Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[263]

 

 

 

Torati na Amri ya Kumi

(Toleo La 2.0 19981011-20120512-20120819)

 

Imeandokwa: Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako. Jarida hili linafafanua mfumo mzima wa Torati an Shria za Mungu, kama inavyotakiwa au kuendana na Amri zake kama zilivyoelezewa na Manabii na jinsi Agani hili linavyoendana na agizo la Usomaji wa Torati katika mwaka wa Saba ambao hujulikana pia kama mwaka wa Sabato.

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Haki Miliki © 1998, 1999, 2012  Wade Cox)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki..

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 


Torati na Amri ya Kumi

 


Imeandikwa: “Usitamani”

Kutoka 20:17 Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.

 

Kumbukumbu la Torati 5:21 Wala usimtamani mke wa jirani yako; wala usiitamani nyumba ya jirani yako, wala shamba lake, wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng'ombe wake, wala punda wake, wala kitu cho chote alicho nacho jirani yako

 

Amri hii ya kumi inaielezea au kuiweka Torati kwenye kiwango chake cha juu cha kiroho na kimtazamo. Inaifanya Torati ikae akilini na mioyoni na inatoa mwongozo wa jinsi ya kutembea au kuishi kwa wateule wake. Kitendo cha kuvunja amri hii inayohusu kutamani, kama zilizo amri nyingine zote zilizoorodheshwa, ni tendo lililo sawa na kuvunja amri hizi zote nyingine.

Warumi 7:7 Tusemeje, basi? Torati ni dhambi? Hasha! Walakini singalitambua dhambi ila kwa sheria; kwa kuwa singalijua kutamani, kama torati isingalisema, Usitamani.

 

Utaratibu ulioko kwenye amri hii ya kumi unafuatiwa na ule wa Amri Kuu Mbili, na ni sawa tu na kama zilivyo amri nyingine zote tisa zilizotangulia, na mbazo zimetuama tu kwenye upendo wa Mungu.

Mathayo 22:36-38 Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? 37 Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. 38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza

 

Utaratibu wa Mungu na Mamlaka yaliyo kwenye Torati

Mungu ameweka sheria zake hadi utimilifu na ukamilifu wote wa mpango wake kwa kipindi chote na ufufuko wa maisha na hukumu.

Mathayo 5:17-32 inasema: Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. 18 Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie. 18 Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. 20 Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. 21 Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu.  22 Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto. 23 Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako, 24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako. 25 Patana na mshitaki wako upesi, wakati uwapo pamoja naye njiani; yule mshitaki asije akakupeleka kwa kadhi, na kadhi akakupeleka kwa askari, ukatupwa gerezani. 26 Amin, nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho. 27 Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake. 29 Jicho lako la kuume likikukosesha, ling'oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum. 30 Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum. 31 Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka; 32 lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.

 

Utaratibu wote na mkamilifu wa Torati ulifasiriwa vyema na kuwekwa kwenye mtazamo wa kiroho na Masihi. Alimpa Torati nabii Musa na hatimaye Masihi akamuwezesha kuzielewa wa jinsi zilivyokuwa zinatakiwa kuadhimisha au kutunzwa.

Kumukumbu la Torati 27:26 Na alaaniwe asiyeyaweka imara maneno ya torati hii kwa kuyafanya. Na watu wote waseme, Amina.

 

Mamlaka na uweza wote ni wa Mungu, hata kwa uweza wote unaoonekana kuwanao Shetani kwa pale anaporuhusiwa kuuonyesha na kwa Wateule wa siku za mwisho. Mungu sio mlinzi wa mtu kama tulivyojionea kwenye maandiko yafuatayo: (Walawi 19:15; Kum. 1:17; 16:19; 2Sam. 14:14; 2Nya. 19:7; Mithali 24:23; 28:21; Warumi 2:11; Waefeso 6:9; Wakolosai 3:25; Yakobo 2:1; 2:9; 1Pet. 1:17). Mungu hutoa nguvu na fursa katika mipango yake.

 

Imani ya Waamini Mungu Mmoja au Monotheism ni imani inayoamini kuwa makududio yote yanatokana na mipango aliyoikusudia Mungu Mmoja Wapekee na wa Kweli, afanyaye kazi kupitia kwa Yesu Kristo aliyemtuma (Yohana 17:3).

 

Mateso ya watu wa Mungu yafanywayo kwa chuki

Kutoka 1:1-14 inasema: Basi majina ya wana wa Israeli walioingia Misri ni haya; kila mtu pamoja na jamaa zake walikuja pamoja na Yakobo. 2 Reubeni, na Simeoni na Lawi, na Yuda; 3 na Isakari, na Zabuloni, na Benyamini; 4 na Dani, na Naftali, na Gadi, na Asheri. 5 Na nafsi zile zote zilizotoka viunoni mwa Yakobo zilikuwa ni nafsi sabini; na huyo Yusufu alikuwa huko ndani ya Misri tangu hapo. 6 Yusufu akafa, na ndugu zake wote, na watu wote wa kizazi kile. 7 Na wana wa Israeli walikuwa na uzazi sana, na kuongezeka mno, na kuzidi kuwa wengi, nao wakaendelea na kuongezeka nguvu; na ile nchi ilikuwa imejawa na wao. 8 Basi akainuka mfalme mpya kutawala Misri, asiyemjua Yusufu. 9 Akawaambia watu wake, Angalieni, watu wa wana wa Israeli ni wengi tena wana nguvu kuliko sisi. 10 Haya! Na tuwatendee kwa akili, wasije wakaongezeka; tena, ikitokea vita, wao nao wasije wakashikamana na adui zetu na kupigana nasi, na kutoka katika nchi hii. 11 Basi wakaweka wasimamizi juu yao wawatese kwa mizigo yao. Nao wakamjengea Farao miji ya kuwekea akiba, Pithomu na Ramesesi. 12 Lakini kwa kadiri ya walivyowatesa ndivyo walivyoongezeka na kuzidi kuenea. Nao walichukiwa kwa sababu ya wana wa Israeli.
13 Wamisri wakawatumikisha wana wa Israeli kwa ukali; 14 wakafanya maisha yao kuwa uchungu kwa kazi ngumu; kazi ya chokaa na ya matofali, na kila namna ya kazi ya mashamba; kwa kazi zao zote walizowatumikisha kwa ukali.

 

Farao na Wamisri hapa waliwatendea Israeli kwa hila ya hali ya juu. Ni sawa tu, na kutamani ukuaji na hali njema waliyokuwanaye na kuuogopa uweza waliokuwanao watu wa Mungu mtu anayetamani, ndipo adui akaweka mpango wa kuwaangamiza. Hata hivyo, Bwana akawawekea mpango wa kuwaokoa watu wake hawa katika kipindi chake muafaka kilivyofika.

 

Kutoka 2:16-25  Basi kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao wakaja wakateka maji, wakazijaza birika maji, wapate kunywesha kundi la baba yao. 17 Wachungaji wakaja wakawafukuza; lakini Musa akasimama, akawasaidia, akalinywesha kundi lao. 18 Walipofika kwa Reueli baba yao, akasema, Imekuwaje hata mkarejea mapema leo? 19 Wakasema, Mmisri mmoja alituokoa katika mikono ya wachungaji, tena zaidi ya hayo, akatutekea maji, akalinywesha kundi. 20 Akawaambia binti zake, Yuko wapi basi? Mbona mmemwacha mtu huyo? Mwiteni, ale chakula. 21 Musa akawa radhi kukaa kwake mtu yule, naye akampa Musa binti yake, Sipora. 22 Huyo akamzalia mwana, akamwita jina lake Gershomu, maana alisema, Nimekuwa mgeni katika nchi ya ugeni. 23 Hata baada ya siku zile nyingi mfalme wa Misri akafa; wana wa Israeli wakaugua kwa sababu ya ule utumwa, wakalia; kilio chao kikafika juu kwa Mungu kwa sababu ya ule utumwa. 24 Mungu akasikia kuugua kwao, Mungu akakumbuka agano lake alilolifanya na Ibrahimu na Isaka na Yakobo. 25 Mungu akawaona wana wa Israeli, na Mungu akawaangalia.

 

Kutoka 3:1 Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.

 

Ndipo Mungu alipomuita mkombozi wake kwa lengo lake maalumu alilolipanga. Mungu akafanya ukombozi kwa kipindi chake alichokiweka mwenyewe na kilichokuwa mwafaka kwake. Amri hii ya kumi inafundisha uvumilivu na subira kwenye mambo na mipango ya Mungu.

 

Hiyari za kuasi

Tendo la kukusudia kufanya uasi kwa kuyaasi maelekezo au Mapenzi ya Mungu Mmoja na wa Pekee na wa Kweli ni kama kufuata imani au itikadi ya kuamini Miungu wengi maarufu kama. Polytheism, ambao unatafuta tu jinsi ya kufanya mambo kinyume na ilivyo au yatokanayo mbali na mapenzi ya Mungu Mmoja wa Pekee na wa Kweli. Kristo aliyatenda na kuyatii mapenzi ya Baba kwa kila namna (Yohana 6:38-40).

 

Mungu anayajua tunayohitaji na kila jambo limewekwa kwenye mpango maalumu wa mipangilio yake. Tamaa inapingana na imani kwa kuwa inaoneashaka uwezo wa Mungu kutupa mahitaji yetu na mambo mema alayotukusudia na kuyapanga kwetu. Wana wa Israeli walipewa mana ili kwamba mkate wao na maji view ni vitu vya uhakika kwao kuvipata, jambo ambalo ndilo alilotuahidi sisi kwenye kipindi hiki cha mwisho tulicho hapa jangwani (Zaburi 37:25; Isaya 33:16; sawa na Hesabu 11:1-35).

 

Tunapaswa kushukuru kwa kila jambo—yaani kuwa na tabia ya shukrani kwa yale yote ambayo Bwana, Mungu ametupa. Kwa kuwa tamaa ya mwili nay a mali ni machukizo na vinawasha hasira ya Mungu.

 

Uasi umefananishwa na dhambi ya uchawi (1Samweli 15:23). Kwa hiyo, dhambi ya uchawi na ulozi au ushirikina unazuia uwezekano wa kutimilizwa kwa yale aliyoapanga na kuyakusudia Mungu. Matendo ya kishirikina ya kutazama nyakati na kuzichunguza nyakati kwa kupiga bao ni mambo yanayofanyika kwa tama ya kujua mambo yajayo ili kuchukua hatua kwa kufanya matendo yaliyo kinyume na mapenzi ya Mungu.

Kumbukumbu la Torati 18:10-14 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, 11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu. 12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako. 13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako. 14 Maana mataifa haya utakaowamiliki huwasikiliza wanaoshika nyakati mbaya na kutazama bao; bali wewe, Bwana, Mungu wako, hakukupa ruhusa kutenda hayo

 

Tendo la kupandisha mapepo ili kuwasiliana na maroho yanapingana na imani, na wwenye haki wataishi kwa imani (Warumi 1:17; 2Cor. 5:7).

 

Sabato kama Ishara ya Mungu na Uweza wake

Mungu aliweka utaratibu wake kwa mujibu wa nyakati zake muafaka na kwa kuifuata kalenda yake na sio kwa mujibu wa kalenda ya mungu wa dunia hii. Ndio maana kwamba kalenda ypte ya mfumo wa dunia hii, ikiwemo ile potofu ya mfumo wa Hilelli iliyo chini ya baraza la Kiyahudi la Talmudi, ni lazima iondolewe ama kurudishwa kwenye mfumo wa kalenda iliyotumika kipindi cha Hekalu (sawa na Ufunuo 23:1-44; Hesabu 15:3; 29:39; 1Nyakati 23:31; Ezra 3:5; Nehemia 10:33). Kalenda inayofuata mfumo wa Juan a Kalenda ya Wahilleli ya Kiyahudi zote hizi zinapingana au ziko kinyume na Mapenzi ya Mungu na Mungu anasema kwamba anazichukia sikukuu zao (Isaya 1:14) kwa kuwa wamezitia unajisi Sikukuu Zake.

 

Mfumo mzima wote wa kuabudu siku za Jumapili umetuama kwenye teolojia ya kipagani ambao ni kinyume kabisa na mapenzi ya Mungu na sheria zake zilivyo zilizotolewa kwenye maagizo au maelekezo yaliyo kwenye amri ya nne (soma jarida la Torati na Amri ya Nne (Na. 256) [Law and the Fourth Commandment (No. 256))].  Teolojia yoyote inayokingia kifua ibada hizi za siku ya Jumapili ziko kinyume na zinapingana na kugeuza mafundisho yenye uzima nay a kweli yaliyoko kwenye Maandiko Matatifu na yanapotosha maelekezo ya uumbaji ambayo yanatuama kwenye mapumziko yz Sabato ya Mungu katika siku ya saba na ambayo ni Sabato. Siku ya kwanza ya juma haina misingi kwenye maelekezo haya, zaidi ya kuwa tu ni siku ya kuanza juma jipya lenye siku saba nyingine kama yanavyoeleza maelezo haya. Dhana ya siku hii yenyewe inatokana na mawazo ya watu wenye tama ya kimapepo, ambayo ni uvunjaji tena wa amri hii ya kumi.

 

Jinsi tamaa inavyopelekea Uvunjifu wa Amri Kuu ya Pili

Tamaa ya mwili inapingana na amri au sheria kwa mtindo wa kiroho na unaifanya nia ya mtu kuserereka chini hadi kuwaka tamaa za kimwili ambayo hupelekea kutenda dhambi. Sisi ni watu wa Mungu na tumekusudiwa tumuabudu kwa Roho na kweli.

 

Imeandikwa:

Mathayo 22:39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako

 

Warumi 13:9 Maana kule kusema, Usizini, Usiue, Usiibe, Usitamani; na ikiwapo amri nyingine yo yote, inajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako.

 

Msisitizo wa umuhimu wa sheria kumefungamanishwa kwenye maelezo haya: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.” Ni kwa kiasi gani basi amri hii ya kumi inahusiana na dhana hii?

 

Kumkosea au kumkwaza jirani

Mambo ya Walawi 19:13 Usimdhulumu jirani yako, wala kumnyang'anya mali yake; ijara yake aliyeajiriwa isikae kwako usiku kucha hata asubuhi.

Makosa ya msingi ya udanganyifu na wizi ni kama tulivyojionea hapo juu ni, matendo yanayofanywa kwa mwili na lakini yote yametuama kwenye mchakato wa kimawazo ambao unampelekea mtu kutenda dhambi. Dhambi inashambulia mahusiano ya jamii na kuathiri uhuru wa watu.

 

Nguvu za taifa inatokana na hali ya uhuru na utushelevu wa watu. Utumwa ni laana kwa mujibu wa mfumo na mapenzi ya Mungu na roho ya kurithi laana za mababu katika familia, ambayo inaipatiliza mawazo ya wana wa Mungu. Tendo la kumtamani mtumwa wa mwingine linaingilia uwezo wa mtu kufanya kazi na kuzishika amri na sheria hizi.

 

Mtumwa aliyemtoroka bwana wake anadhaniwa amefanya hivyo kwa sababu ya haki, na mtumwa huyo haruhusiwi kurudishwa kwa bwana wake na wale waliomuona; bali badala yake anapaswa kupewa hifadhi na msaada anaohitaji na wale waliomuona au aliowakimbilia kujihifadhi kwao.

Kumbukumbu la Torati 23:15-16 Usimrudishe kwa bwana wake mtumwa aliyejiponya kutoka kwa bwana wake kuja kwako; 16 na akae nawe, katikati yako, ndani ya malango yako mojawapo, mahali atakapochagua palipo pema machoni pake; usimwonee.

 

Sharia hii inaenda pia hadi kwenye roho au hali ya ukimbizi kwa mkimbizi aliyetoroka kwa sababu za halali, kwa kulinda na kuyahifadhi maisha au uhai wake, bali haimfanyi kumwondolea mwenendo usio muhimu kwa kujitafutia umaarufu wa hali bora zaidi ya kimaisha. Wengi wa wale wanaokimbia nchi zao wanakuwa na sababu za msingi hasa zinazotokana na taifa lao kushindwa kuzishika au kuziogopa amri za Mungu kwa namna moja au nyingine.

 

Dhambi au uovu

Sheria ya “jicho kwa jicho” iliwekwa mahali pa kushughulikia makovu yaliyotokana na sababu zilizotokana na dhambi hii ya kutamani.

Mambo ya Walawi 24:19-20  Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo; 20 jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo.

 

Kristo alikuwa na mengi ya kusema kuhusu mtazamo wetu kwa ajili ya makosa au dhambi hizi na upendo wetu kwa jirani yetu na wajibu wetu katika kutoa msamaha. Hata hivyo, sheria imewekwa ili itumike chini ya mazingira yanayoifanya iwe sahihi.

 

Jinsi tamaa inavyofananishwa na ibada ya sanamu

Utaratibu huo uko kwenye kiwango cha juu kwenye amri ya kumi na ukweli huu mara nyingi umesifiwa sana.

 

Waefeso 5:5 Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.

Tendo hili la tama ya mwili ni ibada ya sanamu na inamtenganisha mtu na ufalme wa Mungu.

 

Utaratibu wa sheria na zawadi au kipawa cha Mungu mara nyingi umewekwa na kufanyizwa kwa hali ya kumstahi mtu pasipo kuwadhalilisha watu.

Mathayo 20:13-16 Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari? 14 Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe. 15 Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema? 16 Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.

 

Sisi sote tunafanya kazi kwa ajili kupokea mshahara wa aina moja nasi sote tumeahidiwa wokovu, ambao ni kipawa cha Mungu tunaoupata kwa neema tu. Ni sawa tu na haijalishi ni kwa muda gani au ni vigumu kiasi gani tunatumika kwenye shamba hili la mizabibu la Bwana Mungu wetu. Thawabu yetu pia imeelezwa kuwa ni kupewa miji. Hata hivyo, wote tumeokolewa kwa damu ya Kristo tukiwa kama miongoni mwa warithi kulioruzukiwa kwa kazi zetu. Kuzitii sheria za Mungu au Torati yake hakutufanyi kuupate wokovu au uzima wa milele. Hata hivyo, kuzitii sheria za Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo ni utaratibu ambao kwao tunajipatia kipawa cha neema na wokovu wa milele. Hatuokolewi kwa ajili ya kuzishika kwetu sheria au amri. Na wala hatuokolewi kwa matendo yetu au kazi zetu. Hata hivyo, tunaruzukiwa kipawa na kuwa na sehemu kwenye ufalme kwa jinsi vile tunavyoendelea kuzitii amri hizi za Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo (Ufunuo 12:17; 14:12) na hii ni tofauti kuu na ya msingi kati ya imani na matendo, jambo ambalo halieleweki na Wakristo walio kwenye mrengo wa kuabudu siku ya Jumapili, marabi wa Kiyahudi na Waislamu wanaoamini Hadidhi za kidini. Na tunajua kwamba imani pasipo na matendo imekufa (Yakobo 2:17).

 

Wale ambao hawamtukuzi Mungu bali wanatafuta kujitukuza wao wenyewe au wengine walio kwenye daraja lake kwa namna ya kutamani kimwili ni wajinga. Watu wengi walioitwa wameangukia kwenye hasara ya kupoteza sehemu yao kwenye ufalme kwa kupitia makosa haya ya kufikiri (soma Warumi 1:22; 8:29-30).

 

Jinsi tamaa ya mwili inavyoleta madhara na kuiathiri Familia

Tamaa ya mwili isiachiwe ikiingilia na kuathiri ustawi wa familia, ambayo ni msingi na chanzo cha taifa.

Kutoka 21:3-11 Kwamba aliingia kwako peke yake tu, atatoka hivyo peke yake; kwamba ameoa, mkewe atatoka aende pamoja naye. 4 Kwamba ni bwana wake aliyempa huyo mke, naye amemzalia wana, wa kiume au wa kike; yule mke na wanawe watakuwa ni mali ya bwana wake, naye mume atatoka peke yake. 5 Lakini huyo mtumwa akisema waziwazi, Mimi nampenda bwana wangu, na mke wangu na watoto wangu; sitaki mimi kutoka niwe huru; 6 ndipo hapo huyo bwana wake atamleta mbele ya Mungu na kumleta mlangoni, au penye mwimo wa mlango; na bwana wake atalitoboa sikio lake kwa uma; ndipo atamtumikia sikuzote. 7 Mtu akimwuza binti yake awe kijakazi, hatatoka yeye kama watumwa wa kiume watokavyo. 8 Kwamba bwana wake hakupendezewa naye, akiwa amemposa, ndipo atakubali akombolewe; hana amri yeye kumwuza aende kwa watu wageni maana amemtenda kwa udanganyifu. 9 Kwamba amposa mwanawe, atamtendea kama desturi zipasazo binti zake.
10 Kwamba ajitwalia mke mwingine, chakula chake huyo, na nguo zake, na ngono yake, hatampunguzia. 11 Kwamba hamfanyii mambo haya matatu, ndipo atatoka aende bure, pasipo kutolewa mali.

 

Totari au sheria hairuhusu mtu yeyote kutendewa vibaya kwa matamanio au kudhalilishwa. Wazo lolote linalopinga wokovu kwa Wamataifa kwa nia ya kuwafanya waendelee kutozwa riba na malipo ya ziada—hata kwa kiasi cha kukanusha jinsi wanavyotakiwa kuitwa na kuwanacho chenye kuwaokoa maisha yao kwa dharura kama tuliyoiona kwa Watalmudi wa Kiyahudi (soma jarida la Torati na Amri ya Sita (Na. 259) [Law and the Sixth Commandment (No. 259)] – wanaotokana na mabadiliko au upotoshaji mkubwa wa sheria za Mungu na makufuru dhidi ya mfumo na taratibu zake upendo na utaratibu. Ndiyo maana Masihi alilaumiwa na kushitakiwa na Mafarisayo, na ndoyo maana walimuua badala ya kutubu. Ni aina hiyohiyo ya mawazo au fikra potofu ziliinua kwa lengo lililokuwa kinyume na imani ya kiyahudi na Uislamu na kusababusha mateso ya Wakristo.

 

Jinsi Tamaa inavyohusiana na Uuaji na Uzinifu

Mauaji yote yanatokana na hasira na tama za mwili au chuki. Hili ndilo somo la msingi na alilokazia sana kwenye mafundisho yake Masihi.

Mathayo 5:21-28 Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu. 22 Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto. 23 Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako, 24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako. 25 Patana na mshitaki wako upesi, wakati uwapo pamoja naye njiani; yule mshitaki asije akakupeleka kwa kadhi, na kadhi akakupeleka kwa askari, ukatupwa gerezani. 26 Amin, nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho. 27 Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.

 

Mawazo haya yanaendela hadi kufikia kiwango cha kumchukia jirani. Neno Raca limeachwa bila kufasiriwa na watu wa Magharibi kwa kuwa hawakuliewa maana yake. Ni neno lenye asili ya Kiaramu ambalo maana yake ni “jichune uso wako.” Lilikuwa linatumika kwenye mapatano ya kuomba punguzo la bei na ni neno lililotumiwa kuomba punguzo la bei kwenye masuala ya kibiashara lililotumiwa na watu wa upande mwingine (soma na ujionee lilivyotumiwa kwenye kamusi maarufu ya Tafsiri ya Lamsa kwenye toleo la kamusi ya Peshitta).

 

Ni neno tunalolitumia sisi ambalo limepunguzwa maana yake.

Mathayo 15:10-20 Akawaita makutano akawaambia 11 Sikilizeni, mfahamu; Sicho kiingiacho kinywani kimtiacho mtu unajisi; bali kitokacho kinywani ndicho kimtiacho mtu unajisi. 12 Ndipo wanafunzi wake walipomwendea, wakamwambia, Wajua ya kuwa Mafarisayo walipolisikia neno lile walichukizwa? 13 Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang'olewa. 14 Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili. 15 Basi Petro akajibu, akamwambia, Tueleze mfano huo. 16 Yesu akasema, Hata sasa ninyi nanyi mngali hamna akili? 17 Hamjafahamu bado ya kuwa kila kiingiacho kinywani hupita tumboni, kikatupwa chooni? 18 Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi. 19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano; 20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi.

 

Hapa tunajionea kwamba nguvu za mawazo na kutamani ni kuielewa hali ya kiroho chetu.

Mika 2:1-2 Ole wao wakusudiao mambo maovu, na kutenda mabaya vitandani mwao! Kunapopambazuka asubuhi huyafanya, kwa sababu ya katika uwezo wa mikono yao. 2 Nao hutamani mashamba, na kuyashika; na nyumba pia, nao huzichukua; nao humwonea mtu na nyumba yake, naam, mtu na urithi wake.

 

Hii ilipewa nguvu zaidi na mke wa Ahabu, Yezebeli (1Wafalme 21:1-29) na pia na Daudi na mke wa Uria Mhiti (2Sam. 11:1-12:9). Kwenye matukio haya yote mawili tunaona kwamba tama ya mwili ilipelekea au ilisababisha mauaji, ingawaje ushahidi wa uwongo na matumizi mabaya ya mamlaka na cheo dhidi ya mtu aliyetoka kwenye familia ya kifalme vilifanyika. Kwenye kila moja ya matukio haya Bwana alimuinua au kumtuma nabii akashughulike na matatizo haya ya matumizi mabaya ya madaraka.

 

Kila ilipookiukwa na kuvunjwa kwa amri hii ya kumi kwa njia hii ya kuwaka tamaa kulitokea matokeo ya uzinifu, kama alivyoonekana Daudi na Bersheba.

Mathayo 5:27-28 Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; 28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake

Sheria hii ya juu inashindana na maandalizi ya mawazo yalivyo na roho katika uwajibikaji wake kwa Mungu.

 

Jinsi kutamani kunavyofafana na Wizi

Tamaaa inampelekea mtu kufanya dhambi ya wizi pia, kama tunavyoona kwenye tukio la 1Wafalme 21 jinsi alivyofanya Ahabu katika kudhulumu shamba. Pia tamaa inamsababisha mtu avunje taratibu au kanuni za Mungu na kumfanya apoteze sehemu yake katika ufalme wa Mungu, kama tilivyokwisha kujionea kwenye tukio la Akani (Yoshua 7:19-21).

 

Utaratibu wote uliowekwa wa utoaji wa zaka ya fungu la kumi na kuwekwa kwenye amri za Mungu ni chanzo au mlango wa kuinyesha nia ya kupenda kuishika sheria na ni amri ya kwanza kuanguka kwayo wakati moyo wa kupenda kuishika sheria inapokuwa inavunjwa. Kwa hiyo, sheria inaendelea kutoka kwa Mungu na inashikiliwa na kusababisha ukamilifu wa kiroho na utimilifu wa amri ya kumi.

 

Mambo ya Walawi 6:1-7 Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 2 Mtu awaye yote akifanya dhambi, na kuasi juu ya Bwana, akamdanganya mwenziwe katika jambo la amana, au la mapatano, au la kunyang'anya, au kumwonea mwenziwe; 3 au kuzumbua kitu kilichopotea na kutenda la uongo juu yake, na kuapa kwa uongo; katika mambo hayo yote mojawapo atakalolitenda mtu, na kufanya dhambi kwalo; 4 ndipo itakapokuwa, akiwa amefanya dhambi, na kupata hatia, atarudisha hicho alichokipata kwa kunyang'anya, au kitu kile alichokipata kwa kuonea, au ile amana aliyowekewa, au kitu kile kilichopotea alichokizumbua yeye, 5 au kitu cho chote ambacho amekiapia uongo; atakirudisha hata kwa utimilifu wake, kisha ataongeza na sehemu ya tano zaidi juu yake; naye atampa huyo mwenyewe, siku hiyo ambayo atakapohukumiwa kuwa mwenye hatia. 6 Kisha ataleta sadaka yake ya hatia kwa Bwana, ni kondoo mume wa katika kundi lake, mkamilifu, sawasawa na hesabu utakayomwandikia, kuwa sadaka ya hatia, na kumpa kuhani; 7 na huyo kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana, naye atasamehewa; katika jambo lo lote alifanyalo hata akapata kuwa mwenye hatia kwalo.

 

Tumekwisha jionea kwenye jarida la Torati na Amri ya Nane na maandiko haya yanaonyesha marejesho makamilifu ya kimwili au ya kibinadamu. Maandiko yaliyo kwenye aya za 6 na 7 yanaelezea kuhusu sadaka ya dhambi, ambayo inaendeiea hadi kwenye kuponya yaliyovunjwa kwenye amri ya kumi na athari zake za kimawazo na masharti ya kiroho.

 

Dhambi zote hutoka kati yetu sisi na Munbu. Taifa linaangamia na watu wanashindwa kufikia kiwango husika na kuondolewa kwenye agano na kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu.

 

Mambo ya Walawi 20:10-11 Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na mwanamke aziniye, hakika watauawa. 11 Na mtu mume atakayelala pamoja na mke wa baba yake amefunua utupu wa baba yake; wote wawili hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.

Hii ni hukumu mbaya sana. Kristo alituonyesha kwamba ilikuwa hairuhusiwi kabisa kwa mujibu wa sheria au torati. Alionesha jinsi makatazo au uwekaji marufuku huu ulivyoshughulikiwa na ulivyochukuliwa wakati mwanamke mzinzi alipofanya toba, na akasema kwamba yeyote miongoni mwao anayejiona kuwa hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe. Tunaweza kufikiria ni nini kilichokuwa kinatokea pale. Hata hivyo, kitendo cha kukutwa na hatia ya dhambi mioyoni mwa kila mmoja wao, kilisababisha kundi lote litawanyike (Yohana 8:1-11). Jinsi hii ya kushughulika na torati inatuonyesha ukamilifu wa kinia na kimatendo.

 

Tendo la kuwaita ndugu kwa wageni au wasafiri walio kwenye nchi yao linaonekana kwenye Mambo ya Walawi 25:35-55. Kwa hiyo utozaji wa riba na malipo ya ziada havipaswi kufanywa kwa mtu yeyote yule katika nchi, wakiwemo wageni na wapitaji tulionao hata kwetu.

 

Tumekwisha jionea umuhimu wa sheria hii kwenye jarida la Torati na Amri ya Nane. Mkazo wote uliowekwa kwenye sheria hii ni kutuonyesha jinsi wazaliwa au wazawa wa Israeli walivuochukuliwa kuwa ni kitu cha thamani mno, na kwamba hakuna mtu aliyeweza kuwa mzaliwa na akaruhusiwa kuwa mwabudu sanamu. Kukataliwa kwa mawazo yasemayo kuwa fursa ya wokovu iliendelea na kuwafikia hadi Wamataifa kupitia kwa Yesu Kristo, lilipingwa kwa itikadi kali iliyokusudia na kupenda tu kupinga dhana hii ya kwamba wokovu unaweza kuwa na kwa mataifa mengine pia, jambo lililotokana na tamaa ya kutaka mali zao kwa kutumia maneno yasiyo na haki au ya kuwadhulumu. Mawazo ya namna hii yanaendelea kuwepo hata leo.

 

Watu wote wanaoishi kwenye taifa wanakusudiwa kuwa wana wa Mungu na taifa linapawa kuwaandaa kwa kazi hiyo. Wokovu ni wa ajili ya Wamataifa na Israeli wote wanapaswa kufurahia wanaoona kwamba hii imeruhusiwa.

 

Kutoka kwenye maandiko ya Kutoka  22:1-15 (soma jarida la Torati ya Amri ya Nane (Na. 261) [Law and the Eighth Commandment (No. 261)] tumeona sheria ya marejesho ya mali au kitu kilichopotea kwa kuibiwa. Sehemu kubwa ya andiko hili linaelezea upotevu uliotokea kwa matokeo ya moja kwa moja ya uvunjifu wa amri hii ya kumi na hasa kwa ajili ya udanganyifu au utapeli. Maandiko haya yanaeneo linayolezea pia madai yasiyo halali ya sheria. Iwapo kama mtu atadai umiliki wa kitu na kumbe akiwa sio mmiliki halali, basi akigundulika atatakiwa kutozwa faini mara mbili ya thamani ya kitu anachodai kuwa ni chake (Kutoka 22:9). Sheria hii ya ahabu inasaidia kuzuia kitendo hiki cha kujaribu kudai uhalali wa umiliki wa kitu kwa njia ya uwongo unaotokana na ushawishi wa tamaa mbaya na hila.

 

Kwenye maandiko haya tunajionea pia upotevu unaotokana na tamaa ya kupenda kufanywa mzuri na sheria, na madai ya uwongo yanayochochewa na tamaa yakitozwa faini. Kwenye maandiko haya hapa tunaenda mbali zaidi pia hadi kwenye mtazamo wa kuharibu kitu kwa kukichoma motoni na kukipoteza kwa makusudi, na kukiwa na uharibifu unaoonekana kuwa ni chanzo au sababu ya pili. Dhana ya uangalizi bora wa mali kwa anayehusika au mlindaji au kwa anayeishi karibu yake unaonekana hapa, na hii inafuatia pia kwenye amri ya kumi. Kujali au kutunza mali ya jirani yako kunatokana na upendo na hali ya kutilia maanani au kujali. Uharibifu mara nyingi unatokana au unasababishwa na tamaa ya mwili na mawazo mapotofu yaliyo moyoni mwa mtu.

 

Uharibifu wa mali kwa kuchoma moto kwa makusudi unatokana na athari ya magonjwa ya akili, haitajalisha, kama upotevu huo umefanywa kwa kuchoma moto kwa makusudi, kutafidiwa tu kwa kuchukuliwa kuwa ni uharibifu. Uchomaji moto kwa makusudi pamoja na wizi na ni vitendo vya uharibifu tu kwa ujumla wake, na mbavyo vinatokana na wivu au husuda. Wivu na husuda ni vitendo vinavyotokana na hali ya kupenda kuchukua au kuwa na kitu alichonacho mtu mwingine, wakati husuda maana yake ni kitendo cha kutaka kuangamiza kitu fulani au mtu fulani hasa anapokuwa mtu yule anamiliki kitu ambacho mwenye husuda anakuwa hana. Uvunjaji huu wa amri ya kumi ni tatizo kubwa sana linalotokana na akili ya mtu anapokuwa kati ya watu, na inamzuia aina hii ya mtu kuwa na sehemu kwenye Ufalme wa Mungu.

 

Hali hii ya tamaa inampelekea mtu hata kuiba ardhi na milki, ya maongeo na mifugo.

Kumbukumbu la Torati 27:17 Na alaaniwe aondoaye mpaka wa jirani yake. Na watu wote waseme, Amina.

 

Kumbukumbu la Torati 19:14 Usiiondoe alama ya mpaka wa jirani yako, waliouweka watu wa kale katika urithi wako, utakaorithi ndani ya nchi akupayo Bwana, Mungu wako, uimiliki.

 

Maqmbo ya Kiroho na Torati yote

Kusudi na nia ya sheria inaendambali hadi kufikia kuelekeza umuhimu wa kulinda mali ya adui zetu, sawa na kama tunavyolinda mali za ndugu zetu. Tunapoitazama na kuitafakari Torati hii ya Mungu jinsi inavyotenda kazi ulimwenguni kote kwa mtazamo wa Kiroho na kuifanya, basi tunakuwa tumetimiliza mapenzi ya Mungu.

Kumbukumbu la Torati 22:1-4 Umwonapo ng'ombe wa nduguyo au kondoo wake akipotea, usijifiche kama usiyemwona; sharti utamrudisha kwa nduguyo. 2 Na kwamba yule nduguyo hayupo karibu nawe, au ukiwa humjui, umchukue kwenu nyumbani kwako, uwe naye hata aje nduguyo kumtafuta, nawe mrudishie. 3 Tena fanya vivyo kwa punda wake; tena fanya vivyo kwa mavazi yake; tena fanya vivyo kwa kila kitu kilichopotea cha nduguyo, kilichompotea ukakiona wewe; usijifiche kama usiyekiona. 4 Umwonapo punda wa nduguyo, au ng'ombe wake, ameanguka kando ya njia, usijifiche kama usiyemwona; sharti umsaidie kumwinua tena.

 

Tunahitajika kurejesha kila kilichoharibika tunachokiona pasipo hata kuombwa na tunatakiwa kuwalinda maadui zetu kama tunavyojilinda sisi wenyewe.

 

Hakuna mtu anayetakiwa kujipatia faida kwa kupitia mgongo wa mwingine, iwe kwa njia ya wizi au kwa kutoza riba, kitendo ambacho ni wizi pia, na chenye nia ya kujipatia faida kwa kupitia nguvu za wengine.

Kutoka 22:25 Ukimkopesha mtu aliye maskini, katika watu wangu walio pamoja nawe; usiwe kwake mfano wa mwenye kumdai; wala hutamwandikia faida.

 

Na hakuna ahadi inayotakiwa iingilie uhuru au utulivu wa mwingine, au maisha yake au mambo yake binafsi au ya sirini mwake, na wala haipaswi kumpunguzia uwezo wake wa kuishi au wa kimaisha.

Kutoka 22:26-27 Ikiwa wewe kwa njia yo yote wapokea nguo ya jirani yako rehani, lazima utamrudishia mbele ya jua kuchwa; 27 maana hiyo nguo ni kifuniko chake, hiyo peke yake ni nguo ya ngozi yake; je! Atalalia nini? Itakuwa, hapo atakaponililia mimi, nitasikia; kwa kuwa mimi ni mwenye rehema

 

Tabia ya kutamani inamuondolea mtu mwenye tabia hii uweza wa kuingia kwenye ufalme wa Mungu, na unampelekea kwenye uvunjifu wa amri nyingine na, kwa ujumla kuzivunja sheria au amri nyingine zote.

q


 


 

HITIMISHO



Wakati Mungu alipowapa Israeli nchi ya ahadi waimiliki waliamriwa wazishike amri zake, kama tunavyoona kwenye Kumbukumbu la Torati 26. Israeli walifanywa kuwa kielelezo na mfano kwa mataifa na walipaswa kuwa ni sehemu ya Yahova na ni kiini na kielelezo cha Mpango wa Mungu.

 

Pamoja na baraka walizopewa na Mwenyezi, Mungu, kulikuwa na matendo ashirivu, kama tunavyoyaona kwenye Kumbukumbu la Torati sura za 11 na 27 (soma pia majarida ya Torati na Amri ya Sita (Na. 259) na Torati na Amri ya Tano (Na. 253) [Law and the Sixth Commandment (No. 259) and Law and the First Commandment (No. 253)].

Kumbukumbu la Torati 11:26-32  Angalieni, nawawekea mbele yenu hivi leo baraka na laana; 27 baraka ni hapo mtakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wenu, niwaagizayo leo; 28 na laana ni hapo msiposikiza maagizo ya Bwana, Mungu wenu, mkikengeuka katika njia niwaagizayo leo, kwa kuandama miungu mingine msiyoijua. 29 Tena itakuwa, atakapokuleta Bwana, Mungu wako, na kukutia katika nchi uendeayo kuimiliki, ndipo uiweke baraka juu ya mlima wa Gerizimu, na laana uiweke juu ya mlima wa Ebali. 30 Je! Haiwi ng'ambo ya Yordani? Nyuma ya njia ya machweo ya jua, katika nchi ya Wakanaani waketio katika Araba kuelekea Gilgali, kando ya hiyo mialoni ya More? 31 Kwani ninyi mtavuka Yordani mwingie kuimiliki nchi awapayo Bwana, Mungu wenu, nanyi muimiliki na kuketi humo. 32 Nanyi angalieni mzifanye amri na hukumu zote niwawekeazo leo mbele yenu.

Gerizimu palikuwa ni mahali pa baraka za watu ambao waliamriwa waitikie “Amina” kwa kila baraka ilipotamkwa. Hadi leo unapofika mwezi wa Abibu, Wasamaria wanaiadhimisha Pasaka majira ya alasiri ya siku ya  Kumi na Nne kwenye Usiku wa Kukumbukwa Sana (kama ilivyokusudiwa na kuamriwa tangu zamani kwa kitendo cha kukesha usiku kucha) kwenye Mlima wa Gerizimu. Wanashinda usiku mzima wakikesha pasipo kulala usingizi na wakilinda, na wanarudi majumbani mwao asubuhi kwenye maadhimisho ya Siku Takatifu na Sikukuu ya Pasaka. Na hatimaye wanabakia wakiikumbuka Sikukuu—sherehe inayoitwa Idi ya Mikate Isiyotiwa Chachu—hadi Siku Takatifu ya Mwigho ya Mikate Isiyotiwa Chachu.

 

Baraka na laana zilizoandikwa kwenye maandiko haya ni zile zijazo kwa sababu ya asili ya matendo ambayo yangeweza kufanywa kwa siri, wakati taifa lilikuwa linataraji na kuweza kuingia kwenye milki yake likiwa pamoja na watu waliokubali kukiri wazi wazi na wenye nia njema sirini au mioyoni mwao. Makuihani na Walawi walisimama kwenye ukingo wa bonde na wakafanya matangazo, ambayo yaliitikiwa kwa sauti za juu kila upande wa milima yote miwili kwa mwitikio ulioongizwa na watu waliotoka kwenmye makabila yote kumi na mawili, yaliyokuwa yamesimama kila upande makabila sita.

 

Ukiri wa waziwazi wa Torati ya Mungu kwa ujumla na ukamilifu wake wote ulifanywa katika mahali palipokuwa pamesimamishwa madhabahu. Zile mbao mbili kubwa za mawe zilisimamishwa pia mahali pa wazi pamoja na utaratibu wote mzima wa maagizo ya Torati ulivyoandikwa ndani yake ukiwa kama ni mwongozo wa taifa zima lote. Kwa hiyo, torati yote ya Mungu ilitakiwa itangazwe hadharani na ifanyiwe ukiri wa hadharani kuwa wataitii. Wazo la kuwa na mapokeo ya siri—ambayo yanaendelezwa kwenye hadhara hii na na utaratibu ulioandikwa wa sheria na haki—ni upuuzi na ni mateto au shutuma dhidi ya mababa zetu waliotutangulia nyuma yetu, ambao walianzisha wakiwa chini ya maongozi ya Mungu Mooja na Wapekee na wa Kweli.

 

Mungu aliwapa ahadi ya totari kwa Israeli, pamoja na maelekezo ya kina ya baraka na laana kwenye Kumbukumbu la Torati 28:1-68.

 

Mungu aliwatenga Israeli kwa kuwapeleka jangwani wakiwa ni mfano kwetu, na wawe kielelezo kwa kuja kwake Masihi na Yubile arobaini za jangwani za kuongozwa na Roho Mtakatifu (soma Matendo 7:1-60). Roho Mtakatifu alikuwa ni wa muhimu na wa lazima ili kuweza kuzitunza amri na sheria vizuri. Sheria ya Mungu inaendelea Mungu mwenyewe na inaendana na asili yake. Kwa hiyo, mwonekano wa Mungu, ingawaje Roho Mtakatifu ni wa muhimu katika ushikaji na utii kwenye Torati, ambayo kwayo Mungu ameiandika mioyoni mwetu (Yeremia 31:31-40).

 

Ndipo Roho alitolewa kwa wote siku ya Pentekoste mwaka 30 BK. Tangu mwaka 27 BK, Mungu alianza kuwaita masalio ya wateule wake, kama ilivyosemwa na manabii na mitume (soma Yoeli 2:28-31).

Matendo 2:16-36 inasema: Lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli, 17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto. 18 Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri. 19 Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi. 20 Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri. 21 Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa. 22 Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua; 23 mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua; 24 ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao. 25 Maana Daudi ataja habari zake, Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike. 26 Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa, ulimi wangu ukafurahi; Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini. 27 Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu; Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu. 28 Umenijuvisha njia za uzima; Utanijaza furaha kwa uso wako. 29 Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo. 30 Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi; 31 yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu. 32 Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake. 33 Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia. 34 Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume. 35 Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako. 36 Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.

 

Aya ya mwisha ya maandiko haya kwenye Yoeli yanawaelezea masalio ambao Bwana atawaita na wokovu wa namna hiyohiyo kutoka Yerusalemu.

Yoeli 2:32 Na itakuwa ya kwamba mtu awaye yote atakayeliita jina la Bwana ataponywa; kwa kuwa katika mlima Sayuni na katika Yerusalemu watakuwako watu watakaookoka, kama Bwana alivyosema; na katika mabaki, hao awaitao Bwana.

 

Kuna wale walioitwa kwenye agano la Mungu, ambao walikuwepo pale Sinai na wakaendelea na Masihi na hata kipindi cha baadae (Kumbukumbu la Torati 29).

 

Utawanyiko wa Israeli ulitabiriwa tangu mwanzo, na Mungu alisema kwamba kutokana na Torati hii uelewa na ufahamu wao vitawarudia. Sheria hizi zinapaswa ziandikwe mioyoni na mawazoni mwa watu wake na Roho Mtakatifu na hatimaye wamngeweza kurejeshwa upya.

 

Tunajua kutokana na Kumbukumbu la Torati 30:1-20 kwamba kutokana na kuichukulia na kuishika Torati, Israeli wataokoka na kufanywa upya. Kwa hiyo zile laana zilizowekwa kwa mataifa waliowatesa wao kipindi cha utawanyiko wao wataadhibiwa. Mfano wa kondoo na mbuzi ilioandikwa kwenye Mathayo 25 unatokana na andiko hili.

Mathayo 25:31-46 inasema: Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake; 32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; 33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto. 34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; 35 kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; 36 nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia. 37 Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha? 38 Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika? 39 Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia? 40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi. 41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake; 42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe; 43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama. 44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie? 45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi. 46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.

Tunaona kwenye maandiko haya kipindi cha mpito cha tangia zama za Israeli kama taifa la Mungu linaloteswa na mataifa ya duniani, hadi kipindi cha Israeli kama wateule wa Mungu wanaoteseka, na hatimaye kwa mataifa yanahukumiwa kwa ajili ya matendo yao waliyowafanyia Israeli. Hapa tunamashahidi wawili, mmoja ni taifa la kimwili na la kisiasa la Israeli na lenye makabila mbalimbali ndani yake, na ushahidi wa pili ni Israeli kama Kanisa. Mambo haya mawili yanaendelea hadi kwenye siku za mwisho.

 

Tunaona kwamba Musa aliwaambia Israeli mambo yajayo na aliwafundisha Israeli Wimbo wake, pamoja na Wimbo wa Utukufu wa Bwana ambao alipewa awafunze. Nyinbo hizi mbili zinaashiria wateule wa Siku za Mwisho na kipindi cha ufufuo wa wafu. Kipindi chake Mwanakondoo, Wimbo mpya utatolewa na kuimbwa na wazee ishirini na wanne (Ufunuo 5:9) na Wimbo huo watapewa wale 144,000 (Ufunuo 14:3). Hadi kipindi kile, nyimbo hizi mbili zinaweka msingi wa wateule wa ubatizo wa Masihi (soma Kumbukumbu la Torati 31:1-30).

 

Mungu aliona toka mbali yote yaliyokuwemo kwenye taifa. Tumeamriwa tuisome Torati kwenye kila mwisho wa mwaka wa saba wa mzunguko wa kalenda kwenye Sikukuu ya Vibanda au Idi ya Vibanda, ili kwamba watu wasiweze kusahau au kupoteza mwelekeo wa mafundisho ya Torati au wakaacha kumcha Bwana, Mungu wao.

 

Tatizo moja kuhusiana na sheria za Mungu ni kwamba watu wanajaribu kutilia mkazo sehemu tu ya hizi, huku wakiondoa yale ambayo hawayataki au yale ambayo  hawakubaliani nayo. Kwa mfano, mfumo at utaratibu wa kuzitunza Sabato uliondolewa tangu kipindi cha kwanza cha mwanzo wa Kanisa kwa kisingizio cha kwamba Kristo aliibadili Sabato na kuanzisha ibada za Jumapili jambo ambalo hakuna hata mtu mmoja aliyewahi kutoa ushahidi wa kimaandiko wa madai haya. Mfumo wote wa Kalenda ya Mungu uliondolewa mbali kwa lengo la kuushamirisha ule wa kipagani na kuwawezesha kuziingiza siku zao takatifu zilizo kwa muono wao. Sheria zilizokuwa zinasimamia mambo ya fedha zilibadilishwa kwa lengo la kuwatumikisha watu kama watumwa na kuwapunja au kuwadhulumu kwa kutumia sheria zilizopotoka. Makasisi wazinifu na walawiti walizipindisha na kuzipunguzia nguvu sheria kwa lengo la kuruhusu matendo yao ya uzinifu. Israeli ilichukuliwa kabisa na mfumo huu potofu; jambo lililowapelekea sasa kuwa kwenye utumwa wa dhambi—ambako ni kutenda mambo kinyume kabisa na maelekezo ya Torati na sheria zake Mungu—na la kusikitisha ni kwamba hawaelewi kabisa ukweli huu. Sayar yote hii imearibiwa na dini ya uwongo, na sheria za Mungu hakuna zinapotiliwa mkazo au kufundishwa. Wakati lilipoanzishwa Kanisa la Rumi, kizazi cha mwisho cha ndugu wa Masihi (waliosalia) waliuawa wote kwa hila mmoja baada ya mwingine, tendo lililofanywa baada ya wao kutoa mwito wa kurejeshwa maongozi ya Torati kwenye Ukristo. Matukio haya ya kutisha yalikwisha tabiriwa mapema na mmoja wapo wa nabii zilizotolewa na Musa.

 

Kama ikiwezekana, Wimbo huu wa Musa unaweza kutumiwa kuuimba kwa Kiebrania asilia cha kale tunapoufikia mwaka wa saba na tunapokuwa Tunaisoma Torati, na hatimaye ue;ezewe maana yake. Wimbo wa Musa unapatikana kwenye kumbukumbu la Torati 32:1-52 (pia tazama kwenye jarida la Torati na Amri ya Kwanza (Na. 253) [Law and the First Commandment (No. 253)].

.

Jangwa la Sini (au Zini) ni ishara ya uharibifu wa mfumo au imani ya uwongo wa ibada unaojulikana kwa imani ya kuabudu siku ya Jumapili, na maadhimisho ya sikukuu ya Ishta au Easter, na ibada za kumuabudu mungu wa utatu. Tumekuwa jangwani kwa kipindi cha mfululizo cha zaidi ya miaka elfu mbili. Masihi atakuja hivi punde na atawashughulikia Israeli na mataifa. Ndipo sisi tutawekwa kwenye urithi wetu stahiki, kwa pande zote mbili, yaani ndani na nje ya Israeli.

 

Kutakuwa na Msafara mwingine mpya ujulikanao kama Kutoka, na ule wa kwanza hautakumbukwa kabisa mioyoni na akilini mwetu.

Isaya 66:1-24 inasema: Bwana asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani? 2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu. 3 Yeye achinjaye ng'ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao. 4 Mimi nami nitachagua mapigo yao, nitaleta hofu zao juu yao; kwa sababu nilipoita, hawakuitika; na niliponena, hawakusikia; bali walifanya yaliyo maovu machoni pangu, na kuyachagua nisiyoyafurahia. 5 Lisikilizeni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa sababu ya neno lake; Ndugu zenu wawachukiao ninyi, waliowatupa kwa ajili ya jina langu, wamesema, Na atukuzwe Bwana, tupate kuiona furaha yenu; lakini watatahayarika. 6 Sauti ya fujo itokayo mjini! Sauti itokayo hekaluni! Sauti ya Bwana awalipaye adui zake adhabu! 7 Kabla hajaona utungu alizaa; Kabla maumivu yake hayajampata, Alizaa mtoto mwanamume. 8 Ni nani aliyesikia neno kama hili? Ni nani aliyeona mambo kama haya? Je! Nchi yaweza kuzaliwa siku moja? Taifa laweza kuzaliwa mara? Maana Sayuni, mara alipoona utungu, Alizaa watoto wake. 9 Je! Mimi nilete wana karibu na kuzaliwa, nisizalishe? Asema Bwana; mimi nizalishaye, je! Nilifunge tumbo? Asema Mungu wako. 10 Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake; 11 mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake. 12 Maana Bwana asema hivi, Tazama, nitamwelekezea amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa; na juu ya magoti mtabembelezwa. 13 Mfano wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi mtafarijiwa katika Yerusalemu. 14 Nanyi mtaona, na mioyo yenu itafurahi, na mifupa yenu itasitawi kama majani mabichi; na mkono wa Bwana utajulikana, uwaelekeao watumishi wake, naye atawaonea adui zake ghadhabu. 15 Maana Bwana atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto. 16 Kwa maana Bwana atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga wake; nao watakaouawa na Bwana watakuwa wengi. 17 Watu wale wajitakasao, na kujisafisha katika bustani, nyuma yake aliye katikati; wakila nyama ya nguruwe, na machukizo, na panya; watakoma pamoja, asema Bwana. 18 Nami nayajua matendo yao na mawazo yao; wakati unakuja nitakapokusanya mataifa yote na lugha zote; nao watakuja, nao watauona utukufu wangu.19 Nami nitaweka ishara kati yao, nami nitawatuma hao waliookoka kwa mataifa, Tarshishi, na Puli, na Ludi, wavutao upinde, kwa Tubali na Yavani, visiwa vilivyo mbali; watu wasioisikia habari yangu, wala kuuona utukufu wangu; nao watahubiri utukufu wangu katika mataifa. 20 Nao watawaleta ndugu zenu wote kutoka mataifa yote, kuwa sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, na katika magari, na katika machela, na juu ya nyumbu, na juu ya wanyama wepesi, mpaka mlima wangu mtakatifu Yerusalemu, asema Bwana; kama vile wana wa Israeli waletavyo sadaka yao nyumbani kwa Bwana katika chombo safi. 21 Na baadhi ya hao nitawatwaa kuwa makuhani na Walawi, asema Bwana. 22 Kama vile mbingu mpya na nchi mpya, nitakazofanya, zitakavyokaa mbele zangu, asema Bwana, ndivyo uzao wenu na jina lenu litakavyokaa. 23 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana. 24 Nao watatoka nje na kuitazama mizoga ya watu walioniasi; maana funza wao hatakufa, wala moto wao hautazimika nao watakuwa chukizo machoni pa wote wenye mwili.

 

Bwana ataweka utaratibu wake, na Sabato zake na Miandamo ya Mwezi Mpya, na watu wote wataziadhimisha Sikukuu zake. Mataifa yote watatuma wawakilishi au wajumbe wao kwenye Sikukuu hizi huko Yerusalemu, vinginevyo watakosa mvua maana haitanyesha kwao kwa majira yake muafaka, na pia watapigwa maradhi mabaya au tauni ya Wamisri.

Zekaria 14:16-21 Hata itakuwa, ya kwamba kila mtu aliyesalia wa mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu, atakwea mwaka baada ya mwaka ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, na kuishika sikukuu ya Vibanda. 17 Tena itakuwa, ya kwamba mtu awaye yote wa jamaa zote zilizomo duniani, asiyekwea kwenda Yerusalemu ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, mvua haitanyesha kwao. 18 Na kama jamaa ya Misri hawakwei, wala hawaji, pia haitanyesha kwao; itakuwako tauni, ambayo Bwana atawapiga mataifa, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda. 19 Hii ndiyo adhabu ya Misri, na adhabu ya mataifa yote, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda. 20 Siku hiyo katika njuga za farasi yataandikwa maneno haya, WATAKATIFU KWA Bwana; navyo vyombo vilivyomo ndani ya nyumba ya Bwana vitakuwa kama mabakuli yaliyoko mbele ya madhabahu. 21 Naam, kila chombo katika Yerusalemu, na katika Yuda, kitakuwa kitakatifu kwa Bwana wa majeshi; nao wote watoao dhabihu watakuja kuvitwaa vile vyombo, na kutokosa nyama ndani yake; wala siku hiyo hatakuwamo tena mfanya biashara ndani ya nyumba ya Bwana wa majeshi.

Utoaji wa dhabihu utaanza tena huko Yerusalemu, ila itakuwa ni dhabihu ya asubuhi tu ndiyo itakuwa inatolewa. Sisi tutakuwa tumepewa tayari uzima wa milele na Ufufuo wa Kwanza wa wafu—ambayo inawakilishwa na dhabihu ya jioni –ambayo itakuwa imepita na haitakuwepo tena. Utii utatolewa kwenye maagizo yote yaliyoko kwenye Torati ya Mungu nay a Masihi, au vinginevyo, mataifa yale yatakaoziasi yatakubwa na baa la njaa. Tutazihubiri Sheria na Ushuhuda, na mataifa yote yatajua njia za Mungu kazi itakayofanyika kwa.kipindi cha miaka elfu moja. Kisha wafu wengine wote waliobalia watafufuliwa na wataletwa katika hukumu ya wale walioadibishwa kwa njia ya mateso au machungu.

Ufunuo 20:4-15 inasema: Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. 5 Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. 6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu. 7 Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; 8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari. 9 Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala. 10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele. 11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.

Huu ndiyo mwisho wa Sheria au Torati yote na Manabii. Watu wote waweze kuufikia na kuupata wokovu na wamuone Mungu. Musa na manabii walikuwepo hadi kuja kwa Masihi (Kum. 34), na hatimaye Torati iliandikwa kwenye mioyo yqa wateule. Kila mmoja wao alijaribiwa kwa kupitia maeso, na ikaendelea hadi kipindi cha Yubile arobaini, ambaco kiliwakilisha na kipindi cha miaka arobaini ya maisha ya Musa.

 

Mesihi alikuwa na Waisraeli walipokuwa jangwani, na hata sasa bado yoko nao.

1Wakorintho 10:1-24 inasema: Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; 2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari; 3 wote wakala chakula kile kile cha roho; 4 wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. 5 Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani. 6 Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani. 7 Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze. 8 Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. 9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka. 10 Wala msinung'unike, kama wengine wao walivyonung'unika, wakaharibiwa na mharabu. 11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. 12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke. 13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili. 14 Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu. 15 Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo. 16 Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, je! Si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? 17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja. 18 Waangalieni hao Waisraeli walivyokuwa kwa jinsi ya mwili; wale wazilao dhabihu, je! Hawana shirika na madhabahu? 19 Basi niseme nini? Ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu? Au ya kwamba sanamu ni kitu? 20 Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani. 21 Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani. 22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye? 23 Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo. 24 Mtu asitafute faida yake mwenyewe, bali ya mwenzake. 

 

Tunatakiwa kutafuta msaada wa Mungu kila mara, na tunapaswa kuwafanyia wengine kama tunavyopenda sisi tutendewe.

Mathayo 7:7-12  Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; 8 kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. 9 Au kuna mtu yupi kwenu, ambaye, mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe? 10 Au akiomba samaki, atampa nyoka? 11 Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao? 12 Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; maana hiyo ndiyo torati na manabii.

 

Mwisho wa Torati yote ni huu:

Nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote.

Na mpende jirani yako kama nafsi yako. Maana hiyo ndiyo Torati na Manabii. AMINA.