotosheka. Miaka ya sitini ilishuhudia mlipuko kwenye soko la muziki, michezo, sinema na runinga na kusema kweli na soko la mihadarati. “Vichekesho” vilikuwepo pia. Muziki ulielezea hadithi. Kutajwa kwa mihadarati, mitindo, vyote vilipelekea kuwepo kwa ‘ukimya’ wa matumizi ya mihadarati.

 

Vijana walijua kwamba nguvu zao mpya pamoja na kupendaji wa matembezi au safari za Leary maeneo yote ya nchi wakieneza ‘injili’ yake ya ‘kuenea kwa hali ya kihisia’, kulikuwa na ongezeko kubwa la matumizi ya mihadarati au madawa ya kuongeza nguvu. Tindikali na LSD vilikuwepo na kuonekana kama vitu vya kawaida miongoni mwa vijana wa umri wa miaka chini ya ishirini kama ulivyokuwa ulevi. Hisia iliyokuwa imetiwa nguvu au kusisitizwa, mtizamo mpya au jinsi ya kuiona upya dunia. Hekima bandia au ya uwongo, kutokuwa na hukumu sawa wa kitaifa au aina yoyote ya msingi na yenye mashiko, bali walijisikia kuwasiliana na kuwa karibu zaidi, kuwa huru zaidi na hivyo uasi uliendelea.

 

Hata hivyo, mambo yalianza kushindwa kidogo katika maiak ya sabini. Shule au makundi ya wenye kufikiri yalijitokeza miongoni mwa desturi na mila za vijana. Moja, ma daraja la wafanyakazi lisilo na aina za kitaaluma lililofundisha mafundisho ya Malaika wa Kuzimuni na mengine kama hayo – waliyaeneza yote kwa pamoja. Ndoto ya Wamarekani haikuwepo waikuweza kufikiwa na walijua hivyo. Waeneaji wa mihadarati wa miaka ya sitini walitoa mwanya wa matumizi mabaya ya bangi, vileo na dawa za kulenya aina ya heroin – walemewaji wote au waathirika. Hali inayoendelea ilikuwa ni vurugu au machafuko, hasira, chuki, dalili ya matendo ya jakamoyo la kisaikolojia matendo yanayodhalilisha mambo haya madogo yote kabisa yaliyosababisha au kupelekea hivo.

 

Kundi lingine lilikuwa la aina ya Berkeley, walioinukia. Waligundua kuwa maandamano ya kisiasa ya kiama ya sitini ya maua na sherehe au matamasha ya rocki yalikuwa ya makelele na yalisomewa ili kukidhi haja ya kiuchumi ya miaka ya sabini na themanini – mtindo wa YUPPIE ulianza au ulizaliwa. Ni ndivyo ilivyokuwa pia kwa wanamitindo wa mihadarati - madawa ya kulevya aina ya cocaine, madawa aina ya ecstasy na kubobea kwenye matendo na kubobea nayo kulianza kutokana na hali hii.

 

Kulikuwa na uharibifu na mporomoko mkubwa wa maadili kwa muda mfupi sana. Sasa tunajionea mifano kutokana na yale yaliyojitokeza ambayo yametajwa hapo kabla – madhara ya ndani ya uasi wa vijana. Tuaweza sasa jinsi inavyosema Biblia kuhusu ujana na ale tunayoyaona leo na tutajionea jinsi vijana wetu wanavyoweza kufanya kesho.

 

Je, neno ujana lina maana gani?

Biblia ina maneno mengi yanayoelezea ujana -

 

bahur, na'ar, yeled, neanias, neunfskos. Maneno haya yanamaanisha msichana, mvulana, kinana, kijana shujaa, mwanajeshi, mtumishi, mvulana, mtoto na mwanaume.

 

neoterus, alma, nea, neotera.  Maneno haya yote yanamaana ya kijana wa kike, mwanamwali, mjakazi, bikira, -pia msichana, mjakazi, mwanamke mtarajiwa kuoewa.

 

bhurot, nurim, nour, nvrot, sird, yaldot, neotes.  Yote yanamaanisha kijana, utoto, mtoto, uvulana. Neno la Kiyunani kuhusu ujana ni neoterikos. Maneno yanayotumika kwenye Biblia kuhusu mwanaume kijana alinionyesha mchoro wa wazi kwa kila moja na linguine na halimaanishi umri wa mtu kwa ukamilifu wake. Kwa mfano, hebu na tuliangalie neno la Kiebrania la na'ar na lile la kike, na'arah. Maneno haya yameteonnyeshwa kwenye makundi ya umri tofauti. Hebu na tusome kwenye andiko la Kutoka 2:6

 

Akakifungua, akamwona mtoto, na tazama, mtoto yule analia. Basi akamhurumia...

 

Neno lililotumika hapa kwa mtoto mchanga ni na'ar na linamaanisha mtoto wa umri wa miezi mitatu.

 

1Samweli 1:22 Bali Hana hakukwea; maana alimwambia mumewe, Sitakwea mimi hata mtoto wangu atakapoachishwa maziwa, hapo ndipo nitakapomleta, ili ahudhurie mbele za Bwana, akae huko daima.

 

Hapa tunaona neno lililotumika kumuelezea mtoto mdogo, mtoto aliye bado mchanga, na tena kwenye 1Samweli 2:11.

 

Kisha Elkana akaenda Rama nyumbani kwake. Na yule mtoto akamtumikia Bwana mbele yake Eli, kuhani.

 

Samweli hapa anafanya ibada kama vile ni mtu aliyekuwa anamsaidia kuhani mkuu – akiwa kijana mdogo bado.

 

Mwanzo 25:27 Watoto wakakua, Esau alikuwa mtu ajuaye kuwinda wanyama, mtu wa nyikani, na Yakobo alikuwa mtu mtulivu, mwenye kukaa hemani.

 

Hapa neno na'ar linaonyesha wavulana wanaoelekea kubalehe. Kwenye Mwanzo 21:17 tunasoma:

 

Mungu akasikia sauti ya kijana. Malaika wa Mungu akamwita Hajiri kutoka mbinguni, akamwambia,...

 

Hapa neno hili linatumika kumuelezea Ishmaeli akiwa na umri wa miaka 14 au zaidi.

 

Mwanzo 37:2 Yusufu, aliyekuwa mwenye miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo....

 

Kutoka 33:11 Naye Bwana akasema na Musa uso kwa uso, kama vile mtu asemavyo na rafiki yake. Kisha akageuka akarejea hata maragoni; bali mtumishi wake Yoshua, mwana wa Nuni, naye ni kijana, hakutoka mle hemani.

 

Matumizi ya neno na'ar yalikuwa ya mara nyingi, ile si wakati wote, kwa mtu mzima.

 

Tunaona hapa kwamba maana ya neno kijana ni yule tuliyenae tangu kuzaliwa kwake hadi tunapofikia umri wa utu uzima. Watafsiri wa kamusi ijulikanayo kama Dictionary of the Bible [Kamusi ya Biblia], ukurasa wa 928, inasema kuwa ujana ni Wakati, usio na kikomo, baada ya utoto uchanga na kabla ya kipindi cha mtu kufikia utu uzima, kipindi cha nguvu nyingi na umajimoto na cha fursa, kisichoteweza kuhukumu na utu uzima. Ukuu unasemwa hapa sio tu kuwa unataja nguvu za kimwili.

 

Kwa hiyo, dhana ya ujana ni pan asana. Ni nini kinachoanzisha utu uzima?

 

Watafsiri wa Kamusi ya Biblia yaani The Interpreters Dictionary of the Bible, Vol. 4, page 925 inasema kwamba

 

Hesabu ya umri uliokusudiwa haueleweki vizuri. Neno la na’ar linatumika kwa nyakati hata kwa watoto wachanga au watoto na wadogo sana (Kutoka 2:6; Waamuzi 13:8; 1Samweli 1:22; 4:21), na kwa wengine kuna maneno mengine pia (tazama panaposema Mtoto), lakini linatumiwa kwa mtu aliyekua tayari (sawa na Mwanzo 34:19; 2Samweli 18:5). Walawi 27:1-8 naweza kupendekeza umri wa miaka ishirini kuwa ni kama kipindi ambacho mtu anakuwa amepita kwenye ujana kuelekea ukubwani. Hapo kwa lengo la kuainisha usawa wa thamani ya mzani mtu na kugawanya kwenye makuni kulinganisha na umri, na miaka ishirini inaonekana kama ni umri wa chini unaofanya kikomo cha aina ya kundi linalothaminiwa sana, kwa hiyo, linachukuliwa kuwa ni mwanzo wa maisha. Wahesabuji wa idadi ya watu walihesabu ongozeko la watu tangu waliofikia umri wa miaka ishirini na kwenda juu (Kutoka 30:14). Hawa walitakiwa kulipa kodi, na wanaume wa umri huu ‘waliweza kwenda vitani’ (Hesabu 1:3). Kutokana na Hesabu 14:29 tunweza kuona pia majukumu haya yakiwafikia pia walio na umri wa miaka ishirini. Lakini Walawi hawakuruhusiwa kuhudumu kwenye hema la kukutania hadi wafikie umri wa miaka ishirini na mitano (Hesabu 8:24). Lakini walipuuzia umri huu walioambiwa kwenye Hesabu 1:3, mlinzi mara nyingi aliitwa na’ar, na mwenye umri wa juu ya hapo kwenye ‘ujana’ hakuwa kwene idadi kamili.

 

Inawezekana sana kwamba huena neno hili ‘kijana’ wakati mwingine lilitumika mara chache kumaanisha uchanga au hali ya kutokomaa. Watu kadhaa kwenye biblia wanajionyesha wenyewe kuudhalilisha ‘vijana’. Yeremia haelezei vizuri kuhusu miaka ya umri wake anapojitetea kwa kusema: ' Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto’. (Yeremia 1:6), wala Mfalme Sulemani alipokuwa anaomba: ‘Na sasa, Ee Bwana, Mungu wangu, umenitawaza niwe mfalme .... nami ni mtoto mdogo tu' (1Wafalme 3:7); wanaonyesha tu hali ya kuwa waaminifu na wanyenyekevu. Sawa na kama ilivyo kwenye Waamuzi 6:15.

 

Ni kama ‘Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi’. (Mithali 20:29), na wakati ’ Siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kwa kiu' (Amosi 8:13), wote watakumbwa k

na maafa kuwafikia.

 

Vijana waliopo hawatajizoeza hekima ya wazee wao; kwa hiyo maonyo ya mara kwa mara kama ya kwenye kitabu cha Mithali, ambapo ‘wana’ wanatajwa kama watoto wa kila mwanaume (mfano Mithali 7:24). Vijana hawa wanaalikwa au wanapewa wito wa kuitafuta hekima ili wapate kuelewa (Mithali 8:32-36 na mara nyingi), na wameonywa wajiepushe na ‘wanawake wafujaji’ wanaowasubiri wakiwasubiria vijana wajinga (Mithali 7:4-12).

 

Lakinii Kohelethi, anaujua udhaifu wa umri wa uzee (soma jarida la Umri, Uzee) amsihipo Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo. Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako’ (Mhubiri 11:9; 12:1).

 

Sio mara ningi, historia ya mwanzoni ya Israeli imeelezewa kiushairi kuhusu ‘vijana’ wake na ama walisikitika kama wakati wa ukengeufu wa kitaifa (Ezekieli 23:19) au walikumbuka kwa uchungu kama wakati wa imani nzuri kati ya Mungu na watu (Hosea 2:15-17), kwa mujibu wa hisia ya mwandishi au lengo lake.

 

Kwa hiyo tunaona kwamba, kufikia umri wa utu uzima, yatupasa kuamua na kujikubali kuachana na umajimoto na utukutu au utundu ambavyo ni sehemu ya tabia za ujana.

 

Majukumu na Wajibu wa Kijana

Ni muhimu kuyajua majukumu na wajibu tunaopaswa kuwanao kwenye jamii ili tupate nafasi sahihi ya kibiblia. Kwenye Luke 22:26 Yesu anasema hivi:

 

Lakini kwenu ninyi sivyo; bali aliye mkubwa kwenu na awe kama aliye mdogo; na mwenye kuongoza kama yule atumikaye.

 

Tafsiri ya NIV Study Bible, kwenye ukurasa wa ufafanuzi wake kuhusu kifungu hiki inafurahisha sana. Inasema:

 

Yesu aliwasihi na kuwaonyesha mfano wa kiongozi mtumishi -  usaliti ambao haukuwa wa kawaida kuliko ilivyo siku zetu hizi.

 

Hata hivyo, usaliti huu ni unatendeka Kanisani na ni budi ufanyike. Maneno haya ya Yes uni ya muhimu kwa jinsi anavyotuambia sisi kuhusu hali na msimamo wa vijana kwa alivyoona Yesu. Alikuwa anamaanisha kwamba kijana anapaswa kutenda majukumu ya kujitoa na kujinyenyekesha. Matendo 5:5,10 imeandikwa tena hivi.

 

5 Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya. wale vijana wakaingia wakamkuta amekufa, wakamchukua nje, wakamzika pamoja na mumewe.  

 

10 Mara akaanguka miguuni pake akafa; wale vijana wakaingia wakamkuta amekufa, wakamchukua nje, wakamzika pamoja na mumewe.

 

Hii inaonyesha kuwa vijana yanapasa kujifunza kutumika kabla hawajatumikiwa au kuhudumiwa kimwili wao wenyewe. Mchakato huu wa utumishi ni ndipo kijana anavyopata hekima au busara.

 

Kwenye maeneo yote ya kitabu cha Mithali, inasema baba ni mwalimu, mtoto ni mwanafunzi. Utaratibu huu ndio anaotutaka sisi Mungu tuwenao.

 

Mithali 4:1 Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu, Tegeni masikio mpate kujua ufahamu.

 

Yampasa kijana kumsikiliza mwalimu wake kwa moyo wa unyenekevu wa kukubali na kupambanua kwa mujibu wa Biblia. Nyakati hizi ni ngumu kwa vijana sasa.

 

Mhubiri 11:7-10 Kweli nuru ni tamu, tena ni jambo la kupendeza macho kutazama jua. 8 Naam, mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie yote; lakini na azikumbuke siku zijazo za giza, kwa maana zitakuwa nyingi. Mambo yote yajayo ni ubatili. 9 Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni. 10 Kwa hiyo ondoa majonzi moyoni mwako, nawe uuondoe ubaya mwilini mwako; kwa maana ujana ni ubatili, na utu uzima pia.

 

Mhubiri 12:1 Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo

 

Huenda hivi ndivyo ilivyotokea. Vijana walifaidi wakati wao bali walimsahau Muumba wao. Ujana ni wakati wa kuufurahia na kufaidi, lakini unaendana mkono kwa mkono na hali ya kujitoa kwenye kweli. Inapendeza kugundua kwamba historia ya mwanzoni ya Israeli inaitwa ya ‘ujana’ na inakumbukwa sana kwa mazuri yake au inasikitisha kutegemea na mtazamo wako. ‘Vijana’ wa Israeli walipotoshwa kwa mujibu wa Ezekieli 23:19, lakini Hosea 2:15-17 anakumbuka kwa wema sana ujana kuwa ni kama wakati wa imani nzuri. Kwa hiyo thamani ya ujana ni kutumia uthubutu wetu na nguvu zetu ili kutumikia jamii zetu, kutumia nguvu zetu na hari yetu ili kujitoa na kujifunza ili kwamba wakati wetu utumike vizuri hapa uniani na hukumu yetu sio kubwa sana.

 

Waandishi wa Biblia, walipokuwa wanamuelezea kijana kwa maana ya shujaa/mtumishi walitumia neno na'ar (Waamuzi 7:10). Hii inaonyesha jinsi vijana walivyokuwa wanachukuliwa. Umuhimu wa nguvu zao ulikuwa mkubwa. Nguvu zao na misisimko yao iliwafanya vijana kuwa wafanyakazi wakuu sana na walifanya kazi kwa bidii na kwa nguvu kwenye jamii zao. Wazee kwa busara yao iliyotokana na uzoefu wao, waliyasimamia mambo ya kijamii na waliwategemea vijana kwa usalama wao na vijana waliwategemea wazee kuwaelimisha au kuwashauri. Utaratibu huu unaendelea kudumu.

 

Watu wote/wanawake walilihudumia jamii kwa ujumla kulitenda kazi kwa mtazamo sahihi na halisi wa Kimungu. Mahali pengine, utaratibu huu ulikiukwa.

 

Vijana hawakujua kwamba kuupenda kwao uhuru, uelewa na kupevuka kiutuuzima, kabla hekima haipo husababisha machafuko, matatizo ya mihadarati na jamii kwa ujumla tabia wanayojisikia nayo ni potofu. Miaka ya sitini ilikuwa ni kipini ambacho hali ya kupenda fedha na mali kwa vijana iliibuka. Vitu kama Muziki, magari, mitindo, michezo, nk, vilipenwa na kuhitajika kila mahali, na tasnia za watuwazima wa kwenye jamii zetu ziliipokea hali hii kwa ulafi na kwa kujilimbikizia na kujijali wenyewe.

 

IWafalme 12:6-14 Mfalme Rehoboamu akataka shauri kwa wazee waliokuwa wakisimama mbele ya Sulemani, baba yake, alipokuwa hai, akasema, Mwanipa shauri gani ili niwajibu watu hawa? 7 Wakamwambia wakasema, Ukikubali kuwa mtumishi wa watu hawa leo, na kuwatumikia, na kuwajibu, na kuwapa maneno mazuri, basi watakuwa watumishi wako daima. 8 Lakini akaliacha shauri lile la wazee, walilompa, akataka shauri kwa wale vijana waliokua pamoja naye, na kusimama mbele yake. 9 Akawaambia, Mwanipa shauri gani ili tuwajibu watu hawa, waliosema nami, wakinena Utufanyie jepesi kongwa lile alilotutwika baba yako? 10 Na wale vijana waliokua pamoja naye wakamwambia, wakasema, Uwaambie hivi watu wale waliokuambia, wakisema, Baba yako alilifanya zito kongwa letu, bali wewe utufanyie jepesi, uwaambie hivi, Kidole changu cha mwisho ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu. 11 Basi kama vile baba yangu alivyowatwika kongwa zito, mimi nitaongeza kongwa lenu; baba yangu aliwapiga kwa mijeledi, bali mimi nitawapigeni kwa nge. 12 Basi, Yeroboamu na watu wote wakamfikia Rehoboamu siku ya tatu, kama mfalme alivyoamuru, akisema, Mnirudie siku ya tatu. 13 Mfalme akawajibu watu wale kwa ukali, akaliacha shauri lile wazee walilompa; 14 akawajibu kama vile walivyomshauri vijana, ...

 

1Wafalme 12:19. Hivyo Israeli wakaasi juu ya nyumba ya Daudi hata leo.

 

Tunasoma hapa matokeo ya kusikiliza ushauri wa vijana na watoto wadogo ambao hawajapevuka bado. Mfalme aliukataa ushauri wa busara wa wazee na akauchukua ule wa vijana waovu. Matokeo yake yalikuwa ni vurugu na chuki katika jamii. Mioyo ya mababa iliwachukia watoto wao, na watoto wakawachukia baba zao. Vijana walilazimisha na kumshauri na viongozi wakawasikiliza.

 

Vijana wanauona unafiki kwenye uongozi wao. Watu hhuko Marekani, waliojidai kuwa ni wacha Mungu na watu wenye amani sana – na bado watoto wanajificha chini ya meza ili kujikinga na vita vya mabomu ya nyukilia na kwamba Mungu wao anawapenda Wakristo waliofanya kazi kubwa ya kupangilia. Wakati vijana walipoasi – kuliko kujifanya kuwa watumishi na kutumikiana wenyewe kwa wenyewe kwa uongozi, hekima na nidhamu – waligeukia kwenye mambo yao wenyewe na ndipo umbali kati ya vijana na watu wazima uliongezeka. Wanaiita hali hii umbali wa kiuzawa kati ya kizazi kimoja na kingine.

 

Machafuko yote yaliyopo sasa hapa duniani kwene desturi ya kutumia mihadarati kwa vijana yanatokana na dhambi moja – dhambi ambayo waovu wote wameianzisha. Wakati Shetani alipochagua kujiona yeye mwenyewe kuwa ni mkubwa kuliko walivyokuwa wao. Desturi ya vijana kwenye miaka ya sitini ilijaribu kujiona wao wenyewe kuwa wakubwa na vijana walidai usawa na watu wazima – ni wazo sawa tu na alilokuwanalo Shetani – ni wazo hilohilo linalowafanya wanadamu kumfanya Yesu kuwa sawa na Mungu. Kwa kufanya hivyo, tunahalalisha udhaifu na dhambi zetu za kiburi na tama kwa kujitukuza au kwa utukufu wetu wenyewe.

 

Wito wa vijana ni kuona maono na kutaka kwa bidii hekima kwa gharama yoyote. Hekima ndiyo wito wetu mkuu.

 

Mithali 8:1-22 Je! Hekima halii? Ufahamu hatoi sauti yake? 2 Juu ya mahali palipoinuka karibu na njia, Penye njia panda, ndipo asimamapo. 3 Karibu na malango, mahali pa kuingia mjini, Mahali pa kuyaingilia malango anapiga kelele. 4 Enyi watu, nawaita ninyi; Na sauti yangu ni kwa wanadamu. 5 Enyi wajinga, fahamuni werevu, Nanyi wapumbavu, mpate moyo wa kufahamu. 6 Sikieni, maana nitasema yaliyo mazuri, Na kufumbua midomo yangu kutakuwa maadili. 7 Maana kinywa changu kitasema kweli, Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu. 8 Maneno yote ya kinywa changu yana haki; Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi. 9 Yote humwelea yule afahamuye, Yote huelekea mbele yao waliopata maarifa. 10 Pokea mafundisho yangu, wala si fedha, Na maarifa kuliko dhahabu safi. 11 Maana hekima ni bora kuliko marijani; Wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo. 12 Mimi, hekima, nimefanya werevu kuwa kao langu; Natafuta maarifa na busara. 13 Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia. 14 Shauri ni langu, na maarifa yaliyo sahihi; Mimi ni ufahamu, mimi nina nguvu. 15 Kwa msaada wangu wafalme humiliki, Na wakuu wanahukumu haki. 16 Kwa msaada wangu wakuu hutawala, Na waungwana, naam, waamuzi wote wa dunia. 17 Nawapenda wale wanipendao, Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona. 18 Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. 19 Matunda yangu hupita dhahabu, naam, dhahabu safi, Na faida yangu hupita fedha iliyo teule. 20 Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu. 21 Niwarithishe mali wale wanipendao, Tena nipate kuzijaza hazina zao. 22 Bwana alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake, Kabla ya matendo yake ya kale.

 

Utumishi ni mchakato pekee. Vijana wanapaswa kujifunza kuwatumikia tena wakubwa wao yaani watu wazima na hawa watu wazima vivyohivyo wanapaswa wajifunze kuwahudumia vijana wao. Vinginevyo, imani haitadumu.

 

Kwa nini ilitokea hivi?

Mtazamo ni kwamba The view is uasi wa vijana uliachiliwa utokee kwa tukio muhimu sana katika nyakati za mwisho. Matokeo ya uasi huu yamekuwa makubwa sana nay a kutisha. Desturi ya kutumia mihadarati yamepelekea ubadhirifu, mauaji, kujiua, fujo mitaani, kutoroka majumbani na wadokozi wa majumbani, udokozi wa kukwapua vitu, wizi, na kadhalika wa kadhalika, kiasi kwamba wanaweza hata kuwapiga watu wazima na kuwaibia mali zao ili na wao waweze kujinufaisha kimahitaji.

 

Hatimaye, serikali itavunjika kwa namna utaratibu huohuo unaoumiliki. Serikali inaweza kusema kwamba vijana wamefanya machafuko haya na miili yenye kuharibika waiwezi kwendana nao. Hivyo uhalalisho wa kwanza wa utawala wa mnama na imani yake umeanza.

 

Kile wanachetakiwa vijana kukifanya kama wako makini na wanapenda kusaidia kulitatua tatizo ni kuitafuta hekima kwa maombi na gharama yoyote ile. Tangu washirika na watu wenye busara, waitafute kweli kwenye Biblia. Kuna kazi kubwa sana ya kufanya katika kusaidia matatizo ya ndani ya yene athari kubwa ya uasi unaoendelea sasa wa watu kumuasi Mungu, uasi ulioanza miaka mingi iliyopita. Hadi leo watu wangali wakihangaikia madaraka na mamlaka juu ya binadamu wenzao.

 

Ukikubali kuwa mtumishi wa watu hawa leo, na kuwatumikia, na kuwajibu, na kuwapa maneno mazuri, basi watakuwa watumishi wako daima.

 

Kumbuka: nukuu za biblia zimechukuliwa kutoka biblia ya Kiswahili ya Union Version.