Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[121]
Mika
5:2-3
(Toleo La 1.1 19950624-19991009)
Jinsi andiko wanavyolitumia Wabinitarian
kumeainishwa na kuonyeshwa kuwa siyo sahihi kabisa. Maelekezo ya uzushi wa guvu
za namna Mbili yameonekana kuwa ni uwongo. Jarida hili linaelezea kuhusu ulio
kwenye andiko hili na jinsi yanavyohusiana na Masihi na uhusiano wake na Mungu.
Christian Churches of God
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 1995,
1999 Wade Cox)
(tr. 2016)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na
tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza
kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka
maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia
yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Mika 5:2-3
Tunajua kwamba
maandiko ya Mika 5:2-3 yamekarabatiwa kimakosa na watumishi au wahubiri wa Kibinitarian
ili kuhalalisha imani yao ya Kibinitarian au mafundisho ya kizushi ya Nguvu
Kuwili kama ilivyokuwa imejulikana hapo zamani. Ni kubisha kwamba kuna Miungu
miwili idumuyo milele huko mbinguni, ikiwa kwamba ama kuna miungu miwili
waishio milele ama la wanaodaiwa kuwa hivyo kwenye imani ya Kiutatu au
Utrinitarian. Mafundisho haya ya kizushi kimsingi yanapinga au kushuku uweza wa
kuwa na nguvu zote alionao Mungu na yanajaribu kupingana na maandiko yaliyo
kwenye Yohana 17:3 na 1Yohana 5:20 yanayoelezea na kusisitiza kwamba kuna Mungu
mmoja tu, wa Pekee na wa Kweli, na kwamba Yesu Kristo ni Mwanae wa pekee.
Yohana 17:3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
1Yohana 5:20 Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele.
Andiko hili
limetafsiriwa ili kufanya ionekane kwamba neno Mungu wa Kweli, na uzima wa milele huenda lilikuwa linamlenga Kristo,
jambo ambalo sivyo. Zaidi sana ni kwamba vitabu cha Ufafanuzi vya Douay-Reims
Bible (yaani, Heydock) vinajaribu kuonyesha kwamba makala yenyewe halisi,
inatumika hapa kumtaja Mungu wa Pekee na wa Kweli, ikimkusudia Kristo, hambo
ambalo sivyo kabisa.
Mungu wa Kweli,
ndiye Mungu wa Pekee na wa Kweli na siyo Yesu Kristo aliyemtuma. Hakuna mtu
aliyewahi kumuona yeye, Mungu, na wala atakayeweza kumuona (Yohana 1:18). Ni yeye
tu, peke yake ndiye hafi wala kupatwa ma madhara. Anaonekana tu katika Roho.
1Timotheo 6:13-16 Nakuagiza
mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu,
aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato, 14
kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa
kwake Bwana wetu Yesu Kristo; 15 ambako yeye kwa
majira yake atakudhihirisha, yeye aliyehimidiwa, Mwenye uweza peke yake, Mfalme
wa wafalme, Bwana wa mabwana; 16 ambaye yeye peke yake
hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna
mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata
milele. Amina.
Ikumbukwe hapa
kwamba ni Mungu ndiye atoaye uzima kwa viumbe na vitu vyote. Yeye ni mbarikiwa
na ni Mtukufu, Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana. Ni yeye peke yake ndiye
hafi wala kupatwa na madhara. Kwa hiyo, ni yeye pekee ndiye atoaye uzima kwa
viumbe vyote. Na ni yeye peke
yake ndiye aliyempa uzima hata Kristo.
Kuendelea kudai
kwamba Kristo ana umilele sawa na Mungu kunapingana na ni kama kunashambulia
moyo au kiini cha utukufu wa kipekee wa Mungu Mmoja, wa Pekee na wa Kweli na ni
kitendo na tabia ya waabudu na waamini miungu mingi. Kristo alipaa mbinguni ili
afanyike kuwa Mwana wa Mungu mwenye uweza kutokana na kufufuka kwake kutoka kwa
wafu (Warumi 1:4). Madai ya kwamba nabii Mika anauelezea umilele wa Kristo pia,
yanatafuta kupinga andiko lililo kwenye 1Timotheo 6:16 linaloonyesha kwamba ni
Mungu tu peke yake ndiye hafi wala kupatwa na madhara. Madai haya yanatokana na
hali ya kutafsiri na kuyaelezea vibaya na kimakosa Maandiko Matakatifu.
Hebu na tulipitie
andiko lenewe lisemavyo.
Mika 5:2-3 Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo
kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa
mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale,
tangu milele. 3 Kwa sababu hiyo atawatoa, hata wakati wa
kuzaa kwake aliye na utungu; ndipo hayo mabaki ya nduguze watawarudia wana wa
Israeli.
Madai haya
yanatuama kwenye maandiko yaliyo kwenye tafsiri ya KJV ambayo inaaminiwa au kuchukuliwa
kwamba inajaribu kuyafanya madai haya yawezekane na kukubalika.
Mika 5:2-3 Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo
kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa
mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale,
tangu milele. 3 Kwa sababu hiyo atawatoa, hata wakati wa
kuzaa kwake aliye na utungu; ndipo hayo mabaki ya nduguze watawarudia wana wa
Israeli.
Andiko
lililotafsiriwa hapa kuwa kama ambaye matokeo
yake yamekuwa tangu zamani za kale milele na milele.
Tafsiri ya RSV imeandikwa
andiko hili kuwa ni Ambaye matokeo yake
yamekuwa tangu zamani za kale. Kwa hiyo, uingizaji wa maneno yanayokusudia
kumaanisha umilele yanatokana na marekebisho yaliyo kwnye tafsiri ya KJV yasemayo
umilele ambayo kwa jinsi yalivyo tu
yenyewe kuwa marekebisho yaliyofanyizwa kwa upotoshaji kutokana na lugha ya
Kingereza.
Andiko hili limetafsiriwa
kwenye Biblia tafsiri ijulikanayo kama Interlinear Bible kama
Bali wewe,
Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe
atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake
yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.
Kutoka kwenye
siku za umilele imetafsiriwa kwa maneno mawili ya Kiebrania. Neno la kwanza ni miymy (*/*/) linalotokana na kamusi ya SHD 3117 yowm (.&*) linalomaanisha siku (hizo), tangu mawio ya
jua hadi mawio yanayofuatia, likiwa linatokana na maana ya chimbuko
lisilotumika kuwa moto. Neno la pili
kwa mujibu wa kamusi ya SHD 5769 ni ‘owlawm
(.-&3) ambalo maana
yake yamefutwa au kuondolewa, au kwenye kiwango cha kuondolewa. Inamaanisha kipindi au mda ulio nje ya mawazo au umilele
unaojulikana (kamusi ya Strongs) ambqacho
mara zote, au kutoka nyakati za kale, nk. Andiko halina jinsi ya kukanushwa kuwa
linakusudia kuutaja umilele wa kiumbe ambaye aliyeumbwa na kuwa msaidizi wa
Mungu wa Pekee wa Kweli. Masihi anaweza kuchukuliwa kutokana na andiko hili
kuwa amewahi tu kuwa alikuwepo kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi hapa
duniani, nyakati za kale. Halimaanishi kufundisha kuwa ana umilele sawa na
Mungu. Kwa kweli, kutokana na andiko hili tunaweza kuona kwamba Kristo anatoaka
kwa Mungu na ametumwa naye, hivyo hawezi kuwa sawa naye. Kudai kwamba kiumbe
huyu amukuwepo milele sawa na alivyo Mungu wa Pekee wa Kweli kunamuondolea
hadhi ya uweza wake (Mungu) usioshindwa na nguvu nyingine yoyite.
Tafsiri ya
Soncino imetafsiri andiko hili la Mika 5:1[2] kama Ambaye
matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale,
Na kulitafsiri
andiko hili kuwa:
Matokeo yakeyamekuwa, yaani .mstari.
Tangu zamani za kale. Inawezekana kwamba kufungu hiki kilesababisha
kuinuka kwa mafundisho ya Kiyahudi yasemayo kwamba Masihi alikuwepo kwenye
mawazo ya Mungu tangu wakati mwingi usioweza kutajika, akiwa kama sehemu ya mpango
wa Muumba kwenye ubunifu wa jinsi utakavyokuwa ulimwengu. Kwenye tafsiri ya Talmud,
jina la Masihi ni miongoni mwa mambo saba yaliyokuwepo au kubuniwa kabla ya ulimwengu
haujaanza kukaliwa na kiumbe chochote.
Ni Mungu pekee
ndiye anayeishi na kudumu milele
Isaya 57:15 15 Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye
jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo
patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili
kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.
Neno hili umilele
limeandikwa kwenye kamusi ya SHD 5703 kama ‘ad
($3) ambalo linamaanisha
dhana ya kitu kisicho mwisho na likimaanisha
kipindi endelevu au cha kudumu kwa maana ya umilele, ambavyo ni milele au kudumu (milele). Dhana hii ni kama tunavyoona ilienea kwa roho zote
zenye toba na zilizo na unyofu ili kufufua moyo wa unyenyekevu na toba. Kwa
hiyo, uwezo huu wa kuishi au kudumu milele ni mkanganyiko uliuowekezwa tu kwa
kila mmoja ili kuwezekane kuwa na wokovu wa kila mmoja. Neno ‘owlawm linatumika kwa kanuni za kawaida
za kimwili pia, ambazo tunazijua kuwa si vitu vya kiroho milele. Neno umilele wa agano la milele linalitajwa kwenye Mwanzo 9:16;
17:7-8,13,19 linatumika pia kwa Mungu wa Milele kwenye Mwanzo 21:33.
Mwanzo 21:33 Ibrahimu akapanda mkwaju huko Beer-sheba, akaliitia huko jina la Bwana
Mungu wa milele.
Bado tunajua
kwamba hakuna bado wala hakuna mwenye mwili wala ardhi iliyo ya kudumu milele,
iwe tangu mwanza au kwa wakati mwingine wowote. Hivyo basi, matumizi ya neno
hayaashirii kuwepo kwa umilele wowote pamoja na Mungu wa Pekee wa Kweli. Kwa
kweli, kama Masihi alikuwa wa milele sawa na Mungu, basi asingeweza kuwa Mwana,
na kwa hiyo hakuna kitu kingalichoweza kutabiriwa kuwa kwenye uhusiano ule.
Zaidi sana, ni ukweli wa kwamba kulikuwa na idadi kubwa ya wana tangu kuwekwa
kwa msingi ambao wangedai pia kuwekwa kwenye mfumo huo wa miungu mingi ulio
kwenye muundo wa uhusiano wa kimilele wa kiwana. Kristo kama elohim alikuwa na
washiriki wenzake (Waebrania 1:8-9 sawa na Zaburi 45:6-7). Alitiwa mafuta kuwa elohim na elohim wake. Madai yatokanayo na mafundisho ya kizushi ya kuwa na
mamlaka kuwili yanatokana kabisa na Wanotheist (Yanahusisha na kuabudu malaika
kwa kudai kuwa wana sifa ya kuishi milele mbali na Mungu). Madai ya kwamba ya
kwamba Mungu, kama Elohimu, yanatokana na vitu viwili vya muhimu na lazima
kwamba mmoja wa hawa elohim alikuwa ni Malaika wa Yehova, kama inavyosema
Zekaria 12:8 wakitokana na Malaika wa Yehova akiwa elohim.
Zekaria 12:8 Katika
siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni
mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu,
kama malaika wa Bwana mbele yao.
Zekaria 12:8 Katika
siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni
mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu,
kama malaika wa Bwana mbele yao.
Andiko hili
linaonyesha kwamba watu wa nyumbani mwa Daudi watakuwa Elohim, kama Makaila wa
Yehova (aliyetafsiriwa kama Bwana), kabla
au mbele yao au vichwani mwao.
Tafsiri ya Soncino inasema na kumtaja elohim
hapa kama kiumbe anayefanana na Mungu. Kwa
hiyo, neno elohim limeeleweka kuenea hadi kwa wengine.
Ni Masihi ndiye
anayeiongoza Nyuma ya Daudi. Kiumbe huyu wa kimbinguni au kiongozi
anayetangulia mbele ya wateule kama Malaika wa Yehova ndiye huyuhuyu Masihi. Hakuna
kiwango chochote anachoonekana kwamba awe ni wa nyumba ya Daudi au Malaika wa
Bwana, kwa kuwa kiumbe au kufanyika kuwa elohim waliofanana sawa na Eloa ambaye
ni Mungu Baba (Mithali 30:4-5). Eloa peke yake ndiye anayestahili kulengwa
kwenye ibada za hekaluni (Ezra 5:1-8), ambalo lilikuwa ndilo hekalu lake (Ezra
6:16-18). Eloa ndiye alikuwa mlengwa kwenye matoleo ya dhabihu (Ezra 6:9-10), Mungu
wa mbinguni na chanzo cha Sheria au aliyetoa Torati (Ezra 7:14). Madai ya
kwamba Mika 5:2-3 inamaanisha uwepo wa usawa wa umilele ni makosa yanayotokana
na upotoshaji wa kimaandiko kwa kuyaondoa au kuyatenganisha na maandiko mengine
mengi yanayopinga uwezekano kama huo.
Ni muhimu kuitathimini
dhana usawa wa umilele. Usawa wa umilele unadai kwamba Masihi alikuwa ni Mungu
mwingine aliyeishi na kudumu peke yake mbali na Mungu wa Peke wa Kweli. Kwa hiyo,
andiko lifundishalo kuhusu Mungu wa Pekee wa Kweli linapuuzwa. Ndipo kwa kweli
ingepasa kuwe na miungu wawili wa Pekee na wa Kweli, lakini Maandiko yanasema
kuna Mungu Mmoja tu, wa Pekee na wa Kweli (Kumbukumbu la Torati 6:4; Yohana
17:3). Basi kama hakuna Miungu Wawili wa Kweli na wa Pekee ndipo kiumbe mmoja
atakuwa anamtegemea mwenzake ili aweze kuishi. Kwa hiyo, mmoja atakuwa ndiye
Mungu na mwingine atakuwa ni wa kuumbwa au aliyeumbwa na mwenzake. Kwa kuwa
Mwana ndiye aliyeumbwa na Baba na ndivyo ilivyo pia kwamba ni mwana aliye tunda
la Baba au aliyeumbwa naye. Kuna wana wengi wa Mungu tangu mwanzo (Ayubu 1:6;
2:1; 38:4-7), walio washirika wa karibu na Kristo (Zaburi 45:6-7; Waebrania
1:8-9). Na ndivyo ilivy pia kwamba ilikuwa ni Mungu Baba kwa kuumbwa kwao.
Tafsiri ya Soncino inaitaja Zaburi 45:7[8] kuwa ni ya Kimahisi. Kimchi inasema
Mafuta yalikuwa ni ishara
ya furaha (Isaya lxi. 3) na Mtunga Zaburi anakusudia kwamba Mungu kwa kumtia
kwake mafuta Masihi awe Mfalme wake, atamuinua juu yaw engine wote na kuanzisha
furaha ya ulimwengu.
Ufalme huu wa
wana wengi wa Mungu ni kitu ambacho kimeongelewa kuwa kama ufalme wa milele (Zaburi
145:13), lakini bado hakuwa na umilele pamoja naye. Agano la Mungu na Ibrahimu
lilikuwa la milele au ni agano lenye uhusiano (‘owlawm) (Zaburi 105:10), hata hivyo, haiashirii kuwa na usawa
wowote na Mungu. Zaburi 93:2 inasema kuwa Bwana tu ndiye aliyekuwepo tangu
milele yote. Dhana iliyopo kwenye andiko hili ni kuhusu utawala wa Mungu
ulikuwepo tangu milele na milele (inarudi
hadi nyuma kwenye mwanzo wa nyakati; Soncino) hata ingawaje masomo yalikuwa
hayajatungwa bado. Dhana hii ilieleweka kutoka kwenye Isaya 9:6 kutokana na
maneno yake ya Ajabu, Mshauri, Mungu mwenye nguvu (Eli), Baba wa milele, Mfalme
wa Amani,. Maneno kama wa Ajabu, Mshauri yameandikwa kwenye Septuagint (LXX) kama
Mjumbe wa Shauri Kuu (Megales boules
aggelos). Neno Eli mwenye nguvu halimaanishi kuwa na usaw wowote na Eloah au
Mungu. Wala neno hili Baba wa Milele
halimaanishi kutambulisha kitu chochote, na kama, Mungu Baba. Kuna aina nyingi
sana ya ubaba mbinguni na hata hapa duniani. Kila mmoja ametajwa na Mungu Baba
(patria Waefeso 3:15). Kristo amepewa
Ubaba wa wote wenye mwili. Kristo hakuwa wakati wote Baba wa milele, ingawaje
cheo hicho alipewa. Kwa hiyo, jina hili halimaanishi uweza wa kutokufa au
kupatwa na madhara zaidi ya vile lilivyochukuliwa kwa ajili ya Mungu. Andiko
hili lilikusudiwa kwenye tafsiri ya Soncino (Isaya 9:5[6]) kama
Na jina lake ataitwa Pele-joez-gibbor-Abi-ad-sar-shalom.
Soncino inasema
Maana ya maneno ya
Kiebrania ni ‘Mshauri wa Ajabu ni Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mtawala
wa Amani.’ Mtoto huyu atakuwa na majina haya ya maana ili kuwapa watu ujumbe
waliokusudiwa (Arbarbanel).
Andiko hili kwa
hiyo linachukuliwa kuwa na mamlaka yaliyokusudiwa. Kwa kulifafanua andiko hilo,
linalofuatia aya hii inayoitwa tangu hapo
hata milele na milele, Rashi anasema kwamba neno la Kiebrania olam linamaanisha pia wakati au kipindilso cha mhimu. Maelezo haya yanatokana na jaribio la
kulifanya au kulizeuza andiko hili na kulilinganisha na utawala wa mfalme Hezekia.
Hata hivyo, maelezo ya maana yake yana maana sana.
Kwa hiyo inaweza
kuonekana kwamba matumizi ya andiko hili la Mika 5:2-3 kuyafanya yamaanishe
umilele wa Masihi na hivyo kuupa mashiko Ubinitarianism au mafundisho ya
kizushi ya Nguvu Kuwili kuwa ni kama kukatisha au kuondoa sifa kuu ya Mungu ya
kuweza kila jambo na kutoshindwa na nguvu nyingine yoyote ile na kuuvunja au
kuupotosha mfumo mzima wa Umonotheism au imani juu ya Mungu mmoja na asiye na
mshirika. Inapuuzia au kupotosha malaika au watakatifu muhimu walioelezewa
kwenye Maandiko Matakatifu inayoonyesha tafsiri kuwa ina makosa au imekosewa.