Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[121]

 

 

 

 

Mika 5:2-3

(Toleo La 1.1 19950624-19991009)

 

Jinsi andiko wanavyolitumia Wabinitarian kumeainishwa na kuonyeshwa kuwa siyo sahihi kabisa. Maelekezo ya uzushi wa guvu za namna Mbili yameonekana kuwa ni uwongo. Jarida hili linaelezea kuhusu ulio kwenye andiko hili na jinsi yanavyohusiana na Masihi na uhusiano wake na Mungu.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki © 1995, 1999 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


 

Mika 5:2-3

 

 


Tunajua kwamba maandiko ya Mika 5:2-3 yamekarabatiwa kimakosa na watumishi au wahubiri wa Kibinitarian ili kuhalalisha imani yao ya Kibinitarian au mafundisho ya kizushi ya Nguvu Kuwili kama ilivyokuwa imejulikana hapo zamani. Ni kubisha kwamba kuna Miungu miwili idumuyo milele huko mbinguni, ikiwa kwamba ama kuna miungu miwili waishio milele ama la wanaodaiwa kuwa hivyo kwenye imani ya Kiutatu au Utrinitarian. Mafundisho haya ya kizushi kimsingi yanapinga au kushuku uweza wa kuwa na nguvu zote alionao Mungu na yanajaribu kupingana na maandiko yaliyo kwenye Yohana 17:3 na 1Yohana 5:20 yanayoelezea na kusisitiza kwamba kuna Mungu mmoja tu, wa Pekee na wa Kweli, na kwamba Yesu Kristo ni Mwanae wa pekee.

Yohana 17:3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.

 

1Yohana 5:20 Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele.

Andiko hili limetafsiriwa ili kufanya ionekane kwamba neno Mungu wa Kweli, na uzima wa milele huenda lilikuwa linamlenga Kristo, jambo ambalo sivyo. Zaidi sana ni kwamba vitabu cha Ufafanuzi vya Douay-Reims Bible (yaani, Heydock) vinajaribu kuonyesha kwamba makala yenyewe halisi, inatumika hapa kumtaja Mungu wa Pekee na wa Kweli, ikimkusudia Kristo, hambo ambalo sivyo kabisa.

 

Mungu wa Kweli, ndiye Mungu wa Pekee na wa Kweli na siyo Yesu Kristo aliyemtuma. Hakuna mtu aliyewahi kumuona yeye, Mungu, na wala atakayeweza kumuona (Yohana 1:18). Ni yeye tu, peke yake ndiye hafi wala kupatwa ma madhara. Anaonekana tu katika Roho.

1Timotheo 6:13-16 Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato, 14 kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo; 15 ambako yeye kwa majira yake atakudhihirisha, yeye aliyehimidiwa, Mwenye uweza peke yake, Mfalme wa wafalme, Bwana wa mabwana; 16 ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.

 

Ikumbukwe hapa kwamba ni Mungu ndiye atoaye uzima kwa viumbe na vitu vyote. Yeye ni mbarikiwa na ni Mtukufu, Mfalme wa Wafalme na Bwana wa Mabwana. Ni yeye peke yake ndiye hafi wala kupatwa na madhara. Kwa hiyo, ni yeye pekee ndiye atoaye uzima kwa viumbe vyote. Na ni yeye peke yake ndiye aliyempa uzima hata Kristo.

 

Kuendelea kudai kwamba Kristo ana umilele sawa na Mungu kunapingana na ni kama kunashambulia moyo au kiini cha utukufu wa kipekee wa Mungu Mmoja, wa Pekee na wa Kweli na ni kitendo na tabia ya waabudu na waamini miungu mingi. Kristo alipaa mbinguni ili afanyike kuwa Mwana wa Mungu mwenye uweza kutokana na kufufuka kwake kutoka kwa wafu (Warumi 1:4). Madai ya kwamba nabii Mika anauelezea umilele wa Kristo pia, yanatafuta kupinga andiko lililo kwenye 1Timotheo 6:16 linaloonyesha kwamba ni Mungu tu peke yake ndiye hafi wala kupatwa na madhara. Madai haya yanatokana na hali ya kutafsiri na kuyaelezea vibaya na kimakosa Maandiko Matakatifu.

 

Hebu na tulipitie andiko lenewe lisemavyo.

Mika 5:2-3 Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele. 3 Kwa sababu hiyo atawatoa, hata wakati wa kuzaa kwake aliye na utungu; ndipo hayo mabaki ya nduguze watawarudia wana wa Israeli.

Madai haya yanatuama kwenye maandiko yaliyo kwenye tafsiri ya KJV ambayo inaaminiwa au kuchukuliwa kwamba inajaribu kuyafanya madai haya yawezekane na kukubalika.

Mika 5:2-3  Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele. 3 Kwa sababu hiyo atawatoa, hata wakati wa kuzaa kwake aliye na utungu; ndipo hayo mabaki ya nduguze watawarudia wana wa Israeli.

Andiko lililotafsiriwa hapa kuwa kama ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale milele na milele.

 

Tafsiri ya RSV imeandikwa andiko hili kuwa ni Ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale. Kwa hiyo, uingizaji wa maneno yanayokusudia kumaanisha umilele yanatokana na marekebisho yaliyo kwnye tafsiri ya KJV yasemayo umilele ambayo kwa jinsi yalivyo tu yenyewe kuwa marekebisho yaliyofanyizwa kwa upotoshaji kutokana na lugha ya Kingereza.

Andiko hili limetafsiriwa kwenye Biblia tafsiri ijulikanayo kama Interlinear Bible kama

Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.

Kutoka kwenye siku za umilele imetafsiriwa kwa maneno mawili ya Kiebrania. Neno la kwanza ni miymy (*/*/) linalotokana na kamusi ya SHD 3117 yowm (.&*) linalomaanisha siku (hizo), tangu mawio ya jua hadi mawio yanayofuatia, likiwa linatokana na maana ya chimbuko lisilotumika kuwa moto. Neno la pili kwa mujibu wa kamusi ya SHD 5769 ni ‘owlawm (.-&3) ambalo maana yake yamefutwa au kuondolewa, au kwenye kiwango cha kuondolewa. Inamaanisha kipindi au mda ulio nje ya mawazo au umilele unaojulikana (kamusi ya Strongs) ambqacho mara zote, au kutoka nyakati za kale, nk. Andiko halina jinsi ya kukanushwa kuwa linakusudia kuutaja umilele wa kiumbe ambaye aliyeumbwa na kuwa msaidizi wa Mungu wa Pekee wa Kweli. Masihi anaweza kuchukuliwa kutokana na andiko hili kuwa amewahi tu kuwa alikuwepo kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi hapa duniani, nyakati za kale. Halimaanishi kufundisha kuwa ana umilele sawa na Mungu. Kwa kweli, kutokana na andiko hili tunaweza kuona kwamba Kristo anatoaka kwa Mungu na ametumwa naye, hivyo hawezi kuwa sawa naye. Kudai kwamba kiumbe huyu amukuwepo milele sawa na alivyo Mungu wa Pekee wa Kweli kunamuondolea hadhi ya uweza wake (Mungu) usioshindwa na nguvu nyingine yoyite.

 

Tafsiri ya Soncino imetafsiri andiko hili la Mika 5:1[2] kama Ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale,

Na kulitafsiri andiko hili kuwa:

Matokeo yakeyamekuwa, yaani .mstari.

Tangu zamani za kale. Inawezekana kwamba kufungu hiki kilesababisha kuinuka kwa mafundisho ya Kiyahudi yasemayo kwamba Masihi alikuwepo kwenye mawazo ya Mungu tangu wakati mwingi usioweza kutajika, akiwa kama sehemu ya mpango wa Muumba kwenye ubunifu wa jinsi utakavyokuwa ulimwengu. Kwenye tafsiri ya Talmud, jina la Masihi ni miongoni mwa mambo saba yaliyokuwepo au kubuniwa kabla ya ulimwengu haujaanza kukaliwa na kiumbe chochote.

 

Ni Mungu pekee ndiye anayeishi na kudumu milele

Isaya 57:15 15 Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu; tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea, ili kuzifufua roho za wanyenyekevu, na kuifufua mioyo yao waliotubu.

 

Neno hili umilele limeandikwa kwenye kamusi ya SHD 5703 kama ‘ad ($3) ambalo linamaanisha dhana ya kitu kisicho mwisho na likimaanisha kipindi endelevu au cha kudumu kwa maana ya umilele, ambavyo ni milele au kudumu (milele). Dhana hii ni kama tunavyoona ilienea kwa roho zote zenye toba na zilizo na unyofu ili kufufua moyo wa unyenyekevu na toba. Kwa hiyo, uwezo huu wa kuishi au kudumu milele ni mkanganyiko uliuowekezwa tu kwa kila mmoja ili kuwezekane kuwa na wokovu wa kila mmoja. Neno ‘owlawm linatumika kwa kanuni za kawaida za kimwili pia, ambazo tunazijua kuwa si vitu vya kiroho milele. Neno umilele wa agano la milele linalitajwa kwenye Mwanzo 9:16; 17:7-8,13,19 linatumika pia kwa Mungu wa Milele kwenye Mwanzo 21:33.

Mwanzo 21:33 Ibrahimu akapanda mkwaju huko Beer-sheba, akaliitia huko jina la Bwana Mungu wa milele.

 

Bado tunajua kwamba hakuna bado wala hakuna mwenye mwili wala ardhi iliyo ya kudumu milele, iwe tangu mwanza au kwa wakati mwingine wowote. Hivyo basi, matumizi ya neno hayaashirii kuwepo kwa umilele wowote pamoja na Mungu wa Pekee wa Kweli. Kwa kweli, kama Masihi alikuwa wa milele sawa na Mungu, basi asingeweza kuwa Mwana, na kwa hiyo hakuna kitu kingalichoweza kutabiriwa kuwa kwenye uhusiano ule. Zaidi sana, ni ukweli wa kwamba kulikuwa na idadi kubwa ya wana tangu kuwekwa kwa msingi ambao wangedai pia kuwekwa kwenye mfumo huo wa miungu mingi ulio kwenye muundo wa uhusiano wa kimilele wa kiwana. Kristo kama elohim alikuwa na washiriki wenzake (Waebrania 1:8-9 sawa na Zaburi 45:6-7). Alitiwa mafuta kuwa elohim na elohim wake. Madai yatokanayo na mafundisho ya kizushi ya kuwa na mamlaka kuwili yanatokana kabisa na Wanotheist (Yanahusisha na kuabudu malaika kwa kudai kuwa wana sifa ya kuishi milele mbali na Mungu). Madai ya kwamba ya kwamba Mungu, kama Elohimu, yanatokana na vitu viwili vya muhimu na lazima kwamba mmoja wa hawa elohim alikuwa ni Malaika wa Yehova, kama inavyosema Zekaria 12:8 wakitokana na Malaika wa Yehova akiwa elohim.

Zekaria 12:8 Katika siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana mbele yao.  

 

Zekaria 12:8 Katika siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana mbele yao.

 

Andiko hili linaonyesha kwamba watu wa nyumbani mwa Daudi watakuwa Elohim, kama Makaila wa Yehova (aliyetafsiriwa kama Bwana), kabla au mbele yao au vichwani mwao. Tafsiri ya Soncino inasema na kumtaja elohim hapa kama kiumbe anayefanana na Mungu. Kwa hiyo, neno elohim limeeleweka kuenea hadi kwa wengine.

 

Ni Masihi ndiye anayeiongoza Nyuma ya Daudi. Kiumbe huyu wa kimbinguni au kiongozi anayetangulia mbele ya wateule kama Malaika wa Yehova ndiye huyuhuyu Masihi. Hakuna kiwango chochote anachoonekana kwamba awe ni wa nyumba ya Daudi au Malaika wa Bwana, kwa kuwa kiumbe au kufanyika kuwa elohim waliofanana sawa na Eloa ambaye ni Mungu Baba (Mithali 30:4-5). Eloa peke yake ndiye anayestahili kulengwa kwenye ibada za hekaluni (Ezra 5:1-8), ambalo lilikuwa ndilo hekalu lake (Ezra 6:16-18). Eloa ndiye alikuwa mlengwa kwenye matoleo ya dhabihu (Ezra 6:9-10), Mungu wa mbinguni na chanzo cha Sheria au aliyetoa Torati (Ezra 7:14). Madai ya kwamba Mika 5:2-3 inamaanisha uwepo wa usawa wa umilele ni makosa yanayotokana na upotoshaji wa kimaandiko kwa kuyaondoa au kuyatenganisha na maandiko mengine mengi yanayopinga uwezekano kama huo.

 

Ni muhimu kuitathimini dhana usawa wa umilele. Usawa wa umilele unadai kwamba Masihi alikuwa ni Mungu mwingine aliyeishi na kudumu peke yake mbali na Mungu wa Peke wa Kweli. Kwa hiyo, andiko lifundishalo kuhusu Mungu wa Pekee wa Kweli linapuuzwa. Ndipo kwa kweli ingepasa kuwe na miungu wawili wa Pekee na wa Kweli, lakini Maandiko yanasema kuna Mungu Mmoja tu, wa Pekee na wa Kweli (Kumbukumbu la Torati 6:4; Yohana 17:3). Basi kama hakuna Miungu Wawili wa Kweli na wa Pekee ndipo kiumbe mmoja atakuwa anamtegemea mwenzake ili aweze kuishi. Kwa hiyo, mmoja atakuwa ndiye Mungu na mwingine atakuwa ni wa kuumbwa au aliyeumbwa na mwenzake. Kwa kuwa Mwana ndiye aliyeumbwa na Baba na ndivyo ilivyo pia kwamba ni mwana aliye tunda la Baba au aliyeumbwa naye. Kuna wana wengi wa Mungu tangu mwanzo (Ayubu 1:6; 2:1; 38:4-7), walio washirika wa karibu na Kristo (Zaburi 45:6-7; Waebrania 1:8-9). Na ndivyo ilivy pia kwamba ilikuwa ni Mungu Baba kwa kuumbwa kwao. Tafsiri ya Soncino inaitaja Zaburi 45:7[8] kuwa ni ya Kimahisi. Kimchi inasema

Mafuta yalikuwa ni ishara ya furaha (Isaya lxi. 3) na Mtunga Zaburi anakusudia kwamba Mungu kwa kumtia kwake mafuta Masihi awe Mfalme wake, atamuinua juu yaw engine wote na kuanzisha furaha ya ulimwengu.

 

Ufalme huu wa wana wengi wa Mungu ni kitu ambacho kimeongelewa kuwa kama ufalme wa milele (Zaburi 145:13), lakini bado hakuwa na umilele pamoja naye. Agano la Mungu na Ibrahimu lilikuwa la milele au ni agano lenye uhusiano (‘owlawm) (Zaburi 105:10), hata hivyo, haiashirii kuwa na usawa wowote na Mungu. Zaburi 93:2 inasema kuwa Bwana tu ndiye aliyekuwepo tangu milele yote. Dhana iliyopo kwenye andiko hili ni kuhusu utawala wa Mungu ulikuwepo tangu milele na milele (inarudi hadi nyuma kwenye mwanzo wa nyakati; Soncino) hata ingawaje masomo yalikuwa hayajatungwa bado. Dhana hii ilieleweka kutoka kwenye Isaya 9:6 kutokana na maneno yake ya Ajabu, Mshauri, Mungu mwenye nguvu (Eli), Baba wa milele, Mfalme wa Amani,. Maneno kama wa Ajabu, Mshauri yameandikwa kwenye Septuagint (LXX) kama Mjumbe wa Shauri Kuu (Megales boules aggelos). Neno Eli mwenye nguvu halimaanishi kuwa na usaw wowote na Eloah au Mungu. Wala neno hili Baba wa Milele halimaanishi kutambulisha kitu chochote, na kama, Mungu Baba. Kuna aina nyingi sana ya ubaba mbinguni na hata hapa duniani. Kila mmoja ametajwa na Mungu Baba (patria Waefeso 3:15). Kristo amepewa Ubaba wa wote wenye mwili. Kristo hakuwa wakati wote Baba wa milele, ingawaje cheo hicho alipewa. Kwa hiyo, jina hili halimaanishi uweza wa kutokufa au kupatwa na madhara zaidi ya vile lilivyochukuliwa kwa ajili ya Mungu. Andiko hili lilikusudiwa kwenye tafsiri ya Soncino (Isaya 9:5[6]) kama

Na jina lake ataitwa Pele-joez-gibbor-Abi-ad-sar-shalom.

 

Soncino inasema

Maana ya maneno ya Kiebrania ni ‘Mshauri wa Ajabu ni Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mtawala wa Amani.’ Mtoto huyu atakuwa na majina haya ya maana ili kuwapa watu ujumbe waliokusudiwa (Arbarbanel).

 

Andiko hili kwa hiyo linachukuliwa kuwa na mamlaka yaliyokusudiwa. Kwa kulifafanua andiko hilo, linalofuatia aya hii inayoitwa tangu hapo hata milele na milele, Rashi anasema kwamba neno la Kiebrania olam linamaanisha pia wakati au kipindilso cha mhimu. Maelezo haya yanatokana na jaribio la kulifanya au kulizeuza andiko hili na kulilinganisha na utawala wa mfalme Hezekia. Hata hivyo, maelezo ya maana yake yana maana sana.

 

Kwa hiyo inaweza kuonekana kwamba matumizi ya andiko hili la Mika 5:2-3 kuyafanya yamaanishe umilele wa Masihi na hivyo kuupa mashiko Ubinitarianism au mafundisho ya kizushi ya Nguvu Kuwili kuwa ni kama kukatisha au kuondoa sifa kuu ya Mungu ya kuweza kila jambo na kutoshindwa na nguvu nyingine yoyote ile na kuuvunja au kuupotosha mfumo mzima wa Umonotheism au imani juu ya Mungu mmoja na asiye na mshirika. Inapuuzia au kupotosha malaika au watakatifu muhimu walioelezewa kwenye Maandiko Matakatifu inayoonyesha tafsiri kuwa ina makosa au imekosewa.