Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[275]
Sadaka
(Toleo La 1.0
20060923-20060923)
Kumbukumbu la Torati 16:16: “Mara tatu kwa
mwaka na watokee wanawaume wako wote mbele za Bwana, Mungu wako, mahali
atakapochagua; katika sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, na katika sikukuu ya
majuma, na katika sikukuu ya vibanda; wala wasitokee mbele za Bwana mikono
mitupu."
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © Wade
Cox)
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Sadaka
Maratatu kila
mwaka Mungu ametumuru kukusanyika pamoja mahali ambapo Mungu amepachagua
alikalishe jina lake. Sikukuu hizo tatu ni: Sikukuu ya Pasaka na Mikate
Isiyotiwa Chachu; Idi au Sikukuu ya Majuma; na Sikukuu ya Vibanda. Tunatakiwa
kuondoka na kuziach nyumba zetu na kwenda mahali alipopachagu Bwana. Kumbukumbu
la Torati 16:16-17:
“16 Mara tatu kwa mwaka na watokee wanawaume
wako wote mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua; katika sikukuu ya
mikate isiyotiwa chachu, na katika sikukuu ya majuma, na katika sikukuu ya
vibanda; wala wasitokee mbele za Bwana mikono mitupu. 17 Kila
mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako,
alivyokupa”
Maelekezo haya
tumepewa kwa zaidi ya sehemu moja kwenye Maandiko Matakatifu. Zaidi ya yote,
amri au agizo kuhusia na jinsi Sikukuu hizi zitakavyokuwa linategemeana na
makabila yalivyo. Tumeamriwa kuwa tusiende huko mbele za Mungu tukiwa mikono mitupu.
Kumbukumbu la Torti
12:1-18 “1 Hizi ndizo amri na hukumu mtakazotunza
kuzifanya katika nchi aliyokupa Bwana, Mungu wa baba zako, uimiliki, siku zote
mtakazoishi juu ya nchi. 2 Vunjeni kabisa mahali
pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima
mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi; 3 nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na
maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao
zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo. 4 Wala
msimfanyie hivyo Bwana, Mungu wenu. 5 Lakini mahali
atakapochagua Bwana, Mungu wenu, katika kabila zenu zote, apaweke jina lake,
maana, ni makao yake, elekezeni nyuso zenu hapo, nawe wende huko; 6 pelekeni huko sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu
zenu, na zaka zenu, na sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu, na
sadaka zenu za hiari, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ng'ombe na ya
kondoo; 7 na huko mtakula mbele za Bwana, Mungu
wenu, nanyi furahini katika yote mtakayotia mikono yenu, ninyi na wa nyumbani
mwenu, aliyokubarikia Bwana, Mungu wako.”
Kwa hiyo ni wazi
sana basi, wakati tulipopewa milki zetu kufuatana na makabila yetu, mataifa
yalipaswa kujua au kuchagua mahala pao pa kufanyia ibada na iliwapasa
kujihudhurudhisha kwenye maeneo hayo kwa sikukuu.
8 Msifanye kwa kufuata mambo yote tuyafanyayo hapa
leo, kila mtu kama aonavyo vema machoni pake; 9 kwani
hamjafikilia bado katika raha na urithi akupao Bwana, Mungu wako. 10 Lakini mtakapovuka Yordani na kukaa katika nchi anayowarithisha
Bwana, Mungu wenu, akawapeni raha, akiwaokoa na adui zenu pande zote, mkakaa
salama;
Kwa hiyo, mahala
pa urithi na milki palipaswa kuchaguliwa na hapa, ni mahala pale pa milki au
urithi, ndipo tunapaswa kumuabudu Mungu.
11 wakati huo itakuwa kwamba mahali pale atakapopachagua
Bwana, Mungu wenu, alikalishe jina lake, hapo ndipo mtakapoleta kila kitu
ninachowaamuru; sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu zenu, na zaka zenu, na
sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu zote teule mtakazoweka kwa
Bwana. 12 Nanyi mtafurahi mbele za Bwana, Mungu
wenu, ninyi, na wana wenu, na binti zenu, na watumishi wenu wanawaume na
wanawake, na Mlawi aliyemo malangoni mwenu; kwa kuwa hana sehemu wala urithi
kwenu. 13 Ujihadhari usitoe sadaka zako za kuteketezwa
katika kila mahali upaonapo; 14 bali katika mahali
atakapopachagua Bwana katika kabila zako mojawapo, ndipo utakapotoa sadaka zako
za kuteketezwa, ndipo utakapotenda yote nikuamuruyo.
Watu wote
walitakiwa wakajihudhurishe mbele za Mungu pamoja na makuhani wao ambao
waliwajibika kuwahudumia. Kanisa lilipewa mamlaka haya na lilifundisha kwamba lilikuwa
limepewa mamlaka haya tangu mwanzoni kabisa (soma jarida la Utoaji wa Zaka (Na. 161)).
Andiko hili
halikukataza ulaji wa nyama zilizotolewa kama dhabihu za helaku la Mungu kama
tunavyoona kwenye maandiko yanayofuatia mara tu baada ya andiko hili. Bali ni
kwamba nyama ziliagizwa na kuruhusiwa kuchinjwa na kuliwa kwenye miji yote ya
urithi wa Israeli.
15 Pamoja na haya waweza kuchinja nyama na
kula ndani ya malango yako yote, kwa kufuata yote yatamaniwayo na roho yako,
kwa mfano wa baraka ya Bwana, Mungu wako, aliyokupa; aliye tohara na asiye
tohara ana ruhusa kula katika nyama hiyo, kama ya paa na ya kulungu. 16 Lakini msiile damu; imwageni juu ya nchi kama maji.
Agizo na amri
iliyokuwepo ni kwamba unapaswa kwenda kwenye sikukuu ili ukale Zaka yako ya
Pili.
17 Usile ndani ya malango yako zaka ya nafaka
zako, wala ya divai yako, wala ya mafuta yako, wala wazaliwa wa kwanza wa
makundi yako, ya ng'ombe wala ya kondoo, wala nadhiri zako uwekazo zo zote,
wala sadaka zako za hiari, wala sadaka ya kuinuliwa ya mkono wako; 18 lakini hivyo mtakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali
atakapochagua Bwana, Mungu wako, wewe, na mwanao mume na mke, na mtumwa wako
mume na mke, na Mlawi aliye ndani ya malango yako; nawe furahi mbele za Bwana,
Mungu wako, katika yote utakayotia mkono wako.
Nano hili la
"mahali atakapopachagua" limekuwa likibadilika kwa nyakati kadhaa
mbalimbali na linategemea na maeneo na mataifa ambayo Mungu ametupa ili
tuyamiliki. Kumbuka, Mungu aliwahi kuwtawanya Israeli na kuyaangamiza kabisa
Mahekalu yote mawili, lile la Yerusalemu na lile la Samaria lililokuwa kwenye
Mlima Gerizi, na pia lile la Misri. Mungu alihyadamishia mamlaka yote ya
utaratibu na mfumo wa Hekalu kwenye Kanisa. Baraka za mataifa yote zimeondolewa
kutoka Yuda na kutoka kwa Wasamaria na waliangamizwa kama watu. Baraka za
Efraimu na Manase hazipo kwa Wasamaria wanaodai utambulisho huo wa Baraka.
Wasamaria waliangamizwa na wa Byzantines na sasa hesabu yao ni ya watu wachache
sana mno. Hakuna hata mmoja kati yao anayehesabiwa kwenye makanisa ya Mungu.
Sikukuu hizi
zinaadhimishwa kwenye mataifa tuliyopewa na tunayoishi na hayahusiani na
Yerusalemu. Wakti Hekalu liliposimamishwa pale kulikuwa na mahekalu meingine
huko Misri yaliyokuwa yamedumu kwa karne nyingi kadhaa nyuma, kwa vipindi vyote
viwili, yaani kipindi cha kuwepo kwa Hekalu huko Yerusalemu na kile cha kutokea
kwa ukengeufu wake. Mungu aliamuru lijengwe Hekalu huko Misri na Sikukuu
zilikuwa zinaadhimishwa huko, na Kristo mwenyewe aliziadhimisha huko wakati
alipokuwa kitoto kichanga akiwa na wazazi wake, kwa kuwa imeandikwa katika Hosea:
"Kutoka Misri Nilikuita Mwanangu". Baada ya Kanisa kuanza, lilikuwa
ni Hekalu la kiroho – Kanisa – ndilo lililoamua masuala yahusuyo maadhimisho ya
Sikukuu na kuchagua mahala pa kuziadhimishia. Ukuhani wa Melkizedeki na Hekalu
la Kiroho ulichukua mahala pa ule w a Lawi na Hekalu la kimwili.
Mungu anatuambia
sisi pia kwamba umbali usiwe sababu ya kutuzuia, kwa hiyo tunapaswa kulitia
hilo mioyoni wakati tunapokuwa tunajiandaa kwa ajili ya kuziadimisha Sikukuu
hizi kila mwaka. Wengi wetu tunalazimika kusafiri umbali mrefu ili kuweza kujihudhurisha
kwenye Sikukuu. Na hii ndiyo maana katika mwaka wa tatu tunaziweka zaka zetu
kwenye mfuko wa kusaidia jamii ya wasiojiweza au maskini ili kuwasaidia
wahitaji waweze kuhudhuria Sikukuu, na ikiwezekana au ikilzimu, kuwapatia
misaada mingine yoyote itakayohitajika.
Kumbukumbu la Torati
14:23-26 Nawe
utakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake,
zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa
makundi yako ya ng'ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha Bwana, Mungu
wako, daima. 24 Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze
kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua Bwana, Mungu wako,
apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia Bwana, Mungu wako; 25 ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende
nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako; 26 na zile fedha zitumie kwa cho chote itakachotamani roho
yako, ng'ombe, au kondoo, au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako cho
chote; nawe utakula huko mbele za Bwana, Mungu wako; tena furahi, wewe na
nyumba yako;
Sehemu ya
kuziandaa Sikukuu hizi zote ni kutilia maanani Baraka ambazo Mungu Baba yetu
ametuahidi kuwa atatufanyia, tunapaswa kwenda kumtolea sadaka au dhabihu
zinazolingana sawasawa na Baraka alizotubarikia. Tusijitokeze tu kwenye hizi
Sikukuu pasipo mpangilio na kufanya maamuzi ya haraka ya papohapo katika kutoa
sadaka zatu kwa kulinganisha na kile tulichonacho mifukoni mwetu kwa wakati
ule, au kuandika hundi ya fedha tukadhani kuwa tumeshatimiza wajibu wetu
unaotupasa kuufanya sisi kama Wakristo. Inatupasa tutilie maanani au
kulinganisha na jinsi Mungu alivyotutendea na ndipo tumtolee dhabihu au sadaka
inayolingana kwayo.
2Wakorintho 9:7 Kila
mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa
lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.
Kwa maneno
mengine, ni kwamba tunapoamua kutoa sadaka zetu tunapaswa kuwa na furaha na heshima
ili tuweze kutoa kile tunachoweza kusaidia ama kuitegemeza huduma tuliyopewa. Je, ni huduma au majukumu gani basi hayo? (Soma
jarida la Majukumu ya Kanisa (Na. 171).)
Mathayo 28:18-20 Yesu
akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa
wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi;
na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.
Jambo linguine na
la muhimu sana kuhusu utoaji wa sadaka zetu kwa Mungu ni kuhusu uhusiano wetu
na kila mmoja wetu.
Mathayo 5:22-24 Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye
ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa
baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto. 23 Basi
ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno
juu yako, 24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu,
uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako.
Ili kulitimiliza
Agizo Kuu la Kanisa tunapaswa kufanya kazi pamoja kama kikundi au timu. Timu
inategemea sana na jinsi uhusiano ulivyo wa washiriki waalio kwenye ile timu
katika ufanyaji kazi wake wa kiumakini na ushirikiano.
Tazama isemavyo 1Wakorintho
sura ya 3.
Hatutaweza
kusaidiana sisi kwa sisi kuwa Wakristo tusipopendana (Mathayo 22:39).
Yohana 14:15 "Mkinipenda,
mtazishika amri zangu.”
Hii inaturudisha
nyum hadi kwenye amri iliyo kwenye Kumbukumbu la Torati 16:16 kwamba na tusitokee
mbele za Bwana mikono mitupu.
Kanuni ya
kumpenda Mungu na kumpenda Kristo ni sharti tupendane. Hii sio hisia ya juujuu
tu na yakimsisimko kuonyeshana kia mtu na mwenzake, bali ni kuchukuliana mizigo
kikamilifu na kuhudumia au kuwap mahitaji kwa wengine wenye uhitaji; huwaheshimu
wengine kwa kujali utu wao na kuwafanyia mema kwa kuwaona bora kuliko sisi
wenyewe. Inatupasa kulia pamoja na waliao na kufurahi na wafurahio. Inatupasa
kushiriki mateso kwa kuwafariji waumizwao. Yatupasa kuombeana na kuridhika na
ale tulipofikia na tulivyonavyo, na tusiwadhulumu wengine au tusiwiwe kitu na
mtu yeyote.
Mwenendo na nia
yetu kwa hiyo ni wa muhimu sana na ni kit kinachoamua na kuona iwapo kama
sadaka zetu zitakubalika na Mungu au hapana. Hatuwezi kuchukulia utoji wetu wa
sadaka kuwa ni kitu kidogo na kisichohitaji kutilia maanani. Inatupasa kuchukulia
hali yetu ya kiroho kwa umakini na uzito mkubwa.
Hakuna hata mmoja
miongoni mwetu aliye tajiri sana na tunahangaika tuwezavyo ili tuweze
kujihudhurisha kwenye Sikukuu, kutoa zaka kama tulivyoamriwa, na kujipatia
sadaka. Hatuwezi kupata kiasi kikubwa cha sadaka lakini hii haimaanishi kwamba
sadaka zetu zinadharauliwa na kuhesabiwa kuwa si kitu kwa Mungu.
Marko 12:41-44 Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi. 42 Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa. 43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina; 44 maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.
Ni myoyo wetu
ndiyo Mungu anaouangalia na wala sio utajiri wetu.
Sisi, tukiwa kama
sehemu ya mwili wa Kristo ndani ya Kanisa lake Mungu, tunao wajibu wa kuihubiri
injili kwa kila kiumbe. Mkakati huu wa kuihubiri injili inagharama. Wengi wetu
tunafanya kazi za kujitolea, tukiliachia Kanisa litumie akib yake kulipia zile
huduma ambazo sisi wenyewe hatuna ujuzi wa kuzifanya. Ili tuweze kuihubiri
injili kwa kila kiumbe, basi ni lazima itafsiriwe kwa lugha zote. Kuna gharama
inayoendana na shuhuli hii ya kutafsiri maandishi na machapisho yote ambayo
yameandikwa na kuchapishwa na Kanisa kwenye lugha mbalimbali za ulimwengu. Hata
hivyo inafurahisha na kutia moyo kuona jinsi ilivyofanyika kwa kiasi kikubwa.
Lakini tunapaswa kufanya bidii kubwa ili kukamilisha kazi na wajibu wetu.
Wakati tunapotoa
sadaka zetu, ndipo tunategemeza na kuwezesha kufnyika kwa sehemu muhimu sana ya
kazi ambayo Kanisa limegizwa na kuamriwa kuifanya. Hatutaweza kulichukulia
agizo hili kijuujuu na kulipa uzito mwepesi.
Mathayo 24:14 Tena
habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa
mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.
Kila mmoja wetu anawajibika
kutoa sadaka na kuwafikiria mahitaji ya Kanisa, mahitaji ya familia, na
mahitaji yaw engine walio nje ya familia yetu ambayo ni nje ya Mkutano wa kundi
la Mungu.
Injili itahubiriwa
ulimwenguni kote. Maandiko Matakatifu yanasema hivyo, na maandiko hayawezi
kutanguka. (Yohana 10:35). Hebu na tufanye kazi sasa wakati tukiwa
tunahakikisha kuwa hilo linatimilika. Muda uliobakia i mfupi sasa na kama
hatutafanya kazi Mungu atawainua watu wengine waifanye.
Ni sehemu ya shindano
la mbio tunakimbia (Waebrania 12:1) na Mtume Paulo anasema kwenye 1Wakorintho
9:24-27:
Je! Hamjui, ya kuwa
wale washindanao kwa mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate. 25 Na kila ashindanaye katika michezo
hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo;
bali sisi tupokee taji isiyoharibika. 26 Hata
mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si
kama apigaye hewa; 27 bali nautesa mwili
wangu na kuutumikisha; isiwe kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye
tuzo ni, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.
Tunakimbia
shindano la imani kwa ajili ya thawabun ijayo na tuliyoahidiwa. Nayo ni uzima
wa milele kwenye Ufalme wa Mungu. Tunapiga mbio kwa imani ili tuweze kuwa na
sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu, ambao umetajwa kuwa ni ufufuo mwema.
Tunazidi kupiga mbio ili tuweze kufanana na Kristo zaidi na tunapiga mbio hii
kwa unyenyekevu mkubwa kwa Mungu na Amri zake kama tulivyopewa na Kristo.
Kristo anasema
hivi kwenye Ufunuo 3:11-12:
Naja upesi. Shika
sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. 12 Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo
katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika
juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu
mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile
jipya.
Basi na
tutazitunza sadaka hizi tangu sasa ili kwamba Baba yetu aweze kutubariki,
kutusaidia na kutuwezesha tuendelee kufanya kazi kwa mwongozo wa Kristo katika
kukamilisha agizo lake. Hebu na tufurahi sasa mbele za Mungu, hapa kwenye
Sikukuu hii, mahali alipopachagua kwa kipindi hiki sawasawa na amri zake, na
hebu na tufurahi na kusherehekea kwa kuweza kushiriki kipindi hiki pamoja na
kwa amani na nia moja.
q