Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[021i]
Ufafanuzi wa Kitabu
cha Sefania
(Toleo La 1.0
20141003-20141003)
Unabii huu muhimu
uliandikwa kwenye kipindi cha takriban dazani moja ya miaka kabla ya kuanguka
kwa Ninawi, na kabla ya kipindi cha utumwa wa Yuda. Nabii huyu wa mwisho wa
kabla ya kipindi cha utumwa aliwataja moja kwa moja makasisi waliojulikana kama
Chemarim au Makuhani au makasisi wavaa
Majoho Meusi wa Baali na Ashtorethi au Easter, wa dini au imani potofu ya
Mungumke. Makuhani hawa bado wapo na wanahudumu huko Yerusalemu kwa maelfu na
wataondolewa mara moja hivi punde na kulazimika kutubu na kuachana mafundisho
ya uzushi na hawatayafundisha kamwe tena kabisa.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)
(tr. 2015)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Sefania
ameorodheshwa kuwa ni wa Nane miongoni mwa manabii waliokubalika kwenye kanuni
ya Agano la Kale. Uzao wake umeorodheshwa kwa zaidi ya vizazi vinne kwa kuwa
neno la mababa zke kwenye tafsiri ya KJV ni neno hilohilo kwenye Kiebrania kama
Hezekia na watawala walivyothibitisha alikuwa ni kitukuu wa Hezekia Mfalme wa
Yuda.
Imethititishwa na
E.A. Leslie (kwenye kamusi yake ya Interp. Dictionary of the Bible, Bk. IV, pp. 951ff.) kwamba huduma
yake imekadiriwa tarehe kwa harakati za uvamizi za Scythian mnamo mwaka 630-625
KK. Harakati za ibada na dini za Baali na Mungu Mke wa a dini za Waashuru na
Wababeloni zilikuwa zimeingia katika Yuda baada ya kupanuka kwa dola ya
Waashuru na Manase kuzijenga madhabahu na magari kwenye nyumba ya juu ya Mfalme
Ahazi ili kuliabudu Juan a dini za kisiri. Waliliabudu jua, mwezi na sanamu
zote za kizodiaki na Malaika wote wa Mbinguni (2Wafalme 23:11ff). Mkazo mpya
ulitolewa kwenye dini za Mungu Mke pamoja na sherehe au sikuku za Ashtorethi au
Easter na za Baali zilizoingia kutoka kwenye imani mchanganyiko wa Waashuru na Wababeloni
zilizosisitizwa kwa nguvu na mkazo mkubwa. Dini hizi zikafanyika kuwa maarufu
kwa haraka na zikaingia katika familia za watu wa Yudea na wakazishiriki pamoja
na kila mshiriki walijitahidi kufanya wawezavyo kwa namna hii hii tunayoiona
wakifanya leo kwenye hizi dini za waadubu Jua na waamini Utatu wanavyoitukuza
kwa kuiadhimisha tarehe 25 Disemba siku ya Krismas na kwa jinsi hii hii kama
wanavyofanya leo kama ilivyokuwa na kulaaniwa na nabii Yeremia (Yeremia 7:17ff,
10:1-9) ambaye alikuwa nabii kwa kipindi kimoja na Sefania.
Kabila la Scythians
walikuwa wasio na ustaarabu kutoka Kaskazini ambalo lilivamia Asia Ndogo kwenye
mipaka ya Misri. Farao Psammetichus I wa Misri (Herodotus I, 103-106) aliwapa
rushwa na waliafikiana kwa mkataba kutoka mipakani mwake na wakaishambulia na
kuiteka Ashkeloni na Beth-shean.
Unabii haukuishia
kukemea Yuda tu kwa kipindi kile cha uvamizi wa hawa Scythian na kabla ya
kuanguka kwa dola ya Waashuru mwaka 605 KK na Wababeloni. Yalikuwa ni makemeo
kwa wanadamu wotekwa uasi wao uliotokana na kutatanishwa na Dini za Waabudu Jua
kama tunavyoona kwenye Sefania 1:2-3.
Neno
la Bwana lililomjia Sefania, mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria,
mwana wa Hezekia; katika siku za Yosia, mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda.
Kwa hiyo ndiyo maana tunaamini kukiweka kipindi
hiki kuwa klikuwa ni kile cha Yosia, mfalme wa Yuda (642/1–609). Marejesho ya
Yosia katika mwaka huu wa 18 yalikuwa hayajaisha bado kama tunavyoona kwenye
mlinganisho na 2Wafalme 23. Kwa hiyo, andiko hili liliandikwa mapema kabla ya kipindi
cha Marejesho bali huenda yawezekana sana kuwa ni kipindi kile cha kuonekana
kwa Kitabu cha Torati kuelekea kwenye Marejesho kwenye Yubile ya mwaka 624 KK.
Unabii wake kwa Ninawi ulitimilika kwa kuanguka
kwa Ninawi na kuangamizwa kwake na Wamedi na Wababeloni mwaka 612 KK. Wababeloni
waliwapiga kabisa na ushawishi wa Wamisri kwenye Mapigano ya Karchemishi mwaka
605 KK mzunguko mmoja wa Sabato baadae. Utajwaji wake kwenye Sefania hakupo kwa
moja kwa moja kama vile ilivyo kwenye unabii wa Nahumu ambako umeelezewa kwa
kina zaidi kwenye unabii wake kuhusu kuanguka kwa Ninawi.
Huu ni unabii
unaohusu Siku za Mwisho:
2 Nitavikomesha kabisa vitu vyote, visionekane juu
ya uso wa nchi, asema Bwana. 3 Nitamkomesha mwanadamu
na mnyama; nitakomesha ndege wa angani, na samaki wa baharini, na hayo makwazo
pamoja na wabaya; nami nitamkatilia mbali mwanadamu, asionekane juu ya uso wa
nchi, asema Bwana. 4 Nami nitaunyosha mkono wangu juu
ya Yuda, na juu ya watu wote wakaao Yerusalemu; nami nitayakatilia mbali mabaki
ya Baali, yasionekane mahali hapa, na hilo jina la Wakemari pamoja na makuhani;
5 na wale walisujudiao jeshi la mbinguni juu ya dari
za nyumba; na hao waabuduo, waapao kwa Bwana na kuapa pia kwa Malkamu;
Malkamu ni neno
la Kiebrania kwa Mungu wa kitaifa wa Waamoni, yaani Moleki. Alihusishwa na
Nyota ya Mungu Remphan ambaye ni Nyota Sita Zinazoonyeshwa na ambayo sasa
inaonekana kwenye Bendera ya Israeli na kiupotoshaji inajulikana kama Nyota ya
Daudi. Kungu aliwakasirikia Yuda na akawapeleka utumwani huko Babeli na
wanapaswa kutendewa ipasavyo katika siku ya Bwana. Huu sio Utumwa wa Babeli,
sio Utumwa wa Warumi, bali ni wa namna wa wote wawili, na kwa kupitia
utawanyiko wao katika Siku za Mwisho. Siku ya Bwana imenenwa kwenye jarida la Siku ya Bwana na Siku za Mwisho (Na. 192). Kuna sehemu takriban ishirini
zinazoitaja Siku ya Bwana (kwa Kiebrania Yom Yahovah) kuna mifano takriban 16 kuanzia
kwenye andiko kama vila Isaya 2:12 (kisha tena Isaya 13:5; Yoeli 1:15; 2:1,11;
3:14; 4:14; Amosi 5:18,20; Obadia 15; Sefania 1:7,14,14; Malaki 4:5). Kwenye vifungu
vinne ni pamoja na neno la Kiebrania la Lamed (yani Sefania 2:12; Ezekieli
30:3; Sefania 14:1,17) ambako ni siku
inayojulikana na Yahova na kwenye sehemu nyingine imejuluishwa na maneno hasira au kisasi.
Kwenye Agano
Jipya imejitokeza mara nne kwenye 1Wathesalonike 5:2, 2Wathesalonike 2:2, 2Petro
3:10, Ufunuo 1:10, na Bullinger anaiona hii kuwa kama kiashirio cha namba nne
na kila kitu kinafanyika ili kumshusha mwanadamu na kumuinua Yahova kwa
matumizi yake na unabii ambao inatokea.
6 na hao waliorudi nyuma, na kuacha kumfuata
Bwana; na hao wasiomtafuta Bwana, wala kumwulizia. 7 Nyamaza
kimya mbele za Bwana MUNGU; Kwa maana siku ya Bwana i karibu; Kwa kuwa Bwana
ameweka tayari dhabihu, Amewatakasa wageni wake. 8 Na
itakuwa, katika siku ile ya dhabihu ya Bwana, nitawaadhibu wakuu, na wana wa
mfalme, na watu wote waliovaa mavazi ya kigeni. 9 Na
katika siku ile nitawaadhibu hao wote warukao juu ya kizingiti, waijazao nyumba
ya bwana wao udhalimu na udanganyifu. 10 Na katika
siku ile, asema Bwana kutakuwako sauti ya kilio kutoka lango la samaki, na mlio
mkuu katika mtaa wa pili, na mshindo mkuu kutoka milimani. 11
Haya! Lieni, ninyi mkaao katika Makteshi, maana wafanya biashara wote
wameangamia; hao wote waliokuwa na mizigo ya fedha wamekatiliwa mbali.
Maandalizi ya
dhabihu ya Bwana yalifanyika na Kristo na utakatifushaji wa Wageni wa Bwana
kulifanyika kwenye Pentekoste ya mwaka 30 BK.
Mwaka 597 KK
walikwenda utumwani huko Babeli kuwaandaa Yuda na kuwarejesha mioyo ili wadumu
hadi Masihi na waingie hukumuni na Kanisa lianzishwe. Kisha Yuda washughulikiwe
kama kanisa lilivyofanyiwa kwa kuchaguliwa na kutolewa kwa kipindi cha yubile
40 tangu mwaka 27 BK hadi 2027 BK. Kipindi cha mwisho kitakuwa ni cha kutoka
kipindi cha Vita vya Mwisho hadi kile cha kumiminwa Vitasa vya ghadhabu chini
ya Masihi kitakachoishia kwenye Siku ya Upatanisho ya mwaka 2024. 2025 utakuwa
ni mwaka wa Mavuno Makuu abato na Yubile ya mwaka 2026 na 2027. Yerusalemu ilitwaliwa
na kisha ikafanwa upya na kisha ikaangamizwa kabla haujaangamizwa kabisa. Dini
ya Kiyahudi ikaanzishwa ikiwa sasa kama dini potofu na ya uwongo na
itaangamizwa pia kati ya mwaka 2015-2024.
12 Kisha itakuwa wakati ule,
nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami nitawaadhibu watu walioganda juu ya sira
zao; wasemao katika mioyo yao, Bwana hatatenda mema, wala hatatenda mabaya. 13 Na huko utajiri wao utakuwa mateka, na nyumba zao
zitakuwa ukiwa; naam, watajenga nyumba, lakini hawatakaa ndani yake; nao
watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.
Siku za Mwisho
haitakuwa na kingine chochote kabla ya hii na hata kama Yerusalemu ilikatiliwa
mbali na wazelote waliwasha uporaji wao na kuharibu Sadaka za Daima kwa mashambulizi
ya Warumi na ndivyo wengi watataabika tena. Tukio kuu moja wapo lilikuwa ni
Mauaji ya kupangwa ya kuwaangamiza Wayahudi yajulikanayo kama Holocaust mwaka
1941-1945. Mungu kwa sasa anashughulika na Mashariki ya Kati na makabila yanayoizunguka
na mataifa kama ilivyokuwa inaenda kwa miaka 2520 tangu kuanguka kwa Hekalu
mwaka 597 hadi mamlaka ya Wapalestina mwaka 1922/23. Mwaka 1922 Palestina
ilikabidhiwa kwa Waingereza (wakati kwamba mwaka 1917 kulishuhudiwa azimio la
Balfour). Mwaka 1948 uhuru wa Israeli ulitangazwa na mwaka 1967 ulishuhudia
Yerusalemu ikifanywa upya na kurejeshwa kwa Yuda chini ya Vita ya Siku Sita.
Hiki ni kipindi kinachowakilisha kile cha maombolezo ya Haruni ba Yerusalemu ukirejeshwa
tena lakini ukuhani wa kweli hauna uthibiti na utaratibu wa ibada za Hekalu
haukuweza kurejeshwa. Hii ilianzisha Kipindi cha Marejesho na kisha Vita vya
Siku za Mwisho vilianza baada ya kipindi cha miaka ya Thelathini ya Mwisho cha
Maombolezo ya Musa kuanza mwaka 1997 baada ya mwisho wa Kipindi cha Wamataifa (Soma
jarida la Kuanguka kwa Misri Kuanguka kwa Misri Sehemu ya II: Vita vya Mwisho (Na.
036_2).)
14 Hiyo siku ya Bwana iliyo kuu
i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya Bwana;
Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko! 15 Siku ile ni
siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya
giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu, 16 Siku
ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu
sana. 17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata
watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao
itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi. 18 Fedha
yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana;
bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu
wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha.
Ni katika wakati huu
Masihi atatumwa kushughulika na wanadamu kwa Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu.
(Soma jarida la Vita vya Siku za Mwisho na Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu (Na. 141B).)
Sura inayofuatia
inashughulikia hali na mwonekano wa watu wa nchi na jinsi wanyenyekevu na
wapole watakavyoirithi nchi. Amri hapa ni kutafuta upole na utakatifu.
Kifuatacho hapo
kinahusu na Gaza na Palestina. Ushughukiaji huu utakuwa ni kutoka Gaza hadi
kaskazini mwa miji ya pwani ya Lebanoni.
Sefania
Sura ya 2
Jikusanyeni, naam, jikusanyeni, Ee taifa lisilo na
haya; 2 kabla haijazaa hiyo amri, kabla haijapita siku
ile kama makapi, kabla haijawajilia hasira kali ya Bwana, kabla haijawajilia
siku ya hasira ya Bwana. 3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote
mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki,
utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya Bwana.
Kwa hiyo, ni
wapole na watakatifu ndio wanalindwa Siku ya Hasira ya Mungu.
Kumbuka majina ya
makundi ya kikabila na kile kitakachotokea na kuwapata. Maelezo haya pia ni kwa
mujibu wa unabii wa wengine wa kundi la Manabii Kumi na Mbili.
Katika Siku za
Mwisho Gaza chini ya Hamas imeleta maangamizi na kulimaliza yenyewe. Ndivyo
ilivyo pia kwa Waashuru na Wababeloni na Waajemi na kisha Warumi walishuka kuja
kushinda na kukaa na ndivyo itakavyokuwa pia katika Siku za Mwisho ndipo hawa
Wapalestina wanaojifanya kuwa Waarabu wataishusha Ghadhabu ya Mungu kuifanya
ije juu yao tena. Machafuko haya yasiyo na maana yataendelea na hayatakoma hadi
Gaza ikiwa tupu na maganjo matupu na Mfalme wa Kaskazini ataitwaa hii na
kutandaza hema yake ya ufalme kama ilivyotabiriwa na nabii Danieli (11:40-45).
Itaenea kutoka Gaza hadi Ashkeloni na Ashidodi na Ekroni haitakuwa na wa
kubakia ndani yake anayeshikilia sasa na nguvu au uweza wa mnyama wa mwisho wa
Mfalme wa Kaskazini ataimiliki Yerusalemu kama tunavyojionea kwenye Danieli.
Mji wa Ekroni ulikuwa
kaskazini kabisa ya Palestina (Joshua 13:3) kilometa 14 mashariki mwanzoni mwa
Bonde la Soreki kuelekea Yerusalemu. Huenda ni mji wa zamani sana katika
Kanaani kama tunavyojionea kutoka kwenye Yoshua 13:3 (na soma kitabu cha Joseph.
Antiq., V.iii.1).
Inaweza kupingwa
kwamba Waashuru chini ya Senikarebu aliutwaa huu na kuwaweka waasi waliouteka
chini ya Hezekia awaue na ndipo ilikomesha mchakato huu lakini hii haikuwezekana.
Andiko hili linazitaja Siku za Mwisho. Eneo hilo kwa hiyo lilikaliwa na Mfalme
wa Kaskazini katika Siku za Mwisho zinazotajwa hapa na kwenye Danieli anaenea
kutoka kusini mwa Gaza hadi kwenye eneo la Ekroni na hadi Yerusalemu.
4 Kwa kuwa Gaza utaachwa, na
Ashkeloni utakuwa ukiwa; wataufukuzia mbali Ashdodi wakati wa adhuhuri, na
Ekroni utang'olewa.
Kundi la Wakerathi ndilo linalotajwa hapa.
5 Ole wao wakaao karibu na
pwani ya bahari, taifa la Wakerethi! Neno la Bwana li juu yenu, Ee Kanaani,
nchi ya Wafilisti; mimi nitakuangamiza, asibaki mtu akaaye kwako.
Andiko hili hapa linataja taifa la Wakerithi.
Wakerithi na Wapalestina walikuwa sehemu ya Jeshi binafsi la Daudi ambao
waliwakusanya na kuwaingiza wageni na waongofu hawa wawili kutoka Ufilisti na
walithibitisha utii wao mkubwa kwake. Walikuwa ni sehemu ya waliomfuata kwenye
msafara wake wakati alipokaa huko Yerusalemu. Benaiya mwana wa Yehoyada alikuwa
kiongozi wao (2Samweli 8:18; 20:23). Wakerithi walikaa kusini mwa Yudea huko
Negebu. Wao ni sehemu ya Wakazi wa pwani ya Bahari na yawezekana kabisa kuwa
hata jina lao limechukuliwa kutoka kwa Wakariti ambao pia waliwahi baadae kuwa
wafanyakazi wa kujitolea kutoka eneo la kaskazini mwa Asia Ndogo. Unabii unawaelezea
watu hawa kuwa huenda ni wa nje ya Ufilisti ya zamani itafanywa upya.
Unabii huu
unayataja maeneo yote ya makundi haya kwenye nyumba ya Yuda na kwamba watakuja
chini ya kundi la kimkoa la Yuda kwenye Muungano wa Kitaifa wa Israeli kwa kipindi
cha Milenia.
6 Na hiyo nchi ya pwani itakuwa malisho, yenye vibanda
vya wachungaji, na mazizi ya makundi ya kondoo. 7 Na
hiyo nchi ya pwani itakuwa nchi ya watu wa nyumba ya Yuda waliosalia; watalisha
makundi yao huko; watalala katika nyumba za Ashkeloni wakati wa jioni; kwa
maana Bwana, Mungu wao, atawajilia na kuwarudisha wafungwa wao.
Unabii huu unaonekana kuwahusu Waashikeloni kwenye
muungano wa taifa la Israeli chini ya Yuda. Bahati za wote zitarejeshwa upya.
8 Mimi nimeyasikia
matukano ya Moabu, na dhihaka za wana wa Amoni, ambazo kwa hizo wamewatukana
watu wangu, na kujitukuza juu ya mpaka wao.
Mabishano ya kikanda ya Wapalestina na kuendelea
kukataa kuwa na amani na kuafikiana kutashuhudia wao walishughulikiwa katika
siku zijazo. Matokeo yake kwenye ujio wa vita ardhi za ukanda wa mashariki
itaangamizwa vibaya sana. Israeli wataikalia na wataunda sehemu pia ya
shirikisho la Israeli.
Andiko lifuatalo kwa kweli linasomeka kuwa “Ni Neno
la Yahova, Mungu wa Israeli.”
9 Basi kama niishivyo, asema Bwana wa majeshi, Mungu
wa Israeli, Hakika Moabu atakuwa kama Sodoma, na wana wa Amoni kama Gomora,
yaani, milki ya upupu, na mashimo ya chumvi, ukiwa wa daima; watu wangu
waliosalia watawateka nyara, na watu wa taifa langu waliobaki watawarithi. 10 Mambo hayo yatawapata kwa sababu ya kiburi chao, kwa kuwa
wamewatukana watu wa Bwana wa majeshi, na kujitukuza juu yao.
Maeneo haya yatabidi kufanywa upya na kiburi cha
Amoni na Moabu kitawashusha chini na kuwafanya duni.
Hazitakuwa na rutuba kama zilivyokuwa hapo zamani wakati
Lutu alipokaa hapo kwanza maeneo hayo. Bado unabii unaonekana kulenga moja kwa
moja kwenye uwezekano wa kuangamizwa kwa miungu ya dunia hii ili kuzinufaisha
nchi hizi.
11 Bwana atakuwa mwenye
kuwatisha sana; kwa maana atawafisha kwa njaa miungu yote ya dunia; na watu
watamsujudia yeye, kila mtu toka mahali pake; naam, nchi zote za mataifa.
Anayetajwa hapa
kuwa “Yeye” ni Masihi akiwa ni Kuhani Mkuu wa Mungu Mmoja wa Kweli na ambaye
ataitiisha dunia na kuitawala sawasawa na unabii wa Sefania 14:16-19 wakati
watakapowatuma wajumbe ambao ni wawakilishi wao kwenda Yerusalemu kila mwaka
kwenye Sikukuu ya Vibanda.
Andiko kwa hiyo
linageukia Kusini kwa Waethiopia na kisha Kaskazini kwa Waashuru. Hii ni kwenye
Vita vya Siku za Mwisho tunajua kwamba Waashuru wanatokea Kaskazini, mkono kwa
mkono na Waisraeli na Waethiopia wanatawaliwa wakati wa Siku za Mwisho kwa
sambamba na Mfalme wa Kaskazini kama walivyo wakazi wa Afrika Kaskazini kutoka
Libya magharibi na kisha kutawaliwa na Masihi.
12 Na ninyi Wakushi pia,
mtauawa kwa upanga wangu. 13 Naye atanyosha mkono wake
juu ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza Ashuru; naye ataufanya Ninawi kuwa
ukiwa, kuwa mahali pakavu kama jangwa. 14 Na makundi
ya wanyama watalala kati yake, wanyama wote wa mataifa; mwari-nyuni na nungu
watakaa juu ya vichwa vya nguzo zake; sauti yao itasikiwa madirishani;
vizingitini mwake mtakuwa ukiwa; kwa maana ameifunua kazi ya mierezi.
Tunaona Ninawi iliangamia lakini hii sio nabii zote
unaihusu Ashuru. Ni vitovu vyao vya ibada za sanamu ndizo zitaangamizwa.
15 Huu ndio mji ule wa furaha, Uliokaa pasipo
kufikiri, Uliosema moyoni mwake, Mimi niko, Wala hapana mwingine ila mimi.
Jinsi ulivyokuwa ukiwa, Mahali pa kulala pa wanyama wa bara! Kila mtu apitaye
atazomea, Na kutikisa mkono wake.
Ni sahihi kwamba
Ninawi iliangamia mwaka 612 KK na kumbukumbu zinaweza kuelekeza kwenye ukaaji
wa mwanzoni wa Ethiopia lakini unabii kuhusu Siku za Mwisho uko wazi. Wakati
Mungu akiungamiza Ninawi ndipo atawarejesha kutoka kaskazini katika Siku za
Mwisho na kuwafanya tena kuwa sehemu ya ushirika wa biashara wa sitini na
Israeli na Misri. Mungu anasema kuwa atawarudisha tena Yuda na Efraimu na
Israeli wote kutoka Misri na kutoka Ashuru kutoka kaskazini na kuwafanya wawe
taifa tena (Zekaria 10:10-11) na watabarikiwa kama washirika wa kibiashara kwenye
utawala utakaoongozwa na Masihi watakapokuwa waneunganishwa na njia kuu kutoka
Misri hadi Ashuru; na Israeli itakuwa mshirika wa tatu wa ushirikiano huu na
baraka za nchi ambayo Bwana wa Majeshi atawabariki akisema, “Israeli atakuwa wa
tatu pamoja na Misri na Ashuru, watakuwa baraka kati ya dunia;”(Isaya
19:23-25).
Mungu kwa hiyo
anaushughulikia Yerusalemu kwenye kifungu hiki cha mwisho.yerusalemu
umelaumiwa. Dini ya kiyahudi haikubali wala kupokea maonyo yoyote kwa kipindi
chote cha miaka 2000 tangu Masihi hadi kuja kwake na maonyo ya mwisho.
Unakaribia sasa kupata ijara yake lakini kwa masharti yanayowekea ukomo mataifa
kwa kile yanachoweza kufanya. Makuhani wa Yuda na Walawi wameihalifu na kuitia
unajisi Kalenda na Agano na wamejiwekea baraza la Talmud na kujitungia sheria
zisemazo mambo ambayo haisemi na wamezipotosha na kuigeuza sheroa.
Sefania
Sura ya 3
Ole wake yeye aliyeasi na kutiwa unajisi, mji wa
udhalimu! 2 Hakuitii sauti; hakukubali kurudiwa;
hakumwamini Bwana; hakumkaribia Mungu wake. 3 Wakuu
wake walio ndani yake ni simba wangurumao; makadhi wake ni mbwa-mwitu wa jioni;
hawasazi kitu cho chote hata siku ya pili. 4 Manabii
wake ni watu hafifu, wadanganyifu; makuhani wake wamepatia unajisi patakatifu,
wameifanyia sheria udhalimu.
Hapa Mungu
anafananisha matendo yake na hali ya wafalme wake, makuhani na manabii wake na
hali zao za kupenda.
5 Bwana kati yake ni mwenye haki; hatatenda
uovu; kila asubuhi hudhihirisha hukumu yake, wala hakomi; bali mtu asiye haki
hajui kuona haya. 6 Nimekatilia mbali mataifa, buruji
zao zina ukiwa; nimeziharibu njia kuu zao, hata hapana mmoja apitaye; miji yao
imeangamizwa; hamna mtu hata mmoja, wala hapana akaaye huko.
Ndipo anawasihi kwamba watubu hakika lakini
hawakutubu.
7 Nalisema, Hakika utaniogopa,
utakubali kurudiwa; ili yasikatiliwe mbali makao yake, sawasawa ya yote
niliyoagiza katika habari zake; lakini waliondoka mapema na kuyaharibu matendo
yao yote.
Andiko hili
hatimaye linaonyesha kwamba atainuka katika siku za mwisho na kushughulika na
mataifa yote na kwa hiyo hatuna mashaka kwamba andiko hili linamtaja Masihi.
Hivi ni Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu vilivyoandikwa kwenye kitabu cha Ufunuo.
8 Basi ningojeni, asema Bwana,
hata siku ile nitakapoondoka kuteka mateka; maana nimeazimia kuwakusanya
mataifa, ili nizikutanishe falme, nipate kuwamwagia ghadhabu yangu; naam, ukali
wote wa hasira yangu; kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa wivu wangu.
Kisha Mungu atazibadili lugha za mataifa na kuwa
ndimi safi zisemazo kweli na kisha atawashughulikia mataifa.
9 Maana hapo ndipo
nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la Bwana,
wamtumikie kwa nia moja.
Tunaona hapa kwenye andiko hili kwamba atayarudia
yale aliyoyasema kwenye sura zilizopita kuhusu Waethiopia na kwa wale wote
wanaomrudia yeye kutoka nchi zilizo mbali na mipaka ya Ethiopia na Afrika yote
na mbele ya mipaka yake.
10 Maana toka nchi iliyo mbali
na mito ya Kushi, waniombao dua, yaani, binti za watu wangu waliotawanyika,
wataleta matoleo yangu. 11 Siku ile hutatahayarikia
matendo yako yote uliyoniasi; maana hapo nitawaondoa watu wako wanaotakabari na
kujivuna, wasiwe kati yako, wala hutatakabari tena katika mlima wangu
mtakatifu. 12 Lakini nitasaza ndani yako watu
walioonewa na maskini, nao watalitumainia jina la Bwana. 13 Mabaki
ya Israeli hawatatenda uovu, wala kusema uongo; wala ulimi wa hadaa
hautaonekana kinywani mwao; kwa maana watakula na kulala, wala hapana mtu
atakayewaogofya. 14 Imba, Ee binti Sayuni; piga
kelele, Ee Israeli; Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, Ee binti
Yerusalemu. 15 Bwana ameziondoa hukumu zako, Amemtupa
nje adui yako; Mfalme wa Israeli, naam, yeye Bwana, yu katikati yako; Hutaogopa
uovu tena. 16 Katika siku ile Yerusalemu utaambiwa,
Usiogope, Ee Sayuni; mikono yako isilegee. 17 Bwana,
Mungu wako, yu katikati yako shujaa awezaye kuokoa; Atakushangilia kwa furaha
kuu, Atakutuliza katika upendo wake, Atakufurahia kwa kuimba. 18 Nitawakusanya wanaousikitikia mkutano wa ibada, hao
waliokuwa wa kwako; ambao mzigo uliokuwa juu yake ulikuwa fedheha kwao. 19 Tazama, wakati huo nitawapatiliza watu wote wanaokutesa;
nami nitamponya yeye achechemeaye, nami nitamkusanya yeye aliyefukuzwa; nami
nitawafanya kuwa sifa na jina, hao ambao fedheha yao ilikuwa katika dunia yote.
20 Wakati huo nitawaingizeni, na wakati huo
nitawakusanya; kwa maana nitawafanya ninyi kuwa sifa na jina, miongoni mwa watu
wote wa dunia, nitakapowarudisha wafungwa wenu mbele ya macho yenu, asema
Bwana.
Ni kwa wakati huu
ambapo Mungu, kwa kupitia Masihi na wateule, watamkusanyikia yeye aliye
mwaminifu na na kuongea naye maneno mazuri kwa lugha mpya kwamba amewaondolea
maafa na aibu yao. Kwenye andiko hili tunauona unabii kwenye Isaya 65:17-25 ambapo
Mungu anaahidi kuzifana mbingu mpya na nchi mpya kwakuwa zitakuwa zimeharibika
kwa hali yake yenyewe ya hewa na mazingira na ndivyo itakuwa hata kwa dunia yote
na bahari zake zote.
q