Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[284]
Kumbukumbu La Torati 12:17-28
(Toleo La 1.0 19990910-19990910) Imerekodiwa Kwenye Tepu
Andiko hili linahusu wajibu wetu
tuliopewa kuufanya chini ya sheria kuhusiana na ushiriki wetu kwenye sikukuu.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 1999 Wade Cox)
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Mungu ametoa
maelekezo ya wazi kwa kile anachotutaka tufanye kuhusu kuadhimisha sikukuu.
Wakati mwingine maandiko yaliyo kwenye Torati yanalohusiana na maadhimisho ya
sikukuu yanapotoshwa au kutumiwa vibaya au pengine ni kwamba hayaeleweki tu na
walengwa.
Kumbukumbu La Torati
12:17-28 Usile ndani ya
malango yako zaka ya nafaka zako, wala ya divai yako, wala ya mafuta yako, wala
wazaliwa wa kwanza wa makundi yako, ya ng'ombe wala ya kondoo, wala nadhiri
zako uwekazo zo zote, wala sadaka zako za hiari, wala sadaka ya kuinuliwa ya
mkono wako; 18 lakini hivyo mtakula mbele za Bwana,
Mungu wako, mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, wewe, na mwanao mume na
mke, na mtumwa wako mume na mke, na Mlawi aliye ndani ya malango yako; nawe
furahi mbele za Bwana, Mungu wako, katika yote utakayotia mkono wako. 19 Jilinde nafsi yako usimwache Mlawi siku zote uishizo
katika nchi yako. 20 Bwana, Mungu wako,
atakapoongeza mpaka wako, kama alivyokuahidi, nawe utakaposema, Nataka kula
nyama, kwa kuwa roho yako yatamani kula nyama; waweza kula nyama, kwa kufuata
yote inayotamani roho yako. 21 Na mahali
atakapochagua Bwana, Mungu wako, apaweke jina lake, pakiwa mbali nawe mno,
ndipo utakapochinja katika kundi lako la ng'ombe na kondoo alilokupa Bwana kama
nilivyokuagiza, nawe utakula ndani ya malango yako, kwa kufuata yote
inayotamani roho yako. 22 Kama vile aliwavyo
paa na kulungu, ndivyo utakavyoila nyama hii; asiyekuwa tohara na aliye tohara
wataila pia. 23
Ila ujihadhari kwamba usile damu, kwani ile damu ndiyo uhai; na
uhai usile pamoja na nyama. 24 Usiile; imwage juu
ya nchi kama maji. 25 Usiile; ili upate
kufanikiwa, na watoto wako baada yako utakapofanya yaliyoelekea machoni pa
Bwana. 26 Ila vitu vyako vitakatifu ulivyo navyo,
na nadhiri zako, uvitwae ukaende mahali atakapochagua Bwana; 27 nawe zisongeze sadaka zako za kuteketezwa, nyama na
damu, juu ya madhabahu ya Bwana, Mungu wako; na damu ya dhabihu zako uimwage
juu ya madhabahu ya Bwana, Mungu wako, na wewe utakula nyama yake. 28 Maneno haya nikuagizayo yote yatunze na kuyasikiza, ili
upate kufanikiwa na watoto wako baada yako milele, hapo uyafanyapo yaliyo mema
na kuelekea machoni pa Bwana, Mungu wako.
Andiko hili
linaeleza kwa wazi sana kile ambacho mtu anaweza kukifikiria. Aya ya 17 inasema
wazi kuwa zaka isiliwe kwenye malango yetu yoyote. Hii inaelezea wazi kuhusu
zaka ambayo inaweza kuliwa kama kinyume na zaka ile ambayo inahusu kuwapa
Walawi na ambayo wanapewa hao pekeyao. Zaka hii inajulikana kama zaka ya pili
ambayo hutumuwa na mtu mwenyewe tu binafsi yake. Mtu anatakiwa kuitenga zaka
hii kando, mahali, ili kwamba aendenayo kwenye sikukuu ya Bwana, mara tatu kila
mwaka kama ilivyoamriwa. Jambo hili limeelezewa kwa kina kwenye majarida ya Utoaji wa Zaka (Na. 161) na Torati na Amri ya Nne (Na. 256) [Tithing (No.
161) and Law and the Fourth Commandment (No. 256)].
Kuna wajibu
lililopewa taifa na makuhani wake ya kupachagua mahali patakapoazimishwa
sikukuu ili kila mtu apajue mahala hapo na aende kama alivyoamriwa.
Mara hizi tatu na
sikukuu zake tatu zileelekezwa kwenye Kumbukumbu La Torati 16:1-17.
Kumbukumbu La Torati
16:1-8 Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka Bwana, Mungu wako, kwa kuwa
ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku Bwana; Mungu wako. 2 Nawe umchinjie pasaka Bwana, Mungu wako, katika kundi la
kondoo na la ng'ombe, mahali atakapochagua Bwana apakalishe jina lake. 3 Usimle
pamoja na mikate iliyotiwa chachu; siku saba utakula naye mikate isiyotiwa
chachu, nayo ni mikate ya mateso; kwa maana ulitoka nchi ya Misri kwa haraka;
ili upate kukumbuka siku uliyotoka nchi ya Misri, siku zote za maisha yako. 4 Wala
isionekane kwako chachu muda wa siku saba katika mipaka yako yote; wala katika
hiyo nyama uchinjayo siku ya kwanza jioni, kisilale cho chote usiku kucha hata
asubuhi. 5 Usimchinje pasaka ndani ya malango yako
yote akupayo Bwana, Mungu wako; 6 ila mahali
atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake, ndipo mtakapomchinja
pasaka jioni, katika machweo ya jua, kwa wakati kama uliotoka Misri. 7 Nawe umwoke na kumla mahali atakapochagua Bwana, Mungu
wako; kisha asubuhi yake ugeuke uende hemani mwako. 8 Siku
sita utakula mikate isiyotiwa chachu; na siku ya saba na uwe mkutano mtukufu
kwa Bwana, Mungu wako, usifanye kazi yo yote.
Kipengele hiki cha
Pasaka kinaelezewa kwa wazi sana kuwa hakiwezekani kuwa inaliwa ndani ya
malangoni. Kwa maneno mengine ni kwamba kila mtu anapaswa awe nje ya makazi
yake kwa ajili ya jambo hili. Wasamaria wamekuwa wakiifuata sheria hii
kikamilifu na kwa uaminifu wao wote tangu siku ya 14 Nisani kwa zaidi ya siku
nzima na hadi asubuhi ya siku ya 15 Nisani, kwa kipindi cha zaidi ya miaka elfu
mbili. Wanaondoka na kuwa nje ya makazi au nyumba zao na inawezekana kuwa
walikuwa wanakwenda kwenye Mlima Gerizimu kwa ajili ya mkesha. Idi ya Mikate
Isiyo na Chachu inafuatia. Kipindi hiki kinajumuisha pia maadhimisho ya Mganda
wa Kutikiswa yanayofanyika siku ya Jumapili ya wakati wa Idi ya Mikate isiyotiwa
Chachu, ambayo inakuwa ndiyo mwanzo wa kuhesabu siku za kufikia maadhimisho ya
Idi ya Majuma au Pentekoste, ambayo pia huadhimishwa siku ya Jumapili na ambayo
ilikuwa pia inaadhimishwa na Wayahudi na Wasamaria siku ya Jumapili kwa kipindi
chot cha zama za Hekalu.
9 Jihesabie majuma saba; tangu wakati uanzao kutia
mundu katika mmea utaanza kuhesabu majuma saba. 10 Nawe
sikukuu ya majuma umfanyie Bwana, Mungu wako, kwa kutoa sadaka ya hiari ya
mkono wako, utakayotoa kwa kadiri akubarikiavyo Bwana, Mungu wako; 11 nawe utafurahi mbele ya Bwana, Mungu wako, wewe na mwana
wako na binti yako, na mtumwa wako na mjakazi wako, na Mlawi aliye ndani ya
malango yako, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio
katikati yako, katika mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina
lake. 12 Nawe kumbuka kwamba ulikuwa mtumwa huko
Misri; tena zishike amri hizi kwa kuzifanya.
Kwa hiyo, tunaona
hapa kwamba Idi au Sikukuu ya Pentekoste inahusiana pia na dhana ya utumwa na
kukombolewa kwao kutoka utumwani Misri. Tunaona pia hapa kwamba watu wote walipaswa
kuhudhuria Sikukuu zote. Watu wote waliokuwa wanaishinao majumbai mwao na pia
kwenye sikukuu zote tatu za kila mwaka. Hata hivyo, wanaume ndiyo peke yao
waliotajwa kwa uzito wake maalumu kuwa ni lazima wajihudhurishe kila sikukuu
kwa mujibu wa Torati kama tuonavyo hapo chini.
13 Fanya sikukuu ya vibanda siku saba,
utakapokwisha kuyakusanya yatokayo katika sakafu yako ya nafaka, na katika kinu
chako cha divai; 14 nawe utafurahi katika sikukuu yako, wewe,
na mwanao, na binti yako, na mtumwa wako, na mjakazi wako, na Mlawi, na mgeni,
na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani ya malango yako. 15 Siku saba mfanyie sikukuu Bwana, Mungu wako, mahali
atakapochagua Bwana; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, atakubarikia katika maongeo
yako yote, na katika kazi zote za mikono yako, nawe uwe katika kufurahi kabisa.
Kwa hiyo tunaona
kwamba, sikukuu zote mbili, yaani Pasaka na utaratibu wa kuhesabu hadi kufikia
Pentekoste na Idi ya Vibanda, watu wote waishio kwenye nyumba wametajwa kushiriki.
Wanapaswa kwenda hadi mahali ambapo Bwana amepachagua. Tunaona hili sasa kwa
kuwa amri ilitolewa moja kwa moja kwa wanaume.
16 Mara tatu kwa mwaka na watokee wanawaume
wako wote mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua; katika sikukuu ya
mikate isiyotiwa chachu, na katika sikukuu ya majuma, na katika sikukuu ya
vibanda; wala wasitokee mbele za Bwana mikono mitupu. 17 Kila
mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako,
alivyokupa.
Vipindi vimeorodheshwa
kuwa ni Idi za Mikate Isiyotiwa Chachu, Pentekoste na Idi ya Vibanda. Hii
ilifanyika ili kwamba tusiachwe na mashaka yoyote, ambacho kilikuwa ni kipindi
kamili na wanaume hawana uchaguzi kuhusu jambo hili. Wanawake wanaweza kuchagua
au kuamua kutokwenda kwa kuwa wanaweza kuwa kwenye kipindi cha uzazi wa watoto
au mambo mengine mengi, lakini wanaume hawana chaguo wa hiyari ya kwenda huko.
Suala ni kitu
kingine chochote kilichojiinua au kujitokeza: Oo, ni sawa, kwa anayechagua. Tunaawezaje
kujua kuwa ni kweli Mungu ameuweka mkono wake pale? Jagwani ilikuwa ni rahisi. Nguzo
ya Moto na Wingu viliwaashiria Israeli wakati wa kuondoka na sehemu ya
kuelekea. Katika nchi ya ahadi Mungu aliwapa muelekeo wao kwa kwenda kwa
kupitia Manabii. Aliwaelekeza kuuchagua Yerusalemu baada ya Daudi kuiondoa au
kuihamisha maskani kwa kuipeleka huko kutoka Hebroni. Mungu pia alilihusuru
Hekalu na kuamuru kuanza kwa kanisa. Kanisa lile lilikuw na wajibu wa
kupatangaza mahali pa kufanyia maadhimisho ya sikukuu na kuiandia hapo.
Kwa ajili hii sehemu iliyofuatia ya andiko la Kumbukumbu la Torati 16 inaonekana jinsi inavyofanya.
Kumbukumbu La Torati
16:18-20 Weka waamuzi na maakida katika malango yako yote akupayo Bwana, Mungu
wako, kwa hesabu ya kabila zako; nao wawaamue watu kwa maamuzi ya haki. 19 Usipotoe
maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa
hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza daawa ya wenye haki. 20 Yaliyo haki kabisa ndiyo utakayoyafuata, ili upate
kuishi na kuirithi nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.
Nia iko wazi
sana. Taifa lina wajibu wa kuhakikisha kwamba linawachagua waamuzi na maafisa
ili kuhakikisha kwamba Torati ishikwe na watu wazifuate sheria za Mungu katika
Haki na Kweli. Hii inaendana sawa tu na kuhusianishwa na Torati na kuhaguliwa
kwa kanisa na shughuli zake za kumfanyia Mungu ibada.
Tumeona kwamba sikukuu
ni kusanyiko lililoamriwa. Sikukuu zote tatu zimeamriwa na kuagizwa na kwamba
wanaume wote wanatakiwa kujitokeza
na watu wote wa nyumbani mwao wanatakiwa
kuhudhuria na maamrisho ni kwamba wanaume wanatakiwa kuhakikisha eneo
linatengwa kwa wanaume na wanawake hata kwenye huduma za mahali pamoja ili
waweze kujitokeza na kuhudhuria.
Sehemu
inayofuatia ya uhudhuriaji ni ile ya wawakilishi wa eneo.
Kabla
hatujatafakari jambo hilo inatupasa tutafakari suala la umbali na utaratibu
kuhusu umbali.
Kwenye andiko la
Kumbukumbu La Torati 12:17-19 tunaona kwamba hizi sikukuu ni ya kuhudhuria
wakazi wote wa nyumba ile, sawasawa na ilivyoamriwa kwenye Kumbukumbu La Torati
16:16.
Kutoka kwenye aya
ya 20 tunaona kwamba inaonekana kuwa ni ya kipekee ya aina yake, lakini ndivyo
ilivyo? Hebu na tulitafakari andiko hili.
Kumbukumbu La Torati
12:20-22 Bwana, Mungu wako,
atakapoongeza mpaka wako, kama alivyokuahidi, nawe utakaposema, Nataka kula
nyama, kwa kuwa roho yako yatamani kula nyama; waweza kula nyama, kwa kufuata
yote inayotamani roho yako. 21 Na mahali atakapochagua
Bwana, Mungu wako, apaweke jina lake, pakiwa mbali nawe mno, ndipo
utakapochinja katika kundi lako la ng'ombe na kondoo alilokupa Bwana kama
nilivyokuagiza, nawe utakula ndani ya malango yako, kwa kufuata yote
inayotamani roho yako. 22 Kama vile aliwavyo
paa na kulungu, ndivyo utakavyoila nyama hii; asiyekuwa tohara na aliye tohara
wataila pia.
Hapa tunaona
kwamba andiko linasema kwamba kama mahali patakuwa ni mbali sana na kama
unataka kumla akiwa na hali ya ubichibichi, ndipo unaweza kumuua na kama mnyama
aliye kwenye makundi yako, hata katika mademe ya paa na ayala nk. Mgeni na
asiyetohara anaruhusiwa pia kuwala. Kwa maneno mengine ni kusema kwamba sikukuu
inawahusu pia wasio tohara na wamataifa, watakaokwenda hekaluni.
Je, kwahiyo hii
inamaanisha kwamba hupaswi kwenda mahali palipocchakuliwa kufanyiwa sikukuu?
Hapana, haimaanishi hivyo kabisa.
Hebu na angalia
kwa kina na kwa umakini mkubwa andiko hili hapa chini.
Kumbukumbu La Torati
12:23-29 Ila ujihadhari kwamba usile damu, kwani ile damu ndiyo uhai; na uhai
usile pamoja na nyama. 24 Usiile; imwage juu
ya nchi kama maji. 25 Usiile; ili upate
kufanikiwa, na watoto wako baada yako utakapofanya yaliyoelekea machoni pa
Bwana.
Hapa tunaona
ufafanuzi. Nyama inaweza kuliwa nyumbani. Hata hivyo, vitu vitakatifu
ulivyonavyo na ainazote za nadhiri unazomfanyia Mungu unapaswa kwendanazo
mahali alipopachagua Bwana, Mungu wako.
26 Ila vitu vyako vitakatifu ulivyo navyo, na
nadhiri zako, uvitwae ukaende mahali atakapochagua Bwana; 27 nawe
zisongeze sadaka zako za kuteketezwa, nyama na damu, juu ya madhabahu ya Bwana,
Mungu wako; na damu ya dhabihu zako uimwage juu ya madhabahu ya Bwana, Mungu
wako, na wewe utakula nyama yake. 28 Maneno haya
nikuagizayo yote yatunze na kuyasikiza, ili upate kufanikiwa na watoto wako
baada yako milele, hapo uyafanyapo yaliyo mema na kuelekea machoni pa Bwana,
Mungu wako. 29 Bwana, Mungu wako, atakapoyakatilia mbali
hayo mataifa mbele yako, huko uingiako kuyamiliki, nawe ukawatwaa, na kuketi
katika nchi yao;
Kwa hiyo,
kinachoonekana kuwa ni kifungu kinachotolewa hakikutolewa kabisa. Unafana kile
inachoweza kukibeba na kiliho Kitakatifu na kilicho kwenye nadhiri na utoke na
kwendanacho kwenye mahali itakapokuwa kambi la sikukuu ambapo pametengwa na
kuandaliwa kwa ajili yako.
Jambo hili
limeelezewa kwa kina kwenye andiko linguine pia.
Kumbukumbu La Torati
14:22-29 Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako,
yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka. 23 Nawe
utakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake,
zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa
makundi yako ya ng'ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha Bwana, Mungu
wako, daima. 24 Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze
kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua Bwana, Mungu wako,
apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia Bwana, Mungu wako; 25 ndipo
uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata
mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako; 26 na
zile fedha zitumie kwa cho chote itakachotamani roho yako, ng'ombe, au kondoo,
au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako cho chote; nawe utakula huko
mbele za Bwana, Mungu wako; tena furahi, wewe na nyumba yako; 27 na Mlawi aliye ndani ya malango yako usimwache, kwani
hana fungu wala urithi pamoja nawe. 28 Kila mwaka wa tatu,
mwisho wake, toa fungu la kumi lote la maongeo yako ya mwaka huo, uliweke ndani
ya malango yako; 29 na Mlawi kwa kuwa hana fungu wala urithi
pamoja nawe, na mgeni, na yatima, na mjane aliyefiliwa na mumewe, walio ndani
ya malango yako, na waje wale na kushiba; ili kwamba Bwana, Mungu wako,
akubarikie katika kazi yote ya mkono wako uifanyayo.
Hapa tunaona maelekezo sahihi. Unakuza na kukibadili kuwa fedha ile ulichonacho na kukichukua hadi mahali palipoachaguliwa kufanyika sikukuu na unaruhusiwa kununua chochote unachokitaka. Tahadhari tu iliyotolewa hapa kwenye andiko hili na kwamba ni katika ule mzunguko wa mwaka wa Saba tu wakati sikukuu inapoweza kuliwa nyumbani na mwendelezo wake unajiri kwenye zaka ya tatu ya kuwasaidia maskini (sawa na jarida la. Utoaji wa Zaka (Na. 161) [Tithing (No. 161)].
Kwa hiyo kama mtu atakuwa ni mwanaume hatakiwi kutafuta udhuru maana hatasamehewa. Kama maeneo yako mbali na makundi yanayokusudiwa kiasi kwamba hata wameamua kujifanyia makambi yao wenyewe kama jamii, tunaiona kanuni ningine pia. Kitendo ha kukataa kwenda mahali alipohaguliwa na kanisa ni kuikataa haki ya kanisa ya kupachagua mahali pale.
Zekaria ameweka wazi kwa kile kitakachotokea kwa mtu au jamii itakayoshindwa kwenda kujihudhurisha na kuzishika sikukuu hizi, au wasiotuma wawakilishi wao.
Zekaria 14:16-19 Hata itakuwa, ya kwamba kila mtu aliyesalia wa
mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu, atakwea mwaka baada ya mwaka
ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, na kuishika sikukuu ya Vibanda. 17 Tena itakuwa, ya kwamba mtu awaye yote wa jamaa zote
zilizomo duniani, asiyekwea kwenda Yerusalemu ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa
majeshi, mvua haitanyesha kwao. 18 Na kama jamaa ya
Misri hawakwei, wala hawaji, pia haitanyesha kwao; itakuwako tauni, ambayo
Bwana atawapiga mataifa, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda. 19 Hii ndiyo adhabu ya Misri, na adhabu ya mataifa yote,
wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda.
Kama taifa
halitapata mvua kwa wakati wake, kama Misri, ambayo inategemea mmiminiko wa
maji ya Mto Nile, Mungu atawapiga kwa tauni hadi watakapotubu. Hali hii
itatokea kwa kipindi cha miaka 1,000 ya utawala wa Milenia hapa duniani.
Kama Mungu
atayaadhibu mataifa hayo yasiyozishika sikukuu kwa vifo na njaa, basi Mungu
atawezaje kuonyesha upendeleo kwa wateule?
Mungu hana
upendeleo. Mtu yeyote atakayeshindwa kuchukua hatua ya kwenda kuzishika sikukuu
na kuwawezesha familia yake kwenda kuishika sikukuu, atachukuliwa kama mtu wa mataifa
na ataondolewa mbali na wateule na Kuondokwa na Roho Mtakatifu.
Mtu yeyote anayepinga sheria hii ya kuhudhuria kwenye maadhimisho ya sikukuu nje ya malango yake, anajitoa mwenyewe na kujiweka nje ya Baraka za Torati na kuzivunja Amri za Mungu na kuwa mbali na wateule waliotajwa kwenye Ufunuo 12:17 na 14:12. Yeyote anayepinga haki ya kanisa ya kuchagua maeneo hayo ya kuandaa sikukuu, wanajitoa nje ya ushirika wa kanisa.
Kila mtu kisheria ametakiwa asaidiwe ili ahudhurie kwenye sikukuu, lakini ni lazima aonyeshe kuwa yeye mwenewe ana nia ya dhati na amechukua hatua fulani katika kujiandaa kwa mujibu wa sheria.
Kinachoonekana kutolewa nje kwa wale wasiopenda kujihudhurisha, ni kwa kweli ni maelekezo ya jinsi wanavyotakiwa kuhudhuria.
Angalia sasa Kutoka 34:23-24 inavyosema.
Kutoka 34:23-24 Mara tatu kila mwaka watu waume wako wote
watahudhuria mbele za Bwana MUNGU, Mungu wa Israeli. 24 Kwa
kuwa mimi nitazitupa nje taifa za watu mbele yako, na kuipanua mipaka yako;
wala hapana mtu ye yote atakayeitamani nchi yako, hapo utakapokwea kwenda
kuhudhuria mbele za Bwana Mungu wako mara tatu kila mwaka.
Hakuna mtu
atakayetamani mali au ardhi yako. Ni suala la imani tu kwamba wewe uiache numba
yako na kwenda hadi mahali alipopachagua Bwana na hapo ndipo ukaziadhimishe idi
zake.
Msimamo wa wale
wanaotaka kukwepa kuzishika sikukuu na kuwapinga watu wa Mungu, mara zote
unaonekana kwenye sababu zilezile za wakati kambi ya sikukuu inapofanika kwenye
maeneo jimo yao kwa namna zozote. Dhana na mawazo kama hayo ndiyo hayana mahali
wala kutakiwa kwene kanisa la Mungu.
q