Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[067B]
Masihi wa Uwongo
(Toleo La 2.0 20100109-20100804)
Maranyingi
tumekuwa tukikabiliana na nameno ya propaganda kutoka kwa Marabi kuhusu kile
ambacho Yahoshua (Yesu/Iesou au Yoshua) Kristo hakukitimiliza kutoka kwenye
Maandiko Matakatifu na ambacho kwacho kinamfanya asistahili kuwa Masihi. Basi
huu ni wakati mzuri kushughulika na uwongo huu na kuzifunua baadhi ya
propaganda za marabi kwa udanganyifu wanaoutumia kuhalalisha madai yao na kule
yalikoelekezwa.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Barua Pepe au Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2010 Wade Cox)
(tr. 2013)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Mungu anakaribia
kushughulika na taifa la Yuda na masuala yake yote yaliyo muhimu yanayohusiana
na Hekalu na ujenzi wake na ukaidi wao wanaozifanya shingo zao kuwa ngumu kwa
kuziacha desturi au mapokeo yao na wasizifuate sheria na amri za Mungu na
wakaamua kuachana na mapokeo yao ya kidini. Mapokeo waliyonayo ni yale
wanayoyaita Sheria au Amri za Kimapokeo ambazo hufanywa kwa kufundishana tu kana
kwamba Mungu hakuziandika amri zake na akatupa sisi ili tuzijue na kuzielewa
kwa wazi. Bali wao wanazibadili na kuzifanya zionekane upande mweusi uwe mweupe
na kugeuza upande mweupe uwe mweusi kwa kupitia mafundisho yanayotokana na
baraza la kidini la Talmud.
Uandishi wa
kirida ulioandikwa na Rabi wa Kiyahudi aitwaye Rabi Shraga Simmons aliyeandika
makala isemayo Hivi ni Kwanini Wayahudi
Hawamwamini Yesu ni moja wapo ya mfano mzuri wa mchanganyo wenye utata
unaoendelea kudumu kwenye mawazo ya walio katika imani ya kiyahudi, jambo
ambalo kwa ukweli Agano Jipya limeshughulika kufundisha na ndilo jambo kuu
ambalo Ukristo ndiyo kiini chake.
Hebu na tuwe wazi
na wakweli kuhusu kitu kimoja. Ukwisto wa waamini Utatu na waabudu siku za
Jumapili haumo kwenye imani ya wale wanaoitwa na Yesu Kristo na haikuwepo
kwenye Kanisa la Mungu la Karne ya Kwanza. Mbinu hii ya kushamirisha mafundisho
ya uwongo na tafsiri potofu na za uwongo za Biblia hazitaweza kamwe kabisa
kushawishi fikra za watu wanaopenda na kuyafuata mafundisho yenye uzima kwa
wingi wao, na hata kwa Wayahudi, wala kwa kweli hata kwa Mwislamu, na wala hata
kwa mtu yeyote aliye na imani na lengo la dhati la kudumu kwenye imani kamilifu
nay a kweli ya Kikristo. Madhara yake ni jambo lililosawa na ukosefu wa uadilifu
unaofananishwa kama na kipande cha mlo.
Kuna uwanja ulio
wakawaida ambao tunaweza kukubaliana nao; Shraga Simmons ameandika hilo kwenye
mtandao wa wavuti ifuatayo ya http://www.simpletoremember.com/articles/a/jewsandjesus/
“Je, Ninani hasa aliye Masihi?
Nono au jina “Masihi”
linatokana na mlinganisho wa neno la Kiebrania lijulikanalo kama “Mashiach”,
lenye maana ya ‘Mtiwa Mafuta.’ Ni jina ambalo kwa kawaida linamtaja mtu ambaye
amewekwa kwenye huduma ya kumtumikia Mungu kwa tukio linalofanywa kwa kutiwa
mafuta kichani mwake (Kutoka 29:7, I Wafalme 1:39, II Wafalme 9:3)
Kwa kuwa kila Mfalme
na Kuhani Mkuu walikuwa wametiwa mafuta haya, basi kila mmoja wao alichukuliwa
kuwa ni ‘mtiwa mafuta’ (ni Mashiach au Masihi). Kwa mfano: ‘Mungu
alinikataza kwamba Mimi [Daudi] nisimnyooshee mkono Masihi wa Bwana [Sauli]...’
(I Samweli 26:11. Sawa na. II Samweli 23:1, Isaya 45:1, Zaburi 20:6)
Je, dhana hii ya
Masihi ilitokea wapi katikati ya Wayahudi? Mojawapo ya jumbe mzito zinazobeba maana
ya nabii za Kibiblia ni ahadi ya zama zijazo za ukamilifu utakaokuwa wa amani
kamilifu ya ulimwenguni mwote na itakayofanya na kutambulika na Mwenyezi Mungu (Isaya
2:1-4; Sefania 3:9; Hosea 2:20-22; Amosi 9:13-15; Isaya 32:15-18, 60:15-18; Mika
4:1-4; Zekaria 8:23, 14:9; Yeremia 31:33-34)
Nyingi ya haya
maandishi ya kinabii zinawataja wazaliwa wanaotoka kwenye uzao wa Mfalme Daudi atakayewatawala
Israeli katika zama ya utawala mkamilifu (Isaya 11:1-9; Yeremia 23:5-6,
30:7-10, 33:14-16; Ezekieli 34:11-31, 37:21-28; Hosea 3:4-5)”
Kwa hiyo, mtu
huyu anatafuta kutenganisha yaliyoko hapo juu na kwa maelezo yanayomhusu Masihi.
Pia anapuuzia yale yaliyoandikwa kwenye Zekaria 12:8 ambayo yanaongelea kwa
uwazi sana kwamba hata Daudi mwenyewe atafufuliwa na kwamba ni yeye mwenyewe
ndiye atakayetawala kwa mamlaka ya Malaika wa Yahova mwenyewe na ambaye ndiye
atakayetangulia huko mjini Yerusalemu na kwenye nyumba ya Daudi kama elohim.
Kitendo cha kutotenganisha
au kuyaacha maandiko yaliyo kwenye Danieli 9:25 kuonyesha makosa ya kiutafsiri
yanayofanywa na wanazuoni wa mrengo wa Waamini Utatu na kwahiyo wanafikia
kudiriki kuyaacha maandiko haya yanayomhusu au kumtaja Yesu Kristo kwa dhahiri
sana. Ungekuwa ni mfano mzuri sana kunukuu katika kuonyesha kwamba maandiko
haya matakatifu yametafsiriwa kimakosa katika tafsiri ya kimaandiko yanayomlenga
Kristo mwenyewe.
Hata hivyo, hili
lisingeweza kufanywa na Myahudi na hasa kwa vile ilivyoweza kuutambulisha au
kuuonyesha unabii unaoelezea au kuonyesha historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu na
kwamba kulikuwa na matiwa mafuta wawili kwenye maandiko haya. Zaidi sana, walidumu
katika kuiweka au kuichukulia historia kwa mlinganisho sahihi wa Kibiblia ambao
ungweza hata kuuonyesba unabii huu kwa kipindi chake halisi na sahihi cha
utimilifu wa mambo na sababu zilizomfanya Mungu awaangamize. Ilionekana pia
kwamba mmojawapo kati ya watiwa mafuta, au mamasihi, hawa alikuwa ni Nehemia ambaye
alifanya kazi kubwa ya kuujienga tena Yerusalemu na Hekalu lake ambalo Ezra aliutabiri mwaka wake kamili katika
kipindi cha utawala wa Artashasta II. Mwingine
wa pili aliyekusudiwa kuwepo kama ni mtiwa mafuta ni Yule aliyekatiliwa mbali,
lakini sio kwa ajili yake mwenyewe, kama alivyokuwa ametabiriwa kwenye
maandiko. Hata hivyo, huo ulipaswa kuwa ni unabii uliotarajiwa uliomhusu Yesu
Kristo. Kipindi muafaka kilichowekwa kataka mwaka uliotarajiwa ni cha juma moja
la miaka kabla ya kuangamizwa kwake mji wa Yerusalemu na kwa Hekalu
kulikofanywa na Warumi mwaka 70 BK; ambao ulikuwa ni mwaka 63/64 BK.
Mtiwa mafuta huyu
anapaswa kuwa ndiye Yule mtiwa mafuta aliyetajwa kwenye tafsiri iliyoko hapo
juu. Katika mwaka ule kulikuwa na mtu mmoja tu ambaye alistahili kwa kutimiza
vigezo vyote vinavyohusu uzao wa Daudi na mtu Yule alikuwa ni wa kabila la Yuda
na wa uzao wa Daudi, lakini alikuwa ni mtumishi wa Mungu na ni Kristo. Alikuwa
ni ndugu wa Yesu Kristo na askofu wa Yerusalemu, ambaye ni Yakobo, mwana wa
Yusufu na Mariamu.
Ili kuelezea au
kuweka wazi makosa haya ya kiutafsiri kutawalazimu marabi wakumbane na jambo hili
kubwa na la muhimu na ambalo lingelazimika kuzua hali tete na ambao kwamba kila
mtu angehitaji kutegea sikio lake kiasi kwamba maandiko yaliyo kwenye kitabu
cha nabii Danieli yatimilike na watu waliohusika ni wa uzao wa Daudi na maafa
ya Hekalu yakatuama mikononi mwa Mungu. Hukumu yake imeangukia katika Yuda na
Yerusalemu kwa sababu ya dhambi zao na makosa yao na hawawezi kufikilia ukweli na
kwamba walihukumiwa kwa kuwa walitenda dhambi
na walihukumiwa na Kristo. Yeye alikuwa ni mwanadamu Yahoshua aliyeitwa
pia kuwa ni Iesuo na Wayunani na
Warumi na neno Joshua ni la Kiingereza linalotaja jina lake hilohilo.
Hawauelezei unabii kwa kuwa hawawezi kuuelezea au kulifafanua hili ndani ya
hali yao ya mkanganyiko [hebu jisomee jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya
wa Hekalu Na. 013 (Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the
Temple (No. 013)].
Kwenye swali lao
au kujiuliza kwao kuhusu Masihi na Ujenzi Mpya wa Hekalu kwa kiasi fulani pia
wanautegemea unabii wa Ujenzi Upya wa Sinagogi la Hurva mjini Yerusalemu. Unabii
wa Wayahudi wa leo unalihusisha tukio hili na mwanzo wa ujenzi wa Hekalu la
Tatu.
Sinagogi la Hurva
lilijengwa zamani katika karne ya 18 mjini Yerusalemu. Vilna Gaon, rabi aliyeheshimika
sana katika jopo au baraza la malmaka ya marabi, alitabiri kwamba Sinagogi hili
la Hurva lingeharibiwa na kujengwa tena mara mbili, na kwamba Hurva lingekamilika
kwa mara ya tatu, ujenzi huu wa Hekalu la Tatu kungeanza.
Sinagogi la Hurva liliharibiwa kwanza kipindi kifupi tu mara baada kuanza kwa
ujenzi wake wakati Waislamu kudai warudishiwe madeni yao, na ndipo
wakalivunjilia mbali. Hatimaye Sinagogi hili lilijengwa tena miaka mia kadha iliyofuatia
baadae. Lifanyika kuwa ni mahali au nyumba muhimu sana pa ibada ya Wayahudi katika
Nchi Takatifu. Hatahivyo, lilivunjwa vipande vipande na wanajeshi wa Jordan katika
kipindi cha Vita ya Waisraeli ya mwaka 1948 vya kupigania Uhuru.
Mnamo mwaka wa
2001, Israeli hatimaye waliamua kujenga timazi, ambayo leo imesimama katikati ya
Makao Makuu ya Wayahudi katika Mji wa Kale wa Yerusalemu. Ujenzi wa jengo hili
ulipangwa ukamilike na Sinagogi la Hurva liwekwe wakfu kwa mara ya tatu mnamo
tarehe 15 Machi 2010. Mwonekano au Mwandamo wa Mwezi Mpya wa Abibu ulifanyika saa
5:01 ya usiku kwa muda wa saa za Yerusalemu mnamo tarehe 15 Machi. Hii
ingepelekea tendo hili la kuwekwa wakfu kwake kuangukie siku ya mwisho ya mwezi
wa Adari katika Mwaka wa 32 wa Yubile ya 120. Kwa hiyo, Hekalu lilitabiriwa
lianze ujenzi wake tangu siku ya 16 ya mwezi Machi, ambayo pia ni siku ya Mwandamo
wa Mwezi wa Abibu ya mwaka wa 33 wa Yubile ya 120. Swali ni kwamba ni wapi
wanapoijenga Sibagogi hili? Kama ni
mahali Patakatifu basi itawalazimu kuuondoa Msikiti na ndipo kutaanza vita na
mapigano mabaya. Kana ni hivyo basi, hili litakuwa ni chukizo kubwa la
uharibifu litakalosimamishwa Mahali Patakatifu. Sinagogi hili na utaratibu wake
mzima wa Marabi na wa baraza la Kitalmudi utatuama katika mapokeo ya dini za
Kibabeli. Kalenda ya Kibabeli pamoja na siku zake za kuabudu vitaingizwa
vitumike kwenye Mahali hapa Patakatifu. Litakapotokea jambo hilo ndipo ukumbuke
kuwa Biblia imelielezea wazi na kutoa wito kwamba tutoke na kukimbia huko
Yerusalemu (Mat. 24:15; Mk. 13:14). Nyota ya sita inayoonyeshwa ya mungu Remphan
au Kiuni utakuwepo hapo ikiwa ni ishara au alama ya sadaka au kafara ya
wanadamu na machukizo.
Kutokana na maelezo
ya Kristo yaliyonukuliwa alionya kwamba uwezekano mkubwa wa kutukia jambo hili
ni wakati wa baridi au siku ya Sabato. Mwandamo wa Mwezi wa Mwezi wa Kumi wa mwaka
2010 ni siku ya Jumatatu, tarehe 6 Desemba na Sabato ziliangukia siku za tarehe
4, 11, 18 na 25 Desemba, au siku za sikukuu ya kipagani inayoitwa Krismas. Iwapo
kama haya ndiyo majira yaliyoongelewa na Kristo basi ungekuwa ni wakati mkamilifu
katika kuuharibu mfumo wote mzima, ukianzia tangu Yerusalemu, katika suku ya
ibada potofu na ya uwongo ya imani ya mungu Jua inayoitwa ya Krismas.
Kwa hiyo, kabila
la Yuda litaanza kushughulikiwa kwa kiasi kikubwa. Hatahivyo, tunamatatizo na
hizi nabii za Kiyahudi. Je, rabi huyu anasemaje kuhusu Kristo? Anasema kwamba
Jesu Kristo hakutimiliza vigezo vya nabii zilizotolewa kuhusu Masihi.
Anaingiza maswali
yafuatayo:
“Je, ni kitu gani ambacho Masihi alitakiwa kutimiliza?”
Biblia inasema
kwamba atatimiliza yafuatayo:
A.Atalijenga Hekalu la Tatu (Ezekieli 37:26-28).
B. Atawakusanya Wayahudi wote na kuwarudisha kwenye Nchi yo ya Ahadi ya Israeli (Isaya 43:5-6).
C. Atakomesha maasi na uganganyifu wote ulioko ulimwenguni, na ataleta amani ulimwenguni, na kukomesha chuki, dhuluma, mateso na magonjwa. Kama yanavyosema maandiko kwamba: " taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe." (Isaya 2:4)
D. Ataeneza uwezo wa kuelewa ulimwenguni kote
na kueneza maarifa ya wanadamu kumjua Mungu wa kweli wa Israeli, maarifa
yatakayoweza kuwaunganisha wanadamu wote pamoja na kwa umoja. Maandiko
yanatuambia kwamba: “Naye
Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina
lake moja.” (Zekaria 14:9).”
Wakati Masihi atakapokuja
mjini Yerusalemu atafanya kile ambacho kwa mujibu wa Maandiko ya Biblia, kutakuwa
Hekalu limeshajengwa tayari. Na hii inaonyesha wazi kabisa kwamba Wayahudi, ili
kufanya madai ya unabii na ujenzi wa Hekalu, watadai kuwepo kwa Masihi mpya na
wa uwongo.
Wayahudi wanadai
kwamba Yesu hakuweza kutimiliza nabii hizi zinazomhusu Masihi hata moja. Ukweli
ni kwamba angweza kufanya lile tu au kungekuwa na maana tu, kuanzisha
kutimiliza kile kilichotajwa kwenye kipengele D hapo juu. Kwa hiyo, Roho Mtakatifu
anapaswa awepo tangia kwenye dhabihu hadi kwa mataifa yote. Na ndipo maarifa ya
kumjua Mungu yalifanywa yawepo tangia kipindi hicho.
Wakagundua kwamba
mafundisho ya Wakristo yanadai na kuamini kwamba Kristo ataufanya upya mji wa Yerusalemu
na atalijenga tena Hekalu hapo atakapokuja. Hata hivyo, wao wanadai kwamba
vyanzo vilivyopo kwenye itikadi ya Kiyahudi vinaonyesha kuwa Masihi atautimiliza
unabii mara moja kwa kipindi kimoja tu cha kuwepo kwake na kwamba hakuna
fundisho wala dhana ya kurudi kwake mara ya pili iliyoko. Maelezo haya yenye
upotevu mkubwa yanapuuzia na kuyakataa maandiko mengine yaliyoandikwa kwenye
Biblia ambayo baadhi yake hata yanaeleza kwa wazi kabisa na kuonysha kwamba
Masihi ameandikiwa kuwa ataketi katika Mkono wa Kuume wa Mungu hadi
atakapowaweka maadui zake wote wawe chini ya miguu yake.
Yahova wa Israeli
anaelezea kwa mpangilio mwanana kwamba Yahova wa Majeshi atamtuma yeye ili awaokoe
Israeli na kisha ndipo watajua kwamba Yahova wa Majeshi amemtuma kwao (Zekaria
2:6-13). Hii inaonyesha kwamba kuwa Yahova wawili wanaohusika na Yahova huyu wa
pili ametumwa na Yahova wa Majeshi. Jambo hili halieleweki na waamini Utatu na
Wayahudi wanajionea kuwa ni vigumu sana na haiwezekani jinsi ya kuielezea. Kumbe
huyu alikuwa ni Malaika wa Uwepo wake ambaye ndiye aliyetoa Torati na kumpa nabii
Musa na alikuwa ni hadhi iliyosawa kuitwa elohim wa Zaburi 45:6-7. Anajulikana Masihi
kwenye Waebrania 1:8-9. Alitumwa ili aufanye upya mji wa Yerusalemu na kwamba
tukio hili la mwisho litatukia katika Siku za Mwisho. Tunajionea kwenye sura ya
3 inayofuatia jinsi inavyohusianisha na urudishaji wa huduma ya Kuhani Mkuu
chini ya Tawi na hili maandiko linalofuatia ambalo pia linahusianisha na sura
ya 2 ya unabii wa kipindi cha kuruhusiwa kwake na cha kufanya haya marejesho
mapya.
Yale
yaliyotabiriwa kwenye sura ya 12 yanaonyesha kwamba kipindi cha maendelezo ya
nabii Zekaria ni kile cha tangia Ufufuo wa Kwanza wa wafu na wa kujungwa kwake
upya mji wa Yerusalemu, kama Daudi yuko hai na kumfanya kuwa ni kiongozi wao
nao watakuwa kama elohim na kama Malaika wa Bwana aliye kwenye uongozi
akiwaongoza wateule. Ni andiko hili ndilo linaloonyesha katika siku hizo watu
wa nchi watamtazama yeye waliyemchoma mkuki ubavuni mwake. Andiko hili linahusu
na tendo la utakaso wa mataifa utakaofanya na Masihi alinayetokea kwenye nyumba
ya Daudi kupitia kabila la Nathani na nyumba ya Lawi kupitia Kwa Shimei. Utakaso
huu ni maombolezo ya Yuda kwa toba yao kwa hali itakayowapata ya kuelewa kwamba
walimuua Masihi wao humo mjini Yerusalemu. Siku ile ya maombolezo, utaratibu wote
wa kiimani utabadilika na kamwe hawatakuwepo tena manabii katika nchi yote ya Israeli.
Imani ya Kiyahudi
inashikilia kudai na kuamini kwamba Yesu hakuwa na vigezo kwa nafsi yake
vinavyomfanya akubalike na kustahili kuitwa au kuwa Masihi. Marabi wanasema na
kudai kwamba:
“Yesu hakuwa nabii.
Unabii uliweza kuaminika na kubakia katika Israeli kipinci cha zama za kale za
ulimwengu wa mavumbuzi ya ubora wa Dhahabu ba Usonara. Wakati wa Ezra (yapata
kama mwaka 300 KK), wakati ambao Wayahudi wengi walikataa kuondoka kutoka
utumwani Babeli na kwenda kwenye nchi yao ya ahadi ya Israeli, unacii uliishia
katika kipindi cha mwisho cha manabii—Haggai, Zekaria na Malaki.
Yesu alijitokea
baadae kwenye miaka takriban 350 baada ya unabii kukoma.”
Kwa hiyo ndipo
mikono ya Mungu ilifungwa kwa ukweli kwamba alitarajiwa kuwashughulikia hawa
Yuda kwa kupiti manabii wengine zaidi. Ukweli ulikuwa ni kwamba
aliwashughulikia sawa hawa Wayahudi na kwa kupitia nabii kahaa wa kadha
zikiwatabiria kwamba wangeweza kukabiliwa na balaa la kufukuzwa kutoka nchini
mwao na kwamba Hekalu lingeweza kuhusuriwa kwa kubomolewa na kuangushwa kabisa,
tukio ambalo lilikuja kutimilika mwaka 70 BK, mwaka ambao unabii ulitimilika
kabisa na likaangamizwa. Kwa jinsi hii, hakutakuweko kamwe na nabii katika nchi
ya Israeli kwa vile idadi kubwa ya Wayahudi wako nje ya nchi hii inayojulikana
eo kama taifa la kawaida tu la Israeli. Mungu hana la kushndwa na mataifa ya
wanadamu na hususan wale wanaozigeuza Sheria zake.
Rekodi ya kuwepo
kwa unabii zimeonekana kuwepo kwenye Aganno Jipya na nabii zote hizi zinasimama
kama ushahidi dhidi ya Yuda na mfumo wao wa kiimani uliopotoka. Makaila wa
Bwana alitumwa kwa Kuhani Mkuu wa kundi la Abia na akaambiwa kuwa ataongeza
nabii mwigine na kwamba mjomba wa mke wake pia atakuwa ni mama wa Masihi. Hii
iliandikwa kama kitu cha kweli kwenye hizi injili. Uzao wake umeandikwa pia
kwenye hizi injili na mabaraza ya marabi yanaikiri kuwa orodha ya wale
walioandikwa kwenye ya Luka 3 kuwa ni ya kweli na kwamba huyu Mariamu
aliyeandikwa hapa ni mama yake Yesu Kristo (soma jarida la Orodha ya Uzao wa Masihi (Na. 119) [Genealogy of
the Messiah (No. 119)].
Kristo alitumwa
kwa watu wa Yuda sawa na kana vile nabii Yona alivyotumwa kwa watu wa Ninawi na
aliwaambia Yuda hakika ya ukweli ule. Kuna idadi kubwa ya nabii zinazoilaumu
Yuda na hawatalijua hilo kwa kuwa wataangukia kuukubali ukweli na kutubu.
Kwanza kabisa,
uharibifu wa orodha ya uzao wa Yuda ulichukuliwa kwenye mchakato wa Herode kama
ni suala la kihistoria; ilichukuliwa hivyo sio kwa sababu nyingine yoyote, bali
ni kwa kufuta na kuondoa migongano muhimu katika nyumba ya kifalme ya Yuda. Mnyororo
wa ufalme wa Yuda ulikoma kuwa kwenye kiti cha ufalme wa Yuda na Yerusalemu
kama alivyoandika mwandishi maarufu aitwaye Exilarchs aliyeandika habari zake
kipindi ambacho Masihi alipokuwa bado yungali hai. Ni juu ya jinsi inavyosema
Historian a rekodi za kinasaba (soma jarida la Tangu Daudi na Exilarchs hadi kwenye Nyumba ya Windsor (Na. 67) [From David
and the Exilarchs to the House of Windsor (No. 67)]. Kuzaliwa kwake kuliandikwa kuwa
ni kama kitu kilitabiriwa Hekaluni na nabii aliyekuwako mule. Hili
lingetosha kuwaeleza kwamba kitu fulani. Hata hivyo, walipuuzia unabii huu. Kwa
bahati mbaya, Herode hakuupuuzia unabii huu na aliwaua watu wengi kama
inavyotuambia historia.
Hatimaye Yuda
wakatumiwa Yohana Mbati ambaye aliwatabiria kuhusu ujio wake. Alianza kuhubiri
katika Mwaka wa Yubile na alimbatiza ndugu yake Yahoshua aitwaye Kristo katika
mto wa Yordan kama ilivyoandikwa na kuelezewa vyema. Alifungwa gerezani na
kuuawa na Wahasmonea. Kristo alianza huduma yake sawa na kama ilivyoandikwa, baada
ya kufungwa kwake Yohana Mbatizaji, kitendo kilichotokea baada ya Pasaka ya
mwaka 28 BK. Aliwaambia kwamba walikuwa wanatenda dhambi kupitia mapokeo yao na
akaanzisha Kanisa katika kuchukua mahala pa huduma ya kikuhani ya Walawi. Taifa
lote zima la Yuda lilikuwa na nakala ya maandiko yaliyoko kwenye Biblia na
nabii zilizowaambia kwamba Hehalu lilikuwa hatarini kuhusuriwa au kubomolewa.
Waliletewa Kristo
akiwa kama ni nabii mkuu kuliko wengine wote waliowahi kuwepo hapo kabla. Aliwahubiria
kwa kipindi cha takriban miaka miwili, kama alivyohubiri Yona huko Ninawi kwa
siku mbili baada ya kutembea kwa mwendo wa siku moja ndani ya Ninawi na kuanza
kuhubiri. Yona aliandaliwa na samaki mkubwa alikuwa ameandaliwa kwa ajili yake
na akaingia tumboni mwake na akachukuliwa akafanya kazi yake huko Ninawi. Na
ndivyo hivyohivyo sawa na Kristo alivyojitoa katika kipindi chake cha mwanzo
akionekana kama Malaika Mkuu wa Maagano aliyetoa Sheria au Torati kwa Musa huko
Sinai na alidumu kuwepo kwenye tumbo la mwanamwali bikira na kuchukuliwa tumboni
kwa muda wa miezi tisa na hatimaye akazaliwa huko mjini Bethlehem, ambako ndiko
kwenye kiti na urithi wa kifamilia Daudi. Kristo alizaliwa kama ni mfalme wa Yuda
wa kutoka katika orodha ya uzao wa Yese na Daudi. Ahadi ya urithi wake ilikuwa
ni kuwa taifa zima lote la Israeli na ukamilifu wote wa Mataifa unapaswa kuwa
juu yao kama ilivyotabiriwa na Yakobo alipokuwa akimbariki Efraimu na sio Yuda
(Mwanzo 48:13-22, hasa ile aya ya 19). Urithi huu ni kama mmoja wapo wa wana wa
Mungu alivyowahi kuandika kwenye Kumbukumbu la Torati 32:8 na kama
ilivyoandikwa kwenye maandiko ya Septuagint (LXX) na kwenye gombo linnloitwa
Gombo Lililovumbuliwa kwenye Bahari ya Chumvi [Dead Sea Scrolls (DSS)] nah ii ndiyo
maana marabi walikuwa wanabalisha tafsiri ya Maandiko ya Masoretic (MT) na
kuubadili ukweli wa kwamba Yahova wa Israeli aliwapa nchi ya Israeli ili iwe ni
urithi wao na Mwenyezi Mungu. Pia walibadili maana ya Maandiko ya Maandiko ya Mesoretic
na kukiongezea kifungu cha 132 ili kugeuza maana ya uhusiano wa Yahova na
Yahovi (soma jarida la Malaika wa YHVH (Na. 24) [Angel of YHVH (No. 24)]. Alikuwa ni yule malaika aliyetajwa
kukutana na Yakobo alipombariki kwenye Mwanzo 48:16 na kuwa ndiye aliyemlinda
yeye kipindi chake chote cha maisha yake. Hawatafanya lolote lile linguine
zaidi tu ya kukubali juu ya uhusiano huu ulio kwenye maandiko ya Agano la Kale.
Kanisa la waamini
Utatu wanakubaliana na madai ya Wayahudi ambayo yanaharibu uelewa wao kwa kiasi
kikubwa mno.
Madai ya Wayahudi
yanasema hivi:
“Kwa mujibu wa
maandishi yanayoaminiwa na Wayahudi, yanasema kwamba Masihi atazaliwa kutoka
kwa wazazi wanadamu na ni wazazi watakaokuwa na miili ya kawaida tu ya
kibinadamu na mwonekano wao utakuwa ni kama wa watu wengine wote tu. Na wala hatakuwa
na nasaba ya kimungu ndani yake, (1) na wala hatakuwa na chembe yoyote ya uweza wa kimiujiza ndani yake.
Lazima Masihi atokee upande wa baba yake, yaani kutoka kwenye orodha ya uzao wa Mfalme Daudi 49:10 na Isaya 11:1). Kwa mujibu wa madai ya Wakristo yanasema kwamba kuzaliwa kwa Yesu kunatokana na matokeo ya uzao wa mwanamwali bikira, na kwamba wala hana baba—na kama ni hiyo basi kunalifanya jambo hili lisiweze kuwa sawa au kutimilika katika kufikia vigezi vya Kimasihi vya kuwa alishuka kutoka juu kwa baba alitokana na orodha ya uzao wa Mfalme Daudi! (2)” (ibid.).
Hii inapelekea kuweka nia ya kukataa uwepo wa ile hali isiyo ya asili wala kawaida ya Masihi. Kristo asingeweza kuyatumia mamlaka ya kifalme kama wa uzao wa Yekonia hadi pale alipofikia kuwa na kiwango maalumu cha uhusiano wa kinasaba na Mungu. Aliweza kufikia kiwango hicho kwa kuwa na uhusiano wake wa kinasaba na Yusufu ambaye alikuwa ni baba wa kimalezi tu. Yufusu alikuwa ni wa kutoka kwenye uzao wa Konia na kumfanya mtoto huyu asiweze kuwa mfalme pasipokuwa na uhusiano wa moja kwa moja kutoka kwa Mungu. Masihi alipaswa awe na uhusiano wa kinasaba pia na uzao wa Lawi kupitia kwa Shimei pia (tazama namba 119 ibid).
Isaya 11:1 inasema kwamba ilimpasa Masihi atokane
na kiini cha kinasaba cha Yese baba wa Daudi na kutoka kwenye shina
linalotokana na mizizi yake. Ni kweli kwamba ni wanaume tu ndio wanaochukua
vipimo vya nasaba vya YDNA vya baba. Ktisto alikuwa na uhusiano wa aina hii na
Mungu peke yake katika kuumbwa kwake na vipimo hivi vya YDNA na katika kuonyesha
kwamba yeye ni wa uzao wa Daudi, ni kama alivyokuwa Adamu kutegemea tu uzao
wake kwa Mungu na kwa vipimo hivi vya YDNA. Tena Wayahudi walikuwa wanadai tu kwa
wazi kabisa kwamba mtu hawezi kukubalika kuwa ni Myahudi kama hatazaliwa na
mwanamke au mama Myahudi, na ndipo atakapoirithi ile hali ya kinasaba ya
Kiyahudi ambayo ataipata kutoka kwa mama yake. Ikumbukwe pia kwamba Masihi alizaliwa
akitokea katika familia ya Kilawi kwa Shimei. Tunajua kutokana na ukweli kwamba
Mariamu alikuwa na nasaba za aina mbili, yaani alikuwa za uzao wa Kiyahudi kutoka
kwa mama yake, kwa kuwa mama yake Mariamu alikuwa ni dada na Elizabeth
aliyekuwa mke wa Kuhani Mkuu wa uzao wa Abiya na mama yake Yohana Mbatizaji. Milolongo
hii miwili ya makuhani waliolewa na hawa wanaume waliotokana na kabila la Lawi
au Walawi. Na ukweli ni
kwamba Mariamu alimudu kuwa na mambo haya mawili muhimu.
Pia Masihi alikuwa
ni Mwana wa Mungu na hili ni jambo la muhimu sana. Mwana wa Mungu alimaanisha
kuwa alikuwa ni Yahova wa Israeli, ambayo ndiyo urithi wake. Alikuwa ni kama
mungu mdogo na ni Mwana wa Mungu, ambaye alitarajiwa kuwa kwenye mateso na
kuchukua huduma ya Ukuhani Mkuu. Agano Jipya linasema pia kwamba Kuhani Mkuu
alitabiri katika mwaka ule kwamba itampasa mtu mmoja afe kwa ajili ya wokovu wa
taifa zima. Ayubu alisema karne nyingi sana zilizokuwa zimepita kwamba mtu
mmoja katj ya maelfu atamkomboa yeye na pia kwamba alitabiri kuhusu Ufufuo na
kwamba angeweza kumwona Masihi kwa macho yake mwenyewe na sio kwa macho ya
mwingine na kwamba atamuomba Eloa na atapata kibali kutoka kwake na kwamba
atauona uso wa Eloa kwa furaha kuu. Hii inamaana kwamba atakuwa ni kiumbe
katika ulimwengu war oho ili aweze kumuona Eloa na aishi. Hakuna mtu
atakayeweza kumuona Eloa na wala hakuna mtu aliyewahi kumona yeye na wala
hakuna atakayekuja kumuona yeye akiwa na macho haya ya kimwili (soma Ayubu 33:23-28).
Eloa ndiye muumbaji au aliyevifanya vyote viwepo (Ayubu 35:10). Wana wa Mungu
na Nyota ya Alfajiri walikuwepo hata kabla ya uumbaji wa hii dunia (Ayubu 38:4-7), na waliumbwa na Eloa .
Tendo la kuchomwa
mkuki kwa Masihi lilitabiriwa kwa kuandikwa kwenye Zaburi 22 na kwenye Zekaria
12. Kristo aliutimiliza unabii huu wa Zaburi 22. Aliunukuu alipokuwa kwenye mti
wa mateso na ulikamilika. Inaelezea kuhusu kuuawa kwa Masihi na namna ya pekee
ya makovu haya na kifo chake yalikuwa yamefanya maumivu sana katika historia ni
kwa kuwa kwenye “mti wa kuhuzunisha” au mti wa mateso ambao ulikuwa
umetengenezwa kwa namna ya kishenzi sana ya kimauaji yaliyofanywa kwa
mashambulizi ya Wafoeniki. Warumi waliongeza kipande kingine cha ubao
uliokinzana na kuonekana kuwa ni msalaba na walifanya hivyo miaka mingi sana
baada ya kifo cha Kristo. Kristo aliweza kuja tu kwa kipindi kile alichofanya
hivyo na kupata mateso kama alivyofanya. Baraza la Masoretes wailibadili jina
la Yahova (Yehova) na kumuita Adonai kwenye Zaburi hii marambili (kwenye aya za
19 na 30) ili kubadili kilichokusudiwa zaidi. Andiko limeandika kwamba Mungu hakugeuza
uso wake na kuangalia pembeni na kumuacha bali ukweli ni kwamba alimuokoa kwa tangazo
la haki yake kwa kweli lilitangazwa kwa watu ambao walikuwa hawajazaliwa bado.
Madaia ya Wayahudi
kwamba Zaburi 22:16 (17) isemayo “wameichoma mikono yangu na miguu” kwamba
ilivyotafsiriwa kimakosa kutegemea na kiwango cha fasiri ya marabi ya maandiko
haya kama: “Kama simba wako miguuni mwangu”. Neno lililotumika hapa ni ‘ariy (SHD 738) ambalo maana yake ni simba
mdoo, lakini maana yake ni imechukuliwa kutoka kwenye maandiko ya chini ambayo
yana maana ya kuchoma mikononi na miguuni ambayo ndivyo walivyomfanyia Kristo kwa kumpigilia
misumari pale mtini. Jina hili limechukuliwa kutoka kwenye kitabu cha fasiri
cha SHD 717 maana yake ni kukusanya au kutawanya. Inaonekana kuwa
matumizi ya mabari kuwa yafanyika ili kuficha ile maana yake nyingine. Matumizi
ya mbwa na simba kwa pamoja yanawataja watu na matendo yao katika kifo cha
Masihi na ni jambo linalodumu sana ambalo mapokeo yao yanapenda.
Zaburi 82:6 ilikuwa
ni andiko elekezi kwa kile kilichompelekea Kristo kuuawa. Alijitangaza mwenyewe
kuwa ni elohim ambaye ataihukumu dunia na kuyarithi au kuyatawala mataifa yote (Zaburi
82:8). Huyu elohim alisimama kwenye kusanyiko la elohim na kuwahukumu watu wote.
Malaika walioasi au mapepo watahukumiwa naye na watatupwa shimoni sawa kama
watu wengine wowote tu watakavyofanyiwa. Lakini elohim huyu alifanywa kuwa ni elohim
na Yeye Aliye Juu Sana, Elyon, ambaye ni Eloa. Huyu elohim ni yule elohim wa
Zaburi 45:6-7 ambaye ni Mungu wa Daudi ambaye ni wa uzao wake pia. Kama hana
sifa ya kuwa alikuwepo huko nyuma kabla na kuwahukumu miungu midogomidogo, angewezaje
basi kuwa ni mwanadamu tu asiyekuwa kwanza na uwepo wake huko nyuma? (Tazama
jarida la Uwepo wa Yesu Kristo Hapo Kabla (Na. 243) The Pre-Existence of Jesus Christ
[(No. 243)].
Iwapo kama yeye
ni Mwana wa Daudi tu, inakuwaje basi Daudi akiongozwa na Roho Mtakatifu alimuita
yeye kuwa ni Bwana? Anaposema “Bwana alimwambia Bwana wangu” (Zaburi 110:1). Baraza
la Sanhedrin halikuweza kulijibu hili na kwa hiyo na hawawezi kulijibu hili
sasa. Iwapo kama hana haishi kwa wateule inakuwaje sasa aweze kutukiri sisi mbele
ya Baraza la Elohim? Inatuatia kuaminika kwamba ni lazima awe aliishi na kufa
wakti alipofanya na kama alivyofanya na kwamba ni lazima atakuwa aliwahi kuishi
kwa Wateule na akaketi Mkono wa Kuume wa Mungu wakati wateule wanazaliwa kwa kusudi
la kutimiliza unabii na mpango wa Mungu. Na iwapo kama Masihi angekuwa ni
mwanadamu aliyezaliwa katika siku hizi za mwisho ndipo Maandiko yangeweza
kutanguka. Walioifasiri Biblia ya LXX walielewa kwamba Masihi alikuweko huko
nyuma kabla kama inavyosema Isaya 9:5-6 walitafsiri andiko hili ili lisomeke
kama Malaika wa Shauri Kuu (soma
jarida la Isaya (Na. 9:6 224) [Isaiah 9:6 (No 224)].
Nabii Isaya
ameweka wazi kwenye ile sura ya 53 kwa jinsi alivyosema kwamba Masihi hakuna na
umbo wala mwonekano wa utanashati na pia hana hata uzuri. Wayahudi walidhania kuwa
alikuwa amepigwa na Mungu mnamo mwaka wa 30 BK na bado wanaendelea kuamini
kwamba alipigwa kwa ajili ya makosa yake mwenyewe na kwamba hakuwa Masihi aliyetabiriwa
kwenye unabii huu. Lakini Isaya alisema wazi kwenye utabiri wake kwamba aliumizwa
kwa ajili ya makosa na maovu yetu, na alichubuliwa kwa ajili ya maovu yetu. Maongeo
ya amani yetu yalikuwa juu yake na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. Kwa kuwa sote tumefanya dhambi
na maovu yetu yote yamewekwa kwa Kristo (Isaya 53:3-6).
Pia Isaya
anaonyesha kwa wazi sana kwenye sura ya 53 kwamba itambidi Masihi afe kwa ajili
yetu. Ilimpasa pia afungwe, apigwe mijeledi, ateswe akiwa kimya bila
purukushani, ahukumiwe na akuhumiwe na afe, kitendo ambacho tunakijua sana
kwamba kilipaswa kifanyike kwa kupigwa na kupigiliwa misumari mikononi na
miguuni, na jambo hili lililazimu lifanyike kwa yeye kuwmbwa mtini. Alihukumiwa
na wanadamu wenye udhaifu kisha akazikwa kwenye kaburi jipya lililochongwa
mwambani kwenye eneo wanalozikwa watu maarufu na matajiri. Yesu Kristo alitimiliza
haya yote na ni jambo lisilowezekana kabisa kwa Myahudi yeote kuweza
kuzitimiliza nabii hizi. Ikiwa kama Yesu hakuwa Kristo, kama marabi
wanavyosema, basi hawajui lolote kuhusu ni nani basi anayeweza kufaa kuwa na
wadhifa huu. Kristo amefanyika kuwa sadaka ya dhambi kwa kifo chake na Eloa
alimfufua kutoka kaburini na alitakiwa auone uzao wake, ambani ni wateule ambao
ni Kanisa na mafundisho na nabii alizokuwa akifundisha. Ataishi milele na
kumfanya aendeleze siku zake kama zilivyotabiriwa. Mafundisho yake yameiwapa haki
watu wengi. Aliwekwa wakfu na kuchaguliwa ili awe na sehemu yake kwa wenye
nguvu na kugawanya mateka na na wenye mamlaka kwakuwa aliitoa roho yake hadi
kufa na alihesabiwa na waovu na akachukua mzigo wa dhambi za wengi na kuwaombea
wakosefu (soma Isaya 53:7-12). Unabii huu
haufuniki maeneo yote ya maisha ya mtu wa kawaida na unajumuisha tukio la
ufufuo kutoka kwa wafu.
Kukubaliana na
dhana kwamba andiko hili linafuatana na sura ya 52, inayouelezea utumwa wa
Babeli na kuwa haihusiani na Kristo na kifo chake ni kitendo cha kupamba tu
kama ulivyo utaratibu wake kwenye sura ya 52 inavyoendelea kuelezea hadi
kufanywa kwake upya mji wa Yerusalemu na Sayuni na kisha inamuelezea Masihi
kama ni mtu asiyeweza kufananishwa na kwamba kwa kupitia yeye mataifa yote
yatajua kile ambacho hakikuelezwa kwao nao wataona na kujua na kukiona kile
walichokuwa hawajakisikia (Isaya 52:14-15). Kwa kupitia yeye na kwa sadaka yake
Roho Mtakatifu atawapa uelewa. Hii ndiyo imefanya umuhimu wa sura ya 53. Jambo hili
limeelezewa kwa kina zaidi kwenye jarida la Maana ya Neno Mwana wa Mungu (Na 211) [The
Significance of the Term Son of God (No. 211)].
Wayahudi
wameendea kuifanya Sabato kuwa ni mzigo na kuzifanya Amri za Mungu zisiwe na
maana au umuhimu zaidi ya mapokeo yao. Wanafanya hivyo hadi leo na lakini
wanafanya zaidi ya hayo, na wanatenda dhambi bila kukoma kwa kupitia mapokeo
yao na upotoshaji wa sheria za Mungu. Wanaendelea kuyafanya makosa yale yale
hadi sasa ambayo kama walivyofanya wakati alipokuwa anawatabiria na
kuwashutumu, kama alivyotumwa ili afanye hivyo na Mungu.
Ni kama mwandishi
maarufu Simmons anavyojitahidi kutoa mwongozo:
“Je, ni wapi ambapo
kosa la kufasiri limefanyika? Mt. Gregory, Askofu wa Nazianzus katika karne ya 4
aliandika hivi: ‘Jina lenye cheo lenye istilahi ni jambo lililo la muhimu peke
yake kuwaelezea watu. Kadiri wanavyoendana nalo ndivyo watakapozidi kushangaa’"
Ni jambo lisilo na
maana. Madai ya waamini Utatu wa kwanza waliokuweko katika fursa nzuri katika
karne ya nne yanashangaza sana lakini yanamaanisha kwamba yalikuwa na mvuto
kwenye karne hii ya nne ilivyofuatia Ukristo jambo lililo sawa na kuzidharau
fikra za wenye akili timamu. Dhana hii ya marabi haina maana kabisa na ilikuwa
na mengi ya kuyalaumu kwa kuwa ilipelekea kuanzishwa kwa Uislamu sambamba na
kuzuka kwa imani ya Utatu tangia mwaka 381-451 BK.
Mwandishi R.
Shraga Simmons alisema hivi kwa ajili ya umuhimu wa kuitunza na kuishika Torati:
“Masihi atawaongoza
Wayahudi kipindi watakapoishika Torati kikamilifu. Torati inasema kwamba mitzvot
(amri) zote zitaendelea kutuhusu tuzifanye milele, na yeyote atakayetokea
kuibadilisha Torati mara moja atachukuliwa na kuchukuliwa kuwa ni nabii wa
uwongo (Kum. 13:1-4)
Katika Agani Jipya
lote, Yesu anaikinzanisha Torati na anasema kwamba amri zake hazina umuhimu
tena. (soma Yohana 1:45 na 9:16, Matendo 3:22 na 7:37) kwa mfano, Yohana
9:14 immeandika kwamba Yesu alifanya nukuu rejesho katika kuihalifu Shabato, jambo
ambalo liliwasababisha Mafarisayo kusema (kwenye aya ya 16), ‘Hazishiki Sabato!!’"
Sasa mtu huyu
twaweza kumchukulia kuwa ama hajui aliyokuwa anayasema Kristo na waliyokuwa
wanayasema mitume katika Agano Jipya au ni kwamba amefanya makusudi tu
kuyatafsiri vibaya maandiko haya. Anaonekana kwamba anaunga mkono madai ya wa Gnostiki
kwa mujibu wa maandiko ya Paulo na Sheria na kuyatumia hayo kwa kuwa yanaendana
naye. Masihi anawajibu wa kuwapelekea wokovu Wamataifa na Wayahudi wanataka
wamshikilie kwa watu wa Yuda peke yao.
Kristo alisema
waziwazi kabisa kwamba: “Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja (mfano;
kidoti au koma) wala nukta moja ya torati haitaoondoka, hata yote yatimie (soma
Mat. 5:17,18; Lk. 16:17). Aliwashutumu Mafarisayo kwa kuwa na sheria alizopewa
Musa lakini wakawa hawazishiki (Yohana 7:19:24). Wanalaumiwa kwa ajili ya
kuyang’ang’ania mapokeo yao ambayo hayana nuru ndani yake (Isaya 8:20) (soma
jarida la Mkutano wa Baraza wa Matendo 15 (Na. 69) na PAULO: Sehemu ya I Paulo na Torati (Na. 271)
[The Acts 15 Conference (No. 69) and PAUL: Part I Paul and the Law (No. 271)].
Wayahudi
wanapinga kwa kusema kwamba maandiko ya kiebrania ni lazima yasomwe kutoka
kwenye uandishi wake wa asili na kwamba mengi yake yametafsriwa kimakosa
yanapomuandika au kumtaja Kristo.
Isaya 7:14 mara
nyingi limetolewa kama mfano. Linaeleza jinsi mwanamwali atakapozaa mtoto na
makanusho yanafanyika kama ifuatavyo:
“Wazo la Wakristo la
kuzaliwa mtoto na mwanamwali bikira limetokana na maandiko ya Isaya 7:14 inapomwelezea kama ‘alma’ kama
kujifungua mwana. Neno hili ‘alma’ mara zote linamaanisha binti kijana au msichana,
lakini wana teolojia wa Kikristo walikuja katika kipindi zama cha karne kadhaa
zilizofuatia na lilitafsiriwa kama ‘bikira.’ Hili lilikuwa ni pamoja na
kuzaliwa kwa Yesu na wazo lililotokana na wapagani wa karne ya kwanza la
hadithi ya kiumbe kisichokufa lichopewa mimba na miungu.” (Simmons, ibid.)
Tatizo ni kwamba
kuna maneno mawili yanayotumika kuelezea jambo hili la bikira katika maandishi
ya lugha ya Kiebrania. La kwanza ni bethuwlah
(SHD 1330) lenye maana ya kutenganisha
maana bikira mmoja anayetoka kutoka
mafichoni, na wakati mwingine ni bibi
arusi pia na kwa namna ya mfano ni mji
au jimbo; ambaye ni mjakazi au mwanamwali
bikira.
Jina lililotumika
kwenye kitabu cha fasiri cha (SHD 1330) limetumika kwenye kila tukio likimtaja
mwanamwali bikira kwenye lugha ya Kiebrania kwa mwonekano wa kijakazi au bibi
arusi au mwanamwali bikira au mabikira wenye hali maalumu wa mifano mine wakati
kwamba neno lililo kwenye kitabu fasiri cha (SHD 5959), “alma” (sic) linatumika.
Mojawapo ya hili lipo kwenye Mwanzo 24:43 pale linapouelezea mfano wa uhusiano
wa Rebeka unapofunuliwa kuwa ni mke wa Isaka kwa mtumishi wa Ibrahimu na
maandiko yameweka wazi sana alikuwa ni mwanamwali bikira. Jambo hili lina maana
ya kiroho kwa wateule wa Mungu. Andiko la pili linaloelezea liko kwenye Wimbo
Ulio Bora 1:3; na 6:8 ambao unataja kwa wazi sana wanawali mabikira wa kiroho
ambao wanampenda Masihi (soma jarida la Wimbo Ulio Bora (Na. 145) [Song of Songs
No. (145)]. Andiko hili limependwa na kujulikana sana na
marabi wengi kama maabdiko ya Kimasihi. Kwenye matukio yote mawili imeandikwa
kwa mwonekano wa uwingi na linaelezea kuhusu upendo wa wanawali mabikira kwenye
uandishi.
Andiko la pili ni
lile la Isaya 7:14. Andiko hili linamhusu mama wa Masihi. Mfano ulio kwenye
tukio la kwanza ni la ubikira wa mama wa wana wa kiume wa kimwili wa Isaka
ambao ni urithi wake Masihi na andiko lililoko kwenye Isaya linamuelezea mama
huyu wa Masihi kama alivyoelezewa kwenye unabii. Matumizi ya Wimbo Ulio Bora yanamaana
yake kwa wateule katika uhusiano wao na Masihi. Neno hili limetafsiriwa pia
kama “mjakazi” kwenye Kutoka 2:8 ambapo neno limehusishwa na Miriamu, dada yake
Musa ambaye alikuwa ni bikira na pia nabii wa Israeli kutoka kabila la Lawi.
Katika kila tukio lina mwingiliano wa mpangilio wa wateule au wale waliotengwa
na kutakaswa na Mungu wadumu kwenye huduma ya kumuokoa mwanadamu kwa imani. Kuna
idadi kadhaa ya ya maneno yaliyotumiwa kutaja hali ya ujakazi, na kadhalika,
lakini neno hili moja lililo kwenye kitabu cha fasiri cha (SHD 5959) ni adimu sana.
Limetumika mara 5 kwenye uandishi wake, na limetumika zaidi sana katika kuiendeleza
dhana ya mtazamo wa kiroho wa uanawali ukiwemo mtazamo wake wa kimwili. Mtazamo
wa Wayahudi ni wa uwongo na kwa kweli kwa wapinga Umasihi ili kugeuza dokezo
lake.
Watu
wanaoikumbatia itikadi ya Kiyahudi wanadai kwamba imani ya Kiyahudi ndiyo dini
pekee iliyo na mwelekeo halisi katika ufunuo wa moja kwa moja wa Mungu kwa
taifa lao lote. Imani ya Kiyudea haikuweka itikadi yake kwa kulingana na Sheria
au Torati ya Mungu na kwenye ufunuo wa moja kwa moja kutoka kwa Mungu alionao
kwa taifa la Israeli. Huu ni opotoshaji wa moja kwa moja wa kila kitu muhimu
ambacho Mungu aliwaambia na kuwaagiza Israeli wafanye.
Kumbe Yule Yule (Kristo)
aliyeongea kwa mababa zao na kuwapa Torati Israeli katika mlima wa Sinai ndiye
alitumwa na Mungu avae mwili wa kibinadamu. Alilirudi kwa Mungu na akaletwa
tena hapa duniani kwa kuingizwa kwenye tumbo la mwanamwali bikira wa Kiyahudi
aliyechaguliwa aliyetoka kwenye Nyumba ya Daudi. Akawafundisha watu wa Yuda na
Walawi na pia kwa Wakanaani na waedomu na Wafoenike miongoni mwao. Lakini
matokeo yake ni kwamba sio tu kuwa wengi wao hawakumsikiliza, bali pia
walimuua, na hatimaye baaya ya kupewa kwao kipindi cha miaka 40 hadi mwezi ili
watubie uovu wao, walikataa kufanya hivyo. Walimuua ndugu yake miaka saba kabla
ya kuangamizwa kwa Hekalu, na hatimaye walipelekwa utumwani, kama ilivyokuwa
imetabiriwa na nabii Danieli na hawakuweza kuelewa kosa walilolifanya. Hata
hivyo, la kushukuru kwao ni kwamba Walawi walijiunga na kujumuishwa,
wakalianzisha Kanisa la Mungu ambalo litamtumikia yeye milele.
Yuda na masalio ya
watu wa kabila la Lawi pamoja na makabila mengine miongoni mwao walipewa mashahidi
wawili ambao ni Yohana Mbatizaji na Kristo. Ndugu yake Kristo ambaye pia
alikuwa ni wa nasaba moja ya damu na ambaye apikuwa ni wa ukoo mmoja huo huo wa
Daudi ambao ni wa Yuda na ambaye alibakia katika zamu yake akiwa ni shahidi wa Yuda
na Yerusalemu kwa kipindi cha miaka 33. Kwa mujibu wa Danieli 9:25, inasema
kwamba katika mwisho wa juma la 69 la miaka, alikuwa amekatikliwa mbali, lakini
sio kwa ajili yake mwenyewe. Ndipo Kanisa baada ya kifo cha Klopa, mume wa Maria,
dada wa Mariamu, alikimbilia huko Pella akawa na Simeon, mwana wa Klopa. Alikuwa
ni mjomba wa Kristo.
Ndipo Yuda
ikaangamizwa na Hekalu likaangushwa hadi chini. Tangu hapo marabi waibuka na kuunda
au kuanzisha na kuendeleza itikadi na kundi la Mafarisayo, ambao walikuwa ni
watangulizi wao. Imani ya Kiyudea nayo ikaibuka na wakafanyika kuwa wana wa
mapepo mara mbili zaidi ya kile walichokifanya Mafarisayo huko nyuma yao.
Madai ya kwamba
Ukristo unatatanisha imani na teolojia ya Kiyahudi yanazitatanisha Sheria na
Torati ya Mungu. Hata hivyo, kwa Myahudi kufanya madai kwamba imani za Utatu au
Utrinitaria, Ubinitariani au Udihei kuwa ni Ukristo yametokana tu na makosa na
kutoijua kwake Biblia na kutolijua kwake Kanisa la Mungu. Imani ya Utatu na Wapinga
sheria au Torati sio Wakristo kabisa kuliko imani ya Kiyudea ilivyokuwa ni dini
iliyotokana na mafundisho ya Musa nay a Manabii.
Imani ya Kiyudea ina
makosa kwa sababu zifuatazo:
1.
Haikubaliani na mtazamo wa kiuwingi na tofauti
iliyopo kati ya Eloa na wana wa Mungu ambao ni elohim.
2.
Imesababisha kwa kuianzisha kalenda ya Kibalelonia
kwa makosa waliyoyafanya katika kuweka nyongeza ya siku na kile wanachikiita
uhairisho mapokeo waliyoyaweka kwenye
Kalenda na kuwapotosha watu wote wanaoutafuta ukweli ili wamjue na kumfuata
Mungu matokeo yake wamepotoka na kushindwa kuzitunza Sikukuu na Siku Nyingine
Takatifu kwa siku sahihi na maranyingi sana wamekuwa wanazitunza hata miezi
mingine ambayo siyo yenyewe. Wameachana na agizo la kuadhimisha Miandamo ya
Mwezi ili iwasaidie kufikia lengo lao la kuishamirisha kalenda yao hii ya
uwongo.
3.
Inapelekea kudharau Sheria au Torati ya Mungu na
kuifanya kuwa haina maana yoyote kwa kupitia mapokeo yao.
Madai ya Wayahudi
kwamba Wakristo wanapinga kwamba mwanadamu ni Mungu yanatokana na kutoielewa
Biblia na maandiko matakatifu.
Zekaria 12:8 inasema
wazi kabisa kwamba mwanadamu atafanyika kuwa mungu mdogo (elohim). Hakuna shaka
kwamba hatima yetu sisi sote ni kwamba tutafanana na mungu au tutakuwa ni
miungu wadogo (elohim) (soma jarida la Wateule kama Elohim (Na. 001) [The Elect
as Elohim (No. 001)].
Kuna aina tofauti
ya hawa miungu wadogo au elohim, bali kuna Mungu au Eloa Mmoja tu na Wapekee
ambaye anajitosheleza na mwenye kuwaruzukia Malaika na wateule wake wote, walio
wa namna zote mbili, yaani wakiroho na wakimwili, wanapokuwa karika ulimwengu
wa roho. Yeye ndiye Ha Elohim mwenye wana wengi wa Mungu tangu mwanzo wa
uumbaji wa Kiroho marabi wanashindwa hata kuelewa maana iliyoko kwenye Biblia
yao yenyewe.
Ukweli ni kwamba
Mungu na Kristo ni wamoja (Yohana 10:30) ni kama sisi sote tulivyo wamoja, nasi
tutakuwa miungu wadogo (elohim) wakati wa ufufuo wa wafu. Lakini wao wahajalielewa
hili bado na hawataweza kulielewa kwa sasa. Siku moja na ambayo imekaribia sana
magamba yanayowazuia kuona machoni mwao yataondolewa na watatubu na kuongoka.
Hawajui kwamba
alikuwa ni huyu elohim ndiye aliyekuwanao pale kwenye Mlima wa Sinai na ndiye aliyewatokea
Israeli na kuwapa amri, na ndiye aliyekuja kwao kwa umbo la Yesu Kristo. Alikuwa
ni Yule kiumbe aliyewatokea na hata kushindana nao kwa mieleka mababa zao wa
zamani.
Torati inasema:
"Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute;” (Hesabu 23:19a). Wayahudi wanatumia sehemu yake
ya kwanza ya andiko hili ili kujaribu kujenga hoja ya kuwapinga waamini Utatu
na huku wakiacha kwa makusudi pale inaposema au kutaja Mwana wa Adamu ambapo
inaonyesha kumaanisha kuwa ni Mwana wa Adamu ametajwa kuwa ni Kristo na ambaye
yuko tofauti na huyu Mungu wa Pekee na wa Kweli. Toba yake aliyoifanya na
majuto yote yalikuwa ni kwa ajili ya dhambi za watu wote duniani na huu ulikuwa
ni unabii uliotolewa mapema sana huko nyuma kuhusu kazi na majukumu ya Masihi,
kama ilivyoandikwa kwenye Isaya Kristo ws use the first section of this half 53
na sehemu nyingine nyingi.
Imani ya Kiyudaea
inasema kwamba Masihi atazaliwa na wazazi wanadamu, na ayakuwa na mwili wa
kawaida kama watu wengine. Hatakuwa mungu-mdogo, na hatakuwa na hali yoyote isiyo
ya kawaida asilia. Kwa kweli, ni mtu mmoja anayeishi katika zama za vizazi vyote
ambaye anauweza wa kufanya mambo yamhusuyo Masihi (soma kitabu cha Maimonides –
Sheria za Wafalme 11:3).
Dini hii ya
Kiyahudi imefasiri vibaya makosa yanayofanywa na Wakatoliki wa Roma juu ya
maombi yao ya kuombea dua, kwa mtindo ulio kinyume kabisa maelekezo aliyoyatoa
Kristo. Maelekezo ya Kristo yanasema kwamba hakuna atakayekuja kwa Baba
aspoitwa na yeye alikuwa anamaanisha ni kwa njia upatanisho wa dhambi kupitia
kifo na kufufuka kwake, kumepuuzwa na kwa lengo lake la makusudi kama lilivyo
kwenye maelezo yake yanayohusu kuwa maombi yetu yawe yanamlenga Baba kwa jina
la Kristo.
Ni kweli kwamba
maombi ni jambo la siri kati ya mwanadamu na Mungu. Mungu yupo karibu na wale
wanaomuita (Zaburi 145:18). Madai kwamba ile Amri ya Kwanza inayosema: “Usiwe
na miungu mingine ila mimi” inamaanisha kuwa imekatazwa kuwa na mbombezi kati
ya Mungu na mwanadamu yanatokana na kutoelewa maana ya mwombezi kwenye Agano
Jipya, na yamesababisha kuzuka kwa mafundisho ya uwongo yaliyo kwenye Kanisa
Katoliki la Roma yanayounga mkono imani potofu ya kuomba vitu mbali mbali,
jambo linaloonekana kwa wazi kabisa kuwa ni kinyume na mafundisho yake Kristo
kuhusu maombi.
Upotovu wa Kanisa
Katoliki la Roma kuhusu Kuabudu Sanamu za kuchonga na useja ni kinyume kabisa
na maagizo yaliyo kwenye Biblia na ni jambo na wenyewe hawaoni kuwa ni muhimu
na wanaona kuwa hayana tija kushughulika na mabishano au hoja potovu zinalizotungwa
kwa makusudi na watu dhid ya Ukatoliki inayojiona kuwa kama ni uwakilishi wa
imani ya kikristo, jambo ambalo sio la kweli kabisa.
Ni jambo lililo
wazi kwamba kuna mambo mawili yameelezwa kwenye maandiko ya Biblia na ambayo
yanatokea kwenye matukio ya dunia katika Siku za Mwisho. Mambo haya mawili ni
kuibuka kwa Nabii wa Uwongo ambaye atafanya kazi take na Mnyama kwa malengo ya
kuwafanya watu waipokee chapa yake (Ufunuo 19:20) Nikaona roho tatu za
uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika
kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo. Hizo ndizo
roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu
wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi. Tazama, naja kama
mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione
aibu yake.) Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni (Ufunuo 16:13-16). Yule anayejulikana kama
mtu wa kuasi (mara nyingine anajulikana
kutokana na kazi yake kuwa ni mpingakristo) ameelezwa pia kwenye 2Wathesalonike
sura ya 2. Kuja kwa Kristo kutatanguliwa na kuwepo kwake huyu mtu wa kuasi,
ambaye ametajwa kwa jina lake linguine kama mwana
wa uharibifu. Mtu huyu atafanya kazi ya kupinga na atajinua nafsi yake juu ya
kila kiitwacho mungu na kila kinachostahili kuabudiwa. Ataweka kiti chake
kwenye Hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kuwa yeye ni Mungu (aya ya 4).
Kuna uwezekano wa
aina mbili tu uliopo katika kupata maana ya utimilifu wa andiko hili. Moja wapo
ni uwezekano wa kujengwa kwa Hekalu lenyewe Kabisa, na mwingine ni ule wa
kwamba mtu huyu atatokea kwenye moja ya Kanisa la Mungu. Uwezekano tarajiwa ni
kwamba tutakuwa tunajionea utendaji wa kazi zake huyu nabii wa uwongo ukianzia
huko Yerusalemu na pia tutajionea makao ya mamlaka kazi ya Mnyama, ambaye
anaweza kuwa ndiye huyohuyo ama mwingine. Ni lazima atakuwepo msemaji mkuu atakayefanya
kazi kwenye mamlaka ya Mnyama. Muundo wa Nabii huyu wa Uwongo na ule wa dini ya
ulimwengu utafikia kwenye malengo ya kuliwezesha Kanisa la Mungu likue na
kuenea kwa nguvu zaidi katika Siku za Mwisho kwenye kipindi cha kabla ya
kurudia kwa Masihi na hili litakuwa ni Kanisa la Mpingakristo. Hii inatuama katika
ukweli kwamba Kanisa linazishika Sheria au Amri za Mungu na halimkani Kristo. Na
Kristo atakuja kuwaokoa watu hawa.
Nguvu za Mnyama huyu mwanzoni zitalitumia Kanisa Katoliki la Roma na huku
ni kujaribu kuliendesha kwa kipindi hiki nyeti na cha mwisho. Hata hivyo, nguvu
hizi zitaendelea na kuenea zaidi ya hapo kama ilivyotabiriwa katika Ufunuo 18.
Vita vya Siku za Mwisho vitaiangamiza Roma na hatimaye Papa wa Mwisho, ambaye watadai
ya kuwa yeye ni Petro wa Roma na huenda hata jina lake ataitwa Pius XIII. Ataondoa kutoka Roma akipita juu ya
miili ya makuhani wake. Utawala wake utakoma na kuwa msiba mkubwa na maangamizo
na ndio utakuwa mwisho uimara wa Kanisa hili la Utatu na wafuasi wake wote (soma
pia jarida la Papa wa Mwisho (Na. 288) [The Last
Pope (No. 288)].
Matukio haya yote
yatatokea kwa kipindi kilichowekwa na kutabiriwa cha siku hizi za mwisho cha
kati ya miaka 2010 na majejezo mapya ya mwisho ya mwaka 2025, na majira ya mavuno
makuu ya Yubile ya mwaka 2027 na Milenia mwaka 2028. Tangia kipindi hiki na kuendelea
mbele Hekalu litajengwa na Masihi mwenyewe wa kweli na Torati ya Mungu na
sheria zake zitatumika.
Yule nabii wa
uwongo/Mtu wa Kuasi atafunuliwa na kuwekwa wazi kupitia watu wawili
waliotabiriwa kwenye Biblia wanaojulikana kama Mashahidi Wawili (Ufunuo 11:2; soma
jarida lar Mashahidi Wawili (pamoja na Mashahidi Wawili) (Na. 135) [The Witnesses
(including the Two Witnesses) (No. 135)].
Ni ukweli
uliodhahiri kwamba, ili kuufanya ulimwengu ulikubali Hekalu Jipya, Masihi huyu
wa Uwongo itamlazimu afanikishe kwanza mbinu zake za kudanganya sehemu kubwa ya
Waisraeli wa aina zote mbili, yaani wale wa Kiroho na wale wa Uzawa Asilia. Ndipo
baada ya kufanikiwa hilo kiumbe huyu ataketi kwenye Hekalu hili la Mungu na
kujifanya kuwa yeye ni Mungu.
Mesihi huyu wa Uwongo
au Nabii wa Uwongo atafanya kazi pamoja na Joka Mwekundu pamoja na mapepo walio
kenye mashikiano na yule Mnyama ili kuwakusanya watu wote kwa vita ya Armagedon.
Matukio na harakati hizi zitaanza kujitokeza katikati ya Pasaka ijayo na ujio
wa Masihi wa Kweli. Mara baada ya kukauka mto Frati na mamlaka hii imekwisha
waangamiza Wafalme wa Mashariki, ndipo atashuka hadi Megido. Ttukio hili hata hivyo
litaihusisha kwa kuijumuisha nguvu au watawala wa upande wa Kaskazini baada ya
kumwangamiza mfalme wa Kusini na hatimaye wale wote walioko upande wa Kaskazini
ya Mashariki. Baada ya kuangamizwa hawa wafalme wa Kaskazini, ndipo wafalme wa
Mashariki wataletwa hadi Megido. Tutafafanua majira ya matukio haya kwenye
majarida mengine huko mbele.
Hatua inayofuatia
kwenye mchakato huu ni ya kumchagua mtu aitwaye Nasi au Mfalme wa Yuda. Mchakato
huu ulishaanza kufanywa katika kipindi walichoanza kuijenga Hurva mwaka 2001. Mwandishi
wa habari hii alijulishwa na wale waliohusika wakamwambia kwamba huyu Nasi
alitarajiwa kuchagulia kwenye mkutano mkuu wa mwaka 2005. Mmoja wa wagombea wa
wadhifa huu alitakiwa atoke kwenye Nyumba au ukoo wa Dayan. Nyumba au ukoo
mwingine ulikuwa ni ule wa Salathiel. Tatizo kubwa lilijitokeza wakati vipimo
vya kuhakiki nasaba ya mtu vya DNA vilipochukuliwa na ikaonekana kwamba watu
wote waliopimwa kwenye vipimo hivi hawatoki kwenye nasaba ya uzao wa Kiyahudi. Walikuwa
ni wa nasaba ya Kihiti yaani Hg. R Hittite/Celts (soma jarida la Chimbuko la Nasaba Uzao wa Mataifa (Na. 265) [The
Genetic Origin of the Nations (No. 265)]. Kuna tatizo kubwa katika eneo lile la Kaskazini mwa Wahiti na kipima
nasaba cha DNA na tatizo kubwa ni ukoo mkubwa wa ukoo wa kifalme wa Yuda. Jambo
hili limeelezwa vema kwenye jarida letu la Wahiti Katika Nyumba ya Daudi (Na. 67C) [Hittites in the House of David
(No. 67C)]. Mchako wa uchaguzi unaendelea na utatanganzwa
hivi karibuni na wakati wowote baada ya Mwaka Mpya unaofuatia baada ya
kukamilika kwa ujenzi wa Sinagogi la Hurva Mk. III.
Ni kwa jinsi gani
basi Wayahudi wanakusudia au kupenda wafanane na Wamataifa na kuwashawishi
wamkubali Masihi wa uwongo na “kujiunga’ na kile kinachoitwa misingi ya imani
ya Biblia?
Jibu la swali hili
ni rahisi na wameishaanza kufanya madai ulimwenguni kwa kile kinachoitwa “Sheria
Saba za Nuhu.” Hiki kinachojulikana kama sheria za Nuhu ni jaribio la wazi sana
katika kuhitimisha mchakato wao wa kuziondoa kabisa Sheria au Torati ya Mungu
kwa mataifa. Hii ni kwa ajili ya kuificha siri ya Uovu na Ukengeufu.
Wanashikilia
kuamini kwamba:
“Imani
ya Kiyahudi haimlazimishi mwongofu yeyote kuwa kwenye dini yao. Torati ya Musa
ni ukweli kwa kila mwanadamu, awe Myahudi ama la. Mfalme Sulemani alimuomba
Mungu kuwa ayasikilize maombi hata ya mtu asiye Myahudi anapokuja kwenye Hekalu
lake Takatifu (1 Wafalme 8:41-43). Naye nabii Isaya analitaja Hekalu kuwa ni
“Nyumba ya sala kwa mataifa yote.”
Shughuli za ibada Hekaluni
wakati wa Sikukuu ya Vibanda au Sukkot iligharimu kuchinjwa ng’ombe dume 70 kama
sadaka, idadi inayomaanisha uwakilishi wa mataifa 70 ya duniani. Baraza la Talmud
linsema kwamba kama Warumi wangegundua ni faida ya kisi gani walichokuwa wanapata
kutoka Hekaluni, basi wasingeweza kamwe kuliteketeza na kuliangamiza kabisa.
Kamwe Wayahudi
hawakuwa na tabia au mikakati ya kuwatafuta watu waingie au kujiunga na imani
yao ya Kiyahudi kwakuwa Torati iliweka wazi mlango au njia kwa wamataifa
kuifuata, ijulikanayo kama “Sheria au Kanuni Saba za Nuhu.” Maimonides anafafanua
kwamba kila mwanadamu anayezishika kikamilifu na kwa uaminifu sheria hizi
ambazo msingi wake ni katika maadili mema, basi atakuwa na nafasi nzuri huko
mbinguni.” (Simmons, ibid.)
Hizo zinazoitwa
Sheria Saba za Nuhu ni:
1.
Kufanya ngono bila kujizuia; (zikiwemo za aina
yeyote ile);
3. Kuiba;
4. Kuabudu Sanamu;
5. Kukufuru (Kulitukana na Kulilaani Hilo Jina);
6. Kula viungo vya mnyama anayeendelea kuishi;
7. Umuhimu wa kuweka taratibu na sheria kwenye jamii.
Sheria hizi saba ni kitu cha kipuuzi na hazina maana yoyote kabisa na ni kitu ambacho hakijawahi kuwepo wala kusemekana tangu siku za Nuhu, na Mababa wote wa imani walikuwa walikuwa mbele zaidi wakizishika sheria walizopewa mbali ya hizi za hawa marabi waliopagawa na kuziweka kwenye imani yao ya Kiyahudi na kututaka sisi tuziamini. Nuhu aliiwaweka kwenye safina pea saba za wanyama walio safi na pea moja kwa wanyama walio najisi. Sheria za gharika ziikuwepo tangu kipindi cha Uumbaji (soma jarida la Gharika (Na. 15) [The Foodlaws (No. 15)] na pia lila la Imani ya Kula Mbogamboga tu na Biblia (Na. 183) [Vegetarianism and the Bible (No. 183)]. Kwa hiyo ilikuwa pia ni uelewa wa uumbaji na kalenda kwa kina. Josephus aliandika kwamba kuna nguzo mbili za mawe ambayo ni matofali msingi yanayoionyesha au ilikuwa ni kalenda iliyosimamishwa na Sethi, na nguzo ya mawe inayoelezea utengenezwaji wa nguzo zote mbili na zilikuwepo bado huko Siriad (Syria) katika siku zake (Josephus, A. of J., Bk. 1; 2.3).
Sheria ya kuabudu sanamu ni machukizo makubwa yanayopaswa kukataliwa na imewekwa kwa lengo la kuihalifu amri ya pili, na hii ndiyo desturi yao Wakatoliki, na hadi wanafikia kwenye wazo lwa kwamba inakubalika kujiwekea vinyago au sanamu machoni pao wanapokuwa wanapofanya maombi, na hasa mwanapokuwa wakimuomba “Mariamu” au wale wanaowaita watakatifu waombezi wao.
Na zaidi sana wanadai kwamba utaratibu wa kuhesabiwa Haki kwa mataifa ya Wamataifa ni juu yao kwa kadiri wanavyoendelea kuzishika zile sheria Saba zilizoorodheshwa kwenye amri za Nuhu au Amri Saba za Nuhu. Na ndipo wanahakikishiwa kuwa na “sehemu yao mbinguni” jambo ambalo ni dhana au imani ya kipagani kabisa na iliyo kinyume kabisa na imani ya Wakristo wa kwanza na kwenye Biblia.
Mungu alisema kupitia watumishi wake manabii, kwamba kalenda yote—ya Sabato, Miandamo ya Mwezi na Sikukuu—ni lazima ziadhimishwe na mataifa yote katika kipindi cha mambo yote kufanywa Upya cha Milenia cha utawala wa Masihi na mataifa watakufa iwapo kama hawataziadhimisha siku hizi (Isaya 66:23; Zekaria 14:16-19).
Udanganyifu huu wa Sheria za Nuhu ungali bado unaendelea kwa kweli, na hata baraza la kutunga sheria la Marekani limezieidhia na kuziingiza kwa kuwa zinakidhi haja ya imani ya waamini Utatu, na kufanya kwao hivyo wanadhani kwamba wako kwenye uwanja au nafasi nzuri. Hata Bunge la Ireland limeipitisha sheria mbovu na isiyowezekana kwa kufuru. Katiba yao ni ya kuiunga mkono imani ya Utatu na inaipendelea imani ya Utatu, ambayo iligombaniwa kwa nguvu zote na Wakatoliki wanaoliamini Kanisa la Roma tangu mwaka 1937.
Torati ilikuwpo tangu siku za Adamu na ilitunzwa na Mababa wote wa imani na iliagizwa tena kwa ufasaha na ufafanuzi mzuri na Musa pale Sinai na Yesu Kristo ambaye alikuwa pamoja nao walipokuwa jangwani (1Wakorintho 10:4).
Soma maandiko yafuatayo.
Amri Saba za Nuhu (The Seven Laws of Noah)
Ufuatao ni mtazamo wa kawaida wanaouamini Wayahudi kuhusu kuja kwa Masihi:
Wanachukulia mambo kwamba Maimonides wanaamini kwamba imani za kikristo na Uislamu ziko kwenye mpango wa Mungu ili kueneza dhana na mafundisho ya Torati ulimwenguni kote, ili kuzifanya jamii zote ziwe mahali pakamilifu. Zote hizi zinachukuliwa kwamba zipo kwenye mpango wa matayarisho ya kuanzishwa kwa Zama ya Masihi ambayo wanaamini kuwa haijakuwepo bado bali inakuja siku za usoni (kama Biblia inavyosema), na wanapinga fundisho la kurudi kwa Masihi kwa kuwa wanaendelea kuamini kuwa bado hajaja.
Simmons anasema:
“Kwa kweli, dunia ipo kwenye hali ya kukata tama na inahitaji Ukombozi wa Masihi. Vita na machafuko yanaitishia sayari yetu. Ubinafsi na machafuko vinaziletea madhara maisha ya familia zetu. Kiasi kwamba tunayajua matatizo yaliyo kwenye jamii zetu, kiasi kwamba tutahitaji tu ukombozi. Kama baraza la Talmud linavyosema, moja ya maswali ya kwanza anayoulizwa Myahudi kuhusu Siku ya Hukumu ni kwamba: ‘Je, unajua na kujiandaa kwa ajili ya kurudi kwa Masihi?’
Tunawezaje kuharakisha ujio wa Masihi? Njia bora zaidi ni kuwapenda watu wote kwa ukarimu mkubwa, kushika maagizo yote {mitzvoth} ya Torati (kwa uwezo wetu wote tuwezavyo), na kuwatia moyo wengine wafanye hivyo pia.
Mabishano yanaendelea, dunia inaonekana kutarajia zaidi ukombozi. Ishara moja iliyo wazi sana ni kwamba Wayahudi wamerejea kwenye katika Nchi ya Israeli na uifanya ichipuke tena. Na zaidi sana ni kwamba, kuna vuguvugu kubwa la vijana wa Kiyahudi wanaopiga mbio kukimbilia au kuirudia Torati na mafundisho yake.
Masihi anaweza kuja
wakati wowote, na hii yote itategemea na matendo yetu. Mungu yuko tayari pale
tulipo. Ni kama anavyosema Mfalme Daudi kwamba “Ukombozi utakuja leo—ikiwa kama
utaisikiliza sauti yake” (sawa na anavyosema R. Shraga Simmons Inapatikana kwa
zaidi kwenye wavuti ya Aish.com)
Kumbuka kwamba melezo yanaihusu mtazamo wa mafundisho ya Torati. Tabgia
siku ya 1 ya mwezi wa Abibu mwaka huu wa 2010, baada ya kumalizika kwa ujenzi
wa sinagogi la Hurva huko Yerusalemu, majaribio kadhaa yatafanywa ili kulijenga
Hekalu kwenye Mlima wa Sayuni. Ili kufanikisha mkakati huu inabidi Masihi wa
uwongo atalazimu kutangazwa kwanza katika mwaka wake wa karibu mbele yake.
Atakuwa kiongozi machachari na mwenye uwezo na ndiye pia nabii wa uwongo ambaye
ataingilia miongozo ya tangazo la Agizo la Mfumo Mmoja Ulimwenguni.
Tangia
kipindi cha kabla ya Desemba ya mwaka wa 2010 kutatokea uamsho mkubwa wa kidini
na hali ya mambo itadorora. Katika kipindi kifupi kijacho tutashuhudia mapigano
mengi yakiibuka hapa na pale, na tutajionea kukaliwa kwa maeneo ya Gaza kutoka
kwenye baharini ikiwemo Yerusalemu na majeshi ya Mfalme wa Kaskazini atakayekuwa
na wadhifa wa “Mpingakristo.”
Dola au
milki ya Mnyama itaanzishwa kwa mabavu, mkakati ulioanza kwa mijadala ya huko Copenhagen
tangia tarehe 2 Disemba 2009. Makubaliano tayatiwa saini mnamo mwezi Julai ya mwaka
2010 yatakayosababishwa na mwonekano wa mdororo wa kiuchumi na Agizo la Mfumo
Mmoja wa Mambo Ulimwenguni utakaoshika hatamu. Vita ya III ya Dunia itakuwa inaendelea
na itakuwa kubwa kiasi cha kukaribia kuiangamiza dunia yote.
[Kumbuka kuwa
Umoja wa Kibunge wa Kimataifa (IPU) unaaandaa Kongamano la Dunia la Maspika wa
Mabunge yote ya Dunia na watakaa kikao chao kuanzia tahere 19 hadi 21 Julai. Dhumini
na kusudio kubwa la Kongamano hii ya mwaka 2010 lilikuwa sawa na kauli mbiu yao
isemayo Mabunge yaliyo
kwenye ulimwengu wenye matatizo na midororo: Jinsi ya kuulinda uwajibikaji wa
kidemokrasia ulimwenguni kote kwa manufaa mema. Soma ripoti yake yote kikamilifu kwenye wavuti hii
http://www.ipu.org/splz-e/speakers10.htm & http://www.iisd.ca/recent/recentmeetings.aspx
(Ed.)]
Dini hii
potofu na mfumo wake utawadanganya na kuwapotosha yamkini hata walio wateule,
kwa jinsi utakavyokuja kwa hila na mbinu za kijanja.
Utakuwa na
Msihi wa uwongo ambaye ataishi huko Yerusalemu na ambaye ataishika kalenda ya
uwongo yenye muundo wa Kibabeli na yenye mapokeo mengi ya kidini. Itamkana
Kristo aliyetuokoa sisi sote.
Makanisa ya
Mungu yatakayokuwa yamedanganyika na Wachungaji waabudu sanamu na walioharibiwa
kimafundisho ya ki—Ditheism na kuishika Kalenda ya Ki—Hilleli hawataweza
kushinda na kusimama. Ni wale tu walio kwenye kundi la Wafiladelfia ndio
watakaowezeshwa kushinda. Hawatalikana jina lake (Ufunuo 3:8). Wengi miongoni
mwa Wasardi na Walaodikia watashindwa kwa kuwa walikuwa wameishaharibiwa tayari
na mafundisho haya ya wa—Ditheism na wengi
wao wataanguka.
Na hata
sasa, wengi wanaendelea kuanguka kwa upande mmoja na wengine wanakuwa Wayahudi
na huku wakimkana Kristo aliyewaokoa. Wanangojea kipindi hiki cha kudanganywa na
Masihi huyu wa uwongo. Wanaweka matumaini yao kwa Wamarekani ambako dini ya
kujipenda na kujiabudu mwenyewe imeshika kasi na kuharibu wengi yakiwemo
Makanisa ya Mungu pia.
Muda ni mfupi.
Kuna kazi kubwa ya kuganya mbele yetu.
Hebu na mtoke
ninyi nyote mlioko mashimoni na mliojeruhiwa, kuumizwa na kuchoka. Kuna vita
kubwa moja mbele yetu na tunatakiwa kupigana.
q