Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[076D]

 

 

 

 

Madhara Yaliyoyakumba Makanisa ya Mungu Katika Karne ya 20 Kuhusu Fundisho la Asili ya Mungu

 

(Toleo La 1.0 20110312-20110312)

 

Kwenye jarida hili tutaainisha baadhi ya makosa mkubwa kwenye Makanisa ya Mungu yaliyoingia katika karne ya 20 pamoja na imani ya Kiditheism ya Herbert Armstrong.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hatimiliki ©  2011 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Madhara Yaliyoyakumba Makanisa ya Mungu Katika Karne ya 20 Kuhusu Fundisho la Asili ya Mungu


 

Tuliyaeleze makosa ya Herbert Armstrong kwenye jarida la Imani ya Kiditheism (Na. 76B).

 

Kosa hili la Uditheism limeelezewa kwa kina kwenye kile kinachoonekana kuwa ni hata kama nj kufuru kubwa sana kwa upande wa mtumishi wa zamani wa lililokuwa kanisa la WCG na ambaye alikuwa ni muumini mwaminifu wa Herbert Armstrong, lililoonekana sana kuwa ni sehemu ya ibada ya sanamu. Sambamba na makaribisho ya maelekezo ya uwongo na sababu za uwongo, mtumishi huyu pia alidai kwa wazi sana kwamba Herbert Armstrong alivuviwa na Mungu kwenye muono wake na hususan kwenye suala hili la Asili ya Mungu. Alipinga kwamba kwa kiasi fulani na mabashiri ya Armstrong inamaana kwamba mtu anamchukia Armstrong. Ni suala la kufikiri tu kwamba kutokubaliana na nafasi ya kitu chochote hakumaanishi kwamba mtu anamchukia mtu anayefanya makosa. Ka kweli, huu ni msimamo wa Kibiblia au makatazo kwa wateule wote na ulitolewa kwa Waberoya walioyatafiti Maandiko Matakatifu kila siku ili kuona kama kilichosemwa kilikuwa ndivto kilivyo.

aliufuata mtazamo wa kaaida wa Armstrong kwamba Mungu Baba hakua anajidhihirisha kwenye Agano la Kale kwa mtazamo kwamba Amri ya Kwanza yaimtaji Mungu Baba bali kwa Yesu Kristo. Kwa hiyo, usemi wa kwamba “Usiwe na miungu mingine ila Mimi” unamaanisha kwamba usiwe na mingu mingine ila Yesu Kristo.

Hakuna yeyote miongoni mwa maafisa wa CCG aliyelielezea WCG kwamba wamelijadili jambo hili na alisikia kufuru hii ikitamkwa kwenye kanisa la WCG au kwenye makanisa yaliyochipuka hapo kabla yake. Baadhi ya fafanuzi zao zimeorodheshwa hapo chini.


sasa inaweza kuwa kwamba mwamini utatu au Mtrinitarian anaweza kudai kwamba amri hii inamlenga Baba, Mwana na Roho Mtakatifu wakiwa kama mkusanyiko wa Utatu. Lakini hatujawahi kusikia kabisa hata Mtrinitarian akidai kufuru kama hiyo.

 

Hii ngito misingi ya madai ya mhubiri wa zamani wa WCG. Mtu huyu hana kanisa na hivyo anaweka sawa na kufundisha msimamo wake pasipo mamlaka yoyote ya kimpangilio. Jambo hili linahitaji kulielezea kama upanuzi mzuri wa Uditheism wa Armstrong nan i uzushi mkubwa sana.

 

Mtunzi: Frank W. Nelte


tarehe: Machi 1994


MUNGU KENYE AGANO LA KALE NA UELEWA WA WAYAHUDI


“Sasa hebu na tutazame kwenye Kutoka sura ya 20.


5) Kumbuka kuwa Kutoka 20 kwa kweli inasema hivi:


Mungu akanena maneno haya yote akasema, Mimi ni Bwana, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. Usiwe na miungu mingine ila mimi. (Kutoka 20:1-3)


A) Ni MANI aliyekuwa anayanena maneno hayo? Jibu lake ni kwamba YESU KRISTO!


B) Ni kwa namna GANI basi Kristo alijitambisha mwenyewe kwa Waisraeli? Jibu ni kama kwamba "YHWH Elohim wenu aliyewaleta Israeli mtoke kutoka Misri".

 

UTAMBULISHO HUU NI WA MUHIMU SANA!


C) KWANINI utambulisho huu imetuama kwenye amri 10 za Mungu? Tutaona zababu ya jambo hili kwa kipindi kifupi.


D) Ni NINI kwa kweli kinacholengwa au kukusudiwa na andiko la Kutoka 20:3? ... "Usiwe na miungu mingine ILA MIMI"? ni NANI anayesema maneno haya?


je, ni Yesu Kristo ndite Msemaji wa aya hizi, akisema: ‘usiwe na miungu mingine ila Mungu Baba’?

HAPANA, hicho sicho alichosema! Kristo aliwaambia israeli ‘mbele YANGU’!


Tunaweza kuishikilia tafsiri ya wazi ya Kutoka 20:3? Israeli hawakujua kwamba kulikuwa na ‘Mungu Baba’.

 

Alikuwa hajafunuliwa kwao na Kristo. Yesu Kristo Mwenyewe alikuwa anashughulika na taifa la Israeli, na aliwaambia wasiwe na miungu mingine ila yeye, Yesu Kristo.


Aliamua kujidhihirisha kwao kama ‘YHWH, Elohim wako’ aliyewatoa kutoka nchi ya Misri.


E) Je, Kristo alikuwa anajiweka mwenyewe mbele za Mungu Baba kwa kuwaambia Israeli wamwabudu yeye, Yesu Kristo?


HAPANA, sivyo kabisa! Mungu Baba na Yesu Kristo waliamua na kukubaliana kwamba Kristo ndye awe wa kufanya uumbaji wote;- Kristo ndiye angekuwa wa kushughulika na wanadamu hadi mpango mzima wote wa wokovu utakapokamilika;

- Kristo alijidhihirisha mwenyewe kwa Waisraeli;

- Kristo kwa mapema sana kabla ya ujio wake wa kwanza, angekuwa na uwepo wa Baba uliofichwa na Baba katika Israeli kwa ujumla;

- Kwenye Agano la Kale, nyakati za Kristo zingedhihirika tu kwa wateule wale wale tu wachache waliochaguliwa, kwa sababu azijuazo Mungu mwenyewe;

- Ni kwa ujio wake huu tu ndipo Kristo angeudhihirisha uwepo wa Mungu Baba kwa wanadamu;...”


Madai ya nyingeza yanatuama kwenye mikururu ya matukio ya uwongo ya sababu za uwongo na madai ya uwongo kwamba Mungu Baba hakufunuliwa kwenye Agano la Kale. Kumbuka kwamba fafanuzi zilizotiliwa chumvi ni kwamba kulikuwa na mjadala na Kristo alikubali kufanya uumbaji wote na kwamba ‘alishughulika na wanadamu hadi pale mpango wote mzima wa Wokovu ulikamilika.”

 

Kisha madai ya uwongo yalifanywa kwamba Kristo alifanya uwepo wa Baba ufichwe na usijulikane na Waisraeli kwa ujumla. Aliudhihirisha uwepo wa Baba kwa wateule wachache tu. Sasa ilikuwa ni kwa kutokana na uwongo huu wa teolojia potofu na ya uwongo ya Armstrong fundisho hili lilijengwa na lilikuwa ni kinyume na yanavyosema maandiko mengi kadhaa kwenye Agano la Kale na nukuu za Agano jipya zilizotoholewa kama rejea kutoka kwenye Agano la Kale. 

 

Madai meingine yanayofuatia ya uwongo ni yale yanayodai kwamba elohim ni wa “uwingi wenye muunganiko” na neno linalotumika linaonyesha kumhusu Yesu Kristo peke yake. Ukweli ni kwamba ni neno la uwingi. Hakuna kitu kama hicho kisemwacho kuwa ni uwingi jumuisho wala neno kama hilo isipokuwa ni kwamba neno elohim linataja washiriki wa daraja fulani. Wakati linapotumika na kiambishi cha kama Ha Elohim, kama Elohim Mwenyewe, inaaminika kuwa inamtaja Baba. Kuna idadi kadhaa ya maneno kwenye Agano la Kale yanayotumika kwa ajili ya Mungu kwamba yanamtaja Baba peke yake kama Mungu Mmoja wa Kweli na majina yanaonyesha tofauti iliyopo kati ya Mungu na elohim ambao ni wana wa Mungu. 

 

Baba ndiye muumbaji na anajulikana kwenye Agano la Kale kwa maeneo mengi sana. Kushindwa kuyajua majina ya Mungu walikokuwanako kanisa la WCG na tofauti iliyokuwepo kati ya Baba na wana wa Mungu ambao ni elohim ni kosa au tatizo kubwa sana kwenye teolojia na upotoshaji wa maelezo yao kuhusu Mpango wa Mungu na kuyaelewa maagano ya Kale na Jipya. Ilikuwa ni kwa sababu hii ndipo hawakuweza kumshawishi mtu yeyote kuwaami kutoka jamii ya Kiislamu, au mtu yeyote bali ni msaada mkubwa kutoka kwa wa SDA na vikundi vingine vya Makanisa ya Mungu na wachache sana kutoka kwenye dini ya Kiyahudi.

 

Dalili za makosa haya ni mafundisho mapotofu na mtazamo huu haukuwa umesikika kamwe kabisa yakitangazwa kwa wazi sana na kimakosa kabisa kama ilivyokuwa kwenye huduma ya WCG au makanisa yaliyochipuka kwenye kanisa hilo ya huko Australia au kutangazwa kutoka Marekani. Waandishi wengine wa jarida la Uditheism (Na 076B) waliulizwa kama waliwahi kusikia mafundisho haya mapotofu yakifundishwa kwenye kanisa la WCG au kwenye makanisa haya yaliyochipuka kutoka kwenye kanisa hilo kongwe. 

 

Mmoja wa Makodineta wa CCG nchini Marekani aliulizwa kuhusu jambo hili. Alizaliwa kwenye kanisa la WCG, na akahudhuria mafunzo kwenye chuo kilichojulikana kama Ambassador College, na akakitangaza chuo hicho kwenye jimbo la AC na kukipeleka huko nchini Jordan. Mtazamo wake ulikuwa ni kama ifuatavyo:

 

“Baada ya kuyasoma baadhi ya maandiko yake, kwa kweli sikuweza kushangazwa sana kama kitu kama hicho kinatokea kwa mchungaji wake wa zamani wa kanisa la WCG wakati teolojia yake ilipotuama kwenye ukweli wa kwamba kitu chochote anachokisema Herbert Armstrong hakimfanyi yeye kumuona mzee wa kanisa afananishe na kile kinachosemwa na maandiko matakatifu kuhusu masuala yahusuyo asili ya Mungu na ya watoto wake wakati Armstrong alipokuwa anasimamia kwenye msimamo kwamba Mungu alikuwa na mtoto mmoja tu, licha ya maandiko kwenye Ayubu na penginepo kueleza watoto wengi wa Mungu kuepo kabla ya kuja na kuzaliwa kwa Kristo ulimwenguni (Mwanzo 6:2,4, Ayubu1:6, 2:1, 38:7) kinyume kabisa na imani ya Herbert.


Msimamo rahisi na wa pekee kwamba Yesu Kristo ni mwana wa Mungu ungemaanisha kwamba aliumbwa na a kwamba aliumbwa na Mungu Baba. Na hiki ndicho wanachokifanya mababa - wanazaa watoto. Vinginevyo utakuwa umejiunga na filosofia ya waamini Utatu ya uwingi wa miungu na ya kupenda. Ahh, lakini kama Armstrong hakuwahi kufikiri hivyo, basi ukweli ni lazima uwe umeyumbishwa au kupotoshwa.


kisa hiki cha wachungaji kuwapofusha watu kwa kuwaingiza kwenye ibada za sanamu, watu wa kada zote za madaraja na kuyatafsiri maandiko kwa kutumia mitazamo waionayo wao kuwa ina mashiko kwenye tafsiri ya maandiko matakatifu.


Usemi au maelezo haya ya kwamba amri ya kwanza haikusudii kumtaja Mungu Baba na badala yake inamtaja au kumlenga Yesu Kristo ni wazi sana kwa mara ya kwanza niliisikia kwenye kanisa la WCG. Hii inanifanya nishangae kwamba ni watumishi wangapi wa lililokuwa hapo zamani kanisa la WCG huenda walikuwa karibu sana na imani hii. Hawezi kua ndiye huyu wa pekee na wa kweli.


kwa kweli hii inaonyesha dalili ya kwamba tunapaswa kumwabudu Yesu Kristo, na tena inakwenda moja kwa moja kinyume na mafundisho ya Kristo ya kwamba tumwabudu Mungu (Baba) peke yake kwa kuwa ni yeye tu ndiye aliye mwema (Mathayo 19:17, Marko 10:18, Luka 18:19), na maelekezo aliyyotupa Kristo katika kumuomba Mungu Baba. Hii inanifanya mimi nifikirie kwamba mtu anayeamini hivi anaweza kuwa anamuomba Yesu Kristo.


mfuasi yeyote wa Herbert Armstrong kwa kweli angedhani na kuona kama ni kufuru kusema kuwa Kristo alikuwa ni mwana wa Mungu aliyekuwepo tangu hapo nyuma kabla ya kuzaliwa kwake rasmi duniani aliyekuwepo pamoja na wana wengine wengi wa Mungu na Kristo akiwa ni kama ndugu yao, au mshirika au ndugu pamoja nao. Lakini tunajua ni wapi inakoelekea. Ni mkakati wa kuwapofusha tu kunakofanywa na upotoshaji wa makusudi wa maandiko matakatifu wakati akisema azi kabisa kwamba Mungu Baba, Mungu wa Yesu Kristo ambaye yu wa chini ya Mungu na ndiye mwana wa Mungu, alitiwa mafuta na kuinuliwa kuliko ndugu na wenzake wote (Waebrania 1:9). Kimsingi inasema kwamba kabla ya mtiwa mafuta huyu kutoka kwa Mungu wake alikuwa ni wa daraja sawa tu na hawa wenzake.

Ni kweli, hii ni sahihi, na siyo teolojia ya Herbert Armstrong ya mfumo wa imani ya kwamba miungu ya kweli ni wawili, na kama haikubaliki kwenye mafundisho yasiyo na mashiko na mapotofu ya Herbert Armstrong, teolojia inayopinga na kwendana kinyume na biblia haitaingia akilini kwao pasi kujalisha ni maandiko mengi kiasi gani yaliyokosekana kuthibitisha jambo hili la kufuru.”

 

Mtazamo wa maafisa kuhusu andiko la Waebrania 1:9 unaendana kabisa na wa Frank Nelte aliyekwenda kulinganisha na Zaburi 45:6-7. Tumesikia pia wengine wakionyeshwa kwenye Zaburi 45:7 wakidai kuwa andiko hilo linawataka wateule wa kanisa lililotajwa hapo juu ambamo Kristo alitukuzwa na kuinuliwa juu. Hata hivyo, andiko la Waebrania linafanya hilo lisiwezekane au iwe vigumu na inathibitisha pia Baba kuwa alijulikana kwenye Agano la Kale kama ilivyokuwa imenukuliwa kwenye Waebrania 1:5, hususan ukweli kuhusu Mungu na Mwana wa Mungu. Uhusiano huu ulithibitishwa pia kwenye Mithali 30:4-5 ambako jina la Baba lilitambulika kwa wazi sana kama Eloa, Mungu wa Agano la Kale.

 

Waebrania 1:1-4 inasema:

[1] Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, 2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. 3 Yeye kwa kuwa ni mng'ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu; 4 amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao.

 

(Tafsiri ya RSV inatumia neno kotekote vinginevyo ni kama imenena kinyume chake.)

 

Kristo anatajwa hapa kuwa amefanyika kuwa ni bora zaidi ya malaika kwa maana kwamba hakuwa wakato wote hivyo. Ni kweli kwamba alikuwa ni sehemu ya Malaika akiwa ni kama Malaika wa Uwepo wake, au Malaika wa Bwana, katika Israeli.

 

Kumbuka kuwa Mungu anaonekana hapa kama anaongea ka kupitia manabii wa zamani. Kwa hiyo kitendo cha kudai kwamba manabii hawakujua kuwa Mungu alikuwepo ni madai ya kipuuzi kutokana na andiko la Agano Jipya lenyewe. Kristo hapa alifanywa kuwa ni mrithi wa mambo yote. Sisi pia tu warithi pamoja naye. Maneno yaliyo kwenye tafsiri ya KJV ya “Kwa yeye mwenyewe” na “yetu” yameongezewa kwenye maandiko ambayo hayakuwepo kwenye maandiko ya zamani na yaliongezewa na Watrinitarian kwa lengo la kuhalalisha maandiko waliyoyakusudia kuyaanikisha. 

 

Andiko hili kwa Kiebrania yamepotoshwa au kutumiwa vibaya na Watrinitarian na Waditheis/Wabinitarian wakidai kwamba Kristo kila wakati alikuwa ni wa tofauti na pia juu ya Jeshi la Malaika wakati Biblia inseam wazi sana kwamba siyo kweli. Mtazamo wa namna hiyohiyo uliingia kwenye imani ya Kikristo ukitokea kwa waongofu aliotokea kwenye imani ya mungu Attis wa huko Roma na ikaanza kuenea mnamo mwaka 170 BK. Habari hii imeelezwa kwa kina kwenye jarida la Imani za Ubinitarian na Utrinitarian (Na. 076) na hasahasa kwenye jarida la Upotoshaji wa Wabinitarian na Watrinitarian Kuhusu Teolojia ya Zamani ya Uungu (Na. 127B).

 

Andiko lililoko kwenye Waebrania 1:2 limepotoshwa na kutafsia vibaya kusema “kwa yeye aliyeiumba dunia pia,” wakati neno lenyewe halisemi dunia bali ni kiambishi cha aion lenye maana ya zama au umri.

 

Andiko hili hapa linaonyesha kuwa uwepo wa Baba ulijulikana na kutangazwa kutoka kwenye maandiko mengi ya Agano la Kale lakini mifano hii imepuuziliwambali na wafuasi wa Armstrong.


Waebrania 1:5 Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana?

 

Aya ya 5 imeinukuu Zaburi 2:7[8] (kwenye tafsiri ya the Septuagint (LXX), soma tafsiri ya Brenton). Zaburi 2:2 pia inamtaja Bwana Yahova na dhidi ya mtiwa mafuta wake, ikiwataja viumbe wawili, na aya ya 7 inaonyesha kuwa andiko hili linawataja Baba na Mwana. Hivyo kwenye andiko hili tunajionea wazi sana kwamba Baba na Kristo wanatajwa na Yahova kwenye aya ya 2 ni Baba kama jina au neno la kiuzaa tu. Neno Yahova kwenye aya ya 4 lilipotoshwa kwa kubadilishwa kuwa Adonai kwenye tafsiri ya the Sopherim kwenye kipindi cha baada ya kuangamizwa kwa Hekalu ili kupotosha maana halisi iliyokusudiwa. Andiko lililotafsiriwa mwana wa pekee lina maana ya moja kwa moja ya aliyekuzaa. Maneno haya yamechukuliwa na Bullinger kuwa ni kwenye Ufufuo wa Wafu wakati Kristo atakapokuwa “kiongozi wa taifa huru tukufu wa aina mpya ya viumbe” (kutokana na Matendo 13:33; soma tafsiri ya Companion Bible sawa na Waebrania 1:5). Andiko hilo liloendelea kwenye aya ya 5 na linasema “Na tena, Mimi nitakuwa kwake baba, Na yeye atakuwa kwangu mwana” linatohoa kwenye 2Samweli 7:14 ambalo linamhusu Mungu na kumtaja Kristo. Mungu anajidhihirisha kwa Nathan kwamba uzao wa Daudi utamzalia yeye mwana kutoka kwenye aya za 12-16.

 

Kwa hiyo Daudi aliambiwa na Mungu, kwa kumtumia Roho Mtakatifu kwa kupitia Nathan kwamba Mungu atamleta Mwanae (Kristo) kutoka kwenye uzao wa Daudi. Kwa hiyo madai ya Armstrong ndipo yanathitika tena kuwa ni ya uwongo.

 

2Samweli 7:12-17 Nawe siku zako zitakapotimia, ukalala na baba zako, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayetoka viunoni mwako, nami nitaufanya imara ufalme wake. 13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu, nacho kiti cha enzi cha ufalme wake nitakifanya imara milele. 14 Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu; akitenda maovu nitamwadhibu kwa fimbo ya binadamu na kwa mapigo ya wanadamu; 15 lakini fadhili zangu hazitamwondoka, kama vile nilivyomwondolea Sauli, niliyemwondoa mbele yako. 16 Na nyumba yako, na ufalme wako, vitathibitishwa milele mbele yako. Nacho kiti chako kitafanywa imara milele. 17 Kwa maneno hayo yote, na kwa maono hayo yote, ndivyo Nathani alivyonena na Daudi.

 

Andiko la Waebrania 1:6 linalitaja andiko hilo kama prototokos au mzaliwa wa kwanza ilivyonukuliwa kutoka kwenye Kumbukumbu la Torati 32:43 kwenye tafsiri ya the LXX (cf. Ps. 97:7).

 

Waebrania 1:6 Hata tena, amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu malaika wote wa Mungu.

 

Andiko la kwenye tafsiri ya the LXX linasema kwenye aya hii: “Furahini enyi mbingu pamoja naye na Malaika wote wa Mungu na wamwabudu (proskuneo – msujudie) yeye. Furahini enyi Mataifa pamoja na watu wake na hebu ana wote wa Mungu ajitie nguvu katika yeye.”

 

Neno la asili lililotumiwa kutaja wana wa Mungu ni pantes uioi theou. Hili lina maanishwa wazi kuwa ni wana wote wa Mungu na viumbe hawa siyo Kristo ila ni wana wengine wa Mungu ambao ni tofauti kabisa na Wamataifa na Waisraeli na hivyo wanakuwa ni viumbe tu wa kiroho ambao ni Malaika wanaotajwwa tu kwenye Ayubu 1:6, 2:1 na 38:4-7. Andiko hili pia lilighushiwa kwenye tafsiri ya Maandiko ya Masoretic Text (MT) kama ilivyokuwa kwenye Kumbukumbu la Torati 32:8 ambalo lilibadilishwa kutoka kwenye maneno sawasawa na idadi ya wana wa Mungu kwa maneno yaliyo sawa na idadi ya Wana wa Israeli. Walilichukua andiko kutokana na aya hii ya 43 ili kubadilisha au kupotosha kutoka kwenye ukweli ufuatao: Wana wa Mungu walio kwenye aya ya 8 sio kuwa walikuwa na mataifa waliyopewa na Israeli walitolewa kwa Yahova wa Israeli, lakini, kutokana na aya ya 43, kwamba wokovu ulifunuliwa na kuwa wazi kwa Wamataifa, pamoja na Waisraeli na pia kwa wana wa Mungu wakiukubali. Tulikuwa na kweli kwenye andiko la tafsiri ya LXX kuthibitisha andiko kwenye Waebrania, lakini Watrinitaian hawakujali hali hii ya kugushi, na liliwapendeza tu. Waamini imani ya Kiditheism na wafuasi wa Armstrong hawakumudu kujua tu vya kutosha jinsi ya kulifanya andiko hili. Hata hivyo, hakuna shaka kwa vyovyote vile kwamba andiko hili la Waebrania linanukuu moja kwa moja andiko liilo kwenye tafsiri ya LXX na andiko kamili linaloangaza kwenye maana iliyo kwenye Waebrania. Gombo zijulikanazo kama za Bahari ya Chumvi (The Dead Sea Scrolls (DSS)] linathibitisha pia andiko lililo kwenye tafsiri ya LXX na inaonyesha kuwa tafsiri hii ya MT ni tafsiri iliyofanywa baadae kwa kazi ya kughushi ya Wayahudi. Tafsiri ya RSV imesahihisha andiko lililo kwenye aya ya 8 kwa misingi hiyo.

 

Waebrania 1:7 imetoholewa kwenye Zaburi 104:4. Rejea hii inathibitisha pia pasi shaka kabisa kwamba Baba anayetajwa kwenye Zaburi na Kitabu cha Waebrania vinaonyesha na kuthibitisha ukweli huo kama inavyonekana kwenye Zaburi 104 inayomtaja Baba kama muumbaji Aliyeiweka misingi ya dunia (Zaburi 104:5a).

 

Waebrania 1:7 Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye malaika zake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa miali ya moto.

 

Zaburi 45 imefanyiwa rejea kwenye aya 8 na inaonyesha kuwa mwana anayefunuliwa, na hivyo na Baba pia. Kwa hiyo, elohim ambaye ni elohim wa Kristo anaweza kuwa ni Baba tu, peke yake. Kwa hiyo kwa mara nyingine tena kwa mifano saba mingine iliyo tofauti kwenye sehemu ya kwanza ya Waebrania sura ya 1, uthibitisho wa kwamba Baba hakufunuliwa kwenye maandiko ya Agano la Kale imethibitika kuwa ni uwongo. 

 

Waebrania 1:8-9 [8] Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.

 

Aya za 10-12 zinafanya rejea kwenye Zaburi 102:25-27. Ni jambo lililo wazi sana kwamba andiko hili linamtaja Baba kama lilivyotumiwa hapa kwenye Waebrania kwa kumkanganya na mwana ambaye hatimaye anatajwa tena kwenye aya ya 13 likifanya rejea kwenye Zaburi 110:1 na malaika kwenye aya ya 14.

 

Waebrania 1:10-14 Na tena, Wewe,Bwana,hapo mwanzo uliitia misingi ya nchi, Na mbingu ni kazi za mikono yako; 11 Hizo zitaharibika, bali wewe unadumu; Nazo zote zitachakaa kama nguo, 12 Na kama mavazi utazizinga, nazo zitabadilika; Lakini wewe u yeye yule, Na miaka yako haitakoma. 13 Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? 14 Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

 

Ni kwa jinsi gani basi hawa Baba na Mwana hawakujulikana kutoka kwenye mambo yaliyo kwenye maandiko haya? Kwa nini Baba hajulikani kwenye Zaburi 110 kwenye Agano la Kale? Swali hili ni la kipuuzi. Andiko lililo kwenye Zaburi 102:27 limetafsiriwa kutoka kwenye maneno Lakini Wewe U Yeye yule; ili kugeuza ukweli kwamba tunaongelea kuhusu Mungu wa Pekee wa Kweli na sio mfumo au imani ya Utatu.

 

Andiko lenyewe lilikuwa kwa bahati mbaya ni kama lilivyotumika kwenye tadsiri fulani kadhaa ili kumuinua Kristo juu ya Malaika na kudai kwamba ilikuwa hivyo kila wakati wakati maandiko yalipoonyesha kuwa yeye alikuwa ni mmoja wao wakiwa kama wana wa Mungu. Lengo la andiko ni kuonyesha kwamba Kristo, akiwa kama mmoja wao, alifanywa kuwa wa chini kidogo kuliko malaika, na kisha akainuliwa juu yao kwa kupitia sadaka yake. Walionyeshwa na kutajwa kwenye tafsiri ya LXX kuwa ni wana wa Mungu kama sehemu ya kiumbe Malaika akiwa ni tofauti na wanadamu, wa namna mbili zote, yaani Mwisraeli na Mmataifa. Tutaona tena kwa kuyaelewa maandiko haya na kisha kwenda mbele kuonyesha kwa kina utambulisho wa Baba kama Mungu wa Kweli na wa Pekee wa Agano la Kale.

 

Tukirudi nyuma kwenye suala la Amri ya Kwanza inayomtaja Kristo: mmoja wa makoodineta wa CCG huko California alilazimika kusema hivi:


“Sijawahi kuskia kabisa jambo hilo kwenye kanisa la Worldwide COG au kwenye machipukizi yake kwamba Amri ya Kwanza iliyo kwenye Kutoka 20 ilitolewa na Kristo na siyo na Baba hadi niliposoma hivyo kwenye makala ya Frank Nelte, ya MPANGO WA MUNGU WA WOKOVU WA MWANADAMU & KURUDI KWA KEISRO. Nimewahi kuwa na waumini wachache walio kwenye matawi yaliyoibuka kutoka kwenye kanisa la WCG na sikuweza kusikia kabisa kufuru kama hii.

Lakini hainishangazi mimi kwa kuwa nilisoma kwenye maandiko ya maandalizi ya mahubiri kutoka kwenye mikururu ya mahubiri ya John Ritenbaugh kuhusu Uhusiano uliopo wa Baba/Mwana kwamba ni vyema au Sawa tu kumuomba Kristo. Mtazamo huu ulikuwa haujahuniriwa wala kufundishwa kabisa kwenye kanisa la Worldwide kipindi cha uhai wa Herbert Armstrong. Ilikuwa ikifundishwa wakati wote na kanisa hili kumuomba Baba kwa jina la Yesu Kristo ni kama ilivyofundishwa na Kristo mwenyewe.”


kanisa la WCG lilifundisha, kama yalivyofanya Makanisa yote ya Mungu kwa kipindi cha takriban miaka elfu mbili, kwamba ilikuwa imekatazwa kabisa kumuoba Kristo. Maombi yote yalilengwa kwa Baba kwa jina la Mwana wake Yesu Kristo.

mara tu unapofanya kosa hili na unapomuinua Kristo na kumfanya kuwa ni sawa na Mungu wa Pekee wa Kweli ndipo kwamba unaendelea kushamirisha kiwango hili cha kufuru. Na kwa kadiri watumishi hawa wavyofanya kazi kimakosa na upotoshaji na huku wakikosa mwongozo wa bodi au naraza la wazee na kujiweka kando au nje ya kinara cha taa cha Kanisa la Mungu, wanafanya makosa na hivyo haishangazi kile walichokipata kwenye mwisho huu wa kiumauti. Mtu aliye mlenhwa wa muainisho huu hata anakana kwamba jina Eloa linamaanisha Mungu Baba kwa maana hii iliyosababisha kujiuliza maswali. Anapinga pia kwamba kulikuwa na Kalenda ya Hekaluni na tutauainisha uwongo huu pia.

 

Koodineta mwingine aliyekuwa na uzoefu na kulijua Kanisa lililoita Kanisa la Mungu la Kimataifa almaarufu kama Church of God International (CGI) alisema kuwa hajawahi kusikia kabisa ikisemwa hivyo, wakati alipokuwa kwenye Kanisa la Mungu la Kimataifa, yaani Church of God, International. Kwenye kanisa hilo ilifundishwa kwamba Amri ya Kwanza inawataja wote wawili, yaani Baba na Kristo kwa kuwa Kristo naye alichukuliwa kuwa ni Mungu kutokana na kutolielewa vyema andiko la Yohana 1. Yohana 1:1 inasema tu kwamba Kristo (Neno) ni theos/elohim, kama walivyo wana wengine wa Mungu (malaika) kutokana na Ayubu 1:6, 2:1, 38:7 na Zaburi 82.

 

Kristo ni anabadilishwa kutoka kuwa Baba, ambaye ndiye Mungu aiye kwenye Yuhana 1:1 kama Ton Theon/Ha Elohim.


Tatizo ambalo lilikabiliwa kanisa la CGI ni kwamba amri inasema kwamba usiwe na elohim mwingine ila mimi.
Andiko linasema: Mimi ni Yahova Elohim wako, Usiwe na miungu mingine ila mimi. .

Ni kweli kwamba Yahova ni jina lililotumiwa kwa wana wengi wa Mungu na Manzo 18 na 19 zinawataja Yahovah wanne kwa wakati mmoja. Mmoja aliishi na Ibrahimu na wawili walikwenda kwa Lutu huko Sodoma na kisha waliuita moto ushuke kutoka kwa Yahova Mbinguni. Habari hii imeainishwa kwa kina kwenye jarida la
Malaika wa YHVH (Na. 024).

Kwa hiyo, lugha ya andiko hili inakubali kuwa ni udogo wa Yahova wa Israeli; hata hivyo, lama maneno yaliyo kwenye Amri ya Kwanza yalikuwa yanatokana au kummaanisha Kristo au Yahova mwingine ni dhahiri shahiri kwamba ni ibada ya sanamu na ni Dhambi ya Shetani.

mtazamo kama huo unatokana na madai ya uwongo na mapotofu kwamba Mungu wa Agano la Kale alikuwa ni Yesu Kristo, ambavyo ni teolojia ya uwongo na potofu ya Armstrong inayolenga moja kwa moja kinyume na maandiko ya Agano la Kale. Wakati madai yakiwa yanafanywa kwamba Yahova hapa inamtaja Kristo na siyo Mungu kama Ha Elohim ndipo tunakabiliwa na ukweli kwamba andiko hili, likiwa ni umoja, linamfanya Kristo adai kwamba yeye anastahili kuabudiwa na Waisraeli na siyo Mungu wa Pekee wa Kweli.

Andiko lenye maana au lugha mbili haliwezi kuwa linavitaja viumbe wawili, ingawaje madai ya kwamba walikuwa ni viumbe wawili kama mmoja ni hoja ya uwongo mkubwa ambayo wanatuama kwayo. Uelewa halisi wa Agano la Kale yamegubikwa na makosa au upotofu wa Armstrong yakiwa yamekuwa akiendelea kwa utetezi huu uliokubalika kwa kupofushwa sana kuyakubali na kuyajengea juu yake kama tunavyoona. Hatuna mashaka kwamba Armstrong mwenyewe aliuulaumu au kuuponda mtazamo huu wa kwamba Amri ya Kwanza inamtaja Kristo.

 

Ni kama ilivyokuwa imenyooshwa hapa, suala lenyewe lapasa liwe wazi sana kwa mtu yeyote kama iwapo kama hizo zilikuwa ni amri za Kristo, kwa hiyo kumwabudu Baba kungekuwa ni makosa kwa kuwa tungekuwa tukimwabudu Baba badala ya Kristo. Ni dhana ya kipuuzi. Tunaposoma Ezra sura za 4-7 tunaona kwamba Hekalu lilikuwa la Mungu (SHD #433 Eloahh, Eloah), na sheria zilikuwa ni zile za Mungu, na kwenye Yohana 17:3 Kristo alimuita Mungu huyu kuwa ni Mungu wa Pekee wa Keli. Kristo pia alimtaja Mungu huyu kuwa ni Mungu wake kwenye Yohana 20:17 na kama ni hivyo hii ingemfanya Mungu huyu kuwa ndiye aliye Muumba Kristo na amemfanya Kristo kuwa ni elohim mdogo saidizi ambaye anatenda kazi kwa niaba ya Muumba wake. Kwa hiyo sheria hizo zinakuwa ni sheria tu za Mungu Baba na kwamba Kanisa la Karne ya Kwanza lilimchukulia Kristo kuwa ni Malaika Mkuu wa Agano la Kale aliyempa Musa Torati, kama inavyosema Biblia.

 

Mungu wetu ndiye Mungu wa Kristo. Tuna Mungu Mmoja tu wa Pekee na wa Kweli. Tunamtimikia yeye, kama afanyavyo Kristo.

 

Uzishi huu mkubwa na usio na haya wa kufundisha kuwa kuna miungu miwili wa kweli na uwongo wa kwamba Baba hajatajwa kwenye Agano la Kale umekuwa ukienezwa na watu hawa kwa kiasi cha kwamba tunaona kwamba mtu mmoja au wawili wa waumini wa Makanisa ya Mungu barani Afrika wamekuwa wakifikiwa kwa njia ya Internet na mtu mmoja waliokuwa waumini wa lililokuwa kanisa la zamani la WCG, wakionekana kabisa kuwa huko Afrika Kusini, wanaojaribu kueneza uwezekano wa kwamba Amri ya Kwanza inamuelezea Kristo. Kwa bahati nzuri sana yamekuwa yakikataliwa na kuonekana kuwa ni uzushi mkubwa sana na wale tunao wajua.

 

Biblia imeweka wazi sana kwamba kuna Mungu Mmoja tu wa Kweli na kwamba Mungu huyo ametajwa kwenye Agano la Kale kuwa ni Baba na muumbaji na jina lake ni Eloa, na ana mtoto wake mwanadamu. Mithali 30:4 moja kwa moja inamtaka kila mmoja anayedhania kua anayeyaelewa maandiko alitangaze jina la Baba na jina la Mwana wake. Hatimaye andiko hili linaendelea kumtaja yeye kwa jina kuwa ni Eloa ambalo ni jina la umoja na inakubali kuwa hakuna uwingi na inamtaja Baba peke yake. Kulijua jina hili la Mungu ni kigezo cha uelewa katika Roho Mtakatifu. Waditheist au Wabinitarian hushindwa mtihani huu. Wanapinga na kufundisha kimakosa jambo hili.

 

Eloa ni Mungu wa Hekaluni na tunajua kutokana na Kumbukumbu la Torati 32:15 kwamba yeye ni muumbaji na kwenye Kumbukumbu la Torati 32:17 kwamba yeye ndiye mlengwa wa sadaka tuzitoazo. Yeye ndiye Mungu wa kwenye Biblia.


Yeye ndiye Mungu Aliye Juu Sana (Eleyon au Elyon) na kuna Mungu mmoja tu Aliye Juu sana kwa maelezo na mashiko ya lugha. Aliyagawanya mataifa sawasawa na idadi ya wana wa Mungu (Kumbukumbu la Torati 32:8 tafsiri za RSV na DSS). Aliwapa mahitaji Waisraeli kutoka kwa Yahova. Kwa hiyo, Elyon na Yahova, wakiwa kama Mungu na mwana wa Mungu, wanawekwa mahala pake hapa kwenye Torati ambako Yahova wa Israeli ni mmoja wa wana wa Mungu na Eloah anafanywa kuwa ni kama muumbaji. Kwa sababu hii tafsiri ya MT ilighushiwa kwenye andiko hili kwenye kipindi cha baada ya Hekalu na ndiyo sababu tafsiri ya KJV ni potofu na ya uwongo.


Ayubu anamtaja Eloah sehemu mbalimbali 45. Mkombozi ameorodheshwa kama mmoja wa Maelfu na siyo Eloah kwenye Ayubu (Ayubu 33:23).


jina hili ni la umoja kwa namna yoyote ile. Maandiko yana haribu kabisa fumbo aliloliweka Armstrong, lisemalo kwamba Agano la Kale lilimtaja Kristo peke yake ambaye alikuwa ndiye Mungu wa Agano la Kale na Baba kakujulikana kwenye Agano la Kale. Huu ni uwongo.


Ezra anamtaja Eloah kuwa ni Mungu wa Hekalu na anaendelea kwenye maandiko yaliyo kwenye Ezra 4:24 kulionyesha Hekalu kama Nyumba ya Eloah; Mungu (Eloah) wa Israeli (Ezra 5:1). Manabii wa Nyumba ya Eloah ni manabii wa Eloah (Ezra 5:2). Ni “jicho” la Eloah ambalo linaona na kuamuru harakati na kazi zote zinazofanyika Hekaluni.

 

Dario aliombwa asaidie ujenzi wa Nyumba ya Eloah Mkuu huko Yerusalemu (Ezra 5:8).


Wayahudi walijua na walisema kuwa watumishi wa Eloah Mkuu wa Mbinguni na Duniani (Ezra 5:11). Lakini alikuwa ni mababa wa Yuda ndio waliomkasirisha Eloah wa Mbinguni na kumtia hasirani (Ezra 5:12).
Kuna Eloah mmoja tu wa Mbingu na Duania na ni Baba. Kudhania vinginevyo ni ibada ya sanamuna kufuru kubwa.

Wayahudi walitambua kuwa alikuwa ni Koreshi ndiye aliyetoa amri ya kuijenga Nyumba ya Eloah huko Yerusalemu (Ezra 5:13). Vyombo vya Nyumba ya Eloah vilirudishwa kwa mfalme wa Yuda (Ezra 5:14) na akaamuru virudishwe kwenye Nyumba ya Eloah kama ilivyojengwa mahala pake (Ezra 5:15). Ombi lilifanywa kuwa ni iwapo kama tangazo la Koreshi lilidumu kuhusu Nyumba ya Eloah (Ezra 5:17).

Dario aliamuru kufanyike utafiti na tangazo la Koreshi lilikutwa likiamuru ujenzi wa Nyumba ya Eloah huko Yerusalemu (Ezra 6:3), pamoja na vyombo vya dhahabu na vya fedha vilivyochukuliwa na Nebukadneza kutoka kwenye Hekalu la Eloah vikiwa vimekarabatiwa na kurudishwa kwenye Nyumba ya Eloah (Ezra 6:5). Hivyo, Hekalu la zamani na hekalu jipya yote mawili yalikuwa ni Nyumba za Eloah.

 

Ndipo maadui wakaamriwa waache kuijenga Nyumba ya Eloah na ndipo Wayahudi pekeyao walibakia kuijenga Nyumba hii ya Eloah (Ezra 6:7). Kodi iliyokuwa inatolewa ng’ambo ya mto iliamriwa itumike kwenye ujenzi wa Nyumba ya Eloah (Ezra 6:8) na pia kwa kutoa dhabihu za utakaso kwa Eloah wa Mbinguni (Ezra 6:9-10).

Ni Eloah ndiye aliyesababisha jina lake liwekwe humo kwenye Nyumba ya Eloah na mamia ya mitamba walitolea sadaka kwa maelekezo ya Nyumba ya Eloah (Ezra 6:12,16-17). Makuhani na Walawi waliwekwa kwenye makundi ili wamtumikie Eloah huyo Yerusalemu (Ezra 6:18).

 

Artashasta alimjua na kuwamini Ezra kuwa ni mwandishi wa Torati ya Eloah wa Mbinguni (Ezra 7:12). Ezra alitumwa kuipeleleza Yerusalemu sawasawa na Torati ya Eloah ambayo ilikuwa mkononi mwake (Ezra 7:14) na mfalme na washauri wake walitoa sadaka ya vito vya fedha na dhahabu kwa Eloah wa Israeli ambaye ndiye Eloah wa Mbinguni ambaye makao yake yapo Yerusalemu (Ezra 7:15). Iliwalazimu kununua wanyama kwa ajili ya sadaka kwa Eloah huko Yerusalemu (Ezra 7:17) na ndio walipofanya mapumziko sawasawa na Mapenzi ya Eloah (Ezra 7:18). Pia walitoa vyombo wakampa Eloah mbee ya Nyumba ya Eloah huko Yerusalemu (Ezra 7:19). Chochote kile kilichokuwa cha muhimu kulileta kwenye Nyumba ya Eloah (Elahh) kilichukuliwa kutoka kwenye nyumba ya hazina ya mfalme kama alivyoamuru ifanyike na Ezra mwandishi wa Torati ya Eloah (Ezra 7:20-21). Chochote kilichoamriwa na Eloah wa Mbinguni kilifanyika kwa umakini mkubwa kwa ajili ya Nyumba ya Eloah wa Mbinguni (Ezra 7:23).

 

Pia makuhani, Walawi, waimbaji na wahunzi, Wanefini, waliokuwa akihudumu kwenye Nyumba ya Eloah na haikuruhusiwa kuwatoza ushuru, kodi au riba kwao (Ezra 7:24). Ezra aliamriwa kutenda mambo sawasawa na busara na hekima ya Eloah katika kuwachagua maliawali na waamuzi au mahakimu. Yeyote asiyeishika sheria ya Torati ya Eloah na sheria za mfalme alihukumiwa kifo kwa haraka sana na wao (Ezra 7:25-26). Kiumbe huyu aitwaye Eloah ndiye Mungu wa Pekee wa Kweli.


Jina lake linaonyesha kuwa halina uwingi kwa namna yoyote ile na Torati inatoka kwake na yeye ndiye mlengwa tunayemtolea sadaka Hekaluni. Kristolitaja Hekalu kama ni Nyumba ya Baba yake. Makuhani, pamoja na Kristo kama Kuhani Mkuu wa mfano wa Melkizedeki, humwabudu yeye na kumtumikia yeye. Elohim wanatokana na yeye wakiwa kama Ha Elohim. Wao ni Elohim, ambalo ni neno la uwingi, nao ni wana wa Mungu na ni baraza la Elohim wa kwenye Zaburi na ni Baraza la kwenye Ufunuo sura ya 4 na ya 5.

 

Ni wazi sana kwamba madai au malumbano ya Herbert Armstrong kwamba Mungu wa Agano la Kale ndiye Kristo ni uzushi wa wazi kabisa na inaonyesha upungufu mkubwa wa kulijua maandiko ya Agano la Kale. Kwenye maandiko ya kanisa la WCG kwenye Mafunzo yake ya Kozi ya Muda Mrefu, kwenye Somo la 8, kanisa la WCG linasema kwamba neno Eloah lilikuwa ni neno la umoja la Mungu ambalo hapo mwanzoni asili ya jina Elohim. Somo hili lilibakia bila kubadilishwa kutoka kwenye uasilia wake kwenye toleo lake la mwisho lililochapishwa chini ya usimamizi wa Tkach Snr. Herbert Armstrong hakubadilisha kabisa wala kuliondoa. Ilionekana kuwa hakujua maana ya andiko kama somo lililofuatia lililokuwa kwenye muundo au mtindo wa Kiditheism. Hata hivyo, washirika wasaidizi wake, kama vile Herman Hoeh, walijua kuwepo kwake lakini huenda siyo maana zake. Kwa bahati mbaya sana, hawakuuendeleza kabisa mfumo wa Agano la Kale kama walivyotakiwa kuwa. Kulikuwa maadiko mengine yanayoelezea kuhusu miungu wawili wa Israeli kama vile Zekaria 2 na wengine wanaoelezea nafasi ya Kristo kama ni Malaika wa Yahova kama ilivyo kwenye Torati na kwenye Zekaria 12:8.

 

Tofauti kati ya Yahova na Yahovi

 

Tofauti ya Yahovi (SHD 3069) na Yahova (SHD 3068) hawakujulikana na Armstrong na hata wasaidizi wake.

 

Ni kama ilivyosemwa hapo juu, kuna Yahova wengi. Kwenye Mwanzo sura ya 18 na 19 tunaona kuwa kulikuwa na takriban Yahova wanne (SHD 3068) wanaotajwa kwa wakati mwingine wowote. Watatu walimtembelea Ibrahimu walipokuwa wanakwenda Sodoma. Mmoja alibakia na yeye na Yahova wawili wengine walikwenda kwa Lutu na Yahova wa Nne aliyebakia mbinguni aliunyesha moto kutoka mbinguni na kuingamiza miji ya Sodoma na Gomora.

Jambo hili limeelezewa kwa kina kwenye jarida la Malaika wa YHVH (Na. 24).


Kutoka 3:14 ipo kwenye mwandiko wa 'eyeh 'asher 'eyeh ambayo imeundwa kwenye muundo wa nafsi ya kwanza ikimaanisha Mimi niko (au nitakuwa) ambaye nitakuwa. Kuna maelezo kwenye tafsiri ya Oxford Annotated RSV kwenye msisitizo huo. YHVH ni nafsi ya tatu ya muundo wake. Kwa maneno mengine Mungu anafanyika kuwa kitu fulani. Anafanyika kuwa kiumbe enezi.

kila mmoja wa malaika aliyetumwa kwa wanadamu alikuwa na haiba ya kuheshimika ya Yahova kama alivyo mfanya kuwa. Neno Yahovi (SHD 3069) linammanisha Mungu wa Pekee wa Kweli peke yake.

Jina Yahova ni mfumo wa nafsi ya tatu ya vebu linalomaanisha kwamba anasababisha au kufanikisha iwe. Halimhusu kabisa Mungu Baba wakati linapomaanishwa Yahova wa Majeshi au kwa mazingira machache kuwa Yahova Elohim.

ni kama ilivyosemwa, kenye Somo Nambari 8 la Mafundisho Marefu ya Kozi za kanisa la WCG iliyoelezewa kwamba Neno kuhusu Mungu lilikuwa Eloah na la uwingi Elohim lilitoholewa kutoka kwenye neno hili, lakini kwenye Somo la 9 walijikita kwenye Uditheism. Kozi ile na somo hilo vimebakia bila kubadilishwa wakati wote wa kuwepo kwa kanisa la WCG hadi Tkach alipoyaingiza na kuyaanzisha kwenye miaka ya 1993-5.

Wakati Wayahudi walipoyasoma maneno Yahovi SHD 3069 walisoma Elohim, na wanaposoma SHD 3068 Yahova wanasoma Adonai kwa hiyo isikanganye viumbe hawa. walibadilisha jina Yahova kuwa Adonai kwenye takriban sehemu 134 kwenye Agano la Kale ili kupotosha au kubadilisha uhusiano pia. Maeneo hayo yamenukuliwa na kuonyeshwa kwenye kurasa za nyongeza za tafsiri ya biblia ya Companion Bible na Bullinger anaonyesha maeneo hayo kwenye bango kitita.

Upande mmoja unaoelezea maana ya jambo hili kwenye andiko la Kutoka 4:10 na pia 4:13 ambapo neno Yahova anafanana na Malaika wa Uwepo anayenena na Musa ambavyo maeneo mawili kati ya 134 yamelibadilisha jina Adonai na hivyo kuonyesha kwamba walielewa ukweli wa kwamba alikuwa ni Kristo ndiye aliyenena na Musa na siyo Mungu wa Pekee wa Kweli ambaye kwa yeye Mungu alimtumia. Vinginevyo maneno haya yangeweza kuzuiwa na kusomeka elohim. Huu ni mfano tu mwingine wa makosa ya imani ya uwili ya Armstrong. Kila moja ya maandiko haya 134 linaoneyesha uhalisia wa tofauti zilizopo kati ya miungu hii.

 

Yahova wa Majeshi Kama Eloah, na the Elohim


Yahovi ni Elyon, au Ha Elohim au Yahova wa Majeshi ambaye ndiye Mungu wa Pekee wa Kweli, Eloah. Yahovi ni Mungu wa wale wote alinaoitwa Yahova au Elohim. Elohim ambaye ndiye alikuwa Kristo aliyetajwa kwenye Zaburi 45:6-7 ana elohim wake ambaye ni Ha Elohim na ana elohim mwingine akiwa kama mshirika wake kama andiko lile la kwenye Waebrania 1:8-9 linasema wazi sana kabisa.

Hili ni jambo la maana na linaloeleweka. Kuwa elohim wengi lakini kuna ELOAH Mmoja tu. Jina lenyewe linakubaliana kuwa halina uwingi kabisa. Muundo wa Wakaldayo wa Eloah ni Elahh. Muundo wa Wakaldayo wa Elohim ni Elahhin. Elahh unakubaliana kuwa hakuna uwingi kabisa na Elahhin kwenye mwonekano wa uwingi anaowafunika Elahhin wote kama wana wa Elahh. Wakaldayo kwa sababu ya Kiaramu cha Kimashariki na Kiebrania waliendeleza Kiaramu cha Kimagharibi.

Kiaramu cha Mashariki kiliendelezwa kwenye Kiarabu. Hiyo ndiyo ilikuwa ni sababu iliyopelekea neno Allah' litumike kwenye Korani ili kuwaonyesha waamini Utatu kwamba hakukuwa na uwingi kabisa kwenye jina la huyu Mungu wa Pekee wa Kweli. Maneno ya Eloahh, Elahh, na Allah’ yanataja Uweza au Mungu, ambaye ni ndiye Mungu Mmoja, na wa Kweli. Korani kama ilivyo kwenye Biblia, haina tatizo na Elahhin, au Elohim, wakiwa ni ana wa Mungu. Kosmolojia ya Kikaldayo ilikuwa inafanana sana kama ya Kiebrania na ya Ibrahimu alichukuliwa kama mfalme wa Elohim kama tunavyoona kutoka kwenye maandiko ya Kiebrania kwenye Mwanzo 23:6 ambapo yeye ni mfalme wa elohim. Danieli anatumia Kikaldayo kuwaelezea wana wa Mungu pia. 

 

Inakuwa wazi sana kwamba huduma ya Armstrong na teolojia yake havikuendana na maana na muundo wa majina ya Mungu na Malaika zake. Ala hawakuelewa utaratibu wa Hekaluni na kwa hiyo hawakuweza kuendananayo kisawasawa na muundo wa Waamini Mungu Mmoja, yaani wa Kimonotheist, ambayo ni wajibu au kazi ambayo inabidi ifanye na Makanisa ya Mungu na Mashahidi katika Nyakati za Mwisho. Herbert Armstrong alikusudia sana kujitangaza yeye mwenyewe kuwa ni shahidi mkuu na kuwa yeye ni nabii Eliya ajaye kuliko kuelea au kuijua kweli na umuhimu wa Mpango wa Mungu. Huo ndio ulikuwa ubatili uliotiwa moyo na kuungwa mkono na uchanga wake, ambao msimamo wake ulihusiana na makosa au upotoshaji ambao tumeuona pia uliendelezwa hapa (soma kwenye majarida ya Je, ni Eliya? (Na. 233) na Kweli 18 Zilizorejeshwa za Herbert W. Armstrong (Na. 233B)).

 

Kristo mwenyewe analitangaza Hekalu la Yerusalemu kuwa ni Nyumba ya Baba yake. Ni la Mungu wa Kristo na Baba yake (Yohana 20:17) ambaye ni Mungu wa taratibu za huduma za Hekalu kwa vipindi vyote viwili, yaani Agano la Kale na Jipya. Hakuna shaka kwamba Israeli walijua kuwa Hekalu ni Nyumba ya Mungu mmoja, wa Pekee na wa Kweli na kwamba elohim wa Israeli alikuwa ni msaidizi wake ambaye ndiye alikuwa mjumbe wa Elyon aliyewapa wao torati mlimani Sinai, na Kristo na mitume waliunena ukweli huo (linganisha na 1 Wakorintho 10:4).

 

Kwenye Yohana 2 aya ya 13, Kristo na wanafunzi wake alisafiri kwenda Yerusalemu kwenda kuishika sikukuu ya Pasaka. Ilikuwa hapa kwamba anatangaza kwamba Hekalu la Yerusalemu ni Nyumba ya Baba yake, na alilisafisha Hekalu kwa kuwafukuza waliokuwa wanafanya biashara ya kubadilisha fedha na wanyama (aya za 14-16). Kristo alikuwa na wivu wa Nyumba ya Baba yake, kama Yohana 2:17 ilivyoinukuu Zaburi 69:9.


Yohana 2:13-17 (tafsiri ya Complete Jewish Bible [Biblia Kamili ya Kiyahudi]).
13 Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; naye Yesu akakwea mpaka Yerusalemu. 14 Akaona pale hekaluni watu waliokuwa wakiuza ng'ombe na kondoo na njiwa, na wenye kuvunja fedha wameketi. 15 Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng'ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao; 16 akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, Yaondoeni haya; msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara. 17 Wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa imeandikwa, Wivu wa nyumba yako utanila.

 

Ayubu 33:23 inamtaja Mmoja wa maelfu ambao walimkomboa Ayubu. Kiumbe huyu anaonekana pia kwenye Mwanzo 48:15-16 kama elohim aliyetembea pamoja na Mababu wa imani na ndiyo waliomlisha Yakobo na ambaye Yakobo alimsema kuwa alikuwa ni Malaika aliyemkomboa yeye. Hawa elohim ni wana wa Mungu. Elohim wa Yaboko alikuwa ni mjumbe wa Mungu wa Pekee wa Kweli na Biblia inaonyesha kwamba ili kuwa hivyo kwenye hatua ya mwazoni sana ya maandiko.

 

Kwenye Waebrania 1:8-9 tunajua bila shaka kwamba kiumbe huyu anayetajwa kwenye Zaburi 45:6-7 ni Kristo kama elohim lakini alikuwa elohim aliye juu yake kama Elohim wake au Mungu wake na kwamba pia ana wenzake hawa au ndugu zake ambao walikuwa ni sawa na yeye lakini aliye juu yake yeye aliyemtia mafuta. Alikuwa ni nani basi?

Wao wangali bado ni ndugu zake au washirika wake. Biblia inatuambia ni akina nani hawa na sio wanadamu kama hawa Waditheists wanavyojaribu kudai. Wafuasi wa Armstrong walioamini Uditheism, kama vile kina Frank Nelte, (na Wabinitarians) wanajaribu kulitenganisha neno chabbar iliyotafsiriwa kuwa Wenzake na Ndugu zake kuwa hayana maana sawa kwenye Kiingereza na kwa kweli inaibua madai haya ya uwongo ya kwamba wao ni wafuasi wake wa kimwili.

 

Hata hivyo, neno hili lilikuwa sawa na la Kiyunani kwenye tafsiri za maagano yote mawili, yaani Agano la Kale na Jipya. Wanazuoni wote wanakubali kwamba chabbar (SHD 2271) linafanana kikamilifu sana na Kiingereza ambalo linakubaliana na lile la Kiyunani lililotumiwa. Ina maana ya washirika, au marafiki. Linatokana na neno ambishi la msingi la chabar (SHD 2266). Kiambishi hiki cha “kuambatana na”, au “kujumuika”, au “kujiunga pamoja, au kwenye shingano”. Kwenye kila matumizi ya maneno yatokayo kwenye mzizi wa neno humaanisha wenzake au washirika au marafiki. Hakuna ubahatisho mwingine au matumizi na mlingano wa Kiingereza unbeba maana yake vizuri sana.

 

Neno lake la Kiyunani ni metoxous (SGD 3353). Kiyunani kina maana yake maalumu ya mshiriki ambayo imechukuliwa kwayo na maana ya mshirikishwaji na kwa kumaanisha mshiriki ambaye ni mwenzake, mrithi au rafiki. Tafsiri ya kionyesha dalili humini yake bashara e Greek has a specific meaning of a participant which carried with it the meaning of a sharer and by implication the LXX inatumia neno hilohilo kwenye tafsiri na Brenton analitafsiri kama wenzake na tafsiri ya Agano Jipya inasema kuwa ni marafiki (Knoch, na Marshall's Interlinear) na ndugu  (kwenye tafsiri za KJV, RSV).

Neno hili la Kiyunani linauhusiano halisi kwenye Kiingereza kama ilivyoelezewa hapa na Kiebrania kina uhusiano kama huo huo kamili. Neno hili la Kiebrania lina maana yake maalumu kutoka kwenye chanzo maalumu na kudai kwamba halifanani kwenye Kiingereza ni maezo yenye uwongo mkubwa. Madai ya kwamba halifanani hayana mashiko kwenye lugha au si ya kweli. Wahubiri watasema wazi kabisa kitu chochote ili ili kugeuza maandiko matakatifu ili kuyafanya yaendane na mafundisho ya uwongo ya Armstrong.

 

Kwa hiyo, kwenye andiko hili, Kristo anaonyeshwa kuwa ana marafiki au ndugu walio pamoja naye ambao walishiriki nafasi yake na zaidi ya yote ni kwamba alichaguliwa na kutiwa mafuta. Umuhimu mkubwa wa suala hili kimsingi ni kwamba haezi kuwa wakati wote juu yao. Alikuwa ni mmoja wao hadi alipotiwa mafuta kuwa yu juu yao. Kwa hiyo, hawa ni kina nani?

 

Ni wazi kabisa kuwa wapo kwenye 1Petro 3:21-22 kwamba kutiwa mafuta kwa Kristo kulifanyika baada ya kufufuliwa kwake na Baba yake, akapaa mbinguni akiifanya sadaka yake ikubaliwe na baba, na kisha akaketi mkono wa kuume wa Baba yake. Hili limekubalika na wasomi au wanazuoni wote wa Biblia.

 

1Petro 3:21-22  Mfano wa mambo hayo ni ubatizo, unaowaokoa ninyi pia siku hizi; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo.22 Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu, amekwenda zake mbinguni, malaika na enzi na nguvu zikiisha kutiishwa chini yake.

 

Kuinuliwa huku kumefanyika tangu kufufuka kwake Kristo kutoka kwa wafu. Alifufuka na kuinuliwa juu zaidi ya wana wengine wote wa Mungu, kama tutakavyokwenda kuona hapo chini.

 

Kutoka kwenye Kumbukumbu la Torati 32:15-17 tunaona kwamba alikuwa ni Eloah ambaye alikuwa ni Mungu aliyewaumba wao, na ni Mungu ambaye walimtolea sadaka. Kwenye aya ya 8, Eloah Baba, ni Mungu Aliye Juu Sana aliyeyaweka mataifa na kwenye aya ya 9 aliwatoa Israeli na kumpa Bwana wetu Yesu Kristo. Kwenye Kutoka 34:5-6 tunauona mfano ambapo Kristo alipaa mawinguni na akasimama pamoja na Musa, na kisha akapita mbele ya Musa, na akatangaza “Bwana, Bwana Mungu"...

Hakuwa anajitangaza mwenyewe; alikuwa anamtangaza Baba mbele ya Musa, ni Baba yule yule ambaye Musa alimuita kuwa Eloah kwenye Kumbukumbu la Torati 32. Kwa hiyo tunaposoma kwenye Kutoka 20:3 tunaona kuwa kwa kweli Israeli walijua kwamba kulikuwa na Mungu Baba au Mwenyezi ambaye alikuwa ni juu ya Kristo kwa kuwa Kristo alikuwa amejidhihirisha mwenyewe kwao. Kristo alikuwa ni taswira ya utukufu wake. Bodi yote mzima ya taifa la Israeli walijua kuwa kiumbe aliyeongea nao pale Sinai alikuwa ni Malaika wa Bwana ambaye alimdhihirisha au kumwakilisha Elyon, Mungu wa Israeli kwao. Huu ni mtazamo wa kila wakati wa Makanisa ya Mungu kwa zaka kadhaa zilizopita.

 
Kwenye Ezra 7:21 torati inaonekana pia kama ni sheria ya Elahh (SHD 426 Chald.) ambaye ni Eloah (SHD 433) anayetajwa mahala pengine popote kwenye maandiko na Ezra. Yeye ni Mungu Mkuu. Kwa hiyo ile amri inayosema: "Usiwe na miungu mingine ila Mimi" ni amri ya Mungu Baba, Mungu wa Pekee na wa Kweli wa Mbinguni na Duniani.


kumbukumbu la Torati 32:8 inaonyesha kwamba Elyon alikuwa ni Mungu aliyeyatenga mataifa na kuwapa wana wa Mungu. Kuna Mungu mmoja tu Aliye Juu sana naye siye Kristo kwa maana hii. Kristo siyo Eloah wa Mbingu na Dunia. Kiumbe huyu anaweza kuwa ni Mungu tu ambaye ni Baba. Baba, Elyon, aliwatoa Israeli na kumpa Elohim ambaye alikuwa ni Kristo. Andiko hili liliteuzwa au kutotoshwa na jopo la Sopherim baada ya kuanguka kwa Hekalu ili kuvunja moyo fundisho la wokovu wa Wamataifa na nafasi ya Kristo kama Yahovah wa Israeli. Kwa hiyo walighushi andiko hili ili lisomeke sawasawa na idadi ya wana wa Israeli badala ya sawasawa na idadi ya wana wa Mungu. Hawa walikuwa thenashara zaidi ya kuwa 70[na wawili] wa wana wa Mungu kama ilivyoonekana pia kwenye baraza la wazee, ambalo linawaashiria wao. Baraza hilo lilikuwa ni la Sanhedrin lililowekwa Waisraeli huko Sinai ili kuwakilisha serikali ya Mungu kama Kristo alivyomuonyesha Musa.

 

Uhusiano kati ya Baba kama Yahova a Majeshi na Kristo kama Yahova wa Israeli unaonekana kwenye Zekaria sura ya 2:7-12:


7 Haya! Ee Sayuni, jiponye, wewe ukaaye pamoja na binti Babeli. 8 Kwa maana Bwana wa majeshi asema hivi, Ili nitafute utukufu amenituma kwa mataifa wale waliowateka ninyi; maana yeye awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake. 9 Kwa maana, tazama, nitatikisa mkono wangu juu yao, nao watakuwa mateka ya hao waliowatumikia; nanyi mtajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma. 10 Imba, ufurahi, Ee binti Sayuni; maana, tazama, ninakuja, nami nitakaa kati yako, asema Bwana. 11 Na mataifa mengi watajiunga na Bwana katika siku ile, nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yako, nawe utajua ya kuwa Bwana wa majeshi amenituma kwako. 12 Na Bwana atairithi Yuda, iwe sehemu yake katika nchi takatifu, naye atachagua Yerusalemu tena.

 

Kumbuka kuwa kiumbe huyu mdogo hapa ananena kwa niaba ya Yahova wa Majeshi na alisemekana kuwa Yahova wa Majeshi alimtuma yeye kuwalinda. Kwa hiyo Yahova wa Majeshi anamtambua yeye na anamtuma kuwashughulikia wale wanaoigusa mboni ya jicho lake. Kwa kweli Bullinger aliliainisha kwamba andiko hilo kama “mboni ya jicho langu” kwenye bango kitita la andiko hilo lenyewe. Yahova msaidizi wa Israeli anaonyekana kuwa ni kama elohim wa Daudi na kuwaongoza ateule waonekane kama Malaika wa Yahova vichwani mwao kwenye Zekaria 12:8.


Zekaria 12:7-8 [7] Naye Bwana ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili utukufu wa nyumba ya Daudi, na utukufu wa wenyeji wa Yerusalemu, usipate kutukuzwa kuliko Yuda. 8 Katika siku hiyo Bwana atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Bwana mbele yao.   

Huyu elohim ni Malaika wa Bwana akiiongoza nyumba ya Daudi atakayefanyika pia kuwa elohim.

sasa, wahuriri wa lililokuwa kanisa la WCG hawakulifundisha KABISA andiko hili au andiko lililoko kwenye sura ya 2. Iliharibu kabisa dhana yao na kwa hiyo waliachana nalo na kujikita kwenye kile ambacho Agano la Kale lilisema. Pia walipuuzia ukweli wa kwamba hawa ndugu au marafiki wa Kristo walijulishwa kwenye Ufunuo sura ya 4 na ya 5. Mzunguko wa ndani wa wale 70 ulikuwa ni thelathini ambao ulikuwa umeashiriwa au kuonyeshwa kwenye Hekalu la Eloah huko Yerusalemu. Karibu na kiti cha enzi cha Eloah kulikuwa na Makerubi au viumbe wenye uhai wanne. Kulikuwa ni makerubi wenye vichwa vya Tai upande wa Kaskazini, kerubi mwenye kichwa cha Dume la ng’ombe upande wa Magharibi, kerubi mwenye kichwa cha Simba upande wa Mashariki na kerubi mwenye kichwa cha Mwanadamu upende wa Kusini. Makerubi hawa wawili wa mwisho waliasi na hukumu yao na kuchukuliwa kwa nafasi zao kumewekewa taswira kwenye mapambo ya Hekaluni sambamba na Mtende ambao ulikuwa unamwakilisha Kristo na utambulisho wao unaonyeshwa kwenye andiko la Kiebrania ya Agano la Kale. Upya au Kerubi aliyezibaji hombwe n kina Ibwahimu na Musa. Walikuwa ni watumishi tu wa Mungu ambao waliitwa kuwa elohim kwenye maandiko (soma Mwanzo 23:6 kwenye lugha ya Kiebrania na Kutoka 4:16; 7:1).


wazee ishirini na nne wenye Mataji zilizovikwa na kusimama mbele za Mungu wamewakilishwa na makuhani wakuu ishirini na wanne wa Hekalu ya Yerusalemu. Walisimama mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na Mwanakondoo yuko pale akiwa kama wa ishirini na tano na Kuhani Mkuu mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Hawa ni washirika wenzake Kristo ambapo yeye aliinuliwa juu ya wote hawa akiwa kama Kuhani Mkuu aliye mfano wa Melkizedeki. Hawa wote ni wana wa Mungu. Wanasema kwamba Kristo ametukomboa sisi, yikiwa ni wanadamu wateule, ili tuwe taifa la Wafalme na Makuhani na tutatawala hapa duniani. Hawa ni marafiki washiriki wa Kristo ambao mbele yao Kristo anatukiri kama tulivyoona kwenye Zaburi 82:1-6 na wote hao ni wana wa Yeye Aliye Juu Sana (Elyon) kama wana wa Mungu (Kumbukumbu la Torati 32:8; Ayubu 1:6; 2:1; 38:4-7; Luka 12:8). Elohim wa Israeli yu pamoja na elohim (Zaburi 86:8). Andiko hili liliaminika kuwa linawajata waamuzi wa Israeli na baadhi ya Waamini Utatu, na wanafunzi waliofundishwa na Armstrong na kuamini imani ya Kiditheist. Hata hivyo, Kristo hakua na sehemu kabisa kwenye baraza la Sanhedrin au kama hakimu. Baraza hili ndil lenyewe lililotajwa kwenye Ufunuo 4 na 5. Wanazuoni ndiyo kwa hakika una ushauri kwamba Baraza la elohim lililo kwenye Zaburi ni lile lililo mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na ni wengi.

 

Ikitokea kama kuna mashaka yoyote kama kwa jinsi alivyo na hai ya kwamba ni Malaika wa Yahova awaongozaye Israeli kwenye Zekaria 12:8 mtu anaweza kusoma tu kwenye andiko linalofuatia ambalo linamtaja Masihi na unabii wake akiwa amechomwa mkuki na anapoyashughulikia mataifa ambayo yanakuja kuikabili Yerusalemu. Hakuna shaka kwamba kiumbe huyu ni msaidizi wa Elohim wa Israeli.

 

Zekaria 12:9-14 9 Hata itakuwa siku hiyo, ya kwamba nitatafuta kuwaangamiza mataifa yote watakaokuja kupigana na Yerusalemu. 10 Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza. 11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido. 12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao; 13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao. 14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao.

 

Huyu ni Masihi. Yeye ni msaidizi wa Elohim wa Israeli na Malaika wa Uwepo wake aliyemkomboa Yakobo.

 

Mwanzo 48:14-16  Israeli akanyosha mkono wake wa kuume akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, aliyekuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto akauweka juu ya kichwa cha Manase, huku akijua atiavyo mikono; maana Manase ndiye aliyezaliwa kwanza. 15 Akambariki Yusufu, akasema, Mungu ambaye baba zangu, Ibrahimu na Isaka, walienenda mbele zake, yeye Mungu aliyenilisha, maisha yangu yote, hata siku hii ya leo, 16 naye Malaika aliyeniokoa na maovu yote, na awabariki vijana hawa; jina langu na litajwe juu yao, na jina la baba zangu, Ibrahimu na Isaka; na wawe wingi wa watu kati ya nchi.

 

Hakuna siri na hakuna shaka ya yule tunayemsema. Malaika wa Ukombozi aliye kwenye Ayubu 33:23 na Mwanzo 48:15-16 ni mmojawapo wa ana wa Mungu, elohim anayetajwa kama Malaika wa Bwana.

 

Kuna Mungu Mmoja tu kwenye Yohana 17:3, aliyemtuma Yesu Kristo, na mtume Paulo anatuambia kwamba Mungu huyu ni kiumbe pekee ambaye hawezi kufa wala kupatwa ma madhara yoyote (1Timotheo 6:16).

 

Kwa hiyo, kumlinganisha kiumbe mwingine na huyu Mungu ni kukufuru. Kudai kwamba mwana wa Mungu, ambaye mwenyewe alidai kuwa anamtegemea huyu Mungu wa Pekee wa Kweli maishani au kwa kuishi kwake (Yohana 6:57), ni sawa tu na kuwa na yeye ni Mungu wa Kweli, anayetoa uhai kwenye vitu vyote (1Timotheo 6:13) ambavyo ni kukufuru kabisa.


kudai kwamba mwana wa Mungu naye ni Mungu tunayemwabudu mahali pa Mungu wa Pekee wa Kweli ni kufuru kubwa sana kwa kuwa Kristo alituambia tumwabudu Baba ambaye ndiye Mungu wake (Yohana 20:17).


Haya ni maneno yake kwenye Yohana 4:21-24:
21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu. 22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi. 23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu. 24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.


Kristo aliliweka wazi sana kwamba wamwabuduo wa kweli wamwabudu Baba. Wanamwabudu Baba katika roho na kweli, na Baba anawatafuta watu kama hao wamwabudu yeye.


Kristo alisema kuwa Wayahudi wamlijua waliyekuwa wakimwabudu na hawakuwa wanawaabudu wana wa Mungu; na walijua kuwa Hekalu lilikuwa ni Nyumba ya Mungu Baba.
Kristo aliliita Hekalu kuwa ni Nyumba ya Baba yake kwenye Yohana 2:16.


kwahiyo, kudai kwamba Kristo ni Mungu aliyetolewa sadaka na ni Mungu ambaye anapaswa kuabudiwa katika roho na kweli ni kufuru kubwa sana.

 

Ni kitu gani basi kilichomfanya Kristo atengwe mbali maalumu na wana wengine wa Mungu kwenye Jeshi la Malaika wa Mbinguni? Jibu lake ni kwamba alikuwa ameinuliwa juu kuliko wana wengine wa Mungu kwa kufufuliwa kwake kutoka kwa wafu na kuchaguliwa kwake kuwa Kuhani Mkuu wa Wateule na Malaika wa mfano wa Melkizedeki. Tutakuwa wote elohim (Yohana 10:34-35) na kufaana na Malaika (SGD 2465 yaani. SGD 2470 + SGD 32 sawasawa au kama malaika) (Luka 20:36; Mathayo 22:30; Marko 12:25) ambao ni elohim pia kwa hiyo nan i kama wana wa Mungu na Baraza la elohim aliye kwenye maandiko ya Agano la Kale. Kristo atatukiri sisi mbele ya malaika hawa wa Mungu (Luka 12:8). Wametajwa kuwa ni wana wa Mungu kwa maeneo mengi mbalimbali kwenye Agano la Kale na sisi tulio wana wa Mungu tutakuwa kama elohim kama ilivyoelezwa kwenye maagano yote mawili, la Kale na Jipya. Wataletwa na Kristo hapa duniani atakaporudi (Mathayo 13:41; 25:31). Kristo anatukiri mbele yao ili kwamba tuweze kukubalika katikati yao kama elohim.

 

Tatizo lililopo kwenye imani za Kiditheism na Kibinitarianism ni kwamba mafundisho ya uwongo yametafuta kumuinua juu Kristo zaidi ya wana wengine wa Mungu na kuanzisha upotofu ambao umeingizwa imani ya Kikristo na wafuasi wa mungu Attis wa huko Roma na ambayo haikuwahi kuwepo kabisa hadi kufikia mwaka 170 BK. Uditheism wa Armstrong haukuwa KABISA sehemu ya mafundisho ya Kanisa la Mungu kwa kipindi chake chote cha miaka 1900 kabla hajaanzisha kufundisha uzushi huu. Ubinitariani ulikuja kutoka kwa waabudu mungu Attis wa huko Roma yapata mwaka 170.

 

Tunaweza kuonyesha ukweli huo kwa kuainisha Teolojia ya Kanisa la Kwanza na nyaraka na rejea za maaskofu waliofundishwa na kanisa huko Smirna kama vile akina Polycarp, Irenaeus na Hippolytus ambani ni Waamini wahafidhina wa Uyunitarian. Hata mwanateolojia mashuhuri Mtrinitarian anakubali kabisa kuwa Kanisa la Kwanza lilikuwa ni la Mrengo wa Kiyunitarian. Kwa kushughulikia maandiko yahusuyo Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu na kuonyesha kutokuwa na mashaka kwamba Smirna ilifundisha wanateolojia na kwamba walikuwa ni wa Imani ya Uyunitarian ya Biblia, Waditheist hawa waliongezea malumbano au hoja ya uhominemu kama vile hivi ifuatavyo:

·   Kwa kuwa wanazuoni na wasomi mahiri wa Kitrinitaria kama vile kile kina Calvin na Harnack wanatangaza hadharani kwamba kanisa la kwanza lilikuwa ni la mrengo wa Kibiblia wa Kiyunitarian wanaweza kupuuzwa kwa kuwa wao ni Watrinitarian. Vivyohivyo Brunner anayeuonyesha ukweli huo na kukubali naye pia hakuaminika kwa kushambuliwa na nyongeza ya hominemu. Ukweli wa kwamba Mwanateolojia wa Kittinitarian ni mwaminifu vya kutosha kiasi cha kukubali kwamba kanisa la kwanza lilikuwa ni la mrengo wa Kiyunitarian ni kwa heshima yake. Mashambilizi ya hominemu ya wahubiri hawa waliofundishwa na Armstrong wanalaumiwa kiasi cha kuhuzunisha na watu kujiuliza kuhusu uadilifu wao wa kiakili.

·   Mwonekano wa Uyunitarian kwa maaskofu waliofundisha huko Smirna kunaelezewa kama hivyo na mashambulizi ya kihominemu kwa ukweli kwamba walihusika kwenye malumbano ya Kuartodecimen mnamo mwaka 192 BK (soma kwenye jarida la Hoja za wakuartodecimen (Na. 277)). Irenaeus wa huko Lyon alikuwa Muumini mzuri sana wa Kiyunitarian kama alivyokuwa Polycarp aliyemfundisha na kama alivyokuwa Hippolytus, ambaye alifundishwa pia kwenye Shule ya Smirna chini ya Polycrates. Mmoja wa watu hawa hata alimshambulia Hippolytus kwa sababu ya kwamba alikuwa ni askofu wa Roma, kwa mujibu wa Wikipedia. Makosa na upotoe huo umeainishwa muda mrefu uliopita. Hippolytus hakuwa askofu wa Roma KABISA. Alichaguliwa kuwa askofu wa Ostia Attica, ambao ulikuwa ni mji wa bandari wa Roma umbali wa maili kadhaa nje. Aliwadharau maaskofu huko Roma na aliwashambulia wazi wazi na mara kwa mara.

·   Ili kuishambulia imani ya Kiyunitarian na kuutetea Uditheism, Nelte, kwa mfano, alianzisha malumbano ya mthafidhina na kumshambulia Anthony Buzzard teolojia yake ya Uyunitarian wa Kihafidhina wa Zama za Baada ya Matengenezo na alijaibu kudai kuwa Uyunitarian unapinga dhana ya kwamba Kristo alikuwepo hapa duniani hata kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi tukujuako wote wakati kuna aina moja tu maalumu ya Uyunitarian wa zama za Baada ya Matengenezo ambayo imaamini hivyo. Kuna idadi kadhaa ya Wayunitarian Wahafidhina kwenye imani ya kanisa la WCG na kwenye vikundi vilivyoibuka baada ya kufa kwa kanisa hili. Uyunitarian halisi wa Kibibia ulitangaza kwa nguvu zake zote dhana hii ya uwepo wa Kristo kwenye kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake rasmi duniani kama tuonavyo hapo juu (soma pia kwenye jarida la Uwepo wa Kristo Kipindi cha Kabla ya Kuzalia Kwake Rasmi Duniani (Na. 243).

 

Kushindwa kwa kiakili kwa kanisa la WCG na vikundi vilivyoibuka kutoka kwake ni kizuizi cha ukuaji wa Makanisa ya Mungu na inaonekana kuwa ni sababu iliyopeleka yaangamie. Imani yao ya Uditheism ni utani. Ubinitarian wao ni mbinu ya kuvukia kuelekea kwenye uzushi wa imani ya mungu wa Utatu ambaye amekuja kuibukia kwenye Ubinitarian wa mungu Attis. Watetezi wa kwenye vikundi hivi vilivyoibuka wanazidi kuendelea kwa kuyahuisha upya mafundisho potofu ya mungu Attis, Adonis, Osiris na Baali/ Mithra wa dini za waabudu jua na kuyaingiza kwenye Makanisa ya Mungu. Madai ya kwamba Kristo ameinuliwa juu ya wana wengine wa Mungu kama Jeshi la Malaika ni hoja inayoendelea ambayo imekuja ikitokea kwenye dini za waabudu jua na ambazo zilitumiwa na Wakatoliki wafuasi wa Athanasias kwenye Baraza Kuu la Mtaguso wa Nicaea mwaka 325 BK na ambayo ilikataliwa kwa kuonekana kama ni uzushi na Makanisa ya Mungu kwa kipindi cha karne kadhaa sasa. Mtazamo huo ulikataliwa na kuchukuliwa kuwa ni uzushi na ukatupiliwa mbali nje na kanoni zote za baraza la halmashauri kuu mwaka 327 BK.

 

Wahubiri hawa wa machipuko ya kanisa la WCG au watu mmoja mmoja wasiokubaliana walifanya makosa makubwa sana ya upotoshaji wakidai kuhalalisha kushindwa na makosa ya kanisa la WCG na imani za makanisa mengine yaliyoibuka kwenye kanisa hilo kwa kushindwa kurejesha upya maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi Mpya na Yubile na Mizunguko ya Miaka ya Sabato kwa kufuata Kalenda ya Hekalu. Wengine hata wamejaribu  kupinga kwamba kalenda ya Hekalu haikuwepo na kwamba utaratibu wa kalenda ya Hekaluni haukuwa na maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi kabisa, bali ilikuwa na maadhimisho ya Sabato peke yake. Tutaelezea mambo hayo mahali pengine. Wengine wamejaribu kudai kwamba utaratibu ulioko kwenye kalenda ya Hileli ndiyo ulikuepo kwenye huduma na shughuli za Hekaluni na kwamba ndivyo alivyoshika na kuadhimisha hata Kristo. Madai haya ni ya uwongo nan i ya kujihesabia hakitu wao wenyewe. Hayana misingi yoyote kwenye ukweli wa kihistoria.

 

Herbert Armstrong alithibika kuwa ni nabii wa uwongo nan i kiongozi asiyeelea mambo yalivyo na ukweli wake (soma pia kwenye majarida ya Unabii wa Uwongo (Na. 269) na lile la Imani ya Kiditheism (Na. 076B)). Hakuwa amewekwa wakfu kabisa na afisa yeyote wa Kanisa lililojulikana kama Church of God (Seventh Day). Alibatizwa na mhubiri mwaamini Utatu na akawekwa wakfu kwa kuwekewa mikono kwenye hema ya kukutania ya mchana kutwa. Kanisa lake la COG (SD) likamkubalia kwa kitambo kifupi sana baada ya hapo. Mamlaka na nguvu zake zilisababishwa au kuwezeshwa na waumini waliobatizwa ambao walimwekea mikono, kwa maana ya kwamba Mungu alikikubali kitendo kile. Hakuwa na sifa za kawaida zainazotambulika. Historia ya maisha yake ya huko nyuma inathibitisha mambo haya. Teolojia yake ya Uditheism na madai vinaonyesha ukweli huo, ni kama wanavyofa pia wafuasi wake kwa namna ya madai wanayoyafanya pia, kama yalivyoonyeshwa hapo juu. Ufafanuzi uliopo hapo juu hauna nia ya kumpakazia au kumdhalilisha. Bali ni maelezo tu yenye ukweli. Mamlaka na nguvu za Makanisa yote ya Mungu yanatokana na katiba iliyothibishwa na kukubaliwa na waumini waliobatizwa wanaounda shirika, chini ya mamlaka ya Agano Jipya waliyopewa na Kristo ya kufunga na kuachilia au kusamehe. Makanisa ya Mungu yana historia yake ya mafundisho ambayo yamekanunishwa na kanisa la WCG pamoja na machipuko yake ni wa imani za Kiditheisn tu kwenye historia yetu yote.

 

Madai ya uwongo ya Wabinitarian na Watrinitarian yanaweza kuonekana kwenye jarida la Makosa ya Kimahubiri ya Wabinitarian na Watrinitarian Kuhusu Teolojia ya Mwanzo ya Uungu (Na. 127B).

 

Soma pia jarida la  Biblia (Na. 164) kwa rejea zaidi za maandiko.

                                                                                                                                    q