Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[021i]

 

 

 

Ufafanuzi wa Kitabu cha Sefania

 

(Toleo La 1.0 20141003-20141003)

 

Unabii huu muhimu uliandikwa kwenye kipindi cha takriban dazani moja ya miaka kabla ya kuanguka kwa Ninawi, na kabla ya kipindi cha utumwa wa Yuda. Nabii huyu wa mwisho wa kabla ya kipindi cha utumwa aliwataja moja kwa moja makasisi waliojulikana kama Chemarim au Makuhani au makasisi wavaa Majoho Meusi wa Baali na Ashtorethi au Easter, wa dini au imani potofu ya Mungumke. Makuhani hawa bado wapo na wanahudumu huko Yerusalemu kwa maelfu na wataondolewa mara moja hivi punde na kulazimika kutubu na kuachana mafundisho ya uzushi na hawatayafundisha kamwe tena kabisa.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2014 Wade Cox)

(tr. 2015)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Ufafanuzi wa Kitabu cha Sefania



Utangulizi

Sefania ameorodheshwa kuwa ni wa Nane miongoni mwa manabii waliokubalika kwenye kanuni ya Agano la Kale. Uzao wake umeorodheshwa kwa zaidi ya vizazi vinne kwa kuwa neno la mababa zke kwenye tafsiri ya KJV ni neno hilohilo kwenye Kiebrania kama Hezekia na watawala walivyothibitisha alikuwa ni kitukuu wa Hezekia Mfalme wa Yuda.

 

Imethititishwa na E.A. Leslie (kwenye kamusi yake ya Interp. Dictionary of the Bible, Bk. IV, pp. 951ff.) kwamba huduma yake imekadiriwa tarehe kwa harakati za uvamizi za Scythian mnamo mwaka 630-625 KK. Harakati za ibada na dini za Baali na Mungu Mke wa a dini za Waashuru na Wababeloni zilikuwa zimeingia katika Yuda baada ya kupanuka kwa dola ya Waashuru na Manase kuzijenga madhabahu na magari kwenye nyumba ya juu ya Mfalme Ahazi ili kuliabudu Juan a dini za kisiri. Waliliabudu jua, mwezi na sanamu zote za kizodiaki na Malaika wote wa Mbinguni (2Wafalme 23:11ff). Mkazo mpya ulitolewa kwenye dini za Mungu Mke pamoja na sherehe au sikuku za Ashtorethi au Easter na za Baali zilizoingia kutoka kwenye imani mchanganyiko wa Waashuru na Wababeloni zilizosisitizwa kwa nguvu na mkazo mkubwa. Dini hizi zikafanyika kuwa maarufu kwa haraka na zikaingia katika familia za watu wa Yudea na wakazishiriki pamoja na kila mshiriki walijitahidi kufanya wawezavyo kwa namna hii hii tunayoiona wakifanya leo kwenye hizi dini za waadubu Jua na waamini Utatu wanavyoitukuza kwa kuiadhimisha tarehe 25 Disemba siku ya Krismas na kwa jinsi hii hii kama wanavyofanya leo kama ilivyokuwa na kulaaniwa na nabii Yeremia (Yeremia 7:17ff, 10:1-9) ambaye alikuwa nabii kwa kipindi kimoja na Sefania.

 

Kabila la Scythians walikuwa wasio na ustaarabu kutoka Kaskazini ambalo lilivamia Asia Ndogo kwenye mipaka ya Misri. Farao Psammetichus I wa Misri (Herodotus I, 103-106) aliwapa rushwa na waliafikiana kwa mkataba kutoka mipakani mwake na wakaishambulia na kuiteka Ashkeloni na Beth-shean.

 

Unabii haukuishia kukemea Yuda tu kwa kipindi kile cha uvamizi wa hawa Scythian na kabla ya kuanguka kwa dola ya Waashuru mwaka 605 KK na Wababeloni. Yalikuwa ni makemeo kwa wanadamu wotekwa uasi wao uliotokana na kutatanishwa na Dini za Waabudu Jua kama tunavyoona kwenye Sefania 1:2-3.

 

Sefania Sura ya 1

Neno la Bwana lililomjia Sefania, mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia; katika siku za Yosia, mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda.

 

Kwa hiyo ndiyo maana tunaamini kukiweka kipindi hiki kuwa klikuwa ni kile cha Yosia, mfalme wa Yuda (642/1–609). Marejesho ya Yosia katika mwaka huu wa 18 yalikuwa hayajaisha bado kama tunavyoona kwenye mlinganisho na 2Wafalme 23. Kwa hiyo, andiko hili liliandikwa mapema kabla ya kipindi cha Marejesho bali huenda yawezekana sana kuwa ni kipindi kile cha kuonekana kwa Kitabu cha Torati kuelekea kwenye Marejesho kwenye Yubile ya mwaka 624 KK.

Unabii wake kwa Ninawi ulitimilika kwa kuanguka kwa Ninawi na kuangamizwa kwake na Wamedi na Wababeloni mwaka 612 KK. Wababeloni waliwapiga kabisa na ushawishi wa Wamisri kwenye Mapigano ya Karchemishi mwaka 605 KK mzunguko mmoja wa Sabato baadae. Utajwaji wake kwenye Sefania hakupo kwa moja kwa moja kama vile ilivyo kwenye unabii wa Nahumu ambako umeelezewa kwa kina zaidi kwenye unabii wake kuhusu kuanguka kwa Ninawi.

Huu ni unabii unaohusu Siku za Mwisho:

2 Nitavikomesha kabisa vitu vyote, visionekane juu ya uso wa nchi, asema Bwana. 3 Nitamkomesha mwanadamu na mnyama; nitakomesha ndege wa angani, na samaki wa baharini, na hayo makwazo pamoja na wabaya; nami nitamkatilia mbali mwanadamu, asionekane juu ya uso wa nchi, asema Bwana. 4 Nami nitaunyosha mkono wangu juu ya Yuda, na juu ya watu wote wakaao Yerusalemu; nami nitayakatilia mbali mabaki ya Baali, yasionekane mahali hapa, na hilo jina la Wakemari pamoja na makuhani; 5 na wale walisujudiao jeshi la mbinguni juu ya dari za nyumba; na hao waabuduo, waapao kwa Bwana na kuapa pia kwa Malkamu;

 

Malkamu ni neno la Kiebrania kwa Mungu wa kitaifa wa Waamoni, yaani Moleki. Alihusishwa na Nyota ya Mungu Remphan ambaye ni Nyota Sita Zinazoonyeshwa na ambayo sasa inaonekana kwenye Bendera ya Israeli na kiupotoshaji inajulikana kama Nyota ya Daudi. Kungu aliwakasirikia Yuda na akawapeleka utumwani huko Babeli na wanapaswa kutendewa ipasavyo katika siku ya Bwana. Huu sio Utumwa wa Babeli, sio Utumwa wa Warumi, bali ni wa namna wa wote wawili, na kwa kupitia utawanyiko wao katika Siku za Mwisho. Siku ya Bwana imenenwa kwenye jarida la Siku ya Bwana na Siku za Mwisho (Na. 192). Kuna sehemu takriban ishirini zinazoitaja Siku ya Bwana (kwa Kiebrania Yom Yahovah) kuna mifano takriban 16 kuanzia kwenye andiko kama vila Isaya 2:12 (kisha tena Isaya 13:5; Yoeli 1:15; 2:1,11; 3:14; 4:14; Amosi 5:18,20; Obadia 15; Sefania 1:7,14,14; Malaki 4:5). Kwenye vifungu vinne ni pamoja na neno la Kiebrania la Lamed (yani Sefania 2:12; Ezekieli 30:3; Sefania 14:1,17) ambako ni siku inayojulikana na Yahova na kwenye sehemu nyingine imejuluishwa na maneno hasira au kisasi.

 

Kwenye Agano Jipya imejitokeza mara nne kwenye 1Wathesalonike 5:2, 2Wathesalonike 2:2, 2Petro 3:10, Ufunuo 1:10, na Bullinger anaiona hii kuwa kama kiashirio cha namba nne na kila kitu kinafanyika ili kumshusha mwanadamu na kumuinua Yahova kwa matumizi yake na unabii ambao inatokea.

 

6 na hao waliorudi nyuma, na kuacha kumfuata Bwana; na hao wasiomtafuta Bwana, wala kumwulizia. 7 Nyamaza kimya mbele za Bwana MUNGU; Kwa maana siku ya Bwana i karibu; Kwa kuwa Bwana ameweka tayari dhabihu, Amewatakasa wageni wake. 8 Na itakuwa, katika siku ile ya dhabihu ya Bwana, nitawaadhibu wakuu, na wana wa mfalme, na watu wote waliovaa mavazi ya kigeni. 9 Na katika siku ile nitawaadhibu hao wote warukao juu ya kizingiti, waijazao nyumba ya bwana wao udhalimu na udanganyifu. 10 Na katika siku ile, asema Bwana kutakuwako sauti ya kilio kutoka lango la samaki, na mlio mkuu katika mtaa wa pili, na mshindo mkuu kutoka milimani. 11 Haya! Lieni, ninyi mkaao katika Makteshi, maana wafanya biashara wote wameangamia; hao wote waliokuwa na mizigo ya fedha wamekatiliwa mbali.

 

Maandalizi ya dhabihu ya Bwana yalifanyika na Kristo na utakatifushaji wa Wageni wa Bwana kulifanyika kwenye Pentekoste ya mwaka 30 BK.

 

Mwaka 597 KK walikwenda utumwani huko Babeli kuwaandaa Yuda na kuwarejesha mioyo ili wadumu hadi Masihi na waingie hukumuni na Kanisa lianzishwe. Kisha Yuda washughulikiwe kama kanisa lilivyofanyiwa kwa kuchaguliwa na kutolewa kwa kipindi cha yubile 40 tangu mwaka 27 BK hadi 2027 BK. Kipindi cha mwisho kitakuwa ni cha kutoka kipindi cha Vita vya Mwisho hadi kile cha kumiminwa Vitasa vya ghadhabu chini ya Masihi kitakachoishia kwenye Siku ya Upatanisho ya mwaka 2024. 2025 utakuwa ni mwaka wa Mavuno Makuu abato na Yubile ya mwaka 2026 na 2027. Yerusalemu ilitwaliwa na kisha ikafanwa upya na kisha ikaangamizwa kabla haujaangamizwa kabisa. Dini ya Kiyahudi ikaanzishwa ikiwa sasa kama dini potofu na ya uwongo na itaangamizwa pia kati ya mwaka 2015-2024.

 

12 Kisha itakuwa wakati ule, nitauchunguza Yerusalemu kwa taa; nami nitawaadhibu watu walioganda juu ya sira zao; wasemao katika mioyo yao, Bwana hatatenda mema, wala hatatenda mabaya. 13 Na huko utajiri wao utakuwa mateka, na nyumba zao zitakuwa ukiwa; naam, watajenga nyumba, lakini hawatakaa ndani yake; nao watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.

 

Siku za Mwisho haitakuwa na kingine chochote kabla ya hii na hata kama Yerusalemu ilikatiliwa mbali na wazelote waliwasha uporaji wao na kuharibu Sadaka za Daima kwa mashambulizi ya Warumi na ndivyo wengi watataabika tena. Tukio kuu moja wapo lilikuwa ni Mauaji ya kupangwa ya kuwaangamiza Wayahudi yajulikanayo kama Holocaust mwaka 1941-1945. Mungu kwa sasa anashughulika na Mashariki ya Kati na makabila yanayoizunguka na mataifa kama ilivyokuwa inaenda kwa miaka 2520 tangu kuanguka kwa Hekalu mwaka 597 hadi mamlaka ya Wapalestina mwaka 1922/23. Mwaka 1922 Palestina ilikabidhiwa kwa Waingereza (wakati kwamba mwaka 1917 kulishuhudiwa azimio la Balfour). Mwaka 1948 uhuru wa Israeli ulitangazwa na mwaka 1967 ulishuhudia Yerusalemu ikifanywa upya na kurejeshwa kwa Yuda chini ya Vita ya Siku Sita. Hiki ni kipindi kinachowakilisha kile cha maombolezo ya Haruni ba Yerusalemu ukirejeshwa tena lakini ukuhani wa kweli hauna uthibiti na utaratibu wa ibada za Hekalu haukuweza kurejeshwa. Hii ilianzisha Kipindi cha Marejesho na kisha Vita vya Siku za Mwisho vilianza baada ya kipindi cha miaka ya Thelathini ya Mwisho cha Maombolezo ya Musa kuanza mwaka 1997 baada ya mwisho wa Kipindi cha Wamataifa (Soma jarida la Kuanguka kwa Misri Kuanguka kwa Misri Sehemu ya II: Vita vya Mwisho (Na. 036_2).)

 

14 Hiyo siku ya Bwana iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya Bwana; Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko! 15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu, 16 Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana. 17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi. 18 Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha.

 

Ni katika wakati huu Masihi atatumwa kushughulika na wanadamu kwa Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu.

(Soma jarida la Vita vya Siku za Mwisho na Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu (Na. 141B).)

 

Sura inayofuatia inashughulikia hali na mwonekano wa watu wa nchi na jinsi wanyenyekevu na wapole watakavyoirithi nchi. Amri hapa ni kutafuta upole na utakatifu.

 

Kifuatacho hapo kinahusu na Gaza na Palestina. Ushughukiaji huu utakuwa ni kutoka Gaza hadi kaskazini mwa miji ya pwani ya Lebanoni.

 

Sefania Sura ya 2

Jikusanyeni, naam, jikusanyeni, Ee taifa lisilo na haya; 2 kabla haijazaa hiyo amri, kabla haijapita siku ile kama makapi, kabla haijawajilia hasira kali ya Bwana, kabla haijawajilia siku ya hasira ya Bwana. 3 Mtafuteni Bwana, enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya Bwana.

 

Kwa hiyo, ni wapole na watakatifu ndio wanalindwa Siku ya Hasira ya Mungu.

 

Kumbuka majina ya makundi ya kikabila na kile kitakachotokea na kuwapata. Maelezo haya pia ni kwa mujibu wa unabii wa wengine wa kundi la Manabii Kumi na Mbili.

 

Katika Siku za Mwisho Gaza chini ya Hamas imeleta maangamizi na kulimaliza yenyewe. Ndivyo ilivyo pia kwa Waashuru na Wababeloni na Waajemi na kisha Warumi walishuka kuja kushinda na kukaa na ndivyo itakavyokuwa pia katika Siku za Mwisho ndipo hawa Wapalestina wanaojifanya kuwa Waarabu wataishusha Ghadhabu ya Mungu kuifanya ije juu yao tena. Machafuko haya yasiyo na maana yataendelea na hayatakoma hadi Gaza ikiwa tupu na maganjo matupu na Mfalme wa Kaskazini ataitwaa hii na kutandaza hema yake ya ufalme kama ilivyotabiriwa na nabii Danieli (11:40-45). Itaenea kutoka Gaza hadi Ashkeloni na Ashidodi na Ekroni haitakuwa na wa kubakia ndani yake anayeshikilia sasa na nguvu au uweza wa mnyama wa mwisho wa Mfalme wa Kaskazini ataimiliki Yerusalemu kama tunavyojionea kwenye Danieli.

 

Mji wa Ekroni ulikuwa kaskazini kabisa ya Palestina (Joshua 13:3) kilometa 14 mashariki mwanzoni mwa Bonde la Soreki kuelekea Yerusalemu. Huenda ni mji wa zamani sana katika Kanaani kama tunavyojionea kutoka kwenye Yoshua 13:3 (na soma kitabu cha Joseph. Antiq., V.iii.1).

 

Inaweza kupingwa kwamba Waashuru chini ya Senikarebu aliutwaa huu na kuwaweka waasi waliouteka chini ya Hezekia awaue na ndipo ilikomesha mchakato huu lakini hii haikuwezekana. Andiko hili linazitaja Siku za Mwisho. Eneo hilo kwa hiyo lilikaliwa na Mfalme wa Kaskazini katika Siku za Mwisho zinazotajwa hapa na kwenye Danieli anaenea kutoka kusini mwa Gaza hadi kwenye eneo la Ekroni na hadi Yerusalemu.

 

4 Kwa kuwa Gaza utaachwa, na Ashkeloni utakuwa ukiwa; wataufukuzia mbali Ashdodi wakati wa adhuhuri, na Ekroni utang'olewa.

 

Kundi la Wakerathi ndilo linalotajwa hapa.

 

5 Ole wao wakaao karibu na pwani ya bahari, taifa la Wakerethi! Neno la Bwana li juu yenu, Ee Kanaani, nchi ya Wafilisti; mimi nitakuangamiza, asibaki mtu akaaye kwako.

 

Andiko hili hapa linataja taifa la Wakerithi. Wakerithi na Wapalestina walikuwa sehemu ya Jeshi binafsi la Daudi ambao waliwakusanya na kuwaingiza wageni na waongofu hawa wawili kutoka Ufilisti na walithibitisha utii wao mkubwa kwake. Walikuwa ni sehemu ya waliomfuata kwenye msafara wake wakati alipokaa huko Yerusalemu. Benaiya mwana wa Yehoyada alikuwa kiongozi wao (2Samweli 8:18; 20:23). Wakerithi walikaa kusini mwa Yudea huko Negebu. Wao ni sehemu ya Wakazi wa pwani ya Bahari na yawezekana kabisa kuwa hata jina lao limechukuliwa kutoka kwa Wakariti ambao pia waliwahi baadae kuwa wafanyakazi wa kujitolea kutoka eneo la kaskazini mwa Asia Ndogo. Unabii unawaelezea watu hawa kuwa huenda ni wa nje ya Ufilisti ya zamani itafanywa upya.

 

Unabii huu unayataja maeneo yote ya makundi haya kwenye nyumba ya Yuda na kwamba watakuja chini ya kundi la kimkoa la Yuda kwenye Muungano wa Kitaifa wa Israeli kwa kipindi cha Milenia.


6 Na hiyo nchi ya pwani itakuwa malisho, yenye vibanda vya wachungaji, na mazizi ya makundi ya kondoo. 7 Na hiyo nchi ya pwani itakuwa nchi ya watu wa nyumba ya Yuda waliosalia; watalisha makundi yao huko; watalala katika nyumba za Ashkeloni wakati wa jioni; kwa maana Bwana, Mungu wao, atawajilia na kuwarudisha wafungwa wao.

 

Unabii huu unaonekana kuwahusu Waashikeloni kwenye muungano wa taifa la Israeli chini ya Yuda. Bahati za wote zitarejeshwa upya.

 

8 Mimi nimeyasikia matukano ya Moabu, na dhihaka za wana wa Amoni, ambazo kwa hizo wamewatukana watu wangu, na kujitukuza juu ya mpaka wao.

 

Mabishano ya kikanda ya Wapalestina na kuendelea kukataa kuwa na amani na kuafikiana kutashuhudia wao walishughulikiwa katika siku zijazo. Matokeo yake kwenye ujio wa vita ardhi za ukanda wa mashariki itaangamizwa vibaya sana. Israeli wataikalia na wataunda sehemu pia ya shirikisho la Israeli.

 

Andiko lifuatalo kwa kweli linasomeka kuwa “Ni Neno la Yahova, Mungu wa Israeli.”


9 Basi kama niishivyo, asema Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, Hakika Moabu atakuwa kama Sodoma, na wana wa Amoni kama Gomora, yaani, milki ya upupu, na mashimo ya chumvi, ukiwa wa daima; watu wangu waliosalia watawateka nyara, na watu wa taifa langu waliobaki watawarithi. 10 Mambo hayo yatawapata kwa sababu ya kiburi chao, kwa kuwa wamewatukana watu wa Bwana wa majeshi, na kujitukuza juu yao.

 

Maeneo haya yatabidi kufanywa upya na kiburi cha Amoni na Moabu kitawashusha chini na kuwafanya duni.

 

Hazitakuwa na rutuba kama zilivyokuwa hapo zamani wakati Lutu alipokaa hapo kwanza maeneo hayo. Bado unabii unaonekana kulenga moja kwa moja kwenye uwezekano wa kuangamizwa kwa miungu ya dunia hii ili kuzinufaisha nchi hizi.

 

11 Bwana atakuwa mwenye kuwatisha sana; kwa maana atawafisha kwa njaa miungu yote ya dunia; na watu watamsujudia yeye, kila mtu toka mahali pake; naam, nchi zote za mataifa.

 

Anayetajwa hapa kuwa “Yeye” ni Masihi akiwa ni Kuhani Mkuu wa Mungu Mmoja wa Kweli na ambaye ataitiisha dunia na kuitawala sawasawa na unabii wa Sefania 14:16-19 wakati watakapowatuma wajumbe ambao ni wawakilishi wao kwenda Yerusalemu kila mwaka kwenye Sikukuu ya Vibanda.

 

Andiko kwa hiyo linageukia Kusini kwa Waethiopia na kisha Kaskazini kwa Waashuru. Hii ni kwenye Vita vya Siku za Mwisho tunajua kwamba Waashuru wanatokea Kaskazini, mkono kwa mkono na Waisraeli na Waethiopia wanatawaliwa wakati wa Siku za Mwisho kwa sambamba na Mfalme wa Kaskazini kama walivyo wakazi wa Afrika Kaskazini kutoka Libya magharibi na kisha kutawaliwa na Masihi.

 

12 Na ninyi Wakushi pia, mtauawa kwa upanga wangu. 13 Naye atanyosha mkono wake juu ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza Ashuru; naye ataufanya Ninawi kuwa ukiwa, kuwa mahali pakavu kama jangwa. 14 Na makundi ya wanyama watalala kati yake, wanyama wote wa mataifa; mwari-nyuni na nungu watakaa juu ya vichwa vya nguzo zake; sauti yao itasikiwa madirishani; vizingitini mwake mtakuwa ukiwa; kwa maana ameifunua kazi ya mierezi.

 

Tunaona Ninawi iliangamia lakini hii sio nabii zote unaihusu Ashuru. Ni vitovu vyao vya ibada za sanamu ndizo zitaangamizwa.


15 Huu ndio mji ule wa furaha, Uliokaa pasipo kufikiri, Uliosema moyoni mwake, Mimi niko, Wala hapana mwingine ila mimi. Jinsi ulivyokuwa ukiwa, Mahali pa kulala pa wanyama wa bara! Kila mtu apitaye atazomea, Na kutikisa mkono wake.

 

Ni sahihi kwamba Ninawi iliangamia mwaka 612 KK na kumbukumbu zinaweza kuelekeza kwenye ukaaji wa mwanzoni wa Ethiopia lakini unabii kuhusu Siku za Mwisho uko wazi. Wakati Mungu akiungamiza Ninawi ndipo atawarejesha kutoka kaskazini katika Siku za Mwisho na kuwafanya tena kuwa sehemu ya ushirika wa biashara wa sitini na Israeli na Misri. Mungu anasema kuwa atawarudisha tena Yuda na Efraimu na Israeli wote kutoka Misri na kutoka Ashuru kutoka kaskazini na kuwafanya wawe taifa tena (Zekaria 10:10-11) na watabarikiwa kama washirika wa kibiashara kwenye utawala utakaoongozwa na Masihi watakapokuwa waneunganishwa na njia kuu kutoka Misri hadi Ashuru; na Israeli itakuwa mshirika wa tatu wa ushirikiano huu na baraka za nchi ambayo Bwana wa Majeshi atawabariki akisema, “Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru, watakuwa baraka kati ya dunia;”(Isaya 19:23-25).

 

Mungu kwa hiyo anaushughulikia Yerusalemu kwenye kifungu hiki cha mwisho.yerusalemu umelaumiwa. Dini ya kiyahudi haikubali wala kupokea maonyo yoyote kwa kipindi chote cha miaka 2000 tangu Masihi hadi kuja kwake na maonyo ya mwisho. Unakaribia sasa kupata ijara yake lakini kwa masharti yanayowekea ukomo mataifa kwa kile yanachoweza kufanya. Makuhani wa Yuda na Walawi wameihalifu na kuitia unajisi Kalenda na Agano na wamejiwekea baraza la Talmud na kujitungia sheria zisemazo mambo ambayo haisemi na wamezipotosha na kuigeuza sheroa.

 

Sefania Sura ya 3

Ole wake yeye aliyeasi na kutiwa unajisi, mji wa udhalimu! 2 Hakuitii sauti; hakukubali kurudiwa; hakumwamini Bwana; hakumkaribia Mungu wake. 3 Wakuu wake walio ndani yake ni simba wangurumao; makadhi wake ni mbwa-mwitu wa jioni; hawasazi kitu cho chote hata siku ya pili. 4 Manabii wake ni watu hafifu, wadanganyifu; makuhani wake wamepatia unajisi patakatifu, wameifanyia sheria udhalimu.

 

Hapa Mungu anafananisha matendo yake na hali ya wafalme wake, makuhani na manabii wake na hali zao za kupenda.


5 Bwana kati yake ni mwenye haki; hatatenda uovu; kila asubuhi hudhihirisha hukumu yake, wala hakomi; bali mtu asiye haki hajui kuona haya. 6 Nimekatilia mbali mataifa, buruji zao zina ukiwa; nimeziharibu njia kuu zao, hata hapana mmoja apitaye; miji yao imeangamizwa; hamna mtu hata mmoja, wala hapana akaaye huko.

 

 

Ndipo anawasihi kwamba watubu hakika lakini hawakutubu.

 

7 Nalisema, Hakika utaniogopa, utakubali kurudiwa; ili yasikatiliwe mbali makao yake, sawasawa ya yote niliyoagiza katika habari zake; lakini waliondoka mapema na kuyaharibu matendo yao yote.

 

Andiko hili hatimaye linaonyesha kwamba atainuka katika siku za mwisho na kushughulika na mataifa yote na kwa hiyo hatuna mashaka kwamba andiko hili linamtaja Masihi. Hivi ni Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu vilivyoandikwa kwenye kitabu cha Ufunuo.

 

8 Basi ningojeni, asema Bwana, hata siku ile nitakapoondoka kuteka mateka; maana nimeazimia kuwakusanya mataifa, ili nizikutanishe falme, nipate kuwamwagia ghadhabu yangu; naam, ukali wote wa hasira yangu; kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa wivu wangu.

 

Kisha Mungu atazibadili lugha za mataifa na kuwa ndimi safi zisemazo kweli na kisha atawashughulikia mataifa.

 

9 Maana hapo ndipo nitakapowarudishia mataifa lugha iliyo safi, wapate kuliitia jina la Bwana, wamtumikie kwa nia moja.

 

Tunaona hapa kwenye andiko hili kwamba atayarudia yale aliyoyasema kwenye sura zilizopita kuhusu Waethiopia na kwa wale wote wanaomrudia yeye kutoka nchi zilizo mbali na mipaka ya Ethiopia na Afrika yote na mbele ya mipaka yake.

 

10 Maana toka nchi iliyo mbali na mito ya Kushi, waniombao dua, yaani, binti za watu wangu waliotawanyika, wataleta matoleo yangu. 11 Siku ile hutatahayarikia matendo yako yote uliyoniasi; maana hapo nitawaondoa watu wako wanaotakabari na kujivuna, wasiwe kati yako, wala hutatakabari tena katika mlima wangu mtakatifu. 12 Lakini nitasaza ndani yako watu walioonewa na maskini, nao watalitumainia jina la Bwana. 13 Mabaki ya Israeli hawatatenda uovu, wala kusema uongo; wala ulimi wa hadaa hautaonekana kinywani mwao; kwa maana watakula na kulala, wala hapana mtu atakayewaogofya. 14 Imba, Ee binti Sayuni; piga kelele, Ee Israeli; Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote, Ee binti Yerusalemu. 15 Bwana ameziondoa hukumu zako, Amemtupa nje adui yako; Mfalme wa Israeli, naam, yeye Bwana, yu katikati yako; Hutaogopa uovu tena. 16 Katika siku ile Yerusalemu utaambiwa, Usiogope, Ee Sayuni; mikono yako isilegee. 17 Bwana, Mungu wako, yu katikati yako shujaa awezaye kuokoa; Atakushangilia kwa furaha kuu, Atakutuliza katika upendo wake, Atakufurahia kwa kuimba. 18 Nitawakusanya wanaousikitikia mkutano wa ibada, hao waliokuwa wa kwako; ambao mzigo uliokuwa juu yake ulikuwa fedheha kwao. 19 Tazama, wakati huo nitawapatiliza watu wote wanaokutesa; nami nitamponya yeye achechemeaye, nami nitamkusanya yeye aliyefukuzwa; nami nitawafanya kuwa sifa na jina, hao ambao fedheha yao ilikuwa katika dunia yote. 20 Wakati huo nitawaingizeni, na wakati huo nitawakusanya; kwa maana nitawafanya ninyi kuwa sifa na jina, miongoni mwa watu wote wa dunia, nitakapowarudisha wafungwa wenu mbele ya macho yenu, asema Bwana.

 

Ni kwa wakati huu ambapo Mungu, kwa kupitia Masihi na wateule, watamkusanyikia yeye aliye mwaminifu na na kuongea naye maneno mazuri kwa lugha mpya kwamba amewaondolea maafa na aibu yao. Kwenye andiko hili tunauona unabii kwenye Isaya 65:17-25 ambapo Mungu anaahidi kuzifana mbingu mpya na nchi mpya kwakuwa zitakuwa zimeharibika kwa hali yake yenyewe ya hewa na mazingira na ndivyo itakuwa hata kwa dunia yote na bahari zake zote.

 

                              q