Makanisa Ya
Kikristo Ya Mungu
[042]
Heri Walioalikwa
(Toleo La 1.0 20020914-20020914)
Mwanzo sura ya 24
ni hadithi ya Ibrahimu akimtafutia mke mwanae Isaka kwa kumtumia mtumishi wake.
Hadithi yenyewe ina utajiri mwingi wa vielelezo na mifano. Tutajionea kusudi
kuu linaloonyeshwa na kufanywa kwenye hadithi hii ya kumtafutia mke Isaka. Ina
uhusiano unaoingiliana na jinsi Mungu anavyomtafuatia bibi arusi Mwanae, Yesu
Kristo.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2002 Peter Donis. ed. Wade Cox)
(tr. 2015)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu
bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza
kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka
maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Heri Walioalikwa
Hebu na tuanze safari
kuanzia Mwanzo sura ya 24.
Mwanzo 24:1-4 Basi Ibrahimu alikuwa mzee mwenye miaka mingi, na
Bwana alikuwa amembariki Ibrahimu katika vitu vyote. 2 Ibrahimu akamwambia mtumishi wake, mzee wa nyumba
yake, aliyetawala vitu vyake vyote, Tafadhali uutie mkono wako chini ya paja
langu, 3 nami
nitakuapisha kwa Bwana, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia
mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao; 4 bali enenda hata nchi yangu, na kwa jamaa
zangu, ukamtwalie mwanangu Isaka mke.
Ibrahimu alikuwa
na umri wa miaka 100 wakati alipozaliwa Isaka (Mwanzo 17:17). Ibrahimu alikuwa
na takriban miaka 140 ya umri wake wakati alipomwambia mtumishi wake aende
kumtafutia mke mwanae. Isaka alikuwa na umri wa miaka 40 wakati huu. Kama
tutaichukua yubile (miaka 50) na kuilinganisha kwa kila mwaka wa umri wa Isaka,
tangu kuzaliwa kwake hadi alipokutana na kumuoa mke wake, tunafika kwenye idadi
ya miaka 2000 kamili.
Kuna mlinganisho wenye kuvutia sana kwenye maisha ya Kristo na maisha ya
Isaka. Kristo alizaliwa karibu na yubile ya 40 au miaka 2000 iliyopita. Rebeka ni
mfano wa kanisa. Isaka alimuwa na umri wa miaka arobaini alipomuoa Rebeka. Kristo
tangu kuzaliwa kwake, amesubiri yubile 40 (sawa na miaka 2000) ili kuungana na
bibi arusi wake, kanisa. Wakati tunapoisoma aya inayohusiana na yubile, inajiri
na tangazo la uhuru kwa ulimwengu wote wakati Kristo atakaporudi (Walawi
25:10).
Akiwa na umri wa
miaka 40 Isaka alikuwa na uwezo na akili timamu ya kumuwezesha kujitafutia mke
mwenyewe, lakini bado Ibrahimu alimtuma mtumishi wake kwenda Harani akamtafutie
Isaka mke huko. Alikuwa Ibrahimu kwa kupitia mtumishi wake, aliyemletea mke
mwanae. Ni sawa na ilivyo kwa Kristo. Baba Mungu (ambaye hapa anafananishwa na
Ibrahimu), kwa uweza wa Roho wake (anaonekana kwa taswira ya mtumishi)
anawaleta watu, anayefanya bodi au bibi arusi wa Kristo (Yohana 6:44).
Mtumishi mku sana
anayetajwa hapa anaweza kuwa ni Eliezeri. Ibrahimu alimtuma mtumishi kwa kuwa
yeye alikuwa ni mwabudu Mungu pia (Mwanzo 24:26, 52). Kama alikuwa ni Eliezeri,
ndipo uadilifu wake ni kitu ambacho tunaweza kukitilia maanani. Alikuwa
anamtafutia mke mwanae ambaye alikuwa alimtaka hapo nyuma awe ni mrithi wa mali
za Ibrahimu (Mwanzo 15:2).
Mke huyu anapaswa
asiwe Mkanaani. Wakanaani walikuwa wamelaaniwa (Mwanzo
5:8-15). Ibrahimu alikuwa anamwambia mtumishi wake kumtafutia mke mwanae
Isaka kwa watu wanaomuabudu Mungu mmoja na anayemwabudu yeye.
Mwanzo 24:5-6 Yule mtumishi akamwambia, Labda yule
mwanamke hatakubali kufuatana nami mpaka nchi hii, je! Nimrudishe mwanao mpaka
nchi ulikotoka? 6 Ibrahimu akamwambia, Ujihadhari, usimrudishe
mwanangu huko.
Eliezeri anaweza kuchukuliwa kama ni mtu asiyeongoka,
tusiwaruhusu wenzi wetu wasioongoka kutuzuia tusitoke Misri au kutushawishi au
kutusababisha turudi Misri. Tumeitwa
tutoke gizani na kuwa kwenye nuru ya ajabu sana ya Mungu (1Petro 2:9).
Mwanzo 24:7 Bwana, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya
babangu, na kusema nami katika nchi niliyozaliwa, aliniapia akisema, Nitawapa
uzao wako nchi hii; yeye atampeleka malaika wake mbele yako, nawe utamtwalia
mwanangu mke tokea huko;
Ni Mungu Baba anayetuita sisi na kututoa
kutoka nyumba zetu za zamani za utumwa. Sisi sote tunayeyatenda mapenzi ya
Mungu Mmoja, wa Pekee na wa Kweli tunaonekana kama uzao au watoto wa kiroho wa
Ibrahimu. Hapa Ibrahim anamuonyesha Kristo kama Malaika wa Mungu.
Mwanzo 24:8 na
yule mwanamke asipokubali kufuatana nawe, basi, utafunguliwa kiapo changu hiki;
lakini usimrudishe mwanangu huko.
Mwanamke huyu ni taswira ya wale walioitwa na sio
waliochaguliwa. Roho wa Mungu atafanyakazi na watu mmoja mmoja ili kumuongoza
yeye apende kubatizwa. Hapa Eliezeri anakuwa taswira ya Roho wa Mungu,
anayetuonyesha sisi kuwa kama mtu hapendi kufuata, ndipo Roho Mtakatifu
“alishuka au kutolewa” kutoka kwa mtu huyo.
Mwanzo 24:9 Yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la Ibrahimu bwana wake,
akamwapia katika neno hilo.
Kutokana na kubatizwa kwetu, ndipo tunatolewa na kuingizwa kwa Kristo.
Kristo anaishi ndani yetu (Wagalatia 2:20). Tunaingia kwenye agano la kumtii
Mungu. Hatuwezi kurudi nyuma kwenye njia zetu za zamani, wakati tulikuwa tumekwisha
kufa kwa mambo maovu (Waefeso 2:5) kumuweka Kristo nyuma kwenye hali yetu ya kimaisha
ya nyuma (Wagalatia 5:1).
Mwanzo 24:10 Kisha huyo mtumishi akatwaa ngamia kumi
katika ngamia za bwana wake akaenda zake, maana mali zote za bwana wake
zilikuwa mkononi mwake, akaondoka, akaja mpaka Mesopotamia, mpaka mji wa
Nahori.
Tarakimu hii
“kumi” inajulikana kama ni tarakimu ya ukamilifu na ni mwanzo mpya kama ilivyo
tarakimu ya “1” kwenye awamu mpya. Ngamia wanaashiria mataifa ya wamataifa. Kwa
maneno mengine, ni kwamba wanawakilisha mataifa yote. Ngamia anachukuliwa kuwa
ni najisi kwenye torati (Walawi 11:4). Mtu anachukuliwa kuwa ni kiumbe najisi kwa
kuwa hazishiki sheria.
Raslimali zote za
bwana wake zilikuwa mikononi mwa mtumishi wake. Hii ingeweza kujumisha pia
ahadi zote za kiroho. Kwa kupitia Ibrahimu mataifa yote yatabarikiwa. Eliezeri
alionyesha kuwa alikuwa ni wokovu wa jumuia yote ya wanadamu kwa uangalizi wake.
Mwanzo 24:11 Akawapigisha magoti ngamia nje ya mji karibu na kisima cha maji wakati wa
jioni, wakati ambapo wanawake wanakwenda kuteka maji.
Ndipo alimwinamisha ngamia wake. Eliezeri anayeonekana kuwa ni
mfano wa Roho Mtakatifu yupo kwenye maelekezo na mwongozo wa Kristo hapa.
Kristo atayafanya mataifa yake (ngamia)
yapige magoti, nje ya Yerusalemu Mpya. Kwa kuwa mataifa yote ni mali ya Mungu (Zaburi
82:8). Mamlaka yote na uweza amepewa Kristo. Ni wale waliozifua nguo zao tu
ndio wataruhusiwa kuingia kupitia malangoni ya mji ule (Ufunuo 22:14). Ni wale
wanaoshinda tu, peke yao watafanyika kuwa nguzo kwenye hekalu la Mungu. Kuna
mji mmoja tu tuliowekewa, Yerusalemu Mpya (Ufunuo 3:12). Watu wengine wote
waliosalia watakuwa na mahala pao pa kutosha nje ya mji huu.
Kisima cha maji
ni maji (roho) ambayo Kristo anayatoa, yanayotuongoza kwenda kwenye uzima wa milele
(Yohana 4:14). Mwanamke aliyechota maji analiwakilisha kanisa. Katika ziku za
zamani, kuchota maji na kuyaleta nyumbani kwa ajili ya familia yake, ilikuwa ni
kazi ya mwanamke. Katika kipindi cha millennia kanisa litashirikisha majukumu ya
kuchota maji ya kweli na maisha ili kuwapa mataifa. Sisi kama kanisa tunachota
maji sasa, tukiwa tumejazwa na Roho Mtakatifu (Matendo 2:4, 13:52).
Haya yote yalifanyika
majira ya jioni, ambao una maana yake fulani. Kazi ilikoma (Ruth 2:17); wafanyakazi
walilipwa (Kumbukumbu la Torati 24:15); dhabihu za jioni zilitolewa (Kutoka
29:38-42, Hesabu 28:3-8); taratibu za
utakaso zilikoma (Walawi 11:24-28). Isaka alitoka nje kwenda kutafakari
(Mwanzo 24:63). Kristo alijitenga mbali kuomba (Mathayo 14:23). Tunaweza kupata
mambo yanayofanana kutoka kwenye maandiko haya.
Watu wa mataifa
wataletwa kisimani, kazi zao za kufungiwa nira ya utumwa inakoma (Wagalatia
5:1). Watashiriki kwenye dhabihu ya Yesu Kristo; kipindi chao cha kukoma kwa
utaratibu zisizo za utakaso. Watakuja kulitafakari neno la Mungu, na maombi
kufanywa mbele za Mungu kama uvumba, kuinua mikono juu kama dhabihu za jioni (Zaburi
141:2) ili kushukuru rehema na uwezo
wa kumjua Mungu (Hosea 6:6).
Mwanzo 24:12 Naye akasema, Ee Bwana, Mungu wa bwana wangu Ibrahimu, nakuomba mambo yangu
uyajalie yawe heri leo, ukamfadhili bwana wangu Ibrahimu.
Maombi ya Eliezeri
kwa Mungu wa Pekee na wa Kweli. Anamtambua pia Eloa, Mungu Aliye Juu Sana, kama
Mungu wa Ibrahimu. Ibrahimu alimuabudu Mungu Mmoja, Wapekee na wa Kweli. Ni
Mungu huyuhuyu ndiye tunayemuomba hata sisi, na si mwingine. Tunaomba kwa jina
la mwanae, ila hatumuombi huyo mwana.
Tunaambiwa kwenye
Biblia jinsi tupasavyo kuomba (Mathayo 6:9-13). Wakati tunapoomba kwa ajili ya
awengine, zaidi kuliko sisi wenyewe, Baba atatujazi mahitaji yetu yote. Hii
inamaanisha kuutafuta kwanza Ufalme wa Mungu, na mengine yote tutapewa (Mathayo
6:33). Ni kitendo cha kujitoa sadaka. Hivi ndivyo alivyofanya Kristo. Aliutoa
uhai wake, kwa ajili yetu. Hii ndiyo namna ya moyo tunaopasa kuushindania.
Mwanzo 24:13-14 Tazama! Nimesimama karibu na kisima cha
maji, na binti za watu wa mjini wanatoka kuteka maji, 14 basi na iwe hivi; yule msichana
nitakayemwambia, Tua mtungi wako, nakuomba, ninywe; naye akasema, Unywe, nami
nitawanywesha na ngamia zako pia; basi huyu na awe ndiye uliyemchagulia
mtumishi wako Isaka; na kwa hayo nitajua ya kuwa umemfadhili bwana wangu.
Kitendo cha Eliezeri
kusimama kisimani kinaonyesha taswira ya makanisa mengi yanayokuja kuchota maji
kwenye kisima cha uzima. Lakini roho (mtumishi) anatenganisha kati ya makanisa
(wanawake). Kanisa halipaswi tu kuwa na ushuhuda, bali linapaswa kuzaa matunda
ya roho (Mathayo 7:20). Mwanamke aliyesema: Unywe, nami
nitawanywesha na ngamia zako pia, ndiye alikuwa na ushuhuda.
Ufalme wa Mungu unajengwa na watu waliotayari kutumika, na sio wale wanaotaka
kutumikiwa. Hivi ndivyo anavyopenda Mungu (Mathayo 20:28).
Mwanzo 24:15 Ikawa, kabla hajaisha kunena, tazama, Rebeka anatokea, binti wa Bethueli
mwana wa Milka, mkewe Nahori, ndugu wa Ibrahimu, naye ana mtungi begani pake.
Mungu Baba yetu anajua kile tunacho hitaji
hata kabla hatujaomba (Mathayo 6:8). Mstari wa uzao wa Rebeka unaonyesha kuwa
alikuwa ni uzao na jamii ya Ibrahimu, lakini la muhimu sana ni kwamba alikuwa
anamuabudu Mungu wa Pekee na wa Kweli, kama uzao wa kiroho.
Alitoka
nje. Hii inamuonyesha yeye kuwa ametoka nje ya
familia yake na kwenye ulimwengu huu. Alikuja kuifanya kazi yake. Alitoka nje
ili kuchota maji kisimani, ambayo ndiyo ilikuwa imani yake. Kitendo
chake cha kubeba mtungi kinaonyesha kuwa alikuwa na kifaa na nguvu za kuchota
maji yeye mwenyewe, na hakuwa anamtegemea mtu mwingine yeyote.
Mwili wetu wa kidunia unachukuliwa kama
chombo au silaha iliyotengenezwa kutoka kwenye udongo (Isaya 64:8). Udongo, kwa
hali yake ya asili, unatumika mara chache kutengenezea vyungu au vitu vya
ufinyanzi. Sisi kama wanadamu hali yetu yenye asili ya kimwili haiwezi kuurithi
ufalme wa Mungu (1Wakorintho 15:50). Udongo umechanganyika na maji, na kisha
inachujwa ili kiondoa mawe na takataka nyingine kubwakubwa. Ni kwa uweza wa
Roho Mtakatifu ndipo tunaweza kupondwapondwa na kubadilishwa, huku mioyo yetu
ikinyunyiziwa usafi kutokana na dhamira na mawazo mauvu na miili yetu ikiwa
imeoshwa kwa maji safi (Waebrania 10:22).
Udongo unaweza
kuchongwa na kurudishwa kwenye umbo lake, na unaweza kukaushwa unapowekwa kwenye
joto kali. Joto hili kali ni kuimarishwa ambako tunapitia maishani mwetu.
Tunapitia kwenye taratibu au awamu mbalimbali, ili kwamba uhalisia na uaminifu
wa imani yetu ijaribiwe kwa moto. Matokeo ya mwisho yatasifiwa na utukufu na
heshima atakaporudi Kristo (1Petro 1:7). Wakati tutakapotiwa kwenye moto
kiasi cha kutosha na kusubuliwa uozo wetu wa kiroho utabadilika. Na ndipo
tutapapokuwa na tabia ya kaka yetu Yesu Kristo (Warumi 8:29) ambaye yeye mwenyewe
alijaribiwa kwa kile alichoteseka kwacho na anaweza kutusaidia sisi (Waebrania
2:18) na tukafanyiwa kuwa wakamilifu (Waebrania 5:9).
Mwanzo 24:16 Naye yule msichana alikuwa mzuri sana uso
wake, bikira, wala mwanamume hajamjua bado; akashuka kisimani, akajaza mtungi
wake, akapanda.
Aya hii inahusiana
na hali ya mtu ya kiroho kabla ya ubatizo. Kabla ya ubatizo tunapasa kuzaa
matunda yatokanayo na toba (Mathayo 3:8). Aya inayoulizwa
inamaanisha hali ya kutengana na mtu. Mwanamke anawakilisha mtu binafsi
aliyetolewa au kuchotwa na Mungu, na akawa tayari kutolewa kwa Kristo.
Sasa alikuwa
ni mzuri sana kumshika. Kimuonekano
wa kimwili, Rebeka anaweza kuwa alikuwa na muonekano mzuri kwa nje. Lakini
tunaangalia hali na tabia yake ya kiroho: Utu wake wa ndani. Neno ambao sasa linaloionyesha hali yake. Kama
tunampenda Mungu kwa moyo wetu wote na kumpenda jirani yetu, ndipo sasa tutachukuliwa kuwa wazuri.
Tunapoanza tu kuonyesha
kuwa tunazaa matunda yapasayo toba, na kuanza kuzishika sheria za Mungu, kujua
jinsi Mungu alivyo na maperzi yake, ndipo tutachukuliwa kuwa wathamani machoni
pa Bwana. Tunastahili uzito wetu ni wa thamani kama dhahabu (Yakobo 1:25).
Hakuna mtu aliyemjua hapo kwanza. Sisi tunaomwabudu Mungu Mmoja
na wa Kweli tunafananishwa na wanawali mabikira (Ufunuo 14:4). Sisi tunaompenda na kumtii Mungu Baba, wanamwabudu yeye
kupitia kwa mwanae Yesu Kristo. Kama tukibakia kuwa waaminifu tutachukuliwa
kama wanawali mwabikira.
Kwa suala la
ibada ya ubatizo, tunashuka kwenda chini
kwenye kisimani au kwenye bwawa lenye kina kirefu lenye maji. Tunapaswa
kuzama mwili wote. Tunapopanda kutoka humo
majini, tunapewa Roho Mtakatifu (Matendo 8:39). Kwa hiyo, aliliona hitaji la kujaza
chombo chake maji ya kisima, ambayo ni Roho Mtakatifu.
Kwenye injili ya
Mathayo tunasoma tukio la Roho wa Mungu akishuka chini kama hua na kumkalia
Kristo mabegani mwake (Mathayo 3:16). Hii ilikuwa ni kuonyesha kuwa Kristo alikuwa
hapa duniani katika mwili na alipokea Roho Mtakatifu kwa hali hiyo.
Mwanzo 24:17 Ndipo yule mtumishi akapiga mbio kwenda kumlaki, akasema, Tafadhali unipe
maji kidogo katika mtungi wako
Na mtumishi
akamkimbilia na kukutana naye – huu ni mwendelezo. Mara tu tunapopanda kutoka
majini, tunakuwa burudikoni, au kukutana na Roho. Roho ndiye anayetupekelea
kwenye ubatizo. Kabla ya ubatizo unapofanywa ndani yetu, lakini nje yetu. Baada
ya ubatizo wa kuzamishwa majini pamoja na kitendo cha ‘kuwekewa mikono’ Roho
huja ndani yetu na kufanyika kuwa sehemu yetu.
Kristo alipanda kutoka majini na Roho wa Mungu alishuka juu yake.
Rebeka “alipanda na kuja” na mtumishi (Roho wa Mungu) akamkimbilia na
kukutana naye. Neno alikimbia inaonyesha kasi ambayo ilitumika.
Ilikuwa ni haraka, mara moja. Tumepewa Roho Mtakatifu na tumetolewa kwa Kristo anayeishi
ndani yetu (Wagalatia 2:20).
“Tafadhali
nipe ninywe kidogo kwenye mtungi wako” (aya ya 17). Inatupasa kila wakati kuwa
kwenye mazingira ya kiroho tunapoweza kuwasaidia wengine kwa siri za Mungu.
Haitupasi kabisa kukimbia mbele tukiwa watupu. Vifaa vyetu vinatakiwa vijae
Roho wa Mungu wakati wote.
Rebeka alijaza mtungi wake na kuubeba
begani mwake. Aliifanya kazi yake kikamilifu na kwa uaminifu mkubwa, kiusahihi
na kwaufanisi mkubwa. Tumepewa kazi ya kufanya na haitupasi kuruhusu sisi
wenyewe kuiharibu au kujikanganya kutoka kwenye wito wetu na kutoka kwenye kazi
tuliyopewa. Yatupasa kushikilia kile tulichonacho, ili mtu asiitwae taji yetu (Ufunuo
3:11).
Kwa kweli, Rebeka
hakumpa Yule mtumishi kinywaji. Bali aukijaza mtungi wake na halafu aliondoka
na kurudi nyumbani. Wakati mwingine hata sisi inatupasa kuwa waangalifu sana na
mtu tunayempa kinywaji kutoka mtungini mwetu. Hatupaswi kutupa lulu zetu mbele
ya nguruwe (Mathayo 7:6). Kama mtu ana kiu ya neno la Mungu, ni yeye ndiye
atakayeomba kinywaji, na inatupasa sisi kuwapa kinywaji ili kuzima kiu chao.
Sio kila mtu anapenda kunywa maji yaliyo kwenye kisima cha uzima. Bali kama
“mtu anakiu”, ndipo inatupasa kumsaidia na kukomesha kiu cha kuitafuta kweli
aliyonayo.
Mtumishi
alimtazama Rebeka alipokuwa anaujaza mtungi wake, na ndipo alijua kwamba mtungi
wake aulikuwa umejaa maji. Wale waliokaribu yetu wanapasa kuona kwamba
tumejazwa na roho aliye tofauti na wao, roho wa kweli. Alimwangalia akiwa anakwenda
kwenye shughuli zake za kila siku na kuona kwamba alikuwa ni mwanamke
mchapakazi na anaweza kufanya kazi zake. Ndivyo ilivyo, watu wanapoyaona
matendo yetu jinsi tunavyoishi watakuja kwetu, wakiitaka kata ili wanywe maji
tunayokunywa sisi kutoka kisimani.
Mwanzo 24:18 Naye akasema, Unywe, bwana wangu, akafanya haraka, akatua mtungi wake
mkononi mwake, akamnywesha.
Kwa haraka sana
akamwambia kunywa, bwana wangu.
Hatupaswi kumkataza mtu yeyote anayetuomba amjue Bwana. Rebeka alionesha kwa mfano
roho ya Kanisa. Yatupasa kutoa msaada kwa hofu, kicho na kutetemeka (Ufunuo
22:17).
Rebeka alimwamini
na kumuonyesha heshima mtuishi wa Ibrahimu na kumuona kuwa bora kuliko yeye mwenyewe.
Kwa kumuita kwake ‘bwana’ alijinyenyekeza mwenyewe na kujishusha kiasi cha kuwa
kama mtumwa au mtumishi. Yatupasa kusaidiaana na kutumikiana kila mmoja na
mwenzake kwa upendo (Wagalatia 5:13).
Tunaweza pia kuona kwamba aliutua mtungi wake chini mikononi mwake.
Tunapowatumikia wengine, inatupasa kuweza kusaidia kwa mikono yetu wenyewe au
uwezo wa kuweza kunena hivyo.
Rebeka hakumpa Eliezeri mtungi wake ili
ajihudumie mwenyewe. Alikimwaga. Watu wengine hawana ujuzi au kuwa imara vya
kutosha kwenye neno la Mungu kuweza kujisaidia wenyewe. Yatupasa kujua hili na
kujenga kile tunachoweza (Matendo 20:32).
Kristo alikuwa
bwana wetu na mkuu wetu, lakini aliwaosha miguu wanafunzi, kitendo
tunachotakiwa kila mwaka kwenye adhimisho la Ushirika wa Meza ya Bwana, tunapomkumbuka
(Yohana 13:14). Hatimaye aliutoa uhai wetu kwa ajili yetu. Hii ni tabia
anayoitaka Baba tuwenayo (1Yohana 3:16).
Kristo hakuona kuwa
sio tu kuwa aliwaona wale walioitwa na Baba kuwa wana kiu ya maji ya uzima,
bali aliyaona pia mataifa (ngamia) kuwa walihitaji kunywa kwenye kisima cha
uzima. Alijua kwamba ilimpasa kuutoa uhai wake, kwa ajili yetu ili tumpokee
Roho Mtakatifu wa Baba, iwe kama sisi tulikuwa Wayahudi au Wayunani.
Mwanzo 24:19 Hata alipokwisha kumnywesha akasema, Na ngamia zako nitawatekea, hata watakapokwisha kunywa.
Hapa Rebeka alikuwa anaonyesha kwamba yeye alijua
na kuelewa mahitaji ya kiu kwa ngamia. Hii ilikuwa ni zaidi ya tendo la wema au ukarimu.
Mithali 12:10 Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama
wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili.
Tumeitwa
ili tuwe watakatifu na inatupasa kufikirie maisha na hali au mambo ya wengine.
Kuweka kiusahihi sana, kunamaanisha dhana ya “mpende jirani yako kama
unavyojipenda mwenyewe,” (Kumbukumbu la Torati 6:4). Kristo hakufa kwa ajili ya
watu wa daraja moja maalumu la kimaisha. Bali alikufa kwa ajili ya watu wote.
Inatupasa kuwa wema kwa watu wote na sio kwa kuwabagua wengine. Tumeambiwa
kuwapenda hata adui zetu (Mathayo 5:44).
Kwa upendo aliomuonyesha huyu mgeni na
wanyama wake, Rebeka kwa kweli alikuwa anatafuta urithi wake mwenyewe. Kanisa
(Rebeka) linatafuta urithi wake (Mataifa). Kwa kuwapenda majirani zetu sasa,
tunawatafuta wale watakaokuwa kwenye uangalizi wetu (Ufunuo 2:26-27).
Mwanzo 24:20 Akafanya haraka, akamwaga maji ya mtungi
wake katika birika, akapiga mbio kisimani ateke, akawatekea ngamia zake wote.
Rebeka kwa
haraka sana alimwaga mtungi wake kwenye chombo. Yatupasa wakati wote kuipa
kipaumbele tabia ya kuwasaidia wengine. Hatuwezi kuruhusu wale wanaoomba
mwongozo wa kiroho wafe kwa kiu. Yatupasa kuchukua hatua mara moja. Mungu
amewaita watu kutoka kwenye mataifa yote, na yatupasa kufanya kila
linalowezekana kuona kwamba wote wanaweza kupokea maji yatoayo uzima aliyonayo
Mungu kwa Mwanae Yesu Kristo (1Wakorintho 12:13).
Tunaona kwamba hakuna tofauti kati ya
vitakatifu na vilivyo najisi. Ngamia wa Eliezeri alikunywa maji kutoka kwenye kisima
hichohicho. Tumepewa Roho huyohuyo, lakini kwa uwezo na vipawa tofauti.
Rebeka aliweza kukijaza na kumwaga mara
kadhaa. Watu wengine wanaomtoa Roho kwenye kuwahudumia wengine wanaona ni
vigumu kutosheleza roho yao. Lakini haitupasi kuchoka kuwatumikia wengine.
Yatupasa tuweze kuonyesha roho ya huruma na kupendana sote.
Mwanzo 24:21 Basi yule mtu akamkazia macho, akanyamaza, ili ajue kwamba Bwana
ameifanikisha safari yake ama sivyo.
Tunaweza kujifunza kutoka kwenye aya hii kwamba
mtu huyu anamuwakilishwa hapa Kristo, kama sisi sasa tulivyotolewa kwake. Tumebatizwa
kwenye mwili wa Kristo. Hii inatuonyesha kuwa ni Baba peke yake ndiye mwenye
uweza wa kujua kila jambo (ajuaye kila jambo). Kristo hajui matokeo ya kila
kitu. Ni Baba aliye mbinguni peke yake ndiye anajua mambo yote (Mathayo
24:36).
Mwanzo 24:22 Ikawa, ngamia walipokwisha kunywa, yule mtu akatwaa pete
ya dhahabu, uzani wake ulikuwa nusu shekeli, na vikuku viwili kwa mikono yake,
uzani wake ulikuwa shekeli kumi za dhahabu, 23 akasema,
U binti wa nani wewe? Tafadhali uniambie. Je! Iko nafasi katika nyumba ya baba
yako tupate mahali pa kukaa kwa muda?
Utoaji wa vikuku mikononi
mwake na “pete puani” mwake au kiusahihi zaidi vito kwenye paja la uso; sawa na
linavyosema jarida la Chimbuko la Uvaaji wa Ndewe na Vito
vya Thamani Nyakati za Kale (Na. 197), inahusiana na ununuzi wa mwanadamu
mzima inayoulizwa na kufanya upatanisho.
Tunahukumiwa kwa
matendo yetu, ambayo kwa namna mbalimbalia yanahusika na mkono, ikiwakilisha
mtu mzima yote (Zaburi 24:4, Matendo 2:23). Mkono unaweza kuwakilisha kikundi;
“mkono wa maadui zangu,” (Zaburi.31:15); taifa; “mkono wa Wamisri,” (Kutoka 3:8); na inatumika kuelezea wakati, “Tubuni
kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia,” (Mathayo 3:2, Mathayo 4:17). Mkono
unamaanisha pia njia ambayo Kristo alitumia kuponya: “Yesu alinyoosha mkono
wake na kumkamata” (Mathayo 14:31); "Binti
yangu ndiye kwanza amekufa, lakini njoo uweke mkono wako juu yake naye atakuwa
hai" (Mathayo 9:18). Sisi pia tunaitumia mikono yetu tunapoomba (Mwanzo
14:22). Mkono unamaanisha udhaifu au uweza na unatumika kwa baraka (Mwanzo
48:14,17); na kwenye ibada (Walawi 14:26,27).
Vikuku viwili
vinawakilisha pande mbili zote, yaani upande wa kuume na kushoto, vinaashiria
udhaifu wa kimwili (kushoto) na uimara wetu wa kiroho (kuume).
Waebrania wote
wawili, yaani mwanamke na mwanamume walivaa vikuku. Kanisa limefanyika kwa
mkusanyiko wa wanaume na wanawake nasi ni Wayahudi wa kiroho (Waebrania)
(Warumi 2:29). Vikuku ni nishani ya hadhi ya juu au unyenyekevu (2Samweli
1:10). Tumefanywa kuwa ni makuhani wa kifalme (1Petro 2:9) wa nyumba ya Daudi.
Vikuku vinatengenezwa kwa malighafi ya thamani. Sisi ni wa thamani machoni pa
Bwana (Zaburi 116:15; Zaburi 35:17). Vikuku vinatengenezwa kwa dhahabu. Mungu
Mwenyezi atakuwa dhahabu yetu, yaani tajiri wa imani (Ayubu 22:25).
Katika siku za
kale, vikuku, ambazo zinaashiria umuhimu vilivaliwa mkononi. Vikuku
vilivyozoeleka kuvaliwa na mwanamke vingeweza kuvaliwa mkononi, kama ilivyo
leo. Rebeka alipewa vikuku mikononi mwake kama zilivyokuwa zikivaliwa na
wanawake wa kawaida yeyote angaliyeona hivyo. Bali hii ilikuwa ni kuonyesha
kuwa Mungu anavitumia vitu dhaifu vinavyoonekana kuwa vya muhimu (vya kawaida)
ili kuwashinda wenye hekima na wenye nguvu (1Wakorintho 1:27).
Vikuku vilipimwa
kwa shekeli kumi, kwa kulinganisha na bei ambayo mtu inampasa kuilipa kwa ajili
ya mwanamke aliye na umri wa kati ya miaka mitano hadi ishirini (Walawi 27:1-5).
Kristo alilipa gharama ya kutununua sisi, wakati alipoyatoa maisha yake. Vikuku
na pete za puani zinahusiana pia katika kufanya upatanisho (Hesabu 31:49-50).
Mwanzo 24:24-25 Akasema, Mimi ni binti wa Bethueli
mwana wa Milka, aliyemzalia Nahori. 25 Tena akamwambia, Kwetu kuna majani na
malisho ya kutosha, na mahali pa kukaa wageni. 26
Wote wawili, yaani Eliezeri na Rebeka
walikuwa wa imani moja. Sisi tulio wa imani moja haitupasi kufungiwa nira
pamoja na wasioamini. Pia yatupasa kuzishika sikukuu zilizoamriwa na Bwana kwa
pamoja kila inapowezekana.
Mwanzo 24:26-27 Yule mtu akainama akamsujudu Bwana. 27 Akasema, Na atukuzwe Bwana, Mungu wa bwana
wangu Ibrahimu, ambaye hakuacha rehema zake na kweli yake kwa bwana wangu.
Bwana akaniongoza mimi nami njiani hata nyumba ya nduguze bwana wangu.
Hapa mtumishi anamshukuru Mungu. Ni
dhahiri sana kwamba mtumishi aliona kwamba vitu hivi vilivyotokea havikuwa
vimetokea kwa nasibu vyote, na kwamba Mungu Baba alikuwa anajua na ameviruhusu
kutokea kwenye mchakato huu wote. Anatoa kile kinachotakiwa na cha muhimu kwa
wanaokihitaji. Nasi pia yatupasa kutoa shukurani kwa kila jambo.
Mtumishi ‘akiwa
njiani’ inaonyesha kuwa alikuwa kweye njia ya kweli. Alikuwa kwenye njia ya
wokovu. Tunapokuwa tunazitoa njia zetu kwa Bwana, mawazo yetu atayathibitisha (Mithali
16:3). Kristo anawaongoza wale wote walio wake.
Mwanzo 24:28 Basi yule msichana akapiga mbio,
akawaambia watu wa nyumba ya mama yake mambo hayo.
Kanisa linalinda
kweli ambayo limeaminiwa kwayo na Roho Mtakatifu anayekaa ndani yetu (2Timotheo
1:14). Tunawajibu na kazi ya kuitangaza
na kuihubiri njia hii ya wokovu (Watendo 16:17). Kanisa linatoa ushuhuda ili
kumshuhudia Yesu Kristo kwa Israeli wa namna zote mbili, yaani wa kimwili na
kiroho.
Mwanzo 24:29-31 Na Rebeka alikuwa na kaka, jina lake
Labani. Labani akatoka mbio kumwendea yule mtu kisimani. 30 Ikawa, alipoiona ile pete, na vikuku
mikononi mwa nduguye, akasikia maneno ya Rebeka nduguye, akisema, Hivyo ndivyo
alivyoniambia mtu huyo, basi akamjia mtu yule, na tazama, amesimama karibu na
ngamia kisimani. 31 Akasema, Karibu, wewe uliyebarikiwa na Bwana,
mbona unasimama nje? Kwa maana nimeiweka nyumba tayari, na nafasi kwa ngamia.
Israeli wa
kimwili walitaka kuona utajiri wa kimwili wa Mungu, kabla hawajamuacha mioyoni
mwao (nyumba). Labani hakuwa na tofauti. Hakuwa anayajali mambo mazito na
muhimu yaliyoagizwa kwenye sheria, haki na rehema na imani (Mathayo 23:23). Alikuwa
amependezwa au kuvutiwa na kujilimbikizia utajiri au mali, zaidi, badala ya
kuzihifadhi kwa ajili ya kujiwekea utajiri mbinguni (Mathayo 6:20). Israeli wa kale
walimjua jinsi alivyokuwa Mungu Baba, kwa kuwa walipewa torati kutoka kwa Adamu.
Labani anazijua ahadi za Mungu, kwa kupitia maneno ya
dada yake Rebeka. “Ndipi mtu aliniambia,” kunaweza kumaanisha Torati iliyonenwa
na Mungu, ambayo ilipitishwa chini. Dada yake Rebeka, kwenye mfano huu
anawataja watu kama Henoko na Nuhu, ambao Roho wa Mungu alinena nao, kupitia Malaika wake, ambaye hatimaye alifanyika
mwanadamu Yesu Kristo (Matendo 3:18-21).
Anaweza
kufana milinganisho rahisi kutoka kwenye hadithi hii kwa jinsi inavyohusiana
kwene maelekezo ya maadhimisho ya Pasaka. Kristo anawaambia wanafunzi wake
waende mjini. Eliezeri alikuwa kisimani ambapo wanawake wa mji walikwenda (Mwanzo
24:15). Kristo alisema “mtakutana na
mwanamume akichukua mtungi wa maji; mfuateni mkaingie katika nyumba
atakayoingia yeye.” (Luka 22:10). Eliezeri mtumishi
alimkuta mwanamke aliyekuwa amebeba gudulia la maji (Mwanzo 24:15) alimfuata
kwa nyuma hadi nyumbani kwake.
Wanafunzi
wa Kristo walimuomba washinde usiku kucha pale na kuhusu chumba cha wageni (Luka
22:11). Eliezeri alimuuliza kama kulikuwa na mahali (chumba cha kulala mgeni)
ambapo angeweza kulala yeye pamoja na watu wake (wanafunzi).
Mwanzo 24:32 Na
mtu yule akaingia katika nyumba, akawafungua ngamia; naye akatoa majani na
malisho kwa ngamia, na maji ya kuoshea miguu yake, na miguu ya watu waliokuwa
pamoja naye.
Kristo
ambaye anashabihishwa na huyu mwanaume. Yeye ni mume wa kanisa la kiroho.
Lakini alikuja kama mtumishi. Kristo kupitia Roho Mtakatifu, alijua pa kwenda. Kristo
alikuja kwenye nyumba ambapo
wanafunzi walikuwepo jioni ile (Marko 14:17). Huu ulikuwa ni wakati wakati
Eliezeri alikutana na Rebeka na kisha akaenda nyumbani kwake.
Majani
makavu na malisho au chakula alichopewa ngamia huyu kinaweza kuwakilisha
chakula kikuu, kama vile mkate na mvinyo, ishara tunayoitumia kwa maadhimisho
ya Meza ya Bwana. Mfano unaolinganishwa na ngamia unatuonyesha kuwa tulikuwa
viumbe najisi kabla ya kutolewa dhabihu kwa Yesu Kisto. Tunaona mfano linganisho
huohuo ukitumika na nabii Yeremia akiwaelezea watu ambao hawakuwa watii kwa
Mungu wa Pekee na wa Kweli (Yeremia 2:20-24).
Maji yatolewa ili
kuosha miguu ya watu waliokuwa pamoja
naye. Kristo, katika usiku wa kabla ya Pasaka, aliwaosha wanafunzi wake
miguu, watu waliokuwa pamoja naye, (Yohana
13:5). Kama tutaangalia kwa mtazamo wa kiroho kwenye ayah ii, tunaona kuwa
ngamia walikuwa mfano wa wanafunzi pia kama viongozi wa makabila na kisha mataifa
kwenye hali yao ya unajisi wa kiroho.
Ni wale
waliobatizwa tu ndio wanaruhusiwa kushiriki ibada hii ya kuosha miguu. Wale wanaoshiriki
mlo hawalazimiki kuwa wamebatizwa. Hii inaongezeka kutokana majani
waliyopewa na kuwalisha ngamia. Tunaonyeshwa kwa wazi sana, kwamba tunachukuliwa kuwa ni safi kiroho,
wakati tunapobatizwa na kuwa sehemu ya ibada kua kuoshana miguu (1Petro
2:10; Matendo 11:9).
Mwanzo 24:33-34 Akaandaliwa
chakula, lakini akasema, Sili mpaka niseme kwanza maneno yangu. Akamwambia,
Haya, sema. 34 Akasema, Mimi
ni mtumwa wa Ibrahimu,
Hii inafanya taswira
ya Kristo kwenye mlo wake wa mwisho. Kristo alijua hangeweza kuula mlo wa
Pasaka akiwa na wanafunzi wake, kwa sababu yeye mwenyewe alikuwa ni Mwanakondoo
wa Pasaka, aliyeuawa hata kabla ya kuwekwa misingi ya dunia (1Petro 1:20; Luka.
22:14-16).
Kristo alikuwa
anasema kuwa angeila hii pamoja nao hapo yote yatakapotimilika. Na ndivyo
ilikuwa kwa Eliezeri hakuweza kula chakula hadi mpango wake wa kumtafutia Isaka
mke ukamilike.
Eliezeri anatangaza kuwa amekuja pale kwa
jina la Bwana wake Ibrahimu. Hii inamuashiria Kristo aliyetumwa na Mungu Baba.
Mtumishi si mkuu kulikb Bwana wake (Mathayo 10:24). Eliezeri, kama Kristo, alikuja
kwa jina la Bwana wake. Hakusema maneno kwa mamlaka yake mwenyewe, au mapenzi
yake mwenyewe. Bali aliyatenda mapenzi ya yeye aliyempeleka (Yohana 6:38).
Ni kama Kristo, Eliezeri anakuwa ni taswira
ya Roho Mtakatifu aliihubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu, kama alivyoelezea
kwenye kadamnasi ya watu waliokuwa kwenye nyumba hiyo sababu iliyomleta pale na
kile alichotumwa kuja kukifanya. Pia alielezea maelezo ya jinsi alivyokutana na
Rebeka kama ilivyoelezwa kwa kina kwenye Mwanzo 24:35-49. Kuna mambo muhimu
yanayofanana hapa na wanafunzi na jinsi walivyoishi na Kristo kwenye injili za
Agano Jipya.
Kristo alikuwa anaihubiri injili kwenye
nyumba ya Labani. Hii inatuambia sisi kuwa mataifa waliujua mpango wa wokovu.
Walitumiwa kila mara watumishi ili kuwafunulia mapenzi ya Baba.
Mwanzo 24:50-51 Ndipo Labani na Bethueli wakajibu
wakasema, Neno hili limetoka kwa Bwana, wala sisi hatuwezi kukuambia neno jema
wala baya. 51 Tazama, huyo
Rebeka yuko mbele yako, umchukue, ukaende zako awe mke wa mwana wa bwana wako,
kama alivyosema Bwana.
Kristo alijitibitisha mwenyewe kuwa ni
Mwana wa Mungu. Alikuwa amehitimisha kazi yake wakati alipoishi hapa duniani.
Alikamilisha yote yaliyoandikwa kwenye maandiko matakatifu. Kila kitu
kilifanyika sawa na kama Mungu alivyosema huko nyuma kwa kupitia manabii wake.
Mwanzo 24:52-53 Ikawa
mtumishi wa Ibrahimu aliposikia maneno yao, akainama hata nchi mbele za Bwana. 53 Kisha huyo mtumishi akatoa vyombo vya fedha, na
vyombo vya dhahabu, na mavazi, akampa Rebeka; na vitu vya thamani akampa
nduguye na mamaye pia.
Rebeka ndipo sasa
akaposwa na Isaka. Nasi tu
wachumba wake Kristo. Tumepambwa kama bibi arusi.
Mwanzo 24:54 Wakala wakanywa, yeye na watu waliokuwa pamoja naye, nao wakakaa usiku.
Wakaondoka asubuhi, naye akasema, Nipeni ruhusa niende kwa bwana wangu.
Tunaweza kudhania
hapa na kusema kuwa watu waliokula chakula pamoja naye, ni wale walioshiriki
maadhimisho ya mlo wa Meza ya Bwana. Kwa jinsi hiyohiyo ndivyo wanafunzi
walikuwa pamoja na Kristo, wakishinda usiku kucha, ili kutuonyesha sisi kwamba
Meza ya Bwana ni sehemu ya maadhimisho ya Sikuuu ya Pasaka. Yatupasa kuuadhimisha
usiku huu siku ya 14 ya mwezi wa Kwanza. Wote walikuwa pamoja kama tunavyofanya
kwenye maadhimisho ya siku takatifu.
Kristo alifufuka
toka kwa wafu siku ya Jumamosi adhuhuri, baada ya kushinda kwa siku tatu, usiku
na mchana kwenye tumbo la kaburi. Tunaweza kudhani kwa udadisi kwa haya
yafuatayo: Kisha akaamka
asubuhi - Krist alipaa kwenda
mbinguni mnamo saa za mapema za siku ya Jumapili. “Nipeleke mbali kwa Bwana wangu” - Kristo alipokuwa anafufuka kimwili,
alijiandaa kwenda kwa Baba. Kristo alitaka arudi mbinguni kwa Mungu wake.
Alikuwa amefufuka, na sasa alipaswa atolewe kama Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa,
wakati wa asubuhi. Alipaswa
kuwakilisha limbuko la kwanza la malimbuko yote.
Mwanzo 24:55 Ndugu
yake na mama yake wakasema, Msichana na akae kwetu kama siku kumi, zisipungue,
baadaye aende.
“Msichana na akae kwetu kama siku kumi,
zisipungue " inahusika
na mlolongo wa wakati. Tunajua kuwa siku moja ni sawa na miaka elfu kwa Bwana
na ndivyo ilivyo kinyume chake (2Petro 3:8).
Kitendo cha
kumchukua mke kutoka kwenye familia ya Ibrahimu kilifanyika kwenye wastani wa
takriban miaka 4000 iliyopita. Wale ambao walimfanya bibi arusi, wliochaguliwa
na Mungu, walianza kwa kiasi kikubwa tangu kipindi cha Ibrahimu (lakini
walikuwepo wengine kabla yake). Bibi arusi huhu alikuwa ndiyo kwanza kwenhye
umri wake wa utoto. Alikuwa ni kijana, kwa hiyo kulikuwa ni kipindi kirefu cha
yeye kutunzwa. Hii ni kutuonyesha sisi kwamba Kanisa lingekuwepo na kubakia
hapa duniani kwa siku chache au kwa kitambo kipindi kinacholinganishwa na miaka
elfu nne. Kanisa limepitia kipindi cha miaka elfu mbili cha kuandaliwa kwake na
kipindi kingine cha miaka elfu nne ya kuitwa na kutolewa nje.
Usemi wa kwamba Hata kwa siku kumi; baada ya hapo anaweza kwenda unatuambia kwamba kanisa lingeweza
kubaki hapa hadi kila kitu kikamillike (10) hadi wateule wengine waliosalia watakapoletwa
kutoka waliko. Baada ya hapo anaweza
kwenda. Baada ya yote wateule watakuwa wametiwa mhuri, ndipo tunaweza kwenda, kama wana wa ufufuo, na kuolewa kimfano na Kristo.
Mwanzo 24:56 Naye akawaambia, Msinikawilishe, mradi
Bwana amefanikisha njia yangu; nipeni ruhusa niende kwa bwana wangu.
Bwana Mungu
ameifanikisha njia ya mtumishi kwa hiyo alikuwa na hamasa ya kwenda nyumbani
kwa Bwana wake Ibrahimu. Kristo alitaka arudi nyuma kwa Mungu wake. Alikuwa
amekwisha fufuka tayari, na sasa alikuwa anataka kupaa kwenda mbinguni ili
kwenda kuchukua urithi wake akiwa kama limbuko la kwanza la malimbuko yote.
Mwanzo 24:57 Wakasema, Na tumwite huyo msichana, tumwulize mwenyewe. 58 Wakamwita Rebeka wakamwuliza, Je! Utakwenda na mtu huyu? Akasema, Nitakwenda.
Wasiwasi au swali
lililokuwa kama Rebeka angekuwa radhi kuolewa na Isaka. Neno wkaimuita linatuonyesha kuwa Mungu Baba
yetu anatuita kwa kila mmoja peke yake na kutuuliza kama kumfuata Kristo. Ni
uamuzi wa kila mmoja peke yake. Ulimwengu huu uliobakia una wito wake wenyewe.
Rebeka alijua
kuwa walikuwa wanaingia kwenye agano la muda mrefu. Wakati tunapoitwa, tumepewa
fursa ya kuingia kwenye agano la kupendwa na Mungu na Kristo wake. Wakristo
hatushurutishwi kinume na tupendavyo ili kumfuata Kristo. Tumepewa uchaguzi.
Mungu anampenda aina ya mtu aliyetayari kutoa kila kitu kwa ajili yake, na kuungana
na mwanae, Yesu Kristo.
Mwanzo 24:59-61 Ndipo wakampeleka Rebeka ndugu yao, na yaya wake, na
mtumishi wa Ibrahimu, na watu wake. 60 Wakambarikia Rebeka, wakamwambia, Ndugu
yetu, uwe wewe mama wa kumi elfu, mara elfu nyingi, na wazao wako waurithi
mlango wa hao wawachukiao. 61 Rebeka akaondoka na vijakazi wake, nao
wakapanda juu ya ngamia, wakamfuata yule mtu. Naye huyo mtumishi akamchukua
Rebeka akaenda zake.
(Tafsiri ya NRSV inatafsiri
sentensi ya mwisho kama; Naye huyo
mtumishi akamchukua Rebeka akaenda zake)
Usemi kwamba Ndipo Rebeka na mtumishi wake wakainuka kuondoka. Tulivhukuliwa
kama mtu aliyekufa kiroho (Waefeso 2:5; Wakolosai 3:3). Tangu tunapobatizwa tunapewa Roho Mtakatifu,
kwa njia ya Kristo. Sikukuu ya Pentekoste ni taswira ya ukweli huu. Tumetakaswa
sasa.
Rebeka
alibarikiwa kuwa ni mama wa makumi elfu na maelfu na uzao wake uliambiwa
utamiliki malango ya adui zao. Baraka hii iliendelea hadi kwa kupitia mataifa
yaliyoinuka kutoka kwake. Kwenye uzao wake ndipo makabila yaliyaongoza mataifa
ya wamataifa na mataifa yote ya dunia yaliyoingia Kanisani kama bibi arufi wa
Kristo kwa Roho Mtakatifu kwenye Ufufuo wa Wafu.
Ndipo tunasoma
kuwa Rebeka alipanda juu ya ngamia (mataifa) na kumfuata mtu ni taswira ya Roho
Mtakatifu na akaenda kwa Isaka anayemwakilisha Kristo mfufuka.
Kabla
hatujazaliwa, tulitakaswa. (Yeremia 1:5). Ingawa tunaishi duniani hatumo sehemu
yah ii. Na dniyo maana
tumepanda na kuwaendesha ngamia. Sisi tumetengwa, wtakatifu. Tumetumwa
kuyaendea mataifa, kuwaamsha ili wamjue Mungu, kupitia Kristo. Yatupasa
tuwaongoze kwenye neema iokoayo katika Kristo.
Ukweli wa kwamba wajakazi wa Rebeka waliinuka na kwenda naye, unatuonyesha kuwa wageni pia wameruhusiwa
kuhudhuria na kuadhimisha sikukuu (Yohana 12:20; Matendo 2:5-11). Tunaruhusiwa kuwa
na watu kwenye sikukuu ambao hawajabatizwa ambao pia ni washirika kwenye mwili
wa Yesu Kristo. Kutajwa kwa wajakazi kunatuambia kuwa wanawake wanatakiwa
kuhudhuria sikukuu zilizoamriwa (1Samweli 1:3,9; Luka
2:41-42). Ilieleweka na Waisraeli wa zamani kuwa jinsia zote mbili, yaani wanaume,
wanawake hata pia na wageni walio ndani ya malango yao, wanapaswa kujihudhurisha
kwenye sikuku. Kwa kufafanua, ni kwamba hii iliendelea hadi kwa wateule wakiwa
kama Israeli wa kiroho. Ni wanaume tu ndio wamelazimishwa kuhudhuria sikukuu na
Torati. Wanawake wanaweza kusamehewa kutokana na sababu za kimaumbile au za
kimwili kwa wakati fulani, lakini nao wanatarajiwa kuhudhuria.
Tunatolea nje na
kutoka. Hii inaashiria kuwa ni tukio la kutoka ya pili itakayokuja kutokea. Rebeka
analiwakilisha kanisa la kiroho na wale wajakazi wake wanawakilisha taifa
halisi la kimwili la Israeli. Walipanda
juu ya ngamia, inaonyesha kuwa kwa njia ya mataifa, tutarudi nyuma nyumbani
kwetu, ambako kutoka huko tulifarakana na kutawanyika. Hebu na tumfuate Kristo.
Ndipo mtumishi
akamchukua Rebeka. Neno akamchukua
linatokana na SHD 3947. Linaweza kuwa na idadi kadhaa ya maana zake, ambayo
yanaweza kuhusiana na taswira yote iliyoko ya mwanadamu. Tumetwaliwa kutoka kwenye imani potofu, tukanunuliwa kwa bei, kwa
ajili ya Kristo, tukiandaliwa kwa arusi.
Sisi tumechaguliwa, kizazi kiteule kitakachopelekwa kwenye ndoa.
Kutokana na neno
hili la kutwaliwa tunaweza kuona
dhana inayofanana kutoka kwenye hadithi ya uumbaji, kwenye Bustani ya Edeni,
wakati Bwana alipoutwaa ubavu kutoka
kwa Adamu. Neno hilihili limetumika, kwa uzito kwene Mwanzo 24:61 ‘ndipo mtumishi
akamchukua Rebeka’.
Mwanzo 2:21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi
mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali
pake, 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana
Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 23 Adamu
akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu,
basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.
Mungu alisababisha
usingizi mzito aupate Adamu ili amfanyie mke. Akachukua mmoja ya ubavu wake na akamfanyia (inasomeka “kumjengea”
kwa Kiebrania) mwanamke. Kutokana na hii twaweza kutofautisha kutwaliwa kwa kanisa. Kanisa limeondolewa
na mwanadamu (mtu) wakati usingizi mzito wa kiroho uliwaangukia wao. Tunajua
kwamba Adamu wa kwanza alitenda dhambi, na kwa hiyo Kristo alikuja ili awe
Adamu wa pili. Ni kama vile Mungu alivyoutwa ubavu mmoja, ndivyo hata sisi
tumetwaliwa tutoke (duniani). Tunafanyika kuwa washirika binafsi wa mwili wa
Kristo (1Wakorintho 12:27).
Neno ubavu linatokana na kamusi ya SHD 6763 tsela na lina maana mbalimbali. Tafsiri ya The Authorised Version inalitafsiri neno hili kama 1.upande, ubavu, bimu. 1A Ubavu (wa mwanadamu). 1C upande wa chumba au seli (za[li] muundo wa hekalu). Sisi ndio Hekalu hilo la Mungu (1Wakorintho 3:17).
Mwanzo 24:62 Basi Isaka alikuwa amekuja kwa njia ya Beer-lahai-roi, maana alikaa katika nchi ya kusini.
Kristo alkuja
kutoka, kuwa kwamba aliumbwa na kutumwa aje, kutoka kwenye njia, ambayo ndiye Baba aliye “kisima cha uzima na
maono” (Lahai Roi). Kwa kuwa Eloa ni kiini cha uzima. Mungu wa Milele, (1Timotheo
6:16) anayemwangalia kwa jicho lake mwenye haki na mtakatifu wake, akitungoja
sisi ili tumuone yeye pia, wakati Kristo atakaporudi (Matendo 22:14).
Mwanzo 24:63 Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni; akainua macho yake, akaona, kuna ngamia wanakuja.
Isaka alitoka
nje ili atafakari shambani wakati wa jua kupunga. Tunaweza kujipatia maarifa
makubwa ya tukio hili, wakati tunapoipitia aya hii ili kuipata taswira halisi.
Kuelewa kile kinachomaanisha kwenye kifungu hiki kisemacho alitoka nje na kujua kinachokusudia, kutatusaidia kuifafanua maana
ya aya hii.
Kwa mujibu wa kamusi ya (SHD 3318) toka nje, ondoka. Kuondoka
na kwenda (kwenda mahali),kuendelea na kwenda (kwendamahali au kwenye kitu fulani). 1A4 kuja au kwenda mbele
(kwa nalengo au matokeo). Kutoa nje, kusukumia
nje. 1B2 kutoo nje ya. 1B3 kusukumia nje.1B4 kutoa, kutolewa
nje au kusukumwa mbele.
Strong, J. (1996). Enhanced Strong's Lexicon
(H3318). Ontario: Woodside
Bible Fellowship.
Kristo alitoka
nje kutoka kwa Baba. Aliondoka kutoka
mbinguni na akatoka kuelekea (mahali), duniani. Ndipo Kristo aliendelea, akiwa kama
kondoo wa kuchinjwa. Tangia kufufuka kwake, alifanyika kuwa limbuko la
malimbuko yote (kwa au kwa ajili ya kitu Fulani) akaenda kwa Baba na kuwa
ni mleta wokovu. (ambalo ndilo lengo au matokeo) kwa wote wenye mwili.
Kristo sasa anakuwa na jukumu la kuwatoa watu, na kupeleka
nje ya ulimwengu huu, kuwatoa nje kutoka gizani, na kuwatoa
kutoka utumwani, hivyo kuwatoa, kutolewa na kutengwa kama taifa
takatifu.
Isaka alitoka nje kutafakari uwanjani majira ya adhuhuri. Yatupasa kuliangalia jambo hili neno kutafakari maana yake. Linatoka kwenye SHD 7742 suwach. Inalitafsiri kama “kutafakari” mara moja. Kutafakari, kufikiri, kupata hisia, kuongea, kulaumu. (Strong, J. (1996). Enhanced Strong's Lexicon (H7742). Ontario: Woodside Bible Fellowship.)
Tunapoliendeleza kila neno linaloleta maana ya kutafakari kwa upana kidogo, tunaiona taswira ikiendelea.
1.Kutafakari = fikiri, ashiria, weka huru, fikria, waza
2.Kikundi cha watu = jamii, wasiliana, semezana, shamba la jamii
3.Sema = semezana, zungumza, wasiliana papo kwa papo,
ambia
4.Lalamika = pinga, kosoa,
tafuta au gundua makosa
Tunauona mwandamano wa matukio. Kile tunachoweza kukipunguza ni muda
muafaka na kusudi au lengo la kurudi kwa Kristo. Kristo anawazia tu kuyatenda mapenzi ya Baba. Anaonyesha uhalisia wake. Anarudi kwenye jamii ambayo aliishi nayo, shamba
la jamii ambalo ni mwanadamu, tungaliweza kusema. Kipindi hiki atayasema mambo
yote yamhusuyo mwanadamu, lakini wakati anapoongea, itakuwa na upanga wenye makali kuwili. Kristo amekuja
kuiokoa dunia. Anakuja kwa namna ya upinzani,
kwa utovu wetu wa nidhamu. Kwa kuwa amelikuta kosa kwa jinsi tunavyoishi.
Shamba darasa liko mbali na kuingiliwa au kukanganywa. Wakati
tunapotafakari na kujumuika pamoja kwenye siku za ibada, yatupasa kuweza kufikiri,
kuwa kielelezo cha neno la Mungu na kuwasiliana kila mmoja na mwenzake, kwa
njia ya kimazingira kutokana na mikanganyo ya mwingiliano na vishawishi vya
ulimwengu huu.
Tunajua kwamba wakati Kristo atakaporudi, atarudi huko Yerusalemu. Wale ngamia waliokuwa wanakuja, tunajua sasa
kuwa ni mataifa yatakayojikusanya karibu au kuuzunguka mji wa Yerusalemu ili
kufanya vita au kupigananao (Ufunuo 16:12). Kuna idadi fulani ya matukio
yatakayodhihirika wakati Kristo atakaporudi.
Mwanzo 24:64 Rebeka akainua macho, naye alipomwona
Isaka, alishuka juu ya ngamia.
Tunaona mataifa yalijongea ili kuusogelea mji wa Yerusalemu. Ni sawa kama
ule mfano wa mtini, tunaweza kuyaona matukio haya yakidhihirika. Sisi tuliodumu
kuwa waaminifu kwa Mungu, na kuufanya mwili wa Kristo, tutashuhudia. Hakuna
mwingine yeyote alyetajwa. Hakutajwa suria wake wala mtumishi awaye yote. Hii
inalilenga moja kwa moja kanisa (Luka 21:27-28). Ni ukombozi wetu, sio wa mataifa. Kristo
anakuja kuwaokoa wateule (Mathayo 24:22).
Sasa tunaona jambo linguine la matukio yanayojidhihirisha wakati Kristo
atakaporudi. Tunapomuona Kristo, tunakuwa tumeshushwa, au maelezo yanayofaa
zaidi ni kwamba tumefufuka kutoka kwa mataifa.
Ngamia tunaowaendesha ni mataifa tunayoishi kwayo. Ni Rebeka tu ndiye
aliyeshuka; hakuna mtu mwingine aliyefanya. Tunaona kuwa tumefufuliwa kutoka
kila moja ya mataifa yetu. Tunaona kuwa Rebeka
alishuka kutoka
juu ya ngamia wake. Hii
inatuonyesha kuwa sisi kama mmoja mmoja tupo kwenye mataifa yetu wenyewe. Hivi
ndivyo inavyomaanisha hapa. Hatujakusanywa wote pamoja tukikaa juu ya ngamia
mmoja. Tumetawanyika kwenye mataifa mbalimbali. Hakuna mahali pa usalama. Vinginevyo,
angekuwa amekalishwa na wengine juu ya ngamia mmoja.
Wakati Rebeka alipoinua macho yake juu, inatuambia kitu fulani. Alijua kuwa alikuwa anakwenda kuolewa na mrithi wa utajiri na
mali nyingi, ila bado alibakia kuwa mnyenyekevu. Kwenye safari yetu hatupaswi
kuvimba vichwa vyetu kwa majivuno na kiburi, ila tujishushe chini kwa
unyenyekevu (Isaya 2:11).
Kumbuka kuwa Rebeka hakuwahi kumuona Isaka hapo kabla. Lakina wakati
alipomuona tu akiwa kondeni, alishuka kutoka juu ya ngamia wake. Asingeweza
kushuka kwa mtu mwingine yeyote tu kwa
kuwa alimwambia yule mtumishi akamuuliza “je, mtu huyu ni nani?” Yeye (kanisa) alijua kuwa alikuwa Isaka
(Kristo).
Mwanzo 24:65 Akamwambia
mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye
bwana wangu. Basi akatwaa shela yake akajifunika.
Hadithi hii ipo kwenye Yohana 6:15-20 inaelezea jinsi Kristo alivyokuja
kwetu, wakati tulipokuwa kwenye matatizo. Wakati tulipokuwa katikati ya mahali
pasipojulikana, pasipo na tumaini, alitembea juu ya maji, ili atupate sisi.
Anatenda miujiza. Wakati anapokuja kwetu wakati tunapokata tama, kwa haraka sana
alipelekwa nchini, ambavyo ni salama.
Ni kama Isaka alipotembea kondeni ili akutane na Rebeka, Kristo alitembea
juu ya maji ili akutane na sisi. Wanafunzi wake waliogopa. Haitupasi kuogoa.
Kristo kwa makusudi mazima alitupokea sisi.
Siku zetu za mashaka na kukata tama zimekwisha. Waliletwa kwa haraka sana kwenye nchi,
waliyokuwa wanaiendea. Nasi tunapelekwa kwenye nchi yetu ya kiroho,
Yerusalemu. Huko ndiko tunakokwenda.
Mwanzo 24:65 Akamwambia mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni
kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye bwana wangu. Basi akatwaa shela yake
akajifunika.
Neno la Kiebrania la shela au kilemba (SHD 6809), kutoka
kwenye shina lake lisilotumika linamaanisha “kujifunga juu.” Inaweza kujulikana
kama kufunika au kujizinga.
Tafsiri ya The American Standard Version inasema
alichukua shela yake. Kwa hiyo aliichukua shela na kujifunika.
Kanisa linachukuliwa au kufananishwa na mwanamke, nasi tunalifanya liwepo
Kanisa la Mungu. Ni kama tulivyokwisha soma tayari, sisi ni wanawali mabikira
wa kiroho. Anaonyesha heshima na unyenyekevu anapokutna na mume wake.
Wakati Kristo atakaporudi, ndipo tutafufuliwa, na kuchukua shela za kubalidika kwetu na kuwa viumbe wa kiroho. Hii
ndiyo ile shela tutakayojifunika kwayo. Miili yetu ya zamani sasa itakuwa imeondoka,
na tutabadilika na kuwa wana wa Mungu wa Kiroho. Hili ndilo vazi letu jipya.
Hatutakuwa wa damu na mwili tena, ila wa kiroho.
Zaburi 140:7 Ee
MUNGU Bwana, nguvu za wokovu wangu, Umenifunika kichwa changu siku ya vita.
Siku hii inafananishwa kama siku ya vita. Ni
wakati Kristo atakaporudi kuchukua kile kilicho haki yake na kitakatifu sana.
Atakichukua kwa nguvu. Mapepo hawaendi kumpa kwa urahisi. Tunafarijika kwa kuwa
Mungu atakifunika kichwa chetu wakati Kristo atakaporudi. Kichwa chetu
kinamaanisha mawazo yetu na hali zetu za mwili.
Mwanzo 24:66 Yule mtumishi akamwambia Isaka mambo yote aliyoyatenda.
Ni kwa njia ya Roho wa Baba ambayo vitu vyote
vitafunuliwa (1Wakorintho 2:10). Baba yu ndani mwa Kristo, na Kristo yu ndani
yake (Yohana 10:38)
Mwanzo 24:67 Isaka
akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake, Sara, akamtwaa Rebeka, akawa
mkewe, akampenda; Isaka akafarijika kwa ajili ya kufa kwa mamake.
Isaka alimchukua Rebeka na kumpeleka kwenye hema
ya mama yake, kama sisi tunavyochukuliwa na Kristo kwenye Yerusalemu Mpya, Mama
wa sisi sote.
Wazo la kuishi kwenye vibanda (hemani) lilikuwa ni
kushinikiza utegemezi wa Israeli kwa Mungu, wakati walipokuwa wageni na
wasafiri jangwani.
(Aya ya 67)….. Isaka akamwingiza Rebeka katika hema ya mama yake,
Mama anawakilisha
taifa la kimwili la Israeli. Kristo alikuja akitokea kwenye kabila la Yuda (Mathayo
2:1). Mwanamke aliye kwenye kitabu cha
Ufunuo anawakilisha Israeli wa kimwili (na wa kiroho) (Ufunuo 12:13).
Israeli wa kale hawakuupata wokovu kwa ujumla. Ni baadhi yao wakiwa mmoja mmoja
waliweza kufanikisha. Tunaweza kuiita zama hii kuwa ni kama cha kufa. Kanisa
lilimfariiji Kristo.
Kwa hili tunaweza
kusema kwamba Kristo alifarijika baada ya kifo cha mama yake. Yerusalemu ile
iliangamizwa na Yerusalemu Mpya itatujia kama Mji wa Mungu (soma jarida la Mji wa Mungu (Na. 180)). Sikukuu ya Mkutano wa Makini au Siku
Iliyokuu ya Mwisho inawakilisha hukumu ya haki ya ulimwengu na kuondolewa kwa
mwisho na ukomo wa dhambi. Inawakilisha ujio wa Mungu duniani na Mji wa Mungu
utajiunga kwenye marejesho mapya ya mwisho. Marejesho haya ya mwisho ni matokeo
ya mwisho ya Mpango wa Mungu.
q