Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

 

[021F]

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu cha Mika

 (Toleo La 1.0 20150107-20150107)

 

Mungu aliwatumia Mika na Isaya kutoa unabii unaofanana mmoja baada ya mwingine. Nabii Isaya anafuatiwa na Mika takriban miaka kumi na saba baadae na jinsi unabii wao unavyofanana imeelezewa kwenye kurasa za nyongeza za jarida hili. Kwa hiyo, Amosi, Hosea na Isaya walimtangulia Mika na muundo wote mzima wa mpangilio wa unabii unaojiri kutoka kipindi cha utumwa wa Waashuru hadi katika Siku au Ntakati za Mwisho na kurudi wa Masihi na kuanza kwa utawala wa Milenia.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2015 Wade Cox)

(tr 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Ufafanuzi wa Kitabu cha Mika


Utangulizi

Nabii Mika alitokea kwenye ukand wa nyanda za chini wa Shefela karibu na mpaka wa Wafilisti. Alihudumu kutoa unabii wakati wa utawala wa wafalme Yothamu, Ahazi na Hezekia (739-693 KK). Alikuwa mdogo kwa manabii wenzake waliohudumu wakati mmjo kina Hosea na Amosi (soma Soncino ukurasa wa 153).  Mika ana mengi ya msingi pamoja na manabii wawili waliomtangulia na tunaona kutoka kwenye maandiko kwamba aliulaumu utaratibu na makuhani na ushawishi au kwa walivyovutiwa na dini za waabudu Jua ya Baali na unabii kwa jinsi Mngu anavyowashughulikia Israeli. Isaya anafananishwa na Mika kwenye ukurasa wa nyongeza.

 

Muundo wa uandishi wa kitabu

Kitabu cha Mika kama vilivyo vya manabii wote wengine kinajumuisha muundo mkuu wa ukemeaji na mapatano kwa uande mmoja na kisha kuwafariji na kuwaahidi kwa upande mwingine. Sura za 1-3 (isipokuwa kwenye aya mbili) kunahusisha makemeo ya dhambi na tangazo la hukumu. Sura za 4 na 5 zina maneno ya matumaini nay a hamasa na sura za 6-7 zina mambo mawili. Wakosoaji wa siku hizi wanadai kuwa kazi ilikusanywa na nabii au wafuasi wake kwa utaratibu wenye mashiko zaidi ya utaratibu wenye mpangilio na ulio sawa na pale walipokuwa wametolewa.  

 

Kama tulivyoona kutoka kwa mwingine kati ya manabii Kumi na mbili utaratibu kwa kweli unahusiana na yatakayofanyika siku zijazo ya Mungu na Waisraeli na Yuda na sasa inampasa Mungu kushughulikia na watu kwenye historia nzima hadi kwenye Nyakati za Mwisho na Ujio wa Masihi na kwenye matukio mwngine hadi kufikia kwenye kiindi cha millennia, Amosi na Hosea ni watangulizi kwenye utiisho na urejesho mpya wa taifa. Waandishi wa tafsiri ya Soncino waliona kuwa ufafanuzi haukuwa sahihi na kuuliza, kwa mfano, kwa nini tuna tafsiri nyingi kwa ghafla na mabadiliko ya maana halisia ambayo hayakuwa yametarajiwa kwenye mpangilio wa kiutunzi. Wanauliza, kwa mfano, ni kwa nini kuna mapatano na aya za utumwani 9 nk. Miongoni mwa unabii wa Masihi wa sura ya 4. Tutaona kwa nini hili linatokea kadiri tunavyoendelea.

 

Pia wanauliza swali ya kuwa kwa nini kulikuwa na maonyo au hasira kwenye sura ya 6:9-7:6 ambayo haikujumuishwa na maonyo au hasira kwenye sura 1-3. Jibu ni kwamba zinahusiana na nyakati nyingine na kujikita kwenye dhambi nyingine za taifa. Mungu huliadhibu taifa kwa viwangi vya kurudiarudia kwa mfululizo.  Hata hivyo, makuhani wanafundisha kwa nia ya kujipatia mshahara kama tunavyoona na wanalaumiwa na Mungu kwa ajili hii. Utaratibu wa unabii uliangiliwa kwa utaratibu ambao Mungu aliouweka kwao kwa nabii na kurejesha kwenye mlolongo wa hukumu na ufumbuzi uliopo mbele kwenye karne ishirini na nane nyingine.

 

Kipindi cha unabii

Kwenye karne ya nane KK, Israeli ilifanyika kuwa taifa lenye mafanikio sana kutokna na misingi iliyowekwa na Yeroboamu II (mwaka 783-743) kwa amani na usalama wa Israeli na kuanzishwa na Uzia (778-740 KK) kwa Yuda.

 

Walitawala kutoka Damascus hadi Bahari ya Shamu na kutoka kwenye bahari ya Mediterranean hadi kwenye Jangwa la Waebrania kisha waliamuru kufanyika kwa misafara mirefu ya kibiashara za wakati ule.

 

Hata hivyo, waliharibiwa na dhambi na hali ya kutojali maagizo ya torati ya Mungu na uwezo wa kimaono, hisani, na upendano wa ndugu. Sheria ziliyoagizwa kwenye Biblia za ardhi ambazo zinahaikikishia jamii ya wapenda usawa zilipuuziwa na jamii iligawanyika kwenye makundi ya madaraja ambayo Biblia imewalinda watu kutoka kuwa hivyo. Marajiri walizijenga nchi kwa msaada wa mahakama zilizobobea na kuharibika kwa ufisadi. Walijenga nyumba kwa nyuma na shamba kwa shamba kama walivyokatazwa kufanya na jamii iliashiria maovu yote tunayoyaona kwenye jamii zetu sasa kwenye nakati hizi za mwisho. Hakukuwa na kuwafidia kwa masikini.

 

Miji ilijengwa na wasio na ardhi walilazimishwa kuwa hmo kwa kutafuta maisha, kama ilivyo leo. Utajiri na anasa viliishi kimkabala na dhambi na vibarua na maskini walikuwa anawasifu kwa sababu ya hii.

 

Utaratibu wa biashara uliletwa pamoja nayo miungu ya uwongo ya wapagani hasahasa kutoka kaskazini na imani ya mchanganyiko wa Kiashuru na Kibabeloni na pia ya Kimisri. Baali na Ashtorethi (au Ishtar) aliishambulia Israeli na kulichanganya taifa hili lote na imani ya utajirisho wa biashara iliyofanyika na kuletwa.

 

Kuitwa kwa Mika

Kutokana na dhambi hii Mungu aliwachagua manabii hawa; Amosi, Hosea, Isaya na kisha Mika. Alimchagua Mika ambaye alikuwa ni mwananhi mzawa na akampa ujumbe sio kwa ajili ya ibada za sanamu tu bali zaidi sana kwa ajili ya uvunjaji wa maagizo ya torati au sheria za Mungu mambo yaliyoharibu upande wa nchi na utaratibu mahalia wa Sheria au Torati ya Mungu. Mika aliathirika kwa kiasi kikubwa sana kwa matendo ya wananchi wenzake na kwa mateso na uharibifu au upotoshaji ambayo kwamba jamii yenye tamaa ya tajiri iliwatesa watu wao wenyewe.

 

Aliona kwamba jamii iliyojengwa kwenye vitisho, ufisadi au dhuluma na viwango visivyolingana vya afya na vya uwongo iliangamizwa na Mungu na maangamizo na huu ulikuwa ni ujumbe ambao aliaminiwa kwao. Mika hakuelekezwa dhidi ya ibada za sanamu na mavuguvugu ya kisiasa lakini zaidi sana ni kwa kupitia Mika, Mungu anawakemea wanaowavunja moyo wengine kwa kutumia utajiri ambao unaathiti na kuharibu kiini au chanzo kikubwa cha mahali pa muhimu au pa lazima wa mwanadamu na Mungu tangu mwanzoni. Mika ametumiwa na Mungu kushambulia hali hii bandia ya jamii iliyoharibika na kuchanganyikiwa. Kwa kupitia Mika Mungu anakemea unyang’anyi au utaifishaji wa nyumba zote na nchi zote, matumizi mabaya ya sheria kwa kuwanyang’anya au kuwapora wenyeji asilia, upotoshaji wa haki ya wadai madeni na haki kuwadhulumu masikini na udhalimu wa watawala na mahakimu na hali ya kustusha ya makuhani na manabii na ulaji wa rushwa na kujipatia utajiri kwa kujipendekeza kwa kuwasifia mno matajiri. 

 

Hapa ndipo Mungu alipowatumia Amosi na Hosea kuelezea uwezo wa Israeli na Yuda na ibada zao za sanamu na ukengeufu, alimtumia Mika kukemea kwa nguvu ufisadi na uharibifu wao huu wa matengenezo ya kijamii kwa kutumia vibaya muundo wao wa kijamii na maagizo yaliyotolewa kwa sheria na torati ya Mungu. Ni kama ilivyokuwa kwa miaka 2800 iliyopita ndivyo ilivyo sasa vibaya au vibaya zaidi na Yuda na Israeli na utaratibu wao wa kijamii potofu na isiyo matumaini kabisa na sifa au tofauti za matajiri kwa maskini. Mabenki yaliichukua nchi na ili wasiwe na haki kuichukua kwa sheria za Mungu. Utajiri ilimiliki ya raslimali za watu ambazo ulipewa kurithi wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Waliumiliki utajiri huu kwa njia za wizi na ufisadi. Asilimia 10 ya watu wa daraja la juu humiliki takriban asilimia 80 ya utajiri wa nhi ya Marekani. Ndivyo hata ilivyokuwa katika siku za Mika na ndivyo ilivyo hata sasa na kile kilichosemwa na Mungu na kisha kwa kupitia Mika zilikomeshwa kwa  viongozi wa mataifa leo na kuendelea hadi kipindi cha kuja kwa Masihi na kwa watu wanaosema kuwa wao ni Wayahudi lakini sivyo, watakwenda utumwani. Hata hivyo, Mika anapewa maono ya siku za mwisho na hatima njema ya taifa wakati Masihi atakapoanzisha tena chini ya utaratibu wa Mungu na sheria za Mungu kwenye kipindi cha utawala wa millennia.

 

Tunaona kuwa Mika (ni kifupi cha Mikaya ambaye maana yake ni nani aliye kama Mungu) alikuwa anatoka katika mji wa Moreshethi-gathi (aya ya 14) (Maresha aya ya 15) au alikuwa anatabiri kwenye maeneo ya Yudea karibu na Shefela kwanza kuhusu Samaria na kisha Yerusalemu.

 

Mika Sura ya 1

1 Hili ndilo neno la Bwana lililomjia Mika, Mmorashti, katika siku za Yothamu, na Ahazi, na Hezekia, wafalme wa Yuda; maono aliyoyaona katika habari za Samaria, na Yerusalemu.

Kipindi cha kuitwa kwake kilikuwa ni cha kutoka utawala wa Yothamu na Ahazi hadi cha Hezekia ambacho ni tangu mwaka 739-693 KK. Maono yake ilihusisha nchi zote mbili, yaani Samaria na Yerusalemu na mapatilizo yao. Bado Samaria ilikuwa ni mji mkuu wa taifa la Israeli na iliishia kwenye tukio la kwenda utumwani mwaka 722/1 KK.

Adhabu na mapatilizo yaliwakumba wote, yaani Israeli na Yuda kwa ajili ya dhambi za Samaria na Yerusalemu. Mika anawaona haa wote wakieelekea kwa haraka kwa kukimbizwa kwenda utumwani, Samaria ambayo ilifanywa kuwa maganjo yaliyobomoshwa mwaka 722 na kisha kuangamia kwa Yerusalemu kulitabiriwa pia (3:12) lakini haikutokea hivyo hadi kipindi cha Wababeloni mwaka 597 bado hata hivyo haikuwa na uhakika kama tunavyoona kwenye aya ya 9 hapo chini. Ilitabiriwa na kutangazwa kwa kipindi cha miaka 100 kabla ya kutokea kwake. Maafa na kuanguka kwa Samaria kulitabiriwa kama onyo kwa Yerusalemu balia kuanguka kwa falme mbili zote kulitabiriwa na unabii na kisha ilichukuliwa kuihusisha Yuda na Yerusalemu . mika anaelekezwa kwa Israeli wote kwenye miji mbalimbali na maangamizo makubwa yatakayotokea na kuutesa ulimwengu wote kwa sababu ya uasherati wa Israeli (sawa na aya za 2-4). Kwa hiyo hukumu itaupata ulimwengu wote tangu mashambulizi ya Waashuru hadi kwenye Nyakati za Mwisho chini ya Masihi.

2 Sikilizeni, enyi watu wa kabila zote; sikiliza, Ee dunia, na vyote vilivyomo; Bwana MUNGU na ashuhudie juu yenu, yeye Bwana kutoka hekalu lake takatifu. 3 Kwa maana, angalieni, Bwana anakuja akitoka mahali pake, naye atashuka, na kupakanyaga mahali pa dunia palipoinuka. 4 Na hiyo milima itayeyuka chini yake, nayo mabonde yatapasuliwa, kama vile nta iliyo mbele ya moto, kama maji yaliyomwagika tena kutelemka gengeni. 5 Kwa sababu ya kosa la Yakobo yametokea haya yote, na kwa sababu ya makosa ya nyumba ya Israeli. Nini kosa la Yakobo? Je, silo Samaria? Na nini mahali pa Yuda palipoinuka? Sipo Yerusalemu? 6 Kwa ajili ya hayo nitafanya Samaria kuwa kama chungu katika shamba, na kama miche ya shamba la mizabibu; nami nitayatupa mawe yake bondeni, nami nitaifunua misingi yake. 7 Na sanamu zake zote za kuchonga zitapondwa-pondwa, na ijara zake zote zitateketezwa kwa moto, na sanamu zake zote nitazifanya ukiwa; kwa kuwa amezikusanya kwa ujira wa kahaba, nazo zitaurudia ujira wa kahaba. 8 Kwa ajili ya hayo nitaomboleza na kulia, Nitakwenda nimevua nguo, ni uchi; Nitafanya mlio kama wa mbweha, Na maombolezo kama ya mbuni.

Ni ukahaba wa waabudu sanamu wa Israeli huko Samaria kama wa kibiashara na ustaarabu wa mijini ambayo ni jeraha chungu katika Yuda kama tuonavyo leo, na ukahaba wa kibiashara na ukahaba wa uabudu sanamu wa imani mchanganyiko za Kiashuru na Kibabeloni utaiangamiza dunia kwa hasira ya Mungu. Israeli waliwekwa huko ili kuzuia maangamizo na ukahaba wake utashindwa. Yeremia 4:23 nk inaonyesha jinsi Mungu anavyoonyesha kwa kupitia manabii kwamba kushindwa na ukahaba wa Israeli ni sababu ya maafa ya matetemeko ya ardhi na maangamizi ambayo yamepunguza ulimwengu mzima (soma aya za 4-5 hapo juu). Kwa hiyo waliruhusu kuendelea kwa ibada za Mahali pa Juu kama ibada za sanamu pia.

Kutoka kwenye aya ya 9 andiko lipo kwenye unabii uliotimia yanaonyesha kwamba utakwenda kutimia na hakuna kitakacho lisimamisha. Yerusalemu ni lango la watu wa Israeli na Yuda kama kiti cha Hekalu la Mungu.

9 Kwa maana jeraha zake haziponyekani; Maana msiba umeijilia hata Yuda, Unalifikia lango la watu wangu, Naam, hata Yerusalemu. 10 Msiyahubiri haya katika Gathi, msilie kamwe; Katika Beth-le-Afra ugae-gae mavumbini. 11 Piteni; uende ukaaye Shafiri, hali ya uchi na aibu; Hivyo akaaye Saanani hajatokea nje; Maombolezo ya Beth-eseli yatawaondolea tegemeo lake; 12 Maana akaaye Marothi ana utungu wa mema; Kwa kuwa msiba umeshuka toka kwa Bwana, Umefika mpaka lango la Yerusalemu. 13 Mfungie gari la vita farasi Aliye mwepesi, ukaaye Lakishi; Alikuwa mwanzo wa dhambi kwa binti Sayuni; Maana makosa ya Israeli yameonekana kwako. 14 Kwa hiyo utaipa Moresheth-Gathi zawadi ya kuagia; Nyumba za Akzibu zitakuwa kijito kidanganyacho wafalme wa Israeli. 15 Bado, ukaaye Maresha, nitakuletea yeye atakayekumiliki; Utukufu wa Israeli utafika mpaka Adulamu.  16 Jifanyie upaa, jikate nywele zako, Kwa ajili ya watoto waliokufurahisha; Panua upaa wako kama tai; Kwa maana wamekwenda mbali nawe utumwani.

Andiko hili linasheheneza kwenye Paronomasia au linajiri kwenye maneno na haiwezekani kuiwekwa kwenye tafsiri.

Maneno yasemayo Usiseme jambo hili katika Gathi unafananishwa na andiko lililo kwenye 2Samueli 1:20. Gathi ulikuwa umetwaliwa kutoka kwa Wafilisti na mfalme Uzia (2Nyakati 26:6) na ndipo hawakuwa huko kabisa na yawezekana ni maneno tu ya mdomo ya sasa (soma Soncino fn.).

Usemi wa hatukuzishika kabisa (Usemi rahisi ni kwamba Muombolezaji asiomboleze (kwa Kiebrania Bacho al tibku); tafsiri ya the LXX inaonyesha kuwa usemi wa msiomboleze kwenye Mujibu wake) Utajwaji wake huenda ulikuwa unamtaja Baali, ambaye ni Mungu Jua pia (likiruka neno ‘ain’) kwa kumtaja Baali, ambaye ni Mungu Jua (soma Soncino fn.) na kwa maangamizi yanayokuja.

 

Jina la beth-le-afra maana yake ni nyumba ya vumbi na haijulikani. Huenda inayataja mahekalu ya Baali na Dagoni wa Wafilisti. Ni kethib hithpallashti au nimejiviriga mwenyewe lakini inaonekana kuwa ni ashirio la maneno yaliyowataja au kumaanisha kuwa ni Wafilisti.

Aya ya 11 inasema pitilia mbali linalochukuliwa kumaanisha utumwani. Hii ni kwa falme zote mbili, yaani Israeli na Yuda.

Neno uchi linachukuliwa kumaanisha kwenye mkatale wa utumwa (soma aya ya 8).

Zaanani inachukuliwa kumaanisha Zenani ambayo ni Shefela (Yoshua 15:37).  Msije ni neno linalotokana na vebu Yatsa kama kwenda. Zaanani linapuuzwa na kuomboleza kutoka Beth-ezel (Nyumba ya karibu ya jirani) linawavunja moyo.

Marothi (aya ya 12) ni uchungu lililo kinume na mwma au msaada.

Funga magari (aya ya 13) limechukuliwa kumanisha jiandae kwa vita. Hata hivyo, lina maana ya kina. Mji wa Laishi ulikuwa ni Kitovu cha kaskazini mwa Dani karibu na jangwa la mapepo la Hermoni. Lakishi ni mji katika Yuda ulio njiani kati ya Yerusalemu na Gaza lakini dunia pia ni jumuisho la Larecheshi hadi feleji za kuchuja. Yuda walipaswa kuitegemea Misri kwa farasi wa vita. Ilikuwa ni ngome za upande za mbele au umuhimu wa kimbinu kati ya Yuda na Misri iliyojengwa kwa kuzungushiwa na Daudi na kisha na Rehoboamu (2Nyakati 11:9) na huenda Asa aliuimarisha (14:7).  Sanekarebu aliuufanya kuwa Makao Makuu yake ya muda mwaka 701 KK. Inaweza kuonekana kuelekea katika kuwafunga mapepo. Hili linasaidiwa na neno chanzo wa dhambi ambayo inachukuliwa kama awamu isiyojulikana na wachambuzi. Chanzo cha dhambi kinatokana na mapepo kwenye Mlima wa Hermoni. Wanazuoni mahiri wa ufafanuzi wa Kiyahudi wanasema kwamba Lakishi ilikuwa ni kiti cha aina ya ibada za sanamu (ambayo tunaijua kama Ndama wa Dhahabu wa Dani ambaye alipewa jina kutokana na mungu Mwezi aitwaye Sin, kama Yeriko ilivyo pia Mji wa Mwezi). Ni kituo cha zamani sana na ulitumika katika utawala wa Hyksos na unatajwa kama La-ti-sa kwenye Kizazi cha kifalme cha 18 cha Ahmosid. Ulikuwa chini ya utawala wa Wamisri na wa Hyksos tangu kizazi cha kifalme cha 12 hadi cha 22.

Moreshath-Gathi ulikuwa kwenye eneo la Wafilisti na ni mji usio na umuhimu au dinu wa Akizibu huko Shefela (Yoshua 15:44) ni usemi unaomaanisha kitu cha uwongo ambacho ni akizabu ambayo ni sio mkondo wa kudumu (sawa na Yeremia 15:18). Kwa leo ni mwiba kwa Waisraeli.

Mika anapewa maono kutoka kwenye mji wa nyumbani kwake na anaona mbali kwa kina kutokana na mashambulizi ya ya Siku za Mwisho. Miji hii iliyotajwa hapa toka aya ya 10-15 haipo katikati ya Samaria na Yerusalemu bali ni kati ya malango ya Yerusalemu na pwani mwa bahari uwanda wa Wafilisti. Huu ulikuwa ni msafara ambao kwamba washambuliaji wa Yudea waliokuja kutika Sargon (719 KK dhidi ya Misri na mwaka 711 dhidi ya Ashdodi), na Senakaribu mwaka 704-1 wakati alipoishambulia Shefela kwa mfululizo pamoja na kushambuliwa kwa Yudea; kulikofanywa na Wamisri na Warumi chini ya Vespasian na kipindi cha Zama-Kati chini ya Saladin na Richard (kwa mjibu wa G.A. Smith; sawa na Soncino fn). Unabii huu unaonyesha kuwa Mika anaona mbele kwenye mashambuliaji yote na jinsi yatavyotokea katika Siku za Mwisho na hatimaye kwenye kipindi cha Utawala wa Mnyama na cha Mfalme wa Kaskazini wa Danieli 11:40-44.

Sura ya 2 ni mwendelezo zaidi wa dhambi ambazo hazijatubiwa bado zilizo kwenye sura ya 1. Inajulikana kwa kuzivunja sheria Mungu kuhusu Yubile umiliki wa ardhi na mashamba. Kwa ajili ya dhambi yao Mungu aliwapeleka utumwani. Hawana wa kumtumikia kwenye Mkutano wa Mungu kwa kura. Hii inajiri na marejesho mapya ya ardhi kwa kupigiwa kura kwenye Yubile. Kwa kuwa hiyo pia ilikuwa ni nchi ya Kanaani iliyogawanywa miongoni mwa makabila. Hata hivyo, hawakuzishika sheria za Mungu na hawakurejesha familia na watumishi kwenye Sabato na Yubile. Hadi leo, makanisa ya Mungu na kuifuata kalenda ya uwongo ya Yud wa sasa. Kwa dhambi hizi watahukumiwa. Wimbo wa dhihaka ni wimbo wa maombolezo au maombolezo yaliyochukuliwa kama tuonavyo pia kwenye Yeremia 9:9; Amosi 5:1. Mashamba makubwa ilipata kinyume na haki kabisa kutatawanyika na kupangiliwa kwa majeshi ya ushindi ya mataifa yenye dhambi.

 

Mika Sura ya 2

1 Ole wao wakusudiao mambo maovu, na kutenda mabaya vitandani mwao! Kunapopambazuka asubuhi huyafanya, kwa sababu ya katika uwezo wa mikono yao. 2 Nao hutamani mashamba, na kuyashika; na nyumba pia, nao huzichukua; nao humwonea mtu na nyumba yake, naam, mtu na urithi wake. 3 Basi Bwana asema hivi, Angalia, nakusudia jambo baya juu ya jamaa hii, ambalo hamtazitoa shingo zenu, wala hamtakwenda kwa kiburi; kwa maana ni wakati mbaya. 4 Siku hiyo watatunga mithali juu yenu, na kuomboleza kwa maombolezo ya huzuni nyingi, na kusema, Sisi tumeangamizwa kabisa; Yeye analibadili fungu la watu wangu; Jinsi anavyoniondolea hilo! Awagawia waasi mashamba yetu. 5 Kwa hiyo hutakuwa na mtu atakayeitupa kamba kwa kura katika mkutano wa Bwana. 

Hapa tunaiona fursa kwenye unabii wa Mika ikitokea kwa makuhani waovu na manabii. Wanafundisha kwamba kuaibisha hawatawapiku wao bali ni Mungu anayewakemea na sio Mika. Nyumba zinazopendeza ni familia yenye furaha wanaziangamiza. Haya ni maambukizi leo na kwa hiyo watakwenda utumwani na kupambanua utajiri wao.

6 Msitabiri, ndivyo watabirivyo; wasiyatabiri mambo haya; lawama hazikomi. 7 Je! Litasemwa neno hili, enyi nyumba ya Yakobo, Roho ya Bwana imepunguzwa? Je! Haya ni matendo yake? Je! Maneno yangu hayamfai yeye aendaye kwa unyofu? 8 Lakini siku hizi mmeinuka kama adui za watu wangu; mwaipokonya joho iliyo juu ya nguo za hao wapitao salama kama watu wasiopenda vita. 9 Wanawake wa watu wangu mwawatupa nje ya nyumba zao nzuri; watoto wao wachanga mwawanyang'anya utukufu wangu milele. 10 Ondokeni, mwende zenu; maana hapa sipo mahali pa raha yenu; kwa sababu ya uchafu mtaangamizwa, naam, kwa maangamizo mazito sana. 11 Mtu akienda kwa roho ya uongo, akinena maneno ya uongo, akisema, Nitakutabiria habari ya mvinyo na kileo; mtu huyu atakuwa nabii wao watu hawa. 12 Hakika nitakukusanya, Ee Yakobo, nyote pia; Bila shaka nitawakusanya waliobaki wa Israeli; Nitawaweka pamoja kama kondoo wa Bozra; Kama kundi la kondoo kati ya malisho yao; Watafanya mvumo kwa wingi wa watu; 13 Avunjaye amekwea juu mbele yao; Wamebomoa mahali, wakapita mpaka langoni, Wakatoka nje huko; Mfalme wao naye amepita akiwatangulia, Naye Bwana ametangulia mbele yao.

 

Kutega na kuwanasa kwa hila mbovu za riba, baraza la rehani, na usaidizi wa mashahidi nay a rushwa kwenye kutoa hukumu unafuatiwa kwa haraka na utekelezaji

 

Makuhani na manabii huwahubiria uwongo na kuwabiria utajiri, mafanikio na vinywaji vikali na kuwatumia vibaya wanawake na watoto na kuchukua mali, ambao ni Israeli wa Mungu, na kuitumia vibaya.

 

Kisha kwenye Sura ya 3 tunaona uovu uliofanywa katika Israeli kwa watu maskini na wahitaji.

 

Mika Sura ya 3

1 Nikasema, Tafadhali sikieni, enyi vichwa vya Yakobo, mnaoitawala nyumba ya Israeli. Je! Haiwapasi ninyi kujua hukumu? 2 Ninyi mnaoyachukia mema, na kuyapenda mabaya; ninyi mnaowachuna watu ngozi yao, na nyama mifupani mwao. 3 Naam, mnakula nyama ya watu wangu, na kuwachuna ngozi zao, na kuivunja mifupa yao; naam, kuwakata vipande vipande kama kwa kutiwa chunguni, na kama nyama sufuriani. 4 Ndipo watakapomwomba Bwana, asiwaitikie; naam, atawaficha uso wake wakati huo, kwa kadiri walivyotenda mabaya kwa matendo yao.

 

Waalimu wa dini na hasahasa manabii huihubiri amani kwa makelele mengi wanapokuwa wamelishwa vizuri lakini huwatangazia vita wale wasiowalisha kwa sababu ya maovu yao. Na ndivyo lilivyo Kanisa la Mungu kwa kuwa kwa zaidi ya kipindi cha karne moja ya Siku za Mwisho. Wanajitangaza kuwa ni manabii wa Mungu kwenye makanisa ya Mungu tulimo kwenye yale ya Ufunuo sura 10 ambao wanautoa unabii kuwa mtamu kama asali midomoni lakini matumbo yatakuwa machungu kwa ajili yake. Mungu atashughulika na waalimu hawa wa uwongo katika Siku za Mwisho. Sio mara moja kwenye karne ya ishirini kwa manabii hawa wa uwongo wa makanisa ya Mungu kutoa kiusahihi unabii na waliwaongoa watu kutoka gizani (soma jarida la Unabii wa Uwongo (Na. 269)).

 

5 Bwana asema hivi katika habari za manabii wanaowakosesha watu wangu; hao waumao kwa meno yao, na kulia, Amani; na mtu awaye yote asiyetia kitu vinywani mwao, wao humwandalia vita. 6 Kwa hiyo itakuwa usiku kwenu, msipate kuona maono; tena itakuwa giza kwenu, msiweze kubashiri; nalo jua litawachwea manabii, nao mchana utakuwa mweusi juu yao. 7 Na hao waonaji watatahayarika, na wenye kubashiri watafadhaika; naam, hao wote watajifunika midomo yao; kwa maana; hapana jawabu la Mungu. 8 Bali mimi, hakika nimejaa nguvu kwa roho ya Bwana; nimejaa hukumu na uwezo; nimhubiri Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake. 9 Sikieni haya, tafadhali, enyi vichwa vya nyumba ya Yakobo, mnaoitawala nyumba ya Israeli, mnaochukia hukumu, na kuipotosha adili. 10 Wanaijenga Sayuni kwa damu, na Yerusalemu kwa uovu. 11 Wakuu wake huhukumu ili wapate rushwa, na makuhani wake hufundisha ili wapate ijara, na manabii wake hubashiri ili wapate fedha; ila hata hivyo watamtegemea Bwana, na kusema, Je! Hayupo Bwana katikati yetu? Hapana neno baya lo lote litakalotufikia. 12 Basi, kwa ajili yenu, Sayuni utalimwa kama shamba lilimwavyo, na Yerusalemu utakuwa magofu; na mlima wa nyumba utakuwa kama mahali palipoinuka msituni.

 

Ufisadi unaongezeka sana kwenye mataifa ya dunia kiasi kwamba inabidi hukumu ya kifo irudi tena ili kwamba wanasiasa wote na wakiritimba wa vichwa ngunu na mahakimu na wenye vichwa vikorofi na mafisadi wahukumiwe kifo na wauawe ili kuyaondoa maovu kama haya katika yetu.

 

Sura ya 4 kisha inaenda mbele kwenye Nyakati za Mwisho wakati mlima wa nyumba ya Bwana utakapoanzishwa huko Sayuni kipindi cha utawala wa Masihi. Sheria zilizoagizwa kwenye Torati ya Mungu zitaanza kutumika na ulimwengu wote utazishika pamoja na taratibu zote na Sikukuu au vinginevyo wataadhibiwa na hawatapata mvua kwa majira muafaka na watataabika kwa magonjwa au tauni ya Misri kama Mungu anavyowaonyesha wanadamu kupitia nabii Zekaria, na walimuua kwa sababu ya unabii wake. Kikanuni, makuhani na manabii wa Israeli wamekuwa ni chanzo cha uovu zaidi a kuwa ufumbuzi. Ni wao ndio waliwaua manabii ambao Mungu aliwatuma kwao na kuwatesa wateule wa kanisa la Mungu. Walibobea kumuabudu Baali na kumwamini Mungu Jua na kuacha kuzishika sheria na Ushuhuda wa Mungu.

 

Unabii huu ni wa millennia kutokana na tukio na mchakato wa nyakati za utumwa.

 

Mika Sura ya 4

1 Lakini itakuwa katika siku za mwisho, ya kwamba mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na watu wa mataifa watauendea makundi makundi. 2 Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, na nyumbani kwa Mungu wa Yakobo; naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake; kwa maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana litatoka Yerusalemu. 3 Naye atafanya hukumu kati ya watu wa kabila nyingi, naye atawakemea mataifa wenye nguvu walio mbali; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe. 4 Bali wataketi kila mtu chini ya mzabibu wake, na chini ya mtini wake; wala hapana mtu atakayewatia hofu; kwa kuwa kinywa cha Bwana wa majeshi kimesema hivi. 5 Kwa maana mataifa yote watakwenda, kila moja kwa jina la mungu wake, na sisi tutakwenda kwa jina la Bwana, Mungu wetu, milele na milele. 6 Katika siku ile, asema Bwana, nitamkusanya yeye achechemeaye, nami nitamrudisha yeye aliyefukuzwa, na yeye niliyemtesa. 7 Nami nitamfanya yeye aliyechechemea kuwa mabaki, na yeye aliyetupwa mbali kuwa taifa lenye nguvu, na Bwana atawamiliki katika mlima Sayuni tangu sasa na hata milele. 8 Na wewe, Ee mnara wa kundi, kilima cha binti Sayuni, utajiliwa; naam, mamlaka ya kwanza yatakuja, ufalme wa binti Yerusalemu. 9 Sasa mbona unapiga kelele? Je! Hakuna mfalme kwako, mshauri wako amepotea, hata umeshikwa na utungu kama mwanamke wakati wa kuzaa? 10 Uwe na utungu, utaabike ili uzae, Ee binti Sayuni, kama mwanamke mwenye utungu; maana sasa utatoka mjini, nawe utakaa katika mashamba; utafika hata Babeli; huko ndiko utakakookolewa; huko ndiko Bwana atakakokukomboa katika mikono ya adui zako. 11 Na sasa mataifa mengi wamekusanyika juu yako, wasemao, Na atiwe unajisi; macho yetu na yaone shari ya Sayuni. 12 Lakini wao hawayajui mawazo ya Bwana, wala hawafahamu shauri lake; kwa maana amewakusanya kama miganda sakafuni. 13 Haya, simama upure, Ee binti Sayuni; kwa maana nitafanya pembe yako kuwa chuma, na kwato zako kuwa shaba; nawe utaponda-ponda mataifa mengi, na faida yao utaiweka wakfu kwa Bwana, na mali zao kwa Bwana wa dunia yote.

 

Kwa hiyo Yuda waliambiwa mapema kuwa watakwenda utumwani na hawakutubu na ndipo walirudi ili kuanzisha mchakat kwa ajili ya Masihi na kisha uteka au utumwa wa pili na utawanyiko ulitokea tangu mwaka 70 BK mwishoni mwa majuma 70 ya miaka ya nabii Danieli 9:23-27 (pia soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Tena wa Hekalu (Na. 013)).

 

Sura ya 5 nayo inaendelea kwa kueleza kwa kina ujio wa Masihi na mahali pa ukoo wake huko Bethlehemu Ef’rata. Ndipo unabii unaendelea mbele kwa kina na Masihi akatolewa (soma Zaburi 110:1ff) hadi ndugu zake wote, ambao ni wateule wa Mungu (wa Zekaria 12:8) wanapelekwa kwenye Yubile ya 40 ya kanisa kuwa jangwani sawasawa na unabii wa Ishara ya Yona ya Yubile moja kuilinganisha na mwaka mmoja.

 

Mika Sura ya 5

1 Sasa utajikusanya vikosi vikosi, Ee binti wa vikosi; yeye amemhusuru; watampiga mwamuzi wa Israeli shavuni mwake kwa fimbo. 2 Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele. 3 Kwa sababu hiyo atawatoa, hata wakati wa kuzaa kwake aliye na utungu; ndipo hayo mabaki ya nduguze watawarudia wana wa Israeli. 4 Naye atasimama, na kulisha kundi lake kwa nguvu za Bwana, kwa enzi ya jina la Bwana, Mungu wake; nao watakaa; maana sasa atakuwa mkuu hata miisho ya dunia. 5 Na mtu huyu atakuwa amani yetu; wakati Mwashuri atakapoingia katika nchi yetu, na kuyakanyaga majumba yetu, hapo mtaondokesha wachungaji saba juu yake, na wakuu wanane. 6 Nao wataiharibu nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake; naye atatuokoa na Mwashuri, atakapoingia katika nchi yetu, na kukanyaga ndani ya mipaka yetu. 1 Sasa utajikusanya vikosi vikosi, Ee binti wa vikosi; yeye amemhusuru; watampiga mwamuzi wa Israeli shavuni mwake kwa fimbo. 2 Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele. 3 Kwa sababu hiyo atawatoa, hata wakati wa kuzaa kwake aliye na utungu; ndipo hayo mabaki ya nduguze watawarudia wana wa Israeli. 4 Naye atasimama, na kulisha kundi lake kwa nguvu za Bwana, kwa enzi ya jina la Bwana, Mungu wake; nao watakaa; maana sasa atakuwa mkuu hata miisho ya dunia. 5 Na mtu huyu atakuwa amani yetu; wakati Mwashuri atakapoingia katika nchi yetu, na kuyakanyaga majumba yetu, hapo mtaondokesha wachungaji saba juu yake, na wakuu wanane. 6 Nao wataiharibu nchi ya Ashuru kwa upanga, na nchi ya Nimrodi katika malango yake; naye atatuokoa na Mwashuri, atakapoingia katika nchi yetu, na kukanyaga ndani ya mipaka yetu.

 

Kwa hiyo ni budi kuwa Masihi alikuwepo hata kabla ya kuzaliwa kwake duniani na alisimama kwa uweza wa Bwana Mungu wake (kama tulivyoona kwenye Zaburi 45:6-7; pia soma Zaburi 72:7; Isaya 9:6-7; Zekaria 9:10). Pia soma jarida la Mika 5:2-3 (Na. 121).

 

Masihi amepewa wachungaji saba wanaouathiri na kuipiga vita imani mchanganyiko ya Waashuru na Wababeloni na pia wafalme wanane wa wanadamu. Ukweli ni kwamba kuna malaika saba wa Makanisa Saba na zama saba za uwepo au vipindi vya Makanisa ya Mungu. Hawa wanaiathiri na kuitokomeza imani na mapokeo ya kidini ya dini za waabudu Jua na Imani za Kisirisiri na Kifumbo. Na pia wafalme nane wa wanadamu ni nguvu iliyopo kutoka kwa watu wa Mungu chini ya kiongozi wao kwenye Nyakati za Mwisho. Wanaunda mataifa manane na vikosi vinane vya majeshi. Nguvu za imani na mfumo mchanganyiko wa Kiashuru na Kibabeloni vitaangamizwa na kusukumiwa tena huko Mashariki ya Kati.

 

Masalia wa Yakobo watatumiwa katika mataifa ili kwamba Wamataifa waletwe ndani na Waefraimu watasimama kama jumuia ya mataifa na kwa yeye Mataifa watawatumainia (Mwanzo 48:15-16).

 

7 Na hayo mabaki ya Yakobo yatakuwa kati ya kabila nyingi mfano wa umande utokao kwa Bwana, mfano wa manyunyu katika manyasi; yasiyomngojea mtu, wala kuwakawilia wanadamu. 8 Na hayo mabaki ya Yakobo yatakuwa kati ya mataifa, kati ya kabila nyingi, mfano wa simba kati ya wanyama wa msituni, kama mwana-simba kati ya makundi ya kondoo, ambaye, akiwa anapita katikati, hukanyaga-kanyaga na kurarua-rarua, wala hakuna wa kuokoa. 9 Mkono wako na uinuliwe juu ya adui zako, na adui zako wote wakauliwe mbali. 10 Kisha itakuwa katika siku hiyo, asema Bwana, nitawakatilia mbali farasi zako watoke kati yako, nami nitayaharibu magari yako ya vita; 11 nami nitaikatilia mbali miji ya nchi yako, na ngome zako zote nitaziangusha; 12 nami nitakatilia mbali uchawi, usiwe mkononi mwako; wala hutakuwa tena na watu wenye kutabana; 13 nami nitakatilia mbali sanamu zako na nguzo zako, zitoke kati yako; wala hutaiabudu tena kazi ya mikono yako. 14 Nami nitayang'oa maashera yenu, yasiwe kati yako; nami nitaiangamiza miji yako. 15 Nami nitajilipiza kisasi katika hasira na ghadhabu juu ya mataifa wasiosikiliza.

 

Ila Utaratibu na imani yote itatakaswa kwenye hivi Vata vya Nyakati za Mwisho na Vikombe vya Ghadhabu ya Mungu (Na. 141B)Imani na dini za waabudu siku ya Jumapili ya Mungu Siri wa Jua  ambayo pia ni waadhimishaji wa Krismas na Easter zitangamizwa na kukomeshwa na kila kasisi wa imani ile atatubu au vinginevyo atakufa. Watazishika Sabato na Miandamo ya Mwezi Mpya, la sivyo watakufa (Isaya 66:23-24). Wataziadhimisha sikukuu za Mungu vinginevyo watakufa (Zekaria 14:16-19).

 

Kila minara mirefu na zakhari zilizosimikwa juu ya majengo ya makanisa madogo, makanisa mkubwa wanayosalisha maaskofu wakuu, mahekalu au misikiti na kila sanamu na alama kuu za kidini, vitaangamizwa na kutokomezwa. Hakuna kasisi asiyetubu, wala rabi, wala imamu, au sheikh, gombera au mtawa atakayeachwa akiwa hai.

 

Sura ya 6 ndipo Bwana anawataka Israeli na waliosalia humo wa kuingilia kwake kati na wokovu wake kwao na hawakumsikiliza wala hawakumshukuru.

 

Mika Sura ya 6

1 Basi sasa, sikieni asemavyo Bwana; Simama, ujitetee mbele ya milima, vilima navyo na visikie sauti yako. 2 Sikieni, enyi milima, mateto ya Bwana, na ninyi, enyi misingi ya dunia iliyo imara; kwa maana Bwana ana mateto na watu wake, naye atahojiana na Israeli. 3 Enyi watu wangu, nimewatenda nini? Nami nimewachosha kwa habari gani? Shuhudieni juu yangu. 4 Kwa maana nalikupandisha kutoka nchi ya Misri, na kukukomboa utoke katika nyumba ya utumwa, nami naliwapeleka Musa, na Haruni, na Miriamu, watangulie mbele yako. 5 Enyi watu wangu, kumbukeni sasa alivyouliza Balaki, mfalme wa Moabu, na alivyojibu Balaamu, mwana wa Beori; kumbukeni toka Shitimu hata Gilgali, mpate kuyajua matendo ya haki ya Bwana. 6 Nimkaribie Bwana na kitu gani, na kuinama mbele za Mungu aliye juu? Je! Nimkaribie na sadaka za kuteketezwa, na ndama za umri wa mwaka mmoja? 7 Je! Bwana atapendezwa na elfu za kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je! Nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa kosa langu, mzao wa mwili wangu kwa dhambi ya roho yangu?

 

Mungu amewaonyesha kuwa hahitaji dhabihu kubwa bali anataka haki na rehema na kuenenda kwa unyenyekevu na Mungu wetu. Anataka utii na sio sadaka ama alivyosema kupitia nabii Samweli.

 

8 Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako! 9 Sauti ya Bwana inaulilia mji, na mtu mwenye akili ataliona jina lako; isikieni hiyo fimbo na yeye aliyeiagiza. 10 Je! Hata sasa hazina za uovu zingalimo nyumbani mwa wabaya, na kipimo kilichopunguka, ambacho ni chukizo? 11 Je! Naweza kuwa safi nami nina mizani ya udhalimu, na mfuko wa mawe ya kupimia ya udanganyifu? 12 Kwa maana matajiri wake wamejaa jeuri, na wenyeji wake wamesema uongo, na ulimi wao una udanganyifu kichwani mwao.

 

Hatimaye Mungu anawalaumu na kuwakemea watawala na matajiri wa Israeli wa makundi yote mawili, yaani wa kabila na wa mji. Walikuwa walaghai sana na waongo na utajiri wao ulikuwa na maovu mengi. Vipimo vy udanganyifu na mizani ya uwongo zilikuwa pamoja nao na ushahidi wa uwongo uliongezeka miongoni mwao. Mungu aliwatangazia maafa yao. Ameanza kuwapiga na atawafanya kuwa ukiwa kwa sababu ya dhambi zao. Atatuadhibu kwa njaa na hatutaweza kuokoka na kila tunachokifanya ni kujiingiza kwenye mkatale wa upanga. Ziku zote za Nyakati hizi za Mwisho mambo haya yataongezeka ili kwamba kama Masihi hakurudi mapema, basi hakuna mwenye mwili atakayebakia hai.

 

 13 Basi, kwa ajili ya hayo, mimi nami nimekupiga kwa pigo liumizalo sana; nimekufanya kuwa ukiwa, kwa sababu ya dhambi zako. 14 Utakula, lakini hutashiba; na fedheha yako itakuwa kati yako; nawe utahama, lakini hutachukua kitu salama; na hicho utakachochukua nitakitoa kwa upanga. 15 Utapanda, lakini hutavuna; utazikanyaga zeituni, lakini hutajipaka mafuta; na hizo zabibu, lakini hutakunywa divai. 16 Kwa maana amri za Omri ndizo zishikwazo, na matendo yote ya nyumba ya Ahabu, nanyi mnakwenda katika mashauri yao; ili nikufanye kuwa ukiwa, na wenyeji waliomo humo kuwa zomeo; nanyi mtayachukua matukano waliyotukanwa watu wangu.

 

Kumbuka kuwa wanazishika sheria za uwongo na potovu za mataifa na za dini za miungu Jua, Dini za Kisirisiri za Ahabu na Yezebeli lakini sio Torati ya Mungu. Wanazishika sheria zilizotungwa na Wababeloni na zile za Mataifa Yaliyoungana na kuiacha Torati ya Mungu. Kwa sababu hii wataadhibiwa wote. Kila kitu kinachotumika kwenye dini hizi za waabudu Jua na Dini za Imani Fumbo vitaondolea mbali na kufutwa chini ya mbingu.

 

Kwenye sura ya 7 tunaona kwamba hakuna wachamungu walioachwa juu ya dunia wa namna yoyote au kiwango. Hakuna mwenyehaki au mchamungu aliyeachwa. Wanadanganya wakivizia damu na kila mmoja anamuwinda ndugu yake kwa wavu. Kwa hiyo, ni sasa na kwa ulimwengu wote na Wasemitiki wamebadilika kuwa wadhalimu na washenzi. Uadilifu na uchamungu na haki vimekimbia kutoka kwa wanadamu. Rushwa na ufisadi vimetawala ulimwenguni kote.

 

Usimwamini mtu yeyote hata Yule wa kifuani mwako. Hata kwenye makanisa ya Mungu tumewaona watoto wakiwafanyia wazazi wao vibaya na tumewashuhudia waliokufa wakiwa vijana kwa sababu ya uzushi wao.

 

Hata hivyo, mwenyehaki ataishi kwa imani na watakombolewa na Mungu kama tunavyoona hapa.

 

Mika Sura ya 7

1 Ole wangu! Maana mimi ni kama hapo walipokwisha kuyachuma matunda ya wakati wa hari, kama zabibu zichumwazo baada ya mavuno; hapana shada la kuliwa; roho yangu inatamani tini iivayo kwanza. 2 Mtu amchaye Mungu ametoweka, asionekane katika nchi, wala hapana mtu mwenye adili katika wanadamu; wote huotea ili kumwaga damu; kila mtu humwinda ndugu yake kwa wavu. 3 Mikono yao inayashika mabaya wayatende kwa bidii; mtu mkuu aomba rushwa, kadhi yu tayari kuipokea; mtu mkubwa hunena madhara yaliyomo rohoni mwake; hivyo ndivyo wayafumavyo hayo pamoja. 4 Mtu aliye mwema miongoni mwao ni kama mbigili; mtu aliye mwenye adili miongoni mwao ni mbaya kuliko boma la michongoma; hiyo siku ya walinzi wako, yaani, siku ya kujiliwa kwako, imefika; sasa kutatokea kufadhaika kwao. 5 Msimwamini rafiki, msimwekee kiongozi tumaini; ilinde milango ya midomo ya kinywa chako ili mkeo alalaye kifuani mwako asijue habari. 6 Kwa maana mwana humwaibisha babaye, na binti huondoka ashindane na mamaye; na mwanamke aliyeolewa hushindana na mavyaaye; adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe. 7 Lakini mimi, nitamtazamia Bwana; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia. 8 Usifurahi juu yangu, Ee adui yangu; niangukapo, nitasimama tena; nikaapo gizani, Bwana atakuwa nuru kwangu. 9 Nitaivumilia ghadhabu ya Bwana, kwa kuwa nimemwasi; hata atakaponitetea teto langu, na kunifanyia hukumu; atanileta nje kwenye nuru, nami nitaiona haki yake.

 

Kumbuka kuwa yatupasa kuwa na hasira ya Bwana kwa kuwa tumetenda dhambi sisi sote. Mtu yeyote mkali anayesema kuwa hana dhambi ni muongo na kweli haimo ndani yake (1Yohana 1:8-10).

 

Kwa kupitia upendo na utauwa wa wateule watu wote watarudi kwenye nchi ya Israeli kutoka ulimenguni kote. Dunia itabaki ukiwa na maganjo kwa sababu ya dhambi zake lakini watarudi ili warejeshwe tena na miujiza ya Mungu chini ya Masihi italeta toba kwa mataifa.

 

10 Ndipo adui yangu ataliona jambo hilo, na aibu itamfunika, yeye aliyeniambia, Yuko wapi Bwana, Mungu wako? Macho yangu yatamtazama; sasa atakanyagwa kama matope ya njia kuu. 11 Ni siku ya kujengwa kuta zako! Siku hiyo mpaka utasongezwa mbali. 12 Siku hiyo watakujia kutoka Ashuru na miji ya Misri, na kutoka Misri mpaka huo Mto, na kutoka bahari hii mpaka bahari hii, na kutoka mlima huu mpaka mlima huu. 13 Hata hivyo nchi itakuwa ukiwa kwa sababu ya hao wakaao ndani yake, kwa sababu ya matunda ya matendo yao. 14 Walishe watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako, wakaao peke yao, mwituni katikati ya Karmeli; na walishe katika Bashani na Gileadi, kama siku za kale. 15 Kama katika siku zile za kutoka kwako katika nchi ya Misri nitamwonyesha mambo ya ajabu. 16 Mataifa wataona, na kuzitahayarikia nguvu zao zote; wataweka mikono yao juu ya vinywa vyao, masikio yao yatakuwa na uziwi. 17 Watayaramba mavumbi kama nyoka, kama vitu vitambaavyo juu ya nchi watatoka katika mahali walimojificha, wakitetemeka; watakuja kwa Bwana, Mungu wetu, kwa hofu, nao wataogopa kwa sababu yako. 18 Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu, na kuliachilia kosa la watu wa urithi wake waliosalia? Hashiki hasira yake milele, kwa maana yeye hufurahia rehema. 19 Atarejea na kutuhurumia; atayakanyaga maovu yetu; nawe utazitupa dhambi zao zote katika vilindi vya bahari. 20 Wewe utamtimilizia Yakobo kweli yako, na Ibrahimu rehema zako, ulizowaapia baba zetu tangu siku za kale.

 

Utawala au kipindi cha milenia utaendeshwa kutoka Yerusalemu na kwa kuwatumia wana wa Yakobo na uzao wa Ibrahimu kutoa viongozi na utaratibu kupitia Masihi na wateule.

 

Sehemu ya Nyongeza ya Ufafanuzi wa Kitabu cha Mika

Mika anatoka karibu kwenye zama moja hiyohiyo na Isaya na Amosi. Maisha ya Isaya kwenye kitabu yanafananishwa kwa sehemu na 2Wafalme hususan 18:13-20:21. Inadhaniwa kuwa alizaliwa Yerusalemu mnamo mwaka 760 au kabla yake. Wito wake aliupata katika mwaka ambao Mfalme Uzia alifariki (yaani mwaka 742). Alioa na anamtaja mke wake kuwa ni nabii mke (Isaya 8:3). Huduma yake idumu kwa miaka 40 wakati wa tawala za wafalme Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia (Isaya 1:1). Tunapomsikia Isaya kwa mara ya mwisho ni kwenye kitisho cha Senakaribu kuuitishia Yerusalemu mwaka 701 KK.

 

Alipata wito wake akiwa Hekaluni karibu na mahali patakatifu au maskani. 

 

Anaripotiwa kuwa aliuona nusu wakati wa utawala wa Manase mwana wa Hezekia (687-642 KK) (sawa na Waebrania 11:37 na 2Wafalme 21:16 na Yoshua Antiq. x, 3.1). Manase alikuwa na umri wa miaka 12 wakati alipoanza kuwa mfalme na alipendezwa na ibada za Waashuru na alirudisha ibada za Baali na kupajenga tena Mahali pa Juu pa kumfanyia ibada. Bila shaka alipingwa na kukemewa na nabii Isaya na manabii wengine na inaripotiwa kuwa aliwaua wengi sana miongoni mwao.

 

Pia Yeremia aliyanukuu moja kwa moja maandiko ya Mika 26:16-19 na kudhania kuhusu baadhi ya maandiko ya Mika yasiyoandikwa na yeye mwenyewe ni mambo yanayodhaniwa kuwa ya uwongo.

 

Inaonekana kwamba Isaya na Mika walichaguliwa na Mungu ili kuweka hukumu yake kwenye modomo ya mashahidi wawili (soma Isaya 1:1 na Mika 1:1).

 

Aliona kuwa Mika alikuwa ni wa kutoka mara tu kabla ya mwisho wa utawala wa Yothamu mwaka 735 tangu mwaka 739-693 KK. Kwa hiyo Isaya alikuwa ameitwa na kuanza kutumika rasmi tangu mwaka 742 KK na Mika alifuatia miaka kadhaa baadae na aliishia miaka minane baada ya tuliposikia mara ya mwisho kutoka kwa Isaya lakini huenda ni miaka michache tu baada ya kufa kwake. Tarehe alizokadiria Bullinger sio sahihi kwa sababu hii. Kwa vyovyote vile, amefanya ulinganisho yanayotumika kwenye maandiko yaliyo kwenye tafsiri ya the Companion Bible.

 

Bullinger anasema kuwa tunaweza kuona “kwa kulinganisha Mika 4:10 na Isaya 39:6, tuna jambo linguine lenye maneno yanayofanana linalojitokeza kwa manabii wawili tofauti, na mengine yamehitimishwa kwamba nabii mmoja alinukuu kutoka kwa mwenzake, inatokana na hii, ni dhana fulna iliyojengeka kwa watu hadi leo, nk. Lakini hakuna mabishano yaliyopo yanaweza kuchukuliwa kuwa msingi kwenye matukio kama haya; kwa sababu rahisi ambazo hatushughuliki nazo na maneno ambayo Mungu anayanena ya manabii, lakini maneno ambayo Mungu aliyanena kwa kuwatumia wao (Waebrania 1:1, nk). Kwa hakika Mungu anaweza kunena maneno hayohayo, hata kwa maneno yanayolingana tu, kwa manabii wake wawili, watatu au hata zaidi. Kama mahitaji yalikuwa ni sawa, ni kwanini basi maneno yasilingane?" kama tulivyoona kipindi karibu kinajiri kwa Mika na Isaya kilikuwa ni cha karibu ni kilekile kabisa. “Si ajabu basi kwamba mzingira yalihitaji maneno hayohayo, yakisisitiza uthibitisho wa Neno la Yehova ‘kwa kinywa cha mashahidi wawili au watatu’. Wote wawili walikuwa peke yao, wakiwa hawana wazo la ‘kunukuu’ aliyoyasema mmoja wao na kuyatia kwa mwingine, kama inavyodaiwa na mwandishi wa kitabu shajara toleo la kumi na moja maarufu kama The Encyclopedia Britannica, eleventh (Cambridge) edition, 1910, 1911, vol. xviii, p. 357, anayesema: ‘haiwezekani kuwa hivyo, kama moja ya kurasa hizi (Mika 4-7) zinaweza kumwelezea Mika mwenyewe’. Hii inasemekana kwenye uso wa ukweli kwamba Yeremia (Mika 26:16-19) yawezekana alinukuu na kumtaja Mika.

 

Maandiko yafuatayo kutoka kwenye milinganisho inayotumika:

Mika 1:9-16, Isaya 10:28-32.

Mika 2:1, Mika 2:2, Isaya 5:8.

Mika 2:6, Mika 2:11, Isaya 30:10,11.

Mika 2:11, Isaya 28:7.

Mika 2:12, Isaya 10:20-23.

Mika 3:5-7, Isaya 29:9-12.

Mika 3:12, Isaya 32:14.

Mika 4:1, Isaya 2:2.

Mika 4:4, Isaya 1:20 .

Mika 4:7, Isaya 9:7.

Mika 4:10, Isaya 39:6.5.

Mika 2-4, Isaya 7:14.

Mika 5:6, Isaya 14:25.

Mika 6:6-8, Isaya 58:6, Isaya 58:7.

Mika 7:7, Isaya 8:17.

Mika 7:12, Isaya 11:11.

 

Notisi za Bullinger kutoka kwenye tafsiri ya Companion Bible ni kama zifuatavyo.

 

Maangamizi katika Israeli na Yuda Mika 1:1

Neno la BWANA. Mahali pekee palipojitokeza usemi huu kwenye kitabu hiki: kunatufanya tupokee hii kutoka kwa Yehova, na sio Mika, na kuiona kalamu ya Mika lakini ikiandika maneno ya Yehova.

BWANA. Kwa Kiebrania Yehova, ukurasa wa Nyongeza 4.

Mika = Ni nani kama Yehova? Ni kifupi cha Mikaiya (2Nyakati 18:7, nk.); limeatumika kwenye Yeremia 26:18 (kwa Kiebrania). Linganisha na 7:18.

Watata: Mareshah (aya ya 15) au Moreshethi-gathi (aya ya 14); sasa ni Tel Sandahanna, huko Shefela, au uwanda, kati ya Yudea na Ufilisti. Kwenye uchimbuzi katika Sandahanna jina la zamani linalonekana kama Marissa. Marissa lilikuwa ni koloni la Wasidoni (karne ya 3 KK), na baadae ulitumika kama mji mkuu wa Idumea ya Waedomu wakati wa utumwa wa Yuda (tazama Taarifa za Nyuma, au Records of the Past, vol. iv, part x, pp. 291-306).

Aliyoiona. Linganisha na Isaya 1:1. Obadia 1:1. Nahumu 1:1.

Kuhusu, nk. Hii inahitimisha somo au fundisho.

 

Mika 1:2

Sikieni watu wote. Mika anaanza kwa kuweka maneno ya kuhitimisha na mengine ya Mika au Mikaya (1Wafalme 22:28), na inarudiwa kwenye 3:1, 9; 6:1, 2. Mara tano, sio mara tatu, kama wanavyosema wengine; na hawafanyi namna yoyote ya kimuundo wa kitabu chote. Rejea kwenye vitabu vya Torati. (Kumbukumbu la Torati 32:1). Nyongeza 92.

Ninyi nyote = enyi watu, wao wote.

watu = enyi watu wote. Inajumuisha na sisi wenewe.

Vyote vilivyomo ni = utimilifu wake.

Mungu na awe shahidi. Rejea kwenye vitabu vya Torati, (Mwanzo 31:50).

Bwana. Kwa Kiebrania Adonai. Nyongeza na. 4.

MUNGU, kwa Kiebrania Yehova, Nyongeza na. 4.

BWANA*. Moja ya maeneo 134 ambayo Sopherim anasema waliyabadilisha "Yehova" kwenye maandiko ya zama kale na kuandika "Adonai". Tazama Nyongeza na. 32.

Kutoka kwenye hekalu lake takatifu. Linganisha na Zaburi 11:4. Yona 2:7. Habakuki 2:20.

Takatifu. Tazama kwenye Kutoka 3:5.

 

Mika 1:4 milima, nk. Aya hii inatabiri maafa au msiba wa kwenye 2Wafalme 17 na 25.

 

Mika 1:5

Kutenda maovu = uasi. Kwa Kiebrania pasha'. Nyongeza na. 44.

Dhambi. Kwa Kiebrania chata'. Nyongeza na. 44. Aramu, na Syria soma imba.

Nini = Ambaye.

Je, sio Samaria? = je, sio za Wasamaria [ibada za sanamu]? Lugha ya mfano. Erotesis. Nyongeza na. 6.

Mahali pa Juu. Linganisha na 1Wafalme 12:31; 14:23. Ezekieli 6:6. Hii ilidumu katika Yerusalemu (Yeremia 32:35); ndiyo kutajwa kwao kwenye maswali zaidi. Lugha ya mfano. Erotesis. Linganisha na 2Wafalme 16:4.

Je, hao sio Yerusalemu? = Je, hii sio ya Yerusalemu [madhabahu za vinyago]?

 

Mika 1:6

Gundua, nk. Hii sasa ni ya hivi karibuni (1911) ilifanwa ni kilimwengu na wauza mvinyo Warabu.

 

Mika 1:7

Sanamu za kuchonga. Kwa kiebrania pesilim. Rejea kwenye vitabu cha Torati. (Kutoka 20:4). Nyongeza na. 92.

Warithi. Ni neno la kitaaluma la kwenye vitabu vya Torati linalomaanisha ajira ya kahaba, ambayo kwayo ibada za sanamu zinalinganishwa kwayo. Linganisha na Hosea 8:9, 10; 9:1. Rejea kwenye Kitabu cha Torati. (Kumbukumbu la Torati 23:18). Linganisha na Nyongeza 92.

Watarudi, nk.: yaani, mali au utajiri uliopatikana kutokana na ibada za sanamu utachukuliwambali na waabudu sanamu wa Kiashuru.

 

Mika 1:8

Lia kwa huzuni = ombolaza. Linganisha na Muundo hapo juu; na kufanya uzito wa “mzigo” wa nabii.

Majoka = mbweha.

Bundi. Kwa Kiebrania ni kilio cha mabinti makahaba.

 

Mika 1:9

Jeraha = mshituko. Kwa Kiebrania makkah (maarufu)

Hiki. Kwa KiaAramu na Kisyria husomeka "yeye mwanamke". Inamaanisha mstuko wake, ambao ni maarufu.

Yeye mwanaume = mwanaume, inataja wale maadui wasiotajwa. Kwa Kiaramu na Kisyria husomeka, “mwanamke”, ikionyesha “mshituko” wa hukumu.

Lango. Linganisha na Obadia 1:11, 13.

 

Mika 1:11

Unipitie mbali: yaani kwenda utumwani.

Saphir, kupata aibu yako, nk. Hapa tunakuwa na mkanganyo. Saphir = Mji mzuri, aibika pamoja na uzuri wake; sasa es Suafir.

Mkazi wa Zaanani ambaye hajaja bado. Kwa Kiebrania hajaenda . . . Zaanani. Kwa Kiebrania. Kwa lugha fumbo ni Paronomasia (Nyongeza na. 6): lo yatz'ah . . . tz'anan = hajatoka nje [kuomboleza] ana mkazi wa Nyuma ya nje.

Asubuhi . . . kiwango chake. Inaanza na sentensi nyepesi hapa; “matatizCo ya Beth-ezeli (Mji-jirani) utakuwa ni jirani asiyefaa". Mkuu "kwa mapenzi ya nyumba ya Bystander, kutoka kwako nenda kwenye chumba cha kusimama au sebuleni".

Atapokea, nk; au atachukua kutoka kwao msaada wake.

 

Mika 1:12

Maroth alingojea kwa uangalifu mkubwa. Wanawake wakazi wa mji Mchungu muuzunikie kwa uchungu mwingi kwa bidhaa zake [alizonyang’anywa].

Uovu = maafa makubwa. Kwa Kiebrania ra'a'. Nyongeza 44.

BWANA. Kwa Kiebrania Yehova. Nyongeza 4. Sio kwa nasibu.

Lango la Yerusalemu. Kwnye Silinda ya Taylor, Senakarebu anataja kuvunjika kwa lango lake (col. iii, lines 22:23).

 

Mika 1:13

Mwanaume mkazi = mwanamke mkazi.

Lakishi . . . chekecha maziwa. Kumbuka kugha Fumbo Paronomasia (Nyongeza na. 6). Kwa Kiebrania larekesh . . . lakish = [funga gari la farasi] kwenye nyumba, Ewe Mwanamke mkazi wa Mji wa farasi,

Lakishi. Sasa Ummtum Lakisi, au Tell el Hesy. Soma notisi kwenye 2Wafalme 14:19; 19:8.

mwanamke. Kwa dhahiri ni Samaria. Linganisha na aya ya 5:9; 6:16.

 

Mika 1:14

Toa wakilisha kwa = toa raslimali kwa.

Akizib . . . uwongo. Kumbuka lugha Fumbo ya Paronomasia, = nyumba ya mji wa Uwongo ('Akzib) atabaini uwongo (iakzab).

Achzib. Sasa es Zib (Yoshua 15:44; 19:29. Waamuzi 1:31).

 

Mika 1:15

Mrithi . . . Mareshah. Kwa Kiebrania mmliki (hayyoresh) . . . Ee Raslimali (Mareshah). Mmiliki ambaye Yehova angemleta ilikuwa ni Ashuru.

Atakuja, nk. Utukufu: yaani muungwana (Isaya 5:13) wa Israeli atakwenda (au kukimbilia) kwenye [pango] la Adulamu; kama Daudi alivyofanya (1Samweli 22:1).

 

Mika 1:16

Nyoeni vipara, nk. Ishara ya kuomboleza. Linganisha na Ayubu 1:20. Isaya 15:2; 22:12. Yeremia 7:29; 16:6; 47:5; 48:37). Hii imeelekezwa kwa Yuda. Ilikatazwa chini ya sheria (Kumbukumbu la Torati 14:1). Yuda wamekuwa kama wamataifa: na waomboleze kama wamataifa wapagani.

Watoto = wana.

 

Olee kwa Wadhulumaji  Mika 2:1

Uovu. Kwa Kiebrania 'aven. Nyongeza na. 44. Sio neno linalofanana kama lilivyo kwenye 3:10. Kumbuka uponzi kwenye aya za 1, 2. Soma muundo uliopo, ukurasa wa  1253.

Kazi = mpango.

Uovu = udhaifu. Kwa Kiebrania ra'a'. Nyongeza ya 44.

Ni = uwepo. Kwa Kiebrania yesh. Soma andiko la Mitahli 8:21.

Kwa nguvu za mikono yao. Kiambishi cha vitabu vya Torati. Rejea kwenye kitabu cha Torati (Mwanzo 31:29). Linganisha na Mithali 3:27. Nehemia 5:5. Halionekani pengine popote.

 

Mika 2:4

Chukulia kama mfano. Rejea kwenye kitabu cha Torati (Hesabu 23:7, 18; 24:3, 15, 20, 23). Imetokea mara mbili kwenye Ayubu (Ayubu 27:1; 29:1); mara moja kwenye Isaya (Isaya 14:4); mara moja kwenye Habakuki (Habakuki 2:6). Halipo pengine popote. Nyongeza ya 92. Kumbuka lugha ya Mafumbo FigChleuasmos (Nyongeza ya 6).

Omboleza kwa maobolezo na huzuni. Kumbuka lugha Fumbo Polyptoton na Paronomasia (Nyongeza ya 6), kwa msisitizo. Kwa Kiebrania venahah nehi nihyah = sikitika masikitiko ya ole.

Badilika = badilika [kwa ubaya]. Kwa Kiebrania mur; sio halaph = imebadilika [kwa uzuri]. Soma Walawi 27:10.

Kugeukia mbali = kuwa mpagani mmataifa: yaani adui wetu Muashuru.

 

Mika 2:5

Pigia kura mnyororo. Inamaanisha desturi, ambayo, inayokizunguka kila kijiji katika Palestina, nchi ligawanywa kwa kura kila mwaka kwa familia mbalimbali; kwa hiyo, maelezo yaliyo kwenye Zaburi 16:6, "kamba" lililowekwa kwa lugha Fumbo ya Metonymy (kwa kweli), Nyongeza ya 6, kwa eneo au kipande cha ardhi kilichowekwa alama na hiyo. Ni kwa hiyo = gawanya urithi wako. Rejea kwenye Torati (Hesabu 26:55, 56). Nyongeza ya 92.

Kusanyiko = mkusanyiko. Linganisha na Kumbukumbu la Torati 23:1-3, Kumbukumbu la Torati 23:8.

 

Mika 2:6

Unabii = Sio kubwabwaja.

Wakiasemezana wao kwa wao unabii = kwa hiyo walisemasema hovyo.

Hawatatabiri. Sio neno la kawaida kwa unabii, lakini kwa Kiebrania ni nataph.

Wao: yaani hawa manabii wa uwongo.

Wao = kama kwa vitu hivi: yaani matendo haya ya Yehova.

Kwamba, nk. Kuwapa, "[usemi], ni lazima awaondolee mbali hawa watesaji na wadhulumaji".

 

Mika 2:7

Yakobo. Tazama maandiko ya Mwanzo 32:28; 43:6; 45:26, 28.

Ni Roho, nk.? Reja kwenye Totati (Hesabu 11:23, ni neno moja hilihili). Nyongeza ya 92.

Roho. Kwa Kiebrania ruach. Nyongeza ya 9.

Haifanyi = hawataki?

Yangu. Tafsiri ya Septuagint inasomeka "Yake", kama kwenye fungu lililotangulia: au = si maneno yangu mazuri [asema Yehova]?

Tenda mema = ya kupendeza.

 

Mika 2:8  

Hata kwa kuchelewa = Ni jana tu, au hivi karibuni: ukabaji na uporaji huu wa barabarani ni mpya na uovu wa hivi karibuni.

 

Mika 2:10

Inuka wewe, nk. Kwa kawaida imenukuliwa kimakosa kwa nia njema; ila Muundo unaonyesha hii kuwa ni sehemu ya maombolezo (ukurasa wa 1253).

Hii = hii [nchi]. Rejea kwenye Torati. (Kumbukumbu la Torati 12:9). Nyongeza ya 92.

yake: yaani hii [nchi].

Imechafuliwa. Rejea kwenye Torati. (Walawi 18:27, 28, ni neno moja). Nyongeza ya 92.

Itaangamiza. Rejea kwenye Torati (Walawi 18:28; 20:22; 26:38). Linganisha na Ezekieli 36:12-14.

 

Mika 2:11

Mvinyo. Kwa Kiebrania yayin. Nyongeza ya 27.

Kinywaji kikali. Kwa Kiebrania shekar. Nyongeza ya 27.

Nabii = kubwabwaja; kama kwenye 2:6. Kwa rahisi mletaji  [wa maneno].

 

Mika 2:12

Nitafanya, nk. Tazama Utaratibu, ukurasa wa 1253.

Israeli. Tazama maandiko ya Mwanzo 32:28; 43:6; 45:26, 28.

ya Bozra: au, kwenye Septuagint, kwenye dhiki au mateso. Mshirika (aya za 12, 13) haiongelei rehema, lakini ya hukumu, ikienda sambamba na mshirika (1:2-4). Sio "mabadiliko kamili", na hakuna "ahadi kwa waliosalia" linganisha na Isaya 34:6. Amosi 1:12.

Piga kelele kubwa = kuwa kwenye rabsha.

Wanaume = wanadamu. Kwa Kiebrania 'adam. Nyongeza ya 14.

 

Mika 2:13

Mvunjaji = Mtu anayefanya mavunyiko au anayevunja. Muashuru. Kwa Kiebrania paratz, kama kwenye Kutoka 19:22, 24; 2Samweli 5:20. 1Nyakati 14:11; 15:13. Kwa ujumla ni maana au mtazamo mbaya.

Iliyovunjika = iliyovunjwa.

Tolewa nje = tolewa kwa shuruti . . . [kwenda utumwani].

Itapita = imepita.

Juu ya = kwenye: kwa kuwa ni hukumu ya Yehova. Linganisha na 1:2-4.

 

Watawala Walimshutumu  Mika 3:1

Sikia. Hii haina dalili ya Kimuundo. Ni uendelezaji wa vitisho dhidi ya watawala (3:1-4, ukurasa wa 1253, kufananisha na "-3", 3:9-12, hapo chini).

Wafalme = waamuzi.

 

Mika 3:3  wakatekate vipande, kama wanakwenda kupikwa kwenye chungu = watawanyie mbali, kama nyama za mwili kwa kuipika kenye chungu.

 

Mika 3:5

Kusea = potoka.

Uma kwa meno yao. Kuwapotosha kwa matendo ya kuabudu sanamu za wamataifa wazungukao madhabahu za Baali, wakiuuma mzabibu kwa vinywa vyao na walihubiri “amani”, ambapo mzabibu ukiwa ni mfano wake (Mfano 8:11). Linganisha na Zekaria 9:7.

Na yeye, nk = lakini ni kinyume chake asiyeweka [mzabibu] kinywani mwake waliotangaza vita.

Vita = ya kupigania dini au ya kidini.

 

Mika 3:6   kwamba hatakuwa wa mbinguni. Rejea kwenye Torati, (Kumbukumbu la Torati 18:10,14. Hesabu 22:7; 23:23). Nyongeza ya 92.

 

Mika 3:10 uovu = udanganyifu. Kwa Kiebrania. 'aval. Nyongeza ya 44. Sio neno moja na lililo kwenye 2:1.

 

Mika 3:12

Sayuni. Soma Nyongeza ya 68.

Kulimwa kama shambani. Hii ni kweli kwenye kiwanja cha Ofeli, lakini sio kweli kwa kiwanja kilichozoeleka kusini magharibi mwa Yerusalemu. Tazama jarida la Nyongeza la 68. Linganisha na 1:6. Yeremia 26:18.

Yerusalemu. Mji ulio sawa na Mlima wa Moria.

Misaada = maangamizo. Kumbuka lugha ya Mfano Paronomasia (Nyongeza ya 6). Kwa Kiebrania yirushalaim 'iyyin. Linganisha na 1:6.

Mlima wa nyumba. Moria na Hekalu. Soma Nyongeza ya 68.

Mahali pa juu msituni = kimo cha urefu wa msitu.

 

Maandiko kweeye tafsiri ya Companion Bible 1909, imasema hivi:

Mika 4:

Siku Zinazokuja za Amani

Mika 4:1

Katika siku za mwisho = katika mwisho wa siku zote. Hapa kunapelekwa kwenye siku fulani iliyo mbele yetu. Rejea kwenye Torati (Mwanzo 49:1, ni andiko hilohilo. Hesabu 24:14). Nyongeza 92. Linganisha na Isaya 2:2, nk. Ezekieli 38:8, 16. Hosea 3:5

Mlima, nk. Linganisha na 3:12; na soma Isaya 2:2-4. Nabii zote mbili zinajitegemea, na ni ujalizo (soma Zaburi 24:3. Ezekieli 28:16).

BWANA. Kwa Kiebrania Yehova. Nyongeza 4.

Imeanzishwa: kujikita sana: sio kwa wakati fulani tu.

Watu = manabii.

 

Mika 4:8

Mnara wa kundi. Kwa Kiebrania  mnara wa 'Eder. Rejea kwenye Torati (Mwanzo 35:21; hakuna mahali pengine). Umetumika hapa kwa Bethlehemu (linganisha na Mwanzo 35:19 na 5:2); hapa imejumuishwa na "Opheli" kwenye fungu la maandiko, "mahali alipozaliwa Daudi" na ni "Mji wa Daudi".

Ngome kuu. Kwa Kiebrania 'Ophel. Soma Nyongeza 68 na Nyongeza 54, mstari wa 21, "ngome", ukurasa 78. Soma maandiko ya 2Nyakati 27:3.

Kwanza = zamani. Kwa kuandika hii linganisha na Kutoka 34:1 (meza). Hesabu 21:26 (wafalme). Kumbukumbu la Torati 4:32; 10:10, nk. (siku). 2Nyakati 9:29; 16:11; 20:34 (matendo).

 

Mika 4:9

Kwanini wewe Unalia? Hii inamaanisha maumivu ya uzazi ya taifa jipya litakalorudishwa tena katika siku hiyo na kwa wakati ule. Linganisha na Isaya 13:8; 21:3, nk.

 

Mika 4:10

Sasa = wakati huohuo: yaani kabla ya siku ile. Linganisha na 4:11 na 5:1.

Hata kwa = kwa kadiri ya. Linganisha na Isaya 39:7; 43:14.

Babeli. Yawezekana "ilivyokuwa machoni na upeo wa kisiasa wa Mika", lakini ilikuwa ni ya Yehova. Linganisha na Amosi 5:25-27. Matendo 7:42, 43.

Hapa . . . kule. Sio marudio ya msisitizo: yaani kule na kisha katika siku za mbele zijazo.

Komboa = komboa [kama ndugu wa damu wa karibu]. Kwa Kiebrania ga'al. Soma Kutoka 6:6.

 

Mika 4:11

Sasa = Wakati huohuo: kama ilivyo kwenye 4:10; 5:1. Rejea kwenye hali ya haraka na kusukiza inayoashiria uadui.

Mataifa mengi. Linganisha na Isaya 33:3. Maombolezo 2:16. Obadia 1:11-13.

Jicho. Kwa hiyo baadhi ya maandiko, zenye machapisho mawili yaliyochapishwa ya zamani kwa lugha za, Kiaramu., Kisyria, na Vulgate; lakini kwenye maandiko ya Kiebrania inasomeka "machos". Linganisha na Zaburi 54:3.

 

Mika 4:12

Hawajui kitu chochote. Linganisha na Isaya 55:8. Yeremia 29:11.

Mawazo = makusudio, au mipango: yaani kwa Israeli kwa kulitakasa kutokana na ibada za sanamu kwa dhiki na mateso yake.

Mashauri: yaani pamoja na wao wenyewe. Sababu inayofuatia.

Kwa: au, kile.

Sakafu = sakafu ya kupuria nafaka.

 

Mika 4:13

Kupura = kupura kama kwa kumtumia maksai.

Pembe . . . kwato. Inammnisha nguvu za ng’ombe dume maksai, na kwenye uhitimisho wa mapatilizo au maangamizi. Rejea kwenye Torati (Kumbukumbu la Torati 25:4). Nyongeza 92. Linganisha na Isaya 41:15. Yeremia 51:33.

Nitafanya. Kwa Kiaramu, Septuagint, Kisyria, na kwenye Vulgate inasomeka "utafanya".

Kutakasa = kujitoa; kama ilivyo kwenye Yoshua 6:19, 24. Linganisha na Zekaria 14:14. Rejea kwenye Torati (Walawi 27:28).

BWANA. Kwa Kiebrania 'Adon. Jina takatifu, linalohusiana na mamlaka au utawala wa duna. Soma jarida la Nyongeza 4.

 

Mika 5:

Kuzaliwa kwa Mfalme katika Bethlehemu

Mika 5:1

Sasa = Wakati huohuo; kama kwenye 4:10, 11. Inaonyesha kuwa 5:1 inahusiana na kipindi cha mpito kati ya kile kipindi kilichopo na “siku ile” ya 4:1, 6.

Jikusanyeni pamoja, nk: au, nanyi mtakumbana na dhiki kubwa (kwa dhambi zenu), binti zenu watateseka.

Yeye mwanaume: yaani adui. Muashuru.

Sisi. Nabii anajijumuisha mwenyewe.

Mwamuzi. Liwali ambaye ndiye mtawala (linganisha na 1Wafalme 22:24. Maombolezo 3:30; 4:20; 5:8, 12), ambaye alikuwa ni mfano wa Masihi (Mathayo 27:30).

Fimbo = fimbo ya enzi ya mfalme. Kwa Kiebrania shebet = rungu (la kujilindia), kama ilivyo kwenye 7:14; kwa hiyo, au ofisi; na sio fimbo, bakora au fimbo (ya kusaidia), kama ilivyo kwenye 6:9. Soma andiko la Zaburi 23:4.

 

Mika 5:2

Lakini wewe. Hii inaonyesha Muundo au Utaratibu. Linganisha na 4:8 na 5:2. Imenukuliwa kutoka kwenye Mathayo 2:5, 6. Yohana 7:42.

Beth-lehemu Efrata. Jina kamili illopewa kama kwenye Mwanzo 35:19, ambalo linahusiana na Mwanzo 35:21 na 4:8.

Jina = alichukua jina la cheo [hadi kwenye cheo kilichopo]. Linganisha na 1Wakorintho 1:27-29.

Maelfu = wilaya kadhaa (1Samweli 23:23). Kama ilivyo kwenye migawanyiko ya Kiingereza cha zamani, iliyoitwa “mamia”. Linganisha na Kutoka 18:25. Rejea kwenye Torati (Kutoka 18:25).

Jikusanyeni mje. Ione tofauti hapa kati ya neno la Kiebrania (yatza) na bo' = jongeeni mje, kwenye Zekaria 9:9. Matukio yote yaliyo katikati ya hizi mbili yanafanya kipindi tunachokiita “Ujio wa kwanza”, na huu ni tasira ya ule “Ujio wa pili”; ujio wa mtu aliyeandikwa kwenye 1Wathesalonike 4:16, na ujio wa mtu aliyeandikwa kwenye 1Wathesalonike 5:2, 3, na 2Wathesalonike 2:8, mtu wa kale aliye kwenye neema, hatimaye hukumuni. Kipindi cha namna hiyohiyo kitatokea kwa ujio wa mtu ambaye siye mfano wa ujio wa kipindi cha mfano 5:2, na Zekaria 9:9.

Ndani yake = kwa.

Milele. Linganisha na Zaburi 90:2. Mithali 8:22, 23. Yohana 1:1, 2.

 

Mika 5:3

Hadi ufike wakati: yaani mwishoni mwa "wakati huohuo" (aya ya 1).

Yeye asafiriye. Linganisha na 4:9, 10-, hapo juu na ona hapa; pia kwenye Yohana 16:21, 22, na Ufunuo 12:1-6.

Watoto = wana.

 

Mika 5:4

Yeye mwanaume: yaani Mchungaji wa Israeli. Rejea kwenye Torati (Mwanzo 49:24). Nyongeza 92. Linganisha na Zaburi 80:1. Yeremia 31:10. Ezekieli 34:23.

Lisha = tunza au chunga, au mchungaji (kama kundi). Linganisha na 7:14. Isaya 40:11; 49:10.

BWANA. Kwa Kiebrania Yehova. Nyongeza 4.

Mungu. Kwa Kiebrania. Elohim. Nyongeza 4.

Wao. Israeli, Kundi lake.

Watakaa. Kwa ilinzi wa milele.

Atakuwa Mkuu. Linganisha na Zaburi 22:27; 72:8; 98:1. Isaya 49:5, 7; 52:13. Zekaria 9:10. Luka 1:32. Ufunuo 11:15.

 

Mika 5:5

Mtu huyu, nk. = huyu [Mchngaji mkuu wa Israeli]. Linganisha na Zaburi 72:7. Isaya 9:6, 7. Zekaria 9:10.

Muashuru. Hii imesisitizwa kwenye Kiebrania.

Wakati, nk. Linganisha na Isaya 7:20 8:7-10; Isaya 37:31-36.

Kisha, nk. Linganisha na Isaya 44:28; 59:19. Zekaria 1:18-21; Zekaria 9:13; 10:3; 12:6.

Wachungaji saba . . . wanaume. Wakati wakati huo utakapokuja maana ya hii itaonekana.

Watu wanaume. Kwa Kiebrania 'adam. Nyongeza 14.

 

Micah 5:8

Itakuwa, nk. Hii inamaanisha kuwarejesha au kuwafanya upya Israeli "katika siku hiyo"; sio kwa watu wengine wowote wale sasa.

Watu. Kwa Kiebrania = watu wenhi.

Kama simba, nk. Rejea kwenye Torati (Hesabu 23:24; 24:9). Nyongeza 92.

 

Mika 5:9

Watatolewa na kupelekwa mbali. Tazama lugha ya Mfano Anaphora (Nyongeza 6), kwenye marudio, "ondolewa mbali", mara nne kwenye aya za 9-13. Yote yanayotajwa haya hatimaye yanawarejesha Israeli.

 

Mika 5:10

Katika siku ile. Utaratibu huu unahusiana na 5:10-14 pamoja na 4:6 -- 5:8, na inaonyesha kuwa ni sawasawa, na tena kwenye wakati ujao, iliyoitwa kwenye 4:1 "siku za mwisho".

Asema BWANA = [ni] nabii wa Yehova.

Nitawakatiliambali, nk. Oma kwenye 5:9. Rejea kwenye Torati (Kumbukumbu la Torati 17:16). Nyongeza 92. Linganisha na Isaya 2:7. Zekaria 9:10.

 

Mika 5:12

Uchawi = ushirikina au matendo ya kichawi. Rejea kwenye Torati (Kutoka 22:18. Walawi 19:26. Kumbukumbu la Torati 18:10). Nyongeza 92.

Mkono. Mandiko kwenye tafsiri ya Septuagint, na Kisyria, zinasonasomeka "mikono".

Wabashiri au wapiga ramli; yaani watumiaji wa picha za zenye tafsiri nyingine ya siri au sanaa za kiokaliti.

 

Mika 5:14

Kuchukua au uchukuzi = kung’oa, au kuangusha chini.

Glovu zako = 'Ashera zako. Nyongeza 42. Rejea kwenye Torati (Kutoka 34:13. Kumbukumbu la Torati 7:5; 12:3).

Miji yako. Ginsburg anadhani "vinyago vyenu". Bango kitita zilizo kwenye tafsiri ya A. V. Inasema "maadui".

 

Mika 6:

Shutuma ya Mungu kwa Watu Wake

Mika 6:4

Niliwaleta huku, nk. Rejea kwenye Torati (Kutoka 12:51; 14:30; 20:2. Kumbukumbu la Torati 4:20). Nyongeza 92.

Na aliwakomboa inyi. Rejea kwenye Torati (Kutoka 6:6; 13:13-16).

Nyumba ya watumishi = nyumba ya utumwa. Rejea kwenye Torati (Kutoka 13:3, 14; 20:2. Kumbukumbu la Torati 5:6; 6:12; 7:8).

Niliwatuma mbele . . . Miriamu. Rejea kwenye Torati (Kutoka 15:20, 21. Hesabu 12:4, 10, 15; 20:1; 26:59). Miriamu hakutajwa baada ya Kumbukumbu la Torati 24:9, isipokuwa kwenye 1Nyakati 6:3.

 

Mika 6:5

Kumbuka sasa, nk. Rejea kwenye Torati (Heabu 22:5; 23:7; 24:10, 11; 25:1; 31:16. Kumbukumbu la Torat 23:4, 5). Nyongeza 92.

Balaki. Hakutajwa tangu kwenye Waamuzi 11:25.

Balaamu. Hakutajwa tangu kwenye Yoshua 24:9, 10, isipokuwa kwenye Nehemia 13:2. Linganisha na 2Petro 2:15, na Yuda 1:11. Ufunuo 2:14.

Utakatifu = mwenendo wa haki au mtakatifu.

 

Mika 6:8

Mtu mwanaume. Kwa Kiebrania 'adam. Nyongeza 14.

Neema = kupenda wema, au rehema.

Kuenenda kwa unyenyekevu. Usemi wa Kiebrania ni (hatzene' leketh) inaonekana hapa peke yake. Aya hii inajumuisha kanuni zinazotawala maongozi ya Yehova chini ya Torati au Sheria, ila sio chini ya Injili. Sasa inatubidi kuwa na imani ili kumweka Mbadala wake yeye aliyemtoa kwa ajili ya wenye dhambi; na haki yake ni budi iweondolewa kutoka kwenye neema. Soma Nyongeza 63. IX: na 72. Linganisha pia na Warumi 3:23, 24. Waefeso 2:3-9. Tito 3:5-8, nk.

 

Mika 6:9

Mji. Limewekwa kwa lugha Mfano Metonymy (ya Somo), Nyongeza 6, kwa wakazi.

Mtu mwenye hekima ataliona Jina lako = [kama inavyopasa kuwa] uthabiti (au usalama) vitalizingatia Jina lako. Tafsiri ya Mugah Codex,ilinukuu kutoka kwenye tafsiri ya Massorah (Nyongeza 30), inayosomeka: "ni kama kutoa heshima kubwa".

Hekima. Kwa Kiebrania tushiyah. Soma andiko la Mithali 2:7.

Yako. Tafsiri ya Septuagint linasomeka: "na yeye (BWANA) atawaokoa kama mtaliheshimu jina lake".

Fimbo. Kwa Kiebrania matteh = bakora (ya kusaidia au ya kuadhibia). Sio neno moja na lililo kwenye 5:1; 7:14. Vinginevyo linaweza kuwekwa kwa lugha Mfano ya Metonymy (kwa sababu yake), nyongeza 6, kwa kuadhibia adhabu stahiki, au kutoa Umboyai kwamba: "sikieni enyi fimbo, na [yeye] mwenye kupanga [adhabu], “kiambishi cha vebu, ‘hiki’, ni kangaga.; wakati "fimbo" ni harakoa. Kwa hiyo tunaweza kutoa “adhabu” (kwa Kiebrania tokahath), ambayo ni fem.

 

Mika 6:10

Uovu . . . muovu = ukengeufu . . . kengeuka. Kwa Kiebrania rasha'.

Kipimo kidoho, nk. Tazama neno "machukizo" hapo chini. Kwenye muundo hiuu, ni kwenye Mithali 22:14 peke yake.

Kipimo = efa. Tazama Nyongeza 51.

Machukizo. Rejea kwenye Torati. Kutokana na maneno yaliyotoholewa, kwenye Kiebrania za'am limechaguliwa kwenye Hesabu Num 28:7, 8, 8, "najisika" = limenajisika. Limejitokeza mara nane peke yake mahala penginepo. Nyongeza 92.

 

Mika 6:14

Utakula, nk. Rejea kwenye Torati (Walawi 26:26).

Utashushwa chini = kutoridhika kwako au kuwatupu na kupungukiwa. Kwa Kiebrania yeshach. Linatokea hapa peke yake.

Nitakuwa katikati yenu = [nitabakia] pamoja nanyi.

Shikilia. Nyaraka zingine zikiwa na toleo moja ya machapisho ya zamani (gombo za Marabi), zinasomeka "chukua milki au tamalaki".

 

Mika 6:16

Muundo. Kwa Kiebrania hukkoth = kwa mtazamo wa kidini (Walawi 20:8. 2Wafalme 17:34. Yeremia 10:3).

ya Omri. Linganisha na 1Wafalme 16:31, 32, kama kwenye ibada ya Baali.

Ilishikwa = ilishika kikamilifu. Linganisha na Hosea 5:4.

Nyumba ya Ahabu. Linganisha na 1Wafalme 16:30. nk.; 21:25, 26. Tazama Nyongeza 65.

Ndipo ningeweza kufanya, nk. Rejea kwenye Torati (Kumbukumbu la Torati 28:37).

 

Mika 7:

Nabii Anaijua Siri za Israeli

Micah 7:3

Uovu. Kwa Kiebrania ra'a'. Nyongeza 44.

Anaomba = anaomba [zawadi]. Rejea kwenye Torati (Kumbukumbu la Torati 16:19). Nyongeza 92. Linganisha na 3:11. Hosea 4:18.

Mwamuzi anaomba = mwamuzi [anahukumu], nk. Dhana ya lugha ya Mfano ya Umboyai. Linganisha na 3:11. Isaya 1:23.

Zawadi = hongo au rushwa.

Tamaa mbaya sisyotimilika = kutofikisha hamu ya moyo wake. Kwa Kiebrania nephesh. Nyongeza 13. Linganisha na 3:9-11.

Wao: yaani mfalme na mwamuzi.

Zinga kwa kuzungushia = ifume pamoja. Linaonekana hapa peke yake.

Hiki. Kwa kiambishi cha Kiebrania ni fem., kwa hiyo inatupasa kutoa nauni kangaga: kwa mfano zimmah = kusudi la kidhalimu, au kitendo kiovu. Isaya 32:7.

 

Mika 7:4

Siku ya walinzi wangu. Imewekwa kwa lugha Mfano ya Metonymy (ya Kiunganisho), nyongeza 6:. siku [ya hukumu] iliyotabiriwa na walinzi.

 

Mika 7:5

Msimwamini = Msimtumainie. Kwa Kiebrania ni 'aman. Soma Nyongeza 69.

Msimtegemee yeye. Kwa Kiebrania batah. Soma Nyongeza 69. Kwa hiyo tafsiri ya Wamasori wa Magharibi. Watu wa Mashariki, wakiwa na matoleo matatu ya kale, yaani, Septuagint, Syria, na Vulgate, inasomeka "kuondoa au kutoiweka", nk. Imenukuliwa kutoka kwenye Mathayo 10:35, 36; Luka 12:53.

 

Mika 7:6

Kutoheshimu au kudharau, nk. Rejea kwenye Torati (Kutoka 20:12. Kumbukumbu la Torati 5:16). Nyongeza 92.

Ni ya mtu mwanaume. Kwa Kiebrania ish. Nyongeza 14. II.

Mwanaume. Kwa Kiebrania ni uwingi wa 'enosh. Nyongeza 14. III. Aya ya 6 haiishi "ghafla sana", wala hapa haitendi "yawn karne moja". Aya ya 7 inatoa ahueni ya kweli kinyume na ahueni zisizopo kwenye aya za 5, 6.

 

Mika 7:8

Wakati niangukapo: yaani kwenye maangamizo; sio kwenye dhambi. Kwa usemi wa Moja kwa moja ni Nimeanguka, Nimeinuka; ingawa naweza kuketi gizani, YJehovah, nk.

 

Mika 7:11

Amri = ilielezea au kumaanisha kikomo au mpaka. Kwa hiyo, kitabu cha Oxford Gesenius, uk. 349. Linganisha na Ayubu 26:10; 38:10. Mithali 8:29. Isaya 24:5. Yeremia 5:22. Kwa Kiebrania chok.

Ondolewa mbali = kuwa mbali: yaani kuongezwa. Soma kitabi cha Oxford Gesenius, uk. 935. Kwa Kiebrania rachak, kama ilivyo kwenye Isaya 26:15. Tazama lugha ya Mfano ya Paronomasia (Nyongeza 6), yir'chok.

 

Mika 7:12

Yeye = mmoja. Lakini husasan usomaji mbalimbali inaitwa Sevir (Nyongeza ya 34), inasomeka "wao": yaani watumwa wako waliouhamishoni, wanakuja = rudini nyumbani; kama kwenye 1Samweli 11:5. Zaburi 45:15. Mithali 2:10, au, kwenye Baraka; kama ilivyo kwenye Zaburi 69:27. Hakuna “kilichoangukia chini” kwenye andiko!

Ashuru. Tazama neno “adui” kwenye 7:10.

Miji yenye maboma = miji ya Matzor (yaani yenye maboma) weka Minsri. Linganisha na Isaya 19:6; 37.

 

Mika 7:14

Kuwekwa huru, nk. Kumbuka hapa, maombi ya Mika. Utoaji  Umbo yai: "[Ndipo Mika aliomba, na kusema: Ee Yehova] Na uwaweke huru Watu wako", nk.

Weka huru = wachungaji wako (mwanaume).

Fimbo. Kwa Kiebrania shebet, kama ilivyo kwenye 5:1; sio kama kwenye 6:9. Hapa ni kanuni inayosemwa.

Inayokaa, nk. = uwe nasi (kangaga): yaani "kundi". Kwa Kiebrania tz'on (linganisha na jinsia).

Upweke = pweke. Rejea kwenye Torai (Hesabu 23:9. Kumbukumbu la Torati 33:28). Nyongeza 92.

Kama ilivyo kwenye siku za zamani = kama ilivyo kwenye zama zilizopita: ndivyo itakavyokuwa tena kwenye siku ya usoni ya kuungana kwake Israeli; sio katika siku za Mika, wakati Israeli walikuwa kwnye umiliki wa Bashani, nk. Hakuna jinsi kwa hiyo, ya kuweka tarehe yalivyofanyika maombi haya “kwenye kipindi cha karibu sana kwa historia ya Israeli, siku za nabii Hagai na Zekaria", kama inavyodaiwa.

 

Mika 7:15

Kwa mujibu, nk. Aya za 15-17 ni majibu ya Yehova kama kutiishwa kwa maadui wa Israeli. Rejea kwenye Torati. Soma maandiko kwenye 6:4. Nyongeza 92. Sio mwendelezo wa maombi ya Mika.

Nitajionyesha kwake. Rejea kwenye Torati (Kutoka 34:10).

 

Mika 7:16

Wawawekea mikono yao, nk weka kwa lugha ya Mfano Metonymy (ya Kiunganisho), nyongeza 6, kwa ukimya, ambao ulikuwa ni usemi uliosikiwa masikioni mwao. maandiko fulani, ambazo kwenye ishara nne zilizochapishwa. Soma Ayubu 21:5; 29:9; 40:4.

Masikio yao. Baadhi ya nyaraka au maandiko, pamoja na hasira zilizochapishwa hapo kale, zinasomeka "na zao".

 

Mika 7:17

Ramba vumbi. Imewekwa kwa lugha ya Mfano Metonymy (ya Kiunganisho), kwa upole na unyenyekevu wa hali ya juu, kama ilivyo kwenye Mwanzo 3:14. Linganisha na Zaburi 72:9. Isaya 49:23.

Ondoa = njoo kwa kutetemeka.

Mashimo = ukazaji. Kwa Kiebrania misgereth.

Minyoo. Rejea kwenye Torati (Kumbukumbu la Torati 32:24, ni neno moja hilohilo). Limejitokeza sehemu hizi mbili peke yake.

 

Mika 7:20

Ingawa atafanya, nk. Imenukuliwa kutoka kwenye Luka 1:72, 73.

Kuapishwa kwa mababa zetu. Rejea kwenye Torati (Mwanzo 50:24. nk.) nyongeza 92. Soma Zaburi 105:9, 10, 42,

                                                            q