Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[189]

 

 

Hatuokolewi Kwa Ajili ya Matendo Yetu Mema

(Toleo La 1.2 19970610-20000712)

Usemi n mafundisho ya kwamba Huokolewi kwa kupitia juhudi zako katika kuzitunza Sabato, ingawaje bado ipo, vimekuwa ukitumika sana hadi kufikia kiwango cha muwako usio wa lazima, na jinsi yanavyotumiwa leo ni kwa kupotosha watu kuliko kwa kuwasaidia. Mojawapo ya jinsi usemu huu unavyotumiwa siku hizi ni kwa kuyateka mawazo ya wasikilizaji na kuwaondoa kutoka kwenye jambo muhimuu tunalolihitaji kulizingatia katika kuziokoa roho zaidi ya kukuza tofauti za kimafundisho. Lakini umuhimu wa jambo na mtazamo vinabakia kwa wasikilizaji na walengwa tunaowapelekea au kuwalenga. Imani yetu iko kwenye matarajio ya aina ya imani ambayo inalinganishwa kimfano wake na Sabato kuwa ni ishara pekee inayowaonyesha wale wanaomtii na kumuabudu Mungu. Bwana wetu alikuwa mtii hadi kufa kwake, akiwa kama mmoja wetu, hadi mauti ya msalaba.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

(Hati Miliki © 1997 by Roy A. Marrs)

Editor of the Bible Advocate, the official organ of the Church of God, Seventh Day (edited by Wade Cox)

(tr. 2013) 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 

 


Hatuolewi Kwa Ajili ya Matendo Yetu Mema


Usemi n mafundisho ya kwamba Huokolewi kwa kupitia juhudi zako katika kuzitunza Sabato, ingawaje bado ipo, vimekuwa ukitumika sana hadi kufikia kiwango cha muwako usio wa lazima, na jinsi yanavyotumiwa leo ni kwa kupotosha watu kuliko kwa kuwasaidia. Wakati mafundisho haya yalipoanza kuzunguka huku na kule kwa mara ya kwanza katikati yetu, yalichukuliwa kuwa ni kitu cha kustaajabisha na yalisababisha “msituko”, na huenda ilitakiwa kusemwa kuwa lilikuwa ni jambo lililolenga kuteka fahamu zetu, bali kwamba ni suala tu la kuwa kama yalikuwa yakitumika au yakuwa bado hata wakati huu yanaendelea kutumia kama inavyotakikana. Mojawapo ya jinsi usemu huu unavyotumiwa siku hizi ni kwa kuyateka mawazo ya wasikilizaji na kuwaondoa kutoka kwenye jambo muhimuu tunalolihitaji kulizingatia katika kuziokoa roho zaidi ya kukuza tofauti za kimafundisho.

Nyraka za Paulo, Petro, Yakobo, Yohana, Yuda, na kitabu cha Waebrania ni nyaraka za mafundisho yalizoandikwa mahsusi ili kuyanafundisha Makanisa. Mkazo wake mkubwa ulikuwa wajue matatizo yaliyoletwa na kusababishwa na dhambi, mpango wa wokovu, utii, kuyafanya mafundisho yawe moja kwa moja, na kuwaonya ili wazae matunda kwa matendo mema. Sio nyaraka walizoandikiwa wasioongoka bado, na mtazamo wake haukuwalenga watu wasioongoka bado.

 

Huu ni ukweli tunaopaswa kuuwakilisha tunaposimama madhabahuni. Ni ukweli unaotakiwa kuzingatiwa hata wakati tunapochapisha gazeti la Bible Advocate au machapisho ya vipeperusgi. Na kwa kiasi kikubwa, tunashughulika na waumini na jumbe zetu zinawalenga waumini. Tunapolihuria Kanisa, kile kinachotakiwa na Kanisa, kuhusu imani ya waumini inatakiwa iendelee kuwepo kama ilivyikuwa siku za misume.

 

Ni kweli kabisa, tunatakiwa kujumuisha maonyo tunapokuuwa madhabahuni na kwenye machapisho tunayowagawia watu tunapowashuhudia. Tunatakiwa kulitia moyo na hamasa Kanisa lipande mbegu; lakini kwa kufanya hivyo, tunakwenda kukuta, kama alivyofanya Paulo, hitaji la kuimarisha ulelewa wa mafundisho ya waamini ambao kwao sisi ni watumishi wake, iwe kwenye madhehebu ya dini au kama ni nje ya madhehebu hayo. Hilo ni tendo moja halisi la mwinjilitti, na Paulo alijikuta karibu apatwe na mkasa wa ,afumdisho ya uwongo na matatizo ya kimwenendo kwenye ua ndishi wake.

 

Mtazamo wa maagano yote, yaani Agano la Kale na Jipya ni kuhusu watu wa Mungu, na yote yameelekeza kwenye makutaniko ya Israeli na kwa Kanisa. Ingawaje wanahusiana na wasioongoka, mtazamo wo mkuu ni kwenye mwenendo na imani ya watu wa Mungu.

 

Hata injili zote zinaelekea kwenye uelewa halisi kuhusu Mungu na Kristo wake na taraja la kwamba tunamtii Bwana wetu, sehemu ya kile kinachotuhusu kupanda mbegu na kufanya kazi kwenye shamba la mavuno yake.

 

Ndiyo maana ukaliaji tena wa kile kinachoshindwa kutuokoa wakati tunapojaribu kuelekea kile kinachoweza kutuokoa? Ni matumaini yetu kwamba wale waliombele yetu wakitusikiliza na wanaoitwa kwa jina la Kristo hawajaokolewa, kwa kuwa wanatumainia matendo yao mema kuwaokoa? Kama ni hivyo, mtazamo wa mawasiliano yetu inapaswa uwe ni kwa vitu vinavyookoa, na sio kwa vile vinavyoshindwa kuokoa. Huenda, ni kwa kuweka mtazamo kwenye vitu visivyoweza kuokoa zaidi kuliko, tunakuwa tukifanya makosa kutazama jambo kwa kujaribu kumfanya amtu asiyeongoka aishike Sabato! Tunataka watu wasioongoka waache dhambi, ili tusiache kuelezea ukweli wa kwamba kwa kuacha kuzini tu hakuwezi kumwokoa mtu.

 

Hebu na tufikirie kwa kina mashiko yaliyopo kwenye “utunzaji wa Sabato peke yake kusikoweza kuokoa” ulivyo na ukosefu wa kimtazamo juu ya jambo hili. Ni jambo lisilo na maana kusema tu kwamba, Huwezi kuokolewa kwa ajili ya kuwaheshimu tu wazazi wako, na wala kutaweza kuokolewa kwa kuishika tu amri moja nyingine yeyote. Tunapomsihi mtu yeyote aishike amri ya kupendana, ni kwa nini basi hatuwatahadharishi kuwa, Wajue kwamba kwa kufanya hivyo peke yake, hakutaweza kuwaokoa? Ukweli mwingine ni kwamba, kumpenda jirani peke yake hakuwezi kukuokoa. Ni kwa nini basi hatuthubutu kusema?

 

Kanisa linaloitwa Church of God, Seventh Day, HALIFUNDISHI kuwa tendo la kuzishika amri kumi au aina nyingine zote za sheria, kutoka kote kuwili, yaani Agano la Kale au jipya, ni kigezo cha wokovu—na kwa jinsi ninavyojua mimi, halijawahi kufundisha hivyo. Tumekuwa tukishutumiwa kimakosa sana na mafundisho mengi na wanaoamini hivyo. Maandiko mengi ya machapisho hata ya baadhi ya watu wetu sisi wenyewe, yanaonyesha kuashiria tafsiri hii potofu kwetu na kwenye mafundisho yetu.

Hebu na nionyeshe uwepo wa hoja za wanaotushutumu kimakosa. Tilia maanani maneno aliyoyasema Paulo kwa Wagalatia.

 

Wagalatia 5:3-4 Tena namshuhudia kila mtu atahiriwaye, kwamba ni wajibu wake kuitimiza torati yote.  Mmetengwa na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika hali ya neema.

 

Wanaotushutumu kwa uwongo wanaweka hoja yao kwamba iwapo kama tutaitunza Sabato basi tunadaiwa kuzishika sheria zote—zikiwemo na zile za utoaji dhabihuna nyingine nyingi zote.

 

Bali wao wanafundisha bado kwamba tusizini na amri nyingine nane miongoni mwa amri hizi kumi. Iwapo kama kwa matendo kabisa, kitendo cha kuitunza Sabato (moja ya amri kumi) inatutaka tutoe dhabihu na sadaka, basin a ndivyo ilivyo kwenye amri inayotuambia “usiue” na pia inatutaka kutoa dhabihu na sadaka! Sawa tu na kwamba mafundisho ambayo hatutakiwi kuyafanya kimatendo yaani ufiraji, na kisha tuzishike sheria zote za Musa ziwe zile zilizo kwenye zile amri kumi au kwenye sehemu nyingine ya sheria za Musa, na kwenye amri nyingine za Musa, na haziko kwenye zile nyingine kumi, ambazo tunazikuta kwenye zile kumi na ambazo tunazikuta kuwa ni amri ambazo zinatutaka tusishiriki ngono na wajamaa za karibu yetu na kufanya ufiraji.

 

Hoja za kila mara za wanaotushutumu hazituami kwenye kanuni ile ile kwao wenycwe ya kwamba (ishike moja ili uzishike na nyingine zote) inausaliti mtazamo wao wa kibagua utunzaji wa Sabato. Zaidi sana, wanatushutumu sisi kwa kujaribu kujihesabia haki (kuokolewa) kwa ajili ya utunzaji wetu wa Sabato.

 

Ili kudumisha mabishano wangepaswa pia waseme kwamba wale wote wanaofundisha watu hawapaswi pia kuua kimatendo (wawe wenye kuchukia) na wasifanye kwa matendo kitendo cha kuiba (bali watamani tu), na wasishirki kimatendo kufanya uzinzi (bali wabakie kumtamani tu mwanamke wanaomtazama). Kama tunajaribu kuokolewa kwa njia ya kuzitunza Sabato, moja ya amri kumi, basi ni kwamba yale yote tunayoyafundisha kuhusu kuzitii na kuzitenda kwa matendo hizi nyingine tisa ni sawa na kujaribu kutafuta kuokolewa kwa njia ya kuyatii matendo ya sheria. Au umuhimu wa kuzitenda sheria hizihizi kwa maadui zetu!

Tohara haipo kwenye amri hizi kumi na hivyo badi haiku miongoni mwa mambo yanayofananishwa na kuitii amri ya Sabato. Bali Sabato imo miongoni mwa amri kumi na wahubiri kina Billy Graham, John McArthur, Chuck Swindoll na wenyine wengi wanaziponda kwenye ibada zao wakidhania kwamba amri kumi bado zinafasiri dhambi.

 

Ni kweli, kwamba amri nyingine zote zinatatakiwa kuadhimishwa na kutunza kwa matendo, bali utunzaji wa Sabato sasa unapaswa utimilike kwa kwa kutafuta pumziko kwa Kristo, wakisema kuwa mtu hawezi kwa sasa kuitimiliza amri hii ya nne kwa kuitunza kimatendo kwa kuiadhimisha siku hii ya saba kuwa ni Sabato; bali kwa namna nyingine, wakiiadhimisha kimatendo kabisa siku ya Jumapili na kuifanya kuwa ni siku yao ya mapumziko na huku wakiifanya kuwa ni ya makusanyiko ya kiroho ingawaje Biblia haiagizi wala kusema kuwa kumekuwa na mabadiliko na Jumapili imechukua mahala pa Sabato.

 

Kwa nini tunaona matumizi haya yasiyo na uwiano ya mtazamo wa sheria wa maadhimisho ya Sabato, kuonyesha kwamba matendo na ushikaji wa ushikaji wa sheria sio mambo muhimu kwa kuupata wokovu? Ni kwa nini basi watumishi hawa wanatufundisha na kututaka sisi tukatae utoaji wa mimba na ufiraji na huku wakiwa hawajisikiii kabisa kusema, Wanalewa, hata hivyo, wakikataa kukubali ama kuwapingana na ushoga kuwa haitakufanya uupate wokovu? Ni kwa nini basi tusiseme kwamba, Tendo la kukataa kuitoa mimba iliyokwisha kutungwa hakutaweza kukuokoa? Ni jambo linaloonekana kana kwamba wanasema hivyohivyo tu kwamba, Kukataa kuua au kutoua mtu hakutakuokoa wewe, sawa na kama wanavyosema kwamba Tendo la kuitunza Sabato halitaweza kukuokoa– lakini hakuna mtu anayefanya hivyo kwa kuwa wanapenda kuishika amri ya Mungu inayokataza kuua.

 

Je, tunataka kuthibitisha na kuipa mashiko dhana na utunzaji wa Sabato? Kama ni hivyo, tunatakiwa kuiongelea kwa upande wa chanya kuhusu umuhimu wa kuitunza Sabato! Kuomgelea vile itakavyofanyika, zaidi kuliko kusema yale yasiyowezekana. Kamwe Mungu hakuielezea Sabato haina maana kwa mchakato wa wokovu wetu, kwa kuwa kufanya hivyo ni kutoka nje ya mstari wa fundisho, na haifai kuweka matamko ambayo hakuyatamka. Ni sawa tu na ukweli kuhusu huduma ya Yesu. Sio mara moja ameelezea yale yatakayojiri kwa kushindwa kuitunza Sabato na kile ambaccho hakiwezi kufanyika kwa mwanadamu.

 

Kwa hiyo, haiwezi kuhitimishwa kuwa kuna mambo mawili muhimu yasiyo sahihi kimwonekano kwenye jambo hili kwa waumini na waalimu wa madhehebu ya kiinjili kama yafuatayo:

1)      Kutenda nmatendo mema hakutaweza kukuokoa.

2)      Kuzishika sheria au torati hakutaweza kukuokoa.

 

Kwa yote mawili, nia inayoonekana ndani yao hasa ni kupinga utunzaji wa Sabato. Utunzaji wa Sabato unaonekana kuwa ni mlengwa pekee na Wakristo wengi huku wakifundisha utendaji wa matendo mema (ambavyo ndivyo hata Biblia imetuhakikishia kuwa inafundisha).

 

Hakuna mahali popote kabisa ambapo Biblia inapinga utendaji wa matendo mema, lakini baadhi ya wahubiri wa siku hizi, wakiwemo pia hata baadhi yao kutoka kwenye Makanisa ya Mungu, karibia sana na hali isiyo ya kawaida na bila udhuru kwanza wanadiriki kueleza kinyume na dhana hii ya utendaji na umuhimu wa matendo mema kwa mtazamo kwamba hayawezi kukuokoa, na kisha wakati mwingine wakiwazidi hata wale wanazuoni watetea dini wakikanganyikiwa kwa kusema kwamba, Lakini simaanishi kuwa myapuuzie matendo mema.

 

Kwa hiyo, ni kwa nini basi waanze kwa kutumia usemi huu?

 

Je, kwa hili tunataja mahali ambapo Biblia inaelezea hivyo? Je, tunajaribu kunyamaza pale ambapo Biblia imanyamaza bila kusema lolote? Huenda tunataka kuirudisha hii kwenye mkazo huu: Tunaongea SAWA na vile Biblia inavyosema, na HATUSEMI pale ambapo Biblia imenyamaza kimya bila kusema lolote! Ni kama kilivyo kistuli chenye mguu mmoja vigumu kukisimamisha kwa namna yeyote ile!

 

Umuhimu wa matendo mema umeelezewa mara kumi na sita kwenye maandiko ya Agano Jipya (kwenye tafsiri ya KJV na kwenye nakala za Kiyunani):

Mathayo 5:16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.

 

Yohana 10:32 Yesu akawajibu, Kazi njema nyingi nimewaonyesha, zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe?

 

Matendo 9:36 Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.

 

Warumi 13:3 Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake;

 

Waefeso 2:10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza

 

1Timotheo 2:10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.

 

1Timotheo 5:10 naye ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni, ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa bidii kila tendo jema.

 

1Timotheo 5:25 Vivyo hivyo matendo yaliyo mazuri ya dhahiri; wala yale yasiyo dhahiri hayawezi kusitirika.

 

1Timotheo 6:18 Watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo;

 

2Timothy 3:17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.

 

 Tito 2:7 katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu,

 

Tito 2:14 ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.

 

Tito 3:8 Ni neno la kuaminiwa; na mambo hayo nataka uyanene kwa nguvu, ili wale waliomwamini Mungu wakumbuke kudumu katika matendo mema. Hayo ni mazuri, tena yana faida kwa wanadamu.

 

Tito 3:14 Watu wetu nao wajifunze kudumu katika matendo mema, kwa matumizi yaliyo lazima, ili wasiwe hawana matunda.

 

Waebrania 10:24 tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri;

 

1Petro 2:12 Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.

Kumbuka kuwa maneno ya Kiyunani yaliyotumika kwenye vifundu au aya hizi, ni ya ama namna ya kalos ergos, au agathos ergos. Matendo mema ni tafsiri au maana bora zaidi ya maandiko haya.

Kila kifungu hapo juu kinaelezea umuhimu wa matendo mema kwa msisitizo mzuri na chanya. Hakuna hata moja kati ya maandiko hayo iliyoonyesha kuwa matendo mema kuwa ni kitu cha kukiwekea mjadala kuhusu neema na sheria! Mjadala kuhusu taji za dhahabu kwa matendo mema unaonekana kwenye Tito 2:14:

(Yesu) ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.

 

na Waefeso 2:10:

Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

 

Iwapo kama tutapenda kuzifananisha na injili kama ilivyotolewa na Yesu, waandishi wa injili, na eneo lingine lote lililobakia la Maandiko Matakatifu ya Agano Jipya, wakati wote tutayaongelea matendo mema kwa mtazamo chanya—bila udhuru!

 

Kinyume chake tunaonywa kuwa tusitafute kufanya matendo ya watu waovu, matendo yanayofanywa ili yaonekane na watu na hasa yanayotendwa kwa dhamira mbaya, mwisho wetu utakuwa sawa na matendo yetu, na wote tumeonywa kuwa tutapewa thawabu sawasawa na matendo yetu, zikiwa ni njema au mbaya, na sote tumetakiwa kutenda matendo nayayoendana na toba yetu.

 

Wakati kwamba Paulo alisema wazi sana kwamba hatuokolewi kuokana na matendo mema au kwa kuishika torati, basi anaharakia kuonyesha jinsi tunavyoweza kuokolewa. Anaweka uzani kwa kufafanua kwamba tunadumu kuishika torati kwa imani; na kwa kusema kwake kuhusu kufanyika kuwa kiumbe kipya kwa jinsi tulivyofanyika kwa kupitia Kristo ni kwa kutenda kwetu katendo mema. Mtume Paulo anasema kuwa Kristo alikufa ili atukomboe sisi kutoka kwenye dhambi na uovu, na kuwatakasa watu wa namna ya kipekee wenye kuonyesha nia na bidii ya kutenda matendo mema. Inawezaje basi watu wafanye bidii ya kuwa na matendo mema iwapo kama matendo mema ni kitu kisichohitajika na sio muhimu? Ni sawa tu na kujiuliza kwamba inamaana gani basi watu kuzitii amri za Mungu ikiwa jambo kuu na muhimu tunaloliongelea ni kwamba kuzitunza ama kuzishika hakutaweza kutuokoa?

 

Ili kupata uwepo wa ushahidi wake kwenye neno la Mungu, yatupasa kujua kwamba Mungu huutuza utii wetu na matendo yetu mema, na kitendo cha kuyaona matendo mema kama hayana maana wakati Mungu alimtoa mwana wake afe ili atubadilishe ili tuweze kuyatenda matendo haya mema ni kitendo cha kuukiuka ujumbe wa injili.

 

Kama jambo hili kwa kweli limefanywa na baadhi ya watumishi miongoni mwetu wakisema kuwa utunzaji wa Sabato hauna umuhimu, basi tunapaswa kuwa wa kweli kuhusu jambo hili na kusema hivyo. Kama tunaamini kuwa bado ni ya muhimu na iko kwenye mapenzi ya Mungu katika maisha yetu, na kwamba sio tu ni kitu kizuri tu kukifanya, na huku kila mara mtu anakuambia kuwa hutaweza kuokolewa kwa kuzitunza Sabato, basi mtu huyo anatakiwa akuthibitishie kuwa aio tu kuwa ni mapokeo mazuri tu kuwemo Kanisani (Mtazamo wa Ulimwengu wote), bali mhubiri anatakiwa asisitize kuwa wanaomuamini Mungu wanatakiwa bado waitunze Sabato (na sio mtindo tu wa Ulimwenguni kote), na kwamba utunzaji wa Sabato ni amri. Je, ipo au haipo? Na kama ipo basi hatupaswi kuiongelea kinyume .

 

Iwapo kama ungeulizwa swali kwamba Je, ungeweza kuifia Sabato? Ungejibuje? Ungepaswa kujibu kwa umakini na tahadhari. Nyuma ya swali kuna swali linguine kubwa zaidi kusema: Je, uko tayari kufa kuliko kumuasi Mungu? Kusema kuwa, Hapana, sipo tayari kuifia Sabato pasipo kutoa maelezo kunaweza kuacha ujumbe wazi wa masuala ya kimaadili kwenye mawazo ya vijana na watu wazima kuwa utii haumaanishi kukifia kitu. Tunatakiwa kila mara kuongea kwa moyo mwema na matendo.

 

Tumaini letu ni kwamba ni muhimu kufa tukionyesha utii wetu kwa Mungu. Kama Yesu alikubali kufa ili kuturekebisha dhambi na uasi wetu, basi ni muhimu kwetu kufa ili kuepuka kuuonyehsa uasl wetu kwake. Ni ukweli unaojiri kwenye historia kwamba mitume wengi na karibu wote waliyatoa maisha yao wakichagua kutii.

 

Iwapo kama tutapunguza uzito wa amri yoyote ya Mungu ambayo inabakia kuwepo, Mungu aatatupatiliza kwa ukali sana akituonyesha kuwa kila alichotuamuru sisi kukifanya ni cha lazima na muhimu (tazma Mathayo 5:18-19; Ufunuo 12:17; 14:12; 22:11-14,19 nk). Inaonekana kwamba kuna watu wanayachukulia maneno ya watu kwamba Kuitunza Sabato hakutaweza kukuokoa, wakimaanisha kuwa Sabato ni jambo la hiyari na sio muhimu sana. Sio kitu cha hiyari kuishika, bali ni amri ya Mungu. Sababu iliyowekwa na kuaminiwa na mababa wa Kanisa la Mungu ilikuwa muhimu na yenye mashiko. Ilimaanisha kitu fulani kama ifuatavyo:

Yakobo 2:10-11 Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria.

 

Imani hii inadumu kuwa na mashiko pale tu inapofanyiwa kazi kama hivi, Kwa kuwa yeye aliyeisema, 'Usiwe na miungu mingine ila mimi,'ndiye alisema pia, 'usijifanyie sanamu ya kuchonga'; au, yeye alisema, 'Waheshimu baba yako na mama yako' ndiye aliyesema pia 'ikumbuke siku ya Sabato na uitakase.'

 

Hitimisho Muhimu Kutiliwa Maanani

Jinsi tunavyozungumza kuhusu matendo mema na utunzaji wa Sabato ni muhimu sana kwa ajili ya amani ya Kanisa. Kama hatuna habari na kulijua hilo, basi tujue kwamba namna tunavyofanya na kuhubiri madhabahuni, kuandika kwenye makala kama vile kwenye majarida ya Bible Advocate au mafundisho ya Shule ya Sabato, yawe ama yanakuwa ya upotoshaji, yenye kuelimisha au kuharibu. Kwa mara chache na kidogokidogo huonekana kuwa ni asilia. Mtazamo wetu wa kimafundisho kuhusu dhana hii ya kwamba utunzaji wa Sabato na matendo mema havitaweza kutuokoa umekosa mizani, na vyote vimekuwa ni vyenye kuwakanganya watu na kuwapoteza na kuwaharibu, kwa kukosa mashiko na matumizi mema yaliyokusudiwa kutumika.

 

Tunatakiwa kuziongelea kwa mtazamo chanya kuhusu vitu tunavyofundisha, na yale tunayosisitizia, na yale tunayoyaamini.

 

Tunatakiwa kutofautisha kati ya yale yanayoweza kutuokoa na yale yanayotuhukumu. Ni mambo tofauti. Ni ukweli ulio dhahiri kutoka kwenye Biblia kwamba hatuokolewi kwa sababu ya matendo yetu mema, bali pia ni wazi kabisa kwamba Biblia inatuambia kwamba Mungu anapenda na kutoa thawabu kwa ajili ya matendo mema na ambavyo anatutarajia sisi tuyatende, na kwamba sisi tunajulikana kuwa tunaendelea kuyatenda na kumpendeza Mungu kwa hayo au vinginevyo tutakuwa hatuko pamoja naye kupitia matendo yetu. Ni jambo lililowazi kwamba tunahukumiwa kutokana na kutoyatenda matendo mema na ni kama ilivyo wazi pia kwamba matendo mema peke yake hayawezi kutuokoa sisi.

 

Wakati kwamba matendo mema ni siyo matendo yaliyo muhimu kwenye mchakato huu wa wokovu, bali kutotenda matendo mema au matendo mabaya yote mawili yanatoa mwelekeo wa hatima ya mtu kwenye wokovu wake! Tendo la kumuasi Mungu ni sababu inayopelekea hitaji la wokovu.

 

Iwapo kama Mungu anapenda tuzitunze Sabato, hebu na tuwe na tuendelee mbele na kusema hivyo kwa namna iliyo na mtazamo chanya! Iwapo kama utunzaji wa Sabato sio jambo linalotokana na mapenzi ya Mungu, basin a tuendelee mbele kwa kusema hivyo!

 

Mtume Paulo aliandika, "Kwa sababu hiyo, naandika haya nisipokuwapo, ili, nikiwapo, nisiutumie ukali kwa kadiri ya uwezo (mamlaka) ule niliopewa na Bwana, kwa kujenga wala si kwa kubomoa." (2Wakorintho 13:10). Hebu basi nia zetu na juhudi za matendo yetu yatumike kwa lengo la kuelimisha.

 

Iwapo kama unataka kutaniko lako lianze kushuhudia zaidi kuliko kuwa washiriki kwenye mtazamo wao, wainue kwa mkono na kusema, Ndugu, hebu na twende na kumtafuta mdhambi tumshuhudie. Ni jambo la maana zaidi kuliko kuwaambia walioongolka kuwa yahawezi kuwaokoa.

 

[Katika kulifanyia kazi andiko hili nilimuandikia  Roy Marrs kuhusu umuhimu wa matendo na nikamuonyesha fafanuzi zenye kuunga mkono zifuatazo na ambazo zingemhakikishia na jinsi zinacvyohusiana kwa mujibu sawa na mapenzi yake (ed.).]

 

Kuzitii amri za Mungu ni tendo linaloonyesha imani. Yeye aliyetupa sisi sheria alifanya hivo kwa kuwa sheria zinatokana na asili yake ilivyo. Sisi ni warithi wa siri na mambo ya mbinguni (2Petro 1:4). Kitendo cha kuzitii sheria ni matokeo ya maongozi ya Roho Mtakatifu na tunazishika sheria kutoka mioyoni mwetu. Hatuhitaji tena mtu wa kutufundisha kwa kuwa tuna Roho Mtakatifu. Sabato ni moja wapo ya mambo yaliyoamrishwa kwenye amri za Mungu na ambayo ndiyo yaliyoanzia na kuongezewa kwenye amri na sheria za Agano la Kale na kuweka msingi wa wajibu tunaouchukua sisi wenyewe wakati tunapokuwa sehemu na washiriki kwenye Ufalme wa Mungu. Hatuhesabiwi haki kwa njia ya sheria. Bali tunahesabiwa haki kwa njia ya imani. Mababa wa kale na wengine wote waliozishika walihesabiwa haki kwa njia ya imani (Waebrania 11:1-39). Imani ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayo (Waebrania 11:1). Lakini hawakuzipokea zile ahadi kwa kuwa Mungu aliwakusudia kitu kingine kizuri zaidi kwa ajili yetu, ambacho mbali na sisi wasingeweza kufanyika wakamilifu (Waebrania 11:39). Kwa imani, tunautarajia mfumo wa maongozi ya torati na utawala utakaokuwa unaongozwa kwa mujibu wa mapenzi halisia ya Mungu. Kwa imani, dhabihu zetu zinafanyika kuwa ni mawe yaliyo hai kwenye Hekalu la Mungu ambayo kwayo sisi tuko na tunatawaliwa kama maongozi ya sheria za Mungu mioyoni mwetu na kwenye nia zetu.

 

Sabato ni amri ya majaribio kwa kuwa inaonyesha mfumo na kanuni za Mungu. Wale wanaodai kuwa na imani, na kuhu wakiwa hawaishiki Sabato, wanapungukiwa na utukufu wa Mungu. Kwa matendo yao wanatuonyesha jinsi imani yao ilivyo na mapungufu. Sisi kwa matendo yetu tunaonyesha imani yetu (Yakobo 3:18). Imani yetu iko kwenye matarajio ya mfumo mpya unaoonyeshwa kwa ishara ya Sabato ikiwa kama ni ishara ya utii ya watu wa Mungu. Bwana wetu alitii hadi kufa, akiwa ni mmoja wetu, hadi mauti ya mtini au msalabani (Wafilipi 2:5-8). Sabato ni alama ya utaratibu wa mapumziko ambayo Mungu ameanzisha kwa ajili yetu katika Yesu Kristo.

q