Makanisa ya Kikristo ya Mungu

 

[093]

 

 

 

Maandalizi ya Mlo wa Pasaka

Katika Usiku wa Kuangaliwa Sana

 

(Toleo:1.0 20020324-20020324)

 

Mlo huu wa kila mwaka wa Pasaka, ukiandaliwa na kuadhimishwa kwa usahihi sana, unaweza kutoa mazingira bora zaidi ya kuwafundisha watoto na wale ambao hawajaongoka.hii ni fursa nzuri sana kuwawezesha wote wakuze ufahamu wao na uwezo wao katika kushuhudia sababu iliyowapelea kuamini.

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

 

(Copyright © 2002, Diane Flanagan, ed. Wade Cox)

(Tr. 2005)

 

Masomo haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kutufa maneno. Jina la mchapishaji na anuami yake pamoja na hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya maelezo na kilugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia ynapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:

http://www.logon.org au http://www.ccg.org

 

 


Maandalizi ya Mlo wa Pasaka

Katika Usiku wa Kuangaliwa Sana


Utangulizi

Maandalizi yanayofanywa kwa ajili ya maadhimisho sahihi katika siku ya 15 ya mwezi wa Kwanza (Abibu) yanaanzia na tendo la kuupambanua mwili wa Kristo au kanisa (1Kor.11:29) na kukusanyika mahali ambapo Mungu  amelikalisha juna lake (Kum. 16:5-6). Aina yoyote ya masalia ya chachu au amira lazima yatupwe nje ya makazi yetu ya kudumu mapema kabla ya kuondoka kwenda kwenye Sikukuu (Kut. 12:15,19; Kum. 16:4)), Wapendwa waliobatizwa kukusanyika na wenzao ili kushiriki Ushirika wa Meza ya Bwana mara baada ya giza kuingia katika siku ya 14 ya mwezi wa Kwanza yaani wa Abibu.

 

Sehe mu ya masaa ya wakati wa mchana wa siku ya 14, ibada ta kukumbuka Kifo cha Mwana Kondoo itaanza majira ya saa 9:00 alasiri, huu ni muda halisi ambao mwana kondoo alitolewa sadaka (Kut. 12:6; Kum.16:6). Sadaka ya kwanza kati ya zile tatu za mwaka huchukuliwa mapema wakati wa asubuhi (Kut. 23:18; 34:23; Kum. 16:16). Tunaweza kupata fursa ya kuleta na kuto sadaka zetu za hiyari mbele za Mungu Baba.

 

Mkumbu Mkumbushaji wa sehemu ya masaa ya mchana wa siku ya 14 ya mwezi wa kwanza atakuwa sasa amefunuliwa kwa kutoa maelezo zaidi.

 

Majukumu yanayotakiwa yatimizwe

Tunajukusanya katika matuo ta muda na tunakusanya na kuhakikisha kuwa tumeondoa aina zote za mazalia ya chachu yaani hamira zisiwepo katika vyumba vyetu tulivyopanga (Kut. 12:15,19; Kum.16:3-4). Aina yoyote ya nembo inayoashiria kutukuza sanamu na au miungu ya uwongo ni lazima viondolewe au kufunikwa wakati wote wa Sikukuu inapokuwa inaendelea. Tukisha ondoka huko nyuma yetu mwenyewe anahiyari ya kuzirudishia tena sehemu zake au kuzifunua tena lakini hii itatokea tunapokuwa sisi tumesha maliza maadhimisho na kuondoka.

 

Wakati wote wa kila kundi linapoamua kuandaa Pasaka na mlo wa siku ya Sabato

 

inayofuatia inakuwa ni chaguo la kila mtu binafsi yake, isipokuwa jambo la kuangalia tu ni kwamba pasiwepo na aina yoyote ya mazalia ya kitu chenye chachu ndani yake. Chakula ni lazima kipikwe na vitu visivyo na chachu ndani yake kwa vile tunavyokula vitu visivyotiwa chachu kwa muda wote wa siku siku saba (Kut.12:15; 13:6-7; 23:15; 34:18; Law. 23:6-8; Hes. 28:17; Kum. 16:3).

 

Siku ya 15 ya Mwezi wa Kwanza ni Sabato ya Siku Tukufu ambayo ni Siku ya Kwanza ya Mikate isiyotiwa Chachu. Huu ni usiku ule ambao Malaika alipita juu ya Misri na kuuwa kila mzaliwa wa kwanza wa binadamu na wanyama katika Misri. Israeli waliponywa na hukumu hii kutokana na kuua kwao na kumla mwana-kondoo wakiwa katika malangoni mwao (Kut. 12:7-13).

 

Kwa hiyo, tunao wajibu mkubwa wa kuhakikisha kuwa tunanunua na kutayarisha chakula chote kabla ya giza halijaanza jioni ya siku ya 14 ya mwezi wa Abibu (Law.23:6-8; Hes.28:16-18). Haturuhusiwi kuuza wala kununua siku ya Sabato (Neh. 10:28-31; Amosi 8:5). Wala haturuhusiwi kufanya aina yoyote ya kazi ya utumishi siku ya Sabato (Kut. 20:8-11; Kum.5:12-15). Kuna masharti muhimu na maalumu kwa ajili ya ushiriki wa mlo wa Pasaka katika ule Usiku wa Kuuangalia Sana kama ilivyoelekezwa hapo chini.

 

Mnyama kutoka katika kundi lako la mifugo

Mlo huu unatakiwa kujumlisha na mnyama kutoka katika kundi lako la mifugo, kwa maana nyingine ni kusema kwamba awe miongoni mwa wanyama wenye kwato zilizopasuka katikati na anayecheua na atapikwa katika mahali pale ambapo Mungu amelikalisha Jina lake (Kum. 16:2,6-7). Inatakiwa aokwe na asipikwe kwa maji wala kwa kuchemshwa na masalia ya nyama yake isibakie hadi kufikia asubuhi (Kut. 12:8-11; Hes. 9:11-14; Kum. 16:7).

 

Kwa jinsi ilivyoanza siku yenyewe ya kwanza, hakuna nyma au mifupa ya mwana kondoo iliyotolewa dhabihu kule Misri ilikuwa imesalia hadi asubuhi. Kila kilichosalia kilichomwa kwa moto na kuteketezwa kabisa; mateketevu makuu katika kila nyumba yalifanyika kwa namna ya kutisha kabisa. Hii iliweza kuzuia kila mtu aliyetaka kutumia sehemu yoyote ya sadaka hii ya mwana kondoo asiichukue na kuitoa kama sadaka kwa miungu ya mingine ya uwongo au katika kuendeleza aina yoyote ya shughuli zozote za ibada za kipagani kutoka katika masalio ya dhabihu hii. Mara tu baada ya hawa wana kondoo wakisha tolewa dhabihu kabisa, kama ilivyokuwa kwa dhabihu ya Masihi ilivyokuwa tayari imeishatolewa (Ebr. 7:27-28; 9:12; 10:10-19; 1Pet. 3:18). Ilitosheleza mambo yote muhimu yaliyotakiwa na taratibu zote zilizohitajika kwa ajili ya dhabihu. Aina yoyote ya mnyama aliye safi kutoka kwenye kundi lako la mifugo kama vile nyama ya ng’ombe, nyama ya kondoo, ya mbuzi, nk, zinakubaliwa kutumika (Wal. 11:1-8; Kum. 14:4-8).

 

Tumetengwa kutoka na familia au makundi madogomadogo ili kuadhimisha na kuula mlo wa Pasaka (Kut. 12:3-4). Kwa hiyo, inatakiwa kuandaliwe nyama ya kutosha ili kwamba itoshe kuliwa yote na wale walioko.

 

Kwa mara ile ya kwanza, damu ilichukuliwa na kupakwa juu ya miimo ya milango kama alama (Kut. 12:7,23). Tunajua vizuri sana kwamba damu ya Kristo imetutakasa sisi, na kupitia hiyo watu wote walionasi katika familia zetu wale ambao hawajaongoka wanatakaswa kupitia kwetu.

 

Hakuna mfupa unaotakiwa kuvunjwa (Kut.12:46; Hes. 9:12; Zab. 34:20; Yoh. 19:33,36) na kwa hakika ni mwana kondoo asiye na mfupa ndiye anayefaa kuandaliwa.

 

Pangilia kipimo cha wastani wa wakia 4 (kama gramu 125 hivi) za nyama ya kondoo na umpe kila mtu mzimauwa. Kwa mfano, kwa watu 12 mmoja anaweza kuhitaji mguu usio na mfupa wa uzito wa wastani wa paundi 3 (au kg 2.5) iliyookwa kwa kipimo cha pimajoto cha digrii za Falnati nyuzi 325 (sawa na Setigredi nyuzi 200). Uokaji unahitajika kutumia wastani wa dakika 40 au 45 kwa mkupuo mmoja au hadi pale kipimo cha joto kifikie na kuonyesha alama ya Falnati nyuzi 170-180. Kisha iachilie nyama ipoe kwa wastani wa dakika 10-20 kabla hujaanza kuikatakata vipande.

 

Kuna maelekezo mbalimbali kuhusiana na jinsi ya kuandaa nyama ya kondoo. Hapa chini ni baadhi tu tunayoweza kutolea mfano.

 

Kondoo wa Kiaustralia

Ijalize wastani wa gramu 150 za jagi la Marashi Moto ya Kiingereza juu ya kipande chote cha nyama, kisha kichovye chote kabisa kwa ua la waridi kisha ioke kwa mujibu wa maelekezo yaliyotolewa hapo juu. Mafuta yatajitenga na nyama kadiri inavyoendelea kupikwa na kila mmoja atachuja mafuta mwenyewe wakati anajihudumia (Law.3:17). (Jagi zenye Marashi Moto ya Kiingereza zinapatikana katika mgahawa ujulikanao kwa jina la Queen’s Pantry huko Leavenworth Kansas na vistoo vinavyofanana na hii huko Marekani).

 

Nyama ya Kondoo na Viungo

Kwa kutumia aina ya kisu kikali, tengeneza seleti au visahani vya wazi juu ya kondoo huyu. kisha tia marashi yaliyotengenezwa kwa karafuu na vituu saumu yaliyotiwa karafuu kwa ndani kabisa ya nyama. Chagiza nyama kwa mchanganyiko wa unga wa kitunguu saumu, unga wa kitunguu maji, chumvi na pilipili [tumia wastani wa kipimo cha kijiko 1 cha chai kwa (mintaarafu ya kipimo cha ujazo wa maji kiitwacho milgram 5) ya kila kiungo kwa paundi 3 (kilogramu 1 ni sawa na gramu 500) za nyama]. Iliyookwa kama isemavyo hapo juu.

 

Mafuta lazima yachujwe mbali na nyama ya kondoo baada ya kupikwa vinginevyo nyama itakauka kwa ukaufu.

 

Mboga za Uchungu

Vilevile tumeelekezwa kutumia mboga chungu katika mlo wetu (kut. 12:8). Hii inahitaji kujumlisha kuwepo na mchunga m’bichi na sahani ya mboga za majani chungu kama vile mchunga na aina nyingine yoyote unayoifahamu ya mboga zenye uchungu lakini zinazolika na bila kuleta madhara zilizoko katika maeneo yako.

 

Mikate Isiyotiwa Chachu

Kwa mujibu wa neno la Mungu, tumeamriwa wakati huu kula mikate isiyotiwa chachu tu yaani vitu visivyotiwa amira katika ule Usiku wa Kuuangalia Sana (Kut. 12:8, 15, 39) na kwa siku nyingine sita zinazofuatia za Sikukuu (Kut.12:15; 13:6-7; 23:15; 34:18; Law. 23:6-8; Hes. 28:16-18; Kum. 16:3). Katika kitabu cha Kutoka tunaona kuwa ule mkate ulikuwa hauna chachu kwa sababu waliondoka kwa haraka (Kut.12:34). Katika Kumbukumbu la Torati inaelezewa kama “Mkate wa mateso” (Kum. 16:3).

 

Maelekezo kuhusu Mikate isiyotiwa Chachu

Andaa vikombe 4 vyenye unga wenye kutosheleza mlo mzima.

Tia viini vya mayai 2 ndani yake

Tia jibini vijiko vikubwa 2 ndani yake

Tia kijiko 1/2 vya chai ndani yake

Tia milgramu 220 ya maji au maziwa

Ongezea chumvi kwenye unga,

Mega siagi katika vipande vidogovidogo kisha ongezea kwenye unga.

Koroga viini vya mayai, mafuta na maziwa au maji kwa pamoja.

Ongezea kuukoroga ule unga jongeza vizuri na kisha ukande kande.

Gawanya lile bonge katika vipande vipande ukubwa sawa na wa mpira wa magongo na kisha uponde kwa mlingano wa kimvuto mwembamba.

Kisha oka kwa kutumia jokofu lenye moto mkali kiasi cha nyuzi joto za Setigredi 180 (sawa na Falnati 350) hadi ionekane kwa rangi ya dhahabu samawati.

(kwa mujibu wa Dale Nelson)

 

kwa maelekezo mengine zaidi tafadhali soma jarida la maelekezo kwa ajili ya Mikate isiyotiwa Chachu (Na. R2).

 

Dhabihu za mikate ya nafaka iliofanywa kwa ajili ya kumtolea Mungu haikuwa inatiwa aina yoyote ya chachu wala asali (Law. 2:11)

 

Chumvi

Dhabihu zote zilitakiwa kutiwa chumvi kwa ajili hiyo basi chmvi ya agano la Mungu wetu haikutakiwa ikosekane (Law. 2:13). Chumvi hii ya agano ni ya milele (Hes. 18:19). Angalia mistari rejea ya chini katika Biblia iitwayo “Companion Bible” katika Hesabu 18:19 kuhusiana na chumvi ya agano. Tunatakiwa sisi sote tukolee munyu (Mk. 9:49-50).

 

Divai

Sasa tunafahamu kwa vizuri sana kwamba tumeamriwa kulirudia agano letu la ubatizo kwa Mungu kwa njia ya kushiriki Meza ya Bwana. Pale tunakunywa divai, ambayo ni ishara ya damu ya Masihi. Mwanzoni kabisa, sadaka ya vinywaji ilitolewa na dhabihu za aina mbalimbali (Kut. 20:40; Law.23:12; Hes. 15:5, 7, 10; 28:7, 14). Baadae katika siku za mbele, dhabihu za asubuhi zita rejeshwa tena kama inavyo onyeshwa katika Ezekieli 46 wakati tendo au wazo la sadaka ya kinywaji litakapotimilizwa, kwa sababu vitakuwa havipo kutoka katika aina nyingine ya dhabihu. Hii inaonekana kumuashiria Masihi na wateule kutimiliza ishara zote za sadaka ya vinywaji.

 

Tumeambiwa kujihudhurisha kwenye sikukuu na kula mbele za Mungu zaka ya nafaka zetu, mafuta na divai mpya kwa furaha (Kum. 14:23,26). Pia tunapaswa kuwasaidia wale wote walio yatima na wajane ambao kutoka na dhati ya mioyo yao wanashindwa kabisa kuhudhuria kwa uwezo wao wenyewe (Kum. 14:28).

 

Mahitaji mengine Muhimu

Mlo huu waweza kuhusisha na vitu vingine kama vile viazi mbatata, na viavi vitamu (vitu visivyo na chachu), lakini orodha yote ya vitu vilivyoko hapo juu imeamriwa viwepo kwa mujibu wa maandiko matakatifu. Kama ilivyo kwa mahitaji yoyote katika maisha ya mwanadamu, maandalizi ya mlo huhusisha mipangilio na maandakizi na mipangilio ili kukiwezesha kiwe tayari kwa wakati muafaka, ili kwamba wote waweze kushiriki chakula hicho mara tu giza linapoingia, tena iwe mapema vya kutosha ili kwamba watoto waweze kuwa na muda mzuri wa kujifunza maana ya Pasaka (Kut. 12:26). Usiku wa Kuuangalia Sana uliamriwa uadhimishwe na wana wa Israeli milele (Kut. 12:42).

 

Usiku wa Kuuangalia Sana

Chakula kinachofutia baada ya giza. Hiki ndicho mlo wa Pasaka (Kut. 12:6-11). Pia unaitwacho ni Usiku wa Kuuadhimisha sana au ni Usiku wa Kuuangalia (Kut. 12:42; 13:3) (angalia rejea za chini za Biblia inayoitwa “Companion Bible” kitabu cha Kutoka 12:42; vile vile jarida lisemalo Usiku wa Kuuadhimisha Sana [101].

 

Huu ni usiku kwa watoto na wale ambao hawajaongoka bado kujihudhurisha na kujifunza zaidi kuhusu mpango ya Mungu Mwenyezi katika kuwakomboa wanadamu wote na wote walioanguka.

 

Inapokaribia mwisho wa mlo huu watoto (au yeyote mmojawapo wa wale ambao hawajaongoka wa umri wowote) watauliza “maana yake ninini kufanya mambo haya yote?” (Kut. 12:26), kadiri inavyoelekea kuhusiana na matukio ya ule nlo (Kut. 12:8).Maana ya yule mwana kondoo aliyetolewa dhabihu (Kut. 12:27), maana ya ule mkate usiotiwa Chachu (Kut. 12:39) na maana ya kuzila zile mboga za uchungu (Kut. 1:14) kisha watafafanuliwa. Kasha wote watajifunza na kumcha Mungu (Kum. 6:10-16; 14:23; 17:19).

 

Kila mmoja aliyemo chumbani au ukumbini mle lazima akae kimya ili kwamba maswali yanayoulizwa yaweze kusikiwa vizuri na pia kama ikilazimika yaweze kusomwa kutoka katika Biblia na watu binafsi wanaweza kuombwa washuhudie kuhusu jinsi walivyomgeukia Bwana na kuhusu imani wanayo amini (Flp. 1:6; 1Pet. 3:15).

 

Washiriki mbalimbali kutoka kwenye makundi mbalimbali wapewe nafasi ya kushuhudia au kuelezea mafafanuzi mbalimbali kuhusiana na kwenye maswali yaliyo ilizwa. Hii inatakiwa hasa ipangiliwe mapema kabla ya muda kufika, lakini wengine wanaweza kuongezea mahali pale ambapo pamezungumziwa. Hii huwafanya kila mmoja ajifunze kushiriki na kujifunza kushuhudia wengine sababu hasa iliyowapelekea wao kudumu katika imani. Hii ingefaa kufantika kwa njia ya utaratibu maalumu lakini ikiwa inatoka moyoni,ikitolewa kwa aina inayofaa ili kwamba vijana watiwe akili na iwasisimue kusikia na kutafakari jinsi ulivyo mzuri mpango wa Mungu.

 

Mwelekeo unatakiwa ulenge katika kusoma na kufundisha zaidi kuliko kuiletea bughudha kwenye majadiliano na mazungumzo haya. Tutatakiwa kuendelea na mazungumzo haya kwa kipindi angalau cha hadi usiku wa manane muda ambao Mungu Aliye Juu sana kihistoria alionyesha uweza wake wa kuwakomboa wana wa Israeli (Kut. 11:4-5, 12-29).

 

Mawazo yanayotakiwa kujadiliwa yanahusika na lakini hayafungiki na haya:

 

1 Nini hasa maana ya Ushirika wa Meza ya Bwana, Pasaka, Mganda wa Kutikiswa na Siku za Mikate isiyotiwa Chachu ambayo ni ishara za milele (Kut. 13:9-10).

2. Maana ya Ukombozi wa kwanza kabisa kwa kila mzaliwa wa kwanza (Kut.15:13; Kum. 21:8, Luka 1:68) na hatimaye ni kwa wote kwa wakati wao wenyewe, maana ya taratibu hizi, au maelekezo (1Kor. 15:23).

 

3. Kwa nini tunatoka nje kwa haraka (Kut. 12:11, 33).

 

4. Maana ya kusema Kumbuka tulikuwa watumwa katika Misri na mlitoka nje ya mfumo. Tunatakiwa kuelekeza kila wiki kuhusu kitabu cha Kutoka wakati wa Sabato (Kum. 5:15; 16:3; Zab. 81:10).

 

5. Maana ya Mkate wa Mateso (Kum. 16:3).

 

6. Nini maana ya Mkate usiotiwa Chachu ulio liwa kwa muda wa siku 7 (Kut. 12:15; 13:6-7; 23:15, 34:18; Law. 23:6-8; Hes. 28:16-18; Kum. 16:3)

 

7. Nini maana ya kula mboga za uchungu (Kut. 1:14).

 

8. Nini maana ya Damu ya agano (Kut. 24:8; Zek.9:11; Mk. 14:24-25; Lk. 22:20; 1Kor. 11:25-29; Efe. 1:7; Kol. 1:14-20; Ebr. 9:14- 22; 10:29; 13:20-21; Ufu.1:5; 5:9; 12:11).

 

9. Maana ya imeadhimishwa na wote kwa vizazi vyote (Kut. 12:14, 17, 23-27).

 

10. fanya marudio ya jinsi ukuu wa ule msafara wa watu wanaotoka utumwani na hali halisi ambayo Israeli na wale kundi mchanganyiko walivyo walivyoachwa pamoja. Inaashiria nini kwetu leo? Je, tunahitaji kusubiria msafara mwingine wa Kutolewa Utumwani? (Isa. 66:18-24).

 

11. utakaso wetu, unaopatikana kwa njia ya:

 

. Mungu Baba (Kut. 31:13; 1Pet. 1:2)

. kuhusu Kristo (Efe.5:25-27; Ebr. 10:10; 13:12)

. Kuhusu Roho Mtakatifu (Rum. 15:16; 2The. 2:13)

. Kuhusu Imani (Mdo. 26:15-18)

. Kuhusu Kweli (Yoh. 4:23; Yoh. 17:17, 19)

. Kuhusu kufunga (Yoeli 2:15)

. Kuhusu Maombi (2Nya. 30:18-20)

 

Usiku wa Kuuangalia Sana unatakiwa uadhimishwe kiusahihi sana na matokeo yake ni kwamba wote watanufaika.

 

Ni jambo la baraka sana kwa kweli kufahamu, kuelewa na kuweza kuwa katika sehemu ya walio kayika mpango wa Mungu wa Pekee na wa Kweli wa ukombozi katika sayari hii. Hebu basi wote na tujifunze jinsi ya kumuishia Mungu na kumwabudu kikamilifu na katika usahihi wake.

 

q