Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[109]

 

 

Swali Kuhusu

Unenaji kwa Lugha

(Toleo La 2.0 19950422-20000619)

 

Jarida hili linafafanua kikamilifu na kujibu suala kuhusu maana ya unenaji wa kugha na historia yake ilivyokuwa kanisani na kwenye karne na karne. Maandiko ya Biblia yanaelezea kwa kuktadha wake kwenye jambo hili kama lilivyoonyeshwa.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hatimiliki ©  1995, 2000 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Swali Kuhusu Kunena kwa Lugha

 


Kwenye Marko 16:15-18 tunakuta imeandikwa hivi:

15 Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. 16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. 17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; 18 watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.

 

Kamusi iitwayo The Interpreter’s Dictionary of the Bible inasema kwamba:

Uelewa wa kibiblia kuhusu ‘unenaji wa lugha’ unajumuisha mambo yafuatayo (a) utendaji wake kama sehemu ya urembesho wa kimwili wa mwanadamu utokanao na ulaji na unywaji wake (Waamuzi 7:5; Isaya 41:17); (b) ajira yake au kuchukuliana kwake kama neno la ‘kilugha’ na kwa hiyo dhana au na’dharia’; (c) mtindo wa utendaji kazi wa Roho; (d) matumizi yake kwa utendaji kazi na nguvu kwa maisha yote ya mwanadamu, na (e) matimizi yake kama alama ambayo kwamba imefikia ukomo kwa mtazamo wa vitu vinavoonekana.’

 

Kunena kwa lugha kumekuwa kukieleweka vibaya kwa muda mrefu sana na kwa siku hizi kunakutikana kwenye makanisa mengi ambako waumini wake huamini kwamba pasipo karama hii mtu anakuwa hajampokea bado Roho Mtakatifu. Inaonekana pia kwamba kila mtu binafsi kwenye makanisa haya ambayo wananena kwa lugha mara kwa mara, wakati mwingine kwa wakati huohuo wakiwa hawajielewi wala kutilia maanani kuhusu umumihu wa kuyaelewa maana yake. Lakini tunapojifunza kwa bidii na umakini vifungu vya Biblia tunakuta kwamba tendo hili la kunena kwa lugha limechukuliwa kwa kutiliwa maanani sana na kwa kweli Mtume Paulo kwenye 1Wakorintho 14:39 anasema kwamba isikatazwe. Kwa hiyo, inapaswa ipate nafasi, tlakini yapasa mtu ajiulize ni sababu ipi iliyopo hapo inayompelekea apayuke payuke tu pasi kueleweka maana yake na mtu yeyote, mbali ya huyo anenaye ambaye ni mmoja tu, peke yake? Kwa hiyo basi, hivi tunaongea nini na Biblia inasemaje hasa?

 

Kwanza kabisa, hebu na tuone kile kinachonenwa na vitabu vya tafsiri vijulikanavyo kama encyclopaedias. Kwenye Catholic Encyclopaedia kwenye makala yake ya kiuandishi kuhusu Lugha, au Glossolalia, (Vol. xiv, pp. 776/7) inasema kwamba wale waliokuwako kipindi cha wanafunzi walipokea karama hii au karama hizi:

Waliwasikia wanafunzi wakinena mambo ‘makuu ya Mungu’ kwa lugha zao wenyewe, ikimaanisha kwa jinsi walivyozaliwa navyo. ......  inaitwa Glossolalia, (ambayo kwa kifupi inamaanisha kipawa cha kunena kwa lugha), kwa hiyo ilielezewa kihistoria, ikijumuishwa na kuanishwa.

 

La kufurahisha sana ni kwamba makala hii inasema:

Kwamba Mtakatifu Frances Xavier anasemekana kuwa waliwahi kumhubiria kwa lugha asiyoielewa na Mtakatifu Vincent Ferrer aliitumia lugha aliyozalwa nayo ya kienyeji na ikaeleweka na wengine.

Paulo aliwaagiza Wakorintho wamwajiri mtu yeyote bali waombe kupewa tafsiri na wasitumie unenaji usio na tija kwa kutoeleweka na mtu (1Wakorintho 14:9) na wajiepushe na matumizi kama hayo Kanisani kwa kuwa hata asiyeamini na mwongofu mpya hataweza kuelewa kinachonenwa (aya ya16).

 

Kwa hiyo, hii ilikuwa ni ishara iliyokusudiwa kwa wasioamini na sio kwa wanaoamini. Kifungu hiki kinaendelea mbele kuonyesha kwamba Kanisa la Korintho linaonekana kuwa liliruhusu misisimko hii kuendelea au kufanyika kwa michanganyiko mipayuko isiyo na maana wala faida yoyote na ambayo wakati mwingine hata ungeweza kuwaingiza kwenye kufuru (1Wakorintho 12:3), jambo lililomsukuma Paulo kuwarekebisha na kuwafundisha njia bora ya kutumia.

 

Kitabu cha Tafsiri na Ufafanuzi kinachoitwa The International Standard Bible Encyclopaedia kwenye makala yake kuhusu dhana hii ya unenaji kwa Lugha au Tongues (Vol. 4, pp. 871-875) kinasema hivi:

Matumizi ya matendo haya yanayojulikana kama Mhemko yanakutikana kwa Washaman, Waseer na Manabii. Kwa ujumla, hali hii ya kuhemka inahusiana na nguvu za kimungu au hali ya kuwa katika roho na uvuvio.

 

Inaendelea kuelezea kwa kusema hivi:

Hakuna ushahidi kwamba waandishi wa Agano la Kale walijua lolote kuhusu ‘unenaji kwa lugha’, ingawaje walijua sana kazi na harakati za kinabii ambayo ilihusiana au kwendana pamoja na hali au aina mbalimbali za utendaji wakuhemka, kama vile lile kundi kubwa la manabii waliokuwa wanaimba na tukio la Sauli baada ya roho wa Yahwe alipomshukia na ‘akambadilisha na kuwa mtu mwingine’ akimuwezesha kutabiri, (1Samweli 10:5-13 sawa na 19:20-24).

 

Hata hivyo, kwenye dini za Kiyunani, dini za Delphi na Pythian zilijua hali hii ya mtu kufanya mhemko na unenaji ulikuwa ni kitu cha wazi tu na ulichukuliwa kuwa ni mvuvio wa kimungu na Apolo. Unenaji wa lugha au lugha zisiotafsiriwa kulikofanyika huko Korintho ulieleweka wazi sana na baadhi yao ikiwa ni dalili iliyotosheleza ya kuwa kulikuwa na maongozi ya na roho na kwamba mtu aliyefanya hivyo alikuwa na roho, na ndiyo maana ilichukuliwa kuwa ni suala ya kiroho (1Wakorintho14:4-6).

 

Maelezo yake yanaendelea kuelezea maana au dhumuni la kutolewa kwa karama na mwongozo wake wa jinsi ya kuzitumia na pia kwenye mitazamo ya kina Marko na Luka. Inasema pia kwamba:

Irenaeus alijionea uwepo wake katika wale walioishi na kuenenda sawa na sheria na maelekezo au mahudhui ya injili. Tertullian aliiorodhesha hali hii kuwa ni kama malumbano au hoja ya utetezi wa imani ili kuuwezesha uhafidhina wa kiitikadi uendelee kuwepo, wakati Origen (kwenye kitabu chake cha Ufafanuzi wa Warumi 1:13; 7.6 var.) aliiona hali hii kuwa ni kama daraja la kuwezesha kuvuka vizuizi vya mahubiri ya kitamaduni.

 

Dhana hii imetajwa pia kwenye nyaraka mbalimbali za kiofisi za papa za nyakati za zama za kati na kusababisha zirudiwe kuonekana kwenye vikundi mbalimbali vya watawa na kwenye dini zenye hamasa au ushupavu za kihafidhina. Kwenye muonekano wa siu hizi hali hii imafanyika ijulikane sana na iwe mashuhuri hasa kwenye karne ya 20 ulipoinuka Upentekoste.

 

Kitabu hiki pia kinasema kuwa:

Nyaraka alizoandika Paulo zinaeleweka kuwa zilifundisha kuwa kunena kwa lugha ni karama waliyopewa Wakristo peke yao.   

 

Kamusi ya The Interpreter’s Dictionary of the Bible kwenye maelezo yake kuhusu Lugha, Karama zake, yaani Tongues, Gift of (Vol. 4, pp. 771/2) inasema kuwa:

Kitendo au hana hii haikuwahusu Wakristo peke yao bali ilionekana pia kwenye imani na dini nyingi za ulimwengu wa kale. Popote pale ilipojitokeza, jambo la kwanza lililochukuliwa kimtazamo lilikuwa ni imani kwamba roho wa mungu waliyekuwa wanamwabudu amempagaa huyo muumini, ili anene na watu kwa kupitia yeye, na mara nyingi alimfanya mpagawaji afane miondoko au mitingishio fulani ya mwili wake na matendo mengine yasiyo ya kawaida. Wakati huu mtu huyu anapokuwa kwenye hali hii ya kuhemka koo lake la kutolea sauti liliathirika au kubadilika, ulimi nao ulitoka kana kwamba kulikuwa na operesheni ya nguvu zisizoweza kudhibitiwa na akili zake huyu aliyepagawa, na ndipo hatimaye alianza kutoa maneno na kumwambia mhusika au watazamaji wengine waliojihudhurisha mahali hapo, mara nyingi maneno au ujumbe uliotolewa haukuwapendeza wale waliokuwa hawako sawa kiimani.

 

Hadithi iliyo kwenye kitabu cha Matendo io sahihi kabisa. Unenaji wa lugha mpya uliofanyia siku ya Pentekoste ulifanwa kwa lugha za wageni, zilijulikana na waliozisiia na ziliwashangaza sana makutano. Lakini wakati unenaji huu huu wa ‘Lugha’ ulipofanyika huko Kaisaria na Efeso (Matendo 10:46; 19:6), Petro alijionea mwenewe, pasipo linganisha na mahala penginepo pote aina kama hii ya muujiza wa kupewa uweza wa kunena lugha nyingi. Wala hakukuwa na uhitaji kama huo kwa kuwa lugha za Kiyunani na Kiaramu zilitisha kabisa kuzitumia kwa huduma za kanisani.

 

Kwa sababu ya msisitizo uliotiliwa chumvi mno kuhusu unenaji kwa lugha uliojulikana kama glossolalia huko Korintho, Mtume Paulo alilazimika kulishughulikia jambo hili. anafanya hivyo kwa kuelezea kuwa anatambua umuhimu wake kwa kusema kwake hivi:

 

(a) kipawa halisi cha Roho, isikatazwe, na anatambua na kuwatia moyo kwamba hata yeye mwenyewe anashirikiana kwa mambo ya karama (1Wakorintho 14:5, 18, 39);

                                                                               

(b) ni msaada mkubwa kwa mtu anapojitoa au kujikabidhi kwenye tafakari, yaani ni njia ya kuwasiliana na Mungu, na ni fursa ya kuelezea mawazo na hisia ambayo yasingeweza kutopata majawabu kwa njia za kawaida (1Wakorintho 14:4: sawa na Warumi 8:26-27);

 

(c) ni ishara kwa wasioamini (1Wakorintho 14:22); na ni ushahidi wa madhihiriko ya nguvu za kimungu, ambayo ni kama ‘ishara ya Yona’ (Mathayo 12:39), ingawaje kwa kusema kweli zilikuwa hazijakubalika sana kihivyo kwa ugumu wa mioyo yao na kutokana na waliimu wa mafundisho ya uwongo na wasioamini na wakosoaji.

 

Paulo aliziona hatari za jinsi wanavyozitumia tena kwa wazi sana kabisa kuliko uzuri wake. Hakuruhusu ifanyike hivyo kama kigezo muhimu kwenye ibada na aliwakataza wasifanye hivyo kwenye ibada za hadharani pia (1Wakorintho 14:19, 28).

 

Anafundisha hivi utaratibu wa kuthibiti:

(a) Kwa kuzifuata kanuni kuu na taratibu zake. Matumizi ya karama za kiroho lazima zifanywe kwa mujibu wa mahitaji yake yaliyopo ili kulijenga kanisa ‘kwa upendo’ (1Wakorintho 13; 14:4-5,17-19; Wakolosai 3:14; sawa na Waefeso 4:16).  Matumizi ya Lugha ni ya kibinafsi mno, yakiukuza utu wa ndani wa kiroho chake na umuhimu wake na yamekusudiwa kujenga mshikamano wa ibada za Kikristo na umoja wao (Warumi 12:3; 1Wakorintho 13:5; Wafilipi 2:3-4).

 

(b) Kwa kusimamia utaratibu wa ibada kulielimisha kanisa ni jambo la muhimu na la kwanza. Yeye anayena ni lazima aweze kujizuia mwenyewe au vinginevya anamaze kimya kusipokuwa na mwenye kutafsiri (Wakorintho 14:27-28).  Wakati ibada inapokuwa haieleweki, au inapowakwaza na kuwaondoa kutoka kwenye kweli, basi inakuwa imeshindwa. Utaratibu na heshima ni vitu vya muhimu sana (1Wakorintho 14:13-19, 23-33, 40).

 

(c) Kwa kuupa umuhimu karama ya kutafsiri lugha. Uwezo wa kutafsiri lugha ulikuwa ni kipawa cha kipekee cha aina yake waliyopewa wau wachache sana (1Wakorintho 12:10,30; 14:28) – uwezo wa kuwa na hali inayotarajiwa ya uaswa wa kile kilichosemwa, hususan kwa kuhamishwa kimawazo hasahasa kwa mtengamano wa kiroho. Mwenye aina hii ya kuhemka anapungukiwa karama hii na yampasa aiombe, kwa kuwa anawajibu wa mambo mawili, yaani kwa yeye mwenewe na kwa kanisa (1Wakorintho 14:13-14).

 

Hizi ni baadhi tu ya vipengele vilivyowekwa na wanazuoni lakini vinaonyesha kuwa ka6rama hizi ni za muhimu na haifai zieleweke vibaya na kutumiwa vibaya na zinapasa zitumiwe kwa uangalifu mkubwa. Zaonekana kuwa kuna kiwango fulani cha nadharia kinachohusiswa, na hususan dhana ya kunena kwa lugha, inaonekana kwamba hakujaeleweka vizuri sana na kikamilifu. Sasa hebu na tutazame kwene Biblia (hususan tafsiri ya Kiingereza ya RSV).

Matendo 2:3-4  Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. 4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.

 

Ilikuwa ni kipindi hiki ambacho wanafunzi walifanika kuwa waongofu na walianza kuhubiri kwa watu wote. Ilikuwa ni Pentekoste, Sikukuu au Idi ya Majuma, na Wayahudi wa huko Yerusalem walikuwa ni wa mataifa yote waliokuwa wanaongea lugha ningine yoyote ile, hivyo, unaweza kupata taswira jinsi walivyoshangazwa wakati walipowasikia Maandiko Matakatifu yakisomwa kwa lugha na ndimi zao wenyewe. Kitabu cha tafsiri cha Catholic Encyclopaedia kinasema kwamba inaaminika kuwa walikuwa ni watu wa kutoka takriban mataifa kumi na tano. .

Matendo 2:5-11 Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. 6 Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. 7 Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? 8 Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo? 9 Warparthi na Wamedi na Waelami, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia, 10 Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu, 11 Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu.

 

Jambo la muhimu hapa ni kwamba Biblia inasema kwamba Wayahudi waliyasikia Maandiko Matakatifu yakifundishwa kwa lugha zao wenyewe. Matendo 10:46 inaanikiza hivi.

Matendo 10:46 inasema: Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu,

 

Kwa hiyo walishangazwa lakini wengine walidhihaki na wakasema kuwa huenda wanafunzi walikuwa wamelewa. Lakini Petro akawatetea akinukuu Maandiko Matakatifu kutoka kitabu cha nabii Yoeli na akawakumbusha kuhusu unabii huu na akawahubiria (Matendo 2:12-47) na wengi wao wakatubu na kubatizwa.

 

Haiishii hapo tu, bali Matendo 10 inaelezea kuhusu maono aliyoonyeshwa Mtume Petro ya wanyama najisi, yaliyofuatiwa na ubatizo wa Kornelio pamoja na familia yake na marafiki zake wa karibu nao pia walinena kwa lugha mpya na walimpokea Roho Mtakatifu (soma Matendo 10:44-47). Hii ilikuwa inaonyesha kuwa Mungu alikuwa anawajali na kutenda kazi na Wamataifa. Sehemu inayofuatia kuelezewa unenaji kwa lugha ni kwenye Matendo 19:6.

Matendo 19:6 Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri.

 

Ni wazi kwamba hii ni karama inayotolewa na Roho Mtakatifu inayofuatia kuwekewa mikono, ingawa hajapewa mtu yeyote. 1Wakorintho 7:7 inasema::

7 Ila nipendalo ni kwamba watu wote wawe kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa Mungu, huyu hivi, na huyu hivi.

 

Mtume Paulo kwenye 1Wakorintho 12 anafafanua kwamba vipawa au karama mbalimbali zimetolewa kwa watu mbalimbali tofauti tofauti sawasawa na mapenzi ya Mungu.

1Wakorintho 12:1-31 Basi, ndugu zangu, kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose kufahamu. 2 Mwajua ya kuwa mlipokuwa watu wa Mataifa, mlichukuliwa kufuata sanamu zisizonena, kama mlivyoongozwa. 3 Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. 4 Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. 5 Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. 6 Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. 7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. 8 Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; 9 mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja; 10 na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha; 11 lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.      

 

Rejea yapaswa ifanywe pia kwenye Warumi  12:6-8:

6 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; 7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; 8 mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.

 

1Wakorintho 12 inaendelea kueleza ikisema:

12 Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. 13 Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi, au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja. 14 Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi. 15 Mguu ukisema, Kwa kuwa mimi si mkono, mimi si wa mwili; je! Si wa mwili kwa sababu hiyo? 16 Na sikio likisema, Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si la mwili; je! Si la mwili kwa sababu hiyo? 17 Kama mwili wote ukiwa jicho, ku wapi kusikia? Kama wote ni sikio ku wapi kunusa? 18 Bali Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka. 19 Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? 20 Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni mmoja. 21 Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi. 22 Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi. 23 Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana. 24 Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa; 25 ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe. 26 Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho. 27 Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake. 28 Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha. 29 Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza? 30 Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri? 31 Takeni sana karama zilizo kuu. Hata hivyo nawaonyesha njia iliyo bora.

 

Wenye Sura ya 13 Mtume Paulo anaendelea kufafanua kuwa karama hizi zote zinapasa ziandamane na upendo wa Mungu vinginevyo vitakuwa havina maana.

1Wakorintho13:1-13 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. 3 Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. 4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. 8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. 9 Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; 10 lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika. 11 Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto. 12 Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana. 13 Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo..

 

Sura ya 14 inaendelea kusema:

1Wakorintho 14:1-18 Ufuateni upendo, na kutaka sana karama za rohoni, lakini zaidi kwamba mpate kuhutubu. 2 Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake. 3 Bali yeye ahutubuye, asema na watu maneno ya kuwajenga, na kuwafariji, na kuwatia moyo. 4 Yeye anenaye kwa lugha hujijenga nafsi yake; bali ahutubuye hulijenga kanisa. 5 Nami nataka ninyi nyote mnene kwa lugha, lakini zaidi sana mpate kuhutubu, maana yeye ahutubuye ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha, isipokuwa afasiri, ili kusudi kanisa lipate kujengwa.

 

Kwenye 1Wakorintho 14:6 ndipo Paulo anafafanua umuhimu wa kuitumia vizuri karama hii ya kunena kwa lugha. Kama mtu atakuwa anaitumia kwa kunena mambo yasiyojulikana ndipo inakuwa haina umuhimu wa kiroho wala haiwatajenga wanaomsikiliza. Hata hivyo, ilionekana kuwa Paulo alikuwa haongelei kuhusu unenaji huo usio na malengo lakini alikuwa anaongelea kuhusu lugha fulani lengwa ambazo zinaweza kueleweka na wanaoiongea lugha hiyo na ambayo mtafsiri anaweza kupatikana.

 

Hata kama hilo halina umuhimu, Paulo anasisitiza umuhimu wa kufundisha kwa ajili ya kuwaelimisha ndugu waumini. Kama hakutakuwa na kuelewa kokote basi hakutakuwa na uelimishaji wala kujenga.

6 Ila sasa, ndugu, nikija kwenu na kunena kwa lugha, nitawafaidia nini, isipokuwa nasema nanyi kwa njia ya ufunuo, au kwa njia ya elimu, au kwa njia ya hotuba, au kwa njia ya fundisho? 7 Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, ikiwa ni filimbi, ikiwa ni kinubi, visipotoa sauti zilizo na tofauti, itatambulikanaje ni wimbo gani unaopigwa kwa filimbi au kwa kinubi? 8 Kwa maana baragumu ikitoa sauti isiyojulikana, ni nani atakayejifanya tayari kwa vita? 9 Vivyo hivyo na ninyi, msipotoa kwa ulimi neno lililo dhahiri, neno lile linenwalo litajulikanaje? Maana mtakuwa mkinena hewani tu. 10 Yamkini ziko sauti za namna nyingi duniani, wala hakuna moja isiyo na maana. 11 Basi nisipoijua maana ya ile sauti nitakuwa kama mjinga kwake yeye anenaye; naye anenaye atakuwa mjinga kwangu. 12 Vivyo hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa. 13 Kwa sababu hiyo yeye anenaye kwa lugha na aombe apewe kufasiri. 14 Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina matunda. 15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia. 16 Kwa maana wewe ukibariki kwa roho, yeye aketiye katika mahali pa mjinga ataitikaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, akiwa hayajui usemayo? 17 Maana ni kweli, wewe washukuru vema, bali yule mwingine hajengwi. 18 Namshukuru Mungu ya kuwa nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote;

Ni dhahiri sana hapa kwamba karama hii amepewa Paulo ili aweze kunena kwa lugha nyingi ambazo hajawahi kujifunza kwazo ili aweze kuwahubiria Injili wale atakao wafikia vinginevyo aweze kuelewa. Kuna jambo lingine hapa ambalo Paulo ameliingiza nalo ni mahala pake muafaka kufanyia maombi haya. Hii imeandikwa kwenye kamsi ya Interpreter’s Dictionary of the Bible kuwa ni kama ilivyoelezwa mwanzoni kwenye kipengele (b) kinachoelezea kuwa ni namna ya kimsada kwa mtu anapojitoa kimaombi 1Wakorintho 14:4 sawa na Warumi 8:26-28 ambayo inasema:

Warumi 8:26-28 Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. 27 Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu. 28 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.

 

1Wakoritho 14:19-33 inaendelea kusema:

19 lakini katika kanisa napenda kunena maneno matano kwa akili zangu, nipate kuwafundisha wengine, zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha. 20 Ndugu zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima. 21 Imeandikwa katika torati, Nitasema na watu hawa kwa watu wa lugha nyingine, na kwa midomo ya wageni, wala hata hivyo hawatanisikia, asema Bwana. 22 Basi, hizi lugha ni ishara, si kwao waaminio, bali kwao wasioamini lakini kuhutubu si kwa ajili yao wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio. 23 Haya! Ikiwa kanisa lote limekusanyika pamoja, na wote wanene kwa lugha, kisha ikawa wameingia watu wajinga au wasioamini, je! Hawatasema ya kwamba mna wazimu? 24 Lakini wote wakihutubu, kisha akaingia mtu asiyeamini, au mjinga, abainishwa na wote, ahukumiwa na wote; 25 siri za moyo wake huwa wazi; na hivyo atamwabudu Mungu, akianguka kifudifudi, na kukiri ya kuwa Mungu yu kati yenu bila shaka.

 

Kwa dhahiri kabisa, matumizi yasiyotakiwa ya lugha yanaonekana kuwa ni kama ishara ya uchanga au kutoimarika hapa. Kifaa muhimu zaidi cha wongofu ni unabii wa wazi. Mtume Paulo anaendelea mbele kufafanua kanuni za kutumia unenaji kwa lugha au lugha mpya ya kigeni.

26 Basi, ndugu, imekuwaje? Mkutanapo pamoja, kila mmoja ana zaburi, ana fundisho, ana ufunuo, ana lugha, ana tafsiri. Mambo yote na yatendeke kwa kusudi la kujenga. 27 Kama mtu akinena kwa lugha, wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na mmoja na afasiri. 28 Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na anyamaze katika kanisa; aseme na nafsi yake tena na Mungu. 29 Na manabii wanene wawili, au watatu, na wengine wapambanue.
30 Lakini mwingine aliyeketi akifunuliwa neno, yule wa kwanza na anyamaze. 31 Kwa maana ninyi nyote mwaweza kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe. 32 Na roho za manabii huwatii manabii. 33 Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu.

 

1Wakorintho 14:39:40:

39 Kwa ajili ya hayo, ndugu, takeni sana kuhutubu, wala msizuie kunena kwa lugha. 40 Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu.

 

Kwa hiyo ilionekana kwamba kunena kwa lugha ni sehemu inayoruhusiwa kwenye Mahubiri ya Injili, lakini wamepewa mtu mmojammoja binafsi kwa makusudio fulani maalumu kwa kuwa zote hizi ni karama za Mungu. Kwenye eneo la kanisa ambako wote wananena au ambapo angalau wanaelewa kwa angalau kiwango cha kutosha lugha inayoongelewa au kutumiwa na watu wa huko basi hakuna sababu ya kufanyika jambo hili. 

 

Tunajua kwamba kwenye Kanisa la Transcarpathia walisemekana kuwa walikuwa wananena kwa lugha. Tunajua kwamba walinena kwa mtindo au aina ya kizamani ya lafudhi Kanisani. Muujiza kama huo waweza kuwa ni wa muhimu, au ni wa muhimu kule lakini sio hapa.

 

Mtume Paulo aliliweka jambo hili kuwa ni kipawa chenye thamani ndogo na alionyesha kuwa kinaweza kutumiwa vibaya na walionacho. Karama hii inaweza kutumiwa tu kwa maongozi na utaratibu ulioelezewa na kuelekezwa na yeye kwa kulijenga kanisa. Warumi 12:6-9 inasema:

Warumi 12:6-9 6 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; 7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; 8 mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha. 9 Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema.

 

Kwahiyo sasa ni kwa kusikia au kunena au yote mawili? Ni lazima iwe ni yote mawili. Mahali pake, ni wakati inavyofanyika kwa moyo wa upendo wa Mungu, yapasa kuwa ni kwenye kuhubiri Injili kwa mataifa yote.

  

Sababu ya pili inatokana na swali kuhusu Lugha na kwamba ni kuhusu hamasa iliyoelezwa kwenye Marko 16:9-20. Biblia ningi hazijumuishi sehemu ya mwisho ya Marko kwenye maandiko yao au zinaijumuisha sehemu hii kwa bango kitita. Maandiko haya hayaonekani kwenye nakala halisi na asilia za kale.

Wakosoaji wengi wa siku hizi wanakubali kwamba aya kumi na m6bili za6 mwisho za Marko 16 hazipo sahihi; na si sehemu ya Injili yake (Companion Bible, Appendix 168, p. 190).

 

Aya hizi zimeonekana kwenye tafsiri za lugha ya Kisyria au Kiaramu na Peshitto inahesabu tangu mapema sana kama hata huenda miaka ya 170 BK na nakala ya Curetonian Syriac ya marne ya tatu. Aya hizo zilikuwa zinataja mamlaka nyingi au waandishi wa zama kale. Kwa mujibu wa tafsiri ya Companion Bible sehemu ya Nyongeza inasema hivi:

 

·         Papius (yapata mwaka 100 AD) anainukuu aya ya 18 (kwa mujibu wa Eusebius, Hist. Ecc. iii 39).

·         Justin Martyr (AD 151) anainuku aya ya 20 (Apol. I. c. 45).

·          Irenaeus (AD 180) anainukuu na kutoa maelezo kwenye aya ya 19 (Adv. Her. lib. iii. c.x.).

·         Hippolytus (AD 190-227) ananukuu aya za 17-19 (Lagarde’s ed. 1858, p. 74).

·         Vincentius (AD 256) anazinukuu aya mbili kwenye Mkutano Mkuu wa saba wa Carthage uliosimamiwa na Cyprian.

·         The ACTA PILATI (sentensi ya 2) anazinukuu aya za 15, 16, 17, 18 (Tischendorf’s ed. 1853, pp. 243, 351). Katiba ya Mitume(senti. 3 au 4) inazinukuu aya za 16,17,18.

·         Eusebius (AD 325.) anazijadili aya hizi, kama zilivyonukuliwa na Marinus kutoka kwenye sehemu iliyopotea ya Historia hii.

·         Aphraartes (AD 337) akofu wa Syria, alizinukuu aya za 16-18 kwenye Mahubiri yake ya kwanza (Dr Wright’s ed., 1869, I., p. 21).

·         Ambrose (AD 374-97) Askofu Mkuu wa Milan, alizinukuu bure kabisa aya za 15 (mara nne), 16, 17, 18 (mara tatu), na aya ya. 20 (mara moja).

·          Chrysostom (AD 400) anaifanyia rejea aya ya.9; na anasema kwamba aya za 19, 20 ni “mwisho wa Injili”. Jerome (b. 331, d.420) anazijumuisha aya hizi kumi na mbili kwenye tafsiri yake ya Kilatini, nambali ya akizinukuu aya za 9 na 14 kwenye maandiko yake mengine.

·         Augustine (fl. AD 395-430) ni zaidi ya kuzinukuu. Alizijadili kuwa ni kazi ya uandishi wa Mwinjilisti MARKO, na anasema kwamba zilisomwa hadharani makanisani.

·         Nestorius (sentesi ya 5) anainukuu aya ya.20; na,

·         Cyril wa Alexandria (AD 430) anakubaliana na kunukuu huku.

·         Victor wa Antioch (AD 425) anaonyesha wazo la Eusebius, kwa kutaja MSS nyingi alizoziona, na hivyo kwamba ametosheka nazo kuwa aya kumi na mbili za mwisho zimerekodiwa kutoka humo.

 

Tafsiri ya Companion Bible inazitetea aya hizi kumi na mbili za mwisho kwa msingi kwamba zilikuwepo kwenye tafsiri ya Kisyria na zilitumika kwenye kanisa la kwanza na kwa hiyo aya hizi zingeondolewa na mamlaka zilizofuatia kama matunda yake yasingekuwepo kwenye nakati za mitume na kwenye Kanisa la kwanza. Hoja kama hizi zingekuwa pia kweli kuhusu miujiza ya mitume na manabii.

 

Utetezi mwingine wa aya hizi umoendelezwa zaidi na makanisa ya kiuamsho ya siku hizi. Utegemezi wake unatokana pia kwenye maandiko au kitabu cha Ivan Panin (cha Aya Kuminambili za Mwisho za Marko..., Shirika la Watu wa Agano, yaani The Last Twelve Verses of Mark..., The Association of the Covenant People). Maandiko haya yaliungwa mkono na Panin kwa mchanganuo wa kimahesabu ambao unawezesha kuwa na thamani ya kitarakimu ya aya hizi kwenye andiko. Inaonekana kuwa andiko hili limetuama kwenye tarakimu saba saba na kuna michanganuo mikubwa iliyofanywa na Panin ambayo inataka kudai kuwa maandiko haya yana uvuvio kwa sababu ya huu msingi ulioenezwa kwa kitarakimu. Inaonekana kuwa ni kundi la watu wanaopotoshwa wakiwa hawajijui kwa baadhi ya maandiko ya Agano la Kale kutokana na uandishi wa siku za hivi karibuni katika Israeli nay a Vitabu vya Torati lakini sio waainishaji wakuu wa Agano Jipya uliofanywa hadi sasa. Zaidi ya yote, andiko lililo kwenye Marko yapasa liwe na mlingano uliothibitishwa. Lakini ikiwa kwamba aya hizi kumi na mbili zitakuwa ni sehemu ya Injili halisi na kinyume chake kina ukweli sawia. Vitabu vingine vimeandikwa au kufanywa lakini sio kazi kubwa sana na zenye mamlaka ya kuvihitimisha. Kitabu cha Panin kinajaribu kuonyesha kuwa andiko lote zima limetathiminiwa na limeonyeshwa kuwa linalingana. Kitabu cha Panin kingekuwa na ushawishi zaidi kama maandiko haya yote yangekuwa yamethibitishwa. Inapotokea kutokuwa na kiambishi kinacholingana kikionyeshwa kuwa kipo inaweza tu kupelekea kuonekana kufanya hitimisho kwamba andiko hilo liliandaliwa kwa namna hiyo kwa kusudi la kuweka nyongeza kwenye Injili kwa malengo yaliyoungwa mkono na maandiko yaliyotungwa kwenye aya hizo. Na jambo lenyewe ni wazi sana kwamba linahusu unenaji kwa lugha. Hadi ukamilishaji wa ushahidi kwa hali hii ya mhamasiko kwenye Marko 16:9-20 imeonekana kujitokeza inaweza kudhaniwa tu kwamba aya hizi kumi na mbili za mwisho zinathibitisha ukweli wa kwamba ziliandaliwa mapema wakati fulani kipindi cha mwishoni mwa karne ya kwanza ili kuunga mkono mtindo wa ibada unaohusisha unenaji kwa lugha na ambao hakuna mamlaka ya kibiblia yaliyokuwepo na ambayo yaliaingizwa ili kufifisha mwongozo halisi uliowekwa kusimamia jambo hili, utaratibu au mwongozo uliotolewa na Mtume Paulo. Hivyo basi, aya hizi kumi na mbili za mwisho ndipo zikaongezwa kwenye Injili hii ya Marko, ambazo ni aya za 9-20, ambazo zinafaa zana kuwa zitumiwe kwa tahadhari kubwa na wala zisitumiwe kwa lengo la kuanzisha aina yoyote ya mafundisho. Fundisho kuhusu unenaji kwa lugha kwa kweli limeainishwa wazi sana kwenye uandishi wa kijarida hiki na karama zinazoelezewa zinahusiana tu na masuala ya lugha inayotumiwa tu kwa maelekezo ya waumini wakati lugha inapohitajika ili kuwafundisha na kwa kuwaongoa wasioamini. Matokeo yake ni kuonekana kwa nidhamu na utaratibu wa Roho Mtakatifu kwa nguvu na uweza, kwa heshima na kwa utaratibu.