Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

 

[042]

 

 

 

Heri Walioalikwa

 (Toleo La 1.0 20020914-20020914)

 

Mwanzo sura ya 24 ni hadithi ya Ibrahimu akimtafutia mke mwanae Isaka kwa kumtumia mtumishi wake. Hadithi yenyewe ina utajiri mwingi wa vielelezo na mifano. Tutajionea kusudi kuu linaloonyeshwa na kufanywa kwenye hadithi hii ya kumtafutia mke Isaka. Ina uhusiano unaoingiliana na jinsi Mungu anavyomtafuatia bibi arusi Mwanae, Yesu Kristo.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

(Hati Miliki © 2002 Peter Donis. ed. Wade Cox)

(tr. 2015)

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Heri Walioalikwa


Hebu na tuanze safari kuanzia Mwanzo sura ya 24.

Mwanzo 24:1-4  Basi Ibrahimu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, na Bwana alikuwa amembariki Ibrahimu katika vitu vyote. 2 Ibrahimu akamwambia mtumishi wake, mzee wa nyumba yake, aliyetawala vitu vyake vyote, Tafadhali uutie mkono wako chini ya paja langu, 3 nami nitakuapisha kwa Bwana, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao; 4 bali enenda hata nchi yangu, na kwa jamaa zangu, ukamtwalie mwanangu Isaka mke.

 

Ibrahimu alikuwa na umri wa miaka 100 wakati alipozaliwa Isaka (Mwanzo 17:17). Ibrahimu alikuwa na takriban miaka 140 ya umri wake wakati alipomwambia mtumishi wake aende kumtafutia mke mwanae. Isaka alikuwa na umri wa miaka 40 wakati huu. Kama tutaichukua yubile (miaka 50) na kuilinganisha kwa kila mwaka wa umri wa Isaka, tangu kuzaliwa kwake hadi alipokutana na kumuoa mke wake, tunafika kwenye idadi ya miaka 2000 kamili. 

Kuna mlinganisho wenye kuvutia sana kwenye maisha ya Kristo na maisha ya Isaka. Kristo alizaliwa karibu na yubile ya 40 au miaka 2000 iliyopita. Rebeka ni mfano wa kanisa. Isaka alimuwa na umri wa miaka arobaini alipomuoa Rebeka. Kristo tangu kuzaliwa kwake, amesubiri yubile 40 (sawa na miaka 2000) ili kuungana na bibi arusi wake, kanisa. Wakati tunapoisoma aya inayohusiana na yubile, inajiri na tangazo la uhuru kwa ulimwengu wote wakati Kristo atakaporudi (Walawi 25:10).

                               

Akiwa na umri wa miaka 40 Isaka alikuwa na uwezo na akili timamu ya kumuwezesha kujitafutia mke mwenyewe, lakini bado Ibrahimu alimtuma mtumishi wake kwenda Harani akamtafutie Isaka mke huko. Alikuwa Ibrahimu kwa kupitia mtumishi wake, aliyemletea mke mwanae. Ni sawa na ilivyo kwa Kristo. Baba Mungu (ambaye hapa anafananishwa na Ibrahimu), kwa uweza wa Roho wake (anaonekana kwa taswira ya mtumishi) anawaleta watu, anayefanya bodi au bibi arusi wa Kristo (Yohana 6:44).

 

Mtumishi mku sana anayetajwa hapa anaweza kuwa ni Eliezeri. Ibrahimu alimtuma mtumishi kwa kuwa yeye alikuwa ni mwabudu Mungu pia (Mwanzo 24:26, 52). Kama alikuwa ni Eliezeri, ndipo uadilifu wake ni kitu ambacho tunaweza kukitilia maanani. Alikuwa anamtafutia mke mwanae ambaye alikuwa alimtaka hapo nyuma awe ni mrithi wa mali za Ibrahimu (Mwanzo 15:2).

 

Mke huyu anapaswa asiwe Mkanaani. Wakanaani walikuwa wamelaaniwa (Mwanzo 5:8-15). Ibrahimu alikuwa anamwambia mtumishi wake kumtafutia mke mwanae Isaka kwa watu wanaomuabudu Mungu mmoja na anayemwabudu yeye.

Mwanzo 24:5-6 Yule mtumishi akamwambia, Labda yule mwanamke hatakubali kufuatana nami mpaka nchi hii, je! Nimrudishe mwanao mpaka nchi ulikotoka? 6 Ibrahimu akamwambia, Ujihadhari, usimrudishe mwanangu huko.

Eliezeri anaweza kuchukuliwa kama ni mtu asiyeongoka, tusiwaruhusu wenzi wetu wasioongoka kutuzuia tusitoke Misri au kutushawishi au kutusababisha turudi Misri. Tumeitwa tutoke gizani na kuwa kwenye nuru ya ajabu sana ya Mungu (1Petro 2:9).

 

Mwanzo 24:7 Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya babangu, na kusema nami katika nchi niliyozaliwa, aliniapia akisema, Nitawapa uzao wako nchi hii; yeye atampeleka malaika wake mbele yako, nawe utamtwalia mwanangu mke tokea huko;

 

Ni Mungu Baba anayetuita sisi na kututoa kutoka nyumba zetu za zamani za utumwa. Sisi sote tunayeyatenda mapenzi ya Mungu Mmoja, wa Pekee na wa Kweli tunaonekana kama uzao au watoto wa kiroho wa Ibrahimu. Hapa Ibrahim anamuonyesha Kristo kama Malaika wa Mungu.

 

Mwanzo 24:8 na yule mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi, utafunguliwa kiapo changu hiki; lakini usimrudishe mwanangu huko.

 

Mwanamke huyu ni taswira ya wale walioitwa na sio waliochaguliwa. Roho wa Mungu atafanyakazi na watu mmoja mmoja ili kumuongoza yeye apende kubatizwa. Hapa Eliezeri anakuwa taswira ya Roho wa Mungu, anayetuonyesha sisi kuwa kama mtu hapendi kufuata, ndipo Roho Mtakatifu “alishuka au kutolewa” kutoka kwa mtu huyo.

 

Mwanzo 24:9 Yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la Ibrahimu bwana wake, akamwapia katika neno hilo.

Kutokana na kubatizwa kwetu, ndipo tunatolewa na kuingizwa kwa Kristo. Kristo anaishi ndani yetu (Wagalatia 2:20). Tunaingia kwenye agano la kumtii Mungu. Hatuwezi kurudi nyuma kwenye njia zetu za zamani, wakati tulikuwa tumekwisha kufa kwa mambo maovu (Waefeso 2:5) kumuweka Kristo nyuma kwenye hali yetu ya kimaisha ya nyuma (Wagalatia 5:1).

 

Mwanzo 24:10 Kisha huyo mtumishi akatwaa ngamia kumi katika ngamia za bwana wake akaenda zake, maana mali zote za bwana wake zilikuwa mkononi mwake, akaondoka, akaja mpaka Mesopotamia, mpaka mji wa Nahori.

 

Tarakimu hii “kumi” inajulikana kama ni tarakimu ya ukamilifu na ni mwanzo mpya kama ilivyo tarakimu ya “1” kwenye awamu mpya. Ngamia wanaashiria mataifa ya wamataifa. Kwa maneno mengine, ni kwamba wanawakilisha mataifa yote. Ngamia anachukuliwa kuwa ni najisi kwenye torati (Walawi 11:4). Mtu anachukuliwa kuwa ni kiumbe najisi kwa kuwa hazishiki sheria.

 

Raslimali zote za bwana wake zilikuwa mikononi mwa mtumishi wake. Hii ingeweza kujumisha pia ahadi zote za kiroho. Kwa kupitia Ibrahimu mataifa yote yatabarikiwa. Eliezeri alionyesha kuwa alikuwa ni wokovu wa jumuia yote ya wanadamu kwa uangalizi wake.

Mwanzo 24:11 Akawapigisha magoti ngamia nje ya mji karibu na kisima cha maji wakati wa jioni, wakati ambapo wanawake wanakwenda kuteka maji.

 

Ndipo alimwinamisha ngamia wake. Eliezeri anayeonekana kuwa ni mfano wa Roho Mtakatifu yupo kwenye maelekezo na mwongozo wa Kristo hapa. Kristo atayafanya mataifa yake (ngamia) yapige magoti, nje ya Yerusalemu Mpya. Kwa kuwa mataifa yote ni mali ya Mungu (Zaburi 82:8). Mamlaka yote na uweza amepewa Kristo. Ni wale waliozifua nguo zao tu ndio wataruhusiwa kuingia kupitia malangoni ya mji ule (Ufunuo 22:14). Ni wale wanaoshinda tu, peke yao watafanyika kuwa nguzo kwenye hekalu la Mungu. Kuna mji mmoja tu tuliowekewa, Yerusalemu Mpya (Ufunuo 3:12). Watu wengine wote waliosalia watakuwa na mahala pao pa kutosha nje ya mji huu.

 

Kisima cha maji ni maji (roho) ambayo Kristo anayatoa, yanayotuongoza kwenda kwenye uzima wa milele (Yohana 4:14). Mwanamke aliyechota maji analiwakilisha kanisa. Katika ziku za zamani, kuchota maji na kuyaleta nyumbani kwa ajili ya familia yake, ilikuwa ni kazi ya mwanamke. Katika kipindi cha millennia kanisa litashirikisha majukumu ya kuchota maji ya kweli na maisha ili kuwapa mataifa. Sisi kama kanisa tunachota maji sasa, tukiwa tumejazwa na Roho Mtakatifu (Matendo 2:4, 13:52).

Haya yote yalifanyika majira ya jioni, ambao una maana yake fulani. Kazi ilikoma (Ruth 2:17); wafanyakazi walilipwa (Kumbukumbu la Torati 24:15); dhabihu za jioni zilitolewa (Kutoka 29:38-42, Hesabu 28:3-8); taratibu za utakaso zilikoma (Walawi 11:24-28). Isaka alitoka nje kwenda kutafakari (Mwanzo 24:63). Kristo alijitenga mbali kuomba (Mathayo 14:23). Tunaweza kupata mambo yanayofanana kutoka kwenye maandiko haya.

Watu wa mataifa wataletwa kisimani, kazi zao za kufungiwa nira ya utumwa inakoma (Wagalatia 5:1). Watashiriki kwenye dhabihu ya Yesu Kristo; kipindi chao cha kukoma kwa utaratibu zisizo za utakaso. Watakuja kulitafakari neno la Mungu, na maombi kufanywa mbele za Mungu kama uvumba, kuinua mikono juu kama dhabihu za jioni (Zaburi 141:2) ili kushukuru rehema na uwezo wa kumjua Mungu (Hosea 6:6).

Mwanzo 24:12 Naye akasema, Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, nakuomba mambo yangu uyajalie yawe heri leo, ukamfadhili bwana wangu Ibrahimu.

 

Maombi ya Eliezeri kwa Mungu wa Pekee na wa Kweli. Anamtambua pia Eloa, Mungu Aliye Juu Sana, kama Mungu wa Ibrahimu. Ibrahimu alimuabudu Mungu Mmoja, Wapekee na wa Kweli. Ni Mungu huyuhuyu ndiye tunayemuomba hata sisi, na si mwingine. Tunaomba kwa jina la mwanae, ila hatumuombi huyo mwana.

 

Tunaambiwa kwenye Biblia jinsi tupasavyo kuomba (Mathayo 6:9-13). Wakati tunapoomba kwa ajili ya awengine, zaidi kuliko sisi wenyewe, Baba atatujazi mahitaji yetu yote. Hii inamaanisha kuutafuta kwanza Ufalme wa Mungu, na mengine yote tutapewa (Mathayo 6:33). Ni kitendo cha kujitoa sadaka. Hivi ndivyo alivyofanya Kristo. Aliutoa uhai wake, kwa ajili yetu. Hii ndiyo namna ya moyo tunaopasa kuushindania.

Mwanzo 24:13-14 Tazama! Nimesimama karibu na kisima cha maji, na binti za watu wa mjini wanatoka kuteka maji, 14 basi na iwe hivi; yule msichana nitakayemwambia, Tua mtungi wako, nakuomba, ninywe; naye akasema, Unywe, nami nitawanywesha na ngamia zako pia; basi huyu na awe ndiye uliyemchagulia mtumishi wako Isaka; na kwa hayo nitajua ya kuwa umemfadhili bwana wangu.

 

Kitendo cha Eliezeri kusimama kisimani kinaonyesha taswira ya makanisa mengi yanayokuja kuchota maji kwenye kisima cha uzima. Lakini roho (mtumishi) anatenganisha kati ya makanisa (wanawake). Kanisa halipaswi tu kuwa na ushuhuda, bali linapaswa kuzaa matunda ya roho (Mathayo 7:20). Mwanamke aliyesema: Unywe, nami nitawanywesha na ngamia zako pia, ndiye alikuwa na ushuhuda. Ufalme wa Mungu unajengwa na watu waliotayari kutumika, na sio wale wanaotaka kutumikiwa. Hivi ndivyo anavyopenda Mungu (Mathayo 20:28).

Mwanzo 24:15 Ikawa, kabla hajaisha kunena, tazama, Rebeka anatokea, binti wa Bethueli mwana wa Milka, mkewe Nahori, ndugu wa Ibrahimu, naye ana mtungi begani pake.

 

Mungu Baba yetu anajua kile tunacho hitaji hata kabla hatujaomba (Mathayo 6:8). Mstari wa uzao wa Rebeka unaonyesha kuwa alikuwa ni uzao na jamii ya Ibrahimu, lakini la muhimu sana ni kwamba alikuwa anamuabudu Mungu wa Pekee na wa Kweli, kama uzao wa kiroho.

 

Alitoka nje. Hii inamuonyesha yeye kuwa ametoka nje ya familia yake na kwenye ulimwengu huu. Alikuja kuifanya kazi yake. Alitoka nje ili kuchota maji kisimani, ambayo ndiyo ilikuwa imani yake. Kitendo chake cha kubeba mtungi kinaonyesha kuwa alikuwa na kifaa na nguvu za kuchota maji yeye mwenyewe, na hakuwa anamtegemea mtu mwingine yeyote.

 

Mwili wetu wa kidunia unachukuliwa kama chombo au silaha iliyotengenezwa kutoka kwenye udongo (Isaya 64:8). Udongo, kwa hali yake ya asili, unatumika mara chache kutengenezea vyungu au vitu vya ufinyanzi. Sisi kama wanadamu hali yetu yenye asili ya kimwili haiwezi kuurithi ufalme wa Mungu (1Wakorintho 15:50). Udongo umechanganyika na maji, na kisha inachujwa ili kiondoa mawe na takataka nyingine kubwakubwa. Ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu ndipo tunaweza kupondwapondwa na kubadilishwa, huku mioyo yetu ikinyunyiziwa usafi kutokana na dhamira na mawazo mauvu na miili yetu ikiwa imeoshwa kwa maji safi (Waebrania 10:22).

 

Udongo unaweza kuchongwa na kurudishwa kwenye umbo lake, na unaweza kukaushwa unapowekwa kwenye joto kali. Joto hili kali ni kuimarishwa ambako tunapitia maishani mwetu. Tunapitia kwenye taratibu au awamu mbalimbali, ili kwamba uhalisia na uaminifu wa imani yetu ijaribiwe kwa moto. Matokeo ya mwisho yatasifiwa na utukufu na heshima atakaporudi Kristo (1Petro 1:7). Wakati tutakapotiwa kwenye moto kiasi cha kutosha na kusubuliwa uozo wetu wa kiroho utabadilika. Na ndipo tutapapokuwa na tabia ya kaka yetu Yesu Kristo (Warumi 8:29) ambaye yeye mwenyewe alijaribiwa kwa kile alichoteseka kwacho na anaweza kutusaidia sisi (Waebrania 2:18) na tukafanyiwa kuwa wakamilifu (Waebrania 5:9).

Mwanzo 24:16 Naye yule msichana alikuwa mzuri sana uso wake, bikira, wala mwanamume hajamjua bado; akashuka kisimani, akajaza mtungi wake, akapanda.

Aya hii inahusiana na hali ya mtu ya kiroho kabla ya ubatizo. Kabla ya ubatizo tunapasa kuzaa matunda yatokanayo na toba (Mathayo 3:8). Aya inayoulizwa inamaanisha hali ya kutengana na mtu. Mwanamke anawakilisha mtu binafsi aliyetolewa au kuchotwa na Mungu, na akawa tayari kutolewa kwa Kristo.

 

Sasa alikuwa ni mzuri sana kumshika. Kimuonekano wa kimwili, Rebeka anaweza kuwa alikuwa na muonekano mzuri kwa nje. Lakini tunaangalia hali na tabia yake ya kiroho: Utu wake wa ndani. Neno ambao sasa linaloionyesha hali yake. Kama tunampenda Mungu kwa moyo wetu wote na kumpenda jirani yetu, ndipo sasa tutachukuliwa kuwa wazuri.

 

Tunapoanza tu kuonyesha kuwa tunazaa matunda yapasayo toba, na kuanza kuzishika sheria za Mungu, kujua jinsi Mungu alivyo na maperzi yake, ndipo tutachukuliwa kuwa wathamani machoni pa Bwana. Tunastahili uzito wetu ni wa thamani kama dhahabu (Yakobo 1:25).

 

Hakuna mtu aliyemjua hapo kwanza. Sisi tunaomwabudu Mungu Mmoja na wa Kweli tunafananishwa na wanawali mabikira (Ufunuo 14:4). Sisi tunaompenda na kumtii Mungu Baba, wanamwabudu yeye kupitia kwa mwanae Yesu Kristo. Kama tukibakia kuwa waaminifu tutachukuliwa kama wanawali mwabikira.

 

Kwa suala la ibada ya ubatizo, tunashuka kwenda chini kwenye kisimani au kwenye bwawa lenye kina kirefu lenye maji. Tunapaswa kuzama mwili wote. Tunapopanda kutoka humo majini, tunapewa Roho Mtakatifu (Matendo 8:39). Kwa hiyo, aliliona hitaji la kujaza chombo chake maji ya kisima, ambayo ni Roho Mtakatifu.

 

Kwenye injili ya Mathayo tunasoma tukio la Roho wa Mungu akishuka chini kama hua na kumkalia Kristo mabegani mwake (Mathayo 3:16). Hii ilikuwa ni kuonyesha kuwa Kristo alikuwa hapa duniani katika mwili na alipokea Roho Mtakatifu kwa hali hiyo.

 

Mwanzo 24:17 Ndipo yule mtumishi akapiga mbio kwenda kumlaki, akasema, Tafadhali unipe maji kidogo katika mtungi wako

 

Na mtumishi akamkimbilia na kukutana naye – huu ni mwendelezo. Mara tu tunapopanda kutoka majini, tunakuwa burudikoni, au kukutana na Roho. Roho ndiye anayetupekelea kwenye ubatizo. Kabla ya ubatizo unapofanywa ndani yetu, lakini nje yetu. Baada ya ubatizo wa kuzamishwa majini pamoja na kitendo cha ‘kuwekewa mikono’ Roho huja ndani yetu na kufanyika kuwa sehemu yetu.

 

Kristo alipanda kutoka majini na Roho wa Mungu alishuka juu yake. Rebeka “alipanda na kuja” na mtumishi (Roho wa Mungu) akamkimbilia na kukutana naye. Neno alikimbia inaonyesha kasi ambayo ilitumika. Ilikuwa ni haraka, mara moja. Tumepewa Roho Mtakatifu na tumetolewa kwa Kristo anayeishi ndani yetu (Wagalatia 2:20).

 

“Tafadhali nipe ninywe kidogo kwenye mtungi wako” (aya ya 17). Inatupasa kila wakati kuwa kwenye mazingira ya kiroho tunapoweza kuwasaidia wengine kwa siri za Mungu. Haitupasi kabisa kukimbia mbele tukiwa watupu. Vifaa vyetu vinatakiwa vijae Roho wa Mungu wakati wote.

 

Rebeka alijaza mtungi wake na kuubeba begani mwake. Aliifanya kazi yake kikamilifu na kwa uaminifu mkubwa, kiusahihi na kwaufanisi mkubwa. Tumepewa kazi ya kufanya na haitupasi kuruhusu sisi wenyewe kuiharibu au kujikanganya kutoka kwenye wito wetu na kutoka kwenye kazi tuliyopewa. Yatupasa kushikilia kile tulichonacho, ili mtu asiitwae taji yetu (Ufunuo 3:11).

 

Kwa kweli, Rebeka hakumpa Yule mtumishi kinywaji. Bali aukijaza mtungi wake na halafu aliondoka na kurudi nyumbani. Wakati mwingine hata sisi inatupasa kuwa waangalifu sana na mtu tunayempa kinywaji kutoka mtungini mwetu. Hatupaswi kutupa lulu zetu mbele ya nguruwe (Mathayo 7:6). Kama mtu ana kiu ya neno la Mungu, ni yeye ndiye atakayeomba kinywaji, na inatupasa sisi kuwapa kinywaji ili kuzima kiu chao. Sio kila mtu anapenda kunywa maji yaliyo kwenye kisima cha uzima. Bali kama “mtu anakiu”, ndipo inatupasa kumsaidia na kukomesha kiu cha kuitafuta kweli aliyonayo.

 

Mtumishi alimtazama Rebeka alipokuwa anaujaza mtungi wake, na ndipo alijua kwamba mtungi wake aulikuwa umejaa maji. Wale waliokaribu yetu wanapasa kuona kwamba tumejazwa na roho aliye tofauti na wao, roho wa kweli. Alimwangalia akiwa anakwenda kwenye shughuli zake za kila siku na kuona kwamba alikuwa ni mwanamke mchapakazi na anaweza kufanya kazi zake. Ndivyo ilivyo, watu wanapoyaona matendo yetu jinsi tunavyoishi watakuja kwetu, wakiitaka kata ili wanywe maji tunayokunywa sisi kutoka kisimani.

 

Mwanzo 24:18 Naye akasema, Unywe, bwana wangu, akafanya haraka, akatua mtungi wake mkononi mwake, akamnywesha.

Kwa haraka sana akamwambia kunywa, bwana wangu. Hatupaswi kumkataza mtu yeyote anayetuomba amjue Bwana. Rebeka alionesha kwa mfano roho ya Kanisa. Yatupasa kutoa msaada kwa hofu, kicho na kutetemeka (Ufunuo 22:17).

 

Rebeka alimwamini na kumuonyesha heshima mtuishi wa Ibrahimu na kumuona kuwa bora kuliko yeye mwenyewe. Kwa kumuita kwake ‘bwana’ alijinyenyekeza mwenyewe na kujishusha kiasi cha kuwa kama mtumwa au mtumishi. Yatupasa kusaidiaana na kutumikiana kila mmoja na mwenzake kwa upendo (Wagalatia 5:13).

 

Tunaweza pia kuona kwamba aliutua mtungi wake chini mikononi mwake. Tunapowatumikia wengine, inatupasa kuweza kusaidia kwa mikono yetu wenyewe au uwezo wa kuweza kunena hivyo.

 

Rebeka hakumpa Eliezeri mtungi wake ili ajihudumie mwenyewe. Alikimwaga. Watu wengine hawana ujuzi au kuwa imara vya kutosha kwenye neno la Mungu kuweza kujisaidia wenyewe. Yatupasa kujua hili na kujenga kile tunachoweza (Matendo 20:32).

 

Kristo alikuwa bwana wetu na mkuu wetu, lakini aliwaosha miguu wanafunzi, kitendo tunachotakiwa kila mwaka kwenye adhimisho la Ushirika wa Meza ya Bwana, tunapomkumbuka (Yohana 13:14). Hatimaye aliutoa uhai wetu kwa ajili yetu. Hii ni tabia anayoitaka Baba tuwenayo (1Yohana 3:16).

 

Kristo hakuona kuwa sio tu kuwa aliwaona wale walioitwa na Baba kuwa wana kiu ya maji ya uzima, bali aliyaona pia mataifa (ngamia) kuwa walihitaji kunywa kwenye kisima cha uzima. Alijua kwamba ilimpasa kuutoa uhai wake, kwa ajili yetu ili tumpokee Roho Mtakatifu wa Baba, iwe kama sisi tulikuwa Wayahudi au Wayunani.

Mwanzo 24:19 Hata alipokwisha kumnywesha akasema, Na ngamia zako nitawatekea, hata watakapokwisha kunywa.

 

 Hapa Rebeka alikuwa anaonyesha kwamba yeye alijua na kuelewa mahitaji ya kiu kwa ngamia. Hii ilikuwa ni zaidi ya tendo la wema au ukarimu.

 

Mithali 12:10 Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.

 

Tumeitwa ili tuwe watakatifu na inatupasa kufikirie maisha na hali au mambo ya wengine. Kuweka kiusahihi sana, kunamaanisha dhana ya “mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe,” (Kumbukumbu la Torati 6:4). Kristo hakufa kwa ajili ya watu wa daraja moja maalumu la kimaisha. Bali alikufa kwa ajili ya watu wote. Inatupasa kuwa wema kwa watu wote na sio kwa kuwabagua wengine. Tumeambiwa kuwapenda hata adui zetu (Mathayo 5:44).

 

Kwa upendo aliomuonyesha huyu mgeni na wanyama wake, Rebeka kwa kweli alikuwa anatafuta urithi wake mwenyewe. Kanisa (Rebeka) linatafuta urithi wake (Mataifa). Kwa kuwapenda majirani zetu sasa, tunawatafuta wale watakaokuwa kwenye uangalizi wetu (Ufunuo 2:26-27). 

Mwanzo 24:20 Akafanya haraka, akamwaga maji ya mtungi wake katika birika, akapiga mbio kisimani ateke, akawatekea ngamia zake wote.

 

Rebeka kwa haraka sana alimwaga mtungi wake kwenye chombo. Yatupasa wakati wote kuipa kipaumbele tabia ya kuwasaidia wengine. Hatuwezi kuruhusu wale wanaoomba mwongozo wa kiroho wafe kwa kiu. Yatupasa kuchukua hatua mara moja. Mungu amewaita watu kutoka kwenye mataifa yote, na yatupasa kufanya kila linalowezekana kuona kwamba wote wanaweza kupokea maji yatoayo uzima aliyonayo Mungu kwa Mwanae Yesu Kristo (1Wakorintho 12:13).

 

Tunaona kwamba hakuna tofauti kati ya vitakatifu na vilivyo najisi. Ngamia wa Eliezeri alikunywa maji kutoka kwenye kisima hichohicho. Tumepewa Roho huyohuyo, lakini kwa uwezo na vipawa tofauti.

 

Rebeka aliweza kukijaza na kumwaga mara kadhaa. Watu wengine wanaomtoa Roho kwenye kuwahudumia wengine wanaona ni vigumu kutosheleza roho yao. Lakini haitupasi kuchoka kuwatumikia wengine. Yatupasa tuweze kuonyesha roho ya huruma na kupendana sote.

 

Mwanzo 24:21 Basi yule mtu akamkazia macho, akanyamaza, ili ajue kwamba Bwana ameifanikisha safari yake ama sivyo.

 

Tunaweza kujifunza kutoka kwenye aya hii kwamba mtu huyu anamuwakilishwa hapa Kristo, kama sisi sasa tulivyotolewa kwake. Tumebatizwa kwenye mwili wa Kristo. Hii inatuonyesha kuwa ni Baba peke yake ndiye mwenye uweza wa kujua kila jambo (ajuaye kila jambo). Kristo hajui matokeo ya kila kitu. Ni Baba aliye mbinguni peke yake ndiye anajua mambo yote (Mathayo 24:36). 

Mwanzo 24:22 Ikawa, ngamia walipokwisha kunywa, yule mtu akatwaa pete ya dhahabu, uzani wake ulikuwa nusu shekeli, na vikuku viwili kwa mikono yake, uzani wake ulikuwa shekeli kumi za dhahabu, 23 akasema, U binti wa nani wewe? Tafadhali uniambie. Je! Iko nafasi katika nyumba ya baba yako tupate mahali pa kukaa kwa muda?

 

Utoaji wa vikuku mikononi mwake na “pete puani” mwake au kiusahihi zaidi vito kwenye paja la uso; sawa na linavyosema jarida la Chimbuko la Uvaaji wa Ndewe na Vito vya Thamani Nyakati za Kale (Na. 197), inahusiana na ununuzi wa mwanadamu mzima inayoulizwa na kufanya upatanisho.

 

Tunahukumiwa kwa matendo yetu, ambayo kwa namna mbalimbalia yanahusika na mkono, ikiwakilisha mtu mzima yote (Zaburi 24:4, Matendo 2:23). Mkono unaweza kuwakilisha kikundi; “mkono wa maadui zangu,” (Zaburi.31:15); taifa; “mkono wa Wamisri,” (Kutoka 3:8); na inatumika kuelezea wakati, “Tubuni kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia,” (Mathayo 3:2, Mathayo 4:17). Mkono unamaanisha pia njia ambayo Kristo alitumia kuponya: “Yesu alinyoosha mkono wake na kumkamata” (Mathayo 14:31); "Binti yangu ndiye kwanza amekufa, lakini njoo uweke mkono wako juu yake naye atakuwa hai" (Mathayo 9:18). Sisi pia tunaitumia mikono yetu tunapoomba (Mwanzo 14:22). Mkono unamaanisha udhaifu au uweza na unatumika kwa baraka (Mwanzo 48:14,17); na kwenye ibada (Walawi 14:26,27).

 

Vikuku viwili vinawakilisha pande mbili zote, yaani upande wa kuume na kushoto, vinaashiria udhaifu wa kimwili (kushoto) na uimara wetu wa kiroho (kuume). 

 

Waebrania wote wawili, yaani mwanamke na mwanamume walivaa vikuku. Kanisa limefanyika kwa mkusanyiko wa wanaume na wanawake nasi ni Wayahudi wa kiroho (Waebrania) (Warumi 2:29). Vikuku ni nishani ya hadhi ya juu au unyenyekevu (2Samweli 1:10). Tumefanywa kuwa ni makuhani wa kifalme (1Petro 2:9) wa nyumba ya Daudi. Vikuku vinatengenezwa kwa malighafi ya thamani. Sisi ni wa thamani machoni pa Bwana (Zaburi 116:15; Zaburi 35:17). Vikuku vinatengenezwa kwa dhahabu. Mungu Mwenyezi atakuwa dhahabu yetu, yaani tajiri wa imani (Ayubu 22:25).

 

Katika siku za kale, vikuku, ambazo zinaashiria umuhimu vilivaliwa mkononi. Vikuku vilivyozoeleka kuvaliwa na mwanamke vingeweza kuvaliwa mkononi, kama ilivyo leo. Rebeka alipewa vikuku mikononi mwake kama zilivyokuwa zikivaliwa na wanawake wa kawaida yeyote angaliyeona hivyo. Bali hii ilikuwa ni kuonyesha kuwa Mungu anavitumia vitu dhaifu vinavyoonekana kuwa vya muhimu (vya kawaida) ili kuwashinda wenye hekima na wenye nguvu (1Wakorintho 1:27).

 

Vikuku vilipimwa kwa shekeli kumi, kwa kulinganisha na bei ambayo mtu inampasa kuilipa kwa ajili ya mwanamke aliye na umri wa kati ya miaka mitano hadi ishirini (Walawi 27:1-5). Kristo alilipa gharama ya kutununua sisi, wakati alipoyatoa maisha yake. Vikuku na pete za puani zinahusiana pia katika kufanya upatanisho (Hesabu 31:49-50).

 

Mwanzo 24:24-25 Akasema, Mimi ni binti wa Bethueli mwana wa Milka, aliyemzalia Nahori. 25 Tena akamwambia, Kwetu kuna majani na malisho ya kutosha, na mahali pa kukaa wageni. 26

 

Wote wawili, yaani Eliezeri na Rebeka walikuwa wa imani moja. Sisi tulio wa imani moja haitupasi kufungiwa nira pamoja na wasioamini. Pia yatupasa kuzishika sikukuu zilizoamriwa na Bwana kwa pamoja kila inapowezekana.

Mwanzo 24:26-27  Yule mtu akainama akamsujudu Bwana. 27 Akasema, Na atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, ambaye hakuacha rehema zake na kweli yake kwa bwana wangu. Bwana akaniongoza mimi nami njiani hata nyumba ya nduguze bwana wangu.

 

Hapa mtumishi anamshukuru Mungu. Ni dhahiri sana kwamba mtumishi aliona kwamba vitu hivi vilivyotokea havikuwa vimetokea kwa nasibu vyote, na kwamba Mungu Baba alikuwa anajua na ameviruhusu kutokea kwenye mchakato huu wote. Anatoa kile kinachotakiwa na cha muhimu kwa wanaokihitaji. Nasi pia yatupasa kutoa shukurani kwa kila jambo.

 

Mtumishi ‘akiwa njiani’ inaonyesha kuwa alikuwa kweye njia ya kweli. Alikuwa kwenye njia ya wokovu. Tunapokuwa tunazitoa njia zetu kwa Bwana, mawazo yetu atayathibitisha (Mithali 16:3). Kristo anawaongoza wale wote walio wake.

Mwanzo 24:28 Basi yule msichana akapiga mbio, akawaambia watu wa nyumba ya mama yake mambo hayo.

 

Kanisa linalinda kweli ambayo limeaminiwa kwayo na Roho Mtakatifu anayekaa ndani yetu (2Timotheo 1:14). Tunawajibu na kazi ya kuitangaza na kuihubiri njia hii ya wokovu (Watendo 16:17). Kanisa linatoa ushuhuda ili kumshuhudia Yesu Kristo kwa Israeli wa namna zote mbili, yaani wa kimwili na kiroho.

Mwanzo 24:29-31 Na Rebeka alikuwa na kaka, jina lake Labani. Labani akatoka mbio kumwendea yule mtu kisimani. 30 Ikawa, alipoiona ile pete, na vikuku mikononi mwa nduguye, akasikia maneno ya Rebeka nduguye, akisema, Hivyo ndivyo alivyoniambia mtu huyo, basi akamjia mtu yule, na tazama, amesimama karibu na ngamia kisimani. 31 Akasema, Karibu, wewe uliyebarikiwa na Bwana, mbona unasimama nje? Kwa maana nimeiweka nyumba tayari, na nafasi kwa ngamia.

 

Israeli wa kimwili walitaka kuona utajiri wa kimwili wa Mungu, kabla hawajamuacha mioyoni mwao (nyumba). Labani hakuwa na tofauti. Hakuwa anayajali mambo mazito na muhimu yaliyoagizwa kwenye sheria, haki na rehema na imani (Mathayo 23:23). Alikuwa amependezwa au kuvutiwa na kujilimbikizia utajiri au mali, zaidi, badala ya kuzihifadhi kwa ajili ya kujiwekea utajiri mbinguni (Mathayo 6:20). Israeli wa kale walimjua jinsi alivyokuwa Mungu Baba, kwa kuwa walipewa torati kutoka kwa Adamu.

 

Labani anazijua ahadi za Mungu, kwa kupitia maneno ya dada yake Rebeka. “Ndipi mtu aliniambia,” kunaweza kumaanisha Torati iliyonenwa na Mungu, ambayo ilipitishwa chini. Dada yake Rebeka, kwenye mfano huu anawataja watu kama Henoko na Nuhu, ambao Roho wa Mungu alinena nao, kupitia Malaika wake, ambaye hatimaye alifanyika mwanadamu Yesu Kristo (Matendo 3:18-21).

 

Anaweza kufana milinganisho rahisi kutoka kwenye hadithi hii kwa jinsi inavyohusiana kwene maelekezo ya maadhimisho ya Pasaka. Kristo anawaambia wanafunzi wake waende mjini. Eliezeri alikuwa kisimani ambapo wanawake wa mji walikwenda (Mwanzo 24:15). Kristo alisema mtakutana na mwanamume akichukua mtungi wa maji; mfuateni mkaingie katika nyumba atakayoingia yeye. (Luka 22:10). Eliezeri mtumishi alimkuta mwanamke aliyekuwa amebeba gudulia la maji (Mwanzo 24:15) alimfuata kwa nyuma hadi nyumbani kwake.

 

Wanafunzi wa Kristo walimuomba washinde usiku kucha pale na kuhusu chumba cha wageni (Luka 22:11). Eliezeri alimuuliza kama kulikuwa na mahali (chumba cha kulala mgeni) ambapo angeweza kulala yeye pamoja na watu wake (wanafunzi).

Mwanzo 24:32  Na mtu yule akaingia katika nyumba, akawafungua ngamia; naye akatoa majani na malisho kwa ngamia, na maji ya kuoshea miguu yake, na miguu ya watu waliokuwa pamoja naye.

Kristo ambaye anashabihishwa na huyu mwanaume. Yeye ni mume wa kanisa la kiroho. Lakini alikuja kama mtumishi. Kristo kupitia Roho Mtakatifu, alijua pa kwenda. Kristo alikuja kwenye nyumba ambapo wanafunzi walikuwepo jioni ile (Marko 14:17). Huu ulikuwa ni wakati wakati Eliezeri alikutana na Rebeka na kisha akaenda nyumbani kwake.

 

Majani makavu na malisho au chakula alichopewa ngamia huyu kinaweza kuwakilisha chakula kikuu, kama vile mkate na mvinyo, ishara tunayoitumia kwa maadhimisho ya Meza ya Bwana. Mfano unaolinganishwa na ngamia unatuonyesha kuwa tulikuwa viumbe najisi kabla ya kutolewa dhabihu kwa Yesu Kisto. Tunaona mfano linganisho huohuo ukitumika na nabii Yeremia akiwaelezea watu ambao hawakuwa watii kwa Mungu wa Pekee na wa Kweli (Yeremia 2:20-24).

 

Maji yatolewa ili kuosha miguu ya watu waliokuwa pamoja naye. Kristo, katika usiku wa kabla ya Pasaka, aliwaosha wanafunzi wake miguu, watu waliokuwa pamoja naye, (Yohana 13:5). Kama tutaangalia kwa mtazamo wa kiroho kwenye ayah ii, tunaona kuwa ngamia walikuwa mfano wa wanafunzi pia kama viongozi wa makabila na kisha mataifa kwenye hali yao ya unajisi wa kiroho.

 

Ni wale waliobatizwa tu ndio wanaruhusiwa kushiriki ibada hii ya kuosha miguu. Wale wanaoshiriki mlo hawalazimiki kuwa wamebatizwa. Hii inaongezeka kutokana majani waliyopewa na kuwalisha ngamia. Tunaonyeshwa kwa wazi sana, kwamba tunachukuliwa kuwa ni safi kiroho, wakati tunapobatizwa na kuwa sehemu ya ibada kua kuoshana miguu (1Petro 2:10; Matendo 11:9).

Mwanzo 24:33-34  Akaandaliwa chakula, lakini akasema, Sili mpaka niseme kwanza maneno yangu. Akamwambia, Haya, sema. 34 Akasema, Mimi ni mtumwa wa Ibrahimu,

 

Hii inafanya taswira ya Kristo kwenye mlo wake wa mwisho. Kristo alijua hangeweza kuula mlo wa Pasaka akiwa na wanafunzi wake, kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa ni Mwanakondoo wa Pasaka, aliyeuawa hata kabla ya kuwekwa misingi ya dunia (1Petro 1:20; Luka. 22:14-16).

 

Kristo alikuwa anasema kuwa angeila hii pamoja nao hapo yote yatakapotimilika. Na ndivyo ilikuwa kwa Eliezeri hakuweza kula chakula hadi mpango wake wa kumtafutia Isaka mke ukamilike.

 

Eliezeri anatangaza kuwa amekuja pale kwa jina la Bwana wake Ibrahimu. Hii inamuashiria Kristo aliyetumwa na Mungu Baba. Mtumishi si mkuu kulikb Bwana wake (Mathayo 10:24). Eliezeri, kama Kristo, alikuja kwa jina la Bwana wake. Hakusema maneno kwa mamlaka yake mwenyewe, au mapenzi yake mwenyewe. Bali aliyatenda mapenzi ya yeye aliyempeleka (Yohana 6:38).

 

Ni kama Kristo, Eliezeri anakuwa ni taswira ya Roho Mtakatifu aliihubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu, kama alivyoelezea kwenye kadamnasi ya watu waliokuwa kwenye nyumba hiyo sababu iliyomleta pale na kile alichotumwa kuja kukifanya. Pia alielezea maelezo ya jinsi alivyokutana na Rebeka kama ilivyoelezwa kwa kina kwenye Mwanzo 24:35-49. Kuna mambo muhimu yanayofanana hapa na wanafunzi na jinsi walivyoishi na Kristo kwenye injili za Agano Jipya.

 

Kristo alikuwa anaihubiri injili kwenye nyumba ya Labani. Hii inatuambia sisi kuwa mataifa waliujua mpango wa wokovu. Walitumiwa kila mara watumishi ili kuwafunulia mapenzi ya Baba. 

  

Mwanzo 24:50-51 Ndipo Labani na Bethueli wakajibu wakasema, Neno hili limetoka kwa Bwana, wala sisi hatuwezi kukuambia neno jema wala baya. 51 Tazama, huyo Rebeka yuko mbele yako, umchukue, ukaende zako awe mke wa mwana wa bwana wako, kama alivyosema Bwana.

 

Kristo alijitibitisha mwenyewe kuwa ni Mwana wa Mungu. Alikuwa amehitimisha kazi yake wakati alipoishi hapa duniani. Alikamilisha yote yaliyoandikwa kwenye maandiko matakatifu. Kila kitu kilifanyika sawa na kama Mungu alivyosema huko nyuma kwa kupitia manabii wake.

 

Mwanzo 24:52-53  Ikawa mtumishi wa Ibrahimu aliposikia maneno yao, akainama hata nchi mbele za Bwana. 53 Kisha huyo mtumishi akatoa vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na mavazi, akampa Rebeka; na vitu vya thamani akampa nduguye na mamaye pia.

 

Rebeka ndipo sasa akaposwa na Isaka. Nasi tu wachumba wake Kristo. Tumepambwa kama bibi arusi.

 

Mwanzo 24:54 Wakala wakanywa, yeye na watu waliokuwa pamoja naye, nao wakakaa usiku. Wakaondoka asubuhi, naye akasema, Nipeni ruhusa niende kwa bwana wangu.

 

Tunaweza kudhania hapa na kusema kuwa watu waliokula chakula pamoja naye, ni wale walioshiriki maadhimisho ya mlo wa Meza ya Bwana. Kwa jinsi hiyohiyo ndivyo wanafunzi walikuwa pamoja na Kristo, wakishinda usiku kucha, ili kutuonyesha sisi kwamba Meza ya Bwana ni sehemu ya maadhimisho ya Sikuuu ya Pasaka. Yatupasa kuuadhimisha usiku huu siku ya 14 ya mwezi wa Kwanza. Wote walikuwa pamoja kama tunavyofanya kwenye maadhimisho ya siku takatifu.

 

Kristo alifufuka toka kwa wafu siku ya Jumamosi adhuhuri, baada ya kushinda kwa siku tatu, usiku na mchana kwenye tumbo la kaburi. Tunaweza kudhani kwa udadisi kwa haya yafuatayo: Kisha akaamka asubuhi - Krist alipaa kwenda mbinguni mnamo saa za mapema za siku ya Jumapili. “Nipeleke mbali kwa Bwana wangu” - Kristo alipokuwa anafufuka kimwili, alijiandaa kwenda kwa Baba. Kristo alitaka arudi mbinguni kwa Mungu wake. Alikuwa amefufuka, na sasa alipaswa atolewe kama Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa, wakati wa asubuhi. Alipaswa kuwakilisha limbuko la kwanza la malimbuko yote.

Mwanzo 24:55 Ndugu yake na mama yake wakasema, Msichana na akae kwetu kama siku kumi, zisipungue, baadaye aende.

 

Msichana na akae kwetu kama siku kumi, zisipungue " inahusika na mlolongo wa wakati. Tunajua kuwa siku moja ni sawa na miaka elfu kwa Bwana na ndivyo ilivyo kinyume chake (2Petro 3:8).

 

Kitendo cha kumchukua mke kutoka kwenye familia ya Ibrahimu kilifanyika kwenye wastani wa takriban miaka 4000 iliyopita. Wale ambao walimfanya bibi arusi, wliochaguliwa na Mungu, walianza kwa kiasi kikubwa tangu kipindi cha Ibrahimu (lakini walikuwepo wengine kabla yake). Bibi arusi huhu alikuwa ndiyo kwanza kwenhye umri wake wa utoto. Alikuwa ni kijana, kwa hiyo kulikuwa ni kipindi kirefu cha yeye kutunzwa. Hii ni kutuonyesha sisi kwamba Kanisa lingekuwepo na kubakia hapa duniani kwa siku chache au kwa kitambo kipindi kinacholinganishwa na miaka elfu nne. Kanisa limepitia kipindi cha miaka elfu mbili cha kuandaliwa kwake na kipindi kingine cha miaka elfu nne ya kuitwa na kutolewa nje.

 

Usemi wa kwamba Hata kwa siku kumi; baada ya hapo anaweza kwenda unatuambia kwamba kanisa lingeweza kubaki hapa hadi kila kitu kikamillike (10) hadi wateule wengine waliosalia watakapoletwa kutoka waliko. Baada ya hapo anaweza kwenda. Baada ya yote wateule watakuwa wametiwa mhuri, ndipo tunaweza kwenda, kama wana wa ufufuo, na kuolewa kimfano na Kristo.

 

Mwanzo 24:56 Naye akawaambia, Msinikawilishe, mradi Bwana amefanikisha njia yangu; nipeni ruhusa niende kwa bwana wangu.

Bwana Mungu ameifanikisha njia ya mtumishi kwa hiyo alikuwa na hamasa ya kwenda nyumbani kwa Bwana wake Ibrahimu. Kristo alitaka arudi nyuma kwa Mungu wake. Alikuwa amekwisha fufuka tayari, na sasa alikuwa anataka kupaa kwenda mbinguni ili kwenda kuchukua urithi wake akiwa kama limbuko la kwanza la malimbuko yote.

Mwanzo 24:57 Wakasema, Na tumwite huyo msichana, tumwulize mwenyewe. 58 Wakamwita Rebeka wakamwuliza, Je! Utakwenda na mtu huyu? Akasema, Nitakwenda.

 

Wasiwasi au swali lililokuwa kama Rebeka angekuwa radhi kuolewa na Isaka. Neno wkaimuita linatuonyesha kuwa Mungu Baba yetu anatuita kwa kila mmoja peke yake na kutuuliza kama kumfuata Kristo. Ni uamuzi wa kila mmoja peke yake. Ulimwengu huu uliobakia una wito wake wenyewe.

 

Rebeka alijua kuwa walikuwa wanaingia kwenye agano la muda mrefu. Wakati tunapoitwa, tumepewa fursa ya kuingia kwenye agano la kupendwa na Mungu na Kristo wake. Wakristo hatushurutishwi kinume na tupendavyo ili kumfuata Kristo. Tumepewa uchaguzi. Mungu anampenda aina ya mtu aliyetayari kutoa kila kitu kwa ajili yake, na kuungana na mwanae, Yesu Kristo.   

 

Mwanzo 24:59-61  Ndipo wakampeleka Rebeka ndugu yao, na yaya wake, na mtumishi wa Ibrahimu, na watu wake. 60 Wakambarikia Rebeka, wakamwambia, Ndugu yetu, uwe wewe mama wa kumi elfu, mara elfu nyingi, na wazao wako waurithi mlango wa hao wawachukiao. 61 Rebeka akaondoka na vijakazi wake, nao wakapanda juu ya ngamia, wakamfuata yule mtu. Naye huyo mtumishi akamchukua Rebeka akaenda zake.

(Tafsiri ya NRSV inatafsiri sentensi ya mwisho kama; Naye huyo mtumishi akamchukua Rebeka akaenda zake)

 

Usemi kwamba Ndipo Rebeka na mtumishi wake wakainuka kuondoka. Tulivhukuliwa kama mtu aliyekufa kiroho (Waefeso 2:5; Wakolosai 3:3). Tangu tunapobatizwa tunapewa Roho Mtakatifu, kwa njia ya Kristo. Sikukuu ya Pentekoste ni taswira ya ukweli huu. Tumetakaswa sasa.

 

Rebeka alibarikiwa kuwa ni mama wa makumi elfu na maelfu na uzao wake uliambiwa utamiliki malango ya adui zao. Baraka hii iliendelea hadi kwa kupitia mataifa yaliyoinuka kutoka kwake. Kwenye uzao wake ndipo makabila yaliyaongoza mataifa ya wamataifa na mataifa yote ya dunia yaliyoingia Kanisani kama bibi arufi wa Kristo kwa Roho Mtakatifu kwenye Ufufuo wa Wafu.

 

Ndipo tunasoma kuwa Rebeka alipanda juu ya ngamia (mataifa) na kumfuata mtu ni taswira ya Roho Mtakatifu na akaenda kwa Isaka anayemwakilisha Kristo mfufuka.

 

Kabla hatujazaliwa, tulitakaswa. (Yeremia 1:5). Ingawa tunaishi duniani hatumo sehemu yah ii. Na dniyo maana tumepanda na kuwaendesha ngamia. Sisi tumetengwa, wtakatifu. Tumetumwa kuyaendea mataifa, kuwaamsha ili wamjue Mungu, kupitia Kristo. Yatupasa tuwaongoze kwenye neema iokoayo katika Kristo.

 

Ukweli wa kwamba wajakazi wa Rebeka waliinuka na kwenda naye, unatuonyesha kuwa wageni pia wameruhusiwa kuhudhuria na kuadhimisha sikukuu (Yohana 12:20; Matendo 2:5-11). Tunaruhusiwa kuwa na watu kwenye sikukuu ambao hawajabatizwa ambao pia ni washirika kwenye mwili wa Yesu Kristo. Kutajwa kwa wajakazi kunatuambia kuwa wanawake wanatakiwa kuhudhuria sikukuu zilizoamriwa (1Samweli 1:3,9; Luka 2:41-42). Ilieleweka na Waisraeli wa zamani kuwa jinsia zote mbili, yaani wanaume, wanawake hata pia na wageni walio ndani ya malango yao, wanapaswa kujihudhurisha kwenye sikuku. Kwa kufafanua, ni kwamba hii iliendelea hadi kwa wateule wakiwa kama Israeli wa kiroho. Ni wanaume tu ndio wamelazimishwa kuhudhuria sikukuu na Torati. Wanawake wanaweza kusamehewa kutokana na sababu za kimaumbile au za kimwili kwa wakati fulani, lakini nao wanatarajiwa kuhudhuria.

 

Tunatolea nje na kutoka. Hii inaashiria kuwa ni tukio la kutoka ya pili itakayokuja kutokea. Rebeka analiwakilisha kanisa la kiroho na wale wajakazi wake wanawakilisha taifa halisi la kimwili la Israeli. Walipanda juu ya ngamia, inaonyesha kuwa kwa njia ya mataifa, tutarudi nyuma nyumbani kwetu, ambako kutoka huko tulifarakana na kutawanyika. Hebu na tumfuate Kristo.

 

Ndipo mtumishi akamchukua Rebeka. Neno akamchukua linatokana na SHD 3947. Linaweza kuwa na idadi kadhaa ya maana zake, ambayo yanaweza kuhusiana na taswira yote iliyoko ya mwanadamu. Tumetwaliwa kutoka kwenye imani potofu, tukanunuliwa kwa bei, kwa ajili ya Kristo, tukiandaliwa kwa arusi. Sisi tumechaguliwa, kizazi kiteule kitakachopelekwa kwenye ndoa.

 

Kutokana na neno hili la kutwaliwa tunaweza kuona dhana inayofanana kutoka kwenye hadithi ya uumbaji, kwenye Bustani ya Edeni, wakati Bwana alipoutwaa ubavu kutoka kwa Adamu. Neno hilihili limetumika, kwa uzito kwene Mwanzo 24:61 ‘ndipo mtumishi akamchukua Rebeka’.

Mwanzo 2:21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.

Mungu alisababisha usingizi mzito aupate Adamu ili amfanyie mke. Akachukua mmoja ya ubavu wake na akamfanyia (inasomeka “kumjengea” kwa Kiebrania) mwanamke. Kutokana na hii twaweza kutofautisha kutwaliwa kwa kanisa. Kanisa limeondolewa na mwanadamu (mtu) wakati usingizi mzito wa kiroho uliwaangukia wao. Tunajua kwamba Adamu wa kwanza alitenda dhambi, na kwa hiyo Kristo alikuja ili awe Adamu wa pili. Ni kama vile Mungu alivyoutwa ubavu mmoja, ndivyo hata sisi tumetwaliwa tutoke (duniani). Tunafanyika kuwa washirika binafsi wa mwili wa Kristo (1Wakorintho 12:27).

Neno ubavu linatokana na kamusi ya SHD 6763 tsela na lina maana mbalimbali. Tafsiri ya The Authorised Version inalitafsiri neno hili kama 1.upande, ubavu, bimu. 1A Ubavu (wa mwanadamu). 1C upande wa chumba au seli (za[li] muundo wa hekalu). Sisi ndio Hekalu hilo la Mungu (1Wakorintho 3:17).

Mwanzo 24:62 Basi Isaka alikuwa amekuja kwa njia ya Beer-lahai-roi, maana alikaa katika nchi ya kusini.

Kristo alkuja kutoka, kuwa kwamba aliumbwa na kutumwa aje, kutoka kwenye njia, ambayo ndiye Baba aliye “kisima cha uzima na maono” (Lahai Roi). Kwa kuwa Eloa ni kiini cha uzima. Mungu wa Milele, (1Timotheo 6:16) anayemwangalia kwa jicho lake mwenye haki na mtakatifu wake, akitungoja sisi ili tumuone yeye pia, wakati Kristo atakaporudi (Matendo 22:14).

 

Mwanzo 24:63 Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni; akainua macho yake, akaona, kuna ngamia wanakuja.

Isaka alitoka nje ili atafakari shambani wakati wa jua kupunga. Tunaweza kujipatia maarifa makubwa ya tukio hili, wakati tunapoipitia aya hii ili kuipata taswira halisi. Kuelewa kile kinachomaanisha kwenye kifungu hiki kisemacho alitoka nje na kujua kinachokusudia, kutatusaidia kuifafanua maana ya aya hii.

Kwa mujibu wa kamusi ya (SHD 3318) toka nje, ondoka. Kuondoka na kwenda (kwenda mahali),kuendelea na kwenda (kwendamahali au  kwenye kitu fulani). 1A4 kuja au kwenda mbele (kwa nalengo au matokeo). Kutoa nje, kusukumia nje. 1B2 kutoo nje ya. 1B3 kusukumia nje.1B4 kutoa, kutolewa nje au kusukumwa mbele.

Strong, J. (1996). Enhanced Strong's Lexicon (H3318). Ontario: Woodside Bible Fellowship.

Kristo alitoka nje kutoka kwa Baba. Aliondoka kutoka mbinguni na akatoka kuelekea (mahali), duniani. Ndipo Kristo aliendelea, akiwa kama kondoo wa kuchinjwa. Tangia kufufuka kwake, alifanyika kuwa limbuko la malimbuko yote (kwa au kwa ajili ya kitu Fulani) akaenda kwa Baba na kuwa ni mleta wokovu. (ambalo ndilo lengo au matokeo) kwa wote wenye mwili. Kristo sasa anakuwa na jukumu la kuwatoa watu, na kupeleka nje ya ulimwengu huu, kuwatoa nje kutoka gizani, na kuwatoa kutoka utumwani, hivyo kuwatoa, kutolewa na kutengwa kama taifa takatifu.

 

Isaka alitoka nje kutafakari uwanjani majira ya adhuhuri. Yatupasa kuliangalia jambo hili neno kutafakari maana yake. Linatoka kwenye SHD 7742 suwach. Inalitafsiri kama “kutafakari” mara moja. Kutafakari, kufikiri, kupata hisia, kuongea, kulaumu. (Strong, J. (1996). Enhanced Strong's Lexicon (H7742). Ontario: Woodside Bible Fellowship.)

 

Tunapoliendeleza kila neno linaloleta maana ya kutafakari kwa upana kidogo, tunaiona taswira ikiendelea.

1.Kutafakari = fikiri, ashiria, weka huru, fikria, waza                                          

2.Kikundi cha watu = jamii, wasiliana, semezana, shamba la jamii                      

3.Sema = semezana, zungumza, wasiliana papo kwa papo, ambia

4.Lalamika = pinga, kosoa, tafuta au gundua makosa

 

Tunauona mwandamano wa matukio. Kile tunachoweza kukipunguza ni muda muafaka na kusudi au lengo la kurudi kwa Kristo. Kristo anawazia tu kuyatenda mapenzi ya Baba. Anaonyesha uhalisia wake. Anarudi kwenye jamii ambayo aliishi nayo, shamba la jamii ambalo ni mwanadamu, tungaliweza kusema. Kipindi hiki atayasema mambo yote yamhusuyo mwanadamu, lakini wakati anapoongea, itakuwa na upanga wenye makali kuwili. Kristo amekuja kuiokoa dunia. Anakuja kwa namna ya upinzani, kwa utovu wetu wa nidhamu. Kwa kuwa amelikuta kosa kwa jinsi tunavyoishi.

Shamba darasa liko mbali na kuingiliwa au kukanganywa. Wakati tunapotafakari na kujumuika pamoja kwenye siku za ibada, yatupasa kuweza kufikiri, kuwa kielelezo cha neno la Mungu na kuwasiliana kila mmoja na mwenzake, kwa njia ya kimazingira kutokana na mikanganyo ya mwingiliano na vishawishi vya ulimwengu huu.

Tunajua kwamba wakati Kristo atakaporudi, atarudi huko Yerusalemu. Wale ngamia waliokuwa wanakuja, tunajua sasa kuwa ni mataifa yatakayojikusanya karibu au kuuzunguka mji wa Yerusalemu ili kufanya vita au kupigananao (Ufunuo 16:12). Kuna idadi fulani ya matukio yatakayodhihirika wakati Kristo atakaporudi.

Mwanzo 24:64 Rebeka akainua macho, naye alipomwona Isaka, alishuka juu ya ngamia.

Tunaona mataifa yalijongea ili kuusogelea mji wa Yerusalemu. Ni sawa kama ule mfano wa mtini, tunaweza kuyaona matukio haya yakidhihirika. Sisi tuliodumu kuwa waaminifu kwa Mungu, na kuufanya mwili wa Kristo, tutashuhudia. Hakuna mwingine yeyote alyetajwa. Hakutajwa suria wake wala mtumishi awaye yote. Hii inalilenga moja kwa moja kanisa (Luka 21:27-28). Ni ukombozi wetu, sio wa mataifa. Kristo anakuja kuwaokoa wateule (Mathayo 24:22).

Sasa tunaona jambo linguine la matukio yanayojidhihirisha wakati Kristo atakaporudi. Tunapomuona Kristo, tunakuwa tumeshushwa, au maelezo yanayofaa zaidi ni kwamba tumefufuka kutoka kwa mataifa.

Ngamia tunaowaendesha ni mataifa tunayoishi kwayo. Ni Rebeka tu ndiye aliyeshuka; hakuna mtu mwingine aliyefanya. Tunaona kuwa tumefufuliwa kutoka kila moja ya mataifa yetu. Tunaona kuwa Rebeka alishuka kutoka juu ya ngamia wake. Hii inatuonyesha kuwa sisi kama mmoja mmoja tupo kwenye mataifa yetu wenyewe. Hivi ndivyo inavyomaanisha hapa. Hatujakusanywa wote pamoja tukikaa juu ya ngamia mmoja. Tumetawanyika kwenye mataifa mbalimbali. Hakuna mahali pa usalama. Vinginevyo, angekuwa amekalishwa na wengine juu ya ngamia mmoja.

Wakati Rebeka alipoinua macho yake juu, inatuambia kitu fulani. Alijua kuwa alikuwa anakwenda kuolewa na mrithi wa utajiri na mali nyingi, ila bado alibakia kuwa mnyenyekevu. Kwenye safari yetu hatupaswi kuvimba vichwa vyetu kwa majivuno na kiburi, ila tujishushe chini kwa unyenyekevu (Isaya 2:11).

Kumbuka kuwa Rebeka hakuwahi kumuona Isaka hapo kabla. Lakina wakati alipomuona tu akiwa kondeni, alishuka kutoka juu ya ngamia wake. Asingeweza kushuka kwa mtu mwingine yeyote tu kwa kuwa alimwambia yule mtumishi akamuuliza “je, mtu huyu ni nani?” Yeye (kanisa) alijua kuwa alikuwa Isaka (Kristo).

Mwanzo 24:65 Akamwambia mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye bwana wangu. Basi akatwaa shela yake akajifunika.

Hadithi hii ipo kwenye Yohana 6:15-20 inaelezea jinsi Kristo alivyokuja kwetu, wakati tulipokuwa kwenye matatizo. Wakati tulipokuwa katikati ya mahali pasipojulikana, pasipo na tumaini, alitembea juu ya maji, ili atupate sisi. Anatenda miujiza. Wakati anapokuja kwetu wakati tunapokata tama, kwa haraka sana alipelekwa nchini, ambavyo ni salama. 

Ni kama Isaka alipotembea kondeni ili akutane na Rebeka, Kristo alitembea juu ya maji ili akutane na sisi. Wanafunzi wake waliogopa. Haitupasi kuogoa. Kristo kwa makusudi mazima alitupokea sisi. Siku zetu za mashaka na kukata tama zimekwisha. Waliletwa kwa haraka sana kwenye nchi, waliyokuwa wanaiendea. Nasi tunapelekwa kwenye nchi yetu ya kiroho, Yerusalemu. Huko ndiko tunakokwenda.

Mwanzo 24:65 Akamwambia mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye bwana wangu. Basi akatwaa shela yake akajifunika.

Neno la Kiebrania la shela au kilemba (SHD 6809), kutoka kwenye shina lake lisilotumika linamaanisha “kujifunga juu.” Inaweza kujulikana kama kufunika au kujizinga.

 

Tafsiri ya The American Standard Version inasema alichukua shela yake. Kwa hiyo aliichukua shela na kujifunika.

Kanisa linachukuliwa au kufananishwa na mwanamke, nasi tunalifanya liwepo Kanisa la Mungu. Ni kama tulivyokwisha soma tayari, sisi ni wanawali mabikira wa kiroho. Anaonyesha heshima na unyenyekevu anapokutna na mume wake.

Wakati Kristo atakaporudi, ndipo tutafufuliwa, na kuchukua shela za kubalidika kwetu na kuwa viumbe wa kiroho. Hii ndiyo ile shela tutakayojifunika kwayo. Miili yetu ya zamani sasa itakuwa imeondoka, na tutabadilika na kuwa wana wa Mungu wa Kiroho. Hili ndilo vazi letu jipya. Hatutakuwa wa damu na mwili tena, ila wa kiroho.

Zaburi 140:7 Ee MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu, Umenifunika kichwa changu siku ya vita.

 

Siku hii inafananishwa kama siku ya vita. Ni wakati Kristo atakaporudi kuchukua kile kilicho haki yake na kitakatifu sana. Atakichukua kwa nguvu. Mapepo hawaendi kumpa kwa urahisi. Tunafarijika kwa kuwa Mungu atakifunika kichwa chetu wakati Kristo atakaporudi. Kichwa chetu kinamaanisha mawazo yetu na hali zetu za mwili.

Mwanzo 24:66 Yule mtumishi akamwambia Isaka mambo yote aliyoyatenda.

 

Ni kwa njia ya Roho wa Baba ambayo vitu vyote vitafunuliwa (1Wakorintho 2:10). Baba yu ndani mwa Kristo, na Kristo yu ndani yake (Yohana 10:38)

 

Mwanzo 24:67 Isaka akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake, Sara, akamtwaa Rebeka, akawa mkewe, akampenda; Isaka akafarijika kwa ajili ya kufa kwa mamake.

 

Isaka alimchukua Rebeka na kumpeleka kwenye hema ya mama yake, kama sisi tunavyochukuliwa na Kristo kwenye Yerusalemu Mpya, Mama wa sisi sote.

 

Wazo la kuishi kwenye vibanda (hemani) lilikuwa ni kushinikiza utegemezi wa Israeli kwa Mungu, wakati walipokuwa wageni na wasafiri jangwani.

 

 (Aya ya 67)….. Isaka akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake,

Mama anawakilisha taifa la kimwili la Israeli. Kristo alikuja akitokea kwenye kabila la Yuda (Mathayo 2:1). Mwanamke aliye kwenye kitabu cha Ufunuo anawakilisha Israeli wa kimwili (na wa kiroho) (Ufunuo 12:13). Israeli wa kale hawakuupata wokovu kwa ujumla. Ni baadhi yao wakiwa mmoja mmoja waliweza kufanikisha. Tunaweza kuiita zama hii kuwa ni kama cha kufa. Kanisa lilimfariiji Kristo.

 

Kwa hili tunaweza kusema kwamba Kristo alifarijika baada ya kifo cha mama yake. Yerusalemu ile iliangamizwa na Yerusalemu Mpya itatujia kama Mji wa Mungu (soma jarida la Mji wa Mungu (Na. 180)). Sikukuu ya Mkutano wa Makini au Siku Iliyokuu ya Mwisho inawakilisha hukumu ya haki ya ulimwengu na kuondolewa kwa mwisho na ukomo wa dhambi. Inawakilisha ujio wa Mungu duniani na Mji wa Mungu utajiunga kwenye marejesho mapya ya mwisho. Marejesho haya ya mwisho ni matokeo ya mwisho ya Mpango wa Mungu.

q