Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[230]
Matumizi ya Neno Uungu Shirikishi
(Toleo La 1.0 19971214-19971214)
Uungu Shirikishi, yaani Hypostasis ni neno la msingi wa kiimani
linalotumiwa na waamini imani ya Utatu. Mungu anachukuliwa
kuwa yupo kwenye uungu shirikishi na wengine,
yaani hypostases la ousia moja. Maneno haya yanatokana na maneno ya kifilosofia
ya Kiyunani. Yanatujmika kwenye Agano Jipya na kwenye tafsiri
ya Septuagint (LXX). Yanamaana gani
basi?
Christian Churches of God
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 1997 Wade Cox)
(tr. 2016)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu
bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu
fupi zaweza kuwekwa toka kokote
ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila
kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana
Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Matumizi ya Neno Mjumuiko wa Uungu
Uungu Shirikishi, yaani Hypostasis asili
yake ni neno la Kistoiki ambalo linahusiana na neno la Kiplatoniki la ousia. Yote mawili yanamaanisha
uwepo wa kiumbe. Yametoholewa kwenye matumizi ya kidini kutokana na hoja za waamini
utatu au watrinitariani, yaliyokusudia kutafuta kuelezea maana ya Uungu kwa kutuama kwenye
matumizi ya maneno yanayotofautisha. Imani za Uungu Shirikishi
za Kistoiki zilitumika ili kuwakilisha udhihirisho wa Mungu. Neno
la Kiplatoniki la ousia lilitumiwa
ili kuwakilisha utimilifu wa Uungu.
Kwa hiyo, Uungu ulichukuliwa kuwa na udhihiriko
wa aina tatu, yaani Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.
Kila moja ya madhihirisho
haya ilichukuliwa kuwa ni namna tu ambayo kwamba mmoja wao
alichagua kujiwakilisha mwenyewe. Kwa hiyo
Baba, Mwana na Roho Mtakatifu walichukuliwa kuwa ni wenye hadhi na
uweza sawa na wanadhihirika sawa kama kitu
kimoja. Tofauti iliendelea kukuzwa sana kwamba wakati mmoja
anapotenda jambo ndipo wote walitenda jambo hilo pasi kutenganishwa na kwamba hakukuwa
na uwezekano wa kuwatenganisha kimatndo na mwenendo
wao. Hapo ndipo dhana hii
ya kipuuzi na ya uwongo iliendelezwa kwamba mjumuiko wa uungu waweza
kuwa tofauti lakini sio kuwatenganisha.
Dhana iliyopo,
ndiyo inayokataa uwezekano wa wateule
kufanyika kuwa elohim au theoi
kama ilivyokuwa ukifundishwa na Kanisa la kwanza na ndivyo ilivyoeleweka
na Irenaeus (soma jarida la Mteule Kama Elohim (Na. 1) kwa rejea zaidi). Kristo
alichukuliwa kuwa hakuwa mwana kwa
maana moja sawa na kuwa Wana
wengine wa Mungu ambavyo wanaweza
kuwa Malaika na wateule wengine
(soma pia kwenye jarida la Usosinianism, Uarianism na Uyunitarianism
(Na. 185)).
Kuna idadi
kadhaa ya mifano ya neno hili uungu shirikishi linavyojitokeza
kwenye Agano Jipya na pia kwenye
tafsiri ya Septuagint
(LXX). Neno hili limejitokeza kwenye Zaburi 68 (69):3 (LXX).
Inaonekana pia
kwenye Ezekieli 43:11. Dhana iliyolibeba neno hili ni kwamba:
kupangilia au kuweka chini ya; kuweka vitu chini
ya, msingi mkuu au msingi: Zaburi.
lxviii (lxix) 3; [tou oikou], Ezekieli xliii,11... (kwa mujibu wa Thayer’s Greek English Lexicon, pp. 644-645).
Maana yake
ya pili ni kwamba:
kile kilicho na msingi, ni imara;
hivyo, ni kile kilicho na uwepo,
kinachoishi, kiumbe cha kweli: ... b. Kiwango na kitu madhubuti,
asili, chochote cha kipekee. au kitu
kwa hiyo
limetumiwa kwenye Waebrania 1:3 ambapo Mwana anawakilisha uhalisia wa Mungu.
Andiko hili
linasomeka [kwenye machanganyiko wa Kirumi na Kiyunani]
os oon apaugasma tes dozes
ambaye ndiye [hakika] na uhalisia
wa utukufu [wake]
kai
charakter tes hupostaseoos
autou,
na uwakilishi wa uhalisia wake
pheroon te ta panta too remati tes dunameoos
na akachukua vitu vyote kwa neno la uweza
wake
autou, katharismon toon amartioon poiesameos
kwa yeye kusafisha dhambi zote zilizofanywa
ekathisen en dezia tes megaloosunes
akaketi mkono wake wa kuume
wa ukuu wake
en upselois,
mahali pa juu
hivyo, neno atajwaye hapa
kwa kweli ni halisi. Kwa hiyo Kristo ni mwakilishi wa uhalisia
wa Mungu. Ni sawa tu na kama kusema kwamba wewe
ni mwakilishi wa uhalisia wa Kanisa
na kusema kwamba ninyi nyote wawili,
yaani wewe na Kanisa ni Mungu kwa kuwa ninyi
nyote wawili mnajumuika pamoja kiushirika, au uungu shirikishi, wa muundo wote mzima.
Waamini Utatu
au Watrinitarians wanajaribu
kukataa tofauti hiyo na uwakilishi kwa kutumia neno
ambalo linaonyesha wazi uhalisia wa
kiumbe. Ni neno la mashara au la mchezo.
Kuna ukweli
wa maana kwa ukweli kwamba
wewe binafsi yako na Kanisa kwa ujumla wote
ninyi ni mawaka wa Mugu.
Lakini Watrinitariani wanapinga mtambuka huu. Wanatafuta kuyafanya matumizi ya neno hili
yamaanishe muungano wa vitu vitatu. Na kwamba Roho Mtakatifu
sio utendaji bali ni washirika pamoja kiuungu
mwingine mbali na hao. Kwa hiyo
kufanya kuwe na uwongo, uzushi na kujiuliza kuna sababu gani ya kuwa na hali
sawa ya uwepo
au kuwepo na uhusiano kati ya mteule
na mwamini Utatu kuwe hakuwezekani.
Neno hili
limetumika kwenye kitabu cha Josephus
cha Zamakale za Wayahudi [Antiquities
of the Jews]
18:1,6; inamaana ya kujiamini au tumaini kuu kwenye 2Wakorintho 9:4 (tumaini) na pia kwenye 11:17. Waebrania 3:14 inalitumia neno hili kama tumaini au hakikisho (Marshall) kama ilivyo kwenye
Waebrania 11:1 inamaanisha kuwa ni uhalisia (Marshall) au uhakika (RSV), ambavyo kwamba imani ni uhalisia au ni kuwa na hakika na mambo yatarajiwayo. Kutokana na andiko hili ni wazi kabisa
kwamba madhihirisho yoyote ya uungu,
ama yawe ya kiimani, au Kristo, au Roho Mtakatifu, au kwa uhakika angalivu
wa mteule, yote hayo ni uungu shirikishi Mungu
hujidhihirisha kwa ushirika wa pamoja wa zaidi
ya aina tatu za imani ya uungu shirikishi. Watrinitariani
kwa hiyo ni wana uchaguzi wa
kuchekesha.
Matumizi ya
neno hili yanapatikana pia kwenye Ruthu 1:12 (LXX) (kwenye SHD
8615; tiqvah)
ambapo anasema kama ningepata
mume hata usiku huu, inamaanisha
chukulia kama msingi wa ukweli.
Dhana itokanayo na msingi wa kiumbe
kama ilivyokuwa. Ezekieli 19:5 (LXX) inatumia uungu shirikishi kwa andiko hili
kama tumaini au matarajio. Zaburi 38[39]:8 inalitumia (kwenye SHD 8431; towcheleth) ambapo linamaanisha kama msingi au mahala pa tumaini
amba7ye ni Mungu. Kwenye Ezekieli 19:5 (LXX) tumaini la
samba jike wa Israeli alituama kwenye samba kijana aliyeshindwa (apooleto e hupostasis).
Kwa hiyo,
imani kama ilivyo yenyewe tu ni washirika wa uungu kama kiini cha uhalisia
ambao ni Mungu.
Mteule kwa
tumaini hili kwenye imani katika
Roho Mtakatifu wote wanakuwa washirika pamoja wa Mungu Mmoja, wa
Pekee na wa Kweli (Warumi 8:17; Wagalatia 3:29; Tito 3:7; Waebrania
1:14; 6:17; 11:9; Yakobo 2:5; 1Petro 3:7).
q