Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[021D]
Ufafanuzi wa Kitabu cha Obadia
(Toleo La 1.0 20140906-20140906)
Maandiko ya kitabu hiki yanaelezea juu ya maafa ya Edomu katika Siku za
Mwisho na kwa kweli ni mrejesho wa muunganiko wa kundi la Yuda katika Siku za
Mwisho kutoka kwenye utawanyiko wa Kurudi kwa Masihi na kurudi kwake huko
Yerusalemu.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)
(tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ufafanuzi
wa Kitabu cha Obadia
Utangulizi
Jina Obadia maana
yake ni mtumishi wa Bwana. Ni jina la
watu kumi na mbili tofauti kwenye Agano la Kale. Hatuna uhakika kuhusu nabii
huyu alikuwa ni yupi hasa kati yao.
Haijulikani pia
ni lini na wakati gani kitabu hiki kiliandikwa na aya za 1-9 zinaelezea juu ya
unabii uliotabiriwa kwenye Yeremia 49:7-22 hasahasa kwenye sura za 49:9, 14-16 ambako
kuna maneno ya wazi yaliyonukuliwa (sawa na ilivyo kwenye tafsiri ya Soncino). Kazi
ya uandishi wake imegubikwa na wito au mahudhui ya haki na hukumu kwa Edomu.
Mapambano na chuki
ya Edomu kwa ndugu na pacha wake vilijitokeza kutoka kwenye misuguano yao hata
kipindi wakiwa tumboni bado na yaliendelea hata kwenye nyanja za historia kwa
migogoro isiyotarajiwa kuonekana kwa watu walio ndugu wa damu.
Migongano kama
hii ilitokea pia kwa Daudi kwa namna zote mbili, yaani kwa Sauli na baadae
kwene utawala wake ha hadi kwenye vita vyake na Wahasmoneans mnmo mwaka 130 KK na
kilio cha kila mara cha manabii wakitoa mwito wa kuwalipizia kisasi Waedomu au
vinginevyo wakisihi kupinduliwa kwake.
Amosi anawalaumu Edom
kwa kuwa walikuwa na hasira wakiwachukia Israeli milele (Amosi 1:11).
(Maandiko mengine
yamenukuliwa kutoka kwenye tafsiri ya Soncino kuwa ni kama kwenye Isaya sura ya
34; Ezekieli 35; Zaburi 137:7; Maombolezo 4:21.)
John Hyrcanus yapata
mwaka 130 KK aliwashinda na kuwatiishwa Waedomiu na Waidumeani na waliletwa
kwenye dini ya Kiyahudi kwenye Karne ya Pili KK na pia wakafanyika kuwa ni sehemu
ya washirika wa kibiashara wa Wafoenike. Herode Mkuu alijikusanya na
kujiimarisha kwenye nafasi yake na Roma kwenye mapigano au Vita ya Actium na
akafanikiwa kuwa mfalme wa Yudea, tangu wakati huu ufalme wa Kusini wa watu wa
Yuda ulijumuisha idadi kubwa ya wa Waidumeani au Waedomu. Wagalilaya
waliokuwepo, idadi yao ilikuwa ni ndogo kuliko hawa. Makabila yote mawili,
Edomu na Yuda walichukiana na kudharauliana kila upande dhidi ya mwingine. Wakati
Wayahudi wengi wakiwa wameingia na kujiunga kwenye imani ya Kikristo, Yuda
wenyewe walikuwa na idadi kubwa ya Waedomu na Wayahudi wa leo waliopo idadi yao
yaweza kuwa ni chini zaidi ya asilimia 18 ya Wayahudi na sehemu nyingine ya
asilimia 10 ni Waedomu na wengine waliobakia ni wale wa jamii isiyo ya Kiyahudi
wala Waedomu na way a kipindi cha utawanyiko. Waliosalia ni Wahamiti kutoka
Kaskazini mwa Afrika au Kanaani au Wahiti kutoka kwenye dola iliyoanguka ya
Wahiti huoko Troy, Mji Mkuu wa Wilusia au Khazars, kutokana na kuongoka kwao
mwaka 730 BK.
Kwa jambo hilo
kuwa moyoni inapasa kujulikana au kugunduliwa kwamba nabii hizi za baadae zinazohusu
Edomu zinataja pia na ukaliwaji wa Palestina katika siku za mwisho na Wazayoni.
Hawa ni watu ambao Kristo anawaongelea kwenye Ufunuo 3:9 ambao ni wa sinagogi
la Shetani na wanaosema wao ni Wayahudi lakini wasema uwongo. Watafanywa waje
kuwasujudia na kuwaheshimu walio kwenye Kanisa la Filadelfia la Siku za Mwisho.
Nabii zinazowahusu
Israeli wa kweli ni kazi za manabii wengine kama vile Nahumu, Isaiya, Yeremia na
manabii wengine kuhusu siku za mwisho. Kipimo cha nasaba cha DNA kinaonyesha
Wayahudi wa siku hizi na habari zake zimeandikwa kwa kina kwenye majarida ya Chimbuko la Kinasaba za Mataifa (Na. 265) na Kizazi cha Ibrahimu Sehemu ya V: Yuda (Na. 212E).
1 Maono
yake Obadia. Ndivyo asemavyo Bwana MUNGU juu ya Edomu; Tumepata habari kwa
Bwana, Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, Akisema,Haya,inukeni ninyi;Na
tuinuke tupigane naye.
Maneno yasemayo Ndivyo asemavyo Bwana MUNGU yaonekana
ama ni marudio ya utambuzi wa maandiko ya Yeremia ya andiko lisemalo Bwana amesema au marudio ya agizo na
mamlaka ya Mungu ya moja kwa moja. Kunaonekana mashaka kidogo kwamba Obadia
anaongelea kwa mamlaka ya moja kwa moja ya Mungu. Nii inaonyesha mashaka kidogo
kwamba Obadia anaongelea kwa mamlaka ya moja kwa moja ya Mungu. Matumizi ya
neno sisi linaweza kuwataja manabii
wengine au kwetu sisi Wayahudi. Umoja
unakutikana kwenye gombo la Yeremia. Neno mjumbe
ametumwa au maka tafsiri ya MT ilivyotafsiri wakati mwingine kuwa balozi ametumwa inaonyesha kutoeleweka
wazi matumizi ya mawazo au dhana ya Mungu kuyainua mataifa yapigane na Edomu
kwenye vita ya kumuadhibu Esau kama Edomu.
2 Tazama, nimekufanya mdogo
kati ya mataifa; Umedharauliwa sana.
Andiko hili
lilitimia mnamo mwaka 70 BK kwa kuwatawany na kupelekwa kwa wingi kwa Wayahudi
wote kwa kushindwa baada ya mwaka 135 BK baada utawanyiko wa Hadrian. Mungu
anawafanya wawe hawana maana kwa idadi kwa walivyokuja na kuingia kwenye imani
ya Kiyahudi na walikuwa tayari yamekwisha dhalilishwa.
3 Kiburi cha moyo wako
kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Mwenye makao yako juu
sana; Asemaye moyoni, Ni nani atakayenishusha mimi?
Mji mjuu wa Edomu
ulikuwa ni Petra na mji huu ulikuwa ni ngome uliokuwa inaingiwa kwa eneo
jembamba, na ulitumika kwa kuwaua wafungwa waliotekwa kwa kuuwa kwa kuwatupa
kwenye maporomoko ya mawe na majabali. Walikuwa wanajulikana na kujulikana kama
wametengwa na hifadhi ya utajiri. Ulinzi wao ulitegemea mkingo wa mawe makubwa,
mapango na miamba ambayo iliwawezesha kuwapa ulinzi. Nguvu na uweza wa
Wamakabayo uliharibiwa. Uelewa wao uliharibiwa kabisa na Mafarisayo baada ya
kuanduka kwa Hekalu kama ilivyokuwa lile la Wayahudi.
4 Ujapopanda juu kama tai,
Ijapokuwa kioto chako kimewekwa kati ya nyota, Nitakushusha kutoka huko; asema
Bwana.
Ingawaje wajibu
na uweza wa kumlinda mwanadamu ni wa Mungu ambaye anawashusha chini kwenye
uharibifu na maangamizo (soma pia Amosi 9:2 kwa ajili ya dhana hii. Kifungu
kisemacho fanya au tengeneza (au jifanyie) kiota linaonekana kwenye Hesabu
24:22; sawa na tafsiri ya Soncino).
5 Kama wevi wangekujilia, kama
wanyang'anyi wangekujilia usiku, (jinsi ulivyokatiliwa mbali!) Je! Wasingeiba
kiasi cha kuwatosha? Kama wachumao zabibu wangekujilia, je! Wasingeacha baadhi
ya zabibu, ziokotwe?
Maana yake ni
kwamba wezi wa kawaida na wakabaji wangeweza kuacha kitu fulani pale walipo
watekaji nyara wa Edomu walipochukua kila kitu. Ndipo ilipowalipa kisasi kwa
vichwa vyao wakiwa hawana wa kuwasaidia. Torati ya Mungu imewakataza wavunaji
kuendelea kuvuna maogeo yachipukayo mara ya pili, bali waache kitu fulani kwa
ajili ya watu maskini (Kumbukumbu la Torati 24:21). Masalia ya Edomu walichukua
kila kitu.
6 Jinsi watu wa Esau
wanavyotafutwa-tafutwa! Jinsi hazina zake zilizofichwa zinavyoulizwa-ulizwa!
Mahala palipofichika panapoelezwa palihusu kuhifadhi mali za Edomu
iliyopatikana kutoka kwenye misafara ya kibiashara na wizi wao. Inaweza kutafsiriwa
kama utajiri au akiba iliyofichika.
7 Watu wote wa mapatano yako
Wamekufukuza, hata mipakani; Wale waliofanya amani nawe Wamekudanganya, na
kukushinda; Walao mkate wako wameweka mtego chini yako; Wala hana ufahamu wa hayo
ndani yake.
Usaliti wa mwaka 70
BK pamoja na maangamizo ya Hekalu ulikofanwa na Warumi na kuharibiwa na
maangamizo makuu ya Yerusalemu kwa kuchochea mapigano kuliwashuhudia Waedomu wakiacha
maeneo yao kama ilivyoelezewa na kufafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Vita na Roma na Kuanguka kwa Hekalu (Na. 298).
Warumi
waliendelea mbele na kuwaangamiza wote waliowapinga na wakaishia kwa kuuzingira
na kuuangusha Masada.
Kusudi au
fundisho kuu la jumla kwenye aya za 6-7 ni kwamba mahali walipokuwa na ngome ya
kuwalinda hapakufanywa na hazina yao. Mapumziko rahisi na makamilifu ni tatizo
la kweli la watafsiri na fafanuzi za marabi. Ilikuwa ni aya ya 7 ambayo ni
jambo rahisi tu linalokamilisha na lilikuwa na kupinduliwa kwa Waedomu kulikuwa
kumekwisha hitimika tayari (ambako hakukutokea hadi kupinduliwa kwao
kulikofanywa na John Hyrcanus) vinginevyo nabii hizi kamilifu zinaonyesha
kupinduliwa kwao hapo baadae? Tatizo la wafafanuzi wa jamii ya marabi ni kwamba
wanajua kwamba hata kabla ya John Hyrcanus mapinduzi yalihusishwa na kutekwa
kwa Edomu katika Yuda na kwamba hiyo ingeweza kuhusisha mkwamo wa kinabii wa
Yuda na hii maana ya kweli na walipaswa kuendelea mbele kwa karne kadhaa na
awamu ya mwisho ipo kwenye Siku za Mwisho za Waisraeli wa siku hizi (sawa pia
na tafsiri ya Soncino hadi aya ya 7, ukurasa wa 130). Tafsiri fulani ni kwamba
washirika walikwenda Edomu kwenye mipaka na waliwatekeleza na kuwaacha mikononi
mwa maadui (kwa hiyo Metsudath David). Aliwaamini marafiki ambao Walao mkate wako wameweka mtego chini yako;
Wala hana ufahamu wa hayo ndani yake. (kwenye maandiko ya chini ya RV yanaelezea
kwamba kwa Kiebrania inasema wazi kuwa mkate wako (sawa na Zaburi 41:10 kwenye
tafsiri ya Soncino). Mithali ya kuwalaghai kuwadhihaki Waedomu (Yeremia
49:7) ilishindwa kupambanua hali siyokuwa ya kutehemeka kwa washirika wao.
Vifungu
vinavyofuatia vinachukuliwa kwendana na aya ya 15 na kuichukulia kama ni unabii
unaohusu Hukumu ya Mungu kwa Edomu katika siku za mwisho zaidi ya kuwa aya zinazotangulia
(sawa na tafsiri ya Soncino kuhusu aya za 8-9). Usemi wa Katika siku hiyoy
unakusudia au unamaanisha Siku za Mwisho (aya ya 15) na ulimaanisha kutaja
kurudi kwa Masihi au hata kwenda mbele zaidi kuutaja Ufufuo wa Pili wa Wafu.
Inawezekana pia kuwa inataja harakati na matendo ya \masihi yatakavyokuwa kabla
ya kipindi cha utawala wa Milenia kama inavyowahusisha pia Yuda kwenye maone ya
Hekalu la nabii Ezekieli. Tatizo ni kwamba Edomu wamo miongoni mwa Yuda nah ii
inamaana kuwa kuna matatizo mengine yanayopelekea kuwakumba Israeli wa sasa
katika Siku za Mwisho (mauaji ya Holocaust yalikuwa ni moja ya yaho). Kwahiyo,
Edomu ni jina linalotumika kuwaita watu walio ndani ya taifa na imani ya
Kiyahudi.
Kutajwa kwa
andiko la kifungu kinalofuatia kwa mtu aitwaye Temani kunalitaja jimbo lililoko
upande wa kaskazini mwa Edomu (sawa na isemavyo pia Amosi 1:12)
8 Siku hiyo, je!
Sitawaangamiza watu wenye akili katika Edomu, na wenye ufahamu katika kilima
cha Esau? Asema Bwana. 9 Na mashujaa wako, Ee Temani,
watafadhaika, hata iwe kila mtu akatiliwe mbali kwa kuuawa katika kilima cha
Esau.
(Ikilinganishwa
na Zefania 1:9,10; 3:16; Hagai 2:23). Edomu alijulikana tena kwa kuwa na watu
wenye busara (Yeremia 49:7).
Andiko hili
lawezekana kabisa kuwa linataja kutiishwa kwa Edomu kulikofanywa na John
Hyrcanus walipokuwa wanaishi huko Negebu. Walikuwa wameteseka kama adhabu kama tunayoona.
Walikoma kuishi kama taifa linalojitegemea tangu kipindi cha utawanyiko na
kuendelea.
10 Kwa sababu ya udhalimu aliotendwa ndugu yako
Yakobo, aibu itakufunika, nawe utakatiliwa mbali hata milele. 11 Siku ile uliposimama upande, siku ile wageni walipochukua
mali zake, na watu wa kabila nyingine walipoingia katika malango yake, na kumpa
kura juu ya Yerusalemu, wewe nawe ulikuwa kama mmoja wao.
Torati inasema
kuwa Usimchukie Mwedomi; kwa kuwa ni
ndugu yako; (Kumbukumbu la Torati 23:7). Edomu walitafuta kuangamiza na
kufaidika kutokana na vipindi vya Yuda kwenda utumwani na kwa kila wakati Yuda
walipokwenda utumwani na walihukumiwa na kulaumiwa kwa ajili hiyo. Walisimama
nyuma na kuwaruhusu au kuwasababisha wengine wanapopige huku wakikusudia
wanufaike kutokana na mateka wao. Wengi walifanya hivyohivyo katika Vita Vya I
na vya II vya Dunia,lilipa gharama yake (sawa na ilivyoandikwa pia kwenye
Zaburi 137:7; Isaya 34:5-7; 63:1-6; Moabolezo. 4:21; Ezekieli 25:12-14; Malaki
1:2-5); na Amosi 1:11-12 kwenye kipindi cha mwanzoni kabisa cha nanabii.
Yuda walikwenda
utumwani mara mbili kwa sababu ya dini yao ya uwongo na kuasi kwao. Mara ya
mwisho ilikuwa ni kwa Warumi na ingawaje walijaribu kutafuta kutoroka, Waedomu
wakaenda utumwani pamoja na hawa Yuda na wakabakia huko hadi leo. 12 Lakini usiitazame siku ya ndugu yako, siku
ya mashaka yake, wala usisimange juu ya wana wa Yuda siku ya kuangamizwa kwao;
wala usinene maneno ya kiburi katika siku ya shida yao. 13 Usiingie
katika lango la watu wangu, siku ya msiba wao; naam, usiyatazame mateso yao,
siku ya msiba wao; wala usitie mikono yako juu ya mali zao, siku ya msiba wao. 14 Wala usisimame penye njia panda, ili kuwakatilia mbali
watu wake wakimbiao; wala usiwatoe watu wake waliosalia, katika siku ya dhiki.
Hili ni shitaka mara
nane zaidi kwa Edomu waliyopewa kwa kulazimishwa. Kwa hiyo Edomu wanahukumiwa
lakini tunaona sasa kwamba hii inaendelea hadi kwenye Siku hizi za Mwisho. Kwa
hiyo, andiko hili linawaelezea tu Yuda wa leo katika Israeli. Ni kama yuda
walivyoutia unajisi Mlima \Mtakatifu wa Mungu na kujiharibia na kuzivuruga siku
zake za kuabudu na kuihalifu Kalenda yake, na ndivyo atakavyohukumiwa na
kushughulikiwa chini ya mashahidi wawili, yaani Eliya na Henoko na chini ya Masihi
aliye kichwa na kongozi wa Watakatifu na kwenye kipindi cha kumiminwa kwa
Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu.
15 Kwa maana hiyo siku ya Bwana
i karibu juu ya mataifa yote; kama ulivyotenda, ndivyo utakavyotendwa; malipo
yako yatakurudia juu ya kichwa chako mwenyewe. 16 Kwa
maana kama vile mlivyokunywa juu ya mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote
watakavyokunywa daima; naam, watakunywa na kubabaika, nao watakuwa kana kwamba
hawakuwa kamwe.
Kilichonenwa
kwenye aya ya 15 ni kilekile kilichotajwa pia kwenye Yoeli 4:14. Kumbuka hapa
kuwa Mlima wa Sayuni utakuwapo na utafanywa kuwa mtakatifu nah ii inaweza tu
kuwa ni kipindi cha marejesho mapya yatakayofanywa na Masihi yaliyotajwa kwenye
vitabu na unabii wa Ezekieli na Zekaria (sawa pia na Yeremia 25:15; 49:12; Ezekieli
35:15 cha Ghadhabu ya Mungu) .
Aya za 17-21 zinataja
marejesho mapya ya Israeli. Aya ya 17 inaelezea hali tunayoiona kwenye Yoeli
4:17.
17 Bali katika mlima Sayuni
watakuwako wenye kuokoka, nao utakuwa mtakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki
milki zao.
18 Na nyumba ya Yakobo itakuwa
moto, na nyumba ya Yusufu itakuwa mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa
mabua makavu, nao watawaka kati yao, na kuwateketeza; wala hatasalia mtu awaye
yote katika nyumba ya Esau; kwa kuwa Bwana amesema hayo.
Kutajwa kwa
upungufu wa idadi ya waliookoka katika Esau na ushindi wa Yakobo na Yusufu kunaelezea
kuhusu kufutiliwa kabisa kwa imani ya sasa ya Kiyahudi pamoja na Kalenda yao
potofu na ya Uwongo ya Hilleli na upotoshaji wa imani sahihi ya mababa zao kina
Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Kunatakiwa
kuwe na marejesho kamili na muunganiko wa taifa la Israeli.
Ndipo tunaendelea
mbele kujionea kile kinachofanyika kuwa ni nchi ambayo inajulikana sasa kuwa ni
Israeli. Wale walio upande wa Kusini wataumiliki Mlima wa Esau ambao upo upande
wa Kusini mwa Yordani. Baada ya utumwa wa Yuda waliotumikia huko Babeli,
Waedomu waliyachukua maeneo ya Negebu na ilikuwa ni huko walikopigwa na
kushindwa vita na huyu John Hyrcanus. Kwa hiyo mabaki ya Waedomu katika Yuda, baada
ya kipindi cha marejesho, watarudishwa kwenye Mlima wa Esau. Wafilisti waliliteka
na kulitwaa eneo la Shefe’la au nyanda za chini ambalo lilikuwa ni ukanda wa
bahari.
19 Na watu wa Negebu
wataumiliki mlima wa Esau; na watu wa Shefela watawamiliki Wafilisti;
Nchi za ukanda wa
bahari litakaliwa tena likiwa kama ni sehemu ya nchi za Yakobo. Yusufu watapewa
kulimiliki eneo la Samaria na upande wa Kaskazini na Benyemini watavuka Yordani
na kumiliki Gileadi, Ukanda wa Mashariki ambao hapo zamani ulikuwa ni moja na
maeneo mengine ya kikabila yaliyokuwa mali ya Manase, baba wa Makiri, baba wa
Gileadi. Kwa hiyo Benyamini wanaonekana kumiliki sehemu ya urithi wa Manase
pia. Yordani kama ilivyo
Amoni na Moabu itakuwa sehemu ya Israeli pia.
19b nao
watalimiliki konde la Efraimu, na konde la Samaria, na Benyamini atamiliki
Gileadi.
Kwa hiyo utumwa
wa Israeli watarudi katika nchi ya Israeli na kuyatwaa tena maeneo yao.
Andiko lililo
kwenye aya ya 20 limetafsiriwa vizuri kwa mujibu wa tafsiri za biblia za AV na
RV kwenye nukushi zake za chini ya kurasa kwa kuandika kuwa “Na mateka wa jeshi
hili la wana wa Israeli watamiliki kile kilicho mali ya Wakanaani hata hadi
huko Zarefathi” nk., na tafsiri ya Soncino inakubaliana na tafsiri yao na
inasema: “Maana ya zaidi hapo ni kwamba watumwa wa Ufalme wa Kaskazini
watawashinda wa Kaskazini na watumwa wa Yuda wa Kusini.”
20 Na watu wa jeshi hili la
wana wa Israeli waliotekwa, walio kati ya Wakanaani, watamiliki mpaka Sarepta;
na hao watu wa Yerusalemu waliotekwa, waliomo Sefaradi, wataimiliki miji ya
Negebu.
Maandiko ya
Kiebrania hayaeleweki lakini Halah iko Kaskazini mwa Mesopotamia (sawa na 2Wafalme
17:6; sawa na inavyosema tafsiri ya biblia ya Annotated Oxford RSV). Kwa hiyo wafungwa
wa Kaskazini watarudi. Zar’efathi ni mji wa Wafoenike ulio kwenye uwanda wa
pwani kati ya Tiro na Sidoni huko Lebanoni (sawa na inavyosema Soncino) na kuanzisha
ukomo wa Kaskazini ya Ufalme Ulioanzishwa tena kutoka Lebanoni iliyoko Mesopotamia
katika Frati. Andiko hili litakuwa ni lile ambalo nabii Yoeli anaonyesha sababu
inayosababisha Maandiko Matakatifu ya Agano la Kale yashambuliwe na Waarabu
ambao ni Waislamu bandia.
21 Tena waokozi watakwea juu ya mlima Sayuni ili
kuuhukumu mlima wa Esau; na huo ufalme utakuwa ni mali ya Bwana
Huyu Mwokozi
anayatajwa hapa akipanda kwenye Mlima Sayuni anayetajwa hapa ni Masihi pamoja
na Jeshi lake la watakatifu. Hii kiteolojia inaonekana kuutaja utawala Masihi
akiwa kama Mfalme wa mataifa yote (sawa na inavyosema Zaburi 22:28; 47;
99:1-2). Baadhi ya Marabi Wasomi (kama vile Metsudath David) wanakubaliana
kwamba hii ndiyo maana ya andiko hili na ni Masihi anayeongelewa hapa.
q