Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[074]

 

 

 

Fikra Iliyopo Kwenye Imani Potofu ya Kalti

(Toleo La 2.0 19941029-20000108)

Jarida hili linachambua dhana au mawazo waliyonayo kwenye imani au dini potofu kwa waumini au watu wanaoshirikiana na makanisa yasiyo husishwa na mapokeo yake na kuishika kweli. Maana au tafsiri ya imani potofu imefafanuliwa kama ni utendaji wa kisasa wa neno hilo. Nguvu kuu ya kuweka kitu chochote kabla upendo wa Baba haujaonekana kama kulionyesha na kulifanya litambulike kundi kuwa ni dini au imani potofu.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1994, 2000 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Fikra Iliyopo Kwenye Imani Potofu ya Kalti


 


Dini hizi za imani potofu zinadumu kutokana na hali ya kukamatwa kwa mawazo ya watu wanaojikusanya amoja. Imani hizi zinaanza na watu wanaojikusanya kama kikundi cha watu wenye mtazamo wa namna moja na imani ya namna moja wanaofanya shughuli zao kwa wasiwasi na woga wa mpotofu na za uwongo.

 

Kuna mtazamo unaoendelea kwenye Ukristo makanisa yenye imani kongwe za kale ambao wanalitumia neno hili imani potofu kwa kuyalenga makanisa au dini zisizo mojawapo ya hizi zenye imani kongwe, ambazo zinatofautiana kimafundisho wayayofundisha wao. Dini hizi zote za imani kongwe na za kikale zilizochipuka kutokana na wahubiri mashuhuri wa zamani kina Knox na Calvin na waanndishi mashuhuri wa zama za Matengenezo (kama Luther), na mahafudhina wengine wote kutoka kwenye mashirika yalioamini na kufundisha Utatu yaliyoendeleza imani hiyo na kuwapa watu alama mbaya na majina mabaya wale ambao hawakukubaliana nao imani zao potofu. Sisi mara zote tumebakia kuwa kwenye imani iliyojulikana kama watu wa njia ile. Mtume Paulo alisema hivyo. Dini hizi za Kalti ni kitu kingine tofauti na ni cha pamoja zaidi. Watu wengi wanakosea kujua aina ya watu wa kuwaita jina hili.

 

Matumizi ya jina hili yanakosewa sana. Uelewa wa kweli na utendaji wake unayazingira makundi yote mawili kisawasawa, yaani, ya Ukristo mkongwe za zamani na kwa vikundi vidogo pia. Tofauti ya kweli kati yake vile vilivyo na visivyo imani potofu zipo kwenye ukweli uliodhahiri sana na unalitofautisha kanisa la kweli la Mungu na makundi haya yote ya imni hizi zote potofu, yakiweko nay ale ya kinachoitwa Ukristo mkongwe wa tangu zama kale.

 

Kamusi maarufu iitwayo The Oxford Universal Dictionary inalitafsiri neno hili la kalti au imani potofu kutoka kwenye ukurasa 1617. [ad. L. cultus kuabudu Mnamo karne ya 19 mara nyingi ilitamkwa culte kama ilivyo kwenye Kifaransa.]  1. Ibada - 1683. 2. Aina fulani ya ibada za dini; husu inapotaja sheria zake za kimapokeo kwa nje na maadhimisho yake 1679. 3. hamisha. Kujitoa kwa mtu fulani au kitu, sasa hususan. Ni kama mwili au kikundi cha wanaodaiwa kushikamana 1711.

 

Kwa hiyo tunaaina hiyo ya ibada kwa haki za namna yake fulani na maadhimisho yanayofanywa na kundi la wale wanaojiita watu waadilifu—wanaotokana na mashirika ya kikanisa. Maranyingi sana, muundo mzima wa kidini na kiimani na uliofanyika kuwa mashuhuri hapa duniani umeungwa na waanzilishi wa imani hizi potofu za kikaltiki.

 

Tafsiri yake imeelezewa kwa kina kwenye Kamusi maarufu ya Kiingereza ijulikanayo kama the Oxford English Dictionary Nyongeza kujumuisha maana ya: cult [kalti], sb. Ikiongeza 2.b.  Sasa linatumika mara kwa mara likimaanishwa na waandishi kwenye kanuni za imani za kikaltiki na wavumbuzi wa zama kale za ukaltiki...

Mifano yake ni kutokana na maelezo yanayoelezeka ya kuabudu miungu mingine tofauti, ya kike nay a kiume kwa mtindo unaobadilikabadilika na wa mazingira tofautitofauti.

 

Tofauti muhimu ya imani hizi ya kikalti ni kwamba ni mitindo yake fulanifulani maalumu na wanayoitilia maanani kwenye taratibu zao za kiibada na kidini, hasahasa katika kuonyesha sheria walizonazo na zile zilizo nje na taratibu zao za jinsi wanavyoadhimisha wanapoabudu au jinsi wanavyomnyenyekea mtu au kitu fulani. Kwa ghafla tu jambo hili linaivunja amri ya kwanza kwenye shirika hili lililoanzishwa na mtu ambaye anaweza kudai uaminifu wa mtu au kudai watu wamtii na kuwa juu ya mambo yote ya kiimani na kiroho ya kalti na kuwa ni mtu mwenye kusikilizwa zaidi ya kweli ambayo Mungu ameiweka kwenye Biblia. Na ndipo sasa inahusiana na tofauti iliyopo kati ya miundo iliyoigizwa au kuingizwa kwenye mshikamano wa mwili.

 

Kwa namna moja au nyingne mifumo yote ya kidini ya kalti. Tofauti kati ya imani za kalti na wateule ni unyofu tu kwenye bodi au mwili wa kile kinachodaiwa kuwa ni zaidi ya mshikamano na juu ya kweli ya kweli iliyo kwenye biblia na kusimamia mwenendo na madai ya mteule.

 

Tofauti inaonekana wakati mtu anapoyaweka madai ya mtu kuwa kwenye bodi au kundi kabla ya mtu hajadai kwenye ukweli uliodhahiri na kuelekea hadi kwenye sheria za kibiblia na ushuhuda.

 

Tofauti ya kinabii inapatikana kwenye gombo la nabii Isaya.

Isaya 8:16-20 Ufunge huo ushuhuda, ukaitie muhuri sheria kati ya wanafunzi wangu. 17 Nami nitamngojea Bwana, awafichaye uso wake nyumba ya Yakobo, nami nitamtazamia. 18 Angalieni, mimi na watoto hawa niliopewa na Bwana tu ishara na ajabu katika Israeli, zitokazo kwa Bwana wa majeshi, yeye akaaye katika mlima Sayuni. 19 Na wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong'ona; je! Haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? Je! Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai? 20 Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi.

 

Hii ingetikea na Mungu alisema ingetokea na kwa mambo mengine Mungu anafanya kwa makusudi mazima kabisa itokee ili kwamba watu hawa wasiingie hukumuni. Wanaruhusiwa kuwa wa imani hizi za kalti na wanaondolewa na kutolewa kwenye kundi la wateule. Hawaitwi hukumuni na kwa hiyo wanabakizwa kuingia hukumuni kwenye ufufuo wa pili wa wafu.

 

Andiko hili lapasa lieleweke vyema kutoka kwenye tafsiri ya KJV.

Isaya 8:16-20 Ufunge huo ushuhuda, ukaitie muhuri sheria kati ya wanafunzi wangu. 17 Nami nitamngojea Bwana, awafichaye uso wake nyumba ya Yakobo, nami nitamtazamia. 18 Angalieni, mimi na watoto hawa niliopewa na Bwana tu ishara na ajabu katika Israeli, zitokazo kwa Bwana wa majeshi, yeye akaaye katika mlima Sayuni.

 

Huu ni unabii. Kristo amewapa wateule na Bwana wa Majeshi kama ishara na maonyo kwa Israeli na ulimwengu. Sheria na ushuhuda vimewekwa juu yetu. Tunalazimishwa kutenda mambo sawasawa na isemavyo sheria na ushuhuda.

 

19 Na wakati watakapokuambia, Tafuta habari kwa watu wenye pepo na kwa wachawi; waliao kama ndege na kunong'ona; je! Haiwapasi watu kutafuta habari kwa Mungu wao? Je! Waende kwa watu waliokufa kwa ajili ya watu walio hai?

 

Hili ndilo linalotokea huko kipindi hiki na ilitabiriwa na kutokea kwa msingi endelevu. Israeli waliigeukia miungu ya uwongo na kuziandama imani na dini za uwongo. Walianza kuyatenda na kuyaandama mambo yote mageni kama vile kusimamisha au kuanzisha tena dini na imani zote potofu za babeli mamboleo, wakianzisha imani na dini za uwongo za kimizimu na kuyaomba maroho ya watu waliokufa (ambao ni mapepo), kama wanavyofanya sasa.

 

20 Na waende kwa sheria na ushuhuda; ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, bila shaka kwa hao hapana asubuhi.

 

Kama mtu akiwa haneni kwa kweli ya Mungu, kama hawajitoi na muhuri haujatiwa vipajini mwao, basi wao hawapo miongoni mwa wateule.

 

Andiko lililo kwenye tafsiri ya RSV halionyeshi kikamilifu umuhimu wa sheria na ushuhuda kwa wanafunzi wa Mungu. Wakati kundi la watu, ambao mwanzoni walidai sheria na ushuhuda, kuwa wanaanza kufundisha kinyume na Biblia wakati ambapo hakuna nuru ndani yao. Wao ni waumini wa kalti. Wale wanasalia ndani ya makundi hayo wakieendelea kung’ang’ania mafundisho ya uwongo hawamo tena kwenye ufuasi wa Mungu na sio wateule. Bali hawa ni wafuasi na wanachama tu wa imani hizi za kalti na kwa namna hiyohiyo ambayo kundi linguine la wasiofanya ibada zilizoelekezwa au kuamriwa na biblia ya walio kwenye imani inayoshikamana na kalti.

 

Kutokana na tafsiri hii wakati dini za Kikristo zilianza kuiga mfumo na imani ya Utatu, kufuatia na mafundisho mabaraza ya kanisa, wakaanza kuwa kalti. Wakati dini za Ukristo mkongwe zilipoanza kuliunda Baraza la Mtaguso wa Nikea na walianzisha mafundisho na mfumo wao wa kiteolojia na kifilosofia ambao ulikuwa ni kinyume kabisa na maagizo ya biblia na wakafanyika kuwa kalti kamili kabisa. Wakati kiasi kingi cha makanisa yalipoiga na kujiunga kwenye mfumo huu wa mabaraza na kukubaliana na imani hii ya Utatu kenye kipindi kilichojulikana kama cha Mafundisho ya Baraza la Mtaguso wa Kalkedoni yote yalikuwa ni kalti na hakuna miongoni mwao aliyekuwa ni sehem ya wateule.

 

Kama sisi tumo kwenye ushirika wa mashirika haya basi tunapendezwa n mafundisho haya. Kama sisi tu wanachama wa mashirika haya yanayofundisha imani ya Utatu basi tuje kuwa tunaunga mkono mafundisho haya mapotofu kwa kujihudhurisha kwetu. Ukweli ni kwamba kitendo chetu cha kujihudhurisha kwenye ibada zao na uanachama wetu kwenye makanisa haya kunafanya ionekane kuwa tunachukuliana au kukubaliana na mafundisho haya; kwakuwa ukimya wetu unafanya yakubalike mafundisho haya.

 

Kwahiyo, Makanisa ya Roman Katholiki, Anglikana, na Greek Orthodox ni kalti, na ndivyo ilivyo pia kwa makanisa mengine yote ya mrengo wa waabudu miungu mingi au kwa vikundi vinavyouabudu utatu ni kalti. Ukubwa na uwingi walionao si kitu au kigezo cha kushindwa kuitwa kuwa wao ni kalti. Ukweli wa kwamba kundi linamtegemea au kuweka imani yao kwa kiongozi mmojana kuwa juu ya kila kitu hata kuwa juu ya maagizo yaliyo kwenye kweli ya biblia ni alama mojawapo ya imani hii ya kalti. Haijalishi jinsi kiongozi huyo alivyo au atakavyoitwa, awe Papa au Askofu Mkuu, au Kiongozi wa wa Ulimwenguni kote, au Jones asiye sawasawa.

 

Wateule wamebatizwa kwenye mwili wa Kristo na sio kwa kanisa lolote au dhehebu. Maneno hayo yananenwa kila mteule anapokuwa anabatizwa. Kwa hiyo wateule wanaunganishwa kwenye mwili wa Yesu Kristo kwenye ibada ya kumuabudu Mungu Mmoja, Wapekee na wa Kweli aliyeandikwa kwenye Yohana 17:3. Kwa hiyo wakati wateule wanapoungana amoja kwenye makanisa mahalia, walikuwa wameunga sana kwa msingi wa kuungamana kwao kwenye kweli na kumuabudu Mungu Mmoja, Wapekee na wa Kweli na kumtumikia Mwanae wa pekee Yesu Kristo.

 

Wakati kanisa lilipokabiliwa na mafundisho yaliyojaribu au kukusudia kumuweka Kristo nje ya hali yake ya kawaida na halisi, na kujaribu kumfanya awe zaidi ya hali yake halisi ya Uwana wa Mungu na kumfanya awe sawa na Mungu na kuutenganisha ubinadamu wake kutoka kwenye utakatifu wake, ndipo wateule walilazimika kujiunga upya kwa kuanzisha kanisa tena na kujitenga na wale wanaooyaanzisha mafundisho ya uwongo, ambayo yalijulikana wazi na kuitwa kama mafundisho ya Mpingakristo.

 

Msingi wa imani ni ukweli na hawaendi gizani kakwe kabisa wale wanaotembea kwenye kweli. Sababu inayotupelekea tuenende kwa mujibu wa 1Yohana ni kwa kuwa malumbano haya yaliingia kanisani kipindi ambacho Mtume Yohana akiwa kiongozi. Ilimpasa kuyashughulikia kikamilifu mafundisho haya mapotofu na fundisho kuhusu Uungu tangu mwanzoni kabisa mwa hatua ya kanisa. Hakuna lililo jipya. Malumbano haya yalipata ufumbuzi wake kwenye kanisa la Yohana, wakati walipojatibu kutenganisha ubinadamu wa Yesu Kristo na kumfanya kuwa alikuwa na utu wa kimbinguni. Walijaribu kusema na kufundisha kwamba alikuwa ni mtu wa asili mbili ya kibinadamu na kimbinguni ambavyo ni kwamba upande huu wa kibinadamu ndiyo ulikuwa Yesu Kristo na huu upande mwingine alikuwa ni Mungu kamili na kwa hiyo kwamba alikuwa ni sawa kabisa na Mungu na kwamba sehemu hii ya kimungu haikufa alipotundikwa pale mtini. Huu ulikuwa ni uzushi na mafundisho haya ya kizushi ambayo yamedumu hadi leo; na Mtume Yohana aliyashughulikia sana kuyakanusha na kuwafundisha watu ukweli kama tutakavyoone kwenye maandiko yanayofuatia. Tutakwenda kujionea pia jinsi yalivyo mafundisho ya Mpingakristo. Tutaona kuwa mafundisho ya utatu ni mwendelezo wa mafundisho mbalimbali ya yanayojigeuzageuza sura yake tu ya Mpingakristo. Dhana ya Umamboleo na ya kimitindo ni fundisho linguine linalobadilikabadilika tu la huyuhuyu Mpingakristo. Kwa vyovyote vile, dhana na imani ya Utatu ni mafundisho ya Mpingakristo nah ii ndiyo sababu kubwa inayotufanya tutoe mwito wa kutoka ndani yake.

 

1Yohana 1:1-10  Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima; 2 (na uzima huo ulidhihirika, nasi tumeona, tena twashuhudia, na kuwahubiri ninyi ule uzima wa milele, uliokuwa kwa Baba, ukadhihirika kwetu); 3 hilo tuliloliona na kulisikia, twawahubiri na ninyi; ili nanyi pia mpate kushirikiana nasi: na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana wake Yesu Kristo.

 

Ukweli huo ndiyo unaoutofautisha au kuufanya ujulikane ushirika wa wateule wake Mungu na Mwanae. Huu ndiyo umuhimu na maana ya aya hii.

 

4 Na haya twayaandika, ili furaha yetu itimizwe. 5 Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kwake, na kuihubiri kwenu, ya kwamba Mungu ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake. 6 Tukisema ya kwamba twashirikiana naye, tena tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatuifanyi iliyo kweli;

 

Wakati tunapokuwa tu mali ya shirika la kidini linaloyakumbatia mafundisho potofu ni uwongo. Sio kweli na bado tunaenenda katika giza, na kwa hiyo hatuwezi kuwa tunatembea na Mungu. Hatupo kwenye ushirikiano na Mungu au hatuna ushirika na Mwanae. Na ndiyo maana hatuwezi kukaa na watu kwenye ushirika wetu, wanaoendelea kuendekeza kutembea gizani.

 

7 bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote. 8 Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. 9 Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. 10 Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu.

 

Kwa hiyo ni wajibu na lazima kabisa kwa wapendwa waende pamoja kwenye kweli. Hatuna fursa ya kuchagua. Ni maelekezo ya lazima ya Roho Mtakatifu aliyotupa kupitia Yohana.

1Yohana 2:1-29  Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, 2 naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote. 3 Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua yeye, ikiwa tunashika amri zake. 4 Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake. 5 Lakini yeye alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake. 6 Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda.

 

Kristo ni wakili wetu anayetuombea na kututete kwa Baba. Wakili ananena mambo kwa mamlaka akimwakilisha mwingine nay eye mwenyewe hawezi kuwa ni mamlaka ya kufanya hivyo. Kwa hiyo ni wazi sana kwamba Kristo akiwa kama wakili hawezi kuwa ni mamlaka yanayoweza kunasihi mashitaka, au kunena kwa niaba ya watu wanaohusika. Hawezi kuwa Mungu na akawa pia ni wakili wa kuwatetea wateule kwa Mungu kwa jinsi hii inayoonekana hapa.

 

7 Wapenzi, siwaandikii amri mpya, ila amri ya zamani mliyokuwa nayo tangu mwanzo. Na hiyo amri ya zamani ni neno lile mlilolisikia. 8 Tena nawaandikia amri mpya, neno lililo kweli ndani yake na ndani yenu; kwa kuwa giza linapita na ile nuru ya kweli imekwisha kung'aa. 9 Yeye asemaye kwamba yumo nuruni, naye amchukia ndugu yake, yumo gizani hata sasa. 10 Yeye ampendaye ndugu yake, akaa katika nuru, wala ndani yake hamna kikwazo. 11 Bali yeye amchukiaye ndugu yake, yu katika giza, tena anakwenda katika giza, wala hajui aendako, kwa sababu giza imempofusha macho.

 

Pendo lionyeshwalo kwa kupendana kila mmoja na mwenzake ni ishara au alama ya mteule. Mahali ambapo kundi la watu au kikundi kinapojikita katika kulipenda shirika lao au viongozi wao zaidi kuliko kupendana wenyewe kwa wenyewe na kutoitilia maana kweli, ndiyo alama ya kuwa kalti. Mahali ambapo watu wanadumu kwenye mfumo wa kiushirikiano unaohubiri mfundisho haya ya uwongo na watu hao wakayavumilia makosa hayo na wayanapenda sehemu au baadhi ya mafundisho au mambo yaliyo kwenye kalti na kuvumilia kwa kujihudhurisha na kuwepo huko, basi wanakuwa ni washiriki wa uovu woe unaofanyika hapo.

 

Mtume Yohana anaandika kuhusu neno la Mungu likae kwa wingi kwenye mioyo ya wateule na kwa kufanya hivyo watamshinda muovu.

12 Nawaandikia ninyi, watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu, kwa ajili ya jina lake. 13 Nawaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nawaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu. Nimewaandikia ninyi, watoto, kwa sababu mmemjua Baba. 14 Nimewaandikia ninyi, akina baba, kwa sababu mmemjua yeye aliye tangu mwanzo. Nimewaandikia ninyi, vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu linakaa ndani yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu. 15 Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

 

Kwa hiyo hatuwezi kulipenda shirika hapa duniani, vinginevyo na kumpenda Baba hakumo ndani yetu. Yatupasa kuipenda kweli itokayo kwa Baba zaidi kuliko shirika lolote au hii dunia. Hakuna kitakacho ingilia kati au kukwaza uhusiano wetu na Baba, yakuna hata ushusiano wetu na Yesu Kristo. Kwa kuwa Yesu Kristo ni mmoja na Baba jambo hilo haliwezekani kabisa kutokea. La muhimu na la kulitilia maanani kwenye uhusiano wetu ni kuwa katika Mungu kwa njia ya Yesu Kristo na kwa ukomo wake. Ndiyo maana Yohana anasema.


16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia. 17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa za ke, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

 

Chimbuko au kiini cha upendo wa wateule ni Baba pekeyake. Msingi wa upendo wa wateule wa kupendana wao kwa wao ni Roho Mtakatifu aliye ndani ya kila moja wao, kutoka kwa Kristo na kuendelea kwa wengine. Kristo alijitoa mwenyewe kwa dunia kwa kupitia upendo wa Baba. Yohana 3:16 inasema kwamba Baba alimtoa Mwana.

Yohana 3:16  Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. \

 

Ni usemi wa kawaida na uliozoeleka au wa zamani kwenye imani ya Ukristo mkongwe, lakini ni usemi wenye nguvu sana na unayasuta matendo yao.

 

Hatuwezi kutoa kile tusichokuwanacho. Hakuna usawa kwenye karama za Mwana na Baba. Zaidi ya yote, Kristo alitumwa na Baba yake kwa hiyari na maelekezo.

Yohana 4:34 Yesu akawaambia, Chakula changu ndicho hiki, niyatende mapenzi yake aliyenipeleka, nikaimalize kazi yake.

 

Kwa hiyo kazi ni ya Baba na yapasa ifanywe na wateule. Ni kwa namna gani basi wateule wanaweza kubaki kwenye shirika linalofundisha mafundisho yaliyo kinyume kabisa na sheria na ushuhuda na huku bado wakiifanya kazi ya Baba? Kazi hiyo itakuwa na maana gani? Yohana aliliona hilo kuwa ilikuwa ni muhimu alipoandika. Ni kwa kiasi gani basi basi jinsi ilivyo leo? Kwa kujihudhurisha kimya kimya kwenye kalti, ambazo hata zimekuwa kama vilabu vya burudani, uwezo wa taifa la Israeli na kutokana na wao ulimwedgu wote mzima kufikia toba kumechelewa au kubebakia kuwa kitu kisichowezekana.

 

Hata kuna maneno mengine yanayozua mabishano makubwa sana ya uwongo na kujidanganya wanayopenda kuyatumia baadhi ya wateule, ambayo yanasemekana kama ifuatavyo. Mimi sijabatizwa kwenye shirika lolote bali nimebatizwa kwenye mwili wa Kristo. Kwa hiyo, mahali popote walipo wateule naweza kuwapo na kujiunganano bila kujali kile linachofundisha shirika hilo.

 

Watu wanaosema wao si washirika au wanachama wa shirika lolote bali wao ni wa mwili wa Kristo tu, na huku wakibakia bado kwenye imani za kalti zinazofundisha kinyume na torati na ushuhuda, wanafanya kazi ya Shetani. Wanakuwa ni kikwazo na kukanganya uwezo wa wateule wa kuihubi kweli. Wanajidanganya wenyewe kwa malumbano yaliyofanywa ili kuepuka ukweli yaliyoanzishwa kwa lengo la kuchelewesha maamuzi yasiyo muafaka. Kwa ufupi, wao ni waoga. Wametumwa na Kristo ili wawe kama kondoo kati ya mbwa mwitu ili wafanye kazi yao ya uvunaji. Kwa kuwepo kwao kwenye mashirika yaliyokengeuka, ambayo kwa ufafanuzi ni pamoja na mashirika yoyote ya waamini Utatu, hawa hawaifanyika kabisa kazi ya Baba. Wanakinza na kukwaza wito wa wateule. Kwa ufupi ni kwamba watu hawa wameichimbia ili kuizika talanta yao designed to delay uncomfortable decisions.

 

Taifa hili linapaswa kuitwa watubu na watendakazi ni wachache.

18 Watoto, ni wakati wa mwisho; na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga Kristo yuaja, hata sasa wapinga Kristo wengi wamekwisha kuwapo. Kwa sababu hiyo twajua ya kuwa ni wakati wa mwisho. 19 Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu. 20 Nanyi mmepakwa mafuta na Yeye aliye Mtakatifu nanyi mnajua nyote. 21 Sikuwaandikia ninyi kwa sababu hamwijui iliyo kweli, bali kwa sababu mwaijua, tena kwamba hapana uongo wo wote utokao katika hiyo kweli.

 

Hivi ndivyo walivyotumwa na kupelekwa. Walianza kuhubiri uwongo. Haijalishi idadi yoyote waliyonayo. Haijalishi kama wanatushurutisha kujiunga na kuanzisha tena. Walikuwa na idadi kubwa tayari tangu kipindi cha Mtaguso wa Nikea. Kwa kweli, tangu mwaka 381 ulipoitishwa Mtaguso wa Constantinople wao walishakuwa na idadi kubwa ya wafuasi tayari. Lakini uwingi wa idadi yao hauwezi kuwafanya wawe ni sehemu ya mwili. Wanapata uwezo mkubwa wa kutoka nje na kuyafikia mataifa mengi kwa kuwa wanafundisha uwongo. Ni kwa hii kweli ndiyo inayotufanya tuwe kwenye mwili wa Yesu Kristo na kujumuika kwetu na watu wenye mtazamo na nia inayofanana ndiko kunakotuwezesha sisi tubakie kwenye Yesu Kristo, tukiifanya kazi ya Yesu Kristo. Kama tutaacha kuitenda kazi ya Yesu Kristo, tukiuhuisha mwili wa Yesu Kristo, vinginevyo hatutakuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu.

 

22 Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo, yeye amkanaye Baba na Mwana. 23 Kila amkanaye Mwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia.

 

Tutawezaje basi kumkiri huyu Mwana tukiwa tunasema kuwa wao ni viumbe jumuisho, walioungana pamoja na kuwa kiumbe mmoja, na Mungu mmoja; na kwamba wao ni udhihirisho tu wa kitu kimoja. Tunamkana Mwana na kwa kufanya kwetu hivyo tunakuwa hatuna Baba kwa maana tunamkana pia. Haya ni mafundisho ya Mpingakristo.

 

24 Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba. 25 Na hii ndiyo ahadi aliyotuahidia, yaani, uzima wa milele. 26 Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza. 27 Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake. 28 Na sasa, watoto wadogo, kaeni ndani yake, ili kusudi, atakapofunuliwa, mwe na ujasiri, wala msiaibike mbele zake katika kuja kwake.  29 Kama mkijua ya kuwa yeye ni mwenye haki, jueni ya kuwa kila atendaye haki amezaliwa na yeye

 

Hapa dhana ya kutoka na kwenda kutoka kwetu inaendelezwa na Mtume Yohana. Mafundisho yaliyoyafundisha na kuyaendelea Kanisani Mtume Yohana hayakuwa yanahusu mambo ya Uungu kabisa ayakuhusiana kuhusu uhusiano uliopo kati ya Baba na Mwana. Malumbao haya yalikuwa ni mwanzo au uanzishwaji wa imani ya Utatu. Yalijaribu kutenganisha nasaba ya ubinadamu wa Kristo na uungu. Zaidi ya hayo ilijaribu kumfana Kristo kuwa ni sehemu ya Mungu na kuwa yu sawa naye. Haya ni mafundisho la Mpingakristo. Ilikuwa ni kuhusianisha kwa wazi na imani ya Utatu ambao maandiko ya 1Yohana 4:1-2 yalibadilishwa ili kupindisha na kupotosha ukweli. Jaribio la kuwa ni sehemu ya mteule ni kwa mwenendo wa haki, yeye atendaye haki ni mtakatifu.

Yeyete atendaye dhambi ni wa ibilisi (diabolos). Kwa hiyo haiwezekani kuwa sehemu ya mshirika kwenye shirika ambalo haliihubiri kweli. Kwa kuwa amri ya Mungu ni ya muhimu sana. Dhambi maana yake ni kile kitendo cha kuvunja amri au kwa hapa ni ukengeufu. Amri ya kwanza inakusiana na jinsi ya kumuabudu na kumpenda Mungu. Tutawezaje kumuabudu Mungu Mmoja, wa Pekee na wa Kweli ikiwa kama tuko sehemu ya imani ya wale wanaojaribu kumshutumu Kristo kwa kujaribu kujaribu kumlinganisha kuwa sawa na Mungu wa Pekee na wa Kweli na kuwa kwenye mkumbo wa kutenda dhambi hiyohiyo ambayo Shetani aliifanya? Kwa hiyo inatupasa kujitakasa kama Kristo alivyo mtakatifu. Tutawezaje kujitakasa sisi wenyewe huku tukiwa kwenye ushirika wa klabu ya starehe? Tunawezaje kumtumikia Mungu na kumtolea zama zetu Baali?

 

1Yohana 3:1-24 Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye. 2 Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo. 3 Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu. 4 Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi. 5 Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake. 6 Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua. 7 Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye; atendaye haki yuna haki, kama yeye alivyo na haki; 8 atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi. 9 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.

 

Huu ni usemi wa maana sana. Tunatenda dhambi wakati wote. Ni tabia na sili ya Mungu ndiyo inayotushuhudia dhambi zetu. Tunajua kuwa wakati tunapofikiria kitu kibaya kwa ajili ya asili yetu ya uasi kwa yale tunayoyafanya na dhamira zetu (Roho Mtakatifu) ikitukataza ikisema hapana, hapana, hapana, hivi sio vizuri. Tunasujisikia kusutwa na dhamiri kwa kuwa tumetenda dhambi. Si kwamba hatuwezi kutenda dhambi tunaweza kupitiliza ushuhuda ule lakini tunayajua yale tunayoyatenda na tunajitenga sisi wenyewe mbali na Mungu kujitenga mbali na wateule kwa ajili ya dhambi, na inatupasa kutubu. Dhambi zinazorudiwa rudiwa haziwezi kutuwekwa mahalia pa kuwezesha kwa kuwa hatuwezi kumfanya Kristo ayarudie mateso ya kusulibiwa mara ya pili tena.

 

10 Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake. \

 

Kwa hiyo tuna mambo mawili tuliyoagizwa – la kwanza ni kuwapenda ndugu zetu na matendo mengine yaliyo mema na hak. Kile kilicho sahihi na haki kipo wazi sana na kinashughulikiwa na torati au sheria. Hatupaswi kuwa kwenye shirika lililokengeuka.

 

Iwapo kama tutakuwa hatutendi mema ndipo tutakuwa si wa Mungu. Hatutaonyesha kuwa tunawapenda watu kama hatutaweza kulihubiri neno la Mungu kwao kwa kweli isiyo na michanganyo au kughoshiwa.

 

Hatuwezi kumtumikia Mungu na huku tukiyanena mambo yaliyo nje ya midomo yetu. Sio jambo gumu kusema yeye aliye na sikio na asikie. Kweli itakayohubiriwa nyakati za mwisho yapasa ihubiriwe kwa wazi kwa wateule na ihubiriwe kwa taifa kwa maneno ya wazi. Kufikiri kinyume chake au vinginevyo ni kujidanganya wenyewe. Vipawa na wito wa Mungu hautolewi ili kuburudisha mikaka ya kwenye vilabu vya starehe au kwa ajili ya mashindano ya kujipatia umashuhuri.

 

11 Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi; 12 si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake. Naye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki. 13 Ndugu zangu, msistaajabu, ulimwengu ukiwachukia. 14 Sisi tunajua ya kuwa tumepita toka mautini kuingia uzimani, kwa maana twawapenda ndugu. Yeye asiyependa, akaa katika mauti. 15 Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake. 16 Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu. 17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli. 19 Katika hili tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, nasi tutaituliza mioyo yetu mbele zake, 20 ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote. 21 Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu; 22 na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake. 23 Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri. 24 Naye azishikaye amri zake hukaa ndani yake yeye naye ndani yake. Na katika hili tunajua ya kuwa anakaa ndani yetu, kwa huyo Roho aliyetupa.

 

Mungu yu tofauti na Mwanae kwa maana kwamba ni viumbe wawili tofauti, Mungu tunayezishika amri zake na kutembea kwenye kweli yake. Kitendo cha kutembea kwenye kweli akiwezi kufikiwa kwa kunyamaza kimya ndani ma mashirika au madhehebu yaliyoanguka kiimani na kukengeuka. Kwa kunyamaza kimya tutakuwa tunamkana Kristo kabisa. Udhaifu kama huo alikuwanao Mtume Petro alipokuwa kabla hajaongoka. Hata hivyo, si jambo linalokubalika kwa wateule.

 

Wakati Petro alipomkana Kristo alikuwa hajaongoka bado. Alikuwa kwenye fursa ndogo kuliko sisi na wateule wote tulivyo. Wala hakutarajiwa kuwa atakuwa imara; kwa kuwa alikuwa hajaongoka. Tunahukumiwa kwa kiwango cha juu kuliko alivyokuwa Petro wakati ule alipokuwa anasulibiwa Yesu Kristo. Hili ni jambo mhimu sana kufanyika. Kuwa sehemu ya wateule wa Mungu si jambo la mzaha.

 

Wateule wajnatakiwa ili kuijaribu au kuipima roho ili kuona kama ni za Mungu. Kama kuna mtu yeyote akituambia sisi kwamba Kristo ni Mungu na yuko sawa na wanahali sawa na Mungu wa Pekee wa Kweli, ndipo tutajua kuwa si Roho wa Mungu. Wateule wanapaswa kujitenganao. Watu hawa wanatoka kwetu kwa kile wanachosema, kinyume na wanavyoketi. Ukweli ni kwamba hali hii ua ukengeufu kushika hatamu za maongozi haiwezi kubadili hali na kuwafanya wao kuwa ni watu wa Mungu, na wala kwamba wanastahili kujumika au kusaidiwa na wateule. Kwa kweli, kinyume cha hapo ndilo hali halisi yenyewe. Wao kwa matendo yao wamekwishajitoa tayari kwetu ili waonyeshe kwamba hawakuwa wa kwetu kabisa. Kitendo cha kuwatenga watu wenye  mafundisho haya mapotofu hakumaanishi kuwa hawa walliotengwa hawapendwi au wanachukiwa, la. Bali wale ambao Mungu anawapenda anawakemea na kuwarudi. Mara nyingi kitendo hiki cha kukemea kinafanywa kwa wale walioimara kiroho na kwenye neno la Mungu.

1Yohana 4:1-21 Wapenzi, msiiamini kila roho, bali zijaribuni hizo roho, kwamba zimetokana na Mungu; kwa sababu manabii wa uongo wengi wametokea duniani. 2 Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. 3 Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo ambayo mmesikia kwamba yaja; na sasa imekwisha kuwako duniani.

 

Kwenye kipindi cha Yohana, roho hii ya Mpingakristo ilijaribu kusema kuwa sehemu ya mwili wa Yesu Kristo haikuwa kwenye hali ya kimwili, bali ilibakia kuwa kule juu kwa hali yake. Roho ile ingali bado ipo leo na ni sehemu ya imani na mfumo au utawala wa mwanamke kahaba. Ni sehemu ya dini potofu. Ni fundisho la Mpigakristo.

 

Andiko hili kuhusu mafundisho ya Mpingakristo limekuwa likibadilishwa kwenye maandiko ya kale. Hili ni moja ya maandiko ya kwanza waliyoyageuza na kuyapotosha kwa kuyaghushi kwa kuwa andiko hili ndilo linatuambia sisi kwamba mafundisho ya Utatu yanatokana na mafundisho ya Mpingakristo, kwa hiyo iliwalazimu kubadilisha uandishi wa aya na andiko hili. Andiko sahihi linaweza kuonekana kwenye uhalisia aliouandika mwandishi mashuhuri aitwaye Irenaeus (soma kitabu chake cha the Ante-Nicene Fathers, Vol 1, fn. p. 443). Andiko hili linasomeka hivi:

Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; Na kila roho inayomkiri Yesu Kristo kuwa ametokana na mwili hi ya Mungu; na kila roho inayomtenganisha Yesu Kristo siyo ya Mungu bal ni ya Mpinga Kristo.

 

Mwanahistoria mashuhuri Socrates anasema (VII, 32 p. 381) kwamba ayah ii au kifungu hiki kimepotoshwa na wale waliokusudia kuitenganisha nasaba ya kimwili ya Yesu Kristo na uungu wake. Kwa hiyo madai yanayosema kuwa Kristo alikuwa sehemu moja na nasaba ya mbinguni akiwa kama sehemu ya Mungu, mbali na ubinadamu wake na kifo chake pale msalabani, unapingana kabisa na kukanusha ufufuo wan a mafundisho ya Mpingakristo. Kwa hiyo imani ya Utatu yanaangukia wazi sana kuwa ya Mpingaktisto.

 

4 Ninyi, watoto wadogo, mwatokana na Mungu nanyi mmewashinda, kwa sababu yeye aliye ndani yenu ni mkuu kuliko yeye aliye katika dunia. 5 Hao ni wa dunia; kwa hiyo wanena ya dunia na dunia huwasikia. 6 Sisi twatokana na Mungu. Yeye amjuaye Mungu atusikia; yeye asiyetokana na Mungu hatusikii. Katika hili twamjua Roho wa kweli, na roho ya upotevu.

 

Kwa hiyo, roho wa kweli anahitajika kumtenganisha kutokana na roho wa upotevu. Jaribu hili kwa wateule ili kuwaonyesha jinsi walivyo na ni nani hasa walio wateule na walioitwa na siyo kuchaguliwa.

 

7 Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. 8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo. 9 Katika hili pendo la Mungu lilionekana kwetu, kwamba Mungu amemtuma Mwanawe pekee ulimwenguni, ili tupate uzima kwa yeye. 10 Hili ndilo pendo, si kwamba sisi tulimpenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda sisi, akamtuma Mwanawe kuwa kipatanisho kwa dhambi zetu. 11 Wapenzi ikiwa Mungu alitupenda sisi hivi, imetupasa na sisi kupendana. 12 Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu. 13 Katika hili tunafahamu ya kuwa tunakaa ndani yake, naye ndani yetu, kwa kuwa ametushirikisha Roho wake. 14 Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu. 15 Kila akiriye ya kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu, Mungu hukaa ndani yake, naye ndani ya Mungu. 16 Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake. 17 Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu. 18 Katika pendo hamna hofu; lakini pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa maana hofu ina adhabu; na mwenye hofu hakukamilishwa katika pendo.

 

Kama tunatishika kuhusu kama shirika ni mali ya kile kinachoitwa mashirika ili kuimarisha mahala petu, na kuogopa kile kinacho kuhusu kuamua kwenda kwa usalama, na kukiogopa kle kiachokwenda kutokeza duniani na mateso na dhana kwamba tunaweza kujiepusha nacho, kwa hiyo hatuwezi kuwa na upendo kamili na hatufikiri vizuri sana. Hatumwangalii au kumtegemea Mungu.

 

19 Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza. 20 Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. 21 Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.

 

Wale walio na upendo kamili hawaogopi tena, wakiwaacha peke yao wale dhambini na kukosea kikimya kimya na wakibakia bado kwenye shirika hilo. Mtu anaweza tu kuwa mshirika wa kalti na siwe tena kuwa sehemu ya mwili wa Kristo.

 

Vigezo vya kuushinda ulimwengu vimeelezwa wazi kwenye 1Yohana 5:1-5.

1Yohana 5:1-21 Kila mtu aaminiye kwamba Yesu ni Kristo amezaliwa na Mungu. Na kila mtu ampendaye mwenye kuzaa, ampenda hata yeye aliyezaliwa na yeye. 2 Katika hili twajua kwamba twawapenda watoto wa Mungu, tumpendapo Mungu, na kuzishika amri zake. 3 Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito. 4 Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu. 5 Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu?

 

Kama tunampenda Mungu tutazishika amri zake. Kwa hili tunajua kuwa tunawapenda watoto wa Mungu. Tunapozaliwa katika Mungu yatupasa kuushinda ulimwengu. Kuushinda ulimwengu yatupasa kuamini kuwa Masihi ni Mwana wa Mungu. Kwa hiyo uhusiano ni muhimu. Hali ya udanganyifu inayotafuta kutokuwa na haja au uhitaji huu unaoonekana miongoni mwa waamini Utatu unakutikana kwenye ubadilishaji au upotoshaji uliofanywa kwenye maandiko ya biblia, au kwenye tafsiri yao potofu mbali na maana iliyowazi ya maneno kama tunavyoona hapo chini (hasa hasa kwenye 1Yohana 5:7. Linganisha na hapo chini na maandiko yaliyopotoshwa kwenye tafsiri ya KJV).

 

6 Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu. 7 Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli. 8 Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. 9 Kisha wako watatu washuhudiao duniani], Roho, na maji, na damu; na watatu hawa hupatana kwa habari moja. Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe. 10 Yeye amwaminiye Mwana wa Mungu anao huo ushuhuda ndani yake. Asiyemwamini Mungu amemfanya kuwa mwongo, kwa kuwa hakuuamini huo ushuhuda ambao Mungu amemshuhudia Mwanawe. 11 Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; na uzima huu umo katika Mwanawe. 12 Yeye aliye naye Mwana, anao huo uzima; asiye naye Mwana wa Mungu hana huo uzima. 

Kumbuka kuwa Mungu alitupa sisi uzima wa milele na uzima huu umo hatika mwanae. Kwa hiyo mwana ana uzima wa milele kutoka kwa Baba, ambao tumepewa pia sisi kwa namna hiyohiyo.

13 Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu. 14 Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. 15 Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba. 16 Mtu akimwona ndugu yake anatenda dhambi isiyo ya mauti, ataomba, na Mungu atampa uzima kwa ajili ya hao watendao dhambi isiyo ya mauti. Iko dhambi iliyo ya mauti. Sisemi ya kwamba ataomba kwa ajili ya hiyo. 17 Kila lisilo la haki ni dhambi, na dhambi iko isiyo ya mauti. 18 Twajua ya kuwa kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi; bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda, wala yule mwovu hamgusi. 19 Twajua ya kuwa sisi tu wa Mungu; na dunia yote pia hukaa katika yule mwovu. 20 Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele. 21 Watoto wadogo, jilindeni nafsi zenu na sanamu.

 

Dhana hii hapa kuhusu dhambi ya mauti imechukuliwa na Wakatoliki kwenye imani au dhana ya kuwa na dhambi ya mauti nay a milele. Kle Yohana anachojaribu kukitofautisha hapa ni kwamba mchakato wa kufikia ukamilifu wa wateule ni lazima upitie kwenye makosa ya kimaisha ya siku hadi siku. Makosa hayo ni sehemu ya ushindi wetu. Tunatenda dhambi kila siku. Dhambi ya mauti kwa mtazamo huu (ni dhambi ile itakayomfanya mtu asiwe na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu bali awe kwenye ufufuo wa pili) ni wakati tunapotenda dhambi kwa kiwango ambacho mwili wa Kristo, kwa kupitia wazee, waseme kwamba hatuwezi tena kabisa kuhukumu na inaturudisha duniani ili kwamba tunatolewa kwa adui, ili kwamba maisha yetu yaokolewe katika siku za mwisho. Tunarudishwa nyuma kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Hiki ndicho kilichotokea kwenye 1Wakorintho 5:5. Tunapokuwa tunatenda dhambi kwa makusudi ndipo tunakwenda kwenye dhambi aa mauti ambazo hatuwezi kuzishinda na zinaturudisha nyuma duniani. Kwa hiyo tunaondolewa kwenye hukumu. Ni kwa rehema zake.

 

Kwa hiyo wateule wapo chini ya hukumu kwa kile wanachokitenda, kunena na kuwaza. Matendo yao yanapimwa kila wakati na Roho Mtakatifu. Kitendo cha kujiunga kwa wateule kwenye makundi la watu yanayotenda na kuenenda kinyume na Maandiko Matakatifu yanamfanya mteule awe hukumuni. Kwa hiyo mteule hapaswi kuwa mashirika wa vikundi vya imani hizi potofu za kikalti vinavyofuata na kutenda mambo yanayopangwa na wanadamu hata yakiwa ni kinyme au yanapingana kabisa na Maandiko Matakatifu na kweli yake.

 

Tunapojiunga kwenye shirika au kanisa linalofundisha na kuzihalifu sheria za Mungu, tunajiweka wenyewe kwenye hukumu. Hakuna tofauti kati ya kuwa kwenye shirika au kanisa linaloivunja amri ya kwanza na kuwa mwanachama wa kanisa linaloivunja amri ya saba, au ya nane, au ya tisa. Hakuna tofauti kati ya kuwa mshirika wa kikundi cha kalti ya kidini kinachoabudu miungu wa uwongo na kuwa mshirika au mhusika wa waliofanya mashambulizi ya mauaji, au kuwa kwenye kundi la waporaji na wanyang’anyi, au kuwa kwenye kundi la wazinzi. Wote hawa ni wanachama wa kalti na ni wavunjaji wa Amri ya Kumi na wote hawatakuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu bali ni hadi ule wa pili wa hukumu ili wahukumiwe.

 

Kuna mchakato wa udhanganyifu na upotofu unaowashinda na kuwaangusha watu walio kwenye imani hizi za kalti, ambao unawafanya wasiijali kweli na kuipuuzia. Ni kama tulivyoona, kwamba kalti ni kundi la waamini wanaoongozwa kwa kufuata mawazo ya watu na mapokeo ya taratibu za kidini na hawajali kulisikiliza neno la Mungu

 

Mungu anachukiwa sana na kuwashutumu kwa matendo haya kwenye Isaya 66:4

Isaya 66:4 Mimi nami nitachagua mapigo yao, nitaleta hofu zao juu yao; kwa sababu nilipoita, hawakuitika; na niliponena, hawakusikia; bali walifanya yaliyo maovu machoni pangu, na kuyachagua nisiyoyafurahia.

 

Neno hili lililotafsiriwa kuwa maovu hapa linamaana hasa ya uchokozi au ukali au mateso kama lilivyo kwenye yafsiri ya RSV.

 

Kuchagua kutomfuata na kumuasi Mungu kutampelekea Mungu kuchagua kututesa. Mateso haya yameorodheshwa kama kutangatanga kwa ajili ya makosa kwenye 2Wathesalonike 2:11.

2Wathesalonike 2:9-10 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo; 10 na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa.

 

Mtu wa kuasi anaweza kutokea tu kutoka kwa wateule kwa kuwa washirika wanaotangatanga na kudai kuwa ni mwili wa Kristo kwenye nyakati za mwisho hawatakuwa sehemu ya wateule. Hawataipenda kweli ili waokolewe. Watatumiwa nguvu ya upotevu na Mungu.

2Wathesalonike 2:11  Kwa hiyo Mungu awaletea nguvu ya upotevu, wauamini uongo;

 

Neno hili lililotafsiriwa nguvu ya upotevu kwa kweli imekwishaanza kufanya kazi yake ya kuwapotosha watu (energeian planes, soma kitabu cha Marshall's Interlinear). Walipewa nguvu za kimkakati za kutenda kazi ya kupotosha na Mungu kwa kuwa hawakuipenda kweli, ili wasiingie hukumuni, kwa kuwa hawakuokolewa.

 

Kama tunawafuata wanadamu na mapokeo yao kuliko kuipenda kweli, hatuaweza kuokolewa hakika. Haitakuwa wazi sana. 

 

Makanisa kwenye vuguvugu la kipindi cha karne ya ishirini yaliyazifanya dini kama biashara na kuyafanya mafundisho kuwa ni kama kitu cha kuwavutia tu wateja. Hii kwa kweli ilikuwa ni mtindo lilioufanya kanisa la Rumi kwenye kipindi chake cha karne ya nne na Ukristo uliharibiwa kwa sababu ya mtindo huu, kama ulivyo mfumo wa imani kongwe za kale.

 

Mkakati huu wa udanganyifu au mbinu za kiulaghai, unapelekea kuwepo kwa ongezeko la aina ya malumbano kwenye kitabu cha ufafanuzi maarufu kama kitabu cha ufafanuzi wa Biblia cha G.L. Haydock, [yaani the G.L. Haydock, to the Douay-Rheims Bible (1850 reprint of the 1819 version)], kuhusu Yohana 17:3.

Aya ya 3. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. [Kwa maneno haya Waariani wamejifanya kuamini kuwa Baba peke yake ndiye Mungu wa Pekee na wa Kweli]. S Aug. and diverse others answer, that the sense and construction is, Wakujue wewe, na pia Yesu Kristo Mwanao ili awe Mungu wa Pekee na wa Kweli We may also expound them with S. Chrys. and others, so that the Father is here called the only true God, not to exclude the Son, and the Holy Ghost, who are the same one true God with the Father; but only to exclude the false God's of the Gentiles. Let the Socinians take notice that (1John v, 20), the Son of God, Christ Jesus, is expressly called the true God, even with the Greek article, upon which they commonly lay so much stress.

 

Marfa tu tunapofika kwenye uharibifu wa hii kweli, ndipo tutaamili kila kitu. Kumbuka pia matumizi mabaya ya lebo bandia, kama vile ya  Arian, kutafuta ku-obviate au kukataa uhalali wa imani ya Uyunitariani iliyo kwenye Biblia. Hakuna uwezekano kwamba Mungu wa Pekee na wa Kweli aliyetajwa kwene Yohana 17:3 au 1Yohana 5:20 haimtaja Yesu Kristo kabisa wala kumaanisha yeye, ndani ay nje ya kifungu hiki. Ukweli wa kwamba tafsiri wa toleo la Douay-Rheims ni tafsiri ya Kiyunani ya Vulgate na kwa hiyo makala imetoholewa kutoka kwenye lugha ya Kilatini haikutajwa. Neno na makala havimtaji wala kumaanisha Kristo, bali zaidi tu ni kwa Mungu wa Pekee na wa Kweli ambaye Mwana wake ni Kristo. Ni muhimu kwa waamini Utatu kusalia kwenye udanganyifu kama huu ili kurekebisha nafasi yao machoni pa maandiko. hili si jambo jipya.

 

1Yohana 5:20 Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele.

 

Yeye aliye wa kweli ni yeye Mungu wa Pekee na wa Kweli. Tunamjua nasi tu ndani yake, yeye aliye wa kweli na katika Mwanawe Yesu Kristo.

 

Enyi watoto wadogo, hebu jiepusheni na kujilinda na ibada za sanamu; zile za wanadamu na za mapepo na acheni uwongo na udanganyifu wa imani hizi potofu za kikalti. Tikeni kati yake, enyi watu wangu (Ufunuo 18:4)

Ufunuo 18:4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.

 

Huyu mwanamke kahaba aliyetajwa na kufananishwa kama Babeli Mkuu, Mama wa Makahaba na Machukizo ya Nchi ni kiongozi wa imani na mfumo wa dini hii potofu ya ulimwenguni. Utaratibu na mfumo huu umekuwa ukijulikana kuwa msingi wake ni kwenye dini potofu ya uwongo ya mungu wa Utatu kwa kipindi cha karibu zaidi ya miaka elfu mbili. Kwa kipindi chote hiki wateule hawajawahi kuikubalia wala kushirikanaina dini hii. Wito uliotolewa ni wa kutoka ndani yake ili kwamba wateule wasishiriki mapigo na maafa yake makubwa ambayo yatamiminwa juu ya waamini Utatu na dini yao potofu katika siku za mwisho – mabinti makahaba wa huyu mwanamke kahaba ni wale waliojiengua katika kipindi kilichojulikana kama cha Wanamatengenezo. Watumishi hawa hawa walianza kwa kufundisha kinyume na imani na mfumo huu hapo mwanzoni. Ila sasa wanafundisha mafundisho haya Utatu na kusisitiza kuhusu fedha na mali; hawapo miongoni mwetu sisi. Hebu na tuwahubirie na kutoka kwenye mifumo na imani yao.

q