Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[021]
Manabii Kumi na Mbili
(Toleo La 1.0
20150314-20150314)
Manabii Kumi na Mbili ni wa mwisho
kwenye utaratibu wa mpangilio wa Kanuni ya mpangilio wa vitabu lakini haina
maana kuwa wao ni wadogo au duni kwenye umuhimu wa Manabii wa Mungu.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati
Miliki © 2015 Wade Cox)
(tr.
2015)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Manabii
Kumi na Mbili
Utangulizi
Orodha ya Kikanuni ya mpangilio wa
Manabii Kumi na Mbili wanaoitwa au kujulikana kama Manabii Wadogo imeorodheshwa
kwa mpangilio ufuatao:
Hosea
Yoeli
Amosi
Obadia
Yona
Mika
Nahumu
Habakuki
Sefania
Hagai
Zekaria
Malaki.
Wamewekwa kwenye utaratibu au muundo
wa manabii watatu, kisha manabii sita na hatimaye manabii watatu.
Mpangilio uliotumika katika kuwapanga
sio mpangilio ambao Mungu aliutumia alipowatuma. Mungu alimtuma Amosi kwanza
wakati anaonekana kuwa watatu kwenye Kanuni hii ya mpangilio kwa mfano. Ni
sawa tu na kama Zekaria alipouawa na makuhani na manabii. Wengine waliteswa
vibaya mno.
UTARATIBU WA KIMPANGILIO WA MANABII.
Israeli walipewa miaka arobaini
kuwaonya tangu mwaka 761-721 KK kama tulivyoona kwa manabii wa mwanzoni, kina
Yona na Amosi. Abraham ibn Ezra mwanazuoni wa enzi ya zama kati alimuweka
kwenye miaka arobaini kabla ya kuanguka kwa Samaria lakini wanazuoni waliofuatia
wanamuwekwa kwenye miaka thelathini ya kabla ya kuanguka kwake Samaria
(750-720) (linganisha na Soncino, Tangu Utangulizi hadi ukurasa wa 1).
Hakuna shaka kwamba Mungu aliwaonya
Israeli kwa kipindi cha miaka arobaini kabla ya anguko la Samaria sawasawa na
utaratibu wa kiunabii.
Israeli walipewa miaka 40 na ndivyo
pia walivyopewa Yuda tangu mwaka 30 BK wakati wa Pasaka ya kifo cha Kristo hadi
mwaka 70 BK kwenye mwisho wa majuma Sabini ya miaka na kuangamizwa kwa Hekalu
kulikofanywa na Warumi (soma majarida ya Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Upya wa Hekalu (Na.
013) na Vita na Warumi na Kuanguka kwa Hekalu (Na. 298)).
Ndivyo ilivyokuwa pia Ishara ya Yona iliyoendelea kwa kipindi
cha yubile 40 kwenye Yubile ya miaka inayoendana kwa msingi wa kipindi cha
Kanisa kuwa jangwani kama ilivyokuwa kwa Israeli kuwa jangwani kipindi cha
Kutoka. Ndivyo ilivyokuwa pia kwa Makanisa ya Mungu limepewa miaka 40 ya
Upimaji wa Hekalu tangu mwaka 1987 hadi kwenye Yubile ya mwaka 2027 (soma pia
jarida la Upimaji wa Hekalu (Na. 137)).
Manabii wote Kumi na Mbili waliudumu
tangu miaka 40 kabla ya kuanguka kwa Samaria hadi kwenye Siku za Mwisho na ujio
wa Masihi na kutwaliwa au kutekwa ya mji wa Yerusalemu. Kisha Zekaria anaanza
mchakato wa utawala wa milenia.
Yona
Maonyo kwa Waashuru ambao walitumika
kwenye mkakati wa kuiangusha na kuikomesha dola ya Israeli yalifanywa na Yona
na kwa hiyo na maonyo yake yalifanana na ya Amosi.
Kama tutakavyoona kwenye jarida la
ufafanuzi wa kitabu cha Yona mwana wa Amitai akiwa kama mtu anayejulikana sana
kwenye historia. Ametajwa kwenye 2Wafalme 14:25. Alikuwa anatokea Gath-hefa ambao
ni mji wa mpakani na Zabuloni (sawasawa na Yoshua 19:13). Huenda
inaonyesha na Kiribeti ez Sura’ ambao ni mahala pakubwa sana
ulio maili tatu Kaskazini-Mashariki ya Nazarethi, ambao ulikuwa katika
Galilaya. Maneno ya Mafarisayo kwenye Yohana 7:52 yalikuwa ni ya
uwongo ule. Kristo alitokea eneo la Nazarethi ya Galilaya, kama alivyokuwa
Yona. Ulikuwepo wakati wa Zama za Chuma, awamu zote za I na II yaani miaya ya 1200-600 KK na ndicho
kipindi cha Yona na kabla ya hapo kwenye kipindi kilichofuatia cha Zama za
Shaba tangu mwaka 1550 KK na kuendelea. Yona alikuwa anahudumu kipindi kimoja
na Yeroboamu II mfalme wa Israeli (793-775 KK) na miaka ya mwanzoni ya utawala
wa Uzia (775-757 KK). Upo umbali mfupi upande wa kaskazini mwa kijiji kilichobakia
cha Meshedi ambacho ni mahala ambapo kimapokeo ndipo lilipo Kaburi la Yona.
Ni kama tulivyoona kwenye jarida
la Kuanguka kwa Misri (Na. 036), na
ilivyoelezewa tena kwenye jarida la ufafanuzi wa kitabu cha Yona, mwaka
732 KK mfalme Tiglathi Pileser III wa Ashuru aliungana na
Wadameski ili kuwatoza kodi Israeli na Yuda. Mwaka 729
KK Tiglath Pileser III aliungana na Wababeloni
na Shalmaneser V (tangu mwaka 724-721 KK) akajiunga na Israeli
mwaka 722 KK. Mrithi wake Sargon II aliyahamisha makabila kumi na mbili.
Ushuhuda wa Yona ulikuwa kwa kipindi
cha zaidi ya miaka arobaini tangu utawala wa Yeroboamu II (793-775) hadi Uzia
(775-753) na tawala zingine mchanganyiko zilikuwa kwa kipindi cha miaka arobaini
pamoja na kipindi cha matazamio tangu mwaka wa tatu wa utawala wa Uzia yapata
kama mwaka 772-732 hadi kwenye kipindi cha Kutozwa kodi hadi cha Waashuru.
Israeli walipelekwa utumwani Ashuru kwa kipindi cha kuanzia mwaka 722 KK
ambacho kilikuwa ni cha wastani wa miaka 40 na kisha miaka 50 au yubile ya
tangia unabii wa Yona kwa Israeli. Ilimpasa Yona ajifunze kutokana na huduma
yake ya Ninawi na kuwaonya Israeli kwa kile Mungu alichowafanyia na kile
ambacho hatimaye kingalichowatokea Israeli lakini hawakusikiliza kama Yuda
wasivyomsikiliza kwa kipindi chote cha miaka arobaini walichopewa kwa ajili ya
toba (soma pia jarida la Kuujua Mzunguko wa Nyakati (Na. 272)).
Inaonekana kwamba Yona na Amosi
walikuwa wakihudumu kuwaonya kwa wakati mmoja wakiwa sehemu zote mbili, yaani
Ashuru na Israeli na kwa kipindi ambacho walipewa cha kuwaonya kwa miaka 40
kabla ya hukumu.
Kama tunavyoona kwenye maandiko au
jarida la Ufafanuzi wa Kitabu cha Hosea na tafsiri za Talmud na Midrash zina
mirejesho mingi inayomtaja Hosea na humo anachukuliwa kuwa ni mkuu zaidi kwa
unabii wake uliotolewa kwa wakati mmoja na wengine (linganisha na jarida namba
87a). Wafafanuzi wanaamini kuwa baba yake Beeri kuwa naye pia alikuwa nabii na
unabii wake umejmuishwa kwenye Isaya 8:19ff (sawa na kitabu cha Lev. Rabba 6,
xv, 2). Wadadisi na wafafanuzi wanadhana kwamba sio nabii zote za Hosea
zimeandikwa kwa mpangilio mzuri wa kimatukio ila tutaona kama hilo linamashiko
likinganishwa na historia. Tafsiri ya Talmud inakubali kuwa Mpangilio huu
Kikanuni haujaendana sawasawa pia (B.B 14a). Rejea kwenye kitabu cha Fafanuzi.
Yoeli anashughulika na maandalizi ya
wateule hasahasa tangu Masihi na kwenye nyakati za mwisho kuna mambo ya muhimu
ya kulitakasa kundi la Israeli kama Hekalu la Mungu na kutanguliwa na ni kwa
wakati mmoja wake na wa maandalizi ya maandiko ya Ezekieli. Bullinger anakiweka
hiki pamoja na Ezekieli tangu mwaka wa tano wa kwenda utumwani kwa Yehoyakimu
lakini haukuhesabiwa. Marabi wengine wanauweka mwaka huu mahali pengine. Kanuni
ya kupangilia vitabu inauweka katikati ya Hosea na Amosi. Sisi hata hivyo
tunajua kwamba Amosi na Yona waliwatangulia.kina Hosea na Yoeli ambao tarehe
zao hazijaandikwa na kuhusu matukio yajayo baadae kimsingi yanaangukia
kidogokidogo kwa Hosea. Kwa hiyo Mpangilio wa mambo unadhaniwa kuwa ni kama
Amosi, Yona, Hosea. Inaonekana hata hivyo huenda mpangilio wa kweli ni Yona,
Amosi na Hosea.
Amosi
Amosi kwa ujumla anachukuliwa kuwa
kitabu chake kiliandikwa kati ya miaka ya 765 na 750 KK kwenye utawala wa
Yeroboamu II (782-743). Kitabu chake kimeorodheshwa cha tatu kwenye
Kanuni ya uorodheshaji bali anachukuliwa kuwa ni wa kwanza wa manabii wengine
na kazi yake inamtenga mwenyewe na manabii wa zamani wa kabla yake ambao kwao
mkanganyo ulizisibu shule zao kama tunavyojionea kutokana na uandishi wake.
Kukataa kwake kuwa si nabii hakumaanishi kuwa hakuwa hivyo, bali alikuwa
anasikitishwa na kuwashutumu kwa ajili ya ufisadi wao na alikuwa anawaonyesha
kuwa yeye hayupo miongoni mwao.
Tetemeko la nchi alilokuwa
analiongelee kwenye 1:1 linaaminika kuwa lilitokea wakati wa Uzia (Zekaria
14:5). Kupatwa kwa jua kulikoongelewa kwenye 8:9 inahesabiwa kuwa kulitokea
mwaka 763 KK (linganisha na Soncino Utangulizi hadi ukurasa wa
81).
Tena tunaona kipindi cha miaka
thelathini na arobaini kikiwa cha muhimu kwa toba ya Israeli (linganisha pia na
jarida la Cox la Ufafanuzi wa kitabu cha Yona). Maonyo haya
yalifanyika mwaka 763-2 KK na mnamo kwama 733 Waashuru waliuteka mji wa Dameski
na kuwafanya kuwa nchi ya kuitoza kodi. Mwaka 723-2 waliingia Samaria na mwaka
722 KK Israeli walichukuliwa kwenda utumwani na wapelekwa eneo la kaskazini mwa
Araxes na hawakurudi hadi Ujio wa Pili wa Masihi.
Mika
Nabii Mika alitokea nyanda za chini za
Shefela karibu na nchi ya Wafilisti, mpakani. Alitabiri kipindi cha utawala wa
Yothamu, Ahazi na Hezekia (739-693 KK). Alikuwa
kijana mdoho akihudu wakati moja na Hosea na Amosi (soma Soncino,
uk. 153). Mika ana meingi yanayofanana na manabii wawili
waliomtangulia na tunaona kutoka kwenye maandiko kwamba anaulaumu utaratibu
uliokuwepo na wa makuhani na ushawishi wao au walivyokuwa wanavutiwa na imani
ya Baali ambaye dini ya waabudu Juan a unabii wa jinsi Mungu anavyotaka
kushughulika nao Israeli. Nabii Isaya analinganishwa na Mika kwenye fafanuzi za
Nyongeza. Inaonekana kabiwa kwamba walihudumu wakati mmoja, au kwa kipindi
kimoja.
Tutamuweka nabii huyu kutoka kwa Isaya
kila mara. Manabii Yeremia, Danieli, na Ezekieli wanadhaniwa walihudumu kipindi
hiki na wapo hadi kuanguka kwa dola ya Yuda na Wababeloni.
Andiko lililo kwenye Obadia
linaonekana kuwa liliandikwa wakati wa Yeremia ingawaje hatuna uhakika wa ni
lini liliandikwa na aya za mwanzoni za 1-9 zinarudia unabii ulionenwa kwenye
Yeremia 49:7-22 hasa hasa kwenye 49:9, 14-16 ambako unaongelewa kwa mdomo (sawa
na Soncino). Kazi imejawa na maneno yanayosisitiza haki
na hukumu ya Edomu.
Kama ilivyoonyeshwa kwenye ufafanuzi
kuhusu mashindano na chuki za Edomu kwa ndugu zake wawili mapacha kulionekana
kutokana na jinsi walivyoshindana tumboni na jinsi yalivyoendelea kwa kipindi
chote cha historia kwenye mgogoro ambao haujawahi kuonekana kati ya ndugu.
Mgongano huu ulijitokeza pia kwa Daudi
alipokuwa chini ya Sauli na baadae kwenye utawala na hadi kwenye vita vya
Wahasmonean yapata mwaka130 KK na manabii waliendelea kupiga kelele
kuwataka wajilipizie kisasi kwa Waedomu au wajitukuze kwa kupindualiwa kwao.
Amosi anawachutumu Waedomu kwakuwa
walikuwa wakiwachukia Israeli milele (Amosi 1:11).
(maandiko mengine yanachukuliwa na Soncino kama
kwenye Isaya sura ya 34; Ezekieli 35; Zaburi 137:7; Maombolezo 4:21.)
Tunapaswa kudhania kwamba andiko hilo
mara nyingi linaonekana kwa Yeremia na Obadia likimnukuu yeye zaidi ya kwamba
ni kinyume chake.
Nahumu
Wanazuoni wengi wanakubali kwamba
tarehe ya mwanzoni sana inayokadiriwa kuwa kimeandikwa ni mwaka 663 KK wakati
wa kuanguka kwa Thebes hadi Ashuru. Tarehe ya karibu sana inayodhaniwa ni
wakati wa kuanguka kwa Ninawi mwaka 612 KK. Dola mamboleo ya Babeli maarufu
kama Neo-Babylonian ilianzishwa na Nabopolasa mwaka 625 KK na, kuyakusanya
pamoja majeshi ya Wababeloni, aliuvuka mto Frati hadi Qablinu ambako
aliliangamiza Jeshi la Waashuru kwa maangamizo makubwa na kuwashinda. Wamedi
walianza kushambulia kutoka Mashariki na mwaka 614 waliuchukua na kuukamia mji
wa Asshuri. Nabopolasa alifanya muungano hatimaye na mfalme. Pamoja na Wamedi
na Wakaldayo aliendelea kushambulia hadi Ninawi ilipoanguka mwaka 612 KK. Mwaka
625 KK ni mwaka unaodhaniwa sana kwa wote wawili, yaani Nahumu na Sefania kwa
mujibu wa Gombo lililovumbuliwa la Torati tayari kwa marejesho mapya
yaliyofanywa na Yosia katika mwaka wa 18 wa utawala wake. Hivyo basi, ilikuwa
ni mwanzoni mwa kujiimarisha kwao Wababeloni ambavyo yalitumika katika kuiangamiza
Ashuru.
Bullinger anaamini kwamba maovu na
machukizo yaliyotajwa kwenye 1:11 kwa kweli inamkusudiac au kumaanisha
Rab-sheka aliye kwenye 2Wafalme 18:26-28 huyu anayeonekana kama Myahudi
aliyekengeuka au kukufuru ambaye alifanyika kuwa kiongozi mkuu au afisa wa
kisiasa wa Senakarebu na alifanya machukizo makubwa sana
kwa Yahova wa Israeli. Bullinger aliupa tarehe ya uandishi wa kitabu
hiki kuwa ni mwaka wa 14 wa utawala wa Hezekia na kwa hiyo ni mwaka
wa 704/3 KK. Hii huenda ni mapema sana ila ni baada ya
kuanguka kwa ufalme wa Israeli.
Obadia
Jina Obadia maana yake ni Mtumishi
wa Bwana. Ni jina la watu tofauti kumi na mbili kwenye Agano la Kale.
Hatuna hakika kuhusu nabii huyu ni yupi kati yao.
Haijulikani pia kwamba ni wakati gani
kitabu hiki kiliandikwa na aya za mwanzoni za 1-9 zinakazia unabii uliotolewa
kwenye Yeremia 49:7-22 hususan kwenye 49:9, 14-16 ambako imenenwa kwa mdomo
(sawa na Soncino). Uandishi wake umetuama mkazo wa haki na
hukumu ya Waedomu. Kwa kuujua ukweli huu yatupasa tudhanie kuwa kiliandikwa
baada ya Yeremia na huenda baada ya kugunduliwa kwa gombo au kitabu cha torati
Hekaluni kwa ajili ya marejesho mapya. Kwa hiyo kiliandikwa kabla ya Sefania.
Sefania
Kutokana na ilivyo hapo juu kwa hiyo
inatupasa kudhania kuwa ni Safania. Kama tunavyoona kwenye ufafanuzi wa kitabu
hiki cha Sefania, imeorodheshwa mara tisa miongoni mwa manabii walio kwenye
mpangilio wa kikanuni wa Agano la Kale. Mlolongo wake wa kiuzawa umeorodheshwa
kwa zaidi ya vizazi vinne kwakuwa neno la wazazi wake wa kale kwenye tafsiri ya
KJV ni neno hilihili lililo kwenye Kiebrania kama Hezekia na mamlaka
yanajiamini alikuwa ni kitukuu wa Hezekia Mfalme wa Yuda.
Inachukuliwa na kuaminika na E.A. Leslie (Kamusi ya Interp.
Dictionary of the Bible, Bk. IV,
pp. 951ff.) kwamba kitabu chake kimekadiriwa kuwa kiliandikwa harakati za
ushambulizi wa Scythian yapata mwaka 630-625 KK. Harakati na matendo ya Baali na
imani au dini ya Mungu Mke wa Waashuru na Wababeloni, dini zilizokuwa zimeingia
katika Yuda baada ya kupanuka kwa dola ya Waashuru na Manase wakajenga
madhabahu na kujitengenezea magari ya farasi mahala pa juu pa Mfalme Ahazia ili
kuabudu Jua na kushamirisha imani au dini potofu ya Siri. Waliliabudu jua,
mwezi na ishsra zote za mbinguni za kizodaki na Jeshi lote la mbinguni (2Wafalme
23:11ff).
Habakuki
Inaonekana kwamba Habakuki alitabiri
kidogo baada ya gombo la torati lililookotwa Hekaluni wakati wa utawala wa
Yosia mwaka 621 KK. Marejesho ya Yosia yalidumu kwa kipindi kifupi na wakati wa
Yehoyakimu watu walianza kuabudu tena sanamu na ukengeufu alizidi na
ulikubalika sana kipindi hiki. mfalme alibadilisha mambo na kutukuza maovu kwa
shuruti na hatimaye wakasalimu amri au kufanyika watumwa wa Nebukadneza (soma 2Wafalme
14:1).
Seder Olam zinafundisha kwamba Yoeli, Nahumu na Habakuki wote walitabiri katika
siku za Manase (soma Soncino Intro., p. 211). Mfalme huyu alikuwa
muovu sana na inadaiwa kuwa waliliruka jina lake kwenye vitabu vyao. Mchakato
unaodhaniwa zaidi unaanza baada ya mwaka 621 na unaanza kwa kuinuka au ujio wa
Wakaldayo. Wengine wanadhani kwamba huenda ilikuwa katikati ya Mapigano ya Carchemish
mwaka 605 KK na kuangamizwa kwa Hekalu mwaka 586 KK; tuseme ni kama mwaka 600 KK
wakati wa utawala wa Yehoyakimu.
Hata hivyo, kuna mambo mengi sana kwenye
unabii huu kuliko ulivyopunguzwa na mamlaka ya marabi. Ukomo wao kwa kipindi
cha baada ya Carchemish inavyoweza kuhitimishwa kwenye unabii kama tunavyoona
kutokana na ushindi au uvamizi wa Nabopolasa, mfalme wa 1 wa kizazi
cha Wakaldayo na Wamedi.
Hagai
Kata tutakavyoona kwenye jarida
la Ufafanuzi wa kitabu cha Hagai, jina la Hagai linatokana na neno Hag au sikukuu,
au karamu au sherehe.
Andiko hili linatokana na hali ya Mwandamo wa Mwezi Mpya, lakini Bullinger anakosea
sana kwa kusema kwenye uandishi wake kwamba linahusiana kuutaja mwezi mkamilifu
ambavyo ni makosa (soma tafsiri ya Companion Bible, fn. 1). Ni
mwezi wa Sita au mwezi wa Eluli. Ni katika mwaka wa Pili wa Dario Mwajemi
(Dario II) wakati agizo na maelekezo ya kuimalizia ujenzi wa Hekalu yalitolewa
na Yahova kwa kupitia nabii Hagai.
Andiko hili ndilo maelekezo au
agizo kutoka kwa Yahova kwa Yuda kwa kuukataa unabii uliotolewa na Zekaria.
Agizo limetolewa katika mwaka wa
Kwanza wa Yubile ya 71. Utaratibu kamili wa kimpangilio wa Yubile 71
tangu kufungwa kwa bustani ya Edeni umekamilika na Yubile ya mwaka 424/3 KK, na
Hekalu sasa linapasa kujengwa tena. Hili ni agizo la pili kutolewa na Mungu
lakini kazi ilisimamishwa kwa kitambo tangu agizo au tangazo la Koreshi hadi kipindi
cha Artashasta I aliyesimamisha ujenzi, na ulisimama hadi mwaka wa Pili wa Dario
Mwajemi (soma jarida la Ishaya ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na.
013)).
Kipindi
cha Dario na Manabii
Kama
tulivyoona kwenye majarida yote mawili ya ufafanuzi wa vitabu vya Hagai na Zekaria,
Dario II alipata kiti cha ufalme mwishoni mwa mwaka 424 au mapema ya mwaka 423 KK.
Agizo hili lilitolewa ili kuanzisha ujenzi mnamo mwaka 422 KK (Ezra 6:1 na
4:24) (yaani mwaka wake wa pili). Majuma 70 ya miaka inaanza tangu tarehe hii.
Kutokana na Ezra 5 inaonekana kwamba unabii wa Hagai na Zekaria mwaka 423 KK na
mwaka 422 KK. Majuma 70 ya miaka inaanzia tangu mwaka 423/22 KK (yaani mwaka wa
kwanza wa kipindi cha Yubile mpya). Ujenzi uliisha katika mwaka wa sita wa
Dario Mwajemi (Ezra 6:15) siku ya 3 Adari, yaani mwezi Marchi wa mwaka 418 KK.
Dario alifariki kwenye kipindi cha tangu mwishoni mwa mwaka 405 hadi majita ya
machipuko ya mwaka 404 (soma jarida la Ishara
ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 013):.
Mpangilio wa Bullinger sio wa kweli kwa jinsi hii kama ilivyo sawasawa na
kurasa za nyongeza).
Unabii huu
kwa hiyo unafungamana na ujenzi mpya wa Hekalu na unafanya sehemu Msingi wa
Nyumba ya Daudi imani na utaratibu wa unabii na maongozi yanayoendelea hadi
Siku za Mwisho na ujenzi mpya wa mwisho wa Hekalu (soma jarida la Utawala
wa Wafalme Sehemu ya III: Sulemoni na Ufunguo wa Daudi (Na. 282C)).
Sehemu ya
kwanza inatokana na mwanzo wa ujenzi na inaishia katika mwaka wa 2 wa ujenzi
kwa kiwango nusu. Sehemu ya pili ni ile inayotolewa kwa kipindi cha zaidi ya
nusu ya ujenzi na inafungamana na unabii hadi kwenye marejesho mapya ya Israeli
na Yuda chini ya Masihi, na Kanisa ambayo yamenenwa hapa kwenye maandiko kama
ni kutawala na Masihi huko Yerusalemu.
Hagai anahusika
pia kwenye unabii kwa kipindi kama tulivyoona.
Malaki
Malaki
alikuwa ni nabii wa mwisho na alihudumu kwenye miaka ya karibu nay a mwisho wa
uhai wa Ezra. aliishi kwenye wakati ambao Zekaria aliuawa.
Mathayo 23:35 inasema kwamba Zekaria aliuawa kati ya hekalu na
madhabahu. Aliuawa kabisa na makuhani, ili kukomesha kazi na huduma yake.
Mathayo 23:33-36
Enyi nyoka, wana wa
majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum? 34 Kwa sababu
hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na
wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika
masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji; 35 hivyo
ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili,
yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya
patakatifu na madhabahu.
Kristo anawaambia makuhani na hii hatua ya
maana sana. Inaonekana kuwa Zekaria aliuawa kwa jinsi ya kikatili sana. Zekaria
1:7 inaonyesha kuwa alikuwa ni Zekari'a mwana wa Barakia, mwana wa Ido, nabii.
(Soma kitabu cha Josephus, cha Vita vya Wayahudi, 4.5.4 kwa maelezo
zaidi, pia soma bango kitita za kitabu cha Bullinger.) hii imetajwa kama
inaanzisha tatizo kwenye vitabu vya Malaki na Zekaria.
Kwenye sura za Zekaria kuna madiliko
kidogo kwenye mtindo na kile kinachodhaniwa ni kwamba Malaki alichukua wajibu wake
na kuanza kuandika na kumaliza sura kadhaa za mwisho za kitabu cha Zekaria na
kisha akamalizia utaratibu wake kwa kitabu chake, ambacho hatimaye kilifanyika
kuwa ni cha mwisho kwenye Mpangilio huu wa uandishi. Ilikuwa ni wakati
alipofariki Iskanda Mkuu ambao ulikuwa ni sawasawa na mwaka 323 KK. Ezra mwandishi
alifariki wakati huu huu. Kitabu cha Sedum Olam Rabbah inaonyesha kwamba
walifariki wakati mmoja. Kisha walihitimisha Agano la Kale na kuweka
kilichoitwa Kanuni ya Agano hilo tangu wakati wa kifo hik mwaka 323 KK. Vitabu
viliorodheshwa na kuchapishwa na kutolewa mnamo mwaka 321 KK.
Malaki ni mmoja wa manabii sita ambao
hawajapewa tarehe za hawa Kumi na Mbili wanaojulikana au kuitwa kama Manabii
“Wadogo”. Kitabu chake kinaonyesha kwamba ibada za Hekalu na sadaka zake
zilirejeshwa zote kikamilifu bali utaratibu wa kiibada na unafiki ambao
ulishika kasi kipindi ch huduma ya Bwana wetu vilionekana kushika kasi na
kuwepo kipindi hiki cha Malaki. Sio kwa haraka sana walipingamiza ushawishi wa
Ezra na Nehemia kuondolewa zaidi ya ufisadi ulioanza na vita iliyoendelea kwa
kina iliyoshuhudiwa kwenye Malaki 1:7-8 na
3:8 nk.
Kwa hiyo, Mpangilio wa orodha ya Manabii Kumi na Mbili
ni:
Amos na Yona huenda walihudumu wakati
mmoja.
Hosea
Mika
Yoeli
Nahumu
Obadia
Sefania
Habakuki
Hagai
Zekaria
Malaki
Isaya
Isaya alikuwa anatabiri pia kipindi
hiki. Wanazuoni wa siku hizi wanajaribu kumtenganisha Isaya kwenye maandiko
matatu na sehemu ya kwanza ni kipindi cha kabla ya utumwa na nyingine ni ya
baada ya utumwa. Kuna mashaka kidogo kwamba alikuwa anaandika mahali fulani
kabla ya kuanguka kwa Hekalu na wakati wa utumwa lakini alikuwa hado ndani ya
Palestina. Zaidi ya kushughulika na jambo hapa tutashughulika na kuhesabu
tarehe za nyakati za Isaya na manabii wengine wa utumwani kwenye ufafanuzi wao.
Nyongeza
Nukuu ya Bullinger ni Manabii Kumi na
Mbili.
Manabii wa Agano la Kale wamegawanyika
kwenye Biblia ya Kiebrania makundi MAWILI:
I. Manabi wa “ZAMANI" (Yoshua hadi
Wafalme. Zekaria 1. 4; 7. 7, 12). Soma maandiko ya ukurasa wa 289, na Jalada la
Nyongeza 1. II; na kwa hiyo kwa kupendekeza,
II. Manabii “WALIOFUATIA” (Isaya hadi Malaki)
kwenye mlolongo usiovunjika (Danieli akiwa kwenye mpangilio wa mwanadamu na
orodha na kuwa kwake Hagiographa). Soma Jalada
la Nyongeza 1. III
Kwenye maandiko yote ya Kiebrania, na
Biblia zilizochapishwa za Kiebrania, Manabii Wadogo Kumi na Mbili (au wenye
vitabu vifupi) wameandikwa, na kuchapishwa kwa utaratibu usiojulikana; na mara zote wamekuwa wakihesabiwa, na
wamekuja chini kwetu, kama kitabu kimoja
.
Ni kama kila Kabila moja lilikuwa ni kitu cha tofauti katika Israeli,
nab ado yote kumi na mbili kwa pamoja yaliunda Taifa moja na ndivyo Manabii
hawa Kumi na Mbili kwa pamoja wanaunda kitabu kimoja
.
Kama ilivyokuwa
zamani (Makabila kumi na mbili) yakiitwa "dodekaphulon" =
makabila kumi na mbili, na (kutokana na neno dodeka = kumi na
mbili, na phule = kabila), Luka 22. ndivyo; Matendo 26. 7 ; na
Yakobo 1. 1 ; kwa hiyo baadae baadae (manabii kumi na mbili) wanaitwa “dodeka
propheton" (Mhubiri 49.10). alipokuwa anawasifia “watu
mashuhuri", mwandishi (Yesu, mwana wa Sirach) alisema "na hawa
manabii kumi na mbili (ton dodeka propheton) hebu na ukumbusho wao ubarikiwe, na
mifupa iimarike tena na itoke nje ya mahala pake; kwa kuwa wamemfariji Yakobo
(yaani Taifa la makabila kumi na mbili) na kuwakomboa kwa tumaini la
uhakika."
Maandiko ya Kiebrania
ya kitabu hiki chenye mkusanyiko wa vitabu kumi na mbili yamegawanyika kwa Sedarim ishirini
na moja (au sehemu kwa ajili ya usomaji wa hadharani au wa watu wote), nah
ii inasomeka pasipo kujali mwanzoni wala mwishoni mwa vitabu vingine vya
pembeni, na ndipo inaonyesha kwamba vitabu kumi na mbili vinapasa vichukuliwe
kama kitabu kimoja. Hizi Sedarim ishirini na moja ni kama
zifuatavyo :-
1. Hosea 1.1-15. 2. ″ 6.1-10.11. 3. ″ 10.12-14.6. 4. ″ 14.7
-Yoeli 2.26. 5.
Yoeli 2.27-Amosi 2.9. 6. Amosi 2.10-5.13. 7. ″ 5.14-7.14. 8. ″ 7.15-Obadia
20. 9. Obadia 21-Yona
4.11. 10. Mika 1.1-4.4. 11. ″ 4.5-7.19. |
12.Mika 7.20-Nahumu
3.19. 13.Habakuki 1.1-3.19. 14. Sefania 1.1-3.19. 15. ″ 3.20-Hagai 2.22. 16. Hagai 2.23-Zekaria 4.1. 17. Zekaria 4.2-6.13. 18. ″ 6.14-8.22. 19. ″ 8.23-11.17. 20. ″ 12.1-14.20. 21. ″ 14.21-Malaki
4.6. |
Kutokana
na Sedarim ishirini na moja hapo juu itapasa ikumbukwe kwamba ni
vitabu vinne peke yake vinaanza
na Seder (Hosea, Mika, Habakuki, na Sefania); wakati saba wengine wanazidi, na kujumuishwa
sehemu ya vitabu viwili (kama kwa suala la Namba 5: 8, 9, 12, 15, 16, na 21).
Soma maandiko kwenye kurasa za 366 na 616.
§
Inatafuta Muundo wa taratibu za Kanuni zao kwa ujumla, itakumbukwa kwamba sita
kati yao wamewekwa kwenye tarehe
(Hosea, Amosi, Mika, Sefania, Hagai, na Zekaria), na sita wengine hawajapangiwa
tarehe (Yoeli, Obadia, Yona, Nahumu, Habakuki, Malaki). Hawa
kumi na mbili wamegawanyika tena kwenye makundi mawili; wanane wao ni kabla ya
kipindi cha Utumwa na watatu wao ni
baada ya utumwa. Kwa unabii uliojulikana tarehe zake, mbili kati yake
umewajumuisha Wafalme wa Israeli, na nyingine mbili nyingine zinawajumuisha
Wafalme wa Wamei na Waajemi peke yao.
Kwa
hiyo, makundi matatu yamewekwa ili
kufanya vitabu vitatu (1);
vitabu sita (2); na vitabu vitatu (3).
Ni kama
hii ilivyotokea au kuonekana kwenye ukurasa wa 1206, uhusiano zaidi utakumbukwa
kama kitu muhimu na mtazamo wa jumla wa nabii fulani kadhaa, kama
vilivyoonyeshwa kwenye herufi au nyaraka muhimu zilizoaambatanishwa.
q