Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[299B]
Vita Kuu Ya III Sehemu Ya II:
Mwanamke Kahaba Na Mnyama
(Toleo Na 1.0 20100331-20100331)
Sehemu hii ya II inaendelea kuelezea utaratibu wa lile shirika
litakaloshika hatamu za uongozi wa kidini katika Siku za Mwisho chini ya huyu
Mwanamke Kahaba na kukomeshwa kwa utaratibu wake hapo atakapokuja Masihi.
Email: secretary@ccg.org
(Haki Miliki © 2010 Wade Cox)
(tr. 2012)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili
yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Mwanamke
Kahaba na Mnyama
Kwenye
sehemu ya I tumejionea kwamba Dola ya Mnyama inavyoanza kuinuka na jinsi
inavyoweka mfumo wa Serikali inayothibiti mambo yote ya kiunchumi hapa duniani.
Wakati mgongano ulioanzishwa au kuchochewa na mfumo huu utakapoleta maafa
kwenye nchi nyingi na watakapokuwa wameanzisha nfuno bandia na kuuthibiti kwa
kuukalia nji wa Yerusalemu kwa kipindi cha miezi 42 na kisha wataangamizwa.
Katika
kipindi hiki cha miezi 42 cha utawala wao watakuwa wanapingwa na Mashahidi
Wawili watakaotumwa na Mungu. Na baada ya siku 1260 watauawa na Kristo ndipo
atakapoingilia kati kwa kurudi kwake. Tunajionea uingiliaji kati huu kwenye
kitabu cha Ufunuo 14, ambayo imemalizia Sehemu yetu ya I.
Wateule
ambao idadi
Baada ya
kuanguka huku kwa mji wa Babeli, Malaika wa Tatu atatangaza maafa
yatakayowapata wale watu wote walioikubali na kuipokea ile chapa ya Mnyama
kwenye kipindi hiki chote cha siku 1263.
Sehemu inayofuatia
inaonyesha jinsi Mwanamke huyu maarufu
Wateule
watakaomshinda huyu Mnyama ndipo watakirimiwa thawabu ya kuwa na Kristo wakati
mataifa yatakapokuwa yanahukumiwa.
Hata hivyo,
kabla Mwanamke huyu kahaba hajaangamizwa kwenye jaribio
Ufunuo 15 inasema:
1Ndipo nikaona ishara nyingine
kubwa ya ajabu mbinguni, malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa
sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika. 2Nikaona kile kilichoonekana kama
bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa
wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu
ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu. 3Nao wakaimba wimbo wa Mose, mtumishi
wa Mungu na wimbo wa Mwana-Kondoo wakisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, matendo Yako
ni makuu na ya ajabu Mfalme wa zamani zote, njia Zako Wewe
ni za haki na za kweli! 4Ni nani
ambaye hatakuogopa Wewe Bwana na kulitukuza Jina Lako? Kwa kuwa Wewe peke yako
ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo
yako ya haki yamedhihirishwa.’’ 5Baada
ya haya nikatazama, nalo hekalu la hema la ushuhuda lilikuwa limefunguliwa
mbinguni, 6ndani ya lile hekalu
wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za
kitani ing’aayo na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao. 7Ndipo mmoja wa wale wenye uhai wanne
akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu,
Yeye aishiye milele na milele. 8Nalo
lile hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake,
wala hakuna ye yote aliyeweza kuingia mle hekaluni mpaka yale mapigo saba ya
wale malaika saba yalipomalizika.
Ni katika kipindi
hiki ndipo malaika mkuu aliye miongoni mwa wale viumbe hai wanne wanaoonekana
wamechukua vitasa saba vya ghadhabu ya Mungu na kuwapelekea malaika wale saba
watakaotoa mapigo ya mwisho.
Kristo
atamuangamiza huyu Mpingakristo na yule Nabii wa Uwongo wakati atakaporudi
ambao pia ni wakati wa ule Ufufuo wa Kwanza. Ni katika kipindi hiki ambapo wale
wote walio kwenye imani ya Utatu na Kanisa lao vitaharibiwa na kukomeshwa kabisa.
Vitasa hivi vya
ghadhabu ya Mungu ni mkomesho wa mwisho wa mfumo huu wa uwongo na mafundisho
yake na kama tunavyoona kwamba hakuna hata mmoja anayefanya toba kutubia hali
hii. Kitasa cha kwanza kitafunguliwa na kumimina ghadhabu yake kwa wale wote
walioipokea chapa ya Mnyama na hawakujutia wala kuitubia hali hii.
Ufunuo 16 inasema:
1Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mle hekaluni ikiwaambia wale malaika
saba, “Nendeni, mkayamwage duniani hayo mabakuli saba ya ghadhabu ya Mungu.’’ 2Malaika wa kwanza
akaenda akalimwaga hilo bakuli lake juu ya nchi. Majipu mabaya yenye maumivu
makali yakawapata wale watu wote waliokuwa na chapa ya yule mnyama na kuiabudu
sanamu yake. 3Malaika wa pili akalimwaga bakuli lake baharini, nayo ikabadilika kuwa damu
kama ya mtu aliyekufa na kila kiumbe hai kilichokuwa ndani ya bahari kikafa. 4Malaika wa tatu
akalimwaga bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, nazo zikawa damu. 5Ndipo nikamsikia
malaika msimamizi wa maji akisema, “Wewe una haki katika hukumu hizi ulizotoa,
wewe uliyeko, uliyekuwako, uliye Mtakatifu, kwa sababu umehukumu hivyo, 6kwa kuwa walimwaga
damu ya watakatifu Wako na manabii Wako, nawe umewapa damu wanywe kama
walivyostahili.’’ 7Nikasikia madhabahu ikiitikia, “Naam, Bwana Mungu
Mwenyezi, hukumu Zako ni kweli na haki.”
Hukumu hii ni dhidi ya wanadamu itakayotokana kama kisasi
cha mambo ya mateso waliyowafanyia waeule wa Mungu na kuwauwa watumishi wake
Mungu na madhabahu ikawalilia kwa jambo hilo.
Janga la mabadiliko ya Tabia Nchi
Tunaona kwamba janga hili la Mabadiliko ya Tabia Nchi
linalotangazwa na kunadiwa sana na wanasayansi linaanza kujitokeza kwa hivi sasa
na litaendelea hivyo chini ya malaika wa nne hadi pale wanadamu watakapounguzwa
na kuteketezwa kabisa kwenye joto la jua na jehanamu ya moto na kwa aina yote ya
maangamizo yatakayowakumba itakayotokea baada ya hapo.
8Malaika wa nne akamimina bakuli lake kwenye jua, nalo likapewa nguvu za
kuwaunguza watu kwa moto. 9Watu wakaunguzwa na hilo joto kali, lakini
wakalaani Jina la Mungu, aliyekuwa na uwezo juu ya mapigo haya, wala hawakutubu
na kumtukuza Mungu.
Wanamlaani Mungu kwa ajili hii na la kusikitisha ni kwamba hawazitubii
dhambi zao hizi wala kumpa utukufu. Ni jambo lililowekwa bayana kwenye unabii
kwamba jua ndilo chanzo kikuu cha hali hii ya Mabadiliko ya tabia Nchi na wala
sio kitu kinachofanywa na wanadamu lakini mapepo wametunga sababu za kisayansi
za uwongo iliwawapate kuwadanganya watu kupitia kwenye unabii (tazama jarida la
Mabadiliko ya
Tabia Nchi na Nabii za Kwenye Biblia (Na. 281) [Global Warming and Bible Prophecy (No. 218)] na Mabadiliko ya
Tabia Nchi: Mzunguko Wake wa Kihistoria (Na. 218b) [Global Warming: Historical Cycles (No. 218b)].
10Malaika wa tano
akamimina bakuli lake kwenye kiti cha enzi cha yule mnyama, nao ufalme wake
ukagubikwa na giza. Watu wakatafuna ndimi zao kwa ajili ya maumivu 11wakamlaani Mungu wa mbinguni kwa sababu ya
maumivu na majeraha yao, wala hawakutubu kwa ajili ya matendo yao maovu
Pamoja na mateso na maumivu haya yote lakini bado hawaonyeshi kuyatubia
matendo yao maovu waliyoyafanya.
Dola hii imeweka ngome yake huko Ulaya na Umoja wa Mataifa unaandaliwa
kukomeshwa na inatakiwa ifikie mwisho wake na watu hawa waovu na waliomwasi
Mungu. Kwa hiyo, Mfalme wa Mashariki ataenda kumkabili Kristo na wateule wake.
Ukanda wote wa Mashariki ya Kati utakauka na utaharibiwa na wafalme wa watapita
ndani yake.
12Malaika wa sita
akamimina bakuli lake kwenye mto mkubwa Eufrati, maji yake yakakauka ili
kutayarisha njia kwa ajili ya wafalme watokao mashariki.
Tendo hili litafanyika ili kajeshi yote ya duniani yakusanyike yakiwa
yamevuviwa na roho za Joka Mkuu, na Mnyama na Nabii wa Uwongo. Kifungu fulani
kwenye aya hii ya 15 kinaonyesha kwamba ni katika kipindi hiki ndipo Kristo
atakapokuja na kuwaangamiza watu hawa ambao walisababisha kuwepo kwa hali hii.
Kwa nasibu njema mchakato huu utachukua kipindi kifupi sana.
13Kisha nikaona roho wachafu watatu waliofanana na vyura wakitoka katika
kinywa cha lile joka na katika kinywa cha yule mnyama na katika kinywa cha yule
nabii wa uongo. 14Hizo ndizo roho za pepo wachafu zitendazo miujiza.
Nazo huwaendea wafalme wa ulimwengu wote na kuwakusanya tayari kwa ajili ya
vita katika siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi. 15“Tazama, naja kama
mwivi! Amebarikiwa yeye akeshaye na kuziweka tayari nguo zake ili asiende uchi
na kuoenekana aibu yake”. 16Ndipo wakawakusanya wafalme pamoja mahali paitwapo
“Armagedoni’’a kwa Kiebrania.
Vita ya Armagedoni ndiyo itakayohitimisha kipindi hiki. Baada ya hapo mambo
yote yatahitimishwa.
Ufunuo 16 (inaendela
kusema)
17Malaika
wa saba akamimina bakuli lake angani na sauti kubwa ikatoka mle hekaluni katika
kile kiti cha enzi, ikisema, ‘‘Imekwisha kuwa!’’ 18Kukawa na mianga ya umeme wa radi, ngurumo, radi na
tetemeko kubwa la ardhi. Hapajawa kamwe na tetemeko la ardhi kama hilo tangu
mwanadamu awepo duniani, hivyo lilikuwa tetemeko kubwa ajabu. 19Ule mji mkubwa ukagawanyika katika
sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikaanguka. Munguakaukumbuka Babeli ule
uliokuwa mkuu na kuupa kikombe cha hasira na ghadhabu Yake. 20Kila kisiwa kikatoweka wala milima
haikuonekana. 21Mvua kubwa ya
mawe, mawe yenye uzito wa talanta mojab
yakaanguka kutoka mbinguni, yakawaangukia wanadamu. Nao wanadamu
wakamlaani Mungu kwa ajili ya hayo mapigo ya mvua ya mawe, kwa sababu pigo hilo
lilikuwa la kutisha.
Kwenye kipindi hiki chs kumiminwa kitasa cha mwisho ndipo mfumo wote wa
dunia utaangaka na kukoma. Miji mikuu ya nchi za dunia pamoja na uongozi wao
mbovu na sheria zake za kidunia na mifumo yake vitakomeshwa vote.
Hukumu ya Mwanamke Huyu Kahaba
Sura inayofuata
ya 17 inaelezea hukumu ya mwaname huyu kahaba.
Inaelezea matukio
yake na dhambi zake. Inatupeleka nyuma kwenye kipindi chake na kuendelea hadi
kwenye matukio ya utendaji kazi wake na jinsi alivyowatesa watu wa Mungu. Huu
ni mfumo wa Dini kuu ya Siri ya Babeli inayoendelea kikamilifu kwenye hatua
zote zilizonenwa na nabii Danieli sura ya 2 iliyodumu na kupitia kwenye dola za
Wababelonia, Wamedi na Waajemi na Wayunani, ambao walifarakana na hatimaye Dola
ya Warumi ambayo ndiyo ile miguu ya chuma na hatimaye ni udongo, na Dola ya
mwisho ya Mnyama yenye vidole kumi. Hatimaye Kristo atakuja akiwa ni lile jiwe
lisilofanywa kwa mkono wa mwanadamu na litaikomesha kadhia yote ya mfumo wa
siku za mwisho.
Mfumo huu wa
imani ya Utatu uliotungwa na Manamke Kahaba umeua watumishi wa Mungu wengi sana
na kwa ajili ya jambo hilo atahukumiwa.
Ufunuo 17 inasema:
1Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli
saba akaja akaniambia, ‘‘Njoo, nitakuonyesha adhabu ya yule kahaba mkuu,
aketiye juu ya maji mengi. 2Yule ambaye wafalme wa dunia
walizini naye na watu wakaao duniani walilewa kwa mvinyo wa uzinzi wake.’’ 3Kisha yule malaika
akanichukua katika Roho akanipeleka nyikani. Huko nikamwona mwanamke mmoja
ameketi juu ya mnyama mwekundu aliyejaa majina ya kumkufuru Mungu mwili mzima.
Mnyama huyo alikuwa na vichwa saba na pembe kumi. 4Huyo mwanamke alikuwa
amevaa mavazi ya rangi ya zambarau na nyekundu, akimetameta kwa dhahabu, vito
vya thamani na lulu. Mkononi mwake alikuwa ameshika kikombe cha dhahabu
kilichojaa mambo ya machukizo na uchafu wa uzinzi wake. 5Kwenye kipaji chake
cha uso palikuwa pameandikwa jina: “SIRI, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA
MACHUKIZO YA DUNIA.’’ 6Nikaona kuwa huyo mwanamke alikuwa amelewa kwa
damu ya watakatifu, yaani, damu ya wale watu waliouawa kwa ushuhuda wa Yesu. Nilipomwona
huyo mwanamke, nilistaajabu sana.
Malaika
anamuelezea kwa wazi kabisa jinsi alivyo. (Soma jarida la Imani-Hila za Siri (B7 1) [Mysticism (B7_1)]
(pia soma kitabu cha Dini-Hila za Siri (Mysticism), kilichochapishwa
nasi Makanisa ya Kikristo ya Mungu.
Ufunuo 17 inasema:
7Ndipo
yule malaika akaniambia, ‘‘Kwa nini unastaajabu? Nitakufafanulia siri ya huyo
mwanamke na huyo mnyama aliyempanda, mwenye vichwa saba na pembe kumi. 8Huyo mnyama, ambaye ulimwona, wakati
fulani alikuwepo, lakini sasa hayupo, naye atapanda kutoka katika lile shimo
lisilo na mwisho na kwenda kwenye maangamizo. Watu waishio duniani ambao majina
yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima tangu kuumbwa kwaulimwengu
watastaajabu kumwona huyo mnyama, kwa maana alikuwepo, wakati fulani na sasa
hayupo, lakini atakuja. 9‘‘Hapa
ndipo penye akili pamoja na hekima. Vile vichwa saba ni vilima saba ambavyo
huyo mwanamke amevikalia. 10Pia
hivyo vichwa saba ni wafalme saba ambao miongoni mwao watano wamekwisha
kuanguka, mwingine hajaja bado, lakini atakapokuja, atalazimika kukaa kwa muda
mfupi. 11Yule mnyama aliyekuwepo
wakati fulani na ambaye sasa hayupo, yeye ni mfalme wa nane. Ni miongoni mwa
wale saba, naye anakwenda kwenye maangamizi. 12‘‘Zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi ambao bado
hawajapokea ufalme, lakini ambao watapokea mamlaka kuwa wafalme kwa wakati
mmoja pamoja na yule mnyama. 13Hawa
wana nia moja, nao watamwachia yule mnyama nguvu zao na mamlaka yao. 14Watafanya vita na Mwana-Kondoo,
lakini Mwana-Kondoo atawashinda kwa sababu Yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme
wa wafalme. Yeye atakuwa pamoja na watu wake walioitwa ambao ni wateule wake na
wafuasi wake waaminifu.’’ 15Kisha
yule malaika akaniambia, ‘‘Yale maji uliyoyaona, yule kahaba akiwa ameketi juu
yake ni jamaa za watu, makutano, mataifa na lugha. 16Zile pembe kumi ulizoziona, pamoja na huyo mnyama, watamchukia
huyo kahaba, watamfilisi na kumwacha uchi, watamla nyama yake na kumteketeza
kwa moto. 17Kwa maana Mungu
ataweka mioyoni mwao kutimiza kusudi lake kwa kukubali kumpa yule mnyama
mamlaka yao ya utawala mpaka maneno ya Mungu yatakapotimia. 18Yule mwanamke uliyemwona ni ule mji
mkubwa unaotawala juu ya wafalme wa dunia.’’
Haihitaji mtu
kuwa na elimu kubwa sana au uwezo mkubwa sana wa ajabu kiakili ili kuujua mji
huu ambao ni makao makuu na ya taasisi hii ijulikanayo kama milima saba na
inatawala na kumiliki wafalme saba wa dunia.
Kuna mji mmoja tu
unaojiri kuwe nao ni mji wa Roma na dini inayoiwakilisha ni ile iliyo kwenye
mfumo wa Kibabeloni ulioirithi.
Ufunuo 18 inasema:
1Baada
ya haya nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, akiwa na mamlaka
makuu na dunia ikamulikiwa na mng’ao wake. 2Naye akalia kwa nguvu kwa sauti kubwa, akisema: ‘‘Umeanguka!
Umeanguka Babeli ulio mkuu! Umekuwa makao ya mashetani na makazi ya kila pepo
mchafu, makazi ya kila ndege na kila mnyama achukizaye. 3Kwa maana mataifa yote yamekunywa
mvinyowa uasherati wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye, nao
wafanyi biashara wa dunia wametajirika kutokana na wingi wa utajiri wake.’’ 4Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka
mbinguni ikisema: “Tokeni katikati yake, enyi watu wangu, ili msije
mkashiriki dhambi zake, ili usije ukapatwa na pigo lake lo lote, 5kwa kuwa dhambi zake zimelundikana
hadi mbinguni, naye Mungu ameukumbuka uhalifu wake. 6Mtendee kama yeye alivyotenda, umlipe mara mbili kwa ajili ya
yale aliyotenda. Katika kikombe chake mchanganyie mara mbili ya kile
alichochanganya. 7Mpatie mateso
na huzuni nyingi sawa na utukufu na anasa alizojipatia. Kwa kuwa moyoni mwake
hujivuna akisema, ‘Mimi ninatawala kama malkia, mimi si
mjane wala sitaona huzuni kamwe.’ 8Kwa
hiyo mapigo yatampata kwa siku moja: mauti, maombolezo na njaa. Naye
atateketezwa kwa moto, kwa maana amhukumuye ni Bwana Mungu Mwenyezi. 9“Wafalme wa dunia waliozini naye na
kushiriki anasa zake watakapoona moshi wa kuungua kwake, watamlilia na
kumwombolezea. 10Watasimama
mbali na kulia kwa hofu kutokana na mateso yake na kusema: “
‘Ole! Ole Ee mji mkuu, Ee Babeli mji wenye nguvu! Hukumu yako
imekuja katika saa moja!’ 11“Na
wafanyi biashara wa duniani wanalia na kuomboleza kwa sababu hakuna anunuaye
bidhaa zao tena. 12Bidhaa za
dhahabu, za fedha, za vito vya thamani na vya lulu, kitani safi, nguo za rangi
ya zambarau, hariri, nguo nyekundu, aina zote za miti ya manukato, vifaa vyote
vya pembe za ndovu, vifaa vyote vya miti yenye thamani kuliko yote, shaba
nyeusi, chuma na marmar, 13mdalasini,
vikolezi, uvumba, manemane, uvumba wenye harufu nzuri, divai, mafuta ya
zeituni, unga mzuri na ngano, ng'ombe na kondoo, farasi na magari, watumwa, pia
na roho za wanadamu. 14‘‘Watasema,
‘Yale matunda ambayo roho yako iliyatamani yamekoma. Utajiri wako wote na
fahari yako vimetoweka, wala haviwezi kupatikana tena kamwe!’ 15Wale wafanyibiashara wauzao bidhaa
hizo na kupata utajiri wao kutoka kwake watasimama mbali naye kwa hofu ya
mateso yanayompata. Watalia na kuomboleza wakipiga kelele wakisema: 16‘‘ ‘Ole! Ole, Ee, mji mkubwa,
uliyekuwa umevikwa mavazi ya kitani safi, ya rangi ya zambarau na nyekundu,
ukimetameta kwa dhahabu, vito vya thamani na lulu! 17Katika muda wa saa moja utajiri wote mkubwa kama huu
umeangamia!’ ‘‘Kila nahodha, mabaharia wote wasafirio baharini na wote wafanyao
kazi melini watasimama mbali naye. 18Watakapoona
moshi wa kuungua kwake watalia wakisema, ‘Je, ulipata kuwako mji mkuu kama
huu?’ 19Nao watajirushia mavumbi
vichwani mwao huku wakilia na kuomboleza wakisema: ‘‘ ‘Ole, Ole, Ee mji mkubwa,
mji ambao wote wenye meli baharini walitajirika kwa kupitia mali zako! Katika
saa moja tu umeangamizwa! 20Furahia
uharibifu wake, Ee mbingu! Furahini ninyi watakatifu na mitume na manabii! Kwa
kuwa Mungu ameutendea kama vile ulivyowatendea ninyi.’ ’’ 21Kisha malaika mmoja mwenye nguvu
akainua jiwe kubwa kama la kusagia akalitupa baharini akisema: “Hivyo ndivyo
mji mkubwa Babeli utakavyotupwa chini kwa nguvu wala hautaonekana tena. 22Nyimbo za wapiga vinubi na waimbaji,
wapiga filimbi na sauti za wapiga tarumbeta hazitasikika ndani yako tena. Ndani
yako kamwe hataonekana fundi mwenye ujuzi wa aina yo yote. Wala sauti ya jiwe
la kusagia kamwe haitaisikika. 23Mwanga
wa taa hautaangaza tena ndani yako. Wala sauti ya bwana arusi na bibi arusi
kamwe haitasikiwa ndani yako. Kwa kuwa wafanyi biashara wako walikuwa watu
maarufu wa dunia na mataifa yote yalidanganyika kwa uchawi wako. 24Ndani yako ilionekana damu ya
manabii na ya watakatifu na watu wote waliouawa duniani.’’
Ufunuo 19 inasema:
Baada ya haya nikasikia sauti
kama sauti ya umati mkubwa wa watu mbinguni ikisema kwa nguvu :
“Haleluya! Wokovu na utukufu na
uweza ni vya Mungu wetu, 2kwa
maana hukumu Zake ni za kweli na za haki. Amemhukumu yule kahaba mkuu
aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake. Mungu amemlipiza kisasi kwa ajili ya
damu ya watumishi wake.’’ 3Wakasema
tena kwa nguvu: “Haleluya! Moshi wake huyo kahaba unapanda juu milele na
milele.’’
Watakatifu wakiimba
wimbo wa kumsifu Mungu wakimsifu kwa kumhukumu mwanamke huyu kahaba na kwa
kuwaangamiza watu na makuhani na mfumo wake kahaba huyu.
Kuanguka kwa Mwanamke Kahaba
Hebu na tuangalie
historia yake huko nyuma hadi kwenye mwanguko wa mfumo huu utakavyokuwa kwenye
siku za mwisho kwa mujibu wa fafanuzi za wanazuoni na wanahistoria. Alipaswa
kuandika kitabu akilenga kuyabadili mambo fulani alizozitaja lakini hatimaye
anuakiri ukweli wake. Hatimaye aliuawa..
Kutoka kwenye Nyumba nayopeperushwa kwa Upepo Kama Alivyoandika Malachi
Martin
Utaratibu uliofanyika katika kuuanzisha muundo wa Mnyama huyu
ulikuwa ni muundo wa kumweka manamke huu kahaba.
Tarehe 25 Machi 1957
Kulikuwa na Mawaziri wa Mabo ya nje sita waliokutanika huko Roma kutia
saini Mkataba wa kuunda Jumuia ya Kiuchumi ya Nchi za Ulaya. Nao walikuwa ni
hawa wafuatao:
Ubelgiji Paul-Henri Spaak
Uholanzi
Luxembourg
Italia
Ufransa Robert
Schuman & Jean Monet
Ujerumani Magharibi
Konrad Adenauer
Baada ya hapo walifanya kikao cha faragha na Papa Pius XII ambaye baada ya
kuondoka kwao aalimwambia mjeswiti wa Kijerumani na aliyekuwa amemshirikisha
jambo hili kwa ukaribu kwamba “Baba, Ulaya mpya itakuwa na siku yake ndogo.
Lakini itakuwa na siku moja tu…”
Waweza kujionea hilo pia kwenye jarida letu kwenye tovuti ya:
http://www.historiasiglo20.org/europe/traroma.htm
Dola hii ya Mnyama
itaungana na kutawala kwa kipindi cha saa moja tu. Alikuwa anamaanisha kwa
kuilinganisha na siku. Inaweza kudumu hadi mwezi mmoja lakini haitadumu. Lakini
papa huyu aliitabiria kuwa itadumu kwa siku moja tu. e ni Empire of the Beast
will come together
Mwaka 1960
Kwenye mdahalo wake Papa Yohana XXIII kwenye kile kilichojulikana kwa lugha
ya Kilatini kama re 3rd Secret of Fatima, (Mkakati wa Siri wa 3 wa
Fatima) ambao ulitakiwa utangazwe rasmi na Papa huyu mwaka 1960, kuliamriwa
kwamba hali ya mabo ilivyokuwa huko Urusi yalikuwa yanatatanisha. Na matokeo ya
shinikizo lililotolewa na sista Lucia wa Kikatoliki kwa kile alichokiita kuwa
kutoka wa “Malkia wa Mbinguni” linaweza kuwa ni sawa na kuinoa au kuipa makali
nchi ya Urusi na kumfanya kiongozi wake Nikita Khrushchev afanye matendo ya
kihalifu. Matokeo yake yalikuwa ni kufunguliwa kwa matendo ya kutesa watu na
siri yake haijawekwa wazi bado hadi sasa.
Hata hivyo nchi ya Urusi iliwekwa wakfu kwa Mungumke na ndiyo kwa kweli
itakuwa sehemu ya sababu ya vita vya siku za mwisho (soma jarida la Vita yar of Hamon-Gogu (Na. 294) [War of Hamon-Gog (No. 294)].
Tarehe 11 Oktoba 1962 hadi 8 Disemba
1965
Kwa mujibu wa Tovuti yetu ya: http://religion.wikia.com/wiki/Second_Vatican_Council
Mtaguso wa Pili wa Vatican wa Majumuisho na Dini
Nyingine, au pengine unaitwa Vatican
II, ulikuwas ni Mtaguso wa ishirini na moja,
maarufu kama Baraza la Muunganosho wa Dini kufanywa na Kanisa Katoliki la Roma. Lilifunguliwa
na Papa Yohana
XXIII mnamo Octoba 11, 1962 na na kufungwa na Papa Paulo VI Disemba 8, 1965. Takriban mapapa wanne waliofuatia
baadae walihusika katika kuweka mkakati wa kulifungua baraza hili wakihudhuria
vikao vyake kuvifungua na kuvifunga. Kardinali Giovanni Battista Montini, ambaye
alimrithi Papa Yohana XXIII alichukua jina la Paulo VI; Askofu Albino Luciani, aliyeurithi upapa baadae alijiita
Papa Yohana
Paulo I; Askofu Karol
Wojtyła, aliyefuatia alijiita Papa Yohana
Paulo II; na Padri Joseph
Ratzinger, aliyeko sasa ambaye kitaaluma ni mshauri na mwanateolojia, ambaye
alijiita Papa
Benedict XVI.[1][2]
Tarehe
29 Juni 1963 soma kurasa za 7-20 ili kujua mchakato
wake.
Siku
ya karamu ya hufanywa kwenye makanisa madogo yaliyoko ndani ya Mwatakatifu
Petro na Paulo na
iliyodumu siku 7 ambayo hufanyika mara baada tu ya kufanyika uchaguzi wa papa.
Kinachofavnyka
humo ni tendo la kumtawaza mwakilishi wa Malaika Mkuu Muasi yaani Lusifeli ili
achukue uongozi na utawala wa
Huu
unakuwa ndio “Muda wa Muafaka”. Kwenye kipindi hikihiki ndipo sherehe ya
kuhamisha mamlaka na kurekebisha au kubadilisha mambo fulani pia ilifanyika
kwenye kitengo kilichoko huko Karolina Kusini nchini Marekani.
Tarehe 6 Agost 1978 papa huyu alikufa.
Iliwahi
kutokea kuingia Papa “Kimakosa” ambaye alichaguliwa na akafa au
kuuawa baada ya kukaa kwenye kiti hiki kwa mudawa siku 33 tu. Kwenye kitabu
chake David Yallop chwnye kichwa cha maneno Kwa
Jina La Mwenyezi Mungu (Jonathan Cape, 1984) kilichandikwa
kwa maombi na ushauri wa wanazuoni na watafiti kuihusu Vatican wakidai kuwa
alikuwa ameuawa na wanaelezea ukweli wa jambo hili.
Kutoka
mwenye mahojiano kwenye magazeti kuhusu mapapa hawa wawili uliofanywa ni Waziri
wa Mambo ya Nje ya baraza la Makardinali (na mbaye alihusika kikamilifu na
mbaye hatimaye alikufa huko mjini Mablon tarehe 19 Machi 1979), inaonekana kuwa
miongoni mwao, au huenda papa Yohana Paulo 1, alijua kutawazwa kwake.
Papa
Yohana Paulo II pia hakuwa ni papa “muafaka” waliomtaka wao kwa mujibu wa
kitabu hiki cha mwandishi Martin.
Tendo la
kutawazwa rasmi Lusifeli awe Mungu, tendo lililofanywa na ridhaa ya
Ukweli ni
kwamba hakuna mgogoro wala uhasama kati ya hawa Freemason na Vatican bali lao
ni moja tu na wanashirikiana vizuri
Zaidi ya
yote, ni kwamba mikakati yote ya kisera ya nchi ya Marekani inafanya kazi bega
kwa bega na taasisi za kimataifa za Mnyama.
Mapapa
waliopita hivi karibuni hawakuweza kushirikishwa kwenye mikakati ya watu hawa,
bali nguvu za kishetani zilitumika kuuwezesha mkakati huu wa kudhibiti maongozi
ya dunia. Na hii ndiyo iliyomsababishia Yallop atakiwe kutoa maelezo kuelezea
kifo cha Papa Yohane Paulo 1, na kwa nini Papa Yohane Paulo II alifanikiwa
kuwekwa madarakani na akajulikana kuwa ni Papa wa Kislavia yaani asiye Mrumi.
Kile
kilichoonekana
Inayabana
mataifa kumi na tatu yanayochukuliwa kuwa ni muhimu zaidi katika kuipatia
malighafi muhimu kwa usalama wa Marekani n ani nchi muhimu kwa soko la Bidhaa
na Kihuduma kwa Nchi za Magharibi. Nchi hizo ni India, Pakistan, Bangladesh, Nigeria, Mexico, Indonesia,
Brazil, Ufilipino, Thailand, Misri, Uturuki, Ethiopia, na Columbia. Jambo muhimu
lililotiliwa maanani kwenye Mkataba huo ni kuangalia kuwa kasi ya ongezeko la
watu kwenye mataifa haya liko juu sana na linaweza kuathiri usalama. Kwa hiyo,
mkakati huu wa NSSM 200 iliweka wazi msimamo wake kuhusu hali hii.
Ikaidhinisha kupitia baraza linaloshughulikia masuala ya fedha ili litoe
fedha kupitia serikali ya Marekani na zipelekwe kwenye nchi hizi na hata kwa
nchi nyingine ili kuongeza kasi yao ya kiwango chao cha matumizi ya vidonge vya
kuzuia mimba, matendo utoaji mamba, matumizi ya ngono bandia au kutumia mipira
kwenye ngono na waendelee kutafiti njia nyingine zaidi zenye madhara.
Kwa hiyo, mpango huu wa kuzuia ongezeko la watu duniani kwa kisingizio
maarufu kama uzazi wa mpango kwa watu wa mataifa meingine ulikuwa ni muhimu
kwenye mkakati wa usalama wa Marekani na kama ilivyokuwa ni muhimu pia kwa hakika
ya usalama ya eneo lake. Sera hii ilipita kwenye mirengo yote miwili ya siasa.
Mwezi Novembea 26 1976 Rais Ford akitumia Kipengele cha Katiba chemye Maamuzi ya
Mkakati wa Usalama wa Taifa Namba 314 (NSDM 314) alianzisha mkakati huu
ujulikanao kama NSSM 200 ukiwa kama ni mwongozo muhimu kwa uwakilishi wa sera
za Marekani. Ulilenga kwenye Taasisi za Nchi za Kifedha, Ulinzi, Kilimo, Afya
na Huduma za Jamii, Uwakilishi kwenye shughuli za Kimaendeleo za Kimataifa na
kwenye Baraza la Uchumi la Rais. Matokeo yake Marekani ikajikuta ikizitumia
zaidi ya nchi nyingine zote kuziingiza kwenye mkakati huu wa kupunguza idadi ya
watu duniani maarufu kama uzazi wa mpango
(ameandika. Martin, kwenye kurasa za 430-431).
Nchi nyingi ziliunga mkono mkakati huu na kwa kupitia fedha zilizoithinishwa
na kutolewa na mfuko maalumu wa Umoja wa Mataifa kama ule unaoitwa Mfuko wa
Umoja wa Mataifa wa Idadi wa Kudhibiti Idadi ya Watu (Kwa kimimbo UNPF), Shirika
la Fedha la Kimataifa (IFM), Benki ya Dunia (WB), Shirikisho la Uzazi wa Mpango
(PPF) na wengine wengi kutoka kwenye mashirika na taasisi binafsi yaliyotafuta
fursa ya kushiriki mkakati huu wa upunguzaji wa idadi ya watu duniani kwa
kutumia mbinu zozote zitakazowezekana.
Tatizo linalojitokeza ni kwamba lengo la baadhi ya mapapa haw ani kwamba
wamekuwa wakiendeleza kuficha ukweli na kudanganya kwa maslahi ya mataifa
yaliyoendelea na kwa kuyanufaisha mashirika ya kishetani wanayoyategemea katika
kujiendesha na Vatican yenyewe.
Lengo la harakati za Kibinadamu kwenye mikakati ya Vatican ni kukomesha
makundi yao kwa kuwatumia vibaya wanawake kwa nyakati zake zote. Kwenye miaka
ya 1990, papa wa Kislovia alikabiliwa na wanaharakati na kufikishwa mahali pa
kukubaliana kwa ujumla mpango huu wa udhibiti wa idadi ya watu. Nchi ya Marekani
na papa huyu wa Kislocia walifikishwa mahali pa kuweka mjadala kwamba mataifa yote
yaingizwe kwenye mkakati huu wa dunia nzima wa kudhibiti ongezeko la watu na
inaelezwa kwamba alichaguliwa mtu aitwaye Rosicrucian Gibson Appleyard ili aanhae
mjadala au mdahalo huo (kitabu cha Martin, ukurasa wa 431).
Papa huyu wa Kislavia alichaguliwa kama ni mtu mwafaka sana kulishughulikia
jambo hili, na kama alivyokijukana kwenye kumbukumbu zake za kuwa ni “mwenye
kupendelea mpango huu kushibiti ongezeko la watu…akiwa pia na mtazamo wa kukomesha
uwezekano wa kutokea kwa maafa ya kimazingira unaotokana na ongezeko kubwa la
watu duniani” (kitabu cha Martin, ukurasa wa 435).
Kwa hiyo tatizo hili la madawa lilipojitokeza walihusika.
Kile kinachijulikana kama uvumilivu, licha ya jinsi alivyosema wakati
alivyoenda kwenye makanisa ya Kikatoliki iliashiria kuwa inaweza kutumika pia
(sura na ukurasa huohuo.
Hata hivyo tunaona kwamba walikuwa wanajua kwamba kulikuwa na mbinu kadhaa
za kudhibiti uzazi na uwepo wa mkakati wa kuharibu uwezo wa mbegu za uzazi kwa
kutumia matimizi ya madawa na vipodozi ni mambo yaliyozingatiwa sana. Watawala
wa Marekani haikuwa na wasiwasi wowote na wala hawakuwa wa viwanda vya
kutengeneza vipodozi wala mihadarati.
Hata hivyo, kulikuwa na hamasa ndogo kwa Vatican pale lilipokuwa
linaongelewa suala lolote linalohusu kuwatumia au kutowatumia mabinti waimbaji
wa kwaya makanisani kwenye mpango huu wa kuwaingiza kwenye matendo ya usagaji
au ngono za kishoga wafanyiwe na makasisi wao na wale makasisi waliobobea
kwenye shughuli za Kifreemason, maelekezo yao yasiyo na woga wa kufanya aina
hizi za ngono kufuru, na waliobobea kwenye mafundisho yao mapotofu na matumizi
ya simu yenye lengo la kumsisimua mtu kingono yenye wastani w amara 50,000 kwa
mwaka na kuendeleza hali hiyo.
Awamu ya pili ya mkakati huu wa kuzuia ongezeko la watu inatumia madawa
yanayotengenezwa huko Marekani na inahusisha pia makubaliano ya Biashara ya
Pamoja yanayozihusiaha pia nchi za Australia na nchi nyingine zilizoendelea.
Lilikuwa ni tendo ambalo kwamba makanisa na Mashirika ya
bahati na Sib una mashirika mengine ya huruma yalihusishwa kutoa madawa kila siku
ambayo yalihitajika na yaliwekwa alama na kupelekwa na wataalamu na mabingwa wa
elimu ya madawa ili watoe ushauri kwenye mataifa yanayoendelea ili watumike
kwenye kazi ya kuwahudumia watu maskini, na vifaa ambavyo vingewasababisha
watoto kuharibikiwa akili zao kwa kupitia magonjwa kama vile homa ya malaria na
magonjwa mengineyo.
Kampuni Kubwa na Maarufu sana la Madawa la Marekani lilitumia haiba yake ya
umaarufu kuzuia ufungishaji mizigo na kusaidia mkakati huu wa ugawaji wa madawa
na kulazimisha yaharibiwe tendo ambalo lilisababisha vifo vya watu wengi sana
kwa ajili ya uchoyo wao huu na mkakati wao wa kudhibiti ongezeko la watu.
Jambo hili halikutokea kwa bahati mbaya. Bali hii ilikuwa ni sera iliyowekwa
kwa makusudi kabisa. Na ndivyo ilivyotokea pia kwenye tukio la upigaji marufuku
wa matumizi ya dawa aina ya DDT ulikuwa ni mkakati wa makusudi ulioingizwa
kisiasa ukilenga kuendekeza kwa lazimma kutokee vifo vitokanavyo na ugonjwa wa
malaria kwenye nchi zinazoendelea hali iliyosababisha vifo vya watu zaidi ya
milioni moja kwa hali ambayo ingeweza kuepukwa na kila mwaka makatazo haya yaliendelea
kulazimishwa, na Umoja wa Mataifa iliiridhia na kuruhusu jambo hili. Hatimaye
walilazimishwa na wanasayansi kuhusu jambo hili ili kuendeleza marufuku hii na
kuendeleza mkakati huu wa kudhibiti hali ya ongezeko la watu kwa kubuni mkakati
wa vifo vinavyotokana na ugonjwa wa malaria. Mambo yote haya yanatokana na
mkakati huu wa makusudi wa udhibiti wa kiwango zha ongezeko la watu jambo
ambalo wanaweka mkakati mwingine wa kudhibiti ongezeko wa idadi ya madhehebu ya
kidini wakioanisha na mkakati wao huu wa kuwaongezea uwezo wa kudhibiti
ongezeko la watu. Huu ni uhailifu mkubwa dhidi ya ubinadamu.
Kuna mageuzi ya
kijamii yanayoendelea hivi sasa na ambayo yamesababisha
kuanzishwa kwa mfumo wa Kibenki wa kile kinachojulikana kama Tangazo Jipya la
Mfumo Mmoja Duniani unaolenga kuharibu kabisa hali ya umoja kwenye jamii zetu.
Vuguvugu la wanaharakati wanaotetea haki za wanawake wanawashawishi wanye
mabenki wawape kipaumbele cha kuwakopesha wanawake na kuwaingiza kwenye maeneo
muhimu kiuchumi kwenye jamii zetu jambo ambalo hatimayake ni kuharibu hali ya
umoja kwenye familia. Hali hii ilikamilika lengo lake baada ya Vita Kuu ya II
ya Dunia na hali ilisaidia kuiunganisha tena Ulaya na upande wa Magharibi kwa
ujumla. Vuguvugu hili la wanaharakati hawa wa haki za wanawake wataurudisha
mfumo ule dhidi yake wenyewe kwa kutumia mafundisho ya utoaji mamba na kwa
uvunjifu wake wenyewe.
Kile
kitakachotokea kwenye siku za mwisho ni mifumo mitatu ya kidini. Hali ya
kuushanbulia utaratibu wa kawaida na kuubadili kwenye mifumo ya Kiutatu
imekueudiwa na waabudu Shetani walioko kwenye mfumo huu wa Kiutatu wenyewe.
Madhehebu ya Kiprotestant yamedharauliwa na kuingiliwa na vuguvugu la ndoa za
jinsia moja na usagaji na ushoga hata ulawiti. Kinacholengwa na kulazimishwa hapo
ni kuweko na migawanyiko miongoni mwao hawa Waprotestant sawa na kama walivyo
kwa wanaharakati wanaotetea maisha ya kitamaduni wakubalike na wajumuishwe
kwenye mambo yaliyodumu kwa muda mrefu na yasiyobadilika ya Warumi. Watoto
makahaba ambao ni wana way ule kahaba mkuu watajumuishwa kwa lazima kwenye
vuguvugu hili la wana Utatu.
Katika
kulifanikisha hilo, kanisa la Roma linajiandaa sasa kwa mpango wa kimageuzi
makubwa wa kuwaruhusu makasisi wao kuoa ili hatimaye liwe ni kanisa
linaloongozwa na makasisi waliooa.
Vuguvugu la
wanaharakati wanaotetea haki za wanawake na mashoga na wasagaji nao
watalazimisha wanawake aruhusiwe kuwa makasisi.
Kwa hiyo ni vyema
kujua kwamba vuguvugu hili la “waliberali” litabadili kabisa mfumo wa kidini
ili kufanya madhehebu mengi ya kile kinachoitwa na kujulikana kama mfumo wa
Kikristo wajiundie madhehebu mengi lukuki yanayoamini na kufundisha mfumo mpya
ujulikanao kama vuguvugu la itikadi ya kidini kisasa au inayoendana na wakati
inayojumuisha pia mafundisho ya kutokula nyama na kusisitiza ulaji wa
mbogamboga tu, na mfumo wa ndoa utabadilishwa pia ili kuupa nafasi mfumo wa
ndoa za jinsi moja za ushoga na usagaji na kuwafundisha watu waone kuwa ni
kawaida tu kama ilivyokwisha anzishwa sasa na wanaharakati hawa na unavyoonekana
kushamiri kwenye jamii.
Jambo la tatu
kuonekana kwenye mfumo huu litakuwa ni mfumo na hali ya mwisho litakalokuwanayo
Kanisa la Mungu katika siku za mwisho.
Mfumo utakalokuwanao utaanza kwa muonekano mdogo sana hapa mwanzoni lakini
utaendelea na kukua hadi juhudi za makusudi na za pamoja zitakapofanywa ili
kuliangamiza na kulikomesha na ndipo Kristo atarudi ili kuwaokoa. Kipindi cha
Wafiladefia ndicho kanisa hili litakapopata nguvu na kujiunga na kukua.
Mafundisho yake yataimarika na mfumo wa imani yake vitaanzishwa. Hatimaye
litafarijiwa na wale Mashahidi na litakuwa ni chanzo cha mgawanyiko wa mfumo wa
kiuchumi.
Kutakuwa na makundi makuu mawili yatakayojitokeza kugawanyika kiuchumi
kwtika siku za mwisho, nayo ni kati ya waamini Utatu na wale watakaotoka kwenye
harakati za utitiri wa muungano wa kidini utakaotokana na tama ya kimaslahi
itakayochochewa na mfumo wa kifedha wa huyu Mnyama.
Na kwa hali hiyohiyo, watu wanaojiona kuwa wanatofautiana
na Kanisa la Mungu watalazimika tu kujiunga kwenye mfumo na imani ya Makanisa
ya Mungu kwa ajili ya ulazima
utakaotokana na uhitaji wa kuijua na kuifuatisha Kalenda ya Mungu ili waweze
kuendelea vizuri na kuepuka kutiwa chapa ya Mnyama. Kalenda itatumika kwa minajili
ya kujipatia mkate wa Mana katika siku za Sabato, Mwandamo wa Mwezi na kwenye
Sikukuu Zilizoamriwa na Mungu. Mtu anaweza kubisha hadi sura yake ikabadilika
rangi na kuwa ya bluu, bali ukweli ni kwamba itakuwepo au hautakuwepo.
Na wale wote ambao hawataweza kununa au kuuza watatakiwa kumtegemea Mungu
na Kalenda Yake ili waendeleekuishi. Ni kama Israeli walivyokuwa jangwani
ndivyo litakavyokuwa Kanisa la Mungu katika siku za mwisho. Mkate wetu na
chakula vitapatikana kwa uhakika na tutaulisha mwili wa Kristo kwa kipindi hiki
chote. Kamwe Mungu hafanyi jambo pasipo kutoa mlango wa kutokea naye atafanya
hivyo ili kutuokoa. Tutalazimika kuzitunza Sabato zake na Miandamo ya
Mwezi na Sikukuu zake Takatifu na
hatutakuwa na mashaka kujua zitakuwa lini ingwa kutakuwa hakuna chakula katika
siku hizo. wakati huo. Tutaishi kwa imani kwa miezi 42 kipindi hiki ambacho
Mnyama atakuwa anashikilia hatamu za uongozi duniani. Baada ya wale mashahidi
kumaliza kazi yao kwenye kipindi cha mwisho, ndipo Masihi atarudi nasi
tutafufuliwa na kufanywa wapya.
Ndipo Kristo atawashughulikia kuwahukumu manabii wote wa uwongo na yule
Mpingakristo kipindi hiki cha kurudi kwake.
Ni katika kipindi hiki ndipo huyu Mnyama atamgeukia yule Mwanamke Kahaba.
Mkuu wa dini ya Roma ataangamizwa pia.
Matatizo yanaanza kujitokeza kwenye kipindi hiki cha sasa cha upapa wa
Benedict XVI. Papa atakayefuatia atapewa jina la Petro Mrumi, atakayechukua
jina hili kwa mujibu wa Unabii wa Kirumi wa Pius XIII, usemao kuwa ataondoka
Roma na miili ya makasisi na ndiye atakuwa ni papa wa mwisho. (soma jarida la Papa wa Mwisho (Na. 288) [The Last Pope
(No. 288)].
Roma yenyewe itaangamizwa yote kabisa. Itakubwa na maafa ya kiasili.
Nanabii waliitabiria kuwa itangaamizwa kwa mafuriko.
Kwa sasa kuna vuguvugu la volcano kwenye kiini cha Bahari ya Tyrrhenian.
Volcano ya Masili ilipaa juu kwa futi 9800. Ilienda umbali wa maili 44 na
kusambaa maili 19 na kufikia kiasi cha robo maili (chini ya mita 500) chini ya
usawa wa bahari na inaweza kuangamiza kabisa eleo lote la Kusini mwa Italia
pamoja na miji ya Naples na Roma. Wafanya biashara wakuu watakaokuwa na mnyama
huyu wataangamizwa na maafa makuu yatokanayo na maovu yao waliyoyatenda.
Inaweza kutokea hata kesho.
Maangamizo ya Rumi yatatokea kwa siku moja tu. Itaangamizwa. Itashambuliwa
kwanza na majeshi ya Kiislamu na wananchi wenye hasira watawageukia makasisi
wao pia na kisha Rumi yenyewe itaangamizwa kabisa. Utaangamizwa kwa mabomu na
kisha utamaliziwa kwa mafuriko.
Kitabu cha nabii Danieli kinamtaja mrithi huyu wa dola ya Babeli na
Mwanamke huyu kahaba.
Mfumo wake umeelezewa kwenye kitabu cha nabii Danieli sura ya 2 ukiendelea
hadi kwenye siku za mwisho na tumemwelezea huyu mnyama mwenye kichwa cha
dhahabu hadi chini kwenye vidole kumi vya chuma iliyochanganika na udongo;
tumemwelezea kwenye majarida yaliyopita. Vidole vya sanamu ile vilikuwa ni vya
udongo vilivyochanganika na udongo ambavyo vilikuwa na maana ya yule
atakayeirithi Dola hii ya Rumi, nk. Ile waliyoiita kuwa Dola Takatifu ya Kirumi
na sola ya mwisho yenye vidole kumi ndiyo Dola hii ya Mnyama inayotafuta jinsi
ya kumwangamiza huyu Mwanamke kahaba ambaye ni Kanisa hili la Utatu lililotokwa
kwenye Dola yenye makao yake makuu huko Roma na Constantinople.
Ni ile hadithi ya Mfalme wa Kaskazini
na wa Kusini waliobebwa kwenye kitabu cha Danieli sura ya 11. Maelezo ya kina
kuhusu jambo hili yametolewa kwenye jarila lihusulo habari za unabii wa Danieli
sura ya 11.
Kwenye ile vita ya Wafalme wa Kaskazini na wa Kusini tunaowaona kwenye sura
ya 11:30 ikiwataja wafalme ambao meli za Kitimu zililetwa, ni katiks kipindi
ambacho Mfalme wa Kaskazini ataubadili nfumo wa vita uwe kwenye vurugu za
kidini ukipinga Agano Takatifu na watu wa Mungu. Kutakuwa na mateso makali sana
na ya muda mrefu watakayofanyiwa wateule yatakayochechewa na mfumo huu wa Dini
ya Kaskazini.
Kipindi hiki Kanisa la Mungu litaingiliwa wapelelezi wasio na nia njema na
wale watakaotokea kwenye dini ya uwongo ya Mwanamke Kahaba. Wengi watakuwa
kwenye mateso lakini watazifanya nguo zao kuwa nyeupe kwa damu ya mwana kondoo.
Hali hii ilishagawahi kutoke kwenye karne ya ishirini na inatarajia kutokea
tena katika siku hizi za mwisho kinachotarajiwa kutokea kwenye miaka michache
tu ijayo.
Danieli 11 inasema:
30Meli za nchi za Kitimu zitampinga, naye atavunjika moyo. Ndipo atageuka
nyuma na kutoa wazi hasira yake dhidi ya agano takatifu. Atarudi na kuonyesha
fadhili kwa wale waliachao agano takatifu. 31Majeshi yake yenye
silaha yatainuka ili kunajisi ngome ya hekalu na kuondolea mbalisadaka ya
kuteketezwa ya kila siku. Ndipo watalisimamisha chukizo la uharibifu
lisababishalo ukiwa. 32Kwa udanganyifu atapotosha wale walionajisi agano,
lakini watu wanaomjua Mungu wao watampinga kwa uthabiti. 33Wale wenye hekima
watawafundisha wengi, ingawa kwa kitambo watauawa kwa upanga au kuchomwa moto,
au kukamatwa na kufanywa mateka. 34Watakapoanguka, watapokea msaada kidogo, nao wengi
ambao si waaminifu wataungana nao. 35Baadhi ya wenye hekima watajikwaa, ili kwamba
waweze kusafishwa, kutakaswa na kufanywa wasio na waa mpaka wakati wa mwisho,
kwa maana bado litakuja kwa wakati ulioamuriwa. 36Mfalme atafanya
apendavyo. Atajikweza na kujitukuza mwenyewe kujihesabu mwenye nguvu zaidi juu
ya kila mungu naye atasema vitu ambavyo havijasikiwa dhidi ya Mungu wa miungu.
Atafanikiwa hadi wakati wa ghadhabu utimie, kwa maana kile kilichokusudiwa
lazima kitokee. 37Hataonyesha heshima kwa miungu ya baba zake au kwa
yule aliyetamaniwa na wanawake, wala hatajali mungu ye yote, bali atajikweza
mwenyewe juu yao wote. 38Badala ya kuwajali hao miungu, ataheshimu mungu wa
ngome, mungu ambaye hakujulikana na baba zake, atamheshimu kwa dhahabu na
fedha, kwa vito vya thamani na zawadi za thamani kubwa. 39Atashambulia ngome
zenye nguvu mno kwa msaada wa mungu wa kigeni naye atawaheshimu sana wale
watakaomkubali yeye. Atawafanya watawala juu ya watu wengi na atagawa nchi kwa
kulipia.
Mfumo wa utawala
watapewa waabudu sanamu hawa waliogawanyika vikundi mbalimbali, na wale
watakaoiunga mkono dini hii ya uwongo ya mwanamke huyu Kahaba ndio watakaopewa
mamlaka na uwezo wa kumiliki na kudhibiti ugawaji wa ardhi.
Tunaenda
kuangalia nyakati hizi za mwisho na mgogoro huu mkuu wa mwisho vitakavyotokea
kipindi cha mwisho cha mateso.
Danieli 11 inasema:
40“Katika wakati wa mwisho mfalme wa Kusini
atapigana naye vita, naye mfalme wa Kaskazini atamshambulia kwa magari ya vita
na askari wapanda farasi na idadi kubwa ya meli. Atavamia nchi nyingi na
kukumba nchi hizo kama mafuriko. 41Pia
ataivamia Nchi yakupendeza. Nchi nyingi zitapinduliwa, bali Edomu, Moabu na
viongozi wa Amoni wataokolewa kutoka katika mkono wake. 42Atapanua mamlaka yake juu ya nchi nyingi, Misri haitaepuka. 43Atamiliki hazina za dhahabu, fedha
na utajiri wote wa Misri, pamoja na Walibia na Wakushi kwa kujisalimisha. 44Lakini taarifa kutoka mashariki na
kaskazini zitamshtua, naye ataondoka kwa ghadhabu nyingi ili kuangamiza na
kuharibu kabisa wengi. 45Atasimika
mahema yake ya kifalme kati ya bahari na mlima mtakatifu wa kupendeza. Hata
hivyo, atafikia mwisho wake, wala hakuna ye yote atakayemsaidia.
Mfalme wa Kusini
ndiye atakayeianzisha Vita hii ya Mwisho. Itawajumuisha Wamisri walioenenda
kinyume na Mfalme huyu wa Kaskazini mwaka 1956 kwenye mgogoro wa kugombea
mfereji wa Suez na waliomudu kuchukua udhibiti wa mfereji huu wa Suez. Huu
ulikuwa ni mlolongo wa kipindi cha miaka 40 cha nyakati za mataifa (soma jarida
la Kuanguka kwa Misri: Unabii wa Farao Aliyevunjika
Mikono (Na. 036) [The Fall of Egypt: The Prophecy of Pharaohs Broken Arms (No.
036)].
Dola hii ya
Mnyama ilianza kuwekwa kwenye mchakato wa kuianzisha tangia kipindi hiki pia
mgogoro huu mkubwa na wa mwisho unaendela tangia mwaka 2001 hadi 2025.
Katika kipindi
hiki ndipo kutakuwa na Ufufuo wa Kwanza wa wafu.
Malaika mkuu
Mikaeli ataongoza mapambano na kuwakomboa Waisraeli.
Danieli 12 inasema:
1“Katika
wakati huo Mikaeli, mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako, atainuka.
Kutakuwako wakati wa taabu ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati
huo. Lakini wakati huo, watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa
limeandikwa kwenye kitabu, ataokolewa. 2Watu
wengi ambao wamelala kwenye mavumbi wataamka, baadhi yao kwa uzima wa milele,
wengine kwenye aibu na kudharauliwa milele. 3Wale wenye hekima watang'aa kama mwanga wa mbingu, nao wale ambao
huwaongoza wengi kutenda haki, watang'aa kama nyota milele na milele. 4Lakini wewe Danieli, yafunge na
kuyatia muhuri maneno ya kitabu hiki mpaka wakati wa mwisho. Wengi watakwenda
huku na huko na maarifa yataongezeka.’’
******************
Kipindi hiki
nguvu zetu kama Watu Watakatifu zitavunjika na Ufufuo wa Kwanza utatokea.
Mapambano yataendelea tangia hapo na ndipo Kristo atauangamiza na kuukomesha
Mfumo wa kidini wa Kirumi na kuiangamiza Dola hii ya Mnyama na ya Mpingakristo
na ya Nabii wa Uwongo.
Danieli 12 inasema:
5Ndipo mimi Danieli,
nikaangalia, nako mbele yangu walisimama wengine wawili, mmoja katika ukingo
huu wa mto na mwingine ukingo wa pili wa mto. 6Mmoja wao akasema na yule mtu aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa
juu ya maji ya mto, “Je, itachukua muda gani kabla mambo haya ya kushangaza
hayajatimizwa?’’ 7Kisha mtu yule
aliyevaa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, akainua mkono wake wa
kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni, nami nikamsikia akiapa kwa
jina lake Yeye aishiye milele, akisema, “Itakuwa wakati, nyakati mbili na nusu
wakatia. Nguvu za watu watakatifu zitakapokuwa zimevunjwa kabisa, ndipo
mambo haya yote yatakapotimizwa.’’ 8Nilisikia,
lakini sikuelewa. Kwa hiyo nikauliza, “Bwana wangu, matokeo ya haya yote
yatakuwa nini?’’ 9Akajibu,
“Danieli, enenda zako, kwa sababu maneno haya yamefungwa na kutiwa muhuri mpaka
wakati wa mwisho. 10Wengi watatakaswa na kuondolewa mawaa na kuwa safi,
lakini waovu wataendelea kuwa waovu. Hakuna mmoja wa waovu atakayefahamu,
lakini wale wenye hekima watafahamu. 11“Tangu wakati ule wa kukomeshwa dhabihu ya kila siku na
kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu kutakuweko siku 1,290. 12Amebarikiwa mtu yule atakayevumilia
hadi kufikia mwisho wa hizo siku 1,335. 13“Kuhusu
wewe, enenda zako mpaka mwisho. Utapumzika, nawe ndipo mwisho wa hizo siku
utafufuka ili kuupokea urithi uliowekwa kwa ajili yako.’’
***************
Mwanamke huyu Kahaba atatafuta jinsi ya kufanya udhibiti na kuwaangamiza
Watakatifu wa Mungu na atafanikiwa kwa kitambo na yule Mnyama atamgeukia huyu
Mwanamke Kahaba na kumwangamiza kwa kuwa Shetani atakuwa amemchukia Kahaba huyu
ila ataweka utaratibu kukomesha ukuaji wa Kanisa la Mungu na alikuwa
anashurutishwa kufanya hivyo na atanuia pia kuzichoma moto Biblia kuwaua wale
wote wanaoitwa wateule wa Mungu.
Mwishoni kabisa wakati kipindi chake kikifikia mwisho, atamwangamiza yule
Kahaba kwa kuwa ameisha timiza leno lake na kumwona kuwa sio wa muhimu tena
kwake.
Kwenye Sehemu ya III A na B tutaorodhesha mambo yatayosababisha vita na
masuala ya kuchumi yaendelee, na mwanguko wa kijamii wa Mfumo wa Dunia na jinsi
Masihi atakavyouchukulia hatua atakaporudi.
q