Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[003b]
Maswali na
Majibu
Kuhusu
Imani ya Kikristo
(Toleo La 1.0 20120101-20120101)
Watu wengi watashangaa watakapokuta yale wanayoyaamini
hayapo kwenye Biblia na wala hayana uhusiano nayo wowote au wala hayakuaminiwa
hivyo na kanisa kwenye kipindi chake chote cha kihistoria. Hebu yajibu maswali
yaliyoandikwa kwenye mtihani huu mdogo na uone jinsi ulivyo karibia sana kwenye
imani ya kweli waliyopewa watakatifu mara moja tu.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 2012 Christian
Churches of God, ed. Wade Cox)
(tr.
2016)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na
tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.
Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala
yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika
tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Maswali
na Majibu Kuhusu Imani ya Kikristo
Mungu
1) Je, Mungu Baba
ndiye Mungu wa pekee na wa Kweli na hana ushirika na mwingine, au Yesu ndiye
huyu Mungu wa Kweli kama alivyo Mungu?
Jibu: Ndiyo, Mungu peke yake ndiye Mungu wa
Kweli.
(1Timotheo 2:5;
1Wakorintho 8:4; Wagalatia 3:19-20; Kumbukumbu la Torati 4:35,39; Waefeso 4:6;
Yohana 17:3; Kumbukumbu la Torati 32:39; Malaki 2:10; Zaburi 90:2; Zaburi
93:1).
2) Je, ni Mungu peke yake ndiye aliyeziumba Mbingu na Dunia au Mungu aliziumba
Mbingu na Nchi kwa kupitia Yesu Kristo?
Jibu: Ndiyo, ni Mungu peke yake ndiye
aliyeziumba Mbingu na Nchi (Isaya 44:24; 51:13; 40:22; Mithali 30:4;
Ayubu 9:8; Ayubu 38:1-7; Zaburi 104:2; Yeremia 51:15; Mwanzo. 1:1;
1Wakorintho 8:6a; Ufunuo 10:6).
Ni wakati Dunia
ilipofanyika kuwa tohu na bohu ndipo Yesu Krim wengine waliumba kwa kuelekezwa
na Mungu ili mwanadamu aweze kuishi ndani yake.
Jibu: Hapana, Mungu huyu wa Pekee
na wa Kweli haonekani (Wakolosai 1: 15; 1Timotheo 1:17; 6:16),
na hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu huyu wa Pekee wa Kweli au aliyewahi
kuisikia sauti yake wakati
wowote (Yohana 5:37, 1Yohana 4:12, Yohana
1:18, 6:46).
4) Je,
Mungu wa Pekee na wa Kweli, Mungu baada ya kufufuka kwake na kuketi mkono wa
kuume wa Mungu?
Jibu: Ndiyo, Mungu wa Pekee wa
Kweli ni Mungu wa Kristo (Waefeso 1:17; Waefeso 4:6; Zaburi 45:7;
Waebrania 1:9; Yohana 17:3).
Hata
baada ya kufufuka kwa Kristo kutoka kwa wafu, Mungu wa Pekee wa Kweli ni Mungu
wake Kristo (Yohana 20:17).
Kuna Mungu mmoja tu na Baba wa wote na ni Mungu wake Kristo (Warumi 15:6; 2Wakorintho 1:3; Waefeso 1:3; Wakolosai 1:3; 1Petro 1:3).
Roho Mtakatifu
1)
Mtakatifu ni Mungu?
Jibu: Hapana, huyu Roho wa kweli
aliyetoka kwa Baba na kuletwa hapa duniani na Kristo siyo Mungu (Yohana
15:26; Yohana 16:13).
2) Je, Roho Mtakatifu ni mshirika kwenye Uungu?
Jibu: Hapana, Roho wa Mungu siyo mshirika
kwenye Uungu (Ufunuo 5:6; Kutoka 31:3; Kutoka 35:31; Mika 3:8; Luka 1:15; Matendo 4:8; Matendo 7:55; Matendo 13:9; Matendo 4:31; 2Nyakati 24:20).
3)
Je, tunapaswa kumuomba au kumwabudu Roho Mtakatifu?
Jibu: Hapana, Kristo alisema kuwa
Baba yake ndiye anayestahili kuabudiwa peke
yake (Yohana 4:23; 1Wakorintho 6:19).
4) Roho Mtakatifu ni nini?
Jibu: Roho Mtakatifu ni nguvu tu
za Mungu (Yohana 20:22;
Matendo 8:17-21; Matendo 1:8; Matendo 2:4; Matendo 4:25;
Luka 4:14; Warumi 15:19; 1Wakorintho 2:4).
Roho
Mtakatifu ni tabia za Mungu (2Petro 1:3-4).
Yesu
1)
Je, Kristo ana wadhifa sawa na Mungu?
Jibu: Hapana, Kristo hana usawa
wowote na Mungu (Yohana
14:28; 1Wakorintho 15:27; Wafilipi 2:6; Matendo 7:56; 1
Petro 3:22).
2) Je, Kristo anasifa ya kuishi milele pamoja na Mungu?
Jibu: Hapana, Kristo si wa milele
kama Baba yake ambaye ni Mungu wake pia (Mithali 30:4; Mika 5:2;
Zaburi 45:7).
3)
Je, Kristo alikuwa na mwanzo wake?
Jibu: Ndiyo, Kristo alikuwa na
mwanzo wake (Ufunuo 3:14).
4)
Je, Kristo aliumbwa na Mungu?
Jibu: Ndiyo, Kristo aliumbwa kwa
mfano wa Mungu (Wakolosai 1:15).
5) Je, Kristo alikuwepo kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake kama mwanadamu?
Kama ni hivyo, kwenye kipindi hiki yeye alikuwa kama nani?
Jibu: Ndiyo, alikuwepo kipindi cha
kabla ya kuzaliwa kwake kuwa mwanadamu
(Yohana 8:58; 1Wakorintho 15:47; Yohana 17:4,24; Yohana 3:13). Kabla
hajafanyika kuwa mwanadamu, Kristo6 alikuwa kwenye umbo la elohim
(Wafilipi 2:6; Zaburi 45:7), yaani, Mwana wa Mungu (kwa
mujibu wa Yohana 10:33-36).
Kristo alitajwa
na Mtume kama Malaika wa Bwana, mwombezi aliyemtokea nabii Musa na akamkabidhi Torati
ya Mungu
(Matendo 7:35,38; Waebrania 2:2; W6agalatia 3:19-20; 1Timotheo 2:5).
6)
Je, Kristo ni Mwana wa pekee wa Mungu?
Jibu: Hapana. Kristo ni Mwana wa Mungu.
Lakini Mungu aliumba wana wengine wengi
(Ayubu 1:6; 2:1; 38:4-7; Zaburi 86:8-10; 95:3; 96:4; 135:5), na
Mungu akafanyika kuwa Mungu Baba kwa viumbe hawa waliofanyika kuwa ni wana wa
kiroho (Waebrania 12:9).
Kwa
hiyo, Kristo alikuwa ni kiumbe alikuja akiwa kama mwana pekee wa Baba. Hii ni
kusema, yeye ni mwana pekee wa Mungu aliyezaliwa katika mwili.
7)
Je, Kristo alifufuliwa kutoka kwa wafu?
Jibu: Ndiyo, Mungu Baba alimfufua
Kristo kutoka kwa wafu (1Wakorintho 15:15;
Warumi 4:24; Matendo 2:24,32; 1Wakorintho 15:3-9).
8)
Je, inatupasa kumuomba au kumwabudu Kristo?
Jibu: Hapana, Kristo alitufundisha
yule anayestahili na tunayepasa kumuomba na jinsi ya kuomba. Na ni Mungu Baba
peke yake ndiye tunapaswa kumuomba na kumuimbia tenzi za sifa, au kumwabudu (Mathayo 6:9; Yohana
14:13; Warumi 16:27; Waebrania 13:15-16).
9) Je, Malaika wanamwabudu au kumuomba Kristo?
Jibu: Hapana, malaika au wanadamu
wanampa heshima tu Kristo inayojulikana kama proskuneo au kumsujudia (Waebrania 1:6; Mathayo 2:11),
na kama ilivyo kwenye Ufunuo 3:9 ambapo wale walio wa sinagogi
la Shetani watakuja kusujudu, yaani proskuneo mbele za
wateule; inamaanisha neno hilihili moja. Kitendo hicho ni ishara ya utumwa au
kutoa heshima, na sio kitendo cha kuabudu.
Yatupasa
kumwabudu Mungu Baba peke yake na wala tusiabudu mungu mwingine yeyote (Luka 4:8; Yohana 4:21-24; Wafilipi 3:3; Waefeso 5:19-20;
Ufunuo 22:9).
Kristo
alisema kuwa ni Baba yake pekee ndiye anayestahili kuabudiwa
(Yohana 4:23; 1Wakorintho 6:19).
10)
Je, ni Mungu ndiye alimkabidhi nabii Musa Torati Mlimani Sinai?
Jibu: Ndiyo, Mungu ndiye aliyemkabidhi Torati
nabii Musa Mlimani Sinai.
11) Je, Mungu
alimkabidhi Torati hii yeye mwenyewe, au ni kwa kupitia kiumbe mwingine? Na
kama ni hivyo, kiumbe huyo alikuwa ni nani?
Jibu: Hapana, siye Mungu wa Pekee
na wa Kweli mwenewe ndiye aliyemtokea Musa huko Sinai. Imenenwa kwa wazi kabisa
kwamba kiumbe aliyenena na kumtokea nabii Musa alipewa jina na cheo la
’malaika’, na kiumbe huyo si mwingine ila ni Yesu Kristo (Matendo 7:35-38;
1Wakoro 10:4; Matendo 7:53; Wagalatia3:19; Waebrania 2:2).
12)
Ni nani inayemtaja Biblia kuwa ni Malaika Mkuu aliyewaongoza au kuwa pamoja na
Waisraeli Jangwani na aliyewalisha?
Jibu: Biblia inasewa wazi sana
kwamba Yesu Kristo ndiye malaika aliyemtokea Musa kwenye kichaka na kusemanaye
na ni malaika huyuhuyu ndiye aliyenena na Musa kwenye Mlima wa Sinai, na
inathibitisha mahali pengine kwenye maandiko pana mengi sana ya kumuelezea.
Neno malaika au malak linamaanisha mjumbe. Kwenye Mwanzo 48:15-16 tunasoma
hivi, “Akambariki Yusufu,
akasema, Mungu ambaye baba zangu, Ibrahimu na Isaka, walienenda mbele zake,
yeye Mungu aliyenilisha, maisha yangu yote, hata siku hii ya leo, naye Malaika
aliyeniokoa na maovu yote, na awabariki vijana hawa; jina langu na litajwe juu
yao, na jina la baba zangu, Ibrahimu na Isaka; na wawe wingi wa watu kati ya
nchi.” Kiumbe huyu aitwaye pia mungu ni
“Malaika” aliyewakomboa Israeli kutokna na uovu wote” alikuwa ni mjumbe
aliyetumwa na MUNGU WA PEKEE WA KWELI. Malaika huyu ni Yesu Kristo (soma pia
kwenye jarida la Malaika wa YHVH (Na. 24)).
13)
Je, ni kitendo cha kukufuru kumtaja au kumfananisha Kristo kuwa ni kama
malaika?
Jibu: Hapana, na kinyume cha fikra
hiyo ni dhana ya kibiblia kabisa. Yesu Kristo NI Malaika wa Bwana aliyekuwa anaongea na
Musa.
Siku ya kuabudu
1) Ni
siku ipi aliyetuamuru Mungu kukutanika pamoja kumwabudu na kumtukuza yeye?
Jibu: Ni siku ya Saba ya juma ambayo
wakati wote inaangukia siku ya Jumamosi
(Kutoka 20:10-11; Waebrania 4:3-40).
2) Je, tunaruhusiwa kukutanika siku ya J6umapili ili kumwa6budu na kumtukuza
Mungu?
Jibu: Hapana, siku inayojulikana
kama Jumapili siyo siku ya Saba ya juma, bali ni siku ya
kwanza ya juma (Mathayo 28:1).
3) Je, tunaruhusiwa kukutanika pamoja siku nyingine yoyote ile ya juma ili
kumwabudu Mungu?
Jibu: Hapana. Siku ya mapumziko
ambayo ni Sabato, ni siku takatifu kwa Bwana
(Kutoka 35:2; Kutoka 31:14; Nehemia 13:22) na ni siku
pekee takatifu ya juma iliyoamriwa kufanyiwa kutaniko takatifu (Mambo ya
Walawi 23:3; Isaya 56:2).
4)
Je, tumepewa uhuru wa kuamua kufanya kazi au kutofanya kazi kwenye siku hii
ambayo Mungu ameitenga na kuitakasa kwa ajili ya kumwabudu yeye?
Jibu: Hapana, hatuna uhuru huo.
Bali tumeamriwa kwamba tufanye kazi siku sita
za juma (Kutoka 23:12). Chochote mkono wako unachotaka kukifanya,
kifanye kwa nguvu zako zote (Mhubiri 9:10).
Haipaswi
kufanywa kazi yoyote siku ya Sabato na mtu yeyote (Marko 2:27).
5)
Je, inaruhusiwa kuwatumikisha watu kazi kwa niaba yetu siku ya Sabato?
Jibu: Hapana. Yatupasa tupumzike
sote siku ya Sabato, tangu Ijumaa jioni giza linapoanza hadi Kumamosi wakati
jua linapozama na giza kuanza.
Lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako; siku hiyo usifanye kazi
yo yote, wewe, wala mwanao, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi
wako, wala ng'ombe wako, wala punda wako, wala mnyama wako ye yote, wala mgeni
aliye ndani ya malango yako, ili mtumwa wako na mjakazi wako wapumzike vile
vile kama wewe. (Kumbukumbu
la Torati 5:14).
6)
Tunaitiaje unajisi Sabato?
Jibu: Kwa kufanya kazi zetu siku
hii, na kwa kuwafanya wengine watufanyie kazi zetu (kama vile kwenye kwenye
kigahawa ili kwenda kula vyakula), na kwa kushughulika na mambo mengi sana
kuwaza na kupangilia kimawazo na kwa kutomfanya Mungu kuwa ni wa kwanza kwenye
fikra na mawazoni mwetu siku hiyo (Isaya 58:13).
Sikukuu
1)
Sikukuu za Mungu ni zipi?
Jibu: Kuna Sikukuu Tatu tu kwa
kila mwaka:
• Pasaka/Mikate Isiyotiwa Chachu
• Pentekoste
• Sikukuu ya Vibanda
au ya Mabua
(Kutoka
23:14-19; Kumbukumbu
la Torati 16:1-17;
Mambo ya Walawi 23:1-44)
2)
Je, inatupasa kuondoka majumbani mwetu tunapoziadhimisha Sikukuu za Mungu?
Jibu: Ndiyo, yatupasa kujitenga na
dunia na mara tatu kila mwaka tunakwenda mahali alipopachagua Mungu na kuliweka
Jina lake ili kuzishika Sikukuu zake Mungu (Kumbukumbu la Torati 16:2,6-7).
Kanisa
linawajibika kupafanyia aina zote za usafi mahali itakapoadhimishwa Sikukuu na
kupaandaa. Hatupaswi kuishika Pasaka tukiwa majumbani au malangoni mwetu (Kumbukumbu la Torati 16:5-6).
3)
Je, inatupasa tuwe katika mahali inapoadhimishwa Sikukuu yake Mungu kwa kipindi
chote cha siku 7 za Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu na siku zote za Sikukuu
ya Vibanda na siku 2 za Pentekoste)?
Jibu: Ndiyo, (Matendo 20:6; 1Wakorintho 5:8; Matendo 2:1). Hatupaswi kurudi nyumbani
au kwenda kazini hadi siku zilizoamriwa kuadhimisha Sikukuu za Mungu ziishe.
4)
Je, tumeamriwa kutoa sadaka kwenye sikuu hizi tatu za kila mwaka?
Jibu: Ndiyo, tusitokee mbele za
Mungu mikono mitupu tuendapo kwenye sikukuu hizi. Kila mtu na atoe kama
awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako, alivyokupa. Kumbukumbu la Torati 16:16-17).
5)
Je, imeruhusiwa kusherehekea Krismasi?
Jibu: Hapana.
Yeremia 10:2-5 Bwana
asema hivi, Msijifunze njia ya mataifa, wala msishangae kwa sababu ya ishara za
mbinguni; maana mataifa hushangaa kwa sababu ya ishara hizo. 3 Maana
desturi za watu hao ni ubatili, maana mtu mmoja hukata mti mwituni, kazi ya
mikono ya fundi na shoka. 4 Huupamba
kwa fedha na dhahabu; huukaza kwa misumari na nyundo, usitikisike. 5 Mfano wao
ni mfano wa mtende, kazi ya cherehani, hawasemi; hawana budi kuchukuliwa, kwa
sababu hawawezi kwenda. Usiwaogope; kwa maana hawawezi kutenda uovu, wala
hawana uwezo wa kutenda mema.
6) Je, tunaweza kushiriki chochote
kwenye maadhimisho ya Easter?
Jibu: Hapana. Easter ni sikukuu ya
kipagani ya mungumke Ishar ambaye mwenza (mume) wake alikufa siku ya Ijumaa na
alivumishwa kwa uwongo kuwa alifufuka siku ya Jumapili. Hatimaye Pasaka
ilibadilishwa na kuingizwa Easter wakati kulipozuka malumbano kanisani kuhusu
siku ya kuadhimisha Ushirika wa Meza ya Bwana.
7)
Je, tunaweza kusherehekea au kuadhimisha siku za kuzaliwa?
Jibu: Hakuna mahali kwenye Biblia
tulipoamriw66a kuadhimisha siku za kuzaliwa. Kwa kweli, mifano iliyo kwenye
Biblia inaashiria kwamba haitupasi kuadhimisha siku hizi za kuzaliwa (Mwanzo 40: 20; Ayubu 1:4; Mathayo 14:6; Marko 6:21).
Tunaambiwa
kulikumbuka tukio la kifo cha Yesu (Luka 22:19), na tunafanya hivyo kila
mwaka kwenye adhimisho la Pasaka, lakini hatujaamriwa kusherehekea wala
kuadhimisha kuzaliwa kwa Yesu.
8) Je, inaruhusiwa kuadhimisha sikukuu ya Mwaka Mpya ya mwezi Januari?
Jibu: Hapana, Mungu anatuambia
kuwa tusijifunze au tusiige njia za mataifa (Yeremia 10:2; 2Wafalme 17:33; 1Wafalme 14:24; Kumbukumbu la Torati 18:9).
9) Ni upi Mwaka mpya kwa mujibu wa Maandiko Matakatifu?
Jibu: Ni mwezi mpya uliokaribu
sana na majira ya machipuko unaporudi Yerusalemu (au majira ya jua kuwa kwenye
ncha ya kaskazini mwa dunia) (soma Kutoka 23:15; Kutoka 12:2).
10) Mwezi Mpya ni nini?
Jibu: I wakati mwezi mwandamo
unapokuwa katikati ya mstari wa jua na mwezi (Zaburi 81:3).
Neno Kehseh lililo kwenye aya ya 3
linatokana na neno la shina ambalo ni Kacah.
Halimaanishi na maana ya mwezi mkamilifu, lakini zaidi tu ni kipindi ambacho
mwezi unakuwa ”umefichwa” kutoka usoni petu.
11) Je, tunaweza kufanya kazi siku za Mwezi Mpya?
Jibu: Hapana, Mwezi Mpya ni siku
tunazotakiwa kuziadhimisha kwa kutofanya kazi zetu (Amosi 8:5).
12)
Je, tunaruhusiwa kuwatumia watu watufanyie kazi siku za Mwezi Mpya?
Jibu: Hakuna biashara
iliyoruhusiwa kufanyika siku za Sabato na Mwezi Mpya (Amosi 8:5).
Vyakula
1) Je, kuna mahala kwenye Agano Jipya ambapo Mungu ameruhusu kula kitu chochote
tupendavyo?
Jibu: Hapana. Kristo alisema hivi: Msidhani ya kuwa
nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. (Mathayo 5:17).
2) Je, vyakula safi na najisi vimeondolewa?
Jibu: Hapana. Kila kiumbe cha
Mungu, kilchotakaswa kwa neno la Mungu kinafaa kwa kuliwa na
hakitakiwi kukataliwa (soma 1Timotheo 4:4-5).
Mahala waendako wafu
1)
Wakati mtu anapokufa, je roho yake inakwenda mbinguni kama alikuwa mwema au
jehanamu kama alikuwa muovu?
Jibu. Hapana, wafu wanafanana kama
wamelala au hawana ufahamu au hawajui chochote
(Danieli 12:2,13; 1Wakorintho 15:20-22).
Wala hakuna mtu aliyepaa mbinguni, ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni,
yaani, Mwana wa Adamu. (Yohana 3:13).
HAKUNA
YEYOTE anayekwenda mbinguni, siyo sasa tu, na wala haijatokea hata huko nyuma.
Ni Mungu peke yake ndiye alitakayeshuka hapa Duniani wakati kile kitu
kimefanywa upya (Ufunuo
22).
2) Je, mfano wa Lazaro na Tajiri unamaanisha kwamba watenda dhambi wataungua
moto milele, wakiteseka jehanamu?
Jibu. Hapana, kwa kuwa Mungu anataka
watu wote waokolewe na waijue kweli (1Timotheo 2:4). Kwa hiyo, watu
wote wenye mwili wanafursa ya kutubu (1Timotheo 4:10).
3) Je,
roho inaweza kufa?
Jibu. Ndiyo, roho inaweza kufa au
kuangamizwa (Ezekieli 18:4).
Kristo
alisema: Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho;
afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza
mwili na roho pia katika jehanum. (Mathayo 10:28).
Mwanadamu
anaweza kusababisha kuyapoteza maisha lakini hawezi kuiangamiza roho – ni Mungu
tu ndiye anaweza kufanya hivyo.
4)
Jehanamu ni nini basi?
Jibu. Neno sahihi linalopaswa kuiita
Jehanamu ni Sheol, na
linamaana ya kaburi ambako wafu wanazikwa
ndani yake. Hades, au Kuzimuni lilikuwa
ni neno la Kiyunani lililotumiwa kumaanisha kaburi. Neno la tatu
lililotafsiriwa kama jehanamu kwenye Biblia ni Gehenna, ambalo
lilikuwa ni jalala la kutupia takataka lililokuwemo nje ya mji wa Yerusalemu
ambako walikuwa wanawachomea mbwa pia pamoja na takataka nyingine. Neno
linguine lililotumika kwenye Biblia ni tartaros au tartaroo,
ambalo likuwa ni shimo lililotengwa na malaika kwa hifadhi yao. Hakuna kitu kama
hicho cha Jehanamu ya kuchomea watu.
5)
Je, Paradiso ni nini nayo?
Jibu. Ni Nyumba ya Mungu, Mlima Mtakatifu wa
Mungu, Mlima wa Sayuni Mji wa Mungu Aliyehai, Yerusalemu ya Mbinguni
(2Wakorintho 12:2,4; Ufunuo
4:2-11; Ufunuo 21; Ufunuo 2:7; Waebrania 12:22; Ps.
125:1).
6) Je, Mauti ya Pili ni nini?
Jibu. Ziwa la Moto ambavyo maana yake ni
kitendo cha kuunguzwa hadi kubakia majivu ya miili ya wafu wale wanaokataa
kutubu na kuifuata njia ya Mun6gu katika kipindi cha mwishoni mwa Ufufuo wa
Kwanza wa wafu na cha Hukumu ya Kitu cha Enzi Kikubwa na Cheupe.
Mauti
na Kuzimu vitakuwa vimeangamizwa zote kabisa pia (Ufunuo 20:14).
7) Je, malaika nao wanakufa?
Jibu. Ndiyo, malaika wanakufa, na
hata pia wale Malaika walioasi mbinguni watakufa
pia (Ezekieli 28:16,18; Isaya 14:15) kama wafanyo
wanadaamu.
Ufufuo wa Wafu
1)
Je, wanadamu wote waliowahi kuishi ulimwenguni watgafufuka kutoka kwa wafu?
Jibu. Ndiyo, ni kama
ilivyoandikwa: Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama
ya wafu ililetwa na mtu. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na
katika Kristo wote watahuishwa. (1Wakorintho 15:21; 1Yohana 2:2; Warumi 11:32).
2) Kuna aina ngapi za Ufufuo wa wafu zilizoandikwa?
Jibu. Biblia inasema kuwa
kutakuwa na aina mbili za ufufuo wa wafu.
Ufufuo wa
Kwanza (Ufunuo 20:6) ni wa watakatifu peke yao, hivyo ni kusema
kwamba, ni wa wale waliozishika amri za Mungu na ushuhuda wa Yesu (Ufunuo
14:12; 12:17), na wa wale walioyapenda maisha yao hadi
kufa (Ufunuo 12:11).
Ufufuo mwingine ni ufufuo wa
Hukumu (Yohana 5:24,29). Watu wote ambao hawakufufuka kwenye Ufufuo
wa Kwanza, ambao ni ufufuo wenye heri (Waebrania 11:35), watafufuka
toka mautini kwa ajili ya kuhumu ya kurudiwa na sio ya kukemewa.
Wakati
huo, malaika watapewa fursa ya wokovu katika Kristo
(1Petro 3:19; 2Petro 2:4) ili kwamba wafikie uwezo wa
kuielewa kweli na kumrudia Mungu (1Wakorintho 6:2-3; Yuda 6).
3)
Je, Mungu atamtuma Kristo mara ya pili aje hapa Duniani?
Jibu. Ndiyo, Mungu atamtuma Kristo mara ya pili aje
hapa Duniani (Waebrania 9:28; Yohana
14:3; Matendo 1:11; Matendo 15:16).
4) Je, kisha Kristo atawachukua watakatifu na kwenda naye hadi mahala alipo
Mungu huko Mbinguni na watakuwa huko pamoja na Mungu?
Jibu. Hapana, watakatifu watakuwa
pamoja na Bwana Jesu, pale atakapokuwa yeye (Yohana
14:3; 1Wathesalonike 4:17; Ufunuo 14:1). Kristo
ataweka makao yake huko Yerusalemu (Ufunuo 14:1) kutoka huko
ulimwengu utatawaliwa.
5) Ni kazi gani atakayokuja kuifanya Kristo atakaporudi hapa Duniani?
Jibu. Kristo (pamoja na
watakatifu waliofufuka) wataitawala dunia yote kutoka
Yerusalemu (Ufunuo 11:15; Ufunuo 19:11-16; Ufunuo 5:10; Ufunuo 20:4).
6) Ni kwa muda gani Mungu amempa Kristo kuifanya kazi hii?
Jibu. Kristo atatawala hapa
Duniani kwa miaka elfu (Ufunuo 20:6).
Kanisa
1)
Kanisa ni kitu gani?
Jibu. Kanisa ni muunganiko wa watu
wanaofanya kutaniko au umma wa watu wa Mungu. Siyo jingo. Kristo alisema kuwa
atalijenga kanisa lake juu ya mwamba na Mungu ndiye huo mwamba (Zaburi 18:1-2).
Kanisa linaongozwa na wazee na mashemas, waliochaguliwa na waumini (Matendo
1:22,26, 6:3,5-6, 15:22; 1Wakorintho 16:3; 2Wakorintho 8:19,23). Roho
Mtakatifu anawafanya kuwa waangalizi wa kundi ambalo ni Kanisa lake Mungu
(Matendo 20:28).
2)
Wajibu na kazi gani basi limepewa kanisa?
Jibu. Kanisa limepewa agizo moja kuu
na Yesu Kristo.
Mathayo
28:18-20 Yesu akaja kwao,
akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. 19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi,
mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; 20
na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo
pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
3)
Je, Wakristo wanatakiwa kutoa zaka ili kusaidia kuendeleza kazi ya Kanisa la
Mngu?
Jibu. Ni wajibu wa kila Mkristo
Kusaidia kazi ya Kanisa (soma
Kumbukumbu la Torati 12:5-19). Kuna zaka ya kwanza nay a pili. Zaka ya kwanza
wanapewa makuhani walio kwenye nchi husika. Zaka ya pili ni kwa ajili ya kila
mtu binafsi yake ili imuwezeshe kushiriki kwenye Sikukuu. Yeyote asiyetoa zaka
anamuibia Mungu (Malaki 3:8-10).
4)
Je, ubatizo wa makanisa ya Waamini Utatu unakubalika na kuchukuliwa kuwa
unafaa?
Jibu. Hapana,
ubatizo wa kumzamisha mtu kwenye maji mengi kwa jina la Baba na Mwana na Roho
Mtakatifu (Mathayo 28:19) unamaana kwamba ubatizo unafanywa kwa Jina la Baba
katika mwili wa Mwana, aliyeombwa kwa jina la Mwana, kwa nguvu na uweza wa Roho
Mtakatifu.
Hii ni maana sahihi ya tangazo la Kristo, na haina uhusiano wowote na imani
ya Utatu.
5) Je, waamini Utatu wanapaswa kubatizwa tena?
Jibu. Ndiyo,
pamoja na wale waliobatizwa kwenye imani za makanisa ya Kibinitarian au
Wadiheist, nk.
6) Kwa mujibu wa Bilia, je inaruhusiwa kumbatiza mtoto au mvulana aliye
chini ya miaka 20?
Jibu. Hapana.
Kwa mujibu wa Maandiko Matakatifu yatupasa tuwe watu wazima kwanza wenye sifa
za kwenda vitani na ni umri wa utu uzima unaanzia miaka 20 kwa mujibu wa
Maandiko Matakatifu (Hesabu 1:1-3,18; Ezra 3:8).
Watakatifu hawapasi kupigana vita vya mwili na damu na wanajipanga kwa vita
dhidi ya wafalme, dhidi ya nguvu, dhidi ya watawala wa ulimwengu huu wenye
giza, dhidi ya malaika waovu walio mahala pa juu (Waefeso 6:11-13; 1Timotheo
6:12; 2Timotheo 4:7; Ufunuo 3:21; Ufunuo 12:11; Ufunuo 15:2).
7) Kwa mujibu wa Biblia, ni umri gani ambao mtu anaweza kuanza huduma ya
kumtumikia Mungu Kanisani?
Jibu. Tunaweza
kuchukua ofisi ya utumishi au huduma ya kuanza kufundisha kwenye hekalu la
Mungu tangu umri wa miaka thelathni kwa mujibu wa maelekezo ya Torati ya Mungu
(Hesabu 4:3,23,30; 1Nyakati 23:3). Watakatifu sasa ndio Hekalu la Mungu
(1Wakorintho 3:16; 2Wakorintho 6:16).
8) Je, mtu aliyeoa kihalali zaidi ya mke mmoja anaweza kuwekwa wakfu
kutumikia Kanisa la Mungu?
Jibu. Hapana,
Agano Jipya linaweka kikomo cha idadi ya mtumishi kuwa na wake ambacho ni mke
mmoja tu ndiyo wanaruhusiwa kuwa nao wazee wa kanisa. Hakuna anayeruhusiwa
kuwekwa wakfu kutumika kama mzee wa kanisa kama atakuwa ana wake zaidi ya
mmoja, (1Timotheo 3:2,12; Tito 1:6).
Wazee wa kanisa wanatakiwa wawe wameoa, kwa kuwa ndoa ni wajibu waliopewa
watu wote kwa amri au agizo alilopewa Adamu.
9) Je, wanawake wanaruhusiwa kuwekwa wakfu kuwa watumishi kwa lengo la
kuhudumu kwenye Ibada ya Kuabudu kwenye Kanisa la Mungu?
Jibu. Hapana. Yatupasa tujue kwamba
kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha kila m6wanam6ke ni mum6e
wake, na kichwa cha Kristo ni Mungu (1Wakorintho 11:3; Waefeso 5:23).
Utaratibu
wa kuandaa na kuendesha ibada kwenye kanisa la CCG unapaswa kufanana
ulimwenguni kote.
Kwa
hiyo, utaratibu na mtiririko wake unapasa uwe kama ifuatavyo.
Mambo au taratibu
zote zinatanguliwa au zinaanza kwa ‘Maombi ya Kufungulia Ibada’ kwanza, kisha
hufuatiwa na wimbo mmoja au nyingine kadhaa.
Nyimbo au Tenzi hizi
ni za namna ya kuabudu.
Kisha ndipo
m6ajarida yatatakiwa yasomwe kwa kujifunza.
Maswali
yanaruhusiwa na kujibiwa mwishoni mwa mafundisho kwa kawaida, lakini mtu
anayeshughulikia na ufundishaji au kutayarisha masomo anaweza kuyachukua
maswali na kuyajibu iwapo kama yataonekana kuwa yana umuhimu kuyafafanua iwapo
kam6a hakuna kumbukumbu itakayofanyika.
Wote wawili,
yaani wanaume na wanawake wanaweza kuuliza m6aswali kwenye kipindi cha Maswali
na Majibu kama watakuwa ni wanawake wasio na wanaume zao waliohudhuria kwenye
ibada hizo na vinginevyo basi maelekezo ya Mtume Paulo yatakuwa hatafuatwi na
sisi kikamilifu.
Wanawake
wanapaswa kuwashauri waume zao kama ikiwezekana.
Ufungaji
wa ibada unafanywa kwa kuimba wimbo wa tenzi na kisha kufanywa maombi.
Maombi yote ya
kufungulia na kufunga ibada yapasa yafanywe na wanaume kama wapo.
Kwenye ibada au
vipindi vyovyote wanavyohudhuria wanawake peke yao, ni dhahiri sana kwamba
wanawake ndio watashughulika na shughuli zote za ufundishaji na kufanya maombi
haya yote ya kufungua na kufunga na watajibu maswali yoyote
yatakayojitokeza.
Wanafunzi mara
nyingi wapewe fursa ya kufanya maombi ya kufungua na kufunga ibada kama sisi
wenyewe tunavyomuomba Mungu awe pamoja nasi kwa Roho wake Mtakatifu.
10) Ni kalenda
ipi basi ambayo Kanisa la Mungu linapasa kuifuata: Kalenda ya Mungu inayotokana
na mwanzo wake siku za kutoonekana Mwezi Mpya, au Kalenda ya Gregorian, au
Kalenda ya Hillel, au Kalenda ya Kiislamu? Je, tunapaswa kusherehekea au
kuadhimisha mavuno ya shayiri ya Yerusalemu ili itusaidie kuamua mwanzo wa
Mwezi Mpywa wa Abibu?
Jibu. a) Hapana, hatuadhimishi mavuno majira ya
shayiri ya Yerusalemu ili tuamue mwanzo wa Mwezi Mpya wa Abibu. Nuhu aliingia
kwenye Safina na kisha ikafungwa (Mwanzo 7:16), lakini mwishoni mwa gharika
kuu, alijua siku ambayo Mwaka Mpya ulianza. Kisha ndipo alifunua kifuniko cha
Safina (Mwanzo 8:13). Uwezo huu wa kuijua siku ya kuanza kwa Mwaka Mpya
haukutokana na hali ya kuangalia alama au ishara na kwakweli haikutokana na
kuyaona kwake mavuno ya shayiri karibu na Yerusalemu mwishoni mwa gharika au
mahali pengine popote pale.
Mwanzo wa mwaka
HAUHUSIANI na ukomavu wa mavuno ya shayiri kwenye israeli ya sasa. Unaweza
kutofautiana kwa majuma kadhaa hadi mwaka mmoja na kwa wengine na inafanya
isiwezekane kuchapisha kalenda na maelekezo ya Siku Takatifu.
Leo, watu wanazitumia mbegu za kisasa zinazokomaa kwa viwango mbalimbali na
kutofautiana kwa kiasi kikubwa sana na punje za nyakati za kale. Wengine
huzipanda, kwa kweli, kwenye mazingira yaliyotunzwa sana na kulindwa wakijaribu
kutunza dhana zao. Hata hivyo, mazingira fulani yanabadilisha shauku yao kwa
kweli.
Mwaka wa saba wa
mzunguko wa miaka ni mwaka wa sabato wakati ambapo hatuvuni mavuno ya kila
mwaka kwa mujibu wa sheria na amri za Tirati ya Mungu. Kwene kipindi cha
Milenia, hakuna mtu atakayepanda mbegu za kila mwaka kama vile shayiri. Matokeo
yake, hakuna atakayeweza kuona kiwango cha umeaji na ukuaji wa shayiri kuwa
inakuwa miezi ya Marchi au Aprili, kwenye mwaka wa Sabato na kwenye mwaka wa
Yubile. Kujua kwake hakuhitajiki na hakutahitajika ili kuanza mwaka na
kutangaza Sikukuu na hata Siku Takatifu.
b) Haturuhusiwi
kuahirisha maadhimisho ya Siku Takatifu, Mwezi Mpya na Sabato. Kwa hiyo,
Kalenda ya Hillel ni upotofu na machukizo.
c) Kalenda ya
Gregorian imetungwa na wanadamu, na haitokani na Maandiko Matakatifu.
d) Ni jambo la
kihistoria kabisa kwamba Kristo na Kanisa la Mungu wakati wote waliifuata
Kalenda ya H^ekaluni ambayo ilianza miezi yake kwa kipindi cha Kutoonekana
Mwezi na ndipo walianzia Mwezi Mpya kutokea Yerusalemu.
Ndoa
1) Je, Kristo
anaruhusu wanandoa waishi kwa uhusiano bandia au wa kimada?
Jibu. Hapana. Kanuni za makanisa ya Mungu ni
zilezile kwa kipindi chote cha miaka 2000. Mshirika wa mwili wa Kristo anapaswa
awe ameoa ndoa halali ya mwenzi mmoja na ajiepushe na zinaa hadi watakapokuwa
wameoana rasmi.
Kristo alitoa
maelekezo ya wazi sana kuhusu ndoa na hakuitambua sheria iliyo ya kawaida kwa
wengi au ndoa bandia ya watu kuishi vimada kuitambua kuwa kuna ndoa hapo.
Alipokuwa anaongea na yule mwanamke kisimani huko Sikari ya Samaria Kristo
alisema: “Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa. Yule mwanamke akajibu,
akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume; kwa maana umekuwa
na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli” (Yohana 4:16-19).
Kwa hiyo Kristo
alijua kwamba mwanamke huyu alikuwa anaishi kwa uhusiano wa kimada na mtu huyu
kama inavyoonekana kwa usemi wa “naye uliye naye sasa siye mume wako”.
Kuwakataza
watu wasioe ni moja wapo ya mafundisho ya mapepo (1Timotheo 4:1,3).
Meza ya Bwana
1) Ni watu gani peke walioruhusiwa wawepo kwenye chumba kilichoandaliwa kwa
ajili ya ushiriki wa mlo wa mkate na mvinyo?
Jibu. Tendo
hili la Ushirika wa Meza ya Bwana linahudhuriwa na waumini watu wazima na
waliobatizwa peke yao. Inapasa patengwe mahali maalumu patakapotumika kuwazuia
watoto wakati huu wa ibada hii.
2) Je, juisi ya
zabibu inaweza kutumiwa badala ya mvinyo kwenye maadhimisho haya ya Ushirika wa
Meza ya
Bwana?
Jibu. Hapana. Juisi ya zabibu
haikutumiwa kabisa wakati wa Pasaka na Myahudi yoyote wala Mwisraeli, akiwemo
Kristo mwenyewe, Mitume au Kanisa la Agano Jipya. Juisi ya zabibu imekufa,
wakati kwamba mvinyo una uzima na unaashiria damu iliyo hai ya Yesu Kristo kama
mwanadamu.
3) Huu Usiku wa Kuuangalia au Uaiku wa Kuuangalia sana ni kitu gani (Kutoka.
12:42)?
Jibu. Dhana ya kulinda au
kukesha inatokana na kitendo cha Malaika wa mauti kupita juu yao, na matarajio
ya kukombolewa kwa watu wetu. Kristo alikufa muda wa saa 9 alasiri wakati ambao
wanakondoo walikuwa wanauawa au kuchinjwa kwa ajili yam lo wa Pasaka
uliyofanyika jioni ile iliyotanguliwa na huu Usiku wa Kuukumbuka Sana wa siku
ya Kumi na Tano ya mwezi wa Kwanza. Nia siyo kwamba tuiadhimishe siku hii kwa
kukesha lakini zaidi tu ni kwamba usiku umeendelezwa kwa kujisomea na kutafakari
kwa kina. Siyo sahihi sana kwenda kulala mapema usiku huu.
4) Je, Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa una maana gani?
Jibu. Sadaka ya
mwanakondoo na kitendo cha kuutikisa mganda wa malimbuko vinamwashiria Kristo
kama limbuko aliyepaa Mbinguni kwa Mungu wake (Mambo ya Walawi 23:9-14). Yalikuwa ni
malimbuko ya kwanza ya malimbuko ya mavuno ya shayiri na mwanzo wa mavuno ya
wote wenye mwili na wa Malaika kwenye familia ya Mungu. Mganda wa Kutikiswa
unaashiria pia kipindi cha mpito kuelekea Pentekoste na kila mara inatokea siku
ya Kwanza ya Juma ya wakati wa maadimisho ya Mkate Usiotiwa Chachu.
q