Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[048]

 

 

 

 

Mafundisho ya Mapepo katika siku za Mwisho


(Toleo la 2.0 19940813-1999129)

 


Mafundisho ya mapepo yaliyoorodheshwa na Biblia yametathiminiwa kimsingi kwamba yamewekwa  kwa madhumuni ya kudhoofisha  imani. Kimsingi, somo hili lashugulika na mafundisho mawili ya kishenzi yanayohusu ndoa na nyama.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369 WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Barua Pepe: secretary@ccg.org

 

 

(Hati Miliki © 1994, 1999 Wade Cox)

(tr. 2012)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakaotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Mafundisho Ya Mapepo Katika Siku Za Mwisho



Kwa kweli Watu hawajafahamu maana ya maendeleo ya mafundisho ya mapepo. Tunafaa kufahamu kuwa Paulo aliandika maandiko matakatifu kwa pumzi ya Roho Mtakatifu kwa ajili ya manfaa yetu na kufahamu jinsi mafundisho ya mapepo yalivyo na vile yangejitokeza wazi katika  siku za mwisho.

 

Paulo anasema katika 1 Timotheo 4:1-5

Sasa Roho wazi (katika maneno (‘retoos))

Yasema kwamba katika nyakati za baadaye wengi wataiaja imani na kutii roho za uwongo na mafundisho ya mapepo, kwa madai ya uwongo ambayo madhumuni yake ni ya kuharibu (aidha pia umaanisha ushuhuda wa uwongo kiunafiki (pseudologoon) ambayo utia nia kwenye dhamiri (kekausteriasmenoon ten Indian suneidesin)), ni nani anaye kataza  nyama pamoja na kujihepusha na vyakula ambavyo Mungu aliviumba ili viweze kupokelewa na shukurani kwa wanaofahamu na   kusadiki ukweli. Kwa kuwa kila kitu kilicho umbua na Mungu ni bora na hakuna chochote kitakachokataliwa ikiwa kitapokelewa kwa ajili ya shukurani; kwa maana kimetakazwa na neono la Mungu kwa njia ya maombi 

 

Roho Mtakatifu ulitamka maneno kwa nguvu  aukimwambia Paulo kwamba katika siku za mwisho mafundisho muhimu aina mbili ya mapepo yatatokea hata hivyo  lazima yatapingwa na kudhihirishwa na wateule waliofahamu ukweli.

 

Mapepo hayakuamua kutoa mafundisho haya hivi. Nayo si havivu. Katika kutekeza kazi azke yanagonga ile nafsi ambayo ni ya maana kwa Mungu  katika mpango wa ukombozi na pia inayostahili kafara ya Yesu Kristo. Mafundisho haya ni kosa mbili maalum, yaliyo tafuta jinsi ya kudunisha maana ya uumbaji.

 

Mafundisho ya kwanza ya mapepo ni mafundisho kwamba watu wajitenge na Ndoa. mafundisho haya ni ya kishetani yanayo tafuta muungano wa kiroho au kufananishwa kuwa kama ni mwenyewe. Kusudi la fundisho hili la mapepo ni kujaribu kuingilia msingi wa mwanzo wa masomo ambayo mungu amechangua kushughulikia kama mfano wa mfumo wake.  Umoja ni familia. Kwa kuharibu usalama wa kifamilia, mapepo yanaharibu jengo la msingi la jamii yetu.Tunatazama jamii hii ikijikuwaa majoni petu sababu watu wameanza kuishi pamoja inche ya ndoa. Ni muhimu tukifahamu mwanzo kabisa na kuelewa uhusiano wetu na Yesu Kristo na kwa ibada zetu kwa Mungu kwamba umoja wa kifamilia sharti ufahamike vizuri. Kwanguka kwa familia pamoja na mifumo ya kitaifa huelekeza katika upotovu kama wa Sodoma na Gomorra.

 

Mchakato wa fundisho hili umeshirikishwa na ibada ya sanamu. Hilishitawishwa na Paulo katika Warumi 1:1-32. Mafungu haya yanausiana na swala nzima la ibada na kilicho sababisha kuanzishwa kwa usherati katika jamii. Ni msingi unaofanana na usherati wa kiroho katika uhusiano wetu na Mungu, ambayo ni ibada ya sanamu pamoja na ujawi..

 

Warumi 1:1-32 Paulo, mtumwa wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume, na kutengwa aihubiri Injili ya Mungu; (Biblia Takatifu)

 

Ni inchili ya Mungu na ilikabidhiwa kwa Yetu Kristo. Na sisi sote tumetengwa kwa lengo hilo

 

2 ambayo Mungu amekwisha kuiahidi kwa kinywa cha manabii wake katika maandiko matakatifu; 3 yaani, habari za Mwanawe, aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili,   4 na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu;

 

Kristo alikuwa mwana wa Mungu, moja kati ya wana wengi wa Jeshi, kabla hajaabishwa. Hayo yote aliacha na akawa kama mwanadamu. Hatutasema Kristo alibaki na sehemu yoyote ya nafsi yake katika Uungu au nje yake mwenyewe. Paulo amenena  hapa kimasomaso kwamba Kristo alikuwa mwana wa Mungu katika nguvu kulingana na Roho Matakatifu, kwa njia ya kufufuka kwake kutoka mauti aliweka kando kuwa mwana wa Mungu ili kufanyika mwanadamu kwamba aweze kuwa mwana wa Mungu wa kwanza katika ubinadamu. Hiyo ndiyo ilikuwa maana. Hakuna kitu chochote cha Yesu Kristo kilichobakia nje ya uwepo wake wa kibinadamu. Na hii ni mafundisho kwamba Kristo anayo sehemu yake ilio kando na kule kuwa binadamu na kiasi fulani alibaki kuwa na sehemu ya Mungu nje ya uwepo wake wa kimwili. Hata hivyo hakufanya hivyo.

 

5 ambaye katika yeye tulipokea neema na utume ili mataifa yote wapate kujitiisha kwa imani, kwa ajili ya jina lake;

 

Tena Imani ilielekezwa kwa mataifa. Ilikuwa muundo wa utiifu wa imani. Imani yetu ni tiifu kwa Mungu na kutambuwa kwamba Mungu pekee ndiye Mungu wa kweli, hitaji letu la kutuwezesha kuriithi uzima wa milele kutoka Yohana 17: 3 ni kumjua Mungu wa kweli na mwanawe Yesu Kristo aliyemtuma. Biblia imedhihirisha wazi kwamba Yesu Kristo si Mungu pekee wa kweli. Ni wazi kuwa imani yenye utiifu kwa Mungu moja wa kweli, ambaye ni Mungu Baba, Mungu mwenyezi aliye juu, ni hitaji kwetu litakalotuwezeza kupokea kuitwa wana wa Mungu ukombozi wa miili yetu, kutoka Warumi 8:29. Hiyo inajumuisha wale wote walioitwa kumstahili Yesu Kristo katika

 

6 ambao katika hao ninyi mmekuwa wateule wa Yesu Kristo; 7 kwa wote walioko Rumi, wapendwao na Mungu, walioitwa kuwa watakatifu. Neema na iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.

 

Hapo tunaona Uungu katika mistari saba ya kwanza na ufahamu wa imani ya Mungu moja wa kweli, na kwamba Kristo aliweka kando kuwa mwana wa Mungu ili kuwa bindamu na kufanywa kuwa mwana tena kutokana na ukombozi wa mwili wake katika kufufuka kwake. Hakuna uwepo wa Yesu Kristo nje ya ubinadamu wake hadi wakati wa kufufuka kwake.  Kuthibitisha hayo wamekana kafara ya Yesu Kristo na kukana kabisa ufufuo wake, ambapo sasa hayo ni mafundisho ya kishetani. Utatu pia nimafundisho ya uongo na kutoka kwayo mafundisho mengine mawili yanafuata

 

8 Kwanza namshukuru Mungu wangu katika Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa kuwa imani yenu inahubiriwa katika dunia nzima. 9 Kwa maana Mungu, nimwabuduye kwa roho yangu katika Injili ya Mwana wake, ni shahidi wangu jinsi niwatajavyo pasipo kukoma,

 

Bila shaka katika dhamiri ya Paulo alimtumikia Mungu vile ilivyoelezewa na mkuu wake ambaye ni Yesu Kristo. Hakukuwa na utata wowote katika dhamiri ya Paulo juu ya kuwepo kwa Mungu wawili au kwamba Kristo alikuwa Mungu wa kweli. Hakuna kabisa taswishi yoyote.

 

10 siku zote katika sala zangu, nikiomba nije kwenu hivi karibu, Mungu akipenda kuifanikisha safari yangu. 11 Kwa maana ninatamani sana kuwaona, nipate kuwapa karama ya rohoni, ili mfanywe imara;

 

Mbona alikusudia kufanya hivyo? Kanisa lilikuwa Rumi, katikati ya utawala wa juma, uliofuata utawala wa shaba ambao tunaona ukiashiriwa kimfano katika Danieli (Dane 2:1-49). Utawala wa juma uliangusha chini na kuharibu kila kitu na makao yake yalikuwa ngome ya ibada ya sanamu. Watakatifu pale waliitaji kutiwa nguvu na ufahamu.

 

12 yaani, tufarijiane mimi na ninyi, kila mtu kwa imani ya mwenzake, yenu na yangu. 13 Lakini, ndugu zangu, sipendi msiwe na habari, ya kuwa mara nyingi nalikusudia kuja kwenu, nikazuiliwa hata sasa, ili nipate kuwa na matunda kwenu ninyi pia kama nilivyo nayo katika Mataifa wengine.

 

Fahamu kwamba mafungu yamekatwakatwa kwa mpangilio. Kuna mafungu saba ya kutambua Mungu mkuu, tena mengine tano. Tunakabiliana na saba na tano hadi kumi na mbili yanayohusu kazi ya wingi wa Rehema na Roho . Hayo yanahusu mafumbo pia.

 

14 Nawiwa na Wayunani na wasio Wayunani, nawiwa na wenye hekima na wasio na hekima. 15 Kwa hiyo, kwa upande wangu, mimi ni tayari kuihubiri Injili hata na kwenu ninyi mnaokaa Rumi. 16 Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia. 17 Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani.

 

Hapa tunaona kanuni za imani na matakwa ya kupongesana kiurafiki pamoja na ukweli kwamba imani uelekeza katika haki. Ni imani ile Mungu anayotoa, imani ianyodokeza kuwa neno la Mungu ni kweli na kwamba Mungu ametoa neno lake kwa ajiri ya kuwaelimisha watakatifu wake. Imani hiyo utupa sisi uwezo wa kuwa wenye haki, kupitia kwa utiifu wa sheria chini ya rehema ya Yesu Kristo.

 

18 Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.

 

Fungu hilo pia limetafsiriwa “zuia ukweli kwa wasio haki”. Paulo anadokeza hapa kuwa watu wale ambao wanazuia ukweli, uficha taarifa. Paulo yu wazi hapa kwamba yeyote anaye ficha ukweli kati ya wasiohaki hatapatana na ghadhabu ya mbinguni. Hii ni ahadi Mungu amefanya kupitia Paulo.

 

19 Kwa kuwa mambo ya Mungu yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa maana Mungu aliwadhihirishia. 20 Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru;

 

Sasa tunatoka kwa muundo wa Mungu mkuu (kutoka kwa Mungu moja wa kweli) na imani, kuenda kwa utunzaji wa Mungu mkuu na hakikisho kutoka kwa uumbaji. Kadiri ujuzi wetu unavyo ongezeka, kwa kweli ndivyo tunadhihirisha uwepo wa Mungu. Mageuzi yametupiliwa mbali tunapoendelea. Kimsingi yanatenganishwa na hayana maana. Wasayansi wanauweka katika kaburi la sahau. Tunapata kuwa mbingu na ardhi zinaonyesha nguvu za Mungu wanachopishania wasayansi ni swala hili (asiri ya Mungu.)

 

21 kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza. 22 Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika; 23 wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo.

 

Badiliko hili halitatokea hivi tu kuwa la moja kwa moja. Ni jambo la pole pole na lilichukuliwa muda mrefu kuafikiwa. Walitoka kwa kumtambua Mungu kama Mungu, ndani ya Ukristo badala yake wakinua Yesu Kristo kuwa Mungu na wakaanza kumuabudu. Wakishafanya hivyo tena waliwainua watakatifu kati hali moja na wakaanza kuwaabudu mwisho wakaanza kwemba kwa sanamu za maria na miungu mingine kama hiyo, wakapoteza maono kabisa ya ufahamu wa ufufuo. Mariam, visivyo anitwa Maria, amekufa! (cf. Masomo Bikira Maria na Familia ya Yesu Kristo [232]). Mariamu, anayeiitwa maria, atafufuliwa kwanza. Yseu Kristo ni ntu wa pekee aliyefufuka kwenda mbinguni (Yohana 3:13).

 

Hapo matokeo ya kuabudu sanamu polepole umedidimia katika dhamiri ya watu wanaousika. Dhamiri zao zimepungukiwa nasi sahihi.

 

24 Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.

 

Hii ndio utokea tunapoanzaia katika hatua zilizo katika mstari wa 24 na 25. Mara tukifikia kudidimia wa ibada za miungu, tunapewa tamaa sisizo za kawaida. Hii uelekeza kwa usherati na hapo tena kwa upotovu na utaendelea kuwa mbaya zaidi na zaidi. Watu hawajafahamu mlolongo wa kuendelea  kudhoofika. Mafundisho ya kishetani mwanzo uanzia kushambilia kichua cha uungu na kwendelea pande zingine. Na hapo Mungu ukabidhi watu kufuata tamaa zao. Tunaona katika kizazi hiki ambapo watu wamekosa uadilifu wa kimbingu. Walakini hawajafanya hivyo bila adabu. Jamii yao iliporomoka wakawa wamepotoka kabisa. Jamii sharti itubu kwa ajiri ya upotovu. Mtu lazima arejeshe uhusiano wake na  Mungu ili kushinda haya na hatutaweza kushinda dhiki hizi mpaka tumtambue Mungu na tutubu na kurejesha uhusiano wetu na Mungu kupitia kwa Yesu Kristo. Ikiwa tunamwabudu Yesu Kristo tunafanya sawa na kuabudu yeyote kati ya miungu, isipokuwa Mungu Baba. Tunafanya dhambi kwa Kristo tulivyofanya kwa Shetani.

25 Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina. 26 Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; 27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao. 28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.

 

Katika sentensi moja tunajulizwa taarifa yote. Katika kukosa ufahamu wa Mungu ambaye ni kichwa haya ni matokeo ya uvunjaji wa misingi ya jamii.

 

29 Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, 30 wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, 31 wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema;

 

Mambo haya yote ufuata uvunjaji wa uhusiano baina yetu na Mungu. Mambo haya yote ukumbana na uhusiano wa hatua ya familia na hatua ya utangamano na ndio matokeo ya mwisho ya shida za Mungu kama kichwa.

 

32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao. (Biblia Takatifu BT)

 

Inafikia sasa hali ambayo watu wanasema mazuri ni mabaya na mabaya ni mazuri. Wale watu ambao wanakemea vitendo hivi wanakataliwa wenyewe.

 

Tunaona kutoka kwa wazo hili kwamba mchakato wa ibada ya sanamu umeendelezwa kuwa hule wa tama zizizo za kawaida. Michakato hiyo inakuwa wazi kadri mchakato wenyewe ukikatiswa. Mafundisho ya useja wa wakuhani ni hatua ya ndani ya mwozo. Useja ni jambo linguine tofauti kando na mafundisho ya kishetani, lakini useja wa wakuhani ni hatua ya ndani ya mwonzo. Useja wa wakuhani uenyewe si fundisho la kimsingi. Hata hivyo, useja wa wakuhani na umoja ni mafundisho ya kishetani. Paul anasema “ni vyema usioe lakini kama inalazimu oa”.

 

Hivyo sasa kuwabfundisho la kuhitajika kuhepuka kuoa, hili peke yake ni mafundisho ya kishetani.

 

Biblia ianelezea wazi kwamba fundisho hili halijafaulu kabisa kwa kuwa watu bado wanaoa wakati wa kurudi kwa Masihi (Mat.24:30-39). Hata hivyo, ni fundisho kuu na la mshangao mkuu katika siku za mwisho. Ndoa ni takatifu iliowekwa wakfu na Mungu kuonyesha uhusiano kati ya ubinadamu na Yesu Kristo na kuunganishwa kwa mataifa chini ya Baba. Kile ambacho mafundisho ya kishetani yananuia kufanya ni kuharibu ufahamu wa huu mchakato kumzingizia Mungu kwa kusema mfano aliouazisha wastahili kutunzwa na unaleta sitofahamu katika jamii. Wanadai kuwa ushababisha ghasia mbaya kwa dana yoyote ya kisasi, wa urithi, wa utaratibu na wa usalama. Unajenga kutoamini kabisa na imani yeyote katika dhamiri ya mtu.

 

Sababu ya kushindwa kwa jamii ya Sparitani ni kwamba walingilia umoja wakifamilia. Sparita ilikuwa serikali ya kijeshi. Waume wote walikuwa wamefundishwa kwa ajiri ya vikozi vya jeshi. Ni nchi yenye ukosefu wa nidhamu ambao ulimwengu haujawahi  shuhudia ilijiharibu yenyewe sababu ilitupilia mbali umoja wa kifamilia.

 

Mchakato mwingine ni ule wa mafundisho ya kuacha nyama zilizoanzishwa kupokelewa kwa shukrani. Nyama hizi zimetambuliwa na Biblia katika Walawi 11 na kumbu 14.

 

Mchakato huu wa utakaso ni wa zamani kushinda ukristo. Ulijkuwa sehemu ya mfumo wa Pythogorani wa wagiriki na unadhihiirika katika wabuda. Mchakato huu sasa unaitwa wakukula mboga (Taz somo la Wanaokula mboga na Biblia (Nam. 183).

 

Mchakato hu umekosa viungo muhimu kwa ajiri ya kufanya kazi kiusawa kwa ubongo. Liwe liwalo, mafundisho yanagonga mfumo ule ule ya kwamba Mungu alianzisha  adamu kutoka mwanzo. Imezingatiwa bayana pale kwamba Kaini alikuwa mkulima wa shamba na Abeli alikuwa mfungaji. Kafara ya Abeli ilikubaliwa machoni pa Mungu zaidi kuliko ile ya Kaini. Hii ndio ilisababisha asira ya Kaini na ndio sababu alimuua abeli (mwanzo 4:1-16).

 

Maana ya huindinishaji wa upaguzi unalenga kafara ya Masihi. Mfano wote wa upadri ulianzishwa kudhihirisha damu ya kafara ya Masihi na kudhihirisha muundo wa vyakula vilivyo kusudiwa kuchukuliwa na kuliwa.

 

Mchakato wa mboga unaibua swala la ukweli na ufahamu wa mchakato wa ukombozi na mfumo wote wa kafara za hekalu na muundo ulionzishwa na Mungu. Kinachosemwa kiusahihi hapa ni: ulipata kumwelewa vibaya umekosea, we ni mkali. Hitaji la kafara ya damu inaitajika” au, “tunakataa kuwa ni sharti tule nyama. Kwa njia nyingine, ulipata kuelewa muundo wote vibaya na hatutafikia kukamilisha kwa mpango wa ukombozi tukifuata maelezo yako”. Hiyo ndio walaji wa mboga wanambia Mungu.

 

Anayekula mboga anajiweka juu kama hakimu wa Mungu, kukataa kabisa mfumo wa sheria za vyakula na kukataa ufahamu wa uumbaji na uwezo wa mwili wa mwadamu kujisoesha na kujiusisha na vyakula vilivyopeanwa kwa ajiri ya shukrani. Inanena kwa Mungu hukuelewa muundo na kuwa mwili utaharibika kwa kufuata maelekezo ya mungu. Maswali yanayo wekwa mbali ni bure kabisa. Yanajaribu kudunisha matendo ya siku za mwisho na kuibwa swali la uwezo wa masihi kuanzisha tu mifumo. Unabii uko wasi kwamba masihi ataanzisha mfumo Fulani na kutokuwa na kula nyama wakati wa kipindi cha miaka elfu moja, na kututokea urejesho na kuwa Masihi atarejesha kafara. Maswala yote haya yanasababisha swala la vitendo na ufahamu wa Masihi na mpango wa Mungu. Inashitaki Mungu na Masihi na kabisa hii ni kupinga Ukristo.

 

Swala la uwezekano wa kula aina sote za nyama kutoka kwa kifungu cha Biblia ni kweli. Matendo 10 na 11 uonyesha kuoshwa kwa watu wa mataifa kwa kukubalika kuingia katika ufalme wa Mungu. Kifungu hiki hakina lolote kuambatana na vyakula jinsi ilivyo wazi kutoka mitendo 11. Ni baana kuwa maono alionyeshwa Petero yaliosha watu wa mataifa na si vaykula. Swala zima la kukubaliwa kwa vyakula vinavyosunguka ukweli kwamba maana kuu ni kwamba nyama zilitolewa kafara kwa sanamu kabla ya kuuzwa au kuliwa. Mafundisho ya Biblia yaliwekwa ili weteule wangeweza kula nyama bila kujali kuwa ilitolewa kafara kuwa chakula.

 

Warumi 14:1-4 Yeye aliye dhaifu wa imani, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake. 2 Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga. 3 Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali. 4 Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.

Sasa fungu hili haliezi haswa kuwa udhaifu wa ulaji wa mboga. Biblia inoredhesha ulaji wa mboa kama mafundisho ya kishetani. Cha maana katika fungu hili ni kweli kwamba udhaifu si kutokana na matumizi ya mboga bali kutoka kwa ukweli kuwa mshiriki alikuwa na imani pungufu, kule kutojali ikiwa nyama ilitolewa kafara kwa sanamu au la. Hapo maana ni kwamba italiwa pamoja na kutoa shukwrani ndani ya maagizo yaliyotolwa na sheria ya vyakula.

 

Mipangilio iliyoigwa na wayuda katika kafara na mchakato wa kuchinjwa haukuwa kwa watu wa mataifa. Paulo aliweka maelezo madogo kwao kuajana na damu n asana ili ilichanganyika na kafara za snamu (mitendo 15:20,29; 21:25). Hapo tunakumbana na dhana mbili kuhusu matumizi ya nyama ilipotolewa kafara kwa sanamu.

 

Ikichulikana, na kuwa jambo linalohusu uma na linaweza kusababisha ndugu kujikuwaa au kuonekana kama kuidisha vitendo vya dini ya kipangani, hapo sasa itakataliwa na kuhitajiaka kuachwa kabisa. Kama aiambatani na mchakato, itachukuliwa kuwa isiona na maana na bila umuhimu wowote. Chakula inapaswa kuliwa kwa imani, na kama haitaliwa kwa imani hapo ushikanishaji umehukumiwa.

 

Hivyo ulaji wa mboga unatazamiwa kuwa dhambi katika swala la kupekuwa vyakula zinahusu nyama katika mfumo wa kipangani. Kwa njia nyingine ni mafundisho yaliyo wazi. ya mafundisho ya kishetani wakati yanahubiriwa kuwa kuacha nyama kwa ajiri ya utakazo au hitaji la kibiblia au sababu za kiafya. Dhana ya kuwa Mungu hakuanzisha mchakato wa matumizi ya nyama kutoka mwanzo au na kuendelesha huo mchakato kupitia. Gharika ni kosa la kibiblia au ufumi (mw 7:2). Dhan ya kuwa mungu angeanzisha mchakato usio wa kiafya pia ni fukizo didhi ya asiri yake.

 

q