Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[CB5]

 

 

 

Hapo Mwanzo

(Toleo La 2.0 20030706-20061230)

 

Hapo mwanzo Mungu aliumba. Jarida hili limetokana na Sura ya 1 ya Hadithi ya Biblia Toleo la 1 lililoandikwa na Basil Wolverton likachapishwa na idara ya machapisho ya Ambassador College. Dhana au wazo limeongezwa na kuendelezwa kwa mujibu wa mafundisho ya Biblia na mafundisho ya shirika hili hili la Makanisa ya Kikristo ya Mungu.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2003, 2006 Christian Churches of God,  ed. Wade Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Hapo Mwanzo


 


Hadithi ya uumbaji

Ni kama kulivyokuwa na wakati ambao mji wetu na wazazi wetu walikuwa hawajazaliwa na kuwepo bado, kulikuwa na wakati pia ambao hii sayari tunayoikaa na kuishi ndani yake ilikuwa haijawepo bado. Wengi wetu huenda tunashangaa jinsi vitu vilivyokuwa huko nyuma kabla hakujakuwa na kitu chochote kwenye anga lisilo na kitu la ulimwengu wetu huu tulionao sasa. Vilikuwa wapi basi jua mwezi na nyota na vilitokea wapi? Ni vigumu sana kwa akili zetu kuweka taswira kwa kurudisha nyuma mawazo yetu hadi kwenye kipindi hiki kirefu cha wakati ambacho hakukuwa na kitu chochote cha kukiona ila ni baridi iliyo tupu tu, kwenye anga la giza. Lakini kulikuwa na kitufulani kingine hapo kilichochukua nafasi ya hizo nyota na sayari nyinginezo.

 

Ni nani au ni kitu gani basi chaweza kuwa kilikuwepo hapo? Jibu ni kwamba ni Eloa, Mungu wa Pekee na wa Kweli (Yohana 17:3; 1Yohana 5:20). Ni Mungu ndiye alikuwa hapo kwanza kwa kuwa ndiye aiyeumba kila kitu kilichokuwepo na kilichopo (Mwanzo 1:1; Nehemia 9:6, Zaburi 124:8; Isaya 40:26, 28; 44:24; Matendo 14:15; 17:24, 25; Ufunuo 1:8; 4:11; 14:7).

 

Huenda mojawapo ya vitu vya kwanza tunavyovishangaa ni swali kuu tulilonalo kwamba ni wapi basi huyu Mungu alikotokea. Jibu ni kwamba yeye hakutokea mahali popote na wala hatokani na kitu chochote. Ingawa kila kitu kina mwanzo wake, lakini Mungu amekuwepo wakati wowote (Zaburi 90:2). Kulikuwa na wakati ambao aliishi pekeyake. Hakuhitaji kitu chochote ili kumuwezesha awe hai au apate nguvu. Mungu anaishi na kudumu milele (Isaya 57:15). Mungu amekuwepo wakati wote na atazidi kuwepo. Yeye ni mwanzo na mwisho (Ufunuo 1:8). Yeye huishi milele na hafi (1Timotheo 6:16). Hii maana yake ni kwamba hawezi kufa.

 

Kwa kuwa sisi tu viumbe wa kimwili, mambo haya ni vigumu sana kwetu kuyaelewa. Inatupasa tu kuelewa kwamba kuna mambo mengine ambayo Mungu ameyaweka kuwa siri tusiyajue. Mengi ya mambo hayo ametufunulia, hasa wakati tunapokuwa watiifu kwake (Mithali 16:3).

 

Swali linguine ni kwamba, hivi Mungu anafananaje? Tunajua jinsi wanadamu walivyo kwa kuwa tunawaona. Wazazi wetu, kaka zetu na dada zetu ni familia au jamii ya kibinadamu walioumbwa kwa mwili na damu kwa sura na mfano wa Mungu (Mwanzo 1:26). Hii haimaanishi kwamba Eloa, Mungu wa Pekee wa Kweli anafanana na sisi. Inamaanisha kwamba wanadamu waliumbwa kwa namna ya kimungu (elohim), wakati wanyama wengine wote waliumbwa kwa namna yao wenyewe tu nyingine. Kwa ajili hii, wanadamu wamekuwa ni watofauti sana kabisa kulinganisha na wanyama walioumbwa na Mungu.

 

Mungu si mwanadamu, bali ni kiumbe wa Roho kamilifu na takatifu. Viumbe wa kiroho hawahitaji kanuni za wakati wala eneo au anga kuweza kufanya mambo yao. Wanadamu kwa kawaida hawawaoni au kuwwahisi au kuwasikia hawa roho, ila wanaweza kuvutwa ama kushawishiwa nao. Hii ndiyo sababu mojawapo ya kwa nini Shetani anaitwa mfalme wa nguzu za anga (Waefeso 2:2). Anawashawishi watu waziasi Sheria za Mungu.

 

Kwa hiyo, hatuwezi kumuona Mungu kwa kuangalia angani kwa kutafakari mamilioni ya miaka iliyopita, ingawaje Mungu alikuwepo wakati huo wote. Hata hivyo, tunaweza kuyaona mambo ambayo Mungu ameyaumba. Mungu alijua jinsi angalivyofanya hilo. Anauweza wote na hakuna kinachomshinda na asichokiweza yeye Mungu (Luka 1:37). Soma jarida la Mungu ni Nani? (Na. CB1).

 

Hatujui ni lini hasa ulimwengu huu ulipoumbwa, au ilichukua muda gani kuuumba ulimwengu huu wote. Lakini Biblia inatueleza kuhusu uumbaji. Ulimwengu ni mkubwa sana kiasi kwamba tunaweza kuona sehemu tu ya mambo ulionayo. Mawazo yetu hayawezi hata kuanza kugundua ukubwa wake wa ajabu, lakini hii na itupe sisi fikra ya ni kwa kiasi gani basi Muumbaji alivyo na busara kubwa na uweza mkubwa kuliko sisi (Ayubu 22:12; 33:12; 38:4-6).

 

Miongoni mwa makundi ya nyota zinazoipendeza Dunia yetu ziliumbwa. Wanadamu wamekuwa na mawazo mengi na nadharia mbalimbali ya jinsi dunia ilivyofanyika hadi kuumbwa kwake na jinsi hizi nyota zilivyoweza kuwa pale. Wajinga wengi huamini na kufundisha kuwa nyota zote ni sayari “zilizotokea” tu zenyewe pasipo Mungu kuziumba. Biblia haikuweka shaka ya kwamba kama kuna Mungu, ila inasema kuwa kuna Mungu aliyekuwepo tangu mwanzo wa yote na kwenye mwanzo wa uumbaji. Ni mpumbavu tu ndiye anayesema kuwa hakuna Mungu (Zaburi 53:1).

 

Kama tungeiona jinsi Dunia ilivyokuwa baada ya kuumbwa kwake, basi tungeuona ulimwengu mkubwa wenye mchanganyiko wa rangi za bluu na kijani wenye uzuri mkubwa ukining’inia dhidi ya kile wasomi wa mambo ta nyota na anga wanachokielezea kuwa zilidondoka kutoka angani. Tusingeweza kutambua hata mabara yaliyoko kwenye sayari yetu au mipaka yake, kwa kuwa ilipoumbwa mara ya kwanza ilikuwa ni tofauti sana na hivi ilivyo leo.

 

Ili kuviumba vitu vyote ulimwenguni, Mungu angehitaji akusanye vifaa mbalimbali kama mafundi seremala wanavyohitaji vifaa vya kujengea nyumba tunazoishi ndani yake (Waebrania 11:3). Kama tulivyokwisha kujua tayari, Mungu ni Roho. Na kama nuru inavyomulika kutoka kwenye taa na kukijaza chumba chote, ndipo Roho Mtakatifu wa Mungu alivyotoka kutoka kwake na kuenea ulimwenguni. Uweza huu ambao ni siri na wa ajabu ndio asili halisia ya Mungu. Kwa uweza wake ulimwengu uliumbwa na kutokana na huo kila nguvu za kimwili na na mwili mwili huu dhaifu unathibitiwa. Soma jarida la Roho Mtakatifu ni Nini? (Na. CB3).

Mwanzo wa Uumbaji

 

Mwanzo 1:1-2 Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. 2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

 

Hapa tunaona mwanzo wa uumbaji wa Mbingu na Nchi. Hii inaelezea kuhusu dunia ambayo ilikuja kuwa (2Petro 3:5-6) kabla haijawa tohu na bohu au ikwa tupu bila kuwa na umbo na tupu. Ilikuwa imeumbwa kwa siku nyingi sana zilizopita. Lakini ilikujakuharibiwa (soma jinsi ilivyoandikwa kwenye aya ya 1 na 2 ya Biblia ya The Companion Bible). tutaielelezea sababu ya hiyo kadiri tunavyoendelea mbele.

 

Wana wa Mungu

Mungu hakuiumba huu ulimwengu kwa kubahatisha ili hatimaye aishangae kazi yake. Kwa namna fulani Mungu anapenda kuifanya familia kwa ajili yake mwenyewe. Kwanza kabisa aliumba mamilioni ya viumbe wa kiroho ili waishi kwenye huu ulimwengu. Wengi wao walimtumikia kwenye Mbingu ya tatu, mahali alipoweka Kiti chake cha Enzi (2Wakorintho 12:2). Hatuambiwi ni mahali gani ilipo Mbingu hii ya tatu, lakini huenda iko mahali fulani kwenye anga la mawingu ya pande za mbali za Kaskazini (Isaya 14:13). Tunajua kwamba ni mahali ambapo mwanadamu hawezi kupaona kwa macho yake ni kama viumbe wa kiroho tusivyoweza kuwaona (2Wakorintho 4:18).

 

Mungu alijua pia kwamba viumbe wake aliowauba watakuja wajibika kutenda kazi zao kwa kufuata Sheria zake. Viumbe hawa walikuwa ni wana wa Mungu (elohim) na walipewa Roho Mtakatifu ili waweze kuwasiliana na Baba na wao kwa wao. Mungu aliwatia mafuta watoto wake wawili kati ya wale wengine ili wawe ni Kerubi Wafunikao wa Baraza la Elohim. Mmoja wao ni huyu aliyekuja hatimaye kuwa ni Masihi (Wakolosai 1:15) na mwingine alikuwa ni huyu kiumbe (Lusifa) tunayemjua sasa na kumuita kuwa ni Shetani (Ezekieli 28:14-16). Soma pia majarida ya Yesu ni Nani? (Na. CB2) na Uumbaji wa Familia ya Mungu (Na. CB4).

 

Mungu alimfanya Lusifa kuwa ni wa Dunia iliyofanywa tena, ambayo mamilioni ya malaika walipelekwa kuishi ndani yake. Lusifa ndiye alipewa jukumu la kuwatawala na kuwasimamia malaika hawa hapa Duniani kwa kuzisimamia sheria na amri zote za Mungu. Lusifa alikuwa ni mwerevu sana, mzuri na mwenye uwezo. Alikuwa mkamilifu katika njia zake wakati alipoumbwa, na alikuwa na uwezo mkubwa wa kiujuzi na kimuonekano wa umbo lake jina Lusifa maana yake ni Mleta Nuru, au Nyota Ing’aayo ya Mapambazuko.

 

Kwakuwa Mungu aliumba na kuumiliki ulimwengu, basi yeye ni mtawala mkuu na bora wa huu ulimwengu. Mwanzoni huko Lusifa alikuwa anamtii. Alifanya yote ambayo Mungu alikuwa anamuamuru. Kulikuwa na kipindi cha miaka na miaka ya furaha na kurithika katikati ya malaika wakati wao na Lusifeli walikuwa wanatii kila moja ya Sheria za Mungu. Hii ni kwa kuwa Sheria za Mungu zimetolewa ili kuwafanya viumbe wafurahi. Mambo yalienda vizuri sana kwa kadiri Lusifeli alipokuwa anazitii sheria au kanuni za Mungu na maelekezo yake (Ezekieli 28:13-15).

 

Lakini katika kipindi alichoyaruhusu mawazo maovu kuingi moyoni mwake. "Mimi ni mfalme wa mamilioni ya malaika," alidhani. "Pamoja nao maunda jeshi kubwa na lenye nguvu vya kutosha kuwashambulia na kuwashinda malaika wa Mungu wanaotupinga. Na kama nitakitwaa kiti cha enzi cha Mungu huko Mbinguni na kumuondoa Mungu, basi nitafanyika kuwa mtawala bora wa ulimwengu wote!" (Isaya 14:12-14).

 

Wazo la kumshinda Mungu na kuchukua nafasi yake lilisababisha majivuno na kiburi kwa kiasi kikubwa sana na kuibuka kwa machukizo. Kwa kadiri wazo hili lilipozidi kukua na tamaa hii na muwako wa shauku ya kuonyesha muwako wa shauku na matamanio yake.

 

Hatimaye Lusifeli anaufanya mpango wake ujulikane na wale waliokuwa wanaonyesha kupenda kumsikiliza na huku akijaribu kuwaahidi kuwa atawafanya kuwa watawala, kwenye utawala wake, kwenye ulimwengu mwingine, na kuwapa nyadhifa za juu hata huko Mbinguni wale wote watakaoasi pamoja nay eye. Aliwarubuni kiasi cha kufanikiwa kuwapata theluthi moja ya malaika wote wakapumbazika vya kutosha kujitoa mhanga kwa kuhatarisha furaha yao kwa kujiunga na mpango wake muovu (Ufunuo 12:4; Ayubu 4:18). Theluthi mbili nyingine walibakia watiifu kwa Muumba wao.

 

Kiburi, majivuno na ulafi vilivyotokana na mawazo mabaya viliifanya busara kubwa ya Lusifa kubadilika. Vinginevyo, angeweza kujua kwamba kuifanikisha vita ya kupigana na Muumbaji isingewezekana. Fikra zake zilibadilika sana hasa ni kutokana na kwamba  fikra na mawazo yake yalikuwa ni mabaya. Huku akiwa amejazwa na mawazo ya kwamba angeweza kumshinda Muumba wake, Lusifa akaendelea na mchakato wa kuandaa mipango yake ya uasi. Akiwa pamoja na mamilioni ya malaika waliokuwa tayari kumtii yye badala ya Mungu, aliichafua Mbingu na wenzake hawa na kuanzisha mashambulizi.

 

Vita hii ilipeleke idadi kubwa ya viumbe wa kiroho waongezeke, ni kitu cha kusikitisha sana. Wanadamu hawajui chochote kilicho kigeni na majeshi haya yenye kusababisha maafa makubwa yaliyotumika. Hata mbomu ya haidrojeni na kobalti hayawezi kulinganishwa na nguvu zilizo kwenye amri ya Mungu. Mara zote Mungu amekuwa na viumbe wenye nguvu nyingi sana wakiwemo. Hakuja majeshi ya wanadamu au rogo zilizo na nguvu nyingi za kuweza kumuondoa kwenye kiti chake cha enzi.

 

Lusifeli alipitia kwenye kipindi kibaya cha kushindwa. Nguvu nyingi zisizoweza kulinganishwa z Muumba iliwaangukia na kuyakamia majeshi haya kiasi kwamba washambulizi wake walipigwa bumbuazi kwa kipigo kiasi cha kuparaganyika na kutojielewa na ndipo wakafukuzwa kutoka Mbinguni na wakatupwa hapa Duniani (2Petro 2:4; Isaya 14:15).

 

Mungu hakuishia hapo tu katika kuwashughulikia malaika hawa waasi, hata hivyo, dhambi ya Lusifa ya uasi dhidi ya mamlaka na utawala wa Mungu ilimfanya ajikute akiwa hapa duniani na milki zake. Alipaswa kuitawala Dunia wakati tulipoletwa na kufanyika kuwa chini yake na kutolewa mbali na utawala wake kwa wakati mwingine na kutawala pamoja na Kristo ambaye siku moja atachukua mahala pake. Kwa matendo yake hayo kwa sehemu hii ya Mpango wa Mungu, yeye pamoja na wafuasi wake watahukumiwa.

 

Jina lake lilibadilishwa na kuwa Shetani ambalo maana yake ni adui kwa Kiebrania (Ufunuo 12:9), kwa kuwa amekuwa ni adui wa watu wa Mungu. Wale malaika waliomfuata walikuwa kutoka kwenye kundi la walioitwa baadae kuwa ni washitaki au wafanya mashitaka ya uwongo dhidi ya wanadamu. Kwa Kiyunani neno linalotumika kuwaelezea ni diabolos. Neno la Kiebrania litumikalo kuwaita roho hawa ni shade au shades. Pia waliitwa kama mabeberu au mazimwi, kutokana na ibada zinazoonekana kwenye imani za kipagani za mungu aitwaye Pan wa jangwani. Neno pepo linatokana na maana ya Kiyunani ya mungu au mungu mdogo. Manno yaliyochukuliwa kutoka kwenye maana hii ni kushawishika au kuvutiwa, au kuzoelezwa na mungu aliyeasi au "pepo". Maneno ya kiyunani yanayotokana kutoka kwenye neno asili la daimon ambalo lilitumika kama roho au nguvu za kimungu na lilitumika kwa maana zote mbili, yaani kwa maana mbaya na njema. Luka 4:33 inatumia neno pepo mchafu na neno linguine la pepo kuonyesha kuwa inaongelea roho mchafu.

 

Mapepo hawakuumbwa wakiwa waovu. Ni kama Kristo pamoja na watoto wote wa Mungu waliumbwa na uwezo wa kujua mema na mabaya. Lakini wengine wamechagua kutenda dhambi kwa kuasi na hii ilisababisha kuwepo na vita kubwa mbinguni, na ambayo bado inaendelea hata leo. Uasi huu ulisababisha mgawanyiko kwenye serikali ya Mungu. Na hii ilipelekea kuanza kwa dini nyingi za uwongo na miungu wa uwongo na dunia kujawa na maovu.

 

Hukumu ya kutisha ya dhambi

Popote ambapo Sheria za Mungu zinavunjwa, mateso, dhiki na maangamizo havinabudi kufuatia. Wakati wa ambano kuu wakati Shetani na mapepo wake walijaribu kupigana Mungu ili wamshinde, ndipo mabadiliko makubwa nay a kuhuzunisha yalikuja Duniani (Mwanzo 1:2). Ile iliyokuwa ni sayari ya kupendeza ilibadilika na kuwa mahali pa mavunjiko. Hatuna uhakika ni nini kilisababisha maangamizi haya. Hali ya hewa na mazingira yalichafuka. Inaonekana kuwa maasi ya Shetani na theluthi moja ya Malaika wa huko Mbinguni yalipelekea maangamizo makubwa ya uumbaji asilia uliokuwa hapo mwanzoni.

 

Uhai kidogo au wa kimwili ungeweza kumudu kwenye kipindi kile cha hatari; kwa kitambo dunia yetu ilibakia imezikwa au kufunikwa na blanketi au hewa, moshi na maji. Bahari ziliifunika Dunia yote. Haikuwepo tena ardhi kavu. Hali ya hewa ilikuwa ni imegubikwa sana mawingu ya mgandano au ukungu mdogomdogo kiasi kwamba hakuna nuru ingaliyoweza kuifikia bahari. Hatujui ni kwa muda gani hali hii ilidumu, lakini hatimaye ulikuja muda ambao Mungu alianza kuandaa kwa ajili ya tukio la muhimu sana kwenye Mpango wake Mkuu. Nao ulikuwa ni kumfanya mwanadamu awepo na kuishi.

 

Mungu alikuwa na upendo mkubwa sana wa kuuumba ulimwengu bora na wenye kupendeza kwa ajili ya viumbe wake. Angeweza kuumba tena pamona na elohim wake zama au ulimwengu mwingine ambao kwa sasa wanadamu wanaishi ndani yake.

 

Kuna sayari kadhaa nyingine sambamba na Dunia zilizo kwenye mzunguko zikilizunguka jua letu, na huenda kuna nyingine zaidi hapa ulimwenguni. Kwa kadiri tujuavyo, Dunia ilikuwa ni sayari pekee Mungu aliyoichagua na kuiandaa iwe kamao ya mwanadamu aliyeumbwa kwa sura na mfano wake.

 

Uumbaji wa zama hizi

"Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji." Kisha kwennye Mwanzo 2:1 tunasoma: "Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote". Uumbaji huu ulikuwa ni wa zama tulizonazo leo (2Petro 3:7) na ulifanyika kwa muda wa siku sita za uumbaji wa Mungu (siku za kazi) kabla hajapumzika siku ya saba ya juma hili.

 

Kwa hiyo, kutokana na Mwanzo 1:2-31 tunaona mwanzo mpya baada ya uasi na ulimwengu ulifanyika mtupu na wenye giza. Mbingu na Nchi hapa ni zile tunazozijua sasa (2Petro 3:7). Uliharibiwa tena katika siku za Nuhu kwa gharika kuu, lakini tutaliona hilo kwenye masomo mengine.

 

Kwa siku tano Mungu alisaidiwaa na elohim, au familia au miungu wadogo akiwaumba kama baba yao, akifanya kazi kama ya kuiumba Dunia mahala ambapo ingekuwa sahihi kwa kuishi mwanadamu (Mwanzo 1:23). Iligharimu nguvu kubwa na na nguvu za masikitiko kubadilisha uso wote wa sayari hii kwa kipindi cha chini ya juma moja.

 

Baba ana mpango mkamilifu na bora sana. Aliamua kile cha kufanya. Kisha alimuambia mjumbe maalumu, au malaika (ndilo neno la Kiyunani lenye maana ya mjumbe) ambaye anajulikana kama “Neno la Mungu” kwa kuwa alipaswa kuwa ni msemaji, asemaye kama anavyomuamuru Baba. Malaika huyu Mkuu ndiye Yule aliyewatokea Mababa wa imani na ndiye aliyempa Musa Torati. Hatimaye alizaliwa kama mwanadamu, na akafanyika kuwa Yesu Kristo. Mara hiyo, Roho Mtakatifu mwenye nguvu na uweza wote akafanya kitokee chochote ambacho Neno anakiamuru kitendeke. Hivyo ndivyo Mungu alivyoumba na kufana kila kitu kilichopo siku hizi kwa kupitia Yesu Kristo (Yohana 1:3).

 

Katika siku ya kwanza ya kuufanya uso wa Dunia, Mungu alisema, "Iwe nuru." Akaitenga nuru na giza na akaiita ile nuru ‘mchana’ na giza akaliita ‘usiku’. Kwa hiyo vile vimelea vya mchanganyiko wa moshi na gesi na mambo mengine ambayo yaliijaza mawingu viliondolewa mbali. Kwa hiyo nuru ndogo iliuja kwa kupitia Dunia kwa mara ya kwanza tangu Shetani na mapepo wake walipotupwa kutoka Mbinguni hadi hapa chini hapa duniani (Mwanzo 1:2-5).

 

Katika siku ya pili Mungu alifanya tabaka kubwa la hewa safi kwenye Dunia. Kwa kupitia hiyo maji mengi sana yalitiririka kwa mwendo kasi kutoka ardhini kuja juu ili kufanyiza mawingu makubwa na mengi angani juu mawinguni, na yenye hewa ya afya njema ambayo ilikuwa ni salama kwa kuivuta. Mchanganiko huu wa gesi yend day God produced a vast layer of fresh air over thye afya ulikuwa ni wa muhimu ili kumfanya mwanadamu aishi (Mwanzo 1:6-8). Mungu aliliita hili anga Mbingu (Mwanzo 1:8). Aliongelea pia kuhusu mbingu nyingine mbili, moja ni anga iliyo zaidi ya anga letu (Mwanzo 1:14), na lingine linaitwa Mbingu ya tatu, ambapo ndipo Kiti chake cha Enzi kilipo (Matendo 7:49; 2Wakorintho 12:2). Hatuambii wapi kilipo, na wataalamu wa mambo ya anga hawajawahi kukiona kamwe kwa kuwa hakionekani kwa macho ya kimwili kama utaratibu wa kiroho. Vitu vinavyoonekana vimefanywa kutoka kwenye vitu visivyoonekana.

 

Katika siku ya tatu, Muumba aliufanya uso na umbo la Dunia ili kwamba sehemu nyingine iwe juu na nyingine iwe chini. Tabaka kuu la maji likaizunguka dunia lilitiririka kuelekea maeneo ya chini yakisababisha mwonekano wa sura mbalimbali za bahari. Maeneo makubwa ya ardhi yaliachwa yakiwa juu ya maji, yakifanya migawanyo ya nchi kavu (Mwanzo 1:9-10). Katika nchi kavu Mungu alifanya kuwe na uoto – miti, vichaka, maua na nyasi –zimee kutoka ardhini. Katika siku ile ile ardhi ikaanza kuwa ya kijani na yenye uoto wa kila aina ulichipuka juu kutoka kwenye udongo (Mwanzo 1:11-13).

 

Katika siku ya nne Muumbaji aliifagia sehemu ya mwisho ya vumbi na hewa yenye madhara mawinguni, ambavyo ni kulifanya jua, mwezi na nyota zing’ae kwa mg’ao wake kamili ardhini na baharini. Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza. Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Kwa kweli hii inaongelea kuhusu jua na mwezi. Kisha aliziumba nyota (Mwanzo 1:14-19). Hapa tunaona kuwa Kalenda ya Mungu inawekwa na kuanza tangi mwanzoni tu. Pia soma Zaburi 104:19.

 

Katika siku ya tano aliumba nyangumi na aina zote za viumbe wa baharini. Katika siku hiyo aliumba pia aina mbalimbali ya ndege warukao angani. Mara tu ndipo angani na majini kukafurika na viumbe hai.

 

Muumbaji akaufanya kuwa mpya uso wa Dunia na kuujaza aina mbalimbali ya viumbe hai na uhai wenyewe kwa kipindi cha siku tano tu. Mwishoni kabisa alikuwa anakaribia kabisa kumfanya mwanadamu uwepo. Lakini kabla ya kumuumba mwanadamu katika siku ya sita, kulikuwa na udongo maalumu ambao viumbe watatakiwa watokane kwao. Hawa ni pamoja na tembo, ng’ombe, farasi, nguchito, minyoo, wadudu na kila aina ya kitu kinachotembea, chenye kutambaa na kutembea kwa tumbo (Mwanzo 1:24-25).

 

Manadamu anaumbwa

Hatimaye Mungu alifanya kazi ya mhimu sana ya kazi ya mikono yake. Akitumia vifaa kutoka kwenye kitu alichokiumba yaani Dunia, alimuumba mwanadamu! (Mwanzo 1:26-28).

 

Mbingu na Nchi ziliumbwa na elohim aliyesema, "Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi." (Mwanzo 1:26). Wanadamu wameamriwa kwenda na kuiongeza (kuijaza) Dunia (Mwanzo 1:28; sawa na Zaburi 8 na Waebrania 2:6-8).

 

Ingawa elohim alikuwa na kazi na majukumu ya namna mbalimbali kwenye uumbaji, Mungu wa Pekee na wa Kweli aliiumba Dunia kwa uweza wake na hekima yake.

Yeremia 10:12-13 Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu. 13 Atoapo sauti yake, pana mshindo wa maji mbinguni, Naye hupandisha mawingu toka ncha za nchi; Huifanyia mvua umeme, Huutoa upepo katika hazina zake. 

 

Bwana Mungu alimfanya mwanadamu wa kwanza kutoka kwenye mavumbi ya ardhi na kumpulizia pumzi ya uhai kwenye mianzi ya pua kisha akawa nafsi hai na mwanadamu akawa kiumbe shenye uhai (Mwanzo 2:7).

 

Mungu alimuita mwanadamu huyu wa kwanza kuwa ni Adamu. Ni mwanadamu wa kwanza kuishi miongoni mwa wote wenye mwili hapa duniani (1Wakorintho 15:45). Muumba alikuwa amekwishaandaa tayari bustani mzuri sana kwa ajili ya Adamu ili aishi na kufanya kazi humo (Mwanzo 2:8). Hapa palikuwa ni Edeni, nchi iliyoko huko Mashariki ya Kati pamoja na ile inayojulikana sasa kuwa maeneo ya Israeli na ni kaskazini mwa kingo za Tigri na Frati.

 

Mungu aliuw amepanga kuwaumba wanadamu. Alijua kuwa Adamu angekuwa ni mpweke iwapo kama angekuwa ni mwanadamu pekeyake lakini aliamua kupitia yeye amuumbe mwingine pia. Alichukua mojawapo ya mbavu za Adamu, wakati alipokuwa amelala na kuitumia kumuumba mwanamke. Akapewa Adamu kuwa ni mshirika na mwenzi wake. Adamu akamuita mwanamke huyu jina lake kuwa ni Hawa (Mwanzo 2:18-22).

 

Vitu hivi vyote alivitengeneza Mungu na aliviumba kwa muda wa siku sita za kazi. Kila siku na kisha na kwa hiyo ilikuwa na urefu wa saa ishirini na manne na zilikuwa ni ujsiku na mchana ni kama zilivyo siku hizi. Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. (Mwanzo 1:31).

 

Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote (Mwanzo 2:1).

 

Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. (Mwanzo 2:2-3). Aliita siku ya saba kuwa ni Sabato (Kutoka 16:26), kwa hiyo akaiichagua siku maalumu ya mapumziko na kuitenga kama ni kipindi cha saa ishirini na nne kama Siku yake maalumu ya Mapumziko. Akaweka Sheria kwamba mwanadamu anapaswa kuiheshimu na kuiadhimisha siku hii kiola wiki kwa kupumzika na kukutanika kwa ibada katika siku hii ya saba. Mungu aliifanya siku ile kuwa ni kipindi kitakatifu, na kuwaamuru watu wote kuiadhimisha kwa kuitakatifuza. Kama tulivyojua tayari kuwa Amri ya Nne inatuambia kuitunza siku ya Sabato na kuitakatifuza. Siku sita za kwanza zilikuwa ni kwa ajili ya wanadamu kufanya kazi na kucheza, lakini siku ya saba nay a mwisho ya juma Mungu aliitenga kwa ajili yake mwenyewe (Kutoka 20:8-11). Soma pia jarida la Siku ya Sabato (Na. CB21).

 

Tunaambiwa kwamba siu ya saba (Sabato) ni ukumbusho wa kutukumbusha kuhusu mapumziko ya Bwana kutoka kwenye kazi na mwishoi mwa juma la uumbaji. Lakini Kristo anatuambia sisi kwenye Biblia kwamba yeye amoja na Baba wangali wanafanya kazi bado (Yohana 5:17). Kwa hiyo, mapumziko haya ni ya endelevu na ni ishara ya mapumziko yajayo mbeleni (soma Waebrania 4:1-4).

 

Kwa hiyo inahitimisha juma la kwanza katika historia ya uumbaji na mpangilio wa sayari ambayo kwamba wanadamu wameishi ndani yake sasa kwa kipindi cha miaka elfu sita.

 

Kama tutaangalia kwa uangalifu na kwa ukaribu sana kwenye juma hili la kwanza la uumbaji tutauona Mpango wa Mungu wa Uokovu. Juma la uumbaji lilianzia siu ya kwanza ya juma (Jumapili) na likaendelea hadi siku ya saba ambayo ni Sabato (Jumamosi). Biblia inatuambia kwamba kwa Bwana, siku moja ni kama miaka elfu (2Petro 3:8). Juma la uumbaji linaonekana kama taswira ya miaka elfu saba, ambayo ndiyo Mpango wa Mungu kwa mwanadamu.

 

Kwa hiyo, miaka elfu sira ya kwanza mwanadamu yupo chini ya utawala wa Shetani na mapepo. miaka mingine elfu moja ya mwisho inaitwa Siku ya Bwana. Hii itakuwa ni Milenia itakayokuwa chini ya utawala wa Yesu Kristo na wateule wake, wakati atakapokuja kumnyang’anya Shetani na kuchukua mamlaka aliyonayo sasa. "nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu" (soma Ufunuo 20:4).

 

q