Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[245]
Marejesho ya Yosia
(Toleo La 2.0
19980422-20081122)
Marejesho yaliyofanywa chini ya
uongozi wa Mfalme Yosia yana idadi kadhaa ya mafundisho yanye maana ambayo ni
muhimu kwetu katika kuuelewa Ukristo wetu leo.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati
Miliki © 1998, 2008 Wade Cox)
(tr. 2014)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili
yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama
yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa.
Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana
zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya
haki miliki.
Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya::
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Marejesho ya Yosia
Kwenye jarida la Utakasaji wa Hekalu tumeelezea kwa kina
kuhusu mchakato wa Utakaso na Marejesho yaliyofanywa kwa kipindi cha idadi
kadhaa ya watawala. Jarida lile pia limetathmini na kuelezea umuhimu wa kufanya
marejesho kwa viumbe kwa kuanzia siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza na matendo
au matukio ya haraka ya Mungu kwenye mchakato huu. Tangu kipindi kilichoko
katikati ya Hezekia na marejesho ya Ezra kulikuwa na marejesho yaliyofanywa na
Yosia ambayo yalikuwa ya mwisho kuwahi kufanyika kwenye Hekalu la Sulemani.
Ndani ya miongo michache baada ya marejesho ya Hezekia,
taifa likakumbwa na ukengeufu mkubwa uliotokea kipindi cha utawala wa Waashuru.
Waashuru walionywa kupitia nabii Yona na Ninawi ulisamehewa na kuachwa kutokana
na toba waliyoionyesha. Hata hivyo walirudi nyuma na kuiadhimisha Easter na
kushamirisha Dini ya kuliabudu Jua ambapo Israeli na Yuda waliwaiga na kuwafuata.
Israeli wengi walitekwa na kuchukuliwa utumwani na hawa Waashuru.
Yeroboamu alikuwa ndiye mfalme wa Israeli aliyejikita sana
kwenye mimani hizi kiasi cha kuanzisha na kufadhili ibada zilizoathiri
utaratibu na imani ya Mungu lakini alianzisha imani hii ndani ya ibada za
kuaudu Ndama wa Dhahabu ambayo ilikuwa ni sehemu ya dini ya Wababeloni wa kale
waliokuwa wanaabudu mungu Mwezi aliyejulikana kwa jina la Sin (sawa na
ilivyoandikwa kwenye jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222) [The Golden Calf (No. 222)].
Pia aliweka sikukuu mwezi wa nane kama tulivyoona kwenye
jarida la Yeroboam na Kalenda ya Hilleli (Na. 191) (sawa na
lisemavyo jarida la Goligotha, Mahali pa Fuvu la
Kichwa (Na. 217) [Golgotha: the Place of the Skull (No. 217)].
1Wafalme
12:32-33 Yeroboamu akaamuru
kushika sikukuu katika mwezi wa nane, siku ya kumi na tano ya mwezi, mfano wa
sikukuu iliyokuwa katika Yuda, akapanda juu ili kuiendea madhabahu. Akafanya
vivyo katika Betheli akiwatolea dhabihu wale ng'ombe aliowafanya; akawaweka
katika Betheli wale makuhani wa mahali pa juu alipokuwa amepafanya. 33 Akatoa dhabihu juu ya ile madhabahu aliyoifanya katika
Betheli, siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane, mwezi aliouwaza moyoni mwake
mwenyewe; akawaamuru wana wa Israeli waishike sikukuu hiyo, akapanda kuiendea
madhabahu, ili kufukiza uvumba.
Wakati wa kipindi hiki cha ukengeufu na ufumo au imani
hii ya dini ya uwongo iliyoanzishwa na Yeroboamu, Mungu alimuinua na kumpeleka
nabii akawaonye ukengeufu huu. Mungu hafanyi jambo lolote katika kuwahukumu
watu pasipo kuwaonya kwanza watu wake kwa kupitia watumishi wake manabii, kabla
hajaamua kuchukua hatua.
1Wafalme
13:1-6 Na tazama,
akatoka mtu wa Mungu katika Yuda kwa neno la Bwana, akafika Betheli. Naye
Yeroboamu alikuwa akisimama penye madhabahu, afukize uvumba. 2
Basi mtu huyo akapiga kelele juu ya madhabahu, kwa neno la Bwana
akasema, Ee madhabahu, madhabahu, Bwana asema hivi, Angalia, mtoto atazaliwa
katika nyumba ya Daudi, jina lake Yosia; na juu yako atawachinja makuhani wa
mahali pa juu, wanaofukiza uvumba juu yako, na mifupa ya watu itateketezwa juu
yako. 3 Akatoa ishara siku ile ile, akasema, Hii ndiyo
ishara aliyoinena Bwana, Tazama, madhabahu itapasuka, na majivu yaliyo juu yake
yatamwagika. 4 Ikawa, mfalme Yeroboamu alipoyasikia maneno
ya yule mtu wa Mungu, alipopiga kelele juu ya madhabahu huko Betheli, alinyosha
mkono wake pale madhabahuni, akasema, Mkamateni. Basi ule mkono wake
aliounyosha ukakatika, wala hakuweza kuurudisha kwake tena. 5
Madhabahu ikapasuka, majivu ya madhabahuni yakamwagika, sawasawa na
ishara aliyoitoa mtu wa Mungu kwa neno la Bwana. 6 Mfalme
akajibu, akamwambia yule mtu wa Mungu, Umsihi sasa Bwana, Mungu wako,
ukaniombee, ili nirudishiwe mkono wangu tena. Yule mtu wa Mungu akamwomba Bwana
mkono wa mfalme ukarudishwa tena, ukawa kama ulivyokuwa kwanza
Na ndivyo vivyohivyo, hata hawa manabii wenyewe inawapasa
kufuata maelekezo ya Mungu bila ya kuyaacha na kwenda mkono wa kushoto wala wa
kuume wa kile walichambiwa na kutakiwa kukifanya. Nabii huyu aliambiwa wazi
kabisa kile akachokifanya kuhusu jambo hili kama tunavyojionea kutoka kwenye
aya ya 9.
1Wafalme
13:7-10 Mfalme
akamwambia mtu wa Mungu, Karibu nyumbani kwangu ujiburudishe, nami nitakupa
thawabu. 8 Mtu wa Mungu akamwambia mfalme, Ujaponipa
nusu ya nyumba yako, sitaingia pamoja nawe, wala sitakula chakula, wala
sitakunywa maji mahali hapa; 9 maana ndivyo
nilivyoagizwa kwa neno la Bwana, kusema, Usile chakula cho chote wala usinywe
maji, wala usirudi kwa njia ile uliyoijia. 10 Basi
akaenda zake kwa njia nyingine, wala hakurudi kwa njia ile aliyoijia Betheli.
Wakati nabii anapokuwa na ujumbe kutoka kwa Mungu
anatakiwa kutii hata kama nabii mwingine akimwambia kuwa ana maelekezo mengine
aliyoyapokea amayo yapo kinyume na na yale aliyoyapokea kwa Bwana. Kwenye tukio
hili, tunaona kwamba nabii aliponzwa na mmoja wa manabii wenzake.
1Wafalme
13:13-32 Akawaambia
wanawe, Nitandikieni punda. Wakamtandikia punda, naye akampanda. 14 Akamfuata mtu wa Mungu, akamkuta ameketi chini ya
mwaloni, akamwambia, Je! Wewe ndiwe yule mtu wa Mungu aliyetoka katika Yuda?
Akamwambia, Mimi ndiye. 15 Akamwambia, Karibu kwangu
nyumbani, ule chakula.16 Naye akamwambia, Siwezi
kurudi pamoja nawe, wala kuingia pamoja nawe; wala sili chakula wala sinywi
maji pamoja nawe hapa; 17 kwani nimeambiwa kwa neno la
Bwana, Usile chakula wala usinywe maji huko, wala usirudi kwa njia ile
uliyoijia. 18 Akamwambia, Mimi nami ni nabii kama
wewe, na malaika akaniambia kwa neno la Bwana, kusema, Mrudishe pamoja nawe
nyumbani kwako, ale chakula, akanywe maji. Lakini alisema uongo. 19 Basi mtu yule akarudi pamoja naye, akala chakula, akanywa
maji nyumbani mwake. 20 Hata ikawa, walipokuwa
wameketi mezani, neno la Bwana likamjia nabii yule aliyemrudisha; 21 akamlilia yule mtu wa Mungu aliyetoka katika Yuda, akinena,
Bwana asema hivi, Kwa sababu umeiasi kauli ya Bwana, wala hukuishika amri ile
aliyokuamuru Bwana, Mungu wako, 22 bali umerudi, ukala
chakula ukanywa maji, hapo alipokuambia, Usile chakula, wala usinywe maji;
maiti yako haitaliingia kaburi la baba zako. 23 Basi
ikawa, alipokwisha kula chakula na kunywa maji, yule nabii aliyemrudisha
akamtandikia punda. 24 Na alipokuwa amekwenda zake,
simba alimkuta njiani, akamwua. Maiti yake ikatupwa njiani, na yule punda
akasimama karibu naye; na yule simba naye akasimama karibu na maiti. 25 Na tazama, watu wakapita, wakauona mzoga umetupwa njiani,
na yule simba akisimama karibu na mzoga, wakaenda, wakatoa habari katika mji
ule alimokaa yule nabii mzee. 26 Na yule nabii
aliyemrudisha njiani alipopata habari, akasema; Ndiye yule mtu wa Mungu,
aliyeiasi kauli ya Bwana; kwa hiyo Bwana amempambanisha na simba, simba
akamrarua, akamwua, sawasawa na neno la Bwana alilomwambia. 27
Akawaambia wanawe, akasema, Nitandikieni punda. Wakamtandikia. 28 Akaenda, akamwona yule maiti ametupwa njiani, na punda na
simba wamesimama karibu na maiti; yule simba alikuwa hakumla maiti, wala
hakumrarua punda. 29 Nabii yule akamtwaa maiti wa yule
mtu wa Mungu, akamweka juu ya punda wake, akamrudisha; yule nabii mzee akaenda
mjini mwake, kukaa matanga, na kumzika. 30 Akamweka
maiti katika kaburi lake mwenyewe; wakamlilia, wakisema, Aa! Ndugu yangu! 31 Hata ikawa, alipokwisha kumzika, akawaambia wanawe,
akasema, Nikifa mimi, nizikeni katika kaburi hili alimozikwa yule mtu wa Mungu;
iwekeni mifupa yangu kando ya mifupa yake. 32 Kwa
maana neno hilo alilolia juu ya madhabahu katika Betheli, kwa neno la Bwana, na
juu ya nyumba zote za mahali pa juu zilizo katika miji ya Samaria, hakika
litatimizwa.
Nabii huyu wa Israeli alikuwa anamjaribu nabii kutoka
Yuda ili ajue kama kile alichokuja kukisema kilikuwa kweli. Ukweli ni kwamba
alisema uwongo na ilimgharimu kupoteza uhai wa huyu nabii mgeni na
kilichomsababisha kufanya hivyo ilikuwa ni kutafuta uhakika wa ujumbe wake.
Hata hivyo, ilikuwa ni kweli na majesho yalifanyika vizuri sana na Yosia ambaye
alitajwa na kuchaguliwa na Mungu na kuahidiwa kama mtoto atakaye tawala na
kuwarejesha Israeli kutoka Nyumba ya Daudi.
Baada ya mwinsho wa kipindi hiki cha kutisha kwa ibada za
sanamu kwa pande zote mbili, yaani Israeli na Yuda, mfalme wa Yuda alikuwa
Manase na huyu sio tu kuw3a aliwaongoza na kuwapelekesha Yuda kuabudu sanamu,
bali alimwaga sana damu ya wasio na hatia na kuijaza Yerusalemu kwa damu kutoka
mmoja hadi mwingine (2Wafalme 21:16). Alikufa na Amoni mtoto wake
akatawala mahala pake na alifanya hayohayo.
2Wafalme
21:19-26 Amoni alikuwa
na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala; akatawala miaka miwili
huko Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Meshulemethi, binti Haruzi wa
Yotba. 20 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, kama
Manase babaye alivyofanya. 21 Akaiendea njia yote
aliyoiendea baba yake, akazitumikia sanamu alizozitumikia baba yake,
akaziabudu. 22 Akamwacha Bwana, Mungu wa babaze, wala
hakuiendea njia ya Bwana. 23 Nao watumishi wa Amoni
wakafanya fitina juu yake, wakamwua mfalme ndani ya nyumba yake mwenyewe. 24 Lakini watu wa nchi wakawaua wote waliofanya fitina juu
yake mfalme Amoni, watu wa nchi wakamfanya Yosia mwanawe awe mfalme mahali
pake. 25 Basi mambo yote ya Amoni yaliyosalia,
aliyoyafanya, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda? 26 Akazikwa kaburini mwake katika bustani ya Uza. Na Yosia
mwanawe akatawala mahali pake.
Jina Amoni linaloonekana hapa (linamaana ya
fundi au mtu aliyeandaliwa kwa kufundishwa ufundi wa kazi za
mokono) aliuawa na watumishi wake. Watu walioonekana wanependekezwa
kumrithi Amoni kutoka kwenye mnyororo wa uzao wake, hatimaye waliwaua wale
mtumishi.
Kwa hiyo, hapa unabii unaanzia. Mtoto anaketishwa kwenye
kiti cha enzi na Mungu na hatimaye anaanza kufanya kazi naye.
2Wafalme
22:1-2 Yosia alikuwa na umri
wa miaka minane alipoanza kutawala; akatawala miaka thelathini na mmoja katika
Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Yedida, binti Adaya wa Bozkathi. 2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, akaenda katika njia
yote ya Daudi baba yake, wala hakugeuka upande wa kuume wala wa kushoto.
Mfalme aliwekwa kwa namna iliyo kwenye mpango wa Mungu
kutoka kipindi cha ujana wake na wala hakukengeuka wala kupotoka. Aliandaliwa ili
atumike kwa namna hii na wakati ulionyesha njia ya namna atakavyoifanya kazi
hii.
Katika mwaka huu wa kumi na nane wa kutawala kwake,
alitumiwa na Mungu akiwa na umri wa kiujana wa miaka ishirini na tano, ukiwa ni
mwaka muafaka kwake kuwekwa kwenye huduma ya hekaluni kama alivyofanya Hezekia
kipindi cha matengenezo yake (sawa na jarida la Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. [Sanctification of the
Temple of God (No. 241)].
Kwa hiyo Yosia alitumika tangu alipokuwa na umri wa miaka
25, katika mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake. Mungu alimtumia kwa njia
hii:
2Wafalme
22:3-13 Ikawa, katika mwaka
wa kumi na nane wa mfalme Yosia, mfalme akamtuma Shafani, mwana wa Azalia,
mwana wa Meshulamu, mwandishi, nyumbani kwa Bwana, akisema, 4
Enenda kwa Hilkia, kuhani mkuu, ili aihesabu fedha yote inayoletwa
nyumbani mwa Bwana, ambayo mabawabu wameipokea kwa watu; 5 tena
waitie ile fedha katika mikono ya wafanya kazi wanaoisimamia nyumba ya Bwana;
wakapewe wafanya kazi waliomo ndani ya nyumba ya Bwana, ili wapate
kupatengeneza mahali palipobomoka ndani ya nyumba; 6 wapewe
maseremala, na wajenzi, na waashi; ili kununua miti na mawe yaliyochongwa
wapate kuitengeneza nyumba. 7 Lakini hawakuulizwa
habari za ile fedha waliyokabidhiwa; maana walitenda kazi kwa uaminifu. 8 Naye Hilkia, kuhani mkuu, akamwambia Shafani, mwandishi,
Nimekiona kitabu cha torati katika nyumba ya Bwana. Hilkia akampa Shafani kile
kitabu, naye akakisoma. 9 Shafani mwandishi akamwendea
mfalme, akamletea mfalme habari tena, akasema, Watumishi wako wamezitoa zile
fedha zilizoonekana ndani ya nyumba, nao wamewakabidhi wafanya kazi
wanaoisimamia nyumba ya Bwana. 10 Kisha Shafani
mwandishi akamwambia mfalme, akasema, Hilkia kuhani amenipa kitabu. Shafani akakisoma
mbele ya mfalme. 11 Ikawa, mfalme alipokwisha
kuyasikia maneno ya kitabu hicho cha torati, alirarua nguo zake. 12 Mfalme akamwamuru Hilkia kuhani, na Ahikamu, mwana wa
Shafani, na Akbori, mwana wa Mikaya, na Shafani mwandishi, na Asaya, mtumishi wa
mfalme akasema, 13 Enendeni, mkamwulize Bwana kwa
ajili yangu, na kwa ajili ya watu hawa, na kwa ajili ya Yuda yote, katika
habari za maneno ya kitabu hiki kilichoonekana; kwa kuwa hasira ya Bwana ni
kubwa aliyotukasirikia, kwa sababu baba zetu hawakuyaangalia maneno ya kitabu
hiki, kufanya kama hayo yote tuliyoandikiwa.
Mungu aliweka moyoni mwa Yosia ni na moyo wa kimtii.
Wakati Yosia alipoona kwamba Yuda walikuwa hawazitii Sheria za Mungu, aliweza
kuchukua hatua kuishughulikia hali na taarifa ile aliyoipata na kutubu na
kufanya mabadiliko muhimu yanayohitajika kurejea kwa Mungu na kwenye Torati
yake.
Alijua kwamba kama hawataonyesha toba Mungu
angewaangamiza. Kwa kupitia kwa washauri wake, ndipo walitafuta ushauri kutoka
kwa manabii.
2Wafalme
22:14-20 Basi Hilkia kuhani,
na Ahikamu, na Akbori, na Shafani, na Asaya, wakamwendea Hulda, nabii mke,
mkewe Shalumu, mwana wa Tikva, mwana wa Harhasi, mtunza mavazi ya mfalme; (naye
alikaa Yerusalemu katika mtaa wa pili;) wakasema naye. 15 Akawaambia,
Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi; Mwambieni mtu yule aliyewatuma ninyi
kwangu, 16 Bwana asema hivi, Tazama, mimi nitaleta
uovu juu ya mahali hapa, na juu yao wakaao hapa, naam, maneno yote ya kitabu
alichokisoma mfalme wa Yuda; 17 kwa sababu wameniacha
mimi, wameifukizia uvumba miungu mingine, ili wapate kunikasirisha kwa kazi
yote ya mikono yao; kwa hiyo hasira yangu itawaka juu ya mahali hapa,
isizimike. 18 Lakini yule mfalme wa Yuda, aliyewatuma
ninyi kumwuliza Bwana, mtamwambia hivi, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi,
Kwa habari ya maneno yale uliyoyasikia, 19 kwa kuwa
moyo wako ulikuwa mwororo, nawe ukajinyenyekesha mbele za Bwana, hapo
ulipoyasikia maneno niliyoyanena juu ya mahali hapa, na juu ya wenyeji wake, ya
kwamba watakuwa ukiwa na laana, nawe ulizirarua nguo zako, ukalia mbele zangu;
basi, mimi nami nimekusikia wewe, asema Bwana. 20 Kwa
hiyo tazama, nitakukusanya pamoja na baba zako, nawe utawekwa kaburini mwako
kwa amani; wala macho yako hayatauona uovu huo wote nitakaouleta juu ya mahali
hapa. Basi wakamletea mfalme habari tena.
Kwa toba ya wazi ya viongozi uovu ulikuwa umezuiwa kwa
mtazamo unaoonekana. Kwa hiyo Yosia alichukua hatua kwa imani kwa maneno ya
manabii na Torati ya Mungu.
Kutokana na sura ya 23 tunaona kiusahihi sana kwamba
kunajisika kwa Israeli kulikuwepo. Ilikuwa ni imani ya kuabudu jua ya
Wababelonia na Wamisri, kama tunavyojionea kutoka pale Sinai kama
walivyoonekana kama Ndama wa Dhahabu (soma jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222) [The Golden Calf (No. 222)]. Imani
hii bado inaendelea karika Israeli na kwa watu wetu na itasababisha maangamizo
yetu (sawa na jarida la Chimbuko la Krismas na Uaster
(Na. 235) [The Origins of Christmas and Easter (No. 235)].
Tunaona ia kutoka kwenye maandiko kwamba kipindi hiki
kilikuwa ni kile cha kuelekea kwenye maadhimisho ya Pasaka lakini hii haikuwa
ni Pasaka ya kawaida. Jina Yosia kwa kweli linaandika na kutamkwa Yo’shiYah (SHD
2977) maana yake ni Aliyeanzisha na Yah au Zawadi au Kipawa
cha Yah au linatokana na shina la neno asa, maana yake ni uponyaji
wa Yah. Unabii huu ulifanywa ili tuweze kuona kwamba marejesho haya
yalianzishwa au yalifanywa na Yah. Kama jina la Yah lilivyo la umoja linalotokana
na jina Yahova linalotumika kwa matumizi ya uwingi.
Kutokana na marejesho haya Hekalu pia lilisafishwa au
kutakasika kutoka kwenye machukizo na machafu yake.
2Wafalme
23:1-20 Kisha, mfalme
akatuma wajumbe, nao wakamkusanyia wazee wote wa Yuda na wa Yerusalemu. 2 Mfalme akapanda kwenda nyumbani kwa Bwana, na watu wote wa
Yuda, nao wote waliokaa Yerusalemu, pamoja naye, na makuhani, na manabii, na
watu wote, wadogo kwa wakubwa; akasoma masikioni mwao maneno yote ya kitabu cha
agano kilichoonekana katika nyumba ya Bwana. 3 Mfalme
akasimama karibu na nguzo, akafanya agano mbele za Bwana, kumfuata Bwana, na
kuyashika maagizo yake, na shuhuda zake, na amri zake, kwa moyo wake wote, na
kwa roho yake yote, na kuyathibitisha maneno ya agano hilo yaliyoandikwa katika
kitabu hicho; nao watu wote wakalikubali agano lile. 4 Kisha,
mfalme akamwamuru Hilkia, kuhani mkuu, na makuhani wa daraja ya pili, na
walinzi wa mlango, kwamba watoe katika hekalu la Bwana vyombo vyote
vilivyofanywa kwa ajili ya Baali, na kwa ajili ya Ashera, na kwa ajili ya jeshi
lote la mbinguni; akavipiga moto nje ya Yerusalemu, katika mashamba ya Ridroni,
akayachukua majivu yake mpaka Betheli. 5 Akawaondosha
wale makuhuni walioabudu sanamu, ambao wafalme wa Yuda waliwaweka ili kufukiza
uvumba katika mahali pa juu, ndani ya miji ya Yuda, na katika kila mahali,
pande zote za Yerusalemu; na hao pia waliomfukizia uvumba Baali, na jua, na
mwezi, na sayari, na jeshi lote la mbinguni. 6 Naye
akaiondoa Ashera katika nyumba ya Bwana, nje ya Yerusalemu, mpaka Kidroni,
akaipiga moto penye kijito cha Kidroni, na kuiponda-ponda iwe mavumbi,
akayatupa mavumbi yake juu ya makaburi ya watu. 7 Akaziangusha
nyumba za mahanithi, waliokuwamo nyumbani mwa Bwana, wanawake walipofuma
mapazia ya Ashera. 8 Akawatoa makuhani wote katika
miji ya Yuda, akapanajisi mahali pa juu, makuhani walipokuwa wamefukiza uvumba,
tangu Geba hata Beer-sheba; akapavunja mahali pa juu pa malango, palipokuwapo
penye kuingia lango la Yoshua, liwali wa mji, palipokuwa upande wa kushoto wa
mtu langoni pa mji. 9 Walakini hao makuhani wa mahali
pa juu hawakupanda madhabahuni kwa Bwana katika Yerusalemu, bali wakala mikate
isiyo na chachu katikati ya ndugu zao. 10 Naye
akainajisi Tofethi, iliyomo katika bonde la wana wa Hinomu, ili mtu asipitishe
mwana wake au binti yake motoni kwa Moleki. 11 Akawaondoa
farasi ambao wafalme wa Yuda waliwatoa kwa jua, hapo pa kuingia nyumbani mwa
Bwana, karibu na chumba cha Nathan-Meleki, towashi, kilichohuwako kiungani;
akayapiga moto magari ya jua. 12 Nazo madhabahu
zilizokuwako darini juu ya chumba cha juu cha Ahazi, wafalme wa Yuda
walizozifanya, nazo madhabahu alizozifanya Manase katika behewa mbili za nyumba
ya Bwana, mfalme akazivunja, akazitelemsha huko nje, na kuyatupa mavumbi yake
katika kijito cha Kidroni. 13 Na mahali pa juu
palipokuwapo mbele ya Yerusalemu, palipokuwa upande wa kuume wa mlima wa
uharibifu, alipopajenga Sulemani, mfalme wa Israeli, kwa Ashtorethi, chukizo la
Wasidoni, na Kemoshi, chukizo la Moabu, na Milkomu, chukizo la wana wa Amoni,
mfalme akapanajisi. 14 Akazivunja-vunja nguzo,
akayakata-kata maashera, akapajaza mahali pake mifupa ya watu. 15 Tena zaidi ya hayo, ile madhabahu iliyokuwako Betheli, na
mahali pa juu alipopafanya Yeroboamu, mwana wa Nebati, aliyewakosesha Israeli,
madhabahu hiyo aliibomoa; na mahali pa juu alipateketeza, akapaponda-ponda hata
pakawa mavumbi, akaiteketeza ile Ashera.
Utaratibu wote wa kuabudu Baali na Ashtorethi unaoendana
ma ibada za Easter na imani ya kumuabudu Venus ajulikanaye pia kama Nyota ya Alfajiri
na Mungu Mwezi aliyeitwa Sin au Molkom na Kemoshi na kuabudu Dume la
Ng’ombe aliyechinjwa na dini ya kuabudu
jua; imani tunazoziona wazi kuwa zilikuwepo kwa Waaryani na hata siku hizi bado
zinaendelea huko Ulaya kwenye vizazi vyao. Kilichofuatia kutoka kwenye imani au
dini hii ilikuwa ni dini au ibada zilizofanywa kwa matendo ya uasherati na
matendo ya ufiraji ambayo yaliletwa na kufanyika hata kwenye hekalu hili la
Mungu. Gari la farasi la Apollo na Sanamu lake lililokutikana pande za
kaskazini na huko Ulaya zilikuwa hapa Sayuni na Hekaluni.
Dini au imani yote ya Waashuru/Wababeloni tunayoiona sasa
kushamiri huko Ulaya iliendelezwa miongoni mwao na walizidisha umuhimu au
kuwazidishia mziho Waashuru. Ilikuwa imevutia kiasi kwamba watu hawakugundua kwamba
imani yao ilikuwa ni harufu ichukizayo kwenye mianzi ya pua ya Mungu. Wamekuwa
wakiabudu kwa namna hiyo kwa kipindi cha karne kadhaa za vipindi vtote viwili,
yaani cha kabla ya baada ya matengenezo ya Hezekia. Hawakujua au hawakupenda
kujua kwamba walikuwa ni waabudu sanamu na kwamba walikuwa kwenye hatari ya
uharibifu au kuangamizwa. Na hii ndiyo hasa imani iliyoko leo. Makasisi wanajua
na hawapendi kusema ukweli na watu wanaangamia kwa kukosa maono. Kwa ajili hii
ndipo Yosia aliona umuhimu wa kufanya matengenezo. Mungu alimtumia alipofikia
kipindi cha umri muafaka kwa mujibu wa torati kama alivyomtumia Hezekla hapo
nyuma kabla yake.
Ni wazi sana pia kwamba Mungu alisaidia imani ya Yosia na
kuwadhoofisha Waashuru wasiweze kuimiliki Yuda kwa kadiri alivyoenenda katika
kweli na kuishika Torati ya Mungu.
16
Naye Yosia alipogeuka,
aliyaona makaburi yale yaliyokuwako huko, juu ya mlima; akatuma watu, akaitoa
ile mifupa katika yale makaburi, akaiteketeza juu ya madhabahu, akainajisi,
sawasawa na lile neno la Bwana, alilolinena yule mtu wa Mungu, aliyetamka mambo
hayo. 17 Kisha akasema, Ni kumbukumbu la nani, hili
ninaloliona? Na watu wa mji wakamwambia, Ni kaburi la yule mtu wa Mungu,
aliyetoka Yuda, akayanena mambo hayo uliyoyatenda wewe juu ya madhabahu ya
Betheli. 18 Akasema, Mwacheni; mtu awaye yote
asiiondoe mifupa yake. Basi wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya yule
nabii aliyetoka Samaria. 19 Na nyumba zote pia za
mahali pa juu palipokuwa katika miji ya Samaria, wafalme wa Israeli
walizozifanya, ili kumkasirisha Bwana, Yosia aliziondoa, akazitenda kwa mfano
wa mambo yote aliyoyatenda katika Betheli. 20 Akawaua
na makuhani wote wa mahali pa juu waliokuwako huko, juu ya madhabahu,
akateketeza mifupa ya watu juu yake; kisha akarejea Yerusalemu.
Yosia alifanya kile alichoamriwa na Mungu kukifanya kuhusu
Makuhani hawa wanaopendezwa na matendo ya Kisodoma. Aliwauilia mbali. Unabii
ulitimilika na ilijulikana kwamba ni mwendelezo kutoka kipindi ambacho
ilifanvika hivyo kilikamilika.
Kipindi cha marejesho
Kipindi cha marejesho kina maana sana. Yosia
alitawala katika Yuda tangu mwaka 640-609 KK.
Yosia alianza kumtafuta Mungu wa Baba yake Daudi kuanzia
mwaka wa nane wa utawala wake (yapata takriban mwaka 632 KK kama inavyosema 2Nyakati
34:3a). Mungu aliwapa thawabu kwa imani yao kwa kuwadhoofisha Waashuru
wasiyamiliki majimbo ya pande za Kusini na Magharibi (sawa na kamusi inayoitwa Interpreters
Dictionary of the Bible, art, “Josiah”, vol. 2, p. 997). Hii iliimarisha
uwezo wake na nguvu iliyoendelea hadi mwaka 628.
Katika mwaka wa ishirini wa kutawala kwake (yapata mwaka 628
KK), (sawa na pale alipofikia umri wa utu uzima wa miaka ishirini), alianza
kuwatakasa Yuda na Yerusalemu (2Nyakati 34:3b-5).
2Nyakati
34:3-5 Kwa kuwa katika
mwaka wa nane wa kutawala kwake, naye akali mchanga, alianza kumtafuta Mungu wa
Daudi babaye; hata katika mwaka wa kumi na mbili akaanza kusafisha Yuda na
Yerusalemu kwa kuondoa mahali pa juu, na kwa kuondoa maashera, na sanamu za
kuchora, nazo za kusubu. 4 Wakazibomoa madhabahu za
mabaali machoni pake; na sanamu za jua, zilizoinuliwa juu yake, akazikata-kata;
na maashera, na sanamu za kuchonga, nazo za kusubu, akazivunja-vunja,
akaziponda kuwa mavumbi, akayamimina juu ya makaburi ya hao waliozichinjia
dhabihu. 5 Akaiteketeza mifupa ya makuhani madhabahuni
mwao, akasafisha Yuda na Yerusalemu.
Baada yah ii ndipo alieneza juhudi zake kwenye maeneo ya
masalio ya Manase, Efraimu na hata kwa Wanaftali.
2Nyakati 34:6-7 Na katika miji ya Manase, na
Efraimu, na Simeoni, mpaka Naftali, akafanya vile vile; na katika maganjo yake
pande zote. 7 Akazibomoa madhabahu, akaponda-ponda
maashera na sanamu kuwa mavumbi, akazikata-kata sanamu zote za jua katika nchi
yote ya Israeli, kisha akarejea Yerusalemu.
Kwa kuonekana Kitabu
cha Torati hekaluni, katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake (mwaka 622)
alifanya matengenezo makubwa ya kidini ambayo yalikuwa na dalili za mamlaka ya
utawala wa nchi pia (2Nyakati 34:8-35:19; sawa na kamusi ya Interp.
Dict., ibid.).
Habari iliyoko kwenye vitabu vya Nyakati inasema kwamba
Manase ameziondoa sanamu na alama zote za ibada za Waashuru na inaeleza tu kuwa
ni Wakanaani ndio walioondolewa na Yosia nah ii inaonekana kuwa ndiyo yaliyomo
kwenye 2Wafalme ambapo Yosia anasemekana kuwa aliwaondoa wengi. Jibu liko wazi
kabisa.
Manase mwana wa Hezekia aliwaongoza kwene toba lakini
hayakuwa marejesho na Amoni na maongozi yalichukua mkondo wake na ni kwa
sababu hii ndiyo maana aliuawa (sawa na 2Nyakati 33:23).
Matukio yaliyo kwenye 2Wafalme haya0tangui mchakato wa
matengenezo kama tunavyoona kwenye vitabu vya Nyakati. Inaonekana kwenye
matukio mawili kutoka kwenye mwaka wa kumi na nane iliyotangulia kuelekea
kwenye miji ya Samaria. Jibu hapa ni kwamba mchakato huu kwa kweli ulikuwa
haujafanikiwa kabisa hadi katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake. Miji ya
Samaria kwa kipindi hiki ilikuwa pia imekajiwa na Wacutheans na Wamedi
ambao waliwekwa na Waashuru (tazama jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na.
13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No.
13)] na utakaso huu haukuwa na nguvu sana
hadi mwaka 622 KK.
Kulikuwa na matukio kadhaa yaliyohitaji kutimilizwa kwa
muunganiko na marejesho na ni Mungu tu ndiye angeweza kulifanya hilo.
Mwanzo wa kudhoofika kwa nguvu za Waashuru ulikuwa ni
kifo cha mfalme Assurbanipal ambayo inaweza kuaminika ilikuwa mwaka 630 KK (Interp.
Dict., ibid.). kwa mujibu wa Vitabu
Vya Historia ya Waashuru, Babeli ilifanya uasi dhidi ya Waashuru na
wakamuweka Nabopolassa kwenye kiti cha enzi cha ufalme, ambaye alikuwa ni mtu
wa Babeli, siku inayodhaniwa kufantika tukio hili ni Novemba 22/23 626 KK. Kwa
kipindi cha takriban mwaka mmoja kumeandikwa kuwa “kulikuwa hakuna mfalme katika
nchi” (ibid).
Kwa hiyo, kutokana na matendo yaliyomaanisha ya Yosia
ndipo tunayaona matukio mbalibali yakitokea wakati Assurbanipal alipokufa, dola
ya Ashuru ikizidi kudhoofika na kulikuwa hakuna mfalme katika nchi mwaka 627 KK.
Katika mwaka huu Ashuru ilikuwa imekumbwa na matukio au mikasa kutoka Mashariki
na Mungu kwa kweli alikuwa amewaondolea ushawishi wao kwa Yuda upande wa kusini
magharibi akimuandaa Yosia kuanzisha mchakato wa ukombozi au kupata uhuru
uliopelekea marejesho ya mwaka
622.
Mwaka wa Yubile ulikuwa ni ule wa 624 KK. Mchakato wa
marejesho ulikuwa mrefu maandalizi yake. Marejesho ya Hezekia yanaweza pia kuwa
ya muhimu kwenye maandalizi ya kukilinda Kitabu
cha Torati na dira ya kuelekea kwene marejesho. Hii huenda ilikutikana kwenye
matengenezo ya Hezekia (mwaka 715-687 KK)
yaliyofanywa na Hilkia. Inadhaniwa kuwa kuna baadhi ya watu walioandaliwa wakati
wa utawala wa Manase, miaka hamsini iliyotangulia (Interp. Dict. ibid.
p. 997). Kwa hiyo, mchakato wa marejesho ulikuwa sawa sawa. Hezekia alianza
marejesho yake siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wa mwaka mtakatifu 715/14 wakati
alipoanza pia kutawala. Marejesho haya yalianza mwaka wa tisa wa wa mzunguko wa
Yubile iliyopita. Haikuwa na uhusiano na Yubile bali ilikuwa na umuhimu wake
kwenye marejesho yalitofuatia yaliyochukua mahala pake miaka tisini na moja
iliyofuatia.
Maswali makubwa pia hapa ni kwamba: Nabii Yeremia alikuwa
wapi wakati huu wa marejesho? Ni kwa nini walikuwa wanamuuliza nabii mdogo
wakati nabii mkuu sana wa Israeli kipindi kile alikuwa yu hai bado? Jibu halisi
ni kwamba Yeremia hakuwepo. Hili ni jambo jingine. Alikuwa na hili tu kusema kuhusu
Yosia alipokuwa ananena kuhusu Yosia alipokuwa anamwambia Yehoyakimu mwana wa
Yosia, yafuatayo:
Yeremia 22:15-16 Je! Utatawala kwa sababu unashindana na
watu kwa mierezi? Baba yako, je! Hakula na kunywa, na kufanya hukumu na haki?
Hapo ndipo alipofanikiwa. 16 Alihukumu
maneno ya maskini na mhitaji; hapo ndipo alipofanikiwa. Je! Huku siko kunijua,
asema Bwana?
Nabii Sefania anaaminika pia kuwa alikuwepo nayeye pia hakuulizwa
wala kuombwa ushauri.
Ni kutokana na
marejesho haya ya Yosia ndyo wanazuoni wa siku hizi wanadai kuwa ilikuwa ni
kitabu cha Kumbukumbu la Torati na kazi ya wanazuoni na Waandishi wa Kitabu cha
Torati kuwa viliandika kuanzia mwaka 560 KK (ibid., na sawa na jarida la Biblia (Na 164) [The Bible (No. 164)].
Sababu iliyoko nyuma ya mtazamo huu ni maelezo ya kina ya
vitabu vya Nyakati dhidi ya maelezo yaliyo kwenye 2Wafalme. Kwa kweli, marejesho
yaliyofanywa chini ya usimamizi wa Hezekia yalichukuliwa kutoka kanuni halisi
ya Maandiko Matakatifu hata kwenye Mithali za Sulemani (sawa na Interp. Dict.ibid., art.
“Hezekiah”, p. 598). Kazi ya Waandishi kwenye marejesho. Kulikuwa na mambo
mawili muhimu kwenye matcngenezo yaliyotangulia Yubile iliyokuwa kipindi cha
Yosia na marejesho ya kila mara kwenye mwaka wa kwanza wa Yubile mpya. Kwa
marejesho haya kulikuwa na kiwango kikubwa cha harakati kuwepo kwa kipindi cha
miaka mingi iliyokuwa kwenye Yubile zilizopita. Harakati hizi zenyewe zilifuatia
kutoka na juhudi kubwa zilizofanywa kwenye Yubile iliyopita ya kipindi cha
Hezekia na harakati au juhudi nyingine zilizofanywa na Manase kwenye kipindi
chake cha kuwaongoza watu kwenye ukengeufu na kurudi nyumba kwa kuiacha imani
ya kweli.
Tunachokiona hapa ni kwamba ukweli ni kwamba hakukuwa na Pasaka
iliyochelewa na utakaso wa hekalu kwa kweli ulikuwa mkubwa kwa kiasi kikubwa
sana. Kipindi cha mpito kilikuwa cha muhimu ili kujua kile kilichotokea.
Tangu mwaka 633/32 KK, mwaka mmoja kabla ya ule wa Sabato (ambao
ungehusisha na usomaji wa torati ambayo haikuwa) na kupelekea kwenye mwaka wa
kwanza wa mzunguko wa mwisho wa mtaratibu wa Yubile. Yosia alianza kumfuata
Mungu na kurejesha imani. Hii ilihusisha kwanza kabisa, kulitiisha eneo ambalo
kwa kweli halikuwa kipindi cha Hezekia, kwa kuwa Israeli walikuwa wamepelekwa
mbali utumwani.
Yosia alifanya hivi hadi mwaka 628/27 KK, ambao ulikuwa ni mwaka
wa arobaini wa mzunguko. Mnamo mwaka wa 627/26, ambao ndio ulikuwa mwaka wa hamsini
wa mzunguko na wa mavuno makuu, aliisafisha nchi iliyokuwa na sanamu na
kuzichoma moto na kuzisaga hadi zikawa mavumbi. Katika miaka ya 625 na 624 kulikuwa
na mwaka wa Sabato na ni mwaka wa Yubile wa kuuadhimisha. Mwaka wa 623/22, mwaka
wa kurejea wa Yubile mpya, alianza marejesho. Huenda hii
ilianza baada ya kupigwa baragumu ya Yubile kwenye Siku ya Upatanisho ya mwaka 624.
Huu ulikuwa ni mwaka wa kumi na nane wa utawala wake. Kamusi ya the Interpreters
Dictionary (ibid., p. 997) inasema kwamba ulikuwa ni mwaka wa 622 ambao
inawezekana kuwa ni kutoka mwanzoni mwa utawala wake katika mwaka mtakatifu wa 640/39
KK.
Marejesho yalikuwa na kishindo kikubwa sana kama
tunavyoyaona kwenye hali ya utukufu wa hekalu. Mnamo siku ya 1 Nisan 623/2, ukiwa
ni mwaka wa kwanza wa Yubile Mpya, aliwasafisha Israeli na kuwarejesha kwenye
imani. Pasaka kwa mara nyingine tena ilikuwa imeanza Hekaluni na manabii wa
uwongo na waabudu sanamu waliondolewa au kuuawa.
Sikukuu ya Pasaka imeonyesshwa kwenye 2Nyakati 35:1-19.
2Nyakati
35:1-19 Naye Yosia akamfanyia
Bwana pasaka huko Yerusalemu; wakachinja pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi wa
kwanza. 2 Akawasimamisha makuhani katika malinzi yao,
akawatia moyo kufanya utumishi wa nyumba ya Bwana. 3 Akawaambia
Walawi, waliowafundisha Israeli wote, waliotakasika kwa Bwana, Wekeni sanduku
takatifu katika nyumba aliyoijenga Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli;
hamtakuwa tena na mzigo mabegani; sasa mtumikieni Bwana, Mungu wenu, na watu
wake Israeli. 4 Mkajiweke tayari kwa kadiri ya nyumba
za baba zenu, kwa zamu zenu, kama alivyoandika Daudi mfalme wa Israeli, na kama
alivyoandika Sulemani mwanawe. 5 Mkasimame katika
patakatifu, kama walivyogawanyika ndugu zenu, wana wa watu, kufuata nyumba za
mababa, kadiri ya mgawanyiko wa kila nyumba ya baba, ya Walawi. 6 Mkachinje pasaka, mkajitakase, mkawatengenezee ndugu zenu,
kutenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Musa. 7 Tena
Yosia akawapa wana wa watu, matoleo ya makundi, wana-kondoo na wana-mbuzi, yote
yawe kwa ajili ya matoleo ya pasaka, wote waliokuwako, wakipata thelathini
elfu, na ng'ombe elfu tatu; hao walitoka katika mali za mfalme. 8 Na wakuu wake wakawapa watu, na makuhani na Walawi matoleo
ya hiari. Hilkia na wana na Yehieli, wakubwa wa nyumba ya Mungu, wakawapa
makuhani, kuwa matoleo ya pasaka, wana-kondoo elfu mbili na mia sita, na
ng'ombe mia tatu. 9 Konania naye, na Shemaya, na
Nethaneli, ndugu zake, na Hashabia, na Yeieli, na Yozabadi, wakuu wa Walawi,
wakawapa Walawi, kuwa matoleo ya pasaka, wana-kondoo elfu tano, na ng'ombe mia
tano. 10 Hivyo huduma ikatengenezwa, wakasimama
makuhani mahali pao, na Walawi kwa zamu zao, kama alivyoamuru mfalme. 11 Wakachinja pasaka, nao makuhani wakamimina damu
waliyopokea mikononi mwao, Walawi wakachuna. 12 Wakaziondoa
sadaka za kuteketezwa, wawape wana wa watu, kama walivyogawanyika kufuata
nyumba za mababa, ili wamtolee Bwana, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha
Musa. Nao ng'ombe wakawafanya vivyo hivyo. 13 Wakaioka
moto pasaka kama ilivyo sheria; wakatokosa matoleo matakatifu vyunguni, na
masufuriani, na makaangoni, wakawachukulia upesi wana wa watu wote. 14 Baadaye wakajiandalia wenyewe, na makuhani; kwa sababu
makuhani, wana wa Haruni, walikuwa na kazi ya kutoa sadaka za kuteketezwa, na
mafuta hata usiku; kwa hiyo Walawi wakajiandalia wenyewe, na makuhani, wana wa
Haruni. 15 Nao waimbaji, wana wa Asafu wakasimama
mahali pao, kama alivyoamuru Daudi, na Asafu, na Hemani, na Yeduthuni mwonaji
wa mfalme; nao mabawabu walikuwa katika kila lango; hawakuhitaji kuondoka
katika huduma yao, kwa kuwa ndugu zao Walawi wakawaandalia. 16
Basi huduma yote ya Bwana ikatengenezwa siku ile ile, kuifanya pasaka,
na kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana, kama alivyoamuru
mfalme Yosia. 17 Wana wa Israeli waliokuwapo wakafanya
pasaka wakati ule, na sikukuu ya mikate isiyochachwa muda wa siku saba. 18 Wala haikufanyika pasaka kama ile katika Israeli tangu
siku za nabii Samweli; wala wafalme wa Israeli hawakufanya hata mmoja wao
pasaka kama ile Yosia aliyoifanya, pamoja na makuhani, na Walawi, na Yuda wote
na Israeli waliokuwapo, na wenyeji wa Yerusalemu. 19 Katika
mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake Yosia ikafanyika pasaka hiyo
Kuondoa kabisa hali ya kuabudu sanamu na kurudi nyuma au
kumuacha Mungu ilikuwa karibu ishindikane kwa kuwa watu walikuwa walikuwa
wamewekezwa ama kurithishwa ibada hizi za sanamu. Dini ya Israeli na Yuda
ilikuwa imeathirika sana kwa kuwa ilikuwa imeunganishwa na ibada za waabudu Jua
ya Waaryani kwa kipindi cha millennia baada ya kuanzishwa kwa Babeli na hata
kabla kipindi kilichokubalika cha gharika kuu.
Mataifa ya Ulaya bado yamezingirwa kwenye imani hizi za ibada
za sanamu na inaenea na kuelekea kwenye mapokeo ya Kiislamu na kwenye dini za
Mashariki na za Kimarekani. Fundisho tunalojifunza kutokana na matengenezo ya
Yosia ni umuhimu wa Kuinya dunia hii ya siku za mwisho na marejesho mapya
yatakayofanyika kipindi cha Masihi.
Kuanguka kwa WaaAshuru
Mungu hakuwa mbali na marejsho haya. Waashuru walikuwa wamekwishaonywa
na nabii Yona na walitubu kama Israeli walivyofanya kipindi cha Hezekia. Hata
hivyo, hawakubakia kuishi maisha ya toba na walirejea kwene inani za dini yao
ya uwongo na kuiingiza katika Israeli na Yuda baada ya wao kutumiwa na Mungu
kuwaadibisha Israeli kwa ajili ya ukengeufu wao huu.
Ufalme wa Babeli ulianza kupata nguvu ya Waashuru na
habari zilizo kwenye Vitabu vya Historian
a Mambo ya Wababelonia zinatoa taswira ya ufalme ule tangu mwaka 626-623 KK.
Mvinjiko ulifuatia kwenye habari zilizolandikwa kwenye mwaka 616 KK (Interp.
Dict., ibid., p. 997).
Mnamo mwaka 614 Ashuru iliangushwa na Cyaxares mfalme wa Wamedi. Mji ulianguka hata kabla ya kuwasili kwa Nabopolassa
lakini njama zilifanywa kati ya Wamedi na Wababelonia. Mwaka 612 Ninawi ulianguka
mikononi mwa majeshi ya ushirika na Waashuru wakaondolewa na kusukumiwa huko
Harani ambako Ashuruballit II alijaribu kuirejesha tena Dola ya Waashuru.
Alilazimishwa kuondoka huko Harani mwaka 610 licha ya kushurutishwa na Wamisri.
Wababeloni na Wamedi waliuteka mji na kuushikilia na kuulinda dhidi ya majeshi
yenye nguvu ya Waashuru na Wamisri mwaka 609 KK.
Yosia alikumbwa na mauti kwenye vita ya Megido.
Alijisikia msukumo kutoka ndani yake wa kwenda kupigana akijaribu kuwazuia
Wamisri waliokuwa wanaongozwa na Farao Neko aliyekuwa amekusanya majeshi kwenda
kupigana na Waashuru. Yosia huenda alikuwa anajaribu kuwasaidia Wababeloni
aliyewaona kuwa ni wa washirika muhimu. Yosia, hata pamoja na nguvu hizi zote
alizokuwa amepewa na Mungu, hakuweze kuyasikiliza maonyo aliyopewa na Mungu, hata
kupitia kwene mdomo au kinywa cha Neko mwenyewe. Bali alitafuta jinsi ya
kuingilia kati mapigano akienda kuwasaidia Wababeloni ambao walikuja kuwa
maadui na watakaoiangamiza Yuda na imani yake ya kidini kama ilivyotabiriwa huko
nyuma na na kama tuonavyo huko mbele na nabii Danieli (sawa na Danieli sura ya
2). Wamisri waliletwa na Mungu na aliwatumia ili kuandaa njia ya kulipeleka
taifa utumwani.
2Nyakati
35:20-27 Baada ya hayo
yote, alipokwisha Yosia kulitengeneza hekalu, Neko, mfalme wa Misri, akakwea
ili kupigana Karkemishi karibu na Frati; naye Yosia akatoka juu yake. 21 Lakini yeye akatuma kwake wajumbe, kusema, Ni nini niliyo
nayo mimi na wewe, Ee mfalme wa Yuda? Sikuja juu yako leo, lakini juu ya nyumba
niliyo na vita nayo; naye Mungu ameniamuru nifanye haraka; acha basi kumpinga
Mungu, aliye pamoja nami, asikuharibu. 22 Walakini
Yosia hakukubali kumgeuzia uso mbali, akajibadilisha apate kupigana naye,
asiyasikilize maneno ya Neko, yaliyotoka kinywani kwa Mungu, akaja kupigana
bondeni mwa Megido. 23 Nao wapiga upinde wakampiga
Yosia; naye mfalme akawaambia watumishi wake, Niondoeni; kwani nimejeruhiwa
sana.24 Basi watumishi wake wakamtoa garini, wakamtia
katika gari la pili alilokuwa nalo, wakamleta Yerusalemu; naye akafa, akazikwa
makaburini mwa babaze. Wakamlilia Yosia Yuda wote na Yerusalemu. 25 Naye Yeremia akamlilia Yosia; na waimbaji wote waume kwa
wake wakamtaja Yosia katika maombolezo yao, hata leo; hata wakayafanya kuwa ada
kwa Israeli; nayo, tazama, yameandikwa katika maombolezo. 26 Basi
mambo yote ya Yosia yaliyosalia, na matendo yake mema, sawasawa na yote
yaliyoandikwa katika torati ya Bwana, 27 na mambo
yake, ya kwanza na ya mwisho, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa
Israeli na Yuda.
2Wafalme 23:29 inasema kuwa aliuawa na watumishi wake na
wakamchukua hadi Yerusalemu ambako alizikwa. 2Nyakati inaonyesha kwamba
alijeruhiwa vibaya sana mapiganoni na watumishi wake walimchukua kumrudisha
Yerusalemu na Yuda wote na Yerusalemu walimuombolezea
Yosia (2Nyakati 35:24). Jibu halisi kutokana na mgogoro wowote hapa ni
kwamba alikuwa amejeruhiwa sana na alifariki alipokuwa anarudi Yerusalemu.
Yosia aliandaliwa ayatangaze na kuyaweka kuwa sheria ya
nchi matengenezo lakini unabii ulikuwa umeisha mtaja kuwa atakuwepo. Mungu
alikuwa anakwenda kuwaacha Yuda waende utumwani kwa ababu ya kujiuza kwao
kuabudu sanamu, na imani ya dini yao ya uwongo. Imani ile bado inaendelea
kudumu hapa duniani na ni dini inayojulikana na kuwa na watu wengi zaidi na ni
imani iliyoenea na kujulikana sana hapa duniani.
Mungu analeta mabadiliko au mageuzi makubwa na matengenezo,
yaliyo makubwa zaidi ya haya marejesho ambayo tumepewa kwa mfano wetu. Israeli
walikwenda utumwani Ashuru yapata kama mwaka 721 KK. Yuda walitubu na ilisalia
na kulindwa lakini wakaingia au kuangukia kwenye ibada za sanamu na wakawafuata
wenzao Israeli miaka takriban ishirini na tano baada ya Yubile iliyotangulia marejesho
ya Yosia. Tangu Yubile ya mwaka 724 KK Israeli walichukuliwa utumwani ili
kwamba tangia mwaka 721 wawe kuwa ni taifa lililo utumwani. Tangu mwaka 715 Mungu
aliwarejesha Yuda ili kwamba utumwa wa Yuda uwe umechelewa na Yuda waweze
kutengwa mbali na tofauti na ndugu zao Israeli. Yuda hawakushindwa vita hadi
kipindi cha kuanguka kwa dola ya Waashuru na tangu mwaka 612 KK tunawaona
Waashuru na Wahiti na makabila yao washirika wakipotea kutoka kwenye matukio na
nafasi yao ikichukuliwa na Wababeloni na Wamedi na Waajemi.
Harakati zilizokuweko kwenye karne ya nane KK zinaendana
na zile za karne ya ishirini inayotuongoza kuelekea kwenye maadhimisho ya
Yubile ya mwaka 2027/28. Wababeloni walichukua madaraka chini ya Nebukadneza
kwenye vita ya Karkemish mwaka 605 KK. Mnamo mwaka 525 wakiwa chini ya Cambyses
waliutwaa Misri na wakawa ni watawala au dola yenye nguvu. Utaratibu huu ulipaswa
uishie kwa nyakati saba au miaka 2520 hadi kufikia mwaka 1996.
Tangu mwaka 632 KK nguvu za utawala wa Waashuru ilianza
kuharibiwa na kwa kipindi cha zaidi ya miaka ishirini na saba, Ashuru
iliangamiazwa na Babeli ilianza. Ili kufanikisha hili, vita viliwadhoofisha
Israeli na walipelekwa utumwani na kipindi kirefu cha miaka mia moja na
ishirini ya mwanzoni.
Katika karne a ishirini ulimwengu wa watu wanaoongea
lugha ya Kiingereza wamedhoofishwa na mlolongo wa Vita Vikuu vya Dunia vimemwaga
damu ya weupe na pamoja na mauaji ya Holocaust hadi mwaka 1945 na vita nyingi
nyinginezo ndogondogo.
Hivi karibuni, dunia yote itafikia toba. Vivyohivyo,
Misri ililetwa ipite kwenye bonde la Megido na kumuua Yosia, na ndivyo itakavyokuwa
pia kwamba mataifa wataletwa washuke chini kwene bonde la Megido na
kuangamizwa. Imani za kidini za ulimwengu huu zilizoanzishwa kwa muunganiko wa
Waashuru na Wababeloni na Wamisri utaangamizwa. Kutoka Yubile ijayo, kutakuwa
na marejesho ambayo tutakayojionea marejesho mapya ya kidini na utaratibu
utaanzishwa na dunia itatawaliwa na utaratibu wa tofauti wa kisheria panoja na
na utaratibu mpya wa kidini ambao utatuama kwenye haki na utakatifu na mwenendo
sahihi. Hii pia inaashiria marejesho ya ujenzi na matumizi au huduma za Hekalu
la pili la Ezra na Nehemia. itakuwa hiyohiyo pia na Utakaso wa Hekalu (sawa na
lisemavyo jarida la Utakaso wa Hekalu la Mungu
(Na. 241) [Tanctification of the Temple of God (No. 241)] unapaswa
kuanza na makuhani na hekalu la Mungu na kuenea duniani kupitia harakati zao.
Ni sawasawa tu na ilivyo kwa sasa kwamba dunia inaandaliwa.
Mungu aliiangamiza dunia kwa gharika na ilipofika siku ya
kwanza ya mwezi wa kwanza, Safina ilifunguliwa kifuniko chake na nchi ilikauka (Mwanzo
8:13). Ilikuwa hata hivyo katika mwezi wa pili, siku ya ishirini nnna saba ya
mwezi ambapo nchi ilikuwa imekauka kabisa kiasi cha mtu kutembea juu yake na
ndipo wana wa Nuhu waliweza kukamyaga miguu yao na kuishi tena duniani (Mwanzo
8:14-19). Marejesho haya yanaonyesha kwamba kipindi cha kuweka makazi kilikuwa
ni cha siku hamsini tangu siku ya utakaso wa hekalu na cha toba kwa ajili ya
dhambi zilizofanywa kwa kupotoshwa kwa dunia ambayo ni siku ya saba ya mwezi wa
Nisan, na sio tangu Pasaka na pia sio siku ya kwanza ya ya mwezi wa kwanza. Kwa
harakati za wateule, ndipo ulimwengu unaweza kuwa tayari kwa kumpokea Masihi.
Siku kumi kabla ya Pentekoste ambayo inajulikana pia kama ni siku hamsini tangu
siku ya Saba Nisan, ndipo Kristo alipaa kwenda mbinguni ili kufanya iwezekane
kwa mwanadamu kuuingia ufalme wa mbinguni.
Tangu Mwezi wa Kwanza hadi Mwezi wa Saba
Mchakato huu wa marejesho ya kwanza ulifikia kilele chake
kwa Masihi. Mchakato wa kipindi hiki unaonekana kama taswira ya mchakato wa
mwezi wa kwanza.
Mwezi wa kwanza siku ya kwanza ya mwezi, Utakaso wa
Hekalu la Mungu unafanyika, Hekalu ambalo ni sisi (1Wakorintho 3:16; 6:19).
Siku ya saba ya mwezi ni siku ya utakaso kwa ajili ya dhambi
zilizofanywa kwa kutojua ama kwa kupotoshwa. Harakati hizi zinatakiwa kwa
viumbe walioumbwa hata sasa na pia kwenye kipindi cha millennia na ni moja ya
mikanganiko miwili iliyoko kati ya miezi ya Nisan na Tishri ambao kwa namna
fulani unaashiria mpango uleule na matendo.
Siku ya kumi ya mwezi wa kumi kunaonekana kuchaguliwa na
kumtenga mbali mwanakondoo ambayo inaanzisha mchakato wa okombozi na kipindi
ambacho malimbuko yanatakiwa kutolewa na kukubalika na Mungu.
Siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza ni Sikukuu ya
Pasaka. Marejesho yote kwa kipindi hiki yanaanza kutoka mwanzoni na yanahusisha
mwezi wa kwanza yaliongoza kwenye dhabihu na kuula mwili na damu ya Kristo
ikiwa ni sakramenti ya pili ya wateule. Sakramenti ya kwanza ya wateule ni
ubatizo ambao ni hatua ya kwanza wa utakaso wa hekalu ambao maana yake halisi
ni kufanyika baada ya majira ya Sikukuu na baadae kidogo hadi katikati ya siku
ya kwanza na ya saba Nisan na mapema kabla ya siku ya 14 ya mwezi wa Kwanza.
Sikukuu ya Pasaka na Mikate Isiyo na Chachu zimeunganishwa
kwa siku moja na ni kipindi cha siku saba. Kipindi hiki kinaashiria dhabihu na
maandalizi ya wateule na kuondoa kwa dhambi na kisha kujiweka sawa kwa
Pentekoste na Mavuno ya wateule katika yubile ya arobaini jengwani.
Kuna Siku Takatifu za mwanzo na mwish wa Sikukuu hii ya
Mikate Isiyo na Chachu pamoja na siku ya kwanza au Siku ya Pasaka ambayo ni ya 14
Nisan ambayo ni siku ya maandalio. Wateule wasipokuwa watakatifu hawaruhusiwi
kushiriki mkate usio na chachu wa Pasaka ambao tumeuona kwenye matengenezo ya
Yosia ambapo makuhani wa Mahali pa Juu hawakuruhusiwa kwenda Hekaluni kwenye
Pasaka. Kwa hiyo ibada za sanamu zilipunguza idadi ya makuhani kwenye
maadhimisho ya Pasaka Hekaluni.
Tofauti iliyopo kati ya miezi wa kwanza na wa saba ni kusanyiko
la Siku ya Baragumu ambalo linafanyika tena katika siku ya Mwandamo wa Mwezi
Mpya au siku ya kwanza ya mwezi, ambayo inatangaza kipindi ambacho Masihi
ataingilia kati maongozi ya dunia. Ataingilia kati na kuchukua uongozi kwa kuwa
wateule na uwepo wao na ushiriki wao wakiwa kama watu wa Mungu. Wanajulikana
kutokana na matendo yao na kazi zao walizopangiwa na inayoonekana wazi kama
Sabato, Miandamo ya Mwezi, Sikukuu na harakati zao kuanzia Mwezi wa Kwanza na
kuendelea pamoja na kumpokea kwao Roho Mtakatifu siku ya Pentekoste na kwa
Sikukuu na Torati ya Mungu kwa ujumla.
Hakuna mfungo wa saumu siku ya saba ya mwezi katika mwezi
wa saba. Hakuna kitu anachoweza klukifanya mwanadamu sasa kilichofanananacho. Mwanakondoo
amekwisha tolewa sadaka tayari na ndipo saumu ya siku ya kumi ya mwezi wa saba
wakati siku ya kwanza imetengwa tu mbali kwa ajili ya dhabihu ya siku ya kumi
na nne. Mnamo mwezi wa saba, Yule mwanakondoo aliyechaguliwa na kuwekwa kando
huko mbinguni akiwa kama mfalme mshindaji, aliyeonyeshwa kwa ishara ya baragumu
inayopigwa siku ya kwanza ya mwezi wa saba. Katika siku ya kumi ya Upatanisho
dunia ilipatanishwa na inaandaliwa kwa ajili ya utawala wa Milenia. Tazama pia
jarida la Lafudhi ya Musa (Na. 70) [The Ascents
of Moses (No. 70)].
Mataifa yanashughulikiwa kwa kiwango endelevu. Kama Yosia
alivyolirejesha hekalu na torati tangu Pasaka na kuendelea hadi miaka mingine
kumi na tatu ya nyongeza baada ya mwaka 623/2 KK hadi alipokwenda Megido mwaka 609
KK kuyakabili mataifa na kufa, na ndivyo ilivyo pia kwamba ufalme utapita
mikononi mwa wafalme hadi kwenye mikono ya Masihi ambaye haki ni yake.
Sikukuu ya Kutaniko inapaswa ifanyike pamoja na sadaka
wakati wa jioni ya kwanza ya sikukuu. Siku ya kwanza ya sikukuu ya Vibanda ni
siku Takatifu ambayo hakuna harakati wala kazi yoyote inayopaswa kufanywa na
mwanadamu zaidi ya kutafakari na kujiandaa kwa mkusanyiko na kutoa sadaka
ambayo haitakiwi ibakie hata asubuhi.
Siku ya Saba ya Sikukuu ya Vibanda ni kipindi kinachofananishwa
na kipindi cha millennia ya siku saba ya Mikate Isiyo na Chachu. Kwenye mfano
wa kwanza Masihi alikufa ili kuiwezesha Sikukuu ya Pasaka. Matendo ya wanadamu
ni ya muhimu ili kutoka nje ya dunia.
Katika mwezi wa saba sikukuu inaashiria au kuwakilisha
utawala wa Masihi hapa duniani ambapo hakuna umuhimu kutoka nje ya dunia wakati
dunia yote itakapokuwa chini ya utawala wa haki na maongozi ya torati ya Mungu.
Kwa hiyo, siku ya saba au ya mwisho wa maadhimisho ya
Sikuu ya Vibanda sio siku takatifu kwa kuwa inawakilisha kipindi ambacho dunia
itarudi kwenye zama za uadui na vita.
Siku Iliyo Kuu ya Mkutano wa Makini kwa namna nyingine ni
siku ya nane ambayo ni tofauti na maadhimisho ya Mkate Usio na Chachu ni ya
mwisho na sio ya kwanza na ni siku takatifu. Pentekoste kwa namna nyingin e sio
siku takatifu kwa kuwa inawakilisha kazi ya Masihi kwenye wokovu wa mwanadamu.
Siku ya Mkutano wa Makini ni Takatifu kwa kuwa inawakilisha
ashirio la siku ya hukumu ya haki itakayotolewa kwa haki kwa walimwengu na ni
ondoleo la mwisho la dhambi. Inawakilisha ujio wa Mungu hapa duniani na Mji wa
Mungu utaunganishwa kwenye marejesho haya ya mwisho.
Marejesho haya ya mwisho ni matokeo ya mwisho katika
mpango wa Mungu.
Ndipo tunayaona Marejesho na Pasaka Kuu Saba zilizo
kwenye Bbiblia zinamaana kwene harakati hizi na mlolongo huu wa Mpango wa Mungu.
Soma jarida la Pasaka Kuu Saba za Biblia (Na.
141) na Baragumu Saba (Na. 107) [The Seven Great
Passovers of the Bible (No. 107)].
Ingawa Yosia alitubu bado alipaswa afe kama utaratibu
wote mzima aliouongoza kuurejesha kikamilifu kwa kuyaangamiza mataifa na Yuda
hawakuwa na uwezo wa kufanya hivyo kabisa.
Hezekia alianza mchakato na mwanae Manase alijaribu bali
alishindwa. Mwanae Amoni ndiye alikuwa ni mbaya zaidi ya Manase kwa uovu wake.
Yosia aliahirisha kutokea kwa maafa yasiyoweza kuepukika. Hata hivyo ilitokea
kipindi cha Wababeloni. Hekalu lilihusuriwa na marejesho yaliyofuatia yalipaswa
yawe kwenye Hekalu linguine na lenye muundo tofauti, kama tunavyoona kwenye
vitabu vya kina Ezra na Nehemia. Hii ilikuwa ni ashirio na ilikuwa inamlenga
Kristo. Mambo yote yaliyokuwa yanafanywa kwenye hekalu lile yalikuwa yanamlenga
Masihi na mhukumu au mwamuzi wa Yuda kwene kipindi cha majuma sabini ya miaka
iliyoishia mwaka 70 BK (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi upya wa Hekalu (Na.
13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No.
13)].
Tunaelekea kwenye marejesho ya Masihi. Ni kama
yalivyokuwa marejesho ya Yosia, nasi haya yetu yanaelekea kwenye Yubile, lakini
kutakuwa na mlipuko wa maasi na upinzani dhidi ya marejesho haya katika vipindi
vyote viwili, yaani mwanzoni mwake, na ambayo yata yatakuwa na umuhimu wake utachukua taswira ya
Ezra, na pia mwishoni mwa Milenia itakayoitangulia hukumu. Hii ni hadithi
nyingine.
Ili kutusaidia angalia masomo mlinganisho tunayopaswa
kujionea mafuatano yake kwenye mtindo wa jedwali. Marejesho ya Ezra na Nehemia
yalikuwa ni ya hekalu jipya na la pili.
Marejesho ya Hezekia yalikuwa na mchocheo wa Mungu.
Marejesho haya yalifuatiwa na mwanzo wa marejesho mengine tena ya unabii
uliovuviwa. Haya yalitanguliwa na kipindi cha mzunguko wa miaka saba kilichotangulia
Yubile. Hii tena iliwakilishwa na kipindi cha miaka saba kinachoonekana kwenye
Baragumu na kimeelezewa kwenye majarida ya Kuanguka Kwa Yeriko (Na. 142) na pia Mihuri Saba (Na. 140) na
Baragumu \\\Saba (Na, 141) [The Fall of Jericho (No. 142) and
also The Seven Seals (No. 140) and The Seven Trumpets (No. 141).
Masihi anazipunguza siku za mwisho kwa kurudi kabla ya
Yubile ya Milenia ijayo kwa mfano miaka saba mapema kabla ya kuifka Yubile ya
mwaka 2027/28 huenda kabla ya mwaka 2019/20. Dini inayompinga Masihi itauona
mfumo na imani mpya vikiwekwa na kuchukua mahali pake katika kipindi hiki cha
Milenia kama Ezra na Nehemia walivyotumiwa na fanya.
Jedwali la ulinganisho linaonekana kama hivi
lilivyofungamanishwa na matukio yajayo yanaweza kuonekana kabisa kama yale
yaliyoorodheshwa kwene jedwali hili:
Marejesho ya Israeli chini ya wafalme
715/16 KK marejesho ya Hezekia.
Israeli walimuacha Mungu na kurudi nyuma chini ya Manase na Amoni.
632 Marejesho ya Yosia yanaanza.
630 Mfalme wa Waashuru anakufa.
627 Hakuna mfalme kwenye kiti cha enzi cha ufalme wa
Kaskazini.
624 Taifa la Israeli na Wasamaria wanaadibishwa na
kutolewa kwenye sanamu.
624/23 Yubile inatangazwa na marejesho ya dini ya
kishindo yanafuatia.
623/22 Pasaka ya Marejesho inafanyika (kiwango cha rekodi
kinavunjwa)
616 Wamedi wanajitokeza kuwa viongozi dhidi ya Waashuru
na Misri inajipanga kuikabili Ashuru.
614 Assur aliangukia
mikononi mwa Cyaxares mfalme wa Wamedi kwa
mkakati uliofanywa na Wamedi na Wababeloni chini ya Nabopolasa aliyekuja akiwa
amechelewa kumuangusha Assur.
612 Ninawi unaangusha na majeshi ya muungano na Ashuru
inaondolewa kwenda Harani ambako Ashuruballit II alijaribu kuirejesha tena
Dola ya Waashuru.
610 Ashuruballit II anaondoka Harani licha ya
msaada aliokuwa anaupata wa Wamisri na mji ukaangukia mikononi mwa Wamedi na
Wababelonia.
609 Yosia anajeruhiwa na kuondolewa mapiganoni huko
Megido. Wamedi na Wababeloni wanakabiliana na mashambulizi ya majeshi ya ushirika ya Wamisri na Waashuru.
605-525 Kipindi cha Utimilifu wa Mataifa kinaanza.
598/97 Yuda inaangushwa na Wababeloni na utaratibu wa
kale wa Hekalu unaondoshwa au kukomeshwa.
539 Babeli unatekwa na Koreshi na Dario Mmedi mwana wa Astyages na
mjomba wa Korshi.
423-410 Hekalu la Pili linajengwa. Juma la Saba la miaka
linaanza na kuishia mwaka 70 BK.
398-373/2 Ezra na Nehemia wanaurudisha utaratibu wa ibada
Hekaluni chini ya Artashasta II.
Marejesho chini ya Masihi
1914/18 Vita Kuu ya I ya Dunia. Vita vya mwisho wa
dunia vimeanzia.
1917 Kuichukua tena Palestina kwa msaada wa Majeshi ya
Jumuia ya Madola ya Mwingereza na kutangazwa kwa Nchi au Taifa la Wayahudi.
1939 Vita Kuu ya II ya Dunia ilianza.
1942 Mauaji ya Holocaust yalianza.
1945 Vita Kuu ya II ya Dunia iliisha.
1953 Misri ilitangaza uhuru wake.
1956 Mgogoro wa kugombea mfereji wa Suez.
1996 Mwisho wa Kipindi cha Utimilifu wa Mataifa cha miaka
2000 au yubile arobaini tangu kuzaliwa kwa Masihi. Maadhimiso ya mwaka wa 3000
tangu Daudi alipoingia Yerusalemu.
1997 Mwezi wa Miaka Ulianza. Kuondolewa kwa mfumo wa
ibada za kidunia wa Makasisi, Wafalme na Manabii kulianza.
1998 Mwaka wa Sabato na ni mwaka wa 21 wa Yubile ya 39 tangu
huduma ya Yohane Mbatizaji na Masihi katika Yubile ya mwaka 27/28 BK. Usomaji
wa Torati kwa Mara ya Kwanza ulifanyika kwenye Sikukuu ya Vibanda tangu kipindi
ch karne nyingi zimepita.
1999-2019 Vita ya wafalme wa Kaskazini na Kusini na
kuangamia kwa mataifa kulianza na kunaendelea.
2019/20 Masihi ataanza kuyatiisha na kuyaadibisha mataifa
na wito wa Megido.
2027/28 Yubile ya 40 itatangazwa kwa kupigiwa mbiu.
2028 Kipindi na Utawala wa Milenia Utaanza. Kipindi zama
cha Utawala wa Haki chini ta Torati au Sheriza za Biblia kitaanza.
Vita vya waasi.
Matengenezo na ujenzi wa Hejalu.
2997 + Shetani atafunguliwa.
2997-3027 Vita ya Waasi au Uasr wa Mwisho.
3028 Ufufuo wa Pili wa Hukumu ya Malaika na Ulimwengu.
3127 Kukabidhi kila kitu kwa Eloa na kushuka kwa Mji
wa Mungu.
3128 Pasaka Kuu ya Kwanza ya Watakatifu.
Kwa kujisomea zaidi haya, jisomee pia majarida yafuatayo:
Maelezo ya Ratiba ya Zama na Matukio Yake (Na. 272) [Outline
Timetable of the Age (No. 272)]
Ujio wa Masihi Sehemu ya 1 (Na. 210A) [Advent of the
Messiah: Part I (No. 210A)]
Yubile ya Dhahabu na Milenia (Na. 300) [The Golden Jubilee
and the Millennuim (No. 300)]
q