Makanisa
ya Kikristo ya Mungu
[189]
Hatuokolewi Kwa Ajili ya Matendo Yetu Mema
(Toleo La 1.2
19970610-20000712)
Usemi n mafundisho ya kwamba Huokolewi kwa kupitia juhudi zako katika
kuzitunza Sabato, ingawaje bado ipo, vimekuwa ukitumika sana hadi kufikia kiwango
cha muwako usio wa lazima, na jinsi yanavyotumiwa leo ni kwa kupotosha watu
kuliko kwa kuwasaidia. Mojawapo ya jinsi usemu huu unavyotumiwa siku hizi ni
kwa kuyateka mawazo ya wasikilizaji na kuwaondoa kutoka kwenye jambo muhimuu
tunalolihitaji kulizingatia katika kuziokoa roho zaidi ya kukuza tofauti za kimafundisho.
Lakini umuhimu wa jambo na mtazamo vinabakia kwa wasikilizaji na walengwa
tunaowapelekea au kuwalenga. Imani yetu iko kwenye matarajio ya aina ya imani
ambayo inalinganishwa kimfano wake na Sabato kuwa ni ishara pekee inayowaonyesha
wale wanaomtii na kumuabudu Mungu. Bwana wetu alikuwa mtii hadi kufa kwake, akiwa
kama mmoja wetu, hadi mauti ya msalaba.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki ©
1997 by
Roy A. Marrs)
Editor of the Bible Advocate, the official organ of
the Church of God, Seventh Day (edited by Wade Cox)
(tr. 2013)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la
haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa
au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya
lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Hatuolewi Kwa Ajili ya Matendo
Yetu Mema
Usemi n
mafundisho ya kwamba Huokolewi kwa
kupitia juhudi zako katika kuzitunza Sabato, ingawaje bado ipo, vimekuwa
ukitumika sana hadi kufikia kiwango cha muwako usio wa lazima, na jinsi
yanavyotumiwa leo ni kwa kupotosha watu kuliko kwa kuwasaidia. Wakati
mafundisho haya yalipoanza kuzunguka huku na kule kwa mara ya kwanza katikati yetu,
yalichukuliwa kuwa ni kitu cha kustaajabisha na yalisababisha “msituko”, na huenda
ilitakiwa kusemwa kuwa lilikuwa ni jambo lililolenga kuteka fahamu zetu, bali
kwamba ni suala tu la kuwa kama yalikuwa yakitumika au yakuwa bado hata wakati
huu yanaendelea kutumia kama inavyotakikana. Mojawapo ya jinsi usemu huu
unavyotumiwa siku hizi ni kwa kuyateka mawazo ya wasikilizaji na kuwaondoa
kutoka kwenye jambo muhimuu tunalolihitaji kulizingatia katika kuziokoa roho
zaidi ya kukuza tofauti za kimafundisho.
Nyraka za Paulo,
Petro, Yakobo, Yohana, Yuda, na kitabu cha Waebrania ni nyaraka za mafundisho
yalizoandikwa mahsusi ili kuyanafundisha Makanisa. Mkazo wake mkubwa ulikuwa
wajue matatizo yaliyoletwa na kusababishwa na dhambi, mpango wa wokovu, utii,
kuyafanya mafundisho yawe moja kwa moja, na kuwaonya ili wazae matunda kwa
matendo mema. Sio nyaraka walizoandikiwa wasioongoka bado, na mtazamo wake haukuwalenga
watu wasioongoka bado.
Huu ni ukweli
tunaopaswa kuuwakilisha tunaposimama madhabahuni. Ni ukweli unaotakiwa
kuzingatiwa hata wakati tunapochapisha gazeti la Bible Advocate au
machapisho ya vipeperusgi. Na kwa kiasi kikubwa, tunashughulika na waumini na
jumbe zetu zinawalenga waumini. Tunapolihuria Kanisa, kile kinachotakiwa na
Kanisa, kuhusu imani ya waumini inatakiwa iendelee kuwepo kama ilivyikuwa siku
za misume.
Ni kweli kabisa,
tunatakiwa kujumuisha maonyo tunapokuuwa madhabahuni na kwenye machapisho
tunayowagawia watu tunapowashuhudia. Tunatakiwa kulitia moyo na hamasa Kanisa lipande
mbegu; lakini kwa kufanya hivyo, tunakwenda kukuta, kama alivyofanya Paulo, hitaji
la kuimarisha ulelewa wa mafundisho ya waamini ambao kwao sisi ni watumishi
wake, iwe kwenye madhehebu ya dini au kama ni nje ya madhehebu hayo. Hilo ni
tendo moja halisi la mwinjilitti, na Paulo alijikuta karibu apatwe na mkasa wa
,afumdisho ya uwongo na matatizo ya kimwenendo kwenye ua ndishi wake.
Mtazamo wa
maagano yote, yaani Agano la Kale na Jipya ni kuhusu watu wa Mungu, na yote yameelekeza
kwenye makutaniko ya Israeli na kwa Kanisa. Ingawaje wanahusiana na
wasioongoka, mtazamo wo mkuu ni kwenye mwenendo na imani ya watu wa Mungu.
Hata injili zote
zinaelekea kwenye uelewa halisi kuhusu Mungu na Kristo wake na taraja la kwamba
tunamtii Bwana wetu, sehemu ya kile kinachotuhusu kupanda mbegu na kufanya kazi
kwenye shamba la mavuno yake.
Ndiyo maana
ukaliaji tena wa kile kinachoshindwa kutuokoa wakati tunapojaribu kuelekea kile
kinachoweza kutuokoa? Ni matumaini yetu kwamba wale waliombele yetu
wakitusikiliza na wanaoitwa kwa jina la Kristo hawajaokolewa, kwa kuwa
wanatumainia matendo yao mema kuwaokoa? Kama ni hivyo, mtazamo wa mawasiliano
yetu inapaswa uwe ni kwa vitu vinavyookoa, na sio kwa vile vinavyoshindwa
kuokoa. Huenda, ni kwa kuweka mtazamo kwenye vitu visivyoweza kuokoa zaidi
kuliko, tunakuwa tukifanya makosa kutazama jambo kwa kujaribu kumfanya amtu
asiyeongoka aishike Sabato! Tunataka watu wasioongoka waache dhambi, ili
tusiache kuelezea ukweli wa kwamba kwa kuacha kuzini tu hakuwezi kumwokoa mtu.
Hebu na tufikirie
kwa kina mashiko yaliyopo kwenye “utunzaji wa Sabato peke yake kusikoweza
kuokoa” ulivyo na ukosefu wa kimtazamo juu ya jambo hili. Ni jambo lisilo na
maana kusema tu kwamba, Huwezi kuokolewa kwa ajili ya kuwaheshimu tu wazazi
wako, na wala kutaweza kuokolewa kwa kuishika tu amri moja nyingine yeyote.
Tunapomsihi mtu yeyote aishike amri ya kupendana, ni kwa nini basi
hatuwatahadharishi kuwa, Wajue kwamba kwa
kufanya hivyo peke yake, hakutaweza kuwaokoa?
Ukweli mwingine ni kwamba, kumpenda
jirani peke yake hakuwezi kukuokoa. Ni kwa nini basi hatuthubutu kusema?
Kanisa linaloitwa
Church of God, Seventh Day, HALIFUNDISHI kuwa tendo la kuzishika amri kumi au
aina nyingine zote za sheria, kutoka kote kuwili, yaani Agano la Kale au jipya,
ni kigezo cha wokovu—na kwa jinsi ninavyojua mimi, halijawahi kufundisha hivyo.
Tumekuwa tukishutumiwa kimakosa sana na mafundisho mengi na wanaoamini hivyo.
Maandiko mengi ya machapisho hata ya baadhi ya watu wetu sisi wenyewe,
yanaonyesha kuashiria tafsiri hii potofu kwetu na kwenye mafundisho yetu.
Hebu na nionyeshe
uwepo wa hoja za wanaotushutumu kimakosa. Tilia maanani maneno aliyoyasema Paulo kwa
Wagalatia.
Wagalatia 5:3-4 Tena namshuhudia kila mtu atahiriwaye,
kwamba ni wajibu wake kuitimiza torati yote. Mmetengwa
na Kristo, ninyi mtakao kuhesabiwa haki kwa sheria; mmeanguka na kutoka katika
hali ya neema.
Wanaotushutumu
kwa uwongo wanaweka hoja yao kwamba iwapo kama tutaitunza Sabato basi tunadaiwa
kuzishika sheria zote—zikiwemo na zile za utoaji dhabihuna nyingine nyingi zote.
Bali wao wanafundisha
bado kwamba tusizini na amri nyingine nane miongoni mwa amri hizi kumi. Iwapo
kama kwa matendo kabisa, kitendo cha kuitunza Sabato (moja ya amri kumi)
inatutaka tutoe dhabihu na sadaka, basin a ndivyo ilivyo kwenye amri
inayotuambia “usiue” na pia inatutaka kutoa dhabihu na sadaka! Sawa tu na
kwamba mafundisho ambayo hatutakiwi kuyafanya kimatendo yaani ufiraji, na kisha
tuzishike sheria zote za Musa ziwe zile zilizo kwenye zile amri kumi au kwenye
sehemu nyingine ya sheria za Musa, na kwenye amri nyingine za Musa, na haziko
kwenye zile nyingine kumi, ambazo tunazikuta kwenye zile kumi na ambazo
tunazikuta kuwa ni amri ambazo zinatutaka tusishiriki ngono na wajamaa za
karibu yetu na kufanya ufiraji.
Hoja za kila mara
za wanaotushutumu hazituami kwenye kanuni ile ile kwao wenycwe ya kwamba
(ishike moja ili uzishike na nyingine zote) inausaliti mtazamo wao wa kibagua
utunzaji wa Sabato. Zaidi sana, wanatushutumu sisi kwa kujaribu kujihesabia
haki (kuokolewa) kwa ajili ya utunzaji wetu wa Sabato.
Ili kudumisha
mabishano wangepaswa pia waseme kwamba wale wote wanaofundisha watu hawapaswi
pia kuua kimatendo (wawe wenye kuchukia) na wasifanye kwa matendo kitendo cha
kuiba (bali watamani tu), na wasishirki kimatendo kufanya uzinzi (bali wabakie
kumtamani tu mwanamke wanaomtazama). Kama tunajaribu kuokolewa kwa njia ya
kuzitunza Sabato, moja ya amri kumi, basi ni kwamba yale yote tunayoyafundisha kuhusu
kuzitii na kuzitenda kwa matendo hizi nyingine tisa ni sawa na kujaribu kutafuta
kuokolewa kwa njia ya kuyatii matendo ya sheria. Au umuhimu wa kuzitenda sheria
hizihizi kwa maadui zetu!
Tohara haipo
kwenye amri hizi kumi na hivyo badi haiku miongoni mwa mambo yanayofananishwa
na kuitii amri ya Sabato. Bali Sabato imo miongoni mwa amri kumi na wahubiri
kina Billy Graham, John McArthur, Chuck Swindoll na wenyine wengi wanaziponda kwenye
ibada zao wakidhania kwamba amri kumi bado zinafasiri dhambi.
Ni kweli, kwamba
amri nyingine zote zinatatakiwa kuadhimishwa na kutunza kwa matendo, bali
utunzaji wa Sabato sasa unapaswa utimilike kwa kwa kutafuta pumziko kwa Kristo,
wakisema kuwa mtu hawezi kwa sasa kuitimiliza amri hii ya nne kwa kuitunza
kimatendo kwa kuiadhimisha siku hii ya saba kuwa ni Sabato; bali kwa namna
nyingine, wakiiadhimisha kimatendo kabisa siku ya Jumapili na kuifanya kuwa ni
siku yao ya mapumziko na huku wakiifanya kuwa ni ya makusanyiko ya kiroho ingawaje
Biblia haiagizi wala kusema kuwa kumekuwa na mabadiliko na Jumapili imechukua
mahala pa Sabato.
Kwa nini tunaona
matumizi haya yasiyo na uwiano ya mtazamo wa sheria wa maadhimisho ya Sabato, kuonyesha
kwamba matendo na ushikaji wa ushikaji wa sheria sio mambo muhimu kwa kuupata
wokovu? Ni kwa nini basi watumishi hawa wanatufundisha na kututaka sisi tukatae
utoaji wa mimba na ufiraji na huku wakiwa hawajisikiii kabisa kusema, Wanalewa, hata hivyo, wakikataa kukubali ama
kuwapingana na ushoga kuwa haitakufanya uupate wokovu? Ni kwa nini basi
tusiseme kwamba, Tendo la kukataa kuitoa
mimba iliyokwisha kutungwa hakutaweza kukuokoa? Ni jambo linaloonekana kana
kwamba wanasema hivyohivyo tu kwamba, Kukataa
kuua au kutoua mtu hakutakuokoa wewe, sawa na kama wanavyosema kwamba Tendo la kuitunza Sabato halitaweza kukuokoa–
lakini hakuna mtu anayefanya hivyo kwa kuwa wanapenda kuishika amri ya Mungu
inayokataza kuua.
Je, tunataka
kuthibitisha na kuipa mashiko dhana na utunzaji wa Sabato? Kama ni hivyo,
tunatakiwa kuiongelea kwa upande wa chanya kuhusu umuhimu wa kuitunza Sabato!
Kuomgelea vile itakavyofanyika, zaidi kuliko kusema yale yasiyowezekana. Kamwe
Mungu hakuielezea Sabato haina maana kwa mchakato wa wokovu wetu, kwa kuwa kufanya
hivyo ni kutoka nje ya mstari wa fundisho, na haifai kuweka matamko ambayo
hakuyatamka. Ni sawa tu na ukweli kuhusu huduma ya Yesu. Sio mara moja
ameelezea yale yatakayojiri kwa kushindwa kuitunza Sabato na kile ambaccho hakiwezi
kufanyika kwa mwanadamu.
Kwa hiyo, haiwezi
kuhitimishwa kuwa kuna mambo mawili muhimu yasiyo sahihi kimwonekano kwenye
jambo hili kwa waumini na waalimu wa madhehebu ya kiinjili kama yafuatayo:
1) Kutenda nmatendo mema
hakutaweza kukuokoa.
2) Kuzishika sheria au
torati hakutaweza kukuokoa.
Kwa yote mawili,
nia inayoonekana ndani yao hasa ni kupinga utunzaji wa Sabato. Utunzaji wa
Sabato unaonekana kuwa ni mlengwa pekee na Wakristo wengi huku wakifundisha
utendaji wa matendo mema (ambavyo ndivyo hata Biblia imetuhakikishia kuwa
inafundisha).
Hakuna mahali popote
kabisa ambapo Biblia inapinga utendaji wa matendo mema, lakini baadhi ya
wahubiri wa siku hizi, wakiwemo pia hata baadhi yao kutoka kwenye Makanisa ya
Mungu, karibia sana na hali isiyo ya kawaida na bila udhuru kwanza wanadiriki
kueleza kinyume na dhana hii ya utendaji na umuhimu wa matendo mema kwa mtazamo
kwamba hayawezi kukuokoa, na kisha wakati mwingine wakiwazidi hata wale
wanazuoni watetea dini wakikanganyikiwa kwa kusema kwamba, Lakini simaanishi kuwa myapuuzie matendo mema.
Kwa hiyo, ni kwa
nini basi waanze kwa kutumia usemi huu?
Je, kwa hili tunataja
mahali ambapo Biblia inaelezea hivyo? Je, tunajaribu kunyamaza pale ambapo
Biblia imanyamaza bila kusema lolote? Huenda tunataka kuirudisha hii kwenye
mkazo huu: Tunaongea SAWA na vile Biblia
inavyosema, na HATUSEMI pale ambapo Biblia imenyamaza kimya bila kusema lolote! Ni kama kilivyo kistuli chenye
mguu mmoja vigumu kukisimamisha kwa namna yeyote ile!
Umuhimu wa matendo
mema umeelezewa mara kumi na sita kwenye maandiko ya Agano Jipya (kwenye tafsiri
ya KJV na kwenye nakala za Kiyunani):
Mathayo 5:16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya
watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
Yohana 10:32 Yesu
akawajibu, Kazi njema nyingi nimewaonyesha, zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya
kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe?
Matendo 9:36 Na
mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi
(yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.
Warumi 13:3 Kwa maana watawalao hawatishi watu kwa
sababu ya matendo mema, bali kwa sababu ya matendo mabaya. Basi, wataka
usimwogope mwenye mamlaka? Fanya mema, nawe utapata sifa kwake;
Waefeso 2:10 Maana
tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea
awali Mungu aliyatengeneza
1Timotheo 2:10 bali
kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.
1Timotheo 5:10 naye
ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni,
ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa
bidii kila tendo jema.
1Timotheo 5:25 Vivyo
hivyo matendo yaliyo mazuri ya dhahiri; wala yale yasiyo dhahiri hayawezi
kusitirika.
1Timotheo 6:18 Watende
mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane
na wengine kwa moyo;
2Timothy 3:17 ili
mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.
Tito 2:7 katika mambo yote ukijionyesha wewe
mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha
usahihi na ustahivu,
Tito 2:14 ambaye
alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na
kujisafishia watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo
mema.
Tito 3:8 Ni neno la
kuaminiwa; na mambo hayo nataka uyanene kwa nguvu, ili wale waliomwamini Mungu
wakumbuke kudumu katika matendo mema. Hayo ni mazuri, tena yana faida kwa
wanadamu.
Tito 3:14 Watu wetu nao wajifunze kudumu katika matendo mema, kwa matumizi yaliyo lazima, ili wasiwe hawana matunda.
Waebrania 10:24 tukaangaliane
sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri;
1Petro 2:12 Mwe na
mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya,
wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.
Kumbuka kuwa
maneno ya Kiyunani yaliyotumika kwenye vifundu au aya hizi, ni ya ama namna ya kalos
ergos, au agathos ergos. Matendo mema ni tafsiri au maana bora zaidi ya maandiko haya.
Kila kifungu hapo
juu kinaelezea umuhimu wa matendo mema
kwa msisitizo mzuri na chanya. Hakuna hata moja kati ya maandiko hayo
iliyoonyesha kuwa matendo mema kuwa
ni kitu cha kukiwekea mjadala kuhusu neema na sheria! Mjadala kuhusu taji za
dhahabu kwa matendo mema unaonekana kwenye Tito 2:14:
(Yesu) ambaye
alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe na maasi yote, na kujisafishia
watu wawe milki yake mwenyewe, wale walio na juhudi katika matendo mema.
na Waefeso 2:10:
Maana tu kazi yake,
tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu
aliyatengeneza ili tuenende nayo.
Iwapo kama
tutapenda kuzifananisha na injili kama ilivyotolewa na Yesu, waandishi wa
injili, na eneo lingine lote lililobakia la Maandiko Matakatifu ya Agano Jipya,
wakati wote tutayaongelea matendo mema kwa mtazamo chanya—bila udhuru!
Kinyume chake tunaonywa
kuwa tusitafute kufanya matendo ya watu waovu, matendo yanayofanywa ili
yaonekane na watu na hasa yanayotendwa kwa dhamira mbaya, mwisho wetu utakuwa
sawa na matendo yetu, na wote tumeonywa kuwa tutapewa thawabu sawasawa na
matendo yetu, zikiwa ni njema au mbaya, na sote tumetakiwa kutenda matendo
nayayoendana na toba yetu.
Wakati kwamba Paulo
alisema wazi sana kwamba hatuokolewi kuokana na matendo mema au kwa kuishika
torati, basi anaharakia kuonyesha jinsi tunavyoweza kuokolewa. Anaweka uzani
kwa kufafanua kwamba tunadumu kuishika torati kwa imani; na kwa kusema kwake
kuhusu kufanyika kuwa kiumbe kipya kwa jinsi tulivyofanyika kwa kupitia Kristo
ni kwa kutenda kwetu katendo mema. Mtume Paulo anasema kuwa Kristo alikufa ili atukomboe
sisi kutoka kwenye dhambi na uovu, na kuwatakasa watu wa namna ya kipekee wenye
kuonyesha nia na bidii ya kutenda matendo mema. Inawezaje basi watu wafanye
bidii ya kuwa na matendo mema iwapo kama matendo mema ni kitu kisichohitajika
na sio muhimu? Ni sawa tu na kujiuliza kwamba inamaana gani basi watu kuzitii
amri za Mungu ikiwa jambo kuu na muhimu tunaloliongelea ni kwamba kuzitunza ama
kuzishika hakutaweza kutuokoa?
Ili kupata uwepo
wa ushahidi wake kwenye neno la Mungu, yatupasa kujua kwamba Mungu huutuza utii
wetu na matendo yetu mema, na kitendo cha kuyaona matendo mema kama hayana
maana wakati Mungu alimtoa mwana wake afe ili atubadilishe ili tuweze kuyatenda
matendo haya mema ni kitendo cha kuukiuka ujumbe wa injili.
Kama jambo hili
kwa kweli limefanywa na baadhi ya watumishi miongoni mwetu wakisema kuwa
utunzaji wa Sabato hauna umuhimu, basi tunapaswa kuwa wa kweli kuhusu jambo
hili na kusema hivyo. Kama tunaamini kuwa bado ni ya muhimu na iko kwenye
mapenzi ya Mungu katika maisha yetu, na kwamba sio tu ni kitu kizuri tu
kukifanya, na huku kila mara mtu anakuambia kuwa hutaweza kuokolewa kwa
kuzitunza Sabato, basi mtu huyo anatakiwa akuthibitishie kuwa aio tu kuwa ni
mapokeo mazuri tu kuwemo Kanisani (Mtazamo wa Ulimwengu wote), bali mhubiri anatakiwa asisitize kuwa wanaomuamini
Mungu wanatakiwa bado waitunze Sabato (na sio mtindo tu wa Ulimwenguni kote), na kwamba utunzaji wa Sabato ni amri. Je, ipo au
haipo? Na kama ipo basi hatupaswi kuiongelea kinyume .
Iwapo kama
ungeulizwa swali kwamba Je, ungeweza
kuifia Sabato? Ungejibuje? Ungepaswa kujibu kwa umakini na tahadhari. Nyuma
ya swali kuna swali linguine kubwa zaidi kusema: Je, uko tayari kufa kuliko kumuasi Mungu? Kusema kuwa, Hapana, sipo tayari kuifia Sabato pasipo
kutoa maelezo kunaweza kuacha ujumbe wazi wa masuala ya kimaadili kwenye mawazo ya vijana na watu wazima kuwa
utii haumaanishi kukifia kitu. Tunatakiwa kila mara kuongea kwa moyo mwema na
matendo.
Tumaini letu ni
kwamba ni muhimu kufa tukionyesha utii wetu kwa Mungu. Kama Yesu alikubali kufa
ili kuturekebisha dhambi na uasi wetu, basi ni muhimu kwetu kufa ili kuepuka
kuuonyehsa uasl wetu kwake. Ni ukweli unaojiri kwenye historia kwamba mitume
wengi na karibu wote waliyatoa maisha yao wakichagua kutii.
Iwapo kama
tutapunguza uzito wa amri yoyote ya Mungu ambayo inabakia kuwepo, Mungu
aatatupatiliza kwa ukali sana akituonyesha kuwa kila alichotuamuru sisi kukifanya
ni cha lazima na muhimu (tazma Mathayo 5:18-19; Ufunuo 12:17; 14:12;
22:11-14,19 nk). Inaonekana kwamba kuna watu wanayachukulia maneno ya watu
kwamba Kuitunza Sabato hakutaweza
kukuokoa, wakimaanisha kuwa Sabato ni jambo la hiyari na sio muhimu sana.
Sio kitu cha hiyari kuishika, bali ni amri ya Mungu. Sababu iliyowekwa na
kuaminiwa na mababa wa Kanisa la Mungu ilikuwa muhimu na yenye mashiko. Ilimaanisha
kitu fulani kama ifuatavyo:
Yakobo 2:10-11 Maana
mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja,
amekosa juu ya yote. Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue.
Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria.
Imani hii inadumu
kuwa na mashiko pale tu inapofanyiwa kazi kama hivi, Kwa kuwa yeye aliyeisema, 'Usiwe
na miungu mingine ila mimi,'ndiye alisema pia, 'usijifanyie sanamu ya kuchonga';
au, yeye alisema, 'Waheshimu baba yako na mama yako' ndiye aliyesema pia 'ikumbuke
siku ya Sabato na uitakase.'
Hitimisho
Muhimu Kutiliwa Maanani
Jinsi tunavyozungumza kuhusu matendo
mema na utunzaji wa Sabato ni muhimu sana kwa ajili ya amani ya Kanisa.
Kama hatuna habari na kulijua hilo, basi tujue kwamba namna tunavyofanya na
kuhubiri madhabahuni, kuandika kwenye makala kama vile kwenye majarida ya Bible
Advocate au mafundisho ya Shule ya Sabato, yawe ama yanakuwa ya upotoshaji,
yenye kuelimisha au kuharibu. Kwa mara chache na kidogokidogo huonekana kuwa ni
asilia. Mtazamo wetu wa kimafundisho kuhusu dhana hii ya kwamba utunzaji wa
Sabato na matendo mema havitaweza kutuokoa umekosa mizani, na vyote vimekuwa ni
vyenye kuwakanganya watu na kuwapoteza na kuwaharibu, kwa kukosa mashiko na
matumizi mema yaliyokusudiwa kutumika.
Tunatakiwa kuziongelea kwa mtazamo chanya kuhusu vitu tunavyofundisha, na
yale tunayosisitizia, na yale tunayoyaamini.
Tunatakiwa kutofautisha kati ya yale yanayoweza kutuokoa na yale
yanayotuhukumu. Ni mambo tofauti. Ni ukweli ulio dhahiri kutoka kwenye Biblia
kwamba hatuokolewi kwa sababu ya matendo yetu mema, bali pia ni wazi kabisa
kwamba Biblia inatuambia kwamba Mungu anapenda na kutoa thawabu kwa ajili ya
matendo mema na ambavyo anatutarajia sisi tuyatende, na kwamba sisi
tunajulikana kuwa tunaendelea kuyatenda na kumpendeza Mungu kwa hayo au
vinginevyo tutakuwa hatuko pamoja naye kupitia matendo yetu. Ni jambo
lililowazi kwamba tunahukumiwa kutokana na kutoyatenda matendo mema na ni kama
ilivyo wazi pia kwamba matendo mema peke yake hayawezi kutuokoa sisi.
Wakati kwamba matendo mema ni siyo matendo yaliyo muhimu kwenye mchakato
huu wa wokovu, bali kutotenda matendo mema au matendo mabaya yote mawili yanatoa
mwelekeo wa hatima ya mtu kwenye wokovu wake! Tendo la kumuasi Mungu ni sababu
inayopelekea hitaji la wokovu.
Iwapo kama Mungu anapenda tuzitunze Sabato, hebu na tuwe na tuendelee mbele
na kusema hivyo kwa namna iliyo na mtazamo chanya! Iwapo kama utunzaji wa
Sabato sio jambo linalotokana na mapenzi ya Mungu, basin a tuendelee mbele kwa
kusema hivyo!
Mtume Paulo aliandika, "Kwa sababu hiyo, naandika haya nisipokuwapo,
ili, nikiwapo, nisiutumie ukali kwa kadiri ya uwezo (mamlaka) ule niliopewa na
Bwana, kwa kujenga wala si kwa kubomoa." (2Wakorintho 13:10). Hebu basi
nia zetu na juhudi za matendo yetu yatumike kwa lengo la kuelimisha.
Iwapo kama unataka kutaniko lako lianze kushuhudia zaidi kuliko kuwa
washiriki kwenye mtazamo wao, wainue kwa mkono na kusema, Ndugu, hebu na twende na kumtafuta mdhambi tumshuhudie. Ni jambo la
maana zaidi kuliko kuwaambia walioongolka kuwa yahawezi kuwaokoa.
[Katika kulifanyia kazi andiko hili nilimuandikia Roy Marrs kuhusu umuhimu wa matendo na
nikamuonyesha fafanuzi zenye kuunga mkono zifuatazo na ambazo zingemhakikishia
na jinsi zinacvyohusiana kwa mujibu sawa na mapenzi yake (ed.).]
Kuzitii amri za Mungu ni tendo linaloonyesha imani. Yeye aliyetupa sisi
sheria alifanya hivo kwa kuwa sheria zinatokana na asili yake ilivyo. Sisi ni warithi
wa siri na mambo ya mbinguni (2Petro 1:4). Kitendo cha kuzitii sheria ni
matokeo ya maongozi ya Roho Mtakatifu na tunazishika sheria kutoka mioyoni
mwetu. Hatuhitaji tena mtu wa kutufundisha kwa kuwa tuna Roho Mtakatifu. Sabato
ni moja wapo ya mambo yaliyoamrishwa kwenye amri za Mungu na ambayo ndiyo
yaliyoanzia na kuongezewa kwenye amri na sheria za Agano la Kale na kuweka
msingi wa wajibu tunaouchukua sisi wenyewe wakati tunapokuwa sehemu na
washiriki kwenye Ufalme wa Mungu. Hatuhesabiwi haki kwa njia ya sheria. Bali
tunahesabiwa haki kwa njia ya imani. Mababa wa kale na wengine wote waliozishika
walihesabiwa haki kwa njia ya imani (Waebrania 11:1-39). Imani ni kuwa na
hakika na mambo yatarajiwayo (Waebrania 11:1). Lakini hawakuzipokea zile ahadi
kwa kuwa Mungu aliwakusudia kitu kingine kizuri zaidi kwa ajili yetu, ambacho
mbali na sisi wasingeweza kufanyika wakamilifu (Waebrania 11:39). Kwa imani,
tunautarajia mfumo wa maongozi ya torati na utawala utakaokuwa unaongozwa kwa
mujibu wa mapenzi halisia ya Mungu. Kwa imani, dhabihu zetu zinafanyika kuwa ni
mawe yaliyo hai kwenye Hekalu la Mungu ambayo kwayo sisi tuko na tunatawaliwa
kama maongozi ya sheria za Mungu mioyoni mwetu na kwenye nia zetu.
Sabato ni amri ya majaribio kwa kuwa inaonyesha mfumo na kanuni za Mungu.
Wale wanaodai kuwa na imani, na kuhu wakiwa hawaishiki Sabato, wanapungukiwa na
utukufu wa Mungu. Kwa matendo yao wanatuonyesha jinsi imani yao ilivyo na
mapungufu. Sisi kwa matendo yetu tunaonyesha imani yetu (Yakobo 3:18). Imani
yetu iko kwenye matarajio ya mfumo mpya unaoonyeshwa kwa ishara ya Sabato ikiwa
kama ni ishara ya utii ya watu wa Mungu. Bwana wetu alitii hadi kufa, akiwa ni
mmoja wetu, hadi mauti ya mtini au msalabani (Wafilipi 2:5-8). Sabato ni alama
ya utaratibu wa mapumziko ambayo Mungu ameanzisha kwa ajili yetu katika Yesu
Kristo.
q