Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[299C]

 

 

 

Ufafanuzi Kuhusu Danieli

Sura ya 7

                                                                                                                     

(Toleo La 1.0 20140327-20140327)

 

Danieli sura ya 7 inahusiana na matukio ya siku za mwisho na vita vitakavyotangulia kabla ya kurudi kwa Masihi.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)

(tr. 2014)

 

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ufafanuzi Kuhusu Danieli Sura ya 7



Utangulizi

Danieli sura ya 7 ni mwendelezo wa tukio lililotangulia kabla yake ya kisa na habari ya kukombolewa kwa Danieli kutoka kwenye tundu la Simba kilichotokea wakati wa utawala wa Dario na inaendelea kuelezea mambo mengine yaliyojiri kipindi cha Koreshi Muajemi. Maandiko yanauelezea mwaka wa Kwanza wa Belshaza mwana na kukaimu na kutawala pamoja na Nabonidus, Mfalme wa Mwisho wa Babeli (555-539 KK). Nabonidus alirithiwa na Koreshi na Dario aliyetajwa kwenye sura ya 6 aliyetawa baada ya Koreshi. Belshaza hakurithishwa na baba yake, bala walitawala kwa pamoja wote wawili nay eye akiwa kama ndiye Mfalme Liyetawazwa rasmi. Nabonidus aliondoka kutoka mji mkuu wao mara tu baada ya kuinuka kwake na kuchukua ufalme, upande wa magharibi, na hakuwepo mjini na wala hakujihudhurisha kwenye Sherehe za Mwaka Mpya kwa kipindi cha miaka saaba. Kwa hiyo, mwaka wa Kwanza wa kukaimu huenda ulikuwa ni mwaka wa pili wa utawala wa Nabonidus takriban mwaka 554 KK na unaweza pia kuwa ni tangu mwaka 555. Nebukadneza alitawala tangu mwaka 605 KK hadi mwaka 562 KK na alirithiwa na mwanae Evil-Merodaki 562-560KK. Nabonidus peke yake ndiye anayemtaja Nebukadneza na Neriglissar kama wana wa ufalme wawili waliofuatia na hawamtaji mfalme huyu na wala masalia au sehemu ya habari zao kwenye vitabu vya Historia ya Nyakati za Wababeloni hazimtaji. Neriglissar alikuwa ni mfalme tangu mwaka 560-555 KK. Danieli ialikuwepo wakati huu wote tangu mwaka 597 akiwa kijana mdogo hadi mwaka 555/4 wakati alipofikia umri wa takriban miaka 62 wakati alipoyaona maono haya na ambayo yamefuatiwa kutoka na maandiko yaliyo kwenye sura ya 2. Ni muhimu kujua kuwa mandiko haya yanahusiana na mlolongo wa matukio yaliyopo kwenye sura ya 2:42-43.

 

Sura ya 7 imeandikwa kwa lugha ya Kikaldayo na inafuatia matukio ya kwenye sura ya 2:42-43 ambayo yanahusiana na Falme au Dola zitakazoinuka ambazo sasa zinainuka katika Siku hizi za Mwisho. Kipindi cha kujiri kwa matukio haya ni kile cha siku za mwisho cha utimilifu wa Wamataifa chenye jumla ya miaka 2520 kijulikanacho kama cha Nyakati za Wamataifa na cha uanzishaji wa dola za siku za mwisho iliyoanzia tangu mwaka 1914-1918 na mwisho wao ni mwaka 1996 na ndio mwanzo wa kipindi cha Dola ya mwisho ya Mnyama kuanzia mwaka 1997 (soma jarida la Kuanguka kwa Dola ya Misri Sehemu ya II: Vita vya Meisho (Na. 036_2)).

 

Danieli 7:1-28

1 Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danielii aliona ndoto, na maono ya kichwa chake, kitandani mwake; basi akaiandika ndoto, akatoa habari ya jumla ya mambo hayo. 2 Danielii akanena, akisema, Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa. 3 Ndipo wanyama wakubwa wanne wakatoka baharini, wote wa namna mbalimbali. 4 Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu.

 

Hii inachukua sura ya Kibabeloni na mfumo au imani yake yenye Miguu ya Chuma kwenye sanamu iliyoandikwa kwenye sura ya 2 ambayo ilikuwa ni Dola ya Rumi na nyayo zake za mchanganyiko wa Chuma na Udongo ilikuwa ni iliyokuwa inaitwa kuwa ni Dola Takatifu ya Roma ambayo ilidumu na ilikuwa ni budi idumu tangu mwaka 590 KK hadi 1850 huko Roma na kisha akarishwa na Mnyama ambayo iliundwa kutoka mfuo huko Ulaya. Ilikuwa ni kuwa Dola hii ya mwisho iliyoundwa kutoka kwenye unguvu nyingine kwa kipindi chote cha zaidi karne ya 19 na 20. Ilikuwa ni Dola iliyokusudiwa kuwa ni ya Mfalme wa Kaskazini ikiwa kama ni Mnyama wa Nne wa maandiko haya. Kumbuka kuwa aliinuliwa juu na kuwezesha isimame kwa miguu yake na akapewa moyo wa mwanadamu katika siku za mwisho. Na kwa hiyo inaibadili hadhi yake na imefishwa tena na tena na kufanyika kuwa ni muunganiko wa Mnyama wa Nne.

 

5 Na tazama, mnyama mwingine, wa pili, kama dubu, naye aliinuliwa upande mmoja, na mifupa mitatu ya mbavu ilikuwamo kinywani mwake katika meno yake; wakamwambia mnyama huyo hivi, Inuka, ule nyama tele.

 

Hii ilikuwa ni bara la Ulaya lililoundwa kutoka kwenye mfumo wa Kirusi na iliua jozi nyingi za mamilioni ya watu kwenye kipindi ambacho iliundwa kwayo. Mbavu tatu zilizobanwa kinywani mwake zinahusiana na hizi Nchi zinazojulikana kuwa ni za Kibaltiki na zinaweza zinaweza kutanjwa pia na maeneo mengine zaidi za uliokuwa muungano wa umoja wa Kisovieti pia. Inayofuatia inahusiana na ya Tatu nay a mfumo wa Kiasia.

 

6 Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.

 

Huyu alikuwa ni Mnyama wa Tatu aliyetokana na Yule aliyepewa mamlaka au ufalme na aliyetokea Baharini ambao ni idadi kubwa ya wanadamu. Chui ni kama alama ya kinembo inaweza kuwa simba au duma. Inaoashiria mfumo au dini za Kihindi au Kiasia na inaenea kutoka Mashariki ya Kati hadi Mashariki ya Mbali.

 

Katika siku za mwisho, Mnyama wa Nne anatokea kutoka kwa ule mfumo wa tatu wa kwanza waliopita na ni vidole hivi kumi vya chuma vilivyochanganyika na udongo na ambavyo vinaunda kutoka kwenye sura ya 2.

 

Imekuwa ikiwezeshwa kuchukua madaraka na utawala kwa kipindi cha zaidi ya miaka thelathini iliyopita ya mwisho wa mfumo na utawala wa kidunia. Iliwekewa mkakati wake kwenye kile kinachoitwa kama Klabu ya Roma mnamo mwaka 1956 ikiwa kama miungano ya kiuchumi zinazozisukuma na kupekelesha uweza au nguvu za kitaifa la kila taifa linguine lolote. Hata hivyo, inatumia nguvu za kijeshi za Mfalme wa Kaskazini ambayo kwa hakika kabisa inamaanisha kuwa ni umoja wa kujihami wa NATO.

 

7 Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi. 8 Nikaziangalia sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang'olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu.  

 

Maandko yaliyo kwenye Danieli sura ya 8 yanaonyesha mgongano uliokuwepo kati ya Wamedi na Waajemi walipoichukua na kuitamalaki dola ya Babeli. Sura ya 9 inaelezea unabii kuhusu Hekalu na kuanguka kwa Yerusalemu baada ya majuma sabini ya miaka kwenye mwaka mtakatifu wa 70-71 BK. Kwenye sura ya 10 Danieli alipewa au kuonyeshwa maono katika Mwaka wa Tatu wa Koreshi na inaelezea kuwa maandiko yanayofuatia yalikuwa ni kwa kipindi cha mbali cha siku zijazo katika siku za mwisho, na alipewa uwezo wa kuelewa kwamba Wayunani wangechukua utawala baada ya hawa Waajemi na Yule mfalme aliyeelezewa kwenye Danieli angefanya vita na mfalme wa atakaye watawala Wayunani pia. Mchakato huu ulianza kutoka kwenye Vita ya Wagranicus na ulifuatia jumla ya siku 2300 jioni na asubuhi iliyoelekea na kuendelea mbele hadi kwenye marejesho mapya ya Yerusalemu mwishoni tangu mwaka 1967 (soma pia jarida la Maelezo ya Ratiba ya Nyakati (Na. 272)). Kisha unabii unakwenda kwenye mlolongo wa vita vya wafalme wa Kaskazini na vya Kusini ambavyo vinachukua mlolongo na mfuatano wote mzima wa vita kutoka kwenye ushindi juu ya Waajemi hadi kwenye vita vya siku za mwisho.

 

Amdiko la Danieli sura ya 7:7 linahusu matukio yaliyo kwenye Danieli 11:40-45. Kuna vita vya siku mwisho na jinsi Dola ya Mnyama inashika hatamu na kuzitiisha dola nyingine tatu na kuimiliki Nchi Takatifu na dunia tangu kipindi cha miezi 42.

 

Danieli 11:40-45

40 na wakati wa mwisho mfalme wa kusini atashindana naye; na mfalme wa kaskazini atamshambulia kama upepo wa kisulisuli, pamoja na magari ya vita, na wapanda farasi, na merikebu nyingi; naye ataingia katika nchi hizo, na kufurika na kupita katikati. 41 Tena ataingia katika hiyo nchi ya uzuri, na nchi nyingi zitapinduliwa; lakini nchi hizi zitaokolewa na mkono wake, Edomu, na Moabu, na wakuu wa watu wa Amoni. 42 Naye ataunyosha mkono wake juu ya nchi hizo, hata na nchi ya Misri haitaokoka. 43 Lakini atakuwa na nguvu juu ya hazina za dhahabu na fedha, na juu ya vitu vyote vya Misri vyenye thamani; na Walibia na Wakushi watafuata nyayo zake. 44 Lakini habari zitokazo mashariki na kaskazini zitamfadhaisha; naye atatoka kwa ghadhabu nyingi, ili kuharibu, na kuwaondolea mbali watu wengi. 45 Naye ataweka hema zake za kifalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa uzuri; lakini ataifikilia ajali yake, wala hakuna atakayemsaidia.

 

Kipindi cha kutamalaki na kutiisha ulimwengu cha Mnyama wa Pili na wa Tatu kitatokea kwa kipindi kifupi cha vita katikati ya wakati atakapoenda mbele kuelekea kutoka Mashariki ya Kati kuyatiisha mataifa ambayo yanampigia kelele kutokana na habari za kutoka Mashariki. Hi ni kipindi kilichotajwa kwenye Ufunuo kama ni Timetable of the Agita za Baragumu ya Tano nay a Sita. Thelithi moja ya watu watauawa kwenye vita hivi. Kwa kipindi cha miezi 42 ambacho Mnyama na Nabii wa Uwongo na Mpingakristo watatawala kutoka Yerusalemu watakuwa wanapingwa na Mashahidi Wawili watakaotumwa na Mungu kusimama mbele yao. Hawa ni Henoko na Eliya ambao walitumwa kusimama mbele ya Mungu wa Dunia hii (soma jarida la Mahahidi (wakiwemo wale Mmashahidi Wawili (Na. 135)).

 

Kwa hiyo ndipo tutakabiliwa na ujio wa Masihi kuja kushika hatamu za kuitawala hii dunia na kuurejesha Ufalme wa Mungu (soma jarida la Kungojea Ujio wa Masihi (Na. 210A)).

 

9 Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao. 10 Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.

 

Vitabu vilifunguliwa ili kuwaja wale walio kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu. Hawa ni wale waliochaguliwa (soma jarida la Mbingu, Jehanamu au Ufufuo wa Wafu (Na. 143A)). Katika kipindi hiki cha ujio wa Masihi, Mpingakristo na Nabii wa Uwongo wataangamizwa na Dola ya Mnyama itaangamia yote kabisa. Haya pia ni matukio yaliyoelezewa kwenye Danieli sura ya 12:1-13. Matukio ya nyakati moja, nyakati mbili na nusu wakati ni jumla ya siku 1260 za Mashahidi wa nyakati za mwisho wakati Watakatifu watakapotawanyika. Ni baada ya miaka hii mitatu na nusu ambayo tutakuwa tumefufuliwa kama ilivyoelezewa kwenye sura ya 12.

 

11 Nikatazama wakati huo; kwa sababu ya sauti ya yale maneno makubwa iliyoyasema ile pembe; nalitazama hata mnyama yule akauawa, mwili wake ukaharibiwa, akatolewa ateketezwe kwa moto.

 

Kumbuka kutoka kwenye maandiko kwamba Wanyama watatu waliopita hawakuuawa na uhai au maisha yao yaliongezwa. Ni kwenye kipindi hiki wakati Dola ya Mnyama ikiangamizwa ndipo Kristo atakapoanza kuyashughulikia mataifa yaliyo chini ya Wanyama hawa.

 

12 Na kwa habari za wale wanyama wengine, walinyang'anywa mamlaka yao; walakini maisha yao yalidumishwa kwa wakati na majira.

 

Ndipo tutamuona Masihi akija akitokea mbele ya Mzee wa Siku na akiwa amepewa mamlaka kamili ya kuitawala dunia.

 

13 Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye. 14 Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.

 

Kisha Danieli anapewa ufafanuzi wa maana yake.

15 Basi, mimi Danieli, roho yangu ilihuzunika mwilini mwangu, na hayo maono ya kichwa changu yakanifadhaisha. 16 Nikamkaribia mmoja wa hao waliosimama karibu, nikamwuliza maana ya kweli ya hayo yote. Basi akaniambia, akanijulisha tafsiri ya mambo hayo. 17 Wanyama hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani. 18 Lakini watakatifu wake Aliye juu wataupokea ufalme, na kuumiliki huo ufalme milele, naam hata milele na milele.

 

Kisha tunaona kwamba utawala na dini ya Mnyama ni ule wa Mpingakristo ndiyo inayofanya vita na kanisa.

 

19 Kisha nalitaka kujua maana ya yule mnyama wa nne, aliyekuwa mbali na wenziwe wote, mwenye kutisha sana, ambaye meno yake yalikuwa ya chuma, na makucha yake ya shaba; aliyekula, na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; 20 na habari za zile pembe kumi zilizokuwa kichwani mwake, na ile pembe nyingine iliyozuka, ambayo mbele yake zilianguka pembe tatu; yaani, pembe ile yenye macho, na kanwa lililonena makuu, ambayo kuonekana kwake kulikuwa hodari kuliko wenzake.

 

Vita hivi vitakomeshwa kwa kuingiliwa na Mungu na Watakatifu wataokolewa kwa iungiliaji huu wa Mungu nao watahukumiwa. Ufalme wa Nne wa Mnyama nao unaelezewa.

 

21 Nikatazama, na pembe iyo hiyo ilifanya vita na watakatifu, ikawashinda; 22 hata akaja huyo mzee wa siku, nao watakatifu wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia watakatifu waumiliki ufalme. 23 Akanena hivi, Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia, utakaokuwa mbali na falme zile zote, nao utakula dunia yote, na kuikanyaga, na kuivunja vipande vipande. 24 Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu. 25 Naye atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.

 

Mnyama huyu na mfumo wake chini ya Mpingaktisto watawatawala watakatifu kwa kipindi cha miaka 1260 yangu mwaka 590 BK hadi mwaka 1850 BK ya Dola Takatifu ya Rumi na pia kwenye vita vya mwisho kwa kipindi chote cha siku 1260 na zote mbili, yaani Vita ya II ya Dunia ya Manazi na kipindi cha siku 1260 za Mashahidi kabla ya Kuja kwa Masihi.

 

26 Lakini hukumu itawekwa, nao watamwondolea mamlaka yake, kuipoteza na kuiangamiza, hata milele. 27 Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii. 28 Huu ndio mwisho wa jambo lile. Nami, Danielii, fikira zangu zilinifadhaisha, na uso wangu ulinibadilika; lakini naliliweka jambo hilo moyoni mwangu. [

 

Kipijndi hiki ni cha utawala wa Milenia wa Kristo na Kanisa kutoka Yerusalemu tangu mwaka 2018 hadi 3027 na miaka mia moja ya Ufufuo wa Pili wa watu na Hukumu (soma jarida la Ufufuo wa Pili wa Wafu na Kiti cha Enzi Kikubwa Cheupe cha Hukumu (Na. 143B)).

 

Kwa hiyo ni kutokana na yubile inayofuatia wakati wa tukio Kubwa la Kutoka (sawa na ilivyo pia kwenye Isaya 65).

 

Zekaria 10:10-12

10 Tena nitawarudisha toka nchi ya Misri, nitawakusanya na kuwatoa katika Ashuru; nami nitawaingiza katika nchi ya Gileadi na Lebanoni; ila nafasi ya kuwatosha haitaonekana. 11 Naye atapita kati ya bahari ya mateso, na kuyapiga mawimbi ya bahari, na vilindi vyote vya mto wa Nile vitakauka; na kiburi cha Ashuru kitashushwa; na fimbo ya enzi ya Misri itatoweka. 12 Nami nitawatia nguvu katika Bwana; nao watatembea huko na huko katika jina lake, asema Bwana.

                                   

Zekaria 11:1-3

1 Ifungue milango yako, Ee Lebanoni, Ili moto uiteketeze mierezi yako. 2 Piga yowe, msunobari, maana mwerezi umeanguka, Kwa sababu miti iliyo mizuri imeharibika; Pigeni yowe, enyi mialoni ya Bashani, Kwa maana msitu wenye nguvu umeangamia. 3 Sauti ya wachungaji, ya uchungu mwingi! Kwa maana utukufu wao umeharibika; Sauti ya ngurumo ya wana-simba! Kwa maana kiburi cha Yordani kimeharibika.                       

 

Kumbuka kuwa Mnyama wa Siku za Mwisho ni muunganiko wa mambo haya tofauti ya Wanyama hawa watatu.

 

Ufunuo 13:1-10

1 Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya makufuru. 2 Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi. 3 Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa jeraha la mauti, na pigo lake la mauti likapona. Dunia yote ikamstaajabia mnyama yule. 4 Wakamsujudu yule joka kwa sababu alimpa huyo mnyama uwezo wake; nao wakamsujudu yule mnyama, wakisema, Ni nani afananaye na mnyama huyu? Tena ni nani awezaye kufanya vita naye? 5 Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili. 6 Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na maskani yake, nao wakaao mbinguni. 7 Tena akapewa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na jamaa na lugha na taifa. 8 Na watu wote wakaao juu ya nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia. 9 Mtu akiwa na sikio na asikie. 10 Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.

 

Kumbuka kwamba Mnyama huyu anaabudiwa na ulimwengu wote na anafanyika kuwa yeye mwenyewe ni mtu wa kuabudiwa na awe kwenye mfumo wa kidini. Anabidi kuangamizwa kabisa na wote wanaogongwa mhuri wake hawataurithi ufalme wa Mungu na hawataingia kwenye kipindi cha utawala wa Milenia. Mambo haya yameandikwa kwenye majarida yaliyotajwa hapa (soma pia majarida ya Vita Vya III vya Dunia Sehemu ya I: Dola ya Mnyama (Na. 299A) na pia Vita vya III vya Dunia Sehemu ya II: Mwanamke Kahaba  na Mnyama (Na. 299B)).

                                                            q