Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[231]
Kipeperushi cha
Zamani cha Mafundisho ya Kanisa la Mill Yard
(Toleo La 1.0 19971224-19971224)
Shukurani zetu
zimwendee Thomas McElwain kwa kutupatia kipeperushi kilichoambatanishwa,
ambacho ni kabrasha la zamani sana la Kiingereza la Kanisa la Sabato.
Inaonyesha kuwa haihitaji kupingwa wala kuonewa mashaka kwamba mafundisho
halisia ya zamani ya Kanisa la Kibaptist la Sabato lijulikanalo kama “the Mill
Yard Seventh Day Baptist Church” kuhusu Uungu yalikuwa ya mrengo wa Kiyunitarian
kama wanateolojia wenyewe wa kanisa hili la Mill Yard walivyoshuhudia na kwa
sawasawa na mafundisho ya Makanisa ya Kikeisto ya Mungu, yaani Christian
Churches of God.
Christian Churches of God
Email: secretary@ccg.org
(tr. 2016)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na
tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.
Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala
yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia
yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Dagoni aliyeangukia kizingitini: au Udadisi na
hoja za wanadamu, waziwezi kusimama mbele ya amti ya kwanza ya Mungu isemayo,
Usiwe na miungu mingine ila mimi.
Na Edward Elwall wa Wolverhampton
Iliyochapishwa mwaka 1726
Usiwe na miungu
mingine ila Mimi.
Amri hii Takatifu
ilinenwa na kutolewa na Mungu mwenyewe, hivyo tu, bali iliandikwa kwa chanda au
kidole cha Mungu, kwa hiyo, wale wote Wampendao yeye kwa Mioyo yao yote, na
Mioyo yao, na guvu zao, waweze kuamini na kuzitii Sheria zake.
Sasa hebu na watu
weote wamche Mungu, chukua Notisi maalumu na za muhimu, kwamba neno hili la mwisho
kabia la Torati tukufu, pamoja (nami) ni kiasi fulani cha Kuwakanusha wale wanaomfanya
Mungu aliye juu sana kuwa ni wa afsi ya uwingi: Kwa kuwa Neno Mimi,
halimjumuishi kabisa Mtu au nafsi yoyote kwa kumfanya awe Mungu, bali huyu
mmoja Mimi; na hawezi kuwa wawili, wala watatu, wala wanne. Na kwa
kulithibitisha hilo kama Mtawala wa ndani wa Binadamu wote, Mungu alinena kwa
Kinywa cha Nabii Musa, Kumbukumbu la Torati 32, 39. "Fahamu sasa ya kuwa
Mimi, naam, Mimi ndiye, Wala hapana Mungu mwingine ila Mimi." Tusimruhusu Mtu yeyote aupotoshe
kwa wazi, dhahiri, kiuwazi, Maana ya Maneno yake, kwa kuwa hakuna miungu
mingine ila Mimi kunaonyesha ushahidi wa wazi wa kutomjumuisha na Mtu au nafsi
nyingine yoyote ila Mimi peke yangu.
Mwokozi wetu Yesu
Kristo anatoa ushuhuda kama huohuo, kwa kuwa wakati mtu fulani alipomuuliwa
kwamba ni Amri ipi iliyo Kuu na ya kwanza kuliko zote, alitoa Maelezo kama
hayohayo, kama ilivyokuwa ikiaminiwa na imani nzuri ya zamani ya mtu mwaminifu
Musa ilivyokuwa hapo kabla, isemayo, "Sikiza, Ee Israeli;
Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja." Marko 12:29, na aya ya 32 inasema, "Yule
mwandishi akamwambia, Hakika, Mwalimu, umesema vema ya kwamba Mungu ni mmoja,
wala hakuna mwingine ila yeye;."
Kutokana na hiyo
ndipo nimechukua Magizo ya asili; kwamba hakuna mwingine ila Mungu ni mmoja tu,
na hakuna mwingine ila Yeye tu.
Kwa hiyo, yeyote
anayemfanya huyu Mungu Mmoja kuwa ana Nafsi nyingine yoyote zaidi kuliko alivyo
Yeye mmoja, anapotoka na kukosea kabia na fikra yake si ya kweli kabisa; na
anajaribu Kuukanganya na kuupigwa kwa wazi Ushuhuda wa Yesu Kristo.
Sasa, Sheria ya
milele iliyotiwa kwenye Sanduku la Agano la Mungu, ni hii, isemayo, Usiwe na
miungu mingine ila Mimi; lakini mashambulizi wa Wanadamu, yalipelekea
wamsimamishe Dagoni; lakini alianguka mbele ya Sanduku la Agano. Na ndipo
walimsimamisha na kumrudisha sehemu yake tena, lakini Asubuhi ilipofika,
tazama, Dagoni alianguka tena Uso wake kifudifudi Ardhini, mbele ya Sanduku la
Agano la Mungu, na hivyo ndivyo itakavyokuwa kwenye Mavumbuzi au maagizo ya
wanadamu wote.
Sasa, Maneno ya
Mungu wa Kweli, kwenye Amri ya Nne ni haya, Siku ya Saba ni Sabato ya Bwana
Mungu wako; lakini Mavumbuzi na maagizo ya Wanadamu, yameifanya Siku ya Sita
kuwa ni Sabato, na wengine wakaifanya Siku ya kwanza kuwa ni Sabato. Karibia
Dola Kuu zote za Dunia, zilizo chini ya Waturuki, Waajemi, Wamoguli, na Mataifa
mengi mengine, wameifanya Siku ya Sita, kuwa ni Sabato; na karibia Mataifa yote
yaliyo bado, au yaliyowahi kuwa chini ya Papa, na yaliyoyashika maagizo yake,
yaliifanya Siku ya Kwanza kuwa ndiyo Sabato. Maamuzi yote hayo Yanapingana na
Sheria takatifu ya Mungu, iliyotuambia wazi sana, na kwa Kinywa chake mwenyewe
kuwa, Siku ya Saba ni Sabato.
Na kwapmb
tusisahau kabisa, wala kujifanya kuwa hatulijui agizo hili, alipenda kuiandika
kwa rehema zake na kwa Chanda cha mkono wake kwenye Mbao za Mawe, na akaagiza
itiwe kwenye Sanduku la Agano la Mungu, wakati ambapo kabla ya Sheria yoyote ya
Kidini na kiibada haikjaja, bali ilikuwa ni Sheria hii tu takatifu peke yake ya
Amri Kumi; ambayo Kristo anatuambia pia kwamba, Lakini ni vyepesi zaidi
mbingu na nchi vitoweke, kuliko itanguke nukta moja ya torati, Luka 16.17. na anatuambia kwenye Mat.
5;17. Kwamba hakuja kuitangua, bali kuitimiliza, ambavyo ni kuitenda
Kwa kifupi, jinsi
inavyopotoshwa, ndivyo jinsi itakavyomuathiri Mtu mwadilifu, kwa kuwaona watu
wakichagua kuyafanya na kuyafuata Maagizo mapotofu yanayoamriwa kwenye Dini
zao, badala ya kuzishika amri takatifu za Mwenyezi Mungu.
Ni kwa kiasi gani
basi Roho yangu inateseka kwa Huzuni, ninapofikiria ni watu wengi kwa kiasi
gani wanaoelekea kwennye Nyumba za Minara, na huko wanawasikiliza Makasisi wao
wakiinenea kinyume Amri hii ya Nne, isemayo, Ikumbuke siku ya Sabato
uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni
Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, nk, nab ado Watu wanaomba na kusema, Bwana
Utuhurumie, na tunaitoa Mioyo yetu kuishika Sheria hii; na ambavyo ikionekana
wazi kabisa, wanaifanya hii kuwa ni Sheria au amri ya Mungu, au vinginevyo, Ni
kwa nini wanamuomba na wakiizuia Mioyo ishiishike? Na bado kwa wakati huo huo,
hakuna kitu kingine chochote kwa hakika, zaidi ya vile walivyokusudia kuishika,
au kuitii amri hii.
Watu kadhaa wenye
hekima na busara na wema, wameungana na mimi kwenye Somo hili la Linalombelezewa
na kusikitisha, na wakaomba kutokee Matengenezo; na, kwa kweli, Siandiki jambo
hili ili kumuudhi au kumchokoza Mtu yeyote, lakini ni zaidi tu, ni kwamba, ili
waiweke Moyoni, na waichukulie kiukamilifu kwa Kicho na Hofu, ili Mungu
asitukanwe; na kwamba waovu wasifanywe mioyo yao kuwa migumu na kutiwamoyo, kwa
Kuivunja Sheria ile Takatifu, kwa kuzivunja na nyinginezo pia.
Kwa kuwa ni
vizuri kuyashika Maneno ya Mtume Yakobo yasemayo, Maana mtu awaye yote
atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.
11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema,
Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria, Yakobo 2:10,11.
Sasa, inaweza
kuwa imesemwa kwenye yoyote kati ya Amri hizi Kumi’ ya Nne na ya Tano, pamoja
na ile ya Sita na ya Saba. Lakini uwiano wa ujumla wa Wanadamu waliokuwanao
zaidi ya kuchukulia Dini zao nje ya Almanack, zaidi nje ya Sheria Takatifu ya
Mungu; Kwa kuwa Mamilioni ya watu watazishika Siku zilizochorwa Maandishi
Mekundu, ambazo Papa mwenye Maagizo ya kibinadamu amezipangia, lakini Siku
Takatifu ya Sabato, ambayo Mungu mwenyewe ameiamuru, hawataishika, wala
kuitilia Maanani kwa Kuiadhimisha.
Sawa tu na ndivyo
hivyohivyo wanavyofanywa kwenye Amri ya 2, ambapo Mungu anasema, Usijifanyie
sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala
kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala
kuvitumikia; nk. lakini Mafundisho ya
Mapapa, Maaskofu na Makasisi, yamesababisha kutengenezwe maelfu ya Sanamu za Kuchonga;
na sio tu kwamba wazisujudie kwa kuzipigia magoti na wanadamu, bali hata
wazipige busu. Na kwa kuivunja Amri ya 3, sasa imekuwa kama kitu cha
Kuambukiza, na cha Ulimwengu wote, ikipuuziwa kwamba Nafsi inayo nyenyekea kwa
hakika inaweza kusema na abii wa Zamani, Isaya, xxiv.3. kusema; Dunia
imenajisiwa na Wanaoikalia, kwa kuwa wamezihalifu Sheria, na kubadili Amri, ...
Isaya 29:13.14.15.16.
Hebu na watu wote
wema wachukue Notisi kadhaa, jinsi Mungu anavyopendezwanao wote, ambao Wanamcha
na kumhofu yeye, kinyume na inavyofundishwa na Maagizo ya Wanadamu: Ambavyo ni,
kama Maneno ya Bwana wetu yasemavyo, Hayo yote ni Mafundisho, Amri za Wanadamu.
Lakini wote walio
wema, wanyofu wa Roho, wanaompenda Mungu Aliyehai, watayainua Macho yao
kumtazama Mungu Aliye Juu sana, na kwa Manabii wake, na kwa Kristo na Miyume
wake, ili kuitafuta Amri Takatifu, na mambo yote yahusuyo Imani yao na Wokovu,
Ibada yao, au kitu chochote kinachohusiana na Hatima yao ijayo; Na kwma kwenye
Maagizo yoyote ya Wanadamu, kwa masuala ya Kidini, iwe ni Wafalme au Mapapa,
Maaskofu au Makasisi, au Yeyote yule, tusishughulike nao, wala Watunga Kanuni
za Imani.
Lakini kwa mambo
yote ambayo yana Tabia za muda mfupi, na zinazohusiana na Hali zetu za Kijamii,
Siasa za Serikali za Kidunia, zihakikishe zinatii Sheria na maagizo ya Wanadamu
kwa ajili ya Bwana; na kutii kikamilifu kinachoamriwa na Mahakama, kutoka kwa
mfalme aliye kwenye Kiti cha Enzi, hadi chini kwa Mjumbe mwenye mamlaka ya Ardhi
au eneo lako.
Lakini kwenye
mambo yoyote ya Kiroho, mfanye Mungu wetu mwema kuwa Mshauri wako, na usimuite
mtu yeyote Baba hapa Duniani, kwa kuwa Baba yako ni Mmoja tu ambaye ni Mung; na
wala usimuite mtu yeyote Bwana, kwa kuwa unaye Bwana wako Mmoja, Kristo; na
kumbuka wakati wote kwamba Ufalme wake sio wa Dunia hii.
Na kama Watu
watadiriki kuachana na Mapokeo au maagizo ya Wanadamu, na wakaziamini au kuzitii
Amri Takatifu za Mungu, na kuyachagua Maneno ya Kristo na Mitume wake, badala
ya Maneno na maagizo ya Mapapa na Mabaraza yake; ndipo wataweza kabisa
kuugundua upumbavu ulio kwenye Mafundisho ya Utrinitarian, pamoja na kwa
walivyoona kwamba Mkate na Divai Hugeuka kuwa mwili na damu halisi; na kwamba
ya kwanza hayastahili kushindwa kuliko iliyofuatia, lakini yote ni kama haina
mashiko, Hayatokani na Maandiko, na Hayana uhalisia, ambavyo ni kinyume kabisa
na maana yoyote njema Iliyokusudiwa na Kufikirika.
Kwa kuwa sio yote
kwa pamoja ni ujinga kusema kuwa, Mungu Mmoja anaweza kuwa na Nasfi Tatu, ni
sawa na kusema kuwa, Mkate na Mvinyo ni Mwili na Damu ya Kristo? Hapana, ndipo
Watu wangesema wazi kwamba Kweli halisi, Hivi sio Upumbavu mkubwa kusema, Mungu
Mmoja wa Mbinguni na Duniani, ni Nafsi Tatu au ne, kama kusema, Mfalme Mmoja wa
Uingereza na Ireland, ni Watu au afsi tatu au Nne? Hivi siyo zamani zote kuwa
ni uwongo na zaidi?
Oo, Mungu Uliyehai,
nakutafuta kwa unyenyekevu wote, yafungue Macho ya Mwananchi mwenzangu kwa
kweli, na Watu wengine wote kwa ujumla, ili waweze kuona, na kumchukia Kahaba
mkuu, Mama wa Makahaba, na wa Machukizo yote na Mafundisho yake yote potofu
yaliyoshika dau hapa Duniani; kwa kuwa hivi ni baadhi ya Vikombe vya Mvinyo wa
Uasherati wake, ambazo amekuwanavyo hapa na huko mbeleni, na angali bado
anatunywesha sisi, na Mataifa mengi Jirani zetu; aliyoyanywesha kwa uchafu wa Uasherati
wake, na Mafundisho yake yote ya Uwongo.
Oo Bwana Mungu
Mwenyezi, Hukumu zako ni za kweli na za haki; harakisha Muda, nakuomba, kisha
uzitukuze Sheria zako, na uzifanye ziheshimiwe; wakati Wafalme wa Dunia watakapomchukia
Kahaba huyu Mkuu, na kuyaasi Maagizo yake Yachukizayo na machafu yake yote ya
Uasherati wake.
Oo, ili Watu wako
watoke kwenye dini hii ya Siri ya Kibabeloni, ili wasiwe sehemu ya Dhambi zake,
na kwamba wasipokee Mapigo yake, kwa kuwa Dhambi zake zimefika hadi Mbinguni,
na Mungu atayakumbuka Maovu yake.
Ni wewe, Ee Roma
mchafu, nayashitaki Maagizo haya yote ya upotofu, ya Kuvunja Mpangilio wa
Kwanza wa Amri Kumi, kwa kumfanya Mungu Aliye Juu Sana, Mtakatifu wa Israeli,
kuwa ni wa Nafsi Nyingi; kinyume kabisa na isemavyo Amri ya Kwanza, nawe
ukawafanya watu wako wajifanyie Sanamu za Kuchonga na Wazisujudie; kinyume na
isemavyo Amri ya Pili, na kwa kuwaruhusu walitajea bure Jina takatifu la Mungu,
kwenye Viapo vyao vingi, na kulitukana au kulidhalilisha kwa Makusudi kwa
kuliona la Kawaida tu mwenye Taratibu zao nyingi, kinyume kabisa na isemavyo
Amri ya Tatu.
Kwa kuibadilisha
Sabato Takatifu, kutoka Siku ya Saba (ambayo Mungu anapumzika kwayo, na
kuibariki na kuitakasa kwa Matumizi Matakatifu) na kuipeleka hadi Siku ya
Kwanza, ambayo ilikuwa ni moja ya Siku za Mungu za Kazi; (na inayopasa kuwa ni
moja ya Siku za Kazi za Mwanadamu, milele) Hiyo, nawe umezibadili Amri za
Mungu, na kulivunja Agano la Milele, ambavyo ni kinyume kabisa na maagizo ya
amri Nne za Kwanza za Mungu.
Pamoja na Maagizo
yako mashuhuri na yaliyo kinyume yaliyoandikwa hata kwa rangi Nyekundu kwenye
Maandiko, Siku za Watakatifu, na Siku zako zote ulizoziita Takatifu; ambazo
wala hakuna hata moja aliyoiamuru Mungu iadhimishwe kati yake. Nakupa
changamoto kwa kukutaka, Ewe Roma pamoja na Wafuasi wako wote, unionyeshe
Ulipoagizwa na Mungu, au kutoka kwa abii wake yeyote, au kutoka kwa Mtume wake
yeyote, alipokuagiza yeyote hata Moja tu kati ya Siku zako zote ulizoziwekea
Maandiko Mekundu ukiashiria kuzifanyia maadhimisho ya Watakatifu, Ama ya Kuzaliwa
kwa Kristo, au Siku ya Kusulibiwa kwake, au Siku ya Kufufuka kwake, au Siku ya
Kupaa kwake Mbinguni, au yoyote ile iliyoko kwenye mlolongo wote wa Kundi la
Siku za Watakatifu, na Nyinginezo; ambazo kama tungezishika japo nusu yake,
basi tungekuwa wabaya zaidi kuliko wasiowapatia mahitaji familia zao, wala
kuomba ili tusamehewe Makosa yetu; ili kwamba badaya sisi kuwa Watakatifu sisi
wenyewe, basi tungekuwa waovu, tusio na haki na Wadhambi, na wenye kumchukiza
Mungu. Pia imani yako ya kuwaomba unaowaita wewe Watakatifu, na kwa Mariamu
Mama wa Kristo, Ewe Roma Umchukizaye mno Mungu, amka sasa na unijibu; Wewe
uliyewaua wafuasi waaminifuwa wa Mwanakondoo, hebu niambie ni wapi mtumishi
yeyote wa Mungu au Watu wa Zamani, walipomuomba hata Abeli, au Enoshi, au uhu,
au Ibrahimu, Isaka au Yakobo, au Mtumishi mwaminifu wa Mungu Musa, au Nabii
yeyote yule? Je, ilishawahi kutokea kwamba mmoja wa miungu aliyekuwa na wafuasi
kwa idadi fulani waliowaomba mmoja kati hao? Je, walikwisha wahi kushika Siku
ya Watakatifu, kwa yeyote kati ya hawa?
Sasa je, wewe sio
Uso wa yule Kahaba Mkuu, ambaye ana Jereha la Kichwa mwake; kwa kuwa unajua
kutoka Moyoni mwako kuwa hawajawahi kuwaomba, wala kuzishik Siku, zozote kati
ya hizo za hawa wanaoitwa Watu Watakatifu, kwa kuwa Mungu Mwenyezi hakuziagiza
wala kuziamuru.
Lakini kama
Wafuasi wowote wa kanisa la Roma, au hawa wanaojifanya kuwa Waprotestant, wangeniambia,
Rafiki yetu Elwall, kwa nini unayahalifu Mapokeo ya Wazee; kwa kufungua Duka
lako, na unafanya kazi Zako zote Siku za kwanza za juma, na Siku za Watakatifu,
na Siku nyingine zote zilizowekewa Maandishi
Mekundu; Siku ya Kusulibiwa na Siku ya Kufufuka, na Siku ya Kupaa kwake
Mbinguni, nitawajibu kwa kutumia Maneno ya Bwana wangu, kwenye Mt. 15:3 isemapo;
Mbona
ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu? Kwa kuwa Mungu Aliamuru, akisema, Ikumbuke siku
ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku
ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, Lakini ninyi mnasema, yeyote afanyaye kazi
siku hii itakuwa huru.
Nanyi mwzifanya Amri za Mungu
kuwa hazina Umuhimu kwa Mapokeo yenu; lakini mwaniabudu bure, Wakifundisha mafundisho
Yaliyo maagizo ya wanadamu, Mat.
15.9.
Hapa kwa kweli ni kila Roho ya Kidini inaweza kuona, kwamba Bwana wetu
mpendwa Yesu Kristo, asingeweza kuwa na Wanafunzi wake mwenyewe na Wafuasi wa kuzishika Amri za Wanadamu
kwa mambo yote ya Kidini, wala moja ya Mapokeo yao yasiyo na maana, lakini
aliwasisitiza, kuzishika sheria na Amri za Mungu.
Kwa kuwa mtu
alipomjia Kristo na kusema, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa
milele? Akamjibu; ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. Mat. 19.17.
Lakini hapa
nawasihi Watu wote kuchukua otisi fulani, kwamba Kristo Alimkemea huyu Kijana
kwa kumuita yeye mwema, akasema, kwa nini unaniita mimi mwema? Hakuna alye
mwema ila ni Mmoja tu, naye ndiye Mungu: Sas Maneno haya ya Kristo Yanaonyesha
kwamba yeye sio MUNGU; kwa kuwa yeye ambaye Cheo hiki cha sifa ya Wema hawezi
kuwa nacho kabisa, hawezi yeye kuwa Mungu aliye juu; lakini ni kwa Maneno ya
Bwana wetu mwenyewe, anatuonyesha kuwa Cheo hiki sio chake, lakini kinamhusu
Mungu peke yake, na hakuna Mungu mwingine ila Mimi.
Nahofia kwamba
Dini haitaweza kabisa kuirudia hali yake ya Utakaso ya kale, hadi pale ya
uchafu iwekwe kando, na Huduma Huru iwepo; ndipo hapo Makasisi wasanii na
wapole wa Kujionyesha na wanafiki watakapoondolewa mbali; Wakati Watu
watakapohubiri kwa Jicho moja, na Shauku timilifu ya kuendelea mbele kwenye Ufalme
wa Kristo, na kuwaleta Viumbe Wenzao ndani yake, na kuwapa bure kabisa hivyo
Vitu vya Kiroho, wamepokea bure kabisa pasipo kununua kwa Fedha, na bila kutoa
Gharama; Ndipo kwa kweli itasemwa, umeanguka Babeli, umeanguka! Na Maaskofu
wake wote, na Makasisi, wa Aina zote, pamoja na Mafundisho yao yote ya kipuuzi,
na Mateso yao ya kikatili, vyote vitaangushwa na kupondwapondwa chini Ardhini,
na kuanguka kama Jiwe la kusagia Baharini.
Ni Upumbavu wa
kiasi gani unaweza kuwa Duniani, zaidi ya kusema, Kwamba Mungu Aliye Juu sana,
Sababu ya Kwanza au Mungu Mkuu wa Vitu vyote, ni Undumbe vyote ni kuamini shirika
ya Mungu wa Uwili, Utatu, au Urobo wa Nafsi, na Dini Iliyodhihirika
inayotuambia sisi, Kuna Mungu Mmoja tu, na hakuna mwingine ila yeye. Marko 12:32.
Na sio mafundisho ya wanadamu kusema kama Katekisimu ya kanisa la Assemblies, inavyosema,
"Kuna Nafsi Tatu kwenye Uungu" na kwamba wao wako "Sawa kwa
Uweza na Utukufu: Wakati kwamba Kristo anatuambia sivyo, na kwamba Baba ni mkuu
kuliko yeye.
Na Nabii Isaya
anatuambia, Kwamba Mungu hana wa kufanana naye: Na Mtakatifu Paulo anatuambia
sisi, kwamba Kuna Baba Mmoja tu, 1Kor. 8:6. Sasa iwe kama tunaiamini Katekisimu
hii Potofu, au kama tunaamini maneno ya Yesu Kristo, Isaya, na Paulo, nitawaachia
Watu makini kuhukumu.
Sasa, kwa kweli,
imefanya Uchungu na huzuni Kifuani mwangu, na kwa wanyofu kadhaa, Watu wenyekuzijua
sheria, wameomboleza pamoja nami, kwamba maskini Watoto wasio na hatia, wanafundishwa
Mafundisho haya yasio ya kweli, na yasiyo ya kibiblia, yanayomchanganya Mungu
na Manabii wake, Kristo na Mitume; Kwa kuwa Mungu alisema, Usiwe na miungu
mingine ila Mimi: Na Kristo alisema, Baba yake ndiye alikuwa Mungu wa Pekee na
wa Kweli: Na Musa alisema, Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja: Na Paulo alisema, Hakuna Mungu Mwingine
ila Mmoja, 1Kor. 7:5.
M6aandiko
Matakatifu yanatuambia, Kwamba Kristo alikuwa ni Nabii, imara kwenye Vitendo na
kwenye Neno, mbele za Mungu na kwa Watu wote, Luke 24:19. Hata kama Mungu
alivyokuwa ameahidi kwa kupitia Mtumishi wake Musa, aliyetuambia sisi kuwa, Bwana, Mungu
wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi;
msikilizeni yeye.
Sasa, huyo
aliyeahidiwa kuwa Nabii, hangeweza kuwa ni Mungu mwenyewe: Ni mkanganyo kwenye
Tabia na sili ya Vitu kudhania hivyo; kwa kuwa Israeli wangesema kabisa kuwa
Musa alikuwa Mungu, ambavyo siye Mmoja Israeli waliyewahi kumthibitisha na
kumkubali, ingawaje alikuwa amependwa sana na Mungu, na kupendwa na Watu wote
wema, ambavyo alisemewa kwamba, Wala hajainukia abii mwingine katia Israeli,
ambaye Bwana alimjua na kuongeanaye Uso kwa Uso; na ambaye kwa yeye Mungu
alifanya Miujiza na ajabu nyingi, ambayo haikuwa kufanyika huko nyuma kabla
yake, kama vile ya kuigawanya Bahari ya Shamu, nk. na hivyo, vyote viwili,
yaani Maandiko Matakatifu, na Agano la Kale na Jipya vinathibitisha, Kwamba
Kristo alikuwa Nabii kama alivyo Musa, na alikuwa na uweza wa Kimatendo na na katika
Neno, na kwa hiyo tusilogeke na
Mafundisho mapotofu ya wanadamu, tuliyoyadhania kuwa ni hayana maana kabisa
japo ni Mashuhuri hapa Duniani, kusema kwamba (yeye aliyekuwa abii, na ambaye
alikuwa Mtumishi wa Mungu na ambaye Mungu alimuinua, na ambaye Mungu alimtia
mafuta; na ambaye Mungu alimtuma, na yeye ambaye asingefanya chochote yeye
mwenyewe, na yeye aliyesema, Baba yake ni mkuu kuliko yeye; na yeye ambaye
Mungu alimfufua toka kwa Wafu; na yeye ambaye hakuwa na Uweza wowote kwa yeye
mwenyewe wala Mamlaka lakini kile alichopokea toka kwa Mungu, na yeye ambaye
Mungu alimuinua awe Mfalme na Mwokozi, na yeye ambaye Mungu amemfanya kuwa
Bwana na Kristo, ambaye ni Mwanadamu Yesu Kristo, ambaye Mungu amempa mamlaka
ya Kuhukumu wote, na aliyemuamuru kuuhukumu Ulimwengu; Mungu amempokea huko
mbinguni kwa Utukufu, ambako Mungu amemtunukia aketi au asimame, Mkono wake wa
Kuume, na yeye ambaye ni Kuhani Mkuu wetu Milele; na yeye ambaye anaendelea
Kutuombea mbele za Mungu) awe ni Mungu yeye mwenyewe.
Nasema,
Kusingeweza Madai haya Kumpa Amani moyoni kwa aina hii yote ya Upumbavu na
upotofu ambavyo hayakuwa kamwe mafundisho ya Wanadamu?
Bwana mwema wa
Mbinguni na Duniani, na awafungue Macho yao Watu wote walio waaminifu, tena
zaidi na zaidi, ili waweze kuuona Ukweli wa Mungu kutoka kwenye Maneno yake
Matakatifu, na wasipotoshwe kabisa na Mapapa, Maaskofu, au Makasisi, kwa Mungu
waiweke Imani yao; lakini wakati wote wamchukue Bwana wetu mpenzi kuwa Mshauri,
na wasimuite Mwanadamu yeyote Baba hapa Duniani, kwa kuwa Baba yet uni Mmoja
tu. Ambaye ni Mungu, na wasimuite Mtu yeyote Bwana hapa Duniani, kwa kuwa Bwana
wet uni Mmoja ambaye ni Kristo. Na kisha Maneno yake ya busara, yanamfanya mtu
awe na Kicho au hofu ya Asilia, Isichukue kamwe Kanuni zako za Kidini kutoka
kwa Wanadamu, bali wakati wote kutoka kwa Mungu na Manabii wake, Kristo na
Mitume wake.
Kwa kuwa kama
mngekuwa Watu Watakatifu, basi Mngefundishwa na Mungu, na kama mkiyageuza Macho
ya nia zenu kwake, na kusema mioyoni mwenu, Bwana, Nia yako na Mapenzi yako ni
yapi? Hebu nijalie kujua zaidi, nami nitafanya hivyo.
Ndipo huyu Mungu
mwema anayeona hata Mateso yaliyo ndani ya Roho zenu, na jinsi mlivyo na kiu
cha mumtafuta yeye, yeye ana Huruma nyingi na Upendo, naye atakuja, na kwa Roho
wake mwema atafanya Makao nyani yako. Kwa hiyo, hakikisha kuwa unayakumbuka
Maneno ya Bwana wetu mpendwa. Na kama (anasema yeye) Mtazishika Amri zangu
mtakaa katika Pendo langu, kama mimi nilivyozishika Amri za Baba yangu, na
kukaa kwenye Pendo lake.
Kristo alituambia,
kama mnataka kuupata uzima wa milele zishikeni Amri za Mungu: Ambazo tunajua
kwamba ni Amri Kumi, kwa kuwa tunakuta amezielezea kwa kina sana, na
kuzielekeza kiungwana sana kwa wengi wao. Na kwenye Yohana 17:3. Kristo anatuambia
sisi, Kwamba Baba yake ni Mungu wa Pekee na wa Kweli.
Sasa, kama
tukimwamini Kristo, ndipo ni hakika, hakuna Mtu mwingine aliye Mungu wa Kweli
ila ni Baba yake peke yake.
Na kama Bwana
wetu Yesu alivyokuwa makini wakati wote kumpa Utukufu Mungu wake na Baba yake
wa Mbinguni, basin a sisi, tukiwa ni Wafuasi wake wa kweli, hebu na tumpe
Utukufu huyu MUNGU wa pekeena asiye na mshirika, na ambaye hana wa
kufanananaye, na wala hakuna mungu mwingine aliye kama yeye: kwa kuwa ni yeye
tu peke yake ndiye mwenye Uzima na uhai ndani yake, ambaye haupati uhai huo
kutoka kwa Mwingine: a ni yeye tu peke yake Anajitosheleza au Hahitaji msaada wowote,
na anaweza kufanya Vitu vyote yeye mwenyewe: a kwa kuwa ni yeye peke yake ndiye
Anaishi kwa Uweza wake mwenyewe, na wala Hatokani Mwanzo wake, au kushirikisha
Uweza wake, kutoka kwa yeyote yule; bali yeye ni Mfalme Anayejitosheleza, Aliyeko,
wa Milele, Hafi wala Kupatwa na madhara, Haonekani kwa macho, na ni Mungu Pekee
mwenye busara.
Yeye ndiye Mungu
wa Mababa wa Imani waliopita, na wa Manabii, naye sio tu Mungu wa Ibrahimu, na
Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, peke yao, bali pia ni Mungu na Baba wa
Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye ametangaza kwa wazi sana, Kwamba anapewa na
kuupokea Uweza wake wote, kwa sehemu zote mbili, yaani Mbinguni na Duniani, kutoka
kwa Mungu; na kwamba kwa yeye peke yake hawezi kufanya neno lolote; na kwamba
Mwishoni, atayatoa Ufalme kwa Mungu, aliye Baba: a kwamba Mwana mwenyewe
atajinyenyekesha kwake na kumpa Vitu vyote yeye, ili Mungu afanyike kuwa yote
katika yote na ndani ya yote1Kor. 11:.24, hadi 29.
Iwapo kama Mtu
mwadilifu yeyote atasoma Aya Tano za hapo juu, ataijionea kwa dhahiri sana
Kweli ambayo nimeidai na kuielezea; Kwamba kama ilikuwa ni Mungu Baba aliyetoa
Uweza Mikononi mwa Kristo; hivyo Mwishoni, Kristo atamrudishia Mamlaka yote
Mungu, kwa Ushuhuda wa yeye kufanyika kwa Utiifu wote kwake, na kwamba Mungu
afanyike kuwa yote katika yote.
Kwa hiyo huyo ni
kama Dagoni aliyeanguka mbele ya Sanduku la Agano la Mungu, ndivyo
itakavyoonekana Mwishoni, Maagizo yote ya kipumbavu ya Wanadamu, hayataweza
kusimama kinyume cha Amri Takatifu na ya Kweli ya Mungu:
Usiwe na miungu
mingine ila Mimi.
Na sasa, Ee Bwana
Mungu Mwenyezi, nakutafuta kwa unyenyekevu mkubwa, kwa njia ya Yesu Kristo,
kuuombea Moyo wa kila Mtu aliyemaanisha, Mwanaume na Mwanamke, anayeusoma
Ushuhuda huu ili akupende wewe na Sheria yako takatifu. Na kwamba iwe vizuri
kwao kuliko maelfu ya Dhahabu na Fedha, na kwamba Sheria ya Kinywa chako (wewe
uliye Chemichemi ya Mema yote na Kweli) uweze kuwa mbele ya Maagizo yote ya
kijinga na yasiyo na maana ya Wanadamu.
Ewe uliye Kiumbe
mkamilifu na usiye na doa, wewe ndiwe Mungu wa pekee uishiye na wa kweli,
unayenipa mimi Pumzi, na ambaye unaweza kuitwa tena, wakati, na mahali, na
jinsi unavyopendezwa, Nakuomba, hebu Ongoalea mbali Hofu ya kuwaogopa Watu
Moyoni mwangu, wanaoweza kuua Mwili wangu tu, na nianze kujifunza kuhusu Mwana
wako Yesu Kristo, kumuogopa yeye na Mungu wa wote wenye mwili, yeye pekee
anayeweza kuua vyote viwili, yaani Mwili na Roho.
Mungu mwenye huruma
yako, upemdo na uweza wote. Aliyemlinda na kumuokoa Danieli, na Watumishi wako
Waaminifu, kwenye kila Zama za Ulimwengu, nisaidie Bwana na nitie nguvu Kumbe
wako dhaifu, ili niweze bado kuusikia Ushuhuda wangu wa kweli kwako, na kwa Sheria
yako Takatifu kwa uaminifu mkubwa, hadi Mwisho wa Maisha yangu.
Nashindwa kutoa
sauti yangu kulia kama walivyofanya Manabii wa Zamani, Ezekieli 22:26. Makuhani
wake wameihalifu sheria yangu, wametia unajisi vitu vyangu vitakatifu;
hawakuweka tofauti ya vitu vitakatifu na vitu vya kutumiwa sikuzote; wala
hawakuwafundisha watu kupambanua vitu vichafu na vitu vilivyo safi, nao
wamefumba macho yao, wasiziangalie sabato zangu, nami nimetiwa unajisi kati
yao.
Wakati umewadia Bwana atende kazi; Kwa kuwa wameitangua sheria yako. Zaburi 119:126.
HITIMISHO
Edward Elwall, aliyejulikana
kama "Myunitarian mwanakikundi wa Kweka [Quaker]" alikuwa mshirika wa
Kanisa la Kibaptist la Sabato la Mill Yard mjini London. Kipeperushi hiki cha
mafundisho ya dini kimenukuliwa kwa mkono kutoka kwenye nakala iliyohifadhiwa
kwenye Maktaba yajulikanayo kama Dr. Williams's Library huko London na Thomas
McElwain, anayewajibika kwa nukuu zote za kimakosa zinazoweza kukutikana. Maandishi
ulalo kwenye nakala asilia yamepuuzwa kuwa sio ya muhumu sana.
q