Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[038B]
Ishara
za Mbinguni za Mhuri wa Sita Kwa Muktadha Wake
(Toleo La Edition
1.0 20120801-20120801)
Jarida hili ni
Sehemu ya II ya somo hili la Ishara za Mbinguni na linaziwekwa kwa muktadha wake
na unabii na Maonyo ya Siku za Mwisho zinazoonyesha ashirio la kurudi kwa
Masihi.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2012 Wade Cox)
(tr.
2014)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na
tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza
kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka
maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ishara za
Mbinguni za Mhuri wa Sita Kwa Muktadha Wake
Kwenye jarida la I
(soma jarida la Ishara za Mbinguni Sehemu ya I (Na. 38A)) tuliona nadharia au dhana ya matukio ya upatwaji
wa jua unavyotokea katika Siku Takatifu kwenye mzunguko huu unaofuatia na wa
pili wa Usomaji wa Torati katika mwaka 2019 na maana zake kwa kuhusianisha na uwezekano
wa kuja au kurudi kwa Masihi.
Inaonyesha kweli
fulani zenye mashiko na zakuvutia na hitimisho yapaswa itolewe iashiriayo
kwamba ishara zapaswa zifanywe zinazohusiana na kipindi cha kufuatia kuandama
kwa Mwezi amayo ni Ishara kuu ya Mbinguni ambayo iliwekwa kule katika kuweka
mwelekeo wa kutumiwa wa Kalenda ya Mungu iliyotumika kama Kalenda ya Hekaluni
hadi kipindi cha kuvunjwa na kuharibiwa kwa Hekalu kwa mara ya mwisho ya
historia ya Kale ya Israeli huko Yerusalemu, na Hekalu la huko Heliopolis nchini
Misri lilifungwa kwa amri ya Vespasian kabla ya Pasaka ya mwaka 71 BK.
Kalenda ya Mungu ilishikwa
na kutumiwa na Makanisa ya Mungu tangu wakati huu na kuendelea kwa mujibu sawa
na Kalenda ya Hekaluni. Hawakupumbazwa na mafundisho mapotofu nay a kizushi ya
Wayayhudi kama walivyokuwa wanaishika Kalenda ya Hekaluni kwa kipindi cha miaka
331 kabla ya muda huu. Wayahudi walikuwa hawajaitunga Kalenda ya Hilleli hadi
wakati Rabi Hilleli wa II alipopewa maono ya kuanzisha kalenda ya uwongo na
potofu kutokana na marabi wawili wa Kibabeloni mwaka 344 BK na ilirekebishwa
ili kukithi mapokeo ya Wayahudi, na ikatolewa na kurekebishwa zaidi na zaidi tangu
mwaka 358 BK hadi kwenye karne ya 12. Marabi waligundua kuwa Kalenda ya Hilleli
haikuwa sahihi, lakini walidai kwamba ilipaswa kusubiriwa hadi Masihi
atakapojumuishwa. Hili ni jambo lisilokubalika, kwa kuwa Mungu sio wa machafuko.
Kalenda ya uwongo
haikushikwa kamwe na Makanisa ya Mungu hadi kipindi ulipotokea ukengeufu kati
yao kama ilivyotokea katika karne za 18-19 huko Transylvania na katika karne ya
20 huko Marekani na kutoka huko uliingia huko Yerusalemu na Nigeria (soma
majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. 156); Kalenda na Mwezi Mwandamo: Miahirisho au Sikukuu?
(Na. 195) na Kubadilishwa kwa Kalenda ya Mungu Katika
Yuda (Na. 195B)).
Ratiba ya Siku
za Mwisho
Ratiba ya matukio
ya siku za mwisho yalionyeshwa kutoka kwenye nabii za Danieli na pia kuhusu
Kuanguka kwa Misri.
Tunajua kwamba nabii
za Danieli zilianzia kwa kuonyesha habari za falme au dola za Babeli na sanamu
ya Danieli 2 ambapo kulionekana dola zilizokuwa chini ya kichwa cha dhahabu ya
Babeli iliyoanzishwa na Nebukadreza ambaye ndiye alikuwa kile kichwa cha
dhahabu. Alianza kutawala tangu kwenye Vita ya Carchemish mwaka 605 KK. Dola hizo
zilikuwa ni Babeli tangu mwaka 605 KK yenye mikono miwili ya miaka 40 kuhusu
jinsi ilivyoitawala Misri tangu mwaka 605 hadi uhuru wa Misri ya kale wa mwaka 565
KK na Mashambulizi ya Kambise mwaka 525 KK.
Mchakato huu ulikuwa ni unabii wa Mikono Iliovunjika ya Farao ambayo
imeorodheshwa kwenye mwandamano wa majarida ya Kuanguko kwa Misri (Na. 36) na Kuanguka kwa Misri Sehemu ya II: Vita vya Mwisho (Na. 36_2).
Mara saba za dola
ya Babeli zilienda kutoka kipindi cha mwaka 605-525 KK cha miaka 2520 hadi kile
cha miaka ya 1916-1996 BK hadi kwene Nyakati za mwisho za utimilifu wa Mataifa.
Mwaka 1997 ulikuwa ni mwanzo wa kile kinachojulikana kama Agizo Jipya la Mufumo
wa Ulimwengu na Dola ya Mnyama kama inavyoelekea kuchukua hatamu ya kuingoza dunia
na hatimaye kuelekea kwenye maangamivu kamili wakati atakapokuja Masihi na
kipindi cha Utawala wa Milenia wa Mungu kwenye Yubile ya mwaka 2027.
Mwandamano wa
nyakati za dola hizi ulikuwa ni mwanzo pia au kufunguliwa kwa ratiba hii.
Ufalme wa Wamedi
na Waajemi uliendelea tangu utawala wa Koreshi. Agizo la kulijenga tena Hekalu
lilitolewa na Koreshi lakini shughuli hii ya kulijenga upya ilisimamishwa na
Koreshi Makroka [Cyrus Macrocheir] aliyejulikana pia kama Artashasta I na
Wayunani. Ujenzi huu ulisimamishwa hadi wakati wa utawala wa Dario II Mwajemi
kwenye mwaka wake wa pili na amri ya kulijenga tena Hekalu ilitolewa na Artashasta
II kama tunavyoona kutokana na unabii wa Danieli sura ya 9. Nehemia alikuwa ndiye mtiwa mafuta wa kwanza
ambaye alitumwa kwenda kuanzisha ujenzi huu wa Hekalu mwishoni mwa majuma saba
ya miaka. Unabii huu na tafsiri potofu iliyofanywa kwenye tafsiri ya Biblia ya
Tafsiri ya Mpya ya Mfalme Yakobo [KJV] ya Danieli 9:25 vimefafanuliwa kwenye jarida
la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13).
Ile Dola
iliyoonyeshwa kama Kondoo Mume ya Wayunani ambayo imeiangamiziliambali Dola ya Kondoo
mume ya Waajemi kama ilivyotabiriwa kwenye Danieli 8:5-8 (na pia kwenye Danieli
sura ya 11) ilikuwa ni ile ya Iskanda Mkuu. Yeye pamoja na Ezra alifariki wakati
mmoja katika mwaka 323 KK.
Dola ya Mbuzi
mume ilikuwa ni ile ya Wayunani na iliyoonyeshwa kuwa ya Shaba. Ziliendelea
hadi kuifikia ile ya Warumi ambayo ni dola iliyoishwa kuwa yenye Miguu ya
Chuma. Dola iliyofuatia ilikuwa yenye Nyayo zilizochanganyika Chuma na Udongo
ambayo ni ile iliyokuwa ikijulikana kama Dola Takatifu ya Rumi iliyodumu
kuanzia mwaka 590 BK hadi mwaka 1850. Dola hii ilifungwa na maandalizi yalianza
rasi ya Vita vya Mwisho ambayo ilianzia kwa Vita Kuu ya I ya Dunia. Dola hii
ilipasa ifuatiwe na Dola ya Dunia ambayo itaundwa kwa Vidole Kumi vya Chuma na
Udongo vitakavyounda Dola Kuu ya Dunia ya Siku za Mwisho na ambayo itaangamizwa
na Kristo atakaporudi akiwa ni lile jiwe lisilofanywa kwa mikono ya mwanadamu
na ambalo litaipiga ile sanamu ile ya mfumo mpotofu litakaloipiga miguuni mwake
na kwenye vidole vyake na kuisagasaga milele.
Daraja ambalo huyu
Beberu wa mbuzi alilitumia kumshambulia huyu Kondoo mume lilikuwa ni Daraja la Granicus
na kutokana na mapigano yale unabii wa jioni 2300 na asubuhi zake kwa hesabu za
siku moja kuwa mwaka zinatufikisha hadi kwenye karne ya 20 hadi
katika mwaka 1967. Vita ya wakati ule iliendeleza pia mchakato wa wakati wa
Nyakati za Mwisho (soma jarida la Kuelezea Juu ya Ratiba ya Nyakati (Na. 272)).
Miaka 40 ya
kwanza ya mkono wa Kwanza ilienda kwenye matayarisho ya vipindi vya kuanzia
miaka ya 1912-1914-16. Mwaka 1916 Vita Kuu ya Somme upande wa magharibi ya
Ulaya na vita kadhaa vya mashariki vilianzisha mwanzo wa mfululizo wa Vita vya
Mwisho. Miaka 40 ilienda tangu mwaka 1916 hadi uhuru wa Misri tangu mwaka 1953-1956
na mgogoro wa kugombania mfereji wa Suez. Tangu wakati ule Misri na imani ya
Kiislamu ilichukua mahala pa Mfalme wa Kusini aliyeandikwa kwenye Danieli sura
ya 11.
Mnamo mwaka 1917
Palestina ilitwaliwa na na kuwa kwenye Dola ya Ottoman na majeshi ya muungano
ya Jumuia ya Madola na iliyojulikana kama Azimio la Balfour kwa ajili ya
Palestina lilishuhudia nchi au taifa la asili la Wayahudi likitangazwa.
Mwaka 1947 Israeli
walizidisha harakati za kujipatia uhuru na walipigana vita vyake vya kwanza vya
kupigania uhuru hadi walipoupata mnamo mwaka wa 1948.
Ni kama
tuliojionea kwenye Sehemu ya I ya jarida hili la Ishara za Mbinguni za Mhuri wa
Sita ulianza kufanya kazi tangu wakati huu.
Maana ya mwonekano
wa ishara hizi ambazo ni utungu tu yameripotiwa kwenye makala iliyoelezewa
kwenye Sehemu ya I. Ishara hiyohiyo ya damu nyekundu na miezi yake ilitokea
baada ya \israeli kufanyika kuwa taifa mwaka 1948 na ilitokea hivyo katika
miezi ya Kwanza na Saba za miaka ya 1949 na 1950.
Mara ya mwisho
mfululizo huu wa matukio ya kupatwa kwa mwezi kutokea yalikuwa na maana na
umuhimu wake sana kwa Wayahudi walioko huko Israeli. Ishara hii ilifuatiwa na
nita ya mwaka 1967 na kuunganishwa kwa Yerusalemu tangu mwaka ule kulihusiana
na Pasaka ya mwaka 1968. Kipindi kilikuwa ni cha miaka 9.5 kabla ya Yubile
iliyotuatia ya Siku ya Upatanisho ya mwaka 1977. Ulikuwa ni mwaka wa sita wa
Mzunguko wa Sabato na mji wa Yerusalemu ulikuwa mikononi mwa Israeli tayari kwa
mwaka wa Sabato wa mzunguko mmoja wa kabla ya Usomaji wa Torati na Yubile ya
mwaka 1977. Ni kweli kwamba Yuda hawakuwa wanazishika Sabato wala Usomaji huu
wa Torati lakini hii haiendani wala kufanana na Marejesho na watafanya kama
watakavyoambiwa kwenye kipindi hiki chote. Tukio la kupatwa kwa Mwezi mara zote
linakuwa la rangi nyekundu kwa wale waliofananisha mlinganisho wa rangi.
Miaka kumi tangu
Yubile ya mwaka 1977 matika mwaka wa Tatu wa Mzunguko wa Pili wa Yubile ya 120
upimaji wa Hekalu la \Mungu ulianza katika Siku za Mwisho. Jambo hili limeelezewa
kwa kina kwenye jarida la Upimaji wa Hekalu (Na. 137).
Wakati wote Mungu
hufanya mabadiliko katika mwaka wa Tatu wa mzunguko wa Sabato ili kufanya kuwa
Torati iwe bado inadumu na kushikwa licha ya mabadiliko magumu yanayotokea.
Mwaka 1993-4 Makanisa
ya Mungu yalikuwa yametawanyika na kinara cha taa kiliwekwa mnamo mwaka 1994 ili
kutayarisha mchakato wa Maonyo ya Siku za Mwisho yaliyotabiriwa kwenye Yeremia
4:15 (soma jarida la Maonyo ya Siku za Mwisho (Na. 44)).
Kipindi cha
kuanzia mwaka 1967 hadi 1997 kilikuwa ni kile kilijulikana kuwa ni cha Kumuombolezea Haruni kilichokitangulia
kipindi cha kinabii cha Maombolezo ya Musa
ambacho kilikuwa ni miaka Thelathini ya Mwisho tangu mwaka 1997 hadi 2027 (soma
pia jarida la Miaka Thelathini ya Mwisho: Pambano la Mwisho (Na. 219)).
Kipindi cha miaka
arobaini jangwani kilikuwa kinaashiria au taswira ya kimahesabu ya Yubile
Arobaini za Kanisa kuwa jangwani na kipindi cha siku thelathini mbili, na tukio
la kuingia nchi ya Kanaani kulikuwa ni kuashiria miaka sitini ya mwisho ya
Yubile ya Arobaini.
Yerusalemu
lirudishwa kwene mikono ya Yuda mwaka 1967 ili kuwaandaa kwa ujio wa Masihi na
kuwaandaa kwa wongofu wao. Jambo hili limefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Ujio wa Masihi Sehemu ya I (Na. 210A).
Mwaka 1997 tangazo
lijulikanalo kama the New World Order (NWO) au Agizo Jipya la Ulimwengu
lilianza kutekelezwa kwa kinachoonekana kama Awamu ya Mwisho ya Dola ya Mnyama.
Soma jarida la Vita Kuu ya III ya Dunia Sehemu ya 1: Dola ya Mnyama (Na. 299A).
Muundo wa mwisho
wa kidini ulianza kushika hatamu yake ya kidola. Soma jarida la Vita Kuu ya III ya Dunia Sehemu ya II: Mwanamke Kahaba na Mnyama (Na. 299B).
Mwaka 1998 Usomaji
wa Torati ya Mungu kwene Miaka ya Sabato ulianza tena. Hii ilitokea pia tena
kwenye miaka ya 2005 na 2012.
Tangu mwaka 2001 Vita
vya Mwisho vilianza.
Mchakato wa
mfululizo wa Utakaso kwa kipindi cha siku za miaka ishirini na moja ulianza
tangu mwaka 2006.
Mchakato
unaofuatia unahusu Ishara hizi za Mbinguni.
Tangu mwaka 2006 hatima ya muundo wa dunia uliwekwa kwa kushindwa ili
kwamba uangukie kwenye hili Agizo Moja Jipya Ulimwenguni (NWO) kwa kile kinachojulikana
sasa kuwa Mgogoro na Mfilisiko wa Kiuchumi Duniani. Mporomoko wa muundo na
taratibu za kifedha uliratibiwa kiasi kwamba bara la \Ulaya lililazimika
kuingia kwenye mkanganyiko mkubwa wa kimpangilio ili kwamba utaratibu na hila
zilizokusudiwa au kupangiliwa zichukue mkondo wake na kufanikishwa kirahisi na
uanze rasmi mnamo mwaka 2013. Agizo hli
la Mfumo Mmoja Ulimwenguni linaenda kwa wafalme wadogo au maliwali kumi wa dola
yenye vidole kumi. Haya ni mataifa kumi yenye nguvu za kiuchumi na kifedha yanayoendeshwa
kwa ukiritimba mkubwa au kwa masharti magumu.
Mashariki ya \Kati imejiunda upya kwa mageuzi na mapinduzi ya kuanzia mwaka
2011 hadi 2012. Vita vya Mwisho vimeratibiwa ili kwamba Awamu za Mwisho za Vita
vya wafalme wa Kaskazini na Kusini vianze na vikie kikomo au kilele chake tangu
mwaka 2013, na Mfalme wa Kaskazini ashike hatamu kutoka baharini huko Gaza hadi
Yerusalemu, na awamu ya mwisho ya uwekaji makazi yao ni miezi 42.
Tangu mwaka 2012-2013
Vita vya Mpigakristo vinaendelea kwene awamu zake za mwisho za Vita Kuu ya III
ya Dunia. Kuitwaa na kuikalia Mashariki
ya Kati kunaendelea (Danieli 11:40-43). Hata hivyo, ilivunjwa na habari kutoka
upande wa Mashariki na Kaskazini za Danieli 11:44. Ukomeshaji huu au mauaji ya
wengi utatokea na utafantika kwa muunganiko na mfululizo wa matukio ambayo
tunayaona tangu mwanzo wa vita vya Baragumu ya Tano na ya Sita.
Theluthi ya wanadamu
watauawa kwa vita hivi. Wakati vita hivi vitakapoendelea na kushika kasi,
ishara za mbinguni zilizotabiriwa na nabii Yoeli zitaanza kuchukua nafasi yake
kwenye vita hivi.
Kabla ya kurudi Masihi matetemeko makubwa ya ardhi yatatangulia. Haya
yatasababisha moto na moshi na pia mlipuko wa matope ya moto milimani na
vuguvugu litasababisha mlipuko wa miali myekundu utokee.
Ongezeko la Ishara utawezesha uimara mkubwa uonekane kwamba ujio wa \Kristo
utarajiwe kuwa utatokea mara moja na wakati wowote. Kristo atakuwa pale mapema
kabla ya Mavuno ya mwaka Mkuu wa 2025 mwishoni mwake.
Tukio la Kristo kumtokea Yoshua huko Yeriko kinaashiria mapigano au vita ya
Megido na kufuatia baadae na namna fulani ya Vita vya Hamon-Gogu (soma jarida
la Vita vya Hamon-Gogu (Na. 294)). Siku saba za kuuzunguka Yeriko zinaashiria
kwamba Kristo atabidi awe huko katika miaka saba tangu Yubile na hivyo kwamba
mnamo mwaka wa 2019 kwa ajili ya Sabato na huenda itakuwa mwaka 2018 kuhitimisha
nabii zilizotolewa (soma jarida la Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142)).
Baadhi ya Ishara muhimu za Mbinguni zitatokea mapema kabla ya mwa 2018 na
zinaweza kusaidia kuelekeza vipindi hivi maalumu. Matukio haya ya kupatwa kwa
mwezi hutokea sawasawa na mujibu wa Kalenda ya Hekalu ikihusiana na kipindi cha
Mpito hadi kuonekana tena mwezi.
Mwaka 2014 kuna
upatwaji kamilifu wa mwezi wakati wa Sikuku ya Pasaka kama tulivyoona kutoka
kwenye Sehemu ya I. Pia kuna upatwaji kamili wa mwezi katika Siku Takatifu ya
Kwanza ya Sikukuu ya Vibanda.
Mwaka 2015, kupatwa
kamili kwa jua kutatokea pia katika Mwaka Mpya hapo tarehe 20 Marchi 2015 na
upatwaji kamili wa mwezi mnamo tahere 4 Aprili 2015, ambayo ni siku itakayokuwa
baada ya Siku Takatifu ya Kwanza inapoanza Sikukuu ya Mikate Isiyo na Chachu. Kutakuwa
na upatwaji wasehemu wa jua utakaofanyika kwenye Siku ya Upatanisho siku ya
Jumapili ya tarehe 13 Septemba 2015. Siku ya Jumapili, tarehe 27 Septemba 2015 Siku
Takatifu ya Kwanza ya Sikukuu ya Vibanda, kutakuwa na upatwaji kamili wa mwezi.
Tahere 9 Marchi
2016 siku ya 1 Abibu kutakuwa na kupatwa kwa mwezi. Tahere Marchi 23 wakati wa Pasaka
kutakuwa na kupatwa kwa mwezi. Tarehe 1 Septemba 2016 wakati wa Sikukuu ya
Baragumu kutakuwa na kupatwa kwa mwezi. Tarehe 16 Septemba 2016 kutakuwa
kupatwa kwa jua siku ya pili ya Sikukuu ya Vibanda.
Tarehe 11 Februari
2017 kutakuwa na kupatwa kwa jua, siku ya 15 ya Adari 1 ambayo ndiyo
siku ya maadhimisho ya Purimu. Tarehe 26 Februari 2017 kutakuwa na kupatwa kwa
jua siku ya Mwandamo wa Mwezi wa Adari 2. Katika kipindi cha Mwezi Kamili wa Abu,
tahere 7 Augosti 2017 kutakuwa na kupatwa kwa jua. Jioni ya tarehe 21 Augosti kutakuwa
na kupatwa kwa mwezi utakaoambatana na Mwandamo wa Mwezi wa Eluli, Mwezi wa Sita,
unaoweka kipindi cha kupaa cha mwisho ya Musa (soma jarida la Kupaa kwa Musa (Na. 70)).
Tukio hili la kupatwa
jua na mwezi litatokea katika siku muhimu ya Kalenda ya Hekalu tangu mwaka 2014-2017
na zaidi ili kwamba kipindi kingine chochote cha historia ya sasa.
Kama tulivyoona,
inamaana sana kwamba hakukuwa na ishara za kiastronomicali kwenye miaka ya 1600
hadi kwenye karne ya ishirini. Ishara za miaka ya 1500 hazikutokea kwenye
Sikukuu yeyote za Kalenda Takatifu. Mungu alitoa ishara kwenye Marejesho Mapya.
Ndipo mbinguni kulikuwa kimya kuhusiana na imani kwa kipindi cha karne kadhaa
na kisha kwenye siku zenyewe ambazo zilikuwa za muhimu sana kwenye unabii kwa
kulinganisha na mwaka 2300 jioni na asubuhi zake na kwenye nabii za Danieli na
Ezekieli ishara hizi za kupatwa jua na mwezi zilitangulia kutokea.
Ishara za Mbinguni zitaendelea kwa kusababisha matetemeko ya ardhi hadi
mwaka 2025. Tumekijadili na kutathimini kile kinachoitwa Ishara za
Mbinguni hadi mwaka 2017. Kutakuwa na ishara nyingi nyingine
zitakazoendelea hadi kurudi kwa Masihi. Kama tulivyosema,, tunatarajia kumuona
kabla ya Yubile ya mwaka wa 2027. Hebu na tuone na kusubiri na kuomba kwa ujio wake.
Sasa tutaendelea kuelezea naendeleo ya Vita ya III ya Dunia kipindi chote
kilichobakia cha muda huu maalumu.
q