Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[CB5]
Hapo Mwanzo
(Toleo La
2.0
20030706-20061230)
Hapo
mwanzo Mungu aliumba. Jarida hili limetokana na Sura ya 1 ya Hadithi ya
Biblia Toleo la 1 lililoandikwa na Basil Wolverton likachapishwa na idara
ya machapisho ya Ambassador College. Dhana au wazo limeongezwa na kuendelezwa
kwa mujibu wa mafundisho ya Biblia na mafundisho ya shirika hili hili la
Makanisa ya Kikristo ya Mungu.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2003, 2006 Christian Churches of
God, ed. Wade Cox)
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Hapo Mwanzo
Hadithi ya
uumbaji
Ni kama
kulivyokuwa na wakati ambao mji wetu na wazazi wetu walikuwa hawajazaliwa na
kuwepo bado, kulikuwa na wakati pia ambao hii sayari tunayoikaa na kuishi ndani
yake ilikuwa haijawepo bado. Wengi wetu huenda tunashangaa jinsi vitu
vilivyokuwa huko nyuma kabla hakujakuwa na kitu chochote kwenye anga lisilo na
kitu la ulimwengu wetu huu tulionao sasa. Vilikuwa wapi basi jua mwezi na nyota
na vilitokea wapi? Ni vigumu sana kwa akili zetu kuweka taswira kwa kurudisha
nyuma mawazo yetu hadi kwenye kipindi hiki kirefu cha wakati ambacho hakukuwa
na kitu chochote cha kukiona ila ni baridi iliyo tupu tu, kwenye anga la giza.
Lakini kulikuwa na kitufulani kingine hapo kilichochukua nafasi ya hizo nyota
na sayari nyinginezo.
Ni nani au ni
kitu gani basi chaweza kuwa kilikuwepo hapo? Jibu ni kwamba ni Eloa, Mungu wa
Pekee na wa Kweli (Yohana 17:3; 1Yohana 5:20). Ni Mungu ndiye alikuwa hapo
kwanza kwa kuwa ndiye aiyeumba kila kitu kilichokuwepo na kilichopo (Mwanzo
1:1; Nehemia 9:6, Zaburi 124:8; Isaya 40:26,
28; 44:24; Matendo 14:15; 17:24, 25; Ufunuo 1:8; 4:11; 14:7).
Huenda mojawapo
ya vitu vya kwanza tunavyovishangaa ni swali kuu tulilonalo kwamba ni wapi basi
huyu Mungu alikotokea. Jibu ni kwamba yeye hakutokea mahali popote na wala
hatokani na kitu chochote. Ingawa kila kitu kina mwanzo wake, lakini Mungu
amekuwepo wakati wowote (Zaburi 90:2). Kulikuwa na wakati ambao aliishi
pekeyake. Hakuhitaji kitu chochote ili kumuwezesha awe hai au apate nguvu.
Mungu anaishi na kudumu milele (Isaya 57:15). Mungu amekuwepo wakati wote na
atazidi kuwepo. Yeye ni mwanzo na mwisho (Ufunuo 1:8). Yeye huishi milele na
hafi (1Timotheo 6:16). Hii maana yake ni kwamba hawezi kufa.
Kwa kuwa sisi tu
viumbe wa kimwili, mambo haya ni vigumu sana kwetu kuyaelewa. Inatupasa tu
kuelewa kwamba kuna mambo mengine ambayo Mungu ameyaweka kuwa siri tusiyajue.
Mengi ya mambo hayo ametufunulia, hasa wakati tunapokuwa watiifu kwake (Mithali
16:3).
Swali linguine ni
kwamba, hivi Mungu anafananaje? Tunajua jinsi wanadamu walivyo kwa kuwa
tunawaona. Wazazi wetu, kaka zetu na dada zetu ni familia au jamii ya kibinadamu
walioumbwa kwa mwili na damu kwa sura na mfano wa Mungu (Mwanzo 1:26). Hii
haimaanishi kwamba Eloa, Mungu wa Pekee wa Kweli anafanana na sisi. Inamaanisha
kwamba wanadamu waliumbwa kwa namna ya kimungu (elohim), wakati wanyama wengine
wote waliumbwa kwa namna yao wenyewe tu nyingine. Kwa ajili hii, wanadamu
wamekuwa ni watofauti sana kabisa kulinganisha na wanyama walioumbwa na Mungu.
Mungu si
mwanadamu, bali ni kiumbe wa Roho kamilifu na takatifu. Viumbe wa kiroho
hawahitaji kanuni za wakati wala eneo au anga kuweza kufanya mambo yao.
Wanadamu kwa kawaida hawawaoni au kuwwahisi au kuwasikia hawa roho, ila
wanaweza kuvutwa ama kushawishiwa nao. Hii ndiyo sababu mojawapo ya kwa nini
Shetani anaitwa mfalme wa nguzu za anga (Waefeso 2:2). Anawashawishi watu
waziasi Sheria za Mungu.
Kwa hiyo,
hatuwezi kumuona Mungu kwa kuangalia angani kwa kutafakari mamilioni ya miaka
iliyopita, ingawaje Mungu alikuwepo wakati huo wote. Hata hivyo, tunaweza
kuyaona mambo ambayo Mungu ameyaumba. Mungu alijua jinsi angalivyofanya hilo.
Anauweza wote na hakuna kinachomshinda na asichokiweza yeye Mungu (Luka 1:37).
Soma jarida la Mungu ni Nani? (Na. CB1).
Hatujui ni lini
hasa ulimwengu huu ulipoumbwa, au ilichukua muda gani kuuumba ulimwengu huu
wote. Lakini Biblia inatueleza kuhusu uumbaji. Ulimwengu ni mkubwa sana kiasi
kwamba tunaweza kuona sehemu tu ya mambo ulionayo. Mawazo yetu hayawezi hata
kuanza kugundua ukubwa wake wa ajabu, lakini hii na itupe sisi fikra ya ni kwa
kiasi gani basi Muumbaji alivyo na busara kubwa na uweza mkubwa kuliko sisi
(Ayubu 22:12; 33:12; 38:4-6).
Miongoni mwa
makundi ya nyota zinazoipendeza Dunia yetu ziliumbwa. Wanadamu wamekuwa na
mawazo mengi na nadharia mbalimbali ya jinsi dunia ilivyofanyika hadi kuumbwa
kwake na jinsi hizi nyota zilivyoweza kuwa pale. Wajinga wengi huamini na
kufundisha kuwa nyota zote ni sayari “zilizotokea” tu zenyewe pasipo Mungu
kuziumba. Biblia haikuweka shaka ya kwamba kama kuna Mungu, ila inasema kuwa
kuna Mungu aliyekuwepo tangu mwanzo wa yote na kwenye mwanzo wa uumbaji. Ni
mpumbavu tu ndiye anayesema kuwa hakuna Mungu (Zaburi 53:1).
Kama tungeiona
jinsi Dunia ilivyokuwa baada ya kuumbwa kwake, basi tungeuona ulimwengu mkubwa
wenye mchanganyiko wa rangi za bluu na kijani wenye uzuri mkubwa ukining’inia
dhidi ya kile wasomi wa mambo ta nyota na anga wanachokielezea kuwa zilidondoka
kutoka angani. Tusingeweza kutambua hata mabara yaliyoko kwenye sayari yetu au
mipaka yake, kwa kuwa ilipoumbwa mara ya kwanza ilikuwa ni tofauti sana na hivi
ilivyo leo.
Ili kuviumba vitu
vyote ulimwenguni, Mungu angehitaji akusanye vifaa mbalimbali kama mafundi
seremala wanavyohitaji vifaa vya kujengea nyumba tunazoishi ndani yake
(Waebrania 11:3). Kama tulivyokwisha kujua tayari, Mungu ni Roho. Na kama nuru
inavyomulika kutoka kwenye taa na kukijaza chumba chote, ndipo Roho Mtakatifu
wa Mungu alivyotoka kutoka kwake na kuenea ulimwenguni. Uweza huu ambao ni siri na wa ajabu ndio asili
halisia ya Mungu. Kwa uweza wake ulimwengu uliumbwa na kutokana na huo kila
nguvu za kimwili na na mwili mwili huu dhaifu unathibitiwa. Soma jarida la Roho
Mtakatifu ni Nini? (Na. CB3).
Mwanzo wa Uumbaji
Mwanzo 1:1-2 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na
nchi. 2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na
giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso
wa maji.
Hapa tunaona
mwanzo wa uumbaji wa Mbingu na Nchi. Hii inaelezea kuhusu dunia ambayo ilikuja
kuwa (2Petro 3:5-6) kabla haijawa tohu na bohu au ikwa tupu bila
kuwa na umbo na tupu. Ilikuwa imeumbwa kwa siku nyingi sana zilizopita. Lakini
ilikujakuharibiwa (soma jinsi ilivyoandikwa kwenye aya ya 1 na 2 ya Biblia ya The
Companion Bible). tutaielelezea sababu ya hiyo kadiri tunavyoendelea mbele.
Wana wa Mungu
Mungu hakuiumba
huu ulimwengu kwa kubahatisha ili hatimaye aishangae kazi yake. Kwa namna
fulani Mungu anapenda kuifanya familia kwa ajili yake mwenyewe. Kwanza kabisa
aliumba mamilioni ya viumbe wa kiroho ili waishi kwenye huu ulimwengu. Wengi
wao walimtumikia kwenye Mbingu ya tatu, mahali alipoweka Kiti chake cha Enzi
(2Wakorintho 12:2). Hatuambiwi ni mahali gani ilipo Mbingu hii ya tatu, lakini
huenda iko mahali fulani kwenye anga la mawingu ya pande za mbali za Kaskazini
(Isaya 14:13). Tunajua kwamba ni mahali ambapo mwanadamu hawezi kupaona kwa
macho yake ni kama viumbe wa kiroho tusivyoweza kuwaona (2Wakorintho 4:18).
Mungu alijua pia
kwamba viumbe wake aliowauba watakuja wajibika kutenda kazi zao kwa kufuata
Sheria zake. Viumbe hawa walikuwa ni wana wa Mungu (elohim) na walipewa Roho
Mtakatifu ili waweze kuwasiliana na Baba na wao kwa wao. Mungu aliwatia mafuta
watoto wake wawili kati ya wale wengine ili wawe ni Kerubi Wafunikao wa Baraza
la Elohim. Mmoja wao ni huyu aliyekuja hatimaye kuwa ni Masihi (Wakolosai 1:15)
na mwingine alikuwa ni huyu kiumbe (Lusifa) tunayemjua sasa na kumuita kuwa ni
Shetani (Ezekieli 28:14-16). Soma pia majarida ya Yesu ni Nani? (Na. CB2) na Uumbaji wa
Familia ya Mungu (Na. CB4).
Mungu alimfanya
Lusifa kuwa ni wa Dunia iliyofanywa tena, ambayo mamilioni ya malaika
walipelekwa kuishi ndani yake. Lusifa ndiye alipewa jukumu la kuwatawala na
kuwasimamia malaika hawa hapa Duniani kwa kuzisimamia sheria na amri zote za
Mungu. Lusifa alikuwa ni mwerevu sana, mzuri na mwenye uwezo. Alikuwa mkamilifu
katika njia zake wakati alipoumbwa, na alikuwa na uwezo mkubwa wa kiujuzi na
kimuonekano wa umbo lake jina Lusifa maana yake ni Mleta Nuru, au
Nyota Ing’aayo ya Mapambazuko.
Kwakuwa Mungu
aliumba na kuumiliki ulimwengu, basi yeye ni mtawala mkuu na bora wa huu
ulimwengu. Mwanzoni huko Lusifa alikuwa anamtii. Alifanya yote ambayo Mungu
alikuwa anamuamuru. Kulikuwa na kipindi cha miaka na miaka ya furaha na
kurithika katikati ya malaika wakati wao na Lusifeli walikuwa wanatii kila moja
ya Sheria za Mungu. Hii ni kwa kuwa Sheria za Mungu zimetolewa ili kuwafanya
viumbe wafurahi. Mambo yalienda vizuri sana kwa kadiri Lusifeli alipokuwa
anazitii sheria au kanuni za Mungu na maelekezo yake (Ezekieli 28:13-15).
Lakini katika
kipindi alichoyaruhusu mawazo maovu kuingi moyoni mwake. "Mimi ni mfalme
wa mamilioni ya malaika," alidhani. "Pamoja nao maunda jeshi kubwa na
lenye nguvu vya kutosha kuwashambulia na kuwashinda malaika wa Mungu
wanaotupinga. Na kama nitakitwaa kiti cha enzi cha Mungu huko Mbinguni na
kumuondoa Mungu, basi nitafanyika kuwa mtawala bora wa ulimwengu wote!"
(Isaya 14:12-14).
Wazo la kumshinda
Mungu na kuchukua nafasi yake lilisababisha majivuno na kiburi kwa kiasi
kikubwa sana na kuibuka kwa machukizo. Kwa kadiri wazo hili lilipozidi kukua na
tamaa hii na muwako wa shauku ya kuonyesha muwako wa shauku na matamanio yake.
Hatimaye Lusifeli
anaufanya mpango wake ujulikane na wale waliokuwa wanaonyesha kupenda
kumsikiliza na huku akijaribu kuwaahidi kuwa atawafanya kuwa watawala, kwenye
utawala wake, kwenye ulimwengu mwingine, na kuwapa nyadhifa za juu hata huko
Mbinguni wale wote watakaoasi pamoja nay eye. Aliwarubuni kiasi cha kufanikiwa
kuwapata theluthi moja ya malaika wote wakapumbazika vya kutosha kujitoa mhanga
kwa kuhatarisha furaha yao kwa kujiunga na mpango wake muovu (Ufunuo 12:4;
Ayubu 4:18). Theluthi mbili nyingine walibakia watiifu kwa Muumba wao.
Kiburi, majivuno
na ulafi vilivyotokana na mawazo mabaya viliifanya busara kubwa ya Lusifa
kubadilika. Vinginevyo, angeweza kujua kwamba kuifanikisha vita ya kupigana na
Muumbaji isingewezekana. Fikra zake zilibadilika sana hasa ni kutokana na
kwamba fikra na mawazo yake yalikuwa ni
mabaya. Huku akiwa amejazwa na mawazo ya kwamba angeweza kumshinda Muumba wake,
Lusifa akaendelea na mchakato wa kuandaa mipango yake ya uasi. Akiwa pamoja na
mamilioni ya malaika waliokuwa tayari kumtii yye badala ya Mungu, aliichafua
Mbingu na wenzake hawa na kuanzisha mashambulizi.
Vita hii
ilipeleke idadi kubwa ya viumbe wa kiroho waongezeke, ni kitu cha kusikitisha
sana. Wanadamu hawajui chochote kilicho kigeni na majeshi haya yenye
kusababisha maafa makubwa yaliyotumika. Hata mbomu ya haidrojeni na kobalti
hayawezi kulinganishwa na nguvu zilizo kwenye amri ya Mungu. Mara zote Mungu
amekuwa na viumbe wenye nguvu nyingi sana wakiwemo. Hakuja majeshi ya wanadamu
au rogo zilizo na nguvu nyingi za kuweza kumuondoa kwenye kiti chake cha enzi.
Lusifeli alipitia
kwenye kipindi kibaya cha kushindwa. Nguvu nyingi zisizoweza kulinganishwa z
Muumba iliwaangukia na kuyakamia majeshi haya kiasi kwamba washambulizi wake
walipigwa bumbuazi kwa kipigo kiasi cha kuparaganyika na kutojielewa na ndipo
wakafukuzwa kutoka Mbinguni na wakatupwa hapa Duniani (2Petro 2:4; Isaya
14:15).
Mungu hakuishia
hapo tu katika kuwashughulikia malaika hawa waasi, hata hivyo, dhambi ya Lusifa
ya uasi dhidi ya mamlaka na utawala wa Mungu ilimfanya ajikute akiwa hapa
duniani na milki zake. Alipaswa kuitawala Dunia wakati tulipoletwa na kufanyika
kuwa chini yake na kutolewa mbali na utawala wake kwa wakati mwingine na
kutawala pamoja na Kristo ambaye siku moja atachukua mahala pake. Kwa matendo
yake hayo kwa sehemu hii ya Mpango wa Mungu, yeye pamoja na wafuasi wake
watahukumiwa.
Jina lake
lilibadilishwa na kuwa Shetani ambalo maana yake ni adui kwa Kiebrania
(Ufunuo 12:9), kwa kuwa amekuwa ni adui wa watu wa Mungu. Wale malaika
waliomfuata walikuwa kutoka kwenye kundi la walioitwa baadae kuwa ni washitaki
au wafanya mashitaka ya uwongo dhidi ya wanadamu. Kwa Kiyunani neno
linalotumika kuwaelezea ni diabolos. Neno la Kiebrania litumikalo kuwaita
roho hawa ni shade au shades. Pia waliitwa kama mabeberu au
mazimwi, kutokana na ibada zinazoonekana kwenye imani za kipagani za mungu
aitwaye Pan wa jangwani. Neno pepo linatokana na maana ya Kiyunani ya
mungu au mungu mdogo. Manno yaliyochukuliwa kutoka kwenye maana hii ni
kushawishika au kuvutiwa, au kuzoelezwa na mungu aliyeasi au "pepo".
Maneno ya kiyunani yanayotokana kutoka kwenye neno asili la daimon ambalo
lilitumika kama roho au nguvu za kimungu na lilitumika kwa maana zote mbili,
yaani kwa maana mbaya na njema. Luka 4:33 inatumia neno pepo mchafu na
neno linguine la pepo kuonyesha kuwa inaongelea roho mchafu.
Mapepo
hawakuumbwa wakiwa waovu. Ni kama Kristo pamoja na watoto wote wa Mungu
waliumbwa na uwezo wa kujua mema na mabaya. Lakini wengine wamechagua kutenda
dhambi kwa kuasi na hii ilisababisha kuwepo na vita kubwa mbinguni, na ambayo
bado inaendelea hata leo. Uasi huu ulisababisha mgawanyiko kwenye serikali ya
Mungu. Na hii ilipelekea kuanza kwa dini nyingi za uwongo na miungu wa uwongo na
dunia kujawa na maovu.
Hukumu ya kutisha ya dhambi
Popote ambapo
Sheria za Mungu zinavunjwa, mateso, dhiki na maangamizo havinabudi kufuatia.
Wakati wa ambano kuu wakati Shetani na mapepo wake walijaribu kupigana Mungu
ili wamshinde, ndipo mabadiliko makubwa nay a kuhuzunisha yalikuja Duniani
(Mwanzo 1:2). Ile iliyokuwa ni sayari ya kupendeza ilibadilika na kuwa mahali
pa mavunjiko. Hatuna uhakika ni nini kilisababisha maangamizi haya. Hali ya
hewa na mazingira yalichafuka. Inaonekana kuwa maasi ya Shetani na theluthi
moja ya Malaika wa huko Mbinguni yalipelekea maangamizo makubwa ya uumbaji
asilia uliokuwa hapo mwanzoni.
Uhai kidogo au wa
kimwili ungeweza kumudu kwenye kipindi kile cha hatari; kwa kitambo dunia yetu
ilibakia imezikwa au kufunikwa na blanketi au hewa, moshi na maji. Bahari
ziliifunika Dunia yote. Haikuwepo tena ardhi kavu. Hali ya hewa ilikuwa ni
imegubikwa sana mawingu ya mgandano au ukungu mdogomdogo kiasi kwamba hakuna
nuru ingaliyoweza kuifikia bahari. Hatujui ni kwa muda gani hali hii ilidumu,
lakini hatimaye ulikuja muda ambao Mungu alianza kuandaa kwa ajili ya tukio la
muhimu sana kwenye Mpango wake Mkuu. Nao ulikuwa ni kumfanya mwanadamu awepo na
kuishi.
Mungu alikuwa na
upendo mkubwa sana wa kuuumba ulimwengu bora na wenye kupendeza kwa ajili ya
viumbe wake. Angeweza kuumba tena pamona na elohim wake zama au ulimwengu
mwingine ambao kwa sasa wanadamu wanaishi ndani yake.
Kuna sayari
kadhaa nyingine sambamba na Dunia zilizo kwenye mzunguko zikilizunguka jua
letu, na huenda kuna nyingine zaidi hapa ulimwenguni. Kwa kadiri tujuavyo,
Dunia ilikuwa ni sayari pekee Mungu aliyoichagua na kuiandaa iwe kamao ya
mwanadamu aliyeumbwa kwa sura na mfano wake.
Uumbaji wa zama hizi
"Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji." Kisha kwennye Mwanzo 2:1 tunasoma:
"Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote". Uumbaji huu
ulikuwa ni wa zama tulizonazo leo (2Petro 3:7) na ulifanyika kwa muda wa siku
sita za uumbaji wa Mungu (siku za kazi) kabla hajapumzika siku ya saba ya juma
hili.
Kwa hiyo,
kutokana na Mwanzo 1:2-31 tunaona mwanzo mpya baada ya uasi na ulimwengu
ulifanyika mtupu na wenye giza. Mbingu na Nchi hapa ni zile tunazozijua sasa
(2Petro 3:7). Uliharibiwa tena katika siku za Nuhu kwa gharika kuu, lakini
tutaliona hilo kwenye masomo mengine.
Kwa siku tano
Mungu alisaidiwaa na elohim, au familia au miungu wadogo akiwaumba kama baba
yao, akifanya kazi kama ya kuiumba Dunia mahala ambapo ingekuwa sahihi kwa
kuishi mwanadamu (Mwanzo 1:23). Iligharimu nguvu kubwa na na nguvu za masikitiko
kubadilisha uso wote wa sayari hii kwa kipindi cha chini ya juma moja.
Baba ana mpango
mkamilifu na bora sana. Aliamua kile cha kufanya. Kisha alimuambia mjumbe
maalumu, au malaika (ndilo neno la Kiyunani lenye maana ya mjumbe) ambaye
anajulikana kama “Neno la Mungu” kwa kuwa alipaswa kuwa ni msemaji, asemaye
kama anavyomuamuru Baba. Malaika huyu Mkuu ndiye Yule aliyewatokea Mababa wa
imani na ndiye aliyempa Musa Torati. Hatimaye alizaliwa kama mwanadamu, na
akafanyika kuwa Yesu Kristo. Mara hiyo, Roho Mtakatifu mwenye nguvu na uweza
wote akafanya kitokee chochote ambacho Neno anakiamuru kitendeke. Hivyo ndivyo
Mungu alivyoumba na kufana kila kitu kilichopo siku hizi kwa kupitia Yesu
Kristo (Yohana 1:3).
Katika siku ya
kwanza ya kuufanya uso wa Dunia, Mungu alisema, "Iwe nuru." Akaitenga nuru na giza na akaiita ile nuru
‘mchana’ na giza akaliita ‘usiku’. Kwa hiyo vile vimelea vya mchanganyiko wa
moshi na gesi na mambo mengine ambayo yaliijaza mawingu viliondolewa mbali. Kwa
hiyo nuru ndogo iliuja kwa kupitia Dunia kwa mara ya kwanza tangu Shetani na
mapepo wake walipotupwa kutoka Mbinguni hadi hapa chini hapa duniani (Mwanzo
1:2-5).
Katika siku ya
pili Mungu alifanya tabaka kubwa la hewa safi kwenye Dunia. Kwa kupitia hiyo
maji mengi sana yalitiririka kwa mwendo kasi kutoka ardhini kuja juu ili
kufanyiza mawingu makubwa na mengi angani juu mawinguni, na yenye hewa ya afya
njema ambayo ilikuwa ni salama kwa kuivuta. Mchanganiko huu wa gesi yend day
God produced a vast layer of fresh air over thye afya ulikuwa ni wa muhimu ili
kumfanya mwanadamu aishi (Mwanzo 1:6-8). Mungu aliliita hili anga Mbingu
(Mwanzo 1:8). Aliongelea pia kuhusu mbingu nyingine mbili, moja ni anga iliyo
zaidi ya anga letu (Mwanzo 1:14), na lingine linaitwa Mbingu ya tatu, ambapo
ndipo Kiti chake cha Enzi kilipo (Matendo 7:49; 2Wakorintho 12:2). Hatuambii
wapi kilipo, na wataalamu wa mambo ya anga hawajawahi kukiona kamwe kwa kuwa
hakionekani kwa macho ya kimwili kama utaratibu wa kiroho. Vitu vinavyoonekana
vimefanywa kutoka kwenye vitu visivyoonekana.
Katika siku ya
tatu, Muumba aliufanya uso na umbo la Dunia ili kwamba sehemu nyingine iwe juu
na nyingine iwe chini. Tabaka kuu la maji likaizunguka dunia lilitiririka
kuelekea maeneo ya chini yakisababisha mwonekano wa sura mbalimbali za bahari.
Maeneo makubwa ya ardhi yaliachwa yakiwa juu ya maji, yakifanya migawanyo ya
nchi kavu (Mwanzo 1:9-10). Katika nchi kavu Mungu alifanya kuwe na uoto – miti,
vichaka, maua na nyasi –zimee kutoka ardhini. Katika siku ile ile ardhi ikaanza
kuwa ya kijani na yenye uoto wa kila aina ulichipuka juu kutoka kwenye udongo
(Mwanzo 1:11-13).
Katika siku ya
nne Muumbaji aliifagia sehemu ya mwisho ya vumbi na hewa yenye madhara
mawinguni, ambavyo ni kulifanya jua, mwezi na nyota zing’ae kwa mg’ao wake
kamili ardhini na baharini. Mungu
akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu
akatenga nuru na giza. Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Kwa kweli hii inaongelea kuhusu jua na mwezi. Kisha
aliziumba nyota (Mwanzo 1:14-19). Hapa tunaona kuwa Kalenda ya Mungu inawekwa
na kuanza tangi mwanzoni tu. Pia soma Zaburi 104:19.
Katika siku ya
tano aliumba nyangumi na aina zote za viumbe wa baharini. Katika siku hiyo
aliumba pia aina mbalimbali ya ndege warukao angani. Mara tu ndipo angani na majini kukafurika na
viumbe hai.
Muumbaji
akaufanya kuwa mpya uso wa Dunia na kuujaza aina mbalimbali ya viumbe hai na
uhai wenyewe kwa kipindi cha siku tano tu. Mwishoni kabisa alikuwa anakaribia
kabisa kumfanya mwanadamu uwepo. Lakini kabla ya kumuumba mwanadamu katika siku
ya sita, kulikuwa na udongo maalumu ambao viumbe watatakiwa watokane kwao. Hawa
ni pamoja na tembo, ng’ombe, farasi, nguchito, minyoo, wadudu na kila aina ya
kitu kinachotembea, chenye kutambaa na kutembea kwa tumbo (Mwanzo 1:24-25).
Manadamu anaumbwa
Hatimaye Mungu
alifanya kazi ya mhimu sana ya kazi ya mikono yake. Akitumia vifaa kutoka
kwenye kitu alichokiumba yaani Dunia, alimuumba mwanadamu! (Mwanzo 1:26-28).
Mbingu na Nchi
ziliumbwa na elohim aliyesema, "Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa
baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye
kutambaa kitambaacho juu ya nchi." (Mwanzo 1:26). Wanadamu wameamriwa kwenda na kuiongeza (kuijaza)
Dunia (Mwanzo 1:28; sawa na Zaburi 8 na Waebrania 2:6-8).
Ingawa elohim
alikuwa na kazi na majukumu ya namna mbalimbali kwenye uumbaji, Mungu wa Pekee
na wa Kweli aliiumba Dunia kwa uweza wake na hekima yake.
Yeremia 10:12-13
Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa
ufahamu wake amezitandika mbingu. 13 Atoapo sauti yake, pana mshindo wa maji mbinguni,
Naye hupandisha mawingu toka ncha za nchi; Huifanyia mvua umeme, Huutoa upepo
katika hazina zake.
Bwana Mungu
alimfanya mwanadamu wa kwanza kutoka kwenye mavumbi ya ardhi na kumpulizia
pumzi ya uhai kwenye mianzi ya pua kisha akawa nafsi hai na mwanadamu akawa
kiumbe shenye uhai (Mwanzo 2:7).
Mungu alimuita
mwanadamu huyu wa kwanza kuwa ni Adamu. Ni mwanadamu wa kwanza kuishi miongoni
mwa wote wenye mwili hapa duniani (1Wakorintho 15:45). Muumba alikuwa
amekwishaandaa tayari bustani mzuri sana kwa ajili ya Adamu ili aishi na
kufanya kazi humo (Mwanzo 2:8). Hapa palikuwa ni Edeni, nchi iliyoko huko
Mashariki ya Kati pamoja na ile inayojulikana sasa kuwa maeneo ya Israeli na ni
kaskazini mwa kingo za Tigri na Frati.
Mungu aliuw
amepanga kuwaumba wanadamu. Alijua kuwa Adamu angekuwa ni mpweke iwapo kama
angekuwa ni mwanadamu pekeyake lakini aliamua kupitia yeye amuumbe mwingine
pia. Alichukua mojawapo ya mbavu za Adamu, wakati alipokuwa amelala na kuitumia
kumuumba mwanamke. Akapewa Adamu kuwa ni mshirika na mwenzi wake. Adamu
akamuita mwanamke huyu jina lake kuwa ni Hawa (Mwanzo 2:18-22).
Vitu hivi vyote
alivitengeneza Mungu na aliviumba kwa muda wa siku sita za kazi. Kila siku na
kisha na kwa hiyo ilikuwa na urefu wa saa ishirini na manne na zilikuwa ni
ujsiku na mchana ni kama zilivyo siku hizi. Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama,
ni chema sana. (Mwanzo 1:31).
Basi mbingu na nchi
zikamalizika, na jeshi lake lote (Mwanzo 2:1).
Na siku ya saba
Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha
kufanya kazi yake yote aliyoifanya. (Mwanzo 2:2-3). Aliita siku ya
saba kuwa ni Sabato (Kutoka 16:26), kwa hiyo akaiichagua siku maalumu ya
mapumziko na kuitenga kama ni kipindi cha saa ishirini na nne kama Siku yake
maalumu ya Mapumziko. Akaweka Sheria kwamba mwanadamu anapaswa kuiheshimu na
kuiadhimisha siku hii kiola wiki kwa kupumzika na kukutanika kwa ibada katika
siku hii ya saba. Mungu aliifanya siku ile kuwa ni kipindi kitakatifu, na
kuwaamuru watu wote kuiadhimisha kwa kuitakatifuza. Kama tulivyojua tayari kuwa
Amri ya Nne inatuambia kuitunza siku ya Sabato na kuitakatifuza. Siku sita za
kwanza zilikuwa ni kwa ajili ya wanadamu kufanya kazi na kucheza, lakini siku
ya saba nay a mwisho ya juma Mungu aliitenga kwa ajili yake mwenyewe (Kutoka
20:8-11). Soma pia jarida la Siku ya Sabato (Na. CB21).
Tunaambiwa kwamba siu ya saba (Sabato) ni
ukumbusho wa kutukumbusha kuhusu mapumziko ya Bwana kutoka kwenye kazi na
mwishoi mwa juma la uumbaji. Lakini Kristo anatuambia sisi kwenye Biblia kwamba
yeye amoja na Baba wangali wanafanya kazi bado (Yohana 5:17). Kwa hiyo, mapumziko haya ni ya endelevu na
ni ishara ya mapumziko yajayo mbeleni (soma Waebrania 4:1-4).
Kwa hiyo
inahitimisha juma la kwanza katika historia ya uumbaji na mpangilio wa sayari
ambayo kwamba wanadamu wameishi ndani yake sasa kwa kipindi cha miaka elfu
sita.
Kama tutaangalia
kwa uangalifu na kwa ukaribu sana kwenye juma hili la kwanza la uumbaji
tutauona Mpango wa Mungu wa Uokovu. Juma la uumbaji lilianzia siu ya kwanza ya
juma (Jumapili) na likaendelea hadi siku ya saba ambayo ni Sabato (Jumamosi).
Biblia inatuambia kwamba kwa Bwana, siku moja ni kama miaka elfu (2Petro 3:8).
Juma la uumbaji linaonekana kama taswira ya miaka elfu saba, ambayo ndiyo
Mpango wa Mungu kwa mwanadamu.
Kwa hiyo, miaka
elfu sira ya kwanza mwanadamu yupo chini ya utawala wa Shetani na mapepo. miaka
mingine elfu moja ya mwisho inaitwa Siku ya Bwana. Hii itakuwa ni Milenia
itakayokuwa chini ya utawala wa Yesu Kristo na wateule wake, wakati atakapokuja
kumnyang’anya Shetani na kuchukua mamlaka aliyonayo sasa. "nao wakawa hai,
wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu" (soma Ufunuo 20:4).
q