Makanisa Ya
Kikristo Ya Mungu
[004]
Kuichagua Huduma
(Toleo La 2.0 20000419-20110701)
Kwenye zama hizi za leo za upashanaji wa kisasa
tunaweza kushangazwa tu kuona idadi kubwa ya vikundi na makanisa ulimwenguni
yanayolitumia jina la Kristo. Hata kama tukiyaondoa au kutoyahesabia yale
yasiyoyatumia maneno “Kanisa la Mungu” kwenye majina yao, bado tutabakiwa na
idadi kubwa kwa mamia. Lakini lakujiuliza ni kwamba je, haya yote yanasifa na vigezo stahiki? Je,
tutawezaje kuchagua huduma halisi na sahihi ili ituongoze kwa Kristo? Je,
tungoje tu mstari mrefu unaoendelea wa viongozi walioitwa na kupewa majukumu mfululizo
kutoka kwa Kristo hadi kwenye nyakati zote na zama zote? Tunawezaje kuwajaribu
watu hawa, na kulikuta Kanisa la kweli?
Christian Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2000 Pieter Voges and Wade Cox, ed. Wade Cox)
(rev.
2011; tr. 2015)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu
bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza
kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka
maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Kuichagua Huduma
Kwenye zama hizi za leo za upashanaji wa kisasa tunaweza
kushangazwa tu kuona idadi kubwa ya vikundi na makanisa ulimwenguni
yanayolitumia jina la Kristo. Jambo hili lilitabiriwa kuwa litatokea.
Mathayo
24:4-5 Yesu akajibu,
akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina
langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.
Wengine wamegundua kwamba jina linapaswa liwe sawasawa na
kama alivyolitumia Mtume Paulo.
2Wakorintho 1:1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu,
na Timotheo ndugu yetu; kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na
watakatifu wote walioko katika nchi yote ya Akaya.
1Wahesalonike 2:14 Maana ninyi, ndugu, mlikuwa
wafuasi wa makanisa ya Mungu yaliyo katika Uyahudi, katika Kristo Yesu;
Hata kama tukiyaondoa au kutoyahesabia yale yasiyoyatumia
maneno “Kanisa la Mungu” kwenye majina yao, bado tutabakiwa na idadi kubwa kwa
mamia. Lakini
lakujiuliza ni kwamba je, haya yote yanasifa na vigezo stahiki? Je, vikundi na
makanisa haya yote yameanzishwa na Kristo? Je, Kristo amegawanyika? Tunawezaje
kuwajaribu watu hawa, na kulikuta Kanisa la kweli?
Je, Ni Mwendelezo wa
Mstari Ulioahidiwa na Kukusudiwa?
Wengine wanaweza kuhisi kwamba wamekuwa ni mwendelezo wa mstari
wa mfululizo ulizokusudiwa na kuwekwa kutoka kwa Kristo na kuelekea chini kwa
zama na zama. Bahati mbaya sana hili sio jambo la wakati wote. Wakati mwingine,
kiongozi anayechukua uongozi kutoka kwa mwingine anakuwa fisadi na muovu, na
kuliongoza kanisa kuelekea kwenye unpangiliwapointments from Christ down
through the akengeufu. Jambo hili linajitokeza kwenye mwisho wa kila zama ya
Kanisa, kwa mujibu wa Ufunuo sura za 2 na 3. Hebu na tuyatathimini matukio ya
ukengeufu wa Kanisa la kwanza.
Yuda 3-4 Wapenzi, nilipokuwa nikifanya
bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona
imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa
watakatifu mara moja tu. 4 Kwa maana kuna watu
waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri,
wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake
Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo.
Kweli ilikuwa imepuuzwa na kuachiliwa mbali, na hatimaye ilikataliwa.
Waliongozwa na wengine kwenye huduma hizi kuamini kwamba neema maana yake ni ruhusa
ya wao kuendelea kuziishia dhambi. Matatizo haya yalitokea ili kwamba waumini
wa uwongo wajlikane, kwa kuwa watafuata ukengeufu wao na kuuamini na kuupenda
kwa furaha kuu.
1Wakorintho 11:18-19 Kwa maana kwanza mkutanikapo
kanisani nasikia kuna faraka kwenu; nami nusu nasadiki; 19 kwa
maana lazima kuwapo na uzushi kwenu, ili waliokubaliwa wawe dhahiri kwenu.
Hatimaye kinara cha taa kitaondolewa kutoka kwa kiongozi
aliyewekwa, na kupewa mwingine.
Ufunuo 2:5 Basi, kumbuka ni wapi
ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo,
naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu.
Kwa hiyo, ilitokea hivyo nyakati zilizopita kwamba Kristo
alipaswa kulianzisha kwa kulifufua Kanisa kutoka mautini kwa kuwatumia viongozi
wapya.
Alimwambia Baba yake, yeye Mwamba ambao Kanisa limejengwa
juu yake, na Kristo akiwa ndiye jiwe kuu la pembeni, Kristo alimwambia Patro,
mfano huu kwa wakati ule:
Mathayo 16:17-18 Yesu akajibu, akamwambia, Heri
wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba
yangu aliye mbinguni. 18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe
Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu
haitalishinda.
Hii inaonyesha dalili ya kwamba kwa wakati ule itampasa
Kristo kulilinda Kanisa kutokana na tofauti kubwa sana na ya muhimu au mauti,
iliyoelezwa na kumaanishwa kwa jina la “jehanamu”, yaani, kaburi au kuzimuni.
Uongozi wa Kanisa unapaswa kuchukuliwa kama ulikufa kiroho na haukuruhusiwa
kuweka kiongozi mpya aliyekubaliwa na Kristo. Kiongozi aliyekengeuka atakuwa anawafukuza
viongozi wengine wa kweli na wapenda kweli, kama ilivyotokea.
3Yohana
9-10 Naliliandikia
kanisa neno, lakini Diotrefe, apendaye kuwa wa kwanza kati yao, hatukubali. 10 Kwa hiyo, nikija,
nitayakumbuka matendo yake atendayo, atoavyo upuzi juu yetu kwa maneno maovu;
wala hatoshwi na hayo, ila yeye mwenyewe hawakaribishi hao ndugu, na wale
watakao kuwakaribisha, huwazuia, na kuwatoa katika kanisa.
Wakati Kanisa linapofikia kiwango hiki, wakati hata
kichwa na fikra za mwanadamu zinapokuwa zimezama kwenye ukengeufu, ni dhahiri
kabisa kwamba yeye hatamchagua kiongozi mpya atakayeyathibitisha na
kuyaendeleza makosa ya zamani yaliyofanywa na kiongozi aliyepita. Kwahiyo,
kwenye mabadiliko ya kutoka kwenye kipindi cha zama moja ya Kanisa ilivyo
kwenye Ufunuo 2 na 3 na kuanza zama ya Kanisa linguine, ilipasa kiongozi
mwingine mpya mwanadamu achaguliwe kutoka kwenye kundi la waliosalia kutunza
uaminifu na waliofukuzwa kwenye imani ya kiongozi mkengeufu. Mamlaka ya
kuchagua viongozi yamepewa Kanisa na kitendo cha kubatiza ni njia ya kumhamisha
Roho Mtakatifu kwa mbatizwaji. Mungu aliliambia Kanisa akiwaambia walengwa
wote, yaani viongozi na wapendwa waumini kuwa:
Mathayo
16:18-20 Nami nakuambia,
Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango
ya kuzimu haitalishinda. 19 Nami nitakupa wewe funguo
za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa
mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni. 20 Ndipo alipowakataza sana wanafunzi wake wasimwambie mtu
ye yote ya kwamba yeye ndiye Kristo.
Mitume kwa pamoja
waliunda bodi ya uongozi. Hoja hapa ilikuwa imetumika kuendeleza suala
lililotokana na tabia ya Petro ya kimbelembele. Hatahivyo, yatupasa kurejea
kwenye maandiko yaliyo kwenye Waefeso 2:20 na Ufunuo 21:14.
Mtindo uliotumika kuyaandika maneno haya ni wa lugha ya
Kiaramu kuelezea Mwamba na jiwe dogo. Maana halisi ya maneno ni Petros kwa
Mwamba na petras kwa jiwe dogo, ambayo inamaanisha Petro.
Mwamba wa kweli wa Kanisa, Kefa, ulikuwa ni Mungu
mwenyewe na ilikuwa ni kwa mapenzi na mpango wake Mungu kuwa Kristo alilijenga,
na jambo hili au ukweli huu umepotoshwa kwa makusudi na imani ya waamini Utatu
ambayojikuta yenyewe ikijumuika na kuwa chini ya mfumo na mafundisho ya Papa
ili istahimili kumudu kuendelea. Petro aliteuliwa kuwa askofu wa Anthiokia na orodha
ya mambo yake mengi haionekani wala kujulikana kabisa na alikuwa na wadhifa wa
juu kimaongozi zaidi ya askofu wa Roma (kama ilivyo kwenye Orodha ya Mapapa na
Wapinga-Mapapa kwenye jarida la Jarida la Nyongeza A (Na. 288a)).
Mamlaka hapo
mwanzoni kabisa ilitolewa na Kristo na aliwapa mitume sabini alipowasimika, na hatimaye
kwa Kanisa zima lote na kwa yeyote ambaye Kanisa linamuweka wakfu sawasawa na
vigezo vya kimbuni (soma Luka 10:1,17). Malaika wote waasi ambao sasa ni
mashetani na mapepo waliwatii hawa mitume sabini. Walifanyika kuwa ni bodi kamili
ya kuliongoza Kanisa ambayo ilichukua mamlaka na shughuli zote za utendaji kazi
ambao hapo mwanzoni mamlaka na uweza huu ulikuwa chini ya baraza la Sanhedrin la
Waisraeli. Tangu hapa, Israeli walifanyika
pia kuwa ni sehemu ya umma wa kiroho na Wokovu ukaenea na kuwafikia Wamataifa.
Sasa tunaona kwamba mamlaka yalitolewa kwa waumini wote
walio kwenye bodi au ushirika wa Kanisa. Tunaona kwamba bodi hii iliweka na kutawaza
viongozi na waliwekwa wakfu na uongozi uliokuwa kwenye muundo huu wa uongozi. Mamlaka
ya kufunga na kufungua limepewa Kanisa.
Mathayo
18:15-20 Na ndugu yako
akikukosa, enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu; akikusikia, umempata
nduguyo. 16 La, kama hasikii, chukua pamoja nawe tena
mtu mmoja au wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno
lithibitike. 17 Na asipowasikiliza wao, liambie
kanisa; na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako kama mtu wa mataifa na
mtoza ushuru. 18 Amin, nawaambieni, yo yote
mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua
duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. 19 Tena
nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote
watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni. 20 Kwa
kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo
katikati yao.
Mamlaka ya kufunga na kufungua imetolewa na limepewa
Kanisa kwa ujumla na kwa viongozi wake waliowekwa wakfu. Dhana iliyojengeka ya
kuwa mamlaka hii imepitia kwa mkondo wa mtu mmoja hadi mwingine ni ya kishirikina
na na sio fundisho la kweli la imani ya kweli ya Kikristo (soma jarida la Abrakadabra: Maana ya Majina (Na.
240)).
Kwahiyo, hatuwezi kutarajia mwendelezo endelevu wa
uwekaji wakfu kutoka kwa Kristo hadi kipindi hiki cha sasa. Itatupasa tu
kuthibitisha ukweli na kisha tuthibitishe na kulijua Kanisa la kweli jinsi
lilivyo.
Mathayo 7:15-21 Jihadharini na manabii wa uongo,
watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu
wakali. 16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu
huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti? 17 Vivyo
hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya. 18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu
kuzaa matunda mazuri. 19 Kila mti usiozaa tunda zuri
hukatwa ukatupwa motoni. 20 Ndiposa kwa matunda yao
mtawatambua. 21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana,
atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba
yangu aliye mbinguni.
Tumeelekezwa kuwa tuitafute ilipo huduma ya kweli
inayomtii Mungu, Baba, na inayozishika Amri zake zote.
Watumishi
Wanaolihudumu Neno Lote Kikamilifu
Manabii wa zamani wamekwishatupa tayari vigezo vyake.
Huduma ya Mungu na Mwanawe aliyemchagua ataishi na kufundisha sawasawa na kila
lisemavyo Neno la Mungu, akitenda kwa kuifuata kanuni na Sheria hii.
Isaya 8:20 Na waende kwa sheria na ushuhuda;
ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi.
Huduma ya kweli itaishi kwa kila Neno litokalo kwa Mungu.
Mathayo 4:3-4 Mjaribu akamjia akamwambia, Ukiwa
ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate.4 Naye
akajibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno
litokalo katika kinywa cha Mungu.
Watazitii na kuzifundisha amri za Mungu. Watajua na kuelewa
kwamba maana ya Ukristo ni kufanana au kuwa kama Kristo, kwa kumpenda Mungu na
kuzishika amri zake.
Ufunuo 12:17 Joka akamkasirikia yule mwanamke,
akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za
Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.
Ufunuo 14:12 Hapa ndipo penye subira ya
watakatifu, hao wazishikao amri za Mungu, na imani ya Yesu.
Kwa hili tuna muongozo wa kutosha ili kuligundua Kanisa la
kweli. Kwa mfano, litakuwa ni Kanisa linalozitunza Sabato, kuadhimisha Miandamo
ya Mwezi Mpya na kuziadhimisha Siku Takatifu zilizoamriwa na Mungu kwa mujibu
wa Kalenda aliyoiweka Mungu. (soma jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156)). Tunaona kwamba kwa uwingi
mkuu na wa jumla ulilikosoa Kanisa la kwanza kwa kufanya kwake hivyo.
Wakolosai 2:16 Basi, mtu asiwahukumu ninyi
katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;
Kanisa limekuwa ni bodi inayoonekana na kutambulika kwa
kipindi cha zaidi ya milenia mbili, likiteswa kwa ajili ya utii wake kwenye
Amri za Mungu na Ushuhuda wa Mungu au imani yake kwa Yesu Kristo (Ufunuo 12:17;
14:12) (soma jarida la Wajibu wa Amri ya Nne Kwenye Historia
ya Makanisa ya Mungu Yanayozitunza Sabato (Na. 170)).
Kuanzisha Huduma
Huduma inaanzishwaje? Je, Biblia inatupa mwongozo wowote?
Je, kuna utaraticu wowote wa kuchagua ambao kwamba washirika wa Kanisa la kweli
wanachaguliwa kwenye huduma?
Jibu ni kwamba “Ndiyo” upo. Tutauangalia utaratibu huo.
Mitume wa kwanza wa Kristo
Tunauona uchaguzi wa kwanza kwenye
uingizaji wa walio mbadala wa watu wa Yuda.
Matendo 1:15-20 Siku zile akasimama Petro kati ya hao ndugu (jumla
ya majina ilipata mia na ishirini), akasema, 16 Ndugu,
ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha
Daudi, katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu; 17 kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata
sehemu ya huduma hii. 18 (Basi mtu huyu
alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake
yote yakatoka. 19 Ikajulikana na watu wote wakaao
Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde
la damu.) 20 Kwa maana imeandikwa katika chuo cha
Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa, Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo;
Jinsi tutakavyoona mchakato wa uchaguzi.
Nafasi ya juu zaidi
ya mwanadamu
Kwanza kabisa, inatupasa kujua kwamba wakati Kristo
alipotembea juu ya nchi, alikuwa ni mamlaka ya juu sana akiwa na umbo la
kibinadamu. Aliwaambia (au kuwapa majukumu) mitume waunganenaye, kama
walivyokuwa wametolewa na kupewa Kristo. Kibinafsi yeye aliwajulisha kuhusu
kuitwa kwao. Mungu aliwachagua mitume kumi na mbili. Kristo aliwajulisha kuhusu
kuchaguliwa kwao. Hata hivyo, Kristo hakujionyesha mwenyewe kwao kama kwenye
hatua hii alivyofanya uchaguzi wake mwenyewe kwa dhahiri na kumchagua mtume
atakayechukua nafasi yake. Zaidi ya yote, mitume kumi na mbili wengine walikuwa
na mamlaka sawa hadi wakati huu. Kwa hiyo, hakuna hata mmoja wao angeweza kuwa
na mamlaka ya kumsimika mwingine aliye chini yake, kwa kuwa mitume hawa kumi na
mbili walikuwa na cheo sawa kwa kila kabila moja ya makabila kumi na mbili ya
Israeli.
Mathayo 19:28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia
ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa
Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na
viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.
Kwa hiyo, kwa nafasi hii ya juu sana kuliko, mapenzi ya
Mungu yalitafutwa. Hili lilifanyika kwa mchakato wa namna mbili.
1. Weka kigezo cha kuitwa na kuchaguliwa
2. Kama kuna mmoja anayefikia vigezo kuliko wengine, piga
kura ili kutafuta chaguo kutoka kwenye mamlaka yanayofuatia ya pili, ambayo ni
Kristo.
Hili lilifanyika sawasawa na maelekezo ya torati, kama
kuhani mkuu alivyokuwa kila mara akichaguliwa, akiitwa kwa kupigiwa kura.
Kuweka Kigezo
Kwanza kabisa, kigezo cha uchaguzi kinapaswa kiwekwe.
Matendo 1:21-22 Basi katika watu waliofuatana
nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu, 22 kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile
alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka
kwake pamoja nasi.
Kama mtu mmoja akipendekezwa anayetimiza vigezo, ndipo
alipoweza kuwa chaguo. Lakini wakati mwingine ilijitokeza kuwa na watu zaidi ya
mmoja wanaoonekana kukidhi vigezo hivyo, na kwa kuwa mamlaka ya pili nay a juu
zaidi yalikuwa ni Kristo, ndipo shauri liliweza kuhitimika kwa muujiza kutoka
mbinguni kwa jambo hili.
Matendo 1:23-26 Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye
Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya. 24 Kisha
wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani
uliyemchagua katika hawa wawili, 25 ashike mahali katika
huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe. 26 Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye
akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja.
Hii ni njia ambayo kwayo nafasi ya juu sana ya sasa ya
mwanadam inawekwa. Ni dhahiri kabisa kwamba mitume hawa kumi na mbili tayari
walikidhi vigezo vya nafasi zao, na hawapo kabisa tena. Nafasi hizo zilichukuliwa.
Hata hivyo, kwa zama zote za Kanisa kama vilivyo kwenye Ufunuo sura za 2 na 3, kuongozi
mpya wa kibinadamu alipaswa kuchaguliwa, kwa kuwa sisi sote tunakufa hatimaye.
Hawa sabini waliunda uongozi wa Kanisa kwa kipindi cha miaka elfu mbili na hawa
ia wanaunda jopo la watu 70 jumlisha 2 ili kufikisha idadi ya wateule 144,000 wa
maongozi ya Mungu (soma jarida la Mavuno
ya Mungu, Dhabihu ya Mwandamo wa Mwezi Mpya, na ya Wateule 144,000 (Na. 120)).
Vipi kuhusu huduma
nyinginezo?
Mara tu baada ya kiongozi wa kibinadamu anapowekwa,
anaiweka sehemu yote ya huduma iliyobakia kwa viongozi wa kuteuliwa. Tena
kigezo cha kuteuliwa kwao kinawekwa na kuwekewa kigezo chao kutokana na matunda
waliyonayo viongozi hao waliopendekezwa. Viongozi hao walioteuliwa ndipo
wanawekwa wakfu.
Matendo 6:1-6 Hata siku zile wanafunzi
walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung'uniko ya Wayahudi wa
Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya
kila siku. 2 Wale Thenashara wakawaita jamii ya
wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani.
3 Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu,
walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya
jambo hili; 4 na sisi tutadumu katika kuomba na
kulihudumia lile Neno. 5 Neno hili likapendeza machoni
pa mkutano wote; wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na
Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa
Antiokia; 6 ambao wakawaweka mbele ya mitume, na
walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao.
Tunaona pia kwamba mchakato huu wa kuweka kigezo na
kuwachagua viongozi ulifuatiwa na ukuaji wa Kanisa.
Tito 1:5 Kwa sababu hii nalikuacha Krete,
ili uyatengeneze yaliyopunguka, na kuweka wazee katika kila mji kama vile
nilivyokuamuru;
Kwa hiyo, mtumishi hawezi kuwa mtu aliyejichagua au
kujiteua mwenyewe. Inampasa athibitishwe na watakatifu wa kweli wanaounda bodi
ya uongozi wa Kanisa, na awekwe na uongozi wenye mamlaka ya Kanisa.
Jambo Muhimu na la Kipekee
Wakati mwingine kunaweza kusiwe na kusanyiko la kumpendekeza
kiongozi kutoka kwenye daraja lao. Wakati mwingine kunaweza kuwa na mtu mmoja
tu kwenye eneo la kijiografia. Ni wazi sana kwamba hapa panakuwa na mtu mmoja
tu pekee wa kumchagua.
Utaratibu Usiowezekana
Watu mara nyingi wanayashangaa maandiko matakatifu
yafuatayo:
Waebrania 5:4 Na hapana mtu ajitwaliaye
mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama vile Haruni.
Ndipo swali linaibuka sasa kwamba ni kwa jinsi gani mtu
anaweza kuwa na uhakka kama mtu ameitwa na Mungu kumtumikia. Hata hivyo, hii
sio sahihi kwa kile linachikusudia andiko hili. Hebu na tuliangalie jambo hili
kwa jinsi lilivyo:
Waebrania 5:1-10 Maana kila kuhani mkuu
aliyetwaliwa katika wanadamu amewekwa kwa ajili ya wanadamu katika mambo
yamhusuyo Mungu, ili atoe matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi; 2 awezaye kuwachukulia kwa upole wao wasiojua na wenye
kupotea, kwa kuwa yeye mwenyewe yu katika hali ya udhaifu; 3 na
kwa sababu hiyo imempasa, kama kwa ajili ya watu, vivyo hivyo kwa ajili ya
nafsi yake mwenyewe, kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi. 4 Na
hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe heshima hii, ila yeye aitwaye na Mungu, kama
vile Haruni. 5 Vivyo hivyo Kristo naye hakujitukuza
nafsi yake kufanywa kuhani mkuu, lakini yeye aliyemwambia, Ndiwe mwanangu, Mimi
leo nimekuzaa. 6 kama asemavyo mahali pengine, Ndiwe
kuhani wa milele Kwa mfano wa Melkizedeki. 7 Yeye,
siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika
mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi
alivyokuwa mcha Mungu; 8 na, ingawa ni Mwana,
alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata; 9 naye
alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote
wanaomtii; 10 kisha ametajwa na Mungu kuwa kuhani mkuu
kwa mfano wa Melkizedeki.
Kwenye kifungu hiki Paulo anaongele kuhusu kuhani mkuu,
mtu anayehusika kuendesha ibada ya kutoa sadaka za dhambi za watu. Ni Kristo
peke yake anayeweza na amekamilisha kazi hii. Kwa hiyo, aya ya 5 inamuelezea
Mtiwa mafuta ambaye ni Kristo, Masihi, na sio huduma iliyopo sasa ya kibinadamu
hapa duniani. Huduma zote za Kanisa zinasimama kwa Kristo, kama Makuhani walio
mfano wa Melkizedeki kwakuwa hakuna anayeweza kuwa Kuhani Mkuu wa mfano wa mtu
asiyeweza kuwa makuhani. Kwa hiyo wateule kama walivyo tu wao wenyewe wapo wa
mfano wa Melkizedeki kama warithi pamoja na Kristo (soma jarida la Melkizedeki (Na. 128)).
Hitimisho
Baada ya zama ya uongozi kupitia kwenye zama ya
ukengeufu, ilimpasa Kristo kulifufua Kanisa na kuweka uongozi mpya. Waumini
wanaoyajua mafundisho ya kweli waliyopewa watakatifu wa kwanza wa karne ya
kwanza walichagua viongozi wazuri kutoka watu waliokuwa kati yao walioendana na
vigezo vilivyoonyeshwa kwenye Biblia.
1Timotheo 3:1-7 Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka
kazi ya askofu, atamani kazi njema. 2 Basi imempasa
askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa
utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha; 3 si mtu
wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala
asiwe mwenye kupenda fedha; 4 mwenye kuisimamia nyumba
yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu; 5 (yaani,
mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?) 6 Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna
akaanguka katika hukumu ya Ibilisi. 7 Tena imempasa
kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa
Ibilisi.
Iwapo kama kuna watu zaidi ya mtu mmoja anayeonekana kuwa
kwenye kiwango na daraja moja la maendeleo ya kiroho, ndipo viongozi itawapasa
wapige kura baada ya kufunga saumu na kuomba, ili kwamba Mungu kupitia kwa
Kristo awachagulie kiongozi.
Kiongozi huyu ndipo ataomba ushauri au
mapendekezo ya kutoka kwenye kundi ili kuwapata viongozi, na shauri lake ndipo
litawagundua watu na kuwasimika wanaokidhi vigezo na kuzaa matunda, kutegemea
na matendo yanayohitajika kutendwa.
Kwa suala la Kanisa kutenda kazi kwenye shughuli zake,
kama Makanisa ya Kikristo ya Mungu na mengine ya mahalia yanayosaidia kwenye
mataifa yote, mchakato umeanza kwa katiba iliyoandikwa na mamlaka yamewekwa
kwenye uongozi wa Kanisa. Viongozi, kama Mwangalizi Mkuu (Coordinators-General)
anashikilia vyeo na mamlaka yote na kazi zote na mipango yote pamoja na
kuwateua viongozi wa Kanisa kama mitume, wainjilisti na wachungaji, ili kwamba
wao waweze kuwachagua na kuwasimika wengine kwa kazi zote zilizo sawasawa na
mapenzi yaliyoelezewa ya Kanisa. Wao wenyewe wanachaguliwa kwa kupigiwa kura
kwenye kila mwaka wa Sabato ambao pia ni wa usomaji wa Torati, kwa kufuata
mujibu wa sheria ya Mungu
.
Tumeitwa ili tuwe taifa la wafalme na makuhani, la watu
watakatifu (Ufunuo 1:6; 5:10) na imeandikwa kwamba kila mtu anayekwenda kuwa
mfalme inampasa ajiandalie wenyewe Torati ya Mungu (Kumbukumbu la Torati 17:18)
ili kwamba aweze kuzifuata na kuzishika amri za Mungu anapochaguliwa. Kwa hiyo
ni sawa na sisi na kama tulivyochaguliwa na kusimikwa kwenye Makanisa ya Mungu
na kuachana na sheria zetu.
Huduma zote zinashikilia ofisi zao kwa maslahi ya Kanisa
na kupewa majukumu kama linavyokusudia Kanisa.
Kuna vyeo viwili vya huduma, Wazee wa Kanisa na Maaskofu
na Mashemasi. Maafisa hawa wanaweza kubeba majukumu na kazi au utendaji ambazo
wamesimikwa kwazo.
Askofu au Mzee wa Kanisa wanaweza kuchukua wadhifa wowote
wa Kanisa na wanaweza kuwasimika au kuwaweka wakfu wengine kwenye ofisi kama
ilivyokusudiwa na Kanisa.
Shemasi anaweza kushikilia majukumu ya kiofisi au kazi ya
Muinjilisti, au Mchungaji, au Kiongozi na anaweza kufanya shughuli za wakfu za
Kanisa ambazo anastahili, kwenye eneo aliloruhusiwa na kikomo alichopewa nay
eye, Askofu au Mzee wa Kanisa (soma jarida la Wakfu au Sakramenti za Kanisa
(Na. 150)).
Mashemasi wanaruhusiwa kubatiza waongofu wapya kama
alivyofanya Filipo kwenye Matendo 8:26-40. Kwenye mifano mingine maaskofu
wanaweza kuwaelekeza mashemasi na kuwaruhusu kubatiza, na kuwaweka akiba kwa
ajili shughuli za kuwawekea watu mikono kama kutakuwa na tatizo kubwa, kama
ilivyokuwa kwenye tukio la Simoni Mchawi na Mwana mazingaombwe (soma Matendo
8:12-17). Hata hivyo, haikuwa inafanyika hivyo wakati ule. Mashemasi hubatiza
kwa sababu zao wenyewe. Haijalishi kinachofanyika inafanywa kwa utukufu wa
Mungu, sawasawa na mapenzi yake na kwa wateule wake.
Haijalishi kinachofanyika kiache na kifanyike hivyo
kwenye ubinadamu wote na acha wote wawaheshimu wale waliowekwa wakfu na
kusimikwa kuwatumikia wao.
Mpendane na tuwafanye wote watumikiane kwa unyenyekevu na
wampende Mungu.
Hesabu 8:24-26 Mambo yawapasayo hao Walawi ni haya;
tangu waliopata umri wa miaka ishirini na mitano na zaidi wataingia ndani ili
watumike utumishi katika kazi ya hema ya kukutania; 25 tena
tangu waliopata umri wa miaka hamsini wataacha kutumika huo utumishi,
wasitumike tena; 26 lakini watatumika pamoja na ndugu zao
katika hema ya kukutania, kushika ulinzi, lakini wasitumike katika huo utumishi
tena. Ndivyo utakavyowafanyia Walawi katika mambo ya ulinzi wao.
Inapasa mtu awe na umri wa miaka thelathini kabla hajaruhusiwa
kuanza kufundisha. Kristo mwenyewe hakuwa na udhuru kwa hili. Kwenye kanuni za
Kilawi waliingia kwenye huduma akiwa na umri wa miaka ishirini na tano na
aliacha huduma akiwa na umri wa miaka hamsini. Baada ya miaka hiyo hamsini
walidumu kwenye huduma ya ndugu zao.
Hata hivyo, uwekaji
wakfu unaweza kufanyika kabla ya kufikia umri wa miaka thelathini, kama ilivyokuwa
kwa shauri la Timotheo ambaye alikuwa amewekwa wakfu kabla hajaufikia umri,huu ulioelekezwa,
tunaouona kwenye 1Timotheo 4:12. Tunaweza kuona kuwa hii ilikuwa muhimu kwakuwa
alikuwa apelekwe kwenye huduma ya umisheni na kwa hiyo ilimlazimu kusimikwa na
kuwekwa wakfu.
1Timotheo 4:12 Mtu awaye yote asiudharau
ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na
katika upendo na imani na usafi.
Tuna dhana na
wazo la mamlaka na huduma na sisi pia tunadhana ya matumizi au kuwatumia
wanawake Kanisani. Kwenye 1Timotheo 2:11-13 tunasoma:
1Timotheo 2:11-14 Mwanamke na ajifunze
katika utulivu, akitii kwa kila namna. 12 Simpi
mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika
utulivu. 13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza,
na Hawa baadaye. 14 Wala Adamu hakudanganywa, ila
mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa.
Hoja iliyotolewa ni kwamba Mashemasi wa kike waliwekwa
wakfu kuhudumu Kanisani ili kuwaongoza na kuwafundisha wanawake. Hawakuruhusiwa
kufundisha wala kuwa na mamlaka juu ya wanaume, lakini walikuwa nanafanya kazi
Kanisani na walifanya huduma ya kuwafundisha wanawake kwa kipindi cha karne
kadhaa.
Suala la kufndisha Kanisani inaweza kuonekana kwenye 1Timotheo
sura ya 5 (hasa tafsiri ya KJV).
1Timotheo 5:1-2 Mzee usimkemee,
bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu; 2 wanawake
wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote.
Andiko hilo ndipo
linaenda mbali kupitia kwenye utaratibu wa kuwahudumia wajane kanisani na
utaratibu na mwenendo mzuri wa watu kanisani (soma aya za 3-16).
Inaendelea 1Timotheo
5:
17 Wazee watawalao vema na wahesabiwe
kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.
Wazee wa Kanisa kanisani walihudumu kwenye kazi
mbalimbali. Wale waliokuwa wakilihudumu neno na kufundisha (kufundisha na
kupangilia) walihesabiwa kustahili heshima maradufu.
18 Kwa maana andiko lasema,
Usimfunge kinywa ng'ombe apurapo nafaka. Na tena, Mtenda kazi astahili ujira
wake.
Suala hili lote
kuhusu wazee kupewa zawadi ni kwa ajili ya kazi mbalimbali na wanapangiwa
kufanya kazi kanisani. Si vyema kumtumia mzee wa kanisa kwa kutomjali, yaani
bila kumpa zawadi.
Pia kwenye 1Timotheo
5:19ff. Tunasoma kwe habari ya makato au malipo hivi.
1Timoteo 5:19 Usikubali
mashitaka juu ya mzee, ila kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu.
Mambo haya ni ya muhim sana
kwa utaratibu mzuri. Kama tujuavyo kuwa wazee wa kanisa wamekuwa ni walengwa
kwa miaka mingi kadhaa.
20 Wale wadumuo kutenda dhambi uwakemee mbele ya wote, ili na wengine waogope.
21 Nakuagiza mbele za Mungu, na mbele za Kristo Yesu,
na mbele za malaika wateule, uyatende hayo pasipo kuhukumu kwa haraka; usifanye
neno lo lote kwa upendeleo. 22 Usimwekee mtu mikono
kwa haraka, wala usizishiriki dhambi za watu wengine. Ujilinde nafsi yako uwe
safi. 23 Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia
mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara. 24 Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda
hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata. 25 Vivyo hivyo
matendo yaliyo mazuri ya dhahiri; wala yale yasiyo dhahiri hayawezi kusitirika.
Mpangilio ulio kwenye andiko hili ni kuifanya huduma iheshimike: kuwafanya wawe
kwenye uangalizi; kutoonyesha upendeleo kumpendelea mtu kwenye huduma yote na
kufanya mashitaka kuishitaki huduma kwa uangalizi unaostahili. Mambo haya yote
hufanyika kwa utaratibu kanisani.
Utaratibu wa
Kanisa umechukuliwa na huduma na ndugu wapendwa wanaowasaidia, ili lisiwe ni
kanisa lililofarakana, bali wote wanafanya kazi pamoja kwa utukufu wa Mungu. Mambo
haya ni ya muhimu katika kujua yanayotupasa kufanya kwene huduma kwenye
kuchaguliwa, wanayofundisha na uongozi wao wa muda mrefu na msaada wa wapendwa
wengi.
Yatupasa tuombe wote kuiombea huduma na kufanya kazi
pamoja kusaidiana katika kumtumikia Mugu. Kila mmoja wetu anabudi kuwasaidia
watumishi wa Mungu wetu, na sio kuwalaumu tu kila mara na kuwashitaki na kwa
kweli si kwa kutafuta kuwakuta na makosa na kuidharau huduma na watumishi wake.
q