Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[234]

 

 

 

Bonde la Mifupa Mikavu

 

(Toleo La 1.0 20060927-20060927)

 

Mungu alinena kwa kupitia nabii Ezekieli sura ya 37 akilitaja Bonde lenye Mifupa Mikavu. Hii inajulikana kama Ufufuo wa Wafu. Hata hivyo, ni ufufuo upi basi huu na utafanyika lini na wakati upi, na una maana gani kwa kuuhusianisha na Ufufuo wa Israeli?

 

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

 

(Hatimiliki © 2006 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org


Bonde la Mifupa Mikavu

 


Harakati zilizo kwenye Ezekieli sura ya 37 mara zote zimekuwa zikitafsiriwa kama zinahusiana na tukio la ufufuo wa wafu. Neno lililotumika kwa makaburi kwenye aya ya 12 ni neno la Kiebrania la qeber (kehber, SHD 6913) na sio Sheol. Kuna marudio yaliyoko, yanayochukuliwa na wanazuoni kujumuisha Ufufuo pia na Marejesho mapya, katika nchi ya Israeli (yaani kwenye nchi ya Israeli (Kwa Kiebrania ‘admath) (sawa na kwa mfano wa Bullinger, Comp. Bible, fn. to 37:12).

 

Kuna watu wamelitafsiri andiko hili walihusianisha na Ufufuo wa Pili wa Wafu, wa mwishoni mwa Milenia.

 

U6andikaji wa andiko kwa kuhusianisha na sura zingine za kitabu kunaonyesha kwamba kuna mrejesho wa kijeneriki kwa marejesho mapya ya Israeli ya migawanyo yote miwili, na hatimaye kunajumuisha Ufufuo wa Kwanza wa wafu.

 

Neno la Bwana liliwajia wachungaji wa Israeli kwenye Ezekieli 34. Andiko hili limeainishwa kwa kina kwenye jarida la Upimaji wa Hekalu (Na. 137).

 

Ndipo Mungu aimwambia Ezekieli ayaonye mataifa yanayozunguka Israeli, na kisha awajulishe marejesho mapya ya nchi ya Israeli.

 

Kwenye sura ya 35 Mungu anauonya Mlima Seiri, au taifa la Edomu, ambao ni wana wa Esau.

 

Edomu waliwachukia Israeli na kuwafuatilia kwa nia ya kumwaga damu. Mungu aliamua kuwaadhibu Edomu kwa kuwa walikuwa wanafuatia Israeli kwa kipindi ambacho uovu wao ulikuwa umefikia mwisho (Ezekieli 35:5). Walipigwa na Yuda chini ya uongozi wa John Hyrcanus na wakaingizwa kwenye imani ya kiyahudi. Walijichanganya na watu wa kabila la Yuda huko Yudea, na wafalme wa Yudea wakati wa Warumi walikuwa ni Waedomu au Waidumeani. Herode Mkuu alikuwa ni wa uzao wa Esau. Wakati wa kutawanyika kwao Yuda Waedomu walishirikiana na Wazelote na wakaitwaa Yuda iliyoko Yerusalemu (soma kwenye jarida la Vita Dhidi ya Warumi na Kuangamizwa kwa Hekalu (Na. 298)).

 

Edomu iliamriwa ifanywe kuwa ni maganjo milele na miji yao isirejeshwe, na ndipo wangejua kuwa Bwana ndiye Mungu. Edomu alitafuta jinsi ya kuzipata Baraka za Israeli na Yuda, ingawaje Bwana alikuwepo hapo  (Ezekieli 35:10). Hii ilikuwa ni rejea ya shauku ya Edomu kushindania tena haki ya uzaliwa wa kwanza ambayo Esau aliiuza kwa Yakobo. Bwana alikuwepo hapo kama shahidi, na alikuwa kwenye nchi wakati walipokuwa wanajaribu kuitwaa.

 

Kwahiyo, ilibidi Mungu awahukumu Edomu kwa ajili ya chuki zao na na hasira na kufuru zao. Aliamua kuwaangamiza Edomu. Ahadi yake ilikuwa ni kwamba, wakati nchi yote itakapokuwa ikifurahi, ndipo ataifanya Edomu kuwa maganjo, sehemu zote mbili, yaani kwenye Mlima wa Seiri na huko Idumea.

 

Edomu aliwa kote kuwili, yaani katika Edomu na Yudea na kwenye dola au mataifa yafanyayo biashara ya Wafoenike.

 

Watafanyika maganjo wakati ulimwengu wote ukiwa kwenye furaha. Hivyo basi, hata kwenye kipindi cha marejesho mapya yajayo, watabakia maganjo.

 

Kisha, kwenye sura ya 36, Yahova anamwambia na kumwelekeza Ezekieli ayatamke maneno ya Yahova Adonai.

 

Mataifa walitafuta na kudai wawe na Mahali pa Juu pa kale au vilima vya Israeli, waliyoahidiwa (Mwanzo 49:26; Kumbukumbu la Torati 13:13; 33:15).

 

Kwa kuwa mataifa walikuwa wameimeza Israeli na kuifanya kuwa maganjo kwa pande zake zote, na walifanyika kuwa ni milki ya wamataifa na kuwa matukano na watu wote, Mungu aliamua kuingilia kati. Hili ni jambo lilelile tunaloliona kwenye Kitabu cha Zekaria (soma jarida la Ufafanuzi wa Kitabu cha Zekaria (Na. 021K)).

 

Ndipo hatimaye Mungu aliyaambia mataifa ya wamataifa yaliyoizunguka Israeli, ikiwemo Idumea, na kuwatangazia hukumu yao.

 

Ezekieli 36:1-38

Na wewe, mwanadamu, itabirie milima ya Israeli, useme, Enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Bwana. 2 Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu adui amesema juu yenu, Aha! Na, Mahali pa juu pa zamani pamekuwa petu tupamiliki; 3 basi tabiri useme, Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu, naam, kwa sababu wamewafanya ninyi kuwa ukiwa, na kuwameza pande zote, mpate kuwa milki kwa mabaki ya mataifa, nanyi mmeambwa kwa midomo yao waongeao, na kwa masingizio ya watu; 4 kwa sababu hiyo, enyi milima ya Israeli, lisikieni neno la Bwana MUNGU; Bwana MUNGU aiambia hivi hiyo milima na vilima, mifereji ya maji na mabonde, mahali palipoharibika na kuwa ukiwa, na miji iliyoachwa na watu, ambayo imekuwa mateka, na kuzomewa na mabaki ya mataifa, walio karibu pande zote; 5 basi Bwana MUNGU asema hivi; Hakika kwa moto wa wivu wangu nimenena juu ya mabaki ya mataifa, na juu ya Edomu yote, waliojiandikia nchi yangu kuwa milki yao, kwa furaha ya mioyo yao yote, kwa jeuri ya roho zao, ili waitupe nje kuwa mawindo; 6 basi katika kutabiri habari za nchi ya Israeli, uiambie milima na vilima, mifereji ya maji na mabonde, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nimenena katika wivu wangu na hasira yangu, kwa sababu mmechukua aibu ya mataifa; 7 basi Bwana MUNGU asema hivi; Nimeinua mkono wangu, kusema, Hakika, mataifa walio karibu nanyi pande zote, wao watachukua aibu yao. 8 Lakini ninyi, enyi milima ya Israeli, mtachipuza matawi yenu na kuwapa watu wangu Israeli matunda yenu; maana wa karibu kuja. 9 Maana, tazama, mimi nasimama upande wenu, nami nitawaelekea, nanyi mtalimwa na kupandwa mbegu; 10 nami nitaongeza watu juu yenu, nyumba yote ya Israeli, naam, yote pia; nayo miji itakaliwa na watu, na mahali palipoharibika patajengwa. 11 Nami nitaongeza juu yenu mwanadamu na mnyama, nao watazidi na kuzaa; nami nitawakalisha watu ndani yenu, kwa kadiri ya hali yenu ya kwanza, nami nitawatendea mema kuliko mema ya mianzo yenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.

 

Kisha Mungu akatangaza Baraka zake kwa Israeli. Milima itabarikiwa na wana wa Israeli ndipo watarudi nyumbani mara moja. Hiki ni kipindi cha Nyakati za Mwisho kwenye Ufufuo wa wafu.

 

Ndipo Israeli wataongezeka idadi yao na watoto wao wahatakufa kabisa na Israeli hawataombolezewa tena kabisa. Hiki kitakuwa ni kipindi cha mwishoni cha mauaji ya kutisha ya Holocaust kilichowaua wana wa Israeli.

 
12 Naam, nitaleta watu watembee juu yenu, naam, watu wangu Israeli; nao watakumiliki, nawe utakuwa urithi wao, wala hutawafisha watoto wao tena tangu leo.

 

Kipindi hiki cha amani kitashuhudia Israeli wakiwa hawawauwi tena watu na kupoteza watoto wake.

 

13 Bwana MUNGU asema hivi; Kwa kuwa watu hukuambia, wewe nchi u mwenye kula watu, nawe umekuwa mwenye kufisha watu wa taifa lako; 14 basi hutakula watu tena, wala hutafisha watu wa taifa lako tena, asema Bwana MUNGU; 15 wala sitakusikizisha tena aibu yao wasioamini, wala hutachukua matukano ya watu tena; wala hutalikwaza taifa lako tena, asema Bwana MUNGU.

 

Kwa hiyo Waisraeli hawatakuwa wakilaumiwa tena na mataifa, kama ilivyo sasa, na makuhani wake hawatawasababishia kujikwaa kwa kuwakosesha au kuwapotosha.

 

Israeli waliadhibiwa kwa ukengeufu wao wakati walipokuwa wakiishi kwenye nchi yao wenyewe, na walifukuzwa na kupelekwa nchi ya mbali kwa sababu ya ukenngeufu wao huo na kwaajili ya kuabudu sanamu kwao. Walitawanya kwenye mataifa mbalimbali kwa sababu ya mapokeo na desturi hizihizi ambazo Masihi aliwakemeanazo sana, na mbazo walimuua kwazo. Walifukuzwa na kuadhibiwa kwa mwenendo wao na matendo yao. Mwenendo na matendo ya watu wa Yuda, tangu hapo, hadi kufikia hivi karibuni, yalikuwa yasiyostahili kuwahurumia kabisa kama tunavyojionea kwenye jarida la Vita Dhidi ya Warumi na Kuangamizwa kwa Hekalu (Na. 298).

 

16 Tena, neno la Bwana likanijia, kusema, 17 Mwanadamu, nyumba ya Israeli walipokaa katika nchi yao wenyewe, waliitia uchafu kwa njia yao na kwa matendo yao. Njia yao mbele zangu ilikuwa kama uchafu wa mwanamke wakati wa kutengwa kwake. 18 Kwa hiyo nalimwaga hasira yangu juu yao, kwa ajili ya damu waliyoimwaga juu ya nchi, na kwa sababu wameitia uchafu kwa vinyago vyao. 19 Nikawatawanya katika mataifa, wakatapanyika katika nchi nyingi; kwa kadiri ya njia yao, na kwa kadiri ya matendo yao, naliwahukumu. 20 Nao walipoyafikilia mataifa yale waliyoyaendea, walilitia unajisi jina langu takatifu; kwa kuwa watu waliwanena, wakisema, Watu hawa ni watu wa Bwana, nao wametoka katika nchi yake. 21 Lakini, naliwahurumia kwa ajili ya jina langu takatifu, ambalo nyumba ya Israeli walikuwa wamelitia unajisi katika mataifa waliyoyaendea.

 

Mungu aliamua kuifanya upya Israeli, siyo kwa faida yao, na licha ya mafundisho yao ya kizushi na mapokeo yao mapotofu. Aliwarejesha na kuwafanya wapya tena kwa ajili ya Jina Lake Takatifu, ambalo walilisababishia litukanwe na wengine kulikufuru kati ya mataifa. Wakati huo ni sasa, ni juu yetu tu.

 

Israeli inafanywa upya kabla ya kipindi chake cha kuongoka. Marejesho haya yatakuwa makubwa sana kutokana na matendo ya Efraimu kuanzia mwaka 1916.


22 Kwa hiyo; waambieni nyumba ya Israeli, Bwana MUNGU asema hivi Sitendi hili kwa ajili yenu, Ee nyumba ya Israeli, bali kwa ajili ya jina langu takatifu, mlilolitia unajisi katika mataifa mliyoyaendea. 23 Nami nitalitakasa jina langu kuu, lililotiwa unajisi katika mataifa, mlilolitia unajisi kati yao; nao mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, asema Bwana MUNGU, nitakapotakaswa kati yenu mbele ya macho yao. 24 Maana nitawatwaa kati ya mataifa, nami nitawakusanya na kuwatoa katika nchi zote, na kuwarudisha katika nchi yenu wenyewe.

Mkutaniko huo unachukua mkondo wake sasa na utaendelea kwa kipindi fulani kifupi kijacho.

 

Kisha ndipo watatakasika, watapewa moyo wa toba na wataongoka kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

 

25 Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; nitawatakaseni na uchafu wenu wote, na vinyago vyenu vyote. 26 Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama. 27 Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda. 28 Nanyi mtakaa katika nchi ile niliyowapa baba zenu, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.

 

*Kumbuka: tafsiri ya Knox inasema kwenye aya ya 25: “Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; ….”

 

Kumbuka kuwa mchakato wa wongofu utajumuisha na Israeli kuenenda na Amri na Sheria za Mungu, kama alivyozitoa kwa Kristo, na kwa Musa pale Sinai. Utii huu ni wa kama ulivyo kwenye Ufunuo 12:17 na 14:12.

 

Mungu atawatakasa na kuifanya milima iwamwagie kwa uwingi wao. Hawataweza kukumbwa tena na baa la njaa. Kwa jinsi hiyo watayakumbuka maovu yao na dhambi zao.


29 Nami nitawaokoeni na uchafu wenu wote; nitaiita ngano, na kuiongeza, wala sitaweka njaa juu yenu tena. 30 Nami nitazidisha matunda ya miti, na mazao ya mashamba, msipate tena kutukanwa na mataifa kwa sababu ya njaa. 31 Ndipo mtazikumbuka njia zenu mbaya, na matendo yenu yasiyokuwa mema, nanyi mtajichukia nafsi zenu kwa macho yenu, kwa sababu ya maovu yenu na machukizo yenu.

 

Mungu anasema hafanyi mambo yake kwa faida ya Israeli, bali ni kwa kuwathibitishia, na kuaaibisha.

 

32 Ijulikane kwenu ya kuwa silitendi neno hili kwa ajili yenu, asema Bwana MUNGU; tahayarikeni, na kufadhaika, kwa sababu ya njia zenu, Enyi nyumba ya Israeli. 33 Bwana MUNGU asema hivi; Siku ile nitakapowatakaseni na maovu yenu yote, nitaifanya miji ikaliwe na watu, na palipobomolewa pajengwe tena. 34 Nchi iliyokuwa ukiwa italimwa, ijapokuwa ilikuwa ukiwa mbele ya macho ya watu wote waliopita. 35 Nao watasema, Nchi hii, iliyokuwa ukiwa, imekuwa kama bustani ya Adeni; nayo miji iliyokuwa mahame, na ukiwa, na magofu, sasa ina maboma, inakaliwa na watu. 36 Ndipo mataifa, waliobaki karibu yenu pande zote, watajua ya kuwa mimi, Bwana, nimejenga mahali palipoharibika, nami nimepanda mbegu katika nchi iliyokuwa ukiwa; mimi, Bwana, nimesema hayo; tena nitayatenda. 37 Bwana MUNGU asema hivi, Tena kwa ajili ya jambo hili nitaulizwa na nyumba ya Israeli, ili niwatendee; nami nitawaongeza kwa watu kama kundi la kondoo. 38 Kama kundi lililo tayari kutolewa sadaka, kama kundi la Yerusalemu katika sikukuu zake zilizoamriwa; ndivyo itakavyojazwa watu, miji ile iliyokuwa maganjo; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.

 

Ndipo taifa hili litajua na kuelewa kuwa Mungu ndiye aliyefanya hivyo. Miji iliyosalia itafurika watu kama kundi la wanyama wa kutolewa dhabihu kama huko Yerusalemu. Watu hawa watawekwa wakfu na Mungu kwa Roho Mtakatifu. Watayaacha mapokeo na desturi zao kama makapi machafu, na kurudi na kugeuza mioyo yao na kubatizwa na kuongoka.

 

Awamu inayofuatia ya Marejesho ni ile ya ufufuo wa wafu atakaporudi Masihi.

 

Ufufuo

Sehemu hii inaelezea Mifupa Mikavu (aya ya 1-14) na fimbo mbili (aya ya 15-28) kwenye Ezekieli 37.

 

Unabii kuhusu mifupa mikavu ikifuatiwa kama mkururo ufuatao:

  1. Maono yaliyofunuliwa (aya ya 1,2).
  2. Swali na jibu la nabii (aya ya 3).
  3. Amri ya kuitabiria mifupa (aya ya 4) (Kwa Kiebrania ‘al).
  4. Maneno ya unabii (aya ya 5,6).
  5. Utii wa nabii (aya ya7).
  6. Matokeo (aya ya 7-8).

 

Kisha sehemu ya mwisho inarudia kutoka 3:

  1. Amri ya kutabiria (‘el) Roho; yaani, Mungu anauelekeza uweza na nguvu zake kwa wakati muafaka (aya ya 9).
  2. Maneno ya unabii (aya ya 9).
  3. Utii wa nabii (aya ya 10).
  4. Matokeo (aya ya10).

 

Kisha maono yanafafanuliwa (aya ya 11).

 

Swali na jibu la Yahova ndipo vinatokea (aya ya 12-14).

 

Sasa Bwana ananena kwa Roho Mtakatifu (soma pia 1:1,3; 8:3; 11:24-25; 40:2-3). Maelekezo kwenye maandiko haya yanaonyesha maana ya Ufunuo 1:10 (soma pia kitabu cha Bullinger, andiko la Companion Bible hadi aya ya 1).

 

Ezekieli 37:1-28

Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanichukua nje katika roho ya Bwana, akaniweka chini, katikati ya bonde; nalo limejaa mifupa; 2 akanipitisha karibu nayo pande zote; na tazama, palikuwa na mifupa mingi katika ule uwanda! Nayo, tazama, ilikuwa mikavu sana. 3 Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe. 4 Akaniambia tena, Toa unabii juu ya mifupa hii, uiambie, Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Bwana. 5 Bwana MUNGU aiambia mifupa hii maneno haya; Tazama, nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi. 6 Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na kuwafunika ngozi, na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. 7 Basi nikatoa unabii kama nilivyoamriwa; hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu; na tazama, tetemeko la nchi, na ile mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe. 8 Nikatazama, kumbe! Kulikuwa na mishipa juu yake, nyama ikatokea juu yake, ngozi ikaifunika juu yake; lakini haikuwamo pumzi ndani yake. 9 Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa, wapate kuishi. 10 Basi nikatabiri kama alivyoniamuru; pumzi ikawaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno.

 

Neno linalotaja mauaji hayo ya kuchinja ya wanaomtumikia Mungu. Wanakuwa wamekufa, kwa vifo vya machafuko. Tafsiri ya Septuagint inalitaja jambo hili kuwa ni tous nekrous, ambayo ni tofauti na neno nekrous pasipo makala, inayowataja wale waliokuwa wazima hapo mwanzoni. Lakini kwa jinsi hii, pamoja na makala, inaitaja mizoga. Bullinger anaweka tofauti (kwenye hitimisho la aya ya 9). Linganisha andiko hili na kile alichokuwa anakisema Kristo kwenye Mathayo 22:31-32 na Luka 24:5 (ni sawa pia na 1Wakorintho 15:29, 35, 42, 52).

 

Andiko hili linautaja Ufufuo wa Kwanza wa wafu na mahali pake kwenye maongozi, na pia marejesho mapya ya Israeli kwa namna fulani za kimiujiza.

 

Huu ni mwisho wa maono yaliyoonyeshwa na mkururo wa kwanza. Watu hawa ni watiifu walio kwenye Nyumba ya Israeli.

 

Maono haya yanafafanuliwa sasa.

 

Matumizi ya neno “nyumba yote” yanaonyesha pia kulitaja Kanisa, ambalo ni shamba la mizabibu la Bwana pia, likiwa kama Israeli ya kiroho.


11 Kisha akaniambia, Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli; tazama, wao husema, Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yametupotea; tumekatiliwa mbali kabisa.

 

Wanaona kuwa wamekatiliwa mbali lakini sivyo, na utambulisho wao na mistari yao ya kiuzawa yapasa irejeshwe.


12 Basi tabiri, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitafunua makaburi yenu, na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli. 13 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu, enyi watu wangu.

 

Tendo hili la kimiujiza linahusu ufufuo sawasawa na uumbwaji wa Adamu. Huu ni ufufuo sawa na lile la Lazaro na la mteule wakati wa Masihi, wakati wale waliokuja kutoka makaburini waliishi tena na wakafa kwa kifo cha asili, au waliuawa.

 

Mkururo unaofuatia ahadi za Yahova ili:

  1. Kutangaza tendo (aya ya 12).
  2. Ahadi ya ufufuo (aya ya 12).
  3. Ahadi ya kuwafanya tena upya Israeli (aya ya 12).
  4. Umuhimu na matokeo ya kumjua Bwana (aya ya 13).

 

Kisha inakuja ahadi ya kumjua ikifuatiwa kutoka kwenye kitendo.

  1. Wakati nilipoyafungua makaburi yenu (aya ya 13).
  2. Na nilikuweka kwenye nchi yako mwenyewe (aya ya 14).
  3. Ndipo watajua (aya ya 14).
  4. Anamtangaza Bwana Mungu (aya ya 14).


14 Nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi, nami nitawawekeni katika nchi yenu, nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, nimesema hayo, na kuyatimiza, asema Bwana.

 

Hapa ufufuo unahusisha na kumuweka Roho Mtakatifu katika Israeli. Hivyo, ndivyo wongofu wa Israeli, pande mbili zote, yaani Yuda na Efraimu, inayoongelewa hapa. Sasa tunajionea hiyo ikielezewa.

 

Hili pia ni tukio la Kutoka lililotabiriwa na nabii Isaya (Isaya 66:18-24).

 

Fimbo Mbili

Fimbo mbili zimechukuliwa kuwakilisha mataifa mawili ya Yuda (na sehemu ya kabila la Benyamini na kabila la Lawi) na Efraimu na makabila kumi yanayojumuikanayo. Pande hizi mbili zitaungana pamoja tena baada ya umoja wao kuvunjika kama tulivyoona kwenye unabii wa Uzuri na Vifungo (soma jarida la Ufafanuzi wa Kitabu cha Zekaria (Na. 021K)).

 

15 Neno la Bwana likanijia tena, kusema, 16 Na wewe mwanadamu, twaa kijiti kimoja; ukaandike juu yake, Kwa Yuda, na kwa wana wa Israeli wenzake; kisha, twaa kijiti cha pili; ukaandike juu yake, Kwa Yusufu, kijiti cha Efraimu, na kwa nyumba yote ya Israeli wenzake; 17 ukaviunge pamoja kwa ajili yako hiki na hiki viwe kijiti kimoja, viwe kimoja katika mkono wako. 18 Na wana wa watu wangu watakapokuambia, wakisema, Je! Hutatuonyesha maana ya mambo hayo utendayo? 19 Waambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitakitwaa kijiti cha Yusufu, kilicho mkononi mwa Efraimu, na kabila za Israeli wenzake, nami nitawaweka pamoja nacho, yaani, pamoja na kijiti cha Yuda, na kuvifanya kuwa kijiti kimoja; navyo vitakuwa kimoja mkononi mwangu. 20 Navyo vijiti, ambavyo uliandika juu yake, vitakuwa mkononi mwako mbele ya macho yao.


Kwahiyo, yataunganika na kujumuika kwa kauli na nia moja, na watachukuliwa na kutolewa kutoka nchi na mataifa yote ya dunia ambako wametawanyikia kwayo.

 

21 Ukawaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nitawatwaa wana wa Israeli toka kati ya mataifa walikokwenda, nami nitawakusanya pande zote, na kuwaleta katika nchi yao wenyewe; 22 nami nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi hiyo, juu ya milima ya Israeli; na mfalme mmoja atakuwa mfalme wao wote; wala hawatakuwa tena mataifa mawili, wala hawatagawanyikana kuwa falme mbili tena, hata milele.


Kwa hiyo, ndipo watafanyika kuwa taifa moja na ufalme mmoja na kuwa chini ya mamlaka moja. Muungano huu utafanyika katika Nyakati za Mwisho atakapokuja Masihi.

 

Kisha ndipo watajitakasa kutokana na ibada zao za sanamu, mapokeo na desturi zao na imani zao potofu za kisirisiri.

 

23 Wala hawatajitia uchafu tena kwa vinyago vyao, wala kwa vitu vyao vichukizavyo, wala kwa makosa yao mojawapo; lakini nitawaokoa, na kuwatoa katika makao yao yote, ambayo wamefanya dhambi ndani yake, nami nitawatakasa; basi watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.


Daudi atakuwa mfalme akiwatawala.

 

Na kama Daudi alivyo kwamba amekufa kwa kipindi cha takriban milenia tatu, basi ni dhahiri sana kwamba tunachokiongelea hapa ni ufufuo wa wafu na Masihi, mwana wa Daudi. Chini ya Kristo, watafuata sheria za Torati ya Mungu kama zilivyotolewa kwa Israeli.

24 Na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mfalme juu yao, nao wote watakuwa na mchungaji mmoja; nao wataenenda katika hukumu zangu, na kuzishika amri zangu, na kuzitenda. 25 Nao watakaa katika nchi niliyompa Yakobo, mtumishi wangu, walimokaa baba zenu; nao watakaa humo, wao na watoto wao, na watoto wa watoto wao, milele; na Daudi, mtumishi wangu, atakuwa mkuu wao milele.


Daudi atafufuliwa, na Masihi atakuwa Bwana wao, na wateule watakuwa watu wa nyumbani mwa Daudi kama elohim (soma Zekaria 12:8; pia soma kwenye jarida la
Wateule Kama Elohim (Na. 1)).

 

Ndipo itapasa agano lirudiwe na kuwekwa upya milele. Yahova wa Israeli atakuwa pamoja nao, na Yahova wa Majeshi atakuwa hapo kwa Roho wake Mtakatifu, na Hekalu litakuwa ni wateule wenyewe, na Hekalu la Kimwili la Jengo litakuwa ni mfano wa Hekalu la Kiroho, Hekalu ambalo ni sisi.

 

26 Tena nitafanya agano la amani pamoja nao; litakuwa agano la milele pamoja nao; nami nitawaweka na kuwazidisha, na patakatifu pangu nitapaweka katikati yao milele. 27 Tena maskani yangu itakuwa pamoja nao; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 28 Na mataifa watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, mimi niwatakasaye Israeli, patakatifu pangu patakapokuwa katikati yao milele.

 

Mataifa watakuja kwenye Nchi Takatifu mwaka hadi mwaka ili kumwabudu Bwana wa Majeshi, na watajua kwamba Mungu yupo pale katikati yao milele na milele.

 

Kisha, wakati Bwana anapoanza kuifufua tena Israeli, na atakaporudi Masihi na mkutaniko wa wateule, vita ya Milenia vitatokea.

 

Hadithi iliyo kwenye Ezekieli sura ya 38 na 39 inaelezea vita hivi, ambayo ni vita ya Hamon-Gogu (soma jarida la Vita Vya Hamon-Gogu (Na. 294)).

 

Ezekieli 39:25 inaonyesha kwamba vita vitakavyoanza kabla ya kuanza rasmi kwa Milenia na kuukomesha kabisa utumwa wa Yakobo chini ya Mungu, kama Nyumba nzima yote Israeli kwenye Nchi Takatifu. Hawa watu wa Nyumba Yote ya Israeli wanawakilisha pia wateule. Kwa hiyo Mungu ataitumia vita hii ili kuwaunganisha na kuwafanya Israeli kuwa ni Taifa Lake Takatifu.

 

Ezekieli 38:1-16

Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, kaza uso wako, umwelekee Gogu, wa nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki, na Tubali, ukatabiri juu yake, 3 useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ewe Gogu, mkuu wa Roshi, na Mesheki, na Tubali; 4 nami nitakugeuza na kutia kulabu katika mataya yako, nami nitakutoa, pamoja na jeshi lako lote, farasi na hao wapandao farasi, wote wamevaa silaha za namna zote, jeshi kubwa sana, wenye ngao na kigao, wote wakishika upanga; 5 Uajemi, na Kushi, na Putu, pamoja nao; wote wana ngao na chapeo; 6 Gomeri, na vikosi vyake vyote; nyumba ya Togarma, pande za mwisho za kaskazini, na vikosi vyake vyote; naam, watu wengi pamoja nawe. 7 Ujiweke tayari, naam, jiweke tayari, wewe na majeshi yako yote waliokukusanyikia, nawe uwe jemadari wao. 8 Na baada ya siku nyingi utajiliwa; katika miaka ya mwisho, utaingia nchi iliyorudishiwa hali yake ya kwanza, baada ya kupigwa kwa upanga, iliyokusanywa toka kabila nyingi za watu, juu ya milima ya Israeli, iliyokuwa ukiwa wa daima; lakini imetolewa katika kabila za watu, nao watakaa salama salimini wote pia. 9 Nawe utapaa juu, utakuja kama tufani, utakuwa kama wingu kuifunika nchi, wewe, na vikosi vyako vyote, na kabila nyingi za watu pamoja nawe.


Israeli inajenga miji, na mataifa ya kaskazini wanaijia juu kinyume chake. Utambulisho wa mataifa haya umefafanuliwa kwenye jarida la
Vita ya Hamon-Gogu (Na. 294) na itatanda pande mbili zote mbili za mgogoro. Pande mbili zote zitatiishwa, kama tutakavyojionea kwenye jarida la hilo.

 

10 Bwana MUNGU asema hivi; Itakuwa katika siku hiyo, mawazo yataingia moyoni mwako, nawe utakusudia kusudi baya; 11 nawe utasema, Nitapanda juu niiendee nchi yenye vijiji visivyo na maboma; nitawaendea watu wanaostarehe, wanaokaa salama, wote wakikaa pasipo kuta, ambao hawana makomeo wala malango; 12 ili kuteka mateka, na kuwinda mawindo; uugeuze mkono wako juu ya mahali palipoharibika, ambapo sasa panakaliwa na watu, na juu ya watu waliokusanyika toka mataifa, waliopata ng'ombe na mali, wakaao katikati ya dunia. 13 Sheba, na Dedani, na wafanya biashara wa Tarshishi, pamoja na wana-simba wake wote, watakuambia, Je! Umekuja kuteka mateka? Umekusanya jeshi lako, ili kuwinda mawindo? Kuchukua fedha na dhahabu, kuchukua ng'ombe na mali, kuteka mateka mengi sana? 14 Basi, mwanadamu, tabiri, umwambie Gogu, Bwana MUNGU asema hivi; Katika siku ile watu wangu, Israeli, watakapokaa salama, hutapata habari? 15 Nawe utakuja kutoka mahali pako, kutoka pande za mwisho za kaskazini, wewe, na watu wa kabila nyingi pamoja nawe, wote wamepanda farasi, kusanyiko kubwa, na jeshi kuu; 16 nawe utapanda juu uwajilie watu wangu, Israeli, kama wingu kuifunika nchi; itakuwa katika siku za mwisho, nitakuleta upigane na nchi yangu, ili mataifa wanijue, nitakapotakaswa kwako, Ewe Gogu, mbele ya macho yao.

 

Vita Kuu ya Hamon-Gogu itatokea mwanzoni mwa Milenia. Hata hivyo, tunajua pia kutokana na Ufunuo sura ya 20 kwamba vita kubwa itatokea mwishoni mwa Milenia pia, kabla ya Ufufuo (wa Pili) wa wafu Wote. Ufunuo sura ya 20 inafafanua Ezekieli sura za 36-39. Ezekieli sura za 40-41 zinaonyesha mfumo wa Hekalu kwamba utakuwepo na kwamba litajengwa kipindi hiki cha Milenia.

 

Ufunuo 20:1-15

Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu; 3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache.

 

Marejesho haya yataanzia kwa kufungwa kifungoni kwa Shetani atakaporudi Masihi. Wateule watakuwa wamefufuka na kuhukumiwa hukumu ya watakatifu. Huu ni mwanzo wa marejesho mapema kabla ya utawala wa millennia.


4 Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu. 5 Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. 6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu.

 

Kwa hiyo, utawala wa millennia wa watakatifu utakuwa ni mwanzo wa kipindi hiki cha Milenia. Hayo ni marejesho na kuifanya upya Israeli, yaliyoitwa kuwa ni utumwa wa Yakobo. Kristo atarudi ili kuwachukua watumwa utumwani.

 

Shetani atafunguliwa tena kwa ajili ya vita ya mwisho mwishoni mwa kipindi hiki cha Milenia.

 

7 Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; 8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari. 9 Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala. 10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.

 

Kwa hiyo, Vita ya Gogu na Magogu ni vita endelevu na inaendelea, kwa nyakati zote mbili, yaani wakati wa utawala wa Shetani na tena atakapofunguliwa Shetani. Maafa yatakayowakumba Shetani na Mnyama, na nabii wa uwongo, na kifo cha nadharia au dhana ya mwisho wa miaka elfu saba ya mfumo na imani za kidunia zilizopo leo hapa duniani. Ufufuo wa wote hauhusiani na mataifa na imani au mifumo na mambo kama hayo. Utahusika na hukumu na kuwarudi watu kwa kipindi kifupi maalumu kilishofupishwa na kinaitwa cha Hukumu ya kwenye Kiti cha Enzi, Kikubwa Cheupe. Soma jarida la Ufufuo wa Pili wa Wafu na Kiti cha Enzi, Kikubwa Cheupe cha Hukumu (Na. 143B).

 

11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.

 

Makanisa ya Mungu katika karne ya 20 yalifanya makosa makubwa kwa kutenganisha matukio yaliyo kwenye aya ya 12 na 13, na kufundisha kuwa kuna Ufufuo wa Tatu kwa lengo la kuwathibiti na kuwatawala waumini wao kwa kuwatia hofu (soma jarida la Uwongo Potoshi Kuhusu Ufufuo wa Tatu (Na. 166)). Hata hivyo, ni dhahiri sana kutokana na mashiko ya kimaandiko kwamba aya ya 13 inaongelea tu kuhusu wale waliokufa baharini kuwa nao watafufuliwa ili wahukumiwe pamoja na wale waliokufa katika nchi au ardhi ya kawaida. Wale wasiotubu mwishoni mwa kipindi hiki watakataliwa kwenye uzima wa milele na watakufa, na watachomwa kama takataka kwenye moto wa Jehanamu, jina linalotokana na shimo la jalala la kutupiwa takataka lililokuwa nje ya mji wa Yerusalemu.

 

13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.

 

Kwa hiyo, Ezekieli hapa anaongelea juu ya ufufuo wa aina mbili zote, yaani wa mwanzoni mwa Milenia wa marejesho mapya na wa mwishoni. Vita vitatangulia marejesho yatakayoenda kwa wakati wote wa Milenia. Marejesho yatakayofanywa kwenye vita yameandaliwa na kukusudiwa kuianzisha yumba ya Mungu yenye utukufu milele.

Ezekieli 38:17-23

17 Bwana MUNGU asema hivi; Je! Wewe ndiwe niliyemnena zamani za kale, kwa vinywa vya watumishi wangu, manabii wa Israeli, waliotabiri siku zile kwa muda wa miaka mingi, ya kwamba nitakuleta upigane nao? 18 Itakuwa katika siku hiyo, Gogu atakapokuja kupigana na nchi ya Israeli, asema Bwana MUNGU, ghadhabu yangu itapanda katika mianzi ya pua yangu. 19 Kwa maana katika wivu wangu, na katika moto wa ghadhabu yangu, nimenena, Hakika katika siku ile kutakuwako tetemeko kubwa katika nchi ya Israeli; 20 hata samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama wa kondeni, na vitu vyote vitambaavyo juu ya nchi, na wanadamu wote walio juu ya uso wa nchi, watatetemeka mbele ya uso wangu; nayo milima itatupwa chini, na magenge yataanguka, na kila ukuta utaanguka chini. 21 Nami nitaita upanga, uje juu yake katika milima yangu yote, asema Bwana MUNGU; nao upanga wa kila mtu utakuwa juu ya ndugu yake. 22 Nami nitamhukumu kwa tauni, na kwa damu; nami nitanyesha mvua ifurikayo, na mvua ya mawe makubwa sana, na moto na kiberiti juu yake, na vikosi vyake, na watu wa kabila nyingi walio pamoja naye. 23 Nami nitajitukuza, na kujitakasa, na kujidhihirisha, mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.

 

Utawala wa millennia ndipo utaanza na mataifa yatajinyenyekesha na kutii maelekezo na sheria na amri za Mungu na yataandaliwa kwa ajili ya Ufufuo wa Pili wa Wafu Wote, utakaotanguliwa na vita ya mwisho ya Gogu na Magogu.

 

Mwisho wa matokeo ya mchakato huu ni ujio wa Mji wa Mungu (soma jarida la Mji wa Mungu (Na. 180)).

q