Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu

[286]

 

 

 

Maana ya Mwaka wa 2000

(Toleo La 1.0 20000101-20000101) Imerekodiwa Kwenye Tepu

 

Papa ameutangaza mwaka 2000 kuwa ni mwaka wa yubile. Mabingwa na wangwiji waliobobea wanasema kuwa kwa kweli ni mwaka 2001 hata hivyo. Je, Milenia ya kweli ni lini hasa na inamaana gani hasa? Ni nani basi anayesema kuwa ilikuwa ni mwaka 2000 hata hivyo mbali ya kasisi aliyapata mwanzo wa tarehe yake kuwa una makosa.

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Hati Miliki © 2000 Wade Cox)

 (Tr. 2014)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Maana ya Mwaka wa 2000


 


Tunatarajia kuingia mwaka 2000. Michakato na Mahangiko meingi yamefanywa kuhusu mwaka huu zaidi ya mwingine wowote kuwahi kutokea. Watu wanakimbia huko na huko wakisema kuwa Masihi anakuja na dunia inafikia mwisho wake. Waisraeli wanalisikia hili pia na wanakaribia kutok kwa watu wengi na wanapokea wageni wanaofikia kiasi ha zaidi ya milioni 2 au 3, waliokwenda huko kwenye changamoto au mchocheo wa Yohana Paulo II ili kusherehekea hii inayojulikana kama mwaka wa yubile ya Utatu.

 

Je, jambo hili la kipuuzi lina maana gani hasa? Ni kwa nini Yohana Paulo anawataka watu kufanya jambo lisiloendana na Maandiko Matakatifu na ambalo ni la uwongo mkubwa ambapo anajua na huku akijua kuwa ni uwongo mkubwa na ambao chimbuko lake ni linamakosa yaliyofanywa kwa kipindi cha takriban miaka 1600 iliyopita?

 

Jibu lake ni siasa na uanzilishwaji wa mtafaruku kwenye madhabahu ambao utashughulika na mpasuko wa kiuelewa na matarajio ya Masihi na imani kwenye unabii wa kibiblia.

 

Kanisa Katiliki la Romalimeanza kutengeneza njia na Biblia na kujaribu kuwaingiza Yuda na imani yao kwenye itikadi ya Utatu tangu mapema sana takriban miaka 600 baada ya kutangazwa kwa iliyokuwa ikijulikana kama Dola Takatifu ya Rumi mwaka wa 590 BK.

 

Kwanini tunazitumia tarehe hizi na kwanini baadhi ya watu hutumia neno AD na wengine BK na ni kwa sababu tofauti? Na ni kwa jinsi gani tunaipata kalenda hata hivyo? Je, msingi au chimbuko lake ni nini?

 

Uwekaji wa Kalenda

Je. Tuliwezaje basi kujua kuwa huu ulikuwa ni mwaka wa 2000? Inadaiwa kuwa hii ni miaka elfu mbili baada ya kuzaliwa kwa Kristo. Walakini Kristo hakuzaliwa katika mwaka wa 1 na hata kama alikuwa amezaliwa mwaka huu, basi Milenia isingekuwa imeisha hadi 2001 hata hivyo. Kuamua uanzaji wa kile tunachokijua au kijulikanacho kama mwaka 1 AD ulikuwa ni makosa ya karne hadhaa. Inawezekana kuwa Kristo hakuzaliwa mapema kabisa ya kabla ya siku ya 1 Nisani (au Abibu) ya mwaka 4 KK. Tunajua hilo kwa uhakika. Tunajua hilo kutokana na rekodi ya Biblia kuwa Kristo alizaliwa kabla hajafa Herode, na Herode alifariki kati ya siku ya 1 hadi 13 Nisani, mwaka 4 KK. Kristo alikuwa na umri wa hadi miaka miwili wakati tukio lile lilipotokea lakini kuzaliwa kwake huenda kulikuwa katika mwaka 5 BK karibu na kipindi cha maadhimisho ya Idi ya Vibanda (soma jarida la Chimbuko la Krismas na Easter (Na 235) [The Origins of Christmas and Easter (No. 235)].

 

Kwa hiyo Milenia ya pili tangu Kuzaliwa kwa Kristo ilianza siku ya 1 Nisani 1997. mwaka 2000 kwa kweli ulikuwa ni 1996, ambao ulikuwa ni miaka 3000 tangu Daudi alipoingia Yerusalemu kwa shangwe na ushindi, na ni miaka 2000 tangu mwaka kamili wa kuzaliwa kwake Kristo. Mchakato huu umeelezewa kwa kina kwenye jarida la Mchakato wa Majira ya Nyakati (Na. 272) [Outline Timetable of the Age (No. 272)].

 

Je, Makosa yalitokeaje?

Mpangilio wa kalenda ya kale zaidi tuliyonayo ni kwamba ilitungwa na Filocalus ya mwaka 354, ambayo ilikuwa ni chapisho la mara nyingine tena la ile ya mwanzoni na asilia ya mwaka 336. Damasus wa Roma alimuajiri Furius Dyonisius Filocalus ili afanye kazi kadhaa ikiwemo ya makaburi ya wafia dini (soma kitabu ha Fasihi cha Encyc. Of Religion and Ethics (ERE), art. Calendar (Christian). Kwenye maandiko hayo tunaona kuwepo na tarehe fulani zilizopewa siku na miaka ya kuzaliwa na kufa kwa Kristo.

 

Huko Italia, mnamo mwaka 536, Dionysius Exiguus alifana michakato miwili mikuwa ya ukusanyaji, mmoja ulikuwa ni wa kanuni na mwingine ni wa agizo au nyaraka za papa hadi kufikia makati wa Anastasius II (496-498) na hizi mbili wakati zilipounganishwa ziliweza kubuni au kuunda kile kinahoitwa kuwa ni maandiko rasmi ya kitabu cha Warumi ambacho kinelezea haya mengine yote (Kamusi ya ERE, Vol. 7. p. 836). Alipewa kazi ya kubuni meza ya miaka 95 ya maadhimisho ya Easter. Wakati huo na kwa millennia inayopita huko numa, utaratibu wa kuhesabu ulikuwa ni kwa miaka ya utawala wa wafalme. Hii ilikuja kuingizwa kwenye utaratibu wa kuhesabu tangu mwanzoni mwa utawala wa Diocletian, ambao ulisemekana kuwa ni mwaka wa 1 ambao ni mwaka wa 284. Dennis Mfupi, ambapo ndiyo maana ya jina lake, au Dennis Mdogo kama alivyokuwa anaitwa na marafiki zake, aliweka utaratibu wa kuhesabu tarehe kwa kuupa neno la Anno Domini na kuifanya au kuweka tarehe ya kubahatisha nay a holela kuwa ni mwaka wa 1 kwa kile alichodhania kuwa ungewezakuwa ni mwaka wa kuzaliwa kwake Kristo na kurudisha nyuma taratibu kutoka mwaka wa 1 pia. Na ndipo kilipokuja kutungwa hiki kilichokuja kujulikana hatimaye kama Kabla.ya Kristo au KK. Kisha akamwandikia askofu Petronius kwa kile tunachokijua sisi kuwa ni mwaka 531 au 247 anni Diocletiani akulalamikia utaratibu au mfumo huo. Alishindania kwamba Diocletian alikuwa ni mtesaji mashuhuri na aliyejulikana sana na wengi kuwa aliwatesa Wakristo na kwa hiyo alielezea kwenye waraka huu kuwa yeye alikuwa:

Ilipendekezwa kuhesabu na kuanzia hesabu ya miaka tangu alipotungwa mimba na kuzaliwa Bwana wetu, kwa dhumuni la kuweka msingi wa tumaini letu ijulikanayo sana na sababu ya wokovu wetu na wa mwanadamu uliowazi sana kwa kila mtu (sawa na tafsiri ya andiko hili ya David Ewing Duncan, kwenye kitabu chake cha, The Calendar, (Kalenda), Fourth Estate London, 1998, p. 100)

 

Dennis hakuuweka mwaka 0 kwenye kalenda kwenye kipindi ha mpito, kwa kuwa sifuri ilikuwa haijagunduliwa umuhimu wake.

Iwe isiwe, bali mfumo huu ulitumika kwa namna isiyorasmi kama mapokeo tusiyoyajua, wala hatujui ni wapi watu hawa walipata taarifa zake zilizozitumia kwazo kwenye uwekaji wa hesabu zao. Hata hivyo, yeye alikuwa ni wa kwanza tunayemfahamu kuwa ndiye aliye aliyeweka mfumo wakati alipotengeneza meza au chati za Easter zijulikanazo kama, anni Domini nostri Jesu Christi (miaka ya Bwana wetu Yesu Kristo) 532-627 (ibid.).

 

Alikuwa ni huyu rafiki yake Cassiodorus ambaye kwanza alitumia utaratibu ulio kwenye kazi iliyochapishwa kwenye vijitabu vyao katika mwaka 562 vya jinsi ya kuamua siku ya Easter na tarehe nyingine; maarufu kama Computus Paschalis.

 

Kimsingi mfumo huu ulizuiwa na Wakristo waliopenda na kuipendekeza hii anni Diocletiani kuwa ni kama walivyoielezea ndani yake kuwa ni kama Zama ya Wafia dini na walihesabu na kuzipa siku na tarehe vitu vyote kwa mtindo na utaratibu huu (ukurasa huu huu wa 101). Kwa kweli, Kanisa la Wakristo wa Koptiki wa Misri bado wanahesabu tarehe zao kuanzia kipindi hiki kijulikanacho kama Zama ya Wafia dini na kwa wao ni mwaka wa 1716. Kwa taratibutaraibu, utaratibu uliopo sasa ulienea hadi Utaliano kote kwa miongo kadhaa iliyofuatia na hatimaye kwa taratibu sana ulimwenguni kote (ukurasa huohuo). Wakatoliki waliiingiza nchini Uingereza tangu mwaka 595 na baada ya kuukubali kwake kwa mkataba wa shuruti wa huko Whitby mwaka 664 kutokana na imani ya kweli. Imani hii ilifika huko Gaul kwenye karne ya nane na haikuwa kwenye matumizi yaliyoenea huko Ulaya hadi katika karene ya kumi. Kwenye baadhi ya majimbo yaliyoelezwa na sehemu ya Uhispania haikuweza kuja kutumika hadi kwenye miaka ya 1300. Uwekaji wa kifupisho cha KK (BC) kuwa na maana ya Kabla ya Kristo hakikuwa kikitumika hadi kufikia mwaka 1627 wakati mtaalamu wa mambo ya nyota au mnajimu Denis Petau alipoutambulisha ua kuufundisha mfumo huu kwenye Chuo cha Clermont (the Collège de Clermont) huko Paris (Duncan ibid., p. 101-102).

 

Uataratibu ulioposasa wa kuhesabu tarehe ilikujakuunea kwa kasi pande za mashariki mwa dunia. Matengenezo mapya ya Kalenda yaliyofanyika hini ya Gregory XIII hayakuweza kusahihisha makosa ya mfumo huu. Inaonekana kwamba hayakuelezewa mengi kwenye maandiko yoyote ya hivi karibuni. Hata hivyo, makosa haya yanawezakuwa hayajulikani kwa kuwa yanaendana na lengo la utendaji wake usiokuwa na siku au tarehe halisi nay a uhakika na kalenda kueleweka.

 

Mwaka Mpya

Mwaka Mpya ulikuwa hausheherekewi siku ya tarehe 1 Januari na waliokuwa wanaitii Biblia au imani ya Kanisa. Ilianzishwa kutoka Roma ikitokana na mfumo wa Julian. Ilikuwa haisheherekewi huko Uingereza hadi alipoileta Normans akiwa pamoja nao mwaka 1066. Iliondolewa na sio yote kwa wakati usio mrefu zaidi na baada ya Mwaka Mpya kurudi nyuma hadi mwezi Machi, tarehe 25 Machi ambayo ilikuwa ndiyo siku ya ikwinoksi ya kale iliyoingizwa pia kwene Kalenda ya Wasamaria. Hii ilibakia hivyo hadi karne ya kumi na nane (kwa habari zaidi soma jarida la Mwezi Mwandamo na Mwaka Mpya (Na. 213) [The Moon and the New Year (No. 213)].

 

Mwaka Mpya wa kweli kwa mujibu wa Biblia ni mwandamo wa mwezi wa Abibu, ambao ndio mwezi wa kwanza wa mwaka na unaandama katikati ya miezi ya Machi na Aprili kwa mujibu wa kalenda hii ya kidunia inayotokana na mizunguko ya Mwezi na Jua.

Kwa hiyo ndiyo maana ulimwengu wa magharibi unafuata kalenda ya kipagani iliyoanzishwa na Warumi inayoitumia tarehe kuwa ni Mwaka Mpya kinyume na agizo kuu lililotolewa na Mungu na sawasawa na utaratibu wa miaka, ambayo inaiweka kando miaka minne kwenye uhesabuji wake.

 

Yubile

Kuutangaza mwaka 2000 kuwa ni yubile ni jambo lililo na makosa ya wazi kabisa. Yubile inahesabiwa kutoka na maandio kadhaa ya Biblia na zinaangukia kwenye miaka ya 27 na 77 ya zama zetu hizi.

Jinsi ya kuzipata hizi jubile imeelezwa kwa kina kwenye jarida la Usomaji wa Torati Ulivyofanywa na Ezra na Nehemia (Na. 250) [Reading the Law with Ezra and Nehemiah (No. 250)].

 

Yubile inayofuatia itakuwa katika mwaka wa 2027/8 na kuangukia kwenye Idi ya Upatanisho na itachukua miezi kumi na miwili itakayoishia kwenye nyakati za upandaji wa mashamba kwa ajili ya mavuno ya Pasaka ya mwaka unaofuatia.

 

Kwa hiyo tuna tarehe ya uwongo ya mwaka. Mwaka Mpya ulio kinyume kabisa na sheria na amri za Mungu, na yubile isiyoendana na utaratibu aliouweka Mungu na inayoendana kinyume kabisa na maelekezo ya Biblia ya utaratibu wa jinsi ya kuzipata yubile.

 

Je, makosa kama haya anakusudia nini?

Sio kana kwamba hawajui ukubwa wa makosa na matendo yao. Ni nini basi makusudi yake? Ni kwa nini wanafanya hivi? Je, hawamuogopi Mungu? Jibu ni hapana. Hawana hofu ya Mungu ndani yao. Maadhimisho haya ya hii millennia yao ni utimilifu wa unabii mwingine wa Masihi.

 

Luka 18:8 kuna unabii inaoelezea kuhusu kupotea kwa imani kutakakotokea katika siku za mwisho.

Luka 18:7-8 Na Mungu, je! Hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku, naye ni mvumilivu kwao? 8 Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?

 

Itawezekanaje kuifikia? Kumbuka kuna mambo mawili yanayoelezewa kwenye usemi huu. La kwanza, linaongelea kuhusu mateso ya wateule. Mateso haya yatakayokuwa kwenye Mhuri wa Tano wa kitabu cha Ufunuo yataendelea hadi kurudi kwa Masihi kuwaokoa wale wanaomgojea kwa hamu na wakiwa kwenye imani thabiti.

 

Andiko lililo kwenye Mathayo linaonyesha kwamba tutakuwa tukikimbia huku na huko wakati huu wa kipindi cha mateso hadi pale Mwana wa Adamu atakapokuja.

Mathayo 10:23 Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia, Hamtaimaliza miji ya Israeli, hata ajapo Mwana wa Adamu.

 

Mateso ya Mhuri wa Tano yalianza tangu karne ya ishirini. Awamu za kwanza za mwanamke aliye jangwani anayefuatwa na joka wa Ufunuo 12 (hususan 12:17) ilikuwa ni ya kipindi cha miaka 1260 ya kudumu kwake iliyojulikana kama Dola Takatifu ya Roma iliyojitangazia na kuanza tangu mwaka 590 hadi 1850. Katika kipinhi kicho kanisa lilikimbia kutoka mji mmoja hadi mwingine na kutoka taifa moja hadi linguine au lilijiendesha kwa sirisiri chini kwa chini hasa huko Ulaya. Awamu iliyofuatia ilikuwa ni ile ya mauaji ya kuangamiza binadamu maarufu kwa jina la Holocaust. Awamu hii ilidumu kuanzia mwaka 1927 hadi 1945 huko Uturuki na Ulaya na mwaka 1953 huko Urusi yakiongozwa na Stalin. Makanisa ya Wakatoliki la Roma na Kilutheri yalitumika kama chombo kizuri cha kutekeleza mauaji haya. Waliwasaidia wote wawili, yaani Bunge maalumu la chama cha Nazi lililoshiriki kupitisha kufanyika kwa mauaji maarufu kama SA na kundi lililojulikana kama schutzstaffel lililohusika kutoa walizi kuwalinda Manazi likijulikana kama SS katika utekelezaji wao na waliwasaidia kutoroka waalifu waliofanya matendo ya jinai kwenye vita ya walinzi hawa wapambe wa Kinazi au SS mwishoni mwa Vita Kuu ya 2 ya Dunia (soma jarida la Holocaust: Mhuri wa Tano wa Mateso [The Holocaust: The Fifth Seal of Persecution)].

 

Mauaji haya ya Holocaust yaliratibiwa na kuchochewa na kanisa kuu la Kiutatu yalikusudia kuondoa na kukomesha ushikaji wa Sheria za Mungu huko barani Ulaya na warithi wao watajaribu sasa kuiondoa maeneo mengine yote ya ulimwenguni.

 

Ili kulifikia lengo hili wanalazimika kuanzisha mfululizo wa matukio yanaokusudia kuonyesha kwamba nabii zilizo kwenye Biblia zimekosa kueleweka au zimeeleweka vibaya na ujio wa Masihi haukukusudiwa kuwa kwenye miaka hii ya 2000 au kuwa kwenye yubile ya arobaini ambacho ni kipindi maalumu kilicho kwenye mpangilio kwa mujibu wa unabii wa Ishara ya Yona.

 

Bwana Wangu Anachelewa Kuja

Unabii wa kuchelewa umerudiwa kwenye maandiko ya Mathayo 24:48 na Luka 12:45.

Mathayo 24:48 Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;

Tunaona kifungu hiki hapa kisemacho Bwana Wangu anachelewa kuja kwake. Tunjua kuwa Mungu atamtuma Kristo kwa wakati wake muafaka na uliokusudiwa. Kwa hiyo, kutakuwa na jambo fulani litakalotokea ambalo litatoa ashirio la kuonekana kuchelewa kwa ujio wa Masihi katika siku za mwisho litakalosababisha kwa kiasi kikubwa kubadilisha au kupotosha namna ambayo mtazamo wa Wakristo na kuanza kusalitiana.

Hebu na tuliangalie andiko la Luka.

Luka 12:35-49 Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka; 36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara. 37 Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia. 38 Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao. 39 Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa. 40 Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu. 41 Petro akamwambia, Bwana, mithali hiyo umetuambia sisi tu, au watu wote pia? 42 Bwana akasema, Ni nani, basi, aliye wakili mwaminifu, mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya utumishi wake wote, awape watu posho kwa wakati wake? 43 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta anafanya hivyo. 44 Kweli nawaambia, atamweka juu ya vitu vyake vyote. 45 Lakini, mtumwa yule akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia kuja, akaanza kuwapiga wajoli wake, wanaume kwa wanawake, akila na kunywa na kulewa; 46 bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wasioamini. 47 Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana. 48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi. 49 Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi?

Kwa hiyo tunaona hapa sababu ya kuchelewa. Kristo alitaka iwe imekwisha washwa tayari. Watu wanaokuchukulia kuchelwa huku kama sababu ya kuwekea udhuru wa kuwaadhibu wale ambao wanajaribu pia kumtumikia Mungu kupitia Kristo wataondolewa na kutupwa waliko waovu na wasiowaaminifu. Hii inapasa iwe ni onyo tosha kwa makanisa makongwe ya Waorthodox wa zamani waliowatesa na kuwaua na kuwaadhibu kwa mateso makali wateule wa Mungu, kwa kuwa tu walikataa kuzikubaliana na mtazamo wa Wakatoiki na Waprotestanti wa kutaka kuzibadilisha na kuzipotosha Sheria za Mungu. Mtazamo huu ambao uko mioyoni mwa wapinga usemitiki ulikuwa ndiyo sababu ya kutokea mauaji haya makubwa ya kutisha yajulikanayo kama Holocaust na mateso ya Kanisa na Wayahudi walioishi maeneo yote ya Ulaya (soma kitabu cha S. Kohn, cha Wasabato wa Transylvania, [The Sabbatarians in Transylvania], (foreword by W. Cox, trans. T. McElwain and B. Rook, CCG Publishing, 1998).

 

Nia ni kuweka kigezo kikubwa kuuhusu mwaka 2000 kufuatia na makosa ya kimhesabu ya kalenda na kujaribu kuanzisha upinzani mkubwa wa hitimisho au kilele. Tutajionea kukijitokeza matatizo yaliyobuniwa ili kuondoa heshima stahiki ya wanafunzi au wasomaji wa Biblia na kuzitupilia mbali Sheria za Mungu kwenye uovu. Wakati wa kuanzishwa kwa mkakati wa Agizo Jipya la Ulimwengu maarufu kama New World Order, msukumo utaletwa wa kubebwa na Washika Sabato wote na ambao sio waamini Utatu. Mwaka huu unamaanisha kuwa ni mwanzo wa mchakato huu. Sababu za kuanzishwa tena kwa Baraza la Hukumu na Mateso ya kidini ziliwekwa kwenye waraka maalumu wa kipapa wa Yohana-Paulo mwaka 1993, na ambao ulipingwa na watafakari maarufu wa kanisa hili Katholiki la Roma kama vile kina Morris West.

 

Tunapaswa wote tuwekwe pamoja kwenye mchakato huu wa mfumo mmoja wa ulimwengu ambao ni mgeni na haupo kabisa kwenye Biblia na kwenye Torati ya Mungu. Papa huyu ameweka mkakati thabiti kuhusu jambo hili. Na ndiyo maana nabii wa Kikatoliki Malachy alimuita yeye jina lake kuwa ni Kutoka Kwenye Kazi ya Jua, na papa anayemfuatia atajionea hii ikiwa inaendelea vizuri na kamilifu kama Kutoka Kwenye Utukufu wa Mzabibu (soma jarida la Papa wa Mwisho: Alivyoelezewa na Nostradamus na Malachy (Na. 288) [The Last Pope: Examining Nostradamus and Malachy (No. 288)].

 

Ukweli wa mambo ni kwamba mfumo huu na dini yake ya uwongo una kipindi cha miaka michache tu mbele yetu cha kwenda kwenye Ishara ya Yona (soma jarida la Ishara ya Yona na Historia ya Ujenzi Mpya wa Hekalu (Na. 13) [The Sign of Jonah and the History of the Reconstruction of the Temple (No. 13)]. Kisha ndipo mfumo wote wa makasisi wavaa majoho meusi wa Baali na imani ya kumuabudu Mungu Mke wa dini za kuliabudu jua vyote hivyo vitaangamia (soma jarida la Ujumbe wa Ufunuo 14 (Na. 270) [The Messages of Revelation 14 (No. 270)].

 

Yerusalemu ilizingirwa na majeshi siku ya 1 Abibu, 70 BK, sawasawa na unabii wa Ishara ya Yona, miaka arobaini baada ya kifo cha Masihi. Uliangamizwa kabisa sawasawa na majuma sabini ya miaka iliyotabiriwa kwenye Danieli 9:25-26. Yerusalemu utazingirwa tena na majeshi ya mbinguni kwa kumilikiwa kikamilifu chini ya Masihi mnamo mwaka 2027, sawasawa na unabii wa Ishara ya Yona na ni yubile 40 kamili tangu kutangazwa kwa Mwaka wa Bwana Uliokubaliwa wa yubile iliyofuatia kuzaliwa kwa Masihi.

 

Mwaka 2000 na kwa kweli ni mwaka 2004 ni angalau tu na hauna uhusiano na kalenda ya kweli au na sheria za Mungu na ushuhuda ya Kristo. Ni kitu bandia tu kilichoweka na cha kimapepo kinacholenga kushusha hari ya mioyo ya wateule na kutokea kana kwamba ionekane kana kwamba Kristo amechelewa kurudi kwake. Umebuniwa hivyo ili ionekane kwamba Kanisa la Orthodox liwe na uendelevu wa namna yake baada ya kufanya kioja cha kwamba hawa Wanautatu na waabudu Jumapili wameunda ili kumuasi Mungo na Masihi. Hatua yao inayofuatia hapo mbele ni kumtangaza au kumrasimisha Munhu wao Mke ajulikanaye kama Malkia wa Mbinguni achukue mahala pake pa zamani kwa kutumia mbinu bandia ya kumuita jina la Mariamu (kwa kisingizio cha Mariamu aliyekuwa ni Mama halisi wa Kristo). Imani waliyonayo ni nakala ya ibada za Easter au imani za Ishta za waabudu Baali-Ashtorethi chini ya Yezebeli akiwa kama kuhani mwanamke, aliyeuawa na Eliya. (soma majarida ya: Bikira Mariamu na Familia ya Yesu Kristo (Na. 232), Chimbuko la Krismas na Easter (Na. 235), Ndama wa Dhahabu (Na. 222)  Jeshi la Gideoni na Siku za Mwisho (Na. 22) na [The Virgin Mariam and the Family of Jesus Christ (No. 232), The Origins of Christmas and Easter (No. 235), The Golden Calf (No. 222), and Gideon's Force and the Last Days (No. 22).

 

Kazi yetu ni kuishikilia kwa bidii imani iliyotolewa kwa watakatifu mara moja tu na kuionya dunia kwa kufunguliwa au kufikia hitimisho lake kutakakofanyika ghafla na kwa mara moja.

 

q