Makanisa ya Kikristo ya Mungu

                                                                             [A1]

       

MATAMKO KUHUSU IMANI YA KIKRISTO

                                                                

CHRISTIAN CHURCHES OF GOD

P.O.BOX 369 WODEN ACT 2606, AUSTRALIA

 

Coordinator-General: Wade Cox

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

In North America

 

PO Box 1537, Blue Springs, MO 64013-1537, United States of America

 

 

Copyright © 1994,1995,1996,1997, Christian Churches of God

 

 

 

Karatasi hii inaruhusiwa kunukuliwa na kusambazwa kwa yeyote mradi tu kama itanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kuondoa maana halisi. Jina la mchapishaji na anuani yake na tangazo la hati miliki lazima vijumlishwe. Hakuna gharama yoyote ipaswayo kuchangiwa na mtumiaji na hairuhusiwi kuuzwa nakala zake kwa msomaji. Nukuu chache zaweza kuchukuliwa katika makala zinazo tofautiana kimtazamo na kimaoni bila kukiuka maadili ya haki miliki.

This Paper is available from the World Wide Web page:

Karatasi hii inapatikana pia katika Tovuti zetu popote Duniani

http://www.logon.org  and  http://ccg.org

 

MATAMKO YA IMANI YA MAKANISA YA KIKRISTO

 

YALIYOMO

                                                                                                                                                                                                                   

Utangulizi

Sura 1. Uungu

1.1 Mungu Baba

1.2 Yesu Mwana wa Mungu

1.3 Roho Mtakatifu

1.4 Uhusiano kati ya Roho Mtakatifu, Kristo na Binadamu

1.5 Uhusiano kati ya Kristo, Shetani na Jeshi la Mungu

1.5.1   Kristo kama Mwana wa Mungu

1.5.2   Mafundisho ya mpinga Kristo

1.5.3   Jina na Ukuu wa Mungu

 

Sura 2.  Mpango wa Wokovu

2.1 Anguko la Mwanadamu

2.2 Wokovu wa Mwanadamu

2.3 Biblia Kama Ukweli ulio Vuviwa

2.4 Kutubu na Kuongoka

2.5 Ubatizo

 

Sura 3. Mafundisho Kuhusu Wajibu wa Mwanadamu

 3.1 Maombi na Kuabudu

3.1.1.Mungu Kama Mlengwa apaswaye Kuombwa na kuabudiwa

3.1.1.1  Lengo La Maombi

3.1.1.2  Lengo La Ibada

3.1.1.3  Maombi ya Binafsi na ya wengi Kwaniaba ya Wengine

3.2 Uhusiano Kati ya Wokovu na Sheria

3.2.1  Mungu ndiye Mwamba wetu

3.2.2  Wokovu Kwa Neema

3.2.3  Ulazima wa kuwa chini ya Sheria

3.2.3.1  Kwanini ni lazima Wakristo washike Sheria

3.2.3.2  Wakristo kama Hekalu la Mungu

3.2.4 Amri Kumi

3.2.5 Sheria Nyingine zitawalazo Mwenendo wa Mwanadamu

3.2.5.1  Sheria ya Vyakula

3.2.5.2  Sabato

3.2.5.3  Mwandamo wa Mwezi

3.2.5.4. Siku Takatifu za Mwaka

3.2.5.5. Ndoa

3.2.6  Uwakili wa Mali

3.2.6.1  Kwaajili ya Mungu

3.2.6.2  Kwaajili ya Wengine

3.2.7  Mambo ya Vita na Uchaguzi

3.2.7.1  Vita

3.2.7.2  Uchaguzi

 

Sura 4. Mafundisho Kuhusu Masihi

4.1  Kuwepo kwa Kristo tangu Mwanzo

4.2  Kusulibiwa na Kufufuka

4.3  Kuja kwa Kristo Mara ya Pili

4.4  Utawala wa Milenia

 

Sura ya 5. Matatizo ya Uovu

5.1  Kuwepo kwa Uovu baada ya Uasi

5.2  Fundisho Kuhusu Kuchaguliwa Tangu Mwanzo

5.3  Hali ya Wafu

5.4  Ufufuo wa Wafu

5.5  Hukumu ya Waovu

 

Sura  6. Kanisa

6.1  Je,Kanisa ni nani au ninini?

6.2  Kanisa kama Shirika

6.3  Makusudio na Malengo ya Kanisa

6.4  Utakaso

 

Sura 7. Ufalme wa Mungu

7.1  Kuanzishwa kwa Ufalme wa Mungu

7.1.1  Ufalme wa Kiroho

7.1.2  Utawala wa Milenia wa Kristo

7.1.2.1  Kurudi Kwa Masiha

7.1.2.2  Kutaniko La Israeli

7.1.2.3  Siku ya Bwana

7.1.3  Utawala wa Milele wa Mungu

7.1.3.1  Ujio wa Mungu

7.1.3.2  Dunia Mpya na Yerusalem mpya

7.1.3.3  Hatima ya Wanadamu

Maongezo    

 

Utangulizi

Kwa muda wa miaka mia saba, Ukristo umefungwa katika mfumo wa Teolojia ambao umeshikilia Falsafa za Kiyunani na mfumo shirikishi na fikra za Kiplatoni mamboleo. Mbinu za ki Unitariani za kupelekea Ujumbe wa Biblia na ukiambatana na ufunuo wa Mungu kwa mwanadamu katika Maagano yote imebadilishwa na kutumiwa kwa maslahi ya kuendeleza nguvu na mamlaka ya kiutawala ya Dunia.

Hatimaye matokeo yake ni kile kilichoeleweka kuwa ni muundo ulio anzishwa na braza la Nikea (451AD), Laodikia (366AD), Costantinopo (381AD), na Kalkedoni (451AD). Mfumo huo ulibadili mwelekeo wa Mungu kuhusu mlolongo wa kinasfi hatimaye kukaanzishwa imani ya Utatu. Baraza la Laodikia (canon 29) vilevile liliondoa Sabato na badala yake vikaingizwa na kukubalishwa sikukuu za Kipagani kutoka ibada za Jumapili hadi Mwezi Desemba sikukuu ya Juana mfumo wa Easter mahali pa Pasaka. Kingine kilichokuwa kimebadilishwa, ni jinsi ya kuelewa mfumo wa Kibiblia na kwamba sheria zilipaswa zitafsiriwe. Sheria zilizotolewa na Musa zikachukuliwa kuwa zimepitwa na wakati na maandiko ya Agano Jipya yakatafsiriwa vibaya ili yaunge mkono uwepo wa matendo ya kipagani.

Kwa mfano, Sheria ya vyakula ikaondolewa kwa kunukuu vibaya Matendo ya Mitume 10 na aya nyinginezo. Madhara katika afya ya mwanadamu yakaonekana maramoja. Hatahivyo, matokeo ya mwisho ya mazingira yalianza kuonekana kwa hakika baada ya miaka elfu mbili hivi. Uvunjaji wa kanuni za utaratibu wa vyakula vilichangia pia kwa kiasi kikubwa sana, kwaajili ya ulaji wa vyakula vilivyo katazwa chini ya Sheria za Kibiblia.

Mmomonyoko wa mfumo wa ardhi unaweza kuonekana kikamilifu baada ya ardhi inapokuwa imechoka kwaajili ya kushindwa kuadhimisha mfumo wa Jubilee na sabato za ardhi kwasababu walizivunja na na kufuata mfumo wa kalenda zenye mzunguko wa miezi kuminatisa. Kuanzishwa kwa mfumo wa kalenda za jua (solar) ilikuwa yenyewe tu ni hatua kubwa sana katika kuharibu isieleweke mfumo na mzunguko ambao Mungu aliuweka kwa jinsi ya mpangilio wa asili.

Ukristo uliopo leo kwa wingi au kwa uchache haufanani na ule Ukristo wa asili wa zamani. Kuibuka kwa Uislam na vita vya baadae na waislam kulikuwa ni matokeo dhahiri ya mfumo wa Ukristo wa uwongo ulioanzilishwa na Ulaya na Asia Magharibi na mfumo wa falsafa za Kiyunani kwa kutumia teolojia ya Wakapadokiani iliyoamini Mungu wa nafsi Tatu na kwamba kuna mahusiano ya siri na Mungu na ni ndio Mungu. Mfumo huu wa ki-Utatu hauwezi kufanya kazi. Matokeo ya mwisho ya miaka elfu moja na mia saba ya mafundisho haya ya uwongo yamekuwa ni kukaribia uharibifu wa Sayari na kuteswa kwa watu ambao wanajaribu kwa dhati ya moyo kutii sheria za kibiblia.

Madhumuni ya kazi hii ni kuutoa kwa uwazi na kwa njia rahisi iwezekanavyo ujumbe halisi wa Biblia na wa Kanisa la Agano jipya chini ya Yesu Kristo na Mitume. Bilashaka baadhi ya mambo yaliyo elezewa ndani yake yataleta changamoto na yatafishwa. Kazi imeandikwa ili kwamba iwe karibu iwezekanavyo, mafuatano ya maelezo ya kibiblia au mafafanuzi ambayo yanapata uungwaji mkono na aya zilizo nukuliwa. Kwa njia hii inachukuliwa kwamba kitabu hiki kimekamilika bila kutumia lugha za mafumbo na malengo yetu yako wazi kabisa. Ilipowezekana sehemu nyingine vitabu vingi vya biblia vimeorodheshwa ili kuepukana na nukuu chache. Baadhi ya aya za biblia zimekosewa kiuwazi kabisa. (mf. 1Jn. 5:7 KJV; 1Tim 3:16 KJV; kutokana na Codex A), au zingine zimetafsiriwa visivyo (mf. 1Kor.15:28 RSV, kadhalika Ufu.3:18 NIV ni baadhi tu ya zile zingine), zilifanywa hivyo ili ziunge mkono fundisho la Utatu au mfumo wa Wakapadokiani vinavyotaka kuonekana haviendani.

Wakati Masihi ajapo tena atakuja kurudisha tena mfumo wa sheria alizompa Musa pale Sinai.Kila Mkristo anao wajibu kudhihirisha na kuendeleza mfumo wa jinsi ya kuishi na na kuabudu sawa na ilivyo elekezwa katika Biblia. Makristo analazimika kujitahidi kupita njia ya maisha Yesu Kristo na kuishi katika mfumo ule ambao Kristo alifundisha na alivyoishi kama mwanadamu na aliyetoka juu. Kitabu hiki kimetolewa ili kuelezea mfumo mzima wa jinsi tunavyoishi kwa nia ya kutulinda na mfumo wa uwongo mpotofu na mfumo ule ambao kwa miaka elfu moja na mia saba utupiliwe mbali na njia halisi nay a kweli iweze kujulikana na ianze kufanya kazi ndani ya maisha ya watu haijaliishi nini walifanya nini huko nyuma. Jukumu letu ni kuwaita watu kwenye toba na upya wa uzima.                                        

 

Sura ya 1

Uungu

1.1  Mungu Baba

Nafasi ya juu sana Ulimwenguni iliyo bora na kutukuka sana kwahabari ya mambo ya Uungu ni ya Mungu. Yeye ndiye mwenge nguvu zote, Muumbaji na na mwenye kuvifanya viendelee kuwepo Mbingu, dunia na vyote vilivyomo ndani yake (Mwa.1:1; Neh.9:6; Zab.124:8 Isa.40:26,28; 44:24; Mdo.14:15; 17:24-25; Ufu.14:7). Yeye pekee ndiye mwenye kuishi milele bila kufa (1Tim. 6:16). Yeye ndiye Mungu na Baba yetu, na pia ndiye Mungu na Baba wa Yesu Kristo (Yoh. 20:17). Yeye ndiye Mungu aliye juu sana zaidi vitu vyote (Mwa. 14:18; Hes.24:16; Kum.32:8; Mk.5:7) na ni Mungu wa pekee wa kweli (Yoh.17:3; 1Yoh.5:20).

1.2  Yesu Mwana wa Mungu

Yesu ni mzaliwa wa kwanza (proototokos) katika uumbaji (Kol. 1:15) yaani kuanzia mwanzo (arche) wa uumbaji wa Mungu (Ufu.3:14). Yeye ndiye mzaliwa pekee (monogene) Mwana wa Mungu (Mat. 3:17; Yoh. 1:18; 1Yoh. 4:9), aliyetungiwa mamba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu akazaliwa na bikira Mariamu (Lk. 1:26-35). Yeye ndiye Kristo au Masihi (Mat. 16:16; Yoh.1:41), aliyetumwa kutoka kwa Mungu awe Mwokozi na Mkombozi wetu (Mat.14:33; Yoh.8:42; Efe.1:7; Tit.2:14). Anaitwa ni Mwana wa “Mungu aliye juu sana” (Mk. 5:7). Alikuwa ni Mwana wa Mungu aliyekirimiwa uweza wa Roho ya Utakatifu na kufufuliwa kutoka mautini (Rum.1:4). Emepewa kiti cha enzi cha Daudi ili kutawala nyumba ya Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho (Lk. 1:32).

1.3  Roho Mtakatifu

Roho Mtakatifu (Mdo. 2:4) ni kiini au nguvu za Mungu ambaye Kristo aliahidi kumtuma kwa wateule (Yoh.16:7). Yeye siyo nafsi au mtu, lakini ni mgawanyo tu wa nguvu za Mungu zilizo hai. Ni kwakupitia yeye sisi tunafanyika kuwa warithi wa Asili ya mambo ya Mbinguni (2Pet. 1:4), kujazwa na Roho Mtakatifu (Mdo.9:17; Efe.5:18) na hivyo  sote kufanyika watoto wa Mungu (Ayu.38:7; Rum.8:14; 1Yoh.3:1-2) na warithi pamoja na Kristo (Rum.8:17; Gal.3:29; Tit.3:7; Ebr.1:14, 6:17, 11:9; Yak.2:5; 1Pet.3:7) Hutolewa na Mungu kwa wale wamuombao (Lk.11:9-13) na wanao mtii, Hukaa ndani yao wale wanazishika Amri za Mungu (1Yoh.3:24; Mdo.5:32). Roho Mtakatifu ni mfariji ambaye huwaongoza watumishi wa Mungu na kuwatia katika kweli yote (Yoh. 14:16,17,26).  Roho Mtakatifu hutia nguvu za kushuhudia (Mdo.1:8). Hushughulika na maongozi ya karama kama zilivyo elezewa katika 1Wakorintho 12:7-11 na anayo matunda kama ilivyoelezewa katika Wagalatia 5:22-23, hatolewi kwa kipimo (Yoh. 3:34 RSV; Rum.12:6) Kwakupitia yeye hatimaye Mungu hufanyika ni yote katika yote (1Kor.15:28; Efe 4:6).

1.4  Uhusiano kati ya Roho Mtakatifu, Kristo na Binadamu

Roho Mtakatifu hufanya kazi kwa mtu hata kabla ya Ubatizo. Roho humleta mtu binafsi yake kwa Mungu kupitia Kristo (Ebr. 7:25)

Matunda ya kwanza ya Roho hutolewa kwa mwanadamu pale anapobatizwa, kama isemavyo Warumi 8:23, ambapo inasema waziwazi kuwa kufanyika mwana hakutimiliki hadi ukombozi wa mwili.

Hivyo basi tumezaliwa mara ya pili lakini tunaendelea kukua katika Roho kila siku katika Kristo Yesu hadi kuufikia utukufu wa Mungu. Roho Mtakatifu ni Roho wa Mungu (Rum. 8:14) na ni Roho wa imani (2Kor. 4:13) ambaye huchunguza mambo yote na hufahamu mambo yote (1Wak.2:10-11, 12:3ff.).

Hivyo basi, Roho Mtakatifu siyo kuwa ni kitu kinacho jitegemea cha Mungu mwenye mfumo wa Utatu, lakini ni njia ambayo sisi tumefanyika kuwa ni elohim (Zek. 12:8). Roho huwakilisha kwa Mungu uelewa wa mawazo yetu na uanadamu wetu, tukiwezeshwa kupitia Yesu Kristo kama mwombezi na mpatanishi wetu yaani elohim au theos (Zab. 45:6-7; Zek.12:8; Ebr.1:8-9) anamuwezesha Kristo kutusaidia, kutufundisha na kutufariji na kutuwezesha kuzifanyia kazi nguvu za Mungu. Roho hutoa kwa kila mtu tabia njema kama apendavyo Mungu ili kuufaidia mwili wa Kristo kama inavyosema 1Wakorintho 12:7-11.

Roho anaweza kuzimwa (1The. 5:19) kwa kukataliwa au kwa kuhuzunishwa (Efe. 4:30) hivyo basi aweza kuona faida na hasara katika nafsi ya mtu.

Tunda la Roho Mtakatifu ni Upendo kama isemavyo wagalatia 5:22. Hivyo basi, kama hatupendani sisi wenyewe Roho Mtakatifu hayupo mahali hapo.

Roho ni njia ambayo kwayo kwayo kwayo tunamuabudu mungu kama inavyoelekezwa katika Wafilipi 3:3. hivyo basi hawezi kuwa Mungu kiasi cha kuwa mlengwa katika ibada kiasi cha kuabudiwa na hivyo kuwa sawa na Mungu Baba. Ni nguvu imtiayo nguvu Kristo. Pale isemwapo kuwa Kristo ni Baba wa Milele, (Isa. 9:6) ni kwamba kuna aina nyingi ya ubaba mbinguni na duniani (Efe. 3:15). Kristo amefanyika kuwa Baba wa Milele kwa njia ya uwakilishi.

Aina hizi zote za ubaba au familia zimetumika kumtaja Mungu Baba hii ndiyo maana tunapiga goti mbele zake Mungu Baba na kumuabudu (Efe. 3:14-15).

Kristo mzaliwa wa kwanza au mzaliwa wa kwanza katika Uumbaji. Kwakuwa katika yeye viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni viti vya enzi,au usultani, auenzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwaajili yake. Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye. (Kol. 1:16-17). Lakini ilikuwa ni Mungu aliye mfanyiza na aliyerithia kwmba uumbaji udumu na uwepo katika Kristo. Hivyo basi, Kristo siyo Mungu kwa namna yeyote ile kama Mungu Baba alivyo Mungu na kwamba yeye tu pekeyake mwenye kuishi milele bila kufa (1Tim. 6:16) huishi bila kutegemea kitu chochote katika umilele.

Wakristo wameitwa kutoka katika dunia hii ili waishi maisha ya utumishi na kujitoa wakfu. Walioitwa ni wengi lakini wateule ni wachache (Mat. 20:16, 22:14). Wakristo ni watu waliochaguliwa kama vile Kristo alivyokuwa amechaguliwa na Mungu (Lk. 23:35). Wateule wamechaguliwa na Kristo (Yoh. 6:70, 15:16,19), kwa maongozi ya Mungu. (1Pet. 2:4).

Ili kulisaidia Kanisa, wateule ambao ndio Kanisa au ecclesia, wamepewa majaliwa ya kuzijua siri za Mungu. Roho Mtakatifu ndiyo anayefanya kazi hiyo ya kuwawezesha kuelewa siri za Mungu na za Ufalme wa Mungu (Mk. 4:11). Kwakuwa hekima ya Mungu huongelewa kwa njia ya mafumbo (1Kor. 2:7), ambayo hutafafanuliwa na watumishi wa Mungu (1Kor. 2:7, 15:51). Kwakuwa mapenzi ya Mungu yameelezewa kwa njia ya mafumbo (Efe. 1:9) ambayo Mungu aliwapa watumishi wake kwa njia ya ufunuo . Zaidi ya yote, siri hizo ziko katika utumishi wa Kristo kupitia wateule. Mtume Paulo aliandika:

…ikiwa mmesikia habari ya uwakili wa neema ya Mungu niliyopewa kwaajili yenu; ya kwamba kwakufunuliwa nalijulishwa siri hiyo, kama nilivyotangulia kuandika kwa maneno machache.Kwahayo, myasomapo, mtaweza kuutambua ufahamu wangu katika siri yake Kristo. Siri hiyo hawakujulishwa wanadamu katika vizazi vingine; kama walivyofunuliwa mitume wake watakatifu na manabii zamani hizi katika Roho; ya kwamba Mataifa ni warithi pamoja nasi wa urithi mmoja, na wa mwili mmoja na washiriki pamoja nasi wa ahadi yake iliyo katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili; (Efe. 3:2-6).

1.5  Uhusiano Kati ya Kristo, Shetani na Jeshi la Mungu

Kuna aina mbalimbali ya matumizi ya neno Elohim au Theoi lilivyo tumika katika Biblia likitumiwa kwa maana ya miungu. Kristo ni miongoni mwa watu wanaoonekana kutujumuishwa katika kundi hili katika rejea za Agano La Kale kama Elohim (tazama Zek.12:8). Kristo anatajwa tena katika rejea za Agano Jipya kama ni Nyota mpya ya Afajiri katika kurudi kwake duniani. Atawashirikisha daraja hili la heshima wateule wake (Ufu. 2:28, 22:16).

Mungu anasisitizwa katika Biblia kuwa ni Mungu na Baba wa Kristo (soma Rum.15:6; 2Kor.1:3, 11:31; Efe.1:3, 17; Kol.1:3; Ebr.1:1 ff; 1Pet.1:3; 2Yoh.3; Ufu.1:1,6, 15:3) Kristo alitoa uhai wake, nguvu na mamlaka kwa amri ya Mungu Baba (Yoh.10:17-18). Kristo aliyatiisha mapenzi yake yaendane na vile Mungu alipenda ambaye ni Baba (Mat. 21:31, 26:39; Mk.14:36; Yoh.3:16, 4:34). Mungu amempa Kristo wateule wote kuwa wake na Mungu ni mkuu kuliko Kristo (Yoh. 14:28) na ni mkuu kuliko vitu vyote (Yoh.10:29). Hivyo basi, Mungu alimtuma mwanawake wa pekee (monogene) duniani ili sisi tuishi kupitia yeye (1Yoh. 4:9). Ni Mungu ndiye ampaye heshima na kumtukuza Kristo (Yoh. 8:54), Mungu akiwa ndiye mkuu kuliko Kristo (Yoh. 14:28).

Mungu ni Mwamba (sur) kama Jabali au Mlima ambalo wengine wote wametokana kwayo, jiwe la gumegume la Yoshua 5:2 lililo watahiri Israeli, kanuni na sababu kuu muhimu (Kum. 32:4). Mungu ndiye Mwamba wa Israeli, Mwamba wa wokovu (Kum. 32:15), Mwamba ule uliowazaa (Kum. 32:18,28-31). 1Samweli 2:2 hutuonyesha kuwa Mungu wetu ndiye Mwamba wetu, Mwamba wa milele (Isa. 26:4). Ni kutokana na Mwamba huu ndipo wengine wote wametokea kama wote ni wana wa Abraham kwa njia ya imani (Isa. 51:1-2). Masihi ametokana na katika Mwamba huu (Dan. 2:34,45) ili kuzitiisha tawala zote za dunia. Mungu ni Mwamba au timazi ambayo msingi umewekwa na ambapo Kristo atalijenga kanisa lake (Mat. 16:24) na ambapo yeye mwenyewe huweka makao na kupumzika. Masihi ndiye Jiwe Kuu la Pembeni la Hekalu la Mungu, ambalo wateule ni Naos au Patakatifu pa Patakatifu, wakimtuinia Roho Mtakatifu. Mawe yote ya Hekalu yametokana ndani ya Mwamba ambao ni Mungu, kama ilivyokuwa kwa Kristo, na wamekabidhiwa kwa Kristo, mwamba war oho (1Kor. 10:4), jiwe likwazalo, na mwamba uangushao; (Rum. 9:23) ili kujenga Hekalu.

Kristo analijenga Hekalu ili Mungu awe yote katika yote (Efe. 4:6). Mungu amemfanya Kristo kuwa ni yote katika yote (panta kai en pasin Kol. 3:11) akivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake (1Kor.15:27) akimfanya wewe kuwa ni kichwa juu ya mambo yote katika Kanisa ambalo ndio Mwili wake, utimilifu wake ambao unaokamilisha mambo yote katika yote (Efe.1:22-23).Wakati Mungu alipo vitiisha vitu vyote chini ya Kristo, ilikuwa inaashiria kuwa Mungu alimteua yeye mwenyewe ili avitiishe vitu vyote chini ya miguu ya Kristo (1Kor. 15:27).

Wakati Kristo anapovitiisha vitu vyote ndipo hatimaye Kristo mwenyewe atajitia chini ya Mungu aliye vitiisha vitu vyote kwa Kristo ili Mungu awe yote katika yote (panta en pasin 1Kor. 15:28 sio sawa na vile tafsiri ya RSV). Hapa ndipo mafundisho ya Waplatoni yanapotafuta kuchanganyisha kati ya Mungu na Kristo katika maandiko yanayojichanganya kuhusu Utatu. Kristo atakaa mkono wa kuume wa Mungu, kwa maongozi ya Mungu (Ebr. 1:3, 13, 8:1, 10:12, 12:2; 1Pet.3:22) ambacho ni kiti cha enzi cha Mungu (Zab.45:6-7; Ebr.1:8) au Mungu yuko juu ya kiti chake cha enzi imetafsiriwa kuwa kiti chako cha enzi ee Mungu (angalia rejea za chini “footnote” katika Biblia ya RSV).

Mungu, ambaye anatuma ni mkuu kuliko yeye anayetumwa (Yoh. 13:16), mtumwa hawi mkuu kuliko Bwana wake (Yoh.15:20)

Kristo alishindana na Shetani na kukutana na majaribu makuu ambayo Shetani aliyaandaa. Shetani ambaye alikuwa ni Nyota ya Asubuhi, Lusifa au mleta nuru katika dunia hii (Isa. 14:12) kama alivyokuwa mlinzi na mwalimu, kikamilifu kabisa, mmoja kati ya Elohim ambaye alikuwa chimi ya Mungu Baba.

Kristo alikuwa ndiyo ambayo ilikuwa itokee katika nyumba ya Yakobo (katika Hesabu 24:17). Hivyo basi, iliashiriwa katika Vitabu vya nabii Musa kuwa mojawapo ya Nyota ya Asubuhi ambayo imetajwa kuwa itakuwepo katika mwisho wa hii sayari hii (katika Ayubu 38:7), mmojawapo wa elohim, alipaswa afanyike kuwa mwanadamu katika Yakobo na katika Daudi (Ufu.22:16).

Huyu elohim tumjuaye kama Yesu Kristo alikuwa bado sio Nyota ya Asubuhi ya sayari hii. Cheo kilishikiliwa na Shetani (soma Isa.14:12 na Eze.28:2-10).

Kristo alipakwa mafuta kuwa ni elohim wa Israel usomapo Zaburi 45:7 na mpakwa mafuta juu ya washiriki wake au watendakazi pamoja naye. Hata hivyo, Kristo kwakweli hakuwa katika cheo cha kuwa Nyota ya Asubuhi na hataweza kuzifanya kazi hizo hadi pale atakapo rudi mara ya pili. Cheo na majukumu ilipaswa vishirikishwe kati ya Kristo na wateule, ambao wamejumuishwa katika asili yake kama Nyota ya Asubuhi katika mioyo yao (imetafsiriwa kama Nyota ya Mchana katika 2Pet.1:19). Wateule wameahidiwa kushirikishwa katika uweza huu usomapo Ufunuo 2:28.

Shetani, kama Nyota ya Asubuhi, alishindana na Mungu Mkuu Aliye juu sana au Mungu Baba kama tunavyoambiwa katika Isaya 14:12. Alijaribu kujikweza au kukiinua kiti chake cha enzi, kiti cha enzi cha Mungu, juu ya Nyota za Mungu au baraza la Elohim. Baraza hili ni Kusanyiko la Elohim au Miungu kama inavyosema Zaburi 82:1. Ni jambo la kufurahisha sana kufahamu kuwa Irenia mwanafunzi wa Polycarp, mwanafunzi wa Mtume Yohana, alishikilia kwamba Zaburi 82:1 inapelekea kwa Theoi au miungu ambayo ilijumuisha vilevile wateule, kwa jina la wale waliofanywa wana (kinyume na Mafundisho PotofuHeresies’, Bk.3, Ch.6, ANF, Vol.1, p.419).  

Kuna aina mbalimbali ya Wana wa Mungu (kulingana na Ayubu 1:6, 2:1, 38:7; Zab.86:8-10, 95:3, 96:4, 135:5) waliojulikana kama Bene Elyon au Wana wa aliye juu sana. Binadamu wateule vilevile wamejumlisha pamoja na Jeshi la mbinguni kama Wana wa Mungu (Rum. 8:14). Hivyo basi Kristo na wateule kama Wana wa Mungu ni wamoja na Mungu kupitia Roho Mtakatifu, waliokusudiwa tangia mwanzo wa kuwekwa misingi ya dunia. Kristo aliachia chini uweza wake na kufanyika kuwa mwanadamu. Yeye pamoja na wateule wote wamepokea Uwana kwa uweza kulingana na Roho ya Utakatifu kwa kufufulika kwake kutoka na nguvu za mauti (Rum. 1:4).

Katika Matendo 7:35-39 alikuwa ni malaika aliyesema na Musa katika mlima wa Sinai na malaika huyo ni Kristo. Katika wagalatia 4:14 Paulo hujifananisha na malaika wa Mungu vilevile Yesu Kristo.

Vilevile sisi tutakuwa kama malaika (Mat. 22:30) kama amri au isaggelos (Lk. 20:36) kuwa warithi pamoja na Kristo (Rum. 8:17; Gal.3:29; Tit.3:7; Ebr.1:14, 6:17, 11:9; Yak.2:5; 1Pet.3:7). Agano la Kale linamtaja malaika wa YHWH kwa namna zote Yehova na Elohim (Kut. 3:2,4-6 wakati Mungu au elohim hapa alikuwa ni malaika; mfano Zek.12:8).

Zabiri 89:6-8 hutuonyesha kuwa kuna Baraza la Watakatifu (qedosim au qadoshim, vilevile imetumika kama wanadamu) hujumlishwa na yote mawili baraza la ndani na la nje. Hii inajulikana kuwa ni Baraza la kimbinguni la Elohim wa haki.

1.5.1 Kristo kama Mwana wa Mungu

Shetani alipania kumjaribu Kristo kwa njia mbalimbali. Kwanza kabisa shetani alimtaja yesu kama Mwana wa Mungu (Mat.4:3, 4:6; Lk.4:3). Mapepo pia walimtaja Kristo kama Mwana wa Mungu (Mat. 8:29; Lk.4:41; Mk.3:11). Shetani aliojaribu kumfanya Kristo athibitishe sehemu yake kama Mwana wa Mungu kwa njia ya kutumia vibaya mamlaka yake, kwakuwa Mungu aliahidi kuwa atamtumia malaika zake wamlinde  (Zab. 91:11-12). Shetani akaruka pale inaposema kukulinda katika njia zako zote na akaongeza neno wakati wote. Hivyo basi kwa njia hii ya kupindisha maandiko Shetani alikuwa anajaribu kuchukua uhai wa Kristo.

Kristo hawa mara moja hakumsahihisha Shetani wala mapepo kwa kudai yeye alikuwa ni Mungu badala ya Mwana wa Mungu. Kwahakika, hakuna pepo aliye wahi kudai udanganyifu wa kuwa Kristo alikuwa Mungu Mkuu bora kabisa mpaka baada ya kifo chake na nia yake ilikuwa ni kuanzisha fundisho linalosema kuwa Kristo alikuwa Mungu katika namna moja ya kwamba Mungu Baba ni Mungu na kwamba amekamilika baada ya kifo chake, ni udanganyifu ambao Kristo angeukanusha maisha. Katika kila jaribu moja nia ilikuwa kudhoofisha utii wa Kristo kwa Mungu na kwa ile nia yake njema ili avunje maandiko. Shetani alikuwa anajaribu kumfanya Kristo amuabudu yeye. Alimuahidi Kristo kumpa utawala wa dunia hii iwapo tu kama Kristo angekubali kumuabudu.

Kristo hakubishania haki yake ya kutawala hii dunia au kuwa kwakweli yeye alikuwa ni mtawala. Badala yake Kristo alijibu:

…imeandikwa Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.        

Kristo hakumwambia Shetani kuwa ilpaswa Shetani amsujudie Kristo lakini badala yake alimpeleka kwenye nukuu za vitabu vya sheria. Kristo katika hatua yoyote ya huduma yake kamwe hajadai wala kujitangaza kuwa yeye ni Mungu. Alisema kuwa yeye ni Mwana wa Mungu. Na ni kwasababu hii ndiyo ilimfanya kuingia matatani.

Ni kama vile ilivyoandikwa katika Mathayo 27:43

Alimtegemea Mungu; na amwokoe sasa, kama anamtaka; kwa maana alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu’.

 Hapa ndipo Kristo alipolia ili kutimiliza andiko katika Zaburi 22:1

           Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?

Kristo ni dhahiri kabisa hakujiita wala kujichukulia mwenuewe kuwa ni Mungu. Kutia dhana hii kuwa yeye alikuwa ni sehemu ya uungu kwamba alidai hivyo na kuwa yeye yuko cheo sawa, ni ujinga.

1.5.2  Fundisho la Mpinga Kristo

Fundisho la Mpinga Kristo limeelezewa katika 1Yohana 4:1-2. Kulingana na maandiko yaliyoko katika Gombo halisi za zamani, 1Yohana 4:1-2 kadiri ilivyo sanifiwa na Irenia, Sura 16:8 (ANF, Vol.1, fn. p. 443).         

Hivyo basi mfahamuni Roho wa Mungu: Kila roho inayokiri kuwa Yesu Kristo amekuja katika mwili ni ya Mungu; na kila roho inayomtenga Yesu Kristo sio ya Mungu ni ya Mpinga Kristo.

Mwana historia mmoja aitwaye Socrates alisema (katika VII, 32, p. 381) aya hii changanywa na wale waliotaka kutenganisha ubinadamu wa Yesu Kristo kutoka katika uhali yake ya kimbinguni.

Kristo kama Mwana na siyo Mungu Mmoja wa pekee (Yoh.17:3).

Pia katika Luka 22:70, wakasema wote,Basi, wewe ndiwe Mwana wa Mungu?

Akawaambia, Ninyi mwasema kwamba mimi ndiye.

Alijulikana kama Mwana wa Mungu pia katika:

* Mathayo 27:54 ambapo inasema Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.

* Marko 1:1 inasisitiza Injili kuwa ni Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.

* Luka 1:35 inaelezea kuwa Mtakatifu atakaye zaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.

Kufahamu kuwa Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu, ni ufunuo kutoka kwa Mungu.

Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu   akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona, kwakuwa mwili na damu havikukufunulia hili; bali Baba yangu aliye Mbinguni. (Mat.16:16-17)

Vilevile Mathayo 11:27 inasema:

Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu, wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia.

Hivyo basi, Baba huwafunulia mambo watu binafsi na humpa Kristo watu hao ambaye hatimaye huwafunulia Baba watu hao.

1.5.3  Jina na Ukuu wa Mungu

Hakuna shaka yoyote kuwa Mungu ni mmoja na ni mkuu. Mithali 30:4-6 inatuonyesha jina la Mungu nanikuwa anaye mtoto.

            Ninani aliyepanda mbinguni na kushuka chini?

Ninani aliyekamata upepo na makonzi yake?

                Ninani aliyefunga maji ndani ya nguo yake?

                Ninani aliyefanya imara ncha zote za nchi?

                Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwanawe, kama wajua?

                Kila neon la Mungu [ELOAH] limehakikishwa;

                Yeye ni ngao yao wamwaminio.

                Usiongeze neno katika maneno yake;

                Asije akakulaumu, ukaonekana u mwongo.

Biblia hujitafsiri yenyewe na jina la Mungu linaonyeshwa waziwazi ikifuatilia maelezo ya swali na ni wazi kuwa uungu sio kitu cha muunganiko wa vitu vingi pamoja kama vile Baba na Mwana, lakini zaidi sana ni kwamba anaye Mwana.

Zaidi ya yote, Agano jipya huelezea waziwazi kuwa ni Baba anayepaswa kuabudiwa. Kristo alimuonya Mwanamke Msamaria katika Yohana 4:21 kwamba saa inakuja ambayo hamtamuabudu Baba katika mlima huu (Samaria), wala kule Yerusalemu. Lakini kwa msisitizo kabisa anasema katika Yohana 4:23:

Lakini saa inakuja inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba   katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

Kristo anaelekeza hapa kuwa anayepaswa kuabudiwa hapa ni Baba na sio yeye mwenyewe. Hivyo basi tunaona kuwa ni kufuru kubwa kudai kuwa anayepaswa kuabudiwa hapa ni Kristo aliye inuliwa na itkuwa ni kwenda kinyume na Yohana 3:14 isemapo kuwa Mwana wa Adamu alipaswa kuinuliwa juu kama vile Musa alivyo muinua yule nyoka jangwani. Kusudi la kusulibishwa ilikuwa ni ili mwanadamu apate uzima wa milele, na sio ili hatimaye Kristo awe ndiye mlengwa katika kuabudiwa kama inavyo fundishwa kwa uwongo. Kutokana na mtazamo huu wa potofu, pia imedaiwa kwa namna potofu sana kuwa Wakristo wanaabudu mwili wa Kristo na damu yake wakati wanaposhiriki Ekaristi.

Eloah ni Mungu wa Agano la Kale na Hekalu na ni Mungu wa Yesu Kristo wa Agano Jipya. Hekalu lililokuwako Yerusalemu lilikuwa ni nyumba ya Eloah (Ezra 4:24; 5:2,13,15,16,17; 6:3,5,7,8,16,17; 7:23). Alikuwa ni Eloah wa Israeli (Ezra 5:1; 7:15), Eloah Mukuu wa Mbinguni (Ezra 5:8,12). Alikuwa ndiye mlengwa katika kumtolea na kupokea sadaka katika Hekalu (Ezra 6:10) mahali alipokuwa amelikalisha Jina lake (Ezra 6:12). Yeye ndiye aliye amuru ujenzi wa Hekalu (Ezra6:14) na kusimamisha kwa ukuhani ili kumtumikia yeye (Ezra 6:18; 7:24) na wafanye mapenzi yake (Ezra 7:18). Torati ni Sheria za Eloah wa Mbinguni (Ezra 7:12-14). Wale wanaozijua sheria za Eloah walipaswa kuwafundisha wale wote wasiozifahamu (Ezra 7:25) na hukumu zilipaswa kufuata sheria za Eloah (Ezra 7:26). Anayetajwa hapa ni Baba ambaye ni Eloah mmoja na ni Mungu Aliye Juu Sana, Baba wa Masihi na wa watoto wa Mungu wote.

 

Sura ya  2

Mpango wa Wokovu

2.1 Anguko la Mwanadamu                                                                                                                                                                                                                 

Mwanadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu na kufanana naye (Mwa. 1:26-27). Adamu na Hawa walilaaniwa kwasababu kutotii (Mwa. 3:16-19). Matokeo ya uasi huu, dhambi na mapatilizo ya mauti iliwapata wanadamu   wote (1Kor. 15:22; Rum.5:12).

2.2  Wokovu wa Mwanadamu

Mungu hapendi mtu yeyote apotee (1Pet. 3:9). Ili kwamba mwanadamu aepukane na hukumu ya dhambi, Mungu aliandaa mpango wa wokovu ukihusisha na sadaka ya kifo na ufufuko wa Mwanae Yesu Kristo (Yoh. 3:16). Mpango huo ni kwa kutoa malimbuko ambayo ilikuwa ni Kristo ambaye ni malimbuko ya wote walio lala mautini (1Kor. 15:20). Mpango huu wa wokovu unaonekana kwa kioo kupitia Sikukuu takatifu za kila mwaka zilizoko katika Biblia (Law. 23).

2.3  Biblia kama Ukweli uliovuviwa

Kristo alisema: …imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu (Mat. 4:4; Lk.4:4). Biblia hujulikana kama Maandiko Matakatifu (Dan. 10:21), na yanayomuongoza mtu ili kuupata wokovu na madhihirisho ya nguvu za Mungu (Kut.9:16; Rum.9:17). Njia pekee ya kuupata wokovu ni Yesu Kristo (Rum.10:11) ambaye alitabiriwa na Maandiko Matakatifu kuanzia Musa na Manabii wengine (Lk.24:27), unabii katika Maandiko Matakatifu (Mat. 26:56; Rum.1:2). Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema (2Tim. 3:16).

Maandiko Matakatifu wakati wa Kristo na Mitume yalikuwa ni ya Agano la Kale tu (Mat. 21:42; Mk.12:10; Mdo 17:2). Maandiko Matakatifu ya Agano la Kale ndiyo yaliyokuwa yanaoelezewa kuwa ni pumzi ya Mungu au yamevuviwa katika 2Timotheo 3:16. Agano Jipya ni nyongeza ya Agano la Kale. Halichukui nafasi mbadala ya Agano la Kale.

Agano la Kale liliandikwa siku za mapema zaidi likilenga kutupa maelekezo, ili kwamba kwa kusimama kwetu imara huku tukitiwa moyo na maandiko haya tupate tumaini (Rum.15:4). Kupotea ni matokeo ya kutoyajua Maandiko (Mat. 22:29; Mk.12:24). Watu wa Beroya waliyachunguza Maandiko kila siku, ili waone kuwa kama yale yanayosemwa ni ya kweli. Hali hii ilifanya waonekane kuwa ni wastaarabu (Mdo.17:11). Mtazamo mzima wa Biblia umechukuliwa kutokana na maeneo yote ya Maandiko Matakatifu, fundisho hadi fundisho, msitari hadi msitari (Isa. 28:10). Maandiko hueleza kuwa kwamba Yesu alikuwa Masihi au Kristo (Mdo.18:28). Ni Kristo kwa njia ya Roho Mtakatifu, anaye fungua ufahamu wa wateule akianzia na Mitume, ili kwamba Maandiko Matakatifu yaweze kueleweka. (Lk. 24:45).

Maandiko ya Agano la Kale lazima yatimizwe (Mat. 26:54,56; Mk.12:10; 14:49) na hayawezi kutanguka (Yoh.10:35). Maandiko mengi sana yalimuelekea na yalitimilizwa kwa Kristo au yata timilizwa na Kristo atakapo kuja mara ya pili (Ufu.1:7, 12:10, 17:14, 19:11-21), ambapo itakuwa katika uweza na utukufu (Mat. 24:30)

2.4  Kutubu na Kuongoka

Kwa Mwanadamu kuishi au kupata uzima wa milele, Mungu anahitaji ni sharti iwepo toba. Bila toba ni kuangamia (Lk.13:3-5)

Kristo alitumwa ili kuwaalika watu wote watubu (Lk. 11:32). Kristo alianza huduma yake baada ya Yohana Mbatizaji kutiwa gerezani (Mat. 4:12). Yohana alitiwa gerezani yapata baada ya Pasaka ya mwaka 28 BK (Yoh. 3:22-24, 4:12) ambayo ni Pasaka baada ya kuanzishwa kwa huduma ya Yohana katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio (Lk.3:1). Tangia wakati ule, Yesu alianza kuhubiri akisema Tubuni kwa maana ufalme wa Mungu umekaribia (Mat. 4:17). Kristo akawatuma wanafunzi wake wakahubiri Injili ya toba, akiwapa mamlaka juu ya mapepo au roho chafu (Mk. 6:7,12; Lk.10:1,17-20).                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                     

Toba i11720).u roho chafu (Mk.wake wakahubiri Injili ua Yohana katika mwaka wa kuminatano                                           lifundishwa kama ni kitu cha lazima katika kufutiwa dhambi (au madhaifu) (Matendo 8:22) ili kwamba wakati wa kujiburudisha awe akitokea kwenye uwepo wa Bwana, ili kwamba amtume Kristo aliye mchagua kwaajili yetu (soma pia Matendo 15:3).

Kanisa la Efeso waliambiwa watubu na kukumbuka pale walipoanguka, na kufanya kazi walizo fanya hapo mwanzo (Ufu. 2:5). Vilevile Kanisa la Pergamo liliambiwa litubu  (Ufu. 2:16). Vilevile kama ilivyo kuwa Kanisa la Thiatira (Ufu. 2:21-22) ambalo mwana wa ukengeufu alitupwa juu ya kitanda chake na waalimu wa dini za uwongo. Kanisa la Sardi vilevile liliambiwa watubu vinginevyo Kristo angekuja kama vile mwivi ajavyo usiku na wao wasingeijua saa ya kuja kwake (Ufu. 3:19). Toba ndicho kitu kinachotiliwa mkazo kwa Makanisa yote ya Mungu, kama ni wajibu wa kwanza kabisa wa wote (Yak. 5:19-20).

2.5  Ubatizo

Mamlaka yote alipewa Kristo ikifuatiwa na ufufuko wake (Mat. 28:18). Aliwaamuru wanafunzi wake waende Ulimwenguni kote wakawafanye Mataifa yote kuwa wanafunzi na Kuwabatiza Katika Jina La Baba Katika Mwili wa Mwana Katika Nguvu za Roho Mtakatifu (Mat. 28:19). Na kuwafundisha kuyashika yote Kristo aliyo waamuru. Na kwamba atakuwa pamoja nao hadi ukamilifu wa dahari (Mat. 28:20).

Toba ni lazima iendane sambamba na Ubatizo vikiambatana na vipawa vya Roho Mtakatifu (Mdo. 2:38). Huwezi kumpokea Roho Mtakatifu hadi utubu na ubatizwe, ambako ni kuzaliwa mara ya pili. Usipo zaliwa mara ya pili huwezi kuuingia ufalme wa Mungu (Yoh. 3:3-5). Toba ni sharti lisiloepukika ili mtu abatizwe na kumpokea Roho Mtakatifu. Ndiyo maana ubatizo wa watoto hauna maana na ni kinyume kabisa cha vile Biblia inavyo sema. Toba yenye masharti ilisisitizwa katika huduma ya Yohana Mbatizaji ambaye alishuhudia mara moja ubatizo wa Roho Mtakatifu kwa Kristo (Mk. 1:4,8). Yohana alisema kuwa Kristo atawabatiza watu kwa Roho Mtakatifu na kwa moto, kuhusu wale wasiotubu (wameelezewa kama makapi) (Lk. 3:16-17), Roho Mtakatifu huwezeshwa kufanya maongozi ya Mungu. Kwa njia ya maombi, huonekana kwa njia ya kuwekewa mikono, Roho Mtakatifu humshukia mtu binafsi yale. Hivyo basi Roho huweza kufanya aina yoyote ya kazi njema. Roho Mtakatifu huanza kufanya kazi hata kabla ya ubatizo akishughulika na mtu binafsi. Roho huwaleta wateule kwa Kristo (Ebr. 7:25). Sehemu ya kwanza ya tunda la Roho atapewa muamini wakati ule wa ubatizo, kama isemavyo Warumi 8:23, ambapo inasema kuwa kufanywa wana hakukamiliki hadi pale ukombozi wa mwili. Hivyo basi, sisi tumezaliwa mara ya pili lakini bado tunaendelea kukua katika roho kila siku katika Kristo Yesu hadi tutakapo ufikilia utukufu wa Mungu.

Hali hii ya utendaji kazi wa Roho Mtakatifu wakati wa ubatizo ni maji ya kisima cha wokovu kama ilivyoahidiwa na Mungu kupitia manabii wake (Isa. 12:3). Maji haya ya Roho Mtakatifu ni ahadi ya Mungu kwa Yakobo kama ilivyoandikwa katika Isaya 44:3. Bwana Mungu ndiye chemichemi ya maji ya uzima (Yer. 2:13, 17:13; vilevile Zek.14:8) Huu ndio mto wa maji ya uzima (Ufu. 22:1). Kristo anaongelea kwa habari ya Roho (Yoh. 7:39), alisema kutoka kwake maji yaliyo hai hutiririka (Yoh. 4:10-14; 7:38 cf. Isa.21:3; 55:1; 58:11; Eze. 47:1) Israeli wamesafishwa kiroho katika maji kulingana na andiko la Ezekieli 36:25,  ambaye ni maji ya uzima au Roho Mtakatifu. Wateule huchota maji haya bila kulipa kitu (Ufu. 22:17).

 

Sura ya 3

Mafundisho Kuhusu Majukumu ya Mwanadamu

3.1  Maombi na Kuabudu

3.1.1 Mungu ipasavyo kuwa ni mlengwa katika Kusifiwa na Kuabudiwa

3.1.1.1 Lengo la Kuabudu

Sehemu ya kwanza na kanuni inayo ashiria kwa mteule ni kwa wakati wote awe ni imani juu ya Mungu mmoja tu, imani ambayo chanzo chake ni mahusiano na Yesu Kristo. Tusiabudu Elohim mwingine zaidi ya Mungu (Kut. 34:14; Kum.11:16) vinginevyo tutaangamia (Kum 30:17-18). Mungu alitoa amri ya kwanza ikisema:

Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya Utumwa. Usiwe na Miungu (elohim) mingine ila mimi. (Kut. 20:2-3)

Wazo hapa kusema mbele yangu inamaanisha kuwa sambamba yaani kufanya kitu m’badala au bila mamlaka ya Mungu tunayemulewa kuwa ni Mungu Baba.

Tunapaswa kumpenda Bwana Mungu wetu na kumtumikia kwa mioyo yetu yote na kwa roho zetu zote, yaani kwakuwepo kwetu, ilituweze kupata vyua kwa yake tuweze kupata mazao na malisho kwa mifugo yetu. Kwa maneno mengine ni kwamba tutakula vitu vingi (Kum.11:13-15). Lakini tunalo Agano jipya ambalo Bwana anaweka Sheria zake katika nia zetu na kuziandika mioyoni mwetu. Yeye ndiye Mungu wetu na sisi ni watumishi wake, ili tumuabudu yeye, kwa kuzishika Sheria zake katika hali yetu hii tuliyonayo (Ebr.8:10-13).

Inapaswa kumuabudu Bwana Mungu wetu (Kum. 26:10; 1Sam.1:3; 15:25). Mungu huyu ni Mungu mmoja ambaye ni wapekee wa kweli ambaye ni Mungu Baba. Sharti la kuupate uzima wa milele ni kwamba, lazima tumjue yeye (Mungu) na Mwanae Yesu Kristo (Yoh.17:3). Tunampatia Bwana, utukufu wa Jina lake; tunamuabudu Bwana kwa uzuri na utakatifu (Zab. 29:2; 96:9). Dunia yote inamuabudu yeye na humwimbia nyimbo za sifa kulisifu Jina lake (Zab. 66:4). Huu ni unabii na utakuja timilika. Mataifa yote aliyoyafanya yatakuja kumsujudia, kwa kutetemeka mbele zake (Zab. 96:9), yakilitukuza Jina lake, kwakuwa yeye peke yake ndiye Mungu (Zab. 86:9-10), Bwana Muumbaji wetu. Yeye ndiye Mungu wetu sisi ni kondoo wa malisho yake (Zab. 99:5,9). Yeye ni Mtakatifu (Zab. 99:5,9). Kuelewa ni nani tunaye muabudu vilevile kumeonyeshwa katika ishara kuu mbili ambazo kwa pamoja na kuelewa asili ya Mungu kunako fanyiza kuwekwa muhuri kwa wateule. Alama hizo mbili ni:

1. Sabato (soma Kutoka 20:8,10-11; Kum. 5:12). Sabato ni ishara kati yetu na Mungu atutakasaye (Kut. 31:12-14); na

2. Pasaka. Pasaka ni ishara au muhuri ambapo katika Kutoka 13:9,16, Pasaka inajumlishwa na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, ni ishara ya sheria ya sheria ya Bwana (Kum.6:8) na alivyo wakomboa Israeli (Kum. 6:10) ambayo katika Agano Jipya, inamaanisha ni kwa wote walio ndani ya Kristo (Rum.9:6; 11:25-26).

Ishara hizi za sheria, Sabato na Pasaka, viliwekwa kwa makusudi kabisa ili kuwalinda na ibada za sanamu (Kum.11:16). Ishara hizi mbili ni muhuri waliogongwa wateule katika mikono yao na vipaji vya nyuso zao, na kwa Roho Mtakatifu, itakuwa ndio msingi katika kuwatia muhuri kwa wale watakatifu 140,000 wa siku za mwisho walioandikwa katika Ufunuo 7:3. Zinatuongoza kuelekea katika Siku takatifu za mwisho.

Kristo alisema: Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake (au kumtumikia)  (Mat. 4:10; Lk.4:8). Vivyo basi kumtumikia ni kuabudu katika lugha ya Kibiblia.

Kumwabudu Mungu kwa nia ya kuonekana na watu ni ibada isiyo na maana (Mat. 15:8-9). Kwakuwa Baba hupendezwa watu wamwabudu katika roho na kweli (Yoh. 4:21-24). Kwakuwa sisi tu tohara ya kweli tumwabuduo Mungu katika roho na ukufu katika Kristo Yesu (Flp. 3:3). Baraza lote la wazee, pamoja na Kristo, humwabudu Mungu aliye viumba vitu vyote na ambaye kwa yeye vilifanyika na huishi (Ufu. 4:10). Kwa amri ya Kristo, kwa njia yoyote kati ya mbili hizi yaani kwa sheria (Kut. 20:3) na kwa ufunuo, tunamwabudu Mungu (Ufu. 22:9).

3.1.1.2  Mlengwa katika Maombi

Mwanadamu hupaswa kumwomba Bwana Mungu (Zab.3 9:12; 54:2) ambaye anasikia. Lolote uliombalo katika maombi utpokea kama ukiwa na imani (Mat. 21:22). Mfano wa jinsi ya kuomba unapatikana katika Sala ya Bwana ambayo ni muongozo au mfano wa jinsi ya kuomba uliotolewa na Kristo (Lk.11:2-4).

Mhimili wa kwanza kabisa wa mteule au huduma ni maombi na huduma au kuhudumia neon (Mdo.6:4). Baraza la wazee limepewa wajibu wa kuratibu mkakati wa maombi wa watakatifu (Ufu. 5:8).

3.1.1.3  Maombi ya Binafsi na ya pamoja Kuwaombea Wengine

Maombi ya pamoja kwa moyo mmoja ni mfano kama walivyofanya mitume (Mdo. 1:14). Hii hufanyika kwa ushiriki wa kanisa lote (Mdo. 12:5).

Maombi sio kwa ajili ya Kanisa tu; bali pia ni kwa wale wenye bidii lakini hawajatiwa nuru na kujitia chini ya haki ya Mungu. Kwakuwa Kristo ndio mwisho (au mlengwa) wa sheria ambaye kila amwaminiye ahesabiwe haki (Rum 10:1-4).

Maombi huleta msaada. Mibaraka inayotokana na majibu ya maombi mengi, inafaa ishukuriwe pia kwa maombi mengi ya shukurani (2Kor. 1:11). Maombi lazima yawe katika roho (Efe.6:18). Lazima yawe maombi ya uvumilivu (Kol.4:2-4). Na hii ni silaha yenye kuwezesha kusimama imara katika kweli na utakatifu (Efe. 6:14).

Maombi ya mwenye haki yana nguvu katika kutenda kazi. Maombi yatokanayo na imani yanaweza kuponya mgonjwa na hutoa hakika ya msamaha wa dhambi. Kwahiyo tunaungamiana dhambi zetu sisi kwa sisi na kuombeana ili tupate kuponywa (Yak. 5:15-16).

3.2  Uhusiano kati ya Wokovu na Sheria

3.2.1 Mungu ndiye Mwamba Wetu

Mungu ndiye Mwamba wetu, nguvu zetu na wokovu wetu ambaye kwa yeye tunapata kimbilio letu (Zab.18:1-2). Kunamwamini yeye na hatuogopi (Isa. 12:2). Ufahamu kuhusu wokovu ni kazi ya Kristo na manabii (Lk. 1:77). Ufahamu huu limepewa Kanisa ambako watakatifu ni watumishi wa siri za Mungu (1Kor. 4:1). Wokovu unatoka kwa Wayahudi (4:22). Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine lolote chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokoleawa kwalo  (Mdo. 4:12). Hivyo basi wokovu hupatikana kupitia Injili, kama ni uweza wa Mungu uletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia. Kwa njia ya Injili, haki ya Mungu inadhihirishwa kwa imani kwakuwa mwenye haki ataishi kwa imani (Rum.1:14-17). Mungu hakumkusudia mwanadamu akutane ha hasira, bali apate wokovu kupitia Yesu Kristo (1The. 5:9).

Kumwelewa Mungu husababisha mtu kujisikia sononeko la kimungu, ambayo huleta toka liletalo ondoleo la dhambi (2Kor. 7:10). Vivyo basi, Injili ni neno la kweli na ni pia ni Injili ya wokovu ambayo humfanya kila anayetubu apingwe muhuri na Roho Mtakatifu (Efe.1:13). Wokovu hupatikana kwa kuyaamini maandiko matakatifu. Kwa kuvuviwa na Mungu, Maandiko yaweza kumwelekeza mfanya toba kwenye wokovu kwa njia ya imani katika Yesu Kristo (2Tim. 3:15-16). Na, ingawa ni Mwana, alijifunza kutii kwa mateso yaliyo mpata; naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii; (Ebr. 5:8-9).

Kwahiyo alitolewa mara moja tu ili azichukue dhambi na atakuja tena mara ya pili, sio kuja kuchukua dhambi ila kuja kuwaokoa wale wote ambao walikuwa wanamngea kwa uaminifu na hamu (Ebr. 9:28). Kwahiyo Wokovu ni muhimu kwa wote na umetolewa mara moja tu kwa watakatifu (Yuda 3). Hivyo basi, hakuna tena ufunuo wa aina yoyote mpya ambao alipewa Yesu Kristo na Mungu na akampa Mtume Yohana. Chochote kile kinacho husu wokovu wa mwanadamu kimeandikwa katika Biblia. Wokovu, nguvu na utukufu ni vya Mungu na ame wafunulia watumishi wake kupitia Kristo na inatakiwa kushikilia visibadilike (Ufu.22:18-19).

Kutiwa muhuri kwa mara ya mwisho kwa watakatifu ni kupitia Roho Mtakatifu sawasawa na sheria za Mungu kama zilivyo funuliwa katika Biblia katika Agano la Kale vikithibitishwa na sheria.

Kristo alitoa sheria pale Sinai kama Malaika wa Agano au Uwepo wa Malaika wa Yahweh. Alisema kwamba:

…Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati havitaondoka, hata yote yatimie. Basi mtu yeyote atakaye vyunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni. (Mat. 5:18-19).          

Ndiyo maana Kristo kwa namna yoyote ile hakuvunja sheria. Alizishika sheria na aliwaamuru watu kufanya vivyohivyo. Torati na manabii vilikuwepo mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema za Ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu (au hujichomeka humo) (Lk.16:16).

Lakini ni vyepesi zaidi mbingu na nchi vitoweke, kuliko itanguke nukta moja ya torati  (Lk. 16:17).

Sheria ilitolewa na kupitia Musa, ila hazikushikwa (Yoh. 7:19). Wale watendao dhambi chini ya sheria, wataangamia chini ya sheria (Rum. 2:12) kwakuwa dhambi ni uasi au ni uvunjaji wa sheria (1Yoh.314). Tohara ni ya moyoni na ushikaji wa misingi ya sheria ni kipimo cha tohara hiyo. Yeye ashikaye sheria amesha pata tohara ya moyoni, na yule aliyetahiriwa kimwili lakini hazishiki sheria ni sawa na mgumu ambaye si mwaminifu. Wale walio Wayahudi ni wale wazishikao sheria tokea mioyoni mwao ni Wayahudi wa kiroho. Hivyo basi, wale wasemao kuwa ni Wayahudi, na kumbe sio, watahukumiwa Ufu.3:9) na watakuja jinyenyekesha kwa watakatifu. (Aina hii ya kunyenyekea inatafsiriwa pia kama kusujudu na itafanya kwa Kristo na watakatifu).

Torati ni takatifu na hizi amri ni takatifu na za haki na ni njema (Rum. 7:12). Kwahiyo, Torati haisababishi mauti lakini ni ile dhambi ambaya tafsiri yake ni uvunjaji wa sheria, inayofanya kazi ndani ya moyo wa mtu (Rum. 7:13).

Torati ni ya kiroho lakini mwanadamu ndio aliye ni wa kimwili, aliye uzwa katika utumwa wa dhambi (Rum.7:14). Mwongofu wa kweli ni lazima ataifurahia sheria ya Mungu moyoni mwake (Zab.119:1ff.; Rum.7:22). Kwakuwa sheria huwaongoza watu kaw Kristo ambaye ndiye mwisho wa sheria (Rum. 10:4). Kuongozwa na Roho humuweka mtu huru na sheria (Gal. 5:18). Siyo kuwa Roho huiondoa ile sheria, la hasha bali hutuwezesha kishika ile sheria kirahisi toka moyoni na kwa matendo mema katika asili yetu (Ebr. 8:10-13). Sheria za Mungu hufuatwa kwa njia ya imani na sio kwa kazi au matendo (Rum. 9:32). Kuzitii sheria ni kitu muhium katika kumpendeza Roho Mtakatifu akaaye ndani yao wazishikao Amri za Mungu (1Yoh.3:24; Mdo.5:32). Kwahiyo, haiwezekani kuwa Mkristo na kumpenda na Kristo bila kushika sheria za Torati. Hii ni muhimu, ikijumlisha na ushikaji wa Sabato kama ni amri ya nne.

3.2.2  Wokovu Kwa Neema

Maana neema ya Mungu iwaokowayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tama za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa; tukilitazama tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu; (Tit. 2:11-13, soma Biblia iitwayo Marshall’s RSV Interlinear Greek-English New Testament). Kwahiyo Kristo ni mwonekano wa utukufu wa Mungu Mkuu ambaye ni Mwokozi wetu (Tit. 2:10). Kwahiyo, neema ni matokeo ya kazi ya Yesu Kristo.

Kanisa linalindwa kwa nguvu za Mungu kwa njia ya imani kwa wokovu utakao funuliwa katika siku za mwisho (1Pet. 1:5). Matokeo ya imani ni wokovu wa roho. Manabii walitabiri kuhusu wokovu lakini hawakujua majira wala mtu huyu Masihi wakati wakitabiri mateso yake na ukuu wa ukufu wake (1Pet.1:9-10).

Dhambi ziliingia duniani kupitia Adamu na zilitawala kuanzia Adamu hadi Musa. Mauti ilikuwa ndio matokeo ya dhambi (Rum. 5:12). Dhambi ilikuwepo kabla Torati haijatolewa kwa Musa (Rum.5:13). Kwahiyo, matokeo ya Torati yalikwisha fahamika tayari tokea Adamu, kuwa dhambi hazihesabiwi pasipo sheria. Kwahiyo, neema imetolewa kwa wingi kwa sababu ya kumkomboa mwanadamu na dhambi na sheria. Wakati dhambi zilivyokuwa nyingi, chini ya sheria, neema ilikuwa nyingi (Rum. 5:15-21). Kwa kutii kwake mtu mmoja wengi wamewezeshwa kupata haki kwa neema itokanayo na haki hadi uzima wa milele katika Yesu mpakwa mafuta. (Rum. 5:20-21). Sasa basi, hakuna hukumu ya dhambi juu yao walio katika Kristo Yesu (Rum. 8:1). Kwahiyo, sheria imetimilika kwetu sisi tunao enenda katika Roho (Rum. 8:4).

Roho huongoza nia zetu ili ziyafanye mapenzi yake (Rum. 8:5). Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu wala haiwezi kuitii (Rum. 8:7). Hivyo basi, mawazo ya kimwili au ya mtu asiye ongoka hujulikana pale yanapo shindana katika kukubaliana na kuzishika sheria za Mungu.

Lakini, ikiwa Roho wake yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu (Rum. 8:11). Kwakuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu (Rum. 8:14) nah ii ni kwa neema ya Mungu. Kwakuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo (Yoh. 1:17). Kwahiyo twalia Aba, yaani Baba, kuendeleza hali hii ya uwana (Rum. 8:15) kama ilivyotolewa kwa kaka yetu Yesu Kristo.

Torati yenywe peke yake haitoi haki. Mtu huhesabiwa haki kwa njia ya imani katika Yesu Kristo (Gal. 2:16). Maisha wanayoishi ni kwa imani kupitia Mwana wa Mungu (Gal. 2:20). Maana mimi kwa njia ya sheria nalifia sheria ili nimwishie Mungu (Gal. 2:19). Siibatili neema ya Mungu; maana, ikiwa haki hupatikana kwa njia ya sheria, basi Kristo alikufa bure (Gal. 2:21). Tunashika sheria kwasababu Roho hutuongoza na sheria hutangulia mbele ya ili asili ya Mungu ambayo ambayo tumewekwa ndani yake na sisi tukiwa ni warithi (2Pet. 1:4) kama ilivyo kwa Kristo.

Tumeokolewa sio kwa sheria bali ni kwa neema ya Yesu Kristo (Mdo.15:11).  Dhambi haziwatawali wateule kwasababu hawapo chini ya sheria bali chini ya neema na wamejitia chini ya haki ya Mungu (Rum.6:14-15). Walakini, hatufanyi dhambi kwa kuvunja sheria kwa sababu sisi ni watumwa wa Mungu na haki na sio watumwa wa dhambi, tukitii kutoka mioyoni mwetu sawa na kiwango cha mafundisho ambayo tumejitoa kwayo (Rum. 6:17-18). Hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, mmeokolewa kwa neema (Efe. 2:5). Ametufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu waroho, katika Kristo Yesu; ili katika zamani zinazo kuja audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasi kwa neema yake kwetu sisi katika Kristo Yesu (Efe.2:6-7). Wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu (Efe.2:9). Kwahiyo, tunashika sheria kwa Roho wa Mungu kwa neema.

3.2.3  Ulazima wa kuwa Chini ya Sheria

Kuna ulazima usio na mwisho wa kuishika sheria, wa kudumu milele kama ilivyoandikwa (Mat. 3:18; Lk.16:17). Haikuwa inashikwa sawasawa na Wayahudi wakati ule wa Kristo (Yoh.7:19), ilikuwa imechanganywa na mapokeo (Mat.15:2-3,6; Mk.7:3,5,8-9,13). Waalimu wa Kiyahudi wa zama zile waliwatwisha mizigo na kongwa ikawafikisha mahali pa kumjaribu Mungu (Mdo.15:10).Kuna amri au agizo kutoka juu ya kushika amri za Mungu. Zinadumu na kamwe hazitapita mpaka ukamilifu wa dahari wa kuwepo kwa mwanadamu.

3.2.3.1 Kwanini Wakristo Washike Sheria

Wakristo wameokolewa kwa neema na sio kwa sheria. Kwa nini basi ionakane kuwa ni muhimu kushika sheria? Ni kulingana na sababu zifuatazo:

Sheria za Mungu ziliwekwa kulingana na asili ya wema wake.

Sheria za Mungu inatokana na asili yake Mungu na hivyo basi inasimama milele kwakuwa Mungu mwenyewe habadiliki, akiwa ni mwema sana akiwa ni kituo cha wema na upedo. Katika Marko 10:18, Kristo alisema: kwanini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu au kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. Lakini ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri (Mat.19:17). Asili ya Mungu ni wema usio badilika. Jeshi la mbinguni limerithi asili yake hii ya kimbinguni. Wanafanyika wakati wote kuwa katika asili hii ya kimbinguni ambayo ni ya wema.

Kwa jinsi hiyo, Kristo ni yeye yule habadiliki jana, leo na katika zama zote (aioonas) (Ebr.13:8). Wateule, katika kurithi kuhu asili ya kimbinguni (Pet. 1:4), hufanyika kuwa ni sehemu ya ukuhani wa kimbinguni, ule wa Melkizedeki ambao hudumu milele na haubadiliki (oparabaton) au haubadiliki kizazi hadi kizazi (aioona) (Ebr. 7:24). Kristo aweza kuwaokoa wote wamnjiao Mungu kupitia yeye (soma, Ebr. 7:25 katika Marshall’s Greek-English Interlinear) Lakini yeye sio mlengwa katika kuabudu wala Mungu hajaamuru kufanyika jambo namna hiyo kuwa ni mapenzi yake.

Sheria ya Mungu ni ya kuifuata kwa imani na sio kwa kazi (Rum. 9:32). Tunalo Agano Jipya ambalo Bwana ameweka sheria zake ndani ya mawazo yetu na kuziandika mioyoni mwetu. Yeye ni Mungu nasi ni watumishi wake, tumuabuduye kwa kuzishika sheria zake katika hali yetu ya asili (Ebr. 8:10-13). Kwahiyo, hakuna ishara nyingine ya nje ila ni kwa kuzishika amri za Mungu kati yetu ambazo ndio tohara yetu (1Kor. 7:19) kama Wakristo na washirika wa Israeli ya kiroho. Ni wale wanao mkasirisha joka kwa kuzishika amri za Mungu. Ushikaji wa amri za Mungu huwatambulisha katika kipindi cha mateso (Ufu.12:17). Hawa ndio watakatifu wazishikao amri za Mungu na subira (Ufu. 14:12).

 

3.2.3.2  Wakristo kama Hekalu la Mungu

 

Watakatifu ni Hekalu au Sinagogi naos, la Mungu na Roho wa Mungu anakaa ndani yake. Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana Hekalu la Mungu ni takatifu ambalo ndilo ninyi (1Kor.31617). Kwa ajili hiyo kuna ulazima kwa Wakristo kutunza miili yao kiafya kama apendavyo Roho wa Mungu kwakuwa Mungu alisema yeye atakaa ndani yetu na kutembea pamoja nasinaye atakuwa Mungu wetu. Tunapaswa kuishi katika utakatifu na kujitenga na mambo ya ulimwengu huu. Mungu awe ni Baba yetu na sisi tuwe watoto wake (2Kor. 6:16-18 sehemu nyingi imenuu aya za Agano la Kale, Walawi 26:12; Eze.37:27; Isa.52:11; 2Sam.7:14).

 

Kwa ajili hiyo, Wakristo wanatakiwa wasifungiwe nira pamoja na wasioamini kwa jinsi isivyo sawasawa (2Kor. 6:14). Yawapasa kajitakasa na kila aina ya unajisi wa mwili na roho, ili kutunza kikamilifu utakatifu katika kicho cha Mungu (2Kor.7:1). Kwahiyo wamechaguliwa tangia mwanzo na kuokolewa kwa njia ya utakaso na Roho kwa kuiamini kweli (2The. 2:14). Kuiamini kweli ni muhimu katika kupata afya ya akili na ni alama kwa wateule. Inaonekana wazi kuwa Biblia na amri zilizoko ndani yake zina umuhimu na malengo katika maisha. Upimaji wa Hekalu la Mungu hufanyika kupitia sheria hizi (Ufu.11:1).

 

3.2.4  Amri Kumi Za Mungu

 

Kanisa linatakiwa kuzishika amri kumi za Mungu kama zilivyo elekezwa katika Kutoka 20:1-17 na Kumbukumbu la Torati 5:6-21.

 

Amri ya kwanza inasema:

Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. Usiwe na miungu mingine ila mimi.

 

Mungu Baba ni Mungu wa pekee wa kweli (Yoh.17:3) na hakuna elohim mwingine kuwepo kabla yake, au aliye sawa naye. Kwakweli hairuhusiwi kukiabidu au kuonba kiumbe kingine chochote akiwemo Yesu Kristo.

 

Amri ya Pili inasema:

                                                          

Usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia; kwakuwa mimi, BWANA, Mungu waku ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.

 

Kwahiyo basi, tunaona kwamba hairuhusiwi kujifanyia sanamu ya kuchonga au mfano wa kitu wa kitu chochote kwa matumizi yoyote yale, iwe ni ibada za kidini au kwa ajiliya nembo ya kidini. Hii inamaanisha pia kuwa hata msalaba ni miongoni mwa vitu vilivyo katazwa kutumiwa kama nembo ya Kanisa.

 

Hizi amri zenyewe tu zinaunda utambulisho wa mfumo wa kidini na zote zinazungushiwa hivyo.

 

Amri ya Tatu inasema:

Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.

 

Jina la Bwana Mungu lina mamlaka na kwahiyo amri hii sio tu kuwa inashughulika na namna tu ya makufuru, bali inafikia hata kwenye hatua ya kuhusikana na matimizi mabaya ya mamlaka ya Kanisa na wale wote wanaoenenda vibaya tofauti na maelekezo ya Mungu kupitia Yesu Kristo.

 

Amri ya Nne inasema:

Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana kwa siku sita BWANA alifanya mbingu na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwahiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.

 

Sabato ya kila siku ya saba ya juma, ni ya muhimu sana kwa wokovu na imani yetu. Hakuna Mkristo anayedai kuwa anamuishia Mungu na huku akishindwa na kudharau kuishika Sabato, ambayo kwa kalenda za leo inaangukia siku ya Jumamosi. Tendo la kuanzilisha siku nyingine na kuifanya kuwa ni ya ibada tofauti na ile ya siku ya saba ya juma sio tu kuwa inaitia unajisi bali inakuwa ni miongoni ya ibada ya sanamu ambayo ni chukizo na ni kuyaasi mapenzi ya Mungu. Ni tendo la uasi ambao umefananishwa na dhambi ya uchawi (1Sam.15:23). Ikiunganishwa na amri ya pili ambayo inaongelea kuhusu kumuabudu Mungu peke yake hivyo kukiuka amri ya nne ni ibada ya sanamu. Tendo la kutunga kalenda nyingine ambayo inaiyumbisha kalenda halisi ya wiki kwa kuongeza siku moja mbele katika mzunguko halisi kuna endeleza maana ileile.

 

Amri hizi nne za mwanzo zinahusu mahusiano kati ya mwanadamu na Mungu na zinajulikana kama ni kundi la amri ya kwanza iliyo kuu isemayo kuwa: Nawe pende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, (na kwa nguvu zako zote Mk 12:30). Hii ndio amri iliyokuu tena ni ya kwanza (Mat. 22:37-38).

 

Njia pekee ya kujionyesha kuwa mtu kuwa anamjua na kumtii Mungu ni kwa kuzishika hizi amri, na kuangalia kutozivunja.

Amri kuu ya pili ni:

Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi      (Mat.22:39; Mk.12:31).

Amri kuu ya pili inahusu uhusiano uliotajwa katika amri zile sita za mwisho kati ya kumi ambazo zinahusu mahusiano kati ya wanadamu.

Amri ya tano inasema:

Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.

Uhusiano katika familia ni tofali la muhimu katika ujenzi wa msingi katika jamii na inaashiria msimamo wa kimaadili wa jinsi dini ilivyo mahali popote pale duniani.

Amri ya Sita inasema:

Usiue

Hukumu imewekwa juu ya Wakristo wenye kuvunja amri inayosema usimuonee hasira ndugu yako. Kuwaka hasira ni kufanya fujo au kugombana na jirani yako. Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanam ya moto (au kaburi au kuzimu) (Mat.5:22)

Amri ya Saba inasema:

Usizini

Hukumu imewekwa juu ya Wakristo wenye kuvunja amri inayosema usiwakiane tamaa na mtu mwingine ambaye sio mwenzi wako wa ndoa (Mat.5:28).

Amri ya Nane inasema:

Usiibe

Kuiba ni kutenda kosa kwa jirani yako, jambo linalo pelekea wewe kujunja uhusiano wako na Mungu.

Amri ya Tisa inasema:

Usimshuhudie jirani yako uongo

Utakatifu na haki ni maneno kwakweli yaliyochua maana moja tu katika lugha ya Kiebrania. Inamaana kuwa Kristo hawezi kuwa mtakatifu bila kuwa ni mtu wa haki. Hali ya kugeuza haki kwa kutoa ushahidi wa uongo kunaathirivi maisha ya wokovu wa Mkristo.

Amri ya Kumi inasema:

Usitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala chochote alichonacho jirani yako.

Tamaa ni hatua inayo wapelekea watu hatimaye kuiba vitu au kufanya mahusiano ya kiuasherati na kuathiri uhusiano na Mungu. Kwa minjiri hii hii inakuwa ni ibada ya sanamu. Inafanya kiwepo kitu kingine cha kukilenga katika kutimiliza haja zako huku ikienda kinyume na zile amri nyingine. Kwa mtazamo huu utaona kuwa amri hizi zinaenda kwa mzunguko unao tegemeana na hivyo uhusiano wa tamaa unakuwa ni chanzo cha kuvunja zile nyingine, na hivyo uvunjaji wa amri moja tu kati ya hizi, humaanisha kuwa umevunja nyingine zote pia. Kwahiyo hakuna ruhusa yoyote kuhusisha na dhambi. Dhambi ni uasi au uvunjaji wa sheria. Kristo alifundisha jinsi unavyoweza kufahamu sheria kiukweli katika Mathayo 5:21-48; zikihusiana na Kutoka 20:13; Kumbukumbu la Torati 5:17, 16:18 na vilevile Luka 12:57-59.

Amri hizi zinapaswa wazazi wawafundishwe watoto wao kwa bidii, kadiri watoto wanavyokua. Yawe dalili juu ya mikono na kama utepe ktikati ya macho yako (kwa nadharia na matendo) na yaandikwe juu ya miimo ya nyumba (Kum.6:7-9).

 

3.2.5  Sheria nyingine zitawalazo Mwenendo wa Mwanadamu

3.2.5.1  Shera ya Vyakula

Sheria ya vyakula inapatikana katika Walawi 11:1-47 na Kumbukumbu la Torati 14:4-21. Zinamahusiano na mfumo wa kiafya katika mwili wa mwanadamu, katika kuufanya uwe ni mahali pa kuaminika kiafya na zinauthibitisho wenye uwiano na kanuni za muhimu kimaumbile ya mwili. Amri ilikuwa ni kuwa mtakatifu na mwenye mwili wenye afya bore kumwezesha Roho Mtakatifu akae ndani yake. Zina  uwiano na uthibitisho wa kisayansi ndani ya sheria hizi za vyakula. Ulaji wa damu umekatazwa katika Kumbukumbu la Torati 12:16 na pamoja na mafuta yake imekatazwa katika Walawi 3:17. Nyamafu au mnyama aliyeraruliwa pia havikuruhusiwa kuliwa (Eze.44:31). Sheria hizi zina maongozi ya kiroho.

3.2.8.5.2  Sabato

Sabato ya Siku ya saba ya juma inapaswa kuitunza na kuiadhimisha (kulingana na Kutoka 20:8-11; Kum.5:12-15) kama inavyoelezewa kuwa ni amri ya kila mara ya Bwana na ni mojawapo kati ya amri kumi za Mungu. Amri hizi ni za milele kwa kila mtu na hazitzkiwi kuvunjwa. Sabato ni takatifu. Kila anayeitia unajisi Sabato atauawa na kukatiliwa mbali na watu wake (Kut.31:14-15). Ni agano la milele kati ya wana wa Israeli na ni ishara ya milele kati yao na Mungu, wakikumbuka kuwa yeye ndiye muumbaji (Kut.31:15-16). Wakristo wote ni Waisraeli wa kiroho na Wamataifa wote wanatakiwa waje katika taifa hili la Israeli. Kwahiyo, Sabato ni ishara kati ya Mungu na watu wake kwa wakati wote. Hukumu kwa ajili ya kuitia unajisi ni kifo ni sawa na ile ya kumkufuru Roho Mtakatifu ambayo itatolewa wakati ule wa ufufuo wa pili (soma Ufu.20:5). Sabato ni ya lazima na inatakiwa kuiheshimu kama Siku Takatifu ya Bwana. Isifanywe kuwa ni siku ya pumziko la kivivu bali ni la kufanya kutaniko takatifu (Isa.58:13-14). Kazi na isifanywe wala mizigo isibebwe katika siku hiyo (Yer.17:21-22).

Bwana wetu alizitunza Sabato katika siku zake (Mk.6:2). Kadhalika Mitume walizitunza Sabato (na Siku Takatifu) nasi ni lazima tuzishike Sabato. Bwana atazianzisha tena sheria za Sabato, Siku za Mwezi Mpya na Siku Takatifu kwa nguvu wakati wa utawala wa Milenia katika siku za mwisho za utawala wa Masihi, akiyahukumu mataifa ambayo walipinga na kudharau (Isa.66:22-23; Zek.14:16-19).  

3.2.5.3 Mwandamo Wa Mwezi

Kila mwandamo wa Mwezi Mpya yapaswa kuuadhimisha na kuutunza kulingana na sheria (Hes.10:10, 28:11-15; 1Nya.23:31; 2Nya.2:4, 8:13, 31:3). Shughuli za biashara zote husimama kama ilivyo ka siku ya Sabato (Amosi 8 ;5). Israeli waliishika sikukuu za Miandamo ya Mwezi Mpya (Isa.1:13-14; Ezra 3:5; Neh.10:23; Zab.81:3; Hos.2:11), kama lilivyofanya Kanisa kwa Karne mbalimbali. Kanisa lilishika siku za Mwezi Mpya na Sabato na Siku Takatifu (Kol.2:16). Siku za Mwandamo wa Mwezipia zitaadhimishwa na kutunzwa chini ya Masihi kama zilivyo Sabato (Isa.66:23; Eze.45:17, 46:1, 3,6).

3.2.5.4  Siku Takatifu za Mwaka

Siku Takatifu za Mwaka zinapatikana katika Mambo ya Walawi 23:1-44. Siku hizi Takatifu ni kioo cha mpango wa Mungu wa wokovu. Sikukuu hizo ni hizi:

* Pasaka na Sikukuu ya Mikate isiyotiwa Chachu 

* Pentekoste

* Sikukuu ya Baragumu

* Siku ya Upatanisho

* Sikukuu ya Vibanda au Maskani

* Siku ya Mwisho iliyo Kuu

Siku hizi ni za lazima na zinachukua umuhimu ulio wazi kabisa kama ishara kati ya Mungu na watu wake. Siku hizi Takatifu huadhimishwa kama Sabato.

3.2.5.5  Ndoa

Ndoa ni taasisi takatifu. Ni mfano wa muungano wa Kristo na kanisa chini ya Mungu (Ufu.19:7,9). Mfano huu umeelezewa katika Mathayo22:2-14. Ni taasisi inayoendelea na Kristo (Mat.25:10) inayo tegemea utayari wa kiroho. Kuanzia wakati wa mwisho wa upatanisho, hakutahitajika tena kuoana. Ndoa aliwekewa mwanadamu na sio taasisi ya Malaika (Mat.22:30). Kwahiyo, watu watakao fufuka kutoka kwa wafu hawatahitaji kuoa wala kuolewa (Mk.12:25). Hii ni wakati ule watakapo hesabiwa wanastahili kuingia katika ulimwengu ujao kwa njia ya ufufuo. Watafanana na malaika nao ni wana wa Mungu (Lk.20:34-36).

Kwahiyo, ndoa ni taasisi aliyo wekewa mwanadamu na itaishia pale zama hizi za maisha yake aliyoumbiwa itakapo isha. Tangia kuumbwa kwake Adamu, taasisi hii ilianzishwa ili kwamba mwanaume atamuacha baba yake na mama yake na kuambatana na mke wake, nao watakuwa mwili mmoja (Mwa.2:24).

Mke ni mke wa maagano na Bwana anatamani kuona uzao wenye kumcha Mungu ukitokea ndani yake.Bwana Mungu anachukia kuachana, ambayo ni hiyana (Mal.2:16). Talaka iliruhusiwa na Musa lakini Wakristo hawakuruhusiwa kuachana na wenzi wao isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati (Mat.5:31-32). Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe (Mat.19:3-12). Ikitokea mwenzi asiyeamini akakubali kuishi na mwenzi aliyeamini ndoa hiyo iendelee wasiachane (1Kor.7:10-16).

3.2.6  Uwakili wa Mali

3.2.6.1  Kwa ajili ya Mungu

Uwajibikaji kwa ajili ya mali za Mungu unakutikana katika Kumbukumbu la Torati 12:5-19. Ni wajibu wa kila Mkristo kuchangia shughuli za Kanisa. Kanuni yake imeelezewa kuwa zaka ni budi itolewe kwa Mungu kupitia makuhani na walawi walio katika malango ya Israeli (Kum.12:9-14) halafu ni kwa Hekalu. Kodi ya Hekalu ilikuwa inachukuliwa katika siku ya Upatanisho. Michango ilikuwa kama inavyosema Nehemia 10:32. kazi anaendelea hadi wakati wa kuanzishwa utawala wa Milenia wa Masihi (Mal.3:16). Katika Malaki 3:7, Mungu analiamuru taifa limrudie Yeye na kwamba yeye ange warudia pia. Kumrudia huku kunaendana na ufanyaji wa kazi ya Mungu na uchangiaji kazi ile kwa zaka (Mal.3:7). Kutomtolea Mungu zaka kumefananishwa na kumuibia Mungu (Mal.3:8-10).

Utoaji wa zaka katika mahali pale ambapo utaratibu wa kukusanya unafanyika kwa uaminifu, unatoa uhakika kwamba kazi ya Mungu yaweza kusonga mbela na matunda au mavuno ya nchi yana uhakika kukutwa na Mungu arudipo (Mal.3:10-12).

Uwajibikaji wa Kanisa kwa Mungu umeanza siku za mitume ingawa sio kila mara umekuwa unafanyika, au ulikuwa unabadilika na huduma (2Kor.12:13-18). Kristo aliwatuma wazee waende wawili wawili, na ilibidi wategemezwe katika kazini kulekule katika kundi lile ambalo walilihudumia (Lk.10:1-12). Wale wafanyao kazi za Hekaluni na kuihubiri Injili yapaswa wapate riziki zao katika Injili (1Kor.9:13-14). Ni wajibu wa Kanisa kuwategemeza watumishi wake wadumuo katika kuhubiri na kufundisha kwa wakati wote (1Tim.5:17-18; cf, Kum.24:14-15).

3.2.6.2  Kwa ajili ya Wengine

Lakini mtu yeyote asiye watunza watu wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiye amini (1Tim.5:8).

Mkristo haruhusiwi kudhulumu au kuzuia mshahara wa mtu mwingine (Kum.24:15). Wanapaswa kulipa fedha zote wanazo daiwa na Mwaka wa Sabato ukifika wanatakiwa kuasamehe madeni yote wanayo daiana yaani ndugu walio katika imani (Kum.15:1-3).

Utoaji zaka kwaajili ya Sikukuu umeagizwa katika maandiko mengi sana. Fungu la pili la zaka haliruhusiwi kulila ndani ya malango yako lakini mpaka mahali ambapo Bwana amepachagua (Kum.12:17-19).

Katika mwaka wa tatu wa mzunguko wa miaka ya Sabato, zaka itolewayo hutumiwa kwa kusaidia masikini (Kum.14:28, 26:12). Mzunguko huu wa mwaka wa tatu wa Sabato huangukia katika miaka ya 1994-95, 2001-02, 2008-09, 2015-16, 2022-23, 2030-31. mwaka mtakatifu wa 2030-31 ni mwaka wa kwanza wa mwaka wa tatu wa zaka wa mzunguko wa Yubile mpya au Milenia mpya. Hii ni kutokana na mzunguko wa Yubile ulioangukia katika miaka ya 27-28, 77-78 kutokana na Ezekieli 1:1. Agizo la zaka ya tatu linaweza kubadilika au kuahirishwa kulingana na jinsi Kanisa lilivyo jengwa au mfumo wa kiulinzi ulivyo katika maeneo hayo.

Mwaka wa Sabato ni mwaka wa kupumzika ardhi, mizabibu na mizeituni ili kwamba masikini waweze kula na watakacho saza wale wanyama wa kondeni Kut.23:10-11). Miaka ya Sabato huangukia katika miaka mitakatifu ya 1998-99, 2005-06, 2012-13, 2019-20, 2026-27 pamoja na miaka ya Yubile inayo angukia mwaka 2027-28.

Amhurumiaye maskini humkopesha Bwana, Naye atamlipa kwa matendo yake mema (Mithali 19:17) na hatapungukiwa na kitu (Mit.28:17), pia atakuwa na hazina yake mbinguni (Mk.10:21). Mungu anaweza kutoa kwa kila kazi njema sio tu kuwapatia mahitaji ya watakatifu bali ili tuweze kumshukuru Mungu (2Kor.9:6-12).

3.2.7  Mambo ya Vita na Uchaguzi

3.2.7.1 Mambo ya Vita

Watakatifu ni makluhani wa Mungu aliye juu sana. Si vema kwa Mkristo yeyote kukatiza uhai wa mtu mwingine kwa sababu yeyote ile (Hes.20:13; Mat.5:38-48; Lk.6:27-36). Kama wanafunzi wa Kristo wangekuwa ni wa dunia hii wangepigana ili wasikabidhiwe kwa mamlaka ya ulimwengu huu (Yoh.18:36). Ingawa wanaishi humu ulimwenguni, hawachukui majukumu ya vita vya ulimwengu huu (2Kor.10:4). Hatahivyo, Wakristo wanatakiwa kuisaidia serikali ya nchi yao na kuliombea utii wa dhati kwaajili ya maendeleo ya nchi yao ili kwamba Mungu awalinde kwa uweza wake.

3.2.7.2  Uchaguzi

Wakristo wanatakiwa kuziheshimu sheria za nchi isipokuwa ni pale tu zinapoonekana kwenda kinyume na sheria za Biblia. Pale inapotakiwa na sheria za nchi kupiga kura, Wkristo washiriki kama haitapingana na kanuni za Biblia. Tendo la kuchagua viongozi kwa njia ya kura, limechuliwa katika Kumbukumbu la Torati 1:9-14 na katika unabii wa siku za mwisho au wa Hosea 1:11. Lakini tendo la kujiingiza katika shughuli na ukerekwtwa wa kisiasa huonekana kama muendelezo wa machafuko.

Sura Ya 4

Mafundisho yamhusuyo Masihi

4.1  Kuhusu Kuwepo kwake tokea mwanzo

Yesu Kristo alikuwepo tangu mwanzo kama mwanadamu katika ulimwengu war oho. Alikuwepo tangia mwanzo wa uumbaji (Yoh.1:1) akiwa ni mzaliwa wa kwanza katika uumbaji (Kol.1:15) na kwa hiyo ni mwanzo wa uumbaji wa Mungu (Ufu.3:14). Yeye ni yule aliye onekana mara kwa mara katika Agano la Kale kama Malaika wa Yahweh, Malaika aliye pamoja nasi, au wa Agano. Alikuwa ni yule Malaika aliye watoa Israeli kutoka Misri na kuwavusha katika Bahari ya Shamu. Alikuwa ni yule Malaika aliyekuweko kwenye mawingu aliyesema na Musa katika Mlima wa Sinai (Mdo.7:35-38). Alikuwa ni El Bethel au El, Mungu au Kuhani Mkuu wa Nyumba ya Mungu (Mwa. 28:17, 21-22, 31:11-13; Ebr.3:1). Kriasto Malaika wa Haelohim (Mwa.31:11-13). Aliteuliwa kama elohim na elohim wake (Zab.45:6-7) ambaye alikuwa Mungu Baba. Alikuwa mwaminifu kwake yeye aliye mweka, kama Musa naye alivyokuwa, katika nyumba yote ya Mungu (Ebr.3:2) lakini kama mtumishi.

Kristo alikuja hapa ulimwenguni ili aishuhudie kweli (Yoh.18:37). Ufalme wake umekaribia kuja duniani. Alikusudiwa kabla ya kuwekwa kwa misingi ya dunia kama ni tendo la uumbaji wa Kimungu (Ufu.13:8).

Wanadamu wasipo kiri na kuamini kuwa Kristo ni Masihi watakufa katika dhambi zao (Yoh.8:24).

Kristo alikufa kwaajili ya dhambi zetu kama yasemavyo maandiko na akazikwa na kufufuka katika siku ya tatu kama yanenavyo maandiko (1Kor.15:3-4), kasha akawatokea kwa watu zaidi ya elfu tano (1Kor.15:5-6). Kristo alikuwa amefufuka tayari kabla ya siku ijulikanayo leo kama Jumapili au siku ya kwanza ya juma (Yoh.20:1; angalia pia nukuu swali Mk.16:9-10, angalia nukuu isemayo mara baada ya kufufuka kwake). Alitabiriwa kuwemo kwa siku tatu kamili usiku na mchana katika moyo wa nchi kawa Ishara ya Yona (Mat.12:39-40; pia ona Lk.24:6-8).

Kristo alisulibiwa (Mat.27:32-50; Mk.15:24-37; Lk.23:33-46; Yoh.19:23-30) kuanzia majira ya saa tatu yaani saa 3 asubuhi (Mk.15:25), hadi saa 9 alasiri (Mk.15:33), siku ya 14 mwezi wa Nisan. Hakuna uthibitisho kuwa alisulibiwa katika msalaba, au juu ya mti mnyofu au mti wenye alama ya T. Hata kama ikiwa vyovyo vile, bado ni makosa kuufanya msalaba kuwa ni nembo ya imani ya Ukristo, kama walivyofanya wapagani wa zamani katika shughuli za kishirikina.

Kristo alisulibiwa na alifufuka (Mk.16:6). Hatimaye alipaa juu kwa Baba yake ambaye pia ni Baba yake na kwa Mungu wake ambaye ni Mungu wetu (Yo.20:11-18). Ameketi katika mkono wa kuume wa Mungu pamoja na malaika, mamlaka na uweza viko juu yake (1Pet.3:22).

Kristo ametoa uweza wa kusamehe na ondoleo la dhambi kwa Kanisa kupitia mitume (Yoh.20:22-23).

4.3 Kurudi kwa Yesu Mara ya Pili

Kristo alikuja kwa mara ya kwanza kufanyika sadaka ya ukombozi wa dhambi. Hakuja mara ile ya kwanza kama Mfalme Masihi nah ii ilieleweka vibaya na wayahudi wa siku zake. Wao walimtegemea mfalme mshindi (Mat.27:11,29,37; Lk.23:2-3, 37-38; Yoh.19:14-16). Hata hivyo, alitambuliwa na wengine kupitia Roho Mtakatifu, kama mfalme wa Israeli (Yoh.1:49, 12:13-15) ili kutimiliza unabii (Zek.9:9).

Yesu atakuja tena kwa uweza, akifuatana na Jeshi la mbinguni (Mat.25:31) kama Mfalme Masihi (Ufu.17:14). Ujio wake utakuwa dhahiri kama umeme wa mawiguni (Mat.24:27). Atatawala kwa mamlaka pamoja na watakatifu walio fufuka (Ufu.20:4).

Atamharibu mwana wa kuasi atakapo kuja (2The.2:8) na kutamalaki mamlaka za ulimwengu. Mwana wa uharibifu (asi) atakuja kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uwongo (2The.2:9). Ukengeufu huu utasimama katika Hekalu la Mungu kwasababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa. Kwahiyo Mungu aliwaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo (2The.2:10-12). Bwana ataharibu mfumo huu wa ukengeufu kwa pumzi ya kinywa chake, na kwa ufunuo wa kuwepo kwake (2The.2:8).

4.4  Utawala wa Milenia wa Kristo 

Kristo ataanzisha utawala katika sayari hii kwa kipindi cha miaka elfu moja pamoja na watakatifu walio fufuliwa (Ufu.20:3-4). Shetani atafungwa kwa kipindi cha miaka elfu moja na kutupwa kuzimuni kuitwako pia tartaroo, yaani ni mahali pa malaika walioanguka au mapepo na majini (2Pet.2:4). Watakatifu wale waliokatwa vichwa kwa ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya  neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu (Ufu.20:5). Huu ndio ufufuo wa jumla wa wote.

Kipindi hiki cha miaka elfu moja, Kristo ataanzisha tena Ufalme wenye kufuata sheria na amri za kibiblia zilizotolewa Sinai. Tukio hili litaanzia tangia pale atakapo tokea na kusimama juu ya Mlima wa Mizeituni (Zek.14:4,6 ff). Mataifa yatajipanga kwa vita kwa ajili ya mji wa Yerusalemu na yata angamizwa (Zek.14:12). Kila mtu atakayesalia wa mataifa yote, watakwea mwaka baada ya mwaka ili kumwabudu mfalme, BWANA wa majeshi, na kuishika sikukuu ya vibanda (Zek.14:16). Sabato, Miandamo ya Mwezi na Siku Takatifu vitakuwa ni lazima na amri itatolewa kutoka Yerusalemu. Mataifa yale ambayo hayatapeleka wajumbe kuwawakilisha kwenda Yerusalemu kuishika Sikukuu ya Vibanda vyua haita nyesha kwao kwa wakati muafaka (Zek.14:16-19).

Katika kipindi hiki cha mwisho wa Milenia, Shetani atafunguliwa atoke kifungoni ili awadanganye mataifa wakaao juu ya dunia yote (Ufu.20:7-8). Watajikusanya tena kwa vita, laniki wataangamizwa kwa moto (Ufu.20:9); hatimaye Shetani ataangamizwa. Kisha ufufuo wa watu wote utachukua nafasi, na kasha Hukumu (Ufu.20:13-15).

 

Sura ya 5

Tatizo la Uovu

5.1 Kuwepo Kwa Maovu Baada Ya Uasi

Shetani alitupwa kutoka mbinguni kwaajili ya dhambi ya uasi ambapo alitaka kujifanya awe sawa au zaidi ya Mungu Baba, ni ibada ya sanamu (au uchawi kana ilivyo elrzewa katika 1Sam.15:23). Shetani alijaribu kujifanya awe sawa na Mungu Aliye Juu sana au Mungu Baba. Kristo kwa namna nyingine hakujaribu kujifanya awe sawa na Mungu alijishusha chini ya mapenzi yake. (Yoh.4:34).

Ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa anamfano wa wanadamu; tena alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam mauti ya msalaba. Kwahiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina…(Fil.2:6).

Hivyo basi Mungu alimtukuza Kristo kupitia utii kwavile hakujikweza kuwa sawa na yeye na hakutaka kumshusha Mungu kama mshiriki mwenza wa sehemu ya tatu ya elohim na bene elohim kama alivyotaka kufanya.

Katika Luka 10:18 Kristo anasema alimuona shetani akianguka kama umeme kutoka mbinguni. Shetani alizoa theluthi moja ya Malaika au Nyota za Mbinguni (Ufu.12:4). Malaika hawa walitupwa pamoja na Shetani chini, hapa  duniani (Ufu.12:9). Anguko hili limefananishwa na anguko lililo andikwa katika Ufunuo 8:10 ambapo malaika wa tatu anaonyesha tena kuanguka kwa Nyota kutoka Mbinguni ikiangukia theluthi moja ya viumbe. Jeshi hili liliharibiwa na uasi. Kusanyiko hili ni Maskani ya Mungu Mbinguni. Uasi ule ulishuhudia theluthi moja kuondolewa na mfumo wa dunia kunena makufuru kinyume chake jina la Mungu na maskani yake nao wakaao mbinguni (Ufu.13:6). Kwahiyo, Mungu hukaa katika maskani ya mbinguni na kwa wateule ambao ni maskani ya Mungu hapa duniani.

5.2  Mafundisho kuhusu kuchaguliwa tangu mwanzo

Ni Mungu kupitia Kristo, kwa njia ya Roho Mtakatifu, anayefunua akili za wateule kuanzia kwa mitume, ili kwamba maandiko yaweze kueleweka (Lk.24:45). Kristo alisema kwa mafumbo ili kwamba wale ambao hawakuchaguliwa na Mungu wasielewe. Wasije wakageuka na kuokoka (Mat.13:10-17) ili kwamba wasije waka hukumiwa. Mungu ni mwenye rehema na hapendi mtu yeyote apotee. Hivyo kwa mpango wake wa kimungu, kila mmoja ameitwa sawasawa na makusudi yake. Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, na wale aliowaita, hao aliwahesabia haki; na wale aliowahesabia haki; nao akawatukuza. Basi tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? (Rum.8:28-31).

5.3 Mahala Waendako Wafu

Wafu huenda kwenyekimya (Zab.115:17) ni kwenye giza (Zab.143:3). Hakuna roho inayoishi milele. Wote wanalo tukio moja (Mhu.9:3). Wafu hawajui chochote (Mhu.9:5)

Baadhi ya wafu waliokufa zamani hawatafufuka (Isa.26:14; soma nukuu za Biblia iitwayo Companion Bible).

Wafu ambao ni watakatifu huitwa waliolala au wale walio lala (ona Mwa.9:24; Yoh.11:11; 1Kor.11:30, 15:6,18,51; 1The.4:13-15; 2Pet.3:4).

5.4 Ufufuo Wa Wafu

Mungu atafanya muujiza wa kuwafufua wafu na wale waliolala watafufuliwa ili waweze kumsifu (Zab.88:10). Upendo wake mkuu utaonyeshwa hata kaburini (Zab.88:11) wakati wafu watakapo fufuliwa. Ayubu alijua kuwa mtetezi wake yu hai (Ayu.19:25) na kwamba hatimaye atasimama juu ya nchi. Baada ya Ayubu kupatwa na maafa, alijua kuwa katika hali ya mwili wake atamuona Mungu ambaye alikuwa upande wake, na kwamba macho yake yangemuona yeye na siye kwa [macho ya] mwingine (Ayu. 19:25-27).

Kristo alifufua wafu ilitujue kuwa yeye ni Masihi (Mat.11:4-5). Lazaro alikuwa ni mmojawapo wa mfano huu wa uweza wake (Yoh.11:11). Wazo hili la ufufuo kama lilivyofanywa na Masihi lilijulikana na mamlaka ya wakati wake (Mat.14:2).

Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, …wakati wa parapanda ya mwisho (1Kor.15:51). Kwahiyo wapendwa watapitia katika vizazi hata vizazi wakilala, lakini siku ya mwisho Masihi atakuja na kuwakuta watakatifu wengine wakiwa hai. Kisha wote watabadilishwa na kuvaa mwili usioharibika wa kiroho (1Kor.15:44ff.). Waliolala watafufuliwa kwanza. Kasha waliohai walioachwa hadi kuja kwake Bwana hawatawatangulia wale waliolala (1The .4:13-15). Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko wa sautu ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kasha sisi tuliohai tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao ili kumlaki Bwana hewani; hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele (1The. 4:16-17).

Kuanzia kipindi hiki cha ufufuo, kipindi cha utawala wa milenia utaanza. Watakatifu watatawala mataifa kwa fimbo ya chuma (Ufu.2:26-27).

Katika ufufuko hakutakuwepo kuoa (Mat.22:30). Watakatifu watafufuliwa wakiwa na mwili mpya kiroho. Kristo alikufa kwaajili yetu ili kwamba tutakapoamka toka usingizini tuishi naye (1The.5:10). Ni muhimu kuelewa kuwa ni watakatifu tu ndio watakao fufuka ufufuo huu wa kwanza. Mneno haya “Wenyehaki” (zedek) na “Haki” katika lugha ya Kiebrania ni neno moja tu. Yanamaanisha kitu kimoja tu. Hivyo basi, hali ya kutotubu mteule akoseapo kutoa haki, humnajisi mteule kiasi cha kumkosesha mteule katika ufufuo huu wa kwanza.

5.5  Hukumu Ya Watenda Dhambi

Mwanadamu ameumbiwa hali ya kutunza na kujifunza na kutenda haki. Mungu hapendi mwenye mwili yeyote apotee bali wafanye toba. (2Pet.3:9).

Kama Mungu akimchukua Roho wake wanadamu wote wataangamia na kurudi kwenye mavumbi (Ayu.34:15) na roho haiishi.

Sio kwamba wanadamu wote watafufuliwa katika ule ufufuo wa kwanza, ambao ni ufufuo ulio heri (Ebr.11:35), wengine watafufuliwa katika ufufuo wa pili ambao utakuwa baada ya utawala wa milenia wa Masihi. Hiki ni kipindi cha hukumu kitachua muda wa miaka miamoja (Isa.65:20). Huu ni ufufuo wa hukumu (Yoh.5:29) ni wakati wa kujisahihisha na kujifunza ili kwamba watu wote waweze kujitayarisha kupokea uzima wa milele. Nano litumikalo kwa hukumu (kriseoos) (linamaanisha ni hukumu kali ya milele katika KJV), inamaanisha ni kitu mtu alicho chagua au kuamua.

Ukweli ni kuhusu kusahihisha makosa na dhana au maamuzi yalitotolewa kutokana na matendo yaliyo tendeka. Inaweza kuwa na maana ya hukumu au maonyo. Hata hivyo, wale ambao hawakupata nafasi ya kumjua Mungu hawataweza kwakweli kuadhibiwa vikali. Waovu waweza ku pata adibisho. Kama hawakutubu katika kipindi hiki cha miaka mia moja kilicho ruhusiwa katika ufufuo wa pili wataruhusiwa kufa na miili yao itaharibiwa kwa kutupwa Jehanamu la moto (imetafsiriwa ziwa la moto) (Mat.5:22,29,30, 10:28, 18:9, 23:15,33; Mk.9:43,45,47; Lk.12:5; Yak.3:6).

Kuna maneno matatu katika Agano Jipya ambayo yametafsiriwa kama kuzmu. Ambayo ni (SGD 86) kuzimu ambayo ni sawa na (SHD 7585) shimo au shimo la kaburi, mahali ambapo miili iliyokufa huhifadhiwa. Aya nyingine mbili ni (SGD 1067) Gehena ambalo kwa Kiebrania chimbuko lake ni Bonde la Hinomu. Hapa palikuwa ni jalala la takataka ambalo maozea na na nyamafu kutoka Yerusalemu vilikuwa vinachomwa moto. Neno ambalo Yesu alilitumia katika lugha ya fumbo kwa maana ya  sehemu ya kutupa mizoga kwa maana zote mwili na roho (Mat.10:28) baada ya hukumu. Sehemu ya tatu ni (SGD 5020) tartaros maana yake ni mahabusu ambako malaika walifungwa baada ya uasi.

Hukumu ya milele (kolasin mateso ya milele) ambayo inaongelewa katika Mathayo 25:46 ni kinyume cha uzima wa milele. Ina maana ya kifo. Dhana ya hukumu kama ya timoria  katika Waebrania 10:29 inatokana na kupatikana na hatia. 2Korintho 2:6 inatumia neno epitimia katima heshima ya uraia. Kwahiyo adhabu ina asili hii ya kuondoa heshima ya uraia.

Kwahiyo hakuna mahali pasemapo kuhusu mateso ya milele kwa wafu. Watakatifu wataitwa katika ufufuo wa kwanza kufanya kazi ya kufundisha katika kipindi cha Milenia ili kwamba mapepo yahukumiwe kulingana na matendo dunia ione kiwango halisi ambacho watakiwekea kipimo. Hawa hawatakufa kwa maana kuwa wanahukumiwa sasa. Watakuwa kwenye kundi la wale waliolala.

Wengine waliosalia ulimwenguni, ambao sio sehemu ya wateule, hawata hukumiwa sasa. Waliosalia wote duniani watafufuka katika ufufuo huu wa pili (Ufu.20:12-13). Hakuna ufufuo mwingine tena wala hukumu zaidi ya ile ya ufufuo wa pili au ufufuo wa jumla wa watu wote. Waliofanya toba watarithi uzima wa milele na watakatifu wa ufufuo wa kwanza na wasiotubu watakufa hakika na miili yao itachomwa moto. Baada ya hayo, kifo, mauti na kuzimu vitaondolewa (Ufu.20:14). Wenye dhambi watakaokuwa hai wakati wa kuja kwake Masihi wataangamizwa (Mal.4:3) na kusubiri ufufuo wa pili.

Ufufuo wa pili ni hukumu iliyotolewa kwa Yuda kwa sababu walimkataa Kristo. Walikuwa ni wana wa ufalme waliotupwa katika giza la nje (Mat.8:12). Watahesabiwa kuwa taifa katika ufufuo wa pili badala ya kuchukua ili asili ya kimbinguni (2Pet.1:4) na ufufuo wa kwanza. Licha ya kufanywa kuwa taifa miongoni mwa wateule (Ufu.7:5), Yuda hawana sehemu katika huu ufufuo wa kwanza. Walioitwa ni wengi bali wateule ni wachache kufanya kazi hii (Mat.22:13-14). Wengi wanamshuhudia Kristo lakini wakiwatenda mabaya wateule wake, au ambao hakujitoa kikamilifu (Mat.25:30) watawekwa katika ufufuo wa pili (Mat.24:51, 25:30) ni wengi wameachwa (Lk.13:26-28) na hata wale walio katika ufufuo wa kwanza, wakwanza atakuwa wa mwisho na wa mwisho atakuwa wa kwanza (Lk.13:30).

 

Sura ya 6

Kanisa

6.1  Kanisa ni Nini au Nani       

Kristo alisema atalijenga Kanisa lake juu ya mwamba ambalo nguvu za kuzimu hazitaweza kulishinda (Mat.16:18). Mungu ndio mwamba huo ambao Kanisa limejengwa juu yake. Kanisa ni mkusanyiko wa watu mmoja mmoja au umoja wa washirika. “Kanisa la Mungu” ni jina ambalo kila kanisa la mahali pamoja ndivyo lilivyoitwa (1Kor.1:2; 2Kor.1:1; na vilevile 1Kor.11:22 kulingana na nukuu za Kanisa la Korintho). Kwa ujumla, yalijulikana kwa namna zote mbili yaani “Kanisa la Mungu” (Mdo.20:28; Gal.1:13; 1Tim.3:5), na “Makanisa ya Mungu” (1Kor.11:16, 1The.2:14; 2The.1:4). 1Korintho 14:33 inaita “Makanisa ya Watakatifu” akimtaja mmoja mmoja waliokuwepo. Makanisa yalikuwa mengi na kila moja lilijitegemeza.

Mtu huitwa na Mungu na hukabidhiwa kwa Kristo (Yoh.17:11-12; Ebr.2:13, 9:15). Bwana huliongeza Kanisa kila siku wale waliokuwa wakiokolewa (Mdo.2:47). Makanisa yaliitwa kwa majina ya maeneo yao (Rum.16:1; 1Kor.1:2; 1The.1:1; 2The.1:1; 1Pet.5:13) na yalikuwa mara nyingi ni madogo madogo au Makanisa ya nyumbani (Rum.16:5,23; 1Kor.16:19; Kol.4:15; Flm1:2). Kristo aliwekwa kuwa kichwa cha mambo yote yahusuyo Kanisa. (Efe.1:22). Mungu hudhihirisha uweza wa kimbinguni na busara yake kwa Kanisa (Efe.3:10). Kristo ndio kichwa cha Kanisa, ambalo ndio mwili wake, na linapaswa kumtii Kristo. Kristo alijitoa nafsi yake kwa ajili ya Kanisa, kama mkuu wa nyumba anavyo angalia nyumba yake (5:23-26). Kanisa linatakiwa lijitoe kwa Kristo pasipo mawaa wala kunyanzi liwe takatifu lisilo na mawaa (Efe.5:27). Kanisa hulishwa na Kristo (Efe.5:29). Kristo kama kichwa cha Kanisa alikuwa ni mzaliwa wa kwanza kutoka  kwa wafu ili kwamba atutangulie. Kwahiyo, Kanisa ni mwili wa Kristo , ni bibi arusi wa Kristo kama kundi katika ufufuo wa kwanza wakati bwana arusi ajapo (Mat.25:1-10; Kol.1:18,24). Kanisa limeundwa kama Kanisa la wazaliwa wa kwanza na majina yao yameandikwa mbinguni (Ebr.12:23). Nyumba ya Mungu ni Kanisa la Mungu aliye hai,ni nguzo na uwanja wa ukweli. Kwahiyo Kanisa la Mungu limejengwa katika msingi wa ukweli (1Tim3:16)

6.2  Kanisa Kama Shirika

Kanisa kama taasisi hai inayo wajibu wa kuhudumia watu wake (1Tim.5:16). Hii ni katika mtazamo wa kusanyiko la pamija.

Kanisa huongozwa na wazee na mashemasi, waliochaguliwa na wapendwa (Mdo.1:22,26, 6:3,5-6, 15:22; 1Kor.16:3; 2Kor.8:19,23), ambao huombea na kupaka mafuta wagonjwa waamini kwa jina la Bwana (Yak.5:14). Roho Mtakatifu ndiye anaowafanya wao kuwa waangalizi wa kundi ambalo ni Kanisa la Mungu (Mdo.20:28). Kanisa linapaswa kuwa na fungamano kubwa lenye nguvu ya dhati (3Yoh.1:9-10). Kazi ya uongozi wa Makanisa hufanywa na mashemasi wakiume na wakike (Rum.16:1), ambao wamethibitishwa na ofisi hii (Flp.1:1; 1Tim.3:8-13). Kanisani kuna aina mbalimbali wa utendaji kazi vikiwemo manabii na waalimu (Mdo.13:1), kisha miujiza, masaidiano, maongozi na aina ya ligha (1Kor.12:28). Ufundishaji katika Kanisa unafanyika katika lugha inayo eleweka au kwa ndimi inayo amriwa na kueleweka pia lazima zifasiriwe kwa walioko (1Kor.14:4-5).

Makanisa yanayo wajibu kusaidia kazi za wanafunzi au wainjilisti waliopewa kuhudumia maeneo makubwa kuliko yale yaliyo katika maeneo mamoja (Mdo.14:23,27, 15:3,4,22, 18:22, 20:17; 1Kor.4:17).

 Kristo alitoa ujumbe maalumu kwa kila Kanisa moja moja akatoa malaika wa kusimamia kila moja ili kuhudumia mfano kama afanyavyo kwa wateule (Ufu.2:1,8,12,18, 3:1,7,14).

 

Kazi za kuhukumu na kupanga zamu kwa mambo ya kila siku yapaswa yafanywe na waumini wa kawaida wa Kanisa, ilikwamba waweze kukua kiuwezo kwa shughuli za utoaji wa hukumu kwa Jeshi (1Kor.6:4).

6.3  Makusudi Na Malengo Ya Kanisa

Lengo la kwanza la Kanisa ni kuihubiri Injili ya Ufalme wa Mungu kama ilivyoagizwa na Yesu Kristo (Mat.4:17, 10:7, 11:1; Mk.1:38-39; 3:14, 16:15; Lk.4:43, 9:60).

Kanisa lapaswa kuhubiri habari njema kwa wanyenyekevu, kuwaganga waliovunjika moyo, kwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao (au walio umizwa) (Isa.61:1). Na  vipofu kupata kuona tena (Lk.4:18). Ni kuponya wagonjwa (Lk.9:2).

Ni kuutangaza mwaka wa Bwana uliokubalika (Lk.4:19) na kushuhudia kuwa ni Kristo aliyewekwa wakfu na Mungu kuwahukumu wazima na wafu (Mdo.10:42).

Kulilisha Kanisa ni jukumu la pili la wazee (Mdo.20:28) ambao huenda kufundisha kila mahali na kila Kanisa (1Kor.4:17). Karama za 1Wakorintho 12:28 zilitolewa ili kusaidia maendeleo ya Kanisa. Karama hizi za rohoni inabidi ziendelezwe kwa bidii kwaajili ya maendeleo ya Kanisa (1Kor.14:12). Usimamizi wa nyumba yake mtu ndicho kipimo cha usimamizi wake kwa Kanisa la Mungu (1Tim.3:5).

6.4 Utakaso

Waumini wa Kanisa walioitwa na Roho Mtakatifu (Rum.15:16) kuwa watakatifu wametakaswa (1Kor.1:2) na Mungu Baba na wanalindwa na Yesu Kristo (Yuda 1).

Watakatifu wametakaswa na Mungu kupitia damu ya agano (Ebr.10:29) na mwili wa Yesu Kristo (Ebr.10:9-10). Watakatifu kwahiyo wanaokolewa katika ubatizo (1Kor.6:11). Kwahiyo Roho Mtakatifu ni roho wa Mungu wetu, na kupitia jina la Yesu Kristo wateule hutakaswa na kuoshwa kwa sadaka inayoendelea kwa njia ya imani kupitia Mungu (Mdo.26:18).

Wateule wamekirimiwa msamaha wa dhambi kwa neema na kutunza wokovu huo kwa imani itakasayo pande zote mbili yaani kwa Kanisa na kwa familia (1Kor.7:14). Kwahiyo mwenzi asiyeamini na watoto wametakaswa kwaajili ya mwenzi aliye amini. Wateule hutakaswa kupitia mwili wa Kristo nao huwa mwili mmoja katika Kristo (Rum.12:5; 1Kor.12:20-27), hivyo basi utakaso hautegemei kufuata utaratibu fulani uliobuniwa.

 

Sura Ya 7

Ufalme Wa Mungu

7.1  Kuanzishwa Kwa Ufalme Wa Mungu

Kuanzishwa kwa Ufalme wa Mungu kulitabiriwa kama kukomeshwa kwa tawala za kidunia kwa ujio wa Masihi katika ukamilifu wa dahari (Dan.2:44). Ufalme wa Mungu ulishahubiriwa na Kristo ambaye alisema umekaribia (Mk.1:14-15). Kwahiyo Ufalme una maana mbili. Maana ya kwanza ni Ufalme wa Kiroho na ya pili ni Ufalme halisi wa kipindi cha Milenia chini ya Masihi.

7.1.1  Ufalme Wa Kiroho

Miaka ya nyuma kabla ya mwaka 30 BK ni manabii tu au viongozi wa Israeli walipewa Roho Mtakatifu na ni kwa makusudi maalumu. Hakukuweko taifa jingine, hadi wakati wa kukubaliwa kwa Wa-mataifa Kanisani kuanzia mwaka 30 BK walikuwa na Roho Mtakatifu. Hawa wote wanahusishwa na ufufuo wa pili au ufufuo wa wote katika Ufunuo 20:4 ff.

Roho Mtakatifu alitolewa kwa wote wenye mwili tangia kifo cha Kristo, kama awamu ya kwanza siku ya Pentekoste mwaka 30 BK (Mdo.2:1-4) ambaye walimuona akishuka kwa nguvu (Mk.9:1). Inapaswa kila muumini ampokee kwa bidii na ufahamu kama mtoto mdogo (Mk.10:15). Mtu asipozaliwa mara ya pili, kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu (Yoh.3:3-5).

Siri za Ufalme wa Mungu wamepewa wateule na ufahamu hutolewa na Roho Mtakatifu, na Biblia imeandikwa kwa lugha za fumbo (Lk.8:10). Ufalme wa Mungu sio kula na kunywa, bali ni haki, amani na furaha katika Roho Mtakatifu (Rum.14:17). Sio katika maneno bali ni katika uweza (1Kor.4:20).

Toba ni kitu cha muhimu sana ili kuingia katika huu Ufalme. Wenye dhambi waliotubu watawatangulia kuingia Ufalme wa Mungu kuliko wale wanaojihesabia haki mbele za Mungu (Mat.21:31-32). Jinsi ya kupokea wito wateule ni kwa njia ya jumla ni kama mpanzi alivyo panda mbegu (Mat.13:3-9). Hutawanyika na hupokelewa kwa bidii kubwa kupitia Roho Mtakatifu (Mat.13:44-46). Kwahiyo walioitwa ni wengi lakini wateule kwakweli ni wachache (Mat.20:16, 22:14). Wito hukusanya wengi, kadhalika na wateule, waliochujwa kwa siku za mwisho karibu na kurudi kwake Masihi au kwa wale waliokufa wakati wa ufufuo (Mat.13:25-30,36,38-40,47-50). Wateule walikusudiwa tangu mwanzo, wakaitwa na kuhesabiwa haki na kutukuzwa (Rum.8:29).

 

Wakati Ufalme utolewapo na Roho Mtakatifu, unafanana na punje ya haradali ambayo hukua hadi kufikia mti mkubwa sana au umefanana na chachu ambayo huchachusha donge zima (Mat.13:31-32), hivyo humfanya Mungu awe ni yote katika yote (1Kor.15:28) (soma Biblia ya Marshall’s Interlinear, Efe.46).

Jambo la muhimu ni kuutafuta kwanza Ufalme wa Mungu na haki zake na mengine yote mtapewa kwa ziada (Mat.6:33). Uweza dhidi ya mapepo ni ishara ya Ufalme wa Mungu kwa mtu binafsi (Mat.12:28). Kuyafanya mapenzi ya Mungu ni kitu cha muhimu sana kama tunataka kuurithi Ufalme wa Mungu kupitia Roho Mtakatifu. Kama hatumtumii vizuri ataondoka kwetu na kupewa watu wengine watakao mzalia matunda (Mat.21:31-43).

Ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza, lakini umo ndani ya kila mmoja (Lk.17:20-21). Ufalme wa Mungu pia unaitwa ni Ufalme wa Mbinguni, haupatikani kwa njia ya kumjua tu Kristo kuwa ni Bwana, bali kwa kuyatenda mapenzi ya Mungu Baba (Mat.7:21). Kwa kunyenyekea na kuyafanya mapenzi ya Mungu mtu hufanyika mkuu katika Ufalme wa Mungu (Mat.18:3-4).

Mambo yanayoweza kumzuia mtu kuingia Ufalme wa Mungu yameelezewa katika waziwazi katika 1Wakorintho 6:9-10, Wagalatia 5:21 na Waefeso5:5.

7.1.2  Utawala Wa Milenia Wa Kristo

Utawala wa Milenia wa Masihi umeelezewa wazi katika Ufunuo 20:2-7.  Kipindi hiki cha miaka elfu moja kinajulikama kama Milenia au Chiliad.

7.1.2.1  Kurudi Kwa Masihi

Marejesho ya mfumo wa Kibiblia kupitia kurudi kwake Masihi, kunapatikana katika Zekaria 14:4. Kristo alisema kwa mifano, kwamba alipaswa yeye aondoke kwanza kasha arudi tena (Lk.19:12).

Masihi atafikia katika Mlima wa Mizeituni. Pamoja na wateule ataanzisha Serikali yake. Atalijenga Hekalu (Mdo.15:16). Ataurudisha tena utaratibu wa Kibiblia vikiwemo Sabato, Miandamo ya Mwezi na vipindi vya Siku Takatifu za Mwaka. Mataifa yote yatalazimika kupeleka wawakilishi wao Yerusalemu ili kushika Sikukuu ya Vibanda kama hawatafanya hivyo, basi vyua haitanyesha kwa majira muafaka katika nchi zao (Zek.14:16-19).

Ujio wake utakuwa na ishara kuu na ajabu katika uweza na utujufu mkuu (Mat.24:27-30; Ufu.1:7). Kurudi kwake kutakuwa kwa dhahiri kukifuatiwa na  ishara za mbinguni (Ufu.6:12). Nguvu za mbingu zitatikisika. Jua litatiwa giza na mwezi hautatoa mwanga wake (Mat.24:29; Mdo.2:20). Ataketi mkono wa kuume kwa uweza na atakuja toka mawingu, mbinguni. Hivyo Mungu amempa kristo uweza (Mat.26:64; Lk.14:62; Lk.21:27; Mdo.1:11).

Kristo atakuja na sauti kuu ya malaika mkuu Mikaeli katika parapanda ya mwisho (1The.4:16-17; Ufu.11:15).

Wakati mwana wa Adamu atakapo kuja katika utukufu wake, kuja kutukuzwa na watakatifu wake (2The.1:10), pamoja na malaika wake, atawatenga watu na kuwashughulikia (Mat.25:31-46).

Wateule, walio wa Ufalme wa Mungu, waliopewa Roho Mtakatifu kupitia toba na ubatizo wa watu wazima, wakizishika amri, watafufuka Kristo ajapo. Huu ndio ufufuo wa kwanza. Wafu waliosalia hadi pale mwisho wa Milenia. Huu ndio ufufuo wa pili (Ufu.20:4 ff). Wateule ni tumaini na sababu ya kuja kwa Masihi (1The.2:19; Ufu.22:20). Wateule wanatakiwa wasiwe na mawaa katika utakatifu tayari kwa ujio wa Kristo na Jeshi (1The.3:13; 1The.5:23). Kuipenda kweli ni jambo la muhimu ili kupata wokovu (2The.2:10) Bwana atawaangamiza waovu kwa pumzi ya kinywa chake (2The.2:8). Kanisa limetakiwa likeshe, lisilale usingizi kwakuwa halijui saa ya kuja kwake Bwana (Mk.13:35-37; Ufu.3:3,11). Kristo atarudi na hukumu ya haki na atafanya vita na wale wote waliokataa kuzishika amri za Mungu (Zab.96:13; 19:11). Kristo atarudi na kushughulika na wanadamu katika mambo yao yote (Ufu.22:12).

7.1.2.2  Mkusanyiko Wa Israeli

Wakati wa kurudi kwake Masihi wateule na masalia ya Waisraeli wa kimwili, ambao wengine wao watatumika kama makuhani, watakusanyika Yerusalemu katika pembe nne za nchi (Isa.11:12,66:19-21).

7.1.2.3  SikuYaBwana

Kabla ya haijafika siku ya Bwana, kutatokea usi au ukengeufu, na kudhihirishwa kwa mwana wa ukengeufu (mpingakizi – apostasia) mwenye kuwafundisha watu wasishike kweli na sheria za Mungu na kuwapoteza yamkini hata wateule. Asi, mwana wa uharibifu, (anomias), aitwa hivyo kwa kazi yake ya kuwapoteza watu mbali na sheria za Mungu kupitia mafundisho yake kwa wateule, atadhihirishwa (2The.2:3-8). Ataketi katika Hekalu la Mungu na kijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu. Ataangamiza na Masihi atakapokuja.

Bwana atawaangamiza wale wote wasioutakia mema Yerusalemu. Watakao angamizwa watashituka na kurudi kuwashambulia wenzao (Zek.14:12-13). Hii itatokea bila kutarajiwa kabisa (1The.5:2).

Uharibifu utatokea katika nchi. Wanadamu watajificha katika milima na miamba kwasababu Kristo amekuja na hasira na hakuna mmoja atakayewaza kusimama (Ufu.6:15-17), kutatolewa baragumu na mapigo ya magonjwa Mungu atakayo mwaga juu ya wanadamu katika siku za mwisho (Ufu.8:7-21; Ufu.16:1-20). Katika mwisho wa siku ya Bwana, ambao unadumu hadi Milenia, tutashuhudia mwisho wa dunia kama tunavyofahamu. Sayari itaangamizwa kwa moto (2Pet.3:7-10,12), hivyo kuondoa masalia yote ya makazi ya mwanadamu.

Mafuatano yote ya kipindi cha Siku ya Bwana yamepangwa ili kutoa hukumu kwa dunia na kuwarekebisha wateule (Yuda 14:16). Wateule wale waliofanya dhambi hukabidhiwa kwa mfumo wa dunia watapewa nafasi ya kuokoka katika kipindi hiki cha Siku ya Bwana, kwa kurekebishwa katika kipindi cha ufufuo wa pili (1Kor.5:5). Kwahiyo, kuna aina mbili tu za ufufuo.

7.1.3  Utawala Wa Milele Wa Mungu

7.1.3.1  Kuja kwake Bwana

Wakati Kristo atakapo kabidhi utawala wote na mamlaka, atamrudishia tena Mungu mfumo wote mzima (1Kor.15:24-28). Kasha Mungu atakuja duniani na kufanya makao ya mbinguni yawe hapa duniani. Kwahiyo dunia yote itajawa na utukufu wake (Isa.6:3) na Mungu na Mwana kondoo watia nuru dunia nzima (Ufu.21:23).

7.1.3.2  Dunia Mpya Na Yerusalemu Mpya

Isaya 65:17 inasema kuwa kutakuweko na mbingu mpya na nchi mpya vitafanyizwa. Uzao wa Israeli vitasalia mbele za Mungu wakati wa kuweko kwa mfumo huu (Isa.66:22) mpaka mwisho wa Milenia ambapo miili yote itakapoharibiwa. Mungu ataweka makao yake Sayuni na utaitwa jina lake ni mji mwaminifu (Zek.8:3). Mji huu wa Yerusalemu mpya utashuka kutoka mbinguni (Ufu.3:12). Yerusalemu hii ni Mji Mtakatifu ushukao chini katika uumbaji wa mbingu mpya na nchi mpya (Ufu.21:1-4,7,10). Kasha maskani ya Mungu yatakuwa pamoja na wanadamu. Mambo yote ya kale hayatakumbukwa tena (Isa.65:17). Tunatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambamo haki yakaa ndani yake, kama ilivyoahidiwa (2Pet.3:13). Wengi wa watakatifu walioshinda watafanyika kuwa nguzo katika Hekalu la Mungu (Ufu.3:12). Kwahiyo itakuwa ni kutaniko la kiroho.

7.1.3.3  Hatima Wa Wanadamu

Wateule watapewa uongozi wa duniani hapa wakati wa Milenia (Lk.19:17,19), watafanana na malaika (Mat.22:30), wakiirithi nchi na kumuona Mungu kikamilifu, wakiwa ni Wana wa Mungu (Mat.5:3-11). Nafasi hii itaenea katika mataifa yote (Mat.8:11). Haya ni mapenzi ya Mungu Baba (Lk.12:32). Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu (Rum.8:14).

Utawala wa Milenia wa Masihi ndio fundisho kuu kama chombo katika kumuandaa mwanadamu kwaajili ya wajibu wake wa mwisho, ili kutimiliza mwelekeo wao na mpango wa Mungu ambao aliuweka kabla ya kuwekwa misingi ya dunia.

Hatima ya mwanadamu ni kuandaliwa ili kuchukua sehemu yao katika mfumo huu mkamilifu wa kimungu, na kuchukua sehemu yao katika urithi wao halali ambao ni mwendelezo na utawala wa dunia hii (Zab.8:1-9; Dan.2:44-45) na mpango wa amri mpya ya ulimwengu (Dan.7:27, 12:3).

 

 

Maongezo

Roho iliyo ndani ya Waamini Imani ya Utatu

Waamini Utatu waliitenganisha Theolojia kwa kitu kinachoitwa uchumi wa wokovu katika kufanyika mwanadamu halisi kwa Yesu Kristo. LaCugna (GOD FOR US  The Trinity and Christian Life, Harper, San Francisco, 1991), katika kushughulikia na maendelezo ya fundisho la Utatu na kuitenganisha elimu ya theolojia na mpango wa wokovu (au soteriology)  kama ilivyo funuliwa katika kufanyika kwake Kristo kuwa mwanadamu, ilichukuliwa kuwa theolojia tegemevu ya Wakapadokia ambayo ilichangia zaidi kutenganisha kati ya uchumi na theolojia. Kisa hiki kilifikilisha katika:

Kupitia kinyume cha U-Dionisia wa uwongo na hatimaye, kwenye theolojia ya Gregory wa Palamas (Sura ya 6).

Katika Magharibi ya Ulatini, katika kipindi mara tu baada ya mtaguso wa Nikea, wana theolojia kamavile Hilary wa Poittier nap engine kwa kiwango kikubwa kilichokosa kiasi, Marsela wa Ansira, alishikilia uhusiano kati ya uungu na uchumi wa wokovu. Augustino alizindua kikamilifu mwelekeo mpya. Hatua yake ya kuanzia haikuwa tena utumishi wa Baba bali uungu uliohusisha vitu vitatu kwa pamoja vinavyo shiriki usawa katika nafsi tatu [msisitizo uliongezwa]. Badala ya kupata asili ya theolojia kama ilivyo funuliwa katika dhana ya kufanyika kwa Kristo kuwa mwanadamu na kufundishwa na Roho Mtakatifu [mkazo iliongezwa]. Augustino alionba aongezee kuandika neno Utatu likapatikana na kuaminika katika kila mwanadamu. Mvuto wa Augustino uliegemea kuweka ulinganisho wa ‘kisaikolojia’ kwa mfano wa utatu wa kibinadamu yaani mwili nafsi na roho unavyo husiana ingekuwa na maana kwanba fundisho la utatu hivyo lingehusu na uhusiano wa ndani kwa ndani katika Uungu ulio unganishwa kwakile tunacho kijua katika Mungu kupitia Kristo katika Roho (LaCugna, p. 44)

Theolojia ya Kilatini wakati wa miaka ya kati (Medieval) iliyofuatia ile ya Augustino na utenganisho wa theolojia ya uchumi na wokovu. Mfumo mzima ulifungamanishwa na u-Plato mamboleo na usiri.

Nukuu muhimu za LaCugna ni zile zilizotoka kwa Augustino Mtawa kwamba ukuu wa Baba haukuwa na maana tena. Utatu uliaminika kuwa ni usawa. Hii ulikuwa ni hatua ya pili kufuatia madai ya uwongo kuhusu usawa. Wazo sahihi lilikuwa la kufikiri kuwako kwa madhihiriko ya Uungu kuweko katika kila mmoja wao, kusema kuwa katika utendaji kazi wa Baba kwa kumtumia Roho Mtakatifu aliyefunuliwa kwa njia ya Yesu Kristo. Uelekeo huu kupitia Yesu Kristo ulimfanya Kristo kumsimamia na kumuongoza kila mmoja sawa na mapenzi ya Mungu aliyeishi ndani ya kila mteule.

Kristo hakuwa asili ya Roho Mtakatifu. Yeye ni mwombezi msimamizi. Hufanya mambo kwaajili ya Mungu kama alivyofanya wakati wote kulingana na mapenzi ya Mungu. Lakini hakuwa Mungu. Waamini Utatu wamepoza muelekeo kuhusu ukweli huu, kama kwakweli walielewa jambo hili. Kama LaCugna alivyosema:

Thelojia ya Utatu wa Mungu yaonekana imeongezewa katika tafakari ya Mungu mmoja (p.44).

Hii iliathiri msingi wa jinsi Wakristo walivyoomba. Wakawa sasa hawaombi kwa Baba pekeyake (Mat.6:6,9) katika jina la Mwana kama Biblia inavyoelekeza (katika Lk.11:12), kumuabudu Baba (Yoh.4:23), lakini kwa jina la Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Zaidi kabisa, wanazuoni waliendeleza dhana ya theolojia ya uwongo. Lakini lengo lilikuwa ni kuigeuza Biblia. Ndiomaana waamini Utatu kamwe hawatumii maandiko ya Biblia hasa kusimamia wanapo fundisha na wanatafsiri kwa makosa au kunukuu ki makosa aya nyingine, huku wakipuuzia zile ambazo zinazo wapinga kwa dhahiri. Laniki mfumo wao umesimamia zaidi katika madai ya Kifumbo na Kiplatoni. LaCugna anasema:

Wakapadokia (pia ni Augustino) walikwenda mbali mno na uelewa wa kimaandiko katika kuchukulia suala la uchumi hadi kuliweka katika mahusiano ya Mungu na Mwana (na Roho) katika kiwango sawa cha uungu (p.54).

Mungu mmoja aishiye kama ousia ni mwenye nafsi tatu hypostases. Tunaona katika (Cox, The elect as Elohim) kuwa msemo wa Kiplatoni ousia na wa Kistoini hypostases humaanisha chanzo cha kitu kimoja.

Roho ni wa muhimu katika utendaji kazi. Kukataa kuwa Roho hana sehemu katika utendaji kazi, kutamaanisha kuwa wawezi kushiriki katika asili ya mambo ya Mungu kama Kristo anavyoshiriki katika asili ile. Madai kama haya ni kwenda kinyume na maandiko. wateule hushiriki katika asili ya mbinguni (2Pet.1:4).

Katika Waefeso 1:22 Mungu alivitia vitu vyote chini ya miguu ya Kristo na akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya Kanisa. Mungu alimfufuaKristo toka kwa wafu:

Akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya Kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.

Kwahiyo, Kristo amepewa mamlaka juu ya majina yote, kama jina lake lenywe linavyo beba mamlaka. Amepewa mamlaka juu ya vitu vyote ili kwamba Kanisa lifikie kwenye haki ya urithi kupitia Kristo ambaye katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili (Kol.2:9). Neno hili limetafsiriwa Uungu hapa ni theotetos linamaanisha uungu au hali ya kuwa Mungu.

Sasa Thayer anasema kwamba uungu (theot) kama kiini, hutofautiana na umbinguni (theiot) kama kiini kinavyo tofautiana na ubora au tabia (Thyer’s, p.288). hapa ina maana kuwa utimilifu wote wa Mungu upo kwa jinsi ya kimwili ndani ya Kristo. Ni aina hii ya ukamilifu ndiyo tuliyopewa ili kwamba watu wote wapewe asili hii mpya ya Mungu (Kol.3:10). Haijalishi kuwa ni Myahudi au Myunani lakini wote ni wa Kristo kwasababu yeye ni yote katika yote (Kol.3:11). Huwaundeleza watu. Kupitia nguvu za Roho Mtakatifu, ili hatimaye Mungu awe yote katika yote (1Kor.15:28).

Wakati vitu vyote vitakapo vitakapo mtii yeye,Mwana mwenyewe atajinyenyekesha kwake yeye aliyeviweka vitu vyote chini yake, ili Mungu awe ni [yote katika yote KJV] (panta en panta) [ukisoma Marsall’s Interlinear na vile vile Kol.3:11 (panta kai en pasin)].

Waamini Utatu wameanza kutafsiri aya hii isomeke kilakitu kwa kilamtu ili kuepuka ukweli halisi kuwa Mungu ni kiini cha uwepo wa watu wote kama ilivyo kwa Kristo kulingana na ayah ii.

Ni Kristo anaye tujaza sisi ukamilifu wa Mungu (Efe.3:19). Utimilifu wa Kristo kuwa mfano wa sura ya Mungu Baba (Efe.4:13). Kwa jinsi hii sisi pia tunafanyika mfano wa sura eikon ya Baba kama alivyokuwa Kristo nasi ni watoto wa Mungu na warithi pamoja na Kristo katika Ufalme wa Mungu (Rum.8:17; Yak.2:5). Ni warithi kutokana na ahadi (Gal.3:29) wa wokovu (Ebr.1:14) na warithi pamoja wa neema (1Pet.3:7).

 

Wana wa Mungu baada ya kuwa Baba wa Milele (Isa.9:6) akiwa ni kichwa cha ubaba wa mwanadamu, maskani yatakayo kuwepo mkabala na ubaba mwingine uwao wote wa mbinguni waliko jeshi kubwa (Efe.3:14).

Kwa hiyo nampigia Baba magoti, ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa.

Neno familia hapa ni patria au ubaba. Kwa hiyo cheo baba, iwe ni nyumba nzima wa nyumba yote ya Mungu, ni cheo kilichotolewa kikionyesha umuhimu wa wajibu wa kila kiongozi wa taasisi yoyote ile au familia. Kwa hiyo, amri ni kutoka kwa Mungu kwenda kwa Kristo kwenda kwa mwanaume kiongozi wa nyumba (1Kor.11:3) ambaye ni lazima awajibike kwa Mungu kama afanyavyo kwa Kristo na kwa Watoto wengine wa Mungu ambao ni elohim na ni njia amboyo hao elohim waweze kuwatoe wajibu wao walio chini yao.

Roho Mtakatifu ni njia inayo tuunganisha na kutuwezesha katika u-elohim wa kila Malaika. Hakuna swali kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu katika aina yeyote tofauti na mwanadamu na kujaliwa uhusiano wa kiuungu wa muungano wa nafsi tatu. Wote ni Wana wa Mungu, ni warithi pamoja na Kristo katika jinsi ileile. Ibada ya kumuabudu Roho Mtakatifu, ingekuwa ni kwa maana sawa na kujitukuza badala ya kumpa nafasi hiyo Mungu aliye yote katika yote.

Kwahiyo kumuabudu kumekatazwa kabisa kama ni kujitukuza kwavile ni sehamu ya kitu binafsi. Ni nguvu tu au tabia iliyoshirikishwa na sio Mungu mwenyewe. Roho Mtakatifu hutuwezesha kuwa na uweza wa kuwa Elohim au Theoi.

Uungu ni mfumo unaoendelea hadi kweye Baraza. Braza lile limeelezwa katika Zaburi na katika aya nyingine zinazoelezea Kiti cha enzi cha Mungu na Baraza la Wazee limeelezewa katika Ufunuo 4:1 hadi 5:14. baraza hili linamjumlisha Yesu Kristo kama Mwana Kondoo, na Kuhani Mkuu (soma Ebr.8:12), wakimtumikia na kumuabudu Bwana Mungu wa Majeshi (Ufu.4:8-11). Katika kumtumikia Mungu, Kristo aliutoa uhai wake, kama ilivyokuwa inampasa kila kuhani kutoa kitu fulani kwa Mungu kama sadaka (Ebr.8:3).

Ufunuo 4:8-11 kinasema kuwa Bwana Mungu wa Majeshi enzi yake iko juu sana kuliko wazee wote ambao pia wamepewa enzi. Tena wameweka taji zao chini ya Bwana Mungu wa Majeshi ambao kupitia wao aliumba vitu vyote. Yeye ni Bwana Mungu wa Yesu Kristo na wa hili Baraza.

Kuna aina Wana wengi wa Mungu pamoja na Jeshi la mbinguni (Ayu.1:6, 2:1, 38:7; Zab.86:8-10, 95:3, 96:4, 135:5) ambao wamejulikana kama Bene Elyon au Wana wa Aliye Juu sana (soma Sabourin SJ, The Psalms: Their Origin and Meaning, Alba House, NY, pp. 72-74). Uchaguzi wa wanadamu unajumlishwa na Jeshi la mbinguni na Wana wa Mungu (katika Rum.8:14).

Kristo alikuwa ni mzaliwa wa kwanza au mzaliwa wa kwanza wa pekee wa kwanza katika uumbaji. Kwakuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni viti vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. Naye alikuwako kabla ya vitu vyote na vitu vyote hushikamana katika yeye (Kol.1:16-17). Lakini ilikuwa ni Mungu aliye mkirimia na kupenda kuwa uumbaji uwepo na upitie kwa Kristo. Kwahivyo bas, Kristo sio Mungu kwa aina yoyote ya mtazamo kulinganisha na vile Mungu Baba alivyo Mungu na kwamba ni yeye tu ndiye mwenyekuishi milele (1Tim.6:16) na ni mkuu kuliko wote (Yoh.10:29).

Kwa hiyo, Mungu alimtuma Mwana wake wa pekee (monogene) hapa ulimwenguni ili tuishi kwa ajili yake (1Yoh.4:9). Ni Mungu ambaye aliye mheshimu Kristo, Mungu akiwa ni mkuu (Yoh.8:54).

Kristo aliachilia mamlaka yake kama Mwana wa Mungu kule Mbinguni na akawa mwanadamu, kashuaka katika mbari ya Daudi katika mwili (Rum.1:3). Alidhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwaba wetu (Rum.1:4).

Mungu ni Mwamba (sur) kama jiwe kuu au mlima ambao kwake wengine wote walitokea, ni gumegume la Yoshua 5:2, lililo watahiri Israeli, myenye haki na adili (Kum.32:4, Mainmonedes, Guide of the Perplexed, University of Chicago Press, 1965, Ch.16, pp. 42 ff). Mungu ndiye Mwamba wa Israeli, Mwamba wa wokovu wao (Kum.32:15), Mwamba ulio wazaa (Kum.32:18, 30-31). 1Samweli 2:2 yatuonyesha kuwa Mungu wetu ni Mwamba wetu, Mwamba wa milele (Isa.26:4). Ni kutokana na Mwamba huu wengine wote walichongwa kama wote ni wana wa Ibrahim wa imani (Isa.51:1-2). Masihi alitokea katika Mwamba huu (Dan.23:4-45) ili kuzitiisha falme za dunia. Ni Mungu, wala sio Petro,wala Kristo, wala sio mtu awayeyote, ni Mwamba au msingi ambao juu yake Kristo atalijenga atalijenga Kanisa lake (Mat.16:18) ambapo yeye mwenyewe aweka msingi wake.

Masihi ndiye Jiwe Kuu la Hekalu la Mungu, ambalo wateule ni Naos au Patakatifu pa Patakatifu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. Mawe ya Hekalu yamechongwa kutoka katika Mwamba ambaye ni Mungu, kama ilivyokuwa kwa Kristo, na kupewa Kristo, mwamba war oho (1Kor.10:4), jiwe likwazalo na mwamba unaoangusha (Rum.933) kufanya Hekalu. Kristo atalijenga Hekalu ili Mungu awe ni yote katika yote (Flp.4:6). Mungu amemfanya Kristo kuwa yote katika yote  (panta kai en pasin Kol.3:11) akiweka mambo yote chini ya miguu yake (1Kor.15:27) akamfa kuwa kichwa cha cha kilakitu kwa Kanisa ambalo ni Mwili wake, ili kumkamilisha yeye awe yote katika yote (Efe.1:22-23). Wakati Mungu alipoweka mambo yote chini ya Kristo, ni udhhihirisho kuwa Mungu anatarajiwa kuwa ndiye aliviweka vitu vyote chini ya miguu ya Kristo (Kor.15:17).

Wakati Kristo atakapo vitiisha vitu vyote, kasha Kristo mwenyewe atajinyenyekeza kwa Mungu aliyeviweka vitu vyote chini ya. Kristo ili Mungu awe ni yote ndani ya yote (panta en pasin 1Kor.15:28 si kama ilivyo katika Biblia ya RSV). Kwahiyo, mafundisho ya Waplotini yanayotafuta muunganisha Mungu na Yesu katika Utatu huchanyanya Maandiko. Kristo ataketi mkono wa kuume wa Mungu wa kuume wa Mungu, kwa maelekezo ya Mungu (Ebr.1:3,13, 8:1, 10:12, 12:2; 1Pet.3:22) na kushiriki kiti cha enzi cha Mungu kama wateule watakavyo shiriki kiti cha enzi alichopewa Kristo (Ufu.3:21) ambacho ni kiti cha enzi cha Mungu (Zab.45:6-7; Ebr.1:8 au Mungu ndio kiti chako cha enzi kama ilivyotafsiriwa na Kiti chako cha enzi O Mungu, angalia nukuu za chini za Biblia ya ”annotatoted” RSV).

Mungu aliyemtuma ni mkuu kuliko yeye aliyetumwa (Yoh.13:16), mtumwa hawezi kuwa mkuu kuliko Bwana wake (Yoh.15:20). Ni upuuzi usio kifani kuelezea kuwa Mungu anaweza kujitoa sadaka kwake mwenyewe. Tendo la namna hiyo kwa watu wenye akili na kufamu mambo wataelewa kuwa ni kujinyonga yaani kujitoa mhanga au kwa Waamini Utatu ni sehemu ya uharibifu. Tena basi fundisho hili linapinga ufufuo hususan kulinganisha na 1Wakorintho.15.

Kwahiyo, tofauti kati ya kusulibiwa na kufufuka ni ya lazima na nikamilifu. Ufufuko ni lazima uwe katika mwili ukihusishwa na tafiri ya nikama Sadaka ya Kutikiswa, vinginevyo hakuwezekani kuwepo na wokovu na hakuna mazao endelevu. Matayarisho ya kunyakuliwa kwa Kristo kwenda kwa Mungu wake ambaye ni Baba yetu (Yoh.20:17) ulikuwa ni kweli, halisi na ni wa kipekee.