Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[095]

 

 

 

Kipindi cha Milenia na Dhana ya Unyakuo

(Toleo La 2.0 19950311-20000107)

 

Jarida hili linachambua kuhsusu nafasi ya waamini mafundisho yahusuyo kipindi cha millenia kwenye Kanisa dhidi ya dhana au mafundisho yaliyotapakaa ya siku hizi yajulikanayo kama unyakuo. Mafundisho ya zama kale yanaendelezwa kutoka kwa waandishi wa zamni. Chanzo au chimbuko la fundisho hili la unyakuo kinachambuliwa pia. Utunzi wa mafundisho ya siku hizi au ya kisasa na pia harakati za makasisi wa kimajeswiti  kina Ribera na mwenzake Bellarmine zinaelezew pia. Harakati za mtu aitwaye Samuel Maitland katika kuanzisha au kuzua mafundishohaya ya uwongo pia kunachambuliwa kwenye jarida hili.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 1995, 2000 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Kipindi cha Milenia na Dhana ya Unyakuo


 


Fundisho halisi la Kanisa la kwanzalilikuwa ni la imani juu ya kipindi cha utawala wa millennia. Kanisa lilingojea kwa hamu kurudi kwa Kristo na ufufuo wa watakatifu wakati atakaporudi. Na ndipo watakatifu watakapotawala Dunia kwa kipindi cha miaka elfu moja, na baada ya hapo ndipo Ufufuo wa (Jumla) wa Wafu ndipo utatokea, na kuhumu itafuatia baada ya kipindi hiki cha miaka elfu moja.

 

Kuna Maandiko Matakatifu mengi ya Agao la Kale yanayoshabihiana na maneno yaliyoandikwa kwenye Ufunuo 20 aya za 1-15 na kushabihiana na aya hizo. Tusipoelewa vizuri kuhusu fundisho ju ya ufufuo wa wafu na kipindi cha Milenia hatutaweza kuelewa kinachotokea wakati wa kuja kwake Masihi. Kwa mfano, hatutaweza kuelewa maana ya yaliyoandikwa kwenye Zekaria 14:16-19 kuhusu kuendelea kuadhimishwa kwa Sikukuu ya Vibanda na ulazima au umuhim wa kuwapeleka wawakilishi huko Yerusalemu. Waadventista Wasabato hawawezi kuyaelewa Maandiko haya Matakatifu. Na pia hawawezi kuelewa maana ya andiko la Isaya 66:20 na kurudishwa tena kwa maadhimisho ya Sabato na Miandamo ya Mwezi Mpya, kwa kuwa wao wanaamini uzushi wa Milenia ya mbinguni. Hawawezi kuelewa hata kidogo kuhusu maana ya nabii hizi za Agano la Kale zinazihsiana na marejeo ya Masihi, kwa kuwa hawawezi kuelewa hali yenyewe halisi na mazingira ya jinsi itakavyokuwa atakaporejea.

 

Watu wengi sana huko je wamepotoshwa, na tatizo ni kwamba, dhana ya imani yao imesimama kwenye mawazo ya kudhania na kufikirika tu na yasiyo halisi na yanayotokana na msukumo wa kimawazo wa kwenye Dunia hii wanayokaa, inavyoamini kuhusu ujio wa Masihi. Shetani amelishambulia sana fundisho la kweli kuhusu jambo hili na kufanya liwe ni makosa na chanzo cha upotoshaji kwa kipindi cha takriban miaka 2,000. Fundisho hili ni mojawapo ya mambo yanayolionyesha Kanisa la kweli na Ukristo wa kweli na linaloelewa vizuri mafundisho ya Biblia.

 

Sasa hebu na tuone Ufunuo 20:1-15.

Ufunuo 20:1-15

Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu; 3 akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache.

 

Hapa tunaona kuwa Shetani amewadanganya mataifa kwa kipindi chota hadi kuanza kwa kipindi hiki cha Milenia na kurudi kwake Yesu Kristo. Moja na fundisho analolipiga vita, na ambalo kwalo hulitumia kuwadanganya mataifa, ni la Mundo wa Serikali ya Mungu na uwepo wake katika Siku za Mwisho. Na hii ndiyo sababu kubwa itakayompelekea yeye kutupwa kwenye shimo refu lisilo na mwisho maarufu kama kuzimuni, kwa kuwa yeye ni mdanganyifu na ambaye dini ya uwongo inatokana na yeye.

 

4 Kisha nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, wakatawala pamoja na Kristo miaka elfu.

 

Andiko hili ni kiini au chanzo kikubwa sana cha mkanganyiko uliopo. Iliamriwa na baadhi ya waamini fundisho hili la Milenia wa Kanisa la kwanza kuwa ufufuo huu wa wafu na utawala au ufalme ni thawabu watakayopewa wafia dini peke yao. Yaani ni kwamba itamlazimu mtu kuuawa kwa kukata kichwa kwa ajili ya kumshuhudia Yesu ndipo atakuwa na sehemu kwenye Ufufuo huu wa Kwanza wa wafu. Hilo ndilo lilikuwa fundisho la mwanzoni mwa uchanga wa Kanisa katika karne ya kwanza. Hata hivyo, inaweza kusomeka hivyo kwa namna kama hiyo kwa kusema kuwa wale waliouawa kwa kukata vichwa watakuwa sehemu nyingine tofauti na wale waliokataa kumsujudia mnyama. Hawa ni wale walio na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanz wa Wafu.

 

Hii inamaana kuwa nguvu za mnyama italazimu kuendelea na kudumu kwa kipindi cha miaka 2,000, vinginevyo watakatifu hawatajaribiwa kwa kipindi hiki chote, na idadi kubwa ya watakatifu hawatakuwa na sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu, bali ni wafiadini peke yao. Kwa hiyo nguvu za mnyama ni lazima zitende kazi. Dhana hii ya kutenda kazi kwa nguvu za mnyama haipaswi kuonekana kuwa ni tafsiri ya waona mbali wa matukio ya Nyakati za Mwisho peke yao. Nguvu za mnyama zinapaswa kuwa ni kutu kinachoendelea kutokea na kuendelea pia, ili kwamba huyu mnyama aweze kuungana na kutenda kazi bega kwa bega na mkakati wa dini ya uwongo. Kwa hiyo, nguvu za mnyama wa nyakati za mwisho ni budi awe mwendelezo wa mkakati wa imani ya dini ya uwongo, lakini kuna atakayeukomesha muundo huu wa dini ya uwongo katika Siku za Mwisho.

5 Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. 6 Huo ndio ufufuo wa kwanza.

 

Kwa hiyo ni  wazi sana kwamba aina mbili za ufufuo wa wafu; wafu waliosalia watakuwa kwenye kipindi cha mwishoni cha Milenia. Kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu ni wa wale tu walioifia dini na waliokataa kuipokea alama ya Mnyama. Kwa hiyo ni wazi sana kabisa kuwa yatupasa sisi tujarbiwe hadi kufa, au tuikatae chapa ya mnyama, ili tuwe na sehem kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu.

6 Huo ndio ufufuo wa kwanza. Heri, na mtakatifu, ni yeye aliye na sehemu katika ufufuo wa kwanza; juu ya hao mauti ya pili haina nguvu; bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye hiyo miaka elfu.

 

Hii hi dhahiri shahiri. Kunakwenda kuwa na makuhani wa Mungu na wa Kristo na watatawala na Kristo kwa kipindi cha miaka elfu. Wanakwenda kuwa makuhani wa mambo mengine. Mtu hawezi kuwa kuhani kwa au wa Mungu, pasipo kuwa na kitu kinachompelekea yeye kuwa kuhani wake, kama mkusanyiko.

7 Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; 8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari.

 

Ni wazi sana kuwa kuna nguvu zilizo je ambazo ni nguvu za kimwili. Kwenye mwishoni wa miaka hii elfu kutakuwa na watu wenye mwili watakaochukua silaha na kuwaendea watakatifu kwa nia mbaya.

Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala. 10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.

 

Mnyama na nabii wa uwongo watakuwa ndio watasimamia mfumo wa uongozi, na imani na kuisimamia mikakati ya unabii wa uwongo. Hawatakuwa peke yao au mmoja mmoja. Nia inayokusudiwa kwenye maandiko haya imefafanuliwa kwa kina kwenye majarida ya Ufufuo wa Wafu (Na. 143) na Hukumu ya Mapepo (Na. 80).  Watu hawatupwi kwenye ziwa la moto, ispokuwa ni wakiwa na miili iliyokufa ya wale waliokataa kuokolewa. Hakuna kitu kinachoitwa au kujulikana kuwa ni mateso ya milele ya watu watakaokuwa kwenye hali ya roho watakaotupwa kwenye ziwa la moto.

11 Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

 

Hakuna ufufuo wa tatu wa wafu unaokusudiwa kufundishwa kutokana na andiko la Ufunuo 13. Fundisho hilo ni la kuzushwa kulikofanywa na baadhi ya wazushi kwenye Mkanisa ya Mungu ambalo limetokana na hisia zao za woga na linaweza kuitwa kuwa ni fundisho la uzushi na la woga (soma jarida la Uzushi Kuhusu Ufufuo wa Tatu wa Wafu (Na. 166)).

14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.

 

Kuna wazo linalowashwa kwenye ziwa la moto. Ni kwa mfumo mzima wote Duniani na kwenye mchakato wake wa kimwili unaozidi kuendelea.

15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.

 

Hii ilitolewa na Mungu na kumpa Yesu Kristo na ikaandikwa kwa kutofautisha na mtume Yohana. Hii imesaidiwa na maandiko kwenye kitabu cha Isaya na Zekaria na kwenye Injili, lakini kwa udogo au upana imetupilia mbali.

 

Mtazamo wa kurudi kwa Masihi umefikia kuharibiwa, na mtazamo asilia wa Kanisa ukafanyika kupewa jina la imani ya kuamini ujio wa Masihi kipindi cha kabla ya Milenia. Fundisho la utawala wa kipindi cha Milenia au itikadi ya kuamini utawala wa Milenia lilikuwa ndiyo mtazamo uliodumu na kuaminiwa na Kanisa la Wasabato. Ilifikia kiasi cha kupingwa na kugeuzwa au kupotoshwa na hata jina ililochukua na mafundisho ya uwongo na Teolojia ya Kiutatu.

 

Mtaaamo wa kwamba watakatifu wanaotawala walikuwa ni wale tu walioifia imani ulikuwa sio mtazamo Kanisa la Agano Jipya. Paulo alisema kuwa wale waliokuwa hai wasingewatangulia (au kuwazuia kama ilivyoqandika kwenye tafsiri ya Kiingereza ya KJV) waliokufa katika Kristo, lakini watakufanyika pamoja nao ili kuwa na Bwana na kuwa pamoja nae milele (1Wathesalonike 4:15-18). Hii ndiyo ilikuwa imani asilia ya waamini kipindi cha millennia na mtazamo wa Kanisa.

 

Waamini kipindi cha utawala wa Milenia au wale wamaitwa waandishi wa mrengo wa Milenia walikuwa ni Apollinaris, Commodianus, Hippolytus, Irenaeus, Justin Martyr (Mfiadini), Lactantius, Methodius (ambao walikiona kipindi hiki cha Milenia kama siku ya hukumu), Montanus, Nepos, Barnabas wa bandia, Tertullian na Victorinus. Dhana au fundisho la kuchelewa kwa juma la 70 linahusiana na andiko la Danieli 9:25 kwa Kristo hapo mwanzoni lilifundishwa na Hippolytus.

 

Fundisho hili liliendelezwa au kukuzwa kwenye kile kinachoitwa Uchiliadi, ambalo kimsingi kabisa ni fundisho la kile kinachoitwa Umilenianismu. Milenia ni neno lenye maana ya miaka elfu moja na kuna jina linguine pia linaloitwa Chiliadi na hili lina maana pia ya miaka elfu moja. Lakini kulikuwa na majina mengine mawili tofauti. Chiliadi ilichukuliwa pia baadae kwenye mafundisho ya waamini utawala wa miaka elfu wa Milenia, ambayo yalikuwa na mambo ya ziada na ya kimwili kwake. Wanostiki walianza kuendeleza imani hii ya Uchilism ambapo walikuwa na ziada ya namna ya kimwili na kipagani wa kuishi kwa kipindi cha miaka elfu moja. Iliangukia kwa kumvunjia heshima au kumdhalilisha kwa sababu ya waandishi wa Kinostiki.

 

Satani alilishambulia fundisho hili la Millennia kwa kutumia ukweli ulio kwenye fundisho hili kwa kuliongeza ili kuufananisha na mambo ya kimwili kwa namna zisizo za kawaida. Fundisho la waamini melinia lilitofautiana kwa fundisho hili la Uchliani kutokana na watakatifu walioifia imani watakavyotawala Dunia pamoja na Kristo, yakiwa yakienea mara nyingi kwa maandishi ya Wakristo ya zama ziliofuatia na kuwajumuisha Wakristo wengine wote watakaokutwa hai wakati atakapokuja Kristo, badala ya wale waliokwisha kufa kwa kuuawa wakiwa wanamshuhudia Kristo au wafia imani. Maandiko yaliyofuatia ya Uchiliani, hasahasa yale ya Lactantius na ya zama zake, yaliangukia kwenye malumbano ya ziada yaliyoufananisha na utawala wa kidunia ulioko Yerusalem, na wengine walifanya ionekane kuwa ni mafundisho ya kimwili zaidi kutokana na maandiko waliyoyachukua kutoka kwenye vyanzo vingine visivyo vya kbiblia.

 

Hatimaye Kanisa Katoliki likadai kuwa dhana hii ya utawala wa Milenia ilikuwa ni fundisho-tata na lisiloeleweka lililo kwenye imani ya Kiyahudi na wakapinga nia ya moja kwa moja ya tafsiri ya kitabu cha Ufunuo.

Wakasema: Ingawa ni vigumu kuitazama mara moja taswira iliyotumika kwenye Ufunuo na mambo yaliyoelezwa na wao, bado kunaweza kusiwe na mashaka kwamba maelezo yao yote yanayolinganishwa na mambo ya kiroho yanayolinganishwa na Kristo na Kanisa kwa upande mmoja na nguvu zenye madhara na maumivu za jehanamu na ulimwengu kwa upande mwingine. Hata hivyo, idadi kubwa ya Wakristo wa kipindi cha baada ya Mitume ,hasa huko Asia ndogo, walijikita. kwenye mafunuo ya kimapokeo ya Wayahudi; wakijaribu kuyapa maana au tafsiri za moja kwa moja kwenye maelezo na maandiko haya ya Ufunuo wa Yohana; na matokeo yake yake yalikuwa ni kwambaimani ya waamini millennia ilienea na ikapata utetezi wa nguvu sio kwa miongoni mwa wazushi peke yao, bali hata na Wakristo Wakatoliki pia. (Catholic Enc.,Vol. X Millennium, p. 308)

 

Hii inatuonysha sisi viwango vya upotoshaji. Kwa kweli Kanisa la Mwanzoni lilikuwa ni la waamini millennia. Sababu iliyolifanya Kanisa Katoliki lisipende ufunuo huu wa Wayahudi ni kwa sababu nguvu na mamlaka yake yaliegemea kwenye nchi na serikali ya Kiruma na Rumi ilikuwa ni Dolan a haikupenda ifundishwe hivyo (kuwa itatokea hivyo huko mwishoni) dhana hii ya utawala wa miaka elfu duniani na kwamba makao yake yatakuwa huko Yerusalemu. Wazo la Kristo kutawala kipindi cha miaka elfu moja hapa duniani na makao yake yakiwa Yerusalemu hi tatizo endelevu na lene dosari kwa zama moja hadi nyingine kwa Wakristo wa Ulaya. Hawapendi Kristo awe Myahudi na autawale ulimwengu akitokea Yerusalemu . na ndiyo maana watu hawa wanayapinga maana iliyo wazi ya Biblia ya kuwepo kwa kipindi cha Milenia.

 

Cerinthus Mnostiki alichora au kuchapisha picha za matukio ya Milenia kwa rangi angavu sana (C.E. ibid.) (Caius in Eusebius, “Hist. Eccl.”, III, 28; Dionysius Alex. in Eusebius ibid., VII, 25).

 

Askofu Papius wa Hierapolis, mwanafunzi wa Yohana alikuwa ni mtetezi mzuri wa imani hii ya Milenia. Anadaiwa kuwa alikuwa Mkatoliki na J.P. Kirsch CE. (ibid.); hata hivyo hilo haliwezekani kupewa mbinu za kimafundisho ya Athanasians kama kanisa. Wote wawili, yaani Papius na Irenaeus walidaiwa kuwa walijifunza mafundisho ya Milenia kutoka kwa Yohana. Irenaeus ameandika kuwa Mzee (Presbyteri) mwingine ambaye alimuona na kumsikiliza mwanafunzi wa Yohana na aliyejifunza kutoka kwake alifundisha na mwenyewe kuwa wa imani hii ya Milenia na hili alilifanya kuwa ni sehemu ya fundisho alilofundisha Bwana.

 

Kwa hiyo hapa tuna mashahidi wawili. Irenaeus anasema wazi sana maaskofu wengine wote na viongozi wa makanisa kuwa walimuona na kumsikia Yohana akiwafundisha fundisho hili la Milenia yeye mwenyewe. Kuna shuhuda wa macho. Mtu fulani aliyemuona Yohana alijifunza kutoka kwake, na kwa wanafunzi wake. Walikuwa na mafundisho ya Yohana ambayo yalikuwa ni mafundisho ya Milenia na kuwa yalikuwa ni sehemu mafundisho muhimu ya Bwana, na kisha walisema kuwa ni mafundisho ya Kanisa ya kwanza.

 

Kwa mujibu wa Eusebius (Hist. Eccl., III, 39), Papius, kwenye kitabu chake, anadai kwamba ufufuo wa wafu ungefuatiwa na kipindi cha ufalme mtukufu sana kuwahi kutokea ulimwenguni ambao ni wa Kristo, na kwa mujibu wa Irenaeus (Adv. Her V, 32-33), alifundisha kwamba watakatifu nao wangefaidi raha au starehe nyingi zisizoelezeka za hapa duniani kipindi hiki cha Milenia (soma pia kitabu cha Cath. Enc. op.cit.). kwa hiyo hata watakatifu wa hapa duniani wanaweza, kwa mujibu wa Irenaeus, kuchukua umbo la kimwili na kuwa na sehemu kwenye utawala ule.

 

Injili ya Mt. Barnaba inadaiwa pia kuwa na dhana hii ya kimilenia. Dhana ya kuwa na siku sita za kazi za kila jma na Sabato kuwa ni siku ya ibada na mapumziko inaonekana kudumu kwa kpindi cha miaka elfu sita ya Mpango wa kazi ya Mungu, na kipindi cha miaka elfu cha mapumziko ya Milenia. Kwa hiyo kipindi cha miaka elfu saba ni dhana na fundisho lililokuwa kwenye imani na mafundisho ya Wakristo wa zamani wa Kiyahudi.

 

Kanisa la kwanza lilielewa kwamba Sabato ya kila juma ilikuwa ni taswira ya kipindi hiki cha miaka elfu sita cha utawala wa Shetani na cha kazi ya Mungu, na ile siku ya saba ilikuwa ni taswira ya kipindi cha miaka elfu moja ya Milenia. Huu umekuwa ndio mtazamo na imani ya Kanisa la Mungu, kwa kipindi cha takriban miaka 2,000 na hii ndiyo sababu lilikuwa linashambuliwa. Fundisho hili limekuwa likipingwa wakati wote, kwa kuwa tunaelewa hilo. Na ndio maana Sabato inapingwa na kushambuliwa, kwa sababu Sabato pia ni taswira ya kipindi cha Milenia.

 

Mfiadini Justin wa Roma kwenye mdahalo wake alioufanya na Trypho (Ukurasa wa 80-81) anafafanua mahala pa Milenia kwenye Biblia. Anagundua kuwa hata hivyo kulikuwa na Wakristo wengi sana ambao hawakuamini fundisho hili.

 

Melito, askofu wa Sardi katika karne ya pili, alielezea mafundisho ya millenia na akafuatiwa na Irenaeus kwenye mtazamo wake.

 

Waumini wa mafundisho ya Montani walikuwa pia waaminifu na waliosimama imara wanaoamini fundiho hili la Milenia. Tertullian aliyekuwa nguli au kiongozi wa waamini mafundisho ya Montani aliyafundisha kwa kina mafundisho haya kwenye kitabu chake ambacho kwa sasa kimepotezwa cha De Spe Fidelium na kwenye kitabu cha Adv. Marcionem, IV.

 

Kitendo cha kuyakataa mafundisho na itikadi ya Milenia kimsingi kilitokana na imani ya Wanostiki (soma pia kitabu cha Cath. Enc. op. cit.). Hata hivyo, chanzo kikuu cha kukataa huku ni hawahawa wapinga imani ya Kiyahudi au Usemitiki. Ilipingwa pia na Alogi huko Asia Ndogo, na walikataa sio Ufunuo peke yake (wakimuonesha au kumlinganisha na Cerinthus) bali pia Injili ya Yohana. Vita dhidi ya imani ya Milenia ilienda mkono kwa mkono na vita dihi ya wafuasi wa Montana waliujlikana kama wa Montanists. Mafundisho ya uzushi yaliibuka ambayo nayo yalifundisha imani ya Milenia. Ni tabia ya Shetani kufanya kazi zake kwa namna hii kila mara. Atalianzisha kundi lenye mafundisho ya kizushi mengi yanayochanganya na kweli ndani yake, na kuwakutanisha pamoja na kisha wakaanza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe. Kwa hiyo kwenye vuguvugu hili la kweli kuchanganywa na uwongo hatimaye ile kweli inaondolewa mbali na uwongo unashinda.

 

Kuelekea mwishoni mwa karne ya pili na mwanzoni mwa karne ya tatu, mzee maarufu wa kanisa la Kirumu kwa jina Caius aliyashambulia sana mafundisho haya ya Milenia pamoja na mwingine aliyeitwa kwa jina Hyppolytus wa hukohuko Roma wakiyazuia yasiendelee wala watu wake wasiyatetee.

 

Mpinzani aliyekuwa na nguvu sana kupinga imani hii ya Umilenia alikuwa Origen wa Alexandria. Kwa hiyo basi hii ilipelekea mgawanyiko wa kimafundisho huko Alexandria, ambao uliishia kukomeshwa na sundisho la Uungu, ambalo lilishambulia pia maana halisi yaliyoko kwenye Maandiko Matakatifu.

Kwa mtazamo wa kile kinachojulikana kama Neo-Platonism ambayo kwayo ndipo mafundisho yake yalitokana na mtindo wa tafsiri yake iliyojlikana sana kama ni ya kuyatafsiri maandiko kwa kiroho peke yake ailioutumia katika kuyachambua Maandiko Matakatifu, na asingeweza kushiriki kwenye imani ya Milenia. Aliyashikilia mafundisho haya kwa kusisitiza sana na kuibuka na ushawishi mkubwa ambavyo maandiko ya vitabu vyake yalituama kwenye teolojia ya kikanisa hasa kwenye nchi za Mashariki, ndipo fundisho la millennia lilitoweka kidogokidogo kwenye mawazo na mafundisho ya Wakristo wa Mashariki (Cath. Enc. ibid., p. 309).

 

Nepos, askofu wa Misri, aliupinga mtindo wa kuyachambua maandiko kwa tafsiri ya kiroho wa Origen kwenye karne ya tatu akilitetea fundisho la millennia, akisisitiza umuhim wake huko Arsinoe. Ilikuwa ni kwa kupitia mafundisho yaliyojulikana kama uplatoni wa kisasa ndipo fundisho la Utatu lilianza kufundishwa. Origen alikuwa ni muumini wa mafundisho haya ya uplatoni mpya. Kwa hiyo ndivyo tulipopata mafundisho haya ya uwongo na kuingizwa kwake Kanisani yakipinga na kushambulia mafundisho ya kweli, yaliyoanzishwa na kufundishwa na Kristo ya kuwa atatawala hapa duniani. Hili ndilo lilikuwa lengo la mashambulizi yao. Dionysius wa Alexandria alionekana kwa kiasi kikubwa sana kupendezwa na fundisho la Milenia na kuachana na mtazamo wao wa kuzuia hila (Eusebius Hist. Eccl. VII, 14).

 

Mafundisho ya Milenia yalibakia huko Misri kwa kipindi fulani na Methodius, askofu wa Olympus na mpinzani mkubwa wa Origen aliutetea Umilenia kwenye Mdahalo wake (IX, 1, 5, in Migne, Patr. Graec, XVIII, 178 sqq.). Apollinaris, askofu wa Laodikia aliutetea Umilenia kwenye kipindi kilichofuatia cha karne ya kwanza hadi karne ya nne. Maandiko yake yaliwekewa rejea na Basil wa Kaisaria (Waraka ( Epist.) wa CCLXIII, 4, in Migne, Patr. Graec.XXXII, 980); sma pia kweenye Epiphaneus (Her. LXX, 36, in Migne loc. cit. XLII, 696); na Jerome (In Isa. XVIII, in Migne Patr. Lat. XXIV, 627). Jerome anasema pia kwamba Mileniam ilikuwa ni fundisho yaliyoenea na kujulikana, lakini baada ya hapo Kanisa lilifanya juhudi kubwa ya kukatisha tamaa umhimu wake kimafundisho. Ni fundisho lililokutokana huko Magharibi, kwa mfano huko Commodian (Instructiones (Mafundisho) 41,42,44 Migne ibid. V, 231 sqq) na huko Lactantius (Institutiones (Vyuo Vikuu) VIII, Migne ibid. Vi, 739 sqq.) ambao pia waliyachukua kutoka kwenye unabii wa Sybilline, ambao walikuwa ni Wanamilenia wa Kanisa la Kwanza. Nabii za Sibilline kimsingi zimeorodheshwa kwenye Maandiko Bandia ya yasiyokubalika ya Agano la Kale. Ni nabii za Kimasihi. Iwe ni hivyo au hapana, wao walikuwa ni Wakristo ni dhana ya kila mmoja. Ni wafuasi wa Masihi wenye asili ya Kiyahudi na wanazifania rejea kanuni za kimwili za Masihi. Fundisho hili linapatikana hasahasa kwenye Kanisa la mrengo wa Kiyunitari pia.

 

Kwa sababu ya makosa makubwa na upotoshaji wa makanisa ya siku hizi, kurudi kwa Kristo na marejesho mapya ya kipindi cha Milenia, wanateolojia wengi wa siku hizi, wanadiriki kuzikumbushia ahadi zilizotolewa kwenye Agano la Kale wakiziingiza kwenye matengenezo mapya kuwa ni kitu cha ajabu kisichowezekana, na wengi hulichanganya  neno Israeli na Wayahudi. Hawajui kuwa Wayahudi ni sehemu tu ya Israeli na kwamba makabila kumi yaliyopotea yapo nje bado na kwamba makabila haya yanaunda shirika, na kuna mtazamo wa ujumla wa Kibiblia wa ulimwengu wote kufanyika kuwa Waisraeli.

 

Wanadiriki kuziwekea matabaka ahadi za Mungu kwenye Agano la Kale, ni ushahidi wa zaidi wa ushawishi wa Waetruscan na Waajemi kwenye mafundisho na hivyo, kuidunisha asili yao iliyovuviwa. Mara nyingi sana, wakati mwandishi anapoyadunisha Maandiko Matakatifu ya Agano la Kale hitimisho lao linakuwa kituko na si la kibiblia. Ni kama tulivyojionea mara nyingi, kwa kweli, Maandiko Matakatifu yanamaanisha Agano la Kale na Injili imejumuisha kwayo. Mitume walikuwa na Maandiko Matakatifu, yaani, Agano la Kale na ndilo walilolitumia kufundishia. Maandiko ya Mtume Paulo yalikuwa hayajakusanywa bado na nyaraka zake sio Maandiko Matakatifu yanayostahili kuizidi Biblia. Bali ni nyongeza tu za Biblia. Yatupasa kulijua hilo vizuri sana.

 

Ili kulipinga n kulishambulia fundisho la Milenia, kwa kweli inawapasa kukiamini Kitabu cha Ufunuo. Hiyo ilipandekezwa kuwa ni ufumbuzi na kwa kipindi fulani walijaribu kukiondoa kitabu hiki cha Ufunuo kutoka kwenye Biblia. Kuna mambo kidogo yanayotatanisha maana yake kwenye kitabu hiki cha Ufunuo. Ni jambo la wazi na muhim na linaloshutumu au kuzikemea kwa ukali imani na dini za uwongo, na ni wazi kabisa kuwa Kristo anakwenda kushughulikia ulimwengu huu.

 

Kuondolewa kwa kitabu cha Ufunuo kwenye Mchakato wa Kuyarasmisha Maandiko maarufu kama Kanuni au Canon

Ilikuwa ni kutokana na madai haya ya ziada ya Kichiliasm ndipo Ufunuo (kitabu cha Ufunuo) kiliondolewa kutoka kwenye orodha ya vitabu vilivyokubaliwa na hili waliloliita Baraza la Kanuni Takatifu kwa muda fulani, ingawaje sababu ya kweli yawezekana kabisa ni mapokeo ya Kimithraiki yalikuwa kujitilia chumvi mno yenyewe kwenye Kanisa na kitabu cha Ufunuo kilikuwa wazi sana na kilikuwa kinaeleweka kinavyosema. Mwishoni mwa karne ya pili kitabu cha Ufunuo kilitambuliwa na kukubalika kuwa ni kitabu chenye ujumbe wa kitume na kimevuviwa na Kanisa zima lote, isipokuwa nakala iliyoandikwa kwa lugha ya Kisyria kilijikuta kikiangukia kwa muda kwenye kudunishwa na kutoaminika, kwa sababu ya upinzani uliokuwepo wa kuwapinga Wamilenia wenye itikadi ya Kichiliani yaliyofanywa na Dyonisius wa Alexandria (aliyefariki mwaka 265). Wote wawili, yaani Cyril wa Yerusalemu (aliyefariki mwaka 368) na Gregory wa Nazianzus (aliyefariki mwaka 389) walikitenga kitabu cha Ufunuo utoka kwenye orodha yao ya vitabu vya Agano Jipya na Chrysostom (aliyefariki mwaka 407) hakuweka nukuu mahali popote kutoka kwnye kitabu hiki (soma jarida la Uasili na Usawa  na Baba (Na. 81)).

 

Ni kina nani watu hawa? Gregory wa Nazianzus na Gregory wa Nissa na Basil wa Kaisaria, walikuwa ni watu watatu walioanzisha fundisho la Utatu. Watu hawa kwa wazi waliyaendeleza mafundisho ya Utatu na walieneza uvumi wa umuhimu wake ili wayaendeleze (kama anavyosema Basil mwenyewe) kuwa ni Mungu. Walikuwa ni mojawapo ya waanzilishi wa Kanisa Katoliki.

 

Mtaguso wa Laodikia (mwaka 366) ulikiacha na kukitenga orodha ya vitabu vilivyokubalika na kutambuliwa na Kanuni.

 

Kipengele cha kanuni cha 29 cha maraza hilo kilisema kuwa Wakristo hawatafuata seria za Kiyahudi na kupumzika siku ya Sabato, bali wafanye kazi siku hiyo; lakini wakaiweka Siku nyingine ya Bwana ambayo watapaswa kuiadhimisha kwa makini na ambayo inaweza kuwa ni siku ya ibada za Wakristo, ambayo ikiwezekana kwayo hawatafanya kazi yoyote siku ya dominika. Na kama watakutikana kwa namna yoyite wakiyashika maagizo ya dini ya Kiyahudi, basi watatengwa na kanisa na kutangazwa kuwa wamelaaniwa na Kristo.1

Kumbuka kuwa tarakim 1. Hefele kwenye Historia ya Mabaraza ya Kanisa [Councils of the Church, Volume 2, page 316] ameitaja siku ya Sabato kuwa ni Jumamosi na akalitumia neno “wafukuziwembali na kufungiwa nje ya Kristo".

 

Kwa hiyo baraza hili lilikipiga marufuku kitabu cha Ufunuo na kuipiga marufuku Sabato. Hii inawapa wanafunzi wa Biblia wazo muafaka la nia ya kiroho ya Baraza la Mtaguso wa Laodikia.

 

Kanuni nyingine za Mtaguso huo zilitoa ruhusa ya usomaji wa Maandiko Matakatifu yanayotoa mkate wa kipindi cha Kwaresma; na kuwaadhimisha wafia dini kwenye ibada za Sabato na zile za Jumapili. Baraza hili likuwa linaona bado Sabato kuwa ni siku takatifu loitunza Sabato, lakini huku likiifanya na kuitangaza kuwa ni siku ya watu kufanya kazi ba huku ikiipigia chapuo kwa hila zote siku ya Jumapili na kuitangaza kuwa ndiyo siku ya mapumziko na ibada za kanisa.

 

Hivyo ilikomesha au kuhitimisha makosa na upotove wa Mtaguso wa Nikea wa mwaka 325 BK wakato walipoketi kikao cha jakamoyo kilichoitishwa na Constantine tangu mwaka 321 BK. Ushindi haukuwa kamili, hata hivyo, kwa kuwa Athanasius katika mwaka 367 BK aliijumuisha hii kwenye orodhai yake na kwenye Mtaguso wa Hippo (mwaka 393) na wa Carthage (mwaka 397) waliitangaza kuwa inakubalika Kikanuni.2

Notisi namba 2. Dondoo za historia iliyokumbana na matatizo ya kitabu cha Ufunuo yalijumuishwa kwenye kitabu cha Askofu B F Westcott cha Udadisi wa Jumla wa Historia ya Kanuni ya Agano Jipya 1875 ukurasa wa.2C.

 

Walishinda vita waliyohitaji kushinda na mnamo mwaka 367 mwaka mmoja baada ya Mtaguso wa Laodikia, Athanasius ambaye alikuwa ni mmoja kati ya mababa waanzishi wa Kanisa Katoliki (wanaitwa Waathanisani kwa kuwa walikuwa waamini Utatu) kisha wakakiachilia mbali kitabu cha Ufunuo na kuktoa kwenye Kanuni hii.

 

Constantine aiharibu Imani

Ilikuwa ni Constantine pia ndiye aliyeharakisha kukomeshwa kwa fundisho la kipindi cha Mileniai na mauti au iifo cha kusikitisha ya Imani yetu ya mwanzoni kutokea. Kuongezeka kwa mafundisho ya mali na utajirisho, Uchiliasm kulisukuma upinzani na kwanza ilionekana kwa mwonekano wa Origen wa Alexandria. Kwa kufanya tafsiri ya kiroho na tafsiri ya kiroho na yenye kutilia chumvi alilifanya Kanisa kwenye barabara inayoelekea upande wa chini ya kilima. Dhana ya kwamba Ufalme wa milele wa Mungu unamaana ya uwepo wa Kanisa Linaloendelea Kudumu Duniani lililotokana kwa mlango wa nyuma wa maandiko ya Tichonius na yalianzishwa na Eusebius yakifuatiwa na “mjadala” wa Constantine kwa Wakristo. Constantine alibatizwa na Eusebius wa Nicomedia alipookuwa mahututi mahutihuti. Alibatizwa akiwa na imani ya Kiyunitariani (yaani kile kinachitwa iamani ya Uariani au Ueusebiani) na sio Ukatoliki. Constantine hakuwa Mkatoliki kabisa na aliikataa imani yao na kwa kweli aliitwa Mueusebiani. Alikuwa Myunitariani. Aurelius Augustine, Askofu wa Hippo, kwenye jhudi yao ya kupinga imani ya kichiliastiki uliansiahi wenye hamasa kwenye maandiko yake ya kutafsiri kirohoroho kila kitu pamoja na Milenia yenye msingi wake kwenye theory iliyena iliyofundishwa na Tichonius. Hii inaonyesha kuwa kitabu cha Ufunuo kinajirudia chenyewe kikiandika matukio yote ya zama ya Wakristo chini ya alama ya makanisa saba, mihuri saba, baragumu saba, wanyama na kisha Milenia. Kwa hiyo kutokana na watu hawa na umashuhuri au heshima ya Constantine, Shetani wa bandia alizaliwa na fundisho la utawala wa kipindi chaa baada ya milenia yaliibuka na kuenea.

 

Milenia ya Mbinguni

Sambamba na uibukaji wa mafundisho ya kuwepo kipindi cha baada ya millennia, kulikuwa na malumbano yaliyoibuliwa na Jerome kwamba kipindi hii Milenia itafanyika mbinguni na sio duniani. Hoja yake ilituama kwenye dhana tu au theory na ni wazi sana kwamba alimshawishi na kumvutia Augustine kwenye maandiko yake. Inaendelea kudumu hata sasa na kuwezesha sarakasi au mtafaruku wa kifikra kuhusishwa, ya kwamba yatupasa kuzipuuza au kuzikataa nabii zote za Agano la Kale.

 

Ni jambo la kusisimua kuona kuwa hata Augustine alikuwa mwamini fundisho hili la Milenia (Kitabu cha City of God [Mji wa Mungu], XX, 7). Hata hivyo, anaonekana kudaiwa kuwa aliamini kuwa kipindi cha Milenia kitakuwa baada ya ufufuo wa wafu Wote na ni huenda ni kiroho zaidi (Sermo, CCLIX, in Migne, ibid., XXXVIII, 1197). Anaaminika pia kuwa alikuwa anasaidia mrendo wa waamini milenia ya baada ya kipindi cha ufufuo wa wote na anaungwa mkono pia na baadhi ya wanazuoni wa elimu ya mambo ya siku za mwisho kwa kuanzisha au kufundisha theory ya milenia. Watu wengi wanaenda nyuma hadi kipindi cha Augustine na kudai uungwaji mkono wa mitazamo yao kutoka kwake.

 

Wakati wa zama iliyojlikana kama ya Matengenezo wote walikwenda kwa Augustine na hawakurudi nyuma hadi kwenye Kanisa la Kwanza. Matengenezo haya bado yamewajumuisha au kuwakumba watu na kuwatia kwene imani ya Utatu (na Waabudu Jumapili), kwa kuwa hawakurudi nyuma hadi ya nyakati za Augustine. Imani ya milenia ya baada ya Ufufuo wa wote haikuwa imani rasmi ya Kanisa Katoliki la Roma, hadi baada ya Thomas Aquinus alipowashinda wapinzani wake na haikuwa imekubalika kiujumla hadi baada ya mwaka 1700. Kitabu Wakatoliki kilichojulikana kama “The new Catholic Commentary on Holy Scripture, 1953 p.1207”, Kitabu kipya cha Ufafanuzi wa Maandiko Matakatifu cha mwaka ulioandika hapo, kinawashauri viongozi wake kwa kusema hivi: “kuhusu mabadiliko ya Shetani na utawala wa Watakatifu kwa kipindi chote kunajiri kwa taratibu na dhana ya mabadiliko ya maumblle ya mtu kupitia kwenye kchakato kadhaa hadi awe mwanadamu".

 

Kutokana na madai ya kubadilika kimchakato hadi kuzaliwa kwa Kristo au incarnation, na kufufuka kwa Kristo, na matokeo ya mavuno mengi ya Kanisa, Kanisa Katoiki la Roma linadai kuwa na serikali, mamlaka na uweza wa kimamlaka sasa. Imani yao ni kwamba wao ni mamlaka inayotawala na yenye nguvu, na kwamba Milenia (Ufalme wa Mungu) ni sasa na uko haoahapa duniani.

 

Imani ya Milenia Mchanganyiko

Imani ya mchanganyiko wa kipindi cha milenia inachekesha sana na ni fundisho potofu na la uwongo. Wanafundisha kwamba Ufunuo 20 inafundisha tu ukweli wa kiroh kwa lugha ya ishara. Inadai kuwa hakuna millennia yenyewe hasa wala utawala wake, au vinginevyo inachukuliwa kama ni makosa na upotofu ulioko kwenye imani ya Kikristo iliyodumu kwa vipindi vyote. Aina mbili za ufufuo wa wafu inaunganishwa kwenye mmoja tu na Kristo anakuja katika mwisho wa dahari kuhukumu ulimwengu. Mtindo huu wa kuunganisha mambo unakuwa unatimika na kupendwa na watumishi au wahubiri wa kimagharibi na waamini Utatu kwa ujumla.

 

Tofauti iliyoko kati ya waamini millennia ya baada ya kipindi  cha ufalme wa mbinguni duniani na hawa wanaounganisha kipindi cha milenia ni ndogo saana, lakini hata haijalishi kama wanatofautiana.

 

Mabadiliko Kwenye Imani ya Milenia ya Baada Kiyama

Waamini milenia ya baada ya kiyama wamekwenda wakibadilika badilika, na mnamo mwaka 1190, Joachim wa Flores na Joachimite Spirituals, waliamua kuanzisha kanisa lisilo na doa. Masalia wa Kanisa la Roma waliwasukuma wale waliojisikia kuwa wanaishi katika Kristo kutafuta kitu kingine zaidi cha ziada. Huku wakiwa mabaki ya kiuchanga au kimwili viongozi wa Kanisa waliojulikana kama wafalme wa Kanisa na utendaji kazi wa aliyejipachika cheo cha kuwa ni Mwakilishi wa Kristo hapa duniani, mtu asingekuwa na namna nyingine bali ni kutarajia tu kwamba kulikuwa na maelezo mengine ya Mpango wa Mungu hapo juu na zaidi kipindi cha milenna, ambacho kilidhaniwa kuwa kiwango cha juu sana cha hamasa ya mwanadamu iliashiriwa kwenye Serikali ya Kanisa la Rumi.

 

Mafundisho ya Utatu na ya Kanisa Lisilo na Doa

Kanisa jipya lisilo na doa, hata hivyo lilkuwa limetuama kwenye mafundisho na imani ya Utatu na mapokeo yake mbalimbali yanayotuama kwenye utofautishaji; umri wa Mungu Baba, umri wa Mwana wake na umri wa Roho Mtakatifu. Joachim alishikilia kuamini kuwa umri wa Roho Mtakatifu ulikuwa ni kuanzia mwaka 1260 BK kwa kanuni ya hesabu yamwaka mmoja sawa na siku moja. Umri ujao wa Roho Mtakatifu ulielezwa pia na Wafransiskani wa Kiroho. Wakati huu Kanisa lilikuwa linajihusisha na kutoa maelezo au mafundisho ya kuwezesha kuaminika kwa mafundisho ya kizushi ya Utatu kwa namna zote mbili, yaani kiasili na kiufunuo. Aya iliyo kwenye 1Yohana 5:8 kwenye tafsiri ya Biblia ya the Textus Receptus na kisha kwenye King James inayosema: "Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja," ilikuwa ni aya ya kughushi au iligushiwa. Ilijumuisha maandishi mengine zaidi, kwa kuwa hakukuwa na aya nyingine kwenye Biblia iliyosaidia dhana hii ya miungu ya imani za Kimisri, ambazo zilikuwa zimekwisha anza kuchanganywa na kukubalika kwenye Ukristo wa Kirumi. Tarakumu hii ya tatu ilikuwa pia na maana yake kwenye dini ya kale ya mngu mke, ambaye alionekana wazi kabisa kuwa ni mwenye umbo la kike na ni desturi shirikishi iliyojmisha asili ya ibada na maumbo ya uasilia au ubinadamu, ambayo hatimaye ilionyoshwa kama ishara ya ushirikina. Kwa hiyo bila ya kuwa na msingi wa ki biblia kwa ajili ya kulifikia lengo hili la kuwapotosha watu kwa imani hii ya Utatu waliama kuigushi aya hii.

 

Msingi wa kitendo cha wana vuguvugu hawa wa kiroho ilikuwa ni kutoka kwenye kipindi zama cha muongo moja uliokuwa kwenye kanisa la zama za kati. Wafransiskani, waliponywa na Pierre Jean D’Olivi (aliyefakiri mwaka 1298), aliyeiona ile hali ya vyeo au madaraja ya kanisa ni kama siri za kimafumbo ya Kibabeloni, na Ubertino wa Casale (yapata mwaka 1312) aliyemfananisha na kumchukulia Papa kama alama ya Mnyama, pamoja na Joachimites, walikuwa wamechefuliwa sana na upotkatishaoshaji mkubwa na Kanisa lilikuwa linazama au kudidimia, na ndipo waliona umuhimu wa kufanya matengenezo. Kwa hiyo mengi yalifanywa ili kuleta msukumo na kwamba wengi waliwaona mapapa kama Wapingakristo. Hiki ndicho kilio kilichosikika kutoka kwenye Makanisa ya Kiprotestanti, wakitoa mwito kwamba watoke kutoka kwenye ukengeufu wa Kibabeloni.

 

Kosa la kiteoojia la Waprotestanti lilikuwa kwamba hawakuenda mbali na kwa kina kuangaza historia ya nyuma kwenye mkakati wao huu wa kuurejesha ki kwelikweli ukweli uliopotoshwa na kupotea kwenye Kanisa, zaidi ya kumnuku Augustine wa Hippo na ambaye asingeweza kuwaokoa kutokana na makosa au upotofu uliofanywa na mabaraza ya Nikea, Laodika, Constantinople na Kalkedoni. Kwa hiyo hawakurejesha Ukristo wa Kanisa la kwanza kabisa, na wakashindwa.

 

Kilio kikubwa cha kulisafisha Kanisa la hawa wazushi wa kwanza kilisikika kupigwa wangwi na Milicz wa Kremsier (alifariki mwaka 1374) kabla ya ulaji wake haujaathirika.

 

Edward Gibbon anasema anaposhughulikia kuenea kwa ushawishi wa Vatican, “wakati wa karne kumu za upofu na utumwa, Ulaya ilipokea ushauri wake wa kidini kutoka kwa unabii au mafundisho ya Vatican, na ni mafundisho hayohayo, tayari yamekwisha futiliwa mbali na kutu ya uovu yaliyoingizwa bila kupingwa kwenye ukiri wa imani ya wana matengenezo walioukataa uhalali wa mamlaka ya Papa wa Roma”. Sinodi ya Kalkedoni ingali bado inashika dau la Makanisa ya Kiprotestanti. Wallfanya matengenezo ya kinafiki, lakini hawakurudi kwenye ushikaji wa Amri za Mungu na hadi leo wanaendelea kuzinajisi Sabato, pasipo na mamlaka nyingine zaidi ya ile ya Askofu wa Roma.

 

Arnold wa Villanova aliyefariki mwaka 1313 akitarajia kutokea kwa matengenezo ya ndani ya Kanisa, huenda angechefuliwa na kuchukizwa sana na matengenezo haya bandia yaliyopokelewa mahala pake, ambayo, yaliponywa au kuokomeshwa na baraza la mahakama ya kidini, lililoua maelfu ya watu wa Mungu ambao habari zao hazisimuliwi kwa njia mbalimbali na za hatari ambayo watesaji na wauaji waliizitumia. Kanisa lisolo na doa la waamini Milenia lilichuja na kufifia kidogokidogo kutokana na mateso haya. Walikuja kuwakilishwa na vikundi vilivyopoa kama vile cha wa Anabaptists.

 

Upinzani dhidi ya imani ya Kirumi ulikutikana huko Ulaya na Wasabato ambao walikuwa ni Wayunitariani (soma jarida la Jukum la Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu ya Washika Sabato (Na. 170)). Kimsingi, wa Waldensians walikuwa ni sehemu ya Wasabato na walikuwa Way8unitari wa imani ya Milenia. Kitendo chao cha kulikataa fundisho na imani ya Utatu kilikuwa ni moja ya kile kilichoitwa “uzushi” wa wa Waldensians, (Kwa mujibu wa kitabu cha Rev. A.C. Shannon  cha Papa na Mafundisho ya Uzushi Katika Karne ya Kumi na Tatu [The Pope and Heresy in the Thirteenth Century, p.7]).

 

Wachilisti Wenye Wivu wa Kupindukia

Imani yaw a Milenia ilikwenda kwenye msononeko baada ya hii, hususan baada ya Wanamatengenezo wa Kiprotestanti waliouona wivu wa Wachiliasti kuwa wanakata tama na kufadhaika. Hasahasa wale waliojulikana sana walikuwa wa Munsterites kwenye Bara, na hatimaye wamonaki au Watawa wa Kwanza wanaume wa Uingereza ambao walijaribu kuanzisha Ufalme wa Mungu hapa Duniani kwa kutumia njia za ksiasa na za kijeshi kwa wakati wao walioishi.

 

Uhamiaji

Mtazamo wa Wachiliastiki, hata hivyo, ulikuwa ni kuanzisha kwa njia ya Mikusanyiko na kendesha ibada zao kwa njia hii na hatimaye wakawa Wabaptist, ambao baadhi yao walikwenda Marekani. Wabaptisti wengine walikuwa ni washika Sabato ambao kutokana nao walianzisha kanisa lililojulikana kama Seventh Day Baptists. Kutikana na kikundi hiki ndipo walitokea Waadventista Wasabato (SDA) na Makanisa meingine ya Mungu ya washika Sabato yalitokea pia. Lakini Waadventista Wasabato hawapo miongon mwa hawa Wachilialisti, bali zaidi sana wao wameyachukua na kuyaamini mafundisho na mtazamo wa Jerome wa Miienia ya Mbinguni, bila shaka walisababishwa na kupata msukumo kutokana na kushindwa kut Wachi imia kwa unabii wa mwanzilishi wa kanisa lao William Miller na kusaidiwa na Ellen G. White na matarajio ya kwamba tarehe 22 Octoba 1844 ingekuwa ni siku ya kurudi kwake Kristo duniani.

 

Kuanza Tena kwa Mafundisho ya Kweli na Mabadiliko ya Fikra

Nuru ndogo ya ukweli ilijitokeza tena ikiletwa na Joseph Mede, ambaye aliufundisha mtazamo au imani iliyodumu kwenye historia ya milenia moja ya wakati wa kurudi kwa Mwokozi, bila shaka ni kupingana na mtazamo na mafundisho ya Kanisa la Rumi ya millennia ya baada ya kipindi cha kiyama.

 

Aina mpya ya imani ya millennia ya baada ya kiyama ilianzishwa na kufundishwa na Daniel Whitby mwaka 1703, inayoamini kwamba Kurudi kwa mara ya pili kwa Masihi kutatokea tu baada ya kipindi cha miaka elfu moja na zaidi au kabla kidogo, wakati dunia itakuwa na amani tele, haki, utauwa na wema kwa ujumla wa mwanadamu, ambapo kwamba ulimwengu wote kwa ujumla utakuwa umeongoka na kuingia kwenye imani ya Kikristo. Bilashaka hii inatokana na malsha safi ya dunia, ambavyo itamshinda Shetani, awapate Wayahudi, Waislam na mtu mwingine yeyote na kukomesha vita vyote. Jonathan Edwards na Samuel Hopkins walianzisha mafundisho huko Marekani na mnamo mwaka 1800 ilifanyika kuwa ni mtazamo wa kimafundisho au mafundisho ya msingi. Wandishi hawa walidai kwamba hili tendo la kufungwa na kufunguliwa kwa Shetani ni mfano tu, lakini nguvu za Shetani zinaweza kushinda kwa kitambo kabla ya kurudi kwa Kristo. Waovu wengine waliosalia wanaweza kuangamizwa baada ya kuja kwake na ndipo Ufalme wa Mille wa Mungu utaanza.

 

Wakristadelfians wanadai kwamba Shetani hayupo, kuokoka nl dhana tu, na kwa hiyo inaweza kuangukia kwenye mtazamo wa kutumia akili wa kinamna hiyo au wa kujiuliza akilini, lakini kwa mafundisho tofauti sana na ya kila namna yanayofanana na imani au mtazamo wa kimilenia.

 

Imani au mitazamo kuhusu Ufufuko wa wafu imetiwa giza au kufifishwa kwa namna hiyohiyo na wafuasi hawa wa Whitby. Whitby na Vitringa wanapinga kwamba Yerusalemu Mpya ni Baraka za Kanisa la kwanza kwenye kipindi cha Milenia, wakati kwamba wengine walio kama Brown na Faber wanaamini hii kuwa ni kundi la watakatifu baada ya Milenia.

 

Theori au fundisho hili lilikuwa limeharibiwa zaidi katika karne ya 20 wakati Vita Kuu ya 1 ilipolipuka. Ni kama itakavyoweza kudhaniwa, wakati mwaka 1914 ulipokuja kwenye tetesi zake na dunia ikaingia kwenye vita – Vita Kuu kwa ajili ya ustaarabu – kisha kwa ghafla fundisho zoma lote ilifungiwa na kutopewa nafasi. Sisi tupo kwenye vita na unabii na unabii uhusuo Nyakati za Mwisho. Hawakupenda kuukabili ukweli kwamba nabii hizi zilikuwa wazi na kwamba walikuwa wanakwenda kwenye vita vya mwisho na mtu Yule alikuwa hawezekani au aishindwi, pasipo msaada ya Roho Mtakatifu, wa kuendeleza mfumo au utawala mpya na dunia mpya na kupatawala mahali hapa kwa utawala wa Yesu Kristo. Huenda ilitabiriwa kipindi kirefu cha nyuma kwenye mwaka 1139 wakati Mt. Malachi alipomita Papa wa wakati huo kuwa ni "Religio Depopulata" Mwangamiza Dini. Hata hivyo, vita n, vita ni fundisho la unabii wa kibiblia (soma jarida la Anguka la Misri: Unabii wa Mikono Iliyovunjika ya Farao (Na. 36)).

 

Whitbyists alisema kuwa mwanadam amefanya maendeleo makubwa sana kujaribu kuchokoza iwepo vita nyingine. Waamini wote wa mafundisho ya milenia ya baada ya kiyama tangu Augustine hadi Whitby walikabiliana na tatizo ambalo ulimwengu hauishi kwalo kwenye ubashiri wao na mawazo yao ni kinyume na fundisho la biblia. Biblia iko wazi sana kuhusu kile kinachotokea. Tunafurahi kuona na kutazma mbele kwa kuwa tuajua kitakachotokea. Kwa kuendeleza uhusiano wetu na Mungu tumeona kuwa usalama wetu upo kwa Mungu, na furaha ni jinsi tunavyoweza kuishi pamoja.

 

Kushindwa kwa mafundisho haya kulisababisha kufufuliwa kwa imani ya milenia ya wakati wa kurudi kwa Masihi. Wale waliotazamia kile kilichonenwa na Biblia na kukinukuu walilazimika kugawanyika ki matawi na kuwa wafasiri maandiko kama yalivyo na sio kwa kiroho na walipingwa na wafasiri maandiko kwa kutumia mtindo wa kiroho, lakini kama ilivyo kawaida ni kwamba mawzo ya kujilinda yaliezwa kwa watu wakipuuza na kukataa neno lililoandikwa na kutafsiri ujumbe. Tatizo lililokuwepo kutoka kwa watu walioacha kuyachukulia maandiko kuwa ni kama maneno au usemi wa vile yanavyomaanisha.

 

Mafundisho yaliyofuatia baadae

Mafundisho yaliyofuatia baadae yamejumisha imani waliyodai kuwa ni Unyakuo wa SIri, fundisho lililoanzishwa na Edward Irving, aliyeanzisha kanisa lililojulikana kama Kanisa Katoliki la Mitume au Catholic Apostolic Church mwaka 1832. Aliondolewa kutoka madhabahuni mwaka 1832 na kuondolewa kwenye wadhifa wake wa ukasisi wa Kanisa la Scotland mwaka 1833. Wengi wa wafuasi wake walimfuata kwenye Kanisa lake Jipya. Alifukuzwa kwenye Kanisa la Scotland kutokana na kipeperushi alichokiandika kilichosema kuwa Yesu alikuwa na mwili wa kawaida wa kibinadamu unaoweza kutenda dhambi. Alifundisha kuwa dhiki kuu itatokea kwenye kipindi cha kati ya Ufufuo wa Wenye haki au wa Watakatifu na Kunyakuliwa kwa Watakatifu na kupinduliwa kwa Shetani, tukio ambalo lingefuatiwa na kipindi cha utawala wa Kristo wa Milenia. Kutofautiana kuhusu msimamo wa imani hii ya unyakuo kumeibuka tangu wakati huu, lakini misingi yake ni mimoja. Dhumni lenyewe halisi linaonekana kuwa ni kuuepuka ukweli kuhusu dhiki kuu.

 

Mafundisho yote yanayohusiana na habari hii ya unyakuo, kukiwemo na fundisho la mahali pa usalama yaliyofundishwa na kuvumishwa kwenye Makanisa ya Armstrong, na ndivyo ilivyokuwa kwenye fundisho hili la kunyakuliwa kwa kutumiwa majina tofautitofauti mbalimbali. Ni suala tu la kuachananayo kutoka kwenye dhiki kuu na kuyakwepa mambo yote yasiyopendeza na ya kuchukiza yanayokuja na kujitokeza, kwa kuwa hatupendi kurekebisha mwenendo wetu wa kibinadamu (soma pia jarida la Mahala pa Salama (Na. 194)).

 

Wakati wafuasi wa mafundisho haya wanapokuwa wanakabiliwa dhiki kuu, wao pamoja na makanisa yao wanayoabudu watakuwa na ugumu wa kuwa kwenye nafasi zao na watu wao. Wote wawili, yaani waalim wanaofundisha huu unyakuo wa kabla ya kutokea kwa dhiki kuu, kina J.N. Darby na Irving, ambao walikuwa na ushawishi mkubwa kwa wahaidhina wene msimamo mkali wa imani ya millennia ya kipindi cha kurudi kwa Masihi wa nyakati hizi s. Irving alifariki kwa ugonjwa wa pumu au tibii mwaka 1834.

 

Matawi mengi ya siku zilizofuatia ya waamini milenia ya wakati wa kurudi kwa Masihi yalikua na kuenea kutokana na mtazamo uliotofautiana kama vile:

 

1. Wamileriti, ambao walitetea yasiyo ya muda mfupi na kwenye maneno yao, Milenia isiyo ya Wayahudi (ambayo ilionekana kuonyesha mapungufu yao ya uelewa kwenye mataifa na wajibu au nafasi ya Waisraeli);

2. Ndugu Wapendwa wa huko Plymouth, waliodai kuwa ni watu wenye mtazamo wa kutazama nyakati zijazo, na kufundisha wafundisha mtawanyiko.

 

Tofauti iliyopo kwenye mfundisho na imani hizi za Milenia ya wakati wa kurudi kwa Yesu na ile ya Milenia ya baada ya kiyama inazidi kuongezeka, mtu anaweza kusema, karibu kila siku.

 

Mafundisho ya Irving ya Unakuo wa Siri yanaonekana kuwa yameanzishwa kwa kutokana na maono ya wanaroho wa Bibi Margaret McDonald mnamo Machi 1830, ambaye alinena akiwa amepagawa na kuweweseka kutokana na kile alichokiita kuwa ni Maono ya Ujio wa Kristo. Hii ilikuwa ni ruya aliyoiona na ambayo aliitafsri kiuvumi na uzushi, ambayo hatimaye ilifanyika kuwa fundisho. Haina msingi wowote wa kimaandiko. Ilijipenyeza na kuenea kwa Wapendwa wa huko Plymouth kupitia kwa John Nelson Darby (miaka ya 1800-1882) aliyeyaleta mafundisho haya kwenye tafsiri ya jmla ya kinabii. Kwa hiyo, sisi tuna dhana au mtazamo wa zama kale sana ya Utawanjiko iliyoelezwa na mamilioni kama unabii wa Kimaandiko, ambao kwa kweli hauna msingi wowote ule zaidi ya kuwa tu ruya ya kimaono ya binti mdogo kwenye tukio la kupagawa la Machi 1830, wakati wa kipindi ambacho ilikuwa ni mtindo mzuri kuwa na maono kama hayo. Kwa bahati nzuri, sio Wandugu wote wa huko Plymouth walidanganyika na huyu Dr. S.P. Tregelles alipewa jina hili kwa jinsi ilivyokuwa kwenye mwaka 1864 (kwa mujibu wa kitabu cha Tregelles, The Hope of Christ’s Second Coming, pp. 34-37).

 

Sikujua kuwa kulikuwa na mafundisho yoyote yenye ushawishi mkubwa yaliyosema kuwa kutakuwa na Unyakuo wa Siri wa Kanisa kwenye ujio wake Masihi wa siri hadi ilipofundishwa kwa msisitizo na nipomsikia ikinenwa kwenye kanisa la Bwana Irving kwa kile kilichopokelewa hatimaye kuwa ni kama sauti ya Roho. Bali hata kama kuna yeyote anayedai kit kama hicho au hapana ilikuwa ni kutokana na kile kinachoaminiwa kuwa ni ufunuo ambao fundisho la kisasa na uainishaji wa kisasa vinatilia maanani kuibuka kwa mafundisho haya. Hayakuja kutoka kwenye Maandiko Matakatifu, bali ni kutoka kwenye kile walichokifanya kwa uwongo mkubwa kuwa ni Roho wa Mungu."

 

Darby anatajwa kuwa ni baba wa Mtafaruku, kwa hiyo kwenye upendeleo wowote ule alipasa kulaumiwa kwa uenezaji wake wa uwongo na fundisho la kijinga. Alisimikwa kuwa shemasi kwenye Kanisa la Uingereza mwaka 1825, lakini kwa ajili ya mauaji ya kihafidhina wa wazee na makasisi wa Kianglikana wa wakati ule, yeye pamoja na wenye kuabudu walioondolewa wakfu wao walijikusanya pamoja na vuguvugu jipya lilianza huko Dublin, lakini iliendeleza kituo chake huko Plymouth na kwa hiyo wakajulikana kama Ndugu Wapendwa wa Plymouth.

 

Ilikuwa ni kwa kupitia mtazamo huu ndipo vuguvugu hili jipya ambalo Darby alilienezea mafundisho ya Irving yenye msingi wa “maneno” ya Bi McDonald ila mengi yaliongezwa kwenye Tregelles, aliyakataa. Hawa walikuwa ni miongoni mwa wengine ni B.W. Newton, Charles Spurgeon, William Booth na George Millar, bali hii haikukomesha kuenea kwake hadi huko Marekani na Canada kwenye miaka ya 1860 na-1870. Ni kama Darby mwenyewe alivyotembelea Marekani mara sita, vuguvugu hili linaweza kuwa lilifundishwa kipindi cha mapema sana cha hata kabla ya mwaka wa 1840, lakini hii haieleweki vizuri.

 

Iwapo kama kitu fulani kimenukuliwa mara nyingi vha kutosha, watu walianza kuamini kuwa ilikuwa ni kweli, a baaba ya maandiko ya Charles Henry Mackintosh (miaka ya 1820-1896) watu walianza kuyakubali kwa ujumla. Bado anaendelea kusomwa. Yeye, pamoja na William Blackstone na wafuasi wengine wa mafundish ya Darby kama vile kina Malachi Taylor na J.H. Brooks, walikuwa na ushawishi mkubwa sana kwa Cyrus Ingerson Scofield (1843-1921).

 

Tafsiri ya Scofield inamtajwa na kusifiwa na Darby kuwa ni kama Biblia Bora na nzuri sana ya wanazuoni au wasomi wa nyakati hizi. (Dr C.I. Scofield's Question Box, p. 93) na baada ya kutumika kwenye vita vya kiraia akiwa kama mwanajeshi, alichaguliwa kuwa mwansheria huko Marekani kwenye jimbo la Kansas wakati wa Kuchaguliwa kwa Grant. Alifanyika kuwa mhubiri na kiongozi wa hawa wanaokusanyika Kimakundi mwaka 1882.

 

Ingawa uchapishaji huu wa Biblia iliyojulikana kama Scofield Reference Bible, na hasahasa uanndishi wake kwenye unabii, alisaidia kutokea kwa mateso ya kimafundisho ambayo hayakuwa ya uzima na mapotofu na yasiyotokana na maandiko na yanayoleta mdhara makubwa kwenye ukubalikaji wa muhimu na wa msingi wa Maandiko Matakatifu. Kwa hiyo, wote wawili, yaani kina Darby na Scofield walikuwa watu waaminifu, wapenda kweli na ni watu wene maamuzi magumu na wasioonewa shaka. (utunzi wa vitabu 30 vya Darby unashuhudia hilo.) kwa hiyo walichepuka kutoka kwenye Maandiko Matakatifu inasikitisha sana.

 

Dini na Matengenezo Yaliyofanywa na Mwanadamu

Uendelezaji wa dhana au theory hii iliyofanywa au kuanzishwa na mwanadamu, ambayo imeondoka kutoka kwenye mafundisho ya Mitume, kulitokea kwenye kipindi chote cha karne ya 18. Mapokeo ya wanadam yalishika dau na kuifunika Imani.

 

Inafurahisha kuona maneno ya kimtazamo ya Luther kuhusiana na misingi ya Imani. Wakati alipombiwa ajitokeze mbele ya Diet wa Worms, Martin Luther alitoa jibu lifuatalo wakati alipoambiwa aikane harakati yake,

 

Kwa kuwa wewe mtukufu mheshimiwa sana na uweza wako mkubwa sana hivyo uliponiomba nikupe jibu lililo wazi, la rahisi na lenye kueleweka, nitakupa jibu moja, nalo ni hili: Siwezi kuiweka imani yangu kwa mtu yeyote, iwe ni kwa \papa au kwenye mabaraza, kwa kuwa ni wazi sana kama siku siku waliyoyatenda makosa mfululizo na kujikanganya kila mmoja na mwingine. Ispokuwa hata hivyo, nimeshawishika kwa ushuhuda wa Maandiko Matakatifu au kwa dhamira safi kabisa hadi niliposhawishika kwa kupitia vifungu nilivyo nukuu na isipokuwa kwa yale yanayogusa dhamira yangu inayofungamana kwa neno la Mungu; siwezi na sitoweza kuikana kwa kuwa sio salama kwa Mkristo kunena kinyume na ilivyo dhamira yake. Hapa nasimama, siwezi kufanya kitu kingine chochote zaidi; Mungu nisaidie mimi. Amina. (J.H.Merle D’Aubigne, History of the Reformation of the Sixteenth Century. Book 7, Ch.8.)

 

Matengenezo haya hayakwenda mbali vya kutosha; makanisa yakachukua baadhi ya kweli iliyotangazwa. Kwa namna nyingine ni kwamba matengenezo haya yalikuwa yanarudi nyuma au yanarudi kinyumenyume. Mwaka 1542 Henry VIII alitangaza kuwa Krismas ilikuwa ni sikuku ya Kipagani na akaipiga marufuku kuadhimishwa. Sikukuu hii ilirudishwa upya tena mwaka 1554 baada ya Mkatoliki wa Roma Mary Tudor alipochukua kiti cha enzi cha ufalme. Elizabeth 1 alikosa mbinu za kumuwezesha kumpinga na kurudisha maamuzi yale tena. Cromwell pia akaipiga marufuku tena sikuku hii ya Krismas kwa kipindi cha miaka 12, lakini ilirejeshwa tena na Stuarts na mafundisho ya kizushi yakaendelea.

 

Tunasikitishwa hapa na kufifia pilepole kwa mafundisho ya Kanisa yanayoamini na kufundisha ujio na utawala wa Kristo hapa Duniani.

 

Kuhusu Mpingakristo, fundisho la waamini kunyakuliwa lilitofautiana. Mafundisho ya namna mbalimbali yalisema kwamba Mpingakristo ni mkanamungu au kutoaminika au kukosa uadilifu au Myahudi aliyekengeuka imani. Maelezo haya sio sahihi. Mafundisho haya yanaonekana hadi sasa yanatoka kwenye manabii wa Zama za Giza au wa Zama za Kati za Kanisa na huenda haikuwa sahihi na yalitokana na kuacha kwao kutosikiliza kutoka kwenye vyanzo halisi ili kujifunza chanzo halisi cha kutokea kwa shiku kuu.

 

Mwaka 1534 wa Anabaptists walianzisha huko Munster, Westphalia, Ufalme mpya wa Sayuni, ambao ulihusisha na kitendo cha kugawana mali zao (ilidaiwa kuwa hata) wanawake kwa kawaida, ikiwa ni sharti muhimu kufanywa kwenye Ufalme Mpya wa Kristo (Cath. Enc. loc. cit.). kusitasita kwao kuliwapelekea Wongofu wa kina Augsberg (art. 17) na wa Helvetian (ch. 11) kuyakana mafundisho na hivyo waamini Milenia ya kipindi cha kuja kwake Masihi wakajikuta kuwa hawakubaliki kwenye imani ya Kilutheri na kwenye teolojia za wana Matengenezo (ibid.).

 

Shetani akaanzisha tena kanisa la mafundisho ya kizushi akiwatumia kanuni za kijanja za Mpingakristo, na kisha akachanganya na haya au ndani yake mafundisho ya Milenia ya wakati wa kurudi kwa Masihi. Ndipo yalikataliwa kabisa na halmashauri ku ya kanisa kwa kuwa hawakuwa wanakijua kile ambacho Kanisa la kwanza lilikuwa linakifundisha na hawakuichukulia Biblia kama ilivyo.

 

Malumbano ya Matengezo yalikuwa makubwa sana kuhusiana na jinsi ya kumtambua Mpingakristo na wengi wali waliamini na kufundisha kuwa ni kile cheo cha Upapa, na kwamba mnamo mwaka 1516 Mkutano wa Tano wa Halmashauri Kuu ya Kanisa la Kilutheri ulimwenguni lilipitisha azimio la kukataza mtu yeyote kuandika au kuhubiri somo kuhusu Mpingakristo. Kwa sababu ya uharibifu uliofanywa kwenye Kanisa na Wanamatengenezo wa Kiprotestanti kuhusu suala hili la jinsi ya kumtambua Mpingakristo, mashambulizi ya kitafsiri yalikutikana. Wanateolojia wa kwenye Jamii ya Yesu walifanya hii tafsiri ya kimashambulizi.

 

Mwanzilishi alikuwa Francisco Ribera (miaka ya 1537-1591) wa Salamanca Uhispania, aliyechapisha kitabu cha ufafanuzi chenye kurasa 500 aliyekusudia kujibu kwa mashambulizi mafundisho ya Kiprotestanti uliofundisha kuwa huyu Mpingakristo si mwingine ila ni ofisi ya Papa. Mtu huyu kimsingi ndiye mwanzilishi wa Mtindo wa Tafsiri ya Mambo yajayo, maarufu kama Futurist School of Interpretation (soma pia kitabu cha Encyclopedia Brittannica, 11th Edition, Vol. 23, p.213, article ‘Revelation’ for further comment on the Futurist School).

 

Fundisho lote zima kuhusu unyakuo ni utetezi mtupu, na lililoanzishwa na kuibuliwa tu na wanazuoni wa teolojia ambao ndio walilolikuz fundisho lenyewe na pia kwa wale waliokusudiwa walipinge.

 

Mafundisho ya Ribera yaliendelezwa na Kardinali Robert Bellarmine (miaka ya 1542-1621) wa Italia, Mjesuiti mwenye taaluma ya Kukanganya mafundisho aliyesema kwa Danieli, Yohana, na Paulo walikuwa wameyaacha kuuelezea uweza wa Papa na kwamba unabii wao na mafundisho yao yalituama kwenye kumtaja Mpingakristo atakayekuja baadae katika siku za mwisho.

 

Kasisi mstaafu wa Kikatoliki, Joseph Zacchello anasema kuwa: “Wajesuiti walitaka kupindisha fikra za watu kwa kuonekana utimilifu wa unabii wa Mpingakristo kwenye kanisa la Kipapa. Ribera ameleta imani ya kuona kuwa mambo yatatokea huko mbele, yanayodai kuwa Mpingakristo hajaja bado”. Kwa kusema hivyo anaongeza, “Waprotestanti wanaotetea mafundishohaya ya mambo kutokea baadae wanampendezesha au wanajikomba kwa Papa na wanacheza kwenye mikono ya Roma” (kwa mijibu wa kitabu cha J. Zacchello – cha Ni nani Mpingakristo [Who is the Antichrist] – kilichonukuliwa pia na Woodrow).

 

Ukweli ni kwamba wao ni mchakato endelevu. Biblia iko wazi sana kwamba kuna Wapingakristo wengi. Mpingakristo alikuwepo hata ndani ya Kanisa la Yohana huko Efeso. Wanaendelea kuwepo hadi katika siku za mwisho.

 

Wafasiri mambo kwa mrengo wa siku zinazokuja mbele na misingi yao ya imani ya unyakuo ilikuwa ni mafundisho ya Wakatoliki hadi kwa Mkutubi wa Asfofu Mkuu wa Canterbury, Samuel R. Maitland (miaka ya 1792-1866) kwa zaodi ya kipindi cha miaka ya 1826-30 alifanyika kuwa Mprotestanti wa kwanza kuikubali imani na tafsiri ya waamini kila kitu kitatokea Siku za Mbele yaliyofungwa na Mjesuiti Ribera. Alifuatiwa na Edward Irving mwaka 1832 aliyeendeleza fundisho hili la Unyakuo wa Siri. Maitland lilikuwa kanisa la mrengo wa juu la wanabaraza kuu waliokuwa na mtazamo au msimamo mkali walioshinda vita vya Matengenezo yenye mashindano au malumbano. Mtu huyu kwenye baadhi ya vitabu vyake 50 alifanya uharibifu mkubwa na wa dhahiri kwenye Kanisa la Uingereza na kwenye Makanisa ya Matengenezo kwa ujumla na alisaidia kuongezea na kuzieneza propaganda isiyo ya kimaandiko kwa kiwango ambacho iliwavuna mamilioni ya watu.

 

Msukumo wa msingi ulio nyuma ya mkakati wa kushamirisha na kuyafawezesha kuwa maarufu madundisho haya ya Unyakuo na fikra yake ni kwamba ni ukwepaji. Watu hawawezi kukabili ukweli na kuwa tegemezi kwa rehema na uingiliaji kati wa Mungu. Warumi 8:7 inaonyesha uadui dhidi ya Torati. Hata hivyo, hii inaendana na kushindwa kuikabili kweli. Watatubu au vinginevyo watakabiliwa na maafa makubwa.

 

Baadhi ya wana itikadi hii ya Unyaku wanabashiri ujenzi upya wa Babeli ya Nyakati hizi za Mwisho kwenye jaribio la kuishamirisha imani ya tayaona yaliyoandikwa yatatokea siku za mbele mbali na kuiona Roma kuwa mlengwa. Babeli bado ipo hata sasa ikiwa kama maangamizo makubwa karibu na mji unaojlikana siku hizi kama El Hillah, Iraq. Babeli ya kwenye Ufunuo ni wazi sana kuwa ilikuwepo tangu kipindi cha Kristo, kuelekea mbele hadi kwenye kipindi cha zaidi ya miaka elfu mbili ya mwisho na inaendelea kuwepo hadi leo.

 

Kwa kundi la watu kupinga kuwa Kanisa na Roho wa Mungu yapasa liondolewe kabla ya watu bilioni moja hawajamuongokea Kristo kwenye kipindi cha miaka mitatu na nusu ya dhiki kuu kikiwa kimeanza. Hii ni juhudi kubwa sana kuliko ile ya Kanisa ililoweza kuwa kwenye historia. Hitimisho zaidi ni pia limekubalika kuwa inapasa kuwe na nguvu kuu zaidi Roho wa Mungu au vinginevyo, watu hawa watakuwa sio waongofu, au vinginevyo malumbano haya ni ya uwongo na udanganyifu. Hakuna shaka kwamba malumbano haya ni sahihi na ni kile kile ambacho kinaelezwa kwenye historia; ni sehemu ya propaganda za Kiijesuiti, iliyopangwa na kuwa kwenye mkakati wa makusudi wa wataalamu wa kuitetea dini walio na uweza kama wa kina Maitland, Irving, Darby, Scofield, Estep na waandishi wengi wengine wa kaliba ya chini inayojulikana na kuaminika sana.

 

Waamini Unyakuo wanaweza kuwa sahihi sana kuliko wanavyofikiri, kwa hiyo wataepuka dhiki kuu pekee ya kukabioliana na maafa ya tauni au magonjwa ya ghadhabu ya Mungu, kwa kuwa hawana Mhuri au Alama ya Mungu kwenye vipaji vya nyuso zao, au kwenye mikono yao ya kuume (Kumbukumbu la Torati 6:8), wakiwa wanaendelea kuivunja Amri ya Mungu. Bila shaka waamini Unyakuo ni wakweli, wenye juhudi kumtafuta Kristo na wanasumbukia sana mambo yajayo. Lakini kwa kuzifuata kwao hadithi za kizee zisizo na msingi wa kibiblia, hata hivyo hakutawasaidi mzigo wao kuwa mwepesi; inawaongoza tu kwenye kuyafuata mafundisho ya uwongo na kwenye ukengeufu.

 

“Agano Jipya halifanyi tofauti yoyote kati ya parousia, ufunuo, na hali ya kuonekana na kuwepo siku za nyuma za kabla ya kuzaliwa kimwili ya Yesu Kristo. Majina haya yanaashiria taswira ya mtu mmoja, au mtu binafsi, hali ya kutoonekana ya ujio au kurudi kwa Kristot” (kwa mujibu wa kitabu cha Hans K. La Rondelle, cha Israeli wa Mungu kwenye Unabii; au The Israel of God in Prophecy, p. 188).

 

Utawala wa kipindi cha Milenia utakuwa umeanza. Biblia iko wazi sana na ni kweli na tusipoichukua Biblia na kukielewa kipindi cha millennia na utawala wa Kristo kutoka Yerusalemu kwa kipindi cha miaka elfu moja, ndipo hatutaweza kuuelewa Mpango wa Mungu. Hatutaweza kujua kinachofanyika kwenye Mpango huo na hatutaweza kujua kinachokwenda kutokea kwenye unabii wa Agano la Kale. Wala hatutaweza kuelewa unabii wa Zekaria, Isaya, Yeremia na Ezekieli. Ni muhimu kwamba hatudanganyiki na watu hawa, na kwamba tunajua kulitarajia tumaini letu katika Yesu Kristo na kwamba tunapata hatima yenye utukufu kwa pamoja.

 

Tunalindwa. Ni suala la kuenenda kwa imani na Mungu na kuifanya kazi yetu pia kama tuwezavyo. Sisi sote tuna mahala petu pa usalama, ambapo ni Mungu. Mungu ni mwamba wetu na nguvu yetu na wokovu wetu. Hatuhitaji kitu kingine chochote zaidi. Tunahitajiana kila mmoja na mwingine ili tuweze kukusanyika pamoja, ili tuweze kumwabudu vizuri Mungu wetu wapekee na wa Kweli. Na usipoteze imani kwa nia ya moja kwa moja ya ahadi ya Mungu.

q