Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[275]

 

 

 

 

 

 

 

 

 Sadaka

(Toleo La 1.0 20060923-20060923)

Kumbukumbu la Torati 16:16: “Mara tatu kwa mwaka na watokee wanawaume wako wote mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua; katika sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, na katika sikukuu ya majuma, na katika sikukuu ya vibanda; wala wasitokee mbele za Bwana mikono mitupu."

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © Wade Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Sadaka



Maratatu kila mwaka Mungu ametumuru kukusanyika pamoja mahali ambapo Mungu amepachagua alikalishe jina lake. Sikukuu hizo tatu ni: Sikukuu ya Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu; Idi au Sikukuu ya Majuma; na Sikukuu ya Vibanda. Tunatakiwa kuondoka na kuziach nyumba zetu na kwenda mahali alipopachagu Bwana. Kumbukumbu la Torati 16:16-17:

“16 Mara tatu kwa mwaka na watokee wanawaume wako wote mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua; katika sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, na katika sikukuu ya majuma, na katika sikukuu ya vibanda; wala wasitokee mbele za Bwana mikono mitupu. 17 Kila mtu na atoe kama awezavyo, kwa kadiri ya baraka ya Bwana, Mungu wako, alivyokupa”

 

Maelekezo haya tumepewa kwa zaidi ya sehemu moja kwenye Maandiko Matakatifu. Zaidi ya yote, amri au agizo kuhusia na jinsi Sikukuu hizi zitakavyokuwa linategemeana na makabila yalivyo. Tumeamriwa kuwa tusiende huko mbele za Mungu tukiwa mikono mitupu.

Kumbukumbu la Torti 12:1-18 “1 Hizi ndizo amri na hukumu mtakazotunza kuzifanya katika nchi aliyokupa Bwana, Mungu wa baba zako, uimiliki, siku zote mtakazoishi juu ya nchi. 2 Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi; 3 nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo. 4 Wala msimfanyie hivyo Bwana, Mungu wenu. 5 Lakini mahali atakapochagua Bwana, Mungu wenu, katika kabila zenu zote, apaweke jina lake, maana, ni makao yake, elekezeni nyuso zenu hapo, nawe wende huko; 6 pelekeni huko sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu zenu, na zaka zenu, na sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu, na sadaka zenu za hiari, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ng'ombe na ya kondoo; 7 na huko mtakula mbele za Bwana, Mungu wenu, nanyi furahini katika yote mtakayotia mikono yenu, ninyi na wa nyumbani mwenu, aliyokubarikia Bwana, Mungu wako.”

 

Kwa hiyo ni wazi sana basi, wakati tulipopewa milki zetu kufuatana na makabila yetu, mataifa yalipaswa kujua au kuchagua mahala pao pa kufanyia ibada na iliwapasa kujihudhurudhisha kwenye maeneo hayo kwa sikukuu.

8 Msifanye kwa kufuata mambo yote tuyafanyayo hapa leo, kila mtu kama aonavyo vema machoni pake; 9 kwani hamjafikilia bado katika raha na urithi akupao Bwana, Mungu wako. 10 Lakini mtakapovuka Yordani na kukaa katika nchi anayowarithisha Bwana, Mungu wenu, akawapeni raha, akiwaokoa na adui zenu pande zote, mkakaa salama;

 

Kwa hiyo, mahala pa urithi na milki palipaswa kuchaguliwa na hapa, ni mahala pale pa milki au urithi, ndipo tunapaswa kumuabudu Mungu.


11 wakati huo itakuwa kwamba mahali pale atakapopachagua Bwana, Mungu wenu, alikalishe jina lake, hapo ndipo mtakapoleta kila kitu ninachowaamuru; sadaka zenu za kuteketezwa, na dhabihu zenu, na zaka zenu, na sadaka ya kuinuliwa ya mikono yenu, na nadhiri zenu zote teule mtakazoweka kwa Bwana. 12 Nanyi mtafurahi mbele za Bwana, Mungu wenu, ninyi, na wana wenu, na binti zenu, na watumishi wenu wanawaume na wanawake, na Mlawi aliyemo malangoni mwenu; kwa kuwa hana sehemu wala urithi kwenu. 13 Ujihadhari usitoe sadaka zako za kuteketezwa katika kila mahali upaonapo; 14 bali katika mahali atakapopachagua Bwana katika kabila zako mojawapo, ndipo utakapotoa sadaka zako za kuteketezwa, ndipo utakapotenda yote nikuamuruyo.

 

Watu wote walitakiwa wakajihudhurishe mbele za Mungu pamoja na makuhani wao ambao waliwajibika kuwahudumia. Kanisa lilipewa mamlaka haya na lilifundisha kwamba lilikuwa limepewa mamlaka haya tangu mwanzoni kabisa (soma jarida la Utoaji wa Zaka (Na. 161)).

 

Andiko hili halikukataza ulaji wa nyama zilizotolewa kama dhabihu za helaku la Mungu kama tunavyoona kwenye maandiko yanayofuatia mara tu baada ya andiko hili. Bali ni kwamba nyama ziliagizwa na kuruhusiwa kuchinjwa na kuliwa kwenye miji yote ya urithi wa Israeli.

15 Pamoja na haya waweza kuchinja nyama na kula ndani ya malango yako yote, kwa kufuata yote yatamaniwayo na roho yako, kwa mfano wa baraka ya Bwana, Mungu wako, aliyokupa; aliye tohara na asiye tohara ana ruhusa kula katika nyama hiyo, kama ya paa na ya kulungu. 16 Lakini msiile damu; imwageni juu ya nchi kama maji.

 

Agizo na amri iliyokuwepo ni kwamba unapaswa kwenda kwenye sikukuu ili ukale Zaka yako ya Pili.

17 Usile ndani ya malango yako zaka ya nafaka zako, wala ya divai yako, wala ya mafuta yako, wala wazaliwa wa kwanza wa makundi yako, ya ng'ombe wala ya kondoo, wala nadhiri zako uwekazo zo zote, wala sadaka zako za hiari, wala sadaka ya kuinuliwa ya mkono wako; 18 lakini hivyo mtakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako, wewe, na mwanao mume na mke, na mtumwa wako mume na mke, na Mlawi aliye ndani ya malango yako; nawe furahi mbele za Bwana, Mungu wako, katika yote utakayotia mkono wako.

 

Nano hili la "mahali atakapopachagua" limekuwa likibadilika kwa nyakati kadhaa mbalimbali na linategemea na maeneo na mataifa ambayo Mungu ametupa ili tuyamiliki. Kumbuka, Mungu aliwahi kuwtawanya Israeli na kuyaangamiza kabisa Mahekalu yote mawili, lile la Yerusalemu na lile la Samaria lililokuwa kwenye Mlima Gerizi, na pia lile la Misri. Mungu alihyadamishia mamlaka yote ya utaratibu na mfumo wa Hekalu kwenye Kanisa. Baraka za mataifa yote zimeondolewa kutoka Yuda na kutoka kwa Wasamaria na waliangamizwa kama watu. Baraka za Efraimu na Manase hazipo kwa Wasamaria wanaodai utambulisho huo wa Baraka. Wasamaria waliangamizwa na wa Byzantines na sasa hesabu yao ni ya watu wachache sana mno. Hakuna hata mmoja kati yao anayehesabiwa kwenye makanisa ya Mungu.

 

Sikukuu hizi zinaadhimishwa kwenye mataifa tuliyopewa na tunayoishi na hayahusiani na Yerusalemu. Wakti Hekalu liliposimamishwa pale kulikuwa na mahekalu meingine huko Misri yaliyokuwa yamedumu kwa karne nyingi kadhaa nyuma, kwa vipindi vyote viwili, yaani kipindi cha kuwepo kwa Hekalu huko Yerusalemu na kile cha kutokea kwa ukengeufu wake. Mungu aliamuru lijengwe Hekalu huko Misri na Sikukuu zilikuwa zinaadhimishwa huko, na Kristo mwenyewe aliziadhimisha huko wakati alipokuwa kitoto kichanga akiwa na wazazi wake, kwa kuwa imeandikwa katika Hosea: "Kutoka Misri Nilikuita Mwanangu". Baada ya Kanisa kuanza, lilikuwa ni Hekalu la kiroho – Kanisa – ndilo lililoamua masuala yahusuyo maadhimisho ya Sikukuu na kuchagua mahala pa kuziadhimishia. Ukuhani wa Melkizedeki na Hekalu la Kiroho ulichukua mahala pa ule w a Lawi na Hekalu la kimwili.

 

Mungu anatuambia sisi pia kwamba umbali usiwe sababu ya kutuzuia, kwa hiyo tunapaswa kulitia hilo mioyoni wakati tunapokuwa tunajiandaa kwa ajili ya kuziadimisha Sikukuu hizi kila mwaka. Wengi wetu tunalazimika kusafiri umbali mrefu ili kuweza kujihudhurisha kwenye Sikukuu. Na hii ndiyo maana katika mwaka wa tatu tunaziweka zaka zetu kwenye mfuko wa kusaidia jamii ya wasiojiweza au maskini ili kuwasaidia wahitaji waweze kuhudhuria Sikukuu, na ikiwezekana au ikilzimu, kuwapatia misaada mingine yoyote itakayohitajika.

Kumbukumbu la Torati 14:23-26 Nawe utakula mbele za Bwana, Mungu wako, mahali atakapochagua apakalishe jina lake, zaka ya nafaka zako, na divai yako, na mafuta yako, na wazaliwa wa kwanza wa makundi yako ya ng'ombe na ya kondoo; ili upate kujifunza kumcha Bwana, Mungu wako, daima. 24 Na njia ikiwa ndefu mno nawe, usiweze kuzichukua kwa kuwa mahali ni mbali nawe mno atakapochagua Bwana, Mungu wako, apakalishe jina lake, hapo atakapokubarikia Bwana, Mungu wako; 25 ndipo uzibadili ziwe fedha, na kufunga zile fedha uende nazo mkononi mwako, hata mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako; 26 na zile fedha zitumie kwa cho chote itakachotamani roho yako, ng'ombe, au kondoo, au divai, au kileo, au roho yako itakacho kwako cho chote; nawe utakula huko mbele za Bwana, Mungu wako; tena furahi, wewe na nyumba yako;  

 

Sehemu ya kuziandaa Sikukuu hizi zote ni kutilia maanani Baraka ambazo Mungu Baba yetu ametuahidi kuwa atatufanyia, tunapaswa kwenda kumtolea sadaka au dhabihu zinazolingana sawasawa na Baraka alizotubarikia. Tusijitokeze tu kwenye hizi Sikukuu pasipo mpangilio na kufanya maamuzi ya haraka ya papohapo katika kutoa sadaka zatu kwa kulinganisha na kile tulichonacho mifukoni mwetu kwa wakati ule, au kuandika hundi ya fedha tukadhani kuwa tumeshatimiza wajibu wetu unaotupasa kuufanya sisi kama Wakristo. Inatupasa tutilie maanani au kulinganisha na jinsi Mungu alivyotutendea na ndipo tumtolee dhabihu au sadaka inayolingana kwayo.

2Wakorintho 9:7 Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.

 

Kwa maneno mengine, ni kwamba tunapoamua kutoa sadaka zetu tunapaswa kuwa na furaha na heshima ili tuweze kutoa kile tunachoweza kusaidia ama kuitegemeza huduma tuliyopewa. Je, ni huduma au majukumu gani basi hayo? (Soma jarida la Majukumu ya Kanisa (Na. 171).)

 

Mathayo 28:18-20 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. 19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.

 

Jambo linguine na la muhimu sana kuhusu utoaji wa sadaka zetu kwa Mungu ni kuhusu uhusiano wetu na kila mmoja wetu.

Mathayo 5:22-24 Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto. 23 Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako, 24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako.

 

Ili kulitimiliza Agizo Kuu la Kanisa tunapaswa kufanya kazi pamoja kama kikundi au timu. Timu inategemea sana na jinsi uhusiano ulivyo wa washiriki waalio kwenye ile timu katika ufanyaji kazi wake wa kiumakini na ushirikiano.

 

Tazama isemavyo 1Wakorintho sura ya 3.

Hatutaweza kusaidiana sisi kwa sisi kuwa Wakristo tusipopendana (Mathayo 22:39).

Yohana 14:15 "Mkinipenda, mtazishika amri zangu.”

 

Hii inaturudisha nyum hadi kwenye amri iliyo kwenye Kumbukumbu la Torati 16:16 kwamba na tusitokee mbele za Bwana mikono mitupu.

 

Kanuni ya kumpenda Mungu na kumpenda Kristo ni sharti tupendane. Hii sio hisia ya juujuu tu na yakimsisimko kuonyeshana kia mtu na mwenzake, bali ni kuchukuliana mizigo kikamilifu na kuhudumia au kuwap mahitaji kwa wengine wenye uhitaji; huwaheshimu wengine kwa kujali utu wao na kuwafanyia mema kwa kuwaona bora kuliko sisi wenyewe. Inatupasa kulia pamoja na waliao na kufurahi na wafurahio. Inatupasa kushiriki mateso kwa kuwafariji waumizwao. Yatupasa kuombeana na kuridhika na ale tulipofikia na tulivyonavyo, na tusiwadhulumu wengine au tusiwiwe kitu na mtu yeyote.

 

Mwenendo na nia yetu kwa hiyo ni wa muhimu sana na ni kit kinachoamua na kuona iwapo kama sadaka zetu zitakubalika na Mungu au hapana. Hatuwezi kuchukulia utoji wetu wa sadaka kuwa ni kitu kidogo na kisichohitaji kutilia maanani. Inatupasa kuchukulia hali yetu ya kiroho kwa umakini na uzito mkubwa.

 

Hakuna hata mmoja miongoni mwetu aliye tajiri sana na tunahangaika tuwezavyo ili tuweze kujihudhurisha kwenye Sikukuu, kutoa zaka kama tulivyoamriwa, na kujipatia sadaka. Hatuwezi kupata kiasi kikubwa cha sadaka lakini hii haimaanishi kwamba sadaka zetu zinadharauliwa na kuhesabiwa kuwa si kitu kwa Mungu.

 

Marko 12:41-44 Naye akaketi kulielekea sanduku la hazina, akatazama jinsi mkutano watiavyo mapesa katika sanduku. Matajiri wengi wakatia mengi. 42 Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia senti mbili, kiasi cha nusu pesa. 43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambia, Huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote wanaotia katika sanduku la hazina; 44 maana hao wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi; bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndiyo riziki yake yote pia.

 

Ni myoyo wetu ndiyo Mungu anaouangalia na wala sio utajiri wetu.

Sisi, tukiwa kama sehemu ya mwili wa Kristo ndani ya Kanisa lake Mungu, tunao wajibu wa kuihubiri injili kwa kila kiumbe. Mkakati huu wa kuihubiri injili inagharama. Wengi wetu tunafanya kazi za kujitolea, tukiliachia Kanisa litumie akib yake kulipia zile huduma ambazo sisi wenyewe hatuna ujuzi wa kuzifanya. Ili tuweze kuihubiri injili kwa kila kiumbe, basi ni lazima itafsiriwe kwa lugha zote. Kuna gharama inayoendana na shuhuli hii ya kutafsiri maandishi na machapisho yote ambayo yameandikwa na kuchapishwa na Kanisa kwenye lugha mbalimbali za ulimwengu. Hata hivyo inafurahisha na kutia moyo kuona jinsi ilivyofanyika kwa kiasi kikubwa. Lakini tunapaswa kufanya bidii kubwa ili kukamilisha kazi na wajibu wetu.

 

Wakati tunapotoa sadaka zetu, ndipo tunategemeza na kuwezesha kufnyika kwa sehemu muhimu sana ya kazi ambayo Kanisa limegizwa na kuamriwa kuifanya. Hatutaweza kulichukulia agizo hili kijuujuu na kulipa uzito mwepesi.

 

Mathayo 24:14 Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.

 

Kila mmoja wetu anawajibika kutoa sadaka na kuwafikiria mahitaji ya Kanisa, mahitaji ya familia, na mahitaji yaw engine walio nje ya familia yetu ambayo ni nje ya Mkutano wa kundi la Mungu.

 

Injili itahubiriwa ulimwenguni kote. Maandiko Matakatifu yanasema hivyo, na maandiko hayawezi kutanguka. (Yohana 10:35). Hebu na tufanye kazi sasa wakati tukiwa tunahakikisha kuwa hilo linatimilika. Muda uliobakia i mfupi sasa na kama hatutafanya kazi Mungu atawainua watu wengine waifanye.

 

Ni sehemu ya shindano la mbio tunakimbia (Waebrania 12:1) na Mtume Paulo anasema kwenye 1Wakorintho 9:24-27:

Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate. 25 Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika. 26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa; 27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.

 

Tunakimbia shindano la imani kwa ajili ya thawabun ijayo na tuliyoahidiwa. Nayo ni uzima wa milele kwenye Ufalme wa Mungu. Tunapiga mbio kwa imani ili tuweze kuwa na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu, ambao umetajwa kuwa ni ufufuo mwema. Tunazidi kupiga mbio ili tuweze kufanana na Kristo zaidi na tunapiga mbio hii kwa unyenyekevu mkubwa kwa Mungu na Amri zake kama tulivyopewa na Kristo.

 

Kristo anasema hivi kwenye Ufunuo 3:11-12:

Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. 12 Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya.

 

Basi na tutazitunza sadaka hizi tangu sasa ili kwamba Baba yetu aweze kutubariki, kutusaidia na kutuwezesha tuendelee kufanya kazi kwa mwongozo wa Kristo katika kukamilisha agizo lake. Hebu na tufurahi sasa mbele za Mungu, hapa kwenye Sikukuu hii, mahali alipopachagua kwa kipindi hiki sawasawa na amri zake, na hebu na tufurahi na kusherehekea kwa kuweza kushiriki kipindi hiki pamoja na kwa amani na nia moja.

q