Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[127]
Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu:
Tathmini ya Waandishi wa Kipatristiki na Uainisho Wao
Kuhusu Mungu
(Toleo La 4.0 19950722-1998093-20110104-20110129)
Jarida hili linayatathmini maandiko ya zamani na kuondoa mitizamo yake
kuhusu Mungu. linaainisha pasipo shaka kwamba waandishi wa mwanzoni walikuwa
ama ni Waamini Utatu au Watrinitariani au Waamini Miungu Wawili yaani
Wabinitariani, na hawakuwa wakiamini kwamba Kristo alikuwepo tangu hapo
mwanzoni. Jarida hili linasaidia kuonyeshaa mabadiliko haya ya kiupotoe yanayojitokeza
kidogokidogo ya kiteolojia kwenye muundo wa imani ya Kitrinitarian.
Christian Churches of God
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 1995, 1999, 2011 Wade Cox)
(tr. 2016)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na
tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote
atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja
ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia
yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://ww.ccg.org
Teolojia ya Mwanzoni ya Uungu
Dhana na
Nadharia ya Zamakale ya Mungu wa Utatu au Utrinitariani
Dhana kuu iliyopo kuhusu Ukristo wa Kisasa
ni kwamba Mungu yupo kwenye umbo au muunganiko wa vitu vitatu au hypostases. Kuna mijumuisho mbalimbali
kwenye umoja au mmoja kwenye muungano wa utatu, unaojulikana au kuelezewa kama
Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, ambao wanaelezea kuwa ni nafsi za pamoja. Vitu au watu hawa watatu wanasemekana kuunda Utatu. Utetezi wa usahihi wa madai haya
umefanywa na dhana ya zamakale. Dhana nyingine iliyoeneza sana na iliyo ya
uwongo ulio sawa na hiyo ni kwamba Kanisa la kwanza lilikua la imani ya Kibinitariani
kuliko kuwa ni la Kitrinitariani, na linalodhaniwa kuwa Kristo, alipokuwa ni
msaidizi, hata na wala hakuwa sawa na Mungu. Kwa hiyo wanasema kwamba
kulikuweko na Miungu wawili walioishi kuweko kwa kila upande wakiwa kama Baba
na Mwana. Hiki ndicho kilchojulikana hapo zamani kuwa ni Uzushi kuhusu Nguvu
Mbili zitendazo kazi pamoja. Mafundisho haya mapotofu yanatokana na imani za zama kale za Kinostoki na Dini za
Kisirisiri au za Kimafumbo za waabudu Mungu Juan a hayana uhusiano wowote
kabisa na mafundisho ya Mitume au ya Kanisa la Kwanza. Yanaenda kinyume na
kukanganya andiko la Mtume Yohana (Yohana 17:3 na 1Yohana 5:20) linalosema kwamba
kuna Mungu Mmoja tu wa Pekee na wa Kweli, na kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana
wake, na pia maandiko ya Mtume Paulo yanayosema kuwa ni Mungu tu peke yake
ndiye hafi wala kupatwa na madhara, kwenye 1Timotheo 6:16. Kuelewa yaliyosemwa
na Mitume hawa, yaani Yohana na Paulo na mitume wengine yalifundishwa na
kuaminiwa pia na mitume Yohana na waliowarithi au kuwafuatia baadae, kama
tutakavyoona hapo chini.
Jarida hili linakusudia kuainisha uwepo wa
dhana kama hizo kuhusu Uungu kwenye mintaarafu ya mafundisho ya kibiblia
tuliyoanzanayo tangu hapo mwanzoni na kwa uelewa wa wanateolojia wa zamani au
wa kwanza. Madai ya kwamba Mungu ni mjumuiko wa viumbe au nafsi tatu ambayo
kila moja inakuwa sawa na za milele hayakuwa mafundisho wala imani ya Kanisa la
kwanza la Mitume kama tulivyojionea. Itaonekana pia kwamba hayakuwa ni
mafundisho wala imani ya Kanisa la kwanza. Dhana ya Uungu kuwa ni mjumuisho wa
viumbe watatu kwa kweli halikuwa la imani ya Kikristo na, kwa kweli lilianzia
kipindi cha hata kabla ya kuzaliwa kwa Kristo na karne nyingi sana kabla yake.
Hakuna shaka kanisa kwamba habari na hadithi za mungu wa utatu zinakutikana kwenye ngano za ustaarabu wa zama za
kale zaidi na anajulikana kuwepo pande za mashariki mwa Asia. Waamini wa nadharia
hii kuhusu Mungu wa Utatu waliingia kwenye imani ya Kikristo kwa kishindo
wakitokea kutoka kwenye imani za Kiyunani na imani hii ikapata ushaishi na
kukubalika na Warumi. Kiini au etimolojia ya jina la Yesu linayokana na lugha
na mapokeo ya Kihellenia ya jina Yoshua ambalo ndilo lilikuwa jina la Masihi.
Neno lililo kenye Agano Jipya lililotumika kutafsiri jina la Yoshua ni lile
lililo kwenye Kamusi ya SGD 2424 z30F@ŘH au ’Iesous. Neno hili linatumika
kwa Yoshua Mwana wa Nuni kwenye Waebrania 4:8, na Yoshua (z30F@Ř au ’Iesou)
wa wakati wa Zerubabeli, aliyokuwa miongoni mwa mababu wa Kristo, kwenye Luka
3:29. Neno hili linatimika pia kutafsiri jina la Yusto kwenye Wakolosai 4:11.
Neno la Kiyunani la Iesus linaonekana kuwa linatokana au kushabihiana na neno la
Kiceltiki la Esus, mmoja wa miungu
iliyo kwenye mjumuisho wa miungu inayokutikana kwenye Dini na Imani za Wahaiperborean
(soma kamusi ya ERE, Vol. 3, p. 278).
Imani hizi zilikuwa na nguvu au ushawishi mkubwa sana zikikubalika na Walatini
kisha pamoja na Wateutons (ibid.). Jina Esus huenda liingia kwenye lugha ya
Kiyunani kutoka kaskazini pamoja na imani ya kidini ya Kihaiperborean na dini
za Kisirisiri. Mjumuiko wa kiutawala wa mjumuiko ulijitokeza kwenye imani za Tuatha
de Danann, kama Brian, Iuchair na Iucharbar, wakiwa ni kama wana wa mungumke Danu
(ibid., p. 282). Huyu Tuatha de Danann pia alifanyika kuwa ni mshirika wa mungu
wa Kisiwani Elysium na ndiyo Imani na Dini ya Kisirisiri ya Waelysian (ibid.,
p. 298) na alikuja kujulikana kama watu
wa miungu mitatu (ibid., p. 292).
Waliamini kwa heshima yao yote kutokana,
zaidi ya kuumbwa na miungu (ibid., p. 298). Wadruids walifundisha kuwa Wagauls
walikuwa wameibuka kutoka kwa Dispater, mungu wa chini ya dunia (ibid., pp.
298-299).
Esus alikuwa ni mungu wa bara anayechorwa
picha yake kwenye madhabahu huko Treves, akiwa kama mti uliokata chini shinani
ambao ni kichwa cha dume la ng’ombe na korongo watatu (mchoro unaoashiria mungu
mke Morrigan, malkia wa kijiamizi anayejumuishwa
kwenye utatu pamoja na Brigit na Anu, ibid., p. 286). Reinach anasema kuwa
muunganiko huu ndiyo dhana ile ile moja iliyokutikana kwenye madhabahu za huko Paris
(ibid. p. 296). D'Arbois (R. Cel.,
xix, p. 246) inayoonekana kwenye rejea hizi kwa Tain. Esus ni Cuchilainn anayeukata
na kuuangusha chini mti ili kuwaonyesha maadui zake. Ng’ombe huyu dume ni Dume la rangi ya Udhurungi la
Cualnge. Kwa hiyo, Esus anaushirika jumuisgi na dini za Kisirisiri na dini za
dume la ng’ombe linalochinjwa. Dume hili la ng’ombe pamoja na wapingaji walionekana
pia kwa Wahelvi, kama ni mzunguko wa kuzaliwa kiumbe tena na tena kwa kundi au jamii ya sid (nguruwe-watu) ambao kwamba
walikuwa na asili ya kimbinguni (ERE,
ibid., p. 296). Baadae, dume huyu wa ng’ombe aliunganishwa au kujumuishwa
pamoja na mungu Medros (ibid.). waselti waliviunganishwa vichwa na dhabihu ya
wanadamu, ambao nyama yao ilikuwa inaliwa, kwa vikundi vya watatu watatu wakiienzi
imani na dhana ya utatu (ibid., p. 300).
Rejea ya
Kwanza kuhusu Dhana ya Utatu Utatu Kwenye
imani ya Kikristo
Mfano wa kwanza wa rejea au kutajwa kwa
Uungu wa Kikristo kuwa ni wa mjumuiko wa viumbe watatu kulifanywa na Theophilus
wa Antioch (yapata kama mwaka 180 BK) aliyelitumia neno JD4"H au trias
ambaye neno la kilatini la trinitas linachukuliwa
kuwa ndilo limetafsiriwa kwalo. Neno hili alilitumia alipokuwa anaongelea kuhusu
trias ya Mungu, Neno lake na Hekima yake (kwa kujibu wa waraka wa Theophilus kwa Autolycus. Tafsiri ya ANF hapa inatafsiri neno hili trias kama utatu). Mfano unaofuatia wa matumizi ya neno hili ni ule wa
Tertullian (De Pud, c. xxi, P. G.,
II, 1026). Tertullian alikuwa ni wa kwanza kudai moja kwa moja umuhimu wa
ujumuisho wa “nafsi” tatu, ila hoja yake na sababu zake vilikwa na umuhumu wa
kujumuisha na kuweka usaidizi (soma kitabu cha Schaff, cha History of the Christian Church [Historia ya Kanisa la Kikristo],
Vol. II, p. 570). Usawa ulio wa karibu zaidi na fundisho lililopitishwa kwenye mkutano
wa baraza kuu la Nicene ha haikuwa imeonekana hapo kabla hadi ilivyopendekezwa
na Askofu wa Kirumi Dionysius (mwaka 262BK) ambaye alikuwa ni Myunani kwa
kuzaliwa. Alikusudia kuufutilia mbali mchakato wa kupunguza viumbe vitatu ili
kuitenganisha Miungu (Schaff, ibid.).
Madai ya kwamba Mungu ni kiumbe
anayejumuika na viumbe wengine wawili na kwamba ni nafsi au persona kama roho au nguvu unayotokea
kutoka kwa mmoja au kwa wote wawili ni madai ya baadae ya waamini Utatu ya
karne ya nne, tano, na ya sita. Madai haya yalifanywa ili kutambuli au
kuonyesha asili na chimbuko la trias
(hapo juu) aliyeachwa kama asiyeshabihiana. Kosmolojia zote mbili za kiutatu na
ya Utatu, kama zinavyojulikana sasa hazina madhiko yoyote yale ya kibiblia, ni
sawa tu na kama ilivyo imani ya Kibinitariani.
Dhana ya utatu inaeza kuelezewa kwa njia
mbili vifuatazo:
1. "Nafsihai Tatu ambao wako sawa wote na
wenye asili ya kimbinguni". Huu unachkuliwa kuwa ni mtazamo uliozoeleka na
kuaminika sana tangu kwenye mkutano mkuu wa Mabaraza ya Nicća na
Constantinople.
2. Mwana na Roho
wanatokana na Baba ambaye ndiye asili ya pekee na chimbuko la Uungu. Huu ni
mtazamo kingifu wa Mababa wapinzani wao wajulikanao kama Ante-Nicene na Kanisa
ka ujumla hadi kufikia mtaguso wa Nicća (mwaka 325 BK) (soma kitabu cha G.H.
Joyce, The Catholic Encyc.(C.E.) makala ya ‘Trinity’, Vol. XV, p.
51, ambapo panasema kuwa “Chini ya suala hili, Baba akia ni kama chimbuko la
hawa wote, anaweza kuitwa kuwa ni mkuu zaidi kuliko Mwana").
Fundiksho la Utatu linatokana na mfululizo
wa mkururu wa nadharia potofu na za uwongo zilizotungwa kinyume kabisa na
ushahidi wa kibiblia. Nadharia kuu mbili za uwongo zilizo wazi kutokana na
nukuu zilizofanywa ni hizi hapa chini:
kwamba
maneno yaliyotafsiriwa Mungu yanamhusu
mmoja , wawili au watatu au viumbe jumuishi, na
kwamba
Kristo ni Mungu mwenye haiba sawa ya umilele na usawa kama alivyo Mungu Baba
nan i Mungu.
Kutokana na uainisho kwenye Kitabu cha Mungu Aliyedhihirishwa, Kitabu cha Kwanza tunaona kwamba nadharia
na mawazo haya hayana msingi wowote wa kibiblia na kwa kweli yanapingana na
Maandiko Matakatifu. Dhana ya pili hapo juu inatokana na imani ya Kibinitariani
ya Kisirisiri na za Dini waabudu Jua.
Kutathimini
Dhana ya Ushirikishi wa Usawa na Umilele
Waandishi wengi wa Kipastriki walipimga
dhana hii ya usawa wa Mwana na Baba, na walipinga kwa hoja zenye nguvu na zenye
mashiko usawa huu shirikishi. Vifungu sawa tu kama hivyo kama ifuatavyo. Mfumo
wa imani ya Kibinitariani umechukuliwa au kutoholewa kutoka Roma kutoka kwenye
ibada za mungu Attis na siyo kutoka kwenye Ukristo.
Justin
Mwalimu wetu katika masuala haya ni Yesu Kristo, ambaye
pia alizaliwa kwa ajili hii, na kusulubiwa chini ya Pontio Pilato wa Uyahudi,
wakati wa Tiberio Kaisari; na kuwa tunamuabudu, tukifahamu kuwa ni mwana wa
Mungu wa kweli, na kumimshikia katika nafasi ya pili, na roho mtakatifu kuwa
katika nafasi ya tatu, tutahakikisha kwani wakaushtumu uwazimu wetu kuweko
hapa, eti kuwa tunaipeana nafasi ya pili kwa mtu aliyesulubiwa kutoka kwa Mungu
asiyebadilika na aishiye milele, muumbaji wetu sote, kwa kuwa hawafahamu
maajibu yaliyoko humo, ambamo kwamo, tunavyokueleteza wazi, tunaomba usadiki
(Apol I, xiii).
Na mamlaka ya kwanza baada ya Mungu Baba na Bwana wa wote ni Neno [8@(@H au logos],
ambaye pia ni Mwana. (Apol., I,
xxxii).
Kwa hiyo ni makosa kuelewa kwamba Roho na mamlaka ya Mungu, kuwa ni kama kitu
kinginecho mbali ya Neno [8@(@H au
logos], ambaye pia ni mzaliwa wa
kwanza wa Mungu. (Apol., I, xxxiii).
Kwahiyo, Justin anadhania Logos kuwa ni
kama taswira ya Mungu ambaye ni uwingi wa mjumuiko wa wengi ili kulipa mashiko
wazo hili la Roho kwa ujumla na hasahasa la Kristo. Hata hivyo anasema:
Wote, yeye (Mungu) na Mwana (ambaye alishuka kutoka kwake
na kutufunza mambo haya, na mwenyeji wa malaika wote wazuri ambaye waliumbwa
kama yeye, na wanafuata), na roho wa unabii, kuwafahamu ki sababu na ki kweli
na kakiri bila kibari kwa yeyote anuiaye kufunza kama nasi tulivyofunzwa.
Kwahiyo, malaika alichukuliwa pia kuwa
wana namna ya sura na mfano wa Mungu. Kutokana na Sura za 13, 16 na 61 za
kitabu chake, Justin hakutetea ibada za kuwaabudu Malaika (soma pia sura ya 3 kwenye
kamusi ya ANF, Vol. 1, p. 164). Neno kuabudu limetoholewa kutoka kwenye neno lililo
kwenye Ufunuo 3:9 lililotuama kwenye maana ya proskuneo, linaloitwa BD@F6L<ZFTF4< au
proskunesoosin (Marshall), linalomaanisha
atapiga magoti mbele ya wateule wa Kanisa
la Filadelfia. Kwa hiyo, neno hili halimanishi kuwaabudu malaika au Kristo bali
ni kuonyesha heshima na unyenyekevu kwa kusujudu kifudifudi kimwili; kwa maneno
mengine, ni kuonyesha heshima. Kwa hiyo, viumbe vilivyotajwa hapa vitapewa
heshima yao stahiki ikia ni kama sehemu ya Malaika wanyenyekevu na watiifu wa
Mungu. Malaika wanaotajwa kwenye kitabu hiki cha Ufunuo wa Yohana kua
walijizuia kufanya hivyo bali zaidi tu ni kwamba walimwabudu Mungu (Ufunuo
22:9). Hivyo basi, wateule humwabudu Mungu peke yake. Justin anaelezea juu ya
kutoa heshima stahiki tu na siyo kuwaabudu. Ahadi waliyopewa Kanisa la
Filadelfia ilitokana na sababu za kwamba Wayahudi ambao walidai kuwa ni
Wayahudi, bali walikuwa ni sinagogi la Shetani, walikuwa wameanzisha michakato
ya dini za Kisirisiri za Merkabah zinazoendesha imani yake kimafumbo au za
wapanda Magari ya Farasi wa Mungu, na za matulizo au uheri wa malaika kwa
madaraja saba, (soma kitabu cha Mysticism).
Kosa na upotovu huu ulienea hadi kwenye Kanisa la Wakolosai kwa sehemu. Ibada
ya Kanisa la Mungu inatakiwa imlenge Mungu na haipaswi imlenge hata Kristo, zaidi
ya kumpa tu heshima yake anayostahili kama kiongozi na bwana. Lakini la muhimu
sana ni kwamba Justin anaujumuisha mwili akijumuisha Malaika watiifu. Hii kwa
hiyo ni uwiano wa karibu kwenye mafundisho ya biblia ya Roho kuwa anaweza
anapopewa nafasi kama mtendaji kuwakumbatia wateule wanaokwenda kufanyika kuwa theoi, kama Kristo alivyo mmoja wa theoi mdogo na msaidizi kwa theos wake ambaye ni Mungu Baba.
Kimsingi sana, yeye hata hivyo ni wa pili kwenye daraja la juu sana la theos, akiwa ni kama kuhani mkuu.
Yaonekana sana kabisa kwamba Justin
ndiye aliyekuwa wa kuanzisha ibada ya jumapili (Taz bacc anatinoman views”
kuhusiana na sabato kuwa adhabu kali; matazamo wake haukuungwa mkono na
wakristo katika kipindi hicho na Nacchiocchi ana shikilia kuwa wakristo hawa
jawahi kubadili uongo kama hao, (P. 225) kukiri kuwa Mungu anaiazisha tohara na
sabato katika msingi wa uovu wa Wayahudi tu kama alama ya utambulisho dhidi ya
mataifa na sisi wakristo ili wao tu ndio waweze kutoabika (Dial 16:1; 21:1
tazama pia Bacchiocchi Ibid). kwamtia Mungu kosa la utovu wa nidahamu kwa
binadamu na kinyume cha sheria za toba za uongofu. Licha ya kosa hili, mtazamo
wake kwa uongozi wa Mungu bado ya walakini wa ubadala. Hata hivyo anabuni mvuto wa hisia ambao unaenda
sambamba na hii “Antinomianist approach”. Kama tulivyoona, Justin, hata hivyo,
alizipiga mafundisho ya Roho kuendelea kuishi baada ya kufa nay ale ya kwenda
mbinguni kuwa siyo ya Kikristo, falsafa ambazo zinachipua kutoka katika dini
potofu za kisirisiri (Dial. LXXX).
Irenćus alikuwa ni mwanafunzi kutoka Smirna
aliyefundishwa na Polycarp, mwanafunzi wa Yohana, na kwa ukaribu sana tunapata
teolojia asilia yenyewe.
Irenćus amamwambia Mungu
Kwa kuwa aliamrisha, na wakaumbwa, alizungumza na
wakatengenezwa. Alimwamrisha nani? Neno bila shaka na nani, anasema mbingu
ziliumbwa na nguvu za pumzi ya kunywa chake (Zab 33:6). (Adu haer, iii, viii,
3).
Irenćus alishikilia kuwa:
imehakikishwa vyema kuwa si manabdii bali ni tume wapeana
jina kuwa Mungu mwenine au kumwita Bwana, bali Mungu wa kweli na wa pekee…..
ila vitu vilivyobaniwa ni tofauti naye aliyevibini, na vilivyo yeye mwenyewe
hakuumbwa, hana mwanzo wala mwisho; na anachukilia kitu. Yeye ni safi kwake
mwenyewe, na zaidi anawapa uwepo wengine wote, ila vitu vilivyoptengenezwa naye
(Ibid).
Irenaeus alikizidisha kiwango cha kuwa Mungu (theos an Elohim) hadi kwenye
“Logos|” kitu baki kutoka katika vitu vingine vilivyofanywa (ibid). alikuwa
tayari ameshafanya nafasi ya Mungu nay a mwana na wana wote wa Mungu kutoka
kwenye Kitabu III, Sura ya vi.
Kwa hivyo si Bwana wala roho mtakatifu wala mitume
wamewahi kumpa jina Mungu, bila shaka, yeye ambaye hakuwa Mungu, labda ikiwa
alikuwa Bwana wake wa kimwili, ila Mungu Baba atawalaye kute vote, na mwanawe
aliyepeanwa naye Mungu juu ya viumbe vyote, kama isemavyo taarifa ijuatayoi.
Neno la Bwana kwa Bwana wangu, ukae mkono wangu kuume hata niwafanyapo adui
zako kuwa chini ya miguu yako (Zab 110:1). Hapa, maandiko yanawalakisha
maongoze ya Baba kwa mwana, aliyepewa urithi ya ulimwengu, na adui zake wote
kulengeshwa kwake.
Irenaeus akaendelea kusema kusema roho mtakatifu aliwataja aliyezungumza na
Abrahamu kabla ya kutekofwa kwa Sodoma na alipokea nguvu (Kutoka kwa Mungu)
kuwahukumu wa Sodoma kwa uovu wao. Tazama kufungu kifuatacho.
inasema ukweli huo huo; “kiti chako cha enzi, Mungu ni
cha milele na milele fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya achili, umependa haki,
umeichuka dhaluma, kwa hiyo Mungu, Mungu wako amekupaka mafuta (Zab 45:6), kwa
kuwa roho anaambalisha wote kwa jina Mungu (Theus an Elohim) wote, aliyepakwa
mafuta na yule aliyeyapaka mafuta, ambaye ni Baba na tena, Mungu anasimama
katika kusanyiko la katikati ya Mungu, anahukumu (Zab 45:6), yeye hapa
yamaanisha Mungu, mwana na wale waliopewa uwezo kuwa wana; lakini hili ndilo
kanisa ambalo ndiyo sinagogi ya Mungu ambalo Mungu mwana mwenyewe amekusanya,
na anawaambia Mungu, Mungu Bwana amenena, ametiita nchi toka maawio ya jua hadi
machweo yake……. (Zab 50:1) katika kifungu hiki, Mungu ni nani? Anawaambia Mungu
mwana alisema, watu wasionitaka wanamliza habari zangu (Isa 65:1) lakini
aaongea juu ya Miungu wapi? Ni Miungu wa wale awasemeao ‘mimi ninasema ndiyi
Miungu na wana wa aliye juu’ (Zab 82:6). Kwa hao, Bila shaka , wale ambayo
wamepokea amani wa “ Kupokewa, ambayo tuko Abba Baba” (Warumi 8:15) ( Agaisnst
Heresies, Bk.iii, ch.vi, ANF, Vol. I,pp. 418-419).’’
Hapana shaka kuwa irenasus ilikuwa na mtazamo wa ushirikiano wa utawala wa
Mungu na akaendelea neno ‘Mungu’ kujumuisha mwana na wale waliopewa uwezo kuwa
wana. Kujumuisha mwana na wale waliopewa uwezo kuwa wana. Anaonekana kuashiria
kuwa wana. Ananena kuwa kuashiria kuwa Ksristo akawakusanya wateule, bali sisi
twajua kuwa ni Mungu ndiye amepanye Kristo wa teule (Yn 17:11-12, Waibi 2:13;
9:15) matumizi ya neno hili kwa wateule wa kimwili huenda yasisiwe sawa
tukiuzingatia mtazamo wa irenaeuos hapa. Wenyeji wazalendo pia wamehusishwa
katika baraza tukitumia uelewavu wa ufunuo 4 na 5- hivyo wenyeji wazalendo ndio
“Ecclesia” wa Mungu. Hapana shaka kuwa maneno “Elohim” au “Theoi” yalimaanishwa
kuenea hadi kanisani na kuwa ulikuwa ni uelewevu ya kanisa la karne ya kwanza
kutoka kwa Yohana na Polycarp, walionifunza irenaeous, na kuingia katika karne
ya pili na karne zilifuata.
Kihistoria hili limekuwa likifahamika kama baraza la Elohim ambao ni wana
wa Mungu.
Ni dhahiri sana kwamba Ireneaus
aliamini kwamba ni Mungu Baba peke yake ndiye Mungu wa kweli wa kwenye Biblia
na ndiye Muumbaji wa vitu vyote.
Kwenye Kitabu cha V sura ya 25
tunasoma kwenye sura ya 2:
2. Zaidi ya
yote, yeye (Mtume) ameonyesha pia jambo hili nililolionyesha kwa namna nyingi,
kuwa Hekalu la Yerusalemu lilijengwa kwa maelekezo ya Mungu wa kweli. Kwa kuwa
mtume mwenyewe, ananena kwa nafsi yake mwenyewe, kwa namna tofauti sana aliitwa
kwenye hekalu la Mungu. Sasa nimeonyesha kwenye kitabu cha tatu, kuwa hakuna
mwingine aliyeitwa na mitume Mungu walipokuwa wakijiita mwenyewe, isipokuwa kwake yeye ambaye ndiye
Mungu wa kweli, Baba na Bwana, ambaye kwaye, maelekezo ya ujenzi wa hekalu la
Yerusalemu yalitumika kwenye kulijenga kwa malengo hayo ambavyo nimekwisha
yaelezea tayari; ambavyo kwamba adui wa (hekalu) ataketi, akijaribu kujionyesha
yeye mwenyewe kuwa ni Kristo, kama Bwana alivyomtaja pia kwamba: Basi hapo
mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli,
limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu), ndipo walio katika Uyahudi
na wakimbilie milimani; naye aliye juu ya dari asishuke kuvichukua vitu
vilivyomo nyumbani mwake; wala aliye shambani asirudi nyuma kuichukua nguo
yake. Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo! Ombeni, ili kukimbia kwenu
kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato. Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo
dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa,
wala haitakuwapo kamwe.
Bila shaka kwamba kanisa la
kwanza lilikuwa ni saidizi au dogo na kwamba wale aliofundishwa huko Smirna na
mitume na wale waliokuwa kama mitume kama vile Polycarp walikuwa ni wa mrengo
wa Uyunitariani wa Kibiblia na waliamini kwamna ni Baba tu pekeyake ndiye
alikuwa Mungu wa Pekee wa Kweli, na kwamba wengine wote, akiwemo Kristo,
waliruzukiwa tu uzima wa milele na Baba.
Irenćus alinena
kinyume kupanuka kukubwa kupya kwa Ubinitariani unaotokana na dini za waabudu
Jua za huko Roma na kile kinachojulikana kama mafundisho ya Kibinitariani kama
uzushi na imani yao kulikoendelea mbele kwenye mwenelezo kamilifu wa
Utrinitariani wa Mungu wa Utatu. Haya ni mafundisho ya Mpingakristo na mfumo
wake sahihi na halisia unaoonekana kutoka kwa Irenćus. Fundisho hili lilijipengeza kwenye makanisa
ya Mungu mwishoni mwa karne ya ishirini yakitokea Marekani.
Irenaeus, Sura ya 16:8 (ANF,
Vol. 1, fn. p. 443) inasema:
Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo
kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu. Na kila roho
isiyomkiri Yesu haitokani na Mungu. Na hii ndiyo roho ya mpinga Kristo.
Socrates
mwanahistoria anasema (VII, 32, p. 381) kwamba kifungu hiki kimekanganywa na
wale waliopenda kutenganisha ubinadamu wa Yesu Kristo kutoka kwenye haiba yake ya
kimbinguni.
Clement wa Alexandria anasema:-
Kwa kuwa mwana ndiye nguvu ya Mungu, na kuwa ndiye neno
la kale zaidi la Baba, kabla ya kufanywa chochote na Bwana yake. Hivyo anaitwa
mwalimu wa waumbile yake. Sasa nguvu za Bwana lina marejeleo katika mwezi, na
mwana ni nguvu za Baba (“Strom.”, VII,ii,P.G., IX, 410).
Hata hivyo Clement alielewa kuwa hatima ya wateule ni kuwa miungu.
Alipoongea kuhusu ‘gnosis’ alishikilia kuwa ingepatikana na mwanadamu katika kanisa
kwake kwenye nchi au dunianii:
Hafika upeo baada ya mauti ya kimwili, nafasi ya
(gnoostikis) ilihusiwapo kuenda mahali pake rasmi, ambapo, baada ya kuwa Mungu,
itafarijika, katika mapumziko yasio na mwisho. (S.R.C Lilla
Clement of Alexander, a study in Christian platonisan and grosticison, Oxford
1971, P 142).
Hivyo tunaona hapa mchanganyiko wa ‘gnosis’ ya kigiriki na tamaduni za kale kuwa tutakuwa ‘theoi’ Elhim. Hapakuwa maoni kuwa Kristo wala theoi wengine kuwa sawasawa na tutakatifu wa jua zaidi.
Hippolytus asema
Kwa kuwa sasa Neotus anahakikisha kwamba mwana
na Baba walikuwa sawa, hakuna asiyejua. Ila amamtoa maelezo ‘wakati Baba hakuwa
amezaliwa, alikuwa ameshahakikiwa kwa haki kuwa Baba; na kuendeleza vizuri
kulipoupendeza, kwa alikuwa wa pekee yeye mwenyewe akawa mwanawe, kulingana na
kipindi cha ‘visiccitude’ (Hippolytus anarudia wazo hili katika utupisho wa
kitabu chake X) (Con. Neot, n, 14, “The refutation of all Heresies Bk ix. Ch,
v, ANT, Vol, v, pp 127-128);
Wakwanza na wa pekee (Mungu mmoja), muumba na
Bwana wa wote hakuwa na chochote “coeval” ndani yake……… ila alikuwa mmoja na
pekee yake. Kwa zoezi la mapenzi yake, aliviumba vitu ambavyo havikuwepo
mwanzoni yapokuwa alimwa viwepo kwani anafahamu yake fika na chochote ambacho
kinakaribia kutendeka, ufahamu wa kimbele pia anao (Hippolytus, ibid, x,
xxviii, p 150).
Kwa hivyo huyu Mungu mwenzake yote, kwa uakizi
mwanzo alileta ‘logos’ si neno kwa kufanywa na sauti bali kama uswazisho wa
ulimwengu, uliofanywa na kupewa makao akilini. Yeye mwenye alichumbuka kutoka
katika vitu vilivyo; kwa kuwa Baba mwenye alikuwa ndiye uwepo, na kuzaliwa
ndiko kulisababisha vingine kuwapo. Logos ilikuwa ndani ya Baba mwenyewe,
kushikilia mapenzi ya mwelekezi wake na si kuwa na ufahamu duni wa akili ya
Baba.
Sambamba na uwezo wake kutoka kwa mwelekezi
wale, na kuwa yeye ndiye mwanambee wa mwelakazi hiyo. Na hivyo ndivyo
ilivyokuwa, kuwa Baba aliponuru kuwekko ulimwengu, logos, mmoja baada ya
mwingien wakaukamilisha uumbaji hivyo kumfarahosha Mungu.
(Hyppolytus idid, x, xxix).
Ni kupitia kwa mwandishi huyu ambayo tunaingiwa
na kwa kuwa Kristo ndiye mali ya Baba na kuwa maumbile mengine ya mbinguni ni
humbaji wa mwana na hivyo hawana ushirika katika mazingira kama mwana. Kutokana
na kosa hili, tunaduni ya utatu ulianza kujengeka. Elohim ni wenyeji wengi
ambamo kwao wana kondoo ndiye kuhani mkuu, ila yeye ni mmoja wao na kwao ni
mwenzi au rafiki, ingawa mpangilia wa uyeo ulikengwa nay eye, ndani yake na
kwake yeye (Wakolosai 1:15). Watakatifu pia walikuwa wenzi wa Kristo kutoka
Waibi 3:14 na hivyo ndoyo wa mwenyeji (Ufunuo 12:10) na warithi kama Kristo (Warumi
8:17) mbingu na vyote vilikuwema, na vilivyotajwa kuwa viliumbwa na mwana na 1
Wakorintho 8:6 ikirejelea ulimwengu na wanadamu. Wakolosai 1:15-17 inatengesha
uumbaji wa vitu vyote, vinavyoonekana na visivyooneknana. Uumbaji wa vitu vya
ufalme, ubwana, uongozi, watawala kupitia kwake, kwa ajili yake, haiwezi
kulirejelea baraza la Elohim uumbaji wa Kristo wa ubwana hauhusiani na haya.
Kama ulivyokuwa hivyo, ingehushisha uumbaji wa
Mungu hivyo tunambaka na nguvu na si nafsi. Viti vya ufalme na mana ya mbingu na serikali
yake.
Waefeso 1:22 na 3:9 inaonyesha kuwa ni Mungu aliyeumba vitu vyote na
kuliweka minguu pa kristo na akafanya kwa kiongozi wa vitu vyote, kwa ajili ya
kanisa. Haya yalijengwa ili utawala wa mbinguni waufahamu uwezo na nguvu za
Mungu. Vitu hivi vilifanywa ili kuonyesha kuwa Mungu ni Kristo aliyeinuliwa
(Wafil 2:10). Ambaye hangeweza kuwa chapo awali. Mungu alimwita Kristo kama
mali ghafi ya uumbaji (Waeb 113) Kristo akauumba ulimwengu (Waeb 1:2) na
naakisi nuru ya Bwana na anao muhuri wa muumbile yake (Waeb 1:3) Waebrania 2:10
iarejelea vitu vyote ukiwemo ulimwengu.
Waebrania 2:11 inasema kwamba Maana yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia
watoka kwa mmoja. (©<ÎH BV<J,H or enos
pantes). Waebrania 11:3 inaaminika
kuwa inasema kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu (ŐZ:"J4 2,@Ř au pneumati theou) (soma kitabu cha Marshall). Hii Logos haionekani kama
inakuwa ikihusishwa na hasahasa neno lililotafsiriwa kama iliumbwa inaonyeshwa hivyo na Marshall likimaaisha kuwa limerekebishwa (6"J0DJ\F2"4 au katertisthia)
na neno halikurekebishwa bali zaidi ni
suala tu la zama mbalimbali ("Ćä<"H au aionas). Kwa hiyo, hizi zama
ndio zilizorekebishwa kwa neno la Mungu ili kwamba kile kinachoonekana kuwa
kilifanywa kutoka kwa vitu visivyoonekana. Hivyo ndiyo dhana ya uumbaji kwa kurekebisha anga/wakati
au majira yaliyo sawa. Warumi 11:36 inamtaja Mungu kuwa ni kama chimbuko na
mlengwa wa mambo yote, na siyo Kristo.
Elohim wengine
wanaotajwa kwenye Biblia wana usaidi lakini wana mamlaka shirikishi na Kristo.
Wanamamlaka kwenye muundo mtakatifu wa kimbinguni. Ushirika huu wa elohim
(chini ya mamlaka ya Yesu Kristo) umefanywa kwa mujibu sawia na mapenzi ya
Mungu. Mmoja wao ni kerubi mwenye mbawa zinazofunika anayeitwa Shetani, na wale
walio wadogo wasaidizi wake, ambao wameumbwa kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu,
kimahusiano (soma harida la Uumbaji: Kutoka kwenye Teolojia ya Kianthropomofiki Hadi Anthropolojia ua
Kitheomofiki (Na. B5)). Ni upuuzi mkubwa sana kufikiria kwamba Kristo aliumbwa na hali isiyo na
dhambi wala kosa lolote, na lakini washirika wake wengine ambao ni Malaika
wakapewa uhuru wa kuchagua kwamba wachague kutii au kutenda dhambi. Mafanikio
ya Kristo yalitokana na utii wake na siyo kwaajili ya hali yake ya kukamilika
na kutotenda dhambi. Mafanikio yake yalijulikana kutokanao na uweza wa Mungu wa
kujua kila jambo hata ya mambo yaliyokusudiwa tangu mwanzoni. Amepewa mamlaka
halisi kutokana na utii wake na imani. Utawala au mamlaka dhidi ya viumbe wote
waliopo na ambazo ni uweza wa Kristo na Malaika kwenye uumbaji yapasa uenee kwa
wanadamu baada ya ufufuo wa pili wa wafu kutokana na Kumbukumbu la Torati 4:19.
Kamusi ya the New Catholic Encyclopedia (N.C.E.) article ‘Trinity, Holy’, Vol. XIV, McGraw Hill, N.Y., 1967, p. 296, inafanya jambo kubwa linalodaiwa lisilo la kawaida kuhusu fundisho la Hippolytus.
Hippolytus kwenye ukanushaji wake Noetus (10) na utambulisho uliotiliwa chumvi wa Kristo pamoja na Baba, anasisitiza kuwa Mungu alijiongeza tangu mwanzoni.
Ni uwongo tu kutokana na ulinganisho na andiko halisi la Hippolytus (C. Noetus 10) hapo juu. Mamlaka hayohayo yanaelezea kwamba:
Tertullian, anakuwa na msimamo huohuo (Adv. Prax. 5), wate isipokuwa ufanywaji kiunafsi uwingi huu wa milele. Neno linasimama au kubakia kuwa limesimama na zaidi kuliko katika Uungu kwa maana iliyoshauriwa mwonekano wa kibinadamu, kama mjadala wa ndani ulivyo kwa namna hiyohiyo nyingine, pa pili kwenye ongezeko kwa kila mtu peke yake, ingaaje bado ni ndani ya kila mmoja peke yake.
Aina au mtindo huu unahusu mashiko hayohayo ya Unoetianism na Usabellianism na inatofautiana sana.
Tertullian anaelezea kwenye kitabu chake cha Against (Adv.) Praxeas kwamba:
Huyu mmoja ni Mungu pekee aliye pia Mwana, Neno lake, aliyetokana na yeye mwenyewe, ambaye kaye ni vitu vyote vimeumbwa...Wote ni wa mmoja, kwa umoja (ambaye ni) mdogo au msaidizi; wakati siri ya utawanyiko ingali bado inalindwa, ambayo unatoa au unaanzisha au kusababisha Utatu ndani ya Utatu, akiweka kwenye utaratibu wao wa Nafsi tatu-Baba, Mwana na [Roho] Mtakatifu: watatu hata hivyo, hawamo kwenye masharti bali kwa kiwango; siyo kwa udogo bali kwa utaratibu au kanuni; siyo kwa uweza au kwa nguvu bali ni kwa utendaji; lakini bado wakia ni kitu kimoja, na wenye sharti moja, na wenye nguvu moja ni kama alivyo Mungu ni Mmoja, ambaye kwa yeye viwango hivi na aina hizi na mambo yake yamebubalika, chini ya jina la Baba, na la Mwana na la [Roho] Mtakatifu... (II);
Pia Tertullian anasema kwamba Baba alimfufua Mwana kutoka mautini (II). Kwahiyo Tertullian anaiweka tofauti ya muhimu sana kwenye mfungamano wa kimahusiano wa vitu vitatu ambao ndiyo walengwa harakazi na kazi za Mungu kwa kiwango. Mwana na Roho ni mwendelezo kutoka kwa Baba na ni viumbe wadogo au wasaidizi wa udhihirisho wake. Tertullian aliipa imani ya Utatu pgangilio wa kinumerali na migawanyo (III). Na pia alishikilia uamini kwamba Umonaki wa Mungu ulikuja kutoka kwa Baba (III). Lakini hii ilikuwa ni sawa tu na huyu Mwana kuchukuliwa kuwa ni wa namna zote mbili (III) akiwa ametolewa kwa Mwana na Baba (IV).
Tertullian aliamini kuwa Roho Mtakatifu alishuka kutoka kwa Baba kwa kupitia kwa Mwana. Tertullian aliamini (IV) kuwa Baba na Mwana ni wawili, yaani ni viumbe waliotofauti kila mmjoja wao. Kwa hiyo, ilipasa idaiwe na kuaminika kuwa imani ya kweli ya Kiditheism (inayoitwa pia Ubinitariani) ilianzishwa na Tertullian (soma Zaburi 45:6-7).
Yeye ambaye wanamtii (viumbe wote) nay eye ambaye walikuwa wamemtii – ni lazima wawe ni Viumbe wawili walio tofauti.
Hata hivyo, Tertullian anasema kuwa Sura ya
V kwamba kabla ya kuwepo vitu vyote Mungu alikuwepo.
Kwa kuwa kabla ya
kuwepo kwa vitu vyote Mungu alikuwa peke yake – akiwa ndani yake mwenyewe na
kwa ajili yake yeye mwenyewe ulimwenguni, na kwenye anga na kwa vitu vyote.
Zaidi ya yote ni kwamba, alikuwa peke yake kwa kuwa hakukuwa na kitu chochote nje
yake bali ni yeye tu peke yake.
Ukweli wa kwamba sababu aliyopewa ilimfanya kwa kweli asiwe peke yake na Tertullian anasema
kuwa mrengo huu wa kufikiri unaoitwa
kwa Kiyunani logos ulikuwa ni muono
wa tangu mwanzo ambao ulikuwa ni sahihi zaidi kifikra kuliko neno kama
alipokuwa anafikiria lakini hakusema. Hivyo, Tertullian anaweka tofauti kwamba
Kristo ni fikra ya Mungu na kwamba sababu hii ni lazima iwe imehusiana na
chimbuko la kimungu tangu mwanzo. Hoja au mjadala uko wazi kwa vipingamizi
mbalimbali. Kosa la kwanza ni kwamba Kristo alikuwa ndiye mlengwa pekee na Neno
na Hekima na sio tu ni udhihirisho wa hao wote. Lakini alikuwa Logos kama sehemu
ya Logon (ikifuatia tofauti halisia/iliyopendekezwa kama tulivyojionea kutoka
kwenye kitabu cha Kwanza cha Mungu Amedhihirika, yaani God Revealed, Book One). Logos iliyojitokeza
kwa mwanadamu alikuwa Kristo. Kama Kristo alikuwa pamoja na Mungu kipindi cha
kabla ya mwanzo wa uumbaji, kama asemavyo Tertullian kwamba Mungu alikuwa na sababu
hata kabla ya mwanzo wa uumbaji, ndipo
Kristo ni mlengwa wa Mungu ambavyo inawezekana kwenye mgawanyo bali haiwezekani
kwenye utenganifu kwa kitu kimoja. Ni upuuzi kudhania kuwa Kristo mbali na
Mungu anaweza kuwa Mungu pasipo kufikiri au hekima na hivyo hawezi kuwa Mungu.
Kristo alikuwa mwanzo wa uumbaji wa Mungu (Ufunuo
3:14). Kwa hiyo tumekuwa tumeelewa au kujulishwa mwanzo kama ulivyoeleweka na
wanateolojia wa zamani kama mwanzo wa uumbaji ulioanzisha majira na nyakati zake.
Tertullian anashikilia kuamini kwamba ni Mungu tu ndiye aliyeishi au kuwepo
kipindi cha kabla ya uumbaji na akiwepo kiumilele (V), akiwa wa tofauti na
mkubwa zaidi kumliko Mwana (IX) aliye ni wa namna zote mbili, yaani, Neno na Hekima (VI). Mungu hakufanyika kuwa Baba hadi kipindi cha baada ya Uumbaji wa Neno (VII) hasahasa kenye
uumbaji wenyewe (Adv. Hermog. 3). Kwa hiyo Mungu Baba ndiye aliyesimama
nje ya wakati na viumbe wote wengine haakuwa hivyo. Ni yeye tu peke yake ndiye
Mungu Mkuu wa wa Pekee. Kitabu au jarida la N.C.E. linasema kuwa
Mnamo karne ya 3, kama mtu anavyoweza kuona ikionyeshwa kwenye kitabu cha
kutisha cha Novatian cha De Trintate,
Kanisa la Kirumi, hapo mwanzoni sana lilipunguza mguvu kuhusu jakamoyo yale
kwenye uwingine na uwingi, lilikuja kujishirikisha na busara au muono mkuu wa
Tertullian. Hata hivyo, Novatian, anasisitiza (kwenye sura ya 31) kwa uwazi
sana kuhusu umilele usio sawasawa wa baba na mwana kwenye Uungu. (op. cit., p.
297)
Ni kama inavyoonekana hapo juu, mafundisho
ya baadae, yakiwa yanashirikisha na baadhi ya mitazamo au hisia za Tertullian,
yakafanyika kuwa kwenye msingi wa nadharia ya Novatian kuhusu umilele ulio sawa
akipinga maelekezo ya maneno ya Tertullian. Kwahiyo, dhana ya fundisho la dogma
ilikuwa ni nadharia tu ya kuitunga na kuitengeneza kiubandia iliyoanzishwa kwenye
Kanisa la karne ya tatu. Hayakuwa na msingi wake kwenye mafundisho ya biblia
bali ni kutoka kwenye mwendelezo ulioingia taratibu wa makosa ya kiteolojia.
Ufafanuzi uliopo hapo juu unaashiria kwamba mamlaka yametamkwa kimakosa, yakirudia
kiukamilifu kabisa maana ya maandiko, ambayo yanaashiria kwa kiasi kikubwa sana
kuwa yamechaguliwa kusomwa.
Mrengo wa mashariki umetuama kwenye nadharia
ya Alexandria na maandiko yaliyo karibu na wakati wa Hippolytus na Tertullian alikuwa
na aliyashirikisha mafundisho yamhusuyo Clement (hapo juu), ya Mwana kama uzao
wa Baba. Lakini Clement alikuwa msaidizi, kama walivyokuwa wanateolojia wote wa
mwanzoni. Mrithi wa nafasi ya Clement alikuwa Origen.
Origen anaunga mkono
kwa wazi sana akisema hivi:
Tunatangaza kwamba
Mwana si mkuu kuliko Baba, bali ni mdogo kwake. Na imani hii tunaijenga kwenye
maneno aliyoayasema Yesu mwenyewe: 'Baba aliyenituma mimi ni Mkuu kuliko mimi.'
(Con. Cels.,VIII, xv)
Tunajua, kwa hiyo
kwamba yeye ni Mwana wa Mungu, na kwamba Mungu ni Baba yake. Na kwamba hakuna
aliye na ubora wa kumzidi au wa kutokufanyika taswira ya Mungu kwenye mafundisho
ya kwamba angeweza kuwa ni mzaliwa kama ni Mwana wa pekee, na hakuna
atakayetushawishi sisi kwamba huyo mmoja siyo Mwana wa pekee wa Mungu na Baba.
Na iwapo kama Celsus amesikia kitu fulani cha watu fulani wakishikilia kuamini
kwamba Mwana wa Mungu siyo Mwana wa Muumbaji wa ulimwengu, hili ni suala au jambo
linalotuama kati yake nan a wasaidizi wa dhana au nadharia kama hiyo. (Con. Cels., VIII, xiv)
Origen akiwa ni
mrithi au aliyemfuatia Clement kwenye Shule ya Alexandrian anasema hivi:
Aliufanya ulimwengu
uone sawa na maono ya aaminye mistari ya Kineoplatoni ya daraja la kicheo la kiubashiri.
Kwenye kilele timilifu cha upeo wa juu, kuna Mungu Baba (De Princ. 1.1.6), ni pekee mwenye chanzo au mwanzo usio na chimbuko
lake, au kwa kutumia maneno aliyoyapenda sana kuyatumia Origen (kwa mfano
kwenye kitabu chake cha Ioan.
2.10.75), hajiongezi (•(X<<0J@H au agennetos). Lakini (De Princ. 1.2.3) Baba anatokana na umilele wote aliomuumba Mwana,
na (Kwenye Ioan. 2.10. 75) kutokana
na huyu Mwana kunatoka Neno, ndiye alimleta au kumtuma Roho Mtakatifu. tatu ni
kwamba, Origen anaendeleza kivungu hikihiki, kuwa ni watatu walio tofauti kile mmoja
wapo [yaani nafsi zao] au *hypostases [sawa na ilivyo Kwenye Ioh. 2,10,75]. kwa upande mwingine (Frag. in Hebr.), kwa rejea rahisi hapa kuhusu Baba na Mwana,
wanashirikiana kwa pamoja ‘jamii ya msikamano’ kwa Mwana, anaongeza kipindi
hiki baadae kua ni ‘cha kiini hikihiki’ [*homoousios Ď:@@bF4@H] na Bab. (N.C.E., p.297).
J. N. D. Kelly (kwenye kitabu chake cha Early Christian Doctrines [Mafundisho ya
Mwanzoni ya Kikristo]) anasema kuhusu mtazamo au nadharia ya Origen kuhusu Hypostases kwamba:
Uthibitisho huu wa
kwamba hawa Watatu ni nafsi au hypostasis tofauti kwenye umilele wowote, siyo
tu kuwa (kama walivyoamini kina Tertullian na Hippolytus) kuwa walionekana au
kudhihirika kwenye ‘ubanifu’, kuwa ni kama moja ya tabia kuu am mwelekeo wa
mafundisho yake, na anatuama moja kwa moja kwenye dhana ya kizazi cha milele. Hupostasis na ousia mwanzoni kabisa walikuwa wako sawa, Wastoiki wa mwanzoni na
hatimaye akawa Waplatoniki, ikimaanisha kuwapo kiuhalisia au chimbuko na kiini
chake, jambo ambalo ndilo kitu chenyewe; lakini wakati hupostasis inaporudi kwenye mtiririko huu wa kikanuni kwenye ule wa
Origen [yaani Kwenye Ioh 20,22,182f.;
32,16,192f.], ndipo mara nyingi sana anaipa mashiko ya kusaidiana kila mmoja na
mwenziwe, na uwepo wa kila mmoja. Makosa au upotoe wa nadharia ya Kimamboleo,
anapinga [ibid.. 10,37,246: cf. ib. 2.2.16;
In Matt. 17,14.], inatuama kwenye hali ya kuwachukulia Watatu hawa kama ni
idadi isiyobadilika (:¬ *4"NXD,4<
Jč •D42:č au mimi diapherin kuwa ariethmo), aliwa
wanatofautiana kwenye mawazo na fikra tu, peke yake, mmoja akiwa hayupo lakini
akiwa kwenye uwepo tu '...(p. 129)
Kutokana na kitabu cha De Orat. 15,1; C. Cels. 8,12, Origen anashikilia kuamini mafundisho ya kweli kuwa
ni kwamba Mwana "si hana zaidi ya kuwa msaidizi tu kuliko kuwa Baba".
Baba na Mwana ni “wawili tofauti kimtazamo wa Kinafsi, bali ni amoja kwenye ushirikiano,
utendaji wa pamoja na kwenye kuonyesha mapenzi na nia " (soma pia kitabu
cha Kelly, ibid.). Kelly anasema hivi:
Hivyo basi, kwa kuwa
kuna tofauti ya kweli, basi Watatu hawa wanatokana na mtazamo mwingine wa mtu; ni
kama anavyoelezea [Dial. Heracl. 2],
'hatuogopi kuelezea kwa maana moja ya miungu miwili, na kwa upande mwingine ni
kwa mrengo wa Mungu mmoja' (ibid.).
Kwa hiyo Origen aliamini kuwa Baba kuwa ni
kipaumbele kwenye teolojia kwa Mwana na kwamba Mwana alitokana na Baba.
Aliamini kuwa umoja ulikuwa ni wa lazima zaidi kuliko ilivyodhiwa na mshikamano
wa Kimamboleo. Origen anahusianisha ufungaji wa ndoa wa mwanaume na mkewe
wakawa mwili mmoja kuwa ni mfano wa jambo hili na pia ni sawa na uhusiano wa
mwanadamu na wa mteule na Kristo na kuwa kwenye roho mmoja. Hivyo basi, kwa
kiwango cha juu sana tena, Baba na Mwana ingawa wako tofauti bali ni Mungu
mmoja. Kelly anaamini kuwa ingawa Origen anaonekana kuongelea kuhusu Kristo
kuwa ni kama kiumbe tu, hili ni kama wazo au dhana iliyopo kwenye kifungu cha
Mithali 8:22 na Wakolosai 1:15 na kwamba haipasi kupuuziwa. Anashiriki kwenye
asili ya kimungu kwa kuwa muunganiko na asili ya Baba (In Ioh. 2,2,16; 2,10,76; 19,2,6). Kelly anasema kwamba:
Yampasa mtu awe
makini, hata hivyo, haipasi kunasibisha
na Origen kwa fundisho lolote la kuwa mmoja na Baba na Mwana.
Mlinganisho wa Origen wa Baba na Mwana ni
moja ya upendo, utashi na tendo (Kelly, anayachukulia maandiko yanayoendelea
kudumu na tafsiri iliyoonyumbuishwa ya Kilatini, ibid., p. 130). Origen anasema
kuhusu Roho Mtakatifu (Frag. in Hebr. PG 14, 1308):
Anawapa wale ambao, kwa
ajili yake na ushiriki wao wake, wameitwa kuwa wametakaswa na jambo, kama
ningelielezea, neema yao. Jambo hili hili la neema limehitajika na kuwekewa
umuhimu mkubwa na Mungu, limetumikiwa na Kristo, na kufikiwa na kila mmoja
aliyelifikilia (ßN,FJfF0H au huphestoses) kam Roho
Mtakatifu.(soma pia kwenye kitabu hichohicho cha Kelly ibid.).
Kelly (kurasa za 130-131) anaamini
kutokana na kitabu hiki kwamba uwanja wote mzima wa kuwa Roho Mtakatifu ni Baba
lakini hii imechukuliwa kwa kina kuwa ni Roho na Mwana, ambaye kutokana na yeye
Roho anachukua tabia zote (sawa na ilivyo kwenye ibid., 2,10,76).
Watatu hawa ni wa milele na wana tofautiana
sana lakini hawapo kuwa ni viumbe walio na mwambatano wa Kiiutatu au Triad. Makosa
yapo kwenye hitimisho la kwamba Mwana ana ushabihiano na Roho kwenye tabia zake
zote zaidi ya kuwa tu ni mwongozaji wa wateule. Dhana ya umilele ulio sawa
kimsingi imebuniwa tu. Kushindwa kuelewa tabia na majukumu ya Roho kwenye
maongozi ya kimonotheist ya mteule ni kosa kubwa sana kuliko yote hapa.
Mtazamo wa Kiplatoni unasema kuwa utaratibu
huu ulianzia kwenye muundo huu kutoka kwa Baba na hivyo Roho akafanyika kuwa
nafsi ya tatu kuliko kuwa amekuwa ni mwakilishi tu na kiungo ambacho kwaye
ndipo Kristo alifanyika kuwa ni mmoja na Mungu. Kwa njia ya Roho, ndipo
mwanadamu alifanyika kuwa mmoja ni kama Kristo alivyofanyika, lakini ni kwa
misingi yenye masharti ambayo kwayo Wayunani wanaonekana kuwa waliyakataa.
Kuingizwa au kubuniwa kwa imani ijulikanayo kama Uplatoni mamboleo kwenye Ukristo
kumeenea kwa kina ulimwanguni kote (soma kitabu cha Imani za Siri au Mysticism).
Kitendo cha kutoielewa tofauti iliyofanywa na Origen hapo juu kulisababisha
kuwepo kwa fursa kwenye Baraza la Halmashauri Kuu la Mtaguso wa Nicća ulioitishwa
na kukaliwa miaka 100 iliyofuatia baadae. Umoja wa jambo hili ulikuwa ni umoja
uliotajwa na uwepo wa Roho Mtakatifu, ambao ulikuwa kwa wenyewe tu ni tabia ya
Mungu. Origen aliamini kuwa ni Baba tu, peke yake ndiye Mungu atokanaye na yeye Mwenyewe ("ŰJ`2,@H au autotheos);
(Kwenye Kitabu cha Ioan. 2.2.17);
Na kwenye fikra za Origen
(C. Cels. 5.39) Wakristo wanatajwa
moja kwa moja kwa Mwana akiwa kama ‘wa pili’ (*,bJ,D@H au deuteros)
deity. (N.C.E., ibid.).
Dhana au madai ya Origen ya uumbaji wa
milele unaendanga kinyume na dhana ya usawa wa milele wa Kristo. Augustine hatimaye
aliamini kuwa wakati au zama ilianza kwa vuguvugu la malaika. Dhan hii ni
sahihi sana kwamba nyakati zilianza kwa uumbaji wa malaika wa elohim. Ni Mungu Baba au Eloah peke yake ndiye aliyewahi kuwepo
nje ya kipindi hiki cha zama na alikuwepo kwenye umilele ule wa kabla ya
uumbaji. Kwa hiyo, yeye ndiye mwenye uweza wa kipekee wa kuelewa kila kitu na
Kristo alikuwa wa pili au deuteros theos.
Dhana ya kuwa Roho Mtakatifu anatokana na Kristo ilipelekea kuwa na hitimisho
potofu au la kimakosa na kusema kwamba kwa hiyo Kristo ndiye alimuumba Roho
Mtakatifu. Kutokana na hapo juu, ni kwamba Roho Mtakatifu anatokana na Baba
peke yake. Roho ametolewa kama kitu cha kutusaidia na anatokana au anaendelea
kuwa msaidizi wa elohim kwa Wana wa
Mungu. Imani na mtazamo huu ulikuwa ni tofauti sana na ule wa Jeshi la malaika
waliokuwepo kabla ya kuumbwa kwa mwanadamu. Kulikuwa na Wana wengi sana wa
Mungu, akiwemo Shetani mwenyewe (Ayubu 1:6), wakijulikana kama Nyota za Asubuhi
wakati wa uumbaji wa dunia (Ayubu 38:7). Suala la kwamba lilijitokeza baadae na
ambalo lilifanyika kuwa la muhimu sana kwenye kipindi cha katikati ya karne ya
tatu ilikuwa ni iwapo kama kiumbe huyu mdogo na msaidizi alikuwa ni mmoja wa
viumbe au ni kama alikuwa ni mmojawapo tu ya utaratibu wa kumiliki. Wayunani
waliichukulia muono wa Oregon kwenye kipindi kilichofuatia baadae cha nuru ya
karne ya tatu. Hivyohivyo, wanazuoni kama akina Theognostus wa shule ya kateksomu
ya huko Alexandria, walisisitiza Uwana wake na Baba. Hata hivyo, Mwana
alichukuliwa kuwa ni kama ni kiumbe mwenye harakati zake zenye ukomo kwa viumbe
wa aina fulani. Na alitangaza pia kwamba udogo na usaidizi wake au ousia (akutumia neno la Kiplatoniki
zaidi kuliko neno hypostases) alitokana
na usaidizi wa Baba (soma kitabu cha Kelly cha, Early Church Doctrines [Mafundisho ya Kanisa la Kwanza], ukurasa
133). Wengine walisisitiza dhana ya udogo na usaidizi wake.
Mwanafunzi wa Origen aitwaye Dionysius, Papa
wa Alexandria, alyetokana na kuparaganyika kwa imani ya Kisabelliani kwenye
Pentapolis ya Kilybia mwishoni mwa miaka ya mwishoni ya hamsini ya karne ya
tatu, aliandika akiupinga Umodalism. Alikanusha kabisa utofauti wa kinafsi wa
kati ya Baba na Mwana kwa kiasi kikubwa sana. Wasabellian walikuwa na moja ya
nyaraka zake alizowaandikia maaskofu Ammonius na Euphranor alielezea kwa kina
jambo hili ambalo Kelly (p. 134) anadai kuwa lilikuwa haliwezekani wala
kustahili. Dionysius, Papa wa Roma, alimwandikia Dionysius, Papa wa Alexandria,
(Papa kilikuwa ni cheo cha kawaida tu walichopewa Maaskofu wakuu hasa wale
waliokuwepo huko Alexandria tangu kipindi cha Heraclus yapata mwaka 233-249 (kwa
mujibu wa kitabu cha Eusebius, cha Historia
ya Kanisa [Church History], vii, 7,4)), kinatoa uhakika kwamba wafuasi wa
Origen walisisitiza juu ya mjumuisho au uwepo wa viumbe watatu kila mmoja akiwa
peke yake na ambao wanaonekana kuwa kila mmoja yupo kivyake pasi kutegemeana na
wala hawaungamaniki na kile kinachoita au kujulikana kama umilele ulio sawa (apud. Athan., De decr. Nic. syn. 26). Alexandria inakubalika kwa kiasi fulani kwa
majibu yake (apud. Atan., De sent. Dion. 14-18). Wasabellian
walilalamika kwamba wafuasi wa Origen walikuwa wanaweka migawanyiko midogo iwe
mikubwa ili kuwatenganisha kati ya Baba na Mwana. Jambo hili lilipingwa na
kuthibitiwa na Wanovationist wa huko Roma waliomshawishi au kumvutia Askofu Dionysius,
Papa. Athanasius alijaribu (kwenye kitabu chake cha De sent. Dion. 4) kumtakasa Dionysius wa Alexandria karne nyingine
moja iliyofuatia lakini Basil (Ep.
9.2) aliendelea kutetea kwamba alikuwa amegeukia kwenye upande mwingine wa
uhafidhina mkubwa wa wenye juhudi ya kuupinga Usabellian.
Ni kwanini habari ya nafasi au pahala pa
Kristo kuhusiano wake na Mungu iwe na umuhimu mkubwa kiasi hiki kama itakuwa
haina msingi wa kibiblia? Kwa nini iwe kwamba ya muhimu sana kihivyo katika
kipindi cha katikati mwa karne ya tatu? Jibu lake linatuama kwenye dini za siri
za mungu jua.
Imekuwa
ikionekana hivyo tangu kwenye maendeleo ya zama za kwanza, na zaidi, kwamba
Biblia na wanateolojia wa Kanisa la kwanza walikuwa ni wa mirengo ya kuamini
usaidizi na Uyunitarian. Mungu Baba alikuwa ni Mungu na Baba wa Masihi ambaye
ndiye alikua mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi (Warumi 8:29). Roho
Mtakatifu ni kifaa ambacho kamba Wana wote a Mungu, pamoja na malaika,
wanaifikia nafasi yake ya kuunganika na Mungu. Kristo alikuwa ni miongoni mwa
Wana wengi wa Mungu, lakini alikuwa ni mzaliwa wa pekee (monogenes) (Mwana wa) Mungu (ambaye ndiye monogenese theos), mzaliwa
wa kwanza (prototokos) kati ya
Malaika wa mbinguni akiwa kama kuhani mkuu wa elohim. Elimu hii na uelewa wake
vimeanza kupotea kwa kupitia mbinu za kimapokeo ya Kanisa la kwanza. Dini potofu
za kisirisiri zilishika hatamu na zilikuwepo kwenye teolojia na kanuni za
kidini za Kanisa la kwanza. Habari hii imeelezewa kwa kina kwenye kitabu cha Dini za siri cha Mysticism.
Bacchiocchi (loc. cit.) alionyesha uwepo
wa dini hizi za mungu Jua kwenye kipindi cha mpito cha mabadiliko ya kutoka
ibada za siku za Sabato hadi sasa kuwa Jumapili na uingizwaji wa sikukuu za
kipagani kama vile Krismas na Easter. Maadhimisho ya Krismas hayakuwepo
makanisani hadi maka 475 huko Syria. Easter iliingizwa kwenye Ukristo huko Roma
mnamo mwaka 154 chini ya Anicetus na hila ilifanywa mnamo mwaka 192 BK wakati
wa Victor. Mabadiliko ya kuifanya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu na Pasaka
kubalishwa kwa kuiingiza Easter yaliendelea kwa kasi kubwa. Waongofu alioingia
kwenye Ukrito wakitokea kwenye dini potofu za Kisiri na za waabudu Jua aliongeza
shinikizo kwa kutumia mbinu za uhamasishaji kwa kuondoa misimamo ya Kiyahudi ya
sharia au torati na za sikukuu (soma kitabu cha Bacchiocchi, op. cit.) ambazo
zilikuwa zinatokana na kalenda ya mwandamo wa mwezi na siyo ya mzunguko wa jua.
Ujazaji wa mafundisho ya kisynkretiki ulipelekea kufikiwa kwa kilele chake kwenye
Mtaguso wa Nicća. Kosmolojia ya kibiblia ilituama kwenye mamlaka yote na
kuinuliwa kwa Eloah. Jambo hili lilikuwa na maana kubwa sana kwa tabia isiyochukiza
ya sharia au torati. Kubadilisha kwa utaratibu kungekua na maana ya kuwepo
kwake tu iwapo kama mchakato ungeanza kwa kumuinua na kumtukuza Kristo kwa
kumfananisha kuwa sawa na Mungu na hatimaye kulipa mamlaka Kanisa ya kuyatengea
kazi mamlaka kama hayo ni kama ilivyoeleweka na kutafsiriwa kimakosa kuwa
limepea Kanisa.
Utata wa kwanza kuhusu sheria ulikuwa ni kuhusu
Pasaka na Sabato ya juma. Kuingizwa au kuanzishwa kwa ibada za Jumapili na
kufanya kuwa ni siku muhimu na ya lazima ya kuabudu kulianzishwa na Mtaguso wa
Halmashauri Kuu ya Elvira (mwaka 300). Haikuwa bahati mbaya tu kwamba mtaguso
wa Nicća uliamua suala la Pasaka na kuanzishwa kwa maadhimisho ya sikukuu ya
kipagani ya Easter. Haikua ni kwa bahati mbaya tu kwamba jambo lililofuatia
lilikuwa ni kuihusu Sabato ambapo, kwenye Mtaguso wa Laodicea mwaka 366 (tarehe
hazikumbukwi vizuri), Mtaguso, kwenye Kanoni ya 29, ulipiga marufuku
kuiadhimisha Sabato na ulianzisha na kuitangaza rasmi Jumapili kuwa ndiyo siku
rasmi ya kuadhimishwa kwa ibada za Kanisa. Kwa hiyo, hatua ziliwekwa na
kupangiliwa kwa kile kilivhokuwa kikionekana kama kuondolewa kwa kile kilichokuwa
kinaitwa chembechembe za itikadi na imani za Kiyahudi kwenye imani ya Kikristo.
Kilichojitokeza na kuonekana ni Upagani ndani ya Ukristo.
Endelea ili ujionee jinsi waandishi waliofuatia walivyodanganya Ukristo
kama kwenye historia kwenye jarida hili la Makosa ya Kiutafsiri ya Ubinitarian na Utrinitarian Kuhusu Teolojia ya
Mwanzoni ya Uungu (Na. 127B).
.
q