Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

 [005]

 

 

 

Uchoraji wa Tatuu Mwilini

(Toleo La 1.0 20000513-20000513)

Uchoraji wa Tatuu au Kujiweka Michoro ya Tatuu mwilini ni jambo la kizamani sana na ina maana yake maalumu ya kiroho. Kwa sababu njema sana Biblia imekataza kitendo hiki.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2000 Wade Cox)

(tr. 2014)

 

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Uchoraji wa Tatuu Mwilini



Tatuu ni neno linalotokana na asili ya Kipolynesiani na lilitolewa na Kapteni Cook baada ya kutembelea kwake kule. Neno hili asili yake linatokana na neno Tatu ambalo maana yake ni kujigonga chapa au kuweka alama au kujichora picha kwenye ngozi na limechukuliwa kutoka kwenye neno la Kitahiliani la tatau, ambalo limefupishwa kutoka kwenye neno ta linalomaanisha kugonga (kwa kujibu wa kamusi ya Encyclopaedia of Religion and Ethics (ERE), Vol. 12, article ‘Tatuing,’ pp. 208ff).

 

Kitendo hiki kina ukale au uzamani kubwa sana ikionekana miongoniwa Waaustralia wa jamii ya Kiaboriginals ambao wanaichanja na kuipamba miili yao kwa miaka ya zama kati, na desturi hii inakutikana katikati ya Wapolynesiani na Wajapani, ambayo kwao ni mtindo mzuri sana wa uchoraji na sanaa kwao.

 

Kwenye zama za nyuma za kabla ya mwanzo wa uzao wa kifalme wa Wamisri, tatuu zilionekana kwenye mumiani iliyobakia, kw mfano ya mwanamke huko Tukh (ERE ibid., p. 208b). Kwenye dola ya Theban Wamisri walijichora michoro hii ya tatuu kwenye maeneo ya matiti kwa kujiandika majina, au kujiweka alama au kuandika miungu yao na kadhalika (ERE ibid.). kwenye kipindi kilichoonekana kama cha kilele cha maisha kwao tatuu za mapambo zilikuwa adimu kwa Wamisri waliosalia.

 

Hawa ERE wanafanya uchunguzi wa sababu iliyopelekea kutakazwa na Biblia kama inavyosema:

Makatazo yaliyotamkwa kwene Mambo ya Walawi 19:28, ‘Msichanje chale yo yote katika nyama ya miili yenu kwa ajili ya wafu, wala msiandike alama miilini mwenu;’ inaashiria kuwa Wayahudi walikuwa wameyaonaa matendo haya yakifanywa na wamataifa wasiomcha Mungu ambao wapo kwenye maeneo iliyoangukia kura yao na huenda hata wao wenyewe walikuwa wameanza kujifania kwa kuwaiga (ERE, ibid).

 

Hawa ERE wanaendelea mbele zaidi kuona migawanyo mikuu ya mambo haya na malengo ya kiuandishi yangepaswa pia yaashirie chimbuko asilia mawazoni na kusudi ambalo kwalo zilikuwa zinatumiwa kwayo. Bila shaka kabisa kwamba matendo kama haya yalikuwa yakitumika ili kuonyesha alama ya kitatuu ya ukoo fulani kwa kuutofautisha na koo nyongine katika Australia. ERE wanaendelea kusema yafuatayo:

Kuna mwonekno na dondoo nyingi za uchoraji wa kimadaraja ya tatuu kwa wakazi wa Ulaya. Herodotus anaandika kuhusu wanawake wa Thracian kuwa walikuwa wanachorwa tatuu zikiwa kama ni ishara ya ustaarabu au uungwana. Pliny anasema kwamba wanaume wa Dacians na Sarmatians walichanja miili yao (‘corpora sua inscribunt’). Kwamba tatuu ilikuwa inajulikana na Wapictones na makabila mengine ya wa Gaul yanaonekana kwa ushahidi ya machapisho ya kwenye arafu. Mapokeo ya Wachina yanasema kwamba shujaa mwingine wa Kichina aitwaye Tschaipe alizikuta tatuu miongoni mwa wa Ainus wa Japan ambao kwa kweli walikuwa wanajichora hadi siku za leo. Huko Uchina kitendo hiki kilikoma tabgu siku za kale na za nyuma sana kuwa ni mtindo unaopendwa wa mapambo na kuendelea tu kama kama ni mtindo wa kuchapa au kuchora alama mbalimbali na zinazotofautiana. A. T. Sinclair anasema kwamba miongoni mwa hadithi za kale za huko West Indies, Mexico na Amerika ya Kati uchoraji wa tatuu ulikuwa umeenea kama sio ulimwenguni kote. Ilikuwa inafanywa hivyo na wakazi wa zmani wa Amerika ya Kusini, kama ilivyoonekana kwenye makabila ya pande za pwani ya Ecuador na Peru ya kale (ibid).

 

Tunajua kwamba ilionyesha mgawanyiko kama huo na ambao ulienea miongoni mwa watu wa maeneo ya pwani au pengine huenda kwa wao.

G. Elliot Smith analikuta hilo pamoja na wakazi wa pwani kwa sehemu kubwa ya dunia na ikijumuisha kwenye desturi na mila mchanganyiko ya ‘kitu kutoka juani (ERE ibid.).

 

Nukuu hii ina maana sana. Neno kutoka juani au heliolithic kuhusiana na zama ya kubuni isiyo rasmi na kwenye jambo hili umri wa jua na safari za waabudu jua za kihujaji zilichukua kiwango chake cha mgawanyiko au uingiaji. Uhusiano wao na nchi za pwani unaonyesha kuwa wanahusiana na mjumuiko wa watu wa pwani. Tunaweza kujipunguza kutoka na hili na ukale wa matukio au matendo tunayoshughulikanayo kwa vipindi vya wafalme wa kale wa baharini mapema kabla ya maendeleo ya dola kuu za kimabara ya Wababelonia na ya Wamedi na Waajemi na ya Wayunani na Warumi.

 

Darwin kwenye masomo yake alisema kuwa ilikuwa imeeenea sana ulimwenguni kote kwamba hakuna nchi moja kuu inayoweza kuitwa ambayo kwamba waaboriginali hawakujichota tatuu (ERE ibid.).

 

Tumeona na kuelewa sasa kwamba ilikuwa inaambukiza miongoni mwa Wamisri wa zamani na miongoni mwa wa Thracians, wa Picts na wakazi wa Amerika ya Kusini. Katika Amerika ya Kasakazini inakutikana pia kwa Wahindi hususan kwa wa Iriquois, wa Pricked Pawnees, wa Delawares na wengineo wengi (ibid.).

 

Kimsingi, watu wenye ngozi ya rangi nyeusi walifanya uchanjaji huu wa kimichoro, wakati wale wenye ngozi nyeupe ama angavu walikuwa wanajichora hizi tatuu.

 

Uhusiano wa matendo ya zama kale unaweza kukutikana hata sasa na tunaweza rkuanzisha utamaduni wa kujichora tatuu uliokatazwa kwenye Biblia kwenye Mambo ya Walawi 19:28.

 

Flinders Petrie ameguswa na kuwa makini kwenye ufananishaji kati ya muonekano wa Waalgeria ulioelezewa na Lucien Jacquot na wale walio kwenye muonekano wa kike waliokutikana huko Tukh (waliotajwa hapo juu) na kwa Walibya kwenye kaburi la Seti 1. Huyu Farao Seti 1 alikuwa ni wa Kizazi cha Kifalme cha XIX, takriban mwaka 1300 KK na anahushwa na wanazuoni na kpindi cha tukio la Kutoka akifuatiwa na kipindi cha utawala wa Manetho. Kwa hiyo tunaona mlolongo wa matukio ya huko Misri tangu wakati wa zama ya Mababa hadi siku hizi huko Afrika Kaskazini.

 

Hata hivyo, tunaweza kuidhania hii pia kuwa ni chanzo halisi cha dini halisi miongoni mwa imani kuu yenye mchanganyiko wa Kiashuru na Kibabeloni, ambayo ilikatazwa na Mungu, kwa kupitia Malaika wa Uwepo wake na Musa. Tumejionea ya kwamba ilikuwa ni ugonjwa huko Misri ya kale kuiwaklisha miungu, hususan katika kipindi cha wa Theban. Hii ni muhimu sana kwa aina yake kama mtindo wa ibada ulioenea kutoka Frigia hadi Misri na hadi huko Ulaya kwenye dini ya Kiseltiki nay a Picts.

 

Tunajua pia kuna ushahidi wa hitimisho la jumla la biashara ya kimataifa nay a kimabara na mawasiliano tangu mwaka 1000 KK kati ya Masharik ya Kati na Amerika ya Kusini. Ni vizuri na salama sana kudhania kwamba mueneo wa kipwani wa tendo hili ulikwenda na wachuuzi na imani ya dini ya waabudu jua waliyokuwanayo.

 

Mitindo iliojulikana na kupendwa huko Algeria ni

Msalaba na alama iliyofanana na inzi, ambazo zinadhaniwa kuwa mambo zimetokana na wa swastika – chombo kilichosambazwa sehemu nyingi barani Afrika na kwingineko, na yenye hali ya uzamani sana, kama inavyoonyeshwa katika uonekanaji wake kwenye mwonekano ulioongoza kwenye mji wa pili wa Troy (yapata kama mwaka 2500-2000 KK) na kwa kulindwa kwake huko Crete ya kale (ERE, ibid, p. 210).

 

Ni rahisi kuona kutoka kwenye rejea hizi na tarehe na alama, tunazo shughulika nazo na imani za zama kale kama zilivyotokea kutoka kwenye mchanganyiko wa Waashuru na Wababeloni huko Mashariki ya Kati. Ilijumuisha dini siri za kale na dini za jua zilizoonyeshwa kwa alama kwa msalaba, na kama ilivyotengenezwa kwa mtindo Swastika, na alama ya Baali-Zeebubu Bwana wa Inzi, mungu wa Ekroni (soma majarida ya Msalaba: Chimbuko Lake na Maana Yake (Na. 39) na  Daudi na Goliathi (Na. 126).  

 

Tunaiona dini ya Wafilisti, wenyeji wa maeneo ya pwani ya bahari waliokuja Kanaani na Misri kwa njia ya visiwa vya Mashariki ya Kati na ambao imani yao ilienea miongoni mwa waumini wote waabudu Baali na Ashtoreth au Astarte, Ishtar au Easter. Hii ilikuwa ni dini ya Watrojani. Watu hawa waliondoka Mashariki ya Kati na wakaingia na kuweka makazi yao huko Ulaya. Tunawaona watoto wao wakiuita mji kwa jina la shujaa wao Paris na linguine la baada ya ule Troy wa kale. Wao, pamoja na Wahiti, Wahati au Wakalti, Wakeltoi, ambao wengi wao waliondoka na kwenda Ulaya pamoja na Waashuru na sehemu kubwa ya Waisraeli wakati wa kuanguka kwa Dola ya Waparthi na wakajulikana kwenye historia kama Waaryans (soma jarida la Vita vya Wayunitariani na Watrinitariani (Na. 268)).

 

Imani hii inaonekana kwenye maadhimisho ya Easter na Christmas, hususan kwa wafuasi wa kile kilichoingia kwenye Uktisto kama sikukuu na maadhimisho ya Easter, inayotokana na ibada ya mungu Attis. Dini ya Siri na ya kuabudu Jua zilikuwa na kanuni na desturi hizi na tunazikuta kwenye dini potofu na za uwongo za Kiorphik, ya Dionysian, zile za Attis na pia zile za Adonis.

 

Makuhani matowashi wa mungu Attis walijipamba kwa michoro ya tatuu za mti wa mdaha au muivy ambao ulikuwa ni mtakatifu kwenye imani ya Wadruidiki wote na kwenye imani na Dini za waabudu Jua kwa ujumla. Neno Attis maana yake ni baba. Kwa hiyo, jina Papa au pope linatokana na dini hizi za kisiri na kifumbo. Neno au cheo hiki cha baba pia ni cheo cha daraja imani ya dini ya Mithras na kwa hiyo ujumuisho wa Dini za Siri na fumbo za waabudu Jua.

 

James George Frazer anaiweka hii kwenye mtazamo wa kazi hii The Golden Bough (third edition, Macmillan, 1976 print, v. p. 277).

Chimbuko na muonekano wa huyu Attis ni kama roho ya mti uliojitokeza wazi kwa nje kwa sehemu ambapo mti wa msonobari unaonyesha umuhimu wake, kanuni yake na sanamu zake. Hadithi inayodai kuwa alikuwa ni mwanadamu aliyebadilika kuwa mti wa msonobari ni moja pekee kati ya zile zinazojaribu kuweka wazi katika kuhusianisha na imani za zamani na ambazo zimetukuta sisi mara kwa mara kwenye mafundisho ya mizimu na mazimwi. Kitendo cha kuuingiza mti wamsonobari kutoka kwenye mbao zilizotengenezwa kwa mchanganyiko wa makapi na hariri, ni sawa kama kuuingiza au kuuleta mti wa May au mti wa majira ya Joto kwenye desturi ya makundi ya kisasa na kinyago au sanamu iliyoambatanishwa kwenye mti wa msonobari ambao ulikuwa umefanywa kuwa muwakilishi war oho ya mti wa Attis. Baada ya kuwa umekazwa kwenye mti, ndipo sanamu au kinyago kilitunzwa kwa mwaka mmoja na kisha ulichomwa moto…. (p. 277)

 

Imani hii imefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235). Dhana ya mzimu wa mti na mungu wa Utatu imeelezwa kwa kina na kuendelezwa kwenye jarida la Fundiho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya I Bustani ya Edeni (Na. 246).

 

Kushamiri kwa imani ya kidini ilikuwa ni kwa kuwa ilikuwa ni imani ile ile ya mwanzoni asilia. Ilitokana na imani kale za mchanganiko wa Waashuru na Wababwloni iliyotujia hadi sisi kama Waaryani na dini yao iliyoenea hadi kwenye maeneo ya mbali ya Wahiti na Waashuru na kwenye Makabila Kumi ya Israeli kutoka Mashariki ya Karti na katika kingo za kati za Ulaya hadi India.

 

Frazer alikuwa na mtazamo kwamba nia ya kwanza ya desturi iliyoelezwa hapo juu na kwa Msonobari kuwa mti mtakatifu kwa Attis, ilikuwa ni kuendeleza roho ya uoto kwenye maisha kwa mwaka wote mzima. Hamu hii indelevu ya kuziomba roho ya uzima na imani ya kutokufa ilijulikana na kuaminika sana miongoni mwa Waaryani ni kama ilivyokuwa dhana yote nzima isemayo Hutakufa hakika.

Frazer anaongeza kuwa:

Kwa sababu hizohizo ndpo huenda Ivy ulikuwa mtakatifu kwa Attis; kwa matukio yote tumesoma kwamba kulikuwa na makuhani matowashi waliochorwa tatuu zenye alama ya majani ya mti wa (ibid. p. 278).

 

ERE inasema:

Daraja zote huamini kwamba inafaa ya tatuu inafanya mwendelezo zaidi ya maisha yaliyoko leo hadi yale ya ulimwengu ujao, ambao wanatumika kama ilivyowekwa alama za utambulisho – kama, Nagas wa Manipur, Kayans wa Borneo, Wahindi wa Amerika Kaskazini, na wengine wengi, au ni kama mwongozo au ni kama kwa sasa inavyowawezesha wafanikisha safari yao.

 

Kwa hiyo, ingekuwa isemekane tu kwamba sababu ya kuweka tatuu hapo kale ilikuwa ni kama alama ya utambulisho, inayomfanya mtu aliyechorwa tatuu kwenye dini au imani yake kwa mungu au kwa mapepo ambayo ilikuwa inaombwa. Hii ilifanywa ili kwamba miungu au mungu au mapepo wachukue roho ya mwenye kuteseka na magonjwa na kuirejesha upya roho ile kwenye utaratibu wa maisha baada ya kufariki, iliyo kwenye mfumo au muundo war oho au ka. Hii ilifanyika ndani ya ufafanuzi kuhusu uzima wa milele uliotolewa na watu wa zamani kwenye ibada za Mungu wa Utatu, ambaye yeye mwenyewe anahusiana kama mungu kwene mti. Mungu utatu aliye kwenye mti anaonekana kutoka na rekodi yetu kwa zamani sana kabla ya kuishi kwa Wahindu waliokuwepo kwenye kngo za huko Harappa na Mohenjo Daro tangu kipindi cha kale cha majira ya Joto yapata mwaka 2000 KK. (soma pia jarida la Fundisho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya I Bustani ya Edeni (Na. 246)).

 

Hutu Mungu wa Utatu alitokea kuwa ni kama imani kuu ya huko Roma kama walivyo wengine kina Jupiter Juno na Minerva na pia kwa umbo la mungu mke aitwaye Hecate, mungu mwenye sura tatu kwenye jedwali la chemchabongo.

 

Kwa hiyp tunaona kusudi halisi ni kuweka alama au kutambulisha ushikaji wa imani na hasahasa kwa makuhani matowashi kuwa wamejitoa mhanga kwenye imani, kwa hiyo wametambulika kwenye maisha baada ya kufa au maisha yajayo.

 

Ni nyongeza kutoka kwenye mfumo wa imani wa kimapepo na uliwekwa ili kuendeleza au kutukuza fundiho la kuwa roho inaendelea kuishi na dhana yake na ni uwongo mkubwa sana uliotumika pale Edeni kuwa: Hakika hutakufa.

 

Kwa sababu hii Mungu amelaani na kukataza jambo hili, kwa kuwa ni ibada ya sanamu.

q