Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[139]
Makusanyiko [139]
(Toleo 2.0 19940908- 19990904)
Sadaka hii ambyo inayofanyika mwanzoni mwa Sikukuu ya Vibanda imewekwa kwa mujibu wa sheria na inamwandamano wake wa mambo muhimu ambayo Mkristo anatakiwa ajue. Utaratibu wa sadaka kuu tatu pia umewekwa. Jarida hili linaelezea utaratibu unaohusika na Sikukuu ya Makusanyiko au kwa jina lingine inajulikana kama Sikukuu ya Mavuno, hesabu na kodi ya siku ya Upatanisho, mwezi mpevu, Pentekoste, Baragumu, hukumu ya Shetani, kazi ya waliofufuliwa, mafunzo katika jeshi la Mungu.
Christian Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Copyright © 1994, 1995,
1996, 1998, 1999 Wade Cox)
(Tr. 2005)
Masomo
haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kutufa maneno. Jina la mchapishaji na anuami
yake pamoja na hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya maelezo na kilugha
lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia ynapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti
yetu ya:
http://www.logon.org
au http://www.ccg.org
Mavuno au Makusanyiko
Kuna majira makuu matatu ya kuadhimisha sikukuu. wa tatu wa kujisongeza mbele za Bwana, wakati ujulikanao kama Sikukuu ya Vibanda au Sikukuu ya Sikukuu ya Vibanda vya nyasi (Kut. 23:14-16; 34:22-23; Law.23:33-44).
Walawi 23:33-44 inasema: 33 kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia, 34 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba ni sikukuu ya vibanda muda wa siku saba kwa BWANA. 35 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu; msifanye kazi yoyote ya utumishi. 36 Mtamsongezea BWANA sadaka kwa moto siku saba; siku ya nane kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; nanyi mtamsongezea BWANA sadaka kwa moto; ni mkutano wa makini huu; msifanye kazi yoyote ya utumishi. 37 Sikukuu za BWANA ni hizi, ambazo mtazipigia mbiu ya kuwa ni makutaniko matakatifu, ili amsongezee BWANA sadaka kwa moto, sadaka ya kuteketezwa, na sadaka ya unga, na dhabihu, na sadaka ya kinywaji, kila sadaka kwa siku yake; 38 zaidi ya hizo Sabato za BWANA, na zaidi ya matoleo yenu, na zaidi ya hizo nadhiri zenu zote, na zaidi ya sadaka zenu za hiari, ambazo mwampa BWANA. 39Lakini siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, hapo mtakapokuwa mmekwisha kuyachuma mavuno ya nchi, mtaweka sikukuu ya BWANA muda wa siku saba; siku ya kwanza kutakuwa na kustarehe kabisa, na siku ya nane kutakuwa na kustarehe kabisa. 40 Nanyi siku ya kwanza mtajipatia matunda ya miti mizuri, na makuti ya mitende, na matawi ya miti minene, na mierebi ya vijitoni; nanyi mtafurahi mbele za BWANA, Mungu wemu, muda wa siku saba. 41 Nanyi mtaishika kuwa sikukuu kwa BWANA muda wa siku saba katika mwaka; ni amri ya milele katika vizazi vyenu; mtaishika katika mwezi wa saba. 42 Mtaketi katika vibanda muda wa siku saba; wazalia wote wa Israeli wataketi katika vibanda; 43 ili vizazi vyenu vipate kujua ya kuwa niliwaketisha wana wa Israeli katika vibanda, hapo nilipowaleta kutoka nchi ya Misri; mimi ndimi BWANA, Mungu wenu. 44 Naye Musa akawaambia wana wa Israeli hizo sikukuu za BWANA.
Inapaswa ijulikane hapa kuwa Israeli wameamriwa kuishi kwenye vibanda vya nyasi wakati wote wa sukukuu hii. Mwanzoni kabisa hii ilikuwa na matawi yake, lakini baadae ilifanyiwa mabadiliko na kutumiwa mahema, huenda hii ilifanyika kwa kuzingatia sababu za kimazingira na sababu za kiusalama. Hosea katika (Hos. 12:9), anaelezea kwamba Israeli waliishi kwenye mahema katika kipindi hiki na waliamriwa waishi kwenye mahema au maskani ya vibanda kama walivyokuwa wanafanya wawapo kwenye siku za sikukuu. Ukaaji wa kwenye vibanda vya nyasi ulilazimishwa wakati wa kipindi cha marejesho kilichofanywa na Nehemia (Neh. 8:14-17).
Wazo hasa lililopelekea wao kukaa kwenye vibanda vya nyasi lilikuwa ni kulazimisha tena uhuru wa Israeli katika kumuabudu na kumuishia Mungu, wakati walipokuwa wanasafiri jangwani. Kwa wao, tendo la marejesho liliwakumbusha msafara mwingine wa kutoka utumwani ambao ulikuwa ni sawa na ule wa Israeli waliokuwa wanatoka Misri. Wakati huu utakuwa kama alivyoonyeshwa nabii Isaya katika sura ya 66:18-24. Msafara huu wa kutoka utumwani utakuwa ni mkuu sana kuliko kuliko ule msafara wa kwanza na utachukua pahala pa mfasafara wa kwanza. Hii ndiyo maana vibanda vya nyasi vinatumiwa wakati wa Sikukuu ya Vibanda au Maskani. Sikukuu hii kwa sasa inawakilisha ile awamu ya mwisho kufanyika chini ya Masihi kwa ajili ya utawala wa Milenia ambao kwayo, sheria zote zitatokea Yerusalemu. Ni katika siku ijulikanayo kama Siku Iliyokuu ya Mwisho ndiyo vibanda hivi vya nyasi havi hitajiki tena kabisa kwa mujibu wa sheria za Mungu. Hii ni kwa sababu Siku Iliyo kuu ya Mwisho hutoa mfano wa marejesho ya mwisho na upatanisho kati yetu na Mungu. Tendo la kukaa kwenye vibanda ni la muhimu na ni sharti la sikukuu hii.
Sura yote ya Walawi 23 inahusika na kufafanua jinsi ambavyo kila sikuu itakavyoendesha taratibu zake, hadi kufikia sikukuu ya vibanda na ile ya Siku Iliyokuu ya Mwisho, ikifafanua utaratibu wa mavuno. Siku ya Makusanyo ilikuwa ni ya mavuno ya mwisho. Tutajionea, katika mafuatano haya, na kuelewa ni kwa nini kulikuwa na makusanyo ya sadaka yaliamriwa kufanyika katika kila mwaka. Kwa kweli, ni makosa kufanyiza matoleo mengine yoyote na kwa wakati mwingine wowote nje na haya makusanyo matakatifu ya sadaka zitolewazo mara tatu tu kwa mwaka.
Hela zinazotolewa kama sadaka maalumu inayotumika kujua idadi ya waliohudhuria itolewayo Siku ya Upatanisho ni kodi. Angalia jarida linalosema: Upatanisho [138] ambalo linashughulika kufafanua kuhusu utaratibu mzima wa kuhesabu na kodi hii inayolipwa na kwa nini inachukuliwa, na inaelezea kuhusu ni kwa nini ni makosa kutoza watu sadaka kwa siku nyingine yeyote zaidi katika Siku ya Upatanisho. Hii kwakweli ni matukano ya dhahiri shahiri kumfanyia Yesu Kristo na ni sawa na kuitoa kasoro dhabihu ambayo Yesu Kristo aliitoa. Kristo ataianzisha tena kodi ya Hekalu wakati atakaposimama juu ya mlima wa Sayuni.
Hivyo basi kitendo cha kuweka vipindi vya kutoa matoleo ya sadaka mara saba kwa mwaka yaani kwa kila makutaniko ya kila Siku Takatifu, ni tendo baya kuliko, au hata ile ya kila juma ni kufanya mambo yaliyo kinyume sana na Maandiko Matakatifu. Hii ni kinyume kabisa na maelekezo ya Yesu Kristo akiwa kama ni Malaika wa Agano.
Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba ni siku ambayo mwezi unakuwa mkamilifu. Mara nyingi sikukuu hizi kwa mujibu wa kalenda za Kiyahudi hufanyika wakati mwezi mwandamo ukiwa mpevu au zikiwa zimesalia siku moja au mbili kufikia kuwa mpevu kamili. Sheria iliyohusu jinsi ya kufanyia maamuzi siku gani kuwepo na sikukuu ni dhahiri kabisa kulitegemea Miandamo ya Mwezi Mpya, na wala haikutegemea mfumo wa Kiyahudi wa kuhesabu mwelekeo wa mwezi wa Tishri. Mambo ya Walawi 23:33-35 inasema:
Mambo ya Walawi 23:33-35: 33 kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia, 34 Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba ni sikukuu ya vibanda muda wa siku saba kwa BWANA. 35 Siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu; msifanye kazi yoyote ya utumishi.
Sikukuu hizi ni mfano kwetu kuwa tunatoka katika mfumo wa kidunia. Kristo ametukomboa tutoke kwenye utumwa kama ule wa Misri kama walivyofanya Israeli. Ile ilikuwa ni ishara ya kimwili ya ukombozi ujao. Alitutoa na kutukomboa mara moja tu, na anaenda kututoa nje tena, kiroho na kimwili. Aliyekuwa ni limbuko la kwanza ni Yesu Kristo. Mganda wa Kutikiswa, hufanyika wakati wa Pasaka, ulikuwa unamwakilisha Yesu Kristo aliye ni limbuko la kwanza la malimbuko.
Sikukuu ya Pentekoste ni mavuno YETU – na sio sikukuu ya Vibanda. Mavuno yetu yalikuwa ni Pentekoste kama inavyozidi kuendelea mbele. Sababu iliyopelekea kuwa katika Pentekoste ni kwa sababu watu wetu wote, wateule walivunwa kuanzia mwaka 30 BK; kuanzia kifo cha Yesu Kristo njia zote hadi kufikia siku za leo. katika Pentekoste ya mwaka 30 BK tulipewa Roho Mtakatifu. Haya yalikuwa ni matokeo kwa ajili ya malimbuko ya wito wetu na ya imani yetu. Wale waliolala mavumbuni walikuwa ndio haya malimbuko. Kwa hiyo, si jambo la busara kwa sisi kuiona Sikukuu ya Vibanda au ya Vijumba vya Nyasi kuwa inawakilisha mavuno yetu. Tumekwisha kuvunwa tayari tangia siku ya Pentekoste. Tutaungana na Kristo wakati atakapo kuja. Lakini bado kuna kazi kubwa inatakiwa kufanyika nasi tutachukua mahala pa mavuno ya wakati huu.
Sababu hasa ya msingi kwa nini hatukusanyi sadaka siku ya sikukuu ya Baragumu au Upatanisho ni kwamba hainachochote kinachohusiana kufanyika na sisi. Matendo yote yaliyoko kwenye sikukuu ya Baragumu au Upatanisho ni yale yaliyoko katika neema iokoayo ya Yesu Kristo kwa kufuatana na maelekezo ya Mungu. Hatuna lolote la kufanya kwa ajili yake. Amekuja kutuokoa. Kwa hiyo, hatuna chochote cha kumtolea zaidi ya kule kujitoa kwetu sisi wenyewe. Hii ndio sababu sikukuu ya Baragumu haikuorodheshwa kama inatakiwa kutolewa matoleo na ndio sababu pia haifanyiki pia kwenye siku ya Upatanisho. Kwa kweli, izingatiwe kuwa imekatazwa kabisa kuchukua matoleo siku ya Upatanisho wakati mtu mwingine anapotoa zaidi ya mwingine. Wateule wanabidi kuelewa kwamba katika makanisa mengine na waliliona hilo kama dhana na waliuliza: je, ni kwa nini tunafanya hivi, watati kwamba imekatazwa kiwaziwazi kabisa? Yaani kwamba hakuna mtu anayeruhusiwa kutoa matoleo zaidi au chini ya kile kiwango kwa kulinganisha na mwingine. Ni kodi maalumu ya namna yake. Makosa yalikuja kujiingiza hatimaye miongoni mwa wateule kwasababu walikuwa hawaifuati kweli. Badala yake, walikuwa wanafuata maneno ya wanadamu.
Wazo kuu kuhusiana na mavuno haya, ni kama ilivyo kwa siku ya Makutaniko, ni kuanzisha kwa zama mfumo wa kimilenia ambao haki inakaa ndani yake. Kutapewa uweza wa kuitawala hii sayari. Kisha tutaweza kutoa mavuno ambayo pengine yangeweza kutolewa na Yuda ambao wangeweza kuchukua pahala pake mapema. Dhana kama hii hutatiza kwa sababu vitu vyote hufanyika kwa kulingana na mtazamo uliotathminiwa mapema sana wa kisayansi na kwa kutuata maongozi ya Mungu. Watu wanaitwa kwa wakati maalumu na kwa ajili ya kufanya kazi maalumu. Nani anayeweza kuhoji kuwa ni kwa nini kuna idadi maalumu ya wateule katika kila wakati Fulani? Nani anaweza kuhoji kuwa kunakuwa na watu fulani maalumu kwenye maeneo maalumu wanaoelewa na kufanya, na kwa nini wengi sana hawaelewi? Kwa nini idadi yao ni ndogo sana? Ni nani ajuaye kile ambacho Mungu anafanya?
Tunachotakiwa kufanya ni kwamba sisi tufanye tu ile kazi yetu na tuzifuate hizi sheria kwa uaminifu wetu wote na kuelewa maana yake ya kiroho. Mungu humuita kila mmoja wetu kwa wakati muafaka ili afanye lililo la wajibu wake kwa ajili ya mpango ulioandaliwa wa wokovu. Kwa ajili hii ndio maana Kristo aliongea kwa njia ya mifano na ndio maana siri za Mungu zimefunuliwa kwa kipimo na kwa wachache (tazama jarida lisemalo: Siri za Mungu [131]. Wayahudi hufuata sheria, kwa hiyo wanazisema na kuzikariri, lakini hawaelewi maana zake za kiroho. Na ndio maana wanazichanganya na mapokeo yao.
Sisi sasa tunafahamu ni kwa nini kwamba
sadaka hii inatakiwa itolewe kwa jioni ya kwanza ya Sikukuu ya Vibanda.
Inawakilisha mavuno makuu ya tatu. Katika kitabu cha Kutoka 23:17-19 inasema
kama ifuatavyo:
Kutoka 23:17-19 inasema:17 Mara tatu katika mwaka watu waume wako wote watahudhuria mbele za BWANA MUNGU. 18 Usisongeze damu ya dhabihu zangu pamoja na mkate usiotiwa chachu, wala mafuta ya sikukuu yangu usiyaache kusalia hata asubuhi. 19Ya kwanza ya malimbuko ya nchi utayaleta na kuyatia ndani ya nyumba ya BWANA, Mungu wako. Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
Hivyo ni kwa mujibu wa Biblia tafsiri ya Union Version nukuu zote zilizomo katika tafsiri hii ya Kiswahili, ambayo kwa lile jarida la Kiingereza imetolewa katika Biblia ya Tafsiri ya Mfalme Yakobo (KJV) na RSV.
Tafsiri hizi zote zimenukuu aya hii kwa pale inaposema Usimtokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake iliyoko katika aya ya 19 na haipo pale kwa bahati mbaya tu na kwamba haina sababu. Mlo uliotolewa rejea zake hapa ulitokana na desturi ya kidini zilizokuwepo wakati ule upande wa mashariki iliyokuwa inatumiwa kwa namna ya kisiri za Wababelonia. Wala haina lolote linaloagiza kuhusiana na kuchanganya kati ya nyama na maziwa. Dhabihu hizi pia zilikuwa zinatokoswa. Kwahiyo tendo la kumtokosa mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake kwa wakati huu wa kutoa sadaka ungekuwa na maana na kwa kutoa sadaka kwenye tafrija za risi na kuwa na maana sawa na ibada ya sanamu. Kwa hiyo ilikatazwa, na inajitokeza kwenye aya hii ikimaanisha kuunga mkono wazo hili.
Pia kuna dhana nyingine katika aya hii.
Katika moja wapo ya tafsiri inasema dhabihu na nyingine inasema sikukuu
(Tafsiri ya Mfalme Yakobo yaani KJV, inasema dhabihu; wakati ile ya
RSV inasema sikukuu). Biblia ijulikanayo kama Interlinear Bible
inashughulika na jambo hili. Hii pia inasema dhabihu.
Inasema hivi: Usisongeze damu ya dhabihu zangu pamoja na mkate usiotiwa
chachu, wala mafuta ya sikukuu yangu usiyaache kusalia hata asubuhi.
Wazo hili linafungamanishwa kuonyesha nini ni sikukuu na nini ni dhabihu.Neno lililotumika kuelezea sikukuu katika kamusi iitwayo Strong’s Hebrew Dictionary (SHD 2282) inasema khawg yenye maana ama ya sikukuu au madhabuha au muanga. Kundi la vijana lipo katika dhabihu, kwa mujibu wa Biblia ya KJV. Maandiko yajulikanayo kama ya Masoretic kwa mujibu wa tafsiri ya Interlinear Bible, limeandika neon hili sawa na ilivyoandikwa katika kamusi ya Strong’s Concordance. Nia kwa hiyo haipo dhahiri. Kitabu cha fafanuzi kiitwacho Sancino kinaelezea kama maarifa. Maandiko haya yanaelekezea kote kuwili kwenye mafuta ya kondoo wa Pasaka (Rashbam) na kwa sadaka ya watu wasafirio au wageni wanaohudhuria sikukuu kwa mujibu wa mwanazuoni aitwae (Abraham ibn Ezra). Rash anashikilia kuamini kuwa dhabihu isibakie kwa usiku mzima view mbali na madhabahu kwa mujibu wa (Sancino).
Ukielewa maandiko haya kunakufanya uelewe ni wakati gani Makusanyiko yafanyike na pia kuelewa madhumuni yake. Maana yake yako wazi kwa mujibu wa maandiko. Inatakiwa makusanyiko yafanyike katika jioni ya siku ya kwanza na isisimame hadi asubuhi. Kuna maana ya sehemu zote mbili yaani ya kimwili na kiroho kwa jambo hili.
Ni katika sikukuu ambapo sehemu ya kwanza ya malimbuko huletwa ndani. Hivyo ni lazima kuwepo na maandalizi ambayo yamefanywa mapema kabla ya sikukuu. Ni lazima tuweze kuzishika sikukuu ili kwamba kusanyiko lifanyike kwa wakati huu. Panatakiwa pawe ni mahala pa kutoa mfano wa mavuno, na kitu fulani chaweza kuletwa ili kuanzisha mfumo wa wakati wa milenia.
Vilevile, dhana iliyoko ni kwamba kwa kipindi hiki chote cha sikukuu cha siku nane. Ikiwa ulikileta ndani baadae kungekuwa na kazi ya uongozi isio ya lazima kwa siku takatifu. Ingewezekana kama ungefanya kwa usahihi chini ya mazingira ya kimavuno. Sasa wakati tunapoitambulisha tena sheria hii, wakati Bwana wetu ajapo na tunaweka utaratibu huu, hatutakuwa tunachukua fedha kwenye bank na kuziweka katika kikapu. Tutakuwa tunaleta magunia ya nafaka na wanyama na tutakuwa tunaleta malimbuko kama familia kwenye sikukuu zilizo amriwa na tutazileta ndani na kuzitoa kwa makuhani, ambao ni Walawi wapya.
Baadhi yetu tutakuwa ni wafalmw wa kikweli wa kimwili, makuhani, zaidi sana vijana tunao ujumbe mkuu sana na baraka ndani yake. Mara nyingi sana tumekuwa tukisikia habari kuhusu jinsi kanisa litakaponyakuliwa mbali kwenda mahali paitwapo Petra au mahali pengine popote, nasi sote tutakuwa ni viumbe wa jinsi kiroho. Watoto wagodo wataachwa wakifikiri; je, kwa sisi itakuwaje? Mimi bado sija batizwa, nami sio mzee kiasi cha kutosha. Vijana mara chache wameambiwa kwamba wanaenda kuwa wafalme na makuhani. Watoto watakuwa viongozi katika ulimwengu huu wa kimwili, katika mavuno makuu, Makutaniko makuu. Watakuwa ni sehemu katika korban ya Makutaniko.
Utaratibu wote mzima utafanyika mwanzoni mwa Milenia kwahiyo kilamtu yuko pale na mavuno ni mengi. Sababu ya sisi kuweza kufanya hili katika usiku wa kwanza ni kwamba makuhani wote au viongozi waweze kujipanga sawa. Inatolewa wakati wa jioni ili kwamba watu na vikundi vya kikuhani waweze kula. Ni suala tu la ugawaji. Hatutakuwa na mtunza fedha atakaekwenda kwenye bank katika siku inayofuata, na kuchukua fedha zilizoingizwa mwaka uliopita. Hatutachukua mavuno ya nafaka za mwaka uliopita isipokuwa ni kwa miaka ya Sabato. Makusanyo vilevile ni mavuno ya kimwili na tunatakiwa kuyaandaa. Tunatakiwa kufikiria njia ile kwasababu tunatakiwa kuhakikisha kuwa watu wanaohusika wamejiweka sawa na tunajua kwamba haya yanatokea. Hii inafanywa kwasababu kama mataifa hawata adhimisha sikukuu hizi, sisi kama wateule wa kiroho tunaenda kujiweka tayari kuona kuwa hakutakuwa na mvua kwa msimu huo wote. Hii ni ahadi kutokana na unabii ulivyotabiriwa na Zekaria 14:16-19.
Kama mataifa hawatatuma wawakilishi wao kwenda Yerusalemu ili kushika sikukuu, tutakwenda kukosa chanzo chenye kuleta mvua katika mataifa hayo. Baadhi yetu tutakuwa waangalizi wa kusimamia na kuongoza mataifa. Tunakwenda kufanya kazi ya namna ileile ambayo hata mapepo wasingeweza kuifanya. Tunakwenda kuhakikisha kuwa mambo haya yote yanatokea. Tutakuwa tunashika dau katika utaratibu wa shughuli kwa kipindi cha miaka elfu na tutakuwa tunahukumiwa kulingana na matendo yetu kwa jinsi ile tulivyofanya katika uzuri au ubaya wake. Tutashughulikiwa na Yesu Kristo kwa vizuri kiasi gani tunavyofanya. Tutawajibika mbele za Masihi lakini zaidi sana, mapepo na mashetani wote watahukumiwa kwa ajili ya matendo yetu mema tunayoyafanya na kwa kazi yetu njema.
Tutaweka kiwango kulingana na vile watakavyopimwa; kama vile ambavy Jesu Kristo alivyoweka viwango kinyume na vile Shetani alivyopimwa katika vita vya jangwani wakati walipo simama pale jangwani. Kwa kile ambacho Kristo alikifanya katika maisha yake, katika huduma yake yatosha kabisa kusema kuwa aliweka kiwango kinachotakiwa. Ndio maana alisema kuwa Shetani amekwisha kuhukumiwa. Shetani alikuwa ndiye peke aliyekwisha kuhukumiwa. Mapepo wengine weliobakia wanahukumiwa kwa sababu ya ushiriki wao katika matendo ya ibilisi: kama sisi tulivyo wafuasi wa mema. Sisi ni maadui wa mapepo nao wanahukumiwa kwa namna ileilemoja. Shetani alihukumiwa kwa ajili ya kushindwa kwake kufikia kiwango chake cha kufanya mashitaka juu ya Yesu Kristo. Mapepo wanahukumiwa kwa kukosakwao kwao kuwa na kitu cha kutushitaki sisi. Kama tukishindwa kuzishika amri za Mungu basi hatustahili kuwa waamuzi katika mfumo utakaotumika kipindi cha Milenia.
1Yohana 2:1-5 inasema: Kila mtu aaminiye ya kwamba Yesu ni Kristo amezaliwa na Mungu. Na kila mtu ampendaye mwenye kuzaa, ampenda hata yeye aliyezaliwa na yeye. 2 Katika hili twajua ya kwamba twawapenda watoto wa Mungu, tumpendapo Mungu, na kuzishika amri zake; wala amri zake si nzito. 4 Kwa maana kila kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. 5 Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu?
Kama tutakuwa hatuzishiki sheria za Mungu na kudai kuwa tunamjua Mungu tutakuwa tunasema uwongo. Na uzima wa Milele ni huu yaani kumjua Mungu wa pekee na wakweli na Yesu Kristo aliyemtuma (Yoh. 17:3). Kama tukisema tunamjua Mungu na huku tukiwa hatuzishiki sheria zake basi tutakuwa ni waongo.
Ukusanyaji wa mavuno kunawakilisha kazi za mikono yetu. Hii ndiyo maana tunatakiwa kuelekeza hisia zetu juu yake. Katika jioni ya siku ya Makusanyiko tunatakiwa kuelekeza hisia zetu kwenye mavuno haya. Hakuna mavuno katika Siku ya Mwisho iliyo Kuu kwa sababu kazi yetu imkwisha fanyika kuanzia siku ya Makusanyiko hadi siku ijulikanayo kama Siku ya Mwisho iliyo Kuu. Siku ya Mwisho iliyokuu Kuu ni mfano wa ufufuo wa wafu. Siku ya ufufuo wa wafu na hukumu vimeelezewa katika majarida mengine. Hakuna mavuno yanayoanzia kipindi cha hukumu. Hukumu ni hitimisho la mlolongo wote. Kwa hiyo weak na kupangilia. Hii ni utendaji wa mavuno na ina maana na ishara zake za kiroho. Hii ndiyo maana ya kuweka mara tatu kwa mwaka. Wazo hili limesisitizwa kwa sababu hatuwezi kukua hadi pale tumefanya mambo kwa njia ile ambayo Biblia inavyoagiza ifanywe. Hatuwezi kufikia kwenye hatua ya pili kiroho na kimwili.
Kwa bila kujali vile Biblia kuna makanisa mengine yameweka sheria za kimaongozi ya kiutawala na kusema kuwa watakuwa na makusanyo ya sadaka mara saba kwa sababu yana tia fedha nyingi mfukoni. Lakini hii haiendani kwa kutegemeana na maamuzi ya viongozi. Hii ni amri iliyotolewa na Mungu kwetu kupitia Yesu Kristo. Sisi hatuwezi kufanya maamuzi kwa kufuatana na maamuzi ya viongozi kuhusiana na mambo yanayohusu sheria. Sio nukta moja au ndogo ya sheria itakayopitishwa hadi pale zote zitakapo kamilishwa. Tunachotakiwa kufanya ni kuzitii kikamilifu. Ni kwa njia ya utii ti ndipo tunaweka mambo yote katika mahala patakapo tufikiliza tukue katika maarifa na ufahamu katika nia zetu na katika nia za wapendwa wenzetu.
Tulipokuwa tunaishika Pasaka kikamilifu, kwa mara ya kwanza, basi tulianza kukua katika vikwazo na vipingamizi kwa namna ya maarifa. Kama hatutatenda katika kweli Roho atatuacha. Usomaji wa mara kwa mara na kwa bidii kutatuwezesha kupata ufunuo mpya. Kama tutaendeleza yale tunayoyafahamu, kisha tutapandishwa hadi kwenye hatua ya pili ya kuelewa. Mavuno haya ni chanzo muhimu katika kuelewa matendo ya kiroho yatakayotokea kipandi cha Milenia. Mara tu tunapotilia hili lote katika mahali pa uelewa nia na malengo yake yote. Sikukuu hizi ni mfano wa haki na utauwa katika mfumo wa Masihi. Tunaenda kushirikisha sheria zote katika ujumla wake. Kilakitu Masihi, kama Malaika wa Yahova (Yehova) wa Sinai, aliyempa Musa sheria hizi, zitaanzishwa tena katika imani timilifu nasi tutazifanya.
Kristo hakumpa Musa mkono mbaya wenye kumtakia kutofanikiwa. Mfumo wa Ukristo Mamboleo unasema ilikuwa ni vizuri sana kwa Israeli na kwamba sheria zilikuwa kwa ajili ya Wayahudi ni kama wanoshughulika na deki ya runinga iliyo haribika. Wana utaratibu wa sheria na mfumo ambao sio mzuri na sasa, pengine, twaweza kuwa tunafahamu vizuri zaidi. Ukweli wa mambo ni kwamba ni kwamba Kristo alitoa mfumo mkamilifu wa sheria za Musa ili kwamba ziweze kutumika katika hii sayari ili kwamba ziweze kuanzisha mfumo wa milenia hatimaye. Somo hapa ni kwamba, tunahitaji Roho Mtakatifu wa Mungu ili atuwezeshe kuzishika sheria hizi. Kama ingekuwa ulimwengu wote ungekuwa umeingia kwenye uongofu katika Israeli, kama ungeshikilia imani na ukaachana na huko ulikoenda mbali kuamini miungu wa kigeni, na sio kushindwa, ushwishi wao hapa duniani ungekuwa umeigwa na kutumiwa na wengi. Kamwe tusingekuwa kwenye vita kila mahali hapa duniani kama tunavyoona ilivyo sasa. Hii sayari isingekuwa inaendelea kufa. Lakini hawakudumu katika imani. Na wala hawakufanya wajibu wao. Bali waliendelea kuziweka sheria hizi mbali na kupoteza muelekeo kuhusu maana ya hizi sikukuu. Waliacha hata kuishika Sikukuu ya Vibanda kwa karne kadhaa. Sikukuu hizi zilianzishwa tena na Nehemia. zilitabiriwa na zikafundishwa tena na nabii Ezekieli. Nabii Ezekieli alikuwa anaongelea katika mtazamo wa Kimilenia.
Nehemia na Ezra waliweka utaratibu wa Hekalu na kuuokoa na kuulinda mji wa Yerusalemu. Wakakikuta kitabu cha sheria ambacho walikisoma baada ya kufanya maandalizi na kuwakutanisha watu. Watu wakatokwa na machozi. Taifa lote zima wakasimama mbele ya makuhani wakisiliza sheria zikisomwa (sawa na lisemavyo jarida la Kusomwa kwa Sheria na Ezra na Nehemia [250]. Kuna umuhimu na ni agizo kwamba kila mwaka wa Sabato zisomwe sheria.
Makanisa ya Mungu katika ujumla wake huwa hayafanyi hivi. Hakukuwa na usomwaji wa sheria katika miaka ya Sabato kwa kanisa lolote katika sayari yetu hii kwa kipindi cha karne nyingi. Hatimaye ilisomwa kwa mara ya kwanza katika mwaka wa Sabato wa 1998-99 baada ya kuachwa kusomwa kwa kipindi cha karne nyingi wakati wa Sikukuu ya Vibanda. Ilifanywa kwa uaminifu mkubwa na sasa inachapishwa kwa Lugha nyingi.
Kama ilivyoanza tokea mwanzo, sasa tunaunganishwa na kuimarishwa kama kundi. Mungu ataendelea kushughulika na sisi kwa kadiri tunapokuwa tuko tayari. Kama tukiwa hatupo sawa kiroho, Mungu atatuengua mbali na jingo. Hatutaweza kuongezwa kwa idadi kubwa hadi pale tutakapokuwa tupo tayari. Mungu atatuongeza sawasawa na mpango wake. Lile tunalotakiwa kulifanya ni kusema na kufundisha kweli. Ni wajibu wetu kuendeleza kiwango chetu cha kiroho na kukua ili kwamba tujiandae kwa mavuno haya. Sisi ni askari katika jeshi la Mungu, katika mafunzo ili kufikia mahali ambapo tunaweza kufaa kutumika na kusimama na Yesu Kristo. Kama tutakavyoona kutokana na chanzo na utaratibu wa sikukuu, haitaweza kutokea kwa kila mmoja aketiye chini na kukubali kujongelea meza.
Utawala wa Milenia hautaweza kuletwa ili kufikia kima cha utulivu na amani. Inabidi tuelewe hilo na tujiandae kwa hilo. Ishar hii ya makusanyo ya kiroho ni la muhimu katika hali ya uelewa wa nyakati. Ni Sheria ya Mungu kwamba tuwemo kwenye ushiriki wa sikukuu katika shughuli hizo.
q