Makanisa ya Kikristo ya Mungu

 

[107]

 

 

Pasaka Kuu Saba za Biblia

 

(Toleo 3.0 19950421-19970207)

 

Jarida hili linaelezea mfululizo wa Pasaka Kuu Saba zilizomo katika Biblia na maana zake katika kujenga dhana ya ujio wa Masihi katika hali ya Kutungiwa mimba na Kuzaliwa kibinadamu. Maana zake tangulizi za Pasaka zime fafanuliwa na kisha maana zilizo nyuma ya Pasaka katika msafara wa Kutoka utumwani, kuanguka kwa mji wa Yeriko, habari za Gideoni, wafalme Hezekia na Yosia, nabii Ezra na hatimaye Masihi, zote zime fafanuliwa. Utimilifu wa kazi za Pasaka zimefafanuliwa zikihusianishwa na maisha ya mwanadamu, mfumo wa Yubile na usemi wa kimfano kutokana na vitabu vya Mwanzo 2:9; Zekaria 4:3-6; na Luka 3:7-14 pia zime fafanuliwa. Miaka ya mti iliyosimuliwa katika Luka 13:6-9 imeweza kufafanuliwa kwa kina kirefu au kulinganishwa katika jarida hili.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Copyright © 1994, 1995, 1997 Wade Cox)

 

(Tr. 2005)

 

Masomo haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kutufa maneno. Jina la mchapishaji na anuami yake pamoja na hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya maelezo na kilugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia ynapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 


Pasaka Kuu Saba za Biblia [107]

 


Maana Kivuli za Pasaka

Dalili ya kitu kinachohitajika katika kuhamisha mamlaka ya mfumo wa ulimwengu inapatikana katika kitabu cha Mwanzo 3:15 ambapo inasema: nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; nao utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.

 

Neno uzao hapa husomeka kama zer’a ambayo ni neno linalo onyesha nafsi ya umoja. Kwa hiyo ni dhahiri kabisa kuwa tunashughulikia hapa na dhana inayo onekana kuwa ni nafsi ya umoja yaani mbegu au uzao, mf. Kristo na mwanamke wote ni Israeli na Kanisa. Wamataifa wameitwa na kuwa Israeli wa kiroho. Kanisa ndiyo hiyo Israeli. Lakini sio taifa lote la Israeli ni watoto wa kimwili wa Yakobo, waliomo bado Kanisani. Kanisa hilo limeunganishwa wote na wote ni wamoja. Tunashughulikia jinsi ya kukabidhi mamlaka ya mfumo wa dunia kwa hatua hii. Makabidhiano haya ya mamlaka yatakomesha zama hii ya tambo la ulimwengu na kuanza kwa zama nyingine la Milenia.

 

Pasaka ilianzishwa hata kabla ya sheria hazija kabidhiwa  katika mlima wa Sinai. Kwa hiyo basi, Pasaka inasimama kama mhimili katika sheria za Musa, na katika sgughuli zote za Mungu kama ni kitu kilicho pewa nafasi muhimu iliyotangulia kabla sheria za Musa kama ilivyo kwa Sabato zake na mavuno katika ujumla wake. Siku takatifu hutoa ishara mabadilishano ya mamlaka kutoka kwenye mfumo uliopo na ujio wa mfumo wa Kimasihi. Mfumo ule utakuwa na makao yake makuu mjini Yerusalemu. Hii ndio sababu kuwa hizi Sikukuu, Mwandamo wa Mwezi Mpya na Sabato zake zinapigwa vita na kubadilishwa na mfumo ulioko sasa unaodai kuwa ni wa kikristo. Hawajui ni nini kinachoendelea. Wakati unaposimama kuzishika sheria za Mungu zilizo elekezwa katika amri kumi za Mungu, kwa kuzishika zote kabisa, na kila kilicho elekezwa katika sheria hizi na manabii, basi uelewa wako huondolewa.

 

Walijihoji nafsi zao pia hata katika Pasaka ile ya mwanzo wa msafara wa Kutoka utumwani ambao walijichunguza sana.

 

Anguko la Sodoma na Gomora

Mfano wa mambo yaliyokuwa yamehusishwa katika mabadiliko ya mamlaka na kuhukumiwa kwa mfumo wa dunia kunaonekana katika anguko la miji ya Sodoma na Gomora. Kitabu cha Mwanzo 19:3 inadokeza kuwa tunajionea pale muundo wa Pasaka kama kitu kinachotangulia kwenye utaratibu halisi wa Pasaka kutoka katika kitabu cha Kutoka. Maandiko haya yote yako pale kwa sababu maalumu.

 

Mwanzo 19:3 inasema: 3Akawasihi sana, nao wakaja, wakaingia nyumbani mwake. Akawafanyia karamu, akawapikia mikate isiyochachwa, nao wakala.

 

Mkate usiotiwa Chachu uko hapa kwa sababu maalumu. Hakutakiwi kuweko na mkate usiotiwa chachu ukatolewa sadaka (Kut. 23:18; 34:25; Law. 2:11; nk). Tukio hili lilitumika kuwakilisha dhabihu. Kulikuweko na Pasaka kuu saba lakini hii ilikuwa inatangulia kwa umuhimu kwa hizi saba nyingine kwa namna ile ile ambayo Kristo alikuwa mtangulizi kwa makanisa saba kama ni wa nane. Dhana ya wazo hili inachukuliwa kutoka kwenye Hekalu la mfalme Sulemani ambako kulikuwa na vinara kumi vya taa au mishumaa vyenye taa saba kila kimoja. Masikani iliyojengwa na Daudi ilikuwa na moja tu na ilikuwa katika mkazo muhimu katika muendelezo wa maskani iliyokuweko jangwani. Kinara cha kwanza kilimwakilisha Kristo, na vile vingine saba vinavyofuatia vinawakilisha makanisa saba na yale mawili ya mwisho yana simama mahali pa mashahidi wawili. Utaratibu huu uliendelezwa kuanzia kwa Kristo hadi kwenye marejesho ya kurudi kwake. Vile vinara saba vilikuwa na mishumaa au taa sabini ambazo ziliwakilisha ongezeko la baraza la wazee. Kwa hiyo basi, uwakilishi huu unaofanywa kwa Kanisa ulitabiriwa kama ni kuondolewa kwa mamlaka kutoka kwenye baraza la wazee sabini wa Kiyahudi likijulikana kama Sanhedrin na kupewa Kanisa. Hawa wazee sabini wenyewe walikuwa ni wawakilishi wa mfumo wa kidini kama tunavyoona katika kitabu cha Waebrania (tazama pia katika jarida lisemalo Mabashiri ya Mungu [184].

 

Dhabihu iliyofanywa mbele ya malaika iliuangusha chini mji wa Sodoma na kuangamiza eneo lote la ardhi la upande wa mashariki ya ukingo wa Yordani. Lutu alikuwa amechukua ardhi yote yenye rutuba na tajiri ya wakazi wa Sodoma. Abrahamu alimpa yeye fursa ya kwanza ya kuchagua. Kristo alikuwa akishughulikia kumwonyesha Lutu kile alichotakiwa kufanya wakati aliposhindana na mataifa kwa ajili ya ardhi yao, na kuitoa kwa familia ya Abrahamu.

 

Pasaka ya 1: Kuanguka kwa Misri

Pasaka kuu ya kwanza ilikuwa ni kuanguka kwa Misri ambayo ilihusu kwa kitambo (tazama jarida la Musa na miungu ya misri [105] na pia lisemalo  Pasaka [098].

 

Pasaka ya 2: kuanguka kwa Yeriko

Pasaka ya pili ilifanyika wakati ambapo nchi ya ahadi imekabidhiwa kwa wana wa Israeli. Hivyo ni kusema kwamba Pasaka ya kwanza ilifanyika kwa ukombozi na hii Pasaka ya pili ni kwa kuingizwa kwao katika nchi yao. Yoshua 5:7 inasema 7Na watoto wao, aliowainua badala yao ndio hao alio watahiri Yoshua; kwa kuwa wao walikuwa hawajatahiriwa, kwa maana walikuwa hawakuwatahiri njiani.

 

Israeli wali tanga tanga jandwani kwa muda wa miaka arobaini. Wote waliachwa bila kutahiriwa. Hii ilikuwa ni namana ya kukigawa au kukitofautisha kizazi kimoja na kingine. Ilikuwa ni mfano wa kuweko kwa Yubile ya arobaini ya Kanisa kuweko jangwani kuanzia wakati wa Masihi, Wamataifa au watu wasiotahiriwa ambao wangeweza kuuingia ufalme wakati ambapo walio tahiriwa wakishindwa kufanya hivyo. Wakati ule ubao ulitumika ili kupimia urefu wa muda wa matazamio ya ujio kati ya Masihi mmoja, Masihi wa Haruni au Masihi-Kuhani, na matarajio ya ujio wa pili wa Masihi wa Israeli kama mfame na mshindi. Wale waliotahiriwa walioanguka jangwani wakati walikuwa ni Yuda. Walipewa fursa ya kuwepo Kanisani chini ya Masihi na walikataa fursa ile. Waliangukia katika jangwa la Yubile ya arobaini chini ya Kanisa. Walikuwa wasio tahiriwa, Wamataifa, ambao waliletwa ndani. Kwa hiyo basi, zama za hawa wasiotahiriwa ilikuwa ni kuelekeza kuelekea Wa-Mataifa warudishwa katika Israeli. Kila Muisraeli anapaswa kujua kupitia maandiko haya, kuwa wa-mataifa walikuwa wanaenda kurejeshwa kuwa Waisraeli.

 

Wakati wa kuingia Kaanan, wanaume wa Israeli walifanyiwa tohara pale Gilgali kwa kutumia jiwe la gumegume. Maana ya neon Gilgali ni njia iliyozungushiwa au mzingo. Kwa hiyo hili jiwe la gume gume aliloli lizinga Mungu dhambi, au mashitaka ya Misri, mbali na Israeli. Sisi tuna anzisha muda kwa usahihi kabisa. Ilikuwa wakati wa Pasaka ndipo waliichukua Yeriko.

Yoshua 5:10-11 inasema: 10 Basi wana wa Israeli wakapanga hema zao huko Gilgali; nao wakala sikukuu ya Pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi, jioni, katika nchi tambarare ya Yeriko. 11 Nao wakala katika mazao ya nchi siku ya pili ya kuiandama hiyo sikukuu ya Pasaka, mikate isiyotiwa chachu, na bisi, siku hiyo hiyo.

 

Walikula mkate wa mada jangwani. Hatimaye

katika siku ileile baadae waliyokula mazao ya Kaanani, ile mana ilikauka. Kwa hiyo, katika siku ya kwanza ya Mikate isiyotiwa Chachu walianza kula mahindi na nafaka za Kaanani, kisha ile mana ikakoma kushuka juu ya nchi.walikuwa na namna moja tu ya kujipatia chakula kwa kipindi chote cha miaka arobaini. Kisha walipewa mkate au matunda ya nchi ya ahadi. Tendo hili lilihusisha ama kwa kula nafaka za zamani au ilikuwa vile vile ni Sadaka ya Mganda wa Kuinuliwa inayo angukia kufanyika katika siku ya kwanza ya juma ambayo ni kama Sikukuu ya kwanza ya Mikate isiyotiwa Chachu. Inachukuliwa kama ni siku ya kula nafaka za zamani. Nafaka mpya haziwezi kuliwa hadi Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa iwe imetolewa.

 

Yoshua 5:13-15 inaonyesha kuwa Bwana alikuwa anaingilia kati katika uanzishwaji wake. Huyu alikuwa ni Kristo kama Kamanda wa jeshi la Mungu.

Yoshua 5:13-15 inasema: 13 Ikawa hapo Yoshua alipokuwa karibu na mji wa Yeriko, akavua macho yake na kuangalia, na tazama, mtu mume akasimama kumkabili mbele yake, naye alikuwa na upanga wazi mkononi mwake; Yoshua akamwendea, na kumwambia, Je, wewe u upande wetu, au upande wa adui zetu? 14 Akasema, La, lakini nimekuja sasa, ni amiri wa jeshi la BWANA. Yoshua akapomoka kiusouso hata nchi, naye akasujudu,akamwuliza, BWANA aniambia nini mimi mtumishi wake? 15 Huyo amiri wa jeshi la BWANA akamwambia Yoshua, vua viatu vyako miguuni mwako; kwa kuwa mahali hapa ulipo ni patakatifu. Yoshua akafanya vivyo.

 

Hii ilikuwa ni kitu kimoja kilekile ambacho Musa alisema pale Sinai.

 

Yoshua 6:1-16 inatuonyesha kuwa Bwana aliishatoa mji kwa Israeli. Pasaka ni mfano wa tendo la kwanza katika kuanguka kwa mataifa. Malimbuko ni Kristo na Kristo alikuwa ni lile jiwe ambalo liliangamiza na kukomesha tawala za dunia zinazo onekana katika kitabu cha nabii Danieli ile sura ya 2. Kristi alikuwa ni chanzo kikuu cha kwanza katika kuanguka kwa mataifa katika baragumu ya saba ya Ufunuo wa Yohana, ambaye ni mwenye kuangusha na mshindi wa falme zote za kidunia, anguko la mfumo wa dunia mwishoni mwa zama hii tuliyonayo. Tunacho kitafakari sana hapa ni ishara iliyo mfano wa Pasaka. Mfano unaotoa kielelezo unaohusiana na siku ya mwisho, mf. Siku ya mwisho ya sikukuu ya Mikate isiyotiwa Chachu. Pasaka ilikuwa ni lazima iadhimishwe ili kwamba mji wa Yeriko uweze kuanguka. Ni wakati ule tu tunapoadhimisha Pasaka vyema ndipo mataifa yataanguka katika siku za mwisho. Mji wa ya Yeriko ilianguka katika siku ya mwisho ya Mikate isiyotiwa Chachu. Utaratibu huu unasigishana na hatua za kurudi kwa Masihi kama Kamanda wa Jeshi la watakatifu.

 

Pasaka ya 3: Siku za Gideoni

Pasaka inayofuatia ni ile ya Gideoni. Katika kitabu cha Waamuzi 6:1, katika Pasaka ya pili, Israeli wanapewa mashamba au maeneo ya urithi au milki yao. Wa kwanza aliwaona wakitwaliwa kutoka katika Misri. Yule wa tatu Israeli wakipoteza milki zao kwa ajili ya kujitia na kufanta uovu.

 

Waamuzi 6:1-3 inasema: Kisha wana wa Israeli walifanya yaliyo maovu mbele za macho ya BWANA; BWANA akawatia mikononi mwa Midiani muda wa miaka saba. 2 Mkono wa Midiani ulikuwa mzito juu ya Israeli; tena kwa sababu ya Midiani wana wa Israeli walijifanyia hayo mashimo yaliyo milimani, na hayo mapango, na hizo ngome. 3 Basi ikawa, hapo Israeli walipokuwa wamepanda mashamba, Wamidiani wakakwea, na Waamaleki, na hao wana wa mashariki; wakakwea juu yao;  

 

Israeli walikombolewa kutoka mikononi mwa Wamidiani kwa kipindi cha miaka saba. Hawa wakikuwa watoto wa Ketura alio mzalia Abraham. Wao ni sawa kama ilivyo kwa Waamaleki ni wakatili. Waliangamiza kila kitu kilichoonekana mbele yao. Mungu aliwatumia katika kuwa adibisha Israeli. Israeli walianzisha na kuendeleza mahandaki au mapango ili kuweza kupigana na watu hawa. Wamidiani waliwaotea kinyume chao kisha wakapora ardhi yao kwa mabavu. Hatimaye Israeli walimlilia Bwana. Israeli wakatubu dhambi zao za kuabudu sanamu. Mungu anawaonyesha kwa njia ya mfano huu kwamba, kwa toba atarejesha milki yetu.

 

Waamuzi 6:8-10 inasema: 8 BWANA akamwambia nabii aende kwa hao wana wa Israeli; naye akamwambia, BWANA, yeye Mungu wa Israeli asema hivi, Mimi niliwaleta ninyi mkweem kutoka Misri, nikawatoa kutoka katika nchi ya utumwa; 9 nami niliwaokoa na mkono wa Wamisri, na mikono ya wote waliokuwa waliwaonea, nami niliwafukuza watoke mbele zenu, nami niliwapa ninyi nchi yao; 10 kisha niliwaambia, Mimi ndimi BWANA, Mungu wenu; msiiche miungu ya Waamori, ambayo mwaketi katika nchi yao; lakini hamkuitii sauti yangu.

 

Walitumikishwa kwa kazi za shokoa kipindi cha miaka saba. Hawakuzisikiliza ahadi ya Mungu. Matokeo yake yapo dhahiri kupitia maandiko. Mungu alimtuma Malaika wa Bwana (ni Yesu Kristo, mf, Zek. 12:8; Ebr. 1:8-9), na akasema na mwana wa Yoashi (ndiye Gideoni).

 

Waamuzi 6:12-13 inasema: 12 Malaika wa BWANA akamtokea, akamwambia, BWANA yu pamoja nawe, Ee shujaa. 13 Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu, ikiwa BWANA yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliyotuhadithia baba zetu, wakisema, Je, siye BWANA aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa, naye ametutia katika mikono ya Midiani.

 

Hawakuacha kuabudu sanamui zao na misiba au mikosi! Hawakujua kuwa walikuwa ni waabudu sanamu. Dhana hii imechukuliwa sana na watu wa mataifa katika siku hizi. Nchi hii ilitolewa kama urithi ili kwamba wateule waweze kupandikizwa. Lakini wakati wateule wanapofuata miungu ya uwongo na mifumo ya uwongo, basi ulinzi unaweza kuondolewa na kasha tutapelekwa katika utumwa hadi pale tutakapotubu. Wateule wenyewe hawaonekani kuelewa kweli ile. Kwa njia hii basi ndipo Bwana atatuhukumu. Atawapa maadui zetu mioyo ya jiwe ili watutese. Kwa mfano, katika siku za leo, baadhi ya makanisa ya kimamboleo yanaweka nembo au minara kama zinavyojitokza na kuonekana katika juu ya majengo ya makanisa yao. Lakini mambo haya yamekatazwa. Kumbukumbu la Torati 16:21 imekataza tendo hili la kujisimamishia minara au nembo. Inatambuliwa kwa lugha nyingine kuwa ni Ashera amhayo imetafsiriwa kwa makosa kuwa miti. Ashera nembo za makanisa, mnara mtakatifu wa kengele mambo ambayo ni sawa na yaliyokuwa yakituka zamani vilivyokuwa wakfu kwa mungu jua (vikijulikana kama ben au benben na Wamisri; tazama kamusi ya Interpreter’s Dictionary of the Bible, art. Obelisk, na Companion Bible, App.42).

 

Tunatakiwa tugeuke mbali kutokana na matendo haya ya ibada za sanamu au vinginevyo tutapoteza haki yetu ya kumiliki ambayo tumepewa kwa kipindi cha miaka mia mbili ya mwisho. Kile kinachotokea kwa taifa ni picha ambayo sisi wateule tunafanya. Usitawi wa nchi unategemea na matendo ya wateule. Mungu anahitaji utii. Kila mtu anafanya kinacho onekana kuwa  sawa machoni mwake mwenyewe katika siku hizi na watu wataangamia.

 

Hesabio la utendaji mambo katika kitabu cha Waamuzi kuna mahusiano ya karibu na Pasaka na ambayo taifa liliacha kuvitunza.

Waamuzi 6:20-21 inasema: 20 Naye Malaika wa Mungu akamwambia, itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uiweke juu ya mwamba huu, ukaumwage huu mchuzi. Akafanya hivyo. 21 Ndipo malaika wa BWANA akanyosha ncha ya fimbo ile iliyokuwa mkononi mwake, akaigusa ile nyama na ile mikate; moto ukatoka mwambani, ukaiteketeza ile nyama na ile mikate; malaika wa BWANA akaondoka mbele ya macho yake.

 

Walichofanya ilikuwa ni kuzigeukia idaba za sanamu na kusahau kuzitunza sikukuu hizi. Kristo, kwa njia ya matendo yake, alianzisha tena sheria ya Pasaka.

 

Waamuzi 6:27:Ndipo Gideoni akatwaa watu kumi miongoni mwa watumishi wake, akafanya kama BWANA alivyo mwambia; lakini ikawa, kwa sababu aliwaogopa watu wa nyumba ya baba yake, na watu wa mji, hakuweza kuyatenda hayo wakati wa mchana, basi aliyatenda usiku.

 

Namba kumi ni idadi ya kimapokeo ya watu wanaotakiwa kuwepo katika kila familia kwa ajili ya dhabihu ya Pasaka.

 

Gideoni alikuwa anaogopa kufanya majira ya mchana kazi ya kuibomoa madhabahu ya Baali na kuvunja-vunja chukizo hili lenye kukwaza. Ashera ni kitu kilichopo hapa na sio kichala cha miti. Ni mnara wa nguzo. Watu walianza kuviabudu vitu hivi katika Israeli na wakafikia mahali pa kudhani kuwa ni makufuru kuviondoa viyu hivi! Ni mazingira kama hayahaya ndiyo yanatokea kwa wengi leo. Badala ya watu kumwabudu Mungu kwa utaratibu aliouacha Kristo, watu badala yake wameshawishika kufuata desturi za miungu wa uwongo kuanzia toka imani ya Utatu hadi kwenye mafundisho ya imani inayojengwa katika mali na utajiri ambavyo vimefanyika kuwa ni miongoni mwa miungu ya taifa hili. Wamepofushwa na hawawezi kuona. Inapotokea tu kuwa mfumo wa uwongo ume shirikishwa, Biblia inasema kuwa unapewa nguvu ya upotevu ili uuamini uwongo. Kadhalika watu hawa walitaka kumuadhibu Gideoni kwa uamuzi wake wa kuondoa vinyago au, hasa zaidi sana ilikuwa ashera. Ashera au minara viliitwa viunga vya miti ili kupunguza maana halisi ki maandiko.

 

Waamuzi 6:30-31 inasema:30 Ndipo watu wa mji wakamwambia Yoashi, Mlete mwanao afe; kwa sababu ameibomoa madhabahu ya Baali na kwa kuwa ameikata ile Ashera iliyokuwa karibu nayo. 31Yoashi akawaambia watu wote waliokuwa wakishindana naye, Je! Mtamtetea Baali? Au mtamwokoa ninyi? Yeye atakaye mtetea na auawe hivi asubuhi; kama yeye ni Mungu na ajitetee nafsi yake, kwa sababu mtu mmoja ameibomoa madhabahu yake.

 

Yoashi alimtaka Baali ajitetee mwenyewe. Kama huyu angekuwa ni Mungu wa kweli basi angeweza kupanga vita na Malaika wa Bwana! Lakini hiyo haikuwezekana kufanyika. Kwa hiyo, malaika wa Mungu aliwakomboa Israeli na utumwa mikononi mwa Wamidiani. Ni sehemu ya mwandamano wa matukio. Kwa kweli, ingawaje katika wamu hii ya tatu Israeli walirejeshwa.

 

Uanzishwaji wa Sheria na Taratibu za Hekalu

Habari hii inachukua nafasi hadi kufikia zama za utawala wa Daudi na Sulemani. Daudi alianzisha taratibu za Hekalu. Kutoka 1 Nyakati 23:24 tunaona jinsi Daudi alivyoanzisha mfumo ambao uliishia wakati wa Kristo. Bwana Mungualisema na Daudi kwamba Israeli wangekaa Yerusalemu milele. Alianzisha taratibu za Miandamo ya Miezi Mipya, Sabato, nk.

 

1Nyakati 23:31: inasema: 31 na kumtolea BWANA sadaka zote za kutekeyezwa, katika siku za Sabato, na mwezi mpya, na za sikukuu zilizo agizwa , kwa hesabu kadiri ya agizo lake, daima mbele za BWANA.

 

Daudi aliziweka sheria lakini hakulijenga Hekalu. Kazi hii aliachiwa Sulemani ili alijenge Hekalu hili. Hekalu hili lililoitwa Hekalu la Sulemani lilikuwa na vinara kumi vya taa. Daudi alikuwa na moja. Daudi bado alikuwa chini ya sheria za Musa. Katika 1Nyakati 8:12-13 tunaona kuwa Sulemani ana anzisha taratibu nyingine na kanuni ndogondogo za Hekaluni. Tunaona kupitia utaratibu huu kwamba kulikuwa na makundi matatu ya Pasaka. Kisha uanzishwaji wa Hekalu.

 

2Nyakati 8:12-13 inasema: 12 Ndipo Sulemani akamtolea BWANA sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya BWANA, aliyoijenga mbele ya ukmbi.

 

Utaratibu wa kimfano wa Agano Jipya ulianzishwa hapa lakini hakukukuwa na mabadiliko ya ki-utaratibu wa kiibada. Msingi wa mpango ulibakia kuwa uleule kwa sababu haukuwa umebadilika. Utaratibu mpya ulifanyika kuwa ni kama mwongozo mkuu kwa watu. Lakini mpango wa wokovu umedhihirishwa kutoka katika Agano la Kale na pia katika Agano Jipya. Unaweza kujionea mwenyewe kutoka katika kila mojawapo katika kuhakikisha kuwa utaratibu huu haugeuzwi.

 

Pasaka ya 4: Siku za Hezekia

Pasaka hii ya nne ilifanyika baada ya ujenzi wa Hekalu wakati wa enzi ya mfalme Hezekia. Taifa hili lilijiingiza kuamini ibada za sanamu wakati wa utawala wa mfalme Ahazi. Ilitokea kuwa kitu kibaya sana kuwa Hekalu halikuweza kutengenezwa tena kwa ajili ya kutoa dhabihu katika siku ya 14 ya mwezi wa Nisan. Kwa hivyo walekosea kufanya Pasaka kwa muda wa siku mbili. Israeli walinajisika! Walikuwa wameenda mbali sana kuelekea mstari wa ukengeufu kutokana na makosa ya kikuhani ambayo ilihitajika wajitakase nafsi zao tena. Na hili ndilo tatizo lililoko katika karne yetu hii. Israeli na makuhani wao wako katika hali ya kifo cha kiroho. Utaratibu huu wa kujitakasa upya ni jambo lililo dhahiri linalotakiwa kufanyika katika  Pasaka.

 

2Nyakati 29:17 inasema: 17 Basi akaanza kutakasa siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, hata siku ya nane ya mwezi wakafika katika ukumbi wa BWANA; wakaitakasa nyumba ya BWANA katika muda wa siku nane; wakamaliza siku ya kumi na sita ya mwezi wa kwanza.

 

Katika siku ya saba ya mwezi wa Nisan ilikuwa na siku maalumu kwa ajili ya utakaso kwa ajili ya dhambi zote zilizo fanywa na wenye kukwaza. Ilitakiwa utakaso uhesabiwe kuwa ni kitu muhimu maana unafanya kuchukua mambo haya yote.

 

Hezekia aliitisha dhabihu ya mafahali saba ya ng’ombe, kondoo saba, nk, ili kufanya utakaso kwa ajili ya taifa. Anguko hili kuu la ki ukengeufu, huonyesha kama mfano wa anguko kuu la ki ukengeufu wa wateule kutokea katika siku za mwisho. Hii inamahusiano makubwa sana na kinachoitwa ukengeufu kwa lugha nyingine huitwa apostasia. Sio ukengeufu unaochukuliwa kutokana na kupungua kwa idadi ya waaminio bali unaosababishwa na ukosefu wa uelewa.

 

2Nyakati 29:22-24 inasema: 22 Basi wakawachinja ng’ombe, na makuhani wakaipokea damu, wakainyunyiza madhabahuni; wakawachukua kondoo waume, na kunyunyiza damu madhabahuni, wakawachukua na wana kondoo, na kunyunyiza damu madhabahuni. 23 Wakawaleta karibu mabeberu wa sadaka ya dhambi mbele ya mfalme na kusanyiko, wakawawekea mikono yao; 24 na makuhani wakawachinja, wakawatoa damu yao kuwa sadaka ya dhambi madhabahuni ili kuwafanyia Israeli wote upatanisho; maana mfalme aliwaamuru Israeli wote wafanyiwe sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya dhambi.

 

2Nyakati 29:30 inasema: 30 Tena Hezekia mfalme na wakuu wakawaamuru Walawi, wamwimbie BWANA  sifa kwa maneno ya Daudi, na ya Asafu mwonaji. Wakaimba sifa kwa furaha, wakainama vichwa na kusujudu.

 

Zaburi 133 inajulikana kama wimbo wa Hezekia (wasifa wake) hushabihiana na hali hii. Hezekia alifanya marekebisho katika ufalme ili kupoke baraka za Kristo akiwa kama Malaika wa Yahova (Yehova). Walikuwa hawajatakasika vyovyote. Tunaweza kuondoa dhabihu ya Kristo kwa kushindwa kwetu kama walivyofanya wao! Zaburi 133 inasema: Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, na kwa umoja. 2Ni kama mafuta mazuri kichwani, Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni, Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake. 3Kama umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni, Maana ndiko BWANA alikoamuru baraka, Naam, uzima wa milele.

 

Hivyo basi hapa tunashuhudia kufanywa upya kwa taifa.

 

Pasaka ya 5: Siku za Yosia

Pasaka ya tano ni ile iliyofanyika katika siku za  Mfalme Yosia (2Nyakati 35:1). Tunaona katika 2Nyakati 35:10-18 kuwa walishika Sikukuu ya Mikate isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba. Pasaka ilikuwa imeokwa (soma 2Nyakati 35:13) lakini lakini sadaka nyingine takatifu iliwekwa kwenye masufuria au chunguni. Huu unawezekena kuwa ndio ulikuwa mwanzo wa mchanganyo katika kutumia dhana potofu kuhusu matumizi ya neno mapishi. Makuhani walikuwa na harakari nyingi sana alasiri yote ya siku ya 14 Nisan. Kwa hiyo, Walawi walijiandaa nafsi zao, na kwa ajili ya makuhani wana wa Haruni, na kwa ajili ya waimbaji wana wa Asafu. Makuhani walikuwa kwenye harakati kubwa hadi kufikia usiku. Siku zote za siku ya 14 Nisan maandalizi yaliendelea kwa mtindo mmoja. Kwa hiyo, hitimisho la yaliyokuwemo katika siku ya 14 Nisan yakichukuliwa kama ni ya wakati wa dhabihu ya Pasaka itakuwa haileti maana.

 

2Nyakati 35:18, inasema: 18 Wala haikufanyika Pasaka namna ile katika Israeli tangu siku za nabii Samweli; wala wafalme wa Israeli hawakufanya hata mmoja wao Pasaka kama ile Yosia aliyoifanya, pamoja na makuhani, na Walawi na Yuda wote na Israeli waliokuwapo, na wenyeji wa Yerusalemu.

 

Waliiadhimisha Pasaka na Sikuu ya Mikate isiyotiwa Chachu kwa muda wa siku saba (2Nyakati 35:17). Mwaka wa 18 ya Yosia, tofauti kabisa na dhana nyingine zinazokosea kuelewa, ilikuwa sio Yubile. Bali ulikuwa na mwaka wa kwanza wa Yubile mpya, au ni mwaka wa kurudi. Ulikuwa kabisa sio mwaaka wa Yubile. Marejesho ya Yubile yalifanyika kipindi hiki. Kipindi cha Yubile kinawenza kufahamika kwa kuzingatia Ezekieli 1:1. Huu ulikuwa ni mwaka wa 30 wa Yubile. Kifanyika katika kipindi kijulikanacho kama siku ya kuchukuliwa kwenda utumwani kwa mfalme Yehoyakini. Kwa hiyo basi, Yubile itarejeshwa tena ili kutilia umuhimu utaratibu katika maisha ya watu kwaenye zama mpya ya Milenia. Pasaka hii ni marejesho ya pili ya Hekalu. Hekalu lilipaswa kufanyiwa marekabishwo mara tatu! Pasaka ya kwanza ilikuwa ni kwaajili ya kuanzishwa kwa taifa. Marejesho haya yalikuwa yanaelezea kuhusu muendelezo wa maendeleo ya ufalme kwa sehemu zote mbili yaani kwa mataifa na kwa kila mtu binafsi yake.

 

Marejesho ya tatu yalikuwa kama ilivyoandikwa katika Ezra 6, kuanzia mstari wa 3 na Ezra sura ya 9. Kutokana na kifungu hiki kinatoa mwanzo wa dhana ya kwamba sisi tunashughulika na kutumika katika nyumba ya Eloah na katika matengenezo yake. Wakati huu Hekalu lilikuwa limeisha haribiwa tayari. Israeli walikuwa wamepelekwa mbali sana kwenye utumwa katika nchi za watu wenye desturi za kuabudu sanamu. Mungu hakuliinua taifa ili kuongoza na kuwatawala wakiwa katika nchi yao. Bali walichukuliwa mbali katika nchi ya mbali kwa sababu hawakujifunza tutukana na makosa yao. Hivyo basi Israeli na wateule wanashughulikiwa kwa njia ya mtazamo endelevu hadipale tulipopata ujumbe. Hekalu ni nyumba ya Mungu [Elaha (Chad) au Eloah (kwa Kiebrania)]. Katika Ezra 7:12 tunaona kuwa ilikuwa vilevile ni sheria ya Mungu (Eloah au Elah). Tunazungumzia kuhusu Mungu Baba. Ni mapenzi yakle na nyumba yake. Katika Ezra 6:9-12 tunaona kuwa dhabihu zinatolewa ili kuanzisha na kuendeleza ufalme. Katika kitabu cha Ezra 6:15-22 tunaona kuwa Hekalu lilikuwa limekwisha malizika kujengwa wakati wa utawala wa mfalme Dario.

 

Ezra 6:15 inasema: 15 Nyumba hiyo ilikamilika siku ya tatu ya mwezi Adari, katika mwaka wa sit wa kutawala kwake mfalme Dario

 

Adari ulikuwa ndio mwezi wa mwisho wa mwaka. Taifa liliweka wakfu Hekalu (Ezra 6:16-17), tunaona kutolewa kwa dhabihu kwa mafahali ya ng’ombe 100, nk, na kufanya kwa migawanyo ya ki maeneo (Ezra 6:18), kasha waliadhimisha sikukuu (Ezra 6:19).

 

Ezra 6:19 inasema: 19 Kisha, wana wa uhamisho wakafanya Pasaka, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi.

 

Kwa hapa tunaona kuwa Pasaka inafanyika kama ilivyoandikwa katika Gombo za kale kama zilizovyo andikwa katika nyaraka za lugha ya Kiaramu kutoka kwa mujibu wa maandishi yajulikanayo kama Elephantine yenye maana ya ukubwa au yaliyoandikwa kwa kutumia pembe za tembo kwa mujibu wa (tr.Ginsbury, Pritchard waandishi wa zamani wa ukanda wa Mashariki ya Karibu nk., Vol.1).

 

Ezra 6:22 inasema: 22 wakaifanya sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu kwa furaha, kwa muda wa siku saba; kwa kuwa BWANA amewafurahisha, na kumgeuza moyo mfalme wa Ashuru, awaelekee, ili awatie nguvu mikono yao katika kazi hiyo ya nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.

 

Makuhani walitakaswa. Hili lilikuwa ni sharti endelevu. Walikuwa wamenajisika. Mtu anaweza kujiuliza kama hili: Kwa nini walikuwa wanaanguka kila mara kasha Mungu akiwainua tena?

 

Wakati wa kujengwa kwa Hekalu ulikuwa dhahiri. Ni jambo la maana sana kuanzisha muda kwa kuzingatia na uhusiano wake na yale majuma sabini ya miaka yaliyo katika Danieli 9:25. Marejesho haya ya sita yanatupelekea hadi ujio wa Masihi. Mfale aliyekuweko wakati huo alikuwa Dario II, sio yule Dario I (tazama Ezra 4 ili kuthibitisha usemi ukweli huu: pia tazama jarida lisemalo Ishara zaYona na Historia ya Ujenzi upya  wa Hekalu [013]. Juma la saba la miaka lanaendana toka wakati wa Dario II hadi mwaka 70 BK. Hekalu linalo onyeshwa katika kitabu cha nabii Isaya (Isaya 19:19), lilikuwa lijengwe Misri, na ni kweli unabii huu ulitimia kwa hekalu hili kujengwa huko Misri katika mahali panapoitwa Heliopolis katika kiwanja cha Leontopolis na Onias IV ambaye alikimbia kutoka mjini Alexandria wakati wa utawala wa mfalme Ptolemy Philometor. Hekalu hili lilidumu kutumika kama kuanzia mwaka wa 160 KK hadi 71 BK wakati lilipofungwa na mfalme Verspasian (tazama Machapisho ya nyongeza namba 81 katika Biblia ijulikanayo kama Companion Bible). Matoleo ya dhabihu hii katika viwanya vyote viwili kwa wakati ule. Kristo, aliwa mtotot mchanga alihudhuria katika Hekalu hili kipindi kile ambacho familia yake ilikuwa huko Misri. Walifanyia bidii yote ili kukuza imani kikamilifu wakiwa kule (na wakati wake wote wa maisha yake) ili kuutimiliza unabii unaosema, Kutoka Misri.nilimwita mwanangu (Hosea 11:1; na Mathayo 2:15). Wayahudi waliokuwa wanaishi mjini Yerusalemu walikuwa na wivu sana na Hekalu hili, hata hivyo lilihitajika kufungwa mnamo mwaka 71 BK ili kwamba juma lile la saba la miaka likamilike na mamlaka yapelekwe kwa Kanisa. Juma hili la mwisho la miaka kalenda zake zilikosewa na makundi yote mawili yaani Wayahudi na Wakristo. Wakristo walifundisha kuwa kipindi hiki kindeishia mwaka wa 27 BK. Huu ni mwaka unaoaminika kuwa ulikuwa ndio mwanzo wa hududuma ya Kristo. Hii inaendana sambamba na unabii ulio katika Danieli 9:25 kama unabii unaomlenga Masihi (Soma Biblia ya KJV) jambo ambalo sio. Yohana Mbatizaji alianza kuhubiri kuanzia mwezi wa Oktoba ya mwaka 27 BK. Kristo alianza kuhubiri kuanziwa kipindi cha Yohana Mbatizaji alipotiwa gerezani baada ya Pasaka mwaka 28 BK, ambao ulikuwa ni mwaka wa kurejeshwa kwa Yubile mpya. Kristo alianza matengenezo yake katika mzunguko mpya wa Yubile ya arobaini.

 

Pasaka ya 7: ya Masihi

Ili kuweka mwisho wa mfumo wa dunia hii na kufanya upatanisho juu ya dhambi, Mungu alitoa Pasaka kuu ya mwisho ambaye ni Kristo. Na ambayo ni kuleta haki yote kwa Kristo. Ni jambo la muhimu kuelewa uhakika wa kazi yenyewe. Kipindi cha maswali kilikuwa ni kutoka matengenezo ya Hekalu hadi wakati wa Yesu Kristo. Kuna wakati maalumu na mafuatano ambayo yanahitaji kufanyiwa maamuzi kila moja pekeyake. Matazamio ya ujio wa Masihi yako katika kipindi hiki cha Pasaka ya saba. Kitabu cha Mwanzo 3:15 kilionyesha ya kuwa Yesu Kristo alikuwa ni uzao wa mwanamke. Mwana kondoo wa Pasaka ni wazo lililoanzishwa vyema hadi kufikia kitabu cha Ufunuo. Kitabu hiki cha Ufunuo 21:14 kinaonyesha kuwa wale mitume walikuwa ni Wana Kondoo. Ufunuo 22:3 inaonyesha kuwa kile kiti cha enzi kilikuwa ni cha Mungu na Mwana kondoo. Kwa hiyo dhana ya Mwana kondoo wa (Pasaka) ni hadithi iliyoweka mizizi katika mpango wa Mungu. Jina lake litaandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao. Wateule watatiwa muhuri na Mwana kondoo chukua nafasi katika kiti cha enzi cha Mungu. Anaketi pale kama Mwana kondoo wa Mungu. Habari hii inachimbuko lake katika Pasaka. Wateule wote wanashiriki katika Nyota ya Asubuhi na Kristo wakati anapochukua mamlaka ya uongozi (1Pet. 1:19 (hutajwa nyota ya siku), Ufu. 2:28; 22:16).

 

Jinsi ya kufahamu Utendaji kazi wa Pasaka hizi zote

 

Maisha ya Mtu

Jumla ya siku za maisha ya mtu ni miaka 70. Ulikuwa na umri wa miaka 20 kabla hujawa bado mtu mzima na miaka 50 ya utu uzima. Hii ni Yubile ya mzunguko wa saba wa miaka sabasaba. Kwa kipindi hiki chote, kila watu binafsi yao wanashughulikiwa na Mungu. Dhana ile inahusiana na ujenzi tena wa Hekalu. Je, hivi vipimo vina maana gani na mahusiano ya mwanadamu ni jambo lililo mbali nayo. Mzunguko huu pia unaeleweka kupitia hizi Pasaka.

 

Mwanadamu na Yubile

Kwa kadiri ile unavyoshughulika na mwandamano huu wa hizi Pasaka saba, sasa utapata mfumo wa mizunguko mikuu saba. Kila mzunguko mmoja una miaka saba hivyo kufanya kuwa kipindi cha Yubile cha miaka 49 na kujumlisha mwaka mmoja wa mapumziko ya ardhi ambao ni wa hamsini. Katika kila moja wapo ya hiyo miaka kuna Siku Takatifu saba. Vilevile hizi zinahusiana na Yubile. Yubile hii huelezea maisha ya mwanadamu kadiri anavyohudumiwa na Mungu. Mfano wa mafuatano haya yako mbali kando kama ilivyo kwa yale Makanisa saba katika Ufunuo sura za 2 na 3.

 

Miti

Maendeleo ya mwanadamu yameelezewa katika fundisho la fumbo la miti.

 

Kitabu cha Mwanzo 2:9 kinasema: 9 BWANA, Mungu akachipusha katika nchi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.

 

Mwanzo 2:9 inaelezea kuhusu mti wa uzima na ule wa ujuzi wa mema na mabaya. Mti wa mzeituni hufanyika kama ishara ya hitimisho la maarifa na umwagiko wa nguvu za Roho Mtakatifu.

 

Zekaria 4:3-6 inasema: 3 na mizeituni miwili karibu yake, mwingine upande wa kuume wa lile bakuli, na mmoja upande wake wa kushoto. 4 Nami nikajibu, nikamwambia yule malaika aliyesema nami, nikasema, Ee, Bwana wangu, vitu hivi ni nini? 5 Ndipo malaika akasema nami akajibu, akaniambia, Hujui vitu hivi ni nini? Nikamwambia, La, Bwana wangu. 6 Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neon la BWANA kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali kwa roho yangu asema BWANA wa majeshi.

 

Mafuta haya ya mzabibu yalikuwa ama ndani ya bakuli ambayo imetiwa mafuta ya Roho Mtakatifu. Wateule ndio lile bakuli. Ishara imechukuliwa katika mtazamo wa wale mashahidi wawili katika Ufunuo 11:3. Miti ile miwili ya mizeituni ni mfano wa aina mbili ya ufufuo wa wafu na matazamio ya ujio wa Mashihi wawili, wakitanguliwa na manabii wawili. Yohana Mbatizaji alikuwa ni mtangulizi mwenza wa shughuli hii. Katendo haya yatarudiwa tena katika Roho ya Eliya (Mal. 4:5-6). Ni kwa namna gani utendaji-kazi ule utachukuliwa na kufanyika bado haijawa katika hali iliyo dhahiri sana. Kitabu cha nabii Yeremia 4:15 inatoa dokezo, la angalau kazi zile za kwanza.

 

Dhana ihusuyo mifano ya miti ni muhimu sana kwetu ili kuwezesha kuelewa kama kumetokea maendeleo yoyote ya kiroho.

 

Luka 3:7-14 inasema: 7 Basi aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliye waonya ninyi kuikimbia hasira inayokuja? 8 Basi, toeni matunda yapatanayo na toba; wala msianze kusema mioyoni mwenu, Tunaye baba ndiye Ibrahimu; kwa kuwa nawaambia ya kwamba katika mawe haya Mungu aweza kumuinulia Ibrahimu watoto. 9 Na sasa hivi shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usio zaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni. 10 Makutano wakamwuliza, Tufanye nini basi? 1 1Akawajibu akawaambia, Mwenye kanzu mbili na ampe asiye na kanzu; na mwenye vyakula na afganye vivyo hivyo. 12Watoza ushuru nao wakaja kubatizwa, wakamwuliza, Mwalimu, tufanye nini sisi? 13 Akawaambia, Msitoze kitu zaidi kuliko mlivyo amriwa. 14 Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msimdhulumu mtu, wala msishitaki kwa uwongo; tena mtosheke na mishahara yenu.

 

Tusiwe tu tunahubiri kuhusu maonyo yahusuyo watu waikimbie hasira inayo kuja. Bali tuna kazi ya ziada kuifanya. Kurekebusha mienendo yetu na kufundisha toba kwa watu duniani. Usiwajibike tu na yanayohusiana na mahali au usalama. Sisi ni watoto tuliochukuliwa kutoka katika mawe kwa sababu Yuda (Wayahudi) waligeuka kwa Kristo. Kama Wayahudi wangetubu, basi leo hadithi ingekuwa ya tofauti. Wayahudi wangekuwa ni makuhani. Kwa hiyo kusinge wezekana ukuhani huu uwaendee watu wengine nje ya wale wa kabila la Lawi. Lakini Mungu alijua isinge wezekana mambo kuwa katika hali katika hali za namna ile na kwa hakika hakukusudia jambo hili liwe katika mazingira kama hayo. Kwa hiyo, shoka lilikuwa limewekwa katika miguu ya mti wa Yuda. Kwa vile haukuweza kuzaa matunda. Makuhani na manabii walipewa taifa jingine, ambao ni Israeli wa kiroho. Kwa hiyo, kanisa linabidi kufanikisha. Mawe mapya yatatokea ili kuchukua mahala pa wale walioshindwa kufanikisha. Hatahivyo, Yuda wataelewa katika siku za mwisho na kuja katika urithi. Iwapo kama Roho Mtakatifu angekuwepo katika Yuda, basi wangeweza kueneza habari za wokovu kwa Watu wa mataifa, lakini hawakufanya. Lakini hawakuweza hata kula nao.

 

Miaka Saba ya Mti

Israeli wa kiroho huendelezwa kulingana na muandamano wa mzunguko wa miaka saba kama ilivyofafanuliwa katika fundisho fumbo la mti.

 

Luka 13:6-9 inasema: 6 Akasema mfano huu; mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu, akaenda akatafuta matunda juu yake asipate. 7 Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu, uukate, mbona hata nchi waiharibu? 7 Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi; 9 nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa ndipo uukate.

 

Katika Luka 13:6-9 inasema kuwa ule mtini haukutakiwa ukatwe na kuangushwa chini. Miaka mitatu ya kwanza ilikuwa ni miaka ya kukuza. Mwaka wa nne ulikuiwa ni wa kukatia vichele vya matawi ya miti na kutilia mbolea. Mwaka wa tano ulikuwa ni mwaka wa neema. Mwaka wa sita ni mwaka wa mtu anapokuwa ametupwa nje nyuma ya kiwango cha maendeleo. Huu ni mtihani. Ni mwaka wa majaribu kujiipima sisi wenyewe. Mwaka wa saba ni mwaka wa mapumziko ya ardhi. Hii hufanyika katika mizunguko saba. Kila wakati utaendelea kwenda mbele kufikilia ukuaji wa kiroho. Kila Pasaka unayokuwanayo utatumika kwenye wajibu wowote unaotakiwa kuwanao. Kwa jinsi hiyo, utaweza kuzaa matunda yanayoendana na toba uliyoifanya. Hii kwa kiasi fulani inaonekana kama inaleta mchanganyo lakini imeweza kurahisishwa kwa nia ya kufahamu moondo wenyewe. Ujenzi wa Hekalu umetegemeana na maelekezo yalitoko katika mfumo huu. Hekalu ni kielelezo cha kimwili cha maendeleo ya wateule hadi watakapo kwenye utimilifu wa Patakatifu pa Patakatifu. Utaratibu wake umeelekezwa pia katika jarida lisemalo Samson na Waamuzi [073].

 

Ili kupata maendeleo sharti moja ni kwamba tunatakiwa tufanye kazi kwa bidii. Tumeitwa kutoka katika hali mbalimbali za uwezo wa uelewa. Njia moja kuu na muhimu kuizingatia ni kwamba tujitahidi kusaidiana kila mmoja na mwenzake. Kusiwe na mashindano ya kufanya wengine waonekane kuwa ni washindi au wameshindwa. Tunahitajika sisi sote tusaidiane kwa moyo wote mmoja kwakuwa tumo safarini. Kila Pasaka ijapo tunahitajika kwa kweli tuelekee kwenye hatua au ndazi ya pili. Tunapaswa kusaidiana hasahasa katika ule mwaka wa sita wa majaribu. Ni hakika kuwa Mungu atakuacha uingie kwenye majaribu makubwa, ili akuone kama unaweka katika matendo kanuni na sheria zinazohusu upendo, subira, wema na ukweli. Ikiwa kama hatuna upendano katikati yetu, basi Mungu ataruhusu majaribu ili kufikiliza kwenye hatua hii. Lakini hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo, atawapa mlango wa kutokea (1Kor. 10:13). Kabla ya Pasaka, mkono wa Mungu utainuliwa juu-ili kutusaidia sisi tukue. Tunayaona madhaifu yetu. Lakini hatupaswi kukata tamaa! Wala hatupaswi kujihesabia haki sana kwaajili ya matendo yetu tunayofanyiana. Raslimali kuu uliyokuwa nayo ni ule uhusiano wako na Yesu Kristo na kule kuwemo kwako katika utumishi kumtumikia Mungu. Raslimali ya pili ni ule uhusiano wako wewe na wenzako katika Roho Mtakatifu. Ni kweli kwamba tunahitaji kupiga mbio ili tuweze kushinda lakini tunapaswa kupitia kwenye mstari mmoja kwa umoja yaani mkono kwa mkono. Tunahitajika sana kufanya hivyo.

q