Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[299C]
Ufafanuzi Kuhusu Danieli
Sura ya 7
(Toleo La 1.0 20140327-20140327)
Danieli sura ya 7 inahusiana na matukio ya siku za mwisho na vita
vitakavyotangulia kabla ya kurudi kwa Masihi.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)
(tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ufafanuzi
Kuhusu Danieli Sura ya 7
Utangulizi
Danieli sura ya 7 ni mwendelezo wa tukio
lililotangulia kabla yake ya kisa na habari ya kukombolewa kwa Danieli kutoka
kwenye tundu la Simba kilichotokea wakati wa utawala wa Dario na inaendelea
kuelezea mambo mengine yaliyojiri kipindi cha Koreshi Muajemi. Maandiko
yanauelezea mwaka wa Kwanza wa Belshaza mwana na kukaimu na kutawala pamoja na Nabonidus,
Mfalme wa Mwisho wa Babeli (555-539 KK). Nabonidus alirithiwa na Koreshi na
Dario aliyetajwa kwenye sura ya 6 aliyetawa baada ya Koreshi. Belshaza
hakurithishwa na baba yake, bala walitawala kwa pamoja wote wawili nay eye
akiwa kama ndiye Mfalme Liyetawazwa rasmi. Nabonidus aliondoka kutoka mji mkuu
wao mara tu baada ya kuinuka kwake na kuchukua ufalme, upande wa magharibi, na
hakuwepo mjini na wala hakujihudhurisha kwenye Sherehe za Mwaka Mpya kwa
kipindi cha miaka saaba. Kwa hiyo, mwaka wa Kwanza wa kukaimu huenda ulikuwa ni
mwaka wa pili wa utawala wa Nabonidus takriban mwaka 554 KK na unaweza pia kuwa
ni tangu mwaka 555. Nebukadneza alitawala tangu mwaka 605 KK hadi mwaka 562 KK na
alirithiwa na mwanae Evil-Merodaki 562-560KK. Nabonidus peke yake ndiye
anayemtaja Nebukadneza na Neriglissar kama wana wa ufalme wawili waliofuatia na
hawamtaji mfalme huyu na wala masalia au sehemu ya habari zao kwenye vitabu vya
Historia ya Nyakati za Wababeloni hazimtaji. Neriglissar alikuwa ni mfalme
tangu mwaka 560-555 KK. Danieli ialikuwepo wakati huu wote tangu mwaka 597 akiwa
kijana mdogo hadi mwaka 555/4 wakati alipofikia umri wa takriban miaka 62 wakati
alipoyaona maono haya na ambayo yamefuatiwa kutoka na maandiko yaliyo kwenye
sura ya 2. Ni muhimu kujua kuwa mandiko haya yanahusiana na mlolongo wa matukio
yaliyopo kwenye sura ya 2:42-43.
Sura ya 7 imeandikwa kwa lugha ya Kikaldayo na
inafuatia matukio ya kwenye sura ya 2:42-43 ambayo yanahusiana na Falme au Dola
zitakazoinuka ambazo sasa zinainuka katika Siku hizi za Mwisho. Kipindi cha kujiri
kwa matukio haya ni kile cha siku za mwisho cha utimilifu wa Wamataifa chenye
jumla ya miaka 2520 kijulikanacho kama cha Nyakati za Wamataifa na cha
uanzishaji wa dola za siku za mwisho iliyoanzia tangu mwaka 1914-1918 na mwisho
wao ni mwaka 1996 na ndio mwanzo wa kipindi cha Dola ya mwisho ya Mnyama
kuanzia mwaka 1997 (soma jarida la Kuanguka kwa Dola ya Misri Sehemu ya II: Vita vya
Meisho (Na. 036_2)).
Danieli 7:1-28
1 Katika
mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danielii aliona ndoto, na maono
ya kichwa chake, kitandani mwake; basi akaiandika ndoto, akatoa habari ya jumla
ya mambo hayo. 2 Danielii akanena, akisema, Naliona
katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni
zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa. 3 Ndipo
wanyama wakubwa wanne wakatoka baharini, wote wa namna mbalimbali. 4 Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya
tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi,
akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa
kibinadamu.
Hii inachukua sura ya Kibabeloni na mfumo au
imani yake yenye Miguu ya Chuma kwenye sanamu iliyoandikwa kwenye sura ya 2
ambayo ilikuwa ni Dola ya Rumi na nyayo zake za mchanganyiko wa Chuma na Udongo
ilikuwa ni iliyokuwa inaitwa kuwa ni Dola Takatifu ya Roma ambayo ilidumu na
ilikuwa ni budi idumu tangu mwaka 590 KK hadi 1850 huko Roma na kisha akarishwa
na Mnyama ambayo iliundwa kutoka mfuo huko Ulaya. Ilikuwa ni kuwa Dola hii ya mwisho
iliyoundwa kutoka kwenye unguvu nyingine kwa kipindi chote cha zaidi karne ya 19
na 20. Ilikuwa ni Dola iliyokusudiwa kuwa ni ya Mfalme wa Kaskazini ikiwa kama
ni Mnyama wa Nne wa maandiko haya. Kumbuka kuwa aliinuliwa juu na kuwezesha
isimame kwa miguu yake na akapewa moyo wa mwanadamu katika siku za mwisho. Na
kwa hiyo inaibadili hadhi yake na imefishwa tena na tena na kufanyika kuwa ni
muunganiko wa Mnyama wa Nne.
5
Na tazama, mnyama mwingine, wa pili, kama dubu,
naye aliinuliwa upande mmoja, na mifupa mitatu ya mbavu ilikuwamo kinywani
mwake katika meno yake; wakamwambia mnyama huyo hivi, Inuka, ule nyama tele.
Hii ilikuwa ni bara la Ulaya lililoundwa kutoka
kwenye mfumo wa Kirusi na iliua jozi nyingi za mamilioni ya watu kwenye kipindi
ambacho iliundwa kwayo. Mbavu tatu zilizobanwa kinywani mwake zinahusiana na
hizi Nchi zinazojulikana kuwa ni za Kibaltiki na zinaweza zinaweza kutanjwa pia
na maeneo mengine zaidi za uliokuwa muungano wa umoja wa Kisovieti pia.
Inayofuatia inahusiana na ya Tatu nay a mfumo wa Kiasia.
6
Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama
chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama
huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.
Huyu alikuwa ni Mnyama wa Tatu aliyetokana na
Yule aliyepewa mamlaka au ufalme na aliyetokea Baharini ambao ni idadi kubwa ya
wanadamu. Chui ni kama alama ya kinembo inaweza kuwa simba au duma. Inaoashiria
mfumo au dini za Kihindi au Kiasia na inaenea kutoka Mashariki ya Kati hadi
Mashariki ya Mbali.
Katika siku za mwisho, Mnyama wa Nne anatokea
kutoka kwa ule mfumo wa tatu wa kwanza waliopita na ni vidole hivi kumi vya
chuma vilivyochanganyika na udongo na ambavyo vinaunda kutoka kwenye sura ya 2.
Imekuwa ikiwezeshwa kuchukua madaraka na utawala
kwa kipindi cha zaidi ya miaka thelathini iliyopita ya mwisho wa mfumo na
utawala wa kidunia. Iliwekewa mkakati wake kwenye kile kinachoitwa kama Klabu
ya Roma mnamo mwaka 1956 ikiwa kama miungano ya kiuchumi zinazozisukuma na
kupekelesha uweza au nguvu za kitaifa la kila taifa linguine lolote. Hata
hivyo, inatumia nguvu za kijeshi za Mfalme wa Kaskazini ambayo kwa hakika
kabisa inamaanisha kuwa ni umoja wa kujihami wa NATO.
7
Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama,
mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa
na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na
kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale
wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi. 8 Nikaziangalia
sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa
ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang'olewa kabisa;
na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na
kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu.
Maandko yaliyo kwenye Danieli sura ya 8 yanaonyesha
mgongano uliokuwepo kati ya Wamedi na Waajemi walipoichukua na kuitamalaki dola
ya Babeli. Sura ya 9 inaelezea unabii kuhusu Hekalu na kuanguka kwa Yerusalemu
baada ya majuma sabini ya miaka kwenye mwaka mtakatifu wa 70-71 BK. Kwenye sura
ya 10 Danieli alipewa au kuonyeshwa maono katika Mwaka wa Tatu wa Koreshi na
inaelezea kuwa maandiko yanayofuatia yalikuwa ni kwa kipindi cha mbali cha siku
zijazo katika siku za mwisho, na alipewa uwezo wa kuelewa kwamba Wayunani
wangechukua utawala baada ya hawa Waajemi na Yule mfalme aliyeelezewa kwenye
Danieli angefanya vita na mfalme wa atakaye watawala Wayunani pia. Mchakato huu
ulianza kutoka kwenye Vita ya Wagranicus na ulifuatia jumla ya siku 2300 jioni
na asubuhi iliyoelekea na kuendelea mbele hadi kwenye marejesho mapya ya
Yerusalemu mwishoni tangu mwaka 1967 (soma pia jarida la Maelezo ya Ratiba ya Nyakati (Na. 272)). Kisha unabii
unakwenda kwenye mlolongo wa vita vya wafalme wa Kaskazini na vya Kusini
ambavyo vinachukua mlolongo na mfuatano wote mzima wa vita kutoka kwenye
ushindi juu ya Waajemi hadi kwenye vita vya siku za mwisho.
Amdiko la Danieli sura ya 7:7 linahusu matukio
yaliyo kwenye Danieli 11:40-45. Kuna vita vya siku mwisho na jinsi Dola ya
Mnyama inashika hatamu na kuzitiisha dola nyingine tatu na kuimiliki Nchi
Takatifu na dunia tangu kipindi cha miezi 42.
Danieli 11:40-45
40
na wakati wa mwisho mfalme wa kusini atashindana
naye; na mfalme wa kaskazini atamshambulia kama upepo wa kisulisuli, pamoja na
magari ya vita, na wapanda farasi, na merikebu nyingi; naye ataingia katika
nchi hizo, na kufurika na kupita katikati. 41 Tena
ataingia katika hiyo nchi ya uzuri, na nchi nyingi zitapinduliwa; lakini nchi
hizi zitaokolewa na mkono wake, Edomu, na Moabu, na wakuu wa watu wa Amoni. 42 Naye ataunyosha mkono wake juu ya nchi hizo, hata na nchi
ya Misri haitaokoka. 43 Lakini atakuwa na nguvu juu ya
hazina za dhahabu na fedha, na juu ya vitu vyote vya Misri vyenye thamani; na
Walibia na Wakushi watafuata nyayo zake. 44 Lakini
habari zitokazo mashariki na kaskazini zitamfadhaisha; naye atatoka kwa
ghadhabu nyingi, ili kuharibu, na kuwaondolea mbali watu wengi. 45 Naye ataweka hema zake za kifalme kati ya bahari na mlima
mtakatifu wa uzuri; lakini ataifikilia ajali yake, wala hakuna atakayemsaidia.
Kipindi cha kutamalaki na kutiisha ulimwengu cha
Mnyama wa Pili na wa Tatu kitatokea kwa kipindi kifupi cha vita katikati ya
wakati atakapoenda mbele kuelekea kutoka Mashariki ya Kati kuyatiisha mataifa
ambayo yanampigia kelele kutokana na habari za kutoka Mashariki. Hi ni kipindi kilichotajwa
kwenye Ufunuo kama ni Timetable of the Agita za Baragumu ya Tano nay a Sita. Thelithi
moja ya watu watauawa kwenye vita hivi. Kwa kipindi cha miezi 42 ambacho Mnyama
na Nabii wa Uwongo na Mpingakristo watatawala kutoka Yerusalemu watakuwa
wanapingwa na Mashahidi Wawili watakaotumwa na Mungu kusimama mbele yao. Hawa
ni Henoko na Eliya ambao walitumwa kusimama mbele ya Mungu wa Dunia hii (soma
jarida la Mahahidi (wakiwemo wale Mmashahidi Wawili (Na. 135)).
Kwa hiyo ndipo tutakabiliwa na ujio wa Masihi
kuja kushika hatamu za kuitawala hii dunia na kuurejesha Ufalme wa Mungu (soma
jarida la Kungojea Ujio wa Masihi (Na. 210A)).
9
Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja
aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele
za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na
gurudumu zake moto uwakao. 10 Mto kama wa moto ukatoka
ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi
wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.
Vitabu vilifunguliwa ili kuwaja wale walio
kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu. Hawa ni wale waliochaguliwa (soma jarida la Mbingu, Jehanamu au Ufufuo wa Wafu (Na. 143A)). Katika
kipindi hiki cha ujio wa Masihi, Mpingakristo na Nabii wa Uwongo wataangamizwa
na Dola ya Mnyama itaangamia yote kabisa. Haya pia ni matukio yaliyoelezewa
kwenye Danieli sura ya 12:1-13. Matukio ya nyakati moja, nyakati mbili na nusu
wakati ni jumla ya siku 1260 za Mashahidi wa nyakati za mwisho wakati
Watakatifu watakapotawanyika. Ni baada ya miaka hii mitatu na nusu ambayo
tutakuwa tumefufuliwa kama ilivyoelezewa kwenye sura ya 12.
11
Nikatazama wakati huo; kwa sababu ya sauti ya yale
maneno makubwa iliyoyasema ile pembe; nalitazama hata mnyama yule akauawa,
mwili wake ukaharibiwa, akatolewa ateketezwe kwa moto.
Kumbuka kutoka kwenye maandiko kwamba Wanyama
watatu waliopita hawakuuawa na uhai au maisha yao yaliongezwa. Ni kwenye
kipindi hiki wakati Dola ya Mnyama ikiangamizwa ndipo Kristo atakapoanza
kuyashughulikia mataifa yaliyo chini ya Wanyama hawa.
12
Na kwa habari za wale wanyama wengine,
walinyang'anywa mamlaka yao; walakini maisha yao yalidumishwa kwa wakati na
majira.
Ndipo tutamuona Masihi akija akitokea mbele ya
Mzee wa Siku na akiwa amepewa mamlaka kamili ya kuitawala dunia.
13
Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja
aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo
mzee wa siku, wakamleta karibu naye. 14 Naye akapewa
mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na
lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe,
na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.
Kisha Danieli anapewa ufafanuzi wa maana yake.
15
Basi, mimi Danieli, roho yangu ilihuzunika mwilini
mwangu, na hayo maono ya kichwa changu yakanifadhaisha. 16 Nikamkaribia
mmoja wa hao waliosimama karibu, nikamwuliza maana ya kweli ya hayo yote. Basi
akaniambia, akanijulisha tafsiri ya mambo hayo. 17 Wanyama
hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani. 18 Lakini watakatifu wake Aliye juu wataupokea ufalme, na
kuumiliki huo ufalme milele, naam hata milele na milele.
Kisha tunaona kwamba utawala na dini ya Mnyama
ni ule wa Mpingakristo ndiyo inayofanya vita na kanisa.
19
Kisha nalitaka kujua maana ya yule mnyama wa nne,
aliyekuwa mbali na wenziwe wote, mwenye kutisha sana, ambaye meno yake yalikuwa
ya chuma, na makucha yake ya shaba; aliyekula, na kuvunja vipande vipande, na
kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; 20 na habari za
zile pembe kumi zilizokuwa kichwani mwake, na ile pembe nyingine iliyozuka,
ambayo mbele yake zilianguka pembe tatu; yaani, pembe ile yenye macho, na kanwa
lililonena makuu, ambayo kuonekana kwake kulikuwa hodari kuliko wenzake.
Vita hivi vitakomeshwa kwa kuingiliwa na Mungu
na Watakatifu wataokolewa kwa iungiliaji huu wa Mungu nao watahukumiwa. Ufalme
wa Nne wa Mnyama nao unaelezewa.
21
Nikatazama, na pembe iyo hiyo ilifanya vita na
watakatifu, ikawashinda; 22 hata akaja huyo mzee wa
siku, nao watakatifu wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia
watakatifu waumiliki ufalme. 23 Akanena hivi, Huyo
mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia, utakaokuwa mbali na falme
zile zote, nao utakula dunia yote, na kuikanyaga, na kuivunja vipande vipande. 24 Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo
wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali
na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu. 25 Naye
atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake
Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake
kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.
Mnyama huyu na mfumo wake chini ya Mpingaktisto
watawatawala watakatifu kwa kipindi cha miaka 1260 yangu mwaka 590 BK hadi
mwaka 1850 BK ya Dola Takatifu ya Rumi na pia kwenye vita vya mwisho kwa
kipindi chote cha siku 1260 na zote mbili, yaani Vita ya II ya Dunia ya Manazi
na kipindi cha siku 1260 za Mashahidi kabla ya Kuja kwa Masihi.
26
Lakini hukumu itawekwa, nao watamwondolea mamlaka
yake, kuipoteza na kuiangamiza, hata milele. 27 Na
ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa
watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye
mamlaka watamtumikia na kumtii. 28 Huu ndio mwisho wa
jambo lile. Nami, Danielii, fikira zangu zilinifadhaisha, na uso wangu
ulinibadilika; lakini naliliweka jambo hilo moyoni mwangu. [
Kipijndi hiki ni cha utawala wa Milenia wa Kristo na Kanisa kutoka
Yerusalemu tangu mwaka 2018 hadi 3027 na miaka mia moja ya Ufufuo wa Pili wa
watu na Hukumu (soma jarida la Ufufuo wa Pili wa Wafu na Kiti cha Enzi Kikubwa
Cheupe cha Hukumu (Na. 143B)).
Kwa hiyo ni kutokana na yubile inayofuatia
wakati wa tukio Kubwa la Kutoka (sawa na ilivyo pia kwenye Isaya 65).
Zekaria 10:10-12
10
Tena nitawarudisha toka nchi ya Misri,
nitawakusanya na kuwatoa katika Ashuru; nami nitawaingiza katika nchi ya
Gileadi na Lebanoni; ila nafasi ya kuwatosha haitaonekana. 11
Naye atapita kati ya bahari ya mateso, na kuyapiga mawimbi ya bahari, na
vilindi vyote vya mto wa Nile vitakauka; na kiburi cha Ashuru kitashushwa; na
fimbo ya enzi ya Misri itatoweka. 12 Nami nitawatia
nguvu katika Bwana; nao watatembea huko na huko katika jina lake, asema Bwana.
Zekaria 11:1-3
1
Ifungue milango yako, Ee Lebanoni, Ili moto uiteketeze mierezi yako. 2 Piga yowe, msunobari, maana mwerezi umeanguka, Kwa sababu
miti iliyo mizuri imeharibika; Pigeni yowe, enyi mialoni ya Bashani, Kwa maana
msitu wenye nguvu umeangamia. 3 Sauti ya wachungaji,
ya uchungu mwingi! Kwa maana utukufu wao umeharibika; Sauti ya ngurumo ya
wana-simba! Kwa maana kiburi cha Yordani kimeharibika.
Kumbuka kuwa Mnyama wa Siku za Mwisho ni muunganiko wa mambo haya tofauti
ya Wanyama hawa watatu.
Ufunuo 13:1-10
1
Kisha nikaona mnyama akitoka katika bahari, mwenye pembe kumi, na vichwa saba,
na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na juu ya vichwa vyake majina ya
makufuru. 2 Na yule mnyama niliyemwona alikuwa mfano
wa chui, na miguu yake ilikuwa kama miguu ya dubu, na kinywa chake kama kinywa
cha simba, yule joka akampa nguvu zake na kiti chake cha enzi na uwezo mwingi. 3 Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa
jeraha la mauti, na pigo lake la mauti likapona. Dunia yote ikamstaajabia
mnyama yule. 4 Wakamsujudu yule joka kwa sababu alimpa
huyo mnyama uwezo wake; nao wakamsujudu yule mnyama, wakisema, Ni nani
afananaye na mnyama huyu? Tena ni nani awezaye kufanya vita naye? 5 Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya makufuru.
Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake miezi arobaini na miwili. 6
Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na
maskani yake, nao wakaao mbinguni. 7 Tena akapewa
kufanya vita na watakatifu na kuwashinda, akapewa uwezo juu ya kila kabila na
jamaa na lugha na taifa. 8 Na watu wote wakaao juu ya
nchi watamsujudu, kila ambaye jina lake halikuandikwa katika kitabu cha uzima
cha Mwana-Kondoo, aliyechinjwa tangu kuwekwa misingi ya dunia. 9 Mtu akiwa na sikio na asikie. 10 Mtu
akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa
upanga. Hapa ndipo penye subira na imani ya watakatifu.
Kumbuka kwamba Mnyama huyu anaabudiwa na
ulimwengu wote na anafanyika kuwa yeye mwenyewe ni mtu wa kuabudiwa na awe
kwenye mfumo wa kidini. Anabidi kuangamizwa kabisa na wote wanaogongwa mhuri wake
hawataurithi ufalme wa Mungu na hawataingia kwenye kipindi cha utawala wa Milenia.
Mambo haya yameandikwa kwenye majarida yaliyotajwa hapa (soma pia majarida ya Vita Vya III vya Dunia Sehemu ya I: Dola ya Mnyama (Na. 299A) na pia Vita vya III vya Dunia Sehemu ya II: Mwanamke
Kahaba na Mnyama (Na. 299B)).
q