Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[A3]
Mwongozo Uliopo wa Kuliendesha Kanisa la CCG
(Toleo La 1.0 20090718-20090718)
Ili kuweza kuendana na muundo kamilifu wa Sheria za kibiblia, Mwongozo
ufuatao wa Jinsi ya Kuliendesha Kanisa kwa mujibu wa Ktiba ya CCG inatakiwa
kutiliwa maanani.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2009 Wade Cox)
(tr. 2014)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la
haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa
au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya
lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Sura ya
1: Shirika
Kanisa la CCG limeweka
maongozi yake kwa muundo wa ngazi za kitaifa unaozingatia muundo wa kibiblia
kama walivyoelekezwa wana wa Israeli.
Kutoka 18:12-27
Yethro mkwewe Musa
akamletea Mungu sadaka ya kuteketezwa na dhabihu; na Haruni akaja, na wazee
wote wa Israeli, wale chakula pamoja na mkwewe Musa mbele za Mungu. 13 Asubuhi yake Musa akaketi ili awapishie hukumu watu; na
hao watu wakasimama kumzunguka Musa tangu asubuhi hata jioni. 14 Mkwewe Musa alipoyaona yote aliyowafanyia watu, akasema,
Ni jambo gani hili uwatendealo hao watu? Kwani wewe kuketi hapo peke yako, na
watu wote kusimama kwako tangu asubuhi hata jioni? 15 Musa
akamwambia mkwewe, Ni kwa sababu watu hunijilia mimi wapate kumwuliza Mungu; 16 wakiwa na neno, hunijilia; nami naamua kati ya mtu na
mwenziwe, nami nawajuvisha amri za Mungu, na sheria zake. 17 Mkwewe
Musa akamwambia, Jambo hili ufanyalo si jema. 18 Huna
budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia; maana jambo hili ni
zito mno kwako; huwezi wewe kulitenda peke yako. 19 Sikiza
sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe kwa
ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao; 20
nawe utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo
inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kuifanya. 21 Zaidi
ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu,
watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu
wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi; 22 nao wawaamue watu hawa sikuzote; kisha, kila neno lililo
kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno dogo wataliamua wenyewe; basi kwako
wewe mwenyewe utapata nafasi zaidi, nao watauchukua huo mzigo pamoja nawe. 23 Kwamba utafanya jambo hili, na Mungu akikuagiza hivyo,
basi utaweza kusimama wewe, na watu hawa wote nao watakwenda mahali pao kwa
amani. 24 Basi Musa akasikiza neno la mkwewe,
akayafanya yote aliyokuwa amemwambia. 25 Musa
akawachagua watu wenye uwezo katika Israeli yote, akawaweka wawe vichwa juu ya
watu, wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi. 26 Nao wakawaamua watu sikuzote; mashauri magumu wakamletea
Musa, lakini kila neno dogo wakaliamua wenyewe. 27 Kisha
Musa akaagana na mkwewe; naye akaenda zake, mpaka nchi yake mwenyewe.
Tunaona
kuchaguliwa kwa viongozi waliotokana na uchaguzi na mapendekezo ya watu, kutoka
kwa Musa na maandiko.
Kumbukumbu la Torati
1:9-17
Nami wakati ule niliwaambia, nikasema, Siwezi mimi mwenyewe kuwachukua peke
yangu. 10 Bwana, Mungu wenu, amewafanya kuwa wengi,
nanyi, angalieni, mmekuwa leo mfano wa nyota za mbinguni kwa wingi.11 Bwana, Mungu wa baba zenu, na awafanye kuwa wengi mara
elfu kuliko mlivyo, na kuwabarikia, kama alivyowaahidi. 12 Nitachukuaje
peke yangu mimi mwenyewe udhia wenu, na mzigo wenu, na mateto yenu? 13 Jitwalieni watu wenye akili na fahamu, watu
wanaojulikana, kwa kadiri ya kabila zenu, nami nitawafanya wawe vichwa juu
yenu. 14 Nanyi mkanijibu, mkaniambia, Jambo ulilonena
ni jema la kufanya. 15 Basi nikatwaa vichwa vya kabila
zenu wenye akili, waliojulikana, nikawafanya wawe vichwa juu yenu, maakida ya
elfu elfu, na maakida ya mia mia, na maakida ya hamsini hamsini, na maakida ya
kumi kumi, na wenye amri, kwa kadiri ya kabila zenu. 16 Nikawaagiza
wakati ule waamuzi wenu, nikawaambia, Sikizeni ninyi maneno kati ya ndugu zenu,
mkaamue kwa haki kati ya mtu na nduguye, na mgeni aliye pamoja naye. 17 Msitazame nafsi za watu katika hukumu; mwasikize wadogo
na wakubwa sawasawa; msiche uso wa mtu awaye yote; kwa kuwa hukumu ni ya Mungu;
na lile neno liwashindalo mniletee mimi, nami nitalisikiza.
Kwa sababu hii
tunawashirikisha wapendwa waumini wetu katika kuwachagua viongozi
watakaowaongoza.
1.1.
1.1.1. Hii
inatokana na mfano wa maandiko matakatifu kwamba kila Halmashauri Kuu ya Taifa
kama itaweza kutunga katiba inayoendana na maongozi ya kamati yake ya uongozi,
muundo wa kishirika ulio chini ya kiongozi wa maelfu.
1.1.2. Kila kundi
la hawa elfu linapaswa kuundwa kutokana na muundo wa mgawanyo wa watu mia mia
na ulio na vikundi vya hamsinihamsihi na kisha watu kumikumi.
1.1.3. Muundo huu
wa watu utahusiana na hesabu ya wanaume watu wazima sawasawa na inavyotuambia
Biblia kuhusu kuwahesabu wanaume watuwazima wanaozidi umri wa miaka 20.
1.1.4. Wanaume wenye
umri wa kati ya miaka 20 hadi 50 wanastahili kuchukua majukumu yote ya
kimaongozi kama wataonekana wanafaa kuchukua uongozi na kuhudumu.
1.1.5. Wanaume
wenye umri wa miaka 50 hadi 70 nanachukuliwa kuwa wanafaa kusaidia kwenye
shughuli za kuongoza au kuhudumu kwenye ibada.
1.1.6. Hali ya
kupatwa na maradhi aua madhara inayothibitishwa na watabibu inaweza kumfanya
mtu asihusishwe na mambo ya kihuduma.
1.1.7. Wanawake
wanajumuishwa pamoja kwa uangalizi wa wanaume kwenye huduma zote zinazowahusu
wanawake, na wanaweza kuongezwa kwenye huduma kama wasaidizi tu hasa kwenye
huduma za mapishi, masuala yanayohusu usafi na afya za watu, kuangalia nyumba,
usafi wa vyakula, mambo yanayohusu wanawake na kuwaelekeza watoto an kuwapa
miongozo mbalimbali kama watakavyohitajika na kulingana na jinsi mazingira
yatakavyoruhusu.
1.2.
1.2.1. Mwenyekiti
wa Taifa ni Amirijeshi Mkuu wa kusimamia muundo huu, akisaidiwa na kamati yake.
1.2.2. Kila jumla
ya watu elfu kama wanavyojulikana na kuitwa ‘eleph
au kundi la familia kwa kumaana ya kimaongozi. Neno hili linatokana na neno la
Kiebrania linalomaanisha kundi la ng’ome wenye nguvu au maksai au familia na
pia ni tarakimu ya 1000. Vikundi hivi kwa kawaida vinaundwa kutoka kwenye wilaya
na mijini. Vinapaswa kuitwa kwa majina ya wiiaya ilea ma kata ilea ma na kitu
kitakachoweza kutambulisha mahala walipo, mfano kinaweza kuitwa ni Kikundi cha
Familia “x”. jedwali linaloonyesha namna ya kupangilia vikundi limeonyshwa hapo
chini kwenye ukurasa wa Nyongeza ama Appendix 1. Kwa kweli ni kusanyikon la
Maelfu au ni parishi zinazounda mwanzo wa kundi zima lote.
1.2.3.1. Kila
kikundi kinatakiwa kiwe na mgawanyo wa vikundi vidogovidogo kumi vya vikundi
vya familia. Vikundi hivi vitajulikana kama Makanisa ya Mahali Pamoja. Kwa
mujibu wa utaratibu huu, kanisa lililo kwenye mgawanyo mdogo litajumuisha
wastani wa wanaume wenye uwezo na mwitikio wapatao 100 na familia zao na ni
watu wa zamani wa eneo lile. Hili lilijulikana kama la mamia kwa lugha ya kale
ya Kianglo-Saxon na hawa Mamia walifanyika kuwa ni chanzo cha kuwepo kwa mfumo
Mzima. Hawa “Mia” kimsingi wanamaanisha sawa na parishi na wanachimbuko lake
kwa wale mamia walioko kwenye biblia kwenye mwongozo huu
1.2.3.2. Wakati
kanisa linapokuwa na zaidi ya vikundi vidogovidogo vitatu (kama vile wanaume
wenye uwezo zaidi bove 150) kwa kawaida kanisa jipya linatarajiwa lianzishwe
kutokana na sehemu ya lile kundi dogo. Kutegemea na eneo, vinginevyo, uwekaji
wa kundi hili dogo linaweza kuwa na maeneo la idadi ya wanaume kumi dadi ya
kumi ili kuanzisha kanisa jipya. Kundi hlvi dogo la vikundi vitatu linaweza kuundwa
kutokana na idadi ya wanaume 100 na 150 na kiongozi anayejulikana kama kamanda
wa kundi dogo. Kanisa moja linaweza kujukuisha vikundi hivi vidogovidogo viwili
au zaidi kutegemea na umbali wake utakavyokuwa. Kwa sababu hii, Msimamizi au
Kamanda wa hawa Mia atamsaidia Kiongozi Mkuu au Kodineta Mkuu. Haipendezi kuona
kwamba kundi moja likiwa kubwa sana na linakuwa kivyakevyake au kipekeepekee.
1.2.3.3. Kanisa
lililo kwenye kundi dogo linakuwa kwenye ukubwa wa wastani unaoweza kuwafanya
waandae vizuri sikukuu na kujipikia kama kundi. Kundi la familia la wnaue Elfu
Moja ndilo kubwa sana linalojumuisha watu wengine wanaostahili na wenye vifaa
vya kupikia waliokusanyika kutoka kwenye vikundi vidogovidogo. Hawa wanaweza
kutenganishwa kwenye vikundi vidogovidogo wakati wanaposhiriki mlo kutokana na
aina ya vyombo vya kulia vilivyo hata hivyo.
1.2.3.4. Mambo
yanayohusiana na uadibisho na maongozi yanaweza kushughulikiwa na ngazi hii au
yatashughulikiwa kama ni mambo makubwa sana.
1.2.3.5. Hawa
makamanda ni makodineta wa kanisa pamoja na makamanda wa vikundi wanaojulikana
kama makodineta wakubwa.
1.2.3.6. Kila kanisa
lililo kwenye jumuia ndogo litagawanywa kwa jumuia yenye makundi mawili ya watu
hamsini walio chini ya makoodineta wasaidizi.
1.2.3.7. Kila
jumuia ndogo ya kanisa inatakiwa kuwa na mgawanyo zaidi wa vikundi vidogo vya
kumikumi (kwa Kiebrania ehser) wanaume
walio chini ya amri ya shemasi kiongozi au ‘acolyte’ shemasi msaidizi aliwa
kama mtumishi aliyepitia mafunzo. Msaidizi anaweza kuchaguliwa kama ni msaidizi
wa kamanda wa wa jumuia ndogo kutoka kwenye moja ya vikundi hivi. Kundi hili ni
kundi la msingi kwa maadhimisho yam lo wa Pasaka katika jioni ya siku ya 15
Abibu, ambao ndio Mwezi wa Kwanza.
1.2.3.8. Wanawake
walioolewa wanatakiwa kuwatii waume zao kama wanavyomtii Bwana (Waefeso
5:22-24, NIV). Wajane na wanawake wasiiilewa
ambao hawaishi na wazazi wao watahudumiwa na mashemasi wa kike wanaotoa ripoti
zao kwa viongozi wao au kwenye jumuia ndogondogo na makamanda wa kanisa
1.3.1. Maafisa
wote wanachaguliwa kwa maelekezo ya Koodineta Mkuu na Kamati ya Halmashauri ya
Taifa.
1.3.2. Maafisa
wote wanatathminiwa tena baada ya kila miaka saba ya kwenye Kikao cha
Halmashauri Kuu ya Mwaka wa Sabato.
1.3.1. Uchaguzi
au uteuzi wa wazee wa kanisa na maaskofu unafanywa na Koodineta Mkuu pamoja na
jopo la Baraza ya Wazee wa Halmashauri Kuu ya Dunia.
1.4.1.1. Kama CCG
ilivyo na mataifa yenye jumla wa wafuasi zaidi ya efu ishirini na kwa hiyo
inakuwa na zaidi ya migawanyo kumi ya kieneo, itakuwa na ulazima wa kuwaweka
pamoja wale walio kwenye maeneo hayo na Makoodineta wa Eneo kwenye kila nchi au
jimbo au kwenye eneo husika. Viongozi hawa wasichanganywe na Makoodineta wa
Kanda anayeangalia eneo la zaidi ya nchi moja na aliyeteuliwa na Halmashauri
Kuu ya Dunia kwa kazi au malengo ya kimisionari.
.
1.4.1.2. Muundo
wa kawaida wa baraza kuu umeorodheshwa kwenye maandiko matakatifu.
Watu waliokuwa na
Daudi wakutegemeka walikuwa elfu sita (1Samweli 23:13).
Waliongozwa
vizuri na Mashukjaa au Watu wenye Uweza katika Israeli.
Kanisa la CCG lina
Halmashauri za Kitaifa zenye watu kumi na wawili. Hawa wanawajibika kwenye
maongozi na huduma za kitaifa za makanisa wakiwa chini ya kamanda wao wa taifa.
Mwenyekiti wa Halmashauri
ya Taifa ana mamlaka ya kiuangalizi na ndiye Kamanda wa hawa Watatu (sawa na
isemavyo 2Samweli 23:8-17).
Hawa Watatu ni
makamanda wa viongozi Watatu wa Kundi la Taifa.
Sehemu ya Mia
sita ya Komandi Mkuu ya Taifa wapo chini ya mamlaka ya komandi ya Tatu, kwa
hiyo ile mia sita inagawanywa kwa makundi Matatu ya Ishiriniishirini (30 x 20 =
600).
Kwa hiyo, kila
mmoja wa Watatu hawa ni kamanda wa kumi wa Thelathini (1 x 10 x 20 = 200).
Watu 600 wanakuwa
na uwezo wa kuwa Makapteni wa Mamia na Makapteni wa Maelfu na hatimaye kuwa
Makapteni wa Maeneo-jimbo. Kwa hiyo, kila taifa litakalokuwa na uwezo wa kuwa
na jeshi kuu la watu 14,400,000 pamoja na makanmanda wao, au linawezakuwa na
jumla ya vikundi 100 vikundi vya watu 144,000. Hili ni Jeshi la Mungu
litakalokuwepo kwenye marejesho ya ulimwengu mpya chini ya Masihi. Kuna idadi
ya migawanyo Maelfu 24 kwenye muundo wa Migawanyo wa Jeshi la Bblia na
Migawanyo 200 ya Jeshi la Biblia la migawanyo Mitatu, pamoja na Migawanyo
mingine 600 ya Halmashauri iliyo chini ya komandi kwa mazingira mengine yoyote
(tazama chati iliyoambatanishwa).
Kila mojawapo ya
vikundi hivi vitatu vya watu Mia Sita vitakuwa na kiongozi mkuu mmoja
aliyechaguliwa kuwa kiongozi wao. Hawa ni wale walio kwenye Kundi la Pili la
yale Matatu (2Samweli 23:20-23). Kundi la Tatu la watu 200 liliunda Jeshi la
Ulinzi la Daudi. Linaitwa Jeshi la Ulinzi la Mwenyekiti linalotokana na
uchaguzi wake hadi Ufufuo wa Kwana wa Wafu.
Muundo huu wa
hawa Thelathini wameorotheshwa kwenye 2Samweli 23:24-39. Wamwisho kati ya hawa
Thelathini alikuwa ni Uria, Mhiti, mume wa Bathsheba, mama wa Sulemani. Ndugu
zake wa damu wawatoto wa Bathsheba, wanapatikana kwenye Nyumba ya Daudi hadi
hivi leo. Anaweza kuwa wa kundi la nasaba-damu la RxR1 ambalo lilitawanyika
baada ya mwaka 900 KK, likiwa na alama za nasaba-damu za R1b na R1a za kundi la
kinasaba-damu cha YDNA ni miongoni mwa wa ukoo wa Daudi, na hasa kupitia kwa
binti wa Daudi. Wanapatikana kwenye koo za Dayan na Salathiel/Shealtiel hadi
leo katika taifa la Israeli. Kwa hiyo ilionekana kuenea kwa kupitia damu za
wanawake na uzao uliopitia kwao.
2Samweli 23:8-19
Haya ndiyo majina ya
mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethia, Mtahkemoni alikuwa ndiye kiongozi
wa wale watatu, yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua kwa
siku moja. 9Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodaib Mwahohi. Akiwa
mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati
walipowadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pasi-Daminu kwa ajili ya
vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma, 10lakini yeye alisimama imara
akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. BWANA
akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara
za waliokufa. 11Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee Mharari. Wafilisti
walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya
Israeli viliwakimbia. 12Lakini Shama akasimama imara katikati ya shamba. Akatetea
na kuwaua Wafilisti, naye BWANA akawapatia ushindi mkubwa. 13Wakati wa mavuno,
viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka wakamwendea Daudi katika
pango la Adulamu, wakati ambapo kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi
kufika Bonde la Refaimu. 14Wakati huo Daudi alikuwa ndani ya ngome, nao askari
walinzi wa ngome wa Wafilisti walikuwa huko Bethlehemu. 15Daudi akatamani maji,
akasema, “Laiti kwamba mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kile kisima
kilicho karibu na lango la Bethlehemu!’’ 16Basi mashujaa hao watatu wakapenya
katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwenye kile kisima kilicho
karibu na lango la Bethelemu na kumletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa,
badala yake, aliyamimina mbele za BWANA. 17Akasema, “Iwe mbali nami, Ee BWANA ,
kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha
maisha yao? Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu. 18Abishai
ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye aliyekuwa kiongozi wa hao watatu. Aliinua
mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama
hao watatu. 19Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa
jemadari wao, ingawa hakuwekwa miongoni mwao
Tunaona kwamba
kulikuwa na kundi la pili la hawa watatu kutoka kwenye aya zinazofuatia za
2Samweli 23:
20Benaya mwana wa
Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabzeeli, ambaye alifanya mambo mengi
ya ushujaa. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia
alishuka Shimoni siku kulipokuwa na barafu na kumwuua simba. 21Pia alimwua
Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya
alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumwua
kwa mkuki wake mwenyewe. 22Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa
Yehoyada, naye pia alikuwa maarufu sawa na wale mashujaa watatu. 23Alipata
heshima kubwa zaidi kuliko ye yote wa wale Thelathini, lakini hakuwekwa
miongoni mwa wale watatu. Daudi alimweka kuwa kiongozi wa walinzi wake
mwenyewe. 24Miongoni mwa wale thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu,
Elhana mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu. 25Shama Mharodi, Elika Mharodi, 26Helesi
Mpalti, Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa, 27Abiezeri kutoka Anathothi, Mebunai
Mhushathi, 28Salmoni Mwahohi, Muharai Mnetofathi, 29Heledi mwana wa Baana
Mnetofathi, Ithai mwana wa Ribai kutoka Gibea katika Benyamini, 30Benaya
Mpirathoni, Hidai kutoka vijito vya Gaashi, 31Abi - Alboni Mwarbathi, Azmawethi
Mbarhumi, 32Eliaba Mshaalboni, wana wa Yasheni, Yonathani 33mwana wa Shama
Mharari, Ahiamu mwana wa Sharari Mharari, 34Elifeleti mwana wa Ahasbai
Mmaakathi, Eliamu mwana wa Ahithofeli Mgiloni, 35Hezro Mkarmeli, Paarai Mwarbi 36Igali
mwana wa Nathani kutoka Soba, mwana wa Hagri, 37Seleki Mwaamori, Naharai
Mbeerothi, aliyekuwa mchukuzi wa silaha za Yoabu mwana wa Seruya, 38Ira
Mwithri, Gerebu Mwithri 39na Uria Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu
thelathini na saba.
Andiko
linaonyesha kwamba 2Samweli 23:20 inawataja ariels wawili au watu
wanaofananishwa na samba wa Moabu waliouawa na mmoja wa hawa mashujaa watatu.
Hata hivyo, mahala pengine ambapo neno hili limetumika ni kwenye Isaya 29:1,2
ambapo panautaja Mji aliokuwa anaishi Daudi. Jina asilia la mji wa Yerusalemu
ni Har-El linalomaanisha milima ya kale ya Wamisri. Neno Ariel linaweza
kumaanisha pia kuwa au ni samba wa Mungu kama huenda inavyoonekana hapa au
madhabahu ya juu ya Mungu kama ilivyo kwenye Ezekieli 43:15-16.
Muundo huu wa kiuongozi ndio tunaoutarajia
kuwa utatumika wakati atakaporudi Masihi na kutawala hapa duniani kwa mamlaka
ya Daudi.
Miongozo mingine
zaidi kuhusu muundo huu ni kama ifuatavyo:
Kwa hiyo kila
kikosi kilipaswa kiundwe na wanaume elfu arobaini na nne.
1.4.1.3.
Walitakiwa wafundishwe au kuandaliwa kwa kazi na kuhudumu mwezi hadi mwezi,
kama vilivyowekwa vikosi kwa mujibu wa biblia.
1.4.1.4. Hadi
kufikia vikosi ishirini na vinne waliweka makamanda wa maelfu ili wafanye kazi
za wakuu wa vikosi pamoja na Maelfu wao. Hawa Elfu hawakuwa na nguvu kamili,
bali walipaswa wajengwe na hili kundi la hawa Mamia. Kila mmoja wa hawa Maelfu
atatumika kama mtianguvu wa kila komandi ya hivi vikosi. Haawa Maelfu ishirini
na nne wanapaswa waundwe kwanza kwenye muundo wa eneo la Kitaifa.
Hivi Vikosi kwa
ujumla vinaweza kuundwa kwa maana mbili, bali vinaweza kuwa vimeundwa kwa
sababu fulani maalumu na Sababu hasa ya kuundwa kwa kila Kikosi ni kwa kutoa
huduma za Madawa au Kitabibu na Utoaji Elimu au Uelimishaji.
Vyo vikuu
vinapaswa pia kuanzishwa vikiwa kama ni kitu tegemezi cha muhimu kwa shughuli
za uelimishaji, utabibu na kwa mchakato wa kisayansi ya muundo wa kijamii. Hizi
zinaweza pia kuwa na umuhimu wa kuwa ni vyenye kusaidia tu na sio vipaumbele.
Wanawake wote wanapaswa kupewa fursa ya elimu. Mafunzo na uelimishaji vinapaswa
kuwa ni shughuli endelevu kwa wafanyakazi au wahudumu wa ngazi zote.
1.4.1.5.
Halmashauri ya Taifa inatakiwa kuwaweka Mahakimu na Mawakili wenye uwezo ili
washughulikie masuala ya hukumu na kufanya ufumbuzi wa mabishano na kuanzisha
mahakama itakayosikiliza madai au mambo ambayo hayajapatiwa ufumbuzi kwenye
Kikundi chao na Eneo lao la Kijimbo.
1.4.1.6. Mahakama
Kuu ya Rufaa ni Halmashauri Kuu au Makao Makuu ya Kanisa Ulimwenguni ambayo
inajumuisha Wazee waliobobea kuzijua kanuni za kisheria.
1.4.1.7. Bodi
yote ya Kanisa inapaswa kuuundwa kwa maamuzi ya mchakato wa kimahakama ya
Kanisa ambao unapaswa uwe wa mujibu wa sheria za biblia na kanuni zake.
1.4.2. Maeneo
yanaweza kupangiliwa ndani ya sharika na makoodineta wa majimbo au nchi kama
itakavyoonekana inafaa au kwenye muundo wa sehemu nyingine nyingi kadhaa na
Makamanda Wasimamizi waliokubalika. Yanweza kuundwa kutoka na eneo lolote la
muundo wa Kidivisheni kama mazingira yatakavyolazimika kuwa
1.4.3.1. Pale
ambapo kuna maeneo matatu ya komandi watatoa ripoti zao moja kwa moja kwa
Koodineta wa Taifa. Pale ambapo kuna zaidi ya maeneo matatu ya komandi
zinazoundwa kwa divisheni zenye zaidi ya wanaume 24,000. Inatakiwa kuwe na
divisheni 24 kwenye eneo maalumu lililogawanywa kwa divisheni mbili maeneo
fulani katika nchi. Majimbo yanapaswa kujumuishwa kwa malengo yale. Hawa ni
jumla ya watu 576,000 ambao ni wanaume na familia zao kutokana na muudo huu wa
jeshi imara na lenye ngivu.
1.4.3.2. Kwa hiyo
kutaweza sasa kuwa na divisheni mbili iliyokabidhiwa majukumu ya kila wakati na
kwenye eneo la masuala ya kidini na kijamii, na watapewa majukumu yote ya kila
jambo ambao ni wawili kwa kila mwezi watakaopangiwa sawa miongoni mwa Watatu
hadi zitapapoundwa nyingine zaidi ya nane kwenye kila Tatu na kisha zitachukuliwa
kama mbili kwa wakati mmoja hadi kufikia kwenye Ishirini ya kila Tatu. Nyingine
Maelfu zinaweza kuundwa kama maeneo mengine yatakayoonekana kuna walioongoka
baada ya kufikiwa na imani.
1.4.4. Pale
ambapo kuna zaidi ya divisheni tatu katika lila mgawanyo wa Tatu zinaweza
kuundwa na Makamanda wa Kundi na Kundi waliochaguliwa kutoka kwa kila divisheni
mbili au zaidi. Mkuu wa hawa Kumi anazisimamia komando zinazoweza kufikia hadi
tano hadi Kundi. Kunatalkiwa kuwe na miundombinu ya ziada kusaidia ya wanaume
walioko kwenye hawa makamanda wa Makundi ya vikundi vidogovidogo
1.4.5. Hawa
watatu wanajulikana kama Maafisa wa Huduma-kazi wa Taifa waliopangiwa kusimamia
vikundi kadhaa na vitendea kazi vya misaada. Hadi pale shuguli za uongofu
itakapokamilika msingi wa muundo wa mataifa utatofautiana kadiri kali ya
wongofu inapoendelea na kuwa ni wa dunia nzima.
2.1. Namna za
utendaji inatakiwa zifantike sawasawa na zilivyo programu zilizoamuliwa na Halmashauri
ya Taifa na kazi za Kimisionari kama zilivyopangwa na kuagizwa na Halmashauri
Kuu ya Dunia/ kazi hizo zinaweza kujuisha yafuatayo:
2.1.1. Ujenzi wa
majengo kwenye maeneo kama ilivyoelekezwa kwa matumizi ya nyumba, shule,
hospitali na wanyama wa kufugwa kama ilivyoamuliwa.
2.1.2. Ujenzi wa
miradi ya mashamba kama ilivyoamuliwa wakiwemo mabwawa ya samaki, miradi ya
uvuvi, ufugaji wa kuku, miradi ya kufuga, miradi ya maziwa, matunda na bustani
ya mbogamboga.
2.1.3. Kununua
vifaa au zana za elimu za viwango vyote.
2.1.4. Kununua na
kutumia vifaa vya utabibu n vya hospitali.
2.1.5. Ugawaji na
usambazaji wa vifaa vya kupashiana Habari kama ilivyoelekezwa na Halmashauri
Kuu ya Dunia na Halmashauri ya Taifa kwa mujibu wa katiba ilivyo.
2.1.6. Kushughulika
na kuangalia utendaji kazi wa shughuli za ujenzi na utendaji kazi wa mashine
kubwa na vifaa vya kufundishia.
2.1.7. Kuendeleza
program za ugawaji wa chakula na mavazi.
2.1.8.
Kushughulika na miradi ya mazao na
uzalishaji wa vifaa vya ujenzi.
2.1.9.
Kushughulika na usimamizaji wa warsha kwa uzalishaji na utengenezaji wa HIKI
kwa mujibu sawa na vifaa vya kuzalishia tena na vya mawasiliano.
2.1.10. Kuendesha
shughulika za kiusafiri na vifaa vya kila namna.
2.1.11. Kuendesha
na kutengeneza mashine kubwakubwa na nzitonzito.
2.1.12.
\kushughulika na kutengeneza mazalia au mimea kwa ajili ya kuzalisha nguvu za
umeme, maji na makapi yaliyosazwa na kutokuwa na maana au matumizi au mifereji
michafu.
2.2.1. Mnyororo
wa kamandi na nidhamu unatakiwa uanzishwe pamoja na mashitaka na ukataji wa
rufani kwa kila ngazi.
2.2.2. Mahakama
ya usuluishi yanatakiwa yafanye kwa kufuata mujibu wa katiba.
2.2.3.
Ikiwezekana, idara ya sheria inatakiwa iendelezwe na kufundishwa.
2.2.4. Pale
ambapo kanisa la CCG litakuwa limeshika hatamu kwenye majimbo lote, mahakimu
watabidi wawekwe na kama itawezekana na waumini wa CCG.
2.3.1. Kila
halmashauri ya kitaifa inawajibika katika kujihudumia kwa mahitaji yake.
Ulinzi na Usalama
2.4.1. Kila
kikundi kinawajibika katika kuwalinda na kuwapa usalama watu wake na kanisa lao
na kanisa linawjibika kuhakikisha kuwa ulinzi imara na usalama unakuwepo kwenye
nchi yao.
2.5.1. Kila
halmashauri ya taifa ya CCG inapaswa kuwachagua na kuwapa mafunzo watu wake kwa
kadri iwezekanavyo.
2.5.2. Uwezo wa
mkufunzi unapaswa ujaribiwe katika kumudu mafunso ya ufundi yaliyotolewa kama
msaada kwenye ngazi ya juu sana iwezekanavyo.
2.5.3. Wanawake
wanapaswa kuelimishwa kadri iwezekanavyo na wana fursa ya namna moja ya kupata
elimu kama waliyonayo wanaume.
2.5.4. Maeneo ya
Kitaifa ya CCG wanapaswa watumie uwezo wao wa uzalishaji mali katika kujenga
taasisi au vyuo vya mafunzo na kununua vifaa vya elimu. Majengo haya yanaweza
kutumika kwa matumizi aina mbili yakiwemo ya kuyatumia kama majengo ya makanisa
kwa kuwa hayatatumika sikn za Sabaro, Mwandamo wa Mwezi Mpyana siku za Sikukuu
zilizoamriwa.
2.5.5. Mafunzo
yanapaswa kujumuisha mambo yote yanayohusu ufundi wa umeme, umakanika sambamba
na ujuzi ama uhandisi wa kujenga, pamoja na useremala na ufundibomba na aina
nyingine zote za ufundi wa mikono, pamoja na namna zote za utoaji wa elimu ya
juu.
2.1. Namna za
utendaji inatakiwa zifantike sawasawa na zilivyo programu zilizoamuliwa na
Halmashauri ya Taifa na kazi za Kimisionari kama zilivyopangwa na kuagizwa na
Halmashauri Kuu ya Dunia/ kazi hizo zinaweza kujuisha yafuatayo:
2.1.1. Ujenzi wa
majengo kwenye maeneo kama ilivyoelekezwa kwa matumizi ya nyumba, shule, hospitali
na wanyama wa kufugwa kama ilivyoamuliwa.
2.1.2. Ujenzi wa
miradi ya mashamba kama ilivyoamuliwa wakiwemo mabwawa ya samaki, miradi ya
uvuvi, ufugaji wa kuku, miradi ya kufuga, miradi ya maziwa, matunda na bustani
ya mbogamboga.
2.1.3. Kununua
vifaa au zana za elimu za viwango vyote.
2.1.4. Kununua na
kutumia vifaa vya utabibu n vya hospitali.
2.1.5. Ugawaji na
usambazaji wa vifaa vya kupashiana Habari kama ilivyoelekezwa na Halmashauri
Kuu ya Dunia na Halmashauri ya Taifa kwa mujibu wa katiba ilivyo.
2.1.6. Kushughulika
na kuangalia utendaji kazi wa shughuli za ujenzi na utendaji kazi wa mashine
kubwa na vifaa vya kufundishia.
2.1.7. Kuendeleza
program za ugawaji wa chakula na mavazi.
2.1.8. Kushughulika
na miradi ya mazao na uzalishaji wa vifaa
vya ujenzi.
2.1.9. Kushughulika
na usimamizaji wa warsha kwa uzalishaji na utengenezaji wa HIKI kwa mujibu sawa
na vifaa vya kuzalishia tena na vya mawasiliano.
2.1.10. Kuendesha
shughulika za kiusafiri na vifaa vya kila namna.
2.1.11. Kuendesha
na kutengeneza mashine kubwakubwa na nzitonzito.
2.1.12. \kushughulika
na kutengeneza mazalia au mimea kwa ajili ya kuzalisha nguvu za umeme, maji na
makapi yaliyosazwa na kutokuwa na maana au matumizi au mifereji michafu.
2.2.1. Mnyororo
wa kamandi na nidhamu unatakiwa uanzishwe pamoja na mashitaka na ukataji wa
rufani kwa kila ngazi.
2.2.2. Mahakama
ya usuluishi yanatakiwa yafanye kwa kufuata mujibu wa katiba.
2.2.3. Ikiwezekana,
idara ya sheria inatakiwa iendelezwe na kufundishwa.
2.2.4. Pale
ambapo kanisa la CCG litakuwa limeshika hatamu kwenye majimbo lote, mahakimu
watabidi wawekwe na kama itawezekana na waumini wa CCG.
2.3.1. Kila
halmashauri ya kitaifa inawajibika katika kujihudumia kwa mahitaji yake.
Ulinzi na Usalama
2.4.1. Kila
kikundi kinawajibika katika kuwalinda na kuwapa usalama watu wake na kanisa lao
na kanisa linawjibika kuhakikisha kuwa ulinzi imara na usalama unakuwepo kwenye
nchi yao.
2.5.1. Kila
halmashauri ya taifa ya CCG inapaswa kuwachagua na kuwapa mafunzo watu wake kwa
kadri iwezekanavyo.
2.5.2. Uwezo wa
mkufunzi unapaswa ujaribiwe katika kumudu mafunso ya ufundi yaliyotolewa kama
msaada kwenye ngazi ya juu sana iwezekanavyo.
2.5.3. Wanawake
wanapaswa kuelimishwa kadri iwezekanavyo na wana fursa ya namna moja ya kupata
elimu kama waliyonayo wanaume.
2.5.4. Maeneo ya
Kitaifa ya CCG wanapaswa watumie uwezo wao wa uzalishaji mali katika kujenga
taasisi au vyuo vya mafunzo na kununua vifaa vya elimu. Majengo haya yanaweza
kutumika kwa matumizi aina mbili yakiwemo ya kuyatumia kama majengo ya makanisa
kwa kuwa hayatatumika sikn za Sabaro, Mwandamo wa Mwezi Mpyana siku za Sikukuu
zilizoamriwa.
2.5.5. Mafunzo
yanapaswa kujumuisha mambo yote yanayohusu ufundi wa umeme, umakanika sambamba
na ujuzi ama uhandisi wa kujenga, pamoja na useremala na ufundibomba na aina
nyingine zote za ufundi wa mikono, pamoja na namna zote za utoaji wa elimu ya
juu.