Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[228]

 

 

 

Lazaro na Tajiri

(Toleo La 1.0 19971120-19971120)

Mfano wa Lazaro na Tajiri umekuwa ukitumika sana na Ukristo wa kimapokeo kwa sababu kadhaa zisizosahihi. Umekuwa ukitumika kwa lengo la kuyapa mashiko mafundisho yaliyoshamiri ya Roho kueendelea kuishi na pia kusaidia au kuyapa mashiko mafundisho wafu kwenda Mbinguni na Jehanamu mtu anapokuwa amekufa. Je, mfano huu una maana gani hasa? Ni nani aliyelengwa kuelezwa?

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1997  Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayopewa.  Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Lazaro na Tajiri

 


Ili kuuelewa mfano uliotolewa kuhusu Lazaro na Tajiri na pia sababu zilizompelekea Kristo kutoa mfano huu na kuhusu Yule anayekusudiwa, inatupasa kwanza kuijua historia ya Lazaro. Hapa tunaona kwamba idadi kubwa ya jumbe na mafundisho yamelenga sana kwenye mafundisho ya Kanisa na ia kwenye ujumbe wa Kristo kwa Wayahudi.

 

Hadithi hii haiungi mkono wala haitaunga mkono mafundisho ya imani ya roho kuendelea kuishi milele na uwepo wa uwezekano wa wafu kwenda mbinguni na jehanamu wanapokufa kama tutakavyoona.

 

Habari au hadithi ya Lazaro

Tunaiona hii ikiwa ni hadithi inyojulikana sana kwenye sura za Yohana sura za 11 na 12.

 

Muujiza huu ulikuwa ni muujiza mkubwa ambao uliwafanya Wayahudi watafute jinsi ya kumuua Kristo. Tunaona kwenye hadithi hii harakati za makusudi na mipango ya kumuua Masihi.

 

Yohana 11:1-4  Basi mtu mmoja alikuwa hawezi, Lazaro wa Bethania, mwenyeji wa mji wa Mariamu na Martha, dada yake. 2 Ndiye Mariamu yule aliyempaka Bwana marhamu, akamfuta miguu kwa nywele zake, ambaye Lazaro nduguye alikuwa hawezi. 3 Basi wale maumbu wakatuma ujumbe kwake wakisema, Bwana, yeye umpendaye hawezi. 4 Naye Yesu aliposikia, alisema, Ugonjwa huu si wa mauti, bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu atukuzwe kwa huo. 

 

Hapa kutaona kwamba Masihi anachukua hatua inayoendana na mpango wao wa makusudi kwa utukufu wa Mungu na kujitambulisha yeye mwenyewe kama Mwana wa Mungu. Kwa kweli, ulikuwa ni muujiza huu ndio uliomtambulisha na watu wamjue kuwa ni Masihi na kwamba ni yeye ndiye kuhani mkuu Kayafa ndiye alimkusudia kumtaja kwenye unabii wake.

 

Mariamu, kwenye andiko hili, anaonekana akimuomba moja kwa moja Masihi kwa ajili ya ndugu yao kwa kutilia maanani upendo aliokuwa akimpenda marehemu. Andiko linaonyesha wazi kabisa na moja kwa moja kwamba Masihi aliitilia maanani na kushikaman na familia hii yote kwa kiasi kukibwa sana. Lakini tunaona kwamba wakati aliposikia kuwa Lazaro hawezi, yaani mgonjwa mahututi alichelewa kwa siku mbili kabla hajaenda Bethania ya Yudea. Alikuwa hatarini huko kwa kuwa walikuwa wanamtafuta ili wampige mawe na wanafunzi wake walijua jambo hili kama tunavyoona kwenye aya ya 8.

Yohana 11:5-8  Naye Yesu alimpenda Martha na umbu lake na Lazaro. 6 Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo. 7 Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena. 8 Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena? 

 

Yesu hakuogopa na hiyo haikuwa sababu kwake na alikwenda. Alifundisha kuhusu kuwa nuru ya ulimwengu. Na hapa alifundisha kuhusu urefu wa siku. Alifanya rejea kuhusu fundisho la mchana na usiku na kwa hali za kiroho za nuru na giza.

John 11:9-11 Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu. 10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake. 11 Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.

 

Alitaja kulala hapa lakini alimaanisha kufa. Alikuwa anaonyesha kwamba Lazaro alikuwa ni mfano wa Kanisa. Kwa Kanisa, kifo kilikuwa ni kulala tu, na kungojea ufufuo wa wafu. Kwa kitendo hiki alikuwa analenga kwenye ufufuo wa wafu wa Kanisa waka atakapokuja Masihi. Wanafunzi hawakuuelewa ujumbe huu bado. Wala hawakuweza kudhania au kujua anachokwenda kukifanya. Walifikiri tu kwamba kama Lazaro ataweza kuamka kutoka usingizini basi angebarikiwa.

Yohana 11:12-13 Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona. 13 Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi. 

Hakuwa amelala hata hivyo. Alikuwa amekufa na Kristo hatimaye akawaambia wazi jambo hilo.

Yohana 11:14-16  Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa. 15 Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake. 16 Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, Twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye. 

 

Masihi akaliweka jambo hili wazi hapa kwamba anafurahi kwa kuwa hakuwepo huko, kwakuwa ingekinza uonyeshaji wa uweza wake kwenye muujiza wa kumfufua mfu.

 

Haipo wazi kwenye maelezo ya ufafanuzi ya Thomaso kwamba kama Thomaso alikuwa anakejeli ama la. Kukosekana kwa dalili yoyote ya kukejeli kwenye Kiyunani kunaonyesha uwezekano mkubwa wa kama inamaanisha kuwa Thomaso ambaye ni pacha wa kuzaliwa alijionea mara moja umuhimu wa ufufuo wa wafu na kusudi la Masihi la kufanya muujiza ule muhimu na wenye maana sana.

 

Waliacha baada ya kufuata muda wa kutosha kwa ajili ya Lazaro kuzikwa kwa muda wa siku tatu kaburini. Na kwa hiyo kwa kawaida na kisheria alikuwa amekufa kabisa – kwa kuwa kwake kaburini kwa kipindi cha siku tatu. Mji wa Bethania ulikuwa na umbali wa kilometa tatu kutoka Yerusalemu upande mwingine wa Mlima wa Mizeituni, na kwa hiyo kulikuwa na fursa kubwa ya kuwashuhudia Wayahudi wa Yerusalemu na Hekaluni.

Yohana 11:17-19 Basi Yesu alipofika, alimkuta amekwisha kuwamo kaburini yapata siku nne. 18 Na Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu, kadiri ya maili mbili hivi; 19 na watu wengi katika Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Mariamu, ili kuwafariji kwa habari ya ndugu yao. 

 

Walikuwa na Mariamu na Martha. Lakini alikuwa Martha peke yake ndiye alikuja kumlaki Kristo akiwa na maneno ya ukiri wa imani wa kimuujiza wa ufufuo mdomoni mwake. Nyongeza ya neno lisemalo bado kwenye tafsiri ya KJV na RSV halipo kwenye maandiko hasilia ya Kiyunani na linaonyesha dalili ya kuwa Mariamu hakuwa na imani sana na inamuonyesha kuwa na mtazamo asi kwamba hakutumaini muujiza huu kwa asilimia zote. Inaonyesha zaidi tu kana kwamba alidumu kwa kuwashughulikia wageni wengine tu na waombolezaji waliokuja kuwafariji tu.

 

Yohana 11:20-28 Basi Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alikwenda kumlaki; na Mariamu alikuwa akikaa nyumbani. 21 Basi Martha akamwambia Yesu, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa. 22 Lakini hata sasa najua ya kuwa yo yote utakayomwomba Mungu, Mungu atakupa. 23 Yesu akamwambia, Ndugu yako atafufuka. 24 Martha akamwambia, Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho. 25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi; 26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo? 27 Akamwambia, Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni. 28 Naye alipokwisha kusema hayo, alikwenda zake; akamwita umbu lake Mariamu faraghani, akisema, Mwalimu yupo anakuita. 

Hapa tunaiona nia ya kweli iliyokuwa nyuma ya kitendo cha Mariamu kubnya siri sana kumuita Martha na kumjulisha. Hawakupenfa kuonyesha dalili yoyote kuonyesha kuwa Kristo alikuwa pale kwa kuwa ingepelekea kufanyika kwa nyama nyingine ya kumpiga mawe jambo lililoonyesha kuwa huenda lilimtisha sana Thomaso. Mariamu akafanya haraka sana. Imani ya wanawake hawa wote ilikuwa kwenye uwez awa Masihi akiwa kama Mwana wa Mungu mwenye mamlaka dhidi ya mauti kwenye ufufuo wa wafu na hii ndiyo ilikuwa habari na sababu kuu yenyewe. Ni wazi kabisa kuwa Mariamu alikuwa amekata tama na kuchoka na mwitikio wa wageni waliokuja kuomboleza unalithibitisha jambo hili.

Yohana 11:29-32  Naye aliposikia, aliondoka upesi, akamwendea. 30 Na Yesu alikuwa hajafika ndani ya kijiji; lakini alikuwa akalipo pale pale alipomlaki Martha. 31 Basi wale Wayahudi waliokuwapo na Mariamu nyumbani, wakimfariji, walipomwona jinsi alivyoondoka upesi na kutoka, walimfuata; huku wakidhania ya kuwa anakwenda kaburini ili alie huko. 32 Basi Mariamu alipofika pale alipokuwapo Yesu, na kumwona, alianguka miguuni pake, akamwambia, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa. 

Hapa tunashuhudia maonyo au makemeo ya watu kuendelea na huzuni na kuambiwa wauamini uweza wa Kristo lakini ilikuwa haijaonekana bado nguvu dhidi ya mauti. Masihi akalia na kuhuzunika katika roho kwenye tatizo hili kwa sababu ilimuathiri na kumuuzunisha sana Mariamu.

Yohana 11:33-36 Basi Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliofuatana naye wanalia, aliugua rohoni, akafadhaika roho yake, 34 akasema, Mmemweka wapi? Wakamwambia, Bwana, njoo utazame. 35 Yesu akalia machozi. 36 Basi Wayahudi wakasema, Angalieni jinsi alivyompenda. 

 

Neno lisemalo akalia machozi au embrimaomi hapa lilikuwa sio kuhuzunika bali ilikuwa ni kuguguna kama afanyavyo farasi na hivyo ni jinsi ya kuonyesha hisia kali, uchungu, woga au hasira. Hisia hii kali ilimpelekea mtu kutokwa na machozi.

 

Maelezo yafuatayo huenda ni matokeo ya mawazo na hisia ambayo Kristo yalimpata na ambayo yalisababisha uchungu na hisia yake kuwa kali. Utoaji wake sauti ya hisia kali tena ulimsababishia kujihisi afanye jambo.

Yohana 11:37-38 Bali wengine wao wakasema, Je! Huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife? 38 Basi Yesu, hali akiugua tena nafsini mwake, akafika kwenye kaburi. Nalo lilikuwa ni pango, na jiwe limewekwa juu yake. 

Mchakato huu wote ulielekezwa kwenye tukio la kuuawa na kuteswa hadi kufia imani kwa wateule kwa kipindi chote hadi kuja kwake. Lazaro alikuwa ni mfano wa Kanisa. Wafuasi wake ni kama ulimwengu wote, ambao wanapatwa na mauti kwa ajili ya dhambi au kushindwa kwa Adamu.

 

Wangepata uzima kwa kupitia yeye na ujio uliofuatia wa Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste.

 

Ingawa Masihi aliye Adamu wa pili, ndipo kwaye wangeuona ufufuo wa pili wa wafu. Hata hivyo, wafuasi wake ambao ni ulimwengu walitafuta jinsi ya kumuua kama walivyofanya kwa kumuua. Mchakato huu uliendelea zaidi au kwa kiasi kidogo haukuangaliwa hadi alipokuja tena kuwaokoa wale wanaomngojea kwa hamu kubwa. Wakati huu wa ujio wake wa kwanza alikuja kushughulika na dhambi. Aliona mbele kwa kupitia Yubile hadi kurudi kwake na hiyo ndiyo iliyomsababishia Masihi kuhuzunika. Alimfufu Lazaro lakini vifo vya wateule lilikuwa ni suala la Mungu sawa na kama ilivyokuwa kwake yeye mwenyewe.

 

Sasa tunaendelea kuielezea miujiza yenyewe. Martha alipewa maelekezo na ingawa alieleza kama mtu anayeamini kuwa uweza ulikuwa mkononi mwake na kumuomba atende muujiza, wakati ilipokuwa karibu kufanyika hakuweza kuelewa alichokuwa anakwenda kukifanya. Hili kama lilivyo lenyewe tu lilionyesha hali ya kiroho ya Kanisa katika siku za mwisho mapema kabla ya kurudi kwa Masihi na ufufuo wa kwanza wa wafu wa wateule.

Yohana 11:39-40  Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne. 40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu? 

Hapa Masihi anamkemea kwa kutoikumbuka ahadi aliyomuahidi. Hili pia ni tatizo la Kanisa katika siku hizi za mwisho. Martha ni mfano wa Kanisa lifanyalo kazi likitaabishwa na masubufu ya dunia na linalopoteza mwelekeo na macho ya kuiona ahadi ya Mungu na kurudi kwake hivi karibuni mfalme kwa utukufu na kuanzisha utawala wake kwa nguvu.

 

Yohana 11:41-42 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia. 42 Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma. 

Tunaona hapa mjadala ulionukuliwa na kuandikwa sio kwa ajili ya kumuelimisha Mungu bali ni kutuelimisha sisi. Ujumbe uliokusudiwa pale ni kuonyesha uweza wa Masihi kama mwana wa Mungu na ia kufanya kitendo cha maombi na uhusiano wetu na Mungu ambaye anatusikia kila mara.

 

Yohana 11:43-44 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. 44 Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake. 

Hii lazima iwe kuwa ni muono unaoendelea. Jaribu, kwa kweli, lilikuwa ni kwamba wale wasio na shoka la kukatia walilichukua tukio hili kwa thamani ya machoni tu na wale walio na mkoba wa kikuhani waliliona kama ni kosa.

 

Yohana 11:45-46 Basi wengi katika Wayahudi waliokuja kwa Mariamu, na kuyaona yale aliyoyafanya, wakamwamini. 46 Lakini wengine wakaenda zao kwa Mafarisayo, wakawaambia aliyoyafanya Yesu. 

Kwa hiyo hili lilifanyika wakati wa Pasaka. Waliona kuwa wanapaswa kutenda kitu. Kama watu walimuamini Kristo kama makuhani wasingekuwa na la kufanya zaidi kwa kuwa ujumbe wake uliwashutumu kwa kazi wanazozifanya. Hili bado ni tatizo lao Yuda hadi leo, na hata linaelekea hadi kwa walei, kwa kuwa wokovu umewajia Wamataifa.

 

Yohana 11:47-48 Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi. 48 Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu.

 

Hapa tunaona kuogopwa na kuhani mkuu kwa kutoa wito wa kijinga kwa watu wake mwenyewe. Hakuyaelewa Maandiko Matakatifu yaliyosema kuwa inampasa Masihi afe akiwa kama Masihi kuhani kwanza, kabla hajaja kwa huduma ya Masihi mfalme. Aliwaambia kwa maongozi ya Roho Mtakatifu akiongozwa na Mungu.

Yohana 11:49-52 Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote; 50 wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima. 51 Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo. 52 Wala si kwa ajili ya taifa hilo tu; lakini pamoja na hayo awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika, ili wawe wamoja. 

Hapa kunaona kuwa haikuwa kwa taifa la Yuda peke yake bali kwa ajili ya wana wa Mungu ambao walitawanyika ulimwenguni kote. Kwa hiyo ilionyesha dalili ya kueleweka kidogo kwamba makabila yalitawanyika na kwa hiyo wokovu ulienea pia mbali na Yuda na ukuhani wa Walawi. Kwa ajili hiyo walifanya yale yaliyokuwa yanafanywa wakati wote kwa manabii nay ale waliyojaribu kuyafanya baadae Kanisani. walitafuta kumuua.

Yohana 11:53-54 Basi tangu siku ile walifanya shauri la kumwua. 54 Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake. 

Sio kwa nasibu tu kwamba hatimaye Masihi alikwenda huku na huko katika mji wa Efraimu.

 

Alionyesha kwamba nguvu za Roho zilikuwa zinaenda kuchukuliwa na kupewa taifa litakaloweza kuzaa matunda ya Ufalme wa Mungu na Roho Mtakatifu.

 

Yohana 11:55-56  Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; na wengi wakakwea toka mashambani kwenda Yerusalemu kabla ya Pasaka, ili wajitakase. 56 Basi wao wakamtafuta Yesu, wakasemezana hali wamesimama hekaluni, Mwaonaje? Haji kabisa sikukuu hii? 

Mchakati huu wa utakaso ilifanyika kwa mujibu wa maagizo ya torati. Utakaso kwa ajili ya dhambi ndogo zilizofanywa kwa kupotoshwa ulifanyika katika siku ya saba ya mwezi wa kwanza. Kutengwa na kuwekwa mbali kwa Masihi kama mwanakondoo kulifanyika siku ya kumi ya mwezi huu.

 

Yohana 11:57 Na wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri ya kwamba mtu akimjua alipo, alete habari, ili wapate kumkamata.

 

Tunaona habari hii ilofanyika siku sita kabla ya Pasaka huko Bethania. Hapa palikuwa nyumbani kwa Lazaro na dada zake. Kwa hiyo tunaona kwamba Mariamu ndiye Yule aliyemtia mafuta ya mazuri ikifuatiwa na muujiza wa kumfufua kaka yake. Pia alijua kuwa alipaswa afe kwa ajili ya muujiza ule.

Yohana 12:1-6 Basi, siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alifika Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye Yesu alimfufua katika wafu. 2 Basi wakamwandalia karamu huko; naye Martha akatumikia; na Lazaro alikuwa mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye. 3 Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu. 4 Basi Yuda Iskariote, mmojawapo wa wanafunzi wake, ambaye ndiye atakaye kumsaliti, akasema, 5 Mbona marhamu hii haikuuzwa kwa dinari mia tatu, wakapewa maskini? 6 Naye aliyasema hayo, si kwa kuwahurumia maskini; bali kwa kuwa ni mwivi, naye ndiye aliyeshika mfuko, akavichukua vilivyotiwa humo. 

Yuda alikamatwa kwa ajili ya tamaa yake. Alikuwa mtu mwenye tabia za kimwili, na alitaka Masihi atawale na kisha ampe mamlaka hatimaye. Hana tofauti yoyote na hawa wainjilisti wengi wanaojiyangaza kwa kutumia runinga na huduma inayoenea kwenye ulimwengu unaotumia lugha ya Kiingerza, na hususan nchini Marekani. Alimuuza Masihi kwa kuwa alijua na kuwa na uhakika kwamba walikuwa wanakwenda kupata mateso wote. Kanisa la Mungu limekuwa likiangukia kwenye mtego huu wa mabadiliko mazuri ya hali bora ya kifedha kwa karne nyingi sana sasa.

 

Yohana 12:7-11 Basi Yesu alisema, Mwache aiweke kwa siku ya maziko yangu. 8 Kwa maana maskini mnao sikuzote pamoja nanyi; bali mimi hamnami sikuzote. 9 Basi watu wengi katika Wayahudi walipata kujua ya kuwa yeye yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili yake Yesu tu, ila wamwone na Lazaro, ambaye Yesu alimfufua katika wafu. 10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye; 11 maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu. 

Lazaro alikuwa ndiye chanzo cha huu ushuhuda wa muujiza naye alipaswa alipaswa kufa. Lazaro alikuwa ni mfano wa Kanisa na aliteswa kwa uhusiano wake na Masihi na ushuhuda lililoutoa.

 

Siku iliyofuatia ilikuwa ni siku ya tano kala ya Pasaka au siku ya kumi ya mwezi na ndyo aliyotengwa mbali kama mwanakondoo tangu siku hii. Alichukuliwa kuwa kama mfalme kwa wale walioiona miujiza yake aliyoitenda. Walimtarajia achukue nafasi na majukumu ya kifalme akiwa kama mfalme Masihi – na siyo awe sadaka.

Yohana 12:12-19  Nayo siku ya pili yake watu wengi walioijia sikukuu walisikia ya kwamba Yesu anakuja Yerusalemu; 13 wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, Hosana! Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli! 14 Naye Yesu alikuwa amepata mwana-punda, akampanda, kama vile iliyoandikwa, 15 Usiogope, binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda. 16 Mambo hayo wanafunzi wake hawakuyafahamu hapo kwanza; lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka ya kwamba ameandikiwa hayo, na ya kwamba walimtendea hayo. 17 Basi wakamshuhudia wale mkutano waliokuwapo pamoja naye alipomwita Lazaro kutoka kaburini, akamfufua. 18 Na kwa sababu hiyo mkutano walikwenda kumlaki, kwa kuwa wamesikia ya kwamba ameifanya ishara hiyo. 19 Basi Mafarisayo wakasemezana wao kwa wao, Mwaona kwamba hamfai neno lo lote; tazameni, ulimwengu umekwenda nyuma yake. 

Mafarisayo, ambao baadae waliunda baraza la makuhani, waliiona hatari itakayoikumba nafasi yao. Uelewa kuhusu ujuio wa kuhani Masihi ulikuwa umekwishajengewa tayari na Essene (soma kitabu cha Geza Vermes, cha The Dead Sea Scrolls in English [Gombo Zilizochimbuliwa Kwenye Bahari ya Chumvi Nakala ya Kiingereza] re Damascus Rule VII and the fragment from cave IV). Inaonekana kuwa Wazolete wanauhusiano na wao kutoka na kile tunachokijua kukutikana kwa Geniza huko Masada.

 

Habari ilienea hadi kwenye nchi za mbali walizotawanyikia na watu walikuwa wanapenda kumuona. Hii ilikuwa ni ishara kwa Masihi kuwa majira yalikuwa yamewadia.

Yohana 12:20-26 Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu. 21 Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu. 22 Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu. 23 Naye Yesu akawajibu, akasema, Saa imefika atukuzwe Mwana wa Adamu. 24 Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi. 25 Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele. 26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu. 

 

Ujumbe huohuo limepewa Kanisa. Kwa ushuhuda na kifo cha, matunda mengi yalizaliwa. Ndivyo ilivyo pia, tunazaa matunda kutokana na kujitoa kwetu sadaka kama Wakristo. Hakuna atakayeweza kutuokoa kutoka kwenye majukumu tuliyopewa kama Kanisa. Ilimpasa Lazaro auawe kwa ajili ya kushiriki kwake na Kristo. Lakini maana yake ilikuwa ni kwamba yeye na mtu mwingine yeyote yule walijua kwamba Masihi alikuwa na uweza wa kumfufua yeye kutoka kwa wafu wakati majira yalipofika kwa maelekezo na maongozi ya Mungu wa pekee na wa kweli.

 

Yohana 12:27-29 Sasa roho yangu imefadhaika; nami nisemeje? Baba, uniokoe katika saa hii? Lakini ni kwa ajili ya hayo nilivyoifikia saa hii. 28 Baba, ulitukuze jina lako. Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena. 29 Basi mkutano uliosimama karibu wakasikia, walisema ya kwamba kumekuwa ngurumo; wengine walisema, Malaika amesema naye. 

Sauti kutoka mbinguni haikuwa Mungu Baba kwa kuwa hakuna mtu aliyewahi kuisikia sauti yake. Andiko linatuambia kwamba ni Malaika ndiye aliyenena ili kwamba ushuhuda utolewe kwa wanadamu wa kuwepo na maongozi ya Baba kwenye tukio hili.

 

Yohana 12:30-33  Yesu akajibu, akasema, Sauti hiyo haikuwako kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu. 31 Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo; sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje. 32 Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu. 33 Aliyanena hayo akionyesha ni mauti gani atakayokufa. 

Hapa tunaona unabii unaohusu mtawala wa dunia hii kuwa ataondolewa. Hatimaye aliondolewa na kutupwa chini na kumfuata mwanamke kwa hasira.

 

Kristo alijua jinsi atakavyokufa na kwa hiyo kuonyesha uthibiti wa Mungu kuwa umehusika kwenye jambo hili.

Yohana 12:34-36 Basi mkutano wakamjibu, Sisi tumesikia katika torati ya kwamba Kristo adumu hata milele; nawe wasemaje ya kwamba imempasa Mwana wa Adamu kuinuliwa? Huyu Mwana wa Adamu ni nani? 35 Basi Yesu akawaambia, Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako. 36 Maadamu mnayo nuru, iaminini nuru hiyo, ili mpate kuwa wana wa nuru. Hayo aliyasema Yesu, akaenda zake, akajificha wasimwone. 

Watu walikuwa wanaanza kujiuliza kile ambacho Kristo anakusudia kusema. Hawakupenda mwana wa Adamu ambaye alikuwa anakwenda kusulibiwa. Walikuwa wanamtaka mwana wa Mungu ambaye alikuwa anakwenda kuwa mshindi. Walikuwa wanataka kuwa huru kutoka kwenye kongwa ya Warumi na pia kutoka kwenye minyororo ya Waedomu.

 

Yohana 12:37-41  Walakini ajapokuwa amefanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, hawakumwamini; 38 ili litimie lile neno la nabii Isaya alilolisema, Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu; Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani? 39 Ndiyo sababu wao hawakuweza kusadiki; kwa maana Isaya alisema tena, 40 Amewapofusha macho, Ameifanya mizito mioyo yao; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakafahamu kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya. 41 Maneno hayo aliyasema Isaya, kwa kuwa aliuona utukufu wake, akataja habari zake. 

Mfano huu ulikuwa unaonyesha kwamba wateule walikuwa ni kundi dogo la waliochaguliwa na ilikuwa imetabiriwa kwamba kutakuwa na wateule wachache. Yuda waliipoteza nafasi yao kwa kipindi cha takriban miaka elfu mbili. Ni mtu mmoja mmoja tu angefanikisha katika kuwa sehemu ya kundi la Masihi akiwa ni mteule. Wengi walitaabika kama Lazaro. Watawala wengi na waliokuwa wa mrengo wa kiaristokrats ambao walikuwa pia ni Masadukayo walimuamini Masihi.

 

Yohana 12:42-43  Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi. 43 Kwa maana walipenda utukufu wa wanadamu kuliko utukufu wa Mungu. 

Tatizo kubwa lililolikumba Kanisa limekuwa kwamba wengi wa wanaoingia ndani yake wanapenda kusifiwa na wanadamu kuliko kusifiwa na Mungu. Hii imepelekea kuibuka kwa dhana nyingi za migongano mingi na mafarakano kuliko kitu kingine chochote kile.

 

Imani ni kwamba wale wanaomwamini Kristo hawamwamini yeye tu bali wanamwamini Mungu pia aliyemtuma.

Yohana 12:44-45  Naye Yesu akapaza sauti, akasema, Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi bali yeye aliyenipeleka. 45 Naye anitazamaye mimi amtazama yeye aliyenipeleka. 

Mtazamo huu na andiko havieleweki na Wakristo wa imani kongwe za kale.

 

Kristo hawahukumu wale wanaosikia na hawaamini kwa kuwa hawapo chini ya hukumu bado. Kristo hakuja kuuhukumu ulimwengu bali kuuokoa na kwa hiyo, wakati wao wa kuhukumiwa bado haujafika. Ni walio kwenye nyumba ya Mungu tu ndio wanaohukuiwa sasa.

Yohana 12:46-48 Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani. 47 Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu. 48 Yeye anikataaye mimi, asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumuye; neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho. 

Kwa hiyo hukumu yao ipo katika siku ya mwisho na ni kinyume na neno la Mungu ndivyo watahukumiwa. Yao wao ni hukumu ya maamuzi na kurudiwa au inaitwa krisis.

 

Yohana 12:49-50  Kwa sababu mimi sikunena kwa nafsi yangu tu; bali Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema. 50 Nami najua ya kuwa agizo lake ni uzima wa milele; basi hayo ninenayo mimi, kama Baba alivyoniambia, ndivyo ninenavyo.

Baba anaamuru kile Masihi anachokisema na kile tunachokisema sisi ote. Usifikirifikiri jinsi utakavyosema – utapewa. Ni kama alivyofufliwa Lazaro na ndivyo Mungu alivyomfufua Yesu Kristo.

 

Jambo lililokuwako ni kwamba lilionyesha umaana mkubwa wa tukio kwenye historia ya mwanadamu. Maelezo ya kina kuhusu kusulibiwa na kufufuka yametolewa kwenye jarida la Nyakati za Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159).

 

Mfano

Sasa tunaendelea kutafakari mfano wa Lazaro na Tajiri kwa mstakabala wa historia ya hadithi hii ya Lazaro ambayo kwa yenyewe tu inatuama kwenye ufufuo wa wafu.

 

Mfano unakutikana kwenye Luka 16. Mfano huu kwa kweli unafuatia mfano wa mwanzoni na ambavyo yote miwili inafanyiwa rejea zake kutoka kwenye imani na mafundisho ya kiyahudi na Kifarisayo. Tutakwenda kuchambua na kufafanua mifano yote miwili na tutaona kielewa kikamilifu kile Kristo alichokuwa anasema.

Luka 16:1-2  Tena, aliwaambia wanafunzi wake, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyekuwa na wakili wake; huyu alishitakiwa kwake kuwa anatapanya mali zake. 2 Akamwita, akamwambia, Ni habari gani hii ninayosikia juu yako? Toa hesabu ya uwakili wako, kwa kuwa huwezi kuwa wakili tena. 

Hapa Masihi alikuwa anawakusudia makuhani ambao walikuwa watumishi juu ya jube na maelekezo ya Mungu (soma jarida la Jumbe za Kinabii za Mungu (Na. 184)). Walikuwa wameshindwa kwenye utumishi wao na utumishi au huduma ilibidi iondolewe kutoka kwao.

 

Na kwahiyo waliuhalifu utaratibu au mpango na kubadili au kugeuza sheria za Mungu na kuzilinda kazi zao kwa kuzifanya zikubalike zaidi kwenye nyumba nzima yote ya walimwengu. Hatimaye walilifanya hilo kwa kuzihalifu karibu kila neno lililoamriwa kwenye torati na sheria za Mungu. Kalenda ilibadilishwa ili kuhakikisha kwamba hakuna kitakachoadhimishwa kwa siku sahihi. Walilibadili Kanisa ambalo ni ahadi ya agano na wakajaribu kuliharibu.

Luka 16:3-9 Yule wakili akasema moyoni mwake, Nifanyeje? Maana, bwana wangu ananiondolea uwakili. Kulima, siwezi; kuomba, naona haya. 4 Najua nitakalotenda, ili nitakapotolewa katika uwakili, wanikaribishe nyumbani mwao. 5 Akawaita wadeni wa bwana wake, kila mmoja; akamwambia wa kwanza, Wawiwani na bwana wangu? 6 Akasema, Vipimo mia vya mafuta. Akamwambia, Twaa hati yako, keti upesi, andika hamsini. 7 Kisha akamwambia mwingine, Na wewe wawiwani? Akasema, Makanda mia ya ngano. Akamwambia, Twaa hati yako, andika themanini. 8 Yule bwana akamsifu wakili dhalimu kwa vile alivyotenda kwa busara; kwa kuwa wana wa ulimwengu huu katika kizazi chao wenyewe huwa na busara kuliko wana wa nuru. 9 Nami nawaambia, Jifanyieni rafiki kwa mali ya udhalimu, ili itakapokosekana wawakaribishe katika makao ya milele. 

Hapa Masihi alikuwa anaiweka tofauti kwenye imani kati ya wale waliochaguliwa nay a wale wa ulimwengu huu. Kuna mchirizi wa mnyofu unayotembea kwa wana wa nuru. Waovu watenda dhambi wameitwa ila hawajachaguliwa na kwa hiyo wamekusudiwa kushindwa. Hawako hukumuni sasa na, ndiyo maana aliyokusudia Kristo hapa.

 

Wateule wanajaribiwa kwenye utumishi wao kama walivyojaribiwa Walawi na Mafarisayo.

Luka 16:10-12  Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia. 11 Basi, kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli? 12 Na kama hamkuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe? 

Ujumbe uliopo hapa ulikuwa ni kwamba Walawi na Mafarisayo hawakuwa waaminifu kwenye sheria za Mungu. Mamlaka ikaondolewa kutoka Yuda na uongozi wake. Kwa sababu hii kwanza waliambatana na Masihi na hatimaye wakamuua.

 

Luka 16:13-18  Hakuna mtumishi awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana, ama atamchukia huyu na kumpenda huyu, ama atashikamana na huyu na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali. 14 Basi Mafarisayo, ambao wenyewe ni wapenda fedha, waliyasikia hayo yote, wakamdhihaki. 15 Akawaambia, Ninyi ndinyi mnaojidai haki mbele ya wanadamu, lakini Mungu awajua mioyo yenu; kwa kuwa lililotukuka kwa wanadamu huwa chukizo mbele za Mungu. 16 Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu. 17 Lakini ni vyepesi zaidi mbingu na nchi vitoweke, kuliko itanguke nukta moja ya torati. 18 Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini. 

Hapa tunaona tofauti ya kiutaratibu au mfumo wa sheria na manabii na kutangazwa kwa Ufalme wa Mungu. Yuda na makuhani Walawi waliondolewa kutoka kwenye Ufalme ule. Ni mtu binafsi tu ndio walioingizwa ndani yake.

 

Mafarisayo walisikia maneno haya ya Kristo na walimchukia na hatimaye aliwapa mfano wa Kanisa na unabii wa matukio yote mawili ya ufufuo wa Lazaro na uhusiano wake na Kristo na Kanisa.

Luka 16:19-21  Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa. 20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi, 21 naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake. 

Kumbuka hapa pia kuwa Kanisa liliteswa vibaya sana na Wayahudi huko Mashariki ya Kati kipindi chote cha karne za kwanza mwanzoni kokote walikoweza kutamalaki. Kwa sababu hizi, walikwenda utumwani na kudharauliwa. Hawakutubu nab ado hawajatubu.

 

Mfano huu unaendelea kwa kumtaja au kumhusisha Ibrahimu na kisha unatumia ishara ya kitaswira kufafanua uhusiano uliopo kati ya tajiri ambaye alikuwa mpenda fedha na mali zisizo za halali aliyetajwa kwenye mfano wa mwanzo. Lazro anatajwa kwa jina lake hapa kama hadithi inavyoendelea.

 

Luka 16:22  Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. 

Wazo lililoko hapa lilikuwa ni la ufufuo wa wafu kwanza na wa pili. Lazaro alikuwa amechukuliwa na kuwekwa kifuani mwa Ibrahimu. Tajiri naye akafa na akazikwa. Wana wa Ibrahimu wanatajwa kwenye andiko hili wakichukuliwa kama wateule. Wao ni mbegu na wa uzao wa Ibrahimu.

Wagalatia 3:29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.

 

Paulo aliongelea juu dhana hii kwenye waraka wake kwa Warumi tangu mwishoni mwa sura ya 10.

Warumi 10:1-9  Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe. 2 Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. 3 Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu. 4 Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki. 5 Kwa maana Musa aliandika juu ya haki itokayo kwa sheria, ya kuwa, Mtu afanyaye hiyo ataishi kwa hiyo. 6 Bali ile haki ipatikanayo kwa imani yanena hivi, Usiseme moyoni mwako, Ni nani atakayepanda kwenda mbinguni? (Yaani, ni kumleta Kristo chini), 7 au, Ni nani atakayeshuka kwenda kuzimuni? (Yaani, ni kumleta Kristo juu, kutoka kwa wafu.) 8 Lakini yanenaje? Lile neno li karibu nawe, katika kinywa chako, na katika moyo wako; yaani, ni lile neno la imani tulihubirilo. 9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. 

 

Mchakato huu unafanya tofuti kati ya wana wa Ibrahimu na wa aina ya wateule na waliofananishwa na Lazaro na wale waliokuwa kwenye mstari wa kiuzao wa Ibrahimu lakini waliokuwa sio Waisraeli bali wapenda fedha na anasa na wa kwenye ufufuo wa pili wa wafu, kazi kubwa inayokusudiwa kwenye hadithi hii ni juu ya ufufuo wa wafu.

 

Luka 16:23-24 Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake. 24 Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu. 

Kinachotajwa kuwa ni kuzimuni hapa ni kaburi. Hapa ni mahali ambapo ufufuo ulikuwa unafanyika. Hadithi inasema kwamba imani ya Kiyahudi ilikuwa inaamini juu ya ufufuo wa pili wa wafu uliotajwa moja kwa moja na kwa wazi kwenye Ufunuo 20. Ufufuo huu utafanyika mwishoni mwa kipindi cha Milenia. Huu ni ufufuo wa nyumba yote ya Israeli waliotajwa kwenye Ezekieli 37:11 na ni wa mwili.

 

Luka 16:25-26  Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. 26 Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu. 

Hadithi hii hapa ina mifano mingine miwili. Wa kwanza ni wa kondoo na mbuzi ambapo mataifa yamepewa sawasawa na walivyowatendea wateule. Wa pili ni ule wa wateule kupitishwa na kusafishwa kwenye tanuru la moto kwa mateso na dhiki kuu tunayoiona habari zake kwenye kitabu cha Ufunuo sura za 1 hadi 6. Shimo linalotajwa hapa ni utenganisho wenye umbali uliosbabishwa na kushindwa kwa mwili na damu kuurithi Ufalme wa Mungu. Ndiyo maana Mtume Paulo alisema kwamba wana juhudi lakini si katikaa. Hapa tunaingia kwenye kiini cha mfano. Lazaro anaombwa atumwe aende kwenye nyumba ya baba zake ambayo kwa kweli ilikuwa ni Yuda. Majibu yaliyotoka kinywani mwa Ibrahimu ni ya muhimu na ya msingi kama yalivyokuwa kwa hawa ndugu watano.

Luka 16:27-28  Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu, 28 kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso. 

Ndugu watano wa Yuda ni wana wa Lea. Alikuwa na watoto saba, (sita wa kiume na mmoja binti) kama tujuavyo. Ndugu hawa wanaume watano wa Yuda ni Reubeni, Simeoni, Lawi, Isakari na Zabuloni. Yuda, Isakari na Zabuloni ni makabila matatu yaliyokuwa upande wa mashariki na wa kwanza kuondoka kwa desturi ya kuondoka kutoka maragoni safarini na kuanza kutembea (soma Hesabu 10). Reubeni alipoteza haki ya uzaliwa wake wa kwanza na kabila la Simeoni lilitawanyika kwa ajili ya ukatili wake. Tunaona kwamba tunawaongelea wana wa Israeli waliounda taifa linaloitwa la Kiyahudi. Isakari na Zabuloni walijumuika nao na kwa kipindi kile walikuwa wa kaskazini mwa Israeli. Ndugu watano ni rejea tu ya wana wa Lea ambao ni wazi kabisa kwamba angewatambulisha kama Yuda kutoka kwa binamu zake ambao walikuwa ni makabila mengine yaliyobakia.

 

Luka 16:29-31 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao. 30 Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu. 31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.

Hapa tunaona kwamba Ibrahimu anasikika akiwaambia kuwa wanao Musa na manabii wa kuwafundisha. Andiko la wazi na lililo chanya linasema kuwa hawakuwasikia Musa na hawa manabii. Kwa hiyo walikuwa wanazibadili sheria kwa kuitafsiri kinyume nia na mahudhui ya sheria. Hili ndilo hata Mtume Paulo alilolisema.

 

Swali ni halafu liliwekwa kinywani mwa Ibrahimu na Masihi kuhusu uwezekano wenye mashaka kwa wao kumsikia mtu atokaye kutoka kwa wafu kama hawakuisikia torati.

 

Kufufuka kwa Lazaro kwa hiyo kulitolewa kwenye mfano na kisha kufanyika kwenye uhalisia ili kuonyesha uweza wa Mungu na ujumbe wa Masihi kwa utendaji sahihi wa torati. Kristo alikamatwa kwa ajili ya ujumbe huu. Walijua kwamba alikuwa anawaongelea Mafarisayo (ambao baadae walifanyika kuwa jopo la makuhani).

 

Alitenda muujiza na walimchukia kwa hilo na wakashauriana kumkamata yeye pamoja na Yule mtu aliyemfufua na kuwaua. Ndipo hatimaye walimuua na baadae wateule waliomfuata kwa kuwa alikuwa mwana wa Mungu.

 

Hadithi hii haina kitu kingine chochote kinachohusiana na dhana ya wafu kwenda mbinguni au kwenye motoni au na fundisho la roho za wafu kuendelea kuishi. Inahusiana na wokovu wa Yuda na kushindwa kwao kusikiliza maonyo yaliyo kwenye torati na neno la Mungu. Linahusiana na matuku ya kuhamishwa kwao na kwenda uhamishoni. Ni unabii wa moja kwa moja wa Masihi wa ufufuko wa Lazaro ambao ilikuwa ni ishara kubwa na muhimu na maajabu yaliyofanywa na yeye ili kuwaonyesha Yuda hatari iliyokuwa inawakabili.

 

Hawakusikliza kama Wakristo wa imani za makanisa ya kale na makongwe wasivyosikiliza leo.

q