Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[021J]

 

 

 

 

Ufafanuzi Kuhusu Haggai


(Toleo la 2.5 20060910-20140905)

 

Mungu alimuagiza Haggai kutoa unabii juu ya matengenezo na ujenzi wa Hekalu. Maandiko yanamsifu Zakaria pamoja kuwa yu kuwili katika tabia ya asili. Huelekeza katika mfumo wa kipindi cha miaka elfu moja pamoja kuongoka kwa watu wa mataifa.



 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Barua pepe: secretary@ccg.org

 

 

(Hati miliki © 2006, 2014 Wade Cox)

(tr. 2012)

 

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakaotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


 

Ufafanusi Kuhusu Haggai



Utangulishi                                    

Jina Haggai asili yake inatokana na neno Haghu, karamu au sikukuu. Na kifungu hiki kimetokana na mwezi mwandamano, ambayo Bulliger kifupi anakili mwandamizi wa Biblia, fn 1) kuwa kama Sabbato ya mwezi mwandamano. Ni mwezi wa Elul ulikuwa mwaka wa pili wa atamu ya uongozi wa Dario mfalme wa wajemi ndio wakati agizo la kukamilisha hekali ulitolewa na Yehova kupitia kwa Haggai.

 

Andiko hili basi ni agizo kutoka kwa Yehova kwa Yuda ukiendeleshana na ule unabii uliotolewa kupitia Zakaria.

 

Amri hii ilitolewa katika mwaka wa kwanza wa sikukuu sabini (f10) kwanzia kufungwa kwa Edeni unakamilishwa na sikukuu ya mwaka wa 424/3 BCE, na hekala sasa linaudwa upya. Hili ni angizo la pili lililotolewa na Mungu walakini kazi ya ujenzi ilitamatishwa kwa kipindi Fulani tokea kutolewa kwa amri ya Cyrus kimeendelea hadi utawala wa Aritaserises wa kwanza ambaye alitamatisha ujenzi na ujenzi huu ulitamatishwa hadi mwaka wa pili wa utawala wa Dairo mchemi (tazama somo hili Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi mpya wa Hekalu [013]) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)].

 

Kwa ajiri ya kupuusa kwa Wayuda Mungu amenena dhidi yao. Ujumbe huo umejengwa katika sehemu nne.

1.      Neno la Yehova. Andiko tulo limeanza na lawama kwao kwa ajiri ya kuuza maagizo ya Mungu (Hag 1:1-4).

2.      Hapo matamshi ya watu yameshuhudiwa na Yehova.

3.      Tena neno la Yehova limetolewa.

4.      Matamshi ya watu yametolewa na kujibiwa na Yehova.

Mungu kunena kupitia kwa manabii ni msemo wa waibrenia amabayo ni, “kwa mkon wa”. Hapo hapo hubainisha kusudi lililoko kwa kutolewa kwa unabii utakaoandikwa kuwa kumbukumbu ya wakati wote mifano hiyo imo ndani ya maelezo yafuatao kwa Mwandamizi wa Biblia [Companion Bible].

 

Neno lilitolewa kwa Zerubabeli, maana kuapishwa katika Babiloni (hiyo ni Babeli). Alikuwa mzao wa fimilia ya kifalme kwa kubaliwa au kuapishwa katika Babiloni, na kwa Yoshua mwana wa Yosedeki, kuhani mukuu.

 

Jina Yoshua ni sawa na lile Masihi alipewa.

Jina kamili ni Yohoshua au wokovu wa yoho, iliyo jukumu la masihi kama kuhani mkuu pia kama mfalme wa Israeli. Neno mwana katika andiko limetumika pia kwa mejukuu (cf. 1 mambo ya nyakati 3:19 na Ezra 2:2 na 3:2). Tazama pia katika masomo haya Ukoo wa masihi (Nam. 119)[Genealogy of the Messiah (No. 119)].

 

Yosedeki (Yahosedech) inamaanisha Yahova ni mwenye haki. Kwa ukamilifu jina hilo ni Yahoshua, au Yoshua wa Yosedeki. Maan ukombozi ni kupitia Yahova mtakatifu.

 

Yoshua ni kuhani mkuu wa kwanza katika Hekalu katika ule ujenzi mpaya. Wote walikuwa wa wakati huu wa masuto. Masihi atakuwa kuhani mkuu wakati wa rejea Yerusalem mara ya mwisho, ambayo hiyo ni mada ya ujumbe ulio katika kitabu cha Zakaria. Maandiko haya yote hivyo yanaungana hadi kipindi cha miaka elfu ambayo ni cha utawala wa Masihi.

 

Jina Gavana hapa limetokana na neno la wachemi Pechah (kutokana nalo tunapata jina Pasha) kama misimamizi au Liwali.

 

Shealtiel ina maana kilichoombwa kutoka kwa Mungu. Alikuwa mwana wa Yekonia (Jehoichin) aliyechukuliwa mateka uko Babiloni (2 Wafalme 24:15; 1 Mambo ya nyakati 3:17; cf. Ezra 3:2-8; 5:2; Nehemia 12:1; matayo 1:12, Luka 3:27).

 

UJUMBE WA KWANZA

 

Sura ya 1

 

Haggai: 1-4 Katika mwaka wa pili wa Dario mfalme, mwezi wa sita, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana lilimjia Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, kwa kinywa chake Hagai nabii, kusema, 2 Bwana wa majeshi asema hivi, ya kwamba, Watu hawa husema, Huu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujenga nyumba ya Bwana. 3 Ndipo neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema, 4 Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika? (Biblia Takatifu BT)

 

Yudah wameulizwa swali, mbona waliacha nyumba ya Mungu katika mabaki kwa uzuri zaidi ya miaka mia moja badala wangeijenga karne moja mapema walakini, kulikuwa na Hekalu la Yerusalem iliyofanay kazi wakati Hekalu la Yerusalem lilikuwa ukiwa na hilo halipaswi kusahaulika.

 

Yehova hapo tena anawakumbusha kuhusu dalili za hali yao.

 

5 Basi sasa, Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu. 6 Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; na yeye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka-toboka.  7 Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu (Biblia Takatifu BT)

 

Hivyo Yehova uanza na kumalizia kwa maelezo haya “tafakari jinsi umeishi” hawana chochote sababu hawakumstahiki Mungu.” Neno, tafakari limetumika mara tano katika kitabu hiki (Haggai 1:5,7; 2:15, 18,23; cf. Job 1:8; 2:3 na Isaya 41: 22).na maana yake ni weka tayari moyo wako au kuwa mwangalifu. Azimio ni kuhakikisha pale Yuda waliongozwa na matokeo ya yale wanatenda.

 

Yehova hapo tena akatoa amri:

 

8 Pandeni milimani, mkalete miti, mkaijenge nyumba; nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana. (Biblia Takatifu BT)

 

Neno kuonekana katika utukufu wangu ni kusema, nitajitwalia hustahiki/sifa. Jina la Kiebrania ni ekkabda. Hili ni moja ya maneno ishirini na tisa yasio na herufi HJe pale mwisho (Ginsberg’s Massorah, vol1, b 281). Herufi he ni sawa na tano. Bullinger (Comp. Biblia fn.to v 8).

 

Unakili haya kwa kunena kuwa wasomi wa mafundisho ya wayaudi hufikiria kwamba hili ni kwa sababu kulikuwa na vipengee vitano ambavyo vimekosea katika Hekalu la pili ambavyo ni:

 

1.Sanduku la Agano.

2.Moto uliowekwa wakfu/ Moto mtakatifu

3.Shekina.

4.Urim na Thummim/vinyago vitakatifu vilivyowekwa kifuani mwa kuhani enzi zile kwa ajili ya ufunuo wa penzi la Mungu; na

5. Roho ya unabii.

 

Kitu nambari 2 na 3 vinawakilisha Roho mtakatifu na uakilishi wao ndani ya wateule. Kitu na 5, Roho ya unabii, hipo katika kanisa na ukamilifu wake uko katika Yesu Kristo.

 

Oroda uhoji kulinda mwongozo wa neno ulio na herufi He mwisho wake. (mifano hipo katika kitabu cha kutoka 14:4, 17).

 

Katika Hekalu la kipindi cha miaka elfu moja Roho mtakatifu ndani ya wateule kama Hekalu la Mungu uhamisa upeo huu wote. Hili limekuwa Kanisani Tangu mwanzo wa kanisa pale haugwani.

 

Yehova anena kwamba watatafuta mengi na wakapokea havivu. Waliotunza vilipeperushwa mbali. Hapo tena alitoa jib: Sababu nyumba hipo katika maangamizi. Hivyo ni kusema hawajafanya chochote kwa wakati wa karne yote tokea agizo la Cyrus hadi lile la Dario Hystaspes wakati ambapo wangetenda kazi kujenga, na Mungu aliwaadhibu kwa hilo. Ilikuwa tu wakati wa utawala wa Artashasta wa 1 ambapo ujenzi ulikatishwa lakini hawakufanya Juhudi zozote hili kufufua ujenzi baada ya Artashasta alikomesha vita vya wenyewe kwa wenyewe (taz. masomo Nambari 13 ibid/katika lile lililotajwa).

 

9. Mlitazamia vingi, kumbe vikatokea vichache; tena mlipovileta nyumbani nikavipeperusha. Ni kwa sababu gani? Asema Bwana wa majeshi. Ni kwa sababu ya nyumba yangu inayokaa hali ya kuharibika, wakati ambapo ninyi mnakimbilia kila mtu nyumbani kwake. 10 Basi, kwa ajili yenu mbingu zimezuiliwa zisitoe umande, nayo nchi imezuiliwa isitoe matunda yake. 11 Nami nikaita wakati wa joto uje juu ya nchi, na juu ya milima, na juu ya nafaka, na juu ya divai mpya, na juu ya mafuta, na juu ya kila kitu itoacho nchi, na juu ya wanadamu, na juu ya wanyama, na juu ya kazi zote za mikono. (Biblia Takatifu BT)

 

Mungu aliweka ardhi chini ya laana na mafuno yalisuhiliwa kwa ajili ya ukaidi wao.

Wakati Mungu aliwakemea walitubu.

 

12 Ndipo Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, pamoja na hayo mabaki yote ya watu, wakaitii sauti ya Bwana, Mungu wao, na maneno ya Hagai nabii, kama Bwana, Mungu wao, alivyomtuma; nao watu wakaogopa mbele za Bwana. (Biblia Takatifu BT)

 

Hapo watu walikusanyika tayari kutenda kazi. Tena Bwana akanena kupitia Haggai.

 

13 Ndipo Hagai mjumbe wa Bwana, katika ujumbe wa Bwana, akawaambia watu, akisema, Mimi nipo pamoja nanyi, asema Bwana. 14 Bwana akaiamsha roho ya Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na roho ya Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, na roho zao mabaki ya watu; wakaenda, wakafanya kazi katika nyumba ya Bwana wa majeshi, Mungu wao; 15 katika siku ya ishirini na nne ya mwezi, katika mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa Dario mfalme. (Biblia Takatifu BT)

 

Ujumbe na toba vikafanyika kwa siku ya 24 tangia mwezi mwandamano hadi siku ya ishirini na nne ya mwezi wa sita.Tazama pia katika masomo haya Daraja ya Musa [070].

[The Ascents of Moses (No. 70)]

 

Unabii wa Haggai ulikaguliwa tena katika masomo haya Vipaumbele Vya Mungu [184] [The Oracles of God (No. 184)] mradi kushulikia hoja nyingi kuhusu kalenda, na kutumika vibaya kwa unabii wa Haggai na Daniel kwa matukio ya nyakati za mwisho. Maoni yaliyo muhimu kwa Haggai yamenakiliwa hapa.

 

Mafundisho katika sura ya 1 ni kusihi taifa la Yuda ili kuanza kazi ya Hekalu. Taifa halijabarikiwa kwa sababu wametangulisha matakwa yao binafsi juu ya yale ya Mungu. Kunayo mambo mengi katika hadithi ambayo ni sambamba kabisa na ile tabia ya Yuda pamoja na utepetevu wa kazi ya Mungu. Ikiwa unabii huu unauhusu dalili za siku za mwisho, lazima basi urejelee lile Hekalu la Kiroho, ambalo ni Kanisa.Washirika wenyeji katika unabii huu ni Zerubbabel, mwana wa Sheltiel msimamizi wa Yuda, na Yoshua, mwana wa Yosedach kuhani mkuu. Huu wakati ulikuwa mwaka wa pili wa utawala wa Dario II. Jambo hili limeelezewa kwa kina katika masomo haya Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi mpya wa Hekalu [013]. Majina hayo ni ya watu binafsi wa wakati ule wa ukarabati wa Hekalu ya pili (taz. Pia masomo haya Ukoo wa masihi (Nam. 119).

 

Ikiwa unabii ni wa siku za baadaye tunaweza tu kutaja juu ya Hekalu ya kiroho, na haina ya Zerubbabel na Yoshua, kama Kuhani Mkuu. Kuhani Mkuu Yoshua, ni Yeshua au ni Masihi kipeo kwa Yesu Kristo upatikana katika Zakaria wakati wa hukumu. Kristo ni kuwili akiwa mfalme na kuhani akitimisha vipeo vyote. Agizo katika sura ya 1 ya kitabu cha Haggai linanena kwamba taifa la Israeli halitanawili hadi pale watakapofanya kazi ya Masihi katika mategenezo kama sehemu ya Hekalu la Mungu. Laana za ardhi zitaongezeka hadi hilo lifanyike (Haggai 1:10-11). Ishara ya kwanza hipo katikasiku ya 24 ya mwezi wa sita. Hili lilitokea katika Hekalu la pili. Itaweza kuwa imepita au kulenga siku sijazo kama asili ya ishara.

 

Hivyo Haggai anahusika na ujenzi wa Hekalu, na Baraka za Israeli ni matokeo yanayofuata kitendo hicho. Hivyo ni vigumu kuhusisha matukio katika sura ya 2 kwa tukio ambalo alifuatani na tukio katika sura ya 1. Hivyo, kazi ya Nyumba ya Mungu inaheshimiwa katika siku ya 24 ya mwezi wa sita. Sura ya 2 tena inaanzia siku ya 21 ya mwezi wa saba au siku ya mwisho ya sherehe za vipanda. Sikukuu ya mwisho ni siku ya nane ya sherehe” (Vipaumbele Vya Mungu [184].

 

UJUMBE WA PILI

Ujumbe wa pili ulitolewa katika siku ya mwisho ya sherehe za vipinda na kabla ya kuanza kwa siku ya ishirini na mbili ya mwezi wa saba, ambayo ni sikukuu ya mwisho na hua sherehe katika haki ya kipekee. Ilikuwa Ishara kwamba Mungu, alitoa maelekezo kutoka mwezi mwandamano wa awali katika mwisho wa kipindi cha majafuko na muozo na kutawanyisha, na ni baada ya urejesho wao katika Ardhi takatifu.

 

Tena alinena nao katika mwezi wa saba na kile kinakisiwa kama uwakilisho wa mfumo wa millennia na kabla ya kisiwa kuwa kipindi cha ufufuo wa pili wa wafu Walihitajika kutunza sherehe na ni baada ya sherehe za miaka elfu moja ambapo wangeanzisha ujenzi.

 

Ujumbe huu na unabii ulikuwa wa aina mbili  kiasili. Ilikuwa kutazama mbele kuelekea matengenezo ya Yudah katika ardhi takatifu na kuelekeza kwa kukemewa kwao na toba lao katika kipindi cha mwisho kabla ya kurejea kwa Masihi.

 

Tazama katika ujumbe wa Mungu. Ni moja kati ya zile ambazo utia moyo kuhusu vitendo vyake vya wakati wa kutikishwa kwa mbingu na ardhi na mataifa. Hili linahusu vita vya mwisho pamoja na siku za mwisho.Hili halijahusishwa na kuokoka bado bali kuletwa katika kutiishwa na baadaye tena kuletwa katika toba na kuongoka (taz Masomo haya siku ya bwana na siku za mwisho (Nam. 192) [The Day of the Lord and the Last Days (No. 192)] na Miaka thelethini ya mwisho:  Jitihada za Mwisho (Nam. 219).

[The Last Thirty Years: the Final Struggle (No. 219)]

 

Sura ya 2

1 Katika mwezi wa saba, siku ya ishirini na moja ya mwezi, neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha Hagai nabii, kusema, 2 Sema sasa na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda, na Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, na hayo mabaki ya watu, ukisema, 3 Miongoni mwenu amebaki nani aliyeiona nyumba hii katika utukufu wake wa kwanza? Nanyi mnaionaje sasa? Je! Mbele ya macho yenu, siyo kama si kitu? 4 Lakini sasa uwe hodari, Ee Zerubabeli, asema Bwana; nawe uwe hodari, Ee Yoshua, mwana wa Yehosadaki, kuhani mkuu, nanyi iweni hodari, enyi watu wote wa nchi hii, asema Bwana; mkafanye kazi, kwa kuwa mimi ni pamoja nanyi, asema Bwana wa majeshi; 5 kama neno lile nililoagana nanyi mlipotoka katika nchi ya Misri; na roho yangu inakaa kati yenu; msiogope. 6 Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi, Mara moja tena, ni kitambo kidogo tu, nami nitazitikisa hizo mbingu, na hii nchi, na bahari, na nchi kavu; 7 nami nitatikisa mataifa yote, na vitu vinavyotamaniwa na mataifa yote vitakuja; nami nitaijaza nyumba hii utukufu, asema Bwana wa majeshi. 8 Fedha ni mali yangu, na dhahabu ni mali yangu, asema Bwana wa majeshi. 9 Utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko utukufu wake wa kwanza, asema Bwana wa majeshi; na katika mahali hapa nitawapa amani, asema Bwana wa majeshi. (Biblia Takatifu BT)

 

Siri ya mataifa yote imetolewa katika maandiko ya kale kwa kiyunani (LXX) Kama wateule wa mataifa yote. Ni lasima basi kuhihusu Kanisa na uongovu wa watu wa mataifa.

 

Hekalu la roho litasengwa kadili ya sikukuu arobaini za sherehe ya jubilee au mwaka elfu mbili toka 30CE hadi Kristo ataporejea mara ya pili.

 

Nyumba timilifu ya mungu itaundua upya bali utakuwa wakati wa mfumo wa kipindi cha miaka elfu moja ya utawala wa wateule baada ya kurejea kwa masihi mara ya pili na baada ya kutiishwa kwa mataifa yote. Hii ni hema takakatifu ya miaka elfu moja ya utawala wa wateule inavyorejelewa na Ezekiel (cf. comp Biblia fn to 2.77 utukufu wa baadaye utakuwa mkuu kuliko ule wa kwanza (ef. Ezekiel 43:2-5) Nyumba onekanefu haitajengwa kabla ya miaka elfu moja ya utawala wa wateule bali katika wakati wa elfu moja yenyewe. Sherehe za ukumbuzo wa kwanza wa miaka elfu moja itakuwa wakati wa ukumbusho wa sherehe za sikukuu ya mwaka wa hamsini kwa kuwa angizo hili lilikwisha tolewa, Zakaria pia alikabidhiwa mpangilio wa vitendo (taz Ufafanuzi wa Kitabu cha Zekaria [297]  [Commentary on Zechariah (No. 297)] na Yubile Kuu ya Dhahabu na Milenia [300]) [The Golden Jubilee and the Millennium (No. 300)].

 

Hekalu la kiroho la Mungu liliamishwa tangu wakati wa siku za hamsini baada ya pasaka/siku ya roho mtakatifu (30cc Pentecost) ambao ulikuwa mwaka wa tatu wa andamano baada ya sikukuu ya Yumbilee ya 27CE tutaweza kuamini kwamba Hekalu onekanefu na miundo yake vitaasisiwa katika Yerusalemu toka mwaka wa tatu wa ukumbuzo wa sikukuu ya 121 kwa mwandamo wake mfano 2030 wakati huo tutashugulikia utaratibu ulioko katika masomo yenye mada hii.

 

Ujumbe ulirejea tena kupitia Haggai katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa. Ujumbe ulikuwa juu ya kuwekwa wakfu na ukafiri. Hapa inahusu ukombozi wa watu wa mataifa na utakaso wao. Maneno mwili matakatifu katika maandiko ni nyama ya kafara, ambayo uhusiana na wateule wa Mungu baadaye.Neno lasema kwamba mwili mfu ni nephesh au nafsi na ni moja ya mafungu 13 mahali ambapo neno nephesh  linatumika kuashiria nyama mfu. Hapa uleta mtawinyiko kati ya waliokufa ambao  hawakuongoka,  na wateule walio hai ambao wamealikwa na Mungu. Wakati wa kipindi cha miaka elfu moja Yuda na Israel watarejeshwa pia mataifa yote yatarejeshwa na kuletwa katika utakaso na kuwekwa wakfu katika msingi wa kuendelea mbele (taz pia masomo Ufafanuzi wa Kitabu cha Zekaria [297] na Utakaso wa Mataifa [077] [Sanctification of the Nations (No. 77)].

 

10 Siku ya ishirini na nne, ya mwezi wa kenda, katika mwaka wa pili wa Dario, neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha Hagai nabii, kusema, 11 Bwana wa majeshi asema hivi, Waulizeni sasa makuhani katika habari ya sheria, mkisema,
12 Mtu akichukua nyama takatifu katika upindo wa nguo yake, naye akagusa kwa upindo wake mkate, au ugali, au divai, au mafuta, au chakula cho chote, je! Kitu hicho kitakuwa kitakatifu? Makuhani wakajibu, wakasema, La. 13 Ndipo Hagai akasema, Kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti, akigusa kimojawapo cha vitu hivi, je! Kitakuwa najisi? Makuhani wakajibu, wakasema, Kitakuwa najisi. 14 Ndipo Hagai akajibu, akasema, Hivyo ndivyo walivyo watu hawa, na hivyo ndivyo lilivyo taifa hili mbele zangu, asema Bwana; na hivyo ndivyo ilivyo kila kazi ya mikono yao; na kitu hicho wakitoacho sadaka huko ni najisi.(Biblia Takatifu BT)

 

Matabahu yalijengwa mbele ya Hekalu na kafara zimeainishawa kama najisi. Hata hivyo, haya yanalenga mbele katika wakati wa jitihada za kafara zitazotekelezwa na yuda bila toba, uongofu na ubatiso.

 

15 Na sasa nawaomba, tafakarini; tangu siku hii na siku zilizopita; kabla halijatiwa bado jiwe juu ya jiwe katika nyumba ya Bwana; 16 katika wakati huo wote, mtu alipofikia chungu ya vipimo ishirini, palikuwa na vipimo kumi tu; na mtu alipofikia shinikizo apate kuteka divai ya vyombo hamsini, palikuwa na divai ya vyombo ishirini tu. 17 Naliwapiga kwa ukavu, na ukungu, na mvua ya mawe, katika kazi zote za mikono yenu; lakini hamkunielekea mimi, asema Bwana. (Biblia Takatifu BT)

 

Maana Mungu kuwapa mapigo ni mfano tu katika Kumbukumbu la torali 28:22. Hata hivyo, hili litakuwa badili ya toba.

 

18 Tafakarini, nawaomba; tangu siku hii ya leo na siku zijazo; tangu siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kenda, naam, tangu siku hiyo ulipowekwa msingi wa hekalu la Bwana tafakarini haya. 19 Je! Mbegu ingali ghalani? Naam, huo mzabibu, wala mtini, wala mkomamanga, wala mzeituni, haikuzaa kitu; tangu siku hii ya leo nitawabariki. 20 Kisha neno la Bwana likamjia Hagai mara ya pili, siku ya ishirini na nne ya mwezi, kusema, 21 Sema na Zerubabeli, liwali wa Yuda, ukisema, Nitazitikisa mbingu na dunia; 22 nami nitakipindua kiti cha enzi cha falme, nami nitaziharibu nguvu za falme za mataifa; nami nitayapindua magari, na hao wapandao ndani yake; farasi na hao wawapandao wataanguka chini; kila mtu kwa upanga wa ndugu yake. 23 Katika siku ile, asema Bwana wa majeshi, nitakutwaa wewe, Ee Zerubabeli, mtumishi wangu, mwana wa Shealtieli, asema Bwana, nami nitakufanya kuwa kama pete yenye muhuri; kwa kuwa nimekuchagua, asema Bwana wa majeshi. (Biblia Taakatifu BT)

 

Mbegu zitapandwa na Mungu atabariki upanzi huu kabla ya kusanywa na kuletwa ndani na kuzidishwa.

 

Baraka za Yuda zitatokea wakati Yuda wataanza kubariki mataifa na Hekalu likiwa limeanzishwa katika Yerusalemu chini ya Masihi katika siku hiyo. Utajiri/ukuasi wan chi takatifu utaongezeka mara kumi. Uharibifu wote utaponywa na nchi itarejeshwa.

 

Unabii huu basi umeiweka siku ya 24 ya mwezi wa tisa kama asili ya rehema ya Mungu kwa Israel na baraka zake kwa taifa. Kwa kawaida limekuwa likitazamwa kama neno la wakati unaofaa kwamba matengenezo yamekamilishwa. Na ndio iliyosababisha jitihada zilizofanywa kudai taifa la watu wote chini ya Jemedari mkuu Allenbi waliwashinda Yerusalemu mwaka wa 1917 mwezi wa Chisler siku ya 24. Hata hivyo, kuingia Yerusalemu kwa Allenby kulikuwa mwezi wa Chislev, lakini ushindi haukuwa siku ya 24 uvamizi ulianzishwa siku ya 24 mwezi wa chislev kuambatana na mwungano wa mwezi mwandamo, na si kuambatana takuimu ya Hillel. Yamechunguzwa Kinaganaga katika masomo haya Vipaumbele Vya Mungu [184] kusudi maalum ya kimsingi ya masomo hayo ni kushugulikia hoja ya usia wa Mungu na pale ambapo makaazi ya mamlaka ya takuimu.

 

Tutahitajika kutilia maanani maelezo haya yaliyo elezwa kwa kina ambayo ni hesabu kuhusu matengenezo ya Israel katika siku za nwisho.

 

Kunukuu Vipaumbele Vya Mungu [184] tunaona kwamba:

“Ushauri uliotolewa katika unabii huu ni:

 

  • Unabii kuhusu siku za baadaye
  • Siku ya 24 ya chislev ni tarehe maalum ya baadaye.
  • Kulingana na takuimu ya Hillel siku hii ilikuwa siku ambayo Yerusalem walifunguliwa katika mwaka wa 1917, ambayo ilikuwa December 1917 na inaaminika ndio siku ambayo Allemby aliingia Yerusalemu.
  • Baraka zilizotajua na Haggai zilitimishwa.
  • Kivingine hii pia ni mwandamo wa mara ya saba tokea kwanguka kwa Jerusalem.

 

Kutokana na hoja hizo tunahoji kuwa takuimu ya Hillel basi ni pumsi la Mungu na ni usia wake Mungu.

 

Kuambatana na kuanguka kwa Yerusalemu, kwanza, kamusi ya Biblia ya mpiga kinubi imeandikwa Wababiloni waliteka mji wa Yerusalemu mwaka wa 598 BCE, na mji huu ulisawanzishwa katika mwaka 587 BCE. Hakuna kati ya tarehe hizi zote huteta 1917 kwa kujumilisha miandamo mara saba au mwaka 2,520. Tarehe ya kwanza huleta 1923 na tarehe za nyuma zita leta 1933.

 

Tutakavyona sasa mchakato huu ni bora ukitafakariwa kimwandamo. Ni bayana kutokana na uchunguzi wa hadithi ya uhuru wa Yerusalemu ambapo matukio yaliorodheshwa kwa jinsi yalivyotokukia,  ili kutokeza wazo la Mungu akitekeleza kazi ya utimisho wa unabii sababu watu wa wakati huo waliona hilo kama utimilifu wa unabii. Tarehe ya 9 Disemba 1917 ikishawekwa itatumika kuhalalisha takuinu ya Hillel iliyofanya msingi wa uanzilishi wa mara ya kwanza.

 

Katika mwaka wa 1917 nchi takatifu ilifunguliwa na wa Australia, New Zealand na Uingereza, na miungano mingine ya kijeshi waliopiga vita Wauturuki pamoja na vikozi vya Ujerumani vilivyoongezea nguvu kulingana na mpangilio rasmi wa vita (H.S. Gullett, The Australian Imperial Force in Sinai and Palestine, Vol. II of the Official History of Australia in the War of 1914-18, Angus and Robertson Ltd, Sydney, 1937), Gaza na Berisheba walikuwa wamechukuliwa kufikia 31st Octoba hadi 1 Novemba 1917.  Kuteka kwa Wapalestina hakungesuilika. Mnamo tarehe 2 Novemba 1917 tangazo la Balfour juu ya kuasisiwa kwa Boma ya wayaudi ilitolewa na waziri mkuu Balfour kama tangazo lake la kwaza (tangazo la pili lilihusu jumuia ya madola ya Australia chini ya sheria ya Uingereza). Kutekwa kwa Yerusalemu hakukutelezwa hadi Disemba. Maendeleo ya vikozi ni hifuatayo.

 

Vita vya Beersheba               

31 Octoba hadi 1 Novemba

Tel el Khuweilfe

8 Novemba

Kukatokea Ushindi    (Sinai na Palestine 4-8 Nov.)

6-11 Novemba

The Great Drive was made

8-15 Novemba

Pahali Tambalale ba Bahari yaliondozwa                   

11-17 Novemba

Yerusalemu kuendelzwa Zaidi

16-24 Novemba

Nahr Auja na El Buij

24 Novemba - 1 Disemba

Mashamblishi ya mwisho kwa kuuteka mji wa Yerusalemu

 

7 Disemba

Mashambulishi ya mwisho yalianzishwa na vikozi vya jumuia ya madola mnamo tarehe7 Disemba 1917. Kuambatana na mwezi mwandamo wa kweli, 24 Chisler ilikuwa tarehe halisi (takuimu ya Hillel ilianza mwezi wake siku mbili baadaye) Waturuki na Wajerumani walianzisha uamisho ghafla, na kufikia 8 Disemba 1917 Yerusalemu ilikuwa huru. Askari wa nchi kavu walikua wamekita misisi kufikia tarehe 10 Disemba askari wafarasi wenye siraha nyepesi walizidi kuingia ndani kupitia barabara ya Nablus takribani umbali wa maili nane. Waliendeleza mizinga mizito ya Uturuki wakiendelea kuteka kusini kuelekea mpaka wa ponde la Yorodani na walijitahidi kudhibiti vinjia vilivyovuka mto kuelekea leli ya Hejaz na hivyo kudhibiti shughuli za Alleby za upande wa kulia.

 

Hakukuwa na tukio lolote tarehe 9 Disemba 1917 kwa kuwa Yerusalemu tiyare ilikuwa imekombolewa tarehe saba. Wengi wavwanahistoria wa asili ya Kiprotestanti wanaonekana kujaribu kudai kuwa Disemba 9 ilikuwa ndio siku ambayo Allenby aliingia Yerusalemu na kuikomboa.

 

Ukweli wa mambo ni kuwa Allemby aliingia Yerusalemu rasmi mnamo tarehe 11 Disemba  1917. Allenby alikuwa mwangalifu sana juu ya tamasha za majivuno ya jinsi mfalme wa miliki ya Ujerumani Wilhelm (William) alivyoingia Yerusalemu mwaka wa 1908. Makusudi alifanya kuingia kwake kuwa jambo la hali ya chini sana wakipitia kiingilio chembamba cha mlango wa Jaffa kwa barabara ya Jaffa ili kukabiliana na tukio lolote kama litatokea, hivi vikozi vilijumuhishwa na vikozi vya Uingeresha, Scotland, Ireland, Welsh, Ghurkas, Australians na Waitalia. New Zealanders walisika samu zaidi Jaffa ili utawala uweze kubainishwa. Rangi iliyotambulika tu ni ile ya mtengo ya vokosi vya Ufaransa wakiwa na share za rangi ya samawati na nyeupe. Hii mara ya ishirini na nne ambapo Yerusalemu iliingiwia kwa njia ya uvamishi wa kimabavu (Gullett, ibid., p. 523) lakini haikuwa siku ya 24 Chisler 1917. Kulingana na takuimu ya Hillel ilikuwa 26 Chislev, lakini kutoka mwezi mwandamo halisi ilikuwa mnamo 28 Chislev.  Vikozi vyetu kwa kweli waliingia mnamo 24 cheslev, bali kwa njia ya uvamishi. Hayo ni kulingana na muungano halisi na bila kuhairishwa.

 

Yerusalemu katika wakati wa kutekwa hawa kushwa ushahidi wa kulenga umaskini lakini ilikuwa katika hali ya uchafu isiyoeleweka. Ilikuwa ime chafuliwa na wausaji wa  mazao ya kidini na ibada ya kinafiki ambao kawaida walikuwa najisi kwa usaidishi wa desturi za zamani ya askari za uturuki kwa miaka tatu.

 

Kwamba Kakristo wakumbuka kufika kwao kwa mshangao (ibid, masomo 522) Baada ya shughuli za Yerusalemu mji ulikabiliwa na ukosefu wa cakula na waingelesha walilazimika kusafilisha  msaada Yerusalemu kupitia ziwa Meditaranean. Mkopo wetu kutoka kusini ulikuwa unaenda kwa haraka kwamba waturuki hawakuwa na wakati kuwafanya waamiaji wa sehemu za Kusini kuwa bure. Walikuwa wanathibitisha kuwa wao ni wa maana. Agizo la kizionist chini ya Raisi wa muungano wa utawala wa kizionist wa uingereza. Daktari weizmann aliulishwa kwa amri ya serikali la uingereza pamoja na kujenga upya Palestina. Kazi hii iliusisha matengenezo kutokana na uharibifu wa karne ya kumi na nne na nusu (The Times History of the War, Vol. XV, London, 1918, p. 179).

 

Kusudi hapa inaweza onekana  katika mwangaza wa kihistoria ambao hauna  uongo  wa waprotestant wenye hawakuhusika na ambao ni uvumi wa British Israelite ianayotoka Marekani.

  • Haikuwa mwandamo wa mara ya saba tokea kuingia kwa wababiloni welekevu wa mwandamo mara saba umeangaliwa katika masomo haya Kuanguka kwa Misri: Unabii wa Mikono Iliyovunjika ya Farao [036] unabii wa siraha havivu za Pharaoh)
  • Allenby hakuingia Yerusalemu mnamo tarehe 9 Disemba, bali aliingia pale tarehe 11 Dec.
  • Vikozi vya jumuia ya madola vilishamblia mji wa Yerusalemu mnamo tarehe 7 Disemba 1917.
  • Wajerumani na Waturuki walijiondoa mnamo tarehe 8 Disemba.
  • Muungano wa vikozi ulifanyika kutoka 8-10 Disemba.
  • Tarehe halisi ya 24 Chisler1917 ilikuwa 7 Disemba1917 kulingana na takuimu ya Hillele.

 

Katika yote haya, lazima tukumbuke kuwa Yuda haikuwa imebarikiwa katika hatua hii. Ni upotevu kudhani kuwa Mungu angefanya wakati huu kuwa hitimisho la unabii wa Haggai na kuwacha unabii mwingine ambao utatimishwa wakati Yuda Angepitia dhiki za maisha yake kama taifa.

 

Miandamo saba halisi kulainishwa kwa Yerusalemu na wababuloni, chama nazi kitwaa utawala katika Ujerumani na wakaanza utaratibu wa kutesa Wayaudi. Toka 1992 hadi 1945 Ujerumani walitekeleza mauaji yaliyopangwa kwa watu wa ugaidi au tunaweza sema Nchi yoyote iliyoingia katika kumbukumbu za kihistoria. Kuthibitisha hayo hii ilikuwa nia ya Mungu kubariki Yuda, katika kukamilisha unabii wa kitabu cha Haggai, tunaweza sema kwa ufupi kuwa ni njia iliyo patoka mno ikiwa mtu atafikilia kuwa kitabu cha Haggai kimekamilishwa katika vitendo hivi.

  • Takuimu ya Hillel ni kosa
  • Lakini cha umuhimu, Ashkenazim na kwa kweli Bara lote la ulaya zimo nche kabisa ya baraka za Mungu sababu wameasi Roho na kusudi la sheria pamoja na sherehe za sikukuu. Kila laana ucha kwa sababu yake.

 

Hairidishi hata hivyo kusema kwamba kitabu cha Haggai kimetimishwa.

 

Walakini, tunaweza kifupi kuwa tarehe hii 24 Chislev 1917, ilikuwa mwanzo wa kuasisiwa kwa Yerusalemu kama ngome ya makaazi ya Wayaudi iliyotangazwa na Balfour katika tangazo la tarehe 2 November 1917. Tangazo lingine la Balfour lilikuwa kuhusu Australia na katiba yake.

 

Ikiwa tutazama zoezi hili kama mfano wa maagizo ili kujenga Hekalu la zamani jinsi ilivyokuwa toka wakati wa amri ya Cyrus hadi mwanzo wa ujenzi wa Hekalu chini ya Dario Muajemi, hapo tunapata mlolongo wa nyakati inayotanda kipindi chote cha miaka mia moja na kumi na sita. Hivyo kutolewa kwa tangazo la Balfour ni mwanzo wa mfururisho wa maagizo tokea 1917. Kuitangaza kulifanyika katika siku ya kumi na nane ya mwezi wa nane wa mwaka wa arobaini wa sikukuu ya ukumbuzo wa 118 au 2 Novemba 1917. Mwisho wa kipindi cha miaka 116 kuelekea mfumo wa kipindi cha miaka elfu moja ni katika mwaka wa 2033, au mwaka wa sita wa mfumo wa Millenia. Tunaweza  tarajia mwaka wa tatu hadi wa sita wa millennia  kuhusishwa na Hekalu na ujenzi wa makaazi ya utawala wa kimellania kuambatana na unabii. Taz. somo Yubile Kuu ya Dhahabu na Milenia [300] na Ukumbusho wa miaka hamsini na mileniia sehemu II Israeli na mataifa yanayowazingira( (Nam. 300B).

 

Kurejelea kwa pete yenye muhuri ni sambamba na Zakaria 4:7-10 na 6:13 (cf mwanzo 41:42 na Esta 3:10) ufananisho huu unaonekana pia katika wimbo uliobora na Yeremia 22:24.

 

Aliyeteuliwa ni yule mfalme wa kweli na msimamizi wa Isaya 9:6-7 wateule wote wameteuliwa kama Daudi na uzao wake uliteuliwa (Wafalme 8:16, 11:34, cf. pia Zakaria 12:8)

 

Kuzinduliwa kwa Hekalu ambayo imetajua hapo kunaonekana kuwa Hekalu hili lilikuwa kubwa kuliko lile la Solomon huo ulikuwa mdomo tu.

 

Kwa kweli unabii katika Daniel 9:25-27 unaonyesha kwamba Hekalu litajengwa zaidi ya majuma sabini ya miaka. Hakuna tashwishi kwamba Hekalu la pili, na ukarabati wa Herodi havingeweza kulinganishwa na Hekalu la Sulemani. Hekalu linalozugumziwa hapa ni unabii unaopambanisha Hekalu la kiroho chini ya masihi na hile Hekalu la kiroho hile Hekalu Onekanevu pamoja na Agano la kale.

 

Roho wa bwana alikuwa amedumu ndani ya watu na hili lilitokea Kanisani katika miundo msingi thabiti. Haggai 2:6 limeandikwa katika waeberania 12:26-27

 

26 ambaye sauti yake iliitetemesha nchi wakati ule; lakini sasa ameahidi akisema, Mara moja tena nitatetemesha si nchi tu, bali na mbingu pia. 27 Lakini neno lile, Mara moja tena, ladhihirisha kuhamishwa vile viwezavyo kutetemeshwa, kama vitu vilivyoumbwa, vitu visivyoweza kutetemeshwa vikae. (Biblia Takatifu BT)

 

Hii ni onyo la moja kwa moja kutoka kwa masihi kunena kwamba unabii huu unahusu tetemesho la mwisho litakalo tetemesha Mbingu na ardhi hivi kwamba kitu ambacho hakitatikishwa kitadumu. Hili tetemeko litaanzia katika Hekalu la Mungu, ambalo amblo ni Kanisa. Wakiwa naos au Mtakatifu wa Watakatifu (1 Wakorintho 3:17) kwa sababu hii hebu tumshukuru Mungu kwa ajili ya kupokea ufalme ambao hautatetemeka (Waeberania 12:28)

 

Wakati utawadia katika vita vya mwisho na kurejea kwa Masihi mara ya pili. Vita vya kwanza vya dunia vilitajua kama vita vikuu vya ustaharabu sababu watu wakizia kwamba mwisho wa dunia umewadia na 1914-1916 katika unabii ilionekana barabara kama kukamilishwa kwa mara ya saba tokea utawala wa Nebukadresa. Ikianzia mapigano ya karkemish katika mwaka wa 605 BCE mapigano ya mwisho wa dunia kwa kweli yalianzia tokea tarehe hii, lakini yangeedelea kwa wakati uliorefushwa na unabii sanasana uliohusisha matengenezo chini ya Masihi. Tarehe 24 Chisler (mwezi wa tisa) inahusu swala la utakatifu na unajisi (Haggai 2:10-1). Taifa linatazamwa kama najisi, na taifa tokea wakati huu limetakaswa kutokana na unajisi wake. Jambo hili limehusishwa moja kwa moja kwa dhana ile ya kuwekwa jiwe juu la lingine katika Hekalu. Tokea siku hiyo na kuendelea ni ujenzi wa Hekalu. Mpangilio huu hauna huusiano na vitu vinavyoonekana bali kubarikiwa kwa Hekalu kutaendelea. Ndio maana maangamizi ya moto yalitendeka hivyo sababu taifa lilikuwa alijaongoka na baraka za Bwana hazikuwa zimetolewa. Bado kutakuwa na vita zaidi na maagamizi zaidi katika Yuda na katika Israeli hadi pale wote watakapofikia Toba na utakazo kutokana na dhabi zao (Vipaumbele Vya Mungu [184]).

 

Hekalu linaendelea Kujengwa kutumia mawe hai na Mungu hataruhusu muundo onekanevu kutenda kazi katika msingi asili unaoendelea hadi wakati ambapo Masihi atarejea na Yuda akiwa ameongoka. Jitihada za kufanya hivyo zimeshindwa hadi leo hii na kusababisha adhabu kali kwa Yuda. Hakuna Myaudi au mtu wa mataifa asiyeongoka ambaye anaruhusiwa kushiriki katika Hekalu.

 

Wale tu watatubu na kupokea ubatiso ndio wataweza kuwa sehemu ya mchakato huo hili izifanyike najisi. Falme za ulimwengu huu zitaangushwa na kitu kilichoabishwa Babuloni kitafanywa pete yenye muhuri kwa Bwana wa majeshi. Wanajisi watatakaswa na wataitwa watakatifu katika Bwana na watawala kama watakatifu wa Mbiguni, kama wafalme na makuhani ndani na Nche ya Yerusalemu.