Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[084]

 


 


 

Hivi Hamjui?

(Toleo La 1.5 20020731-20110326)

 

Kifungu kisemacho “hivi hamjui au hamfahamu” kimetumika mara 15 kwenye Agano Jipya. Jarida hili linatathmini maana yake na kilichomgusa mwandishi na kuona kuwa ni muhimu kijulikane na waumini wa Kanisa la kwanza.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Hatimiliki © 2002, 2011 Dave Treat, ed. Wade Cox)

(rev. 2011) (tr. 2015)

 

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Hivi Hamjui?

 


Paulo alitumia usemi wa “hivi hamjui ya kuwa” mata kumi na tatu kwenye nyaraka zake kwa makanisa ya Warumi na Wakorintho. Alikuwa anaonyesha kushangazwa kwake kwa alichoshangaa kugundua kuwa alikuwa analazimika kuwafundisha tena mafundisho ya msingi ambayo alidhani kwamba walikuwa wanayajua vizuri sana. Ni mafundisho yapi basi haya na yanaweza kutuathirije sisi leo? Kama tujuavyo kuwa Mungu habadiliki, yatupasa tufikiri mambo ambayo Paulo alikuwa anayataja na jinsi yanavyofanana na siku zetu sisi za leo. Hebu na tuzipitie aya zenye maneno haya ili tujue kile alichokuwa anajaribu kukisema Paulo.

 

Aya ya kwanza yenye maneno haya ni Warumi 6:3 inayosema:

Warumi 6:3 Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

 

Tumeweza kuona kwenye dhana muhimu ambayo kwamba usemi huu umetokana kwao ili kuweka maana yake. Warumi 6:1-13 inasema:

Warumi 6:1-2 Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi? 2 Hasha! Sisi tulioifia dhambi tutaishije tena katika dhambi?

 

Kumbuka kuwa ni Paulo ndiye asemaye hapa. Tunawezaje kuwa wafu katika dhambi na huku tukiwa tunaishi kwa wakati huohuo? Ni kama dhambi inaishi ndani yetu ama la. Haiwezekani kabisa kuwa ni mtu wa namna mbili zote.

Warumi 6:3-13 Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? 4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. 5 Kwa maana kama mlivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake; 6 mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena; 7 kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi. 8 Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; 9 tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. 10 Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. 11 Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu. 12 Basi, dhambi isitawale ndani ya miili yenu ipatikanayo na mauti, hata mkazitii tamaa zake; 13 wala msiendelee kuvitoa viungo vyenu kuwa silaha za dhuluma kwa dhambi; bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama walio hai baada ya kufa, na viungo vyenu kwa Mungu kuwa silaha za haki.  

 

Kitabu cha tafsiri kijulikanacho kama Matthew Henrey’s Commentary kwenye aya ya 3 inasemaon:

Ubatizo hufundisha umuhimu wa mfu katika dhambi, na kwa huo tukazikwa kutokana na mambo yote machafu na yasiyompendeza Mungu na kutoyafuatilia tena mambo machafu na kuanza kutembea na Mungu kwenye upya wa uzima. Maprofesa waovu na watenda dhambi yawezekana kuwa walikuwa na ishara za nje za kufa dhambini, na za kuzaliwa upya kwenye haki na utakatifu, bali hawakuweza kamwe kupita kutoka kwenye familia ya Shetani hadi kwwenye ile ya Mungu. Asili ya dhana au wazo liitwalo mtu wa kale, ni kwa kuwa lilitoholewa kutokana na baba yetu wa kwanza, Adamu, na mtu huyo wa kale alisulibiwa pamoja na Kristo, kwa kila muumini wa kweli, kwa neema iliyotolewa pale mtini. Imedhoofishwa na katika hali ya kufa, kwayo, ila angali anajitahidi kupambana bado awe mzima, na hata ikiwezekana ashinde. Lakini mwili wote wa dhambi, kwa vyovyote vile hauzipendi sheria za Mungu, basi unapasa kuondolewa, ili kwamba muumini asifanyike tena kuwa mtumwa wa dhambi, ila aishi katika Mungu, na kumtumikia kwa furaha.

 

Kumbuka rejea yake kwa ukweli kwamba mwili wa dhambi kwa namna yoyote ile si sehemu ya sheria takatifu na wala hauipendi. Katika siku za Paulo vuguvugu la imani ya Wanostiki lilikuwepo na lilikuwa imara. Moja ya mafundisho makuu ya imani ya Wanostiki lilikuwa ni kwamba torati ya Mungu haifai na kama mtu akiishika anakuwa wa mwilini zaidi. Ili kupambisha juu nia yao ya kutamani na kupenda mali za kidunia, basi inampasa mtu ajitenge kabisa na torati. Hili ni jambo moja ambalo Paulo analifanya hapa anaposema, “Tufanye dhambi ili neema iongezeke?” Neema pekee bila torati ilikuwa ndiyo mtazamo na imani ya Kinostiki na Kiantinomia na waliyaingiza mafundisho haya au kuyapenyeza kwenye kanisa la kwanza na Paulo alikuwa anayapinga mafundisho haya.

 

Hatuwezi kujitosa kwenye tama za dunia na kutenda upotoe na tukadhani kuwa tumefunikwa na neema ya Mungu. Tunatenda dhambi sote na kupungukiwa na utukufu wa Mungu, ila hii haitupi leseni ya kutenda dhambi, kama wanavyomini Wanostiki wahafidhina. Tufanyapo dhambi yatupasa kuomba msamaha na kuenndelea mbele. Hatuendelei kwenye dhambi hiyohiyo kwa jinsi ya mwenendo na matendo yetu. Tumebatizwa kwa mauti ya Kristo. Mtu wa kale haishi tena. Sisi tu kiumbe kipya na tunapaswa kuhakikisha kuwa matendo yetu na nia zetu ni vitu vipya pia. Habari njema ni kwamba nasi tumebatizwa pia kwenye maisha yake. Kama tutavumilia na kuishinda dhambi kutupeleka mbali na ukamilifu maishani mwetu, basi tutaurithi uzima wa milele au Aionian ambao Mungu ametuahidi. [nano hili limetafsiriwa kwa Kiingereza kama “eternal” au “milele” kwenye mifano yote kwenye lugha ya Kiyunani.]

Warumi 6:16 Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii, mmekuwa watumwa wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti, au kwamba ni utumishi wa utii uletao haki.

 

Ili kuielewa aya hii vizuri yatupasa kuziangalia aya zinazoizunguka. Aya za 15-19 kwenye Biblia ni Msingi unaosomeka kwenye lugha ya Kiingereza:

Warumi 6:15-19 Ni nini basi? Tufanye dhambi kwa sababu hatuwi chini ya sheria bali chini ya neema? Hasha! 16 Hamjui ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii, mmekuwa watumwa wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti, au kwamba ni utumishi wa utii uletao haki. 17 Lakini Mungu na ashukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mliitii kwa mioyo yenu ile namna ya elimu ambayo mliwekwa chini yake; 18 na mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki. 19 Nasema kwa jinsi ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wa miili yenu. Kwa kuwa kama mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi mpate kuasi, vivyo hivyo sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate kutakaswa.

 

Tena tunaona kutajwa kwa imani ya Kinostiki kwamba neema imechukua mahala pa sheria na sheria imetanguka. Mtume Paulo  anaonyesha ukweli kwamba kwa kuwa tupo kwenye kipindi cha neema, haituondoi sisi kutoka kwenye majukumu yetu au wajibu wetu wa kuishika sheria kama ananyoonyesha kwenye aya ya 15.

 

Wengi wetu tuliona kilichotokea wakati Kanisa la Mungu kwenye karne ya 20 liliamua kuwa hawakupaswa wala kuhitajika kuzishika sheria. Kanisa lile lilitapikwa kutoka kwenye kinywa cha Mungu, lilitawanyikiambali na viongozi wake waliuawa kipindi cha majuma 40 tu baada ya kutangaza tangazo hili la wazi.

 

Hatuwi chini ya sheria wakati tunapokuwa tukizitii tu. Wengi hujaribu kudai kwamba Paulo aliitangua torati kwa kupitia maandiko yake haya. Wengi wa “Wakristo” mamboleo wanamtaja yeye wakati wanapotoa hoja zao kupinga ushikaji wa sheria za torati. Ni kama tu Paulo alikuwa mwendawazimu, vinginevyo asingeweza kabisa kusema kabisa kuwa torati imetanguka na haina umuhimu tena, kwa kuwa kama tuonavyo kwenye aya zinazofuatia, anapingana moja kwa moja na wazo hilo.

Warumi 7:12 Basi torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya haki, na njema.

 

Tuliona kwenye aya ya 15 ya sura ya 6 kuwa Paulo anatuambia tusiendelee na dhambi. Dhambi ni nini? Ni kitendo cha kutangua au kuvunja sheria za torati. Kama hatuzivunji sheria basi tunatenda dhambi na kwa hiyo hatuyafuati mafundisho ya Paulo au ya Kristo yaliyosema:

 Matthew 5:17 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.

 

Watu wanaojaribu kuyatumia maandiko ya Paulo ili kuhalalisha msimamo wao wa Kiantinomia au hali ya kutoshika sheria, wanafanya hivyo kwa uvunjifu wao wenyewe. Mtume Petro aliandika kwenye 2Petro 3:15-18:

2Petro 3:15-18 Nanyi uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa; 16 vile vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo; katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe. 17 Basi, wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu. 18 Lakini, kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu una yeye sasa na hata milele.

 

Paulo anakuwa ni mmoja wa watu walionukuliwa sana kati ya watu na mitume waliowahi kuishi hapa duniani.

Warumi 7:1 Ndugu zangu, hamjui (maana nasema na hao waijuao sheria) ya kuwa torati humtawala mtu wakati anapokuwa yu hai?  

 

Huu ni mkanusho wa moja kwa moja unaokusudia kupinga imani ya Kiantinomia na ukengeufu wake, hali na mafundisho yaliyokuwa yametapakaa nyakati za Paulo. Paulo anaendelea mbele kwa kusema kwenye aya za 2-25:

Warumi 7:2-6 Kwa maana mwanamke aliye na mume amefungwa na sheria kwa yule mume wakati anapokuwa yu hai; bali akifa yule mume, amefunguliwa ile sheria ya mume. 3 Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine. 4 Kadhalika, ndugu zangu, ninyi pia mmeifia torati, kwa njia ya mwili wa Kristo, mpate kuwa mali ya mwingine, yeye aliyefufuka katika wafu, kusudi tumzalie Mungu matunda. 5 Kwa maana tulipokuwa katika hali ya mwili, tamaa za dhambi, zilizokuwako kwa sababu ya torati, zilitenda kazi katika viungo vyetu hata mkaizalia mauti mazao. 6 Bali sasa tumefunguliwa katika torati, tumeifia hali ile iliyotupinga, ili sisi tupate kutumika katika hali mpya ya roho, si katika hali ya zamani, ya andiko.

 

Hii ni hatua ya kweli na halisi. Sisi tupo chini sheria ya roho, na sio ya waraka. Kristo aliongeza uweza wa kiroho kwenye torati ambao haukuwahi kuwepo hapo zamani.

Warumi 7:7-13 Tusemeje, basi? Torati ni dhambi? Hasha! Walakini singalitambua dhambi ila kwa sheria; kwa kuwa singalijua kutamani, kama torati isingalisema, Usitamani. 8 Lakini dhambi ilipata nafasi kwa ile amri, ikafanya ndani yangu kila namna ya kutamani. Kwa maana dhambi bila sheria imekufa. 9 Nami nalikuwa hai hapo kwanza bila sheria; ila ilipokuja ile amri, dhambi ilihuika, nami nikafa. 10 Nikaona ile amri iletayo uzima ya kuwa kwangu mimi ilileta mauti. 11 Kwa maana dhambi, kwa kupata nafasi kwa ile amri, ilinidanganya, na kwa hiyo ikaniua. 12 Basi torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya haki, na njema. 13 Basi je! Ile iliyo njema ilikuwa mauti kwangu mimi? Hasha! Bali dhambi, ili ionekane kuwa ni dhambi hasa, ilifanya mauti ndani yangu kwa njia ya ile njema, kusudi kwa ile amri dhambi izidi kuwa mbaya mno.

 

Haya ni maelezo mazuri sana yanayotoa mwelekeo mzuri tulionao kuhusu dhambi na matendo yake. Hata kwenye makanisa ya Mungu, dhambi haichukuliwi kuwa ni kitu kiovu kama inavyostahili. Mambo haya hayatushitui tena sisi kabisa. Ni mambo yanayokubalika kabisa kwenye jamii zetu kutoa au kuharibu mimba za vichanga na kuwa na familia za watu wa jinsia moja. Hali hii ya kuvumilia matendo ya dhambi inaziharibu jamii zetu na haitaweza kuvumiliwa milele. Basi na tusikutwe tukiwa na msimamo dhaifu au kuonea aibu dhambi. Itatupeleka upotevuni na kutuangamiza.

Warumi 7:14-25 Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi. 15 Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda. 16 Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema. 17 Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu 18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati. 19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 21 Basi nimeona sheria hii, ya kuwa kwangu mimi nitakaye kutenda lililo jema, lipo lililo baya. 22 Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani, 23 lakini katika viungo vyangu naona sheria iliyo mbali, inapiga vita na ile sheria ya akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya dhambi iliyo katika viungo vyangu. 24 Ole wangu, maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti? 25 Namshukuru Mungu, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.

 

Watu wengi, wanapobanwa sana, wanakubaliana na angalau amri sita, bali wanazichukulia nne za kwanza kuwa zinahusu tu mahusiano yetu na Mungu, jambo ambalo ni kosa. Paulo anasema kuwa sheria ni takatifu na kamilifu.

 

Sheria ndiyo kitu kinachoainisha au kuonyesha dhambi na hiki ndicho anachomaana Paulo. Asingeweza kuijua dhambi kama isingekuwa torati. Anataka kuzitii sheria, ila hata hivyi anatendadhambi kwakuwa mwili ni dhaifu. Ila kama asemavyo Paulo, hahukumiwi na adhabu ya mauti kwa kuwa anatamani kushika sheria moyoni mwake. Ni dhambi ndiyo ikaayo ndani yetu ambayo sasa inatupeleka kwenye hukumu ya mauti. Kristo amezifisha dhambi. Sote tunatenda dhambi, na kama isingekuwa kujitoa sadaka kwa Kristo, basi tungeupokea mshahara wa dhambi, ambao ni mauti. Kristo ametu0okoa kutoka kwenye hukumu hii kwa njia ya kujitoa kwake sadaka. Sasa tuko chini ya sheria ya roho na sio chini ya waraka. Kuwa kwetu chini ya roho ya sheria hakunaanishi kuwa hatuzitii sheria. Bali inamaanisha tu kwamba sheria sasa zimeandikwa mioyoni mwetu. Hatuzitii tena ssheria kwa kuwa tunazo tu bali, kwa kuwa tunazihitaji. Nia za mioyo yetu zimehuishwa upya kwa njia ya Roho Mtakatifu.

1Wakorintho 3:16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?  

 

Hebu na tuwe na mtazamo mzuri kwenye taswira kamili kwa kusoma 1Wakorintho 3:1-19 inayosema:

1Wakorintho 3:1-2 Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. 2 Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi,

 

Kanisa la Mungu katika karne ya 20 lilishindwa kutulisha nyama. Hatukuwa tayari kuila hadi sasa. Haikuwa hivyo hadi katika michache ya mwisho ambapo wengi wetu tuligundua kuwa tulipaswa kujibidiisha kuutunza wokovu sisi wenyewe; na kwamba hatuingia kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu kwa njia ya kujishikilia kingo za makoti ya wahubiri. Tangu tulipogundua hilo na tukaanza kusoma kwa bidii na makini, Mungu ametupa nyama nyingi sana inayohitajika na kuendelea kutufungua macho yetu kwenye kweli zaidi na zaidi.

1Wakorintho 3:3-4 3 kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? 4 Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu?

 

1Wakorintho 3:5-19 Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa. 6 Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. 7 Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. 8 Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe. 9 Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu. 10 Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. 11 Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. 12 Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.13 Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. 14 Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. 15 Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto. 16 Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi. 18 Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima. 19 Maana hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za Mungu. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao.

 

Sisi tu hekalu la Mungu na roho wake anakaa ndani yetu. Yatupasa kuwa waangalifu sana jinsi tujengavyo kwenye msingi uliowekwa na Mitume. Yatupasa kupambanua kati ya kweli na uwongo na kuhakikisha kuwa hatupotoshwi kwa mafundisho ya uwongo. Wajenzi ni watu waliopewa wajibu au jukumu la kufundisha na kuwaongoza watu wa Mungu. Wajenzi wanapaswa kuogopa kutumia vifaa vya ujenzi visivyofaa kwa kuwa vinaweza kuudhoofisha mfumo mzima wa ujenzi. Ili kuwa na jingo imara, inapasa msingi wake wapasa uwe imara na mgumu na kisha kila tabaka na awamu inayoendelea kujengwa kutoka hapo na kuendelea mbele yapasa ijengwe kwa malighafi nzuri. Vifaa vya ujenzi ni mafundisho ya kanisa, Mungu atatupima kwa kigezi cha uelewa wetu na kwa njia ya utii na uaminifu wetu kwenye mafundisho tunayofundisha na kujifunza. Mafundisho yote ya uwongo yataangamizwa ni wajibu wetu kama Wakristo kuhakikisha kabisa kuwa hatuliachilii au kuliruhusu hekalu linajisike kwa mafundisho ya uwongo na mapotofu.

1Wakorintho 5:6 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima?

 

Kwenye 1Wakorintho  5:1-13 tunasoma:

1Wakorintho 5:1-13 Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye. 2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo. 3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo. 4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu; 5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu. 6 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima? 7 Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo; 8 basi na tuifanye karamu, si kwa chachu ya kale, wala kwa chachu ya uovu na ubaya, bali kwa yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli. 9 Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi. 10 Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang'anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia. 11 Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang'anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye. 12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani? 13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu.

 

Mwili wa Kristo, watu wanaounda kanisa, wana wajibu wa kuhakikisha kuwa linafundisha vizuri. Iwapo sisi, kama mwili wa Kristo, tukimuachia mshirika yeyote, wakiwemo watumishi wahubiri wetu, kuenenda kwa makusudi kabisa kinyume na maagizo ya torati ya Mungu nasi tusifanye chochote, basi tutakuwa hatuyaishii mafundisho haya wala watuwajibiki kwa mujibu wa tulivyoagizwa na kuamriwa. Tumeagizwa sio tu kwa kundi, bali ni kwa kila mtu binafsi yake pia, agizo la kumuondoa mtu huyo kutoka kundini. Mwenendo wa dhambi ni sawa na saratani. Itaenea kwenye mwili mzima kama haitaondolewa. Yapasa kuondolewa ili kunusuru uhai na sehemu ya mwili iliyobakia.

 

Dhambi ni kama chachu. Inatakiwa kuwa na kiasi kidogo tu cha chachu ili kuchachusha donge zima. Tunaiondoa chachu ya dhambi mahali tulipo ili kulilinda kutaniko lote, bali pia ili mtu aondolewe ni budi ayaone au kuambiwa makosa yake na atubu. Kama hataamua kutubu ndipo ataachwa ili ahukumiwe kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Kama kwa namna nyingine, akiamua kutubu, ndipo atarejeshwa kundini na kuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu pe of leaven. It only takes a small amount of leaven.

 

Kwenye 1Wakorintho 6:2-3 tunasoma:

1Wakorintho 6:2-3 Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? 3 Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya?

 

Aya hii imepotoshwa kwa kutafsiriwa visivyo kwa wengine kumaanisha kwamba tutawahukumu malaika wote. Ni dhana potofu na uwongo kwa sisi kudhania kwamba tutawahukumu malaika waliobakia watiifu kwa Mungu. Malaika wanaotajwa hapa ni wale walioasi. Wakristo wa kweli wanakwenda kupewa wajibu wa kuuhukumu ulimwengu na malaika waasi kwa ajili ya matendo yao. Hatutapewa mamlaka kabisa ya kuwahukumu malaika watiifu ambao wanatuangalia na kutulinda sisi na maisha yetu yote.

 

Ni nni basi kilikuwa ni jambo la muhimu kumpelekea Paulo aandike hivi? Tunaona hilo kwenye 1Wakorintho 6:1-8.

1Wakorintho 6:1-8 Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu? 2 Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? 3 Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya? 4 Basi, mkiwa na mahali panapohukumiwa mambo ya maisha haya, mwawaweka kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika kanisa? 5 Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo, kwamba kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima, awezaye kukata maneno ya ndugu zake? 6 Bali mwashitakiana, ndugu kwa ndugu, tena mbele yao wasioamini. 7 Basi imekuwa upungufu kwenu kabisa kwamba mnashitakiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali kudhulumiwa? Maana si afadhali kunyang'anywa mali zenu? 8 Bali kinyume cha hayo ninyi wenyewe mwadhulumu watu na kunyang'anya mali zao; naam, hata za ndugu zenu.

 

Wapendwa waumini kwenye kanisa la Korintho walikuwa wanakwenda au kupelekana kwenye mahakama za wamataifa badala ya kuyapeleka mambo yao mbele za mkutano wa kanisa ili yafanyiwe maamuzi au kusuluhishwa. Alichukisudia kuwaambia Paulo ni kwamba, watakatifu wanakwenda kuuhukumu ulimwengu na watawahukumu pia malaika walioasi kutokana na matendo yao. Yatupasa tuweze kuhukumu kati ya mema na mabaya kuanzia mambo ya ulimwengu huu tuliopo. Wapendwa waumini wa Korintho kwa hakika hawakufanya hukumu ya haki kwa kuzitendea kazi kanuni zilizo kwenye sheria ya Mungu na kwa hiyo, wapendwa waliamua kwenda kwenye mahakama za kidunia.

 

Jambo lingine lipasalo kulijua hapa ni kwamba uongozi wa kanisa unawajibu kuhakikisha kuwa hukumu zao ni za haki na takatifu. Mojawapo ya matatizo makubwa yaliyolikkumba kanisa la Mungu kwenye karne ya ishirini lilikuwa ni kutoweza kutoa hukumu za haki. Sisi kama Wakristo tunawajibu wa kusimamia haki na utakatifu. Tusiruhusu dhuluma au hukumu isiyo ya haki kufanyika kanisani, vinginevyo itawafanya waaminio waamue watoke kanisani na kwenda kutafuta hukumu za haki nje ya kanisa. Yanasemaje basi kwa mashirika ya kidini yanayojiita kuwa ni Kanisa la Mungu na huku waumini wake hawapati haki ndani ya kanisa? Yatupasa kujikite sana kwenye kuielewa torati au sheria na kanuni za Mungu ili tuweze kutoa huku za haki na ni wajibu wa kila Mkristo kusoma na kuzielewa kanuni hizi na kuweza kutoa hukumu kwa haki na halali.

1Wakorintho 6:9 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

 

Tunaposoma 1Wakorintho 6:9-14 tunapata uelewa mzuri wa kile kinachosemwa hapa.

1Wakorintho 6:9-14 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, 10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi. 11 Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu. 12 Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si vyote vifaavyo; vitu vyote ni halali kwangu, lakini mimi sitatiwa chini ya uwezo wa kitu cho chote. 13 Vyakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo na vyakula. Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa mwili. 14 Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena atatufufua sisi kwa uweza wake.

 

Hapa tunaona namna ya mienendo itakayotufanya kuwa kwenye hukumu walio kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Tumeoshwa na kusafishwa kwa dhabihu ya Kristo, lakini hatuwezi kuenenda kwa namna walivyoenenda watu hawa. Kama anavyoonyosha Paulo kuwa wengi wetu tuliyatenda mambo haya kabla hatujaitwa na kubatizwa, bali sasa tumeachananayo na kuenenda kwa mwenendo tofauti. Hatuyatendi tena mambo haya. Sisi ni viumbe wapya kwa kupitia Roho wa Mungu.

 

Kwenye aya ya 12 inaonekana kuwa Paulo anasema kuwa vitu vyote vimetakaswa na kuhalalishwa kwa yeye kuvifanya. Hili ndilo suala lenyewe? Tumekwishaona tayari kwamba sheria za Mungu zingali zinatakiwa bado kuheshimiwa na tumeagizwa kama Wakristo kuzitii hizo sheria za torati .

 

Sisi sote tunahali ya kufanya maamuzi kuhusu mambo ya kutenda tunayoyataka. Hii haimaanishi kuwa ni haki na ni vizuri kwetu. Kama Wakristo yatupasa kuchagua kuhusu mwenendo wetu na ni juu yetu kuchagua mema au mabaya; uzima au mauti.

1Wakorintho 6:15 Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.

 

Ni kama miili yetu ilivyo hekalu la Mungu, ndipo mwili wa Kristo, ambalo ni mtu mmojammoja wanaounda kanisa, nao ni aina ya upanuzi wa hekalu. Kila mmoja ni mashirika au sehemu ya mwili mzima. Aya ya 16 hadi 18:

1Wakorintho 6:16-18 Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja. 17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye. 18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe.

 

Anachokisema Paulo hapa ni kina tafsiri ya maana mbili. Tukiwa tunatakiwa kuepuka uzinzi wa kimwili, yatupasa pia kujiepusha na zinaa ya kiroho. Mwanamke kahaba ni mfano wa dini ya uwongo. Wale walioungana kwenye dini hii ya uwongo hufanyika kuwa wamoja nayo. Kama tukiungqanishwa kwenye dini ya uwongo, basi hatuwezi kuungana kwenye arusi tukawa ni bibi arusi wa bwana arusi, Yesu Kristo. Tumeambiwa kuujaribu mwili ambao ni kanisa. Yatupasa kukusanyika pamoja na kushiriki ibada kwenye mwili wa Kristo. Tumeagizwa kujua pale ulipo na ni nani wao na namna pekee tutayoweza kuijua ni kwa mafundisho yao. Ni kama alivyosema Kristo Mathayo 7:16: “utawatambua kwa matendo yao”. Yatupasa kuwa na msingi mzuri kwenye mafundisho ya kweli na kanuni za Mungu ili kuuendeleza mwili huu.

Aya ya 19 inasema:

1Wakorintho 6:19 15 Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!

 

Paulo anasisitiza kuwa miili yet uni hekalu la Mungu na Roho wa Mungu anakaa ndani yetu. Anafanya neno la nyongeza kwa kusema kuwa wala si mali yetu sisi wenyewe. Kwenye aya ya 20 tunasoma:

1Wakorintho 6:20 15 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.

 

Tumenunuliwa kwa gharama. Bei hiyo ilikuwa ni uhai wa Kristo. Alimlipia kila mmoja wetu kwa damu yake. Sisi sasa tu watu wa Mungu. Mwili wetu si wetu wenyewe, ili tumtukuze bwana wetu, Mungu Baba, kwa miili yetu. Tunamtukuza kwa kujiepusha na tama za mwili na matendo ya kidunia na kuzitii sheria zake. Tunayashika yaliyomema na ya haki na kukataa maovu na upotoe wa dunia hii. Mungu anasema watu wake ni watu muhimu wa aina yake. Kama tukifanana na kuendana na watu wengine wa dunia na hakuna anayeona kuwa sisi tu watu wa tofauti, ndipo basi hatuna tofauti yoyote na huenda yatupasa kutathmini maisha yetu ili kuona kuwa tunaishi sawasawa na mujibu wa neno halisi na la kweli la Mungu. Njia ya Mungu ni tofauti sana na ya dunia hivyo ingeweza kuwa dhahiri sana kuwa sisi tu watofauti. Yatupasa kujitahidi kila siku kuwa ni watu wa tofauti na wa aina yake. Kwa kweli, kama tunakiiadhimisha siku ya Mwezi Mpya kwa kuitakatifuza na kudhani kuwa tunaweza kuishika torati ya Mungu, tutaonekana kuwa ni watu wa aina ya kipekee. Na ukweli wa mambo, hata tutaonekana ni wa pekee aina yake hata kwenye Makanisa mengi ya Mungu.

1Wakorintho 9:24 Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

 

Kwenye uwanja wa michezo, riadha inagharimu juhudi ya takriban asilimia 110% ili kushinda shindano. Paulo anatuonya sisi kupiga mbio ili tuweze kupokea zawadi au tuzo. Ni tuzo gani basi anayoisema Paulo hapa? Hebu na tutazame kwenye 1Wakorintho 9:25-27 na tuone anachikisema Paulo.

1Wakorintho 9:25-27 Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika. 26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa; 27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.

 

Taji tunayoishindania na kuikazia mbio haiharibiki ambayo watapewa Wakristo wa kweli ataporudi Kristo. Paulo anasema kuwa anautesa mwili wake. Paulo alipigana vita endelevu, kama sisi, dhidi ya mambo ya kimwili ya mwanadamu na dhambi. Ni wale wanaovumilia hata mwisho ndio wataipokea taji. Ni watendaji wa neno na sio wasikiaji watakaohesabiwa haki.

 

Taji hii si ya kudumu kama baadhi ya wenye imani ya “mtu aokokapo mara moja huendelea milele” wanavyotutaka sisi tuamini. Paulo anasema kwenye aya ya 27 kwamba aliutaabisha mwili wake ili uyatii mambo ambayo yeye hangeweza kuyashinda/ kama hatutakuwa makini na kujibidiisha ili kushinda na kufanana zaidi na viongozi wetu na kaka yetu mkubwa Yesu Kristo, hatutaipokea taji, Paulo anachoongelea hapa. Tutajikuta wenyewe  tukiwa kwenye ufufuo wa 2 wa wafu. Kumbuka kuwa ni ufufuo wa 2 wa wafu. Wengi wamejaribu kutushawishi huko nyuma kuwa kama hatukuishi kama ushirika wa kipekee tutakataliwa kwenye ufufuo wa 3 ambako tutalelelewa, tukionyeshwa jinsi kila mmoja alivyofanya matendo mema na kisha kutupwa kwenye ziwaa la moto. Namna bora tunayoabudu ni neema kubwa sana kulik0o hivyo. Soma jarida la Mafundisho Potofu ya Ufufuo wa Tatu (Na. 166)  ili kupata habari kwa kina zaidi kuhusu jambo hili.

2Wakorintho 13:5 Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa.

 

Hebu na tutazame aya hii kwa kina tena uelewa mzuri wa kile anachokisema Paulo hapa. Tutaona kwenye 2Wakorintho 13:1-14.

2Wakorintho 13:1-9. Hii ndiyo mara ya tatu ya mimi kuja kwenu. Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno litathibitishwa. 2 Nimetangulia kuwaambia; na, kama vile nilipokuwapo mara ya pili, vivyo hivyo sasa nisipokuwapo, nawaambia wazi wao waliotenda dhambi tangu hapo, na wengine wote, ya kwamba, nikija, sitahurumia; 3 kwa kuwa mnatafuta dalili ya Kristo, asemaye ndani yangu, ambaye si dhaifu kwenu, bali ana uweza ndani yenu. 4 Maana, alisulibiwa katika udhaifu, lakini anaishi kwa nguvu za Mungu. Maana sisi nasi tu dhaifu katika yeye; lakini tutaishi pamoja naye kwa uweza wa Mungu ulio kwenu. 5 Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa. 6 Lakini natumaini kama mtajua ya kuwa sisi hatukukataliwa. 7 Nasi twamwomba Mungu, msifanye lo lote lililo baya; si kwamba sisi tuonekane tumekubaliwa, lakini ninyi mfanye lile lililo jema, tujapokuwa sisi tu kama waliokataliwa. 8 Maana hatuwezi kutenda neno lo lote kinyume cha kweli, bali kwa ajili ya kweli. 9 Maana twafurahi, iwapo sisi tu dhaifu, nanyi mmekuwa hodari. Tena twaomba hili nalo, kutimilika kwenu.

 

Ili sisi tuwe na nguvu yatupasa tuweze kujisimamia wenyewe. Kanisa kwa takriban miaka 40 iliyopita au limekuwa linachunga idadi kubwa ya wafuasi na sio mahiri wa kutafakari. Na hii ndiyo sababu iliyowapelekea watu wengi kuwafuta viongozi wa kanisa kwenye ukengeufu. Paulo anatoa mfano wa huduma na ilimaanisha haikuonekana wala kujulikana.

2Wakorintho 13:10–14 Kwa sababu hiyo, naandika haya nisipokuwapo, ili, nikiwapo, nisiutumie ukali kwa kadiri ya uwezo ule niliopewa na Bwana, kwa kujenga wala si kwa kubomoa. 11 Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfarijike, nieni mamoja, mkae katika amani; na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi. 12 Salimianeni kwa busu takatifu. 13 Watakatifu wote wawasalimu. 14 Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.

 

Paulo anaashiria kuwa aliwahi kuwaambia jambo hili waumini wa kanisa la Korintho mara mbili kabla ya kipindi hiki. Inaonekana kuwa kanisa la korintho lilikuwa gumu kidogo au vivu kuelewa. Paulo anarudia tena hapa kukanusha na kukemea mafundisho ya Kinostiki yaliayokuwa wanaenezwa siku hizo. Wanostiki walikuwa hawamwamini Mungu, kwa namna waliyokuwa wanamchukulia Kristo, kuwa aliishi kama mwanadamu halisi. Kiumbe ni muovu kwa mtazamo wao kwa hiyo kimsingyo kimsingi isingewezekana kwa Mungu mtakatifu kuishhi ndani ya mtendadhambi. Paulo alikuwa anajaribu tu kuonyesha ukweli kwamba Kristo anaishi ndani yetu, kinyume na mawazo yaliyokuwa yakifundishwa siku zile. Tumepewa agizo na wajibu wa kujitathimini wenyewe. Tunafanya hivyo kwa kuzitathimini njia zetu na matendo yetu kwa kulinganisha na mneno ya Biblia. Kama mafundisho yetu na imani yetu haifanani na Maandiko Matakatifu, basi tutakuwa sio wafuasi wa Kristo. “Maandiko Matakatifu” yaliyoko hapa yanatokana na yafsiri ya Biblia King James Version. Inajitahidi kuelezea vizuri sana kuwezesha kuipata maana halisi kusudiwa ya maandiko matakatifu. Tunapaswa kuitafuta kweli kwa bidii sana ili tuipate. Si kazi rahisi ila tumeagizwa kufanya hivyo. Ni kama asemavyo Mtume, “Yeye asemaye anamjua Mungu na asizishike amri zake yeye ni mwongo”. Yatupasa kujua bila shaka kwamba amri hizo ni.

1Wathesaloniake 5:21 jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;

 

Yatupasa kuyajaribu mafundisho tunayoyasikia ili kuona kama ni ya kweli au sivyo. Yatupasa pia kujichunguza wenyewe ili kuona kama matendo na mwenendo wetu vinaendana sawa na mafundisho yetu. Hii ni muhimu sana hasahasa kwenye majira ya maadhimisho ya Pasaka. Paulo alisema kwamba tumaini lake ni kwamba Wakorintho walikuwa hawana mashaka kuwa wao ni wa Kristo. Namna pekee tunayoweza kuifanya hivyo ni iwapo kama tutakuwa tunajisomea kwa bidii ili kuthibitisha mafundisho yetu. Yatupasa kuwekeza hela zetu mahali ilipo midomo yetu.

 

Kwa kuhitimisha, tunaona kuwa Paulo hakuwa amependezwa kabisa na tabia au mwenendo wa waumini wa makanisa ya Warumi na Wakorintho.

 

Wapendwa ndugu zangu, sisi tu mwili wa Kristo. Roho wa Mungu anakaa ndani yetu. Tunamtii na kumcha Mungu kwa kuwa tunampenda, na sio kwa kuwa tumehesabiwa haki kwa kuishika sheria yake. Hebu na tujifunze kutokana na makosa na mapungufu yaliyoonekana kwenye makanisa ya Warumi na Wakorintho. Hebu na tukimbie mbio za mashindano haya ili tushinde, na tusiwekwe tu kwenye nafasi ya pili au ya tatu. Hebu na tuendelee kujisomea na kujifunza kama Waberoya, ili tuejitwike majukumu yetu kama washirika wa mwili wa Kristo. Endelea kuendeleza uelewa wa kina wa Biblia na wa kanuni na sheria au torati ya Mungu ili asiwepo mtu wa kutuambia “Hivi Hamjui?”