Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[CB10]
Ibrahimu na Sara
(Toleo La 2.0
20030923-20070123)
Bwana
akamwambia Abramu, “Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya
baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; nami nitakufanya wewe kuwa taifa
kubwa, na kukubariki." Jarida
hili limetokana na sura ya 6 ya jarida la Hadithi za Biblia [The Bible Story
Volume 1] iliyoandikwa na Basil Wolverton, na kuchapishwa na Idara ya
Machapisho ya Ambassador College, na majarida menguine ya Abramu na Sodoma (Na.
91) na Melkizedeki (Na. 128), yaliyochapishwa na CCG.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2003, 2007 Christian Churches of God, ed. Wade
Cox)
(Tr. 2014)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ibrahimu na Sara
Tunaendelea hapa kutoka
kwenye jarida la Nimrodi na Dini ya Uwongo (Na. CB9).
Miaka miwili
baada ya gharika kuu, wakati mwana wa Nuhu Shemu alikuwa na umri wa miaka 100,
Shemu alikuwa na mtoto aliyeitwa Arfaksadi (Mwanzo 11:10). Wakati Arfaksadi alipokuwa
na uri wa miaka 35, alikuwa na mtoto aliyeitwa Sela (Mwanzo 11:12). Vizazi kadha
vilienda kwa jinsi hii. Wakati ya takriban miaka 300 kupita, mtu aliyeitwa
Abramu alizaliwa. Jina la baba yake aliitwa Tera (Mwanzo 11:26).
Abramu alilelewa
kwenye mji au mjini huko Mesopotamia (Matendo 7:2) ulioitwa Uru, sio mbali sana
na mahali ambapo Nimrodi alianza kuujenga mnara wa Babeli (Mwanzo 11:2). Hapa
Abramu, kama alivyokuwa Nuhu, alijifunz kuzitii Sheria za Mungu, wakati kwamba
watu wa ulimwengu ule walikuwa ni waabudu sanamu na wakiishi mbali sana na njia
au maagizo ya Mungu. Abramu alikuwa ni mmoja wa wachache ambao hawakuzishiriki
imani hizi za kipagani. Akiwa huko Mesopotamia Abramu alikuwa na maono yake ya
kwanza au wito kutoka kwa Mungu kuondoka na kuiacha nchi yake na watu wake (Matendo
7:2). Wakati alipokuwa na umri wa takriban miaka sabini na tano, Abramu alikuwa
tena ameambiwa aondoke na familia yake na kwenda nchi nyingine.
Bwana akamwambia
Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako,
uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; (Mwanzo 12:1)
Abramu anamtii
Mungu
Mungu alimuahidi
Abramu kwamba kama atatii amri na maongozi yake yote, basi atajibarikia na
atafanyika kuwa baba wa taifa kubwa (Mwanzo 12:2-3). Kipindi ambacho taifa hili
litafurahia baraka fulani za muhimu na za aina yake, Abramu hakujua ni nchi gani
anayokwenda na ipoje, na pia hakujua ni Baraka gani watakayopewa watu wake,
lakini alimuamini na kumtumaini Mungu na akamtii.
Akiwa pamoja na
mke wake, Sarai, Abramu alimchukua na kwenda naye mpwa wake Lutu na mke wa
Lutu, na wachungaji ili wakachunge mifugo yao pamoja na kondoo zao na watu
mahiri katika shughuli za kuchunga ili wachunge mifugo ya ng’ombe. Sio jambo
dogo kwa Abramu kuondoka na kuiacha familia yake na mali zao na kwenda nchi ya
mbali (Mwanzo 12:4).
Baada ya majuma
mengi ya kusafiri, walifika kwenye nchi ya Kanaani, wakati Mungu alipomwambia
Abramu kuwa anapaswa aondoke (Mwanzo 12:5). Kanaani ilikuwa ni nchi yenye
rutuba sana ambayo ilikuwa na udongo mzuri sana wa kulima na kukuzia vitu.
Lakini watu wan chi ile walikuwa wabaya na watenda dhambi sana. Kwa hiyo Mungu
alisababisha baa la njaa lije kwenye nchi ile. Njaa hii ilitokea mara tu baada ya Abramu kufika
huko Kanaani (Mwanzo 12:10). Ukosefu wa mvua ulisababisha matunda na miti, uoto
wa mbogamboga na nyasi kukauka. Kulikuwa na chakula kidogo kwa ajili ya wanyama
waliokuwanao kina Abramu na Lutu na ambao waliwaleta huko Kanaani. Na
kusingekuwa na ng’ombe na kondoo, kusingekuwa na chakula cha kutosha kwa Abramu
na wengine wote aliokuwanao.
Abramu anaenda
Misri
Habari zililetwa
na wasafiri kwamba katika nchi ya Misri hakukuwa na uhaba wa mvua, kwa hiyo
Abramu na familia yake walishuka na kwenda huko Misri ili kuokoa mifugo yao.
Mungu alikuwa amekwishaweka agano na Abramu la kumpa nchi na kumpa chakula
palepale alipokuwa, lakini bado hakuwa na imani ya kutosha kukaa pale na
kumtumainia Mungu. Hatimaye tutaona kwamba Ibrahimu alikuwa ni mtumishi
mwaminifu na rafiki wa Mungu kupitia utii wake. Soma jarida la Ibrahimu na Isaka: Sadaka Adilifu
(Na. CB11).
Katika nchi ya
Misri ustaarabu mkubwa ulianza na kuwepo mara tu baada ya gharia kuu. Wafalme
wa Misri, au Mafarao, walikuwa matajiri wakubwa licha ya ibada zao za sanamu
walizokuwanazo. Walifaidi mema yote yaliyomea kutoka ardhini. Chochote walichopungukiwa
walikichukua kutoka kwa wengine.
Kwakuwa Sarai alikuwa
ni mwanamke mzuri sana, na Abramu alikuwa anamuogopa mfalme wa Misri na
kumdhania kuwa huenda angempenda na kumchukua awe miongoni mwa wake zake wengi,
alimuomba Sarai aseme kuwa yeye ni dada yake badala ya kumwambia kuwa ni mke
wake (Mwanzo 12:12-13). Sarai kwa kweli alikuwa ni mke ambaye alikuwa ni
dada-binamu na Abramu, kwa kuwa baba yake alikuwa pia ni baba yake Abramu,
lakini mama yake hakuwa ni mama wa Abramu. Abramu alitaka kuitumia fursa hii
kwa kunena nusu ukweli kwakuwa aliogopa kwamba kama itajulikana kwamba alikuwa
ni mume wa Sarai, Wamisri wangeweza kumuua ili kwamba Sarai awe huru kuolewa.
Mfalme ambaye Abramu
alikuwa anamuogopa akatokea maramoja. Ingawa alikuwa na umri wa takriban miaka 65,
Sarai bado alionekana kuwa kama mwanamke kijana na mzuri sana. Alikuwa anavutia
sana kumuangalia. Kabla ya hapo ilisemekana au kulikuwa na uvumi kwamba
mwanamke huyu asiye wa kawaida angepewa upendeleo wa aina yake na Farao, ambaye
aliamuru kuwa aletwe kwenye jumba lake la kifalme.
Farao alifurahishwa
sana na mwonekano na umbo la Sarai na akapanga awe mke wake, na akampa Abramu
zawadi zenye thamani kubwa zikiwemo wanyama wa kufuga, watumishi na makazi
mazuri. Lakini Abramu alitenda dhambi kwa kuwa aliongopa na Farao alitenda dhambi
kwa kumchukua mke wa mtu mwingine. Kwa ajili hii Mungu akaiadhibu kwa magonjwa
nyumba ya Farao. Farao akamkasirikia sana Abramu, lakini akamrudisha Sarai kwa
mume wake, na akawaamuru watu wake wahakikishe kwamba Abramu na familia yake na
mali zake wasindikizwe kwa usalama wanapotoka Misri (Mwanzo 12:14-20). Tunaweza
kuona hapa kwamba ndoa na Sheria za Mungu zilijulikana hata zama hizo.
Kurudi Kanaani
Abramu na Lutu na
wake zao na watumishi wao ndipo waliondoka na mifugo yao na kurejea Kanaani.
Abramu akaenda moja kwa moja mahali apokuwa amemjengea Mungu madhabahu
alipokuja mara ya kwanza huko Kanaani. Ale akaomba msamaha na nguvu (Mwanzo
13:4).
Katika kipindi
hik njaa katika Kaaani ilikuwa imeisha. Mifugo na wanyama aliokuwanao Abramu na Lutu iliongezeka sana. Mungu alimbariki Abramu na Lutu pia kwa
kuwa alikuwa ni sehemu ya familia ya Abramu. Lakini kwa kuwa wanyama walikuwa
ni wengi sana, watumishi wa Abramu na wa Lutu walianza kugombea mahali pa
kuwafugia na malisho, sehemu zilizokuwa na majani mengi mazuri na maji. Abramu
hakupenda kutokee matatizo na mtengano wa kudumu na Lutu, kwa hiyo akamshauri
achague aende sehemu nyingine tofauti nay eye akaishi huko.
Mungu alimuahidi
nchi ile Abramu. Ilikuwa ni haki yake Abramu achague kwanza mahali alipotaka
kwenda ili wanyama wake wakapate malisho, lakini kwa moyo usio na ubinafsi
alimwambia Lutu achague kwanza. Lutu akatazama chini kwenye udongo mzuri na
wenye utajiri kwenye bonde la Mto Yordani, na akasema anaitaka nchi ile. Hii
inamaanisha kwamba alimwachia Abramu uwanda wa juu, lakini Abramu aliridhika
kwa kuwa alimuona Lutu alikuwa ameridhika (Mwanzo 13:5-12).
Hatimaye Mungu
akanena na Abramu tena akimwambia kwamba nchi yote anayoiona pande zote itakuwa
yake milele nay a watoto wake, ambao idadi yao itakuwa kama mchanga au mavumbi
ya Dunia. Kisha Abramu akaliondoa hema lake akaenda Hebroni na huko akamjengea
BWANA madhabahu (Mwanzo 13:14-18). Hii ilikuwa ni ahadi ya ajabu kwa Abramu, ambaye
ata hivyo kwa kipindi hiki alikuwa anakaribia umri wa miaka 80 na akiwa hana
watoto.
Wakati huohuo
Lutu na familia yake wakatweka hema zao karibu na mji wa Sodoma kwenye bonde tajiri
la Yordani. Lutu alidhani kuwa amefanya uchaguzi sahihi na wa busara kwa kwenda
kwake kule. Hakujua kuwa atakumbana na matatizo makubwa na watu wanaoishi huko.
Walikuwa ni wagomvi na wenye tabia mbaya zisizo za kawaida. Akiwa kama
mchamungu, Lutu asingepaswa kwenda na kuishi karibu na watu wale.
Vita inalipuka
huko Kanaani
Muda mfupi tu
baada ya Lutu kwenda maeneo ya Sodoma, vita ikaanza kati ya wafalme wa miji
mitano ya bonde la Yordani na wafalme hawa wane wan chi hii walikuwapo wakati Nimrodi
alipoanzisha ufalme wake. Wafalme wanne waliombali na Yule mwingine walishinda vita.
Watu walioishi kwenye miji ya mabonde makuu mawili, yaani miji ya Sodom na
Gomorrah, walifukuzwa na kukimbilia milimani walikuwa ni baadhi ya wale
walioponyoka na kuokoka. Wengi wao walikamatwa na kufanywa watumwa wa
waliowashinda. Miongoni mwa hawa mateka walikuwa ni Lutu, familia yake na
watumishi wake. Mali zote za Lutu walimnyang’anya na zikachukuliwa.
Wakati ujumbe
ulipomfikia Abramu kuhusu yale yaliyotokea, Abramu alitoka na kuwafuata wale
wafalme walioshinda akiwa na wanaume wa vita takriban 318 (Mwanzo 14:14). Ilihitaji
ujasiri kukabiliana na jeshi lenye wanaume wengi zaidi kiasi kile kuliko wale
aliokuwanao Abramu. Lakini Abramu alimwangalia Mungu amsaidie na Mungu
alimsaidia kwa kumpa fursa ya kuizunguka ki kimyakimya ngome ya wafalme wanne
washambulizi muda wa usiku. Watu wao walichukuliwa kwa mshangao. Kwenye giza
hawakuweza hawakuweza kusimulia ni kwa kiasi gani yale majeshi yalikuwa yanawashambulia.
Kwa kuogopa kwamba huenda walikuwa ni wengi sana, walikimbilia milimani karibu
na Dameski hadi ande za kaskazini, wakiwaacha nyuma mateka na mateka waliotekwa
kwenye bonde la Yordani (Mwanzo 14:13-16).
Mfalme wa Sodoma akaja
pamoja na watu waliobakia ili kupa heshima Abramu kwa kile alichowafanyia maadui.
Hata hivyo, hakujua kwamba Abramu alifanya hivyo kwa sababu ya Lutu na familia
yake. Mkutaniko huu ulifanyika mara moja karibu na mji wa Salemu, ambao
hatimaye ulikujaitwa Yerusalemu.
Melkizedeki, mfalme
wa Salemu, pia alijitokeza kwenda kukutana na Abramu. Watumishi wa Melkizedeki
wakamletea mkate na mvinyo Abramu na watu wake mashujaa (Mwanzo 14:13-16). Melkizedeki
akambariki Abramu kwa kuwaokoa watu ambao walikuwa mateka. Melkizedeki alikuwa sio
mfalme tu bali pia alikuwa ni kihani wa
Mungu Aliye Juu Sana (Waebrania 7:1).
Inapendeza kujua
kwamba Masihi alipaswa kuja na kuwa kuhani wa milele baada ya utaratibu wa Melkizedeki.
Yeye ni Kuhani Mkuu wa milele, lakini hakuwa Melkizedeki aliyekutana na Ibrahimu.
Yeye alikuwa ni kuhani mwingine wa Namna ile (Waebrania 7:11). Yesu alikwenda
kama mtangulizi kwa niaba yetu. Hii inamaana ya kwamba inatupasa sisi pia kuwa
makuhani wa Namna ile. Ukuhani wa Melkizedeki ni sehemu ya ahadi ya Mungu (Waebrania
6:17-20).
Bwana ameapa, Wala
hataghairi, Ndiwe [Masihi] kuhani hata milele, Kwa mfano wa Melkizedeki (Zaburi
110:4)
Maana ya mkate na
divai au mvinyo uliotolewa na kupewa Ibrahimu, inahusiana moja kwa moja na Mkate
na Divai au mvinyo ulioanzishwa kutumiwa na Masihi, kwenye Mlowa Meza ya Bwana.
Tuko hili lilionekana kuelekea kwenye kutolewa kwa Roho Mtakatifu chini ya
huduma mpya ya kikuhani wa Aina ya Melkizeeki, kama ulivyoanzishwa na Masihi.
Abramu alimpa Melkizedeki
fungu la kumi au sehemu ya kumi ya vitu vyote vilivyschwa na washambuliaji na
ambao walikimbia ingawaje Abramu hakujichukulia chochote kiwe mali yake (Mwanzo
14:20-24). Hii ni kutuonyesha kwamba uzao wa Ibrahimu watatoa zaka zao kwa
makuhani. Sheria ya Mungu ta utoaji zaka inasema kuwa mtu yeyote anayeshindwa
kutoa zaka ya mapato yake kwa makuhani wa Mungu anamuibia Mungu (Malaki 3:8). Mali
zote tulizonazo ni za Mungu. Utoaji wa sehemu ya kumi kumrudishia Mungu ni moja
ya njia sahihi za kuonyesha kumtii na kumheshimu yeye.
Mfalme wa Sodoma alitoa
na kumpa zawadi Abramu kwa chochote alichokifanya, lakini Abramu alikataa
kupokea vitu hivyo vyote. Litamani na kuzitaka Baraka za Mungu za utajiri wa
mfalme wa kidunia alizozitoa. Inafurahisha kuona kwamba watu wa Sodoma
walibarikiwa hapa kwa sababu ya Abramu, hata kama walikuwa wanaishi maisha
yaliyo kinyume kabisa na Sheria za Mungu.
Ahadi nyingine kwa Abramu
Miaka kadhaa
mingine iliyofuata, wakati Abramu akiishi maisha ya amani nyingi hemani kwake
kenye milima ya juu ya bonde la Yordani, Malaika wa Bwana alikuja tena na
kuongea naye kwenye maono. Alimuambia kwamba kwasababu ya utii wake basi
atakuwa baba wa taifa kubwa. Abramu na mke wake walikuwa wanaendelea kuzeeka
wakiwa wamepita ule umri wa kuweza kupata mtoto, kwa hiyo Abramu alishangazwa
sana na ahadi hii. Akamkumbusha Yule Malaika kwamba yeye hakuwa na mtoto na
hana mrithi wa kurithi mali zake (Mwanzo 15:1-3).
Abramu aliambiwa
kwamba mrithi wake atakuwa ni mtoto wake mwenyewe, na kwamba kama anaweza
kuzihesabu nyota zilizo gizani usiku, basi angeweza kujua idadi kubwa ya watu
watakaotokana na kizazi chake kutokana na mtoto wake mmoja.
Abramu aliamini
na alibarikiwa kwa ajili hiyo (Mwanzo 15:6; Warumi 4:20-22). Ndipo Abramu akaambiwa
awachinje baadhi ya wanyama waliosafi na ndege na awaangike nje wawe sadaka (Mwanzo
15:9-10).
Abramu alitii
Mara tu usingizi
mzito ulimpata Abramu. Akaota kwamba alikuwa kwenye giza nene sana, na kwamba
sauti ya Malaika ilimjia ikitokea kwenye lil giza, ikimwambia mambo
yatakayotokea miaka mingi baada ya kufa kwake Abramu (Mwanzo 15:12-16).
“Ujue hakika ya
kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale,
nao watateswa muda wa miaka mia nne. Hata na taifa lile, watakaowatumikia,
nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi." (Mwanzo 15:13-16). Ndoto hii
ilikuwa inatabiri uteka na utumwa wa wana wa Israeli katika nchi ya Misri utakaotokea
baadae.
Abramu aakaamka
na akaona moto mkubwa kama tanuru ukipita mbele yake na ukiteketeza zile nyama
za wale wanyama na ndege aliowawamba nje ya hema lake. Wakati alipokuwa
analiona jambo hili la kushangaza, imani yake kwa Mungu iliimarika sana kuliko
mwanzo (Mwanzo 15:17). Na siku hiyohiyo Mungu akafanya agano linguine na Abramu
la kwamba atakuwa na uzao mwingi na watakuwa na mali nyingi na kumiliki nchi
kubwa pamoja na baraka nyingi nyingine za mali.
Mungu mara zote
huwaahidi mambo mazuri wale wanaomtii. Ahadi yake kwa Abramu ni moja ya zile
zilizofanya taadhima kubwa ulimwenguni kote kwa kipindi cha maelfu ya miaka. Katika
vizazi vyote vya uzao wa Abramu vimefaidi utajiri mkubwa na Baraka za mali
kuliko mataifa mengi mengine.
Mtoto wa kwanza wa kiume wa Abramu
Sarai, mkewe Abramu,
alikuwa na umri wa miaka 75 wakati ule. Aliamini kwamba alikuwa amezeeka sana
sasa na hangea tena kuzaa mtoto. Hakuweza kujua kuwa ilikuwa inawezekana kwake
na kwa Abramu kuwa ni wazazi wa mtoto ambaye kutoka kwa huyo mamilioni ya watu
watatokea. Sarai alikuwa na suria wa Kimisri, Hajiri, ambaye alikuwa ni
mwanamke kijana na mdogo. Ndipo Sarai akamwambia Abramu kwamba amchukue huyo
Hajiri ili awe mke wake wa pili, akitarajia kwamba Hajiri atawzalia mtoto
atakayekuwa wa kwao wote, Abramu na Sarai. Wakati huo mara nyingi wanaume
walikuwa wanaoa zaidi ya mke mmoja. Ndipo Abramu akafanya kama Sarai
alivyomshauri, na ndipo Hajiri akawa mzamzito au akapata mimba (Mwanzo 16:1-3).
Hatimaye Hajiri
akaanza kumdharau Sarai kwa kuwa alijidhania kuwa alikuwa bora kuliko Sarai kwa
kuwa sasa alikuwa na mimba yam toto wa Abramu. Ndipo Sarai akamfanyia ukatili
Hajiri na akamkimbia. Lakini Malaika wa Bwana akakutana na Hajiri na akamuuliza
alikuwa anafanya nini pale. Akamueleza kile alichokuwa anafanya pale na Malaika
akamwambia arudi kwa mke wa bwana wake. Hajiri akaambiwa pia kwamba atazaa
mtoto wa kiume na amuite jina lake Ishimaeli. Malaika huyu wa Bwana akamahidi
pia kwamba atambariki na kumpa uzao mwingi, uzao utakaoitwa ni wa Waishimaeli,
na ambao utakuwa unatokana na maseyidi au watoto wake 12. Wakati Hajiri alipomzaa
Ishimaeli, Abramu alikuwa na umri wa miaka 86 (Mwanzo 16:4-15).
Uzao au wana wa Ishimaeli
ni hawa wa mataifa ya Kiarabu wanaotokana na ahadi aliyoitoa Malaika kwa Hajiri.
Malaika huyu alimuita "Mungu anayeona". Huyu alikuwa ni kiumbe
aliyeitoa Torati na kuwapa wana wa Israeli walipokuwa Wanatoka utumwani.
Agano la tohara
Miaka kumi na
tatu ilipita. Wakati Abramu alipofikia umri wa miaka 99, Bwana akamtokea na
kumwambia: "Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu!"
(Mwanzo 17:1).
Tunajua kutoka
kwenye Yohana 1:18 kwamba hakuna mtu aliyewahi kumuona Mungu Baba wakati wowote,
kiumbe huyu aliyeongea na Musa hapa ni akifanya kazi ya ujumbe au Malaika wa
Yahova Aliye Juu Sana.
Huku akitetekema,
Abramu aliinamisha kichwa chake na kusujudu ardhini wakati Malaika alipomwambia
kwamba kwakuwa amezitii Sheria za Mungu, basi ataitunza ahadi aliyomuahidi
miaka mingi nyuma. Akamwambia Abramu kwamba jina lake lapasa libadilike aitwe
Ibrahimu, ambalo maana yake ni baba wa watu wengi (Mwanzo 17:3-6). Na
jina la Sarai libadilike na aitwe Sara, ambalo maana yake ni mfalme mwanamke
au malkia.
Agano alilopewa
Ibrahimu lilikuwa ni kwamba yeye na watu wote wa nyumbani mwake na watoto wake
wajao na uzao wake wote ujao walishike. Ishara ya agano hili ilikuwa ni kwamba
watoto wote wa kiume waliopo watahiriwe. Na kizazi chote kijacho pia wawatahiri
watoto wao wachanga wanapofikia umri wa siku nane (Mwanzo 17:9-14). Hata hivyo,
agano hili liliwekwa kwa kupitia Sara pia na kwa Bwana akasema, "naye
atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa
kabila za watu watatoka kwake." (Mwanzo 17:15-16).
Kisha Mungu
akamahidi Ibrahimu kwamba hakika Sara atazaa mtoto, ingawa alikuwa tayari ana
umri wa miaka themanini na tisa. Mtoto huyu alitakiwa aitwe Isaka (Mwanzo
17:15-16, 19). Soma jarida la Isaka: Mtoto wa Ahadi (CB12).
Wageni watatu
Sio kipindi
kirefu baada ya wageni watatu walipomjia au kutembelea kwenye hema ya Ibrahimu.
Watu hawa walikuwa ni Malaika waliomtokea kwa umbo la wanadamu wanaume (Mwanzo
18:1-2). Katika siku hizo, kwakuwa kusafiri kulikuwa ni jambo gumu sana na
kunachosha, basi ukarimu ulikuwa ni mwingi. Ibrahimu akawakaribisha watatu hawa
wale chakula na kupumzika. Chakula kikaandaliwa kwa ajili yao (Mwanzo 18:3-8). Baada
ya wao kula, Ibrahimu aliarifiwa kwamba ndani ya kipindi cha mwaka mmoja Sara
atakuwa na mtoto. Hii ilikuwa ni habari ya kupendeza na kushangaza kwa Ibrahimu
na Sara. Na hasa Sara kwa hakika ilikuwa ni vigumu sana kwake kuamini habari
hii (Mwanzo 18:9-15).
Wakati watu wame
walipoinuka na kuondo waliiangalia Sodoma. Kisha Bwana akamwambia Ibrahimu kuwa
wale malaika walikuwa wanakwenda Sodoma ili kwenda kujionea ni kwa kiasi gani
watu walivyo waovu watu wanaoishi kule.
"Bwana
akasema… basi, nitashuka sasa
nione kama wanayotenda ni kiasi cha kilio kilichonijia; na kama sivyo, nitajua.
(Mwanzo 18:16-22).
"Ibrahimu
akakaribia, akasema, ...Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji,
utaharibu, wala hutauacha mji kwa ajili ya hao hamsini wenye haki waliomo?
"Bwana
akasema, Nikiona katika Sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha mahali pote
kwa ajili yao.”
Ndipo Ibrahimu akauliza
kama Sodoma inaweza kupona iwapo kama kutakuwa na watu arobaini na watano wema
wakionekana kuwepo ndani yake. Jibu lilikuwa ni kwamba hata kama wangekuwa
wameonekana watu arobaini tu, mji ungeweza kupona. Ibrahimu akaendelea kuuliza
kuhusu jambo hili, kila mara akipunguza idadi ya watu. Hatimaye aliambiwa
kwamba hata kama kama watakutwa watu kumi tu humo Sodoma, basi mji ungeweza
kupona (Mwanzo 18:23-33). Ibrahimu alikuwa anawaombea wenyehaki na wachamungu
waachwe wasiangamizwe wakiwemo watu wa familia ya ndugu yake.
Lutu, mjomba
wake, na ambaye Ibrahimu alimuokoa kutokana na uteka wa wafalme walioishambulia
Sodoma, alifanya uamuzi usio wa busara wa kurudi tena kule na kuishi. Jioni ile
malaika wawili walioonekana kama wanadamu, walifika Sodoma na wakakutana na
Lutu ambaye aliketi kwenye mmoja kati ya malango ya mji ule (Mwanzo 19:1). Lutu
akaona kuwa watu wale walikuwa ni wageni, na akawauliza kwa ustaarabu na upole weingie
nyumbani mwake ili wale chakula. Hakujua kuwa walikuwa ni wajumbe wa Mungu.
Kwanza walisita na kukataa lakini hatimye wakakubali kumfuata Lutu. Lutu
mwenyewe alikuwa anapimwa.
Lutu alikuwa na
chakula maalumu kwa ajili ya wageni hawa. Hatimaye, walipokuwa karibu ya kwenda
kuondoka ili wakalale, kelele kubwa za kundi la watu liliizunguka nyumba ya
Lutu. Watu hawa walikuwa wamekwishajua kwamba kulikuwa na wageni wawili kwenye
numba ile. Wakamuomba na kumshurutisha Lutu awatoe nje mtaani, ambako
walikusudia kuwatendea hawa wageni mambo ya aibu kubwa (Mwanzo 19:4-5).
Lutu akatoka nje
na kuusihi umati ile wa watu waondoke. Lakini kundi hili lililobobea kwenye
maovu halikumsikiliza Lutu. Baadhi ya wanaume wakamkimbilia, wakimzuia mlangoni.
Ndipo wale malaika wawili waliokuwa ndani wakatoka, wakamwingiza Lutu ndani, na
wakafunga vifungo vya mlango (Mwanzo 19:6-10). Kundi lenye hasira likakusanyika
kwenye ile nyumba wakitaka kuivunja ili waingie ndani. Ndipo kitu kigeni
kikatokea. Wale washambuliaji wakaanza kuona giza na kuanza kupigapiga huku na
huko bila kujulikana wanalolifanya. Hasira yao ya kiwazimu ikabadilika kuwa
maombolezo. Wajumbe wa Mungu walikuwa wamewapiga kwa upofu wa ghafla! (Mwanzo
19:11).
Wakati kundi
lililobakia lilipoona kwamba kunakitu cha hatari na cha kuhuzunisha kinatokea,
likaondoka na kurudi nyuma kutoka kwenye nyumba ile. Lakini kitu kingine kibaya
zaidi kilikuwa kinakaribia kutokea. Watu wote wa mji walijiunga na kundi hili (Mwanzo
19:4). Na kwa kuwa watu wote walivyoonekana kuwa na hamu ya kufanya jambo
hilohilo moja, na hii inamaanisha kwamba hakukuwepo kabisa na wale kumi wema
kwenye mji huu wa Sodoma. Kwa hiyo hakukuwa na sababu ya Muungu kuuachilia.
"Basi wale
watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na
wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa; maana tutapaharibu sisi
mahali hapa,…!"
Lutu akatoka nje
kwa haraka na akawakuta vijana waliokuwa waliowachumbia binti zke. Alipowaambia
kile kilichokuwa kinataka kutokea, walikataa kumuani (Mwanzo 19:14). Alikuwa
amekata tama sana na kuchoka kwamba aliamua kukaa nyumbani mwake hadi walipokuja
kuungana naye. Malaika wakamuonya kwamba anatakiwa aondoke mara moja, lakini
Lutu alisitasita. Hata baada ya wao kumkamata, mke wake pamoja na binti zake
wawili ambao walikuwa hawajaolewa na kuwalazimisha watoke nje ya mji, bado Lutu
alitumaini familia yake iliyobakia wakawikawia na kusitasita (Mwanzo 19:15-16).
"Jiponye
nafsi yako usitazame nyuma, wala usisimame katika hilo bonde po pote; ujiponye
mlimani, usije ukapotea.”
"nami siwezi
kukimbilia mlimani nisipatwe na yale mabaya, nikafa. Basi mji huu u karibu,
niukimbilie, nao ni mdogo, nijiponye sasa huko, sio mdogo huu? Na nafsi yangu
itaishi.!" (Mwanzo 19:17-22).
Uvumilivu wa awa
malaika ulikuwa karibu ufikie kikomo kwa Lutu, ambaye alikuwa akitumaini kuwa huenda
wakweze watarajiwa wangemfuata. Wakaharakisha kumtoa. Jua lilikuwa karibu ya
kuchomoza walipoufikia mji wa Soari, maili kadhaa kutoka Sodoma.
Turudi nyuma huko
Sodoma, na huko Gomora, ambao ni mji mwingine mkubwa uliokuwa kwenye ardhi tambarare
kulikuwa na kihoro cha ghafla kutingisha ardhi yao. Inadhaniwa kuwa kwenye
maeneo ya karibu yenye mashimo yawakayo moto chokaa au lami, nchi ilifunua
kinywa chake na kutoa nje mafuta, chumvi na kibiriti au tindikali vyote hivi
vilitoka nje kwa nguvu hadi mawinguni. Kwa ghafla hii ilizichanganya pamoja na
kulipuka kwa mshindo mkubwa usioelezeka, zikivuma, zikilipuka kwa mshindo na
mshindo uliomkubwa na kwa kiwango cha juu sana. Sekune chache baadae vipande
hivi vyenye miali hii ya moto vilinyeha chini kama mvua, kwa mamia viliangukia
na kuilipukia miji hii ya Sodoma na Gomora kama kimondo kinapoanguka. Hakukuwa
na jinsi ya watu waliokuwa ndani au karibu na miji hii kujiponya. Hata hivyo,
Biblia inasema tu kwamba moto uliunyeshea kutoka juu mji huu wa Sodoma, moto
uliotoka kwa Yahova kutoka Mbinguni.
Hata maeneo
mengine mengi ya uwanda tambarare yaliyo karibu na miji miwili ilipatwa na joto
kali na la kutisha sana. Hakuna kiumbe kilichoachwa hai kwenye ukanda ule wote.
Vichaka vilivyokuwa vya kijani na vizuri na nyasi zote ziliwaka moto na
kuungua. Masalia meingine ya lami zilichomwa, ikisababisha mfanyiko wa mnyororo
uliofanya maangamizo makubwa yatokee pale kabisa (Mwanzo 9:24-25). Ndivyo Mungu
alivyowafanyia watu wa kule kwa kuwa walikuwa wanajidhuru wenyewe kwa kuishi
maisha yaliyozifuata njia zao wenyewe badala ya ktuzifuata Sheria zake.
Mwanzoni mwa
mlipuko huu wa moto kama vile Lutu na sehemu ya familia yake walipokuwa
wanakaribia kuingia Soari, mke wa Lutu aligeuka nyuma ili aone jinsi maangamizo
haya yalivyo. Huenda alikuwa anakumbuka vitu vyake alivyoviacha huko nyuma na
huenda anasikitishwa sana kuondoka na kuuacha mji huu muovu, licha ya matendo
yake yote maovu na dhambi. Lutu na binti zake waliahakisha wakimbia kwenda Soari,
lakini mke wa Lutu hakufika kamwe pamoja nao. Akageuka kuwa nguzo ya chumvi,
iliyokuwa na umbo la mwanadamu (Mwanzo 19:26; Luka 17:29). Lakini Mungu ni
mwenye rehema, na alimhurumia sana Lutu kwa kumtoa na binti zake wawili. Somo
na fundisho la kujifunza sisi ni kwamba tunapokuwa tumeitwa na kutoka kwenye
lindi la dhambi tusitamani tena kurudi nyuma na kuirudia, ila na tuziache kabisa
pasipo kuwa na nia ya kuzirudia.
Ibrahimu anauona moto wa kutisha
Akiwa amekaa
nyumbani kwake kwa amani milimni, Ibrahimu aliamka mapema asubuhi na akaangalia
maeneo ya chini upande wa Sodoma. Alishangazwa na kuhofu kuona wingu la moshi
likitoka na kuelekea juu wa uwanda uliochafuliwa kwa weusi na miji yake (Mwanzo
19:27-29). Ilieleweka wazi sana kwake kwamba hakukuwa hata na watu kumi tu
waliokutwa wema humo Sodoma.
baadae Ibrahimu akagundua
kwa furaha kuwa sana kwamba Mungu amejibu maombi yake. Mji wa Soari, ingawaje ulikuwa
kwenye uwanda wa maeneo ya Sodomana Gomora, uliachwa usiangamie ili kwamba Lutu
aweze kuukimbilia huko.
Alipogundua hilo kwa kukaa kwake huko Soari angekuwa anaishi katikati ya watu ambao walikuwa hawamchi wala kumuogopa Mungu, ndipo Lutu na binti zake wakakimbilia milimani (Mwanzo 19:30). Angeweza kuwa tajiri zaidi na asingekuwa na matatizo kabisa kama angechagua kuishi katikati ya watu waovu wa Kanaani.
Kifo
cha Sara
Kisha Ibrahimu aliondoka na kwenda Hebroni
upande wa kaskazini wa nchi ya Kanaani. Hapa Sara alifariki akiwa na umri wa
miaka 127 (Mwanzo 23:1-2). Ibrahimu alinunua shamba kubwa sehemu ile. Kulikuwa na pango mle shambani, na humo
akamzikia mke wake Sara.
Tunaweza
kushangaa ni kwa nini Ibrahimu iliyekuwa mtu tajiri sana na mwenye idadi kubwa
ya mifugo, alikuwa anaondoka kutoka sehemu moja hadi nyingine mara kwa mara.
Ndiyo, ni kitu kimoja huenda kilimsababishia kuwa hivyo wakati mwingine ni
vyema kuondoka na kuhama kwa faida ya mifugo yake. Kama hakukuwa na mvua ya
kutosha, wanyama walikosa kuwa na nyasi za kutosha za kula. Kwa sababu kama
hiyo, Ibrahimu alikuwa anazing’oa tu hema zake na kuipeleka mifugo yake kwenye
malisho nyenye nyasi nyingi zaidi.
Lakini fundisho
la muhimu zaidi zilizompelekea Ibrahimu aishi kwenye mahema na kuhamahama
ilikuwa ni kwamba Mungu alimuelekeza kuondoka kutoka mahali pamoja ha kuhamia
kwingine. Karibu watu wengi wa nchi hizo hawakumjua sana Mungu. Waliabudu
sanamu na Mungu hakutaka Ibrahimu au watu wa familia yake wakae chini na
kuzifuata njia za watu wale.
Kifo cha Ibrahimu
Kipindi ambacho Ibrahimu
alioa mwanamke mwingine ambaye jina lake aliitwa Ketura. Alimzaliwa watoto sita
zaidi wa kiume (Mwanzo 25:1-4).
Ibrahimu alimuachia
kila kitu alichokuwanacho Isaka. Lakini wakati alipokuwa anaishi bado aliwapa
zawadi watoto wake wengine (Mwanzo 24:5-6). Sheria au Torati ilielekeza kuwa
sehemu mara dufu ya mali zilizoachwa na baba apewe mzaliwa wa kwanza wakati
baba anapofariki (Kumbukumbu la Torati 21:15-17).
Miaka yote aliyoishi
Ibrahimu ilikuwa ni jumla ya miaka 175 kisha akafa. Watoto wake Isaka na Ishimaeli
walimzika kwenye pango ambalo Ibrahimu huko nyuma alimzikia Sara mke wake.
Baada ya kufariki Ibrahimu, Mungu alimbariki mtoto wake Isaka ambaye hatimaye
alikwenda kuishi karibu na Beeri Lahai Roi (Mwanzo 24:7-11).
Jifunze zaidi
kuhusu Ibrahimu, uzao wake na ahadi za Mungu kwenye tovuti yetu ya: www.abrahams-legacy.org
q