Makanisa Ya Kikristo ya Mungu

[065]

 

 

 

Chachu ya Pentekoste [065]

 

(Toleo 1.0 230504-230504)

 

Mikate ya Iliyotiwa Chachu ya Boflo ya Pentekoste ilikosekana kueleweka kabisa na Kanisa la Mungu katika kipindi cha nusu ya karne ya ishirini. Uelewa wa kusudi la utiaji-chachu ni ili kufanyika watoto wa Mungu wenye uweza katika Ufufuo wa Wafu kama Kristo alivyo kuwemo mautini kwa kipindi Fulani.

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Copyright © 2004  Wade Cox)

(Tr. 2005)

 

Masomo haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kutufa maneno. Jina la mchapishaji na anuami yake pamoja na hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya maelezo na kilugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia ynapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

 

http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 

 


Chachu ya Pentekoste [065]

 


Mwezi Mpya Mwandamo wa Mwezi wa Tatu wa Mwaka Mtakatifu kwa kawaida huwa unaangukia katika juma la saba la Kipimo cha kuhesabu kuelekea Pentekoste. Kwa miaka mingi, Sabato iliyokuwa inafuatia na Siku ya Kwanza ya juma iliyokuwa inafuata ilikuwa inafanywa kuwa ni siku mbili mfululizo za Sikukuu ya Majuma au Pentekoste. Kama ambvyo tungalivyoweza kuona, neno Pentekoste lina maana “hesabu ya hamsini” au kuhasabu hadi hamsini. Kwa kipindi hiki tunajiweka tayari kwa kumpokea Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste. Kuna idadi ya mambo tunayo ya hitaji ili kukifikia utimilifu katika Kipimo hiki cha hasabu. Upendo na umoja miongoni mwa wapendwa vina umuhimu mkubwa sana na pia kukifuatiwa upendo wetu kwa Mungu.

 

Tunahitajika kushiriki maadhimisho ya Pasaka tukiwa tumejitakasa mioyo yetu tangia Mwaka Mpya katika siku ya Kwanza ya Mwezi wa Abibu. Tunatakiwa kufunga saumu katika siku ya Saba ya Mwezi wa Abibu. Baadhi ya Makanisa ya Mungu kwa kweli yameacha kushiriki mambi ya utakaso kwa ajili ya Dhambi zilizofanywa kwa Kukoseshwa au kwa Kutokujua, yaani zitokanazo na ujinga ambapo tunatakiwa kufunga saumu, na badala yake wameanzisha mfungo wa saumu katika siku ya Sabato ya siku ya kwanza ya Mwanzo wa hesabu ili kuridhisha haja ya mapokeo waliyojuwekea. Mungu anahitaji utii zaidi ya dhabihu au sadaka. Wakati anaposema juu ya kulitakasa kutaniko kwa njia ya mfungo wa saumu na kuitunza siku ya Saba ya mwezi wa Abibu kwa kumfanyia mfungo wa saumu kwa toba ya dhambi Zilizofanywa kwa Kupotoshwa, huwa anamaanisha vivyo hivyo na si vema kufanya vinginevyo.

 

Kwa kipindi chote cha siku ishirini na moja  katika Mwezi wa Kwanza wa Abibu ni kipindi kinachohusika na mambo ya utakaso. Tunatakiwa kukipa uhumimu kipindi hiki na kukielewa. Tunatakiwa kuondoa kila aina ya chachu za uovu na nia mbaya na kushiriki adhimisho la sikukuu kwa moyo wa dhati na kweli (tazama jarida la Chachu ya Kale na Mpya [106a]). Kwa jinsi hii hesabu ya kipindi hiki cha kuelekea kwenye Pentekoste inaanzishwa kwa msingi wenye maana. Utaratibu wake ni kwamba unaanzia kwenye sikukuu, ambako tumepewa chachu za Ufalme wa Mbinguni. Kristo alisema akiufananisha Ufalme wa Mbinguni na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga hata ukachachwa wote pia (Mt. 13:33). Katika fafanuzi za Bullinger kuhusiana na andiko hili katika biblia iitwayo Companion Bible iko tofauti kabisa kwa kweli na maneno ya Kristo.

 

Kwa kipindi cha miaka mingi sasa Maakanisa ya Mungu yameshindwa kufikia kwenye kukubaliana na maana hasa ya mfano wa chachu ya uovu na nia mbaya yanavyoweza kuendana na maaana halisi ya chuachu ya Roho Mtakatifu, ambaye ni Ufalme wa Mbinguni na ambaye yuko kati yetu. Zaidi ya kushindikana huku kumeangukia na matokeo mengine ya moja kwa moja ya kushindwa kuadhimisha Sikukuu hii kikamilifu kwa siku zote nane kamilifu kuanzia siku ya 14 Abibu hadi siku ya 21 mwezi uu huu wa Abibu. Ni kwa njia ya utii tu katika kushika Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba, na kuwepo kwetu kwenye ushirika, ndipo tunapofikia kwenye kiwango cha uelewa. Usishangae wakati kwa hao walio kwenye Makanisa ya Mungu wanaelewa utaratibu huu hata kwa kiasi kidogo sana. Hawaelewi kwa sababu hawamtii Mungu. Hebu ukumbuke ukweli huu kwenye andiko lisemalo “Mkabidhi BWANA kazi zako, Na mawazo yako yatathibitika” (Mit. 16:3). Hakuna njia nyingine iliyoko. Wala haisemi: “Hebu fikiria habari za Mungu kidogo naye atazithibitisha njia zako”. Hivi sivyo inavyokwenda au mambo yanavyokuwa. Fanya hivyo na kasha tutakuelewa.

 

Ukweli ni kwamba Mungu ameamuru kutiwa kwa chachu kwenye mikate miwili ya uwonyesho katika siku ya Pentekoste. Je, ni kweli kwamba sisi tunadai kikweli kweli kwamba Mungu angeweka maana mfano wa kuwa dhambi kwenye moja wapo ya dhabihu zake? Je, sisi tunajaribu kuifanya ifanane na dhambi tunamsaidia Mungu kuweka maana nyingine kwa kumkosoa vile alivyoweka yeye au kumshawishi abadilishe?

 

Sadaka itolewayo siku ya Pentekoste inalilenga Kanisa, ambalo watu wake ndilo Hekalu la Mungu. Utiwaji wa chachu kwenye mikate ya wonyesho ya siku ya Pentekoste inalenga muelekeo wa asili inayokwenda pamoja kati ya Maandiko Matakatifu, na mwenendo wa mwanadamu na Mungu kupitia Roho Mtakatifu. Pia inataja kwenye mwenendo huo wa pamoja kati ya mambo yahusuyo jeshi lililoko  mbinguni na la duniani kwenye mji wa Mungu (tazama jarida la Mji wa Mungu Na. 180). Vipimo vitatu vya mlo huwakilisha namna tatu za aina ya Ufalme wa Mungu. kristo alikuwepo kama Mfalme, Kuhani na Nabii (tazama jarida la Yesu ni Kristo, Mfalme, Kuhani na Nabii, Na. 180). Kwa hiyo, kwa kadiri ile tulivyoitwa na kuchaguliwa kuwa taifa la wafalme na makuhani, na tunautendea kazi unabii ulioko kati yetu na ni kitu muhimu cha tatu kwa Kanisa na watu wake.

 

Roho Mtakatifu hufanya kazi ndani ya kila mtu ili kufanya mshiriki wa mwili wa Kristo na hutuwezesha kama wafalme, makuhani na manabii. Kwa jinsi hii, sisi kama waandishi wa Kanisa, wenye elimu katika Siri za Mungu. Tumefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vikale (Mt. 13:52).

 

Katika siku za Kristo, mambo yalikuwa yanaongelewa kwa mifano ili kwamba watu wasione na kuelewa, wakageuka na kuokoka kabla ya nyakati zao. Kanisa pia limelizuiwa lisonene mambo wazi wazi kwa kipindi cha miaka mingi kwa matendo yafanywayo na maadui. Kupitia mateso Kanisa lililindwa na mafumbo na achilio la taratibu la maelekezo. Kwa matukio mengi, Kanisa lenyewe halikuelewa pia kwa ajili ya uasi wa kutotii viongozi wao na watu. Kanisa linafanana na mwezi, mng’aro na ufifi katika uelewa kwa vipindi vya karne nyingi.

 

Wanafunzi wakamwuliza Kristo “Kwa nini unasema nao kwa Mifano?”

 

Kristo akawajibu:

Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali hao hawakujaliwa. Kwa maana yeyote mwenye kitu atapewa, naye atazidishiwa tele; lakini  ye yote asiye na kitu, hata kile alichonacho atanyang’anywa. Kwa sababu hii nasemanao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa. Na neno la nabii Isaya litatimia kwao, likisema, kusikia mtasikia, wala hamtaelewa. Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito. Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka nikawaponya. Lakini heri macho yenu kwa kuwa yanaona, na masikio yenu, kwa kuwa yanasikia. (Mt.13:10-16; sawa na Isa. 6:9-10, na vile vile tafsiri za Yoh. 12:39-40, Mdo.28:26).

 

Maendeleo ya Kanisa kila wakati yamekuwa yakifikiwa kwa hali ya udhati wa moyo na ukweli. Chachu ya kale ya uovu na uchafu wa moyo yameondolewa. Sikukuu huadhimishwa katika hali ya udhati wa moyo na ukweli, na kwa kupitia njia hii ya udhati wa moyo na kweli tunaelekea kwenye chachu ya Roho Mtakatifu, anaye mwezesha mtu kuwa ni mtu mpya mwenye kuweza kufanya yote. Kwa kupitia chachu tunafanyika waongofu na kuwa viumbe vipya au watu wapya. Kristo alimwambia Petro:

Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani mewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano; lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako. (Luka 22:31-32)

 

Tunatakiwa sote tuishike kweli na kuendelea nayo. Pilato aliuliza: “Je, kweli ni nini?” kwa sababu alikuwa ameona mambomengi sana ya uwongo na mawazo mapotofu. Kanisa la Mungu lazima liweze kupambanua kweli na kuligawa neno la Mungu katika utakatifu. Uongofu ni tendo la mwanadamu kumrudia Mungu (kama isemavyo Mt. 18:3). Kuwa kama mtoto mdogo ni kukubali kuja kwa Mungu katika hali isiyo na hila na hamu ya kujifunza. Mtu hawezi kukua kwa namna ya kuishupazia shingo kweli. Ni kweli ya Mungu tu ndiyo itatuweka huru (tazama jarida la: Kweli, Na. 168). Ni kwa kupitia kwenye kweli tu na hali ya kuipenda kweli niyo itakayomwezesha mtu kuongoka  na kumgeukia Mungu (tazama jarida la: Uongofu na Kweli [072]).

 

Tunaona kwamba kuna tofauti kati ya hali ya kawaida ya mawazo ya kimwili wa wana wa Mungu. Kuna idadi ya mitazamo na Naandiko Matakatifu yanayo husiana au kufafana na mfano wa mafundisho ya katika Mathayo 13.

 

Ni sisi tuliohuishwa kwa chachu ya Roho Mtakatifu.

 

Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa ya dhambi zenu; 2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi; (Efe. 2:1-2).

 

Kwa kweli mshitaki na adui wetu ametupofusha sote kama mtume Paulo anavyosema katika 2Wakorintho

ambao ndani yao mungu wa dunia hii amewapofusha fikra zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura ya Mungu. (2Kor. 4:4).

 

Kwa jinsi hii, Injili ya utukufu wa Kristo ndio kitu kinachotufanya kufunguliwa kifikra.

 

Wengi wetu tumeitwa kwenye imani na wengine wamechaguliwa. Hawa ndio wale wanaosikia na kuona, na mbegu zinazozaa matunda.

 

Fundisho kuu la mfano katika Mathayo 13 linafuatia katika kuunganishwa na wanafunzi kuhusiana na hali ya kuona na kuona na kuweza kuongoka (tazama hapo juu) ilivyokuwa kwa mpanzi.

Siku ile Yesu akatoka nyumbani, akaketi kando ya bahari. 2 Wakamkusanyikia makutano wengi, hata akapanda chomboni, akaketi; na ule mkutano wote wakasimama pwani. 3 Akawaambia mambo mengi kwa mifano, akisema, Tazama, mpanzi alitoka kwenda kupanda. 4 Hata alipokuwa akipanda, mbegu nyingine zilianguka karibu na njia, ndege wakaja wakazila; 5 nyingine zikaanguka penye miamba, pasipokuwa na udongo mwingi, mara zikaota, kwa udongo kukosa kina; 6 na jua lilipozuka ziliungua; na kwa kuwa hazina mizizi zikanyauka. 7 Nyingine zikaanguka penye miiba; ile miiba ikamea, ikazisonga; 8 nyingine zikaanguka penye udungo mzuri, zikazaa moja mia, moja sitini, moja thelathini. 9 Mwenye masikio na asikie. (Mathayo 13:1-9).

 

Kanisa lililoshikilia uaminifu mkubwa sana katika Makanisa ya Mungu ni lile lililotajwa kama la Wafiladelfia, kwa sababu walikuwa na upendo mkubwa kati yao. Lilikuwa na nguvu kidogolakini liliishikilia imani na kujitoa wakfu kwenye nguvu za Roho Mtakatifu.

 

Nayajua matendo yako, Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kifogo, nawe umelitunza neno langu, wala hukulikana jina langu .(Ufu. 3:8).

 

Kinachotutenga sisi mbali ni Roho Mtakatifu ili kwamba tuweze kuzishika amri za Mungu na kuwa waaminifu na kushika ushuhuda wa Yesu

 

Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari. (Ufu. 12:17).

 

Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, na hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.(Ufu. 14:12),

 

Utaratibu uliopo kuelekea kwenye ubatizo na toba unatuleta mahali ambapo Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yetu. Tunazifua kanzu zetu kwa damu ya Mwana kondoo kwa dhabihu iliyotuwezesha kuingia Hukumuni na huduma ambayo Roho Mtakatifu, ambaye hatimaye hufanya kazi ndani yetu.

Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima na kuingia mjini kwa milango yake.(Ufu. 22:14).

 

Ni kwa kusikiliza neno katika Roho, na kulitendea kazi, kwa hiyo tunaweza kuelewa. Mathayo 13:10-23 inasema:

Wakaja wanafunzi, wakamwambia, Kwa nini unasema nao kwa Mifano? 11 Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni, bali hao hawakujaliwa. 12 Kwa maana yeyote mwenye kitu atapewa, naye atazidishiwa tele; lakini  ye yote asiye na kitu, hata kile alichonacho atanyang’anywa. 13 Kwa sababu hii nasemanao kwa mifano; kwa kuwa wakitazama hawaoni, na wakisikia hawasikii, wala kuelewa. 14 Na neno la nabii Isaya litatimia kwao, likisema, kusikia mtasikia, wala hamtaelewa. 15 Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito. Na kwa masikio yao hawasikii vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka nikawaponya. 16 Lakini heri macho yenu kwa kuwa yanaona, na masikio yenu, kwa kuwa yanasikia. 17 Kwa maana, amin, nawaambia, Manabii wengi na wenye haki walitamani kuyaona mnayoyaona ninyi, wasiyaone; na kuyasikia mnayoyasikia ninyi, wasiyasikie. 18 Basi ninyi sikilizeni mfano wa mpanzi. 19 Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia. 20 Naye aliyepandwa penye miamba, huyo ndiye alisikiaye lile neno, akalipokea kwa furaha, 21 lakini hana mizizi ndani yake, bali hudumu kwa muda; ikitokea dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara huchukizwa. 22 Naye aliyepandwa penye miiba, huyo ndiye alisikiaye lile neno; na shughuli za dunia, na udanganyifu wa mali hulisonga lile neno; likawa halizai. 23 Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyu ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo, yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sabini, na huyu thelathini.

 

Kwa kuelewa, tunazaa matunda kwa matendo. Mathayo 13:24-30 inasema:

Akawaambia mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; 25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake. 26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu. 27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu? 28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye? 29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu na kuzing’oa ngano pamoja nayo. 30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu mkayafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

 

Mbegu hii hukua ndani ya mtu binafsi na kisha inakuwa yote katika yote, na hatimaye anakuwa elohim (tazama jarida la Kuchaguliwa kama Elohim Na. 1). Hili ni lengo la mwisho la wito wetu kama kwa jinsi tunavyoona pia katika Zaburi 82.

 

Mathayo 13:31-32 inasema:

Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake; 32 nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.

 

Mungu aliangamiza dunia na vitu vyote vilivyokuwemo kwenye gharika, kwa sababu maovu yalipita kiwango cha kawaida ya kuvumilika. Kitabu cha Mwanzo 6:5 kinatuonyesha kuhusu uovu wa moyo wa mwanadamu pia.

 

BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoyni mwake ni baya tu siku zote.

 

Hata vivyo, Mungu aliahidi kutukomboa sisi na akamtuma Kristo kufanya kile ambacho tunachofanya.

 

Injili ya Mathayo 13:33 inatuonyesha Kanisa, kama mwanamke aliye na chachu ya Ufalme wa Mbinguni, aliyeigawanya katika mafungu matatu ya vipimo.

 

Akawaambia mfano mwingine; Ufalme wa mbinguni umefanana na chachu aliyoitwaa mwanamke, akaisitiri ndani ya pishi tatu za unga, hata uka chacha wote pia.

 

Vibaba hivyo vitatu huwakilisha huduma tatu zitendazo kazi Kanisani. Haya ni majukumu ya Kristo kama Mfalme, Kuhani na Nabii.

 

Wateule wamekombolewa miongoni mwa watu kama washiriki wa baraza la wafalme na makuhani, na kwalo wamepewa roho ya unabii. Kwa hiyo Kanisa linajiandaa kwa kazi yake kwa hii awamu ya huduma tatu kwa pamoja, ambako Roho Mtakatifu huendeleza karama na vipaji na kuvitoa kwa kila mtu kulingana na mahitaji ya Kanisa na kwa wakati ule.

 

Machungu ya kushikilia imani hayaepukiki kama bidii katika wokovu wetu sote.

 

Yohana 16:21 inasema: Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika; lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni.

 

Mwanamke ni Kanisa la Mungu, na bibi arusi wa Kristo. Kwa sababu hii adui hulitesa Kanisa kwa mfano tunao uona katika kitabu cha Ufunuo 12:13 inavyosema:

Na joka yule alipoona ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

 

Ufunuo wa Yohana 12:17 inasema:

Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.

 

Mbegu ambayo ni Kristo na Kanisa itashinda juu ya adui zao na mfumo wao kama tutakavyo kwenda kuona. Unabii wa Zekaria 5:5-11 unatuonyesha kuwa kinachotaka kutokea. Aliunuliwa kwa ajili ya kutia moyo mataifa baada ya kurudi kwao kutoka utumwani. Andiko haliashirii chochote wala kutaja kuhusu Utumwa Babeli ila unaonyesha ni kwa Siku Zinazokuja. Mwanamke anayetajwa hapa ni mfumo mbovu wa ukengeufu na unakatiliwa mbali na midomo yake inafungwa kwa talanta ya risasi na wanamchukua hadi kwenye nchi ya Shinari na wawili ambao walikuwa kama ndege aina ya korongo. Kipimo cha efa kama mfano wa biashara unaoungana pamoja dini ya uwongo ya adui imewekwa na kuelezewa kama mfumo wa Kibabeli. Ni Kanisa la Mungu lenye wajibu mkuu wa kukosoa na kusahihisha makosa hayo yote ya mfumo huu wa uwongo.

 

Zekaria 5:5-11 inasema:

Ndipo yule malaika aliyesema nami akatokea, akaniambia, Inua macho yako sasa, uone ni kitu gani kitokeacho. 6 Akasema, Ni kitu gani? Akasema, kitu hiki ni efa itokeayo. Tena akasema, Huu ndio uovu wao katika nchi hii yote; 7 na tazama, talanta ya risasi iliinuliwa; na tazama, mwanamke akaaye katikati ya hiyo efa. 8 Akasema, Huyu ni Uovu; akamtupa chini katikati ya ile efa; akalitupa lile jiwe la risasi juu ya mdomo wa ile efa. 9 Ndipo nikainua macho yangu, nikaona, na tazama, wanawake wawili walitokea, nao upepo ulikuwa katika mabawa yao; na mabawa yao yalikuwa kama mabawa ya korongo; wakaiinua ile efa kati ya dunia na mbingu. 10 Ndipo nikamwambia yule malaika aliyesema nami, Hawa wanaipeleka wapi efa hii? 11 Akaniambia, Wanakwenda kumjengea nyumba katika nchi ya Shinari; tena ikiisha kutengenezwa, atawekwa huko mahali pake mwenyewe.

 

Tunatiwa unajisi katika jamii zetu kama tuonavyo katika Hagai 2:13:

Ndipo Hagai akasema, Kama mtu aliyetiwa unajisi kwa kugusa maiti, akigusa kimojawapo cha vitu hivi, je! Kitakuwa najisi? Makuhani wakajibu, wakasema, Kitakuwa najisi.

 

Dhambi ni unajisi na jambo hili lilifundishwa kwa msisitizo mkubwa katika Israeli kwa kuhitajika kufanyika kwa sheria ya utakaso kama tunavyoona katika kitabu cha Mambo ya Walawi 22:4-6: kikisema.

 

Mtu yeyote wa kizazi cha Haruni aliye mwenye ukoma, au mwenye kisosono; yeye asile katika vitu vitakatifu, hata atakapokuwa safi. Tena mtu awaye yote atakayekinusa kitu kilicho na unajisi kwa sababu ya wafu, au mtu ambaye shahawa humtoka; 5 au mtu amgusaye mnyama atambaaye, wa kumpatia unajisi, au kwamba amgusa mtu wa kumpatia unajisi, kwa unajisi wowote alio nao; 6 huyu mtu atakayegusa kitu cho chote namna hiyo atakuwa najisi hata jioni, naye hatakula katika vitu vitakatifu, asipooga mwili wake majini.

 

Mambo haya yanahitaji toba kama tunavyoweza kuangamia kwa ajili ya dhambi. Kanisa la Wakorintho, lilikuwa na mfano fulani maalumu wa jambo hili na halikuweza kuona maana yake kama tunavyoona katika 1Wakorintho 5:1-6:

Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye. 2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo. 3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo. 4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu, 5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu. 6 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui hamjui kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima?

 

Kwa mtazamo huu inamaanisha kuwa mbingu ilikuwa mwashiriki wa waliofanya dhambi na ilikuwa inauchafulia mwili wa Kanisa, ambao haukuona tatizo kama mtume Paulo alivyoliona. Lakini dhambi maana yake imeenda mbali zaidi ya ile ya uasherati, na yeye mwenye hasira na mwenye amchukiaye ndugu yake hayo ni kama makosa tu.

 

Kuna aina mbili za mashindano ya chachu. Chachu ya Shetani inalenga kutufanya sisi tusiwe sawa kwa ajili ya chachu ya Roho Mtakatifu, ambaye ni Ufalme wa Mbinguni, na unaondoka mbali na sisi nasi tuweze kuharibika zaidi.

 

Mathayo 13:34-58 inasema:

Hayo yote Yesu akiwaambia makutano kwa mifano; wala pasipo mfano hakuwaambia neno; 35 ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema, Nitafumbua kinywa changu kwa mifano, Nitayatamka yaliyositirika tangu awali. 36 Kisha Yesu akawaaga makutano, akaingia nyumbani; wanafunzi wake wakamwendea, wakasema, Tufafanulie maana ya magugu ya kondeni. 37 Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni Mwana wa Adamu, 38 lile konde ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme, na yale magugu ni wana wa yule mwovu; 39 yule adui aliyeyapanda ni Ibilisi; mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika. 40 Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia. 41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi, 42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. 43 Ndipo wenye haki watakapong’aa kama jua katika ufalme wa Baba yao. Mwenye masikio, na asikie. 44 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyositirika katika shamba; ambayo mtu alipoiona, aliificha, na kwa furaha yake akaenda akauza alivyonavyo vyote, akalinunua shamba lile. 45 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara, mwenye kutafuta lulu nzuri; 46 naye alipoona lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua. 47 Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna; 48 hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakawakusanya walio wema vyomboni. 49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki, 50 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. 51 Yesu akawauliza, Mmeyafahamu hayo yote? Wakamwambia, Naam. 52 Akawambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye elimu ya ufalme wa mbinguni amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale. 53 Ikawa Yesu alipoimaliza mifano hiyo, akatoka akaenda zake. 54 Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii? 55 Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda? 56 Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote? 57 Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia, Nabii hakosi kupata heshima, isipokuwa katika nchi yake, na nyumbani kwake mwenyewe. 58 Wala hakufanya miujiza mingi huko; kwa sababu ya kutokuami kwao.

 

Matumizi ya neno chachu pia linahusu masomo au mafundisho ya dini. Mafundisho ya maandiko ya Biblia kama chachu ya Ufalme wa Mbinguni sio tu kuwa inahusiana na Roho Mtakatifu kama nguvu za Mungu zikiwa ni Ufalme wa Mungu ukipanuka kwa wote wenye mwili lakini pia ni wa kweli na mafundisho anayoshirikisha. Uelewaji wa Maandiko Matakatifu ilivurugwa au kuchanganywa na Mafarisayo na kupitia kwa Masadukayo waliokuwa na kalenda sahihi ili kwamba Hekalu liweze kufanya kazi, hata hivyo mafundisho yao yalikuwa ni kinyume na Ufalme wa Munngu na hivyo ile chachu ambayo ilitakiwa iepukwe.

 

Kwa mujibu wa Injili ya Mathayo 16:6-12 tunasoma:

Yesu akawaambia, Angalieni, jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo. 7 Wakabishana wao kwa wao wakisema, Ni kwa sababu hatukuchukua mikate. 8 Naye Yesu akafahamu, akawaambia, Mbona mnabishana ninyi kwa ninyi, enyi wa imani chache, kwa sababu hamna mikate? 9 Hamjafahamu bado, wala hamkumbuki ile mikate mitano kwa wale elfu tano, na vikapu vingapi mlivyoviokota? 10 Wala ile mikate saba kwa watu elfu nane, na makanda mangapi mliyaokota? 11 Imekuwaje hamkufahamu ya kuwa si kwa sababu ya mikate naliwaambia? Ila jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo. 12 Ndipo walipofahamu ya kuwa hakuwaambia kujilinda na chachu ya mikate, bali na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.

 

Wazo la kuifananisha chachu kuwa dhambi lilichukuliwa katika aya za maandiko ambazo ni kama hizi; ambazo ilikuwa ni uongo na sio sahihi na kama zikiendelezwa zinamharibu mtu.

 

1Wakorintho 5:6-8 inasema

Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui hamjui kwamba chachu kidogo huchachusha donge zima? 7 Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyokuwa hamkutiwa chachu. Kwa maaana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, kristo; 8 basi na tuifanye karamu, si kwa chachu ya kale, wala kwa chachu ya uovu na ubaya, bali yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli.

 

Dhabihu ya chachu kama dhabihu safi na takatifu ya Shukurani haikuwa ni ya Pentekoste peke yake, bali pia ilimaanisha “usafi” wa moyoni mwa mwenye kufanya toba katika Israeli. Ingawa kwa kupitia nabii Amosi, Mungu alisema kile alichokiitaji katika Israeli. Katika chachu za Sadaka ya Shururani, alikuwa anaelekeza tena kwenye moyo safi uliojazwa na Roho Mtakatifu na hii ilifananishwa na chachu zilizoko ndani ya sadaka ya Shukurani.

 

Amosi 4:1-5 inasema:

Lisikieni neno hili, enyi ng’ombe wa Bashani mkaao juu ya mlima wa Samaria, mnaowaonea maskini, na kuwaponda wahitaji; mnaowaambia bwana zao. Haya! Leteni tunywe. 2 Bwana, MUNGU ameapa kwa utakatifu wake, ya kuwa, tazama, siku zitawajilia, watakapowachukua ninyi kwa kulabu, na mabaki yenu kwa ndoana. 3 Nanyi mtatoka kwenye mahali palipobomolewa, kila mwanamke moja kwa moja mbele yake; nanyi mtajitupa katika Harmoni, asema BWANA. 4 Njoni Betheli, mkakose, njoni Gilgali, mkaongeze makosa; kaleteni dhabihu zenu kila asubuhi, na zaka zenu kila siku ya tatu; 5 mkachome sadaka ya shukurani, ya kitu kilichotiwa chachu; mkatangaze sadaka mtoazo kwa hiari na kuzihubiri habari zake; kwa maana ndivyo viwapendezavyo ninyi, enyi wana wa Israeli, asema Bwana, MUNGU.  

 

Amosi anawafananisha watesi wao kama wanyama au ng’ombe wa Bashani. Mtazamo au msimamo huu huwaridhisha wanadamu lakini kamwe haumfurahishi Mungu. Habu jifunze kile ambacho Amosi alichotaka kukisema kuhusu utaratibu na njia bora ya uadhimishaji wa Sabato za Bwana na Miandamo ya Mwezi Mpya (Amosi 8:5).

 

Sasa pia tazama kuhusu ni nini maana ya Sadaka ya Pentekoste. Katika Mambo ya Walawi 23:15-16, tunaona maelekezo ya hesabu ifanyikayo kuelekea kwenye Pentekoste. Inaenda kwa ndani zaidi kuelezea maana halisi ya kwamba ile Mikaye ya Wonyesho ilikuwa inawakilisha nini.

 

Katika Mambo ya Walawi 23:17-22 inasema:

Mtatoa katika makao yenu mikate miwili ya kutikiswa, itakuwa ya sehemu za kumi mbili za efa; itakuwa ya unga mwembamba, itaokwa na chachu, iwe malimbuko kwa BWANA. 18 Nanyi, pamoja na hiyo mikate, mtasongeza wana kondoo saba, walio wakamilifu, wa mwaka wa kwanza, na ng’ombe mume mmoja, na kondoo waume wawili; watakuwa sadaka ya kuteketezwa aka zao kwa BWANA, pamoja na sadaka yao ya unga, na sadza kinywaji, sadaka ya harufu ya kupendeza iliyosogezwa kwa BWANA kwa njia ya moto. 19 Nanyi mtamsongeza mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wana kondoo wawili waume wa mwaka wa kwanza kuwa dhabihu ya sadaka za amani. 20 Kisha kuhani atawatikisa pamoja na hiyo mikate ya malimbuko kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za BWANA, pamojana wale kondoo wawili; watakuwa watakatifu kwa BWANA , wawe wa huyo kuhani. 21 Nanyi mtapiga mbiu siku iyo hiyo; kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; msifanye kazi yoyote ya utumishi; ni amri ya milele katika makao yenu yote, katika vizazi vyenu. 22 Nanyi hapo mtakapovuna mavuno ya nchi yenu, msivune kabisa kabisa pembe la shamba lako, wala msiyakusanye masazo ya mavuno yako; utayaacha kwa ajili ya huyo masikini, na mgeni, mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

 

Hii ni Mitate ya wonyesho ya Malimbuko. Ni mifano iliyo dhahiri kabisa yenye maana ya Malimbuko, baada ya Kristo, ni Kanisa la Mungu na wana wakilishwa na chachu kwenye mikate ya wonyesho. Vyote viwili, yaani Kristo katika Pentekoste hufanyika mkate wa wonyesho uliotiwa chachu. Hii chachu yaweza tu pia kuwakilisha chachu za ufalme wa Mungu, ambaye ni Roho Mtakatifu. Vile vile fahamu hili kuhusu mambo mengine muhimu yanayotakiwa kwa kuufikilia utakatifu, na hasahasa utaratibu wa utoji zaka. Dhabihu zetu sisi ni maombi na kufunga saumu na sadaka za hiyari.

 

Sisi sote hutenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu. Jitahidi kuzishinda na. Mtumie Roho Mtakatifu kwa mambo mazuri. Usimhuzinishe wala kumzima, lakini fanya toba yaani utubu na uwe na nia safi. Kuwa mshindi na utiwe nguvu kwa huyo Roho Mtakatifu.

 

Waraka kwa Warumi 7:14-25 unasema:

Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi. 15 Maana sijui nifanyalo, kwa sababu nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalo litenda. 16 Lakini nikilipenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema. 17 Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati. 19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 21 Basi nimeona sheria hii, ya kuwa kwangu mimi nitakaye kutenda lililo jema, lipo lililo baya. 22 Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani, 23 lakini katika viungo vyangu naona sheria iliyo mbali, inapiga vita na ile sheria ya akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya dhambi katika viungo vyangu. 24 Ole wangu, maskini mimi! Ni nani atakaye niokoa na mwili huu wa mauti? 25 Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.

 

Kwa hiyo, mtume Paulo anaonyesha jinsi mambo haya yote mawili yanavyo gongana kati ya chachu ya Shetani na chachu ya Ufalme wa Mbinguni, ambaye ni Roho Mtakatifu. Hii ni kusema kwamba ufalme unaweza kuwa katikati yetu.

 

Sisi sote hufanya makosa kama watu wenye mwili. Yehova, Mungu wetu huangalia na kuchunguza mawazo kwa ajili ya tunayoyafanya na kuwaza.

 

Yeremia 17:9-10 inasema:

Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugojwa wa kufisha; nani awezaye kuujua? 10 Mimi, BWANA, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.

 

Sisi kama tulivyo tu pekeyetu wenyewe hatuwezi kushinda pasipo Mungu kuingilia kati kwa kupitia Roho wake Mtakatifu.

 

Yeremia 10:23-24 inasema:

Ee BWANA, najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu. 24 Ee BWANA, unirudi kwa haki, si hasira yako, usije ukaniangamiza.

 

Mungu alituahidi kwa kupitia mtumishi wake nabii Isaya kwamba atamimina Roho Wake Mtakatifu juu ya mbegu, ambalo ni mwili wa Kristo yaani Kanisa. Mwili huu unafananishwa na mkate. Mkate unaoliwa wakati wa Pasaka hauruhusiwi kutiwa chachu ndani kwa sababu tumetatakiwa kuondoa chachu za uovu na mawazo mabaya katikati yetu. Ni kwa ile siku ya mwisho ya Mikate Isiyotiwa Chachu ambayo ni siku ya 21 ya mwezi wa Abibu, wakati tukiwa tumeondolewa chachu za dhambi za kale na ubinafsi, tunaweza sasa kuendelea na Pentekoste ambapo Roho Mtakatifu huwepo nasi tunatiwa chachu na nguvu za Mungu. Kwa hiyo ni muhimu kuwa tunaadhimisha kuzitunza siku nane zote kikamilifu za sikukuu, ili tuweze kujiandaa vizuri sisi wenyewe kwa maadhimisho ya Pentekoste.

 

Isaya 44:3 inasema:

Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa.

 

Dhabihu ya dhambi iliwafanya wale waliokuwa wanaigusa hii wawe watakatifu (Law. 6:24-27) na ilikuwa inaashiria kwamba Kristo angefanyika ondoleo la dhambi na kuwafanya Israeli na watu wa ulimwwengu wote kuwa watakatifu. Hata hivyo, kusudiola kutayarishwa kwake imevunjika na kuachwa, kama sisi wenyewe tutakavyofanyika wanadamu tulioko kwenye ulimwengu wa roho.

 

Mambo ya Walawi 6:28 inasema:

Lakini hicho chombo cha udongo ambacho hiyo nyama ilipikwa ndani yake kitavunjwa; na kama ikipikwa katika chombo cha shaba kitasuguliwa, na kuoshwa kwa maji.

 

Walawi waliokuwa wanasaidia kuandaa dhabihu kwa ajili ya dhambi walikuwa wakitakaswa pia kama sisi wenyewe leo tunavyo takiwa tuwe tumetakasika.

 

Nawe utawafanyia mambo haya ili kuwatakasa; nyunyiza juu yao maji yatakasayo dhambi, nao wajinyoe kwa wembe mwili wote, kisha wazifue nguo zao, na kujitakasa. (Hesabu 8:7).

 

Maana ya kumfanya Kristo awe ni njia ya ili tuweze kuingia na kumpatata Roho Mtakatifu aliyetolewa kwetu jangwani.

 

Hesabu 20:8-11 inasema:

Twaa ile fimbo, ukawakusanye mkutano; wewe na Haruni ndugu yako, ukauambie mwamba mbele ya macho yao utoe maji yake, nawe utawatokezea maji katika mwamba, na hivyo utawanywesha maji mkutano na wanyama wao. 9 Musa akaitwaa hiyo fimbo kutoka mbele ya BWANA kama alivyowaamuru. 10 Musa na Haruni wakawakusanya kusanyiko mbele ya mwamba, akawaambia, Sikieni sasa, enyi waasi; je! Tuwatokezee maji katika mwamba huu? 11 Musa akainua macho yake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na wanyama wao pia.

 

Kwa hiyo pia Nehemia anasema walipewa chakula toka mbinguni, ili kwamba waweze kuirithi ahadi yao ya haki yao ya uzaliwa wa kwanza.

Ukawapa chakula toka mbinguni, kwa ajili ya njaa yao, na kwa ajili yao ukaleta maji kutoka mwambani, kwa sababu ya kiu yao, ukawaamuru kwamba waingie katika nchi na kuimiliki, ambayo umeinua mkono wako kuwapa .(Neh. 9:15).

 

Na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.

 

wote wakanywa kinywaji kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. (1Kor. 10:4).

 

Na kile kilikuwa ni kisima cha nadhiri.

16 Kutoka huko wakasafiri kwenda Beeri; ni kisima ambacho BWANA alimwamuru Musa, Ukawakutanishe, nami nitawapa maji (Hes. 21:16).

 

Tunaona hapa kuwa mfano huu wa maji ya Roho unaelekeza roho iliyoko ndani ya mwanadamu.

 

Waamuzi 15:19 inasema:

Lakini Mungu akapasua mahali panye shimo palipo katika Lehi, pakatoka maji; naye alipokwisha kunywa, roho yake itamrudia, akaburudika; kwa hiyo jina la mahali pale litaitwa Enhakore, napo pa katika Lehi hata hivi leo.

 

Chachu hii ya Roho Mtakatifu pia inafananishwa na mafuta yanayojazwa katika taa za wateule.

 

Mathayo 25:I-13 inasema:

Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi. 2 Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara. 3 Wle waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao; 4 bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao. 5 Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi. 6 Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki. 7 Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao. 8 Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika. 9 Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie. 10 Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa. 11 Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie. 12 Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi. 13Basi kesheni, kwa sababu hamjui siku wala saa.

 

Kristo alituonyesha kuwa maji yalikuwa ni mfano wa maji yaliyohai ya Roho Mtakatifu, ambayo wakati wa hukumu inawakilishwa na Siku ya Mwisho iliyo Kuu, ambayo itatolewa kwa watu wote.

 

Yohana 7:37-39 inasema:

37 Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe. 38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake. 39 Na neno hilo alilisema katika habari za Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.

 

Hivyo pia akaendeleza kipawa kile kwa Mataifa wasio Waisraeli.

 

Yohana 4:10-15 inasema:

Yesu akawajibu, akawaambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai. 11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo maji yaliyo hai? 12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake na wanawe pia, na wanyama wake? 13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena; 14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemichemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele. 15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, nipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.

 

Kwa hiyo tumebatizwa kwa Roho Mtakatifu na nguvu ile hutujaa na hutufanya kuwa viumbe vipya. Tumetiwa chachu kwa chachu mpya na nguvu mpya na kutufanya kuwa mkate wa wonyesho, ulio pia ni mwili wa Kristo na Mana kutoka Mbinguni.

 

Mathayo 3:11 inasema:

Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sisahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.

 

Marko 1:8 inaelezea kuwa.

Mimi niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.

 

Wakati ambapo Luka anasema katika Luka 3:16:

Yohana akajibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu ya viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto;

 

Waefeso 5:26 inatuonyesha jinsi utakaso unavyoweza kutokea.

ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno ;

 

Kuwa mwangalifu pia kwa mifano ya hao walao nasi na wasio na Roho Mtakatifu.

 

Yuda 12 nasema:

Watu hawa ni miamba yenye hatari katika karamu zenu za upendo walapo karamu zenu za upendo walapo karamu pamoja nanyi, wakijilisha pasipo hofu; ni mawingu yasiyo na maji, yachuliwayo na matunda, iliyokufa mara mbili, na kung’olewa babisa;

 

Mungu anasema kwa kupitia Kristo katika Ufunuo wa Yohana 21:6 kuwa:

Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima bure.

 

Tumepewa Roho Mtakatifu bure kabisa kadiri tunavyoshinda.

 

Vilevile anasema katika Ufunuo 21:17 kuwa:

Akaupima ukuta wake, ukapata dhiraa mia na arobaini nne, kwa kipimo cha kibinadamu, maana yake, cha malaika.

 

Tutakuwa kama malaika na watoto wa Mungu pamoja na jeshi adilifu kama viumbe katika ulimwengu wa roho.

 

Waraka wa 1Wakorintho 6:11 unatuonyesha kuwa sisi sote tumeoshwa na kutakaswa na kuhesabiwa haki kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, katika Roho wa Mungu wetu.

Lakini nasema hayo, kwa kutoa idhini yangu, si baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.

 

Sote tumefanyika kuwa mwili mmoja kwa kuwa Roho ni mmoja.

 

1Korintho 12:13 inatuonyesha umoja wetu katika Roho.

Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweeshwa Roho mmoja.

 

Kwa jinsi hii sisi tu wamoja na ndugu kwa pamoja, na bibi arusi wa Kristo, sisi sote. Sisi tu mikate ya wonyesho iliyotiwa chachu ya Pentekoste ambayo jeshi la mbinguni kama Malimbuko kwa Mungu.

 

(Maswali yame wekwa kwa kumujibu wa Biblia iitwayo Amertcan Standard Version 1901 lakini ikafanyiwa marekebisho na kusomeka Yahovah. Hakuna herufi “j” katika Lugha ya Kiebrania na tunalijua hilo katika uchimbaji kiutafiti jina la zamani lilikuwa “Yaho” au “Yahova”, na sio “Jah” na “Jehovah”, au hata “Yahweh” kama pia inavyodaiwa).

 

q