Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[038B]

 

 

 

Ishara za Mbinguni za Mhuri wa Sita Kwa Muktadha Wake

 

(Toleo La Edition 1.0 20120801-20120801)

 

Jarida hili ni Sehemu ya II ya somo hili la Ishara za Mbinguni na linaziwekwa kwa muktadha wake na unabii na Maonyo ya Siku za Mwisho zinazoonyesha ashirio la kurudi kwa Masihi.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki ©  2012 Wade Cox)

(tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ishara za Mbinguni za Mhuri wa Sita Kwa Muktadha Wake


Utangulizi

Kwenye jarida la I (soma jarida la Ishara za Mbinguni Sehemu ya I (Na. 38A)) tuliona nadharia au dhana ya matukio ya upatwaji wa jua unavyotokea katika Siku Takatifu kwenye mzunguko huu unaofuatia na wa pili wa Usomaji wa Torati katika mwaka 2019 na maana zake kwa kuhusianisha na uwezekano wa kuja au kurudi kwa Masihi.          

 

Inaonyesha kweli fulani zenye mashiko na zakuvutia na hitimisho yapaswa itolewe iashiriayo kwamba ishara zapaswa zifanywe zinazohusiana na kipindi cha kufuatia kuandama kwa Mwezi amayo ni Ishara kuu ya Mbinguni ambayo iliwekwa kule katika kuweka mwelekeo wa kutumiwa wa Kalenda ya Mungu iliyotumika kama Kalenda ya Hekaluni hadi kipindi cha kuvunjwa na kuharibiwa kwa Hekalu kwa mara ya mwisho ya historia ya Kale ya Israeli huko Yerusalemu, na Hekalu la huko Heliopolis nchini Misri lilifungwa kwa amri ya Vespasian kabla ya Pasaka ya mwaka 71 BK. 

 

Kalenda ya Mungu ilishikwa na kutumiwa na Makanisa ya Mungu tangu wakati huu na kuendelea kwa mujibu sawa na Kalenda ya Hekaluni. Hawakupumbazwa na mafundisho mapotofu nay a kizushi ya Wayayhudi kama walivyokuwa wanaishika Kalenda ya Hekaluni kwa kipindi cha miaka 331 kabla ya muda huu. Wayahudi walikuwa hawajaitunga Kalenda ya Hilleli hadi wakati Rabi Hilleli wa II alipopewa maono ya kuanzisha kalenda ya uwongo na potofu kutokana na marabi wawili wa Kibabeloni mwaka 344 BK na ilirekebishwa ili kukithi mapokeo ya Wayahudi, na ikatolewa na kurekebishwa zaidi na zaidi tangu mwaka 358 BK hadi kwenye karne ya 12. Marabi waligundua kuwa Kalenda ya Hilleli haikuwa sahihi, lakini walidai kwamba ilipaswa kusubiriwa hadi Masihi atakapojumuishwa. Hili ni jambo lisilokubalika, kwa kuwa Mungu sio wa machafuko.

 

Kalenda ya uwongo haikushikwa kamwe na Makanisa ya Mungu hadi kipindi ulipotokea ukengeufu kati yao kama ilivyotokea katika karne za 18-19 huko Transylvania na katika karne ya 20 huko Marekani na kutoka huko uliingia huko Yerusalemu na Nigeria (soma majarida ya Kalenda ya Mungu (Na. 156); Kalenda na Mwezi Mwandamo: Miahirisho au Sikukuu? (Na. 195) na Kubadilishwa kwa Kalenda ya Mungu Katika Yuda (Na. 195B)).

                                   

Ratiba ya Siku za Mwisho   

Ratiba ya matukio ya siku za mwisho yalionyeshwa kutoka kwenye nabii za Danieli na pia kuhusu Kuanguka kwa Misri.

 

Tunajua kwamba nabii za Danieli zilianzia kwa kuonyesha habari za falme au dola za Babeli na sanamu ya Danieli 2 ambapo kulionekana dola zilizokuwa chini ya kichwa cha dhahabu ya Babeli iliyoanzishwa na Nebukadreza ambaye ndiye alikuwa kile kichwa cha dhahabu. Alianza kutawala tangu kwenye Vita ya Carchemish mwaka 605 KK. Dola hizo zilikuwa ni Babeli tangu mwaka 605 KK yenye mikono miwili ya miaka 40 kuhusu jinsi ilivyoitawala Misri tangu mwaka 605 hadi uhuru wa Misri ya kale wa mwaka 565 KK na Mashambulizi ya Kambise mwaka 525 KK.  Mchakato huu ulikuwa ni unabii wa Mikono Iliovunjika ya Farao ambayo imeorodheshwa kwenye mwandamano wa majarida ya Kuanguko kwa Misri (Na. 36) na Kuanguka kwa Misri Sehemu ya II: Vita vya Mwisho (Na. 36_2).

 

Mara saba za dola ya Babeli zilienda kutoka kipindi cha mwaka 605-525 KK cha miaka 2520 hadi kile cha miaka ya 1916-1996 BK hadi kwene Nyakati za mwisho za utimilifu wa Mataifa. Mwaka 1997 ulikuwa ni mwanzo wa kile kinachojulikana kama Agizo Jipya la Mufumo wa Ulimwengu na Dola ya Mnyama kama inavyoelekea kuchukua hatamu ya kuingoza dunia na hatimaye kuelekea kwenye maangamivu kamili wakati atakapokuja Masihi na kipindi cha Utawala wa Milenia wa Mungu kwenye Yubile ya mwaka  2027.

 

Mwandamano wa nyakati za dola hizi ulikuwa ni mwanzo pia au kufunguliwa kwa ratiba hii.

 

Ufalme wa Wamedi na Waajemi uliendelea tangu utawala wa Koreshi. Agizo la kulijenga tena Hekalu lilitolewa na Koreshi lakini shughuli hii ya kulijenga upya ilisimamishwa na Koreshi Makroka [Cyrus Macrocheir] aliyejulikana pia kama Artashasta I na Wayunani. Ujenzi huu ulisimamishwa hadi wakati wa utawala wa Dario II Mwajemi kwenye mwaka wake wa pili na amri ya kulijenga tena Hekalu ilitolewa na Artashasta II kama tunavyoona kutokana na unabii wa Danieli sura ya 9.  Nehemia alikuwa ndiye mtiwa mafuta wa kwanza ambaye alitumwa kwenda kuanzisha ujenzi huu wa Hekalu mwishoni mwa majuma saba ya miaka. Unabii huu na tafsiri potofu iliyofanywa kwenye tafsiri ya Biblia ya Tafsiri ya Mpya ya Mfalme Yakobo [KJV] ya Danieli 9:25 vimefafanuliwa kwenye jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13).

 

Ile Dola iliyoonyeshwa kama Kondoo Mume ya Wayunani ambayo imeiangamiziliambali Dola ya Kondoo mume ya Waajemi kama ilivyotabiriwa kwenye Danieli 8:5-8 (na pia kwenye Danieli sura ya 11) ilikuwa ni ile ya Iskanda Mkuu. Yeye pamoja na Ezra alifariki wakati mmoja katika mwaka 323 KK. 

 

Dola ya Mbuzi mume ilikuwa ni ile ya Wayunani na iliyoonyeshwa kuwa ya Shaba. Ziliendelea hadi kuifikia ile ya Warumi ambayo ni dola iliyoishwa kuwa yenye Miguu ya Chuma. Dola iliyofuatia ilikuwa yenye Nyayo zilizochanganyika Chuma na Udongo ambayo ni ile iliyokuwa ikijulikana kama Dola Takatifu ya Rumi iliyodumu kuanzia mwaka 590 BK hadi mwaka 1850. Dola hii ilifungwa na maandalizi yalianza rasi ya Vita vya Mwisho ambayo ilianzia kwa Vita Kuu ya I ya Dunia. Dola hii ilipasa ifuatiwe na Dola ya Dunia ambayo itaundwa kwa Vidole Kumi vya Chuma na Udongo vitakavyounda Dola Kuu ya Dunia ya Siku za Mwisho na ambayo itaangamizwa na Kristo atakaporudi akiwa ni lile jiwe lisilofanywa kwa mikono ya mwanadamu na ambalo litaipiga ile sanamu ile ya mfumo mpotofu litakaloipiga miguuni mwake na kwenye vidole vyake na kuisagasaga milele.

 

Daraja ambalo huyu Beberu wa mbuzi alilitumia kumshambulia huyu Kondoo mume lilikuwa ni Daraja la Granicus na kutokana na mapigano yale unabii wa jioni 2300 na asubuhi zake kwa hesabu za siku moja kuwa mwaka zinatufikisha hadi kwenye karne ya 20 hadi katika mwaka 1967. Vita ya wakati ule iliendeleza pia mchakato wa wakati wa Nyakati za Mwisho (soma jarida la Kuelezea Juu ya Ratiba ya Nyakati (Na. 272)).

 

Miaka 40 ya kwanza ya mkono wa Kwanza ilienda kwenye matayarisho ya vipindi vya kuanzia miaka ya 1912-1914-16. Mwaka 1916 Vita Kuu ya Somme upande wa magharibi ya Ulaya na vita kadhaa vya mashariki vilianzisha mwanzo wa mfululizo wa Vita vya Mwisho. Miaka 40 ilienda tangu mwaka 1916 hadi uhuru wa Misri tangu mwaka 1953-1956 na mgogoro wa kugombania mfereji wa Suez. Tangu wakati ule Misri na imani ya Kiislamu ilichukua mahala pa Mfalme wa Kusini aliyeandikwa kwenye Danieli sura ya 11.

 

Mnamo mwaka 1917 Palestina ilitwaliwa na na kuwa kwenye Dola ya Ottoman na majeshi ya muungano ya Jumuia ya Madola na iliyojulikana kama Azimio la Balfour kwa ajili ya Palestina lilishuhudia nchi au taifa la asili la Wayahudi likitangazwa.

 

Mwaka 1947 Israeli walizidisha harakati za kujipatia uhuru na walipigana vita vyake vya kwanza vya kupigania uhuru hadi walipoupata mnamo mwaka wa 1948.

 

Ni kama tuliojionea kwenye Sehemu ya I ya jarida hili la Ishara za Mbinguni za Mhuri wa Sita ulianza kufanya kazi tangu wakati huu.

 

Maana ya mwonekano wa ishara hizi ambazo ni utungu tu yameripotiwa kwenye makala iliyoelezewa kwenye Sehemu ya I. Ishara hiyohiyo ya damu nyekundu na miezi yake ilitokea baada ya \israeli kufanyika kuwa taifa mwaka 1948 na ilitokea hivyo katika miezi ya Kwanza na Saba za miaka ya 1949 na 1950.

 

Mara ya mwisho mfululizo huu wa matukio ya kupatwa kwa mwezi kutokea yalikuwa na maana na umuhimu wake sana kwa Wayahudi walioko huko Israeli. Ishara hii ilifuatiwa na nita ya mwaka 1967 na kuunganishwa kwa Yerusalemu tangu mwaka ule kulihusiana na Pasaka ya mwaka 1968. Kipindi kilikuwa ni cha miaka 9.5 kabla ya Yubile iliyotuatia ya Siku ya Upatanisho ya mwaka 1977. Ulikuwa ni mwaka wa sita wa Mzunguko wa Sabato na mji wa Yerusalemu ulikuwa mikononi mwa Israeli tayari kwa mwaka wa Sabato wa mzunguko mmoja wa kabla ya Usomaji wa Torati na Yubile ya mwaka 1977. Ni kweli kwamba Yuda hawakuwa wanazishika Sabato wala Usomaji huu wa Torati lakini hii haiendani wala kufanana na Marejesho na watafanya kama watakavyoambiwa kwenye kipindi hiki chote. Tukio la kupatwa kwa Mwezi mara zote linakuwa la rangi nyekundu kwa wale waliofananisha mlinganisho wa rangi.

 

Miaka kumi tangu Yubile ya mwaka 1977 matika mwaka wa Tatu wa Mzunguko wa Pili wa Yubile ya 120 upimaji wa Hekalu la \Mungu ulianza katika Siku za Mwisho. Jambo hili limeelezewa kwa kina kwenye jarida la Upimaji wa Hekalu (Na. 137).

 

Wakati wote Mungu hufanya mabadiliko katika mwaka wa Tatu wa mzunguko wa Sabato ili kufanya kuwa Torati iwe bado inadumu na kushikwa licha ya mabadiliko magumu yanayotokea.

 

Mwaka 1993-4 Makanisa ya Mungu yalikuwa yametawanyika na kinara cha taa kiliwekwa mnamo mwaka 1994 ili kutayarisha mchakato wa Maonyo ya Siku za Mwisho yaliyotabiriwa kwenye Yeremia 4:15 (soma jarida la Maonyo ya Siku za Mwisho (Na. 44)).

 

Kipindi cha kuanzia mwaka 1967 hadi 1997 kilikuwa ni kile kilijulikana kuwa ni cha Kumuombolezea Haruni kilichokitangulia kipindi cha kinabii cha Maombolezo ya Musa ambacho kilikuwa ni miaka Thelathini ya Mwisho tangu mwaka 1997 hadi 2027 (soma pia jarida la Miaka Thelathini ya Mwisho: Pambano la Mwisho (Na. 219)).

 

Kipindi cha miaka arobaini jangwani kilikuwa kinaashiria au taswira ya kimahesabu ya Yubile Arobaini za Kanisa kuwa jangwani na kipindi cha siku thelathini mbili, na tukio la kuingia nchi ya Kanaani kulikuwa ni kuashiria miaka sitini ya mwisho ya Yubile ya Arobaini.

 

Yerusalemu lirudishwa kwene mikono ya Yuda mwaka 1967 ili kuwaandaa kwa ujio wa Masihi na kuwaandaa kwa wongofu wao. Jambo hili limefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Ujio wa Masihi Sehemu ya I (Na. 210A).

 

Mwaka 1997 tangazo lijulikanalo kama the New World Order (NWO) au Agizo Jipya la Ulimwengu lilianza kutekelezwa kwa kinachoonekana kama Awamu ya Mwisho ya Dola ya Mnyama. Soma jarida la Vita Kuu ya III ya Dunia Sehemu ya 1: Dola ya Mnyama (Na. 299A).

 

Muundo wa mwisho wa kidini ulianza kushika hatamu yake ya kidola. Soma jarida la Vita Kuu ya III ya Dunia Sehemu ya II: Mwanamke Kahaba na Mnyama (Na. 299B).

 

Mwaka 1998 Usomaji wa Torati ya Mungu kwene Miaka ya Sabato ulianza tena. Hii ilitokea pia tena kwenye miaka ya 2005 na 2012.

 

Tangu mwaka 2001 Vita vya Mwisho vilianza.

 

Mchakato wa mfululizo wa Utakaso kwa kipindi cha siku za miaka ishirini na moja ulianza tangu mwaka 2006.

Vita hivi vya mwisho vitaendelea na kushika kasi hadi hii inayojulikana kama Agizo Jipya la Mfumo wa Ulimwengu (NWO) liwe limekwisha tekelezwa, na mnamo mwaka 2012 juhudi za makusudi zilifanywa kuudanganya ulimwengu kupitia kwa Nabii wa Uwongo na Mpingakristo afanaye kazi zake kwa uweza wa mapepo na ambaye wamemuweka wao wenyewe. Soma jarida la Mwaka 2012 na Mpingakristo (Na. 299D).

 

Mchakato unaofuatia unahusu Ishara hizi za Mbinguni.

 

Tangu mwaka 2006 hatima ya muundo wa dunia uliwekwa kwa kushindwa ili kwamba uangukie kwenye hili Agizo Moja Jipya Ulimwenguni (NWO) kwa kile kinachojulikana sasa kuwa Mgogoro na Mfilisiko wa Kiuchumi Duniani. Mporomoko wa muundo na taratibu za kifedha uliratibiwa kiasi kwamba bara la \Ulaya lililazimika kuingia kwenye mkanganyiko mkubwa wa kimpangilio ili kwamba utaratibu na hila zilizokusudiwa au kupangiliwa zichukue mkondo wake na kufanikishwa kirahisi na uanze rasmi mnamo mwaka 2013.  Agizo hli la Mfumo Mmoja Ulimwenguni linaenda kwa wafalme wadogo au maliwali kumi wa dola yenye vidole kumi. Haya ni mataifa kumi yenye nguvu za kiuchumi na kifedha yanayoendeshwa kwa ukiritimba mkubwa au kwa masharti magumu.

 

Mashariki ya \Kati imejiunda upya kwa mageuzi na mapinduzi ya kuanzia mwaka 2011 hadi 2012. Vita vya Mwisho vimeratibiwa ili kwamba Awamu za Mwisho za Vita vya wafalme wa Kaskazini na Kusini vianze na vikie kikomo au kilele chake tangu mwaka 2013, na Mfalme wa Kaskazini ashike hatamu kutoka baharini huko Gaza hadi Yerusalemu, na awamu ya mwisho ya uwekaji makazi yao ni miezi 42.

Mchakato wa mwisho utafuatia tangu mwaka 2012 hadi Yubile ya mwaka 2027 kwenye mfululizo wa awamu. Mwaka 2012 unafanya mwisho wa zama za mpito wa Venus kama ulivyokusudiwa na kupangiliwa kwenye kalenda ya Wahindi wenye asili ya Kimarekani na ni Zama Mpya ya kipindi cha \Mpito cha Venus akiwa kama Nyota ya Asubuhi chini ya kiongozi mpya wa mbinguni anayedaiwa kuwa ameanza.

 

Tangu mwaka 2012-2013 Vita vya Mpigakristo vinaendelea kwene awamu zake za mwisho za Vita Kuu ya III ya Dunia.  Kuitwaa na kuikalia Mashariki ya Kati kunaendelea (Danieli 11:40-43). Hata hivyo, ilivunjwa na habari kutoka upande wa Mashariki na Kaskazini za Danieli 11:44. Ukomeshaji huu au mauaji ya wengi utatokea na utafantika kwa muunganiko na mfululizo wa matukio ambayo tunayaona tangu mwanzo wa vita vya Baragumu ya Tano na ya Sita.

 

Theluthi ya wanadamu watauawa kwa vita hivi. Wakati vita hivi vitakapoendelea na kushika kasi, ishara za mbinguni zilizotabiriwa na nabii Yoeli zitaanza kuchukua nafasi yake kwenye vita hivi.

 

Kabla ya kurudi Masihi matetemeko makubwa ya ardhi yatatangulia. Haya yatasababisha moto na moshi na pia mlipuko wa matope ya moto milimani na vuguvugu litasababisha mlipuko wa miali myekundu utokee.

 

Ongezeko la Ishara utawezesha uimara mkubwa uonekane kwamba ujio wa \Kristo utarajiwe kuwa utatokea mara moja na wakati wowote. Kristo atakuwa pale mapema kabla ya Mavuno ya mwaka Mkuu wa 2025 mwishoni mwake.

 

Tukio la Kristo kumtokea Yoshua huko Yeriko kinaashiria mapigano au vita ya Megido na kufuatia baadae na namna fulani ya Vita vya Hamon-Gogu (soma jarida la Vita vya Hamon-Gogu (Na. 294)). Siku saba za kuuzunguka Yeriko zinaashiria kwamba Kristo atabidi awe huko katika miaka saba tangu Yubile na hivyo kwamba mnamo mwaka wa 2019 kwa ajili ya Sabato na huenda itakuwa mwaka 2018 kuhitimisha nabii zilizotolewa (soma jarida la Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142)).

 

Baadhi ya Ishara muhimu za Mbinguni zitatokea mapema kabla ya mwa 2018 na zinaweza kusaidia kuelekeza vipindi hivi maalumu. Matukio haya ya kupatwa kwa mwezi hutokea sawasawa na mujibu wa Kalenda ya Hekalu ikihusiana na kipindi cha Mpito hadi kuonekana tena mwezi.

 

Mwaka 2014 kuna upatwaji kamilifu wa mwezi wakati wa Sikuku ya Pasaka kama tulivyoona kutoka kwenye Sehemu ya I. Pia kuna upatwaji kamili wa mwezi katika Siku Takatifu ya Kwanza ya Sikukuu ya Vibanda.

 

Mwaka 2015, kupatwa kamili kwa jua kutatokea pia katika Mwaka Mpya hapo tarehe 20 Marchi 2015 na upatwaji kamili wa mwezi mnamo tahere 4 Aprili 2015, ambayo ni siku itakayokuwa baada ya Siku Takatifu ya Kwanza inapoanza Sikukuu ya Mikate Isiyo na Chachu. Kutakuwa na upatwaji wasehemu wa jua utakaofanyika kwenye Siku ya Upatanisho siku ya Jumapili ya tarehe 13 Septemba 2015. Siku ya Jumapili, tarehe 27 Septemba 2015 Siku Takatifu ya Kwanza ya Sikukuu ya Vibanda, kutakuwa na upatwaji kamili wa mwezi.

 

Tahere 9 Marchi 2016 siku ya 1 Abibu kutakuwa na kupatwa kwa mwezi. Tahere Marchi 23 wakati wa Pasaka kutakuwa na kupatwa kwa mwezi. Tarehe 1 Septemba 2016 wakati wa Sikukuu ya Baragumu kutakuwa na kupatwa kwa mwezi. Tarehe 16 Septemba 2016 kutakuwa kupatwa kwa jua siku ya pili ya Sikukuu ya Vibanda.

 

Tarehe 11 Februari 2017 kutakuwa na kupatwa kwa jua, siku ya 15 ya Adari 1 ambayo ndiyo siku ya maadhimisho ya Purimu. Tarehe 26 Februari 2017 kutakuwa na kupatwa kwa jua siku ya Mwandamo wa Mwezi wa Adari 2. Katika kipindi cha Mwezi Kamili wa Abu, tahere 7 Augosti 2017 kutakuwa na kupatwa kwa jua. Jioni ya tarehe 21 Augosti kutakuwa na kupatwa kwa mwezi utakaoambatana na Mwandamo wa Mwezi wa Eluli, Mwezi wa Sita, unaoweka kipindi cha kupaa cha mwisho ya Musa (soma jarida la Kupaa kwa Musa (Na. 70)). 

 

Tukio hili la kupatwa jua na mwezi litatokea katika siku muhimu ya Kalenda ya Hekalu tangu mwaka 2014-2017 na zaidi ili kwamba kipindi kingine chochote cha historia ya sasa.

 

Kama tulivyoona, inamaana sana kwamba hakukuwa na ishara za kiastronomicali kwenye miaka ya 1600 hadi kwenye karne ya ishirini. Ishara za miaka ya 1500 hazikutokea kwenye Sikukuu yeyote za Kalenda Takatifu. Mungu alitoa ishara kwenye Marejesho Mapya. Ndipo mbinguni kulikuwa kimya kuhusiana na imani kwa kipindi cha karne kadhaa na kisha kwenye siku zenyewe ambazo zilikuwa za muhimu sana kwenye unabii kwa kulinganisha na mwaka 2300 jioni na asubuhi zake na kwenye nabii za Danieli na Ezekieli ishara hizi za kupatwa jua na mwezi zilitangulia kutokea.

 

Ishara za Mbinguni zitaendelea kwa kusababisha matetemeko ya ardhi hadi mwaka 2025. Tumekijadili na kutathimini kile kinachoitwa Ishara za Mbinguni hadi mwaka 2017. Kutakuwa na ishara nyingi nyingine zitakazoendelea hadi kurudi kwa Masihi. Kama tulivyosema,, tunatarajia kumuona kabla ya Yubile ya mwaka wa 2027. Hebu na tuone na kusubiri na kuomba kwa ujio wake.

 

Sasa tutaendelea kuelezea naendeleo ya Vita ya III ya Dunia kipindi chote kilichobakia cha muda huu maalumu.

q