Makanisa ya Kikristo ya Mungu

 

[130]

 

 

Kutiamoyo na Kuvunjamoyo

(Toleo Namba 1.1 19950812-19980613-20070818)

 

Majaribu ni kitu cha lazima na hayaepukiki kwa maendeleo yetu tuwapo Wakristo, hata hivyo, mara nyingi yamekuwa yakisababisha hali ya kukata tamaa na kuvunja moyo. Ili kuishinda hali hii, ni muhimu tujizoeze kutoa na kupokea utiwaji moyo ambao ni kama silaha ya upendo. Utiajimoyo unasaidia kumtia hamasa mtu, kwa kutoa hisia ya kujiona kustahili au kujirudishia matumaini tena, na kuinua au kuongeza hamasa na hata ustawi na ubora wa kimwili na kisihia.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

 

(Hati Miliki © 1995, 1998, 2007 CCG, ed. Wade Cox)

(tr. 2017)

 

Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.

 

 

Jarida hili linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


 

Kutiamoyo na Kuvunjamoyo


 

Kutiamoyo ni kitendo cha kutia nguvu ujasiri na hali ya kumfanya mwingine ajiamini. Kunasaidia kumtia hamasa mtu ili afanye kazi kwenye mazingira magumu na kumpa matumaini ya kuwa na hatima njema. Kila mtu kwa wakati fulani anahitaji hali hii ya kutiwamoyp. Yatupasa kuelezea au kuwafisia au kuwashukuru wengine kila mara. Kitendo hiki cha kutiamoyo humsaidia mtu afanye kazi kwa bidii kubwa na kufikia malengo kusudiwa zaidi. Kunasaodia kumpa mtu ahueni kutokana na matatizo aliyonayo au huenda hata kubalidisha mtazamo au hatima ya maisha yake. Biblia inatuagiza kwamba tunapaswa kufarijiana na kutiana moyo, kama kwa kweli anavyowafanyia Mungu wale wamwaminio na wanaomtii yeye.

 

Mungu anatujaribu ili kuithibitisha imani au kuthibitisha kujitoa kwetu kwake. Tupo kwenye mchakato wa kujifunza kuendeleza tabia ua kimungu.

 

Warumi 5:4 na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;

 

Kujenga tabia kunamaanisha kutii hata kwenye wakati wa mateso. Kumtii Mungu wakati tunapokuwa tunaumia kunaonyesha imani. Ni rahisi sana kumtii Mungu akati mambo yanapokuwa yanakwenda vizuri, lakini jaribu la kweli hutokea wakati tunapokuwa tumefungwa na kubanwa zaidi ya kipimo cha kawaida.

 

Mfano mkuu wa imani ni Ibrahimu. Mungu alimjaribu kwa kumtaka amtoe mwanae sadaka ya kuteketezwa (Mwanzo 22:1ff.). ibrahimu alikuwa amejiandaa kumtii Mungu kwa jambo hili, hata kwa maumivu makali sana yatakayo mkabili kwa kuwa alikuwa amemtumaini Mungu na kujua kwamba mwanawe angefufuka hatimaye. Lakini Ibrahimu alililishinda jaribu hili la imani na Mungu akalibatilisha ombi hilo kupitia kwa Malaika.

Mwanzo 22:12 Akasema, Usimnyoshee kijana mkono wako, wala usimtendee neno; kwa maana sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.

 

Hadithi au habari ya Ayubu ni mfano wa mtu anayeteseka, mtiifu na mwelewa. Ayubu hakujua sababu iliyopelekea kupatwa na majaribu haya lakini Mungu alimruhusu Adui amjaribu.

 

Baada ya Ayubu kupoteza mali zake zote na watoto wake, marafiki zake walimwendea ili kumlilia na kuomboleza pamoja naye. Walimfariji kwa kuwepo kwao pale .

Ayubu 2:11-13 Basi ikawa hao rafikize Ayubu watatu walipopata habari ya mabaya hayo yote yaliyomfikilia, wakaja kila mtu kutoka mahali pake; nao ni Elifazi Mtemani, na Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi; wakapatana pamoja ili waende kumlilia Ayubu na kumtuliza moyo. 12 Basi walipovua macho yao, nao wakali mbali, wasimtambue, wakainua sauti zao na kulia; kila mmoja akararua joho yake, wakarusha mavumbi juu ya vichwa vyao kuelekea mbinguni. 13 Kisha wakaketi nchi pamoja naye muda wa siku saba, mchana na usiku, wala hapana mmoja aliyenena naye neno lo lote; kwa maana waliona ya kuwa mashaka yake aliyo nayo ni makuu mno.  

 

Ayubu hakuwa peke yake akikabiliana na misukosuko na mateso yake makubwa. Wala siyo kwamba ni wadhaifu tu ndiyo wanaojaribiwa na kwamba wenye nguvu za kiroho hawakumbwi na misukosuko kama hiyo. Watu wakuu sana kwenye historia ya Israeli walikabiliwa na misukosuko na majaribu na wakajiona wenyewe kuwa hawafai kwa kazi zao .

 

Waisraeli kwenye suala la mateso yao waliyoteswa na Wamisri, walikuwa wamekata tamaa sana.

Kutoka 6:9 Musa akawaambia wana wa Israeli maneno haya; lakini hawakumsikiliza Musa kwa ajili ya uchungu wa moyo, na kwa ajili ya utumwa mgumu.

 

Lakini, Mungu alikisikia kilio chao na kwa kweli aliutumia utumwa wao kwa kuwaongeza na kuwazidisha wawe wengi wakiwa kwenye utumwa huu. Aliwainulia mkombozi lakini hawakumsikiliza. Kama ilivyokuwa kwa Musa ndivyo ilivyokuwa pia kwa Kristo.

 

Musa alijiona mwenyewe kama hafai wakati alipopelekwa kuifanya huduma yake kwa Waisraeli.

Kutoka 4:10 Musa akamwambia Bwana Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.

 

Alipewa Haruni awe kama nabii, na yeye mwenyewe alifanywa kuwa kama elohim kwa Haruni na kwa Wamisri (Kutoka 4:16; 7:1). Lakini, bado alikuwa amekata tamaa chini ya adui.

 

Wakati watu walipotamani kula nyama, alikasirika na kuanza kumlaumu Mungu.

Hesabu 11:11-15 Musa akamwambia Bwana, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? Kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu? 12 Je! Ni mimi niliyewatungisha mimba watu hawa wote je! Ni mimi niliyewazaa, hata ikawa wewe kuniambia, Haya, wachukue kifuani mwako, mfano wa baba mwenye kulea achukuavyo mtoto anyonyaye, uende nao mpaka nchi uliyowaapia baba zao? 13 Nipate wapi nyama ya kuwapa watu hawa wote? Kwani wanililia, wakisema Tupe nyama, tupate kula. 14 Mimi siwezi kuwachukua watu hawa wote peke yangu, kwa kuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda. 15 Na kama ukinitenda hivi, nakuomba uniulie mbali, kwamba nimepata fadhili mbele ya macho yako; nami nisiyaone haya mashaka yangu.

 

Hata hivyo, Mungu alimpa Musa ujasiri wa kuubeba mzigo. Pia Mungu alimuwezesha kuyatoa maji ya Roho kutoka kwenye mwamba -- ambao ni Kristo -- kuwaokoa Israeli. Kwa sababu hii Musa hakuweza kuiingia Kanaani, siyo kwa kuhukumiwa, bali ni kama mfano kwetu sisi. Kwanza kabisa, ilikuwa hivyo ili kwamba Waisraeli wasiitumie mifupa yake kama sanamu. La pili, ilikuwa ni kutuonyesha sisi kwamba hatutaiingia nchi ya Israeli ya kimwili, bali ni kwamba tutafanyika kuwa roho kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu. Kukata tamaa kwa Musa kulijitokeza mara nyingi kwa kuwa hakuwa ameona mbali sana kilichokuwa mbele yake.

 

Ni sawa tu na wakati Eliya alipokimbia kutoka kwa Yezebeli kwenda jangwani, alikaa chini ya mti wa mretemu na akaomba afe.

1Wafalme 19:4 Lakini yeye mwenyewe akaendelea katika jangwa mwendo wa siku moja, akaenda akaketi chini ya mretemu. Akajiombea roho yake afe, akasema, Yatosha; sasa, Ee Bwana, uiondoe roho yangu; kwa kuwa mimi si mwema kuliko baba zangu.  

 

Eliya alisikiwa na Bwana na alitiwamoyo. Pia alisaidiwa. Alilishwa na kunguru kama mfano. Alilishwa na malaika na alipewa kuuona uweza wa Mungu na jinsi Mungu anavyotenda kazi.

1Wafalme 19:7-12 Malaika wa Bwana akamwendea mara ya pili, akamgusa, akasema, Inuka, ule; maana safari hii ni kubwa mno kwako. 8 Akainuka, akala, akanywa, akaenda katika nguvu za chakula hicho siku arobaini mchana na usiku hata akafika Horebu, mlima wa Mungu. 9 Akafika kunako pango, akalala ndani yake. Na tazama, neno la Bwana likamjia, naye akamwambia, Unafanya nini hapa, Eliya? 10 Akasema, Nimeona wivu mwingi kwa ajili ya Bwana Mungu wa majeshi; kwa kuwa wana wa Israeli wameyaacha maagano yako, na kuzivunja madhabahu zako, na kuwaua manabii wako kwa upanga; nami nimesalia, mimi peke yangu; nao wanitafuta roho yangu, waiondoe. 11 Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za Bwana. Na tazama, Bwana akapita; upepo mwingi wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja miamba mbele za Bwana; lakini Bwana hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo, tetemeko la nchi; lakini Bwana hakuwamo katika lile tetemeko la nchi; 12 na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto; lakini Bwana hakuwamo katika moto ule; na baada ya moto sauti ndogo, ya utulivu.  

 

Mungu hakuwa kwenye upepo uliovuma kwa nguvu wala kwenye tetemeko la ardhi, wala kwenye moto. Alikuwa kenye sauti ndogo. Sauti ile ilifanya kazi katika Israeli na kwa mataifa kwa milenia kadhaa. Eliya alidhani kwamba amebakia yeye peke yake. Lakini, bado kulikuwapo bado na 7000 wengine waliobakia na Bwana. Aliambiwa akamtie mafuta Elisha. Elisha alimuomba upako mara dufu wa roho yake, ili umsaidie kukabiliana na tatizo alilokuwanalo la kujifikiria mwenyewe. Hata hivyo, Eliya alikuwa ni shahidi aliyepewa jukumu la kuushuhudia ulimwengu na ni mfano wa uweza wa Mungu aliyepamoja naye na anayemwezesha .

 

Mfano mwingine ni ule wa Yona. Alijaribu kukimbia kwenda mbali na alikotumwa, ni sawa na kama wengi wetu tunavyofanya. Mungu alimshughulikia kwa kumfanyia kitendo cha sawa tu na kumuua na kumfufua tena kama mfano wa Masihi ajaye. Mungu alijua kile alichokitenda na na aliandaa mwelekeo wake mpya. Lakini, licha ya muujiza huu, Yona aliamua kwamba alijua vizuri kuliko Mungu na alitaka kuona Waninawi wakiangamia ili ajisikie kuwa hakukosea. Baada ya kuwahubiria watu wa Ninawi, hakujisikia vizuri na alijikuta amekata tamaa kwa kuwa hawakuangamizwa.

Yona 4:3,8 Basi, sasa, Ee Bwana, nakuomba, uniondolee uhai wangu; maana ni afadhali nife mimi kuliko kuishi. Basi ikawa, jua lilipopanda juu, Mungu akaweka tayari upepo wa mashariki, wenye hari nyingi; jua likampiga Yona kichwani, hata akazimia, naye akajitakia kufa, akasema, Ni afadhali nife mimi kuliko kuishi.

 

Majaribu haya yote yalihitimisha kazi ya Mungu. Wengine ni rahisi kuona; wengine hawako rahisi kumtambua juhudi za mtu. Nasi pia tunaweza kuuawa na kufufuliwa kwenye huduma na utumishi wake Mungu. Yatupasa kuhakikisha kuwa tunaifanya kazi yetu na kwamba tupo kwenye ufufuo ulio sahihi.

 

Licha ya ugumu mkubwa au sababu ya mateso au majaribu yetu, yatupasa tuendelee kumtii Mungu.

Ayubu 2:10 Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.  

 

Dhana yenyewe ni kwamba hatutapewa mzigo au jaribu ambalo hatutaweza kulibeba  (1Wakorintho 10:13).

 

Mungu anajua udhaifu wetu, hofu zetu na kukata tamaa kwetu na atatusaidia.

Zaburi 103:13-14 Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao. 14 Kwa maana Yeye anatujua umbo letu, Na kukumbuka ya kuwa sisi tu mavumbi.

 

Zaburi 34:18 Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa.

 

Upendo wa Mungu na huruma yake inazidi mamlaka zote na hatupaswi kuionea mashaka kabisa.

Warumi 8:31-39 Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? 32 Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye? 33 Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki. 34 Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea. 35 Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? 36 Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. 37 Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. 38 Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, 39 wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.   

 

Kama Mungu yupo upande wetu, ni nani atakuwa kinyume chetu? Hii haimaanishi kwamba tunakwenda kupata mteremko. Mkate wetu na maji vitakuwa vya uhakika (Isaya 33:16). Hayo yote ndiyo ya uhakika. Iwe ama tunaishi au tunakufa ni sawasawa na kusudi la Mungu.

 

Hali ya kujihisi hufai au hustahili ni rahisi sana kumpata mtu yeyote. Kukatatamaa kunaweza kujitokeza kutokana na matarajio yasiyojulikana na ambayo hayana uhusiano wowote na uhalisia wa mambo au Mpango wa Mungu.

Mithali 13:12 Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua. Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.

 

Malengo yetu yapasa yawe halisia na yanaoendana sawa na njia ya Mungu ya uzima. Mungu alitupa mlolongo wa amri zihusuzo masuala ya kijamii na kimaadili.

Zekaria 7:9-10 Bwana wa majeshi amesema hivi, ya kwamba, Fanyeni hukumu za kweli, kila mtu na amwonee ndugu yake rehema na huruma; 10 tena msimdhulumu mjane, wala yatima, wala mgeni, wala maskini; wala mtu awaye yote miongoni mwenu asiwaze mabaya juu ya ndugu yake moyoni mwake.

 

Tunaishi kwenye nyakati za jakamoyo sana, na Maandiko yafuatayo yanaonyesha taswira isiyopendeza ya wakati huu.

Warumi 1:29-31 Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, 30 wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, 31 wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema

 

2Timotheo 3:2-3 Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, 3 wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,

 

Daudi aliwashughulikia watu wasiojisikia.

Zaburi 69:20 Laumu imenivunja moyo, Nami ninaugua sana. Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu.  

 

Chanzo hiki cha mambo hakikuwa kimesemwa kwetu sisi. Yatupasa kuonyesha kujali, na inapasa ionekane wazi sana kwamba tunajali. Yatupasa kujiepusha na hali ya kujihesabia haki sisi wenyewe wakati wote.

 

Sisi sote tunapenda kushukuriwa na kuona kazi zetu zikitambuliwa. Kushukuriwa na kutiwamoyo ni mambo yaliyo rahisi kuyatoa na hayagharimu chochote. Ni mara nyingi kiasi gani tunakumbuka tumetumia zana hii? Ni rahisi kuwavunjamoyo wengine na pia kuchochea hamasa nyema. Ulimwengu umejawa na watu wenye mitazamo hasi walio rahisi kuwadunisha au kuwashushamoyo wengine. Mambo madogomadogo ndiyo yanayokumbukwa na kushukuriwa zaidi. Kupelekeana kadi au vijimemo, kupenana maua au zawadi, miito ya simu, tabasamu, maneno mazuri, au kukumbatiana, hivi vyote vinaonyesha kutianamoyo. Wakati mwingine hata ‘uwepo wako tu, kuwa pale’ kunatosha.

 

Kulisoma neno la Mungu kunafariji kwa kuwa ni mungu anasema na sisi.

Warumi 15:4-5 Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini. 5 Na Mungu mwenye saburi na faraja awajalie kunia mamoja ninyi kwa ninyi, kwa mfano wa Kristo Yesu;

 

Paulo aliujua sana umuhimu wa kutiamana moyo.

1Wathesalonike 2:11-12 vile vile, kama mjuavyo, jinsi tulivyomwonya kila mmoja wenu kama baba awaonyavyo watoto wake mwenyewe, tukiwatia moyo na kushuhudia; 12 ili mwenende kama ilivyo wajibu wenu kwa Mungu, mwenye kuwaita ninyi ili mwingie katika ufalme wake na utukufu wake.

 

Hivyo, yatupasa tufanye kama anavyosema Paulo kuhusu kutiana moyo.

1Wathesalonike 5:11 Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya.

 

Mungu anapenda familia yake iwe msaaida na iweza kutiana moyo.

 

Barnaba, ambaye jina lake lina maana ya mwana wa faraja (Matendo 4:36), alitumwa na Kanisa la Yerusalemu aende Anthiokia na aliwatiamoyo wote wabakie kwenye imani na wabakie wakweli kwa Bwana (Matendo 11:23-24).

 

Matendo 11:23-24 Naye, alipokwisha kufika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo. 24 Maana alikuwa mtu mwema amejaa Roho Mtakatifu na imani; watu wengi wakaongezeka upande wa Bwana.

Kumbuka kuwa Barnaba alikuwa mtu mzuri na mwema kwa kuwa alikuwa amejawa na Roho Mtakatifu na imani.

 

Ili kuwatiamoyo wengine yatupasa tujitiemoyo sisi wenyewe, ili tuweze kujiandaa kupokea faraja tutakazopewa. Mara nyingi watu hudhania kutiamoyo kwa namna ya kukubali au kuidhinisha itolewe kwa wengine kua wanastahili. Jiepushe na kudhania kuwa utiajimoyo endelevu ni budi uwe haukosolewi. Hayo ni makosa makubwa.

 

Kutiamoyo huenda ni aina ya faraja. Mungu alimfariji Daudi na atafanya vivyohivyo kwetu pia.

1Samweli 30:6 Naye Daudi akafadhaika sana; kwa sababu watu walikuwa wakisema kwamba apigwe kwa mawe, kwa maana nafsi za hao watu wote walisononeka, kila mtu kwa ajili ya wanawe na binti zake; lakini Daudi alijitia nguvu katika Bwana, Mungu wake.  

Huu ni mchakato wa uweza wa Roho Mtakatifu.

2Wakorintho 4:16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.  

 

Waebrania 10:24-25 tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri; 25 wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.

 

Wafilipi 4:13 Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.

 

Tunayaweza mambo yote katika yeye atutiaye nguvu, ambavyo ni kwa kupitia Roho Mtakatifu wa Mungu.

 

Kama Wakristo, yatupasa tujiyajali matatizo ya wengine na tujue jinsi ya kuwafikia na kuwasaidia kwa njia chanya, kwa kuwa kuna wakati ambapo tulikuwa hatuzijui ahadi za Mungu au kuzijua Sheria zake. Hata hivyo, Mungu alitukomboa na kutuchukua kutoka kwenye giza na kutuleta kwenye nuru yake.

Waefeso 2:12 kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani.

 

Mithali 3:27 Usiwanyime watu mema yaliyo haki yao, Ikiwa katika uwezo wa mkono wako kuyatenda.

 

1Wakorintho 13 inaorodhesha upendo kuwa ni kama karama kuu zaidi ya Mungu kuliko nyingine zote alizotupa sisi. Mungu ametupa upendo wake bure kabisa pasipo malipo na anatutarajia tuwapende wengine kwa namna hiyohiyo. Yohana 13:35 inaliweka jambo hili wazi sana.

Yohana 13:35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.

 

Baadhi ya watu walioumizwa wanaweza wasiwe tayari kusimulia matatizo yao. Lakini yatupasa tukubaliane na hali ilivyo na sio kuwahukumu kw mazingira ambayo wanayokutana nayo. Yatupasa tuwe na weledi mkubwa wa kushirikishana vipindi vizuri na vigumu. Fundisho la kwamba ‘kuumwa ni matokeo ya dhambi’ sio fundisho la Mungu. Ni fundisho la mapepo. Mara nyingi watu hutaabika kwa magonjwa yanayojulikana sababu zake kwa wazi kutokana na ujinga wao. Hata hivyo, ni kweli kwamba kua wakati mwingine yanawapata kutokana na dhambi zilizoko duniani. Kama mtu ni mgonjwa, sio kwamba Mungu anamhukumu au kumpatiliza. Mafuudisho haya ya kujihesabia haki ni silaha inayokatisha tamaa zaidi kuwahi kuonekana miongoni mwa watu wa Mungu. Yatupasa kuwapa msaada pasipo kuhukumu kwa kufananisha mateso yao na dhambi.

Warumi 12:15 Furahini pamoja nao wafurahio; lieni pamoja nao waliao.

 

Wagalatia 6:2 Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo.

 

Waefeso 4:25 Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake.  

 

Daudi aliwaombolezea maadui zake wakati walipopatwa magonjwa au walipourwa, hata alifunga saumu kwa ajili yao.

Zaburi 35:13-14 Nalijifanya kama kwamba ni rafiki au ndugu yangu, Naliinama nikilia kama aliyefiwa na mamaye. 15 Lakini nikijikwaa hufurahi na kukusanyana, Walinikusanyikia watu ovyo nisiowajua, Wananipapura wala hawakomi.

 

Hakuna mtu anayetakiwa akumbane na vipindi vigumu peke yake.

Ayubu 6:14 Kwake huyo atakaye kuzima roho inapasa atendewe mema na rafiki; Hata kwake huyo aachaye kumcha Mwenyezi.  

 

Mungu anatushughulikia kwa kutupa faraja kubwa na njia ya rehema licha ya mapungufu yetu yote. Kwa hiyo juhudi zetu za kuwasaidia wengine yapasa iwe ya mtazamo chanya na yenye kumuinua mtu moyo wake. Twaweza kusaidia au kuzuia mkabala wetu.

Warumi 15:1-2 Basi imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wao wasio na nguvu, wala haitupasi kujipendeza wenyewe. 2 Kila mtu miongoni mwetu na ampendeze jirani yake, apate wema, akajengwe.

 

Wafilipi 2:1-5 Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema, 2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja. 3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. 4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. 5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

 

Tunaweza kushangaa Mungu yuko wapi tunapokuwa kwenye vilindi vya kuvunjika moyo na kusahau kutiwa moyo. Anatoa kwa kupitia ndugu wa kiume au dada. Yatupasa tuuone upendo wa Mungu likiwemo kwa Mkristo mwingine.

1John 4:16 Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

 

Wagalatia 6:10 Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.

 

Paulo alifarijiwa kwa ujio wa Tito akiwa na habari njema.

2Wakorintho 7:6 Lakini Mungu, mwenye kuwafariji wanyonge, alitufariji kwa kuja kwake Tito.

 

Waristo ni watu ambao Mungu huwatumia kuwafariji wengine.

Yohana 17:22-23 Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja. 23 Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.

 

Mungu nashughulika na kila mmoja wetu kwa upendo. Faraja ni kitu muhimu na kama silaha ya upendo ambao alimpa Kristo. Huenda ni vigumu sana kwetu kuchukuliana na vile alivyo Mungu kwa kuwa Mungu ana upendo uleule kwetu sisi kama ulivyo kwa Yesu Kristo.

John 17:26 Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.

 

1Yohana 4:7-8,12 Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu. 8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo. Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote. Tukipendana, Mungu hukaa ndani yetu, na pendo lake limekamilika ndani yetu.

 

Kupendana siyo kitu tulichonacho kama hatushikamani. Tumeamriwa kupendana.

Yohana 13:34-35 Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo. 35 Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.

 

Upendo huu ni unatoa, ushirikiano, kusaidia na kuutoa uhai wake. Ukiwa kama tabia kwenye upendo wa Mungu inatulazimu kuwasaidia wengine.

1Yohana 3:16-18 Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu. 17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo? 18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.

 

Upendo wa Mungu unaonekana unapenda kuwa na wale wanaozishika amri zake. Mama yetu na kaka zetu na dada zetu ni wale wanaoyatenda mapenzi ya Baba yetu wa Mbinguni.

 

Sehemu ya upendo ni huruma. Huruma ni hali ya kuonyesha masikitiko na kuchukuliana mizigo na mtu aliye kwenye mateso na shauku ya kuchukuliana maumivu. Tunahitaji kuonyesha uhusika wetu kwa kiasi cha kujihusisha. Kwa huruma tunahitaji kuonyesha masikitiko na tunajaribu kusaidia kuchukuliana mizigo na mtu aliyeko taabuni.

 

Kristo alikuwa na huruma sana kwa wanadamu. Mifano ya huruma ya Kristo ni hii hapa:

Mathayo 9:36 Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.

 

Mathayo 14:14 Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.

 

Mathayo 15:32 Yesu akawaita wanafunzi wake, akasema, Nawahurumia mkutano, kwa kuwa yapata siku tatu wamekaa pamoja nami, wala hawana kitu cha kula, tena kuwaaga wakifunga sipendi, wasije wakazimia njiani.

 

Luka 7:13 Bwana alipomwona alimwonea huruma, akamwambia, Usilie.

Kwenye mifano hii Kristo anatoa msaada kwa njia ya kufanya miujiza kwa Roho Mtakatifu kwa kuwaponya wagonjwa, kuwalisha wenye njaa na kuwafariji waliokuwa taabuni.

 

Hadithi ya Msamaria Mwema (Luka 10:25-37) inasisitiza hitaji la kunyoosha mikono yetu na kuwasaidia wote, na siyo kwa wapendwa wa imani moja na sisi peke yao. Msamaria alionyesha huruma kwa njia ya matendo na siyo kwa maneno matupu. Ilimgharimu Msamaria kuutoa muda wake, fedha zake na usumbufu mwingi ili kumsaidia adui. Kristo aliwaambia wale waliokuwa wanamsikiliza “Nenda kafanye hivyo. yatupasa kuwahurumia walio kwenye mateso, pasi kujali sababu inayowapelekea kuteseka.

 

Ni mara ngapi tumekuwa tukiwatia moyo wengine? Yapasa iwe kila siku na kuwa kitu endelevu .

Waebrania 3:13 Lakini mwonyane kila siku, maadamu iitwapo leo; ili mmoja wenu asifanywe mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.  

 

Tabia ya kutiamoyo inapasa uwe ni endelevu na inaweza kuwa na chimchuko la uponyaji. Kwa kutumia mbinu ya kumkabili mtu iliyo sahihi, tunaweza kuwaelekeza watu kwa Mungu wetu ambaye ndiye Mungu wa tumaini. Inahitaji ujasiri kufikia hatua ya kujiamini na kumtumaini Mungu na kuunyoosha mkono wetu wa msaada kwa wengine. Ni vigumu kubakia tukiwa wajasiri na tukiwa tumetiwamoyo kwa hiyari yetu wenyewe. Tunapomtii Mungu anatupa Roho wake ili tuweze kutiwamoyo na kua wajasiri kila siku, kama tukiomba na kuisoma Biblia. Kwa nyakati nyingine, mengi yamefikiwa kwa hali ya kuonyesha huruma tu. Wakati mwingine maombi ni kitendo pekee tunachoweza kukifanya, lakini kama tutakuwa na la zaidi kulifanya tunaeza kufanya hivyo pia.

 

Mtumaini Mungu Unapokata Tamaa

Kukata tamaa kunaweza kupelekea kutoka kwa haraka na hali ya kushindwa kufanikisha au wakati tunapotakiwa kufanya mabadiliko katika maisha yetu ambayo hayajazoeleka kwetu. Tunaweza pia kukata tamaa tunapokuwa tunakosa pakukimbilia--mahali salama. Kwa maneno mengine ni kwamba tunamhitaji mtu mwingine ambaye anayetulewa na kutusikiliza. Watu waliokata tamaa hawapendi kukosolewa. Ni rahisi kuikwaruza roho ya mtu kwa maneno tunayoyasema. Maneno yetu yanaweza kumsifu Mungu na kuwainua wengine au yanaweza kuharibu na kuwakatisha tamaa wengine. Yatupasa kufanya uamuzi sahihi.

Mithali 12:25 Uzito katika moyo wa mtu huuinamisha; Bali neno jema huufurahisha.

 

Kwenye Zaburi 31, Daudi alimuita Mungu ili apate ukombozi kwa wakati wake wa uhitaji na wakati marafiki zake walipomuacha. Akiwa mtu mwenye shida na matatizo, Daudi aliona kimbilio lake li katika Bwana. Akiwa na Mungu alijihisi kulindwa, salama na kutiwa moyo.

Zaburi 31:2 Unitegee sikio lako, uniokoe hima. Uwe kwangu mwamba wa nguvu, Nyumba yenye maboma ya kuniokoa.

Isome Zaburi hii yote ya 31.

 

Ingawaje twaweza hata kupata kukubaliwa na utiwaji moyo kutoka kwa wengine, tunajua kwamba Mungu anaona yote na ameahidi kutupa thawabu kama tutavumilia na kudumu kwenye imani na mwenendo wa Kikristo.

 

Mifano mingine ya Mungu alipotiamoyo na makusudi au malengo kwetu sisi kumesaidia sana.

Waefeso 2:10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.

 

Zaburi 16:11 Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako ziko furaha tele; Na katika mkono wako wa kuume Mna mema ya milele.

 

Wagalatia 6:9 Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.

 

Waebrania 6:10 Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia.

 

Zaburi 37:25 Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee, Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa Wala mzao wake akiomba chakula.

 

1Timotheo 6:6-8 Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa. 7 Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu; 8 ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.

 

Waebrania 13:15-16 Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake. 16 Lakini msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu.

 

2Petro 3:9 Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.

 

Warumi 8:28-30 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. 29 Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. 30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza. 

 

Kama tutatuliza mawazo yetu na kufumbia macho kimwili na kujikita kwenye mitazamo ya kiroho tungekuwa na ujasiri kujua kuwa hatuko peke yetu, lakini yatupasa tufanye sehemu yetu. Ni juu yetu kuyatumia maisha yetu kwa utukufu wa Mungu.

1Yohana 2:15-17 Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. 16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia. 17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

 

Siri ya kuridhika hauhusiani na vitu vya dunia hii. Sisi sote tunamtegemea Mungu.

Wafilipi 4:11-12 Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo. 12 Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa.

 

Matukio ya kukata tamaa kwenye maisha haya ya kimwili hayapasi kuyukatisha tamaa tena kabisa wakati tunapokuwa na mwelekeo sahihi. Tutakuwa tumejifunza, kama Paulo, kwamba kwa kupitia uhusiano wetu na Kristo tutakabiliana na kuvirudisha, kwa kuwa tunakuwa hatuvithamini tena vitu hivyo kwa kiwango cha juu sana.

Waebrania 13:5-6 Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa. 6 Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?  

 

Kama Mungu anaona tutabakia kuwa waaminifu kwenye madhaifu yetu. Anajua kuwa tutakuwa waaminifu wakati wote.

2 Wakorintho 1:8-10 Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi. 9 Naam, sisi wenyewe tulikuwa na hukumu ya mauti katika nafsi zetu ili tusijitumainie nafsi zetu, bali tumtumaini Mungu, awafufuaye wafu, 10 aliyetuokoa sisi katika mauti kuu namna ile; tena atatuokoa; ambaye tumemtumaini kwamba atazidi kutuokoa;

 

Uhusiano na Mungu ni kwenye kupenda wema na rehema. Hii iko hivyo ili kwamba tusikatishe tamaa.

Yeremia 10:24 Ee Bwana, unirudi kwa haki; si kwa hasira yako, usije ukaniangamiza.

 

Tunaweza kuwafanya wadogo zetu au wanaotusaidia na watoto wetu wakate tamaa kwa kupitia kitendo hiki cha kuwakatisha tamaa. Lakini Bwana angali anaadibisha bado na kwa hiyo yatupasa tufanye vivyohivyo, lakini ni kwa upendo na uzuri au wema.

Waebrania 12:5-6 tena mmeyasahau yale maonyo, yasemayo nanyi kama kusema na wana, Mwanangu, usiyadharau marudia ya Bwana, Wala usizimie moyo ukikemewa naye; 6 Maana yeye ambaye Bwana ampenda, humrudi, Naye humpiga kila mwana amkubaliye.

 

Mungu hapendi sisi tushindwe. Siyo kusudio lake kwamba sisi tujikwae na kushindwa.

Waebrania 12:2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.

Thawabu ya Kristo, kwa wale watakaopitia mateso hadi kufa, ni kuketi kwenye mkono wa kuume kwenye Kiti cha Enzi cha Mungu.

 

Mungu ametuahidi sisi kwamba tuwe na uhakika wa kupitia mateso na majaribu. Lengo ni kumtayarisha mtu awe mzuri na kumleta karibu kwa Mungu.

1Wakorintho 10:13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.

 

Wakati mwingine ni vigumu kuelea ni kwa nini Mungu anaruhusu tupatwe mateso. Na wala kilamara tunaona njia ya kujiepusha palepale. Watu wengine hukata tamaa wakati shinikizo linapokuwa kubwa sana na wanakuwa hawamtumaini Mungu kuwaona wanapoyapitia mateso haya na majaribu. Mara nyingi wanakuwa hawayaoni makusudio yake kwa sababu ya utofauti uliopo kati ya mwonekano wa nje na sisi.

Isaya 55:8-9 Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana. 9 Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu. 

 

Lakini Mungu wetu mkuu ni Mungu wa faraja na kama tutafanya sehemu yetu, ndipo naye atafanya sehemu yake.

2Wakorintho 1:3-4 Na ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa rehema, Mungu wa faraja yote;
4 atufarijiye katika dhiki zetu zote ili nasi tupate kuwafariji wale walio katika dhiki za namna zote, kwa faraja hizo, tunazofarijiwa na Mungu.

 

Jinsi ya kujiepusha kutoka na majaribu ni kumtegemea Mungu. Anaweza kubadilisha hali iliyopo au vinginevyo hawezi kufanya hivyo, lakini Roho wake atatusaidia kustahimili.

Wagalatia 5:22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

 

Majaribu hayatakoma milele, yapo kwa majira na majira kadha wa kadha. La muhimu ni kujifunza somo kutokana na majaribu hayo.

1Petro 1:6-7 Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali; 7 ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.

 

Ayubu alilijua jambo hilo:

Ayubu 23:10 Lakini yeye aijua njia niendeayo; Akisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.

 

Mungu anahusika binafsi yake kabisa maishani mwetu. Kila mmoja wetu ni wa muhimu kwa Mungu. Sisi sote tupo sawa na ni binadamu tuliotofautiana. Daudi alilijua hilo.

Zaburi 139:13-16 Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu, Uliniunga tumboni mwa mama yangu. 14 Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha. Matendo yako ni ya ajabu, Na nafsi yangu yajua sana, 15 Mifupa yangu haikusitirika kwako, Nilipoumbwa kwa siri, Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi; 16 Macho yako yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.

 

Daudi alitiwamoyo kwa nguvu nyingi za Mungu.

Zaburi 29:10-11 Bwana aliketi juu ya Gharika; Naam, Bwana ameketi hali ya mfalme milele. 11 Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani.

Paulo aliujua pia uweza wa Mungu na alitusihi tuuelewe.

Waefeso 1:18-19 macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo; 19 na ubora wa ukuu wa uweza wake ndani yetu tuaminio jinsi ulivyo; kwa kadiri ya utendaji wa nguvu za uweza wake;

 

Waefeso 6:10 Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.

 

Kwa kupitia magumu na mateso tunajifunza kumtumainia Mungu na kumtegemea atuokoe. Wakati mwingine wakati tunapokuwa tukipelekea kuwa kwenye kiwango cha chini sana kwamba tunamtafuta Mungu. Lakini yatupasa tumtafute yeye kwa namna mbili zote, kwa nyakati mbaya na nzuri zote. Jaribu lolote laweza kuwa ni kikwazo kama tutaliruhusu. Ni wazi sana kwamba Shetani anataka tushindwe. Anajua kuwa tunahitaji kuyajaza mawazo na nia zetu na Roho wa Mungu ili tusishindwe na kuangukia kama wahanga wa mashaka ya Shetani anayojaribu kutuingizia akilini mwetu. Tunapomuacha mlinzi wetu mbali na kumuacha, ndipo tunakuwa mawindo mazuri ya kukamatwa. Mungu yupo ili kutusaidia kwa wakati wote, kwa hiyo, badala ya kufikiri ni lazima tushindwe, yatupasa tuwe ni watu wenye matarajio makubwa na kutazamia mambo mema na mazuri.

 

Maneno ya kushukuru, ya kutiamoyo na ya kusifia ni ya muhimu kusikika kwenye hisia zetu kwa kujisikia kuwa tunastahili. Maneno mazuri ya mrengo chanya ya upendo yanaweza kumfanya mtu kuwa hata na afya njema na kupata upomyaji wa kihisia.

 

Mithali 12:18 Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya.

 

Mithali 16:24 Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; Ni tamu nafsini, na afya mifupani.

 

Mafanikio yetu yanatokana na imani yetu kwa Mungu na kwa jinsi tunavyosaidiana sisi kwa sisi kwa maongozi ya Yesu Kristo kwa njia ya Roho Mtakatifu.

q