Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[108B]

 

 

 

Ezekieli 34 na Wachungaji

wa Israeli

 

(Toleo La 1.0 20100520-20100520)

 

Nabii Ezekieli alipewa unabii wa muhimu sana kuhusu Wachungaji wa Israeli. Unabii huo unatusuta hata sisi moja kwa moja leo.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hatimiliki ©  2010  Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ezekieli 34 na Wachungaji wa Israeli




Utangulizi Sehemu A

Andiko lililo kwenye Ezekieli 34 ni karipio au onyo la moja kwa moja kwa Wachungaji wa Israeli. Andiko lililo kwenye Ezekieli linatupeleka hadi kwenye Siku za Mwisho na kwenye kipindi cha Milenia.

 

Jaribio hapa ni kusema kwamba Ezekieli 34 ni kuwaonya Israeli kwenye kipindi cha Ezekieli.

 

Tatizo kwenye hali hii halisi ni kwamba Ezekieli alikuwa akiwatabiria wakati Wachungaji wa Israeli wakati wakiwa wamekwenda utumwani kwa muda mrefu uliopita mbali ya Araxes na hawakuwa wameamriwa na utaratibu wa Kilawi Hekaluni. Kulikuwa na koo ishirini na moja zilizokwenda utumwani na ni tatu tu ndizo zilizokuwa zimesalia Yudea na ambazo zilikuwa ni za masalia ya Walawi. Kutokana na koo hizi tatu ni koo ishirini na nne tu ndizo zilizorejeshwa na kutengenezwa tena.

 

Wa hiyo ni upuuzi sana kudai kwamba Wachungaji wa Israeli walikuwa ni masalia walioachwa katika Yudea kwenye utumwa wa Wababeloni.

 

Kwa hiyo andiko hili ni unabii kwa Wachungaji wa Israeli katika Siku za Mwisho na hivyo inakitaja kipindi cha Kanisa katika Siku za Mwisho kwa kuwa hakukuwa na Hekalu na hakujawahi kuwepo Hekalu katika Israeli tangu mwaka 722 KK.  

 

Unabii huu unahusiana moja kwa moja na zama za makanisa ya Siku za Mwisho.

 

Mbili kati ya zama hizi zimekataliwa na Mungu kama matokeo ya matendo yao. Zama moja ya Wasardi, ya kanisa lililoonekana kuwa limekufa na nyingine ya Walaodikia, ambayo ni yenye nguvu kubwa na utajiri, ni ya uvuguvugu, na Mungu alilitapika litoke kinwani mwake. 

 

Tutaona hapa kwamba Mungu anawatawanya na kuwaondoa kondoo watoke kwenye vikundi hivi na kuwakusanya pamoja wawe kwenye kanisa la tatu ambalo lina nguvu kidogo na watahukumiana wenewe kwa wenyewe.

 

Andiko hili moja kwa moja linataja Ufunuo sura ya 3 na zama hizo za makanisa hayo matatu, na yapasa yasomwe kwenye nuru ile.

 

Makanisa kwenye karne ya 20 yalikuwa ni wawakilishi wa moja kwa moja wa mambo yote mabaya ambayo Mungu aliyakemea hapa kwa kupitia nabii Ezekieli. 

 

Tazama jinsi walivyowafanyia kondoo tajiri na wadhaifu au wasio na kitu na jinsi walivyofanya kwenye wajibu wao wa kuwalisha kondoo.

 

Ezekieli 34

Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa unabii, uwaambie, naam, hao wachungaji, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo? 3 Mnawala walionona, mnajivika manyoya, mnawachinja walionona; lakini hamwalishi kondoo. 4 Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala.

 

Bila shaka ndugu wapendwa wa karne ya 20 wangedai hili kuwa hivyo hususan tangu katikati hadi mwishoni mwa karne. Walitawanyika kwa kuwa hawakuwa na mchungaji wa kuwaangalia na huduma zao zilikuwa ni za kitoto au kibabaishaji na za bandia bandia tu kwene mwili wa Kristo. 

 

Maandiko na rekodi yao ziko kinyume na wachungaji kwa jinsi walivyoenenda nab ado jinsi wanavyoenenda.

 

Andiko linalofuatia linaonyesha kwamba ilitokea kwene uso wote wa dunia.

 

5 Nao wakatawanyika, kwa sababu hapakuwa na mchungaji; wakawa chakula cha wanyama- mwitu, wakatawanyika. 6 Kondoo zangu walitanga-tanga katika milima yote, na juu ya kila kilima kirefu; naam, kondoo zangu walitawanyika juu ya uso wote wa dunia; wala hapakuwa na mtu aliyewaulizia, wala kuwatafuta.

 

Ndipo Mungu aliwatangazia hukumu yao. Hukumu hii ilianzia kuchukua mkondo wake mwaka 1987 mwanzoni mwa miaka 40 ya Kizazi cha Mwisho kilichonenwa na Kristo. 

 

7 Basi, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana; 8 Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, kwa sababu kondoo zangu walikuwa mateka, kondoo zangu wakawa chakula cha wanyama-mwitu wote, kwa sababu hapakuwa na mchungaji, wala wachungaji wangu hawakutafuta kondoo zangu, bali wachungaji walijilisha wenyewe wala hawakuwalisha kondoo zangu; 9 kwa sababu hiyo, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana; 10 Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu ya wachungaji; nami nitawataka kondoo zangu mikononi mwao, nami nitawaachisha hiyo kazi ya kuwalisha kondoo; nao wachungaji hawatajilisha wenyewe tena; nami nitawaokoa kondoo zangu vinywani mwao, wasiwe tena chakula chao.  

 

Mungu anasema kwenye andiko hili maneno makuu matatu:

  1. Atawadai na kuwahukumu wachungaji kwa kosa la kupotea kondoo na kuwahukumu kama sawasawa na makosa yao.
  2. Atawazuia asifundishe na kuwapotosha zaidi kondoo. Kondoo hawatawasikiliza tena kabisa.
  3. Na ndipo wachungaji hawataweza kujilisha tena kabisa wao wenyewe kutoka kwa kondoo na kondoo wataokolewa kutoka vinywani mwao na kulindwa wawe salama.

 

Kisha Mungu anaendelea kutofuta jinsi ya kuwaokoa kondoo hao yeye mwenyewe, akiwatafuta kutoka kila mahali ambako wametawanyikia. Hatimaye atawaweka mahala penye malisho mazuri.

 

11 Maana, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi mwenyewe, naam, mimi, nitawatafuta kondoo zangu, na kuwaulizia. 12 Kama vile mchungaji atafutavyo kondoo zake, siku ile anapokuwa kati ya kondoo zake waliotawanyika; ndivyo nitakavyowatafuta kondoo zangu; nami nitawaokoa katika mahali pote walipotawanyika, katika siku ya mawingu na giza.

 

Kumbuka kuhusu aya hizi kwamba kondoo hawa watatolewa nje kutoka kwa watu na kuwakuwasanya kwenye mataifa au nchi mbalimbali.

 

13 Nami nitawatoa katika watu wa mataifa, na kuwakusanya katika nchi zote, nami nitawarudisha katika nchi yao wenyewe; nami nitawalisha juu ya milima ya Israeli, kando ya mifereji ya maji; na katika mahali pote pa nchi panapokaliwa na watu. 14 Nami nitawalisha malisho mema, pa juu ya milima ya mahali palipoinuka pa Israeli litakuwa zizi lao; huko watalala katika zizi jema; nao watakula malisho mema, juu ya milima ya Israeli. 15 Mimi mwenyewe nitawalisha kondoo zangu, nami nitawalaza, asema Bwana MUNGU.

 

Kumbuka kwamba aya za 13-15 Mungu anaelezea au kuonyesha utaratibu atakaoufuata.

  1. Kwanza kabisa atawapokonya kondoo watoke mikononi mwa wachungaji hawa.
  2. Kisha atawaweka mahali palipo salama na kuwakusanya kwa kuwaondoa kutoka kwa watu walio karibu yao. Mwa naneno mengine ni kwamba waakusanywa na sio chini ya wachungaji hawa waovu na waongo waliowachuna hadi kwenye kwato zao.
  3. Watalishwa vizuri na kuhukumiwa, kama tutakavyojionea, kwa jinsi wanavyohudumuana.
  4. Knisha ndipo Mungu atawaleta hadi kwenye nchi yao wenyewe na watalishwa kwenye milima ya Israeli.
  5. Watalishwa kwenye malisho mazuri na kwenye nchi za kupendeza na Mungu mwenyewe atawafundisha.

 

Mungu atawatibu maumivu yote ya wateule wake nay a watu wote wanaoliitia jina lake. Atawaponya wadhaifu na viwete na kuwapiga upofu na kuwalisha na kuwaangalia walio na nguvu ili wasiweze kuwasukuma tena wale walio wadhaifu na kuwadhalilisha.

 

16 Nami nitawatafuta waliopotea, nitawarudisha waliofukuzwa, nitawafunga waliovunjika, nitawatia nguvu wagonjwa; nao wanono na wenye nguvu nitawaharibu; nitawalisha hukumu.

 

Tazama jinsi Mungu atakavyowahukumu kondoo.

 

17 Na kwa habari zenu, Enyi kundi langu, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nahukumu kati ya mnyama na mnyama, kondoo waume na mbuzi waume pia.

 

Kipindi hiki cha kuhukumu ni zama ya Wafiladelfia. Ni zama ya kondoo kuhukumiwa dhidi ya kondoo na hakutakuwa na wachungaji watakaowalisha na hakuna atakayewatumia na kuwadhalilisha. Ni hukumu itakayotolewa au kufanywa kwa kuzingatia upendo wa kidugu na utaendelea hadi utaratibu wote wa utawala wa kipindi hicho uanze chini ya Masihi.

 

Kisha hapa ndipo Mungu anaelezea kuhusu kondoo matajiri na wanono kwenye kifungu hiki cha mwisho:

 

18 Je! Mwaona ya kuwa ni neno dogo ninyi kulishwa malisho mema, hata mkawa hamna budi hukanyaga kwa miguu yenu yaliyosalia? Na kuwa mmekunywa maji yaliyo safi, nanyi hamna budi kuyatibua kwa miguu yaliyobaki? 19 Na kwa habari za kondoo zangu, wao wanakula hayo mliyoyakanyaga kwa miguu yenu, nao wanakunywa maji mliyoyatibua kwa miguu yenu.

 

Hiki ni kiambishi tunachoendana nacho sasa ambapo kondoo wanapowafutia wengine malisho kwa bidii na uangalifu. Kondoo hao wote watahukumiwa kwa ajili hiyo na kondoo waliokonda watalindwa.

 

20 Kwa sababu hiyo, Bwana MUNGU awaambia hivi; Tazama, mimi, naam, mimi, nitahukumu kati ya wanyama walionona na wanyama waliokonda. 21 Kwa kuwa mmesukuma kwa ubavu, na kwa mabega, na kuwapiga wenye maradhi kwa pembe zenu, hata mkawatawanyia mbali;

 

Kipindi hiki cha kutawanyika kiko njiani kinakuja kwa miongo kadhaa, na hakipo mbali.

 

Mungu anakiona na anasema:


22 basi mimi nitaliokoa kundi langu, wala hawatakuwa mateka tena; nami nitahukumu kati ya mnyama na mnyama.

 

Kipindi hiki ki awamu ya mwisho ya hukumu ya kabla ya ufufuo wa wafu wa Masihi. Kisha tutahukumiwa na wanaostahili watafufuliwa. Kuna andiko linaloelezea jambo hili hata pia kwenye Zekaria 12:8.

 

23 Nami nitaweka mchungaji mmoja juu yao, naye atawalisha, naam, mtumishi wangu, Daudi; yeye atawalisha, naye atakuwa mchungaji wao. 24 Na mimi, Bwana, nitakuwa Mungu wao, na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mkuu kati yao; mimi, Bwana, nimesema haya. 25 Nami nitafanya agano la amani nao, nami nitawakomesha wanyama wakali kati yao; nao watakaa salama jangwani, na kulala misituni. 26 Nami nitawafanya wao, na mahali palipo pande zote za mlima wangu, kuwa baraka, nami nitaleta manyunyu kwa wakati wake; yatakuwako manyunyu ya baraka.

 

Hivyo basi, watu waanchi wataipata amani na ulinzi na watakuwa salama.

 

Kumbuka kuwa Mungu anasema kwamba nchi itazaa maongeo yake na miti itatoa matunda yake. Kwa hiyo ndipo nchi haitakuwa na laana tena kabisa. Na zaidi sana ni kwamba wanadamu hawatatiwa utumwani tena na wala hawatakuwa kwenye kongwa la mizigo mizito.


27 Na mti wa kondeni utazaa matunda yake, nayo ardhi itatoa mazao yake, nao watakuwa salama katika nchi yao; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya kongwa lao, na kuwaokoa katika mikono ya watu wale waliowatumikisha. 28 Hawatakuwa mateka ya makafiri tena, wala mnyama wa nchi hatawala; bali watakaa salama salimini, wala hapana mtu atakayewatia hofu.

 

Kwa hiyo, tutajionea marejesho mapya ya watu wa Mungu walitolewa kwenye kongwa na Kristo ataletwa ili kuchukua watumwa walioko utumwani.

 

Mungu atakuwasanya watu wake na hawatapata mashutumu tena wala kulaumiwa na mataifa. Tutashuhudia jinsi jambo hili litakapofanyika na jinsi watu wa Mungu watakavyofanyiwa na kuhesabiwa kwenye mwili wa Kristo kwa Mashahidi na kwa njia ya dhiki kuu ya Nyakati za Mwisho.

 

Ni kama Mungu alivyoahidi:

29 Nami nitawainulia miche iwe sifa njema, wala hawataangamizwa kwa njaa katika nchi yao tena, wala hawatachukua tena aibu ya makafiri. 30 Nao watajua ya kuwa mimi, Bwana, Mungu wao, ni pamoja nao, na ya kuwa wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana MUNGU. 31 Na ninyi, kondoo zangu, kondoo za malisho yangu, ni wanadamu, na mimi ni Mungu wenu, asema Bwana MUNGU. 

 

Hitimisho

Kutokana na andiko hili la Ezekieli 34 inaonekana wazi kabisa kwamba katika Nyakati za Mwisho hakuna watumishi wa Makanisa ya Mungu watakaoruhusiwa kuwaacha ndugu wapendwa waaminio. Kondoo wote watatolewa au kupokonywa kutoka mikononi mwa wachungaji kwa ajili ya dhuluma zao na mafundisho yao ya uwongo.

 

Kwa hiyo inafuatia kwamba kanisa la mwisho la Nyakati za Mwisho ambalo kwamba Mungu amewaweka kondoo litakuwa ni huduma isiyolipwa iliyohukumiwa sawasawa na jinsi inavyowatumikia waumini wake na jinsi wanavyohudumiana na kuchukuliana wote na jinsi wanavyoendelea kushikilia mafunndisho ya Makanisa ya Mungu.

 

Tathmini zaidi ambayo mchakato wake tunaoweza kuyageukia Makanisa yaliyo kwenye kitabu cha Ufunuo.

 

Makanisa kwenye Nyakati za Mwisho

Hebu na tuyaangalie sasa maandiko yaliyo kwenye Ufunuo sura ya 3 kwa Makanisa ya Nyakati za Mwisho.

 

Kwenye Ufunuo 2 tunaambiwa kwamba kanisa la Thiatira halitabebeshwa mzigo wowote mwingine kama walivyoteseka sana kwenye mateso waliyokabiliana nayo kwenye karne kadhaa za nyuma. Watakusanywa na kuwekwa mahali na Wafiladelfia kwenye mwisho wa majaribu yao.

 

Twaweza kujionea kwenye andiko la Ufunuo sura ya tatu kwamba ujumbe uliopo unayahusu makanisa matatu ya mwisho.

 

Jambo hili limeainishwa kikamilifu zaidi kwenye jarida la Nguzo za Filadelfia (Na. 283). Imeshauriwa kwamba jarida hilo lisomwe sambamba na jarida hili.

 

Ufunuo 3

 

Sardi

Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa. 2 Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu. 3 Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako. 4 Lakini unayo majina machache katika Sardi, watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa wamestahili. 5 Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake. 6 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.

 

Hivyo tunaona kwamba imani ya Wasardi imekufa ingawaje wanaendelea kuonekana kama wako “hai.” Kuna kanisa moja tu katika historia ambalo lina jina hili la Kanisa “Hai” la Mungu. Huu ni mfano au kivuli cha zama ya kanisa la Wasardi. 

 

Kuna baadhi walio kwenye imani hii wanaostahili na watatolewa watoke nje ya imani hii kama sehemu ya mchakato huu wa kuwapokonya kondoo kutoka mikononi mwa wachungaji hawa.

 

Zama hii imepita kwa muda wa karne nyingi lakini lilikuwa limekufa na halikufanya kitu chochote kwa zaidi ya imani nyingi.

 

Filadelfia

Kanisa hili lina idadi ya mambo kadhaa yanayoludi. Lina nguvu au uweza wa kufungua na kufunga kwenye Makanisa ya Mungu na mataifa na uweza dhidi ya mapepo na kuzimuni.

 
7 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye. 8 Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe umelitunza neno langu, wala hukulikana jina langu.

 

Kanisa hili linakabiliana na nyakati za mateso ya Siku za Mwisho na dhiki kuu itakayoukabili mwili wa Kristo na halijalikana jina lake.

 

Imani hii itawachukua walio kwenye sinagogi la Shetani na kulishughulikia na katika siku za mwisho watawafanya waje kujipendekeza na kujiunga nao. Kanisa hili litachukuliwa na kuwa na sehemu kwenye ufufuo wa wafu na linalindwa litoke saa ya mateso ya kujaribiwa. Makanisa meingine mawili hakuachwa na hayana sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu.

 
9 Tazama, nakupa walio wa sinagogi la Shetani, wasemao kwamba ni Wayahudi, nao sio, bali wasema uongo. Tazama, nitawafanya waje kusujudu mbele ya miguu yako, na kujua ya kuwa nimekupenda. 10 Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.

 

Kanisa hili linastahili na litakuwa na sehemu wakati wa kurudi kwake Kristo:

 
11 Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. 12 Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya. 13 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.



Watu hawa wanafanyika kuwa nguzo muhimu na kufanyika kuwa nguzo za muhimu kwenye Hekalu la Mungu.

 

Laodikia

Laodikia ni kanisa kubwa sana miongoni mwa makanisa ya Sabato na wanadhani kuwa ni matajiri, bali hawako hivyo kabisa, bali ni maskini, mnyonge na mwenye mashaka, kipofu na uchi. Wale anaowapenda Mungu huwaondoa kanisani na kuwaweka pia kwenye kanisa la Filadelfia.

 

14 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu. 15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. 17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. 18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. 19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu. 20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. 21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.

 

Wale walio na juhudi na bidii na wanaotubu wanaondolewa kutoka kwao na wanaunganishwa na Wafiladelfia ambako hawatatoka na kuondoka tena kamwe, kabisa.

 

Fanya rejea ya jarida la Nguzo za Filadelfia (Na. 283).                     

 

Mungu anashughulika na makanisa na anayaandaa kwa ajili ya Ufufuo wa Kwanza baada ya kuhukumiwa yao ambayo katika Nyakati za Mwisho yatajaribiwa kwa upendo wa kidugu na uaminifu wao kwenye mafundisho. Imani zote mbili au makundi haya ya kanisa yamekataliwa kwa ajili ya upotofu wao.

q