Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[108B]
Ezekieli
34 na Wachungaji
wa Israeli
(Toleo La 1.0 20100520-20100520)
Nabii Ezekieli alipewa unabii wa muhimu sana kuhusu Wachungaji wa Israeli. Unabii huo unatusuta hata sisi moja kwa moja leo.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hatimiliki © 2010 Wade Cox)
(tr. 2016)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na
tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.
Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala
yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia
yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Andiko lililo kwenye Ezekieli 34 ni karipio au onyo la
moja kwa moja kwa Wachungaji wa Israeli. Andiko lililo kwenye Ezekieli
linatupeleka hadi kwenye Siku za Mwisho na kwenye kipindi cha Milenia.
Jaribio hapa ni kusema kwamba Ezekieli 34 ni kuwaonya
Israeli kwenye kipindi cha Ezekieli.
Tatizo kwenye hali hii halisi ni kwamba Ezekieli alikuwa
akiwatabiria wakati Wachungaji wa Israeli wakati wakiwa wamekwenda utumwani kwa
muda mrefu uliopita mbali ya Araxes na hawakuwa wameamriwa na utaratibu wa
Kilawi Hekaluni. Kulikuwa na koo ishirini na moja zilizokwenda utumwani na ni
tatu tu ndizo zilizokuwa zimesalia Yudea na ambazo zilikuwa ni za masalia ya
Walawi. Kutokana na koo hizi tatu ni koo ishirini na nne tu ndizo
zilizorejeshwa na kutengenezwa tena.
Wa hiyo ni upuuzi sana kudai kwamba Wachungaji wa Israeli
walikuwa ni masalia walioachwa katika Yudea kwenye utumwa wa Wababeloni.
Kwa hiyo andiko hili ni unabii kwa Wachungaji wa Israeli
katika Siku za Mwisho na hivyo inakitaja kipindi cha Kanisa katika Siku za
Mwisho kwa kuwa hakukuwa na Hekalu na hakujawahi kuwepo Hekalu katika Israeli
tangu mwaka 722 KK.
Unabii huu unahusiana moja kwa moja na zama za makanisa
ya Siku za Mwisho.
Mbili kati ya zama hizi zimekataliwa na Mungu kama
matokeo ya matendo yao. Zama moja ya Wasardi, ya kanisa lililoonekana kuwa
limekufa na nyingine ya Walaodikia, ambayo ni yenye nguvu kubwa na utajiri, ni
ya uvuguvugu, na Mungu alilitapika litoke kinwani mwake.
Tutaona hapa kwamba Mungu anawatawanya na kuwaondoa
kondoo watoke kwenye vikundi hivi na kuwakusanya pamoja wawe kwenye kanisa la
tatu ambalo lina nguvu kidogo na watahukumiana wenewe kwa wenyewe.
Andiko hili moja kwa moja linataja Ufunuo sura ya 3 na
zama hizo za makanisa hayo matatu, na yapasa yasomwe kwenye nuru ile.
Makanisa kwenye karne ya 20 yalikuwa ni
wawakilishi wa moja kwa moja wa mambo yote mabaya ambayo Mungu aliyakemea hapa
kwa kupitia nabii Ezekieli.
Tazama jinsi walivyowafanyia kondoo tajiri na wadhaifu au
wasio na kitu na jinsi walivyofanya kwenye wajibu wao wa kuwalisha kondoo.
Ezekieli 34
Neno la Bwana
likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, toa unabii juu ya wachungaji wa Israeli, toa
unabii, uwaambie, naam, hao wachungaji, Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao
wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha
kondoo? 3 Mnawala walionona, mnajivika manyoya, mnawachinja walionona; lakini
hamwalishi kondoo. 4 Wagonjwa hamkuwatia nguvu, wala hamkuwaponya wenye
maradhi, wala hamkuwafunga waliovunjika, wala hamkuwarudisha waliofukuzwa, wala
hamkuwatafuta waliopotea; bali kwa nguvu na kwa ukali mmewatawala.
Bila shaka ndugu wapendwa wa karne ya 20 wangedai hili
kuwa hivyo hususan tangu katikati hadi mwishoni mwa karne. Walitawanyika kwa
kuwa hawakuwa na mchungaji wa kuwaangalia na huduma zao zilikuwa ni za kitoto au
kibabaishaji na za bandia bandia tu kwene mwili wa Kristo.
Maandiko na rekodi yao ziko kinyume na wachungaji kwa
jinsi walivyoenenda nab ado jinsi wanavyoenenda.
Andiko linalofuatia linaonyesha kwamba ilitokea kwene uso
wote wa dunia.
5 Nao wakatawanyika, kwa sababu hapakuwa na mchungaji; wakawa chakula cha wanyama- mwitu, wakatawanyika. 6 Kondoo zangu walitanga-tanga katika milima yote, na juu ya kila kilima kirefu; naam, kondoo zangu walitawanyika juu ya uso wote wa dunia; wala hapakuwa na mtu aliyewaulizia, wala kuwatafuta.
Ndipo Mungu aliwatangazia hukumu yao. Hukumu hii ilianzia kuchukua mkondo
wake mwaka 1987 mwanzoni mwa miaka 40 ya Kizazi cha Mwisho kilichonenwa na
Kristo.
7 Basi, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana; 8 Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, kwa sababu kondoo zangu walikuwa mateka, kondoo zangu wakawa chakula cha wanyama-mwitu wote, kwa sababu hapakuwa na mchungaji, wala wachungaji wangu hawakutafuta kondoo zangu, bali wachungaji walijilisha wenyewe wala hawakuwalisha kondoo zangu; 9 kwa sababu hiyo, enyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana; 10 Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu ya wachungaji; nami nitawataka kondoo zangu mikononi mwao, nami nitawaachisha hiyo kazi ya kuwalisha kondoo; nao wachungaji hawatajilisha wenyewe tena; nami nitawaokoa kondoo zangu vinywani mwao, wasiwe tena chakula chao.
Mungu anasema kwenye andiko hili maneno makuu
matatu:
Kisha Mungu anaendelea kutofuta jinsi ya
kuwaokoa kondoo hao yeye mwenyewe, akiwatafuta kutoka kila mahali ambako
wametawanyikia. Hatimaye atawaweka mahala penye malisho mazuri.
11 Maana, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi mwenyewe, naam, mimi, nitawatafuta kondoo zangu, na kuwaulizia. 12 Kama vile mchungaji atafutavyo kondoo zake, siku ile anapokuwa kati ya kondoo zake waliotawanyika; ndivyo nitakavyowatafuta kondoo zangu; nami nitawaokoa katika mahali pote walipotawanyika, katika siku ya mawingu na giza.
Kumbuka kuhusu aya hizi kwamba kondoo hawa
watatolewa nje kutoka kwa watu na kuwakuwasanya kwenye mataifa au nchi
mbalimbali.
13 Nami nitawatoa katika watu wa mataifa, na kuwakusanya katika nchi zote, nami nitawarudisha katika nchi yao wenyewe; nami nitawalisha juu ya milima ya Israeli, kando ya mifereji ya maji; na katika mahali pote pa nchi panapokaliwa na watu. 14 Nami nitawalisha malisho mema, pa juu ya milima ya mahali palipoinuka pa Israeli litakuwa zizi lao; huko watalala katika zizi jema; nao watakula malisho mema, juu ya milima ya Israeli. 15 Mimi mwenyewe nitawalisha kondoo zangu, nami nitawalaza, asema Bwana MUNGU.
Kumbuka kwamba aya za 13-15 Mungu anaelezea au
kuonyesha utaratibu atakaoufuata.
Mungu atawatibu maumivu yote ya wateule wake nay
a watu wote wanaoliitia jina lake. Atawaponya wadhaifu na viwete na kuwapiga
upofu na kuwalisha na kuwaangalia walio na nguvu ili wasiweze kuwasukuma tena
wale walio wadhaifu na kuwadhalilisha.
16 Nami nitawatafuta waliopotea, nitawarudisha
waliofukuzwa, nitawafunga waliovunjika, nitawatia nguvu wagonjwa; nao wanono na
wenye nguvu nitawaharibu; nitawalisha hukumu.
Tazama jinsi Mungu atakavyowahukumu kondoo.
17 Na kwa habari zenu, Enyi kundi langu, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, nahukumu kati ya mnyama na mnyama, kondoo waume na mbuzi waume pia.
Kipindi hiki cha kuhukumu ni zama ya
Wafiladelfia. Ni zama ya kondoo kuhukumiwa dhidi ya kondoo na hakutakuwa na
wachungaji watakaowalisha na hakuna atakayewatumia na kuwadhalilisha. Ni hukumu
itakayotolewa au kufanywa kwa kuzingatia upendo wa kidugu na utaendelea hadi
utaratibu wote wa utawala wa kipindi hicho uanze chini ya Masihi.
Kisha hapa ndipo Mungu anaelezea kuhusu kondoo
matajiri na wanono kwenye kifungu hiki cha mwisho:
18 Je! Mwaona ya kuwa ni neno dogo ninyi kulishwa malisho mema, hata mkawa hamna budi hukanyaga kwa miguu yenu yaliyosalia? Na kuwa mmekunywa maji yaliyo safi, nanyi hamna budi kuyatibua kwa miguu yaliyobaki? 19 Na kwa habari za kondoo zangu, wao wanakula hayo mliyoyakanyaga kwa miguu yenu, nao wanakunywa maji mliyoyatibua kwa miguu yenu.
Hiki ni kiambishi tunachoendana nacho sasa
ambapo kondoo wanapowafutia wengine malisho kwa bidii na uangalifu. Kondoo hao
wote watahukumiwa kwa ajili hiyo na kondoo waliokonda watalindwa.
20 Kwa sababu hiyo, Bwana MUNGU awaambia hivi; Tazama, mimi, naam, mimi, nitahukumu kati ya wanyama walionona na wanyama waliokonda. 21 Kwa kuwa mmesukuma kwa ubavu, na kwa mabega, na kuwapiga wenye maradhi kwa pembe zenu, hata mkawatawanyia mbali;
Kipindi hiki cha kutawanyika kiko njiani
kinakuja kwa miongo kadhaa, na hakipo mbali.
Mungu anakiona na anasema:
22 basi mimi nitaliokoa kundi langu, wala hawatakuwa
mateka tena; nami nitahukumu kati ya mnyama na mnyama.
Kipindi hiki ki awamu ya mwisho ya hukumu ya
kabla ya ufufuo wa wafu wa Masihi. Kisha tutahukumiwa na wanaostahili
watafufuliwa. Kuna andiko linaloelezea jambo hili hata pia kwenye Zekaria 12:8.
23 Nami nitaweka mchungaji mmoja juu yao, naye atawalisha, naam, mtumishi wangu, Daudi; yeye atawalisha, naye atakuwa mchungaji wao. 24 Na mimi, Bwana, nitakuwa Mungu wao, na mtumishi wangu, Daudi, atakuwa mkuu kati yao; mimi, Bwana, nimesema haya. 25 Nami nitafanya agano la amani nao, nami nitawakomesha wanyama wakali kati yao; nao watakaa salama jangwani, na kulala misituni. 26 Nami nitawafanya wao, na mahali palipo pande zote za mlima wangu, kuwa baraka, nami nitaleta manyunyu kwa wakati wake; yatakuwako manyunyu ya baraka.
Hivyo basi, watu waanchi wataipata amani na
ulinzi na watakuwa salama.
Kumbuka kuwa Mungu anasema kwamba nchi itazaa
maongeo yake na miti itatoa matunda yake. Kwa hiyo ndipo nchi haitakuwa na
laana tena kabisa. Na zaidi sana ni kwamba wanadamu hawatatiwa utumwani tena na
wala hawatakuwa kwenye kongwa la mizigo mizito.
27 Na mti wa kondeni utazaa matunda yake, nayo ardhi
itatoa mazao yake, nao watakuwa salama katika nchi yao; nao watajua ya kuwa
mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya kongwa lao, na kuwaokoa katika
mikono ya watu wale waliowatumikisha. 28 Hawatakuwa mateka ya makafiri tena,
wala mnyama wa nchi hatawala; bali watakaa salama salimini, wala hapana mtu
atakayewatia hofu.
Kwa hiyo, tutajionea marejesho mapya ya watu wa
Mungu walitolewa kwenye kongwa na Kristo ataletwa ili kuchukua watumwa walioko
utumwani.
Mungu atakuwasanya watu wake na hawatapata
mashutumu tena wala kulaumiwa na mataifa. Tutashuhudia jinsi jambo hili
litakapofanyika na jinsi watu wa Mungu watakavyofanyiwa na kuhesabiwa kwenye
mwili wa Kristo kwa Mashahidi na kwa njia ya dhiki kuu ya Nyakati za Mwisho.
Ni kama Mungu alivyoahidi:
29 Nami nitawainulia miche iwe sifa njema, wala hawataangamizwa kwa njaa katika nchi yao tena, wala hawatachukua tena aibu ya makafiri. 30 Nao watajua ya kuwa mimi, Bwana, Mungu wao, ni pamoja nao, na ya kuwa wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana MUNGU. 31 Na ninyi, kondoo zangu, kondoo za malisho yangu, ni wanadamu, na mimi ni Mungu wenu, asema Bwana MUNGU.
Hitimisho
Kutokana na andiko hili la Ezekieli 34 inaonekana wazi kabisa kwamba katika
Nyakati za Mwisho hakuna watumishi wa Makanisa ya Mungu watakaoruhusiwa
kuwaacha ndugu wapendwa waaminio. Kondoo wote watatolewa au kupokonywa kutoka
mikononi mwa wachungaji kwa ajili ya dhuluma zao na mafundisho yao ya uwongo.
Kwa hiyo inafuatia kwamba kanisa la mwisho la Nyakati za Mwisho ambalo
kwamba Mungu amewaweka kondoo litakuwa ni huduma isiyolipwa iliyohukumiwa
sawasawa na jinsi inavyowatumikia waumini wake na jinsi wanavyohudumiana na
kuchukuliana wote na jinsi wanavyoendelea kushikilia mafunndisho ya Makanisa ya
Mungu.
Tathmini zaidi ambayo mchakato wake tunaoweza kuyageukia Makanisa yaliyo
kwenye kitabu cha Ufunuo.
Hebu na tuyaangalie sasa maandiko yaliyo kwenye Ufunuo sura ya 3 kwa Makanisa
ya Nyakati za Mwisho.
Kwenye Ufunuo 2 tunaambiwa kwamba kanisa la Thiatira halitabebeshwa mzigo
wowote mwingine kama walivyoteseka sana kwenye mateso waliyokabiliana nayo
kwenye karne kadhaa za nyuma. Watakusanywa na kuwekwa mahali na Wafiladelfia
kwenye mwisho wa majaribu yao.
Twaweza kujionea kwenye andiko la Ufunuo sura ya tatu kwamba ujumbe uliopo
unayahusu makanisa matatu ya mwisho.
Jambo hili limeainishwa kikamilifu zaidi kwenye jarida la Nguzo za Filadelfia (Na. 283). Imeshauriwa kwamba jarida hilo lisomwe sambamba na jarida hili.
Ufunuo
3
Sardi
Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa. 2 Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu. 3 Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako. 4 Lakini unayo majina machache katika Sardi, watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa wamestahili. 5 Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake. 6 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.
Hivyo tunaona kwamba imani ya Wasardi imekufa
ingawaje wanaendelea kuonekana kama wako “hai.” Kuna kanisa moja tu
katika historia ambalo lina jina hili la Kanisa “Hai” la Mungu. Huu ni mfano au
kivuli cha zama ya kanisa la Wasardi.
Kuna baadhi walio kwenye imani hii wanaostahili
na watatolewa watoke nje ya imani hii kama sehemu ya mchakato huu wa
kuwapokonya kondoo kutoka mikononi mwa wachungaji hawa.
Zama hii imepita kwa muda wa karne nyingi lakini
lilikuwa limekufa na halikufanya kitu chochote kwa zaidi ya imani nyingi.
Filadelfia
Kanisa hili lina idadi ya mambo kadhaa
yanayoludi. Lina nguvu au uweza wa kufungua na kufunga kwenye Makanisa ya Mungu
na mataifa na uweza dhidi ya mapepo na kuzimuni.
7 Na kwa malaika wa kanisa
lililoko Filadelfia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa
kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye,
naye afunga wala hapana afunguaye. 8 Nayajua matendo yako.
Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye
kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe umelitunza neno langu, wala
hukulikana jina langu.
Kanisa hili linakabiliana na nyakati za mateso ya
Siku za Mwisho na dhiki kuu itakayoukabili mwili wa Kristo na halijalikana jina
lake.
Imani hii itawachukua walio kwenye sinagogi la
Shetani na kulishughulikia na katika siku za mwisho watawafanya waje
kujipendekeza na kujiunga nao. Kanisa hili litachukuliwa na kuwa na sehemu kwenye
ufufuo wa wafu na linalindwa litoke saa ya mateso ya kujaribiwa. Makanisa
meingine mawili hakuachwa na hayana sehemu kwenye Ufufuo wa Kwanza wa wafu.
9 Tazama, nakupa walio wa sinagogi la Shetani,
wasemao kwamba ni Wayahudi, nao sio, bali wasema uongo. Tazama, nitawafanya
waje kusujudu mbele ya miguu yako, na kujua ya kuwa nimekupenda. 10 Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu,
mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia
ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.
Kanisa hili linastahili na litakuwa na sehemu
wakati wa kurudi kwake Kristo:
11 Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije
mtu akaitwaa taji yako. 12 Yeye ashindaye,
nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena
kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu
wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina
langu mwenyewe, lile jipya. 13 Yeye aliye na
sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.
Watu hawa wanafanyika kuwa nguzo muhimu na
kufanyika kuwa nguzo za muhimu kwenye Hekalu la Mungu.
Laodikia
Laodikia ni kanisa kubwa sana miongoni mwa
makanisa ya Sabato na wanadhani kuwa ni matajiri, bali hawako hivyo kabisa,
bali ni maskini, mnyonge na mwenye mashaka, kipofu na uchi. Wale anaowapenda
Mungu huwaondoa kanisani na kuwaweka pia kwenye kanisa la Filadelfia.
14 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu. 15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. 17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. 18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. 19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu. 20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. 21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.
Wale walio na juhudi na bidii na wanaotubu wanaondolewa kutoka kwao na
wanaunganishwa na Wafiladelfia ambako hawatatoka na kuondoka tena kamwe, kabisa.
Fanya rejea ya jarida la Nguzo za Filadelfia (Na. 283).
Mungu anashughulika na makanisa na anayaandaa kwa ajili ya Ufufuo wa Kwanza
baada ya kuhukumiwa yao ambayo katika Nyakati za Mwisho yatajaribiwa kwa upendo
wa kidugu na uaminifu wao kwenye mafundisho. Imani zote mbili au makundi haya
ya kanisa yamekataliwa kwa ajili ya upotofu wao.
q