Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[021C]

 

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu cha Amosi

(Toleo La 3.0 20141212-20141225-20150110)

 

Amosi ni kitabu cha Tatu kwa mujibu wa Kanuni ya Mpangilio wa Manabii Kumi na Mbili wa Agano la Kale, lakini kinachukuliwa kuwa ni kitabu cha Kwanza kati yao kwa wakati ule. Maana yake yameelezewa kwa kina.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2014, 2015 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Ufafanuzi wa Kitabu cha Amosi



Utangulizi

Jina la Amosi linadhaniwa kuwa linatokana na jina Amazia (7:10) au Amasia (2Nyakati 17:16). Marabi wa baraza la Talmudi waliamua kuwa anawezekana kuwa alikuwa mzito wa kuongea kama alivyokuwa Musa (sawa na Soncino Intro., uk. 81). Alikuwa mfugaji wa mifugo na mkulima na mmwagiliaji wa mikuyu (1:1, 7:14). Wakati alipokuwa ameajiriwa kuifanya kazi hii ndipo Mungu alipomuita na kumtuma awaendee Israeli na kuwaarifu kuwa kikombe chao cha uovu kilikuwa kimejaa na kama hawatatubu kwa haraka na kumrudia Mungu watakumbana na mapatilizo makali na kupelekwa utumwani. Wito huu wa kumtumikia Mungu ulimlazimu aiache nyumba yake na kuondoka na kwenda pande za kaskazini mwa Yuda na kuishi huko Samaria na Betheli ili avishughulikie vituo hivi ambavyo vilikwa ni maeneo ya ibada za sanamu na vitala na upagani na ibada za sanamu.

 

Kitabu hiki cha Amosi kinakubalika kwa ujumla kuwa kiliandikwa katikati ya miaka ya 750 KK wakati wa utawala wa Yeroboamu II (782-743).  Kitabu hiki kileorodheshwa kuwa ni cha tatu kwenye Kanuni ya mpangilio lakini anakubalika kuwa alikuwa wa kwanza kati ya manabii na kazi yake ilimtenganisha yeye mwenyewe na manabii wa mwanzoni ambao upotofu au ukengeufu ulikuwa umeyakumba mafundisho yao kama tunavyoona kutoka kwenye mandiko yake. Kukataa kwake kuwa yeye hakuwa miongoni mwa manabii haumaanishi kuwa ni kweli hakuwa miongoni mwao bali ni dhahiri tu kuwa alikuwa analaumu na kukemea ukenyeufu wao na kuwa yeye hakuwa mmoja wao.

 

Tetemeko la ardhi analolitaja kwenye sua ya 1:1 lnaaminika kuwa lilitokea wakati wa Uzia (Zekaria 14:5). Tukio la kupatwa kwa jua linalotajwa kwenye sura ya 8:9 linahesabiwa kuwa lilitokea mwaka 763 KK (soma kitabu cha Soncino Intro., p. 81). 

 

Mara tu tunapoona kipindi cha miaka thelathini au arobaini kinafanyika kwenye toba ya taifa la Israeli (sawa pia na jarida la Cox la Ufafanuzi wa Kitabu cha Yona (Commentary on Jonah). Maonyo haya yanaonekana kuwa yalifanyika mwaka 763-2 KK na 733 wakati Waashuru walipoitwaa Damascus na kuifanya Israeli kuwa ni nchi ya kuitoza kodi. Katika mwaka 723-2 waliondoka na kwenda Samaria na mwaka 722 KK Waisraeli walichukuliwa utumwani na wakapelekwa pande za kaskazini, huko Araxes na hawajarudi hadi leo na hadi hapo kipindi cha Kurudi kwake Masihi Mara ya Pili.

 

Anajulikana kama ni nabii aliyekuwa anawashambulia makuhani na manabii wakengeufu kwenye maandiko yake na kwamba aliuawa kwa kipigo alichopigwa na chuma kizito usoni. Mtazamo wa kwanza ni kwamba inaaminika kuwa aliuawa kwa kupigwa chuma kizito usoni mwake na Uzia. Dhana ya pili inaamini kuwa aliuawa kwa kupigwa kitu kizito usoni na Amazia kuhani wa Betheli. Mitazamo haya yote miwili inakubaliana na jinsi alivyouawa na kwamba ni watawala tu ndio waliosababisha na kuhusika (soma kitabu cha Soncino, ibid). Yawezekana kuwa ama aliuawa na mfalme aliyepigwa ukoma wa Yuda au kuhani mkengeufu wa Israeli. Na jinsi hii ya mauaji ilikuwa ya kawaida kwa manabii wa Mungu waliuawa waliuawa kwa ajili ya kazi zao walizokuwa wakizifanya.

 

Ujumbe

Ni muhimu kunukuu mtazamowa marabi kwenye hilo ingawa wanaelewa na kuija kweli wa ujummbe wanaoukataa na kuupuzia Yuda nab ado wanalaumiwa kwa sababu ya hilo. Ukristo wa Mimamboleo pia umelaumiwa sana na Manabii Kumi na Mbili na Amosi kwa ujmla.

 

Akiwakama mwelekezaji wa mambo ya kimaadili na kijamii ya kidini umuhimu wa Amosi unatangulia. Mungu sio Mungu wa Waisraeli peke yao, bali ni wa ulimwengu wote. Wala agano lake kwa Israeli halitakoma. Wataadhibiwa kwa ajili ya dhambi zao tena kwa ukali sana kuliko mataifa mengine, na uovu yanayostahili kuadhibiwa vikali ni dhuluma kwenye jamii. Maadimiso au uadhimishaji wa uangalifu na makini kwa taratibu au mapokeo ya kiibada hayataweza kuwaokoa. Amosi anaweka msisitizo wakati alipokemea udanganyifu kwamba mapokeo au utaratibu kama ulivyo tu wenyewe yanaweza kumthibitisha au kumpendeza Mungu ambaye anahitaji haki, utakatifu na rehema. Ni kweli kwamba Israeli walikuwa ni wateule wake, bali ukamilifu wa umuhimu wa fursa.

 

Ujumbe huu wa uingizaji ndani ni ni jamii ile, kama itakuwa inadumu, inapasa iwe kwenye haki kati ya mtu na mtu, sawasawa na ilivyo kati ya mataifa. Kwa uaminifu wa Amosi na kuwatendea kwake watu bila upendeleo ilikuwa ni majira muhimu kwa ustawi wa kitaifa. Kipindi chake cha Kilele ni moja ya nyakati ambazo mawazo ya wenye hekima na ya urahisi wa maisha wamekuwa wakipatana kiushabihisho.”(Soncino, ibid).

 

Hata hivyo, ni Mung ndiye anayetoa unabii mwishoni mwa wakati ambao Amosi anawaambia Israeli moja kwa moja na mbali na unabii tulioutaja kutlioutaja kutoka kwenye vitabu vya Torati na kutajwa kwa manabii wa zamani waliohudumu hapo kale kabla ya nabii Samweli, na kwenye Wafalme na Mambo ya Nyakati, kama Amosi anavyovijua kuwa ni nabii za zamani sana zilizodumu hadi sasa.

 

Kitabu hiki kinajikuta kikiangukia moja kwa moja kwenye migawanyo mitatu. Sura mbili za kwanza zinachukuliwa kama dibaji ya uandishi wa nabii au kiusahihi zaidi twaweza kusema kuwa ni maandalizi ya Mungu kupitia kwa nabii ili kuwashughulikia Israeli.

 

Israeli wa mataifa yote waliendelea kufanya ukahaba wa kuabudu sanamu na kama yalivyo mataifa mengine yote hawakujiepusha, wala kwa Israeli na Mungu yu karibu kuwashughulikia kwanza Israeli kwa kulitumia taifa ambalo lilikuwa ndivyo lilikuwa limekwisha laumiwa tayari. Kisha sisi tutakwenda kuyahukumu mataifa yote kama tunavyoona kutoka kwa hawa Manabii Kumi na Mbili. Hakuna hata moja kati ya dini hizi zinazoendeleza ukahaba itakayobakia na zote zitaangamizwa na kutokomezwa kabisa.

 

Sura nne zinazofuatia zinashughulika na watu waliokuwa wanaoangalia utajiri wao wenyewe kuwa ni kama amala na ishara ya utakatifu wao. Hali hii inaedelea kuwa ni msingi muhimu wa kimtazamo wa mataifa ya Israeli ambao wanakuwa bado hara sasa hawajui kuwa walichopewa kuwa chao ni kwa mujibu wa haki yao ya urithi kutoka kwa Ibrahimu na Mababa zao wa imani wa zamani na haina uhusiano wowote na thamani yao kama watu na kuwa majirani zao kuwa ni kama uchafu machoni pa Mungu. Uozo ulioanzia kutoka Ulaya Magharibi kupitia kwenye Jumuia ya Madola na kwenye mataifa yote na hasa Marekani. Imani ya kiantinomia ambayp haijali kuzifuata sheria za Mungu ya kile kinachoitwa Ukristo wa Kisasa inakaribia kuhukumiwa na nabii Amosi anaona kutoka mbali tangu kwenye utumwa wa Ashuru hadi nyakati za vita ya mwisho na ujio wa Masihi hakuwezi kuwa na haki na kubakia mtakatifu bila kuwepo Sheria ya Mungu na Haki. omianism of the so-called Modern Christians is about to be punished and Amos looks forward from the Assyrian captivity to the final war of the end and the Messiah. There can be no righteousness without God’s Law and Justice. Tsedek (au Zedeki) ni neno moja tu kwenye Kiebrania lenye maana na dhana mbili.

 

Kumbuka kile andiko linalomtambulisha yeye kuwa ni mchungaji wa Tekoa. Hii ni sehemu ya mapokeo ya manabii na Kurani inasema kuwa hakuna nabii ambaye hajawahi kuwa mchungaji.

 

Amosi Sura ya 1

Maneno ya Amosi, aliyekuwa mmoja wa wachungaji wa Tekoa; maono aliyoyaona katika habari za Israeli, siku za Uzia, mfalme wa Yuda, na siku za Yeroboamu, mwana wa Yoashi, mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la nchi. 2 Naye alisema, Bwana atanguruma toka Sayuni, Atatoa sauti yake toka Yerusalemu; Na malisho ya wachungaji yataomboleza, Na kilele cha Karmeli kitanyauka. 3 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Dameski, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameipura Gileadi kwa vyombo vya kupuria vya chuma; 4 lakini nitapeleka moto uingie katika nyumba ya Hazaeli, nao utayateketeza majumba ya Ben-hadadi. 5 Nami nitalivunja komeo la Dameski, na kuwakatilia mbali wenyeji wa bondeni mwa Aveni, na yeye aishikaye fimbo ya enzi katika Beth-Adini; na watu wa Shamu watakwenda hali ya kufungwa hata Kiri, asema Bwana. 6 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Gaza, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu waliichukua katika hali ya kufungwa kabila nzima, wawatie katika mikono ya Edomu; 7 lakini nitapeleka moto juu ya ukuta wa Gaza, nao utayateketeza majumba yake. 8 Nami nitamkatilia mbali mwenyeji katika Ashdodi; na yeye aishikaye fimbo ya enzi katika Ashkeloni; nami nitaugeuza mkono wangu uwe juu ya Ekroni; na mabaki ya Wafilisti wataangamia, asema Bwana MUNGU. 9 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Tiro, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameitia kabila nzima katika mikono ya Edomu, wala hawakulikumbuka agano la udugu; 10 lakini nitapeleka moto juu ya ukuta wa Tiro, nao utayateketeza majumba yake. 11 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Edomu, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu alimfuatia ndugu yake kwa upanga, akatupilia mbali huruma zake zote; hasira yake ikararua-rarua daima, akaishika ghadhabu yake milele; 12 lakini nitapeleka moto juu ya Temani, nao utayateketeza majumba ya Bosra. 13 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya wana wa Amoni, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wamewapasua wanawake wa Gileadi wenye mimba, ili wapate kuongeza mipaka yao; 14 lakini nitawasha moto katika ukuta wa Raba, nao utayateketeza majumba yake; pamoja na kupiga kelele siku ya vita, pamoja na tufani katika siku ya chamchela; 15 na mfalme wao atakwenda utumwani, yeye na wakuu wake wote pamoja, asema Bwana.

 

Hitimisho

Kwa hiyo ndipo mataifa ya kaskazini walichukuliwa utumwani kama onyo kwa Israeli lakini hawakujali maonyo hayo.

 

Nchi ya Wamoabu wana wa Lutu iliangamizwa kwa ajili ya kuwatesa kwao Waedomu. Yuda nao walitabiriwa kufikwa na maafa lakini maangamizo yao yalikuja baadae, baada ya kuangamizwa kwao Israeli kwa kuondolewa kwao na kupelekwa utumwani mwaka 722 na Yuda hawakuangamia hadi mwaka 586 KK.

 

Waashuru na Wafilisti na Waedomu waliangamizwa, kama ilivyokuwa kwa watu wa Tiro. Adhabu hizi zilirudiwa tena na tena ma zitaendelea kwenye vipindi vyote hadi mwishoni katika Siku za Mwisho. Miaka 40 ya Toba ya Waashuru ilitolewa kutoka tangu mwishoni mwa vita iliyopiganwa wakati wa Sikukuu ya Kiyahudi iitwayo Yom Kippur ya mwaka 1974 mwezi Mei na vita vya kuiangamiza Syria iliendelea tangu Mei 2014. Gaza ilikutatizwa au kuzongwa kama ilivyofanywa Lebanon. Edom sasa ni sehemu ya itikadi ya Uzayoni au ya Kiyahudi.

 

Wamoabu waliokuwa kwenye ukingo wa mashariki mwa Yordani waliongea kwa lafundhi ya Kiyahudi na walikuwa chini ya mamlaka ya Israeli hadi kipindi cha utawala wa Ahabu. Masi yaliyofanywa na Mfalme Mesha dhidi ya mamlaka ya Ahabu kulitajwa kwenye 2Wafalme 3 na pia kwenye jiwe la Wamoabu.

 

Amosi Sura ya 2

Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Moabu, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu aliichoma moto mifupa ya mfalme wa Edomu hata ikawa chokaa; 2 lakini nitapeleka moto juu ya Moabu, nao utayateketeza majumba ya Keriothi; na Moabu atakufa pamoja na mshindo, na kelele, na sauti ya tarumbeta; 3 nami nitamkatilia mbali mwamuzi atoke kati yake, nami nitawaua wakuu wake pamoja naye, asema Bwana. 4 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Yuda, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wameikataa sheria ya Bwana; wala hawakuzishika amri zake; na maneno yao ya uongo yamewakosesha, ambayo baba zao waliyafuata; 5 lakini nitapeleka moto juu ya Yuda, nao utayateketeza majumba ya Yerusalemu.

 

Andiko la 2.1

Aya ya 4: Amosi anaendelea kuitabiri kuhusu hukumu itakayowakumba Yuda kwa dhambi zao walizozifanywa kwa kuikataa Torati. Tendo hili linaendelea hadi katika Siku za Mwisho pia. Hadi siku hii ya leo, wanaigeuza Torati kichwa chini kwa kutumia Talmud na kuibadili na kuitia unajisi kalenda kwa kutumia mapokeo yao na taratibu za miahirisho za Kibabeloni. Kwenye Isaya 5:24 na Hosea 4:6 tunaona mabadiliko hayahaya kama yalivyo kwenye kitabu cha Amosi kuhusu mambo ya kimaadili ya sheria.

 

Uwongo na upotofu wao vimetajwa kwa ibada zao za sanamu na miungu wao wa uwongo. Vimeshamiri hadi leo na watu hawawezi hata kujua chimbuko lao.

 

Aya ya 5:  Moto uliotajwa kuwateketeza Yuda unamaanisha maangamizo ya Wababeloni yaliyofanywa mwaka 586 KK.

 

6 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kwa makosa matatu ya Israeli, naam, kwa manne, sitaizuia adhabu yake isimpate; kwa sababu wamewauza wenye haki kwa fedha, na maskini kwa jozi ya viatu; 7 nao hutwetea mavumbi yaliyo juu ya vichwa vya maskini, na kuipotosha njia ya mwenye upole; na mtu na baba yake humwendea mwanamke mmoja, hata kulitia unajisi jina langu takatifu; 8 nao hujilaza karibu na kila madhabahu juu ya nguo zilizowekwa rehani, na katika nyumba ya Mungu wao hunywa divai ya watu waliotozwa fedha. 9 Lakini nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini naliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini. 10 Pia naliwapandisha ninyi kutoka nchi ya Misri, nikawaongoza muda wa miaka arobaini jangwani, ili mpate kuimiliki nchi ya Mwamori. 11 Nami nikawainua watu miongoni mwa wana wenu wawe manabii, na katika vijana wenu wawe Wanadhiri; je! Sivyo hivyo, enyi wana wa Israeli? Asema Bwana. 12 Lakini mliwapa Wanadhiri mvinyo wanywe; mkawaamuru manabii, mkisema, Msifanye unabii. 13 Tazameni, nitawalemea ninyi, Kama gari lilemeavyo lililojaa miganda. 14 Naye apigaye mbio atapotewa na kimbilio; Wala aliye hodari hataongeza nguvu zake; Wala shujaa hatajiokoa nafsi yake; 15 Wala apindaye upinde hatasimama; Wala aliye mwepesi wa miguu hataokoka; Wala apandaye farasi hatajiokoa nafsi yake; 16 Naye mwenye moyo mkuu miongoni mwa mashujaa Atakimbia uchi siku ile, asema Bwana.

 

Hitimisho

Moabu walihukumiwa hapa. Waamoni walikuwa wamehukumiwa kwenye Sura ya 1. Hukumu ilikuwa kali sana kwa kuwa Israeli waliagizwa kuwa wasiwashambulie lakini wao waliwashambulia Israeli  (Kumbukumbu la Torati 2:4 nk.). kwa hiyo nchi yote ya Yordani inahukumiwa na kushughulikiwa vilivyo katika kipindi hiki. Waliambiwa wasiwashambulie Israeli kwenye vita ya mwaka 1967 lakini waliwashambulia na wakajiepusha baada ya Vita iliyopiganwa wakati wa Sikuku ya Yom Kippur ya mwaka 1973/4. Kujitoa au kujiepusha katika Siku za Mwisho kutawatoa nje ya mikono ya nguvu za Mnyama wa kutoka Kaskazini lakni wataletwa chini ya Taifa la Israeli chini ya Masihi kutokana na jarida la Vita ya Hamon –Gogu (Na. 294).

 

Kumbuka kuwa Israeli wamehukumiwa kutokana na dhambi ya kimwili kama sisi tulivyoutia unajisi Unazarayo wetu wa kidini na kushindwa kwetu kuenenda sawasawa na unabii wa Mungu na kuwatweza manabii na kwa kweli kuwaua manabii hawa kama walivyomtendea Amosi mwenyewe. Baba na mwana wanashirikiana mwanamke mmoja na wanawatesa watakatifu wenye haki na kuwauza kwa fedha. Wanazichukua nguo au mavazi ya walioweka rehani na kwendanazo kwenye madhabahu ya Bwana kama watakatifu. Israeli wa leo ni waovu zaidi kuliko walivyokuwa kipindi kitabu hiki kikiandikwa. Mungu alizivunja nguvu na uweza wao wa kijeshi waliokuwa wakiutegemea na atafanya hivyo tena katika Siku za Mwisho.

 

Kile wanachokitumainia kitapokwa kutoka kwao na watalazimishwa kumtumaini Mungu peke yake.

 

Kisha kwenye Sura ya 3 Mungu anaiambia nyumba yote ya Israeli aliyoitoa kutoka utumwani Misri nah ii inaijumuisha Yuda. Kwenye Sura hii Mungu anasema kuwa hafanyi chochote ili kuokoa, bali kwanza kabisa anawaonya kwanza kwa kupitia manabii wake.

 

Ukweli ni kwamba hakuna laana inayokuja pasipo kuwa na sababu (Mithali 26:2).

 

Amosi Sura ya 3

Lisikieni neno hili alilolisema Bwana juu yenu, enyi wana wa Israeli, juu ya jamaa yote niliowapandisha kutoka nchi ya Misri, nikisema, 2 Ni ninyi tu niliowajua katika jamaa zote zilizo duniani; kwa sababu hiyo nitawapatiliza ninyi maovu yenu yote. 3 Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana? 4 Je! Simba atanguruma mwituni, asipokuwa na mawindo? Mwana-simba atalia pangoni mwake, ikiwa hakupata kitu? 5 Je! Ndege ataanguka mtegoni juu ya nchi, mahali asipotegewa tanzi? Mtego utafyatuka juu ya nchi, bila kunasa kitu cho chote? 6 Je! Tarumbeta itapigwa mjini, watu wasiogope? Mji utapatikana na hali mbaya, asiyoileta Bwana? 7 Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lo lote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake. 8 Simba amekwisha kunguruma, ni nani asiyeogopa? Bwana MUNGU amenena, ni nani awezaye neno ila kutabiri? 9 Tangazeni habari katika majumba ya Ashdodi, na katika majumba ya nchi ya Misri, mkaseme, Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria, katazameni, ni mishindo mikubwa kama nini iliyomo humo, na udhalimu mwingi kama nini uliomo ndani yake. 10 Kwa maana hawajui kutenda haki, asema Bwana, hao wawekao akiba ya jeuri na unyang'anyi katika majumba yao. 11 Basi, haya ndiyo asemayo Bwana MUNGU; Atakuwako adui, kuizunguka nchi pande zote; naye atazishusha chini nguvu zako zikutoke; na majumba yako yatatekwa nyara. 12 Haya ndiyo asemayo Bwana; Kama vile mchungaji apokonyavyo kinywani mwa simba miguu miwili, au kipande cha sikio; ndivyo watakavyopokonywa wana wa Israeli, wakaao Samaria katika pembe ya semadari, na juu ya mito ya hariri ya kitanda. 13 Sikieni, mkashuhudu juu ya nyumba ya Yakobo, asema Bwana, MUNGU wa majeshi. 14 Kwani katika siku ile nitakapompatiliza Israeli makosa yake, nitazipatiliza pia madhabahu za Betheli, na pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali, na kuanguka chini. 15 Nami nitaipiga nyumba ya wakati wa baridi pamoja na nyumba ya wakati wa hari; na hizo nyumba za pembe zitaangamia, nazo nyumba kubwa zitakuwa na mwisho, asema Bwana.

 

Hitimisho

Wenyeji wa nchi za Wafilisti na Misri walisihiwa waje na kushuhudia kuangamia kwa Israeli. Hii ilikuwa inasimama pia kama somo kwao kwenye Siku za Mwisho. Nchi hizi mbili ziliadhibiwa na kuangamizwa na Israeli walikumbuka kuangamia kwao na halafu katika Siku za Mwisho nchi yao yote itachukuliwa hatimaye.

 

Milima ya Samaria: Walikuwa wanamudu kuviona vilele vyake wakiwa Samaria kutoka kwenye milima iliyowazunguka. Nchi ilikuwa imezama kwenye makanganyiko wa machafuko kwa ajili ya ufisadi na shuruti. Hisia zao za kimaadili zilikuwa zimeharibika kabisa.

 

Pembe za madhabahu ndizo zilizoshikiliwa na wale waliokuwa wanatafuta utakatifu wa mahali patakatifu kutoka kwa Mungu. Uwezo wa kutafuta utakatifu kutoka kwa Mungu utaondolewa. Vyanzo hivyohivyo vya marabi hata vinadai kwamba misingi ya madhabahu imeondolewa.

 

Nyumba ya wakati wa baridi imetajwa tena kwenye Yeremia 36:22. Yaonyesha kuwa inautaja utajiri mkubwa wa watu walio kwenye madaraja ya utawala dhidi ya maskini wasio na kitu. Utajiri wao utaondolewa na hawa walio kwenye madaraja ya utawala wataachwa watupu.

 

Makabila yaliadhibiwa kwa ajili ya kuabudu kwao sanamu na imani yao ya mungue Jua kwa kuwa ndivyo walivyofanya huko Betheli. Katika utumwa huu, sehemu kubwa ya Walawi walikwenda utumwani pia divisheni au tarafa 24 zilianzishwa tena kutoka kwenye divisheni au tarafa tatu zilizoko bado katika Yuda ili kwamba huduma za Makuhani zifanyike Hekaluni. Ulikuwa ni mlipuko mkubwa kwa Walawi nchini kote Israeli. Weote walikwenda utumwani eneo la mbali zaidi huko Araxes na walichanganyika pamoja na Wahiti au Waseltiki.

 

Kwenye aya ya 11 na 12 tunaona kwamba unabii ulitimia na baada ya miaka thelathini Syria ilizingirwa na kutekwa na Waashuru baada ya kuzingirwa kwa miaka mitatu. Samani zenye thamani kubwa za Samaria ambao lizidharauliwa na kupuuzwa na Amosi zilivunjiliwa mbali na Waashuru.

 

Kwenye maandiko yaliyo kwenye Sura ya 4 yanaonyesha kuwa Mungu yupo kinyume sana na wanawake wa Israeli Ng’ombe wa Bashani ambao wanawadhulumu maskini. Wanapelekwa utumwani na kuadhibiwa kwa ajili ya kuabudu kwao sanamu na vinyago huko Betheli zilizoingizwa na Yezebeli kwenye Dini za waabudu Jua. Upotofu wa Samaria ulikuwa wazi na ulitajwa na Amosi kuwa ni kama uanzishaji au mwanzo wa choyo kwa wanawake wao na wanafananishwa na ng’ombe wa Bashani.

 

Ibada hizi za sanam zinaonekana katika Israeli hadi siku hizi za leo.

 

Amosi Sura ya 4

Lisikieni neno hili, enyi ng'ombe wa Bashani, mnaokaa juu ya mlima wa Samaria, mnaowaonea maskini, na kuwaponda wahitaji; mnaowaambia bwana zao, Haya! Leteni, tunywe. 2 Bwana MUNGU ameapa kwa utakatifu wake, ya kuwa, tazama, siku zitawajilia, watakapowaondoa ninyi kwa kulabu, na mabaki yenu kwa ndoana. 3 Nanyi mtatoka kwenye mahali palipobomolewa, kila mwanamke moja kwa moja mbele yake; nanyi mtajitupa katika Harmoni, asema Bwana. 4 Njoni Betheli, mkakose; njoni Gilgali, mkaongeze makosa; kaleteni dhabihu zenu kila asubuhi, na zaka zenu kila siku ya tatu; 5 mkachome sadaka ya shukrani, ya kitu kilichotiwa chachu; mkatangaze sadaka mtoazo kwa hiari na kuzihubiri habari zake; kwa maana ndivyo viwapendezavyo ninyi, enyi wana wa Israeli, asema Bwana MUNGU. 6 Mimi nami nimewapa usafi wa meno katika miji yenu yote, na kutindikiwa na mkate mahali penu pote; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 7 Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikatika. 8 Basi kutoka miji miwili mitatu walitanga-tanga kuendea mji mwingine wapate kunywa maji, wasipate ya kuwatosha; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 9 Nami nimewapiga kwa ukavu na koga; wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 10 Nimewapelekea tauni, kama tauni ya Misri; vijana wenu nimewaua kwa upanga, na farasi wenu nimewachukulia mbali; nami nimeupandisha uvundo wa matuo yenu na kuuingiza katika mianzi ya pua zenu; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 11 Baadhi yenu nimewaangamiza, kama hapo Mungu alipoiangamiza Sodoma na Gomora, nanyi mkawa kama kinga kilichonyakuliwa motoni; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana. 12 Basi nitakutenda hivi, Ee Israeli, na kwa sababu nitakutenda hivi, ujiweke tayari kuonana na Mungu wako, Ee Israeli. 13 Kwa maana, angalia, yeye aifanyizaye milima, na kuuumba upepo, na kumwambia mwanadamu mawazo yake, afanyaye asubuhi kuwa giza, na kupakanyaga mahali pa dunia palipoinuka; Bwana, Mungu wa majeshi, ndilo jina lake. 

 

Hitimisho

Kumbuka kuwa Bwana wa Majeshi anawashughulikia Israeli kwa msingi au muono wa kiuchaguzi na aliwalazimisha kwa makundi na miji lakini bado hawakutubu na kumrudia.

 

Andiko lililo kwenye aya za 4-13 linaanza kwa kusema Njooni Betheli. Mwelekeo huu uko sawa na ule wa Eliya kwenye Mlima wa Karmeli (1Wafalme sura ya 18). Inakemea ibada zao za kutukuza sanamu pamoja na sheria zake au mapokeo ya kiibada ambazo kwazo waliziiga na hazikuwarithisha na zilikataliwa na Mungu ambaye aliwakemea na kuwaadhibu kwa ukame na moto, tetemeko la ardhi, baa la nyaa, tauni, na kwa vita. Na bado hawakumzikiliza.

 

 Kwa ujumbe wa kuhusu Gilgali tunaona andiko kwenye Hosea 4:15.

 

Dhabihu zilitolewa kwa miungu wa uwongo na zaka ilitolewa ili kuiwezesha dini ya uwongo ya Baali katika Israeli nab ado inafanyika hivyo hadi siku hizi. Mzingiro wa matendo ya dhambi zao ambayo ndiyo yalikuwa makusudio ya watu wa Gilgali yakuwa wamezingiriwa mbali.

 

Sura ya Tano inaendelea kuuelezea utaratibu au mfumo jinsi yatakavyotokea maafa. Hakutakuwa na mtu atakayeliinua na kuifufua Israeli. Taifa zime lote linapasa kuangamizwa. Aya za kwanza ni wimbo wa maombolezo ya kuwaombolezea Israeli kwa kuwa kwa maombolezo. Isreali imeanguka. Vebu iliyo iliyo kwenye utimilifu wa kinabii na ndipo inlionyesha kama nna kamilika au kutimilika. Uwongo wake umekataliwa. Andiko hili ndipo linaelekea hadi kwene unabii.

 

Taifa ya kuwaua wajumbe wa kila watu kumi na kwa hiyo lilikusudiwa lisiwe lenye nguvu tena.

 

Mungu anatoa maelekezo ya haraka kwa Israeli akisema kwamba wasiende Gileadi karibu na Yordani kama walivyokuwa wanakaribia kwenda utumwani kabla ya Samaria.  Wala hawakuomba msaada kutoka kwa waabudu sanamu wenzao wa Betheli wala hawakuruhusiwa kwenda Yuda na kuishi kwenye nchi za kusini huko Gilagali na Beersheba. Hakuna hata mmoja aliyewasaidia. Washirika wao hawatawasaidia na Bwana wa Majeshi atawafuata popote waendapo na kuwatesa.

 

Kama watamrudia Mungu wataishi lakini hawatadumu kama hawatafana hivyo. Mungu atawapiga kwa mabaa ya njaa na ukame katika Israeli yote hadi watakapotubu nah ii itaendelea hadi katika Siku za Mwisho.

 

Amosi Sura ya 5

Lisikieni neno hili nilitamkalo liwe maombolezo juu yenu, enyi nyumba ya Israeli. 2 Bikira wa Israeli ameanguka; hatainuka tena; Ameangushwa katika nchi yake; hakuna mtu wa kumwinua. 3 Kwa kuwa Bwana MUNGU asema hivi; Mji uliotoka nje wenye watu elfu, utasaziwa watu mia, na mji uliotoka wenye watu mia, utasaziwa watu kumi, kwa nyumba ya Israeli. 4 Maana Bwana awaambia hivi nyumba ya Israeli, Nitafuteni mimi, nanyi mtaishi; 5 bali msitafute Betheli, wala msiingie Gilgali, wala msipite kwenda Beer-sheba; kwani Gilgali hakika yake itakwenda utumwani, na Betheli itakuwa ubatili. 6 Mtafuteni Bwana, nanyi mtaishi; asije akawaka kama moto katika nyumba ya Yusufu, nao ukateketeza, asiwepo mtu awezaye kuuzima katika Betheli.,

 

Endelea na andiko la 5.1

Imani hii ya kidini ambayo imeiharibu na kuipotoa Israeli kutoka Betheli imeenepokelewa na kukubalika katika Israeli na hawakuitubia na waliishamirisha imani na itikadi ya uovu na dhuluma nyuani mwao (malangoni mwao).

 

Dini za kuliabudu Jua za mungu Baali ambazo hadi leo zinaizunguka Israeli na wanaabudu siku ya Juan a wanaadhimisha Sikukuu za Krismas na Easter na kwa ajili hiyo wataadhibiwa (soma jarida la Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235)).

 

7 Ninyi mnaogeuza hukumu kuwa uchungu, na kuiangusha haki chini, 8 mtafuteni yeye afanyaye Kilimia na Orioni, na kukigeuza kivuli cha mauti kuwa asubuhi, na kuufanya mchana kuwa giza kwa usiku; yeye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; Bwana, ndilo jina lake; 9 yeye aletaye uharibifu wa ghafula juu yao walio hodari, hata uharibifu uipate ngome.

 

Endelea na andiko la 5.2

Itikadi zao za udhalim na dhuluma ziliwagunguka. Ufisadi ukashamiri kila mahali na wale walio madarakani wakachukia kukemewa. Kweli ikaondolewa na kufunikwa chini. Mwishoni, Mungu akalazimika kuingilia kati. Hali hii inaendelea hadi kwenye Siku za Mwisho kama tunavyouona unabii unaotupeleka kwenye kipindi cha Siku ya Bwana. Tunaambiwa tuwe na busara na kuchukia uovu na tupende mema na Bwana wa Majeshi atakuwa pamoja nasi. Wadhalimu walioishi kwenye karne za kabla ya kufanya Makazi yao huko Canada na Marekari na hukf Australia na New Zealand walikuwa wakimuogopa au kumcha na Mungu aliutumia udhalilishaji ule ili kuwamilikisha tena maskini nchi nyingine na kuyaokoa mataifa mengi hadi nyakati za mwisho.

 

Wamewatesa wenye imani na waliokuwa wanaihubiri na kuifundisha kweli na waliokuwa wanaishika sheria ya Mungu kwa karne nyingi.

 

10 Wao humchukia yeye akemeaye langoni, nao humzira anenaye maneno ya adili. 11 Basi, kwa kuwa mnamkanyaga maskini, na kumtoza ngano; ninyi mmejenga nyumba za mawe yaliyochongwa, lakini hamtakaa ndani yake; ninyi mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu, lakini hamtakunywa divai yake. 12 Maana mimi najua jinsi maasi yenu yalivyo mengi, na jinsi dhambi zenu zilivyo kubwa; ninyi mnaowaonea wenye haki, mnaopokea rushwa, na kuwageuza wahitaji langoni wasipate haki yao. 13 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya. 14 Tafuteni mema, wala si mabaya, mpate kuishi; hivyo Bwana, Mungu wa majeshi, atakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo. 15 Yachukieni mabaya; yapendeni mema; mkaithibitishe haki langoni; yamkini kwamba Bwana, Mungu wa majeshi, atawafanyia fadhili mabaki ya Yusufu. 16 Kwa ajili ya hayo, asema Bwana, Mungu wa majeshi, aliye Bwana; Kutakuwako maombolezo katika njia kuu zote; nao watasema katika njia zote, Ole! Ole! Nao watamwita mkulima aje kuombolea, na hao walio hodari wa kulia waje kuomboleza. 17 Tena katika mashamba yote ya mizabibu kutakuwako kulia; kwa maana mimi nitapita katikati yako, asema Bwana.

 

Endelea na andiko la 5.3

Ufisadi upo kila mahali katika Siku hizi za Mwisho na wenye hekima hawathubutu kusema lolote. Ni watenda haki tu walio nyuani mwa Israeli ndio watakaookolewa. Na kama inavyozidi kushamiri udhalimu ndivyo watakavyoadhibiwa.

 

Ukame uliwafanya wakulima waomboleze na wakulima wa mizabibu wataomboleza.

 

Siku ya Bwana sio kitu ambacho watu wanapaswa kukitamani kwa kuwa itwakuta wakiwa hawajatubu.

 

18 Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru. 19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma. 20 Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga.

 

Endelea na andiko la 5.4

Mungu anatangaza kwamba anazichukia na kuzidharau sikukuu zao. Makanisa mengi ya Mungu wameanzisha kalenda ya uwongo na sikuku zao haziangukii kwenye siku muafaka zilizoamriwa kama walivyofanya kwenye Kalenda ya Hilleli katika Yuda. Katika Israeli wengi wao wanatangaza makusanyiko yao kama zilivyo sheria au mapokeo ya ibada za dini za Kipagani za Baali kama walivyokuwa wakiwaabudu huko Betheli kwenye Dini za Jua na Ibada za Sirisiri na Krismas na Easter ya mungumke. (Soma majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. 156)Kalenda na Mwezi Mwandamo: Ni Uahirisho au Sikukuu (Na. 195)Ubadilishaji wa Kalenda ya Mungu Katika Yuda (Na. 195B) na Chanzo cha Maadhimisho ya Krismas na Easter (Na. 235).)  Mungu hatawakubalia kitu chochote mahali popote.

 

21 Mimi nazichukia sikukuu zenu, nazidharau, nami sitapendezwa na makutano yenu ya dini. 22 Naam, ijapokuwa mnanitolea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za unga, sitazikubali; wala sitaziangalia sadaka zenu za amani, na za wanyama walionona. 23 Niondoleeni kelele za nyimbo zenu; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu.

 

Endelea na andiko la 5.5

Ni lazima kuwa haki na maadili mema na mwenendo mwema vinatokea kwenye kiini au katikati ya Israeli na kwenye imani yake ya kidini na sio kuwa gamba tupu kama ilivyo sasa.

 

24 Lakini hukumu na itelemke kama maji, na haki kama maji makuu. 25 Je! Mliniletea dhabihu na sadaka jangwani muda wa miaka arobaini, enyi nyumba ya Israeli? 26 Naam, mtamchukua Sikuthi, mfalme wenu, na Kiuni, sanamu zenu, nyota ya mungu wenu, mliojifanyizia wenyewe. 27 Kwa sababu hiyo nitawahamisha, hali ya kufungwa, mwende mbali kupita Dameski, asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi

 

Hitimisho

Utaratibu wa kuabudu katika Israeli ulikengeushwa na Mungu hatawakubalia.

 

Sakkuthi na Kaiwani ni miungu ya kipagani na nyota ya Kiiuni au Kaiwani au Remfani wangali wakitumika na kuabudiwa bado katia Yuda hadi sasa. Hii ni miungu ya Wababeloni na Waashuru inayokutikana hadi leo na ingali bado ikiabudiwa kwa pamoja. Walishurutishwa waibebe miungu yao ya uwongo hadi Ashuru na zaidi ya huko, kaskazini mwa Araxes.  Wataadhibiwa tena katika Siku za Mwisho kwa ajili ya dhambi hizihizi.

 

Kumbuka kuwa Sura ya Sita inaendelea hadi kwenye makemeo waliyokemewa Yuda katika Sayuni pamoja na wenyeji wa Samaria kwa pamoja kwa kuwa ibada hizi zilikuwa zimejiingiza na kukubalika kote kuwili.

 

Amosi Sura ya 6

Ole wao wanaostarehe katika Sayuni, na hao wanaokaa salama katika mlima wa Samaria, watu mashuhuri wa taifa lililo la kwanza, ambao nyumba ya Israeli huwaendea. 2 Piteni hata Kalne, mkaone; tena tokea huko enendeni hata Hamathi iliyo kuu; kisha shukeni hata Gathi ya Wafilisti; je! Ninyi ni bora kuliko falme hizi? Au mpaka wao ni mkubwa kuliko mpaka wenu?

 

Ufafanuzi juu ya Andiko la 6.1

Miji ya Kalne na Hamathi zilianguka mwaka 738 na  720 KK. Kwa hiyo, ni kutokana na hiyo yalipaswa kukumbwa mapema na maafa anayoyataja nabii Amosi

(soma kitabu cha Soncino fn.). Gathi ni mku mkuu wa Wafilisti (soma 1:6) na andiko lilipasa lisomwe ili kuashiria swali lenye mashiko kwa Israeli, yaani; je, mnadhani kuwa ninyi ni bora kuliko ninyi mtakaoatoroka maafa watakayoyaleta?

 

3 Ninyi mnaoiweka mbali siku hiyo mbaya, na kulileta karibu kao la udhalimu; 4 ninyi mnaolala juu ya vitanda vya pembe, na kujinyosha juu ya masemadari yenu; ninyi mnaokula wana-kondoo wa kundi, na ndama waliomo zizini; 5 ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi; 6 ninyi mnaokunywa divai katika mabakuli, na kujipaka marhamu iliyo nzuri; lakini hawahuzuniki kwa sababu ya mateso ya Yusufu. 7 Basi kwa ajili ya hayo sasa watakwenda utumwani pamoja na wa kwanza watakaokwenda utumwani, na kelele za machezo za hao waliojinyosha zitakoma. 8 Bwana MUNGU ameapa kwa nafsi yake, asema Bwana, Mungu wa majeshi; Naizira fahari ya Yakobo, nachukizwa na majumba yake; kwa sababu hiyo nitautoa huo mji, pamoja na wote waliomo ndani yake. 9 Hata itakuwa, wakisalia wanaume kumi katika nyumba moja, watakufa.

 

Endelea na andiko la 6.2

Kwa hiyo. Mali na nguvu walizokuwanazo matajiri pia matajiri wa Israeli katika Siku za Mwisho vitakuwa vya kwanza kuangamizwa. Wale wanaolala kwenye vitanda vya pembe na kujificha kwenye maangamizo watachukuliwa na kuchomwa moto kama watakavyofanywa kwenye Siku za Mwisho pia.

 

Watakufa na hakuna hata nyumba moja itakayosalia, na watategemea ndugu zao kuwachomwa moto kwa sababu ya tauni watakayoteswa kwayo; na hususan katika Siku za Mwisho mapigo hayo ya magonjwa yatakuwa makubwa sana.

 

 10 Na mjomba wa mtu atakapomwinua, yaani, yeye amchomaye moto, ili atoe mifupa yake nyumbani, naye atakapomwambia yeye aliye katika pande za ndani za nyumba, Je! Yuko mtu ye yote pamoja nawe? Naye atakaposema, La, hapana; ndipo atasema, Nyamaza kimya; maana hatuna ruhusa kulitaja jina la Bwana. 11 Kwa maana, angalia, Bwana atoa amri, na nyumba kubwa itapigwa na kuwa na mahali palipobomolewa, na nyumba ndogo nayo itapigwa iwe na nyufa.

 

Endelea na andiko la 6.3

Mungu amegeuka na kuwatega mgongo na maombi yao yatageuka kuwa hukumu.

 

Kwa mjibu wa Targum Nyumba Kuu inayotajwa inamaanisha Israeli na hii Nyumba Ndogo ni Yuda. Wote watakatwakatwa vipande. Andiko linataja upotoshaji wa utoaji wa haki. Ni jambo la hatari sana kupoka au kugeuza haki kama ilivyo kuwaendesha farasi kwenye miamba na nikazibure kama ilivyo kulima baharini kwa maksai. Israeli na Yuda wameipotosha Haki na Utakatifu kwa kuiifisha kwa sumu na kwa kimnyoo. Wao ni sawa tu na Tsedek.

 

12 Je! Farasi watapiga mbio juu ya mwamba? Je! Mtu atalima na ng'ombe huko? Hata mmegeuza hukumu kuwa uchungu, na matunda ya haki kuwa pakanga; 13 ninyi mnaolifurahia jambo lisilo na maana, msemao, Je! Hatukujipatia pembe kwa nguvu zetu wenyewe? 14 Maana, angalia, nitaondokesha taifa juu yenu, enyi nyumba ya Israeli, asema Bwana, Mungu wa majeshi, nao watawatesa ninyi toka mahali pa kuingilia katika Hamathi hata kijito cha Araba.

 

Hitimisho

Lo debar ni kitu kisichofaa au kisichokuwepo. (Si watu wangu, Kumbukumbu la Torati 32:21). Wanahusika na hali ya kutopatilizwa na ya kipuuzi kwa kile kinachokosesha akiba. 

 

Jina Karnaim maana yake ni pembe na ni neno la fumbo alilolitumia Amosi ili kuyataja majina ya Israeli. Graetz inadhaniwa kuwa ni Lo Debar na Karnaim ni mahali palipoitwa Gileadi. Lidbiri na Lo Dabari imeorodheshwa kwenye Yoshua 13:26; 2Sawueli 9:4f; 17:27.  AshtarothKarnaimu umetajwa kwenye Mwanzo 14:5 na unahusiana na mungumke Ashtarothi au Easter mshirika wa Baali anayeabudiwa katika Israel hadi leo. Gileadi ulikuwa kwenye mazingira ya vita tangu kipindi cha Yeroboamu II na Waashuru na Amosi alitabiri kinyume chao kwa kutumia maneno ya fumbo. Neno “taifa” linamaanisha Syria na kuendelea hadi katika Siku za Mwisho (soma kitabu cha Soncino fns).

 

Neno la Hamathi kwenye Kitabu cha Arabah linafananishwa na Dani hadi Beersheba.  Kwa hiyo nchi yote ambayo kwayo Israeli anatawala itatawaliwa zaidi (sawa na 2Wafalme 14:25). Unabii huu wa maangamizo inahitimisha sehemu hii ya unabii.

 

Utangulizi wa Sura ya 7

Kifungu cha andiko kinaanza na Maono ya Kwanza. Tauni na Nzige.

 

Kuingilia kati na muhimu kwa Amosi kunawezesha kusimamisha kwa pigo hili la tauni. Kwa hiyo Mungu anaonyesha kwamba ni kwa uingiliaji kati tu wa watumishi wake ndipo wataweza kuokoka.

 

Hii inaendelea tangu hapo hadi mwishoni na ni kwa maombi tu peke yake ya wateule ndipo wanaweza kuokolewa.

 

Kuna maono matano. 

 

Tukio la nzige lililotumika hapa linaonyesha kuwa Mungu alikuwa anawatengeneza ilikuwa ni  Gobai pia iliyotumika kwenye Nahumu 3:17. Kukua kwa baadae (kwa Kiebrania Lekesh, mizizi inayojitokeza kutoka kwenye malkosh kama “mvua baadae”) inataja na kuonyesha ukuaji wa mazao ya majira ya Baridi.

 

“Fagio au Fekeo za Mfalme” ilikuwa ni kodi au ushuru uliotolewa kwa hiyari na upendo kwa wafalme wa Israeli kwa malisho au majani ya wanyama kwa kikosi cha magari ya deraya (sawa na 1Wafalme 18:5). Baada ya kodi hii ikiwa imekwisha lipwa, watu walikata majani kwa ajili ya matumizi yao lakini nzige walikuja na kuyala (Dereva).

 

Amosi Sura ya 7

Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama, aliumba nzige mwanzo wa kuchipuka kwake mimea wakati wa vuli; na tazama, ilikuwa mimea ya wakati wa vuli baada ya mavuno ya mfalme. 2 Ikawa, nzige walipokwisha kula majani ya nchi, ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, samehe, nakusihi; Yakobo atasimamaje? Kwa maana ni mdogo. 3 Bwana akaghairi katika jambo hili. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana.

 

Endelea na andiko la 7.1

Neno la Kiebrania lililotafsiriwa jani hapa linaandikwa na kutamkwa herb (mboga) kwenye Mwanzo 1:12 na ni neno la jumla kwa mbogamboga.

 

Kimsingi Amosi alisema akitumia neno inuka kuwa “Ni kivipi Israeli watajinasua kutoka kwenye maafa kama haya.” Pia alijua kuwa hukumu ilikuwa inakuja na kufanywa na Mungu kwa watu wenye dhambi na ndipo aliwaombea msamaha watu wote. Alidai kwamba licha ya mtazamo wao wa kiutajiri na mali raslimali zao zilichukuliwa kuwa ni kidogo sana kuweza kufaa kwenye maafa.

 

Hawa nzige walikuwa ni taswira ya maadui kutoka Kaskazini kama ilivyotumika kwenye unabii uliofuatia baadae, kama alivyotabiri Nahumu kwa Waashuru wote na mashambulizi ya Wababeloni.

 

Kwa hiyo Amosi aliingilia kati kwa niaba ya Israeli.  Walisazwa kutoka kwa Nzige wa Kaskazini lakini Yuda waliruhusiwa kurejea kwenye nchi yao baada ya maangamizo ya Wababeloni ili wamone na kumshuhudia Masihi kwenye nchi yao wenyewe. 

 

Kisha Bwana Mungu alimuonyesha Amosi kuwa hawajatubu. Ndipo Bwana aliwatawanya Yuda ulimwenguni kote na kuuhusuru Yerusalemu kwa kuuangamiza kwa moto na akalitawanya hata kanisa pia. 

 

4 Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama, Bwana MUNGU aliita ili kushindana kwa moto; nao ukavila vilindi vikuu, ukataka kuiteketeza nchi kavu. 5 Ndipo nikasema, Ee Bwana MUNGU, acha, nakusihi; Yakobo atasimamaje? Kwa maana ni mdogo. 6 Bwana akaghairi katika jambo hili pia. Jambo hili halitakuwa, asema Bwana MUNGU.

 

Endelea na andiko la 7.2

Tafsiri ya Soncino inaweka neno hapa kuwa Mungu wakati wote anawaonya watu kabla ya kumwagwa kwa kamio la Hukumu (mfano ni Isaya 3:13; Yeremia 2:9; Hosea 4:1 Mika 6:1). Neno “Kina kirefu” linadhaniwa kuzitaja bahari ambayo kwayo dunia imetolewa na wakosoaji wanadhani kuwa ilikuwa imetuama kwenye kakosa ya kisayansi. Hata hivyo, kina kirefu hatimaye kimekuja kugundulika na wanasayansi kuwa ni ghala kubwa ya maji iliyoko chini ya maji huko kwenye bara la Amerika ya Kaskazini. Hii inaweza kuwa ni hukumu kali na ya kutisha itakayotolewa katika Siku za Mwisho ambayo itaikumba dunia.

 

Inaweza pia kumaanisha watu wa ulimwengu miongoni mwa sehemu ambazo Yuda na Israeli.

 

Maono ya pili yalihusu Timazi.  Hii ilikuwa hi taswira ya hukumu ya Mungu kwa Nyumba ya Isaka na ilikuwa kwamba Israeli walikuwa wamekwisha hukumiwa kwenda utumwani kwa ajili ya ibada zao za sanam zilizoongozwa na wafalme wao na makuhani waona watu wake.

 

Ndipo Amazia Kuhani wa Betheli alijaribu kufanya hila za kumua Amosi na kutafuta jinsi ya kuzuia wasiende utumwani. Kwa jinsi hii hii, ndipo makuhani wa uwongo na manabii walijaribu kulinyamazisha neno la Mungu katika Israeli.

 

7 Haya ndiyo aliyonionyesha; na tazama, Bwana alisimama karibu na ukuta uliojengwa kwa timazi, mwenye timazi mkononi mwake. 8 Bwana akaniambia, Amosii, unaona nini? Nikasema, Naona timazi. Ndipo Bwana akasema, Tazama, nitaweka timazi kati ya watu wangu Israeli; sitawapita tena kamwe; 9 na mahali palipoinuka pa Isaka patakuwa ukiwa, na mahali patakatifu pa Israeli pataharibika; nami nitaondoka nishindane na nyumba ya Yeroboamu kwa upanga. 10 Ndipo Amazia, kuhani wa Betheli, akapeleka habari kwa Yeroboamu, mfalme wa Israeli, akisema, Amosii amefanya fitina juu yako kati ya nyumba ya Israeli; nchi haiwezi kustahimili maneno yake yote. 11 Kwa maana Amosii asema hivi, Yeroboamu atakufa kwa upanga, na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali, hali ya kufungwa, atoke katika nchi yake. 12 Tena Amazia akamwambia Amosii, Ewe mwonaji, nenda zako, ikimbilie nchi ya Yuda, ukale mkate huko, ukatabiri huko; 13 lakini usitabiri tena huku Betheli; kwa maana ni mahali patakatifu pa mfalme, nayo ni nyumba ya kifalme. 14 Ndipo Amosii akajibu akamwambia Amazia, Mimi sikuwa nabii, wala sikuwa mwana wa nabii; bali nalikuwa mchungaji, na mtunza mikuyu; 15 naye Bwana akanitwaa, katika kufuatana na kundi; Bwana akaniambia, Enenda uwatabirie watu wangu Israeli. 16 Basi, sasa lisikie neno la Bwana; Wewe unasema, Usitabiri juu ya Israeli, wala usitoe neno lako juu ya nyumba ya Isaka; 17 kwa hiyo, Bwana asema hivi, Mke wako atakuwa kahaba mjini, na wana wako na binti zako wataanguka kwa upanga, na shamba lako litagawanywa kwa kamba; na wewe mwenyewe utakufa katika nchi iliyo najisi; na bila shaka Israeli atachukuliwa mbali hali ya kufungwa kutoka nchi yake. 

 

Hitimisho

Mngu aliitamka hukumu yake kwa Israeli na kwa manabii wa uwongo wanaomtumikia na kumabudu mungu Jua katika Israeli na hukumu itatolewa juu yao katika Siku za Mwisho pia.

 

Wakati kwenye sura inayofuatia Mungu anawambia Amosi mbali ya utawanyiko utakaofanywa na Waashuru ambako anawafananisha Israeli na kikapu cha matunda wakati wa hari. Huu ni wakati wa mwisho. Ni Maono ya Nne.

 

Amosi Sura ya 8

Haya ndiyo aliyonionyesha Bwana MUNGU; tazama, kikapu cha matunda ya wakati wa hari. 2 Akaniambia, Amosii, unaona nini? Nikasema, Naona kikapu cha matunda ya wakati wa hari. Ndipo Bwana akaniambia, Mwisho wao umewajilia watu wangu Israeli; sitawapita tena kamwe. 3 Tena nyimbo za hekaluni zitakuwa vilio siku ile, asema Bwana MUNGU; mizoga itakuwa mingi; kila mahali wataitupa, wakinyamaza kimya.

 

Endelea na andiko la 8.1

Sasa Mungu anakataa kuwarehem Israeli. Alikuwa amekwisha liharibu Hekalu la kimwili lakini Zaburi zilikuwa zinaimbwa bado. Miandamo ya Mwezi Mpya na Sabato zilikuwa zinaadhimishwa kikamilifu na kwa siku sahihi zilizoagizwa wakati wote wa maisha ya Kristo na hata baadae kidogo hadi wakati wa kuangamizwa kwa Hekalu. Hawakuwa wamezigeukia au kurudi kwenye maombolezo na masikitiko au kudhihirisha hadi kwenye Nyakati za Mwisho wakati Uprotestanti wa Marekani ulipolifanya ibada za kanisa la Waisraeli kuwa ni kituko kabisa na kufedhehesha na walilupotosha ulimwengu kwa kudhahirisha kwao. Kile kinachoitwa kuwa Ukristo hawazishiki Sabato wala Miandamo ya Mwezi Mpya na waka hawazishiki sikukuu isipokuwa sikukuu za mungu Jua, mungu Baali na Imani za Kisirisiri (soma jarida la Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235)). Zama za Wasardi za Makanisa ya Mungu iliondolea mbali maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi Mpya na Sikuku za Pasaka nay a Mkate Usiotiwa Chachu na waliziadhimisha Siku Takatifu kwenye siku zisizo sahihi wakiambatana na Hilleli nap engine hata kwenye miei mingine isivyo sahihi iliyofuata utaratibu uliojlikana kama uahirisho wa Kibabeloni. Kwa ajili hiyo watakwenda kwenye Ufufuo wa Pili wa Wafu kama itakavyokuwa kwa waliokuwa kwenye zama za Walaodikia.

 

Ndivyo ilivyokuwa kwa Yuda pia ambao waligeuza maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi Mpya kuwa mzaha na Siku Takatifu hazikuadhmishwa tena kabisa kwa siku zake sahihi isipokuwa pale tu ilipoonekana kutokuwa na chaguo linguine au kwa nasibu tu.

 

4 Lisikieni hili, ninyi mnaopenda kuwameza wahitaji, na kuwakomesha maskini wa nchi, 5 mkisema, Mwezi mpya utaondoka lini, tupate kuuza nafaka? Na sabato nayo, tupate kuandika ngano? Mkiipunguza efa na kuiongeza shekeli, mkidanganya watu kwa mizani ya udanganyifu; 6 tupate kuwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu; na kuziuza takataka za ngano.

 

Endelea na andiko la 8.2

Kumbuka pia kuwa udanganyifu juu ya maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi Mpya na Sabato kunaenda sambamba na matuizi ya mizani ya uwongo na vipimo vya uwongo na kudanganya kwenye utaratibu wao wa mwisho. Hivi karibuni kulikuwa na tukio la Marekani kuilipa Ujerumani dhahabu feki baada ya kusababisha Mgogoro wa Kiuchumi au wa Kifedha Ulimwenguni kwenye shirika linalojulikana kama Fraudulent Collateralised Debt Obligations (CDOs). 

 

Mngu hauvumilii mwenendo huu (sawa na Walawi 19:35nk; Kumbukumbu ka Torati 25:13nk; Mithali 20:10). Hii efa ni kama kipimo cha magaloni manane.

 

Ona sasa kwamba Mungu wa Israeli amesema kuhusu kile atakachowafanya wao. Hii ni katika Siku za Mwisho kwenye siku iliyo karibu sana kabisa. Kama Israeli hawatatubu watakuwa kwa wingi na Mungu hatawasaza. 

 

7 Bwana ameapa kwa fahari ya Yakobo, Hakika sitazisahau kamwe kazi zao hata mojawapo. 8 Kwa ajili ya hayo, je! Haitatetemeka nchi, na kuomboleza kila mtu akaaye ndani yake? Naam, itainuka yote pia kama huo Mto; nayo itataabika na kupwa tena kama Mto wa Misri. 9 Tena itakuwa siku hiyo, asema Bwana MUNGU, nitalifanya jua litue wakati wa adhuhuri, nami nitaitia nchi giza wakati wa nuru ya mchana. 10 Nami nitazigeuza sikukuu zenu kuwa maombolezo, na nyimbo zenu zote kuwa vilio; nami nitatia nguo za magunia katika viuno vyote, na upaa katika kila kichwa; nami nitayafanya haya kuwa kama maombolezo kwa ajili ya mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.

 

Endelea na andiko la 8.3

Jambo hili litafanyika katika nyakati za mwisho wakati watu hawataweza kuyasikia maneno ya Mungu Aliyehai kutoka kwenye midomo au vinywa vya watumishi wahudumuo kwenye Makanisa ya Mungu vya manabii watatu wa mwisho (Yeremia. 4:15-16; Ufunuo 11:3-14) atawashughulikia kama Mungu anavyoelekeza. Hii ni njaa ya kulikosa Neno la Mungu ambayo imekuweko kwenye karne iliyopita na makuhani wanapimwa na kuhukumiwa kwa hili. Makasisi wote wa ibada za Jumapili za Baali wanakaribiwa kupatilizwa na kuangamizwa. Na wale wanaowafuata nyuma yao watakumbwa na maafa hayohayo.

 

Kupatwa kwa jua kulikotokea tarehe 15 Juni 763 KK kunadhaniwa kuwa kulichukuliwa kama taarifa ya ukweli huu (sawa na kitabu cha Soncino n. to v. 9).

 

Upara unaotajwa kwenye aya ya 10 ni mfano wa matendo ya kipagani huko Uarabuni na Ugiriki ya kunyoa usoni mbele na kuziacha nywele kaburini kama kufanya agano kati ya walihai na waliokufa hapa imekemewa na Mungu kuwa ni jambo linalostahili hukumu. Kifo cha mtoto wa pekee ni jambo lenye kutia uchungu sana kwa wenzi waliofiwa walitaabishwa nalo mno katika siku za kale (sawa na Yeremia 6:26; Zekaria 12:10).

 

11 Angalia, siku zinakuja, asema Bwana MUNGU, ambazo nitaleta njaa katika nchi; si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya Bwana. 12 Nao watatanga-tanga toka bahari hata bahari; na toka upande wa kaskazi hata upande wa mashariki; watapiga mbio, wakienda huko na huko, kulitafuta neno la Bwana, wasilione. 13 Siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kwa kiu. 14 Na hao waapao kwa dhambi ya Samaria, na kusema, Kama aishivyo Mungu wako, Ee Dani, na, Kama iishivyo njia ya Beer-sheba, hao nao wataanguka, wasiinuke tena.  

 

Endelea na andiko la 8.4

Dhambi au chukizo (Ashemathi) wa Samaria: Ni neno lililotumiwa kuelezea dhambi na kuwa ilikuwa ni ugeuzaji au upotoshaji wa makusudi wa neno Ashima jina la Mungumke wa Waashuru waliomuiga na kumfanya Mungu Mke wa dini ya waabudu Baali (sawa na kwenye 2Wafalme 17:30). Ametajwa kwenye gombo la Papyri lililogunduliwa huko Elephantine na baadhi ya mamlaka ya marabi inaijumuisha hii na Ndaa wa Dhahabu aliyetengenezwa na kutolewa na Yeroboamu 1.  Mungu wako Ee Dani inammaanisha ndama wa Dhahabu aliyesimamishwa huko (1Wafalme 12:29). Huyu Mngu Mwezi aliyeitwa pia Sini na wa Dini potofu za Jua bado zinaushawishi kwa Israeli katika Siku za Mwisho

 

Andiko linalosema: Kama njia ya Beersheba iishivyo linammana ya wageni wasafiri au wahujaji wanaokenda kuhiji kwenye hekalu za sanamu hususan kwenye ibada za Juan a Dini za Sirisiri. Ibada hizi zinafanyika ulimwenguni kote kwenye zama zote za kudumu kwake dini ya Kiislamu hadi siku hii ya leo wakiapa na kuweka nadhiri wakiwa niani kuelekea Maka (G. A. Smith).

 

Hitimisho

Hakuna hata mmoja kati ya watu hawa atafutaye maarifa kutoka kwa makuhani na manabii wao wa uwongo watajifunza na kutubu na kuwa hai. Ni kwa kuwaondoa tu makuhani hawa wa dini za waabudu Jua ndipo tutaishi.

 

Mungu amesema kuwa hakuna hata mmoja wao atakayeiepuka hukumu. Mifumo yao itaangamizwa na watu wake watauawa kwa upanga. Hawataweza kujiepusha.

 

Tunaelekea mbele kwenye maangamizo ya wisho kwenye sura inayofuatia. Maono ya Tano ni Hukumu ya Mungu kwa Israeli.

 

Amosi Sura ya 9

Nalimwona Bwana akisimama karibu na madhabahu; akasema, vipigo vichwa vya nguzo, hata vizingiti vitikisike; vivunje vipande vipande juu ya kichwa cha kila mmoja wao; nami nitamwua mtu wa mwisho wao kwa upanga; hapana hata mmoja wao atakayekimbia, wala hataokoka hata mmoja wao.

 

Endelea na andiko la 9.1

Watachimba mashimo ya kutorokea ya kujificha ili kujilinda kwenye miamba ardhini lakini hawatajiokoa. Hili ni fungu la kwenye Ufunuo linaloonyesha kuwa wafalme wa dunia hujificha mapangoni na kutafuta kujiepusha hasira ya Mungu wakati atakapokuja Masihi, lakini hawataweza kujiepusha. Hawatakuwa na mahali pa kujificha.

 

2 Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko; nao wajapopanda hata mbinguni, nitawatelemsha toka huko. 3 Nao wajapojificha katika kilele cha Karmeli, nitawatafuta na kuwatoa toka huko; na wajapositirika katika vilindi vya bahari nisiwaone, nitamwagiza joka huko, naye atawauma.

 

Endelea na andiko la 9.2

Kumbuka kuwa hata kwenye utumwa utakaokuja kwenye Siku za Mwisho hawatawea kujiepusha. Kuna njia moja tu nayo ni kutubu na kuliitia jina la Mungu na kuzitii Amri na Sheria zake. Hawatakuwa na namna ya kujiepusha.

 

Kila mtu anayetamani kuingia kwenye utawala wa Milenia watakuwa wametubu na kubatizwa na kuzishika Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya na Sikukuu zilizoamriwa na Mungu.

 

Hakuna hata mmoja ajitoaye na kuwa mshirika wa dini za waabudu Jua atakayebakia hai kama hatatubu. 

 

Kuitaja kwake Karmeli kunaonyesha ukweli wa kwamba ulikuwa ni mlima mrefu (wa takriban futi 1800) iliyojizinga kwenye mawe ya chokaa yaliyopindapinda kama joka inayozidi tarakimu 2000 na katika siku za Strabo ambao waliishi na waporaji au wanyang’anyi au waporaji waliojificha mapangoni na miituni (soma kitabu cha Soncino).

 

Kutoroka kwao na kwenda baharini kutajinea tu mashambulizi zaidi na Mungu ataweka macho yake juu yao kwa hokum yao na sio kwa faida.

 

4 Nao wajapokwenda hali ya kufungwa mbele ya adui zao, nitauagiza upanga huko, nao utawaua; nami nitawaelekezea macho yangu niwatende mabaya, wala si mema. 5 Kwa maana Bwana, MUNGU wa majeshi, ndiye aigusaye nchi, nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani yake wataomboleza; nayo itainuka yote pia kama Mto, nayo itakupwa tena kama Mto wa Misri. 6 Yeye ndiye avijengaye vyumba vyake mbinguni, na kuweka misingi ya kuba yake juu ya nchi; yeye ndiye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; Bwana ndilo jina lake. 7 Je! Ninyi si kama wana wa Wakushi kwangu mimi, enyi wana wa Israeli, asema Bwana? Je! Mimi sikuwapandisha Israeli toka nchi ya Misri, na Wafilisti toka Kaftori, na Washami toka Kiri? 8 Angalieni, macho ya Bwana MUNGU yanauangalia ufalme wenye dhambi, nami nitauangamiza utoke juu ya uso wa dunia; lakini sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo, asema Bwana. 9 Kwa maana, angalieni, nitatoa amri, nami nitaipepeta nyumba ya Israeli katika mataifa yote, kama vile ngano ipepetwavyo katika ungo lakini hata chembe moja iliyo ndogo haitaanguka chini. 10 Wenye dhambi wote katika watu wangu watakufa kwa upanga, hao wasemao, Mabaya hayatatupata nyuma wala mbele.

 

Endelea na andiko la 9.3

Ufalme wenye dhambi unaonyssha taifa zima la Israeli na Yuda. Masalia waliobakia hawatakuwa pamoja na Yuda peke yao bali ni kwa maangamizi ya Yuda (soma pia aya ya 11).

 

Punje ya nafaka ya mwisho kwa lugh rahisi ni pebble na utawanyiko wa watu ni sawa punje ya nafaka kupitia kwenye chekecheke. Siku ya Bwana ni kipindi cha uadibisho na utakaso.

 

Kwa hiyo Israeli itachekechwa na wote walio ndani yake wanaotenda dhamb na wasitubu watakufa. Ni wale tu wote ambao watatubu watakuwa hai. Kisha ulimwengu utafika na kushuhudia Ufufuo wa Kwanza wa wafu kufanywa upya kwa Hema au Nyumba ya Daudi. Hii inawataja wana wa Mungu kwenye ufufuo wa Nyumba ya Daudi kulikoelzwa kwenye Zekaria 12:8 ambayo ni kanisa chini ya Yesu Kristo, Malaika wa Bwana vichwani mwao.

 

 11 Siku hiyo nitaiinua tena maskani ya Daudi iliyoanguka, na kuziba mahali palipobomoka; nami nitayainua magofu yake, na kuyajenga kama siku za kale; 12 wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yaitwayo kwa jina langu, asema Bwana, afanyaye hayo.

 

Endelea na andiko la 9.4

Masalia ya Edomu wanaotajwa ni Waedom ambao kwa sasa ni sehemu ya masalia ya Yuda walio katikati ya taifa la Kiyahudi na mataifa yote yanayotajwa kuwa ni wana wa Isaka ambayo kwayo Israeli inajulikana. Ndipo Mungu ataifanya upya Israeli. Marejesho haya ni yale yaliyotajwa kwenye Isaya 65 kwa ukamilifu wake kwenye Ufufuo wa Pili wa Wafu na pia kwenye Zekaria 14:16-19 kipindi cha Milenia.

 

13 Angalieni, siku zinakuja, asema Bwana, ambazo huyo alimaye atamfikilia avunaye, na yeye akanyagaye zabibu atamfikilia apandaye mbegu; nayo milima itadondoza divai tamu, na vilima vyote vitayeyuka. 14 Nami nitawarejeza tena watu wangu Israeli waliohamishwa, nao wataijenga miji iliyoachwa maganjo, na kukaa ndani yake; nao watapanda mizabibu katika mashamba, na kunywa divai yake; nao watafanyiza bustani, na kula matunda yake. 15 Nami nitawapanda katika nchi yao, wala hawatang'olewa tena watoke katika nchi yao niliyowapa, asema Bwana, Mungu wako. 

           

Hitimisho

Kwa hiyo kutoka kurudi kwa Masihi, Israeli na Yuda watachekechwa kama ngano. Watahukumiwa na kufanywa wapya na kurkebishwa.

 

Watakatifu wataunda jamii ya walio kwenye nyumba ya Daudi kama ilivyokuwa huko Sayuni kabla ya kujengwa kwa Hekalu la Sulemani wakiwakilisha aswira ya wateule watakaokuwa kwenye Ufufu wa Kwanza wa Wafu na Hekalu likiwa ni Mji wote wa Mungu.

 

Wanadamu pamoja na Malaika watakatifu ndio wataunda misingi ya Mji wa Mungu na ambao utafanyika kuwa Bustani ya Edeni iakayorurishwa tena kwenye kipindi hiki cha Milenia na Ufufuo wa Kwanza wa Wafu.

 

Maandiko kwenye lugha ya Kiebrania kwenye maandiko asilia

Manabii Yeremia na Ezekieli walilitumia jina la Mungu Yahovih (SHD 3069) ambalo linamaana ya Mungu Mmoja wa Pekee na wa Kweli, Eloah kama Ha Elohim. Linasomwa na Marabi kama Elohim na sio Adonai. Kamusi ya Strong inafanya maaana hii muhimu kwenye kamusi yake ya Exhaustive Concordance kwenye rejea ya 3068 Yahovah na 3069 Yahovih.  Kuna viumbe wawili au watatu.

 

Amosi anaendelea kuliitia jina hili muhimu wakati kwamba wenzake wengine miongoni mwa hawa manabii kumi na mbili wanatumia tu 3069 kwenye Mika 1:2; Sefania 1:7 na Zekaria 9:14. Kwenye uandishi wa nabii Zekaria neno Yahova Sabaiothi linatumka mara 44 kwenye sura za 1-8 na mara tisa kwenye sura za 9-14 ambako ni Yahova Sabaiothi anayenena na ameonekana kwenye unabii wa Zekaria.

 

Kwenye Amosi, neno Yahovih kwa kumtaja Mungu Mmoja wa Kweli limetumika mara 22: kwenye Amosi 1:8; 3:7,8,11,13; 4:2,5; 5:3; 6:8; 7:1,2,4,4,5,6; 8:1,3,9,11; 9:5,8,15. Mifano mingine iliyotumia neno hili elohim kumtaja Mungu wa Majeshi na kwa elohim kwa ujmla. 

 

Kutumiwa kwa Yahovih mara 22 ni tarakimu ya ukamilifu na inamtaja Mungu Mmoja wa Kweli peke yake na ni mhuri wa unabii unaoanza kushika kas kuelekea kwenye Siku za Mwisho. Jina Elohimu linatumika mara 11, likiashira mchakato wa kutokamilika kuhusu elohimu na uumbaji wa Mungu, ambapo unabii umekamilika na kuishia kwenye mchakato kuelekea Siku za Mwisho. Kwa kulinganisha: matumizi ya neno elohimu mara 11 na lilitafsiriwa Mungu kwenye kamusi ya SHD 410 linaonekana mara moja tu kwenye kitabu cha Micah na Yahovih linatumika mra moja tu. Yahova limetumika mara 37 kwenye uandishi huo na limetafsiriwa Bwana kwenye kamusi ya SHD 136 limetumika mara mbili na maneno mengine kuwa Bwana wa Hekalu na Bwana wa Mungu kwenye SHD 113 limetumika mara moja kumuita Bwana wa Dunia Yote.

 

Jina Yahova kwenye 3068 kwenye kitabu cha Amosi limetumika mara 60 na limetafsiwa kama Bwana. Hii ni tarakimu ya mpango wa uumbaji iliyozidishwa kama mlolongo wa matukio. 

 

Kwenye SHD 136 linajitokeza mara 25 na limeungamishwa pamoja na kusomeka Bwana Mungu au Bwana Mungu wa Majeshi.

 

Tarakimu hizi za mlolongo wa matukio ni mihuri ya mamlaka au utawala na zinawatofautisha viumbe na unabii na ni uthibitisho wa mamlaka ya maandiko.

 

Inaonyesha pia kwamba watafsiri walijua kuwa kwenye SHD 3069 Yahovih alikuwa ni Mungu Mmoja wa Kweli na walilitafsiri hili kwa namna hiyo na kuita Yahova kama ilivyo kwenye viabishi.

 

Hii inaonyesha kushindwa kuonyesha busara kwa kumuita hivyo Mungu kwa namna ya kama Yahwe kuwa ni kama jina lisilokuwepo kwenye lugha ya Kiebrania na halina maana mengine kutoka kwenye maneno halisia ya maandiko.

 

Tutafafanua kwa kina mambo mengine kwenye vitabu vya Hosea na Mika.

 

************

 

Maandiko ya Bullinger kutoka kwenye tafsiri ya the Companion Bible ni kama ifuatavyo:

 

Amosi 1:1

JINA LA CHEO. Maneno ya Amosi. Lakini maneno ya Yahova kwa Amosi. Soma 1:3.

Amosi = Mzigo.

herdmen = wachungaji. Kwa Kiebrania nokdim; linaitwa hivyo kutokana na ufugaji wa kipekee wa kondoo wa fusi (wenye sufi nzuri). Mesha uliitwa nakshi, ikijlikana kama "bwana wa kondoo" (2Wafalme 3:4). Soma Nyongeza 54. Linatokea sehemu hizi mbili pekee. Lakini Amosi alikuwa mfugaji, kama inavyoonekana wazi kwenye 7:14; ambapo neno boker linatokana na neno bakar, yaani maksai wa ng’ombe, na kwa hiyo linahusiana na kazi yake ya kulima au kukatua ardhi (1Wafalme 19:19, 21, nk.) Soma andiko kwenye 7:14.

Tekoa. Sasa unaitwa Khan Telkua, ni umbali wa maili tano kusini kwa Bethlehemu, na maili kumi kutoka Yerusalemu. Linganisha na 2Samweli14:2. 2Nyakati 20:20.

ambayo = ambayo [maneno].

aliona = aliona [kwenye maono]. Linganisha na Hesabu 24:4, 16. Isaya 30:10. Ezekieli 12:27.

Israeli. Hili linatupa sisi kichwa cha somo la kitabu. Katika siku za. Linganisha na Hosea 1:1.

Yeroboamu. Soma 7:10.

Miaka miwili kabla ya tetemeko la ardhi: yaani kabla ya lile moja linalojulikana sana na kukumbukwa. Linganisha na Zekaria 14:5.

Tetemeko la ardhi. Kwa lugha ya fumbo ya Hysteresis. Nyongeza 6.

 

Amosi 1:2

BWANA. Kwa Kiebrania Yahova Nyongeza 4. Jina hili si la mtu wa kawaida kwenye kitabu hiki.

unguruma = unguruma kama samba, au radi. Ni kilamara, wakati lilipomtabiri Bwana, liliunganisha na utimlifu wa utawala au zama za Wamataifa. Linganisha na Yeremia 25:30, Yoeli 3:16.

tamka = toa maneno.

makazi = malisho.

wachungani. Si neno moja na lililo kwenye 1:1, lakini ni neno la kawaida (raah = walishaji).

Kilele cha Mlima Karmeli. Mlima Karmeli ulio kaskazini, ambao unaitamalaki nchi yote; sasa ni Yebel Kurmuli; sio Karmeli iliyopo Yuda (kusini mwa Hebroni); sasa ni el Kurmul. Linganisha na 1Samweli 25:2. Isaya 33:9.

kame = nchi kame.

 

Amosi 1:3

Asema BWANA. Maneno ya Yahova: sio maneno ya Amosi. Utaratibu wa kinabii. Tazama sehem ya Nyongeza 82. Soma habari za hawa kumi na mbili na Yahova, kwenye aya za 3:6, 9, 11, 13; 2:1, 4, 6; 8:12; 5:4; 16; 7:17; na wawili na Adonai Yahova kwenye 3:11; 5:3.

watatu . . . wanne. Usemi wa Kiebrania kwa kuelezea idadi kadhaa, au wengi (Ayubu 33:29, soma bango kitita) Linganisha na Mithali 30:15, 18, 21, 29.

Kutenda maovu. Kwa Kiebrania pasha. Nyongeza 44.

geuza = kirudishe nyuma, au kipindishe, pitisha hukumu ju yao. Hakuna Ellipsis iliyotolewa, na haitenganishwi kwa ilivyo kwenye neno la Kiebrania la “uso”. Kwa Kiebrania ni lo' ashibennu, Sitasababisha ligeuke na kurudi: yaani Sitaligeuza.

Pronauni ya “hiki” ni ya kume, ikikubaliana na kutajwa kwa tukio la tetemeko la ardhi (aya ya 1), na linamaanisha Yahova ambaye lilibakia lilivyo bila kuligeuka. Kwa hiyo lilionekana kwenye maeneo yote manane (aya za 3:6, 9, 11, 13; 2:1, 4, 6).

Kupigwa vibaya kwa Gileadi. Linganisha na Yoeli 8:14. Ni neno hilohilo lililotumika kwenye 2Wafalme 13:7.

Pamoja na = [kama ilivyokuwa] kwenye Lugha Fumbo ya Hypocatastasis. Nyongeza 6.

 

Amosi 1:4

Nitauleta moto. Linganisha na 1:7, 10, 12; 2:2, 5. Rejea kwenye Yeremia 17:27; 49:27; 50:32. Hosea 8:14.

Hazaeli. Linganisha na 2Wafalme 8:12; 10:32, 33; 13:3.

Ikulu: au ngome. Kwa Kiebrania 'armon. Limetokea (kwa uwingi) mara kumi na mbili kwenye kitabu cha Amosi (soma Nyongeza 10): 1:4, 7, 10, 12, 14; 2:2, 5; 3:9, 10, 11; 6:8; mara saba na vebu ya "fakamia" (Kwa Kiebrania akal).

Ben-hadadi. Ni jina la cheo la kiofisi la Wafalme wa Ashuru = mwana wa Hadadi, yaani mngu jua. Ben-hadad wa kwenye 2Wafalme 13:3; sio wa kwenye 2Wafalme 8:7-15.

 

Amosi 1:5

Mche. Kumbuka lugha ya Mfano ya Metalepsis (Nyongeza 6), kwa jinsi neno hili "mche" lilivyowekwa kwenye Lugha Fumbo ya Metalepsis, Nyongeza 6, kwa malango, na kisha malango yaliwekwa kwa ulinzi wa mji. Linganisha na Kumbukumbu la Torati 3:5. 1Wafalme 4:13. Yeremia 51:30. Maombolezo 2:9.

Wakazi: au, mtu aliyeketi, yaani mtawala, mwenye kushabihiana na andiko la kwenye mstari.

Avon. Sawa na Beth-aveni, mashariki mwa Beth-eli, unaokaliwa na kabila la Benjamin. Linganisha na Hosea 4:15; 5:8; 10:5, 8.

Nyumba ya Edeni = Beth-edeni.

Kir. Kama ilivyo kwenye 9:7, 2Wafalme 16:9. Isaya 22:6.

 

Amosi 1:6

Gaza (Ghuzzeh), iko Ufilisti.

Utumwa wote = kuuzwa utumwani.

utumwani = watumwa au mateka. Imewekwa kwa Lugha ya Kimafumbo ya Metonymy (ya Muunganisho), Nyongeza 6, kwa kundi lote la watumwa. Soma Yeremia 13:19. Linganisha na Yeremia 47:1. 2Nyakati 21:16, 17; 28:17.

 

Amosi 1:7

Ukutal. Imewekwa kwa lugha ya Mfanp ya Synecdoche (ya Kundi au Sehem), nyongeza 6, kwa mji wote.

 

Amos 1:8

Ashdodi. Baadae uliitwa na Wayunani jina la, "Azoto". Sasa unaitwa Escludi, kwenye uwanda au nchi ya Wafilisti, uko maili thelathini na tano kaskazini mwa Gaza.

Ashkeloni. Sasa unaitwa 'Askalan, upande wa pwani mwa Ufilisti.

Ekroni. Baadae, Wayunani waliuita "Accaron" (1 Wamakabayo 10.89), kwa sasa unaitwa 'Akiri, uko maili sita magharibi ya Gezeri. Huko "Gezeri "soma maandiko ya Bullinger kwenye 1Wafalme 9:15-17.

Asema = amesema.

Bwana MUNGU. Kwa Kiebrania Adonai Yehova. Nyongeza 4. na II. Cheo na Jina hili la Kimungu linatokea mara ishirini na moja (7 x 3. Soma Nyongeza 10) kwenye kitabu hiki (1:8, 3, 7, 8, 11, 13; 4:2, 5; 5:3; 6:8; 7:1-6; 8:1, 3, 9, 11; 9:5, 8). Kwa hiyo "hivi ndivyo asemavyo Adonai Yehova" Soma 3:11.

 

Amosi 1:11

Edomu. Linganisha Isaya 21:11; 34:5. Yeremia 49:8, nk. Ezekieli 25:12-14; Ezekieli 35:2. Yoeli 3:19; Obadia 1:1. Malaki 1:4.

Kwa kuwa, nk. Rejea kwenye Torati (Mwanzo 27:41. Linganisha na Kumbukumbu la Torati 23:7). (sawa na Linganisha tafsiri ya Companion Bible, Nyingeza 92. Linganisha na Malaki 1:2.

Ndugu yake. Rejea kwenye Torati (Mwanzo 25:24-26).

Tawanya milele: au, tawanya [mawindo yake] milele. Ginsburg anadhani = aliishikilia kwa kinyongo chake. Linganisha na 2Nyakati 28:17.

Yeye. Kamusi ya 1611 toleo la A.V. linaruka neno hili la "yeye".

 

Amosi 1:12

Temani. Linganisha na Yeremia 49:7. Obadia 1:9. Habakuki 3:3. Elifazi alikuwa Mtemani (Ayubu 2:11, nk.)

Bozra; Sasa unaitwa el Buseirah, uko kusini mashariki mwa Bahari ya Chumvi.

 

Amosi 1:13

Watoto = wana.

Amoni. Linganisha na 1Saya 11:1.

Raruka au pasuka, nk. Ilitabiriwa kwenye Hosea 13:16. 2Wafalme 8:12; 15, 16.

Kwamba wasiweze kufanya, nk. Linganisha na Yeremia 49:1.

14 Rabba. Kwa sasa unaitwa 'Amman (upo kwenye nyanda za juu ya Gileadi), "mji wa maji mengi", upo maili ishirini na tano kaskazini mwa Bahari ya Chumvi linganisha na 2Samweli 11:1, na 2Samweli 12:26, 27. Yeremia 49:2. Rejea kwenye Torati (Kumbukumbu la Torati 3:10, 11). Nyongeza 92.

Piga kelele au mayowe = kilio cha vita ku.

Siku ya mapigano au ya vita: yaani siku ya mashambulizi ya makelele na mizomeo ya maadui zao.

 

Amosi 1:15

Yeye. Ginsburg anadhani hivyo = makuhani wake, pamoja na kwenye tafsiri ya Septuagint.

(sawa na tafsiri ya Companion Bible).

Mfalme wao (Malkamu). Ni konsonanti hizohizo yenye viwango mbalimbali vya vaweli vinavyompa Milcomu mungu wa Waamoni (1Wafalme 11:5). Hii inadaiwa mno kukusudia kuionyesha sera ya watawala wao kwenye uwakilishi wake lakini inauonyesha mfumo wake wote wa kidini wa watu hawa (sawa na Soncino).

 

Amosi 2:1

Burnedi ...ndimu. ndimu. Kwa hiyo inathibitisha mahali ambapo Wamoabi ambao hawakuruhusu au kuwaacha wafu kupumzika na walihukumiwa hapa kwa kuwa waliichomwa moto mifupa ya Mfalme wa Edom (adui wa Israeli) kunasa au mnaso. Kwa hiyo hukumu hii hapa kwenye kitabu cha Amosi inaonyesha tabia ya kutopendelea ya Mungu kwenye mambo yahusuyo hokumu kwa makabila haya.

 

Amosi 2:2

Kiriothi: maana yake nyingine ni., miji yake. Sasa unaitwa el Kureiyat, au Kiraiathaimu, ulio katikati ya Diboni na Medeba. (sawa na Yeremia 48:24) Umetajwa na Mesha kwenye Jiwe la Wamoabu. (Soma tafsiri ya Companion Bible, Nyongeza 54.) Makao Makuu ya ibada na dini ya Kemoshi.

Kupiga kelele = kilio au kelele za vita. Linganisha na 1:14

Tarumbeta au baragumu. Kwa Kiebrania, shofar.

 

Amosi 2:3

Mwamuzi = mtawala (fimbo ya mfalme-anayeshika fimbo hiyo; Hesabu 24:17)

 

Amosi 2:6

Waliuza. Rejea kwenye Torati. (Walawi 25:39. Kumbukumbu la Torati 15:12). Companion Bible, Ngoneza 92, Myahudi atajiuza mwenyewe, lakini sio ndugu yake au sio amdaiwa aliyefilisika au asiye na uwezo wa kulipa (2Wafalme 4:1; Nehemia 5:5),

Mtakatifu na mwenye haki = mtu wa haki na mtakatifu.

Maskini = mwenye uhitaji. Kwa Kiebrania ni ebyon (sawa pia na Mithali 6:11).

Pea moja ya vitu. Imewekwa kwa lugha ya Mfanp ya Metonymy (ya Kiunganishi), soma kwenye Companio Bible, Nyongeza 6, kwa hatimiliki ya zile zilizoelezewa (linganisha na Ruthu 4:7).

 

Amosi 2:7

Anguka = vunjiko. Kwa Kiebrania shaaph, Na hii Homonymyn, maana yake ni (1) ni mshituko au inayotamani (Ayubu 7:2; 36:20, Zaburi 119:131. Mhubiri 1:5. Yeremia 2:24); (2) kugonga (kama shuph kwenye Mwanzo 3:15 Ikimaanisha "kumeza yote" kwenye 8:4. Ayubu 5:5. Zaburi 56:1, 2; 57:3. Ezekieli 36:3. Kwa hiyo hapa ni = kugonga. Soma kamzi ya Oxford Gesenius, ukurasa 983, vol. 2. Inasema "gonga kichwa cha mtu maskini kwenye mavumbi ya nchi".

Maskini = zenye kusababisha umaskini. Kwa kiambishi cha Kiebrania (uwingi) Tazama neno “umaskini”, Mithali 6:11. Sio neno moja na lile la kwenye 2:6.

Geuka na kuacha = geuza njia yao yote.

Mpole = wapole, kwa Kiebrania ni uwingi wa `ani, Soma andiko kwenye "ufukara", Mithali 6:11

Mtu mwanaume. Kwa Kiebrania 'ish. Nyongeza 14.

Na baba yake. Hii ilifanyika kenye ibada za sanamu za Wakanaani, na wanawake waliohudumu mahekaluni, walioitwa Kadeshoth (uke) na Kadeshhim (uume)

kijana = mtu kijana (mwanaume au mwanamke). Aliitwa hivyo kutokana na nguvu zake au makeke ya kiujana.

Kutia unajisi au kukufuru, nk. Hii inafanya matokeo, na sio makusudio, na inaonesha machukizo/enormity ya dhambi machoni pa Yahova. Rejea kwenye Torati, (Walawi 18:21; 20:3). (sawa na Companion Bible, Nyongeza 92). Linganisha na Isaya 48:11. Ezekieli 20:9, 14; 36:20-23, Warumi 2:24. 1Wakorintho 5:1.

Takatifu. Soma andiko la Kutoka 3:5.

 

Amosi 2:8

Wanajishusha chini wenyewe, nk. Rejea kwenye Torati (Kutoka 22:26. Kumbukumbu la Torati 24:12), (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 92). Kila madhabahu. Dhambi iliyowekwa kwa kweli ilikuwa ni sheria ya madhabahu moja na ilijlikana kuwa ni kama amri ya zamani pamoja na sheria inayohusiana na marejesho mapya ya mavazi ya mnadhiri.

Mvinyo, kwa Kibrania Yayin. Linganisha na Comp. Bible, Nyongeza 27.Mimi na jarida la Mvinyo Kwenye Biblia (Na. 188).

Wa waliokatazwa: au mvinyo uliokubalika.

 

Amosi 2:9

Tena. Baraka za zamani zinatamkwa ili kuonyesha au kukuza uovu wa uasi wao mara tano. Waamoni Rejea kwenye Torati (Hesabu 21:24. Kumbukumbu la Torati 2:32-34). (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 92). Linganisha na Yoshua 24:8. Hawa ni wa uzao wa Wanefili walikusudiwa kuangamizwa wote, ambao na mataifa meingine ya Wakanaani, waliangamizwa kwa upanga wa Israeli. (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 23 na Nyongeza 25).

Wao. Maandiko fulani, zenye matoleo yaliyochapishwa zamani, inasomeka “wewe”.

Urefu. Rejea kwenye Torati (Hesabu 21:24. Kumbukumbu la Torati 2:32-34). (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 92).

 

Amosi 2:11

Niliikuza, nk. Sio mpaka makuhani waliposhindwa kwenye huduma yao ya kufundisha torati. Soma Walawi 10:8, 11. Kumbukumbu la Torati 33:8, 10. Manabii hawakupewa hadhi ya Unazarayo hapo mwanzoni; Rejea kwenye Torati (Hesabu 6:2). (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 92.

Sivyo . . . ?  Neno la Mfano la Erotesis. Nyongeza 6.

Watoto = wana.

Asema Bwana = [ni] mjumbe wa Yahova.

 

Amosi 2:16

Ujasiri au uhodari = kuwa na ujasiri moyoni (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 92).

Kuwa uchi: au, kutovaa silaha ya kujikinga.

(sawa na Bullinger, Companion Bible.)

 

Amosi 3:1

BWANA. Kwa Kiebrania Yahova

Watoto = wana. Gombo nyingine zenye nakala za maandiko yaliyochapishwa zamani sana, za lugha za Kiaram, Kiseptuagint zinasomeka “nyumba”. Aitha, usomekaji huu unaonyesha kuwa sura hizi zinahusiana na taifa la makabila kumi na mbili.

Niliwatoa na kuwaleta, nk. Rejea kwenye Torati (Kutoka 12:51, nk.)

Ni ninyi tu ninaowajua, nk. Soma Mpangilio wahe hapo juu. Rejea kwenye Torati (Kumbukumbu la Torati 7:6). (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 92; sawa na Zaburi 147:19, 20.)

Dunia = ardhi. Kwa Kiebrania addamah.

Kukusukuma = kukutembelea, kama ilivyo kwenye 3:14. Rejea kwenye Torati (Kutoka 32:34). (linganisha na Comp. Bible,  Nyongeza 92)

 Maovu au machukizo. Kwa Kiebrania `avah. (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 44).

 

Amosi 3:3

Yawezekana watu wawili . . . ? Lugha ya Kimfano ya Erotesis (kwa kinyume. Kuimarisha au uimarishaji). Nyongeza 6. Huu ni mfano wa kwanza kati ya mitano. Jibu la kila swali ni ushuhuda unaojishuhudia wenyewe. Kukubaliwa = wamekutanika pamoja kwa ahadi [ya muda na (mahali].

 

Amosi 3:6

Itakuwa . . . ? Kwa lugha ya Mfano ya Erotesis. (sawa na Comp Bible, Ap. 6).

Tarumbeta au baragum. Kwa Kiebrania shofa.

Msiogope = msikimbie pamoja.

Ovu = maafa, kama ilivyo kwenye 5:13. Zaburi 141:5.

Kwa Kiebrania ra'a'. = ovu: isiyoshika maadili, ovu, lakini uovu unabidi kuadhibiwa, (kama ilivyo kwenye 5:13. Isaya 45:7. Yeremia 18:11. Maombolezo 3:38).

Na BWANA hajatenda hili? Kwa maana ya kweli ya neno “uovu” Bullinger haoni kuwa hakuna sababu ya kufankwenye lugha ya Kiebrania ili kuutetea utakatifu au haki ya Yahova ya kushughulika nao.

imefanyika = imeteseka.

 

Amosi 3:8

Samba ameunguruma. Lugha ya Mfano ya Hypocatastasis (kama ilivyo kwenye Comp. Bible, Nyongeza 6).

Bwana MNGU amesema. Lugha ya Mfano ya Hermeneia (sawa na ilivyo pia kwenye Nyongeza 6 ibid). Kuelezea kwa lugha ya Mfano ya Hypocatastasis. Kwenye mstari uliotangulia kabla yake.

Ni nani awezaye zaidi ya kutoa unabii? Lugha ya Mfano ya Erotesis. (sawa na Nyongeza 6 ibid). Wakosoaji wengine wa siku hizi wameibadili maana halisi ya Kiebrania na kuiandika kuwa “kutishwa”, wasijue kwamba ni kwa nia ya unabii ndipo Mungu huongea na watu wake (Waebrania 1:1).

 

Amosi 3:12

Anachukua = anaopoa au kuokoa kutoka hatarini, kama kitu kipya na kizuri kilichoopolewa kutoka kwenye muunguzo wa moto.

Kipande kimoja = safari au msafara.

Kwenye kochi au kiti kikubwa cha kisasa = [kuwa taabani kwa ugonjwa wa] kulala yaani kuwa kwenye raha mstarehe burudanini. Linganisha na 6:1-4. Ellipsis (ya Marudio). (sawa sawa na Nyongeza 6,  ibid).

 

Amosi 4:3

Ng’ombe, yaani mwanamke.

Kwa hiyo ambayo ni kabla ya yake = kila mwanamke kwa uvunjaji [kwenye ukuta wa Samaria].

Kabla yake, yaani pasipo kubadilika kwenye mkono wa kushoto au kume. Linganisha na Yoshua 6:5, 20.

Atammuweka kwenye jumba la kifalme. Jumba la Kifalme au Ikulu kwa Kiebrania ni harmon (tazama kwenye andiko la 1:4). Hapa ni kwamba Ha-Harmonah, linalounda neno la Kimafumbo la Paronomasia (sawa na Comp. Bible, Nyongeza 6) pamoja na 'arman (3:11). Kiambishi hiki yabidi kitafsiriwe kwa 3:11, 12, na 5:27, na kwa hiyo ingepasa lisomeke: "utatupwa mbele kuelekea Ha-Harmon". Mahali hapajulikani, ila yaweza kumaanisha "enyi wanawake mliotulia kwenye majumba yenu ya fahari" (arman, 3:11, 12) mtatolewa na kupelekwa huko Ha-Harmonah: utumwani. Andiko hili si lazima “likanganywe” kwa kuwa haitufanyi tujue mahali lilipokusudiwa jina hilo.

 

Amosi 4:4

Njooni Beth-eli, nk. Hapa tuna mwongozo wa Kimungu, kana kwamba inamaanisha “kijazeni kikombe cha uovu wenu". Linganisha na Mathayo 23:32.

Potosha au tia unajisi . . . upotoshaji au utiaji unajisi. Kwa Kiebrania pasha'. Nyongeza 44.

Beth-eli . . . Gilgali. Linganisha na 3:14; 5:5; Hosea 4:15; 9:15; 12:11.

Baada ya miaka mitatu. Mrejesho wake upo kwenye Torati (Hesabu 28:3. Kumbukumbu la Torati 14:28), (Nyongeza 92 ibid); sio kwenye "siku", au "mahujaji walio kwenye Umma wa Mohammedi".

 

Amosi 4:7

Mvua kubwa za masika hinyesha kutoka mwishoni mwa mwezi Oktoba hadi mwishoni mwa mwezi Februari. “Mvua inayofuatia Baadae” hunyesha mwezi Marchi na Aprili.

Miezi mitatu ya kuendea majira ya mavuno ndio watati ambao ardhi inaahitaji nvua kwa siasi kikubwa. Kukuza jambo huku kunafaanyika inapokuwa hakuhitajiki sana na haufanyiki wakati unapohitajika sana.

 

Amosi 4:9

Kwa nini wanajenga au kulima bustani wakati wanataka kuangamia wote.

Neno Hija au Uhujaji limetajwa pia kwenye Yoeli 1:4.

 

Amosi 4:10

Njia ya Misri ni bota zaidi kwa maana au jinsi  ya Misri (sawa na Isaya 10:24,26)  na ni vibaya sana kama ilivyo Misri (sawa na Kutoka 9:3nk).

 

Amosi 4:12

Andaeni kukutsns nsye, nk, yaani kwenye hukumu. Sawa na ilivyo kwenye Ezekieli 13:5; 22:30. Aya za 11 na 12 hazipo “nje ya nafasi” au ni "uondoaji wa maneno", bali wanalazimishwa au kuamriwa na Maandiko Matakatifu, "M", (Bullinger, ukurasa wa 1236).

 

Amosi 5:5

Betheli. Gilgali. Beer-sheba. Linganisha na Hosea 4:15; 10:8. Haya yalikuwa ni makazi au vituo vya ibada za Israeli waabudu sanamu.

Usipite = usipite mbali; ambapo ilikuwa ilikuwa ni mhimu ili kupata kutoka kaskazini hadi Beer-sheba upande wa kusini. Linganisha na 4:4; 8:14.

Gilgali kwa hakika itakwenda utumwani. Kumbuka lugha ya Mfano ya Paronomasia (Comp. Bible, Ap. 6), kwa msisitizo. Kwa Kiebrania Gilgal galoh yigleh = Rola, inayozinga, litazingilia mbali, yaani kuondolewa kabisa. Hii imesisitizwa kwa lugha ya Mfano ya Polyptoton (Nyongeza 6).

 

Amosi 5:15

Chukieni maovu, Linganisha na Zaburi 34:14; 97:10. Warumi 12:9, Hii inajumuisha onyo la mwisho kati ya nasaha tatu.Inaweza kuwa kwa Kiebrania ulay. Aya yote inajiri na nasaha lakini kwa matamshi ya Kiebrania, inaiondoa sentensi hii, ikitilia maanani, sio kwa kubahatisha kwa upande wa Yahova, bali kwa magumu ya upande wa Israeli; na utaratibu huu ni kuhamasisha utii kwa miito. Linganisha na Kutoka 32:30. 2Wafalme 19:4. Yoeli 2:14.

Jina Yusufu. Limewekwa kw lugha ya Mfano ya Synecdoche (kwa Sehemu), (Nyongeza 6 ibid), kwa sehemu zote za Ufalme wa Kaskazini.

 

Amosi 5:18

Ole. 0le ya kwanza. Tazama Utaratibu kwa siku ya BWANA (sawa na jarida la Siku ya Bwana na Nyakati za Mwisho (Na. 192). (Soma maandiko ya Bullinger kuhusu Isaya 2:12; 13:6. Yoeli 2:1.)

Giza, na si nuru. Kumbuka kuwa hii ni lugha ya Mfano ya aina ya Pleonasm (Nyongeza 6) kwa kukazia. Sawa na Yeremia 30:7. Yoeli 2:2. Sefania 1:15.

 

Amosi 5:25

Mmetoa sadaka, nk . . . . ? lugha ya Mfano ya Erotesis. Nyongeza 6. Hili ni swali lililo kwenye baadhi ya nakala na matoleo matatu ya machapisho ya kale, lakini matoleo mengine manne ya nakala zilizochapishwa hapo zamani, yanasomeka hapa kama usemi imara na thabiti. Kama ni swali, jibu lake litakuwa ni Hapana. Soma Kumbukumbu la Torati 32:17. Yoshua 5:5-7. Yeremia 7:22, 23. Ezekieli 20:8, 16, 24.

Kwangu mimi, na Sio “kwa Mashetani". Rejea kwenye Torati (Walawi 17:7. Kumbukumbu la Torati 32:17). (Nyongeza 92 ibid), (sawa na Zaburi 106:37. 1Wakorintho 10:7).

 

Amosi 5:26

Kiuni. Mungu wa Wamisri na Wayunani sawasawa na alivyokuwa Remphan (kwenye Septuagint ameandikwa Raiphan; spelingi nyingine imebakizwa kwenye Septuagint na kwenye Matendo 7:43). Majina halisi yanayotofautiana kila mara kwenye speling, kwa mfano Ethiopia ni neno la Kiebrania Kushi laweza kuwa pia na maana ya Kikaldayo; Misri ni Mizraim; Mesopotamia na Syria ni'Aramu, au 'Aram-naharaim, nk.

 

Amosi 5:27

Mbele zaidi ya Damascus. Kwenye Matendo 7:43 ng’ambo ya Babeli, ambalo kulikuwa kwa kweli “ng’ambo ya Damascus", na kulijumuisha hii, kuoyesha kile lilochokuwa mpando wa Kimngu kwa maneno ya Yahova (aya ya 27) na Amosi. Zaidi ya yote,, barabara ya kwenda Ashuru ilikuwa inapitia Damascus. Linganisha na 2Wafalme 15:29; 16:9. Isaya 8:4. 3:12. Mtu mmoja anauliza swali. Inaweza asiwe Mungu kupitia Roho Mtakatifu aliyenuku na kuiga maneno yake mwenyewe kama apendavyo?

 

Amosi 6:1

'Ole. Ole ya pili. Soma kwenye 5:18. Wao, yaani wenye hekima wa Yuda, kwa kulinganisha na wenye hekima wa Israeli (katika Samaria) kwenye kifungu kinachofuatia kwenye utulivu na amani = kutojali, linda, au kubali kirahisi.

Tumainia = tegemea. Kwa Kiebrania ni batah. (sawa na Nyongeza 69 kinyume cha cha madai).

Hapa Sehemu. = wao waliothibitisha au kuamini.

Ambao wametajwa majina = [wanaume wa] wanaume, sawa na ilivyo kwenye Hesabu 1:17

Mfalme wa mataifa: yaani Israeli. Rejea kwenye Torati (Kutoka 19:5).(Nyongeza 92 ibid),

Nyumba ya Israeli: yaani Ufalme wa Kaskazini = Watu wa Israeli.

Njooni. Eneza Kimduara wa umbo la yai: "njooni [kwa ajili ya hukumu na haki]", kama ilivyoonyeshwa na idadi iliyobakia ya tarakimu hii ("y1").

 

Amosi 6:10

Mjomba wa mtu = ndugu au jamaa

Yeye, yaani mzoga unaounguzwa motoni. Tazama ilivyoandikwa kwenye 4:10. Hapa na kwenye 1Samweli 31:12 ni sehem mbili pekee ambapo uchomaji moto wa maiti umetajwa, nk. Zote mbili ni kesi za aina yake, ila ilikuwa ni matendo ya kawaida ya Wahiti (Mwanzo 14:6; Kumbukumbu la Torati 2:12, 22) ambako mabaki au masalio yao yanakutikana kwenye kazi ya uchimbuzi wa mambokale huko Gezeri. Tazama kitabu cha Bullinger na maoni yake kuhusu 1Wafalme 9:15-17.

Mifupa; yaani mtu aliyepunguzwa na kuwa skeleton au mifupa mitupu. Linganisha na Ayubu 7:15; 19:20.

Yeye aliyeko, nk, aliyeponoka au kupona.

Kwa pande za = katikati ya, au upende unaozuia.

Yeyote, yaani aliyehai au aliyekufa.

Fanya mtajo wa = itia au hiomba dua. Linganisha na Isaya 26:13; 49:1; 62:6.

 

Amosi 7:9

Mahali pa juu. Palipotumika kwa kujengwa madhabahu za ibada za sanamu, nk.

Isaka . . . Israeli. Imetumika na Amosi peke yake kwa maana hii. Imewekwa kwa lugha ya Kimfano ya Metonymy (ya Kiunganishi), nyongeza ya 6 ibid, kwa taifa la Israeli. Linganisha na Petro 105:9, 10. Yeremia 33:26, nk.

Nitainuka kinyume, nk. Imetimilika kwenye 2Wafalme 15:10. Yeroboamu. Sawa na ilivyo kwenye Hosea 1:4.

 

Amosi 7:10

Kuhani. Kuhani mwongoza ibada za sanamu.

Beth-eli. Linganisha na 3:14; 4:4; 5:5, 6.

Hamasisha = kufanya hila za kuangusha utawala, mapango yaliyounganishwa na sera ya taifa la Israeli (1Wafalme 12:26-33).

Kwa upande wa katikati, nk: yaani kwa wazi sana. Linganisha na 7:8.

Vumilia = stahimili.

 

Amosi 7:11

Yeroboamu atakufa, nk. Mabadiliko haya hayakuwa ya kweli. Linganisha na Matendo 17:6-7; Matendo 24:5. Zingatia kile alichoacha kukifanyia toba Amazia.

 

Amosi 8:3

Hekalu. Toleo la Kamusi ya 1611 la tafsiri ya A.V. inasomeka mahekalu".

 

Amosi 8:9

Sababu ya jua. Inaama nyakati za kutimia kwa "mapatilizo" haya. Soma kwenye Isaya 13:10; 59:9, 10. Yeremia 15:5. Yoeli 2:2; 3:15. Mika 3:6. Yawezekana kuwa hii inamaanisha tetemeko la ardhi la 1:1?

 

Amosi 9:1

BWANA. Moja ya kamusi hizi za 134 inaliweka jina hili pale ambapo tafsiri ya Sopherim inasema waligeuza maana ya jina "Yahova" kutoka kwenye andiko la zama kale na kuandika "Adonai" (Nyongeza ya 2 ibid). Soma pia kwenye tafsiri ya Comp. Bible, Nyongeza 4. na II . Hapa inajumuisha na 'eth = Yahova Mwenyewe.

Inategemea upande, au kwayo.

Madhabahu. Huenda ni madhabahu ile ile sawa na ya Beth-ali ya wakati wa Yeroboamu aliyowahi kjuijenga huko (1Wafalme 13:1). Linganisha na 7:13, linta = kuu au kubwa. Inasema: "upige mji mku, tingisha misingi yake, ikatilie mbali [yaani nguzo zake] kwa kichwa, wote miongoni mwao". Na nitawachinja. Hii ndiyo maana yake tendo hili la mfano.

Neno la mwisho: yaani masalio ya Watu.

 

Amosi 9:11

Katika siku ile. Kwa kupitia kwenye somo au fundisho la marejesho mapya yatakaypfanyika siku zijazo na z mwisho (soma jarida la Siku ya Bwana na Nyakati za Mwisho (Na. 192)). Ilinukuu kutoka kwenye Matendo 15:14-18 kuhusu Daudi. Ilisimamishwa huko Sayuni na Daudi (2Samweli 6:17. Linganisha na 7:6) kabla halijajengwa Hekalu juu ya Mlima wa Moria na Sulemani. Mwaka 7:7-9, ulionekana kuwa "nje ya timazi", kwa hiyo kuwa kwenye nafasi ya kuanguka. Hapa umeanguka chini: kwa hiyo unabii unabii unatolewa tena hapa. Kwenye Matendo 15 wakati ulikuwa umewasili, na watu waliuitikia na kuutii wito wa Petro kwenye 3:18-21. Lakini hatimaye ulikataliwa (Matendo 28:25-28), na unabii huu, kwa hiyo bado unangojea kutimia kwake.

 

Amosi 9:13

Mtu wa kulima, nk. Hii inaonyesha kuwa utimilifu wa unabii huu ni bado haukuwa ukitumika, kwa kuwa Baraka hizi za kitambo ziliahirishwa kwa sababu ya kuukataa kwao wito wa kutubu ulio kwenye Matendo 3:18-26. Linganisha na Matendo 28:25-58. Kumbuka mrejesho wa Torati (Walawi 26:5). Nyongeza 92 ibid.

Milima, nk. Linganisha na Yoeli 3:18.

Mvinyo mtamu = mvinyo mpya. Kwa Kiebrania asis Soma jarida la Mvinyo Kwenye Biblia (Na. 188).

Yeyuka, yaani kubobea kwenye unywaji wa mvinyo na kuyeyushwa kwenye mafuta. Lugha ya Mfano ya Hyperbole (Nyongeza 6), kwa kukazia au msisitizo.

 

Amosi 9:15

Nitapanda. Rejea kwenye Torati (Walawi 25:18, 19; 26:5). Nyongeza 92 ibid.

Nchi yao. Rejea kwenye Torati (Mwanzo 13:15, nk.) nyongeza 92 ibid. Linganisha na Isaya 60:21. Yeremia 24:6; 32:41. Ezekieli 34:28; 37:25. Yoeli 3:20. Mika 4:4.

Hakuna kuvutwa tena. Linganisha na Yeremia 32:41.

Ambayo nimewapa. Hii ni sababu ya Baraka zote. Rejea kwenye Torati (Hesabu 32:7, 9. Kumbukumbu la Torati 3:18; 26:15; 28:52). Nyongeza 92 ibid. Linganisha na Yoshua 2:6, 15; 18:3; 23:13, 15. Yeremia 25:5. Ile inayoitwa “Gombo la ‘Makuhani’”, kwa mujibu wa wakosoaji wa siku hizi, ilitungwa na makuhani huko Babeli, na karibu Torati yote ni ya kipindi cha “baada ya utumwa” (soma kitabu cha Encyclopaedia. Britania, eleventh (Cambridge) edition, vol. 3, p. 852, col. I). Tena ilijulikana sana na Amosi (karne ya 7 KK.) linganisha na 2:4, 7, 8, 12; 4:4, 5; 5:12, 21, 22; 9:4, nk. Wengine hata wanajaribu kutumia kiunganishi hiki ili kuhalalisha chimbuko asilia la Amosi.

anasema = amesema.                                                            

 

                                                            q