Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[031B]

 

 

 

Bwana wa Sabato

 

(Toleo La 1.5 20101204-20101207)

 

Jina au Cheo cha Bwana wa Sabato kama linavyommaanisha Kristo, mara nyingi limepotoshwa na imani ya Kikristo kwa hila yenye lengo la kuuwezesha mfumo wao wa kiimani wa Kiantinomia ufanikiwe vyema. Maana yake halisi na iliyokusudiwa imepotoshwa kabisa na kuwa kinyume chake. Kristo alijitangaza mwenyewe kuwa ni Bwana wa Sabato akimaanisha kuvuta hisia ya kwamba ataiendelewa Sabato na kuipa nguvu zaidi Amri ya Nne pamoja na Sabato zake, Miezi Mipya na Sikukuu zote wakati atakapokuja pasipo kuzipotosha wala kuzibadilisha, wala pasipo kuingiza ibada za sanamu na mapokeo.

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

Email: secretary@ccg.org

 

(Hatimiliki © 2010 Wade Cox)

(tr. 2016)

 

Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.  Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 

 


Bwana wa Sabato


Utangulizi

Kuna sehemu mbili kwenye injili ambapo Kristo alijitangaza mwenyewe kuwa yeye ni Bwana wa Sabato.

 

Waantinomia ambao ni waabudu Miuingu ya Jua wanashikilia kuamini kwamba usemi huu ulimaanisha kuwa Kristo aliruhusu kubadilika kwa Sabato na kuwa Jumapili kwenye imani ya Kikristo na kwamba alizitangua Sabato za Biblia na kuzirihusu au kuzipa nafasi siku nyingine za kuabudu mungu Junna miungu mingine ya Kisirisiri, kwamba ziingizwe tu na zchuiue nafasi ya Sabato za kwenye Biblia. Upotoshaji huu wa makusudi unapasa ubadilishwe kabisa na kukanushwa.

 

Hebu na tutafakari kile alichokisema Kristo na tulione jambo hili kwenye maandiko mengine linamaanisha nini. Hiki ndicho kwa hakika alichokisema Kristo na mazingira yalivyokuwa hadi ikampelekea aseme hivyo:           

 

Marko 2:23-28 Ikawa alipokuwa akipita mashambani siku ya sabato, wanafunzi wake walianza kuendelea njiani wakivunja masuke. 24 Mafarisayo wakamwambia, Tazama, mbona wanafanya lisilokuwa halali siku ya sabato? 25 Akawaambia, Hamkusoma popote alivyofanya Daudi, alipokuwa ana haja, na kuona njaa, yeye na wenziwe? 26 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, zamani za kuhani mkuu Abiathari, akaila mikate ile ya Wonyesho, ambayo si halali kuliwa ila na makuhani, akawapa na wenziwe? 27 Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato. 28 Basi Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia.

 

Luka 6:1-5 Ikawa siku ya sabato moja alikuwa akipita katika mashamba, wanafunzi wake wakawa wakivunja masuke na kuyala, wakiyapukusa-pukusa mikononi mwao. 2 Basi baadhi ya Mafarisayo wakawaambia, Mbona mnafanya lisilo halali siku ya sabato? 3 Yesu akawajibu akawaa mbia, Hamkulisoma hata hilo alilolifanya Daudi, alipokuwa na njaa, yeye na wale aliokuwa nao? 4 Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu, akaitwaa mikate ile ya Wonyesho, akaila akawapa na hao wenziwe, ambayo si halali kuila ila kwa makuhani peke yao. 5 Akawaambia, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato.

 

Vifungu hivi kimsingi vinafanana tu na vinamaana moja hiyohiyo kusuduwa na ujumbe wake ulikuwa unaelekezwa moja kwa moja kwa makuhani na mazingira ambayo kisa hiki cha Sabato kilivyotumiwa na Kristo kwa makusudi ambayo kwayo iliwekwa tanngu mwanzo.

 

Ni Kristo ndiye aliyejitangaza mwenyewe kuwa ni Mwana wa Adamu, na pia kuwa ni Bwana wa Sabato. Na ndipo alielekeza moja kwa moja hoja zake kwa Daudi ambaye ni mkate wa wonyesho na ndipo alipofuatia kujitangaza kwake mwenyewe kuwa ni Bwana wa Sabato. Tendo hili halina udhuru kwa mstari wote mzima wa m6l6olon6go wa mambo.

 

Zekaria 12:8 inasema kwamba Daudi na watu wote wa nyumbani mwake ambao ni wateule watakuwa elohim kama Malaika wa Yahova vichwani mwao. Kwa hiyo alikuwa anajitangaza mwenyewe kuwa ni elohim wa Israeli na kichwa cha ukuhani wa Melkizedeki ambapo kwayo alijitangaza kuwa ni Kuhani Mkuu (soma Waebrania sura za 4-10).

 

Vigezo vya kuwa Kuhani Mkuu wa mfano wa Melikizedeki vinawafanya wale wote walio kwenye Mwili wa Kristo waweze kufanyika kuwa wafalme na makuhani watakaotawala pamoja na Kristo kwa mfano wa Melikizedeki.

 

Vigezo vha kuwa mfano wa Melkizdeki ndio kigezo cha makuhani walio chini yake ili wafae kuwa ni makuhani pamoja na yeye.

 

Maandiko ya Biblia yanatazama mbele kuiashiria siku hiyo na kuuelezea mazingira na utawala ambayo kwamba wateule wake Mungu wakiwa kama makuhani watakaokuwa chini ya Kristo watahudumu na kwa kweli, jinsi Kuhani Mkuu wa mfano wa Melkizedeki atakapojipangia majukumu na kuwapangia majukumu makuhani majukumu yao watakaohudumu kipindi hiki na utaratibu wa ibada.

 

Kwa mtazamo huo, ndipo yeye ni Bwana wa Sabato na atawapangia makuhani wake majukumu ya kushughulikia mambo yote yahusuyo maadhimisho ya Sabato zote, sawasawa na ilivyoamriwa kuadhimishwa kwenye Maandiko Matakatifu. Hivyo basi, maongozi na maelekezo ya Kristo akiwa kama Bwana wa Sabato yanajiri na kama ilivyokusudiwa wakati zilipoanzishwa Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya na Sikukuu zilizoamriwa na kuagizwa kwenye Maandiko Matakatifu, na Kristo pia alisema kuwa Maandiko hayawezi kutanguka. Kwenye maandiko ya Yohana 10:34-35 alisema pia kwamba: “Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu (Zaburi) ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu? 35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka);”

 

Kwa hiyo, wateule watafanyika kuwa elohim na taifa la wafalme na makuhani. Wote watajumuishwa kutumika pamoja na huyu Bwana wa Sabato na kwa kufanya kwao hivyo, watakuwa wanaendeleza maadhimisho ya Sabato ulimwenguni.

 

Pia wataanzisha zama za utawala ambao maongozi na maagizo yake yote yatatokea Yerusalemu.

 

Zekaria 14:1-21 Tazama, siku moja ya Bwana inakuja, ambayo mateka yatagawanyika kati yako. 2 Kwa maana nitawakusanya mataifa yote walete vita juu ya Yerusalemu; na huo mji utapigwa, nazo nyumba zitatekwa, nao wanawake watatendwa jeuri; na nusu ya watu wa mji watatoka kwenda utumwani; ila mabaki ya watu wa mji hawatakatiliwa mbali. 3 Hapo ndipo atakapotokea Bwana, naye atapigana na mataifa hayo, kama vile alipopigana zamani siku ya vita. 4 Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini. 5 Nanyi mtakimbia kwa njia ya bonde la milima yangu; kwa maana bonde lile la milima litaenea hata Aseli; naam, mtakimbia, kama vile mlivyokimbia mbele ya tetemeko la nchi, siku za Uzia, mfalme wa Yuda; na Bwana, Mungu wangu, atakuja, na watakatifu wote pamoja naye. 6 Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba nuru yake haitakuwa na mwangaza na kiwi; 7 lakini itakuwa siku moja, iliyojulikana na Bwana; si mchana, wala si usiku; lakini itakuwa, ya kwamba wakati wa jioni kutakuwako nuru. 8 Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba maji yaliyo hai yatatoka katika Yerusalemu; nusu yake itakwenda upande wa bahari ya mashariki, na nusu yake upande wa bahari ya magharibi; wakati wa hari na wakati wa baridi itakuwa hivi. 9 Naye Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina lake moja. 10 Nchi yote itageuzwa kuwa kama Araba, toka Geba mpaka Rimoni upande wa kusini wa Yerusalemu; naye atainuliwa juu, atakaa mahali pake mwenyewe, toka lango la Benyamini mpaka mahali pa lango la kwanza, mpaka lango la pembeni; tena toka mnara wa Hananeli mpaka mashinikizo ya mfalme. 11 Na watu watakaa ndani yake, wala hakutakuwako laana tena; lakini Yerusalemu utakaa salama. 12 Na hii ndiyo tauni, ambayo Bwana atawapiga watu wote waliofanya vita juu ya Yerusalemu; nyama ya mwili wao itaharibika, wasimamapo juu ya miguu yao, na macho yao yataharibika ndani ya vichwa vyao, na ndimi zao zitaharibika vinywani mwao. 13 Tena itakuwa siku hiyo, ya kwamba mashaka makubwa yatokayo kwa Bwana yatakuwa kati yao; na kila mmoja wao atakamata mkono wa jirani yake, na mkono wake utainuliwa ili kushindana na mkono wa jirani yake. 14 Yuda naye atafanya vita juu ya Yerusalemu; na huo utajiri wa mataifa wa pande zote utakusanyika, dhahabu, na fedha, na mavazi; vitu vingi sana. 15 Na hivyo ndivyo itakavyokuwa tauni ya farasi, na nyumbu, na ngamia, na punda, na ya hao wanyama wote watakaokuwamo matuoni mle, kama tauni hiyo. 16 Hata itakuwa, ya kwamba kila mtu aliyesalia wa mataifa yote, waliokuja kupigana na Yerusalemu, atakwea mwaka baada ya mwaka ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, na kuishika sikukuu ya Vibanda. 17 Tena itakuwa, ya kwamba mtu awaye yote wa jamaa zote zilizomo duniani, asiyekwea kwenda Yerusalemu ili kumwabudu Mfalme, Bwana wa majeshi, mvua haitanyesha kwao. 18 Na kama jamaa ya Misri hawakwei, wala hawaji, pia haitanyesha kwao; itakuwako tauni, ambayo Bwana atawapiga mataifa, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda. 19 Hii ndiyo adhabu ya Misri, na adhabu ya mataifa yote, wasiokwea ili kushika sikukuu ya Vibanda. 20 Siku hiyo katika njuga za farasi yataandikwa maneno haya, WATAKATIFU KWA Bwana; navyo vyombo vilivyomo ndani ya nyumba ya Bwana vitakuwa kama mabakuli yaliyoko mbele ya madhabahu. 21 Naam, kila chombo katika Yerusalemu, na katika Yuda, kitakuwa kitakatifu kwa Bwana wa majeshi; nao wote watoao dhabihu watakuja kuvitwaa vile vyombo, na kutokosa nyama ndani yake; wala siku hiyo hatakuwamo tena mfanya biashara ndani ya nyumba ya Bwana wa majeshi.

 

Ni wazi na dhahiri sana tu kwamba kutokana na aya za 16-19 kwamba Bwana wa Sabato ataamuru kuwe na msisitizo wa kuziadhimisha Sabato za Mungu.

 

Mapatilizo au adhabu itakayowakumba watu kwa kutoziheshimu amri na maagizo haya yatakuwa ni kukumbwa kwa baa la njaa na tauni ya Misri ili kwamba kama unadhani kuwa unaweza kuepukana na baa hili kali la njaa kwa kutumia mbinu za kilimo cha umwagiliaji au kwa kuhifadhi chakula kingi kwenye maghala utakatishwa tamaa sana. Kwa kuwa utauawa kwa mapigo ya magonjwa. 

 

Pia atasisitiza maadhimisho ya Miandamo ya Mwezi Mpya sambamba na Sabato kama tunavyojionea kwenye andiko la Isaya 66:23, na kwenye aya ya 24 tunaona kuwa wanalazimishwa kwa adhabu ya kifo.

 

Isaya 66:23-24 Na itakuwa, mwezi mpya hata mwezi mpya, na sabato hata sabato, wanadamu wote watakuja kuabudu mbele zangu, asema Bwana. 24 Nao watatoka nje na kuitazama mizoga ya watu walioniasi; maana funza wao hatakufa, wala moto wao hautazimika nao watakuwa chukizo machoni pa wote wenye mwili.

 

Jinsi pekee ambayo Waantinomia wanaweza kuyakeepa maandiko haya yaliyo wazi sana ni kwa mbinu za kulipotosha Agano la Kale na kudai kwamba Kristo, kwa kusema kwake kuwa yeye ni Bwana wa Sabato, alikuwa anamaanisha kuwa anamamlaka ya kuitangua na akaziweka siku nyingine za Miungu ya Kisirisiri ya Jua. Bali hata hivyo, tatizo linaendelea kubaki kuwa kwamba Mungu alinena kwa kupitia watumishi wake manabii na akasema kuwa Sabato zitashurutishwa kwa kuwekewa hukumu ya kifo. Kila mwanadamu ambaye hatatubu atapigwa kwa mapigo wakati wa kurejeshwa na kusisitizwa kwa sheria hizi na atakufa.

 

Shetani ni mungu wa dunia hii (2Wakorintho 4:4) na hivyo anauwezo wa kushurutisha imani yake ya kidini hadi atakaporudi tena Kristo. Waantinomia ni sehemu ya itikadi na mifumo ya dini potofu na za uwongo zinazotokana na dini za kishetani za waabudu muingu ya Siri ya Jua ya mungu wa Utatu. Wamejaribu kupingana na sheria na kuweka ushawishi wao kwa watu kuzipinga na kuzikataa au kuzipuuza sheria au torati ya Mungu na utaratibu aliouwaka Mungu wa ibada, kazi walioendelea kuifanya kwa kipindi cha takriban miaka elfu sita iliyopita, lakini bila ya mafanikio, na kwa kipindi kingine cha takriban miata elfu mbili wakijifanya kama Wakristo au wakiitumia dini hii. Hawataweza kushinda au kufanikisha mkakati wao na muda uliobakia na mfupi sana.

 

Pia unabii wa Mungu, aliomtumia nabii wake Ezekieli, kuhusu Marejesho na Matengenezo mapya. Unabii huu unaonyesha utawala wa haki wa mizani na vipimo, na kuwekwa mwa msisitizo wa maadhimisho ya Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya, na Sikukuu zilizoamriwa kwenye kipindi cha utawala wa mfalme. Ni wajibu wa mfalme kuainisha na kusisitiza umuhimu wa kuziadhimisha Sabato na sheria ya ulaji wa vyakula kwa kila mmoja wao kwenye kipindi chote cha matengenezo na marejesho mapya. Ni marejesho mapya ya Nchi iliyo Ahidiwa, kwa nyakati zote mbili, yaani za kabla na wakati wa utawala na kipindi cha marejesho ya milenia.

 

Utaratibu na imani hii ya kidini vitasisitizwa na kuadhimishwa kikamilifu na Kristo wakati atakapokuja hapa na wateule watalazimika kuwajibika kufanikisha mkakati wa kushika maadhimisho haya na utaratibu wake .

 

Ezekieli 45:1-25 Tena, mtakapoigawanya nchi kwa kura iwe urithi, mtamtolea Bwana toleo, sehemu takatifu ya nchi, urefu wake utakuwa urefu wa mianzi ishirini na tano elfu, na upana wake elfu kumi; itakuwa takatifu ndani ya mipaka yake yote pande zote. 2 Katika hiyo itakuwako sehemu kwa mahali patakatifu, urefu wake mia tano, na upana wake mia tano, mraba pande zote; na dhiraa ishirini kwa viunga vyake pande zote. 3 Na kwa kipimo hicho utapima, urefu wa ishirini na tano elfu, na upana wa elfu kumi; na ndani yake patakuwa patakatifu, palipo patakatifu sana. 4 Hiyo ni sehemu takatifu ya nchi; itakuwa ya makuhani, wahudumu wa patakatifu, wakaribiao kumhudumia Bwana; nayo itakuwa mahali kwa nyumba zao, na patakatifu kwa mahali patakatifu. 5 Tena urefu wa ishirini na tano elfu, na upana wa elfu kumi, ni sehemu ya Walawi, wahudumu wa nyumba, iwe milki yao wenyewe kwa vyumba ishirini. 6 Nanyi mtaiandika milki ya mji, upana wake elfu tano, na urefu wake ishirini na tano elfu, kandokando ya mahali palipotolewa, iwe sehemu takatifu; nayo itakuwa ya nyumba yote ya Israeli. 7 Na sehemu itakayokuwa ya mkuu itakuwa upande huu, na upande huu, wa toleo takatifu, na wa milki ya mji, kulikabili toleo takatifu, na kuikabili milki ya mji, upande wa magharibi kuelekea magharibi, na upande wa mashariki kuelekea mashariki; na kwa urefu wake sawasawa na sehemu mojawapo, toka mpaka wa magharibi hata mpaka wa mashariki. 8 Katika nchi hiyo itakuwa milki kwake katika Israeli; wala wakuu wangu hawatawaonea watu wangu tena kabisa; bali watawapa nyumba ya Israeli nchi hiyo, kwa kadiri ya makabila yao. 9 Bwana MUNGU asema hivi; Na iwatoshe ninyi, enyi wakuu wa Israeli; ondoeni dhuluma na unyang'anyi; fanyeni hukumu na haki; ondoeni kutoza kwa nguvu kwenu katika watu wangu, asema Bwana MUNGU. 10 Mtakuwa na mizani ya haki, na efa ya haki, na bathi ya haki. 11 Efa na bathi zitakuwa za kipimo kimoja; ili kwamba bathi ichukue sehemu ya kumi ya homeri, na efa sehemu ya kumi ya homeri; kipimo chake kitakuwa kwa kadiri ya cheo cha kawaida cha homeri. 12 Nayo shekeli itakuwa gera ishirini; shekeli tano zitakuwa shekeli tano, shekeli kumi zitakuwa kumi, na shekeli hamsini zitakuwa mane yenu. 13 Toleo mtakalotoa ni hili; sehemu ya sita ya efa katika homeri moja ya ngano, nanyi mtatoa sehemu ya sita ya efa katika homeri ya shayiri; 14 na sehemu ya mafuta iliyoamriwa, katika bathi ya mafuta, itakuwa sehemu ya kumi ya bathi katika kori moja, ambayo ni bathi kumi, yaani homeri; maana bathi kumi ni homeri moja; 15 na mwana-kondoo mmoja wa kundi katika mia mbili, katika malisho ya Israeli yenye maji; kwa sadaka ya unga, na kwa sadaka ya kuteketezwa, na kwa sadaka za amani, ili kuwafanyia upatanisho, asema Bwana MUNGU. 16 Watu wote wa nchi watatoa toleo hili kwa ajili ya mkuu katika Israeli. 17 Tena itakuwa kazi ya mkuu kutoa hizo sadaka za kuteketezwa, na sadaka za unga, na sadaka za vinywaji, katika sikukuu, na katika mwezi mpya, na katika sabato, katika sikukuu zote za nyumba ya Israeli zilizoamriwa; atatengeneza sadaka ya dhambi, na sadaka ya unga, na sadaka ya kuteketezwa, na sadaka za amani, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli. 18 Bwana MUNGU asema hivi; Mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utatwaa ng'ombe mchanga mume mkamilifu; nawe utapatakasa mahali patakatifu. 19 Na kuhani atatwaa baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi, na kuitia juu ya miimo ya milango ya nyumba, na juu ya pembe nne za daraja ya madhabahu, na juu ya miimo ya lango la ua wa ndani. 20 Nawe utafanya vivyo hivyo katika mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi kwa ajili ya kila mtu akosaye, na kwa ajili ya mtu aliye mjinga, ndivyo mtakavyoifanyia nyumba upatanisho. 21 Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi, mtakuwa na Pasaka, sikukuu ya siku saba; mkate usiotiwa chachu utaliwa. 22 Na siku hiyo mkuu atatengeneza ng'ombe kuwa sadaka ya dhambi, kwa ajili ya nafsi yake, na kwa ajili ya watu wote wa nchi. 23 Tena, katika zile siku saba za sikukuu atamtengenezea Bwana sadaka ya kuteketezwa, ng'ombe saba na kondoo waume saba wakamilifu, kila siku kwa muda wa siku saba, na beberu mmoja kila siku kuwa sadaka ya dhambi. 24 Naye atatengeneza sadaka ya unga, efa moja kwa ng'ombe, na efa moja kwa kondoo mume, na hini moja ya mafuta kwa efa moja; 25 katika mwezi wa saba, siku ya kumi na tano ya mwezi, katika sikukuu atafanya vivyo hivyo kwa muda wa siku saba; sadaka ya dhambi vivyo hivyo, na sadaka ya kuteketezwa vivyo hivyo, na sadaka ya unga vivyo hivyo, na mafuta vivyo hivyo.

 

Hakuna kilicho tofauti au kipya na kilicho kinyume na Maandiko Matakatifu kwenye mwendelezo wa mfumo na imani hii. Kudhania kama wanavyofanya Waantinomia, kwamba Kristo alimpa sheria au torati Musa huko Sinai na kuikazia kwa hukumu ya kifo, ambayo aliitoa na kuisisitiza kwenye baraza la Sanhedrin, na kisha aitangue, ni dhana ya kipuuzi. Alikuwa ni Musa aliyewachagua wazee kwa utaratibu wa 70 (+2) ili wasimamie mambo yahusuyo utoaji wa hukumu. Aliwafukuza na kuwapeleka utumwani kama taifa kwa nyakati kadhaa vipindi tofauti kwa sababu walizivunja sheria zake zihusuzo maadhimisho ya Yubile na maadhimisho ya Sabato.

 

Kisha, wakati Kristo alipofanyika kuwa mwanadamu, alizitunza pia Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya na Sikukuu zilizoamriwa kikamilifu na kwa kuziangalia sana ili zisivunjwe wala kupotoshwa na pia ndivyo walivyofanya mitume wake pia. Makanisa ya Mungu nayo yalizishika pia Sabato, Miandamo ya Mwezi Mpya na Sikukuu zilizoamriwa na wakipitia kipindi cha machungu mengi ya kifo na mateso kwa kipindi cha takriban milenia mbili.

 

Na ndivyo ilivyokuwa pia kwa Yuda, ingawa walikuwa wameipotoa kwa kuichanganya na mapokeo ambayo Kristo aliwakemea kwayo.

 

Wateule wameithibisha imani yao na kuishikilia hadi kufa kwa kipindi cha milenia mbili, na wale wote waliofariki dunia, watafufuliwa na kuendelea kuusisitizia utaratibu na imani ya Biblia kwa fimbo ya chuma kwa kipindi cha miaka elfu moja kwa wote waliohai, na kisha kwa kipindi kile cha miaka 100 ya mwisho, ambacho ni cha Ufufuo wa Pili wa wafu, utakaowakumba watu wote waliowahi kuishi usoni pa dunia kwa kipindi chote cha kudumu kwake.

q