Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[273]
Riboni za Bluu
(Toleo La 1.0 19981212-19981212) Ipo Kwenye Odio
Biblia
imeamuru kwa ukumbusho wa Torati au Sheria za Mungu kwamba tuwe tunavaa vishada
au riboni za bluu zinazotakiwa zibandikwe kwenye sehemu iliyotariziwa au pindo
za nguo au mavazi tunayoyavaa.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1998 Thomas McElwain, John and Theresa Simons, Wade Cox)
(Tr.
2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Riboni za Bluu
Utangulizi
Maelezo yanayoagiza
kufuatia nia ya kuagiza sheria zimeandikwa kwenye aya zifuatazo:
Hesabu 15:38 Nena na wana wa Israeli, na kuwaagiza ya
kwamba wajifanyie vishada katika ncha za nguo zao, katika vizazi vyao, tena ya
kwamba watie katika kila kishada cha kila ncha nyuzi za rangi ya samawi
Hesabu 15:39 nacho
kitakuwa kwenu ni kishada, ili mpate kukiangalia, na kuyakumbuka maagizo yote
ya Bwana, na kuyafanya; tena kwamba msiende kutanga-tanga kuandama mioyo yenu
wenyewe, na macho yenu wenyewe, ambayo mlikuwa mkiyaandama kwa uasherati hapo
kwanza;
Kumbukumbu la
Toratui 22:12 Ujifanyizie vishada katika pembe nne za mavazi yako ya
kujifunika.
Jarida hili kwa
kweli ni myongeza ya lile la Amru Iliyokuu nay a Kwanza na limetokana na dhana
au fundisho lililo kwenye jarida la Amri ya Kwanza.
Ili kuzielewa aya
au maandiko haya kiusahihi, nia iliyokusudiwa kwenye uandishi asilia wa maneno
yaliyotumika kama lazima. Kwenye Mathayo 9:20; 14:36; 23:5; Marko 6:56; na Luka
8:44 neno hem au pindo la vazi limetajwa. Ni neno ambalo kwa Kiyunani
ni kraspedon (kwenye kamusi ya Strong’s Greek Dictionary (SGD)
2899) ambalo linatafsiriwa kwenye kamusi ya Thayer’s Greek Lexicon kwa kina
zaidi au sehemu muhimu ya kitu,
kikomo, upindo wa shketi; kama vile, kitu cha nyongeza au kilichojitokeza kinachoning’inia
chini kutoka ukingoni mwa joho au saa,
kilichotengenezwa kwa sufi iliyochambuliwa;; kirangirangi, kishungi au kishada.
Neno
lililoandikwa kwenye Zekaria 8:23 na 1Samweli 15:27 ni kanaph, ambalo kwenye
kamusi ya Strong Hebrew Dictionary (SHD) 3671 na ambalo linatafsiriwa
kama upindo au mwishoni; maalumu. (au ndege au jeshi) bawa, (la nguo au shuka
ya kitanda) kifuniko, (ya dunia) robo moja, (ya jengo)mnara mferu.
Watafsiri wa
Biblia ya KJV walitumia tafsiri au maelezo yafuatayo kuhusu neno hili kanaph: pindo,
kona, mwisho, yenye manyoya, roborobo zilizotawanyika sana, sketi, sehemu za
mbali sana, chenye mabawa, pamoja na matendo na kazi za ndege, kuruka, mmoja
kwa mwingine, na kitu chochote. Kanaph inatafsiriwa kwenye tafsiri ya Gesenius’
Hebrew Lexicon as 1) mbawa, 2) ukingoni, kikomo – (moja ya) vazi, pindo,
la vazi, sketi; upindo mzima wa vazi 1Samweli 24:5,12; Hesabu 15:38; Kumbukumbu
la Torati 22:12 – pia bila jina vazi. Zekaria 8:23, ‘upindo (wa) yeye aliye
Myahudi.’… b) pindo au kingo za dunia (kama ni wakazi wa dunia mara nyingi
hufananishwa na mweneo wa saa). Isaya 24:16 ‘kingo za dunia’. Hasahas kwenye
umoja katika Ayubu 37:3; 38:13, ‘misingi ya dunia’; na Zaburi 11:12; Ezekieli
7:2, ‘kona au pande nne,’ au ‘misingi yenyewe ya dunia.’
Neno pande nne
za dunia halionyeshi nwala kumaanisha pembe nne za kimwili za dunia, wala
haiwezi kuwa hivyo likionyesha kuwa linamaanisha vazi tulijualo la kimwili.
Neno pindo la
nguo lililotajwa kwenye Hesabu 15:38 kama et al. ni kwenye kamusi ya SHD
6734 (tsitsith), ambalo kwenye kamusi ya Strong inalielezea kama mimea
au flora au kitu kinachoonekana kama bawa, kama vile kshungi cha nywele zilizosokotwa,
shada. Kwenye tafsiri ya KJV watafsiri walichagua maneno mtarazo au msokoto.
Hii Gesenius anaitafsiri kuwa ni kama mtarazo, kitu kilichopangiliwa vizuri
kama ua au nyoya… (1) kishungi kilichojichomoza cha nywele (2) pindo za nguo, pembeni
mlimotariziwa, ambazo Israeli walikuwa wanaziweka kwenye pindo za nguo zao, Hesabu
15:38,39.
Neno mtarazo
lililotajwa kwenye Kumbukumbu la Torati 22:12 kwenye kamusi ya SHD 1434 (gedil)
ambalo kamusi ya Strong inalielezea kama kutoka 1431 (kwa maana ya
kuyumbisha); kukamia, kama vile shada au mambo ya shanga. Wafsiri
walioitafsiri KJV walichagua maneno ya mtarazo na upindo.
Neno ribband
lililo kwenye Hesabu 15:38 kwenye SHD 6616, limeandikwa pathil, ambalo kwenye
kamusi ya Strong inalielezea kama kutoka 6617; msikoto wa kitani. Walioitafsiri
biblia ya KJV walichagua maneno iliyounana, vikukuau bangili, kamba, mstari,
ribband au riboni, nyembamba, na waya.
Neno bluu,
ambalo kwenye SHD 8504, tekheleth, linaelezwa kama kiambishi. Kwenye 7827; misuli ya rangi ya samawi; kama vile, rangi (mchanganyiko)
zipatikanazo huko au fimbo iliyokolezwa rangi ndani yake. Walioitafsiri
bilbia ya KJV maranyingi waliitafsiri hii kuwa ni bluu. Gesenius anasema
kuwa ni samaki mwenye gamba, hasahasa
Yule anayeitwa (helix ianthina,
Linn.), kama vile vipande au sehemu ya misuli zinazopatikana kwenye bahari ya Mediterranean,
zikiwa na gamba la bluu, ambazo kwazo, rangi ya samawi na ya tangi ya papo au
zambarau hutengenezwa,… ambayo ni rangi ya samawi na ya zambarau, na nguo (samawi
zilizoshonwa kwa uzi mwembamba na sufi), zilizochovywa kwenye rangi ya ii
zambarau, Kutoka 26:4,31; Hesabu 4:6, sawa na; Ezekielieli 23:6; 27:7,24.
Neno tekheleth,
lililotafsiriwa kama bluu limetumika na kome za Kimediterranean ammbayo
imetokana na chanzo chake cha mchovyo asilia unaoonewa mashaka (hakuna mfano wa
Kibiblia), kwa nguo zilizochovywa kwenye rangi namna hiyo (Kutoka 25:4; 26:1,4;
nk.), na kwa rangi zenyewe (ni kwenye Esta 1:6 peke yake). Ingawa maandiko haya
yanauelezea mfano wa kuchovya zaidi ya rangi hasahasa iliyoonyeshwa kwenye
utajwaji ulio kwenye mahala popote ulipotajwa muunganiko wa bluu (tekheleth)
na zambarau (argaman), zote mbili na ambazo zinajumuisha tofauti ya hizi
rangi, maneno haya yanaweza kutumiwa kama maneno yaliyo kiutofauti ya rangi. Wimbo
Uliobora 7:5(6) inaonyesha kwamba rangi ya argaman/zambarau ni neno
linaloitaja rangi iliyo nyeusi sana kuliko ile ya tekheleth/bluu. Ukweli
wa kwamba maneno litumikalo kuelezea kuchovya au kikitia rangi kitu zaidi ya
maneno yanayoelezea rangi tofauti linalotumika haliashirii kuwa ni mchovyo
maalumu unaolengwa tu wa kitu uliokusudiwa, kwa vile hakuna maneno nyingine
maalumu ya rangi yaliyokutikana kwenye Biblia ya Kiebrania. Kwenye hesabu, neno
la Kiebrania linaeleweka sana kuashiria kuwa ni rangi ya bluu inayoweza kutofautishika
iliyotafsiriwa kutoka kwenye zambarau na ambayo inajulikana kwa kiwango cha juu
sana. Wayahudi wameyatafsiri maandiko haya kwa namna hiyo kama kuyakanusha
kabisa na kuvaa vishada vyeupe na kwenye shali za maombi yao, sehemu za chini
za mavazi yao.
Neno kasuuth
limetafsiriwa vesture mara moja na kujifunika vazi mara moja. Kwa namna nyingine
zote limetafsiriwa funika. Hii ni kwa mujibu unaolingana na shina la
vebu ambayo kwayo limechukuliwa, ambalo kimsingi linamaana ya kufunika.
Neno beghed ni la kawaida sana, na mara nyingine
sana limetafsiriwa kuwa vazi au nguo. Inatokana pia na vebu yenye maana
ya kufunika. Iko wazi kabisa kuwa ni ufunikaji wan je iliyotumika kwa
namna zote mbili, kama kujifunika wakati wa mchana na ni kama cha kujifunika
usiku. Imeelezewa kigrafiki kwenye hahari au hadithi ya Yusufu kwenye Mwanzo
39:12-18.
Ufunikaji huu wa
nje wa blanketi kwenye matukio mengi unaonekana kuwa ni umilikaji pekee wa thamani.
Kwa hiyo ni maranyingi imechukuliwa kama nadhiri, mara nyingi na kwamba ni neno
hilohilo ambalo linafanana sana na nadhiri, kama kwenye Ayubu 22:6, Mithali
20:16; 27:13; Ezekieli 18:7,16; na Amosi 2:8. Ni nadhiri ya kawaida
iliyojulikana sana kuandikwa kwenye Biblia.
Kutoka 22:26 Ikiwa wewe kwa njia yo yote wapokea nguo
ya jirani yako rehani, lazima utamrudishia mbele ya jua kuchwa; maana
hiyo nguo ni kifuniko chake, hiyo peke yake ni nguo ya ngozi yake; je! Atalalia
nini? Itakuwa, hapo atakaponililia mimi, nitasikia; kwa kuwa mimi ni mwenye
rehema.
Ni hii hii ndiyo
iliyorudiwa kwenye Kumbukumbu la Torati 24:10-17, hususan aya ya 13: apate kulala na mavazi yake, na kukubarikia.
Hili ni neno la kawaida lililotumika kwenye Biblia kwa jinsi tunavyoweza
kudhania kuwa ni kama blanketi la kujifunikia. Idadi ya maneno yametumika kwa
ushinaji au vazi lililoshonwa la nguo.
Mahudhui na
kusudi la amri hii
Kuna utekelezaji wa
aina mbili wa amri. Wa kwanza ni kwamba amri hii inahusiana na utengenezaji na
kulibuni neno kasuuth na beghed kwa jinsi kwamba mtande na sufi
hazishikamani au kufumika, lakini ikaachwa kama mtarazo kwa pande zote nne za
kona ya nguo, ambayo kwayo likuwa salama kwa maana ya vazi jeupe au kitambaa
cha nguo kinachozunguka pande nne zote kwa namna ambavyo kitambaa cha bluu kinabakia
kuonekana wazi na dhahiri linapotumika. Iwe kwa urefu wa mtarazo wala upana wa
kitambaa cha kushonea cha bluu iliyokolea, ni pale vinapoonekana wazi tu vikiwa
kama ni ukumbusho wa kumkumbusha mtu anayevitumia. Amri hii ni kitu cha
kibinafsi kama tulivyoona kutoka kwenye ukweli wa kwamba hakuna adhabu
iliyoelezwa na kwa hiyo sio jambo lililo kwenye sheria za kimahakama.
Lengo la amri
linatofautiana. Kwanza kabisa, mtarazo na kishada cha bluu vinatakiwa vionekane
na kwa hiyo view wazi na dhahiri lakini sheria hii imeelekeza hivyo au ni kwa
kila mtu binanfsi yake. Kusudi na kazi yake hii ni kukumbushia amri zote
zilizotolewa na Bwana. Ukumbushio huu unakusudia kuweka hali ya utiifu kwa
Mungu zaidi ya kuwa ni kuyatii mapenzi au matamanio ya kila mtu binafsi yake au
kujua na kuyapambanua yaliyomema na mabaya.
Utekelezaji wa
amri
Suala la
kutekeleza linageukia kwenye ama amri au sio amri zinazoonekana kufanana, na
kama ni hivyo, jinsi inavyotakiwa kutekelezwa kwenye mazingira ya kisasa. Ushauri
kwenye mambo haya mawili utaamuliwa kwa kudhania tena maya ya pili. Ya kwanza
ni kwamba agano na Israeli linawafunga uzao wote wa waliokuwepo hai kwenye
Mlima wa Sinai wakati Torati ilipotolewa na sio wana wa uzao wa Yuda peke yao. Fikra
ya kabla hapo nyumana ya Pili ni kwamba sheria
ilipaswa itafsiriwe kama ilivyo kama kiuandishi iwezekanavyo.
Neno lisemalo
"katika vizazi vyao vyote" linasema wazi wakati mkubwa unaowezekana
wa kipindi cha uwepo wa amri hii. Zaidi sana ni kwamba Injili zinazoutaja mfano
wa Kristo inauhusiano mkubwa na amri hizi. Mathayo 9:20 "Na tazama,
mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja
kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake." Mathayo 14:36 " nao wakamsihi waguse hata pindo la vazi lake tu;
na wote waliogusa wakaponywa kabisa.."
Lengo la amri hii pia lina umhimu wake muhimu. Kwa hiyo, ni ukubusho unaokumbushia kuzishika amri kuwa ni bado inatumika hata leo kama wakati amri hizo zilipokuwa zimetolewa. Zaidi sana, watu bado wanahimizwa kubakia kwenye vigezo vya kupambanua yaliyomema na mabaya kwa kulinganisha na sheria na maagizo matakatifu. Kwahiyo, umuhimu wa amri unabakia kuwa muhimu. Amri hii inabakia na ni kama amri iliyoko kwenye sheria za biblia na haziwezi kupunguzwa maana na umuhimu wake au kupunguzwa uzito wa utekelezaji wake. Huu ni mtazamo pia wa R. J. Rushdoony kwenye kitabu chake cha The Institutes of Biblical Law [Taasisi za Sheria za Kibiblia]. Anasema Vishada vya Bluu vinavyotakiwa haviwezi kutafsiriwa kiroho kabisa ingawaje kimakosa kabisa anaendelea kuamini kwamba ilikuwa imeonekana kuwa ni muhimu sana kwa ishara mpya za agano kama lilivyokuwa lile la Sabato na tohara. Hata hivyo, anapinga mtazamo na mawazo ya Calvin na anasema kuwa ni sheria za Calvin mars. (kwenye machapisho ya Presbyterian and Reformed Publishing Company, 1973, pp. 22-23)
Jambo
linalofuatia ni utekelezaji wa siku hizi. Ushikaji wa moja kwa moja wa sheria unakinzana
na matumizi ya shada za bluu katikati ya mavazi nap indo kwenye ile ijulikanayo
kama beghed na kasuuth, kwa hiyo, namna wanayofanya wafumaji nguo
wa kufunika zote mbili, yaani mablanketi ya kulalia usiku na kwa kujifunika
mchana. Matumizi mengine yote yanaweza kupingwa kabisa kwa hiyo na kuyaona kuwa
yanakwenda nje na maagizo yaliyotolewa kufanywa kwenye matuzi halisi yaliyoagizwa
na yanahatarisha ugunduzi wa sheria au kanuni mbadala.
Pindo na vishada
vya bluu vimetajwa tu kwa jina la beghed na kasuuth, wakati
kwamba kuna mishono mingine mingi ya nguo ilyotajwa kwenye Biblia. Amri
iliyowazi ni ile ya kuweka shada za bluu kwenye pindo na kona za nguo
wanazoziita beghed na kasuuth. Dokezo lake kwa hiyo inalazimu kwamba shada za
bluu hazipaswi kuwekwa kwenye maeneo mengine ya vazi. Kwa kuwa matumizi ya hizi
beghed na kasuuth yamezuiwa kabisa kwenye matumizi ya siku hizi, utekelezaji wa
moja kwa moja wa amri yanaonekana ni muhimu na muafaka sana kabisa.
Ushauri au muono
mmoja ni kwamba hii shali iliyo kwenye muonekano wa beghed/kasuuth ilitakiwa na
ilitumika kama blanketi la kujifunikia na ni kama mtandio/shali wa mabegani (au
joho lililo kama kawa au hutwa poncho), kwenye matukio mengine yoyote stahiki,
yanayotimiliza amri, na kwamba shada za bluu na pindo zilizoshonewa au kuambatanishwa
kwenye vazi linguine lolote halitimilizi amri. Mtazamo kama huo unahitaji
kwamba sheria haina ulazima wa kuendelea na sio haiendelei kutumiwa kwenye
mavazi. Nguo kama hozi kwa hiyo zingeweza kuonekana kama mtandio, moinganiko
wake wote kamili (kutoka kwenye mafsiri ya kijinga ya kimwili ya neno hilo) na
isiyoshonwa, kufumwa ili kwamba pindo na sufi inayofanya mitandio kwenye sehemu
zake zote nne. Shada ya bluu au riboni kwa hiyo inapaswa ishonewe katikati mitarazo
na nguoni. Kutokana na maonyo yaliyotolewa kwenye Kumbukumbu la Torati 22:5, kunapaswa
kuwa na tofauti ya wazi kati ya mtandio autumiao mwanaume kimavazi na ule wa
mwanamke. Kwa upande mwingine, ni kusema asipo kushonewa, tofauti kati ya
blanketi la mwanaume na mwanamke ni vigumu kulifanya lionekane pasipo uchambuzi
wa kisheria au kanuni. Kwahiyo, kutokana na agizo linguine la Kumbukumbu la Torati
22:5 linapaswa kutekelezwa na nguo zilizoshonwa peke yake na sio kwa mablanketi
ya kujifunikia.
Maandiko yaliyo
kwenye Kumbukumbu la Torati na Hesabu ndipo yanaweza kuchukuliwa kuithibitisha
tofauti na riboni zenye utepe wa bluu zikiwa ni ufungaji wa kibinafsi kwenye pindo
ambao kwa karne ningi na zisizohesabika zimekuwa zinashonewa kwenye mavazi. Kwa
hiyo hizi riboni zimetiwa ndani yao kama ukumbusho kwenye uthibitisho wa sheria.
Kwa kuwa sheria
hii haihusiani na nyakati, mahali, au harakati husika, basi inabakia kuwa ni
utekelezaji wa mtu binafsi. Zaidi sana, hakuna adhabu iliyoagizwa kupewa mtu
anayeivunja au kuipuuzia amri hii. Ikiwa kama kitu cha kumkumbusha mtu binafsi,
hata hivyo, kwa hakika inaelezea shauku ya kukumbuka, upendo, na utimilifu wa
amri za Mungu.
q