Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[063B]
Ufafanuzi
wa Kitabu cha Esta Sehemu ya II:
Purimu
Katika Siku za Mwisho
(Tolao La 2.0 20090207-20090219)
Sehemu ya II inaweka Ufafanuzi wa Kitabu cha Esta katika Siku za Mwisho na
inaielezea siku ya Purimu katia Siku za Mwisho na jaribio la kuwaangamiza kwa
kuwafutilia mbali Waebrania na matokeo yanayofuatia uamuzi huo.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2009 Wade Cox)
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ufafanuzi
wa Kitabu cha Esta Sehemu ya II:
Purimu
Katika Siku za Mwisho
Katika Sehemu ya
I ya Ufafanuzi kuhusu kitabu cha Esta tuliona maana halisi ya Kitabu cha Esta
na jinsi kinavyolingana kwa Masihi na kwa Kanisa la Mungu likiwa kama bibi
arusi wa \kristo. Ilionyesha
pia nafasi ya Wayahudi kwenye mchakato huu na maana ya Sikukuu ya Purimu. Sasa
tutakwenda kujionea uhusiano wa majaribu au mateso yatakayotokea katika Siku za
Mwisho.
Katika Sehemu ya
I tuliwaona wahusika wa hadithi hii na nyadhifa zao kwa upana zaidi na
ikilinganishwa na mambo ya kiroho. Tulimuona Modekai akimuwakilisha Masihi na
Esta akiliwakilisha Kanisa.
Vashti
anaiwakilisha numba ya kifalme ya Yuda ambayo ilikataa wito na ikaachiliwambali
lakini haikuuawa ili kwamba mfalme awe anabakia akimkumbuka tu. Esta aliitwa na
kuchaguliwa achukue nafasi yake akiwa kama Israeli wa Mungu.
Katika Sehemu ya
I, Sura ya 7 tuliona kwamba towashi wa mfalme aitwaye Harbona, aliamriwa amtundike
Hamani kwenye mti alioutengeneza mwenyewe kwa ajili ya Modekai. Mara tu baada
ya Harbona kumtundika Hamani, ndipo hasira za mfalme zilitulia. Ndipo Modekai
akainuliwa na kuwekwa kwenye cheo cha uangalizi wa Nyumba ya Hamani na akapewa
pete yake ya kiofisi. Hii haiwakilishi tu kuuawa kwa kiongozi wa maadui wa
kimwili wa Israeli na Kanisa bali pia inaonyesha mfano wa jinsi Shetani
atakapoyavua mamlaka yake na kuyakabithi kwa Kristo katika Siku za Mwisho.
Harbona anamuwakilisha Malaika Mkuu kwenye Kiti cha Enzi cha Mungu
atakayemariwa kumfanyia hukumu anayostahili Shetani.
Ili kutuweka sawa
kwa andiko husika mwishoni mwa mchakato huu tunasoma maandiko yafuatayo.
Kumbuka kuwa
waraka uliotumwa wenye ujumbe wa kuwaangamiza Wayahudi ulitumwa kwenye majimbo
yote katika dola nzima uliamuru kuwaua Wayahudi wote kokote waliko kwenye dola
yote.
Esta 8 inasema:
Siku ile mfalme
Ahasuero alimpa malkia Esta nyumba yake Hamani, yule adui ya Wayahudi. Mordekai
naye akahudhuria mbele ya mfalme; kwa maana Esta alikuwa amedhihirisha
alivyomhusu. 2 Basi mfalme akaivua pete yake,
aliyompokonya Hamani, akampa Mordekai. Naye Esta akamweka Mordekai kuwa juu ya
mlango wake Hamani.3 Tena Esta akasema na mfalme mara
ya pili, akaanguka miguuni pake, akamsihi kwa machozi ayaondoe madhara ya
Hamani, Mwagagi, na shauri alilowafanyia Wayahudi. 4 Ndipo
mfalme alipomnyoshea Esta fimbo yake ya dhahabu. Basi Esta akaondoka, akasimama
mbele ya mfalme. 5 Akasema, Mfalme akiona vema, nami
nikiwa nimepata kibali machoni pake, na neno likionekana jema mbele ya mfalme,
nami nikimpendeza machoni pake, iandikwe kuzitangua barua za Hamani bin
Hamedatha, Mwagagi, alizotunga na kuziandika ili kuwaangamiza Wayahudi walioko
katika majimbo yote ya mfalme. 6 Kwa maana niwezeje
kuyaona mabaya yatakayowajia watu wangu? Au niwezeje kuyatazama maangamizo ya
jamaa zangu? 7 Mfalme Ahasuero akawaambia malkia Esta
na Mordekai, Myahudi, kusema, Tazama, nimekwisha kumpa Esta nyumba yake Hamani,
naye mwenyewe wamekwisha kumtundika juu ya mti, kwa sababu aliwatia mikono
Wayahudi. 8 Basi waandikieni Wayahudi pia vyo vyote
mpendavyo, kwa jina la mfalme, mkatie muhuri kwa pete ya mfalme; kwa kuwa
andiko lililoandikwa kwa jina la mfalme na kutiwa muhuri kwa pete ya mfalme
hakuna awezaye kulitangua. 9 Basi, waandishi wa mfalme
wakaitwa pale pale, siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa tatu, ndio mwezi wa
Siwani; na kama vile Mordekai alivyoamuru, Wayahudi wakaandikiwa, pamoja na
maakida na maliwali, na wakuu wa majimbo toka Bara Hindi mpaka Kushi, majimbo
mia na ishirini na saba, kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha
yake; na Wayahudi kwa mwandiko wao na kwa lugha yao. 10 Akaandika
kwa jina la mfalme Ahasuero, na kutia muhuri kwa pete ya mfalme, akazipeleka
barua kwa matarishi, wamepanda farasi, wamepanda wanyama wepesi sana
waliotumika kwa huduma ya mfalme, ndio waliozalishwa katika zizi la mfalme. 11 Katika barua hizo mfalme aliwaruhusu Wayahudi wakusanyike
katika kila mji na kuzisimamia maisha zao, kuangamiza, na kuua, na kulifisha
jeshi lote la watu na la jimbo watakaowaondokea, wao na wadogo wao na wanawake;
na kuyachukua mali yao kuwa nyara; 12 siku moja,
katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero, yaani, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa
kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari. 13 Nakili ya
andiko, ya kupigwa mbiu katika kila jimbo, ilitangazwa kwa mataifa yote, na kwa
Wayahudi, wawe tayari siku ile ile kujilipiza kisasi juu ya adui zao. 14 Matarishi wakaondoka, wamepanda wanyama wepesi sana
waliotumika kwa huduma ya mfalme, huku wakihimizwa na kusukumizwa kwa amri ya
mfalme; kukapigwa mbiu huko Shushani ngomeni. 15 Naye
Mordekai akatoka usoni pa mfalme, amevaa mavazi ya kifalme, ya rangi ya samawi
na nyeupe, mwenye taji kubwa ya dhahabu, na joho ya kitani safi na rangi ya
zambarau. Mji wa Shushani wakapaza sauti, wakashangilia. 16 Ikawa
nuru na furaha na shangwe na heshima kwa Wayahudi. 17 Na
katika kila jimbo, na kila mji, po pote palipowasili amri ya mfalme na mbiu
yake, Wayahudi wakapata furaha na shangwe, karamu na sikukuu. Hata wengi wa
watu wa nchi wakajifanya Wayahudi, kwa kuwa hofu ya Wayahudi imewaangukia.
Mchakato uliopo kwenye sura hii ya 8 ulikuwa ni
kuhukumu sawasawa na jinsi ilivyokusudiwa na Shetani na mfumo au taratibu za
kidunia kama ulivyokusudiwa na Hamani Mhagagi. Kinachoonyeshwa hapa ni kwamba ulimwengu
utahukumiwa sawasawa na kinachotoka kinywani mwake. Na kadri majeshi
yalivyojipanga dhidi ya watakatifu na yakikusudia kuwadhuru wateule na ndipo
amri ilitokea kuwa wanapaswa kuhukumiwa sawasawa na walivyohukumiwa.
Mchakato wa wakati katika Siku za Mwisho ni
sehemu ya ujumbe ulioko kwenye kitabu hiki. Maafa haya yalipangwa yatokee
katika mwezi wa mwisho wa mwaka. Kwenye maandiko yaliyo kwenye Sehemu ya I
tulielezea kwa kulinganisha siku 30 za Maombolezo
ya Musa. Kipindi hiki kimeelezewa kwa kina kwenye jarida la Miaka Thelathini ya Mwisho: Mpambano wa Mwisho
(Na. 219) [The Last Thirty Years: The Final Struggle (No. 219)].
Lakini kumbuka kwamba Waraka wa wokovu kwa Yuda
uliandikwa katika mwezi wa Watatu, siku ya ishirini na tatu. Hii ilikuwa ni
baada ya kupita idi ya Pentekoste. Mfano wake ni kwamba hii ilikuwa ni baada ya
siku ya kutolewa kwa Roho Mtakatifu kwenye Kanisa la Mungu na Kanisa likiwa
limefanya maombi na dua kwa Mungu kwa ajili yao Yuda na kwa taifa la Israeli.
Wale wajumbe waliotumwa wanafananishwa na
manabii wa Mungu na wazee wa Makanisa ya Mungu ambayo yanahudumu kwa njia ya
Machapisho na maandiko sambamba na Maandiko Matakatifu vipindi vyote vya
Maagano yote mawili. Wajumbe hawa wataendelea bila kukoma hadi katika Siku za
Mwisho. Watu hawa na mchakato mzima wa mashahidi wa Injili au Habari Njema ya
Ufalme na Sheria au Torati ya Mungu, na habari yake imeelezewa kwa kina kwenye
jarida la Mashahidi (pamoja na wale Wawili) (Na. 135) [The
Witnesses (including the Two Witnesses (No. 135)].
Kiunabii tunapaswa kujua kwamba ni siku 270
kabla ya Purimu au miaka 270 kabla ya Purimu kwa hesabu ya kulinganisha siku
moja kwa mwaka. Tutarudi tena kwenye jambo hili baadae. Mwenendo au mchakato wa
shahidi unaachwa tangu kipindi hiki kwa ulimwengu wote.
Sura ya 9 inaelezea mpambano huu wa mwisho na
tutajaribu kuuelezea wakati wake mahsusi kwenye mchakato wa Siku za Mwisho
(soma pia jarida la Siku ya Bwana na Siku za Mwisho (Na. 192) [The Day
of the Lord and the Last Days (No. 192)].
Esta 9 inasema:
Hata ulipofika mwezi
wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, siku yake ya kumi na tatu, amri ya
mfalme na mbiu yake ilipowadia kutekelezwa; ambayo siku ile adui za Wayahudi
walitumaini kuwatawala, bali kumebadilika kinyume, hata Wayahudi waliwatawala
wale waliowachukia; 2 siku ile ile Wayahudi
wakakusanyika mijini mwao katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero ili kuwatia
mikono wale watu waliowatakia hasara; wala asiweze mtu kuwazuia, kwa kuwa hofu
yao imewaangukia watu wote. 3 Nao maakida wa majimbo,
na majumbe, na maliwali, na wale waliofanya shughuli ya mfalme, waliwasaidia
Wayahudi; kwa sababu hofu ya Mordekai imewaangukia. 4 Maana
Mordekai alikuwa mkuu nyumbani mwa mfalme, na sifa yake imevuma katika majimbo
yote, kwa kuwa huyo Mordekai amezidi kukuzwa. 5 Basi
Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na machinjo, na maangamizo,
wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia. 6 Hata
huko Shushani ngomeni Wayahudi wakawaua watu mia tano, na kuwaangamiza. 7 Wakawaua na Parshandatha, na Dalfoni, na Aspatha, 8 na Poratha, na Adalia, na Aridatha, 9 na
Parmashta, na Arisai, na Aridai, na Waizatha, 10 wana
kumi wa Hamani bin Hamedatha, adui ya Wayahudi; walakini juu ya nyara
hawakuweka mikono. 11 Siku ile mfalme akaletewa hesabu
ya hao waliouawa huko Shushani ngomeni. 12 Mfalme
akamwambia malkia Esta, Wayahudi wamewaua watu mia tano hapa Shushani ngomeni
na kuwaangamiza, pamoja na wana kumi wa Hamani, je! Wamefanyaje basi katika
majimbo ya mfalme yaliyosalia! Basi, una nini uombalo? Nawe utapewa; ama unayo
haja gani tena? Nayo itatimizwa. 13 Ndipo Esta
aliposema, Mfalme akiona vema, Wayahudi walioko Shushani na wapewe ruhusa
kufanya tena kesho sawasawa na mbiu ya leo, na hao wana kumi wa Hamani
watundikwe juu ya mti ule. 14 Mfalme akaamuru
vifanyike vivyo hivyo, mbiu ikapigwa huko Shushani, wakawatundika wale wana
kumi wa Hamani. 15 Basi Wayahudi wa Shushani
wakakusanyika tena siku ya kumi na nne pia ya mwezi wa Adari, wakawaua watu mia
tatu huko Shushani; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. 16
Nao Wayahudi wengine waliokaa katika majimbo ya mfalme walikusanyika,
wakazishindania maisha zao, wakajipatia raha mbele ya adui zao, wakawaua
waliowachukia, watu sabini na tano elfu; walakini juu ya nyara hawakuweka
mikono. 17 Hii ndiyo siku ya kumi na tatu ya mwezi wa
Adari; na siku ya kumi na nne ya mwezi huo wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya
karamu na furaha. 18 Lakini Wayahudi wa Shushani
walikusanyika siku ya kumi na tatu ya mwezi huo, na siku ya kumi na nne pia; na
siku ya kumi na tano ya mwezi uo huo wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya
karamu na furaha. 19 Kwa sababu hii Wayahudi wa
vijijini, wakaao katika miji isiyo na boma, huishika siku ya kumi na nne ya
mwezi wa Adari, kuwa siku ya furaha na karamu, sikukuu ya kupelekeana zawadi. 20 Basi Mordekai aliyaandika mambo hayo; naye akapeleka
barua kwa Wayahudi wote waliokaa katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero,
waliokuwa karibu na waliokuwa mbali, 21 kuwaonya
wazishike siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, na siku ya kumi na tano yake,
mwaka kwa mwaka, 22 ambazo ni siku Wayahudi
walipojipatia raha mbele ya adui zao, na mwezi uliogeuzwa kwao kuwa furaha
badala ya huzuni, na kuwa sikukuu badala ya kilio; wazifanye siku hizo ziwe za
karamu na furaha, za kupeana zawadi na za kuwapa maskini vipawa. 23 Nao Wayahudi wakakubali kufanya kama walivyoanza, na kama
Mordekai alivyowaandikia; 24 kwa sababu Hamani bin
Hamedatha, Mwagagi, adui ya Wayahudi wote, alikuwa amefanya shauri juu ya
Wayahudi ili kuwaangamiza, akapiga Puri, yaani kura, ili kuwakomesha na
kuwaangamiza pia; 25 bali mfalme alipoarifiwa,
aliamuru kwa barua ya kwamba hilo shauri baya alilolifanya juu ya Wayahudi
limrudie kichwani pake mwenyewe; na ya kwamba yeye na wanawe watundikwe juu ya
mti. 26 Hivyo wakaziita siku hizo Purimu, kwa jina la
Puri. Basi, kwa ajili ya maneno yote ya barua hiyo, na kwa yale waliyoyaona
wenyewe juu ya jambo hilo, na mambo yenyewe yaliyowajia, 27 Wayahudi
wakaagiza na kutadariki juu yao wenyewe, na juu ya wazao wao, na juu ya wote
watakaojiunga nao, isikome, ya kwamba watazishika siku hizo mbili sawasawa na
andiko lile, na kwa majira yake kila mwaka; 28 siku
hizo zikumbukwe na kushikwa kwa vizazi vyote na kila jamaa, katika kila jimbo
na kila mji; wala siku hizo za Purimu zisikome katikati ya Wayahudi, wala
kumbukumbu lake lisiishe kwa wazao wao. 29 Ndipo
malkia Esta, binti Abihaili, pamoja na Mordekai Myahudi, alipoandika kwa
mamlaka yote kuithibitisha barua hii ya pili ya Purimu. 30 Akapeleka
barua kwa Wayahudi wote katika majimbo yote mia na ishirini na saba ya ufalme
wake Ahasuero, maneno ya amani na kweli, 31 ili
kuzithibitisha siku hizo za Purimu kwa majira yake, kama Mordekai Myahudi na
malkia Esta walivyoamuru, na kama walivyojiagizia juu yao wenyewe, na juu ya
wazao wao, kwa habari ya kufunga na kilio. 32 Amri
yake Esta ikayathibitisha mambo hayo ya Purimu; ikaandikwa katika kitabu.
Kumbuka kuwa
matukio yaliyo kwenye Sura ya 9 (aya za 7 na 14) yanaonyesha kurudiwa kwa
mauaji ya watoto kumi wa Hamani. Mtafaruku huu unaonyesha hali ya mtafaruku wa
tukio halisi na tukio kinzanifu la mauaji ya siku ya Purimu na linaonyesha
kwenye matukio yatakayotokea katika nyakati za mwisho pamoja na matukio
yatakinzana fananisho repeat of the killing of the ten soayotanguli au
yatakayotokea kwanza.
[aya za 10,15,16]
zinarudia maneno haya: “walakini juu ya nyara hawakuweka mikono” (soma jarida la Ndamba wa Dhahabu (Na. 222) [The Golden Calf (No.
222)].
Kuingizwa na mahali pa Purimu kwenye Vita vya
Mwisho
Tumejua idadi ya
Siku za Maombolezo ya Musa kuwa ni kama miaka thelathini ya mwisho kwa hesabu
ya siku moja sawa na mwaka kwenye Yubile ya mwisho ya miaka elfu sita ya
Utawala wa Shetani. Hiyo ni Yubile ya 120 tangu uumbaji tangu kufukuzwa kwa
wanadamu na kufungwa kwa bustani ya Edeni. Kipindi hiki ni cha Nyakati za
Mwisho za zama na utimilifu wa Mataifa au Nyakati za utawala wa Mataifa ya
dunia. Nyakati hizi ziliishia katikati ya miaka ya 1996-7. Mwaka huu
unachukuliwa kuwa ni mwisho wa Miaka Thelathini wa Maombolezo ya Haruni.
Mwaka 1967
ulikuwa ni mwaka ambao ulihitimisha mapambano na mataifa yaliyo nje ya Nchi ya
Ahadi na kuuteka mji wa Yerusalemu kwa mapambano au Vita ya Siku Sita.
Kumbuka kwamba
Miriamu alikufa baada ya kuweka matuo yao huko Meriba katika mwaka huu Mwezi wa
Kwanza. Waedomu walikataa kuwaruhusu Israeli kupita na wakawatokea kwa vita
(Hesabu 20:1).
Kipindi hiki
kilienda hadi miaka 2520 kutoka Vita ya Karkemishi ya kukomesha mauaji ya
kinyama ya Vita Kuu ya I ya Dunia mwaka 1916 na kutekwa kwa miji ya Beersheba
na Yerusalem mwaka 1917. 1916 ulianzisha kipindi cha mwisho wa miaka themanini
cha utimilifu wa Mataifa (soma pia
jarida la Kuanguka kwa Misri: Unabii wa Mkono
Uliovunjika wa Farao (Na. 36) [The Fall of Egypt: The Prophecy of Pharaoh’s
Broken Arms (No. 36)].
Mnamo mwaka 1967
Yerusalem ulitwaliwa au kukombolewa. Mwaka 1996-7 ulishuhudia ukomo wa Nyakati
Saba walizopewa Mataifa tangu kipindi cha Babeli, kama tulivyokiona kwenye
Danieli Sura ya 2. Mwendelezo wa Misheni ya Kanisa ulianzia kipindi hiki. Mnamo
mwaka 1987 Hekalu liliingia hukumi na lilipimwa au kujaribiwa. Mchakato mzima
kuhusu jambo hili umeelezewa kwa kina kwenye jarida la Kupimwa kwa Hekalu (Na. 137) [Measuring the Temple
(No. 137)].
Kanisa lilijiunda
tena kwa awamu ya mwisho ya Makanisa ya Mungu katika mwaka wa Tatu wa Mzunguko
wa miaka ya Sabato mnamo mwaka 1994.
The end of
the Time of the Nations or the Time of the Gentiles was in 1996/7.
Mwaka 1997 kilianza
kipindi cha Miaka Thelathini ya mwisho kabla ya kuanza kwa kipindi cha utawala
wa millennia katika Nchi Takatifu. Kipindi hiki kwa hiyo kinafananishwa na
mwezi wa Adari au mwezi wa mwisho wa mwaka cha kabla ya kuanza kwa mamlaka
mapya. Katika miaka hii ndipo tunatarajia kuiona Purimu ya mwisho.
Mwaka 1998 kulianzishwa
Marejesho mapya ya Msisitizo wa Torati yake Mungu na ndio mwaka iliposomwa
kwenye mwaka wa Sabato na ilisomwa tena kwa mara ya pili kwenye Mwaka wa Sabato
wa mwaka 2005.
Purimu tunayoiona
hapa ilipasa ianze tangu siku ya 13 ya mwezi na kuendelea hadi siku ya 14 na 15
ya wa Maombolezo ya Musa.
Tangu mwaka 1997
wa hwsabu ya mwaka kwa siku tunafikilia hadi kwenye miaka ya 2009, 2010 na
2011.
Tungetarajia
kuona mwisho wa kipindi hicho, tangu kukoma0kwa vita ya kuangamiza na
kutokomeza watu ya mwaka 1967, kipindi cha maandalizi makubwa ya maadui wa
Watakatifu wake Aliye Juu. Hii inamaanisha kwanza kabisa Makanisa ya Mungu
ambao ni Israeli wa kiroho sambamba na Wayahudi kwa ande zote mbili, yaani Yuda
na Israeli.
Kipindi hiki
kitakuwa na matukio mfululizo nay a kushangaza ya kimikakati ya kuwaangamiza
watu na kuzitokomeza kabisa nguvu za Watu Watakatifu sambamba na kuhujumu au
kudhoofisha uchumi wao na uwezo wao wa kawaida.
Nguvu za majeshi
ya Shetani zimekusudiwa kusababisha maangamizi ya kiuchumi kwa watu wa jamii ya
Kiebrania na mara tu mkakati huu utakapoanza kutekelezwa, kutazingatiwa kufikwa
lengo la kuwaangamiza kabisa kimwili. Jambo hili limeonyeshwa kimfano kwenye
mateso yaliyooanndikwa kwenye Kitasa cha Tano kwenye kitabu cha Ufunuo.
Tungetarajia jaribio
la mwisho kwenye maangamizi haya kutokea na kutekelezwa tangu siku ya 13 hadi
15 Adari au tangu mwaka 2009 hadi 2011 ikiwa ni siku ya 13 hadi 15 za mwezi wa
Adari au mwezi wa Maombolezo ya Musa ya Siku za Mwisho.
Hatima ya Shetani ni muhimu. Marejesho
mapya ya mambo yote ya Eliya na shahidi mwingine yanakuja sambamba na
kuanzishwa kwa Yerusalemu. Kufuatia na siku za Mashahidi Wawili tunatarajia
kuingia na kupewa nafasi kwa Modekai-Masihi akiwa kama Halifa wa Ufalme wa hii
dunia baada ya hukumu ya wale Mashahidi Wawili.
Jaribio kubwa la
mauaji ya halaiki ya kuwaangamiza Wayahudi na katika Israeli na kwenye Vita Kuu
ya II ya Dunia. “Suluhu ya Mwisho” lilipangwa huko Ulaya na kambi
zilizokusudiwa na kulengwa kwanza zilikuwa zimejengwa huko Ujerumani katika mji
wa Hamburg mwaka 1932 na Watrinitariani au waamini Utatu. Madhehebu haya yote
mawili yaani Walutheri na Wakatoliki walihusika na jambo hili lililojulikana
kama “Suluhisho la Mwisho.” Mwisho wake watatoa mwito ili kuwapeleka wahalifu
wa kivita kwenye nchi za Marekani, Australia na Amerika Kusini. Baadhi ya wazee
hawa wanakanusha au kutokea kwa mauaji haya ya kuangamiza wanadamu hata sasa.
Mapapa waliwasaidia kwanza kwa kutoa msaada wa dhahiri na wa wazi kabisa na
kisha wakafumbia macho na kunyamazia.
Ni kama kasisi wa
zamani na Mjesuit aitwaye Malachi Martin amebadilika, mauaji ya wengi yalitajwa
huko St Peters katika karne ya 20 kwa ajili ya kumtawaza na kumpa Kiti cha enzi
Shetani kumfanya kuwa ni mungu. Kasisi huyu aliuawa kabla hajaandika makala ya
pili ya kuliweka wazi tukio hili. Yaliyoandikwa kwenye Isaya 14 na Ezekieli 28
yanarudiwa.
Kwenye mateso ya
Nuremburg kiongozi moja Manazi alisema, wakati alipokuwa anahukumiwa kifo, “Kwa
Hakika, Hii ni Purimu”.
Kwa kweli
majaribio ya kuwaangamiza Wayahudi yalifanywa kwa milolongo endelevu kama
kunavyoonekana kuwa kulikuwepo na vita dhidi ya Uingereza na Anglo-Saxons ambao
wanafanya sehemu kubwa ya watu hawa. Mnamo mwaka 1739 Waingereza walipigana
vita vyao na Uhispania na iliyokuwa Dola Takatifu ya Roma ilishindwa vita
kwenye nchi ya Uturuki. Wazungu wa Ulaya, Warusi na Waturuki walitia saini
makubaliano katika mwaka huu ili kukomesha uhasama. Pia katika mwaka huu
Wayahudi walihusuriwa maisha yao kwa kuhukumiwa vifungo vya maisha huko Lisbon,
nchini Ureno. Maaribio ya kuwaangamiza Waisraeli yamekuwa na mtafaruku mkubwa
kwa namna endelevu. Mwaka 1739 ulikuwa ni mwaka wa 270 tangia mwaka 2009.
Kitabu cha Esta
hakikusema kwamba majaribio ya kuwaua Wayahudi yatakoma. Bali kinasema kwamba
majatibio haya yatashindwa na wale wanaofanya hila hizi watakufa.
Chokocho za Mauaji ya Kimbari
Azimio la Balfour
lilitolewa na Waziri Mkuu Balfour baada kuwashindwa Waturuki huko Beersheba na
Yerusalem mwaka 1917. Linaanzisha dhana na haki na msaada wa Waingereza kwenye
Ardhi ya Wayahudi. Tangu wakati ule na kuendelea mauaji ya kuwaangamiza
Wayahudi yamekuwa yakipangwa na kufanyika sehemu zote mbili, yaani huko Ulaya
na katika Mashariki ya Kati.
Watoto kumi wa
kiume wa Hamani ni sawasawa na zile embe Kumi au wafalme wa Dola ya Mnyama na
vile vidole Kumi vya chuma na udongo za Dola ya Mwisho ya Roma iliyoonyeshwa
kwenye Danieli 2.
Kumbuka kwamba
Kitabu cha Esta knasema kuwa kwene Mji mkuu huko Shushani mauaji yalifanyika
siku ya 14 ya mwezi wa Adar pia. Mauaji kwene miji mingine ya Dola hii
yatatokea na yatachukua muda mrefu na yatakuwa mabaya sana kuliko mengine yote
yaliyotokea nyuma. Tangu vita vya mwisho yatupasa tutarajie migogoro hii kwisha
kwa zaidi ya miaka miwili kuanzia Ulaya hadi Iran.
Jaribio
lililofanywa huko nyuma kuwaangamiza Waingereza, Waceltiki na wa Anglo-Saxon
yamekuwa yalifanywa na Watrinitariani wa Ulaya kwa karne nyingi sasa.
Hawajafanikiwa kabisa lakini watafanya jaribio moja linguine tena la mwisho
katika miaka michache ijayo.
Hujuma na
maangamizi ya kiuchumi ya Marekani na Muungano wa Nchi za Jumuia ya Madola
inayoongozwa na Uingereza zitachukuliwa na watumishi hawa wa Shetani katika
sehemu zote mbili, yaani huko Ulaya na Mashariki ya Kati. Mipango yao na zana
au silaha zao za maangamizi zitatumika dhidi yao na watawanyonga kwenye miti wa
kuwanyongea wao wenyewe kama alivyoangikwa Hamani na watoto wake kumi
walivyoangikwa. Nyayo zilizochangantika chuma na udongo zinawakilisha kukangana
malengo na makusudio na watu na imani kwenye dola hii ya mwisho. Kristo
ataiangamiza na kukomesha uwepo wake na kuitwaa Mashariki ya Kati na
Yerusalemu.
Kwa sasa Iran,
inasaidiwa na washirika wake ambao ni Wasyrin, Walebanon na Wapalestina,
wanatoa mwito wa kuwaangamiza kwa mauaji makubwa Wayahudi. Wanapiga makelele ya
“Hamas, Hamas, Wayahudi wachomwe moto wa gesi”. Harakati za Hamas ni matendo
yanayofanywa kwa makusudi au ugaidi ambao unaenezwa kwa taarifa za vyombo vya
habati kwenye ulimwengu weote wa Kiislamu na nchi za Magharibi na wanajumuisha
mambo ya bandia na yakutunga dhidi ya Waisraeli. Mambo yanayofanyia huko Gaza
na kwa Wapalestina yamepangwa kwa makusudi ili kuhalalisha mauaji ya
kuwaangamiza Israeli. Hakuna taifa hapa duniani linaloweza kuyavumilia
makombora yanayopigwa kila mara yakiwashambulia watu wake kama yanayorushwa na
Hamas kuishambulia Israeli. Ni sera ya chuki ambayo inafumbiwa macho na Umoja
wa Mataifa huku ukijua vema sana kuwa ni uchokozi na uhalifu dhidi ya sheria na
sera za Umoja wa Mataifa na Mkataba wa Geneva. Misri inatumiwa kama bomba au njia
ya kuyaleta makombora ndani ya Gaza.
Kile
kinachofanywa na vyombo vya habari ni kufikisha lengo la kuwagawa Israeli
machoni pa ulimwengu na kuwafanya israeli wawe chini ya mashambulizi ya
kihasama na kwa namna ya kutengwa kiasi cha kwamba sasa itachagua wanasiasa
sahihi sana watakaopigana dhidi ya uwepo wa taifa la Israeli.
Vyombo vya habari
na Umojja wa Mataifa vimehakikisha kwamba falsafa ya uiana dini ya ugaidi wa
Kiislamu imejikita na kuwa imara katika nchi za Kiislamu kutoka Afrika hadi
Indonesia. Vyombo vya -habari vimewaimarisha wapinga falsafa ya Kisemitiki na
kambi za chuki za kidini za Wazungu wa Ulaya.
Israeli ndiyo
nchi pekee duniani ambayo haikuwa na uchumi kama kigezo chake cha kwanza cha
kisiasa katika kipindi cha miezi michache iliyopita kabla ya Pasaka ya mwaka
2009.
Waislamu hawasomi
Biblia na waamini Utatu au Watrinitariani nao pia hawaisomi Biblia. Hawaisomi
kwa kuwa haifaidishi wala kuunga mkono mikaka ti yao. Magaidi wa kidini
wanasutwa kwa yale yaliyoandikwa ndani yake.
Neno lake Mungu
Aliyehai liko wazi sana. Ataruhusu Israeli washughulikiwe nah ii itafanywa au
kuhusisha mataifa yaliyotoka kwenye mchanganyiko wa mataifa hayo. Atawaacha
watokomezwe na kuuawa kwa upanga pamoja na kusumbuliwa na magonjwa ya tauni na
njaa lakini hawataashiwa waangamie kabisa.
Kila taifa
linaloshirikiana au kujiunga na wahafidhina hawa wenye chuki wanaotoa wito au
kujaribu kufanya maangamizi makubwa ya kuwahilikisha Israeli watauawa kwa
upanga. Hii itajumuisha viongozi wa imani ile ya kidini.
Mashariki ya Kati
haitashinda na watajilelea madhara na ungamivu wao wenyewe. Haijalishi ni wapi
ilipangwa na haijalishi ni wapi silaha hizo ya vita zimewekwa kwa mkakati wa
kuwaangamiza na kuwatokomeza watu wa Mungu, wale wanaopanga mkakati huu
watauawa wenyewe kwa kutumia silaha zao wenyewe za mauaji ya kimbari, hata
katika nchi za Uingereza na Marekani kwenyewe.
Tumeelezea kuhusu
kuenea na kuongezeka kwa Israeli kwa mujibu wa unabii, na kuingizwa kwa taifa
ndani yake, kwa kiasi fulani kwenye majarida ya Miaka Thelathini ya Mwisho: Mpambano Mkuu
(Na. 219) na Vita vya Hamon-Gogu (Na. 294) [The Last
Thirty Years: the Final Struggle (No. 219) and War of Hamon-Gog (No. 294)].
Majarida haya yamekuwa ni mwongozo na yanaonyesha chanzo cha Vita Vya
Mwisho. Vita hivi vimetabiriwa kwenye Maandiko Matakatifu na Kristo alisema
kuwa Maandiko hayawezi kutanguka (Yohana 10:35). Mungu amelitoa neno lake kwa
kupitia manabii na mambo haya yatatimilika.
Swali pekee
tulilobakiwanalo sasa ni kwamba kipindi mujarabu kinachongojewa cha ku kumuo
Eliya na mashahidi wenyine hapa duniani? (Soma jaridarida la Mashahidi (pamoja na wale Mashidi Wawili (Na. 135) [The Witnesses
(including the Two Witnesses (No. 135). Je, mwanzo wa mauaji ya
kinyama ya Purimu au ni mwisho? Ratiba hii imetolewa katika mwezi wa mwisho wa
Adari kabla ya Zama Mpya ya utawala wa millennia, ambao ni Mwaka Mpya wa 2009 au
je, itakuwa katika Mwaka Mpya wa 2012? Muundo wa mchakato wa matukio haya umeelezewa
kwa kina kwenye majarida ya Ujio
wa Masihi Sehemu ya 1 (Na. 210A) na Yubile ya Dhahabu na Milenia (Na. 300) [The Advent of the
Messiah Part I (No. 210A) and The Golden Jubilee and the
Millennium (No. 300)].
Kuanza
huduma kwa Mashahidi Wawili kuna maana na ashirio la moja kwa moja la
kujulikana ni lini Masihi atarejea. Ni matukio yanayotegemeana na Maandiko
hayawezi kutanguka. Masihi atarudi ili kuja kuwaokoa wale wanaomngojea kwa hamu.
Kwa
hiyo, kama Mashahidi hawa hayakuanza kazi yao hadi mwaka 2012 au hata pengine
baadae, basi hatuwezi kumtarajia Masihi hadi mwaka 2015 au hata bada ya hapo,
kutegemea ni lini Mashahidi hawa wataanza kazi yao huko Yerusalemu. Tunajua
kuwa Masihi ataingilia kati kwa kukifupisha kipindi hiki cha utawala wa
Shetani. Utawale wake utaishia kwenye Yubile ya 120 mnao mwaka 2027 kwa tukio
lolote. Kwahiyo, Masihi atarejea na kuanzisha utawala wake utakaodumu kwa
millennia huko Yerusalemu kabla ya mwaka 2027. Kutokana na mfano wa kuzingirwa
kwa Yeriko kungeweza kutarajia siku saba za misho za mzee wa siku zianze tangu
angalau mwaka 2019 au mapema kidogo (soma jarida la Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142) [The
Fall of Jericho (No. 142)].
Mashahidi
hawa kwa hiyo hawakuje mapema kabla ya mwaka 2015. Kristo atawashughulikia na
kuweka utaratibu mpya kwenye Nchi Takatifu kwa kutumia matetemeko ya ardhi na
kuujenga upya.
Kwa
hiyo. Kristo atawaleta maadui watakaouchukia utawala na imani ya kidini ya
duniani chini huko Har-magedon na kuwaangamiza, kama ilivyoatabiriwa kwenye
Maandiko Matakatifu. Hii itatokea hivyo kwa kuwa dunia, hata pamoja na miujiza
mingi iliyoshuhudiwa, hawakutubu. Wengi wa hawa wanaodai kuwa ni Wakristo leo watamtangaza
Masihi kuwa ni Mpingakristo kwa kuwa, yeye kama walivyo Mashahidi wengine
waliotangulia kabla yake, atakuja kuzisisitiza na kuzirejesha Amri au Torati ya
Mungu. Mpingakristo wa kweli atakuja kabla yake, na atakuja kwa mwonekano wa
kiongozi mwenye kuheshimika na kuaminika kidini, kwa watu hawa hawa. Kristo
atamuua na nabii wake wa uwongo wakati atakaporudi. Kwa hiyo, yatubidi kudhania
kwamba viongozi hawa mashuhuri wa dini hii potofu nay a uwongo watafanya kazi
au huduma zao kipindi kimoja sambamba na Mashahidi hawa wawili. Tunaweza kudhania
pia kwamba ni lazima Mpingakristo ataanza kutawala pamoja na huyu nabii wa
uwongo wakati wowote tangia mwaka 2012, na kuendelea hadi mwishoni mwa mwaka
2019. Huenda kwa sasa yeye amekwishaanza kwa kuonekana ni mmojawapo kwa kutumia
harakati za kuuonga ulimwengu wa kidini – akiwa kama nabii wa uwongo
anayeonekana kuwa ni kiongozi wa kidini.
Tunweza
kuhitimisha kwamba kutokana na utaratibu wa Yubile kama ulivyoonekana kwenye
historian a kwenye Biblia na – kukataa utaratibu mpotofu wa marabi wa zama ya
baada ya Hekalu ujulikanao kama wa uahirisho wa kila mwaka wa 49 unaotokana na
hesabu za Wababeloni walioamua uwepo wa miaka mirefu na mifupi – iliyojumuishwa
na hesabu za majira ya Purimu na Mwezi wa Mwisho wa Miaka ya mzunguko wa Yubile
na mfano wa Ishara ya Yona na cha Kanisa kuwa jangwani, Mashahidi hawa walipaswa
wawe wamekuja tangia wakati wowote kuazia mwaka 2009 hadi 2015, na Masihi
afuatie tangu hapo wakati wowote tangu miaka hii ya 2012 hadi 2019.
Matukio
haya yote ni kutokana na mujibu wa Mpango na Amri ya Mungu (soma majarida ya Ishara
ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13); Kubadilishwa kwa Kalenda
ya Mungu Katika Yudea (Na. 195B) [The Sign of Jonah and the History of the
Reconstruction of the Temple (No. 13); Distortion of God’s Calendar in
Judah (No. 195B)].
Kitu pekee
tunachoweza kuwa na uhakika nacho ni kwamba majeshi ya Shetani yatashindwa na
kuangamizwa kote kote, yaani katika Asia na huko Mashariki ya Kati na hata yale
ya Waamarekani na kwenye imani yake ya kidini huko Ulaya. Makao yake Makuu
yaliyoko huko Ulaya yataharibiwa na kuangamizwa yote. Mkakati huu wa
kuwaangamiz na kuwatokomeza Israeli hautaruhusiwa kuufanikisha kwa kuwa Modekai
ambaye ni Kristo leo ameimaliza kazi yake na awamu au kipengele cha mwisho
kwenye maombi ya Esta nay a wateule kinakamilika hivi sasa.
Kristo
atatawala kama Kaimu wa Ufalme wa Mungu hapa Duniani. Mungu anaamua kile
kinachotakiwa kifanyike kwa Sheria na Torati yake. Zaka za Mungu zinapaswa zikusanywe
katika nchi na kwenye maeneo ya pwani pamoja na maongeo yake yote.
Esta 10
Basi mfalme Ahasuero alitoza kodi katika nchi
na katika visiwa vya bahari. 2 Na matendo yake yote
yenye nguvu na ya ushujaa, na habari zote za ukuu wake Mordekai ambao alipewa
na mfalme, hazikuandikwa katika kitabu-cha-taarifa cha wafalme wa Umedi na
Uajemi? 3 Kwa maana Mordekai Myahudi akawa wa pili
wake mfalme Ahasuero, na mkuu wa Wayahudi, amependeza mbele ya jamii ya ndugu
zake; ambaye aliwatafuta watu wake wema, na kuiangalia hali njema ya wazao wao
wote.
Kanisa
litatawala na Kristo. Kazi za Kanisa na kuanza kwa kipindi cha utawala wa
millennia kutajumuishwa pamoja. Masihi wa uzao wa Yuda na wa Daudi wa Bethelehem
ya Efrata atatulisha sisi sote na atakuwa ni Mfalme wa Amani.
Ni kwa
ufanisi kiasi gani tunavyofanya kazi yetu sasa ndivyo itaamua jinsi tunavyoishi.
Na sasa
tutaanza kushughulika kuandika majarida ya Vita Kuu ya III ya Dunia: Sehemu
ya I Dola ya Mnyama (Na. 299A) na Vita Kuu
ya III ya Dunia Sehemu ya II: Mwanamke Kahaba na Mnyama (Na. 299B) [World War
III: Part I The Empire of the Beast (No. 299A) and WWIII Part II: The Whore and the
Beast (No. 299B]).
q