Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[102]

 

 

 

Naona Kiu

(Toleo La 1.0 20000416-20000418)

Maneno ya mwisho yaliyonenwa na Kristo alipokuwa anakufa yana maana ya kinabii na yanahusiana na utaratibu wote wa sheria ya utoaji dhabihu na wa ondoleo la dhambi au msamaha na upatanisho wa Mungu, kama ulivyotabiriwa kwenye Zaburi na ushuhuda mwingine.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2000 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Naona Kiu


 


Mtume Yohana ananukuu maneno ya mwisho yaliyotamkwa na Masihi, kabla ya kifo chake pale mtini (au kwenye mti uliosimamishwa wima) alipokuwa anasulibiwa. Alikuwa ni shuhuda aliyeshuhudia kwa macho yake.

 

Kulikuwa na maneno saba aliyoyanena pale mtini. Mathayo 27:46 na Marko 15:34 kumenukuliwa na kuandikwa usemi mmoja.

Mathayo 27:46 Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?

 

Luka ananukuu kwa kuandika maneno mengine matatu kwenye Luka 23: 34, 43, 46.

 

Luka 23:34 Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.

 

Luka 23:43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.

 

Luka 23:46 Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu. Alipokwisha kusema hayo alikata roho.

 

Yohana pia ananukuu semi tatu nyingine hapa kwenye sura za 19:26, 27, 28 na 30.

 

Yohana 19:26-30 Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao. 27 Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake. 28 Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu. 29 Kulikuwako huko chombo kimejaa siki; basi wakatia sifongo iliyojaa siki juu ya ufito wa hisopo, wakampelekea kinywani. 30 Basi Yesu alipokwisha kuipokea ile siki, alisema, Imekwisha. Akainama kichwa, akaisalimu roho yake.

 

Ni wazi sana kutoka kwenye Luka 23:44 kwamba ahadi ya muuaji ilikuwa kabla ya giza.

 

Maneno ya kwenye Zaburi 22:1 yalinenwa mwanoni au kabla ya kufika saa tatu za giza (sawa na tafsiri ya Bullinger, Companion Bible, angalia Yohana 19:30).

 

Bullinger anaichukulia hii kuwa ni kwamba Kristo aliitamka au kuiimba Zaburi yote ya 22 kama ushuhua kwa makuhani wakuu waliokuwepo (Marko 15:31 na Luka 23:35). Kwa kifo chake alifanyika kuwa ushuhuda dhidi ya makuhani hawa na imani iliyoharibika na kupotoka waliyoiachia kuinuka. Kutoka kwenye hatua hii na kuendelea walifanyika kuwa Ishara ya Yona na waliwekwa wenye ukomo wa toba au maangamizo. Ilipofika siku ya 1 Abibu au Nisan, ya mwaka 70 BK, miaka arobaini kamili ilyofuatia, mwanzoni mwa Mwezi wa Kwanza na Mwaka Mpya, Yerusalemu ulizingirwa na Majeshi ya Warumi. Utaratibu wa Hekalu pamoja na makuhani wake walipewa miaka arobaini ya kufanya toba sawa na mlingano wa siku moja kwa mwaka mmoja walizopewa watu wa Ninawi (soma jarida ya Ishara ya Yona na Historia Ujenzi Tena wa Hekalu (Na. 13)).

 

Zaburi 22 ni Zaburi ya Mtesekaji, inayomwelezea Mtesekaji na pia utukufu utakaofuatia.

 

Zaburi 22:1-31 Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu? 2 Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha. 3 Na Wewe U Mtakatifu, Uketiye juu ya sifa za Israeli. 4 Baba zetu walikutumaini Wewe, Walitumaini, na Wewe ukawaokoa. 5 Walikulilia Wewe wakaokoka, Walikutumaini wasiaibike. 6 Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu. 7 Wote wanionao hunicheka sana, Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao; 8 Husema, Umtegemee Bwana; na amponye; Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye. 9 Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni, Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu. 10 Kwako nalitupwa tangu tumboni, Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu. 11 Usiwe mbali nami maana taabu i karibu, Kwa maana hakuna msaidizi. 12 Mafahali wengi wamenizunguka, Walio hodari wa Bashani wamenisonga; 13 Wananifumbulia vinywa vyao, Kama simba apapuraye na kunguruma. 14 Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu. 15 Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti 16 Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; Wamenizua mikono na miguu. 17 Naweza kuihesabu mifupa yangu yote; Wao wananitazama na kunikodolea macho. 18 Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura. 19 Nawe, Bwana, usiwe mbali, Ee Nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia. 20 Uniponye nafsi yangu na upanga, Mpenzi wangu na nguvu za mbwa. 21 Kinywani mwa simba uniokoe; Naam, toka pembe za nyati umenijibu. 22 Nitalihubiri jina lako kwa ndugu zangu, Katikati ya kusanyiko nitakusifu. 23 Ninyi mnaomcha Bwana, msifuni, Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni, Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli. 24 Maana hakulidharau teso la mteswa, Wala hakuchukizwa nalo; Wala hakumficha uso wake, Bali alipomlilia akamsikia. 25 Kwako zinatoka sifa zangu Katika kusanyiko kubwa. Nitaziondoa nadhiri zangu Mbele yao wamchao. 26 Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao Bwana watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele. 27 Miisho yote ya dunia itakumbuka, Na watu watamrejea Bwana; Jamaa zote za mataifa watamsujudia. 28 Maana ufalme una Bwana, Naye ndiye awatawalaye mataifa. 29 Wakwasi wote wa dunia watakula na kusujudu, Humwinamia wote washukao mavumbini; Naam, yeye asiyeweza kujihuisha nafsi yake, 30 Wazao wake watamtumikia. Zitasimuliwa habari za Bwana, Kwa kizazi kitakachokuja, 31 Nao watawahubiri watakaozaliwa haki yake, Ya kwamba ndiye aliyeyafanya.

 

Kwenye maandiko ya Yohana 19:23-24 tunamuona mwingine na unabii wa mwisho ukitimia. Maaskari waligawana nguo zake kwa kuzipigia kura kwa vazi au kanzu zake kama ilivyotabiriwa (Zaburi 22:18). Hii ni sehemu ya mwisho ya unabii na huenda ulitokea baada ya matamshi yake ya Zaburi 22. Lakini Mungu hakumficha uso wake wala kumsahau kama inavyosema Zaburi (Zaburi 22:24).

 

Baada ya kumkabidhi mama yake kwenye uangalizi wa mwanafunzi aliyekuwapo na ambaye alimchukua mara moja kwenye matunzo, ndipo Kristo aliendelea kukamilisha Maandiko Matakatifu na unabii kwa kusema maneno haya, “Naona Kiu”. Kisha walihitimisha kwa kumpitishia sponji iliyojazwa siki, ambayo hatimaye waliitia Hisopo na kumtia kinywani mwake. Wakati Yesu alipoipokea hiyo siki alisema: Imekwisha (teleõ). Hii ilikuwa na maana inayomaanisha kwamba mambo yote yaliyotakiwa kufanyika yalikuwa yamehitimika, kwa kuwa Maandiko hayatanguki (Yohana 10:34-35). Kisha aliinamisha kichwa chake chini, ikimaanisha kuwa kilikuwa bado kinatazama mbele hadi wakati huu na kisha akaitoa roho yake au kukata pumzi yake (paradidõmi). Mathayo anasema akaitoa roho yake (Mathayo 27:50).

 

Andiko pekee ambalo lilikuwa halijatimilika bado halikutimilika hadi alipokuwa tayari na kumtuma roho wake. Hii ilikuwa ni siku ya 14 Nisan ya mwaka 30 BK. Ilianguka siku ya Jumatano. Hakukuwa na mwaka mwingine ambao Kristo angeweza kuuawa kwa mujibu wa rekodi za Biblia, kwa kuwa siku ya 14 Abibu au Nisan iliangukia siku ya Ijumaa (soma jarida la Nyakati za Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159)). Fundisho la Kuteswa na Kuuawa siku ya Ijuma ni sehemu ya imani ya Easter au ibada za Baal-Istar au Easter, imani ya waabudu mungu-mke aliyekuwa anaabudiwa na makuhani wa Attis katika  pande za Magharibi, au ya waabudu Adonis pande za Mashariki (soma jarida la Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235)). Pia ina uhusiano na imani ya Ndama wa Dhahabu (soma jarida la Ndama wa Dhahabu (Na. 222)). Imani hii ilikuwa pia na uhusiano na Wafilisti na ibada za Derceto na Joka, ambapo alama za samaki na njiwa zimetokana na ibada hizi (soma majarida ya Daudi na Goliathi (Na. 126) na Piñata (Na. 276)).

 

Siku ya Alhamisi, katika mwaka 30 BK, ilikuwa Siku Takatifu ikiwa ni Siku Takatifu ya Kwanza ya Sikukuu ya Mikate Isiyo na Chachu. Jioni au usiku ule ulikuwa ni wa kuila Pasaka (soma jarida la Pasaka (Na. 98)).

 

Kwa mujibu wa Torati, siku hii haikupasa itiwe unajisi kwa kugusa maiti au mwili wa mtu aliyekufa. Kwa hiyo, iliwalazimu kuhakikisha kuwa wawe wamekufa ndani ya wakati ulioruhuiwa. Miguu ya wasulibiwa wawili wa kwanza waliokuwa pamoja naye ilivunjwa, lakini walipofika kwa Kristo walimkuta amekwisha kufa tayari na hawakuivunja miguu yake, ila askari mmoja alimchoma mkuki ubavuni mwake na ikatoka damu na maji na kumwagika chini ardhini.

 

Hii ilitokea ili kutimiliza Andiko lingine kuhusiana na kifo chake. Kwanza kabisa, ni kwamba haukupasa mfupa wake uvunjike (sawa na Zaburi 34:20). Andiko la pili lilisema, “Watamtazama yeye waliyemchoma”, ambalo linatoka kwenye Zekaria 12:10. Hii inamaana na dalili kuuhusu mstari wa uzao wa Masihi (soma jarida la Mstari wa Uzao wa Masihi (Na. 119)). Unabii huu una maana yake pia na kumhusu jinsi alivyokuwa Masihi na pia hatima ya wateule kwa kufanyika kwao elohim (Zekaria 12:8; soma jarida la Mteule Kama Elohim (Na. 1)).

 

Kisha alichukuliwa na Yusufu wa Arimathaya, ambaye alikuwa ni mwanafunzi wa riri wa Masihi, na Yusufu akamuoba Pilato ampe mwili wake na alipewa. Na mwanafunzi mwingine Nikodemo aliyeleta marhamu au marashi yenye uzito wa takriban paundi au ratili mia, walimchukua wakamzike kwenye kaburi alilolichonga Yusufu, ambalo lilikuwa jipya. Jambo hili lilikuwa muhimu pia kwa utakaso wake akiwa kama dhabihu. Kwa kuyajua maandiko na dhabihu ndipo tunaiona Zaburi na ubii wake. Zaburi 22 inamhusu au kumlenga Kristo akiwa kama Sadaka ya Dhambi.

 

Kwenye Zaburi 40 tunamuona Kristo akiwa kama Sadaka Kamili Yote ya Kuteketezwa.

 

Zaburi 40:1-17 Nalimngoja Bwana kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu. 2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu. 3 Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumaini Bwana 4 Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake, Wala hakuwaelekea wenye kiburi, Wala hao wanaogeukia uongo. 5 Ee Bwana, Mungu wangu, umefanya kwa wingi Miujiza yako na mawazo yako kwetu; Hakuna awezaye kufananishwa nawe; Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri, Ni mengi sana hayahesabiki. 6 Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo, Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka. 7 Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, (Katika gombo la chuo nimeandikiwa,) 8 Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu. 9 Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa. Sikuizuia midomo yangu; Ee Bwana, unajua. 10 Sikusitiri haki yako moyoni mwangu; Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako. Sikuficha fadhili zako wala kweli yako Katika kusanyiko kubwa. 11 Nawe, Bwana, usinizuilie rehema zako, Fadhili zako na kweli yako na zinihifadhi daima. 12 Kwa maana mabaya yasiyohesabika Yamenizunguka mimi. Maovu yangu yamenipata, Wala siwezi kuona. Yamezidi kuliko nywele za kichwa changu, Na moyo wangu umeniacha. 13 Ee Bwana, uwe radhi kuniokoa, Ee Bwana, unisaidie hima. 14 Waaibike, wafedheheke pamoja, Wanaoitafuta nafsi yangu waiangamize. Warudishwe nyuma, watahayarishwe, Wapendezwao na shari yangu. 15 Wakae hali ya ukiwa, na iwe aibu yao, Wanaoniambia, Ewe! Ewe! 16 Washangilie, wakufurahie, Wote wakutafutao. Waupendao wokovu wako Waseme daima, Atukuzwe Bwana. 17 Nami ni maskini na mhitaji, Bwana atanitunza. Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, Ee Mungu wangu, usikawie.

 

Kwenye Zaburi 69 tunamuon Kristo akiwa kama Sadaka ya Dhambi (huu pia ni mtazam wa Bullingers sawa na ilivyo kwenye Znye Zaburi 69:1).

Zaburi 69:1-36 Ee Mungu, uniokoe, Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu. 2 Ninazama katika matope mengi, Pasipowezekana kusimama. Nimefika penye maji ya vilindi, Mkondo wa maji unanigharikisha. 3 Nimechoka kwa kulia kwangu, Koo yangu imekauka. Macho yangu yamedhoofu Kwa kumngoja Mungu wangu. 4 Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua. 5 Ee Mungu, unajua upumbavu wangu, Wala hukufichwa dhambi yangu. 6 Wanaokungoja Wewe wasiaibishwe, Kwa ajili yangu, Bwana, MUNGU wa majeshi. Wanaokutafuta Wewe wasifedheheshwe, Kwa ajili yangu, Ee Mungu wa Israeli. 7 Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu, Fedheha imenifunika uso wangu. 8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, Na msikwao kwa wana wa mama yangu. 9 Maana wivu wa nyumba yako umenila, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata. 10 Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa laumu juu yangu.

 

Zaburi 69:9 inatajwa au kunukuliwa kwenye Yohana 15:25.

Yohana 15:25 Lakini litimie lile neno lililoandikwa katika torati yao, Walinichukia bure.

 

Zaburi 69:10 inaendelea kusema: Nilipofanya gunia kuwa nguo zangu, Nikawa mithali kwao. 12 Waketio langoni hunisema, Na nyimbo za walevi hunidhihaki. 13 Nami maombi yangu nakuomba Wewe, Bwana, Wakati ukupendezao; Ee Mungu, Kwa wingi wa fadhili zako unijibu, Katika kweli ya wokovu wako. 14 Uniponye kwa kunitoa matopeni, Wala usiniache nikazama. Na niponywe nao wanaonichukia, Na katika vilindi vya maji. 15 Mkondo usinigharikishe, wala vilindi visinimeze, Wala shimo lisifumbe kinywa chake juu yangu. 16 Ee Bwana, unijibu, maana fadhili zako ni njema, Kwa kadiri ya rehema zako unielekee. 17 Wala usinifiche uso wako, mimi mtumishi wako, Maana mimi nimo taabuni, unijibu upesi. 18 Uikaribie nafsi yangu, uikomboe, Kwa sababu ya adui zangu unifidie. 19 Wewe umejua kulaumiwa kwangu, Na kuaibika na kufedheheka kwangu, Mbele zako Wewe wako watesi wangu wote. 20 Laumu imenivunja moyo, Nami ninaugua sana. Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu. 21 Wakanipa uchungu kuwa chakula changu; Nami nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki. 22 Meza yao mbele yao na iwe mtego; Naam, wakiwa salama na iwe tanzi. 23 Macho yao yatiwe giza wasione, Na viuno vyao uvitetemeshe daima. 24 Uimwage ghadhabu yako juu yao, Na ukali wa hasira yako uwapate. 25 Matuo yao na yawe ukiwa, Pasiwe na mtu wa kukaa hemani mwao. 26 Maana wanamwudhi mtu uliyempiga Wewe, Wanasimulia maumivu ya hao uliowatia jeraha. 27 Uwaongezee uovu juu ya uovu, Wala wasiingie katika haki yako. 28 Na wafutwe katika chuo cha uhai, Wala pamoja na wenye haki wasiandikwe. 29 Nami niliye maskini na mtu wa huzuni, Mungu, wokovu wako utaniinua. 30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo, Nami nitamtukuza kwa shukrani. 31 Nayo yatampendeza Bwana kuliko ng'ombe, Au ndama mwenye pembe na kwato. 32 Walioonewa watakapoona watafurahi; Enyi mmtafutao Mungu, mioyo yenu ihuishwe. 33 Kwa kuwa Bwana huwasikia wahitaji, Wala hawadharau wafungwa wake. 34 Mbingu na nchi zimsifu, Bahari na vyote viendavyo ndani yake. 35 Maana Mungu ataiokoa Sayuni, na kuijenga miji ya Yuda, Na watu watakaa ndani yake na kuimiliki. 36 Wazao wa watumishi wake watairithi, Nao walipendao jina lake watakaa humo.

 

Zaburi 69:14-20 inachukuliwa na Bullinger kuhusiana na Gethsemane inayotajwa kwenye Mathayo 26:36-45. Inajiri na matukio ya mateso na kusulibiwa ambapo maadui wa Kristo wakiwa mbele yake.

Mathayo 26:36-45 Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe. 37 Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka. 38 Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami. 39 Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe. 40 Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? 41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu. 42 Akaenda tena mara ya pili, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwa haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisipokunywa, mapenzi yako yatimizwe. 43 Akaja tena, akawakuta wamelala; maana macho yao yamekuwa mazito. 44 Akawaacha tena, akaenda, akaomba mara ya tatu, akisema maneno yale yale. 45 Kisha akawajia wanafunzi wake, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike tazama, saa imekaribia, na Mwana wa Adamu anatiwa katika mikono ya wenye dhambi.

 

Zaburi 69:21 inataja tukio la kusulibiwa (Mathayo 27:34-48; Yohana 19:29). Ni unabii unaobidi utimilike kabla ya kifo chake kama Masihi, kwa kunywesha siki. Kitendo hicho na kumnywesha nyongo iliyotolewa mwanzoni kabisa, inaleta hukumu kwa Yuda. Wamepewa zaidi, kama kabila kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Wanaingia kwenye madaraja au viwango vya mteule wakiwa kila mmoja peke yake tu. Hawahitaji kuwa wamefanya hili.

 

Zaburi 69:25 inamtaja Yuda wa kwenye Matendo 1:20 kama alivyokaririwa hapa. Hili ni suala sasa kwenye maneno ya mitume kumi na wawili. Tuna mitume kumi na mbili watakaoyahukumu makabila. Kuna mtume mkuu mmoja na anayeliwakilisha kila kabila. Kabila la Lawi linauchukua ukuhani, bali kuna makabila kumi na mbili tu yanayohusika. Yuda aliashiria usaliti ambao Yuda waliomfanyia Masihi aliyetumwa kao akiwa ni Mjumbe wa Agano aliyewatoa kutoka utumwani kwenye tukio la Kutoka kwao utumwani. Alikuwa wa kabila la Yuda na wa ukoo uliokuwa katika Bethlehemu ya Efrata. Kwa hiyo ni zaidi hata ya kumtaja tu Yuda anapokuwa anajumuishwa hapa. Zaburi 69:22-28 Bullinger anaichukulia kuwa inashabihiana na Warumi 11:9,10. Nukuu hii inafuatia kutoka kwenye Warumi 11:8 inatoshabihiana na andiko lililoandikwa huko nyuma la Isaya 29:10. Bila shaka hapa unabii huu ulihusiana na kushindwa kwa Yuda kama taifa kumpokea Roho Mtakatifu kama wakati ule na mapokeo yao yalifanyika kuwa mitego kamili kwao.

 

Kila sheria ambayo ilikuwepo kwa ajili ya mambo yao ilifanyika kuwa mtego kwao. Baada ya kuangushwa au kubomolewa kwa Hekalu, Yuda na Lawi waliiharibu au kuobadilisha na kuipotosha kalenda kwa kuweka kipengele cha uahirisho na kuifanya sheria ya ulaji wa vyakula kuwa kitu cha ziada tu hadi leo hii. Hawakuweza kusikia, wala kuelewa, ili wageuke na kuokoka. Hawakuwa na urithi na makazi yao yaliangamizwa na kufanywa ukiwa kwa kipindi cha Milenia. Lakini Mungu atauponya na kuukoa Sayuni na ataijenga miji ya Yuda. Katia siku za mwisho watafanywa upya na Roho Mtakatifu atamwagwa juu yao kwa kupitia Masihi waliyemuua atakayerudi kuwaokoa wale wanaomngojea kwa hamu kubwa. Hawa ni wale wanaozishika amri za Mungu na imani ya Yesu Kristo, au Yoshua Masihi (Ufunuo 12:17: 14:12).

 

 

q