Makanisa La Wakristo Wa Mungu

[CB46_2]

 

 

 

Somo:

Kuzuru Kanaani

 

(Edition 1.0 20060824-20060824)

 

Katika somo hili tutaangazia Kuzuru Kanaani (No. CB46). Watoto watafunziwa juu ya miaka arobaini ambayo Waisraeli waliyachukua kule jangwani na jinsi walivyoweza kuingia katika nchi waliyoahidiwa.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Copyright ã 2006  Leslie Hilburn, ed. Wade Cox)

(Tr. 2008)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


 

Somo:

Kuzuru Kanaani


 

 

Madhumuni:

Watoto watajifunza kuhusu nchi iliyaohidiwa na miaka arobaini jangwani.

 

Lego:

Kuwapa watoto kuelewa pahali nchi ya ahadi upo.

Kuwafanya watoto kuelewa umuhimu wa kumcha Mungu na kumwamini na pia kwa kutambua kuwa kuna madhara ya kutomcha Mungu.

 

Kifaa cha Kutumia:

Kuzuru Kanani (No. CB46).

 

Nukuu za agano zinazohusika:

Hesabu sura 13,14 na 15.

 

Mwenendo:

Kufungua kwa maombi.

Somo kuhusu kuzuru kanani – kujibizana maswali pamoja na watoto.

Zoezi iliyo na funzo kuhusu kuzuru kanani.

Kufunga kwa maombi.

 

Somo:

Soma Nakala hili isipokuwa somo inaweza kuweka kama mahubiri na watoto waliohudhuria. Maswali kwa watoto yameandikwa kwa herufi nzito. Hiyo ni kurejelea yale yaliyoangaziwa katika nakala. Siyo maswali yote yatangaziwa – ni jukumu la mwalimu kuamua maswali yatakayorejelewa.

 

Swali 1: Nchi iliyoahidiwa inaitwaje?

Jawabu: Ardhi ya Kanani.

 

Swali 2: Watu wangopi walitumwa kwenda kuzuru nchi hiyo iliyoahidiwa ili kuleta ripoti kamilifu?

Jawabu: Kumi na wawili. Mmoja kutoka katika kila tabaka (Hesabu 13:1-3).

 

Swali 3: Watu wawili waliteuliwa kuongoza. Walikuwa ni kina nani?

Jawabu: Yoshua na Calebu.

 

Swali 4: Nchi iliyoahidiwa ilikuwaje?

Jawabu: Ilikuwa ina mashamba mazuri na mimea ilikuwa imestahimili. Ardhi ilikuwa yenye kusalisha na pia kulikuwa na ishara ya kuendelea na mali.

 

Swali 5: Wale watu waliotumwa kwenda kuzuru kanani walirudi na nini?

Jawabu: Matunda kama makomango na tini. (v.23-24)

 

Swali 6: Unakumbuka popote katika bibilia ambapo makomanga imezungumziwa?

Jawabu: Chini ya kanzu yenye rangi ya wamawati ya mkuhuni mkuu na zile katika hekalu.

 

Swali 7: Maskauti wale walikuwa wameenda kwa muda gani?

Jawabu: Siku Arobaini. (v 25)

 

Swali 8: Siku zile Arobaini zina maanisha nini?

Jawabu: Ni nambari ya kutubu. Ilikuwa ni kuashiria miaka arobaini ambayo Israeli na Yuda walipewa kutubu, wote wakiwa jangwani na pia kutoka wakati wa Mesia hadi wakati wa kuharibiwa kwa hekalu huko 70 CE.

 

Swali 9: Je Maskauti walileta ripoti nzuri?

Jawabu: La, kumi walileta ripoti ya wongo. Waliogopa majitu na maadui wao wote hawakumwamini Mungu (vv 31-33).

 

Swali 10: Je, Maskauti wote walileta ripoti ya wongo?

Jawabu: La, Yoshua na Kalenu walinena ukweli. Waliwaeleza kuwa nchi ile ilikuwa ina maziwa na asali (Hesabu 14:7-8). Waliwaambia “Msiwaogope wenyeji wan chi ile juu tutawamaliza kwa hile kinga yao haipo tena bali Mungu ya nasi’’ (v.9).

 

Swali 11: Je, Waisraeli waliwaskiza Yashua na Kalebu?

Jawabu: La,walitaka kuwapiga na mawe (Hesabu 14;10).

 

Swali 12: Musa alifanyaje?

Jawabu: Aliomba Mungu ashika usukani na kuweka watu chini ya mamlaka yake.

 

Swali 13: Je, Mungu aliijibuye maombi ya Musa?

Jawabu: Mungu alisema “Nitawapa laana itakayowaongamiza’’. (v. 12)

 

Swali 14: Je, Musa alifanyaje baada ya Mungu kusema kuwa alikuwa anaenda kuangamiza Israeli kwa kutomwamini?

Jawabu: Musa alimwomba Mungu awahurumia na awasemehe dhambi zao. (v. 19)

 

Swali 15: Je Mungu aliitikiaje wito wake Musa?

Jawabu: Mungu alisema hatawaangamiza Waisraeli. Lakini pia alisema hatawapa fursa ya kuingia nchi walioahidiwa kwa vile walikuwa tiari washovinja agano kati yao na pia walishakosa imani. (vv. 22-23)

 

Swali 16: Je Kuna Mwisraeli yeyote aliyeingia katika nchi iliyoahidiwa?

Jawabu: Ndio, wote waliokuwa chini ya umri wa Miaka ishirini na Yoshua na Kalebu. (vv. 29-30)

 

Swali 17: Waisraeli walichukua muda gani kule jangwani?

Jawabu: Miaka arobaini. Kila mwaka ulaashiria siku waliohitaji maskauti waliotumwa kwenda  kuzuru Kanani (vv. 32-34). Adhabu la miaka arobaini jangwani ilikuwa kuwakilisha miaka elfu mbili ya kuteseka kwa Waisraeli hadi kuja kwake Kristo kwa mara ya pili.

 

Swali 18: Je, nini iliwatendeka maskauti wale kumi walioleta ripoti ya uongo?

Jawabu: Mungu aliwamaliza na laana (v.37).

 

Swali 19: Enyewe nini iliwatendekea watu wale waliojaribu kuingia nchi ile iliyoahidiwa?

Jawabu: Walishindwa vitani. Mungu hakuwa nao tu bali alikuwa pia anawapinga (vv. 41-45).

 

Swali 20: Je, Mungu alitoa lile wingu la moto?

Jawabu: La,juu haikuwa madhumuni yake kutowajali Waisraeli milele.

 

Swali  21: Je sisi hufanya nini kama kumbukumbu ya amri kumi za Mungu?

Jawabu: Nyusi za samawati katika mwisho wa mavazi

 

Bwana aliongea na Musa na akasema, “Kupitia kizazi zote zijasho munanifanya nyusi ya kando ya vasi langu, na samawati wa kila vasi. Utakuwa na nyusi kuliangalia na sasa utakumbuka amri zote za Bwan, ili umheshimu na sio kufanya dhambi na kuenda kwa taama za moyo wako na macho yako. Alafu utanikumbuka na kuniheshimu amri zangu zote na utakuwa wakipekee kwa Mungu wako’’ (Hesabu 15:37-40).

 

Zoezi:

 

A. Nchi iliyoahidiwa

Wape watoto ramani na kasha wakaipake rangi nchi iliyoahidiwa. Zungumzia jinsi ilivyowachukua maskauti siku arobaini kuzuru nchi hiyo. Ma pia kuwa wakati ahadi ya urithi ilipeanwa katika zile tabaka kumi na mbili, Manasseh,Gad na Reubebi waliahidiwa urithu uliokuwa katika ule upande mwingine wa mto wa Yordani.

 

B. Nyusi ya samawati

Mpe kila mtoto nyusi ya samawati na vipini kasha waziweka nyusi hizo kwenye mavazi yao na kasha uweleza jinsi wakifanya hivyo kila asubuhi itawakumbusha juu ya amri kumi za Mungu.

 

C. Uwindaji wa mabaki

Hiyo itafanywa nje ya majenge juu inahitaji nafsi kubwa.

 

Funga kwa maombi.

 

 

 

 

q