Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[031B]
Bwana wa Sabato
(Toleo La 1.5 20101204-20101207)
Jina au Cheo cha Bwana wa Sabato kama linavyommaanisha
Kristo, mara nyingi limepotoshwa na imani ya Kikristo kwa hila yenye lengo la
kuuwezesha mfumo wao wa kiimani wa Kiantinomia ufanikiwe vyema. Maana yake
halisi na iliyokusudiwa imepotoshwa kabisa na kuwa kinyume chake. Kristo
alijitangaza mwenyewe kuwa ni Bwana wa Sabato akimaanisha kuvuta hisia ya
kwamba ataiendelewa Sabato na kuipa nguvu zaidi Amri ya Nne pamoja na Sabato
zake, Miezi Mipya na Sikukuu zote wakati atakapokuja pasipo kuzipotosha wala
kuzibadilisha, wala pasipo kuingiza ibada za sanamu na mapokeo.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 2010 Wade
Cox)
(tr. 2016)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na
tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.
Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala
yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia
yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Kuna sehemu mbili kwenye injili ambapo Kristo alijitangaza mwenyewe kuwa
yeye ni Bwana wa Sabato.
Waantinomia ambao ni waabudu Miuingu ya Jua wanashikilia kuamini kwamba usemi
huu ulimaanisha kuwa Kristo aliruhusu kubadilika kwa Sabato na kuwa Jumapili
kwenye imani ya Kikristo na kwamba alizitangua Sabato za Biblia na kuzirihusu
au kuzipa nafasi siku nyingine za kuabudu mungu Junna miungu mingine ya Kisirisiri,
kwamba ziingizwe tu na zchuiue nafasi ya Sabato za kwenye Biblia. Upotoshaji
huu wa makusudi unapasa ubadilishwe kabisa na kukanushwa.
Hebu na tutafakari kile alichokisema Kristo na tulione jambo hili kwenye maandiko
mengine linamaanisha nini. Hiki ndicho kwa hakika alichokisema Kristo na
mazingira yalivyokuwa hadi ikampelekea aseme hivyo:
Marko 2:23-28 Ikawa alipokuwa akipita mashambani siku ya sabato, wanafunzi wake
walianza kuendelea njiani wakivunja masuke. 24 Mafarisayo
wakamwambia, Tazama, mbona wanafanya lisilokuwa halali siku ya sabato? 25 Akawaambia, Hamkusoma popote alivyofanya Daudi, alipokuwa
ana haja, na kuona njaa, yeye na wenziwe? 26 Jinsi
alivyoingia katika nyumba ya Mungu, zamani za kuhani mkuu Abiathari, akaila
mikate ile ya Wonyesho, ambayo si halali kuliwa ila na makuhani, akawapa na
wenziwe? 27 Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya
mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato. 28 Basi
Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia.
Luka 6:1-5 Ikawa siku ya sabato moja alikuwa akipita katika mashamba, wanafunzi wake
wakawa wakivunja masuke na kuyala, wakiyapukusa-pukusa mikononi mwao. 2 Basi baadhi ya Mafarisayo wakawaambia, Mbona
mnafanya lisilo halali siku ya sabato? 3 Yesu akawajibu akawaa mbia, Hamkulisoma hata hilo
alilolifanya Daudi, alipokuwa na njaa, yeye na wale aliokuwa nao? 4 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, akaitwaa
mikate ile ya Wonyesho, akaila akawapa na hao wenziwe, ambayo si halali kuila
ila kwa makuhani peke yao. 5 Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.
Vifungu hivi kimsingi vinafanana tu na vinamaana moja hiyohiyo kusuduwa na
ujumbe wake ulikuwa unaelekezwa moja kwa moja kwa makuhani na mazingira ambayo
kisa hiki cha Sabato kilivyotumiwa na Kristo kwa makusudi ambayo kwayo iliwekwa
tanngu mwanzo.
Ni Kristo ndiye aliyejitangaza mwenyewe kuwa ni Mwana wa Adamu, na pia kuwa
ni Bwana wa Sabato. Na ndipo alielekeza moja kwa moja hoja zake kwa Daudi
ambaye ni mkate wa wonyesho na ndipo alipofuatia kujitangaza kwake mwenyewe
kuwa ni Bwana wa Sabato. Tendo hili halina udhuru kwa mstari wote mzima wa
m6l6olon6go wa mambo.
Zekaria 12:8 inasema kwamba Daudi na watu wote wa nyumbani mwake ambao ni
wateule watakuwa elohim kama Malaika wa Yahova vichwani mwao. Kwa hiyo alikuwa
anajitangaza mwenyewe kuwa ni elohim wa Israeli na kichwa cha ukuhani wa
Melkizedeki ambapo kwayo alijitangaza kuwa ni Kuhani Mkuu (soma Waebrania sura
za 4-10).
Vigezo vya kuwa Kuhani Mkuu wa mfano wa Melikizedeki vinawafanya wale wote
walio kwenye Mwili wa Kristo waweze kufanyika kuwa wafalme na makuhani
watakaotawala pamoja na Kristo kwa mfano wa Melikizedeki.
Vigezo vha kuwa mfano wa Melkizdeki ndio kigezo cha makuhani walio chini
yake ili wafae kuwa ni makuhani pamoja na yeye.
Maandiko ya Biblia yanatazama mbele kuiashiria siku hiyo na kuuelezea
mazingira na utawala ambayo kwamba wateule wake Mungu wakiwa kama makuhani
watakaokuwa chini ya Kristo watahudumu na kwa kweli, jinsi Kuhani Mkuu wa mfano
wa Melkizedeki atakapojipangia majukumu na kuwapangia majukumu makuhani majukumu
yao watakaohudumu kipindi hiki na utaratibu wa ibada.
Kwa mtazamo huo, ndipo yeye ni Bwana wa Sabato na atawapangia makuhani wake
majukumu ya kushughulikia mambo yote yahusuyo maadhimisho ya Sabato zote, sawasawa
na ilivyoamriwa kuadhimishwa kwenye Maandiko Matakatifu. Hivyo basi, maongozi
na maelekezo ya Kristo akiwa kama Bwana wa Sabato yanajiri na kama
ilivyokusudiwa wakati zilipoanzishwa Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya na Sikukuu
zilizoamriwa na kuagizwa kwenye Maandiko Matakatifu, na Kristo pia alisema kuwa
Maandiko hayawezi kutanguka. Kwenye maandiko ya Yohana 10:34-35 alisema pia
kwamba: “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu (Zaburi) ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu? 35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu;
(na maandiko hayawezi kutanguka);”
Kwa hiyo, wateule watafanyika kuwa elohim na taifa la wafalme na makuhani.
Wote watajumuishwa kutumika pamoja na huyu Bwana wa Sabato na kwa kufanya kwao
hivyo, watakuwa wanaendeleza maadhimisho ya Sabato ulimwenguni.
Pia wataanzisha zama za utawala ambao maongozi na maagizo yake yote
yatatokea Yerusalemu.
Zekaria 14:1-21 Tazama, siku
moja ya Bwana inakuja, ambayo mateka yatagawanyika kati yako. 2 Kwa maana nitawakusanya mataifa yote walete vita
juu ya Yerusalemu; na huo mji utapigwa, nazo nyumba zitatekwa, nao wanawake
watatendwa jeuri; na nusu ya watu wa mji watatoka kwenda utumwani; ila mabaki
ya watu wa mji hawatakatiliwa mbali. 3 Hapo
ndipo atakapotokea Bwana, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana
zamani siku ya vita. 4 Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya
mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa
Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi;
litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande
wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini. 5 Nanyi mtakimbia kwa njia ya bonde la milima yangu;
kwa maana bonde lile la milima litaenea hata Aseli; naam, mtakimbia, kama vile
mlivyokimbia mbele ya tetemeko la nchi, siku za Uzia, mfalme wa Yuda; na Bwana,
Mungu wangu, atakuja, na watakatifu wote pamoja naye. 6 Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba nuru yake
haitakuwa na mwangaza na kiwi; 7 lakini
itakuwa siku moja, iliyojulikana na Bwana; si mchana, wala si usiku; lakini
itakuwa, ya kwamba wakati wa jioni kutakuwako nuru. 8 Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba maji yaliyo hai
yatatoka katika Yerusalemu; nusu yake itakwenda upande wa bahari ya mashariki,
na nusu yake upande wa bahari ya magharibi; wakati wa hari na wakati wa baridi
itakuwa hivi. 9 Naye
Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina
lake moja. 10 Nchi yote itageuzwa kuwa kama Araba, toka Geba
mpaka Rimoni upande wa kusini wa Yerusalemu; naye atainuliwa juu, atakaa mahali
pake mwenyewe, toka lango la Benyamini mpaka mahali pa lango la kwanza, mpaka
lango la pembeni; tena toka mnara wa Hananeli mpaka mashinikizo ya mfalme. 11 Na watu watakaa ndani yake, wala hakutakuwako
laana tena; lakini Yerusalemu utakaa salama. 12 Na hii ndiyo tauni, ambayo Bwana atawapiga watu
wote waliofanya vita juu ya Yerusalemu; nyama ya mwili wao itaharibika,
wasimamapo juu ya miguu yao, na macho yao yataharibika ndani ya vichwa vyao, na
ndimi zao zitaharibika vinywani mwao. 13 Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba mashaka makubwa
yatokayo kwa Bwana yatakuwa kati yao; na kila mmoja wao atakamata mkono wa
jirani yake, na mkono wake utainuliwa ili kushindana na mkono wa jirani yake. 14 Yuda naye atafanya vita juu ya Yerusalemu; na huo
utajiri wa mataifa wa pande zote utakusanyika, dhahabu, na fedha, na mavazi;
vitu vingi sana. 15 Na hivyo ndivyo itakavyokuwa tauni ya farasi, na
nyumbu, na ngamia, na punda, na ya hao wanyama wote watakaokuwamo matuoni mle,
kama tauni hiyo. 16 Hata itakuwa, ya kwamba kila mtu aliyesalia wa
mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu, atakwea mwaka baada ya mwaka
ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, na kuishika sikukuu ya Vibanda. 17 Tena itakuwa, ya kwamba mtu awaye yote wa jamaa
zote zilizomo duniani, asiyekwea kwenda Yerusalemu ili kumwabudu Mfalme, Bwana
wa majeshi, mvua haitanyesha kwao. 18 Na
kama jamaa ya Misri hawakwei, wala hawaji, pia haitanyesha kwao; itakuwako
tauni, ambayo Bwana atawapiga mataifa, wasiokwea ili kushika sikukuu ya
Vibanda. 19 Hii ndiyo adhabu ya Misri, na adhabu ya mataifa
yote, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda. 20 Siku hiyo katika
njuga za farasi yataandikwa maneno haya, WATAKATIFU KWA Bwana; navyo vyombo
vilivyomo ndani ya nyumba ya Bwana vitakuwa kama mabakuli yaliyoko mbele ya
madhabahu. 21 Naam, kila chombo katika Yerusalemu, na katika
Yuda, kitakuwa kitakatifu kwa Bwana wa majeshi; nao wote watoao dhabihu
watakuja kuvitwaa vile vyombo, na kutokosa nyama ndani yake; wala siku hiyo
hatakuwamo tena mfanya biashara ndani ya nyumba ya Bwana wa majeshi.
Ni wazi na dhahiri sana
tu kwamba kutokana na aya za 16-19 kwamba Bwana wa Sabato ataamuru kuwe na
msisitizo wa kuziadhimisha Sabato za Mungu.
Mapatilizo au adhabu
itakayowakumba watu kwa kutoziheshimu amri na maagizo haya yatakuwa ni kukumbwa
kwa baa la njaa na tauni ya Misri ili kwamba kama unadhani kuwa unaweza kuepukana
na baa hili kali la njaa kwa kutumia mbinu za kilimo cha umwagiliaji au kwa
kuhifadhi chakula kingi kwenye maghala utakatishwa tamaa sana. Kwa kuwa utauawa
kwa mapigo ya magonjwa.
Pia atasisitiza
maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi Mpya sambamba na Sabato kama tunavyojionea kwenye
andiko la Isaya 66:23, na kwenye aya ya 24 tunaona kuwa wanalazimishwa kwa
adhabu ya kifo.
Isaya 66:23-24 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato
hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana. 24 Nao watatoka nje na
kuitazama mizoga ya watu walioniasi; maana funza wao hatakufa, wala moto wao
hautazimika nao watakuwa chukizo machoni pa wote wenye mwili.
Jinsi pekee ambayo
Waantinomia wanaweza kuyakeepa maandiko haya yaliyo wazi sana ni kwa mbinu za
kulipotosha Agano la Kale na kudai kwamba Kristo, kwa kusema kwake kuwa yeye ni
Bwana wa Sabato, alikuwa anamaanisha kuwa anamamlaka ya kuitangua na akaziweka
siku nyingine za Miungu ya Kisirisiri ya Jua. Bali hata hivyo, tatizo
linaendelea kubaki kuwa kwamba Mungu alinena kwa kupitia watumishi wake manabii
na akasema kuwa Sabato zitashurutishwa kwa kuwekewa hukumu ya kifo. Kila
mwanadamu ambaye hatatubu atapigwa kwa mapigo wakati wa kurejeshwa na
kusisitizwa kwa sheria hizi na atakufa.
Shetani ni mungu wa
dunia hii (2Wakorintho 4:4) na hivyo anauwezo wa kushurutisha imani yake ya kidini
hadi atakaporudi tena Kristo. Waantinomia ni sehemu ya itikadi na mifumo ya
dini potofu na za uwongo zinazotokana na dini za kishetani za waabudu muingu ya
Siri ya Jua ya mungu wa Utatu. Wamejaribu kupingana na sheria na kuweka
ushawishi wao kwa watu kuzipinga na kuzikataa au kuzipuuza sheria au torati ya
Mungu na utaratibu aliouwaka Mungu wa ibada, kazi walioendelea kuifanya kwa
kipindi cha takriban miaka elfu sita iliyopita, lakini bila ya mafanikio, na
kwa kipindi kingine cha takriban miata elfu mbili wakijifanya kama Wakristo au
wakiitumia dini hii. Hawataweza kushinda au kufanikisha mkakati wao na muda
uliobakia na mfupi sana.
Pia unabii wa Mungu,
aliomtumia nabii wake Ezekieli, kuhusu Marejesho na Matengenezo mapya. Unabii
huu unaonyesha utawala wa haki wa mizani na vipimo, na kuwekwa mwa msisitizo wa
maadhimisho ya Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya, na Sikukuu zilizoamriwa kwenye
kipindi cha utawala wa mfalme. Ni wajibu wa mfalme kuainisha na kusisitiza
umuhimu wa kuziadhimisha Sabato na sheria ya ulaji wa vyakula kwa kila mmoja
wao kwenye kipindi chote cha matengenezo na marejesho mapya. Ni marejesho mapya
ya Nchi iliyo Ahidiwa, kwa nyakati zote mbili, yaani za kabla na wakati wa
utawala na kipindi cha marejesho ya milenia.
Utaratibu na imani hii
ya kidini vitasisitizwa na kuadhimishwa kikamilifu na Kristo wakati atakapokuja
hapa na wateule watalazimika kuwajibika kufanikisha mkakati wa kushika
maadhimisho haya na utaratibu wake .
Ezekieli 45:1-25 Tena, mtakapoigawanya nchi kwa
kura iwe urithi, mtamtolea Bwana toleo, sehemu takatifu ya nchi, urefu wake
utakuwa urefu wa mianzi ishirini na tano elfu, na upana wake elfu kumi; itakuwa
takatifu ndani ya mipaka yake yote pande zote. 2 Katika hiyo itakuwako
sehemu kwa mahali patakatifu, urefu wake mia tano, na upana wake mia tano,
mraba pande zote; na dhiraa ishirini kwa viunga vyake pande zote. 3 Na
kwa kipimo hicho utapima, urefu wa ishirini na tano elfu, na upana wa elfu
kumi; na ndani yake patakuwa patakatifu, palipo patakatifu sana. 4 Hiyo
ni sehemu takatifu ya nchi; itakuwa ya makuhani, wahudumu wa patakatifu,
wakaribiao kumhudumia Bwana; nayo itakuwa mahali kwa nyumba zao, na patakatifu
kwa mahali patakatifu. 5 Tena urefu wa ishirini
na tano elfu, na upana wa elfu kumi, ni sehemu ya Walawi, wahudumu wa nyumba,
iwe milki yao wenyewe kwa vyumba ishirini. 6 Nanyi mtaiandika milki
ya mji, upana wake elfu tano, na urefu wake ishirini na tano elfu, kandokando
ya mahali palipotolewa, iwe sehemu takatifu; nayo itakuwa ya nyumba yote ya
Israeli. 7 Na sehemu itakayokuwa ya mkuu itakuwa upande huu, na upande huu, wa
toleo takatifu, na wa milki ya mji, kulikabili toleo takatifu, na kuikabili
milki ya mji, upande wa magharibi kuelekea magharibi, na upande wa mashariki
kuelekea mashariki; na kwa urefu wake sawasawa na sehemu mojawapo, toka mpaka
wa magharibi hata mpaka wa mashariki. 8 Katika nchi hiyo itakuwa
milki kwake katika Israeli; wala wakuu wangu hawatawaonea watu wangu tena
kabisa; bali watawapa nyumba ya Israeli nchi hiyo, kwa kadiri ya makabila yao. 9 Bwana
MUNGU asema hivi; Na iwatoshe ninyi, enyi wakuu wa Israeli; ondoeni dhuluma na
unyang'anyi; fanyeni hukumu na haki; ondoeni kutoza kwa nguvu kwenu katika watu
wangu, asema Bwana MUNGU. 10 Mtakuwa na mizani ya
haki, na efa ya haki, na bathi ya haki. 11 Efa na bathi zitakuwa
za kipimo kimoja; ili kwamba bathi ichukue sehemu ya kumi ya homeri, na efa
sehemu ya kumi ya homeri; kipimo chake kitakuwa kwa kadiri ya cheo cha kawaida
cha homeri. 12 Nayo shekeli itakuwa gera ishirini; shekeli tano zitakuwa shekeli tano,
shekeli kumi zitakuwa kumi, na shekeli hamsini zitakuwa mane yenu. 13 Toleo
mtakalotoa ni hili; sehemu ya sita ya efa katika homeri moja ya ngano, nanyi
mtatoa sehemu ya sita ya efa katika homeri ya shayiri; 14 na
sehemu ya mafuta iliyoamriwa, katika bathi ya mafuta, itakuwa sehemu ya kumi ya
bathi katika kori moja, ambayo ni bathi kumi, yaani homeri; maana bathi kumi ni
homeri moja; 15 na mwana-kondoo mmoja wa kundi katika mia mbili, katika malisho ya
Israeli yenye maji; kwa sadaka ya unga, na kwa sadaka ya kuteketezwa, na kwa
sadaka za amani, ili kuwafanyia upatanisho, asema Bwana MUNGU. 16 Watu
wote wa nchi watatoa toleo hili kwa ajili ya mkuu katika Israeli. 17 Tena
itakuwa kazi ya mkuu kutoa hizo sadaka za kuteketezwa, na sadaka za unga, na
sadaka za vinywaji, katika sikukuu, na katika mwezi mpya, na katika sabato,
katika sikukuu zote za nyumba ya Israeli zilizoamriwa; atatengeneza sadaka ya
dhambi, na sadaka ya unga, na sadaka ya kuteketezwa, na sadaka za amani, ili
kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli. 18 Bwana MUNGU asema hivi;
Mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utatwaa ng'ombe mchanga mume
mkamilifu; nawe utapatakasa mahali patakatifu. 19 Na kuhani atatwaa
baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi, na kuitia juu ya miimo ya milango ya
nyumba, na juu ya pembe nne za daraja ya madhabahu, na juu ya miimo ya lango la
ua wa ndani. 20 Nawe utafanya vivyo hivyo katika mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi
kwa ajili ya kila mtu akosaye, na kwa ajili ya mtu aliye mjinga, ndivyo
mtakavyoifanyia nyumba upatanisho. 21 Mwezi wa kwanza, siku
ya kumi na nne ya mwezi, mtakuwa na Pasaka, sikukuu ya siku saba; mkate
usiotiwa chachu utaliwa. 22 Na siku hiyo mkuu
atatengeneza ng'ombe kuwa sadaka ya dhambi, kwa ajili ya nafsi yake, na kwa
ajili ya watu wote wa nchi. 23 Tena, katika zile siku
saba za sikukuu atamtengenezea Bwana sadaka ya kuteketezwa, ng'ombe saba na
kondoo waume saba wakamilifu, kila siku kwa muda wa siku saba, na beberu mmoja
kila siku kuwa sadaka ya dhambi. 24 Naye atatengeneza
sadaka ya unga, efa moja kwa ng'ombe, na efa moja kwa kondoo mume, na hini moja
ya mafuta kwa efa moja; 25 katika mwezi wa saba,
siku ya kumi na tano ya mwezi, katika sikukuu atafanya vivyo hivyo kwa muda wa
siku saba; sadaka ya dhambi vivyo hivyo, na sadaka ya kuteketezwa vivyo hivyo,
na sadaka ya unga vivyo hivyo, na mafuta vivyo hivyo.
Hakuna kilicho tofauti au kipya na kilicho kinyume na Maandiko Matakatifu
kwenye mwendelezo wa mfumo na imani hii. Kudhania kama wanavyofanya
Waantinomia, kwamba Kristo alimpa sheria au torati Musa huko Sinai na kuikazia
kwa hukumu ya kifo, ambayo aliitoa na kuisisitiza kwenye baraza la Sanhedrin, na
kisha aitangue, ni dhana ya kipuuzi. Alikuwa ni Musa aliyewachagua wazee kwa
utaratibu wa 70 (+2) ili wasimamie mambo yahusuyo utoaji wa hukumu. Aliwafukuza
na kuwapeleka utumwani kama taifa kwa nyakati kadhaa vipindi tofauti kwa sababu
walizivunja sheria zake zihusuzo maadhimisho ya Yubile na maadhimisho ya Sabato.
Kisha, wakati Kristo alipofanyika kuwa mwanadamu, alizitunza pia Sabato,
Miandamo ya Mwezi Mpya na Sikukuu zilizoamriwa kikamilifu na kwa kuziangalia sana
ili zisivunjwe wala kupotoshwa na pia ndivyo walivyofanya mitume wake pia.
Makanisa ya Mungu nayo yalizishika pia Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya na
Sikukuu zilizoamriwa na wakipitia kipindi cha machungu mengi ya kifo na mateso
kwa kipindi cha takriban milenia mbili.
Na ndivyo ilivyokuwa pia kwa Yuda, ingawa walikuwa wameipotoa kwa
kuichanganya na mapokeo ambayo Kristo aliwakemea kwayo.
Wateule wameithibisha imani yao na kuishikilia hadi kufa kwa kipindi cha
milenia mbili, na wale wote waliofariki dunia, watafufuliwa na kuendelea
kuusisitizia utaratibu na imani ya Biblia kwa fimbo ya chuma kwa kipindi cha
miaka elfu moja kwa wote waliohai, na kisha kwa kipindi kile cha miaka 100 ya
mwisho, ambacho ni cha Ufufuo wa Pili wa wafu, utakaowakumba watu wote
waliowahi kuishi usoni pa dunia kwa kipindi chote cha kudumu kwake.
q