Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[185]

 

Imani za Kisosiniani, Kiariani na Kiyunitariani

(Chapisho La 1.0 19961221-19961221)

 

Neno Usosinianism limekuwa likitumiwa bila kutofautisha na sehemu kubwa ya wapinga mafundisho ya Utatu au wapinga imani ya Kitrinitatiani. Suala ama fundisho la Uungu ilikuwa ni jambo muhimu sana kwenye imani ya Kisosiani. Na kwa mtazamo wa makundi yote mawili, yaani Wakatholiki na Waunitariani, walishikilia kwa namna zao zote kwamba kumjua Mungu ni kitu rahisi na hakuna utata. Walihitimisha kwa kusema kwamba utofautishaji wa nafsi ni kitendo cha kuharibu mwelekeo wa ufafanuzi huo. Kwa mtazamo na msimamo wao, waliukataa Utatu kuwa ni imani sahihi. Tofauti liyopo kati ya imani za Kitrinitarini na Uyunitariani ni kwamba heshima anayopewa Kristo inatokana na jinsi uhisiano wake ulivyo na Baba na kwamba ni wa aina ya pili, wakati ambapo Watrinitariani wanashikilia kuamini kwamba unatokana na imani ya kidini ya latria, ambako inaamini naq kufundisha watu wake kwamba yeye kwa hakika ni Mungu sawa na kama alivyo Baba kuwa ni Mungu.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

(Hati Miliki © 1996  Wade Cox)

(tr. 2014)

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 


Imani za Kisosiniani, Kiariani na Kiyunitariani


 

Neno Usosinianism limekuwa likitumiwa bila kutofautisha na sehemu kubwa ya wapinga mafundisho ya Utatu au wapinga imani ya Kitrinitatiani. Neno hili limechukuliwa kutoka kwa mtu aliyeitwa Lelius Socinius (1526-1562) na mjomba wake Faustus Socinius (1539-1604), mkazi wa huko Sienna. Dini iliyoanza siku za kale kabla ya Faustus ilihusiana sana na hii, lakini ilimwia kila mtu kuwa ndani ya hii. Jamii ya kisirisiri ilijiunda huko Vicenza katika dayosisi ya Venice ili kujadili imani na mafundisho ya Utatu. Miongoni mwa washiriki waliokuwepo walikuwemo kina George Blandrata (mwana fizikia), Alciatus, Gentilis na  Lelio Socinius. Lelius (au Lelio) Socinius alikuwa kasisi wa huko Sienna na rafiki wa Bullinger, Calvin na Melancthon. Lengo la kuundwa kwa kikundi kile lilikuwa ni kuanzisha vuguvugu la kupinga imani na mafundisho ya Utatu. Kikundi hiki kilivunjika na wanachama wake wakakimbilia Poland ambako waliteswa sana tena.

 

Ijulikane pia kwamba hawa Waanzilishi wa vuguvugu hili au Nominalists waliokuwa chini ya uongozi wa Abelard walikuwa wahamasishaji na wapinzani wa kweli wa mafundisho na imani hii ya Utatu katika kipindi cha Matengenezo kama walivyowaona Wakatoliki na hivi ndivyo inavyoonekana kwenye mandiko Hugh Pope kwenye makala aliyoandika kuielezea imani ya Kisosiani (Cath. Encyc., Vol. XIV, p. 113). Wale walioitwa kuwa ni wapinga kundi la Wakweli, Wahamasishaji walikataliwa na wanafalsafa wa Kikatoliki. Kazi hii ya uchambuziani ilihusisha na ufafanuzi wa mambo kwa namna ya kila mtu peke yake ili kuupata ukweli ndani wa kila mmoja. Kwa hiyo unapinga uwepo wa dhana ya kuachananayo na ya ulimwengu, na inakataa kukubaliana na ukweli kwamba akili zinauwezo wa kufanya hayo. Kwa hiyo maendeleo ya kimizimu hayajumuishwi pia. Itikadi ana mafundisho yaliyotiliwa chumvi ya Wafuata uhalissia yakaiteka dunia na mawasiliano yenye ukweli na halisi sambamba na mtazamo uliokuwepo wa mawazo ya kidunia. Wakatoliki walikuwa kwenye mrengo wa waamini kwa Ushupavu wa mafundisho haya ya Uhalisia Shupavu wa Kiaristoteli (hasahasa kutoka pipindi cha kina Aquinas na Occam na kuendelea), zaidi sana kuliko imani ya Kishupavu ya Uhalisia wa Waplatoniki. Mchakato huu wa kifikra una dalili mbaya na madhara katika kuifafanua Theori au Dhana fikirika ya nafsi na roho ya dunia. Mawazo ya kisasa ya kisayansi na  ya kinadharia kimsingi yanatuama kwenye kufafanua matukio kwa mtazamo wa kimwili. Wahamasishaji waliendeleza mafundisho yao hasa hasa kupitia kina Hume, Stuart Mill, Spencer, Huxley na Tain. Wakatoliki waliwaona wao kuwa wanazidisha kuweka tofauti hususan ya utendaji wenye mashiko (uozo au uharibifu rahisi wa utoaji mada au mahuribi yaliyogusa mioyo kuhusu mshangazo na kusahau mkubwa ujulikanao au mlinganisho wenye mashiko na mchakato wa utandawazi) (tazama kitabu cha De Wulf, Nominalism, Realism, Conceptualism, Cath. Encyc., Vol. XI, p. 93). Wakatoliki wenye itikadi ya Kiaristoteliani wanajulikana (na wao wenyewe) kutofautisha kwa uangalifu sana kati ya haya yote mawili ya utengaji kazi wa akili. Unominalism hauafikiani na falsafa ya kiroho, na hata kwenye Uanazuoni au Uskolastiki. Nadharia za Kant Anayedhaniwa pia kuharibu vifungo vyote ambazo zingeweza kuliunganisha wazo la ulimwengu wa ndani (De Wulf, ibid.). wakatoliki wameendelea kuamini na kushikilia hivyo hadi kwenye karne hii kwamba hatuwezi kujitoa kwa akili zetu zote na uwezo wetu wa kimaarifa, ila tunazalisha ndani yetu kwa ushawishi wa kiasi fulani kwa kitu kinachojidhihirisha kwetu (ibid.). Hii inaashiria jambo kwenye mapenzi ya Mungu kutufunulia mambo, ambalo ni asili ya Mungu. Maelekezo ya ukweli huu ni ya kiantolojia. Antolojia ni sayansi ya kusomea viumbe au vyanzo au asili ya vitu. Inahusiana na masomo ya kusomea habari za viumbe au asili ya vitu kwa ujumla. Kwa hiyo, dini zote zinahusiana na maelezo haya kwa ujumla. Kwa hiyo, maelezo na ufafanuzi kama huu yanatoa ukweli kuhusu Mungu na wana wa Mungu na mapepo.

 

Uontolojia, ambao unahusiana sana na imani ya Uplatoni Shupavu, unaonyesha kwa kiasi kikubwa kuwa ni aina ya dhana fikirika, inayokuja kwetu kutokana na ulimwengu uliomakini kwa njia ya kimapokeo, pamoja na aina ya dhana fikirika ya kugeuka kihalisia mkate na divai kuwa ni mwili na damu halisi pamoja na asili ya uwepo wa Mungu. De Wulf anaendelea kuamini kwamba tunaunda fikra yetu ya kwanza tukiwa bado hatujamjua Mungu bado. Sisi hatumju sana yeye kiasi kwamba tunapaswa kujifundisha fikra zetu hizi mpya ili kukuza kiwango chetu cha posteriori cha uwepo na chanzo chake. De Wulf anafikiri kwamba Uontolojia umeacha kuishi kwake na kwamba hii dunia sasa inaenda kwa mfumo wa kimajaribio na utafakari ukidhaniwa kuwa utarudi kwenye ndoto za Plato (ibid.). Wakatoliki hawakujua kwenye mtazamo wao kwamba baadhi ya mawazo makuu walikuwa ni Wayunitariani pamoja na wale waliotoa fafanuzi za kisayansi na kifalsafa za ukweli—kina John Locke na Sir Isaac Newton akiwa ni mfano unaojulikana sana na mtu mashuhuri. Kwa hiyo, Wayunitariani (au Waariani kama walivyoitwa na Watrinitariani) wanaonekana kama walikuwa na sehemu kubwa ya kufanya na kushiriki mchakato huu.

 

Mtazamo huu wa maarifa na Theori ya Causal imefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Uumbaji: Kutoka Theori ya Anthropomofia Hadi Kwenye Anthropolojia ya Kitheomofiki (Na. B5) [Creation: From Anthropomorphic Theology to Theomorphic Anthropology (No. B5)]. Wanominalisti walikuwa ni wapinga Utrinitariani kutokana na utafiti wao  uliotuama kwenye salsafa ambazo zinapinga Dini ya Waplatoniki mamboleo. Tofauti iliyoko kati ya Wakatoliki na Dini zinazopinga Utrinitari ulikuwa ni karibu sababu sawa, ya kuwa Mungu alijidhihirisha kwa kupitia ufunuo na kwa wale watu wazima waliobatizwa katika Roho Mtakatifu. Ili wawe  Wanaamini fundisho la mkate na divai kugeuke kuwa damu na mwili halisi.

 

Kwa sababu hii Wakatoliki waliyakomesha haya madai ya wapinga Utrinitariani kwa kufundisha uhusiano wa mwendelezo wa, imani ya mkate na divai kugeuka kuwa damu na mwili halisi  hadi utii na kuwa sawa na Kristo bali akiwa ni mdogo au asiye na hadhi sawa na Mungu. Wakatoliki walikataa matendo haya na kama Mungu alivyofanya na kutegemea kwenye mwendelezo wa kuamini hadithi na imani za kimistiki na kuwa kama Mungu kama ilivyoelezewa na Wakapadokia. Hii ilikuwa ni tofauti ya kidhana ambayo Wakatoliki waliipinga tangu kikipindi cha Wakapadokia (tazama majarida ya Roho Mtakatifu (Na. 117) na Consubstatial na Baba (Na. 81) [The Holy Spirit (No. 117)  and Consubstantial with the Father (No. 81)].

 

Historia inatuonyesha kwamba kwa muda mrefu Kanisa la Mungu limekuwa likitanguliwa na Matengenezo ya Wawaaldensiani mara zote walikuwa ni wapinga Utrinitariani tangu hapo hadi kipindi cha Matengenezo. Hugh Pope anawachukulia Watrinitariani kuwa ni wawakilishi wa Wasabellian, Wamakedonia na Waarian wa zamani. Kwa kweli, Wawaaldensian walishutumiwa kwa au kwenye maelezo ya Waariani katika mwaka 1180 kwa mtazamo wa Bernard wa Fontcaude (Adversus Vallenses et Arianos; tazama jarida la Wajibu wa Anri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Nubgu Yanayoshika Sabato (Na. 170) [The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)].

 

Watu wa huko Ulaya waliwaita wapinga Utatu kuwa ni wanaotokana na ujuzi wakiwa ni matokeo ya wana Matengenezo na wakawa wanashikilia mtazamo tofauti. Na kwahiyo inapotosha kuwaita hawa kuwa ni Wasociani. Ni sawa tu na jinsi Makanisa ya Mungu huko Marekani yalivyofanya tangu kipindi cha kati cha miaka ya 1800 yakijulikana kama Waarmstrong. Alikuwa ni kiongozi wa baadae wa tawi moja. Ni kama alivyokuwa Armstrong, nasi tutajionea kwamba Wasosiani wenyewe walibadilisha mtazamo wao kuhusu asili ya Mungu.

 

Lelius Socinius aliishi kipindi chake kirefu huko Zurich lakini nalikuwa na pia anakipindi cha kuwa na muda wa kuishi huko Cracow. Alifariki mwaka 1562 na wapinga Utatu walipitia mateswa makali kipindi hiki. Mwaka 1570 Wasosinian waliogawanyika na kushawishiwa na John Sigismund, walianzisha huko Racow. Mnamo mwaka 1579 Faustus alikuja Poland pamoja na vitabu vya mjomba wake. Alikuta dini imegawanyika na kwanza alikataa uanachama kwa kuwa alikuwa hajabatizwa mara ya pili. Ubatizo wake wa kwanza kwa hiyo ni lazima uwe ulifanyika akiwa mtu mzima. Mwaka 1574 Wasosinian walianzisha Katekismu ya Wayunitariani. Asili na ukamilifu wa Mungu ulielezwa lakini makabrasha hayakuandika chochote kuhusu tabia za kimbinguni ambayo ilichukuliwa kama siri kubwa (na Wakatoliki). Kristo alichukuliwa kuwa ni kuwa ni mwana wa ahadi na mwombezi wa  wanadamu

 

Faustus Socinius alijiunganishia kazi hizi zote yeye mwenewe tangu mwaka 1579. Alikuwa amealikwa huko Siebenburg (au Siebenburgen) ili kukabiliana na wapinga Utatu waliokuwa chini ya Francis David (au Davidis) (1510-1579). David alikufa huko Deva Castle ambako alikuwa amefungwa gerezani kwa kosa la kuwa na msimamo wake wa tofauti kuhusu asili ya Kristo. Kanisa laSiebenburg, baada ya kifo cha Francis David, aliyeuawa kwa kukata kichwa na Andreas Eossi na hili ndilo lilikuwa Kanisa huko Ulaya Mashariki lililotokea kwenye imani ya Wawaldensian. Tunajua bila shaka kuwa walikuwa ni Wayunitariani (mara ngingine waliitwa Waarian na Wakatoliki). Walizishika Sabato, Sikukuu Takatifu Zilizoamriwa na waliadhimisha Miandamo ya Mwezi Mpya na walikuwa ni Kanisa la Kweli la Mungu hukp Ulaya ambayo kwayo twaweza kuiita ilikuwa ni zama ya Watiathira (soma majarida ya Mgawanyo Mkuu wa Makanisa Yanayoshika Sabato (Na. 122) na Wajibu wa Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu yanayoshika Sabato (Na. 170) [General Distribution of the Sabbath-keeping Churches (No. 122)  and The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)].

 

David alikataa kuukubali upekee wa mafundisho ya imani ya Wasosiniani yasemayo kuwa Kristo, ingawaje sio Mungu anapaswa kuabudiwa. Kanisa la Mungu huko Ulaya halikuwa limekubaliana kwamba Kristo alikuwa na sifa ya kiuungu kiasi cha kuabudiwa au kuombwa kwenye maombi yao. Kukataa kumuabudu Kristo ulikuwa ndiyo mtazamo uliokuwepo kwenye imani ya Kanisa la Mungu kwa kipindi cha karne kadhaa, wakiwemo Wawaldensian ambao imani yao kanisa la Siebenburg lilikuwa miongoni mwao walioamini hivyo. David aufungwa gerezani kutokana na msimamo wake na hatimaye aliuawa akiwa humo gerezani. Hugh Pope aligundua pia kwamba Budnaeus alidharauliwa na kuchukiwa kwa ajili ya kushikilia mtazamo huohuo wa David na alitengwa na kanisa lao mwaka 1584. Wawili hawa walikuwa wameongoka na kungia imani ya wale waliokuwa wanajulikana kama Waorthodoxy.

 

Wasosiniani wa kipingi hiki waliikataa katekisimu ya zamani na kuitengeneza nyingine mpya waliyoiita kuwa ni Kateksimu ya Racow ambayo ingawa iliandikwa na Faustus Socinius ilikuwa haijachapishwa hadi mwaka 1605, mwaka mmoja baada ya kufa kwake. Ilichapishwa kwa mara ya kwanza kwa lugha ya Kipolandi na kisha ikachapishwa tena kwa Kilatini mwaka 1609.

 

Wasosinian walikuwa wamejiimarisha Walijenga vyuo, wakaanzisha sinodi na kumiliki mitambo ya uchapishaji ambazo kwazo walimudu kuchapisha masomo mengi ya mafundisho. Machapisho haya yalikusanywa na Sandius yaliwa na kichwa cha somo Bibliotheca Antitrinitarianorum. Machapisho ya Faustus yamejumuishwa kwenye vitabu vinavyoitwa Bibliotheca Fratrum Polonorum.

 

Kanisa la Mungu huko Siebenburg, kwa upande mwingine, lilikataa mamlaka ya kanisa na kukataa kushirikiana na utaratibu wa kuchapisha machapisho mbalimbali. Eossi aliiandika kazi hii kwa kutumia mikono yake na ilikaririwa na wasaidizi wake.

 

Mwaka 1638 Wakatoliki wakasisitiza kuwa Wasosiniani waangamizwe. Dini hii ilikusudiwa kukomeshwa huko Ulaya lakini Pope anasema kwamba wafalme wengi waliipenda na kuipa msaada mkubwa kwa siri (ibid., p. 114). Ilikuwa ni kama kwa namna fulani ndiyo iliyokuwa inatawala huko Ulaya. Balozi wa Uingereza aliionya serikali ya Uholanzi kuwa Wasisiniani walikuwa wanaelekea huko wakitokea Poland, jambo ambalo lilifanyka kweli mwaka 1639. Mwaka 1653 ilikomeshwa huko kwa kufanyika makatazo ya kutishia watu.

 

Haikuweza kukubalika na kushamiri sana Uingereza, kama alivyojionea Pope, ingawaje mwaka 1612 Leggatt na Wightman walishitakiwa na kuhukumiwa kifo kwa kosa la kukataa uungu wa Kristo. John Biddle alisemekana kuwa walikuwa anachukuliwa kama mfuasi wa imani za Kisosiniani na alifukuzwa na Cromwell na kupelekwa kifungoni Kisiwani Scilly ambako alifungwa hadi alipoachiliwa na kurudi kwa amri ya kiwali wa wakati huo. Lakini alitiwa gerezani tena baada ya zama za Marejesho na alifariki mwaka 1662.

 

Hugh Pope kwa usahihi sana anakumbuka na kuandika (ibid.) kwamba Waunitarian wanajulikana mara zote kuwa ni Wasosniiani, lakini wana mambo muhimu wanayotofautiana kwenye mafundisho yao.

 

Tutaona kwamba neno Wayunitariani mara nyingi linatumika kimakosa na Wakatoliki na Pope analitumia neno hili kwa mtazamo mmoja tu, ambayo tunalichukulia kuwa sio sahihi. Wakatoliki wanachukulia majina haya ya wa Yunitarian, Arian na Socinian kuwa ni imani tofauti na ni maneno tofauti wakati kwamba Schaff, kwa mfano, aliwajumuisha hawa wote kwenye kundi moja tu la Wayunitarian (pamoja na tofauti nyingi walizonazo) kama tunavyoona kutoka kwenye kitabu chake kinachitwa Historia ya Kanisa la Kikristo [History of the Christian Church (Vol. II, pp. 571ff.)].

 

Wasosiniani wanaamini ifuatavyo:

1.      Biblia ina mamlaka yote lakini inatakiwa itafsiriwe kwa kumaanisha.

2.      Walikataa aina yote ya imani fumbo ("Imani fumbo kwa kweli zimeinuliwa na kutukuzwa sana kuliko imani zinazofikirika lakini wao pasipo maana wamezitukuza sana; na pasipo na sababu yoyote wameizima nuru, lakini pia wameitimiliza tu." John Crell (d. 1633) De Deo et ejus Attributis; cf. Pope, ibid.).

3.      Umoja, uhalisia, uweza juu ya yote, haki, na hekima ya Mungu vinapaswa kusisitizwa tangu tunapoongoka na kuwa kwenye imani hii.

4.      Uweza wa Mungu katika ukubwa usio na kikomo na wa kujua kila kitu vilichukuliwa kuwa ni zaidi ya uwezo wa mwanadamu na kwa hiyo  havina umuhimu kwa wokovu.

5.      Haki ya kwanza ilimaanisha kuwa Adamu hakuwa na dhambi na ndiyo kitu kilichomfanya aruzukiwe na tunu ya kipekee ya kuwa mtu mkamilifu; kwa hiyo Socinius alilikataa na kulipinga kwa nguvu zote fundisho la dhambi ya asili.

6.      Kwakuwa imani haipatikani kwa njia nyingine iwayoyote ila ni kwa kumtumainia Mungu, Wasosinian waliyapinga mafundisho ya Wakatoliki ya jinsi ya kuhesabiwa haki kwa maana ya namna waliyoamini wao. Hakukuwa na namna nyingine zaidi ya namna ya kimahakama kwa uopande wa Mungu.

7.      Kulikuwa na sacrament mbili tu lakini hawa walizichukulia kuwa sio muhimu kwa mambo ya imani, kwa kuwa hazikuwa na uwezo wa kumbadilisha mtu kutoka ndani (kwa hiyo, fundisho la imani ya kugeuka kihalisia kwa mkate na divai walilikataa na la uhakika wa kifo kwa mtu mzima anapoingia kwenye ubatizo na huenda kwa maswali).

8.      Waliupinga ubatizo wa watoto wadogo na mafundisho ya kwenda motoni. Bali watenda   dhambi watachomeka na kwisha kama myeyuko.

 

Uungu ni kitu muhimu sana kufundisha kwa wa Sosiniani. Kutokana na mtazamo wa makundi haya yote mawili, yaani ya Wakatoliki na Wayunitariani, waliendelea kuona kuwa Mungu hana utata kumjua kwake na ni mmoja. Walihitimisha kwa kusema kwamba tendo ka kutofautisha nafsi ni la uiharibifu dhana hii ya umoja wake. Kutokana na mtazamo huu wenye mashiko, walipinga fundisho na imani ya Utatu na kuliona halina maana wala mashiko. Wakatoliki wanauona mtazamo huu kuwa ni wa kupotoka kutoka kwenye mafundisho yao ya Tohara au utofautishaji wa Utatu ndani ya Uungu. Imani ya Kiditheist ya Herbert Armstrong, kama ilivyoenea tangu mwaka 1978, inajaribu kuafikianisha tatizo hili la Umoja na Utofauti huku wakijifanya kupinga imani ya Utatu na kumtenga Roho Mtakatifu kutoka kwenye mwambatano huu. Hili ndilo jambo lililolazimisha kuitishwa kwa mtaguso wa Constantinople mwaka 381 na kuishia kwenye imani ya kawaida na iliyiozoeleka na wengi kipindi hicho ya Kitrinitariani (sawa na alivyosema Gregory wa Nazianzus 380 BK, na kunukuliwa kwenye jarida la Maongozi ya Mungu (Na. 174) [The Government of God (No. 174)]. Ni sawa na zama za Wamakedonia ambayo inaitwa pia kama ya Waarian, na kwa hiyo inajaribu kuijumuisha elimu ya kumtukuza Kristo. Wanafunzi na wafuasi wa Armstrong walifikia uamuzi katika mwaka 1990, wa kutangaza kwamba Mungu na Kristo walijadiliana na kuafikiana nani miongoni mwao ashuke hapa chini ili atolewe sadaka (jarida la Worldwide News na ilitangazwa rasmi na mwinjilist G. Waterhouse, huko Canberra, Australia – kwenye Sikukuu ya Vibanda mwaka 1990).

 

Hata hivyo, Wasosinian, waliendelea kuyapinga mafundisho hayo kwa kusema kuwa hakuwezekani kuwa na usawa kati ya kitu kilichotengenezwa na aliyekifanya, na kwamba, hakuwezekani kuwepo dhana hii ya mtu kuishi hapo kabla na kisha aje na kuzaliwa tena maarufu kama Inkanesheni ya Mungu kana kwamba yeye anahitaji ama kudai usawa wa namna hiyo. Hata hivyo, kama kwa kutowezekana kokote, kulikuwa na utofauti wa watu kwnye Uungu, hakuna mtu wa kimbinguni anaeweza kuunganika na mwanadamu kama vile kusivyowezekana kuwa  na muunganiko kati ya watu wawili. Hoja nyingine iko kinyume sana na Maandiko Matakatifu. Aquinas anaelezea jambo la kwanza kutoka kwenye mtazamo wa Wakatoliki wa Summa, I, Q. xii, a. 1 ad 4 am (see Petavius kwa anayekumbuka).

 

Wasocsnian hawajawahi kuwa kile kinachoitwa Waariani kama walivyokuwa kina Campanus na Gentilis. Inaonekana kwamba Gentilis alikuwa ni mmoja wa waliokuwa kwenye jumuia asilia ya kale. Aliuawa kwa kukatwa kichwa huko Berne mwaka 1566 na baadhi walifupisha jina lake na kumuita Mtritheist kwake kama alivyomshuhudia Pope (tazama kitabu kinachoitwa A Short History of Valentius Gentilis the Tritheist, London, 1696 yaani Historia Fupi ya kina Vallentus Gentilis Mtritheist). Mtazamo wa Kiditheist unaweza kuangukia kwenye tatizo hili wakati Roho Mtakatifu akiwa hajalifunua au pale kwenye mafundisho ya imani ya Kitrinitariani. Hii imetokea pia kwenye Kanisa la Waadventista Wasabato ambalo limekuwa la Kiutatu tangu mwaka 1931 baada ya kifo cha Uriah Smith, na kwenye Kanisa la Worldwide Church of God kati ya miaka ya 1978 na 1993 ambalo hatimaye lilikuwa la Kiutatu pia.

 

Wakatoliki wanasema kwamba Socinius hakuwa Myunitariani aliyebobea sana, kama walivyokuwa kina Paulo wa Samostata na Sabellius, alimchukulia Roho Mtakatifu kuwa ni nguvu ya kawaida tu na ni utendaji wa Mungu, nguvu iwezeshayo utakaso.

 

Ilikuwa ni kwa mafundisho kuhusu Kristo ndipo Socinius alitofautiana na Wayunitarian, ingawaje alifundisha kumtukuza au kumwabudu Kristo, jambo ambalo Kanisa la Mungu lilikataa kufanya. Socinius aliamini kwamba Kristo alikuwa ni neno tu au logos lakini alipinga uwepo wake. Akiwa kama Neno wa Mungu, yeye alikuwa ndiye mkalimani au mtafsiri wake. Pope anasema (ibid.) Socinius alimtaja John akimtaja katika ubadilisho peke yake. Bilashaka hii ilichukuliwa kutoka kwenye neno lenye maana ya tohu na bohu kutoka Mwanzo 1:1-2. (Wazo hili limepokelewa sana na masalia yaliyoonekana na wachimbuzi wa siku hizi) kristo hatahivyo alikuwa amezaloiwa na mwanamwali kimiujiza. Alikuwa ni binadamu aliyekamilika. Alikuwa ni mwombezi wetu aliyechaguliwa, ila hakuwa Mungu, bali ni mtu mnyenyekevu. Kwa jinsi hii alipaswa kuheshimiwa kibinabdamu.

 

Wakatoliki wanaamini hii kuwa ni mstari mkubwa sana unaowagawa Wayunitariani na Wasosianisti (tazama kitabu cha Pope, ibid.). wakatoliki wanaamini kuwa Wayunitariani wanapinga kuzaliwa kimuujiza kwa Kristo na kwamba wanakataa kumuomba na kumtukuza kama Mungu. Pope anaamini kwamba kimsingi Wayunitariani wako sahihi sana.

 

Kwa hiyo, Wakatoliki wanaamini utofauti uliopo kati ya Waarian, Wayunitarian na Wasosiniani kuwa:

1.      Waarian wanaaini kuwa Kristo alikuwepo na kuishi zaa za kabla ya kuzaliwa kwake na mwanawali aliwa na Baba. Wakatoliki wanadai kwamba Waariani wanaamini kuwa Roho Mtakatifu anatokana na Mwana. Dhana hii inatokana na maandishi ya wale wanaitwa Waariani lakini ni wafuasi waliokuja baadae wa Ariani.

2.      Waunitarian wanaaminika kuwa wanapinga kuwepo muda kabla ya kuzaliwa kwa Kristo, uweza wa kimbinguni wa kuzaliwa, na pia kumuabudu Kristo. (Tunaiita imani hii ni yaa Uyunitarian wenye Msimamo Mkali na Wakatoliki wanapaswa kutofautisha jambo hili au imani hizi.)

3.      Wasosiniani wanajulikana kuwa wanapinga uwepo wa Kristo wa zama kabla lakini wanakubaliana na kuzaliwa kwake kimiujiza na pia wanamuabudu.

 

Tofauti hizi tutazielewa vizuri zaidi kwa kadiri tunavyoendelea kujifunza hapo chini.

 

Shutuma za kawaida za Wasosiniani haziwezi kuonyesha kwa usahihi sana mafundisho yao kwa kuwalaumu tu kulikofanywa siku za kabla ya kuchapishwa kwa Katekismu ya Racow mwaka 1605. Mashitaka yapo kwenye Katiba  ya Paulo IV, Cum quorundam, 1555 (Denz. 993) iliyoendelezwa na Clement VIII mwaka 1603 Dominici gregis. Zaidi ya yote, inawezekana kuwa hii katekismu isionyeshe maendeleo zaidi ya kimtazamo wa viongozi wa taasisi (tazama kitabu cha Hugh Pope, ibid., p. 115). Kutoka kwenye marufuku hii inaonyesha kwamba ilidhaniwa kwamwa mwaka 1555 na tena mwaka 1603 ndipo Wasosiniani walidai yafuatayo:

a.       Hakuna kitu kinachojulikana kama Utatu;

b.      Kristo hakuwa na uhusiano wa kimungu na Baba na Roho Mtakatifu;

c.       Kwamba hakutungwa mimba yake kwa uwezo wa  Roho Mtakatifu bali alizaliwa na Yusufu;

d.      Kwamba kifo na mateso yake havikufanyika kwa kusudi la kut uletea sisi ukombozi;

e.       Kwamba mwanamwali mbarikiwa sio mama wa Mungu na wala hakurudia hali yake ya uwanawali baada ya kuzaa.

 

Kwenye Katekismu ya mwaka 1605, Wasosiniani walisema wazi kabisa kwamba Kristo alitungwa kwa mimba ya kimiujiza lakini Pope amasema (ibid.) kwa jambo hili haieleweki. Kwa hiyo, wakosoaji wanahoja zisizo sahihi na wanatunia ushahidi usio sahihi. Tatizo linaloonekana kuwa sio sahihi kwenye itikadi hii ya mafundisho ya Wakatoliki ni kwamba wanashikilia kuamini Wasosiniani wanapinga uwepo wa Kristo kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake na mwanamwali duniani. Lakini tunapokuwa tunapotathmini maelezo yao kuhusiana na Yohana kuhusu Masihi condemnations rest on incorrect and contradictory, tunaona kwamba hoja za Wasosiniani zimetuama kwenye Yohana 1:10 inayojulikana kama ni orodha ya kizazi au uzao na haimaanishi kizazi chenyewe halisia. Hii inaonyesha fuindisho la Uungu. Maelezo ya uumbaji yaliyoko kwenye Mwanzo 1:1-2 yanachukuliwa sasa zaidi ya maelezo halisia kutokana na kile tunachokijua umri wake wa duniani na historia yake. Haiwezekani kuafikinisha upingaji wa kutokuwepo hapo kabla kwa Masihi na uzao wa hapa duniani ulioandikwa kwenye Yohana 1:10. Wasosiniani kwa hiyo hawakupaswa kushikilia mafundisho ya Uyunitarian wenye itikadi kali na walipaswa kuwa wanawasaidia Wayunitariani, ambao wamekuwa wanaitwa kimakosa na Wakatoliki kuwa ni Waariani. Msimamo huu kwa hiyo umeyagawa makundi mawili na yanaipa historia ya Waaldensian. Uwezekano mkubwa wa maelezo ni kwamba Wayunitariani wenye msimamo mkali walikuwepo kwa idadi ndogo kwenye maakanisa ya Ulaya lakini hawakuuwakilisha mtazamo wao wa kweli wa uliokuwepo wa kimafundisho. Kwa kiasi kiubwa, kwa namna hiyohiyo wanaendelea kuwepo hata leo kwa idadi ndogo ilikuwa kwenye Makanisa ya Mungu.

 

Kwa mtazamo huu, kama ulivyoorodheshwa na Wakatoliki, Kanisa la Mungu liliyachukulia machache yake na iliaminika kwamba Kanisa la Mungu huko Ulaya, liwe lile la Siebenburg au kama lilivyokuwa lile la Wawaldensian, yalikuwa ama ya wa Socinian ama la Kikatoliki waliojulikana kama ni wa Yunitariani wenye itikadi kali, kama vile, wale wanaopinga uwepo wa Kristo siku za kabla ya kuzaliwa kwake duniani, kama ni makosa ya kiuelewa. Kwa uzuri zaidi ni kwamba ilirahisishwa sana na ilionyesha tofauti kubwa. Inaweza kuwa pia kwamba Wakatoliki wanalifanyia kazi tu neno hili la kuwepo kwa Kristo kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake duniani ili kushamirisha mafundisho yao. Kama neno hili la kuwepo kwake kipindi-kabla ili kumaanisha madai yao ya kuwa alikuwepo hata kabla ya kuumbwa kwa Malaika, badala ya kuonyesha uwepo wake katika zama za kabla ya Kuja kwake na kuzaliwa hapa duniani, na ndipo tuwe na maana fafanuzi ya neno hili. Kama hili ndilo suluhisho la mgongano huu wa kifikra kwenye maelezo ya Wakatoliki ya mafundisho ya kidini ya Wasosinian, kisha tofauti yao uadilifu wao wa kielimu una maswali makubwa. Kwa kiwango chochote mtazamo wa kiitikadi ya Ugeukaji wa \Mkate na divai kuwa mwili na damu halisi pia inafanya kuwepo kwa maswali.

 

Mtazamo wa Kanisa na maeneo mengine vinaweza kuelezewa vizuri sana kama yanafuata.

 

Kanisa la Mungu mara zote limekuwa na uhusiano na Kristo na Mitume, likiwa lenye mrengo wa Kiyunitariani. Lilishikilia kuaminini ifuatavyo:

1.      Kuna Mungu Mmoja tu wa Pekee na wa Kweli na ndiye Baba wa wote.

2.      Kwamba Kristo ni msaidizi na ni Mwana wa Mungu na sio Mungu wa pekee na wa kweli. Bali yeye alikuwa amezaliwa na kuwa mwana wa \Mungu (Yohana 1:18; tazama kitabu cha Irenaeus kwa maandiko sahihi, sawa na Marshall's Greek-English Interlinear RSV).

3.      Kwamba Kristo na Wana wengine wote wa Mungu wametokana na Baba na kwa sababu hii kizazi chao kinatokana na kitendo cha uhiyari na ndilo tendo la uumbaji (Malaki 2:10; Waebrania 2:11 RSV; sawa na Waefeso 3:9 RSV. Kumbuka kwamba tafsiri ya KJV imeongeza neno na Yesu Kristo ambalo halimo kwenye nakala asilia za kale; tazama tafsiri ya Companion Bible, n. hadi aya ya 9 na pia katika Ufunuo 4:11).

4.      Kristo alikuwepo hata kabla ya kuzaliwa kwake duniani aliwa kama Mjumbe wa Mungu na kwamba Yule aliyekuwa akinena na nabii Musa pale Sinai na Malaika wa Anago la Kale (Mwanzo 48:15-16; Isaya 9:6 LXX; Zekaria 12:8; Matendo 7:38; Wagalatia. 3:19). Hakuna mtu aliyewahi kumuona \Mungu (Yohana 1:18; 1Timotheo 6:16). (Tafsiri ya Septuagint (LXX) inamtaja Masihi kutoka kwenye Isaya 9:6 kuwa ni Mjumbe wa Shauri Kuu).

5.      Kristo alikuwa na haiba ya kimbinguni akiwa amezaliwa na mwanamwali bikira ili awe mkombozi wa wenye dhambi.

6.      Mariamu (Maria) alipata mimba na kuzaa watoto wengine na Yusufu ambao wametajwa kwenye Biblia kuwa ni ndugu zake wa kike na wa kiume Kristo.

7.      Wahipinga kitendo cha kuabudu kiumbe kingine zaidi ya kumuabudu Mungu Baba.

8.      Walikuwa na Sakramenti mbili.

 

9.      Hawakuwa na alama ya msalaba wala hawakuitumia.

10.  Mafundisho ya Mkate na divai kugeuka na kuwa damu na mwili halisi hayaonekani kuwa yalifundishwa na wao.

11.  Roho Mtakatifu ilikuwa ni uweza au nguvu itendayo kazi na uweza wa Mungu inayowawezesha watu kuwa wana wa Mungu na kustahili uhusiano wa Baba kama Kristo alivyofanyika kuwa mrithi pamoja na Baba (tazama majarida ya Roho Mtakatifu (Na. 117) na Kurithi Pamaja Baba (Na. 81) [The Holy Spirit (No. 117)  and Consubstantial with the Father (No. 81)].

12.  Kristo hakujaribu kamwe kutafuta usawa wa namna yoyote ile na Mungu, bali alijishusha na kujifanya hana stahili yoyote, akauchukua mwili wa kibinadamu na akawa mtii hadi kufa (Wafilipi 2:6, RSV). Akawa na huduma bora zaidi (Waebrania 8:6). Kwa kujitoa sadaka mwenyewe alifanyika kuwa mpatanishi na mwombezi wa Agano Jipya alitakaswa na viumbe wa mbinguni na sio vya kiduniani (Waebrania. 9:14,15,23). Kristo aliyejitoa sadaka pamoja na wale wote waliojitoa sadaka wote wanaasili moja tu (Waebrania 2:11 RSV). Kristo alikuja ili kuyafanya mapenzi ya Mungu na baada ya kuteswa kwake ili atolewe sadaka mara moja kwa ondoleo la dhambi milele, ameketi mkono wa kuume wa Mungu (Waebrania 10:5-9,12). Kristo aliyavumilia mateso pale mtini kwa neema ya furaha aliyokirimiwa mbele yake na kwa sababu hii ndiyo maana amepewa heshima ya kuketishwa mkono wa kuume wa Mungu (Waebrania 12:2). Mungu anawachukulia Malaika na watakatifu wote kama wana na tu watiifu na mali ya yeye Mungu wa Roho zote na ambaye anaturudi tukoseapo na kutukemea kwa faida yetu. Kristo alivumilia na akawa mwana wa Mungu mwenye uweza uliotokana na kufufuka kwake toka kwa wafu (Warumi 1:4).

 

Jambo hili limeendelea kuaminika hivyo kwa kipindi chote cha historia ya Kanisa kama tunavyoona kutoka kwenye rekodi za mateso ya kidini (tazama jarida la Jukumu la Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu Yanayozishika Sabato (Na. 170) [The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)]. Tunajua kwamba mtazamo au jambo hili liliaminika sana na kanisa la Siebenburg kama tulivyo na hiatoria kamilin ya imani yao kutokana na kazi ya uandishi aliyoifanya Rabi \Mkuu wa Budapest alipokuwa akirudia matukio ya karne iliyopita (DIE SABBATHARIER IN SIEBENBURGEN, Ihre Geschicte, Literatur und Dogmatik, Budapest, Verlag von Singer & Wolfer, 1894’). Hawakuwa Wayunitari wenye imani kali; walikuwa Wayunitari wa msimamo wa kadiri kama tulivo sisi. (Tazama jarida la Wasabato wa Transylvania, AB2 [The Sabbatarians in Transylvania A_B2.)] 

 

Imani nyingine iliibuka huko Ulaya ikaongezeka kwenye imani hizi zote, yaani za Wayunitari wenye itikadi kali na ambayo ilipinga fundisho la kuwepo kwa Kristo siku kabla ya kuzaliwa kwake duniani na Usosinian ambao ulidaiwa kuwa na mafundisho potofu tumeona hapo juu. Imani ya Wamanichean Dualism pia walijiengua kama walivyofanya Wakatharist Montania pamoja na mafundisho mengine mengi ya kiasitiki yaliyotokana na imani ya Kinostiki na Imani fumbo ambayo yameelezewa ka kufafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Imani ya Ulaji wa Mbogamboga Tupu na Biblia (Na. 183) [Vegetarianism and the Bible (No. 183)].

 

Makanisa ya Mungu kwenye karne za kumi na tisa na ishirini yalikuwa na mafundisho kama hayahaya kama yalilvyokuwa yanafundishwa na kanisa kipindi chote cha historia yake. Upotoshaji wa kugeuza uliofanywa na makanisa ya SDA na WCG ulioelezewa hapo juu haukuwepo huko nyuma. Sifa zilizotolewa na Wakatoliki kwa mafundisho ya Wariani ni sahihi, hatimaye Waariani walitofautiana baadae kimafundisho na kanisa la kwanza kwa suala ya Roho Mtakatifu na hawakujua kazi zake. Hii, kwa kweli ilisababisha wafanyiwe propaganda za uwongo za kuchafuliwa na Wakatoliki na kutokuwepo kwa kila maelekezo yanayothibitisha kwenye kanuni zao zinazojulikana kama Thalia au kazi nyingine walizozifanya ama kina Arius, au Eusebius, au Asterius, au za askofu mwingine yeyote wa upande wao. Jina la Waariani limetolewa kutokana na jina la mtu mmoja wa upande wao ambaye alimtangulia kwa kipindi kirefu. Ni mazea waliyonayo Wakatoliki ya kujaribu kuliita Kanisa kwa jina la mtu binafsi ili wafanikishe kuvunja uendelevu wake. Mbinu na tabia hii inasaidiwa na kitengo cha kidini kinachopendelea kuita vikundi vyao kwa majina yao na tabia hii imeshamiri sana hasa huko nchini Marekani.

 

Tofauti ndogo ya msingi iliyopo kati ya hawa Watrinitariani waliobebea kwenye imani hiyo na wale Wayunitariani wa msimamo wa kati kwenye Kanisa ni:

1.      Wote wanaamini kwamba kuna Mungu Mmoja tu wa Pekee na wa Kweli. Hatokani na kitu chochote na anaishi kwa uweza wake mwenyewe (Kutoka 3:14). Hakuna kitu wala mtu yeyote anayelingana au wa kumlinganisha na yeye (Isaya 40:17; sawa na Kitabu cha Hekima 11:23). Mungu ndiye mwanzo na mwisho wa kila kitu (Isaya 48:12; sawa na Ufunuo 1:8). Vitu vingine vyote vinatokana na Mungu Baba na kwake yeye na kwa yeye kupitia kwa Yesu Kristo (Warumi 11:36; 1Wakorintho 8:6; Wakolosai 1:16). Mungu ndiye Bwana aliye yote katika yote na wapekee (Zaburi 46:12; Isaya 44:24; Waebrania 1:10). Kitabu cha fasihi cha Catholic Encyclopedia (Vol. IV, article ‘Creation’, p. 471) kinasema: Kwamba maandiko haya yanayofanana yanadai kwamba Mungu ndiye muumbaji wa vitu vyote yanaonyesha dhahiri kuhitaji maelezo zaidi kufafanua. Andiko haliko sawa kama tunavyoona.

2.      Wote wanakubalia kuwa mwana ni uzao wa Baba.

 

Mambo yaliyoko kwenye jambo hili ni haya yafuatayo:

1.      Watrinitarian wanaamiki kuwa:

·         Mwana alikuwa ni mwana aliye na wadhifa sawa kwenye Uungu. Uzao wake haukuhusiaka na kwenye tendo la uumbaji na wanaamini kuwa alikuwa ni huyu Mungu wa kweli alitokana na Mungu wa kweli (kinyume na inavyosema Yohana 17:3).Mungu alikuwa ni Baba aliye ndani na Krisro alikuwa ni Mwana aliye ndani.

·         Wana wengine wa Mungu hawakutokana na uzao wa Baba na kwa namna hiyohiyo akiwa na uhusiano wenye hadhi sawa na Baba. Hakuna andiko linalowapa mashiko kwa madai yao haya na kigezo chao kimewekwa kwenye falsafa za kina Plato, Aristotle na Plotinus ili kuhalalisha madai yao haya. Tofauti hii haikupata suluhu hadi ulipoitishwa Mtaguso wa Nne wa Lateran mwaka 1215.

·         Tangu kipindi cha Augustine, ndipo vipindi vilihesabiwa kuanzia kipindi cha uumbaji wa Malaika. Kwa hiyo, kuna tofauti ashirio na tofauti isiyoelezeka kati ya kuumbwa wa huyu Mwana na ule wa wana wengine wa Mungu walioko huko Mbinguni. Madai haya yana umuhimu kutokana na andiko linalohusiana na mwanzo wa zama au vipindi.

·         Basi kama Mwana hakuwa ndiye huyu Mungu wa kweli, basi asingeweza kusamehe au kuwahesabia haki watu kwa kuwapatanisha na Mungu. Tena madai haya hayajapewa mashiko na Maandiko Matakatifu bali yanatuama tu kwenye mawazo ya kina Plato na Aristotle.

 

2.      Mitaguso iliyofuatia pia ilitangaza maazimio yafuatayo:

·         Kristo hakuonekana kwenye Agano la Kale au na mtu yeyote yule kipindi chote cha kabla ya Kuzaliwa kwake hapa duniani.

·         Kristo sio yule Malaika wa Yahova, elohim wa Agano la Kale aliyemtokea nabii Musa na kumkabidhi Torati huko Sinai, ikiwa kwamba hakuna aliyewahi kumuona Mungu wakati wowote, na kwa hiyo asingeweza kumuona Kristo kama angekuwa Mungu.

·         Kristo anauweza wa kujua kila jambo na pale aliposema hakujua mambo fulani ilikuwa ni usemi tu wa kimafumbo.

 

Ushahidi wa Kanisa la Kwanza unaonyesha kwamba kulikuwa hakuna mtazamo wa kikalti kuhusiana na malaika na mara chache waliwakilishwa kwenye michoro ya Wakristo hadi kipindi cha Constantine. Michoro ya zamani zaidi ambyo malaika alionekana lilikuwa ni tukio la Kuvumbuliwa (kwenye karne ya pili) kwa kaburi la Prisila (tazama Cath. Encyc., Vol. I, p. 485). Michoro ya malaika mwenye mabawa hakuonekana kipindi cha kabla ya Constantine. Hawakuwa wanajitokeza kamwe hadi kuwe na umuhimu wa kihistoria na hata hivyo haikuwa mara zote wakijitokeza (ibid.). njiwa alikuwa anaonekana kuwakilisha malaika wakiwa tanuruni mwa wana wa Kiebrania katika michoro ya ya kaburi la Prisila. Katika karne ya nne michoro iliyokuwa inaonyesha jambo hilohilo, mkono wa Mungu uliwekwa mahala pa malaika au mjumbe wa mbinguni. Tangu kipindi cha Constantine aina mpya ya malaika mwenye mabawa alionekana kuchorwa kwenye michoro ya Wakristo huenda ilituama kweye kile kilichojulikana kama Ushindi (ibid.). mfano za zamani sana unaojulukana kuwa upo hata sasa wa malaika mwenye mabawa aliyekuwa anaonekana kwenye imani ya bas kutoka Carthage na alionekana kwa muonekano wa pembe za Mikaeli, wote wawili kutoka karene ya nne. Sanamu (kwenye Jumba la Makumbusho la Uingereza) ina fimbo kwenye mkono wake mmoja na kuyashinda ya dunia na msalaba kwa upande mwingine. Kwenye karne ya tano, tunawaona malaika wakishirikishwa pamoja kwenye michoro iliyodaiwa kuwa ni ya Kristo na Bikira Mariamu. Jingo linaloashiria ushindi wa Mary Majors unamuonyesha malaika Gabrieli mwenye mabawa akiruka angani kumwendea Mariamu ambaye amezungukwa na kundi la malaika wenye mabawa. Mnamo karne ya sita michoro iliyojulikana kama Hierachia coelestis ya Dionysius wa uwongo ilifanya kazi kubwa na muhimu katika kudanganya watu kuhusu dhana hii ya malaika. Hadi kipindi hiki mtazamo kuhusu nyadhifa na utendaji kazi wa hawa Malaika wa Mbinguni ulikuwa haujatofautishwa kwa maana kwamba kama tuliyonayo siku za leo kufundishwa kuhusu hali zao na kazi zao. Tangu kipindi kile na kuendelea, uhusiano wa malaika na Mungu uliwakilishwa kutoka na imani za Mashariki kwa namna ya mtenganisho wa viwango au madaraja mbalimbali kimahakama wanapofanyia kazi kulingana na jinsi wanavoonyesha utii wao kwa Wafalme (Cath. Encyc., ibid., p. 485b). Maandiko ya vitabu vya Wakristo wa zamani, sambamba na michoro yake, vilikuwa na habari chache sana zinazowaelezea malaika. Mtazmo na imani ya Wakatoliki ni kwamba pamoja na imani maarufu inayojulikana na kuaminiwa na dini nyingi ni kwamba ilkuwa ni muhimu kuwa msisitiza fulani kuhusu umoja wa Mungu (ibid.).

 

Mwendelezo wa imani kuhusu malaika ulikuwa wa muhimu ili kufanya tofauti njema kati ya Wana wa Mungu walioko Mbinguni na kazi ya Kristo kama ilivyokuja kuamuliwa tangu mwaka 381 kwenye Mtaguso wa Constantinople. Kutoka Mtaguso wa Chalcedon jukumu na utendaji wa wana wa Mungu kama wajumbe na roho zinazohudumia yalipunguzwa kwa kiasi cha kwamba uwepo wao ulikuwa kudharauliwa na neno malaika lilikoma kuwa ni la kazi zinazoeleweka za mwana wa Mungu kukondolewa mpango wa Mungu. Akawa ni mtu tu wa aina yeke mwenyewe ambaye alimudu kuwa na maisha madogo kwenye majukumu muhimu ya Masihi na wateule. Imani hii iliwekwa ili kufikilisha lengo la kuyainua mafundisho ya elimu ya Ukristo na kumuondoa Kristo kwenye uhusika wake wa uumbaji kwa namna yoyote ile kwa mujibu wa mafundisho ya kimapokeo ya waamini utatu. Imani hii haikuwa ya Kanisa la kwanza na neno malaika lilionekana kuwa ni kama utendaji wa wana wa Mungu. Upunguzaji huu wa mabishano ni tatizo moja kubwa hadi leo katika kuelezea kosmolojia ya kweli ya kibiblia kwa wanaoanza ambao hawajaisoma bado Biblia kikamilifu. Justin Martyr (Apol. 1:6) anasema kuwa hawa matakatifu wanaoshirikiana na malaika Wema walishikiliwa kwa heshima kubwa sana. Athenagoras anazielezea kazi za hawa Malaika watiifu ambao Mungu amewaweka kwenye maeneo mbalimbali, ili wajipange wenyewe kwa mambo yote na mbinguni na duniani (Legatio x). Katika karne ya nne, Eusebius wa Caesaria anatofautisha kati ya imni potovu waliyokuwanayo wao na ibada anayofanbyiwa Mungu (Demonstratio evang., III, 3). Mwishoni mwa karne ya nne, Ambrose wa Milan anakubaliana na maombi kwa wao (Cath. Encyc., ibid.). kwa hiyo tunaona kwamba mafundisho kuhusu roho yalijiingiza kwenye Ukristo. Hawa kina Athanasians walipunguza nafasi ya wana wa Mungu na uhusiano wao na Baba na kufanya kuwa kuna viumbe wengine wanaoshirikiana naye kuunda Utatu.

 

Wakati huohuo walianzisha imani potofu iliyoendekeza maombi na ibada za kuwatukuza wao na Mariamu kuwa ni viumbe waliofufuka. Mafundisho ya kwamba damu iko halisi kwenye divai tangu kipindi hiki yaliwaondoa Malaika kwenye ushirikiano wao na Mungu, wakisisitiza imani ya Utatu. Litania nyingi za kale zaidi tangu kipindi hiki zililenga kwenye Utatu na hatimaye kwa Mikaeli (maana yake ni nail kama Mungu) Who is like God) na Gabrieli (maana yake Mtu wa Mungu) na hatimaye Mariamu (ibid.). Tofauti hizi tulizoziona hapo juu zilifanyika kuwa ni msingi wa migawanyiko kati ya Kanisa la Kweli na na Waathanasian (au Ukristo uliochanganya na imani za kale).

 

Haikuwa hivyo hadi katika Mtaguso wa Nne wa Lateran mwaka 1215, uliojadili imani wanayofundisha waumini wa namna Kuwili mingoni mwa Wacathari wa Wakialbigensia kwamba Kanisa la Roma liliotangaza kuwa malaika waliumbwa (kama ilivyopingwa na Kristo ambaye hakuwa emeumbwa) na kwamba wanadamu waliumbwa baada yao (kwa mujibu wa tangazo liitwalo Firmiter; cf. Cath. Encyc., article ‘Angel’, Vol. I, p. 476). Kwa kweli, Kiebrania kina neno rahisi tu la kuwaita hawa la malak linalotokana na sina la neno lak lenye maaaa ya anayekwenda au aliyetumwa, ambaye ni mjumbe. Malaika wa uwepo wake aliyetajwa kwenye Isaya 63:9 na tafsiri ya the LXX inamtaja kuwa ni Masihi, Malaika wa Shauri Kuu. Aquinas anatangaza kuwa malaika hawakuwa na hadhi sawa na Mungu bali walikuwa wameumbwa ex nihilo. Kwa sababu hii Aquinas analinda utofauti uliopo kati ya Kristo na wana wengine wa Mungu. Kutoka kwa Tauler (d. 1361) na wafuasi wake Wadionysian ndipo tofauti ya kimadaraja kati ya Roho ilifuatia.

 

Ibada

Dhana na sababu ya kuabudu inamaanisha ni mchakato wa kutoa heshima. Inaendana na amri. Inapaswa kumuelekezea moja kwa moja Mwenyezi Mungu na kwa ajili hii inapaswa kuwa ni ibada tukufu na yenye unyenyekevu wa hali ya juu sana ya kumtukuza. Ibada hii ya kumuabudu Mungu kitakatifu yaani latria, inapaswa afanyiwe Mungu peke yake (Cath. Encyc., Vol. XV, article ‘Worship’, p. 710). Wakati ibada kama hii (dulia; hyperdulia ya Mariamu) inapoelekezwa kwa wengine, basi haielekezwi moja kwa moja kwa Mungu, bali inaelekezwa kwa wao kwa imani kufananisha uhusiano wao na Mungu. Aina hizi mbili zote zinatokana na dhana ya kumpa heshima yaani proskuneo au ulegevu kutoka kwenye \Kiyunani. Kwa hiyo, heshima wanayopewa Kristo na malaika wateule inatokana tu na uhusiano wao mwema na Mungu. Kwa namna hii, tofauti kati ya Watrinitariani na Wayunitariani ni ile tabia ya kumwabudu Kristo kwa kisingizio tu cha uhusiano wake na Mungu Baba nay a kuwa ni wa pili kihadhi–wakati mwamba W#atrinitaariani kwamba ni imani potofu ya madhehebu yafuatayo  

 

Tofauti ya Waprotestant

Tofauti iliyoko kati ya Wakatoliki na Waprotestant Waamini Utatu inaonekana kuwa endelevu na inaongezeka kutokana na malumbano yaliyopo hapo juu. Uprotestant una mitizamo miwili. Wa kwanza ni ule wa Luther, ambao umechukua mafundisho yaliyofundishwa na Kanisa siku nyingi kabla yake, imani iliyojulikana kama Sola Scriptura, au  ni Biblia peke yake ndiyo mamlaka yetu. Kanisa la Anglikana na mengine yanakubaliana kuwa yaliyoamriwa na Mitaguso yalikuwa sahihi hadi ilipofikia Mtaguso wa Chalcedon mwaka 451 na kuwafanya waungane nao kimafundisho sawa na Wakatoliki wa Roma ila kwa kiwango pungufu kidogo. Kanisa la Kilutheri halifuati mafundisho haya Luther nce are tainted in the same way doctrinally as Roma—vinginevyo wangeweza kuirudisha kweli asilia iliyopotoshwa kuliko ile kidogo waliyoirejesha. Harnack anasema kwamba Ukristo umenajisika kwa imani juu ya miungu wengi au Polytheism na umeingiza mambo mengi kadhaa yanayotokana na imani asilia za kipagani (Das Wesen des Christentums, Berlin, 1900, pp. 126,137-138,148). Hii imesababisha kuwepo malumbano ya kimsingi kati ya kanisa kongwe la kale na Makanisa ya \Mungu kwa kipindi cha karne kadhaa sasa.

 

Imani ya Ubinitariani, ambayo inapaswa pia iungane na malumbano haya, inakuwa ni mchepusho mwingine wa kimhimili ambao hausimami sawasawa na ukweli na, kwa hiyo, haukudumu kimafundisho kwa namna yenye kumaanisha.

 

Kanisa na Ibada

Kristo alianzisha Kanisa moja tu lenye Bwana mmoja na imani moja, ubatizo mmoja na Mungu mmoja Baba wa wote (Waefeso 4:5-6). Ubatizo huu unawakilisha ibada yote, ambao unapaswa kuwa ni mmoja, unaomlenga Mungu mmoja na kwa Kristo huyohuyo (Cath. Encyc., article ‘Worship’, ibid.). imani hii haijabadilika bado Kanisa bado linamuabudu Mungu huyohuyo na ni Baba wa wote. Muntgu anastahili kuabudiwa kama ishara ya utakatifu na haki, na suala hili la kuabudu sio la hiyari kwa viumbe wake wote (Cath. Encyc., op. cit.). haki na utakatifu ni neno moja lenye maana moja pia (tsedek) ni la lugha ya Kiebrania. Kuabudu kifaragha na kwa wazi hakutoshi. Jamii inapaswa imheshimu na Wakristo wanapaswa kukutanika pamoja kumuabudu na mumsifu na kumtafakari yeye (ibid.).

 

Wamontani kwenye karne ya pili walianzisha imani potofu ya kumuabudu Roho Mtakatifu, kama walivyokuwa wakitarajia kitendo cha Roho kuja na kuchukua mahala pa wana na kuitangaza injili iliyokamili zaidi. Imani hii ilishinikizwa na kupelekea kuitishwa kwa Mtaguso wa Nne wa Roma mwaka 380 ambapo Papa Damasus aliwalaani na kumshutumu mtu yeyote anayekataa fundisho la kwamba Roho Mtakatifu anapaswa kuabudiwa pia, sawa na Baba na Mwana (ibid., p. 711). Ndipo mwaka uliofuatia (381) kwenye Mtaguso wa Constantinople, ndipo Roho Mtakatifu aliongezwa kwenye Uungu na kuanza kwa Utatu lakini hauikuwa imefanikiwa sana kama ilivyokuwa Wakapadokia walivyokuwa wamependa. Jambo hili lilianzisha utata uliopelekea tofauti kubwa nyingine kati ya Kanisa na Waamini Utatu.

 

Wakatoliki walikubali (ibid.) kwamba Kristo aliadhimisha kwa umakini sana desturi zote za ibada za Wayahudi (ikiwemo Sabato na Sikukuu zilizoamriwa) kwa kuwa kutoadhimisha yeyote moja wapo kati ya hizo kungeibua upinzani ambao ungeweza hata kuelezewa kwenye maandiko ya Injili. Alichokuwa anapingana nao kilikuwa ni jinsi wanavyoadhimisha lakini sio ukweli ulikuwapo kuhusu maadhimisho ya Sabato.

 

Kanisa la Kweli

Dini ya kikatoliki imejeribu kwa wakati wote kuzika uendelevu wa Kanisa kwa kuliwekea mapingamizi kadhaa kwa kosa la kuyapinga mafundisho yhao. Hesabu za kihistoria na mafundisho haviko sahihi kutokana na kupotoka kwa watu waliohusika na usiri wa Kanisa lililokuwa kwenye mateso. Kanisa Katoliki limekuwa likilitesa Kanisa la Mungu kwa kipindi cha karne nyingi. Mnamo mwaka 1179 Mtagudeo Mkuu wa Tatu wa Lateran ulilipiga marufuku Kanisa linalojulikana la Wavallenses tangu mwaka ule. Papa Lucius III alitoa amri Kuu ya kuwatenga huko Verona mwaka 1184 kwa kuwa marufuku yanayotolewa na Kanisa lililo na ujtii ni ya Mungu na siyo ya mwanadamu na walikataa kuiacha imani yao. Mkutano Mkuu kati ya Kanisa na Wakatoliki uliitishwa na kufanyika mwaka 1191 na ulifuatiwa na ule wa pili wa Parmiers mwaka 1207. Mnamo mwaka 1192 askofu Otto wa Toul aliamuru Wawaaaldenses wote wafungwe minyororo na wapelekwe kwenye mahakama ya kiaskofu. Mwaka 1194 Alphonso II wa Aragon aliamuru wahamishwe na kupndolewa kutoka kwenye maeneo ya utawala wake na kauamuru wanyimwe misaada ya nyuma na chakula. Mtaguso wa Genoa (1197) ulikazia hukumu hii na kuamuru wauawe kwa kuchomwa moto mbele ya Kanisa. Kutoka hapo, walijaribu kuua ama kulikomesha kabisa Kanisa kwa mbinu mbalimbali zilizowezekana. Uwepo wa mafundisho ya kizurshi na vikundi vingi vya upotoshaji vilisababisha muathiriko wa utambulisho uhalisia wa mambo lililoyafanya kanisa Katoliki katika historia yake na historia yake ikawa ya uwongo kabisa wakijaribu kuliunganisha Kanisa lao Petro Waldo na katika karne ya ishirini na kujivunia mafundisho yao na athari zake (tazama majarida ya Mgawanyo wa Makanisa Yanayozishika Sabato (Na. 122) na  Wajibu wa Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu Yanayozishika Sabato (Na 170) [General Distribution of the Sabbath-keeping Churches (No. 122) and The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)].

 

Kristo ana Kanisa moja tu – lililo kwenye mamlaka mbalimbali ya kimaongozi au kiutendaji kama anavyosema Mtume Paulo (1Wakorintho 12:6). Kanisa hilo halijawahi kuacha kufanya kazi zake na wala halijabadili mafundisho yake ya msingi kwa kipindi chote cha miaka elfu mbili sasa. Kanisa Katoliki wanataka watu waamini kuwa wao ndio Kanisa hilo. Madai haya ni ya uwongo. Kristo hajaanza kazi yake karne hii na wala hajabadilisha imani na mafundisho yake. Na Kristo ni yeye yuke, jana, leo na hata milele. Sisi tu warithi wa kweli wa imani hiyo waliyopewa watakatifu mara moja tu (Yuda 3).

q