Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[255]
Torati
na Amri ya Tatu ya Mungu
(Toleo Na 4.0 19981006-20050810-20120520)
Imeandikwa: Usilitaje
bure jina la Bwana, Mungu wako, maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia mtu
alitajaye jina
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1998, 1999, 2005,
2012 Wade Cox et al, ed. Wade Cox)
(tr. 2012)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu
Jarida hili linapatikana Ulimwenguni
kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Torati na
Amri ya Tatu ya Mungu
Imeandikwa:
Kutoka 20:7 Usilitaje bure jina la Bwana, Mungu
wako, maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina
Kumbukumbu la Torati 5:11 Usilitaje bure jina la Bwana,
Mungu wako, maana Bwana hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina
Jina la Mungu liko kwenye tarakimu ya umoja
Malaika wa
mbinguni wanapewa uweza wa kiungu, yaani kuwa elohim wakishirikiana na Eloah,
katika maumbile
Kumbukumbu la Torati 6:4-5 4 Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja. 5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.
Kutoka 3:14 inatuonyesha jinsi Mungu anavyofanyika
kuwa kitu fulani. Hapa anasema, Mimi niko ambaye niko,
yaani “Nitakuwa
Sheria za Mungu-Mfumo wa Utaratibu
Ni tengo ka uvunjajis wa Sheria za Mungu na amri ya tatu ya Mungu kuuweka mfumo wa sheria au imani iliyokinyume na isemavyo Biblia na maelekezo au kanuni zake. Mfumo mzima unaoonekana kugeuza Amri za Mungu. Hairuhusiwi kuweka aina yoyote ya utaratibu wa sheria na kuzichagua nyingine.
Hairuhusiwi kudai kuwa tunamwabudu Mungu Aliyehai kwa jina la Yesu Kristo na wakati huo huo tukizidharau au kutozitunza Sabato na Sikukuu zake, na kuupa nafasi mbadala mfumo wa wa imani zinazotokana na upagani na ibada za kuabudu Jua. Ndivyo ilivyo kwamba ibada za siku ya Jumapili na maadhimisho ya sikukuu za Krismas na Easter sio tu kuwa yanapingana na kuivunja amri ya hii ya Tatu, bali ni kuzivunja amri zote. Mungu anasema kwamba anazichukia Sikukuu na Sabato zao. (Isa. 1:11-20) kwa ajili ya unafiki huu mkubwa.
Sabato ya uwongo haina maana tu ya lile
tendo la kufanya ibada siku nyingine asiyoiamuru Mungu tu,
Mamlaka yote imetakiwa
itumike kwa ajili ya kuyafanya mambo yote yaihusuyo
Torati ya Mungu. Aina yoyote ya imani ya kidini inayopingana na
maudhui ya Biblia na maana zake au inayoathiri au yanayobadili maana iliyo
kwenye torati au utaratibu wake ni yana maana sawa tu na hii ya kulitaja jina
la Mungu huyu wa Pekee na Wakweli bure; na ni kuivunja Amri ya Torati yake
iliyoko kwenye amri ya tatu. Na ni kwamba wanafundisha
kinyume na neno la Mungu na wanalichukua jina
Jina la Mungu
Mambo yote yahusuyo kutumia mamlaka yaliyo kwenye mambo ya Mungu yanafanywa kwa jina lake akiwa ni Yahova na wanayatumia mamlaka yake kwa namna iliyo sawa tu na kama anavyofanya mfalme aitumiapo pete yake itumiwe kama muhuru wa kuidhinisha jambo (sawa na ilivyoandikwa kwenye jarida la Malaika wa YHVH [The Angel of YHVH (No. 24)]; katika kitabu cha Mwanzo sura za 18 na 19).
Mungu anatuonya na kutufundisha sisi. Upole wake hutufanya tuwe wakamilifu na tuna ngao ya wokovu wake. Yeye ni ngome yetu na mkombozi wetu (soma 2Sam. 22:32-35; Zab. 18:34; 144:1). Mamlaka na uweza vyote ni vya Mungu na mamlaka yaliyoko yote ni ya Mungu (Rum. 13:1,2,7).
Kwa hiyo tuapaswa kumtii Mungu kuliko wanadamu (Mdo 5:29). Kisasi ni juu yake yeye na ni yeye awezaye kufidia na kulipiza kwa haki (Kum. 32:35; Zab. 94:1; Ebr. 10:30; Rum. 12:19).
Kumbukumbu la Torati 10:20-22 Mche Bwana,
Mungu wako, umtumikie yeye; ambatana naye, na kuapa
kwa jina lake. 21 Yeye ndiye fahari yako, na yeye ndiye
Mungu wako, aliyekutendea mambo haya makubwa, ya kutisha, uliyoyaona kwa macho
yako. 22 Baba zako walishukia Misri na watu
sabini; na sasa Bwana, Mungu wako, amekufanya kama nyota za mbinguni kwa wingi.
Kwa hiyo, tumekatazwa kulitumia
jina la Mungu bure, au kufanya viapo vya uwongo kwa
jina lake. Yeye ni mtakatifu, na jina
Mambo ya Walawi 19:12 Msiape uongo kwa jina langu, hata ukalinajisi jina la Mungu wako; Mimi ndimi Bwana..
Zaburi 99:2-3
Bwana katika
Sayuni ni mkuu, Naye ametukuka juu ya mataifa yote. Na
walishukuru jina lake kuu la kuhofiwa; Ndiye mtakatifu.
Zaburi 111:9 Amewapelekea watu wake ukombozi,
Ameamuru agano
Yeremia 14:9b Lakini wewe, Bwana, u katikati yetu, nasi tunaitwa kwa jina lako; usituache.
Mungu asiye onekana
Maandiko matakatifu yanatueleza kuwa Mungu hajawahi
kuonekana kamwe kabisa na kwamba hakuna aliyewahi
kuisikia sauti yake. Je, Mungu huyu ni yupi basi na ambaye anajulikana kwa jina
Yohana 1:18a Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote;
Kutoka 33:20 inasema: Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi.
Yohana 5:37 Naye Baba aliyenipeleka amenishuhudia. Sauti yake hamkuisikia wakati wo wote, wala sura yake hamkuiona.
Hapa Kristo anamwelezea baba yake kuwa ni kumbe ambaye hajawahi kuonekana—na wala sura yake wala umbo lake—na wala sauti yake haijawahi kusikiwa.
Maandiko ya Mtume Paulo kwenye Agano Jipya
anamwelezea
Wakolosai 1:15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
1Timotheo 1:17 Sasa kwa
Mfalme wa milele, asiyeweza kuona uharibifu, asiyeonekana, Mungu peke yake, na
iwe heshima na utukufu milele na milele. Amina.
Waebrania 11:27 Kwa imani akatoka Misri, asiogope
ghadhabu ya mfalme; maana alistahimili
Mungu huyu ambaye hakuna mtu aliyewahi kumuona analo jina. Jina la Mungu huashiria tabia yake au jinsi alivyo. Jina la Mungu ni Eloa, au Yahova wa Majeshi. Wakati mwingine jina hili la Mungu hukosewa kuitwa, kwa jinsi watu wanavyomuita kuwa ni Yehova au Yahwe.
Je, ni kwa namna
gani basi jina hili la Mungu linaweza kutumika au kutajwa bure au visivyo? Kitabu
cha fasiri cha Young’s Analytical Concordance kinaelezea jinsi linavyoweza kutumiwa visivyo
·
Ubatili:
Neno hili linatokana na lugha ya Kiebrania la hebel (Yer.10:3)
· Bure, kwa kutangua-kutoka kwenye neno la
Kiebrania chinnam (Eze. 6:10)
· Tupu, linalotokana na neno la Kiebrania la nabab (Ayubu11:11,12)
·
Pasipo
Kitu, bure linalotokana na neno la Kiebrania rig (Zaburi 2:1; Yeremia 51:58)
·
Uwongo
au Udanganyifu kutokana na neno sheqer
(Kutoka 5:9)
·
Kuharibika
au uharibifu, kutoka kwenye neno tohu (Isaya
45:18; sawa na Mwanzo 1:2; Yeremia 4:23)
·
Hasara
au kisichofaa kutoka kwenye neno la Kiyunani mataios
Maneno haya yote yametafsiriwa
Jina la Mungu limeandikwa na sio kutajwa
Jina la Mungu lilikuwa na
maana
Maandiko ya Kiebrania
Wakati jina hili lilipoandikwa Yahovah (SHD 3068) basi kila lilipoandikwa
hivyo lilitamkwa kama “Adonai,” na wakati Mungu
alipotajwa
Hata walipokuwa wanaliandika jina hili la Mungu walipokuwa wanazinukuu sheria za Mungu kwenye maandiko mbalimbali, waandishi walilazimika kuadhimsha au kuzishika shera na taratibu fulani fulani
· Alipaswa kuwa ameoga vizuri na awe msafi.
· Ni lazima awe amezaa mavazi yote yaliyochukuliwa kuwa matakatifu kwa Wayahudi.
· Alipaswa kujihadhari kuwa asiingize peni yake na kutumbukia hadi katikati wakati anapiliandika jina hili la Mungu.
· Ni lazima Mfalme amuelekeze anapokuwa analiandika jina hili la Mungu, na asichukue maneno yoyote mengine anayoyasikia au kuwaza moyoni mwake.
Inadaiwa kuwa taratibu hizi ziliingizwa au
kuwekwa kwa kuwa walidhania kwamba zingezuia watu
kulitaja jina la Mungu bure. Ni jambo lililodhahiri
Biblia maarufu ya wwandishi maarufu Bullinger inayoitwa Bullinga’s Companion Bible (Nyongeza yake ya 32) ina orodha ya nyongeza hizi yanayolitaja jina la Adonai katika kumtaja Yahova na pia utendaji kazi wa elohim. Mtazamo wa jinsi ya kulitamka jina la Mungu sio kitu ambacho amri hii ya tatu inaliongelea au kinachomaanisha.
Mwandishi mwingine aitwaye R.J. Rushdoony [kwenye kitabu chake cha Chuo cha Torati au Sheria ya Biblia (The Institutes of Biblical Law)], ambacho kilichapishwa kwenye machapisho yaliyoitwa kama Presbyterian and Reformed Publishing Company, 1973, ukurasa wa (126) ambayo ilikuwa na maswali yafuatayo:
“Swali
la112. Je, ninini kinachotakiwa kufanyika kwenye amri za tatu?”
“Jibu: Amri ya tatu
inataka kwamba, jina la Mungu, wadhifa wake, haiba yake, amri zake, neno lake, sakramenti
zake, kwenye maombi, viapo vyake, katika kupiga kura, katika kuapa, kazi zake, na
mambo mengineyo yote na ambavyo kwavyo vinamfanya ajulikane kuwa ni mtakatifu na
atumike kwa heshima yake kubwa na kutumika mawazoni, kwenye mawazoni, neno au
uandishi, kwa taaluma takatifu ya kikuhani, na malumbano yasiyojibika, kwenye
utukufu wa Mungu, na kwa faida zetu na za wengine.”
“Swali
la 113. Je, kuna dhambi gani imekatazwa kwenye amri hii ya tatu?”
“Jibu: Dhambi
zilizokatazwa kwenye amri hii ya tatu ni, kutolitumia jina la Mungu kinyume na inavyotakiwa,
na tendo la kulidhalilisha kwa kulitumia kinyume na kijinga, au kulitumia bila
maana au sababu ya maana, kulitumia visivyopasa, kulikufuru, kulitumia kwenye
mambo ya ushirikina, au kulitumia kwenye mambo ya ulozi au kwa matendo yote ya
kutumia cheo chake, wadhiwa wake, kuyatumia maandiko yake au aya na kazi zake
kwa matumizi ya kukufuru, au kufanya maapizo, au katika kuweka nadhiri, viapo,
utiifu au uadilifu, na kutimiliza kama kuna vitu vingine visivyo kwenye
uadilifu, kwenye manung’uniko na migogoro, kwenye udadisi au nasaha, au
kushindwa kutendea kazi, au kwa namna nyingine yoyote inayoligeuza au kupingana
na neno lake, au sehemu nyingine iwayo yote, katika namna ya kukufuru, mabishano
au kwenye maswali yasiyo na faida, kulitumia kinyume na kwa mambo yasiyo ya
lazima au katika kuyatetea mafundisho ya uwongo, kulidharau,, kiumbe au
kitu chochote kilichochini ya jina la Mungu, kulitumia kwa matumizi ya kiuchawi
au kwa dhambi zozote zinazotokana na tama ya mwili na utendaji wake, au kwa
matendo yoyote maovu, udanganyifu, kwa mpindisho au kwa namna nyingine yoyote
inayopingana na kweli ya Mungu, neema na nyinginezo. Kuweka dhana ya
nyadhifa kwenye mambo ya dini ni unafiki au ni kwa kwa
namna nyingine twaweza kusema kwamba hatimayake ni kupelekea kwenye jambo la
aibu au ni aibu kubwa”.
Huenda watu wengi
hawajatilia maanani jambo au utendaji huu mkuu wa amri
hii ya tatu ya Mungu. Tunajua kwamba Mungu anataka kushirikiana na mwanadamu. Na jinsi pekee ya uhusiano huu anaweza kusababisha
mchanganyo ni kwa mtu kuwa na hali ya kujisalimisha
kikamilifu kwa Mungu na kwa mapenzi yake, kwa kuwa na unyenyekevu kamilifu
kwenye Amri zake. Mungu anapendezwa na unyenyekevu na
sio sadaka. Na zaidi
Tendo la
kuyabadili matumizi ya jina la Mungu na kulitumia
pasipo sababu na kimakosa yalianza nyakati za mjukuu wa Adamu aliyeitwa Enoshi,
kwa mujibu wa ilivyoandikwa na kuonekana kwenye kitabu cha Mwanzo 4:26.
Mwanzo 4:26 inasema: Sethi naye
akazaa mwana; akamwita jina
Uandishi
wa neno hili kwenye tafsiri ya Kiingereza ya KJV inaficha
kile ambacho kwakweli kinachoendelea, wakati kwenye tafsiri ya Biblia iitwayo Bullinger’s
Companion Bible, Appendix 21 inatupa
maana kusudiwa ya aya hii. Kwa mujibu wa fafanuzi za kale za Kiyahudi,
zonaonyesha kwamba watu waliacha kuomba kwa kulitumia jina la Bwana (kwa mujibu
wa kitabu cha Targum Onkelos) na pia walijifanyia
vinyago na sanamu za kuchonga na kuziitia kwa jina la Neno la Bwana (kwa mujibu
wa Targum Jonathan). Rashi anasema
kulikuwa na aina ya kufuru katika kuliitia jina la
Bwana. Kwa hiyo, Dabar Yahovah au Neno
la Bwana lilikuwa ni jina linalomaanisha Mungu; na hii
ndiyo kazi ya Yesu Kristo, akiwa ni Neno.
Ilijulikana
vema kwamba katika siku za Enoshi (aliyekuwa miongoni mwa uzao wa Adamu) ndipo watu walianzisha aina ptotfu ya ibada kwa
kulihusianisha jina la Mungu na viumbe vingine vya mbinguni. Inaaminika kuwa
walianza kuiitia miungu
Jinsi ya Kulitamka Jina
la Mungu kwa Lugha ya Kiebrania
Kuna makundi fulani miongoni mwa ndugu wa Makanisa ya Mungu yanayotunza
Sabato, ambao wanashikilia kuamini dhana ya kuwa ni muhimu
Matendo 4:12 inasema: 12
Wala
hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana
hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi
kuokolewa kwalo
Baadhi ya majina yaliyoaminika
kutumiwa na jinsi ya kuyatamka na makanisa haya ni
Kwa Masihi, wanatumia: YaHVaHoshea, Yahushua, Yahshua, Yeshua.
Kulitaja “Jin takatifu
zaidi), makundi haya kwanza wanatumia Yahweh na kwa
Yeye Aliye Juu Sana, na hutumia jina Yahshua ili kumtaja Masihi.
Dhana iliyoko kwenye “majina matakatifu” inadai kwamba tunapaswa kulijua jina
sahihi la Mungu na pia tuweze kulitamka vizuri—pamoja
na kujua jinsi linavyoandikwa—ili tupate kuokolewa. Wazo hili linamdhalilisha
Mwenyezi Mungu na kumfanyia dhihaka, na kumfanya aonekane kuwa hawezi
kuwasiliana na wanadamu kwa lugha nyingine yoyote ila ni kwa Kiebrania tu, na
wanasahau kabisa kuwa ni yeye Mungu ndiye aliyezigawanya lugha za wanadamu
kwenye mnara wa Babeli. Dhana hii pia inapuuzia kilichoelezwa kwenye Isaya 28:11.
Isaya 28:11 inasema: La, bali kwa midomo ya watu wageni, na kwa lugha nyingine atasema na watu hawa;
Wazo na
dhana hii ya kutumia “majina matakatifu” pia inashindwa kujua majina na vyeo
mbalimbali yanayomwakilisha mtu
ambaye hatimaye alijulikana kama Yesu Kristo,
Isaya 9:6 inasema: Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,
Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye
ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye
nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.
Dhana halisi ya kifungu hiki
inaweza kusomwa na kueleweka kwa namna mbalimbali.
Kwenye tafsiri maarufu ya Septuagint (LXX), aya hii ya Isaya 9:6-8 inasomeka
hivi:
Maana
kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme
utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mjumbe wa Shauri Kuu [Malaika wa Shauri
Kuu] kwakuwa nitaleta amani kwa wafalme na afya kwake. 7 Maongeo
ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha
Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki,
Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.
8 Bwana alimpelekea Yakobo neno, likamfikilia Israeli.
Andiko hili linasomeka moja kwa moja
Jina Baba wa Milele haliwezi kueleweka na waamini Utatu au kwa
walio kwenye dini ya Kiyahudi na limeandikwa kikamilifu
Mtoto amezaliwa kwa ajili yaetu,
Tumepewa mtoto,
Na uweza wa
kifalme u mabegani mwake,
Na jina
Pele-joez-el-gibbor-
Abdi-ad-sar-shalom
Kwa hiyo, mfumo mzima unaonekana
Dhana hii inayoupa ulazima wa kutumia “majina matakatifu” inaonyesha kupuuzia kile
kilichoandikwa kwenye Maandiko Matakatifu kwenye Mathayo 1:21 (pia kwenye aya ya 23).
Mathayo 1:21 inasema: Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina
Yesu alifanyika
Mwokozi kwa uteule wake, baada ya kuishi maisha yasiyo
na dhambi na kisha kuyatoa maisha yake yawe sadaka. Kuna Maandiko Matakatifu
yanayoonyesha vizuri kwamba Mungu Baba yetu ni Mwokozi
wetu halisi (Zaburi 106.21; na Isaya 60:16).
Yuda 25 inasema: Yeye aliye Mungu pekee, Mwokozi wetu kwa Yesu Kristo Bwana wetu; utukufu una yeye, na ukuu, na
uwezo, na nguvu, tangu milele, na sasa, na hata milele. Amina.
(sawa na tulivyoandika kwenye jarida la Mungu Mwokozi Wetu (Na. 198) [God Our Saviour (No. 198)].
Mathayo 1:23 inasema: Tazama, bikira atachukua mimba, Naye
atazaa mwana; Nao watamwita jina
Mwna huyu wa Mungu, ambaye
pia ni Masihi na Mwokozi aliyeruzukiwa na Mungu, alifanya pia kuwa ni Kuhani
Mkuu mwenye Cheo sawa na kile cha Melkizedeki, na alifanika kuwa kuhani wetu
Mkuu alipokuja kwa mara yake ya kwanza na atafanyika kuwa Mfalme wetu kipindi
atakapokuja mara ya pili. Kumfanya Masihi awe na jina
moja tu kwa Kiebrania kunavunja amri ya tatu, na ni sawa na kulitaja jina la
Mungu bila sababu ya maana. Kunazuia makusudi ya Mungu na
kuuzuia Mpango wa Mungu uliowekwa kwa kusudi la kuwaokoa watu wote.
Wakati Yesu alipoombwa na wanafunzi wake awafundishe jinsi ya kuomba (Luka 11:1-4),
aliwafundisha kuyawakilisha au kuyapeleka maombi
Tunaona pia kwamba maombi
aliyoyafanya Yesu Kristo katika Yohana 17:1-26 aliyafanya kwa
kumtaja Mungu kuwa ni “Baba.” Na kwenye Mathayo 27:46 tunaona kuwa Yeeu Kristo
alipokuwa anasulibiwa mtini alimlilia Baba kwa lugha
ya Kiaramu, ambayo ilikuwa ni ya kawaida na iliyozoeleka na wengi kwa kipindi
kile akisema “Eloi, Eloi, Lama Sabakthani?” [(Mungu wangu,
Mungu wangu, Mbona umeniacha?) (alinukuu Maandiko
Matakatifu ya Kiebrania)]. Tunaona kwamba wala hakuitumia lugha ya Kiebrania
ili kumtaja Baba. Mtume Mathayo aliandika hivyo kwa kuwa alikuwepo pale wakati alipokuwa anasulibiwa na
alimsikia akitamka hivyo. Yohana pia alikuwepo pale, na
aliandika kwa kunukuu maneno aliyoyasema Kristo ya kuwa “Imekwisha.”
Kwa hiyo, Mungu ana majina
mengi na majina haya yote yanapaswa kutukuzwa. Tendo la kuyataja au kuyatamka
majina haya kwa lugha ya Kiebrania peke yake
halifanikishi dhana ya Kulitukuza jina
la Mungu. Majina wenyewe tu
Kukufuru na kuyatumia vibaya Majina ya Mungu
Mwandishi wa
Zaburi alielezea jinsi wajinga na maadui wa Israeli walivyolikufuru na kulitumia
vibaya jina la Mungu (Zaburi 74:10-18). Ni watu waliochukuliwa mateka na kupelekwa mbali pasipokuwa na makosa na hatimaye
wakakombolewa, ndiyo wanaosema. Watu wa Mungu
walipelekwa utumwani na kulikufuru jina la Mungu. Kwa hiyo watu hawa watalijua
jina
Mfano wa dhairi katika
kulitumia vibaya jina na mamlaka ya Mungu kwa kufanya viapo visivyomuhimu na
kulikufu, unapatikana kwenye kitabu cha 1Wafalme 21:10-13 na Matendo 6:11. tunona kwamba Stefano hakuuliza haki waliyopewa baraza la
kidini ya kumhukumu yeye kifo.
Tunaona pia kwamba Kristo alishitakiwa kwa
makosa ya uwongo ya kukufuru (Mathayo 9:3; 26:65,66; Yohana
10:36). Tunaona pia kwamba aliitaja dhambi nyingine asiyoweza kuwsamehewa mtu
ambayo ni ile ya kumkufuru Roho Mtakatifu (Mathayo
12:22-32; Marko 3:22-30). Hili ni jambo linalotatanisha
kwa namna fulani. Roho Mtakatifu ni wa muhimu
Kuwaheshimu wengine wanaolichukua Majina ya Mungu
Mamlaka ya Mungu
yanatuama kote kuwili, yaani ni kwa watawala wa kada
zote mbili yaani wa kimwili na kiroho
Kutoka 22:28 inasema: Usimtukane Mungu, wala
usimlaani mkuu wa watu wako.
Tendo la kutomtii na kumuasi elohim na watawala wa nchi fulani ni sawa na kukufuru huku kunakoelezwa hapa kwenye jina la Mungu. Tunajionea jambo hili zaidi hapo mbeleni. Kukufuru na kulikufuru jina la Mungu ni matendo yanayofanyika kwa namna nyingi kwenye Maandiko Matakatifu.
Zaburi 74:10 inasema: Ee Mungu, mtesi atalaumu hata lini? Adui alidharau jina
lako hata milele.
Zaburi 74:18 Ee Bwana, uyakumbuke hayo, adui amelaumu, Na watu wapumbavu wamelidharau jina lako.
Isaya 52:5-6 Basi sasa, nafanya nini hapa, asema Bwana, ikiwa watu wangu wamechukuliwa bure? Hao wanaowatawala wanapiga yowe, asema Bwana, na jina langu linatukanwa daima mchana kutwa. 6 Kwa hiyo watu wangu watalijua jina langu kwa hiyo watajua siku ile ya kuwa mimi ndimi ninenaye; tazama ni mimi.
Mfano wa ushahidi wa uwongo uliotolewa kwa faida ya udhalimu unaonekana kwenye tukio la Nabothi. Tukio hili linapingana ama linazivunja amri zote mbili, yaani ya tatu na ya tisa, kwa kuwa ni uvunjifu wa amri ya tisa kwa pale unapotokea ushahidi wa uwongo, na hivyo, kuikinzana na ya tatu ambayo hukumu ile ilitolewa kidhalimu sana.
1Wafalme 21:10-13 inasema: mkainue watu wawili, watu
wasiofaa, ili wamshitaki, na kumshuhudia, kunena,
Umemtukana Mungu na mfalme. Kisha mchukueni nje, mkampige kwa mawe, ili afe. 11 Wale wazee wa mji wake, na walio wenye nguvu waliokaa
mjini mwake, wakafanya kama Yezebeli alivyowaagiza, kama ilivyoandikwa katika
nyaraka alizowapelekea. 12 Wakapiga mbiu ya
watu kufunga, wakamweka Nabothi juu mbele ya watu. 13 Na
hao watu wawili, watu wasiofaa, wakaingia, wakaketi mbele yake; wale watu
wasiofaa wakamshuhudia Nabothi mbele ya watu, wakasema, Nabothi amemtukana
Mungu na mfalme. Ndipo wakamchukua nje ya mji, wakampiga kwa mawe hata akafa.
Kwenye andiko hili tunaona jinsi Yezebeli alivyowaleta walalamikaji wa uwongo ili Mfalme Ahabu afanikishe jama yake ya kulichukua shamba la mizabibu la Nabothi.
Mfano ulio kwenye Agano la Jipya wa mashitaka ya uwongo unaonekana kwenye kitabu cha Matendo sura ya 6.
Matendo 6:8-13 inasema: Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika
watu. 9 Lakini baadhi ya watu wa
sinagogi lililoitwa sinagogi la Mahuru, na la Wakirene, na la Waiskanderia, na
la wale wa Kilikia na Asia, wakaondoka na kujadiliana na Stefano; 10 lakini hawakuweza
kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye. 11 Hata wakashawishi watu
waliosema, Tumemsikia mtu huyu akinena maneno ya kumtukana Musa na Mungu. 12 Wakawataharakisha watu na
wazee na waandishi, wakamwendea, wakamkamata, wakampeleka mbele ya baraza. 13 Wakasimamisha mashahidi
wa uongo waliosema, Mtu huyu haachi kusema maneno ya kufuru juu ya mahali hapa
patakatifu na juu ya torati.
Hapa waliwekwa mashahidi wa
uwingo ili wamshitaki Stefano kwa kumsingizia kuwa walimsikia akikufuru.
Mamlaka iliyokuwepo ilimhukumu auawe lakini walifanya hivyo kinakosa na waliyatumia vibaya mamlaka
Na
Mathayo 9:1-7 inasema: Akapanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao. 2 Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako. 3 Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru. 4 Naye Yesu, hali akijua mawazo yao, akasema, Mbona mnawaza maovu mioyoni mwenu? 5 Kwa maana rahisi ni lipi, ni kusema, Umesamehewa dhambi zako, au ni kusema, Ondoka, uende? 6 Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (amwambia yule mwenye kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako. 7 Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake.
Iwapo kama Jesu alikuwa ndiye Kristo, kwa hiyo asingeweza kusema neno la kufuru. Kuhani Mkuu alitabiri mwaka ule kwamba inampasa mmoja afe kwa ajili ya wengi. Alitegemea mtu huyo kuwa ni Kristo, nah ii ndiyo maana hasa ya kurarua vazi lake. Kuhani Mkuu hapaswi kamwe kulirarua vazi lake, lakini kile alichokifanya kilikuwa ni mfano unaoasihiria sawa na kulirarua vazi lake kwa jinsi alivyofanya hivyo, ilikuwa ni mfano pia wa kuuondoa ukuhani kutoka kwenye kabila la Lawi katika Yudea na kuupeleka kwa Melikizedeki katika Israeli.
Mathayo 26:63-66 inasema: Lakini, Yesu akanyamaza.
Kuhani Mkuu akamwambia, Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe
ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu. 64 Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini
nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa
nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni. 65 Ndipo Kuhani Mkuu akararua mavazi
yake, akisema, Amekufuru; mna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa
mmesikia hiyo kufuru yake; 66 mwaonaje ninyi? Wakajibu, wakasema,
Imempasa kuuawa.
Yesu Kristo alishitakiwa mashitaka ya uwongo kwamba
amekufuru kwa kulikotokana na hali ya wasikilizaji
wake ya kutoyajua Maandiko Matakatifu jinsi yanavyosema. Na wengi wa Wakristo
wa leo wangeweza pia kumuua Kristo kwa kama angekuja kwao leo, angetoa mahubiri
yanayotofautiana na vile wanavyotaka aseme kwa jinsi walivyoongozwa na kufanywa
waamini. Kipindi zama kijulikanacho kama cha
Yohana 10:34-36 inasema: Yesu akawajibu, Kazi njema nyingi
nimewaonyesha, zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya kazi
ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe? 33 Wayahudi wakamjibu,
Kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu
wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu. 34 Yesu
akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi
miungu? 35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na
neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka); 36 je!
Yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru;
kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?
Ujumbe uliko kwenye maneno haya peke yake ungeweza kumfanya ahukumiwe kifo. Alikuwa anashutumiwa kuwa anafanya kazi na miujiza yake kwa kutumia nguvu za Belzebuli, aliyekuwa ni Bwana wa Warukao na Mungu wa Ekroni.
Mathayo 12:22-32 inasema: Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona. 23 Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa
Daudi? 24 Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema,
Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo. 25 Basi
Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake,
hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake,
haitasimama. 26 Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika
juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje? 27 Na
mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu
hiyo hao ndio watakaowahukumu. 28 Lakini mimi nikitoa
pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia. 29 Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye
nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo
atakapoiteka nyumba yake. 30 Mtu asiye pamoja
nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya. 31 Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la
kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa. 32 Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu
atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa
katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.
Yesu Kristo alifundisha
kwamba tendo la kukufuriana mtu na mwenzake ni machukizo
yanayoweza kusameheka lakini tendo la kumkufuru Roho Mtakatifu wa Mungu ni uovu
sioweza kusameheka na unampelekea mtu kwenye hukumu ya mauti. Toba ndicho kitu
kinachohitajika ili mtu aupate wokovu, na tendo la
kuikiri dhambi na kujua umuhimu wa neema iletayo wokovu iliyo kwa Mungu kupitia
kwa Roho wake Mtakatifu ndiyo kiini pekee cha wokovu. Adhabu ya mtu anayekufuru
na asiyetubu ni kali kwa kweli.
Ufunuo 16:9,11,21
inasema: Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao
wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu
wala kumpa utukufu. 11 wakamtukana Mungu wa
mbingu kwa sababu ya maumivu yao, na kwa sababu ya majipu yao; wala
hawakuyatubia matendo yao. 21 Na mvua ya mawe
kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya
wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe;
kwa maana pigo lake ni kubwa mno.
Tendo la
kumkufuru Mungu kikwazo kikubwa cha toba. Dunia imeendesha mambo yake
kwa kadiri ya zinavyosema sheria zake na mfumo wake
kwa takriban kipindi cha miaka elfu sita na zaidi sasa. Wangeweza kuipunguza
dunia hali isiyoweza kukalika na kumilikiwa na kubakia
kuwa jangwa, lakini kamwe hawaoni umuhimu wa kufanya toba na kumpa Mungu
utukufu na kuzishika amri zake. Wanalitumia jina lake pasipo maana kwa kujiwekea mfumo au utaratibu mbovu wa utawala (cf.
Walawi 24:16).
Mungu hafanyi mchezo au
masihara, bali anamaanisha kile anachokisema. Dunia na jumuia zake patakuwa ni mahala salama iwapo tu
Maasi ya Kora kwenye kitabu cha Hesabu 16 kunatuonyesha jinsi ambavyo Mungu hataendela tu kuwa mvumilivu milele kwa wale wanaompinga na kumkufuru.
Hesabu 16:31-33 inasema: Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa
chini
Tunaona hapa kwamba jina la Mungu na la mtikwa mafuta wake walikuwa wananenewa maneno mabaya.
Mungu aliutumia mfano wake kuwafutilia mbali wale waasi ili
iwe ni mfano wa wengine wote watakaokuwa wanamkufuru Mungu. Kukufuru ni zaidi ya kulitumia jina la Mungu na kulitumia kwa mambo
yasiyopaswa, au kulidhalilisha au kulitumia
Nabii Yeremia alichukiwa na manabii wa Anathothi ambao walikuwa ni watu wanaotoka mahali alipotoka yeye pia. Kwa ujumla twaweza kusema kwamba ghasia zilifanyika kwenye nchi chini ya mfumo wake wa kimaongozi. Na katika siku za mwisho mfumo wa kikahaba wa kidini utakuwa imejiharibia wadhifa wake, na mahala pake na mfumo wa kidunia wa mnyama utamgeukia mwanamke huyu kahaba na kumuangamiza. Kwa kuwa mwanamke huyu kahaba amelitumia jina la Mungu Aliye Hai vibaya na kuliondolea heshima yake lililokuwa nayo (sawa na inavyosema Ufunuo 17:16).
Mtume Paulo na Torati
Mtume Paulo aliletwa mbele ya Kuhani Mkuu. Tendo hili linatupa fundisho la muhimu.
Matendo 23:1-5 inasema: Paulo akawakazia macho watu wa baraza, akasema, Ndugu zangu, mimi kwa dhamiri
Je, ni
Shera gani hiyo iliyoandikwa kutomnenea mabaya liwali au mkuu wa watu ama
kiongozi? (Ni kwenye Kutoka 22:28).
Mtume Paulo aliijua
sheria hii. Alifundishwa torati akiwa Farisayo na
Gemalieli (soma Matendo 5:34).
Matendo 22:3 Mimi ni mtu
wa Kiyahudi, nalizaliwa Tarso, mji wa Kilikia, ila nililelewa katika mji huu,
miguuni pa Gamalieli, nikafundishwa sheria ya baba zetu kwa usahihi, nikawa mtu
wa jitihadi kwa Mungu kama ninyi nyote mlivyo leo hivi;
Mtume Paulo hakuwa Myahudi, kwa
kweli yeye alikuwa ni Mbenyamini (Warumi 11:1) wa kabila la Benyamini na sio
Yuda, lakini neno Myahudi linalotumika
hapa lina maana ya kijeneriki zaidi ya kabila. Musa pia hakuwa Myahudi, bali anakuwa na uhusiano na kabila la Lawi. Kuhani Mkuu pia
alikuwa ni Mlawi na pia hakuwa Myahudi, na wala hakuwa kiongozi wa kabila la
Yuda na Benyamini, na pia kwa kabila ya Lawi, na hata hivyo, maongozi ya Kuhani
Mkuu aliyekuwa wa kabila la Lawi hayakuweza kabisa kufanywa baada ya
kuangamizwa ka Hekalu na kutawanyika kwao.
Mtume Paulo alijua
kile alichokuwa amekifanya na mara tu baada ya
kuligundua kuwa amemnenea mabaya Kuhani Mkuu Anasi, na kwamba amemnenea vibaya mkuu wa watu
au mtu aliyepewa mamlaka na Mungu, tendo ambalo limekatazwa kwenye torati
(Kutoka 22:28).
Hatimaye Mtume
Paulo analiandikia Kanisa la Rumi, kwenye Warumi 13:1a
akisema: “Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu” au
Warumi 13:1-2 Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. 2 Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu.
Makatazo ya Mungu ni Amri za Mungu zilizoandikwa kwenye kitabu cha Kutoka 22:28.
Amri hii ni ngumu
Kujifunga kwa kiapo
Mithali 19:28 inasema: Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki
hukumu, Na vinywa vya wasio haki humeza uovu.
“Msingi wa kile kinachoitwa utaratibu wa kisheria unahusisha kile kinachoitwa mabishano ya kienyeji ni kitu kilicho wazi sana kwenye amri hii ya tatu na ingeweza kuchukuliwa kama mjadala kuhusu uhalifu.”
[Hii ni kwa mujubu wa Ingram, kwenye kitabu chake cha Ulimwengu Chini ya Torati ya Mungu, ukurasa wa 46 (World Under God’s Law, page 46)].
Kiapo cha kuingia kwenye wadhifa,
kiitwacho kama ushuhuda wa uaminifu, au ithibitisho katika jamii ni neno
lililozoeleka kwenye jamii likijulikana kama kiapo cha uaminifu na utii na
ukweli, na mfumo wake mzima uliotuama kwenye aina yoyote ya maneno na sio
matendo ya maelekezo yaliyo kwenye dhana ya usafi au ukweli unaotokana na viapo
(au uthibitisho ambao kiapo kinapo
kinaonekana kama tendo hili la kula kiapo linapingana na maelekezo ya Kristo).
Mahali pasipo na kikomo au kanuni za ukweli mahali
ambapo mtu anaweza kuiona kama kiapo ambacho hakikusudii kutuama kwenye maneno
Kwenye miaka ya mwanzoni, kiapo cha Ufalme
au cha ofisi ya Urais (na kila kiapo cha kuchukua wadhifa
ofisini) vilichukuliwa kabisa kwamba vilikuwa vinatokana na amri hii ya tatu na
kwa kweli ilikuwa inaivunja. Kwa kula kiapo mtu aliahidi kuiheshimu kwa neno
Tendo la kudharau kiapo lilichukuliwa kama machukizo makuu sana katika siku za kale. Na ili mtu ashuhudie kiapo kile kwa sababu njema au mbaya mahali popote na ili kusichukuliwe hatua, kulihtajika itilewa sadaka ya upatanisho (Walawi 5:4-7). Kiapo cha uwongo kilikuwa ni kosa na machukizo (assault) kwa maisha ya jamii nzima husika. Umuhimu wa kuchukia kiapo cha uwongo umeelezwa kwenye Zaburi 109.
Zaburi 109:17-18 inasema: Naye alipenda kulaani,
nako kukampata. Hakupendezwa na kubariki, kukawa mbali naye, 18 Alijivika laana kana kwamba ni vazi lake.
Ikamwingilia moyoni kama maji, Na kama mafuta mifupani mwake.
Kutoka 23:1 inasema: Usivumishe habari za
uongo; usitie mkono wako pamoja na mwovu, kuwa shahidi
wa udhalimu.
Namna
sahihi ya kula kiapo imeelekezwa kwenye kitabu chaKutoka 22
Kutoka 22:10-11 inasema: Mtu akimpa mwenziwe punda, au ng'ombe,
au kondoo, au mnyama ye yote, ili amtunzie; yule
mnyama akafa, au akaumia, au akachukuliwa mtu asione; 11 patakuwa
na kiapo cha Bwana katikati ya watu hao wawili, kwamba alipeleka mkono wake
kutwaa
Maana ya neno kukitunza iliyoandikwa kwenye aya ya 10 ni kule kinakojulikana kama kukitunza kiusalama wakati jirani anapokuwa ameondoka. Mchakato mzima wa kula kiapo unatakiwa kuandaliwa ili kiapo kifanyike ili kufikia ufumuzi kwa jamo linalobishaniwa kati ya watwawili, wakati kwamba neno linalobishaniwa hakuna aliyeliona.
Zekaria 8:16-17 inasema: Haya ndiyo mtakayoyatenda; kila mtu na aseme kweli na jirani yake; hukumuni kweli na hukumu ya
amani malangoni mwenu; 17 wala mtu wa kwenu
asiwaze mabaya moyoni mwake juu ya jirani yake; wala msipende kiapo cha
uongo; maana hayo yote ndiyo niyachukiayo, asema Bwana.
Kutokula kiapo kabisa
Je, Yesu Kristo alikuwa na maana gani kwenye mahubiri yake ya Mlimani alipowaambia wanafunzi wake, “Swear not at all”? na kwa vile alikuwa ndio kwanza tu anawaambia kuwa yeye hakuja kuitangua torati. Je, kwa kusema hivi alikuwa anabadili sehemu ya torati hii hapa?
Mathayo 5:34-37 inasema: lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu; 35 wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu. 36 Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37 Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu
Maneno yaliyotumika kwenye tafsiri ya Mfalme Yakobo (KJV) yanasema “Usiape kabisa” sio tafsiri nzuri kutoka kwenye tafsiri halisi ya kiyunani.
Tafsiri
ya Agano Jipya iitwayo The Concordant Literal New Testament inaelezea
kile alichokikusudia Yesu Kristo, na kuelezea kwa
uwazi zaidi kwa kuandika
Mathayo 5:33-37 Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako; 34 lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu; 35 wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu. 36 Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 37 Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.
Kuna aina mbili katika aya hizi, sehemu ya
kwanza inaithibitishba sheria ya kiapo, na sehemu ya
pili inakataza kuapa kwa sababu zisizo na umuhimu (a
frivolous manner) au kula kiapo kwa hali ya mzaha. Sisi
sote tumewasikia watu wakisema kwamba “Waseme kweli.” Je,
hii inamaana kuwa walikuwa hawasemi kweli hapo kabla? Au wanajaribu
kutilia mkazo kwa kusema “Mama yangu na awe kipofu
iwapo
Jamii katika siku za Kristo walikuwa wanatumia
ardhi, Yerusalemu au vichwa vyao ili kujaribu kutilia
mkazo kwenye maneno yao. Na ndivyo ilivyo hata watu wengi leo,
wanatumia maneno ya laana ili kutilia mkazo mambo
Viongozi haohao
wa kanisa wamewafundisha watu kuwa wasiape wanapokuwa mahakamani wakiyachukulia maneno haya, “msiape kabisa” all”. Hii ni tafsiri potofu ya maneno haya. Hata hivyo, mtume Paulo
alipopelekwa mahakamani aliapa na ilikuwa sahihi
kufanya hivyo.
Ruthu alilitumia jina la
Mungu katika kujitangaza wakati alipojitoa kwa Naomi.
Ruthu 1:16-17 Naye Ruthu akasema,
Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na
wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu
wangu; 17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo
hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga
wewe nami.
Sahihi, na kwa
mfano hii tunapaswa hata sisi kufanya vivyohivyo.
Mambo saba
anayoyachukia Mungu
Mithali 6:16-19 inasema: Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana; Naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. 17 Macho
ya kiburi, ulimi wa uongo, Na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; 18 Moyo uwazao mawazo mabaya; Miguu iliyo
myepesi kukimbilia maovu; 19 Shahidi wa
uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.
Mambo ya Walawi 5:1 inasema: Na mtu awaye yote akifanya
dhambi, kwa kuwa ameisikia sauti yenye kuapisha, naye
akawa ni shahidi, kwamba aliona au kujua, asipolifunua neno lile, ndipo
atakapochukua uovu wake mwenyewe;
Mambo ya Walawi 5:4-5 inasema: au, kama mtu akijiapisha, kwa
kutamka haraka kwa midomo yake, kutenda uovu, au kutenda mema, neno lo lote mtu
atakalolitamka kwa kiapo pasipo kufikiri, na neno hilo likamfichamania; hapo
atakapolijua, ndipo atakapokuwa na hatia katika mambo hayo mojawapo; 5 kisha itakuwa, hapo atakapokuwa na hatia katika mambo
hayo mojawapo, ndipo utakapoliungama jambo hilo alilolikosa;
Jambo jema la kulifanya
Mambo ya Walawi 5:6-13 inasema: naye atamletea Bwana sadaka yake ya hatia kwa ajili ya hiyo dhambi yake aliyoifanya, mwana-kondoo wa kike, au mbuzi mke, kutoka katika kundi lake, kuwa ni sadaka ya dhambi; kisha kuhani atamfanyia upatanisho kwa ajili ya hiyo dhambi yake. 7 Lakini asipomweza mwana-kondoo, ndipo atakapomletea Bwana hua wawili, au makinda mawili ya njiwa, kuwa ni sadaka yake ya hatia ya jambo hilo alilolikosa; mmoja wa hao ndege kwa sadaka ya dhambi, na wa pili kwa sadaka ya kuteketezwa. 8 Naye atawaleta kwa kuhani, atakayemsongeza kwanza yule wa sadaka ya dhambi, naye atamkongonyoa kichwa shingoni mwake, lakini asimpasue vipande viwili; 9 kisha baadhi ya damu ya hiyo sadaka ya dhambi atainyunyiza katika ubavu wa madhabahu; na damu iliyosalia itachuruzishwa hapo chini ya madhabahu; ni sadaka ya dhambi. 10 Kisha huyo ndege wa pili atamsongeza kuwa sadaka ya kuteketezwa, sawasawa na sheria; na kuhani atamfanyia upatanisho kwa ajili ya hiyo dhambi yake aliyoifanya, naye atasamehewa. 11 Lakini asipowaweza hua wawili, au makinda mawili ya njiwa, ndipo hapo atakapoleta matoleo yake kwa ajili ya neno hilo alilolikosa, sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba, kuwa sadaka yake ya dhambi; asitie mafuta juu yake, wala ubani usitiwe juu yake; maana, ni sadaka ya dhambi. 12 Naye atamletea kuhani, na kuhani atatwaa konzi yake ya huo unga kuwa ukumbusho wake, na kuuteketeza juu ya madhabahu, juu ya sadaka zilizosongezwa kwa Bwana kwa njia ya moto; ni sadaka ya dhambi. 13 Na huyo kuhani atamfanyia upatanisho kwa ajili ya dhambi yake ambayo katika mambo hayo mojawapo amefanya dhambi, naye atasamehewa; na unga uliosalia utakuwa wa kuhani, kama hiyo sadaka ya unga ilivyokuwa.
Tendo la kuvunja amri
zilizo kwenye Torati na huku ukizijua sio jambo
linaloweza kusamaheka, sawa na tendo la kutomtimizia Bwana nyapo zako
ulizoziweka kwa Mungu, pia hakuna udhuru utakaokubalika kumsamehe mtu wa namna
hii.
Kumbukumbu la Torati 23:21-23 inasema: Utakapoweka nadhiri kwa Bwana, Mungu wako, usiwe mlegevu katika kuiondoa; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, hataacha kuitaka kwako; nayo hivi itakuwa dhambi kwako. 22 Lakini ukijizuia usiweke nadhiri, haitakuwa dhambi kwako. 23 Yaliyotoka midomoni mwako yashike kuyafanya; kwa mfano wa ulivyomwekea nadhiri Bwana, Mungu wako, ni sadaka ya hiari uliyoahidi kwa kinywa chako.
Kuna sheria na maelekezo yaliyowekwa kuhusu familia na mkuu wa familia
kuhusu ulaji wa kiapo
Hesabu 30:1-16 inasema: Kisha Musa akanena na wale
vichwa vya kabila za wana wa Israeli, na kuwaambia, Neno hili ndilo
aliloliagiza Bwana. 2 Mtu atakapomwekea Bwana nadhiri,
au, atakapoapa kiapo ili kufunga nafsi yake kwa kifungo, asilitangue neno lake;
atafanya sawasawa na hayo yote yamtokayo kinywani mwake. 3 Tena
mtu mke atakapomwekea Bwana nadhiri, na kufunga nafsi yake kwa kifungo, naye
aketi katika nyumba ya babaye, katika ujana wake; 4 babaye
naye akasikia nadhiri yake, na kile kifungo chake alichofungia nafsi yake, na
babaye akamnyamazia; ndipo nadhiri zake zote zitathibitika, na kila kifungo
alichofungia nafsi yake kitathibitika. 5 Lakini kama
huyo babaye akimkataza siku hiyo aliyosikia; nadhiri zake ziwazo zote, wala
vifungo vyake alivyoifungia nafsi yake havitathibitika; na Bwana atamsamehe,
kwa kuwa babaye alimkataza. 6 Tena kama amekwisha
kuolewa na mume, wakati huo wa nadhiri zake, au wa neno hilo alilolitamka kwa
midomo yake pasipo kufikiri, alilojifungia; 7 na
mumewe akasikia, naye akamnyamazia siku hiyo aliyosikia neno hilo; ndipo
nadhiri zake zitathibitika, na vile vifungo ambavyo ameifunga nafsi yake
vitathibitika. 8 Lakini kama mumewe akimkataza siku
hiyo aliyolisikia; ndipo ataitangua nadhiri yake iliyo juu yake na neno
alilolitamka kwa midomo yake pasipo kufikiri, alilojifungia; na Bwana
atamsamehe 9 Lakini nadhiri ya mjane, au ya mwanamke
aliyeachishwa mume, kila neno ambalo ameifunga nafsi yake kwalo, litathibitika
juu yake. 10 Tena kama aliweka nadhiri nyumbani mwa
mumewe, au kama aliifunga nafsi yake kwa kifungo pamoja na kiapo, 11 na mumewe alisikia akamnyamazia, wala hakumkataza; ndipo
nadhiri zake zote zitathibitika, na kila kifungo alichojifungia kitathibitika. 12 Lakini kama mumewe alizibatilisha na kuzitangua siku hiyo
aliyozisikia, ndipo kila neno lililotoka midomoni mwake katika hizo nadhiri
zake, au katika kile kifungo cha nafsi yake, halitathibitika; huyo mumewe
amezitangua; na Bwana atamsamehe. 13 Kila nadhiri, na
kila kiapo kifungacho, ili kuitaabisha nafsi ya mwanamke mumewe aweza
kuthibitisha, au mumewe aweza kutangua. 14 Lakini
mumewe akimnyamazia mkewe kabisa siku hata siku ndipo azithibitisha nadhiri
zote za mkewe, au vifungo vyake vyote vilivyo juu yake; yeye amezithibitisha,
kwa kuwa alimnyamazia mkewe siku hiyo aliyozisikia nadhiri zake. 15 Lakini akizibatilisha na kuzitangua baada ya kuzisikia;
ndipo yeye atachukua uovu wa mkewe. 16 Hizi ndizo
amri, ambazo Bwana alimwagiza Musa, kati ya mtu mume na mkewe, kati ya baba na
binti yake, katika ujana wake, ali nyumbani mwa babaye.
Utakatifu wa Sadaka au Dhabihu
Mambo ya Walawi 22:1-33 inasema: Kisha Bwana akanena na Musa, na
kumwambia, 2 Nena na Haruni na wanawe, ili wajitenge
wenyewe na vitu vitakatifu vya wana wa Israeli ambavyo wanitakasia mimi, tena
kwamba wasilinajisi jina langu takatifu; mimi ndimi Bwana. 3 Waambie,
Mtu ye yote wa kizazi chenu chote katika vizazi vyenu, atakayevikaribia vile
vitu vitakatifu, ambavyo wana wa Israeli wamtakasia Bwana, naye ana unajisi,
mtu huyo atakatiliwa mbali asiwe mbele zangu; mimi ndimi Bwana. 4 Mtu ye yote wa kizazi cha Haruni aliye mwenye ukoma, au
mwenye kisonono; yeye asile katika vitu vitakatifu, hata atakapokuwa safi. Tena
mtu awaye yote atakayekinusa kitu kilicho na unajisi kwa sababu ya wafu, au mtu
ambaye shahawa humtoka; 5 au mtu amgusaye mnyama
atambaaye, wa kumpatia unajisi, au kwamba amgusa mtu wa kumpatia unajisi, kwa
unajisi wo wote alio nao; 6 huyo mtu atakayegusa kitu
cho chote namna hiyo atakuwa najisi hata jioni, naye hatakula katika vitu
vitakatifu, asipooga mwili wake majini. 7 Jua likiisha
kuchwa atakuwa safi; kisha baadaye atakula katika vitu vitakatifu, maana ni
chakula chake. 8 Nyamafu au mnyama aliyeraruliwa na
wanyama asile, asijitie unajisi kwa hiyo nyama; mimi ndimi Bwana. 9 Basi kwa hiyo watayashika mausia yangu, wasije wakachukua
dhambi kwa hayo, nao wakafa humo, wakiyanajisi; mimi ndimi Bwana niwatakasaye. 10 Mgeni awaye yote asile katika kitu kitakatifu; mgeni wa
kuhani akaaye kwake, au mtumishi aliyeajiriwa, asile katika kitu kitakatifu. 11 Lakini kwamba kuhani akinunua mtu ye yote, kwa kumnunua
kwa fedha zake, yeye atakula katika hicho; na hao waliozaliwa nyumbani mwake
watakula katika chakula chake. 12 Na binti ya kuhani
kwamba ameolewa na mgeni, asile katika sadaka ya kuinuliwa katika vitu vile
vitakatifu. 13 Lakini kwamba binti ya kuhani ni mjane,
au kwamba ameachwa na mumewe, wala hana mtoto, kisha amerudi na kuketi katika
nyumba ya baba yake, kama vile katika ujana wake, yeye atakula katika chakula
cha baba yake; lakini mgeni awaye yote asile katika chakula hicho. 14 Tena kama mtu ye yote akila katika kitu kilicho
kitakatifu pasipo kukijua, ndipo ataongeza sehemu ya tano juu ya kitu hicho, na
kumpa kuhani kitu hicho kitakatifu. 15 Wala wasivinajisi
vitu vitakatifu vya wana wa Israeli, wavisongezavyo kwa Bwana; 16 hata wakawatwika ule uovu uletao hatia, hapo walapo vitu
vyao vitakatifu; kwa kuwa mimi ndimi Bwana niwatakasaye. 17 Kisha
Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 18 Nena na Haruni
na wanawe, na wana wa israeli wote, uwaambie, Mtu ye yote wa nyumba ya Israeli,
au wa wageni walio katika Israeli, atakayetoa matoleo yake, kama ni nadhiri zao
mojawapo, au kama ni sadaka yo yote ya hiari, watakayomtolea Bwana kuwa sadaka
ya kuteketezwa; 19 ili mpate kukubaliwa, mtaleta mume
mkamilifu, katika ng'ombe, au katika kondoo, au katika mbuzi. 20 Lakini mnyama ye yote aliye na kilema msimtoe; kwa kuwa
hatakubaliwa kwa ajili yenu. 21 Na mtu awaye yote
atakayemtolea Bwana dhabihu katika sadaka za amani, ili kuondoa nadhiri, au
sadaka ya moyo wa kupenda, katika ng'ombe, au katika kondoo, atakuwa mkamilifu,
apate kukubaliwa; pasiwe na kilema ndani yake cho chote. 22 Kipofu,
au aliyevunjika mahali, au kiwete au aliye na vidonda, au aliye na upele, au
aliye na kikoko, hamtamtolea Bwana wanyama hao, wala msiwasongeze kwa Bwana kwa
njia ya moto juu ya madhabahu. 23 Ng'ombe, au
mwana-kondoo aliye na kitu kilichozidi, au aliyepungukiwa na kitu katika vitu
vya mwilini mwake, mna ruhusa kutoa kuwa sadaka ya moyo wa kupenda; lakini kwa
ajili ya nadhiri hatakubaliwa. 24 Mnyama aliyeumia
mapumbu yake, au kusetwa, au kuvunjwa, au kukatwa, msimtolee Bwana; wala
msifanye hivi katika nchi yenu. 25 Wala msisongeze
chakula cha Mungu wenu katika wanyama hao mmojawapo kitokacho mkononi mwa
mgeni; kwa sababu uharibifu wao u ndani yao, wana kilema ndani yao;
hawatakubaliwa kwa ajili yenu. 26 Kisha Bwana akanena
na Musa, na kumwambia, 27 Hapo ng'ombe, au kondoo, au
mbuzi, akizaliwa, atakuwa pamoja na mamaye muda wa siku saba; na siku ya nane
na baadaye atakubaliwa kuwa ni sadaka ya kutolewa kwa Bwana kwa njia ya moto. 28 Tena kama ni ng'ombe, au kama ni kondoo, msimchinje huyo
na mwanawe wote wawili kwa siku moja. 29 Tena
mtakapomchinjia Bwana dhabihu ya shukrani, mtamchinja ili mpate kukubaliwa. 30 Italiwa siku iyo hiyo; msisaze kitu chake hata asubuhi;
mimi ndimi Bwana. 31 Kwa hiyo mtayashika maagizo
yangu, na kuyafanya; mimi ndimi Bwana. 32 Wala
msilinajisi jina langu takatifu; lakini nitatakaswa mimi katika wana wa
Israeli; mimi ndimi Bwana niwatakasaye ninyi, 33 niliyewaleta
mtoke nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu; mimi ndimi Bwana.
Sadaka zote ni takatifu kwa Bwana, na sadaka kuinajisi sadaka ni tendo
lile la kulitaja jina la Mungu bure. Na hiki ndicha hasa chanzo zha malalamiko:
Mungu anawaambia watu wake kwamba wanadai kuwa meza yake imenajisika, kwa kuwa sisi tu wenyedhambi na ni watu tuliokombolewa na
Mungu tukiwa
Matumizi ya Ulimi
Mtazamo wa
amri hii ya tatu unatuama kwenye kile tunachokisema. Maneno
yetu yanadhihirisha kile tunachokifikiria au tunachowaza, wakati kwamba mawazo
yetu huongoza matendo yetu. Kanuni hii imetolewa na
Kristo kwenye Injili ya Luka 6:43-45.
Luka 6:43-45 inasema: Kwa maana hakuna mti mzuri uzaao
matunda mabaya, wala mti mbaya uzaao matunda mazuri; 44 kwa
kuwa kila mti hutambulikana kwa matunda yake; maana, katika miiba hawachumi
tini, wala katika michongoma hawachumi zabibu. 45 Mtu
mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika
hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena
yale yaujazayo moyo wake.
Mtume Paulo anauelezea moyo
mbaya uli ndani ya mwanadamu kwa wapagani waliokuwa
huko Rumi. Anaionyesha matendo yatokanayo na asili ya
mwili wa mwanadamu aliyeamua kujitenga na kuwa kinyume na Mungu.
Warumi 3:10-18 inasema:
Aya hizi zinawaelezea wale
wasiozitii na kuzipenda Amri na Sheria za Mungu.
Ndugu wa karibu sana wa Kristo
aliyeitwa Yakobo na mchungaji wa Kanisa la Yerusalemu na ambaye ndiye alikuwa
msemaji wa makao makuu ya kanisa kama alivyoandikwa kwenye kitabu cha Matendo
ya Mitume 15, alikuwa pia na mengi sana ya kuongea kuhusu matumizi ya ulimi.
Yakobo 1:26 inasema: Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai
Yakobo 2:5-7 inasema: Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao? 6 Bali ninyi mmemvunjia heshima maskini. Je! Matajiri hawawaonei ninyi na kuwavuta mbele ya viti vya hukumu? 7 Hawalitukani jina lile zuri mliloitwa?
Yakobo 3:5-9 inasema: Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana. 6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum. 7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu. 8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti. 9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.
Yakobo 4:11-12 inasema: Ndugu, msisingiziane; amsingiziaye ndugu yake, au kumhukumu ndugu yake, huisingizia sheria na kuihukumu sheria. Lakini ukiihukumu sheria, huwi mtenda sheria, bali umekuwa hakimu. 12 Mtoa sheria na mwenye kuhukumu ni mmoja tu, ndiye awezaye kuokoa na kuangamiza. U nani wewe umhukumuye mtu mwingine?
1Petro 3:10 inasema: Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.
Tunayaona Maandiko haya
Matakatifu yakisema kwamba Mungu anawataka watumishi wake wa
kweli wawe na ulimi
Maombi
Kumuomba Mungu kwa namna iliyo sahihi kulijulikana tangia siku za kale za
kwanza. Hata hivyo maombi yalitumika pia
Isaya 1:15 inasema: Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia;
Unabii wa Uwongo
Mungu alitumia unabii na manabii ili kuwaonya watu kwa ajili ya matukio yanayokuja
mbele
Unabii wa
uwongo umekuwa ni mtego wa kila mara kwa watu wa Mungu. Tukio la Mfalme Balaki wa Moabu la kumuomba Balaamu awalaani kwa laana Israeli kwenye
kitabu cha Hesabu sura ya 22 linaonyesha jinsi Mungu anavyowaona hawa manabii
wa uwongo. Ilimlazimu Mungu amtumie punda ili aongee
na Balaamu
Ulimwengu wa
Wakristo wanaojiita wenye Itikadi Kali au ya Kiorthodoxi umegubikwa na mafundisho
waliyotungwa na wanadamu na ambayo yanapingana na kuivunja mari hii ya tatu na
kuzipinga Sheria na Torati ya Mungu. Tendo lao la kumuomba mtu aliyebandikwa
jina la Mariamu mama wa Mungu na kumfanyiza Kristo bandia na wa uwongo ni jambo
lenye ibatili mkubwa—na mtindi wao wa maombi ya kurudia rudia ni ubatili
mkubwa. Matumizi ya vishada vya shanga vyenye mzunguko-duara kufanyia maombi
yote ni ubatili mkubwa pia na imekatazwa na Biblia
(Mathayo 6:7). Tendo la kukusanyika maelfu ya watu mahali pamoja kwenye viwanja
vya mpira na kuwahubiria ili eti wamkubali na kumpokea
Kristo ni ubatili mkubwa pia—hii ni kulitumia jina la Mungu Aliye hai bure.
Kuna jambo moja pia ambalo
tunapaswa kulijua nalo ni kwamba; nyimbo nyingi
zilizotungwa hivi karibuni na ambazo zinaonekana au kujulikana kuwa ni za
kisasa.na kutumika kanisani wakati wa ibada, na hususani zile za mtindo wa
“Mimi kama nilivyo” au “Mniache
Mahubiri
yanayofanywa siku za Jumapili asubuhi nayayoitwa “mahubiri ya kumhubiri Yesu”
yanalenga jambo hilihili moja la kulitumia jina la Bwana bure. Yesu Kristo wa ukweli wa Agano Jipya anasema kwenye Mathayo 15:9 na Marko
7:7 hivi:
Nao
waniabudu (Kwa Kiyunani-adore) bure,
Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu,
Namna yote ya kile wanachokiita
Muziki wa Injili pamoja na ujumbe wake wanaokazia
kuutoa wa “Yatoe maisha na moyo wako kwa Bwana” na mafundisho
Kusimama Kinyume na Torati
Kuna watu ambao wamediriki
hata kulaumu wakiwema kwamba utaratibu wa Amri Kumi
zilizoandikwa kwenye Torati unajipinga wenyewe na maneno yanayosema (Usifanye
hivi na vile…” Usemi huu umetumika mara kumi kwenye Kutoka 20 na mara kumi tena kwenye Kumbukumbu la Tirati 5. Lakini vipengele vya amri hizi kumi zinaendana pamoja kwenye
utekelezaji wake. Amri hizi Kumi zinapaswa kuheshimiwa, na zina umuhimu wake fulani kwenye jamii kwa mtazamo wa watu
wengi au kwa kila mmoja binafsi yake.
Sheria hizi za Torati
zinapokuwa zinatunwa hunfanya mtu awe mtii na
mnyenyekevu na mwenye kujitoa kwa Mungu. Zinamfanya mtu aendeleze tabia yake ya
utii kutoka ndani, na zinamfundisha mtu namna ya
kujitawala na kuyatii mamlaka. Mwanadamu anapokuwa anamudu kujifunza kuitawala roho
au moyo wake, ndipo ile hali ya kutojali na kuzivunja
sheria na amri zake Mungu hutoweka. Moyo wa mwanadamu
unapaswa uongoke na ubadilike, vinginevyo matendo yote ya mwanadamu huwa ni
ujinga mtupu.
Zaburi 14:1; 53:1a inasema: Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu;
Mithali 14:7 inasema:
Toka mbele ya uso wa mpumbavu, Maana hutaona kwake midomo ya maarifa.
Mithali 17:12
inasema: Afadhali
mtu akutwe na dubu aliyenyang'anywa watoto wake,
Kuliko na mpumbavu katika upumbavu wake.
Mithali 18:6 inasema: Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina, Na kinywa chake huita mapigo.
Mithali 13:20
inasema: Enenda
pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima;
Sheria na Torati ya Mungu imejaa hekima na mtu akiitii inampa mtu
uelewa. Mtu anapoitendea kazi inaleta majibu mema na
mtu anapoiasi kutoa matokeo mabaya.
Sheria ya Mungu hutoa majibu na suluhu ya hali ya mwanadamu kushindwa kujitawala mwenyewe
na kuitawala sayari hii, na amri hii ya tatu ni sehemu kuu na muhimu ya kutawla
huko. Mungu kwa hekima yake ametufunulia Sheria yake. Mwanadamu
anapaswa kujifunza mumcha Mungu na kuzitii Amri zake. (Pia
soma Kutoka 20:10; Kumbukumbu la Torati 5:14; Mithali 1:32; 14:7; 17:12; 10:23;
18:6; 29:11; 13:20; 26:6.)
Haki na
hukumu ya haki
Mfano wa maamuzi ya hukumu ya kifo kwa mwenye kukufuru unapatikana kwenye kitabu cha Mambo ya Walawi 24:10-16.
Mambo ya Walawi 24:10-16 inasema: Ikawa mwana wa mwanamke wa
Kiisraeli, ambaye babaye alikuwa Mmisri, akatokea kati ya wana wa Israeli; na
huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli, na Mwisraeli mmoja, wakapigana pamoja
ndani ya marago; 11 kisha huyo mwana wa mwanamke wa Kiisraeli
akalikufuru hilo Jina, na kuapiza; nao wakamleta kwa Musa. Na jina la mamaye
alikuwa akiitwa Shelomithi, binti ya Dibri, wa kabila ya Dani. 12 Nao wakamtia kifungoni, ili wapate kuambiwa neno
litakalotoka kinywani pa Bwana. 13 Na Bwana akasema na
Musa, na kumwambia, 14 Mtoe huyo aliyeapiza
nje ya marago; na wale wote waliomsikia na waweke mikono yao kichwani mwake,
kisha mkutano wote na wamwue kwa kumpiga kwa mawe. 15 Nawe
nena na wana wa Israeli na kuwaambia, Mtu awaye yote atakayemlaani Mungu wake
atachukua dhambi yake. 16 Na yeye
atakayelikufuru jina la Bwana hakika atauawa; mkutano wote watamwua kwa kumpiga
kwa mawe; kama ni mgeni, kama ni mzalia, hapo atakapolikufuru jina la Bwana
atauawa.
Kitu cha msingi kuhusu aya hii ni kwamba ni Yesu Kristo ndiye alikuwa na hawa Israeli kule Jangwani. Kristo mwenyewe amesema kwamba wala hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu, wala aliyewahi kuisikia sauti yake. Kwa hiyo, ni Kristo ndiye aliyeiweka hukumu hii kupitia kwa Musa, nah ii inaonyesha jinsi Kristo alivyofikiri jinsi ilivyopaswa kusimamiwa.
Musa aliichukulia hukumu hii kama alivyoelekezwa kule jangwani na mtu tunayemdhania au
kumjua kuwa ni Masihi, akiwa
Mambo ya Walawi 24:23 inasema: Musa akanena na wana wa Israeli, nao wakamtoa huyo aliyeapiza nje ya
marago, wakamwua kwa kumpiga kwa mawe. Wana wa Israeli wakafanya kama Bwana
alivyomwagiza Musa.
Iwapo kama huyu Malaika wa Kuwepo kwake alikuwa ni Yesu Kristo,
kwa hiyo amri hii ilisimama imara bila kuzibadilishwa au kuzivunjwa na
kuziathiri zile kumi nyingine zote, ikiwemo nah ii ya Sabato nay a Sikukuu
Takatifu zilizoamriwa, zote zimebakia imara na pasipo kuathiriwa. Kwa ajili hii
ndipo makanisa ya Waamini Imani ya Utatu wa nyakati za Zama za Kati walifanya kuwa
ni tendo la kukufuru kama mtu atasema kuwa Kristo ndiye aliyekuwa na wana wa
Israeli pale jangwani, akiwa kama Malaika wa Yahova au Mjumbe wa Mshauri Mkuu
wa Ajabu aliyetajwa kwenye Isaya 9:6 (LXX). Na ndipo Waamini Utatu hawa wakayatumia
mamlaka ya Mungu na kulitumia jina
Kulaani na kuabudu
Kutoka 21:17 inaonyesha hukumu itokanayo na mtu anayediriki kumlaani baba yake au mama yake. Umuhimu wa kumlaani mtu aliyefanya matendo ya kuliasi taifa umetokana na maandiko ya torati. Hakuna namna yoyote ya kulaani au mashitaka yanayoweza kufanywa pasipofuatwa utaratibu ulioko kwenye torati. Aina nyingine yoyote itakayofanyika itakiuka na kuivunja amri hii ya tatu, na nyingine nyingi ambazo zinaangukia kwenye mambo ya kisheria.
Tendo la Kumtangaza
Mungu na Ibada
Mungu anapoapa kwa nafsi yake mwenyewe, kiapo kile ni lazima kibakia
Isaya 45:23 inasema: Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.
Hapa Mungu anatangaza kwamba
historia ndiyo itakayohitimisha na kuweka kikomo cha
kumuabudu yeye, na kiapo cha kimungu kitakuwa ni msingi wa kila jamii na kila
kabila.
Mika 6:8 inasema: Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!
Yakobo 5:12 inasema: Lakini zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, wala kwa mbingu wala kwa nchi; wala kwa kiapo kinginecho chote; bali ndiyo yenu na iwe ndiyo, na siyo yenu iwe siyo, msije mkaangukia hukumu.
Neno la Mungu
halitarudi bure, na wala jina
Kwenye kila kizazi Mungu amewalinda na kuwatunza wale wote wasioupigia magoti mfumo huu, na wakiwa wamemkubali na kubakia waminifu kwake (1Wafalme 19:18).
1Wafalme 19:18 inasema: Pamoja na
hayo nitajisazia katika Israeli watu elfu saba, kila goti lisilomwinamia Baali,
na kila kinywa kisichombusu.
Mungu amemchagua Yesu Kristo kuwa ni mtiwa mafuta wake na wote watampigia magoti kwa jina la Mungu.
Wafilipi 2:10 inasema:
Kile kinachatakiwa
kijulikane na Mungu ni kuonekana kwa wateule wanaofanya
kazi kwa jina lake. (Warumi 1:19-20). Katika Ufalme unaokuja wa
Mungu watu hawataliitia jina la Mungu kwa uwongo
q