Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

 

[004]

 

 

 

Kuichagua Huduma

(Toleo La 2.0 20000419-20110701)

 

Kwenye zama hizi za leo za upashanaji wa kisasa tunaweza kushangazwa tu kuona idadi kubwa ya vikundi na makanisa ulimwenguni yanayolitumia jina la Kristo. Hata kama tukiyaondoa au kutoyahesabia yale yasiyoyatumia maneno “Kanisa la Mungu” kwenye majina yao, bado tutabakiwa na idadi kubwa kwa mamia. Lakini lakujiuliza ni kwamba je, haya yote yanasifa na vigezo stahiki? Je, tutawezaje kuchagua huduma halisi na sahihi ili ituongoze kwa Kristo? Je, tungoje tu mstari mrefu unaoendelea wa viongozi walioitwa na kupewa majukumu mfululizo kutoka kwa Kristo hadi kwenye nyakati zote na zama zote? Tunawezaje kuwajaribu watu hawa, na kulikuta Kanisa la kweli?

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2000 Pieter Voges and Wade Cox, ed. Wade Cox)

(rev. 2011; tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Kuichagua Huduma


Kwenye zama hizi za leo za upashanaji wa kisasa tunaweza kushangazwa tu kuona idadi kubwa ya vikundi na makanisa ulimwenguni yanayolitumia jina la Kristo. Jambo hili lilitabiriwa kuwa litatokea.

 

Mathayo 24:4-5 Yesu akajibu, akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.

 

Wengine wamegundua kwamba jina linapaswa liwe sawasawa na kama alivyolitumia Mtume Paulo.

 

2Wakorintho 1:1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu; kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko katika nchi yote ya Akaya.

 

1Wahesalonike 2:14  Maana ninyi, ndugu, mlikuwa wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyo katika Uyahudi, katika Kristo Yesu;

 

Hata kama tukiyaondoa au kutoyahesabia yale yasiyoyatumia maneno “Kanisa la Mungu” kwenye majina yao, bado tutabakiwa na idadi kubwa kwa mamia. Lakini lakujiuliza ni kwamba je, haya yote yanasifa na vigezo stahiki? Je, vikundi na makanisa haya yote yameanzishwa na Kristo? Je, Kristo amegawanyika? Tunawezaje kuwajaribu watu hawa, na kulikuta Kanisa la kweli?

 

Je, Ni Mwendelezo wa Mstari Ulioahidiwa na Kukusudiwa?

Wengine wanaweza kuhisi kwamba wamekuwa ni mwendelezo wa mstari wa mfululizo ulizokusudiwa na kuwekwa kutoka kwa Kristo na kuelekea chini kwa zama na zama. Bahati mbaya sana hili sio jambo la wakati wote. Wakati mwingine, kiongozi anayechukua uongozi kutoka kwa mwingine anakuwa fisadi na muovu, na kuliongoza kanisa kuelekea kwenye unpangiliwapointments from Christ down through the akengeufu. Jambo hili linajitokeza kwenye mwisho wa kila zama ya Kanisa, kwa mujibu wa Ufunuo sura za 2 na 3. Hebu na tuyatathimini matukio ya ukengeufu wa Kanisa la kwanza.

 

Yuda 3-4  Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu. 4 Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.

 

Kweli ilikuwa imepuuzwa na kuachiliwa mbali, na hatimaye ilikataliwa. Waliongozwa na wengine kwenye huduma hizi kuamini kwamba neema maana yake ni ruhusa ya wao kuendelea kuziishia dhambi. Matatizo haya yalitokea ili kwamba waumini wa uwongo wajlikane, kwa kuwa watafuata ukengeufu wao na kuuamini na kuupenda kwa furaha kuu.

 

1Wakorintho 11:18-19  Kwa maana kwanza mkutanikapo kanisani nasikia kuna faraka kwenu; nami nusu nasadiki; 19 kwa maana lazima kuwapo na uzushi kwenu, ili waliokubaliwa wawe dhahiri kwenu.

 

Hatimaye kinara cha taa kitaondolewa kutoka kwa kiongozi aliyewekwa, na kupewa mwingine.

Ufunuo 2:5 Basi, kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu.

 

Kwa hiyo, ilitokea hivyo nyakati zilizopita kwamba Kristo alipaswa kulianzisha kwa kulifufua Kanisa kutoka mautini kwa kuwatumia viongozi wapya.

 

Alimwambia Baba yake, yeye Mwamba ambao Kanisa limejengwa juu yake, na Kristo akiwa ndiye jiwe kuu la pembeni, Kristo alimwambia Patro, mfano huu kwa wakati ule:

Mathayo 16:17-18  Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni. 18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.

 

Hii inaonyesha dalili ya kwamba kwa wakati ule itampasa Kristo kulilinda Kanisa kutokana na tofauti kubwa sana na ya muhimu au mauti, iliyoelezwa na kumaanishwa kwa jina la “jehanamu”, yaani, kaburi au kuzimuni. Uongozi wa Kanisa unapaswa kuchukuliwa kama ulikufa kiroho na haukuruhusiwa kuweka kiongozi mpya aliyekubaliwa na Kristo. Kiongozi aliyekengeuka atakuwa anawafukuza viongozi wengine wa kweli na wapenda kweli, kama ilivyotokea.

 

3Yohana 9-10 Naliliandikia kanisa neno, lakini Diotrefe, apendaye kuwa wa kwanza kati yao, hatukubali. 10 Kwa hiyo, nikija, nitayakumbuka matendo yake atendayo, atoavyo upuzi juu yetu kwa maneno maovu; wala hatoshwi na hayo, ila yeye mwenyewe hawakaribishi hao ndugu, na wale watakao kuwakaribisha, huwazuia, na kuwatoa katika kanisa. 

 

Wakati Kanisa linapofikia kiwango hiki, wakati hata kichwa na fikra za mwanadamu zinapokuwa zimezama kwenye ukengeufu, ni dhahiri kabisa kwamba yeye hatamchagua kiongozi mpya atakayeyathibitisha na kuyaendeleza makosa ya zamani yaliyofanywa na kiongozi aliyepita. Kwahiyo, kwenye mabadiliko ya kutoka kwenye kipindi cha zama moja ya Kanisa ilivyo kwenye Ufunuo 2 na 3 na kuanza zama ya Kanisa linguine, ilipasa kiongozi mwingine mpya mwanadamu achaguliwe kutoka kwenye kundi la waliosalia kutunza uaminifu na waliofukuzwa kwenye imani ya kiongozi mkengeufu. Mamlaka ya kuchagua viongozi yamepewa Kanisa na kitendo cha kubatiza ni njia ya kumhamisha Roho Mtakatifu kwa mbatizwaji. Mungu aliliambia Kanisa akiwaambia walengwa wote, yaani viongozi na wapendwa waumini kuwa:

Mathayo 16:18-20  Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. 19 Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. 20 Ndipo alipowakataza sana wanafunzi wake wasimwambie mtu ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.

 

Mitume kwa pamoja waliunda bodi ya uongozi. Hoja hapa ilikuwa imetumika kuendeleza suala lililotokana na tabia ya Petro ya kimbelembele. Hatahivyo, yatupasa kurejea kwenye maandiko yaliyo kwenye Waefeso 2:20 na Ufunuo 21:14.

 

Mtindo uliotumika kuyaandika maneno haya ni wa lugha ya Kiaramu kuelezea Mwamba na jiwe dogo. Maana halisi ya maneno ni Petros kwa Mwamba na petras kwa jiwe dogo, ambayo inamaanisha Petro.

 

Mwamba wa kweli wa Kanisa, Kefa, ulikuwa ni Mungu mwenyewe na ilikuwa ni kwa mapenzi na mpango wake Mungu kuwa Kristo alilijenga, na jambo hili au ukweli huu umepotoshwa kwa makusudi na imani ya waamini Utatu ambayojikuta yenyewe ikijumuika na kuwa chini ya mfumo na mafundisho ya Papa ili istahimili kumudu kuendelea. Petro aliteuliwa kuwa askofu wa Anthiokia na orodha ya mambo yake mengi haionekani wala kujulikana kabisa na alikuwa na wadhifa wa juu kimaongozi zaidi ya askofu wa Roma (kama ilivyo kwenye Orodha ya Mapapa na Wapinga-Mapapa kwenye jarida la Jarida la Nyongeza A (Na. 288a)).

 

Mamlaka hapo mwanzoni kabisa ilitolewa na Kristo na aliwapa mitume sabini alipowasimika, na hatimaye kwa Kanisa zima lote na kwa yeyote ambaye Kanisa linamuweka wakfu sawasawa na vigezo vya kimbuni (soma Luka 10:1,17). Malaika wote waasi ambao sasa ni mashetani na mapepo waliwatii hawa mitume sabini. Walifanyika kuwa ni bodi kamili ya kuliongoza Kanisa ambayo ilichukua mamlaka na shughuli zote za utendaji kazi ambao hapo mwanzoni mamlaka na uweza huu ulikuwa chini ya baraza la Sanhedrin la Waisraeli. Tangu hapa,  Israeli walifanyika pia kuwa ni sehemu ya umma wa kiroho na Wokovu ukaenea na kuwafikia Wamataifa.

 

Sasa tunaona kwamba mamlaka yalitolewa kwa waumini wote walio kwenye bodi au ushirika wa Kanisa. Tunaona kwamba bodi hii iliweka na kutawaza viongozi na waliwekwa wakfu na uongozi uliokuwa kwenye muundo huu wa uongozi. Mamlaka ya kufunga na kufungua limepewa Kanisa.

 

Mathayo 18:15-20  Na ndugu yako akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata nduguyo. 16 La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno lithibitike. 17 Na asipowasikiliza wao, liambie kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru. 18 Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. 19 Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. 20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.

 

Mamlaka ya kufunga na kufungua imetolewa na limepewa Kanisa kwa ujumla na kwa viongozi wake waliowekwa wakfu. Dhana iliyojengeka ya kuwa mamlaka hii imepitia kwa mkondo wa mtu mmoja hadi mwingine ni ya kishirikina na na sio fundisho la kweli la imani ya kweli ya Kikristo (soma jarida la Abrakadabra: Maana ya Majina (Na. 240)).

 

Kwahiyo, hatuwezi kutarajia mwendelezo endelevu wa uwekaji wakfu kutoka kwa Kristo hadi kipindi hiki cha sasa. Itatupasa tu kuthibitisha ukweli na kisha tuthibitishe na kulijua Kanisa la kweli jinsi lilivyo.

Mathayo 7:15-21  Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali. 16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? 17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya. 18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri. 19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni. 20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua. 21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

 

Tumeelekezwa kuwa tuitafute ilipo huduma ya kweli inayomtii Mungu, Baba, na inayozishika Amri zake zote.

 

Watumishi Wanaolihudumu Neno Lote Kikamilifu

Manabii wa zamani wamekwishatupa tayari vigezo vyake. Huduma ya Mungu na Mwanawe aliyemchagua ataishi na kufundisha sawasawa na kila lisemavyo Neno la Mungu, akitenda kwa kuifuata kanuni na Sheria hii.

 

Isaya 8:20  Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi.

 

Huduma ya kweli itaishi kwa kila Neno litokalo kwa Mungu.

 

Mathayo 4:3-4 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.4 Naye akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.

 

Watazitii na kuzifundisha amri za Mungu. Watajua na kuelewa kwamba maana ya Ukristo ni kufanana au kuwa kama Kristo, kwa kumpenda Mungu na kuzishika amri zake.

 

Ufunuo 12:17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.

 

Ufunuo 14:12  Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.

 

Kwa hili tuna muongozo wa kutosha ili kuligundua Kanisa la kweli. Kwa mfano, litakuwa ni Kanisa linalozitunza Sabato, kuadhimisha Miandamo ya Mwezi Mpya na kuziadhimisha Siku Takatifu zilizoamriwa na Mungu kwa mujibu wa Kalenda aliyoiweka Mungu. (soma jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156)). Tunaona kwamba kwa uwingi mkuu na wa jumla ulilikosoa Kanisa la kwanza kwa kufanya kwake hivyo.

Wakolosai 2:16  Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;

 

Kanisa limekuwa ni bodi inayoonekana na kutambulika kwa kipindi cha zaidi ya milenia mbili, likiteswa kwa ajili ya utii wake kwenye Amri za Mungu na Ushuhuda wa Mungu au imani yake kwa Yesu Kristo (Ufunuo 12:17; 14:12) (soma jarida la Wajibu wa Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu Yanayozitunza Sabato (Na. 170)).

 

Kuanzisha Huduma

Huduma inaanzishwaje? Je, Biblia inatupa mwongozo wowote? Je, kuna utaraticu wowote wa kuchagua ambao kwamba washirika wa Kanisa la kweli wanachaguliwa kwenye huduma?

 

Jibu ni kwamba “Ndiyo” upo. Tutauangalia utaratibu huo.

 

Mitume wa kwanza wa Kristo

Tunauona uchaguzi wa kwanza kwenye uingizaji wa walio mbadala wa watu wa Yuda.

 

Matendo 1:15-20 Siku zile akasimama Petro kati ya hao ndugu (jumla ya majina ilipata mia na ishirini), akasema, 16 Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi, katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu; 17 kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii. 18 (Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka. 19 Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.) 20 Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa, Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo;

 

Jinsi tutakavyoona mchakato wa uchaguzi.

 

Nafasi ya juu zaidi ya mwanadamu

Kwanza kabisa, inatupasa kujua kwamba wakati Kristo alipotembea juu ya nchi, alikuwa ni mamlaka ya juu sana akiwa na umbo la kibinadamu. Aliwaambia (au kuwapa majukumu) mitume waunganenaye, kama walivyokuwa wametolewa na kupewa Kristo. Kibinafsi yeye aliwajulisha kuhusu kuitwa kwao. Mungu aliwachagua mitume kumi na mbili. Kristo aliwajulisha kuhusu kuchaguliwa kwao. Hata hivyo, Kristo hakujionyesha mwenyewe kwao kama kwenye hatua hii alivyofanya uchaguzi wake mwenyewe kwa dhahiri na kumchagua mtume atakayechukua nafasi yake. Zaidi ya yote, mitume kumi na mbili wengine walikuwa na mamlaka sawa hadi wakati huu. Kwa hiyo, hakuna hata mmoja wao angeweza kuwa na mamlaka ya kumsimika mwingine aliye chini yake, kwa kuwa mitume hawa kumi na mbili walikuwa na cheo sawa kwa kila kabila moja ya makabila kumi na mbili ya Israeli.

 

Mathayo 19:28  Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

 

Kwa hiyo, kwa nafasi hii ya juu sana kuliko, mapenzi ya Mungu yalitafutwa. Hili lilifanyika kwa mchakato wa namna mbili.

1.      Weka kigezo cha kuitwa na kuchaguliwa

2.      Kama kuna mmoja anayefikia vigezo kuliko wengine, piga kura ili kutafuta chaguo kutoka kwenye mamlaka yanayofuatia ya pili, ambayo ni Kristo.

Hili lilifanyika sawasawa na maelekezo ya torati, kama kuhani mkuu alivyokuwa kila mara akichaguliwa, akiitwa kwa kupigiwa kura.

 

Kuweka Kigezo

Kwanza kabisa, kigezo cha uchaguzi kinapaswa kiwekwe.

 

Matendo 1:21-22  Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu, 22 kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.

 

Kama mtu mmoja akipendekezwa anayetimiza vigezo, ndipo alipoweza kuwa chaguo. Lakini wakati mwingine ilijitokeza kuwa na watu zaidi ya mmoja wanaoonekana kukidhi vigezo hivyo, na kwa kuwa mamlaka ya pili nay a juu zaidi yalikuwa ni Kristo, ndipo shauri liliweza kuhitimika kwa muujiza kutoka mbinguni kwa jambo hili.

 

Matendo 1:23-26  Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya. 24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili, 25 ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. 26 Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.

 

Hii ni njia ambayo kwayo nafasi ya juu sana ya sasa ya mwanadam inawekwa. Ni dhahiri kabisa kwamba mitume hawa kumi na mbili tayari walikidhi vigezo vya nafasi zao, na hawapo kabisa tena. Nafasi hizo zilichukuliwa. Hata hivyo, kwa zama zote za Kanisa kama vilivyo kwenye Ufunuo sura za 2 na 3, kuongozi mpya wa kibinadamu alipaswa kuchaguliwa, kwa kuwa sisi sote tunakufa hatimaye. Hawa sabini waliunda uongozi wa Kanisa kwa kipindi cha miaka elfu mbili na hawa ia wanaunda jopo la watu 70 jumlisha 2 ili kufikisha idadi ya wateule 144,000 wa maongozi ya Mungu (soma jarida la Mavuno ya Mungu, Dhabihu ya Mwandamo wa Mwezi Mpya, na ya Wateule 144,000 (Na. 120)).

 

Vipi kuhusu huduma nyinginezo?

Mara tu baada ya kiongozi wa kibinadamu anapowekwa, anaiweka sehemu yote ya huduma iliyobakia kwa viongozi wa kuteuliwa. Tena kigezo cha kuteuliwa kwao kinawekwa na kuwekewa kigezo chao kutokana na matunda waliyonayo viongozi hao waliopendekezwa. Viongozi hao walioteuliwa ndipo wanawekwa wakfu.

Matendo 6:1-6  Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung'uniko ya Wayahudi wa Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku. 2 Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani. 3 Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili; 4 na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno. 5 Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia; 6 ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao.

 

Tunaona pia kwamba mchakato huu wa kuweka kigezo na kuwachagua viongozi ulifuatiwa na ukuaji wa Kanisa.

 

Tito 1:5  Kwa sababu hii nalikuacha Krete, ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile nilivyokuamuru;

Kwa hiyo, mtumishi hawezi kuwa mtu aliyejichagua au kujiteua mwenyewe. Inampasa athibitishwe na watakatifu wa kweli wanaounda bodi ya uongozi wa Kanisa, na awekwe na uongozi wenye mamlaka ya Kanisa.

 

Jambo Muhimu na la Kipekee

Wakati mwingine kunaweza kusiwe na kusanyiko la kumpendekeza kiongozi kutoka kwenye daraja lao. Wakati mwingine kunaweza kuwa na mtu mmoja tu kwenye eneo la kijiografia. Ni wazi sana kwamba hapa panakuwa na mtu mmoja tu pekee wa kumchagua.

 

Utaratibu Usiowezekana

Watu mara nyingi wanayashangaa maandiko matakatifu yafuatayo:

Waebrania 5:4 Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni.

 

Ndipo swali linaibuka sasa kwamba ni kwa jinsi gani mtu anaweza kuwa na uhakka kama mtu ameitwa na Mungu kumtumikia. Hata hivyo, hii sio sahihi kwa kile linachikusudia andiko hili. Hebu na tuliangalie jambo hili kwa jinsi lilivyo:

Waebrania 5:1-10  Maana kila kuhani mkuu aliyetwaliwa katika wanadamu amewekwa kwa ajili ya wanadamu katika mambo yamhusuyo Mungu, ili atoe matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi; 2 awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na wenye kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe yu katika hali ya udhaifu; 3 na kwa sababu hiyo imempasa, kama kwa ajili ya watu, vivyo hivyo kwa ajili ya nafsi yake mwenyewe, kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi. 4 Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni. 5 Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa. 6 kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe kuhani wa milele Kwa mfano wa Melkizedeki. 7 Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu; 8 na, ingawa ni Mwana, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata; 9 naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii; 10 kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.

 

Kwenye kifungu hiki Paulo anaongele kuhusu kuhani mkuu, mtu anayehusika kuendesha ibada ya kutoa sadaka za dhambi za watu. Ni Kristo peke yake anayeweza na amekamilisha kazi hii. Kwa hiyo, aya ya 5 inamuelezea Mtiwa mafuta ambaye ni Kristo, Masihi, na sio huduma iliyopo sasa ya kibinadamu hapa duniani. Huduma zote za Kanisa zinasimama kwa Kristo, kama Makuhani walio mfano wa Melkizedeki kwakuwa hakuna anayeweza kuwa Kuhani Mkuu wa mfano wa mtu asiyeweza kuwa makuhani. Kwa hiyo wateule kama walivyo tu wao wenyewe wapo wa mfano wa Melkizedeki kama warithi pamoja na Kristo (soma jarida la Melkizedeki (Na. 128)).

 

Hitimisho

Baada ya zama ya uongozi kupitia kwenye zama ya ukengeufu, ilimpasa Kristo kulifufua Kanisa na kuweka uongozi mpya. Waumini wanaoyajua mafundisho ya kweli waliyopewa watakatifu wa kwanza wa karne ya kwanza walichagua viongozi wazuri kutoka watu waliokuwa kati yao walioendana na vigezo vilivyoonyeshwa kwenye Biblia.

 

1Timotheo 3:1-7  Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema. 2 Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; 3 si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha; 4 mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; 5 (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?) 6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi. 7 Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.

Iwapo kama kuna watu zaidi ya mtu mmoja anayeonekana kuwa kwenye kiwango na daraja moja la maendeleo ya kiroho, ndipo viongozi itawapasa wapige kura baada ya kufunga saumu na kuomba, ili kwamba Mungu kupitia kwa Kristo awachagulie kiongozi.

 

Kiongozi huyu ndipo ataomba ushauri au mapendekezo ya kutoka kwenye kundi ili kuwapata viongozi, na shauri lake ndipo litawagundua watu na kuwasimika wanaokidhi vigezo na kuzaa matunda, kutegemea na matendo yanayohitajika kutendwa.

 

Kwa suala la Kanisa kutenda kazi kwenye shughuli zake, kama Makanisa ya Kikristo ya Mungu na mengine ya mahalia yanayosaidia kwenye mataifa yote, mchakato umeanza kwa katiba iliyoandikwa na mamlaka yamewekwa kwenye uongozi wa Kanisa. Viongozi, kama Mwangalizi Mkuu (Coordinators-General) anashikilia vyeo na mamlaka yote na kazi zote na mipango yote pamoja na kuwateua viongozi wa Kanisa kama mitume, wainjilisti na wachungaji, ili kwamba wao waweze kuwachagua na kuwasimika wengine kwa kazi zote zilizo sawasawa na mapenzi yaliyoelezewa ya Kanisa. Wao wenyewe wanachaguliwa kwa kupigiwa kura kwenye kila mwaka wa Sabato ambao pia ni wa usomaji wa Torati, kwa kufuata mujibu wa sheria ya Mungu

.

 

Tumeitwa ili tuwe taifa la wafalme na makuhani, la watu watakatifu (Ufunuo 1:6; 5:10) na imeandikwa kwamba kila mtu anayekwenda kuwa mfalme inampasa ajiandalie wenyewe Torati ya Mungu (Kumbukumbu la Torati 17:18) ili kwamba aweze kuzifuata na kuzishika amri za Mungu anapochaguliwa. Kwa hiyo ni sawa na sisi na kama tulivyochaguliwa na kusimikwa kwenye Makanisa ya Mungu na kuachana na sheria zetu.

 

Huduma zote zinashikilia ofisi zao kwa maslahi ya Kanisa na kupewa majukumu kama linavyokusudia Kanisa.

 

Kuna vyeo viwili vya huduma, Wazee wa Kanisa na Maaskofu na Mashemasi. Maafisa hawa wanaweza kubeba majukumu na kazi au utendaji ambazo wamesimikwa kwazo.

 

Askofu au Mzee wa Kanisa wanaweza kuchukua wadhifa wowote wa Kanisa na wanaweza kuwasimika au kuwaweka wakfu wengine kwenye ofisi kama ilivyokusudiwa na Kanisa.

 

Shemasi anaweza kushikilia majukumu ya kiofisi au kazi ya Muinjilisti, au Mchungaji, au Kiongozi na anaweza kufanya shughuli za wakfu za Kanisa ambazo anastahili, kwenye eneo aliloruhusiwa na kikomo alichopewa nay eye, Askofu au Mzee wa Kanisa (soma jarida la Wakfu au Sakramenti za Kanisa (Na. 150)).

 

Mashemasi wanaruhusiwa kubatiza waongofu wapya kama alivyofanya Filipo kwenye Matendo 8:26-40. Kwenye mifano mingine maaskofu wanaweza kuwaelekeza mashemasi na kuwaruhusu kubatiza, na kuwaweka akiba kwa ajili shughuli za kuwawekea watu mikono kama kutakuwa na tatizo kubwa, kama ilivyokuwa kwenye tukio la Simoni Mchawi na Mwana mazingaombwe (soma Matendo 8:12-17). Hata hivyo, haikuwa inafanyika hivyo wakati ule. Mashemasi hubatiza kwa sababu zao wenyewe. Haijalishi kinachofanyika inafanywa kwa utukufu wa Mungu, sawasawa na mapenzi yake na kwa wateule wake.

 

Haijalishi kinachofanyika kiache na kifanyike hivyo kwenye ubinadamu wote na acha wote wawaheshimu wale waliowekwa wakfu na kusimikwa kuwatumikia wao.

 

Mpendane na tuwafanye wote watumikiane kwa unyenyekevu na wampende Mungu.

 

Kuyajali mambo yaw engine na kuyatilia maanani, au kuangalia umri kwenye huduma, tunagundua kwamba torati inasema kuwa mtu anapasa kuwa na umri wa miaka ishirini na tano kabla hajaingizwa kwenye huduma za Hekaluni (Hesabu 8:24).

Hesabu 8:24-26  Mambo yawapasayo hao Walawi ni haya; tangu waliopata umri wa miaka ishirini na mitano na zaidi wataingia ndani ili watumike utumishi katika kazi ya hema ya kukutania; 25 tena tangu waliopata umri wa miaka hamsini wataacha kutumika huo utumishi, wasitumike tena; 26 lakini watatumika pamoja na ndugu zao katika hema ya kukutania, kushika ulinzi, lakini wasitumike katika huo utumishi tena. Ndivyo utakavyowafanyia Walawi katika mambo ya ulinzi wao.

 

Inapasa mtu awe na umri wa miaka thelathini kabla hajaruhusiwa kuanza kufundisha. Kristo mwenyewe hakuwa na udhuru kwa hili. Kwenye kanuni za Kilawi waliingia kwenye huduma akiwa na umri wa miaka ishirini na tano na aliacha huduma akiwa na umri wa miaka hamsini. Baada ya miaka hiyo hamsini walidumu kwenye huduma ya ndugu zao.

 

Hata hivyo, uwekaji wakfu unaweza kufanyika kabla ya kufikia umri wa miaka thelathini, kama ilivyokuwa kwa shauri la Timotheo ambaye alikuwa amewekwa wakfu kabla hajaufikia umri,huu ulioelekezwa, tunaouona kwenye 1Timotheo 4:12. Tunaweza kuona kuwa hii ilikuwa muhimu kwakuwa alikuwa apelekwe kwenye huduma ya umisheni na kwa hiyo ilimlazimu kusimikwa na kuwekwa wakfu.

1Timotheo 4:12 Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.

 

Tuna dhana na wazo la mamlaka na huduma na sisi pia tunadhana ya matumizi au kuwatumia wanawake Kanisani. Kwenye 1Timotheo 2:11-13 tunasoma:

1Timotheo 2:11-14 Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna. 12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu. 13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye. 14 Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa.

Hoja iliyotolewa ni kwamba Mashemasi wa kike waliwekwa wakfu kuhudumu Kanisani ili kuwaongoza na kuwafundisha wanawake. Hawakuruhusiwa kufundisha wala kuwa na mamlaka juu ya wanaume, lakini walikuwa nanafanya kazi Kanisani na walifanya huduma ya kuwafundisha wanawake kwa kipindi cha karne kadhaa.

 

Suala la kufndisha Kanisani inaweza kuonekana kwenye 1Timotheo sura ya 5 (hasa tafsiri ya KJV).

 

1Timotheo 5:1-2   Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu; 2 wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote.

Andiko hilo ndipo linaenda mbali kupitia kwenye utaratibu wa kuwahudumia wajane kanisani na utaratibu na mwenendo mzuri wa watu kanisani (soma aya za 3-16).

 

Inaendelea 1Timotheo 5:

17 Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.

Wazee wa Kanisa kanisani walihudumu kwenye kazi mbalimbali. Wale waliokuwa wakilihudumu neno na kufundisha (kufundisha na kupangilia) walihesabiwa kustahili heshima maradufu.

18 Kwa maana andiko lasema, Usimfunge kinywa ng'ombe apurapo nafaka. Na tena, Mtenda kazi astahili ujira wake.

Suala hili lote kuhusu wazee kupewa zawadi ni kwa ajili ya kazi mbalimbali na wanapangiwa kufanya kazi kanisani. Si vyema kumtumia mzee wa kanisa kwa kutomjali, yaani bila kumpa zawadi.

 

Pia kwenye 1Timotheo 5:19ff. Tunasoma kwe habari ya makato au malipo hivi.

1Timoteo 5:19 Usikubali mashitaka juu ya mzee, ila kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu.


Mambo haya ni ya muhim sana kwa utaratibu mzuri. Kama tujuavyo kuwa wazee wa kanisa wamekuwa ni walengwa kwa miaka mingi kadhaa.


20 Wale wadumuo kutenda dhambi uwakemee mbele ya wote, ili na wengine waogope. 21 Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu, na mbele za malaika wateule, uyatende hayo pasipo kuhukumu kwa haraka; usifanye neno lo lote kwa upendeleo. 22 Usimwekee mtu mikono kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe safi. 23 Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara. 24 Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata. 25 Vivyo hivyo matendo yaliyo mazuri ya dhahiri; wala yale yasiyo dhahiri hayawezi kusitirika.


Mpangilio ulio kwenye andiko hili ni kuifanya huduma iheshimike: kuwafanya wawe kwenye uangalizi; kutoonyesha upendeleo kumpendelea mtu kwenye huduma yote na kufanya mashitaka kuishitaki huduma kwa uangalizi unaostahili. Mambo haya yote hufanyika kwa utaratibu kanisani.


Utaratibu wa Kanisa umechukuliwa na huduma na ndugu wapendwa wanaowasaidia, ili lisiwe ni kanisa lililofarakana, bali wote wanafanya kazi pamoja kwa utukufu wa Mungu. Mambo haya ni ya muhimu katika kujua yanayotupasa kufanya kwene huduma kwenye kuchaguliwa, wanayofundisha na uongozi wao wa muda mrefu na msaada wa wapendwa wengi.

 

Yatupasa tuombe wote kuiombea huduma na kufanya kazi pamoja kusaidiana katika kumtumikia Mugu. Kila mmoja wetu anabudi kuwasaidia watumishi wa Mungu wetu, na sio kuwalaumu tu kila mara na kuwashitaki na kwa kweli si kwa kutafuta kuwakuta na makosa na kuidharau huduma na watumishi wake.

q