Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[239]
Kwanini Pasaka Ilichelewa Sana Kufanyika Mwaka 1997?
(Toleo La 1.0 19980217-19980217)
Makala ilichapishwa kwenye Jarida lililojulikana kama Robo ya Biblia ya kiyahudi [Jewish Bible Quarterly], Toleo la 25, Namba 1, 1997 na lilirudiwa kuchapishwa kwa kuruhusiwa. Chama cha Biblia cha Kiyahudi, yaani The Jewish Bible Association ina tovuti yao ya http://www.jewishbible.org.
Christian Churches of God
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 1997 Jewish Bible
Association)
Published with permission of Executive Secretary, Jewish Bible Association
(tr. 2016)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama
yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.
Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala
yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org nad http://www.ccg.org
Toleo la 25, Namba 1, 1997
JARIDA
LIJULIKANALO KAMA “JEWISH BIBLE
QUARTERLY”
KWANINI PASAKA ILICHELEWA SANA KUFANYIKA
MWAKA HUU?
SAUL LEEMAN
(Saul Leeman ni Rabi mstaafu aliye kwenye
Jimbo la, R.I.)
Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie
pasaka Bwana, Mungu wako
Unapoisoma aya hii ya Kumbukumbu la Torati 16:1 pamoja
na maandiko mengine ya marabi, mtu anaweza kujihisi yuko sahihi kwa kudhania
kwamba Torati ilikusudia kwamba sikukuu ilipasa ifanyike, kama inavyofanyika
mara nyingi, wakati wa mwezi wa kwanza wa majira ya baridi. Mwaka huu (5757), hata
hivyo, haikuweza kuwa hivyo. Ili kuelewa kwa kina uchelewaji wa kuja kwake
sikukuu hii ya majira ya baridi, maswali fulani yanapaswa kuulizwa:
Ni
kwa nini Pasaka ilichelewa sana mwaka huu?
Pasaka imechelewa sana mwaka huu (Aprili 22) kwakuwa
huu ulikuwa ni mwaka mrefu kwenye Kalenda ya Kiyahudi wenye miezi kumi na
mitatu ukiwa na mwezi wa nyongeza. Katika kila mzunguko wa mwaka wa 19 kuna
miaka 7 mirefu yenye mwezi wa nyongeza: nayo ni mwaka wa 3, wa 6, wa 8, wa 11, wa
14, wa 17, na wa 19.
Ndiyo,
najua hilo. Lakini kwenye suala la miaka 10 iliyopita au zaidi, hii imekuwa ni
namba ya miaka mirefu, na bado sijaona Pasaka ikichelewa kama mwaka huu,.
Imekuwa hivyo kwa kuwa huu ni mwaka wa 19 wa
mzunguko, ni mwaka mrefu unaotokea tu kila baada ya kipindi cha miaka miwili
ukifuatiwa na mwaka mrefu uliopita. Vivyohivyo ni kweli (na hata zaidi sana)
ilivyo kwenye mwaka wa 8 wa mzunguko. Kwa hiyo, kuna miaka hii miwili katika
kila mzunguko ambapo Pasaka inachelewa majira haya ya baridi. Mnamo mwaka 1967
(“mwaka wa 8") Pasala iliangukia tarehe 25 Aprili, uchelewaji mrefu sana
kuwahi kutokea.
Unasema
“ilichelewa sana.” Je, inaweza kumaanisha kuwa Pasaka inaweza kuchelewa hata
ikafanyika baada ya Aprili 25?
Ndiyo, ni kweli – na hili ndilo tatizo kubwa
lililo kwenye kalenda ya Kiyahudi; yaani., hii inategemea na uhesabuji wa mwaka
wa mfumo wa jua ambao hauko sahihi na unaupotofu wa takriban dakika 6½. Ni hali
hii ya mapungufu ndiyo inayopelekea Pasaka kuelekea majira ya joto kwa kiwango
cha takriban siku kamili kwenye kila miaka 200, kukijitokeza tofauti ya
takriban siku 4½ kwa kila miaka 1,000. Hii ina maana ya kwamba kwenye kipindi
cha takriban miaka 1,000, Pasaka itakuwa inaadhimishwa karibia tarehe 1 Mei, na
kwenye miaka 8,000 ijayo, itaadhimishwa mnamo hata tarehe 1 Juni.
Je,
hali hii inaweza kurekebishwa?
Hali hiyo inaweza kurekebishwa kwa kupitia tu
kwenye matengenezo au marekebisho ya kalenda yalituama kwenye hesabu za mfumo
wa kalenda.
Unasema
kuwa matengenezo au marekebisho ya kalenda hatimaye yatakuwa ya lazima.
Kumekisha wahi kufanyika kitu kama hicho kwa siku za hivi karibuni katika historia?
Ndiyo, imewahi kufanyika. Mwaka 1582 kalenda ya Juliani, ambayo ilikuwa
ikitumiwa tangu mwaka 46 KK, ilibadilishwa na kuanza kutumika kwa kalenda ya Gregorian.
Kalenda ya Julian, iliyoanzishwa na Kaisari Julius, ilituama kwenye mahesabu
yaliyotuama kwenye urefu wa mwaka wa mrengo wa jua yenye siku 365 na masaa 6, ambapo
kiuhalisia una upungufu wa dakika 11¼.
Tofauti hii ilipelekea kuwa na makosa ya takriban
siku 3 katika kila miaka 400 (au siku 7½ kwa kila miaka 1,000). Matokeo yake,
mnamo karne ya 16, siku ya ikwinoksi ya majira ya machipuko ilirudishwa nyuma hadi
Marchi 11. Ili kuifarekebisha ili iwe na tarehe sahihi, Papa Gregory XIII alitangaza
kwamba siku inayofuatia Oktoba 4 haitakuwa au kuitwa Oktoba 5 bali itaitwa
Oktoba 15. Kwa tangazo hili, aliirudisha siku ya ikwinoksi ya majira ya baridi
iendelee kuwa Marchi 21, tarehe ambayo ilikuwa kwenye mwaka wa 325 BK ambapo
Baraza la Mtaguso wa Nicea (likilenga kuiingiza Easter isimame badala ya Pasaka)
lilitangaza kwamba utaratibu wa kupangilia tarehe ya kusherehekea Easter ingekuwa
“Jumapili ya kwanza baada ya mwezi mkamilifu wa kwanza na zaidi au baada ya
ikwinoksi ya majira ya baridi."
Kumbuka kwamba lilikuwa ni jukumu lake kuweka siku
maalumu ya kuadhimisha Easter ambayo ilihamasisha marekebisho ya kalenda ya
Papa.
Kukiwa kumeondolewa makosa ya kimpangilio ya siku 10,
kalenda ya Gregorian ilibidi iwezeshe na kuhakikisha kwamba hakuna kitu kama
mwaka wa marejeo ukitokea. Hii ilifanyika kwa kutangaza kwamba miaka ya karne isiwe na mwaka mrefu isipokuwa kama itakuwa
inagawanyika kwa tarakimu 400. Matokeo ya uwezesho huu, ndipo miaka ya 1700,
1800, na 1900 – miaka mirefu kwenye kalenda ya Julian – haikuwa miaka mirefu
kwenye kalenda ya Gregorian. Rejea kati ya mbili sasa ni siku 13. Ifikapo mwaka
2100, tofauti yake itakuwa siku 14.
Lakini
matendo ya kidini ya Kiyahudi hayana uhusiano na kalenda ya jua. Je,
maadhimisho yote ya Kiyahudi yanaendana na kalenda inayotokana na mzunguko wa
mwezi?
Sio kabisa. Kuna maadhimisho ya aina mbili yanayoendana
na kalenda ya mzunguko wa jua. Moja wapo ni ile ya tal umatar, maombi kwa ajili ya umande na mvua. Baraza la Talmud linakusanyika
kwa kufanya maombi ya kurudiarudia kwenye maombi haya ili kuanza siku 60 baada
ya ikwinoksi ya majira ya mvumo wa upepo na kuendelea hadi Pasaka. Kitabu cha
maombi hata hivyo, kinaiweka kwenye orodha hii siku ya tal umatar kwenye Desemba 5 – siku 73 baada ya ikwinoksi (Septemba
23). Tofauti hii ya siku 13 ni tofauti kati ya kalenda za Julian na ya Gregorian,
na tofauti hizi zinaendelea kukua kwa kiwango cha siku 7½ kwa kila baada ya
miaka 1,000.
Kwa siku hii ya tal umatar kuendelea kwenye mwelekeo wa Pasaka kwa kiwango cha siku
7½ kwenye kila miaka 1,000, wapangaji siku hatimaye watafikia hatimaye kwenye takriban
miaka 35,000. Mapema kabla ya hapo, hata hivyo, tarehe ya Pasaka itabidi ifanyiwe
marekebisho, na ndipo hili tatizo la tal
umatar itapata suluhu.
Katika Israeli kuna kiasi kidogo sana cha "mitambo
ya kupiga ashirio" kuhusiana na tatizo hili kwa kuwa kwenye chi Takatifu
majira ya hii tal umatar yanaanza
kwenye juma la kwanza ya mwezi wa Buli au Heshvan na haiungani au kuhusiana
moja kwa moja na kalenda ya mzunguko wa jua kabisa (Soma kitabu cha Bab.
Talmud, Taanit 10a).
Ulisema
kuwa kulikuwa na “maadhimisho mawili” yanayoendana na kalenda ya mzunguko wa jua.
Ni ipi nyingine moja?
Nyingine moja ni Birkat ha-Hammah – Baraka ya Jua, maombi ya dua yanayofanywa kwa kurudiwarudiwa wakati wa ikwinoksi
ya majira ya machipuko mara moja kwa kila kipindi cha miaka 28 wakati kwamba,
kwa mujibu wa mapokeo na desturi, wanaamini kwamba dunia inarudi mahala pake
palepale ikihusiana na jua lililochukua mkondo wakati wa Uumbaji. Ilikuwa
ikiombwa kila mara siku ya Jumatano (waliyoamini kuwa ni siku ambayo jua
liliumbwa). Maombi yake yaliyofanywa kwa siku za hivi baribuni sana ilikuwa
mnamo Aprili 8, 2009. Na haya ni maombi ya kuomba viumbe vilivyo kwenye anga la
juu na yasiyo na maana yoyote kabisa, na ambayo kwa hakika yamewekezwa kwetu
ndani yetu wakati sherehe hizi za Baraka za Jua zilifanyika mnamo Aprili 8,
1953 wakati tulipokuwa ndipo “tunasherehekea siku ya Ikwinoksi ya majira ya Baridi"
– mnamo siku ya 23 ya mwezi wa Abibu au Nisan, siku nane baada ya majilio ya
Pasaka!
Wakati marekebisho muhimu ya kalenda
yatakapofanyika, ndipo Birkat ha-Hammah
itaangukia pia kwenye kipindi cha mwezi
wa kwanza cha mwezi kuwa mkubwa na mkamilifu cha majira ya baridi (na sio cha
mwezi kamili wa pili kama ilivyo kwenye mwaka huu) na Birkat ha-Hammah itawekwa ili itokee kwenye Jumatano ya kwanza ya majira
ya baridi.
Ni
lini ambapo kalenda iliyopo sasa ya Kiyahudi ilianzishwa na ni nani aliyeianzisha?
Kalenda ya Kiyahudi kama tuliyonayo leo, ilitungwa
na Kiongozi wa Kidini au Rabi aliyeitwa Hilleli II, yapata mwaka 359 BK.
Kwa
nini imetuama kwenye mzunguko wa miaka 19?
Kwa kuwa muundo wa msingi wa kalenda ya Kiyahudi
unafuatia miaka 19 ya mzunguko wa jua = au sawa na miezi mwandamo 235 (miaka 19
ya kawaida inayofuata mwandamo wa mwezi kujumlisha na miezi 7 ya nyongeza ya
mwezi mwandamo). Wayunani walikiita kipindi hiki kuwa ni Mzunguko wa Kimetoniki.
Inamaanisha
kwamba kila miaka 19 tarehe za kidunia (ya Gregorian) na “tarehe za Kiyahudi”
zinashabihiana?
Ndiyo, kila miaka 19 ama zinashabihiana kabisa au zinapishana
kwa takriban siku moja.
Kuna
siku ngapi jumla kwenye kalenda ya Kiyahudi?
Inatofautiana. Kwenye mwaka wa kawaida (usio mwaka
mrefu) una siku 353 (mara nyingine), siku 354 (mwaka wa kawaida), au siku 355 (ukizidi
sana). Sawasawa na ilivyo kwenye mwaka mrefu, kuna siku 383, 384, au siku 385.
Ni
nini kinachosababisha hali hii?
Sababu zake ni za kidini. Ya msingi ni [lo 'adu
rosh] ni kwamba Rosh Hashanah haipasi kabisa iangukie siku ya Jumapili, Jumatano,
au Ijumaa. Iwapo kama Rosh Hashanah itaangukia siku ya Jumatano au Ijumaa, basi
Yom Kippur ingetangulia au kufuatia Sabato, ikipelekea au kusababisha mazingira
au hali ambayo ingehusisha ugumu kuiadhimisha. Kama Rosh Hashanah ingeangukia
siku ya Jumapili, basi Hoshanah Rabbah ingeangukia siku ya Sabato na
kungetolewa wito wa kuharibu au kutatiza taratibu
fulani za kidini ambazo marabi wa kifarisayo hawakupenda ziondolewe.
Kwa hiyo, kuyaweka mambo sawa kwa kupunguza
msimamo kulikuwa lazima ilipojitokeza hivyo, na wakati kwamba, kama Rosh
Hashanah zingeangukia siku yoyote kati ya hizi tatu, ingeahirishwa hadi siku
inayofuatia.
Hivyo, kwenye mwaka wa kawaida (wa siku 354), urefu
wa miezi ni kati ya siku 30 na 29. Kwenye mwaka wa kati (wa siku 353), miezi ya
Heshvan na Kisleu kila mmoja una siku 29. Katika mwaka wenye siku nyingi (wa
siku 355), miezi ya Heshvani na Kisleu kila mmoja unakuwa na siku 30.
Kulikuwa
na utaratibu gani kabla ya Rabi Hillel II hajaanzisha na kuitengeneza kalenda
ya sasa ya Kiyahudi?
Kabla ya siku hiyo, tulikuwa na kalenda
isiyopangiliwa vizuri “ya kudumu.” Mwezi mpya ulijulikana kwa kuutafuta na kuangalia hapa na pale. Mashahidi
waliouona walilazimika kwenda Yerusalemu kushuhudia kuwa wameuona. Iwapo kama
baada ya kupeleleza, na Beth Din akakubaliana na taarifa hii ya kuonekana kwake
kutokana na ushuhuda huo, ndipo Mwezi Mpya ulikubalika kuwa umeanza na Rosh
Hodesh ilitangazwa. Beth Din aliketi kwa utayari ili kupokea taarifa za ushuhuda
katika “siku inayokamilisha siku ya 30" ya mwezi unaoishia ili achukue
hatua ya kuamjua kama siku hiyo inaweza kutangazwa kuwa “siku ya kwanza” ya mwezi
unaoanza. Kama uamuzi kama huo haujafanywa siku hiyo, siku inayofuatia
ilitangazwa moja kwa moja (hata kama hakuna anayeshuhudia kuwa ameuona) na kufanyika
kuwa ni adhimisho la Mwezi Mpya au Rosh Hodesh, kwa kuwa mwezi una urefu
usiopungua siku 29 na hauzidi siku 30. (Soma kitabu cha Mishnah Rosh Hashanah, Sura
za 1-2).
Mara tu Mwezi Mpya unapotakaswa au kuadhimishwa,
ndipo habari zilitangazwa kwenye Nchi yote Takatifu.
Ilikuwaje
basi kuhusu Wayahudi waliokuwa wakiishi nje ya nchi Takatifu? Jumbe uliwafikiaje
wao?
Hili ni swali zuri. Mara nyingi kutokana na ugumu
wa kimawasiliano, ujumbe haukuwafikia kwa wakati muafaka, nah ii iliwafanya
Wayahudi waliokuwa wanaishi nje ya ardhi ya Palestina kwenye matatizo makubwa
sana ya kidini. Kwa mfano, wakati ulipofika wakati wa kuadhimisha Pasaka,
iliwabidi kubahatisha kuona kama mwezi uliopita ulikuwa na urefu wa siku 29 au
30. Iwapo kama ulikuwa na siku 29, ndipo Pasaka ingeadhimishwa kwa siku fulani;
na kama ulikuwa wa siku 30, ndipo Pasaka ingeadhimishwa siku inayofuatia. Ni
nini cha kufanya? Ni kuondoa wasiwasi iliyopo, ndipo waliamua “kufanya kitu cha
kuwahakikishia usalama” na kuadhimisha Yom
Tov kwenye siku zote mbili. Ni sawa tu na ilivyo kweli kwenye Shavuoth na
Sukkoth. Kwa hiyo, Wayahudi walioishi Uhamishoni (ukiwaondoa ndugu zetu
Wanamatengenezo) walikuwa na maadhimisho zaidi ya matano ya siku za yom tov kwa mwaka kuliko walivyokuwa
wanafanya Wayahudi walioishi nchini au ndani ya Israeli.
Vipi
kuhusu Rosh Hashanah?
Rosh Hashanah inaadhimishwa kwa muda wa siku mbili
hata huko Israel pia.
Kuna
mengi sana yahusuyo utaratibu wa kuupangia Mwezi Mpya kipindi cha kabla ya
kuanzishwa kwa kalenda. Sasa niambie tafadhali hii miaka mirefu ilipangiliwaje
kabla ya kuandikwa kalenda?
Hapa, pia ilikuwa ni hali ya kimaisha ambapo
marabi waliamua kabla ya kuutangaza mwezi wa Abibu wakitilia maanani iwapo kama
ishara au dalili za majira ya maridi yamefika (kukoma kwa majira ya mvua, kuiva
kwa mazao, kutilia maanani kama siku ya ikwinoksi imekuwepo, nk). iwapo kama
kutaonekana kuwa majira ya machipuko yamechelewa, ndipo Adari ya Pili
iliingizwa ili kufidia mambo haya, na mwaka huu ulifanyika kuwa mrefu (Soma
kitabu cha Bab. Talmud Sanhedrin 11 a & b).
Kwa
nini ilionekana kuwa ni muhimu kuanzisha kalenda isiyo ya kubahatisha?
Kwa kuwa hata mababu waliosimamia uendeshaji wa
dini katika Nchi Takatifu hawakufurahia kabisa hali ile ya kubahatisha na kwa
kuwa serikali ya Kirumi ilikataza na kuthibiti uhuru wa kujiamulia wa baraza la
Sanhedrin katika kushughulikia mambo haya.
Kalenda
ya Kiyahudi haionekani kuwa kama ni ya mrengo wa mzunguko wa jua au mwonekano wa
mwezi. Unaiitaje kalenda hii kuwa ni ya mrengo upi?
Ni kalenda ya mrengo wa mwonekano wa mwezi, miezi yake inahesabiwa kutokana
na mwonekano wa mwezi na mwaka sambamba na mwonekano wa jua.
Umekwishaonyesha
tayari dalili ya kwamba uhesabuji wake wa mwaka unaoenenda kwa mzunguko wa jua unatofautiana
kwa upungufu wa takriban dakika 6½ kutoka kwenye mwaka halisi wa mzunguko wa
anga. Vipi kuhusu mahesabu ya mwezi wa mzunguko wa mwezi mwandamo?
Hapa ni sahihi sana kama inavyoweza kuwa. Kalenda
ya Kiyahudi huhesabiwa mwezi wake kwa siku 29, masaa 12, dakika 44, na sekunde 3.33 -- tofauti yake kutoka kwenye mwezi halisi wa
mrengo wa mznguko wa anga sio chini ya sekunde moja tu na nusu.
Kwa
kurudi nyuma sasa, ni kwamba umejionea nini kuwa ni kama “tatizo kbwa” lililopo
kwenye kalenda ya Kiyahudi --itachukua
muda gani kabla ya kufanyika kwa Pasaka mnmo Juni 21 na tangu hapo inamaana
kwamba haitakuja kurejea tena kwenye majira ya machipuko?
Ni kwa kipindi cha miaka 12,500.
Ni
kweli hivyo, kwa hiyo ni mapema sana kwa sasa kuogopa kuhusu marekebisho ya
kalenda?
Kwa hakika, inaweza kuwa sio mapema sana kufikiria
jambo hili.
Marekebisho
haya ya kalenda yatapaswa kufanyikaje?
Kuna njia mbili: ya kwanza ni ya kiasili, na
nyingine ni ya kimiujiza. Kwa upande mmoja, kunatakiwa kuwe na mkutano wa
sinodi ya ulimwengu mzima ya watu watakaowakilisha itikadi zote zinazoamini
imani ya Kiyahudi ambayo yatafikia kwenye makubaliano kwamba ni jinsi gani au
ni lini watakapoirekebisha kalenda. Kwa upande mwingine, Uliya atakuja na
kutusaidia kurekebisha mambo haya kwa faida yetu.
Nimegundua
kuwa hujaweka wazi shahiri kuhusu uwezekano upi unaodhania utakuwa wa kiasili
na upi wa kimiujiza. Lakini, kwa muono wako, ni upi kati ya hatima hizi mbili
unaonekana unaweza kutokea kabisa?
Kwa kweli, ni suala la kungojea na kuona tu.
q