Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[132]
Miandamo ya Mwezi Mpya Katika Israeli
[132]
(Toleo 2.0 19950826-19990918)
Jarida hili linachukua maendelezo yaliyoko katika jarida la kwanza na inashughulikia na kufundisha maana ya kiroho yanayohusiana na Miandamo ya Mwezi Mpya. Pia limeelezea kuhusu hakikisho la jinsi Kanisa lilivyokuwa linaadhimisha Miandamo wa Mwezi Mpya kwa kipindi cha karne mbalimbali zilizopita.
Christian Churches of God
E-mail:
secretary@ccg.org
(Copyright © 1995, 1999,Wade
Cox)
(Tr. 2005)
Masomo haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia
watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kutufa
maneno. Jina la mchapishaji na anuami yake pamoja na hati miliki ni lazima
iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya
nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya maelezo na kilugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya
hati miliki.
Masomo haya pia ynapatikana
Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org
au http://www.ccg.org
Miandamo ya Mwezi Mpya
Katika Israeli [132]
Mafundisho kuhusu Miandamo ya Mwezi Mpya yameendelezwa katika mfululizo wa majarida yajulikanayo kwa kichwa cha somo kisemacho Miandamo ya Mwezi Mpya [125]. Jarida hili linakusudia kufafanua maana ya kiroho ya Miandamo ya Mwezi mpya. Kanisa limekuwa likiadhimisha Miandamo ya. Mwezi Mpya kwa vipindi.vya karne nyingi na kile kilichoitwa zama. Kanisa la Mitume liliadhimisha Miandamo ya Mwezi Mpya. Paulo alisema kuwa mtu asimhukumu mwingine kwa ajili ya vyakula na vinywaji au Sabato au Mwandamo wa Mwezi au Sikukuu (Kol. 2:16). Tunajua bila ya shaka kuwa Kanisa la Yerusalemu lilikuwa ni Kanisa linaloitunza Sabato hadi kufikia katika karne ya nne kama ndugu yetu na mwanazuoni maarufu Bakioki anavyo onyesha kwenye maelezo ya tafiti zake. Paulo asingeweza kutoa usemi huu kama aina mbalimbali zozote maadhimisho yasingekuwa yanafanyika. Miandamo ya Mwezi ilifikia hatua ya kutoadhimishwa, kama ilivyokuwa kwa Sikukuu hizi zingine, kwa mara ya kwanza kwa amri ya maazimio ya Mtaguso wa Halmashauri kuu ya Baraza kuu la Nikea kwa kanisa lote. Hata hivyo, hii haina maana kuwa walikuwa hawaadhimishi kabisa.
Miandamo ya Mwezi ilikuwa inaadhimishwa kwa mara ya mwisho katika nchi za Ulaya wakristo wa Makanisa ya Hungari na wa huko Transylvania kama ilivyonukuliwa kwa mujibu wa mwanazuoni ambaye alikuwa pia ni Rabi Mkuu wa Budapest aliyeitwa kwa jina la Rabi Saamuel Kohl kwenye jarida liitwalo (DIE SABBATHARIER IN SIEBENBURGEN Ihre Geshichte, Literatur, und Dogmatik, Budapest, Verlag von Singer & Wolfer, 1894; Liepzig, Verlag von Franz Wagner). Mwezi Mpya ulikuwa na umuhimu kiasi kile lakini Sikukuu ya Baragumu haikuorodheshwa katika kitabu chao cha nyimbo kilichojulikana kama Kitabu cha Nyimbo za Kale za Sabato zilizotungwa kwa kufuatana na sikukuu zenyewe. Ilikuwa inahusiana na Miandamo ya Mwezi ambayo, kutokana na jinsi ilivyokuwa inafanyiwa, inaonyesha kuwa Mwezi Mpya ulikuwa unachukuliwa na Kanisa kuwa ilikuwa inatangulia sikukuu hizi. Hii ndio jinsi ambayo Mwezi Mpya ilikuwa inaorodheshwa. Kwa ujumla, iliorodheshwa kibiblia ili itangulie baada ya Sabato na kabla ya hizo sikukuu (tazama 1Nya. 23:31; 2Nya. 2::4; 8:13; 31:3; Ezra 3:5; Neh. 10:33; Isa. 1:13-14; Eze. 45:17 (utaratibu wa marudio); 46:3; Hos. 2:11 (utaratibu wa marejeo na neno la jumla). Katika maskani, Hekalu chini ya Sulemani na kwa kila marejisho, au matengenezo ya kidini Miezi Mipya ilikuwa imeanzishwa kama tunavyoweza kuona kutoka kwenye aya za maandiko matakatifu. Hakuna marejezo yaliyofikia ukamilifu wake pasipo hiyo.
Katika kurasa za 62-67 za jarida la Kohn inasemea kuhusiana na wimbo wa utenzi kama ifuatavyo:
Wimbo huu uliandikwa huko Hungari na [Andreas] Eossi, Enok Alvinczi, Johannes Bokenyi, Thomas Pankotai & Simoni Pechi. … ilichukua jumla ya Tenzi 102. Tenzi 44 zilikuwa ni kwa ajili ya Sabato, 5 za Mwezi Mpya, 11 za Pasaka na Mikate isiyotiwa Chachu, 6 za Sikukuu ya Majuma, 6 za Sikukuu ya Vibanda, 3 za Mwaka Mpya, 1 za siku ya Upatanisho, 26 kwa matumizi yoyote. (hazina ya majarida haya imeongezewa na Gerhard O Marx kwenye jarida lake liitwalo:Iman na matendo ya Kanisa la Mungu la Transylvania katika kipindi cha miaka ya 1588-1623).
Kohn anayaona Makanisa haya kama:
Yaliyorejesha Ukristo wenyewe asilia na ukweli wa neno, ambao kwa kweli waliupokea na kuenenda kwayo maadili na mapokeo ya kidini ya Wayahudi na sheria ambazo Agano la Kale lilielekeza ambayo kwayo, Wakristo wa kwanza asilia walizishika zikiwafungsmanisha na mbazo baadae zilitupiliwa mbali (soma Kohn, p.8)
Andreas Eossi hatimaye akawa kiongozi wa Kanisa la Wanaoamini kuhusu uwepo wa miungu wawili yaani Waunitaria (Unitarian Church) baaada ya kifo cha Francis Davidis katika mwaka 1579. Davidis akaanzisha Kanisa la Waunitaria huko Transylvania mnamo mwaka 1566 kwa msaada Wahungary akitumilia mwanya uliojitokeza wa kiimani kwa kanisa la Hungary wa kukubaliana na mafundisho ya Waunitaria waliotwa Wawaldensia. Eossi aliingia kwenye kukubaliana na mafundisho ya Waunitaria mwaka 1567. Sawa kabisa na ilivyotokea kwa Wawaldensia wa magharibi kwa wakati wa mwanzo wa Matengenezo ya imani, Kanisa la Mashariki ya Ulaya liligawanyika kwa sehemu mbili yaani wale waliorudi nyuma na kuanza kuabudu siku ya Jumapili na wale walioendelea kuishika Sabato kuanzia kifo cha Davidis na Eossi kuwa kiongozi wa Washika Sabato.
Kanisa la Mungu kwa kweli lilipelekea kupata upinzani na kupingwa na hawa Waunitaria washika Jumapili waliokuwa wametumika katika uanzilishi. Vuguvugu la nguvu za mfumo wa Kiprotestanti lilikuwa ndio sababu ya kwanza kupelekea hali hii.
Pia tunaona tofauti ya mabadiliko ya kijanja yakijitokeza kutoka kwenye kambi ya upinzani wa Davidis yakiongozwa na Faustus Socinus mnamo mwaka (1539-1604) wakati alipojiondoa Piedmontese George Blandrata ambaye hatimaye alikuwa kiongozi wa kanisa lililojulikana kama Reformed Church Unitaria mnamo mwaka 1558 mara tu baada liipoanzisha sinodi mnamo mwaka 1556. Imani nyingine iliyokuwa inajulikana kama Wa-anabaptisti wa Ulaya ya kati (maarufu kama The Dutch Anabaptists) wakiongozwa na David Joris wa Delft, mnamo mwaka (1501-1556) walikuwa pia Waunitaria kama tunavyojua. Hawa Wa-anabaptisti walijitenga kutoka kwa Lollards kiongozi wao kuanzia katika karne ya kumi na tano.
Vuguvugu la Waunitaria hatimaye lilijiita Wasocinia kwa jina la Faustus Socinus. Kama tumjuavyo mtu huyu kuwa alimpinga Francis Davidis aliyeponya sehemu kubwa ya wapiganaji waliokuwa wanatetea kuhusu asili hasa ya Kristo. Huenda upinzani huu ulituama katika uridhishaji wa kurudisha ile idadi kama ilivyokuwa msisitizo kwa karne mbili zilizopita. Davidis akatiwa gerezani katika gereza la Deva kwa kukataa kuomba kwa Kristo na hatimaye alifia huko mwezi Novemba 1579. Nasafi yake ikachukuliwa na Eossi. Kwa kweli, Kanisa la Mungu lilikuwa linajulikana kwa jina la Waunitaria kwa kuwa neno hilo lilikuwa halitumiki kama jina hadi lilipotumika na Meltus likaonekana kwa kara ya kwanza kwenye nakala fulani fulani kwenye nakili za Sinodi ya Lecsfalva mwaka 1600. mwanzoni kabisa lilichukuliwa na kutumiwa na Kanisa la Waroma mwaka 1638. Hali ya kutoelewana iliyokuwa imejitokeza kati ya Socinus na Davidis inonekana ilituama na fundisho kuhusu nasafi hasa ya Kristo ni ipi. Lakini wote wawili walikuwa ni Waunitaria. Davidis alizikataa aina zote za mfano au maelekezo ya kikalti kuhusu Kristo. Socinus alikubali neno Mungu kutumika kwa Kristo katika mtazamo wa udogo. Ni kwa mtazamo huu wa Mungu mdogo, yaani kwa Kiyunani deuteros theos, ambalo tumelichukua kutoka katika kazi za Irenaeus. Andreas Eossi, tangia kifo cha Davidis na tangia kuondolewa kwa vuguvugu la wapenda-Jumaoili, aliweza kurejesha Kanisa la Watu wa Ulaya kufikia utukufu wake zaidizi, mapema mno, na umbo lake asilia.
Utaratibu huu ulihusisha Mwezi Mpya kuwa kama sehemu ya lazima katika imani. Ndipo Miandamo ya Mwezi angalau ilichukuliwa kuwa na nafasi sawa na zilivyoonwa zile Siku Takatifu. Sikukuu ya Baragumu haikuorodheshwa kwa kutenganishwa, kama tulivyoona kwenye orodha ya zile tenzi, lakini zaidi sana ilichukuliwa kama Miandamo ya Mwezi, ambayo ni kufanya Mwandamo wa Mwezi wa saba, au Tishri. Ilikuwa ni kwa ajili hii ilikuwa kwenye mawazo ya Makanisa ya watu wa Ulaya, maana ya kiroho ya Miandamo ya Mwezi uliaowekwa katika umuhimu juu yake ambayo iliwakilisha kama muundo, na haikuangukia juu yake, maana ya ujio wa Masihi kama tuonavyo katika Sikukuu ya Baragumu.
Tumeona kutoka katika jarida la kwanza kuwa Miandamo ya Mwezi ilianzishwa kuanzia katika vitabu vya Torati ya Musa. Zilikuwa zinatunzwa kwa maana iliyo karibu sawa tu na ile ya Sabato za wiki (hii ni kwa mujibu wa Hayyim Schauss, Jarida la Historia ya Sikukuu za Kiyahudi na Maadimisho yake, 1885, p.113). Hakuna biashara iliyokuwa inafanyika iwe kwa Siku ya Mwezi Mpya au Sabato (Amosi 8:5). Tutaona kuanzia jarida hili na la baadae kwamba Miandamo ya Mwezi ni ya lazima kwa Mpango wa Wokovu. Sio kwamba tu Miandamo hii ya Mwezi ina maana ya kiroho tu katika kuhusianisha na sehemu waliyonayo Israeli kwenye Mpango wa Wokovu lakini inawakilisha utaratibu kamili wa dhabihu unaoamulia sio tu uwepo wa Makanisa yaliyokati ya Mungu lakini pia inaamulia jinsi ya upatikanaji wa wale 144,000 na kudhihirisha jinsi ya upatikanaji kwa namna zote mbili yaani kwa utaratibu kufuata makabila, sio tu ndani ya Israeli lakini pia kwa mtazamo ulio mpana kama serikali ya mataifa. Miandamo ya Mwezi pia ni ya muhimu katika kufafanua dhabihu zinazohusishwa kwenye Hekalu Jipya la Mungu lililo anzishwa tangia Kufanyika kwake Masihi kuwa mwili na kufufuka kwake. Pia Eliya atarejesha tena maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi au hatakuwa amerejesha vitu vyote (Mal. 4:5; Mat. 17:10-11). Tokea Mwezi Mpya hadi Mwezi Mpya na tokea Sabato hadi Sabato watu wote watakuja na kuabudu mbele yangu asema Bwana (Isa. 66:23). Haya ni marejesho ya kweli. Marejesho haya yatatangulia kabla ya kuja kwake Masihi na yataendelea hadi mataifa yatakapo nyenyekeshwa na kuongoka.
Kushughulika na kupangilia jinsi sikukuu hizi peke yake zinavyotakiwa kuadhimishwa na kuacha Miandamo ya Mwezi ni kukosa kuelewa maana ya mambo yote mawili na nia ya Mungu. Kama hizi Siku Takatifu zinasimamiwa na amri ya nne ndivyo ilivyo pia kwa Miandamo ya Mwezi.
Hebu sasa na tujaribu kuondoa maana nzima ya Miandamo ya Mwezi katika Mpango wa Mungu.
Kitabu cha Mwanzo 1:14 kinaonyesha kuwa Mungu alifanya nuru iwepo katika mbingu ili kutenganisha mchana na usiku na kama ishara ya majira. Miandamo ya Mwezi huweka utaratibu wa majira ya sikukuu na kwa mantiki kamilifu sana huitangulia Sabato ambayo inawakilisha tendo la kumalizia kwa siku ya saba wakati ambapo Miezi hutangulwa na siku ya nne. Nuru iliwekwa ili kutenganisha nuru na giza (Mwa. 1:18). Mwezi ni mfano wa ishara ya nuru ya ulimwengu ukiwa ndani ulumwengu wa giza linalo itawala. Jua linatumika kama ishara ya Kristo (Mal. 4:2).
Malaki 4:2-5 inasema: 2
Lakni kwenu ninyi mnalolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenge kuponya
katika mbawa zake, nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama nda ma wa mazizini.
3Nanyimtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu;
katika siku ile niifanyayo, asema BWANA wa majeshi. 4 Ikumbukeni torati ya Musa, mtumishi wangu, niliyomwamuru huko Horebu
kwa ajili ya Israeli wote, naam, amri na hukumu. 5 Angalieni nitawaletea nabii, kabla haijaja siku ile ile ya BWANA,
iliyokuu na kuogofya.
Hapa maana yake ni kwamba, jua ni Masihi na kicho cha Bwana ni kukumbuka Sheria ya Mungu.
Pia Jua linalinganishwa na Masihi aliyetokea katika Yakobo (Mwa. 32:30-31).
Mwanzo 32:30-31 inasema hivi: 30 Yakobo akapaita mahali pale, Penueli, maana alisema, Nimeonana na Mungu uso kwa uso, na nafsi yangu imeokoka. 31 jua likamzukia akivuka Penueli, akachechemea kwa sababu ya paja la mguu wake.
Hapa alimuona elohim wa Israeli uso kwa uso. Elohim huyu alikuwa ni Masihi.
Miili ya kimbinguni hutofautiana katika utukufu kama miili itumikayo kuashiria ulimwengu tofauti.
1Wakorintho 15:40-50 inasema: 40 Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani; lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ile ya duniani ni mbali. 41 Kuna fahari moja ya jua, na fahari nyingine ya mwezi, na fahari nyingine ya nyota; maana iko tofauti ya fahari hata kati ya nyota na nyota. 42 Kadhalika na kiyama ya watu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutoka kutoharibika; 43 hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu; 44 hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko. 45 Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha. 46 Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili; baadaye huja ule wa roho. 47 Mtu wa kwanza atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni. 48 Kama alivyo yeye wa udongo, ndivyo walivyo walio wa udongo; na kama alivyo yeye wa mbinguni, ndivyo walivyo walio wa mbinguni. 49 Na kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo; kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni. 50 Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kuto kuto kuharibika.
Mwezi hutumika kutolea mfano kwa wote wawili yaani Israeli kama taifa na Israeli kama Kanisa. Yeye, Israeli, atatawala kama Mungu (elohim).
Katika matumizi ya kwanza tunafikia kwenye mfano wa matendo kwa makabila yanayo patikana kwenye kitabu cha Mwanzo kikimuonyesha Yusufu katika Mwanzo 37:9.
Mwanzo 37:5-11 inasema: 5 Yusufu akaota ndoto, akawapa ndugu zake habari, nao wakazidi kumchukia; 6 akawaambia, Tafadhalini, sikieni ndoto hii niliyoiota. 7 Tazama, sisi tulikuwa tukifunga miganda shambani, kumbe! Mganda wangu ukaondoka ukasimama, na tazama, miganda yenu ikazunguka ikainama mbele ya mganda wangu. 8 Ndugu zake wakamwambia, Je! Kweli wewe utatumiliki sisi? Nawe utatumiliki sisi? Wakazidi kumchukia kwa ajili ya ndoto yake, na kwa maneno yake. 9 Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake, akasema, Angalieni, nimeota ndoto nyingine; na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia. 10 Akawaambia baba yake na ndugu zake; baba yake akamkemea akamwambia, Ni ndoto gani hii uliyoiota? Je! Mimi na mama yako na ndugu zako tutakuja tukusujudie hata nchi? 11 Ndugu zake wakamhusudu; bali baba yake akalihifadhi neno hili.
Maana ya miganda inapatikana ikiashiria mavuno ya jumla. Hapa tunaona utawala wa Yusufu ukiwa kama sehemu ya mavuno. Katika mfumo huu tunaona kuwa maana hii inapanuka hadi inahusisha jua, mwezi na nyota za angani. Yakobo anakuwa jua kama mfano wa Masihi. Taifa lake linaitwa atatawala kama Mungu au Israeli. Mke wake anawakilishwa kama mwezi kwa sababu, kama mama wa Israeli, yeye pia anawakilisha taifa. Mke wa Masihi au bibi arusi wa Kristo vilevile ni Kanisa, kama tunavyoona katika Agano Jipya.
Makabila ni nyota za Jeshi. Wao ni nyota Thenashara pamoja na Yusufu akiwa ndio ile nyota ya kumi na mbili.
Sasa tunaweza kuendelea na Ufunuo wa Yohana 12:1-17.
Ufunuo wa Yohana 12:1-17 unasema: Na ishara kuu ilionekana mbinguni; mwanamke aliyevikwa jua, na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili. 2 Naye alikuwa ana mimba, akilia, hali ana utungu na kuumwa katika kuzaa. 3 Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba. 4 Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi. Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili azaapo, amle mtoto wake. 5 Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakayechunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma. Na mtotot wake akanyakuliwa hata kwa Mungu, na kwa kiti chake cha enzi. 6 Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko muda wa siku elfu na mia mbili na sitini. 7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; 8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. 9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye. 10 Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema. Sasa kumekuwa wokovu na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupya chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakie mbele za Mungu wetu, mchana nausiku. 11 Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. 12 Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kwamba ana wakati mchache tu. 13 Na joka yule alipoona ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume. 14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu wakati, mbali na nyoka huyo. 15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, umfanye kuchukuliwa na mto ule. 16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake. 17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama juu ya mchanga wa bahari.
Hapa tunaona kuwa huyu mwanamke amevikwa jua na mwezi ukiwa chini ya miguu yake. Kichwani kwake amevikwa taji ya nyota kumi na mbili. Maana yake hapa ni kuwa; Israeli alikulia nje ya taifa na kufanyika Kanisa. Waisraeli wa kimwili wakawa Israeli wa kiroho. Haki ya uzaliwa wa taifa na makabila ni kuwa pamba au uzuri kwa Kanisa. Mlolongo huu hutokea kwa wakati ulipelekea kwenye sura hii. Taifa na Kanisa vimepata mateso baada ya alipomleta yule mtoto mwanaume na akachukuliwa kwa Mungu na kwenye kiti chake cha enzi. Baada ya kipindi hiki, tunaona kuwa yule mshitaki wa ndugu zetu alitupwa chini. Malaika wanatajwa hapa kwa wateule ni kama ndugu zao. Hivyo basi, tunaongelea hapa uhusiano wa familia unaojumuisha Jeshi la malaika.
Tunaona hapa kuwa uzao wa mwanamke ni wale wanaoshika amri za Mungu na ushuhuda wa Yesu ili kwamba taifa hapa huwa ni Kanisa na kwa hiyo hufungulia mlango kwa Mataifa kuwa ni sehemu ya Israeli. Hivyo basi, uzao wa Israeli wameteswa kwa nyakati mbili na nusu wakati au miaka ya siku za kinabii 1,260. Kama tulivyokwisha ona kuwa kipindi hiki kiliishia mwaka 1850. Hatahivyo, kuna kipindi kingine zaidi yake kitakacho fuatia kitakacho ambatana na vita ya mwisho itakayoongozwa na kile kijulikanacho kama dola ya mnyama. Kipindi hiki kitachukua kitambo hadi ule muhuri wa mwisho kutiwa watakatifu kama ilivyo elezewa katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana 14. Tangia wakati huu, Injili ya milele ya Ufalme wa Mungu itahubiriwa na mfumo wote wa kibabeli utaangamizwa (Ufunuo 14:8).
Haijalishi ni wakati gani unaohusishwa katika utaratibu huu, jua, mwezi na nyota zinawakilisha mambo yote mawili, yaani mwanamke aliyemzaa Masihi na pia uzao wa mwanamke ambao ni Kanisa na bibi arusi wa. Masihi.
Mwezi unatumika kutolea mfano wa taifa la Israeli na pia kwa Kanisa kwa sababu mwezi hautoi mwanga kwa maumbile yake tu wenyewe. Unapewa nuru kwa msaada wa kuhakisiwa kutoka kwenye jua ambalo ni nyota katika mfumo wa kwanza. Jua hili pia ni ile nyota iliyotabiriwa kuwa itatokea katika nyumba ya Yakobo (Hes. 24:17). Kwa hiyo, tunayo nyota katika ule mfumo wa mwanzo unaoweka mbali madaraja ya vyeo na kuwa wokovu wa mfumo mpya. Kwa kupitia utendaji huu mifumo mipya au nyota vimeumbwa kwa kupitia mwanamke ambaye ni taifa au Kanisa. Pasipo kuwa na msukumo au nguvu zitokazo ndani anategemeka kwa uweza aliopewa kutoka kwenye jua ambalo ndi chanzo cha muumbaji. Kwa hiyo, Mungu hutanguliza kwana matukio ya mwandamano wa mambo.
Pia Mwezi ni alama au mfano kwa sababu uko katika awamu. Mwandamo wa Mwezi Mpya kuashiria mwanzo wa shughili za kila mzunguko. Kuna miezi Thenashara katika kila mwaka (ukiondoa ule mwezi wa mwaka maalumu) (1Fal.4:7; 1Nya. 27:1-15). Inaaminika kuwa na urefu wa jumla ya siku 30 kwa kila mwezi (Mwa. 7:11; 8:3-4; Hes. 20:29; Kum. 21:13; 34:8; Est. 4:11; Dan. 6:7-13). Miezi hiyo ni hii:
Mlingano na miezi ya Wababebi na maana zake ni:
Mzunguko wa miezi kumi na miwili ya mwandamo ni (siku 354¼ ) pungufu kidogo kwa kulinganisha na kalenda ya jua yenye mwaka wenye (siku 365 1/enye (siku 365 1/enye (siku 365¼). Kwa sababu sikukuu ya Pasaka-Mazzoth ya majira ya baridi, inayoanzisha mzunguko wa sikukuu za ukulima, hutakiwa iadhimishwe kwa wakati mmoja uliowekwa katika mwaka hii ni sababu iliyo dhahiri ya kwa nini mwezi maalumu umewekwa katika mwezi wa Adari mwishoni mwa mwaka. Pasaka lazima iambatane na malimbuko au mavuno ya kwanza na iwe kwenye mwanzo wa mwaka kutegemeana na eneo la mwezi mwandamo kwa kipindi ambacho mavuno ya shayiri huwa tayari. Maana ya kiroho yako dhahiri. Sikukuu zinategemea na Mwandamo wa Mwezi na sio nyuma mapema yake.
Mwndamo wa Mwezini ‘‘mwanzo wa mwezi mwandamo, mara nyingi kinakuwa katikati ya kiungo kimoja na kingine, urefu ambao umefanyiwa hesabu yakinifu kwenye shule zitoazo elimu ya mambo ya sayari za mbinguni” (kwa mujibu wa Judaeus Philo, jarida lake la Sheria Maalumu II, XXVI, 140, F. H. Colson, Harvard University Press, Cambridge MA, 1937).
Jina la mwezi huu maalumu wa nyongeza ni WeAdar (na Adar) kwa mujibu wa M. Ned VIII.5 (tazama kamusi iitwayo Interpreter’s Dictionary of the Bible, Vol. 1, p. 487). Hesabu za baraza la marabi huonyesha upungufu kwa saba kutokea kwenye kila miaka kumi na tisa kuwe na mwezi wa nyongeza unaoitwa Adar II.
Miezi inayohesabiwa kwa kuzingatia Miandamo ya Mwezi na Mpango mzima wa Wokovu, imethibitishwa kutoka katika kila Mwandamo wa Mwezi Mpya kupitia kwenye hesabu za sikukuu na madhihirisho yake kwenye mzunguko wa mavuno halisi ya kimwili.
Mungu aliushughulikia mfumo wa Wamisri na miungu yake kupitia kipindi cha kuanza kwao Israseli msafara wa Kutoka utumwani. Mungu aliushughulikia mfumo wa Wababeli kwa njia sahihi ya kuwaanzishia kalenda ya Kanisa. Kumbuka kuwa mfumo wa Wababeli ulianzilisha mwaka kuanzia mwezi wa kuanzia, Teshritu au Tishri. Kuanzia mwezi huu Masihi ataanzisha Mwanzo Mpya ambao unatolewa mfano na Sikukuu ya Baragumu, Siku ya Upatanisho, na Sikukuu ya Vibanda.
Mwezi wa Tishri unachukuliwa kama Mwezi Mpya ambao ni wa Baragumu. Mwezi wa kuanzia ulifanywa kuwa mwezi wa saba wa mwandamo ambao unawakilisha awamu saba za Makanisa saba. Kila Mwezi Mpya inawakilisha awamu moja ya kuanzia Masihi na kupitia kila Kanisa hadi kurudi kwake Masihi hiki kipindi cha kumngojelea. Kwa hiyo utaona kwamba hii Miandamo ya Mwezi yenyewe tu inakuwa inawakilisha kwenye Makanisa. Kwa kadiri yoyote ile itumikayo tumika kuamua ni vipindi vya zama mbili tu za maisha ya Kanisa havikuweza kutunza Miandamo ya Mwezi kwa nyakati fulani za kudumu kwa historia yake. Huu ni wakati unaoweza kuitwa ni zama za kanisa la Sardi na Laodikia. Moja kati ya haya imekufa, na moja nyingine Mungu ameiyapika itoke katika kinywa chake.
Mwaka huu iliwekwa ili kuweka mwezi wa kutoa dhabihu ambao uliwakilisha dhabihu ya Pasaka ya Masihi. Mwezi huu ulianzisha uvunaji ambao pia ilikuwa ni mwanzo wa mlolongo wa uvunaji, ambayo ilikuwa ni mavuno ya shayiri. Kwa hiyo Mungu alichukua utaratibu wa mavuno kupitia kwenye kila moja wapo ya awamu hizi ambazo zilikuwa ni awamu tatu za uvunaji. Hizi ndizo Pasaka na Mikate isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma, na Sikukuu ya Vibanda au Kusanyiko. Sikukuu ya Majuma huwa ni kielelzo cha mavuno ya Kanisa kabla ya kurudi kwa Masihi. Huu ni utaratibu endelevu. Kwa hiyo ni kusema kuwa Pentekoste ni amri ya mfuatano wa matukio inayofuatia kupitia miezi miandamo mitano kuanzia mwezi wa Sivan hadi Tishri, ingawa ipo saba kwenye mlolongo wake kuanzia mwezi wa Nisani hadi mwezi wa Tishri. Idadi hii ya tano inawakilisha mawe matano ya Daudi aliyoyachukua kwenye kijito (tazama jarida la: Daudi na Goliathi [126]. Makanisa Srdi na Laodikia yamekatiliwa mbali. Mwezi wa Sivani huanza kazi ya utengenezaji wa matofali kwa ajili ya Hekalu la Mungu. Mlolongo huu hatimaye huhusisha mwanzo wa mwezi wa (Du-uzu: au Tammuzi), kisha mienge (Abu: au Ab), au minara ya Kanisa na utakaso (Elulu: au Elul) wa wateule. Kwa hiyo miezi kuanzia. Simanu (Sivan) hadi Teshritu (Tishri) inahesabiwa kama mifano ya Wakristo iliyoifutilia mbali ile ya Wababeli. Umlikaji wa mienge wa siku ya 9-10 ya mwezi Ab iliruhusiwa kwa sababu ya ibada ya sanamu kwa Israeli kwa matendo ya Wababeli.
Miezi ipo kumi na miwili katika ujumla wake pamoja na ule wa kumi na tatu unaojitokeza mara saba kwa kila kipindi cha miaka kumi na tisa. Kipindi cha miaka kumi na tisa ni alama ya kukamilika kwa mzunguko. Kipindi hiki hufanyizwa na miezi mwandamo yenywewe, kwa kadiri inavyozunguka kupitia majira mbalimbali. Kuna jumla ya miaka kumi na tisa kwenye mzunguko mmoja.
Dhabihu zitatolewa kama ifuatavyo: Sabato hamsini na mbili, Sikukuu za Siku Takatifu saba na Miandamo ya Mwezi kumi na miwili, pamoja na Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa (Law. 23:9-14). Sikukuu ya Baragumu ina dhabihu mbili kwa pamoja ambayo ni kwa yote mawili yaani Sikukuu na Mwandamo wa Mwezi (Hes. 29:1-6).
Hapa tutashughulika na maana ya miezi ya Israeli. Uhusiano wake unategemea na utendaji kazi wa ule mwezi maalumu kama unavyojitokeza katika miezi kumi na miwili ya kawaida. Israeli huwakilishwa katika mfumo huu kupitia makabila kumi na mawili. Israeli ina makabila kumi na mawili. Hivyi ndivyo yalivyo kutokea upande wa Kaskazini: Dani, Asheri, Naftali, Yuda, Isakari, Zebuloni, Reubeni, Simeoni, Gadi, Efraimu, Manase, Benjamini (tazama Hesabu 10:11; sawa na Ezekieli 1:4). Kabila la Lawi limewekwa katikati maskani. Kwa hiyo, kuna makabila kumi na mawili lakini Yusufu ana haki ya uzaliwa na imegawanywa bila kukosea katika urithi na kufanya yawepo jumla ya makabila kumi na mawili pamoja na kabila la Lawi ambalo halikupewa milki yoyote ili waweze kufanya kikamilifu huduma za kikuhani. Kwa hiyo, ramani ya matendo ya Israeli wa kimwili iliwekwa kwenye nyota za uumbaji. Mwezi Adari II unawakilisha ukuhani kama mwezi wa kumi na tatu wa na kabila. Mwezi huu hutokea mara saba katika mzunguko. Mzunguko huu huwakilisha roho saba za Mungu kwa kadiri zifanyavyo kazi zake chuni ya malaika wa yale Makanisa saba. Tatizo hili haliwezi kupata ufumbuzi au kueleweka bila ya kuwa na ufahamu wa Miandamo ya Mwezi Mpya.
Kwa hiyo makabila hutangulia kwenye eneo la kiroho kama ukuhani wote mzima. Hiyo ingeweza kutokea hivyo, ili kumruhusu Lawi kufanya kazi zake za kawaida kama makuhani wa Israeli kwa kuungana na wengine, Yusufu angeweza kuchukua tu mahali pake pa kabila moja na Lawi kufanya la kumi na mbili. Hilo sio kwa kweli linalotokea. Ahadi za uzaliwa wa kwanza ilizotolewa kwa Yusufu pia zinatunwa katika njia ya mfano. Tunaona utaratibu huu kutokana na tathmini ya wale 144,000. Makabila wamewekewa idadi ya wateule 144,000 kwa msingi mwingine zaidi ya 12,000 kwa kabila. Yusufu kwa kweli lilifanyika muunganiko wa Efraim na Manase. Yusufu ni pekee lililowahi kutumika kuashiria kabila mchanganyiko na lile linalo shikilia haki ya uzaliwa.
Migawanyo hii inapatikana katika Ufunuo wa Yohana 7:1-8.
Baada ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizuzuia pepo nne za nchi, upepo usivume juu ya nchi, wala juu ya bahari, wala juu ya bahari, wala juu ya mti wowote. 2 Nikaona malaika mwingine, akipanda kutoka maawio ya jua, mwenye muhuri ya Mungu aliye hai; akawapigia kelele kwa sauti kuu wale malaika wane waliopewa kuidhuru nchi na bahari, 3 akasema, Msidhuru nchi, wala bahari, wala miti, hata tutakapokwisha kuwatia muhuri watumwa wa Mungu wetu juu ya vipaji vya nyuso zao. 4 Nikasikia hesabu yao waliotiwa muhuri katika kila kabila ya Waisraeli, watu mia na arobaini na nne elfu. 5 Wa kabila la Yuda kumi na mbili elfu waliotiwa muhuri. Wa kabila ya Reubeni kumi na mbili elfu. Wa kabila ya Gadi kumi na mbili elfu. 6 Wa kabila ya Asheri kumi na mbili elfu. Wa kabila ya Naftali kumi na mbili elfu. 7 Wa kabila ya Manase kumi na mbili elfu. Wa kabila ya Simeoni kumi na mbili elfu. Wa kabila ya Lawi kumi na mbili elfu. Wa kabila ya Isakari kumi na mbili elfu. 8 Wa kabila ya Zabuloni kumi na mbili elfu. Wa kabila ya Yusufu kumi na mbili elfu. Wa kabila ya Benyamini kumi na mbili elfu waliotiwa muhuri.
Tunaona hapa kuwa malaika wakipewa uweza wa kuidhuru nchi wakiambiwa wasiidhuru nchi hadi pale watumishi wa Mungu wamepigwa muhuri. Idadi hapa walikuwa 144,000. Waliotiwa muhuri katika makabila kumi na mawili. Inabidi ijulikane katika orodha hii kwamba Lawi anachukua idadi ya watu 12,000, ambayo si kawaida kwamba Lawi hakuhesabiwa katika mgawanyo wa nchi wala kwa mgawanyo wa milki miongoni mwa yale makabila kumi na mawili. Hata hivyo, utiwaji huu wa muhuri ni kwa wateule waliokombolewa kama wafalme na makuhani wa Mungu (Ufu. 5:9-10). Hivyo basi, Lawi kiusahihi kabisa anachukua eneo lake. Badala ya Manase kuungana na Efraim na kuunda Yusufu hapa tunaona kuwa baada ya Dani kuungana na Efraim kuunda Yusufu. Hivyi basi, Dani na Yusufu wakakamilika. Manase anakamilika kwa haki yake mwenyewe. Pia na ikumbukwe kuwa Manase, Reubeni na Gadi walichukua milki yao ya kimwili nje ya Israeli kabla ya kuvuka Yordani; pia walienda utumwani kabla Israeli haijawa sawia. Inaaminika kuwa matendo haya yanapelekea matendo ya siku za mwisho.
Utiwaji muhuri wa makuhani katika makabila haya pia hufuatia mfano wa makabila kumi na mawili kufanyiza kabila la kumi na tatu ambalo kwa mtazamo huu ni la Dani na sio la Lawi. Hili kisha huanzia utimilifu wa unabii mwingine unaokutikana katika kitabu cha Mwanzo 49:16.
Mwanzo 49:16-17 inasema: 16 Dani atahukumu watu wake, Kama moja ya makabila ya Israeli; Dani atakuwa nyoka barabarani, Bafe katikati ya njia, Aumaye visigino vya farasi, Hata apandaye ataanguka chali.
Unabii huu unaonyesha kwamba Dani atawahukumu watu wake kama moja ya makabila ya Israeli. Hii ilitokea wakati wa Samsoni. Hata hivyo, hukumu haijato kwa Dani kama kabila. Sheria ya Dani ilikuja kufanyika kuwa ni mfumo wa sheria katika sheria za kawaida miongoni mwa waongeaji wa Kiingereza lakini hii inaonekana kuwa na maana nyingine ambayo bado haijakamilika. Matumizi ya Dani katika mtindo ulio sawa na Lawi, umeoewa asili isiyo ya kawaida ya mgawanyo wa 144,000, kwa kweli unaweza kuwa mfumo uliojulikana hapa katika kitabu cha ufunuo 7. Pengine Yusufu hapa inajumlisha tu Efraimu na Dani au ama pengine Dani amewekwa kwa mujibu wa haki ya uzaliwa hadi kwenye hukumu kama inavyotangulia kutoka Yerusalemu chini ya Masihi ambayo inabidi kuamuliwa tena. Yote yanayoweza kusemwa katika Maandiko Matakatifu hayawezi kutanguka na Dani atawahukumu watu wake akiwa ni mojawapo wa makabila ya Israeli. Mfano mkuu uliopendwa sana ni wa kwamba Dani atahukumiwa na Masihi na wale mitume kumi na wawili watakaopangiwa kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli (Luka 22:30). Kwa hiyo, makabila yanaendelea mbele kama mfano wa kiroho wa taifa ambalo huhusisha Watu wa Mataifa wasio Waisraeli.
Tunachoweza kukiona kwa uwazi ni kwamba mfumo wa ile Thenashara na wa kumi na tatu huwakilisha utaratibu.wa kawaida wa ulimwengu kupitia makabila ya Israeli kama taifa na kama makuhani wa ulimwengu kama ilivyo pangiliwa .katika mbingu kama agano lisilovunjika kwa watu wa Mungu. Mfumo huu ulitangazwa tokea mwanzo. Ilitiwa muhuri na miezi mwandamo katika mwandamano wao. Bila ya Miandamo ya Mwezi hakuwezi kuwa naelimu au uelewa wa kina wa Mpango wa Wokovu. Mungu ametangaza mwisho tokea mwanzoni. Kwa hiyo, Mungu hufanyika kuwa ni Alfa na Omega yaani akiwa ni yote Mwanzo na Mwisho (Ufu.1:8; 21:6; 22:13). Ameweka umilele kwenye akili za mwanadamu bado [kwa njia kama ile] ili kwamba tusiweze kukuta kile Mungu alichokifanya tokea kuanza kwake hadi mwisho wake (Mhu. 3:11).
Mhubiri 3:11 inasema: 11 Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya moyo yao; ila kwa jinsi ya mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.
Kama Mungu aishivyo milele, hakutakiwi kuongeza wala kupunguza. Mungu ameifanya ili kwamba wanadamu wamuche na kumuishia. Kile kilichoko tayari, na kile ambacho hakijafanywa tayari, na Mungu hukitafuta kile kilicho achiliwa mbali (Mhu. 3:14-15).
Mhubiri 3:14-15 inasema: 14 Najua ya kwamba kila kazi aifanyayo Mungu itadumu milele; haiwezekani kuizidisha kitu, wala kuipunguza kitu; nayo Mungu ameifanya ili watu wamche Yeye. 15 Yale yaliyoko yamekuwako; na hayo yatakayokuwako yamekwisha kuwako; naye Mungu huyatafuta tena mambo ya kale yaliyopita.
Miandamo ya Mwezi Mpya hudumu katika umilele chini ya Masihi na wateule wake.
q