Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[245]

 

 

 

 

Marejesho ya Yosia

(Toleo La 2.0 19980422-20081122)

 

Marejesho yaliyofanywa chini ya uongozi wa Mfalme Yosia yana idadi kadhaa ya mafundisho yanye maana ambayo ni muhimu kwetu katika kuuelewa Ukristo wetu leo.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hati Miliki © 1998, 2008  Wade Cox)

(tr. 2014)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya::
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 

 

 

 

Marejesho ya Yosia


 

Kwenye jarida la Utakasaji wa Hekalu tumeelezea kwa kina kuhusu mchakato wa Utakaso na Marejesho yaliyofanywa kwa kipindi cha idadi kadhaa ya watawala. Jarida lile pia limetathmini na kuelezea umuhimu wa kufanya marejesho kwa viumbe kwa kuanzia siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na matendo au matukio ya haraka ya Mungu kwenye mchakato huu. Tangu kipindi kilichoko katikati ya Hezekia na marejesho ya Ezra kulikuwa na marejesho yaliyofanywa na Yosia ambayo yalikuwa ya mwisho kuwahi kufanyika kwenye Hekalu la Sulemani.

 

Ndani ya miongo michache baada ya marejesho ya Hezekia, taifa likakumbwa na ukengeufu mkubwa uliotokea kipindi cha utawala wa Waashuru. Waashuru walionywa kupitia nabii Yona na Ninawi ulisamehewa na kuachwa kutokana na toba waliyoionyesha. Hata hivyo walirudi nyuma na kuiadhimisha Easter na kushamirisha Dini ya kuliabudu Jua ambapo Israeli na Yuda waliwaiga na kuwafuata. Israeli wengi walitekwa na kuchukuliwa utumwani na hawa Waashuru.

 

Yeroboamu alikuwa ndiye mfalme wa Israeli aliyejikita sana kwenye mimani hizi kiasi cha kuanzisha na kufadhili ibada zilizoathiri utaratibu na imani ya Mungu lakini alianzisha imani hii ndani ya ibada za kuaudu Ndama wa Dhahabu ambayo ilikuwa ni sehemu ya dini ya Wababeloni wa kale waliokuwa wanaabudu mungu Mwezi aliyejulikana kwa jina la Sin (sawa na ilivyoandikwa kwenye jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222) [The Golden Calf (No. 222)].

 

Pia aliweka sikukuu mwezi wa nane kama tulivyoona kwenye jarida la Yeroboam na Kalenda ya Hilleli (Na. 191) (sawa na lisemavyo jarida la Goligotha, Mahali pa Fuvu la Kichwa (Na. 217) [Golgotha: the Place of the Skull (No. 217)].

1Wafalme 12:32-33 Yeroboamu akaamuru kushika sikukuu katika mwezi wa nane, siku ya kumi na tano ya mwezi, mfano wa sikukuu iliyokuwa katika Yuda, akapanda juu ili kuiendea madhabahu. Akafanya vivyo katika Betheli akiwatolea dhabihu wale ng'ombe aliowafanya; akawaweka katika Betheli wale makuhani wa mahali pa juu alipokuwa amepafanya. 33 Akatoa dhabihu juu ya ile madhabahu aliyoifanya katika Betheli, siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouwaza moyoni mwake mwenyewe; akawaamuru wana wa Israeli waishike sikukuu hiyo, akapanda kuiendea madhabahu, ili kufukiza uvumba.

 

Wakati wa kipindi hiki cha ukengeufu na ufumo au imani hii ya dini ya uwongo iliyoanzishwa na Yeroboamu, Mungu alimuinua na kumpeleka nabii akawaonye ukengeufu huu. Mungu hafanyi jambo lolote katika kuwahukumu watu pasipo kuwaonya kwanza watu wake kwa kupitia watumishi wake manabii, kabla hajaamua kuchukua hatua.

1Wafalme 13:1-6  Na tazama, akatoka mtu wa Mungu katika Yuda kwa neno la Bwana, akafika Betheli. Naye Yeroboamu alikuwa akisimama penye madhabahu, afukize uvumba. 2 Basi mtu huyo akapiga kelele juu ya madhabahu, kwa neno la Bwana akasema, Ee madhabahu, madhabahu, Bwana asema hivi, Angalia, mtoto atazaliwa katika nyumba ya Daudi, jina lake Yosia; na juu yako atawachinja makuhani wa mahali pa juu, wanaofukiza uvumba juu yako, na mifupa ya watu itateketezwa juu yako. 3 Akatoa ishara siku ile ile, akasema, Hii ndiyo ishara aliyoinena Bwana, Tazama, madhabahu itapasuka, na majivu yaliyo juu yake yatamwagika. 4 Ikawa, mfalme Yeroboamu alipoyasikia maneno ya yule mtu wa Mungu, alipopiga kelele juu ya madhabahu huko Betheli, alinyosha mkono wake pale madhabahuni, akasema, Mkamateni. Basi ule mkono wake aliounyosha ukakatika, wala hakuweza kuurudisha kwake tena. 5 Madhabahu ikapasuka, majivu ya madhabahuni yakamwagika, sawasawa na ishara aliyoitoa mtu wa Mungu kwa neno la Bwana. 6 Mfalme akajibu, akamwambia yule mtu wa Mungu, Umsihi sasa Bwana, Mungu wako, ukaniombee, ili nirudishiwe mkono wangu tena. Yule mtu wa Mungu akamwomba Bwana mkono wa mfalme ukarudishwa tena, ukawa kama ulivyokuwa kwanza

 

Na ndivyo vivyohivyo, hata hawa manabii wenyewe inawapasa kufuata maelekezo ya Mungu bila ya kuyaacha na kwenda mkono wa kushoto wala wa kuume wa kile walichambiwa na kutakiwa kukifanya. Nabii huyu aliambiwa wazi kabisa kile akachokifanya kuhusu jambo hili kama tunavyojionea kutoka kwenye aya ya 9.

1Wafalme 13:7-10 Mfalme akamwambia mtu wa Mungu, Karibu nyumbani kwangu ujiburudishe, nami nitakupa thawabu. 8 Mtu wa Mungu akamwambia mfalme, Ujaponipa nusu ya nyumba yako, sitaingia pamoja nawe, wala sitakula chakula, wala sitakunywa maji mahali hapa; 9 maana ndivyo nilivyoagizwa kwa neno la Bwana, kusema, Usile chakula cho chote wala usinywe maji, wala usirudi kwa njia ile uliyoijia. 10 Basi akaenda zake kwa njia nyingine, wala hakurudi kwa njia ile aliyoijia Betheli.

 

Wakati nabii anapokuwa na ujumbe kutoka kwa Mungu anatakiwa kutii hata kama nabii mwingine akimwambia kuwa ana maelekezo mengine aliyoyapokea amayo yapo kinyume na na yale aliyoyapokea kwa Bwana. Kwenye tukio hili, tunaona kwamba nabii aliponzwa na mmoja wa manabii wenzake.

1Wafalme 13:13-32 Akawaambia wanawe, Nitandikieni punda. Wakamtandikia punda, naye akampanda. 14 Akamfuata mtu wa Mungu, akamkuta ameketi chini ya mwaloni, akamwambia, Je! Wewe ndiwe yule mtu wa Mungu aliyetoka katika Yuda? Akamwambia, Mimi ndiye. 15 Akamwambia, Karibu kwangu nyumbani, ule chakula.16 Naye akamwambia, Siwezi kurudi pamoja nawe, wala kuingia pamoja nawe; wala sili chakula wala sinywi maji pamoja nawe hapa; 17 kwani nimeambiwa kwa neno la Bwana, Usile chakula wala usinywe maji huko, wala usirudi kwa njia ile uliyoijia. 18 Akamwambia, Mimi nami ni nabii kama wewe, na malaika akaniambia kwa neno la Bwana, kusema, Mrudishe pamoja nawe nyumbani kwako, ale chakula, akanywe maji. Lakini alisema uongo. 19 Basi mtu yule akarudi pamoja naye, akala chakula, akanywa maji nyumbani mwake. 20 Hata ikawa, walipokuwa wameketi mezani, neno la Bwana likamjia nabii yule aliyemrudisha; 21 akamlilia yule mtu wa Mungu aliyetoka katika Yuda, akinena, Bwana asema hivi, Kwa sababu umeiasi kauli ya Bwana, wala hukuishika amri ile aliyokuamuru Bwana, Mungu wako, 22 bali umerudi, ukala chakula ukanywa maji, hapo alipokuambia, Usile chakula, wala usinywe maji; maiti yako haitaliingia kaburi la baba zako. 23 Basi ikawa, alipokwisha kula chakula na kunywa maji, yule nabii aliyemrudisha akamtandikia punda. 24 Na alipokuwa amekwenda zake, simba alimkuta njiani, akamwua. Maiti yake ikatupwa njiani, na yule punda akasimama karibu naye; na yule simba naye akasimama karibu na maiti. 25 Na tazama, watu wakapita, wakauona mzoga umetupwa njiani, na yule simba akisimama karibu na mzoga, wakaenda, wakatoa habari katika mji ule alimokaa yule nabii mzee. 26 Na yule nabii aliyemrudisha njiani alipopata habari, akasema; Ndiye yule mtu wa Mungu, aliyeiasi kauli ya Bwana; kwa hiyo Bwana amempambanisha na simba, simba akamrarua, akamwua, sawasawa na neno la Bwana alilomwambia. 27 Akawaambia wanawe, akasema, Nitandikieni punda. Wakamtandikia. 28 Akaenda, akamwona yule maiti ametupwa njiani, na punda na simba wamesimama karibu na maiti; yule simba alikuwa hakumla maiti, wala hakumrarua punda. 29 Nabii yule akamtwaa maiti wa yule mtu wa Mungu, akamweka juu ya punda wake, akamrudisha; yule nabii mzee akaenda mjini mwake, kukaa matanga, na kumzika. 30 Akamweka maiti katika kaburi lake mwenyewe; wakamlilia, wakisema, Aa! Ndugu yangu! 31 Hata ikawa, alipokwisha kumzika, akawaambia wanawe, akasema, Nikifa mimi, nizikeni katika kaburi hili alimozikwa yule mtu wa Mungu; iwekeni mifupa yangu kando ya mifupa yake. 32 Kwa maana neno hilo alilolia juu ya madhabahu katika Betheli, kwa neno la Bwana, na juu ya nyumba zote za mahali pa juu zilizo katika miji ya Samaria, hakika litatimizwa.

 

Nabii huyu wa Israeli alikuwa anamjaribu nabii kutoka Yuda ili ajue kama kile alichokuja kukisema kilikuwa kweli. Ukweli ni kwamba alisema uwongo na ilimgharimu kupoteza uhai wa huyu nabii mgeni na kilichomsababisha kufanya hivyo ilikuwa ni kutafuta uhakika wa ujumbe wake. Hata hivyo, ilikuwa ni kweli na majesho yalifanyika vizuri sana na Yosia ambaye alitajwa na kuchaguliwa na Mungu na kuahidiwa kama mtoto atakaye tawala na kuwarejesha Israeli kutoka Nyumba ya Daudi.

 

Baada ya mwinsho wa kipindi hiki cha kutisha kwa ibada za sanamu kwa pande zote mbili, yaani Israeli na Yuda, mfalme wa Yuda alikuwa Manase na huyu sio tu kuw3a aliwaongoza na kuwapelekesha Yuda kuabudu sanamu, bali alimwaga sana damu ya wasio na hatia na kuijaza Yerusalemu kwa damu kutoka mmoja hadi mwingine (2Wafalme 21:16). Alikufa na Amoni mtoto wake akatawala mahala pake na alifanya hayohayo.

2Wafalme 21:19-26 Amoni alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala; akatawala miaka miwili huko Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Meshulemethi, binti Haruzi wa Yotba. 20 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, kama Manase babaye alivyofanya. 21 Akaiendea njia yote aliyoiendea baba yake, akazitumikia sanamu alizozitumikia baba yake, akaziabudu. 22 Akamwacha Bwana, Mungu wa babaze, wala hakuiendea njia ya Bwana. 23 Nao watumishi wa Amoni wakafanya fitina juu yake, wakamwua mfalme ndani ya nyumba yake mwenyewe. 24 Lakini watu wa nchi wakawaua wote waliofanya fitina juu yake mfalme Amoni, watu wa nchi wakamfanya Yosia mwanawe awe mfalme mahali pake. 25 Basi mambo yote ya Amoni yaliyosalia, aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda? 26 Akazikwa kaburini mwake katika bustani ya Uza. Na Yosia mwanawe akatawala mahali pake.

 

Jina Amoni linaloonekana hapa (linamaana ya  fundi au mtu aliyeandaliwa kwa kufundishwa ufundi wa kazi za mokono) aliuawa na watumishi wake. Watu walioonekana wanependekezwa kumrithi Amoni kutoka kwenye mnyororo wa uzao wake, hatimaye waliwaua wale mtumishi.

 

Kwa hiyo, hapa unabii unaanzia. Mtoto anaketishwa kwenye kiti cha enzi na Mungu na hatimaye anaanza kufanya kazi naye.

2Wafalme 22:1-2 Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala; akatawala miaka thelathini na mmoja katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Yedida, binti Adaya wa Bozkathi. 2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, akaenda katika njia yote ya Daudi baba yake, wala hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.

 

Mfalme aliwekwa kwa namna iliyo kwenye mpango wa Mungu kutoka kipindi cha ujana wake na wala hakukengeuka wala kupotoka. Aliandaliwa ili atumike kwa namna hii na wakati ulionyesha njia ya namna atakavyoifanya kazi hii.

 

Katika mwaka huu wa kumi na nane wa kutawala kwake, alitumiwa na Mungu akiwa na umri wa kiujana wa miaka ishirini na tano, ukiwa ni mwaka muafaka kwake kuwekwa kwenye huduma ya hekaluni kama alivyofanya Hezekia kipindi cha matengenezo yake (sawa na jarida la Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. [Sanctification of the Temple of God (No. 241)].

 

Kwa hiyo Yosia alitumika tangu alipokuwa na umri wa miaka 25, katika mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake. Mungu alimtumia kwa njia hii:

2Wafalme 22:3-13 Ikawa, katika mwaka wa kumi na nane wa mfalme Yosia, mfalme akamtuma Shafani, mwana wa Azalia, mwana wa Meshulamu, mwandishi, nyumbani kwa Bwana, akisema, 4 Enenda kwa Hilkia, kuhani mkuu, ili aihesabu fedha yote inayoletwa nyumbani mwa Bwana, ambayo mabawabu wameipokea kwa watu; 5 tena waitie ile fedha katika mikono ya wafanya kazi wanaoisimamia nyumba ya Bwana; wakapewe wafanya kazi waliomo ndani ya nyumba ya Bwana, ili wapate kupatengeneza mahali palipobomoka ndani ya nyumba; 6 wapewe maseremala, na wajenzi, na waashi; ili kununua miti na mawe yaliyochongwa wapate kuitengeneza nyumba. 7 Lakini hawakuulizwa habari za ile fedha waliyokabidhiwa; maana walitenda kazi kwa uaminifu. 8 Naye Hilkia, kuhani mkuu, akamwambia Shafani, mwandishi, Nimekiona kitabu cha torati katika nyumba ya Bwana. Hilkia akampa Shafani kile kitabu, naye akakisoma. 9 Shafani mwandishi akamwendea mfalme, akamletea mfalme habari tena, akasema, Watumishi wako wamezitoa zile fedha zilizoonekana ndani ya nyumba, nao wamewakabidhi wafanya kazi wanaoisimamia nyumba ya Bwana. 10 Kisha Shafani mwandishi akamwambia mfalme, akasema, Hilkia kuhani amenipa kitabu. Shafani akakisoma mbele ya mfalme. 11 Ikawa, mfalme alipokwisha kuyasikia maneno ya kitabu hicho cha torati, alirarua nguo zake. 12 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani, na Ahikamu, mwana wa Shafani, na Akbori, mwana wa Mikaya, na Shafani mwandishi, na Asaya, mtumishi wa mfalme akasema, 13 Enendeni, mkamwulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa ajili ya watu hawa, na kwa ajili ya Yuda yote, katika habari za maneno ya kitabu hiki kilichoonekana; kwa kuwa hasira ya Bwana ni kubwa aliyotukasirikia, kwa sababu baba zetu hawakuyaangalia maneno ya kitabu hiki, kufanya kama hayo yote tuliyoandikiwa.

 

Mungu aliweka moyoni mwa Yosia ni na moyo wa kimtii. Wakati Yosia alipoona kwamba Yuda walikuwa hawazitii Sheria za Mungu, aliweza kuchukua hatua kuishughulikia hali na taarifa ile aliyoipata na kutubu na kufanya mabadiliko muhimu yanayohitajika kurejea kwa Mungu na kwenye Torati yake.

 

Alijua kwamba kama hawataonyesha toba Mungu angewaangamiza. Kwa kupitia kwa washauri wake, ndipo walitafuta ushauri kutoka kwa manabii.

2Wafalme 22:14-20 Basi Hilkia kuhani, na Ahikamu, na Akbori, na Shafani, na Asaya, wakamwendea Hulda, nabii mke, mkewe Shalumu, mwana wa Tikva, mwana wa Harhasi, mtunza mavazi ya mfalme; (naye alikaa Yerusalemu katika mtaa wa pili;) wakasema naye. 15 Akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi; Mwambieni mtu yule aliyewatuma ninyi kwangu, 16 Bwana asema hivi, Tazama, mimi nitaleta uovu juu ya mahali hapa, na juu yao wakaao hapa, naam, maneno yote ya kitabu alichokisoma mfalme wa Yuda; 17 kwa sababu wameniacha mimi, wameifukizia uvumba miungu mingine, ili wapate kunikasirisha kwa kazi yote ya mikono yao; kwa hiyo hasira yangu itawaka juu ya mahali hapa, isizimike. 18 Lakini yule mfalme wa Yuda, aliyewatuma ninyi kumwuliza Bwana, mtamwambia hivi, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Kwa habari ya maneno yale uliyoyasikia, 19 kwa kuwa moyo wako ulikuwa mwororo, nawe ukajinyenyekesha mbele za Bwana, hapo ulipoyasikia maneno niliyoyanena juu ya mahali hapa, na juu ya wenyeji wake, ya kwamba watakuwa ukiwa na laana, nawe ulizirarua nguo zako, ukalia mbele zangu; basi, mimi nami nimekusikia wewe, asema Bwana. 20 Kwa hiyo tazama, nitakukusanya pamoja na baba zako, nawe utawekwa kaburini mwako kwa amani; wala macho yako hayatauona uovu huo wote nitakaouleta juu ya mahali hapa. Basi wakamletea mfalme habari tena.

Kwa toba ya wazi ya viongozi uovu ulikuwa umezuiwa kwa mtazamo unaoonekana. Kwa hiyo Yosia alichukua hatua kwa imani kwa maneno ya manabii na Torati ya Mungu.

 

Kutokana na sura ya 23 tunaona kiusahihi sana kwamba kunajisika kwa Israeli kulikuwepo. Ilikuwa ni imani ya kuabudu jua ya Wababelonia na Wamisri, kama tunavyojionea kutoka pale Sinai kama walivyoonekana kama Ndama wa Dhahabu (soma jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222) [The Golden Calf (No. 222)]. Imani hii bado inaendelea karika Israeli na kwa watu wetu na itasababisha maangamizo yetu (sawa na jarida la Chimbuko la Krismas na Uaster (Na. 235) [The Origins of Christmas and Easter (No. 235)].

 

Tunaona ia kutoka kwenye maandiko kwamba kipindi hiki kilikuwa ni kile cha kuelekea kwenye maadhimisho ya Pasaka lakini hii haikuwa ni Pasaka ya kawaida. Jina Yosia kwa kweli linaandika na kutamkwa Yo’shiYah (SHD 2977) maana yake ni Aliyeanzisha na Yah au Zawadi au Kipawa cha Yah au linatokana na shina la neno asa, maana yake ni uponyaji wa Yah. Unabii huu ulifanywa ili tuweze kuona kwamba marejesho haya yalianzishwa au yalifanywa na Yah. Kama jina la Yah lilivyo la umoja linalotokana na jina Yahova linalotumika kwa matumizi ya uwingi.

 

Kutokana na marejesho haya Hekalu pia lilisafishwa au kutakasika kutoka kwenye machukizo na machafu yake.

2Wafalme 23:1-20 Kisha, mfalme akatuma wajumbe, nao wakamkusanyia wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu. 2 Mfalme akapanda kwenda nyumbani kwa Bwana, na watu wote wa Yuda, nao wote waliokaa Yerusalemu, pamoja naye, na makuhani, na manabii, na watu wote, wadogo kwa wakubwa; akasoma masikioni mwao maneno yote ya kitabu cha agano kilichoonekana katika nyumba ya Bwana. 3 Mfalme akasimama karibu na nguzo, akafanya agano mbele za Bwana, kumfuata Bwana, na kuyashika maagizo yake, na shuhuda zake, na amri zake, kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, na kuyathibitisha maneno ya agano hilo yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakalikubali agano lile. 4 Kisha, mfalme akamwamuru Hilkia, kuhani mkuu, na makuhani wa daraja ya pili, na walinzi wa mlango, kwamba watoe katika hekalu la Bwana vyombo vyote vilivyofanywa kwa ajili ya Baali, na kwa ajili ya Ashera, na kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni; akavipiga moto nje ya Yerusalemu, katika mashamba ya Ridroni, akayachukua majivu yake mpaka Betheli. 5 Akawaondosha wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali, pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni. 6 Naye akaiondoa Ashera katika nyumba ya Bwana, nje ya Yerusalemu, mpaka Kidroni, akaipiga moto penye kijito cha Kidroni, na kuiponda-ponda iwe mavumbi, akayatupa mavumbi yake juu ya makaburi ya watu. 7 Akaziangusha nyumba za mahanithi, waliokuwamo nyumbani mwa Bwana, wanawake walipofuma mapazia ya Ashera. 8 Akawatoa makuhani wote katika miji ya Yuda, akapanajisi mahali pa juu, makuhani walipokuwa wamefukiza uvumba, tangu Geba hata Beer-sheba; akapavunja mahali pa juu pa malango, palipokuwapo penye kuingia lango la Yoshua, liwali wa mji, palipokuwa upande wa kushoto wa mtu langoni pa mji. 9 Walakini hao makuhani wa mahali pa juu hawakupanda madhabahuni kwa Bwana katika Yerusalemu, bali wakala mikate isiyo na chachu katikati ya ndugu zao. 10 Naye akainajisi Tofethi, iliyomo katika bonde la wana wa Hinomu, ili mtu asipitishe mwana wake au binti yake motoni kwa Moleki. 11 Akawaondoa farasi ambao wafalme wa Yuda waliwatoa kwa jua, hapo pa kuingia nyumbani mwa Bwana, karibu na chumba cha Nathan-Meleki, towashi, kilichohuwako kiungani; akayapiga moto magari ya jua. 12 Nazo madhabahu zilizokuwako darini juu ya chumba cha juu cha Ahazi, wafalme wa Yuda walizozifanya, nazo madhabahu alizozifanya Manase katika behewa mbili za nyumba ya Bwana, mfalme akazivunja, akazitelemsha huko nje, na kuyatupa mavumbi yake katika kijito cha Kidroni. 13 Na mahali pa juu palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa uharibifu, alipopajenga Sulemani, mfalme wa Israeli, kwa Ashtorethi, chukizo la Wasidoni, na Kemoshi, chukizo la Moabu, na Milkomu, chukizo la wana wa Amoni, mfalme akapanajisi. 14 Akazivunja-vunja nguzo, akayakata-kata maashera, akapajaza mahali pake mifupa ya watu. 15 Tena zaidi ya hayo, ile madhabahu iliyokuwako Betheli, na mahali pa juu alipopafanya Yeroboamu, mwana wa Nebati, aliyewakosesha Israeli, madhabahu hiyo aliibomoa; na mahali pa juu alipateketeza, akapaponda-ponda hata pakawa mavumbi, akaiteketeza ile Ashera.

 

Utaratibu wote wa kuabudu Baali na Ashtorethi unaoendana ma ibada za Easter na imani ya kumuabudu Venus ajulikanaye pia kama Nyota ya Alfajiri na Mungu Mwezi aliyeitwa Sin au Molkom na Kemoshi na kuabudu Dume la Ng’ombe  aliyechinjwa na dini ya kuabudu jua; imani tunazoziona wazi kuwa zilikuwepo kwa Waaryani na hata siku hizi bado zinaendelea huko Ulaya kwenye vizazi vyao. Kilichofuatia kutoka kwenye imani au dini hii ilikuwa ni dini au ibada zilizofanywa kwa matendo ya uasherati na matendo ya ufiraji ambayo yaliletwa na kufanyika hata kwenye hekalu hili la Mungu. Gari la farasi la Apollo na Sanamu lake lililokutikana pande za kaskazini na huko Ulaya zilikuwa hapa Sayuni na Hekaluni.

 

Dini au imani yote ya Waashuru/Wababeloni tunayoiona sasa kushamiri huko Ulaya iliendelezwa miongoni mwao na walizidisha umuhimu au kuwazidishia mziho Waashuru. Ilikuwa imevutia kiasi kwamba watu hawakugundua kwamba imani yao ilikuwa ni harufu ichukizayo kwenye mianzi ya pua ya Mungu. Wamekuwa wakiabudu kwa namna hiyo kwa kipindi cha karne kadhaa za vipindi vtote viwili, yaani cha kabla ya baada ya matengenezo ya Hezekia. Hawakujua au hawakupenda kujua kwamba walikuwa ni waabudu sanamu na kwamba walikuwa kwenye hatari ya uharibifu au kuangamizwa. Na hii ndiyo hasa imani iliyoko leo. Makasisi wanajua na hawapendi kusema ukweli na watu wanaangamia kwa kukosa maono. Kwa ajili hii ndipo Yosia aliona umuhimu wa kufanya matengenezo. Mungu alimtumia alipofikia kipindi cha umri muafaka kwa mujibu wa torati kama alivyomtumia Hezekla hapo nyuma kabla yake.

 

Ni wazi sana pia kwamba Mungu alisaidia imani ya Yosia na kuwadhoofisha Waashuru wasiweze kuimiliki Yuda kwa kadiri alivyoenenda katika kweli na kuishika Torati ya Mungu.

 

16 Naye Yosia alipogeuka, aliyaona makaburi yale yaliyokuwako huko, juu ya mlima; akatuma watu, akaitoa ile mifupa katika yale makaburi, akaiteketeza juu ya madhabahu, akainajisi, sawasawa na lile neno la Bwana, alilolinena yule mtu wa Mungu, aliyetamka mambo hayo. 17 Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu, aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya Betheli. 18 Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule nabii aliyetoka Samaria. 19 Na nyumba zote pia za mahali pa juu palipokuwa katika miji ya Samaria, wafalme wa Israeli walizozifanya, ili kumkasirisha Bwana, Yosia aliziondoa, akazitenda kwa mfano wa mambo yote aliyoyatenda katika Betheli. 20 Akawaua na makuhani wote wa mahali pa juu waliokuwako huko, juu ya madhabahu, akateketeza mifupa ya watu juu yake; kisha akarejea Yerusalemu.

 

Yosia alifanya kile alichoamriwa na Mungu kukifanya kuhusu Makuhani hawa wanaopendezwa na matendo ya Kisodoma. Aliwauilia mbali. Unabii ulitimilika na ilijulikana kwamba ni mwendelezo kutoka kipindi ambacho ilifanvika hivyo kilikamilika.

 

Kipindi cha marejesho

Kipindi cha marejesho kina maana sana. Yosia alitawala katika Yuda tangu mwaka 640-609 KK.

 

Yosia alianza kumtafuta Mungu wa Baba yake Daudi kuanzia mwaka wa nane wa utawala wake (yapata takriban mwaka 632 KK kama inavyosema 2Nyakati 34:3a). Mungu aliwapa thawabu kwa imani yao kwa kuwadhoofisha Waashuru wasiyamiliki majimbo ya pande za Kusini na Magharibi (sawa na kamusi inayoitwa Interpreters Dictionary of the Bible, art, “Josiah”, vol. 2, p. 997). Hii iliimarisha uwezo wake na nguvu iliyoendelea hadi mwaka 628.

 

Katika mwaka wa ishirini wa kutawala kwake (yapata mwaka 628 KK), (sawa na pale alipofikia umri wa utu uzima wa miaka ishirini), alianza kuwatakasa Yuda na Yerusalemu (2Nyakati 34:3b-5).

2Nyakati 34:3-5 Kwa kuwa katika mwaka wa nane wa kutawala kwake, naye akali mchanga, alianza kumtafuta Mungu wa Daudi babaye; hata katika mwaka wa kumi na mbili akaanza kusafisha Yuda na Yerusalemu kwa kuondoa mahali pa juu, na kwa kuondoa maashera, na sanamu za kuchora, nazo za kusubu. 4 Wakazibomoa madhabahu za mabaali machoni pake; na sanamu za jua, zilizoinuliwa juu yake, akazikata-kata; na maashera, na sanamu za kuchonga, nazo za kusubu, akazivunja-vunja, akaziponda kuwa mavumbi, akayamimina juu ya makaburi ya hao waliozichinjia dhabihu. 5 Akaiteketeza mifupa ya makuhani madhabahuni mwao, akasafisha Yuda na Yerusalemu.

 

Baada yah ii ndipo alieneza juhudi zake kwenye maeneo ya masalio ya Manase, Efraimu na hata kwa Wanaftali.

2Nyakati 34:6-7 Na katika miji ya Manase, na Efraimu, na Simeoni, mpaka Naftali, akafanya vile vile; na katika maganjo yake pande zote. 7 Akazibomoa madhabahu, akaponda-ponda maashera na sanamu kuwa mavumbi, akazikata-kata sanamu zote za jua katika nchi yote ya Israeli, kisha akarejea Yerusalemu.

 

Kwa kuonekana Kitabu cha Torati hekaluni, katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake (mwaka 622) alifanya matengenezo makubwa ya kidini ambayo yalikuwa na dalili za mamlaka ya utawala wa nchi pia (2Nyakati 34:8-35:19; sawa na kamusi ya Interp. Dict., ibid.).

 

Habari iliyoko kwenye vitabu vya Nyakati inasema kwamba Manase ameziondoa sanamu na alama zote za ibada za Waashuru na inaeleza tu kuwa ni Wakanaani ndio walioondolewa na Yosia nah ii inaonekana kuwa ndiyo yaliyomo kwenye 2Wafalme ambapo Yosia anasemekana kuwa aliwaondoa wengi. Jibu liko wazi kabisa.

 

Manase mwana wa Hezekia aliwaongoza kwene toba lakini hayakuwa marejesho na Amoni na maongozi yalichukua mkondo wake na ni kwa sababu hii ndiyo maana aliuawa (sawa na 2Nyakati 33:23).

 

Matukio yaliyo kwenye 2Wafalme haya0tangui mchakato wa matengenezo kama tunavyoona kwenye vitabu vya Nyakati. Inaonekana kwenye matukio mawili kutoka kwenye mwaka wa kumi na nane iliyotangulia kuelekea kwenye miji ya Samaria. Jibu hapa ni kwamba mchakato huu kwa kweli ulikuwa haujafanikiwa kabisa hadi katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake. Miji ya Samaria kwa kipindi hiki ilikuwa pia imekajiwa na Wacutheans na Wamedi ambao waliwekwa na Waashuru (tazama jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)] na utakaso huu haukuwa na nguvu sana hadi mwaka 622 KK.

 

Kulikuwa na matukio kadhaa yaliyohitaji kutimilizwa kwa muunganiko na marejesho na ni Mungu tu ndiye angeweza kulifanya hilo.

 

Mwanzo wa kudhoofika kwa nguvu za Waashuru ulikuwa ni kifo cha mfalme Assurbanipal ambayo inaweza kuaminika ilikuwa mwaka 630 KK (Interp. Dict., ibid.). kwa mujibu wa Vitabu Vya Historia ya Waashuru, Babeli ilifanya uasi dhidi ya Waashuru na wakamuweka Nabopolassa kwenye kiti cha enzi cha ufalme, ambaye alikuwa ni mtu wa Babeli, siku inayodhaniwa kufantika tukio hili ni Novemba 22/23 626 KK. Kwa kipindi cha takriban mwaka mmoja kumeandikwa kuwa “kulikuwa hakuna mfalme katika nchi” (ibid).

 

Kwa hiyo, kutokana na matendo yaliyomaanisha ya Yosia ndipo tunayaona matukio mbalibali yakitokea wakati Assurbanipal alipokufa, dola ya Ashuru ikizidi kudhoofika na kulikuwa hakuna mfalme katika nchi mwaka 627 KK. Katika mwaka huu Ashuru ilikuwa imekumbwa na matukio au mikasa kutoka Mashariki na Mungu kwa kweli alikuwa amewaondolea ushawishi wao kwa Yuda upande wa kusini magharibi akimuandaa Yosia kuanzisha mchakato wa ukombozi au kupata uhuru uliopelekea marejesho ya mwaka

622.

 

Mwaka wa Yubile ulikuwa ni ule wa 624 KK. Mchakato wa marejesho ulikuwa mrefu maandalizi yake. Marejesho ya Hezekia yanaweza pia kuwa ya muhimu kwenye maandalizi ya kukilinda Kitabu cha Torati na dira ya kuelekea kwene marejesho. Hii huenda ilikutikana kwenye matengenezo ya Hezekia  (mwaka 715-687 KK) yaliyofanywa na Hilkia. Inadhaniwa kuwa kuna baadhi ya watu walioandaliwa wakati wa utawala wa Manase, miaka hamsini iliyotangulia (Interp. Dict. ibid. p. 997). Kwa hiyo, mchakato wa marejesho ulikuwa sawa sawa. Hezekia alianza marejesho yake siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wa mwaka mtakatifu 715/14 wakati alipoanza pia kutawala. Marejesho haya yalianza mwaka wa tisa wa wa mzunguko wa Yubile iliyopita. Haikuwa na uhusiano na Yubile bali ilikuwa na umuhimu wake kwenye marejesho yalitofuatia yaliyochukua mahala pake miaka tisini na moja iliyofuatia.

 

Maswali makubwa pia hapa ni kwamba: Nabii Yeremia alikuwa wapi wakati huu wa marejesho? Ni kwa nini walikuwa wanamuuliza nabii mdogo wakati nabii mkuu sana wa Israeli kipindi kile alikuwa yu hai bado? Jibu halisi ni kwamba Yeremia hakuwepo. Hili ni jambo jingine. Alikuwa na hili tu kusema kuhusu Yosia alipokuwa ananena kuhusu Yosia alipokuwa anamwambia Yehoyakimu mwana wa Yosia, yafuatayo:

Yeremia 22:15-16 Je! Utatawala kwa sababu unashindana na watu kwa mierezi? Baba yako, je! Hakula na kunywa, na kufanya hukumu na haki? Hapo ndipo alipofanikiwa. 16 Alihukumu maneno ya maskini na mhitaji; hapo ndipo alipofanikiwa. Je! Huku siko kunijua, asema Bwana?

 

Nabii Sefania anaaminika pia kuwa alikuwepo nayeye pia hakuulizwa wala kuombwa ushauri.

 

 Ni kutokana na marejesho haya ya Yosia ndyo wanazuoni wa siku hizi wanadai kuwa ilikuwa ni kitabu cha Kumbukumbu la Torati na kazi ya wanazuoni na Waandishi wa Kitabu cha Torati kuwa viliandika kuanzia mwaka 560 KK (ibid., na sawa na jarida la Biblia (Na 164) [The Bible (No. 164)].

 

Sababu iliyoko nyuma ya mtazamo huu ni maelezo ya kina ya vitabu vya Nyakati dhidi ya maelezo yaliyo kwenye 2Wafalme. Kwa kweli, marejesho yaliyofanywa chini ya usimamizi wa Hezekia yalichukuliwa kutoka kanuni halisi ya Maandiko Matakatifu hata kwenye Mithali za Sulemani (sawa na Interp. Dict.ibid., art. “Hezekiah”, p. 598). Kazi ya Waandishi kwenye marejesho. Kulikuwa na mambo mawili muhimu kwenye matcngenezo yaliyotangulia Yubile iliyokuwa kipindi cha Yosia na marejesho ya kila mara kwenye mwaka wa kwanza wa Yubile mpya. Kwa marejesho haya kulikuwa na kiwango kikubwa cha harakati kuwepo kwa kipindi cha miaka mingi iliyokuwa kwenye Yubile zilizopita. Harakati hizi zenyewe zilifuatia kutoka na juhudi kubwa zilizofanywa kwenye Yubile iliyopita ya kipindi cha Hezekia na harakati au juhudi nyingine zilizofanywa na Manase kwenye kipindi chake cha kuwaongoza watu kwenye ukengeufu na kurudi nyumba kwa kuiacha imani ya kweli.

 

Tunachokiona hapa ni kwamba ukweli ni kwamba hakukuwa na Pasaka iliyochelewa na utakaso wa hekalu kwa kweli ulikuwa mkubwa kwa kiasi kikubwa sana. Kipindi cha mpito kilikuwa cha muhimu ili kujua kile kilichotokea.

 

Tangu mwaka 633/32 KK, mwaka mmoja kabla ya ule wa Sabato (ambao ungehusisha na usomaji wa torati ambayo haikuwa) na kupelekea kwenye mwaka wa kwanza wa mzunguko wa mwisho wa mtaratibu wa Yubile. Yosia alianza kumfuata Mungu na kurejesha imani. Hii ilihusisha kwanza kabisa, kulitiisha eneo ambalo kwa kweli halikuwa kipindi cha Hezekia, kwa kuwa Israeli walikuwa wamepelekwa mbali utumwani.

 

Yosia alifanya hivi hadi mwaka 628/27 KK, ambao ulikuwa ni mwaka wa arobaini wa mzunguko. Mnamo mwaka wa 627/26, ambao ndio ulikuwa mwaka wa hamsini wa mzunguko na wa mavuno makuu, aliisafisha nchi iliyokuwa na sanamu na kuzichoma moto na kuzisaga hadi zikawa mavumbi. Katika miaka ya 625 na 624 kulikuwa na mwaka wa Sabato na ni mwaka wa Yubile wa kuuadhimisha. Mwaka wa 623/22, mwaka wa kurejea wa Yubile mpya, alianza marejesho. Huenda hii ilianza baada ya kupigwa baragumu ya Yubile kwenye Siku ya Upatanisho ya mwaka 624. Huu ulikuwa ni mwaka wa kumi na nane wa utawala wake. Kamusi ya the Interpreters Dictionary (ibid., p. 997) inasema kwamba ulikuwa ni mwaka wa 622 ambao inawezekana kuwa ni kutoka mwanzoni mwa utawala wake katika mwaka mtakatifu wa 640/39 KK.

 

Marejesho yalikuwa na kishindo kikubwa sana kama tunavyoyaona kwenye hali ya utukufu wa hekalu. Mnamo siku ya 1 Nisan 623/2, ukiwa ni mwaka wa kwanza wa Yubile Mpya, aliwasafisha Israeli na kuwarejesha kwenye imani. Pasaka kwa mara nyingine tena ilikuwa imeanza Hekaluni na manabii wa uwongo na waabudu sanamu waliondolewa au kuuawa.

 

Sikukuu ya Pasaka imeonyesshwa kwenye 2Nyakati 35:1-19.

2Nyakati 35:1-19 Naye Yosia akamfanyia Bwana pasaka huko Yerusalemu; wakachinja pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. 2 Akawasimamisha makuhani katika malinzi yao, akawatia moyo kufanya utumishi wa nyumba ya Bwana. 3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Israeli wote, waliotakasika kwa Bwana, Wekeni sanduku takatifu katika nyumba aliyoijenga Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli; hamtakuwa tena na mzigo mabegani; sasa mtumikieni Bwana, Mungu wenu, na watu wake Israeli. 4 Mkajiweke tayari kwa kadiri ya nyumba za baba zenu, kwa zamu zenu, kama alivyoandika Daudi mfalme wa Israeli, na kama alivyoandika Sulemani mwanawe. 5 Mkasimame katika patakatifu, kama walivyogawanyika ndugu zenu, wana wa watu, kufuata nyumba za mababa, kadiri ya mgawanyiko wa kila nyumba ya baba, ya Walawi. 6 Mkachinje pasaka, mkajitakase, mkawatengenezee ndugu zenu, kutenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Musa. 7 Tena Yosia akawapa wana wa watu, matoleo ya makundi, wana-kondoo na wana-mbuzi, yote yawe kwa ajili ya matoleo ya pasaka, wote waliokuwako, wakipata thelathini elfu, na ng'ombe elfu tatu; hao walitoka katika mali za mfalme. 8 Na wakuu wake wakawapa watu, na makuhani na Walawi matoleo ya hiari. Hilkia na wana na Yehieli, wakubwa wa nyumba ya Mungu, wakawapa makuhani, kuwa matoleo ya pasaka, wana-kondoo elfu mbili na mia sita, na ng'ombe mia tatu. 9 Konania naye, na Shemaya, na Nethaneli, ndugu zake, na Hashabia, na Yeieli, na Yozabadi, wakuu wa Walawi, wakawapa Walawi, kuwa matoleo ya pasaka, wana-kondoo elfu tano, na ng'ombe mia tano. 10 Hivyo huduma ikatengenezwa, wakasimama makuhani mahali pao, na Walawi kwa zamu zao, kama alivyoamuru mfalme. 11 Wakachinja pasaka, nao makuhani wakamimina damu waliyopokea mikononi mwao, Walawi wakachuna. 12 Wakaziondoa sadaka za kuteketezwa, wawape wana wa watu, kama walivyogawanyika kufuata nyumba za mababa, ili wamtolee Bwana, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Musa. Nao ng'ombe wakawafanya vivyo hivyo. 13 Wakaioka moto pasaka kama ilivyo sheria; wakatokosa matoleo matakatifu vyunguni, na masufuriani, na makaangoni, wakawachukulia upesi wana wa watu wote. 14 Baadaye wakajiandalia wenyewe, na makuhani; kwa sababu makuhani, wana wa Haruni, walikuwa na kazi ya kutoa sadaka za kuteketezwa, na mafuta hata usiku; kwa hiyo Walawi wakajiandalia wenyewe, na makuhani, wana wa Haruni. 15 Nao waimbaji, wana wa Asafu wakasimama mahali pao, kama alivyoamuru Daudi, na Asafu, na Hemani, na Yeduthuni mwonaji wa mfalme; nao mabawabu walikuwa katika kila lango; hawakuhitaji kuondoka katika huduma yao, kwa kuwa ndugu zao Walawi wakawaandalia. 16 Basi huduma yote ya Bwana ikatengenezwa siku ile ile, kuifanya pasaka, na kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana, kama alivyoamuru mfalme Yosia. 17 Wana wa Israeli waliokuwapo wakafanya pasaka wakati ule, na sikukuu ya mikate isiyochachwa muda wa siku saba. 18 Wala haikufanyika pasaka kama ile katika Israeli tangu siku za nabii Samweli; wala wafalme wa Israeli hawakufanya hata mmoja wao pasaka kama ile Yosia aliyoifanya, pamoja na makuhani, na Walawi, na Yuda wote na Israeli waliokuwapo, na wenyeji wa Yerusalemu. 19 Katika mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake Yosia ikafanyika pasaka hiyo

 

Kuondoa kabisa hali ya kuabudu sanamu na kurudi nyuma au kumuacha Mungu ilikuwa karibu ishindikane kwa kuwa watu walikuwa walikuwa wamewekezwa ama kurithishwa ibada hizi za sanamu. Dini ya Israeli na Yuda ilikuwa imeathirika sana kwa kuwa ilikuwa imeunganishwa na ibada za waabudu Jua ya Waaryani kwa kipindi cha millennia baada ya kuanzishwa kwa Babeli na hata kabla kipindi kilichokubalika cha gharika kuu.

 

Mataifa ya Ulaya bado yamezingirwa kwenye imani hizi za ibada za sanamu na inaenea na kuelekea kwenye mapokeo ya Kiislamu na kwenye dini za Mashariki na za Kimarekani. Fundisho tunalojifunza kutokana na matengenezo ya Yosia ni umuhimu wa Kuinya dunia hii ya siku za mwisho na marejesho mapya yatakayofanyika kipindi cha Masihi.

 

Kuanguka kwa WaaAshuru

Mungu hakuwa mbali na marejsho haya. Waashuru walikuwa wamekwishaonywa na nabii Yona na walitubu kama Israeli walivyofanya kipindi cha Hezekia. Hata hivyo, hawakubakia kuishi maisha ya toba na walirejea kwene inani za dini yao ya uwongo na kuiingiza katika Israeli na Yuda baada ya wao kutumiwa na Mungu kuwaadibisha Israeli kwa ajili ya ukengeufu wao huu.

 

Ufalme wa Babeli ulianza kupata nguvu ya Waashuru na habari zilizo kwenye Vitabu vya Historian a Mambo ya Wababelonia zinatoa taswira ya ufalme ule tangu mwaka 626-623 KK. Mvinjiko ulifuatia kwenye habari zilizolandikwa kwenye mwaka 616 KK (Interp. Dict., ibid., p. 997).

 

Mnamo mwaka 614 Ashuru iliangushwa na Cyaxares mfalme wa Wamedi. Mji ulianguka hata kabla ya kuwasili kwa Nabopolassa lakini njama zilifanywa kati ya Wamedi na Wababelonia. Mwaka 612 Ninawi ulianguka mikononi mwa majeshi ya ushirika na Waashuru wakaondolewa na kusukumiwa huko Harani ambako Ashuruballit II alijaribu kuirejesha tena Dola ya Waashuru. Alilazimishwa kuondoka huko Harani mwaka 610 licha ya kushurutishwa na Wamisri. Wababeloni na Wamedi waliuteka mji na kuushikilia na kuulinda dhidi ya majeshi yenye nguvu ya Waashuru na Wamisri mwaka 609 KK.

 

Yosia alikumbwa na mauti kwenye vita ya Megido. Alijisikia msukumo kutoka ndani yake wa kwenda kupigana akijaribu kuwazuia Wamisri waliokuwa wanaongozwa na Farao Neko aliyekuwa amekusanya majeshi kwenda kupigana na Waashuru. Yosia huenda alikuwa anajaribu kuwasaidia Wababeloni aliyewaona kuwa ni wa washirika muhimu. Yosia, hata pamoja na nguvu hizi zote alizokuwa amepewa na Mungu, hakuweze kuyasikiliza maonyo aliyopewa na Mungu, hata kupitia kwene mdomo au kinywa cha Neko mwenyewe. Bali alitafuta jinsi ya kuingilia kati mapigano akienda kuwasaidia Wababeloni ambao walikuja kuwa maadui na watakaoiangamiza Yuda na imani yake ya kidini kama ilivyotabiriwa huko nyuma na na kama tuonavyo huko mbele na nabii Danieli (sawa na Danieli sura ya 2). Wamisri waliletwa na Mungu na aliwatumia ili kuandaa njia ya kulipeleka taifa utumwani.

2Nyakati 35:20-27 Baada ya hayo yote, alipokwisha Yosia kulitengeneza hekalu, Neko, mfalme wa Misri, akakwea ili kupigana Karkemishi karibu na Frati; naye Yosia akatoka juu yake. 21 Lakini yeye akatuma kwake wajumbe, kusema, Ni nini niliyo nayo mimi na wewe, Ee mfalme wa Yuda? Sikuja juu yako leo, lakini juu ya nyumba niliyo na vita nayo; naye Mungu ameniamuru nifanye haraka; acha basi kumpinga Mungu, aliye pamoja nami, asikuharibu. 22 Walakini Yosia hakukubali kumgeuzia uso mbali, akajibadilisha apate kupigana naye, asiyasikilize maneno ya Neko, yaliyotoka kinywani kwa Mungu, akaja kupigana bondeni mwa Megido. 23 Nao wapiga upinde wakampiga Yosia; naye mfalme akawaambia watumishi wake, Niondoeni; kwani nimejeruhiwa sana.24 Basi watumishi wake wakamtoa garini, wakamtia katika gari la pili alilokuwa nalo, wakamleta Yerusalemu; naye akafa, akazikwa makaburini mwa babaze. Wakamlilia Yosia Yuda wote na Yerusalemu. 25 Naye Yeremia akamlilia Yosia; na waimbaji wote waume kwa wake wakamtaja Yosia katika maombolezo yao, hata leo; hata wakayafanya kuwa ada kwa Israeli; nayo, tazama, yameandikwa katika maombolezo. 26 Basi mambo yote ya Yosia yaliyosalia, na matendo yake mema, sawasawa na yote yaliyoandikwa katika torati ya Bwana, 27 na mambo yake, ya kwanza na ya mwisho, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.

 

2Wafalme 23:29 inasema kuwa aliuawa na watumishi wake na wakamchukua hadi Yerusalemu ambako alizikwa. 2Nyakati inaonyesha kwamba alijeruhiwa vibaya sana mapiganoni na watumishi wake walimchukua kumrudisha Yerusalemu na Yuda wote na Yerusalemu walimuombolezea Yosia (2Nyakati 35:24). Jibu halisi kutokana na mgogoro wowote hapa ni kwamba alikuwa amejeruhiwa sana na alifariki alipokuwa anarudi Yerusalemu.

 

Yosia aliandaliwa ayatangaze na kuyaweka kuwa sheria ya nchi matengenezo lakini unabii ulikuwa umeisha mtaja kuwa atakuwepo. Mungu alikuwa anakwenda kuwaacha Yuda waende utumwani kwa ababu ya kujiuza kwao kuabudu sanamu, na imani ya dini yao ya uwongo. Imani ile bado inaendelea kudumu hapa duniani na ni dini inayojulikana na kuwa na watu wengi zaidi na ni imani iliyoenea na kujulikana sana hapa duniani.

 

Mungu analeta mabadiliko au mageuzi makubwa na matengenezo, yaliyo makubwa zaidi ya haya marejesho ambayo tumepewa kwa mfano wetu. Israeli walikwenda utumwani Ashuru yapata kama mwaka 721 KK. Yuda walitubu na ilisalia na kulindwa lakini wakaingia au kuangukia kwenye ibada za sanamu na wakawafuata wenzao Israeli miaka takriban ishirini na tano baada ya Yubile iliyotangulia marejesho ya Yosia. Tangu Yubile ya mwaka 724 KK Israeli walichukuliwa utumwani ili kwamba tangia mwaka 721 wawe kuwa ni taifa lililo utumwani. Tangu mwaka 715 Mungu aliwarejesha Yuda ili kwamba utumwa wa Yuda uwe umechelewa na Yuda waweze kutengwa mbali na tofauti na ndugu zao Israeli. Yuda hawakushindwa vita hadi kipindi cha kuanguka kwa dola ya Waashuru na tangu mwaka 612 KK tunawaona Waashuru na Wahiti na makabila yao washirika wakipotea kutoka kwenye matukio na nafasi yao ikichukuliwa na Wababeloni na Wamedi na Waajemi.

 

Harakati zilizokuweko kwenye karne ya nane KK zinaendana na zile za karne ya ishirini inayotuongoza kuelekea kwenye maadhimisho ya Yubile ya mwaka 2027/28. Wababeloni walichukua madaraka chini ya Nebukadneza kwenye vita ya Karkemish mwaka 605 KK. Mnamo mwaka 525 wakiwa chini ya Cambyses waliutwaa Misri na wakawa ni watawala au dola yenye nguvu. Utaratibu huu ulipaswa uishie kwa nyakati saba au miaka 2520 hadi kufikia mwaka 1996.

 

Tangu mwaka 632 KK nguvu za utawala wa Waashuru ilianza kuharibiwa na kwa kipindi cha zaidi ya miaka ishirini na saba, Ashuru iliangamiazwa na Babeli ilianza. Ili kufanikisha hili, vita viliwadhoofisha Israeli na walipelekwa utumwani na kipindi kirefu cha miaka mia moja na ishirini ya mwanzoni.

 

Katika karne a ishirini ulimwengu wa watu wanaoongea lugha ya Kiingereza wamedhoofishwa na mlolongo wa Vita Vikuu vya Dunia vimemwaga damu ya weupe na pamoja na mauaji ya Holocaust hadi mwaka 1945 na vita nyingi nyinginezo ndogondogo.

 

Hivi karibuni, dunia yote itafikia toba. Vivyohivyo, Misri ililetwa ipite kwenye bonde la Megido na kumuua Yosia, na ndivyo itakavyokuwa pia kwamba mataifa wataletwa washuke chini kwene bonde la Megido na kuangamizwa. Imani za kidini za ulimwengu huu zilizoanzishwa kwa muunganiko wa Waashuru na Wababeloni na Wamisri utaangamizwa. Kutoka Yubile ijayo, kutakuwa na marejesho ambayo tutakayojionea marejesho mapya ya kidini na utaratibu utaanzishwa na dunia itatawaliwa na utaratibu wa tofauti wa kisheria panoja na na utaratibu mpya wa kidini ambao utatuama kwenye haki na utakatifu na mwenendo sahihi. Hii pia inaashiria marejesho ya ujenzi na matumizi au huduma za Hekalu la pili la Ezra na Nehemia. itakuwa hiyohiyo pia na Utakaso wa Hekalu (sawa na lisemavyo jarida la Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. 241) [Tanctification of the Temple of God (No. 241)] unapaswa kuanza na makuhani na hekalu la Mungu na kuenea duniani kupitia harakati zao. Ni sawasawa tu na ilivyo kwa sasa kwamba dunia inaandaliwa.

 

Mungu aliiangamiza dunia kwa gharika na ilipofika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, Safina ilifunguliwa kifuniko chake na nchi ilikauka (Mwanzo 8:13). Ilikuwa hata hivyo katika mwezi wa pili, siku ya ishirini nnna saba ya mwezi ambapo nchi ilikuwa imekauka kabisa kiasi cha mtu kutembea juu yake na ndipo wana wa Nuhu waliweza kukamyaga miguu yao na kuishi tena duniani (Mwanzo 8:14-19). Marejesho haya yanaonyesha kwamba kipindi cha kuweka makazi kilikuwa ni cha siku hamsini tangu siku ya utakaso wa hekalu na cha toba kwa ajili ya dhambi zilizofanywa kwa kupotoshwa kwa dunia ambayo ni siku ya saba ya mwezi wa Nisan, na sio tangu Pasaka na pia sio siku ya kwanza ya ya mwezi wa kwanza. Kwa harakati za wateule, ndipo ulimwengu unaweza kuwa tayari kwa kumpokea Masihi. Siku kumi kabla ya Pentekoste ambayo inajulikana pia kama ni siku hamsini tangu siku ya Saba Nisan, ndipo Kristo alipaa kwenda mbinguni ili kufanya iwezekane kwa mwanadamu kuuingia ufalme wa mbinguni.

 

Tangu Mwezi wa Kwanza hadi Mwezi wa Saba

Mchakato huu wa marejesho ya kwanza ulifikia kilele chake kwa Masihi. Mchakato wa kipindi hiki unaonekana kama taswira ya mchakato wa mwezi wa kwanza.

 

Mwezi wa kwanza siku ya kwanza ya mwezi, Utakaso wa Hekalu la Mungu unafanyika, Hekalu ambalo ni sisi (1Wakorintho 3:16; 6:19).

 

Siku ya saba ya mwezi ni siku ya utakaso kwa ajili ya dhambi zilizofanywa kwa kutojua ama kwa kupotoshwa. Harakati hizi zinatakiwa kwa viumbe walioumbwa hata sasa na pia kwenye kipindi cha millennia na ni moja ya mikanganiko miwili iliyoko kati ya miezi ya Nisan na Tishri ambao kwa namna fulani unaashiria mpango uleule na matendo.

 

Siku ya kumi ya mwezi wa kumi kunaonekana kuchaguliwa na kumtenga mbali mwanakondoo ambayo inaanzisha mchakato wa okombozi na kipindi ambacho malimbuko yanatakiwa kutolewa na kukubalika na Mungu.

 

Siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza ni Sikukuu ya Pasaka. Marejesho yote kwa kipindi hiki yanaanza kutoka mwanzoni na yanahusisha mwezi wa kwanza yaliongoza kwenye dhabihu na kuula mwili na damu ya Kristo ikiwa ni sakramenti ya pili ya wateule. Sakramenti ya kwanza ya wateule ni ubatizo ambao ni hatua ya kwanza wa utakaso wa hekalu ambao maana yake halisi ni kufanyika baada ya majira ya Sikukuu na baadae kidogo hadi katikati ya siku ya kwanza na ya saba Nisan na mapema kabla ya siku ya 14 ya mwezi wa Kwanza.

 

Sikukuu ya Pasaka na Mikate Isiyo na Chachu zimeunganishwa kwa siku moja na ni kipindi cha siku saba. Kipindi hiki kinaashiria dhabihu na maandalizi ya wateule na kuondoa kwa dhambi na kisha kujiweka sawa kwa Pentekoste na Mavuno ya wateule katika yubile ya arobaini jengwani.

 

Kuna Siku Takatifu za mwanzo na mwish wa Sikukuu hii ya Mikate Isiyo na Chachu pamoja na siku ya kwanza au Siku ya Pasaka ambayo ni ya 14 Nisan ambayo ni siku ya maandalio. Wateule wasipokuwa watakatifu hawaruhusiwi kushiriki mkate usio na chachu wa Pasaka ambao tumeuona kwenye matengenezo ya Yosia ambapo makuhani wa Mahali pa Juu hawakuruhusiwa kwenda Hekaluni kwenye Pasaka. Kwa hiyo ibada za sanamu zilipunguza idadi ya makuhani kwenye maadhimisho ya Pasaka Hekaluni.

 

Tofauti iliyopo kati ya miezi wa kwanza na wa saba ni kusanyiko la Siku ya Baragumu ambalo linafanyika tena katika siku ya Mwandamo wa Mwezi Mpya au siku ya kwanza ya mwezi, ambayo inatangaza kipindi ambacho Masihi ataingilia kati maongozi ya dunia. Ataingilia kati na kuchukua uongozi kwa kuwa wateule na uwepo wao na ushiriki wao wakiwa kama watu wa Mungu. Wanajulikana kutokana na matendo yao na kazi zao walizopangiwa na inayoonekana wazi kama Sabato, Miandamo ya Mwezi, Sikukuu na harakati zao kuanzia Mwezi wa Kwanza na kuendelea pamoja na kumpokea kwao Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste na kwa Sikukuu na Torati ya Mungu kwa ujumla.

 

Hakuna mfungo wa saumu siku ya saba ya mwezi katika mwezi wa saba. Hakuna kitu anachoweza klukifanya mwanadamu sasa kilichofanananacho. Mwanakondoo amekwisha tolewa sadaka tayari na ndipo saumu ya siku ya kumi ya mwezi wa saba wakati siku ya kwanza imetengwa tu mbali kwa ajili ya dhabihu ya siku ya kumi na nne. Mnamo mwezi wa saba, Yule mwanakondoo aliyechaguliwa na kuwekwa kando huko mbinguni akiwa kama mfalme mshindaji, aliyeonyeshwa kwa ishara ya baragumu inayopigwa siku ya kwanza ya mwezi wa saba. Katika siku ya kumi ya Upatanisho dunia ilipatanishwa na inaandaliwa kwa ajili ya utawala wa Milenia. Tazama pia jarida la Lafudhi ya Musa (Na. 70) [The Ascents of Moses (No. 70)].

 

Mataifa yanashughulikiwa kwa kiwango endelevu. Kama Yosia alivyolirejesha hekalu na torati tangu Pasaka na kuendelea hadi miaka mingine kumi na tatu ya nyongeza baada ya mwaka 623/2 KK hadi alipokwenda Megido mwaka 609 KK kuyakabili mataifa na kufa, na ndivyo ilivyo pia kwamba ufalme utapita mikononi mwa wafalme hadi kwenye mikono ya Masihi ambaye haki ni yake.

 

Sikukuu ya Kutaniko inapaswa ifanyike pamoja na sadaka wakati wa jioni ya kwanza ya sikukuu. Siku ya kwanza ya sikukuu ya Vibanda ni siku Takatifu ambayo hakuna harakati wala kazi yoyote inayopaswa kufanywa na mwanadamu zaidi ya kutafakari na kujiandaa kwa mkusanyiko na kutoa sadaka ambayo haitakiwi ibakie hata asubuhi.

 

Siku ya Saba ya Sikukuu ya Vibanda ni kipindi kinachofananishwa na kipindi cha millennia ya siku saba ya Mikate Isiyo na Chachu. Kwenye mfano wa kwanza Masihi alikufa ili kuiwezesha Sikukuu ya Pasaka. Matendo ya wanadamu ni ya muhimu ili kutoka nje ya dunia.

 

Katika mwezi wa saba sikukuu inaashiria au kuwakilisha utawala wa Masihi hapa duniani ambapo hakuna umuhimu kutoka nje ya dunia wakati dunia yote itakapokuwa chini ya utawala wa haki na maongozi ya torati ya Mungu.

 

Kwa hiyo, siku ya saba au ya mwisho wa maadhimisho ya Sikuu ya Vibanda sio siku takatifu kwa kuwa inawakilisha kipindi ambacho dunia itarudi kwenye zama za uadui na vita.

 

Siku Iliyo Kuu ya Mkutano wa Makini kwa namna nyingine ni siku ya nane ambayo ni tofauti na maadhimisho ya Mkate Usio na Chachu ni ya mwisho na sio ya kwanza na ni siku takatifu. Pentekoste kwa namna nyingin e sio siku takatifu kwa kuwa inawakilisha kazi ya Masihi kwenye wokovu wa mwanadamu.

 

Siku ya Mkutano wa Makini ni Takatifu kwa kuwa inawakilisha ashirio la siku ya hukumu ya haki itakayotolewa kwa haki kwa walimwengu na ni ondoleo la mwisho la dhambi. Inawakilisha ujio wa Mungu hapa duniani na Mji wa Mungu utaunganishwa kwenye marejesho haya ya mwisho.

 

Marejesho haya ya mwisho ni matokeo ya mwisho katika mpango wa Mungu.

 

Ndipo tunayaona Marejesho na Pasaka Kuu Saba zilizo kwenye Bbiblia zinamaana kwene harakati hizi na mlolongo huu wa Mpango wa Mungu. Soma jarida la Pasaka Kuu Saba za Biblia (Na. 141)  na  Baragumu Saba (Na. 107) [The Seven Great Passovers of the Bible (No. 107)].

 

Ingawa Yosia alitubu bado alipaswa afe kama utaratibu wote mzima aliouongoza kuurejesha kikamilifu kwa kuyaangamiza mataifa na Yuda hawakuwa na uwezo wa kufanya hivyo kabisa.

 

Hezekia alianza mchakato na mwanae Manase alijaribu bali alishindwa. Mwanae Amoni ndiye alikuwa ni mbaya zaidi ya Manase kwa uovu wake. Yosia aliahirisha kutokea kwa maafa yasiyoweza kuepukika. Hata hivyo ilitokea kipindi cha Wababeloni. Hekalu lilihusuriwa na marejesho yaliyofuatia yalipaswa yawe kwenye Hekalu linguine na lenye muundo tofauti, kama tunavyoona kwenye vitabu vya kina Ezra na Nehemia. Hii ilikuwa ni ashirio na ilikuwa inamlenga Kristo. Mambo yote yaliyokuwa yanafanywa kwenye hekalu lile yalikuwa yanamlenga Masihi na mhukumu au mwamuzi wa Yuda kwene kipindi cha majuma sabini ya miaka iliyoishia mwaka 70 BK (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi upya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)].

 

Tunaelekea kwenye marejesho ya Masihi. Ni kama yalivyokuwa marejesho ya Yosia, nasi haya yetu yanaelekea kwenye Yubile, lakini kutakuwa na mlipuko wa maasi na upinzani dhidi ya marejesho haya katika vipindi vyote viwili, yaani mwanzoni mwake, na ambayo yata  yatakuwa na umuhimu wake utachukua taswira ya Ezra, na pia mwishoni mwa Milenia itakayoitangulia hukumu. Hii ni hadithi nyingine.

 

Ili kutusaidia angalia masomo mlinganisho tunayopaswa kujionea mafuatano yake kwenye mtindo wa jedwali. Marejesho ya Ezra na Nehemia yalikuwa ni ya hekalu jipya na la pili.

 

Marejesho ya Hezekia yalikuwa na mchocheo wa Mungu. Marejesho haya yalifuatiwa na mwanzo wa marejesho mengine tena ya unabii uliovuviwa. Haya yalitanguliwa na kipindi cha mzunguko wa miaka saba kilichotangulia Yubile. Hii tena iliwakilishwa na kipindi cha miaka saba kinachoonekana kwenye Baragumu na kimeelezewa kwenye majarida ya Kuanguka Kwa Yeriko (Na. 142) na  pia Mihuri Saba (Na. 140) na Baragumu \\\Saba (Na, 141) [The Fall of Jericho (No. 142) and also The Seven Seals (No. 140) and The Seven Trumpets (No. 141).

 

Masihi anazipunguza siku za mwisho kwa kurudi kabla ya Yubile ya Milenia ijayo kwa mfano miaka saba mapema kabla ya kuifka Yubile ya mwaka 2027/28 huenda kabla ya mwaka 2019/20. Dini inayompinga Masihi itauona mfumo na imani mpya vikiwekwa na kuchukua mahali pake katika kipindi hiki cha Milenia kama Ezra na Nehemia walivyotumiwa na fanya.

 

Jedwali la ulinganisho linaonekana kama hivi lilivyofungamanishwa na matukio yajayo yanaweza kuonekana kabisa kama yale yaliyoorodheshwa kwene jedwali hili:

 

Marejesho ya Israeli chini ya wafalme

715/16 KK marejesho ya Hezekia.

Israeli walimuacha Mungu na kurudi nyuma chini ya Manase na Amoni.

632 Marejesho ya Yosia yanaanza.

630 Mfalme wa Waashuru anakufa.

627 Hakuna mfalme kwenye kiti cha enzi cha ufalme wa Kaskazini.

624 Taifa la Israeli na Wasamaria wanaadibishwa na kutolewa kwenye sanamu.

624/23 Yubile inatangazwa na marejesho ya dini ya kishindo yanafuatia.

623/22 Pasaka ya Marejesho inafanyika (kiwango cha rekodi kinavunjwa)

616 Wamedi wanajitokeza kuwa viongozi dhidi ya Waashuru na Misri inajipanga kuikabili Ashuru.

614 Assur aliangukia mikononi mwa Cyaxares mfalme wa Wamedi kwa mkakati uliofanywa na Wamedi na Wababeloni chini ya Nabopolasa aliyekuja akiwa amechelewa kumuangusha Assur.

612 Ninawi unaangusha na majeshi ya muungano na Ashuru inaondolewa kwenda Harani ambako Ashuruballit II alijaribu kuirejesha tena Dola ya Waashuru.

610 Ashuruballit II anaondoka Harani licha ya msaada aliokuwa anaupata wa Wamisri na mji ukaangukia mikononi mwa Wamedi na Wababelonia.

609 Yosia anajeruhiwa na kuondolewa mapiganoni huko Megido. Wamedi na Wababeloni wanakabiliana na mashambulizi ya majeshi ya ushirika ya Wamisri na Waashuru.

605-525 Kipindi cha Utimilifu wa Mataifa kinaanza.

598/97 Yuda inaangushwa na Wababeloni na utaratibu wa kale wa Hekalu unaondoshwa au kukomeshwa.

539 Babeli unatekwa na Koreshi na Dario Mmedi mwana wa Astyages na mjomba wa Korshi.

423-410 Hekalu la Pili linajengwa. Juma la Saba la miaka linaanza na kuishia mwaka 70 BK.

398-373/2 Ezra na Nehemia wanaurudisha utaratibu wa ibada Hekaluni chini ya Artashasta II.

 

Marejesho chini ya Masihi

1914/18 Vita Kuu ya I ya Dunia. Vita vya mwisho wa dunia vimeanzia.

1917 Kuichukua tena Palestina kwa msaada wa Majeshi ya Jumuia ya Madola ya Mwingereza na kutangazwa kwa Nchi au Taifa la Wayahudi.

1939 Vita Kuu ya II ya Dunia ilianza.

1942 Mauaji ya Holocaust yalianza.

1945 Vita Kuu ya II ya Dunia iliisha.

1953 Misri ilitangaza uhuru wake.

1956 Mgogoro wa kugombea mfereji wa Suez.

1996 Mwisho wa Kipindi cha Utimilifu wa Mataifa cha miaka 2000 au yubile arobaini tangu kuzaliwa kwa Masihi. Maadhimiso ya mwaka wa 3000 tangu Daudi alipoingia Yerusalemu.

1997 Mwezi wa Miaka Ulianza. Kuondolewa kwa mfumo wa ibada za kidunia wa Makasisi, Wafalme na Manabii kulianza.

1998 Mwaka wa Sabato na ni mwaka wa 21 wa Yubile ya 39 tangu huduma ya Yohane Mbatizaji na Masihi katika Yubile ya mwaka 27/28 BK. Usomaji wa Torati kwa Mara ya Kwanza ulifanyika kwenye Sikukuu ya Vibanda tangu kipindi ch karne nyingi zimepita.

1999-2019 Vita ya wafalme wa Kaskazini na Kusini na kuangamia kwa mataifa kulianza na kunaendelea.

2019/20 Masihi ataanza kuyatiisha na kuyaadibisha mataifa na wito wa Megido.

2027/28 Yubile ya 40 itatangazwa kwa kupigiwa mbiu.

2028 Kipindi na Utawala wa Milenia Utaanza. Kipindi zama cha Utawala wa Haki chini ta Torati au Sheriza za Biblia kitaanza.

Vita vya waasi.

Matengenezo na ujenzi wa Hejalu.

2997 + Shetani atafunguliwa.

2997-3027 Vita ya Waasi au Uasr wa Mwisho.

3028 Ufufuo wa Pili wa Hukumu ya Malaika na Ulimwengu.

3127 Kukabidhi kila kitu kwa Eloa na kushuka kwa Mji wa Mungu.

3128 Pasaka Kuu ya Kwanza ya Watakatifu.

 

Kwa kujisomea zaidi haya, jisomee pia majarida yafuatayo:

Maelezo ya Ratiba ya Zama na Matukio Yake (Na. 272) [Outline Timetable of the Age (No. 272)]

Ujio wa Masihi Sehemu ya 1 (Na. 210A) [Advent of the Messiah: Part I (No. 210A)]

Yubile ya Dhahabu na Milenia (Na. 300) [The Golden Jubilee and the Millennuim (No. 300)]

 

q