Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[299A]
Mwaka 2012 na
Mpingakristo
(Toleo la 1.0 20100515-20100515)
Kuna hali ya wasiwasi
inayoandaliwa hivi sasa inayolenga kufanya muonekano ashirio wa
maana ya mwaka wa 2012. Jarida hili linalenga kuitolelea fafanuzi hali hiyo na
kuelezea mtiririko wa matukio na maana ya mwaka 2012, kwa mujibu wa uelewa wa
watu wa dini inayofanya mambo yake kwa siri na fumbo yaani occult ambayo
wanahusisha sana kufanya mambo ya siri kwa maana zao Fulani. Tunafanya kazi hii
ili kutulinda na udanganyifu na pia itusaidie
kumtambua Nabii wa Uwongo na kuujua mfumo wa Mpingakristo hapo utakapoanza
kufanya kazi zake waziwazi hivi karibuni.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Copyright © 2010 Wade Cox)
(Tr. 2012)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia
yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Mwaka 2012 na
Mpingakristo
Ni jambo linalohitaji kujua kwamba Shetani anajiandaa kwa kila hali katika Siku hizi za Mwisho na ameweka utaratibu fulani ambao kwa huo, anase na kuwapoteza yamkini hata walio wateule. Lakini sisi tunaweza kutofautisha jisi vita hivi vilivyo na majira ambayo aliwaambia wanafunzi wake.
Kuna kazi inayoitwa Appollyon Rising 2012, yaani Mchomozo
wa Apoliyon uliotungwa na kuandikwa na mtu aitwaye
Thomas Horn unaohusu na nambari za vitu vyenye maana yake fulani. Kazi hii
inahusianisha na nabii kadhaa zilizotolewa na manabii
wa zamani na baadhi ya mambo yaliyotokana na kazi ya mtu aitwaye Malachi Martin kwenye kitabu kiitwacho Windswept House, yaani Nyumba Iliyochukuliwa na Upepo. Nimeandika
jarida hili ili kuuelezea mwaka wa 2012 unavyotajwa
kwenye Kalenda ijulikanayo kama ya Mayan na nyinginezo nyingi ambazo
nitazielezea pia. Pia tutauangalia unabii wa Zohar, kama ulivyo kwenye kazi ya uandishi ya Horn, na nabii
kadhaa nyingine nyingi.
Nabii za Malachy wa Armagh
zimeandikwa kwenye jarida liitwalo The Last Pope (No.
288) yaani Papa wa Mwisho atakazoweza kuzisoma
kwenye tovuti ya:
http://www.ccg.org/english/s/p288.html.
Huo ni mwanzo mzuri katika kusoma. Mhuri au alama Kuu ya nchi ya Marekani ni ashirio la muundo wa kitu kinachoitwa kama Amri Mpya Ulimwenguni yaani New Word Order na ni muundo wa mfumo wa imani ya Kimasoni. Kujishamirisha kwake na kuiteka kwake Vatican na Waabudu Shetani na hawa wajulikanao kama Freemasons ndiyo kichwa cha somo la aliyoyaandika Martin na pia aliyoandika Horn pamoja na mlolongo na nyakati zake. Muundo wa uongozi wa nchi ya Marekani ni wa Nguvu ya Mnyama kwa upande mmoja, ukienda sambamba na eneo kubwa la Ulaya likiwa ni pea nyingine ya vidole vya dola ya vidole kumi vya Siku za Mwisho. Nguvu za Mnyama huyu ziko kwenye maeneo mawili kwenye pande zote mbili za bahari ya Atlantic na Shetani na watu wa imani ya mambo ya siri yaani Waoccult wamekuwa wakiyaendeleza mambo yao ili waitawale hii dunia. Tutajifunza hayo yote hapo mbeleni.
Mwaka huu wa 2012 ulipaswa kuwa ni mwanzo wa “Majira
ya Taabu yake Yakobo” na kuja kwake Masihi, lakini tutajifunza hayo zaidi huko
mbele.
Kwenye kitabu cha Martin, tutaenda kufunza na kujionea
pia juu ya jinsi Malaika huyu Muasi Lusifa atakavyotawazwa na kupewa mamlaka
kwenye miji au majimbo ya Vatican na South Carolina [Carolina ya Kusini huko
Marikani] akifanyiwa ibada au misa kuu maeneo 33 zitakazosomwa kwa wakati mmoja
ambazo zitajulikana pia kama sherehe za kishetani.
Mwaka 2012 una
maana muhimu kwa waumini wa dini ya waabudu jua.
Tutatathimini nabii nyingi zaidi na kuona zipi
tutakazo jikita nazo kujifunza kwa wakati huu kwa majira yake.
Sote tunataraji
kwamba Mashahidi hawa waje na tujifunze kwao. Tunajua
kwamba Masihi atakuja hapa duniani baada ya hawa Mashahidi watakapokuwa huko
Yerusalemu kwa kipindi cha siku 1263.5. Mashahidi hawa bado hawajaanza kazi zao huko Yerusalemu wakivaa
nguo za magunia. Na hii ndiyo maana tunathubutu kusema kuwa mwaka 2012
hauwezi kuwa ni mwaka wa kurudi kwake Masihi, bali
kunampango tu hapo wa Mpinga-Kristo na Nabii wa Uwongo ndani yake. Kunafuatia
hali tu ya kujiuliza, na ukifikiri kwa kina utagundua
kuwa haikosi watu hawa wa abudu jua wanachotaka kukitafuta au wanachotaka
kukifanya.
Kitu kimoja tunachoweza kukijua sisi ni kwamba
mchakato huu wa kukabidhiana madaraka hautakuwa ni kitu cha rahisi na amani.
Shetani na jeshi lake la mapepo wameweka utaratibu wa
kimchakato wa kupigana na Kristo na Wateule wake. Kupitia
mchakato huo, atafanikiwa kuwadanganya yamkini hata walio wateule.
Kazi aliyoifanya Malachi Martin ina maana
http://www.ccg.org/english/s/p067b.html.
Mfumo wa
Kalenda ya Mayan
Shetani ameweka mfumo katika Siku hizi za Mwisho ambao unaathari kwetu ya moja kwa moja.
Lifuatalo ni
dondoo kutoka kwenye jarida liitwalo Advent of the Messiah (No. 210a) [Kuja kwa Masihi] utasoma kwenye wavuti
yetu ya:
http://www.ccg.org/english/s/p210a.html.
Mfumo wa Jua una umuhimu wake
na jarida hili lina nyongeza yake inayoelezea kwa kina juu ya mfumo wa kalenda
hii ya Mayan pia.
Sehemu ya I: Kipengele cha C: Nyota ya
Alfajiri na Kalenda ya Mayan
Tumejifunza kuhusu kalenda ya Mayan kwenye jarida lile. Kuna mambo ya kuhimu kuyaangalia kuhusu
mfumo ule. Haukukamilika hadi kwenye maandishi ya kitabu cha makala za mambo ya
kale maarufu kama Dresden Codex, takriban 934 BK. Tutajifunza
tena jambo hilo hapa.
Utaratibu wa kipimo cha kuchunguza damu maarufu kama YDNA
kilichogunduliwa na Maya unasema ongezeko la chembe hai Q hutokea wakati chembe
hai P iliyo kwenye kundi la Haplo [Haplogroup] zikitawanyika na kwenda kwenye
chembe hai iitwayo R na Q vikundi vidogovidogo. Kwa maneno mengine, tukisema
kwa mrengo wa kibiblia twaweza kusema kuwa Waamerindian ni wana wa Yafeti na ni
ndugu wa karibu sana wa Waslavi na Wazungu. (Tazama jarida la Genetic Origin of the Nations
(No. 265) [Chimbuko la Mataifa La Kinasaba] kwenye wavuti hii:
http://www.ccg.org/english/s/p265.html).
Kwa hiyo, Kalenda hii ilianzia kipindi cha baada ya gharika kuu ya Nuhu, na iliwekwa kwenye kiwango cha mrengo au kundi la kalenda iliyojulikana kama Dresden Codex, huenda haina mabadiliko ya siku za kale sana.
Inarejesha nyuma kwenye mfumo unaotuamanisha chimbuko la elimu ya mambo kale
kwenye mwaka wa 3114 BK, miaka arobaini kabla ya kifo
cha Adamu. Ni mfumo tatanishi unaofungamanisha na
maamuzi ya Kuchomoza kwa Venua akiwa kama Nyota ya Asubuhi na inahesabu kipindi
kilichopo cha zama za umbaaji au mzunguko Mkuu wa Mwaka Mmoja ambao unafanya
idadi ya migawanyo waliyoiita baktuns 13, ambao unafanya jumla ya miaka 5125 ya
mzingo wa jua.
Idadi hii ya miaka 5125 inadaiwa kuhusiana na Mzunguko
Mkuu ambao ni muendelezo wa vipindi vya masaa kuwa sawa mchana na usiku. Hivyo
basi, inadaiwa kuwa na zama tano za ambazo pia huitwa
aenos ya Mzingo Mkubwa ambayo ina vipindi viitwavyo Baktuns 13. Hii sio sahihi. Migawanyo mitano ya Baktun 13 unafanya
kuweko kwa jumla ya miaka 25,625 ya mfumo wa jua.
Migawanyo 12 ya ukanda wa anga unaopita sayari
hailingani na migawanyo mitano ya Baktun ya Maya. Kuna
utofauti muhimu kwenye jumla ya Mizingo Mikuu ya miaka ya jua 295.
Tarakimu hizi ni sawa na zinaweza kufanya uhusiano
mwingine elekevu unaotokana na kiini cha zamani.
Mwendlezo wa huu mfumo wa siku kuwa na masaa sawa ya usiku na mchana ni kitu
kilichorudi nyuma pole pole ukichukua kipindi cha takriban miaka 2,160 kupita
kwenye ukanda wa anga unaopita sayari, au miaka 25,920 kupita kwenye ukanda huu
wote wa njia inayopitia sayari. Hakuna mabadiliko ya ghafla
wala ya haraka haraka. Dhana ya kuwa na ‘Mwaka
Mkubwa’ uliokuwa kwenye fikra za Wayunani unaweza kuchukuliwa kuwa ni fikra za
Heraclitus lakini nia yake hasa bado haijulikani. “Inaonekana kazi ya undishi wa Plato iliiridhia na dhana hii ya kuwa na ‘Mwaka Mkubwa’
kwa kadiri muda unavyojiri kwa nyota kurejea tena kwenye mahali ilipoanzia
mzunguko wake ulimwenguni (Ti. 39d) na kuonekana ikitoa thamani ya kimahesabu
kwake (Rep.546b-c), [1][25]. Hii ingeashiria umakinifu
wa Plato kwa mbinu zake za ujuzi wa mambo ya
kimbinguni kwa kipindi kikubwa sana na Celsus akaonekana kuwa makini wa kuijua
mwinendo miwili ya mzunguko wa ulimwengu” (Simon Mahoney, An Interpretation of Mithraic Remains. Soma kwenye wavuti hii http://pages.britishlibrary.net/simon.mahony/ma-mith.html).
Mfumo mzima wa Mayan unatuama kwenye idadi ya walioko
kwenye Baraza la Jeshi la mbinguni. Idadi inayowekwa ni
72 au pia huitwa Hebdomekonta [au duo] ya Luka 10:1 na
17. Inaashiria sana na ile idadi ya baraza la Marabi
wa Kiyahudi, maarufu kama Sanhedrin. Baraza hili la Sanhedrin kwa jinsi lilivyo tu laonyesha kuwa limeundwa kwa mtindo
ulioigwa sawa na lile Baraza la Mbinguni, tunalolijua limetajwa kenye Biblia.
Mwaka 3114 KK Adamu alikuwa hai bado. Wazee wetu
wafuatao walikuwa pia wangali hai: Sethi (b. 3874, d. 2964); Enoshi (b. 3769,
d. 2864); Kenani (b. 3679, d. 2768); Mahalaleli (b. 3609, d. 2714); Yaredi (b.
3544, d. 2582); Henoko (b. 3382, t. 3017); Methusala (b. 3317, d. 2348); Lameki
(b. 3130, d. 2353). Yaredi alikuwa ni baba wa Henoko. Nuhu alikuwa hajazaliwa bado hadi mwaka 2948 KK. Kwa hiyo,
mwaka huu wa 3114 kilikuwa ni kipindi ambacho mababa
hawa wote walikuwa wangali hai na kupelekea zama za kuokolewa kwake Nuhu. Anguko
la watu wa Mungu kimapokeo linadhaniwa kuhusishwa na
kipindi cha utwala wa Yaredi na kwamba katika zama zake hizi Wachamungu
waliinuka na kujitwalia wanawake waasi na kufanyanao ngono. Inadaiwa
kwamba baba yake Mahalaleli alimwita jina hili Yaredi kinabii. Kwa
mujibu wa kitabu fasihi, jina la Yaredi maana yake ni anguko au mporomoko wa kiroho, (SHD
3382), na linaashiria mwonekano wa Watu wa Mungu ulivyokuwa siku hizo.
Alizaliwa mwaka 3544 na alikuwa na umri wa miaka 430
kufikia mwaka 3114 KK. Mporomoko na maanguko haya ya
Wachamungu na maingiliano ya kingono yalitokea kipindi hiki cha utawala wake.
Henoko aliahubiria
sana akiwaonya Wachamungu dhidi ya maasi haya na alitwaliwa
na Mungu kama thawabu ya uaminifu wake kwenye mwaka 3017. Maandiko yaliyoko
kwenye kitabu cha wanahistori kijukanacho kama 1Henoko yanaelezea kuhusu unabii
uliotolewa na Henoko kuwa kulikuweko na Gharika wakati alipozaliwa Nuhu, lakini
hili haliwezekani kwa kuwa Henoko alitwaliwa miaka 69 kabla ya kuzaliwa Nuhu,
(1Henoko 106:12-13; na Yubile 4:4:15,22). Kitabu cha
Yubile kinasema kuwa Henoko alitwaliwa ili awe shuhuda
dhidi ya matendo potofu ya vizazi vyote Siku ya Hukumu ya Kiyama. Na kwamba
atafukiza uvumba juu ya Mlima Qatari, ambao ni mmoja
wapo ya Milima ya Mashariki miongoni mwa Milima mkitakatifu minne iliyopo
(ambayo ni Edeni, Mlima wa Mashariki (Qatari), Sinai na Sayuni), ili kutakasa
mataifa kwa ajili ya uumbaji mpya wa Siku za Mwisho (tazama. Yub.
4:24-26). Inaweza kuwa mwaka huu wa 3114 unahusina na
tukio hili na kujitia unajisi kwa Wachamungu huko Tartarus. Kipimo cha muda
kitatuonyesha kwa kadri tu muda unavyoendelea mbele.
Hata hivyo, mwaka wa 3113 ni wa sabini wa kabla ya kuzaliwa kwa Nuhu, na idadi
yake inafikirika kwa kuonyeshwa kama (alama ya kujumlisha, mbili=72) inahusiana
na ile ya Watakatifu walioko Mbinguni na yale mataifa waliyopewa kuyatawala
miaka ijayo mbeleni. Kwa hiyo, hatunabudi kuongelea kanuni ya uumbaji hadi siku
hii ya leo. Ni kuifanya tarehe ya mwanzo wa zama za mwanzo wa kuumbwa kwa ke Shetani akiwa kama Nyota
ya Alfajri aliwa mkuu wa Mapepo wote au Malaika Waasi wote.
Kuchoza kwa Venus kumechangia kipindi kiitwacho 1
Ahau. Tatehe yenye maana ya “wa 1 kwa Bwana".
Ahau ni neno lionekanalo kwenye lugha nyingi na linahusiana
na neno Yaho na laweza kutokana na Elohim wa Majeshi.
Mfumo wake unatuama kwenye mwezi wa siku ishirini, ambao
unajina uinal. Neno hili uinal maana
yake ni nafsi au
mtu-mume. Nambari 20 ni nambari ya mwaka wa kibiblia unaohitajika kabla ya mtu
hajachukuliwa kuwa amekua na kukomaa kikamilifu. Kuna uainal 18 kwenye mzunguko
wa Tun moja au mwaka mmoja wa siku 360. Mwaka wa kinabii ni ule uliowekwa kwa madhumuni la kumuwezesha
mwanadamu kuwa na maendeleo yanayoonekana. Siku tano zimerekebishwa kama ilivyoelezewa kwenye jarida la Nyongeza (Appendix) 210A.
Miaka imewekwa hivyo ili kufanya mizunguko 100 ya siku
72, au uinail 360 (mwaka wa miezi), na kufikia hesabu ya siku 7200, ambayo
inaitwa Katuni moja. Katuni 20 (miaka
ya miezi) sawa na siku 144,000, inayoitwa Baktuni
Kwa hiyo,
wanazuoni wa Biblia wanaweza kujionea kwamba mfumo
mzima imefanyizwa kwa maongozi yanayolenga kukidhi haja ya huyu Nyota ya
Asubuhi ukishikamana na mfumo wa Jua. Inaweka mwelekeo wa
utawala wa huyu Nyota ya Asubuhi anayetawala zama zetu hizi. Huyu Nyota ya
Asubuhi atawalaye siku hizi ni Shetani. Nyota Mpya ya
Asubuhi ni Kristo na wateule wake 1440,000 chini ya
Mitume. Kalenda hii inaonekana kuwa inakusudia kuwalenga watu wanaorudi kwa muonekano wa kimiungu katika siku za mwisho. Hata hivyo,
haina uhusiano shikamanishi na ule wa mwezi.
Mzunguko
wakalenda ya Venus na mchomozo wake, na mchomozo wa
Nyota ya Asubuhi na ashirio la mwanzo wake.
Kwa hiyo, kalenda ya Mayan inaleta mfumo wa Jua ulio chini ya Shetani anayekuja kuhitimisha zama za uumbaji, ukiwa ni Mwaka Mkuu kwao wa 2012. Tarehe ya mwisho katika mwaka 2012 inakusudiwa kuwa ni ile ijulikanayo kama 13.0.0.0.0 inayomaanisha kwamba Baktuni 13 zimepita, na kuwa jumla ya siku 1,872,000.
Hesabu ya kile kinachoitwa Tzolkin inaaminika kuwa imeanza tangia siku ya 4
Ahau na kwamba itaishia tarehe 4 Ahau; hata hivyo,
kuna mabishano makubwa sana yanayoendelea hivi sasa yakisema kwamba mwanzo wa
hesabu hii na mwisho wake vinapaswa ingekuwa ni tarehe 13 Ahau na sio
vinginevyo.
Mwaka Mkuu mwingine unaofuatia utakuwa chini ya na
wenye maana ya Nyota Mpya ya Alfajiri.
Maelezo mengine yaliyo rahisi zaidi yenye maana ya kina zaidi
kuuhusu mfumo huu unavyohusiana yapo kwenye sehemu ya nyongeza ya jarida hili.
Hebu na tuzione sasa nabii kadhaa zilizotolewa kuuhusu mwaka 2012.
Unabii wa Joka Kuu
Machachari la Kihindi
Wahindi wa imani ya Cherokee Indians wana mfumo wao wa
kalenda na imani yao inafanana na na Mesoamericans. Kwenye
kitabu chake Horn kurasa za 311-313 anawaelezea juu ya Joka machachari la hawa Cherokee
au Nabii za Chikamaugan za miaka ya 1811-1812.
Unabii uliotolewa na kabila kwa wakati ule unachukuliwa kuwa ulimaanisha kurudi kwa joka kuu lenye manyoya maarufu kama mungu Quetzelcoatl katika mwaka 2012. Kalenda zote mbili, yani ya Mayan na Cherokee zinaishia mwaka 2012. Horn anaamini kuwa hii itatokea wakati dhana au imani fikirika ya kinajimu itafungamanishwa na Miungu Mikuu ya Warumi ya Jupita, Zuhura (Venus), Orion, na Pleiades wanaosababisha nguvu za mfumo wa nyota “kuamshwa” au kutikisika.
Sehemu mojawapo kuhusu unabii huu wa joka machachari
inasema hivi:
“Kipindi hiki cha
mwaka 2012 cha msukosuko wa mungu Jupita kuwa mfumo wa
[hii] nyota ya Orion utatikisika. Na hii miungu Pleiades na
Orion itafanya vita tena kama walivyofanya hapo kale Jupita na Venus watakapotikiswa
kwenye eneo lao asilia la mzunguko wao uitwao Unitime. Orion atafanya vita na Pleiades, Jupita atafanya vita na Venus…. Katika mwaka
2012 kutakuwa na mfungamano kwa kalenda hizi zote za Cherokee
na iliyo kimbingu ya Kundi la Nyota (Kiunajimu) ya Joka Kuu.... Ni kipindi cha
kujikita kwa joka lenye vichwa viwili. Ni kipindi cha
rangi nyekundu cha Orion na Jupita kupambana na wale
wenye nasaba ya bluu kina pleiades na venus… Mwaka 2012 hili Kundi la Nyota la
hawa Cherokee Joka kuu litachukua mwelekeo wa tofauti.
Joka lenyewe litabakia, hata hvyo, itakuwa ni juu ya
Joka kuu atakayeongezewa kichwani mwake manyoya na, macho yake yatafunguka na
kuwakawaka, mabawa yatafutuka na kuwa joka kuu lenye mabawa. Litakuwa na mikono na viganja na kwenye viganja vyake atashikilia
bakuli moja kubwa. Bakuli hili litakuwa limejaa damu ndani
yake. Kwenye mkia wake wenye kuchacharika kutakuwa na
harakati na mng’aro wa Pleiades
Hatimaye Joka huyu atakuwa ni joka mwenye manyoya au
atakujikana kama Joka Kuu mwenye manyoya wa Zama/Zama hizo [Quetzacoat]
Sambamba na huyu Joka Mkubwa kutakuwa na kipindi cha heri au cha Njia
ya Maziwa. Mkatizo au mpito wa kipindi cha Njia ya
Maziwa kitaonekana mwaka huu wa 2012. Na Kalenda ya Cherokee itaishia mwaka huu
2012… [na] “ujio wa Mharibifu
na Mdanganyifu utatokea”.
Kikomo cha
Kalenda ya Mayan kwa ujumla wake ni tarehe 21 Desemba
2012 na hata ya Cherokee. Ishara hizi za mbinguni ni muhimu sana katika kujua
kurudi kwa joka huyu mwenye manyoya na kumeainishwa kwa nyakati zetu na Mapepo
yanazitumia matukio haya kwa kumneemesha Nabii wa Uwongo na Mpinga Kristo. Huku
muundo wa kidini ukiuunga mkono muundo wa Kisiasa.
Kipindi cha kuanzishwa kwake kinatuama kwenye chanzo chake asilia kutoka kwa
wafuatiliaji ni mwaka huu ujulikanao kama wa Duma (Tiger) kwenye kipindi
kinachokadiriwa kuwa ni cha Desemba na kitaendelea hadi mwisho wa 2012 kwa
mujibu wa nabii zao.
Mwaka 2012 na Waazteki
Kugunduliwa kwa Kalenda ya Jiwe ya Aztec huko Mexico kwenye eneo la hekalu la Watenochtitla chini ya Kanisa Kuu lililoko kwenye mji mkuu wa Mexico ambako kanisa hilo lipo, kumejionea uwezekano zaidi wa kuelezea kipindi hiki. Wahispaniola waliifukia hapo na ikagunduliwa mnamo mwaka 1990. Tarehe 21 Desemba 2012 ni kikomo cha Mgawanyo wa Tano wa mungu Jua aitwaye Tonatiuh, kipindi kilichoanzia mwaka 3114KK, kama ilivyo kwenye mfumo wa Mayan. Imani hii ya Tonatiuh huenda sambamba na utoaji wa damu ya wanadamu kama moja ya sadaka zao (zaidi ya watu 20,000 kwa mwaka) kama sharti muhimu katika kutoa unabii muhimu. Pia alijulikana kama Bwana wa Siku Kumi na Tatu (Mfu 1 kwa Govi 13). Hii inatumika pia kama kitu muhimu na kitakatifu sana kwa imani ya Frimasons.
Hawa wote, yaani Waazteki na Maya waliamini kuwa Kipindi-zama cha Kwanza au Jua la Kwanza kilikuwa ni kile ambacho majitu walipokuwa wanaishi hapa duniani na walifutiliwambali na gharika kuu.
Kipindi hiki cha mwisho na cha Tano kinaishia tarehe 21 Desemba 2012.
Horn ana mahali pazuri sana kuelezea jambo hili kutoka kwenye ukurasa wa 278 na kuendelea kwenye kitabu chake. Kwenye eneo hili anaonyesha jinsi Wajesuiti na Freemasons walivyoshirikiana kwa pamoja kuifanya kazi ya kuupamba mnara mkubwa au kuba ya mjini Washington DC kwa kuweka alama kufuru za siri zilizogunduliwa huko Mexico.
Mnara-Kuba Maarufu na Mnara
Mrefu na Mwembamba
Minara mikubwa au
Kuba (Dome) maarufu na Minara mirefu na myembamba (Obelisk) huwekwa mijini kwa
lengo la kumkumbuka na kumpa heshima kila kiongozi wa daraja la juu wa imani ya
uwekaji wa alama kufuru za kimafumbo aliyewahikupita na kuonyesha kuwa hata
yeye alikuwa ni mungu. Wao huamini kuwa kila mtawala amezaliwa akitokea kwenye
Tumbo la mungu Isis na hii ndiyo hasa maana na nia ya
kuweka aina hii ya minara mikubwa au kuba (Dome) na kuipamba vizuri. Tangu
sherehe ile ya Washington na nyingie zilizofuatia zote
zinanuiliwa kuona kulifanya tendo hili la kufuru la kujifanya kuwa wao sio
wanadamu tena bali wanageuka kuwa miungu au kwa maana yao wao humaanisha kuwa
kila sherehe hii ya kumtawadha mtawala inalenga kufanya maandalizi ya hitimisho
la kufikia kilele cha uungu mwaka 2012. Nia-dhana ya hii minara mirefu na myembamba inatuama kwenye tarakimu 666.
Minara hii ya
obelisk (mwembamba mrefu) na Dome (Kuba) kufuru
inayowakilisha miungu Isis na Osiris, yaani mungu mke na mume. Mnara mrefu na mwembamba ulioko kwenye kanisa la Mt. Petro ni mmoja ya
mifano hai ambalo lilihamishwa kutoka huko Heliopolis ambalo ni Hekalu la mungu
On, na ndilo lililowekwa wakfu mbele ya mungu Ra/Orisis na Isis pia. Minara hii
yote, minene na mirefu huwekwa Mijini kwa madhumuni
hayohayo pia. Duara linalowekwa maranyingi kwenye minara hii mwembamba mirefu
huwakilisha au humaanisha uke wa Isis na Uume wa
Orisis ukianza kupata ashiki na kusimama.
Kuba ya
iliyowekwa jengo jengo maarufu lililo kilimani (Capitol) ilipakwa rangi na Mtaliano, Brumidi
ambaye alipewa maelekezo na uangalizi wa Wajesuiti. Alipelekwa huko
Ni hakika kwamba
wote wanalijua hilo na wote wamehitoa kupiaheshima
miungu ya kipagani wanayoileta. Kamwe mwili wa mtawala
aitwaye Washington haukuwekwa pale. Imefanywa kuwa ni
alama inayoendelea katika kuonyesha kufuruyao ya Kujitukuza na kujiona kuwa wao
ni miungu na kuitukuza itikadi yao wanayoiamini kuwa watafufuka na kwenda
mbinguni kama miungu. Kuna madaraja matatu hapa kama
kuvyo na vyumba maalumu vitatu kwenye mapiramidi ya Misri.
Mwonekano Mbalimbali Wa
Mambo
Mwaka wa 2012 ni
wa muhima na wa maana sana kwa dini hii ya waabudu Shetani na wanaohusika na
taaluma ya kuweka alama imani zenye mana kufuru zinazojulikana maana zake kwa
watu wachache na kwa wengi kuwa siri isiyojulikana yaani okaliti (occult) wa
Kifreemasons na tutayaelezea mambo hayo.
Kwanza na tuone jinsi uhusiano wa mwaka 2012 na alama za kufuru za hawa
waokaliti kwa mujibu wa mitazamo ya wa Kabbalisti dhidi ya ule wa Zohar na kisha
kwa mujibu wa alama na imani kufuru za Mafreemasos kwa jinsi pia vinavyotukuka
na kukumbatiwa na Vatican.
Pia Mwaka wa 2012 umekuta na kipindi cha utengenezaji wa kile kinachoitwa I Ching ambao maana yake ni Kitabu cha Mabadiliko huku kiwango chake kikiwa kimefanyika kuelekea kwenye utimilifu wa Kitabu hiki cha Mabadiliko ambacho kinahusishwa na kitabu cha fafanuzi cha Wen Yen. Kimefanyizwa kwa mfumo wa kipimo cha hexagram 65.
Kuba ilijengwa kwaka 1973 wakati Terrence na Dennis McKenna ndio walioifanya kazi hii, ikiwa ni kazi nyingine mbali ya dhana ya Kalenda ya mayan.
Mabadiliko yalitokea na sehemu ya mwisho yalitokea kwa kifupi tu ilipofika tarehe 11 Septemba 2001 na yakakoma au kutoweka yakisubiria kutokea tarehe 21 Desemba 2012. Inaoeneka kwamba kipindi hiki kutakuwa na mlipuko mkubwa sana unaokusudiwa kwa Siku za Mwisho.
Mradi
wa Mtandao Uvumi
Mradi uliofanyizwa hivi karibuni wa Uvumia ama uwongo umekuwa ukihusisha na muono wa mambo asilia na kwa kutumia mtandao wa Intaneti na kuanza kubuni na kueneza uvumi wa siku ambazo maafa yanaweza kutokea. Mnamo mwezi wa Juni 2001 waliitabiri tarehe za Septemba 11, 2001, na pia wametabiri kuwa maafa makuu yataukumba ulimwengu hapo mwezi Desemba 2012 (Horn, uk. 309).
Jambo linalotuama kwa ukaribu zaidi ni kwamba matukio lililotokea Septemba 11, 2001 yalijadiliwa kwenye mtandao wa intaneti na mtandao wa mtandao huu wa kuvumisha uwongo ukaanza kukusanya vyanzo vya jinsi tukio hili lilivyotokea.
Mwaka
2012 na Zohari
Kazi iliyofanywa na Kabbalist kuhusu Zohar ilifanywa katika kipindi cha zaidi ya miaka 700 iliyopita na kuandikwa kwa lugha ya Kiaramu kwenye miaka ijulikanayo kuwa ni zama za kati. Inahusisha pia na fafanuzi za zisizo wazi za kitabu cha Torati. Kwa kuongezea tu kuhusu fafanuzi za Maandiko Matakatifu kwenye Sura ya “Vaera” (Toleo la 3, sura ya 34) kuna maneno haya: “Ishara za kumtangaza Mashiach (Masihi).” Zohar alitabiri ujio wa Masihi kuwa utakuwa mwaka 2012. Kwa ajili hiyo, tunaweza kutafsiri kuwa inamaanisha Mpinga Kristo atafunuliwa na kutangazwa rasmi tahere 11 Desemba 2012. Watu wa jamii ya Kabbalist hawakumtambua Kristo kuwa ni Masihi bali walikuwa wamependeza na kujikita tu kwenye itikadi ya imani za sirisiri. Horn mwenyewe alidiriki kusema kwamba hii inamaanisha ni kufunuliwa kwa Mpinga Kristo. Alisema aliwahi kujadiliana na jarida lijulikanalo kama J.R. Church of Prophecy News (Jarida la Kanisa la Unabii la J.R) kuhusu Zohar kwenye aya zake za 476-483 ambako kulikuwa na muono kuwa inaashiria kuwa ni Kipindi cha Taabu yake Yakobo, cha Dhiki Kuu, kwa mujibu wa mtazamo wa Zohar kitaanza mwaka 2012 (Horn, uk, 313).
Hii itatanguliwa na tendo la kumtangaza Masihi wa Uwongo kufanyika tangu mwaka 2010-2012 kama ilivyoelezwa kwenye jarida la [Masihi wa Uwongo (Na. 067B) [The False Messiah (No. 067B)] kwenye tovuti ya http://www.ccg.org/english/s/p067b.html.
Papa anayefuatia, ambaye ni Petro wa Kirumi, atakuwa ni papa wa mwisho atakayefuatia kipindi cha kuangamizwa kwa Roma. [tazama jarida la Pap wa Mwisho Na. 288) (The Last Pope (No. 288) kwenye tovuti ya http://www.ccg.org/english/s/p288.html).
Matukio haya yanaonekana kuwa yatatokea.
Kwa mujibu wa unabii wa Kikatoliki, mtu aitwaye Pius XIII, ataiacha au kuondoka Roma akipitia juu ya miili ya makuhani. Nambari 13 ni nambari wanayoitumia watu wa imani ya alama za fumbo za siri wa kiokaliti na ni namba ya uasi.
Inadhaniwa pia kwamba mwaka 2012 utakuwa ni mwisho wa zama hii, na wanaulinanisha na Mathayo 24 kuhusu siku za Nuhu na kuchukuliwa maana yake kuwa mbingu zitakuwa na uasi mkuu sana kama ilivyokuwa siku za Nuhu na mwisho wa dunia au Aeon.
Misingi
ya unabii kwa mwaka 2012
Je, ninini hasa maana ya mwaka 2012 kwa Malaika Waasi au watu waliomuasi Mungu ambao hapo mwanzo walikuwa watiifu kwake na ni kwa nini nambari za waokaliti wengine ziwe ni muhimu sana? Ni kwa jinsi gani wabobea na kujikita kwenye falsafa au imani na mafundisho ya kidini ya Waokaliti?
Shetani anaonyesha urefu wa kipindi alichopewa. Kitolewa na kupimwa kwa Kalenda ya Mungu.
Utaratibu au Mfumo wa
Yubile
Tutaona sasa
jinsi mfumo wa yubile unavyofanya kazi na maana zake kwa
mujibu wa unabii.
Miaka ya yubile
inaendana kwa mtindo wa tarakimu za miaka ya 27 na 77
kwa miaka ilivyo zama hizi, na katika miaka ya KK ilikuwa miaka 24 na 74 KK.
Jinsi zilivyohesabiwa hizi yubile na kuainishwa imefafanuliwa kwenye jarida la Usomaji wa Torati
na Ezra na Nehemia (Na. 250) [Reading the Law with Ezra and
Nehemiah (No. 250)] kwenye tovuti ya
http://www.ccg.org/english/s/p250.html
na pia kwenye jarida la Maana ya Maono ya Ezekieli Na. 108 [The
Meaning of Ezekiel's Vision (No. 108)] kwenye wavuti ya
http://www.ccg.org/english/s/p108.html.
Mungu hatupi sheria tusizoweza kuzifuata au kuzishika na
chochote kinachofanyika ni kwa dhumuni ya kufanya Marejesho ya Torati na
ushuhuda umewekwa tayari kwenye Maandiko Matakatifu.
Utaratibu wa mzunguko wa mwaka wa saba unawekwa kwenye utaratibu wa kundi la
miaka saba ambalo kila moja lina miaka saba-saba na kwenye mwaka wa sita wa
mzunguko wa kundi la saba, tunakirimiwa na Mwenyezi-Mungu kwa kupewa baraka za
mavuno mara tatu ili yatuchukue hadi kutufikisha kwenye Mwaka wa Sabato ya Saba
na kwenye mwaka wa Hamsini wa Yubile. Baragumu la kuutangaza Mwaka wa Yubile hupigwa kwenye Siku ya Upatanisho inayofanyika
katika Mwaka wa Sabato na inaishia kwenye maadhimisho ya Siku ya Upatanisho ya
mwaka unaofuatia ambao ni wa Yubile. Kutoka kwenye siku hii ya Upatanisho ya
mwaka huu wa Hamsini ardhi yote inatakiwa iachwe ipumzike na inalimwa tena
kwenye mwaka wa “nane” ili kufanya kuwe na mavuno kwenye mwezi wa kwanza ambao
ni wa Abibu unaofuatia ambao ni mwaka wa tisa ambao ni mwaka wa kwanza wa
Yubile mpya. Utaratibu huu umefafanuliwa kwa kina
kwenye jarida liitwalo Kalenda ya Mungu (Na. 156) [God's Calendar (No. 156)]
kwenye wavuti ya
http://www.ccg.org/english/s/p156.html
na kwenye jarida la Utoaji wa Zaka Na. 161 [Tithing (No. 161)] kwenye wavuti ya http://www.ccg.org/english/s/p161.html.
Kwenye karne ya pili KK, Mafarisayo wa kwanza alikuwa
wamevutiwa na kuamini imani ya watu wanaoamini kuwa elimu au kujua mambo pekee
kwa weza kumwokoa mtu yaani Kinosis wa Alexandria walianzisha yubile ya uwongo
yenye kuchukua jumla ya miaka 49 na wakajaribu kuvunja
utaratibu ulioagizwa na Torati na utaratibu wake. Ubadilishaji huu wenye
kupotosha na mbinu na kipindi chake vimefafanuliwa kwa
kina kwenye jarida la Upotoshaji wa Kalenda ya Mungu Katika Yudea Na. 195B [Distortion of God's Calendar in
Judah (No. 195B)] kwenye wavuti ya http://www.ccg.org/english/s/p195b.html.
Kazi alizozifanya Josephus zinaonyesha jinsi mabadiliko haya yalivyotokea pale
alipokuwa, akiwa kama Farisayo, anajaribu kuingiza
mawazo yao lakini akipaswa kuelezea kanuni za Warumi kama zilivyotungwa ambazo
zinaionyesha kisahihi sana Kalenda ya Hekalu na karatasi inauonyesha ukweli huu
kama unavyoonyesha uthibitisho wa wataalamu wanaochimbua na kuvumbua mambo ya
kale tulioupata, unaoonyesha uhusiano wake na kalenda ya Hekalu.
Tendo la kuzijua
hizi Yubile na lini zinakuwa, ni jambo muhimu sana ili
kuujua ulivyo mpango wa Mungu. Yubilee hizi zinafungamana na
utaratibu wa juma la uumbaji. Mzunguko huu wa Yubile
ulianza tangu mwanzo wa utawala wa Shetani baada yakufungwa kwa bustani ya Edeni.
Kwa mujibu wa kronolojia ya Biblia inaoneysha uumbaji
wa Adamu na Hawa kuwa ulifanyika mnamo mwaka 4004 KK.
Kronolojia ya Waashuru inaonyeshwa kwenye toleo la Biblia ya Mfalme Yakobo
(KJV) ya mwaka 1611.
Hata hivyo, Shetani hakupewa mamlaka yote hadi kwenye kipindi
kilichofuatia baadae. Shetani alipewa miaka takriban elfu sita ya
kuitawala hii dunia akiwa kama mungu wa dunia hii
(tazama 2 Wakorintho 4:4). Kwa wakati wote Makanisa ya Mungu yameujua ukweli wa
kwamba kila juma moja linamaanisha ni mjumlisho wa siku sita za kazi na siku ya
saba yake ambayo ni Sabato ni kivuli chenye maana ya kipindi cha utawala wa
Milenia wa Kristo. Siku zilijulikana kuwa ni ishara
ashirio la kipindi cha utawala wa miaka elfu kama anavyokitaja Mtume Petro
kwenye waraka wake (2 Petro 3:8). Kwamba kwa Bwana
siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.
Tunapouanngalia utawala huu wa miaka elfu sita wa Shetani kuanzia mwaka 4004 tangu
uumbaji wa Adamu na hadi kufikia mwaka 1996/7, tunaona kuwa kipindi cha Milenia kilipaswa kiwe kimeanza.
Hata hivyo, Adamu asingehukumiwa kwa kufuata sheria
kwa kuwa alikuwa hajatimiza bado umri wa miaka thelathini. Aliumbwa akiwa ni mtu mzima tayari (akiwa na umri wa takriban miaka
ishirini) lakini alipaswa kufikia umri wa thelathini ili kuwa mtu mzima wa
kustahili kuhukumiwa, ni umri muafaka ambao Kristo aliufikia.
Kristo alibatizwa
na kujaribiwa mnamo mwaka 27BK, mwaka alioutangaza
kuwa ni wa Yubile au “mwaka wa Bwana uliokubaliwa” na kisha akaenda kujaribiwa
nyikani. Mnamo mwaka 3976KK, Adamu alijaribiwa na
akashindwa na kuanguka na ile bustani ikafungwa. Na kipindi
kipya cha yubile kwenye dunia iliyolaaniwa kilianza. Na kwa kipindi chote cha yubile 40 dunia ilipewa fursa ya
kutubu lakini haikufanya hivyo, na nddipo Mungu aliiangamiza kwa gharika kuu
dunia ile ya wakati ule, na kisha akamuita Ibrahimu kutoka Uru ya Wakaldayo ili
aandae ujio wa Masihi ambaye hatimaye alikuja baadae katika kipindi cha yubile
40 ziliyofuatia. Kisha Mungu akalianzisha Kanisa lake likiwa ndiyo Hekalu lake
Mungu na akalipa kipindi kingine cha yubile nyine
arobaini za kiindi kijulikanacho kuwa ni cha kanisa kuwa jangwani. Kipindi cha
miaka elfu sita cha utawala wa Shetani kinaishia mwaka
2027. Yubile hizi 120 zinafanya jumla ya miaka elfu sita.
Maadhimisho ya imani ya Yubile ya miaka 49 ni alama ya
mashambulizi na upotofu wa shetani ulilenga Kanisa la Mungu ili lidanganyike na
lisiuelewe mpango wa Mungu. Mungu ametupa mashahidi wawili; au twaweza pia
kuwaona kuwa ni wanne, lakini mmoja amewekwa kwenye
kundi la watatu. Mmoja huyu kati ya mashahidi hawa watatu alikuwepo siku za
nabii Musa na mwingine alikuwa kwenye Maongozi ya
utawala wa Wafame wa Israeli. Maana yake yameelezwa kwenye majarida yafuatayo: Utawala wa Wafalme Sehemu ya I:
Sauli (Na. 282A) [Rule of the Kings Part I: Saul (No. 282A)] kwenye wavuti
ya http://www.ccg.org/english/s/p282a.html;
Utawala wa Wafalme Sehemu ya II:
Daudi (Na. 282B) [Rule of the Kings Part II: David (No. 282B)] kwenye wavuti
ya http://www.ccg.org/english/s/p282b.html;
na Utawala
wa Wafalme Sehemu ya III: Suleimani na Ufunguo wa Daudi (Na. 282C) [Rule of the
Kings Part III: Solomon and the Key of David (No. 282C)] kwenye wavuti
ya http://www.ccg.org/english/s/p282c.html.
Mwaka wa 2012 kwenye mfumo wa
Kichina
Sio jambo lililotokea kwa bahati mbaya tu kuwa mfumo huu ulifanyizwa ili kwamba Mwaka 2012 uwe ni mwaka wa Joka mkuu na mwaka unaofuatia wa 2013 uwe ni Mwaka wa Joka. Mgongano wa kipindi zama cha kuanzia Mwaka wa Duma wa 2010 ni mwanzo wa mgogoro na juhudi kuelekea kwenye mwaka wa 2013. Waokalisti na Waabudu Shetani wanaamni kuwa wataitawala dunia yote kuanzia mwaka 2013.
Mpango wa Shetani
Kwa kweli, hatuna mambo mengi sana kutufanya tuweke wazi sana kuhusu njama zake, bali tunapaswa tu kujua zaidi kuhusu hizi yubile, na kile ambacho Shetani anakusudia kukifanya. Biblia inatuambia kuwa anachotaka kufanya ni kuiangamiza dunia hii yote na itaingia kwenye giza. Shetani anajua pia kwa mujibu wa Biblia kwamba Kristo anatumwa ili kukifupisha kipindi chake, na vinginevyo kusingekuweko na yeyote mwenye mwili angaliyebaki kuwa hai.
Tangu kuangua kwa mji wa Yeriko na maelekezo aliyoyatoa Masihi akiwa ni Kapteni Shujaa wa Jeshi la BWANA tunajua kuwa ni lazima Kristo awepo hapa kwa miaka saba kabla ya ule Mwaka wa Sabato utakaokitangulia kipindi cha utawala wa Milenia. Ili uueleze unabii huu, jisomee jarida letu liitwalo Kuanguka Kwa Yeriko (Na. 142) [The Fall of Jericho (No. 142)] kwenye wavuti ya http://www.ccg.org/english/s/p142.html.
Shetani anajua kuwa ni lazima Torati itasomwa kuwa ushuhuda na kuwa Mungu hana jambo lingine zaidi ya kufanya maonyo tu kwa watu wake, kazi atakayoifanya kupitia watumishi wake manabii. Katika Siku hizi za Mwisho anafanya hivyo kwa kulitumia kanisa. Torati hii imesomwa sasa kwa vipindi viwili vya miaka mitakatifu ya Sabato vya miaka ya nyuma ya 1998 na 2005. Mmwaka unaofuatia wa Sabato utakuwa ni 2012 na Torati itasomwa tena mwaka huo. Hii itakuwa ni mara ya tatu kwa Torati kusomwa tena kwenye Mwaka wa Sabato. Kuanzia siku ya Mwandamo wa Mwezi wa Nane, Shetani ataruhusiwa kuwafungulia Mpingakristo na Manabii wa Uwongo waanze kazi hapa duniani. Ni kipindi kitakachojiri kati ya tarehe 21 Desemba 2012 na Kuja kwa Masihi zikipigwa Baragumu mwaka 2019. Kitakuwa ni kipindi cha Ibilisi kuwadanganya wote wakaao duniani na kuwaangamiza.na kurudi kwakwe Mwokozi.
Anajua pia kuwa wakati huu wa kipindi chake, Mashahidi Wawili watakuja kuwaonya watu dhidi yake. Ndipo Eliya atarudisha na kuyafanya upya mambo yote, ikiwa ni pamoja na kuwaonyesha watu Umuhimu na Heshima ya Torati. Kwa hiyo, wakati Eliya atakapokuja na kufundisha umuhimu wa Torati, utawala wa Shetani utakuwa umekoma kabisa. Ukweli huu unatupa matumaini makubwa kuhusu kipindi hiki. Hata hivyo, hawa vibaraka watapigwa na kushindwa.
Mpango wake ni kuanzisha na kuendeleza Udanganyifu Mkubwa mwishoni mwa kipindi hiki, udanganyifu ambao utawazoa yamkini hata wateule. Pia anajua toka mwanzo kuhusu mlolongo wa mambo wa siku za mwisho ulivyo na kipindi ambacho Heshima na umuhimu wa Torati itakavyorejeshwa na kipindi cha utawala wake kitakavyofika ukingoni. Ameufanya mwaka wa 2012 kuwa ni mwanzo wa mwisho wa kipindi cha kazi zake na ni mwaka atakaouwekea alama kwa watumishi wake wa harakati za kiokaliti wa kufanya mapenzi yake ya kupotoa na kuwaganganya mataifa ili wajitoe zaidi kwake kumwamini na kumtii kikamilifu sana.
Kwa hiyo, wanaharakati chafu wa kiokaliti wote wanapaswa kuwa sawa na mujibu wa mpango wake ulivyo na kwa mujibu wa alama za tarakimu zake na utaratibu wake kwa kufuatia vile zilivyofanywa na Mungu. Tangu mwaka ule mambo mwngi kufuru haribifu katika sayari hii na kumilikiwa kikamilifu na wao ni mchakato uliopangwa.
Malengo
ya Mpango wa Shetani
Mipango ya Shetani imewekwa wazi kwenye kwenye matamko ya watumishi wa harakati potofu za kiokaliti..
Jenerali wa Kimarekani, Albert Pike, aliwahi kuwafanya watu kuvutiwa na kupendezwa na alama ya Vidole viwili vilivyotumiwa na kuonyeshwa na Guiseppe Mazzini. Mwaka 1871, Pike, akiwa na cheo cha digrii ya 33 ya Kamanda Mkuu Mtukuka wa kanuni na tamaduni za Scotland anayeshughulika kuoanisha na Sheria za Wafreemasoni wa pande za Kusini, kazi ambayo aliteuliwa kuifanya tangu mwaka 1859, alimalizia kilele cha kazi yake ya kijeshi kwa kupigana vita vikuu vitatu vya dunia na kufanya mapinduzi kadhaa ya kijeshi sehemu kadhaa ulimwenguni.
Lengo la Kuanzishwa kwa Vita Kuu ya Kwanza Duniani: Lilikuwa ni kuwaondoa na kuliangamiza kabila la Tsar huko Urusi, kama ilivyokuwa imedhamiriwa na kuahidiwa na Nathan Mayer Rothschild mwaka 1815. Na baada ya kuwaangamiza hawa Tsar mahala pao palifanywa pachukuliwe na imani ya Kikomunisti iliyotumika kushambulia harakati zote njema za kidini na Wakristo wa kweli na wenye msimamo sahihi. Vita hii ilifanywa kwa kuwachonganisha wapigane vita Waingereza na Wajerumani.
Vita ya Pili ya Dunia ilifanyizwa kwa mbinu wa kuwagonganisha Mafashisti wajulikanao kuwa ni wa mrengo wa kushoto na Wanasiasa wa mrengo wa Kizayoni. Mauaji ya Wayahudi maarufu kama Holocust yalitumika ili kuvuta hisia za watu ili wawachukie Wajerumani. Lengo lilikuwa ni kukiangamiza kizazi chote cha Kifashisti cha Roths na kuzidisha nguvu za Wazayoni na pia kuendeleza nguvu za Ukomunisti ili uwe na nguvu sawa na ulimwengu mwingine wote qa Kikristo.
Wakati huo huo, ulimwengu uliobakia wa Kikristo uwe unaingiliwa kirahisi na wanaharakati kufuru wa Kiokaliti na wenye alama Mvutio waendelee na kufanikiwa kwenye maeneo yote na daraja zote za watu maarufu. Nchi ya Marekani ni kituo kukii cha kuweka mipango hii ya kuwafanya watu wautumie Ukristo vibaya kama walivyo mapadri wa Kirumi. Kipindi kilichofuatia baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia kilitumika kuendeleza mambo haya kwa nguvu zote na kwa mafanikio makubwa. Mipango hii haikukugundulika hapo mwanzoni kuwa ni sehemu ya mipango ya Pike bali ni ilikuwa na mkono wa Shetani kupangiliwa ukilenga matokeo ya mwisho ambayo tutajifunza hivi punde.
Vita Kuu ya Tatu ilitumika kuwaondoa Waislamu kutoka kwenye ardhi inayojulikana kisiasa kuwa ni ya Wazayoni, na kuuangamiza na kuuharibu ulimwengu wa Kikristo kwa kufanya njama za migongano inayochechewa na kulazimishwa na waokaliti kwa kuwatumia viongozi wao na vyeo vyao vilivyo namna ya kiakili, kimwili, na mfumo wa kidini au kiroho na kiuchumi.
Mnamo tarehe 15 Augost 1871 Pike aliandika waraka, na uko hadi leo kwenye Jumba la Makumbusho la Uingereza, akimwandikia Guiseppe Mazzini alimwambia mambo yafuatayo:
“Tutawaafungulia walewatakayoikufuru na kuikana imani yao na wale wanaoukana uwepo wa Mungu na tutauchochea moyo wa uamsho mkubwa wa jambo hilo kwenye jamii ambao kwa namna yoyote ile ya vitisho tutayaonyesha mataifa yote kwa waziwazi mafanikio makubwa ya imani hii inayomkana Mungu: chanzo au kiini cha ushenzi na zaidi zasa kwa kumwaga damu nyingi.
Kisha hapo, watu watalazimika kujilinda dhidi ya idadi hii ndogo ya watu walioko hapa ulimwenguni na wanamageuzi hawa ulimwenguni na watawakomesha wasiwepo watu hawa watakaoonekana kuwa ni hatari kwa ustaarabu wa dunia na watu wengi watakatishwa tamaa na Ukristo na kuachana nao, uamuzi ambao unatokana na hali ilivyo kwa kipindi kile pasipo kuongozwa muono na mapenzi yanayotoka na miyoni mwao, na pasipo kujua ya kinsi ya kufanya pambo zake, ndipo nuru ya kweli kwa kupitia mwonekano wa kidunia wa mafundisho ya Lusifeli yataletwa hatimaye kwa wazi wazi.
Mwonekano huu utapelekea kuwa na matokeo ya jumla ya harakati itakayofuatia kuangamizwa kwa imani za Ukristo na wakana Mungu, wote wakiwa wameshindwa na kukomeshwa kwa wakati huu.” (pia imeandikwa kwenye kitabu cha A.C. Hitchcock, kiitwacho The Synagogue of Satan [Sinagogi la Shetani], RCP 2009, kurasa za. 73-75)
Pike alikuwa ni Mfrimason mwenye nguvu na kuogopwa kuliko wengine wote huko Marekani na aliendelea kuwa tishio hivyo hadi mwaka 1891.
Kwenye kitabu chake maarufu cha Maadili na Mapokeo ya Zamakale na Kukubalika kwa Taratibu za Dinikale za Frimason wa Kiscotland, [Morals and Dogma of the Ancient and Accepted Rite of Scottish Freemasonry] Pike anaeleza kinagaubaga lengo la kishetani walilonalo Wafrimason. Aliweka taratibu za kidini kwenye ibada zenye lengo la mwelekeo wa kumwabudu Lusifeli lakini jambo hilo lilifanywa kuwa ni siri kwa watu wa kawaida na wenye kujua maana yake ni wale waliofikia kwenye shahada ya 28 hadi 32 ya mgawanyo wa vyeo vyao kuelewa.
Kuhusu masuala ya Maadili na Mapokeo ya dini kale alisema, “jina halisi na la kweli la Lusifeli, Wakabalisti wanasema ni lile ambalo Yahwe amelichukua: kwakuwa Shetani sio mungu mweusi, bali ni kinyume cha Mungu. Kwa utendaji, huyu sio Kiumbe bali ni Nguvu iliyoumbwa kwa ajili ya mambo mema, ambayo pia inaweza kufanya kazi mbaya. Ni chombo kinachofanya kazi za kuwepa watu Uhuru na kutimiza Makusudi yao yenye kukithi Utashi wao…
LUSIFELI, maana yake ni
Mleta-nuru! Jina geni na la siri ililopewa Roho hii ya
Giza! Lusifeli, Mwana wa Alfajiri! Je, si yeye
apelekaye Nuru, na uzuri wake usiovumilika na Roho za
vipofu, wagonjwa, wadhaifu, wapenda anasa na wabinafsi? Ndivyo
ilivyo na hakuna shaka!” (ukurasa
wa 75).
Usishangae kuambiwa kwamba vita hivi vitatu vya Dunia vilipangwa tangia miaka 120 iliyopita huko Marekani na Mwamerika huyu Mfrimason na mbinu za kufanikisha tangu kipindi hicho hadi kukamilika kwake ulifanywa na maafisa waliomfuatia wote hadi wale walioukamilisha.
Matukio yanayoendelea leo dhidi ya Uislamu ni matokeo ya mambo yaliyoratibiwa siku nyingi na mpagao wenye jazba unaojitokeza dhidi ya Uislamu na Ukomunisti kwa upande wa Magharibi ni mambo yaliyoratibiwa na Wamarekani hawa hawa kwa ujanja na mbinu za hali ya juu wakiwa sambamba na waokaliti kwa lengo la makusudi la kumtumikia Shetani wakisaidiwa kiuwezo na taifa la Marekani na kwa mataifa yote yaliyo kwenye Jumuia ya Madola iliyo chini ya dola ya Uingereza.
Taratibu za Kitarakimu za Waokaliti
Tarakimu zenye maana na umuhimu kwa imani hii ya watu waliomuasi na kumkana Mungu 33 na 13. tarakimu hii ya 33 imechukuliwa kama ukumbusho na nembo ya tukio la kukumbushia jinsi Shetani alivyochukua kwenye uasi wake theluthi mojo (moja ya tatu) ya malaika au pengine huandikwa 33.33 ikimaanisha marudio tu yanayosisitizi kumbukumbu ya tendo hili. Hii ndiyo inamaana moja kwa kilichopelekea kipimo cha bikari kimeundwa kwa mtindo wa pembe tatu ililenga kuitukuza tarakimu hii ya 33 ambayo pia ni tarakimu ya mwisho kwa cheo cha juu sana cha ofisa wa juu zaidi wa Frimason kwa mujibu wa mfumo wa vyeo vyao ulivyoratibiwa na waokaliti. Ni tarakimu inayowakilisha anguko la hawa Malaika waasi.
Malaika hawa waovu walishuka na kukutana kwenye mkutano wa Mlima Hermoni. Hii ilichaguliwa kwa kuwa inasimama na kushabihiana na tarakimu hii ya 33.33 yenye nyuzi mlalo za maili 2012 toka kwenye nyuzi 0 za ikweta. Hivyo basi alama hii inaenda sambasamba na utaratibu wa Malaika hawa Waovu na walipewa kipindi maalumu kilitolewa na kikawekwa.
Tarakimu muhimu sana nyingine kwa waokaliti ni 3 ambayo wanamhusisha Henoko aliyekuwa ni shahidi muhimu sana aliyesimama kinyume chao. Henoko alitwaliwa kwa mazingira tatanishi na ya siri kubwa kwa wanachosema wao umbo la siri la Metraton na umbo hili linamaanisha kuwa ni umbo kuu la kifumbo isiyojulikana akilini hata kwa mapepo. Wanaamini kuwa kama ilivyomtokea Metraton, Henoko alifanyika kuwa “Malaika kwenye upepo wa Kisulisuli.” Waokaliti wa kale waliwatumia wanajimu na waliunda vikundi maalumu vya kiokaliti na kamati za watu 300 wasomi kama watu wenye kuwahabarisha mambo muhiumu.
Aina hii ya imani fichivu potofu za siri inahusika pia na utoaji kafara watoto wadogo kwenye ibada zao na imani hii inahusianishwa na sherehe zilizofanywa kwenye Misitu ya Wahemiani na ibada zilizofanywa kwa kuwachoma moto na kuwateketeza watoto wachanga au kwenye ibada za sanamu inaitwa “Kutunza Kinyago”.
Wakati wataalamu wa mambo ya nyota au wanajimu wa kale, na ambao walikuwa wataalamu hasa, walipoweka alama za nyuzi wima za mzingo wa dunia, waliifanya nyuzi 0 ya wima za dunia kuwa kwenye kipimo cha maili 2012 kuelekea pande za magharibi mwa Mlima Hermon katika kuipa heshima zaidi tarakimu hii ya 33.33 inapotumika kama alama ya nyuzi wima na kuifanya tena tarakimu hii ya 33.33 iwe kwenye nyuzi mlalo.
Kilakitu kwenye mfumo wa kalenda zao na kwenye mifumo yao mingine ilifanyizwa kwa kufuata mlingano wa tarakimu hizi. Kwa hiyo, mpango kazi wa muda mrefu ulifanywa kuwa endelevu kwa miaka maelfu iliyopita. Walifanya hivyo kwa kuwa hivyo ndivyo Mungu alivyowapa kuwa ni kikomo cha wakati.
Magonjwa
hatari ya kuambukiza kwa njia ya virusi katika Duniani
Miongoni mwa mambo wanayofanya watu hawa wenye kumuasi Mungu ni mikakati ineyolenga kuangamiza wanadamu kwa kutengeneza virusi vya mangamizi na magonjwa hatari ya kuambukiza. Maafa haya yanafanyizwa kwa makusudi mazima na watu hawa waabudu Mashetani. Wanafanya hivyo kwa maslahi ya kuvipatia faida kubwa viwanda vyao vya madawa. Kwa kufanya hivyo wanakuwa pia wanatimiliza azima yao ya kupunguza idadi ya watu duniani. Lengo lao ni kupunguza idadi ya watu duniani hadi ifikie watu milioni 500 tu, idadi ambayo wanataka iwe Waabudu Shetani hawa, lakini lengo hasa la shetani sio hilo tu bali ni kuwaangamizilia mbali na kumkomesha mwanadamu asiwepo hapa duniani.
Pale kwenye Mnara wa Babeli lilitokea tukio kubwa sana ambapo watu walichafuliwa lugha zaao na ghafla wakajikuta wamebadilika lugha zao na kuanza kusema vingine kwa namna ndimi zao zilivyoongozwa kutamka (Mwanzo 11:1-9). Jambo hili lilifanywa na Yehova.
Namna rahisi sana katika kutimiza lengo hilo ni kwa kupima vinasaba vya ukoo (DNA) kwa mataifa kwa kuwachafulia lugha zao. Nia ilikuwa ni kuwatawanya na kurudisha nyuma kasi yao ya kimaendeleo.
Kwa kweli, Horn anapingana na yanayosemwa kwenye Mwanzo 10:8 inavyosema kuwa Nimrodi alianza kuwa mtu hodari na mwindaji mbele za BWANA, akisema kuwa imetokana na neno Gibbowr (Kamusi ya SHD 1368) ambalo lilitumika kuwaelezea Wanefili, likimaanisha mtu aliyetokana na mabadiliko ya umbo lake na akaanza kuwa ni Mnefili (Kitabu kichohicho cha Horn, uk. 194-195).
Kwa vyovyote vile, viini vya kinasaba na mnururisho sio tu kuwa vinawezekana bali pia ni vitu vilivyo dhahiri.
Mpango wa kupunguza idadi ya watu duniani umekwisha ongelewa tayari na na uko kwenye vipaumbele vya watu wa tabaka hili la waokaliti.
Kitabu cha Mwanzo 6:2 kinasema kwamba Wana wa Ha Elohim au Wana wa Mungu walitwalia binti za wanadamu. Waliowaona kuwa wanafaa kuenezea mchakato wao wa kuzaa na kuongezeka hawa wana wa Mungu.
Ndio maana ilipingwa kuamini kuwa hawa Wanefili au uzao wa viumbe hawa ulitokana na mwingiliano huu wa Kinasaba na mbegu za Wanadam, kama inavyoelezewa kwenye maandiko ya Kitabu cha Henoko, na Kitabu cha Yubile vinaashiria ukweli wa jambo hili. Imeelezewa vema kwenye Kitabu cha Henoko (1 Henoko 10:3-8), na vitabu vya Yubile, Baruku, kitabu-kivuli kisocho rasmi (Apokrifa) cha Mwanzo na viliaminiwa sana na wanazuoni kina Philo na Josephus na tunaikuta hadithi hii pia kwenye kitabu cha Yasheri kwenye sura ya 4:18 ambako panaeleza wazi kuwa mchanganiko mbegu za wanyama ulimkasirisha Bwana.
Ni hakika sana kwamba Nuhu aliokoka kwa kuwa hakujichanganya kinasaba ya damu (DNA) na kuwa alikuwa mkamilifu kwenye uzao wake.
Kile wanachoona wataalamu wa mambo kale kinacyohusiana na jambo hili ni kwamba Maangalizi walianza kufanyia uzoefu wa kimatendo kwa kuchanganya mbegu za wanyama na waliadhibiwa kwa ajili ya kufanya hivyo na pia walipofanya matendo ya kujamiiana na wanadamu wanaume. Inaonekana kuwa watu hawa walianza kuwachukua wanawake na kuchaganya nasaba zao za DNA mbegu za wanadamu na nasaba za wanyama au utaratibu kama huo sambamba na ule wa kwao waliojifanyia.
Jaribio hili la kuchanganya damu kati ya wanyama na wanadamu linapelekea kwenye mwelekeo wa mwisho uleule ulioko sasa wa kama ilivyokuwa kipindi Wanefili walipokuwepo duniani.
Tunaweza kutarajia kuona ikitokea tena. Ipo kwenye mchakato huo sasa na maroboti wanatumiwa kwa matimizi ya kimawasiliano na mengineyo ya kisayansi kwenye mambo ya kivita.
Sayansi itatumika tena katika kupanua wigo na kuendeleza malengo na utawala wa Mapepo.
Horn ameeneza mtazamo huu na kuwanukuu wafuasi wa okaliti kwenye mtazamo huu. Anasema hivi:
“Osiris afufuka toka kwa wafuna kuanza enzi yake akiwa na utukufu na kutawala ulimwengu na watu wake watukufu na wanafalsafa ambao kwao hekima haikomi” (Manly P. Hall, 33 Ofisa Mfrimason mwenye Shahada ya 33).
“Dunia itakuja kwetu kwa hali ya utukufu utakaotokana na Wafalme maarufu na Mapapa. Tutaweka utaratibu utakaoleta usawa katika hii Dunia, na kuwa watawala juu ya Bwana wa hii Dunia” (Albert Pike, Kamdanda Mkuu Mtukuka wa Mapokeo ya Wasotland ya Kifrimason).
Nilikuwepo jana na nipo pia hata Leo, na nina uwezo wa kuzaliwa kwa mara ya pili (Nukuu toka mawazo ya Osiris kutoka kwenye kitabu kiitwacho Kitabu cha Wafu wa Misri [Egyptian Book of the Dead] (nukuu za Horn, ukurasa wa 181).
Kwa kweli, kitabu hiki kinachojulikana kama Kitabu cha Wafu kinamtaja Osiris kuwa alifufuka, na kwa mujibu wa tafsiri ya E. A Wallis Budge ya Kitabu cha Wafu [The Book of the Dead] (Arkana 1986) anasema kwenye Sura ya XVIII (uk. 116) kwenye maandishi ya chini ya kurasa ya kitabu 2 kwamba “Tet” alisimamishwa kwenye maadhisho ya kumbukumbu za kila mwaka ya mwili uliofufuka wa Osiris, maadhimisho yaliyofanyika kila mwaka huko Mendes. Tet anaonyeshwa akiwa na hali ya sanamu lilonakshiwa vizuri kwenye sura ya CLV kwenye ukurasa wa 521 wa kitabu hiki, ambapo kunafuatia maombi ya kumuombea Osiris Afufuke kwenye kurasa za 518-520.
Waabudu Shetani wanaamini pia kuwa wanauwezo dhidi ya ufufuo, yaani watafufuka, na kisha wataitawala tena hii Dunia kwa mfumo endelevu usiokoma.
Kwa hiyo, wanaamini kuwa vita inayofuatia itakuwa ni kwa wao kupigana na wafu ili waitawale hii dunia na vyote vilivyomo.
Mhuri
na Alama Kuu ya Nchi ya Marekani
Mnamo mwaka 1933 Rais Franklyn Delano Roosevelt (inaaminika kuwa huyu Rosenfelt ambaye ni wa uzao wa Claes Martenzen van Roosevelt, Msefarvaimu Myahudi wa Kidachi aliyehamia Marekani) aliamuru kurudishwa kwa Mhuri Mkubwa na Jicho la Horus na kauli-mbiu isemayo Novus Ordo Seclorum iliwekwa kwenye upande wa nyuma wa Sarafu-noti ya Marekani.
Mhuri wa alama ya nchi ya Marekani una mlolongo wa alama za siri za waokaliti na yule ndege anayeonekana ambaye wengi hudhani kuwa ni tai, kwa kweli sio tai bali ni finiki ambaye ni ndege mwenye hadithi yake ndefu kama anavyoonekana jinsi alivyochorwa kwenye uandishi wa kale. Sikusudii kwenda kwa kina kuelezea alama zote hapa ila inatosha tu sasa nishughulike na ile nembo maarufu kama Capstone iliyobandikwa na yenye jicho la Horus ikiwa limewekwa sambamba na mawe sabini na mawili.
Kwa mujibu wa kitabu cha Kumbukumbu la Torati 32:8, mawe sabini na mawili yanawawakilisha wana wa Mungu ambayo ilikujatumiwa na Wakabalisti wa Kisoferimu kuwabadilisha Watu wa Mungu. Hawa sabini na mbili ni wakuu wa mataifa na mpango uliopo ni kuwashirikisha kwenye malengo ya matimizi ya kiokaliti kwa mtindo wa Kitetagrama kama jina la Mungu ili kuwafanya watawaliwe na dunia ishirikishwe kwa malengo fanikishi ya waokaliti ambao ni waabudu Shetani.
Tarakimu hii 1776 sio mwaka wa tukio hili ingawa ni mwaka wa kuanzishwa kwa alama ya vidole viwili vyenye maana na kichawi ya kuvuta watu iliyoanzishwa na Adam Weishaupt.
Mwaka huu ulitukika pia kumtangaza Masihi wa Sibylline Oracles kuwa ni watu wawili wanaoitumia thamani ya kitarakimu ya Sybil kwa jina la Masihi. Tarakimu ya mungu Apollo kuwa ni Masihi inadhaniwa kuwa jumla yake ni 888. Masihi hawa wawili wa tarakimu 888+888=1776. Kwa hiyo, tarakimu hii 1776 ilitumika kuwa ni mwaka wa kutangaza matayarisho kipindi cha kubadilika kutoka Kristo Masihi, na mwanzo wa Apollo akiwa na uweza wa Kishetani mnamo mwaka 2012. Hili lilikuwa ndiyo hasa lengo la kuanzishwa kwa taifa la Marekani.
Kitabu maarufu cha Wabashiri kiitwacho [The Oracles state in Book 1: 324-333]:
Ni hakika kuwa hatimaye Mwana wa Mungu mkuu atakuja, atakuja katika mwili, akifanana na wanadamu wa kawaida wenye kufa hapa duniani, jina lake litakuwa na vokali nne na konsonanti zitakuwa mbili. Nitazitaja kinagaubaga tarakimu zako zote. Kwa yuniti nane na tarakimu sawa na kumi zitaongezwa mbele yake na mia nane watalifunua jina hilo kwa watu wanaokinai uaminifu. Lakini mjue moyoni mwako Mwana wa Aliye Juu, Mungu aishiye milele, asiyeweza Kufa. Yeye ataitimiliza Torati ya Mungu-hata iharibu wala kuikiuka-ataenda kwa kuifuata na kuitii, akienda sawasawa, naye atafundisha kila kitu… kwa mujibu wa mkufunzi J.J. Collins kwenye kitabu cha James H. Charlesworth mwenye shahada ya elimu kiitwacho: Maandiko ya Kiurembo [The Psedepigraphical Writings], Toleo la 1, Mbashiri wa Sibylline [Sibylline Oracles] 1, p. 342 1:324-333).
Kama tulivyojionea wenyewe jinsi waabudu Shetani hawa wanavyoitumia tarakimu hii ya 888 ya Wabashiri wa Kisybile kumchanganya Masihi na kumweka kwenye dhana yao ya kurudi kwa mungu Apollo, na kisha kuongeza umri tangu mwaka 1776 hadi 2012 ambalo ndilo lengo hasa la kuanzishwa kwa taifa la Marekani.
Kuna tarakimu za maana kwenye somo hili na Horn ni mfano mzuri.
Alama Kuu ya taifa la Marekani ni ule mnara mrefu ambao ni alama ishara ya jumuia ya Waokaliti inayofanya kazi na Mafrimason wakishirikiana pamoja na Wailuminati na jumuia ngingine zinazofanya kazi zake kwa siri kubwa kwa ujumla wake.
Horn anamnukuu pia Manly P. Hall (ofisa wa ngazi ya shahada ya 33 wa Grand Master) akisema:
“Sio tu kwamba mwengi wa walioanzisha taifa la Marekani walikuwa ni Frimason, bali pia walipokea misaada iliyotolewa kwa siri na jumuia au taasisi adhimu na yenye heshima kubwa iliyoko Ulaya, taasisi iliyosaidia sana kuundwa kwa taifa hili kwa lengo la kipekee na kwa namna yake ambavyo linatakiwa kujulikana na watu wachache tu. Mhuri ule Mkuu ni saini ya taasisi tukufu-ambayo na haijulikani na wengi-na lile piramidi linaloonekana halijaisha kwa upande wa nyuma ni taasisi inayotegemewa iliyowekwa lengo la kuashiria kazi inayotakiwa ikamilishwe aambayo ndiyo kwayo Serikali ya Marekani ilipewa jukumu lake tangu kuanzishwa kwake.” (Kitabu hicho hicho cha Horn, ukurasa 123)
Kwa hiyo tunaona sasa kuwa taifa la Marekani ni chombo cha kuitumikia na kukamilisha dhana ijulikanayo kama Agizo Jipya Ulimwenguni na kuweka kongwa kwa jamii za wanadamu. Mataifa ya Marekani na Uingereza ni majeshi ya Kivita ya nguvu za Mnyama, kwa kipindi hiki na hadi pale matumizi yake yatakapofikia ukomo.
Kauli mbiu ya hii ijulikanayo kama Agizo Jipya Ulimwenguni iliyo kwenye mhuri kweli inaashiria kuanzisha tena kwa zama ya ujima chini ya nifumo Siri ya waokalisti ambayo kwa kweli inalenga kuyapa heshima mapokeo ya Nimrodi na Osiris na motto wake au kumbe wanayedai alifufuka Horus. Ndiye mungu Apollo na kwa miungu mingine mbalimbali ya kisiri ya dini potofu ambayo kwayo alijigeuza kuwa kama mungu aliyewahi kufa na Akafufuka. Wote hawa ni miungu walewale – Osiris, Apollo, Adonis, Attis na Nimrodi. Apolioni aliyeandikwa kwenye kitabu cha Ufunuo anadhaniwa kuwa ni mungu huyuhuyu (pia tazama kitabu cha Charles Penglase, cha Dini za Siri za Wayunani na Wamesopotamia: Usawa na Ushawishi kwenye Tenzi za Wahomeri na Waheaiodi [Greek Myths and Mesopotamia: Parallels and Influence in the Homeric Hymns and Hesiod]). Penglase anaifungamanisha miungu hii pamoja na kumrudisha nyuma Nirurta, Mfalme Enmerkar wa Uruk, au Nimrodi (soma pia kitabu cha Peter Goodgame, cha Kuvumbuliwa kwa Giza [The Giza Discovery] pia na Horn, ukurasa 135).
Hii ndio sababu mfumo wa taifa la Marekani umefungamanishwa sana imani ya watu wanaoamini miungu Miwili na wa Utatu wa miungu Attis, Adonis, Osiris, Baal na wanajiingiza kwenye kila shirika na taasisi ili kulazimisha mwendelezo wake. Inaweza pia kuwa kanisa la World-wide Church of God ilikubwa na masahibu haya hadi watumishi wake kujikuta wameingia kwenye mfumo wa kinachoitwa Mesoamerican ambao waliupendelea sana.
Miungu hii limwakilisha Horus akiwa kama mungu aliyefufuka kwenye imani yao ya Kimashetani kuwa ni mungu Angojewaye Kurudi ambaye ni “mtoto mtukufu” ajaye toka mbinguni kuja kuanzisha ufalme wake. Picha za mtoto mdogo zimefanywa na mafundi ujenzi mjini Washingaton DC.
Kile kinachosubiriwa na waabudu Shetani hawa ni jambo lililosemwa tangu zamani na ndilo lilikuwa kusudi halisi la kubuniwa kwa taifa la Marekani likiwa chini ya uongozi wake wa Kiokaliti. Waabudu Shetani hawa walio kwenye mkakati wa shirika la Agizo Jipya la Mfumo Mmoja wa Mambo Duniani watajaribu kuleta Agizo Jipya la Mfumo Mmoja wa Mambo Duniani kwenye utawala wa dunia na watatumia mamlaka yake kuharibu moyo mwema wa wanadamu duniani na kutumia nguvu zake zote kuzuia utendaji kazi wake.
Jambo walilokosa kuligundua ni kwamba wanatumika ili waendeleze mamlaka yao na hatimaye waitawale hii dunia ili kwamba mapepo yaweze kumwangamiza kabisa mwanadamu, na pasipo kuwaacha wao.
Horn anaendeleza wazo hilo kwenye kitabu chake cha Ugunduzi wa Giza (Discovery at Giza) kwa kusema kuwa watatumia vipomo vya vinasaba ukoo wa watu (DNA) vitakavyoonekana ili kuweka uthibisho wa Osiris na kumfufua.
Watakachokifanya ni kuweka kitu chenye mwonekano mbadala ili wayaachilie mapepo kutoka kwenye Shimo refu waliko leo waje na kuendeleza mchakato wao wa kuwatesa na kuwaangamiza wanadamu kama ilivyotabiriwa kwenye kitabu cha Ufunuo. Hii itafanyika bila kujali kama wamemkuta Osiris au la. Watakachokifanya ni kuleta kitu kitakachokuwa ni mbadala wake kutokana na mapepo na anaweza kuwa yeyote miongoni mwao.
Hili ndilo kusudi la hawa waabudu Shetani na ndilo wanalolifanyia kazi kwa kipindi cha karne na milenia kadhaa hadi sasa, wakiwa wameanza kipindi kirefu sana hata kabla ya kuundwa kwa taifa la Marekani.
Mwaka
2016 na mikakati ya waokaliti
Mabashiri haya ya kiokaliti kuhusu mwaka 2012 pia yana kipindi tangulizi cha miaka mitatu na nusu kabla ya kuufikia mwaka 2016. Pia kina maashirio mengi yahusuyo matukio yatakayotokea katika siku za mwisho. Jambo hili kwa jinsi lilivyo linaonekana kuwa limetokana na unabii wa uwongo au tasfiri potofu ya Danieli 9:25 inayotumiwa sana na dini zinazoamini Utatu hasa zilizoko Marekani. Juma la miaka lisemwalo kuweko siku za mwisho litatumika kuashiria kipindi cha tangia Sabato ya miaka ya 2012 hadi kwenye mwaka wa Sabato wa 2019. Kuna wengine miongoni mwa hawa waamini Utatu wanamifumo yao ya kuhesabu inayojaribu kuhusianisha kipindi hiki kuwa kinaaanzia mwaka 2009 wakati kazi za Mpingakristo zitakapoashika hatamu zake lakini kama tunavyoona kuwa hadi leo wale Mashadihi Wawili hawajaanza huduma zao mjini Yerusalemu. Waamini Utatu na Unyakuo watajaribu kuweka madai yao kwamba kazi ya Mpingakristo iliamriwa kuanza rasmi mwaka 2009. Hata hivyo, kukomeshwa kwa huzuma-kazi ya Eliya kunabidi kusimame kidogo ili kuwezesha mchakato wake uendane sawia na unavyotakiwa. Horn anaamini kuwa kipindi hiki cha siku tatu na nusu cha kutoka tarehe 21 Desemba 2012 na hadi tarehe 25 Desemba 2012 henda kitakuwa ni cha vifo vya hawa Mashahidi ambao wamebakiwa na siku tatu na nusu (3.5) tu lakini hii haimo kwenye mchakato huu. Inawezekana sana kuamini kuwa kipindi hiki kitadumu kwa miezi 42 ya Mamlaka na uweza wa yule Mnyama na mamlaka yao ya kiutawala yatafikia ukomo kwenye kipindi hiki huko Mashariki ya Kati na Ulaya. Mfumo wa Waamini Utatu hautaonekana kuwa ni wa kweli hasa kwa jinsi wanavyochukulia hesabu za tarehe na nyakati na unasababisha migongano ya kimpangilio (iko kwenye kitabu cha Horn, ukurasa 267 nk.).
Ili kuweka vipindi hivi mahala pake, kupata kipindi cha kizazi fulani, waliongezea kipindi cha miaka sabini cha kuishi kwa mwanadamu na wakitafsiri hivyo Mathayo 24:34. Hatahivyo, kwa mujibu wa mapokeo na kiunabii, kizazi kimoja kinachukua kipindi cha miaka 40 na sio miaka 70. Horn anaeleze pia hivyohivyo kwenye kitabu chake ukurasa wa 270. Kwa hiyo, kipindi hiki kinachukuliwa kuwa ni cha miaka sabini kwa hesabu za kuanzia mwaka 1948 na ndipo lilipoanzishwa tena taifa la Israeli na kitaendelea kudumu hadi mwaka 2018 ambao utaishia kwenye mwaka unaofuatiwa wa 2019 kwenye siku ya Mwisho ya mwezi wa Adari, lakini ni jambo linaloonekana kuoeleweka na wengi (Kitabu cha Horn, ukurasa wa 270). Na kuna wengine wanaodhani kipindi hiki kuwa kitachukua mkondo wake na kudumu kwenye miaka kati ya 2012-2019 kikiwa ni cha kudumu kwa miaka saba. Hatushangai, ni kwa kawaida Mungu huleta mabadiliko makubwa kwa kuitumia Kalenda na yaliyomo kwenye Torati yake na kwa hiyo, mwaka wa Tatu kwa kawaida ni mwaka kuutumia kufanya mabadiliko makubwa ili kwamba amri zake zisivurugwe au kupuuzwa. Tunajionea pia kwamba hata Gharika Kuu ilitokea kwa kufuata mpangilio huuhuu wa Sabato ya miaka. Mwaka wa Tatu wa mzunguko wa pili unaanzia siku ya 1 Abibu ya mwaka 2015 hadi siku ya 1 Abibu ya mwaka 2016. Ikiwa basi kama Huduma-kazi ya Mashahidi hawa itaanza mwaka 2012 ambao ni mara ya Tatu katika kusoma Torati, basi itamaanisha kuwa kipindi cha siku 1263.5 kitaishia ndani ya miaka hii ya 2015/16. Na hii itamaanisha kuwa matarajio ya Masihi kurudi na kukifupisha kipindi hiki na kutawala pamoja nasi akija kwa sauti ya mlio wa Tarumbeta kuwa ni kati ya mwaka 2015 au 2016 au pia inaweza kuwa mapema sana kwenye mwezi wa Abibu wa mwaka 2017, kutegemea ni lini hawa Mashahidi wataanza kazi yao, kama itakuwa ni tangia sikuya 1 Abibu au siku ya Baragumu. Tunachotakiwa kujua tu ni kwamba kipindi hiki kitakuwa ni chenye dhiki ile kubwa kabisa.
Kwenye kabrasha la mikanda ya sinema ya Wakabalist lililotolewa kwenye kijiji cha maigizo cha Wamarekani maarufu kama Hollywood linatoa ashirio fulani kuihusu miaka ya 2012 hadi 2018 kuwa ni kipindi cha mwisho cha hukumu kuu. Hata hivyo, miaka mingi ya huko nyuma kabla yake kipindi hiki kiliaminiwa kuwa kingeishia mwaka wa 2027 (ambao pia ni wa Yubile). Kikomo halisi cha kipindi hiki ni mwaka 2025 kwenye Mavuno ya Kwanza au Malimbuko ya Sabato na Yubile ya mwaka 2026-2027. Miaka saba inayotangulia kabla kufikia kipindi hiki ni Abibu ya mwaka 2018. Kwa hiyo, tunatarajia kurudi kwa Masihi kwenye mwaka wa 2018 na Mashahidi kuanza huduma yao tangia mwaka 2014 kwa mlio wa Baragumu ikiwa ni vitu vitakavyotokea kihalisi na katika ukamilifu wake. Kinatarajiwa kuwa kitaishia kwenye mwaka wa 2025.
Uislamu
na Mwaka huu wa 2012
Horn anachukua nukuu za kusisimua sana kutoka kwa mwandishi maarufu wa Kiislamu ambaye ameandika akichukua mawazo-dhana ya mwandishi mwenzake aliyeandika kijitabu kiitwacho Siku ya Hasira, [The Day of Wrath], kilichondikwa na Safar Ibn ‘Abd Al-Hawali aliyeanika na kukiweka kwenye wavuti yake ya www.IslamicAwakening.com:
“Wakati nabii Danieli alipoonyeshwa kipindi cha kati ya uteka wake na kuachiliwa kwao, kipindi cha kati ya mateso na kubarikiwa kwao, alikionyesha kana kwamba ni cha miaka abobaini na tano tu! Tumejionea pia kuwa alikielezea kipindi cha kuwekwa kwa chukizo la uharibifu kuwa ni kama mwaka 1967, ambao ndio hasa ulivyotokea. Kwa hiyo ni dhahiri sana kwamba hatima-au mwanzo wa mwisho-utakuwa ni mwaka 1967+45=2012.”
Kwa hiyo, tunapaswa kujua kwamba iwapo kama Mpingakristo ataanza kazi zake mwaka 2012, basi Waislamu watakuwa wamepotoshwa kuambiwa kuwa chukizo la uharibifu limeanza kuchukua mahala pake tangu mwaka 1967 wakati mji wa Yerusalemu ulipochukuliwa na jeshi la Israeli kwa nguvu.
Mwaka
2012 na Wabudha wa Kitibeti
Kwa miaka kadhaa sasa tumekuwa tukitaarifa za mara kwa mara kutoka kwa watawa wa Kitibeti wa dini ya Kibudha na kwenye taarifa zao mpya wanasema kuwa dhiki kuu sana itatokea mwaka 2012 na kwamba sayari nyingine zilizo nje ya dunia yetu zilizokuwa mbali na dunia zitafanya zitaingilia kati kuiokoa.
Mtu anaweza kujionea vema kuwa dodoso hizi zinatufanya tuamini kuwa Waangaliaji hawa wanakuja na kuinglia kati kuokoa sayari yetu hii. Swali kuu tunalobaki tukijiuliza ni kwamba ni kina nani hao wanaokuja kutuokoa? Mashetani wanaweza kujitokeza kwa mwonekano wa kama malaika wa nuru kwenye udanganyifu huu mpotofu wa siku za mwisho. Ni hakika tunapaswa kuwatarajia kufanya hivyo.
Maandalizi
ya Kuyumba Kwa Uchumi Mwaka 2012
Matatizo ya Kuyumba kwa Uchumi Duniani ni tukio lililofanyizwa kwa makusudi kabisa kwa mujibu wa mpango ulioanzishwa kwa umakini mkubwa sana na Pike uliolenga kudhoofisha mfumo wa kiuchumi wa dunia. Umesaidia sana fanikisha matokeo lengwa ya uchaguzi mkuu wa Uingereza wa mwaka 2010 uliotoa hakikisho la lengo tarajiwa kwamba yeyote atakayechua madaraka miongoni mwao na kuunda sarikali kupewa kikombe cha sumu na asiweze kuirejesha nchi kwenye ubora wake wa kichumi wala kimfumo. Muungano wa vyama vya Wademocrat na Waliberali ulianza kwa shida kubwa sana toka hook mwanzo. Wayunani wakafanya jambo ka kijinga sana na watu wake wanajijali wenyewe tu na wasione kile kilichokuwa kinaendelea kingeweza kumpata yeyote yule miongoni mwao mataifa ya Umoja wa Ulaya na hatari nyine inayakaribia mataifa mengine kama vile Ureno, Ireland, Italia, na Uhispania, hawa hawapo mbali na kukumbwa na janga hili.
Nia iliyoko ni kuua Muungano wa Nchi za Ulaya kwa kuuporomosha kiuchumi ili umiliki wa nguvu za kiuchumi za dunia ubakie kwao na mfumo wa sarafu moja duniani ufanikiwe na iwe rahisi kuumiliki ama kuuendesha.
Haya yote yanaandaliwa na kufanywa na hawahawa waabudu shetani wakiwa ni chombo chake katika kumtumikisha mwanadamu na kumfanya aendelee kuwa mjinga kiasi cha kudhani wanaweza kummiliki na kuimiliki dunia.
Taifa la Marekani linaangamia kwa ajili ya mfumo wake wa kibenki na inajimaliza kwa makusudi kabisa. Haya yote yameratibiwa na kutokea kwa mwisho fulani na maalumu katika kuutangulia ujio wa mwaka uliokusudiwa tangia mwaka 2010.
Katika kipindi cha kati ya miaka ya 2010 na 2012 uchumi wa dunia utafanywa uonekane kuwa unamatatizo na itafanywa hivyo ili kuuwezesha mfumo wa serikali moja ya dunia ufanikiwe kupitia kile kitakachojulikana kama Matatizo makubwa ya Mabadiliko ya Tabia-nchi Ulimwenguni na watatumia mbinu za uwongo za kisayansi kulazimisha kukubalika kwa mbinu za upunguzaji wa idadi ya watu duniani na kufanyiza mabadiliko ya kijamii yenye lengo la kuziharibu familia na mahala pake kuendeleza mkakati wa kishetani ili kazi zake ziwe na nguvu zaidi kwa mujibu wa vile walivyopanga na kukusudia.
Mataifa yanayoendelea yataenda sambamba na jambo hili kwa kuwa yatafaidika na misamaha itakayotolewa kutokana na madeni wanayodaiwa na nchi za Magharibi na watadanganyika kijinga sana kuamini hivyo.
Utaratibu wa chanjo na huduma za madawa ya binadamu vitatumika sana katika kufanikisha lengo hili la kupunguza idadi ya watu duniani.
Matokeo yake yatakuwa ni mlipuko wa kupungua idadi ya watu utakaofanyika kwa utaratibu wa kijanja na wenye kupangiliwa vema, au kwa maneno mengine ni kwamba kutaratibiwa mauaji ya namna isiyowahi kutoke huko nyuma kabla yetu.
Mwaka
2012 na Mikakati ya Vatican
Kwenye Kitabu kiitwacho Nyumba Iliyopeperushwa na Upepo [Windswept House (cha Broadway, NY, 1996)] Malachi Martin anaelezea kuhusu sherehe iliyofanywa kwa ajili ya kumtawaza Malaika Muasi Lusifeli, wakimtawaza na kumpa kiti cha yeye kuiwa mungu. Hafla hii ilifanyika huko Vatican ikienda sambamba na kwa wakati mmoja na ibada iliyofanyika huko North Carolina nchini Marekani na pia ziliweka maana lengwa ya ishara ya tarakmu ya 33 ambayo ni tarakimu ya juu nay a heshima sana kwao. Sherehe hii ilifanyika tarehe 29, Juni 1963.
Sherehe hii ilifanyika kwa kufuata itifaki yote ya mabashirio ya waabudu Shetani hawa kwa mabashiri yaliyotolewa huko nyuma kwamba Kipindi-zama cha Utawala wa Mwana wa Mfalme kingeanza wakati papa atakapochukua na kujiita jina la Mtume Paulo. Sharti hili lilikuwa ni ishara ya kwamba “kipindi cha Mafaniko” kimeanza (Kitabu cha Martin, uk. 7). Paulo VI ndiye alikuwa huyu papa. Tarakimu yake ya VI ilikuwa na maana ya kiokaliti. Jina la Yohane-Paulo lilikuwa pia na maana ya kufanya endelezo ya mwanzo wa kipindi hiki muhimu.
Kipindi hiku Muhimu kilikuwa ni cha kutoka tukio lile la kutawazwa kwa Lusifeli mwaka 1963 kwa kipindi cha Yubile ya miaka 49.5 hadi tarehe 21 Desemba 2012.
Yubile ya miaka 50 inaishia Juni 2013 kwenye mwaka wa Joka.
Sherehe ile iliyofanyika South Carolina Marekani mwaka 1963 iliandaliwa na kusimamiwa na kundi la maaskofu wa kanisa Katoliki la Roma huku wakiwasiliana kikamilifu na kupewa mwongozo wa jinsi ya kuiendesha na uongozi wa Vatican.
Kwa kweli, ilifanywa kwa kufuata taratibu zote za mapokeo ya Kishetani ilifanywa na waabudu Shetani hawa kwa ushirikiano mkubwa na uongozi wa Kanisa Katoliki la Roma na nchini Marekani.
Kile wanachokiita “Kanisa dogo Linalokusudiwa” kiliandaliwa kwenye eneo la chini la nyuma ya shule ya parokia na likatiwa nakshi vizuri sana tayari kwa ajili ya maadhimisho haya. Maadhimisho ya sherehe hii yalihisisha vitu muhimu lakini ambavyo havitumiki kwenye ibada za kawaida wa Vatican, kama vile makafara yanayoenda sambasamba na matendo ya kulawiti watoto pamoja na upigaji wa makelele na vifijo zenye sauti kwa jinsi ya kishetani mambo ambayo ni muhimu sana kwenye ibada hizi.
Kwenye kitabu chake Martin aliyaandika haya yote kwa kuwa alijisikia vibaya na kusitushwa kuona uhusika wa moja kwa moja wa Kanisa Katoliki la Roma na mahusiano ya kanisa lote la waamini Utatu na hawa waabudu Shetani mahusiano ambayo lengo lake zima ni kuchukua hatamu na kuliondolea nguvu zake kwa kulisababishia tuhuma za kingono na ubakaji wa watoto na rushwa na kila sifa mbaya.
Tangia kipindi hiki kijulikanacho kama ni Kipindi Muhimu tumejionea wenyewe mlipuko wa ongezeko la wanawake wanaotumia madhabahu lilivyo ulimwenguni kote na jinsi wanavyotumiwa huko Marekani kwenye mashindano ambayo yanaporomoa maadili yameshika kasi kubwa ya urembo na kasi ya kuandaliwa kwa matamasha ya ulimbwende yenye nguo za kubana na nusu uchi. Papa wa Kislavi alijaribu kuwapinga lakini alijikuta akinywea na kuwaacha waendelee. Na akabeza makatazo yake na kushiriki kwenye tamasha waliloingia watu wengi kwa kiingilio kikubwa (pesa 50,000 kwa kila mtu) na mambo mengine mengi yaliyosemwa ambako alitumia muda wake kushawishi wazo lengo la kuungana na kufanya kazi pamoja kwa moyo wa kujituma na bidii nyingi na imani kuu wakishirikishwa hata makuhani wa watu wa imani ya voodoo.
Msisitizo wa “papa wa Kislavi” katika kuppinga mkakati wa uzazi wa mpango ulikuwa pia unaenda sambamba na kupinga faida iliyoko kwenye utaratibu wa Kimarekani na Martin anaielezea migongano na matumizi ya wakala, aliyeaminika kuwa ni Rosicrucian (aliyepewa jina la utani na la bandia na Martin la “Gibson Appleyard”) inchini Marekani aliyetumwa aende Roma ili akafanye mazungumzo na papa ili asisitizie na kurahisisha mkakati huu wa uzazi wa mpango.
Papa alipingwa na mawakala wa Umoja wa Mataifa waliongozwa na Bischara Francis kwa lengo la kufanikisha kwa haraka mkakati huu wa uzazi wa mpango ambao ulikuwa ni moja ya mikakati muhimu ya mpango wa kile kinachoitwa Agizo Jipya la Mfumo Mmoja wa Mambo Duniani ambao kusudi lake kuu ni kupunguza idadi ya watu duniani. Mkakati huu unahusisha utoaji mamba ukikusudia hasa kuwalenga watu kutoka nchi za kundi la mataifa yanayoendelea na Umoja wa Mataifa unatumia uwezo wao wa kumiliki uchumi wa dunia kama silaha yao ya kuendeleza jambo hili. Kuna vuguvugu hivi sasa la kubadilisha Katiba ya Jamhuri ya Kenya linalokusudia kuruhusu utoaji mamba kuwa ni kitu muhimu na wanafungamanisha na uanzishwaji wa Sheria za Kiislamu maarufu kama Sharia ili kuwaridhisha Waislamu wavutiwe kuyapigia kura mabadiliko haya ya katiba.
Rais wa Marekani alikuwa anajaribu alikuwa anajaribu kumlazimisha papa ili akubaliane na kutangaza azimio la kwamba utaratibu wa idadi ya watoto wawili kwa kila familia ya mke na mume ndio ufuatwe kwa wtu wote duniani, yaani Wakatoliki na wasio Wakatoliki pia. Papa huyu wa Kislavi alikataa na mazungumzo ili kuweka muafaka yaliendelea kufanywa ili kumshawishi akubaliane na jambo hili.
Yohana Paulo II alisema yafuatayo alipokuwa anajiandaa kufanya ziara yake ya kutembelea nwenye nchi za Russia na Ukraine. Alitangaza waziwazi akiwa kwenye uwanja maarufu uitwao “Appleyard” kuwa ziara yake iliandaliwa na kupata baraka na Malkia wa Mbinguni. Kwa hiyo, alikuwa anafanya manuizo ambukizi yenye mvuto kwa watu kumhusu Mungu-Mke anayeabudiwa kwa siri kwenye dini potofu ya Siri, au kwa maneno mengine twaweza kuiita ya Kimashetani. Na wakati huo huo viongozi wawakilishi wa Vatican wakampa atie saini kwenye Kitabu cha Usajili wa Wageni kwa kuzingatia Itifaki (kitabu cha Martin, ukurasa 521-522). Yohana Paulo II aliridhia na kutoa idhini kuangamizwa kwa Kanisa Katoliki la Roma na kuteketezwa kwa moto waalimu walioonekana kuwa wana mafundisho yasiyokubalika na wao kwenye seminari, kazi iliyotekelezwa na maaskofu na madinari waovu kwenye majumba yao ya ibada. Pia aliruhusu watoto wadogo wafundishwe mashuleni na waalimu kwa mifumo isiyo ya Kikatiliki na watawa wachukuliwe na wimbi la wanaharakati za usawa wa kijinsia. Hakuwalinda hata mmoja wao wala kuyanusuru majengo yao ya ibada, yaani makanisa. Makanisa madogo yaliachwa bila Madhabahu na bila Tabenakulo na bila Kizimba cha maungamo na pia bila kuwa na sabamu za ibada zao (kitabu cha Martin, sura ya 642).
Benedict XVI aliyemrithi kwa mujibu wa
ubashiri wa Malachy naye bado anaendeleza kazi hiyo hiyo mbovu ambyo iko kwa
mujibu wa mikakati ya Wabudu Shetani na Kanisa litajikuta likimezwa na
mishuguliko ya vikundi vya waamini Utatu na kubadilishwa kwa kadiri muda unavyopangiliwa
kuelekea kwenye zama ya kushamirika kwa dini ya Mnyama na utawala wake (tazama
kwenye jarida liitwalo Vita
ya III ya Dunia Sehemu ya II: Mwanamke Kahaba na Mnyama (Na. 299B), [WWIII Part
II: The Whore and the Beast (No . 299B)] kwenye wavuti ya
http://www.ccg.org/english/s/p299b.html).
Matokeo ya mwisho ni kuukomesha Ukristo na watu wake wote na mahala pake kuufanya ulimwengu wote ugeukie kwenye dini ya kidunia inayomwabudu Lusifeli.
Kitabu cha Martin kinafafanua vizuri sana kuhusu juhudi za Vatican katika kumiliki shughuli zote za kisiasa za dunia na mikakati yake katika kuufanya ulimwengu ushawishike na kuvutiwa na itikadi za Kishetani.
Uwongo
ama Udanganyifu wa Mwisho
Wateule watakuwa ndio walengwa wao katika jambo hili.
Jambo hili litawachanganya watu wengi litakapotokea wakati wale Mashahidi watakavyofanya kazi ya kuwahubiria watu kwa Mfululizo na Juhudi kubwa yaliyoandikwa kwenye Torati kwa kipindi cha siku 1263.5 kabla ya kurudi kwake Kristo.
Ni vema na dhana salama kujua kuwa Adui na Mshitaki wetu hatapoteza muda mwingi sana na tujue pia kwamba mkakati wa kuiunda dini hii hatari na potofu unaendelea na uwekaji wa nembo kufuru zenye maana za.
Tunapaswa kuelewa pia kwamba kalenda hii mashuhuri duniani ni miongoni mwa mambo yanayowasaidia katika juhudi zao wa kuufanya ulimwengu uvutwe na kushawishika na dini ya Shetani. Dennis Exiguus au Dennis Mfupi aliyehusika katika kuitengeneza kalenda kwa makosa na kuuweka mwaka 1BK, akikosea kwa kuacha miaka 5 nyuma. Kwa hiyo, tarehe na matukio viliwekwa vyote kwa mujibu walivyopenda hawa Waokaliti sambamba na sababu zao za siri na Ratiba walizojiwekea sambamba na mambo yalivyo kwa siku hizi. Soma jarida la Umri Aliobatiziwa Kristo na Kipindi Alichofanya Huduma yake, (Na. 019) [Christ’s Age at Baptism and the Duration of His Ministry (No. 019)] kwenye wavuti ya http://www.ccg.org/english/s/p019.html na Significance of the Year 2000 (No. 286) kwenye wavuti ya
http://www.ccg.org/english/s/p286.html.
Inapnekana kuwa na mambo yaliyo zaidi ya bahati mbaya kwenye makosa yaliyofanywa na Dennis Mfupi katika kufanyiza zama tulizonazo sasa ukilinganisha na mabashiri mengine ya kitaifa yanayolinganishwa na mwaka huu wa 2012 na mkutano ulifanywa na kundi la waasi kwa Mungu kwenye Mlima wa Hermon kitovu cha dunia.
Watu wanaovuma kwa umaarufu sana duniani na nukuu za misemo maarufu hutokana na hawa waabudu na watumishi wa Shetani. Wamedandanyika sana kwa kiwango wasiokijua watu wengi na wanadanganyika kuwa watakuwa na uweza wa kutawala kwenye kipindi cha utawla wa milenia ni kama tulivyojionea huko nyuma.
Wamedanganyika kijinga mno wakati ambapo ukweli unaweka dhahiri kuwa hawana kipindi kingine kirefu cha kuishi zaidi ya mwaka 2025 wasipozitubia dhambi zao ila wamekuwa wakijifundisha mambo ya ndani sana ya uwongo wa Shetani ambao utawapekelea kwenye hukumu kuu.
q