Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[021]

 

 

 

Manabii Kumi na Mbili

 

(Toleo La 1.0 20150314-20150314)

 

Manabii Kumi na Mbili ni wa mwisho kwenye utaratibu wa mpangilio wa Kanuni ya mpangilio wa vitabu lakini haina maana kuwa wao ni wadogo au duni kwenye umuhimu wa Manabii wa Mungu.

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2015 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Manabii Kumi na Mbili


 


Utangulizi                                      

Orodha ya Kikanuni ya mpangilio wa Manabii Kumi na Mbili wanaoitwa au kujulikana kama Manabii Wadogo imeorodheshwa kwa mpangilio ufuatao:

Hosea

Yoeli

Amosi

Obadia

Yona

Mika

Nahumu           

Habakuki

Sefania

Hagai

Zekaria

Malaki.                                                         

 

Wamewekwa kwenye utaratibu au muundo wa manabii watatu, kisha manabii sita na hatimaye manabii watatu.

 

Mpangilio uliotumika katika kuwapanga sio mpangilio ambao Mungu aliutumia alipowatuma. Mungu alimtuma Amosi kwanza wakati anaonekana kuwa watatu kwenye Kanuni hii ya mpangilio kwa mfano. Ni sawa tu na kama Zekaria alipouawa na makuhani na manabii. Wengine waliteswa vibaya mno.

 

UTARATIBU WA KIMPANGILIO WA MANABII.

 

Israeli walipewa miaka arobaini kuwaonya tangu mwaka 761-721 KK kama tulivyoona kwa manabii wa mwanzoni, kina Yona na Amosi. Abraham ibn Ezra mwanazuoni wa enzi ya zama kati alimuweka kwenye miaka arobaini kabla ya kuanguka kwa Samaria lakini wanazuoni waliofuatia wanamuwekwa kwenye miaka thelathini ya kabla ya kuanguka kwake Samaria (750-720) (linganisha na Soncino, Tangu Utangulizi hadi ukurasa wa 1).

 

Hakuna shaka kwamba Mungu aliwaonya Israeli kwa kipindi cha miaka arobaini kabla ya anguko la Samaria sawasawa na utaratibu wa kiunabii.

 

Israeli walipewa miaka 40 na ndivyo pia walivyopewa Yuda tangu mwaka 30 BK wakati wa Pasaka ya kifo cha Kristo hadi mwaka 70 BK kwenye mwisho wa majuma Sabini ya miaka na kuangamizwa kwa Hekalu kulikofanywa na Warumi (soma majarida ya Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Upya wa Hekalu (Na. 013) na Vita na Warumi na Kuanguka kwa Hekalu (Na. 298)).

 

Ndivyo ilivyokuwa pia Ishara ya Yona iliyoendelea kwa kipindi cha yubile 40 kwenye Yubile ya miaka inayoendana kwa msingi wa kipindi cha Kanisa kuwa jangwani kama ilivyokuwa kwa Israeli kuwa jangwani kipindi cha Kutoka. Ndivyo ilivyokuwa pia kwa Makanisa ya Mungu limepewa miaka 40 ya Upimaji wa Hekalu tangu mwaka 1987 hadi kwenye Yubile ya mwaka 2027 (soma pia jarida la Upimaji wa Hekalu (Na. 137)). 

 

Manabii wote Kumi na Mbili waliudumu tangu miaka 40 kabla ya kuanguka kwa Samaria hadi kwenye Siku za Mwisho na ujio wa Masihi na kutwaliwa au kutekwa ya mji wa Yerusalemu. Kisha Zekaria anaanza mchakato wa utawala wa milenia.

 

Yona

Maonyo kwa Waashuru ambao walitumika kwenye mkakati wa kuiangusha na kuikomesha dola ya Israeli yalifanywa na Yona na kwa hiyo na maonyo yake yalifanana na ya Amosi.

 

Kama tutakavyoona kwenye jarida la ufafanuzi wa kitabu cha Yona mwana wa Amitai akiwa kama mtu anayejulikana sana kwenye historia. Ametajwa kwenye 2Wafalme 14:25. Alikuwa anatokea Gath-hefa ambao ni mji wa mpakani na Zabuloni (sawasawa na Yoshua 19:13). Huenda inaonyesha na Kiribeti ez Sura’ ambao ni mahala pakubwa sana ulio maili tatu Kaskazini-Mashariki ya Nazarethi, ambao ulikuwa katika Galilaya. Maneno ya Mafarisayo kwenye Yohana 7:52 yalikuwa ni ya uwongo ule. Kristo alitokea eneo la Nazarethi ya Galilaya, kama alivyokuwa Yona. Ulikuwepo wakati wa Zama za Chuma, awamu zote za I na II  yaani miaya ya 1200-600 KK na ndicho kipindi cha Yona na kabla ya hapo kwenye kipindi kilichofuatia cha Zama za Shaba tangu mwaka 1550 KK na kuendelea. Yona alikuwa anahudumu kipindi kimoja na Yeroboamu II mfalme wa Israeli (793-775 KK) na miaka ya mwanzoni ya utawala wa Uzia (775-757 KK). Upo umbali mfupi upande wa kaskazini mwa kijiji kilichobakia cha Meshedi ambacho ni mahala ambapo kimapokeo ndipo lilipo Kaburi la Yona.

 

Ni kama tulivyoona kwenye jarida la Kuanguka kwa Misri (Na. 036), na ilivyoelezewa tena kwenye jarida la ufafanuzi wa kitabu cha Yona, mwaka 732 KK mfalme Tiglathi Pileser III wa Ashuru aliungana na Wadameski ili kuwatoza kodi Israeli na Yuda. Mwaka 729 KK Tiglath Pileser III aliungana na Wababeloni na Shalmaneser V (tangu mwaka 724-721 KK) akajiunga na Israeli mwaka 722 KK. Mrithi wake Sargon II aliyahamisha makabila kumi na mbili.

 

Ushuhuda wa Yona ulikuwa kwa kipindi cha zaidi ya miaka arobaini tangu utawala wa Yeroboamu II (793-775) hadi Uzia (775-753) na tawala zingine mchanganyiko zilikuwa kwa kipindi cha miaka arobaini pamoja na kipindi cha matazamio tangu mwaka wa tatu wa utawala wa Uzia yapata kama mwaka 772-732 hadi kwenye kipindi cha Kutozwa kodi hadi cha Waashuru. Israeli walipelekwa utumwani Ashuru kwa kipindi cha kuanzia mwaka 722 KK ambacho kilikuwa ni cha wastani wa miaka 40 na kisha miaka 50 au yubile ya tangia unabii wa Yona kwa Israeli. Ilimpasa Yona ajifunze kutokana na huduma yake ya Ninawi na kuwaonya Israeli kwa kile Mungu alichowafanyia na kile ambacho hatimaye kingalichowatokea Israeli lakini hawakusikiliza kama Yuda wasivyomsikiliza kwa kipindi chote cha miaka arobaini walichopewa kwa ajili ya toba (soma pia jarida la Kuujua Mzunguko wa Nyakati (Na. 272)).

 

Inaonekana kwamba Yona na Amosi walikuwa wakihudumu kuwaonya kwa wakati mmoja wakiwa sehemu zote mbili, yaani Ashuru na Israeli na kwa kipindi ambacho walipewa cha kuwaonya kwa miaka 40 kabla ya hukumu.

 

Kama tunavyoona kwenye maandiko au jarida la Ufafanuzi wa Kitabu cha Hosea na tafsiri za Talmud na Midrash zina mirejesho mingi inayomtaja Hosea na humo anachukuliwa kuwa ni mkuu zaidi kwa unabii wake uliotolewa kwa wakati mmoja na wengine (linganisha na jarida namba 87a). Wafafanuzi wanaamini kuwa baba yake Beeri kuwa naye pia alikuwa nabii na unabii wake umejmuishwa kwenye Isaya 8:19ff (sawa na kitabu cha Lev. Rabba 6, xv, 2). Wadadisi na wafafanuzi wanadhana kwamba sio nabii zote za Hosea zimeandikwa kwa mpangilio mzuri wa kimatukio ila tutaona kama hilo linamashiko likinganishwa na historia. Tafsiri ya Talmud inakubali kuwa Mpangilio huu Kikanuni haujaendana sawasawa pia (B.B 14a). Rejea kwenye kitabu cha Fafanuzi.

 

Yoeli anashughulika na maandalizi ya wateule hasahasa tangu Masihi na kwenye nyakati za mwisho kuna mambo ya muhimu ya kulitakasa kundi la Israeli kama Hekalu la Mungu na kutanguliwa na ni kwa wakati mmoja wake na wa maandalizi ya maandiko ya Ezekieli. Bullinger anakiweka hiki pamoja na Ezekieli tangu mwaka wa tano wa kwenda utumwani kwa Yehoyakimu lakini haukuhesabiwa. Marabi wengine wanauweka mwaka huu mahali pengine. Kanuni ya kupangilia vitabu inauweka katikati ya Hosea na Amosi. Sisi hata hivyo tunajua kwamba Amosi na Yona waliwatangulia.kina Hosea na Yoeli ambao tarehe zao hazijaandikwa na kuhusu matukio yajayo baadae kimsingi yanaangukia kidogokidogo kwa Hosea. Kwa hiyo Mpangilio wa mambo unadhaniwa kuwa ni kama Amosi, Yona, Hosea. Inaonekana hata hivyo huenda mpangilio wa kweli ni Yona, Amosi na Hosea. 

 

Amosi

Amosi kwa ujumla anachukuliwa kuwa kitabu chake kiliandikwa kati ya miaka ya 765 na 750 KK kwenye utawala wa Yeroboamu II (782-743).  Kitabu chake kimeorodheshwa cha tatu kwenye Kanuni ya uorodheshaji bali anachukuliwa kuwa ni wa kwanza wa manabii wengine na kazi yake inamtenga mwenyewe na manabii wa zamani wa kabla yake ambao kwao mkanganyo ulizisibu shule zao kama tunavyojionea kutokana na uandishi wake. Kukataa kwake kuwa si nabii hakumaanishi kuwa hakuwa hivyo, bali alikuwa anasikitishwa na kuwashutumu kwa ajili ya ufisadi wao na alikuwa anawaonyesha kuwa yeye hayupo miongoni mwao.

 

Tetemeko la nchi alilokuwa analiongelee kwenye 1:1 linaaminika kuwa lilitokea wakati wa Uzia (Zekaria 14:5). Kupatwa kwa jua kulikoongelewa kwenye 8:9 inahesabiwa kuwa kulitokea mwaka 763 KK (linganisha na Soncino Utangulizi hadi ukurasa wa 81). 

 

Tena tunaona kipindi cha miaka thelathini na arobaini kikiwa cha muhimu kwa toba ya Israeli (linganisha pia na jarida la Cox la Ufafanuzi wa kitabu cha Yona). Maonyo haya yalifanyika mwaka 763-2 KK na mnamo kwama 733 Waashuru waliuteka mji wa Dameski na kuwafanya kuwa nchi ya kuitoza kodi. Mwaka 723-2 waliingia Samaria na mwaka 722 KK Israeli walichukuliwa kwenda utumwani na wapelekwa eneo la kaskazini mwa Araxes na hawakurudi hadi Ujio wa Pili wa Masihi.

 

Mika

Nabii Mika alitokea nyanda za chini za Shefela karibu na nchi ya Wafilisti, mpakani. Alitabiri kipindi cha utawala wa Yothamu, Ahazi na Hezekia (739-693 KK). Alikuwa kijana mdoho akihudu wakati moja na Hosea na Amosi (soma Soncino, uk. 153).  Mika ana meingi yanayofanana na manabii wawili waliomtangulia na tunaona kutoka kwenye maandiko kwamba anaulaumu utaratibu uliokuwepo na wa makuhani na ushawishi wao au walivyokuwa wanavutiwa na imani ya Baali ambaye dini ya waabudu Juan a unabii wa jinsi Mungu anavyotaka kushughulika nao Israeli. Nabii Isaya analinganishwa na Mika kwenye fafanuzi za Nyongeza. Inaonekana kabiwa kwamba walihudumu wakati mmoja, au kwa kipindi kimoja.

 

Tutamuweka nabii huyu kutoka kwa Isaya kila mara. Manabii Yeremia, Danieli, na Ezekieli wanadhaniwa walihudumu kipindi hiki na wapo hadi kuanguka kwa dola ya Yuda na Wababeloni.

 

Andiko lililo kwenye Obadia linaonekana kuwa liliandikwa wakati wa Yeremia ingawaje hatuna uhakika wa ni lini liliandikwa na aya za mwanzoni za 1-9 zinarudia unabii ulionenwa kwenye Yeremia 49:7-22 hasa hasa kwenye 49:9, 14-16 ambako unaongelewa kwa mdomo (sawa na Soncino). Kazi imejawa na maneno yanayosisitiza haki na hukumu ya Edomu.  

 

Kama ilivyoonyeshwa kwenye ufafanuzi kuhusu mashindano na chuki za Edomu kwa ndugu zake wawili mapacha kulionekana kutokana na jinsi walivyoshindana tumboni na jinsi yalivyoendelea kwa kipindi chote cha historia kwenye mgogoro ambao haujawahi kuonekana kati ya ndugu.

 

Mgongano huu ulijitokeza pia kwa Daudi alipokuwa chini ya Sauli na baadae kwenye utawala na hadi kwenye vita vya Wahasmonean yapata mwaka130 KK na manabii waliendelea kupiga kelele kuwataka wajilipizie kisasi kwa Waedomu au wajitukuze kwa kupindualiwa kwao.

 

Amosi anawachutumu Waedomu kwakuwa walikuwa wakiwachukia Israeli milele (Amosi 1:11). 

(maandiko mengine yanachukuliwa na Soncino kama kwenye Isaya sura ya 34; Ezekieli 35; Zaburi 137:7; Maombolezo 4:21.)

 

Tunapaswa kudhania kwamba andiko hilo mara nyingi linaonekana kwa Yeremia na Obadia likimnukuu yeye zaidi ya kwamba ni kinyume chake.

 

Nahumu

Wanazuoni wengi wanakubali kwamba tarehe ya mwanzoni sana inayokadiriwa kuwa kimeandikwa ni mwaka 663 KK wakati wa kuanguka kwa Thebes hadi Ashuru. Tarehe ya karibu sana inayodhaniwa ni wakati wa kuanguka kwa Ninawi mwaka 612 KK. Dola mamboleo ya Babeli maarufu kama Neo-Babylonian ilianzishwa na Nabopolasa mwaka 625 KK na, kuyakusanya pamoja majeshi ya Wababeloni, aliuvuka mto Frati hadi Qablinu ambako aliliangamiza Jeshi la Waashuru kwa maangamizo makubwa na kuwashinda. Wamedi walianza kushambulia kutoka Mashariki na mwaka 614 waliuchukua na kuukamia mji wa Asshuri. Nabopolasa alifanya muungano hatimaye na mfalme. Pamoja na Wamedi na Wakaldayo aliendelea kushambulia hadi Ninawi ilipoanguka mwaka 612 KK. Mwaka 625 KK ni mwaka unaodhaniwa sana kwa wote wawili, yaani Nahumu na Sefania kwa mujibu wa Gombo lililovumbuliwa la Torati tayari kwa marejesho mapya yaliyofanywa na Yosia katika mwaka wa 18 wa utawala wake. Hivyo basi, ilikuwa ni mwanzoni mwa kujiimarisha kwao Wababeloni ambavyo yalitumika katika kuiangamiza Ashuru.

 

Bullinger anaamini kwamba maovu na machukizo yaliyotajwa kwenye 1:11 kwa kweli inamkusudiac au kumaanisha Rab-sheka aliye kwenye 2Wafalme 18:26-28 huyu anayeonekana kama Myahudi aliyekengeuka au kukufuru ambaye alifanyika kuwa kiongozi mkuu au afisa wa kisiasa wa Senakarebu na alifanya machukizo makubwa sana kwa Yahova wa Israeli.  Bullinger aliupa tarehe ya uandishi wa kitabu hiki kuwa ni mwaka wa 14 wa utawala wa Hezekia na kwa hiyo ni mwaka wa 704/3 KK. Hii huenda ni mapema sana ila ni baada ya kuanguka kwa ufalme wa Israeli. 

 

Obadia

Jina Obadia maana yake ni Mtumishi wa Bwana. Ni jina la watu tofauti kumi na mbili kwenye Agano la Kale. Hatuna hakika kuhusu nabii huyu ni yupi kati yao.

 

Haijulikani pia kwamba ni wakati gani kitabu hiki kiliandikwa na aya za mwanzoni za 1-9 zinakazia unabii uliotolewa kwenye Yeremia 49:7-22 hususan kwenye 49:9, 14-16 ambako imenenwa kwa mdomo (sawa na Soncino).  Uandishi wake umetuama mkazo wa haki na hukumu ya Waedomu. Kwa kuujua ukweli huu yatupasa tudhanie kuwa kiliandikwa baada ya Yeremia na huenda baada ya kugunduliwa kwa gombo au kitabu cha torati Hekaluni kwa ajili ya marejesho mapya. Kwa hiyo kiliandikwa kabla ya Sefania.

 

Sefania

Kutokana na ilivyo hapo juu kwa hiyo inatupasa kudhania kuwa ni Safania. Kama tunavyoona kwenye ufafanuzi wa kitabu hiki cha Sefania, imeorodheshwa mara tisa miongoni mwa manabii walio kwenye mpangilio wa kikanuni wa Agano la Kale. Mlolongo wake wa kiuzawa umeorodheshwa kwa zaidi ya vizazi vinne kwakuwa neno la wazazi wake wa kale kwenye tafsiri ya KJV ni neno hilihili lililo kwenye Kiebrania kama Hezekia na mamlaka yanajiamini alikuwa ni kitukuu wa Hezekia Mfalme wa Yuda.

 

Inachukuliwa na kuaminika na E.A. Leslie (Kamusi ya Interp. Dictionary of the Bible, Bk. IV, pp. 951ff.) kwamba kitabu chake kimekadiriwa kuwa kiliandikwa harakati za ushambulizi wa Scythian yapata mwaka 630-625 KK. Harakati na matendo ya Baali na imani au dini ya Mungu Mke wa Waashuru na Wababeloni, dini zilizokuwa zimeingia katika Yuda baada ya kupanuka kwa dola ya Waashuru na Manase wakajenga madhabahu na kujitengenezea magari ya farasi mahala pa juu pa Mfalme Ahazia ili kuabudu Jua na kushamirisha imani au dini potofu ya Siri. Waliliabudu jua, mwezi na ishsra zote za mbinguni za kizodaki na Jeshi lote la mbinguni (2Wafalme 23:11ff).

 

Habakuki

Inaonekana kwamba Habakuki alitabiri kidogo baada ya gombo la torati lililookotwa Hekaluni wakati wa utawala wa Yosia mwaka 621 KK. Marejesho ya Yosia yalidumu kwa kipindi kifupi na wakati wa Yehoyakimu watu walianza kuabudu tena sanamu na ukengeufu alizidi na ulikubalika sana kipindi hiki. mfalme alibadilisha mambo na kutukuza maovu kwa shuruti na hatimaye wakasalimu amri au kufanyika watumwa wa Nebukadneza (soma 2Wafalme 14:1).

 

Seder Olam zinafundisha kwamba Yoeli, Nahumu na Habakuki wote walitabiri katika siku za Manase (soma Soncino Intro., p. 211). Mfalme huyu alikuwa muovu sana na inadaiwa kuwa waliliruka jina lake kwenye vitabu vyao. Mchakato unaodhaniwa zaidi unaanza baada ya mwaka 621 na unaanza kwa kuinuka au ujio wa Wakaldayo. Wengine wanadhani kwamba huenda ilikuwa katikati ya Mapigano ya Carchemish mwaka 605 KK na kuangamizwa kwa Hekalu mwaka 586 KK; tuseme ni kama mwaka 600 KK wakati wa utawala wa Yehoyakimu.

 

Hata hivyo, kuna mambo mengi sana kwenye unabii huu kuliko ulivyopunguzwa na mamlaka ya marabi. Ukomo wao kwa kipindi cha baada ya Carchemish inavyoweza kuhitimishwa kwenye unabii kama tunavyoona kutokana na ushindi au uvamizi wa Nabopolasa, mfalme wa 1 wa kizazi cha Wakaldayo na Wamedi.

 

Hagai

Kata tutakavyoona kwenye jarida la Ufafanuzi wa kitabu cha Hagai, jina la Hagai linatokana na neno Hag au sikukuu, au karamu au sherehe. Andiko hili linatokana na hali ya Mwandamo wa Mwezi Mpya, lakini Bullinger anakosea sana kwa kusema kwenye uandishi wake kwamba linahusiana kuutaja mwezi mkamilifu ambavyo ni makosa (soma tafsiri ya Companion Bible, fn. 1). Ni mwezi wa Sita au mwezi wa Eluli. Ni katika mwaka wa Pili wa Dario Mwajemi (Dario II) wakati agizo na maelekezo ya kuimalizia ujenzi wa Hekalu yalitolewa na Yahova kwa kupitia nabii Hagai.

 

Andiko hili ndilo maelekezo au agizo kutoka kwa Yahova kwa Yuda kwa kuukataa unabii uliotolewa na Zekaria.

 

Agizo limetolewa katika mwaka wa Kwanza wa Yubile ya 71. Utaratibu kamili wa kimpangilio wa Yubile 71 tangu kufungwa kwa bustani ya Edeni umekamilika na Yubile ya mwaka 424/3 KK, na Hekalu sasa linapasa kujengwa tena. Hili ni agizo la pili kutolewa na Mungu lakini kazi ilisimamishwa kwa kitambo tangu agizo au tangazo la Koreshi hadi kipindi cha Artashasta I aliyesimamisha ujenzi, na ulisimama hadi mwaka wa Pili wa Dario Mwajemi (soma jarida la Ishaya ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 013)).

 

Kipindi cha Dario na Manabii

Kama tulivyoona kwenye majarida yote mawili ya ufafanuzi wa vitabu vya Hagai na Zekaria, Dario II alipata kiti cha ufalme mwishoni mwa mwaka 424 au mapema ya mwaka 423 KK. Agizo hili lilitolewa ili kuanzisha ujenzi mnamo mwaka 422 KK (Ezra 6:1 na 4:24) (yaani mwaka wake wa pili). Majuma 70 ya miaka inaanza tangu tarehe hii. Kutokana na Ezra 5 inaonekana kwamba unabii wa Hagai na Zekaria mwaka 423 KK na mwaka 422 KK. Majuma 70 ya miaka inaanzia tangu mwaka 423/22 KK (yaani mwaka wa kwanza wa kipindi cha Yubile mpya). Ujenzi uliisha katika mwaka wa sita wa Dario Mwajemi (Ezra 6:15) siku ya 3 Adari, yaani mwezi Marchi wa mwaka 418 KK. Dario alifariki kwenye kipindi cha tangu mwishoni mwa mwaka 405 hadi majita ya machipuko ya mwaka 404 (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 013):.  Mpangilio wa Bullinger sio wa kweli kwa jinsi hii kama ilivyo sawasawa na kurasa za nyongeza).

 

Unabii huu kwa hiyo unafungamana na ujenzi mpya wa Hekalu na unafanya sehemu Msingi wa Nyumba ya Daudi imani na utaratibu wa unabii na maongozi yanayoendelea hadi Siku za Mwisho na ujenzi mpya wa mwisho wa Hekalu (soma jarida la Utawala wa Wafalme Sehemu ya III: Sulemoni na Ufunguo wa Daudi (Na. 282C)).

 

Sehemu ya kwanza inatokana na mwanzo wa ujenzi na inaishia katika mwaka wa 2 wa ujenzi kwa kiwango nusu. Sehemu ya pili ni ile inayotolewa kwa kipindi cha zaidi ya nusu ya ujenzi na inafungamana na unabii hadi kwenye marejesho mapya ya Israeli na Yuda chini ya Masihi, na Kanisa ambayo yamenenwa hapa kwenye maandiko kama ni kutawala na Masihi huko Yerusalemu.

 

Hagai anahusika pia kwenye unabii kwa kipindi kama tulivyoona.

 

Malaki

Malaki alikuwa ni nabii wa mwisho na alihudumu kwenye miaka ya karibu nay a mwisho wa uhai wa Ezra. aliishi kwenye wakati ambao Zekaria aliuawa.

 

Mathayo 23:35 inasema kwamba Zekaria aliuawa kati ya hekalu na madhabahu. Aliuawa kabisa na makuhani, ili kukomesha kazi na huduma yake. 

 

Mathayo 23:33-36

Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum? 34 Kwa sababu hiyo, angalieni, mimi natuma kwenu manabii na wenye hekima na waandishi; na wengine wao ninyi mtawaua na kuwasulibisha, na wengine wao mtawapiga katika masinagogi yenu, na kuwafukuza mji kwa mji; 35 hivyo ije juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki, hata damu ya Zakaria bin Barakia, mliyemwua kati ya patakatifu na madhabahu.

 

Kristo anawaambia makuhani na hii hatua ya maana sana. Inaonekana kuwa Zekaria aliuawa kwa jinsi ya kikatili sana. Zekaria 1:7 inaonyesha kuwa alikuwa ni Zekari'a mwana wa Barakia, mwana wa Ido, nabii. (Soma kitabu cha Josephus, cha Vita vya Wayahudi, 4.5.4 kwa maelezo zaidi, pia soma bango kitita za kitabu cha Bullinger.) hii imetajwa kama inaanzisha tatizo kwenye vitabu vya Malaki na Zekaria.

 

Kwenye sura za Zekaria kuna madiliko kidogo kwenye mtindo na kile kinachodhaniwa ni kwamba Malaki alichukua wajibu wake na kuanza kuandika na kumaliza sura kadhaa za mwisho za kitabu cha Zekaria na kisha akamalizia utaratibu wake kwa kitabu chake, ambacho hatimaye kilifanyika kuwa ni cha mwisho kwenye Mpangilio huu wa uandishi. Ilikuwa ni wakati alipofariki Iskanda Mkuu ambao ulikuwa ni sawasawa na mwaka 323 KK. Ezra mwandishi alifariki wakati huu huu. Kitabu cha Sedum Olam Rabbah inaonyesha kwamba walifariki wakati mmoja. Kisha walihitimisha Agano la Kale na kuweka kilichoitwa Kanuni ya Agano hilo tangu wakati wa kifo hik mwaka 323 KK. Vitabu viliorodheshwa na kuchapishwa na kutolewa mnamo mwaka 321 KK.

 

Malaki ni mmoja wa manabii sita ambao hawajapewa tarehe za hawa Kumi na Mbili wanaojulikana au kuitwa kama Manabii “Wadogo”. Kitabu chake kinaonyesha kwamba ibada za Hekalu na sadaka zake zilirejeshwa zote kikamilifu bali utaratibu wa kiibada na unafiki ambao ulishika kasi kipindi ch huduma ya Bwana wetu vilionekana kushika kasi na kuwepo kipindi hiki cha Malaki. Sio kwa haraka sana walipingamiza ushawishi wa Ezra na Nehemia kuondolewa zaidi ya ufisadi ulioanza na vita iliyoendelea kwa kina iliyoshuhudiwa kwenye Malaki  1:7-8 na 3:8 nk.

 

Kwa hiyo, Mpangilio wa orodha ya Manabii Kumi na Mbili ni:

 

Amos na Yona huenda walihudumu wakati mmoja.

Hosea

Mika

Yoeli

Nahumu

Obadia

Sefania

Habakuki

Hagai

Zekaria

Malaki

 

Isaya

Isaya alikuwa anatabiri pia kipindi hiki. Wanazuoni wa siku hizi wanajaribu kumtenganisha Isaya kwenye maandiko matatu na sehemu ya kwanza ni kipindi cha kabla ya utumwa na nyingine ni ya baada ya utumwa. Kuna mashaka kidogo kwamba alikuwa anaandika mahali fulani kabla ya kuanguka kwa Hekalu na wakati wa utumwa lakini alikuwa hado ndani ya Palestina. Zaidi ya kushughulika na jambo hapa tutashughulika na kuhesabu tarehe za nyakati za Isaya na manabii wengine wa utumwani kwenye ufafanuzi wao.

 

Nyongeza

Nukuu ya Bullinger ni Manabii Kumi na Mbili.

 

Manabii wa Agano la Kale wamegawanyika kwenye Biblia ya Kiebrania makundi MAWILI:

I. Manabi wa “ZAMANI" (Yoshua hadi Wafalme. Zekaria 1. 4; 7. 7, 12). Soma maandiko ya ukurasa wa 289, na Jalada la Nyongeza 1. II; na kwa hiyo kwa kupendekeza,

II. Manabii “WALIOFUATIA” (Isaya hadi Malaki) kwenye mlolongo usiovunjika (Danieli akiwa kwenye mpangilio wa mwanadamu na orodha na kuwa kwake Hagiographa). Soma Jalada la Nyongeza 1. III

 

Kwenye maandiko yote ya Kiebrania, na Biblia zilizochapishwa za Kiebrania, Manabii Wadogo Kumi na Mbili (au wenye vitabu vifupi) wameandikwa, na kuchapishwa kwa utaratibu usiojulikana; na mara zote wamekuwa wakihesabiwa, na wamekuja chini kwetu, kama kitabu kimoja

.

    Ni kama kila Kabila moja lilikuwa ni kitu cha tofauti katika Israeli, nab ado yote kumi na mbili kwa pamoja yaliunda Taifa moja na ndivyo Manabii hawa Kumi na Mbili kwa pamoja wanaunda kitabu kimoja

.

Kama ilivyokuwa zamani (Makabila kumi na mbili) yakiitwa "dodekaphulon" = makabila kumi na mbili, na (kutokana na neno dodeka = kumi na mbili, na phule = kabila), Luka 22. ndivyo; Matendo 26. 7 ; na Yakobo 1. 1 ; kwa hiyo baadae baadae (manabii kumi na mbili) wanaitwa “dodeka propheton" (Mhubiri 49.10). alipokuwa anawasifia “watu mashuhuri", mwandishi (Yesu, mwana wa Sirach) alisema "na hawa manabii kumi na mbili (ton dodeka propheton) hebu na ukumbusho wao ubarikiwe, na mifupa iimarike tena na itoke nje ya mahala pake; kwa kuwa wamemfariji Yakobo (yaani Taifa la makabila kumi na mbili) na kuwakomboa kwa tumaini la uhakika."

 

Maandiko ya Kiebrania ya kitabu hiki chenye mkusanyiko wa vitabu kumi na mbili yamegawanyika kwa Sedarim ishirini na moja (au sehemu kwa ajili ya usomaji wa hadharani au wa watu wote), nah ii inasomeka pasipo kujali mwanzoni wala mwishoni mwa vitabu vingine vya pembeni, na ndipo inaonyesha kwamba vitabu kumi na mbili vinapasa vichukuliwe kama kitabu kimoja. Hizi Sedarim ishirini na moja ni kama zifuatavyo :-

 

1. Hosea 1.1-15.

2.       6.1-10.11.

3.       10.12-14.6.

4.       14.7 -Yoeli 2.26.

5. Yoeli  2.27-Amosi 2.9.

6. Amosi 2.10-5.13.

7.          5.14-7.14.

8.         7.15-Obadia 20.

9. Obadia 21-Yona 4.11.

10. Mika 1.1-4.4.

11.        4.5-7.19.

 

12.Mika 7.20-Nahumu 3.19.

13.Habakuki 1.1-3.19.

14. Sefania 1.1-3.19.

15.      3.20-Hagai 2.22.

16. Hagai 2.23-Zekaria 4.1.

17. Zekaria 4.2-6.13.

18.        6.14-8.22.

19.        8.23-11.17.

20.       12.1-14.20.

21.        14.21-Malaki 4.6.

 

 

Kutokana na Sedarim ishirini na moja hapo juu itapasa ikumbukwe kwamba ni vitabu vinne peke yake vinaanza na Seder (Hosea, Mika, Habakuki, na Sefania); wakati saba wengine wanazidi, na kujumuishwa sehemu ya vitabu viwili (kama kwa suala la Namba 5: 8, 9, 12, 15, 16, na 21). Soma maandiko kwenye kurasa za 366 na 616.

 

§ Inatafuta Muundo wa taratibu za Kanuni zao kwa ujumla, itakumbukwa kwamba sita kati yao wamewekwa kwenye tarehe (Hosea, Amosi, Mika, Sefania, Hagai, na Zekaria), na sita wengine hawajapangiwa tarehe (Yoeli, Obadia, Yona, Nahumu, Habakuki, Malaki). Hawa kumi na mbili wamegawanyika tena kwenye makundi mawili; wanane wao ni kabla ya kipindi cha Utumwa na watatu wao ni baada ya utumwa. Kwa unabii uliojulikana tarehe zake, mbili kati yake umewajumuisha Wafalme wa Israeli, na nyingine mbili nyingine zinawajumuisha Wafalme wa Wamei na Waajemi peke yao.

 

Kwa hiyo, makundi matatu yamewekwa ili kufanya vitabu vitatu (1); vitabu sita (2); na vitabu vitatu (3).

 

Ni kama hii ilivyotokea au kuonekana kwenye ukurasa wa 1206, uhusiano zaidi utakumbukwa kama kitu muhimu na mtazamo wa jumla wa nabii fulani kadhaa, kama vilivyoonyeshwa kwenye herufi au nyaraka muhimu zilizoaambatanishwa.

 

 

q