Makanisa
ya Kikristo ya Mungu
[175]
Uhusiano Kati ya Mwezi Tishri na Ikwinoks
(Toleo
La 2.0 19960824-20080404)
Katika kuitetea dhana au mafundisho ya uahirisho uliofanyika
kwenye kalenda ya Hilleli, baadhi ya watumishi wenye hamasa wanaohudumu kwenye
vuguvugu la Makanisa ya Mungu wamekimbilia kwenye tafsiri za Maandiko
Matakatifu wakitafuka kuyapa mashiko madai ya mafundisho yao. Jarida hili
linafafanua na kutathmini kwa kina kuhusu madai haya, pamoja na hali isiyo ya
kawaida inayojitokeza mfano kama ilivyojitokeza mwaka 1997.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki ©
1996, 2008
Wade Cox)
(tr. 2014)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la
haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa
au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya
lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Uhusiano Kati ya Mwezi Tishri na
Ikwinoks
Baadhi ya
watumishi na wahuribi wenye hamasa walio kwenye vuguvugu la Makanisa ya Mungu
wamejitahidi sana kutafuta namna ya kuhalalisha mafundisho yanayojulikana kama
ya uahirisho yaliyoanzishwa na rabi maarufu anayejulikana kwa jina Hilleli na
aliyeanzisha mfumo wa kalenda inayojulikana kwa jina lake hilihili, hali.iayoashiria
nia yao ya kuyapotosha Maandiko Matakatifu. Mojawapo ya madai mapotofu
waliyonayo kwenye mabishano haya yanatuama kwenye mtazamo kwamba jinsi ya
kuweka kigezo cha kuamua siku inayojulikana
Moladi au Siku ya Kwanza ya mwezi huu wa Tishri kwa mujibu wa mafundisho
ya Hilleli inauhusiano wa aina fulani au inaendana kwa kutegemeana na mwenendo
au mpangilio wa majira ambayo siku moja yake masaa ya usiku na mchana
yanalingana ambayo kwa majira ya hari siku hii inaangukia mwezi Septemba na
siku hii inaitwa ikwinoksi. Mwandamo wa Mwezi Mwandamo wa Tishri unajulikana
vema kuwa ni – Mwandamo wa Mwezi Mpya wa Saba. Neno hili Moladi huenda likawa ni muafaka kulitumia kwa kuwa kwa mujibu wa
mafundisho ya kalenda ya Hilleli, ni makosa makubwa kusema kuwa siku ya Kwanza
ya mwezi wa Tishri haiangukii kwenye Mwandamo wa Mwezi Mpya.
Utetezi
unaotumiwa kuhusu fundisho hili la uahirisho na mabadiliko yake yasiyo ya
kawaida yaliyojitokeza mara kadhaa, mfano wa jinsi ilivyotokea mwaka 1997, kumejitokeza
mabishano makubwa sana yasiyo ya kawaida ambayo bado yanaendelea hadi sasa. Mtu
mmoja aliinukuu Kutoka 34:22 kama andiko linalothibitisha Idi ya mwezi wa Saba
lazima ifanyike kwenye kipindi ikwinoksi au baada ya mwezi Septemba. Andiko
hili linasema wazi sana kwamba:
Exodus 34:22 Nawe utaitunza sikukuu ya majuma, nayo ni
ya malimbuko ya mavuno ya ngano, na sikukuu ya kukusanya vitu mwisho wa mwaka
Andiko hili
linaweza pia kutafsiriwa kama ni la marudio ya kila mwaka kwa kulitumia kama teqûphâh (SHD 8622) likimanisha mageuzi (ya jua) muafaka (wa muda) marejeo,
na kumaanisha mzunguko, kuzunguka au hatima. Hii inaweza kumaanisha mwisho
wa majira yanayoendelea au mwisho wa
mayukio ya mwaka. Hakuna jinsi inayofikiliza kuwepo kwa uhusiano halisi na
siku hii ya ikwinoksi au kama ni lazima ifuatiwe na siku hii ya ikwinksi.
Hakuna kanuni
yoyote ile kutoka kwa mifumo yote ya kalenda zote za kale zijulikanazo kama za
Kiebrania, kiyunani, Kibabeloni, au Kikanaani kwa Kanisa ambayo iliwahi
kuahirisha kutangazwa kwa mwezi wa Nisan[u] au Abibu ambao msingi wake
unatokana na kutilia maanani kwa kuuhesabia mwezi wa Saba kwamba ndiyo uamue
katika kuupata mwezi wa Kwanza wa Kiyahudi na hata wa kwenye mifumo ya kalenda
nyingine. Kalenda ya Waseleucidi wa Kimakedonia inaanza mwaka wake kutoka kwenye
mwezi unaoshabihiana na na mwezi Tishri na kwa hiyo, inaonekana kuenenda na
majira joto ya ikwinoksi ya pande za kaskazini. Kalenda hii ilitumika kama ya
nyongeza kwenye mfumo wa Wababelonia katika kuhesabu matukio hayahaya ya Waseleucidi
zaidi ya ile ya historia halisi ya Wayahudi wakati ule wa Wamakabayo na wengineo
(1Wamakabayo; tazama kitabu cha Schürer, History
of the Jewish People in the Age of Jesus Christ [Historia ya Wayahudi katika
Siku za Yesu Kristo], Vol. 1, uk. 18-19 na uk. 125-126 kwa mchanganuo wa
kina). Hata hivyo, Wamakabayo walianza mwaka wao kwenye majira ya pepo za
kaskazi pia (Schürer, ibid.).
Mabishano haya
yanaonekana kukanganya utendaji kazi wa kalenda hii ya Wamakedonia Waseleucidi na mfumo wa Waebrania-Wababelonia. Kanuni za
uahirisho hazina mashiko wala kuhusiana na majira haya ya kipupwe cha pepo za
kaskazini cha ikwinoksi. Kanuni ni kwamba, katika mazingira ya aina yoyote yale
ni kwamba lazima Pasaka iangukiwkwenye kipindi cha ikwinoksi ya majira ya hari (Schürer,
ibid., uk. 590; imetokana na ruhusa ya, Schürer ambayesema: “wakati jua liliposimama kwa ishara ya Aries”,
ibid., uk. 593). Ishara hii ya Aries inaanzia kuonekana kipindi cha takriban
tarehe 21 Machi na huishia tarehe 20 Aprili, kwa usemi wa ki Gregorian. Kwa hiyo,
Pasaka ya tarehe 21 Aprili imekatazwa kabisa kwa mujibu wa kanuni za zama za
kale. (Ikumbukwe pia kwamba elimu ya Nyota na Mambo-anga hazikuweza kutofautishwa
na kutenganishwa hadi kipindi cha Wanamatengenezo. Kwa hiyo, hii ilikuwa ni
kazi ya elimu ya anga na siyo elimu ya unajimu inavyoonekana) Schürer anamtaja Anatolius,
kwa mujibu wa Eusebius (HE, vii 32,
16-19) akisema kwamba huu ni mtazamo usiojulikana kwa wenye mamlaka wote wa
Kiyahudi akiwemo Aristobulus, mwana falsafa aliyeishi siku za Ptolemy
Philometor, na pia Philo na Josephus (Schürer, op. cit.). Kalenda ya
Wamakedonia ilitumika huko Syria tangu mwanzo wa mamlaka ya Waseleucidi hadi
ikaingia kwenye mfumo na zama za Waktisto.
Ilitumiwa kama
ifuatavyo:
(1) kwendana sambamba na miamdamo halisia ya
miezi;
(2) ili kuipata miezi kumi na miwili ya mwaka
unaofuata kalenda ya jua iliyojulikana hapo mwanzo kama kalenda ya Julian, isipokuwa
kwamba mwanzo wake ulikuwa ni siku tofauti. Kalenda ya Waseleucidi wa
Kimakedonia ilikuwa kutofautina nana kila mara kwa majira mamoja hadi mengine,
ambavyo ilionyesha kwamba kanuni haikuhusiana hasa na ile ikwinoksi ya majira
ya hari hata hivyo. Huko Tiro, mwaka ulianza tahere 18 Novemba (Schürer, p.
595), baada ya ikwinoksi. Huko Gaza, na kwenyewe, ulianza tarehe 29 Augost
(Schürer, ibid.; cf. Bickerman, Chronology,
p. 50), ikiwa ni kabla ya ikwinoksi.
(3) Katika siku zilizofuatia baadae miezi ya
kalenda ya Julian ilianza kuitwa kwa majina ya Wamakedonia (Schürer, ibid.). majina
ya Kisyria ambayo yalikuwa yakijulikana sana au haya yale yasiyojulikana ya
Wayahudi yalitumiwa sambamba nay ale ya Wamakedinia.
Kwa hiyo hakuna
kanuni inayoonyesha kwamba Tishri ambao ndiyo mwezi wa Saba, unauhusiano na
ikwinoksi hii ya majira ya hari. Hii ni hoja ya muhimu katika kuipinga itikadi
ya wanaoamini kalenda ya Hilleli, ambayo haina mashiko yoyote. Inatakiwa pia
katika jaribio la kutetea udanganyifu mwingine kuhusu kusulibbiwa kwa mwokozi
mnamo mwaka 31BK kama ilivyoenezwa na Herman Hoeh kwa kufundishwa na Herbert
Armstrong (soma jarida la Majira ya Kusulibiwa na
Kufufuka (Na. 159) [The Timing of the Crucifixion and the Resurrection (No.
159)]. Herman
Hoeh hata anafikia kuanzisha kanuni ya uahirisho kwa maslahi yake kutokana na
nia yake hii (sawa na jarida lisemalo Siku
ya |Kusulibiwa Haikuwa Ijumaa).
Siku ya maandalio
au siku ya 14 Nisan, inaitwa kuwa Siku ya Ushirika wa Meza ya Bwana, na siyo siku ya Pasaka kama inavyofundishwa
na yeye. Haya yalikuwa mafundisho ya uwongo yaliyoenezwa na Herbert Armstrong na
yalitetewa na baadhi ya watumishi wake, lakini yalikuwa yamekosewa mno (soma
jarida la Pasaka (Na. 98) [The
Passover (No. 98)].
Pasaka ya mwaka
1997 iliadhimishwa kabla ya mwezi mmoja kutokana na kalenda ya Wayahudi kwa
kuwa ilikumbwa na mafundisho haya ya uahirisho yaliyofundishwa na kina Hilleli ambayo
hayapo kwenye Biblia wala hayana mashiko yoyote kwenye Maandiko Matakatifu,
wala kwehye historia ya huko nyuma kabla ya katne ya nne ya zama hizi. Kile
wanachokifanya watetea mafundisho haya wanachokifanya kwa bidii zao zote ni
kuanzisha kanuni mpya na kusema kwamba kanuni ama sheria ya kuamua ni wakati
gani uanze mwezi wa Nisan ni kwamba mwanzo
wa mwezi unaanzia pale unapoandama Mwezi Mpya karibu na majira ya ikwinoksi ya
majira ya kipupwe cha pepo za kaskazi ambayo kunaadhimishwa Idi za Pasaka na
Mikate Isiyo na Chachu kukiwa ni mwezi kamili wa kwanza wa mwaka ikifuatiwa na
ikwinoks isipokuwa wakati Sikukuu ya Vibanda inapoangukia ni kabla ya ikwinoks
ya pepo za kaskazi (na hata kama Siku ya Mkutano wa Makini ikiangukia kwenye
ikwinoks), kwa namna yoyote ile bado Pasaka/Mikate Isiyo na Chachu itakuwa kwenye
kipindi cha mwezi mzima unaotuata siku ya ikwinoks ya majira ya baridi. Hakuna
mahali kanuni hii inaonekana kuwa ipo na kwa kweli hata ilipoashiria kuwa
ilikuwepo, na kama ingekuwepo basi ingeisababishia kalenda ipite kwenye kipindi
cha mkanganyiko mkubwa. Maelezo yaliyo kwenye Kutoka 34:22 wanayodhania wafuasi
wa Hilleli kuwa yanaunga mkono itikadi yao hayana mashiko yoyote kabisa na hata
ya kihistoria hawaungwi mkono. Itikadi yao inatokana na mawazo na mapokeo ya
marabi tu yenye kuwapa haki za misingi ya kidunia tu.
Sawasawa na hilo,
namna ya kuipata Moladi ya Tishri ni kazi nyingine iliyoifanywa na imani ya
Hilleli. Hakuna kanuni ya kibiblia ya namna yoyote ile inayotumika kupanga siku
hii ya Moladi ya Tishri zaidi ya ile ya Mwandamo wa Mwezi Mpya huu wa Saba peke
yake. Kwa hiyo hakuna kitu cha ajabu kinachojitokeza cha kushangaza siku hii,
isipokuwa ni umuhimu wake tu wa siku hii kwetu ya mwezi wa Tishri kwa kuwa
ndiyo unaoadhimishiwa Siku ya Upatanisho na Sikukuu nyinginezo. Mafundisho
yanayosema siku hii ya Moladi iwe katikati ya mwezi huu wa Tishri yanatokana na
mapokeo tu ya (kutoka kwa Mafarisayo) kwenye dini ya Kiyahudi, kama ilivyo
kwenye siku ya 6 Siwani ni Pentekoste. Mwezi wa Nisani, au Abibu (na siyo
Tishri) ndio utakuwa mwanzo wa miezi kwenu (Kutoka 12:2); na wala siyo mwezi wa
Kwanza unaanzia tangu mwezi wa Tishri.
Kosa linguine
lililovumishwa kutoka kwenye malumbano haya ni kwamba siku ya 1 Nisan haiitangulii
ikwinoks ya majira ya baridi. Mwandamo wa Mwezi wa Nisan kinaitangulia
ikwinoks, kwa mfano, katika miaka ya 1988, 1991, 1994 na 1996. 1997 ilikuwa ni
mara tano hii katika kipindi cha miaka kumi ya mwisho kwamba 1 Nisan iliitangulia
ikwinoks. Kwa hiyo, inaonekana kuwa ni karibu sawa kuwa hivyo. Ukweli huu pia
unafanya mwanzo wa mwezi Tishri uwe mapema kabla ya ikwinoks mara nyingi.
Mabishano yale yanayolenga kuweka kanuni ama sheria ya mkaribiano wa Idi ya Vibanda
na siku ya ikwinoks ni ya uwongo na yanapingana na ukweli wa kihistoria.
Mwaka wa 1994 Sikukuu
zote za mwezi wa Tishri ziliangukia kabla ya ikwinoks ya mwezi Septemba isipokuwa
siku ya Mkutano wa Makini, ni kama
ilivyojitokeza tena mwaka 1997 na haikupingika pia mwaka 1994, ikichukuliwa pia
kwamba kwa kuwa watu waliohudhuria walijisikia vizuri na jambo hilo kama
ilivyokuwa pia kwa wale marabi. Hali iliyojitokeza mwaka 1994 kinyume na mwaka 1997
inaonyesha kwamba hakuna kanuni kuhusiana na ikwinoks ya mwezi Septemba.
Kuhusu uhusiano au
kwa kufananisha na siku za Mwandamo wa Miezi, Mwandamo wa Mwezi kwa kweli ni
tukio la kinajimu. Habari yake inapatikana kotekote nchini Uingereza, hadi
kwenye shughuli za ulinzi na za kibiashara za nchi, bahari na angani, na idara
inayojulikana kama Her Majesty’s Nautical Almanac Office (HMNAO). Hiki SIYO kile
kitabu kinachojulikana kama the Queen’s
Almanac kama mpendwa wetu mmoja asiye na habari alivyowahi kudhania kuwa
huenda ilikuwa ni kazi ya uandishi iliyofanyika hivi karibuni. Taarifa za
Miandamo wa Mwezi za hivi karibuni zinaweza kupatikana kwa muda wa masaa
yajulikanayo kama Greenwich Mean Time (saa za Kimataifa) na msaada unaweza
kutolewa kwa kina kwa kazi ya kuhesabu ya masaa ya Yerusalemu na masaa mengine
kutoka kwa vyanzo vyote viwili vya kimuunganiko na kkutoka kwa hawa End Evening
Nautical Twilight (EENT) huko Yerusalemu, na pia kwa maeneo ya kinyumbani. Haya
masaa ya EENT yanatakiwa katika kuamua au kupangilia siku kwa nia ya
kutengeneza kalenda. Tukio la muhimu kulitilia maanani ni Mwandamo wa Mwezi na
ndilo linaloweka majira kwa kuunganisha ulimwengu wote. Mwonekano wa mwezi wa
kila mahali enyeji hutofautiana.
Kwenye baadhi ya
kalenda zilizochapishwa, imeonekana kuwa nyakati au masaa hayaonekani, ni kama
vile mfano ni kalenda inayotengenezwa na Frank Nelte, haionekani kufanana na muda
au majira ya mwezi kutoonrkana kama ilivyofanywa na au kuonyeshwa na vyanzo
maalumu kwa namna iliyo wazi sana. Huenda kuna namna ya mkanganyiko kati ya
vipindi vya mwonekano au mchomoko wa mwezi na kile cha kutoonekana mwezi kabisa.
Hiki ni kipindi
chenye fursa njema cha kuondokana na makosa na opotovu mwingine. Mwandamo wa
Mezi Mpya haina maana ya Mwezi mchanga. Sheria hii ya uahirisho wa saa za mchana
inadai kwamba kipindi cha mpito wa kuandama mwezi kinafanyika mchana na ndipo
maamuzi ya kutangaza Mwandamo wa Mwezi kunatangazwa hadi siku inayofuatia.
Sheria hii ya
majira ya mchana inaweka madai yake kwamba inafanya takriban masaa sita
kuwezesha kufanya mwezi mchanga kutoka kwenye sehemu ya giza. Sheria hii
yenyewe tu inajishuhudia na kumaanisha kwamba kipindi hiki cha giza chenyewe tu
sio mwezi mchanga, bali ni kitu kilichopangwa tu.
Inadhaniwa pia
kwamba huenda sheria hii ya uahitisho ilianzishwa na Waasia wenye asili ya
Kiyahudi waliokuwa wanaishi pande za mashariki ya mbali na ambao Mwandamo wa
Mwezi unachelewa kuonekana pengine hata kufikia siku inayofuatia. Kanuni au
utaratibu wa kutegemea kuonekana Mwezi mjini Yerusalemu ndiyo inafanya Mwandamo
wa Mwezi huko Asia uchelewe kwa masaa hadi manane wakati mwingine, na ndipo
inatokea kwamba siku ya kabla yake kwa muonekano huu wa baadae. Kwa hiyo
kalenda inaweza kuonyesha tofauti ya siku moja baada ya Mwandamo wa Mwezi kwa
upande wa Mashariki hususan katika Australia na New Zealand. Hii ndiyo kanuni
pekee ya uahirisho yenye mashiko kwa namna yoyote ya maadhimisho ya kweli. Tatizo lililopo kwenye kalenda ya Hilleli
yameainishwa kwenye jarida la Kalenda ya Mungu (Na. 156)
[God’s Calendar (No. 156)].
Licha ya haki
iliyoko kwenye jambo hili na haifikishi kwenye suluhisho lake kiusahihi na
kuondoa tatizo, Makanisa ya Kikristo ya Mungu yameamua kutumia mwonekano wa
mwezi wa Yerusalemu Regardless of the merits of this sole position, anna
kuhesabu kutoka huko ili kuondokana na matatizo ya kuahirisha na kwa lengo la
kutuweka wote kwenye wakati mmoja tu na unaolingana wa kikalenda miongoni mwa
Makanisa yote ya Mungu kokote yaliko duniani hadi kufikia kipindi kile cha
mkutano mkuu wa Makanisa ya \Mungu ambako tutajadili kwa kina jambo hili.
q