Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[043]

 

 

 

 

Mbinu za Ibilisi

(Toleo La 2.0 19940723-19991006)

 

Misuguano iliyo kati ya nguvu za kimaandiko ambazo Kanisa linakabiliana nazo zimeelezewa. Aina ya mitindo ya Kishetani au uwongo wa kiuhalalisho ambavyo vinazidi kuongezeka na kuzidi kuidharau au kuipuuza Imani kumeelezewa kwa mtazamo wa kibiblia.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © Christian Churches of God 1994, (ed. 1997), 1999 Wade Cox)

 (tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Mbinu za Ibilisi


 


Utangulizi

Kwenye Agano Jipya maana kadhaa mbalimbali zimeonekana tena na tena. Moja ya maana hizo ambazo zinavutia mawazo kwa kiasi kikubwa sana na maandishi ya waandishi ambao kazi zao zimehifadhiwa kwenye Agano Jipya, ni zile zinazosisitiza kuwa Wakristo tumo vitani dhidi ya nguvu za kiroho. Kuna vita ya kweli na yenye nguvu sana inayofanyika hapa duniani leo. Imejulikana kuwa ni kati ya majeshi ya ulimwengu wa nuru na kweli na ule wa giza na upotevu.

 

Hata hivyo, uwanja wa mapambano wa vita hivi sio wa kimwili—ambavyo ni kwamba, sio kati ya uthibiti na umiliki wa kipande chochote cha eneo au ardhi ya dunia hii—wala si ya wakati huu. Bali uwanja wa mapambano uko kwenye mawazo ya mwanadamu na moyoni mwake—akilini mwake na hisia za mwanadamu.

 

Silaha inayotumika kwenye vita hii inajiri kwa kuzunguka mawazoni, mifumo ya mawazo, mitazamo na misimamo. Kwa upande mmoja ni adui-nguvu za giza – Shetani, mapepo yake na roho zake mbaya na potofu. Wanaohusishwa pia kwenye vita hivi ni Wakristo. Ingawaje ushindi wote unaotakiwa kwenye vita hii umekwisha patikana kwa kushinda kwake Kristo na wimbi la kihistoria limeshageuka kabisa kwa kuyashindia majeshi ya upande wa nuru, bali bado kuna vita ndogondogo vinavyopiganwa kwenye maisha ya Wakristo mmoja mmoja. Hii imekuwa ni hali iliyojiri tangia siku za ushindi mkuu na wa muhimu sana wa Kristo na vitaendelea kuwa hivyohivyo hadi atakaporudi tena.

 

Kila mmoja wetu aanatakiwa awe vitani kila siku. Tumeandaliwa tayari kwa kazi yetu kwa Roho wa Mungu – Roho wa upendo, nguvu na utimamu – na Biblia, ambayo ni upanga war oho na mkali kuliko upanga ukatao kuwili. Kama tutajikwa mapiganoni, kapteni wetu tunaye ili kutusaidia na kutupa nguvu na uweza, ila bado tunayo sehemu yetu kwene vita hivi.

 

Uwanja wa mapigano ni miyo yetu – vile tunavyovifikiri na kuamini na mawazo tunayoyadhania kuwa ya kweli na kuyatumainia mawazoni mwetu – na hisia zetu na misimamo yetu yanayotusukuma kutenda kwa kile tunachokiamini.

 

Sasa, kapteni wa upande wa upinzani, Shetani, ana mbinu zote za kudanganya na za ujanja. side, yeye ni bwana wa mbinu na mikakati. Lengo lake ni kuleha maangamizi ya uimara wa kiroho. Hataacha hata siku moja kupigana nasi au kutupinga. Anaujua kila mchezo, na mbinu za kivita na jinsi ya kufanikisha kuliko tuuavyo sisi. Anajua sana na atatumia kila mbinu chafu kenye kitabu na kila mbinu chafu zisizo kwenye kitabu ili atushinde. Yeye ni muongo na mkatili na wala hana huruma kwenye utendaji wake na mwenendo wake. Yeye yu zaidi ya mwanadamu kwenye nguvu zake za udanganyifu:

Ufunuo 12:9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.

 

1Yohana 5:19 Twajua ya kuwa sisi tu wa Mungu; na dunia yote pia hukaa katika yule mwovu.

 

2Wakorintho 4:3-4 Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; 4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.

 

Waefeso 2:1-2 Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; 2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;

 

Wakristo wameonywa kwenye maeneo kadhaa ya starehe kwenye matendo ya Kishetani. Kuridhika ni kutilia chumvi fulani kwa maanguko au maafa na kushindwa kiroho:

1Petro 5:8 Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.

 

2Wakorintho 11:3 Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.

 

1Wakorintho 10-12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.

 

Waebrania 2:1 Kwa hiyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa. 

 

Mithali 4:23 Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.

 

Sasa, kama ilivyoelezwa, ni kwamba moja ya silaha zetu ni Neno la Mungu. Ndani yake tunapata mbinu muhimu ya jinsi adui wetu anavyotenda kazi:

2Wakorintho 2:11 [Yatupasa kuwa tayari kusamehe] Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.

 

Mitindo na mbunu hizi zimeenea kila mahali:

1Timotheo 4:1 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;

 

Waefeso 2:1-2 Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; 2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;

 

Shetani, ingawa mapepo wake wanaeneza na kusambaza mafundisho mengi au mkakati wa mtandao wa mafundisho ya uwongo, nadharia za uwongo na fikra potofu ambazo zinaweza kutupotosha hata sisi kama hatutakuwa makini na kuyaamini na hatimaye kuyatendea kazi. Zaidi sana, ni kama ilivyoelezewa na kufafanuliwa mara nyingi huko nyuma, ni kwamba Shetani anatangaza misimamo yake pia na kuwazoa au kuwapotosha watu kwa namna hiyo.

 

Tutajifunza kuhusu maneno na maelezo haya na masemezano yatokanayo na hila za Shetani kwenye Biblia. Kwenye maneno haya, Shetani anadhihirisha mabo yahusuyo mikakati ya vita vyake na, hasahasa anajilaumu mwenyewe kwa mdomo wake. Kwa kuyasoma maneno haya, tunapata hekima na busara kuhusu elimu yake ya mpangilio na upotoshaji wake lakini ni njia ya kjanja ya kufanya udanganyifu. Kwa kuyajua mambo haya tutakuwa tumeandaliwa vizuri kukabiliana naye pamoja na mawakala wake wa giza, hasa wakati tunapokabiliana nao kwenye vita vyetu vya kila siku vya maisha ya Kikristo.

 

"Mungu hakupendi"

Inasemekana kwamba Shetani anatumia “karibu na ukweli” wenye kiingia akilini na kukubalika ili kuwapata watu wenye kupenda kudadisi. Kazi yake kubwa saba haifanyi kwenye makasino, au kwenye mabaa au kwenye ufunguaji vifungo. Zinafanyika kwenye mawazo ya mwanadamu. Yeye ni mwaribifu na mpotoshaji wa kweli. Yeye ni muongo tangu mwanzoni. Yeye ni “msukumaji” –sio wa kuwasukumia watu kwenye mihadarati peke yake. Anaiamsha hamu na uteja wa kusema uwongo. Tunaouona uwongo wake kwenye sura za wazi za uwepo wa mwanadamu hapa duniani kwenye Mwanzo 3. Shetani alimsogelea Hawa kwa umbo la nyoka na kuanza kumshambulia.

Mwanzo 3:1 Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?

 

Hapa Shetani anatia mashaka kwa kile alichokisema Mungu alipomwelekeza Adamu. Hapo mwanzoni Mungu alisema:

Mwanzo 2:16-17 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, 17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.

 

Shetani anafanya mbinu zote kuligeuza neno hili na kuonyesha kuwa awaambia Adamu na Hawa kuwa wasile tunda lolote kwenye miti yote iliyokuwa kwenye bustani. Biblia inasomeka ikisema hivi:

Mwanzo 3:14 Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;

 

Alichikifana Shetani hapa kilikuwa ni sio ujanja, bali alitia mashaka kwa maagizo na maaelekezo ya Mungu aliyomwambia Adanu hapo kwanza. Alichokuwa akikifanya kwa kweli ni kumwekeza wazo baya na upotofu kwamba Mungu hakupendi. “Mungu ni mfadhili wa huzuni”, Shetani akasema “Amekuweka humu bustanini kwenye kila aina ya matunda mazuri na matamu halafu anakuambia kuwa usiyale. Ni mkatili kiasi gani huyu basi! Ni mkatili na mbaya kiasi gani na asiye hata na rehema huyu!" sio tu kwamba Shetani anaingiza mashaka kwa kile alichokisema Mungu, kwa kweli, bali, pia anawekeza moyo na nia mbaya kwa Mungu wao.

 

Hawa, akiwa anajibu kiusahihi sana kabisa, kwa yale anayotakiwa kula na asiyotakiwa, lakini jinsi ya utoaji wake majibu unaonyesha kuwa alikuwa amekwisha athirika kwa mawazo mabaya aliyoingiziwa kiujanja kwa maswali aliyoulizwa na Shetani:

Mwanzo 3:2-3  Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; 3 lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa.

 

Mungu hakuwa amewaambia Adamu na Hawa kuwa wasiliguse tunda. Bali aliwaambia tu kuwa wasile. Hawa alimwelewa vibaya Mungu kaa kuongeza kwake, "Wala msiguse". Kwa kweli alikuwa alichanga sehemu ya kweli na kuanza kuyumba kwa kuwa kwenye fikra za “Mungu hakupendi”.

 

Sasa, hii ina maana sana. Mwanzoni sana Mungu aliwapa Adamu na Hawa mamlaka na kila walichotaka kwenye bustani yote “Ya Kila mti waweza kuyala ...”. alikuwa karibia amewaruhusu kila kitu kwenye maelezo haya. Kulikuwa na mti moja tu peke yake, aliowakataza. Kwa kweli, Mungu alikuwa amewahakikishia kuwa, "Mimi nipo kwa ajili yenu. Ndiyo, wote ni wako! Endelea mbele na muyafaidi kikamilifu. Kuleni na muyafaidi. Msiangalie nyuma". Kwa kweli aliwapa moyo kwa dhati kabisa kuifurahia bustani. Kulikuwa na dhambi moja tu ambayo Adamu na Hawa waliitenda nayo ni kulila tunda la mti waliokatazwa.

 

Shetani hata hivyo, aligeuza kinyume malengo mazuri na yenye manufaa kwao aliyokuwanayo Mungu kwa kuwaonyesha kuwa Mungu hakuwa anawapenda Adamu na Hawa. Aliwasikilizisha sauti isemayo "Mungu amewaweka kwenye bustani hii ili kuwakatesa na kuwafanya msiifurahie. Ni mkatili sana". Bahati mbaya sana, Hawa akaiingiza dhamira mbaya ya kuwaza hivyo na mawazo yake yakabadilika. Hata hivyo, bado Shetani anaendelea kuisukuma njia hii hata leo kwa namna mbalimbali.

·      Mungu hakupendi na hapendi uyafurahie maisha.

·      Anatoa amri na maelekezo ambayo ni mzigo na vigumu kuyabeba.

·      Haina maana kujaribu kufanya mafanikio ya mradi au jambo lolote kwa kuwa haitafanikiwa hata hivyo.

 

Kwa kweli mafundisho haya ya kishetani yapo kwenye upinzani mkubwa sana yakipinga asili ya kweli ya tabia ya Mungu na ia yake. Mungu hayupo knyume chetu na wala hatuchukii, bali kwetu sisi ni:

Zaburi 37:4 Nawe utajifurahisha kwa Bwana, Naye atakupa haja za moyo wako.

 

Zaburi 84:11 Kwa kuwa Bwana, Mungu, ni jua na ngao, Bwana atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu

 

Warumi 8:31-32 Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? 32 Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?

 

Matokeo ya mafundisho haya mabaya kwa namna yoyote ni maangamizi makubwa. Wengine wamefikia kushawishika kuwa njia za Mungu ni ngumu na mzigo mkubwa, na ni vigumu kuzichukulia. Hii kimsingi huwa hivyo pamoja na jinsi ya kuiadhimisha siku ya Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya na Siku nyingine Takatifu, utoaji wa zaka, na kadhalika. Kristo na Mume Yohana, wote wawili waliyapinga waziwazi mawazo haya:

Mathayo 11:30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.

 

1Yohana 5:3 Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.

 

Inachangia na ukosefu wa unyenyekevu wa kweli kwa upande wetu kwa Mungu na Kristo wake kwa yote waliyofanya na kutufanyia sisi. Ukosefu wa dhamira ni moja ya ishara inayoelezewa kwa nyakati zetu:

Warumi 1:21 kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.

 

2Timotheo 3:1-2 Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. 2 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi,

 

Inasimama wima kinyume na Ukristo wa kweli:

1Wathesalonike 5:18 shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.

 

Roho ya uchungu

Pia kwa kuendeleza na kufanikisha mafundisho maovu ya Shetani ya “Mungu hakupendi” anatumia roho ya kisasi na uchungu, ambavyo ni aina zote mbili za hasira moyoni mwa mwanadamu. Hili ni tatizo kubwa na sugu kwa wanadamu leo, kote kuwili, yaani nje na ndani ya Kanisa la Mungu. Wengi wanajikuta wakiwa na hasira na kisasi kibaya mioyoni mwao kuhusiana na mambo waliyofanyiwa huko nyuma. Wengine maamuzi yao ya hasira na kisasi waliyoyafanya wazazi wao, au maamuzi waliyoyafanya maishani mwao na Kanisa, na wengine wamerudia mwenendo wa waajiri wao waliopita wa zamani.

 

Ingawa mambo ya hatari tunaweza kufanyiwa sisi, na yawezekana kuwa tulitumiwa vibaya au kutendewa vibaya, na ingawa fursa yaweza kuwa imepotea, na miaka ya thamani au ya muhimu inaweza kuwa imekumbwa na, roho mbaya kwenye hisia hatuwezi kupata pumziko. Kama tutang’ang’ania hasira na roho mbaya basi itaendelea kuwa uchungu, na hatimaye kutupelekea kushindwa kiroho mikononi mwa Adui. Shetani analijua hili na ndiyo maana anafana kazi kimkakati ili kuchochea hisia ya hasira na matokeo ya mwisho ya uchungu kwetu. Mtume Paulo alituonya kuhusu mbinu hii au hila za Shetani:

Waefeso 4:26-27 Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; 27 wala msimpe Ibilisi nafasi.

 

Waebrania 12:14-15 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; 15 mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwa unajisi kwa hilo.

 

Bahati mbaya sana, ni kutokana na aina hiihii ya masengenyo mabaya ndivyo Shetani alivyofanikiwa kuwapotosha na kuwaasisha theluthi moja ya Malaika na wakamuasi Baba Mungu. Kwa hiyo, Shetani anajidhihirisha sio kwa kuwa tu ni mpanda mbegu ya mashaka na mwenezaji wa habari mbaya na za uovu, bali pia ni mwanzilishi war oho mbaya ya kisasi, hasira na uchungu. Ni muhimu sana kuzijua hila za mafundisho ya Shetani na nia yake kwa sehemu hii.

 

"Kudhani kuwa Mungu ni Mwongo"

Akiwa amefanikiwa kuwekeza moyo au mawazo ya mashaka kwenye kichwa cha Hawa na mawazoni mwake, Shetani aliipatia makazi faida yake:

Mwanzo 3:4 Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,

 

Ni kweli, kama tujuavyo, Shetani alikuwa anamwambia Hawa kuhusu fundisho la “roho isiyokufa”. Lakini ni kiujanja zaidi kuliko uwongo wa kurithi hali ya kutokufa, na ujanja au werevu wake wa kimafundisho ulimfikisha kumfanya aamini kuwa “Mungu ni mwongo. Hawezi kuaminika. Neno lake si la kweli”.

 

Alichukuwa anakifanya Shetani kilikuwa ni kuwekeza au kumpa elimu ya kiepistemolojia au elimu ya ufahamu. Epistemolojia inatafsiriwa kwenye kamusi kuwa ni elimu ya kusomea maarifa. Shetani alikuwa amemaanisha, kumpa Hawa mwili mbadala wa maarifa au kweli. Hivyo ndivyo anavyoonekana, kuwa na mamlaka mengine zaidi na ya mwisho, “kweli” zaidi kuliko neno la Mungu mwenyewe. Kisha afikie kwenye mkanganyo au kuchanganyikiwa, kulikokuwepo hadi kwenye mawazo ya Pilato katika nyakati za Kristo, anauliza “Kweli ni Nini?” Hii inaweza kusemekana pia kuwa “Ni Nani Utakaye Mwamini? Ni nini unachoamini? Mamlaka ya mwishi yaliyopo ni yapi?” Jibu la kijanja la Shetani kwa maswali kama haya ni kwamba kweli yaweza kuwa kitu chochote pamoja na neno la Mungu.

 

Leo anatoa fursa zake nyingi kuhusu kweli:

·      Ufananishaji– kweli kuwa juu ya mabadiliko

·      Umilikaji – kweli inakuwa kitu cha kibinafsi kabisa

·      Umilki – kweli ni kile tukionacho tu

·      Uwepo na Udumisho – kweli ni kitu tunachokizoea

·      Utakabishaji – kweli ni kitu kinachokubalika akilini tu (kweli ni kitu tunachoweza kukihoji).

·      Madharia ya Kiplato – kweli inajichanganya sana.

·      Ufiirikaji – kweli ni kama matukio.

·      Imani ya miungu wengi – kweli ni kitu sawa na uumbaji.

·      Umonia wa Saikolojia ya Kimwili - kweli ni sawa na chaguo la kitu kinachoonekana na kisichoonekana.

·      Upragmatism – kweli ni kitu chochote kitendacho kazi.

·      nk.

 

Uwongo wa Shetani unasimama kwenye mkanganyo kinyume na ushahidi wa Mungu aliotupa sisi kwenye Biblia:

Yohana 17:17 Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.

 

2Timotheo 3:16-17 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; 17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.

 

Maandiko Matakatifu ndiyo msingi imara wa pekee utupasao kujenga maisha yetu. Bila hayo tutabakia tumechanganyiiwa kwenye kikwazo au kinamasi cha mawazo ya mwanadamu na utiifu wake. Pasipo hayo, hakuna viwango– wala haki, wala uwongo. Hii kwa kweli, ndiyo mstari anaoutaka Shetani. Yatupasa kukaza mwendo na kukazana ili tusiangukie kwenye uamuzi wa kujitenga sisi na Neno la Mungu, ambalo ndilo kitu sahihi cha kutendea kazi kwenye hali zozote. Maisha yetu na kila tatizo na uamuzi tunaokabiliwanao maishani mwetu, yanahitaji kuwa na msingi kwenye Maandiko Matakatifu, iwe kwa waraka au kwa kwenye kanuni na roho. Biblia inapasa iyaongse.mwenendo wetu na ituelekeze kwenye mambo yote yahusuyo maisha yetu. Viwango na mifano vilivyotolewa kwenye Biblia yapasa view ni vitu vile tunavyovipima kwenye ukuaji wetu wa kiroho na ukomavu wetu.

 

"Kutoka Kwenye Kosa Dogo Hadi Kubwa Sana"

Alipokuwa anamwambia maneno haya Hawa, Shetani pia alidhihirisha hila muhimu ya jinsi anavyotenda kazi. Shetani anafanya kazi zake kwa kumpa kwanza mtu mawazo ya mashaka – kushirikiana na sisi kwenye makosa anayotaka kutupatia mawazoni mwetu. Kwa hatua yake ya udhaifu, anaendelea hadi hata kwenye ushindi mkubwa zaidi. Anayatoa malengo yake na vipau mbele vyake kwa mtazamo wa namna kwamba anajitoa kwa moyo wote kwenye furaha yetu na mahitaji yetu. Ni kutokana na "karamu au furaha" yake alivyojihisi kuwa ni "muhumu" kumtahadharisha Hawa kuhuku nia mbaya ya Mungu na kile alichokuwa anakikosa nje na hivyo. Aliahidi uhuru kutoka mautini lakili akiwa anaiua roho yake.

 

Kwa hiyo, ni kwamba Shetani atatutendea kwa njia mbalimbali. Atakuwa akiwasifu na kuwapotosha kila mara kwa mawazo mabaya na dhaifu kwenye dirii zetu ili atushinde. Kwa mfano, chukua mfano wa kucheza michezo ya kubahatisha. Huenda kama kuna mtu amechoka kuishi. Huenda wanapenda kuwa wangekuwa na edha nyingi zaidi za kulipia madeni au kuchukua likizo. Huenda wapenda wawe na bahati au walishambulia madai yaw engine kwa mafanikio yao. Ndipo wanaanza kununua kupuni za bahati nasibu. Nazo zinagharibu kiasi fulani cha dola, na kuna uwezekano wa kushinda wakicheza kwa takriban mara 10 au 20.

 

Huenda mtu akashinda kidogo na akapoteza kidogo, bali hatimaye anasikia changamoto ya kutaka kujaribu bahati yake zaidi tena kwa ujasiri na moyo mkuu na kisha akaanza kufuata utaratibu wa bahati nasibu. Kwa mara nyingi zaidi anajikuta akipoteza zaidi. Kwa mara wengine, dhambi haiendelei kabisa zaidi ya kwamba ikweli ni kwamba anaendelea kupoteza fedha zake kama tabia ya kawaida, kama ilivyo kuvuta sigara. Kwa wengine inaendelea kwa msukumo walioanzanao kwa kiasi kwamba inaanza kumpotezea sio $5 tu au $10 kwa kila juma, bali sasa ni kwa mamia na hata maelfu ya dola na kupelekea madeni, umasikini na kukata tama, kufunikiza, kudanganya na kadhalika.

 

Hii ni kweli kwa dhambi karibia zote. Uuaji unaanzia kwenye kuchanganyikiwa na wivu mbaya na kunahusiana na hali ya kisasi, hasira, uchugu, chuki na hatimaye mauaji. Masengenyo yanaanza kwa “kukusudia kulikopangiliwa vizuri” na kueneza “habari muhimu” lakini kunaishia na tabia ya kikorofi inayowagawanya watu na inayosababisha kutoaminiana na uchungu. Ni sawa tu na iliyvo kitendi cha udhalilishaji. Ni kama kuna mtu aliwahi kusema, hakuna mtu aliyewahi kudanganyika kuingia kwenye tabia za ulevi kwa ajili ya kumpelekea picha ya mtu aliyechoka mbaya kwa ulevi uliopitiliza.

 

Kwa hiyo inatupasa kila mara tujitahidi kuepuka kumpa Shetani uwezo wa kutushinda. Ni kama tulivyojione hapo kabla kwenye tafsiri ya Phillips ya Waefeso 4:27, kuwa kitendo cha kwenda kulala na hasira kinampa Ibilisi nafasi mawazoni mwetu:

Waefeso 4:26-27 Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; 27 wala msimpe Ibilisi nafasi.

 

Si sawa tu na ilivyo kweli na dhambi nyingine zote tunazopenda kuzitaja.

 

"Hakuna kikomo"

Kiwa ameweka mawazo ya mashaka mwenye fira za Hawa na kumpatia wazo baya la kwamba “Mungu ni Mwongo”, Shetani alisonga mble na kumnyang’anya ushindi mapiganoni. Alisema:

Mwanzo 3:5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.

 

Kwa kweli, Shetani alikuwa anamwambia Hawa mambo yafuatayo:

"Hebu ona Hawa. Machoni pa Mungu, wewe hufai. Ni wazi kuwa yeye alikuumba wewe kwa hali yenye ukomo kwa kuwa anapenda akutumie tu wewe na Adamu kama watumwa wake. Anajua kwamba kama utakula tunda hili, utakuwa kama yeye na kuweza kuyaendesha mambo yako wewe mwenyewe. Na ndiyo maana hapendi mle tunda hili. Lakini mimi nipo hapa ili kukuambia kwamba mambo hayatakuwa hivyo. Jina la mchezo ulioko hapa unaitwa kujitawala au uhuru. Jibu peke lililo kwenye harakati hii ni kujitahidi wewe mwenyewe. Jipange mwenyewe! Hutakufa – na bali badala yake ndipo utafanana na Mungu, na utajiweka wewe mwenyewe kwenye usawa na yeye ukiwa na ujuzi na uwezo wa kufikiri. Utamudu kuendesha maisha na mambo yako mwenyewe kwa msingi wako wewe mwenyewe na kwa uzoefu wako na kwa ujuavyo wewe mwenyewe."

 

Hata hivyo, akaangukia kwenye mkondo wa Shetani wa kujiuliza maswali ambayo ni fundisho la uwongo ambapo kwamba hakukuwa hatima au mwisho wa mwanadamu. Shetani alikuwa ameweka mawazo ya kwamba Mungu ni mpenda na mleta huzuni na kwamba ni mwongo. Na sasa anawekeza kwa hila zaidi aina mpya ya kumuonea mashaka na kwa wote, kwamba hakuna lengo au dhumuni la kuwepo mwanadamu. Ni kweli, kwa mtazamo au muono wa Shetani ilikuwa muhimu kuwa aendeleze mafundisho yake na kwa kweli, kumshawishi Hawa kwenye hilo lilikuwa ndilo lengo la mjadala wake kwa kumbadili mawazo. Sababu kwa kweli ni kwamba kuna kusudi kwenye maisha ya mwanadamu, na kusudi hilo ni pamoja na kufikia ukomo wa hali ya kuwa mshitaki au adui (Shetani) na kuponya maumivu kwenye Familia ya Mungu.

 

Tunajua na tuko macho sana na hatima iliyoko ya mwanadamu inayowangoja ndugu zetu wapendwa wanadamu wenzetu na sisi baada ya ufufuo wa wafu. Inatupasa tubadilike na kuwa Wana wa Mungu wa kiroho, tulioumbwa sawa na malaika, na kuvirithi vitu vyote chini ya uongozi na mamlaka ya kaka yetu mkubwa, Yesu Kristo:

Waebrania 2:5-8 Maana hakuuweka chini ya malaika ulimwengu ule ujao tunaounena, ila mtu mmoja ameshuhudia hivi mahali fulani, akisema, 6 Mwanadamu ni nini hata umkumbuke, Ama mwana wa binadamu, hata umwangalie? 7 Umemfanya mdogo punde kuliko malaika, Umemvika taji ya utukufu na heshima, Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako; 8 Umeweka vitu vyote chini ya nyayo zake. Kwa maana katika kuweka vitu vyote chini yake hakusaza kitu kisichowekwa chini yake. Lakini sasa bado hatujaona vitu vyote kutiwa chini yake.

 

Warumi 8:14-17 Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu. 15 Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba. 16 Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; 17 na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.

 

Ufunuo 21:7 Yeye ashindaye atayarithi haya, [mbingu mpya, nchi mpya, Yerusalemu mpya, nk] nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

 

Biblia inatufundisha kuwa kusudi kubwa zaidi ambalo Mungu alimuumba mwanadamu. Lengo hili ni kuwa kama Mungu aliyemuumba mwanadamu. Lengo hili ni kuwa kama Mungu mwenyewe, kufanyika uzima wake usiotengenezwa wa milele, na kushirikiana naye utawala wa dunia. Ni kwa kusudi hili, ambalo Shetani anatafuta kulipotosha.

 

Leo, Shetani yuko tofauti. Amewashawishi mamilioni wengi waamini kuwa hakuna sababu wala lengo la kuishi. Na kwamba mwanadamu ni suala tu la kufikirika; matokeo ya mwisho ya mabilioni ya miaka ya fursa potofu. Lakini hata kwa wale walio pamoja nasi ambao wanaojua na kuamini kuwa kuna kusudi kwa maisha ya mwanadamu, kuna hatari kwenye fundisho hili la Shetani. Ambavyo ni kwamba kama tutapoteza mwelekeo wa kulinganisha utofauti kati ya maisha haya na maisha yajayo.

 

Mara nyingi tunachanganyikiwa kwa kuvutiwa na haya ya leo, na kupoteza mwelekeo kujua kilicho muhimu hakika. Tunapoishia kwa kile kinachoonekana kama tatizo lisilowezekana, tunaweza kujiuliza wenyewe, “je, inastahili kuwa hivi? Mungu yuko wapi? Kwa nii yuko mbali sana hivi?” Sababu, hata hivyo, haiku kweli kwamba, “Mungu yuko wapi?” bali “Fikra zetu ziko wapi?” Sisi ndio tunaoruhusu mambo yaliyopo kuwa na uzito mkubwa mioyoni mwetu kuliko kusudi la milele alilonalo Mungu kwa ajili yetu.

2Wakorintho 4:17-18 Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; 18 tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.

 

Namna nyingine kuhusu fundisho hili inaweza kuonekana ni kwenye mchanganyo na anasa za dhambi. Kwenye jambo hili anasa za muda mfupi hazipimi namna yoyote ya kipindi kirefu kilichoekwa kwenye ukomo wetu na tunapoteza mwelekeo wa sababu ya sisi kuwepo kwetu hapa dunini kwa mahali pa kwanza. Biblia inatuonya kutazama mifano ya wale waliotutangulia kwenye imani, na wakajikana wenyewe wakizikimbia kwa kukaa mbali na anasa za dhambi za dunia kwa ajili ya hatima kuu inayokuja ya milele:

Waebrania 11:24-27 Kwa imani Musa alipokuwa mtu mzima, akakataa kuitwa mwana wa binti Farao; 25 akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo; 26 akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo. 27 Kwa imani akatoka Misri, asiogope ghadhabu ya mfalme; maana alistahimili kama amwonaye yeye asiyeonekana.

 

Waebrania 12:1 Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

 

"Roho ya uongo"

Ili kulifanikisha fundisho hili la uwongo kwa Hawa, Shetani pia alionyesha jambo kwenye tabia yke ya kupotosha ambayo tunapasa kuiona ya kwamba: yeye ni muongo. Shetan anaishi kwa uwongo, usengenyi au majungu, uvumishaji wa habari, tabia za kushambulia na kushitaki. Kwa suala la umbo la Shetani na kuanguka kwake kulikoandikwa kwenye Ezekiel 28 kuna ugeuzo wa kuvutia kwenye kugha asilia ya Kiebrania kwa kile kilichoandikwa kwa jinsi dhambi inavyoendelea na kujitokeza ndani yake wakati alipokuwa akijulikana kama Kerubi Afunikaye hivi:

Ezekieli 28:14-16 Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto. 15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako. 16 Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto.

 

Aya ya 16 inaanza kwa kusema: Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi. Tafsiri ya NKJV imeitafsiri aya hii kama kwa uwingi wa biashara yako uliyofanyika kujawa na udhalimu ndani yako, na ulitenda dhambi. Neno la faida lililo kwenye kifungu hiki lina maana ya uchuuzi (KJV) au biashara (NKJV). Kwa Kiebrania neno hili ni rekulla maana yake ni ushukuzi au usafirishaji. Linatokana na neno rakal maana yake kuelekea mbele. "maelezo yanayovutia na yanayopendeza" ni kwamba kuna neno linguine linalotoholewa kwenye hili la rakal, ambalo ni rakil, linalomaanisha mwongo neno hili linajitokeza mara sita kwenye Agano la Kale (Walawi 19:16; Yeremia 6:28, 9:4; Ezekieli 22:9; na Mithali 11:13a, 20:19a). limetafsiriwa kama mbeba mkia au usengenyaji, lakini nia ilikuwa ni muongo,

Walawi 19:16 Usiende huko na huko katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usisimame kinyume cha damu ya jirani yako; mimi ndimi Bwana.

 

Dalili iliyo kwenye Ezekieli 28 na kutajwa kwa Shetani inaonekana kuhusiana na maana mbili za namna moja. Kwa biashara inayoonekana, nji wa Tiro ulifanyika kuwa ni mji wa wezi na wanyang’anyi na ulijawa na machafuko na fujo. Lakini kwa mpinga taswira ya Lusifa au Shetani, maana inayoonekana hapa kuwa ni kwamba ni kwa ajili ya uwingi huu uwongo wake, kitend chake cha kutoka nje na kusengenya na kuanza kunena maneno mabaya nay a uwongo kuhusu Mungu, ndipo alijawa na maovu ndani yake (kumchukia Mungu) hivyo ukatenda dhambi.

 

Leo Shetani ni chanzo cha aina hii ya mwenendo nmbaya na mpotovu kati ya wanaume na wanawake na hata kwa watoto, wakati (kwa lugha ya mfano) aliwanong’oneza masikioni mwao na kuwasihi waeneze hadithi za uwongo wasingiziane. Shetani ni mshitaki wa ndugu zetu:

Ufunuo 12:10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.

 

Mojawapo ya silaha kali na zenye nguvu sana za Shetani awapo vitani ni kuwatega na kuwanasa Wakristo kwa kuwafanya wajikite kwenye matendo ya kusengenyana na kushutumiana na hata kushitakiana au kuhukumiana kwa mambo yao. Kwa lugha rahisi ni kama kulifanya jeshi la Mungu lianze kupigana wenyewe kwa wenyewe. Kusengenya ni dhambi mbaya. Ni dhambi mbaya sana machoni pa Mungu kama tulivyoona kwenye Walawi 19:16, kitendo cha kusengenya na kusingizia vimechukuliwa na Mungu kama ni sawa na kudhulumu uhai wa jirani yetu – iwe yu ndani au hata nje ya Kanisa:

Walawi 19:16 Usiende huko na huko katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usisimame kinyume cha damu ya jirani yako; mimi ndimi Bwana.

 

Masengenyo na kusingizia kumo kwenye moyo wa watu wengi ambavyo Mungu anachukia sana:

Mithali 6:16-19 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. 17 Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; 18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu; 19 Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.

 

Usengenyi na uwongo ni machukizo na ni uvunjifu wa amri za Mungu na ni sawa tu na kuua machoni pake. Hayatoki tu kwenye kisima cha chemchemu ya upendo na nia njema endelevu kwa wengine, bali kutokana na upotoshaji wa tabia za Shetani. Yesu alituonya kwamba:

Mathayo 15:18-19 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi. 19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;

 

Mathayo 12:33-37 Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri; au ufanyeni mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana. 34 Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake. 35 Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya. 36 Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu. 37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.

 

Yakobo ndugu yake Yesu, alionya pia kuhusu uharibifu huu huu wa tabia hii ya usenhenyaji na kusingizia:

Yakobo 3:8-12 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti. 9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu. 10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. 11 Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu? 12 Ndugu zangu, Je! Mtini waweza kuzaa zeituni, au mzabibu kuzaa tini? Kadhalika chemchemi haiwezi kutoa maji ya chumvi na maji matamu.

 

Ime,uwa ikisemwa kwamba kabla hatujasengenya, kulaumu na kumnyooshea mtu kidole, tunapaswa kufikia vizuri jinsi vidole vinavyojipanga mikononi mwetu na jinsi vinavyoonekana. Kwa kuwa kila kidole kimoja tunachomnyooshea mtu yeyote, vitatu vinaonesha nyuma upande wetu. Imekuwa ikinenwa pia kwamba tunapodhania au kuwahisi wengine na kuwanene vibaya, yatupasa kujua maana ya neno “kuhisi”. Neno hili kuhisi kwa Kiingereza linaundwa na maneno farasi, ni wewe na mimi (yaani ass, u, and me). Tunapohisi kitu kwa mtu mwingine, ni wazi sana kuwa tunakwenda kumtoa farasi ndani yako (wewe) na mimi.

 

Kusengenya na kusingizia ni dhambi mbaya sana mchoni pa \mungu. Lakini tabia hizi zipo, kama alivyosema Yakobo, ni rahisi kuteleza kwenye hayo. Kabla hatujaenda kusema ktu fulani, kwa kweli kitu chochote kile, kuhusu mtu mwingine yeyote yule, kuzinena habari zake kwa wengine, yatupasa tumhitaji “Mpambana na Usengenyi”. Kwa mambo matatu haya:

1.    Ni vile nilivyo kwa nikatakachokisema, ni kweli? Tunauhakika na mambo tunayokwenda kusema? Tunao uhakika wake? Ama sivyo basi tunakwenda kueneza uwongo na umbeya.

2.    Je, niliwahi kusema mambo haya mbele za mtu anayenenewa habari hii? Kama sivyo, kama tunaharakia kusema mambo haya na kwa kuwa yatamuumiza moyo mtu Yule, ndipo tusiyaseme kabisa. Haionyeshi upendo kwa mtu yule anayehusika kumnenea mambo yasiyofaa dhidi yake, hata kama ni ya kweli, lakini kama hawawezi kujitete wenyewe, au iwapo kama yatamkwaza na kumlete usumbufu.

3.    Je, jambo lenewe hili litawaelimisha wale wanaolisikia? Hata kama jambo lenyewe ni la kweli, na hata kama halitamuumiza mtu anayenenewa habari hii, ni muhimu kusema ni pahala pa kwanza? Je, litaleta faida au manufaa kwa wasikilizaji kujifunza kipande hiki cha habari?

 

Kusengenya na uwongo ni mambo tunayopasa kushindaanayo kwa nguvu zote kwa maisha yetu yote. Shetani ni mwanzilishi wa matendo haya mioyoni na atazitumia silaha  hizi ili kutuharibu kama ataweza.

 

"Maarifa ni kila kitu"

Tena kipimo kingine kwenye kauli za Shetani alipomwambia Hawa kwenye bustani ni kwamba Ujuzi ndio uliopo. Maarifa yapo kila mahali. Shetani alisema:

Mwanzo 3:5 kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.

 

Shetani ni kiumbe mwenye majivuno na mtupu. Bila shaka kabisa ni kwamba alipewa na kuwanao uweza mkubwa sana na mamlaka kwenye Ufalme wa Mungu kabla hajaasi. Baadhi ya mamlaka yale yalikuwa na kiini au chanzo chake kwenye maarifa ya mpango wa Mungu na malengo yake, ambapo mengine hayapo kwenye Mashauri au Baraza la Mungu halikui hiyo. Kwa sababu ya kuwa na maarifa haya ndipo kulimpelekea awe ni kiumbe batili na mwenye Majivuno.

 

Zaidi sana, kama tulivyosema hapo kabla, Shetani tangu hapo aliendeleza baraza lake mwenyewe la “kweli” yake, baraza lake la “maarifa” aliyoyatumia kueneza kwa kasi uwongo wake. Kwa kuwa Shetani anasaidia hii kwa “taarifa za kina” – ziwe za kweli au sivyo – analisha tamaa yake na ubinafsi wake. Sisi bilashaka tumezoea kwa mhemuko huu sisi wenyewe. Tunapokuwa tunalijua jambo ambalo mtu mwingine yeyote halijui, au wakati tunapokuwa na maarifa ambayo kwayo watu wengine inawalazimu kutujia ili wajifunze, inafanya kiwango fulani cha uweza, wa kuwa wa tofauti na rasmi aina yake. Shetani anaijua hisia hii na kwa hiyo amerudla mara kwa mara kuwauza wanadamu kwenye maarifa ya kisirisiri na busara. Dunia imejaa dini nyingi za kimafumbo au sirisiri ambayo kwamba makasisi wake wanadai kujua zaidi kuliko waumini wao.

 

Hata hivyo, Shetani atajaribu kutuuza sisi kwa namna hiyohiyo. Maarifa ni kila kitu. Sasa ni kweli kwamba Mungu anatutaka sisi tuikulie neema na maarifa (2Petro 3:18). Ni kweli kuwa maisha halisi na mazuri yanahusisha kuwa na maarifa ya kumjua yeye kuwa ni Mungu wa Pekee wa Kweli na Yesu Kristo mwanawe (Yohana 17:1-3). Lakini kuna tofauti kati ya maarifa yaokoayo na kuongoza kwenye ukuaji wa kiroho na ukomavu, na maarifa yaliyo na faida ya kimaarifa pekee.

 

Yakobo aliandika:

Yakobo 3:13-18 N'nani aliye na hekima na ufahamu kwenu? Na aonyeshe kazi zake kwa mwenendo wake mzuri, katika upole wa hekima. 14 Lakini, mkiwa na wivu wenye uchungu na ugomvi mioyoni mwenu, msijisifu, wala msiseme uongo juu ya kweli. 15 Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani. 16 Maana hapo palipo wivu na ugomvi ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya. 17 Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki. 18 Na tunda la haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.

 

Maarifa ya msingi anayotoa Mungu ni ya jinsi ya kutuongoza kwenye utakatifu, haki, amani, upole, na maisha ya rehema, yaliyojaa na matunda mema. Kuuelewa unabii, au lugha (ambayo ni lugha ya kigeni), au nyinginezo, kitu kama hicho sio lazima kwa wokovu. Kinginechochote kama uelewa wa ziada ni “kuitia keki baridi”. Lakini yatupasa kujua na kujichunga sisi wenyewe ili tusiangukie kwenye mtego wa Shetani:

2Timotheo 2:22-26 Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi. 23 Walakini uyakatae maswali ya upumbavu yasiyo na elimu, ukijua ya kuwa huzaa magomvi. 24 Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu; 25 akiwaonya kwa upole wao washindanao naye, ili kama ikiwezekana, Mungu awape kutubu na kuijua kweli; 26 wapate tena fahamu zao, na kutoka katika mtego wa Ibilisi, ambao hao wametegwa naye, hata kuyafanya mapenzi yake.

 

Yatupasa wakati wote tujue na kutilia maanani kwamba:

lWakorintho 8:1-3 Na kwa habari ya vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu; Twajua ya kuwa sisi sote tuna ujuzi. Ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga. 2 Mtu akidhani ya kuwa anajua neno, hajui neno lo lote bado, kama impasavyo kujua. 3 Lakini mtu akimpenda Mungu, huyo amejulikana naye.

 

1Wakorintho 13:8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.

 

Kama tunaamini kuwa tuna kiwango fulani cha maarifa au busara ndipo haitupasi kujivuna kwa sababu hiyo, wala hatupaswi kujitukuza, bali yatupasa kumtukuza |Mungu aliyetujalia hayo maarifa na uwezo wa kujua au kuelewa. Tusiangukie kwenye mtego wa Shetani wa kujiinua kwa majivuno kwa kuamini kwamba maarifa ni mwisho wa mambo yote.

 

Hitimisho

Tumejifunza na kupitia mambo machache yahusuyo mafundisho ya Shetani na mbinu zake. Kuna michanganuo mingi sana mingine mizuri iliyo kwa ajili yetu kwenye Biblia (soma jarida la Hukumu ya Mapepo (Na. 80)).

 

Yatupasa kuwa na bidii. Lengo la Shetani ni kutupotosha kila mmoja wetu. Amefanikiwa tayari kwa wanadamu wengi. Alifanikiwa kuwazoa takriban theluthi moja ya Malaika. Kama hatatuuza kwenye mafundisho ya uwongo, atajaribu kutuuza kwenye nia mbaya au dhamiara mbaya ambazo zinaendana na kuyaunga mkono mafundisho hayo atajitahidi kutufikia kwa kuamsha hisia za kisasi, hasira, shutuma na lawama, masengenyo, kiburi, kulisahau lengo letu, kukosa shukurani kwa Mungu, kutumainia akili, na njie nyingine zozote ziwezekanazo.

 

Mbinu na mikakati hii tumefunuliwa sisi kwenye kurasa za Neno la |Mungu. Hii pamoja na uweza wa Roho wa Mungu, ni silaha ya vita vyetu. Mstari wa mapambano umechorwa. Tutawezaje kupigana vita vizuri siku ya leo na kwa siku nyingine yoyote?

q