Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[214]
Azazeli na Upatanisho
(Jarida 1.1 19970911-19970913)
Maana ashirio ya mbuzi kwenye
Upatanisho, mara nyingi imekuwa ikichanganywa na jina Azazeli limekuwa mara
nyingi likikosewa kupangiliwa au limekuwa likitumiwa vibaya. Kuna tafsiri ya
kina ya maana yenye kuonyesha mfano ambayo ilianzia kutoka katika Waisraeli wa
kale na inapatikana iliunganishwa na maandiko ya nyakati mbalimbali. Mfano
unaoelezewa nakufafanuliwa hapa unatokana katika utimilifu wake wa Kimasihi na
mfano linganishi wake wa siku za mwisho.
Christian Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Copyright ã 1997 Wade Cox)
(Tr. 2005)
Masomo
haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kutufa maneno. Jina la mchapishaji na anuami
yake pamoja na hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya maelezo na kilugha
lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti
yetu ya:
http://www.logon.org
au http://www.ccg.org
Azazeli na
Upatanisho [214]
Utangilizi kuhusu Upatanisho
Katika
kitabu cha Mambo ya Walawi 16:1-34, tumepewa maelekezo kuhusu jinsi ya utoaji
wa dhabihu ya Upatanisho. Miongoni mwa zile nyingine ni mbuzi wawili ambazo
kura zilipigwa ili kuwezesha kuamua kuhusu ni dhabihu ipi inafaa na itakayoweza
kuchukua dhambi za watu.
Mambo ya
Walawi 16:1-34 inasema:BWANA akanena na Musa, baada ya kufa hao wana wawili wa
Haruni, walipokaribia mbele za BWANA, wakafa; 2 BWANA akamwambia
musa, Sema na Haruni ndugu yako, kwamba msiingie wakati wo wote katika mahali
pa takatifu ndani ya pazia, mbele ya kiti cha rehema, klicho juu ya sanduku,
msije mkafa; maana, mimi nitaonekana kayika lile wingu juu ya kiti cha rehema. 3
Haruni akaingia katika patakatifu na vitu hivi; ng’ombe mume mchanga kwa sadaka
ya dhambi, na kondoo mume kwa sadakaya kuteketezwa. 4 Ataivaa ile
kanzu takatifu ya kitani, atakuwa na zile suruali za kitani mwilini mwake,
atafungwa ule mshipi wa kitani, naye atavaa ile kofia ya kitani; haya ndio
mavazi matakatifu, naye ataoga mwili wake majini, na kuyavaa. 5 Kisha
ataitwaa mikononi mwa mkutano wa Waisraeli mbuzi waume wawili, kwa sadaka ya
dhambi; na kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa. 6 Na Haruni atamtoa
ng’ombe wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, na kwa
ajili ya nyumba yake. 7 Kisha atawatwaa wale mbuzi wawili na
kuwaweka mbele za BWANA mlangoni pa hema ya kukutania. 8 Na Haruni
atapiga kura juu ya wale mbuzi wawili; kura moja kwa ajili ya BWANA; na kura ya
pili kwa ajili ya Azazeli. 9 Na Haruni atamleta yule mbuzi
aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya BWANA, na kumtoa awe sadaka ya dhambi. 10
Bali yule mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Azazeli atawekwa hai
mbele za BWANA ili kumfanyia upatanisho, ili kumpaleka jangwani kwa ajili ya
Azazeli. 11 Na Haruni atamsongeza ng’ombe wa sadaka ya dhambi, aliye
kwa ajili ya nafsi yake, na kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake
mwenyewe, na kwa ajili ya nafsi yake, na kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi
yake mwenyewe, na kwa ajili ya nyumba; naye atamchinja yule ng’ombe wa sadaka
ya dhambi, aliye kwa ajili ya nafsi yake. 12 Kisha atatwaa chetezo
kilichojaa makaa ya moto yatokayo katika madhabahu iliyo mbele za BWANA, na
konzi za uvumba mzuri uliopondwa sana, mikononi mwake, naye atauleta ndani ya
pazia. 13 kisha atatia ule uvumba juu ya moto mbele za BWANA, ili
moshi wa ule uvumba ukisitiri kiti cha rehema kilicho juu ya ushuhuda, asije
akafa. 14 Kisha atatwaa baadhi ya damu ya yule ng’ombe, na kuinyunyizia kwa kidole chake juu ya kiti cha
rehema upande wa mashariki; na mbele ya kiti cha
rehema
atainyunyiza ile damu kwa kidole chake mara saba. 15 Kisha
atamchinja yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya watu, na kuileta
damu yake ndani ya pazia, na kwa damu hiyo atafanya vile vile kama alivyofanya
kwa damu ya ng’ombe, na kuinyunyiza juu ya kiti cha rehema, 16 naye
atafanya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu, kwa sababu ya mambo machafu
ya wana wa Israeli, na kwa sababu ya makosa yao, naam, kwa ajili ya dhambi zao
zote; naye atafanya vile vile kwa ajili ya hema ya kukutania, ikaayo pamoja na
katikati ya machafu yao. 17 Wala hapatakuwa na mtu katika hema ya
kukutania, wakati aingiapo ili kufanya upatanisho katika patakatifu, hata
atakapotoka nje, baada ya kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe,
na kwa ajili ya nyumba yake, na kwa ajili ya mkutano wote wa Israeli. 18
Kisha atatoka na kuiendea madhabahu iliyo mbele za BWANA na kufanya upatanisho
kwa ajili yake; atatwaa baadhi ya damu ya yule ng’ombe, na damu ya yule mbuzi,
na kuitia juu ya pembe za madhabahu pande zote. 19 Tena atanyunyiza
baadhi ya damu juu ya madhabahu kwa kidole chake mara saba, na kuitakasa, ili
machafu yote ya wana wa Israeli yaitoke. 20 Naye akiisha kufanya
upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu, na hema ya kukutania, na madhabahu,
atamleta yule mbuzi aliye hai. 21 Na Haruni ataweka mikono yake
miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na kuungama juu yake uovu wote
wa wana wa Israeli, na makosa yao, naam, dhambi zao zote; naye ataziweka juu ya
kichwa chake yule mbuzi, kisha atampeleka aende jangwani kwa mkono wa mtu aliye
tayari. 22 Na yule mbuzi atauchukua juu yake uovu wao wote, mpaka
nchi isiyo watu; naye atamwacha mbuzi jangwani. 23 Na Haruni
ataingia katika hema ya kukutania, naye atavua mavazi yake ya kitani, aliyoyavaa
alipoingia katika patakatifu, atayaacha humo; 24 naye ataosha mwili
wake kwa maji mahali patakatifu, na kuvaa nguo zake, na kutoka, na kusongeza
sadaka ya kuteketezwa yake mwenyewe, na sadaka ya kuteketezwa ya watu, naye
atafanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake, na kwaajili ya watu. 25
Na mafuta ya sadaka ya dhambi atayateketeza juu ya madhabahu. 26 Na
mtu yule amwachaye mbuzi wa Azazeli aende zake, ataosha nguo zake, na kuosha
mwili wake kwa maji, na baadaye ataingia katika marago. 27 Na yule
ng’ombe wa sadaka ya dhambi, na yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, ambao damu yao
ililetwa ndani ifanye ukumbusho katika patakatifu, watachukuliwa nje ya marago;
nao watachoma moto ngozi zao, na nyama zao, na mavi yao. 28 Na yeye
awachomaye moto atafua nguo zake, na kuosha mwili wake kwa maji, na baadae
ataingia maragoni. 29 Amri hii itakuwa ni amri ya milele kwenu;
katika mwezi wa saba, siku ya kumi ya nwezi, mtajitaabisha roho zenu, msifanye
kazi ya namna yo yote, mzalia na mgeni akaaye kati yenu. 30 Kwa maana
siku hiyo upatanisho utafanywa kwa ajili yenu, ili kuwatakasa; nanyi mtatakaswa
na dhambi zenu zote mbele za BWANA. 31 Ni Sabato ya raha ya makini
kwenu, nanyi mtajitaabisha roho zenu; ni amri ya milele. 32 Na
kuhani atakayetiwa mafuta na kuwekwa wakfu badala ya baba yake, ataufanya huo
upatanisho, naye atayavaa mavazi ya kitani, yaani, yale mavazi matakatifu. 33
Naye atafanya upatanisho kwa ajili ya patakatifu, naye atafanya upatanisho kwa
ajili ya hema ya kukutania, na kwa ajili ya madhabahu, naye atafanya upatanisho
kwa ajili ya makuhani, na kwa ajili ya watu wote wa kusanyiko. 34 Na
amri hii itakuwa amri ya milele kwenu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya wana
wa Isreali kwa sababu ya dhambi zao zote, mara moja kila mwaka. Naye akafanya
vile vile kama BWANA alivyomwamuru Musa.
Siku ya
Upatanisho imeamriwa na sisi tunaiona kutoka kwenye kitabu cha Mambo ya Walawi
23:26-32 kwamba siku ile inakuwa kuanzia jioni hadi jioni ya siku inayo fuata.
Mambo ya Walawi 23:26-32 inasema: Kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia 27 Lakini siku ya kumi ya mwezi huo wa Saba ni siku ya Upatanisho itakuwa kusanyiko takatifu kwenu, nanyi mtazitesa nafsi zenu, nanyi mtasongeza sadaka kwa BWANA kwa njia ya moto. 28 Nanyi msifanye kazi yo yote siku hiyo; kwa kuwa ni siku ya upatanisho, ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu mbele za BWANA, Mungu wenu. 29 Kwa kuwa mtu awayeyote asiyejitolea mwenyewe siku hiyo hiyo, atakatiliwa mbali na watu wake. 30 Na mtu yeyote afanyaye kazi ya namna yeyote siku hiyo, mtu huyo nitamwangamiza atoke katika watu wake. 31 Msifanye kazi ya namna yeyote ni amri ya milele katika vizazi vyenu, katika makao yenu yote. 32 Itakuwa kwenu sabato ya kustarehe kabisa, nanyi mtaziteza nafsi zenu; siku ya kenda ya mwezi wakati wa jioni, tangu jioni hata jioni, mtaishika hiyo sabato yenu.
Kwa
hiyo, hakutakiwi kufanyika kazi ya namna yoyote ile siku hii na wale wote ambao
hawaitii amri hii inatakiwa wakatiliwe mbali na watu wao na kwa Mungu.
Makuhani
wanatakiwa wajitakase na kujiweka wakfu na kuna mfululizo wa mafuatano ya mambo
yanayoendana na utoaji wa dhabihu hizi. Tumeona mahali pengine kuwa mtamba wa
ng’ombe mwekundu alitakiwa atolewe dhabihu akiwa kama dhabihu kwa ajili ya
dhambi (tazama jarida la Masihi na mtamba mwekundu [216]. Kwenye
mwandamano huu wa mambo kunatakiwa kutolewe ng’ombe dume yaani maksai.
Tendo la
kwanza katika kwa mujibu wa aya za kwenye kitabu cha Mambo ya Walawi
kinavyosema ni kwamba watoto wawili wa kiume wa Haruni walikufa kwa ajili ya
kosa la kutenda mambo kwa kubahatisha visivyo katika hali ya uhakika. Tukio
hili linaendana sambamba na jingine lililotokea kule mbinguni viumbe wawili
waliasi na kuwachukua theluthi moja ya Jeshi la malaika. Mkuu au kiongozi wa
viumbe hawa alikuwa ni Shetani yule Joka Jekundu Mkubwa wa Mkuu wa lile Jeshi
(Ufu. 12:3-17) ambaye ndiye mungu wa dunia hii (2Kor. 4:4). Kuielewa Lugha ya
Kiebrania ilikuwa ni daraja lingine la juu iliyokuwa imehusishwa. Jina hili sio
la muhimu. Hata hivyo, kitabu cha Henoko kinaonekana kumtaja kiongozi huyu kwa
jina la Semyanza. Alama hii inaonekana kujiashiria yenyewe kupitia kipindi
chote cha umlimwengu wa zama za kale akioneshwa kama ni viumbe wenye vichwa
vilivyochanganyikana yaani kichwa cha mwanadamu na kichwa cha simba.
Walionekana kwa taswira ya makerubi katika maandiko ya aya za Kiebrania (tazama
Ezekieli 41:19). Jarida la Aeons katika imani za siri za kidini za imani potofu
(tazama jarida la mwandishi David Ulansey la Chimbuko la imani za Siri za
Kimithra, kwa Kiingereza, The origins of the Mithraic. Mysteries,
Oxford, 1989). Kufahamu hata hivyo kunawezakuwa ni sawasawa lakini
kulitazamwa katika mtazamo wa pande tofauti. Mfumo wa Waebrania unaonekana
kulenga kwenye msimamo wao mpya kwenye hekalu la nabii Ezekieli. Kipindi hiki
kinaonekana dhahiri sana kilikuwa ni cha Masihi kwa hiyo, pengine kinaonekana
kama ni cha kujazilia wale viumbe au malaika waasi walioanguka na kuasi.
Karika
mfumo wa imani ya Kiyahudi, Azazeli anachukuliwa au kujulikana ni malaika
miongoni mwa wale wa Jeshi lililoasi na kutupwa chini, kwa mujibu wa Kitabu cha
Henoko. Mtazamo wa kimapokeo ni unaamini kwamba kulikuwa na viumbe wawili
waliofanana na mbuzi wawili walioelezewa hapa katika kitabu cha Mambo ya Walawi
sura ya 16 mmoja kati ya viumbe hawa atambuliwa na Yahova na wa pili
alitambuliwa na Azazeli. Fafanuzi za marabi humjua yeye kama ni miongoni mwa
Jeshi lililoasi na kutupwa hapa duniani. Kura zilikuwa zinapigwa katika
kumchagua mbuzi. Kila kura ilihusisha mmoja kwa Yahova na mwingune kwa Azazeli
(kwa mujibu wa Rashi, Soncino na Walawi 16:8).
Kitabu
cha fafanuzi au commentary ya Soncino kinafafanua aya ya Mambo ya Walawi 16:8
kwa kuonyesha kuwa neno Azazeli linavyoeleweka katika dini ya Kiyahudi lina
maana ya el mwenye nguvu au mwenye uweza. (‘Azaz katika kamusi ya
Kiebrania ya SHD 5811 inaaminika kuwa imechukuliwa kutoka kwenye kamusi
nyingine toleo la SHD 5810 yenye maana ya kukazia iwe ngumu, kuifanya iwe
shupavu, kushinda, kuiimarisha ijisimamie, na hivyo kuwa imara. Hii ni
ngumu sana Kimasihi). Rashi anasema inaashiria kama genge la ukingoni mwa
bahari. Mwana zuoni mwingine wa Kiyahudi anayeitwa Ibin Ezra anaelezea kuwa
ilikuwa ni genge lililokuwa kwenye ukingo wa bahari uliokuwa karibu na Mlima wa
Sinai mahali ambapo mbuzi alikuwa anatelekezwa. Kitendo hiki cha kumtelekeza au
kumtupa mbuzi kwenye genge la ukingoni mwa bahari kwenye mabadiliko ya dondoo
ambayo sio sehemu ya maelekezo ya kibiblia. Bila shaka hii ilikuwa inamzuia
yule mbuzi asirudi tena nyumbani na hivyo kutokea tena katika Ishareli. Hata
hivyo, hii haitokani na maelekezo ya Biblia na kurarua lile wazo lenyewe la
neema ya Mungu.
Mwanazuoni
mwingine Nachmanides anakariri toka kwa Pirke de Rabbi Eliezer kwamba
malaika Sammaeli ambaye alipewa uweza kwa watu wote isipokuwa kwa Israeli
katika Siku ya Upatanisho kama walifanya dhambi. Mbuzi wa pili anaeleweka na
dini ya Kiyahudi kama alivyokusudiwa ili apelekwe kwa Sammaeli [Azazeli au
mungu wa dunia hii] lakini kwa kadiri alivyokuwa haijaletwa kwenye madhabahu ya
patakatifu, alifunguliwa na kuachiliwa aende jangwani. Hii ni ishara au dalili
ya kuondolewa kwa taifa zaidi sana kuliko kutoa sadaka kwa sanamu. Kuondolewa
kwa kiumbe ambaye dhambi ilimsumbua kama alivyoingia kwenye taifa ni kwa wazo
lile lile kama ondoleo au kufungwa kwa Shetani katika siku za mwisho (Ufu.
20:1-10).
Chimbuko
la hii Sammaeli inatokana na mtazamo wa ukengeufu (inafafanua SHD 8037) na, kwa
hiyo, ilisafirishwa na giza na kwa hiyo, kaskazini kwnye upande wa kaskazini
mwa kizio cha dunia au upande wa mkono wa kushoto (SHD 8040). Huu ni upande wa
mkono wa kushoto wa Mungu kama inavyopata upinzani kwa upende wa mkono wa
kushoto. Jina Shammai (kwa mujibu wa SHD 8060) ina maana ya chenye kuharibu (tazama
SHD 8073).
Kristo
alikuwa upande wa mkono wa kuume wa Mungu. Azazeli au Shetani alikuwa upande wa
mkono wa kushoto.
Kwa
hiyo, hakuna shaka yoyote kuwa Azazeli alijulikana na marabi na kwenye hekalu
la pili katika dini ya Kiyahudi kama inavyoonekana kwa kupewa uweza kwa wazo la
mataifa la Israeli kiumbe yule alijulikana kama ni mshitaki wa Israeli,
Shetani. Ilijulikana kama Sammaeli katika nakala za maandiko ya marabi. Jina
hili linaweza kuchukuliwa kwa maana ya Jina au Jina la Mungu, au
Mungu amepewa jina. Kwa hiyo, angeweza kueleweka kuwa imetendwa kwa jina la
Mungu au mamlaka kwa hatua moja. Kiumbe aliyepewa uweza kwenye juu ya Jeshi la
malaika kwenye Kitabu cha Henoko ni Semyaza neno ambalo linaweza kuwa
limechukuliwa kwenye maana ya asili yenye maana sawa na hii. Jina hili la S[h]emyaza
(hzhYmv) maana yake ni Anaona jina au jina lililoonekana
(tazama kwenye jarida la Knibb, p.67-68). Noth (Die Israelitischen
Personnanamen im Rahmen der Gemeinsemitischen Namengebung, Stuttgart, 1928,
p. 123f.; cf. Knibb p. 68) inahusianisha na jina Shem (mv) na jina la kimbinguni HaShem (svh) ambalo lilijulikana
kutoka katika nakala za maandiko Maarufu. Jina hili, kama lilivyo HASHEM, (svh) linatumika kwenye maandiko ya kale ya
kwenye mawe maarufu yalijulikana kama Chumash kwa ajili ya kutaja Yahova.
Majina ya wote wawili, yaani Semyaza na Asaeli yanaonekana kuwa yamebadilishwa
kwenye sura za awali za kitabu cha Henoko. Katika nakala za aya za Kiethipia za
1Henoko 8:3, jina Semyaza limebadilishwa kabisa kutoka maana yake halisi
ya asili. Knibb anadhani kuwa nakala hizi za Kiethiopia zimepotoshwa (Knibb,
p.71). neno Shemu maana yake ni jina moja. HaShem maana
yake ni Jina maarufu. Linatamkwa shame. Wazo linatokana na
mtazamo ulio dhahiri na nafasi iliyo ya wazi sana. Ni jina la kicheo
linalotumika kutofautisha au kuweka alama ya mtu binafsi yake. Wazo ni kwamba, Shemyaza
au yeye aliyeona jina alishindwa kutokana neema na kwa hiyo
akataabika na mabadiliko ya kicheo yaliyotokana na mabadiliko ya jina. Kwa
hiyo, ndivyo ilivyotokea pia kwa Asaeli. Azazeli ni badiliko kwenye cheo cha
kiongozi au kiongozi wa Jeshi lililoasi na kuangushwa. Wazo hili la mabadiliko
ya cheo hayajatathminiwa mahali popote kwa sababu inapingana na mawazo
yaliyokualika kidini ya mfumo wa baadhi yao. Azazeli anaonekana pia kwenye Gombo
lililogunduliwa kwenye Bahari ya Chumvi (kwa kifupi DSS) katika sehemu
ijulikanayo kama 4Q180-181 ambapo panapelekea katika kifungu kingine cha 4Q180.
Inaonekana kuwa ni nukuu za aya za kitabu cha 1Henoko sura za 6-11 na Yubile
4:22 (Mwa. 6:1-2,4). Aya hii (na hasa hasa mistari ya 5-9) inaonekana kuwa na uhusiano
na hii 4Q181 sehemu ya 2, mistari ya 1-4 (kwa mujibu wa Wise, Abegg na Cook
kwenye jarida lao la Gombo la Bahari ya Chumvi: Tafsiri Mpya, ya Hodder
na Stoughton, 1996, pp. 238-239). Hakuna shaka yo yote kuamini kuwa Azazeli
anaaminika kuwa ni kiongozi wa lile Jeshi la malaika waasi, kwa mujibu wa aya
za kwenye lile gombo la DSS na anawajibika kwa dhambi zote zinazofanywa na
wanadamu kama tunavyoweza kuona katika kanuni za Upatanisho.
Matumizi
ya HaShemu kama Jina maarufu badala ya kuongelea jina la Yahova
ambalo linawakilisha mamlaka ya Mungu akiwa kama ni kiumbe anayejitanua
anayeonekana kutokea kwenye matendo ya kale ya kipagani. Matumizi haya
yamenakiliwa kwenye kazi Kubwa na maarufu. Matendo haya pengine yalitokea kote
kuwili yaani kwa Wamisri na Wababeli na hatimaye yakaingia kwa Wayunani na
Warumi. Imehusianishwa na teolojia inayo amini kuhusu “Majina Matakatifu” na
imani za kishirikina za kizamani zinazodai kuwa na uweza wa kimungu kwa
matumizi sahihi ya jina. Kwa hiyo, mungu msimamizi wa Warumi hakutajwa kamwe na
siri ililindwa kwa maumivu ya kifo. Wazo lililokuwepo lilikuwa ni matamshi
sahihi ya jina na maadui kungewawezesha waaguzi wao kumiliki uweza wa ulinzi wa
kimungu na hivyo kwamba wangeweza kukamata taifa kwa maswali. Wazo hili huenda
likawa ni msingi kwa ajili ya matumizi ya nano HaShemu badala ya Yahova
miongoni mwa Wayahudi baada ya utumwa wa Wakaldayo.
Hakuna
tatizo katika kuelewa kile kinachotokea katika Upatanisho uliochukuliwa kutoka
kwenye mafungisho ya teolojia dhaifu zenye mamlaka kwazo zenyewe tu. Beberu la
mbuzi aliyechaguliwa kwa Azazeli alikuwa ni ishara ya taifa iliyowekwa juu ya
kichwa chake na kwa kuhani aliyekuwa kwenye zamu au mwandishi au mwenye hekima
(itategemea jinsi anavyojua) na kupelekwa katika nchi isiyozaa kitu, kama vile
jangwani na kwenye ardhi isiyotoa mazao yoyote. Kwa maneno mengine, mtunda au
matokeo ya mbuzi huyu ilikuwa ni kuachwa ukiwa (tazama Law. 16:21-23 katika
Soncino na nakala zingine).
Ushahidi
wa historia uko kinyume cha tafsiri ya kuwa mbuzi wa Azazeli anamwakilisha
Masihi. Hata hivyo, mtazamo huu umetokana na idadi ya nyanja tunazoweza
kutathmini hapa kwa kushughulika na somo hili. Pia kuna maelekezo ya tatu
ambayo tutayafanyia tathmini pia.
Bullinger,
kwa mfano, alishikilia kuamini kuwa wale mbuzi wawili walikuwa wanamlenga
Kristo. Hata hivyo, utimilifu huo wa mambo mawili unahusisha kupigwa kwa kura
mbili – yaani moja ikiwa ni ya Yahova na nyingine ikiwa ni ya Azazeli. Ili
kuweza kuupa haki utambulisho wa umoja, utambulisho wa jina la pili hufutwa na
kupigiwa kura au kujumlishwa kwa maana ya kuruhusu au kama maana sawa ambayo
haiwezekani kutokana na elimu ya asili ya maneno.
Imekuwa
sasa ni suala la duniani kote kwa kupitia kwenye aya za maandiko matakatifu ni kama
inavyoonekana katika kila mojawapo ya mawazo haya.
Mambo ya
Walawi 16:1 inasema: BWANA
akanena na Musa, baada ya kufa kwa hao wana wawili wa Haruni. walipokaribia
mbele za BWANA, wakafa,
Huyu ni
Yahova anayesema na Musa. Usemi wa Yahova akanena umetumika katika
kitabu hiki cha Mambo ya Walawi mara thelathini na tano kwa nyakati tofauti na
katika njia zenye maana kumi mbali mbali.
Alinena:
Kila
moja ya tofauti hizi zinaeleweka kutoka kwenye maana yake. Bullinger anaweka
alama kwa tofauti hizi hizi kwa jinsi anavyoielezea Mambo ya Walawi 5:14.
Hapa
katika sura hii ya Mambo ya Walawi 16, tunaona kuwa Musa anapewa amri ili ampe
Haruni ili kwamba asisogelee Mahali Patakatifu kiholela, hadi pale tu
atakapopewa maelekezo, kama vile katika siku ya Upatanisho ili asije akafa,
kama Yahova alivyokuwa anatokea kwenye wingu hapo kwenye kiti cha rehema au alivyokuwa
anafunika kwenye Sanduku la Agano (tazama jarida la Sanduku la Agano [196].
Katika
aya ya 1 tunaona kuwa watoto wa Haruni walikufa kwa sababu walitoa sadaka kwa
Yahova. Lugha ya Kiebrania imeiweka karibu (karab). Maneno yasemayo moto
wa kigeni yameongezwa kwenye maandiko ya kale (Onk. Jon., ya Septuagint
yaani LXX, ya Kisyria, na Vulgate kama ilivyoonyeshwa na Bullinger; n. hadi
kwenye 16:1).
Mambo ya
Walawi 16:2 inasema: BWANA
akamwambia Musa, Sema na Haruni ndugu yako, kwamba asiingie wakati wowote
katika mahali patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kiti cha rehema, kilicho juu
ya sanduku, asije akafa, maana, mimi nitaonekana katika lile wingu juu ya kiti
cha rehema.
Hapa aya
hii ina maana sio tu kwa wakati mwingine wowote. Mahali
Patakatifu panapoongelewa hapa ni Patakatifu pa Patakatifu. Sura hii
aitumii neno hili la Patakatifu pa Patakatifu lakini tu neno Mahali
Patakatifu (aya za 3,16 mara mbili, 20,23,27, pia tazama Kut. 3:5, kwa maelezo
ya Bellinder).
Kwa
hiyo, kuna kitu kinacho elezewa hapa kwenye mfano huu ambacho ni kitu cha
kupita. Kijina rehema pia hutumika kijisifa. Usemi wa Nami nitatokea ni Nami
sitatokea (tazama Kut. 25:22).
Mambo ya
Walawi 16:3 inasema: 3Haruni akaingia katika patakatifu na
vitu hivi; ng'ombe mume mchanga kwa sadaka ya dhambi, na kondoo mume kwa sadaka
ya kutekelezwa.
Neno kwa
hiyo kwa kweli lipo nayo. Haruni ameelekezwa kuleta damu za mafali
ya ng’ombe kwa ajili ya dhabihu za dhambi na kondoo waume kwa ajili ya sadaka
za kuteketezwa. Hili lilikuwa ni tendo la utakaso wa Mahali Patakatifu na
kuhani mkuu. Hii ilifanyika kwa maana maalumu na mavazi yalikuwa ni ya aina
maalumu.
Mambo ya
Walawi 16:4 inasema: Ataivaa ile kanzu
takatifu ya kitani, atakuwa na zile suruali za kitani mwilini mwake, atafungwa
ule mshipi wa kitani, naye atavaa ile kofia ya kitani, hayo ndiyo mavazi
matakatifu, naye ataoga mwili wake majini, na kuyavaa.
Vazi la
hariri la kuhani mkuu hapa lina ashiria kama alama ya ujio wa kwanza wa Masihi
wa Haruni, au kama Masihi kuhani. Alikuwa bado hajawa Masihi mfalme. Mfalme
Masihi aliwakilishwa na kanzu ya kifalme ya utawala na hii iliwakilisha ujio wa
pili, na sio wa kwanza. Utendaji huu wenye maana mbili wa Masihi akiwa kwa
sehemu zote yaani kama mfalme na kuhani mkuu ilieleweka na dini ya Kiyahudi
mapema sana kabla ya Kristo.
Sasa
inaeleweka kutoka kwenye lile gombo la bahari ya chumvi yaani DSS kwenye.
Sheria au kanuni za mjini Damascus (VII) na vipande kutoka kwenye pango IV
ambayo Masihi wote wawili ilieleweka kuwa ni Masihi mmoja (tazama jarida la G.
Vermes la Gombo la Bahari ya Chumvi lililoandikwa kwa lugha ya Kiingereza,
toleo la 2., uandishi wa Pelican, 1985, kifungu cha 49).
Mambo ya
Walawi 16:5 Kisha
atatwaa mikononi mwa mkutano wa Waisraeli mbuzi waume wawili, kwa sadaka ya
dhambi; na kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa.
Neno
hili lililotafsiriwa wana mbuzi ni mbuzi waume au beberu wenye fujo
au utukutu.
Mambo ya
Walawi 16:6 inasema: Na Haruni atamtoa yule ng'ombe wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili
ya nafsi yake, na kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, na kwa
ajili ya nyumba yake.
Tunaona
hapa kuwa ng’ombe dume alifanyika kuwa ni sadaka ya Upatanisho kuhani. Hii
ilikuwa ni wawmu ya kwanza. Masihi alistahili kama kuwa na sifa kama kuhani
mkuu kabla haja fanya maombi ya kuombea msamaha.
Dhabihu
hii ya ng’ombe mume na kondoo mume walioelezwa hapa walitumika pia kutathmini
maafa ya nabii katika Israeli kama tuonavyo sasa kutoka kwenye gombo la bahari
ya chumvi yaani DSS (kwa mujibu wa Wise, Abegg na Cook, ibid, kurasa aa
336-337). Josephus kwenye jarida lake la Kupingana na Apioni anasema
katika (1.8; tazama tena kwa Wise, Abegg na Cook, ibid., ukurasa wa 336,
iliyokaririwa kwa makosa kama 1.41).
Kuanzia wakati Artashasta
mpaka siku zetu hizi kumeandikwa historia nyingi sana kamilifu, lakini
hazichukuliwi kama zinazostahili kuaminiwa na nakili za zamani sana kwa sababu
ya kutokuaminika kuhusu ufuasi uliochukua mahala pa manabii waliotangulia.
Kwa
hiyo, manabii waliendelea lakini kulikuwa na mabishano kama katika uthabiti na,
kwa hiyo, kanuni ilifungamanishwa na Ezra katika mwaka huo huo kama mfalme
Iskanda Mkuu (tazama kwenye uandishi wa Seder Olam Rabba 30 na jarida lisemalo Biblia,
[164] na lile la Manabii wa Mungu [184].
Mambo ya
Walawi 16:7-8 inasema: Kisha atawatwaa wale mbuzi wawili na kuwaweke mbele za BWANA
mlangoni pa hema ya kukutania. 8Na Haruni atapiga kura juu ya wale
mbuzi wawili, kura moja kwa ajiri ya BWANA, na kura ya pili kwa ajili ya
Azazeli.
Neno
hili la mbuzi mhanga hapa limetafsiriwa kutoka kwenye neno lililo katika
mrengo wa Lunga ya Kiebrania ambalo linadhaniwa na baadhi kwa kumaanisha kuondoa
kabisa. Kwa mfano, mwandishi Green (katika Biblia ya Intrlinear, ukurasa
wa 102) kumewekwa neno kama lilivyochukuliwa kutoka katika SHD 5799. Neno
hili linamaannisha kwa maana ya namna zote mbili za mbuzi wa mhanga na
pili ni kwa maana ya kuondolewa kabisa (tazama ukurasa wa 102). Hata
hivyo, neno moja linahusishwa, liitwalo al Azazeli (lzazl). Kiuwazi kabisa, neno moja linachukuliwa
kuwa na maana mbili tofauti na halmashauri ya Septuagint yaani LXX, kwa mujibu
wa Biblia tafsiri ya mfalme Yakobo maarufu kama KJV na kwa mujibu wa Green ili
kuwezesha tafsiri hii. Gombo la bahari ya chumvi maarufu kama DSS na aya za
kane ya kwanza KK zinashikilia kuamini kuwa Azazeli waki maanisha kuwa ni
kiongozi wa Jeshi la malaika waasi.
Wasomaji
wa Biblia iitwayo kama Soncino Chmash kusoma aya hii kwa kusema kuwa:
Na Haruni
atawapigia kura mbuzi hao wawili; kura moja ni kwa Bwana na mwingine ni kwa
azazeli.
Wasomaji
wa Biblia ya Kiingereza ya RSV husoma aya hii ikisema:
na Haruni
atapiga kura kwa mbuzi hawa wawili, kura moja ni kwa Bwana na mwingine kwa
Aza’zeli (RSV)
Kwa
hiyo, pia ilipelekea na toleo la Stone ya Chmash isemayo:
Haruni
ataweka kura kwa mabeberu ya mbuzi wawili: kura moja kwa “HASHEMU” na mwingine
kwa “Azazeli”.
Mmbo ya
Walawi 16:9-10 inasema: Na Haruni akaleta
mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya BWANA, na kumtoa awe sadaka ya dhambi.
10 Bali yule mbuzi aliyeangukiwa na kura kwa ajili ya Azazeli
atawekwa hai mbele za BWANA ili kumfanyia upatanisho, ili kumpeleka jangwani
kwa ajili ya Azazeli
Neno
hili fell hapa katika Lugha ya kiebrania lina maana ya njoo hapa. Kwa maneno
mengine, lilitokea kwenye kimkoba kilicho kuwa kinajumuisha Urimu na Thumimu
liliokuwa na maana ya kuchukua kura za Yahova au hukumu (tazama kitabu cha
Kutoka 28:30).
Aya hii
ni kipande chenye matata. Watu wanaweka madai ya kuondolewa kote kwa
Azazeli na hakuna muundo wa neno ambalo wanaweza kuutumia katika kuelezea.
Stone anaonyesha aya hii ikisema:
9 Na Haruni atamleta karibu mbzi mume
aliyeangukiwa kura kwa HASHEMU. Na kumfanya kuwa ni sadaka ya dhambi. 10Na
mbuzi huyu mume aliyeangulkiwa na kura kwa Azazeli atasimamishwa akiwa hai
mbele za HASHEMU, ili kufanya upatanisho kwa yeye, na kumpeleka kwa Azazeli
jangwani.
Hakuna
mashaka kuwa neno limechukuliwa na umaarufu wa marabi wasomi ili kumaanisha Azazeli.
Neno lililotumika kwenye kila tukio ni al Azazeli lzazl.
Stone
anasema neno hili linamaana ya uimara la na uweza (la). Mtazamo huu
unachukuliwa na mamlaka ya kirabi katika kitabu cha fafanuzi cha Soncino pia
(tazama mwanzoni hadi kufikia ukurasa wa 706). Kwa hiyo, Biblia ya Kiingereza
inayoitwa Oxford Annotated ya RSV, Soncino na kwenye chimbuko katika Strong
wote wamekubali. Mtazamo wa mrengo unaopinga umeliweka hili kwenye SHD 5799
ikihitaji tofauti mbili na maana tofauti kwa neno moja ambalo Strong hakuweza
kwa kweli kuelekeza. Kuna kitu fulani kibaya ambacho kwayo uwekaji wa maneno
umehusishwa. Kamusi ya SHD 5799 ambayo kwayo, ‘aza’zeli ameandikwa kama
mjumuidho wa maneno mawili kwa mujibu wa kamusi ya SHD 5795 na 235 na, kwa
hiyo, huleta maana ya mbuzi wa kuondoka. Hii kupelekea mijumuisho kama
maana mbuzi kwa mujibu wa kamusi ya SHD 5795 isemavyo, ‘ez au aze
lenye maana ya jike la mbuzi lenye maguvu ktika muundo wa kisarufi wa
umoja lakini jike kwa maana ya uwingi pia manyoya ya mbuzi. Neno hili
hutokana na kamusi ya SHD 5810 isemayo ‘azaz shina kuu lenye nguvu,
lenye kuwa gumu, au kuwa imara kujiimarisha wenyewe, au kujiimarisha.
Hali hii ya kujitegemea inayoonekana nayo ni wazo la kunyenyekeana katika
mujibu wa sheria. Neno hili linachukuliwa kuwa limeunganishwa na kamusi ya SHD
235 lisemalo ‘azal likiwa ni chanzo kikuu katika kwenda zake, na
hivyo humaanisha kutokomea, kuanguka, kuishilia mbali, kwenda huku na
huko. Neno hili linatoka katika kitabu cha nabii Ezekieli 27:19 kwa
wengi kama kutoka Uzal na kwa wngine kama kitani. Ina maana ya kutokwa
au kutumiwa. Green anasema inaendelea mbele. Biblia ya Kiingereza ya
KJV inasema ni tendo la kutembea huku na huko yaani kutanga tanga.
Bibliia ya Soncino inasema ni kama kitani kwa msingi wa me’uzzal
katika aya za biblia anafahamika kwa kujusha shina azal (na Aleph) kwa
lugha ya Kiaramu azal (na ain), kusokota. Maandiko halisi mbali mbali na
kadhaa ya Kiebrania na Septuagint au LXX husoma me’uzzal, ‘kutoka
Uzzal’. Jina hili lipo katika Mwanzo 10:27 na ni muonekano wa Sanaa, mji mkuu
wa Yemeni katika Kaskazini ya bara Arabu. Tafsiri hatimaye ingekuwa ni Vedan
na Javan uliyetolewa au kupelekwa na majengo ya Uzzal.
Matumizi
ya shina la neno azal ni mbali na uwekaji sawa na muungano wa neno ‘azazel
linaloweza kuwa na maana kujiimarisha yenyewe el na pia mbuzi
wa anguko au mbuzi aendaye huku na huko au kutanga tanga jangwani.
Al’Azazel huweka kijina halisi cha nano. Hii inaonekana kuwa viumbe wawili
halisi iliyohusishwa na wanahusisha mbuzi wote wawili – mmoja akiwa ni kwa
Yahova na wapili ni kwa kwa makusudi mengine au kwa mahali paitwapo al’Azazel.
Hii ingeongeendeleza pia ufafanuzi matumizi ya jinsi ya kutofautisha kati ya
kondoo na mbuzi katika mfano wa jinsi mataifa yatakavyo tenganishwa katika
(Mat. 25:31-34) wakati wote wawili wakiwa wenyewe ni wanyama safi wasio najisi.
Je, kuna
wazo gani linaloelezewa hapa? Neno hili linaonekana pia kujumuisha neno rahisi
tsav katika (SHD 6673) ambalo maana yake ni kuweka njia panda, amri au fundisho.
Hii tsawlatsaw ni fundisho juu ya fundisho kutoka ambako sheria imewekwa
imara (tazama pia jarida lisemalo Wanikolai).
Hapa
tunaonekana kuwa tunaona kuwa neno likabiliana nafundisho ya Mungu. Amri za
Mungu zilizo kwenye sheria ni zile zilizowekwa juu ya mbuzi. Je, ‘Azazeli
lilikuwa na maana gani basi? Tunajua kuwa kulikuwa na mtazamo wa wenye
kuchanganya au kuunganisha majina ya Asaeli las na Azazeli lzaz kwenye nakala za maandiko ya zamani na
Knibb inayoweka alama ya ukweli huu katika tafsiri ya Kitabu cha Kiethipia
cha Henoko (vol. 2, Oxford, p. 73).
Neno
Asaeli maana yake ni Mungu amefanya. Azazeli maana yake ni kitu kingine
tena. Knibb anashikilia kuamini kuwa inaelekea maandishi ya Kiethiopia ya
Henoko katika sura ya 8:1 yametokana na uharibifu wa Asaeli au Mungu
aliyefanya katika nakala za maandiko ya Kiethiopia au Kiyunani. Kwa hiyo
‘Azaeli anafanyika hapa kuwa ni ‘Azazeli kwa mujibu wa Knibb. Mabadiliko huenda
yasiwe uharibifu lakini ni dalili ya mabadiliko ya wadhifa. Badiliko katika
wadhifa huwa sawa na mabadiliko katika jina kitu kilicho sawa na hicho. Kristo
amepewa jina jipya katika kitabu cha Ufunuo kwa sababu aliendana na mabadiliko
ya heshima ya wadhifa wake. Kwa namna inayolingana na hiyo, sisi pia tumepewa
jina jipya linaloashiria wadhifa wetu mpya. Kitabu cha Kiethiopia cha Henoko
kinaonekana kufanana na maandiko ya Mambo ya Walawi 16:21 na pia kinaunda wazo
linalopatikana katika Targumi wa Pseudo Jonathan katika maandiko haya kama
inavyofananishwa katika sehemu ya Dudaeli. Maandiko haya husomeka kama hivi
katika sura ya 10:
4 Na zaidi sana Bwana akamwambia Rafaeli
akasema: ‘Mfunge Azazeli mikono yake na miguu yake, kisha atupwe kwenye giza.
Kisha utenganishe wazi jangwa lililoko dudaeli na umtupe huko. 5 Na
(2v,b20) umtupe ukingoni na kwenye mawe makali, kisha umfunge usoni kwa
kitambaa cha giza; na kisha umwache pale milele, na umfunike uso wake ili
kwamba asione mwanga. 6 Na kisha katika siku iliyokuu ya hukumu
atupwe motoni. 7 Na ifanyiwe matengenezo dunia ambayo iliharibiwa na
malaika waasi au mapepo, (2v, b25) kisha.kutangazwe matengenezo ya ulimwengu,
kwa kuwa nitaitengeneza dunia ili kwamba wana wote wa wanadamu wasiangamizwe na
siri fumbo za kila kitu a,bazo Watazamaji wajulishwe na wawafundishe
watoto wao. (Knibb anaema kuwa maana ya neno wajulishwe au funuliwa ni
ya lazima hapa).
kitu
muhimu kukitilia maanani hapa ni kwamba mbuzi huyu alikuwa hatumiki kwa ajili
ya upatakisho lakini zaidi sana ni kwamba upatanisho ulifanywa kwa ajili hii.
Kwa Kiebrania inasema kwa ajili yake na sio ndani yake. Kwa hiyo,
hatimaye mbuzi aliachiliwa huru.
Kinacho
fikiriwa hapa kuhusu Dudaeli ni kuaminika na Dillmani (ona Tafsiri 100)
ili kuweza kuvumbuliwa na kuiiga kutoka kwenye jina wenye kumpinga Mungu.
Charles katika tafsiri yake ijulikanayo kama (Tafsiri 22) humuunganisha
Dudaeli kutoka jinsi ilivyotajwa na Targumi Pseudo Jonathan kama mahali ambapo
mbuzi aliwekwa wakfu kwa Azazeli alivyoongozwa. Kwa wakati mmoja, Miliki
alikubali ufafanuzi huu na kuchukuliwa jina kutoka kwenye Michongoko au
maporomoko ya Milima ya Mungu. Neno cheza mchezo wa kutupa kwenye
maporomoko na mawe makali linachukuliwa na Knabb kufanya tuhuma zi mkuu
(Ibid, p.87).
Kwa
hiyo, fikra inatuama katika kitabu cha Henoko na Targumi ambavyo vimechukuliwa
kutoka kwenye fikra inayopatikana katika kitabu cha Torati humu kwenye Mambo ya
Walawi 16. Mtazamo huu umethibitika na Gombo la Bahari ya Chumvi maarufu kama
DSS. hata hivyo, mbuzi huyu alikuwa hauawi ila badala yake aliachiliwa aende
zake atange tange jangwani.
Tunaona
mamlaka ya marabi hayakuwa na maida kamili ya maandiko ambayo sasa inapatikana
kwetu lakini walikuwa na wazo linalohusiana na jambo lenyewe kama lilivyokuwepo
kwenye Torati. Jambo muhimu zaidi sana, ni kuwa jina Azazeli ni linaonekana
sana likilenga katika kitabu cha Mambo
ya Walawi 16. Ilikuwa, zaidi ya yote, ilionekana na kueleweka kuwa hapa kutoka
katika maandiko ya kale ya mfumo wa Kiyudea.
Hii
inatuongoza sisi kuelekea kwenye mtihani zaidi wa mchakato endelevu wa majina
ya Jeshi la malaika. Je, ni kwa jinsi gani Asaeli au hata Semyaza limekuja kuwa
kuitwa Azazeli? Je, ni lini basi jambo hili lilikuja kutokea na jambo hili lina
maana gani?
Ni
dhahiri kuwa jina Azazeli liliandikwa kwenye muundo wa zamani wa Torati.
Sptuagint, yaani LXX ilitafsiri maandiko haya kwenda kwenye Lugha ya Kiyunani
kama ikionyesha mbuzi wa mhanga na Kiyunani kinashikilia kumaanisha kuwa ni
kumpeleka mbali kwa ajili ya kumuondoshelea mbali (tazama nakili za tafsiri za
Brenton). Hata hivyo, maoni haya mawili tofauti yana ashiria kwenye maneno
yaliyotafsiriwa kama mbuzi wa mhanga katika Septuagint yaani LXX. Fikwa hizo
hizo zinachukulia kwenye tafsiri ya Biblia ya Kiingereza ya mfalme yakobo maarufu
kama KJV. Kamusi ya Strong inaweka ujenzi unaoegemea kwenye maana ya SHD 5799
kama kuwa kutoka kwenye SHD 5795 na SHD 235 zaidi sana kuliko ilivyokuwa tu
kutoka kwenye SHD 5810 na rahisi zaidi ‘el. Muunganiko wa maneno hauna maana ya
kujiazima yenyewe kiasi cha kufikia matumizi rahisi ya neno el (SHD 410). Neno
hili linaonekana kuwa kwenye ubora wa azel lza
(kutoweka
au kukwea, au vile vile uzal au kitani, kama katika SHD 235, SHD 236). Kwa hiyo
sisi tunaonekana kuwa na shitaka la mbuzi aliyepotea au kutelekezwa.
Tafsiri zenye Maana mbili: majibu yenye maana mbili
kwa pamoja
Kuna
jibu jingine ambalo lingeweza kujumuisha maana zake. Mbuzi mwenye kujiitutumua
pia ni el mwenye kujitegemea. Tatizo ni kwmba mbuzi hawa ni wakiume na sio
majike. Kwa hiyo, neno kuteuliwa sio sahihi kwa vile tu ni mbuzi mmoja ambaye
hana maana nyingine yeyoye ya zaidi. Mbuzi huyu anaweza kuwa ni jike katika
hali ya umoja kama lilivyo kanisa na wakiume katika uwingi kama tulivyo wana wa
Mungu. Mbuzi alitelekezwa jangwani wa Yubile arobaini baada ya kutolewa dhabihu
kwa Masihi, ambaye ni mbuzi wa Yahova. Wote wawili yaani Masihi na kanisa
walijulikana na kukusudiwa tokea mwanzo wa kuwekwa kwa misingi ya dunia. Kwa
hiyo, pia, mpango umepigiwa dira kwa Jeshi lote zima la malaika na ukombozi wao
na upatanisho (tazama jarida la Kondoo Aliyepotea na Mwana Mpotevu, Na. 199).
Yule joka akamfuata yule mwanamke jangwani (Ufu. 12:10-17).
Vile
vile, mshitaki amefanya dhambi tokea mwanzo (1Yoh. 3:8) walakini alikuwa
mkamilifu tokea wakati wa kuumbwa kwake mpaka pale uovu ulipoonekana ndani yake
(Eze. 28:15). Kwa hiyo, mwanzo unaosemwa hapa sio wanzo wa uumbaji.
Kuna pia
jambo lingine la kulitilia maanani. Katika Septuagint, yaani LXX, kuliandikwa
kule Alexandria chini ya uangalizi wa Ptolemy Philometor. Mfumo wa mchanganyiko
kati ya Wayunani usingeweza kuvumilia fikra za kimaongozi za kutoka kwa Yahova
katika Yerusalemu chini ya sheria, na kufungasha kwa utawala wa mataifa. Kwa
sababu hiyo hiyo, kunaona kwamba mfumo wa mwamini utatu mmoja maarufu kama
Christian - iwe kwamba alikuwa ni kutoka Rumi au Canterbury – asingeweza
kukubaliana kuwa utawala wa Masihi haukuwa ni Kanisa chini ya mfumo wake uliopo
wa amri ya sheria lakini zaidi sana ulikuwa unakwenda kuungwa mkono na Azazeli
aliyetolewa kwa kipindi cha maelfu ya miaka. Umilenia (au Uchiliani kama
ulivyokuwa ukiitwa na kanisa la kwanza) umekuwa ukifutwa kama fikra kwa sababu
unapingana na mawazo ya utawala wa Rumi na wa kanisa la kutoka Rumi. Kwa sababu
hiyo hiyo, mamlaka ya marabi yasingeweza kuichukulia hii katika awamu
inayofuata ya tafsiri ni sawa na wangalivyo weza kumtambua Masihi kuwa anakuja
kwa awamu mbili na awamu ya pili ingeweza kuwa kulingana na Kitabu cha Ufunuo
kinavyosema ambacho chenyewe tayari wameisha kukikataa. Kwa hiyo, jambo lenyewe
lilikuwa halijafunuliwa bado katika ufasaha wake kama siri ya Mungu. Wakati
ilipofunuliwa na Masihi, kisha ilikuja kufichika kwa uwazi iwezekanavyo na
waumini wa dini ya Kiyahudi. Kama mbuzi alihusishwa, inahusisha pia fikra ya
kutanga tanga, na kwa hiyo uuaji wa mbuzi ni kwenda kinyume na fikra hii
iliyohusishwa hapa. Upatanisho umefanywa na mbuzi na ameachwa huru, bila
kuuliwa (tazama hapo juu kama anavyosema Bullinger, katika Biblia
iitwayo.Companion Bible, n. hadi v. 10)
Uficgaji
wa marabi wa maana yake katika fikra ya mbuzi anaye uliwa (wakati ambapo katika
Septuagint, LXX haielezei jambo hili kabisa) inaashiria pia katika siri za
baadae za Wayahudi zaidi kuliko wapinzani wa bidii ya waliokuwa katika imani ya
Kimasihi.
Tunaelewa
sasa kitu kilicho zaidi ya mashaka kuwa fikra hii ilikutikana katika ufunuo
20:4 sisi pia tunaelewa kutokana na Gombo la Bahari ya Chumvi yaani, DSS kama
ilivyokuwa katika ufufuo wa wafu na marejesho katika Milenia (tazama 4Q521
kifungu cha 7 na kifungu cha 5 unganisha na sura ya 2; Wise na Abegg na Cook,
kifungu cha 421). Fikra hii ilikutikana kwenye Ufunuo 21:12-13 ambayo pia
hupatikana katika 4Q554 kifungu cha 1 kifungu kidogo cha 1 msitari wa 9 hadi
kisehemu cha 3 mstari wa 10, ibid, pp. 180-182).
Hivyo
basi, Agabo la Kale liliweza kueleweka kwa mtindo huu kama ulivyokuwa ni lazima
kwenye mpango ingawaje injili hizi (hapa kuna maana ya ile ya Mat. 22:30-32),
1Wakorintho 15:12 na Ufunuo zilikuwa bado hazijatolewa.
Kuna
wazo jingine katika mbuzi aliyetolewa kwa ‘Azazeli jangwani. Masihi aliuawa na
kutumika katika upatanisho. Roho Mtakatifu kanisani aliachwa na kutanga tanga
jangwani kwa kipindi cha yubile arobai au miaka elfu mbili na kwa namna hii hii
alipewa Azazeli kwa kutoa kikamilifu dhambi za ulimwengu. Kwa hiyo, hatimaye
tunapata maana za aina mbili kwa sadaka ya na kwa eneo la dhambi kutawanyikia
jangwani. Jangwa ilikuwa ni ishara ya dhambi na uovu (tazama Isa. 13:21; 34:14;
Mat. 12:43; Lk. 8:27; 11:24; Ufu. 18:2). ‘Azazeli alikuwa ni utambulisho wa
yote yaliyokuwa makuu na yakutisha hapa (tazama Kum. 1:19; 8:15; Yer. 2:6). Kwa
hiyo, upatanisho ulikuwa na maana tatu kwa Azazeli, kwa ajili ya Azazeli na
kama azazeli. Hapa Mwana wa Mungu, ni Azazeli au mbuzi aliyeanguka na kuasi.
Kwa
jinsi hii pia, tunauona mfumo wa Upatanisho ukifanyika katika kipindi cha
baadae klichofuata kutoka sadaka ya Pasaka ya Masihi. Uvaaji wa baadae wa
mfalme Masihi baada ya kanuni za upatanisho huu unaonyesha utimilikaji mara
mbili wa Masihi na kwa ujio wake. Bullinger anasema maana yake hapa kwa nakili
hii hadi kwenye aya ya 8 akisema kuwa:
Hii ni
‘kwa’ inaonekana kama majibu ya muonekano dadi ‘kwa Yahova’. Kama huyu atakuwa
ni Muovu ambaye amemaanishwa kisha hii itakuwa ni utukufu wake. Kwa kuwa,
katika upatanisho wa aya ya. 10 umefanywa kwa mbuzi huyu, na anatakiwa
aachwehuru aende. Mahali ulipo upatanisho lazima uwepo msamaha. (Tutaendeleza
mtihani huu katika aya ya 22)
Maelekezo
haya fikra ya rehema na wema wa Mungu. Upatanisho, mwisho wake, umeendelea hadi
kwa Jeshi la malaika waasi kama utandaji wa neema ya wema wa Mungu na utimilifu
wa dhabihu ya Kristo katika zoezi la uwezo wa Mungu wa kuwepo kila mahali
(tazama jarida la Hukumu ya Mapepo, Na. 180).
Mambo ya
Walawi 16:11-12 inasema: Na Haruni atamsongeza ng'ombe wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili
ya nafsi yake, na kufanya upatanisho kwa ajili yanafsi yake mwenyewe, na kwa
ajili ya nyumba yake; naye atamchinja yule ng'ombe wa sadaka ya dhambi, aliye
kwa ajili ya nafsi yake 12 Kisha atatwaa chetezo kilicho na makaa ya
moto yatokayo katika madhabahu iliyo mbele za BWANA, na kozi mbili za uvumba
mzuri uliopondwa sana mikononi mwake, naye atauleta ndani ya pazia.
Moto huu
ulichukuliwa kutoka madhabahuni mahali ambapo dhabihu ya Upatanisho ulifanyika.
Moto ule peke yake ulifaa kuwashia uvumba katika madhabahu ya dhahabu katika
Mahali Patakatifu (tazama Law. 10:1,7 na vile vile nakili za Bullinger hadi
10:1,7). Moto huu ulikuwa unafanana na ule wa Roho Mtakatifu. Moto mwingine
wowote mbali ya huu ulikuwa ni moto wa kigeni. Kumbuka kuwa watoto wa Haruni
waliuawa kwenye dhabihu hii. Tunaona pia kuwa ubatizo wa Yohana mbatizaji
ulikuwa sio wokovu. Roho Mtakatifu alikuwa ametolewa na Mungu moja kwa moja
baada ya ubatizona alichagua kutenganisha na ukuhani mpya moja kwa moja. Yohan
alikuwa ni mtoto wa kuhani mkuu wa Abia na ni Mlawi, hata hivyo ubatizo wake
haukumpeleka kwenye wokovu. Kwa hiyo, zaidi sana, mfano huu unaelekeza kwenye
tukio lile.
Mambo ya
Walawi 16:13 inasema: Kisha atatia ule uvumba juu ya moto mbele za BWANA, ili moshi wa ule
uvumba ukistiri kiti cha rehema kilicho juu ya ushuhuda, asije akafa.
Hakuna
mtu aliyewahi kumuona Mungu (Yoh. 1:18; 1Tim. 6:16; 1Yoh. 5:20). Ni kuhani mkuu
tu alibakia Mahali Patakatifu na kisha na ni kwa siku ya Upatanisho tu na ni
mara moja kwa mwaka. Hii iliashiria kwa Kristo akiwa kama kuhani mkuu na kwa
ajili ya ufufuo wa wafu. Masihi alkkuwa ni mwana wa Mungu mwenye nguvu toka
kufufu kwake kutoka kwa wafu (Rum. 1:4).
Mambo ya
Walawi 16:14 inasema: Kisha atatwaa baadhi ya damu ya yule ng'ombe, na kuinyunyizia kwa
kidole chake juu ya kiti cha rehema upande wa mashariki; na mbele ya kiti cha
rehema atainyunyiza ile damu kwa kidole chake mara saba.
Hapa
tunaona kuwa ng’ombe mume ameuawa – kwanza ni kwa ajili ya ukuhani ili
kumtakasa kuhani mkuu na hatimaye mbuzi aliuawa ili kutakasa kutaniko. Kisha
hii ilikuwa ni utaratibu wa kudumu. Masihi pia alitimiza masharti yote haya.
Utaratibu huu ulilenga kwenye matukio ya Pasaka inayoishia kutoka siku ya wa 14
hadi ya 15 ya mwezi wa Nisani na halafu hadi kufikia kwenye siku ya Sadaka ya
Mganda wa Kutikiswa siku ya Jumapili asubuhi yapata saa 3 kamili ya asubuhi.
Hii halafu inapimwa hadi saa 3 asubuhi ya siku ya Jumapili ya siku ya
Pentekoste, siku hamsini kamili zinazofuata baadae na kanisa linakuwa limeishavunwa.
Hatua hii inaendelea mbele hadi mwishoni mwa ufufuo wa pili. Jeshi la malaika
waasi na kutaniko la jangwani ni kundi ambalo kwalo mbuzi wa pili hufanya
upatanisho. Sisi kwa hiyo, tuna fikra za mkono wa kuume na wakushoto wa Mungu
ambao ni upatanisho wa dhambi. Damu ya mbuzi wa Yahova inaletwa kwenye Mahali
Patakatifu kwa maana ile ile kama damu ya mafahali. Hii ni kwa wana wa Israeli
ambao ni kanisa.
Mambo ya
Walawi 16:15-16 inasema: 15 Kisha atamchinja yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, aliye kwa ajili ya
watu, na kuileta damu yake ndani ya pazia, na kwa damu hiyo atafanya vile vile
kama alivyo fanya kwa damu ya ng'ombe, na kuinyunyiza ndani ya kiti cha rehema,
na mbele ya kiti cha rehema. 16 Naye atafanya upatanisho kwa ajili
ya mahali patakatifu, kwa sababu ya mambo machafu ya wana wa Israeli, na kwa
sababu ya makosa yao, naam, kwa ajili ya dhambi zao zote; naye atafanya vile
vile kwa ajili ya hema ya kukutania, ikaayo pamoja na katikati ya machafu yao.
Tunaona
kutoka kwenye aya hii kwamba hakutakiwi kuwa na mwanaume yeyote, kwa mfano
hakuna ‘adamu au kiumbe, katika hema la kukutania na pengine linaitwa maskani
hadi pale kuhani mkuu atoke nje na amefanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe.
Kwa hiyo, ukuhani ni ni kitu cha chini katika tendo hili na hakuna ukuhani
wenye kuleta maana wakati ambapo mpinga ashirio yuko kwenye pazia (tazama Ebr.
4:14; 6:20; 9:24).
Mambo ya Walawi 16:17-19 inasema: 17Wala hapakuwa na mtu katika hema ya kukutania, wakati aingiapo ili kufanya upatanisho katika patakatifu, hata atakapo toka nje, baada ya kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, na kwa alili ya nyumba yake, na kwa ajili ya mkutano wote wa Israel. 18Kisha atatoka na kuiendea madhabahu iliyo mbele za BWANA na kufanya upatanisho kwa ajili yake; atatwaa baadhi ya damu ya yule ng’ombe, na ya damu ya yule mbuzi. 19Na kuitia juu ya pembe za madbabahu kwa kidole chake mara saba, na kuitakasa, ili machafu yote ya wana wa Israeli yaitoke. .
Wazo la
kuwa takatifu maana yake ni kuwa mbali au kutengwa mbali na vingine. Ni Mungu
tu ndiye aliye Mtakatifu. Matumizi ya neno hili yanahusiana na kile
kilichotengwa mbali kwa ajili ya kazi yake ya utumishi. Kwenye aya inayofuatia
neno kupatana lina maana ya kufanya upatanisho.
Mambo ya
Walawi 16:20-21 inasema: Naye akiisha kufanya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu, na
hema ya kukutania na madhabahu, atamleta, yule mbuzi aliye hai; 21 Na
Haruni ataweka mikono yake miwili juu ya kichwa cha yule mbuzi aliye hai, na na
kuungama juu yake uovu wote wa wana wa Israeli, na makosa yao, naam, dhambi zao
zote; naye ataziweka juu ya kichwa chake yule mbuzi, kisha atampeleka aende
jangwani kwa mkono wa mtu aliye tayari.
Uwekani
juu wa mikono yote miwili ni kwa maadhimisho na linatumika hapa peke yake.
Tendo hili lina maana ya ukamilifu au kutiiliza ambako kwayo Masihi anachukua
jukumu kama kuhani mkuu na ujumla wa uwekaji wa kanisa na Jeshi la watu wa
Mungu mikononi mwake.
Kwa
jinsi hii, mbuzi wote wawili wanaweza kuwakilisha kikamilifu na Kristo na pia
utimilifu wa Kristo na pia utimilifu wa upatanisho wa Jeshi la kibinadamu na la
kiroho. Kwa jinsi hii pia, hukumu ya Jeshi la malaika walioasi imekwisha
kamilika kama kwa kadiri upatanisho ulivyofanywa kwa ajili yao na kasha
wamepewa kanisa na utaratibu mikononi ili kwamba kwa kushughulika kwao waweze
kupimwa na pia sisi tujaribiwe kwayo. Kwa hiyo, ili Kristo aweze kuishi kama na
katika aina mbili ya mbuzi ingawaje huyu mmoja alitolewa kwa ‘Azazeli na
upatanisho ulifanyika pia kwa ajili yake. Mgongano ni kwamba unahusika. Kama mbuzi
mmoja, Kristo aliuawa katika mwili lakini alifanyika hu hai kama kwa roho. Hii
ni kwa njia ya ufufuo ambako amefanyika kuwa ni mwana wa Mungu katika uweza
(Rum. 1:4; 1Kor. 15:45; 1Pet.3:17). Huyu alikuwa ni mbuzi wa kwanza. Alifanyika
kuwa dhambi kwa ajili yetu ili kwamba tufanyike kuwa wenye haki ki namna ya
mbinguni katika yeye (2Kor. 5:21). Kwa jinsi hii, tulipatanishwa na Mungu na
kupelekwa katikati ya mbwa mwitu. Kwa hiyo, pia, wakati ambapo Jeshi lote la
Mungu likipatanishwa na Mungu na halafu ‘Azazeli alikuwa pia akisamehewa, kama
sisi nasi tulivyofanyiwa, ingawaje haikuwa katika nguvu zake hasa bado.
Azazeli
atafungwa kwa kipindi cha miaka 1,000 cha utawala wa Milenia na alipatanishwa
baada ya hiki.
Mambo ya Walawi 16:22 inasema: Na yule mbuzi atachukua juu yake uovu wao wote, mpaka nchi isiyo watu, naye atamwacha mbuzi jagwani.
Neno
atachukua linaelekea kuchukulia mbali (tazama Isa. 53:4). Nchi isikaliwe kwa
Kiebrania lina maana kuwa nchi itakatiliwa mbali. Janwa la dhambi ni nchi
iliyokatiliwa mbali na Mungu. Upatanisho umefanyika au kutokea kwa mbuzi wa
kwanza. Hapa, kuna matatizo yaliyo changanyika. Kiumbe yuko kwenye uhuru lakini
kutanga tanga jangwani ambako ni kwa jina la ‘Azazeli ambaye yeye mwenyewe anao
upatanisho ambao unafanyika kwa ajili yake mwenyewe. Kama kanisa, tulitanga
tanga kwenye jangwa hili kwa kipindi cha Yubile arobaini kama Israeli walivyo
tanga tanga kwenye jangwa la dhambi kwa miaka arobaini kabla hawajaiingia na
kuimiliki nchi ya ahadi. Wakati walipoingia na ulikuwa ni muda wa kutiishwa kwa
mataifa, walipatanishwa kutoka kwenye Pasaka ya Gilagali. Masihi aliungana nao
kama amiri wa Jeshi la BWANA na kwa muda wa siku saba waliuhusuru mji wa Yeriko
(tazama jarida la Kuanguka kwa Yeriko, na. 142).
Mambo ya Walawi 16:23-28 inasema: Na Haruni ataingia katika hema ya kukutania, naye atavua mavazi yake ya kitani, aliyo vaa alipo ingia katika patakatifu, atayaacha humo; 24 naye ataosha mwili wake kwa maji mahali patakatifu, na kuvaa nguo zake, na kutoka na kusongeza sadaka ya kuteketezwa yake mwenyewe, na sadaka ya kuteketezwa ya watu, naye atafanya upatanisho kwa ajili ya nafsi yake, na kwa ajili ya watu. 25 Na mafuta ya sadaka ya dhambi atayateketeza juu ya madhabahu. 26 Na mtu yule amwachae mbuzi wa Azazeli aende zake, ataosha nguo zake, na kuosha mwili wake kwa maji na baadaye ataingia katika marango. 27 Na yule ng'ombe wa sadaka ya dhambi, na yule mbuzi wa sadaka ya dhambi, ambao damu yao ililetwa ndani ifanye ukumbusho katika patakatifu, watachukuliwa nje ya marango, nao watachoma moto ngozi zao, na nyama yao na mavi yao. 28 Na yeye awachomaye moto atafua nguo zake, na kuosha mwili wake kwa maji, na baadaye ataingia marangoni.
Hapa
tunaona mwili na nguo (ukitoa zile za kuhani mkuu ambazo zinabakia Hekaluni) na
vitambaa vyote vya dhabihu hizi viliunguzwa kwa moto na wale waliokabidhiwa
majukumu haya ambao walitakiwa waoge maji. Hivyo tunaona kwamba damu ya dhabihu
za Masihi inatupatanisha sisi sote na ya kwamba kwa kupitia kwa hiyo tunaweza
kuweka mbali mwili kwa ukamilifu wote na kwamba, kwa njia ya ubatizo,
tunatamani na kuuongojea ufufuo wa roho. Viumbe wote watakuwa wamepewa roho na
fursa ya kutubu, hata ‘Azazeli. Mlolongo huu wa mafuatano ya mambo ni kwa amri
katika ndani ya jangwan ambalo limekatiliwa mbali na Mungu. Kunajisika kwa mtu
binafsi hakutaendelea hadi kwa kuhani mkuu ambaye ni tayari amekwisha takasika
wakati alipozikiri dhambi kwa njia ya mbuzi wa pili. Kutoka katika kitabu cha
mambo ya Walawi 10:17, tunaona kwamba Mungu amemtoa kukupa ili kuchukua udhaifu
na maovu ya kutaniko, ili kufanya upatanisho kwa ajili yao. Hivyo basi,
kukabidhiwa kwa majukumu kunaonekana kuhusisha masharti ya utakaso na hii
inaweza kufanyika tu kwa kubatizwa kwenye maji. Hata kuhani mkuu lazima avue
nguo zake na kuziweka kando kisha aoge katika Mahali Patakatifu kabla hajarudi.
Jangwa
lina tafsiri yenye maana mbili. Ya kwnza kabisa, ni kukatiliwa mbali na Mungu
ili kuwa chini ya uadui, pia, inamaaanisha tendo la kuondolewa kwa dhambi.
Jangwa la usahaulifu ni tendo la kutozikumbuka dhambi zetu tena au kuzisahau
(Isa. 43:25, Yer. 31:34). Katika tendo hili aliziharibu nguvu za adui kama
tunavyoona katika Waebrania 2:14; Luka 13:1-9 ambako inaonekana masharti ya
toba kwa ujumla. Hii inahusisha na ukiri wa dhambi. Kwa mtazamo huu tumewekwa
huru kutokana na hukumu za dhamira mbaya ya adui kama ilivyokuwa ni Mungu yule
atuhesabiaye haki (Rum. 8:33-34). Kwa hiyo ni kwamba tumewekwa huru nyuma mbali
ya hukumu za dhamira zilizokuwa zimewekwa juu yetu siku kabla ya upatanisho na
Kristo uliotuweka huru kutoka kwenye ukweli wa toba yetu. Sisi sasa tumewekwa
mfumo wa adui na tunaweza kusema (kama ilivyonakiliwa na Bullinger (n. hadi 22)
anayethubutu kutuua na kwa ajili hii tumehesabiwa haki na Mungu. Na pasipo
kumwagika damu hapakufanyika ondoleo la dhambi au msamaha wa dhambi. Kwa hiyo,
mauti imechukua mahala pa ukombozi wa maovu. Mafundisho haya yanapatikana
kwenye Waebrania 9:15, 22, 26.
Bullinger
anafanya ulinganisho wa ndege wawili katika Mambo ya Walawi 14:51-53 kama mfano
mwingine wa hatua hii kama inavyofanyika kwa taifa lote. Kuhusu hawa ndege,
nyumba ilipona na ugonywa wa tauni. Damu ya ndege wa kwanza ilimwagwa na ndege
aliye hai alizamishwa kwenye maji yanayokimbia na damu ya ndege wa kwanza.
Kasha nyumba ilinyunyiziwa au kupakwa mara saba na nyumba ilioshwa nayo na mbao
ya mti wa mshita na hisopo rangi nyekundu kama damu ya mzee. Mara saba
ilionyesha utakaso wa makanisa saba. Ndege mzima hatimaye aliachiliwa huru
kwenye shamba lililo wazi. Hivyo basi, ndipo nyumba ikatakasika kwa ajili hii
na vitu vingine vyote, vya kibinadamu na vya mbinguni, vitakuja kwenye taifa
moja na vitatawala kama Mungu ambayo ni kwa maana ya jina la Israeli.
Wakti tu
kila utawala na nguvu na mamlaka yanayotii kisha Masihi atayarudisha nyuma hadi
kwenye ufalme wa Mungu yeye ambaye ni peke yake anabakia na mamlaka alyompa
Masihi (1Kor. 15:22-28).
Wakati
mambo haya yatakapokuwa yanatokea, Masihi na Jeshi la watu wa Mungu watakuwa
wanapatanishwa.
‘Azazeli
(au Shetani) hataweza kuendelea kuishi tema. Mahali kama hapa, tutakuwa ni
viumbe vipya na majina mapya, yaliyoandikwa na Mungu. Wala mauti haitakuwapo
tena, wala unabii wa uwongo wala uwongo, wala yule mnyama na mfumo wake. Kama
isemavyo, watakuwa wameisha kufa na kutupwa wakachomwe kwenye ziwa la moto
(tazama Ufu. 19:20; 20:14).
Mambo ya Walawi 16:29-34 inasema: 29Amri hii itakuwa amri ya milele kwenu; katika mwezi wa saba, siku ya kumi ya mwezi, mtajitaabisha roho zenu, msifanye kazi ya namna yo yote, mzalia na mgeni akaaye kati yenu. 30 Kwa maana siku hiyo upatanisho utafanywa kwa ajili yenu, ili kuwatakasa; nanyi, mtatakaswa na dhambi zenu zote mbele za BWANA. 31 Ni sabato ya raha ya makini kwenu, nanyi mtajitaabisha roho zenu; ni amri ya milele. 32 Na kuhani atakayetiwa mafuta na kuwekwa wakfu badala ya baba yake, ataufanya huo upatanisho, naye atayavaa mavazi ya kitani, yaani, yale mavazi matakatifu. 33 Naye atafanya upatanisho kwa ajili ya patakatifu, naye atafanya upatanisho kwa ajili ya hema ya kukutania, na kwa ajili madhabahu, naye atafanya upatanisho kwa ajili ya makuhani, na kwa ajili ya watu wote wa kusanyiko. 34 Na amri hii itakuwa amri ya milele kwenu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya wana wa Israeli kwa sababu ya dhambi zao zote, mara moja kila mwaka. Naye atafanya vile vile kama BWANA alivomwamuru Musa.
Ni kwa
njia ya utaratibu huu tunaweza kuingia kwenye mwili wa Israeli. Hii ndio maana
mtu asiyeiadhimisha Siku ya Upatanisho na kujua maana ya dhabihu ya Kristo na
upatanisho kwa njia ya ubatizo katika Roho Mtakatifu atakatiliwa mbali na
Mungu. Ni kwa njia ya upatanisho huu na ubatizo wenye maana.
Dhabihu
ya Masihi ilipatanisha viumbe vyote na Mungu. Masihi alifanya upatanisho kwa
kila kiumbe akijumlishwa na ‘Azazeli au Shetani, na hii ndio maana katika mbuzi
wale wawili tunayaona matendo ya Masihi na pia bado tunaweza kujionea mpango
endelevu wa Mungu ukikumbatia watoto wake wote. Mpangu huu umetimia na ni
mkamilifu kwa ajili ya uweza wa kujua mambo yote na uweza wake wenye nguvu zote
zisizoshindwa na kitu. Rehema zake na wema wake ni kamilifu na zadumu milele.
q