Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[252]
Amri Kuu ya Kwanza
(Toleo La 2.0 19981005-19990607-20120603-20120804)
Sheria za Mungu zimejumuisha na Amri mbili. Amri hizi Kuu Mbili huunda msingi wa sheria zote na ushuhuda wa manabii yakiwemo maandiko
ambayo Yesu Kristo ameandikwa ndani yake kwa yale yanayoeleweka kwenye Biblia.
Amri hii Kuu ya Kwanza imeandikwa kama: Nawe mpende
BWANA, Mungu wako, kwa moyo wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote
na Amri Kuu ya Pili inafanana na hii: Nawe mpende jirani yako
E-mail: secretary@ccg.org
(Haki Miliki © 1998, 1999, 2012 Wade Cox)
Masomo
haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure
ikiwa tu
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti
yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Amri Kuu ya
Kuielewa Sheria na
makusudio yake kumekuwa na msisitizo unaobadilika kwa vipindi vingi. Inaonekana
kuwa na mabadiliko au myumbisho katika mtazamo kwa
vipindi kadhaa mbali mbali, kiasi kwamba sheria hizi zinaonekana kuwa kana
kwamba zina kuwa tabaka lililowekwa kwa misisitizo tofauti. Kwa usemi wa jumla na haraka na usioonyesha umakini, tunaweza kusema
kuwa manabii wa zamani wanaonekana kuwa aliziona sheria kwa zaidi hasa kwa
kukusudia kuzitumia katika matumizi ya utoaji haki katika maisha ya kijamii.
Manabii waliokuja baada
Simulizi zo zote za sheria zinahitaji
tathmini ya msisitizo wa aina mbali mbali ya maandiko
kwa wakati na kusudio la sheria za asili. Kitu kimoja ambacho ni cha muhimu zaidi na ambacho kwacho yapasa kujua ni
kwamba, Kristo hakuondoa hata yodi moja au kichwa cha somo au nukta moja au
alama wa mkato kwenye sheria.
Katika amri za Mungu, kwa kufuatana na
tathmini za sheria za Mungu, tunaona ambatano linalo fafanua la ujumbe wa
Biblia ukiendelea kwa nyakati mbali mbali ikijulikana
kwamba Sheria za Mungu ni zile zile
hazibadiliki kama zilivyo kwa sasa na kama zilivyowahi kuwa hapo kabla.
Matatizo yote na yaliyo muhimu katika uendeshaji wa taratibu za liturujia na
utakaso na utoaji wa kiukarimu na misingi ya imani vyote vinajibiwa na ufunuo
ulio sahihi kwa njia ya usomaji sheria zinazotolewa kwa kila miaka saba na zikizungushiwa
kwenye shera hizihizi zenyewe kama zilivyo.
Tutaona kuwa hatukuokolewa kwa ajili ya kuzishika sheria peke
yake, bali tumeokolewa kwa neema.
Pasipokuwa na Roho Mtakatifu tusingeweza kuzitunza
sheria
Wakristo wa
ukristo mamboleo kutoka kwenye dini za madhehebu kwa makosa makubwa sana
wamefundisha kuwa sherioa za Mungu eti zilipigiliwa misumari pale msalabani
kutokana na kutafsiri kimakosa ujumbe ulioko kwenye kitabu cha Wakolosai
2:14-15. Ilikuwa ni deni la hali yetu ya kutodaiwa
chini ya sheria, ni cheirographon ndiyo iliyogongomelewa msalabani, sio
Sheria za Mungu
Warumi wakapandikiza dini kwenye dola na wakati hili lilipoharibiwa; walijifanyia sanamu ya Mnyama
ili kuuwezesha mfumo wa kidini utawale vitu vya taifa
wakati ambapo hapo kale kabisa ilikuwa ni kwa dola yanyewe kabisa. Hii
ingefanywa tu kwa kutumia muundo uliofanyizwa upya kikamilifu wa utaratibu wa kibiblia
na wakidini kama sheria zilizopo za Mungu ambazo zinapingwa na kukataliwa mfumo wa kisiasa na wenye mchanganyiko wa Kiyunani
na Kirumi na wakidini chini ya utaratibu wa mungu wa Utatu. Mfumo huu wa uongo wa kidini uliochanganyika na kisiasa ambao bado
unafanyakazi hata sasa huko na Ulaya umewekezwa ili kuushinikiza mfumo huu.
Ni jukumu letu
Amri za Mungu katika sheria
Kinyume na vile ilivyo hadithi au ngano maarufu, Sheria ya Mungu na Amri zake zilikuwa kwenye uwepo, katika ujulma wake, kutoka mwanzoni. Hii imeelezewa kwenye maandiko ya jarida la Fundisho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya 1 Bustani ya Edeni (Na.246) na jarida la Fundisho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya 2 Uzao wa Adamu, (Na.248). Wazo la Sheria za Kinuhu zilizotangulia kipindi cha Sinai ni ghilba za Marabi wa baadae wa dini ya Kiyahudi. Uelewa na kicho cha Mungu ulikuwa katika Israeli tangu kipindi cha Adamu hadi zama za Mababa wa imani, na hadi kipindi cha utumwa wa Misri kama inavyoonekana kwenye mfano wa wakunga (Kutoka 1:17-21).
Kutoka 1:17-21 inasema:
Lakini wale wazalisha walikuwa
wakimcha Mungu, wasifanye kama walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri, lakini
wakawahifadhi hai wale wanaume.
18 Basi mfalme wa Misri akawaita wale
wazalisha na kuwauliza, Kwa nini kufanya jambo hili, na kuwahifadhi watoto
waume wawe hai? 19 Wazalisha
wakamwambia Farao, Ni kwa sababu hao wanawake wa Kiebrania si kama wanawake wa
Kimisri; kwa kuwa ni hodari hao, nao huzaa kabla mzalisha hajapata kuwafikilia.
20 Basi Mungu akawatendea mema wale
wazalisha; na hao watu wakaongezeka sana, wakaendelea na kuzidi kuwa na nguvu nyingi.
21 Ilikuwa kwa sababu wale wazalisha
walikuwa wakimcha Mungu, akawasimamishia nyumba.
Na Mungu akasema na
watumishi wake manabii na hususani na Musa kwa kupitia Malaika wa Yahova
(tazama jarida la Malaika wa YHVH [024].
Kutoka 3:2-22 inasema: Malaika wa BWANA akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei. 4 BWANA alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa. 5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu. 6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu. 7 BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimesikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; 8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. 9 Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. 10 Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri. 11 Musa akamwambia Mungu, mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri? 12 Akasema, Bila shaka mimi nitakuwa pamoja nawe; na dalili ya kuwa nimekutumia ndio hii; utakapokuwa umekwisha kuwatoa hao watu katika Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu. 13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambi nini? 14 Mungu akamwambia MUSA, MIMI NIKO AMBAYE NIKO*; akasema, Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli; MIMI NIKO amenitumw kwenu. 15 Tena Mungu akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli maneno haya, BWANA, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu; hili ndili jina langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata vizazi vyote. 16 Enenda, ukawakusanye wazee wa Israeli pamoja, ukawaambie, BWANA Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenitokea akaniambia, Hakika nimewajilieni, tena nimeyaona mnayotendewa huko Misri; 17 Nami nimesema, Nitawapandisha kutoka katika mateso ya Misri na kuwaingiza katika nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, nchi ijaayo maziwa na asali. 18 Nao watakusikia sauti yako; nawe utakwenda, wewe na wazee wa Israeli kwa mfalme wa Misri na kumwambia, BWANA, Mungu wa Waebrania, amekutana nasi; basi sasa twakuomba, tupe ruhusa twende mwendo wa siku tatu jangwani, ili tumtolee dhabihu BWANA, Mungu wetu. 19 Nami najua ya kuwa huyo mfalme wa Misri hatawapa ruhusa mwende zenu, la, hata kwa mkono wa nguvu. 20 Nami nitaunyosha mkono wangu, na kuipiga Misri kwa ajabu zangu zote, nitakazofanya kati yake, kisha baadaye atawapa ruhusa kwenda. 21 Nami nitawapa watu hao kufadhiliwa mbele ya Wamisri; hata itakuwa, hapo mtakapokwenda zenu hamtakwenda kitupu; 22 lakini kila mwanamke ataomba kwa jirani, na kwa huyo akaaye naye nyumbani, vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na mavazi; nanyi mtawavika wana wenu na binti zenu; nanyi mtawateka nyara Wamisri.
MIMI NIKO AMBAYE NIKO au ‘eyeh ‘asher ‘eyeh au NITAKUWA KAMA VILE NITAKAVYOKUWA (tazama
fn. Hadi
Alimtia mafuta mwanawake wa
kiroho
Zaburi 45:6-7 inasema: Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 7 Umeipenda haki; Umechukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako.
Na akamuweka awe pamoja na wanadamu.
Waebrania 1:8-9 inasema: Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.
Hii ilifanyika ili wote pia waweze kufanyika kuwa ELOHIM.
Zaburi 82:1-6 inasema: Mungu amesimama katika kusanyiko la Mungu; Katikati ya miungu anahukumu. 2Hata lini mtahukumu kwa dhuluma, Na kuzikubali nyuso za wabaya? 3 Mfanyieni hukumu maskini na yatima; Mtendeeni haki aliyeonewa na fukara; 4 Mwokoeni maskini na mhitaji; Mwopoeni mkononi mwa wadhalimu. 5 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani; Misingi yote ya nchi imetikisika. 6 Mimi nimesema, Ndinyi miungu, Na wana wa Aliye juu, nyote pia.
Eloh aliwapa taifa la Israeli mwana wake kama milki yake,
Kumbu kumbu la Torati 32:8-9 inasema: Yeye Aliye Juu alipowapa mataifa urithi wao, alipowabagua wanadamu, Aliweka mipaka ya watu Kwa kadiri ya hesabu ya wana wa Israeli. 9 Maana, sehemu ya BWANA ni watu wake, Yakobo ni kura ya urithi wake.
Wanadamu wanaweza kufanyika kuwa ELOHIM na Maandiko Matakatifu hayawezi kutanguka (Yoh. 10:34-35). Na Mungu alisema na wanadamu kwa kupitia watumishi wake manabii.
Kutoka 4:1-10 inasema: Musa akajibu akasema,
Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawatasikia sauti yangu; maana watasema,
BWANA hakukutokea. 2 BWANA akamwambia, ni
nini hiyo uliyo nayo mkononi mwako? Akasema, ni fimbo.
3 Akamwambia, itipe chini; akaitupa chini, nayo ikawa
nyoka; Musa akakimbia mbele yake. 4 BWANA akamwambia Musa,
Nyosha mkono wako, kamshike mkia; (akanyosha mkono wake akamshika, naye
akageuka kuwa fimbo mkononi mwake;) 5 ili kwamba wapate kusadiki ya
kwamba BWANA, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amekutokea. 6
BWANA akamwambia tena, Sasa tia mkono wako kifuani mwako. Akautia mkono
wake kifuani mwake; naye alipoutoa, kumbe! Mkono wake ulikuwa una ukoma,
umekuwa mweupe
Kutoka 4:29 inasema: Musa na Haruni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa wana wa Israeli
[Note: the sequence of the Exodus is
contained in Exodus chapters 5-10 and the texts relevant to the Law are
contained in the appropriate section.]
Mungu, akiwa kama Eloah, alituma wajumbe
wake,wa namna zote mbili, yaani wakiroho na wakimwili,
akiwa
Kutoka 7:1 inasema: BWANA akamwambia Musa,
Angalia, nimekufanya wewe kuwa kama Mungu kwa Farao;
na huyo ndugu yako Haruni atakuwa
Kutoka wakati huu na
kuendelea, Mungu angefanya kazi ya kuikomboa sayari hii kwa kupitia watu wake
Israeli chini ya mwanae. Kiumbe huyu, kama roho,
alikuwa na jina
Kutoka 11:1-10 inasema: BWANA akamwambia Musa,
Liko pigo moja bado, nitakaloleta juu ya Farao na juu
ya Misri; baadaye atawapa ninyi ruhusa toke huku; naye hapo atakapowapa ruhusa,
atawafukuza mtoke huku kabisa kabisa. 2 Basi nena wewe masikioni mwa
watu hawa, na kila mtu mume na atoke kwa jirani yake,
na kila mwanamke atoke kwa jirani yake, vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu.
3 BWANA akawapa watu hao kibali machoni pa
Wamisri. Zaidi ya hayo, huyo Musa alikuwa ni mkuu
Mungu aliwatumia Israeli ili kufanya ishara na maajabu, na kuonyesha uweza wake kwa mataifa na kwa jeshi la malaika waasi.
Kutoka 14:1-31 inasema: BWANA akasema na Musa, akamwambia, 2 Waambie wana wa Israeli,
kwamba warudi na kupiga kambi yao mbele ya Pi-hahirothi, kati ya Migdoli na
bahari, kukabili Baal-sefoni; mtapanga mbele yake karibu na bahari. 3 Naye
Farao atasema katika habari za wana wa Israeli,
Wametatanishwa katika nchi, ile jangwa imewazuia wasitoke. 4 Nami
nitaufanya uwe mgumu moyo wa Farao, naye atafuata
nyuma
Israeli walibatizwa kwenye utumishi wake
katika Bahari ya Shamu. Alifanyika kuwa ndiye anayestahili kupokea heshima na utukufu kutoka kwao, na kiini cha ibada zao, ili kwamba
waweze kufanyika kuwa ni wateule wake, na viumbe wake wanaoenea kama Elohim,
Kuna nyimbo kumi za kumtukuza Mungu
zilizoandikwa [tazama (1) Kut. 15:1-19; (2) Hes. 21:17-18; (3) Kum. 32:1-43;
(4) Amu. 5:1-31; (5) 1Sam. 2:1-10; (6) 2Sam. 22:1-51; (7) Lk. 1:46-55; (8) Lk.
1:68-79; (9) Lk. 2:29-32; (10) Ufu. 14:3; 15:3]. Kama wimbo wa
Musa ulioko kwenye (Kum. 32:1-43) halafu wimbo wa pili (tazama Kut. 15:1-19)
inaweza kuwa ni Wimbo wa Mwana kondoo,
Ufunuo 15:3-4 inasema: Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa. 4 Ni nai asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu; kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako; kwa kuwa matendo tako ya haki yamekwisha kufunuliwa.
(tazama Zaburi 86:9-12; Isa. 66:15; Zef. 2:11; Zek. 14:16-21).
Kwa utendaji huu tutarejeleza nguvu za nyimbo za utukufu wa Nyota ya Asubuhi katika msingi wa ulimwengu (Ayu. 38:4-7).
Ayubu 38:4-7 inasema: Ulikuwa wapi nilipoiweka
misingi ya nchi? Haya! Sema,
Tutakuwa Elohim na Mungu atakuwa wimbo wetu. Tuta andaa makao na yeye. Yeye ni Elohim wa baba zetu na sisi ni Hekalu lake. Elohim wa elohim wetu ametuchagua sisi kwa mahali pa maskani yake.
Kutoka 15:1-19 inasema: Ndipo Musa na wana wa
Israeli wakamwimbia BWANA wimbo huu wakanena, na kusema, Nitamwimbia BWANA, kwa
maana ametukuka
Israeli
waliokolewa, na kwa tendo hili alipanda mbegu kwenye Urithi
wa Mlima wa Yahova. Yakobo kama Israeli hutawala
kutoka katika mlima wa Mungu (tazama Kum. 32:8). Yakobo kama
Israeli (maana yake ni “yeye atakayetawala
Lakini watu walinung’unikia kukombolewa kwao.
Kutoka 15:20-27 inasema: Na Miriamu, nabii
mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote
wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza. 21 Miriamu
akawaitikia, Mwimbieni BWANA, kwa maana ametukuka
Israeli walipata kupona kutoka katika maovu
Lakini Mungu kwanza aliwakemea kwa chakula kingi
Kutoka 16:9-12 inasema: Musa akamwambia Haruni, Haya, sema na mkutano wote wa wana wa Israeli, Njoni karibu mbele ya BWANA; kwa kuwa yeye ameyasikia manung’uniko yetu. 10 Ilikuwa Haruni aliponena na huo mkutano wote wa wana wa Israeli, wakaangalia upande wa bara, na tazama, utukufu wa BWANA ukaonekana katika hilo wingu. 11 BWANA akanena na Musa, akinena, 12 Nimeyasikia manung’uniko ya wana wa Israeli, haya! Sema nao, ukinena, Wakati wa jioni mtakula nyama, na wakati wa asubuhi mtashiba mkate; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.
Bwana akawalisha manna jangwani kwa kipindi cha miaka arobaini. Wale wote waliokataa urithi wa Mungu walikufa. Kule kuwalisha jangwani kulikuwa ni kivuli cha yale yanayokwenda kutokea, kama ilivyoelekezwa kwa kanisa, kama wateule, na na Roho Mtakatifu kama alivyokuwa ni kiini kwa kipindi cha Yubile arobaini. Hatuwezi kumuona Mungu kwa hali zetu tulizonazo sasa, vinginevyo tutakufa hakika. Hakuna mtu aliyewahi kumuona, au hatakayeweza kumuona kamwe kabisa. Yeye pekee hawezi kufa, aishiye na kukaa ndani yake ni nuru siyosogeleka (1Tim. 6:16).
Tunatakiwa kuitunza
Kutoka 16:32-36 inasema: Musa akasema, Hili ni neno BWANA aliloliamuru, Pishi moja ya kitu hicho na
kiwekwe kwa ajili ya vizazi vyenu; ili kwamba wao wapate kukiona kile chakula
nilichowalisha ninyi barani, hapo nilipowaleta kutoka nchi ya Misri. 33
Basi Musa akamwambia Haruni, Twaa kopo, ukatie pishi moja ya hiyo Mara ndani
yake, uiweke mbele ya BWANA, ilindwe kwa ajili ya
vizazi vyenu. 34
Mungu aliachilia mbali masharti ili kwamba sisi tuweze tuzirithi ahadi zake na ili tuweze kuwa ni hazina ya tofauti ya namna yake kwake.
Kutoka 19:1-25 inasema: Mwezi wa tatu baada ya kutoka Waisraeli katika nchi ya Misri, siku
iyo hiyo wakafika jangwa la Sinai. 2 Nao walipokuwa wameondoka
Refidimu na kufika jangwa la Sinai, wakatua katika
lile jangwa; Israeli wakapiga kambi huko wakiukabili mlima. 3 Musa
akapanda kwa Mungu, na BWANA akamwita toka mlima ule,
akisema, Utawaambia nyumba ya Yakobo, na kuwaarifu wana wa Israeli, maneno
haya. 4 Mmeona jinsi niivyowatenda Wamisri, na
jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi. 5
Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na
kulishika agano langu, hapo ndipo myakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila
yote ya watu; maana dunia yote pia ni
Mungu alitoa sheria zake kwa kupitia Malaika Mkuu, (Malaika wa Shauri Kuu wa Septuagint, yaaani LXX). Kwa njia hii, kwa kupitia mwombezi aliye kati yetu, Mungu aliutoa utaratibu wa sheria akampa Musa, na mwamba wake wa kiroho alikuwa ni Kristo (1Kor. 10:4).
Kutoka 20:1-17 inasema: Mungu akanena maneno haya yote akasema, 2 Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.
[I] 3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
[II] 4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu ya mbinguni, wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usikisujudie wala kukitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
[III] 7 Usilitaje bure jina la
BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina
IIV] 8 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. 9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; 10 lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. 11 Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.
[V] 12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.
[VI] 13 Usiue.
[VII] 14 Usizini.
[VIII] 15 Usiibe.
[IX] 16 Usimshuhudie jirani yako uongo.
[X] 17 Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.
Mgawanyo wa sheria
hizi kwenye Amri Kuu, umetolewa hatimaye kwenye Kumbu kumbu la Torati. Muundo
unnajieleza kwa uwazi sana, kwenye hizi amri nne za kwanza zinazohusika na
upendo wa Mungu, na hizi sita zinazofuatia zinahusiana na upendo wa kila mtu na
mwenzake. Hii kwa hiyo inahusika na watu wa kawaida
(tazama pia kwenye jarida la Pendo na Muundo wa Sheria [200]. Amri ya Tano inaunganisha sehemu mbili kwa
pamoja na kuzifanya ziwe na uhusiano kama wa kifamilia.
Wajibu wetu kwanza ni kwa Mungu, na hatimaye ni kwa ndugu zetu wapendwa. Wajibu wetu ni kujitahidi tufae na tukubalike na Mungu aliye Hai wa walio hai na sio wa waliokufa.
Mathayo 22:29-46 inasema: Yesu akajibu,
akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala
uweza wa Mungu. 30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala kuolewa, bali huwa
Ni kwa jinsi gani basi Daudi alimwita Bwana na elohim? (Zab. 45:6-7; Ebr. 1:8-9).
Bwana alikuwa ni
elohim wa Israeli ambaye alinena na manabii na mababa wa imani. Yeye ndiye
alikuwa ni yule Malaika wa Yahova akiwaongoza Israeli
Sehemu ya kwanza ya sheria inahusiana na upendo kwa Mungu. Hii inatakiwa ifanyike kwa moyo wote na akili na roho. Sehemu ya pili inahusu
kumpenda jirani yako,
1Yohana 4:20-21 inasema: Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo, kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. 21 Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, apenda na ndugu yake.
muundo wa Amri Kuu ya
Mungu anashughulika na huu muundo, kwa maana halisi ya kuwa kwake yeye kuwa ni kiini cha uumbaji na wokovu. Yeye hutoa uzima wa milele kwa ye yote ampendaye, kwa utaratibu aliouweka.
Amri ya kwanza inatengaza muunganiko wa Mungu na ubora wake.
Kutoka 20:1-3 inasema: Mungu akanena maneno haya yote akasema, 2 Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. 3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Amri ya pili inashughulika na kufuru ya ibada za sanamu na matendo ya kuabudu vitu vinavyoonekana. Mungu anataka watu wamwabudu yeye peke yake na kwa roho na kweli.
Inasema hivi: [II] 4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu ya mbinguni, wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usikisujudie wala kukitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.
Amri hii inatuelekeza sisi jinsi ya kuabudu na kile kinachopaswa kuabudiwa. Hatupaswi kujifanyia mfano wa kitu cho chote kwa ajili ya kukipigia magoti, au kukiabudu, au kukifantia maombi. Hii inamaana ya kitu cho chote kama inavyosema: kwa hiyo, msalaba, au nembo ya kitu cho chote, hata kwa vile vinavyodaiwa kuwa vinawakilisha hali fulani ya uwepo wa Mungu au mwakilishi wa Mungu, au Mungu mwenyewe na aina nyingine fulani sio Kristo na wanaoitwa kuwa ni watakatifu waliokufa zamani, ambao kwayo ni Kristo tu ndiye alifufuka.
Amri ya tatu imewekwa kwa
lengo la kulinda uweza wa jina la Mungu, na shughuli zinazohusiana na kutumika
kwa jina lake,
Inaendelea katika [III] 7
Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana
hatia mtu alitajaye jina
Amri ya nne imewekwa ili kuhakikisha kwamba muundo wake wote umefungamanishwa na mtiririko wa Sheria zake, ndani ya kalenda na utaratibu wake. Amri ya nne haielekezi kwenye adhimisho la siku ya Sabato tu, bali inaelekeza utaratibu wa hiyo Sabato, na sheria yote mzima na muundo na utaratibu wake.
Inaendelea katika [IV] 8 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. 9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; 10 lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. 11 Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.
Kwa hiyo, uanzishwaji wa kalenda kwa utaratibu mwingine wowote au msingi ni tendo la kufuru, na uvunjaji wa Sheria na ni ashirio la kuabudu Mungu meingine wa uongo.
Mungu ameziweka Sabato na
Miandamo ya Mwezi Mpya na Sabato za kila mwaka na Sikukuu. Hakuna utaratibu
wowote uliokubalika au kuruhusiwa zaidi ya ule aliouanzisha na
akaupa baraka zake. Utaratibu bandia wa maadhimisho ya
ibada za Jumapili, na maadhimisho ya Christmas na Easter, ni utaratibu wa mfumo
wa Kipagani unaoendana sambamba na Mungu wa Utatu. Ni uvunjaji wa amri zote nne
zilizopo kwenye fungu la Amri Kuu ya Kwanza na ni uvunjaji wa sheria na amri
zote [tazama majarida ya Chimbuko la Christmas na Easter [235];
Fundicho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya 1 Bustani ya Edeni [246] na Fundisho
la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya 2 Uzao wa Adamu [248]. Hakuna mfumo wala muundo ulioruhusiwa zaidi ya ule
alioufanya na kuuweka Mwenyezi Mungu.
Mambo mengi zasa yaliyo kwenye Ukristo wa leo yametuama kwenye mtazamo unaodhania tu kwamba amri za Mungu zimekoma wakti wake na hazina maana au umuhimu tena. Hii inakinzana na hali ya kudharau kukubwa kwa muundu wa sheria na amri hizi za manabii na ujumbe wa Kristo na wa Mitume wake. Kuna utofauti katika Sheria za Mungu kati ya Sheria inayotuama katika Amri Kuu Mbili (na Amri Kumi ambazo zinaziendeleza) kwa upande mmoja na sheria za utoaji wa sadaka unaanzisha kile kinachoitwa Sheria Kuu za muhimu, ambazo zimeanzisha sehemu ya utaratibu wa Hekalu kwa upande mwingine. Sehemu kubwa ya Ukristo mambo leo unachanganya mambo haya na kimakosa sana huifungamanisha Kalenda na mambo mengine makubwa na sheria pamoja na sadaka, katika kujaribu kudharau sheria za Mungu na kuzigeuza na mfumo wa kipagani wa ibaza za Jua na wa Imani za Siri na Fumbo za kidini. Tofauti hizi zimeelezewa kwenye jarida la Tofauti ya Sheria [096] na pia imepimwa katika utaratibu wa majarida ya amri za binafsi zao wenyewe.
q