Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[185]
Imani za Kisosiniani, Kiariani na Kiyunitariani
(Chapisho La 1.0
19961221-19961221)
Neno Usosinianism limekuwa likitumiwa bila
kutofautisha na sehemu kubwa ya wapinga mafundisho ya Utatu au wapinga imani ya
Kitrinitatiani. Suala ama
fundisho la Uungu ilikuwa ni jambo muhimu sana kwenye imani ya Kisosiani. Na
kwa mtazamo wa makundi yote mawili, yaani Wakatholiki na Waunitariani, walishikilia
kwa namna zao zote kwamba kumjua Mungu ni kitu rahisi na hakuna utata. Walihitimisha
kwa kusema kwamba utofautishaji wa nafsi ni kitendo cha kuharibu mwelekeo wa
ufafanuzi huo. Kwa mtazamo na msimamo wao, waliukataa Utatu kuwa ni imani
sahihi. Tofauti liyopo kati ya imani za Kitrinitarini na Uyunitariani ni kwamba
heshima anayopewa Kristo inatokana na jinsi uhisiano wake ulivyo na Baba na
kwamba ni wa aina ya pili, wakati ambapo Watrinitariani wanashikilia kuamini
kwamba unatokana na imani ya kidini ya latria,
ambako inaamini naq kufundisha watu wake kwamba yeye kwa hakika ni Mungu sawa
na kama alivyo Baba kuwa ni Mungu.
Christian Churches of God
PO Box 369,
WODEN ACT 2606, AUSTRALIA
Email: secretary@ccg.org
(Hati Miliki ©
1996
Wade Cox)
(tr. 2014)
Masomo yaliyo kwenye jarida hili yanaruhusiwa kunukuliwa na
kuwapa watu bure bila kulipishwa kitu, ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la
haki miliki ni lazima viwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa
au kuchangia kununua jarida hili au nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi
zilizolazima zaweza kuwekwa kutoka kokote iwapo zitaonekana zitakithi haja ya
lugha husika lakini pasipo kukuka maadili ya ya sheria ya haki miliki.
Jarida hili
linapatikana Ulimwenguni kote kwenye wavuti yetu ya:
http://www.logon.org au http://www.ccg.org
Imani za Kisosiniani, Kiariani na
Kiyunitariani
Neno Usosinianism limekuwa likitumiwa bila
kutofautisha na sehemu kubwa ya wapinga mafundisho ya Utatu au wapinga imani ya
Kitrinitatiani. Neno hili limechukuliwa kutoka kwa mtu aliyeitwa Lelius
Socinius (1526-1562) na mjomba wake Faustus Socinius (1539-1604), mkazi wa huko
Sienna. Dini iliyoanza siku za kale kabla ya Faustus ilihusiana sana na hii,
lakini ilimwia kila mtu kuwa ndani ya hii. Jamii ya kisirisiri ilijiunda huko Vicenza
katika dayosisi ya Venice ili kujadili imani na mafundisho ya Utatu. Miongoni
mwa washiriki waliokuwepo walikuwemo kina George Blandrata (mwana fizikia),
Alciatus, Gentilis na Lelio Socinius.
Lelius (au Lelio) Socinius alikuwa kasisi wa huko Sienna na rafiki wa
Bullinger, Calvin na Melancthon. Lengo la kuundwa kwa kikundi kile lilikuwa ni
kuanzisha vuguvugu la kupinga imani na mafundisho ya Utatu. Kikundi hiki
kilivunjika na wanachama wake wakakimbilia Poland ambako waliteswa sana tena.
Ijulikane pia
kwamba hawa Waanzilishi wa vuguvugu hili au Nominalists waliokuwa chini ya
uongozi wa Abelard walikuwa wahamasishaji na wapinzani wa kweli wa mafundisho
na imani hii ya Utatu katika kipindi cha Matengenezo kama walivyowaona
Wakatoliki na hivi ndivyo inavyoonekana kwenye mandiko Hugh Pope kwenye makala
aliyoandika kuielezea imani ya Kisosiani (Cath.
Encyc., Vol. XIV, p. 113). Wale walioitwa kuwa ni wapinga kundi la Wakweli,
Wahamasishaji walikataliwa na wanafalsafa wa Kikatoliki. Kazi hii ya uchambuziani
ilihusisha na ufafanuzi wa mambo kwa namna ya kila mtu peke yake ili kuupata
ukweli ndani wa kila mmoja. Kwa hiyo unapinga uwepo wa dhana ya kuachananayo na
ya ulimwengu, na inakataa kukubaliana na ukweli kwamba akili zinauwezo wa
kufanya hayo. Kwa hiyo maendeleo ya kimizimu hayajumuishwi pia. Itikadi ana
mafundisho yaliyotiliwa chumvi ya Wafuata uhalissia yakaiteka dunia na mawasiliano
yenye ukweli na halisi sambamba na mtazamo uliokuwepo wa mawazo ya kidunia. Wakatoliki
walikuwa kwenye mrengo wa waamini kwa Ushupavu wa mafundisho haya ya Uhalisia
Shupavu wa Kiaristoteli (hasahasa kutoka pipindi cha kina Aquinas na Occam na
kuendelea), zaidi sana kuliko imani ya Kishupavu ya Uhalisia wa Waplatoniki. Mchakato
huu wa kifikra una dalili mbaya na madhara katika kuifafanua Theori au Dhana
fikirika ya nafsi na roho ya dunia. Mawazo ya kisasa ya kisayansi na ya kinadharia kimsingi yanatuama kwenye
kufafanua matukio kwa mtazamo wa kimwili. Wahamasishaji waliendeleza mafundisho
yao hasa hasa kupitia kina Hume, Stuart Mill, Spencer, Huxley na Tain. Wakatoliki
waliwaona wao kuwa wanazidisha kuweka tofauti hususan ya utendaji wenye mashiko
(uozo au uharibifu rahisi wa utoaji mada au mahuribi yaliyogusa mioyo kuhusu mshangazo
na kusahau mkubwa ujulikanao au mlinganisho wenye mashiko na mchakato wa
utandawazi) (tazama kitabu cha De Wulf, Nominalism,
Realism, Conceptualism, Cath. Encyc.,
Vol. XI, p. 93). Wakatoliki wenye itikadi ya Kiaristoteliani wanajulikana (na
wao wenyewe) kutofautisha kwa uangalifu sana kati ya haya yote mawili ya
utengaji kazi wa akili. Unominalism hauafikiani na falsafa ya kiroho, na hata
kwenye Uanazuoni au Uskolastiki. Nadharia za Kant Anayedhaniwa pia kuharibu
vifungo vyote ambazo zingeweza kuliunganisha wazo la ulimwengu wa ndani (De
Wulf, ibid.). wakatoliki wameendelea kuamini na kushikilia hivyo hadi kwenye
karne hii kwamba hatuwezi kujitoa kwa akili zetu zote na uwezo wetu wa
kimaarifa, ila tunazalisha ndani yetu kwa ushawishi wa kiasi fulani kwa kitu kinachojidhihirisha
kwetu (ibid.). Hii inaashiria
jambo kwenye mapenzi ya Mungu kutufunulia mambo, ambalo ni asili ya Mungu.
Maelekezo ya ukweli huu ni ya kiantolojia. Antolojia ni sayansi ya kusomea
viumbe au vyanzo au asili ya vitu. Inahusiana na masomo ya kusomea habari za viumbe
au asili ya vitu kwa ujumla. Kwa hiyo, dini zote zinahusiana na maelezo haya
kwa ujumla. Kwa hiyo, maelezo na ufafanuzi kama huu yanatoa ukweli kuhusu Mungu
na wana wa Mungu na mapepo.
Uontolojia, ambao
unahusiana sana na imani ya Uplatoni Shupavu, unaonyesha kwa kiasi kikubwa kuwa
ni aina ya dhana fikirika, inayokuja kwetu kutokana na ulimwengu uliomakini kwa
njia ya kimapokeo, pamoja na aina ya dhana fikirika ya kugeuka kihalisia mkate
na divai kuwa ni mwili na damu halisi pamoja na asili ya uwepo wa Mungu. De
Wulf anaendelea kuamini kwamba tunaunda fikra yetu ya kwanza tukiwa bado hatujamjua
Mungu bado. Sisi hatumju sana yeye kiasi kwamba tunapaswa kujifundisha fikra
zetu hizi mpya ili kukuza kiwango chetu cha posteriori
cha uwepo na chanzo chake. De Wulf anafikiri kwamba Uontolojia umeacha kuishi kwake
na kwamba hii dunia sasa inaenda kwa mfumo wa kimajaribio na utafakari
ukidhaniwa kuwa utarudi kwenye ndoto za
Plato (ibid.). Wakatoliki hawakujua kwenye mtazamo wao kwamba baadhi ya
mawazo makuu walikuwa ni Wayunitariani pamoja na wale waliotoa fafanuzi za
kisayansi na kifalsafa za ukweli—kina John Locke na Sir Isaac Newton akiwa ni
mfano unaojulikana sana na mtu mashuhuri. Kwa hiyo, Wayunitariani (au Waariani
kama walivyoitwa na Watrinitariani) wanaonekana kama walikuwa na sehemu kubwa
ya kufanya na kushiriki mchakato huu.
Mtazamo huu wa maarifa na Theori ya Causal imefafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Uumbaji: Kutoka Theori ya Anthropomofia Hadi Kwenye Anthropolojia ya Kitheomofiki (Na. B5) [Creation: From Anthropomorphic Theology to Theomorphic Anthropology (No. B5)]. Wanominalisti walikuwa ni wapinga Utrinitariani kutokana na utafiti wao uliotuama kwenye salsafa ambazo zinapinga Dini ya Waplatoniki mamboleo. Tofauti iliyoko kati ya Wakatoliki na Dini zinazopinga Utrinitari ulikuwa ni karibu sababu sawa, ya kuwa Mungu alijidhihirisha kwa kupitia ufunuo na kwa wale watu wazima waliobatizwa katika Roho Mtakatifu. Ili wawe Wanaamini fundisho la mkate na divai kugeuke kuwa damu na mwili halisi.
Kwa sababu hii Wakatoliki waliyakomesha haya madai ya wapinga Utrinitariani kwa kufundisha uhusiano wa mwendelezo wa, imani ya mkate na divai kugeuka kuwa damu na mwili halisi hadi utii na kuwa sawa na Kristo bali akiwa ni mdogo au asiye na hadhi sawa na Mungu. Wakatoliki walikataa matendo haya na kama Mungu alivyofanya na kutegemea kwenye mwendelezo wa kuamini hadithi na imani za kimistiki na kuwa kama Mungu kama ilivyoelezewa na Wakapadokia. Hii ilikuwa ni tofauti ya kidhana ambayo Wakatoliki waliipinga tangu kikipindi cha Wakapadokia (tazama majarida ya Roho Mtakatifu (Na. 117) na Consubstatial na Baba (Na. 81) [The Holy Spirit (No. 117) and Consubstantial with the Father (No. 81)].
Historia inatuonyesha kwamba kwa muda mrefu Kanisa la Mungu limekuwa likitanguliwa na Matengenezo ya Wawaaldensiani mara zote walikuwa ni wapinga Utrinitariani tangu hapo hadi kipindi cha Matengenezo. Hugh Pope anawachukulia Watrinitariani kuwa ni wawakilishi wa Wasabellian, Wamakedonia na Waarian wa zamani. Kwa kweli, Wawaaldensian walishutumiwa kwa au kwenye maelezo ya Waariani katika mwaka 1180 kwa mtazamo wa Bernard wa Fontcaude (Adversus Vallenses et Arianos; tazama jarida la Wajibu wa Anri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Nubgu Yanayoshika Sabato (Na. 170) [The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)].
Watu wa huko Ulaya waliwaita wapinga Utatu kuwa ni wanaotokana na ujuzi wakiwa ni matokeo ya wana Matengenezo na wakawa wanashikilia mtazamo tofauti. Na kwahiyo inapotosha kuwaita hawa kuwa ni Wasociani. Ni sawa tu na jinsi Makanisa ya Mungu huko Marekani yalivyofanya tangu kipindi cha kati cha miaka ya 1800 yakijulikana kama Waarmstrong. Alikuwa ni kiongozi wa baadae wa tawi moja. Ni kama alivyokuwa Armstrong, nasi tutajionea kwamba Wasosiani wenyewe walibadilisha mtazamo wao kuhusu asili ya Mungu.
Lelius Socinius aliishi kipindi chake kirefu huko Zurich lakini nalikuwa na pia anakipindi cha kuwa na muda wa kuishi huko Cracow. Alifariki mwaka 1562 na wapinga Utatu walipitia mateswa makali kipindi hiki. Mwaka 1570 Wasosinian waliogawanyika na kushawishiwa na John Sigismund, walianzisha huko Racow. Mnamo mwaka 1579 Faustus alikuja Poland pamoja na vitabu vya mjomba wake. Alikuta dini imegawanyika na kwanza alikataa uanachama kwa kuwa alikuwa hajabatizwa mara ya pili. Ubatizo wake wa kwanza kwa hiyo ni lazima uwe ulifanyika akiwa mtu mzima. Mwaka 1574 Wasosinian walianzisha Katekismu ya Wayunitariani. Asili na ukamilifu wa Mungu ulielezwa lakini makabrasha hayakuandika chochote kuhusu tabia za kimbinguni ambayo ilichukuliwa kama siri kubwa (na Wakatoliki). Kristo alichukuliwa kuwa ni kuwa ni mwana wa ahadi na mwombezi wa wanadamu
Faustus Socinius alijiunganishia kazi hizi zote yeye mwenewe tangu mwaka 1579. Alikuwa amealikwa huko Siebenburg (au Siebenburgen) ili kukabiliana na wapinga Utatu waliokuwa chini ya Francis David (au Davidis) (1510-1579). David alikufa huko Deva Castle ambako alikuwa amefungwa gerezani kwa kosa la kuwa na msimamo wake wa tofauti kuhusu asili ya Kristo. Kanisa laSiebenburg, baada ya kifo cha Francis David, aliyeuawa kwa kukata kichwa na Andreas Eossi na hili ndilo lilikuwa Kanisa huko Ulaya Mashariki lililotokea kwenye imani ya Wawaldensian. Tunajua bila shaka kuwa walikuwa ni Wayunitariani (mara ngingine waliitwa Waarian na Wakatoliki). Walizishika Sabato, Sikukuu Takatifu Zilizoamriwa na waliadhimisha Miandamo ya Mwezi Mpya na walikuwa ni Kanisa la Kweli la Mungu hukp Ulaya ambayo kwayo twaweza kuiita ilikuwa ni zama ya Watiathira (soma majarida ya Mgawanyo Mkuu wa Makanisa Yanayoshika Sabato (Na. 122) na Wajibu wa Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa ya Mungu yanayoshika Sabato (Na. 170) [General Distribution of the Sabbath-keeping Churches (No. 122) and The Role of the Fourth Commandment in the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)].
David alikataa kuukubali upekee wa mafundisho ya imani ya Wasosiniani yasemayo kuwa Kristo, ingawaje sio Mungu anapaswa kuabudiwa. Kanisa la Mungu huko Ulaya halikuwa limekubaliana kwamba Kristo alikuwa na sifa ya kiuungu kiasi cha kuabudiwa au kuombwa kwenye maombi yao. Kukataa kumuabudu Kristo ulikuwa ndiyo mtazamo uliokuwepo kwenye imani ya Kanisa la Mungu kwa kipindi cha karne kadhaa, wakiwemo Wawaldensian ambao imani yao kanisa la Siebenburg lilikuwa miongoni mwao walioamini hivyo. David aufungwa gerezani kutokana na msimamo wake na hatimaye aliuawa akiwa humo gerezani. Hugh Pope aligundua pia kwamba Budnaeus alidharauliwa na kuchukiwa kwa ajili ya kushikilia mtazamo huohuo wa David na alitengwa na kanisa lao mwaka 1584. Wawili hawa walikuwa wameongoka na kungia imani ya wale waliokuwa wanajulikana kama Waorthodoxy.
Wasosiniani wa kipingi hiki waliikataa katekisimu ya zamani na kuitengeneza nyingine mpya waliyoiita kuwa ni Kateksimu ya Racow ambayo ingawa iliandikwa na Faustus Socinius ilikuwa haijachapishwa hadi mwaka 1605, mwaka mmoja baada ya kufa kwake. Ilichapishwa kwa mara ya kwanza kwa lugha ya Kipolandi na kisha ikachapishwa tena kwa Kilatini mwaka 1609.
Wasosinian walikuwa wamejiimarisha Walijenga vyuo, wakaanzisha sinodi na kumiliki mitambo ya uchapishaji ambazo kwazo walimudu kuchapisha masomo mengi ya mafundisho. Machapisho haya yalikusanywa na Sandius yaliwa na kichwa cha somo Bibliotheca Antitrinitarianorum. Machapisho ya Faustus yamejumuishwa kwenye vitabu vinavyoitwa Bibliotheca Fratrum Polonorum.
Kanisa la Mungu huko Siebenburg, kwa upande mwingine, lilikataa mamlaka ya
kanisa na kukataa kushirikiana na utaratibu wa kuchapisha machapisho
mbalimbali. Eossi aliiandika kazi hii kwa kutumia mikono yake na ilikaririwa na
wasaidizi wake.
Mwaka 1638 Wakatoliki wakasisitiza kuwa Wasosiniani waangamizwe. Dini hii ilikusudiwa kukomeshwa huko Ulaya lakini Pope anasema kwamba wafalme wengi waliipenda na kuipa msaada mkubwa kwa siri (ibid., p. 114). Ilikuwa ni kama kwa namna fulani ndiyo iliyokuwa inatawala huko Ulaya. Balozi wa Uingereza aliionya serikali ya Uholanzi kuwa Wasisiniani walikuwa wanaelekea huko wakitokea Poland, jambo ambalo lilifanyka kweli mwaka 1639. Mwaka 1653 ilikomeshwa huko kwa kufanyika makatazo ya kutishia watu.
Haikuweza kukubalika na kushamiri sana Uingereza, kama alivyojionea Pope, ingawaje mwaka 1612 Leggatt na Wightman walishitakiwa na kuhukumiwa kifo kwa kosa la kukataa uungu wa Kristo. John Biddle alisemekana kuwa walikuwa anachukuliwa kama mfuasi wa imani za Kisosiniani na alifukuzwa na Cromwell na kupelekwa kifungoni Kisiwani Scilly ambako alifungwa hadi alipoachiliwa na kurudi kwa amri ya kiwali wa wakati huo. Lakini alitiwa gerezani tena baada ya zama za Marejesho na alifariki mwaka 1662.
Hugh Pope kwa usahihi sana anakumbuka na kuandika (ibid.) kwamba Waunitarian wanajulikana mara zote kuwa ni
Wasosniiani, lakini wana mambo muhimu wanayotofautiana kwenye mafundisho yao.
Tutaona kwamba neno Wayunitariani mara nyingi linatumika kimakosa na
Wakatoliki na Pope analitumia neno hili kwa mtazamo mmoja tu, ambayo
tunalichukulia kuwa sio sahihi. Wakatoliki wanachukulia majina haya ya wa Yunitarian, Arian na Socinian kuwa ni
imani tofauti na ni maneno tofauti wakati kwamba Schaff, kwa mfano, aliwajumuisha
hawa wote kwenye kundi moja tu la Wayunitarian (pamoja na tofauti nyingi walizonazo)
kama tunavyoona kutoka kwenye kitabu chake kinachitwa Historia ya Kanisa la Kikristo [History of the Christian Church
(Vol. II, pp. 571ff.)].
Wasosiniani wanaamini ifuatavyo:
1. Biblia ina mamlaka yote lakini inatakiwa itafsiriwe kwa kumaanisha.
2. Walikataa aina yote ya imani fumbo ("Imani fumbo kwa kweli zimeinuliwa
na kutukuzwa sana kuliko imani zinazofikirika lakini wao pasipo maana
wamezitukuza sana; na pasipo na sababu yoyote wameizima nuru, lakini pia
wameitimiliza tu." John Crell (d. 1633) De Deo et ejus Attributis; cf. Pope, ibid.).
3. Umoja, uhalisia, uweza juu ya yote, haki, na hekima ya Mungu vinapaswa
kusisitizwa tangu tunapoongoka na kuwa kwenye imani hii.
4. Uweza wa Mungu katika ukubwa usio na kikomo na wa kujua kila kitu
vilichukuliwa kuwa ni zaidi ya uwezo wa mwanadamu na kwa hiyo havina umuhimu kwa wokovu.
5. Haki ya kwanza ilimaanisha kuwa Adamu hakuwa na dhambi na ndiyo kitu
kilichomfanya aruzukiwe na tunu ya kipekee ya kuwa mtu mkamilifu; kwa hiyo
Socinius alilikataa na kulipinga kwa nguvu zote fundisho la dhambi ya asili.
6. Kwakuwa imani haipatikani kwa njia nyingine iwayoyote ila ni kwa
kumtumainia Mungu, Wasosinian waliyapinga mafundisho ya Wakatoliki ya jinsi ya
kuhesabiwa haki kwa maana ya namna waliyoamini wao. Hakukuwa na namna nyingine
zaidi ya namna ya kimahakama kwa uopande wa Mungu.
7. Kulikuwa na sacrament mbili tu lakini hawa walizichukulia kuwa sio muhimu
kwa mambo ya imani, kwa kuwa hazikuwa na uwezo wa kumbadilisha mtu kutoka ndani
(kwa hiyo, fundisho la imani ya kugeuka kihalisia kwa mkate na divai walilikataa
na la uhakika wa kifo kwa mtu mzima anapoingia kwenye ubatizo na huenda kwa maswali).
8.
Waliupinga ubatizo wa
watoto wadogo na mafundisho ya kwenda motoni. Bali watenda dhambi watachomeka na kwisha kama myeyuko.
Uungu ni kitu muhimu sana kufundisha kwa wa Sosiniani. Kutokana na mtazamo
wa makundi haya yote mawili, yaani ya Wakatoliki na Wayunitariani, waliendelea
kuona kuwa Mungu hana utata kumjua kwake na ni mmoja. Walihitimisha kwa kusema
kwamba tendo ka kutofautisha nafsi ni la uiharibifu dhana hii ya umoja wake.
Kutokana na mtazamo huu wenye mashiko, walipinga fundisho na imani ya Utatu na
kuliona halina maana wala mashiko. Wakatoliki wanauona mtazamo huu kuwa ni wa
kupotoka kutoka kwenye mafundisho yao ya Tohara au utofautishaji wa Utatu ndani
ya Uungu. Imani ya Kiditheist ya Herbert Armstrong, kama ilivyoenea tangu mwaka
1978, inajaribu kuafikianisha tatizo hili la Umoja na Utofauti huku wakijifanya
kupinga imani ya Utatu na kumtenga Roho Mtakatifu kutoka kwenye mwambatano huu.
Hili ndilo jambo lililolazimisha kuitishwa kwa mtaguso wa Constantinople mwaka
381 na kuishia kwenye imani ya kawaida na iliyiozoeleka na wengi kipindi hicho
ya Kitrinitariani (sawa na alivyosema Gregory wa Nazianzus 380 BK, na
kunukuliwa kwenye jarida la Maongozi ya Mungu (Na. 174) [The Government of God
(No. 174)]. Ni sawa na
zama za Wamakedonia ambayo inaitwa pia kama ya Waarian, na kwa hiyo inajaribu
kuijumuisha elimu ya kumtukuza Kristo. Wanafunzi na wafuasi wa Armstrong walifikia
uamuzi katika mwaka 1990, wa kutangaza kwamba Mungu na Kristo walijadiliana na
kuafikiana nani miongoni mwao ashuke hapa chini ili atolewe sadaka (jarida la Worldwide News na ilitangazwa rasmi na
mwinjilist G. Waterhouse, huko Canberra, Australia – kwenye Sikukuu ya Vibanda
mwaka 1990).
Hata hivyo, Wasosinian, waliendelea kuyapinga mafundisho hayo kwa kusema
kuwa hakuwezekani kuwa na usawa kati ya kitu kilichotengenezwa na aliyekifanya,
na kwamba, hakuwezekani kuwepo dhana hii ya mtu kuishi hapo kabla na kisha aje
na kuzaliwa tena maarufu kama Inkanesheni ya Mungu kana kwamba yeye anahitaji
ama kudai usawa wa namna hiyo. Hata hivyo, kama kwa kutowezekana kokote,
kulikuwa na utofauti wa watu kwnye Uungu, hakuna mtu wa kimbinguni anaeweza
kuunganika na mwanadamu kama vile kusivyowezekana kuwa na muunganiko kati ya watu wawili. Hoja
nyingine iko kinyume sana na Maandiko Matakatifu. Aquinas anaelezea jambo la
kwanza kutoka kwenye mtazamo wa Wakatoliki wa Summa, I, Q. xii, a. 1 ad 4 am
(see Petavius kwa anayekumbuka).
Wasocsnian hawajawahi kuwa kile kinachoitwa Waariani kama walivyokuwa kina Campanus
na Gentilis. Inaonekana kwamba Gentilis alikuwa ni mmoja wa waliokuwa kwenye
jumuia asilia ya kale. Aliuawa kwa kukatwa kichwa huko Berne mwaka 1566 na
baadhi walifupisha jina lake na kumuita Mtritheist kwake kama alivyomshuhudia
Pope (tazama kitabu kinachoitwa A Short
History of Valentius Gentilis the Tritheist, London, 1696 yaani Historia Fupi ya kina Vallentus Gentilis
Mtritheist). Mtazamo wa Kiditheist unaweza kuangukia kwenye tatizo hili
wakati Roho Mtakatifu akiwa hajalifunua au pale kwenye mafundisho ya imani ya
Kitrinitariani. Hii imetokea pia kwenye Kanisa la Waadventista Wasabato ambalo
limekuwa la Kiutatu tangu mwaka 1931 baada ya kifo cha Uriah Smith, na kwenye
Kanisa la Worldwide Church of God kati ya miaka ya 1978 na 1993 ambalo hatimaye
lilikuwa la Kiutatu pia.
Wakatoliki wanasema kwamba Socinius hakuwa Myunitariani aliyebobea sana,
kama walivyokuwa kina Paulo wa Samostata na Sabellius, alimchukulia Roho
Mtakatifu kuwa ni nguvu ya kawaida tu na ni utendaji wa Mungu, nguvu iwezeshayo
utakaso.
Ilikuwa ni kwa mafundisho kuhusu Kristo ndipo Socinius alitofautiana na
Wayunitarian, ingawaje alifundisha kumtukuza au kumwabudu Kristo, jambo ambalo
Kanisa la Mungu lilikataa kufanya. Socinius aliamini kwamba Kristo alikuwa ni
neno tu au logos lakini alipinga uwepo wake. Akiwa kama Neno wa Mungu, yeye
alikuwa ndiye mkalimani au mtafsiri wake. Pope anasema (ibid.) Socinius alimtaja
John akimtaja katika ubadilisho peke yake. Bilashaka hii ilichukuliwa kutoka
kwenye neno lenye maana ya tohu na bohu kutoka Mwanzo 1:1-2. (Wazo hili
limepokelewa sana na masalia yaliyoonekana na wachimbuzi wa siku hizi) kristo
hatahivyo alikuwa amezaloiwa na mwanamwali kimiujiza. Alikuwa ni binadamu aliyekamilika.
Alikuwa ni mwombezi wetu aliyechaguliwa, ila hakuwa Mungu, bali ni mtu
mnyenyekevu. Kwa jinsi hii alipaswa kuheshimiwa kibinabdamu.
Wakatoliki wanaamini hii kuwa ni mstari mkubwa sana unaowagawa
Wayunitariani na Wasosianisti (tazama kitabu cha Pope, ibid.). wakatoliki
wanaamini kuwa Wayunitariani wanapinga kuzaliwa kimuujiza kwa Kristo na kwamba
wanakataa kumuomba na kumtukuza kama Mungu. Pope anaamini kwamba kimsingi
Wayunitariani wako sahihi sana.
Kwa hiyo, Wakatoliki wanaamini utofauti uliopo kati ya Waarian,
Wayunitarian na Wasosiniani kuwa:
1. Waarian wanaaini kuwa Kristo alikuwepo na kuishi zaa za kabla ya kuzaliwa
kwake na mwanawali aliwa na Baba. Wakatoliki wanadai kwamba Waariani wanaamini kuwa
Roho Mtakatifu anatokana na Mwana. Dhana hii inatokana na maandishi ya wale
wanaitwa Waariani lakini ni wafuasi waliokuja baadae wa Ariani.
2. Waunitarian wanaaminika kuwa wanapinga kuwepo muda kabla ya kuzaliwa kwa
Kristo, uweza wa kimbinguni wa kuzaliwa, na pia kumuabudu Kristo. (Tunaiita
imani hii ni yaa Uyunitarian wenye Msimamo Mkali na Wakatoliki wanapaswa
kutofautisha jambo hili au imani hizi.)
3. Wasosiniani wanajulikana kuwa wanapinga uwepo wa Kristo wa zama kabla
lakini wanakubaliana na kuzaliwa kwake kimiujiza na pia wanamuabudu.
Tofauti hizi tutazielewa vizuri zaidi kwa kadiri tunavyoendelea kujifunza
hapo chini.
Shutuma za kawaida za Wasosiniani haziwezi kuonyesha kwa usahihi sana mafundisho
yao kwa kuwalaumu tu kulikofanywa siku za kabla ya kuchapishwa kwa Katekismu ya Racow mwaka 1605. Mashitaka
yapo kwenye Katiba ya Paulo IV, Cum quorundam, 1555 (Denz. 993) iliyoendelezwa
na Clement VIII mwaka 1603 Dominici
gregis. Zaidi ya yote, inawezekana kuwa hii katekismu isionyeshe maendeleo
zaidi ya kimtazamo wa viongozi wa taasisi (tazama kitabu cha Hugh Pope, ibid.,
p. 115). Kutoka kwenye marufuku hii inaonyesha kwamba ilidhaniwa kwamwa
mwaka 1555 na tena mwaka 1603 ndipo Wasosiniani walidai yafuatayo:
a. Hakuna kitu kinachojulikana kama Utatu;
b. Kristo hakuwa na uhusiano wa kimungu na Baba na Roho Mtakatifu;
c. Kwamba hakutungwa mimba yake kwa uwezo wa
Roho Mtakatifu bali alizaliwa na Yusufu;
d. Kwamba kifo na mateso yake havikufanyika kwa kusudi la kut uletea sisi
ukombozi;
e. Kwamba mwanamwali mbarikiwa sio mama wa Mungu na wala hakurudia hali yake
ya uwanawali baada ya kuzaa.
Kwenye Katekismu ya mwaka 1605, Wasosiniani walisema wazi kabisa kwamba
Kristo alitungwa kwa mimba ya kimiujiza lakini Pope amasema (ibid.) kwa jambo hili
haieleweki. Kwa hiyo, wakosoaji wanahoja zisizo sahihi na wanatunia ushahidi usio
sahihi. Tatizo linaloonekana kuwa sio sahihi kwenye itikadi hii ya mafundisho
ya Wakatoliki ni kwamba wanashikilia kuamini Wasosiniani wanapinga uwepo wa
Kristo kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake na mwanamwali duniani. Lakini tunapokuwa
tunapotathmini maelezo yao kuhusiana na Yohana kuhusu Masihi condemnations rest
on incorrect and contradictory, tunaona kwamba hoja za Wasosiniani zimetuama
kwenye Yohana 1:10 inayojulikana kama ni orodha ya kizazi au uzao na
haimaanishi kizazi chenyewe halisia. Hii inaonyesha fuindisho la Uungu. Maelezo
ya uumbaji yaliyoko kwenye Mwanzo 1:1-2 yanachukuliwa sasa zaidi ya maelezo
halisia kutokana na kile tunachokijua umri wake wa duniani na historia yake.
Haiwezekani kuafikinisha upingaji wa kutokuwepo hapo kabla kwa Masihi na uzao
wa hapa duniani ulioandikwa kwenye Yohana 1:10. Wasosiniani kwa hiyo
hawakupaswa kushikilia mafundisho ya Uyunitarian wenye itikadi kali na
walipaswa kuwa wanawasaidia Wayunitariani, ambao wamekuwa wanaitwa kimakosa na
Wakatoliki kuwa ni Waariani. Msimamo huu kwa hiyo umeyagawa makundi mawili na
yanaipa historia ya Waaldensian. Uwezekano mkubwa wa maelezo ni kwamba Wayunitariani
wenye msimamo mkali walikuwepo kwa idadi ndogo kwenye maakanisa ya Ulaya lakini
hawakuuwakilisha mtazamo wao wa kweli wa uliokuwepo wa kimafundisho. Kwa kiasi
kiubwa, kwa namna hiyohiyo wanaendelea kuwepo hata leo kwa idadi ndogo ilikuwa
kwenye Makanisa ya Mungu.
Kwa mtazamo huu, kama ulivyoorodheshwa na Wakatoliki, Kanisa la Mungu
liliyachukulia machache yake na iliaminika kwamba Kanisa la Mungu huko Ulaya,
liwe lile la Siebenburg au kama lilivyokuwa lile la Wawaldensian, yalikuwa ama
ya wa Socinian ama la Kikatoliki waliojulikana kama ni wa Yunitariani wenye
itikadi kali, kama vile, wale wanaopinga uwepo wa Kristo siku za kabla ya
kuzaliwa kwake duniani, kama ni makosa ya kiuelewa. Kwa uzuri zaidi ni kwamba
ilirahisishwa sana na ilionyesha tofauti kubwa. Inaweza kuwa pia kwamba Wakatoliki
wanalifanyia kazi tu neno hili la kuwepo
kwa Kristo kipindi cha kabla ya kuzaliwa kwake duniani ili kushamirisha
mafundisho yao. Kama neno hili la kuwepo
kwake kipindi-kabla ili kumaanisha madai yao ya kuwa alikuwepo hata kabla
ya kuumbwa kwa Malaika, badala ya kuonyesha uwepo wake katika zama za kabla ya
Kuja kwake na kuzaliwa hapa duniani, na ndipo tuwe na maana fafanuzi ya neno
hili. Kama hili ndilo suluhisho la mgongano huu wa kifikra kwenye maelezo ya
Wakatoliki ya mafundisho ya kidini ya Wasosinian, kisha tofauti yao uadilifu
wao wa kielimu una maswali makubwa. Kwa kiwango chochote mtazamo wa kiitikadi
ya Ugeukaji wa \Mkate na divai kuwa mwili na damu halisi pia inafanya kuwepo
kwa maswali.
Mtazamo wa Kanisa na maeneo mengine vinaweza kuelezewa vizuri sana kama
yanafuata.
Kanisa la Mungu mara zote limekuwa na uhusiano na Kristo na Mitume, likiwa
lenye mrengo wa Kiyunitariani. Lilishikilia kuaminini ifuatavyo:
1. Kuna Mungu Mmoja tu wa Pekee na wa Kweli na ndiye Baba wa wote.
2. Kwamba Kristo ni msaidizi na ni Mwana wa Mungu na sio Mungu wa pekee na wa
kweli. Bali yeye alikuwa amezaliwa na kuwa mwana wa \Mungu (Yohana 1:18; tazama
kitabu cha Irenaeus kwa maandiko sahihi, sawa na Marshall's Greek-English Interlinear RSV).
3. Kwamba Kristo na Wana wengine wote wa Mungu wametokana na Baba na kwa
sababu hii kizazi chao kinatokana na
kitendo cha uhiyari na ndilo tendo la uumbaji (Malaki 2:10; Waebrania 2:11 RSV;
sawa na Waefeso 3:9 RSV. Kumbuka kwamba tafsiri ya KJV imeongeza neno na Yesu Kristo ambalo halimo kwenye
nakala asilia za kale; tazama tafsiri ya Companion
Bible, n. hadi aya ya 9 na pia katika Ufunuo 4:11).
4. Kristo alikuwepo hata kabla ya kuzaliwa kwake duniani aliwa kama Mjumbe wa
Mungu na kwamba Yule aliyekuwa akinena na nabii Musa pale Sinai na Malaika wa
Anago la Kale (Mwanzo 48:15-16; Isaya 9:6 LXX; Zekaria 12:8; Matendo 7:38; Wagalatia.
3:19). Hakuna mtu aliyewahi kumuona \Mungu (Yohana 1:18; 1Timotheo 6:16). (Tafsiri
ya Septuagint (LXX) inamtaja Masihi kutoka kwenye Isaya 9:6 kuwa ni Mjumbe wa
Shauri Kuu).
5. Kristo alikuwa na haiba ya kimbinguni akiwa amezaliwa na mwanamwali bikira
ili awe mkombozi wa wenye dhambi.
6. Mariamu (Maria) alipata mimba na kuzaa watoto wengine na Yusufu ambao
wametajwa kwenye Biblia kuwa ni ndugu zake wa kike na wa kiume Kristo.
7.
Wahipinga kitendo cha
kuabudu kiumbe kingine zaidi ya kumuabudu Mungu Baba.
8.
Walikuwa na Sakramenti
mbili.
9. Hawakuwa na alama ya msalaba wala hawakuitumia.
10. Mafundisho ya Mkate na divai kugeuka na kuwa damu na mwili halisi hayaonekani
kuwa yalifundishwa na wao.
11. Roho Mtakatifu ilikuwa ni uweza au nguvu itendayo kazi na uweza wa Mungu
inayowawezesha watu kuwa wana wa Mungu na kustahili uhusiano wa Baba kama
Kristo alivyofanyika kuwa mrithi pamoja na Baba (tazama majarida ya Roho Mtakatifu (Na. 117) na Kurithi Pamaja Baba (Na. 81) [The Holy Spirit (No. 117) and Consubstantial with the Father (No. 81)].
12. Kristo hakujaribu kamwe kutafuta usawa wa namna yoyote ile na Mungu, bali
alijishusha na kujifanya hana stahili yoyote, akauchukua mwili wa kibinadamu na
akawa mtii hadi kufa (Wafilipi 2:6, RSV). Akawa na huduma bora
zaidi (Waebrania 8:6). Kwa kujitoa sadaka mwenyewe alifanyika kuwa mpatanishi
na mwombezi wa Agano Jipya alitakaswa na viumbe wa mbinguni na sio vya
kiduniani (Waebrania. 9:14,15,23). Kristo aliyejitoa sadaka pamoja na wale wote
waliojitoa sadaka wote wanaasili moja tu (Waebrania 2:11 RSV). Kristo alikuja
ili kuyafanya mapenzi ya Mungu na baada
ya kuteswa kwake ili atolewe sadaka mara moja kwa ondoleo la dhambi milele,
ameketi mkono wa kuume wa Mungu (Waebrania 10:5-9,12). Kristo aliyavumilia
mateso pale mtini kwa neema ya furaha aliyokirimiwa mbele yake na kwa sababu
hii ndiyo maana amepewa heshima ya kuketishwa mkono wa kuume wa Mungu (Waebrania
12:2). Mungu anawachukulia Malaika na watakatifu wote kama wana na tu watiifu
na mali ya yeye Mungu wa Roho zote na
ambaye anaturudi tukoseapo na kutukemea kwa faida yetu. Kristo alivumilia na
akawa mwana wa Mungu mwenye uweza uliotokana
na kufufuka kwake toka kwa wafu (Warumi 1:4).
Jambo hili limeendelea
kuaminika hivyo kwa kipindi chote cha historia ya Kanisa kama tunavyoona kutoka
kwenye rekodi za mateso ya kidini (tazama jarida la Jukumu la Amri ya Nne Kwenye Historia ya Makanisa
ya Mungu Yanayozishika Sabato (Na. 170) [The Role of the Fourth Commandment in
the Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)]. Tunajua kwamba mtazamo au jambo hili liliaminika sana na kanisa la Siebenburg
kama tulivyo na hiatoria kamilin ya imani yao kutokana na kazi ya uandishi
aliyoifanya Rabi \Mkuu wa Budapest alipokuwa akirudia matukio ya karne
iliyopita (DIE SABBATHARIER IN SIEBENBURGEN, Ihre Geschicte, Literatur und Dogmatik,
Budapest, Verlag von Singer & Wolfer, 1894’). Hawakuwa Wayunitari wenye imani
kali; walikuwa Wayunitari wa msimamo wa kadiri kama tulivo sisi. (Tazama jarida
la Wasabato wa Transylvania, AB2 [The Sabbatarians in
Transylvania A_B2.)]
Imani nyingine iliibuka huko Ulaya ikaongezeka kwenye imani hizi zote,
yaani za Wayunitari wenye itikadi kali na ambayo ilipinga fundisho la kuwepo
kwa Kristo siku kabla ya kuzaliwa kwake duniani na Usosinian ambao ulidaiwa
kuwa na mafundisho potofu tumeona hapo juu. Imani ya Wamanichean Dualism pia walijiengua
kama walivyofanya Wakatharist Montania pamoja na mafundisho mengine mengi ya
kiasitiki yaliyotokana na imani ya Kinostiki na Imani fumbo ambayo yameelezewa
ka kufafanuliwa kwa kina kwenye jarida la Imani ya Ulaji wa Mbogamboga Tupu na Biblia (Na.
183) [Vegetarianism and the Bible (No. 183)].
Makanisa ya Mungu kwenye karne za kumi na tisa na ishirini yalikuwa na
mafundisho kama hayahaya kama yalilvyokuwa yanafundishwa na kanisa kipindi chote
cha historia yake. Upotoshaji wa kugeuza uliofanywa na makanisa ya SDA na WCG ulioelezewa
hapo juu haukuwepo huko nyuma. Sifa zilizotolewa na Wakatoliki kwa mafundisho
ya Wariani ni sahihi, hatimaye Waariani walitofautiana baadae kimafundisho na
kanisa la kwanza kwa suala ya Roho Mtakatifu na hawakujua kazi zake. Hii, kwa
kweli ilisababisha wafanyiwe propaganda za uwongo za kuchafuliwa na Wakatoliki
na kutokuwepo kwa kila maelekezo yanayothibitisha kwenye kanuni zao
zinazojulikana kama Thalia au kazi
nyingine walizozifanya ama kina Arius, au Eusebius, au Asterius, au za askofu
mwingine yeyote wa upande wao. Jina la Waariani
limetolewa kutokana na jina la mtu mmoja wa upande wao ambaye alimtangulia kwa
kipindi kirefu. Ni mazea waliyonayo Wakatoliki ya kujaribu kuliita Kanisa kwa
jina la mtu binafsi ili wafanikishe kuvunja uendelevu wake. Mbinu na tabia hii
inasaidiwa na kitengo cha kidini kinachopendelea kuita vikundi vyao kwa majina
yao na tabia hii imeshamiri sana hasa huko nchini Marekani.
Tofauti ndogo ya msingi iliyopo kati ya hawa Watrinitariani waliobebea kwenye
imani hiyo na wale Wayunitariani wa msimamo wa kati kwenye Kanisa ni:
1. Wote wanaamini kwamba kuna Mungu Mmoja tu wa Pekee na wa Kweli. Hatokani na
kitu chochote na anaishi kwa uweza wake mwenyewe (Kutoka 3:14). Hakuna kitu
wala mtu yeyote anayelingana au wa kumlinganisha na yeye (Isaya 40:17; sawa na
Kitabu cha Hekima 11:23). Mungu ndiye mwanzo na mwisho wa kila kitu (Isaya
48:12; sawa na Ufunuo 1:8). Vitu vingine vyote vinatokana na Mungu Baba na
kwake yeye na kwa yeye kupitia kwa Yesu Kristo (Warumi 11:36; 1Wakorintho 8:6; Wakolosai
1:16). Mungu ndiye Bwana aliye yote katika yote na wapekee (Zaburi 46:12; Isaya
44:24; Waebrania 1:10). Kitabu cha fasihi cha Catholic Encyclopedia (Vol. IV, article ‘Creation’, p. 471) kinasema:
Kwamba maandiko haya yanayofanana yanadai
kwamba Mungu ndiye muumbaji wa vitu vyote yanaonyesha dhahiri kuhitaji maelezo zaidi
kufafanua. Andiko haliko sawa kama tunavyoona.
2. Wote wanakubalia kuwa mwana ni uzao wa Baba.
Mambo yaliyoko kwenye jambo hili ni haya yafuatayo:
1. Watrinitarian wanaamiki kuwa:
·
Mwana alikuwa ni mwana
aliye na wadhifa sawa kwenye Uungu. Uzao wake haukuhusiaka na kwenye tendo la
uumbaji na wanaamini kuwa alikuwa ni huyu Mungu wa kweli alitokana na Mungu wa
kweli (kinyume na inavyosema Yohana 17:3).Mungu alikuwa ni Baba aliye ndani na
Krisro alikuwa ni Mwana aliye ndani.
·
Wana wengine wa Mungu hawakutokana
na uzao wa Baba na kwa namna hiyohiyo akiwa na uhusiano wenye hadhi sawa na
Baba. Hakuna andiko linalowapa mashiko kwa madai yao haya na kigezo chao
kimewekwa kwenye falsafa za kina Plato, Aristotle na Plotinus ili kuhalalisha
madai yao haya. Tofauti hii haikupata suluhu hadi ulipoitishwa Mtaguso wa Nne wa
Lateran mwaka 1215.
·
Tangu kipindi cha Augustine,
ndipo vipindi vilihesabiwa kuanzia kipindi cha uumbaji wa Malaika. Kwa hiyo,
kuna tofauti ashirio na tofauti isiyoelezeka kati ya kuumbwa wa huyu Mwana na ule wa wana wengine wa Mungu walioko huko
Mbinguni. Madai haya yana umuhimu kutokana na andiko linalohusiana na mwanzo wa
zama au vipindi.
·
Basi kama Mwana hakuwa
ndiye huyu Mungu wa kweli, basi asingeweza kusamehe au kuwahesabia haki watu
kwa kuwapatanisha na Mungu. Tena madai haya hayajapewa mashiko na Maandiko
Matakatifu bali yanatuama tu kwenye mawazo ya kina Plato na Aristotle.
2. Mitaguso iliyofuatia pia ilitangaza maazimio yafuatayo:
·
Kristo hakuonekana kwenye
Agano la Kale au na mtu yeyote yule kipindi chote cha kabla ya Kuzaliwa kwake
hapa duniani.
·
Kristo sio yule Malaika
wa Yahova, elohim wa Agano la Kale aliyemtokea nabii Musa na kumkabidhi Torati
huko Sinai, ikiwa kwamba hakuna aliyewahi kumuona Mungu wakati wowote, na kwa
hiyo asingeweza kumuona Kristo kama angekuwa Mungu.
·
Kristo anauweza wa kujua
kila jambo na pale aliposema hakujua mambo fulani ilikuwa ni usemi tu wa
kimafumbo.
Ushahidi wa Kanisa la Kwanza unaonyesha kwamba kulikuwa hakuna mtazamo wa
kikalti kuhusiana na malaika na mara chache waliwakilishwa kwenye michoro ya
Wakristo hadi kipindi cha Constantine. Michoro ya zamani zaidi ambyo malaika
alionekana lilikuwa ni tukio la Kuvumbuliwa (kwenye karne ya pili) kwa kaburi
la Prisila (tazama Cath. Encyc., Vol.
I, p. 485). Michoro ya malaika mwenye mabawa hakuonekana kipindi cha kabla ya Constantine.
Hawakuwa wanajitokeza kamwe hadi kuwe na umuhimu wa kihistoria na hata hivyo haikuwa
mara zote wakijitokeza (ibid.). njiwa alikuwa anaonekana kuwakilisha malaika
wakiwa tanuruni mwa wana wa Kiebrania katika michoro ya ya kaburi la Prisila. Katika
karne ya nne michoro iliyokuwa inaonyesha jambo hilohilo, mkono wa Mungu
uliwekwa mahala pa malaika au mjumbe wa mbinguni. Tangu kipindi cha Constantine
aina mpya ya malaika mwenye mabawa alionekana kuchorwa kwenye michoro ya Wakristo
huenda ilituama kweye kile kilichojulikana kama Ushindi (ibid.). mfano za zamani sana unaojulukana kuwa upo hata
sasa wa malaika mwenye mabawa aliyekuwa anaonekana kwenye imani ya bas kutoka Carthage
na alionekana kwa muonekano wa pembe za Mikaeli, wote wawili kutoka karene ya
nne. Sanamu (kwenye Jumba la Makumbusho la Uingereza) ina fimbo kwenye mkono
wake mmoja na kuyashinda ya dunia na msalaba kwa upande mwingine. Kwenye karne
ya tano, tunawaona malaika wakishirikishwa pamoja kwenye michoro iliyodaiwa
kuwa ni ya Kristo na Bikira Mariamu. Jingo linaloashiria ushindi wa Mary Majors
unamuonyesha malaika Gabrieli mwenye mabawa akiruka angani kumwendea Mariamu
ambaye amezungukwa na kundi la malaika wenye mabawa. Mnamo karne ya sita
michoro iliyojulikana kama Hierachia
coelestis ya Dionysius wa uwongo ilifanya kazi kubwa na muhimu katika
kudanganya watu kuhusu dhana hii ya malaika. Hadi kipindi hiki mtazamo kuhusu
nyadhifa na utendaji kazi wa hawa Malaika wa Mbinguni ulikuwa haujatofautishwa
kwa maana kwamba kama tuliyonayo siku za leo kufundishwa kuhusu hali zao na
kazi zao. Tangu kipindi kile na kuendelea, uhusiano wa malaika na Mungu
uliwakilishwa kutoka na imani za Mashariki kwa namna ya mtenganisho wa viwango au
madaraja mbalimbali kimahakama wanapofanyia kazi kulingana na jinsi
wanavoonyesha utii wao kwa Wafalme (Cath.
Encyc., ibid., p. 485b). Maandiko ya vitabu vya Wakristo wa zamani,
sambamba na michoro yake, vilikuwa na habari chache sana zinazowaelezea
malaika. Mtazmo na imani ya Wakatoliki ni kwamba pamoja na imani maarufu inayojulikana na kuaminiwa na dini nyingi ni kwamba
ilkuwa ni muhimu kuwa msisitiza fulani kuhusu umoja wa Mungu (ibid.).
Mwendelezo wa imani kuhusu malaika ulikuwa wa muhimu ili kufanya tofauti
njema kati ya Wana wa Mungu walioko Mbinguni na kazi ya Kristo kama ilivyokuja
kuamuliwa tangu mwaka 381 kwenye Mtaguso wa Constantinople. Kutoka Mtaguso wa Chalcedon
jukumu na utendaji wa wana wa Mungu kama wajumbe na roho zinazohudumia
yalipunguzwa kwa kiasi cha kwamba uwepo wao ulikuwa kudharauliwa na neno malaika lilikoma kuwa ni la kazi
zinazoeleweka za mwana wa Mungu kukondolewa mpango wa Mungu. Akawa ni mtu tu wa
aina yeke mwenyewe ambaye alimudu kuwa na maisha madogo kwenye majukumu muhimu
ya Masihi na wateule. Imani hii iliwekwa ili kufikilisha lengo la kuyainua mafundisho
ya elimu ya Ukristo na kumuondoa Kristo kwenye uhusika wake wa uumbaji kwa
namna yoyote ile kwa mujibu wa mafundisho ya kimapokeo ya waamini utatu. Imani
hii haikuwa ya Kanisa la kwanza na neno malaika
lilionekana kuwa ni kama utendaji wa wana wa Mungu. Upunguzaji huu wa mabishano
ni tatizo moja kubwa hadi leo katika kuelezea kosmolojia ya kweli ya kibiblia kwa
wanaoanza ambao hawajaisoma bado Biblia kikamilifu. Justin Martyr (Apol. 1:6) anasema
kuwa hawa matakatifu wanaoshirikiana na malaika
Wema walishikiliwa kwa heshima kubwa sana. Athenagoras anazielezea kazi za
hawa Malaika watiifu ambao Mungu
amewaweka kwenye maeneo mbalimbali, ili wajipange wenyewe kwa mambo yote na
mbinguni na duniani (Legatio x). Katika
karne ya nne, Eusebius wa Caesaria anatofautisha kati ya imni potovu
waliyokuwanayo wao na ibada anayofanbyiwa Mungu (Demonstratio evang., III, 3). Mwishoni mwa karne ya nne, Ambrose wa
Milan anakubaliana na maombi kwa wao (Cath.
Encyc., ibid.). kwa hiyo tunaona kwamba mafundisho kuhusu roho yalijiingiza
kwenye Ukristo. Hawa kina Athanasians walipunguza nafasi ya wana wa Mungu na uhusiano
wao na Baba na kufanya kuwa kuna viumbe wengine wanaoshirikiana naye kuunda
Utatu.
Wakati huohuo walianzisha imani potofu iliyoendekeza maombi na ibada za
kuwatukuza wao na Mariamu kuwa ni viumbe waliofufuka. Mafundisho ya kwamba damu
iko halisi kwenye divai tangu kipindi hiki yaliwaondoa Malaika kwenye
ushirikiano wao na Mungu, wakisisitiza imani ya Utatu. Litania nyingi za kale
zaidi tangu kipindi hiki zililenga kwenye Utatu na hatimaye kwa Mikaeli (maana yake ni nail kama Mungu) Who is like God) na Gabrieli (maana yake
Mtu wa Mungu) na hatimaye Mariamu
(ibid.). Tofauti hizi tulizoziona hapo juu zilifanyika kuwa ni msingi wa
migawanyiko kati ya Kanisa la Kweli na na Waathanasian (au Ukristo
uliochanganya na imani za kale).
Haikuwa hivyo hadi katika Mtaguso wa Nne wa Lateran mwaka 1215, uliojadili
imani wanayofundisha waumini wa namna Kuwili mingoni mwa Wacathari wa Wakialbigensia
kwamba Kanisa la Roma liliotangaza kuwa malaika waliumbwa (kama ilivyopingwa na
Kristo ambaye hakuwa emeumbwa) na kwamba wanadamu waliumbwa baada yao (kwa
mujibu wa tangazo liitwalo Firmiter;
cf. Cath. Encyc., article ‘Angel’,
Vol. I, p. 476). Kwa kweli, Kiebrania kina neno rahisi tu la kuwaita hawa la malak linalotokana na sina la neno lak lenye maaaa ya anayekwenda au aliyetumwa,
ambaye ni mjumbe. Malaika wa uwepo wake aliyetajwa kwenye Isaya 63:9 na tafsiri
ya the LXX inamtaja kuwa ni Masihi, Malaika
wa Shauri Kuu. Aquinas anatangaza kuwa malaika hawakuwa na hadhi sawa na
Mungu bali walikuwa wameumbwa ex nihilo.
Kwa sababu hii Aquinas analinda utofauti uliopo kati ya Kristo na wana wengine
wa Mungu. Kutoka kwa Tauler (d. 1361) na wafuasi wake Wadionysian ndipo tofauti
ya kimadaraja kati ya Roho ilifuatia.
Ibada
Dhana na sababu ya kuabudu inamaanisha ni mchakato wa kutoa heshima. Inaendana
na amri. Inapaswa kumuelekezea moja kwa moja Mwenyezi Mungu na kwa ajili hii
inapaswa kuwa ni ibada tukufu na yenye unyenyekevu wa hali ya juu sana ya
kumtukuza. Ibada hii ya kumuabudu Mungu kitakatifu yaani latria, inapaswa afanyiwe Mungu peke yake (Cath. Encyc., Vol. XV, article ‘Worship’, p. 710). Wakati ibada
kama hii (dulia; hyperdulia ya Mariamu) inapoelekezwa kwa wengine, basi haielekezwi
moja kwa moja kwa Mungu, bali inaelekezwa kwa wao kwa imani kufananisha
uhusiano wao na Mungu. Aina hizi mbili zote zinatokana na dhana ya kumpa
heshima yaani proskuneo au ulegevu kutoka
kwenye \Kiyunani. Kwa hiyo, heshima wanayopewa Kristo na malaika wateule
inatokana tu na uhusiano wao mwema na Mungu. Kwa namna hii, tofauti kati ya
Watrinitariani na Wayunitariani ni ile tabia ya kumwabudu Kristo kwa kisingizio
tu cha uhusiano wake na Mungu Baba
nay a kuwa ni wa pili kihadhi–wakati mwamba W#atrinitaariani kwamba ni imani
potofu ya madhehebu yafuatayo
Tofauti ya Waprotestant
Tofauti iliyoko
kati ya Wakatoliki na Waprotestant Waamini Utatu inaonekana kuwa endelevu na
inaongezeka kutokana na malumbano yaliyopo hapo juu. Uprotestant una mitizamo
miwili. Wa kwanza ni ule wa Luther, ambao umechukua mafundisho yaliyofundishwa
na Kanisa siku nyingi kabla yake, imani iliyojulikana kama Sola Scriptura, au ni Biblia
peke yake ndiyo mamlaka yetu. Kanisa la Anglikana na mengine yanakubaliana kuwa
yaliyoamriwa na Mitaguso yalikuwa sahihi hadi ilipofikia Mtaguso wa Chalcedon mwaka
451 na kuwafanya waungane nao kimafundisho sawa na Wakatoliki wa Roma ila kwa
kiwango pungufu kidogo. Kanisa la Kilutheri halifuati mafundisho haya Luther nce
are tainted in the same way doctrinally as Roma—vinginevyo wangeweza kuirudisha
kweli asilia iliyopotoshwa kuliko ile kidogo waliyoirejesha. Harnack anasema
kwamba Ukristo umenajisika kwa imani juu ya miungu wengi au Polytheism na umeingiza
mambo mengi kadhaa yanayotokana na imani asilia za kipagani (Das Wesen des Christentums, Berlin,
1900, pp. 126,137-138,148). Hii imesababisha kuwepo malumbano ya kimsingi kati
ya kanisa kongwe la kale na Makanisa ya \Mungu kwa kipindi cha karne kadhaa
sasa.
Imani ya Ubinitariani, ambayo inapaswa pia iungane na malumbano haya, inakuwa
ni mchepusho mwingine wa kimhimili ambao hausimami sawasawa na ukweli na, kwa
hiyo, haukudumu kimafundisho kwa namna yenye kumaanisha.
Kanisa na Ibada
Kristo alianzisha Kanisa moja tu lenye Bwana mmoja na imani moja, ubatizo
mmoja na Mungu mmoja Baba wa wote (Waefeso 4:5-6). Ubatizo huu unawakilisha ibada yote, ambao unapaswa kuwa ni mmoja,
unaomlenga Mungu mmoja na kwa Kristo huyohuyo (Cath. Encyc., article ‘Worship’, ibid.). imani hii haijabadilika
bado Kanisa bado linamuabudu Mungu huyohuyo na ni Baba wa wote. Muntgu
anastahili kuabudiwa kama ishara ya utakatifu na haki, na suala hili la kuabudu
sio la hiyari kwa viumbe wake wote (Cath.
Encyc., op. cit.). haki
na utakatifu ni neno moja lenye maana moja pia (tsedek) ni la lugha ya Kiebrania. Kuabudu kifaragha na kwa wazi
hakutoshi. Jamii inapaswa imheshimu na Wakristo wanapaswa kukutanika pamoja
kumuabudu na mumsifu na kumtafakari yeye (ibid.).
Wamontani kwenye karne ya pili walianzisha imani potofu ya kumuabudu Roho Mtakatifu,
kama walivyokuwa wakitarajia kitendo cha Roho kuja na kuchukua mahala pa wana
na kuitangaza injili iliyokamili zaidi. Imani hii ilishinikizwa na kupelekea
kuitishwa kwa Mtaguso wa Nne wa Roma mwaka 380 ambapo Papa Damasus aliwalaani
na kumshutumu mtu yeyote anayekataa fundisho la kwamba Roho Mtakatifu anapaswa
kuabudiwa pia, sawa na Baba na Mwana (ibid., p. 711). Ndipo mwaka uliofuatia (381)
kwenye Mtaguso wa Constantinople, ndipo Roho Mtakatifu aliongezwa kwenye Uungu
na kuanza kwa Utatu lakini hauikuwa imefanikiwa sana kama ilivyokuwa
Wakapadokia walivyokuwa wamependa. Jambo hili lilianzisha utata uliopelekea
tofauti kubwa nyingine kati ya Kanisa na Waamini Utatu.
Wakatoliki walikubali (ibid.) kwamba Kristo aliadhimisha kwa umakini sana
desturi zote za ibada za Wayahudi (ikiwemo Sabato na Sikukuu zilizoamriwa) kwa kuwa kutoadhimisha yeyote moja wapo kati
ya hizo kungeibua upinzani ambao ungeweza hata kuelezewa kwenye maandiko ya
Injili. Alichokuwa anapingana nao kilikuwa ni jinsi wanavyoadhimisha lakini
sio ukweli ulikuwapo kuhusu maadhimisho ya Sabato.
Kanisa la
Kweli
Dini ya
kikatoliki imejeribu kwa wakati wote kuzika uendelevu wa Kanisa kwa kuliwekea
mapingamizi kadhaa kwa kosa la kuyapinga mafundisho yhao. Hesabu za kihistoria
na mafundisho haviko sahihi kutokana na kupotoka kwa watu waliohusika na usiri
wa Kanisa lililokuwa kwenye mateso. Kanisa Katoliki limekuwa likilitesa Kanisa
la Mungu kwa kipindi cha karne nyingi. Mnamo mwaka 1179 Mtagudeo Mkuu wa Tatu
wa Lateran ulilipiga marufuku Kanisa linalojulikana la Wavallenses tangu mwaka
ule. Papa Lucius III alitoa amri Kuu ya kuwatenga huko Verona mwaka 1184 kwa
kuwa marufuku yanayotolewa na Kanisa lililo na ujtii ni ya Mungu na siyo ya
mwanadamu na walikataa kuiacha imani yao. Mkutano Mkuu kati ya Kanisa na
Wakatoliki uliitishwa na kufanyika mwaka 1191 na ulifuatiwa na ule wa pili wa
Parmiers mwaka 1207. Mnamo mwaka 1192 askofu Otto wa Toul aliamuru Wawaaaldenses
wote wafungwe minyororo na wapelekwe kwenye mahakama ya kiaskofu. Mwaka 1194 Alphonso
II wa Aragon aliamuru wahamishwe na kupndolewa kutoka kwenye maeneo ya utawala
wake na kauamuru wanyimwe misaada ya nyuma na chakula. Mtaguso wa Genoa (1197) ulikazia
hukumu hii na kuamuru wauawe kwa kuchomwa moto mbele ya Kanisa. Kutoka hapo,
walijaribu kuua ama kulikomesha kabisa Kanisa kwa mbinu mbalimbali
zilizowezekana. Uwepo wa mafundisho ya kizurshi na vikundi vingi vya upotoshaji
vilisababisha muathiriko wa utambulisho uhalisia wa mambo lililoyafanya kanisa
Katoliki katika historia yake na historia yake ikawa ya uwongo kabisa wakijaribu
kuliunganisha Kanisa lao Petro Waldo na katika karne ya ishirini na kujivunia
mafundisho yao na athari zake (tazama majarida ya Mgawanyo
wa Makanisa Yanayozishika Sabato (Na. 122) na Wajibu wa Amri ya Nne Kwenye Historia ya
Makanisa ya Mungu Yanayozishika Sabato (Na 170) [General Distribution of the
Sabbath-keeping Churches (No. 122) and The Role of the Fourth Commandment in the
Historical Sabbath-keeping Churches of God (No. 170)].
Kristo ana Kanisa moja tu – lililo kwenye mamlaka mbalimbali ya kimaongozi
au kiutendaji kama anavyosema Mtume Paulo (1Wakorintho 12:6). Kanisa hilo halijawahi
kuacha kufanya kazi zake na wala halijabadili mafundisho yake ya msingi kwa
kipindi chote cha miaka elfu mbili sasa. Kanisa Katoliki wanataka watu waamini
kuwa wao ndio Kanisa hilo. Madai haya ni ya uwongo. Kristo hajaanza kazi yake
karne hii na wala hajabadilisha imani na mafundisho yake. Na Kristo ni yeye yuke,
jana, leo na hata milele. Sisi tu warithi wa kweli wa imani hiyo waliyopewa
watakatifu mara moja tu (Yuda 3).
q