Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[109]
Swali Kuhusu
Unenaji kwa
Lugha
(Toleo La 2.0 19950422-20000619)
Jarida hili
linafafanua kikamilifu na kujibu suala kuhusu maana ya unenaji wa kugha na
historia yake ilivyokuwa kanisani na kwenye karne na karne. Maandiko ya Biblia
yanaelezea kwa kuktadha wake kwenye jambo hili kama lilivyoonyeshwa.
Christian Churches of God
PO
Box 369, WODEN ACT 2606,
AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 1995, 2000 Wade
Cox)
(tr. 2016)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na
tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.
Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala
yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika
tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Swali Kuhusu Kunena kwa Lugha
Kwenye Marko
16:15-18 tunakuta imeandikwa hivi:
15
Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. 16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.
17 Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina
langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; 18 watashika
nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono
yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.
Kamusi iitwayo The Interpreter’s
Dictionary of the Bible inasema kwamba:
Uelewa wa kibiblia kuhusu ‘unenaji wa lugha’ unajumuisha mambo yafuatayo (a) utendaji wake kama sehemu ya urembesho wa kimwili wa mwanadamu utokanao na ulaji na unywaji wake (Waamuzi 7:5; Isaya 41:17); (b) ajira yake au kuchukuliana kwake kama neno la ‘kilugha’ na kwa hiyo dhana au na’dharia’; (c) mtindo wa utendaji kazi wa Roho; (d) matumizi yake kwa utendaji kazi na nguvu kwa maisha yote ya mwanadamu, na (e) matimizi yake kama alama ambayo kwamba imefikia ukomo kwa mtazamo wa vitu vinavoonekana.’
Kunena kwa lugha kumekuwa kukieleweka vibaya kwa muda mrefu sana na kwa
siku hizi kunakutikana kwenye makanisa mengi ambako waumini wake huamini kwamba
pasipo karama hii mtu anakuwa hajampokea bado Roho Mtakatifu. Inaonekana pia
kwamba kila mtu binafsi kwenye makanisa haya ambayo wananena kwa lugha mara kwa
mara, wakati mwingine kwa wakati huohuo wakiwa hawajielewi wala kutilia maanani
kuhusu umumihu wa kuyaelewa maana yake. Lakini tunapojifunza kwa bidii na umakini
vifungu vya Biblia tunakuta kwamba tendo hili la kunena kwa lugha limechukuliwa
kwa kutiliwa maanani sana na kwa kweli Mtume Paulo kwenye 1Wakorintho 14:39
anasema kwamba isikatazwe. Kwa hiyo, inapaswa ipate nafasi, tlakini yapasa mtu
ajiulize ni sababu ipi iliyopo hapo inayompelekea apayuke payuke tu pasi
kueleweka maana yake na mtu yeyote, mbali ya huyo anenaye ambaye ni mmoja tu,
peke yake? Kwa hiyo basi, hivi tunaongea nini na Biblia inasemaje hasa?
Kwanza kabisa, hebu na tuone kile kinachonenwa na vitabu vya tafsiri
vijulikanavyo kama encyclopaedias. Kwenye Catholic Encyclopaedia kwenye makala
yake ya kiuandishi kuhusu Lugha, au Glossolalia, (Vol. xiv, pp. 776/7)
inasema kwamba wale waliokuwako kipindi cha wanafunzi walipokea karama hii au karama
hizi:
Waliwasikia wanafunzi wakinena mambo ‘makuu ya
Mungu’ kwa lugha zao wenyewe, ikimaanisha kwa jinsi walivyozaliwa navyo.
...... inaitwa Glossolalia, (ambayo kwa kifupi inamaanisha kipawa cha
kunena kwa lugha), kwa hiyo ilielezewa kihistoria, ikijumuishwa na kuanishwa.
La kufurahisha sana ni kwamba makala hii inasema:
Kwamba Mtakatifu
Frances Xavier anasemekana kuwa waliwahi kumhubiria kwa lugha asiyoielewa na
Mtakatifu Vincent Ferrer aliitumia lugha aliyozalwa nayo ya kienyeji na
ikaeleweka na wengine.
Paulo aliwaagiza
Wakorintho wamwajiri mtu yeyote bali waombe kupewa tafsiri na wasitumie unenaji
usio na tija kwa kutoeleweka na mtu (1Wakorintho 14:9) na wajiepushe na
matumizi kama hayo Kanisani kwa kuwa hata asiyeamini na mwongofu mpya hataweza
kuelewa kinachonenwa (aya ya16).
Kwa hiyo,
hii ilikuwa ni ishara iliyokusudiwa kwa wasioamini na sio kwa wanaoamini.
Kifungu hiki kinaendelea mbele kuonyesha kwamba Kanisa la Korintho linaonekana
kuwa liliruhusu misisimko hii kuendelea au kufanyika kwa michanganyiko mipayuko
isiyo na maana wala faida yoyote na ambayo wakati mwingine hata ungeweza
kuwaingiza kwenye kufuru (1Wakorintho 12:3), jambo lililomsukuma Paulo
kuwarekebisha na kuwafundisha njia bora ya kutumia.
Kitabu cha
Tafsiri na Ufafanuzi kinachoitwa The International Standard Bible Encyclopaedia
kwenye makala yake kuhusu dhana hii ya unenaji kwa Lugha au Tongues (Vol. 4,
pp. 871-875) kinasema hivi:
Matumizi ya matendo
haya yanayojulikana kama Mhemko yanakutikana kwa Washaman, Waseer na Manabii.
Kwa ujumla, hali hii ya kuhemka inahusiana na nguvu za kimungu au hali ya kuwa
katika roho na uvuvio.
Inaendelea
kuelezea kwa kusema hivi:
Hakuna ushahidi
kwamba waandishi wa Agano la Kale walijua lolote kuhusu ‘unenaji kwa lugha’,
ingawaje walijua sana kazi na harakati za kinabii ambayo ilihusiana au kwendana
pamoja na hali au aina mbalimbali za utendaji wakuhemka, kama vile lile kundi
kubwa la manabii waliokuwa wanaimba na tukio la Sauli baada ya roho wa Yahwe
alipomshukia na ‘akambadilisha na kuwa mtu mwingine’ akimuwezesha kutabiri,
(1Samweli 10:5-13 sawa na 19:20-24).
Hata hivyo, kwenye
dini za Kiyunani, dini za Delphi na Pythian zilijua hali hii ya mtu kufanya mhemko
na unenaji ulikuwa ni kitu cha wazi tu na ulichukuliwa kuwa ni mvuvio wa
kimungu na Apolo. Unenaji wa lugha au lugha zisiotafsiriwa kulikofanyika
huko Korintho ulieleweka wazi sana na baadhi yao ikiwa ni dalili iliyotosheleza
ya kuwa kulikuwa na maongozi ya na roho na kwamba mtu aliyefanya hivyo alikuwa
na roho, na ndiyo maana ilichukuliwa kuwa ni suala ya kiroho
(1Wakorintho14:4-6).
Maelezo yake
yanaendelea kuelezea maana au dhumuni la kutolewa kwa karama na mwongozo wake
wa jinsi ya kuzitumia na pia kwenye mitazamo ya kina Marko na Luka. Inasema pia
kwamba:
Irenaeus alijionea
uwepo wake katika wale walioishi na kuenenda sawa na sheria na maelekezo au
mahudhui ya injili. Tertullian aliiorodhesha hali hii kuwa ni kama malumbano au
hoja ya utetezi wa imani ili kuuwezesha uhafidhina wa kiitikadi uendelee
kuwepo, wakati Origen (kwenye kitabu chake cha Ufafanuzi wa Warumi 1:13; 7.6
var.) aliiona hali hii kuwa ni kama daraja la kuwezesha kuvuka vizuizi vya
mahubiri ya kitamaduni.
Dhana hii imetajwa
pia kwenye nyaraka mbalimbali za kiofisi za papa za nyakati za zama za kati na
kusababisha zirudiwe kuonekana kwenye vikundi mbalimbali vya watawa na kwenye
dini zenye hamasa au ushupavu za kihafidhina. Kwenye muonekano wa siu hizi hali
hii imafanyika ijulikane sana na iwe mashuhuri hasa kwenye karne ya 20
ulipoinuka Upentekoste.
Kitabu hiki
pia kinasema kuwa:
Nyaraka alizoandika
Paulo zinaeleweka kuwa zilifundisha kuwa kunena kwa lugha ni karama waliyopewa
Wakristo peke yao.
Kamusi ya
The Interpreter’s Dictionary of the Bible kwenye maelezo yake kuhusu Lugha,
Karama zake, yaani Tongues, Gift of (Vol. 4, pp. 771/2)
inasema kuwa:
Kitendo au hana hii
haikuwahusu Wakristo peke yao bali ilionekana pia kwenye imani na dini nyingi
za ulimwengu wa kale. Popote pale ilipojitokeza, jambo la kwanza
lililochukuliwa kimtazamo lilikuwa ni imani kwamba roho wa mungu waliyekuwa
wanamwabudu amempagaa huyo muumini, ili anene na watu kwa kupitia yeye, na mara
nyingi alimfanya mpagawaji afane miondoko au mitingishio fulani ya mwili wake
na matendo mengine yasiyo ya kawaida. Wakati huu mtu huyu anapokuwa kwenye hali
hii ya kuhemka koo lake la kutolea sauti liliathirika au kubadilika, ulimi nao
ulitoka kana kwamba kulikuwa na operesheni ya nguvu zisizoweza kudhibitiwa na
akili zake huyu aliyepagawa, na ndipo hatimaye alianza kutoa maneno na
kumwambia mhusika au watazamaji wengine waliojihudhurisha mahali hapo, mara
nyingi maneno au ujumbe uliotolewa haukuwapendeza wale waliokuwa hawako sawa
kiimani.
Hadithi iliyo kwenye
kitabu cha Matendo io sahihi kabisa. Unenaji wa lugha mpya uliofanyia siku ya
Pentekoste ulifanwa kwa lugha za wageni, zilijulikana na waliozisiia na
ziliwashangaza sana makutano. Lakini wakati unenaji huu huu wa ‘Lugha’
ulipofanyika huko Kaisaria na Efeso (Matendo 10:46; 19:6), Petro alijionea
mwenewe, pasipo linganisha na mahala penginepo pote aina kama hii ya muujiza wa
kupewa uweza wa kunena lugha nyingi. Wala hakukuwa na uhitaji kama huo kwa kuwa
lugha za Kiyunani na Kiaramu zilitisha kabisa kuzitumia kwa huduma za kanisani.
Kwa sababu ya
msisitizo uliotiliwa chumvi mno kuhusu unenaji kwa lugha uliojulikana kama
glossolalia huko Korintho, Mtume Paulo alilazimika kulishughulikia jambo hili.
anafanya hivyo kwa kuelezea kuwa anatambua umuhimu wake kwa kusema kwake hivi:
(a) kipawa halisi
cha Roho, isikatazwe, na anatambua na kuwatia moyo kwamba hata yeye mwenyewe
anashirikiana kwa mambo ya karama (1Wakorintho 14:5, 18, 39);
(b) ni msaada mkubwa
kwa mtu anapojitoa au kujikabidhi kwenye tafakari, yaani ni njia ya kuwasiliana
na Mungu, na ni fursa ya kuelezea mawazo na hisia ambayo yasingeweza kutopata
majawabu kwa njia za kawaida (1Wakorintho 14:4: sawa na Warumi 8:26-27);
(c) ni ishara kwa
wasioamini (1Wakorintho 14:22); na ni ushahidi wa madhihiriko ya nguvu za
kimungu, ambayo ni kama ‘ishara ya Yona’ (Mathayo 12:39), ingawaje kwa kusema
kweli zilikuwa hazijakubalika sana kihivyo kwa ugumu wa mioyo yao na kutokana
na waliimu wa mafundisho ya uwongo na wasioamini na wakosoaji.
Paulo aliziona
hatari za jinsi wanavyozitumia tena kwa wazi sana kabisa kuliko uzuri wake.
Hakuruhusu ifanyike hivyo kama kigezo muhimu kwenye ibada na aliwakataza
wasifanye hivyo kwenye ibada za hadharani pia (1Wakorintho 14:19, 28).
Anafundisha hivi
utaratibu wa kuthibiti:
(a) Kwa kuzifuata
kanuni kuu na taratibu zake. Matumizi ya karama za kiroho lazima zifanywe
kwa mujibu wa mahitaji yake yaliyopo ili kulijenga kanisa ‘kwa upendo’
(1Wakorintho 13; 14:4-5,17-19; Wakolosai 3:14; sawa na Waefeso 4:16).
Matumizi ya Lugha ni ya kibinafsi mno, yakiukuza utu wa ndani wa kiroho chake
na umuhimu wake na yamekusudiwa kujenga mshikamano wa ibada za Kikristo na
umoja wao (Warumi 12:3; 1Wakorintho 13:5; Wafilipi 2:3-4).
(b) Kwa kusimamia
utaratibu wa ibada kulielimisha kanisa ni jambo la muhimu na la kwanza. Yeye
anayena ni lazima aweze kujizuia mwenyewe au vinginevya anamaze kimya
kusipokuwa na mwenye kutafsiri (Wakorintho 14:27-28). Wakati ibada
inapokuwa haieleweki, au inapowakwaza na kuwaondoa kutoka kwenye kweli, basi
inakuwa imeshindwa. Utaratibu na heshima ni vitu vya muhimu sana (1Wakorintho
14:13-19, 23-33, 40).
(c) Kwa kuupa
umuhimu karama ya kutafsiri lugha. Uwezo wa kutafsiri lugha ulikuwa ni kipawa
cha kipekee cha aina yake waliyopewa wau wachache sana (1Wakorintho 12:10,30;
14:28) – uwezo wa kuwa na hali inayotarajiwa ya uaswa wa kile kilichosemwa,
hususan kwa kuhamishwa kimawazo hasahasa kwa mtengamano wa kiroho. Mwenye aina
hii ya kuhemka anapungukiwa karama hii na yampasa aiombe, kwa kuwa anawajibu wa
mambo mawili, yaani kwa yeye mwenewe na kwa kanisa (1Wakorintho 14:13-14).
Hizi ni
baadhi tu ya vipengele vilivyowekwa na wanazuoni lakini vinaonyesha kuwa
ka6rama hizi ni za muhimu na haifai zieleweke vibaya na kutumiwa vibaya na
zinapasa zitumiwe kwa uangalifu mkubwa. Zaonekana kuwa kuna kiwango fulani cha
nadharia kinachohusiswa, na hususan dhana ya kunena kwa lugha, inaonekana
kwamba hakujaeleweka vizuri sana na kikamilifu. Sasa hebu na tutazame kwene
Biblia (hususan tafsiri ya Kiingereza ya RSV).
Matendo 2:3-4 Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila
mmoja wao. 4 Wote wakajazwa Roho
Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.
Ilikuwa ni kipindi hiki ambacho
wanafunzi walifanika kuwa waongofu na walianza kuhubiri kwa watu wote. Ilikuwa
ni Pentekoste, Sikukuu au Idi ya Majuma, na Wayahudi wa huko Yerusalem walikuwa
ni wa mataifa yote waliokuwa wanaongea lugha ningine yoyote ile, hivyo, unaweza
kupata taswira jinsi walivyoshangazwa wakati walipowasikia Maandiko Matakatifu
yakisomwa kwa lugha na ndimi zao wenyewe. Kitabu cha tafsiri cha Catholic
Encyclopaedia kinasema kwamba inaaminika kuwa walikuwa ni watu wa kutoka
takriban mataifa kumi na tano. .
Matendo 2:5-11 Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa,
watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. 6 Basi
sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa
kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. 7 Wakashangaa
wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? 8 Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha
yetu tuliyozaliwa nayo? 9 Warparthi na Wamedi
na Waelami, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia, 10 Frigia na Pamfilia, Misri na pande za
Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu, 11 Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa
wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu.
Jambo la
muhimu hapa ni kwamba Biblia inasema kwamba Wayahudi waliyasikia Maandiko
Matakatifu yakifundishwa kwa lugha zao wenyewe. Matendo 10:46 inaanikiza
hivi.
Matendo
10:46 inasema: Kwa maana
waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu,
Kwa hiyo
walishangazwa lakini wengine walidhihaki na wakasema kuwa huenda wanafunzi
walikuwa wamelewa. Lakini Petro akawatetea akinukuu Maandiko Matakatifu kutoka
kitabu cha nabii Yoeli na akawakumbusha kuhusu unabii huu na akawahubiria
(Matendo 2:12-47) na wengi wao wakatubu na kubatizwa.
Haiishii
hapo tu, bali Matendo 10 inaelezea kuhusu maono aliyoonyeshwa Mtume Petro ya
wanyama najisi, yaliyofuatiwa na ubatizo wa Kornelio pamoja na familia yake na
marafiki zake wa karibu nao pia walinena kwa lugha mpya na walimpokea Roho
Mtakatifu (soma Matendo 10:44-47). Hii ilikuwa inaonyesha kuwa Mungu alikuwa
anawajali na kutenda kazi na Wamataifa. Sehemu inayofuatia kuelezewa unenaji
kwa lugha ni kwenye Matendo 19:6.
Matendo 19:6 Na Paulo, alipokwisha kuweka mikono
yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na
kutabiri.
Ni wazi kwamba hii ni karama inayotolewa
na Roho Mtakatifu inayofuatia kuwekewa mikono, ingawa hajapewa mtu yeyote.
1Wakorintho 7:7 inasema::
7 Ila nipendalo ni kwamba watu wote wawe
kama mimi nilivyo; walakini kila mtu ana karama yake mwenyewe itokayo kwa
Mungu, huyu hivi, na huyu hivi.
Mtume Paulo
kwenye 1Wakorintho 12 anafafanua kwamba vipawa au karama mbalimbali zimetolewa
kwa watu mbalimbali tofauti tofauti sawasawa na mapenzi ya Mungu.
1Wakorintho
12:1-31 Basi, ndugu zangu,
kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose kufahamu. 2 Mwajua
ya kuwa mlipokuwa watu wa Mataifa, mlichukuliwa kufuata sanamu zisizonena, kama
mlivyoongozwa. 3 Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna
mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu
kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. 4 Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni
yeye yule. 5 Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni
yeye yule. 6 Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali
Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. 7 Lakini
kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. 8 Maana
mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo
Roho yeye yule; 9 mwingine imani katika Roho yeye
yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja; 10
na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine
kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha; 11 lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye
yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.
Rejea yapaswa ifanywe pia kwenye
Warumi 12:6-8:
6 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; 7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake; 8 mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha.
1Wakorintho
12 inaendelea kueleza ikisema:
12
Maana kama vile mwili
ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi,
ni mwili mmoja; vivyo hivyo na Kristo. 13 Kwa maana
katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi,
au kwamba tu Wayunani; ikiwa tu watumwa au ikiwa tu huru; nasi sote
tulinyweshwa Roho mmoja. 14 Kwa maana mwili si kiungo
kimoja, bali ni vingi. 15 Mguu ukisema, Kwa kuwa mimi
si mkono, mimi si wa mwili; je! Si wa mwili kwa sababu hiyo? 16
Na sikio likisema, Kwa kuwa mimi si jicho, mimi si la mwili; je! Si la
mwili kwa sababu hiyo? 17 Kama mwili wote ukiwa jicho,
ku wapi kusikia? Kama wote ni sikio ku wapi kunusa? 18 Bali
Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka. 19 Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa
wapi? 20 Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni
mmoja. 21 Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina
haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi. 22 Bali zaidi sana vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa
vinyonge zaidi vyahitajiwa zaidi. 23 Na vile viungo
vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi;
na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana. 24 Kwa
maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha
mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa; 25
ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na
mwenziwe. 26 Na kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote
huumia nacho, na kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
27 Basi ninyi mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila
kimoja peke yake. 28 Na Mungu ameweka wengine katika
Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza,
kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.
29 Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote
ni waalimu? Wote wanatenda miujiza? 30 Wote wana
karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri? 31 Takeni sana karama zilizo kuu. Hata hivyo nawaonyesha
njia iliyo bora.
Wenye Sura
ya 13 Mtume Paulo anaendelea kufafanua kuwa karama hizi zote zinapasa
ziandamane na upendo wa Mungu vinginevyo vitakuwa havina maana.
1Wakorintho13:1-13 Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za
malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. 2 Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri
zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha
milima, kama sina upendo, si kitu mimi. 3 Tena
nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue
moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. 4 Upendo
huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo
yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; 6 haufurahii
udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; 7 huvumilia
yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. 8 Upendo
haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha,
zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. 9 Kwa
maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; 10 lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa
sehemu itabatilika. 11 Nilipokuwa mtoto
mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri
kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya
kitoto. 12 Maana wakati wa sasa
tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa
sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa
sana. 13 Basi, sasa inadumu
imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo..
Sura ya 14
inaendelea kusema:
1Wakorintho
14:1-18 Ufuateni upendo, na
kutaka sana karama za rohoni, lakini zaidi kwamba mpate kuhutubu. 2 Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu, bali husema
na Mungu; maana hakuna asikiaye; lakini anena mambo ya siri katika roho yake. 3 Bali yeye ahutubuye, asema na watu maneno ya kuwajenga, na
kuwafariji, na kuwatia moyo. 4 Yeye anenaye kwa lugha
hujijenga nafsi yake; bali ahutubuye hulijenga kanisa. 5 Nami
nataka ninyi nyote mnene kwa lugha, lakini zaidi sana mpate kuhutubu, maana
yeye ahutubuye ni mkuu kuliko yeye anenaye kwa lugha, isipokuwa afasiri, ili
kusudi kanisa lipate kujengwa.
Kwenye
1Wakorintho 14:6 ndipo Paulo anafafanua umuhimu wa kuitumia vizuri karama hii
ya kunena kwa lugha. Kama mtu atakuwa anaitumia kwa kunena mambo yasiyojulikana
ndipo inakuwa haina umuhimu wa kiroho wala haiwatajenga wanaomsikiliza. Hata
hivyo, ilionekana kuwa Paulo alikuwa haongelei kuhusu unenaji huo usio na
malengo lakini alikuwa anaongelea kuhusu lugha fulani lengwa ambazo zinaweza
kueleweka na wanaoiongea lugha hiyo na ambayo mtafsiri anaweza kupatikana.
Hata kama
hilo halina umuhimu, Paulo anasisitiza umuhimu wa kufundisha kwa ajili ya
kuwaelimisha ndugu waumini. Kama hakutakuwa na kuelewa kokote basi hakutakuwa
na uelimishaji wala kujenga.
6 Ila sasa, ndugu, nikija kwenu na kunena kwa lugha, nitawafaidia
nini, isipokuwa nasema nanyi kwa njia ya ufunuo, au kwa njia ya elimu, au kwa
njia ya hotuba, au kwa njia ya fundisho? 7 Hata vitu
visivyo na uhai vitoapo sauti, ikiwa ni filimbi, ikiwa ni kinubi, visipotoa
sauti zilizo na tofauti, itatambulikanaje ni wimbo gani unaopigwa kwa filimbi
au kwa kinubi? 8 Kwa maana baragumu ikitoa sauti
isiyojulikana, ni nani atakayejifanya tayari kwa vita? 9 Vivyo
hivyo na ninyi, msipotoa kwa ulimi neno lililo dhahiri, neno lile linenwalo
litajulikanaje? Maana mtakuwa mkinena hewani tu. 10 Yamkini
ziko sauti za namna nyingi duniani, wala hakuna moja isiyo na maana. 11 Basi nisipoijua maana ya ile sauti nitakuwa kama mjinga
kwake yeye anenaye; naye anenaye atakuwa mjinga kwangu. 12 Vivyo
hivyo na ninyi, kwa kuwa mnatamani sana kuwa watu wenye karama za roho, takeni
kwamba mzidi sana kuwa nazo ili kulijenga kanisa. 13 Kwa
sababu hiyo yeye anenaye kwa lugha na aombe apewe kufasiri. 14
Maana nikiomba kwa lugha, roho yangu huomba, lakini akili zangu hazina
matunda. 15 Imekuwaje, basi? Nitaomba kwa roho, tena
nitaomba kwa akili pia; mtaimba kwa roho, tena nitaimba kwa akili pia. 16 Kwa maana wewe ukibariki kwa roho, yeye aketiye katika
mahali pa mjinga ataitikaje, Amina, baada ya kushukuru kwako, akiwa hayajui
usemayo? 17 Maana ni kweli, wewe washukuru vema, bali
yule mwingine hajengwi. 18 Namshukuru Mungu ya kuwa
nanena kwa lugha zaidi ya ninyi nyote;
Ni
dhahiri sana hapa kwamba karama hii amepewa Paulo ili aweze kunena kwa lugha
nyingi ambazo hajawahi kujifunza kwazo ili aweze kuwahubiria Injili wale atakao
wafikia vinginevyo aweze kuelewa. Kuna jambo lingine hapa ambalo Paulo
ameliingiza nalo ni mahala pake muafaka kufanyia maombi haya. Hii imeandikwa
kwenye kamsi ya Interpreter’s Dictionary of the Bible kuwa ni kama ilivyoelezwa
mwanzoni kwenye kipengele (b) kinachoelezea kuwa ni namna ya kimsada kwa mtu
anapojitoa kimaombi 1Wakorintho 14:4 sawa na Warumi 8:26-28 ambayo inasema:
Warumi 8:26-28 Kadhalika Roho naye hutusaidia
udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe
hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. 27 Na
yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu
kama apendavyo Mungu. 28 Nasi twajua ya kuwa
katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia
mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.
1Wakoritho
14:19-33 inaendelea kusema:
19
lakini katika kanisa
napenda kunena maneno matano kwa akili zangu, nipate kuwafundisha wengine,
zaidi ya kunena maneno kumi elfu kwa lugha. 20 Ndugu
zangu, msiwe watoto katika akili zenu; lakini katika uovu mgeuzwe watoto
wachanga, bali katika akili zenu mkawe watu wazima. 21 Imeandikwa
katika torati, Nitasema na watu hawa kwa watu wa lugha nyingine, na kwa midomo
ya wageni, wala hata hivyo hawatanisikia, asema Bwana. 22 Basi,
hizi lugha ni ishara, si kwao waaminio, bali kwao wasioamini lakini kuhutubu si
kwa ajili yao wasioamini, bali kwa ajili yao waaminio. 23 Haya!
Ikiwa kanisa lote limekusanyika pamoja, na wote wanene kwa lugha, kisha ikawa
wameingia watu wajinga au wasioamini, je! Hawatasema ya kwamba mna wazimu? 24 Lakini wote wakihutubu, kisha akaingia mtu asiyeamini, au
mjinga, abainishwa na wote, ahukumiwa na wote; 25 siri
za moyo wake huwa wazi; na hivyo atamwabudu Mungu, akianguka kifudifudi, na
kukiri ya kuwa Mungu yu kati yenu bila shaka.
Kwa
dhahiri kabisa, matumizi yasiyotakiwa ya lugha yanaonekana kuwa ni kama ishara
ya uchanga au kutoimarika hapa. Kifaa muhimu zaidi cha wongofu ni unabii wa
wazi. Mtume Paulo anaendelea mbele kufafanua kanuni za kutumia unenaji kwa
lugha au lugha mpya ya kigeni.
26 Basi, ndugu, imekuwaje? Mkutanapo pamoja, kila mmoja ana zaburi, ana
fundisho, ana ufunuo, ana lugha, ana tafsiri. Mambo yote na yatendeke kwa
kusudi la kujenga. 27 Kama mtu akinena kwa lugha,
wanene wawili au watatu, si zaidi, tena zamu kwa zamu, na mmoja na afasiri. 28 Lakini asipokuwapo mwenye kufasiri na anyamaze katika
kanisa; aseme na nafsi yake tena na Mungu. 29 Na
manabii wanene wawili, au watatu, na wengine wapambanue.
30 Lakini mwingine aliyeketi akifunuliwa neno, yule wa
kwanza na anyamaze. 31 Kwa maana ninyi nyote mwaweza
kuhutubu mmoja mmoja, ili wote wapate kujifunza, na wote wafarijiwe. 32 Na roho za manabii huwatii manabii. 33 Kwa
maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika
makanisa yote ya watakatifu.
1Wakorintho 14:39:40:
39
Kwa ajili ya hayo,
ndugu, takeni sana kuhutubu, wala msizuie kunena kwa lugha. 40 Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri
na kwa utaratibu.
Kwa hiyo
ilionekana kwamba kunena kwa lugha ni sehemu inayoruhusiwa kwenye Mahubiri ya
Injili, lakini wamepewa mtu mmojammoja binafsi kwa makusudio fulani maalumu kwa
kuwa zote hizi ni karama za Mungu. Kwenye eneo la kanisa ambako wote wananena
au ambapo angalau wanaelewa kwa angalau kiwango cha kutosha lugha inayoongelewa
au kutumiwa na watu wa huko basi hakuna sababu ya kufanyika jambo hili.
Tunajua
kwamba kwenye Kanisa la Transcarpathia walisemekana kuwa walikuwa wananena kwa
lugha. Tunajua kwamba walinena kwa mtindo au aina ya kizamani ya lafudhi
Kanisani. Muujiza kama huo waweza kuwa ni wa muhimu, au ni wa muhimu kule
lakini sio hapa.
Mtume Paulo
aliliweka jambo hili kuwa ni kipawa chenye thamani ndogo na alionyesha kuwa
kinaweza kutumiwa vibaya na walionacho. Karama hii inaweza kutumiwa tu kwa
maongozi na utaratibu ulioelezewa na kuelekezwa na yeye kwa kulijenga kanisa.
Warumi 12:6-9 inasema:
Warumi 12:6-9 6 Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya
neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani; 7 ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye
kufundisha, katika kufundisha kwake; 8 mwenye kuonya,
katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa
bidii mwenye kurehemu, kwa furaha. 9 Pendo na lisiwe
na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema.
Kwahiyo sasa
ni kwa kusikia au kunena au yote mawili? Ni lazima iwe ni yote mawili. Mahali
pake, ni wakati inavyofanyika kwa moyo wa upendo wa Mungu, yapasa kuwa ni
kwenye kuhubiri Injili kwa mataifa yote.
Sababu ya
pili inatokana na swali kuhusu Lugha na kwamba ni kuhusu hamasa iliyoelezwa
kwenye Marko 16:9-20. Biblia ningi hazijumuishi sehemu ya mwisho ya Marko
kwenye maandiko yao au zinaijumuisha sehemu hii kwa bango kitita. Maandiko
haya hayaonekani kwenye nakala halisi na asilia za kale.
Wakosoaji wengi wa
siku hizi wanakubali kwamba aya kumi na m6bili za6 mwisho za Marko 16 hazipo
sahihi; na si sehemu ya Injili yake (Companion Bible, Appendix 168, p. 190).
Aya hizi
zimeonekana kwenye tafsiri za lugha ya Kisyria au Kiaramu na Peshitto inahesabu
tangu mapema sana kama hata huenda miaka ya 170 BK na nakala ya Curetonian
Syriac ya marne ya tatu. Aya hizo zilikuwa zinataja mamlaka nyingi au waandishi
wa zama kale. Kwa mujibu wa tafsiri ya Companion Bible sehemu ya Nyongeza
inasema hivi:
·
Papius
(yapata mwaka 100 AD) anainukuu aya ya 18 (kwa mujibu wa Eusebius, Hist. Ecc.
iii 39).
· Justin Martyr (AD 151)
anainuku aya ya 20 (Apol. I. c. 45).
·
Irenaeus (AD 180) anainukuu na
kutoa maelezo kwenye aya ya 19 (Adv. Her. lib. iii. c.x.).
·
Hippolytus (AD 190-227) ananukuu
aya za 17-19 (Lagarde’s ed. 1858, p. 74).
·
Vincentius (AD 256) anazinukuu
aya mbili kwenye Mkutano Mkuu wa saba wa Carthage uliosimamiwa na Cyprian.
·
The ACTA
PILATI (sentensi ya 2) anazinukuu aya za 15, 16, 17, 18 (Tischendorf’s ed.
1853, pp. 243, 351). Katiba ya Mitume(senti. 3 au 4) inazinukuu aya za 16,17,18.
·
Eusebius (AD 325.) anazijadili
aya hizi, kama zilivyonukuliwa na Marinus kutoka kwenye sehemu iliyopotea ya
Historia hii.
·
Aphraartes (AD 337) akofu wa
Syria, alizinukuu aya za 16-18 kwenye Mahubiri yake ya kwanza (Dr Wright’s ed.,
1869, I., p. 21).
·
Ambrose (AD
374-97) Askofu Mkuu wa Milan, alizinukuu bure kabisa aya za 15 (mara nne), 16,
17, 18 (mara tatu), na aya ya. 20 (mara moja).
·
Chrysostom
(AD 400) anaifanyia rejea aya ya.9; na anasema kwamba aya za 19, 20 ni “mwisho
wa Injili”. Jerome (b. 331, d.420) anazijumuisha aya hizi kumi na mbili kwenye
tafsiri yake ya Kilatini, nambali ya akizinukuu aya za 9 na 14 kwenye maandiko yake
mengine.
·
Augustine
(fl. AD 395-430) ni zaidi ya kuzinukuu. Alizijadili kuwa ni kazi ya uandishi wa
Mwinjilisti MARKO, na anasema kwamba zilisomwa hadharani makanisani.
·
Nestorius
(sentesi ya 5) anainukuu aya ya.20; na,
·
Cyril wa Alexandria (AD 430) anakubaliana
na kunukuu huku.
·
Victor wa Antioch (AD 425) anaonyesha
wazo la Eusebius, kwa kutaja MSS nyingi alizoziona, na hivyo kwamba ametosheka
nazo kuwa aya kumi na mbili za mwisho zimerekodiwa kutoka humo.
Tafsiri ya Companion Bible
inazitetea aya hizi kumi na mbili za mwisho kwa msingi kwamba zilikuwepo kwenye
tafsiri ya Kisyria na zilitumika kwenye kanisa la kwanza na kwa hiyo aya hizi
zingeondolewa na mamlaka zilizofuatia kama matunda yake yasingekuwepo kwenye
nakati za mitume na kwenye Kanisa la kwanza. Hoja kama
hizi zingekuwa pia kweli kuhusu miujiza ya mitume na manabii.
Utetezi mwingine wa aya hizi
umoendelezwa zaidi na makanisa ya kiuamsho ya siku hizi. Utegemezi wake
unatokana pia kwenye maandiko au kitabu cha Ivan Panin (cha Aya Kuminambili za Mwisho
za Marko..., Shirika la Watu wa Agano, yaani The Last Twelve Verses of Mark...,
The Association of the Covenant People). Maandiko haya yaliungwa mkono na Panin
kwa mchanganuo wa kimahesabu ambao unawezesha kuwa na thamani ya kitarakimu ya
aya hizi kwenye andiko. Inaonekana kuwa andiko hili limetuama kwenye tarakimu
saba saba na kuna michanganuo mikubwa iliyofanywa na Panin ambayo inataka kudai
kuwa maandiko haya yana uvuvio kwa sababu ya huu msingi ulioenezwa kwa
kitarakimu. Inaonekana kuwa ni kundi la watu wanaopotoshwa wakiwa hawajijui kwa
baadhi ya maandiko ya Agano la Kale kutokana na uandishi wa siku za hivi
karibuni katika Israeli nay a Vitabu vya Torati lakini sio waainishaji wakuu wa
Agano Jipya uliofanywa hadi sasa. Zaidi ya yote, andiko lililo kwenye Marko
yapasa liwe na mlingano uliothibitishwa. Lakini ikiwa kwamba aya hizi kumi na
mbili zitakuwa ni sehemu ya Injili halisi na kinyume chake kina ukweli sawia.
Vitabu vingine vimeandikwa au kufanywa lakini sio kazi kubwa sana na zenye
mamlaka ya kuvihitimisha. Kitabu cha Panin kinajaribu kuonyesha kuwa andiko
lote zima limetathiminiwa na limeonyeshwa kuwa linalingana. Kitabu cha Panin
kingekuwa na ushawishi zaidi kama maandiko haya yote yangekuwa yamethibitishwa.
Inapotokea kutokuwa na kiambishi kinacholingana kikionyeshwa kuwa kipo inaweza
tu kupelekea kuonekana kufanya hitimisho kwamba andiko hilo liliandaliwa kwa
namna hiyo kwa kusudi la kuweka nyongeza kwenye Injili kwa malengo yaliyoungwa
mkono na maandiko yaliyotungwa kwenye aya hizo. Na jambo lenyewe ni wazi sana
kwamba linahusu unenaji kwa lugha. Hadi ukamilishaji wa ushahidi kwa hali hii
ya mhamasiko kwenye Marko 16:9-20 imeonekana kujitokeza inaweza kudhaniwa tu
kwamba aya hizi kumi na mbili za mwisho zinathibitisha ukweli wa kwamba ziliandaliwa
mapema wakati fulani kipindi cha mwishoni mwa karne ya kwanza ili kuunga mkono
mtindo wa ibada unaohusisha unenaji kwa lugha na ambao hakuna mamlaka ya
kibiblia yaliyokuwepo na ambayo yaliaingizwa ili kufifisha mwongozo halisi
uliowekwa kusimamia jambo hili, utaratibu au mwongozo uliotolewa na Mtume
Paulo. Hivyo basi, aya hizi kumi na mbili za mwisho ndipo zikaongezwa kwenye
Injili hii ya Marko, ambazo ni aya za 9-20, ambazo zinafaa zana kuwa zitumiwe
kwa tahadhari kubwa na wala zisitumiwe kwa lengo la kuanzisha aina yoyote ya
mafundisho. Fundisho kuhusu unenaji kwa lugha kwa kweli limeainishwa wazi sana
kwenye uandishi wa kijarida hiki na karama zinazoelezewa zinahusiana tu na
masuala ya lugha inayotumiwa tu kwa maelekezo ya waumini wakati lugha inapohitajika
ili kuwafundisha na kwa kuwaongoa wasioamini. Matokeo yake ni kuonekana kwa
nidhamu na utaratibu wa Roho Mtakatifu kwa nguvu na uweza, kwa heshima na kwa
utaratibu.