Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[104]
Andiko Kuhusu Matendo ya Sheria - au MMT
(Toleo La 2.0 19950415-19990618))
Jarida hili linafafanua kile ambacho Mtume Paulo anachokitaja kama Matendo
ya Sheria kwenye nyaraka zake. Somo hili linaloeleweka kimakosa sana
limefafanuliwa kwa mtazamo wa ushuhahidi wa watalamu wa uchimbuzi wa mambo ya
kale au wanaakaelojia waliotumia kile kinachojulikana kama Gombo
zililodunguliwa kwenye Bahari ya Chumvi. Maandiko yaliyotafsiriwa na kina Quimron
na Strugnell imaelezewa habari zake pia. Inaonekana kama Matendo ya Sheria ni
bodi ya nakala za maandiko yaliyodumu tangu katika karne ya kwanza,
yakijulikana kama Miqsat Ma’ase Ha-Torah au
MMT, ambayo yamegunduliwa katika siu
za hivi karibuni sana. Hii inamfanya Paulo aonekane kuwa ni mtu mahiri sana
kwenye Ukristo wa siku hizi.
Christian Churches of God
(Hatimiliki © 1995,
1999 Wade Cox)
(tr. 2016)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo
atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu
fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila
kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia
yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Andiko Kuhusu Matendo ya Sheria – au MMT
Jarida hili ni la
mwisho kwenye mkururu wa majarida yahusuyo sheria au torati. Linabeba dhima ya
dhana ya matendo ya sheria ambayo
anaielezea Mtume Paulo. Imekuwa ikishambuliwa au imekuwa ni mashambulizi
yaliyofanywa ulimwenguni kote, kwa kipindi kirefu sana, wakijaribu kuondoa au
kutangua dhana yoyote inayoonyesha kuwa sheria bado zinahitajika kuzishika, na
kwa kutumia ufafanuzi au maelezo ya Paulo kwenye naraka zake kwa Wagalatia na
kwa Warumi kama msingi wao. Mijadala yenyewe iliyompelekea kuandika hivyo iko
wazi sana kuwa ni uwongo, lakini haieleweki vizuri
Warumi 3:20 kwa
sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya
sheria; kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria.
Mtume Paulo anatumia
neno linaloitwa matendo ya sheria. Wakristo
wengi wa siku hizi wamedhania tu kwamba anachokiongelea hapa ni torati ya Musa.
Wanadhania kwamba anasema kwamba torati imetanguka. Matendo ya sheria sio ni
kitu kisicho na maana, na matendo ya sheria sio sehemu imani yao. Kwa hiyo, mtu
yeyote anayeandika mawazo kama hayo hurudi nyuma hadi kwenye Agano la Kale kwa
ujumla, na anasema kuwa matendo ya sheria hayatuhusu sisi siku hizi. Hoja hizo
hazina usahihi kwa sababu ya hoja zilizo kenye jarida la Tofauti ya Sheria (Na. 96). Kwenye jarida hilo ilionyeshwa jinsi
sheria za Mungu zilivyo za milele, na zinatokana na tabia yake. Ilionyeshwa pia
kuwa sheria ya utoaji dhabihu ndicho kitu kilichogongolelew pale mtini na siyo
sheria za Kimaadili zilizo kwene amri zake. Kuna jambo lingine, linaloitwa matendo ya sheria, ambalo linahusiana na
sheria hii ya utoaji dhabihu, na linalohusiana na sheria za Mungu tu kwa njia ya
moja kwa moja. Dhana ya matendo ya sheria
haijaeleweka vyema, na ni siku hizi tu, kwa kupitia ushahidi wa wataalamu
wa elimu ya mambo ya kale, ndipo tunaweza kuelewa kwamba kile Paulo alichukuwa
anakiongelea hasa. Tunaweza kuonyesha sasa kwamba kwa hakika Paulo alikuwa
anaiongelea bodi ya uandishi, ambayo
ilikuja kuzuiwa kwenye huduma za madaraja ya kisakwamenti ya Kiyahudi,
iliyokuwa na masingi wake kwenye uandishi wa Kumran, na ambayo haikuwa na
uhusiano wowote na marabi wa Kiyahudi. Ilitumiwa kwa kuwa ni Muhimu na wengine
waliikataa Talmud na utaratibu wa Hekaluni wa makuhani. Vilikuwa ni vikundi vinavyotumia
Biblia peke yake vya karne ya kwanza
KK/BK. Tutaona kwamba neno hili la Paulo la matendo
ya sheria linataja mchanganuo aishishi wa kikundi cha kidini wa utakaso wa
kidini ambao hauna uhusiano yoyote wala msingi wa wokovu. Hawazitaji kabisa sheria
sheria za Mungu kwa wokovu wa kiroho. Bali wanataja tu moja kwa moja Siku Takatifu.
Wanataja ju ya sadaka na utakaso, yaani utakaso wa kidini. Tutaona, kutokana na
mlolongo wa mambo ambao ulikuwepo. Kwenye Warumi 3:20 tuna maelezo ya kwanza ya
tabia zake. Inasema kwa hiyo kwa matendo
ya sheria. Tafsiri ningine zinatafsiri
andiko hili kama matendo ya sheria.
Warumi 3:20-27 kwa
sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya
sheria; kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria. 21
Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na
torati na manabii; 22 ni haki ya Mungu iliyo kwa njia
ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti; 23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na
utukufu wa Mungu; 24 wanahesabiwa haki bure kwa neema
yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; 25 ambaye
Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili
aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi
zote zilzotangulia kufanywa. 26 apate kuonyesha haki
yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye
Yesu. 27 Ku wapi, basi, kujisifu? Kumefungiwa nje. Kwa
sheria ya namna gani? Kwa sheria ya matendo? La! Bali kwa sheria ya imani.
Hapa Paulo anasema,
kwa hakika, Kwa sheria ya namna
gani? Kwa sheria ya matendo? La! Bali kwa sheria ya imani. Hii ni muhimu na jambo kuu na ya muhimu
sana kwa wokovu wa mwanadamu. Kisha Paulo anaongelea kuhusu sheria.
Warumi 3:28-31 Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya
sheria. 29 Au je! Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu? Siye Mungu wa
Mataifa pia? Naam, ni Mungu wa Mataifa pia; 30 kama
kwa kweli Mungu ni mmoja, atakayewahesabia haki wale waliotahiriwa katika
imani, nao wale wasiotahiriwa atawahesabia haki kwa njia ya imani iyo hiyo. 31 Basi, je! Twaibatilisha sheria kwa imani hiyo? Hasha!
Kinyume cha hayo twaithibitisha sheria.
Hivyo basi, Paulo
anasisitizia umuhimu wa sheria kwenye Kanisa la Rumi, kisha anasema kwamba matendo
ya sheria hapa hayapo sahihi. Hayasaidii chochote kwenye wokovu. Wokovu
unapatikana kwa imani kwa kumwamini Yesu Kristo. Ni kwa nini Paulo anahusishwa
na hoja hizi? Wengi, kwa ajili ya mgongano ilioko wazi kuhusu kwenye maneno
haya, wanadhania kwamba alikuwa anaelezea kuhusu sheria ya utoaji wa dhabihu
dhidi ya wale waliokuwa wanajeribu kuzuia sheria. Hili ni tatizo ambalo
maelekezo ya Paulo na kiini au msimamo wa Biblia, kwa kuwa yamekuwa ni
mikanganyiko ya wazi kwa kile anachokisema na kukikusudia Paulo. Kwa upande
mwingine, anasema mtu anapaswa na ni lazima azishike amri za \mungu, na kwa
upande mwingine, anasema kwamba haya matendo ya sheria hayaongezei chochote
wala hayafaidishi lolote. Mgongano huu wa wazi wapasa upatiwe ufumbuzi. Jibu la
mwisho, nje ya mgongano wa wazi uliopo kati ya sheria ya Kimaadili na za utoaji
dhabihu tulizozielezea kwenye jarida letu la Tofauti Iliyopo Kwenye Sheria, linalotuama kwenye bodi ya uandishi,
ambayo tulikuwa hatuyajui. Neno alilolitumia hapa ni ergoon nomou, (kwenye Kiyunani chenye mchanganyiko na Kilatini), lenye
maana ya matendo ya sheria. Neno hilo
linalitafsiri neno la Kiebrania, tulilo kutananalo sasa kutoka kwenye Gombo za
Bahari ya Chumvi. Neno lenyewe ni Miqsat
Ma’ase Ha-Torah, au MMT, tafsiri
ambayo, kwa mujibu wa Strugnell na Qimron, ni Ni Sawa tu na Maagizo ya Torati. Halionekani mahali popote pale
kwenye marabi wa Kiyahudi. Haijafanyika kuwa ndiyo mwenendo au tabia tarajiwa
na kwa hiyo uelewa ulipotea kabisa. Hata hivyo, neno miqsat halimaanishi kitu hichohicho
tu. Linapotumiwa kwenye MMT halionyeshi kuwa ni sheria hizohizo bila kutofautiana.
Uelewa wake unaweza kukusanywa kwenye matumizi yake kwenye Talmud. Hivyo,
Martin Abegg anaamini na kuchukulia (kwenye kitabu chake cha Paul,
Works of the Law and MMT [Paulo, Matendo ya Sheria na MMT], Biblical
Archaeology Review, Nov.-Dec. 1994, pp. 52 ff), kwamba tulipaswa kulitafsiri
neno hili kama umuhimu fulani au uvumilivu. Kina Strugnell na Qimron wanakitafsiri
kifungu hiki ma’ase ha torah kama ni maagizo ya Torati. Lawrence Schiffman anadhania
mamlaka halali ya Torati (kutoka
kwaAbegg ibid). Huenda ile ni zaidi ya rafsiri ya kama mahsusi au muhimu kwenye sheria. Lakini matumizi yake kwenye
Kiyunani yametafsiriwa kama ergoon nomou.
Neno hili lilitumiwa kwenye tafsiri ya Septuagint ili kutafsiri neno hili kama ma’ase ha torah. Neno ergoon nomou ni neno lililotumiwa na Paulo
na ndilo lililotafsiriwa kwenye Kiingereza kama matendo ya sheria. Inakujakuwa dhahiri sana kwamba kwa kweli Paulo
alikuwa anaongelea mtazamo wa sheria unaong’ang’aniwa na dini ya Kumran, na
ambayo ilifanyika kuwepo kwenye dini isiyojumuisha marabi wa Kiyahudi wa karne
ya kwanza ya haikuwa sehemu ya mapokeo ya Kitalmud na tafsiri yake. Haikufanyika
kuwa sehemu ya kile tunachokijua leo kama dhana au nadharia kuu ya Kiyahudi
kwenye karne ya kwanza na haikuchukuliwa kuwa ni sehemu ya mapokeo na tafsiri
za Kitalmud. Ndipo, iliondolewa mbali. Ndipo tulisubiria hadi zilipogunduliwa
Gombo za Bahari ya Chumvi na kuona nakala ziliwepo na kutafsiriwa. Kutokana na
ugunduzi huo ndipo tuliweza kumuelewa Paulo kikamilifu. Tutayaonyesha baadhi ya
maandiko hayo, ni halafu tutakwenda kuona Gombo hizi za Bahari ya Chumvi
yanasema nini kuhusu utaratibu au kanuni zilivyo. Tutapata hisia ya idadi ya
vitu fulani amnavyovikemea Paulo. Tutaona kwamba ni zipi anazozisema kwamba
zimeondolewa. Haziongezi wala kupunguza chochote. Havihusiani wala kuongeza
chochote kwenye maana yetu kuhusu wokovu, na taratibu za kwenye Agano la Kale,
zinazotufunika. Inahusu tu na
taratibu za sheria za utakaso wa dhabihu na kidini. Inamfanya mtu atakasike kwa
matendo kwa mujibu wa usomaji mpotofu wa andiko hilo.
Kuna tukio la
kugombea jimbo fulani nchini Marekani lililopelekea kuzuka kwa mapigano
kugombea haki ya Matendo ya Sheria au
tafsiri za hiki kinachojulikana kama. Elisha Qimron na John Strugnell wameandika
habari hiyo. Wanajaribu kudai haki za maandiko ya Qumran. Unaweza kusema “Inatuhusu
nini sisi? Inatuhusu vipi hata kama watachimbua majarida na maandiko ya kwenye
hiyo Qumran? Na kwani inaweza kutuathiri vipi kiimani?” Jibu ni kwamba inatupa
kifaa kingine, silaha au ngao, ya kujikinga dhidi ya wale wanaojaribu kuisambaratisha
imani yetu na sheria. Mara tu
unapoitangua sheria, unakuwa unatangua pia dhana ya dhambi, na unatangua pia
dhana ya maadhimisho ya Siku Takatifu ya Mkate Usiotiwa Chachu. Unakuwa
unapingana na misingi muhimu ya mpango wa Mungu wa wokovu. Kupuuzia kwa maana
yake kunatufanya iwe vigumu sana kwetu kuelewa kile anachotufanyia Kristo sasa,
na jinsi anavyotusogeza mbele.
Mjadala wa ni
kitu gani alichokisema Paulo kwene nyaraka za Warumi na Wagalatia unaweza
kukingiwa kifua na kueleweshwa kwa uelewa unaoongezeka. Maelezo yake ni kwamba
alikuwa anaongelea kuhusu Matendo ya
Sheria – ambayo ni Miqsat ma’ase
ha-torah au MMT, ambayo kwa wazi
sana anamaanisha maandiko ya dini za Qumran, ambazo ziliingia kwenye itikadi za
kidini ya Kiyahudi katika karne ya kwanza, na ikatoweka kuanzia karne ya pili,
ya tatu na ya nne.
Baada ya
utawanyiko, baada ya kuanguka kwa Yerusalemu, na hasahasa, kuanguka kwa Massada,
ndipo MMT ilipotea. Ilisalia kwenye pango la Qumran. Uelewa wa kile alichokuwa
anakisema Mtume Paulo ulifungiliwa mbali, ili kwamba watu waliokusudia
kupotosha na kuitangua sheria ya Mungu waliyatumia maandiko ya Agano Jipya
kuziondoleambali sheria kwa kutumia maneno aliyokuwa anayasema Paulo. Nyaraka
za Agano Jipya zilitumika pia kuipinga nia na dhamiri njema ya Paulo, na kisha
kwa sababu ya hiyo, Wayahudi wenyewe walijisikia kuwa kwenye shinikizo kwa
ajili ya alichokuwa anakisema Paulo. Ilianzisha kile kilichochotokea kuwa
mkanganyiko mkubwa kwenye maandiko ya Biblia. Wagalatia 2:13 inatoa hisia ya
kile kilichotokea.
Wagalatia 2:13 Na
hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa
na unafiki wao.
Walimwendea Barnaba
kwa maneno mengine, kwa hiyo wateule hawakuwa na la kusamehewa kwa sababu hiyo
na kwa kujiuliza kwao.
Wagalatia 2:14-16 Walakini,
nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kweli ya Injili, nalimwambia
Kefa mbele ya wote, Ikiwa wewe uliye Myahudi wafuata desturi za Mataifa, wala
si za Wayahudi, kwa nini unawashurutisha Mataifa kufuata desturi za Wayahudi? 15 Sisi tulio Wayahudi kwa asili, wala si wakosaji wa
Mataifa, 16 hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi
haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini
Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya
sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki.
Sasa nono matendo ya sheria limechukuliwa kwa
ujumla kuwa na maana ya maneno mawili kama, kazi
ya sheria, lakini kwa kweli lipo kama tunavyoliona, jina lake au wadhifa
wake, Matendo ya Sheria, ambalo
limetafsiriwa kwa Kiebrania kama Miqsat
ma’ase ha-torah. Kutoka sasa na kuendelea mbele, tunaweza kulieleza hili
kama ni cheo cha kazi za Kiyahudi kwenye karne ya kwanza, kinachojaribu
kuonyesha haki ya namna fulani kupatikana kwa njia ya matendo. Wagalatia 3:1-14
inatoa ufafanuzi wa kina.
Wagalatia 3:1-14 Enyi
Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa
wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa? 2 Nataka
kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa
kusikia kunakotokana na imani? 3 Je! Mmekuwa wajinga
namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili?
4 Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa
ni bure kweli. 5 Basi, yeye awapaye Roho na kufanya
miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia
kunakotokana na imani? 6 Kama vile Ibrahimu
alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki. 7 Fahamuni basi,
ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu. 8 Na
andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa
kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe
Mataifa yote watabarikiwa. 9 Basi hao walio wa imani
hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani. 10 Kwa
maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana; maana
imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika
kitabu cha torati, ayafanye. 11 Ni dhahiri ya kwamba
hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu Mwenye
haki ataishi kwa imani. 12 Na torati haikuja kwa
imani, bali, Ayatendaye hayo ataishi katika hayo. 13 Kristo
alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu;
maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti; 14
ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo,
tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.
Paulo anamtaja
kwa kumlinganisha Ibrahimu kwenye andiko lake kwa Waalatia, kwa kuwa Ibrahimu
alihesabiwa kuwa mkamilifu na mwenye haki, kutokana na maandiko yaliyo kwenye
kitabu cha Mwanzo. Hali yote ya kuufikia ukamilifu aliyokuwanayo Ibrahimu ilionekana
kwenye Mwanzo 22:16 ambapo Ibrahimu alikubali kumtoa sadaka mwanawe Isaka kwa
amri ya Mungu. Na Abegg analikuza jambo hili kwenye kipengele chake cha kitabu
hichohicho. Anadhania kwamba kuna uwezekano mmoja tu, na ni uwezekano mkubwa sana,
vinginevyo Paulo asingetumia rejea ili kuhusianisha na andiko hili. asingeweza
kuongelea kuhusu matendo ya sheria, na akautumia mfano wa Ibrahimu, kama mfano
ulikuwa unalenga moja kwa moja na matendo na hali ya kuhesabia haki. Ukweli
ulikuwa ulikuwa ni kwamba alihesabiwa mwenye haki kwa matendo aliyokuwa
anayafanya. Abegg anatoa maelezo mazuri sana, na yanaonekana vizuri na kisahihi
kwamba msingi wa matendo ya sheria unawezesha
utakatifu huenda ulikuwa umechukuliwa pia kutoka kwenye Zaburi 106:30-31.
Zaburi 106:30-31 Ndipo
Finehasi akasimama akafanya hukumu; Tauni ikazuiliwa. 31 Akahesabiwa
kuwa ana haki Kizazi baada ya kizazi hata milele.
Cha kufafa
kilichofanywa na imani ya Kiyahudi na Kanisa, kilichukuliwa dhana hii wakati Finehasi
aliposimama, na kwa matendo yake, aliyoyatenda, alihesabiwa kuwa wenye haki kwa
kizazi chake chote. Kwa hiyo ndivyo zilivyokuwa dini na imani ya Qumran na MMT,
na kwa vikundi vilivyodhania kuwa sheria ingeweza kuwapa haki kwa matendo,
wakilichukulia andiko hili na kulitendea kazi kuwa ni kama uhalalisho wa haki
iliyotokana na matendo ya mtu binafsi yake. Wana
wa Sadoki ndilo lilikuwa jina walilojipa na kulitumia wafuasi wa dini ya Qumran.
Hutu Sadoki, Kuhani Mkuu aliyehudumu zama za Daudi na Sulemani, alikuwa ni wa
uzao wa moja kwa moja wa Finehasi, ni fikra inayoupa mashiko mtazamo huu. Paulo
alisema kwamba hakuna mtu anayehesabiwa haki mbele za Mungu kwa matendo ya
sheria. Yeye anayehesabiwa haki kwa imani ni mkamilifu na ataishi.
Kwa hiyo, haki na
utakatifu ni shatri muhimu katika kuzitii sheria kwa njia ya imani. Kuzishika
tu sheria pasipo kuamini kwa kiwango cha juu hakuna maana. Hili ndilo wazo linaloshambuliwa.
Mtazamo huu wa kimwili haki ulichukuliwa licha ya ukweli kwamba kuna maandiko
mengi sana ya biblia kwenye kitabu cha nabii Isaya, hususan Isaya 9:1-6, inayoelezea
kuhusu Masihi, na Isaya 53, inayoelezea kuhusu mateso yake na kuichukua kwake dhambi.
Maandiko haya yote yalionyesha kwelekea ukomaji wa utoaji dhabihu ya kuondoa
dhambi kwa Masihi. Na bado
watu hawa walidhania kwamba matendo yangewafikiliza na kuwapatia haki. Ni kama
alivyosema Paulo kwamba Enyi Wagalatia
msio na akili, ni nani aliyewaloga,? 2 Nataka
kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa
kusikia kunakotokana na imani?” Kisha ndipo anamwongelea Ibrahimu. Paulo anasema kwamba nafasi yao
imetoholewa kutoka kwenye maandiko mawili, ingawa hakumtaja Finehasi. Hata
hivyo, inaonekana kwa namna fulani kwamba andiko linalosema kwamba Ibrahimu
alihesabiwa haki kwa utii wake na matendo yake aliyoyaonyesha kwa kumtoa sadaka
mwanae Isaka, ulikuwa ni msingi wa mawazo. Kwa kweli, kulikuwa na kitu kilichofanyika
kwenye maisha yao ya useja wa Kitawa kwa namna fulani. Huenda kwa kuwatoa
sadaka watoto, kwa kutokuwa na yeyote, unajiweka kwenye maisha ya useja kwa
kutakasika. Kwa hiyo, unahesabiwa kuwa mwenyehaki kwa kitendo cha kuukataa uzao
wako tu. Ni kujidanganya tu zaidi ya unavyodhania. Lakini mtu anaweza kudhania
kwamba inaweza kuwa ni rahisi. Kuna taratibu nyingine nyingi za utakaso, ambazo
zinafanya kuwe na uenezi, kwa kuwa huwezi kutakasika kabisa kwa kufuatisha
taratibu hizi wakati wote, chini ya sheria, inayofanya kuyathibiti kikamilifu
maisha yote ya mwanadamu. Abegg anaonekana kufaweka hoja nzuri kwa chimbuko la
jina hili. Anaonyesha kwamba MMT inatuama kwenye lugha halisi ya kile ambacho
Paulo walikuwa anakipinga hoja kwenye waraka wake kwa Wagalatia (Wagalatia
2:16) (Abegg op. cit. p. 55).
Ndipo mtu anaweza
kuuliza swali: Matendo ya Sheria ni nini?
Qimron na Strugnell have wamefanya marekebisho ya maana ya dhana hii ya Matendo ya Sheria kwenye maandiko ya DSS.
Yanahusika na sehemu tatu. Nazo ni kwanza kabisa kalenda inayobeba mistari ya
idadi inayojiri kwenye tarakimu 1 hadi 21. Cha pili, ni maeneo ya sheria
yanayotuama kwenye seti ya pili ya maandiko ya Kiebrania, yaliyopewa tarakimu 1
hadi 82. Tatu, ina kiahitimisha, kinachotuama kwenye seti ya tatu ya maandiko,
tangu namba 1 hadi 32.
Viambishi vyenye
nakala tofauti sita za hii MMT zilikutikana huko Qumran, kwa hiyo hilo sio
andiko lililoondolewa au kutendanishwa. Kulikuwa na nakala nyingi sana miongoni
mwa hizo. Ziliandikwa kwa kupangiliwa kwa namna mbili, ya kwanza ni kwa tarakimu
ya 4Q, ikionyesha kuwa zinatoka kwenye pango la Qumran 4. Nazo ni 4Q394 hadi
4Q399. Pili, zimeonyeshwa kwa herufi kamili ya f. Kwenye pambizo za kushoto chanzo
cha maandiko kimeonyeshwa kwa herufi na namba 4Q (kwenye mabano). Hivyo,
mistari 18 ya kwanza ya kalenda yanatoka kwenye nakala a, ambayo ni sawasawa na
4Q394. Tarakimu zinazofuatia namba 4Q zinaonyesha nguzo na mistari (mingi
imerudiwa kwenye maandiko mengine) (Nyongeza A).
Mstari mmoja unasomeka
i [(siku) yake ya kumi na sita (yaani ya mwezi wa pili) ni Sabato]. Sasa hizi
hazihusiani na nafasi ya kibiblia. Huenda hivi ni vigezo pia kwa kalenda
inayotokana na jua kwenye Qumran, ambayo ni potofu. Inaonyesha utaratibu wa
kupanga Siku Takatifu nje ya kisima. Hii ndiyo sababu inayopelekea baadhi ya
mifumo ya kalenda iliyoathirika iondolewe. Na hii ndiyo iliyopelekea isiruhusiwe
kuwepo hadi kufikia karne ya pili.
Marekebisho yanasema:
Siku yake ya ishirini
na tat uni Sabato. Siku yake ya [thelathini ni Sabato. Siku ya Saba ya (mwezi)
wa tat uni Sabato—siku ya kumi na nne yake ni Sabato—siku ya kumi na tato yake
ni Idi ya Majuma [ambapo Pentekoste iliangukia siku ya kumi na 14 na 15 ya mwezi
wa tatu kwenye hii Qumran: nah ii ni kinyume kabisa na maelekezo ya Mambo ya
Walawi 23. Andiko linaendelea]. Siku ya ishirini—na moja) yake ni Sabato. Siku
ya ishirini na nane yake ni Sabato. Baada ya siku hii (yaani Sabato) kunafuatiwa
na siku za Jumapili na Jumatatu, [Jumanne iliongezwa (kwenye mwezi huu).
Haya ni marekebisho
(kwenye majina ya siku tunazozitumia, ili kwamba uelewe kwamba siku za juma
zipo kwenye maelezo ya siku hizi). Andiko hili linaendelea hivi:
Na majira
yanaishia-kwenye siku za thamanini na moja. Siku ya kwanza ya mwezi wa nne ni
Siku ya Ukumbusho. Siku ya nne]iii yake [ni Sabato. Siku ya [kumi na moja] yake
ni Sabato, siku ya kumi na nane yake ni Sabato. Siku ya ishirini na tano yake
ni Sabato. Siku ya pili ya mwezi wa tano ni Sabato. Siku ya tatu yake ni
Sikukuu ya Mvinyo (Mpya)...
iv siku ya tisa yake
tisa yake ni Sabato]. Siku yake ya kumi na sita ni Sabato. Siku ya ishirini na
tatu yake ni Sabato siku ya thelathini [yake ni Sabato. Siku ya saba ya (mwezi)
wa sita ni Sabato. Siku ya kumi na tatu yake ni Sabato siku ya kumi na nne yake
ni Sabato ...
Andiko linaendelea
kwa kuorothesha kisha Sabato zote za mwaka wote ,ona hatimaye kuhitimisha mwaka
kwa Sabato zake, kwa kupitia Sikukuu za mafuta mapya na sikukuu za kutoa sadaka
za kuni. Hizi sio Siku za sikukuu Takatifu ambazo Biblia imetuamuru sisi kuziadhimisha
au tunazohitajika kuziadhimisha kwenye vipindi na majira yote ya Siku Takatifu.
Bali kwazo ni mkururu wote tu wa sikukuu zilizo kwenye kalenda zilizopo kwenye
mkururu wa majarida ya Matendo ya Sheria,
ambayo yamesisitizwa kufanywa na watu bila kukatazwa moja kwa moja na
biblia au kwa kiasi kikubwa kwa kutakiwa kuyaendeleza. Yanaonekana kuwa yalimgharimu
Barnaba kwa mambo hayo. Hivyo ndivyo yalivyokuwa maandiko yenye madhara kwenye
karne ya kwanza.
Andiko
linaendelea kwamba:
1 Jinsi hizi zilivyo
baadhi ya kanuni zetu [...] ambazo [baadhi ya kanuni zinazoambatana nazo ni]
2 [maelekezo] na
maagizo ya (Torati) kwa mujibu wa [mapendekezo yetu, na] yote yaliyopo
yanayohusiana nayo [...]
Yampasa mtu
kukumbuka kwamba haya yamechimbuliwa yapata takriban miaka 2,000 iliyopita ya
magombo yajulikanayo kama papyrus, na nakala zake fulani ningine hazionekani.
Inaendelea:
3 na utakaso wa [...
Na kutokana na vipaji vilivyopandwa au kuwekezwa za] punje za ngano mpya [wamataifa
ambao wao...]
4 na hebu na[...] miguso
yao na (kunajisi hakuna anayeweza kukila]
5 kila punje ya
ngano mpya ya [wamataifa yapasa iletwe kwenye maskani takatifu.
Hapa tunapata wao
- usiguse - usile - usionje. Maelezo haya ya Paulo yote yanafanya kuwa
na mashiko sasa. Anaongelea kuhusu Matendo
ya Sheria, jambo ambalo ndilo linalomanishwa kwenye andiko hili. anasema
kwamba huwezi kutoholewa na kupelekeshwa vitu hivi. Inasema – usiguse hiki na usionje kile, na usifanye
hilo. Hii haileti wala kusaidia chochote kwa wokovu wala kumpa mtu haki.
Haki yetu i ndani ya Kristo Yesu. Huu ni ugunduzi mpya wa haraka, na nia andiko
muhimu sana la kiutafsiriwa. Hii ni pia moja ya sababu ambayo maandiko Qumran yalijiri
hadi miaka 50. Andiko hilo linavunjilia mbali hoja za siku za leo za
Waprotestanti. Bali hii inaihalalisha na kupipa mashiko zaidi Sabato tuijuayo
na tuliyoizoea na nafasi ya kuziadhimisha Siku Takatifu Kanisani kwa ujumla.
Wapinga torati au waanti nomia wa siku hizi wameletwa kwenye msimamo mgumu wa
kuyaamini machapisho ya maandiko haya. Hawanaudhuru wowote kabisa wala la
kujitetea.
Tunaenda moja kwa
moja kwenye wazo hili sasa (kwenye mstari wa 5).
Kila punje moja ya ngano
ya wa[mataifa], [wala] haifai iletwe kwenye maskani takatifu. [Na kuhusu
dhabihu ya utakaso]
6 kile wanachopika
kwenye vifaa vya [shaba] [na wana...] ndani yake,
7 nyama aa dhabihu
zao, ambazo wana zi [...] kwenye nyua za Hekalu (?)...
Na kwa hiyo
tunaongelea kuhusu sadaka jinsi walivyokuwa wakizitendea kwenye nyua za Hekalu.
Hawakuwa na jinsi ya kulitamalaki Hekalu! Lakini walifanya uelimishaji mdogo
walioutaja au kuenekez Hekaluni. Walichokuwa wanakifanya ni kutengeneza kanuni na
taratibu kwa kitu ambacho hawakuwa na uthibiti nacho. Lakini kwa kweli,
walikuwa wanawaambia Mafarisayo na mamlaka za marabi jinsi utaratibu huo
unavyotakiwa uwe. Sasa hili limekujakuwa ni jalada la habari yenye mvuto na
ushiwishi mkubwa sana kwenye maeneo yote ya Mashariki ya Kati kipindi cha karne
ya kwanza. Ilimpelekea hadi Paulo kuwafanya sehemu ya Warumi na Wagalatia
walisome vizuri na kwa uangalifu andiko hili. Hii ndivyo jinsi ilivyoenea
ulimwenguni kote ikiwa.
Inaelezea kuhusu
8 sadaka au dhabihu
zao zote. Na kuhusu sadaka zinazotolewa na wamataifa: [tunashauri kwamba] sdaka
9 yaani [...] ni
kama vile ya (mwanamke) aliyezini naye, [Na kuhusu mkururu wa dhabihu] zinazotolewa
Kwa maneno mengine,
walishambulia moja kwa moja kila kitu walichokifanya Wamataifa kwenye dhabihu
zao Hekaluni. Wapinzani wao waliacha mkururu wa dhabihu kutoka siku moja na
inayofuatia. Waliasisitiza kwamba zilipaswa kuliwa kabla ya kuchwa cha jua ya
siku ile iliyotolewa sadaka.
Hata hivyo, mtu
anapata wazo likimjia, kama alilokuwanalo Yohana, ambalo linaelezea kuhusu
mwanamke, dini potofu ya uwongo, ambayo ni kahaba, kwa kuwa Yuda waliichukulia
dini ya uwongo kama ni kahaba ikihusishwa na Mungu na ni kama mwanamke mzinifu.
Inasema kuhusu
sadaka zao za hiyari, ambazo wapinzani wao wanaziacha juu kutoka siku moja hadi
inayofuatia, lakini imeandikwa, kwenye kipengele cha 11, dhabihu zoye
zinazotolewa zinapasa ziliwe baada ya shahamu, na nyama zinazotolewa mchana
ambazo zinatolewa kabla ya kuzama jua. Kwa watoto wa Makuhani wanawajibika
kujitunza na kutilia maanani kuhusiana na jambo hili, ili wasisababishe watu
kuadhibiwa. MMT inaonyesha rejea ya sheria takatifu za ng’ombe anayetolewa
sadaka, yaani, ng’ombe mwekundu. Yeye anayemchinja ng’mbe huyu na yeye
anayemuoka motoni, na yeye anayemkusanya pamoja kwenye majivu, na yeye
anayemnyunyizia maji, kwa kumtakasa, ni baada ya kuzama kwa jua ndipo wote
watakuwa wasafi.
Sasa tunaelewa
vyema kuhusu dhabihu hizi za sadaka za mtamba mwekundu (Hesabu 19:2). Waandishi
wa MMT wanahusika vyakutosha sana na dhabihu hizi. Wanaziwekea utaratibu dhabihu.
Anachokisema Paulo, mara nyingine tena, ni kwamba sadaka hizi zote za utakaso zilikoma.
Ni nakala ya msamaha au cheirographon,
kama ukipenda ni kusamehewa au kufutiwa deni, iliyogongomelewa mtini kama
ilivyoandikwa kwenye Wakolosai. Kitabu au nakala ya msamewa wa madeni, cha
kwamba dhambi zote zimekusanywa na kuwekwa ndani mwake, ndicho iliyogongomelewa
mtini. Lakini mtu anaweza kuoja jinsi ilivyo hatarishi. Dini ziliyofanya seti
ya pili ya kanuni kama za Talmud, ambazo zilifanyika kuwa ni mkururu wa
maandiko yaliyowezesha kusaidia maisha yetu ya kila siku, na ilikuja kuwa kama
mwendelezo wa marabi wa Kiyahudi, lakini ni kinyume chake. Kwa hiyo, wanashikilia
kwa kuosha mikono yao na kwa kuliangalia kile wanachokifanya kula, kile
wanachokwenda kukishirikisha au kukiunganishanacho pamoja na dhabihu zao.
Sasa ndipo wanaelekeza
habari za makuhani. Wanawataja makuhani kama wana wa Haruni. Wanamaelekezo kwa
ajili ya maji ya utakaso na kitovu chake cha Mjadala kilichopo kwenye (18 ff.) kwenye
maficho ya mifugo ya ng’ombe na kondoo. MMT inaelezea kuhusu kuwaleta kwenye
maskani yao takatifu. Pia kwa mfano:
Kuhusu ngozi na
mifupa ya wanyama najisi. Imekatazwa kufanya mikono ya vyombo kutoka mifupani mwao
na ngozi zao.
Huwezi kumbeba
mnama aliyekufa na kutumia mifupa yake na kwato na mikono ya mfupa na kuviweka
kwenye vyombo vya kupikia, kwa kuwa itavifanya vifaa vyote vya kupikia
vichafuke au vinajisike. Kwa hiyo, hivi vyote ni kanuni unazopaswa kuzifanya
kwenye matendo na mwenendo wako wa kila siku. MMT inaichukua Torati na kuienekeza
kwenye taratibu hizi za utakaso.
Na kuhusu ngozi ya
mizoga ya wanyama najisi, yeye anayebeba mizoga kama hiyo ya wanyama waliosafi,
yeye aubebaye mzoga kama huo hataruhusiwa kuingia kwenye chakula safi.
Hivyo basi, hata
mizoga safi, na huruhusiwi kula chakula kilicho safi. Kwa mfano, kutokana na
hii, kama ulikuwa unafanyakazi kwenye machinjio, hutaweza kushriki kula sadaka
ya mkate mtakatifu pamoja na mvyinyo wake. Kwa hiyo, hivi vyote vimeonekana
kuwa havina maana wala umhimu na ambavyo Paulo alivipuuzia na kuvielezea kuwa
havina mashiko yoyote sawa na dhabihu ya Kristo. Hata hivyo, alikuwa hamaanishi
kuwa anazitangua sheria za Agano la Kale. Alikuwa anatangua baadhi ya sheria zilizohusiana
na zama za Agano la Kale peke yake. Sheria ya utoaji dhabihu ni wazi sana kabisa
kuwa iliondolewa au kukomeshwa na Kristo mwenyewe, kama ilivyofundishwa na
mitume, na ni kama nilivyoielezea kwa kina kwenye jarida la Utafauti wa Sheria. Kwa hiyo, una haya
mambo matatu. Tunashughulikia mambo haya matatu tofauti ya sheria kwenye Agano
Jipya. Paulo mwenyewe anaongelea kuhusu mambo matatu tofauti, na ndiyo maana
unapata mkanganyiko wa dhahiri kwenye kile ananachokisema Paulo. Kwa kuwa
hatukujua ni nini hasa maana ya Matendo
ya Sheria. Lakini Matendo ya Sheria tunayoyajua
sasa ni kazi ya uandishi, utunzi na ufafanuzi, kama maandiko ya Talmud,
yanayokanganya Agano la Kale. Sasa ulijuapo hilo, ni rahisi. Twaweza kujionea
kwa kupitia maandiko ya waantinomia ni kwa kuelewa kwetu tu na kwa kulinganisha
kwetu na Biblia kama tufanyavyo. MMT haikutiliwa maanani wakati jarida ya Utofauti wa Sheria lilipokuwa linaandikwa,
lakini ilikuwa ni rahisi sana kuzishambulia hoja za waantonomia pasipo hii. Kwa
pamoja na maandiko ya MMT, hoja za waantinomia zinaharibika na kukosa maana
kabisa. Mtu anaweza kusema na kumwambia mtu yeyote anayesema kwamba sheria imeondolewa
au kutaguka, kwamba hawajui kile wanachokisema. Hii ndiyo mana inayokusudiwa na
MMT. Tunajua sasa kile kilichokusudiwa na jarida la Matendo ya Sheria.
MMT inaendelea
kuhusu habari au mambo ya makuhani na kwa yale yanayowahusu watu, ili
kuwasababisha watu wahukumiwe.
MMT inaweka au
kutenga mahali pa kuchinjia wanyaka ndani ya marago – kwa upande wa kaskazini
mwa marago. Wanaamini kwamba maskani ni lile hema ya kukutania, na kwamba
Yerusalemu ni kambi, na kwamba nje ya marago ni nje ya Yerusalemu.
Haya ndiyo marago ya ukazi wao (29-30). Ni nje ya marago ndiko ambako
mtu aliweza [kutoa dhabihu?] sadaka za utakaso, na kuondoa majivu ya madhabahu
na kuchoma au kuteketeza sadaka za utakaso, kwa kuwa Yerusalemu ni mahali
ambapo amepachagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli.
Inaonekana kuwa
wanafikia kutokana na hili kwamba Yerusalemu ni kituo kinachohamishika, kama
makazi ya Israeli. Hii ina maana sana kwa shughuli zilizopo kwenye nchi ya
utawanyiko.
Wanapinga kupitia
maandiko haya, kuhusu mahali uchinjaji utafanyika, na ni wapi umwagaji wa
majivu utafanyika. Hivyo tunaona kwa wazi sana na kuitazama sheria ya utoaji wa
dhabihu, na sadaka za utakaso unaibuka kutoka kwa wanyama na dhabihu, na
kutokana na wanyama wanaokufa wenyewe. Maandiko ya MMT yanajiri kuhusu sheria za
takaso na usafi kwamba ni jambo kama la ugonjwa ulioenea kwenye jamii ya
Kiyahudi kwa wakati ule. Yatupasa kuwahukumu kwa viwango vyao, na kile tunachokifanya.
Walikuwa
wanajulikana kwa usafi! Wakiwa wanajulikana ubobefu wao kwenye sheria na kanuni!
Ilikuwa ni utimilishaji. Paulo alishughulikia na hilo kwa kuwa Kristo alinuia
kuweka uelewa wao wa kidini kwa msingi wa kifikra na utimamu mkubwa. Mtazamo
huu wa kidini ulikuwa ni kikwazo kwa ulimwengu wote, nab ado ni kikwazo
ulimwengu wote. Ni kwa kulisoma kwako tu mambo ya kama majarida ya Matendo ya Sheria, unagundua ukubwa wa
tatizo alilokabiliana nalo Paulo.
MMT ndipo
inaendelea mbele (kutokana 36) kwa namna ya tabia za kula kuhusu wanyama wenye
mimba. Huwezi kuwatoa dhabihu mama mtu pamoja na kichanga chake kwa siku moja
hiyohiyo. Huwezi kula kichanga kilichokutikana ndani ya tumbo la mnyama
aliyekufa; kinaweza kuliwa tu mara tu baada ya kuchinjwa kihalali. Idadi hii
yote ya mambo kutokana na kanuni zetu za kawaida za uthibiti, havifanywi na sis
kabisa. Lakini hizi ni kanuni na sheria ambazo watu hawakuzitenda hivyo.
Nazi zinahusiana
na habari au mambo ya ni nani anayeweza kuingia kwenye kutaniko. Waliotajwa ni
Waamori, na Wamoabi, na wamamza, na yeyote aliyevunjika mapumbu yaye, na yule ambaye
ni mwanaume aliyetoka nje ambaye hajaingia kabisa kwenye mkutano na kujitwalia
wanawake na kufanyika kuwa mfupa mmoja, na kuingia kwenye maskani. Hapa MMT inaongelea
kuhusu anayeweza kuoa na yule asiyeoa – ambapo sheria na kanuni zake zinavyosema.
Na wanaongelea kuhusu unajisi wa wakazi wenza wao na kwa ukweli kwamba hawawezi
kuungana na Waisraeli. MMT inaorodhesha mambo yaliyokatazwa kwenye muunganiko
au kuoa mataifa mengine. Makatazo ya kuoana makabila au matabaka mbalimbali
tofauti pia kuhusiana na ndoa za nje ya makabila. Pia MMT inaongelea kuhusu kuwapofusha
watu, hivyo watu walioposhwa wawe makini na wajue kuhusu mchanganyiko, na
wasione mchanganyiko unapokuwa unajitokeza. Wanapaswa kuwa na maandalizi ya
sadaka. Kwa hiyo, kama wewe ni kipofu, hutaweza kuchanganya kitu chochote kwa
kuwa itakupasa kujua kwamba unakula na kuvaa. Ni mzogo gani unaoweza kumtwisha
kipofu. Kuna idadi kubwa ya mambo ambayo kwayo yanahusiana na majarida ya Matendo ya Sheria. Sasa unaelewa
alichokuwa anakikanusha Paulo. Kwa nini alikuwa akilaumiwa na kushutumiwa sana.
Wapingaji wa MMT walidhani kuwa hii inamuwezesha mtu kuwa mtakatifu. Hakuna
utakatifu wowote kwenye hiki tunachokisoma kwenye MMT. Sheria za utoaji sadaka
zimetanguliwa. Sheria za utoaji sadaka zinachukuliwa kuwa ni somo la kufutiwa
madeni au hati ya mashitaka, lakini utakatifu na kuhesabiwa haki kumetokana na
Yesu Kristo. Hatupaswi kuchukulia maelezo yoyote ya MMT kuwa ni utakatifu, au
lolote kati yake kuwa hata kiini cha imani yetu au kuhusiana na imani yetu.
MMT inaendelea
kuyapitia swali lote kuhusu vimiminika – mbwa kuingia maragoni – na kuila
mifupa ya mahali patakatifu - Yerusalemu kuwa ni kitovu au maskani ya
Utakatifu, nk. Vimehusika na hayo kama mahala pake pa kimakao. Waliuona
Yerusalemu kama ni makao makuu ya maskani ya Israeli. Walizungumzia kuhusu
matunda ya miti iliyopandwa kwa ajili ya chakula kwenye ardhi au nchi ya
Israeli. Vilipaswa kushughulikiwa na malimbuko sawasawa na haki ya makuhani. Ni
sawa tu pamoja na zaka na mifugo walizopewa
.
Pia, kuhusu wakoma
walioponywa, dini za MMT zilikuwa na wazo kwamba hawataweza kuingia mahali
popote palipo na chakula kitakatifu, lakini kinapasa kutengwa na kuondolewa, na
nje ya kila nyuma (64-70 uk. 59 f.). Kama mtu atahalifu kabisa amri ya marufuku
haya, na sababu au ukweli uliomuepusha yeye, basi alilazimika kuleta sadaka ya
utakaso. [[Na] kuhusu yeye ambaye anazivunja sheria au kanuni kwa makusudi,
imea[ndikwa kwamba anadharau na kukufuru] (70 ibid.).
Kwa hiyo ndipo
tunakwenda na kuelekea mbele kuhusu dhana ya wakoma na wanyama safi na
mchanganyiko na wasio safi, kwa mfano, kupanda mashamba yako kwa mizabibu na
kuchanganya na halua au mazao jamii ya viungo. Huruhusiwi kufanya hivyo pia kutokana
na maandiko ya biblia. Kisha MMT inaongelea kuhusu ulimaji wa kuwatumia wanyama
wasio wa aina moja wakafungiwa nira pamoja. Kuna mkururu wote wa matokeo ya
matendo unayopaswa kuyafanya. Sisi, sasa, kwa ajili ya mazoea yetu ya kuishi
mijini, tunajifungia nira visvyo sawasawa kwa maana ya watu wa malumbano na
mijadala iliyo tofauti. Wao kwanza kabisa waliichukulia hii kwenye dhana au
wazo la kimwilia la kuwa hairuhusiwi kufanya hivyo au kuwatumia chini ya
sheria, na ndipo walifanya taratibu za zaidi sana (kutokana na maelekezo ya
biblia) kuhusiana na kile unachotakiwa kukifanya. Kisha zilikuwepo kanuni na
miongozo ya vile unavyopaswa uje navyo nyumbani mwako. Kulikuwapo na dhana ya
uzinifu au kuzini na wanawake. Makuhani walikatazwa kuoa wanawake najisi au
makahaba au wasio na bikira. Hukuruhusiwa kuchaganya mbegu, kwa hiyo lilikuwa ni
suala la kuchanganya mbegu; na halikuwa ni suala au tatizo la kiroho/la
kimaadili. Dhana au mawazo haya yote yalikuja onekana kwa mtazamo wa kimwili.
Muundo na mfumo mzima wote wa Roho, uelewa wetu wa kile tulichokuwa tunakifanya
kiroho, vilidharauliwa kabisa na andiko hili kuhusu Matendo ya Sheria. Ilipunguza kila kitu kwenye kiwango cha kimwili
na kisicho na kiroho.
Kimsingi, MMT iko
pale ili kuwezesha au kutoa baraka na laana. Wanachokisema wandishi ni kwamba,
wakati inapochemka, ni kwamba baadhi ya Baraka na laana zimekwisha timilika
tayari kama zilivyoandikwa kwene kitabu cha Musa. Baadhi ya Baraka zingine kutoka
Sulemani na baadhi ya laana tangu i na baadhi ya laana tangu Yeroboamu (18-19
op. cit. p. 61). Inataja hadi aya ya (21) nyakati za mwisho wakati watakaporudi
nchini Israeli (22) milele ... na haitaahirishwa (?) lakini wanyonge na watenda
dhambi wanatenda uovu mkubwa. (Kuna matukio ya kupatwa jua kwenye maandiko haya).
MMT inaendelea kuanzia aya ya (23 ibid. p. 61)
23 na [...].
Wafikirini wafalme wa Israeli, na yatafakarini matendo yao; kila mmoja wenu
24 walioitii Torati
waliokolewa kutoka matesoni, na hawa walikuwa ni watafuta Torati
25 enyi aliosamehewa
[maovu yenu. Mtafakarini Daudi ambaye alikuwa mtu mwenye matendo ya haki na
26 yeye ambaye (kwa
hiyo) ameokolewa kutoka kwenye mateso mengi na kusamehewa. (Kwa hakika) sisi
tumekupeleka wewe
27 miongozo mingine
ya Torati kwa mujibu wa maamuzi yetu kwa ajili ya mambo yako na ustawi wa watu
wenu. Kwa kuwa tumeliona (hilo)
28 unayo hekima na
uelewa wa Torati. Tafakari mambo haya yote, na muombe ili akutie nguvu
29 mapenzi yako, na
ondoka kutoka kwako mipango yote miovu na mambo ya Beliali
30 ili uweze
kufurahi mwishoni mwa nyakati, ukikuta kwamba baadhi ya matendo yetu yako
sahihi.
31 na hii itahesabiwa
kama ni matendo makuu yako, kwa kuwa unafanya yanayoelekea na yaliyo mema
machoni pake kwa ustawi wako wewe, na
32 kwa ustawi na
maslahi ya Israeli.
Miongozo ya MMT kuhusu
Sheria, au Matendo ya Sheria, ndipo
imefanyika muongozo wa kufanikisha kufikia utakatifu. Hii sio kweli. Sasa
tunaweza kujua kile alichowa anakipata Paulo a alichokuwa anakisema. Matendo ya Sheria, au MMT au ergon nomou hayamfanyi mtu kuwa mkamilifu wala hayamhesabii haki.
Tunaona kwamba alikuwa anapinga na kile alichokuwa anakifananisha na utakatifu
au haki ipatikanayo kwa njia ya imani. Tumeandaliwa vizuri na kikamilifu sasa
ili kuyapinga masuala ya maana ya nyaraka kwa Warumi na Wagalatia na uadilifu
wa maandiko. Kwenye jarida linaloongelea kuhusu MMT na Utofauti wa Shria, tumeandaliwa
vizuri kukanusha madai haya ya Waprotestanti wa siku hizi. Kwa sasa
unajidhihirisha kwa wazi sana kabisa kwamba wamepotoka na kukosea sana. Siyo
Torati inayowezesha kuwa mkamilifu, na kwa kweli siyo sheria hizi za usafi
zinazowezesha mtu kuwa mkamilifu. Kile kilichofanywa na hivi ni kiambisho au
kurahisisha sheria ya sadaka na ya utakaso kwenye Torati kwa kujaribu na
kuifana kuwa ni sehemu ya uwezeshaji wa kuupata utakatifu au haki.
Ni sheria ya
maadili ya kijamii inayotokana na asili na tabia za Mungu zinazowezesha kuupata
utauwa. Unaweza kufikiria kuwa kwenye karne ya kwanza mkiwa kama Wakristo
alioketi pamoja na watu wakiwa wanazungumzia hilo. Inakuwa ni gumzo la jumla
kwamba tumepewa kufana kitendo hiki au tendo lile. Yatupasa kuwa wasafi.
Hatuwezi kuutumia mfupa ule kufanya mikono kwa lengo hilo. Hatuwezi kumtumia
mnyama hadi mahala fulani. Huwezi kuifanya kazi hii na isiweze kuifanya ile.
Itakuchanganya sana. Tungewasikia watu hawa wakisema kuwa imewezekana kufanyika
kwa kuwa imo kwenye Matendo ya Sheria.
Matendo ya Sheria yanasema. Ni kama mtu anayesema kwamba kiongozi mmoja wa
kidini alisema, au Askofu x alisema. Hii inaonekana kuwa kama ilitokea.
Kama ilivyotupasa
kuzishughulikia kazi au matendo mapotofu ya uwongo kwa suala la Pasaka inayojaribu
kuifanya siku ya 14 Abibu ambayo ni Pasaka kutokana na kifichio cha uwongo, na
ndivyo ilivyo pia kwamba ilitupasa kushughulika na suala la hii MMT. Paulo
alishughulikia kwayo, kwa kuwa ni wazi sana iliingia na kuathiri Kanisa la
Galatia. Haikuwa ni bahati mbaya kwamba hayakuishia Galatia tu bali inasemekana
kuwa yalienea na kufika hadi kwa Warumi kwa kuwa jumuia ya Wayahudi wa Roma
walikuwa mbali sana kutoka Yerusalemu kuliko ilivyokuwa Galatia. Kadiri ilivyokuwa
mbali na matatizo yalipungua, lakini kwa kweli katika Mashariki ya Kati
kulikuwa na matatizo mengi na makubwa. Ulikuwa ndiyo kipindi ambacho Hekalu
liliwekwa alama ya kuangamizwa. Na ndiyo maana kwamba Hekalu na mazingira yake
yote viliangamizwa vyote, kuondolewa mifumo yote iliyowekwa na Wayahudi na
ambayo haikuwa ya kibiblia. Kwa hiyo utaratibu wote mzima uliendelea mbele
kwenye mfumo wa msafishaji, ili kwamba tuweze kuona kwa maana ya kiroho, badala
ya kushikamanishwa kwenye kanuni zote za kidini ya mambo hayo. Hata hivyo, moja
wapo ya majeruhi wa uondoaji ulikuwa ni ujuzi ukweli wa uwepo mambo haya.
Hatukujua kwamba Matendo ya Sheria kwa
kweli lilikuwa ni jarida lililoandikwa. Kilikuwa ni kitabu. Hakikuwa
kinatendewa kazi. Tunaweza sasa kuona kwenye maandiko kwa mtazamo wa ukweli kwamba
huenda Paulo alichokuwa anakisema kilikuwa, kwa kweli rejea ya MMT. Haijumuiki
bado, lakini wasomi wanazuoni sasa wana uhakika – kwamba hivi ndivyo hakika
kinachomanishwa. Dalili zake ni za kimabadiliko badiliko. Siyo kwa Kanisa la
Mungu, wanaojaribu kutangua. Ni suala mtambuka kwa kwa Waprotestanti wa zama
zetu hizi ambao wanapuuzia tofauti kwenye sheria ambayo ilikuwa imeeleweka wazi
sana na wao nyakati za Matengenezo hata kama hawakuielewa Pasaka na Siku
nyingine Takatifu zilizo kwenye mpango wa wokovu kisahihi. Kanisa limeshuhudiwa
kwa kukutwa hivi. Ukristo wa siku hizi ndipo utaweza kuona, kiusahihi zaidi,
kwamba Kanisa la Mungu linafanya vizuri na sahihi sana kwa hakika tangu mwanzo.