Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[021H]
Ufafanuzi
wa Kitabu cha Habakuki
(Toleo La 1.0 201401107-20141107)
Nabii Habakuki aliishi katika kipindi cha zama za
uovu na anamlalamikia Bwana kuhusu hali hii na anaambiwa kuwa Yuda watapelekwa
utumwani Babeli kwa Wakaldayo ambao watachukua nafasi ya utawala wa dunia ya
Waashuru (sawa kama inavyosema Zaburi 73).
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati
Miliki © 2014 Wade
Cox)
(tr.
2015)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ufafanuzi
wa Kitabu cha Habakuki
Utangulizi
Habakuki huenda
alikuwa ni mtu aliyekuwa akiimba Kwaya Hekaluni na kwa hiyo alikuwa ni wa jamii
ya Walawi (sawa na 1:1 na 3:1,19). Neno la karibu sana kwa jina lake la Kiebrania
ni neno chabak maana yake kukumbatia na mapokeo ya marabi yanadai kuwa
alikuwa ni mtoto wa kiume wa Yule mwnamke Mshunami ambaye nabii Eliya alimponya
na akarejesha uhai wake (2Wafalme 4:16). Jina lake linahusiana pia na neno la Kiashuru la hambakuku ambalo ni ua lakini neno chabak ndilo lililokubalika na baraza la marabi. Jina lake
linawezekana kabisa kuwa limekubalika au kukumbatiwa kwa kuwa alikuwa ametumiwa
kama nabii aliyeshughulikia muungano wa Israeli na Yuda ulioanza katika Nyakati
hizi za Mwisho kama tutakavyoona hapo chini.
Kwa ujumla
inaaminika kuwa alikimbilia Misri kwenye kipindi cha mpitoe kilichofuatiwa mwaka 586 KK akarudi baada ya kuondolewa kwa
Wakaldayo. Inasemekana kuwa kaburi lake lipo huko Keila, maili 18 Kusini
Mashariki mwa Yerusalemu.
Inaonekana kuwa
alitabiri mda mfupi baada ya kugunduliwa kwa gombo la Torati Hekaluni wakati wa
utawala wa Yosia mnamo mwaka 621 KK. Matengenezo ya urejesho ya Yosia yalidum
kipindi kifupi na chini ya Yehoyakimu watu walianza kuabudu na kuzitumikia
sanamu tena na ukengeufu ulifanyika kwa kiwango kikubwa sana na kwa kasi kubwa
mno. Mfalme aliyageuza matendo yake maovu kwa ukatili mkubwa a vitisho na
hatimaye akajikuta akiwa kwenye kongwa la utumwa wa Nebukadneza (sawa na ilivyo
kwenye 2Wafalme 14:1).
Ufafanuzi wa Seder Olam unafundisha kuwa Yoeli, Nahumu
na Habakuki wote walitabiri katika siku za Manase (sawa na usemavyo utangulizi
wa kamusi ya Soncino ukurasa wa 211). Kwamba mfalme alikuwa movu sana ikidaiwa
kuwa waliacha kuliandika jina lake kwenye vitabu vyao. Uwezekano mkubwa sana ni
kwamba huenda mchakato huu ulianza baada ya mwaka 621 na inaanza kwa kuinuka
kwa Wakaldayo. Wengine hudhani kuwa huenda ilikuwa ni katikati ya Vita ya
Karkemishi ya mwaka 605 KK na kipindi cha kuhusuriwa kwa Hekalu mwaka 586 KK; tuseme
ni takriban mwaka 600 KK wakati wa utawala wa Yehoyakimu.
Hata hivyo, kuna
mambo mengi sana yanayojiri kuyaelezea kuhusu unabii huu kuliko ilivyoelezewa
au kufafanuliwa na mamlaka ya marabi. Kikomo au zuio lao la kuiweka Kaekemishi
laweza kuwa ni zuio au kikwazo cha kiunabii kama tunavyoona kutokana na uvamizi
na utekaji maeneo haya uliofanywa na Nebopolasa, mfalme wa 1 wa kizazi cha
Wakaldayo na Wamedi.
Mpangilio wa
Kitabu ni kama hivi:
Kuna aya takriban 56 zilizogawanyika kwenye sura tatu ambayo kinyume chake yanaangukia kwenye migawanyo sita, zaidi kuliko ya mipangilio minne ya kimuundo iliyo hapo juu.
Migawanyo yenyewe ilikuwa hivi:
1:2-4 ambapo nabii anamlalamikia Mungu kwa kuwaacha au kuruhusu watu wasio na hatia wateseke na watu waovu wafanikiwe.
1:5-11 ni jibu la Mungu, akisema kuwa ilikuwa ni lazima hasira yake kali imwagwe na kuwafanya hivyo.
1:12-17 inaonekana kuwa nabii anaiiuliza na kuionea mashaka hukumu kwa kuwa ni hakika Mungu hawezi kulachia taifa lipatilizwe kwa kuchukuliwa lote na taifa ambalo ni ovu zaidi kuliko wao.
Habakuki Sura ya 1
Ufunuo aliouona nabii
Habakuki. 2 Ee Bwana, nilie hata lini, wewe usitake
kusikia? Nakulilia kwa sababu ya udhalimu, ila hutaki kuokoa. 3 Mbona wanionyesha uovu, na kunitazamisha ukaidi? Maana
uharibifu na udhalimu u mbele yangu; kuna ugomvi, na mashindano yatokea. 4 Kwa sababu hiyo sheria imelegea, wala hukumu haipatikani;
kwa maana watu wabaya huwazunguka wenye haki; kwa sababu hiyo hukumu
ikipatikana imepotoka.
Mungu anamjibu Habakuki. Anasema kuwa anawaamsha Wakaldayo, na ndivyo
aivyofanya kwa kumtumia Nabpolasa na alisaidiwa na Wamedi wenye harakati zao za
kuwaasi Waashuru kwa upande wa Mashariki na Kaskazini.
5 Angalieni,
enyi mlio kati ya mataifa, katazameni, kastaajabuni sana; kwa maana mimi
natenda tendo siku zenu, ambalo hamtaliamini hata mkiambiwa. 6 Kwa
maana, angalieni, nawaondokesha Wakaldayo, taifa lile kali, lenye haraka kupita
kiasi; wapitao katikati ya dunia, ili wayamiliki makao yasiyo yao. 7 Hao
ni watu wa kutisha sana, wa kuogofya sana; hukumu yao na ukuu wao hutoka katika
nafsi zao wenyewe. 8 Farasi
zao ni wepesi kuliko chui, ni wakali kuliko mbwa-mwitu wa jioni; na wapanda farasi
wao hujitapa naam, wapanda farasi wao watoka mbali sana; huruka kama tai
afanyaye haraka ale. 9 Waja
wote ili kufanya udhalimu; nyuso zao zimeelekezwa kwa bidii yao kama upepo wa
mashariki, nao hukusanya mateka kama mchanga. 10 Naam, huwadhihaki wafalme,
na wakuu ni kitu cha kudharauliwa kwake; huidharau kila ngome; kwa maana
hufanya chungu ya mavumbi, na kuitwaa. 11 Kisha atapita kwa kasi, kama
upepo, atapita na kuwa ana hatia; yeye ambaye nguvu zake ni mungu wake.
Habakuki anajua kwamba Mungu amewaamuru au kuwatuma wao kama ni hukumu
dhidi ya Yuda. Hata hivyo anamlaumu Mungu kwa kunyamaza kwake kimya wakati
wanakabiliwa na watu waovu.
12 Ee
Bwana, Mungu wangu, mtakatifu wangu, wewe si wa milele? Hatutakufa. Ee Bwana,
umemwandikia hukumu, nawe, Ee Jabali, umemweka imara ili aadhibishwe. 13 Wewe
uliye na macho safi hata usiweze kuangalia uovu, wewe usiyeweza kutazama
ukaidi, mbona unawaangalia watendao kwa hila; na kunyamaza kimya, hapo mtu
mwovu ammezapo mtu aliye mwenye haki kuliko yeye; 14 na kufanya wanadamu kuwa
kama samaki wa baharini, kama vitu vitambaavyo, ambavyo havina mtawala? 15 Yeye
huwatoa wote kwa ndoana yake, huwakamata katika wavu wake, na kuwakusanya
katika juya lake; ndiyo sababu afurahi na kupendezwa. 16 Kwa
sababu hiyo huutolea wavu wake sadaka, na kulifukizia uvumba juya lake; kwa
sababu kwa vitu vile fungu lake limenona, na chakula chake kimekuwa tele. 17 Je!
Atawatoa walio katika wavu wake, asiache kuwaua watu wa mataifa daima?
Anajiuliza kuhusu kitendo cha Wakaldayo kuwapora watu na jinsi inavyoonekana
kuwa ni kama wana haki zaidi kulikowao na kisha anauliza iwapo kama wataendelea
kuwa watu wasio na huruma na wataendelea kuwaua watu kikatili vile kuyatenedea mataifa
mengine milele. Na sasa Danieli alidhihirisha kwamba Wakaldayo walikuwa wanakwenda
kuanza kuanzisha usimamizi wa mamlaka ya kidola ya kuitawala dunia na ambayo
itakwenda kudumu kwa kipindi cha nyakati saba juu ya dola yote ya Wababeloni, Wamedi
na Waajemi, Wayunani, iliyojulikana kama Dola Takatifu ya Rumi na dola ya Vidole
Kumi yenye mchanganyiko wa Chuma na Udongo ambayo itaishia kwenye Nyakati za
Mwisho kwa ujio wa Masihi, ambaye ataiangusha na kuikomesha kwa kuipiga
vidoleni na kuikomesha kabsa. Mchakato huu umewekwa kama unabii kwa kuinuka kwa
utawala na dola ya Wakaldayo kabla ya Karkemishi mwaka 605 KK utawala wa Nebukadneza.
Sura ya 2:1-5 inaonyesha
nabii akiwa kwenye hali ya pweke kuendelea na jibu la masali yake.
Kwenye aya ya 4 Mungu
anatoa ujumbe wa maalumu na muhimu wa kimaandiko ambao ni kwamba mwenye haki ataishi
kwa imani. Hivyo basi Mungu anaweza kuamua kumuweka mteule wake katikati ya
wapagani ili amuendeleze na kumkuza kiimani na kuuondoa uovu katikati yao.
Waovu na wakatili hawataweza kuendelea kabisa na hawatawashinda wateule.
Kumbuka kuwa ilipasa yaandikwe maono kwa kuwa ilikuwa bado haujafika wakati
au majira yaliyokusudiwa ingawaje Wakaldayo walikuwa wanaendelea mble za
Wakalkemishi.
Habakuki Sura ya 2
Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu
ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika
habari ya kulalamika kwangu. 2 Bwana akanijibu,
akasema, Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao, ili aisomaye apate
kuisoma kama maji. 3 Maana njozi hii bado ni kwa
wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema
uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia. 4 Tazama, roho yake hujivuna, haina unyofu ndani yake;
lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake. 5 Naam,
pamoja na hayo, divai ni mchumi mdanganyifu, mtu wa kiburi asiyekaa nyumbani
mwake; huongeza tamaa yake kama kuzimu, naye huwa kama mauti, hawezi
kushibishwa; bali hujikusanyia mataifa yote; hujiwekea kabila zote chungu
chungu.
Falme au dola hizi
zitaundwa na watu wote ulimwenguni na zitadumu kwa kitambo. Kwenye kitabu cha
Danieli tunaona kukitajwa Nyakati Saba au miaka 2520.
Kwenye 2:6-20 tunawaona
waathirika wakiwadhihaki watesi wao kwa mlolongo wa matukio ya ole. Mwisho wa utekaji
wao na udhalim wao unatoa fundisho kwa ulimwengu wote kushuhudia. Ni fundisho
kuu dhidi ya mfumo na imani ya Wababeloni kwa jinsi ilivyokuwa hadi kuanguka
kwake katika Nyakati za Mwisho na sio kuwa ni fundisho au somo tu kwa
Nebukadneza aliyeashiriwa kwa Kichwa cha Dhahabu kwenye Danieli sura ya 2 lakini
dhidi ya yote yatupasayo kujifunza kwenye Nyakati hizi za Mwisho na ujio wa
Masihi.
6 Je! Hawa wote hawatapiga
mfano juu yake, na mithali ya kusimanga juu yake, wakisema, Ole wake yeye
aongezaye kisicho mali yake! Hata lini? Na ole wake yeye ajitwikaye mzigo wa
rehani! 7 Je! Hawatainuka ghafula wao watakaokuuma,
hawataamka wao watakaokusumbua, nawe utakuwa mateka kwao? 8 Kwa
sababu umeteka nyara mataifa mengi, mabaki yote ya kabila watakuteka wewe; kwa
sababu ya damu ya watu, na kwa sababu ya udhalimu iliotendwa nchi hii, na mji
huu, na watu wote wanaokaa ndani yake. 9 Ole wake yeye
aipatiaye nyumba yake mapato mabaya, ili apate kukiweka kioto chake juu, apate
kujiepusha na mkono wa uovu! 10 Wewe umeifanyia nyumba
yako kusudi la aibu, kwa kukatilia mbali watu wengi, nawe umetenda dhambi juu
ya roho yako. 11 Kwa maana jiwe litapiga kelele katika
ukuta, nayo boriti katika miti italijibu. 12 Ole wake
yeye ajengaye mji kwa damu, awekaye imara mji mkubwa kwa uovu! 13 Angalieni; je! Jambo hili halikutoka kwa Bwana wa
majeshi, kwamba watu wajishughulikie moto, na mataifa wajisumbue kwa ajili ya
ubatili? 14 Kwa maana dunia itajazwa maarifa ya
utukufu wa Bwana, kama maji yaifunikavyo bahari. 15 Ole
wake yeye ampaye jirani yake kileo, wewe utiaye sumu yako, na kumlevya pia, ili
kuutazama uchi wao! 16 Umejaa aibu badala ya utukufu;
unywe nawe, uwe kama mtu asiyetahiriwa; kikombe cha mkono wa kuume wa Bwana
kitageuzwa ukipokee, na aibu kuu itakuwa juu ya utukufu wako. 17 Kwa maana udhalimu uliotendwa juu ya Lebanoni
utakufunikiza, na kuangamizwa kwao wanyama kutakutia hofu; kwa sababu ya damu
ya watu, na kwa sababu ya udhalimu iliotendwa nchi hii, na mji huu, na watu
wote wanaokaa ndani yake. 18 Sanamu ya kuchora yafaa
nini, hata yeye aliyeifanya ameichora? Sanamu ya kuyeyuka, nayo ni mwalimu wa
uongo, yafaa nini, hata yeye aliyeifanya aiwekee tumaini lake, na kufanya
sanamu zisizoweza kusema? 19 Ole wake yeye auambiaye
mti, Amka; aliambiaye jiwe lisiloweza kusema, Ondoka! Je! Kitu hicho
kitafundisha? Tazama, kimefunikwa kwa dhahabu na fedha, wala hamna pumzi ndani
yake kabisa. 20 Lakini Bwana yumo ndani ya hekalu lake
takatifu; dunia yote na inyamaze kimya mbele zake.
Imani yote ya
mchanganyiko wa dini za Waashuru na Wababeloni ilienea duniani na dini za Siri
na Fumbo za waabudu Juan a ibada zao za sanamu za Mungumke; lakini ulimwengu umeonywa
kubakia kimya mbele za Mungu na Hekalu lake Takatifu. Waliukata na kuuchonga
mwerezi wa Lebanoni na kwa hiyo Mungu anawatia hatiani na watahukumiwa katika
siku za mwisho z dini hizi hadi kufikia mwishoni.
Kwenye 3:2-19 nabii
anaomba na tena anamsihi Mungu aingilie kati kwa niaba ya watu wake. Habakuki
analinganisha staili ya maombi yake na ile ya Yeremia na Ezekieli ambaye
analaumu na kukemea dhambi za watu watu wake na kuendeleza unabii unaoendelea
wa kipindi cha Nyakati za Mwisho za Mataifa na kuanguka kwa Misri kwenye Nyakati
za Mwisho. Yeremia anatupeleka kwenye Nyakati za Mwisho na Maonyo ya Manabii wa
Mwisho (kwenye Yeremia 4:15). Andiko hili linashughulika na dhambi za dini ya
Kibabeloni na ujio wa Mtu wa Dhifa ya Kifalme wa Mungu ili kuuharibu na
kuuangamiza mfmo wa kidini za watenda dhambi za ulimwengu.
Aya za 16-19 zinaonyesha
kujiamini kikamilifu ambayo ni mwenendo wa kimwili wa Waisraeli na sio tu peke
yao kuwa ndiyo wataokolewa na kuanzisha tena.
Maktaba ya ode kwenye
sura hizi za mwisho zinashangaza kwa wataalamu wao wengi wa lugha ya Kiebrania
na wengine kama mwanazuoni mashuhuri Driver anavyotilia maanani hilo kuwa ni
kama shairi au utenzi mzuri sana wa Kiebrania uliotungwa. Tafsiri ya Soncino inathibitisha
pia na kufafanua kwa kumnukuu Driver.
Habakuki Sura ya 3
Sala ya nabii Habakuki nabii kwa Mjibu wa
Shigionothi.
Shigionothi (sawa
na Zaburi 8). Inalinganshwa na ‘shairi au utenzi wa kimtetemo wenye upeo wa
vilio vya mtu anayetangatangaji nyikani’ (sawa na alivyoandika Soncino).
2 Ee Bwana, nimesikia habari
zako, nami naogopa; Ee Bwana, fufua kazi yako katikati ya miaka; Katikati ya
miaka tangaza habari yake; Katika ghadhabu kumbuka rehema. 3 Mungu
alikuja kutoka Temani, Yeye aliye mtakatifu kutoka mlima Parani. Utukufu wake
ukazifunika mbingu, Nayo dunia ikajaa sifa yake.
Teman ni mji ulio
Kaskazini Magharibi ya Edomu na Parani ni magharibi mwa Edomu katikati ya
Peninsula ya Sinai na na Kadeshi-Barnea. Ni kaskazini mwa bandari ya Aqaba kufuatia
upande wa pwani. Huu ni msafara au njia ambayo majeshi ya Jumuia ya Madola aliufuata
kwenye mkakati wao wa kuikomboa Israeli na mji wa Yerusalemu mwaka 1917 na
kufanikiwa kuuteka tena mji wa Yerusalemu hapo siku ya 25 Kisleu 1917 kwa
mujibu wa Kalenda ya Hekaluni, tukio lililohusiana sambamba na kushambuliwa kwa
Waaustralia, baada ya kuitwaa Beersheba (soma pia jarida la Maonyo ya Mungu (Na. 184)). Hii ilianzisha mkakati wa kuirejesha na kuifanya
upya Israeli katika Nyakati za Mwisho tngu mwaka mtakatifu wa 1916/17 hadi
2027. Kutokana na mchakato huu, ndio Masihi atakuja akitokea Mlima wa Mizeituni
tangia kipindi cha mwaka wa 2018/19 ili kuikamilisha kazi.
Hii ilikuwa ni
mara saba kutoka kwenye Vita vya Karkemishi vya mwaka 605 KK vilivyoishia
katika mwaka wa 1916/17; miaka 2520 baada ya vita hivyo na mwanzo wa nyakati za
mwisho za kipindi cha miaka arobaini arobaini kilichonenwa kwenye unabii wa Ezekieli,
kama ulivyochambuliwa kwenye jarida la Anguko la Misri; Mikono Iliyovunjia ya
Farao (Na. 036) kuanza. Hivi vilikuwa ni
Vita vya Nyakati za Mwisho kama tunavyoviona kwenye jarida la Anguko la Misri Sehemu ya II: Vita vya Mwisho (Na. 036_2).
Muungano wa mataifa ya Anglo-Arabu ulianzishwa katika mwaka mtakatifu wa
1916/17.
Mnamo Januari 24, baada ya siku moja ya vita, jeshi la muungano wa Anglo-Arabu
liliutwaa mji wa bandari wa Wejh, ambao ulifanyika kuwa kituo muhimu cha usafirishaji
na cha kimikakati kwa Waarabu. Na kwa karidi Waarabu walivyokuwa wanakusanyika
na kungana, ndipo Jenerali wa Kiingereza aliyejulikana kwa jina la Sir
Archibald Murray aligundua kuwa Waarabu walihitajika kumpa msaada kwa ajili ya
mkakati wake wa huko Sinai wa kuikomboa Rasi ya Suezi na kuwasukuma wanamgambo
wa Ottoman watoke nje ya maeneo ya Gaza. Kazi waliyotakiwa kuifanya Waarabu
ilikuwa ni kuyafungia majeshi ya Fakhri na kuhakikisha yasitoke huko Madina na
kuitwaa na kuifunga Reli ya Hejaz. Hii ilianzisha kutimia kwa unabii wa
Habakuki kwa kuanza kuwakomboa Watoro au Walevanti na kufanya mwisho wa utawala
wa Ottoman. Ilianzia kutoka kusini kama Mungu alivyosema kuwa itafanyika,
kuanzia huko Parani, ambavyo ni kutoka Sinai hadi Kadeshi Barnea na sambamba na
wani ya Aqaba Magharibi ya Edomu na kupitia Temani ambako ni Kaskazini
Magharibi ya Edomu kuelekea Yordani na kulikuwa na maji ya kutosha. Ni njiapanda
ya barabara muhimu iliyotumiwa kwa misafara ya wafanya biashara kwa zama zote
mbili, yaani za kale na za sasa.
Hivyo, Waarabu walijikita kwenye mkakati wa “kuishambulia njia ya reli” kwa
kipindi chote cha mwaka 1917.
Kiongozi wa uasi alibakia kuwa na mtazamo wake mhimu wa kimkakati
ulioonekana kuwa muhimu na tishio; akiendelea kusongambele upande wa kaskazini
na akijipatia kuungwa mkono na ushirikiano na kuwa na ushawishi na makabila na viongozi
wa huko Syria na eneo lote za Mesopotamia. Hali hii, hata hivyo, ililazimu kuwa
na bandari nyingine pya inayomudu kazi. Wakati wakiwa ana dalili ya homa ya ugonjwa
wa kipindupindu, ndipo T. E. Lawrence alianza hila za kuiteka bandari iliyokuwa
kwenye Bahari ya Shamu ya Aqaba, ambayo kwa siku hizi ni sehemu ya Yordani. Aliakataa
au kuacha kuishambulia kutoka majini, wakati Aqaba ilikuwa inalindwa kwa
bunduki kali na nzito. Zaidi sana, mpango wake wa kijasiri uoliwataka askari
kujimega kutoka kwenye Jangwa la Nefudh, ambavyo majeshi ya Ottoman hawakuwa
wametarajia. Sehem mhim ya Lawrence na mashujaa 17 wa Agayl waliondoka kutoka Wejh
mnamo tarehe 10 Mei, 1917 (kutoka Kipindi cha Pasaka ya Pili). Watu walikuwa na
takriban pesa ya Kiingereza, £20,000 iliyotumiwa kuwaingiza jeshini watu wa
jamii ya makabila mapya na, walipokuwa wanaendelea kufanya hivyo, idadi yao
iliongezeka hadi kufikia idadi ya wapiganaji 700. Kiongozi wa idadi ya Waarabu hawa
wa makabila mapya alikuwa ni Auda Abu Tayi chifu wa jami ya Howeitat ambaye
alikubali kujiunga na Jenerali Lawrence kwenye mapigano ya mashambulizi.
Msafara wa umbali wa urefu wa maili 600 ulipitia mazingira ya magumu na
ya ulichukiwa sana kusiko na kuonyeshwa ukarimu wowote kabisa, hata jamii ya Bedouin
(Wabedui) waliuita al-Houl (yaani msafara wa Magaidi). Mwandishi wa historian ya
matukio na maisha wa Lawrence aliyeitwa Michael Asher aliuita mkakati huu kuwa
ni “moja kati ya majaribio magumu na ya hatari sana kuliko ya mashambulizi
kuwahi kujaribiwa kwenye midani ya vita.” Waarabu walifanya mashambulizi yao
kutoka upande wa kaskazini magharibi, waliyafegiliambali kwa kuyakimbiza na
kuyateka majeshi ya Ottoman kwa kuvipoteza vikosi viwili tu vya makabila mnamo
tarehe 5 Julai. Siku iliyofuatia, Waarabu ambao sasa walikuwa na jeshi la watu 2,500,
waliingia Aqaba bila kutumia kitisho cha milio ya bunduki, ngome au askari
walinzi ikiwa imekurupushiliwa mbali. Gaunt, akiwa amechafuka sana, na akiwa
amevaa kazu ya utamaduni wa jamii ya Bedouin, Lawrence aliivuka Sinai na kwenda
hadi Cairo kumpasha habari kamanda mkuu mpya wa majeshi wa Waingereza, Jenerali
Edmund Allenby, kuhusu ushindi wake mkubwa. Na kama zawadi, Waarabu walipokea
walipokea malipo mengine ya ziada yenye thamani ya fedha za Kiingereza £16,000,
na Lawrence alipandishwa cheo hadi kuwa Meja jeshini.
Kwa kipindi hicho tangu kuondoka kwa Lawrence kwenda Allenby huko Cairo na
kurudi kwake, Aqaba ulikuwa umejengewa ngome au ukuta au kuzingirwa na majeshi
yaliyodumu kama bataliani yenye silaha nzito zilizojlikanna kama Kikosi cha Ngamia
cha Mfalme (Imperial Camel Corp), lenye silaha kali na nzitonzito na magari
yaliyo na silaha na kinga pamoja na dhahabu. Kundi au Kikosi hiki cha Ngamia na
Waarabu walimsaidia kwenye harakati hizi tangu kutwaliwa kwa Aqaba hadi
kuendelea kwao kwa kusonga mbele hadi kwenye Bonde la Yordani hadi Damascus ili
kuulinda ubavu ya upande wa kulia wa Allenby.
Allenby wakaamuru majeshi ya Muungano wa Madola yaende huko Sinai na
kile kilichojulikana kama Farasi Mwepesi wa Kiaustralia, [yaani, the Australian
Light Horse] ilikamatwa huko Beersheba na kisha Waaustralia waliendelea mbele
na kuutwaa mji wa Yerusalemu mnamo tarehe 7 Desemba 1917. Hivyo unabii wa Habakuki
wa kurejesha tena himaya ya Levant kutoka Temani na Parani ulitimilika kwa
kipindi cha zaidi ya Nyakati Saba au miaka 2520 tangia Vita ya Karkemishi na
kukaliwa kwa Wakaldayo kujumlisha na mwaka mmoja kuanzia mwaka 1916 na kuitwaa
Yerusalem hapo Desemba 1917. Lawrence aliingia Yerusalemu akiwa na Allenby na
kisha Majeshi ya Muungano yaliendelea mbele na kukabiliana na vikosi vya ulinzi
vya Ottoman na Wajerumani vilivyokuwa vimeweka kambi zao karibu na Galilaya.
Matukio yenye yalikuwa kama ifuatavyo.
Vita vya Beersheba |
31 Oktoba hadi
tarehe 1 Novemba |
Tel el Khuweilfe |
8 Novemba |
Ahueni au ushindi
ulipatikana (Sinai na Palestina 4-8
Novemba) |
6-11 Novemba |
Tukio Kubwa la
Kuwasukuma Maadui lilifanyika |
8-15 Novemba |
Uwanda wa Bahari ulisafishwa |
11-17 Novemba |
Mafanikio zaidi ya
Yerusalemu |
16-24 Novemba |
Nahr Auja na El
Buij |
24 Novemba hadi 1
Desemba |
Mashambulizi ya
mwisho ya kuutwaa Yerusalemu |
7 Desemba |
Shambulio la mwisho lilifanywa na majeshi ya
Muungano tarehe 7 Desemba 1917. Kwa mujibu wa taarifa za kweli za Mwandamo wa
Mwezi Mpya, hii ni tarehe kamili na ni siku ya 24 Kiisleu (kalenda ya Hilleli ilianza
mwezi mpya siku mbili baadae). Waturuki na Wajerumani walianza harakati za
kuondoka haraka na mnamo yarehe 8 Desemba 1917 Yerusalemu ulitwaliwa. Wachanga
au wasioelewa vizuri walichinba kiundani na kujikita na ilipotimu tarehe 10 Desemba,
Farasi Mwepesi alikimbia au alikimbia kuelekea barabara ya kuelekea Nablus, umbali
wa takriban maili nane. Walichukua silaha nzito nzito za Waturuki na za moto.
Walizishikilia wakielekea upande wa kusini mwishoni mwa Bonde la Yordani na walikuwa
wanajaribu kuyazuia majeshi ya Muungano yasiukatishe mto na kwenda hadi
kuifikia reli ya Hejaz na hivyo kuzuia utendaji kazi wa Allenby kwa ubavu wa
upande wa kulia.
Allenby aliingia rasmi mjini Yerusalemu
tarehe 11 Disemba 1917, siku ya 28 ya mwezi Kisleu.
Majeshi ya Muungano yalielekea na kuingia
Lebanoni na Syria na Feisal aliingia Damascus. Mkataba au makubaliano ya
muafaka wa Sikes/Picot kati ya Waingereza na Wafaransa yaliwagawa Levant pamoja
na Suez, Palestina na Mesopotamia ambao walipewa Waingereza na Lebanoni na
Syria ikatolewa kwa Wafaransa. Hii hata hivyo ilisababisha kuwepo na kile
kilichojulikana kama Mkataba au Azimio la Balfour Declaration la mwaka 1917 na
Usimamizi au Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 1922 wa undwaji au uanzishaji
wa Taifa la Israeli kwa kipindi kilichofuatia cha miaka thelathini tangu mwisho
wa Vita ya Kwanza ya Dunia hadi mwaka 1948.
Unabii ulio kwenye Hagai 2:1-23 unahusiana na unabii hu wa Habakuki.
Unabii ulio
kwenye Hagai unaithibitisha Kalenda ya Hekaluni inayotokana na Miandamo ya
Mwezi Mpya kwa kuanzia kipindi cha mpito wa kuonekana mwezi mpya na sio kama
ilivyo kwenye kalenda ya Hilleli.
Habakuki na kundi
la walioachwa masalia walikimbilia Misri mwaka wa 586 KK na wakarudi baada ya
kuondoka kwa Wakaldayo. Huu ni mzungko wa mara moja wa utaratibu wa mizunguko
wa miaka 19 kutoka Karkemishi na
kujumlisha mzunguko mmoja kuelekea kwenye mwanzo wa kipindi cha mwisho. Kwa
hiyo, Nyakati Saba au miaka 2520 tangu mwanzo wa kipindi cha miaka themanini na
mwisho au utimilifu wa mashambulizi ya Cambyses mwaka 525 KK yaliyoishia mwaka
1996/7 kwenye mwisho wa Nyakati au Utilimifu wa Mataifa. Kipindi cha miaka 2520
tangu kuangamia kwa Yerusalemu na kuondoka kwa Wakaldayo, yaani kuanzia mwaka 587/6
KK, ni jumlisha miaka 19. Miaka 2520 tangu mwaka 586 ni mwaka 1937. Mnamo
Januari 30 1933 Hitler alichaguliwa kuwa kiongozi mkuu anayejulikana kama chancellor
wa Ujerumani. Miaka ya 1933-36 ilifanya mwanzo wa matatizo na migogoro katika
Yuda na kuinua kwa utawala na itikazi ya Manazi na kusaidiwa kwa
Wapinga-Wasemitiki huko Afrika Kusini tangu wakati ule na kuendelea. Mikakati
ya kuwamaliza na kuwaua Wayahudi ilikuwa inaendelea na hususan kwenye kipindi
cha miaka ya 1941-1945. Vita dhidi ya Yuda katika Mashariki ya Kati vilisaidiwa
na kuungwa mkono tangu kuzuka kwa itikadi ya Manazi na vita vilifuatia mwaka 1948
na ilipelekea kuwepo kwa azimio la kutangazwa taifa la Israeli.
Mwaka 1967 kipindi
maalum cha nyakati za mwisho kilianza kwa vita ya Siku Sita na madai tena
yaliyotolewa ya haki ya kuumiliki Yerusalemu na jamii ya Yuda nchini Israeli.
Miaka arobaini
baada ya kuibuka kwa itikadi ya Manazi na jarubio la kuwafutilia mbali
ulimwenguni kote Wayahudi, mnamo Octoba 1973, vita iliyojulikana kama ya Yom
Kippur ilianza na, ingawa amani na Misri iliwekwa na kuhakikishwa, vita na Syria
iliendelea na usimamishaji wa mapigano ulikubaliwa tu mnamo Mei 1974. Miaka arobaini
baadae katika mwaka 2014, baada ya majira ya Machipuko ya Uarabuni yakiwa
yameanza, eneo lote la Mashariki ya Kati lilikubwa na dhahama na kile
kilichojlikana kama kutangazwa kwa Dola la Kislamu chini ya Khalifa Mpya wakati
wa kikomo na cha matazamio cha miaka arobaini. Vita mbaya na ya kikatili ya
kuangamiza watu ilianza baada ya mwisho wa Pasaka ya Pili kuadhimishwa kwenye
eneo lote la Syria na Mesopotamia. Mataifa haya sasa yanaletwa kwenye magoti
yao kwenye vita vya msuguano na kikatili ambayo haijawahi kuonekana katika
Mashariki ya Kati kwa karne kadhaa zilizopita. Vita hivi vinaendelea pia kwenye
ncha ya Kaskazini na Mashariki na inaonekana pia kuwa vita vya Baragumu la Tano
na la Sita vinachochewa.
Kama kuna vipindi
viwili vingine vya miaka arobaini kutoka kipindi hiki vilivyowekwa kwa
matarajio ya kufanya toba ndipo sisi tunaweza kutarajia Hatua ya kimbinguni
tangu mwaka 2015/16 kwa marejesho mapya na kuiunganisha Mashariki ya Kati
katika Israeli na hukumu ya Wakaldayo na Waarabu. Hata hivyo, mataifa
yanatikisika kwa ujumla kutokana na aya ya 6. Kwa hiyo ndipo tukio linguine la zaidi na la jumla
yabidi litarajiwe.
Vita vinaendelea
mbele kama tunavyoweza kujionea ikitajwa kwenye kitabu cha Ufunuo.
4 Mwangaza wake ulikuwa kama nuru; Alikuwa na mishale
ya nuru ubavuni pake; Ndipo ulipofichwa uweza wake. 5 Mbele
zake ilikwenda tauni, Na makaa ya moto yakatoka miguuni pake. 6 Akasimama, akaitetemesha dunia; Akatazama, akawasitusha
mataifa; Na milima ya zamani ikatawanyika; Vilima vya kale vikainama; Miendo
yake ilikuwa kama siku za kale. 7 Naliziona hema za
Kushani katika taabu; Mapazia ya nchi ya Midiani yakatetemeka. 8 Je! Bwana aliikasirikia mito? Je! Hasira yako ilikuwa juu
ya mito, Au ghadhabu yako juu ya bahari, Hata ukapanda farasi zako, Katika
magari yako ya wokovu? 9 Uta wako ukafanywa wazi
kabisa; Viapo walivyopewa kabila vilikuwa neno thabiti; Ukaipasua nchi kwa
mito. 10 Milima ilikuona, ikaogopa; Gharika ya maji
ikapita; Vilindi vikatoa sauti yake, Vikainua juu mikono yake. 11 Jua na mwezi vikasimama makaoni mwao; Mbele ya nuru ya
mishale yako ilipotapakaa, Mbele ya mwangaza wa mkuki wako umeremetao. 12 Ulikwenda katikati ya nchi kwa ghadhabu; Ukawapura
mataifa kwa hasira. 13 Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa
watu wako, Kwa ajili ya wokovu wa masihi wako; Ukakiponda kichwa cha nyumba ya
waovu, Ukiuweka wazi msingi hata mwambani. 14 Ukakichoma
kichwa cha mashujaa wake kwa fimbo zao wenyewe; Wakaja kama kisulisuli ili
kunitawanya; Kama wakifurahi kuwameza maskini kwa siri. 15 Ukaikanyaga
bahari kwa farasi zako, Chungu ya maji yenye nguvu. 16 Nikasikia,
na tumbo langu likatetemeka, Midomo yangu ikatikisika kwa sauti ile; Ubovu
ukaingia mifupani mwangu, Nikatetemeka katika mahali pangu; Ili nipate kuingoja
ile siku ya dhiki, Kundi lao washambuliao wakweapo juu ya watu. 17 Maana mtini hautachanua maua, Wala mizabibuni hamtakuwa
na matunda; Taabu ya mzeituni itakuwa bure, Na mashamba hayatatoa chakula;
Zizini hamtakuwa na kundi, Wala vibandani hamtakuwa na kundi la ng'ombe; 18 Walakini nitamfurahia Bwana Nitamshangilia Mungu wa
wokovu wangu. 19 YEHOVA, aliye Bwana, ni nguvu zangu,
Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali
pangu palipoinuka.
Huu ni mwisho wa
Nyakati za Mwisho na vita kuu vya mwisho. Ingawaje kuna uharibifu nabii ni kwa
ajili ya marejesho mapya ya watu wa Mungu na kuyatiisha au kuyanyenyekeza mataifa
ya dunia kwa kupitia Vitasa vya Ghadhabu ya Mungu atakaporudi Masihi.
Kumbuka kuwa mito
itatumika kuyaadhibu na kuyatesa mataifa ni kama zitakavyofanya bahari pia. Hii
inaonyesha na kuashiria kuwepo kwa vita kubwa vitakavyotokea kwenye kingo za
mito ya Tigri na Frati sambamba na vita vya Baragumu la Tano na la Sita ya
Ufunuo.
Hasira kali na
mateso hapa ni dhidi ya watu walio Mashariki ya Kati na Waarabu wa Kushani na
Midiani hadi kueleea nchi ya Ugiriki. Kushani inatumika sambamba na Midiani na
huenda inaonyesha au kuwataja Wakushi walioko Babeloni zaidi kuliko kwa wale
wanaohusiana na wale walioko Sudani na Ethiopia. Mfumo wa Bonde la Ufa uliopo
kutoka Lebanoni hadi kwenye Bahari ya Shamu litapasuka kutokana na matetemeko
makubwa ya ardhi katika Siku za Mwisho wakati atakapokuja Masihi na kutawanyika
kwa Mlima wa Mizeituni. Tukio hili linasababisha kuwepo kwa bonde kubwa upali
wa kilometa 66 kutoka Kaskazini hadi Kusini na kupitia Sinai kwa upande wa
kusini na kuvunja kingo au midomo ya Bonde la Ufa la Bahari ya Shamu na
itafumkilia mbali. Kuna wasiwasi kidogo kuwa watoto wa kiume wa Kiarabu wa
Midiani na Wakushi wanamaanisha kwa kiasi kidogo sana. Midiani ilikuwa ni
kabila kubwa la kabila la Waarabu upade wa Kusini Mashariki ya Edomu (na ambao
pia walikwenda upande wa kaskazini katika nchi ya Iraq); kama walivyo wana wa Ketura
kwa ujumla. Ishmaeli ni kabila Lililofanyika kuwa Waarabu lililo kwenye maeneo
ya Waarabu na sio Waarabu halisi asili yao ambao walikuwa ni wana wa Ketura.
Unabii wa Habakuki
bado haujafunuliwa bado na utaendelea hadi kuja kwa Masihi.
q