Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[CB10]

 

 

 

 

Ibrahimu na Sara

 

(Toleo La 2.0 20030923-20070123)

Bwana akamwambia Abramu, “Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki." Jarida hili limetokana na sura ya 6 ya jarida la Hadithi za Biblia [The Bible Story Volume 1] iliyoandikwa na Basil Wolverton, na kuchapishwa na Idara ya Machapisho ya Ambassador College, na majarida menguine ya Abramu na Sodoma (Na. 91) na Melkizedeki (Na. 128), yaliyochapishwa na CCG.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki ©  2003, 2007 Christian Churches of God, ed. Wade Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ibrahimu na Sara


 


Tunaendelea hapa kutoka kwenye jarida la Nimrodi na Dini ya Uwongo (Na. CB9).

 

Miaka miwili baada ya gharika kuu, wakati mwana wa Nuhu Shemu alikuwa na umri wa miaka 100, Shemu alikuwa na mtoto aliyeitwa Arfaksadi (Mwanzo 11:10). Wakati Arfaksadi alipokuwa na uri wa miaka 35, alikuwa na mtoto aliyeitwa Sela (Mwanzo 11:12). Vizazi kadha vilienda kwa jinsi hii. Wakati ya takriban miaka 300 kupita, mtu aliyeitwa Abramu alizaliwa. Jina la baba yake aliitwa Tera (Mwanzo 11:26).

 

Abramu alilelewa kwenye mji au mjini huko Mesopotamia (Matendo 7:2) ulioitwa Uru, sio mbali sana na mahali ambapo Nimrodi alianza kuujenga mnara wa Babeli (Mwanzo 11:2). Hapa Abramu, kama alivyokuwa Nuhu, alijifunz kuzitii Sheria za Mungu, wakati kwamba watu wa ulimwengu ule walikuwa ni waabudu sanamu na wakiishi mbali sana na njia au maagizo ya Mungu. Abramu alikuwa ni mmoja wa wachache ambao hawakuzishiriki imani hizi za kipagani. Akiwa huko Mesopotamia Abramu alikuwa na maono yake ya kwanza au wito kutoka kwa Mungu kuondoka na kuiacha nchi yake na watu wake (Matendo 7:2). Wakati alipokuwa na umri wa takriban miaka sabini na tano, Abramu alikuwa tena ameambiwa aondoke na familia yake na kwenda nchi nyingine.

 

Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; (Mwanzo 12:1)

 

Abramu anamtii Mungu

Mungu alimuahidi Abramu kwamba kama atatii amri na maongozi yake yote, basi atajibarikia na atafanyika kuwa baba wa taifa kubwa (Mwanzo 12:2-3). Kipindi ambacho taifa hili litafurahia baraka fulani za muhimu na za aina yake, Abramu hakujua ni nchi gani anayokwenda na ipoje, na pia hakujua ni Baraka gani watakayopewa watu wake, lakini alimuamini na kumtumaini Mungu na akamtii.

 

Akiwa pamoja na mke wake, Sarai, Abramu alimchukua na kwenda naye mpwa wake Lutu na mke wa Lutu, na wachungaji ili wakachunge mifugo yao pamoja na kondoo zao na watu mahiri katika shughuli za kuchunga ili wachunge mifugo ya ng’ombe. Sio jambo dogo kwa Abramu kuondoka na kuiacha familia yake na mali zao na kwenda nchi ya mbali (Mwanzo 12:4).

 

Baada ya majuma mengi ya kusafiri, walifika kwenye nchi ya Kanaani, wakati Mungu alipomwambia Abramu kuwa anapaswa aondoke (Mwanzo 12:5). Kanaani ilikuwa ni nchi yenye rutuba sana ambayo ilikuwa na udongo mzuri sana wa kulima na kukuzia vitu. Lakini watu wan chi ile walikuwa wabaya na watenda dhambi sana. Kwa hiyo Mungu alisababisha baa la njaa lije kwenye nchi ile. Njaa hii ilitokea mara tu baada ya Abramu kufika huko Kanaani (Mwanzo 12:10). Ukosefu wa mvua ulisababisha matunda na miti, uoto wa mbogamboga na nyasi kukauka. Kulikuwa na chakula kidogo kwa ajili ya wanyama waliokuwanao kina Abramu na Lutu na ambao waliwaleta huko Kanaani. Na kusingekuwa na ng’ombe na kondoo, kusingekuwa na chakula cha kutosha kwa Abramu na wengine wote aliokuwanao.

 

Abramu anaenda Misri

Habari zililetwa na wasafiri kwamba katika nchi ya Misri hakukuwa na uhaba wa mvua, kwa hiyo Abramu na familia yake walishuka na kwenda huko Misri ili kuokoa mifugo yao. Mungu alikuwa amekwishaweka agano na Abramu la kumpa nchi na kumpa chakula palepale alipokuwa, lakini bado hakuwa na imani ya kutosha kukaa pale na kumtumainia Mungu. Hatimaye tutaona kwamba Ibrahimu alikuwa ni mtumishi mwaminifu na rafiki wa Mungu kupitia utii wake. Soma jarida la Ibrahimu na Isaka: Sadaka Adilifu (Na. CB11).

 

Katika nchi ya Misri ustaarabu mkubwa ulianza na kuwepo mara tu baada ya gharia kuu. Wafalme wa Misri, au Mafarao, walikuwa matajiri wakubwa licha ya ibada zao za sanamu walizokuwanazo. Walifaidi mema yote yaliyomea kutoka ardhini. Chochote walichopungukiwa walikichukua kutoka kwa wengine.

 

Kwakuwa Sarai alikuwa ni mwanamke mzuri sana, na Abramu alikuwa anamuogopa mfalme wa Misri na kumdhania kuwa huenda angempenda na kumchukua awe miongoni mwa wake zake wengi, alimuomba Sarai aseme kuwa yeye ni dada yake badala ya kumwambia kuwa ni mke wake (Mwanzo 12:12-13). Sarai kwa kweli alikuwa ni mke ambaye alikuwa ni dada-binamu na Abramu, kwa kuwa baba yake alikuwa pia ni baba yake Abramu, lakini mama yake hakuwa ni mama wa Abramu. Abramu alitaka kuitumia fursa hii kwa kunena nusu ukweli kwakuwa aliogopa kwamba kama itajulikana kwamba alikuwa ni mume wa Sarai, Wamisri wangeweza kumuua ili kwamba Sarai awe huru kuolewa.

 

Mfalme ambaye Abramu alikuwa anamuogopa akatokea maramoja. Ingawa alikuwa na umri wa takriban miaka 65, Sarai bado alionekana kuwa kama mwanamke kijana na mzuri sana. Alikuwa anavutia sana kumuangalia. Kabla ya hapo ilisemekana au kulikuwa na uvumi kwamba mwanamke huyu asiye wa kawaida angepewa upendeleo wa aina yake na Farao, ambaye aliamuru kuwa aletwe kwenye jumba lake la kifalme.

 

Farao alifurahishwa sana na mwonekano na umbo la Sarai na akapanga awe mke wake, na akampa Abramu zawadi zenye thamani kubwa zikiwemo wanyama wa kufuga, watumishi na makazi mazuri. Lakini Abramu alitenda dhambi kwa kuwa aliongopa na Farao alitenda dhambi kwa kumchukua mke wa mtu mwingine. Kwa ajili hii Mungu akaiadhibu kwa magonjwa nyumba ya Farao. Farao akamkasirikia sana Abramu, lakini akamrudisha Sarai kwa mume wake, na akawaamuru watu wake wahakikishe kwamba Abramu na familia yake na mali zake wasindikizwe kwa usalama wanapotoka Misri (Mwanzo 12:14-20). Tunaweza kuona hapa kwamba ndoa na Sheria za Mungu zilijulikana hata zama hizo.

 

Kurudi Kanaani

Abramu na Lutu na wake zao na watumishi wao ndipo waliondoka na mifugo yao na kurejea Kanaani. Abramu akaenda moja kwa moja mahali apokuwa amemjengea Mungu madhabahu alipokuja mara ya kwanza huko Kanaani. Ale akaomba msamaha na nguvu (Mwanzo 13:4).

 

Katika kipindi hik njaa katika Kaaani ilikuwa imeisha. Mifugo na wanyama aliokuwanao Abramu na Lutu iliongezeka sana. Mungu alimbariki Abramu na Lutu pia kwa kuwa alikuwa ni sehemu ya familia ya Abramu. Lakini kwa kuwa wanyama walikuwa ni wengi sana, watumishi wa Abramu na wa Lutu walianza kugombea mahali pa kuwafugia na malisho, sehemu zilizokuwa na majani mengi mazuri na maji. Abramu hakupenda kutokee matatizo na mtengano wa kudumu na Lutu, kwa hiyo akamshauri achague aende sehemu nyingine tofauti nay eye akaishi huko.

 

Mungu alimuahidi nchi ile Abramu. Ilikuwa ni haki yake Abramu achague kwanza mahali alipotaka kwenda ili wanyama wake wakapate malisho, lakini kwa moyo usio na ubinafsi alimwambia Lutu achague kwanza. Lutu akatazama chini kwenye udongo mzuri na wenye utajiri kwenye bonde la Mto Yordani, na akasema anaitaka nchi ile. Hii inamaanisha kwamba alimwachia Abramu uwanda wa juu, lakini Abramu aliridhika kwa kuwa alimuona Lutu alikuwa ameridhika (Mwanzo 13:5-12).

 

Hatimaye Mungu akanena na Abramu tena akimwambia kwamba nchi yote anayoiona pande zote itakuwa yake milele nay a watoto wake, ambao idadi yao itakuwa kama mchanga au mavumbi ya Dunia. Kisha Abramu akaliondoa hema lake akaenda Hebroni na huko akamjengea BWANA madhabahu (Mwanzo 13:14-18). Hii ilikuwa ni ahadi ya ajabu kwa Abramu, ambaye ata hivyo kwa kipindi hiki alikuwa anakaribia umri wa miaka 80 na akiwa hana watoto.

 

Wakati huohuo Lutu na familia yake wakatweka hema zao karibu na mji wa Sodoma kwenye bonde tajiri la Yordani. Lutu alidhani kuwa amefanya uchaguzi sahihi na wa busara kwa kwenda kwake kule. Hakujua kuwa atakumbana na matatizo makubwa na watu wanaoishi huko. Walikuwa ni wagomvi na wenye tabia mbaya zisizo za kawaida. Akiwa kama mchamungu, Lutu asingepaswa kwenda na kuishi karibu na watu wale.

 

Vita inalipuka huko Kanaani

Muda mfupi tu baada ya Lutu kwenda maeneo ya Sodoma, vita ikaanza kati ya wafalme wa miji mitano ya bonde la Yordani na wafalme hawa wane wan chi hii walikuwapo wakati Nimrodi alipoanzisha ufalme wake. Wafalme wanne waliombali na Yule mwingine walishinda vita. Watu walioishi kwenye miji ya mabonde makuu mawili, yaani miji ya Sodom na Gomorrah, walifukuzwa na kukimbilia milimani walikuwa ni baadhi ya wale walioponyoka na kuokoka. Wengi wao walikamatwa na kufanywa watumwa wa waliowashinda. Miongoni mwa hawa mateka walikuwa ni Lutu, familia yake na watumishi wake. Mali zote za Lutu walimnyang’anya na zikachukuliwa.

 

Wakati ujumbe ulipomfikia Abramu kuhusu yale yaliyotokea, Abramu alitoka na kuwafuata wale wafalme walioshinda akiwa na wanaume wa vita takriban 318 (Mwanzo 14:14). Ilihitaji ujasiri kukabiliana na jeshi lenye wanaume wengi zaidi kiasi kile kuliko wale aliokuwanao Abramu. Lakini Abramu alimwangalia Mungu amsaidie na Mungu alimsaidia kwa kumpa fursa ya kuizunguka ki kimyakimya ngome ya wafalme wanne washambulizi muda wa usiku. Watu wao walichukuliwa kwa mshangao. Kwenye giza hawakuweza hawakuweza kusimulia ni kwa kiasi gani yale majeshi yalikuwa yanawashambulia. Kwa kuogopa kwamba huenda walikuwa ni wengi sana, walikimbilia milimani karibu na Dameski hadi ande za kaskazini, wakiwaacha nyuma mateka na mateka waliotekwa kwenye bonde la Yordani (Mwanzo 14:13-16).

 

Mfalme wa Sodoma akaja pamoja na watu waliobakia ili kupa heshima Abramu kwa kile alichowafanyia maadui. Hata hivyo, hakujua kwamba Abramu alifanya hivyo kwa sababu ya Lutu na familia yake. Mkutaniko huu ulifanyika mara moja karibu na mji wa Salemu, ambao hatimaye ulikujaitwa Yerusalemu.

 

Melkizedeki, mfalme wa Salemu, pia alijitokeza kwenda kukutana na Abramu. Watumishi wa Melkizedeki wakamletea mkate na mvinyo Abramu na watu wake mashujaa (Mwanzo 14:13-16). Melkizedeki akambariki Abramu kwa kuwaokoa watu ambao walikuwa mateka. Melkizedeki alikuwa sio mfalme tu bali pia alikuwa  ni kihani wa Mungu Aliye Juu Sana (Waebrania 7:1).

 

Inapendeza kujua kwamba Masihi alipaswa kuja na kuwa kuhani wa milele baada ya utaratibu wa Melkizedeki. Yeye ni Kuhani Mkuu wa milele, lakini hakuwa Melkizedeki aliyekutana na Ibrahimu. Yeye alikuwa ni kuhani mwingine wa Namna ile (Waebrania 7:11). Yesu alikwenda kama mtangulizi kwa niaba yetu. Hii inamaana ya kwamba inatupasa sisi pia kuwa makuhani wa Namna ile. Ukuhani wa Melkizedeki ni sehemu ya ahadi ya Mungu (Waebrania 6:17-20).

 

Bwana ameapa, Wala hataghairi, Ndiwe [Masihi] kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki (Zaburi 110:4)

 

Maana ya mkate na divai au mvinyo uliotolewa na kupewa Ibrahimu, inahusiana moja kwa moja na Mkate na Divai au mvinyo ulioanzishwa kutumiwa na Masihi, kwenye Mlowa Meza ya Bwana. Tuko hili lilionekana kuelekea kwenye kutolewa kwa Roho Mtakatifu chini ya huduma mpya ya kikuhani wa Aina ya Melkizeeki, kama ulivyoanzishwa na Masihi.

 

Abramu alimpa Melkizedeki fungu la kumi au sehemu ya kumi ya vitu vyote vilivyschwa na washambuliaji na ambao walikimbia ingawaje Abramu hakujichukulia chochote kiwe mali yake (Mwanzo 14:20-24). Hii ni kutuonyesha kwamba uzao wa Ibrahimu watatoa zaka zao kwa makuhani. Sheria ya Mungu ta utoaji zaka inasema kuwa mtu yeyote anayeshindwa kutoa zaka ya mapato yake kwa makuhani wa Mungu anamuibia Mungu (Malaki 3:8). Mali zote tulizonazo ni za Mungu. Utoaji wa sehemu ya kumi kumrudishia Mungu ni moja ya njia sahihi za kuonyesha kumtii na kumheshimu yeye.

 

Mfalme wa Sodoma alitoa na kumpa zawadi Abramu kwa chochote alichokifanya, lakini Abramu alikataa kupokea vitu hivyo vyote. Litamani na kuzitaka Baraka za Mungu za utajiri wa mfalme wa kidunia alizozitoa. Inafurahisha kuona kwamba watu wa Sodoma walibarikiwa hapa kwa sababu ya Abramu, hata kama walikuwa wanaishi maisha yaliyo kinyume kabisa na Sheria za Mungu.

 

Ahadi nyingine kwa Abramu

Miaka kadhaa mingine iliyofuata, wakati Abramu akiishi maisha ya amani nyingi hemani kwake kenye milima ya juu ya bonde la Yordani, Malaika wa Bwana alikuja tena na kuongea naye kwenye maono. Alimuambia kwamba kwasababu ya utii wake basi atakuwa baba wa taifa kubwa. Abramu na mke wake walikuwa wanaendelea kuzeeka wakiwa wamepita ule umri wa kuweza kupata mtoto, kwa hiyo Abramu alishangazwa sana na ahadi hii. Akamkumbusha Yule Malaika kwamba yeye hakuwa na mtoto na hana mrithi wa kurithi mali zake (Mwanzo 15:1-3).

 

Abramu aliambiwa kwamba mrithi wake atakuwa ni mtoto wake mwenyewe, na kwamba kama anaweza kuzihesabu nyota zilizo gizani usiku, basi angeweza kujua idadi kubwa ya watu watakaotokana na kizazi chake kutokana na mtoto wake mmoja.

 

Abramu aliamini na alibarikiwa kwa ajili hiyo (Mwanzo 15:6; Warumi 4:20-22). Ndipo Abramu akaambiwa awachinje baadhi ya wanyama waliosafi na ndege na awaangike nje wawe sadaka (Mwanzo 15:9-10).

 

Abramu alitii

Mara tu usingizi mzito ulimpata Abramu. Akaota kwamba alikuwa kwenye giza nene sana, na kwamba sauti ya Malaika ilimjia ikitokea kwenye lil giza, ikimwambia mambo yatakayotokea miaka mingi baada ya kufa kwake Abramu (Mwanzo 15:12-16).

 

“Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne. Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi." (Mwanzo 15:13-16). Ndoto hii ilikuwa inatabiri uteka na utumwa wa wana wa Israeli katika nchi ya Misri utakaotokea baadae.

 

Abramu aakaamka na akaona moto mkubwa kama tanuru ukipita mbele yake na ukiteketeza zile nyama za wale wanyama na ndege aliowawamba nje ya hema lake. Wakati alipokuwa analiona jambo hili la kushangaza, imani yake kwa Mungu iliimarika sana kuliko mwanzo (Mwanzo 15:17). Na siku hiyohiyo Mungu akafanya agano linguine na Abramu la kwamba atakuwa na uzao mwingi na watakuwa na mali nyingi na kumiliki nchi kubwa pamoja na baraka nyingi nyingine za mali.

 

Mungu mara zote huwaahidi mambo mazuri wale wanaomtii. Ahadi yake kwa Abramu ni moja ya zile zilizofanya taadhima kubwa ulimwenguni kote kwa kipindi cha maelfu ya miaka. Katika vizazi vyote vya uzao wa Abramu vimefaidi utajiri mkubwa na Baraka za mali kuliko mataifa mengi mengine.

 

Mtoto wa kwanza wa kiume wa Abramu

Sarai, mkewe Abramu, alikuwa na umri wa miaka 75 wakati ule. Aliamini kwamba alikuwa amezeeka sana sasa na hangea tena kuzaa mtoto. Hakuweza kujua kuwa ilikuwa inawezekana kwake na kwa Abramu kuwa ni wazazi wa mtoto ambaye kutoka kwa huyo mamilioni ya watu watatokea. Sarai alikuwa na suria wa Kimisri, Hajiri, ambaye alikuwa ni mwanamke kijana na mdogo. Ndipo Sarai akamwambia Abramu kwamba amchukue huyo Hajiri ili awe mke wake wa pili, akitarajia kwamba Hajiri atawzalia mtoto atakayekuwa wa kwao wote, Abramu na Sarai. Wakati huo mara nyingi wanaume walikuwa wanaoa zaidi ya mke mmoja. Ndipo Abramu akafanya kama Sarai alivyomshauri, na ndipo Hajiri akawa mzamzito au akapata mimba (Mwanzo 16:1-3).

 

Hatimaye Hajiri akaanza kumdharau Sarai kwa kuwa alijidhania kuwa alikuwa bora kuliko Sarai kwa kuwa sasa alikuwa na mimba yam toto wa Abramu. Ndipo Sarai akamfanyia ukatili Hajiri na akamkimbia. Lakini Malaika wa Bwana akakutana na Hajiri na akamuuliza alikuwa anafanya nini pale. Akamueleza kile alichokuwa anafanya pale na Malaika akamwambia arudi kwa mke wa bwana wake. Hajiri akaambiwa pia kwamba atazaa mtoto wa kiume na amuite jina lake Ishimaeli. Malaika huyu wa Bwana akamahidi pia kwamba atambariki na kumpa uzao mwingi, uzao utakaoitwa ni wa Waishimaeli, na ambao utakuwa unatokana na maseyidi au watoto wake 12. Wakati Hajiri alipomzaa Ishimaeli, Abramu alikuwa na umri wa miaka 86 (Mwanzo 16:4-15).

 

Uzao au wana wa Ishimaeli ni hawa wa mataifa ya Kiarabu wanaotokana na ahadi aliyoitoa Malaika kwa Hajiri. Malaika huyu alimuita "Mungu anayeona". Huyu alikuwa ni kiumbe aliyeitoa Torati na kuwapa wana wa Israeli walipokuwa Wanatoka utumwani.

 

Agano la tohara

Miaka kumi na tatu ilipita. Wakati Abramu alipofikia umri wa miaka 99, Bwana akamtokea na kumwambia: "Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu!" (Mwanzo 17:1).

 

Tunajua kutoka kwenye Yohana 1:18 kwamba hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu Baba wakati wowote, kiumbe huyu aliyeongea na Musa hapa ni akifanya kazi ya ujumbe au Malaika wa Yahova Aliye Juu Sana.

 

Huku akitetekema, Abramu aliinamisha kichwa chake na kusujudu ardhini wakati Malaika alipomwambia kwamba kwakuwa amezitii Sheria za Mungu, basi ataitunza ahadi aliyomuahidi miaka mingi nyuma. Akamwambia Abramu kwamba jina lake lapasa libadilike aitwe Ibrahimu, ambalo maana yake ni baba wa watu wengi (Mwanzo 17:3-6). Na jina la Sarai libadilike na aitwe Sara, ambalo maana yake ni mfalme mwanamke au malkia.

 

Agano alilopewa Ibrahimu lilikuwa ni kwamba yeye na watu wote wa nyumbani mwake na watoto wake wajao na uzao wake wote ujao walishike. Ishara ya agano hili ilikuwa ni kwamba watoto wote wa kiume waliopo watahiriwe. Na kizazi chote kijacho pia wawatahiri watoto wao wachanga wanapofikia umri wa siku nane (Mwanzo 17:9-14). Hata hivyo, agano hili liliwekwa kwa kupitia Sara pia na kwa Bwana akasema, "naye atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa kabila za watu watatoka kwake." (Mwanzo 17:15-16).

 

Kisha Mungu akamahidi Ibrahimu kwamba hakika Sara atazaa mtoto, ingawa alikuwa tayari ana umri wa miaka themanini na tisa. Mtoto huyu alitakiwa aitwe Isaka (Mwanzo 17:15-16, 19). Soma jarida la Isaka: Mtoto wa Ahadi (CB12).

 

Wageni watatu

Sio kipindi kirefu baada ya wageni watatu walipomjia au kutembelea kwenye hema ya Ibrahimu. Watu hawa walikuwa ni Malaika waliomtokea kwa umbo la wanadamu wanaume (Mwanzo 18:1-2). Katika siku hizo, kwakuwa kusafiri kulikuwa ni jambo gumu sana na kunachosha, basi ukarimu ulikuwa ni mwingi. Ibrahimu akawakaribisha watatu hawa wale chakula na kupumzika. Chakula kikaandaliwa kwa ajili yao (Mwanzo 18:3-8). Baada ya wao kula, Ibrahimu aliarifiwa kwamba ndani ya kipindi cha mwaka mmoja Sara atakuwa na mtoto. Hii ilikuwa ni habari ya kupendeza na kushangaza kwa Ibrahimu na Sara. Na hasa Sara kwa hakika ilikuwa ni vigumu sana kwake kuamini habari hii (Mwanzo 18:9-15).

 

Wakati watu wame walipoinuka na kuondo waliiangalia Sodoma. Kisha Bwana akamwambia Ibrahimu kuwa wale malaika walikuwa wanakwenda Sodoma ili kwenda kujionea ni kwa kiasi gani watu walivyo waovu watu wanaoishi kule.

 

"Bwana akasema… basi, nitashuka sasa nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua. (Mwanzo 18:16-22).

 

"Ibrahimu akakaribia, akasema, ...Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu, wala hutauacha mji kwa ajili ya hao hamsini wenye haki waliomo?

 

"Bwana akasema, Nikiona katika Sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha mahali pote kwa ajili yao.”

 

Ndipo Ibrahimu akauliza kama Sodoma inaweza kupona iwapo kama kutakuwa na watu arobaini na watano wema wakionekana kuwepo ndani yake. Jibu lilikuwa ni kwamba hata kama wangekuwa wameonekana watu arobaini tu, mji ungeweza kupona. Ibrahimu akaendelea kuuliza kuhusu jambo hili, kila mara akipunguza idadi ya watu. Hatimaye aliambiwa kwamba hata kama kama watakutwa watu kumi tu humo Sodoma, basi mji ungeweza kupona (Mwanzo 18:23-33). Ibrahimu alikuwa anawaombea wenyehaki na wachamungu waachwe wasiangamizwe wakiwemo watu wa familia ya ndugu yake.

 

Lutu, mjomba wake, na ambaye Ibrahimu alimuokoa kutokana na uteka wa wafalme walioishambulia Sodoma, alifanya uamuzi usio wa busara wa kurudi tena kule na kuishi. Jioni ile malaika wawili walioonekana kama wanadamu, walifika Sodoma na wakakutana na Lutu ambaye aliketi kwenye mmoja kati ya malango ya mji ule (Mwanzo 19:1). Lutu akaona kuwa watu wale walikuwa ni wageni, na akawauliza kwa ustaarabu na upole weingie nyumbani mwake ili wale chakula. Hakujua kuwa walikuwa ni wajumbe wa Mungu. Kwanza walisita na kukataa lakini hatimye wakakubali kumfuata Lutu. Lutu mwenyewe alikuwa anapimwa.

 

Lutu alikuwa na chakula maalumu kwa ajili ya wageni hawa. Hatimaye, walipokuwa karibu ya kwenda kuondoka ili wakalale, kelele kubwa za kundi la watu liliizunguka nyumba ya Lutu. Watu hawa walikuwa wamekwishajua kwamba kulikuwa na wageni wawili kwenye numba ile. Wakamuomba na kumshurutisha Lutu awatoe nje mtaani, ambako walikusudia kuwatendea hawa wageni mambo ya aibu kubwa (Mwanzo 19:4-5).

 

Lutu akatoka nje na kuusihi umati ile wa watu waondoke. Lakini kundi hili lililobobea kwenye maovu halikumsikiliza Lutu. Baadhi ya wanaume wakamkimbilia, wakimzuia mlangoni. Ndipo wale malaika wawili waliokuwa ndani wakatoka, wakamwingiza Lutu ndani, na wakafunga vifungo vya mlango (Mwanzo 19:6-10). Kundi lenye hasira likakusanyika kwenye ile nyumba wakitaka kuivunja ili waingie ndani. Ndipo kitu kigeni kikatokea. Wale washambuliaji wakaanza kuona giza na kuanza kupigapiga huku na huko bila kujulikana wanalolifanya. Hasira yao ya kiwazimu ikabadilika kuwa maombolezo. Wajumbe wa Mungu walikuwa wamewapiga kwa upofu wa ghafla! (Mwanzo 19:11).

 

Wakati kundi lililobakia lilipoona kwamba kunakitu cha hatari na cha kuhuzunisha kinatokea, likaondoka na kurudi nyuma kutoka kwenye nyumba ile. Lakini kitu kingine kibaya zaidi kilikuwa kinakaribia kutokea. Watu wote wa mji walijiunga na kundi hili (Mwanzo 19:4). Na kwa kuwa watu wote walivyoonekana kuwa na hamu ya kufanya jambo hilohilo moja, na hii inamaanisha kwamba hakukuwepo kabisa na wale kumi wema kwenye mji huu wa Sodoma. Kwa hiyo hakukuwa na sababu ya Muungu kuuachilia.

 

"Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa; maana tutapaharibu sisi mahali hapa,…!"

 

Lutu akatoka nje kwa haraka na akawakuta vijana waliokuwa waliowachumbia binti zke. Alipowaambia kile kilichokuwa kinataka kutokea, walikataa kumuani (Mwanzo 19:14). Alikuwa amekata tama sana na kuchoka kwamba aliamua kukaa nyumbani mwake hadi walipokuja kuungana naye. Malaika wakamuonya kwamba anatakiwa aondoke mara moja, lakini Lutu alisitasita. Hata baada ya wao kumkamata, mke wake pamoja na binti zake wawili ambao walikuwa hawajaolewa na kuwalazimisha watoke nje ya mji, bado Lutu alitumaini familia yake iliyobakia wakawikawia na kusitasita (Mwanzo 19:15-16).

 

"Jiponye nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye mlimani, usije ukapotea.”

 

"nami siwezi kukimbilia mlimani nisipatwe na yale mabaya, nikafa. Basi mji huu u karibu, niukimbilie, nao ni mdogo, nijiponye sasa huko, sio mdogo huu? Na nafsi yangu itaishi.!" (Mwanzo 19:17-22).

 

Uvumilivu wa awa malaika ulikuwa karibu ufikie kikomo kwa Lutu, ambaye alikuwa akitumaini kuwa huenda wakweze watarajiwa wangemfuata. Wakaharakisha kumtoa. Jua lilikuwa karibu ya kuchomoza walipoufikia mji wa Soari, maili kadhaa kutoka Sodoma.

 

Turudi nyuma huko Sodoma, na huko Gomora, ambao ni mji mwingine mkubwa uliokuwa kwenye ardhi tambarare kulikuwa na kihoro cha ghafla kutingisha ardhi yao. Inadhaniwa kuwa kwenye maeneo ya karibu yenye mashimo yawakayo moto chokaa au lami, nchi ilifunua kinywa chake na kutoa nje mafuta, chumvi na kibiriti au tindikali vyote hivi vilitoka nje kwa nguvu hadi mawinguni. Kwa ghafla hii ilizichanganya pamoja na kulipuka kwa mshindo mkubwa usioelezeka, zikivuma, zikilipuka kwa mshindo na mshindo uliomkubwa na kwa kiwango cha juu sana. Sekune chache baadae vipande hivi vyenye miali hii ya moto vilinyeha chini kama mvua, kwa mamia viliangukia na kuilipukia miji hii ya Sodoma na Gomora kama kimondo kinapoanguka. Hakukuwa na jinsi ya watu waliokuwa ndani au karibu na miji hii kujiponya. Hata hivyo, Biblia inasema tu kwamba moto uliunyeshea kutoka juu mji huu wa Sodoma, moto uliotoka kwa Yahova kutoka Mbinguni.

 

Hata maeneo mengine mengi ya uwanda tambarare yaliyo karibu na miji miwili ilipatwa na joto kali na la kutisha sana. Hakuna kiumbe kilichoachwa hai kwenye ukanda ule wote. Vichaka vilivyokuwa vya kijani na vizuri na nyasi zote ziliwaka moto na kuungua. Masalia meingine ya lami zilichomwa, ikisababisha mfanyiko wa mnyororo uliofanya maangamizo makubwa yatokee pale kabisa (Mwanzo 9:24-25). Ndivyo Mungu alivyowafanyia watu wa kule kwa kuwa walikuwa wanajidhuru wenyewe kwa kuishi maisha yaliyozifuata njia zao wenyewe badala ya ktuzifuata Sheria zake.

 

Mwanzoni mwa mlipuko huu wa moto kama vile Lutu na sehemu ya familia yake walipokuwa wanakaribia kuingia Soari, mke wa Lutu aligeuka nyuma ili aone jinsi maangamizo haya yalivyo. Huenda alikuwa anakumbuka vitu vyake alivyoviacha huko nyuma na huenda anasikitishwa sana kuondoka na kuuacha mji huu muovu, licha ya matendo yake yote maovu na dhambi. Lutu na binti zake waliahakisha wakimbia kwenda Soari, lakini mke wa Lutu hakufika kamwe pamoja nao. Akageuka kuwa nguzo ya chumvi, iliyokuwa na umbo la mwanadamu (Mwanzo 19:26; Luka 17:29). Lakini Mungu ni mwenye rehema, na alimhurumia sana Lutu kwa kumtoa na binti zake wawili. Somo na fundisho la kujifunza sisi ni kwamba tunapokuwa tumeitwa na kutoka kwenye lindi la dhambi tusitamani tena kurudi nyuma na kuirudia, ila na tuziache kabisa pasipo kuwa na nia ya kuzirudia.

 

Ibrahimu anauona moto wa kutisha

Akiwa amekaa nyumbani kwake kwa amani milimni, Ibrahimu aliamka mapema asubuhi na akaangalia maeneo ya chini upande wa Sodoma. Alishangazwa na kuhofu kuona wingu la moshi likitoka na kuelekea juu wa uwanda uliochafuliwa kwa weusi na miji yake (Mwanzo 19:27-29). Ilieleweka wazi sana kwake kwamba hakukuwa hata na watu kumi tu waliokutwa wema humo Sodoma.

 

baadae Ibrahimu akagundua kwa furaha kuwa sana kwamba Mungu amejibu maombi yake. Mji wa Soari, ingawaje ulikuwa kwenye uwanda wa maeneo ya Sodomana Gomora, uliachwa usiangamie ili kwamba Lutu aweze kuukimbilia huko.

 

Alipogundua hilo kwa kukaa kwake huko Soari angekuwa anaishi katikati ya watu ambao walikuwa hawamchi wala kumuogopa Mungu, ndipo Lutu na binti zake wakakimbilia milimani (Mwanzo 19:30). Angeweza kuwa tajiri zaidi na asingekuwa na matatizo kabisa kama angechagua kuishi katikati ya watu waovu wa Kanaani.

 

Kifo cha Sara

Kisha Ibrahimu aliondoka na kwenda Hebroni upande wa kaskazini wa nchi ya Kanaani. Hapa Sara alifariki akiwa na umri wa miaka 127 (Mwanzo 23:1-2). Ibrahimu alinunua shamba kubwa sehemu ile. Kulikuwa na pango mle shambani, na humo akamzikia mke wake Sara.

 

Tunaweza kushangaa ni kwa nini Ibrahimu iliyekuwa mtu tajiri sana na mwenye idadi kubwa ya mifugo, alikuwa anaondoka kutoka sehemu moja hadi nyingine mara kwa mara. Ndiyo, ni kitu kimoja huenda kilimsababishia kuwa hivyo wakati mwingine ni vyema kuondoka na kuhama kwa faida ya mifugo yake. Kama hakukuwa na mvua ya kutosha, wanyama walikosa kuwa na nyasi za kutosha za kula. Kwa sababu kama hiyo, Ibrahimu alikuwa anazing’oa tu hema zake na kuipeleka mifugo yake kwenye malisho nyenye nyasi nyingi zaidi.

 

Lakini fundisho la muhimu zaidi zilizompelekea Ibrahimu aishi kwenye mahema na kuhamahama ilikuwa ni kwamba Mungu alimuelekeza kuondoka kutoka mahali pamoja ha kuhamia kwingine. Karibu watu wengi wa nchi hizo hawakumjua sana Mungu. Waliabudu sanamu na Mungu hakutaka Ibrahimu au watu wa familia yake wakae chini na kuzifuata njia za watu wale.

 

Kifo cha Ibrahimu

Kipindi ambacho Ibrahimu alioa mwanamke mwingine ambaye jina lake aliitwa Ketura. Alimzaliwa watoto sita zaidi wa kiume (Mwanzo 25:1-4).

 

Ibrahimu alimuachia kila kitu alichokuwanacho Isaka. Lakini wakati alipokuwa anaishi bado aliwapa zawadi watoto wake wengine (Mwanzo 24:5-6). Sheria au Torati ilielekeza kuwa sehemu mara dufu ya mali zilizoachwa na baba apewe mzaliwa wa kwanza wakati baba anapofariki (Kumbukumbu la Torati 21:15-17).

 

Miaka yote aliyoishi Ibrahimu ilikuwa ni jumla ya miaka 175 kisha akafa. Watoto wake Isaka na Ishimaeli walimzika kwenye pango ambalo Ibrahimu huko nyuma alimzikia Sara mke wake. Baada ya kufariki Ibrahimu, Mungu alimbariki mtoto wake Isaka ambaye hatimaye alikwenda kuishi karibu na Beeri Lahai Roi (Mwanzo 24:7-11).

 

Jifunze zaidi kuhusu Ibrahimu, uzao wake na ahadi za Mungu kwenye tovuti yetu ya: www.abrahams-legacy.org

q