Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[273]

 

 

 

 

Riboni za Bluu

(Toleo La 1.0 19981212-19981212) Ipo Kwenye Odio

Biblia imeamuru kwa ukumbusho wa Torati au Sheria za Mungu kwamba tuwe tunavaa vishada au riboni za bluu zinazotakiwa zibandikwe kwenye sehemu iliyotariziwa au pindo za nguo au mavazi tunayoyavaa.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1998 Thomas McElwain, John and Theresa Simons, Wade Cox)

(Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Riboni za Bluu


 


Utangulizi

Maelezo yanayoagiza kufuatia nia ya kuagiza sheria zimeandikwa kwenye aya zifuatazo:

Hesabu 15:38 Nena na wana wa Israeli, na kuwaagiza ya kwamba wajifanyie vishada katika ncha za nguo zao, katika vizazi vyao, tena ya kwamba watie katika kila kishada cha kila ncha nyuzi za rangi ya samawi

 

Hesabu 15:39 nacho kitakuwa kwenu ni kishada, ili mpate kukiangalia, na kuyakumbuka maagizo yote ya Bwana, na kuyafanya; tena kwamba msiende kutanga-tanga kuandama mioyo yenu wenyewe, na macho yenu wenyewe, ambayo mlikuwa mkiyaandama kwa uasherati hapo kwanza;

 

Kumbukumbu la Toratui 22:12 Ujifanyizie vishada katika pembe nne za mavazi yako ya kujifunika.  

 

Jarida hili kwa kweli ni myongeza ya lile la Amru Iliyokuu nay a Kwanza na limetokana na dhana au fundisho lililo kwenye jarida la Amri ya Kwanza.

 

Ili kuzielewa aya au maandiko haya kiusahihi, nia iliyokusudiwa kwenye uandishi asilia wa maneno yaliyotumika kama lazima. Kwenye Mathayo 9:20; 14:36; 23:5; Marko 6:56; na Luka 8:44 neno hem au pindo la vazi limetajwa. Ni neno ambalo kwa Kiyunani ni kraspedon (kwenye kamusi ya Strong’s Greek Dictionary (SGD) 2899) ambalo linatafsiriwa kwenye kamusi ya Thayer’s Greek Lexicon kwa kina zaidi au sehemu muhimu ya kitu, kikomo, upindo wa shketi; kama vile, kitu cha nyongeza au kilichojitokeza kinachoning’inia chini kutoka ukingoni mwa  joho au saa, kilichotengenezwa kwa sufi iliyochambuliwa;; kirangirangi, kishungi au kishada.

 

Neno lililoandikwa kwenye Zekaria 8:23 na 1Samweli 15:27 ni kanaph, ambalo kwenye kamusi ya Strong Hebrew Dictionary (SHD) 3671 na ambalo linatafsiriwa kama upindo au mwishoni; maalumu. (au ndege au jeshi) bawa, (la nguo au shuka ya kitanda) kifuniko, (ya dunia) robo moja, (ya jengo)mnara mferu.

 

Watafsiri wa Biblia ya KJV walitumia tafsiri au maelezo yafuatayo kuhusu neno hili kanaph: pindo, kona, mwisho, yenye manyoya, roborobo zilizotawanyika sana, sketi, sehemu za mbali sana, chenye mabawa, pamoja na matendo na kazi za ndege, kuruka, mmoja kwa mwingine, na kitu chochote. Kanaph inatafsiriwa kwenye tafsiri ya Gesenius’ Hebrew Lexicon as 1) mbawa, 2) ukingoni, kikomo – (moja ya) vazi, pindo, la vazi, sketi; upindo mzima wa vazi 1Samweli 24:5,12; Hesabu 15:38; Kumbukumbu la Torati 22:12 – pia bila jina vazi. Zekaria 8:23, ‘upindo (wa) yeye aliye Myahudi.’… b) pindo au kingo za dunia (kama ni wakazi wa dunia mara nyingi hufananishwa na mweneo wa saa). Isaya 24:16 ‘kingo za dunia’. Hasahas kwenye umoja katika Ayubu 37:3; 38:13, ‘misingi ya dunia’; na Zaburi 11:12; Ezekieli 7:2, ‘kona au pande nne,’ au ‘misingi yenyewe ya dunia.

 

Neno pande nne za dunia halionyeshi nwala kumaanisha pembe nne za kimwili za dunia, wala haiwezi kuwa hivyo likionyesha kuwa linamaanisha vazi tulijualo la kimwili.

 

Neno pindo la nguo lililotajwa kwenye Hesabu 15:38 kama et al. ni kwenye kamusi ya SHD 6734 (tsitsith), ambalo kwenye kamusi ya Strong inalielezea kama mimea au flora au kitu kinachoonekana kama bawa, kama vile kshungi cha nywele zilizosokotwa, shada. Kwenye tafsiri ya KJV watafsiri walichagua maneno mtarazo au msokoto. Hii Gesenius anaitafsiri kuwa ni kama mtarazo, kitu kilichopangiliwa vizuri kama ua au nyoya… (1) kishungi kilichojichomoza cha nywele (2) pindo za nguo, pembeni mlimotariziwa, ambazo Israeli walikuwa wanaziweka kwenye pindo za nguo zao, Hesabu 15:38,39.

 

Neno mtarazo lililotajwa kwenye Kumbukumbu la Torati 22:12 kwenye kamusi ya SHD 1434 (gedil) ambalo kamusi ya Strong inalielezea kama kutoka 1431 (kwa maana ya kuyumbisha); kukamia, kama vile shada au mambo ya shanga. Wafsiri walioitafsiri KJV walichagua maneno ya mtarazo na upindo.

 

Neno ribband lililo kwenye Hesabu 15:38 kwenye SHD 6616, limeandikwa pathil, ambalo kwenye kamusi ya Strong inalielezea kama kutoka 6617; msikoto wa kitani. Walioitafsiri biblia ya KJV walichagua maneno iliyounana, vikukuau bangili, kamba, mstari, ribband au riboni, nyembamba, na waya.

 

Neno bluu, ambalo kwenye SHD 8504, tekheleth, linaelezwa kama kiambishi. Kwenye 7827; misuli  ya rangi ya samawi; kama vile, rangi (mchanganyiko) zipatikanazo huko au fimbo iliyokolezwa rangi ndani yake. Walioitafsiri bilbia ya KJV maranyingi waliitafsiri hii kuwa ni bluu. Gesenius anasema kuwa ni samaki mwenye gamba, hasahasa Yule anayeitwa (helix ianthina, Linn.), kama vile vipande au sehemu ya misuli zinazopatikana kwenye bahari ya Mediterranean, zikiwa na gamba la bluu, ambazo kwazo, rangi ya samawi na ya tangi ya papo au zambarau hutengenezwa,… ambayo ni rangi ya samawi na ya zambarau, na nguo (samawi zilizoshonwa kwa uzi mwembamba na sufi), zilizochovywa kwenye rangi ya ii zambarau, Kutoka 26:4,31; Hesabu 4:6, sawa na; Ezekielieli 23:6; 27:7,24.

 

Neno tekheleth, lililotafsiriwa kama bluu limetumika na kome za Kimediterranean ammbayo imetokana na chanzo chake cha mchovyo asilia unaoonewa mashaka (hakuna mfano wa Kibiblia), kwa nguo zilizochovywa kwenye rangi namna hiyo (Kutoka 25:4; 26:1,4; nk.), na kwa rangi zenyewe (ni kwenye  Esta 1:6 peke yake). Ingawa maandiko haya yanauelezea mfano wa kuchovya zaidi ya rangi hasahasa iliyoonyeshwa kwenye utajwaji ulio kwenye mahala popote ulipotajwa muunganiko wa bluu (tekheleth) na zambarau (argaman), zote mbili na ambazo zinajumuisha tofauti ya hizi rangi, maneno haya yanaweza kutumiwa kama maneno yaliyo kiutofauti ya rangi. Wimbo Uliobora 7:5(6) inaonyesha kwamba rangi ya argaman/zambarau ni neno linaloitaja rangi iliyo nyeusi sana kuliko ile ya tekheleth/bluu. Ukweli wa kwamba maneno litumikalo kuelezea kuchovya au kikitia rangi kitu zaidi ya maneno yanayoelezea rangi tofauti linalotumika haliashirii kuwa ni mchovyo maalumu unaolengwa tu wa kitu uliokusudiwa, kwa vile hakuna maneno nyingine maalumu ya rangi yaliyokutikana kwenye Biblia ya Kiebrania. Kwenye hesabu, neno la Kiebrania linaeleweka sana kuashiria kuwa ni rangi ya bluu inayoweza kutofautishika iliyotafsiriwa kutoka kwenye zambarau na ambayo inajulikana kwa kiwango cha juu sana. Wayahudi wameyatafsiri maandiko haya kwa namna hiyo kama kuyakanusha kabisa na kuvaa vishada vyeupe na kwenye shali za maombi yao, sehemu za chini za mavazi yao.

 

Neno kasuuth limetafsiriwa vesture mara moja na kujifunika vazi mara moja. Kwa namna nyingine zote limetafsiriwa funika. Hii ni kwa mujibu unaolingana na shina la vebu ambayo kwayo limechukuliwa, ambalo kimsingi linamaana ya kufunika.

 

Neno beghed ni la kawaida sana, na mara nyingine sana limetafsiriwa kuwa vazi au nguo. Inatokana pia na vebu yenye maana ya kufunika. Iko wazi kabisa kuwa ni ufunikaji wan je iliyotumika kwa namna zote mbili, kama kujifunika wakati wa mchana na ni kama cha kujifunika usiku. Imeelezewa kigrafiki kwenye hahari au hadithi ya Yusufu kwenye Mwanzo 39:12-18.

 

Ufunikaji huu wa nje wa blanketi kwenye matukio mengi unaonekana kuwa ni umilikaji pekee wa thamani. Kwa hiyo ni maranyingi imechukuliwa kama nadhiri, mara nyingi na kwamba ni neno hilohilo ambalo linafanana sana na nadhiri, kama kwenye Ayubu 22:6, Mithali 20:16; 27:13; Ezekieli 18:7,16; na Amosi 2:8. Ni nadhiri ya kawaida iliyojulikana sana kuandikwa kwenye Biblia.

 

Kutoka 22:26 Ikiwa wewe kwa njia yo yote wapokea nguo ya jirani yako rehani, lazima utamrudishia mbele ya jua kuchwa; maana hiyo nguo ni kifuniko chake, hiyo peke yake ni nguo ya ngozi yake; je! Atalalia nini? Itakuwa, hapo atakaponililia mimi, nitasikia; kwa kuwa mimi ni mwenye rehema.

 

Ni hii hii ndiyo iliyorudiwa kwenye Kumbukumbu la Torati 24:10-17, hususan aya ya 13: apate kulala na mavazi yake, na kukubarikia. Hili ni neno la kawaida lililotumika kwenye Biblia kwa jinsi tunavyoweza kudhania kuwa ni kama blanketi la kujifunikia. Idadi ya maneno yametumika kwa ushinaji au vazi lililoshonwa la nguo.

 

Mahudhui na kusudi la amri hii

Kuna utekelezaji wa aina mbili wa amri. Wa kwanza ni kwamba amri hii inahusiana na utengenezaji na kulibuni neno kasuuth na beghed kwa jinsi kwamba mtande na sufi hazishikamani au kufumika, lakini ikaachwa kama mtarazo kwa pande zote nne za kona ya nguo, ambayo kwayo likuwa salama kwa maana ya vazi jeupe au kitambaa cha nguo kinachozunguka pande nne zote kwa namna ambavyo kitambaa cha bluu kinabakia kuonekana wazi na dhahiri linapotumika. Iwe kwa urefu wa mtarazo wala upana wa kitambaa cha kushonea cha bluu iliyokolea, ni pale vinapoonekana wazi tu vikiwa kama ni ukumbusho wa kumkumbusha mtu anayevitumia. Amri hii ni kitu cha kibinafsi kama tulivyoona kutoka kwenye ukweli wa kwamba hakuna adhabu iliyoelezwa na kwa hiyo sio jambo lililo kwenye sheria za kimahakama.

 

Lengo la amri linatofautiana. Kwanza kabisa, mtarazo na kishada cha bluu vinatakiwa vionekane na kwa hiyo view wazi na dhahiri lakini sheria hii imeelekeza hivyo au ni kwa kila mtu binanfsi yake. Kusudi na kazi yake hii ni kukumbushia amri zote zilizotolewa na Bwana. Ukumbushio huu unakusudia kuweka hali ya utiifu kwa Mungu zaidi ya kuwa ni kuyatii mapenzi au matamanio ya kila mtu binafsi yake au kujua na kuyapambanua yaliyomema na mabaya.

Utekelezaji wa amri

 

Suala la kutekeleza linageukia kwenye ama amri au sio amri zinazoonekana kufanana, na kama ni hivyo, jinsi inavyotakiwa kutekelezwa kwenye mazingira ya kisasa. Ushauri kwenye mambo haya mawili utaamuliwa kwa kudhania tena maya ya pili. Ya kwanza ni kwamba agano na Israeli linawafunga uzao wote wa waliokuwepo hai kwenye Mlima wa Sinai wakati Torati ilipotolewa na sio wana wa uzao wa Yuda peke yao. Fikra ya kabla hapo nyumana  ya Pili ni kwamba sheria ilipaswa itafsiriwe kama ilivyo kama kiuandishi iwezekanavyo.

 

Neno lisemalo "katika vizazi vyao vyote" linasema wazi wakati mkubwa unaowezekana wa kipindi cha uwepo wa amri hii. Zaidi sana ni kwamba Injili zinazoutaja mfano wa Kristo inauhusiano mkubwa na amri hizi. Mathayo 9:20 "Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake." Mathayo 14:36 " nao wakamsihi waguse hata pindo la vazi lake tu; na wote waliogusa wakaponywa kabisa.."

 

Lengo la amri hii pia lina umhimu wake muhimu. Kwa hiyo, ni ukubusho unaokumbushia kuzishika amri kuwa ni bado inatumika hata leo kama wakati amri hizo zilipokuwa zimetolewa. Zaidi sana, watu bado wanahimizwa kubakia kwenye vigezo vya kupambanua yaliyomema na mabaya kwa kulinganisha na sheria na maagizo matakatifu. Kwahiyo, umuhimu wa amri unabakia kuwa muhimu. Amri hii inabakia na ni kama amri iliyoko kwenye sheria za biblia na haziwezi kupunguzwa maana na umuhimu wake au kupunguzwa uzito wa utekelezaji wake. Huu ni mtazamo pia wa R. J. Rushdoony kwenye kitabu chake cha The Institutes of Biblical Law [Taasisi za Sheria za Kibiblia]. Anasema Vishada vya Bluu vinavyotakiwa haviwezi kutafsiriwa  kiroho kabisa ingawaje kimakosa kabisa anaendelea kuamini kwamba ilikuwa imeonekana kuwa ni muhimu sana kwa ishara mpya za agano kama lilivyokuwa lile la Sabato na tohara. Hata hivyo, anapinga mtazamo na mawazo ya Calvin na anasema kuwa ni sheria za Calvin mars. (kwenye machapisho ya Presbyterian and Reformed Publishing Company, 1973, pp. 22-23)

 

Jambo linalofuatia ni utekelezaji wa siku hizi. Ushikaji wa moja kwa moja wa sheria unakinzana na matumizi ya shada za bluu katikati ya mavazi nap indo kwenye ile ijulikanayo kama beghed na kasuuth, kwa hiyo, namna wanayofanya wafumaji nguo wa kufunika zote mbili, yaani mablanketi ya kulalia usiku na kwa kujifunika mchana. Matumizi mengine yote yanaweza kupingwa kabisa kwa hiyo na kuyaona kuwa yanakwenda nje na maagizo yaliyotolewa kufanywa kwenye matuzi halisi yaliyoagizwa na yanahatarisha ugunduzi wa sheria au kanuni mbadala.

 

Pindo na vishada vya bluu vimetajwa tu kwa jina la beghed na kasuuth, wakati kwamba kuna mishono mingine mingi ya nguo ilyotajwa kwenye Biblia. Amri iliyowazi ni ile ya kuweka shada za bluu kwenye pindo na kona za nguo wanazoziita beghed na kasuuth. Dokezo lake kwa hiyo inalazimu kwamba shada za bluu hazipaswi kuwekwa kwenye maeneo mengine ya vazi. Kwa kuwa matumizi ya hizi beghed na kasuuth yamezuiwa kabisa kwenye matumizi ya siku hizi, utekelezaji wa moja kwa moja wa amri yanaonekana ni muhimu na muafaka sana kabisa.

 

Ushauri au muono mmoja ni kwamba hii shali iliyo kwenye muonekano wa beghed/kasuuth ilitakiwa na ilitumika kama blanketi la kujifunikia na ni kama mtandio/shali wa mabegani (au joho lililo kama kawa au hutwa poncho), kwenye matukio mengine yoyote stahiki, yanayotimiliza amri, na kwamba shada za bluu na pindo zilizoshonewa au kuambatanishwa kwenye vazi linguine lolote halitimilizi amri. Mtazamo kama huo unahitaji kwamba sheria haina ulazima wa kuendelea na sio haiendelei kutumiwa kwenye mavazi. Nguo kama hozi kwa hiyo zingeweza kuonekana kama mtandio, moinganiko wake wote kamili (kutoka kwenye mafsiri ya kijinga ya kimwili ya neno hilo) na isiyoshonwa, kufumwa ili kwamba pindo na sufi inayofanya mitandio kwenye sehemu zake zote nne. Shada ya bluu au riboni kwa hiyo inapaswa ishonewe katikati mitarazo na nguoni. Kutokana na maonyo yaliyotolewa kwenye Kumbukumbu la Torati 22:5, kunapaswa kuwa na tofauti ya wazi kati ya mtandio autumiao mwanaume kimavazi na ule wa mwanamke. Kwa upande mwingine, ni kusema asipo kushonewa, tofauti kati ya blanketi la mwanaume na mwanamke ni vigumu kulifanya lionekane pasipo uchambuzi wa kisheria au kanuni. Kwahiyo, kutokana na agizo linguine la Kumbukumbu la Torati 22:5 linapaswa kutekelezwa na nguo zilizoshonwa peke yake na sio kwa mablanketi ya kujifunikia.

 

Maandiko yaliyo kwenye Kumbukumbu la Torati na Hesabu ndipo yanaweza kuchukuliwa kuithibitisha tofauti na riboni zenye utepe wa bluu zikiwa ni ufungaji wa kibinafsi kwenye pindo ambao kwa karne ningi na zisizohesabika zimekuwa zinashonewa kwenye mavazi. Kwa hiyo hizi riboni zimetiwa ndani yao kama ukumbusho kwenye uthibitisho wa sheria.

 

Kwa kuwa sheria hii haihusiani na nyakati, mahali, au harakati husika, basi inabakia kuwa ni utekelezaji wa mtu binafsi. Zaidi sana, hakuna adhabu iliyoagizwa kupewa mtu anayeivunja au kuipuuzia amri hii. Ikiwa kama kitu cha kumkumbusha mtu binafsi, hata hivyo, kwa hakika inaelezea shauku ya kukumbuka, upendo, na utimilifu wa amri za Mungu.

 

q