Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[074]
Fikra Iliyopo Kwenye Imani Potofu
ya Kalti
(Toleo La 2.0
19941029-20000108)
Jarida hili linachambua dhana au mawazo waliyonayo kwenye
imani au dini potofu kwa waumini au watu wanaoshirikiana na makanisa yasiyo
husishwa na mapokeo yake na kuishika kweli. Maana au tafsiri ya imani potofu
imefafanuliwa kama ni utendaji wa kisasa wa neno hilo. Nguvu kuu ya kuweka kitu
chochote kabla upendo wa Baba haujaonekana kama kulionyesha na kulifanya
litambulike kundi kuwa ni dini au imani potofu.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati
Miliki © 1994, 2000 Wade
Cox)
(tr.
2015)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Fikra
Iliyopo Kwenye Imani Potofu ya Kalti
Dini hizi za imani potofu zinadumu
kutokana na hali ya kukamatwa kwa mawazo ya watu wanaojikusanya amoja. Imani
hizi zinaanza na watu wanaojikusanya kama kikundi cha watu wenye mtazamo wa
namna moja na imani ya namna moja wanaofanya shughuli zao kwa wasiwasi na woga
wa mpotofu na za uwongo.
Kuna mtazamo unaoendelea kwenye
Ukristo makanisa yenye imani kongwe za kale ambao wanalitumia neno hili imani potofu kwa kuyalenga makanisa au
dini zisizo mojawapo ya hizi zenye imani kongwe, ambazo zinatofautiana
kimafundisho wayayofundisha wao. Dini hizi zote za imani kongwe na za kikale
zilizochipuka kutokana na wahubiri mashuhuri wa zamani kina Knox na Calvin na waanndishi mashuhuri wa zama za
Matengenezo (kama Luther), na mahafudhina wengine wote kutoka kwenye mashirika
yalioamini na kufundisha Utatu yaliyoendeleza imani hiyo na kuwapa watu alama
mbaya na majina mabaya wale ambao hawakukubaliana nao imani zao potofu. Sisi
mara zote tumebakia kuwa kwenye imani iliyojulikana kama watu wa njia ile. Mtume Paulo alisema hivyo.
Dini hizi za Kalti ni kitu kingine tofauti na ni cha pamoja zaidi. Watu wengi
wanakosea kujua aina ya watu wa kuwaita jina hili.
Matumizi ya jina hili yanakosewa sana.
Uelewa wa kweli na utendaji wake unayazingira makundi yote mawili kisawasawa,
yaani, ya Ukristo mkongwe za zamani na kwa vikundi vidogo pia. Tofauti ya kweli
kati yake vile vilivyo na visivyo imani potofu zipo kwenye ukweli uliodhahiri
sana na unalitofautisha kanisa la kweli la Mungu na makundi haya yote ya imni
hizi zote potofu, yakiweko nay ale ya kinachoitwa Ukristo mkongwe wa tangu zama
kale.
Kamusi maarufu iitwayo The Oxford Universal
Dictionary inalitafsiri neno hili la kalti
au imani potofu kutoka kwenye ukurasa 1617. [ad. L. cultus kuabudu Mnamo karne ya 19 mara nyingi
ilitamkwa culte kama ilivyo kwenye Kifaransa.] † 1. Ibada - 1683. 2. Aina fulani ya ibada za dini; husu inapotaja sheria zake za kimapokeo kwa nje na maadhimisho
yake 1679. 3. hamisha. Kujitoa kwa mtu fulani au kitu, sasa hususan. Ni kama mwili au kikundi cha wanaodaiwa kushikamana
1711.
Kwa hiyo tunaaina hiyo ya ibada kwa
haki za namna yake fulani na maadhimisho yanayofanywa na kundi la wale
wanaojiita watu waadilifu—wanaotokana na mashirika ya kikanisa. Maranyingi
sana, muundo mzima wa kidini na kiimani na uliofanyika kuwa mashuhuri hapa
duniani umeungwa na waanzilishi wa imani hizi potofu za kikaltiki.
Tafsiri yake imeelezewa kwa kina
kwenye Kamusi maarufu ya Kiingereza ijulikanayo kama the Oxford English
Dictionary Nyongeza kujumuisha maana ya: cult [kalti], sb. Ikiongeza 2.b. Sasa linatumika mara kwa mara likimaanishwa na
waandishi kwenye kanuni za imani za kikaltiki na wavumbuzi wa zama kale
za ukaltiki...
Mifano yake ni kutokana na maelezo
yanayoelezeka ya kuabudu miungu mingine tofauti, ya kike nay a kiume kwa mtindo
unaobadilikabadilika na wa mazingira tofautitofauti.
Tofauti muhimu ya imani hizi ya kikalti
ni kwamba ni mitindo yake fulanifulani maalumu na wanayoitilia maanani kwenye
taratibu zao za kiibada na kidini, hasahasa katika kuonyesha sheria walizonazo
na zile zilizo nje na taratibu zao za jinsi wanavyoadhimisha wanapoabudu au
jinsi wanavyomnyenyekea mtu au kitu fulani. Kwa ghafla tu jambo hili linaivunja
amri ya kwanza kwenye shirika hili lililoanzishwa na mtu ambaye anaweza kudai
uaminifu wa mtu au kudai watu wamtii na kuwa juu ya mambo yote ya kiimani na
kiroho ya kalti na kuwa ni mtu mwenye kusikilizwa zaidi ya kweli ambayo Mungu
ameiweka kwenye Biblia. Na ndipo sasa inahusiana na tofauti iliyopo kati ya
miundo iliyoigizwa au kuingizwa kwenye mshikamano wa mwili.
Kwa namna moja au nyingne mifumo yote
ya kidini ya kalti. Tofauti kati ya imani za kalti na wateule ni unyofu tu
kwenye bodi au mwili wa kile kinachodaiwa kuwa ni zaidi ya mshikamano na juu ya
kweli ya kweli iliyo kwenye biblia na kusimamia mwenendo na madai ya mteule.
Tofauti inaonekana wakati mtu
anapoyaweka madai ya mtu kuwa kwenye bodi au kundi kabla ya mtu hajadai kwenye
ukweli uliodhahiri na kuelekea hadi kwenye sheria za kibiblia na ushuhuda.
Tofauti ya kinabii inapatikana kwenye
gombo la nabii Isaya.
Isaya 8:16-20 Ufunge huo ushuhuda, ukaitie muhuri sheria kati ya
wanafunzi wangu. 17 Nami nitamngojea Bwana, awafichaye
uso wake nyumba ya Yakobo, nami nitamtazamia. 18 Angalieni,
mimi na watoto hawa niliopewa na Bwana tu ishara na ajabu katika Israeli,
zitokazo kwa Bwana wa majeshi, yeye akaaye katika mlima Sayuni. 19 Na wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye
pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong'ona; je! Haiwapasi watu
kutafuta habari kwa Mungu wao? Je! Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu
walio hai? 20 Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa
hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi.
Hii ingetikea na Mungu alisema
ingetokea na kwa mambo mengine Mungu anafanya kwa makusudi mazima kabisa itokee
ili kwamba watu hawa wasiingie hukumuni. Wanaruhusiwa kuwa wa imani hizi za
kalti na wanaondolewa na kutolewa kwenye kundi la wateule. Hawaitwi hukumuni na
kwa hiyo wanabakizwa kuingia hukumuni kwenye ufufuo wa pili wa wafu.
Andiko
hili lapasa lieleweke vyema kutoka kwenye tafsiri ya KJV.
Isaya
8:16-20 Ufunge huo ushuhuda,
ukaitie muhuri sheria kati ya wanafunzi wangu. 17 Nami
nitamngojea Bwana, awafichaye uso wake nyumba ya Yakobo, nami nitamtazamia. 18 Angalieni, mimi na watoto hawa niliopewa na Bwana tu
ishara na ajabu katika Israeli, zitokazo kwa Bwana wa majeshi, yeye akaaye
katika mlima Sayuni.
Huu ni unabii. Kristo amewapa wateule
na Bwana wa Majeshi kama ishara na maonyo kwa Israeli na ulimwengu. Sheria na
ushuhuda vimewekwa juu yetu. Tunalazimishwa kutenda mambo sawasawa na isemavyo
sheria na ushuhuda.
19
Na wakati
watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama
ndege na kunong'ona; je! Haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? Je!
Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?
Hili ndilo linalotokea huko kipindi
hiki na ilitabiriwa na kutokea kwa msingi endelevu. Israeli waliigeukia
miungu ya uwongo na kuziandama imani na dini za uwongo. Walianza kuyatenda na
kuyaandama mambo yote mageni kama vile kusimamisha au kuanzisha tena dini na
imani zote potofu za babeli mamboleo, wakianzisha imani na dini za uwongo za
kimizimu na kuyaomba maroho ya watu waliokufa (ambao ni mapepo), kama
wanavyofanya sasa.
20
Na waende kwa sheria
na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana
asubuhi.
Kama mtu akiwa haneni kwa kweli ya
Mungu, kama hawajitoi na muhuri haujatiwa vipajini mwao, basi wao hawapo
miongoni mwa wateule.
Andiko lililo kwenye tafsiri ya RSV
halionyeshi kikamilifu umuhimu wa sheria na ushuhuda kwa wanafunzi wa Mungu.
Wakati kundi la watu, ambao mwanzoni walidai sheria na ushuhuda, kuwa wanaanza
kufundisha kinyume na Biblia wakati ambapo hakuna nuru ndani yao. Wao ni
waumini wa kalti. Wale wanasalia ndani ya makundi hayo wakieendelea
kung’ang’ania mafundisho ya uwongo hawamo tena kwenye ufuasi wa Mungu na sio
wateule. Bali hawa ni wafuasi na wanachama tu wa imani hizi za kalti na kwa
namna hiyohiyo ambayo kundi linguine la wasiofanya ibada zilizoelekezwa au
kuamriwa na biblia ya walio kwenye imani inayoshikamana na kalti.
Kutokana na tafsiri hii wakati dini za
Kikristo zilianza kuiga mfumo na imani ya Utatu, kufuatia na mafundisho
mabaraza ya kanisa, wakaanza kuwa kalti. Wakati dini za Ukristo mkongwe
zilipoanza kuliunda Baraza la Mtaguso wa Nikea na walianzisha mafundisho na
mfumo wao wa kiteolojia na kifilosofia ambao ulikuwa ni kinyume kabisa na
maagizo ya biblia na wakafanyika kuwa kalti kamili kabisa. Wakati kiasi kingi
cha makanisa yalipoiga na kujiunga kwenye mfumo huu wa mabaraza na kukubaliana
na imani hii ya Utatu kenye kipindi kilichojulikana kama cha Mafundisho ya
Baraza la Mtaguso wa Kalkedoni yote yalikuwa ni kalti na hakuna miongoni mwao
aliyekuwa ni sehem ya wateule.
Kama sisi tumo kwenye ushirika wa
mashirika haya basi tunapendezwa n mafundisho haya. Kama sisi tu wanachama wa
mashirika haya yanayofundisha imani ya Utatu basi tuje kuwa tunaunga mkono
mafundisho haya mapotofu kwa kujihudhurisha kwetu. Ukweli ni kwamba kitendo
chetu cha kujihudhurisha kwenye ibada zao na uanachama wetu kwenye makanisa
haya kunafanya ionekane kuwa tunachukuliana au kukubaliana na mafundisho haya;
kwakuwa ukimya wetu unafanya yakubalike mafundisho haya.
Kwahiyo, Makanisa ya Roman Katholiki,
Anglikana, na Greek Orthodox ni kalti, na ndivyo ilivyo pia kwa makanisa
mengine yote ya mrengo wa waabudu miungu mingi au kwa vikundi vinavyouabudu
utatu ni kalti. Ukubwa na uwingi walionao si kitu au kigezo cha kushindwa
kuitwa kuwa wao ni kalti. Ukweli wa kwamba kundi linamtegemea au kuweka imani
yao kwa kiongozi mmojana kuwa juu ya kila kitu hata kuwa juu ya maagizo yaliyo
kwenye kweli ya biblia ni alama mojawapo ya imani hii ya kalti. Haijalishi
jinsi kiongozi huyo alivyo au atakavyoitwa, awe Papa au Askofu Mkuu, au
Kiongozi wa wa Ulimwenguni kote, au Jones asiye sawasawa.
Wateule wamebatizwa kwenye mwili wa
Kristo na sio kwa kanisa lolote au dhehebu. Maneno hayo yananenwa kila mteule
anapokuwa anabatizwa. Kwa hiyo wateule wanaunganishwa kwenye mwili wa Yesu
Kristo kwenye ibada ya kumuabudu Mungu Mmoja, Wapekee na wa Kweli aliyeandikwa
kwenye Yohana 17:3. Kwa hiyo wakati wateule wanapoungana amoja kwenye makanisa
mahalia, walikuwa wameunga sana kwa msingi wa kuungamana kwao kwenye kweli na
kumuabudu Mungu Mmoja, Wapekee na wa Kweli na kumtumikia Mwanae wa pekee Yesu
Kristo.
Wakati kanisa lilipokabiliwa na mafundisho
yaliyojaribu au kukusudia kumuweka Kristo nje ya hali yake ya kawaida na
halisi, na kujaribu kumfanya awe zaidi ya hali yake halisi ya Uwana wa Mungu na
kumfanya awe sawa na Mungu na kuutenganisha ubinadamu wake kutoka kwenye
utakatifu wake, ndipo wateule walilazimika kujiunga upya kwa kuanzisha kanisa
tena na kujitenga na wale wanaooyaanzisha mafundisho ya uwongo, ambayo
yalijulikana wazi na kuitwa kama mafundisho ya Mpingakristo.
Msingi wa imani ni ukweli na hawaendi gizani
kakwe kabisa wale wanaotembea kwenye kweli. Sababu inayotupelekea tuenende kwa
mujibu wa 1Yohana ni kwa kuwa malumbano haya yaliingia kanisani kipindi ambacho
Mtume Yohana akiwa kiongozi. Ilimpasa kuyashughulikia kikamilifu mafundisho
haya mapotofu na fundisho kuhusu Uungu tangu mwanzoni kabisa mwa hatua ya
kanisa. Hakuna lililo jipya. Malumbano haya yalipata ufumbuzi wake kwenye
kanisa la Yohana, wakati walipojatibu kutenganisha ubinadamu wa Yesu Kristo na
kumfanya kuwa alikuwa na utu wa kimbinguni. Walijaribu kusema na kufundisha kwamba
alikuwa ni mtu wa asili mbili ya kibinadamu na kimbinguni ambavyo ni kwamba
upande huu wa kibinadamu ndiyo ulikuwa Yesu Kristo na huu upande mwingine
alikuwa ni Mungu kamili na kwa hiyo kwamba alikuwa ni sawa kabisa na Mungu na
kwamba sehemu hii ya kimungu haikufa alipotundikwa pale mtini. Huu ulikuwa ni
uzushi na mafundisho haya ya kizushi ambayo yamedumu hadi leo; na Mtume Yohana
aliyashughulikia sana kuyakanusha na kuwafundisha watu ukweli kama tutakavyoone
kwenye maandiko yanayofuatia. Tutakwenda kujionea pia jinsi yalivyo mafundisho
ya Mpingakristo. Tutaona kuwa mafundisho ya utatu ni mwendelezo wa mafundisho
mbalimbali ya yanayojigeuzageuza sura yake tu ya Mpingakristo. Dhana ya
Umamboleo na ya kimitindo ni fundisho linguine linalobadilikabadilika tu la huyuhuyu
Mpingakristo. Kwa vyovyote vile, dhana na imani ya Utatu ni mafundisho ya
Mpingakristo nah ii ndiyo sababu kubwa inayotufanya tutoe mwito wa kutoka ndani
yake.
1Yohana 1:1-10 Lile lililokuwako tangu mwanzo,
tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu
ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima; 2 (na
uzima huo ulidhihirika, nasi tumeona, tena twashuhudia, na kuwahubiri ninyi ule
uzima wa milele, uliokuwa kwa Baba, ukadhihirika kwetu); 3 hilo
tuliloliona na kulisikia, twawahubiri na ninyi; ili nanyi pia mpate
kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake
Yesu Kristo.
Ukweli huo ndiyo unaoutofautisha au kuufanya
ujulikane ushirika wa wateule wake Mungu na Mwanae. Huu ndiyo umuhimu na maana
ya aya hii.
4 Na haya twayaandika, ili furaha yetu itimizwe. 5 Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kwake, na
kuihubiri kwenu, ya kwamba Mungu ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake. 6 Tukisema ya kwamba twashirikiana naye,
tena tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatuifanyi iliyo kweli;
Wakati tunapokuwa tu mali ya shirika
la kidini linaloyakumbatia mafundisho potofu ni uwongo. Sio kweli na bado
tunaenenda katika giza, na kwa hiyo hatuwezi kuwa tunatembea na Mungu. Hatupo
kwenye ushirikiano na Mungu au hatuna ushirika na Mwanae. Na ndiyo maana
hatuwezi kukaa na watu kwenye ushirika wetu, wanaoendelea kuendekeza kutembea
gizani.
7 bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika
nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha
dhambi yote. 8 Tukisema kwamba hatuna
dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. 9 Tukiziungama
dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na
kutusafisha na udhalimu wote. 10 Tukisema
kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo
mwetu.
Kwa hiyo ni wajibu na lazima kabisa
kwa wapendwa waende pamoja kwenye kweli. Hatuna fursa ya kuchagua. Ni maelekezo
ya lazima ya Roho Mtakatifu aliyotupa kupitia Yohana.
1Yohana 2:1-29 Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili
kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba,
Yesu Kristo mwenye haki, 2 naye ndiye
kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za
ulimwengu wote. 3 Na katika hili twajua ya kuwa
tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake. 4 Yeye
asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani
yake. 5 Lakini yeye
alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli.
Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake. 6 Yeye
asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama
yeye alivyoenenda.
Kristo ni wakili wetu anayetuombea na
kututete kwa Baba. Wakili ananena mambo kwa mamlaka akimwakilisha mwingine nay
eye mwenyewe hawezi kuwa ni mamlaka ya kufanya hivyo. Kwa hiyo ni wazi sana
kwamba Kristo akiwa kama wakili hawezi kuwa ni mamlaka yanayoweza kunasihi
mashitaka, au kunena kwa niaba ya watu wanaohusika. Hawezi kuwa Mungu na akawa
pia ni wakili wa kuwatetea wateule kwa Mungu kwa jinsi hii inayoonekana hapa.
7 Wapenzi, siwaandikii amri mpya, ila amri ya zamani
mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Na hiyo amri ya zamani ni neno lile mlilolisikia. 8 Tena nawaandikia amri mpya, neno lililo
kweli ndani yake na ndani yenu; kwa kuwa giza linapita na ile nuru ya kweli
imekwisha kung'aa. 9 Yeye asemaye kwamba
yumo nuruni, naye amchukia ndugu yake, yumo gizani hata sasa. 10 Yeye ampendaye ndugu yake, akaa katika
nuru, wala ndani yake hamna kikwazo. 11 Bali yeye
amchukiaye ndugu yake, yu katika giza, tena anakwenda katika giza, wala hajui aendako,
kwa sababu giza imempofusha macho.
Pendo lionyeshwalo kwa kupendana kila
mmoja na mwenzake ni ishara au alama ya mteule. Mahali ambapo kundi la watu au
kikundi kinapojikita katika kulipenda shirika lao au viongozi wao zaidi kuliko
kupendana wenyewe kwa wenyewe na kutoitilia maana kweli, ndiyo alama ya kuwa
kalti. Mahali ambapo watu wanadumu kwenye mfumo wa kiushirikiano unaohubiri
mfundisho haya ya uwongo na watu hao wakayavumilia makosa hayo na wayanapenda
sehemu au baadhi ya mafundisho au mambo yaliyo kwenye kalti na kuvumilia kwa
kujihudhurisha na kuwepo huko, basi wanakuwa ni washiriki wa uovu woe
unaofanyika hapo.
Mtume Yohana anaandika kuhusu neno la
Mungu likae kwa wingi kwenye mioyo ya wateule na kwa kufanya hivyo watamshinda
muovu.
12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa
sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake. 13 Nawaandikia
ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia
ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto,
kwa sababu mmemjua Baba. 14 Nimewaandikia
ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia
ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi
mmemshinda yule mwovu. 15 Msiipende dunia,
wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo
ndani yake.
Kwa hiyo hatuwezi kulipenda shirika
hapa duniani, vinginevyo na kumpenda Baba hakumo ndani yetu. Yatupasa kuipenda
kweli itokayo kwa Baba zaidi kuliko shirika lolote au hii dunia. Hakuna
kitakacho ingilia kati au kukwaza uhusiano wetu na Baba, yakuna hata ushusiano
wetu na Yesu Kristo. Kwa kuwa Yesu Kristo ni mmoja na Baba jambo hilo
haliwezekani kabisa kutokea. La muhimu na la kulitilia maanani kwenye uhusiano
wetu ni kuwa katika Mungu kwa njia ya Yesu Kristo na kwa ukomo wake. Ndiyo
maana Yohana anasema.
16 Maana kila kilichomo duniani, yaani,
tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba,
bali vyatokana na dunia. 17 Na dunia
inapita, pamoja na tamaa za ke, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata
milele.
Chimbuko au kiini cha upendo wa
wateule ni Baba pekeyake. Msingi wa upendo wa wateule wa kupendana wao kwa wao
ni Roho Mtakatifu aliye ndani ya kila moja wao, kutoka kwa Kristo na kuendelea
kwa wengine. Kristo alijitoa mwenyewe kwa dunia kwa kupitia upendo wa Baba. Yohana
3:16 inasema kwamba Baba alimtoa Mwana.
Yohana 3:16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda
ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali
awe na uzima wa milele. \
Ni usemi wa kawaida na uliozoeleka au
wa zamani kwenye imani ya Ukristo mkongwe, lakini ni usemi wenye nguvu sana na
unayasuta matendo yao.
Hatuwezi kutoa kile tusichokuwanacho.
Hakuna usawa kwenye karama za Mwana na Baba. Zaidi ya yote, Kristo alitumwa na
Baba yake kwa hiyari na maelekezo.
Yohana 4:34 Yesu
akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka,
nikaimalize kazi yake.
Kwa hiyo kazi ni ya Baba na yapasa
ifanywe na wateule. Ni kwa namna gani basi wateule wanaweza kubaki kwenye
shirika linalofundisha mafundisho yaliyo kinyume kabisa na sheria na ushuhuda
na huku bado wakiifanya kazi ya Baba? Kazi hiyo itakuwa na maana gani? Yohana
aliliona hilo kuwa ilikuwa ni muhimu alipoandika. Ni kwa kiasi gani basi basi
jinsi ilivyo leo? Kwa kujihudhurisha kimya kimya kwenye kalti, ambazo hata
zimekuwa kama vilabu vya burudani, uwezo wa taifa la Israeli na kutokana na wao
ulimwedgu wote mzima kufikia toba kumechelewa au kubebakia kuwa kitu
kisichowezekana.
Hata kuna maneno mengine yanayozua
mabishano makubwa sana ya uwongo na kujidanganya wanayopenda kuyatumia baadhi
ya wateule, ambayo yanasemekana kama ifuatavyo. Mimi sijabatizwa kwenye shirika lolote bali nimebatizwa
kwenye mwili wa Kristo. Kwa hiyo, mahali popote walipo wateule naweza kuwapo na
kujiunganano bila kujali kile linachofundisha shirika hilo.
Watu wanaosema wao si washirika au
wanachama wa shirika lolote bali wao ni wa mwili wa Kristo tu, na huku
wakibakia bado kwenye imani za kalti zinazofundisha kinyume na torati na
ushuhuda, wanafanya kazi ya Shetani. Wanakuwa ni kikwazo na kukanganya uwezo wa
wateule wa kuihubi kweli. Wanajidanganya wenyewe kwa malumbano yaliyofanywa ili
kuepuka ukweli yaliyoanzishwa kwa lengo la kuchelewesha maamuzi yasiyo muafaka.
Kwa ufupi, wao ni waoga. Wametumwa na Kristo ili wawe kama kondoo kati ya mbwa
mwitu ili wafanye kazi yao ya uvunaji. Kwa kuwepo kwao kwenye mashirika
yaliyokengeuka, ambayo kwa ufafanuzi ni pamoja na mashirika yoyote ya waamini
Utatu, hawa hawaifanyika kabisa kazi ya Baba. Wanakinza na kukwaza wito wa
wateule. Kwa ufupi ni kwamba watu hawa wameichimbia ili kuizika talanta yao
designed to delay uncomfortable decisions.
Taifa hili linapaswa kuitwa watubu na
watendakazi ni wachache.
18 Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile
mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi
wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho. 19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu.
Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili
wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu. 20 Nanyi mmepakwa mafuta na
Yeye aliye Mtakatifu nanyi mnajua nyote. 21 Sikuwaandikia
ninyi kwa sababu hamwijui iliyo kweli, bali kwa sababu mwaijua, tena kwamba hapana
uongo wo wote utokao katika hiyo kweli.
Hivi ndivyo walivyotumwa na kupelekwa.
Walianza kuhubiri uwongo. Haijalishi idadi yoyote waliyonayo. Haijalishi kama
wanatushurutisha kujiunga na kuanzisha tena. Walikuwa na idadi kubwa tayari
tangu kipindi cha Mtaguso wa Nikea. Kwa kweli, tangu mwaka 381 ulipoitishwa
Mtaguso wa Constantinople wao walishakuwa na idadi kubwa ya wafuasi tayari.
Lakini uwingi wa idadi yao hauwezi kuwafanya wawe ni sehemu ya mwili. Wanapata
uwezo mkubwa wa kutoka nje na kuyafikia mataifa mengi kwa kuwa wanafundisha
uwongo. Ni kwa hii kweli ndiyo inayotufanya tuwe kwenye mwili wa Yesu Kristo na
kujumuika kwetu na watu wenye mtazamo na nia inayofanana ndiko kunakotuwezesha
sisi tubakie kwenye Yesu Kristo, tukiifanya kazi ya Yesu Kristo. Kama tutaacha
kuitenda kazi ya Yesu Kristo, tukiuhuisha mwili wa Yesu Kristo, vinginevyo
hatutakuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu.
22 Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya
kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana. 23 Kila amkanaye Mwana, hanaye Baba;
amkiriye Mwana anaye Baba pia.
Tutawezaje basi kumkiri huyu Mwana
tukiwa tunasema kuwa wao ni viumbe jumuisho, walioungana pamoja na kuwa kiumbe
mmoja, na Mungu mmoja; na kwamba wao ni udhihirisho tu wa kitu kimoja.
Tunamkana Mwana na kwa kufanya kwetu hivyo tunakuwa hatuna Baba kwa maana
tunamkana pia. Haya ni mafundisho ya Mpingakristo.
24 Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo
na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu,
ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba. 25 Na
hii ndiyo ahadi aliyotuahidia, yaani, uzima wa milele. 26 Nimewaandikia
haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza. 27 Nanyi,
mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu
kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote,
tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake. 28 Na sasa, watoto wadogo, kaeni ndani yake,
ili kusudi, atakapofunuliwa, mwe na ujasiri, wala msiaibike mbele zake katika
kuja kwake. 29 Kama
mkijua ya kuwa yeye ni mwenye haki, jueni ya kuwa kila atendaye haki amezaliwa
na yeye
Hapa dhana ya kutoka na kwenda kutoka
kwetu inaendelezwa na Mtume Yohana. Mafundisho yaliyoyafundisha na kuyaendelea
Kanisani Mtume Yohana hayakuwa yanahusu mambo ya Uungu kabisa ayakuhusiana
kuhusu uhusiano uliopo kati ya Baba na Mwana. Malumbao haya yalikuwa ni mwanzo
au uanzishwaji wa imani ya Utatu. Yalijaribu kutenganisha nasaba ya ubinadamu
wa Kristo na uungu. Zaidi ya hayo ilijaribu kumfana Kristo kuwa ni sehemu ya
Mungu na kuwa yu sawa naye. Haya ni mafundisho la Mpingakristo. Ilikuwa ni kuhusianisha
kwa wazi na imani ya Utatu ambao maandiko ya 1Yohana 4:1-2 yalibadilishwa ili
kupindisha na kupotosha ukweli. Jaribio la kuwa ni sehemu ya mteule ni kwa
mwenendo wa haki, yeye atendaye haki ni mtakatifu.
.
Yeyete atendaye dhambi ni wa ibilisi (diabolos).
Kwa hiyo haiwezekani kuwa sehemu ya mshirika kwenye shirika ambalo haliihubiri
kweli. Kwa kuwa amri ya Mungu ni ya muhimu sana. Dhambi maana yake ni kile
kitendo cha kuvunja amri au kwa hapa ni ukengeufu. Amri ya kwanza inakusiana na
jinsi ya kumuabudu na kumpenda Mungu. Tutawezaje kumuabudu Mungu Mmoja, wa
Pekee na wa Kweli ikiwa kama tuko sehemu ya imani ya wale wanaojaribu
kumshutumu Kristo kwa kujaribu kujaribu kumlinganisha kuwa sawa na Mungu wa
Pekee na wa Kweli na kuwa kwenye mkumbo wa kutenda dhambi hiyohiyo ambayo
Shetani aliifanya? Kwa hiyo inatupasa kujitakasa kama Kristo alivyo mtakatifu.
Tutawezaje kujitakasa sisi wenyewe huku tukiwa kwenye ushirika wa klabu ya
starehe? Tunawezaje kumtumikia Mungu na kumtolea zama zetu Baali?
1Yohana 3:1-24 Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa
Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui,
kwa kuwa haukumtambua yeye. 2 Wapenzi, sasa
tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa
atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. 3 Na kila mwenye matumaini haya katika yeye
hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu. 4 Kila
atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi. 5 Nanyi
mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani
yake. 6 Kila akaaye ndani
yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua. 7 Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye;
atendaye haki yuna haki, kama yeye alivyo na haki; 8 atendaye
dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi
hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. 9 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi
dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa
sababu amezaliwa kutokana na Mungu.
Huu ni usemi wa maana sana. Tunatenda
dhambi wakati wote. Ni tabia na sili ya Mungu ndiyo inayotushuhudia dhambi
zetu. Tunajua kuwa wakati tunapofikiria kitu kibaya kwa ajili ya asili yetu ya
uasi kwa yale tunayoyafanya na dhamira zetu (Roho Mtakatifu) ikitukataza
ikisema hapana, hapana, hapana, hivi sio vizuri. Tunasujisikia kusutwa na
dhamiri kwa kuwa tumetenda dhambi. Si kwamba hatuwezi kutenda dhambi tunaweza
kupitiliza ushuhuda ule lakini tunayajua yale tunayoyatenda na tunajitenga sisi
wenyewe mbali na Mungu kujitenga mbali na wateule kwa ajili ya dhambi, na
inatupasa kutubu. Dhambi zinazorudiwa rudiwa haziwezi kutuwekwa mahalia pa
kuwezesha kwa kuwa hatuwezi kumfanya Kristo ayarudie mateso ya kusulibiwa mara
ya pili tena.
10 Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na
watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye
asiyempenda ndugu yake. \
Kwa hiyo tuna mambo mawili
tuliyoagizwa – la kwanza ni kuwapenda ndugu zetu na matendo mengine yaliyo mema
na hak. Kile kilicho sahihi na haki kipo wazi sana na kinashughulikiwa na
torati au sheria. Hatupaswi kuwa kwenye shirika lililokengeuka.
Iwapo kama tutakuwa hatutendi mema
ndipo tutakuwa si wa Mungu. Hatutaonyesha kuwa tunawapenda watu kama hatutaweza
kulihubiri neno la Mungu kwao kwa kweli isiyo na michanganyo au kughoshiwa.
Hatuwezi kumtumikia Mungu na huku
tukiyanena mambo yaliyo nje ya midomo yetu. Sio jambo gumu kusema
yeye aliye na sikio na asikie. Kweli
itakayohubiriwa nyakati za mwisho yapasa ihubiriwe kwa wazi kwa wateule na
ihubiriwe kwa taifa kwa maneno ya wazi. Kufikiri kinyume chake au vinginevyo ni
kujidanganya wenyewe. Vipawa na wito wa Mungu hautolewi ili kuburudisha mikaka
ya kwenye vilabu vya starehe au kwa ajili ya mashindano ya kujipatia
umashuhuri.
11 Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo,
kwamba tupendane sisi kwa sisi; 12
si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake. Naye
alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu
yake yalikuwa ya haki. 13 Ndugu zangu, msistaajabu, ulimwengu ukiwachukia. 14 Sisi tunajua ya kuwa tumepita toka mautini kuingia
uzimani, kwa maana twawapenda ndugu. Yeye asiyependa, akaa katika mauti. 15 Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya
kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake. 16 Katika
hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu;
imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu. 17 Lakini
mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia
huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa
ulimi, bali kwa tendo na kweli. 19 Katika hili
tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, nasi tutaituliza mioyo yetu mbele zake, 20 ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu
kuliko mioyo yetu naye anajua yote. 21 Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu,
tuna ujasiri kwa Mungu; 22 na lo lote tuombalo,
twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo
machoni pake. 23
Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu
Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri. 24 Naye
azishikaye amri zake hukaa ndani yake yeye naye ndani yake. Na katika hili
tunajua ya kuwa anakaa ndani yetu, kwa huyo Roho aliyetupa.
Mungu yu tofauti na Mwanae kwa maana
kwamba ni viumbe wawili tofauti, Mungu tunayezishika amri zake na kutembea
kwenye kweli yake. Kitendo cha kutembea kwenye kweli akiwezi kufikiwa kwa
kunyamaza kimya ndani ma mashirika au madhehebu yaliyoanguka kiimani na
kukengeuka. Kwa kunyamaza kimya tutakuwa tunamkana Kristo kabisa. Udhaifu kama
huo alikuwanao Mtume Petro alipokuwa kabla hajaongoka. Hata hivyo, si jambo
linalokubalika kwa wateule.
Wakati Petro alipomkana Kristo alikuwa
hajaongoka bado. Alikuwa kwenye fursa ndogo kuliko sisi na wateule wote tulivyo.
Wala hakutarajiwa kuwa atakuwa imara; kwa kuwa alikuwa hajaongoka. Tunahukumiwa
kwa kiwango cha juu kuliko alivyokuwa Petro wakati ule alipokuwa anasulibiwa
Yesu Kristo. Hili ni jambo mhimu sana kufanyika. Kuwa sehemu ya wateule wa
Mungu si jambo la mzaha.
Wateule wajnatakiwa ili kuijaribu au
kuipima roho ili kuona kama ni za Mungu. Kama kuna mtu yeyote akituambia sisi
kwamba Kristo ni Mungu na yuko sawa na wanahali sawa na Mungu wa Pekee wa
Kweli, ndipo tutajua kuwa si Roho wa Mungu. Wateule wanapaswa kujitenganao.
Watu hawa wanatoka kwetu kwa kile wanachosema, kinyume na wanavyoketi. Ukweli
ni kwamba hali hii ua ukengeufu kushika hatamu za maongozi haiwezi kubadili
hali na kuwafanya wao kuwa ni watu wa Mungu, na wala kwamba wanastahili
kujumika au kusaidiwa na wateule. Kwa kweli, kinyume cha hapo ndilo hali halisi
yenyewe. Wao kwa matendo yao wamekwishajitoa tayari kwetu ili waonyeshe kwamba
hawakuwa wa kwetu kabisa. Kitendo cha kuwatenga watu wenye mafundisho haya mapotofu hakumaanishi kuwa
hawa walliotengwa hawapendwi au wanachukiwa, la. Bali wale ambao Mungu
anawapenda anawakemea na kuwarudi. Mara nyingi kitendo hiki cha kukemea
kinafanywa kwa wale walioimara kiroho na kwenye neno la Mungu.
1Yohana 4:1-21 Wapenzi,
msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa
sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. 2 Katika
hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika
mwili yatokana na Mungu. 3 Na kila roho
isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo
mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.
Kwenye kipindi cha Yohana, roho hii ya
Mpingakristo ilijaribu kusema kuwa sehemu ya mwili wa Yesu Kristo haikuwa
kwenye hali ya kimwili, bali ilibakia kuwa kule juu kwa hali yake. Roho ile
ingali bado ipo leo na ni sehemu ya imani na mfumo au utawala wa mwanamke
kahaba. Ni sehemu ya dini potofu. Ni fundisho la Mpigakristo.
Andiko hili kuhusu mafundisho ya Mpingakristo
limekuwa likibadilishwa kwenye maandiko ya kale. Hili ni moja ya maandiko ya
kwanza waliyoyageuza na kuyapotosha kwa kuyaghushi kwa kuwa andiko hili ndilo
linatuambia sisi kwamba mafundisho ya Utatu yanatokana na mafundisho ya
Mpingakristo, kwa hiyo iliwalazimu kubadilisha uandishi wa aya na andiko hili.
Andiko sahihi linaweza kuonekana kwenye uhalisia aliouandika mwandishi
mashuhuri aitwaye Irenaeus (soma kitabu chake cha the Ante-Nicene Fathers, Vol 1, fn. p. 443).
Andiko hili linasomeka hivi:
Katika hili mwamjua
Roho wa Mungu; Na kila roho inayomkiri Yesu Kristo kuwa ametokana na mwili hi ya
Mungu; na kila roho inayomtenganisha Yesu Kristo siyo ya Mungu bal ni ya Mpinga
Kristo.
Mwanahistoria mashuhuri Socrates
anasema (VII, 32 p. 381) kwamba ayah ii au kifungu hiki kimepotoshwa na wale
waliokusudia kuitenganisha nasaba ya
kimwili ya Yesu Kristo na uungu wake. Kwa hiyo madai yanayosema kuwa Kristo
alikuwa sehemu moja na nasaba ya mbinguni akiwa kama sehemu ya Mungu, mbali na
ubinadamu wake na kifo chake pale msalabani, unapingana kabisa na kukanusha
ufufuo wan a mafundisho ya Mpingakristo. Kwa hiyo imani ya Utatu yanaangukia
wazi sana kuwa ya Mpingaktisto.
4 Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi
mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika
dunia. 5 Hao ni wa dunia; kwa
hiyo wanena ya dunia na dunia huwasikia. 6 Sisi twatokana na Mungu. Yeye
amjuaye Mungu atusikia; yeye asiyetokana na Mungu hatusikii. Katika hili
twamjua Roho wa kweli, na roho ya upotevu.
Kwa hiyo, roho wa kweli anahitajika
kumtenganisha kutokana na roho wa upotevu. Jaribu hili kwa wateule ili
kuwaonyesha jinsi walivyo na ni nani hasa walio wateule na walioitwa na siyo kuchaguliwa.
7 Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa
Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. 8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana
Mungu ni upendo. 9 Katika hili pendo la
Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili
tupate uzima kwa yeye. 10 Hili ndilo pendo, si
kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma
Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. 11 Wapenzi
ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana. 12 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo
wote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani
yetu. 13 Katika hili
tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu, kwa kuwa
ametushirikisha Roho wake. 14 Na sisi
tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu. 15 Kila akiriye ya kuwa Yesu ni Mwana wa
Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu. 16 Nasi
tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo,
naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake. 17 Katika hili pendo limekamilishwa kwetu,
ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo
tulivyo na sisi ulimwenguni humu. 18 Katika pendo
hamna hofu; lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa maana hofu ina
adhabu; na mwenye hofu hakukamilishwa katika pendo.
Kama tunatishika kuhusu kama shirika
ni mali ya kile kinachoitwa mashirika ili kuimarisha mahala petu, na kuogopa
kile kinacho kuhusu kuamua kwenda kwa usalama, na kukiogopa kle kiachokwenda
kutokeza duniani na mateso na dhana kwamba tunaweza kujiepusha nacho, kwa hiyo
hatuwezi kuwa na upendo kamili na hatufikiri vizuri sana. Hatumwangalii au
kumtegemea Mungu.
19 Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda
sisi kwanza. 20 Mtu akisema,
Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda
ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. 21 Na amri hii tumepewa na yeye, ya
kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.
Wale walio na upendo kamili hawaogopi
tena, wakiwaacha peke yao wale dhambini na kukosea kikimya kimya na wakibakia
bado kwenye shirika hilo. Mtu anaweza tu kuwa mshirika wa kalti na siwe tena
kuwa sehemu ya mwili wa Kristo.
Vigezo
vya kuushinda ulimwengu vimeelezwa wazi kwenye 1Yohana 5:1-5.
1Yohana
5:1-21 Kila mtu aaminiye
kwamba Yesu ni Kristo amezaliwa na Mungu. Na kila mtu ampendaye mwenye kuzaa,
ampenda hata yeye aliyezaliwa na yeye. 2 Katika
hili twajua kwamba twawapenda watoto wa Mungu, tumpendapo Mungu, na kuzishika
amri zake. 3 Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu,
kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito. 4 Kwa
maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko
kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. 5 Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani,
isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu?
Kama tunampenda Mungu tutazishika amri
zake. Kwa hili tunajua kuwa tunawapenda watoto wa Mungu. Tunapozaliwa katika
Mungu yatupasa kuushinda ulimwengu. Kuushinda ulimwengu yatupasa kuamini kuwa
Masihi ni Mwana wa Mungu. Kwa hiyo uhusiano ni muhimu. Hali ya udanganyifu
inayotafuta kutokuwa na haja au uhitaji huu unaoonekana miongoni mwa waamini Utatu
unakutikana kwenye ubadilishaji au upotoshaji uliofanywa kwenye maandiko ya
biblia, au kwenye tafsiri yao potofu mbali na maana iliyowazi ya maneno kama
tunavyoona hapo chini (hasa hasa kwenye 1Yohana 5:7. Linganisha na hapo chini
na maandiko yaliyopotoshwa kwenye tafsiri ya KJV).
6 Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu
Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu. 7 Naye
Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli. 8 Kwa
maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na
watatu hawa ni umoja. 9 Kisha wako watatu
washuhudiao duniani], Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa
habari moja. Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi;
kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe. 10 Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani
yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo
ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe. 11 Na
huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo
katika Mwanawe. 12 Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima;
asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima.
Kumbuka kuwa Mungu alitupa sisi uzima
wa milele na uzima huu umo hatika mwanae. Kwa hiyo mwana ana uzima wa milele
kutoka kwa Baba, ambao tumepewa pia sisi kwa namna hiyohiyo.
13 Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue
ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu. 14 Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba
kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. 15 Na
kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja
tulizomwomba. 16 Mtu akimwona ndugu yake anatenda dhambi
isiyo ya mauti, ataomba, na Mungu atampa uzima kwa ajili ya hao watendao dhambi
isiyo ya mauti. Iko dhambi iliyo ya mauti. Sisemi ya kwamba ataomba kwa ajili
ya hiyo. 17 Kila lisilo la haki ni dhambi, na dhambi
iko isiyo ya mauti. 18 Twajua ya kuwa kila
mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu
hujilinda, wala yule mwovu hamgusi. 19 Twajua ya kuwa sisi
tu wa Mungu; na dunia yote pia hukaa katika yule mwovu. 20 Nasi
twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue
yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya
Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele. 21 Watoto wadogo, jilindeni nafsi zenu na sanamu.
Dhana hii hapa kuhusu dhambi ya mauti
imechukuliwa na Wakatoliki kwenye imani au dhana ya kuwa na dhambi ya mauti nay
a milele. Kle Yohana anachojaribu kukitofautisha hapa ni kwamba mchakato wa
kufikia ukamilifu wa wateule ni lazima upitie kwenye makosa ya kimaisha ya siku
hadi siku. Makosa hayo ni sehemu ya ushindi wetu. Tunatenda dhambi kila siku. Dhambi
ya mauti kwa mtazamo huu (ni dhambi ile itakayomfanya mtu asiwe na sehemu
kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu bali awe kwenye ufufuo wa pili) ni wakati
tunapotenda dhambi kwa kiwango ambacho mwili wa Kristo, kwa kupitia wazee,
waseme kwamba hatuwezi tena kabisa kuhukumu na inaturudisha duniani ili kwamba
tunatolewa kwa adui, ili kwamba maisha yetu yaokolewe katika siku za mwisho.
Tunarudishwa nyuma kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Hiki ndicho kilichotokea
kwenye 1Wakorintho 5:5. Tunapokuwa tunatenda dhambi kwa makusudi ndipo
tunakwenda kwenye dhambi aa mauti ambazo hatuwezi kuzishinda na zinaturudisha
nyuma duniani. Kwa hiyo tunaondolewa kwenye hukumu. Ni kwa rehema zake.
Kwa hiyo wateule wapo chini ya hukumu
kwa kile wanachokitenda, kunena na kuwaza. Matendo yao yanapimwa kila wakati na
Roho Mtakatifu. Kitendo cha kujiunga kwa wateule kwenye makundi la watu
yanayotenda na kuenenda kinyume na Maandiko Matakatifu yanamfanya mteule awe
hukumuni. Kwa hiyo mteule hapaswi kuwa mashirika wa vikundi vya imani hizi
potofu za kikalti vinavyofuata na kutenda mambo yanayopangwa na wanadamu hata
yakiwa ni kinyme au yanapingana kabisa na Maandiko Matakatifu na kweli yake.
Tunapojiunga kwenye shirika au kanisa
linalofundisha na kuzihalifu sheria za Mungu, tunajiweka wenyewe kwenye hukumu.
Hakuna tofauti kati ya kuwa kwenye shirika au kanisa linaloivunja amri ya
kwanza na kuwa mwanachama wa kanisa linaloivunja amri ya saba, au ya nane, au
ya tisa. Hakuna tofauti kati ya kuwa mshirika wa kikundi cha kalti ya kidini
kinachoabudu miungu wa uwongo na kuwa mshirika au mhusika wa waliofanya
mashambulizi ya mauaji, au kuwa kwenye kundi la waporaji na wanyang’anyi, au
kuwa kwenye kundi la wazinzi. Wote hawa ni wanachama wa kalti na ni wavunjaji
wa Amri ya Kumi na wote hawatakuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu
bali ni hadi ule wa pili wa hukumu ili wahukumiwe.
Kuna mchakato wa udhanganyifu na
upotofu unaowashinda na kuwaangusha watu walio kwenye imani hizi za kalti,
ambao unawafanya wasiijali kweli na kuipuuzia. Ni kama tulivyoona, kwamba kalti
ni kundi la waamini wanaoongozwa kwa kufuata mawazo ya watu na mapokeo ya
taratibu za kidini na hawajali kulisikiliza neno la Mungu
Mungu anachukiwa sana na kuwashutumu
kwa matendo haya kwenye Isaya 66:4
Isaya
66:4 Mimi nami nitachagua
mapigo yao, nitaleta hofu zao juu yao; kwa sababu nilipoita, hawakuitika; na
niliponena, hawakusikia; bali walifanya yaliyo maovu machoni pangu, na
kuyachagua nisiyoyafurahia.
Neno hili lililotafsiriwa kuwa maovu hapa linamaana hasa ya uchokozi au
ukali au mateso kama lilivyo kwenye yafsiri ya RSV.
Kuchagua kutomfuata na kumuasi Mungu
kutampelekea Mungu kuchagua kututesa. Mateso haya yameorodheshwa kama
kutangatanga kwa ajili ya makosa kwenye 2Wathesalonike 2:11.
2Wathesalonike
2:9-10 yule ambaye kuja
kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu
za uongo; 10 na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa
hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.
Mtu wa kuasi anaweza kutokea tu kutoka
kwa wateule kwa kuwa washirika wanaotangatanga na kudai kuwa ni mwili wa Kristo
kwenye nyakati za mwisho hawatakuwa sehemu ya wateule. Hawataipenda kweli ili
waokolewe. Watatumiwa nguvu ya upotevu na Mungu.
2Wathesalonike 2:11 Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu,
wauamini uongo;
Neno hili lililotafsiriwa nguvu ya upotevu kwa kweli imekwishaanza kufanya kazi yake ya kuwapotosha
watu (energeian planes, soma kitabu
cha Marshall's Interlinear). Walipewa nguvu za kimkakati za kutenda kazi ya
kupotosha na Mungu kwa kuwa hawakuipenda kweli, ili wasiingie hukumuni, kwa
kuwa hawakuokolewa.
Kama tunawafuata wanadamu na mapokeo
yao kuliko kuipenda kweli, hatuaweza kuokolewa hakika. Haitakuwa wazi
sana.
Makanisa kwenye vuguvugu la kipindi
cha karne ya ishirini yaliyazifanya dini kama biashara na kuyafanya mafundisho
kuwa ni kama kitu cha kuwavutia tu wateja. Hii kwa kweli ilikuwa ni mtindo
lilioufanya kanisa la Rumi kwenye kipindi chake cha karne ya nne na Ukristo uliharibiwa
kwa sababu ya mtindo huu, kama ulivyo mfumo wa imani kongwe za kale.
Mkakati huu wa udanganyifu au mbinu za
kiulaghai, unapelekea kuwepo kwa ongezeko la aina ya malumbano kwenye kitabu
cha ufafanuzi maarufu kama kitabu cha ufafanuzi wa Biblia cha G.L. Haydock,
[yaani the G.L. Haydock, to the Douay-Rheims Bible (1850 reprint of the 1819
version)], kuhusu Yohana 17:3.
Aya ya
3. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu
wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. [Kwa maneno haya Waariani wamejifanya kuamini
kuwa Baba peke yake ndiye Mungu wa Pekee na wa Kweli].
S Aug. and diverse others answer, that the sense and construction is, Wakujue wewe, na pia Yesu Kristo Mwanao ili
awe Mungu wa Pekee na wa Kweli We may also expound them with S. Chrys. and
others, so that the Father is here called the only true God, not to
exclude the Son, and the Holy Ghost, who are the same one true God with the
Father; but only to exclude the false God's of the Gentiles. Let the Socinians
take notice that (1John v, 20), the Son of God, Christ Jesus, is expressly
called the true God, even with the Greek article, upon which they
commonly lay so much stress.
Marfa tu tunapofika kwenye uharibifu wa
hii kweli, ndipo tutaamili kila kitu. Kumbuka pia matumizi mabaya ya lebo
bandia, kama vile ya Arian, kutafuta ku-obviate au kukataa uhalali wa imani ya
Uyunitariani iliyo kwenye Biblia. Hakuna uwezekano kwamba Mungu wa Pekee na wa
Kweli aliyetajwa kwene Yohana 17:3 au 1Yohana 5:20 haimtaja Yesu Kristo kabisa
wala kumaanisha yeye, ndani ay nje ya kifungu hiki. Ukweli wa kwamba tafsiri wa
toleo la Douay-Rheims ni tafsiri ya Kiyunani ya Vulgate na kwa hiyo makala
imetoholewa kutoka kwenye lugha ya Kilatini haikutajwa. Neno na makala
havimtaji wala kumaanisha Kristo, bali zaidi tu ni kwa Mungu wa Pekee na wa
Kweli ambaye Mwana wake ni Kristo. Ni muhimu kwa waamini Utatu kusalia kwenye
udanganyifu kama huu ili kurekebisha nafasi yao machoni pa maandiko. hili si
jambo jipya.
1Yohana 5:20 Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu
amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo
ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu
ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele.
Yeye aliye wa kweli ni yeye Mungu wa
Pekee na wa Kweli. Tunamjua nasi tu ndani yake, yeye aliye wa kweli na katika
Mwanawe Yesu Kristo.
Enyi watoto wadogo, hebu jiepusheni na
kujilinda na ibada za sanamu; zile za wanadamu na za mapepo na acheni uwongo na
udanganyifu wa imani hizi potofu za kikalti. Tikeni kati yake, enyi watu wangu
(Ufunuo 18:4)
Ufunuo
18:4 Kisha nikasikia sauti
nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki
dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.
Huyu mwanamke kahaba aliyetajwa na
kufananishwa kama Babeli Mkuu, Mama wa Makahaba na Machukizo ya Nchi ni
kiongozi wa imani na mfumo wa dini hii potofu ya ulimwenguni. Utaratibu na
mfumo huu umekuwa ukijulikana kuwa msingi wake ni kwenye dini potofu ya uwongo
ya mungu wa Utatu kwa kipindi cha karibu zaidi ya miaka elfu mbili. Kwa kipindi
chote hiki wateule hawajawahi kuikubalia wala kushirikanaina dini hii. Wito
uliotolewa ni wa kutoka ndani yake ili kwamba wateule wasishiriki mapigo na
maafa yake makubwa ambayo yatamiminwa juu ya waamini Utatu na dini yao potofu
katika siku za mwisho – mabinti makahaba wa huyu mwanamke kahaba ni wale
waliojiengua katika kipindi kilichojulikana kama cha Wanamatengenezo. Watumishi
hawa hawa walianza kwa kufundisha kinyume na imani na mfumo huu hapo mwanzoni.
Ila sasa wanafundisha mafundisho haya Utatu na kusisitiza kuhusu fedha na mali;
hawapo miongoni mwetu sisi. Hebu na tuwahubirie na kutoka kwenye mifumo
na imani yao.
q