Makanisa ya Kikristo ya Mungu

 

[190]

 

 

 

Jinsi ya Kuiandaa Pasaka

 

(Toleo 2.019970118-79990213)

 

Kipindi cha Pasaka ni cha wakati wa muhimu sana kwa mujibu wa Kalenda ya Kanisa. Maandalizi yanayomwezesha mtu ashiriki kikamilifu wakati huu wa Pasaka ndio tatizo kubwa linalojitokeza karibu kwa kila Mkristo. Wengi hawafanyi mipngo ya makusudi ili washiriki kipindi hiki cha Pasaka katika ukamilifu wake na kwa miaka mingi inatokea kuwapita wakirudia makosa kama hayohayo bila kujisikia kuhukumiwa mioyoni mwao, au wanafanya uzembe yaani kutotilia maanani kwa mambo haya muhimu ya kiroho.

 

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

Copyright ã  1997, 1999 Wade Cox)

(Tr. 2005)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org and http://www.ccg.org

 


Jinsi ya Kuiandaa Pasaka



Kipindi cha Pasaka ni cha wakati wa muhimu sana kwa mujibu wa Kalenda ya Kanisa. Maandalizi yanayomwezesha mtu ashiriki kikamilifu wakati huu wa Pasaka ndio tatizo kubwa linalojitokeza karibu kwa kila Mkristo. Wengi hawafanyi mipango ya makusudi ili washiriki kipindi hiki cha Pasaka katika ukamilifu wake na kwa miaka mingi inatokea kuwapita wakirudia makosa kama hayohayo bila kujisikia kuhukumiwa mioyoni mwao, au wanafanya uzembe yaani kutotilia maanani kwa mambo haya muhimu ya kiroho. Utaratimu mzima wa kipindi hiki hufikia kilele chake kwa kushiriki Ushirika wa Meza ya Bwana ambayo inamaana ya huadhimishwa kwa mlo wa usiku unaotajwa katika maandiko matakatifu kama ni Usiku wa Kukuumbuka Sana. Sababu ya kwanza inayopelekea umuhimu wa kushiriki Meza hii ya Bwana ni kwamba inawakilisha mamlaka ya Bwana kwa wateule wake ya kuwafanya kuwa wao sasa ndio Israeli wa Kiroho. Sababu ya pili ni kwamba, mlo ule unaoelezewa katika kitabu cha Kutoka 12 unawakilisha leo wokovu kwa wale wote walio chini ya kivuli cha Kristo na kufanyika kuwa ni sehemu ya uzao wa taifa la Israeli ambao wamekombolewa kwa kupitia dhabihu ya Kristo ambaye alitolewa sadaka kwa kifo chake jioni ile.

 

Paulo alisema hivi kuhusu Meza ya Bwana:       

1Wakorintho 11:23-32: 23 Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliyowapa ninyi, ya kuwa Bwana Yesu ule uliotolewa alitwaa mkate, 24 naye akiisha kushukuru akaumega, akasema, Huu ndio mwilim wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu. 25 Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akasema, kikombe hiki ni agano jipya katika damu yanu;  fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu. 26 Maana kila mwulapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, mwaitangaza mauti ya Bwana hata ajapo. 27 Basi kila aulaye mkate huo, au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa amejipatia hatia ya mwili na damu ya Bwana. 28 Lakini mtu ajihoji mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe. 29 Maana alaye na kunywa, hula na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kuto kuupambanua ule mwili. 30 Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio hawawezi na dhaifu, na watu kadha wa kadha wamelala. 31 Lakini kama tungejipambanua nafsi zetu, tusinge hukumiwa. 32 Ila tuhukumiwapo, twarudiwa na Bwana, isije ikatupata adhabu pamoja na dunia.       

 

Kuula mwili na kuinywa damu ya Masihi bila kupambanua, ni kukufuru au kuutia unajisi mwili na damu ya Bwana. Yeye anayefanya hivyo bila kutofautisha na mlo wa kawaida na asiupambanue mwili wa Bwana, hunywea hukumu ya nasfi yake.

 

Je, hii inamaana gani? Inamaana na kusisitiza kuwa tunapaswa kushiriki mwili na damu ya Kristo kwa maana sahihi. Pia tunapaswa kuupambanua mwili kwa kuliona tendo hili kuwa sio la kawaida na milo ya aina nyingine. Hapa kuna amri mbili zinazojiwakilisha zenyewe. Ya kwanza inasema kuwa tunapaswa tujiandae kwa ajili ya kushiriki Meza hii ya Bwana, kwa  maana halisi. Na ya pili ni kwamba lazima tuupambabue mwili wa Bwana.

 

Hebu tuangalie maana ya ku upambanua Mwili

Tuanze kwa kuitafakari amri ya pili kwanza, inayosema kuupambanua mwili wa Bwana.

 

Neno lenyewe kuu linasema hakika kwa yule alaye na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kuto kuupambanua ule mwili. (angalia Kamusi iitwayo Mashall’s Greek-English Interlinear utaelewa zaidi). Hukumu au kwa Kiyunani krima na neno kuupambanua mwili kunaitwa diakrion to soma. Neno diacrinon linamaana ya kutenga au kuweka kitu katika hali tofauti au kutofautisha. Inaweza kuwa na maana ya kupendekeza au kumtenga mtu mbali na wengine. Hapa inamaana ya kufanya maamuzi, kutoa hukumu au kuamua kupingana (angalia kwenye Kamusi ya New Thuyer’s Greek-English Lexicon, p.138). inaweza pia kuwa na maana sawa tu na kusema watu wanaojiondoa kutoka katika ushirika wa jamii ya Wakristo wa kweli (kama ilivyo sawa na tafsiri katika kamusi zilizotajwa hapo juu). Neno hili la Kiyunani soma hapa lina maana ya mwili na linatumika kwa kila nafsi iwe ni mtu au mnyama unaotolewa kwa ajili ya sadaka (soma Ebr.13:11 na Kut. 29:14; Hes.19:3 LXX). Inaweza pia kuwa ni hakalu la Roho Mtakatifu (rudia tena kusoma kamusi ya thayer’s, kama ilivyoonyeshwa hapo juu, p.611).

 

Sababu muhimu hapa iliyopelekea kufanya iwepo tofauti ni katika Wakorintho ni uhusiano wake na 1Wakorintho 11:18-22.

 

1Wakorintho 11:18-22 inasema: 18 Kwa maana  kwanza mkutanikapo kanisani nasikia kuna faraka kwenu; nami nusu nasadiki; 19 Kwa maana lazima kuwapo na uzushi kwenu, ili waliokubaliwa wawe dhahiri kwenu. 20 Basi mkutaniko pamoja haiwezekani kula chakula cha Bwana; 21 Kwa maana kila mmoja hutangulia kukitwaa chakula chake katika kule kula; hata huyu ana njaa, na huyu amelewa. 22 Je! hanma nyumba ya kulia na kunywea? Niwaambieni? Niwasifu? La! Siwasifu kwa ajili ya hayo.

 

Utendaji kazi wake (au muundo) (aireseis kama vile heresies[mafundisho ya uzushi]) yanaruhusiwa yatokee kati yetu ili kuwathibitisha walio wa kweli (dokrimai) kati yetu na Mungu.

 

Hali ya kuupambanua mwili ni uamuzi wa viungo vya mwili ambao uko na nia ya kufanya matendo au makosa yajulikanayo kama mafundisho yamapotofu ya dini zinazodai kuwa zinafundisha neno la Mungu. Neno heresy lenye maana ya mafundisho ya uzushi, halikutumika kwa maana mbaya katika Agano Jipya (tazama sehemu iliyoongezewa katika jarida linalosema Mwanzo wa Mafundisho ya Uzushi katika Kanisa la Mitume, [089]. Yalitumiwa sana na Mafarisayo (Matendo 15:5) na Masadukayo (Matendo 5:17) na kasha kwa Kanisa lenyewe (Matendo 24:5; 26:5; 28:22). Kwa lugha rahisi tuseme ina maana ya kuchagua na kufanya kuwa ni miongoni mwa chaguo lililo rudishiwa ambayo huitwa kwa Kiingereza sect. katika siku za hivi karibuni neon hili heresy lilikuja kubeba maana ya kitu chochote kilicho tofauti na mifumo iliyozoeleka ya kiimani lakini hii haikuwa ndiyo maana yake hasa ya alisi. Hapa ina maana ya kwamba ni kuligawa neon la Mungu na ili kuwajuwa wale waliomaanisha hasa kuwa ni sehemu ya mwili wa Kristo na wanaoshiriki Meza ya Bwana kwa maana sahihi inavyokusudiwa, kwa wakati na kwa njia sahihi. Kuna tofauti ya maongozi (diaconion) lakini Bwana ni yeye yule na tofauti ya kutenda kazi (diaireseis energematon) lakini Mungu ni yeye yule afanyaye mambo yote katika yote (1Kor.12:5). Kwa hiyo inatupasa kupima kila aina ya maongozi na utendaji kazi wake kwa kila kinacho jiinua kudai kuwa ni sehemu ya mwili huu na tushiriki kuumega mkate na wale tu walio na sehemu katika mwili wa Kristo kwa dhati ingawaje sio lazima kuwa wote watokee katika kundi la namna moja au katika uongozi mmoja au huduma moja. Mungu ndiye afanyaye na kukamilisha mambo yote na katika yote. Lakini tunalopaswa sisi kufanya ni kuupambanua mwili wa Kristo na kushiriki kuila Meza ya Bwana kama mwili mmoja ulioweka msingi wa imani kwenye kweli na kwa moyo wa kweli na katika Mungu mmoja wa pekee wa kweli.

 

Majaribu Yanayotangulia Adhimisho La Pasaka

Katika kipindi unachofanya maandalizi kwa ajili ya kuadhimisha Pasaka, Mungu huyaruhusu majaribu na mitihani ikupate. Tunafikia mahali ambapo kila mmoja wetu anaanza kuwaza juu ya hali yake ya kiroho. Mungu hafanyi mambo yote haya kwa mara moja au watu wengi hawataweza kuwa katika hali tambarare. Yawezekana kuwa katika kila mwaka kadiri unavyo jitahidi kupiga hatua zaidi kwenda mbele, unarudishwa nyuma au unakutana na mawimbi, lakini tunatakiwa tushinde. Hali hii na mara chache sana ikaonekana kupendwa na wengi. Katika kipindi hiki, adui wetu anajaribu kufanya bidii sana kutushambulia na kutukatisha tama. Lakini tunapaswa sote tukumbuke kuwa kipindi cha kujaribiwa ni kimoja na kwa kipindi hichohicho ndipo tunatakiwa kuonyesha ushindi wetu; na huko ndiko kukua kiroho na kufikia maendeleo mazuri.

 

Tatizo linalosumbua sana katika jamii ya wakristo siku hizi ni aina mpya ya Injili inayohubiriwa inayofundisha watu kutajirika na kuwa na afya nzuri kila wakati kama ndio kipimo cha imani yao na wengi wamekulia wakilelewa na aina hii ya injili.

 

Kuugua na kuwa masikini kunategemea jinsi uhusiano wako ulivyo na Mungu. Adui wetu shetani na tumgundue kuwa ndio sababu kubwa azizuiae baraka zetu zisitufikie kutoka kwa Mungu. Mungu huruhusu majaribu ili aturekebishe na kutupa nguvu za kiroho na sio utajiri wa mali. Yeye pia huyapatiliza mataifa kwa hukumu kwa njia moja au nyingine kwa vipindi mbalimbali.

 

Hebu na tufikirie jinsi ambavyo Mungu alivyokuwa anawafanyia Yuda na Yerusalemu. Hebu na tukifikirie tunaposoma kitabu cha nabii Ezekieli. Wakati mambo haya yalipoandikwa, ikumbukwe kuwa ni wakati ambapo Israeli walikuwa tayari wameisha enda utumwani kwa karne kadhaa na Yuda walirejea tena kutoka utumwani na wakaanza maisha tena. Tena unabii wa nabii Ezekieli unahusu kutokea utumwa mwingine kuwepo katika siku za usoni na mateso makubwa.

 

Ezekieli 5:1-17 inasema: Nawe mwanadamu, ujipatie upanga mkali, kama wembe wa kinyozi ujipatie, ukaupitishe juu ya kichwa chako na ndevu zako; kisha ukajipatie mizani ya kupima, ukazigawanye nywele hizo. 2 Theluthi ya hizo utaiteketeza katika mji, siku za mazingiwa zitakapo timia; nawe utatwaa theluthi, na kuipiga kwa upanga pande zote; nawe utatatawanya theluthi ichukuliwe na upepo, nami nitafuta upanga nyuma yake. 3 Nawe twaa nywele chache katika hizo, na kuzifunga katika upindo wa mavazi yako. 4 Nawe utatwaa tena baadhi ya hizo, na kuzitupa katikati ya moto, na kuziteketeza katika moto huo; kutoka nywele hizo moto utakuja na kuingia katika nyumba yote ya Israeli. 5 Bwana MUNGU asema hivi; Huu ndio Yerusalemu; nimeuweka kati ya mataifa, na nchi zauzunguka pande zote. 6 Nao ameasi hukumu zangu, kwa kutenda mabaya kuliko mataifa hayo, nao umeasi sheria kuliko nchi hizo ziuzungukazo; maana wamezikataa hukumu zangu, wala hawakuenda katika sheria zangu. 7 Basi, kwa hiyo Bwana MUNGU asema hivi; Kwa sababu ninyi mmefanya ghasia kuliko mataifa wawazungukao ninyi, wala hamkuenda katika sheria zangu, wala hamkuzishika hukumu zangu, wala hamkutenda kama kawaida za mataifa wawazungukao; 8 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Angalia, mimi, naam, mimi, ni juu yako; nami nitafanya hukumu kati yako machoni pa mataifa. 9 Nami nitakutenda yasiyoyatenda zamani, wala sitafanya tena mambo kama hayo, kwa sababu ya machukizo yako yote. 10 Kwa sababu hiyo baba za watu watawala wana wao kati yako, nao wana watawala baba zao; nami nitafanya hukumu ndani yako, na hao wote waliosalia kwako nitawatawanya kwa pepo zote. 11 Kwa sababu hiyo, kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hakika kwakuwa umepatia unajisi patakatifu pangu, kwa matendo yako yote niyachukiayo, na kwa machukizo yako yote, kwa sababu hiyo mimi nitakupunguza; wala jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma. 12 theluthi yenu watakufa kwa tauni, na kwa njaa watakomeshwa ndani yako; na theluthi yenu wataanguka kwa upanga pande zako zote; na theluthi yenu nitawatawanya pepo zote, kasha nitafuta upanga nyuma yao. 13 Hivyo ndivyo ghadhabu yangu itakavyotimia, nami nitatosheleza hasira yangu juu yao, nami nitafarijika; nao watajua ya kuwa mimi, BWANA, nimenena kwa wivu wangu, nitakapokuwa nimeitimiza ghadhabu yangu juu yao. 14 Tena nitakufanya kuwa ukiwa, na aibu, kati ya mataifa wakuzungukao, machoni pa watu wote wapitao. 15 Nayo itakuwa tukano la aibu, na mafundisho ya ajabu, kwa mataifa wakuzukao, hapo nitakapotekeleza hukumu ndani yako, kwa hasira, na kwa ghadhabu, na kwa malaumu ya ghadhabu; mimi, BWANA, nimeyanena hayo; 16 hapo nitakapopeleka mishale mibaya ya njaa juu yao, iletayo uharibifu, nitakayoipeleka ili kuwaharibu ninyi; nami nitaiongeza njaa juu yenu, na tegemeo lenu la mikate nitalivunja. 17 Nami nitapeleka juu yenu njaa na wanyama wabaya, nao watakunyang’anya watu wako; na tauni na damu zitapita ndani yako; nami nitauleta upanga juu yako; nami BWANA, nimeyanena hayo.

      

Katika aya hizi tunachukuliwa hadi mahali panapo tabiri kuhusu maangamivu kuikumba Yerusalemu, ambayo hayakutokea kwa wakati ule mpaka mwaka 70 BK. Maangamizi haya yalikuwa yatimie kwa kufuatana na unabii na kwa muda muafaka wa kutosha sawa sawa na matukio ya Mungu yalivyofuatana (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu [013]; na Ramani ya Ratiba ya Zama Mbalimbal [272]).

 

Kutokana na vile unabii unavyosema, tunaona kwamba kanisa lilikuwa na wajibu wa kufanya walivyokuwa utumwani. Zile nywele ziliashiria watu wa taifa la Yuda. Nywele ziligawanywa katika sehemu kuu tatu. Sehemu ya kwanza ni theluthi moja ambayo ilitakiwa iteketezwe wakati wa kuuzingira. Sehemu nyingine ya theluthi moja ya mji ilikuwa iteketezwe kwa makamio ya mateso ma vita na sehemu nyingine iliyosalia ilitakiwa igawanywe na kuwindwa hadi kuhusuriwa kwa upanga.

 

Kiasi kidogo cha nywele ambazo zilihifadhiwa katika upindo wa nguo walikuwa ni watu wa kanisa wa Masihi ambao walipitia mateso na watu wa Yuda hadi kufikia mwaka 63 BK wakati Yakobo ndugu yake Bwana aliyekuwa pia askofu wa Yerusalemu aliuawa. Kanisa likakimbilia na kujificha mahali panapoitwa Pella chini ya Symeon ndugu mdogo na Kristo, ambaye kwa wakati ule alishakuwa mkubwa wa kuweza kumrithi Yakobo kama kiongozi wa kanisa na kuwa miongoni mwa Viongozi nguzo wa kanisa (Desponsyni) kwa maana nyingine ni wale walio mali ya Bwana (tazama jarida lisemalo Bikira Mariamu na Ukoo wa Kristo [232].

 

Kutokana na utawanyiko huu kanisa lenyewe tu liliweza kuenea na imani ikaingia hadi Israeli kutoka Yudea kama ilivyokuwa imetabiriwa. Tunaona sasa kuwa Mungu alishughulika na Yudea yote na Yerusalemu, kwa kuwa walizibadili sheria na kuzibadili hukumu za Mungu kwa uovu (Eze. 5:6). Walizigeuza Sheria za Bwana na mapokeo na kupatia unajisi patakatifu pake kwa ibada za sanamu na kwa kufuata desturi za mataifa na wakapelekwa utumwani. Mawazo yao yalikuja kukumbuka haya wakati majeshi ya Warumi yalipouzingira na kuhusuru mji wa Yerusalemu siku ya 1 ya mwezi wa Nisan mwaka 70 BK, mwaka wa arobaini kamili baada ya kifo cha Masihi, matendo yao yalikuwa kwa kweli ni vita kupigana wenyewe kwa wenyewe. Walikuwa wanapigana wakati ambapo majeshi ya Warumi yakiwa yameweka kambi karibu yao. Mwana zuoni maarufu wa Kuyahudi katika karne ya kwanza aitwaye Josephus alitoa ushuhuda wake kuwa kwa kweli Warumi hawakufanya uharibifu mkubwa sana kulinganisha na uharibifu waliofanya Yuda wakati walipokuwa wanapigana wenyewe kwa wenyewe.

 

Wakati huu wote wa kutafanyika kwa matukio haya, kanisa lilindwa kwa kiwango kikubwa sana, isipokuwa viongozi. Wengi wao waliteswa kwa kufanyizwa kazi za shuruba na mateso makali hasahasa katika Yudea hadi ikabidi sadaka na michango ifanywe na makanisa yaliyokuwa nje ya Yerusalemu, ili kulisaidia kanisa la Yerusalemu. Takribani Mitume wote isipokuwa Yohana inasemekena waliuawa na kuanzia hapo inaonekana kuwa kila aliyekuwa anashiklilia uongozi wa kanisa aliuawa mateso yenye kuambatana na mauaji yaliyodumu kwa karne na karne. Mungu aliruhusu viongozi wote wa kanisa wauawe isipokuwa mtume Yohana. Katika Ezekieli 6:1-14 tunaona maangamivu ya Israeli yakitabiriwa .

 

Ezekieli 6:1-14 inasema: Neno la BWANA likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, uelekeze uso wako uitazame milima ya Israeli, ukaitabirie, 3 ukisema, Enyi milima ya Israeli, lisikieni neon la Bwana MUNGU; Bwana MUNGU aiambia hivi milima na vilima, na vijito na mabonde; Tazama, mimi, naam, mimi, nitaleta upanga juu yenu, nami nitapaharibu mahali penu palipo inuka. 4 Na madhabahu zenu zitakuwa ukiwa, na sanamu zenu za jua zitavunjika; nami nitawatupa wana wenu waliouawa mbale ya vinyago vyenu. 5 Nami nitaiweka mizoga ya wana wa Israeli mbele ya vinyago vyao; nami nitaitawanya mifupa yenu pande zote za madhabahu zenu. 6 Kila mahali mkaapo miji itaharibika, na mahali palipoinuka patakuwa ukiwa; ili madhabahu zenu zihzribiwe, na kufanywa ukiwa, na vinyago vyenu vivunjwe, na kukoma, na sanamu zenu za jua zikatwe, na kuangushwa, na kazi zenu zifutwe kabisa. 7 Na hao waliouawa wataanguka katikati yenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA. 8 Lakini nitasaza mabaki; maana mtakuwa na baadhi ya watu watakaoukimbia upanga kati ya mataifa, mtakapokuwa mmetawanyika katika nchi za watu. 9 Na hao wakwenu watakaookoka watanikumbuka kati ya mataifa, watakaochukuliwa mateka, jinsi nilivyoiponda mioyo yao ya kikahaba, iliyoniacha, na macho yao, yaendayo kufanya uasherati na vinyago vyao; nao watajichukia nafsi zao machoni pao wenyewe, kwa sababu ya mabaya yao yote, waliyoyatenda kwa machukizo yao wenyewe, kwa sababu ya mabaya yao yote, waliyoyatenda kwa machukizo yao yote. 10 Nao watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA; sikusema bure kama nitawatenda mbaya hayo. 11Bwana MUNGU asema hivi; Piga kwa mkono wako, ipige nchi kwa mguu wako, ukaseme, Ole! Kwa sababu ya machukizo yote ya nyumba ya Israeli; maana wataanguka kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni. 12 Yeye aliyembali sana atakufa kwa tauni; nay eye aliye karibu atakufa kwa upanga; nay eye atakayesalia, na kuhusuriwa katika mji, atakufa kwa njaa; hivyo ndivyo itakavyoitimiza ghadhabu yangu juu yao. 13 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, watu wa kwao waliouawa watakapokuwa kati ya vinyago vyao, pande zote za madhabahu zao, juu ya kila kirefu, juu ya vilele vya milima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi, na chini ya kila mwaloni mnene, pale pale walipovifukizia uvumba mzuri vinyago vyao vyao vyote. 14 Nami nitanyosha mkono wangu juu yao, na kuifanya nchi kuwa maganjo, tena ukiwa mbaya kuliko jangwa upande wa Dibla, katika makao yao yote; nao watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA.

 

Unabii huu unahusu Israeli na sanamu zao. Kanisa haliwezi kutenganishwa na taifa hili katika utendaji kazi wake. Kanisa litakuwa ndani ya taifa hili katika kipindi chake chote cha mateso, hadi kuja kwake Masihi.

 

Masihi mwenyewe alisema kuwa kanisa halitamaliza kukimbia huku na huko katika mateso likipita katika miji mbalimbali ya Israeli hata atakapo kuja.

 

Mathayo 10:21-23 inasema: 21 Na ndugu atamsaliti nduguye ili auawe, na baba atamsaliti mwana, na wana watawainukia wazazi wao, na kuwafisha. 22 Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka. 23 Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia, Hamtaimaliza miji ya Israeli, hata ajapo Mwana wa Adamu.

 

Kifungu hiki cha maandiko kinaonyesha kuwa hali ya kusalitiwa katika kanisa na kwenye ukoo vitaendelea kutokea kwa ubaya zaidi katika siku hizi za mwisho. Moja lililo dhahiri na muhimu sana kulijua ni hali ya kuchukiwa na watu wote itatupata kwa sababu tu kwamba sisi ni wafuasi wa Kristo. Hii pia inamaanisha kuongezeka kwa kiasi kikubwa kwa hali ya kutovumiliana ambako hakujawahi kutokea kabla na zaidi ya upeo wa uelewa wa wengi.

 

Kanisa limechaguliwa na limeitwa kulingana na makusudi ya Mungu. Hivyo basi ukiyajua haya na kuyaweka moyoni utagundua sasa kuwa ukweli ni kwamba hakuna ukweli katika mafundisho yanayo fundishwa siku hizi kuhusu uhakika wa kudumu kwa mtu wa Mungu kuwa hawezi kuwa masikini ama kuugua ama kupatwa na mateso na matatizo ambayo watu wetu wamesababishiwa kukutana nayo. Kwa njinsi hii basi hatuna wajibu wowote wa kujaribu kuyafanyia kazi, au kuyaombea, watu wetu katika mataifa yote wanapaswa kuweka matumaini na shauku yao kwa Masihi ambaye atarudi tena kuja kutuokoa.

 

Hivyo basi, usikate tama unapokutana na majaribu, magumu  na matatizo. Dunia itafikishwa katika magoti yake katika siku hizi za mwisho nasi tukumbuke kuwa bado tunaishi duniani. Tumemriwa tutoke ndani yake lakini lakini bado tungali tunalazimika bado kuishi ndani yake.

 

Jinsi ya kuandaa Meza ya Bwana

Hebu basi sasa na tutafakari agizo la kwanza kati ya mawili tuliyo amriwa kufanya.

-Andaa Meza ya Bwana.

 

Ni dhana iliyo dhahiri kuwa hakuna mtu awezayekushiriki Meza ya Bwana kwa hivihivi tu. Hili ni janbo ambalo linatoa maana yenye kujichanganya kama kusudi litakuwa hivyo yaani kutimiza wajibutu. Lamaana ni kwamba ni kushiriki mlo ambao uliwekewa maana yenye ukweli kwamba sisi tulikuwa wenye dhambi na kwamba tukipewa wokovu kwa neema tu ambayo maana yake ni kwamba sisi hatutaweza kamwe kuwa wema kiasi cha kutosha kiasi cha kustahili kushiriki kuila Meza hii ya Bwana, Lakini hata hivyo, tunalazimika, kushika jembe kwa mikono yetu, kwa kuula mwili na kuinywa damu ya Masihi la sivyo, hatutaweza kuuingia Ufalme wa Mungu. Yesu alisema hivi katika Yohana 6:53-58:

 

Yohana 6:53-58: 53 Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipokula mwili wake mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu. 54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho. 55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha  kweli. 56 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami ndani yake. 57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa baba, kadhalika yeye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi. 58 Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; sio kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele. 

 

Watu wengi waliacha kumfuata Masihi baada ya kusikia maneno haya. Hawakuweza kuelewa maana ya kimafumbo ya jambo hili. Hivyo basi ni ukweli ulio dhahiri kuwa hutaweza kuuingia Ufalme wa Mungu usiposhiriki Meza ya Bwana. Ili kushiriki sakramenti hii kuna masharti kadhaa muhimu unayotakiwa kuyatimiza. Sharti la kwanza ni lazima ubatizwe. Ikiwa kama bado hujabatizwa, unakuwa ni mfu na uko katika utumwa wa dhambi bado na sehemu yako ni katika ule ufufuo wa pili. Ufufuo wa pili ni wa ufufuo wa mateso au wa hukumu. Utaadhibiwa na kuhukumiwa pale kwa yale unayoyajua. Na haitoshi kuupata ubatizo tu kwa sasa au kuahirisha kufanya kwa siku zijazo halafu ukahukumiwa kwa jambo ambalo ulisha liijua na kuezekana kulifanya likiwa katika ufahamu wako. Kwa hiyo watu wote wanao ukataa ubatizo watakuja kuadhibiwa kwa kukataa kwao ukweli huu katika ule ufufo wa pili.

 

Na sasa basi tutatafakari kwa kupitia miandamano hii kwa hatua moja hadi nyingine ili kwamba kila mmoja wetu aushikilie wokovu kwa hofu na kutetemeka (Flp. 2:12).

 

Kama bado hujabatizwa ni vema ufanye maandalizi ya kubatizwa. Na iwapo kama umebatizwa, basi uutafakari kipengele hadi kipengele cha ubatizo wako na ujue ninini maana yake. Soma jarida linalosema Kutubu na Kubatizwa [052] na majarida shirikishi yafuatayo:

. Hatua za Kufuata ili Kushinda Dhambi [011];

. Uhuru na Wajibu [009];

. Uhusiano uliopo kati ya Kuokolewa kwa Neema na Sheria [082]

. Sakramenti za Kanisa [150].

 

Umepewa Roho Mtakatifu kama msaidizi wako katika ukombozi wako kama mwana wa Mungu. Je, hii inamaana gani? Soma jarida lisemalo Roho Mtakatifu [117]; na Mahusiano katika Utendaji kazi na Baba [081].

 

Sasa waweza kuandaa Pasaka kiasi cha kufaa kutumika kama Meza ya Bwana. Pasaka inatakiwa kuwa lini? Soma jarida linalosema Kalenda ya Mungu [156] na majarida yake shirikishi ya:

. Mwezi wa Tishri na Uhusiano wake na Kipindi cha Jua kipita katikati ya dunia [Equinox][175];

. Yeroboamu na Kalenda ya Hillel [19]..

 

Je, Pasaka inaashiria nini kwa mujibu wa Biblia? Je, ninini mpango wake kwa ujumla? Soma jarida linalosema Pasaka Kuu Saba za Biblia [107]. Je, ni upi utaratibu wa kufuata katika kuadhimisha Pasaka? Soma jarida lisemalo Pasaka [098] na vile vile jarida lisemalo Usiku Wa Kuuangalia Sana  [101].

 

Je, Ushirika wa Meza ya Bwana ni ishara ya nini? Soma majarida ya Ishara ya Kuosha Miguu [099] na Ishara ya Mkate na Divai [100]. Pasaka ni ya kwanza kati ya Sikukuu zinazotolewa matoleo ya sadaka. Nabii Malaki anasema kuwa ishara ya kuwa watu wamemrudia Mungu ni utoaji wa zaka (Mal. 3:6-12) inasema:

 

Malaki 3:6-12: 6 Kwakuwa mimi, BWANA, sina kigeugeu; ndio maana hamkuangamizwa, enyi wana wa Yakobo.7 Tokea siku za baba zenu mmegeuka upande, mkayaacha maagizo yangu, wala hamkuyashika. Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi, asema BWANA wa majeshi. Lakini ninyi mwasema, Turudi kwa namna gain? 8 Je! Mwanadamu atamuibia Mungu? Lakini ninyi mnaniibia mimi. Lakini ninyi mwasema, Tumekuibia kwa namna gain? Mmeniibia zaka na dhabihu. 9 Ninyi mmelaaniwa kwa laana; maana mnaniibia mimi, naam, taifa hili lote. 10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema BWANA wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la. 11 Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu wenu hautapukusha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema BWANA wa majeshi. 12 Na mataifa yote watawaiteni heri; maana watakuwa nchi ya kupendeza sana, asema BWANA wa majeshi.      

 

Meza ya Bwana ni sakramenti inayotangaza watu kumrudia Mungu. Wakati ambapo kutoa zaka ni ishara ya nje ya watu kumrudia Mungu. Je, wewe umeisha anzisha uhusiano wako na Mungu kwa kusimama imara? Je, umeishatoa zaka yako tayari na kuandaa sadaka yako tayari kumtolea Mungu katika Sikukuu hii ya Kwanza kati ya Sikukuu tatu za kila mwaka? Kumbuka kuwa kuna wakati wa kumtolea Bwana sadaka mara tatu tu katika kila mwaka. Kila sadaka inatolewa sambamba na kila sikukuu ambayo ama ya Pasaka au Pentekoste au Sikukuu ya Vibanda. Soma jarida lisemalo Utoaji wa Zaka [161] na majarida shirikishi yake kama vile:

. Siku ya Makutaniko [139];

. Utaratibu kuhusuMeza ya Bwana [157];

. Jinsi ya Kuadhimisha Sikukuu [056];

. Amri ya Kwanza: Dhambi ya Shetani [153];

. Maagano ya Mungu [152];

. Dhambi ya Onan [162];

. Sheria na Amri ya Kwanza [253];

. Sheria na Amri ya Nne [256].

 

Unapaswa sasa kuwa tayari Kushiriki Pasaka tayari kushiriki Meza ya Bwana. Soma jarida la Ushirika wa Meza ya Bwana [013]. Majarida yafuatayo niya umuhimu kwa wakati muafaka kutumika kwa Sikukuu ya Pasaka na Mikate isiyotiwa Chachu. Sadaka ya Mganda wa Kutikiswa lazima itolewe saa tatu kamili (3:00) asubuhi, siku ya Jumapili ya Sikukuu ya Mikate isiyotiwa Chachu.

 

Je, ni kwa namna gain Mungu aliwakomboa Israeli siku ya Pasaka? Jisomee jarida la Musa na Miungu ya Misri [105]. je, ilikuwa inafanyikaje ili kuishinda dhambi? Soma majarida haya mengine yasemayo:

. Chachu ya Kale na Mpya [106a];

. Sikukuu ya Mganda wa Kutikiswa [106b];

. Msamaha [112].

 

Muunganiko katika Historia ya Wokovu: zisemavyo Gombo Tano  

Je, ni kwa namna gani historia ya Esther inahusiana na wokovu wa Waisraeli? Kifungu hiki kwa kawaida husomwa wakati wa sikukuu ya Purimu na Wayahudi. Lakini hata hivyo, ni wazi kabisa kuwa ina chimbuko la Kimasihi na kazi yake katika wokovu wa Yuda ni sawa kabisa kusema ni kifungu kihusucho Pasaka. Wimbo uliobora kwa kawaida himbwa wakati wa Pasaka ambayo inawakumbusha Israeli kumfuata Mungu Mwenyezi machoni pa wafanya ibada wa Kiyahudi. Lakini hata hivyo, tunaposoma kitabu cha Wimbo Uliobora, tunaona uhusiano kati ay Masihi na mwanamke ambaye amemposa. Mwanamke huyu tunaona kuwa ni Yuda kama mwili halisi wa Israeli lakini ina maana iliyojificha kwa ndani zaidi ambayo ni mwili wa kiroho ambao ni Kanisa.hivyo basi, Wimbo Uliobora ni kiunganisho kati ya Pasaka na Pentekoste. Kitabu cha Ruthu ni nakala inayohusu Pentekoste au Shevuoth. Inamzungumzia mwongofu mnyenyekevu wa Kimoabu ambaye aliwaacha watu wake na kuishi maisha ya kifukara katika Israeli kisha akafanyika mzao miongoni mwa wahusika katika mstari wa ukoo wa kifalme wa Daudi. Hadithi hii inahusu Kanisa kama taifa lenye wafalme na makuhani. Kitabu cha Maombolezo husomwa siku ya 9 ya mwezi wa Abu (Ab) au katika maadhimisho ya kuanguka kwa Hekalu, na Muhubiri husomwa katika mwezi wa Sukoti (Sukkoth) au Sikukuu ya Vibanda. Soma jarida lisemalo: Mafafanuzi ya Easter [063].

 

Kwa jinsi hii basi inatupelekea kutujenga katika Pentekoste. Orodha itatolewa kwa kutenganishwa na itakavyokuwa orodha ya masomo ya Zaburi:

Zaburi 1-41 (Kitabu cha Mwanzo cha Zaburi). Kazi hii inaweza kusomwa kutoka mwishoni mwa Sikukuu ya Vibanda. Soma Kitabu cha Kutoka cha Zaburi kwa Pasaka na hadi Pentekoste.

Zaburi 42-49, Kwa Maangamizi ya Israeli.

Zaburi 50-60, Kwa ajili ya Mwokozi (rejea kwenye sura ya 45 vilevile).

Zaburi 62-72, Kwa Ukombozi wa Israeli. Zaburi hizi zote zinatupelekea kwenye Pentekoste.

 

Usomaji wa majarida unapaswa umalizikiwe kwa kufuata mwandamano mkamilifu unaotangulia Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu. Wajibu wa maandalizi kufanya Pasaka kamilifu yanatuama juu yako, na jinsi uhusiano wako ulivyo kwa Mungu kupitia Yesu Kristo katika Roho Mtakatifu. Hakuna yeyote atakayefanya jambo hili likamilike kwa ajili yako.

 

q