Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[238]
Kuwaita Watu Waende
Yerusalemu
(Toleo La 1.1 19970920-19980214)
Agizo la sheria kuhusu
haki ya uzaliwa wa kwanza kwa makabila ya nyakati za mwisho ya Zabuloni na
Isakari linajumuisha amri muhimu sana kwao. Utambulisho wa makabila haya mawili
ni wa muhimu sana pia katika kuuelewa unabii.
Christian Churches of God
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1997, 1998 Christian
Churches of God (ed. Wade Cox))
(tr. 2015)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa
watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta
maneno. Jina
la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe
pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote
atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja
ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo
haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Kuwaita Watu
Waende Yerusalemu
Wengi wetu tunazoea kuyajua makabila ya wana wa Israeli. Ni jambo
linaloeleweka na watu wengi wa Uholanzi kwamba jamii ya Wadachi wanajulikana
kuwa ni wa uzao wa kabila la Zabuloni wa Wafriesiani ni wana wa Isakari. Jambo
hili limefanyiwa utafiti na wanazuoni wengi na uthibitisho wake ulioonekana
ndio unaokwenda kuongelewa hapa. Hatutakwenda kuonyesha utambulisho mwingine wa
Isakari ambao makabila ya Finland wala hatutayaongelea wala kuuelezea mfumo na
itikadi za Wajuti au Jutes, ambao aliishambulia Uingereza pamoja na Waanglo-Saxoni
na Wadenes. Hayo yatakwenda kuandikwa kwenye majarida yafuatayo yatakayojiri
kuelezea historian a vuguvugu za makabila.
Tunajumuishwa hapa na agizo la biblia na wana wa Zabuloni na wa Isakari.
Kwa kweli, tunayajua majukumu yao, sio tu kama watu bali pia majukumu yao
wakiwa kama Kanisa la Mungu na wakiwa kama wana wa Mungu kila mmoja wao, wakiwa
kama wanafunzi wa Yesu Kristo.
Mathayo 28:18-20 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. 19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; 20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Hili ni jukumu letu kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo
kwa kuwafundisha kuyafanya yote alichoamuru Yesu. Kwa hiyo tunatakiwa kujua
kila kitu ambacho Yesu Kristo alichotuamuru. Kwa hiyo ni kukizingira kile tunachokijua
kama sheria au Torati na utimilifu wa Sheria, ambayo kwa hiyo hata nukta moja
au nukta moja oeyote haitapita, hadi iwe imetimilika.
Yohana 10:34-36 Yesu
akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi
miungu? 35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa
na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka); 36 je! Yeye ambaye Baba alimtakasa,
akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni
Mwana wa Mungu?
Mathayo 5:17-18 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii;
la, sikuja kutangua, bali kutimiliza. 18 Kwa maana, amin,
nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya
torati haitaoondoka ,hata yote yatimie.
Kuna idadi kadhaa ya unabii ambao haujakamilika bado, au umekamilika kwa sehemu
tu, ukingojea kutimilika kwake kikamilifu. Hii pia ipo kwa baadhi ya ahadi za
haki ya uzaliwa wa kwanza zilizoahidiwa kwa baadhi ya makundi ya watu ambazo
bado hazijakamilika hadi sasa. Kwa kuwa Maandiko Matakatifu hayawezi kutanguka,
haki hizi za uzaliwa wa kwanza bado zinabidi zikumbushiwe, na ndipo zinaweza
kupatikana kisahihi. Ahadi ya haki ya uzaliwa wa kwanza imetolwa kwa makabila
yakiwa kama sehemu ya Israeli kwenye kitabu cha Mwanzo 48 na kadhalika. Yusufu
alibarikiwa kwa watoto wake wawili kwa haki hii ya uzaliwa wa kwanza kwenye
Mwanzo 48:1 na kadhalika, lakini kwenye Mwanzo 49 makabila yote yalibarikiwa.
Nyingi ya Baraka hizi hazikuweza kuanza wala kuonekana kwenye kipindi cha
utawala wa Israeli wala wa Yuda. Ni baadhi yake tu ndizo zilitimilika. Kwa
mfano, ahadi waliyopewa Yuda ilitimilika katika Kristo (Mwanzo 49:10) lakini
mkutaniko wa mwisho wa watu haujatimilika bado na ufalme haujatolewa bado kwa
Shilo.
Makabila ya Lawi na Simeoni yalitawanyika kila mahali
katika Israeli kwa kuwa walikuwa wakatili. Kimsingi, Zabuloni waliahidiwa haki
ya kuishi kwenye eneo la bandari ndogo ya bahari na kwenye mpaka na Sidoni.
Ndiposa, ilikuwa ni bandari kuu ya bahari na watu wanaona kwamba utimilifu wa
baadae ni sasa. Lakini nyingi zinakuja bado. Isakari ni punda hodari na mwenye
nguvu anayejiinamisha katikati ili abebe mizigo na waliyobakia wakimzuia dhidi
ya kuenea zaidi kwa haki yake ya uzawa.
Pia, ahadi walipewa kabila la Dani kwamba
atawahukumu watu wake akiwa kama moja yama kabila ya Iraeli nah ii
haijatimilika bado. Jambo hilo limechambuliwa kwenye majarida mengine yanayohusika
na Milenia na Marejesho mapya ya Masihi.
Kuna ahadi nyingine pia ya haki ya uzaliwa ya makabila ya Zabuloni na Isakari.
Utendekaji wa ahadi hii ya uzaliwa wa kwanza na utilikaji wake utakuwa n ya millennia.
Kwa hiyo, tunaona ahadi ya haki ya uzaliwa wa kwanza ikifanyika kama kituhimu
mkubwa sana kwa wateule kwenye maisha ya kila siku Kanisani na kwa wakati
mwingine unaofuatia baada zama za Milenia. Kwa hiyo, tunaona kuwa haki ya
uzaliwa wa kwanza ikifanyika kuwa kama kitu endelevu kwa kipindi cha maelfu ya
miaka na kwenye utawala wa Masihi atakaporudi akiwa kama Mfalme.
Isakari na Zabuloni ni mawili kati ya makabila mawili ya Numba ya Yakobo.
Walikwenda utumwani kwa sababu ya kumwasi kwao Mungu na Sheria zake, na
yakafanyika kuwa ni mawili kati ya Makabila Kumi Yaliyopotea ya Israeli. Kwa
utumwa huu hawakubahatika kamwe kupata fursa ya kula matunda ya haki yao ya
uzaliwa wa kwanza. Kwa hiyo, matunda ya haki hii ya uzaliwa wa kwanza hayaja
timilika bado na mengi yake yataonekana nyakati zijazo.
Kwenye tafiti nyingine za kina zilizofanyika kuhusu mahali stahiki pa
Makabila Yaliyopotea. Hivi sasa imeaminika na kukubalika kwa ujumla na
wanazuoni kwenye historia ya Wayahudi na vuguvugu la mataifa kwamba Efraimu na
Manase walikuja kuwa kwenye muunganiko wa makabila ya Anglo-Saxon. Mtazamo huu
umekuwa unaaminika na kuchukuliwa wa kawaida miongoni mwa jamii ya watu
Wanaoongea Lugha ya Kiingereza kwa karne nyingi sasa. Ikiwa kama mtazamo, hili
linajulikana kwa kiwango cha chini kwamba uzao wa Zabuloni na Isakari
unajumuisha watu ambao waliyacukua Maeneo ya Chini ya kaskazini magharibi mwa
Ulaya. Waisakari wanafanya jumuisho nchi kadhaa za Wafriesia kwenye maeneo ya
ukanda wa pwani wa Bahari ya Kaskazini.
Haki ya kuzaliwa ya Zabuloni na Isakari ni agizo la muhimu sana kwao. Tunaweza
pia kuona kutoka kwenye historia kwamba Isakari alikuwa na wajibu mkubwa na wa
muhimu sana.
1Nyakati 12:32 Na
wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo
Israeli wayatende;
Kwenye Hesabu 2 tunasoma mpangilio wa makambi ya makabila yakiizunguka
maskani na mchakato wa kupangilia makambi na upangiliaji wa makambi mapya. Hiki
ni kile tunachokijua kuwa ni mpangilio wa jinsi ya kutembea wanapoondoka.
Kabila la kwanza kuanza kuondoka lilikuwa ni la Yuda. Wokovu (Yehoshua) ni wa
kabila hili la Yuda. Kwa hiyo, Yuda ndio walitakiwa kuanza kuondoka kwanza.
Mungu Baba yetu anampa kipaumbele kamili Yesu Kristo, kwa Yehoshua, kwenye
wokovu wa upatanisho na mwanadamu. Yuda wataokolewa kabla ya kuanza kwa Ufalme
katika Israeli ikiwa ni sehemu ya ahadi iliyotolewa. Hakuna kabila litakalo
jitukuza juu ya Yuda.
Kabila la Isakari lilikuwa la tatu kwenye utaratibu wa kuondoka na kufanya
jumla ya makabila matatu ya upande wa kaskazini wa kundi la makabila
yanayoizunguka maskani. Ni hakika kwamba walikuwa wanafahamu ama kuelewa
nyakati za kujua kila Israeli wanachotakiwa kufanya. Kwa hiyo, yawezekana sana
kuwa walipewa majukumu au walikuwa na watu fulani huko ambao walikuwa na
maarifa ya elimu ya nyota na hesabu zake wakitilia maanani kalenda na majira.
Tulipaswa kuielewa hii kuwa ni awamu inayofuatia baada ya wokovu. baada
awamu inayofuatia baada ya wokovu. Baada ya upatanisho kufanywa na Kristo,
inapasa watu wapewe maarifa na uelewa wa mambo aliyoyaanzisha na kuyaamuru
Mungu kwa kuyatii kwa nyakati zake ambazo Mungu aliyaweka.
Ni wajibu wa kila mmoja kuamua na kushika nyakati za maadhimisho ya Sabato
za kila juma, kila mwezi na za kila mwaka. Jukumu hili liliagizwa kwa kupitia neno
la Mungu la kinabii kwa Kanisa kwa wakati wowote itakapokuwa kwa wakati wowote
uliotolewa. Hata hivyo, jinsi ya kujua ilivyowekwa kalenda ni wazi kuwa ulitegemea
kutangazwa na kabila la Isakari kwenye kipindi cha hekalu kabla ya utumwa wa
makabila kumi.
Tutakwenda kujifunza jinsi mambo haya yanavyouathiri wito katika siku za
mwisho. Kuna idadi kubwa ya mavuguvugu ya wana harakati na matengenezo ambayo
yatachipuka kwa nyakati mbalimbali hadi kurudi kwa Masihi na hatimaye kwenye
kipindi cha tukio kuu la pili la kukombolewa kwetu kutoka utumwa wa dunia hii
tunayoishi. Tukio hili limetajwa kwenye Isaya 66:20-22.
Tendo la kumwabudu Mungu na kuzishika au kuziadhimisha Sikukuu za Mungu na
Siku Takatifu nyingine inatakiwa ifanywe kwa mujibu sawa na majira au nyakati
zilizowekwa kwenye Kalenda ya Mungu. Kwenye kalenda hii, Miandamo ya Mwezi Mpya
ni muhimu sana kwa kuzipangilia Sabato za kila mwaka. Katika kumwabudu Mungu
hakuna nafasi ya kuitumia kalenda isiyo sahihi. Siku Takatifu za Sabato za kila
mwaka zinapaswa kuadhimishwa kwenye siku zake sahihi au vinginevyo Mungu
ataabudiwa na kutumikiwa bure au kiubatili, pasipo kukubalika nay eye mwenyewe.
Kama kalenda ya zamani ilipokuwa inatunzwa na kufuatwa katika Israeli ikiwa
katikati ya makabila, ndivyo vivyohivyo, kalenda hiyohiyo itakavyorejeshwa upya
katika siku zijazo. Kalenda potofu ya Hilleli itatomomelea mbali na
haitakumbukwa tena.
Kalenda ilikuwa inaendesha kwa kufuata Miandamo ya
Mwezi Mpya ambayo ilichukuliwa na kuadhimishwa sawasawa na maadhimisho ya
Sabato. Kalenda ndiyo ilichukuliwa ili kujua nyakati za kutoa sadaka na kuabudu
na haikuwa imeachwa kwa Walawi peke yao waamue.
Katika kuweka mwanzo wa mwaka, Mungu aliwaambia Haruni na Musa, Walawi
wawili ifuatavyo.
Kutoka 12:1-2 Bwana akanena na Musa na Haruni katika nchi ya Misri, akawaambia, 2 Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu; utakuwa ni mwezi wa kwanza wa mwaka kwenu.
Huku kulikuwa ni kuweka mpangilio wa mwezi wa kwanza wa Nisani (Abibu) kama
mwezi wa kwanza wa mwaka, kinyume kabisa na Mwaka Mpya wa Wamisri na Wababeloni
ambao ulikuwa unaanza majira ya kipupwe. Tukio la Kutoka lilifanyika katika
majira ya machipuko na ni uamsho wa maisha mapya kwa upatanisho, wakiwa njiani
wanaelekea kwenye Nchi ya Ahadi.
Ni jambo lisilo fikirika kuwa na dhana ya chini ya ujuzi wa elimu ya nyota kwa
watu wa kale kwenye miaka 3,000 iliyopita. Wakati wa tukio la Kutoka Wamisri
walikuwa na namna sahihi sana ya kuhesabu zilizotokana na vyanzo mbalimbali
vilivyotokana na vitu humihu kwenye imani ya kidini, kama ilivyokuwa mfano
mmoja wapo ni kuonekana kwa Sirius ndani ya dakika chache. Ni kwenye miaka
hamsini ya mwisho ndipo ustaarabu wa Kimagharibi uliweza kuthibitisha kwa
wataalamu wa elimu nyota wa Kimisri, wengi wao kwa sababu ya vifaa vya kuonea
mbali au darubini, waliendeleza elimu ya kisasa ya hesabu na kompyuta.
Musa alilelewa, kukulia na kusomeshwa kwenye nyumba ya kifalme ya Wamisri.
Elimu yake akiwa ni sehemu ya mtoto wa nyumba ya kifalme, ni budi ilijumuisha
elimu ya mambo ya anga hususan elimu ya nyota. Maelekezo ya Mungu kwake na kwa
Haruni kuhu ni siku ipi iwe ni siku ya kwanza katika kuuweka mwanzo lakenda ya
Mungu kwa kutumia mzunguko wa mwezi mwandamo yalikuwa wazi sana kwake. Siku
nyingine zilizosalia za mwaka ni budi zilikuwa wazi sana kwake Musa. Maarifa
haya yalihamishwa kwa wazi na kuyawekeza kwa wazee wa Israeli na tunaona kwenye
vitabu vya Mambo ya Nyakati ilikuwa ikiendea katika Isakari katika nyakati za
Daudi, na andiko haliwezi kutanguka.
Kwenye hesabu za kalenda, siku muhimu zaidi ambazo aitakuwa zinawekwa
kielimu nyota ni Siku za Miandamo ya Mwezi Mpya kwa kuwa kutokana na hizo ndipo
Sikukuu zote za kila mwaka zilizoamriwa na Mungu wa pekee na wa kweli
zinatangazwa kwa mwaka wote mzima.
Mathayo 11:13 Kwa maana manabii wote na torati walitabiri mpaka wakati wa Yohana.
Torati na manabii zote zilikuwako hadi wakati wa Yohana. Wayahudi walikuwa
kwenye kibla cha Musa. Tangu kipingi hiki cha Yohana, mamlaka hii imeondolewa
kutoka kwa Lawi na Yuda na imehamishiwa kwa Israeli, ambao ni Kanisa la Mungu.
Mamlaka ya kuitangaza kalenda imehamishwia pia kwenye Kanisa la Mungu, kama
Israeli.
Jukumu hili litarejeshwa tena katika siku za mwisho ili kuwezesha wito kwa
maraifa kwenda Yerusalemu. Jukumu hili litaonekana kuwahusu Isakari na Zabuloni
ambao wataachilia haki yao ya uzaliwa waliyopewa kwa wingi.
Mnamo mwaka 70 BK, Hekalu liliangamizwa kwa kubomolewa. Kwa hiyo haikuwa
rmewezekana tangu kipindi hicho kuutangaza Mwandamo wa Mwezi Mpya kutokea
Hekaluni. Hata hivyo, haki ya kutangaza ilikuwa imehamishiwa tayari kwenye
Kanisa na Yesu Kristo.
Kumekuwa na uhamishaji wa mamlaka na kwenda Kanisani kwenye Mathayo 11:13. Yakobo
na Israeli ni mashahidi wawili wa Mungu (soma jarida la Mashahidi (wakiwemo Mashahidi Wawili) (Na. 135)).
Isaya 44:1-5 Lakini sikia sasa [watu wa kimwili wa makabila kumi na mbili], Ee Yakobo, mtumishi wangu; na Israeli, niliyekuchagua [Kanisa la wateule na kutiwa mhuri pamoja na makabila kumi na mbili]; 2 Bwana, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni [Mtakatifu, Muisraeli asilia], niliyekuchagua. 3 Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu [makabila ya kimwili yatabarikiwa kwa mavuno yaliyotokana na mvua kunyesha kwa wakati wake muafaka]; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa; 4 nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji [mavuno ya kimwili na ya kiroho]. 5 Mmoja atasema, Mimi ni wa Bwana [Kanisa]; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo [watu wa kawaida wa kimwili wa makabila kumi na mbili walioponywa mjeraha yao]; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa Bwana, na kujiita kwa jina la Israeli [kila mtu yeyote aliye nje ya haya makabila kumi na mbili, watakaoongezwa kwenye Kanisa]. nukuu [zilizo kwenye vifungo] zimeongezwa)
Hapa tunaweza kuona kwamba kila mtu anayeamini ataongezwa Kanisani, katika
Israeli, na kwa hiyo kufanyika kuwa mbegu ya uzao wa Ibrahimu.
Kama ilivyoandika, Torati na Manabii vilikuwepo hadi wakati wa Yohana.
Agizo hili limepewa shahidi Yakobo, taifa la kimwili lionekanalo lenye makabila
kumi na mawili. Walishindwa kuhitimisha agizo lao. Baada ya hapo, Yesu Kristo
alianzisha Kanisa lenye ushuhuda na neno la Mungu linalokutikana kwenye amri za
Mungu, sheria zake na hukumu zake. Haya yote yalihamishiwa kwa Israeli, mwili
wa Yesu Kristo na Kanisa la Mungu. Katika Israeli (Kanisa) wateule, waliotiwa
mhuri bado wapo, na wanazijua nyakati. Ndivyo ilivyo, kwamba haijawahi kutokea
wakati wowote kwa Israeli wakose kujua au wasiwe na habari kwa kile Israena
habari kwa kile Israeli wanachopaswa kufana.
Ufunuo 7:4 Nikasikia hesabu yao waliotiwa muhuri katika kila kabila ya Waisraeli, watu mia na arobaini na nne elfu.
Ufunuo 7:7 Wa kabila ya Simeoni kumi na mbili elfu. Wa kabila ya Lawi kumi na mbili elfu. Wa kabila ya Isakari kumi na mbili elfu.
Isakari ametajwa kwa haraka akimfuatia Lawi ambaye amekuwa na makujumu ya
kila mara ya kuhudumu kwenye ibada za Hekaluni na, kwa hata kwenye Sikukuu.
Kutakuwa na utaratibu wa kikuhani ambao Lawi atakuwa ni sehemu tu ya ukuhani
huo. Ilitupasa tuamue tena kwa wakati huu kama Isakari atakuwa anajua tena
kupanua majira, na kama wataweza kuyafanya maarifa haya yawepo tena kwenye
taifa na ukuhani.
Ufunuo 14:1 Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-Kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu mia na arobaini na nne elfu pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao.
Ufunuo 14:4-5... Hawa wamenunuliwa katika wanadamu, malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. 5 Na katika vinywa vyao haukuonekana uongo. Maana hawana mawaa.
Wayahudi na Walawi hawajapewa majukuu yote ya kalenda wakati kabila la Yuda
lilipokuwa katika Israeli mapema kabla ya utawanyiko wao mwaka 70 BK. Tunajua
kuwa kalenda ilikuwa sahihi wakati wa kipindi cha hekalu na hakukuwa na kitu
kilichojulikana baadae kama kalenda ya Hilleli inayotumiwa na Wayahudi leo
kutokana na utaratibu na imani mpya iliyoanzishwa tangu mwaka 358 BK.
Kalenda yoyote yenye msingi wa mapokeo ya Kiyahudi au utaratibu wao wa
kuhesabu ipo kinyume na Maandiko Matakatifu, na ushikaji wa kalenda ya Hilleli
pamoja au bila ya uahirisho ni uvunjifu wa maongozi ya Torati na kwa hiyo ni
dhambi.
Kama tulivyokwisha jionea, Maandiko Matakatifu yanasema kuwa Isakari
alikuwa na uelewa wa nyakati kwenye ufalme huu uliokuwa chini ya Daudi. Historia
imethibitisha kwamba wana wa Isakari waliokuwa wanaishi huko Friesland, walikuwa
ni wazuri sana (mahiri) kwa masuala ya elimu ya nyota na ujuzi wa nyakati
takatifu kama inavyoonekana kwenye kisayari cha Eise Eisinga huko Franeker. Miaka
mia mbili iliyopita hili lilikuwa ni mojawapo ya mafanikio makubwa sana kuwahi
kufanywa hapo kabla yake na wataalamu wa elimu ya nyota na mambo ya anga. Hata
leo ujio wa kisayari hiki utawashangaza watu kuhusu Eise Eisinga.
Ahadi waliyopewa kina Zabuloni
na Isakari
Ahadi waliyopewa Zabuloni na Isakari inavutia sana. Haijatimilika bado na
inahusisha ulimwengu wote.
Kumbukumbu la Torati 33:18-19 Na Zabuloni akamnena, Furahi Zabuloni, katika kutoka kwako; 19 Watayaita mataifa waje mlimani; Wakasongeze huko sadaka za haki; Kwa kuwa watanyonya wingi wa bahari, Na akiba zilizofichamana za mchangani.
Zabuloni na Isakari watawahubiria watu mlimani – na sio Yuda, sio
Waanglo-Saxon, wala sio Wafaransa, na wala sio Wajerumani. Huduma hii itafanywa
na Zabuloni na Isakari, na sio mwingine yeyote. Na watawahubiria watu au
kuwaita watu mlimani. Je, ni watu gani, ni mlima gani, na wito huu una maana
gani? Ni wakati gani? Hii ni ahadi ya kutisha na kipindi cha mwisho cha kuogofya.
Isaya 66:23 Na
itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote
[wotewenyemwili!] watakuja kuabudu
mbele zangu, asema Bwana.
Miili yote ya watu wote na sadaka takatifu na za haki zitakuwa ni maombi na
sala. Mlima utakuwa ni mbele za uso wa Bwana. Na Bwana Mungu atawafariji.
Isaya 66:13 Mfano
wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi
mtafarijiwa katika Yerusalemu.
Watu watafarijika huko Yerusalemu.
Yerusalemu ni mji wa muhimu sana duniani – hususan kwa mtazamo wa kisiasa
na kidini. Hakuna mji mwingine hapa duniani ambao umekuwa na vita vingi sana
kupiganwa kwa mujibu wa historia yote – na hakuna mji uliomwaga damu nyingi
sana – hakuna mji ulioombewa sana; mji ule ulioitwa kitovu cha dunia.
Kila mtu aliyewahi kuwa huko Yerusalemu anapata hisia ya aina yake fulani,
hamu inayomfanya apende kurudi tena na tena. Tunapaswa pia kuwa na hamu hii
wakati wa Sikukuu; ya kupanda kwenda Yerusalemu, kama mwandishi wa Zaburi
anavyosema.
Zaburi 122:1-9 Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa Bwana. 2 Miguu yetu imesimama Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu. 3 Ee Yerusalemu uliyejengwa Kama mji ulioshikamana, 4 Huko ndiko walikopanda kabila, Kabila za Bwana; Ushuhuda kwa Israeli, Walishukuru jina la Bwana. 5 Maana huko viliwekwa viti vya hukumu, Viti vya enzi vya mbari ya Daudi. 6 Utakieni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao; 7 Amani na ikae ndani ya kuta zako, Na kufanikiwa ndani ya majumba yako. 8 Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, Amani ikae nawe. 9 Kwa ajili ya nyumba ya Bwana, Mungu wetu, Nikutafutie mema.
Sikukuu ya Vibanda tunayoiadhisha ni kivuli tu, ni ashirio au taswira ya
kipindi cha millennia. Inaonyesha kwamba tutapanda wote kwenda Yerusalemu,
kwenye Mji wa Mungu, Mji Mkuu wa wa Nchi ya Ahadi. Sisi ni watu tuelekeao kama
wasafiri na kwa Makanisa ya wasafirio, ni kama Ibrahimu alivyosafiri. Ibrahimu
aliishi kwenye hema pamoja na Isaka na Yakobo na waliutarajia mji ambao misingi
yake, rjenzi wake na aliyoifanya ni Mungu. Nasi tunautarajia mji huuhuu, mji
wetu – mji utakaomilikiwa na Mungu na wateule, watu wa Mungu. Wayahudi wanasema
kila mwaka: “Beshana Haba Biyerushalayim”
– “Mwaka mwingine ujao tukutane tena Yerusalemu”. Yerusalemu ni mji mkuu wa
Wayahudi, lakini Yerusalemu pia ni mji wetu tukiwa kama watu wa nyumbani mwa
Daudi.
Ni kama walivyo Wayahudi na Waisraeli, sisi Wamataifa na watu wote duniani
watakuwa na Yerusalemu kama mji mkuu wao na Sayuni kama mlima mtakatifu ambako huko
Sheria itatiokea. Kama Ibrahimu alivyokaa hemani, sisi pia tuko hemani na
tunaitamani Yerusalemu. Tutakutana wote huko Yerusalemu.
Lakini litawezekanaje jambo hilo. kuutamani mji umwagao damu kama huu? Mji
huu utakuwa wa namna gani? Ni lini tutakwenda huko? Unafananaje mji huo?
Kutakuwa na nini kule? Ni lini tutakusanyika huko?
Hebu na kuone pale Yerusalemu ilipo sasa na jinsi utakavyokuwa wakati Masihi
atakaporudi huko Yerusalemu. Hautakuwa kama Yerusalemu ulioandikwa kwenye
kitabu cha ufunuo ikitajwa kuwa utashuka toka mbinguni kwa Mungu. Ni tofauti na
huo.
Yerusalemu sasa
Yerusalem umejengwa vilimani au milimani. Ni kama mji wa Roma, umejengwa
kwenye milima saba. Katika Yerusalemu, mlima muhimu na mashuhuri ni ule Mlima
wa Hekalu. Sehemu zote mbili, yaani Yerusalemu na Mlima wa Hekalu vinaitwa
Mlima wa Sayuni. Hapo mwanzo jina la Sayuni liliitwa pekee mwiba wa kusini
magharibi.
Mlima wa Hekalu upo hadi wakati huu na umekuwa ni kitu muhimu, hasahasa kwa
Wayahudi na Waislamu, kwa kuwa ni kwenye mji huu kuna mahekalu matakatifu zaidi
ya Waislamu, yaani Al Aksah na Msikiti wa Omar. La mwisho, ujengwaji wa dome ya
dhahabu kama alama ya Yerusalemu. Karibia picha zote, hususan zile za Mlima wa
Mizeituni huonyesha hii dome ya dhahabu.
Mlima wa Hekalu sio mlima mrefu sana. Kwakeli uko chini kwa kimo. Ni mfupi
sana kulinganisha na milima inayouzunguka. Kwa hiyo, waweza kuuona Yerusalemu
tu wakati unapoipita milima inayouzunguka, ambayo ni mirefu sana kuuliko.
Leo, Yerusalemu inakaribia kuathirika kutokana na Bonde kubwa la Ufa
linalokatisha mabara ya Asia na Afrika, na maeneo hayo yanazua wasiwasi wa mlipoko
wa tektoniki kubwa. Kwenye mwathiriko huu kuna bonde pamoja na mto Yordani
unaotiririsha maji yake kwenye Bahari ya Chumvi, zaidi ya meta 366 (futi 1,200)
chini ya kiwango cha chini cha usawa wa bahari. Hebu fikiri!
Yerusalemu nyakati
zijazo
Yerusalemu ungali bado umefichwa na dunia kwa milima iliyouzunguka. Unapaswa
kuukaribia na kuwa umeipita milima hii kabla hujauona mji huu wa Yerusalemu.
Haya yote yatabadilika, nguvu za kitektoniki kwenye bonde la ufa zitakuwa zimeondolewa
hivi karibuni kwa tetemeko la ardhi litakalokuwa kubwa kuliko yote ambayo dunia
imewahi kuyashuhudia, au utakayoyaona tena.
Ufunuo 16:18-20 Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo. 19 Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake. 20 Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.
Hii itatokea wakati Yesu Kristo, Yehoshua HaMashiach, akirudi. Wakati huo
kutakuwa na tetemeko kubwa la ardhi. Hili limetabiriwa kwenye Agano la Kale, na
ni muhimu kwa kuutimiliza unabii mwingine.
Isaya 40:3-4 Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, Itengenezeni nyikani njia ya Bwana; Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu. 4 Kila bonde litainuliwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patasawazishwa;
Kila mlima utashushwa kwa tetemeko hili kubwa la ardhi. Na hii itaufanya
Mlima wa Hekalu kuwa ni mrefu kuliko yote, kiasi kwamba utaweza kuonekana
kutoka umbali mrefu. Milima yote iliyouzunguka ndipo itakaposhushwa na
kusawazishwa kabisa. Dunia yote itauona Yerusalemu, Mlima wa Hekalu na Beramu
ya Mungu.
Isaya 2:2-3 Na itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote watauendea makundi makundi. 3 Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana katika Yerusalemu.
Kiumbe huyu atainuliwa juu ya vilima na sio kwenye Mlima wa Hekalu peke
yake. Bali pia juu ya watu wake, juu ya Kanisa lake, Kanisa la Mungu. Kumbuka
kuwa sisi ni Hekalu kwenye Mlima wa Hekalu.
Zekaria 14:9-11 Naye Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina lake moja. 10 Nchi yote itageuzwa kuwa kama Araba, toka Geba mpaka Rimoni upande wa kusini wa Yerusalemu; naye atainuliwa juu, atakaa mahali pake mwenyewe, toka lango la Benyamini mpaka mahali pa lango la kwanza, mpaka lango la pembeni; tena toka mnara wa Hananeli mpaka mashinikizo ya mfalme. 11 Na watu watakaa ndani yake, wala hakutakuwako laana tena; lakini Yerusalemu utakaa salama.
Mji wa Geba uko kilometa 10 (maili 6) upande wa Kaskazini mwa Mlima wa
Hekalu na mji wa Rimoni upo kilometa 40 (maili 25) upande wa kusini. Mtindo wa
utafiti wa kijiolojia ni wa mtindo wa Karst, na ulikubalika na kuaminika siku
za nyuma, nah ii inaweza kusawazishwa kiurahisi sana na tetemeko kubwa la ardhi.
Hata hivyo, kuna milima ambayo haitasawazika kwa tetemeko hili kubwa. Hii
ni ishara ya mataifa magumu ambayo hayatapiga goti kumwabudu Mungu Mkuu wa
Milele. Hapa kutakuwa na agizo la watu wa Mungu, Kanisa la Mungu. Watatumiwa na Mungu kusawazisha milima
mingine na kuelekeza ibada kwa mataifa mengine.
Tumekwishaona tayari kuwa Zabuloni na Isakari wataita watu mlimani, kwenye Mlima
wa Hekalu huko Yerusalemu. Ndipo Yuda watarudishwa kwanza kwa utaratibu wa
kutembea. Zabuloni na Isakari walifuatia na kisha makabila ya Reubeni Simeoni na
Gadi upande wa kusini na hatimaye makundi ya upande wa magharibi na kaskazini
kwa utaratibu wao kama sehemu ya makabila ya urejesho.
Huu ndiyo wito wetu kama kanisa kwa nguvu za roho, kuiangusha na
kusawazisha milima.
Marko 11:22-23 Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu. 23 Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake.
Isaya 41:15-16 Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi. 16 Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia Bwana, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli.
Ndiyo, tutafurahi katika Bwana, baada ya kuiangusha na kuisawazisha milima.
Itakuwa ni kazi yetu, agizo letu na tukiwa na Masihi, tutawapiga wao kidogo.
Tutakuwa chombo cha Mungu kwa kufanya hivi. Hii ni kwa namna zote mbili, yaani
milima ya kimwili na kiroho. Leo, inaonekana kuwa haiwezekani kabisa kwetu. Tunawezaje
kuiangusha na kuisawazisha milima? Inawezekana.
Kwa nguvu nyingi za Roho Mtakatifu, tunaweza kuyaangusha mataifa kabisa na
kuitia chumvi mawinguni na mavuno kwa Mungu. Milima ya kiroho haiwezi kuwa tatizo
kwa Kanisa. Hatupaswi kuogopa bali kukua kwa nguvu za Roho Mtakatifu.
Tunawezaje kuiangusha milima ya kimwili? Mtu anaweza kusema: Mimi nina urefu wa sentimeta 165
tu (futi 5 na nchi 5) na naendelea kuzeeka! Mlima ni mrefu na mkubwa sana.
Najiona kama Mbilikimo! Mungu amefanya uwezesho kwa hilo hata kwa asili, ili
tuweze kuiangusha milima! Yesu alisema hili na limeandikwa kwenye injili ya
Marko kama tulivyoona.
Kulikuwa na mwanasayansi mkubwa aliyeishi, wala hakueleweka kabisa na wale
waliomzunguka. Alifanya mashambulizi kadhaa, na jina lake linajulikana vizuri.
Naye ni Nikola Tesla. Aligundua mashine mbadala za siku hizi na nyingine
ngingi. Aliendeleza kazi ya kufua nguvu za umeme wa Niagara. Moja ya jambo alilojionea na kulizoea ni
umuhimu na matokeo mazuri ya kufikri.
Mfano wa hii ni mwimbaji au mpiga zumari aliye na bilauri ya mvinyo. Kama
kipigio cha kuume kikiguswa, bilauri inaanza kutetemeka au kuimba, hata hadi
inapoacha kupwita. Mfikirie pia mtu mwenye uzito mkubwa kuliko wote
aning’iniapo na kijana mdogo asukumaye kwa wakati muafaka, tena na tena kwa
upande huo huo. Hatimaye, mtu mwenye uzito mkubwa atazidiwa uzito na
kuning’inia juu na kwa haraka, hadi kunapotokea ajali.
Nikola Tesla alikuta sababu ya muhimu kuamini kuwa dunia ina Hertz 8, 14 na
20, namba za mbebeo kwa sekunde. Alikuwa na shughuli nyingi akishughulikia
kuendeleza matengenezo ya mashine ili kufanyiza mbebeo au mbeleko kwa ajili ya
dunia na kuifanya ieleweke na kuingia akilini. Wazo lilikuwa ni kwamba
mitikisiko ya gamba la dunia ingeweza kuzuiwa kutokana na majenzi. Zingeweza
kuachiliwa au kulipuka kabla ya tetemeko la ardhi halijasababisha uharibifu
wowote.
Bwana Tesla alisomea majukumu haya karne moja iliyopita, akidaiwa kusababisha
matetemeko ya ardhi na madai. Huenda alikuwa anatumia 50% ya uwezo wa akili
zake, kulinganishwa na wastani wetu wa mega/meagre 5%. Ni nini kitakuwa ni
nguvu zetu kwa msaada wa Roho Mtakatifu, nguvu za Mungu, iishiyo ndani yetu? Ni
upi itakuwa nafasi yetu iliyolinganishwa na Bwana Tesla, ni marfa 30, 60 au 100;
au 3,000, 6,000 au 10,000% au hata zaidi?
Wakati atakapokuja Masihi, milima yote itashushwa, isipokuwa mmoja tu.
Mlima ule ni Mlima wa Hekalu ambao kwao, Jerusalemu inasimama. Tutashiriki
katika mchakato huu.
Hili ndilo kusudi la Mungu.
Mathayo 5:14 Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.
Na taifa, mtu alishiye mlimani hataweza kujificha pia.
Isaya 11:10 Na itakuwa katika siku hiyo, shina la Yese lisimamalo kuwa ishara kwa kabila za watu, yeye ndiye ambaye mataifa watamtafuta; na mahali pake pa kupumzikia patakuwa na utukufu.
Bendera ni muhimu. Sote tutakusanyika kwenye bendera yetu maalumu. Watu wa
jamii ya Frisian wana namna yao maalumu ya kuweka bendera kwenye milingoti ya
kanisa ambayo haionekani mahala pengine opote nchini Uholanzi, au ulimwenguni.
Bendera inawekwa kwenye mlingoti mrefu sana ikiwa kama alama, ni bebdera kwa watu.
Kwa hakika inapendeza kuiona na kuiangalia. Kileleni mwa mlima kuna Hekalu, na
kileleni mwa Hekalu kwa upande wa kuelekea juu wima kuna bendera. Na bendera ya
Mungu, bendera ya Mungu itakuwa ya kupendeza.
Isaya 4:3-6 Tena itakuwa ya kwamba yeye aliyebaki katika Sayuni, na yeye aliyeachwa ndani ya Yerusalemu, ataitwa mtakatifu; yaani, kila mmoja aliyeandikwa miongoni mwa hao walio hai ndani ya Yerusalemu; 4 hapo Bwana atakapokuwa ameuosha uchafu wa hao binti za Sayuni na kuisafisha damu ya Yerusalemu kati yake, kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza. 5 Tena juu ya makao yote ya mlima Sayuni, na juu ya makusanyiko yake, Bwana ataumba wingu na moshi wakati wa mchana, na mwangaza wa miali ya moto wakati wa usiku; kwa maana juu ya utukufu wote itatandazwa sitara. 6 Kisha kutakuwa na hema kuwa uvuli wakati wa mchana kwa sababu ya hari, na kuwa mahali pa kukimbilia na kujificha wakati wa tufani na mvua.
Ni uwekaji uleule kama ulivyofanywa kwenye tukuio la Kutoka, kwa nguzo ya
wingu mchana na kwa nguzo ya moto usiku. Sikukuu ya Vibanda ni taswira
inayofananishwa na kipindi cha Milenia kinachotarajiwa kuanza mwishoni Yubile
ya arobaini ya jangwanm ya kumgojea Masihi. Sikukuu ya Pasaka ni ya muhimu kwa
kukumbuka tukio la Kutoka na ni miaka arobaini ya kwanza ya kuwa jangwani.
Tutatembea wote kwenye nuru ya Bwana mwishoni mwa kipindi hiki.
Kwa hiyo, wakati tunapoiangalia sasa Yerusalemu ijayo, tunauona mji
ukiinuka juu mahali pa wazi, ambao katikati yake kuna Mlima wa Hekalu, na kinachoonekana
kuinuka kutoka kwenye mlima ule hadi mbinguni ni bendera ya Mungu, bendera
yake, nduzo ya wingu mchana na nguzo ya moto usiku. Hii itakuwa ishara kwa
ulimwengu wote.
Tumeuona pia umuhimu wa Mlima wa Hekalu kwa Yerusalemu. Kuna mlima mwingine
ulio karibu sana na Yerusalemu, ambao una umuhimu mkubwa sana kwa nyakati
zijazo kwa kushirikisha na kuunganisha mataifa yote.
Mlima wa Mizeituni
Zekaria 14:4 Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini.
Tunajua sasa kwamba sio jambo gumu kiasi hicho kuushusha mlima ukitilia
maanani kwamba sisi ni zana sahihi vilivyopo na imani na Roho Mtakatifu. Kwa
hiyo Mlima wa Mizeituni utagawanyika tu kwa aina yake. Kwa nini Mlima huu wa
Mizeituni ugawanyike? Ni ili kuyapa njia
maji, kwa kufanyiza uwingi wa maji ya uzima.
Zekaria 14: Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba maji yaliyo hai yatatoka katika Yerusalemu; nusu yake itakwenda upande wa bahari ya mashariki, na nusu yake upande wa bahari ya magharibi; wakati wa hari na wakati wa baridi itakuwa hivi.
Maji kutoka Yerusalemu! Lawezekaje kutokea na kuwa hivyo jambo hilo? Ni
nini kiini cha maji haya? Je, kuna kisima cha maji huko Yerusalemu?
Ezekieli 47:1 Baadaye akanileta tena mpaka lango la nyumba; na tazama, maji yalitoka chini ya kizingiti cha nyumba, kwa njia ya mashariki, maana upande wa mbele wa nyumba ulielekea upande wa mashariki; nayo maji yakashuka toka chini ya upande wa kuume wa nyumba, upande wa kusini wa madhabahu.
Maji haya ni maji ya uzima, na ni ya aina yake na ya muhimu sana.
Ezekieli 47:9 Tena itakuwa, kila kiumbe hai kisongamanacho, kila mahali itakapofika mito hiyo, kitaishi; kutakuwapo wingi mkubwa wa samaki, kwa sababu maji haya yamefika huko maana maji yale yataponyeka, na kila kitu kitaishi po pote utakapofikilia mto huo.
Na sio tu kwa kile kilichoko majini, bali pia kwa kile kinachoguguswa na
maji haya.
Ezekieli 47:12 Na
karibu na mto, juu ya ukingo wake, upande huu na upande huu, utamea kila mti wa
chakula, ambao majani yake hayatanyauka, wala matunda yake hayatatindika kamwe;
utatoa matunda mapya kila mwezi, kwa sababu maji yake yanatoka mahali
patakatifu; na matunda yake yatakuwa ni chakula; na majani yake yatakuwa ni
dawa.
Isaya 41:19-20 Nitapanda katika jangwa mwerezi, mshita, mhadasi, na mbono; nitatia katika nyika mberoshi, mtidhari, na mteashuri pamoja; 20 ili waone, na kujua, wakafikiri, na kufahamu pamoja, ya kuwa mkono wa Bwana ndio uliofanya jambo hilo. Mtakatifu wa Israeli ndiye aliyeliumba.
Ndiyo, nyika sinalia, zikilia kwa uchungu kutaka maji. Kiasi kingi cha maji
kinahitajika jangwani na kutakuwa na utepetepe au uwingi wa maji jangwani.
Mungu ataotesha mmea huko – mmea wenye maji mengi unaohitaji maji, maji na maji
mengi mengine, au vinginevyo mmea huu wa mitale utanyauka. Huu ni uthibitisho kwamba
penye maji ni pazuri. Kisha ndipo jangwa litachukuza maua mazuri na kutakuwa na
ukarimu. Kisha kutakuwa na ukarimu, kiasi kwamba watu wote wataishi kwa amani.
Uhitaji wa maji mara nyingi umekuwa ndiyo sababu na chanzo cha vita – na
hasa hasa maji ya ordaini. Maji ni ishara ya Roho Mtakatifu pia. Kama mtu
akiyapokea maji ya uzima ya Roho Mtakatifu moyoni mwake, mtu huyo atakua na
kuchanua na kuzaa matunda ili kwamba watu wote akiri kwamba mkono wa Mungu
unafanya hivyo.
Zekaria 13:1 Katika siku hiyo watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, watafunguliwa chemchemi kwa dhambi na kwa unajisi.
Yoeli 3:18 Tena itakuwa siku ile, ya kwamba milima itadondoza divai tamu, na vilima vitatiririka maziwa, na vijito vyote vya Yuda vitatoa maji tele; na chemchemi itatokea katika nyumba ya Bwana, na kulinywesha bonde la Shitimu.
Maji haya yanatiririka kutoka kwenye Hekalu la Mungu, na kwa hiyo yana
matokeo na maana kubwa sana kila mahali yanakokwenda.
Isaya 35:1-2 Nyika na mahali palipo ukiwa patafurahi; jangwa litashangilia na kuchanua maua kama waridi. 2 Litachanua maua mengi, na kufurahi, naam, kwa shangwe na kuimba; litapewa uzuri wa Lebanoni, utukufu wa Karmeli na Sharoni; watauona utukufu wa Bwana, ukuu wa Mungu wetu. 3 Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu, yafanyeni imara magoti yaliyolegea.
Isaya 33:20 Angalia Sayuni, mji wa sikukuu zetu; macho yako yatauona Yerusalemu umekuwa kao la
raha; hema isiyotanga-tanga; vigingi vyake havitang'olewa, wala kamba zake
hazitakatika.
Isaya 33:24 Wala hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa; watu wakaao humo watasamehewa uovu wao.
Ni nani wakazi wa mji huu na ni watu gani hao?
Isaya 33:14-16 Wenye dhambi walio katika Sayuni wanaogopa; tetemeko limewashika wasiomcha Mungu; Ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto ulao; ni nani kwetu sisi awezaye kukaa na moto uteketezao milele? 15 Ni yeye aendaye kwa haki, anenaye maneno ya adili; ni yeye anayedharau faida ipatikanayo kwa dhuluma; akung'utaye mikono yake asipokee rushwa; azibaye masikio yake asisikie habari za damu; afumbaye macho yake asitazame uovu. 16 Huyu ndiye atakayekaa juu; majabali ni ngome yake; atapewa chakula chake; maji yake hayatakoma.
Yoeli 2:28-29 Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono; 29 tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu.
Na wageni watakuja Yerusalemu, kama wanavyokuja leo, lakini sio kama
watalii.
Isaya 14:1-2 Maana
Bwana atamhurumia Yakobo, atamchagua Israeli tena, naye atawaweka katika nchi
yao wenyewe; na mgeni atajiunga nao, nao wataambatana na nyumba ya Yakobo. 2 Na hao mataifa watawatwaa na kuwaleta
mpaka mahali pao wenyewe, na nyumba ya Israeli watawamiliki, na kuwafanya
watumishi na wajakazi katika nchi ya Bwana; nao watawachukua hali ya kufungwa
watu wale waliowafunga wao, nao watawamiliki watu wale waliowaonea.
Isaya 56:6-8 Na wageni, walioandamana na Bwana ili wamhudumu, na kulipenda jina la Bwana, kuwa watumishi wake; kila aishikaye sabato asiivunje, na kulishika sana agano langu; 7 Nitawaleta hao nao hata mlima wangu mtakatifu, na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala; makafara yao na dhabihu zao zitakubaliwa juu ya madhabahu zangu; kwa maana nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote. 8 Bwana MUNGU, akusanyaye waliofukuzwa katika Israeli asema, Pamoja na hayo nitamkusanyia na wengine, zaidi ya hao walio wake waliokusanywa.
Kusanyiko kubwa la watu litakuja Yerusalemu. Watu wengi wataishi mjini.
Hili haliwezi kutokea kwa kufumba na kufumbua tu. Mipangilio mingi na
maandalizi vitatakiwa ili kufanikisha hii. Ujenzi wa mji na wa dunia vinatakiwa
viandaliwe. Kunaweza kuwa na wekundu kama ulimwengu wote unaangukia kwenye
maangamizo. Kila kitu kinaharibika. Ili kuyajenga tena haya yote, kiasi kingi
cha fedha na raslimali vinahitajika.
Je, dunia hii, kwa sababu hii, iwe ni dunia ya mtu maskini?
Zekaria 14:14 Yuda naye atafanya vita juu ya Yerusalemu; na huo utajiri wa mataifa wa pande zote utakusanyika, dhahabu, na fedha, na mavazi; vitu vingi sana.
Makanisa yote ya leo, mashirika yote ya kidini isipokuwa sisi, yote
yanafanya kazi kwa ajili ya faida yetu kwa kitambo kifupi kijacho. Mali na
utajiri wote ambao wanaukusanya ni kwa faida yetu huko Yerusalemu. Hawajui
jambo hili, lakini wanafanya!
Isaya 23:17-18 Hata itakuwa mwisho wa miaka sabini, Bwana ataizuru nchi ya Tiro, naye atarudi apate ujira wake, atafanya ukahaba pamoja na falme zote za ulimwengu juu ya uso wa dunia. 18 Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa Bwana, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za Bwana, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.
Mika 4:11-13 Na sasa mataifa mengi wamekusanyika juu yako, wasemao, Na atiwe unajisi; macho yetu na yaone shari ya Sayuni. 12 Lakini wao hawayajui mawazo ya Bwana, wala hawafahamu shauri lake; kwa maana amewakusanya kama miganda sakafuni. 13 Haya, simama upure, Ee binti Sayuni; kwa maana nitafanya pembe yako kuwa chuma, na kwato zako kuwa shaba; nawe utaponda-ponda mataifa mengi, na faida yao utaiweka wakfu kwa Bwana, na mali zao kwa Bwana wa dunia yote.
Ni kwa kiasi gani na ni kitu gani watakachokula
kwa kuwatosheleza kabisa?
Isaya 25:6 Na katika mlima huu Bwana wa majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.
Yote haya yanahitaji kupangilia. Ni jinsi gani watu hawa wanaotoka ulimwenguni
kote watakuja Yerusalemu? Ni kwa jinsi gani basi chakula chote na mahitaji yote
mengine ya kila siku na mahitaji kwa ajili ya kundi hili yanaweza kusafirishwa
na kugawanywa? Hayataanguka tu kutoka mbinguni. Je, ni kwa namna gani
Yerusalemu utajengwa upya na majengo yake yatakuwa?
Isaya 60:9-11 Hakika yake visiwa vitaningojea, Na merikebu za Tarshishi kwanza, Ili kuleta wana wako kutoka mbali, Na fedha yao na dhahabu yao pamoja nao, Kwa ajili ya jina la Bwana, Mungu wako, Kwa ajili yake Mtakatifu wa Israeli, Kwa kuwa amekutukuza wewe. 10 Na wageni watajenga kuta zako, Na wafalme wao watakuhudumu; Maana katika ghadhabu yangu nalikupiga, Lakini katika upendeleo wangu nimekurehemu. 11 Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; Hayatafungwa mchana wala usiku; Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.
Biblia ya NIV inasema: “ili kwamba watu wawaletee mali na utajiri wa
mataifa.”
Litakuwa ni kusanyiko lisiloweza kuhesabika. Je, hii ndiyo hatima ya
Yerusalemu – mji uliosongwa na kusanyiko la mataifa? Je, hawahitajiki kutoka
tena nje ulimwenguni kote tena, kila mtu nyumbani mwake? Je, watu watarudi kwa
mzunguko wa Yubile au kwa mwaka wa Sabato tena? Kuna mengi zaidi ya kufanya
zaidi ya madhimisho ya sikukuu tu huko Yerusalemu!
Ezekieli 36:33-38 Bwana MUNGU asema hivi; Siku ile nitakapowatakaseni na maovu yenu yote, nitaifanya miji ikaliwe na watu, na palipobomolewa pajengwe tena. 34 Nchi iliyokuwa ukiwa italimwa, ijapokuwa ilikuwa ukiwa mbele ya macho ya watu wote waliopita. 35 Nao watasema, Nchi hii, iliyokuwa ukiwa, imekuwa kama bustani ya Adeni; nayo miji iliyokuwa mahame, na ukiwa, na magofu, sasa ina maboma, inakaliwa na watu. 36 Ndipo mataifa, waliobaki karibu yenu pande zote, watajua ya kuwa mimi, Bwana, nimejenga mahali palipoharibika, nami nimepanda mbegu katika nchi iliyokuwa ukiwa; mimi, Bwana, nimesema hayo; tena nitayatenda. 37 Bwana MUNGU asema hivi, Tena kwa ajili ya jambo hili nitaulizwa na nyumba ya Israeli, ili niwatendee; nami nitawaongeza kwa watu kama kundi la kondoo. 38 Kama kundi lililo tayari kutolewa sadaka, kama kundi la Yerusalemu katika sikukuu zake zilizoamriwa; ndivyo itakavyojazwa watu, miji ile iliyokuwa maganjo; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.
Flavius Josephus anatuambia kuhusu kusanyiko hili akisema.
Kwa hiyo hawa makuhani wakuu, wanapokuja kwenye sikukuu yao inayoitwa Pasaka, wakati wanapoweka pale sadaka, tangu saa tisa hadi saa kumi na moja, lakini kwa kuwa kundi lao lilikuwa la wasiopungua kumi walijumuika kwenye kila utoaji wa kila, (kwa kuwa haikukatazwa na wala haukuwa uvunjifu wa maagizo ya torati wakijibizana nyimbo wawapo kwenye sikukuu na kupokezana,) na sisi wengi wetu tupo ishirini tunaoshirikiana nao, inafanya idadi ya dhabihu zinazotolewa kuwa jumla ya wanyama mia mbili na hamsini na sita elfu na mia tano, ambayo ni posho ya watu wasiozidi kumi walioisherehekea sikukuu ile pamoja, idadi ya watu milioni mbili na mia saba elfu ns mis mbili ambao walikuwa wamejitakasa na watakatifu. (Josephus Wars, Bk. VI, Ch. 9:3, kimetafsiriwa na Whiston)
Isaya 54:1-3 Imba, wewe uliye tasa, wewe usiyezaa; paza sauti yako kwa kuimba, piga kelele, wewe usiyekuwa na utungu; maana watoto wake aliyeachwa ni wengi kuliko watoto wake yeye aliyeolewa, asema Bwana. 2 Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako. 3 Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto; na wazao wako watawamiliki mataifa; wataifanya miji iliyokuwa ukiwa kukaliwa na watu.
Kusanyiko hili lote haliwezi kuishi mjini Yerusalemu, wanahitaji eneo zaidi.
Isaya 49:18-20
Inua macho yako, ukatazame pande zote;
hao wote wanajikusanya na kukujia. Kama niishivyo, asema Bwana, hakika
utajivika na hao wote, kama kwa uzuri, nawe utajifungia hao, kama bibi arusi. 19 Maana katika habari za mahali pako
palipokuwa ukiwa, pasipokaliwa na watu, na nchi yako iliyoharibika hakika sasa
utakuwa mwembamba usiwatoshe wenyeji wako, nao waliokumeza watakuwa mbali. 20 Watoto ulionyang'anywa watasema
masikioni mwako, Mahali hapa ni pembamba, hapanitoshi; nipe nafasi nipate
kukaa.
Sisi kama Kanisa la Mungu tunajua kuhusu mizunguko ya kalenda na ya mwaka
wa Sabato na ya mwaka wa Yubile. Kwenye miaka hii maalumu ya aina yake, kutakuwa
na shughuli nyingi sana huko Yerusalemu kwa ajili ya watu hawa wote wapandao
kwenda Yerusalemu na kurudi kwenye nchi zao. Lakini kila mwaka mataifa
watatakiwa kupeleka wawakilishi wao huko Yerusalemu kwenye Sikukuu (Zekaria
14:16-19). Ndipo yale mataifa ambayo hayatatuma wawakilishi mvua haitanyesha
kwao kwa majira yake muafaka.
Zaburi 24:3-6 Ni nani atakayepanda katika mlima wa Bwana? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake? 4 Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila. 5 Atapokea baraka kwa Bwana, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake. 6 Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao, Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.
I kitu gani kinachowafanya watu wafurahi? Ni wakati upi watakuwa na furaha
kamili? Ni wakati wanapomtafuta Mungu!
Zaburi 15:1-2 Bwana, ni nani atakayekaa Katika hema yako? Ni nani atakayefanya maskani yake Katika kilima chako kitakatifu? 2 Ni mtu aendaye kwa ukamilifu, Na kutenda haki. Asemaye kweli kwa moyo wake,
Isaya 51:3 Maana Bwana ameufariji Sayuni; amepafariji mahali pake palipokuwa ukiwa; amefanya jangwa lake kuwa kama bustani ya Edeni, na nyika yake kama bustani ya Bwana; furaha na kicheko zitaonekana ndani yake, kushukuru, na sauti ya kuimba.
Isaya 51:11 Nao
waliokombolewa na Bwana watarejea, Watafika Sayuni, wakiimba; Furaha ya milele
itakuwa juu ya vichwa vyao; Watapata shangwe na furaha; Huzuni na kuugua
zitakimbia.
Fikiria juu ya sauti ya wimbo na uimbaji. Watu hawa wote wanatakiwa kufundishwa. Ni nani atakuwa mwalimu? Wapo Hekaluni mwa Mungu.
Ufunuo 3:4, 12 Lakini unayo majina machache katika Sardi, watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa wamestahili. Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya.
Kwa hiyo wakufunzi watajulikana kwa majina maalumu:
1. Jina la familia ya Mungu
2. Jina la mji
3. Jina la mtu
Kwa mfano: Yohana, ndugu wa Yehoshua, Elohim, mwana wa Mungu, kutoka Chuo Kikuu cha Hekalu la Yerusalemu, wanawapangia waalimu na kuwaandaa kwa huduma ya Singapore.
Hata hivyo, waalimu wote watakuwa na mwalimu kiongozi.
Zaburi 145:10-12 Ee Bwana, kazi zako zote zitakushukuru, Na wacha Mungu wako watakuhimidi. 11 Wataunena utukufu wa ufalme wako, Na kuuhadithia uweza wako. 12 Ili kuwajulisha watu matendo yake makuu, Na utukufu wa fahari ya ufalme wake.
Na watu watawaona waalimu wao. Hakutakuwa na msaada utahaohitajika kama tufanyavyo leo kwa kutumia tepu au majarida.
Isaya 30:19-21 Kwa maana watu watakaa katika Sayuni huko Yerusalemu; wewe hutalia tena; hakika yake atakuonea rehema nyingi kwa sauti ya kilio chako; asikiapo ndipo atakapokujibu. 20 Na ingawa Bwana atawapeni chakula cha shida na maji ya msiba, lakini waalimu wako hawatafichwa tena, ila macho yako yatawaona waalimu wako; 21 na masikio yako yatasikia neno nyuma yako, likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa kushoto.
Isaya 52:7-9 Jinsi ilivyo mizuri juu ya milima Miguu yake aletaye habari njema, Yeye aitangazaye amani, Aletaye habari njema ya mambo mema, Yeye autangazaye wokovu, Auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki! 8 Sauti ya walinzi wako! Wanapaza sauti zao, wanaimba pamoja; Maana wataona jicho kwa jicho, Jinsi Bwana arejeavyo Sayuni. 9 Pigeni kelele za furaha, imbeni pamoja, Enyi mahali pa Yerusalemu palipokuwa ukiwa; Kwa kuwa Bwana amewafariji watu wake, Ameukomboa Yerusalemu.
Wakati kunapokuwa na uimbaji kwa furaha, ni nini watu watakachoimba?
Ufunuo 15:3-4 Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa. 4 Ni nani asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu; kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako; kwa kuwa matendo yako ya haki yamekwisha kufunuliwa.
Kutakuwa na nyimbo nyinginr nyingi mpya.
Zaburi 96:1 Mwimbieni Bwana wimbo mpya.
Na hizi nyimbo za zamani na mpya zitatuika kama zana, kama vifaa vya kufundishia, na kuelimishia. Hii ni njia bora sana kuliko.
Wakolosai 3:16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.
Na nyimbo vina thamani kubwa sana kwa Mungu kuliko hata sadaka.
Zaburi 69:30-31 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, Nami nitamtukuza kwa shukrani. 31 Nayo yatampendeza Bwana kuliko ng'ombe, Au ndama mwenye pembe na kwato.
Sasa, kuhusu sisi je? Yatupasa tufanye nini?
Zaburi 100:1-2 Mfanyieni Bwana shangwe, dunia yote; 2 Mtumikieni Bwana kwa furaha; Njoni mbele zake kwa kuimba;
Tunakusanyika
machoni pa Mungu. Tunafanya hivi pia kwa kuimba. Ila tupo kwenye makao ya muda. Sisi ni wasafiri.
Tunaelekea Yerusalemu, mji mkuu wa Nchi ya Ahadi. Na tuwapo njiani yatupasa pia
kuimba.
Zaburi 98:1-9 Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Kwa maana ametenda mambo ya ajabu. Mkono wa kuume wake mwenyewe, Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu. 2 Bwana ameufunua wokovu wake, Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake. 3 Amezikumbuka rehema zake, Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli. Miisho yote ya dunia imeuona Wokovu wa Mungu wetu. 4 Mshangilieni Bwana, nchi yote, Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi. 5 Mwimbieni Bwana zaburi kwa kinubi, Kwa kinubi na sauti ya zaburi. 6 Kwa panda na sauti ya baragumu. Shangilieni mbele za Mfalme, Bwana. 7 Bahari na ivume na vyote viijazavyo, Ulimwengu nao wanaokaa ndani yake. 8 Mito na ipige makofi, Milima na iimbe pamoja kwa furaha. 9 Mbele za Bwana; Kwa maana anakuja aihukumu nchi. Atauhukumu ulimwengu kwa haki, Na mataifa kwa adili.
Tunaiangalia Yerusalemu ijayo, baada ya maangamizo na uharibifu ambao
unakuja ulimwenguni kote. Mataifa yakuwaitwa kwenda Sayuni na Yerusalemu.
Yerusalemu uliojengwa utakuwa ni mji wenye Mlima wa Hekalu, na pamoja na Sayuni
itajitandaza juu ya nyanda zinazouzunguka. Kutoka kwenye Hekalu hili, maji ya
uzima yatatiririka, kuieneza dunia kwa maji na Roho Mtakatifu, ili kwamba
kusiwepo kitu na asiwepo mtu atajayekuwa na kiu tena.
Watu watapanda kwenda Yerusalemu na kupeleka utajiri wao. Sheria zitatokea
Sayuni na mataifa yote yataanzisha elimu sahihi. Yerusalemu hii itakuwa Wimbo
Uliobora zaidi ya nyimbo zote, na watu wote watauimba mji wa Yerusalemu kwa
utukufu wa Mungu wa Milele.
Sisi, kama wateule itatupasa kufanya kazi yetu sawasawa na wito wetu, na
itatupasa kuufundisha ulimwengu. Tutatumiwa sisi sote na Mungu sawasawa na nia
yake, sisi sasa na hata kipindi hicho tutakuwa ni sehemu ya Yerusalemu hii ya
kupendeza, kama sehemu ya Hekalu.
Hii ni hatima ya kupendeza na ya ajabu kuwa sehemu ya Yerusalemu hii ya
kupendeza, na kuwa sehemu ya Hekalu zuri. Hebu jiandae kuchukua taji iliyowekwa
tayari imeandaliwa kwa ajili yako.
Ufunuo 3:11 Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako.
Toba
Sasa tunakuja kwenye sehemu ya ujumbe uliomgumu.
Ni wito wa kufanya toba. Wito wa kurudi kwenye msingi ambao kwa huo Yesu Kristo aliuweka ama kuujenga kama jiwe kuu la pembeni nasi tunapaswa kuongezwa ukiwa kama mawe ya Hekalu la Mungu.
Sot tuna hatia kwa kuyaweka matamanio yetu mbele ya Neno la Mungu. Kila
mmoja wetu anakabiliwa na tamaa ya kutamani kwenye mwenendo fulani, desturi
fulani, daraja fulani linaloonekana kufanya mabo yawe rahisi sana kwetu. Msukumo
unaohusishwa mara nyingi unakuja kutoka mioyoni mwetu sisi wenyewe. Moyo huwa
mdanganyifu kuliko vitu vyote na hukukatisha tamaa na uovu. Tunajidanyanya wenyewe
kwa hisia za mioyo yetu. Tukidhania kwamba tunafanya vitu vizuri, tunafunga
barabara ya wengi kuujia wokovu.
Mara nyingi kwa kusikiliza hisia ya mioyo yetu tunapoteza maono ya upendo
ambao umesisitizwa na sheria, na amri za Mungu, miongozo na hukumu. Yatupasa kuweka
kwa upendo wa Mungu, na kuzishika amri zote kwa kusukumwa na upendo.
Yatuoasa tuwahubirie watu mlimani. Tunaweza kufanya hivyo kwa lugha yetu
wenyewe. Tutawaita Wafriesiani mlimani kwa lugha ya Kifriesiani na Kidachi kwa lugha
ya Kidachi na pia kwa mataifa mengine yote ua lugha zake.
Kwahiyo inatupasa kuwaelekeza watu au kuwahubiria kwa kutumia lugha zao na
kumtangaza Yesu Kristo. Ambavyo ni kwa lugha za Friesland na Uholanzi wanamuita
Jezus Christus, kwa Kifaransa Jésus Christ, kwa Kiyunani Ièsous Chreistos, kwa
Kiebrania Yehoshua HaMashiach.
Mtume Paulo ameandika: “Mhahudi kwa Wayahudi na Myunani kwa Wayunani”. Kwahiyo
kama ukiwa Uholanzi utamtangaza kwa kutumia jina la Yehoshua, ndipo idadi kubwa
ya Wadachi wasingeweza kufikiwa, ni kama na sisi tengekuwa tunaongea tofauti
kwa lugha isiyoeleweka. Hatuwezi kuwafundisha watu kwa Kiebrania, ni kama wao
wasivyoweza kutuelewa sisi pia. Biblia ni kitabu kilicho wazi na kueleweka vya
kutosha.
1Wakorintho 14:21 Imeandikwa katika torati, Nitasema na watu hawa kwa watu wa lugha nyingine, na kwa midomo ya wageni, wala hata hivyo hawatanisikia, asema Bwana.
Tunapaswa kuwa kila kitu kwa watu wote kwa maana sahihi: Myahuso kwa Wayahudi
na Mfriesian kwa Wafriesiani na Mdachi kwa Wadachi wenzake. Tunapaswa pia
kutubu kutokana na dhambi iliyo ndani yetu na kutoka kwenye mapkeo
yanayotuzingira; kutubu kwa kutokuwa na upendo na kufikiria na kutilia maanani
hukumu zetu; kwa kushinikiza mitazamo yetu kwa watu wengine na kwa kutokuwa
watumishi kwa kuusahau upendo wa Agape; na kwa kukubali karibu kitu chochote
badala ya kusimama kama mwamba kwa wavunja miamba. Kwa kuogopa kuwakwaza baadhi
ya watu, tunawaudhi wengine.
Mara nyingi mtu anapolisikia andiko: “Wokovu unatoka kwa Wayahudi.” Huu ni
Wokovu wa kweli, ukombozi, Kristo, Masihi, Yesu, Yehoshua, anatoka kwa Wayahudi.
Alikuwa ni dhabihu ya ukombozi kwa wote wenye mwili – na sio kwa Wayahudi peke
yao, wala sio kwa ajili ya makabila mengine ya Israeli – bali ni kwa viumbe
wote.
Tunajua kwamba makabila kumi yalikwenda utumwani na kufungwa huko kwanza
kwa ajili ya kuasi kwao, na walikumbana na hali ya kutalikiwa. Yuda pia
walikwenda utumwani na vifungoni na hawajarudi bado.
Ufalme wa kaskazini sasa ni Yule mwanamke aliyeachwa na kutalikiwa na mjane,
na anakombolewa ili aolewe tena. Yuda pia ilifanyika kuwa mjane na kukombolewa
iolewe tena. Zote mbili ziko kwenye hali moja. Zote mbili zitakuwa Yakobo tena,
na kuwa mmoja, na kuponywa mavunjiko yake. Wao ni wana wa Yakobo, na Wamataifa
wanaweza wote kupandikizwa kwenye mti mzuri wa mzabibu. Mti wa mzabibu wa
Israeli ni Kanisa la Mungu.
Yakobo na Israeli ni mashahidi wa Mungu.
Isaya 44:1-8 Lakini sikia sasa, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na Israeli, niliyekuchagua; 2 Bwana, aliyekufanya, na kukuumba toka tumboni, yeye atakayekusaidia, asema hivi; Usiogope, Ee Yakobo, mtumishi wangu; na wewe, Yeshuruni, niliyekuchagua. 3 Kwa maana nitamimina maji juu yake aliye na kiu, na vijito vya maji juu ya mahali pakavu; nitamwaga roho yangu juu ya wazao wako, na baraka yangu juu yao utakaowazaa; 4 nao watatokea katika manyasi, kama mierebi karibu na mifereji ya maji. 5 Mmoja atasema, Mimi ni wa Bwana; na mwingine atajiita kwa jina la Yakobo; na mwingine ataandika juu ya mkono wake, Kwa Bwana, na kujiita kwa jina la Israeli. 6 Bwana, Mfalme wa Israeli, Mkombozi wako, Bwana wa majeshi, asema hivi; Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu. 7 Naye ni nani kama mimi atakayeita, na kuyahubiri haya, na kunitengenezea, tangu nilipowaweka watu wa kale? Na mambo yanayokuja na yatakayotokea, wayatangaze. 8 Msiogope wala msifanye hofu; je! Sikukuhubiri haya zamani na kuyaonyesha? Na ninyi ni mashahidi wangu. Je! Yuko Mungu zaidi yangu mimi? Hakika hapana Mwamba; mimi sijui mwingine.
Sisi sote tupo kama Yona. Sote tunataka kukimbia na kutokomea kutoka usoni
pa Bwana. Huu ni upuuzi na hairuhusiwi. Ni kitu cha kutisha kuangukia mikononi
mwa Mungu aliyehai. Hapa tunaweza kuona kwa suala la ishara ya Yona.
Yona 3:4-5 Yona akaanza kuuingia mji mwendo wa siku moja, akapaza sauti yake, akasema, Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa. 5 Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu;
Mathayo 12:39 Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona.
Mathayo 12:41 Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona.
Ninawi ilipewa siku arobaini za kutubu, na Ninawi walitubu. Yuda walipewa
siku ya kinabii ya mwaka na wakapewa miaka arobaini za kutubu, na Yuda hawajatubu.
Miaka arobaini baada ya maneno haya ya Yesu Kristo, Yerusalemu na Hekalu la Pili
zilipinduliwa na Warumi.
Sisi kama Kanisa la Mungu tunapaswa kutubu kwa ajili ya maovu yetu. Je, ni
muda gani tuliopewa sisi? Kwenye kitabu cha Ufunuo, Yesu Kristo anasema: “Naja
upesi”. Ni mara ngapi tunatakiwa kutubu? Kama Kanisa yatupasa kusimame kwenye mimamosahihi.
Hatuwezi kuwa na wakati mmoja kama Yuda walivyopewa miaka arobaini. Huenda tuna
siku arobaini tu kama watu wa Ninawi, au majuma arobaini, au hata miezi
arobaini. Hatujui ni muda gani. La msingi t uni kwamba muda ni mfupi. Inaweza
kuwa ni miaka michache tu hata hivyo, kuwa miaka michache tu ijayo. Yatupasa
tutende kama vile ni leo.
Kwa hiyo hebu na tutubu wote na kurudi kwenye ibada, kumuabudu Mungu wa
pekee na wa kweli kwa namna ya uweza, kwa siku sahihi kwa mwaka mzima, tukiutendea
kazi upendo wa Mungu, ili kwamba asiwepo mtu mwenye nafasi ya kuzitwa taji zetu.
Ndipo bado tunaweza kusema:
BESHANA HABA BIYERUSHALAYIM
Mwaka ujao tena Yerusalemu
Ndipo nitasema hivi:
SHALOM CHAVERIM LEHITRAOTH
Amani, marafiki, kwaherini.
Oant sjens!
q