Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[CB9]

 

 

 

Nimrodi na Dini ya Uongo

 

(Toleo 3.0 20030904-20070109-20140223)

 

Na Kushi akamzaa Nimrodi naye akaanza kuwa ntu hodari duniani. Jarida hili limechukua kisa kilichoandikwa kwenye Sura ya 5 ya kitabu cha Historia ya Biblia Toleo la 1 cha Basil Wolverton Kilichochapishwa na Idara ya Uchapaji ya Chuo kilichojulikana kama Ambassador College.

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

 

(Copyright © 2003, 2007, 2014  Christian Churches of God, ed. Wade Cox)

(Tr. 2009, rev. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Nimrodi na Dini ya Uongo

 


Baada ya gharika

Miaka mingi ilipita na watoto wa Nuhu walipata watoto, na watoto wakakua, nao wakapata watoto.  Na kupitia hawa watoto nchi yote ikaanea watu (Mwanzo 9:19).

 

Kwa vile miaka ilipita watu waliongezeka zaidi.  Na wakati huu watu walikuwa na lugha moja n usemi mmoja.  Watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya shinari (Mwanzo 11:1-2).  Watu walianza kujenga nyumba, maghala na manyumba makubwa na aina zote za mijengo.  Baada ya muda mufupi miji ilikuwa imetagawanyika kila pahari.  Familia zilikuja pamoja na kuishi pamoja kama walivyofanya mbele ya gharika.

 

Mawe na miti yalikuwa machache.  Pengine hawangenjenga mji mkubwa ikiwa hawakufahamu vizuri mchanga wa kweli na bora kwa kujenga matofali.  Mchanga ulitengeneza matofali na kugaweka kwa moto au ina ili iweze kukauka.  Watu walitumia matofali badala ya mawe na lami badala ya chokaa (Mwanzo 11:3).  Na wakasema, haya na tujijengee mji, na mnara na kilele chake kifike mbinguni, tujifanyie jina, ili tusipate  kutawanyika usoni pa nchi yote. 

 

Hawakupendeza Mungu.  Mungu alijua watu wakikaa pamoja, hawatapata mazuri alivypumba duniani, kama msituni, milimani, mito ndani ya ziwa na jangwani.  Na tena watu wangevunja amri ya Mungu aliahidi Nuhu na familia yake watawanyike kote ulimwenguni.

 

Nimrodi akawa shujaa

Wakati huu wa historia ya mwanadamu pakaishi mtu kwa jina Nimrodi na alikuwa wa ukoo wa motto wa Nuhu, Ham. Baba yake aliitea Kushi. 

 

Nimrodi, tukiamini ukweli wa majina ya kihebrania, jina Nimrodi linamaanisha wasi ama shujaa kutoka kitabu cha (Strong’s Hebrew Dictionary 5248).

 

Waebrania walihusisha jina hili na nasi, na kwa hivyo jina lenyewe likawa sawa.  Naye Nimrodi aliishi kama jina lake, yaani akawa muasi.

 

Kwa hivyo, hili jina pengine ilitoka Mesopotamia ninurta, ilihusishwa na Mungu wa vita, aliyeitwa mshale, shujaa hodari na aliyesifika na kuenezwa sana wakati wa mwisho wa Karne ya pili BCE.  Jina lake lilionekana katika wafalme wa mwisho na katika ufalme wa assuru, na ndiye alikuwa mfalme wa kwanza kutawala Babeli, akaitwa tukuti-ninurtal (ca. 1246-1206 BCE). Wasomi wamejaribu kusema ya kwamba, huyu mfalme ndiye mwanzo wa jina ninurta.  Kwa hivyo, pengine aliitwa jina la Nimrodi wa hapa awali, na fundisho la uongo la Ninus, Mungu mwingine wa kaskasini na alifananishwa na Ninurta.  Wote Ninurta na Ninus walihusishwa pamoja na Nimrodi wa hapa mwanzo. 

 

Nimrodi alikuwa mtoto wa kuishi; na Farao Amenophis III (1411-1375) amehusisgwa ba yeye, ni wasomi wale wapinga Bibilia.  Hi ni kwa maana watoto wa kushi walihama Mesopotamia na kwenda Ethiopia, hata ingawa wanaonekana kama walitoka kussi, iliyo kaskasini mwa Mesopotamia, na watoto wengine wa kushi walienda kaskasini zaidi karibu na Indus River basin, iitwayo sasa Pakistani na ndani mwa India.

 

Assuru pia iliitwa nchi ya Nimrodi na akajenga miji bakeli, Ereku na Akadi na Kalne katika nchi ya shinari na ndiyo jina la awali la sumeria.  Na ilihusishwa ninawi na kala ni ikawa mji mkubwa wa Assuru wakati wa ufalme wa Assuru.  Nchi hii sasa, iko karibu Iraq ya sasa.

 

Bibilia yasema Nimrodi alikuwa “Hodari kuwinda wanyama mble za Bwana” kwa hivyo akawa mtu mwenye nguvu uwezo na kuogofya hapa duniani.  Kwa anjili ya nguvu, hekima na utalamu kama mwindaji hodari wa wanyama waliovamia watu, alifahamika kama hodari, shujaa na kiongozi wa kabila lao (Mwanzo 10:8-9) kama wengine wa siku zake walijua sheria za Mungu lakini, walisichukia sheria hata kuamini, Nimrodi waliamini wakiishi na sheria za Mungu hatafurahia maisha.  Aliishi na sheria zake na kujaribu kuwafundisha wengine kuishi na kuamini kama wao.

 

 Nimrodi akawa kiongozi wa watu walioishi nchi ya Shinari. Pengine kuna watu hawakufurahia uongozi wa watu walioishi nchi ya Shinari.  Pengine kuna watu hawakufurahia wongozi wake, lakini wanyama walipowavamia Nimrodi na wawindaji wake waliwakinga watu wote.  Nimrodi pia alijenga ukuta kuzunguka mji wote, matendo kama haya yalimfanya kuheshimika kama kiongozi hodari na kufanya familia nyinyi kuketi chini yake.

 

Baada ya miaka michache mji ulienea na kuwa mji mkubwa ilikuwa mji wa kwanza mkubwa kujenga duniani baada ya yule wa gharika.  Ulikuwa mji wa ajabu, watu alitoka mbali kuja kuitazama mijengo, ukuta na manyumba. Nchi hii baadaye iliitwa Babylonia na mji Babeli (Mwanzo 10:10).  Jina hili Akadi mwanzo na maana yake ni “Miango kwa Mungu” (Mwanzo 10:10, 11:9, NIV Study Bible).

 

Nimrodi akaanza kuabudu sanamu

Na akawa mtu wa kuogofya sana ulimwenguni.  Nguvu zake na utajiri wake ukakua kama vile Babeli ilikua.  Alitengeneza sheria na kusema, watu wa Babeli hawataongozwa na Mungu wa Noah tena, mbali wataongozwa na serikali ya binadamu.  Nimrodi tena akawaamuru kutii shetani kwa kuabudu vyombo walivyoona kwa macho yao, kama jua, nyoka na zingine nyingi (Arumi 1:21-23).

 

Jina la Mungu wa Babeli ni Bel na ni kama jina la Mungu Baali au Bwana, jina lingine ni merodach au “Mungu wa vita” (Yer 50:2) kwa jina la kihibiriania ni Baali au Mungu wa jua Ashtoreth, Ishtar or Easter na hapa sikukuu Easter ikaitwa.  Bel ni Mungu hodari katika miungu mingi.  Nimrodi aliheshimika sana kwa kujifanya kuhani mkuu wa Bel au Baali wa Merodach.  Katika Babei mafundusho ya uongo yalianza na imenea kote karibu kwa kila dini na hata siku ya leo watu wengi wale wangetamani kuishi vyema, hawajui jia zao cha kuabudu zinafanana na za kale kwa kuabudu sanamu.  Wakristiano siku ya leo wanaungana na Babeli kwa kuishika siku za Krismas na Ishtar ambayo Yesu mwenyewe alikufa ijumaa na kufufuka jumapili.  Hii imebeba majina mengi ya mafundisho ya uongo kama ya kaskasini Adonis ya wayunani Orpheus na Dionysus kati ya wayunani.

 

Mnara wa Babeli

Hila moja ya Nimrodi ya kukusanya watu pamoja, ili aweze kuwaongoza ilikuwa ni kujenga mnara wa ajabu na kuogofya kwa mtu. Ulikuwa mji na mnara wa kustaajabisha kote duniani na wa Mungu wa jua (Mwanzo 11:5).

 

Watu wakawa watumwa wakijaribu kuweka msingi wa Babezi, baadaye mnara ukainuka pole pole ukiangalia mawingu; Mpango wa Nimrodi ukaendelea vyema na kujenga mnara.

 

 Mungu akaigia kati, aliona Babeli ilikuwa mwanzo tu ya mwanadamu kujifanyia njia na mambo yake bila Mungu.  Wangeachiliwa dunia ingesambaratika na kuishi kwa miaka elfu sita, muda ambao umeruhushiwa shetani kutawala mwanadamu.  Watu wangefanana na miugu na kwa hivyo lazima wangesimamishwa (Mwanzo 11:6).  Tafakali kungekuwa aje ikiwa Nimrodi alikuwa na silaha za kisasa.

 

Kwa hivyo kuabudu kwa uongo kukaingiliwa kati na lugha ikachafuliwa na wakatawanyika  kote ulimwenguni kwa sababu mwanadamu alipata maarifa ya  kuji,aliza kabla ya muda uliowekewa shetani.

 

Usemi wa lugha nyingi ulianza

Bwana akasema, tazama watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja, na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatasuiliwa neon wanalokusudia kulifanya.  Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao (Mwanzo 11:5-5).  Walianza kuongea lugha tofauti moja na yule mwingine, kutoshikizana kukaingia, hata wakapigana na mwishowe wakaacha kujenga yule mnara (Mwanzo 11:7-8). Bwana akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote; kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli, maana hapo ndipo Bwana aliwachafulia lugha. (SHD 894) katika usemi wa Noah Babeli ni kuchafuliwa lugha.

 

Bila kusikizana familia nyingi zilienda mbali kutafuta riziki nah ii ndiyo ilikuwa mapenzi ya Mungu mwanzo 10:25 (Kumbukumbu la torati 32:7-8). Njia ya Mungu ya kuwatawanya kwa kuwachafulia lugha ilikuwa pigo kubwa kwa ufalme wa NImrodi, hata kuishi na kukaa kwa mwanadamu kukageuka.

 

Hata ingawa watu wengi walitawanyika wengine waliachwa huko Babeli na hata wengine kutoka mbari walitembelea Babeli na watu wakaongozeka katika idadi.

 

Mpango wa Nimrodi wa kutawala ulimwengu

Miaka ilipopita Nimrodi akanjenga miji mingine katika nchi tambarare ya shinari huko Babeli.  Ufalme wake ukaenea huko Assuru.  Watoto wa kushi, baba yao na ndugu zao wanenea mpaka Asia na Europe na wengine wakaenda mpaka Misiri na Ethiopia hapa Africa.Kila pahali walipoenea mafundisho ya Nimrodi ya kuabudu shetani ilienea, kuabudu shetaniakiwa jua ama nyoka, Nimrodi aliamini shetani ndiye mwenye uwezo tu wa kufungua na kuongeza watu maarifa ya kisiri.  Jina NImrodi, wasomi wa Bibilia waligundua ya kwamba linamaanisha Petero ama Pawtah na lugha ya chaldea Babeli na Kiebrania.

 

Kwa hakika watu wengine hawakushugulika na hali ya Nimrodi ya kuabudu sanamu, Hao walionana vyema wamwabudu Mungu wa kweli na wengine hawakujali lolote. 

 

Shemu ndiye mtoto wa umri mdogo katika familia ya Nuhu na shemeji mkubwa wa Nimrodi.  Shemu kama kuhani mkuu wa Mungu alienda kinyume na Nimrodi na kukataa habari yake.

 

Kifo cha Nimrodi hakijulikana vyema, lakini alikufa.  Shemu aliye kuhani mkuu wa Mungu, aliishi Jerusalemu na hata wafalme wengine huko wakawa makuhani, kama Melchizedeki ama Adonai-zedeki kumaanisha Bwana yangu ni mtakatifu.  Abrahamu mwishowe alitoa fungu lake la kumi kwa shemu au mmoja wa makuhani wa Yerusalemu.

 

Kifo cha Nimrodi kiliwashangaza wengi  wa wafuasi wake.  Hawakuamini vile Mungu wa jua ama kahani wao aliweza kufa.  Wafuasi wengi wakapoteza imani na Nimrodi na mpango wake wa dini ya uongo ikaisha nguvu na kusambaratika.

 

Naye satani, akukoma kupigana na Mungu kwa kuwafanya wanadamu kuachana na Mungu wa ukweli, hila zake ni kufaulu kwa miaka elfu nyingi. Satani alikuwa na mpango wa kuwa na kanisa la wasioamini Mungu ambaye itakuja kuwa mauurufu san kati ya waamini katita ulimwengu.

 

Mke wa Nimrodi

Jina la Bibi wa Nimrodi ni Ishtar ama Easter.  Bibilia yamtaja kama Ashtoreth.  Watu wengi walimwita Semiramis na Frazer, (The Golden Bough, ii 275).  Njia za hila zake kufanywa kusini mwa Uganda. Jina lingine la Semiramis ni Phrygian Cybele na Assuru Atargati.  Jina Atargati ni la kiyunani, kusema Baali ya Tarsus, huko sasani Assuru.  Jina lake zamani ilikuwa Atheh-Atheh kumaenisha Mungu mwanamke wa Tarsusi.  Mafundisho yake ya uongo ilienea mpaka kaskazini mwa Hieropolis Bambyce karibu na mto Frati (Frazer ibid. v, 162 and n 2,3).

 

Bwana wake alipokufa, bibi alinyakua mamlaka na kwa sababu watu wengi walikuwa wamepoteza matumaini ya Nimrodi kuwa kama Mungu, kama alivyosema.  Seminari aliogopa kupoteza mamlaka yake, na akatafakari hila ya kuondoa ili wamkubali.  Hila ya kuwashtua na miuliza ya kufanya waamini kweli Nimrodi alikuwa Mungu.

 

Baadaye seminari akapata motto wa kiume, Hii ilikuwa njama na hila ya kudanganya wafuasi wake.  Alieneza uvumi ya kwamba motto hakuwa na baba, lakini alizaliwa kwa mimjiza kutokana na miale ya jua.  Alifahamika kama motto wa kurithi ufalme wa Nimrodi.

 

Huu undanganyifu ulikuwa wa hali ya juu wa kuamini, lakini seminari alifaulu kutawala ufalme.  Nimrodi alionekana sana kama motto wa Mungu.  Na kwa ajiri ya juhudi zake za undanganyifu seminari aliabudiwa kama ndiye mama wa Mungu.  Alijuukana kama “Mama Bikira” au malkia wa mbinguni (Jer 7:18, 44:17-19,25).  Ni yeye mama wa kwanza kuwa wa dini ya uongo.  Mafundisho ya uongo yaliyomfuata ni ya “Cybele ka mama Mungu huko kati ya mashariki.

 

Haya yote yametendeka zaidi ya miaka elfu nne iliyopita.  Ulikuwa mwanzo wa kuabudu sanamu na imekuwa na uwezo kwa karne nyingi zilizopita, hata siku ya leo, watu wengi wanamwabudu “Malkia wa mbignuni” hata ingawa hakuna mtu kama huyo.

 

Shetani amefanya hila na njama zake, hata mifano ya kuabudu sanamu, siku, mila, mawao na mapokeo ya zamani na hizi zimechanganywa pamoja katika hali ya kuabudu Mungu siku ya leo.  Haya mambo yamekuwa siri, na imefanya wengi kutoweza kutii Mungu.

 

Siku za wasiojua Mungu zangaliwa kanisani

Mungu ametuonya kupokea mila za wale wanaoabudu sanamu (Kum. 12:30-31)  Viongozi wengi wa kanisa wanatuambia ni ushenzi kutoshika na kuheshimu 25 Decemba kama sikukuu.  Hii siku ilisherekewa na washenzi kwa ajili ya kuzaliwa kwa motto na malkia wa mbinguni aliyehusishwa na Nimrodi kama Mungu wa jua.

 

Seminaris na wafuasi wake wakasema tarehe 25th Decemba mti ulinenepa kwa siku moja huko Baberi na Nimrodi angerudi kwa siri tarehe hiyo kila mwaka kuacha zawadi kwa huyo mti.  Huyu ni mwanzo wa krismasi.  Soma karatasi “Kwa nini tusisherehekee krissimasi. Why we don’t celebrate Christmas (No. CB24).

 

Siku ingine ya kusherehekea ulimwenguni ni ya kuzaliwa kwa Ishtar (Seminari).  Anasema aliishi kama roho kabla ya gharika, na aliteremuka kama yai kubwa kutoka mbinguni na kuanguka mto frati. Mungu aliyekuja kama yai, si mwingine bali ni seminamis. 

 

Easter imeandikwa katika (KJV) (Mitume 12:4) lakini ni makosa ya watafusiri wa Bibilia, wanyea ndika neon pasaka.  Pasaka ndiyo ya kipekee Mungu angetaka tuisherehekee, lakini Easter Jumapili ni ya washenzi (1Cor. 5:7-8), (Angalia karatasi Siku takatifu za Mungu (No. CB22).

 

Sasa tunaweza kuona vile Nimrodi na seminamis walivyotumiwa na shetani kuhandaa ulimwengu kuamini uongo (Ufunuo 12.9) kama vile alivyopelekea hawa kuamini uongo.

 

Miungu mwingine kudanganya binadamu ni Mungu Ahis, aliyejulikana kama Mungu mmoja aliye wote baba na mwana aliyekuja hapa duniani na kuuawa kwa mti na akaingia kusimu siku ya Ijumaa na Jumapili alifufuka.  Hii ni hadithi ya Easter na si kama ya Kristo ya kufa siku ya pasaka,

 

Na tena ni mwanzo wa mafundisho ya utatu wa Mungu.  Huu ni uongo uliopenya duniani.

 

Hata ingawa shetani hataweza kundanganya ulimwengu siku zote. Siku zaja, wakati nguvu zake ztakomeshwa kwa miaka elfu moja (Ufunuo 20:1-3) na mafundisho ya uongo yatakwisha.  Na ulimwengu utafurahia ukweli uliofichwa machoni mwetu. Vitu ambavyo imefichwa kwetu kwa muda mrefu.

 

q