Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[127]

 

 

 

Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu:

Tathmini ya Waandishi wa Kipatristiki na Uainisho Wao Kuhusu Mungu

(Toleo La 4.0 19950722-1998093-20110104-20110129)

 

Jarida hili linayatathmini maandiko ya zamani na kuondoa mitizamo yake kuhusu Mungu. linaainisha pasipo shaka kwamba waandishi wa mwanzoni walikuwa ama ni Waamini Utatu au Watrinitariani au Waamini Miungu Wawili yaani Wabinitariani, na hawakuwa wakiamini kwamba Kristo alikuwepo tangu hapo mwanzoni. Jarida hili linasaidia kuonyeshaa mabadiliko haya ya kiupotoe yanayojitokeza kidogokidogo ya kiteolojia kwenye muundo wa imani ya Kitrinitarian.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki © 1995, 1999, 2011 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://ww.ccg.org

 


Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu

 


Dhana na Nadharia ya Zamakale ya Mungu wa Utatu au Utrinitariani

Dhana kuu iliyopo kuhusu Ukristo wa Kisasa ni kwamba Mungu yupo kwenye umbo au muunganiko wa vitu vitatu au hypostases. Kuna mijumuisho mbalimbali kwenye umoja au mmoja kwenye muungano wa utatu, unaojulikana au kuelezewa kama Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, ambao wanaelezea kuwa ni nafsi za pamoja. Vitu au watu hawa watatu wanasemekana kuunda Utatu. Utetezi wa usahihi wa madai haya umefanywa na dhana ya zamakale. Dhana nyingine iliyoeneza sana na iliyo ya uwongo ulio sawa na hiyo ni kwamba Kanisa la kwanza lilikua la imani ya Kibinitariani kuliko kuwa ni la Kitrinitariani, na linalodhaniwa kuwa Kristo, alipokuwa ni msaidizi, hata na wala hakuwa sawa na Mungu. Kwa hiyo wanasema kwamba kulikuweko na Miungu wawili walioishi kuweko kwa kila upande wakiwa kama Baba na Mwana. Hiki ndicho kilchojulikana hapo zamani kuwa ni Uzushi kuhusu Nguvu Mbili zitendazo kazi pamoja. Mafundisho haya mapotofu yanatokana  na imani za zama kale za Kinostoki na Dini za Kisirisiri au za Kimafumbo za waabudu Mungu Juan a hayana uhusiano wowote kabisa na mafundisho ya Mitume au ya Kanisa la Kwanza. Yanaenda kinyume na kukanganya andiko la Mtume Yohana (Yohana 17:3 na 1Yohana 5:20) linalosema kwamba kuna Mungu Mmoja tu wa Pekee na wa Kweli, na kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wake, na pia maandiko ya Mtume Paulo yanayosema kuwa ni Mungu tu peke yake ndiye hafi wala kupatwa na madhara, kwenye 1Timotheo 6:16. Kuelewa yaliyosemwa na Mitume hawa, yaani Yohana na Paulo na mitume wengine yalifundishwa na kuaminiwa pia na mitume Yohana na waliowarithi au kuwafuatia baadae, kama tutakavyoona hapo chini.

 

Jarida hili linakusudia kuainisha uwepo wa dhana kama hizo kuhusu Uungu kwenye mintaarafu ya mafundisho ya kibiblia tuliyoanzanayo tangu hapo mwanzoni na kwa uelewa wa wanateolojia wa zamani au wa kwanza. Madai ya kwamba Mungu ni mjumuiko wa viumbe au nafsi tatu ambayo kila moja inakuwa sawa na za milele hayakuwa mafundisho wala imani ya Kanisa la kwanza la Mitume kama tulivyojionea. Itaonekana pia kwamba hayakuwa ni mafundisho wala imani ya Kanisa la kwanza. Dhana ya Uungu kuwa ni mjumuisho wa viumbe watatu kwa kweli halikuwa la imani ya Kikristo na, kwa kweli lilianzia kipindi cha hata kabla ya kuzaliwa kwa Kristo na karne nyingi sana kabla yake. Hakuna shaka kanisa kwamba habari na hadithi za mungu wa utatu zinakutikana kwenye ngano za ustaarabu wa zama za kale zaidi na anajulikana kuwepo pande za mashariki mwa Asia. Waamini wa nadharia hii kuhusu Mungu wa Utatu waliingia kwenye imani ya Kikristo kwa kishindo wakitokea kutoka kwenye imani za Kiyunani na imani hii ikapata ushaishi na kukubalika na Warumi. Kiini au etimolojia ya jina la Yesu linayokana na lugha na mapokeo ya Kihellenia ya jina Yoshua ambalo ndilo lilikuwa jina la Masihi. Neno lililo kenye Agano Jipya lililotumika kutafsiri jina la Yoshua ni lile lililo kwenye Kamusi ya SGD 2424 z30F@ŘH au ’Iesous. Neno hili linatumika kwa Yoshua Mwana wa Nuni kwenye Waebrania 4:8, na Yoshua (z30F@Ř au ’Iesou) wa wakati wa Zerubabeli, aliyokuwa miongoni mwa mababu wa Kristo, kwenye Luka 3:29. Neno hili linatimika pia kutafsiri jina la Yusto kwenye Wakolosai 4:11.

 

Neno la Kiyunani la Iesus linaonekana kuwa linatokana au kushabihiana na neno la Kiceltiki la Esus, mmoja wa miungu iliyo kwenye mjumuisho wa miungu inayokutikana kwenye Dini na Imani za Wahaiperborean (soma kamusi ya ERE, Vol. 3, p. 278). Imani hizi zilikuwa na nguvu au ushawishi mkubwa sana zikikubalika na Walatini kisha pamoja na Wateutons (ibid.). Jina Esus huenda liingia kwenye lugha ya Kiyunani kutoka kaskazini pamoja na imani ya kidini ya Kihaiperborean na dini za Kisirisiri. Mjumuiko wa kiutawala wa mjumuiko ulijitokeza kwenye imani za Tuatha de Danann, kama Brian, Iuchair na Iucharbar, wakiwa ni kama wana wa mungumke Danu (ibid., p. 282). Huyu Tuatha de Danann pia alifanyika kuwa ni mshirika wa mungu wa Kisiwani Elysium na ndiyo Imani na Dini ya Kisirisiri ya Waelysian (ibid., p. 298) na alikuja kujulikana kama watu wa miungu mitatu (ibid., p. 292).

 

Waliamini kwa heshima yao yote kutokana, zaidi ya kuumbwa na miungu (ibid., p. 298). Wadruids walifundisha kuwa Wagauls walikuwa wameibuka kutoka kwa Dispater, mungu wa chini ya dunia (ibid., pp. 298-299).

 

Esus alikuwa ni mungu wa bara anayechorwa picha yake kwenye madhabahu huko Treves, akiwa kama mti uliokata chini shinani ambao ni kichwa cha dume la ng’ombe na korongo watatu (mchoro unaoashiria mungu mke Morrigan, malkia wa kijiamizi anayejumuishwa kwenye utatu pamoja na Brigit na Anu, ibid., p. 286). Reinach anasema kuwa muunganiko huu ndiyo dhana ile ile moja iliyokutikana kwenye madhabahu za huko Paris (ibid. p. 296). D'Arbois (R. Cel., xix, p. 246) inayoonekana kwenye rejea hizi kwa Tain. Esus ni Cuchilainn anayeukata na kuuangusha chini mti ili kuwaonyesha maadui zake. Ng’ombe huyu dume ni Dume la rangi ya Udhurungi la Cualnge. Kwa hiyo, Esus anaushirika jumuisgi na dini za Kisirisiri na dini za dume la ng’ombe linalochinjwa. Dume hili la ng’ombe pamoja na wapingaji walionekana pia kwa Wahelvi, kama ni mzunguko wa kuzaliwa kiumbe tena na tena kwa kundi au jamii ya sid (nguruwe-watu) ambao kwamba walikuwa na asili ya kimbinguni (ERE, ibid., p. 296). Baadae, dume huyu wa ng’ombe aliunganishwa au kujumuishwa pamoja na mungu Medros (ibid.). waselti waliviunganishwa vichwa na dhabihu ya wanadamu, ambao nyama yao ilikuwa inaliwa, kwa vikundi vya watatu watatu wakiienzi imani na dhana ya utatu (ibid., p. 300).

 

Rejea ya Kwanza kuhusu Dhana ya Utatu Utatu Kwenye imani ya Kikristo

Mfano wa kwanza wa rejea au kutajwa kwa Uungu wa Kikristo kuwa ni wa mjumuiko wa viumbe watatu kulifanywa na Theophilus wa Antioch (yapata kama mwaka 180 BK) aliyelitumia neno JD4"H au trias ambaye neno la kilatini la trinitas linachukuliwa kuwa ndilo limetafsiriwa kwalo. Neno hili alilitumia alipokuwa anaongelea kuhusu trias ya Mungu, Neno lake na Hekima yake (kwa kujibu wa waraka wa Theophilus kwa Autolycus. Tafsiri ya ANF hapa inatafsiri neno hili trias kama utatu). Mfano unaofuatia wa matumizi ya neno hili ni ule wa Tertullian (De Pud, c. xxi, P. G., II, 1026). Tertullian alikuwa ni wa kwanza kudai moja kwa moja umuhimu wa ujumuisho wa “nafsi” tatu, ila hoja yake na sababu zake vilikwa na umuhumu wa kujumuisha na kuweka usaidizi (soma kitabu cha Schaff, cha History of the Christian Church [Historia ya Kanisa la Kikristo], Vol. II, p. 570). Usawa ulio wa karibu zaidi na fundisho lililopitishwa kwenye mkutano wa baraza kuu la Nicene ha haikuwa imeonekana hapo kabla hadi ilivyopendekezwa na Askofu wa Kirumi Dionysius (mwaka 262BK) ambaye alikuwa ni Myunani kwa kuzaliwa. Alikusudia kuufutilia mbali mchakato wa kupunguza viumbe vitatu ili kuitenganisha Miungu (Schaff, ibid.).

 

Madai ya kwamba Mungu ni kiumbe anayejumuika na viumbe wengine wawili na kwamba ni nafsi au persona kama roho au nguvu unayotokea kutoka kwa mmoja au kwa wote wawili ni madai ya baadae ya waamini Utatu ya karne ya nne, tano, na ya sita. Madai haya yalifanywa ili kutambuli au kuonyesha asili na chimbuko la trias (hapo juu) aliyeachwa kama asiyeshabihiana. Kosmolojia zote mbili za kiutatu na ya Utatu, kama zinavyojulikana sasa hazina madhiko yoyote yale ya kibiblia, ni sawa tu na kama ilivyo imani ya Kibinitariani.  

 

Dhana ya utatu inaeza kuelezewa kwa njia mbili vifuatazo:

1. "Nafsihai Tatu ambao wako sawa wote na wenye asili ya kimbinguni". Huu unachkuliwa kuwa ni mtazamo uliozoeleka na kuaminika sana tangu kwenye mkutano mkuu wa Mabaraza ya Nicća na Constantinople.

2. Mwana na Roho wanatokana na Baba ambaye ndiye asili ya pekee na chimbuko la Uungu. Huu ni mtazamo kingifu wa Mababa wapinzani wao wajulikanao kama Ante-Nicene na Kanisa ka ujumla hadi kufikia mtaguso wa Nicća (mwaka 325 BK) (soma kitabu cha G.H. Joyce, The Catholic Encyc.(C.E.) makala ya ‘Trinity’, Vol. XV, p. 51, ambapo panasema kuwa “Chini ya suala hili, Baba akia ni kama chimbuko la hawa wote, anaweza kuitwa kuwa ni mkuu zaidi kuliko Mwana").

 

Fundiksho la Utatu linatokana na mfululizo wa mkururu wa nadharia potofu na za uwongo zilizotungwa kinyume kabisa na ushahidi wa kibiblia. Nadharia kuu mbili za uwongo zilizo wazi kutokana na nukuu zilizofanywa ni hizi hapa chini:

     kwamba maneno yaliyotafsiriwa Mungu yanamhusu mmoja , wawili au watatu au viumbe jumuishi, na

     kwamba Kristo ni Mungu mwenye haiba sawa ya umilele na usawa kama alivyo Mungu Baba nan i Mungu.

Kutokana na uainisho kwenye Kitabu cha Mungu Aliyedhihirishwa, Kitabu cha Kwanza tunaona kwamba nadharia na mawazo haya hayana msingi wowote wa kibiblia na kwa kweli yanapingana na Maandiko Matakatifu. Dhana ya pili hapo juu inatokana na imani ya Kibinitariani ya Kisirisiri na za Dini waabudu Jua.

 

Kutathimini Dhana ya Ushirikishi wa Usawa na Umilele

Waandishi wengi wa Kipastriki walipimga dhana hii ya usawa wa Mwana na Baba, na walipinga kwa hoja zenye nguvu na zenye mashiko usawa huu shirikishi. Vifungu sawa tu kama hivyo kama ifuatavyo. Mfumo wa imani ya Kibinitariani umechukuliwa au kutoholewa kutoka Roma kutoka kwenye ibada za mungu Attis na siyo kutoka kwenye Ukristo.

 

Justin

Mwalimu wetu katika masuala haya ni Yesu Kristo, ambaye pia alizaliwa kwa ajili hii, na kusulubiwa chini ya Pontio Pilato wa Uyahudi, wakati wa Tiberio Kaisari; na kuwa tunamuabudu, tukifahamu kuwa ni mwana wa Mungu wa kweli, na kumimshikia katika nafasi ya pili, na roho mtakatifu kuwa katika nafasi ya tatu, tutahakikisha kwani wakaushtumu uwazimu wetu kuweko hapa, eti kuwa tunaipeana nafasi ya pili kwa mtu aliyesulubiwa kutoka kwa Mungu asiyebadilika na aishiye milele, muumbaji wetu sote, kwa kuwa hawafahamu maajibu yaliyoko humo, ambamo kwamo, tunavyokueleteza wazi, tunaomba usadiki (Apol I, xiii).

 

Na mamlaka ya kwanza baada ya Mungu Baba na Bwana wa wote ni Neno [8@(@H au logos], ambaye pia ni Mwana. (Apol., I, xxxii).

 

Kwa hiyo ni makosa kuelewa kwamba Roho na mamlaka ya Mungu, kuwa ni kama kitu kinginecho mbali ya Neno [8@(@H au logos], ambaye pia ni mzaliwa wa kwanza wa Mungu. (Apol., I, xxxiii).

 

Kwahiyo, Justin anadhania Logos kuwa ni kama taswira ya Mungu ambaye ni uwingi wa mjumuiko wa wengi ili kulipa mashiko wazo hili la Roho kwa ujumla na hasahasa la Kristo. Hata hivyo anasema:

Wote, yeye (Mungu) na Mwana (ambaye alishuka kutoka kwake na kutufunza mambo haya, na mwenyeji wa malaika wote wazuri ambaye waliumbwa kama yeye, na wanafuata), na roho wa unabii, kuwafahamu ki sababu na ki kweli na kakiri bila kibari kwa yeyote anuiaye kufunza kama nasi tulivyofunzwa.

 

Kwahiyo, malaika alichukuliwa pia kuwa wana namna ya sura na mfano wa Mungu. Kutokana na Sura za 13, 16 na 61 za kitabu chake, Justin hakutetea ibada za kuwaabudu Malaika (soma pia sura ya 3 kwenye kamusi ya ANF, Vol. 1, p. 164). Neno kuabudu limetoholewa kutoka kwenye neno lililo kwenye Ufunuo 3:9 lililotuama kwenye maana ya proskuneo, linaloitwa BD@F6L<ZFTF4< au proskunesoosin (Marshall), linalomaanisha atapiga magoti mbele ya wateule wa Kanisa la Filadelfia. Kwa hiyo, neno hili halimanishi kuwaabudu malaika au Kristo bali ni kuonyesha heshima na unyenyekevu kwa kusujudu kifudifudi kimwili; kwa maneno mengine, ni kuonyesha heshima. Kwa hiyo, viumbe vilivyotajwa hapa vitapewa heshima yao stahiki ikia ni kama sehemu ya Malaika wanyenyekevu na watiifu wa Mungu. Malaika wanaotajwa kwenye kitabu hiki cha Ufunuo wa Yohana kua walijizuia kufanya hivyo bali zaidi tu ni kwamba walimwabudu Mungu (Ufunuo 22:9). Hivyo basi, wateule humwabudu Mungu peke yake. Justin anaelezea juu ya kutoa heshima stahiki tu na siyo kuwaabudu. Ahadi waliyopewa Kanisa la Filadelfia ilitokana na sababu za kwamba Wayahudi ambao walidai kuwa ni Wayahudi, bali walikuwa ni sinagogi la Shetani, walikuwa wameanzisha michakato ya dini za Kisirisiri za Merkabah zinazoendesha imani yake kimafumbo au za wapanda Magari ya Farasi wa Mungu, na za matulizo au uheri wa malaika kwa madaraja saba, (soma kitabu cha Mysticism). Kosa na upotovu huu ulienea hadi kwenye Kanisa la Wakolosai kwa sehemu. Ibada ya Kanisa la Mungu inatakiwa imlenge Mungu na haipaswi imlenge hata Kristo, zaidi ya kumpa tu heshima yake anayostahili kama kiongozi na bwana. Lakini la muhimu sana ni kwamba Justin anaujumuisha mwili akijumuisha Malaika watiifu. Hii kwa hiyo ni uwiano wa karibu kwenye mafundisho ya biblia ya Roho kuwa anaweza anapopewa nafasi kama mtendaji kuwakumbatia wateule wanaokwenda kufanyika kuwa theoi, kama Kristo alivyo mmoja wa theoi mdogo na msaidizi kwa theos wake ambaye ni Mungu Baba. Kimsingi sana, yeye hata hivyo ni wa pili kwenye daraja la juu sana la theos, akiwa ni kama kuhani mkuu.

 

Yaonekana  sana kabisa kwamba Justin ndiye aliyekuwa wa kuanzisha ibada ya jumapili (Taz bacc anatinoman views” kuhusiana na sabato kuwa adhabu kali; matazamo wake haukuungwa mkono na wakristo katika kipindi hicho na Nacchiocchi ana shikilia kuwa wakristo hawa jawahi kubadili uongo kama hao, (P. 225) kukiri kuwa Mungu anaiazisha tohara na sabato katika msingi wa uovu wa Wayahudi tu kama alama ya utambulisho dhidi ya mataifa na sisi wakristo ili wao tu ndio waweze kutoabika (Dial 16:1; 21:1 tazama pia Bacchiocchi Ibid). kwamtia Mungu kosa la utovu wa nidahamu kwa binadamu na kinyume cha sheria za toba za uongofu. Licha ya kosa hili, mtazamo wake kwa uongozi wa Mungu bado ya walakini wa ubadala. Hata hivyo anabuni mvuto wa hisia ambao unaenda sambamba na hii “Antinomianist approach”. Kama tulivyoona, Justin, hata hivyo, alizipiga mafundisho ya Roho kuendelea kuishi baada ya kufa nay ale ya kwenda mbinguni kuwa siyo ya Kikristo, falsafa ambazo zinachipua kutoka katika dini potofu za kisirisiri (Dial. LXXX).

 

Irenćus alikuwa ni mwanafunzi kutoka Smirna aliyefundishwa na Polycarp, mwanafunzi wa Yohana, na kwa ukaribu sana tunapata teolojia asilia yenyewe.

 

Irenćus amamwambia Mungu

Kwa kuwa aliamrisha, na wakaumbwa, alizungumza na wakatengenezwa. Alimwamrisha nani? Neno bila shaka na nani, anasema mbingu ziliumbwa na nguvu za pumzi ya kunywa chake (Zab 33:6). (Adu haer, iii, viii, 3).

 

Irenćus alishikilia kuwa:

imehakikishwa vyema kuwa si manabdii bali ni tume wapeana jina kuwa Mungu mwenine au kumwita Bwana, bali Mungu wa kweli na wa pekee….. ila vitu vilivyobaniwa ni tofauti naye aliyevibini, na vilivyo yeye mwenyewe hakuumbwa, hana mwanzo wala mwisho; na anachukilia kitu. Yeye ni safi kwake mwenyewe, na zaidi anawapa uwepo wengine wote, ila vitu vilivyoptengenezwa naye (Ibid).

 

Irenaeus alikizidisha kiwango cha kuwa Mungu (theos an Elohim) hadi kwenye “Logos|” kitu baki kutoka katika vitu vingine vilivyofanywa (ibid). alikuwa tayari ameshafanya nafasi ya Mungu nay a mwana na wana wote wa Mungu kutoka kwenye Kitabu III, Sura ya vi.

Kwa hivyo si Bwana wala roho mtakatifu wala mitume wamewahi kumpa jina Mungu, bila shaka, yeye ambaye hakuwa Mungu, labda ikiwa alikuwa Bwana wake wa kimwili, ila Mungu Baba atawalaye kute vote, na mwanawe aliyepeanwa naye Mungu juu ya viumbe vyote, kama isemavyo taarifa ijuatayoi. Neno la Bwana kwa Bwana wangu, ukae mkono wangu kuume hata niwafanyapo adui zako kuwa chini ya miguu yako (Zab 110:1). Hapa, maandiko yanawalakisha maongoze ya Baba kwa mwana, aliyepewa urithi ya ulimwengu, na adui zake wote kulengeshwa kwake.

 

Irenaeus akaendelea kusema kusema roho mtakatifu aliwataja aliyezungumza na Abrahamu kabla ya kutekofwa kwa Sodoma na alipokea nguvu (Kutoka kwa Mungu) kuwahukumu wa Sodoma kwa uovu wao. Tazama kufungu kifuatacho.

inasema ukweli huo huo; “kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele na milele fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya achili, umependa haki, umeichuka dhaluma, kwa hiyo Mungu, Mungu wako amekupaka mafuta (Zab 45:6), kwa kuwa roho anaambalisha wote kwa jina Mungu (Theus an Elohim) wote, aliyepakwa mafuta na yule aliyeyapaka mafuta, ambaye ni Baba na tena, Mungu anasimama katika kusanyiko la katikati ya Mungu, anahukumu (Zab 45:6), yeye hapa yamaanisha Mungu, mwana na wale waliopewa uwezo kuwa wana; lakini hili ndilo kanisa ambalo ndiyo sinagogi ya Mungu ambalo Mungu mwana mwenyewe amekusanya, na anawaambia Mungu, Mungu Bwana amenena, ametiita nchi toka maawio ya jua hadi machweo yake……. (Zab 50:1) katika kifungu hiki, Mungu ni nani? Anawaambia Mungu mwana alisema, watu wasionitaka wanamliza habari zangu (Isa 65:1) lakini aaongea juu ya Miungu wapi? Ni Miungu wa wale awasemeao ‘mimi ninasema ndiyi Miungu na wana wa aliye juu’ (Zab 82:6). Kwa hao, Bila shaka , wale ambayo wamepokea amani wa “ Kupokewa, ambayo tuko Abba Baba” (Warumi 8:15) ( Agaisnst Heresies, Bk.iii, ch.vi, ANF, Vol. I,pp. 418-419).’’

 

Hapana shaka kuwa irenasus ilikuwa na mtazamo wa ushirikiano wa utawala wa Mungu na akaendelea neno ‘Mungu’ kujumuisha mwana na wale waliopewa uwezo kuwa wana. Kujumuisha mwana na wale waliopewa uwezo kuwa wana. Anaonekana kuashiria kuwa wana. Ananena kuwa kuashiria kuwa Ksristo akawakusanya wateule, bali sisi twajua kuwa ni Mungu ndiye amepanye Kristo wa teule (Yn 17:11-12, Waibi 2:13; 9:15) matumizi ya neno hili kwa wateule wa kimwili huenda yasisiwe sawa tukiuzingatia mtazamo wa irenaeuos hapa. Wenyeji wazalendo pia wamehusishwa katika baraza tukitumia uelewavu wa ufunuo 4 na 5- hivyo wenyeji wazalendo ndio “Ecclesia” wa Mungu. Hapana shaka kuwa maneno “Elohim” au “Theoi” yalimaanishwa kuenea hadi kanisani na kuwa ulikuwa ni uelewevu ya kanisa la karne ya kwanza kutoka kwa Yohana na Polycarp, walionifunza irenaeous, na kuingia katika karne ya pili na karne zilifuata.

 

Kihistoria hili limekuwa likifahamika kama baraza la Elohim ambao ni wana wa Mungu.

 

Ni dhahiri sana kwamba Ireneaus aliamini kwamba ni Mungu Baba peke yake ndiye Mungu wa kweli wa kwenye Biblia na ndiye Muumbaji wa vitu vyote.

 

Kwenye Kitabu cha V sura ya 25 tunasoma kwenye sura ya 2:

2. Zaidi ya yote, yeye (Mtume) ameonyesha pia jambo hili nililolionyesha kwa namna nyingi, kuwa Hekalu la Yerusalemu lilijengwa kwa maelekezo ya Mungu wa kweli. Kwa kuwa mtume mwenyewe, ananena kwa nafsi yake mwenyewe, kwa namna tofauti sana aliitwa kwenye hekalu la Mungu. Sasa nimeonyesha kwenye kitabu cha tatu, kuwa hakuna mwingine aliyeitwa na mitume Mungu walipokuwa wakijiita  mwenyewe, isipokuwa kwake yeye ambaye ndiye Mungu wa kweli, Baba na Bwana, ambaye kwaye, maelekezo ya ujenzi wa hekalu la Yerusalemu yalitumika kwenye kulijenga kwa malengo hayo ambavyo nimekwisha yaelezea tayari; ambavyo kwamba adui wa (hekalu) ataketi, akijaribu kujionyesha yeye mwenyewe kuwa ni Kristo, kama Bwana alivyomtaja pia kwamba: Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli, limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu), ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani; naye aliye juu ya dari asishuke kuvichukua vitu vilivyomo nyumbani mwake; wala aliye shambani asirudi nyuma kuichukua nguo yake. Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo! Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato. Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.

 

Bila shaka kwamba kanisa la kwanza lilikuwa ni saidizi au dogo na kwamba wale aliofundishwa huko Smirna na mitume na wale waliokuwa kama mitume kama vile Polycarp walikuwa ni wa mrengo wa Uyunitariani wa Kibiblia na waliamini kwamna ni Baba tu pekeyake ndiye alikuwa Mungu wa Pekee wa Kweli, na kwamba wengine wote, akiwemo Kristo, waliruzukiwa tu uzima wa milele na Baba.

 

Irenćus alinena kinyume kupanuka kukubwa kupya kwa Ubinitariani unaotokana na dini za waabudu Jua za huko Roma na kile kinachojulikana kama mafundisho ya Kibinitariani kama uzushi na imani yao kulikoendelea mbele kwenye mwenelezo kamilifu wa Utrinitariani wa Mungu wa Utatu. Haya ni mafundisho ya Mpingakristo na mfumo wake sahihi na halisia unaoonekana kutoka kwa Irenćus.  Fundisho hili lilijipengeza kwenye makanisa ya Mungu mwishoni mwa karne ya ishirini yakitokea Marekani.

 

Irenaeus, Sura ya 16:8 (ANF, Vol. 1, fn. p. 443) inasema:

Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. Na kila roho isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo.

 

Socrates mwanahistoria anasema (VII, 32, p. 381) kwamba kifungu hiki kimekanganywa na wale waliopenda kutenganisha ubinadamu wa Yesu Kristo kutoka kwenye haiba yake ya kimbinguni.

 

Clement wa Alexandria anasema:-

 

Kwa kuwa mwana ndiye nguvu ya Mungu, na kuwa ndiye neno la kale zaidi la Baba, kabla ya kufanywa chochote na Bwana yake. Hivyo anaitwa mwalimu wa waumbile yake. Sasa nguvu za Bwana lina marejeleo katika mwezi, na mwana ni nguvu za Baba (“Strom.”, VII,ii,P.G., IX, 410).

 

Hata hivyo Clement alielewa kuwa hatima ya wateule ni kuwa miungu. Alipoongea kuhusu ‘gnosis’ alishikilia kuwa ingepatikana na mwanadamu katika kanisa kwake kwenye nchi au dunianii:

Hafika upeo baada ya mauti ya kimwili, nafasi ya (gnoostikis) ilihusiwapo kuenda mahali pake rasmi, ambapo, baada ya kuwa Mungu, itafarijika, katika mapumziko yasio na mwisho. (S.R.C Lilla Clement of Alexander, a study in Christian platonisan and grosticison, Oxford 1971, P 142).

 

Hivyo tunaona hapa mchanganyiko wa ‘gnosis’ ya kigiriki na tamaduni za kale kuwa tutakuwa ‘theoi’ Elhim. Hapakuwa maoni kuwa Kristo wala theoi wengine kuwa sawasawa na tutakatifu wa jua zaidi.

 

Hippolytus asema

Kwa kuwa sasa Neotus anahakikisha kwamba mwana na Baba walikuwa sawa, hakuna asiyejua. Ila amamtoa maelezo ‘wakati Baba hakuwa amezaliwa, alikuwa ameshahakikiwa kwa haki kuwa Baba; na kuendeleza vizuri kulipoupendeza, kwa alikuwa wa pekee yeye mwenyewe akawa mwanawe, kulingana na kipindi cha ‘visiccitude’ (Hippolytus anarudia wazo hili katika utupisho wa kitabu chake X) (Con. Neot, n, 14, “The refutation of all Heresies Bk ix. Ch, v, ANT, Vol, v, pp 127-128);

 

Wakwanza na wa pekee (Mungu mmoja), muumba na Bwana wa wote hakuwa na chochote “coeval” ndani yake……… ila alikuwa mmoja na pekee yake. Kwa zoezi la mapenzi yake, aliviumba vitu ambavyo havikuwepo mwanzoni yapokuwa alimwa viwepo kwani anafahamu yake fika na chochote ambacho kinakaribia kutendeka, ufahamu wa kimbele pia anao (Hippolytus, ibid, x, xxviii, p 150).

 

Kwa hivyo huyu Mungu mwenzake yote, kwa uakizi mwanzo alileta ‘logos’ si neno kwa kufanywa na sauti bali kama uswazisho wa ulimwengu, uliofanywa na kupewa makao akilini. Yeye mwenye alichumbuka kutoka katika vitu vilivyo; kwa kuwa Baba mwenye alikuwa ndiye uwepo, na kuzaliwa ndiko kulisababisha vingine kuwapo. Logos ilikuwa ndani ya Baba mwenyewe, kushikilia mapenzi ya mwelekezi wake na si kuwa na ufahamu duni wa akili ya Baba.

 

Sambamba na uwezo wake kutoka kwa mwelekezi wale, na kuwa yeye ndiye mwanambee wa mwelakazi hiyo. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa, kuwa Baba aliponuru kuwekko ulimwengu, logos, mmoja baada ya mwingien wakaukamilisha uumbaji hivyo kumfarahosha Mungu.

(Hyppolytus idid, x, xxix).

 

Ni kupitia kwa mwandishi huyu ambayo tunaingiwa na kwa kuwa Kristo ndiye mali ya Baba na kuwa maumbile mengine ya mbinguni ni humbaji wa mwana na hivyo hawana ushirika katika mazingira kama mwana. Kutokana na kosa hili, tunaduni ya utatu ulianza kujengeka. Elohim ni wenyeji wengi ambamo kwao wana kondoo ndiye kuhani mkuu, ila yeye ni mmoja wao na kwao ni mwenzi au rafiki, ingawa mpangilia wa uyeo ulikengwa nay eye, ndani yake na kwake yeye (Wakolosai 1:15). Watakatifu pia walikuwa wenzi wa Kristo kutoka Waibi 3:14 na hivyo ndoyo wa mwenyeji (Ufunuo 12:10) na warithi kama Kristo (Warumi 8:17) mbingu na vyote vilikuwema, na vilivyotajwa kuwa viliumbwa na mwana na 1 Wakorintho 8:6 ikirejelea ulimwengu na wanadamu. Wakolosai 1:15-17 inatengesha uumbaji wa vitu vyote, vinavyoonekana na visivyooneknana. Uumbaji wa vitu vya ufalme, ubwana, uongozi, watawala kupitia kwake, kwa ajili yake, haiwezi kulirejelea baraza la Elohim uumbaji wa Kristo wa ubwana hauhusiani na haya.

 

Kama ulivyokuwa hivyo, ingehushisha uumbaji wa Mungu hivyo tunambaka na nguvu na si nafsi. Viti vya ufalme na mana ya mbingu na serikali yake.

 

Waefeso 1:22 na 3:9 inaonyesha kuwa ni Mungu aliyeumba vitu vyote na kuliweka minguu pa kristo na akafanya kwa kiongozi wa vitu vyote, kwa ajili ya kanisa. Haya yalijengwa ili utawala wa mbinguni waufahamu uwezo na nguvu za Mungu. Vitu hivi vilifanywa ili kuonyesha kuwa Mungu ni Kristo aliyeinuliwa (Wafil 2:10). Ambaye hangeweza kuwa chapo awali. Mungu alimwita Kristo kama mali ghafi ya uumbaji (Waeb 113) Kristo akauumba ulimwengu (Waeb 1:2) na naakisi nuru ya Bwana na anao muhuri wa muumbile yake (Waeb 1:3) Waebrania 2:10 iarejelea vitu vyote ukiwemo ulimwengu.

 

Waebrania 2:11 inasema kwamba Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. (©<ÎH BV<J,H or enos pantes). Waebrania 11:3 inaaminika kuwa inasema kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu (ŐZ:"J4 2,@Ř au pneumati theou) (soma kitabu cha Marshall). Hii Logos haionekani kama inakuwa ikihusishwa na hasahasa neno lililotafsiriwa kama iliumbwa inaonyeshwa hivyo na Marshall likimaaisha kuwa limerekebishwa (6"J0DJ\F2"4 au katertisthia) na neno halikurekebishwa bali zaidi ni suala tu la zama mbalimbali ("Ćä<"H au aionas). Kwa hiyo, hizi zama ndio zilizorekebishwa kwa neno la Mungu ili kwamba kile kinachoonekana kuwa kilifanywa kutoka kwa vitu visivyoonekana. Hivyo ndiyo dhana ya uumbaji kwa kurekebisha anga/wakati au majira yaliyo sawa. Warumi 11:36 inamtaja Mungu kuwa ni kama chimbuko na mlengwa wa mambo yote, na siyo Kristo.

 

Elohim wengine wanaotajwa kwenye Biblia wana usaidi lakini wana mamlaka shirikishi na Kristo. Wanamamlaka kwenye muundo mtakatifu wa kimbinguni. Ushirika huu wa elohim (chini ya mamlaka ya Yesu Kristo) umefanywa kwa mujibu sawia na mapenzi ya Mungu. Mmoja wao ni kerubi mwenye mbawa zinazofunika anayeitwa Shetani, na wale walio wadogo wasaidizi wake, ambao wameumbwa kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu, kimahusiano (soma harida la Uumbaji: Kutoka kwenye Teolojia ya Kianthropomofiki Hadi Anthropolojia ua Kitheomofiki (Na. B5)). Ni upuuzi mkubwa sana kufikiria kwamba Kristo aliumbwa na hali isiyo na dhambi wala kosa lolote, na lakini washirika wake wengine ambao ni Malaika wakapewa uhuru wa kuchagua kwamba wachague kutii au kutenda dhambi. Mafanikio ya Kristo yalitokana na utii wake na siyo kwaajili ya hali yake ya kukamilika na kutotenda dhambi. Mafanikio yake yalijulikana kutokanao na uweza wa Mungu wa kujua kila jambo hata ya mambo yaliyokusudiwa tangu mwanzoni. Amepewa mamlaka halisi kutokana na utii wake na imani. Utawala au mamlaka dhidi ya viumbe wote waliopo na ambazo ni uweza wa Kristo na Malaika kwenye uumbaji yapasa uenee kwa wanadamu baada ya ufufuo wa pili wa wafu kutokana na Kumbukumbu la Torati 4:19.

 

Kamusi ya the New Catholic Encyclopedia (N.C.E.) article ‘Trinity, Holy’, Vol. XIV, McGraw Hill, N.Y., 1967, p. 296, inafanya jambo kubwa linalodaiwa lisilo la kawaida kuhusu fundisho la Hippolytus.

Hippolytus kwenye ukanushaji wake Noetus (10) na utambulisho uliotiliwa chumvi wa Kristo pamoja na Baba, anasisitiza kuwa Mungu alijiongeza tangu mwanzoni.

Ni uwongo tu kutokana na ulinganisho na andiko halisi la Hippolytus (C. Noetus 10) hapo juu. Mamlaka hayohayo yanaelezea kwamba:

Tertullian, anakuwa na msimamo huohuo (Adv. Prax. 5), wate isipokuwa ufanywaji kiunafsi uwingi huu wa milele. Neno linasimama au kubakia kuwa limesimama na zaidi kuliko katika Uungu kwa maana iliyoshauriwa mwonekano wa kibinadamu, kama mjadala wa ndani ulivyo kwa namna hiyohiyo nyingine, pa pili kwenye ongezeko kwa kila mtu peke yake, ingaaje bado ni ndani ya kila mmoja peke yake.

Aina au mtindo huu unahusu mashiko hayohayo ya Unoetianism na Usabellianism na inatofautiana sana.

 

Tertullian anaelezea kwenye kitabu chake cha Against (Adv.) Praxeas kwamba:

Huyu mmoja ni Mungu pekee aliye pia Mwana, Neno lake, aliyetokana na yeye mwenyewe, ambaye kaye ni vitu vyote vimeumbwa...Wote ni wa mmoja, kwa umoja (ambaye ni) mdogo au msaidizi; wakati siri ya utawanyiko ingali bado inalindwa, ambayo unatoa au unaanzisha au kusababisha Utatu ndani ya Utatu, akiweka kwenye utaratibu wao wa Nafsi tatu-Baba, Mwana na [Roho] Mtakatifu: watatu hata hivyo, hawamo kwenye masharti bali kwa kiwango; siyo kwa udogo bali kwa utaratibu au kanuni; siyo kwa uweza au kwa nguvu bali ni kwa utendaji; lakini bado wakia ni kitu kimoja, na wenye sharti moja, na wenye nguvu moja ni kama alivyo Mungu ni Mmoja, ambaye kwa yeye viwango hivi na aina hizi na mambo yake yamebubalika, chini ya jina la Baba, na la Mwana na la [Roho] Mtakatifu... (II);

 

Pia Tertullian anasema kwamba Baba alimfufua Mwana kutoka mautini (II). Kwahiyo Tertullian anaiweka tofauti ya muhimu sana kwenye mfungamano wa kimahusiano wa vitu vitatu ambao ndiyo walengwa harakazi na kazi za Mungu kwa kiwango. Mwana na Roho ni mwendelezo kutoka kwa Baba na ni viumbe wadogo au wasaidizi wa udhihirisho wake. Tertullian aliipa imani ya Utatu pgangilio wa kinumerali na migawanyo (III). Na pia alishikilia uamini kwamba Umonaki wa Mungu ulikuja kutoka kwa Baba (III). Lakini hii ilikuwa ni sawa tu na huyu Mwana kuchukuliwa kuwa ni wa namna zote mbili (III) akiwa ametolewa kwa Mwana na Baba (IV).

 

Tertullian aliamini kuwa Roho Mtakatifu alishuka kutoka kwa Baba kwa kupitia kwa Mwana. Tertullian aliamini (IV) kuwa Baba na Mwana ni wawili, yaani ni viumbe waliotofauti kila mmjoja wao. Kwa hiyo, ilipasa idaiwe na kuaminika kuwa imani ya kweli ya Kiditheism (inayoitwa pia Ubinitariani) ilianzishwa na Tertullian (soma Zaburi 45:6-7).

Yeye ambaye wanamtii (viumbe wote) nay eye ambaye walikuwa wamemtii – ni lazima wawe ni Viumbe wawili walio tofauti.

Hata hivyo, Tertullian anasema kuwa Sura ya V kwamba kabla ya kuwepo vitu vyote Mungu alikuwepo.

Kwa kuwa kabla ya kuwepo kwa vitu vyote Mungu alikuwa peke yake – akiwa ndani yake mwenyewe na kwa ajili yake yeye mwenyewe ulimwenguni, na kwenye anga na kwa vitu vyote. Zaidi ya yote ni kwamba, alikuwa peke yake kwa kuwa hakukuwa na kitu chochote nje yake bali ni yeye tu peke yake.

Ukweli wa kwamba sababu aliyopewa ilimfanya kwa kweli asiwe peke yake na Tertullian anasema kuwa mrengo huu wa kufikiri unaoitwa kwa Kiyunani logos ulikuwa ni muono wa tangu mwanzo ambao ulikuwa ni sahihi zaidi kifikra kuliko neno kama alipokuwa anafikiria lakini hakusema. Hivyo, Tertullian anaweka tofauti kwamba Kristo ni fikra ya Mungu na kwamba sababu hii ni lazima iwe imehusiana na chimbuko la kimungu tangu mwanzo. Hoja au mjadala uko wazi kwa vipingamizi mbalimbali. Kosa la kwanza ni kwamba Kristo alikuwa ndiye mlengwa pekee na Neno na Hekima na sio tu ni udhihirisho wa hao wote. Lakini alikuwa Logos kama sehemu ya Logon (ikifuatia tofauti halisia/iliyopendekezwa kama tulivyojionea kutoka kwenye kitabu cha Kwanza cha Mungu Amedhihirika, yaani God Revealed, Book One). Logos iliyojitokeza kwa mwanadamu alikuwa Kristo. Kama Kristo alikuwa pamoja na Mungu kipindi cha kabla ya mwanzo wa uumbaji, kama asemavyo Tertullian kwamba Mungu alikuwa na sababu hata kabla ya mwanzo wa uumbaji, ndipo Kristo ni mlengwa wa Mungu ambavyo inawezekana kwenye mgawanyo bali haiwezekani kwenye utenganifu kwa kitu kimoja. Ni upuuzi kudhania kuwa Kristo mbali na Mungu anaweza kuwa Mungu pasipo kufikiri au hekima na hivyo hawezi kuwa Mungu.

 

Kristo alikuwa mwanzo wa uumbaji wa Mungu (Ufunuo 3:14). Kwa hiyo tumekuwa tumeelewa au kujulishwa mwanzo kama ulivyoeleweka na wanateolojia wa zamani kama mwanzo wa uumbaji ulioanzisha majira na nyakati zake. Tertullian anashikilia kuamini kwamba ni Mungu tu ndiye aliyeishi au kuwepo kipindi cha kabla ya uumbaji na akiwepo kiumilele (V), akiwa wa tofauti na mkubwa zaidi kumliko Mwana (IX) aliye ni wa namna zote mbili, yaani, Neno na Hekima (VI). Mungu hakufanyika kuwa Baba hadi kipindi cha baada ya Uumbaji wa Neno (VII) hasahasa kenye uumbaji wenyewe (Adv. Hermog. 3). Kwa hiyo Mungu Baba ndiye aliyesimama nje ya wakati na viumbe wote wengine haakuwa hivyo. Ni yeye tu peke yake ndiye Mungu Mkuu wa wa Pekee. Kitabu au jarida la N.C.E. linasema kuwa

Mnamo karne ya 3, kama mtu anavyoweza kuona ikionyeshwa kwenye kitabu cha kutisha cha Novatian cha De Trintate, Kanisa la Kirumi, hapo mwanzoni sana lilipunguza mguvu kuhusu jakamoyo yale kwenye uwingine na uwingi, lilikuja kujishirikisha na busara au muono mkuu wa Tertullian. Hata hivyo, Novatian, anasisitiza (kwenye sura ya 31) kwa uwazi sana kuhusu umilele usio sawasawa wa baba na mwana kwenye Uungu. (op. cit., p. 297)

 

Ni kama inavyoonekana hapo juu, mafundisho ya baadae, yakiwa yanashirikisha na baadhi ya mitazamo au hisia za Tertullian, yakafanyika kuwa kwenye msingi wa nadharia ya Novatian kuhusu umilele ulio sawa akipinga maelekezo ya maneno ya Tertullian. Kwahiyo, dhana ya fundisho la dogma ilikuwa ni nadharia tu ya kuitunga na kuitengeneza kiubandia iliyoanzishwa kwenye Kanisa la karne ya tatu. Hayakuwa na msingi wake kwenye mafundisho ya biblia bali ni kutoka kwenye mwendelezo ulioingia taratibu wa makosa ya kiteolojia. Ufafanuzi uliopo hapo juu unaashiria kwamba mamlaka yametamkwa kimakosa, yakirudia kiukamilifu kabisa maana ya maandiko, ambayo yanaashiria kwa kiasi kikubwa sana kuwa yamechaguliwa kusomwa.

 

Mrengo wa mashariki umetuama kwenye nadharia ya Alexandria na maandiko yaliyo karibu na wakati wa Hippolytus na Tertullian alikuwa na aliyashirikisha mafundisho yamhusuyo Clement (hapo juu), ya Mwana kama uzao wa Baba. Lakini Clement alikuwa msaidizi, kama walivyokuwa wanateolojia wote wa mwanzoni. Mrithi wa nafasi ya Clement alikuwa Origen.

 

Origen anaunga mkono kwa wazi sana akisema hivi:

Tunatangaza kwamba Mwana si mkuu kuliko Baba, bali ni mdogo kwake. Na imani hii tunaijenga kwenye maneno aliyoayasema Yesu mwenyewe: 'Baba aliyenituma mimi ni Mkuu kuliko mimi.' (Con. Cels.,VIII, xv)

 

Tunajua, kwa hiyo kwamba yeye ni Mwana wa Mungu, na kwamba Mungu ni Baba yake. Na kwamba hakuna aliye na ubora wa kumzidi au wa kutokufanyika taswira ya Mungu kwenye mafundisho ya kwamba angeweza kuwa ni mzaliwa kama ni Mwana wa pekee, na hakuna atakayetushawishi sisi kwamba huyo mmoja siyo Mwana wa pekee wa Mungu na Baba. Na iwapo kama Celsus amesikia kitu fulani cha watu fulani wakishikilia kuamini kwamba Mwana wa Mungu siyo Mwana wa Muumbaji wa ulimwengu, hili ni suala au jambo linalotuama kati yake nan a wasaidizi wa dhana au nadharia kama hiyo. (Con. Cels., VIII, xiv)

Origen akiwa ni mrithi au aliyemfuatia Clement kwenye Shule ya Alexandrian anasema hivi:

Aliufanya ulimwengu uone sawa na maono ya aaminye mistari ya Kineoplatoni ya daraja la kicheo la kiubashiri. Kwenye kilele timilifu cha upeo wa juu, kuna Mungu Baba (De Princ. 1.1.6), ni pekee mwenye chanzo au mwanzo usio na chimbuko lake, au kwa kutumia maneno aliyoyapenda sana kuyatumia Origen (kwa mfano kwenye kitabu chake cha Ioan. 2.10.75), hajiongezi (•(X<<0J@H au agennetos). Lakini (De Princ. 1.2.3) Baba anatokana na umilele wote aliomuumba Mwana, na (Kwenye Ioan. 2.10. 75) kutokana na huyu Mwana kunatoka Neno, ndiye alimleta au kumtuma Roho Mtakatifu. tatu ni kwamba, Origen anaendeleza kivungu hikihiki, kuwa ni watatu walio tofauti kile mmoja wapo [yaani nafsi zao] au *hypostases [sawa na ilivyo Kwenye Ioh. 2,10,75]. kwa upande mwingine (Frag. in Hebr.), kwa rejea rahisi hapa kuhusu Baba na Mwana, wanashirikiana kwa pamoja ‘jamii ya msikamano’ kwa Mwana, anaongeza kipindi hiki baadae kua ni ‘cha kiini hikihiki’ [*homoousios Ď:@@bF4@H] na Bab. (N.C.E., p.297).

J. N. D. Kelly (kwenye kitabu chake cha Early Christian Doctrines [Mafundisho ya Mwanzoni ya Kikristo]) anasema kuhusu mtazamo au nadharia ya Origen kuhusu Hypostases kwamba:

Uthibitisho huu wa kwamba hawa Watatu ni nafsi au hypostasis tofauti kwenye umilele wowote, siyo tu kuwa (kama walivyoamini kina Tertullian na Hippolytus) kuwa walionekana au kudhihirika kwenye ‘ubanifu’, kuwa ni kama moja ya tabia kuu am mwelekeo wa mafundisho yake, na anatuama moja kwa moja kwenye dhana ya kizazi cha milele. Hupostasis na ousia mwanzoni kabisa walikuwa wako sawa, Wastoiki wa mwanzoni na hatimaye akawa Waplatoniki, ikimaanisha kuwapo kiuhalisia au chimbuko na kiini chake, jambo ambalo ndilo kitu chenyewe; lakini wakati hupostasis inaporudi kwenye mtiririko huu wa kikanuni kwenye ule wa Origen [yaani Kwenye Ioh 20,22,182f.; 32,16,192f.], ndipo mara nyingi sana anaipa mashiko ya kusaidiana kila mmoja na mwenziwe, na uwepo wa kila mmoja. Makosa au upotoe wa nadharia ya Kimamboleo, anapinga [ibid.. 10,37,246: cf. ib. 2.2.16; In Matt. 17,14.], inatuama kwenye hali ya kuwachukulia Watatu hawa kama ni idadi isiyobadilika ( *4"NXD,4< Jč •D42:č au mimi diapherin kuwa ariethmo), aliwa wanatofautiana kwenye mawazo na fikra tu, peke yake, mmoja akiwa hayupo lakini akiwa kwenye uwepo tu '...(p. 129)

 

Kutokana na kitabu cha De Orat. 15,1; C. Cels. 8,12, Origen anashikilia kuamini mafundisho ya kweli kuwa ni kwamba Mwana "si hana zaidi ya kuwa msaidizi tu kuliko kuwa Baba". Baba na Mwana ni “wawili tofauti kimtazamo wa Kinafsi, bali ni amoja kwenye ushirikiano, utendaji wa pamoja na kwenye kuonyesha mapenzi na nia " (soma pia kitabu cha Kelly, ibid.). Kelly anasema hivi:

Hivyo basi, kwa kuwa kuna tofauti ya kweli, basi Watatu hawa wanatokana na mtazamo mwingine wa mtu; ni kama anavyoelezea [Dial. Heracl. 2], 'hatuogopi kuelezea kwa maana moja ya miungu miwili, na kwa upande mwingine ni kwa mrengo wa Mungu mmoja' (ibid.).

Kwa hiyo Origen aliamini kuwa Baba kuwa ni kipaumbele kwenye teolojia kwa Mwana na kwamba Mwana alitokana na Baba. Aliamini kuwa umoja ulikuwa ni wa lazima zaidi kuliko ilivyodhiwa na mshikamano wa Kimamboleo. Origen anahusianisha ufungaji wa ndoa wa mwanaume na mkewe wakawa mwili mmoja kuwa ni mfano wa jambo hili na pia ni sawa na uhusiano wa mwanadamu na wa mteule na Kristo na kuwa kwenye roho mmoja. Hivyo basi, kwa kiwango cha juu sana tena, Baba na Mwana ingawa wako tofauti bali ni Mungu mmoja. Kelly anaamini kuwa ingawa Origen anaonekana kuongelea kuhusu Kristo kuwa ni kama kiumbe tu, hili ni kama wazo au dhana iliyopo kwenye kifungu cha Mithali 8:22 na Wakolosai 1:15 na kwamba haipasi kupuuziwa. Anashiriki kwenye asili ya kimungu kwa kuwa muunganiko na asili ya Baba (In Ioh. 2,2,16; 2,10,76; 19,2,6). Kelly anasema kwamba:

Yampasa mtu awe makini, hata hivyo, haipasi kunasibisha  na Origen kwa fundisho lolote la kuwa mmoja na Baba na Mwana.

Mlinganisho wa Origen wa Baba na Mwana ni moja ya upendo, utashi na tendo (Kelly, anayachukulia maandiko yanayoendelea kudumu na tafsiri iliyoonyumbuishwa ya Kilatini, ibid., p. 130). Origen anasema kuhusu Roho Mtakatifu (Frag. in Hebr. PG 14, 1308):

Anawapa wale ambao, kwa ajili yake na ushiriki wao wake, wameitwa kuwa wametakaswa na jambo, kama ningelielezea, neema yao. Jambo hili hili la neema limehitajika na kuwekewa umuhimu mkubwa na Mungu, limetumikiwa na Kristo, na kufikiwa na kila mmoja aliyelifikilia (ßN,FJfF0H au huphestoses) kam Roho Mtakatifu.(soma pia kwenye kitabu hichohicho cha Kelly ibid.).

Kelly (kurasa za 130-131) anaamini kutokana na kitabu hiki kwamba uwanja wote mzima wa kuwa Roho Mtakatifu ni Baba lakini hii imechukuliwa kwa kina kuwa ni Roho na Mwana, ambaye kutokana na yeye Roho anachukua tabia zote (sawa na ilivyo kwenye ibid., 2,10,76).

 

Watatu hawa ni wa milele na wana tofautiana sana lakini hawapo kuwa ni viumbe walio na mwambatano wa Kiiutatu au Triad. Makosa yapo kwenye hitimisho la kwamba Mwana ana ushabihiano na Roho kwenye tabia zake zote zaidi ya kuwa tu ni mwongozaji wa wateule. Dhana ya umilele ulio sawa kimsingi imebuniwa tu. Kushindwa kuelewa tabia na majukumu ya Roho kwenye maongozi ya kimonotheist ya mteule ni kosa kubwa sana kuliko yote hapa.

 

Mtazamo wa Kiplatoni unasema kuwa utaratibu huu ulianzia kwenye muundo huu kutoka kwa Baba na hivyo Roho akafanyika kuwa nafsi ya tatu kuliko kuwa amekuwa ni mwakilishi tu na kiungo ambacho kwaye ndipo Kristo alifanyika kuwa ni mmoja na Mungu. Kwa njia ya Roho, ndipo mwanadamu alifanyika kuwa mmoja ni kama Kristo alivyofanyika, lakini ni kwa misingi yenye masharti ambayo kwayo Wayunani wanaonekana kuwa waliyakataa. Kuingizwa au kubuniwa kwa imani ijulikanayo kama Uplatoni mamboleo kwenye Ukristo kumeenea kwa kina ulimwanguni kote (soma kitabu cha Imani za Siri au Mysticism). Kitendo cha kutoielewa tofauti iliyofanywa na Origen hapo juu kulisababisha kuwepo kwa fursa kwenye Baraza la Halmashauri Kuu la Mtaguso wa Nicća ulioitishwa na kukaliwa miaka 100 iliyofuatia baadae. Umoja wa jambo hili ulikuwa ni umoja uliotajwa na uwepo wa Roho Mtakatifu, ambao ulikuwa kwa wenyewe tu ni tabia ya Mungu. Origen aliamini kuwa ni Baba tu, peke yake ndiye Mungu atokanaye na yeye Mwenyewe ("ŰJ`2,@H au autotheos); (Kwenye Kitabu cha Ioan. 2.2.17);

Na kwenye fikra za Origen (C. Cels. 5.39) Wakristo wanatajwa moja kwa moja kwa Mwana akiwa kama ‘wa pili’ (*,bJ,D@H au deuteros) deity. (N.C.E., ibid.).

Dhana au madai ya Origen ya uumbaji wa milele unaendanga kinyume na dhana ya usawa wa milele wa Kristo. Augustine hatimaye aliamini kuwa wakati au zama ilianza kwa vuguvugu la malaika. Dhan hii ni sahihi sana kwamba nyakati zilianza kwa uumbaji wa malaika wa elohim. Ni Mungu Baba au Eloah peke yake ndiye aliyewahi kuwepo nje ya kipindi hiki cha zama na alikuwepo kwenye umilele ule wa kabla ya uumbaji. Kwa hiyo, yeye ndiye mwenye uweza wa kipekee wa kuelewa kila kitu na Kristo alikuwa wa pili au deuteros theos. Dhana ya kuwa Roho Mtakatifu anatokana na Kristo ilipelekea kuwa na hitimisho potofu au la kimakosa na kusema kwamba kwa hiyo Kristo ndiye alimuumba Roho Mtakatifu. Kutokana na hapo juu, ni kwamba Roho Mtakatifu anatokana na Baba peke yake. Roho ametolewa kama kitu cha kutusaidia na anatokana au anaendelea kuwa msaidizi wa elohim kwa Wana wa Mungu. Imani na mtazamo huu ulikuwa ni tofauti sana na ule wa Jeshi la malaika waliokuwepo kabla ya kuumbwa kwa mwanadamu. Kulikuwa na Wana wengi sana wa Mungu, akiwemo Shetani mwenyewe (Ayubu 1:6), wakijulikana kama Nyota za Asubuhi wakati wa uumbaji wa dunia (Ayubu 38:7). Suala la kwamba lilijitokeza baadae na ambalo lilifanyika kuwa la muhimu sana kwenye kipindi cha katikati ya karne ya tatu ilikuwa ni iwapo kama kiumbe huyu mdogo na msaidizi alikuwa ni mmoja wa viumbe au ni kama alikuwa ni mmojawapo tu ya utaratibu wa kumiliki. Wayunani waliichukulia muono wa Oregon kwenye kipindi kilichofuatia baadae cha nuru ya karne ya tatu. Hivyohivyo, wanazuoni kama akina Theognostus wa shule ya kateksomu ya huko Alexandria, walisisitiza Uwana wake na Baba. Hata hivyo, Mwana alichukuliwa kuwa ni kama ni kiumbe mwenye harakati zake zenye ukomo kwa viumbe wa aina fulani. Na alitangaza pia kwamba udogo na usaidizi wake au ousia (akutumia neno la Kiplatoniki zaidi kuliko neno hypostases) alitokana na usaidizi wa Baba (soma kitabu cha Kelly cha, Early Church Doctrines [Mafundisho ya Kanisa la Kwanza], ukurasa 133). Wengine walisisitiza dhana ya udogo na usaidizi wake.

 

Mwanafunzi wa Origen aitwaye Dionysius, Papa wa Alexandria, alyetokana na kuparaganyika kwa imani ya Kisabelliani kwenye Pentapolis ya Kilybia mwishoni mwa miaka ya mwishoni ya hamsini ya karne ya tatu, aliandika akiupinga Umodalism. Alikanusha kabisa utofauti wa kinafsi wa kati ya Baba na Mwana kwa kiasi kikubwa sana. Wasabellian walikuwa na moja ya nyaraka zake alizowaandikia maaskofu Ammonius na Euphranor alielezea kwa kina jambo hili ambalo Kelly (p. 134) anadai kuwa lilikuwa haliwezekani wala kustahili. Dionysius, Papa wa Roma, alimwandikia Dionysius, Papa wa Alexandria, (Papa kilikuwa ni cheo cha kawaida tu walichopewa Maaskofu wakuu hasa wale waliokuwepo huko Alexandria tangu kipindi cha Heraclus yapata mwaka 233-249 (kwa mujibu wa kitabu cha Eusebius, cha Historia ya Kanisa [Church History], vii, 7,4)), kinatoa uhakika kwamba wafuasi wa Origen walisisitiza juu ya mjumuisho au uwepo wa viumbe watatu kila mmoja akiwa peke yake na ambao wanaonekana kuwa kila mmoja yupo kivyake pasi kutegemeana na wala hawaungamaniki na kile kinachoita au kujulikana kama umilele ulio sawa (apud. Athan., De decr. Nic. syn. 26). Alexandria inakubalika kwa kiasi fulani kwa majibu yake (apud. Atan., De sent. Dion. 14-18). Wasabellian walilalamika kwamba wafuasi wa Origen walikuwa wanaweka migawanyiko midogo iwe mikubwa ili kuwatenganisha kati ya Baba na Mwana. Jambo hili lilipingwa na kuthibitiwa na Wanovationist wa huko Roma waliomshawishi au kumvutia Askofu Dionysius, Papa. Athanasius alijaribu (kwenye kitabu chake cha De sent. Dion. 4) kumtakasa Dionysius wa Alexandria karne nyingine moja iliyofuatia lakini Basil (Ep. 9.2) aliendelea kutetea kwamba alikuwa amegeukia kwenye upande mwingine wa uhafidhina mkubwa wa wenye juhudi ya kuupinga Usabellian.

 

Ni kwanini habari ya nafasi au pahala pa Kristo kuhusiano wake na Mungu iwe na umuhimu mkubwa kiasi hiki kama itakuwa haina msingi wa kibiblia? Kwa nini iwe kwamba ya muhimu sana kihivyo katika kipindi cha katikati mwa karne ya tatu? Jibu lake linatuama kwenye dini za siri za mungu jua.

 

Imekuwa ikionekana hivyo tangu kwenye maendeleo ya zama za kwanza, na zaidi, kwamba Biblia na wanateolojia wa Kanisa la kwanza walikuwa ni wa mirengo ya kuamini usaidizi na Uyunitarian. Mungu Baba alikuwa ni Mungu na Baba wa Masihi ambaye ndiye alikua mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi (Warumi 8:29). Roho Mtakatifu ni kifaa ambacho kamba Wana wote a Mungu, pamoja na malaika, wanaifikia nafasi yake ya kuunganika na Mungu. Kristo alikuwa ni miongoni mwa Wana wengi wa Mungu, lakini alikuwa ni mzaliwa wa pekee (monogenes) (Mwana wa) Mungu (ambaye ndiye monogenese theos), mzaliwa wa kwanza (prototokos) kati ya Malaika wa mbinguni akiwa kama kuhani mkuu wa elohim. Elimu hii na uelewa wake vimeanza kupotea kwa kupitia mbinu za kimapokeo ya Kanisa la kwanza. Dini potofu za kisirisiri zilishika hatamu na zilikuwepo kwenye teolojia na kanuni za kidini za Kanisa la kwanza. Habari hii imeelezewa kwa kina kwenye kitabu cha Dini za siri cha Mysticism.

 

Bacchiocchi (loc. cit.) alionyesha uwepo wa dini hizi za mungu Jua kwenye kipindi cha mpito cha mabadiliko ya kutoka ibada za siku za Sabato hadi sasa kuwa Jumapili na uingizwaji wa sikukuu za kipagani kama vile Krismas na Easter. Maadhimisho ya Krismas hayakuwepo makanisani hadi maka 475 huko Syria. Easter iliingizwa kwenye Ukristo huko Roma mnamo mwaka 154 chini ya Anicetus na hila ilifanywa mnamo mwaka 192 BK wakati wa Victor. Mabadiliko ya kuifanya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu na Pasaka kubalishwa kwa kuiingiza Easter yaliendelea kwa kasi kubwa. Waongofu alioingia kwenye Ukrito wakitokea kwenye dini potofu za Kisiri na za waabudu Jua aliongeza shinikizo kwa kutumia mbinu za uhamasishaji kwa kuondoa misimamo ya Kiyahudi ya sharia au torati na za sikukuu (soma kitabu cha Bacchiocchi, op. cit.) ambazo zilikuwa zinatokana na kalenda ya mwandamo wa mwezi na siyo ya mzunguko wa jua. Ujazaji wa mafundisho ya kisynkretiki ulipelekea kufikiwa kwa kilele chake kwenye Mtaguso wa Nicća. Kosmolojia ya kibiblia ilituama kwenye mamlaka yote na kuinuliwa kwa Eloah. Jambo hili lilikuwa na maana kubwa sana kwa tabia isiyochukiza ya sharia au torati. Kubadilisha kwa utaratibu kungekua na maana ya kuwepo kwake tu iwapo kama mchakato ungeanza kwa kumuinua na kumtukuza Kristo kwa kumfananisha kuwa sawa na Mungu na hatimaye kulipa mamlaka Kanisa ya kuyatengea kazi mamlaka kama hayo ni kama ilivyoeleweka na kutafsiriwa kimakosa kuwa limepea Kanisa.  

 

Utata wa kwanza kuhusu sheria ulikuwa ni kuhusu Pasaka na Sabato ya juma. Kuingizwa au kuanzishwa kwa ibada za Jumapili na kufanya kuwa ni siku muhimu na ya lazima ya kuabudu kulianzishwa na Mtaguso wa Halmashauri Kuu ya Elvira (mwaka 300). Haikuwa bahati mbaya tu kwamba mtaguso wa Nicća uliamua suala la Pasaka na kuanzishwa kwa maadhimisho ya sikukuu ya kipagani ya Easter. Haikua ni kwa bahati mbaya tu kwamba jambo lililofuatia lilikuwa ni kuihusu Sabato ambapo, kwenye Mtaguso wa Laodicea mwaka 366 (tarehe hazikumbukwi vizuri), Mtaguso, kwenye Kanoni ya 29, ulipiga marufuku kuiadhimisha Sabato na ulianzisha na kuitangaza rasmi Jumapili kuwa ndiyo siku rasmi ya kuadhimishwa kwa ibada za Kanisa. Kwa hiyo, hatua ziliwekwa na kupangiliwa kwa kile kilivhokuwa kikionekana kama kuondolewa kwa kile kilichokuwa kinaitwa chembechembe za itikadi na imani za Kiyahudi kwenye imani ya Kikristo. Kilichojitokeza na kuonekana ni Upagani ndani ya Ukristo.

 

Endelea ili ujionee jinsi waandishi waliofuatia walivyodanganya Ukristo kama kwenye historia kwenye jarida hili la Makosa ya Kiutafsiri ya Ubinitarian na Utrinitarian Kuhusu Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu (Na. 127B).

.

q