Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[289]

 

 

 

Ndoa

 

(Toleo La 2.0 20001220-20070730)

 

Ndoa ni taasisi muhimu sana katika taifa. Ni msingi wa taifa na ni taswira ya hali halisi ya watu ilivyo katika uhusiano wetu na Mungu na Kristo kwenye mambo ya kiroho. Ni msingi muhimu kwa wokovu wa mwanadamu wote na imetabiriwa kwenye uelewa sahihi na mwendelezo wa haya mahusiano kwa wateule wakiwa kama mabibi arusi wa Kristo kwenye taifa la Israeli.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2000, 2007 Wade Cox and Erica Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ndoa


 


Kuumbwa kwa Adamu

Tunapoliangalia suala la ndoa, tunapaswa kurudi nyuma kwenye mwanzo wa uumbaji wa mwanadamu.

 

Shetani alikuwa amekwisha muasi Mungu tayari kwenye jambo hili. Alidhania kuwa angeweza kufanya hivyo pia, kama sio vizuri zaidi kazi ya kuiongoza dunia na ulimwengu wote (Ezekieli 28:1-10).

 

Inaonekana kwamba alinuia kufanya uumbaji maeneo ya wanadamu na kutenga kwanza mahala alipojiwekea yeye mwenyewe na kuwaumba pia viumbe wengine wakubwakubwa, maka vile wanyama wanaojulikana kama Dinosaurs, the Neanderthals, mtu aina ya Cro-Magnon man, nk.

 

Shetani aliwepo kwenye Bustani ya Edeni na Adamu na Hawa walionywa vyema sana kuhusu vyakula ambavyo walipaswa kuvila na vile ambavyo hawakupaswa kuvila. Yapaswa ikumbukwe pia kwamba Kibiblia, chakula kinaweza pia kumaanisha kuwa ni chakula cha kiroho, kwa hiyo tunapaswa kupambanua pia kile tunachochagua kujifunza. Ujumbe na wito wa Shetani ulikuwa ni wa chakula walichokatazwa wasikile, alianzia mbinu zake tangu kipindi cha kuumbwa kwake Adamu akinuia kuuharibu uhusiano mzuri uliokuwepo kati ya mwanadamu na Mungu.

 

Kwa kumuumba mke wa Adamu, Mungu alikuwa anaweka mkakati mbinu wa kumuwekea mazingira imara ambao kwao mwanaume na mwanamke wangeweza kukua kwa pamoja kwenye upendo wenye uhusiano ambao watawapa au kuwashirikisha watoto wao. Mojawapo ya masomo ya mwanzoni zaidi kwa Adamu ilikuwa ni kuwapa majina kwa kila kiumbe mmoja mmoja ambayo walipaswa kuitwa kwayo. Kwa kumuonyesha umahiri wake kwenye wajibu wake kwa viumbe hawa na wajibu wake wa kuiunza Bustani, Adamu pia alifikiria kuchukua wajibu katika kushughulikia mahitaji ya kimwili nay a kihisia ya familia yake.

 

Mungu kwa kupitia Kristo mwanae, alitoa orodha ya amri na sheria za kuyatawala na kuyaongoza maisha ya kila mtu mmoja mmoja na jamii iliyo kwenye msingi wa asili yake na kutoa taswira ya aina ya uhusiano tunaotakiwa kuwa nao kumhusu yeye. Kwa hiyo, famiiia ni kiini cha msingi cha kanuni na Sheria za Mungu. Sheria inayohusiana na mambo ya familia ni Amri ya Tano, inayotutaka kuwatii wazazi wetu, ya Sita inahusu kuyalinda maisha au uhai wa wapendwa wetu, watoto wetu, wengine walio kwenye nyumba na familia zetu, jami na taifa; Amri ya Saba ndiyo iliyokataza uzinzi; Amri ya Nane inakataza wizi; Amri ya Tisa inakataza kumshuhudia mtu ushuhuda wa uwongo; na Amri ya Kumi inakataza kumtamani mke wa jirani, nk.

 

Kwa kweli familia inathirika sana pale sheria na amri hizi zinapovunjwa. Hususan katika familia ya Mungu.

 

Uwekaji wa Mamlaka           

Je, familia ni nini? Familia ni mfumo wa maisha ya kikundi. Inaanza na watu wawili, baba na mama walifuatiwa na watoto; lakini ni kubwa zaidi kuliko hiyo. Kamusi ya The Interpreter’s Dictionary of the Bible (Abingdon Press 1962, 1980, pp.238f.) inasema:

 

Kwa kuwa ndoa ni kitu halisi – ikiwa inasimamiwa na baba- katika watu wa Biblia, familia ilikuwa ni jumuia ya watu walio na uhusiano wa kifungamano wa kindoa na kiudugu na wanaongozwa kwa mamlaka ya baba. Familia ya kibiblia, hususan wakati ndoa inapokuwa ya matala, ilikuwa kubwa. Inajumuisha baba na mama au wamama, watoto wa kiume na wakike, (hadi kuolewa kwao), wajukuu, wengine walio kwenye jamii hii kama ndugu, pamoja na watumishi wa nyumbani hapo, Masuria na wageni (watembeleao). Israeli walihimizwa kuwa na familia kubwa, kwa sababu za kiuchumi pamoja na za kidini. Watoto walikuwa kwa Nyanja zote mbili, yaani kwa kuzaliwa na kwa kwa agano lililowekwa na makundi mengine na kila mmoja wao. Mshikamano katika familia ulitengamaa kwa mpangilio wake ulioko kwa uongozi wa baba na kwa kuzitendea kazi kanuni zinazi tathmini haki kwa maana yakuhusianisha uwajibikaji wa familia (nzima) yote.

 

Kama baba atasema kwamba:

Familia ilitenda kazi kama jumuia ya kidini, iliendeleza na kulinda mapokeao ya kale na kuyapitisha yaendelee kwa maelekezo na na mafundisho yote na ibada. Matendo ya shuiuti yanatishia uadilifu  na usalama wa familia, kama vile mabadiliko ya kiunchumi na ushawishi wa tamaduni na dini za kigeni, kulipingwa kwa nguvu zote na wengi wa waandishi wa bilbia. Umuhimu wa familia unapaswa uonekane kwa taswira ya wazo hili zaidi ya mipaka ya familia kwa kweli. Na ndipo inarejea kwenye makabila ya Kiebrania, mataifa ya Israeli na Yuda, mataifa mengine hya mbali, na kwa Israeli wote, waliochukuliwa kama jumuia ya kiimani zaidi ya kuwa ya kitaifa. Kwenye Agano Jipya inaoneshwa kama jumuuia ya Kikristo pia.

 

Kwa hiyo tunaona kwamba familia inaendelea kwenye ukoo, na pia inajumuisha mtumishi yeyote na wageni, ukoo au kabila, na hatimaye kwenye taifa. Ustawi na afya ya vikundi vigodo unakuwa unaonekana katika jamii kwa ujumla. Familia zinafanya kazi zake chini ya Sheria za Mngu na ndivyo ilivyo kwenye taifa pia (sawa na linavyosema jarida la Torati na Amri ya Tano (Na. 258) [Law and the Fifth Commandment (No. 258)].

 

Biblia ijulikanayo kama The Illustrated Bible Dictionary (Inter-Varsity Press, Tyndale House Publishers, 1980, Part I, p. 500) inasema kwamba:

 

Wakati kwenye kipindi cha uumbaji matala yalionekana ndiyo muundo uliokuwa umakusudiwa, ndipo mfumo wa matala (mwanaume kuwa na wanawake wengi na sio mwanamke kuwa na wanaume wengi) ndio unaoonekana.

 

Basi huu haukuwa mpango wa Mungu ulioonyeshwa kwenye maelekezo na nasaha za manabii wa Israeli kama ndiye bibi arusi pekee wa Mungu (Isaya 50:1; 54:6-7; 62:4-5; Yeremia 2:2; Ezekieli 15; Hosea 2:4f.).

 

Hebu na tuwe na mtazamo mfupi kwa mambo haya.

 

Suria

Sheria za biblia na kanuni za kuwa na mtumwa, mtumwa aliyejitoa kutumikia maisha, suria, nk, zilikuwa tofauti na mwanamke huru. Suria alikuwa ni mwanamke aliyekuwa ameuzwa kwa mtu mwingine. Wakati mwingine aliitwa ni mtumishi wa kulipwa.

 

Kutoka 21:8 inaonyesha kuwa wakati mwanamke walipokuwa anauzwa na baba yake ili awe ni mtumishi wa ndani kwa mtu mwingine aliyemchumbia na kama yeye mwenyewe hakumpenda, hakutakiwa amwambie hayo mbele za wageni. Na zaidi sana, kama alinunuliwa kwa ajili ya mwanae ndipo alipaswa amtunze na kumtendea vizuri kama anavyostahili kufanyiwa ninti. Kwenye aya ya 10, inasema kama ataolewa tena, anapaswa kumpa Yule mtumwa chakula, nguo na mahusiano ya kawaida ya kndoa. Kama atashindwa kumpa mojawapo ya mambo haya, basi aliruhusiwa aondke na kuwa huru pasipo kumlipa fidia yoyote.

 

Kama mwanaume alikuwa na uhusiano wa kingono na suria anayetumika kama mtumwa kwao na ambaye alichumbiwa au kuposwa na mwanaume kama inavyoonekana hapo juu, anaweza kukatiliwa mbali na kunyang’anywa suria huyo lakini sio kuuawa, kwa kuwa hakuwa huru.

 

Maandiko Matakatifu yanahusianisha zaidi kuwa uchumba au posa imekutikana kwenye Kumbukumbu la Torati 20:7 na 28:30.

 

Uchumba au Posa

Neno posa au uchumba lilitumika kwenye Agano Jipya likiitwa mnesteuoo (SGD 3423). Haya hivyo, limetumika mata tatu tu kwenye Mathayo 1:18, Luka 1:27 na Luka 2:5. Maandiko haya Matakatifu yanaongelea kuhusu Mariamu akiwa ni bikira aliyechumbiwa ama kuchumbiwa na Yusufu. Mariamu alikuwa ni mke wake ingawaje ndoa ya kawaida ilikuwa haijafanyika bado na alikuwa bado hawaja juana kimwili.

 

Neno mke ni la limetafsiriwa kiujumla ama kwenye Agano Jipya kwa neno lijulikanalo gune (SGD 1135) au la Agano la Kale la 'ishshah (SHD 802). Yote mawili yana maana moja na ni neno la kiuhusiano wa kinasaba lenye maana ya kike ya mke, mwan ke, mwanamwali bikra, au mwanamke aliyechumbiwa au kuposwa na mwanaume fulani mwingine tuja h have the same meaning and it is (tazama Luka 2:5; Kumbukumbu la Toarti 20:7, na maandiko mengine mengi). Bikira ni mke ambaye alichumbiwa akiwa ni mtumwa wa mwanaume. Kwa hiyo, kwa kipindi hiki yeye ni mumewe.

 

Kinyumba

Kuweka kinyumba kunatokea wakati mwanaume anapochukua mwanamke wa pili wakati mke wa kwanza akiwa hana habari au mke wa pili. Hii haikubaliki kwa kujibu wa sheria za karibu nchi nyingi na ndoa ya mke mmoja ndiyo yanayosisitizwa kwenye sheria za nchi nyingi kati ya hizo.

 

Matala

Ndoa za matala zilieenea na kujulikana katika Israeli yote na inamaanisha tu kuwa ndi ndoa ya wake wengi ambayo kwa kawaida hufanyika kwenye ndani ya familia ile ile. Daudi na Sulemani wote wawili waliuwa na wake wengi. Uislamu unaruhusu kuoa wanawake wane na dini ya kale ya Kiyahudi iliruhusu kuoa wanawake zaidi ya wane. Falme aliruhusiwa kuoa hadi wanawake kumi na wanane.

 

1Timotheo 3:2 inasema kuwa Askofu wa Kanisa anapaswa awe ni mume wa mke mmoja tu. Tafsiri ya usemi huu iko kwenye Sheria ya Mungu/ aliruhusiwa kuoa tena anapokufa au kuachika. Sheria za nchi zinapaswa kuzingatia jambo hili, na kwa kweli, inaangalia mfano wa Sara na Hajiri, na Rahelii. s that a Bishop of the Church may be the husband of  na Lea, na ni wazi kwamba sio kila mara ni wazo lililoko (sawa na jarida la Raheli na Sheria (Na. 281) [Rachel and the Law (No. 281)].

 

Kuna amri pia kumtaka mwanaume ahakikishe kuwa mjane wa wa ndugu yake aolewe ili azae mtoto au watoto waendeleze ukoo na urithi wao, kwa mujibu wa sheria za walawi (soma jarida la Dhambi ya Onani (Na. 162) [The Sin of Onan (No. 162)].

 

Maisha ya Ndoa Moja

Wakati taarifa za biblia inaandikwa zinatoa mifano mingi kuhusiana na ndoa za matala, Biblia pia inaonyesha kwamba ndoa ya mke mmoja ilikuwa ndiyo maisha ya jumla yaliyokuwapo. Maelezo ya kitabu cha Mwanzo yanaonyesha wazi kwamba ndoa za mke mmoja ndilo lilikuwa wazo kuu na ndivyo ilivyokuwa (Mwanzo 2:24). Kwa kawaida, kulipaswa kuwepo na sababu muhimu ya kuongezea wake, kama vile kwa kuhitaji awepo mtoto atakayekuwa mrithi wakati mke anapokuwa hazai au tasa au maka mumewake atakufa na kumuacha mjane akiwa hajamuachia hata uja uzito. Hali ya kumlinda mwanamke ilikuwa ni sababu moja wapo. Angano Jipya pia limeonyesha kwa wazi kwamba ndoa ya mke mmoja ilikuwa ndiyo sheria iliyojulikana na kueleweka zaidi, au hata ndiyo iliohamasishwa na kukubalika kwenye maisha ya watumishi waliosimamia huduma.

 

Mungu alianzisha familia ziwe kama msingi ambao kwazo Taifa litajengwa kwazo.

 

Warumi 13:1-7 Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. 2 Hivyo amwasiye mwenye mamlaka hushindana na agizo la Mungu; nao washindanao watajipatia hukumu. 3 Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake; 4 kwa kuwa yeye ni mtumishi wa Mungu kwako kwa ajili ya mema. Lakini ufanyapo mabaya, ogopa; kwa maana hauchukui upanga bure; kwa kuwa ni mtumishi wa Mungu, amlipizaye kisasi mtenda mabaya kwa ajili ya ghadhabu. 5 Kwa hiyo ni lazima kutii, si kwa sababu ya ile ghadhabu tu, ila na kwa sababu ya dhamiri. 6 Kwa sababu hiyo tena mwalipa kodi; kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi iyo hiyo. 7 Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi, kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahiliye hofu, hofu; astahiliye heshima, heshima.

 

(Soma jarida la Torati na Amri ya Sita (Na. 259) [Taw and the Sixth Commandment (No. 259)].

 

Sisi sote tunapaswa kuitii mamlaka. Wanawake wengi leo wanalalamikia kanuni au utataribu wa biblia inayowataka wawatii waume zao. Kuyaelewa vizuri majukumu ya familia na ndoa inatakiwa iepukane na aina yoyote machungu na unyanyasaji kwa wanawake wa Kikristo.

 

Mungu alimuumba Adamu (Mwanzo 2:7) na akamuweka kwenye Bustani ya Edeni. Alipewa majukumu au kazi ya kuwapa na kuwaita majina viumbe wote aliowaumba Mungu. Aliagizwa kuilima ardhi na kujipatia chakula kutoka kwayo. Kwa maneno mengine, wanadamu walipewa mamlaka kwa Dunia na kutawala na kuitiisha, pamoja na kuwatunza viumbe wengine wakiwepo ndege wa angani na viumbe waishio baharini. Hii siyo leseni ya kuwaua na kuwaangamiza kama tupendavyo, bali tunawajibu wa kuwatunza, kuwalisha na kuwasaidia kikamilifu na kuitunza Dunia sawasawa na Sheria za Mungu, na mwanadamu anawajibika kwa Mungu kutokana na wajibu wake huu anavyoufanyia kazi. Adamu alifundishwa vyema kuhusu kanuni na sheria hizi (soma jarida la Fundisho la Asili ya Dhambi Sehemu ya 1 Bustani ya Edeni (Na. 246) [The Doctrine of Original Sin Part I The Garden of Eden (No. 246)].

 

Tangu wakati wa kujaribiwa kwake Hawa kwenye Bustani ya Edeni, Shetani amekuwa akiudharau uhusiano wetu na Mungu. Tumekuwa tukiwa tumejawa au kuzama kwenye imani za dini za uwongo ya serikali kwa karne nyingi kadhaa.

 

Moja wapo ya njia bora zaidi ya kuliharibu taifa ni kuiharibu familia. Kwa kipindi cha zaidi ya miongo kadhaa michahche ndoa imekuwa ikishambuliwa kwa kiwango endelevu. Sio tuhuma tena kwa watu kuishi pamoja wakiwa nje ya ndoa. Sio uhalifu tena kuishi kiuhusiano wa watu wa jinsia moja. Paulo ailiita hii kuwa ni mafundisho ya mashetani, ambayo yalipelekea utata katika Siku za Mwisho (soma jarida la Mafundisho ya Mapepo ya Siku za Mwisho (Na. 48) [The Doctrines of Demons of the Last Days (No. 48)].

 

Lengo ni kuiharibu jamii na kisha kuharibu maono na tumaini na usalama wa kizazi kijacho. Kushambuliwa kwa dhana uumbaji pia kunaharibu maono na tumaini. Kama hakuna kiumbe, je, kutakuwa na lengo gani katika maisha?

 

Uhusiano kati ya mwanadamu na Mungu umeharibiwa na elimu potofu, ambayo matokeo tuliyonayo sasa yamepelekea uwingi wa dini. Kuruhusu matendo ya ngono sio tu kuwa kunaharibu uhusiano, bali pia kunaathiri afya ka mwili na ya kiroho katika taifa na ustawi wa kizazi kinachofuatia.

 

Tunajionea, kuongezeka kwa machafuko. Mabishano ya majumani yanaendelea katika machafuko au malumbano ya kimwili, kusababisha majeraha kwa wake na watoto. Kuongezeka kwa kiwango cha kutalikiana kutokana na machafuko kunakoleta athari ya sehemu zote mbili, yaani kwa wanandoa na watoto.

 

Uonyeshaji wa machafuko unaofanywa na waendesha vyombo vya habari kunaathiri hisia na akili zetu. Watoto wetu hawanahofu tena ya kuu. Wamelion hilo kwenye taarifa za habari, wanayaona hayo kwenye mikanda ya video na kwene michezo yao ya Kompyuta. Ni programu za kuwaharibu mioyo yao, na mwendendo wao na maadili yao yote yanakuwa yameharibiwa pia.

 

Kuna upungufu kwenye dhana ya kuogopa kutoa uhai. Euthanasia ameelezewa au kusemangwa sana katika miaka ya hivi karibuni kujikinga na matendo ya kujamiiana hususan kwa kutumia mwili wa vifaa bandia. Sadaka ya wanadamu ilikuwa ni kawaida kuitoa kwa miaka mingi iliyopita na huenda inatolewa hadi leo. Sikuu zetu za serikali hususan za Wamarekani, zimewekwa kwenye siku ambazo hutolewa sadaka hizi za wanadamu za imani za kipagani.

 

Tunajionea pia mmomonyoko wa maadili na sheria. Kunauhusiano na uvunjifu wa sheria au uhalifu, na ongezeko la matendo ya dhambi. Baadhi ya maovu ‘yanakubalika’ sana kuliko mengine. Biblia inasema kwamba kuivunja Amri moja ni sawa tu na kzivunja nyingine hizi zote.

 

Tunajionea kukubalika na kushabikiwa kwa ukengeufu. Sheria zinazidi kubadilishwa ili kuhalalisha ukengeufu fulani ufanyike. Aina nyingine fulani za ndoa sasa zimehalalishwa. Matendo ya kuwahasili watoto kwa watu wanapokuwa kwenye mahusiano ya namna hii kwa kuwa hawawezi kuzaa sasa kunaruhusiwa. Haya yote yameandaliwa kwa lengo la kuiharibu familia, kuifanya ndoa isiwe kama ilivyokusudiwa, na mahusiano bandia yaweze kukubalika.

 

Kuanzishwa au kuasisiwa kwa ndoa

Mwanaume hakukusudiwa awe peke yake. Hivyo, alipaswa kuwa na msaidizi (Mwanzo 2:18).

 

Mwanzo 2:18-25 Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye. 19 Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake. 20 Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye. 21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake, 22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu. 23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume. 24 Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja. 25 Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.

 

Hii ilikuwa ni ndoa ya kwanza na Mungu alikuwa katikati yao na kiini cha ndoa ile, ni kama alivyo kuwa yeye ni kiini cha ndoa zote.

 

Ndoa ni mahusiano ya kiroho ya mwili mmoja. Kristo alikuwa na mengi ya kusema kuhusu hili na alitoa msisitizo mkali sana kwa wateule kuhusu masuala ya ndoa na talaka (soma jarida la Torati na Amri ya Saba (Na. 260) [Law and the Seventh Commandment (No. 260)].

 

Mathayo 19:1-12 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo, akatoka Galilaya akafika mipaka ya Uyahudi, ng'ambo ya Yordani. 2 Makutano mengi wakamfuata, akawaponya huko. 3 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamjaribu, wakimwambia, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe kwa kila sababu? 4 Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, 5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja? 6 Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe. 7 Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha? 8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi. 9 Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini. 10 Wanafunzi wake wakamwambia, Mambo ya mtu na mkewe yakiwa hivyo, haifai kuoa. 11 Lakini yeye akawaambia, Si wote wawezao kulipokea neno hili, ila wale waliojaliwa. 12 Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.

 

Kwenye muunganiko huu wa mwili inamaana kwamba kila mmoja hapaswi kuwa amefungiwa nira ya pamoja (KJV) au kuunganishwa (2Korintho 6:14-18).

 

2Wakorintho 6:14-18 Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? 15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? 16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,

 

Ndoa kama Agano na Mungu

Kwa hiyo, muumini aliyebatizwa ana wajibu wa kuoa ndani ya watu walio kwenye Imani yake, mwa muumini mwingine aliyebatizwa, ili waweze kufanyika mwili mmoja katika Mungu kupitia kwa Yesu Kristo. Uhusiano huu ni agano lililo ndani ya Mungu la kuvumilia na kuwa mwaminifu sawasawa na Amri za Mungu.

 

Uzaaji wa Watoto

Ndoa haimaanishi kuwa ipo kwa ajili ya kuzaa watoto eke yake. Ingawaje hata hivyo kumetolewa wito kwa kusema zaeni na mkeongexeke na kuijaza nchi, kuzaa watoto kwa kweli ni sehemu au jambo muhimu sana katika ndoa. Uzaaji wa watoto nje ya ndoa unashughulikiwa kwa mujibu wa sheria zinazohusiana na uzinifu na ukahaba (soma jarida la Torati na Amri ya Saba (Na. 260) [Law and the Seventh Commandment (No. 260)]. Amri ya Sita inashughulika na sio tu na umuhimu wa kutoua, bali pia na mwajibiko wa kuyalinda maisha kiumakini. Maisha ya watoto waliokulia nje ya ndoa kwa namna nyingi sana wanaonekana kuwa kama waliokosa fursa njema na wa daraja la chini. Na ndivyo ilivyo pia kwamba kiwango cha maisha kinakuwa duni kwa watoto ambao utalikiano unatokea kwa wazazi wao. Sio kwa tatizo la kiuchumi tu peke yake yanayowakabili watoto hawa walio kwene maisha au familia ya mzazi mmoja ambalo ndilo tatizo kubwa; bali pia ni ile hali ya kuwakosa wapendwa wao na mwajibiko mzuri wa kifamilia ambao kwa kweli unayaathiri maisha yao.

 

Kristo aliongelea kuhusu uhusiano fulani wa maisha ya nyumbani kwenye Yohana 4:16-18.

Yohana 4:16-18 Yesu akamwambia, Nenda kamwite mumeo, uje naye hapa. 17 Yule mwanamke akajibu, akasema, Sina mume. Yesu akamwambia, Umesema vema, Sina mume; 18 kwa maana umekuwa na waume watano, naye uliye naye sasa siye mume wako; hapo umesema kweli.

 

Kristo kwa wazi kabisa anaiona tofauti kati ya ndoa na ‘umakini’ au halia halisi inayotakiwa kwenye mahusiano ya kindoa.

 

Ndoa inaonekana kwamba nMi ya muhimu sana kimwili. Hakuna kuoana baada ya Ufufuko wa Pili wa Wafu (Mathayo 22:29-30). Hata hivyo, tunatakiwa kuangalia mambo ya kiroho kuhusu ndoa kabla hatujaangalia mambo ya kimwili, kwa sababu mambo yote yana maana za kiroho—na hatupaswi kukosea mwelekeo kuhusu mambo haya.

 

Israeli wameolewa na Mungu. Kanisa limeolewa na Masihi, ambaye ndiye alikuwa Yahova wa Agano la Kale. Mataifa yote yanapaswa kuja katika Israeli wakiwa kama Hekalu la siku zijazo la Mungu wakiwa chini ya Kuhani wao Mkuu, ambaye ndiye elohim wa Israeli (soma Zaburi 45:6-7 na Waebrania 1:8-9; na jarida la Torati na Amri ya Saba (Na. 260) [Law and the Seventh Commandment (No. 260)].

 

Waumini wote watu wazima waliopo na waliobatizwa (tangu umri wa miaka 20) ni sehemu ya Mwili wa Kristo. Ni kama wengine wote walivyo kuwa ni bibi arusi wa Kristo (soma jarida la Baragumu (Na. 136) [Trumpets (No. 136)] Sehemu ya II: Ushirika wa Meza ya Bwana ya Mwanakondoo).

 

Kristo hakuoa kama mwanadamu hapa Duniani kwa kuwa alikuwa amekwisha lichumbia Kanisa, ambalo ni wale walio sehemu ya Mwili wa Kristo. Uchumba, kama unavyoelezewa hapo juu, ni ndoa ya mahiri ambayo kwayo ahadi zinakuwa zimetolewa. Kuelewa jambo hili ni muhimu sana, ni kama ndoa za duniani zinafanya taswira ya mambo ya mbinguni.

 

1Wakorintho 11:3 Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu

 

Mwanamke ni mfano wa Kanisa na hiyo linapaswa kuonyesha mfano mzuri. Mwanamume aliya mfano wa Kristo anapaswa pia awe na mwenendo ulio sawasawa na vile alivyo Kristo na anavyowajibika kwa Mungu, kwa hiyo mwanaume ni wa Kristo, na mwanamke ni wa mwanaume—na wote ni wa Mungu. Mungu anawafungamanisha wote hawa amoja, akiwa yeye ni yote katika yote kupitia Roho Mtakatifu.

 

Kristo akiwa kama kichwa cha mwanaume

Kristo ni mfano tuliopewa. Tulipewa ili awe ‘taswira’. Akiwa kama Malaika wa Mungu, alitolewa kwetu kama seti ya Sheria na kanuni ambazo tunaziishia. Sheria hivi tumepewa kwa faida ya afya za miili yetu, kujenga mwili na kuburudika, kuvaa, kupumzika, kujikinga na kujikinga na magonjwa, na pia kwa mahusiano yetu ya kuwahudumiana kila mmoja na mwingine. Biblia inmeandikwa mambo yote yahusuyo maisha yetu na jinsi ya kuyaachilia kwa mujibu wa Sheria. Kristo kama mwanadamu alituonyesha jinsi ya kuziishia sheria hizo. Alikufa bila kufanya dhambi. Alituonyesha mfano kwamba yeyote apendaye kuwa bwana na mkubwa inampasa kuwatumikia wengine (Yohana 13:12-15); na kwamba hakuna upendo mwingine ulio zaidi ya mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake (Yohana 15:13). Kwa mambo yote, alikuwa mwaminifu kwa Mungu. Hii ni hatua kubwa zaidi ya kuwa mtii kwa Mungu.

 

Mwanaume kama kichwa cha mwanamke

Waefeso 5:24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.

 

Mamlaka aliyopewa mwanaume ni kwa manufaa ya mke wake na familia yake na sio kwa ajili ya kujingeza kwake mwenyewe. Mke wake sio mtumwa kwake, bali ni msaidizi wake, msaada wake. Soma jarida la Mithali 31 hapo chini. Yeye ni mfano wa Kanisa na kwa kuwa yeye ni mfano ambao familia yake itajifunza kutokana na mwajibiko wake kwa Mungu. Soma jarida la Mithali 31 (Na. 114).

 

Maamuzi ya mume yanapaswa yafanyike baada ya kujadiliana kirefu na kwa kina na mke wake, akimchkulia kuwa ni mtu mwenye busara apate ushauri na nasaha zake futa hekima yake. Kwenye mahusiano ya kawaida ya kiafya, kila uamuzi unaotolewa unapaswa uwe na makubaliano ya pamoja au ya pande zote mbili. Pale ambapo makubaliano yanashikana, mwanaume anaweza kutoa uamuzi wa mwisho unaoonekana unaweza kuwa na maslahi makubwa kwa familia yote. Huu sio unyenyekevu wa namna ya mtumwa na bwana wake, lakini utii na unyenyekevu wa hiyari wa mwanamke kwenye mamlaka aliyopo ni upendo.

 

Paulo anatuambia kwamba wanawake wanapaswa kunyenyekea waume zao, lakini wanaume hawa nao inawanapasa wawapende wake zao. Kumpenda Mungu maana yake ni kumtumikia Mungu na kumuabudu yeye Mungu peke yake. Upendo wa mume ni kuhudumu kwa kumpa mahitaji mke wake na hali hii inaweza kufananishwa na kazi ya ukombozi ambayo |Kristo amelifanyia Kanisa.

 

Waefeso 5:21-33 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. 24 Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. 25 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27 apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. 28 Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. 29 Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. 30 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. 31 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. 32 Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. 33 Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.

 

Wanaume inawanapasa wakuumbuke kwamba wake zao wana mahitaji maalumu. Na haya hasa ni kipindi kile wanachotumia cha hedhi na cha kubeba mimba au cha ujauzito. Wanawake wanafanya mambo yaliyo nje ya kawaida yao lakini waume zao wanapaswa kuwahakikishia wana amani ya kiroho na kihisia katika vipindi hivi. Mwanaume anao wajibu wa kuangalia afya ya mke wake na kumhudumia inavyopaswa apone (soma jarida la Utakaso na Tohara (Na. 251) [Purification and Circumcision (No. 251)].

 

Mume ana wajibu wa mujimu kwa mambo yote yaliyo kwenye nadhiri yoyote aliyoiweka mke wake.

 

Hesabu 30:1-16 Kisha Musa akanena na wale vichwa vya kabila za wana wa Israeli, na kuwaambia, Neno hili ndilo aliloliagiza Bwana. 2 Mtu atakapomwekea Bwana nadhiri, au, atakapoapa kiapo ili kufunga nafsi yake kwa kifungo, asilitangue neno lake; atafanya sawasawa na hayo yote yamtokayo kinywani mwake. 3 Tena mtu mke atakapomwekea Bwana nadhiri, na kufunga nafsi yake kwa kifungo, naye aketi katika nyumba ya babaye, katika ujana wake; 4 babaye naye akasikia nadhiri yake, na kile kifungo chake alichofungia nafsi yake, na babaye akamnyamazia; ndipo nadhiri zake zote zitathibitika, na kila kifungo alichofungia nafsi yake kitathibitika. 5 Lakini kama huyo babaye akimkataza siku hiyo aliyosikia; nadhiri zake ziwazo zote, wala vifungo vyake alivyoifungia nafsi yake havitathibitika; na Bwana atamsamehe, kwa kuwa babaye alimkataza.6 Tena kama amekwisha kuolewa na mume, wakati huo wa nadhiri zake, au wa neno hilo alilolitamka kwa midomo yake pasipo kufikiri, alilojifungia; 7 na mumewe akasikia, naye akamnyamazia siku hiyo aliyosikia neno hilo; ndipo nadhiri zake zitathibitika, na vile vifungo ambavyo ameifunga nafsi yake vitathibitika. 8 Lakini kama mumewe akimkataza siku hiyo aliyolisikia; ndipo ataitangua nadhiri yake iliyo juu yake na neno alilolitamka kwa midomo yake pasipo kufikiri, alilojifungia; na Bwana atamsamehe 9 Lakini nadhiri ya mjane, au ya mwanamke aliyeachishwa mume, kila neno ambalo ameifunga nafsi yake kwalo, litathibitika juu yake. 10 Tena kama aliweka nadhiri nyumbani mwa mumewe, au kama aliifunga nafsi yake kwa kifungo pamoja na kiapo, 11 na mumewe alisikia akamnyamazia, wala hakumkataza; ndipo nadhiri zake zote zitathibitika, na kila kifungo alichojifungia kitathibitika. 12 Lakini kama mumewe alizibatilisha na kuzitangua siku hiyo aliyozisikia, ndipo kila neno lililotoka midomoni mwake katika hizo nadhiri zake, au katika kile kifungo cha nafsi yake, halitathibitika; huyo mumewe amezitangua; na Bwana atamsamehe. 13 Kila nadhiri, na kila kiapo kifungacho, ili kuitaabisha nafsi ya mwanamke mumewe aweza kuthibitisha, au mumewe aweza kutangua. 14 Lakini mumewe akimnyamazia mkewe kabisa siku hata siku ndipo azithibitisha nadhiri zote za mkewe, au vifungo vyake vyote vilivyo juu yake; yeye amezithibitisha, kwa kuwa alimnyamazia mkewe siku hiyo aliyozisikia nadhiri zake. 15 Lakini akizibatilisha na kuzitangua baada ya kuzisikia; ndipo yeye atachukua uovu wa mkewe. 16 Hizi ndizo amri, ambazo Bwana alimwagiza Musa, kati ya mtu mume na mkewe, kati ya baba na binti yake, katika ujana wake, ali nyumbani mwa babaye.)

 

Mume anawajibika na usalama wa familia yake. Hii ni kwa namna zote mbili, usalama wa kiroho na wa kimwili. Kwenye 2Wathesalonike 3:10, Mtume Paulo anasema kwamba mtu asiyefanya kazi asile; nah ii inamaanisha kwamba mtu huyo familia yake haitakula pia. Kufanya kazi kwa ajili ya familia na kufanya kazi kwa lengo la kulisaidia Kanisa liihubiri Injili kwa mataifa yote yote haya ni sehemu ya agizo hili; mtu aanatakiwa kutoa mahitaji ya kimwili ya familia, na wengine watoe chakula cha kiroho kwa sehemu zote mbili, yaani kwenye familia na taifa na kwa wale tunaopaswa kuwajibika kwao.

 

Pia, mtu Yule asiyewatunza watu wa nyumbani mwake mwenyewe ni mbaya kuliko asiyeamini.

 

1Timotheo 5:8 Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.

 

Mwanaume anatakiwa pia kuendeleza uhusiano wake na mke wake pindi anapomuona tu. Hiki ni kipindi cha kujifunza kuishi pamoja kwa upendo na utangamano.

 

Kumbukumbu la Torati 24:5 Mtu atwaapo mke mpya, asiende vitani pamoja na jeshi, wala asipewe shughuli juu yake yo yote; akae faragha mwaka mmoja nyumbani mwake, apate mfurahisha mkewe aliyemtwaa.

 

Mahali ambapo mamlaka ya kibiblia yanapovunjika, na hali ya kumjua au kucha Mungu na kuzijua Sheria zake kunapoondoa, matokeo yake ni kama tunayoyaona sasa. Ndoa zina vunjika, mahusiano yanakoma, watoto wanachukuliwa kwenda kulelewa na mtu mwingine na babu na bibi wanapoteza wajukuu zao. Familia inagawanyika na kusambaratika kutokana na talaka na kuachana, kama inavyofanywa na mataifa kuungezea uwezekano wa kutokea matatizo haya kwa makusudi kwa kuziondolea mbali Sheria za Mungu. Matokeo yake ni kuwepo kwa mapigano au vita, yawe ndani ya familia, jamii au kuenea katika nchi yote.

 

Kile Biblia kinachotufundisha ni kwamba ndoa iliingizwa kwenye Sheria za Mungu kwa kuwekewa msisitizo mkubwa sana wa uhusiano wenye afya, watoto wenye furaha, ambao watakua kwenye utu uzima wakiwa kwenye mazingira salama na waweze kuwafundisha watoto wao njiaa bora ya kuishi, wakiwa chini ya Sheria za Mungu.

 

Lakusikitisha mno ni kwamba, siyo mamlaka zote zimewekwa na Mungu ni waaminifu, na ndiyo maana hatuna hata jamii yoyote leo inayoishi chini ya dhana yenye utaratibu imewekwa hapa chini duniani kwetu pamoja nasi. Wale walio nasi wanaojaribu kuziweka Sheria za Mungu kwa ajili ya maongozi ya maisha yetu wamekuwa wakiteswa na kuangamizwa kwa kipindi cha maelfu ya miaka na wataendelea kuteswa hivyohivyo hadi atakaporudi Kristo. Lakini hilo lisituzuie sisi.

 

Kwa hiyo, ndoa inapaswa ijengwe kwenye msingi imara, na inatakiwa pia ijengwe kwenye uelewa wa kina wa Sheria za Mungu. Waume na wake wanatakiwa wasome kwa amoja neno la Mungu. Kimtazamo na uelewa, mwanaume lazima aw na ukomavu na mahiri, na mwenye kuweza kumhudumia mke wake kifedha, kihisia au mawazo na kiroho. Anapaswa kuweze kuendeleza na kuweka sawa heshima ya mke wake na ni lazima amhakikishie uwezo wake wa kumpenda. Mungu anachukia kuachana, ni kitendo kiovu kumfanyia mke wake na watoto wake wengine wote walionao. Kugunduliwa kwa matendo ya zinaa ndiyo kitu pekee kilichotolewa ruhusa ya kuatalikiana. Uzinifu ni uvunjifu wa Amri ya Saba. Uwongo, wizi kushuhudia au kusema uwongo, na kumtamani mke wa jirani, mali na rasilimali zake kunaharibu heshima yoyote iliyokuwepo kati ya mtu mmoja na mwingine. Kitendo cha kutomtenda vyema wu kumfanyia ukatili mke wake, kunaonesha kuwa mwanaume huyu hampendi kama inavyompasa kufanya. Anapaswa kumpenda kama kama aupendavyo mwili wake mwenyewe. Ni kama ilivyo kwa mtu anapokuwa anaumwa hawezi kujipiga au kujidhalilisha, ndivyo vivyohivyo mwanaume hatakiwi kuonyesha aina hiyo ya udhalilishaji kwenye maisha ya ndoa mbele za watu walio kwenye familia yake.

 

Wajibu na majukumu ya mke

1Wakorintho 11:11-12 Walakini si mwanamke pasipo mwanamume, wala mwanamume pasipo mwanamke, katika Bwana. 12 Maana kama mwanamke alitoka katika mwanamume, vile vile mwanamume naye huzaliwa na mwanamke; na vitu vyote asili yake hutoka kwa Mungu. Hukumuni ninyi wenyewe katika nafsi zenu.

 

Mwanamke ni msaidizi wa mwanaume, mshiriki mwenza wake, wa kufanana naye. Kwa hiyo, ingawa kimtazamo wanaonekana kuwa kama wako sawasawa kimila na mwonekano, ni muhimu sana wawe na makubaliano kwa mambo ya imani za kidini. Kunapotokea kuwepo tofauti kwenye masuala ya ukiri wa imani, kunahatari kwamba mmoja wapo anaweza kuwapeleka wenzake kwenye ibada za sanamu. Ubada za sanamu zinauhusiano wa karibu sana na matendo ya zinaa na uasherati.

 

Majukumu ya mwanamke yameonyeshwa kwenye Mithali 31.

Mithali 31:10-31 Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani. 11 Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato. 12 Humtendea mema wala si mabaya, Siku zote za maisha yake. 13 Hutafuta sufu na kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo. 14 Afanana na merikebu za biashara; Huleta chakula chake kutoka mbali. 15 Tena huamka, kabla haujaisha usiku; Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula; Na wajakazi wake sehemu zao. 16 Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu. 17 Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi; Hutia mikono yake nguvu. 18 Huona kama bidhaa yake ina faida; Taa yake haizimiki usiku. 19 Hutia mikono yake katika kusokota; Na mikono yake huishika pia. 20 Huwakunjulia maskini mikono yake; Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake. 21 Hawahofii theluji watu wa nyumbani mwake; Maana wote wa nyumbani mwake huvikwa nguo nyekundu. 22 Hujifanyia mazulia ya urembo; Mavazi yake ni kitani safi na urujuani. 23 Mume wake hujulikana malangoni; Aketipo pamoja na wazee wa nchi. 24 Hufanya nguo za kitani na kuziuza; Huwapa wafanya biashara mishipi. 25 Nguvu na hadhi ndiyo mavazi yake; Anaucheka wakati ujao. 26 Hufumbua kinywa chake kwa hekima, Na sheria ya wema i katika ulimi wake. 27 Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu. 28 Wanawe huondoka na kumwita heri; Mumewe naye humsifu, na kusema, 29 Binti za watu wengi wamefanya mema, Lakini wewe umewapita wote. 30 Upendeleo hudanganya, na uzuri ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa. 31 Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu malangoni.

 

Anaaminiwa na mume wake, anaitunza vyema nyumba na watu wa nyumbani mwake, na ananunua na kuuza, na anaweza kuendesha biashara. Anajali mambo na mahitaji ya familia yake, maskini na wahitaji. Anabusara na mwema. Sio mvivu wala mzembe. Mumewe na watoto wake humsifu. Hizi ni sifa nzuri anazotakiwa kuwanazo. Kumbuka kuwa mwanamke ni taswira ya Kanisa pia. Kwa ujumla tu tuseme kwamba ataweza kufanya mabo haya yote kama atakuwa mtiifu na mnyenyekevu kwa Mungu. Akiwa peke yake, mwanamke anawazia jambo hili na ataweza.kwa masaada wa Mungu na mume wake  (pia soma majarida ya Mithali 31 (Na.  114) na Majukumu ya Mwanamke Mkristo (Na. 62) [Proverbs 31 (No.114) and Role of the Christian Woman (No. 62).

 

Wanawake wasipende kutangulia kuzifanya kazi zinazopaswa kufanywa na waume zao. Yeye anatakiwa kuihudumia familia yake, na ajishushe kwa kukubali kuwa nafasi ya chini kazini, vinginevyo kujikweza kwake kazini kwake na tendo la kumuachia kufanya maamuzi na kazi zote, ni ishara ya huyu mwanaume kujidharau yeye mwenyewe. Moja wapo ya majukumu ya mwanamke ni kumuinua na kumtia moyo mume wake. Kwa kitendo hiki cha kumtia moyo anaweza kuketi ‘malangoni’. Hii inamaana ya kumudu kuyatenda majukumu kwenye jamii na kuwa sehemu ya watoa maamuzi akiwa kama mwanachama au mjumbe mwenye kuheshimika kwenye jamii husika.

 

Mke anapaswa kumsaidia mume wake katika mambo yote. Mara tu baada ya kufanyika maamuzi, ndipo wajibu wao wote wawili kuifanya ifanyike. Mahali pasipo na umoja au ushirikiano kati ya wazazi wote wawili, ni watoto ndio wanaoteseka. Kutakuwa na mtangamano kwenye malezi na nidhamu.

 

Unyenyekevu na utii kwa mke ni jambo muhimu sana. Kwa kweli hali ya kutokuwa na utii na unyenyekevu kunapelekea mwanaume kuwa mzinifu. Kuna matukio mengi sana ambapo mke ameifanya huduma ya utumishi impe umaarufu kiasi kwamba imemfanya aone kama yuko mbele zaidi ya mume wake. Makasisi na watumishi hawa wamehamasisha kwa makusudi uhusiano wa aina yake wa kiuasherati. Hii inapata mwanya wakati huduma ya ushauri nasaha inatakiwa iwepo Kanisani na iwapo kam itafanyika na mtu mmoja tu wa Kanisani inapohitajika. Aina yoyote ya huduma ya ushauri wa mambo ya ndoa Kanisani inatakiwa ifanyike wakiwepo wanandoa wote wawili, vinginevyo tatizo halitaweza kutatuliwa.

 

Wanawake wazee wanatakiwa kuwatia moyo mabinti vijana na kuwashauri mabinyi walioingia kwenye ndoa mpya.

 

Tito 2:3-5 Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema; 4 ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; 5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbanimwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.

 

Moja ya jukumu kubwa sana la mke ni kujua majukumu ya umama. Kuhusu watoto ni kazi kubwa sana kuliko lililoko, kama ilivyo hatima ya mataifa. Kama wazazi wakishindwa kuwalea watoto kuwa wananchi wawajibikaji, wazijue Sheria za Mungu na waish maisha ya utii kwao, ndipo watashindwa. Hatuwezi kubeba jukumu ka maamuzi wanayoyafanya wanapokuwa watu wazima, ila tunaweza kuchukua jukumu la kuwafundisha Sheria za Mungu na kisha kuwapa fursa ya kufanya maamuzi sahihi na kuishi maisha ya kumcha Mungu.

 

Majukumu na wajibu huu upo pia kwenye mifumo ya elimu. Hawakufundishwa Amri za Mungu kwa kuwa waalimu we nyewe hawazijui hizi Sheria za Mungu. Je, wanazishika na kuziadhimisha Sabato za Mungu? Je, wanafundisha Sikukuu zilizoamriwa na Mungu na Siku nyingine Takatifu? Au wanafundisha tu kuhusu miungu wa kipagani, pamoja na maadhimisho ya siku za kuzaliwa, Krismasi, Easter, Siku za Mizimu zinazoitwa Halloween na siku nyingine kama hizo za kipagani? (Soma majarida ya Msalaba: Chanzo Chake na Maana Yake (Na. 39); Chanzo cha Krismas na Easter (Na. 235); Pinata (Na. 276; Sherehe za Kuzaliwa Mtu (Na. 287) [The Cross: Its Origin and Significance (No. 39); The Origins of Christmas and Easter (No. 235); The Pinata (No. 276); Birthdays (No. 287)]. Watoto wetu hawapewi fursa wanayostahili. Tunatakiwa kuwahakikishia watoto wetu kzijua Amri za Mungu

 

Wajibu wa watoto

Kumbukumbu la Torati 5:16 Waheshimu baba yako na mama yako; kama Bwana, Mungu wako, alivyokuamuru, siku zako zipate kuzidi, nawe upate kufanikiwa katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.

 

Amri ya Tano ni ya muhimu sana. Sio tu kwamba inatupeleka kwenye uhusiano kati ya watoto wadogo na wazazi wao. Bali pia inawahusisha watu wazima na kuwafundisha uhusiano wao kwa wazazi wao ambao ni wazee wao walio kwenye jamii zao, pia inatuchukua sisi sote hadi kwenye mahusiano yetu na Baba yetu wa Mbinguni na kwa Kanisa.

 

Kama ilivyoelezwa huko nyuma, wazazi wanatakiwa wawafundishe watoto wao Sheria za Mungu. Wanatakiwa wawafundishe kwa bidii zao zote. Wazazi wanatakiwa pia kujiangalia mienendo yao wenyewe kwa kuwa ndipo hawa watoto ndipo watakapowatii na kuwaheshimu. Watoto ni rahisi sana kwao kugundua udhaifu au mwenendo mbaya na unafiki ukifanyika. Tusitegemee watoto kufanya tunato waagiza kufana iwapo kama sisi wenyewe hatutawaonyesha kuwa tunaishi hivyo huku tukiishi kinyume chake kabisa.

 

Mithali 4:1-27 Wanangu, yasikilizeni mausia ya baba yenu, Tegeni masikio mpate kujua ufahamu. 2 Kwa kuwa nawapa mafundisho mazuri; Msiiache sheria yangu. 3 Maana nalikuwa mwana kwa baba yangu, Mpole, mpenzi wa pekee wa mama yangu. 4 Naye akanifundisha, akaniambia, Moyo wako uyahifadhi maneno yangu; Shika amri zangu ukaishi. 5 Jipatie hekima, jipatie ufahamu; usiusahau; Wala usiyakatae maneno ya kinywa changu. 6 Usimwache, naye atakuhifadhi; Umpende, naye atakulinda. 7 Bora hekima, basi jipatie hekima; Naam, kwa mapato yako yote jipatie ufahamu. 8 Umtukuze, naye atakukuza; Atakupatia heshima, ukimkumbatia.9 Atakupa neema kuwa kilemba kichwani; Na kukukirimia taji ya uzuri. 10 Mwanangu, sikiliza, na kuzipokea kauli zangu; Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi. 11 Nimekufundisha katika njia ya hekima; Nimekuongoza katika mapito ya unyofu. 12 Uendapo, hatua zako hazitadhiikika, Wala ukipiga mbio hutajikwaa.13 Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; Mshike, maana yeye ni uzima wako. 14 Usiingie katika njia ya waovu, Wala usitembee katika njia ya wabaya. 15 Jiepushe nayo, usipite karibu nayo, Igeukie mbali, ukaende zako. 16 Maana hawalali isipokuwa wametenda madhara; Huondolewa usingizi, ikiwa hawakumwangusha mtu. 17 Maana wao hula mkate wa uovu, Nao hunywa divai ya jeuri. 18 Bali njia ya wenye haki ni kama nuru ing'aayo, Ikizidi kung'aa hata mchana mkamilifu. 19 Njia ya waovu ni kama giza; Hawajui ni kitu gani kiwakwazacho. 20 Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzisikie kauli zangu. 21 Zisiondoke machoni pako; Uzihifadhi ndani ya moyo wako. 22 Maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote. 23 Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima. 24 Kinywa cha ukaidi ukitenge nawe, Na midomo ya upotovu uiweke mbali nawe. 25 Macho yako yatazame mbele, Na kope zako zitazame mbele yako sawasawa.26 Ulisawazishe pito la mguu wako, Na njia zako zote zithibitike; 27 Usigeuke kwa kuume wala kwa kushoto; Ondoa mguu wako maovuni.

 

Mithali imejaa utajiri mkubwa wa ushauri wenye busara, sio kwa vijana peke yao tu, bali ni hata kwa mtu mzima na mzee pia.

 

Ni muhimu pia kwamba watoto wafundishwe maana ya ndoa kwa maana linganisho na Agano la Mungu. Wakiwa watoto wanakuwa wametakaswa kupitia kwa wazazi wao, lakini wanapotimiza umri wa miaka 20 wanaanza kuwajibika wenyewe kwa mambo ya imani na uhusiano wao na Mungu na wanaanza kuwa sehemu ya mabibi arusi wa Kristo. Wazazi wanatakiwa kuwatia moyo na kuwahamasisha watoto wafanye hivyo. Kuwatenga watoto kwa kutowafundisha na kuwashrikisha kumjua Mungu na Torati yake ni kuwatenga mbali na fursa yao ya kuwepo kwenye Ufufuo wa Kwanza wa Wafu. Wakati Mungu atakapokuwa anaingilia kati sawa na mapenzi yake, tunabakia kuwa ni wajibu wetu wa kuwafundisha vijana wetu kikamilifu na kiusahihi.

 

Watoto waliolelewa na wazazi wasioelewana, waasi wasiomtii Mungu au waliotalikiana, hawataweza kukua wakiwa na uelewa sahihi kama inavyotakikana. Watoto waliolelewa na mzazi mmoja au walio na malezi ya upande mmoja wanakosa huduma ya kimalezi muhimu iliyotakiwa kutolewa na mmoja wa wazazi hawa, kati ya mama au baba na inakuwa ni wajibu wa Kanisa sasa kuwasaidia. Washirika wa kanisa wanatakiwa kuwa mfano mzuri kwa watoto wanaotoka kwenye aina hii ya malezi ya upande mmoja, kwa kuwaonyesha ukarimu na urafiki. Kanisa linaweza kuwapa huduma za kijamii ili kuwahamasisha maendeleo ya kirafiki miongoni mwa vijana. Watoto wahamasishwe kuwaalika marafiki hawa majumbani mwao.

 

Ndoa na mwenzi asiyeamini

Ndoa nyingi hufungwa mapema kabla ya wanandoa hawajaitwa na kuingia kwenye Imani, na pengine zinafanyika wakati mmoja wa wanandoa akiwa ameitwa na kuingia kwenye imani huku mwingine akiwa hajaamini. Hii inasababisha matatizo mengi kwenye maisha haya ya ndoa. Huyu mmoja aliyeitwa anatakiwa kuwa mvumilivu sana na makini. Mwanandoa ambaye hajaitwa bado hawezi kujua umuhimu wa kumuweka Mungu kwenye kipau mbele cha mambo yao kwa kila kitu. Watajikuta kila mara wanatofautiana kwenye mambo kadhaa ya mambo ya ndoa yao. Mfano ni kwamba mume anaweza kupeleka hela Kanisani huku mke akiona kuwa zingefaa kwa matumizi ya familia. Wanawake kuwaacha waume zao wasioongoka nyumani, na hata wakati mwingine watoton wao pia wanapojihudhurisha kwenye Sikukuu na Siku nyingine Takatifu zilizoamriwa. Hawashindi huko kwa masaa machache kama wanavyofanya Kanisani, bali wanakaa huko kwa juma moja na  takriban mara mbili kila mwaka! Je, wezi wao wasioamini watawaelewaje wanapofanya hivyo? Tatizo kubwa zaidi ni matika kutoa maamuzi juu ya watoto kuwa watakuwa wanafundishwa mafundisho ya dini gani.

 

Mtume Paulo anasema katika 1Wakorintho 7:12-16:

Lakini watu wengine nawaambia mimi, wala si Bwana, ya kwamba iwapo ndugu mmoja ana mke asiyeamini, na mke huyo anakubali kukaa naye asimwache. 13 Na mwanamke, ambaye ana mume asiyeamini, na mume huyo anakubali kukaa naye, asimwache mumewe. 14 Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu. 15 Lakini yule asiyeamini akiondoka, na aondoke. Hapo huyo ndugu mume au ndugu mke hafungiki. Lakini Mungu ametuita katika amani. 16 Kwa maana wajuaje, wewe mwanamke, kama utamwokoa mumeo? Au wajuaje, wewe mwanamume, kama utamwokoa mkeo?

 

Wakati Paulo akikiri hili kuwa siyo Roho Mtakatifu, ndiye mshauri mkuu.

 

Talaka

Marko 10:2-12 Basi Mafarisayo wakamwendea, wakamwuliza, Je! Ni halali mtu kumwacha mkewe? Huku wakimjaribu. 3 Naye akajibu, akawaambia, Musa aliwaamuru nini? 4 Wakasema, Musa alitoa ruhusa kuandika hati ya talaka na kumwacha. 5 Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii. 6 Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke. 7 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; 8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.9 Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe. 10 Hata nyumbani tena wanafunzi wakamwuliza habari ya neno hilo. 11 Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake; 12 na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini.

 

Hapa Kristo anaifafanua sheria inayohusu talaka.

 

Kwenye 1Wakorintho 7:10-11, Paulo anasema:

1Wakorintho 7:10-11 Lakini wale waliokwisha kuoana nawaagiza; wala hapo si mimi, ila Bwana; mke asiachane na mumewe; 11 lakini, ikiwa ameachana naye, na akae asiolewe, au apatane na mumewe; tena mume asimwache mkewe.

 

Talaka ni machafuko. Biblia inautaja uzinifu kuwa ni dhambi pekee. Uzinzi wa kiroho ni ibada ya sanamu. Katika uhusiano wetu kwa Mungu, talaka maana yake ni kifo. Kwenye uhusiano wetu kwa kila mmoja na mwenzake ni uharibifu wa maisha yetu na maisha ya watoto wetu. Watoto wanaweza kugawanyika au kusambaratika wakiwafuata mmoja na wengine kwa mwingine, wakichukua maamuzi ya kuachana aitha na baba yao au mama yao, hata na bibi na babu zao na watu wengine walio kwenye ukoo wao. Mara nyingi wamekuwa wakijilaumu wenyewe.

 

Ni Amri ya Mungu isemayo kwamba hakuna anayeruhusiwa kumtaliki mwenzake, sio mwanaume wala mwanamke, hakuna aliyeruhusiwa kumtaliki mwenza wake kwa kisingizio kwamba mwenzi wake wa ndaa haamini imani yake au hajaongoka. Familia inatakaswa kwenye ndoa na mwamini hataweza kamwe kujua ni kwa jinsi gani au iwapo kama ni mfano wa maisha yao ndio unaushuhuda wa nguvu kwa waumi wengine wa familia. Hata hivyo, kama mwezi asiye amini akiamua kuondoka, basi talaka hapo haitaepukika na itaruhusiwa kutolewa.

 

Kunapokuwa na hali ya kudhalilishwa kati ya wanandoa na watoto, hakuna umuhimu wa kuishi maisha ya namna hiyo. Mwenzi mdhalilishaji ajue kwamba kitendo cha namna hiyo hakiwakilishi wajibu au majukumu yake, na iwapo kama ushauri nasaha umeshindikana kufua dafu kukomesha hali hii, basi usalama na utawi wa familia unapaswa kuchukuliwa. Ndipo inaweza kuonekana kuwa ni busara kutalikiana kuruhusiwe.

 

Kuoa mara ya pili au ndoa ya pili

Warumi 7:2-3 Ndugu zangu, hamjui (maana nasema na hao waijuao sheria) ya kuwa torati humtawala mtu wakati anapokuwa yu hai? 2 Kwa maana mwanamke aliye na mume amefungwa na sheria kwa yule mume wakati anapokuwa yu hai; bali akifa yule mume, amefunguliwa ile sheria ya mume. 3 Basi wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa na mume mwingine.

 

Kama mwanaume akimuacha kwa kumtaliki mkewe, basi asioe tena. Kama atakuja kutubu, basi atashauriwa kumrudia mke wake huyohuyo wa zamani na kumuoa tena.

 

Wakati ndoa inapokuwa ni ya kufungiwa nira na asiyeamini, ambavyo ni, wakati mmoja ya wanandoa anapokuwa hajaitwa bado na kuongoka na akachagua kuivunja ndoa hii na kutalikiana, ndipo mwingine aliyebaka anaruhusiwa na yuko huru kuoa au kuolewa tena.

 

Maisha ya useja ya bila kuoa

Ndoa ni uhusiano huru uliokubalika kati ya mwanaume na mwanamke. Mwanaume hakukusudiwa aishi peke yake. Hata hivyo, kuna mazingira ya namna mbalimbali kadhaa yanayopelekea hali hii kutowezekana. Sio dhambi kabisa kwa mtu akiamua kusihi bila kuoa.

 

Mathayo 19:12 12 Maana wako matowashi waliozaliwa hali hiyo toka matumboni mwa mama zao; tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi; tena wako matowashi waliojifanya kuwa matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kulipokea neno hili, na alipokee.

Hata hivyo, ni dhambi kukataza watu kuoana.

 

1Timotheo 4:1-3 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; 2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe; 3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.

 

Paulo alitoa ushauri mwingi tu kuhusu jambo hili.

1Wakorintho 7:27-40 Je! Umefungwa kwa mke? Usitake kufunguliwa. Umefunguliwa? Usitafute mke. 28 Lakini, kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo. 29 Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana; 30 na wale waliao kama hawalii; na wale wafurahio kama hawafurahi; na wale wanunuao, kama hawana kitu. 31 Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita. 32 Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana; 33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe. 34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe. 35 Nasema hayo niwafaidie, si kwamba niwategee tanzi, bali kwa ajili ya vile vipendezavyo, tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine. 36 Lakini mtu awaye yote akiona ya kuwa hamtendei mwanamwali wake vipendezavyo, na ikiwa huyo amepita uzuri wa ujana wake, na ikiwapo haja, basi, afanye apendavyo, hatendi dhambi, na awaruhusu waoane. 37 Lakini yeye aliyesimama kwa uthabiti wa moyo wake, hana sharti, lakini aweza kuyatawala mapenzi yake, tena amekusudia moyoni mwake kumlinda mwanamwali wake, atatenda vema. 38 Basi, hivyo na amwozaye mwanamwali wake afanya vema; na yeye asiyemwoza atazidi kufanya vema. 39 Mwanamke hufungwa maadamu mumewe yu hai, lakini ikiwa mumewe amefariki, yu huru kuolewa na mtu ye yote amtakaye; katika Bwana tu. 40 Lakini heri yeye zaidi akikaa kama alivyo; ndivyo nionavyo mimi, nami nadhani ya kuwa mimi nami nina Roho wa Mungu.

 

Maandiko haya yamekuwa yakipotoshwa maana yake. Mawazo na ushauri wa Paulo hapa ni kwamba mtu anaweza kuishi maisha au hali ambayo mtu alikuwa anaishi kwayo—ambayo ni kwamba, kama alikuwa ameoa aendelee kuishi na ndoa yake na kama alikuwa hajaoa na aendelee kuishi bila kuoa. Hakuna dhambi yoyote kuishi hivyo kabisa. Ila uamuzi huu wa kujitolewaa kuishi hivyo kusichukuliwe kwa kumaanisha kuwa Paulo hakuwa anachukia ndoa au kuwachukia wanawake. Wakati ule alionekana kuamini kwamba kurudi kwake Kristo kulikuwa kumekaribia mno na aliweka msingi wa ushauri wake kwenye mtazamo wa namna hiyo. Anaendelea kwa kutoa ushauri wa ndoa imara. Aliendelea kuweka mahitaji ya muunganiko wa kwanza wa hiyari, muungano wa wanandoa, ambapo unawafanya kuwa ni mwili mmoja.

 

Uhusiano uliokatazwa

Haya ni maonyo na maelekezo yanayozuia kuwa na ndoa bora.

Mambo ya Walawi 18:1-30 Bwana akanena na Musa, na kumwambia, 2 Nena wewe na wana wa Israeli, uwaambie, Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. 3 Nanyi msifanye matendo kama yale ya nchi ya Misri mliyokaa; wala msifanye matendo kama yale ya nchi ya Kanaani, nitakayowapeleka; wala msiende katika amri zao hao. 4 Mtazifanya hukumu zangu, nanyi mtazishika amri zangu, ili mwenende katika hizo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu. 5 Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo mtu akizitumia ataishi kwa hizo; mimi ndimi Bwana. 6 Mtu ye yote aliye wa kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana. 7 Utupu wa baba yako, wala utupu wa mama yako, usifunue, maana ndiye mama yako; usifunue utupu wake. 8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako. 9 Utupu wa umbu lako, binti ya baba yako, au binti ya mama yako, kwamba alizaliwa nyumbani mwenu au kwamba alizaliwa kwengine, utupu wa hao usifunue. 10 Utupu wa binti ya mwanao mume, au wa binti ya binti yako, utupu wao hao usifunue; kwa kuwa ndio utupu wako mwenyewe. 11 Utupu wa binti ya mkewe baba yako, aliyezaliwa na baba yako, yeye ni umbu lako, usifunue utupu wake. 12 Usifunue utupu wa umbu lake baba yako; maana, yeye ni jamaa aliye karibu. 13 Usifunue utupu wa umbu la mama yako; maana, yeye ni jamaa ya mama yako ya karibu. 14 Usifunue utupu wa ndugu ya baba yako, usimkaribie mkewe huyo; yeye ni shangazi lako. 15 Usifunue utupu wa mkweo mwanamke; yeye ni mke wa mwanao; usifunue utupu wake huyo. 16 Usifunue utupu wa mke wa nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo. 17 Usifunue utupu wa mwanamke na binti yake; usimtwae binti ya mwanawe mume, au binti ya binti yake, ili kufunua utupu wake; hao ni jamaa ya karibu; ni uovu mkuu. 18 Wala usitwae mwanamke pamoja na nduguye, awe mtesi wake, na kufunua utupu wake, huyo wa pili atakapokuwa yu hai. 19 Nawe usimkaribie mwanamke kufunua utupu wake wakati wa kutengwa kwa ajili ya unajisi wake. 20 Usilale na mke wa mwenzio, ukajitia unajisi naye. 21 Nawe usitoe kizazi chako cho chote na kuwapisha kwa Moleki, wala usilinajisi jina la Mungu wako; mimi ndimi Bwana. 22 Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo. 23 Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; ni uchafuko. 24 Msijitie unajisi katika mambo hayo hata mojawapo; kwa maana hizo taifa nitakazozitoa mbele zenu zimekuwa najisi kwa mambo hayo yote; 25 na hiyo nchi imekuwa najisi; kwa ajili ya hayo naipatiliza uovu wake juu yake, na hiyo nchi yatapika wenyeji wake na kuwatoa. 26 Kwa hiyo mtazishika amri zangu na hukumu zangu, wala msifanye machukizo hayo mojawapo; yeye aliye mzalia, wala mgeni aketiye kati yenu; 27 (kwa kuwa hao watu wa nchi wameyafanya machukizo haya yote, hao waliotangulia mbele zenu, na hiyo nchi imekuwa najisi;) 28 ili kwamba hiyo nchi isiwatapike na ninyi pia, hapo mtakapoitia unajisi, kama ilivyoitapika hiyo taifa iliyotangulia mbele yenu. 29 Kwani mtu awaye yote atakayefanya machukizo hayo mojawapo, nafsi hizo zitakazoyafanya zitakatiliwa mbali na watu wao. 30 Kwa ajili ya hayo yashikeni mausia yangu, ili kwamba msifanye kabisa desturi hizi zichukizazo mojawapo, zilizotangulia kufanywa mbele zenu, wala msijitie unajisi katika mambo hayo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.

 

Kuna maelekezo zaidi kuhusu ukomo wa kuoa. Kuhani anatakiwa awe ni mume wa mke mmoja tu. Hii, kwa kweli, ni sharti la maana hata kwa wateule. Mambo ya Walawi 21:7-15 inasema kwamba kuhani au kasisi asioe mwanamke kahaba au Malaya au mwanamke aliyeachwa kwa kutalikiwa. Tukiwa kama wateule tunapaswa kuangalia dalili au dokezo hili na kujilinganisha na maisha yetu wenyewe, kwa kuwa tunakwenda kuwa wafalme na makuhani.

 

Mahusiano yasiyo ya kiasili ya maumbile aliyoyafanya Mungu yamekatazwa pia.

 

Mambo ya Walawi 20:13 Tena mtu mume akilala pamoja na mtu mume, kama alalavyo na mtu mke, wote wawili wamefanya machukizo; hakika watauawa; damu yao itakuwa juu yao.

 

Tunaliona hili pia kwenye Warumi 1:18-32:

Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu. 19 Kwa kuwa mambo ya Mungu yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa maana Mungu aliwadhihirishia. 20 Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru; 21 kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza. 22 Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika; 23 wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo. 24 Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao. 25 Kwa maana waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakakisujudia kiumbe na kukiabudu badala ya Muumba anayehimidiwa milele. Amina. 26 Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; 27 wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao. 28 Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. 29 Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, 30 wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, 31 wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; 32 ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.

 

Aya ya 26 inaonyesha kuwa hii inamaanisha pia mahusiano ya ndoa za mwanamke kwa mwanamke maarufu kama usagaji.

 

Uhusiano kati ya mtu na mwenzake

Mapepo wanajaribu kupuuzia na kupotosha maana ya ndoa kwa lengo la kuyazuia mataifa yasiishike Torati.

 

1Timotheo 4:1-3 Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani; 2 kwa unafiki wa watu wasemao uongo, wakichomwa moto dhamiri zao wenyewe; 3 wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli

 

Sisi sote tunawajibika kuenenda na kuwatendea vyema watu wote kama familia.

 

1Timotheo 5:1-16 Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu; 2 wanawake wazee kama mama; wanawake vijana kama ndugu wa kike; katika usafi wote. 3 Uwaheshimu wajane walio wajane kweli kweli. 4 Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu. 5 Basi yeye aliye mjane kweli kweli, ameachwa peke yake, huyo amemwekea Mungu tumaini lake, naye hudumu katika maombi na sala mchana na usiku. 6 Bali, yeye asiyejizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai. 7 Mambo hayo pia uyaagize, ili wasiwe na lawama. 8 Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini. 9 Mjane asiandikwe isipokuwa umri wake amepata miaka sitini; naye amekuwa mke wa mume mmoja; 10 naye ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni, ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa bidii kila tendo jema. 11 Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa; 12 nao wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani yao ya kwanza. 13 Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizunguka-zunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa. 14 Basi napenda wajane, ambao si wazee, waolewe, wazae watoto, wawe na madaraka ya nyumbani; ili wasimpe adui nafasi ya kulaumu. 15 Kwa maana wengine wamekwisha kugeuka na kumfuata Shetani. 16 Mwanamke aaminiye, akiwa ana wajane, na awasaidie mwenyewe, Kanisa lisilemewe; ili liwasaidie wale walio wajane kweli kweli.

 

Ndoa ni muhimu na msingi wa jamii, kama tutajifunza kuhusiana na wenzi wetu wa ndoa na kuwafundisha watoto wetu kikamilifu kama ilivyofundishwa na kuonyeshwa kwenye Biblia, kama sehemu ya jamii yetu, tutaliendeleza kwanza kundi, kisha taifa, na hatimaye ulimwengu mzima wote utakao yapenda mafundisho Kristo. Ukristo utaendelea kusonga mbele na utakuwa na maana ya kweli na ndipo kutakuwa na Bwana mmoja na Imani moja.

 

Waefeso 4:4-6 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu. 5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. 6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.

 

q