Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[267]
Kula Pamoja Kwenye Ibada
(Toleo
La 1.0 20060426-20060426)
Sheria za Mungu
zinatuamuru kula pamoja kwenye ibada. Jinsi tunavyofanya hivyo, kwa utaratibu
wote na namna yake, vyote vinatoa taswira kwetu kama kanisa na kama mabalozi wa
Ufalme wa Mungu hapa Duniani.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2006 Wade Cox)
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Kula Pamoja Kwenye Ibada
Mungu anatuamuru tuzishike Sheria na kukusantika
pamoja kwenye ardhi yoyote tuliyopewa kama urithi wetu katika kumuabudia yeye.
Utaratibu na amri zake tumepewa kutoka kenye Kumbukumbu la Torati Sura ya 12
kwa ujumla wake.
Kumbukumbu la Torati 12:1 Hizi ndizo amri na hukumu mtakazotunza kuzifanya katika nchi aliyokupa Bwana, Mungu wa baba zako, uimiliki, siku zote mtakazoishi juu ya nchi.
Kumbuka kuwa kipindi endelevu hakiishii kwenye
Hekalu na Yerusalemu, bali zaidi sana ni kwa kila taifa tulilopewa, na kwa kila
siku tunazoishi hapa duniani.
2 Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi; 3 nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo. 4 Wala msimfanyie hivyo Bwana, Mungu wenu. 5 Lakini mahali atakapochagua Bwana, Mungu wenu, katika kabila zenu zote, apaweke jina lake, maana, ni makao yake, elekezeni nyuso zenu hapo, nawe wende huko
Kwa hiyo, Bwana atachagua kupaweka mahali kwa kila
kabila na uwenyeji wake. Kitendo cha kuiabudu miungu ya uwongo ni cha kukikataa
na kujiepusha na haifaia kabisa kukiigiza kwenye ibada tumwabudupo Mungu wa
Pekee na wa Kweli. Mataifa yote na watu wake wanapaswa kumfanyia ibada au kumuabudu
kwa mahali popote ambapo Bwana amelikalisha jina lake. Utoaji wa zaka ni muhimu
kama kiini cha ibada hii na utaratibu wa utoaji zaka kwenye ibada hii unapaswa
ufanyike kwa makabila na taifa popote walipo kwenye mimli ya urithi wao.
6 pelekeni huko sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu zenu, na zaka zenu, na sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu, na sadaka zenu za hiari, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ng'ombe na ya kondoo; 7 na huko mtakula mbele za Bwana, Mungu wenu, nanyi furahini katika yote mtakayotia mikono yenu, ninyi na wa nyumbani mwenu, aliyokubarikia Bwana, Mungu wako. 8 Msifanye kwa kufuata mambo yote tuyafanyayo hapa leo, kila mtu kama aonavyo vema machoni pake; 9 kwani hamjafikilia bado katika raha na urithi akupao Bwana, Mungu wako
Kwa hiyo hatupaswi kutenda yaliyomema machoni petu
wenyewe tun pokuwa tumewekwa kwenye milki yetu na palipo salama.
10 Lakini mtakapovuka Yordani na kukaa katika nchi anayowarithisha Bwana, Mungu wenu, akawapeni raha, akiwaokoa na adui zenu pande zote, mkakaa salama; 11 wakati huo itakuwa kwamba mahali pale atakapopachagua Bwana, Mungu wenu, alikalishe jina lake, hapo ndipo mtakapoleta kila kitu ninachowaamuru; sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu zenu, na zaka zenu, na sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu zote teule mtakazoweka kwa Bwana. 12 Nanyi mtafurahi mbele za Bwana, Mungu wenu, ninyi, na wana wenu, na binti zenu, na watumishi wenu wanawaume na wanawake, na Mlawi aliyemo malangoni mwenu; kwa kuwa hana sehemu wala urithi kwenu.
Tumeamriwa kwenda kule ambako Bwana Mungu wetu amepachagua
alikalishe jina lake, na sisi sote tunatakiwa kwenda na sadaka na zaka zetu na
kuzilia huko tukiwa pamoja na wenzetu, wakiwemo watumishi wa Mungu wetu ambao
hawana urithi wowote kumiliki.
Hatupaswi kuyatoa matoleo haya popote yayaonapo
macho yetu, lakini ni mahali pale ambapo Mungu amepchagua kwa madhumuni hayo.
Kwa siku hizi ni sawa na kusema mahali pale palipochaguliwa na kukubalika na
uongozi wa Kanisa likiwa ni chombo pekee kinachosimamia mwendendo wa watu wake
katika kuzishika na kuzishia sheria au Torati ya Mungu kwenye ibada.
13 Ujihadhari usitoe sadaka zako za kuteketezwa katika kila mahali upaonapo; 14 bali katika mahali atakapopachagua Bwana katika kabila zako mojawapo, ndipo utakapotoa sadaka zako za kuteketezwa, ndipo utakapotenda yote nikuamuruyo
Ulajiwa kawaida wa nyama haujakatazwa kwenye amri na
maagizo haya au sheria hii ambayo inaruhusu kuchinja na ulaji wa kila siku wa
nyama kwenye malango yote ya wato wetu.
15 Pamoja na haya waweza kuchinja nyama na kula ndani ya malango yako yote, kwa kufuata yote yatamaniwayo na roho yako, kwa mfano wa baraka ya Bwana, Mungu wako, aliyokupa; aliye tohara na asiye tohara ana ruhusa kula katika nyama hiyo, kama ya paa na ya kulungu. 16 Lakini msiile damu; imwageni juu ya nchi kama maji
Kitu kilichokatazwa tu ni zaka ambazo tumekatazwa
tusizile ndani ya malango yetu ,rna zinatakiwa ziliwe tu mahala pale ambapo
pamechaguliwa mahsusi kwa kumfanyia ibada Mungu wa Pekee wa Kweli.
17 Usile ndani ya malango yako zaka ya nafaka zako, wala ya divai yako, wala ya mafuta yako, wala wazaliwa wa kwanza wa makundi yako, ya ng'ombe wala ya kondoo, wala nadhiri zako uwekazo zo zote, wala sadaka zako za hiari, wala sadaka ya kuinuliwa ya mkono wako;
Zaka na sadaka hizi zinapaswa kuliwa mahali pale
tu pali[otengwa na kuchaguliwa kwa kusudi hilo na Kanisa kwa madhumuni ya
kufanyia makutaniko ya Sikukuu za Bwana zinazoadhimishwa mara tatu kwa kila
mwaka zinazotokana na Kalenda Takatifu (tazama jarida la Kalenda ya ya Mungu na (Na. 156) (Zaka (Na. 161) [God’s Calendar (No. 156) and also Tithing (No. 161)].
18 lakini hivyo mtakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, wewe, na mwanao mume na mke, na mtumwa wako mume na mke, na Mlawi aliye ndani ya malango yako; nawe furahi mbele za Bwana, Mungu wako, katika yote utakayotia mkono wako. 19 Jilinde nafsi yako usimwache Mlawi siku zote uishizo katika nchi yako.
Madai haya hayakuwahuri Israeli peke yao kwenye
kipindi cha cha kwanza kuyaingiza bali ni kwa taifa lote na kwa Israeli wa
Kiroho, ambao ni Kanisa la Mungu, kama tunavyoona kwenye andiko hili. Tunaweza
kuzibadilisha zaka zetu kwa fedha na kwendanazo mahali palipocgaguliwa kwa
ajili yetu bila kujalisha ni wapi tulipo sisi. Kwa kuwa fedha ni kitu pekee na
kilichozoeleka cha kubadilishia siku hizi, hakuna matatizo kulielewa jambo hilo
la kutoa zaka kwa kutumia fedha zile.
Andoko hili linatutaka tuende na tukafurahi mbele
za Bwana Mungu kwa kila tunachokitia mikononi na kukifanya. Kitendo kile tu cha
kwenda huko na kula ni tendo la ibada kwa Mungu Aliyehai na kile tunachokifanya.
Imeandikwa pia kuhusu tendo hili kwenye Zaburi 22:29.
20 Bwana, Mungu wako, atakapoongeza mpaka wako, kama alivyokuahidi, nawe utakaposema, Nataka kula nyama, kwa kuwa roho yako yatamani kula nyama; waweza kula nyama, kwa kufuata yote inayotamani roho yako. 21 Na mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, apaweke jina lake, pakiwa mbali nawe mno, ndipo utakapochinja katika kundi lako la ng'ombe na kondoo alilokupa Bwana kama nilivyokuagiza, nawe utakula ndani ya malango yako, kwa kufuata yote inayotamani roho yako. 22 Kama vile aliwavyo paa na kulungu, ndivyo utakavyoila nyama hii; asiyekuwa tohara na aliye tohara wataila pia. 23 Ila ujihadhari kwamba usile damu, kwani ile damu ndiyo uhai; na uhai usile pamoja na nyama. 24 Usiile; imwage juu ya nchi kama maji. 25 Usiile; ili upate kufanikiwa, na watoto wako baada yako utakapofanya yaliyoelekea machoni pa Bwana.
Taifa zime lote, wote waliokuwepo, yaani waliotoha
na wasio tohara (aya ya 22), waliruhusiwa kuila nyma hii wawapo kwenye sikukuu.
Damu ya wanyama hawa imekatazwa kuliwa au kuliwa.
Zaka na vyote vilivyokubalika mbele za Mungu zilichukuliwa
hadi mahala palipoteuliwa kufanyiwa Sikuuu na palipochaguliwa kwa dhumuni hilo.
Kwa hiyo, tangia sehemu ya kwanza ya andiko kwenye aya ya 17, tunaona kuwa
tumekatazwa kuzila zaka ndani ya malango yetu. Hata hivyo, tunapokuwa wengi na
mahali palipochaguliwa kufanyika sikukuu pakiwa ni mbali sana, ndpo
tunaruhusiwa kuzila zaka zetu ndani ya malango yetu, kama itakuwa ni lazima
saba na hatuna budi kufanya hivyo (aya ya 21), lakini tunatarajiwa kuwepo
mahali palipochaguliwa kufanyika Sikukuu (aya za 26-27). Kwa hiyo, tunapaswa
kufanya juhudi yoyote iwezekanavyo tuende huko, lakini kama hatuwezi kabisa
ndipo tunaweza kuzila zaha majumbani mwetu na tunaruhusiwa. Kama tunaweza
kufanya hivyo, basi tunaweza kubadilisha zaka hiki na kuwa fedha na kuzichukua
na kwenda kuzitoa nadhiri tulizonazo mbele za Bwana, mahala palipochaguliwa.
Kwa mtazamo wa siku hizi, ka nyingi
zinakuwa ni za fedha hata hivyo kwa wafanyakazi na wafanyabiashara wengi.
26 Ila vitu vyako vitakatifu ulivyo navyo, na nadhiri zako, uvitwae ukaende mahali atakapochagua Bwana; 27 nawe zisongeze sadaka zako za kuteketezwa, nyama na damu, juu ya madhabahu ya Bwana, Mungu wako; na damu ya dhabihu zako uimwage juu ya madhabahu ya Bwana, Mungu wako, na wewe utakula nyama yake.
Kuna amri hapa kwenye andiko hili kuhusu
kinachotupasa sisi kuadhimisha sikukuu hizi milele. Kristo alitimiliza sheria
za Mungu na hivyo, aliondoa au kukomesha utoaji wa dhabihu za wanyama, lakini
hakuzikomesha au kuondoa amri ya kuzishika sheria na pia hakuzikomesha sikukuu
kuadhimishwa na pia hakukomesha utoaji wa zaka.
28 Maneno haya nikuagizayo yote yatunze na
kuyasikiza, ili upate kufanikiwa na watoto wako baada yako milele, hapo
uyafanyapo yaliyo mema na kuelekea machoni pa Bwana, Mungu wako. 29 Bwana,
Mungu wako, atakapoyakatilia mbali hayo mataifa mbele yako, huko uingiako
kuyamiliki, nawe ukawatwaa, na kuketi katika nchi yao; 30 ujiangalie,
usije ukanaswa ukawafuata, wakiisha kuangamizwa mbele yako; wala usije ukauliza
habari za miungu yao, ukisema, Mataifa haya waitumikiaje miungu yao? Nami
nifanye vivyo. 31 Usimtende kama haya Bwana, Mungu wako;
kwani kila yaliyo machukizo kwa Bwana, ayachukiayo yeye, wameifanyia miungu
yao; kwa maana hata wana wao na binti zao huiteketezea hiyo miungu yao ndani ya
moto. 32 Neno niwaagizalo lo lote liangalieni
kulifanya; usiliongeze, wala usilipunguze.
Kwa hiyo, ilieleweka mara zote kwamba hatukuambiwa
kuziacha sheria na maadhimisho ya Sikukuu za Mungu na kukutanika pamoja kwenye
ibada kama makutaniko yaliyoamriwa.
Hii ilijulikana hivyo tangu nyakati za zamani
sana. Daudi alikuwa anajua kuwa alikuwa anahitajika kujihudhurisha na
kuadhimisha Karamu za Miandamo ya Mwezi Mpya kwenye ua wa mfalme na mwenyewe
akiwa ni mhusika mkumbwa (1Samweli 20:5,24). Alitakiwa ahudhurie. Kama tutakuwa
tunawaheshimu wenyemamlaka wa hapa dunianina sheria zake, basi tutakuwa
tunatakiwa kiasi gani kuheshimu Mungu na wapendwa wa imani moja nasi?
Kanisa lilikusanyika pamoja kama tunavyojionea
kwenye Matendo 2:42-47.
Matendo 2:42-47 Wakawa
wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega
mkate, na katika kusali. 43 Kila mtu
akaingiwa na hofu; ajabu nyingi na ishara zikafanywa na mitume. 44 Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja,
na kuwa na vitu vyote shirika, 45 wakiuza mali
zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu
alivyokuwa na haja. 46 Na siku zote kwa
moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na
kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe, 47 wakimsifu
Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale
waliokuwa wakiokolewa.
Kadiri walipokuwa waiongezeka Makanisani, ndipo
ilikuwa ni kawaida yao watu kufanya ibada na kisha kushiriki chakula pamoja.
Waliabudu Hekaluni lilikuweko huko Yerusalemu na
kisha wakaenda kwenye nyumba za wapendwa washirika wenzao na kuja chakula humo
kama ilivyokuwa kawaida yao. Waliokuwa wanatoka nje ya Yudea walikutakina
kwenye majumba yao na kula pamoja na kuabudu humo
Kanisa la Anthiokia lilikuwa linazifanya sikukuu
hizi kuwa ni kitu cha mara kwa mara jambo ambalo sivyo na wakaagizwa au
kuambiwa wale majumbani mwao kama hawakuendenda sawasawa na mwenendo
unaostahili.
1Wakorintho 11:20-34
Basi mkutanikapo pamoja haiwezekani kula chakula cha Bwana; 21
kwa maana kila mmoja hutangulia kutwaa chakula chake katika kule kula;
hata huyu ana njaa, na huyu amelewa. 22 Je! Hamna
nyumba za kulia na kunywea? Au mnalidharau kanisa la Mungu, na kuwatahayarisha
hao wasio na kitu? Niwaambieni? Niwasifu? La! Siwasifu kwa ajili ya hayo. 23 Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliyowapa nanyi, ya
kuwa Bwana Yesu usiku ule aliotolewa alitwaa mkate, 24 naye
akiisha kushukuru akaumega, akasema, Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu;
fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu. 25 Na vivi hivi
baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika
damu yangu; fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu. 26
Maana kila mwulapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, mwaitangaza
mauti ya Bwana hata ajapo. 27 Basi kila aulaye mkate
huo, au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa amejipatia
hatia ya mwili na damu ya Bwana. 28 Lakini mtu ajihoji
mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe. 29 Maana
alaye na kunywa, hula na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kutokuupambanua ule
mwili. 30 Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio
hawawezi na dhaifu, na watu kadha wa kadha wamelala. 31 Lakini
kama tungejipambanua nafsi zetu, tusingehukumiwa. 32 Ila
tuhukumiwapo, twarudiwa na Bwana, isije ikatupasa adhabu pamoja na dunia. 33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mkutanikapo mpate kula,
mngojaneni; 34 mtu akiwa na njaa, na ale nyumbani
kwake; msipate kukutanika kwa hukumu. Na hayo yaliyosalia nijapo
nitayatengeneza.
Kwa hiyo, Ushirika wa Meza ya Bwana ulikuwa ni
tukio la maadhimisho, lakini hatimaye lilibadilishwa kuwa ni la kawaida huko
Korintho. Waumini walitakiwa wakutanike pamoja ili kula na waenende kwa
mwenendo unaotarajiwa kuonekana kutoka kwao hususan wanapokutanika na kula kwa
pamoja.
Kwa jinsi hii walitakiwa kuwa ni mabalozi wa Mungu
na wanaoheshimiana.
Kanisa lilijua jambo hili na lakini lilikuwa na
dhana kwamba Ufalme wa Mungu sio suala tu la kula na kunywa, bali ni haki au
utakatifu na amani na amani katika Roho Mtakatifu (Warumi 14:17). Jinsi
tunavyotendeana sisi wenyewe kwa wenyewe, na heshima tunayowaonyesha wapendwa
wenzetu ni ashirio au ishara ya nia yetu tuliyonayo mioyoni mwetu kwa Mungu na
kwa Kristo kwenye Kanisa.
Mwonekano wa Kimavazi
Watu wa Mungu wote walifundishwa jinsi ya kuvaa
kwa sitara. Wanaume hawakuruhusiwa kufuga ama kuwa na nywele ndefu (1Wakorintho
11:14) na walitakiwa kuvaa mavazi yenye heshima. Wanawake walitakiwa wavae
mavazi ya kujistahi na muashirio wa mambo mema.
Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani; 10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.
Neno ‘broided’ (kujipamba)
lilioandikwa kwenye Biblia ya KJV ni neno la Kiyunani linalotamkwa plegma, ambalo maana yake ni kusuka
nywele zilizosokotwa kwa mtindo wa kimapambo. Ilikuwa ni desturi kujipamba vito
vya dhahabu kwenye nywele na pengine hata vito vingine vya thamani, nk. Walengwa
waliokusudiwa sana walikuwa ni wanawake walioolewa au wake za watu zaidi kuliko
wanawake wote kwa ujumla.
Ufafanuzi: Andiko haliashirii kuwa kulikuwa na
makazo yote kabisa ya wao kuvaa vito vya dhahabu au nywele zilizosokotwa, bali
zaidi sana ni kwamba Paulo alikuwa anaweka tahadhari kwenye jamii ambayo mambo
kama hayo yalikuwa yanaashiria ni anasa na ubadhirifu usio wa lazima na ni dalili
ya mtu kuonyesha majivuno au kupenda ulimbwende.
Linganisha pia na inavyosema 1Petro 3:3-5:
Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; 4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu. 5 Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao.
Ndivyo pia mwanamke hakuruhusiwa kuvaa mavazi
yampasayo mwanaume na mwanaume pia hakutakiwa kuvaa mavazi yanayovaliwa na
wanawake, kwa mujibu wa Totati.
5 Mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanamume, wala mwanamume asivae mavazi ya mwanamke; kwa maana kila afanyaye mambo hayo ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako.
Na ni kwa ajili ya makatazo haya na desturi ya
siku nyingi iliyokuwepo kwenye Makanisa ya Mungu walitakiwa waendane na desturi
ya kimavazi iliyokuwepo kwenye desturi ya mataifa ambayo walikuwa wanaishi
ndani yake.
Sikukuu za Sabato za Kanisa zilichukuliwa pia kuwa
kama karamu za sherehe za maarusi ambazo tulizivalia mavazi ya aina na mitindo
ya kabla ya ujio wa Bwana arusi wetu Yesu Kristo, yapasayo kuvaliwa tunapokwenda
kumuabudu Baba yetu, ambaye ndiye Mungu wa Pekee wa Kweli.
Kwa hiyo, kiwango pekee cha wastani kilikuwa ni
suti au vazi lolote zuri tulilokuwanalo kwenye sherehe maalumu. Kwa kiwango
chochote tunachovaa kama tulivyofanya kwenye mishughuliko mbalimbali katika
harakati zetu za kuonyesha kukubaliana au kufanana na wale tunaokula nao na vile
tunavyokula.
Ni kwa miaka ya hivi karibuni tu hii imekuwa ni
mtindo uliopokelewa kwenye nchi fulani kadhaa kuweka sheria au makatazo ya
kutovaa mavazi yanayofunika nusu mwili wanapokwenda kuzishika Sabato na Siku
nyingine Takatifu za Bwana, na hata wanapokwenda kanisani na hata baada ya hapo
wanapokwenda kula chakula kwenye jamii zao. Hata hivyo, hii haiwezi kulifanya
jambo hili kuwa sahihi zaidi. Lakini inamaanisha kuwa tunapunguza viwango vyetu
vya kutotilia maanani yale tunayoamriwa kuyafanya kutoka na Maandiko Matakatifu
na desturi njema zilizowekwa kwenye Makanisa ya Mungu.
Imekuwa kila mara ni desturi ya Makanisa ya Mungu
kwamba wanawake wavae nguo nyepesi na mlegezo siku za Sabato, Miandamo ya Mwezi
na Siku Takatifu lakini wavae mavazi ya kujistahi nay a hesshima wakivaa pia
sketi na bilauzi, pamoja au pasipo na jaketi.
Wanaume kila mara wavae mashati na tai pamoja na
majaketi sehemu za baridi wawapo sehemu zote, yaani kwenye ibada na chakulani.
Kwenye nchi au mataifa ya Asia uvaaji wa kawaida
wa kitaifa kama vile mashati ya batiki au Barongs (huko Ufilipino) inachukuliwa
na kukubalika kama vazi la heshima na la kawaida.
Sarongs na Saris zinakubalika pia kama mavazi ta
kitaifa ya kawaida.
Uvaaji wa nguo safi na maridadi unatakwa kwenye maadhimisho
na mlo wa Sikukuu na hata kwenye maadhimisho na milo siku za Sabato na Siku
nyingine Takatifu.
Kweye mambo ya nje ya nyumba wanawake wanaweza
kuvaa mlegezo na nguo nyepesi na buti.
Majinzi hayaruhusiwi kwa namna yoyote ile ya
matembezi ya kidini bali yanaweza kuvaliwa tu kwenye matembezi ya kibinafsi
kama vile kutembelea kwenye migahawa, kunyoa nywele na mazoezi.
Ndala zimekuwa zikivaliwa tangu kipindi cha kuanzlshwa
kwa mavazi ya miguuni na hazijawahi kuwekewa sheria na utaratibu, lakini hata
hivyo ni vyema zikavaliwa kwa utaratibu mzuri.
Uvaaji wa viatu vya michezo au njumu au mavazi
mepesi unaweza kufanyika tu inapoonekana kuwa ni lazima kwa sababu za kiafya,
sawa na inavyotakiwa kufanywa kwa aina zote za vyakula vya kawaida Kanisani.
Viwango hivi vimechukuliwa kwa makubaliano ya bodi
zote za mataifa za Makanisa ya Mungu na kwenye Halmashauri Kuu ya Makanisa ya
Mungu Duniani.
Kama tutakuwa hatuheshimiani na tukaamua kuvaa
mavazi kwa mtindo usioendana na desturi, basi hemu na kubakie tu majumbani
kwetu. Kumbuka kuwa sisi ni sehemu ya Mwili wa Kristo na uvaaji wetu unapaswa
uonyeshe ukweli huo. Wakati wowote tunapokutanika amoja tujue kuwa tuko mbele
za Mungu na tunapaswa kumheshimu kwa mavazi yetu, pamoja na maneno na mwenendo
wetu.
Kwa kuhitimisha, twaweza kusema kuwa ni juu yetu
kuvaa kwa heshima ili tusimkasirishe Mungu au mpendwa mwenzetu yeyote. Kwa
kweli watu wanapaswa wasaidiwe ili wote waweze kushiriki maadhimisho haya
muhimu ya Sikukuu, kushiriki na kula pamoja kwa msingi wa kawaida wakati wowote
iwezekanavyo, na kuwa na msingi wa muhimu wa maisha, kama tulivyoona kwenye
Matendo 2:45, ili kwamba tusipungukiwe na kitu chochote.
q