Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[230]

 

 

Matumizi ya Neno Uungu Shirikishi

(Toleo La 1.0 19971214-19971214)

 

Uungu Shirikishi, yaani Hypostasis ni neno la msingi wa kiimani linalotumiwa na waamini imani ya Utatu. Mungu anachukuliwa kuwa yupo kwenye uungu shirikishi na wengine, yaani hypostases la ousia moja. Maneno haya yanatokana na maneno ya kifilosofia ya Kiyunani. Yanatujmika kwenye Agano Jipya na kwenye tafsiri ya Septuagint (LXX). Yanamaana gani basi?

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hatimiliki © 1997  Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Matumizi ya Neno Mjumuiko wa Uungu

 


Uungu Shirikishi, yaani Hypostasis asili yake ni neno la Kistoiki ambalo linahusiana na neno la Kiplatoniki la ousia. Yote mawili yanamaanisha uwepo wa kiumbe. Yametoholewa kwenye matumizi ya kidini kutokana na hoja za waamini utatu au watrinitariani, yaliyokusudia kutafuta kuelezea maana ya Uungu kwa kutuama kwenye matumizi ya maneno yanayotofautisha. Imani za Uungu Shirikishi za Kistoiki zilitumika ili kuwakilisha udhihirisho wa Mungu. Neno la Kiplatoniki la ousia lilitumiwa ili kuwakilisha utimilifu wa Uungu. Kwa hiyo, Uungu ulichukuliwa kuwa na udhihiriko wa aina tatu, yaani Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Kila moja ya madhihirisho haya ilichukuliwa kuwa ni namna tu ambayo kwamba mmoja wao alichagua kujiwakilisha mwenyewe. Kwa hiyo Baba, Mwana na Roho Mtakatifu walichukuliwa kuwa ni wenye hadhi na uweza sawa na wanadhihirika sawa kama kitu kimoja. Tofauti iliendelea kukuzwa sana kwamba wakati mmoja anapotenda jambo ndipo wote walitenda jambo hilo pasi kutenganishwa na kwamba hakukuwa na uwezekano wa kuwatenganisha kimatndo na mwenendo wao. Hapo ndipo dhana hii ya kipuuzi na ya uwongo iliendelezwa kwamba mjumuiko wa uungu waweza kuwa tofauti lakini sio kuwatenganisha.

 

Dhana iliyopo, ndiyo inayokataa uwezekano wa wateule kufanyika kuwa elohim au theoi kama ilivyokuwa ukifundishwa na Kanisa la kwanza na ndivyo ilivyoeleweka na Irenaeus (soma jarida la Mteule Kama Elohim (Na. 1) kwa rejea zaidi). Kristo alichukuliwa kuwa hakuwa mwana kwa maana moja sawa na kuwa Wana wengine wa Mungu ambavyo wanaweza kuwa Malaika na wateule wengine (soma pia kwenye jarida la Usosinianism, Uarianism na Uyunitarianism (Na. 185)).

 

Kuna idadi kadhaa ya mifano ya neno hili uungu shirikishi linavyojitokeza kwenye Agano Jipya na pia kwenye tafsiri ya Septuagint (LXX). Neno hili limejitokeza kwenye Zaburi 68 (69):3 (LXX).

 

Inaonekana pia kwenye Ezekieli 43:11. Dhana iliyolibeba neno hili ni kwamba:

 

kupangilia au kuweka chini ya; kuweka vitu chini ya, msingi mkuu au msingi: Zaburi. lxviii (lxix) 3; [tou oikou], Ezekieli xliii,11... (kwa mujibu wa Thayer’s Greek English Lexicon, pp. 644-645).

 

Maana yake ya pili ni kwamba:

 

kile kilicho na msingi, ni imara; hivyo, ni kile kilicho na uwepo, kinachoishi, kiumbe cha kweli: ... b. Kiwango na kitu madhubuti, asili, chochote cha kipekee. au kitu

 

kwa hiyo limetumiwa kwenye Waebrania 1:3 ambapo Mwana anawakilisha uhalisia wa Mungu.

 

Andiko hili linasomeka [kwenye machanganyiko wa Kirumi na Kiyunani]

os    oon            apaugasma  tes               dozes
ambaye ndiye [hakika] na uhalisia wa utukufu [wake]

 

kai           charakter tes           hupostaseoos autou,
na uwakilishi wa uhalisia wake

 

pheroon te   ta panta   too     remati tes dunameoos
na akachukua vitu vyote kwa neno la uweza wake

 

autou, katharismon toon amartioon poiesameos
kwa yeye kusafisha dhambi zote zilizofanywa

ekathisen en         dezia           tes      megaloosunes
akaketi mkono wake wa kuume wa ukuu wake

 

en upselois,

mahali pa juu

 

hivyo, neno atajwaye hapa kwa kweli ni halisi. Kwa hiyo Kristo ni mwakilishi wa uhalisia wa Mungu. Ni sawa tu na kama kusema kwamba wewe ni mwakilishi wa uhalisia wa Kanisa na kusema kwamba ninyi nyote wawili, yaani wewe na Kanisa ni Mungu kwa kuwa ninyi nyote wawili mnajumuika pamoja kiushirika, au uungu shirikishi, wa muundo wote mzima.

 

Waamini Utatu au Watrinitarians wanajaribu kukataa tofauti hiyo na uwakilishi kwa kutumia neno ambalo linaonyesha wazi uhalisia wa kiumbe. Ni neno la mashara au la mchezo.

 

Kuna ukweli wa maana kwa ukweli kwamba wewe binafsi yako na Kanisa kwa ujumla wote ninyi ni mawaka wa Mugu. Lakini Watrinitariani wanapinga mtambuka huu. Wanatafuta kuyafanya matumizi ya neno hili yamaanishe muungano wa vitu vitatu. Na kwamba Roho Mtakatifu sio utendaji bali ni washirika pamoja kiuungu mwingine mbali na hao. Kwa hiyo kufanya kuwe na uwongo, uzushi na kujiuliza kuna sababu gani ya kuwa na hali sawa ya uwepo au kuwepo na uhusiano kati ya mteule na mwamini Utatu kuwe hakuwezekani.

 

Neno hili limetumika kwenye kitabu cha Josephus cha Zamakale za Wayahudi [Antiquities of the Jews] 18:1,6; inamaana ya kujiamini au tumaini kuu kwenye 2Wakorintho 9:4 (tumaini) na pia kwenye 11:17. Waebrania 3:14 inalitumia neno hili kama tumaini au hakikisho (Marshall) kama ilivyo kwenye Waebrania 11:1 inamaanisha kuwa ni uhalisia (Marshall) au uhakika (RSV), ambavyo kwamba imani ni uhalisia au ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayo. Kutokana na andiko hili ni wazi kabisa kwamba madhihirisho yoyote ya uungu, ama yawe ya kiimani, au Kristo, au Roho Mtakatifu, au kwa uhakika angalivu wa mteule, yote hayo ni uungu shirikishi Mungu hujidhihirisha kwa ushirika wa pamoja wa zaidi ya aina tatu za imani ya uungu shirikishi. Watrinitariani kwa hiyo ni wana uchaguzi wa kuchekesha.

 

Matumizi ya neno hili yanapatikana pia kwenye Ruthu 1:12 (LXX) (kwenye SHD 8615; tiqvah) ambapo anasema kama ningepata mume hata usiku huu, inamaanisha chukulia kama msingi wa ukweli. Dhana itokanayo na msingi wa kiumbe kama ilivyokuwa. Ezekieli 19:5 (LXX) inatumia uungu shirikishi kwa andiko hili kama tumaini au matarajio. Zaburi 38[39]:8 inalitumia (kwenye SHD 8431; towcheleth) ambapo linamaanisha kama msingi au mahala pa tumaini amba7ye ni Mungu. Kwenye Ezekieli 19:5 (LXX) tumaini la samba jike wa Israeli alituama kwenye samba kijana aliyeshindwa (apooleto e hupostasis).

 

Kwa hiyo, imani kama ilivyo yenyewe tu ni washirika wa uungu kama kiini cha uhalisia ambao ni Mungu.

 

Mteule kwa tumaini hili kwenye imani katika Roho Mtakatifu wote wanakuwa washirika pamoja wa Mungu Mmoja, wa Pekee na wa Kweli (Warumi 8:17; Wagalatia 3:29; Tito 3:7; Waebrania 1:14; 6:17; 11:9; Yakobo 2:5; 1Petro 3:7).

q