Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[090]

 

 

 

Kuulaani Mtini

(Toleo La 1.0 20020310-20020310)

 

Tendo la kuulaani mtini lililofanywa na Yesu Kristo lina maana kubwa sana kwenye imani na taratibu za Kanisa la Mungu. Kinatuama kwenye mololongo wa Usafishaji na Utakasaji wa Hekalu la Mungu.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Haki Miliki © 2002 Wade Cox)

(tr. 2013)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 

 


Kuulaani Mtini



Utangulizi

Kwenye Injili ya Mathayo sura ya 21 tunasoma habari ya kulaaniwa kwa mtini kwenye mfululizo wa matukio yaliyofuatiwa na kitendo cha kuingia kwake Yesu kwenye mji wa Yerusalemu, na kulisafisha hekalu.

Matthew 21:1-22 Hata walipokaribia Yerusalemu, na kufika Bethfage, katika mlima wa Mizeituni, ndipo Yesu alipotuma wanafunzi wawili akiwaambia, 2 Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mara mtaona punda amefungwa, na mwana-punda pamoja naye; wafungueni mniletee. 3 Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka. 4 Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,

5 Mwambieni binti Sayuni

Tazama, mfalme wako anakuja kwako,

Mpole, naye amepanda punda,

Na mwana-punda, mtoto wa punda.

6 Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru, 7 wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake. 8 Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; na wengine wakakata matawi ya miti, wakayatandaza njiani. 9 Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema,

Hosana, Mwana wa Daudi;

ndiye mbarikiwa, yeye ajaye

kwa jina la Bwana;

Hosana juu mbinguni.

10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu? 11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya.

Yesu Analisafisha Hekalu

12 Yesu akaingia ndani ya hekalu, akawafukuza wote waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni, akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao waliokuwa wakiuza njiwa; 13 akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi. 14 Na vipofu na viwete wakamwendea mle hekaluni, akawaponya. 15 Lakini wakuu wa makuhani na waandishi walipoyaona maajabu aliyoyafanya, na watoto waliopaza sauti zao hekaluni, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi! Walikasirika, 16 wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umekamilisha sifa? 17 Akawaacha, akatoka nje ya mji mpaka Bethania, akalala huko.

Yesu Anaulaani Mtini

18 Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa. 19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; akauambia, Yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. Mtini ukanyauka mara. 20 Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara? 21 Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka, ukatupwe baharini, litatendeka. 22 Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.

 

Tunapojionea uhusiano wake katika Marko 11 tunaona kwamba mchakato huu unabadilika. Na kwamba kuna mlolongo wa matendo yanayojitokeza na ambayo yanarudiwa.

 

Marko 11:1-33

Hata walipokaribia Yerusalemu karibu na Bethfage na Bethania, kukabili mlima wa Mizeituni, aliwatuma wawili katika wanafunzi wake, 2 akawaambia, Nendeni mpaka kile kijiji kinachowakabili; na katika kuingia ndani yake, mara mtaona mwana-punda amefungwa, asiyepandwa na mtu bado; mfungueni, kamleteni. 3 Na mtu akiwaambia, Mbona mnafanya hivi? Semeni, Bwana anamhitaji na mara atamrudisha tena hapa. 4 Wakaenda zao, wakamwona mwana-punda amefungwa penye mlango, nje katika njia kuu, wakamfungua. 5 Baadhi ya watu waliosimama huko wakawaambia, Mnafanya nini kumfungua mwana-punda? 6 Wakawaambia kama Yesu alivyowaagiza, nao wakawaruhusu. 7 Wakamletea Yesu yule mwana-punda, wakatandika mavazi yao juu yake; akaketi juu yake. 8 Watu wengi wakatandaza mavazi yao njiani, na wengine matawi waliyoyakata mashambani. 9 Nao watu waliotangulia na wale waliofuata wakapaza sauti, Hosana; ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana; 10 umebarikiwa na ufalme ujao, wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni. 11 Naye akaingia Yerusalemu hata ndani ya hekalu; na alipokwisha kutazama yote pande zote, kwa kuwa ni wakati wa jioni, akatoka, akaenda Bethania pamoja na wale Thenashara.

Yesu Anaulaani Mtini

12 Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa. 13 Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini. 14 Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia.

Yesu Analisafisha Hekalu

15 Wakafika Yerusalemu, naye akaingia ndani ya hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua ndani ya hekalu, akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao wauzao njiwa; 16 wala hakuacha mtu achukue chombo kati ya hekalu. 17 Akafundisha, akasema, Je! Haikuandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi. 18 Wakuu wa makuhani na waandishi wakapata habari wakatafuta jinsi ya kumwangamiza; maana walimwogopa, kwa sababu mkutano wote walishangaa kwa mafundisho yake. 19 Na kulipokuwa jioni alitoka mjini.

Fundisho kukutokana na Mtini Ulionyauka

20 Na asubuhi walipokuwa wakipita, waliuona ule mtini umenyauka toka shinani. 21 Petro akakumbuka habari yake, akamwambia, Rabi, tazama, mtini ulioulaani umenyauka. 22 Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu. 23 Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. 24 Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu. 25 Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.

Mamlaka ya Yesu Yanaonewa Mashaka

26 Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.] 27 Wakafika Yerusalemu tena; hata alipokuwa akitembea hekaluni, walimwendea wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee, 28 wakamwambia, Ni kwa mamlaka gani unatenda mambo haya? Naye ni nani aliyekupa mamlaka hii uyatende haya? 29 Yesu akawaambia, Nitawauliza neno moja, nanyi mnijibu, kisha nitawaambia ni kwa mamlaka gani nayatenda haya. 30 Ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni, au kwa wanadamu? Nijibuni. 31 Wakasemezana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema, Ulitoka mbinguni, atasema, Mbona, basi, hamkumwamini? 32 Ila tukisema, Ulitoka kwa wanadamu, -- waliogopa watu; maana watu wote walimwona Yohana kuwa nabii halisi. 33 Wakamjibu Yesu, wakasema, Hatujui. Yesu akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani nayatenda haya.

 

Mchakato huu unaonyesha kwamba aliingia Hekaluni kwa mfuatano maalumu wa siku na akalisafisha. Aliingia Hekaluni ili kuhakikisha kuwa limesafishika, tangu siku ya kwanza ya mwezi wa Abibu na kuendelea kwa mujibu wa maelekezo ya Torati na maeneo tuayoona kuwa imeelezwa na kuandikwa ni kwenye Ezekieli 45:18-25:

18 Bwana MUNGU asema hivi; Mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utatwaa ng'ombe mchanga mume mkamilifu; nawe utapatakasa mahali patakatifu. 19 Na kuhani atatwaa baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi, na kuitia juu ya miimo ya milango ya nyumba, na juu ya pembe nne za daraja ya madhabahu, na juu ya miimo ya lango la ua wa ndani. 20 Nawe utafanya vivyo hivyo katika mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi kwa ajili ya kila mtu akosaye, na kwa ajili ya mtu aliye mjinga, ndivyo mtakavyoifanyia nyumba upatanisho. 21 Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi, mtakuwa na Pasaka, sikukuu ya siku saba; mkate usiotiwa chachu utaliwa. 22 Na siku hiyo mkuu atatengeneza ng'ombe kuwa sadaka ya dhambi, kwa ajili ya nafsi yake, na kwa ajili ya watu wote wa nchi. 23 Tena, katika zile siku saba za sikukuu atamtengenezea Bwana sadaka ya kuteketezwa, ng'ombe saba na kondoo waume saba wakamilifu, kila siku kwa muda wa siku saba, na beberu mmoja kila siku kuwa sadaka ya dhambi. 24 Naye atatengeneza sadaka ya unga, efa moja kwa ng'ombe, na efa moja kwa kondoo mume, na hini moja ya mafuta kwa efa moja; 25 katika mwezi wa saba, siku ya kumi na tano ya mwezi, katika sikukuu atafanya vivyo hivyo kwa muda wa siku saba; sadaka ya dhambi vivyo hivyo, na sadaka ya kuteketezwa vivyo hivyo, na sadaka ya unga vivyo hivyo, na mafuta vivyo hivyo.

 

Nukuu-elekezi ya karibu iko kwenye vitabu vya Mwanzo 8:13; na Kutoka 12:18; 29:1-14. Kwenye Ezekieli 43:18 tunaona kwamba kitendo cha utakaso na kuweka wakfu kinaanzia madhabahuni, malali ambako utakaso wa makuhani ulikuwa ni lazima kwa makuhani wanaotokana na uzao wa Walawi kwa mujibu wa Torati (Walawi 8:1-10). Kwa hiyo, hapa tunashughulika na makuhani waliokwisha kutakaswa tayari na kufuatiwa na tendo la utoaji wa dhabihu madhabahuni kwenye utaratibu mpya. Kwa ajili hii, wana wa Sadoki ndio Walawi pekee walioruhusiwa (Ezekieli 40:46; 44:15; sawa na ilivyoandikwa kwenye Ufunuo sura ya 7). Huu ni ukuhani wa Melikizedeki. Ukuhani huu uliutangulia ule wa Lawi, na Lawi alitoa zaka kwake akipitia kwa Ibrahimu. Shemu alikuwa ndiye kuhani wake mkuu tangu kipindi cha Nuhu. Huduma hii ilikuweko huko Yerusalemu hadi kipindi ambacho Daudi aliutwaa na kuutamalaki mji huu wa Yerusalemu. Mfalme alipewa cheo cha Adonai-Sedeki au Melkizedeki kwa cheo cha kudumu kama tunavyojionea kutoka kwenye Maandiko Matakatifu (sawa na ilivyoandikwa kwenye jarida la Melkizedeki (Na. 128) [Melchisedek (No. 128)].

 

Mfalme huyu hakuwa Yesu Kristo kama wanavyodhani na kufundisha wengine, nah ii ni kwa mujibu wa maandiko kadhaa na mengi yanayoonyesha kuwa huyu asingewezekana kuwa ni Yesu Kristo, maana asingewezekana kuwa ni mwanadamu aliyekuwa anaishi huko Yerusalemu na huku anaweza kumtokea Ibrahimu kwa kipindi na wakati huo huo mmoja akiwa kama Malaika wa Yahiva aliyemtembelea Ibrahimu akiwa na wenzake wengine wawili wakienda kuuangamiza mji wa Sodoma. Na zaidi sana, akiwa kama Malaika wa Yahova, alikuwa pamoja na wana wa Israeli pale jangwani, na kwenye utekaji na kuutamalaki mji wa Yeriko na kwa Kanaani nzima yote. Na angewezaje tena awepo huko Yerusalemu akiwa kama  Adonai-Sedeki? Na kusudi la kuzaliwa kwake katika mwili kingekuwa na maana gani kama kungekuwa tayari imekuwa hivyo katika kipindi cha miaka takriban miaka mia tano iliyopita huko nyuma? (Soma pia jarida la Malaika wa YHVH (Na. 24) (The Angel of YHVH (No. 24).)]

 

Kwenye maandiko ya Kutoka 29:36 tunaona kwamba ng’ombe dume alitolewa sadaka katika siku zile saba muhimu na maalumu. Na hapa kwenye Ezekieli 43 tunaona kuwa natolewa mara moja tu na kwenye siku nyingine wanatolewa mbuzi wagodo. Hili linaonekana wazi kabisa kuwa ni Hekalu linguine na ni kwa mlolongo wa shughuli nyingine. Sadaka hizi kwenye Ezekieli 43:18-27 ni za kitaifa na za kikuhani ambapo zile za kikuhani zinawakilisha zile za taifa zima.

 

Bullinger anaona kwamba hazikuwa za kila mtu binafsi yake, na anadhani kuwa hakutakuweko na Siku ya Upatanisho na anaamini kutokana na ukweli huu kwamba hazitatolewa chini ya Sheria. Ingawaje zitatolewa katika kipindi cha millennia na ambacho utekelezaji wa maagizo ya Torati utakuwa na tofauti aina yak echini na kipindi hiki cha utawala wa Kristo kwa habari ya masuala haya ya utoaji dhabihu za wanyama, kwenye sikukuu zote zinazofuatiwa tangia ile ya Psaka hadi Sikukuu ya Vibanda na ya Upatanisho na ya Baragumu ambazo hazikuandikwa wala kutajwa hapa, (Ezekieli 45:24-25) haimaanishi kuwa hazitaadhimishwa (kama ilivyoandikwa kwenye jarida la  Maswali Yaulizwayo Sana Kuhusu Ezekieli Sura za 36-48 na Utakaso wa Hekalu (Na. 292) na Utakaso wa Hekalu la Mungu (Na. 241) [FAQs on Ezekiel Chapters 36-48 and the Sanctification of the Temple (No. 292) and the Sanctification of the Temple of God (No. 241)]. Inapaswa ijulikane pia kwamba siku za Mwandamo wa Mwezi hazikujumuishwa kwenye siku za kazi na sheria hii itatumika zaidi kwenye kipindi hiki cha millennia kama tunavyoona kwenye Ezekieli 45 f, na pia kwenye Isaya 66:23, na wale ambao hawatazitunza vyema kwa kuziadhimisha watakufa (Isaya 66:24).

 

Mchakato huu wa kusafisha ndio haatimaye utachukua mahali pake tangia mwanzoni mwa Mwezi wa Kwanza hadi mwezi wa saba. Kristo alifanya jambo hili siku ya kumi alipokuwa akiingia mjini Yerusalemu. Alikuwa na njaa pia alipokuwa akitimiliza utaratibu huu. Hii ingeweza kutafsiriwa pia kwamba ilikuwa inaonyesha kuwa alikuwa amefunga saumu kwa kipindi hiki.

 

Ni mchakato wa ufungaji saumu ulioeleweka na wale wanaofanya mfungo aina hii. Hata njaa ya kawaida tu ya siku kwa siku ni jambo gumu sana kulivumilia.

 

Inaeleweka sana kwamba alikuwa amefunga saumu ya kipndi kirefu na cha siku nyingi, na hata kwa wao wenyewe. Na ingawaje inaonekana kwamba alikuwa akipita kwenye nyumba kadhaa za marafiki zake akiwa kwenye hali hii na kipindi kile.

 

Injili za Mathayo, Marko na Luka zinatueleza kwamba Kristo alikuwa Hekaluni, akilisafisha na kuhakikisha kuwa liko safi kwa kuwaondoa wale waliokuwa wanafanya biashara ya kubadilisha fedha na shughuli nyingine za haramu na za kiharamia.

 

Kwa hiyo, baada ya Utakaso kwa ajili ya dhambi zlizozifanywa pasi kukusudia ama kwa Kupotoshwa, Kristo aliingia Yerusalemu, aliingia kutoka Yeriko siku ya 8 mwezi Abibu, na akashinda usiku ule nyumbani kwa Zakayo. Uingiaji huu wa kwanza huko Yerusalemu ulikuwa ni kutokea Bethfegi mnamo siku ya 9 ya Abibu (Ijumaa) na sio kutoka Bethania (kama ilivyo kwenye Mathayo 21:8-9). Alijitokea pasi kutarajiwa na akaingia na kulisafisha Hekalu (Mathayo 21:12-16), na kisha aliondoka na kwenda Bethania (Mathayo 21:17). Mchakato huu umeelezewa kwenye midani za jarida la  Kipindi cha Kusulibiwa na Kufufuka (Na. 159) [Timing of the Crucifixion and the Resurrection (No. 159)].

Ilipofika siku ya 11 mwezi wa Abibu, siku ya nne kabla ya maadhimisho ya Pasaka, aliingia Hekaluni na kuliangalia na kisha akarejea Bethania (Marko 11:11). Siku ya 12 Abibu, ambayo ni siku tatu kabla ya Pasaka ya mwaka 30 BK, alijitotokea tena Hekakuni, akalisafisha tena na kisha akawafundisha watu humo Hekaluni (Marko 11:15-17; Luka 19:45-46). Alikutana na vipingamizi vya wakuu wa Hekalu na watawala (Marko 11:18; Luka 19:47-48) na kisha akaondoka kutoka mjini na huenda alienda tena Bethania (Marko 11:19; Luka 21:37-38).

 

Siku ya pili yake kabla ya Pasaka ambayo ni ya 13 Abibu (Jumanne), Kristo alikuwa tena mjini Yerusalemu na Hekaluni (Mathayo 21:23-27; Marko 11:27-33; Luka 20:1-8). Unabii wake mkuu na wa kwanza ndipo ulitolewa humo Hekaluni (Luka 21:5-36).

 

Maelekezo kuhusu utaratibu wa Meza ya Bwana yalitolewa kwenye juma hili (Luka 21:37-38).

 

Kisha unabii mwingine mkuu ulitolewa kwenye Mlima wa Mizeituni (Mathayo 24:1-51; Marko 13:1-37) na ukaendelea hadi (Mathayo 25:1-46).

 

Ktisto, kwa mfano wake ulio wazi kwenye injili hizi, alikuwa analisafisha Hekalu lote kabisa katika kipindi hiki, tangia siku ya 1 Abibu kama ilivyoagizwa kwenye Torati, hadi kufikia siku ya 13 Abibu au mwezi wa Nisan, ambayo ilikuwa ni siku ya mwanzo wa maandalizi ya Psaka. Na mwishoni mwa siku ya 13 Abibu, yeye pamoja na wanafunzi wake walipumzika kwenye chumba cha ghorofani kwa maadhimisho yake ya Mwisho au Ushirika wa Meza ya Bwana na ndipo aliposalitiwa, akateswa na kupelekwa mbele ya wazee wa mabaraza, huyu Masihi, na ndipo aliposulibiwa akiwa ni Mwanakondoo wa Pasaka majira ya alasiri, siku ya 14 Abibu.

 

Fundisho kutokana na Mtini

Fundisho tunalojifunza kutokana na mchakato wa kulaaniwa kwa mtini lilikuwa ni kwamba, uliwekwa ndani yake na kuhusianishwa na mchakato mzima wa maandalizi ya maadhimisho ya Pasaka, na ilikuwa ni sehemu ya mchakato wa utakaso. Maana yaliyopo sambamba na kutokuwepo kwa matunda ndani yake na kuulani lilikuwa ni fundisho kwa Makanisa ya Mungu, kwamba kwenye mchakato huu wa utakaso au kusafisha kile kilishoshindwa kuzaa matunda ni kile kilichoachwa kikinyauka na kufa.

 

Fundisho hili halikuwa na maana sana na muafaka kwenye sehemu ya karne ya ishirini, kipindi ambacho utakaso ulikuwa haufanyiki kabisa, na maandalizi ya Pasaka yalikuwa hayaelekezwi kabisa katika utakaso na wokovu wa Israeli na wa mataifa.

Na ni kwa sababu hii ndipo mifano iliyo kwenye Injili za Mathayo na Marko unafuatia, ikielezea juu ya kuwaajiri watenda kazi wengine na wana wengine. Mmoja aliahidi kuwa atakwenda na kufanya na mwingine alikataa kuahidi. Hata hivyo, Yule aliyeahidi kuwa atakwenda hakwenda nayule aliyekataa kuahidi chochote ndiye aliyekwenda na akaifanya ile kazi kama alivyopenda Baba yake iwe. Mfano huu ulielekezwa kwao makabila ya Yuda na Lawi na kwa Israeli wote. Mfsno mwingine wa mwenye shamba aliyesafiri (Marko 12:1-12) ulikuwa ni wa manabii na Kristo mwenyewe, na lile shamba la mizabibu walikuwa ni nyumba yote ya Israeli (Isaya 5:7) (sawa na ilivyofafanuliwa kwenye jarida la. Agano la Mungu (Na. 152) [The Covenant of God (No. 152)].  

 

Shamba la Mzabibu

Mfano wa Mpangaji

Marko 12:1-12 Akaanza kusema nao kwa mifano; Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akazungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri. 2 Hata kwa wakati wake akatuma mtumwa kwa wale wakulima, ili apokee kwa wakulima katika matunda ya mizabibu. 3 Wakamtwaa, wakampiga, wakamtoa nje, hana kitu. 4 Akatuma tena kwao mtumwa mwingine, na huyo wakamtia jeraha za kichwa, wakamfanyia jeuri. 5 Akamtuma mwingine, huyo wakamwua; na wengine wengi, hawa wakiwapiga na hawa wakiwaua. 6 Basi alikuwa na mmoja bado, mwana mpendwa wake; huyu naye akamtuma kwao mwisho, akisema, Watamstahi mwanangu. 7 Lakini wale wakulima wakasemezana, Huyu ni mrithi; haya, na tumwue, na urithi utakuwa wetu. 8 Wakamkamata, wakamwua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu. 9 basi atafanyaje yule bwana wa shamba la mizabibu? Atakuja na kuwaangamiza wale wakulima, na lile shamba la mizabibu atawapa wengine. 10 Hata andiko hili hamjalisoma,

Jiwe walilolikataa waashi,

Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni.

11 Neno hili limetoka kwa Bwana,

Nalo ni ajabu machoni petu?

12 Nao wakatafuta kumkamata, wakaogopa mkutano; maana walitambua ya kwamba ule mfano amewanenea wao. Wakamwacha wakaenda zao.

 

Hapa tuaona kwamba wapangaji ni nyumba ya Israeli ambao walikuwa ni makuhani na Walawi waliopewa kuifanya kazi ya Mungu, na pia nyumba ya Yuda ambayo iliangushwa chini na Waedomu na matendo ya imani ya Waheleni. Ujumbe ulikuwa ni kwa wateule wa taifa na kisha kwa Kanisa ambao ulipaswa uwafuate.

 

Kumsheshimu na Kumpa kodi kwa Kaisari

Mtenganisho kati ya masuala yanayolihusu Kanisa na wale walio kwenye mambo ya kidunia kwenye kipindi cha maandalizi vilisisitizwa sana kwenye fundisho lihusulo kumpa Kaisari kwenye Injili ya Marko 12:13-17.

13 Wakatuma kwake baadhi ya Mafarisayo na Maherodi, ili wamnase kwa maneno. 14 Hata walipofika walimwambia, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, wala hujali cheo cha mtu; kwa maana hutazami sura za watu; lakini katika kweli waifundisha njia ya Mungu. Je! Ni halali kumpa Kaisari kodi au siyo? 15 Tumpe, tusimpe? Naye, akijua unafiki wao, akawaambia, Mbona mmenijaribu? Nileteeni dinari niione.
16 Wakaileta. Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii na anwani hii? Wakamwambia, Ni ya Kaisari. 17 Yesu akajibu, akawaambia, Mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na yaliyo ya Mungu mpeni Mungu. Wakamstaajabia sana

Mfululizo wa mifano umetolewa, ili kushirikisha mafundisho kwenye Kanisa.

Kanisa la Ufufuo

Kristo alishughulika na Masadukayo pia kipindi kile kuhusu Ufufuo wa wafu katika Marko 12:18-27.

18 Kisha Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza na kusema, 19 Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie ndugu yake mzao. 20 Basi kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao. 21 Wa pili naye akamtwaa akafa, wala yeye hakuacha mzao. Na wa tatu kadhalika; 22 hata na wote saba, wasiache mzao. Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye. 23 Basi, katika kiyama atakuwa mke wa yupi katika hao? Maana wote saba walikuwa naye. 24 Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu? 25 Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni. 26 Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? 27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana.

 

Kwenye andiko hili alizungumzia kuhusu Ufufuo wa wafu (Marko. 12:18-27) na Kanisa kama mzaliwa wa kwanza aliyefufuka kutoka kwa wafu, kwa kuwa alisema kuwa wakati alipokuwa anaongea na Musa kwenye kile kichaka kilichokuwa kinawaka kwamba: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo” Yeye ni Mungu wa walio hai na sio wa wafu, na kwa hiyo Kristo hapa anaeleza juu ya Kanisa—ambalo ni la wale waliolala katika Bwana.

 

Ni mchakato wa maandalio ya Hekalu ambayo yalichukua mahala pake kutoka siku ya 1 Abibu hadi siku ya Pasaka. Kisha Mkate usiotiwa Chachu ukaliwa kwa siku saba tangu siku ya 15 hadi 21 Abibu, na mwezi wa mfungo wa saumu uliofuatia siku ya saba iliyokaribia, uliopelekea kwenye mchakato wa kawaida wa kuhesabu siku na majuma kuelekea Pentekoste na mavuno ya ngano, ambayo ni mavuno ya Kanisa la mzaliwa wa kwanza.