Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[231]

 

 

 

Kipeperushi cha Zamani cha Mafundisho ya Kanisa la Mill Yard

(Toleo La 1.0 19971224-19971224)

Shukurani zetu zimwendee Thomas McElwain kwa kutupatia kipeperushi kilichoambatanishwa, ambacho ni kabrasha la zamani sana la Kiingereza la Kanisa la Sabato. Inaonyesha kuwa haihitaji kupingwa wala kuonewa mashaka kwamba mafundisho halisia ya zamani ya Kanisa la Kibaptist la Sabato lijulikanalo kama “the Mill Yard Seventh Day Baptist Church” kuhusu Uungu yalikuwa ya mrengo wa Kiyunitarian kama wanateolojia wenyewe wa kanisa hili la Mill Yard walivyoshuhudia na kwa sawasawa na mafundisho ya Makanisa ya Kikeisto ya Mungu, yaani Christian Churches of God.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org


Dagoni aliyeangukia kizingitini: au Udadisi na hoja za wanadamu, waziwezi kusimama mbele ya amti ya kwanza ya Mungu isemayo, Usiwe na miungu mingine ila mimi.

 

Na Edward Elwall wa Wolverhampton

 

Iliyochapishwa mwaka 1726

 


Usiwe na miungu mingine ila Mimi.

 

Amri hii Takatifu ilinenwa na kutolewa na Mungu mwenyewe, hivyo tu, bali iliandikwa kwa chanda au kidole cha Mungu, kwa hiyo, wale wote Wampendao yeye kwa Mioyo yao yote, na Mioyo yao, na guvu zao, waweze kuamini na kuzitii Sheria zake.

 

Sasa hebu na watu weote wamche Mungu, chukua Notisi maalumu na za muhimu, kwamba neno hili la mwisho kabia la Torati tukufu, pamoja (nami) ni kiasi fulani cha Kuwakanusha wale wanaomfanya Mungu aliye juu sana kuwa ni wa afsi ya uwingi: Kwa kuwa Neno Mimi, halimjumuishi kabisa Mtu au nafsi yoyote kwa kumfanya awe Mungu, bali huyu mmoja Mimi; na hawezi kuwa wawili, wala watatu, wala wanne. Na kwa kulithibitisha hilo kama Mtawala wa ndani wa Binadamu wote, Mungu alinena kwa Kinywa cha Nabii Musa, Kumbukumbu la Torati 32, 39. "Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam, Mimi ndiye, Wala hapana Mungu mwingine ila Mimi." Tusimruhusu Mtu yeyote aupotoshe kwa wazi, dhahiri, kiuwazi, Maana ya Maneno yake, kwa kuwa hakuna miungu mingine ila Mimi kunaonyesha ushahidi wa wazi wa kutomjumuisha na Mtu au nafsi nyingine yoyote ila Mimi peke yangu.

 

Mwokozi wetu Yesu Kristo anatoa ushuhuda kama huohuo, kwa kuwa wakati mtu fulani alipomuuliwa kwamba ni Amri ipi iliyo Kuu na ya kwanza kuliko zote, alitoa Maelezo kama hayohayo, kama ilivyokuwa ikiaminiwa na imani nzuri ya zamani ya mtu mwaminifu Musa ilivyokuwa hapo kabla, isemayo, "Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja." Marko 12:29, na aya ya 32 inasema, "Yule mwandishi akamwambia, Hakika, Mwalimu, umesema vema ya kwamba Mungu ni mmoja, wala hakuna mwingine ila yeye;."

 

Kutokana na hiyo ndipo nimechukua Magizo ya asili; kwamba hakuna mwingine ila Mungu ni mmoja tu, na hakuna mwingine ila Yeye tu.

 

Kwa hiyo, yeyote anayemfanya huyu Mungu Mmoja kuwa ana Nafsi nyingine yoyote zaidi kuliko alivyo Yeye mmoja, anapotoka na kukosea kabia na fikra yake si ya kweli kabisa; na anajaribu Kuukanganya na kuupigwa kwa wazi Ushuhuda wa Yesu Kristo.

 

Sasa, Sheria ya milele iliyotiwa kwenye Sanduku la Agano la Mungu, ni hii, isemayo, Usiwe na miungu mingine ila Mimi; lakini mashambulizi wa Wanadamu, yalipelekea wamsimamishe Dagoni; lakini alianguka mbele ya Sanduku la Agano. Na ndipo walimsimamisha na kumrudisha sehemu yake tena, lakini Asubuhi ilipofika, tazama, Dagoni alianguka tena Uso wake kifudifudi Ardhini, mbele ya Sanduku la Agano la Mungu, na hivyo ndivyo itakavyokuwa kwenye Mavumbuzi au maagizo ya wanadamu wote.

 

Sasa, Maneno ya Mungu wa Kweli, kwenye Amri ya Nne ni haya, Siku ya Saba ni Sabato ya Bwana Mungu wako; lakini Mavumbuzi na maagizo ya Wanadamu, yameifanya Siku ya Sita kuwa ni Sabato, na wengine wakaifanya Siku ya kwanza kuwa ni Sabato. Karibia Dola Kuu zote za Dunia, zilizo chini ya Waturuki, Waajemi, Wamoguli, na Mataifa mengi mengine, wameifanya Siku ya Sita, kuwa ni Sabato; na karibia Mataifa yote yaliyo bado, au yaliyowahi kuwa chini ya Papa, na yaliyoyashika maagizo yake, yaliifanya Siku ya Kwanza kuwa ndiyo Sabato. Maamuzi yote hayo Yanapingana na Sheria takatifu ya Mungu, iliyotuambia wazi sana, na kwa Kinywa chake mwenyewe kuwa, Siku ya Saba ni Sabato.

 

Na kwapmb tusisahau kabisa, wala kujifanya kuwa hatulijui agizo hili, alipenda kuiandika kwa rehema zake na kwa Chanda cha mkono wake kwenye Mbao za Mawe, na akaagiza itiwe kwenye Sanduku la Agano la Mungu, wakati ambapo kabla ya Sheria yoyote ya Kidini na kiibada haikjaja, bali ilikuwa ni Sheria hii tu takatifu peke yake ya Amri Kumi; ambayo Kristo anatuambia pia kwamba, Lakini ni vyepesi zaidi mbingu na nchi vitoweke, kuliko itanguke nukta moja ya torati, Luka 16.17. na anatuambia kwenye Mat. 5;17. Kwamba hakuja kuitangua, bali kuitimiliza, ambavyo ni kuitenda

 

Kwa kifupi, jinsi inavyopotoshwa, ndivyo jinsi itakavyomuathiri Mtu mwadilifu, kwa kuwaona watu wakichagua kuyafanya na kuyafuata Maagizo mapotofu yanayoamriwa kwenye Dini zao, badala ya kuzishika amri takatifu za Mwenyezi Mungu.

 

Ni kwa kiasi gani basi Roho yangu inateseka kwa Huzuni, ninapofikiria ni watu wengi kwa kiasi gani wanaoelekea kwennye Nyumba za Minara, na huko wanawasikiliza Makasisi wao wakiinenea kinyume Amri hii ya Nne, isemayo, Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, nk, nab ado Watu wanaomba na kusema, Bwana Utuhurumie, na tunaitoa Mioyo yetu kuishika Sheria hii; na ambavyo ikionekana wazi kabisa, wanaifanya hii kuwa ni Sheria au amri ya Mungu, au vinginevyo, Ni kwa nini wanamuomba na wakiizuia Mioyo ishiishike? Na bado kwa wakati huo huo, hakuna kitu kingine chochote kwa hakika, zaidi ya vile walivyokusudia kuishika, au kuitii amri hii.

 

Watu kadhaa wenye hekima na busara na wema, wameungana na mimi kwenye Somo hili la Linalombelezewa na kusikitisha, na wakaomba kutokee Matengenezo; na, kwa kweli, Siandiki jambo hili ili kumuudhi au kumchokoza Mtu yeyote, lakini ni zaidi tu, ni kwamba, ili waiweke Moyoni, na waichukulie kiukamilifu kwa Kicho na Hofu, ili Mungu asitukanwe; na kwamba waovu wasifanywe mioyo yao kuwa migumu na kutiwamoyo, kwa Kuivunja Sheria ile Takatifu, kwa kuzivunja na nyinginezo pia.

 

Kwa kuwa ni vizuri kuyashika Maneno ya Mtume Yakobo yasemayo, Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. 11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria, Yakobo 2:10,11.

 

Sasa, inaweza kuwa imesemwa kwenye yoyote kati ya Amri hizi Kumi’ ya Nne na ya Tano, pamoja na ile ya Sita na ya Saba. Lakini uwiano wa ujumla wa Wanadamu waliokuwanao zaidi ya kuchukulia Dini zao nje ya Almanack, zaidi nje ya Sheria Takatifu ya Mungu; Kwa kuwa Mamilioni ya watu watazishika Siku zilizochorwa Maandishi Mekundu, ambazo Papa mwenye Maagizo ya kibinadamu amezipangia, lakini Siku Takatifu ya Sabato, ambayo Mungu mwenyewe ameiamuru, hawataishika, wala kuitilia Maanani kwa Kuiadhimisha.

 

Sawa tu na ndivyo hivyohivyo wanavyofanywa kwenye Amri ya 2, ambapo Mungu anasema, Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia; nk. lakini Mafundisho ya Mapapa, Maaskofu na Makasisi, yamesababisha kutengenezwe maelfu ya Sanamu za Kuchonga; na sio tu kwamba wazisujudie kwa kuzipigia magoti na wanadamu, bali hata wazipige busu. Na kwa kuivunja Amri ya 3, sasa imekuwa kama kitu cha Kuambukiza, na cha Ulimwengu wote, ikipuuziwa kwamba Nafsi inayo nyenyekea kwa hakika inaweza kusema na abii wa Zamani, Isaya, xxiv.3. kusema; Dunia imenajisiwa na Wanaoikalia, kwa kuwa wamezihalifu Sheria, na kubadili Amri, ... Isaya 29:13.14.15.16.

 

Hebu na watu wote wema wachukue Notisi kadhaa, jinsi Mungu anavyopendezwanao wote, ambao Wanamcha na kumhofu yeye, kinyume na inavyofundishwa na Maagizo ya Wanadamu: Ambavyo ni, kama Maneno ya Bwana wetu yasemavyo, Hayo yote ni Mafundisho, Amri za Wanadamu.

 

Lakini wote walio wema, wanyofu wa Roho, wanaompenda Mungu Aliyehai, watayainua Macho yao kumtazama Mungu Aliye Juu sana, na kwa Manabii wake, na kwa Kristo na Miyume wake, ili kuitafuta Amri Takatifu, na mambo yote yahusuyo Imani yao na Wokovu, Ibada yao, au kitu chochote kinachohusiana na Hatima yao ijayo; Na kwma kwenye Maagizo yoyote ya Wanadamu, kwa masuala ya Kidini, iwe ni Wafalme au Mapapa, Maaskofu au Makasisi, au Yeyote yule, tusishughulike nao, wala Watunga Kanuni za Imani.

 

Lakini kwa mambo yote ambayo yana Tabia za muda mfupi, na zinazohusiana na Hali zetu za Kijamii, Siasa za Serikali za Kidunia, zihakikishe zinatii Sheria na maagizo ya Wanadamu kwa ajili ya Bwana; na kutii kikamilifu kinachoamriwa na Mahakama, kutoka kwa mfalme aliye kwenye Kiti cha Enzi, hadi chini kwa Mjumbe mwenye mamlaka ya Ardhi au eneo lako.

 

Lakini kwenye mambo yoyote ya Kiroho, mfanye Mungu wetu mwema kuwa Mshauri wako, na usimuite mtu yeyote Baba hapa Duniani, kwa kuwa Baba yako ni Mmoja tu ambaye ni Mung; na wala usimuite mtu yeyote Bwana, kwa kuwa unaye Bwana wako Mmoja, Kristo; na kumbuka wakati wote kwamba Ufalme wake sio wa Dunia hii.

 

Na kama Watu watadiriki kuachana na Mapokeo au maagizo ya Wanadamu, na wakaziamini au kuzitii Amri Takatifu za Mungu, na kuyachagua Maneno ya Kristo na Mitume wake, badala ya Maneno na maagizo ya Mapapa na Mabaraza yake; ndipo wataweza kabisa kuugundua upumbavu ulio kwenye Mafundisho ya Utrinitarian, pamoja na kwa walivyoona kwamba Mkate na Divai Hugeuka kuwa mwili na damu halisi; na kwamba ya kwanza hayastahili kushindwa kuliko iliyofuatia, lakini yote ni kama haina mashiko, Hayatokani na Maandiko, na Hayana uhalisia, ambavyo ni kinyume kabisa na maana yoyote njema Iliyokusudiwa na Kufikirika.

 

Kwa kuwa sio yote kwa pamoja ni ujinga kusema kuwa, Mungu Mmoja anaweza kuwa na Nasfi Tatu, ni sawa na kusema kuwa, Mkate na Mvinyo ni Mwili na Damu ya Kristo? Hapana, ndipo Watu wangesema wazi kwamba Kweli halisi, Hivi sio Upumbavu mkubwa kusema, Mungu Mmoja wa Mbinguni na Duniani, ni Nafsi Tatu au ne, kama kusema, Mfalme Mmoja wa Uingereza na Ireland, ni Watu au afsi tatu au Nne? Hivi siyo zamani zote kuwa ni uwongo na zaidi?

 

Oo, Mungu Uliyehai, nakutafuta kwa unyenyekevu wote, yafungue Macho ya Mwananchi mwenzangu kwa kweli, na Watu wengine wote kwa ujumla, ili waweze kuona, na kumchukia Kahaba mkuu, Mama wa Makahaba, na wa Machukizo yote na Mafundisho yake yote potofu yaliyoshika dau hapa Duniani; kwa kuwa hivi ni baadhi ya Vikombe vya Mvinyo wa Uasherati wake, ambazo amekuwanavyo hapa na huko mbeleni, na angali bado anatunywesha sisi, na Mataifa mengi Jirani zetu; aliyoyanywesha kwa uchafu wa Uasherati wake, na Mafundisho yake yote ya Uwongo.

 

Oo Bwana Mungu Mwenyezi, Hukumu zako ni za kweli na za haki; harakisha Muda, nakuomba, kisha uzitukuze Sheria zako, na uzifanye ziheshimiwe; wakati Wafalme wa Dunia watakapomchukia Kahaba huyu Mkuu, na kuyaasi Maagizo yake Yachukizayo na machafu yake yote ya Uasherati wake.

 

Oo, ili Watu wako watoke kwenye dini hii ya Siri ya Kibabeloni, ili wasiwe sehemu ya Dhambi zake, na kwamba wasipokee Mapigo yake, kwa kuwa Dhambi zake zimefika hadi Mbinguni, na Mungu atayakumbuka Maovu yake.

 

Ni wewe, Ee Roma mchafu, nayashitaki Maagizo haya yote ya upotofu, ya Kuvunja Mpangilio wa Kwanza wa Amri Kumi, kwa kumfanya Mungu Aliye Juu Sana, Mtakatifu wa Israeli, kuwa ni wa Nafsi Nyingi; kinyume kabisa na isemavyo Amri ya Kwanza, nawe ukawafanya watu wako wajifanyie Sanamu za Kuchonga na Wazisujudie; kinyume na isemavyo Amri ya Pili, na kwa kuwaruhusu walitajea bure Jina takatifu la Mungu, kwenye Viapo vyao vingi, na kulitukana au kulidhalilisha kwa Makusudi kwa kuliona la Kawaida tu mwenye Taratibu zao nyingi, kinyume kabisa na isemavyo Amri ya Tatu.

 

Kwa kuibadilisha Sabato Takatifu, kutoka Siku ya Saba (ambayo Mungu anapumzika kwayo, na kuibariki na kuitakasa kwa Matumizi Matakatifu) na kuipeleka hadi Siku ya Kwanza, ambayo ilikuwa ni moja ya Siku za Mungu za Kazi; (na inayopasa kuwa ni moja ya Siku za Kazi za Mwanadamu, milele) Hiyo, nawe umezibadili Amri za Mungu, na kulivunja Agano la Milele, ambavyo ni kinyume kabisa na maagizo ya amri Nne za Kwanza za Mungu.

 

Pamoja na Maagizo yako mashuhuri na yaliyo kinyume yaliyoandikwa hata kwa rangi Nyekundu kwenye Maandiko, Siku za Watakatifu, na Siku zako zote ulizoziita Takatifu; ambazo wala hakuna hata moja aliyoiamuru Mungu iadhimishwe kati yake. Nakupa changamoto kwa kukutaka, Ewe Roma pamoja na Wafuasi wako wote, unionyeshe Ulipoagizwa na Mungu, au kutoka kwa abii wake yeyote, au kutoka kwa Mtume wake yeyote, alipokuagiza yeyote hata Moja tu kati ya Siku zako zote ulizoziwekea Maandiko Mekundu ukiashiria kuzifanyia maadhimisho ya Watakatifu, Ama ya Kuzaliwa kwa Kristo, au Siku ya Kusulibiwa kwake, au Siku ya Kufufuka kwake, au Siku ya Kupaa kwake Mbinguni, au yoyote ile iliyoko kwenye mlolongo wote wa Kundi la Siku za Watakatifu, na Nyinginezo; ambazo kama tungezishika japo nusu yake, basi tungekuwa wabaya zaidi kuliko wasiowapatia mahitaji familia zao, wala kuomba ili tusamehewe Makosa yetu; ili kwamba badaya sisi kuwa Watakatifu sisi wenyewe, basi tungekuwa waovu, tusio na haki na Wadhambi, na wenye kumchukiza Mungu. Pia imani yako ya kuwaomba unaowaita wewe Watakatifu, na kwa Mariamu Mama wa Kristo, Ewe Roma Umchukizaye mno Mungu, amka sasa na unijibu; Wewe uliyewaua wafuasi waaminifuwa wa Mwanakondoo, hebu niambie ni wapi mtumishi yeyote wa Mungu au Watu wa Zamani, walipomuomba hata Abeli, au Enoshi, au uhu, au Ibrahimu, Isaka au Yakobo, au Mtumishi mwaminifu wa Mungu Musa, au Nabii yeyote yule? Je, ilishawahi kutokea kwamba mmoja wa miungu aliyekuwa na wafuasi kwa idadi fulani waliowaomba mmoja kati hao? Je, walikwisha wahi kushika Siku ya Watakatifu, kwa yeyote kati ya hawa?

 

Sasa je, wewe sio Uso wa yule Kahaba Mkuu, ambaye ana Jereha la Kichwa mwake; kwa kuwa unajua kutoka Moyoni mwako kuwa hawajawahi kuwaomba, wala kuzishik Siku, zozote kati ya hizo za hawa wanaoitwa Watu Watakatifu, kwa kuwa Mungu Mwenyezi hakuziagiza wala kuziamuru.

 

Lakini kama Wafuasi wowote wa kanisa la Roma, au hawa wanaojifanya kuwa Waprotestant, wangeniambia, Rafiki yetu Elwall, kwa nini unayahalifu Mapokeo ya Wazee; kwa kufungua Duka lako, na unafanya kazi Zako zote Siku za kwanza za juma, na Siku za Watakatifu, na Siku nyingine  zote zilizowekewa Maandishi Mekundu; Siku ya Kusulibiwa na Siku ya Kufufuka, na Siku ya Kupaa kwake Mbinguni, nitawajibu kwa kutumia Maneno ya Bwana wangu, kwenye Mt. 15:3 isemapo; Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu? Kwa kuwa Mungu Aliamuru, akisema, Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni Sabato ya Bwana, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, Lakini ninyi mnasema, yeyote afanyaye kazi siku hii itakuwa huru.


Nanyi mwzifanya Amri za Mungu kuwa hazina Umuhimu kwa Mapokeo yenu; lakini mwaniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu, Mat. 15.9.

 

Hapa kwa kweli ni kila Roho ya Kidini inaweza kuona, kwamba Bwana wetu mpendwa Yesu Kristo, asingeweza kuwa na Wanafunzi wake mwenyewe na Wafuasi wa kuzishika Amri za Wanadamu kwa mambo yote ya Kidini, wala moja ya Mapokeo yao yasiyo na maana, lakini aliwasisitiza, kuzishika sheria na Amri za Mungu.

 

Kwa kuwa mtu alipomjia Kristo na kusema, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate uzima wa milele? Akamjibu; ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri. Mat. 19.17.

 

Lakini hapa nawasihi Watu wote kuchukua otisi fulani, kwamba Kristo Alimkemea huyu Kijana kwa kumuita yeye mwema, akasema, kwa nini unaniita mimi mwema? Hakuna alye mwema ila ni Mmoja tu, naye ndiye Mungu: Sas Maneno haya ya Kristo Yanaonyesha kwamba yeye sio MUNGU; kwa kuwa yeye ambaye Cheo hiki cha sifa ya Wema hawezi kuwa nacho kabisa, hawezi yeye kuwa Mungu aliye juu; lakini ni kwa Maneno ya Bwana wetu mwenyewe, anatuonyesha kuwa Cheo hiki sio chake, lakini kinamhusu Mungu peke yake, na hakuna Mungu mwingine ila Mimi.

 

Nahofia kwamba Dini haitaweza kabisa kuirudia hali yake ya Utakaso ya kale, hadi pale ya uchafu iwekwe kando, na Huduma Huru iwepo; ndipo hapo Makasisi wasanii na wapole wa Kujionyesha na wanafiki watakapoondolewa mbali; Wakati Watu watakapohubiri kwa Jicho moja, na Shauku timilifu ya kuendelea mbele kwenye Ufalme wa Kristo, na kuwaleta Viumbe Wenzao ndani yake, na kuwapa bure kabisa hivyo Vitu vya Kiroho, wamepokea bure kabisa pasipo kununua kwa Fedha, na bila kutoa Gharama; Ndipo kwa kweli itasemwa, umeanguka Babeli, umeanguka! Na Maaskofu wake wote, na Makasisi, wa Aina zote, pamoja na Mafundisho yao yote ya kipuuzi, na Mateso yao ya kikatili, vyote vitaangushwa na kupondwapondwa chini Ardhini, na kuanguka kama Jiwe la kusagia Baharini.

 

Ni Upumbavu wa kiasi gani unaweza kuwa Duniani, zaidi ya kusema, Kwamba Mungu Aliye Juu sana, Sababu ya Kwanza au Mungu Mkuu wa Vitu vyote, ni Undumbe vyote ni kuamini shirika ya Mungu wa Uwili, Utatu, au Urobo wa Nafsi, na Dini Iliyodhihirika inayotuambia sisi, Kuna Mungu Mmoja tu, na hakuna mwingine ila yeye. Marko 12:32. Na sio mafundisho ya wanadamu kusema kama Katekisimu ya kanisa la Assemblies, inavyosema, "Kuna Nafsi Tatu kwenye Uungu" na kwamba wao wako "Sawa kwa Uweza na Utukufu: Wakati kwamba Kristo anatuambia sivyo, na kwamba Baba ni mkuu kuliko yeye.

 

Na Nabii Isaya anatuambia, Kwamba Mungu hana wa kufanana naye: Na Mtakatifu Paulo anatuambia sisi, kwamba Kuna Baba Mmoja tu, 1Kor. 8:6. Sasa iwe kama tunaiamini Katekisimu hii Potofu, au kama tunaamini maneno ya Yesu Kristo, Isaya, na Paulo, nitawaachia Watu makini kuhukumu.

 

Sasa, kwa kweli, imefanya Uchungu na huzuni Kifuani mwangu, na kwa wanyofu kadhaa, Watu wenyekuzijua sheria, wameomboleza pamoja nami, kwamba maskini Watoto wasio na hatia, wanafundishwa Mafundisho haya yasio ya kweli, na yasiyo ya kibiblia, yanayomchanganya Mungu na Manabii wake, Kristo na Mitume; Kwa kuwa Mungu alisema, Usiwe na miungu mingine ila Mimi: Na Kristo alisema, Baba yake ndiye alikuwa Mungu wa Pekee na wa Kweli: Na Musa alisema, Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja: Na Paulo alisema, Hakuna Mungu Mwingine ila Mmoja, 1Kor. 7:5.

 

M6aandiko Matakatifu yanatuambia, Kwamba Kristo alikuwa ni Nabii, imara kwenye Vitendo na kwenye Neno, mbele za Mungu na kwa Watu wote, Luke 24:19. Hata kama Mungu alivyokuwa ameahidi kwa kupitia Mtumishi wake Musa, aliyetuambia sisi kuwa, Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye.

 

Sasa, huyo aliyeahidiwa kuwa Nabii, hangeweza kuwa ni Mungu mwenyewe: Ni mkanganyo kwenye Tabia na sili ya Vitu kudhania hivyo; kwa kuwa Israeli wangesema kabisa kuwa Musa alikuwa Mungu, ambavyo siye Mmoja Israeli waliyewahi kumthibitisha na kumkubali, ingawaje alikuwa amependwa sana na Mungu, na kupendwa na Watu wote wema, ambavyo alisemewa kwamba, Wala hajainukia abii mwingine katia Israeli, ambaye Bwana alimjua na kuongeanaye Uso kwa Uso; na ambaye kwa yeye Mungu alifanya Miujiza na ajabu nyingi, ambayo haikuwa kufanyika huko nyuma kabla yake, kama vile ya kuigawanya Bahari ya Shamu, nk. na hivyo, vyote viwili, yaani Maandiko Matakatifu, na Agano la Kale na Jipya vinathibitisha, Kwamba Kristo alikuwa Nabii kama alivyo Musa, na alikuwa na uweza wa Kimatendo na na katika      Neno, na kwa hiyo tusilogeke na Mafundisho mapotofu ya wanadamu, tuliyoyadhania kuwa ni hayana maana kabisa japo ni Mashuhuri hapa Duniani, kusema kwamba (yeye aliyekuwa abii, na ambaye alikuwa Mtumishi wa Mungu na ambaye Mungu alimuinua, na ambaye Mungu alimtia mafuta; na ambaye Mungu alimtuma, na yeye ambaye asingefanya chochote yeye mwenyewe, na yeye aliyesema, Baba yake ni mkuu kuliko yeye; na yeye ambaye Mungu alimfufua toka kwa Wafu; na yeye ambaye hakuwa na Uweza wowote kwa yeye mwenyewe wala Mamlaka lakini kile alichopokea toka kwa Mungu, na yeye ambaye Mungu alimuinua awe Mfalme na Mwokozi, na yeye ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo, ambaye ni Mwanadamu Yesu Kristo, ambaye Mungu amempa mamlaka ya Kuhukumu wote, na aliyemuamuru kuuhukumu Ulimwengu; Mungu amempokea huko mbinguni kwa Utukufu, ambako Mungu amemtunukia aketi au asimame, Mkono wake wa Kuume, na yeye ambaye ni Kuhani Mkuu wetu Milele; na yeye ambaye anaendelea Kutuombea mbele za Mungu) awe ni Mungu yeye mwenyewe.

 

Nasema, Kusingeweza Madai haya Kumpa Amani moyoni kwa aina hii yote ya Upumbavu na upotofu ambavyo hayakuwa kamwe mafundisho ya Wanadamu?

 

Bwana mwema wa Mbinguni na Duniani, na awafungue Macho yao Watu wote walio waaminifu, tena zaidi na zaidi, ili waweze kuuona Ukweli wa Mungu kutoka kwenye Maneno yake Matakatifu, na wasipotoshwe kabisa na Mapapa, Maaskofu, au Makasisi, kwa Mungu waiweke Imani yao; lakini wakati wote wamchukue Bwana wetu mpenzi kuwa Mshauri, na wasimuite Mwanadamu yeyote Baba hapa Duniani, kwa kuwa Baba yet uni Mmoja tu. Ambaye ni Mungu, na wasimuite Mtu yeyote Bwana hapa Duniani, kwa kuwa Bwana wet uni Mmoja ambaye ni Kristo. Na kisha Maneno yake ya busara, yanamfanya mtu awe na Kicho au hofu ya Asilia, Isichukue kamwe Kanuni zako za Kidini kutoka kwa Wanadamu, bali wakati wote kutoka kwa Mungu na Manabii wake, Kristo na Mitume wake.

 

Kwa kuwa kama mngekuwa Watu Watakatifu, basi Mngefundishwa na Mungu, na kama mkiyageuza Macho ya nia zenu kwake, na kusema mioyoni mwenu, Bwana, Nia yako na Mapenzi yako ni yapi? Hebu nijalie kujua zaidi, nami nitafanya hivyo.

 

Ndipo huyu Mungu mwema anayeona hata Mateso yaliyo ndani ya Roho zenu, na jinsi mlivyo na kiu cha mumtafuta yeye, yeye ana Huruma nyingi na Upendo, naye atakuja, na kwa Roho wake mwema atafanya Makao nyani yako. Kwa hiyo, hakikisha kuwa unayakumbuka Maneno ya Bwana wetu mpendwa. Na kama (anasema yeye) Mtazishika Amri zangu mtakaa katika Pendo langu, kama mimi nilivyozishika Amri za Baba yangu, na kukaa kwenye Pendo lake.

 

Kristo alituambia, kama mnataka kuupata uzima wa milele zishikeni Amri za Mungu: Ambazo tunajua kwamba ni Amri Kumi, kwa kuwa tunakuta amezielezea kwa kina sana, na kuzielekeza kiungwana sana kwa wengi wao. Na kwenye Yohana 17:3. Kristo anatuambia sisi, Kwamba Baba yake ni Mungu wa Pekee na wa Kweli.

 

Sasa, kama tukimwamini Kristo, ndipo ni hakika, hakuna Mtu mwingine aliye Mungu wa Kweli ila ni Baba yake peke yake.

 

Na kama Bwana wetu Yesu alivyokuwa makini wakati wote kumpa Utukufu Mungu wake na Baba yake wa Mbinguni, basin a sisi, tukiwa ni Wafuasi wake wa kweli, hebu na tumpe Utukufu huyu MUNGU wa pekeena asiye na mshirika, na ambaye hana wa kufanananaye, na wala hakuna mungu mwingine aliye kama yeye: kwa kuwa ni yeye tu peke yake ndiye mwenye Uzima na uhai ndani yake, ambaye haupati uhai huo kutoka kwa Mwingine: a ni yeye tu peke yake Anajitosheleza au Hahitaji msaada wowote, na anaweza kufanya Vitu vyote yeye mwenyewe: a kwa kuwa ni yeye peke yake ndiye Anaishi kwa Uweza wake mwenyewe, na wala Hatokani Mwanzo wake, au kushirikisha Uweza wake, kutoka kwa yeyote yule; bali yeye ni Mfalme Anayejitosheleza, Aliyeko, wa Milele, Hafi wala Kupatwa na madhara, Haonekani kwa macho, na ni Mungu Pekee mwenye busara.

 

Yeye ndiye Mungu wa Mababa wa Imani waliopita, na wa Manabii, naye sio tu Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, peke yao, bali pia ni Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye ametangaza kwa wazi sana, Kwamba anapewa na kuupokea Uweza wake wote, kwa sehemu zote mbili, yaani Mbinguni na Duniani, kutoka kwa Mungu; na kwamba kwa yeye peke yake hawezi kufanya neno lolote; na kwamba Mwishoni, atayatoa Ufalme kwa Mungu, aliye Baba: a kwamba Mwana mwenyewe atajinyenyekesha kwake na kumpa Vitu vyote yeye, ili Mungu afanyike kuwa yote katika yote na ndani ya yote1Kor. 11:.24, hadi 29.

 

Iwapo kama Mtu mwadilifu yeyote atasoma Aya Tano za hapo juu, ataijionea kwa dhahiri sana Kweli ambayo nimeidai na kuielezea; Kwamba kama ilikuwa ni Mungu Baba aliyetoa Uweza Mikononi mwa Kristo; hivyo Mwishoni, Kristo atamrudishia Mamlaka yote Mungu, kwa Ushuhuda wa yeye kufanyika kwa Utiifu wote kwake, na kwamba Mungu afanyike kuwa yote katika yote.

 

Kwa hiyo huyo ni kama Dagoni aliyeanguka mbele ya Sanduku la Agano la Mungu, ndivyo itakavyoonekana Mwishoni, Maagizo yote ya kipumbavu ya Wanadamu, hayataweza kusimama kinyume cha Amri Takatifu na ya Kweli ya Mungu:

 

Usiwe na miungu mingine ila Mimi.

 

Na sasa, Ee Bwana Mungu Mwenyezi, nakutafuta kwa unyenyekevu mkubwa, kwa njia ya Yesu Kristo, kuuombea Moyo wa kila Mtu aliyemaanisha, Mwanaume na Mwanamke, anayeusoma Ushuhuda huu ili akupende wewe na Sheria yako takatifu. Na kwamba iwe vizuri kwao kuliko maelfu ya Dhahabu na Fedha, na kwamba Sheria ya Kinywa chako (wewe uliye Chemichemi ya Mema yote na Kweli) uweze kuwa mbele ya Maagizo yote ya kijinga na yasiyo na maana ya Wanadamu.

 

Ewe uliye Kiumbe mkamilifu na usiye na doa, wewe ndiwe Mungu wa pekee uishiye na wa kweli, unayenipa mimi Pumzi, na ambaye unaweza kuitwa tena, wakati, na mahali, na jinsi unavyopendezwa, Nakuomba, hebu Ongoalea mbali Hofu ya kuwaogopa Watu Moyoni mwangu, wanaoweza kuua Mwili wangu tu, na nianze kujifunza kuhusu Mwana wako Yesu Kristo, kumuogopa yeye na Mungu wa wote wenye mwili, yeye pekee anayeweza kuua vyote viwili, yaani Mwili na Roho.

 

Mungu mwenye huruma yako, upemdo na uweza wote. Aliyemlinda na kumuokoa Danieli, na Watumishi wako Waaminifu, kwenye kila Zama za Ulimwengu, nisaidie Bwana na nitie nguvu Kumbe wako dhaifu, ili niweze bado kuusikia Ushuhuda wangu wa kweli kwako, na kwa Sheria yako Takatifu kwa uaminifu mkubwa, hadi Mwisho wa Maisha yangu.

 

Nashindwa kutoa sauti yangu kulia kama walivyofanya Manabii wa Zamani, Ezekieli 22:26. Makuhani wake wameihalifu sheria yangu, wametia unajisi vitu vyangu vitakatifu; hawakuweka tofauti ya vitu vitakatifu na vitu vya kutumiwa sikuzote; wala hawakuwafundisha watu kupambanua vitu vichafu na vitu vilivyo safi, nao wamefumba macho yao, wasiziangalie sabato zangu, nami nimetiwa unajisi kati yao.

 

Wakati umewadia Bwana atende kazi; Kwa kuwa wameitangua sheria yako. Zaburi 119:126.

 

HITIMISHO

 

Edward Elwall, aliyejulikana kama "Myunitarian mwanakikundi wa Kweka [Quaker]" alikuwa mshirika wa Kanisa la Kibaptist la Sabato la Mill Yard mjini London. Kipeperushi hiki cha mafundisho ya dini kimenukuliwa kwa mkono kutoka kwenye nakala iliyohifadhiwa kwenye Maktaba yajulikanayo kama Dr. Williams's Library huko London na Thomas McElwain, anayewajibika kwa nukuu zote za kimakosa zinazoweza kukutikana. Maandishi ulalo kwenye nakala asilia yamepuuzwa kuwa sio ya muhumu sana.

q