Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[026]
Kiti cha Enzi Kimoja,
Walaghai Wawili
(Toleo La 1.0
19890125-20010303)
Mfumo uliopo sasa wa Jumuia ya Ulaya
una mfumo wa kinidi uliotabiriwa kwenye Kanisa la kale huhusu jumuia hii.
Mnyama atakuwa na uwezo mkubwa na wa kustaajabisha kimatokeo kwa watu wengi kwa
kipindi cha zaidi ya miongo mitat ijayo. Mmoja wao atashughulika na mambo ya
kiutawala au ufalme kwa sehemu zote mbili, yaani kutawala Uingereza na mataifa
mengine ya Ulaya.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati
Miliki © 2001 Wade
Cox)
(tr.
2015)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Kiti Kimoja cha Enzi,
Walaghai Wawili
Mengi yameandikwa ya ujio wa Wazungu
wa Ulaya nchini Marekani na kuhusu muungano au umoja wa mataifa ambayo
yanalazimisha. Uvunguni mwa mwonekano wa uadilifu wa namna zote mbili, yaani
kisiasa na kiuchumi, kuna mashinikizo mengi yanayofanya harakati zake kwa nguvu
ili kufanikisha muungano wa kidini na kimfumo, sio wa kisiasa peke yake, bali
pia ni kidini, kwenye mistari ya kihistoria.
Ulaya inaiona dharura hii kuwa ni kama
kutimilika kwa hatima iliyoanzishwa muda mrefu, kuiamsha dola kuu ambayo
ilishagakuwepo ya Ulaya. Maono ya Ulaya ni kuwa na dola moja ambayo
imejitandaza na kunaenea kutoka
kwenye bahari ya Atlantiki hadi Urusi (na kwa wengine wanaamini itajitandaza
hadi Urals). Dola hii ya Muungano wa Ulaya inaonekana kama kimsingi
imejikusanya au kujiunga karibu na ‘Ulaya ya Kati.’
Muunganiko huu kihistoria umeonekana
ni kama muungano wa kidini kati ya Kanisa la Katoliki na marejesho ya mfumo au
muundo wa kifalme, ambapo ‘Mfalme Mkuu’ au Mtawala Mkuu ataitawala Ulaya yote,
akiwa kama upanga wa kiraia unaouwezesha Upanga wa Kikanisa la Roma.
Wengi wamewaangalia wa Hapsburgs kuwa
ni kama warithi wa kiti hiki cha ufalme wa Ulaya na kwa kweli wanafiki
wanaostahili kukirithi kiti hiki cha enzi. Hawa Hapsburgs wamekuwa wakifanya
kila liwezekanalo kuelekea kwenye muungano wa Ulaya na inaweza kuwa ni salama
kusema kwamba wanajiona wenyewe kuwa ni kama warithi asilia na wanaostahili
kukitwaa kiti hiki cha enzi ili kutimiliza unabii uliotolewa hapo kale.
Wao hata hivyo sio walaghai pekee
kwenye kiti cha enzi na kuna nyumba nyingine inayohitimisha kisawa unabii, (au
hata ni zaidi yake) na kwa madhara ya kisiasa, wanaweza kuwazidi hawa Hapsburgs
kwenye madai yao ya kukitwa kiti cha enzi cha Ulaya.
Mtu anayeweza kuidai heshima hii ni
Charles, Mfalme wa Wales; Duke wa Cornwall wa Nyumba ya Windsor. Nyumba ya
Windsor kwa kweli ni ya Ufalme bandia ambao ulianzishwa ili kuwondoa wapinga
maoni na mawazo ya Kijerumani. Charles Mkuu Mjukuu wa Mfalme George V alichukua
jina la Windsor kama lionekane kuwa ni jina la Kiingereza, akitokea kwenye
ugunduzi kwamba Edward III alijiita mwenyewe kuwa ni Edward wa Windsor (Robert
Lacey, Majesty p. 124, BCA, London 1977).
Tangu Mfalme George 1 hadi William IV
Wafalme wa Uingereza walikuwa ni watu wanaojulikana kabisa kuwa wanatoka kwenye
Nyumba ya Hanover. Wakati Victoria, binamu wa William IV alipoanza kutawala na
kuolewa na Mfalme Albert, suala la uhakikisho wa kutoa majina sahihi
lilitatanisha sana. Mfalme Albert alikuwa na majina mawili, jina la familia
yake ni, Wettin na Jina la Nyumba yake la Saxe-Coburg-Gotha, yote yakiashiria
kama ya Kijerumani, na Victoria na aliowazaa Albert walikuwa na majina yake.
Kwa hiyo, George V alikuwa ni wa
Nyumba za Hanover na Saxe-Coburg-Gotha. Ilimbidi amuoe Mary, Binti Mfalme wa
Nyumba ya Teck na alikuwa na uhusiano na wakuu wa Ujerumani. Sebule
yake ilijaa mabinamu waliofanyika kuwa ni wa asili kutoka Ujerumani na Denmark,
waliokuwa na majina kama ya Gleichen, Schleswig-Holstein na Battenburg.
Operesheni kubwa
ya kujificha ambayo iliendelea mapema kabla ya mwaka 1939, iliona kuwa Saxe-Coburg-Gotha
ilikuwa Nyumba ya Windsor. Na wa Battenbergs ilifanyika kuwa
Mountbatten, Tecks ikawa Cambridges na Count Gleichen kwa
sababu fulani ikajikuta tu inakuwa Lord Gleichen na kama Lacey
anavyosema, 'jamii ya Schleswig-Holsteins walisuluhisha tatizo kwa kuyafisha.'
(ibid). hawa walikuwa binti wa kifalme waliozeeka ambao walikujajulikana kama
Helena Victoria na Mary Louise ambao hawakuolewa wala kuwa na nyunba hadi kufa
kwao.
Lacey anasema kuwa Kaiser mara moja
alikuwa na neno la mwisho. Wakati ali[poisikia habari hizi za upotoshaji na
ndugu zake, alishauri kwamba alikuwa anaangalia mbele kwenye ufanisi wa
Wanawake walioolewa Wenye furaha wa Saxe-Coburg-Gotha. (ibid).
Lord Louis Mountbatten alikuwa ni
mtoto wa kiume wa Mjerumani aliyezaliwa huko Louis Battenburg, mjukuu wa
Malkia Victoria, aliyefanyika kuwa mtu wa Kwanza kuwa kwenye wadhifa
unaojulikana kama Lord mwenye Mvuto huko Admiralty kwenye kipindi cha mlipuko
wa Vita Kuu ya Kwanza vya Dunia. Ingawa Louis Battenburg alishinda
cheo chake anachostahili, baada ya miaka arobaini na sita ya huduma
zinazotofautiana pamoja na Jeshi la Mfalme la Wanamaji, alilazimishwa kustaafu
miezi mitatu baada ya hali ya uadui ilivyoanzishwa na Wajerumani mwaka 1914,
kwa sababu ya kilio kikubwa cha hadharani cha watu wale wenye asili ya
Ujerumani. Familia ya Kifalme ilikubana na mashambulizi makali zaidi hata. Lord
Louis Mountbatten kama alivyokuwa George VI alikuwa ni mmoja wa watukuu wa
Malkia Victoria. Mjomba wake Czar Nicholas II (Aliyeitwa Dickie aliyetangazwa
na kuheshimiwa kama kumtofautisha na Nicky, (Mjomba Nicky) kwakuwa Nicholas
lilikuwa jina lake la mwisho).
Elizabeth II, binti wa mfalme George
VI ni mrithi halali wa kiti cha Duchess wa Saxe-Coburg-Gotha, pamoja na kuwa
mrithi ia wa mstari wa wafalme wa Uingereza. Sio kwamba Charles anarithi milki
za mistari na madai yake, bali kutokana na baba yake anarithi mambo mengine
moja kwa moja au sio kwa moja kwa moja hata kwenye mstari wa “wablua.”
Mwanamfale Phillip wa Ugiriki
kiutaalamu hakuwa na damu ya Kigiriki mishipani mwake, bali alikuwa ni kutoka
kwenye Nyumba ya Kifalme ya Wadachi wa huko
Schleswig-Holstein-Sonderburg-Glucksburg. Familia hii inadhaniwa kuwa ilipita
kutokana na wafalme kumi na wa nane wa Denmark na waliotoa mmoja na kuwapa kwa
Wanorway, wane kwa Waswiden, sita kwa Wagiriki wafalme wa Warusi na wakati
huohuo iliwatoa Masuria wa Malkia kwa wafalme wa Uingereza, Ujerumani na
Rumania.
Binamu wa Mwana Mfalme Phillip alikuwa
ni Malkia Alexandria wa Yugoslavia. Impressive yake ya muda mrefu na ukoo
mwingine wa nje kujumuisha alama za umashuhuri kama vile Henry Percy (au Henry
Hotspur), Earl wa Northumberland na anajiweka mwenyewe
kurudi Charlemagne.
Mstari wa kinasaba wa Ufalme wa
Uingereza wanadai, tangu Edward III, kipenzi cha wakazi au wananchi wa Ufaransa
wakati wa kufa kwake Charles IV mwaka 1328, lakini kwa kupitia mazingira
yaliyopoteza hamasa au upendo kwa Phillip wa Valois ambaye alitawazwa kuwa
Phillip VI. Mnamo mwaka 1337 Phillip alimtangaza kutaifishwa kwa Gascony na
mnamo Oktoba ya mwaka ule, Edward ambaye huko nyuma alidai Kntawazwa kuwa
Mfalme wa Ufaransa na kuwagawa majeshi kwa makundi manne pamoja naye, ambayo
ilikuwa ni mwanzo wa vita vya 100. Kwa kuwa Ufaransa ilikuwa ndiyo ufalme wa
kale zaidi, jamii ya Lilies wajulikanao kama Ufaransa ya Kale, walitawaliwa
kijeshi mara ya kwanza na ya nne, na Leopards wa Uingereza mara ya pili nay a
tatu (soma maelezo ya Picha ya 1). Gharama za Majeshi huko Ufaransa
ilibadilishwa kutoka Ufaransa ya Kale falme tatu za Kifaransa za Fleur de Lys,
zilizojulikana kama Ufaransa ya Kisasa na kuongozwa na Charles V mwaka 1376 au
mwishoni mwa mwaka 1394. Ilikuwa sio hadi Henry IV alipoinuka na kuchukua
ufalme wa Uingereza mwaka 1399 ndipo Majeshi ya Mfalme yalibadilishwa
kuimarika. Alama yake ya kwanza ilikuwa ni ile ya mtangulizi wake, bali Mhuti
wake Mkuu wa pili ulipungua ilipofikia mwaka 1406, kuonyesha dola za Kisasa za
Ufaransa na Uingereza Kwasehemu. (Rodney Dennys, Heraldry and the
Heralds, p.100, Cope, London, 1982).
Madai ya kuwa Ufaransa ni yao
yalitolewa na Edward III ambaye mama yake alikuwa ni Isabella, binti wa Phillip
IV (1285-314) na dada wa Wafalme Louis X (1314-16), Phillip V (1316-22) na
Charles IV (1322-28).
Edward alimuoa Philippa wa
Hainault, binti wa William wa Hainault na Jeanne, binti wa Charles wa Valois na
mjukuu wa Phillip III wa Ufaransa, alitoa madai mengine zaidi kwa Lilies wa
Ufaransa.
Alama hii hii ya kale inarudi nyuma
hadi kabla ya ustaarabu kwenye kipindi cha mwanzoni, iliyokutwa kwenye Misri ya
Kale, ambapo ilikuwa ni alama ya Uzima na Ufufuo. Ilitumiwa na Wafalme wa
Byzantine na Warumi na kwa hiyo huko Ulaya, ambako Wafalme wa Carolingian
waliitumia kama kitu cha kurembeshea kwenye fimbo za wafalme na sarafuni.
Ilikuja kuungana na wafalme wa Wafaransa kwa kutojitokeza kwenye Mihuri Mikuu
na muhimu ya Henry I (1031-60) na Louis VII, na zinaonekana, kama Majeshi ya
Mfalme wa Ufaransa kwenye Mhuri Mkuu wa Louis VIII mwaka 1223. Kabla ya mwaka
1300 alijulikana kama 'Fleur de Glaieul,' kama ua jeupe au maua yaliyochukuliwa
kama ua maalumu na mahsusi la Bikira Maria. Walifanyika kuwa hawajulikan tangu
kutoka kipindi zama maarufu cha zama kati, kilichochukiliwa kama Mfalme wa
Clovis lipewa Fleur de Lys alipobatizwa na malaika aliyetumwa kwake kutoka kwa
Mungu. (ibid., p.98). (Mhuri huu na picha vilijulikana sana na Oriflamme ya
Kifaransa, bendera nyekundu ambayo pia inaonyesha nembo hii takatifu). Vita vya
Agincourt vilivyopiganwa tarehe 25 Oktoba 1415, lilikuwa ni tukio ambalo hii
Oriflamme ilipeperushwa kwenye vita. Kwa hiyo Maua yalifanywa kuwa nembo
takatifu ya Warumi nay a Dola Takatifu ya Rumi nay a muhimu, iliyojulikana huko
nyumba kwenye unabii unaohusu Himaya au Ufalme wa Siku za Mwisho.
Kwa kuucharanga pamoja unabii huu
maarufu wa Kanisa Katoliki ambao ulienea kutoka zama kabla ya mwaka 236 AD3
kunaweza kuendeleza taswira ambayo kwayo historia iliyopo inavyosema.
(Hitimisho limisho la nabii hizi linakutikana kwenye kitabu kiitwacho Prophecy
For Today (Unabii kwa Ajili ya Siku Hizi), sura ya 5, ukurasa wa 31, Fresno
1956. Hippolytus(d.235) aliandika kitabu kiitwacho 'The Great French
Monarch [Mfalme Mkuu wa Ufaransa] watakaotamalaki sehemu yote ya Mashariki
watokea kipindi kinachokaribia mwisho wa dunia.’
Catelados wa Tarentino (yapata
mwaka 500) alimtarajia mtu huyu kuwa atakuwa kazini hadi atakapofikia umri wa
miaka arobaini na ni Mfalme wa Nyumba ya Lily. Ataishinda Uingereza na dola za
visiwa vingine. Ataichukua Ugiriki na kufanywa kuwa ni mfalme wake. Ataiteka na
kuitiisha Clochis, Cyprus, Uturuki na Wabarbariani, kuwattisha na
kuwafanya watu wote wamwabudu ‘yeye Aliyesulibiwa’. Kwa kiasi kikubwa ataiacha
taji yake huko Yerusalemu.
Mambo mengi yamenenwa kuhusu mfalme
huyu, mengine yakiwa yanaeleweka pasipo shaka kwa asili ya ulimwengu ni kama
ilivyonenwa na mengine ni mambo ya kufikirika tu.
Hakuna shaaka kwamba Mfalme huyu Mkuu
anatarajiwa kumsaidia Papa, kwenye mkakati wake ya kuutiisha ulimwengu mzima
alianzia huko Ulaya kwenyewe. Mfalme huyu atakuwa ni chombo muhimu kwene
mkakati wa kutenganisha za Kanisa la Rumi. Kwa sasa kuna matawi matatu ya
Kanisa Katoliki, ambayo ni Kanisa Katoliki lenyewe, Kanisa la Anglikana na
Kanisa la Kiorthodox kongwe ambalo linajulikana kama Katoliki inayoendeleza
mafundisho ya Athanasian.
Waandishi hawa wanamjumuisha Kaisari
wa Arles (469-543), na Mwenyeheri Rabanus Maurus (mwaka 856)
amenukuliwa kama 'Madaktari wetu wakuu waliokubali kututangazia kwamba kuelekea
nyakati za mwisho mmoja kati ya wazawa wa Wafalme wa Ufaransa atatawala juu ya
Dola yote ya Rumi, na kwamba atakuwa ni Mfalme Mku sana kati ya Wafalme wote
kuwahi kutawala na kutokea Ufaransa na atahitimisha mbio zake’. Madaktari hawa
wa ghafla wanamjua kuwa ataachia madaraka na taji lake la kifalme na fimbo yake
ya kifalme huko Yerusalemu pia wakati hii itakapoashiria mwisho Dola
iliyochangamana kati ya Rumi na Ukristo.
Hii imerudiwa na
Monk Adso (mwaka 992), aliyesema kwamba “Huu utakuwa ni mwisho na
hatima ya Dola ya Rumi na hatimaye ndipo Mpingakristo atajitokeza mara moja'.
Kitabu cha Matukio ya Nyakati ya
Magdeburg (karne ya 12?) ananukuliwa
akisema 'Kwenye utawala wa umwaji damu mkubwa wa Mfalme Charles Mkuu na Mfalme
wa Urafansa atainuka kama Mfalme aitwaye Charles atakayetawala kifalme huko
Ulaya, ambaye kwa yeye, nchi iliyooza ya Kanisa itaanzishwa na utukufu wa kale
wa Dola utarudishwa tena.'
Aystinger – Mjerumani (pia kwene
karne ya 12) alimuweka mfalme huyu kuwa atatawala katika siku za mwisho, ambaye
ataibuka kutoka kwa Mfalme Charles. Ataihuisha nchi ya ahadi, yaani nchi ya
ahadi Yerusalemu, na kulifanyia matengenezo kanisa akiwa kama Mfalme wa Ulaya.
Abbot 'Merlin' Joachim (mwaka 1202)
aliyaelezea utejeshaji huu wa mamlaka na mahali pa kanisa kwa Papa wa siku za
mwisho, atakayeihuisha Yerusalemu na kuwanganisha tena mamlaka zilizoondolewa kwa
kitambo na kwenye kanisa la pande za Mashariki na Magharibi. Papa huyu
anatarajiwa kuwa ataabudiwa kwa kupigiwa magoti na kutoa uwezo hali ya juu sana
wanaopinga hila na mafundisho ya kizushi ya kidini. (Kwa maneno mengine,
kitendo cha kuanzisha tena Mahakama ya kanisa la Rumi inayoshughulikia Mambo ya
Kukufuru au uasi wa mafundisho yao sasa Mkusanyiko Mtakatifu kwa Fundisho la
Imani).
Papa huyu anatarajiwa kujaza hombwe
hilli la Mfalme Repin kwenye kiti cha enzi cha kuda mfupi ambacho
kinakuwa tupu (au kuwepo). Hata hivyo, mwandishi ni wazi kabisa kuwa anazitaja
harakati au mandendo ya mwanzoni mwa karne hii kutoka kwenye hadithi fupi ya
'Wachungaji Malaika' waliotajwa na Malachi kwenye kitabu chake alichokiandika
katika karne ya 12.
Kwa mujibu wa Werdin d’Otrante (karne
ya 13) Mfalme Mkuu na Papa Mkuu watamtangulia Mpingakristo.
Mataifa yatakuwa vitani kwa kipindi
cha miaka minne na sehemu kubwa ya dunia itaangamizwa. Dini zote zitakoma (bila
shaka zitasaidiwa kwa kiasi ukaribu na kiasi kikubwa na Ofisi Takatifu).
Mwandishi huyu anaelezea mfumo wa imani wa Ulaya chini ya Papa na mtawala wa
kiraia anayekwenda kuratibu na kusimamia mikakati ya vita vya kumpiga
Mpingakristo (ambavyo watashinda). (Hii imewekwa kwenye tarehe za sikukuu
zinazofuatia za mwaka 2038 ambazo zinaonekana kukanganya unabii wa biblia na
kuonekana kuchelewa sana).
Habari hii inendelea mbele kupitia
waandishi kama vila Ndugu au Brother John wa huko Cleft Rock (mwaka 1340); na
Catherine wa Racconigi (mwaka 1547). Telesphorus wa Cozensa (mwaka
1588) haujui mwisho wa muungano wa Ulaya na bilashaka anakosea.
Holzhauser (mwaka 1658) anatoa
maelezo ya kina sana ya kile kiachoonekana kama matengenezo ya kimiujiza ya
kurejesha kanisa na Taifa, baada ya kinachoonekana kama ni kifo au mauti ya
Kanisa Katoliki na falme au tawala umeathirika na viongozi au watawala wao
kuuawa.
Mfalme huyu ni budi awe Mkatoliki,
kutoka uzao wa Louis IX (1214-1270) (tena) wa uzao wa familia ya Ufalme wa kale
wa Ujerumani, aliyezaliwa uhamishoni (yaani hakuzaliwa Ujerumani). Ataongoza na
kusimamia kikamilifu na kwa umahiri mambo ya kipindi kifupi. Papa atatawala kwa
umahiri mkubwa masuala ya kiroho kwa wakati huohuo. Mateso yatakoma na haki
itatawala (kwenye Kanisa Katoliki). Dini inaonekana kuelezewa, bali kwa
mabadiliko ya falme zote, itaimarishwa zaidi.
Ataondoa mafundisho ya uwongo na
kuuangamiza utawala wa Kiislamu. Mfalme huyu Mkuu atakuwa na usaidizi usio wa
kawaida na wa asilia na atakuwa ni mtu asiyeshindwa. Wakati huu umegawanyika
kwa awamu na awamu ya Tano iliyohesabiwa tarehe zake kuanzia Charles V, hadi
utawala wa Mfalme Mkuu na awamu ya Sita tangu utawala wa Mfalme Mkuu hadi
kipindi cha Mpingakristo. (Cheo au mtu huyu anayeitwa Mpingakristo ni taasiri
kubwa na mashuhuri inayojulikana sana na vuguvugu la Wasabato wanaofundisha
kinyume na Kanisa Katoliki la Rumi ambaye kwa mtazamo wao wanamuita
Mpingaktisro). Kwa kweli, mtu huyu anayatenda yote ambayo Kristo amesema
atakuja kuyatenda. Jina la Mpingakristo, yaonekana kuhusiana na taasisi mbili
zilizoonyeshwa kwenye unabii wa biblia, Mpingakristo wa Dani (Nabii anayetokea
kwenye mchanganyiko wa makabila ya Dani na Efraimu kwenye Yeremia 4:15 sawa na
jarida la Maonyo ya Siku za Mwisho (Na. 44) na ni mtawala mahiri wa
ulimwengu au Masihi.) Rudolf Gekner (mwaka 1675) anasema kuwa huyu
mtu anayetarajiwa ni mfalme mkuu wa Kaskazini. Father Larinsky (mwaka
l708) anayaelezea matukio haya kuwa yalikuwepo baada ya kugawanywa kwa nchi ya
Ujerumani.
Fr. Laurence Ricci SJ (mwaka 1775)
alikiweka kipindi hiki kuwa kilikuwa ‘Baada ya utawala wa Napoleon na baada ya
kipindi cha vita, baa la njaa, na magonjwa au tauni,’ ambapo 'mtawala au mwana
wa mfalme shujaa atainuka kutoka kwenye Nyumba ya Ujerumani ya kale ambayo
ilitiishwa na Mfalme wa Ufaransa.' Atarejesha mali na raslimali za kanisa,
Uprotestanti utakoma na (Uislamu) au Dola ya Kiislamu ya Uturuki itaanguka na
kufikia mwisho.
Josepha von Bourg (mwaka l807) anasema
kuwa Mungu atamchagua mtu kutoka kizazi cha Constantine, Pepin na Mtakatifu
Louis ambaye amekuwa akijaribu kwa kipindi kirefu cha kukatisha tama kuja
kutoka uhamishoni ili kuitawala Ulaya, nk..
Abbe Souffranid (mwaka 1828)
anayaelezea matendo ya miujiza na uzalishaji wa kiasi kingi cha zaidi ya
matarajio. Katikati ya vilio kila kitu kinapotea na kila kitu kinaokolewa,
kutakuwa na mwadimiko wa kila mwanya au umabli. Marejeo haya ya muujiza wa
uponyaji umeshatokea tayari huko Ulaya na kuna mengine mengi bado yanakuja.
Brother Louis Rocco (mwaka 184O)
anasema kuwa huyu Mfalme Mkuu HATAKUWA Mjerumani. ‘
Mheshimiwa Magdalene Parzat (mwaka
1850) alitumia mfano kuelezea kuinuka kwa Mfalme na Papa atakayeitawala
dunia, (Ataokoa shingo la dume la ng’ombe), Jamhuri ya Ufaransa (na
jamhuri zote nyingine za kimapinduzi inayowazuia?) na kuurudisha ufalme.
Kwa mujibu wa
Rev. Theophilus Reisenger, OM cap (mwaka 1940) Mfalme huyu Mkuu
alikudhaniwa kuwa angekuwa ni Archduke Franz Ferdinand. Anadai kwamba utawala
wa Mpingakristo uliahirishwa na hata pia huu wa Mfalme Mkuu. Ni wazi sana
kwamba mapokeo haya yamekuwa yakichukuliwa hivyo huko Ulaya kwa kipindi cha
takriban miaka 1750, au sambamba na imani ya Waaathanasian wa Kanisa
Katoliki inayoendelea hadi sasa.
Sababu inayoshinda kabisa ni wa
marejesho makuu ya Ufalme na Kanisa kwenye muungano wa Ulaya, chini ya maongozi
ya Kanisa moja la Kikatoliki na Papa. Hii itaenda sambamba au kufuatiwa na
utokomezaji au kuyakomesha kwa kuyapiga marufuku makanisa yasiyo ya Kikatoliki.
Mkakati wa kuyaunganisha dini na makanisa yote ndiyo ajenda iliyopo kwa sasa.
Nyumba ya Hapsburg-Lorraine au
Hapsburgs, kimapokeo imekuwa ikionekana kuwa ni watawala wanaoitwa kwenye Dola
hii ya mwisho ya Ulaya. Wakati kwamba hii yaweza kuwa hivyo si jambo lililo
bayana kuwa wao ni washindani wa pekee.
Kama ilivyoonyeshwa, Mtawala aliyeko
sasa ambaye ni Mfalme wa Wales anakithi vigezo vyote. Jamii ya wa Saxons na
Goths walikuwa nje ya mstari wa kiuzawa wa Wajerumani wakiwa ni sehemu ya jamii
ya wa Scandinavia, hadi Goths walipohamia huko Ulaya waliwa kama
wa Ostrogoths na Visigoths, wakiwa wanaishi huko Gothe au
Gotha. Jamii ya wa Saxons hawakuwa kabisa sehemu ya Wajerumani, hadi wakati
Charlemagne alipowashinda wao na kuwashirikisha wao kwenye Shirikisho la
Ujerumani, kama sehemu ya iliyokuwa Dola Takatifu ya Rumi mnamo mwaka 771-2 na
kuwashinda ndugu zao, wa Lombards mwaka 773-4. Kwa hiyo kuna mashaka
kuhusu kiwango cha kidaraja cha Wajerumani wa Saxons wa Schleswig-Holstein.
Hata hivyo, dunia inawaweka watu hawa kwenye tabaka la Wajerumani ma wa Nyumba
ya Hanover na Saxe-Coburg-Gotha wakistahili kwa mambo yaliyonenwa kwenye
unabii. Ni kweli kwamba Nyumba ya Ufalme wa Ujerumani na Uingereza zilihusiana
na hakuna la kujiuliza kuhusu uhusiano wa Wafaransa na kiti cha ufalme wa
Uingereza, huenda ilikuwa ni zaidi sana kuliko ilivyo sasa kwa Wafaransa na
jamii ya Austro-Hungary.
Tangu kipindi cha kuungana kwa
Uingereza na Scotland mwaka 1707, warithi waliochukua ufalme walichukuliwa na
kukubalika kuwa ni warithi wa taji za muungano, tangu mara tu baada ya kuzaliwa
kwake, akipewa jina la kicheo la Duke wa Rothesay, Earl wa Carrick, Baron
Renfrew na Seneschal au Steward wa Scotland, wakichukuliwa kama warithi wa
Scotland tangu mwaka 1396.
Jina la kicheo la, Mfalme au Prince wa
Wales, lilitungwa na Royal Charter tarehe 24 Marchi 1305 na lilichukua mahala
pa jina la zama kale la ki Anglo-Saxon la Atheling. Mfalme huyu wa
Wales alipewa kutoka zama za kale, jina la pili la kicheo pia la Duke wa
Normandy kutoka kwenye mshikamano wa Normandy na wa tatu kwenye daraja la
kicheo kutoka kwenye mwanzoni mwa tarehe 18 Mei 1332 mrithi amapewa jina la
kicheo la Earl wa Chester. Duke wa Cornwall ni wa pili kwenye daraja lakini
watatu kwenye kipindi cha zamani kutoka kwenye kipindi cha Mwanzoni mwa tarehe
17 Marchi 1336, akiwa mtangulizi wa kwanza wa uundwaji wa cheo hiki cha Duke wa
Uiingereza, cheo kilichochokuliwa kutoka kwenye cheo cha zamakale cha Kirumi
cha Dux (kutoka neno Duco). Kulikuwa na jumla ya hawa Duces
12 waliokuwa wanasimamia mambo ya kiutawala wa Magharibi ya Dola ya
Warumi.
Che hiki cha Duchy wa Cornwall,
alichopewa Mfalme wa Wales, kilikuwa ni marejesho ya kwanza ya kisasa ya cheo
cha lake cha Kirumi cha Duke Mpigana Vita, ambaye lishindwa kicheo na
kimatumizi. (Alan wa Britane ambacho kilichukuliwa kama ni cheo cha
zamakale zaidi kwa urithi wa Dukedom, mara nyingi sana kiliitwa Kuja au
Comes kuliko Dux, kama walivyokuwa waliomfuatia hadi
wakati Mfalme wa Ufaransa Phillip mwaka 1277 alipokurejesha cheo cha Duke kwenye
familia ile).
Charles, akiwa kama mrithi pia wa
Ufalme wa Uingereza wa Dola ya Uingereza na Ireland aliyekuwa na haki halali
kwenye maeneo mengine zaidi ya Rumi ya Kale nay a Dola Takatifu ya Rumi.
Kisiasa, mwenendo wake ulikuwa na
dalili zilizokuwa zinaashiria. Taji hii ikiwa ni kama kichwa cha Kanisa la
Uingereza lilipaswa kuvaliwa na kwa kuungana harakati na matendo ya Waanglikana
wa mrengo wa Kikatoliki na Wakatoliki wa Rumi na muunganoniko kama hizi
zitatokea ili kuwezesha mafundisho ya Kiorthodox. Ni rahisi zaidi kwa watu wa
Ulaya ambao wana namna ya madai ya viti vya ufalme vya nchi nyingi kama vile
Ugiriki na wenye udugu wa karibu kwa wengine kwenye maeneo yote ya Ulaya.
Inawezekana kuwa Malkia Elizabeth II
atakapofikia kikomo cha utawala au kujiuzulu, kama ilivyokuwa wakati mmoja
kukiongezeka msukumo wa yeye kufanya hivyo, zaidi ya ilivyokuwa zikionekana
dalili kwamba Charles angeweza kuwa mwenye kulihurumia na kuchukuliana sana na
mikakati ya Wakatoliki, kama ilivyoashiria kwenye ziara yake aliyoifanya
alipotembelea Roma. Kitendo chake kilichofuatia baadae cha kujitangaza mwenyewe
kuwa yeye ni Mtetezi wa Imani, kwa
ujumla kimekuwa na maana inayokanganya. Ni Malkia tu ndiye aliyemkataza na
kuzuia nia yake ya kushiriki Meza ya Ushirika pamoja na Papa.
Swali ni kwamba, huu ulikuwa ni
mkakati wa kumtawaza yeye kuwa mfalme wakati ambapo Malkia Elizabeth angali hai
bado, na halafu kisha yeye awe mkuu kumliko yeye Malkia naye awe kwenye nafasi
chuki. Hali hiyo ingeongeza madhara ya kisiasa. Je, Uingereza ingejitoa, jinsi
ya mahala pa kisheria inavyotenda kazi ua pengine wangaliyo kuwa nayo kama Kiti
Chake cha Enzi, au hata yeye Mfalme wa Wales, akawa ni Mfalme wa Ulaya?
Kimkakati, Dola ya Uingereza
ingetakiwa kuchukua Kiti hiki cha Enzi cha Ufalme wa Ulaya yote na hii
ingelazimisha Dola kufikia uamuzi wa kujitangaza yenyewe kuwa ni Jamhuri
ndogondogo.
Mataifa kama vile Australia
yangepelekea kwa hiyo kujiengua kwenye umuhimu wa kuhitaji kiapo, kama
ilivyotakiwa hata na mstari wa uzawa wa zamakale zaidi ambao Mfalme anatokana
kwao na kumuwezesha kuchukua Kiti cha Enzi cha Daudi. Kama katiba ya Australia
ilivyo kuwa ni kifaa muhimu kwenye Bunge la Uingereza, ndipo hata uhuru wake
unaweza kukosolewa. Mamlaka ya kiutawala ya Canada kimkakati
yanaweza pia kwenye nafasi ya uchochezi. Kimkakati, Canada ingefanyika kuwa ni
Koloni la Ulaya na kujitangazia kwake kuwa Jamhuri kungechukuliwa kama uasi.
Kwa hiyo nchi ya Marekani ingejikuta inazingirwa na jeshi la mataifa ya
Wakatoliki.
Kwa hakika kitendo cha Mfalme wa
Uingereza kuwa kwenye kiti cha ufalme wa Ulaya, kunahalalisha kisheria dhana
iliyopo ya mwisho wa taifa la Uingereza kwa kweli. Hii si mara ya kwanza kwamba
Muundo wa Jumia ya Ulaya imepokonywa uwezo na kuchezewa na wazo hili. Hitler
alijaribu kumuweka Edward VIII kwenye maabusu ya Ulaya na ilibidi nafasi yake
ichukuliwe kwa kupitia Wallis Simpson, kisha mapenzi na nia ya kihisia ya watu
wa Uingereza iliyotokea kuangamia vibaya kabisa.
Malengo ya wazungu wengi wa Ulaya (na
wale wa jamii ya Prieure de Sion) hata hivyo, wamekuwa
wakijiandaa kuelekea kwenye kuifanya kuwa ni Marekani ya Ulaya, chini ya
Hapsburgs na kile kinachoitwa Lstari wa Merovingian wa wafalme, yenye kiini cha
Kanisa Katoliki la Rumi.
Wakati huuhuu, watu wanataka kumuweka
Hapsburg kwenye kiti cha enzi cha ufalme, mazingira ya kisiasa nay a kimuangano
yanaweza kutafuta kuyapa nafasi au fursa matumaini ya mnafiki mwingine kwenye
kiti cha enzi cha Ulaya, kwa maelekezo ya umakini mkubwa ya Bunge la Ulaya.
Tungetarajia kuona shinikizo zaidi la kumtaka Malkia
ajiuzulu kwa kadiri muda unavyozidi kwenda, pamoja na uwezekano wa miungano ya
makanisa yakiendelea nyuma ya matukio.
Kwa Charles, kwa kweli Ulaya ‘ingekuwa
inastahili kula Mlo wa Ushirika.' Charles Phillip Arthur George anapewa kazi
hili kwa haraka. Wafalme au viongozzi wa Cornwall na Wales walipewa jina la kicheo
la Joka, yaani Dragon na alama ya upashaji habari ilikuwa ni joka jekundu.
Alimpa jila la maua Phillip, jina maarufu la wafalme walio kwenye Mstari wa
Wafaransa. Alitimiliza umaarufu wa kukumbukwa kwa jamii ya Arthurian wa mfalme
aliyekuwapo na Yule ajaye akiwa sio kwamba ni Pendragon peke yake (au
Mfalme Mkuu) wa Uingereza, bali wa Ulaya chini ya Dola inayoamka tena ya Rumi
na kujumuisha wa upande wa Magharibi na Mashariki mwa Ulaya, ni kama George wa
mwisho wa Wahellenes.
Kuanzishwa tena kwa ufalme huu wa
mwisho wa Wafaransa kama Dola Takatifu ya Rumi haikubaliani na hatima ya taifa
la Israeli.
Hili ni tukio lililowahi kutabiriwa na
nabii Ezekieli kwenye sura ya 21:26-27 kuhusu kukomeshwa kwa ufalme wa Israeli,
baada ya kupinduliwa kwake mara tatu. Kwa kuwa baada ya kuondolewa Visiwa
kulikonenwa na Yeremia na baada ya kupinduliwa tena huko kutoka nchi ya Ireland
hadi Scotland na kutoka Scotland hadi England, bado kuna ukomo uliopo, hadi
atakapokuja Masihi.
Bwana MUNGU asema hivi;
Kiondoe kilemba, ivue taji; haya hayatakuwa tena kama yalivyo; kikweze kilicho
chini, kakishushe kilichoinuka. 27 Nitakipindua,
nitakipindua, nitakipindua; hiki nacho hakitakuwa tena, hata atakapokuja yeye
ambaye ni haki yake; nami nitampa.
Ukomo wa mwisho wa ufalme wa Waisraeli
ulipasa kutarajiwa kwa kutokea tukio la utumwa au uhamisho wa jamii ya watu
wanaoongea lugha ya Kiingereza. Uingereza (na Canada) watakwenda wakiwa chini
ya mfumo wa Wakatoliki wa Ulaya. Kwa shuruti na ukatili mkubwa, jamii mpya ya
Dux Brittanicum watawatumikisha utumwa jamii ya Angles, Saxons, Jutes
na Danes.
Kutakuwa na uhamisho na mateso makubwa
kufanyiwa wale wote ambao hawataukubali Ukatoliki kwenye nchi hizi.. Australia
na New Zealand zitakuwa zimeenezwa na hawa wahamiaji wenye asili ya Kiingereza.
Wito uliotolewa wa kuwataka watu ukisema ‘tokeni kati yake enyi watu wangu’ una
maana mpya. Wazungu wa Ulaya na kama walivyo wahamiaji walipaswa kutarajiwa
kujaribu kuiweka Australia chini na Nguvu za Mnyama wa Ulaya. Hii kama ilivyo
ingekuwa ni jambo lisilokubalika kwa ‘Wafalme wa Jua Linalokucha’ au ‘Wafalme
wa Mashariki’ walioandikwa kwenye Ufunuo 16:12.
Inaonekana kuwa Australia
ingeshambuliwa na kufikia toba kwa kuvaa nguo za magunia na kujitia majivu na
mavumbi vichwani, ila nchi hizi zimefanya kila linaliwezekana kwenye mwandamano
wa matukio ya siku za mwishoni.
Utabiri wa pili uliofuatia
wa Sybilline ulijua jambo hili wakati ulipoandikwa (huenda ni mapema kabla
ya mwaka 150 BK). Baada ya kuelezea ongezeko la maafa ya nyakati za mwisho,
nabii wa uwongo au kiongozi wa kidini mwenye asili ya kutenda kwake shetani
atatenda miujiza na kuleta maafa katika nyakati za mwisho, mambo ambayo
yatawachanganya na kuwadanganya watu wendi, kiasi cha kuwachanganya yamkini
hata wale waliochaguliwa kuirithi neema au wateule ambao pamoja na Waerania
watakuwa wamenyang’anywa. Inasema:
Hasira kali itawajilia
wakayi watu wa makabila kumi watakuja kutoka mashariki ili kuwatafuta watu,
ambao chipikizi wa Ashuru atakapowaangamiza wenzao Waebrania. Mataifa yataangamia
baada ya vitu hivi.
Kutokana na Ezekieli sura ya 29-32 ukaliwaji wa mwisho
wan chi ya Misri na Wafalme wa Kaskazini utapaswa ufanyike sio kwa kitambo
kirefu sana cha siku zijazo, baada ya mgogoro wa Waislamu wa Ulaya kutokea.
Wakati Utabii wa Sybilline ulipokuwa unaandikwa, kulikuwa hakuna mataifa
yalilojulikana kama ni ya Waisraeli mashariki mwa tunapopaita leo Israeli. Ni
makabila kumi pekee au Waisraeli mashariki mwa Yudea ni Waaustralia na wa New
Zealand. Kwa kweli, hakuna taifa lolote linguine ambalo hata kwa mtazamo wa
kiujima lililotiliwa maanani kuwa limemudu kuuhitimisha au kuutimiliza unabii
huu. Uwezekano uliopo hadi sasa ni kwamba nchi ya Marekani inaweza kusaidia kwa
kupitia Australia. Unabii huu umechukuliwa kutoka kwenye unabii ulio kwenye
biblia unaoelezea kuhusu ujio wa Masihi. Hii inahusisha na unabii mwingine
unaohusu kazi za Mungu katika nyakati za mwisho, ambapo kazi ya Mungu itakuwa
na nguvu sana upende wa kusini. Jambo hili limeelezewa kwa kina kwenye jarida
la Moto Kutoka Mbinguni (Na. 28).
Nabii Yeremia anaelezea juu ya maonyo
ya kukaribia kwenye sura ya 4:15, ambapo sauti, mateso yanayotangazwa kutoka
kwenye milima ya Efraimu, yakionya mataifa kwamba anakuja, naye anauhusiano ia
na kabila la Dani.
Hii inashabihiana na bashiri za
Wakatoliki, zinazomwelezea Mpingakristo wa kabila la Dani, anayejaribu
kuzirejesha tena Sheria za Musa anayekuja akitokea nchi ya mashariki iliyo
katikati ya bahari mbili.
Kwa kweli hii ni kweli kama nabii
Isaya alivyowahi kutabiri kwenye sura ya 46:11, ambapo anatangaza mwisho kutoka
mwanzo urejesho wa wito wa Milele ‘ndege mtoza ushuru kutoka mashariki, mtu
atakayeliondoa shauri langu wa kutoka nchi ya mbali'.
Inapasa ikubukwe kwamba ndege tai ni
nembo au alama ya kabila la Dani na hii ‘nchi ya mbali’ ni lugha mfano
inayoashiria kuwa ni nchi ya Australia, kwa matumizi karibu tangu kuanza kwa
makazi yao. Iyaweza kuwa pia inaashiria kuhusu Wafalme wa Mashariki wa unabii
unaofuatia. Hii ni mara tu kabla ya kuja kwa Masihi kama ilivyo kwenye aya ya
13 ambako tunapoambiwa 'Tena nitauleta haki yangu, haitakuwa mbali sana, na
wokovu wangu hautachelewa; na nitauweka wokovu wangu katika Sayuni kwa ajili ya
Israeli utukufu wangu.'
Inaweza kuwa huenda kwamba huyu nabii
mwenye nasaba mchanganyiko ya Dani na Efraimu ni sauti au kundi litakalotokea
mapema kabla ya mashahidi wawili waliotajwa kwenye Ufunuo 11. Wakati wa vita
vya mwisho ambavyo vitashuhudiwa kutokea hivi karibuni, mambo ya kiuchumi na
kimkakati yatajumuishwa pamoja na kuchukuliwa kwa uzito sawa mambo ya kidini.
Dola mpya yenye nguvu kubwa ya Ulaya itakuwa na nguvu z namna zote mbili, yaani
za kiraia au kijamii na kidini, na ukubwa wa mataifa yake na uwezo wake wa
kivita utawashangaza na kuwahadaa watu wengi. Vita hivi vya mwisho kupiganwa hapa
duniani ni vya muhimu sana kiroho na havitapiganwa kwa nguvu za mwili, 'wala si
nguvu bali ni kwa Roho wangu, asema Bwana.’ Vita hii na Waislamu inakuja na
itatokea hivi punde, na ni ‘vita ya mwisho ya wafalme wa kaskazini na kusini\
iliyotabiriwa na Mungu kwa kupitia nabii Danieli.
Kusudi na lengo la jarida hili ni
kupembua unabii usio wa kibiblia. Pia limekusudiwa kuonyesha kuwa kuna mlolngo
wa uwezekano kwenye mgawanyo ujao wa na uadui. Matendo haya ya siku zijazo
yanaweza kufanywa ili kuwavutia au kuwakanganya watumiaji wa lugha ya
Kiingereza na kuathiri kwa kuikomesha nguvu za muungano wa Jumuia ya Madola,
ambayo pamoja na Marekani, na kuendelea hadi leo, imeuwezesha ulimwengu
kujipatia uhuru ambao usingeweza kujipatia kamwe kwenye Ulaya iliyoungana.
Utambulisho au alama ya watu wanaotumia lugha ya Kiingereza ni zana muhimu sana
katika kuielewa Biblia na matendo au harakati zinazowahusu wao katika nyakati
za mwisho.
q
(kushotot) Sarafu ya Zamakale ya Ufaransa na Uingereza ikiwa na migawanyiko ya
roborobo na (kulia) Sarafu
ya Kisasa ya Ufaransa na Uingereza roborobo.