Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[289]
Ndoa
(Toleo
La 2.0 20001220-20070730)
Ndoa ni taasisi muhimu sana katika taifa. Ni msingi wa taifa na ni taswira
ya hali halisi ya watu ilivyo katika uhusiano wetu na Mungu na Kristo kwenye
mambo ya kiroho. Ni msingi muhimu kwa wokovu wa mwanadamu wote na imetabiriwa
kwenye uelewa sahihi na mwendelezo wa haya mahusiano kwa wateule wakiwa kama
mabibi arusi wa Kristo kwenye taifa la Israeli.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2000, 2007 Wade Cox and Erica Cox)
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ndoa
Kuumbwa kwa Adamu
Tunapoliangalia
suala la ndoa, tunapaswa kurudi nyuma kwenye mwanzo wa uumbaji wa mwanadamu.
Shetani alikuwa
amekwisha muasi Mungu tayari kwenye jambo hili. Alidhania kuwa angeweza kufanya
hivyo pia, kama sio vizuri zaidi kazi ya kuiongoza dunia na ulimwengu wote
(Ezekieli 28:1-10).
Inaonekana kwamba
alinuia kufanya uumbaji maeneo ya wanadamu na kutenga kwanza mahala alipojiwekea
yeye mwenyewe na kuwaumba pia viumbe wengine wakubwakubwa, maka vile wanyama
wanaojulikana kama Dinosaurs, the Neanderthals, mtu aina ya Cro-Magnon man, nk.
Shetani aliwepo
kwenye Bustani ya Edeni na Adamu na Hawa walionywa vyema sana kuhusu vyakula
ambavyo walipaswa kuvila na vile ambavyo hawakupaswa kuvila. Yapaswa ikumbukwe
pia kwamba Kibiblia, chakula kinaweza pia kumaanisha kuwa ni chakula cha kiroho,
kwa hiyo tunapaswa kupambanua pia kile tunachochagua kujifunza. Ujumbe na wito
wa Shetani ulikuwa ni wa chakula walichokatazwa wasikile, alianzia mbinu zake
tangu kipindi cha kuumbwa kwake Adamu akinuia kuuharibu uhusiano mzuri
uliokuwepo kati ya mwanadamu na Mungu.
Kwa kumuumba mke
wa Adamu, Mungu alikuwa anaweka mkakati mbinu wa kumuwekea mazingira imara
ambao kwao mwanaume na mwanamke wangeweza kukua kwa pamoja kwenye upendo wenye uhusiano
ambao watawapa au kuwashirikisha watoto wao. Mojawapo ya masomo ya mwanzoni
zaidi kwa Adamu ilikuwa ni kuwapa majina kwa kila kiumbe mmoja mmoja ambayo
walipaswa kuitwa kwayo. Kwa kumuonyesha umahiri wake kwenye wajibu wake kwa
viumbe hawa na wajibu wake wa kuiunza Bustani, Adamu pia alifikiria kuchukua
wajibu katika kushughulikia mahitaji ya kimwili nay a kihisia ya familia yake.
Mungu kwa kupitia
Kristo mwanae, alitoa orodha ya amri na sheria za kuyatawala na kuyaongoza
maisha ya kila mtu mmoja mmoja na jamii iliyo kwenye msingi wa asili yake na
kutoa taswira ya aina ya uhusiano tunaotakiwa kuwa nao kumhusu yeye. Kwa hiyo,
famiiia ni kiini cha msingi cha kanuni na Sheria za Mungu. Sheria inayohusiana
na mambo ya familia ni Amri ya Tano, inayotutaka kuwatii wazazi wetu, ya Sita
inahusu kuyalinda maisha au uhai wa wapendwa wetu, watoto wetu, wengine walio
kwenye nyumba na familia zetu, jami na taifa; Amri ya Saba ndiyo iliyokataza
uzinzi; Amri ya Nane inakataza wizi; Amri ya Tisa inakataza kumshuhudia mtu
ushuhuda wa uwongo; na Amri ya Kumi inakataza kumtamani mke wa jirani, nk.
Kwa kweli familia
inathirika sana pale sheria na amri hizi zinapovunjwa. Hususan katika familia ya Mungu.
Uwekaji wa Mamlaka
Je, familia ni nini? Familia ni mfumo wa maisha ya kikundi. Inaanza na watu wawili, baba na mama walifuatiwa na watoto; lakini ni kubwa zaidi kuliko hiyo. Kamusi ya The Interpreter’s Dictionary of the Bible (Abingdon Press 1962, 1980, pp.238f.) inasema:
Kwa kuwa ndoa ni kitu halisi – ikiwa inasimamiwa na baba- katika watu wa Biblia, familia ilikuwa ni jumuia ya watu walio na uhusiano wa kifungamano wa kindoa na kiudugu na wanaongozwa kwa mamlaka ya baba. Familia ya kibiblia, hususan wakati ndoa inapokuwa ya matala, ilikuwa kubwa. Inajumuisha baba na mama au wamama, watoto wa kiume na wakike, (hadi kuolewa kwao), wajukuu, wengine walio kwenye jamii hii kama ndugu, pamoja na watumishi wa nyumbani hapo, Masuria na wageni (watembeleao). Israeli walihimizwa kuwa na familia kubwa, kwa sababu za kiuchumi pamoja na za kidini. Watoto walikuwa kwa Nyanja zote mbili, yaani kwa kuzaliwa na kwa kwa agano lililowekwa na makundi mengine na kila mmoja wao. Mshikamano katika familia ulitengamaa kwa mpangilio wake ulioko kwa uongozi wa baba na kwa kuzitendea kazi kanuni zinazi tathmini haki kwa maana yakuhusianisha uwajibikaji wa familia (nzima) yote.
Kama baba atasema
kwamba:
Familia
ilitenda kazi kama jumuia ya kidini, iliendeleza na kulinda mapokeao ya kale na
kuyapitisha yaendelee kwa maelekezo na na mafundisho yote na ibada. Matendo ya
shuiuti yanatishia uadilifu na usalama
wa familia, kama vile mabadiliko ya kiunchumi na ushawishi wa tamaduni na dini za
kigeni, kulipingwa kwa nguvu zote na wengi wa waandishi wa bilbia. Umuhimu wa familia
unapaswa uonekane kwa taswira ya wazo hili zaidi ya mipaka ya familia kwa
kweli. Na ndipo inarejea kwenye makabila ya Kiebrania, mataifa ya Israeli na
Yuda, mataifa mengine hya mbali, na kwa Israeli wote, waliochukuliwa kama
jumuia ya kiimani zaidi ya kuwa ya kitaifa. Kwenye Agano Jipya inaoneshwa kama
jumuuia ya Kikristo pia.
Kwa hiyo tunaona
kwamba familia inaendelea kwenye ukoo, na pia inajumuisha mtumishi yeyote na
wageni, ukoo au kabila, na hatimaye kwenye taifa. Ustawi na afya ya vikundi
vigodo unakuwa unaonekana katika jamii kwa ujumla. Familia zinafanya kazi zake
chini ya Sheria za Mngu na ndivyo ilivyo kwenye taifa pia (sawa na linavyosema
jarida la Torati na Amri ya Tano (Na. 258) [Law and the Fifth Commandment (No. 258)].
Biblia ijulikanayo kama The Illustrated Bible Dictionary (Inter-Varsity Press, Tyndale House Publishers, 1980, Part I, p. 500) inasema kwamba:
Wakati kwenye kipindi cha
uumbaji matala yalionekana ndiyo muundo uliokuwa umakusudiwa, ndipo mfumo wa matala
(mwanaume kuwa na wanawake wengi na sio mwanamke kuwa na wanaume wengi) ndio
unaoonekana.
Basi huu haukuwa mpango
wa Mungu ulioonyeshwa kwenye maelekezo na nasaha za manabii wa Israeli kama
ndiye bibi arusi pekee wa Mungu (Isaya 50:1; 54:6-7; 62:4-5; Yeremia 2:2; Ezekieli
15; Hosea 2:4f.).
Hebu na tuwe na mtazamo
mfupi kwa mambo haya.
Suria
Sheria za biblia
na kanuni za kuwa na mtumwa, mtumwa aliyejitoa kutumikia maisha, suria, nk, zilikuwa
tofauti na mwanamke huru. Suria alikuwa ni mwanamke aliyekuwa ameuzwa kwa mtu
mwingine. Wakati mwingine aliitwa ni mtumishi wa kulipwa.
Kutoka 21:8 inaonyesha
kuwa wakati mwanamke walipokuwa anauzwa na baba yake ili awe ni mtumishi wa
ndani kwa mtu mwingine aliyemchumbia na kama yeye mwenyewe hakumpenda, hakutakiwa
amwambie hayo mbele za wageni. Na zaidi sana, kama alinunuliwa kwa ajili ya
mwanae ndipo alipaswa amtunze na kumtendea vizuri kama anavyostahili kufanyiwa
ninti. Kwenye aya ya 10, inasema kama ataolewa tena, anapaswa kumpa Yule mtumwa
chakula, nguo na mahusiano ya kawaida ya kndoa. Kama atashindwa kumpa mojawapo
ya mambo haya, basi aliruhusiwa aondke na kuwa huru pasipo kumlipa fidia yoyote.
Kama mwanaume
alikuwa na uhusiano wa kingono na suria anayetumika kama mtumwa kwao na ambaye
alichumbiwa au kuposwa na mwanaume kama inavyoonekana hapo juu, anaweza
kukatiliwa mbali na kunyang’anywa suria huyo lakini sio kuuawa, kwa kuwa hakuwa
huru.
Maandiko
Matakatifu yanahusianisha zaidi kuwa uchumba au posa imekutikana kwenye
Kumbukumbu la Torati 20:7 na 28:30.
Uchumba
au Posa
Neno posa au
uchumba lilitumika kwenye
Agano Jipya likiitwa mnesteuoo (SGD 3423). Haya hivyo, limetumika mata
tatu tu kwenye Mathayo 1:18, Luka 1:27 na Luka 2:5. Maandiko haya Matakatifu
yanaongelea kuhusu Mariamu akiwa ni bikira aliyechumbiwa ama kuchumbiwa na
Yusufu. Mariamu alikuwa ni mke wake ingawaje ndoa ya kawaida ilikuwa
haijafanyika bado na alikuwa bado hawaja juana kimwili.
Neno mke ni la limetafsiriwa kiujumla ama kwenye Agano
Jipya kwa neno lijulikanalo gune (SGD 1135) au la Agano la Kale la 'ishshah (SHD
802). Yote mawili yana maana moja na ni neno la kiuhusiano wa kinasaba lenye
maana ya kike ya mke, mwan ke, mwanamwali bikra, au mwanamke aliyechumbiwa au
kuposwa na mwanaume fulani mwingine tuja h have the same meaning and it is (tazama
Luka 2:5; Kumbukumbu la Toarti 20:7, na maandiko mengine mengi). Bikira ni mke ambaye alichumbiwa akiwa ni
mtumwa wa mwanaume. Kwa hiyo, kwa kipindi hiki yeye ni mumewe.
Kinyumba
Kuweka kinyumba
kunatokea wakati mwanaume anapochukua mwanamke wa pili wakati mke wa kwanza
akiwa hana habari au mke wa pili. Hii haikubaliki kwa kujibu wa sheria za
karibu nchi nyingi na ndoa ya mke mmoja ndiyo yanayosisitizwa kwenye sheria za
nchi nyingi kati ya hizo.
Matala
Ndoa za matala
zilieenea na kujulikana katika Israeli yote na inamaanisha tu kuwa ndi ndoa ya
wake wengi ambayo kwa kawaida hufanyika kwenye ndani ya familia ile ile. Daudi
na Sulemani wote wawili waliuwa na wake wengi. Uislamu unaruhusu kuoa wanawake
wane na dini ya kale ya Kiyahudi iliruhusu kuoa wanawake zaidi ya wane. Falme
aliruhusiwa kuoa hadi wanawake kumi na wanane.
1Timotheo 3:2 inasema
kuwa Askofu wa Kanisa anapaswa awe ni mume wa mke mmoja tu. Tafsiri ya usemi
huu iko kwenye Sheria ya Mungu/ aliruhusiwa kuoa tena anapokufa au kuachika.
Sheria za nchi zinapaswa kuzingatia jambo hili, na kwa kweli, inaangalia mfano
wa Sara na Hajiri, na Rahelii. s that a Bishop of the Church may be the husband
of na Lea, na ni wazi kwamba sio kila
mara ni wazo lililoko (sawa na jarida la Raheli na Sheria (Na. 281) [Rachel and the
Law (No. 281)].
Kuna amri pia
kumtaka mwanaume ahakikishe kuwa mjane wa wa ndugu yake aolewe ili azae mtoto
au watoto waendeleze ukoo na urithi wao, kwa mujibu wa sheria za walawi (soma
jarida la Dhambi ya Onani (Na. 162) [The Sin of Onan (No. 162)].
Maisha
ya Ndoa Moja
Wakati taarifa za biblia inaandikwa zinatoa mifano
mingi kuhusiana na ndoa za matala, Biblia pia inaonyesha kwamba ndoa ya mke
mmoja ilikuwa ndiyo maisha ya jumla yaliyokuwapo. Maelezo ya kitabu cha Mwanzo
yanaonyesha wazi kwamba ndoa za mke mmoja ndilo lilikuwa wazo kuu na ndivyo
ilivyokuwa (Mwanzo 2:24). Kwa kawaida, kulipaswa kuwepo na sababu muhimu ya
kuongezea wake, kama vile kwa kuhitaji awepo mtoto atakayekuwa mrithi wakati
mke anapokuwa hazai au tasa au maka mumewake atakufa na kumuacha mjane akiwa
hajamuachia hata uja uzito. Hali ya kumlinda mwanamke ilikuwa ni sababu moja
wapo. Angano Jipya pia limeonyesha kwa wazi kwamba ndoa ya mke mmoja ilikuwa
ndiyo sheria iliyojulikana na kueleweka zaidi, au hata ndiyo iliohamasishwa na
kukubalika kwenye maisha ya watumishi waliosimamia huduma.
Mungu alianzisha
familia ziwe kama msingi ambao kwazo Taifa litajengwa kwazo.
Warumi 13:1-7
Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna
mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. 2 Hivyo amwasiye
mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia
hukumu. 3 Kwa maana
watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo
mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa
kwake; 4 kwa kuwa
yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya,
ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu,
amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu. 5 Kwa hiyo ni lazima kutii, si kwa
sababu ya ile ghadhabu tu, ila na kwa sababu ya dhamiri. 6 Kwa sababu hiyo tena mwalipa kodi;
kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi iyo hiyo. 7 Wapeni wote haki
zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu;
astahiliye heshima, heshima.
(Soma jarida la Torati na Amri ya Sita (Na. 259) [Taw and the Sixth Commandment (No. 259)].
Sisi sote
tunapaswa kuitii mamlaka. Wanawake wengi leo wanalalamikia kanuni au utataribu
wa biblia inayowataka wawatii waume zao. Kuyaelewa vizuri majukumu ya familia na
ndoa inatakiwa iepukane na aina yoyote machungu na unyanyasaji kwa wanawake wa
Kikristo.
Mungu alimuumba
Adamu (Mwanzo 2:7) na akamuweka kwenye Bustani ya Edeni. Alipewa majukumu au
kazi ya kuwapa na kuwaita majina viumbe wote aliowaumba Mungu. Aliagizwa
kuilima ardhi na kujipatia chakula kutoka kwayo. Kwa maneno mengine, wanadamu
walipewa mamlaka kwa Dunia na kutawala na kuitiisha, pamoja na kuwatunza viumbe
wengine wakiwepo ndege wa angani na viumbe waishio baharini. Hii siyo leseni ya
kuwaua na kuwaangamiza kama tupendavyo, bali tunawajibu wa kuwatunza, kuwalisha
na kuwasaidia kikamilifu na kuitunza Dunia sawasawa na Sheria za Mungu, na
mwanadamu anawajibika kwa Mungu kutokana na wajibu wake huu anavyoufanyia kazi.
Adamu alifundishwa vyema kuhusu kanuni na sheria hizi (soma jarida la Fundisho la Asili ya Dhambi Sehemu ya 1 Bustani ya Edeni (Na. 246) [The
Doctrine of Original Sin Part I The
Garden of Eden (No. 246)].
Tangu wakati wa
kujaribiwa kwake Hawa kwenye Bustani ya Edeni, Shetani amekuwa akiudharau
uhusiano wetu na Mungu. Tumekuwa tukiwa tumejawa au kuzama kwenye imani za dini
za uwongo ya serikali kwa karne nyingi kadhaa.
Moja wapo ya njia
bora zaidi ya kuliharibu taifa ni kuiharibu familia. Kwa kipindi cha zaidi ya
miongo kadhaa michahche ndoa imekuwa ikishambuliwa kwa kiwango endelevu. Sio
tuhuma tena kwa watu kuishi pamoja wakiwa nje ya ndoa. Sio uhalifu tena kuishi
kiuhusiano wa watu wa jinsia moja. Paulo ailiita hii kuwa ni mafundisho ya mashetani, ambayo yalipelekea
utata katika Siku za Mwisho (soma
jarida la Mafundisho ya Mapepo ya Siku za Mwisho (Na. 48) [The Doctrines of Demons of
the Last Days (No. 48)].
Lengo ni kuiharibu
jamii na kisha kuharibu maono na tumaini na usalama wa kizazi kijacho.
Kushambuliwa kwa dhana uumbaji pia kunaharibu maono na tumaini. Kama hakuna
kiumbe, je, kutakuwa na lengo gani katika maisha?
Uhusiano kati ya
mwanadamu na Mungu umeharibiwa na elimu potofu, ambayo matokeo tuliyonayo sasa
yamepelekea uwingi wa dini. Kuruhusu matendo ya ngono sio tu kuwa kunaharibu
uhusiano, bali pia kunaathiri afya ka mwili na ya kiroho katika taifa na ustawi
wa kizazi kinachofuatia.
Tunajionea,
kuongezeka kwa machafuko. Mabishano ya majumani yanaendelea katika machafuko au
malumbano ya kimwili, kusababisha majeraha kwa wake na watoto. Kuongezeka kwa
kiwango cha kutalikiana kutokana na machafuko kunakoleta athari ya sehemu zote
mbili, yaani kwa wanandoa na watoto.
Uonyeshaji wa machafuko
unaofanywa na waendesha vyombo vya habari kunaathiri hisia na akili zetu.
Watoto wetu hawanahofu tena ya kuu. Wamelion hilo kwenye taarifa za habari,
wanayaona hayo kwenye mikanda ya video na kwene michezo yao ya Kompyuta. Ni programu
za kuwaharibu mioyo yao, na mwendendo wao na maadili yao yote yanakuwa
yameharibiwa pia.
Kuna upungufu
kwenye dhana ya kuogopa kutoa uhai. Euthanasia ameelezewa au kusemangwa sana
katika miaka ya hivi karibuni kujikinga na matendo ya kujamiiana hususan kwa
kutumia mwili wa vifaa bandia. Sadaka ya wanadamu ilikuwa ni kawaida kuitoa kwa
miaka mingi iliyopita na huenda inatolewa hadi leo. Sikuu zetu za serikali
hususan za Wamarekani, zimewekwa kwenye siku ambazo hutolewa sadaka hizi za
wanadamu za imani za kipagani.
Tunajionea pia
mmomonyoko wa maadili na sheria. Kunauhusiano na uvunjifu wa sheria au uhalifu,
na ongezeko la matendo ya dhambi. Baadhi ya maovu ‘yanakubalika’ sana kuliko mengine.
Biblia inasema kwamba kuivunja Amri moja ni sawa tu na kzivunja nyingine hizi zote.
Tunajionea
kukubalika na kushabikiwa kwa ukengeufu. Sheria zinazidi kubadilishwa ili
kuhalalisha ukengeufu fulani ufanyike. Aina nyingine fulani za ndoa sasa
zimehalalishwa. Matendo ya kuwahasili watoto kwa watu wanapokuwa kwenye
mahusiano ya namna hii kwa kuwa hawawezi kuzaa sasa kunaruhusiwa. Haya yote
yameandaliwa kwa lengo la kuiharibu familia, kuifanya ndoa isiwe kama
ilivyokusudiwa, na mahusiano bandia yaweze kukubalika.
Kuanzishwa au kuasisiwa
kwa ndoa
Mwanaume hakukusudiwa
awe peke yake. Hivyo, alipaswa kuwa na msaidizi (Mwanzo 2:18).
Mwanzo 2:18-25 Bwana
Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana
naye. 19 Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi
kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone
atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake. 20 Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege
wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu
aliyefanana naye. 21 Bwana Mungu akamletea Adamu
usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama
mahali pake, 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu
Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 23 Adamu
akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu,
basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. 24 Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye
ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja. 25 Nao
walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.
Hii ilikuwa ni
ndoa ya kwanza na Mungu alikuwa katikati yao na kiini cha ndoa ile, ni kama
alivyo kuwa yeye ni kiini cha ndoa zote.
Ndoa ni mahusiano
ya kiroho ya mwili mmoja. Kristo alikuwa na mengi ya kusema kuhusu hili na
alitoa msisitizo mkali sana kwa wateule kuhusu masuala ya ndoa na talaka (soma
jarida la Torati na Amri ya Saba (Na. 260) [Law and the Seventh Commandment (No. 260)].
Mathayo
19:1-12 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya
Uyahudi, ng'ambo ya Yordani. 2 Makutano mengi
wakamfuata, akawaponya huko. 3 Basi Mafarisayo
wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa
kila sababu? 4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya
kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, 5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye,
ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? 6 Hata
wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu,
mwanadamu asiwatenganishe. 7 Wakamwambia, Jinsi gani
basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha? 8 Akawaambia,
Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu;
lakini tangu mwanzo haikuwa hivi. 9 Nami nawaambia
ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati,
akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini. 10
Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai
kuoa. 11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao
kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa. 12 Maana
wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako
matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya
kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na
alipokee.
Kwenye muunganiko huu wa mwili inamaana
kwamba kila mmoja hapaswi kuwa amefungiwa
nira ya pamoja (KJV) au kuunganishwa (2Korintho 6:14-18).
2Wakorintho
6:14-18 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo
sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika
gani kati ya nuru na giza? 15 Tena
pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu
gani pamoja na yeye asiyeamini? 16
Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa
maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba,
Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao
watakuwa watu wangu. 17 Kwa
hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho
kichafu, Nami nitawakaribisha.18 Nitakuwa
Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,
Ndoa
kama Agano na Mungu
Kwa hiyo, muumini aliyebatizwa ana wajibu
wa kuoa ndani ya watu walio kwenye Imani yake, mwa muumini mwingine
aliyebatizwa, ili waweze kufanyika mwili mmoja katika Mungu kupitia kwa Yesu
Kristo. Uhusiano huu ni agano lililo ndani ya Mungu la kuvumilia na kuwa
mwaminifu sawasawa na Amri za Mungu.
Uzaaji
wa Watoto
Ndoa haimaanishi
kuwa ipo kwa ajili ya kuzaa watoto eke yake. Ingawaje hata hivyo kumetolewa
wito kwa kusema zaeni na mkeongexeke na
kuijaza nchi, kuzaa watoto kwa kweli ni sehemu au jambo muhimu sana katika
ndoa. Uzaaji wa watoto nje ya ndoa unashughulikiwa kwa mujibu wa sheria
zinazohusiana na uzinifu na ukahaba (soma jarida la Torati na Amri ya Saba (Na. 260) [Law and
the Seventh Commandment (No. 260)]. Amri ya Sita inashughulika na sio tu na umuhimu
wa kutoua, bali pia na mwajibiko wa kuyalinda maisha kiumakini. Maisha ya
watoto waliokulia nje ya ndoa kwa namna nyingi sana wanaonekana kuwa kama
waliokosa fursa njema na wa daraja la chini. Na ndivyo ilivyo pia kwamba
kiwango cha maisha kinakuwa duni kwa watoto ambao utalikiano unatokea kwa
wazazi wao. Sio kwa tatizo la kiuchumi tu peke yake yanayowakabili watoto hawa
walio kwene maisha au familia ya mzazi mmoja ambalo ndilo tatizo kubwa; bali
pia ni ile hali ya kuwakosa wapendwa wao na mwajibiko mzuri wa kifamilia ambao
kwa kweli unayaathiri maisha yao.
Kristo aliongelea
kuhusu uhusiano fulani wa maisha ya nyumbani kwenye Yohana 4:16-18.
Yohana 4:16-18
Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa. 17 Yule mwanamke
akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume; 18 kwa maana
umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema
kweli.
Kristo kwa wazi
kabisa anaiona tofauti kati ya ndoa na ‘umakini’ au halia halisi inayotakiwa kwenye
mahusiano ya kindoa.
Ndoa inaonekana
kwamba nMi ya muhimu sana kimwili. Hakuna kuoana baada ya Ufufuko wa Pili wa
Wafu (Mathayo 22:29-30). Hata hivyo, tunatakiwa kuangalia mambo ya kiroho
kuhusu ndoa kabla hatujaangalia mambo ya kimwili, kwa sababu mambo yote yana
maana za kiroho—na hatupaswi kukosea mwelekeo kuhusu mambo haya.
Israeli wameolewa
na Mungu. Kanisa limeolewa na Masihi, ambaye ndiye alikuwa Yahova wa Agano la
Kale. Mataifa yote yanapaswa kuja katika Israeli wakiwa kama Hekalu la siku
zijazo la Mungu wakiwa chini ya Kuhani wao Mkuu, ambaye ndiye elohim wa Israeli
(soma Zaburi 45:6-7 na Waebrania 1:8-9; na jarida la Torati na Amri ya Saba (Na. 260) [Law and the Seventh Commandment (No. 260)].
Waumini wote watu
wazima waliopo na waliobatizwa (tangu umri wa miaka 20) ni sehemu ya Mwili wa
Kristo. Ni kama wengine wote walivyo kuwa ni bibi arusi wa Kristo (soma jarida
la Baragumu (Na. 136) [Trumpets (No. 136)] Sehemu ya II: Ushirika wa Meza ya Bwana
ya Mwanakondoo).
Kristo hakuoa
kama mwanadamu hapa Duniani kwa kuwa alikuwa amekwisha lichumbia Kanisa, ambalo
ni wale walio sehemu ya Mwili wa Kristo. Uchumba, kama unavyoelezewa hapo juu,
ni ndoa ya mahiri ambayo kwayo ahadi zinakuwa zimetolewa. Kuelewa jambo hili ni
muhimu sana, ni kama ndoa za duniani zinafanya taswira ya mambo ya mbinguni.
1Wakorintho
11:3 Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa
cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu
Mwanamke ni mfano
wa Kanisa na hiyo linapaswa kuonyesha mfano mzuri. Mwanamume aliya mfano wa
Kristo anapaswa pia awe na mwenendo ulio sawasawa na vile alivyo Kristo na
anavyowajibika kwa Mungu, kwa hiyo mwanaume ni wa Kristo, na mwanamke ni wa
mwanaume—na wote ni wa Mungu. Mungu anawafungamanisha wote hawa amoja, akiwa yeye
ni yote katika yote kupitia Roho Mtakatifu.
Kristo akiwa kama kichwa
cha mwanaume
Kristo ni mfano
tuliopewa. Tulipewa ili awe ‘taswira’. Akiwa kama Malaika wa Mungu, alitolewa
kwetu kama seti ya Sheria na kanuni ambazo tunaziishia. Sheria hivi tumepewa
kwa faida ya afya za miili yetu, kujenga mwili na kuburudika, kuvaa, kupumzika,
kujikinga na kujikinga na magonjwa, na pia kwa mahusiano yetu ya kuwahudumiana
kila mmoja na mwingine. Biblia inmeandikwa mambo yote yahusuyo maisha yetu na
jinsi ya kuyaachilia kwa mujibu wa Sheria. Kristo kama mwanadamu alituonyesha
jinsi ya kuziishia sheria hizo. Alikufa bila kufanya dhambi. Alituonyesha mfano
kwamba yeyote apendaye kuwa bwana na mkubwa inampasa kuwatumikia wengine (Yohana
13:12-15); na kwamba hakuna upendo mwingine ulio zaidi ya mtu kuutoa uhai wake
kwa ajili ya rafiki zake (Yohana 15:13). Kwa mambo yote, alikuwa mwaminifu kwa
Mungu. Hii ni hatua kubwa zaidi ya kuwa mtii kwa Mungu.
Mwanaume kama kichwa cha
mwanamke
Waefeso
5:24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo
hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
Mamlaka aliyopewa
mwanaume ni kwa manufaa ya mke wake na familia yake na sio kwa ajili ya kujingeza
kwake mwenyewe. Mke wake sio mtumwa kwake, bali ni msaidizi wake, msaada wake. Soma
jarida la Mithali 31 hapo chini. Yeye ni mfano wa Kanisa na kwa kuwa yeye ni
mfano ambao familia yake itajifunza kutokana na mwajibiko wake kwa Mungu. Soma
jarida la Mithali 31 (Na. 114).
Maamuzi ya mume
yanapaswa yafanyike baada ya kujadiliana kirefu na kwa kina na mke wake,
akimchkulia kuwa ni mtu mwenye busara apate ushauri na nasaha zake futa hekima
yake. Kwenye mahusiano ya kawaida ya kiafya, kila uamuzi unaotolewa unapaswa
uwe na makubaliano ya pamoja au ya pande zote mbili. Pale ambapo makubaliano
yanashikana, mwanaume anaweza kutoa uamuzi wa mwisho unaoonekana unaweza kuwa
na maslahi makubwa kwa familia yote. Huu sio unyenyekevu wa namna ya mtumwa na
bwana wake, lakini utii na unyenyekevu wa hiyari wa mwanamke kwenye mamlaka
aliyopo ni upendo.
Paulo anatuambia
kwamba wanawake wanapaswa kunyenyekea waume zao, lakini wanaume hawa nao
inawanapasa wawapende wake zao. Kumpenda Mungu maana yake ni kumtumikia Mungu
na kumuabudu yeye Mungu peke yake. Upendo wa mume ni kuhudumu kwa kumpa
mahitaji mke wake na hali hii inaweza kufananishwa na kazi ya ukombozi ambayo
|Kristo amelifanyia Kanisa.
Waefeso 5:21-33 Kwa
maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni
mwokozi wa mwili. 24 Lakini
kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika
kila jambo. 25 Enyi waume,
wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili
yake; 26 ili
makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27 apate kujiletea Kanisa tukufu,
lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo
na mawaa. 28 Vivyo hivyo
imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe
hujipenda mwenyewe. 29 Maana
hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama
Kristo naye anavyolitendea Kanisa. 30
Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. 31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba
yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. 32 Siri hiyo ni
kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. 33 Lakini kila mtu ampende mke wake
kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.
Wanaume
inawanapasa wakuumbuke kwamba wake zao wana mahitaji maalumu. Na haya hasa ni kipindi kile wanachotumia
cha hedhi na cha kubeba mimba au cha ujauzito. Wanawake wanafanya mambo yaliyo
nje ya kawaida yao lakini waume zao wanapaswa kuwahakikishia wana amani ya kiroho na kihisia katika vipindi hivi. Mwanaume
anao wajibu wa kuangalia afya ya mke wake na kumhudumia inavyopaswa apone (soma
jarida la Utakaso na Tohara (Na. 251) [Purification and Circumcision (No. 251)].
Mume ana wajibu
wa mujimu kwa mambo yote yaliyo kwenye nadhiri yoyote aliyoiweka mke wake.
Hesabu 30:1-16 Kisha Musa akanena
na wale vichwa vya kabila za wana wa Israeli, na kuwaambia, Neno hili ndilo
aliloliagiza Bwana. 2 Mtu atakapomwekea Bwana nadhiri,
au, atakapoapa kiapo ili kufunga nafsi yake kwa kifungo, asilitangue neno lake;
atafanya sawasawa na hayo yote yamtokayo kinywani mwake. 3 Tena
mtu mke atakapomwekea Bwana nadhiri, na kufunga nafsi yake kwa kifungo, naye
aketi katika nyumba ya babaye, katika ujana wake; 4 babaye
naye akasikia nadhiri yake, na kile kifungo chake alichofungia nafsi yake, na
babaye akamnyamazia; ndipo nadhiri zake zote zitathibitika, na kila kifungo
alichofungia nafsi yake kitathibitika. 5 Lakini kama
huyo babaye akimkataza siku hiyo aliyosikia; nadhiri zake ziwazo zote, wala
vifungo vyake alivyoifungia nafsi yake havitathibitika; na Bwana atamsamehe,
kwa kuwa babaye alimkataza.6 Tena kama amekwisha
kuolewa na mume, wakati huo wa nadhiri zake, au wa neno hilo alilolitamka kwa
midomo yake pasipo kufikiri, alilojifungia; 7 na
mumewe akasikia, naye akamnyamazia siku hiyo aliyosikia neno hilo; ndipo
nadhiri zake zitathibitika, na vile vifungo ambavyo ameifunga nafsi yake
vitathibitika. 8 Lakini kama mumewe akimkataza siku
hiyo aliyolisikia; ndipo ataitangua nadhiri yake iliyo juu yake na neno
alilolitamka kwa midomo yake pasipo kufikiri, alilojifungia; na Bwana
atamsamehe 9 Lakini nadhiri ya mjane, au ya mwanamke
aliyeachishwa mume, kila neno ambalo ameifunga nafsi yake kwalo, litathibitika
juu yake. 10 Tena kama aliweka nadhiri nyumbani mwa
mumewe, au kama aliifunga nafsi yake kwa kifungo pamoja na kiapo, 11 na mumewe alisikia akamnyamazia, wala hakumkataza; ndipo
nadhiri zake zote zitathibitika, na kila kifungo alichojifungia kitathibitika. 12 Lakini kama mumewe alizibatilisha na kuzitangua siku hiyo
aliyozisikia, ndipo kila neno lililotoka midomoni mwake katika hizo nadhiri
zake, au katika kile kifungo cha nafsi yake, halitathibitika; huyo mumewe
amezitangua; na Bwana atamsamehe. 13 Kila nadhiri, na
kila kiapo kifungacho, ili kuitaabisha nafsi ya mwanamke mumewe aweza
kuthibitisha, au mumewe aweza kutangua. 14 Lakini
mumewe akimnyamazia mkewe kabisa siku hata siku ndipo azithibitisha nadhiri
zote za mkewe, au vifungo vyake vyote vilivyo juu yake; yeye amezithibitisha,
kwa kuwa alimnyamazia mkewe siku hiyo aliyozisikia nadhiri zake. 15 Lakini akizibatilisha na kuzitangua baada ya kuzisikia;
ndipo yeye atachukua uovu wa mkewe. 16 Hizi ndizo
amri, ambazo Bwana alimwagiza Musa, kati ya mtu mume na mkewe, kati ya baba na
binti yake, katika ujana wake, ali nyumbani mwa babaye.)
Mume anawajibika
na usalama wa familia yake. Hii ni kwa namna zote mbili, usalama wa kiroho na
wa kimwili. Kwenye 2Wathesalonike 3:10, Mtume Paulo anasema kwamba mtu asiyefanya
kazi asile; nah ii inamaanisha kwamba mtu huyo familia yake haitakula pia.
Kufanya kazi kwa ajili ya familia na kufanya kazi kwa lengo la kulisaidia
Kanisa liihubiri Injili kwa mataifa yote yote haya ni sehemu ya agizo hili; mtu
aanatakiwa kutoa mahitaji ya kimwili ya familia, na wengine watoe chakula cha
kiroho kwa sehemu zote mbili, yaani kwenye familia na taifa na kwa wale
tunaopaswa kuwajibika kwao.
Pia, mtu Yule
asiyewatunza watu wa nyumbani mwake mwenyewe ni mbaya kuliko asiyeamini.
1Timotheo
5:8 Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake
hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.
Mwanaume
anatakiwa pia kuendeleza uhusiano wake na mke wake pindi anapomuona tu. Hiki ni
kipindi cha kujifunza kuishi pamoja kwa upendo na utangamano.
Kumbukumbu
la Torati 24:5 Mtu atwaapo mke mpya, asiende vitani pamoja na jeshi,
wala asipewe shughuli juu yake yo yote; akae faragha mwaka mmoja nyumbani
mwake, apate mfurahisha mkewe aliyemtwaa.
Mahali ambapo
mamlaka ya kibiblia yanapovunjika, na hali ya kumjua au kucha Mungu na kuzijua
Sheria zake kunapoondoa, matokeo yake ni kama tunayoyaona sasa. Ndoa zina
vunjika, mahusiano yanakoma, watoto wanachukuliwa kwenda kulelewa na mtu
mwingine na babu na bibi wanapoteza wajukuu zao. Familia inagawanyika na
kusambaratika kutokana na talaka na kuachana, kama inavyofanywa na mataifa
kuungezea uwezekano wa kutokea matatizo haya kwa makusudi kwa kuziondolea mbali
Sheria za Mungu. Matokeo yake ni kuwepo kwa mapigano au vita, yawe ndani ya
familia, jamii au kuenea katika nchi yote.
Kile Biblia
kinachotufundisha ni kwamba ndoa iliingizwa kwenye Sheria za Mungu kwa kuwekewa
msisitizo mkubwa sana wa uhusiano wenye afya, watoto wenye furaha, ambao watakua
kwenye utu uzima wakiwa kwenye mazingira salama na waweze kuwafundisha watoto
wao njiaa bora ya kuishi, wakiwa chini ya Sheria za Mungu.
Lakusikitisha mno
ni kwamba, siyo mamlaka zote zimewekwa na Mungu ni waaminifu, na ndiyo maana
hatuna hata jamii yoyote leo inayoishi chini ya dhana yenye utaratibu imewekwa
hapa chini duniani kwetu pamoja nasi. Wale walio nasi wanaojaribu kuziweka
Sheria za Mungu kwa ajili ya maongozi ya maisha yetu wamekuwa wakiteswa na
kuangamizwa kwa kipindi cha maelfu ya miaka na wataendelea kuteswa hivyohivyo
hadi atakaporudi Kristo. Lakini hilo lisituzuie sisi.
Kwa hiyo, ndoa
inapaswa ijengwe kwenye msingi imara, na inatakiwa pia ijengwe kwenye uelewa wa
kina wa Sheria za Mungu. Waume na wake wanatakiwa wasome kwa amoja neno la
Mungu. Kimtazamo na uelewa, mwanaume lazima aw na ukomavu na mahiri, na mwenye
kuweza kumhudumia mke wake kifedha, kihisia au mawazo na kiroho. Anapaswa
kuweze kuendeleza na kuweka sawa heshima ya mke wake na ni lazima amhakikishie
uwezo wake wa kumpenda. Mungu anachukia kuachana, ni kitendo kiovu kumfanyia
mke wake na watoto wake wengine wote walionao. Kugunduliwa kwa matendo ya zinaa
ndiyo kitu pekee kilichotolewa ruhusa ya kuatalikiana. Uzinifu ni uvunjifu wa
Amri ya Saba. Uwongo, wizi kushuhudia au kusema uwongo, na kumtamani mke wa
jirani, mali na rasilimali zake kunaharibu heshima yoyote iliyokuwepo kati ya
mtu mmoja na mwingine. Kitendo cha kutomtenda vyema wu kumfanyia ukatili mke
wake, kunaonesha kuwa mwanaume huyu hampendi kama inavyompasa kufanya. Anapaswa
kumpenda kama kama aupendavyo mwili wake mwenyewe. Ni kama ilivyo kwa mtu
anapokuwa anaumwa hawezi kujipiga au kujidhalilisha, ndivyo vivyohivyo mwanaume
hatakiwi kuonyesha aina hiyo ya udhalilishaji kwenye maisha ya ndoa mbele za
watu walio kwenye familia yake.
Wajibu na majukumu ya mke
1Wakorintho
11:11-12 Walakini si mwanamke pasipo mwanamume, wala mwanamume pasipo mwanamke,
katika Bwana. 12 Maana kama mwanamke alitoka katika
mwanamume, vile vile mwanamume naye huzaliwa na mwanamke; na vitu vyote asili
yake hutoka kwa Mungu. Hukumuni ninyi wenyewe katika nafsi zenu.
Mwanamke ni
msaidizi wa mwanaume, mshiriki mwenza wake, wa kufanana naye. Kwa hiyo, ingawa
kimtazamo wanaonekana kuwa kama wako sawasawa kimila na mwonekano, ni muhimu
sana wawe na makubaliano kwa mambo ya imani za kidini. Kunapotokea kuwepo
tofauti kwenye masuala ya ukiri wa imani, kunahatari kwamba mmoja wapo anaweza
kuwapeleka wenzake kwenye ibada za sanamu. Ubada za sanamu zinauhusiano wa
karibu sana na matendo ya zinaa na uasherati.
Majukumu ya
mwanamke yameonyeshwa kwenye Mithali 31.
Mithali 31:10-31 Mke mwema, ni nani awezaye
kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani. 11 Moyo
wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato. 12 Humtendea mema wala si
mabaya, Siku zote za maisha yake. 13 Hutafuta sufu na
kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo. 14 Afanana na merikebu za
biashara; Huleta chakula chake kutoka mbali. 15 Tena
huamka, kabla haujaisha usiku; Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula; Na
wajakazi wake sehemu zao. 16 Huangalia shamba, akalinunua;
Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu. 17 Hujifunga
nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu. 18 Huona
kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku. 19 Hutia
mikono yake katika kusokota; Na mikono yake huishika pia. 20 Huwakunjulia
maskini mikono yake; Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake. 21
Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake; Maana wote wa nyumbani mwake
huvikwa nguo nyekundu. 22 Hujifanyia mazulia ya
urembo; Mavazi yake ni kitani safi na urujuani. 23 Mume
wake hujulikana malangoni; Aketipo pamoja na wazee wa nchi. 24
Hufanya nguo za kitani na kuziuza; Huwapa wafanya biashara mishipi. 25 Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake; Anaucheka wakati ujao. 26 Hufumbua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema i
katika ulimi wake. 27 Huangalia sana njia za watu wa
nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu. 28 Wanawe
huondoka na kumwita heri; Mumewe naye humsifu, na kusema, 29 Binti
za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote. 30 Upendeleo
hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye
atakayesifiwa. 31 Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu
malangoni.
Anaaminiwa na
mume wake, anaitunza vyema nyumba na watu wa nyumbani mwake, na ananunua na
kuuza, na anaweza kuendesha biashara. Anajali mambo na mahitaji ya familia yake, maskini na wahitaji. Anabusara
na mwema. Sio mvivu wala mzembe. Mumewe na watoto wake humsifu. Hizi ni sifa
nzuri anazotakiwa kuwanazo. Kumbuka kuwa mwanamke ni taswira ya Kanisa pia. Kwa
ujumla tu tuseme kwamba ataweza kufanya mabo haya yote kama atakuwa mtiifu na
mnyenyekevu kwa Mungu. Akiwa peke yake, mwanamke anawazia jambo hili na ataweza.kwa
masaada wa Mungu na mume wake (pia soma
majarida ya Mithali 31 (Na. 114) na Majukumu ya Mwanamke Mkristo (Na. 62) [Proverbs 31 (No.114)
and Role of the Christian Woman (No.
62).
Wanawake wasipende kutangulia kuzifanya kazi zinazopaswa kufanywa na waume zao. Yeye anatakiwa kuihudumia familia yake, na ajishushe kwa kukubali kuwa nafasi ya chini kazini, vinginevyo kujikweza kwake kazini kwake na tendo la kumuachia kufanya maamuzi na kazi zote, ni ishara ya huyu mwanaume kujidharau yeye mwenyewe. Moja wapo ya majukumu ya mwanamke ni kumuinua na kumtia moyo mume wake. Kwa kitendo hiki cha kumtia moyo anaweza kuketi ‘malangoni’. Hii inamaana ya kumudu kuyatenda majukumu kwenye jamii na kuwa sehemu ya watoa maamuzi akiwa kama mwanachama au mjumbe mwenye kuheshimika kwenye jamii husika.
Mke anapaswa kumsaidia mume wake katika mambo yote. Mara tu baada ya kufanyika maamuzi, ndipo wajibu wao wote wawili kuifanya ifanyike. Mahali pasipo na umoja au ushirikiano kati ya wazazi wote wawili, ni watoto ndio wanaoteseka. Kutakuwa na mtangamano kwenye malezi na nidhamu.
Unyenyekevu na utii kwa mke ni jambo muhimu sana. Kwa kweli hali ya kutokuwa na utii na unyenyekevu kunapelekea mwanaume kuwa mzinifu. Kuna matukio mengi sana ambapo mke ameifanya huduma ya utumishi impe umaarufu kiasi kwamba imemfanya aone kama yuko mbele zaidi ya mume wake. Makasisi na watumishi hawa wamehamasisha kwa makusudi uhusiano wa aina yake wa kiuasherati. Hii inapata mwanya wakati huduma ya ushauri nasaha inatakiwa iwepo Kanisani na iwapo kam itafanyika na mtu mmoja tu wa Kanisani inapohitajika. Aina yoyote ya huduma ya ushauri wa mambo ya ndoa Kanisani inatakiwa ifanyike wakiwepo wanandoa wote wawili, vinginevyo tatizo halitaweza kutatuliwa.
Wanawake wazee wanatakiwa kuwatia moyo mabinti vijana na kuwashauri mabinyi walioingia kwenye ndoa mpya.
Tito 2:3-5 Vivyo hivyo na
wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye
kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema; 4 ili
wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; 5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbanimwao,
kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.
Moja ya jukumu
kubwa sana la mke ni kujua majukumu ya umama. Kuhusu watoto ni kazi kubwa sana
kuliko lililoko, kama ilivyo hatima ya mataifa. Kama wazazi wakishindwa kuwalea
watoto kuwa wananchi wawajibikaji, wazijue Sheria za Mungu na waish maisha ya
utii kwao, ndipo watashindwa. Hatuwezi kubeba jukumu ka maamuzi wanayoyafanya
wanapokuwa watu wazima, ila tunaweza kuchukua jukumu la kuwafundisha Sheria za
Mungu na kisha kuwapa fursa ya kufanya maamuzi sahihi na kuishi maisha ya
kumcha Mungu.
Majukumu na
wajibu huu upo pia kwenye mifumo ya elimu. Hawakufundishwa Amri za Mungu kwa
kuwa waalimu we nyewe hawazijui hizi Sheria za Mungu. Je, wanazishika na
kuziadhimisha Sabato za Mungu? Je, wanafundisha Sikukuu zilizoamriwa na Mungu
na Siku nyingine Takatifu? Au wanafundisha tu kuhusu miungu wa kipagani, pamoja
na maadhimisho ya siku za kuzaliwa, Krismasi, Easter, Siku za Mizimu zinazoitwa
Halloween na siku nyingine kama hizo za kipagani? (Soma majarida ya Msalaba: Chanzo Chake na Maana Yake (Na.
39); Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235); Pinata (Na. 276; Sherehe za Kuzaliwa Mtu (Na. 287) [The Cross: Its
Origin and Significance (No. 39); The Origins of Christmas and Easter (No. 235); The Pinata (No. 276); Birthdays (No. 287)]. Watoto wetu hawapewi fursa wanayostahili.
Tunatakiwa kuwahakikishia watoto wetu kzijua Amri za Mungu
Wajibu wa watoto
Kumbukumbu
la Torati 5:16 Waheshimu baba yako na mama yako; kama Bwana, Mungu wako,
alivyokuamuru, siku zako zipate kuzidi, nawe upate kufanikiwa katika nchi
upewayo na Bwana, Mungu wako.
Amri ya Tano ni
ya muhimu sana. Sio tu kwamba inatupeleka kwenye uhusiano kati ya watoto wadogo
na wazazi wao. Bali pia inawahusisha watu wazima na kuwafundisha uhusiano wao
kwa wazazi wao ambao ni wazee wao walio kwenye jamii zao, pia inatuchukua sisi
sote hadi kwenye mahusiano yetu na Baba yetu wa Mbinguni na kwa Kanisa.
Kama ilivyoelezwa
huko nyuma, wazazi wanatakiwa wawafundishe watoto wao Sheria za Mungu.
Wanatakiwa wawafundishe kwa bidii zao zote. Wazazi wanatakiwa pia kujiangalia
mienendo yao wenyewe kwa kuwa ndipo hawa watoto ndipo watakapowatii na
kuwaheshimu. Watoto ni rahisi sana kwao kugundua udhaifu au mwenendo mbaya na
unafiki ukifanyika. Tusitegemee watoto kufanya tunato waagiza kufana iwapo kama
sisi wenyewe hatutawaonyesha kuwa tunaishi hivyo huku tukiishi kinyume chake
kabisa.
Mithali 4:1-27 Wanangu, yasikilizeni mausia ya
baba yenu, Tegeni masikio mpate kujua ufahamu. 2 Kwa
kuwa nawapa mafundisho mazuri; Msiiache sheria yangu. 3 Maana
nalikuwa mwana kwa baba yangu, Mpole, mpenzi wa pekee wa mama yangu. 4 Naye akanifundisha, akaniambia, Moyo wako uyahifadhi
maneno yangu; Shika amri zangu ukaishi. 5 Jipatie
hekima, jipatie ufahamu; usiusahau; Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu. 6 Usimwache, naye atakuhifadhi; Umpende, naye atakulinda. 7 Bora hekima, basi jipatie hekima; Naam, kwa mapato yako
yote jipatie ufahamu. 8 Umtukuze, naye atakukuza; Atakupatia
heshima, ukimkumbatia.9 Atakupa neema kuwa kilemba
kichwani; Na kukukirimia taji ya uzuri. 10 Mwanangu,
sikiliza, na kuzipokea kauli zangu; Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi. 11 Nimekufundisha katika njia ya hekima; Nimekuongoza katika
mapito ya unyofu. 12 Uendapo, hatua zako
hazitadhiikika, Wala ukipiga mbio hutajikwaa.13 Mkamate
sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako. 14 Usiingie katika njia ya waovu, Wala usitembee katika njia
ya wabaya. 15 Jiepushe nayo, usipite karibu nayo, Igeukie
mbali, ukaende zako. 16 Maana hawalali isipokuwa
wametenda madhara; Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu. 17 Maana wao hula mkate wa uovu, Nao hunywa divai ya jeuri. 18 Bali njia ya wenye haki ni kama nuru ing'aayo, Ikizidi
kung'aa hata mchana mkamilifu. 19 Njia ya waovu ni
kama giza; Hawajui ni kitu gani kiwakwazacho. 20 Mwanangu,
sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu. 21 Zisiondoke machoni pako; Uzihifadhi ndani ya moyo wako. 22 Maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao
wote. 23 Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana
ndiko zitokako chemchemi za uzima. 24 Kinywa cha
ukaidi ukitenge nawe, Na midomo ya upotovu uiweke mbali nawe. 25 Macho yako yatazame mbele, Na kope zako zitazame mbele
yako sawasawa.26 Ulisawazishe pito la mguu wako, Na
njia zako zote zithibitike; 27 Usigeuke kwa kuume wala
kwa kushoto; Ondoa mguu wako maovuni.
Mithali imejaa
utajiri mkubwa wa ushauri wenye busara, sio kwa vijana peke yao tu, bali ni
hata kwa mtu mzima na mzee pia.
Ni muhimu pia
kwamba watoto wafundishwe maana ya ndoa kwa maana linganisho na Agano la Mungu.
Wakiwa watoto wanakuwa wametakaswa kupitia kwa wazazi wao, lakini wanapotimiza
umri wa miaka 20 wanaanza kuwajibika wenyewe kwa mambo ya imani na uhusiano wao
na Mungu na wanaanza kuwa sehemu ya mabibi arusi wa Kristo. Wazazi wanatakiwa kuwatia
moyo na kuwahamasisha watoto wafanye hivyo. Kuwatenga watoto kwa kutowafundisha
na kuwashrikisha kumjua Mungu na Torati yake ni kuwatenga mbali na fursa yao ya
kuwepo kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu. Wakati Mungu atakapokuwa anaingilia
kati sawa na mapenzi yake, tunabakia kuwa ni wajibu wetu wa kuwafundisha vijana
wetu kikamilifu na kiusahihi.
Watoto
waliolelewa na wazazi wasioelewana, waasi wasiomtii Mungu au waliotalikiana, hawataweza
kukua wakiwa na uelewa sahihi kama inavyotakikana. Watoto waliolelewa na mzazi
mmoja au walio na malezi ya upande mmoja wanakosa huduma ya kimalezi muhimu
iliyotakiwa kutolewa na mmoja wa wazazi hawa, kati ya mama au baba na inakuwa
ni wajibu wa Kanisa sasa kuwasaidia. Washirika wa kanisa wanatakiwa kuwa mfano
mzuri kwa watoto wanaotoka kwenye aina hii ya malezi ya upande mmoja, kwa
kuwaonyesha ukarimu na urafiki. Kanisa linaweza kuwapa huduma za kijamii ili
kuwahamasisha maendeleo ya kirafiki miongoni mwa vijana. Watoto wahamasishwe
kuwaalika marafiki hawa majumbani mwao.
Ndoa na mwenzi asiyeamini
Ndoa nyingi
hufungwa mapema kabla ya wanandoa hawajaitwa na kuingia kwenye Imani, na
pengine zinafanyika wakati mmoja wa wanandoa akiwa ameitwa na kuingia kwenye
imani huku mwingine akiwa hajaamini. Hii inasababisha matatizo mengi kwenye
maisha haya ya ndoa. Huyu mmoja aliyeitwa anatakiwa kuwa mvumilivu sana na
makini. Mwanandoa ambaye hajaitwa bado hawezi kujua umuhimu wa kumuweka Mungu
kwenye kipau mbele cha mambo yao kwa kila kitu. Watajikuta kila mara wanatofautiana
kwenye mambo kadhaa ya mambo ya ndoa yao. Mfano ni kwamba mume anaweza kupeleka
hela Kanisani huku mke akiona kuwa zingefaa kwa matumizi ya familia. Wanawake
kuwaacha waume zao wasioongoka nyumani, na hata wakati mwingine watoton wao pia
wanapojihudhurisha kwenye Sikukuu na Siku nyingine Takatifu zilizoamriwa.
Hawashindi huko kwa masaa machache kama wanavyofanya Kanisani, bali wanakaa
huko kwa juma moja na takriban mara
mbili kila mwaka! Je, wezi wao wasioamini watawaelewaje wanapofanya hivyo?
Tatizo kubwa zaidi ni matika kutoa maamuzi juu ya watoto kuwa watakuwa
wanafundishwa mafundisho ya dini gani.
Mtume Paulo anasema
katika 1Wakorintho 7:12-16:
Lakini
watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke
asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache. 13 Na
mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye,
asimwache mumewe. 14 Kwa maana yule mume asiyeamini
hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama
isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu. 15 Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo
ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani. 16 Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo?
Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?
Wakati Paulo akikiri
hili kuwa siyo Roho Mtakatifu, ndiye mshauri mkuu.
Talaka
Marko
10:2-12 Basi
Mafarisayo wakamwendea, wakamwuliza, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe? Huku
wakimjaribu. 3 Naye
akajibu, akawaambia, Musa aliwaamuru nini? 4 Wakasema, Musa alitoa ruhusa
kuandika hati ya talaka na kumwacha. 5
Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia
amri hii. 6 Lakini tangu
mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke. 7 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha
babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; 8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja;
hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.9 Basi alichokiunganisha Mungu,
mwanadamu asikitenganishe. 10 Hata
nyumbani tena wanafunzi wakamwuliza habari ya neno hilo. 11 Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha
mkewe na kuoa mwingine azini juu yake; 12 na mke, akimwacha mumewe na
kuolewa na mtu mwingine, azini.
Hapa Kristo anaifafanua
sheria inayohusu talaka.
Kwenye 1Wakorintho
7:10-11, Paulo anasema:
1Wakorintho
7:10-11 Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana;
mke asiachane na mumewe; 11 lakini, ikiwa ameachana
naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.
Talaka ni
machafuko. Biblia inautaja uzinifu kuwa ni dhambi pekee. Uzinzi wa kiroho ni
ibada ya sanamu. Katika uhusiano wetu kwa Mungu, talaka maana yake ni kifo.
Kwenye uhusiano wetu kwa kila mmoja na mwenzake ni uharibifu wa maisha yetu na
maisha ya watoto wetu. Watoto wanaweza kugawanyika au kusambaratika wakiwafuata
mmoja na wengine kwa mwingine, wakichukua maamuzi ya kuachana aitha na baba yao
au mama yao, hata na bibi na babu zao na watu wengine walio kwenye ukoo wao.
Mara nyingi wamekuwa wakijilaumu wenyewe.
Ni Amri ya Mungu
isemayo kwamba hakuna anayeruhusiwa kumtaliki mwenzake, sio mwanaume wala mwanamke,
hakuna aliyeruhusiwa kumtaliki mwenza wake kwa kisingizio kwamba mwenzi wake wa
ndaa haamini imani yake au hajaongoka. Familia inatakaswa kwenye ndoa na mwamini
hataweza kamwe kujua ni kwa jinsi gani au iwapo kama ni mfano wa maisha yao
ndio unaushuhuda wa nguvu kwa waumi wengine wa familia. Hata hivyo, kama mwezi
asiye amini akiamua kuondoka, basi talaka hapo haitaepukika na itaruhusiwa
kutolewa.
Kunapokuwa na
hali ya kudhalilishwa kati ya wanandoa na watoto, hakuna umuhimu wa kuishi
maisha ya namna hiyo. Mwenzi mdhalilishaji ajue kwamba kitendo cha namna hiyo
hakiwakilishi wajibu au majukumu yake, na iwapo kama ushauri nasaha umeshindikana
kufua dafu kukomesha hali hii, basi usalama na utawi wa familia unapaswa kuchukuliwa.
Ndipo inaweza kuonekana kuwa ni busara kutalikiana kuruhusiwe.
Kuoa mara ya pili au
ndoa ya pili
Warumi 7:2-3
Ndugu zangu, hamjui
(maana nasema na hao waijuao sheria) ya kuwa torati humtawala mtu wakati
anapokuwa yu hai? 2 Kwa
maana mwanamke aliye na mume amefungwa na sheria kwa yule mume wakati anapokuwa
yu hai; bali akifa yule mume, amefunguliwa ile sheria ya mume. 3 Basi wakati awapo
hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa,
amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume
mwingine.
Kama mwanaume
akimuacha kwa kumtaliki mkewe, basi asioe tena. Kama atakuja kutubu, basi
atashauriwa kumrudia mke wake huyohuyo wa zamani na kumuoa tena.
Wakati ndoa
inapokuwa ni ya kufungiwa nira na asiyeamini, ambavyo ni, wakati mmoja ya
wanandoa anapokuwa hajaitwa bado na kuongoka na akachagua kuivunja ndoa hii na
kutalikiana, ndipo mwingine aliyebaka anaruhusiwa na yuko huru kuoa au kuolewa
tena.
Maisha ya useja ya bila
kuoa
Ndoa ni uhusiano
huru uliokubalika kati ya mwanaume na mwanamke. Mwanaume hakukusudiwa aishi
peke yake. Hata hivyo, kuna mazingira ya namna mbalimbali kadhaa yanayopelekea
hali hii kutowezekana. Sio dhambi kabisa kwa mtu akiamua kusihi bila kuoa.
Mathayo
19:12 12 Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo
toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa
matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme
wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.
Hata hivyo, ni
dhambi kukataza watu kuoana.
1Timotheo
4:1-3 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga
na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; 2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri
zao wenyewe; 3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru
wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio
na imani wenye kuijua hiyo kweli.
Paulo alitoa
ushauri mwingi tu kuhusu jambo hili.
1Wakorintho 7:27-40 Je! Umefungwa kwa mke? Usitake
kufunguliwa. Umefunguliwa? Usitafute mke. 28 Lakini,
kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama
hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo. 29 Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi
tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana; 30 na
wale waliao kama hawalii; na wale wafurahio kama hawafurahi; na wale wanunuao,
kama hawana kitu. 31 Na wale wautumiao ulimwengu huu,
kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita. 32 Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa
hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana; 33 bali
yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza
mkewe. 34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na
mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa
mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya
dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe. 35 Nasema
hayo niwafaidie, si kwamba niwategee tanzi, bali kwa ajili ya vile
vipendezavyo, tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine. 36 Lakini mtu awaye yote akiona ya kuwa hamtendei mwanamwali
wake vipendezavyo, na ikiwa huyo amepita uzuri wa ujana wake, na ikiwapo haja,
basi, afanye apendavyo, hatendi dhambi, na awaruhusu waoane. 37
Lakini yeye aliyesimama kwa uthabiti wa moyo wake, hana sharti, lakini
aweza kuyatawala mapenzi yake, tena amekusudia moyoni mwake kumlinda mwanamwali
wake, atatenda vema. 38 Basi, hivyo na amwozaye
mwanamwali wake afanya vema; na yeye asiyemwoza atazidi kufanya vema. 39 Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa
mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu. 40 Lakini heri yeye zaidi akikaa kama alivyo; ndivyo
nionavyo mimi, nami nadhani ya kuwa mimi nami nina Roho wa Mungu.
Maandiko haya yamekuwa
yakipotoshwa maana yake. Mawazo na ushauri wa Paulo hapa ni kwamba mtu anaweza
kuishi maisha au hali ambayo mtu alikuwa anaishi kwayo—ambayo ni kwamba, kama
alikuwa ameoa aendelee kuishi na ndoa yake na kama alikuwa hajaoa na aendelee
kuishi bila kuoa. Hakuna dhambi yoyote kuishi hivyo kabisa. Ila uamuzi huu wa
kujitolewaa kuishi hivyo kusichukuliwe kwa kumaanisha kuwa Paulo hakuwa
anachukia ndoa au kuwachukia wanawake. Wakati ule alionekana kuamini kwamba
kurudi kwake Kristo kulikuwa kumekaribia mno na aliweka msingi wa ushauri wake
kwenye mtazamo wa namna hiyo. Anaendelea kwa kutoa ushauri wa ndoa imara.
Aliendelea kuweka mahitaji ya muunganiko wa kwanza wa hiyari, muungano wa
wanandoa, ambapo unawafanya kuwa ni mwili mmoja.
Uhusiano uliokatazwa
Haya ni maonyo na
maelekezo yanayozuia kuwa na ndoa bora.
Mambo ya Walawi 18:1-30 Bwana akanena na Musa, na
kumwambia, 2 Nena wewe na wana wa Israeli, uwaambie,
Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. 3 Nanyi msifanye matendo
kama yale ya nchi ya Misri mliyokaa; wala msifanye matendo kama yale ya nchi ya
Kanaani, nitakayowapeleka; wala msiende katika amri zao hao. 4
Mtazifanya hukumu zangu, nanyi mtazishika amri zangu, ili mwenende
katika hizo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. 5 Kwa ajili
ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo mtu akizitumia ataishi
kwa hizo; mimi ndimi Bwana. 6 Mtu ye yote aliye wa
kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu;
mimi ndimi Bwana. 7 Utupu wa baba yako, wala utupu wa
mama yako, usifunue, maana ndiye mama yako; usifunue utupu wake. 8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa
baba yako. 9 Utupu wa umbu lako, binti ya baba yako,
au binti ya mama yako, kwamba alizaliwa nyumbani mwenu au kwamba alizaliwa
kwengine, utupu wa hao usifunue. 10 Utupu wa binti ya
mwanao mume, au wa binti ya binti yako, utupu wao hao usifunue; kwa kuwa ndio
utupu wako mwenyewe. 11 Utupu wa binti ya mkewe baba
yako, aliyezaliwa na baba yako, yeye ni umbu lako, usifunue utupu wake. 12 Usifunue utupu wa umbu lake baba yako; maana, yeye ni
jamaa aliye karibu. 13 Usifunue utupu wa umbu la mama
yako; maana, yeye ni jamaa ya mama yako ya karibu. 14 Usifunue
utupu wa ndugu ya baba yako, usimkaribie mkewe huyo; yeye ni shangazi lako. 15 Usifunue utupu wa mkweo mwanamke; yeye ni mke wa mwanao;
usifunue utupu wake huyo. 16 Usifunue utupu wa mke wa
nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo. 17 Usifunue utupu
wa mwanamke na binti yake; usimtwae binti ya mwanawe mume, au binti ya binti
yake, ili kufunua utupu wake; hao ni jamaa ya karibu; ni uovu mkuu. 18 Wala usitwae mwanamke pamoja na nduguye, awe mtesi wake,
na kufunua utupu wake, huyo wa pili atakapokuwa yu hai. 19 Nawe
usimkaribie mwanamke kufunua utupu wake wakati wa kutengwa kwa ajili ya unajisi
wake. 20 Usilale na mke wa mwenzio, ukajitia unajisi
naye. 21 Nawe usitoe kizazi chako cho chote na
kuwapisha kwa Moleki, wala usilinajisi jina la Mungu wako; mimi ndimi Bwana. 22 Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni
machukizo. 23 Wala usilale na mnyama ye yote, ili
kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye;
ni uchafuko. 24 Msijitie unajisi katika mambo hayo
hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi
kwa mambo hayo yote; 25 na hiyo nchi imekuwa najisi;
kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi yatapika wenyeji
wake na kuwatoa. 26 Kwa hiyo mtazishika amri zangu na
hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala
mgeni aketiye kati yenu; 27 (kwa kuwa hao watu wa nchi
wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi
imekuwa najisi;) 28 ili kwamba hiyo nchi isiwatapike
na ninyi pia, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa
iliyotangulia mbele yenu. 29 Kwani mtu awaye yote
atakayefanya machukizo hayo mojawapo, nafsi hizo zitakazoyafanya zitakatiliwa
mbali na watu wao. 30 Kwa ajili ya hayo yashikeni
mausia yangu, ili kwamba msifanye kabisa desturi hizi zichukizazo mojawapo,
zilizotangulia kufanywa mbele zenu, wala msijitie unajisi katika mambo hayo;
mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Kuna maelekezo
zaidi kuhusu ukomo wa kuoa. Kuhani anatakiwa awe ni mume wa mke mmoja tu. Hii,
kwa kweli, ni sharti la maana hata kwa wateule. Mambo ya Walawi 21:7-15 inasema
kwamba kuhani au kasisi asioe mwanamke kahaba au Malaya au mwanamke aliyeachwa
kwa kutalikiwa. Tukiwa kama wateule tunapaswa kuangalia dalili au dokezo hili
na kujilinganisha na maisha yetu wenyewe, kwa kuwa tunakwenda kuwa wafalme na
makuhani.
Mahusiano yasiyo
ya kiasili ya maumbile aliyoyafanya Mungu yamekatazwa pia.
Mambo
ya Walawi 20:13 Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu
mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu
yao.
Tunaliona hili
pia kwenye Warumi 1:18-32:
Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka
mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu. 19 Kwa kuwa mambo
ya Mungu yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa maana Mungu
aliwadhihirishia. 20 Kwa
sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na
kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe
na udhuru; 21 kwa sababu,
walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea
katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza. 22 Wakijinena kuwa wenye hekima
walipumbazika; 23 wakaubadili
utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na
uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo. 24 Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha
katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili
yao. 25 Kwa maana
waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala
ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina. 26 Hivyo Mungu aliwaacha wafuate
tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi
yasiyo ya asili; 27 wanaume nao
vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume
wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki
yao. 28 Na kama
walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao
zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. 29
Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya;
wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye
kusengenya, 30 wenye
kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno,
wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, 31 wasio na ufahamu, wenye kuvunja
maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; 32 ambao wakijua sana hukumu ya haki
ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si
hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.
Aya ya 26 inaonyesha
kuwa hii inamaanisha pia mahusiano ya ndoa za mwanamke kwa mwanamke maarufu
kama usagaji.
Uhusiano kati ya mtu na
mwenzake
Mapepo wanajaribu
kupuuzia na kupotosha maana ya ndoa kwa lengo la kuyazuia mataifa yasiishike
Torati.
1Timotheo
4:1-3 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga
na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; 2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri
zao wenyewe; 3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru
wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio
na imani wenye kuijua hiyo kweli
Sisi sote
tunawajibika kuenenda na kuwatendea vyema watu wote kama familia.
1Timotheo
5:1-16 Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu; 2 wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa
kike; katika usafi wote. 3 Uwaheshimu wajane walio
wajane kweli kweli. 4 Lakini mjane akiwa ana watoto au
wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe,
na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu. 5 Basi yeye aliye mjane kweli kweli, ameachwa peke yake,
huyo amemwekea Mungu tumaini lake, naye hudumu katika maombi na sala mchana na
usiku. 6 Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa
ingawa yu hai. 7 Mambo hayo pia uyaagize, ili wasiwe
na lawama. 8 Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio
wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko
mtu asiyeamini. 9 Mjane asiandikwe isipokuwa umri wake
amepata miaka sitini; naye amekuwa mke wa mume mmoja; 10 naye
ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni,
ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata
kwa bidii kila tendo jema. 11 Bali wajane walio vijana
ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka
kuolewa; 12 nao wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani
yao ya kwanza. 13 Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa
wavivu, wakizunguka-zunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni
wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa. 14 Basi
napenda wajane, ambao si wazee, waolewe, wazae watoto, wawe na madaraka ya
nyumbani; ili wasimpe adui nafasi ya kulaumu. 15 Kwa
maana wengine wamekwisha kugeuka na kumfuata Shetani. 16 Mwanamke
aaminiye, akiwa ana wajane, na awasaidie mwenyewe, Kanisa lisilemewe; ili
liwasaidie wale walio wajane kweli kweli.
Ndoa ni muhimu na
msingi wa jamii, kama tutajifunza kuhusiana na wenzi wetu wa ndoa na kuwafundisha
watoto wetu kikamilifu kama ilivyofundishwa na kuonyeshwa kwenye Biblia, kama
sehemu ya jamii yetu, tutaliendeleza kwanza kundi, kisha taifa, na hatimaye
ulimwengu mzima wote utakao yapenda mafundisho Kristo. Ukristo utaendelea kusonga mbele na utakuwa na
maana ya kweli na ndipo kutakuwa na Bwana mmoja na Imani moja.
Waefeso
4:4-6 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika
tumaini moja la wito wenu. 5 Bwana
mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. 6
Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika
yote na ndani ya yote.
q