Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[021D]

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu cha  Obadia

(Toleo La 1.0 20140906-20140906)

 

Maandiko ya kitabu hiki yanaelezea juu ya maafa ya Edomu katika Siku za Mwisho na kwa kweli ni mrejesho wa muunganiko wa kundi la Yuda katika Siku za Mwisho kutoka kwenye utawanyiko wa Kurudi kwa Masihi na kurudi kwake huko Yerusalemu.

                           

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)

(tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Ufafanuzi wa Kitabu cha Obadia



Utangulizi

Jina Obadia maana yake ni mtumishi wa Bwana. Ni jina la watu kumi na mbili tofauti kwenye Agano la Kale. Hatuna uhakika kuhusu nabii huyu alikuwa ni yupi hasa kati yao.

 

Haijulikani pia ni lini na wakati gani kitabu hiki kiliandikwa na aya za 1-9 zinaelezea juu ya unabii uliotabiriwa kwenye Yeremia 49:7-22 hasahasa kwenye sura za 49:9, 14-16 ambako kuna maneno ya wazi yaliyonukuliwa (sawa na ilivyo kwenye tafsiri ya Soncino). Kazi ya uandishi wake imegubikwa na wito au mahudhui ya haki na hukumu kwa Edomu.

 

Mapambano na chuki ya Edomu kwa ndugu na pacha wake vilijitokeza kutoka kwenye misuguano yao hata kipindi wakiwa tumboni bado na yaliendelea hata kwenye nyanja za historia kwa migogoro isiyotarajiwa kuonekana kwa watu walio ndugu wa damu.

 

Migongano kama hii ilitokea pia kwa Daudi kwa namna zote mbili, yaani kwa Sauli na baadae kwene utawala wake ha hadi kwenye vita vyake na Wahasmoneans mnmo mwaka 130 KK na kilio cha kila mara cha manabii wakitoa mwito wa kuwalipizia kisasi Waedomu au vinginevyo wakisihi kupinduliwa kwake.

 

Amosi anawalaumu Edom kwa kuwa walikuwa na hasira wakiwachukia Israeli milele (Amosi 1:11).

(Maandiko mengine yamenukuliwa kutoka kwenye tafsiri ya Soncino kuwa ni kama kwenye Isaya sura ya 34; Ezekieli 35; Zaburi 137:7; Maombolezo 4:21.)

 

John Hyrcanus yapata mwaka 130 KK aliwashinda na kuwatiishwa Waedomiu na Waidumeani na waliletwa kwenye dini ya Kiyahudi kwenye Karne ya Pili KK na pia wakafanyika kuwa ni sehemu ya washirika wa kibiashara wa Wafoenike. Herode Mkuu alijikusanya na kujiimarisha kwenye nafasi yake na Roma kwenye mapigano au Vita ya Actium na akafanikiwa kuwa mfalme wa Yudea, tangu wakati huu ufalme wa Kusini wa watu wa Yuda ulijumuisha idadi kubwa ya wa Waidumeani au Waedomu. Wagalilaya waliokuwepo, idadi yao ilikuwa ni ndogo kuliko hawa. Makabila yote mawili, Edomu na Yuda walichukiana na kudharauliana kila upande dhidi ya mwingine. Wakati Wayahudi wengi wakiwa wameingia na kujiunga kwenye imani ya Kikristo, Yuda wenyewe walikuwa na idadi kubwa ya Waedomu na Wayahudi wa leo waliopo idadi yao yaweza kuwa ni chini zaidi ya asilimia 18 ya Wayahudi na sehemu nyingine ya asilimia 10 ni Waedomu na wengine waliobakia ni wale wa jamii isiyo ya Kiyahudi wala Waedomu na way a kipindi cha utawanyiko. Waliosalia ni Wahamiti kutoka Kaskazini mwa Afrika au Kanaani au Wahiti kutoka kwenye dola iliyoanguka ya Wahiti huoko Troy, Mji Mkuu wa Wilusia au Khazars, kutokana na kuongoka kwao mwaka 730 BK.

 

Kwa jambo hilo kuwa moyoni inapasa kujulikana au kugunduliwa kwamba nabii hizi za baadae zinazohusu Edomu zinataja pia na ukaliwaji wa Palestina katika siku za mwisho na Wazayoni. Hawa ni watu ambao Kristo anawaongelea kwenye Ufunuo 3:9 ambao ni wa sinagogi la Shetani na wanaosema wao ni Wayahudi lakini wasema uwongo. Watafanywa waje kuwasujudia na kuwaheshimu walio kwenye Kanisa la Filadelfia la Siku za Mwisho.

 

Nabii zinazowahusu Israeli wa kweli ni kazi za manabii wengine kama vile Nahumu, Isaiya, Yeremia na manabii wengine kuhusu siku za mwisho. Kipimo cha nasaba cha DNA kinaonyesha Wayahudi wa siku hizi na habari zake zimeandikwa kwa kina kwenye majarida ya Chimbuko la Kinasaba za Mataifa (Na. 265) na Kizazi cha Ibrahimu Sehemu ya V: Yuda (Na. 212E).

 

Obadia Sura ya 1

1 Maono yake Obadia. Ndivyo asemavyo Bwana MUNGU juu ya Edomu; Tumepata habari kwa Bwana, Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, Akisema,Haya,inukeni ninyi;Na tuinuke tupigane naye.

Maneno yasemayo Ndivyo asemavyo Bwana MUNGU yaonekana ama ni marudio ya utambuzi wa maandiko ya Yeremia ya andiko lisemalo Bwana amesema au marudio ya agizo na mamlaka ya Mungu ya moja kwa moja. Kunaonekana mashaka kidogo kwamba Obadia anaongelea kwa mamlaka ya moja kwa moja ya Mungu. Nii inaonyesha mashaka kidogo kwamba Obadia anaongelea kwa mamlaka ya moja kwa moja ya Mungu. Matumizi ya neno sisi linaweza kuwataja manabii wengine au kwetu sisi Wayahudi. Umoja unakutikana kwenye gombo la Yeremia. Neno mjumbe ametumwa au maka tafsiri ya MT ilivyotafsiri wakati mwingine kuwa balozi ametumwa inaonyesha kutoeleweka wazi matumizi ya mawazo au dhana ya Mungu kuyainua mataifa yapigane na Edomu kwenye vita ya kumuadhibu Esau kama Edomu.

 

2 Tazama, nimekufanya mdogo kati ya mataifa; Umedharauliwa sana.

Andiko hili lilitimia mnamo mwaka 70 BK kwa kuwatawany na kupelekwa kwa wingi kwa Wayahudi wote kwa kushindwa baada ya mwaka 135 BK baada utawanyiko wa Hadrian. Mungu anawafanya wawe hawana maana kwa idadi kwa walivyokuja na kuingia kwenye imani ya Kiyahudi na walikuwa tayari yamekwisha dhalilishwa.

 

3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Mwenye makao yako juu sana; Asemaye moyoni, Ni nani atakayenishusha mimi?

 

Mji mjuu wa Edomu ulikuwa ni Petra na mji huu ulikuwa ni ngome uliokuwa inaingiwa kwa eneo jembamba, na ulitumika kwa kuwaua wafungwa waliotekwa kwa kuuwa kwa kuwatupa kwenye maporomoko ya mawe na majabali. Walikuwa wanajulikana na kujulikana kama wametengwa na hifadhi ya utajiri. Ulinzi wao ulitegemea mkingo wa mawe makubwa, mapango na miamba ambayo iliwawezesha kuwapa ulinzi. Nguvu na uweza wa Wamakabayo uliharibiwa. Uelewa wao uliharibiwa kabisa na Mafarisayo baada ya kuanduka kwa Hekalu kama ilivyokuwa lile la Wayahudi.

 

4 Ujapopanda juu kama tai, Ijapokuwa kioto chako kimewekwa kati ya nyota, Nitakushusha kutoka huko; asema Bwana.

 

Ingawaje wajibu na uweza wa kumlinda mwanadamu ni wa Mungu ambaye anawashusha chini kwenye uharibifu na maangamizo (soma pia Amosi 9:2 kwa ajili ya dhana hii. Kifungu kisemacho fanya au tengeneza (au jifanyie) kiota linaonekana kwenye Hesabu 24:22; sawa na tafsiri ya Soncino).

 

5 Kama wevi wangekujilia, kama wanyang'anyi wangekujilia usiku, (jinsi ulivyokatiliwa mbali!) Je! Wasingeiba kiasi cha kuwatosha? Kama wachumao zabibu wangekujilia, je! Wasingeacha baadhi ya zabibu, ziokotwe?
 

Maana yake ni kwamba wezi wa kawaida na wakabaji wangeweza kuacha kitu fulani pale walipo watekaji nyara wa Edomu walipochukua kila kitu. Ndipo ilipowalipa kisasi kwa vichwa vyao wakiwa hawana wa kuwasaidia. Torati ya Mungu imewakataza wavunaji kuendelea kuvuna maogeo yachipukayo mara ya pili, bali waache kitu fulani kwa ajili ya watu maskini (Kumbukumbu la Torati 24:21). Masalia ya Edomu walichukua kila kitu.

 

6 Jinsi watu wa Esau wanavyotafutwa-tafutwa! Jinsi hazina zake zilizofichwa zinavyoulizwa-ulizwa!

Mahala palipofichika panapoelezwa palihusu kuhifadhi mali za Edomu iliyopatikana kutoka kwenye misafara ya kibiashara na wizi wao. Inaweza kutafsiriwa kama utajiri au akiba iliyofichika.

 

7 Watu wote wa mapatano yako Wamekufukuza, hata mipakani; Wale waliofanya amani nawe Wamekudanganya, na kukushinda; Walao mkate wako wameweka mtego chini yako; Wala hana ufahamu wa hayo ndani yake.

Usaliti wa mwaka 70 BK pamoja na maangamizo ya Hekalu ulikofanwa na Warumi na kuharibiwa na maangamizo makuu ya Yerusalemu kwa kuchochea mapigano kuliwashuhudia Waedomu wakiacha maeneo yao kama ilivyoelezewa na kufafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Vita na Roma na Kuanguka kwa Hekalu (Na. 298).

 

Warumi waliendelea mbele na kuwaangamiza wote waliowapinga na wakaishia kwa kuuzingira na kuuangusha Masada.

 

Kusudi au fundisho kuu la jumla kwenye aya za 6-7 ni kwamba mahali walipokuwa na ngome ya kuwalinda hapakufanywa na hazina yao. Mapumziko rahisi na makamilifu ni tatizo la kweli la watafsiri na fafanuzi za marabi. Ilikuwa ni aya ya 7 ambayo ni jambo rahisi tu linalokamilisha na lilikuwa na kupinduliwa kwa Waedomu kulikuwa kumekwisha hitimika tayari (ambako hakukutokea hadi kupinduliwa kwao kulikofanywa na John Hyrcanus) vinginevyo nabii hizi kamilifu zinaonyesha kupinduliwa kwao hapo baadae? Tatizo la wafafanuzi wa jamii ya marabi ni kwamba wanajua kwamba hata kabla ya John Hyrcanus mapinduzi yalihusishwa na kutekwa kwa Edomu katika Yuda na kwamba hiyo ingeweza kuhusisha mkwamo wa kinabii wa Yuda na hii maana ya kweli na walipaswa kuendelea mbele kwa karne kadhaa na awamu ya mwisho ipo kwenye Siku za Mwisho za Waisraeli wa siku hizi (sawa pia na tafsiri ya Soncino hadi aya ya 7, ukurasa wa 130). Tafsiri fulani ni kwamba washirika walikwenda Edomu kwenye mipaka na waliwatekeleza na kuwaacha mikononi mwa maadui (kwa hiyo Metsudath David). Aliwaamini marafiki ambao Walao mkate wako wameweka mtego chini yako; Wala hana ufahamu wa hayo ndani yake. (kwenye maandiko ya chini ya RV yanaelezea kwamba kwa Kiebrania inasema wazi kuwa mkate wako (sawa na Zaburi 41:10 kwenye tafsiri ya Soncino). Mithali ya kuwalaghai kuwadhihaki Waedomu (Yeremia 49:7) ilishindwa kupambanua hali siyokuwa ya kutehemeka kwa washirika wao.

 

Vifungu vinavyofuatia vinachukuliwa kwendana na aya ya 15 na kuichukulia kama ni unabii unaohusu Hukumu ya Mungu kwa Edomu katika siku za mwisho zaidi ya kuwa aya zinazotangulia (sawa na tafsiri ya Soncino kuhusu aya za 8-9). Usemi wa Katika siku hiyoy unakusudia au unamaanisha Siku za Mwisho (aya ya 15) na ulimaanisha kutaja kurudi kwa Masihi au hata kwenda mbele zaidi kuutaja Ufufuo wa Pili wa Wafu. Inawezekana pia kuwa inataja harakati na matendo ya \masihi yatakavyokuwa kabla ya kipindi cha utawala wa Milenia kama inavyowahusisha pia Yuda kwenye maone ya Hekalu la nabii Ezekieli. Tatizo ni kwamba Edomu wamo miongoni mwa Yuda nah ii inamaana kuwa kuna matatizo mengine yanayopelekea kuwakumba Israeli wa sasa katika Siku za Mwisho (mauaji ya Holocaust yalikuwa ni moja ya yaho). Kwahiyo, Edomu ni jina linalotumika kuwaita watu walio ndani ya taifa na imani ya Kiyahudi.

 

Kutajwa kwa andiko la kifungu kinalofuatia kwa mtu aitwaye Temani kunalitaja jimbo lililoko upande wa kaskazini mwa Edomu (sawa na isemavyo pia  Amosi 1:12)

8 Siku hiyo, je! Sitawaangamiza watu wenye akili katika Edomu, na wenye ufahamu katika kilima cha Esau? Asema Bwana. 9 Na mashujaa wako, Ee Temani, watafadhaika, hata iwe kila mtu akatiliwe mbali kwa kuuawa katika kilima cha Esau.

(Ikilinganishwa na Zefania 1:9,10; 3:16; Hagai 2:23). Edomu alijulikana tena kwa kuwa na watu wenye busara (Yeremia 49:7).

 

Andiko hili lawezekana kabisa kuwa linataja kutiishwa kwa Edomu kulikofanywa na John Hyrcanus walipokuwa wanaishi huko Negebu. Walikuwa wameteseka kama adhabu kama tunayoona. Walikoma kuishi kama taifa linalojitegemea tangu kipindi cha utawanyiko na kuendelea.


10 Kwa sababu ya udhalimu aliotendwa ndugu yako Yakobo, aibu itakufunika, nawe utakatiliwa mbali hata milele. 11 Siku ile uliposimama upande, siku ile wageni walipochukua mali zake, na watu wa kabila nyingine walipoingia katika malango yake, na kumpa kura juu ya Yerusalemu, wewe nawe ulikuwa kama mmoja wao.

 

Torati inasema kuwa Usimchukie Mwedomi; kwa kuwa ni ndugu yako; (Kumbukumbu la Torati 23:7). Edomu walitafuta kuangamiza na kufaidika kutokana na vipindi vya Yuda kwenda utumwani na kwa kila wakati Yuda walipokwenda utumwani na walihukumiwa na kulaumiwa kwa ajili hiyo. Walisimama nyuma na kuwaruhusu au kuwasababisha wengine wanapopige huku wakikusudia wanufaike kutokana na mateka wao. Wengi walifanya hivyohivyo katika Vita Vya I na vya II vya Dunia,lilipa gharama yake (sawa na ilivyoandikwa pia kwenye Zaburi 137:7; Isaya 34:5-7; 63:1-6; Moabolezo. 4:21; Ezekieli 25:12-14; Malaki 1:2-5); na Amosi 1:11-12 kwenye kipindi cha mwanzoni kabisa cha nanabii.

 

Yuda walikwenda utumwani mara mbili kwa sababu ya dini yao ya uwongo na kuasi kwao. Mara ya mwisho ilikuwa ni kwa Warumi na ingawaje walijaribu kutafuta kutoroka, Waedomu wakaenda utumwani pamoja na hawa Yuda na wakabakia huko hadi leo. 12 Lakini usiitazame siku ya ndugu yako, siku ya mashaka yake, wala usisimange juu ya wana wa Yuda siku ya kuangamizwa kwao; wala usinene maneno ya kiburi katika siku ya shida yao. 13 Usiingie katika lango la watu wangu, siku ya msiba wao; naam, usiyatazame mateso yao, siku ya msiba wao; wala usitie mikono yako juu ya mali zao, siku ya msiba wao. 14 Wala usisimame penye njia panda, ili kuwakatilia mbali watu wake wakimbiao; wala usiwatoe watu wake waliosalia, katika siku ya dhiki.

Hili ni shitaka mara nane zaidi kwa Edomu waliyopewa kwa kulazimishwa. Kwa hiyo Edomu wanahukumiwa lakini tunaona sasa kwamba hii inaendelea hadi kwenye Siku hizi za Mwisho. Kwa hiyo, andiko hili linawaelezea tu Yuda wa leo katika Israeli. Ni kama yuda walivyoutia unajisi Mlima \Mtakatifu wa Mungu na kujiharibia na kuzivuruga siku zake za kuabudu na kuihalifu Kalenda yake, na ndivyo atakavyohukumiwa na kushughulikiwa chini ya mashahidi wawili, yaani Eliya na Henoko na chini ya Masihi aliye kichwa na kongozi wa Watakatifu na kwenye kipindi cha kumiminwa kwa Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu.

 

15 Kwa maana hiyo siku ya Bwana i karibu juu ya mataifa yote; kama ulivyotenda, ndivyo utakavyotendwa; malipo yako yatakurudia juu ya kichwa chako mwenyewe. 16 Kwa maana kama vile mlivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote watakavyokunywa daima; naam, watakunywa na kubabaika, nao watakuwa kana kwamba hawakuwa kamwe.

Kilichonenwa kwenye aya ya 15 ni kilekile kilichotajwa pia kwenye Yoeli 4:14. Kumbuka hapa kuwa Mlima wa Sayuni utakuwapo na utafanywa kuwa mtakatifu nah ii inaweza tu kuwa ni kipindi cha marejesho mapya yatakayofanywa na Masihi yaliyotajwa kwenye vitabu na unabii wa Ezekieli na Zekaria (sawa pia na Yeremia 25:15; 49:12; Ezekieli 35:15 cha Ghadhabu ya Mungu) .

 

Aya za 17-21 zinataja marejesho mapya ya Israeli. Aya ya 17 inaelezea hali tunayoiona kwenye Yoeli 4:17.

17 Bali katika mlima Sayuni watakuwako wenye kuokoka, nao utakuwa mtakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki milki zao.

 

18 Na nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu itakuwa mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaka kati yao, na kuwateketeza; wala hatasalia mtu awaye yote katika nyumba ya Esau; kwa kuwa Bwana amesema hayo.

 

Kutajwa kwa upungufu wa idadi ya waliookoka katika Esau na ushindi wa Yakobo na Yusufu kunaelezea kuhusu kufutiliwa kabisa kwa imani ya sasa ya Kiyahudi pamoja na Kalenda yao potofu na ya Uwongo ya Hilleli na upotoshaji wa imani sahihi ya mababa zao kina Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Kunatakiwa kuwe na marejesho kamili na muunganiko wa taifa la Israeli.

 

Ndipo tunaendelea mbele kujionea kile kinachofanyika kuwa ni nchi ambayo inajulikana sasa kuwa ni Israeli. Wale walio upande wa Kusini wataumiliki Mlima wa Esau ambao upo upande wa Kusini mwa Yordani. Baada ya utumwa wa Yuda waliotumikia huko Babeli, Waedomu waliyachukua maeneo ya Negebu na ilikuwa ni huko walikopigwa na kushindwa vita na huyu John Hyrcanus.  Kwa hiyo mabaki ya Waedomu katika Yuda, baada ya kipindi cha marejesho, watarudishwa kwenye Mlima wa Esau. Wafilisti waliliteka na kulitwaa eneo la Shefe’la au nyanda za chini ambalo lilikuwa ni ukanda wa bahari.

19 Na watu wa Negebu wataumiliki mlima wa Esau; na watu wa Shefela watawamiliki Wafilisti;

Nchi za ukanda wa bahari litakaliwa tena likiwa kama ni sehemu ya nchi za Yakobo. Yusufu watapewa kulimiliki eneo la Samaria na upande wa Kaskazini na Benyemini watavuka Yordani na kumiliki Gileadi, Ukanda wa Mashariki ambao hapo zamani ulikuwa ni moja na maeneo mengine ya kikabila yaliyokuwa mali ya Manase, baba wa Makiri, baba wa Gileadi. Kwa hiyo Benyamini wanaonekana kumiliki sehemu ya urithi wa Manase pia. Yordani kama ilivyo Amoni na Moabu itakuwa sehemu ya Israeli pia.

 

19b nao watalimiliki konde la Efraimu, na konde la Samaria, na Benyamini atamiliki Gileadi.

 

Kwa hiyo utumwa wa Israeli watarudi katika nchi ya Israeli na kuyatwaa tena maeneo yao.

 

Andiko lililo kwenye aya ya 20 limetafsiriwa vizuri kwa mujibu wa tafsiri za biblia za AV na RV kwenye nukushi zake za chini ya kurasa kwa kuandika kuwa “Na mateka wa jeshi hili la wana wa Israeli watamiliki kile kilicho mali ya Wakanaani hata hadi huko Zarefathi” nk., na tafsiri ya Soncino inakubaliana na tafsiri yao na inasema: “Maana ya zaidi hapo ni kwamba watumwa wa Ufalme wa Kaskazini watawashinda wa Kaskazini na watumwa wa Yuda wa Kusini.”

 

20 Na watu wa jeshi hili la wana wa Israeli waliotekwa, walio kati ya Wakanaani, watamiliki mpaka Sarepta; na hao watu wa Yerusalemu waliotekwa, waliomo Sefaradi, wataimiliki miji ya Negebu.

Maandiko ya Kiebrania hayaeleweki lakini Halah iko Kaskazini mwa Mesopotamia (sawa na 2Wafalme 17:6; sawa na inavyosema tafsiri ya biblia ya Annotated Oxford RSV). Kwa hiyo wafungwa wa Kaskazini watarudi. Zar’efathi ni mji wa Wafoenike ulio kwenye uwanda wa pwani kati ya Tiro na Sidoni huko Lebanoni (sawa na inavyosema Soncino) na kuanzisha ukomo wa Kaskazini ya Ufalme Ulioanzishwa tena kutoka Lebanoni iliyoko Mesopotamia katika Frati. Andiko hili litakuwa ni lile ambalo nabii Yoeli anaonyesha sababu inayosababisha Maandiko Matakatifu ya Agano la Kale yashambuliwe na Waarabu ambao ni Waislamu bandia.


21 Tena waokozi watakwea juu ya mlima Sayuni ili kuuhukumu mlima wa Esau; na huo ufalme utakuwa ni mali ya Bwana
                        

Huyu Mwokozi anayatajwa hapa akipanda kwenye Mlima Sayuni anayetajwa hapa ni Masihi pamoja na Jeshi lake la watakatifu. Hii kiteolojia inaonekana kuutaja utawala Masihi akiwa kama Mfalme wa mataifa yote (sawa na inavyosema Zaburi 22:28; 47; 99:1-2). Baadhi ya Marabi Wasomi (kama vile Metsudath David) wanakubaliana kwamba hii ndiyo maana ya andiko hili na ni Masihi anayeongelewa hapa.             

 

q