Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[173]
Kipimo Cha Hesabu Kufikia Pentekoste
(Jarida 2. 0
19960803-20031006)
Kwenye miaka ya karne ya ishirini, Makanisa ya Mungu yalipita kwenye myumbo katika kufanya maamuzi kuhusu siku gani ya kuadhimisha sikukuu ya Pentekose kutokana na uanzishwaji wa Kalenda ya Hilleli na kupitia ushawishi wa imani ya Kizayuni ndani ya Makanisa ya Mungu. Jarida hili linafafanua kuhusu makosa na hatua zilizofuatilia mwanzo wake. Jarida hili linachua mahali pa jarida la awali lililoitwa Pentekose Ikilinganishwa na Walawi 23:11-22 kwenye Septuagin,(ambalo lilikuwa na namba kama hii hii [173].
Christian Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Copyright ã 1996, 2003 Wade Cox)
(Tr. 2005)
Masomo
haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kutufa maneno. Jina la mchapishaji na anuami
yake pamoja na hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya maelezo na kilugha
lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia ynapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti
yetu ya:
http://www.logon.org
au http://www.ccg.org
Kipimo Cha Hesabu Kufikia
Pentekoste [173]
Kumekuwko na hali ya kuchanganya miongoni mwa Makanisa ya Mungu katika kipindi cha ile karne ya ishirini kuhusiana na maamuzi ya siku gani tunaweza kuadhimisha Pentekoste. Tatizo lilijitokeza kwa ajili ya kushindwa kwa Kalenda iliyojulikana kama ya Hilleli. Kalenda hii ilianzishwa mwaka 358BK, iliamulia Mwandamo wa Miezi kuangalia muandamo wa mwezi mpevu ambayo kwayo walipunguza uwezekano wa idadi rasmi ya Miandamo ya Mwezi Mpya kwa mujibu wa mfumo na kanuni zilizokuwa zimewekwa kwa kufuata mapokeo ya marabi na siku au tarehe kamili ya Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa.
Kutokea kwa makosa ya wazi katika mfumo wa upangaji wa tarehe kikamilifu ulisababisha upangaji wa Pantekoste ya siku ya 6 ya mwezi wa Sivani, uelewa wa kihistoria wa Kanisa kama kupanga kwa Pentekoste ya kila mara ya siku ya Jumapili hata kwenye ulimwengu wa Wakatoliki, na kupata maagizo sahihi ya jinsi Maandiko Matakatifu yanavyosema, kufanikisha ili ifuate mfumo wa kalenda ya Hilleli katika mtazamo huu.
Kulingana na mwanzo huu wa kimakosa, Makanisa ya Mungu yalifuatisha mfumo huu wa kalenda ya Hilleli katikati ya karne ya ishirini. makosa haya yalitokana na matangazo ya Radio Kanisa la Mungu, na baadae kwa shirika lililojulikana kama Kanisa la Mungu la Ulimwenguni kote kifupisho kwa Kiingereza kilikuwa WCG. Mabadiliko yao katika mwaka 1974 yalisababisha mlolongo wa makosa kuendelea kufundishwa na kuyafanyia kampeni yapate kukubalika kwenye matawi ya makanisa yao.
Tuna makosa makuu mawili yaliyoshikiliwa na kufuatwa na Makanisa ya Mungu na la tatu linatokana na mfumo wa imani ya Wasamaria lililokubalika kufuatwa na kufanywa na kila mtu binafsi yake, zaidi sana kuliko mfumo wa kanisa lolote linalo maanisha.
Makosa hayo matatu yaliyotumika katika kuamua siku ya Pentekoste ni haya yafuatayo:
(1) Kuifanya Nisani 16 kuwa ni tarehe au siku kamilifu, jambo ambalo
limeungwa mkono na Wayahudi waliowengi wanaifuata mfumo wa kimamboleo
(waliochukua nafasi ya marabi wa Mafarisayo), na Wazayuni Fulani wanaotoka
kwenye Makanisa ya Mungu.
(2) Kuiweka kwenye Jumapili ya baada ya Sabato inayoangukia wakati wa
Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Haya yalikuwa ni mafundisho ya shirika hili
la Kanisa la Mungu la Ulimwenguni kote (WCG) waliyokuwa yakifundishwa hata
kabla ya mwaka 1974. Na bado yanaungwa mkono hata leo na baadhi ya vikundi vya
Kimasihi vinavyofuata maadhimisho ya siku ya Jumapili, au Jumatatu ya
Pentekoste.
(3) Kufuata hesabu ya Wasamaria inayoanzia kutokana na Miandamo ya
Mwezi kuanzia kipindi kile cha mchana na usiku kuwa na masaa au urefu sawa
(Equinox) na kuanzia kutoka Jumapili iliyoko katika kipindi cha Sikukuu ya
Mikate Isiyotiwa Chachu hata kama itaadhimishwa kwa namna hyo hiyo katika Mwezi
Unaofuatia.
Jumapili iliyoko kwenye kipindi cha Sikukuu ya Mikate isiyotiwa Chachu sasa inaungwa mkono kama ni siku sahihi ya Mganda wa Kutikiswa ya kihistoria ya Kanisa la Mungu la Ulimwenguni kote. (WCG) kuanzia mwaka 1974, na kwa vikundi vyake mbali mbali vilivyo jitenga baada ya mavinjiko yake makuu yaliyolikumba baadae, ingawaje hawaadhimishi siku ya Mganda wa kutikiswa kama inavyotakiwa kufanywa kwa mujibu wa kitabu cha Mambo ya Walawi 23. Hatahivyo bado wanakosea, hasa kwa sababu ya Uhairishaji, kama ilivyo kwenye mambo yote kuongelewa hapo juu, pamoja na Wasamaria walio imarisha uhairishaji kwa kipindi cha mwezi mzima kwa wastani wa karibu asilimia hamsini ya mambo.makosa ya muhimili wa mfumo wa Hilleli tangia mwaka 358BK au makosa ya Wasamaria kuhusiana na utaratibu wa Mwaka Mpya unaoanzia baada ya siku ile ambayo masaa ya mchana na usiku huwa sawa.
Makanisa ya Mungu, kihistoria, angalau hadi kufikia kipindi cha makosa kilichofanywa na WCG, ambacho kwanza kabisa ni kujaribu kwao kuishika siku ya 6 ya mwezi wa Sivani na halafu Pentekoste ya Jumatatu kuanzia mwaka 1974. Lakini huko nyuma wamekuwa wakiadhimisha lila mara Pentekoste siku ya Jumapili na utaratibu wa Hekalu wakati wote ulihusu kuadhimisha Pentekoste siku ya Jumapili. Hata katika kipindi ambacho Kanisa la Rumi lilipogawanyika na kujitoa kwenye mfumo halisi wa Kanisa la Mungu chini ya utata wa utaratibu wa mgawanyo wa Kumi na Nne (Quarto-deciman) katika mwaka 192BK waliona hakuna sababu ya kubadili njia ya kufanyia maamuzi ya kupata siku ya maadhimisho ya Pentekoste. Tatizo walilokaniliana nalo lilikuwa ni lile tu kwamba ilibadilishwa kwa kwa kufuatia maamuzi ya Easter peke yake (tazama jarida la Mabishano ya Mgawanyo wa Kumi na nne [277].
Nafasi hizi za kihistoria pia zimefanyiwa tathmini kwenye jarida la Majukumu ya Amri ya Nne kwa Makanisa ya Kihistoria Yaishikayo Sabato [170].
Masadukayo walilikimbia Hekalu wakati wa kipindi cha oparesheni yake na wakati wote waliadhimisha Pentekoste siku za Jumapili.
Hekalu lililokuweko Musri pia lilifuata utaratibu huu kama tuonavyo katika maandiko ya Septuagint (LXX) ambayo ilikuwa ni tafsiri rasmi ya lugha ya Kiyunani ya Agano la Kale na ambayo iliagizwa na kutafsiriwa huko Misri kwa ajili ya Wayahidi walioshi katika hali ya utawanyiko kule na Farao.
Ni kwa jinsi hiyo hiyo ndivyo Wasamaria walivyokimbia pia. Pentekoste yao ilikuwa katika siku za jumapili lakini zilitofautiana na tu kwenye ukweli wa kwamba walikuwa wameanzisha utaratibu wa mwanzo wao wa Mwaka Mpya unaoanzia baada ya ile siku ambayo masaa ya mchana na ya usiku yanakuwa sawa (equinox), wakati wote uliofuatia Mwandamo wa Mwezi Mpya baada ya kipindi hiki cha Equinox na sio siku ya karibu sana na siku ya tukio hili, kama ilivyokuwa kwa masuala ya mfumo wa Hekalu. Kwa jinsi hii takribani nusu ya muda walikuwa wanachelewa kiasi cha mwezi mmoja na Pasaka, adhimisho la kila mara la Pasaka ya pili kama ilivyokuwa ile ya kwanza. Hivyo basi uingizaji huu ilikuwa nje ya mlolongo pia hata kwenye mfumo wa Kiyahudi. Kwa hiyo wao waliadhimisha sikukuu katika mwezi wa nane ambayo ni makosa yaliyofanywa na Yeroboamu ambayo kwayo alilaumiwa na kuonywa na Mungu kupiitia manabii wake (tazama jarida la Yeroboamu na Kalenda ya Hilleli [191].
Mfumo wa Hekalu ulikuwa sahihi na ulifuatia sheria zilizoandikwa kama tunavyoona ikichuliwa na Masadukayo. Mfumo wa Hekalu umeafafanuliwa kwenye jarida la Kalenda ya Mungu [156].
Kulikuwa hakuna kuahirishwa ufanyaji kazi wake katika Wakati wote wa Hekalu. Hili liko wazi kutokana na mtungo wa kalenda Mishna mnamo kama mwaka 200 ambayo kutoka kwayo baadae kalenda ya Talmudi ilitungwa ikiwa kama fafanuzi. Inaonekana kama madai ya uongo ya wanazuoni wa bandia wa makanisa yale yale ya Mungu yaliyotafuta kudai kwamba Uhairishaji ulikuwa inafanyika kwenye vipindi vya Hekaluni kwa mujibu wa Talm,udi. Hata hivyo, hayo yalikuwa ni maelezo ya bure ya uongo yaliyochanganywa na ushahidi wa historia na wa Mishna yenyewe.
Mamlaka ya Kiyahudi (Judaeus) kwa mujibu wa
maandiko ya Filo katika Alexandria, yanatuonyesha kwamba mfumo au utaratibu
wote wa hekalu na wa utawanyiko walikuwa na kalenda moja iliyoruhusu kufanyika
ahirisho na udhuru wa Jamii ya Waqumrani walioitwa Essene kwa usawa. Filo
anasema kwa uwazi sana Miandamo ya Mwezi Mpya ilifanyiwa maamuzi kwa
kuhusianisha, ambayo ilikuwa inahesabiwa kwenye shule zilizokuwa zinafundisha
elimu ya mambo ya nyota au unajimu. Mwezi ulikuwa unatokana kuanzia muunganiko
mmoja hadi kwenye muunganiko mwingine. Hakukuwa na uhairishaji na kamwe hakukuwahi
kuwepo uhairishaji kwenye zamu za Hekalu. Jambo hili limefafanuliwa kwenye
jarida la Jarida la Ufafanuzi kuhusu Mafundisho ya UCG: Je Kuna Umuhimu kwa
Wakristo Kuadhimisha Miandamo ya Mwezi Mpya [124].
Filo anasema:
“Huu ni Mwandamo wa Mwezi Mpya, au ni mwanzo wa mwezi mwandamo, wenye maana ya mwanzo wa muunganiko mmoja na wa pili, urefu ambao umukuwa ni sahihi kabisa kama ilivyohesabiwa kwenye shule zinazofundisha unajimu”.(kwa mujibu wa jarida la Kiingereza liitwalo; Judaeus, Philo, The Special Laws, II, XXVI, 140, Treatise by F.H. Colson, Harvard University Press: Cambridge, MA, 1937).
Hii ni ile ijulikanayo kama nafasi ya kihistoria na na ni fursa inayojulikana sana katika mfumo wa Hekalu. Hakuna ushahidi mwingine tena unaoweza kushawishi kuwa pengine hata kudharau au kuacha ahirisho hadi kufikia kuhusuriwa kwa Hekalu, kama tunavyoona kwenye Talmud, kuwa ahirisho ahirisho halikufanyika mpaka baada ya kutungwa kwa Mishna yapata kama mwaka 200BK.
Tukio la uhairishai limeelezewa kwenye jarida la Kalenda ya Mwezi Mwandamo: Ahirisho la Sikukuu? [195] na pia kwenye Maswali (FAQ’s) mbalimbali ya somo lenyewe.
Utaratibu
wa Hekalu kama unavyoelezewa kwenye Septuagint (LXX)
Maandiko yahusuyo jinsi ya Kuhesabu Kipindi cha kuelekea kwenye Pentekoste kwa mijibu wa LXX imeelekezwa kwenye jarida lisemalo Pentekoste kulinganisha na isemavyo Walawi 23:11-22 katika Septuagint, jarida ambalo kwa sasa halipo, na mahala pake pamechukuliwa na jarida hili.
Septuagint ambayo ina maana ya tafsiri yenye kuhusisha idadi ya watu Sabini (LXX) ni tafsiri ya maandiko kutoka kwenye lugha ya Kiebrania kwenda kwenye Kiyunani kazi iliyofanyika huko Alexandria. Kwa hiyo, ilitakiwa, kufuata kama ilivyo kwenye maandiko ya kiebrania. Tofauti zozote zilitakiwa zinukuliwe kwa kuzingatia utoshelevu wa mtazamo wa kiteolojia na hatimaye mawazo ya marabi. Tafsiri ya Septuagint, yyani LXX iliyotumika hapa ni ile ya Sir Lancelot C. L. Brenton (London, 1851), Hendrickson, ikaridiwa kuchapishwa 1992). Maandiko ya Kiyunani yameonyeshwa kwa namna ya Kirumi iki lenga jarida hili.
Mambo ya Walawi 23:15-17 inasema: Nanyi
mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya Sabato, tangu siku hiyo mlioyouleta
mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia Sabato saba, 16 hata siku
ya pili ya hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea BWANA
sadaka ya unga mpya. 17 Mtatoa katika makao yenu mikate miwili ya
kutikiswa, itakuwa ya sehemu za kumi mbili za efa; itakuwa ya unga mwembamba,
itaokwa na chachu, iwe malimbuko kwa BWANA. Tafsiri ya Septuagint, yaani (LXX)
[Tafsiri ya Biblia ya Mfalme Yakobo, yaani KJV hutafsiri kifungu cha mwisho
kama wao ni malimbuko kwa BWANA].
Kaiarithmesete umin apo tes epauriton, ton sabbaton, apo tes emeras es an prosenegkete to dragma tou epithematos, epta ebdomadas oloklerous, eos tes epaurion tes eschates abdomados arthmesete pentekosta emaras, kai prosoisete thusian nean to Kurio.
Tafsiti ta Biblia ya Mfalme Yakobo yaani KJV inaendana sana ile ya Septuagint yaani LXX ni maandiko yaliyosalia na inanukuliwa kwa mlinganisho.
Mambo ya Walawi 23:18-22 inasema: Nanyi, pamoja na hiyo mikate, mtasongeza wana kondoo saba, walio wakamilifu, wa mwaka wa kwanza, na ng’ombe mume mmoja, na kondoo waume wawili; watakuwa [wote, LXX] sadaka ya kuteketezwa kwa BWANA, pamoja na sadaka yao ya unga, na sadza kinywaji, sadaka ya harufu ya kupendeza iliyosogezwa kwa BWANA kwa njia ya moto. 19 Nanyi mtamsongeza mbuzi mume mmoja kuwa sadaka ya dhambi, na wana kondoo wawili waume wa mwaka wa kwanza kuwa dhabihu ya sadaka za amani. Kisha kuhani atawatikisa pamoja na hiyo mikate ya malimbuko kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za BWANA, pamojana wale kondoo wawili; watakuwa watakatifu kwa BWANA, wawe wa huyo kuhani. [Watakuwa mali ya kuhani aliye kati yao, LXX]. 21 Nanyi mtapiga mbiu siku iyo hiyo; kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; msifanye kazi yoyote ya utumishi; ni amri ya milele katika makao yenu yote, katika vizazi vyenu. 22 Nanyi hapo mtakapovuna mavuno ya nchi yenu, msivune kabisa kabisa [kuvuna yote, LXX] pembe la shamba lako, wala msiyakusanye masazo ya mavuno yako; utayaacha kwa ajili ya huyo masikini, na mgeni, mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.
Ni jambo lililo wazi kabisa, kutoka kwenye maandiko ya Septuagint yaani LXX na kutoka tafsiri ya Brenton, kuwa maandiko haya huanzi kwenye kuhesabu siku baada ya Sabato, wiki saba kamili.
Hakuna shaka wala swali lolote kuwa kuhesabu huku kunahusiana na Siku ya Kwanza ya Mapumziko ya Sikukuu isipo kuwa wakati inapoangukia kwenye juma la Sabato.
Neno hili kwa Kiyunani ni Sabbaton na neno hili limetafsiriwa kwa Kiebrania Shabbath. Haiwezi kuwa sikukuu ya Siku ya Takatifu inayomaanishwa kama yasemavyo maandiko ya Kiebrania huliweka wazi kabisa katika kitabu cha Mambo ya Walawi 23 ya kuwa kuna aina tatu za siku za Sabato ambazo maandiko yanazungumzia habari zake. Aina tatu za Shabbath (kama iandikwavyo kwenye SHD, 1676) au Sabato za juma, Shabbathown (kama kwenye SHD, 7677) au siku za Sabato zilizotakatifuzwa, na Sabato kuu za Sabato yaani ziliitwa Shabbath Shabbathown kwa umuhimu wa Siku ya Upatanisho, ambayo ni Sabato iliyotakatifuzwa ya Sabato au Sabato iliyotakatifu sana. Siku ya Upatanisho imewekwa juu ya siku nyingine zote na inatambulika kwa neno moja la Sabato.
Jinsi
ya Kuhesabu kuelekea Pentekoste na Aina Tatu za Sabato Kitabu cha Mambo ya
Walawi 23 kimeweka wazi kabisa juu ya matumizi ya neno lililoko kwenye lugha ya Kiebrania kuhusu jinsi ya kuhesabu siku hadi kufikia Pentekoste (kwa lugha rahisi ni kuhesabu hadi kufikia hamsini) kuhusiana na Sabato saba nzima au kamilifu. Kitabu cha Walawi 23 ni mfano halisi kwa maandiko ya kiebrania kuhusiana na matumizi ya maneno kama Shabbath (Sabato), Shabbathown (Sabato kuu) na Shabbath Shabbathown (Sabato ya Sabato kuu). Neno Shabbathown (Sabato kuu) huonekana katika kitabu cha Mambo ya Walawi 23:24, 39. Hadi kufikia eneo hili la maandiko matakatifu, Sabato hutumika ki sahihi kabisa, ikionekana tu kama Sabato ya wiki ikitofautishwa na Siku Takatifu, ambazo zinaitwa makusanyiko matakatifu au (qodesh miqra’SHD 6944, 4744). Sikukuu ya Baragumu ni Sabato kuu (Shabbathown) na inatajulikana kama ni ‘qodesh miqra’ (matamshi yake ni chodesh mikraw). Kusanyiko takatifu la Sikukuu ya Vibanda na Siku Iliyo kuu ya Mwisho pia yamo miongoni mwa Sabato kuu yaani Shabbathown. kwa hiyo kuna tofauti iliyowazi kati ya Sabato ya kawaida na Sabato kuu ya sikukuu na pia kwa Sabato za Sabato kuu ya Siku ya Upatanisho, ambayo ni Sabato takatifu sana kuliko Sabato zote. Kwa hiyo, Sabato ya Sabato kuu hutumika kwa Sabato na Upatanisho peke yake (Law. 23:3, 32).
Septuagint LXX hufanya tofauti kati ya Sabato ya kawaida na Sabato ile kuu kwa kutumia neno lililotumika katika Hilleli la Shabbaton yaani Sabato ya kawaida kuelezea Sabato na neno anapausis au mapumziko kwa Sabato iliyo kuu wakati ikitumika kwenye Mambo ya Walawi 23 (kama kwenye aya za 24 na 29). Wazo lilikuwa ni kutoa pumziko (kutoka kwenye kamusi ya SGD 373 anapauo, tunaona katika Thayers kifungu cha 40). Septuagins yaani LXX kwa hiyo hufanya tofauti kati ya Sabato na Siku takatifu kwa kutumia neno Sabbaton yaani Sabato ya kawaida na anapausis maneno yote mawili yakimaanisha mapumziko ya Sabato na Sabato kuu. Matumizi haya huonyesha wazi na kwa makusudi kabisa kwamba neno lililotumika kueleza kuhesabu kuhusiana na Pentekoste linahusu na Sabato ya kila wiki pekee na sio kwa Siku Takatifu. Huu ni uthibitisho wa wazi kwamba, kwa wakati wa utungaji wa Septuagint yaani LXX, siku ya 6 ya mwezi wa Sivani ilikuwa haijafikiriwa kwenye mahesabu ya Pentekoste na hii ilieleweka kama kutoka kwenye Sabato ya kila wiki.
Kwenye mahali kuhusiana na Pentekoste ni neno Shabbathown lilitumika. Kwa hiyo ilikuwa haiwezekani kwa Siku Takatifu za sikukuu ya Mikate isiyotiwa Chachu kufikirika kwenye matengenezo ya hesabu, ama kwanzoni mwa Pentekoste yenyewe. Siku ya Pentekoste ni siku ya pili baada ya Sabato ya Saba na huitishwa kutaniko takatifu (SHD 6944; 4744; qodesh miqra; pia tazama kwenye Rangi ya Kijani, mwa biblia hii au Green, The Interlinear Bible). Neno kusanyiko takatifu hapa hufuatana na Sabato ya kila wiki na inajikita mahali hapa ili kufanyia Siku Takatifu tofauti iliyo wazi sana kutoka kwenye Sabato au Sabato ya kila wiki. Septuagint maarufu kama LXX imevunja kifungu hicho ilikusitokee mchanganyo wowote kati ya Sabato ya kawaida ya wiki na kusanyiko takatifu la siku inayofuatia. Maelezo ya quodesh mikra yametolewa kwenye siku ya Upatanisho (Law. 23:24) ambako imetambulishwa kama Sabato ile kuu. Septuagint, LXX hutumia neno anapousis kuelezea Sabato kuu hapa kwenye aya ya 24.
Hakuna maana wala msingi wowote kwa kuweka madai kuwa Septuagint yaani LXX hutofautiana na utaratibu wake katika kuamua siku ya kuwepo kwa Pentekoste au kwamba Siku Takatifu zihusishwe kwenye kuhesabu, au kwamba kuna nyingine zilizo mbali na zile Sabato za majuma zilizohusishwa. Hakuna maana wala msingi wowote kwa kuweka madai kuwa hesabu haianzii na kuishia kwenye siku baada ya ile ya Sabato za wiki. Siku baada ya Sabato ni wakati wote imekuwa, siku ya kwanza ya juma siku ambayo maarufu kama Jumapili kwa kufuatana na mfumo wa Kirumi. Uamuzi wa kuifanya siku ya 6 Sivani ulitokana na makosa ya upangaji yaliyofanywa baadae na Mafarisayo kwa mfumo wa Pentekoste, uliowekewa msingi wake kwenye mapokeo ya marabi, na hivyo kuzuia kuwa na mfumo endelevu wa kuwa na Sabato mbili kwa pamoja. Marabi wa Kiyahudi inaonekana kufanya kwa makusudi makosa ya upangaji wa kalenda chini ya kalenda maarufu kama Hilleli II kwa nia ya kulinda mapokeo yake mtazamo wa haraka wa kibiblia. Maendelezo ya kalenda yameelekezwa kwenye jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156). Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa kutolewa siku ya 16 Nisani kutokana na makosa ya upangaji ya Marabi yaligunduliwa na Josuphus mwanzoni mwa karne ya kwanza, yapata kuwa kama mwaka BK (A of J, Bk. 3, Ch. 10, Pt. 5) na vile vile na Filo kwenye jarida la (De spec. leg, ii 29 (162)) kama mwaka 40BK.
Ngome ya utetezi wa mfumo wa kirabi kwa wakati mmoja na ule wa Mafarisayo wa Kiyahudi kwa Makanisa ya Mungu huacha kielelezo cha historia katika kuamua siku ya kuadhimishwa Pentekoste. Mabishano kuhusu siku ya 6 Sivani kutoka Septuagint LXX hayana msingi Wowote, makubaliano yanayotokana na historia ndiyo yanaweka suluhu.
Historia
ya kale ya Wazayuni Wakristo walivyoiona Pentekoste
Pentekoste iliamuliwa na matawi yote ya wana imani ya Kikristo kuanzia kwenye karne ya za mwanzoni kama ilivyohesabiwa kwenye Jumapili ya mikate isiyotiwa chachu kwa siku hamsini na ilitangazwa siku ya Jumapili iliyofuatia siku ya Sabato ya kwa kanisa lote. Kwa hatua hii inaonyesha kuwa kanisa la kwanza walikataa kufuata matendo ya Mafarisayo. Lk. 4:16 na Matendo 16:13 kunaonyesha kuwa kukamilika kwa majuma kunahusika. Hata kwa ajili ya yale mabishano kuhusu utaratibu wa mgawanyo wa Kumi na Nne (Quarto-deciman)yalikuwepo kwenye karne ya pili, haikuwa kamwe kuafikiana kuwa Jumapili ya Mikate isiyotiwa Chachu ilikuwa ni siku sahihi kwa kuanzia kuhesabu kuelekea siku halisi ya Pentekoste. Ni jambo lililo wazi kuwa Pentekoste ilikuwa inaadhimishwa kila mwaka na matawi yote imani ya Kikristo, siku ya Jumapili kwa karibu kipindi chote cha historia yake. Tofauti ilikuwa kwenye karne ya ishirini tu ndipo Pentekoste ilianza kuhamishwa kwenye Makanisa ya Mungu na hii ilitokana na ujinga au kutujua kwa dhahiri kwa nafasi mihimu ya kihistoria kwa sehemu zote yaani kwa Yuda na kwa Kanisa.
Adhimisho la Pentekoste au Sikukuu ya
Majuma katika karne ya kwanza kabla haujaanza mgawanyiko uliowazi katika siku
hizi kuikumba jamii ya kiyahudi. Mafarisayo waliadhimisha Pasaka siku ya 6
Sivani wakati ambapo Masadukayo waliadhiiadhimisha mara zote Jumapili, siku ya
hamsini baada ya Mganda wa Kutikiswa, ambayo pia aliadhimisha siku ya Jumapili
ya Mikate isiyotiwa Chachu. Wala hata wale Wamisri Watengeneza madawa, au
Wapalestina Shupavu, ambao wale wana taaluma ya Matulizo huwachukulia kama ni
tawi lake, waliiadhimisha Pentetekoste, sikukuu yao kuu, siku ya 6 Sivani.
Walirudi kwenye Sikukuu ya Majuma au Marudio ya Maagano. Walikuwa na mwaka
wenye mzunguko wa siku saba na tano uliokuwa unaishia katika sikukuu ya kilimo
(kwa mujibu wa jarida la Schurer la: Historia ya Wayahudi kwenye zama za
Yesu kristo, Bol. II, pp. 595-597)
Tofauti ya maadhimisho ya Sikukuu ya Majuma kwa aina zote za madhehebu ya Kiyahudi ilisimamia moja kwa moja kutokana na tafsiri ya neno Sabato katika Walawi 23:11, 15. Masadukayo na matawi ya imani ya Waboethusia, waliielewa hii kama Sabato halisi, kwa mfano, Sabato ya kila wiki, (tazama jarida la Schurer, ibid. Vol. II, p. 416), linakataa mapokeo ya Mafarisayo kwa kutumia vifungu vya maandiko matakatifu (ibid, pp. 408-411). Kwa hiyo, Mganda wa Kutikiswa na Pentekoste kila mara iliangukia siku ya kwanza ya juma, maarufu kama Jumapili. Mafarisayo waliuelewa usemi ulio katika kitabu cha Mambo ya Walawi 23:11 kama inavyoelekeza kwenye sikukuu ya siku ya kwanza ya wiki la Pasaka, siku ya 15 ya mwezi wa Nisani (kwa mujibu wa Schurer, Vol. III, pp. 312). Kitabu cha Yubile ambacho kinatangulia kuweka tarehe ya Mishna na wote wawili yaani Filo na Yosefus huitafsiri Sabato kama ni siku ya mwisho ya wiki la Pasaka, siku ya 21 Nisani (Schurer, tena). Schurer anaamini kuwa matendo ya Mafarisayo yanaungwa mkono na tafsiri ya Septuagint ya Walawi 23:11 [le epaurion les protes] nayo ilizuiwa katika siku za Filo (De spec. leg., ii 29(162), na Yosefas A of J. iii 10,5 (248). Kwa mujibu wa Sheria za DSS Damascus, Essene aliitetea kalenda ya Yubile (ibid.) kalenda ya Yubile inaonekana kuwa ilianzia kutoka kuanzia muda kabla ya Essene Hasidim kwenye nusu ya kwanya ya karne ya pili, kwa mfano, yapata kama mwaka 160 KK (kama asemavyo Schuer. Vol. III, p. 314).
Tatizo ni lile linalo onekana kwa wazi kama mgawanyiko miongoni mwa wauminu wa dini ya Kiyahudi walioshikilia kuamini hivyo kuanzia katika karne ya pili KK, ambyo ilishuhudia migawanyiko mitatu. Filo na Yosefas huunga mkkono mtazamo wa Mafarisayo. Masadukayo walikuwa niwenye kufuata kufuata mambo kama yalivyo ambao waliwadharau na kuyadhihaki mapokeo ya Mafarisayo. Walithitika, na miongoni mwa waandishi wa kwanza walio watangulia, kuweza kueneza kanuni halisi ya heshima kwa waandishi wa sheria yaani Tora, kwa sababu ya kukataliwa kwa mapokeo ya Kifarisayo, na kuwakataa manabii. Mtazamo huu kwa sasa umeondolewa na wanazuoni au wasomi mamboleo. Waliwakubali manabii kama kwaajili ya kanuni tu, wakiyakataa mapokeo tu (Schuer, Vol. II, pp 407-408). Hakuna Myahudi au Mkristo asiye zikubali kanuni za Agano la Kale ziingiapo, na Wakristo huziweka hizi na zile za Agano Jipya.
Schurer alikuwa na mtazamo ule wa kwamba Mafarisayo waliamua kuwa Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa ilitolewa kwenye siku ya sikukuu ya kwanza ya juma la Pasaka, yaani siku ya 15 Nisani kwa mujibu wa tafsiri ya Septuagint yaani LXX ya Walawi 23:11 inayosema:
…; siku ya pili baada ya Sabato kuhani atautikisa. (kwa mijibu wa Brenton tafsiri LXX, Walawi 23:11).
Schuer anadhani kuwa hii siku ya 16 Nisani ni siku kkama ni asubuhi ya siku iliyofuatia inadhaniwa kuwa ni Siku Takatifu ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate isiyo na Chachu.
Hata hivyo, Yosefas alisema kiuwazi sana kuwa siku ya 16 Nisani ni siku ya kutoa sadaka ya Mganda wa Kutikiswa na kwamba mtazamo wa Mafarisayo hauwezi kuwa ni maana ya kweli kifungu cha maandiko kwenye Septuagint yaani LXX. Siku ya kwanza ni siku baada ya Sabato, yaani, siku ya kwanza ya wiki, au Jumapili.
Siku ya kwanza ya juma, au maarufu kwa jina la Jumapili, ni ya maana inayoeleweka iliyochukuliwa na Masadukayo na pia na Wakristo wote wa kanisa la kwanza. Kumbuka, Septuagint, LXX walitasfiri maandiko ya kiebrania, ambayo husomeka asubuhi baada ya Sabato atautikisa. Kujiuliza kwa baadae kwa Mafarisayo kulikuwa ni kwa ajili ya mzunguko huu. Tafsiri ya Kiyunani kutoka kwenye maandiko ya Kiebrania ni zile zilizotumika katka kutafsiri tena maana iliyo wazi ya maandiko ya kale. Tafsiri ya Septuagint yaani LXX, inathibitisha, kwa matumizi yake ya neno siku ya kwanza, ambayo ni siku ya kwanza ya juma, yaani, Siku baada ya Sabato (Law. 23:1), iitwayo Jumapili, imehusishwa. Siku ya 16 Nisani sio siku ya kwanza ya juma-ni siku ya pili ya Mikate isiyotiwa Chachu, na kwa kweli, ni siku ya tatu ya siku ya utaratibu wa Pentekoste/Mikate isiyotiwa Chachu kama wakati wa maandalizi na fafanuzi za Agano Jipya zimehesabiwa kwa kuwekewa asingi wake katika Kumbukumbu la torati 16:6. Septuagint yaani LXX, ilieweka ilieleweka katika msimamo na Wakristo wa kanisa la kwanza. Zaidi ya yote, Kristo ndiye alikuwa alikuwa ile Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa na anaonyeshwa bila ya wasiwasi kuwa alipaa kama Mganda wa Kutikiswa asubuhi ya siku ya kwanza ya juma, au Jumapili (le de mia ton Sabbaton; Lk. 24:1; yoh. 20 ;1). Maandiko ya kwenye Walawi 23:15 yanathibitisha mtazamo huu kama tunavyoona kutoka kwenye tafsiri mbalimbali (tazama jarida la Majira ya Kusulibiwa na Kufufuka [159].
Jambo lingine kwa ajili ya Kanisa la karne ya kwanza ni kwamba Sikukuu ya Majuma inayoongelawa kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume 16:12-13, ni ile Sabato ya kawaida (Sabbaton) inayonyeshwa kwa mfumo sarufi wa uwingi kama Sabato iliyoongelewa na Mashall kwenye Maandiko Makuu ya Interlinear. Kutokana na kusuburia huko, sasa ni kwamba inajulikana kuwa kuna umbali kati ya Sabato na Pentekoste. Hii haifuati kutoka kwenye maandiko. Kusubiri kuliendelea hadi kipindi cha Sabato hizi kama muenekano huu wa uwingi ni marejeo ya kweli ya Pentekoste. hivyo basi walielekea mahali kwa ajili ya kufanya maombi siku ya Sabato na waka kamatwa na kutiwa gerezani kwa kile kilichokuwa ni Pentekoste. Neno Sabato ya kawaida (Sabbaton) linahusu kwa ajili ya Sabato ya kila wiki kwa Kiyunani kama tulivyoona na Sabato ya kila wiki pekeyake pengine inayoelezewa hapa, lakini kwa namna yoyote kusubiri kulikuwa kwa ajili ya tukio hili – iwe ama ni Sabato au mwishoni mwa wiki la Pentekoste, kwa namna yoyote ile iliyokuwa. Neno hilohilo limetumika kwenye Injili ya Luka 4:16 (tazama Marshall). Inaonyesha kukusanya zaidi kuliko kutenganisha matukio na pia kungeonyesha Pentekoste iliyofuatia juma la Sabato ya kila wiki.
Kwa hiyo hakuna mtazamo wowote utakao unga mkono Pentekoste ya kufanyika katika siku ya 6 Sivan kutoka kwenye Maaniko Matakatifu. Inategemea yote kabisa kwenye Maneno tu ya Mapokeo ya Mafarisayo, kama mtazamo wa Masadukayo na inavyooshwa na Kanisa la kwanza. Zaidi ya yote, ilichukuliwa kuwa kwa kila jambo lolote pengine ambapo kumemaanishwa kimahususi na Kalenda ya Kiebrania kisha sikukuu imeelezewa kwa namna ya siku maalumu ya mwezi maalumu. Na kuwa hii haitokei kwenye Pentekoste kwenye maelezo yoyote kuwa kuweka siku hakumaanishi au kuingilia au kupunguzia maana yake.
Tatizo jingine lililojitokeza kutoka
matumizi mabaya ya Septuagint, LXX, yalikuwa ni yale ya ulaji wa mkate na
nafaka (kutoka Law. 23:14). Brenton anatafsiri kifungu hiki cha maansiko kama
hivi:
Nanyi msile mikate wala bisi wala masuke machanga, hata siku iyo hiyo, hata mtakapokuwa mmekwisha kuleta sadaka ya Mungu wenu; hii ni amri ya milele katika vizazi vyenu katika makao yenu yote.
Kifungu hiki cha maandiko huitafsiri MT, ambayo inasomeka:
Mambo ya Walawi 23:14 inasema: Nanyi msile mikate wala bisi wala masuke machanga, hata siku iyo hiyo, hata mtakapokuwa mmekwisha kuleta sadaka ya Mungu wenu; hii ni amri ya milele katika vizazi vyenu katika makao yenu yote.
Andiko linaelekeza kwenye yakimaanisha bisi kama tunavyoona kwenye neno la Kiebrania (SHD 3759) karmeli lenye maana ya masuke yaliyojaa kikamilifu ya kijani yaliyoko shambani. Rangi ya kijani huleta tafsiri ya neno nafaka mpya (kwa mujibu wa Biblia ya Interlinear). Neno lililotumiwa kwa ajili ya mkate ni (arton) hutafsiriwa kwa Kiebrania (SHD 1899) lechem lenye maana ya chakula (kwa mwanadamu na mnyama) hasa hasa mkate au nafaka. Inachukuliwa kwa matendo kukiwa hakuna uzao wa nafaka, au hata pengine chakula, kingeweza kuliwa hadi siku ya Mganda wa Kutikiswa. Mtazamo huu ulichanganywa na sheria za biblia. Mtazamo huu unaleta mchanganyo kwa maandiko yenyewe, kwa kutilia maanani kwa milo na sadaka za Pasaka au Siku Takatifu ya kwanza ya Mikate isiyotiwa Chachu (Kut. 12:18; Law. 23:6; Kum. 16:8).
Maandiko yaliyoko katika Yoshua yanaonyesha maana. Mambo yanayo Oanishwa na maandiko hapa yana maana ya nafaka mpya tunaona kwamba ni nafaka mpya na mazao yote iliyofanyika nafaka mpya vimekatazwa. Mikate isiyotiwa chachu na milo uliendelea mpaka kufikia kuwa Mganda wa kutikiswa umetengenezw kutokana na nafaka iliyohifadhiwa ya mwaka uliopita hadi kufikia Jumapili asubuhi wakati nafaka mpya inapoweza kutumiwa.
Yoshua 5:10-12 inasema: Basi wana wa Israeli wakapanga hema zao huko Gilgali; nao wakala sikukuu ya Pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi, jioni, katika nchi tambarare ya Yeriko. 11 Nao wakala katika mazao ya nchi siku ya pili ya kuiandika hiyo sikukuu ya pasaka, mikate isiyotiwa chachu, na bisi siku hiyo hiyo. 12 Ndipo ile mana ikakoma siku ya pili yake, baada ya wao kuyala hayo mazao ya nchi hawakuwa na mana tena; lakini wakala katika viliwa vya nchi ya Kanaani mwaka huo.
Hapa asubuhi baada ya Pasaka, ijulikanayo kama siku ya 15 Nisani, nafaka za zamani zililiwa. Haikuwa inatumika nafaka mpya. Kwa hiyo, nafaka ya zamani inatumika mpaka Mganda wa kutikiswa na hatimaye ndipo nafaka mpya iliwenza kutumika. Makosa haya madogo yalifanyika kwa sababu Mafarisayo hupenda kufuata mapokeo zaidi kuliko Torati, na hii ndiyo sababu waliadhibiwa (Mit.26:2).
Nukta moja isiyo ya kawaida ya kukosea kupangilia (lakini huenda ni mapendekezo zaidi kuliko mabishano ya kuuhusu siku ya 6 ya mwezi wa Sivani) huhusiana na mahali pa kuwa Pentekoste ni siku ya Jumapili. Hii ilichukuliwa kwa mahali pale ambapo hesabu inakubalika kuwa ianzishwe na Jumapili inayofuatia Sabato ya kila wiki katika juma la Mikata Isiotiwa Chachu ikifuatiwa na Sabato ya saba ya kila juma. Mabisha kwa kiasi fulani yalithibitisha ukweli wa kwamba siku hamsini zinajumuisha siku ya Jumapili lakini Siku Takatifu ya Pentekoste haianzi mpaka jioni ya Jumapili, na hivyo kuwezekana kuifanya Siku Takatifu Jumatatu. Maandiko yanaeleza kiuwazi kabisa asubuhi baada ya wiki la mwisho (hebdomados, LXX) kama siku ya Jumapili utaleta sadaka ya nyama mpya kwa Bwana. Septuagint yaani LXX, inaonyesha hapa kuwa wiki ina siku saba na kwamba vipindi hivi vya siku saba saba (yaani hepta hebdomadas; tazama pia Zab 118[119]:164; Mit. 24:16 kwa utaratibu ulioko kwenye Septuagint, yaani LXX, hapa na Thyers, p.247) vimehusishwa. Mtazamo wa Pentekoste ya Jumatatu ulipata msukumo na Herbert Amstrong wa huduma ya Redio ya Kanisa la Mungu (Radio Church of God) kwenye miaka yake ya kwanza lakini baadae ulikataliwa kama kitu cha uwongo au uzushi na yeye na kile kituo cha Radio na hatimaye ikaunda baraza la Kanisa la Mungu la (Ulimwenguni Kote). Baadhi ya wenzake hawakukubali kupokea ukweli wa hata kosa dogo kwa utaratibu wa kufikiri na mtazamo huu hujitokeza mara kwa mara . Haina msingi wowote wa kweli au katika historia, na ni uongo wa kifikra na kiujuzi wa matumizi ya lugha.
Wakati Kalenda ya Hilleli ikibubalika katika mwaka 358BK kutoka kutambulishwa kwake kutoka Babeli ilikoanzishwa yapata kama mwaka 344BK, Kanisa la Kikristo limekuwa likitunza siku sahihi kwa kuendelea hivyo kukitiliwa maanani nafasi za kirabi na sio tu kuwa sio sahihi bali pia sio sawasawa au haikuendana.
Ukweli ambao umefanya mfano wenye maana ya Mganda wa Kutikiswa usieleweke na Waktisto waliowengi. Wameanzisha na kukifanya kikubalike na kujulikana na wengi ni sikukuu iitwayo Easter au Ishtar na mfano wake wenye maana ya Jumapili ya kufufuka kwa inani potofu ya mungu wa rutuba na mazao wakati wa kipindi zha baridi waridi (spring). Neno au jina Eastar linatokana na lafudhi ya lugha ya kale ya mchanganyiko iliyojulikana kama Anglo-saxon ikiitwa Ishtar, ni mfumo wa imani ya kipagani ya kuabudu ambao ulifanikiwa kujiingiza kwenye Ukristo kwenye karne ya pili. Imani hii iliweka utaratibu wake ukianzia siku ya kifo cha Tammuzi ambaye pia aliitwa au Dumuzi aliyekufa siku ya Ijumaa na ufufuko wake kufanyika siku ya Jumapili. Hii ilikuwa inapelekea kipindi cha nafaka na mfano wa mchipikizi mapya ya nafaka. Ile mikate ya Easter imechukuliwa kutoka kwenye uokaji wa keki au mikate midogo midogo mitamu kwa Malkia wa Mbingu kenye sherehe za mungu wao Ishtar kwa ajili ya kumfufua Tammuzi (au Dumuzi kwa mujibu wa lugha ya kale yenye maana sawa ya Waashuru na Wababeli). Imelaaniwa na mujibu wa Biblia (Yer. 7:18; 44:19; kwa mujibu wa SHD 3561 kavvan mikate myembamba ya sadaka au keki). Mikate myembamba ile mikate myembamba hulindwa kwa mfano wa Ekaristi na zile Bilauri. Kumlilia Tammuzi katika Ezekieli 8:14, kunaelekeza utaratibu wa maombolezo na mfano wa kifo/na ufufuko wa Easter.
Kukosea kwa upangaji wa Pasaka na Mikate
Isiyotiwa Chachu, katika mchanganyo wake wa utaratibu wa Easter ya
Ijumaa/Jumapili, hauna uhusiano wowote na utaratibu wa kibiblia au ulazima wa
kufanya adhimisho la kutoa sadaka ya Mganda wa Kutikiswa katika siku ya
Jumapili inayoangukia ndani ya siku saba za juma la Mikate isiyotiwa Chachu
baada ya Sabato ya kila wiki. Ulazima wa kuadhimisha siku za Pentekoste kwenye
Jumapili baada ya Sabato kadhaa kamilifu, au wiki kamili, ni maelekezo
makamilifu ya biblia (Sabato kamilifu ni kipindi cha reveni, kama
vile wiki ya siku saba, tazama jarida la Kalenda ya Mungu [156], pp. 2-3.
Tatizo linaloteta mchanganyo kwa jambo hili hapa ni mwandamano wa matukio wakati hii Jumapili inapoangukia siku ya 15 ya mwezi wa Abibu na Sabato ikiwa siku ya 14 Abibu, ambayo kwa kawaida huwa ni siku ya maandalizi. Kwa hiyo, Siku Takatifu ya Kwanza iinakuwa ni ya Mganda wa Kutikiswa pia. Hii haikuleta tatizo lolote kwa waumini wa dini Kiyahudi, hata hivyo wengine wao kuichukulia Sabato kama ni kuwa nje ya sikukuu kwa mintaarafu hii na ya Mganda wa Kutikisa iliyofuatia Siku ya mwisho, ambayo ni Sabato ndani ya sikukuu. Ukweli ni kwamba, siku ya 14 ni sehemu ya kipindi cha Sikukuu na Mganda wa Kutikiswa pia ilionekana kama kuwa miongoni mwa sikukuu.
Majadiliano kuhusu siku ya 6 ya mwezi wa Sivani yalituama kwenye makosa ya makusudi ya kutafsiri maelekezo ya msingi ya kibiblia katika makosa ya kiungaji ya marabi wa Kiyahudi, ambayo inaonekana kutokubalika na Wayahudi wote. Utetezi wake kwenye Ukristo kumepewa msukumo na hamu ya dhati ya kuchukuliana kikamilifu na kufuata mfumo mwenyewe halisi. Wanapaswa kusifiwa kwa bidii yao lakini ni vema kusahihisha makosa yao.
Kipimo Cha Hesabu Cha Wasamaria Na Pentekoste
Jambo lililokuwa linafuatia kwa Wasamaria, ikionekana kuwa si sahihi kuadhimisha Mwaka Mpya katika siku ya Mwandamo wa Mwezi Mpya na wakati wote kukifuatiwa na muunganiko wa kama walivyofanya kuanzia kipindi cha Hekalu,
Hata hivyo, Kristo hakuyatilia maanani kuwa ni mfumo unaofaa, sawa kama alivyowaona Mataifa wapagani pia, na akatuma wanafunzi kwa kondoo waliopotea wa wa Nyumba ya Israeli na sio kwa Wasamaria, ambao pia walidai kuwa ni uzao wa Israeli na Yusufu (Mt. 10:5-6). Kwa hiyo, uzaliwa wao unaonekana kuwa ni suala linalosubiri muda. Hata hivyo hawakuwa na ukuhani au kuhani wa Kilawi mpaka kufikia siku za karibuni ambazo zilizo semekana kuwa za msitari halisi na zaidi na huenda kuliko Walawi katika Yuda.
Kitabu cha Mambo ya Walawi 23:15
kinazungumzia kuhusiana na Sheria za Torati ya Wasamaria kwa kusema “15 Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili
baada ya Sabato, tangu siku hiyo mlioyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa;
zitatimia Sabato saba,”
Wiki saba za Kipindi cha kuelekea kwenye sikukuu (Omeri) zilihesabiwa kuanzia Jumapili iliyoko ndani ya Sikukuu ya Pasaka na Mikate isiyotiwa Chachu. Kwa hiyo Pentekoste itasherehekewa kwenye Siku ya Kwanza ya Juma, iitwayo Jumapili, ya siku ya nane ya juma. Majina ya majuma kama ilivyotolewa katika maandiko ya Wasamaria kwa kufuata mfumo au utaratibu wao (KS) ni kama ifuatavyo:
“Wiki ya kuvuka kwenye Bahari ya (Shamu)” (Kutuka 14:26-15:21),
“Wiki ya kubadilika maji mara” [machungu] (Kutoka 15:22-26),
“Wiki ya kuwa elim,walipokuta chemi chemi ya visima kumi na mbili na mitende sabini” (Kutoka 15:27-16:3),
“Wiki ya mkate wa mana, iliyowaangukia kutoka mbinguni wakiwa jangwani” (Kutoka 16:4-36),
“Wiki ya kutoka kwa maji kutoka kwenye mwamba” (Kutoka 17:1-7),
“Wiki ya kupigana vita na ‘Waamaleki’” (Kutoka 17:8-17),
“Wiki ya kusisi kwao katika mlima wa Sinai” (Kutoka 19:1),
(hii ni kwa Sylvia Powels. Katika jarida lake la Wasamaria,lililohakikiwa na Alan Crown).
Utaratibu huu wa Kuhesabu siku za Kuelekea
kwenye sikukuu au tukio la kidini umefafanuliwa zaidi kwenye jarida liitwalo Pentekoste
ya Sinai [115].
Mabishano yaliyoko hapo juu, huashiria kwamba utaratibu huu wa Kuhesabu siku za Kuelekea kwenye sikukuu au tukio la kidini huanzia siku ya Jumapili ndani ya Siku za Mikate isiyotiwa Chachu na huishia kwenye Sikukuu ya Pentekoste au Sikukuu ya Majuma kama ilivyokuw inajulikana kwenye siku ya 49 na za 50 ambazo huwa ni siku za Sabato na Jumapili zikihesabika kama siku mbili mfululizo zenye kuheshimika. Hii tumeona mara zote utaratibu, na bado ni utaratibu ulioko kwenye makanisa mengi ya Mngu hata yale yaliofuata makosa ya Kalenda ya Hilleli kwenye heshima mengine.
q