Makanisa ya Kikristo ya Mungu

[252]

 

 

 

Amri Kuu ya Kwanza

 

(Toleo La 2.0 19981005-19990607-20120603-20120804)

 

Sheria za Mungu zimejumuisha na Amri mbili. Amri hizi Kuu Mbili huunda msingi wa sheria zote na ushuhuda wa manabii yakiwemo maandiko ambayo Yesu Kristo ameandikwa ndani yake kwa yale yanayoeleweka kwenye Biblia. Amri hii Kuu ya Kwanza imeandikwa kama: Nawe mpende BWANA, Mungu wako, kwa moyo wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote na Amri Kuu ya Pili inafanana na hii: Nawe mpende jirani yako kama nafsi yako.

 

 

 

 

Christian Churches of God

PO Box 369,  WODEN  ACT 2606,  AUSTRALIA

 

E-mail: secretary@ccg.org

 

(Haki Miliki © 1998, 1999, 2012  Wade Cox)

 

Masomo haya yanaruhusiwa kunukuliwa na kuwagawia watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kutufa maneno. Jina la mchapishaji na anuami yake pamoja na hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpewaji kutoa au kuchangia kwa ajili ya nakala yoyote atakayopewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya maelezo na kilugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.

 

Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org

 


Amri Kuu ya Kwanza

 


Utangulizi

Kuielewa Sheria na makusudio yake kumekuwa na msisitizo unaobadilika kwa vipindi vingi. Inaonekana kuwa na mabadiliko au myumbisho katika mtazamo kwa vipindi kadhaa mbali mbali, kiasi kwamba sheria hizi zinaonekana kuwa kana kwamba zina kuwa tabaka lililowekwa kwa misisitizo tofauti. Kwa usemi wa jumla na haraka na usioonyesha umakini, tunaweza kusema kuwa manabii wa zamani wanaonekana kuwa aliziona sheria kwa zaidi hasa kwa kukusudia kuzitumia katika matumizi ya utoaji haki katika maisha ya kijamii. Manabii waliokuja baada yao wanaweza kuonekana kuelekeza wajibu kwa matumizi ya kiliturujia na matumizi ya kikuhani. Baadhi zimehusika na hukumu za kinabii na kuwarejesha Israeli kwenye sheria za Mungu. Lile linaloitwa Agano Jipya linalenga kwenye mambo ya mamlaka ya Kimasihi na maendelezo ya sheria kwa kinyume na utaratibu mpya mashauri ya kirabi. Injili ya Kicoptiki ya Thomaso inaelezewa kwa swali linalounda muelekeo wa ujumbe wote. Ililenga kuweka muelekeo wa muda unaodhaniwa kufaa kufanya mambo fulani kama vile wakati wa kufanya maombezi ya kila wakati, wakati gani wa kufunga mfungo wa saumu, na kiasi cha kutoa kwa ajili ya matoleo ya hiyari. Mambo haya tote shirikishi yanashikiliwa na kutolewa muhutasari kwenye kitabu cha Qur’an, ambacho kinafanya mzunguko kamili na hurudi nyuma kwenye msisitizo wa haki ya kiraia.

 

Simulizi zo zote za sheria zinahitaji tathmini ya msisitizo wa aina mbali mbali ya maandiko kwa wakati na kusudio la sheria za asili. Kitu kimoja ambacho ni cha muhimu zaidi na ambacho kwacho yapasa kujua ni kwamba, Kristo hakuondoa hata yodi moja au kichwa cha somo au nukta moja au alama wa mkato kwenye sheria. Kama tutakavyoweza kuona, ujumbe wote wa historia ya kibiblia imeshirikishwa na kumfanya mwanadamu ampende na kisha amtii Mungu na jirani yake.

 

Katika amri za Mungu, kwa kufuatana na tathmini za sheria za Mungu, tunaona ambatano linalo fafanua la ujumbe wa Biblia ukiendelea kwa nyakati mbali mbali ikijulikana kwamba  Sheria za Mungu ni zile zile hazibadiliki kama zilivyo kwa sasa na kama zilivyowahi kuwa hapo kabla. Matatizo yote na yaliyo muhimu katika uendeshaji wa taratibu za liturujia na utakaso na utoaji wa kiukarimu na misingi ya imani vyote vinajibiwa na ufunuo ulio sahihi kwa njia ya usomaji sheria zinazotolewa kwa kila miaka saba na zikizungushiwa kwenye shera hizihizi zenyewe kama zilivyo.

 

Tutaona kuwa hatukuokolewa kwa ajili ya kuzishika sheria peke yake, bali tumeokolewa kwa neema. Pasipokuwa na Roho Mtakatifu tusingeweza kuzitunza sheria kama kabila la Yuda na mataifa ya Kipagani walivyoonyesha kukua na kutanuka kwa kipindi cha zaidi ya miaka elfu tatu. Tunazishika sheria kwa sababu tumeamriwa kufanya hivyo katika upando wetu na utiifu wetu kwa Mungu. Kila wakati ilikusudiwa kuwa sisi tufanye hivyo; ni makuhani wa dunia hii tu wamefundisha vingine visivyo au wamezihalifu sheria za Mungu na kalenda yake ili kwamba visiweze kuadhimishwa kiusahihi.

 

Wakristo wa ukristo mamboleo kutoka kwenye dini za madhehebu kwa makosa makubwa sana wamefundisha kuwa sherioa za Mungu eti zilipigiliwa misumari pale msalabani kutokana na kutafsiri kimakosa ujumbe ulioko kwenye kitabu cha Wakolosai 2:14-15. Ilikuwa ni deni la hali yetu ya kutodaiwa chini ya sheria, ni cheirographon ndiyo iliyogongomelewa msalabani, sio Sheria za Mungu kama zilivyo zenyewe. Muundo wa Kirumi wa kile kilichotokea hatimaye na kuitwa kuwa ni Ukristo ulimtafuta Kristo halisi na kumfanya awe kwenye muundo wa mfumo wa kizamani wa kipagani na mwelekeo unaoendelea kuwepo katika mfumo uliopo unaoendelea wa utaratibu wa kisiasa wa Kiyunani na Kirumi. Ili kufanikisha hili ililazimu mudhrau na kuharibu mfumo mzima wote wa kibiblia kwa njia ya hila iliyoonekana kwa kweli kama haujaiharibu kwa kufanya kwake hivyo. Kwa hiyo, hila za kulitumia Agano Jipya na ufutaji wa Sheria za Mungu zikazaliwa. Hatimaye, upangaji upya wa Kalenda ya Biblia ukachukua nafasi pale ambapo Kalenda ya Kipagani ya Dini za waabudu Jua na utaratibu wa sikukuu za Christmas na Easter ukaanzishwa ili kuchukua mahali pa Kalenda ya Mungu na utaratibu wake wa kufanyika kwa ibada.

 

Warumi wakapandikiza dini kwenye dola na wakati hili lilipoharibiwa; walijifanyia sanamu ya Mnyama ili kuuwezesha mfumo wa kidini utawale vitu vya taifa wakati ambapo hapo kale kabisa ilikuwa ni kwa dola yanyewe kabisa. Hii ingefanywa tu kwa kutumia muundo uliofanyizwa upya kikamilifu wa utaratibu wa kibiblia na wakidini kama sheria zilizopo za Mungu ambazo zinapingwa na kukataliwa mfumo wa kisiasa na wenye mchanganyiko wa Kiyunani na Kirumi na wakidini chini ya utaratibu wa mungu wa Utatu. Mfumo huu wa uongo wa kidini uliochanganyika na kisiasa ambao bado unafanyakazi hata sasa huko na Ulaya umewekezwa ili kuushinikiza mfumo huu. Hilo litabadilika kwa kipindi kifupi sana kijacho na ambacho hakitakawia sana.

 

Ni jukumu letu kama ilivyoelezewa chini ya Shera ya Mungu, kusoma na kufafanua sheria. Kwa kufanya hilo tunaona kile kitakachochukua mahala pake kwa muhula mrefu chini ya Masihi. Kama tungefanya hivyo kwa hali endelevu basi tusingeenda msobe msobe au mrama kutoka kwake kwa sehemu ya kwanza na historia yetu ingekuwa ni tofauti.

 

Amri za Mungu katika sheria

Kinyume na vile ilivyo hadithi au ngano maarufu, Sheria ya Mungu na Amri zake zilikuwa kwenye uwepo, katika ujulma wake, kutoka mwanzoni. Hii imeelezewa kwenye maandiko ya jarida la Fundisho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya 1 Bustani ya Edeni (Na.246) na jarida la Fundisho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya 2 Uzao wa Adamu, (Na.248). Wazo la Sheria za Kinuhu zilizotangulia kipindi cha Sinai ni ghilba za Marabi wa baadae wa dini ya Kiyahudi. Uelewa na kicho cha Mungu ulikuwa katika Israeli tangu kipindi cha Adamu hadi zama za Mababa wa imani, na hadi kipindi cha utumwa wa Misri kama inavyoonekana kwenye mfano wa wakunga (Kutoka 1:17-21).

Kutoka 1:17-21 inasema:

Lakini wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, wasifanye kama walivyoamriwa na huyo mfalme wa Misri, lakini wakawahifadhi hai wale wanaume.
18 Basi mfalme wa Misri akawaita wale wazalisha na kuwauliza, Kwa nini kufanya jambo hili, na kuwahifadhi watoto waume wawe hai? 19 Wazalisha wakamwambia Farao, Ni kwa sababu hao wanawake wa Kiebrania si kama wanawake wa Kimisri; kwa kuwa ni hodari hao, nao huzaa kabla mzalisha hajapata kuwafikilia. 20 Basi Mungu akawatendea mema wale wazalisha; na hao watu wakaongezeka sana, wakaendelea na kuzidi kuwa na nguvu nyingi. 21 Ilikuwa kwa sababu wale wazalisha walikuwa wakimcha Mungu, akawasimamishia nyumba.

 

Na Mungu akasema na watumishi wake manabii na hususani na Musa kwa kupitia Malaika wa Yahova (tazama jarida la Malaika wa YHVH [024].

 

Kutoka 3:2-22 inasema: Malaika wa BWANA akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea. 3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei. 4 BWANA alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa. 5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu. 6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu. 7 BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimesikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; 8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. 9 Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. 10 Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri. 11 Musa akamwambia Mungu, mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri? 12 Akasema, Bila shaka mimi nitakuwa pamoja nawe; na dalili ya kuwa nimekutumia ndio hii; utakapokuwa umekwisha kuwatoa hao watu katika Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu. 13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambi nini? 14 Mungu akamwambia MUSA, MIMI NIKO AMBAYE NIKO*; akasema, Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli; MIMI NIKO amenitumw kwenu. 15 Tena Mungu akamwambia Musa, Waambie wana wa Israeli maneno haya, BWANA, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu; hili ndili jina langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata milele, nalo ni kumbukumbu langu hata vizazi vyote. 16 Enenda, ukawakusanye wazee wa Israeli pamoja, ukawaambie, BWANA Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenitokea akaniambia, Hakika nimewajilieni, tena nimeyaona mnayotendewa huko Misri; 17 Nami nimesema, Nitawapandisha kutoka katika mateso ya Misri na kuwaingiza katika nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, nchi ijaayo maziwa na asali. 18 Nao watakusikia sauti yako; nawe utakwenda, wewe na wazee wa Israeli kwa mfalme wa Misri na kumwambia, BWANA, Mungu wa Waebrania, amekutana nasi; basi sasa twakuomba, tupe ruhusa twende mwendo wa siku tatu jangwani, ili tumtolee dhabihu BWANA, Mungu wetu. 19 Nami najua ya kuwa huyo mfalme wa Misri hatawapa ruhusa mwende zenu, la, hata kwa mkono wa nguvu. 20 Nami nitaunyosha mkono wangu, na kuipiga Misri kwa ajabu zangu zote, nitakazofanya kati yake, kisha baadaye atawapa ruhusa kwenda. 21 Nami nitawapa watu hao kufadhiliwa mbele ya Wamisri; hata itakuwa, hapo mtakapokwenda zenu hamtakwenda kitupu; 22 lakini kila mwanamke ataomba kwa jirani, na kwa huyo akaaye naye nyumbani, vyombo vya fedha, na vyombo vya dhahabu, na mavazi; nanyi mtawavika wana wenu na binti zenu; nanyi mtawateka nyara Wamisri.

 

MIMI NIKO AMBAYE NIKO au ‘eyeh ‘asher ‘eyeh au NITAKUWA KAMA VILE NITAKAVYOKUWA (tazama fn. Hadi Oxford Annotated ya Biblia ya kiindereza ya RSV). Ni Mungu wa pekee na wa Kweli ambaye hawezi kufa (tazama Yoh. 17:3; 1Yoh. 5:20; 1Tim. 6:16), Ni Mungu aliye Juu Sana (Elyon) (Kum. 32:8), ELOAH (tazama Ezra 4:24-7:26; Mit. 30:4-5) alikuwa ni mwenye kujieneza mwenyewe ili awe Mungu kama Elohim. Na nafasi hii alitoa kwa wana wake (tazama zab. 82:1,6).

 

Alimtia mafuta mwanawake wa kiroho kama Elohim,

Zaburi 45:6-7 inasema: Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 7 Umeipenda haki; Umechukia dhuluma. Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta, Mafuta ya furaha kuliko wenzako. 

 

Na akamuweka awe pamoja na wanadamu.

 

Waebrania 1:8-9 inasema: Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili. 9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.

 

Hii ilifanyika ili wote pia waweze kufanyika kuwa ELOHIM.

 

Zaburi 82:1-6 inasema: Mungu amesimama katika kusanyiko la Mungu; Katikati ya miungu anahukumu. 2Hata lini mtahukumu kwa dhuluma, Na kuzikubali nyuso za wabaya? 3 Mfanyieni hukumu maskini na yatima; Mtendeeni haki aliyeonewa na fukara; 4 Mwokoeni maskini na mhitaji; Mwopoeni mkononi mwa wadhalimu. 5 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani; Misingi yote ya nchi imetikisika. 6 Mimi nimesema, Ndinyi miungu, Na wana wa Aliye juu, nyote pia.

 

Eloh aliwapa taifa la Israeli mwana wake kama milki yake, kama Yahova wa Israeli.

 

Kumbu kumbu la Torati 32:8-9 inasema: Yeye Aliye Juu alipowapa mataifa urithi wao, alipowabagua wanadamu, Aliweka mipaka ya watu Kwa kadiri ya hesabu ya wana wa Israeli. 9 Maana, sehemu ya BWANA ni watu wake, Yakobo ni kura ya urithi wake.

 

Wanadamu wanaweza kufanyika kuwa ELOHIM na Maandiko Matakatifu hayawezi kutanguka (Yoh. 10:34-35). Na Mungu alisema na wanadamu kwa kupitia watumishi wake manabii.

 

Kutoka 4:1-10 inasema: Musa akajibu akasema, Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawatasikia sauti yangu; maana watasema, BWANA hakukutokea. 2 BWANA akamwambia, ni nini hiyo uliyo nayo mkononi mwako? Akasema, ni fimbo. 3 Akamwambia, itipe chini; akaitupa chini, nayo ikawa nyoka; Musa akakimbia mbele yake. 4 BWANA akamwambia Musa, Nyosha mkono wako, kamshike mkia; (akanyosha mkono wake akamshika, naye akageuka kuwa fimbo mkononi mwake;) 5 ili kwamba wapate kusadiki ya kwamba BWANA, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amekutokea. 6 BWANA akamwambia tena, Sasa tia mkono wako kifuani mwako. Akautia mkono wake kifuani mwake; naye alipoutoa, kumbe! Mkono wake ulikuwa una ukoma, umekuwa mweupe kama theluji. 7 Akasema, Tia mkono wako kifuani mwako tena. Akautia mkono wake kifuani mwake tena, na alipoutoa kifuani mwake, kumbe! Umerudia hali mwili wake. 8 Basi itakuwa, wasipokusadiki, wala kuisikiliza sauti ya kwanza, wataisikiliza sauti ya ishara ya pili. 9 Kisha itakuwa wsipoamini hata ishara hizo mbili, wala kusikiliza sauti yako, basi, yatwae maji ya mtoni uyamwage juu nchi kavu, na yale maji uyatwaayo mtoni yatakuwa damu juu ya nchi kavu. 10 Musa akamwambia BWANA, Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.

 

Kutoka 4:29 inasema: Musa na Haruni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa wana wa Israeli

 

[Note: the sequence of the Exodus is contained in Exodus chapters 5-10 and the texts relevant to the Law are contained in the appropriate section.]

 

Mungu, akiwa kama Eloah, alituma wajumbe wake,wa namna zote mbili, yaani wakiroho na wakimwili, akiwa kama elohim juu ya watu.

Kutoka 7:1 inasema: BWANA akamwambia Musa, Angalia, nimekufanya wewe kuwa kama Mungu kwa Farao; na huyo ndugu yako Haruni atakuwa kama nabii wako.

 

Kutoka wakati huu na kuendelea, Mungu angefanya kazi ya kuikomboa sayari hii kwa kupitia watu wake Israeli chini ya mwanae. Kiumbe huyu, kama roho, alikuwa na jina lake Yahova, anayefanyia kazi mamlaka ya Mungu na alisema kwa ulimwengu kupitia manabii. Hatimaye alifanyika kaa mwili na damu kwa kuonyesha kwake utii kwa Mungu.

 

Kutoka 11:1-10 inasema: BWANA akamwambia Musa, Liko pigo moja bado, nitakaloleta juu ya Farao na juu ya Misri; baadaye atawapa ninyi ruhusa toke huku; naye hapo atakapowapa ruhusa, atawafukuza mtoke huku kabisa kabisa. 2 Basi nena wewe masikioni mwa watu hawa, na kila mtu mume na atoke kwa jirani yake, na kila mwanamke atoke kwa jirani yake, vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu. 3 BWANA akawapa watu hao kibali machoni pa Wamisri. Zaidi ya hayo, huyo Musa alikuwa ni mkuu sana katika nchi ya Misri, machoni pa watumishi wa Farao, na machoni pa watu wake. 4 Musa akasema, BWANA asema hivi, Kama usiku wa manane mimi nitatoka nipite katika Misri, 5 na wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri watakufa, tangu tule mzaliwa wa kwanza wa Farao aketiye katika kiti chake cha enzi, hata mzaliwa wa kwanza wa huyo kijakazi aliye pale nyuma ya jiwe la kusagia; na wazaliwa wa kwanza wote wa wanyama. 6 Ndipo kutakuwa na kilio kikuu katika nchi yote ya Misri, ambacho mfano wake haujakuwa bado majira yo yote, wala hautakuwako mfano wake tena kabisa. 7 Lakini katika wana wa Israeli hapana hata mbwa atakayetoa ulimi juu yao, juu ya mtu wala juu ya mnyama; ili kwamba mpate kujua jinsi BWANA anavyowatenga Wamisri na Waisraeli. 8 Tena hao watumishi wako wote watanitelemkia kwangu mimi, nao watanisujudia, wakisema, Toka wewe, na hawa watu wote wakufuatao; na baada ya hayo nitatoka. Basi akatoka kwa Farao na hasira kuu. 9 BWANA akamwambia Musa, Farao hatawasikiliza ninyi; kusudi ajabu zangu ziongezeke katika nchi ya Misri. 10 Musa na Haruni walifanya ajabu hizo zote mbele ya Farao; BWANA akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, asiwape wana wa Israeli ruhusa watoke nchi yake.

 

Mungu aliwatumia Israeli ili kufanya ishara na maajabu, na kuonyesha uweza wake kwa mataifa na kwa jeshi la malaika waasi.

 

Kutoka 14:1-31 inasema: BWANA akasema na Musa, akamwambia, 2 Waambie wana wa Israeli, kwamba warudi na kupiga kambi yao mbele ya Pi-hahirothi, kati ya Migdoli na bahari, kukabili Baal-sefoni; mtapanga mbele yake karibu na bahari. 3 Naye Farao atasema katika habari za wana wa Israeli, Wametatanishwa katika nchi, ile jangwa imewazuia wasitoke. 4 Nami nitaufanya uwe mgumu moyo wa Farao, naye atafuata nyuma yao; nami nitajipatia utukufu kwa Farao, na kwa jeshi lake lote; na Wamisri watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA. Basi akafanya hivyo. 5 Mfalme wa Misri aliambiwa ya kuwa wale watu wamekwisha kimbia; na moyo wa Farao, na mioyo ya watumishi wake, iligeuzwa iwe kinyume cha hao watu, nao nao wakasema, Ni nini jambo hili tulilotenda, kwa kuwaacha Waisraeli waende zao wasitutumikie tena? 6 Akaandika gari lake, akawachukua watu wake pamoja naye; 7 tena akatwa magari mia sita yaliyochaguliwa, na magari yote ya Misri, na maakida juu ya magari hayo yote. 8 Na BWANA akaufanya moyo wake Farao mfalme wa Misri kuwa mgumu, naye akawafuata wana wa Israeli; kwa sababu wana wa Israeli walitoka kwa jeuri. 9 Wamisri wakafuata nyuma yao, farasi zote na magari yote ya Farao, na askari zake wenye kupanda farasi, na jeshi lake, nao wakawapata hali wamepanga pale karibu na bahari, karibu na Pi-hahirothi, kukabili Baal-sefoni. 10 Hata Farao alipokaribia, wana wa Israeli wakainua macho yao, na tazama, Wamisri wanakuja nyuma yao; wakaogopa sana; wana wa Israeli wakamlili BWANA. 11 Wakamwambia Musa, Je! Kwa sababu hapakuwa na makaburi katika Misri umetutoa huko ili tufe jangwani? Mbona umetutendea haya, kututoa katika nchi ya Misri? 12 Neno hili sio tulilokuambia huko Misri, tukisema, Tuache tuwatumikie Wamisri? Maana ni afadhali kuwatumikia wamisri kuliko kufa jangwani. 13 Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakao wafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele. 14 BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya. 15 BWANA akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele. 16 Nawe inua fimbo yako, ukanyoshe mkono wako juu ya bahari na kuigawanya; nao wana wa Israeli watapita kati ya bahari katika nchi kavu. 17 Nami, tazama, nitaifanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu, nao wataingia na kuwafuatia, nami nitajipatia utukufu kwa Farao, na kwa jeshi lake lote, kwa magari yake na kwa wapanda farasi wake. 18 Na Wamisri watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, nitakapokwisha kujipatia utukufu kwa Farao, na magari yake, na farasi zake. 19 Kisha malaika wa Mungu, aliyetangulia mbele ya jeshi lote la Israeli, akaondoka akaenda nyuma yao, na ile nguzo ya wingu ikaondoka hapo mbele yao, ikasimama nyuma yao; 20 ikafika kati ya jeshi la Misri na jeshi la Israeli; hapo palikuwa na lile wingu na lile giza, lakini lilitoa nuru wakati wa usiku; na hawa hawakuwakaribia hawa usiku kucha. 21 Musa akanyosha mkono wake juu ya bahari; BWANA akaifanya bahari irudi nyuma kwa upepo wa nguvu utokao mashariki, usiku kucha, akafanya bahari kuwa nchi kavu, maji yakagawanyika. 22 Wana wa Israeli wakaenda ndani ya bahari katika nchi kavu; nayo maji yalikuwa ukuta kwao mkono wa kuume, na mkono wa kushoto. 23 Na wale Wamisri wakawafuatia, wakaingia ndani kati ya bahari, farasi zote za Farao, na magari yake, na wapanda farasi wake. 24 Ikawa katika zamu ya alfajiri, BWANA akalichungulia jeshi la Wamisri katika ile nguzo ya moto na ya wingu, akalifadhaisha jeshi la Wamisri. 25 Akayaondoa magurudumu ya magari yao, hata yakaenda kwa uzito; na Wamisri wakasema, Na tukimbie mbele ya Israeli; kwa kuwa BWANA anawapigania, kinyume cha Wamisri. 26 BWANA akamwambia Musa, Nyosha mkono wako juu ya bahari, ili maji yarudi tena juu ya Wamisri, juu ya magari yao, na juu ya farasi zao. 27 Musa akaunyosha mkono wake juu ya bahari, na kulipopambazuka, bahari ikarudi kwa nguvu zake; Wamisri wakakimbia mbele yake; na BWANA akawakukutia mbali hao Wamisri kati ya bahari. 28 Yale maji yakarudi yakafunikiza magari ya wapanda farasi, hata jeshi lote la Farao lililoingia katika bahari nyuma yao; hakusalia hata mtu mmoja. 29 Lakini wana wa Israeli wakaenda katika nchi kavu katikati ya bahari; na hayo maji yalikuwa ni makuta upande wao wa kuume, na upande wao wa kushoto. 30 Ndivyo BWANA alivyowaokoa Israeli siku ile mikononi mwa Wamisri; Waisraeli wakawaona Wamisri ufuoni kwa bahari, wamekufa. 31 And Israel saw that great work which the Lord did upon the Egyptians: and the people feared the Lord, and believed the Lord, and his servant Moses.

 

Israeli walibatizwa kwenye utumishi wake katika Bahari ya Shamu. Alifanyika kuwa ndiye anayestahili kupokea heshima na utukufu kutoka kwao, na kiini cha ibada zao, ili kwamba waweze kufanyika kuwa ni wateule wake, na viumbe wake wanaoenea kama Elohim, kama malaika wa Yahova vichwani mwao (tazama Zek. 12:8).

 

Kuna nyimbo kumi za kumtukuza Mungu zilizoandikwa [tazama (1) Kut. 15:1-19; (2) Hes. 21:17-18; (3) Kum. 32:1-43; (4) Amu. 5:1-31; (5) 1Sam. 2:1-10; (6) 2Sam. 22:1-51; (7) Lk. 1:46-55; (8) Lk. 1:68-79; (9) Lk. 2:29-32; (10) Ufu. 14:3; 15:3]. Kama wimbo wa Musa ulioko kwenye (Kum. 32:1-43) halafu wimbo wa pili (tazama Kut. 15:1-19) inaweza kuwa ni Wimbo wa Mwana kondoo, kama ilivyo kwa wimbo wa kumtukuza Mungu. Nyimbo hizi mbili za Musa na Mwana kondoo ni zile zinazoonyesha utambulisho wa mteule kenye Matengenezo (Ufu. 15:3-4).

 

Ufunuo 15:3-4 inasema: Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa. 4 Ni nai asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu; kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako; kwa kuwa matendo tako ya haki yamekwisha kufunuliwa.

 

(tazama Zaburi 86:9-12; Isa. 66:15; Zef. 2:11; Zek. 14:16-21).

 

Kwa utendaji huu tutarejeleza nguvu za nyimbo za utukufu wa Nyota ya Asubuhi katika msingi wa ulimwengu (Ayu. 38:4-7).

 

Ayubu 38:4-7 inasema: Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema, kama ukiwa na ufahamu. 5 Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake, kama ukijua? Au ni nani aliyenyosha kamba juu yake? 6 Misingi yake ilikuwa juu ya kitu gani? Au ni nani aliyeweka jiwe lake la pembeni, 7 Hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, Na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?

 

Tutakuwa Elohim na Mungu atakuwa wimbo wetu. Tuta andaa makao na yeye. Yeye ni Elohim wa baba zetu na sisi ni Hekalu lake. Elohim wa elohim wetu ametuchagua sisi kwa mahali pa maskani yake.

 

Kutoka 15:1-19 inasema: Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia BWANA wimbo huu wakanena, na kusema, Nitamwimbia BWANA, kwa maana ametukuka sana,; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini. 2 BWANA ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza. 3 BWANA ni mtu wa vita, BWANA ndilo jina lake. 4 Magari ya Farao na jeshi lake amewatupa baharini, Maakida yake wateule wamezama katika bahari ya Shamu, 5 Vilindi vimewafunikiza, walizama vilindini kama jiwe. 6 BWANA, kono wako wa kuume umepata fahari ya uwezo, BWANA, mkono wako wa kuume wawaseta-seta adui. 7 Kwa wingj wa ukuu wako wawaangusha chini wanaokuondokea, Wapeleka hasira yako, nayo huwateketeza kama mabua makavu. 8 Kwa upepo wa mianzi ya pua yako maji yalipandishwa, Mawimbi yakasimama juu wima mfano wa chungu, Vilindi vikagandamana ndani ya moyo wa bahari. 9 Adui akasema, Nitafuatia, nitapata, nitagawanya nyara, Nafsi yangu itashibishwa na wao; Nitafuta upanga wangu mkono wangu utaawangamiza, 10 Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunikiza; Wakazama kama risasi ndani ya maji makuu. 11 Ee BWANA, katika miungu ni nani aliyekama wewe? Ni nani aliye kama wewe, mtukufu katika utakatifu, Mwenye kuogopwa katika sifa zako, mfanya maajabu? 12 Ulinyoosha mkono wako wa kuume, Nchi ikawameza. 13 Wewe kwa rehema zako umewaongoza watu uliowakomboa, Kwa uweza wako uliwaelekeza hata makao yako matakatifu. 14 Kabila za watu wamesikia, wanatetemeka, Wakaao Ufulisti utungu umewashika. 15 Ndipo majumbe wa Edomu wakashangaa. Watu wa Moabu wenye nguvu tetemeko limewapata, Watu wote wakaao Kanaani wameyeyuka, 16 Hofu na woga umewaangikia; Kwa uweza wa ukomo wako wanakaa kimya kama jiwe; Hata watakapovuka watu wako, Ee BWANA, Hata wayakapovuka watu wako ulio wanunua. 17 Utawaingiza, na kuwapanda katika mlima wa urithi wako. Mahali pale ulipojifanyia, Ee BWANA, ili upakae, Pale patakatifu ulipopaweka imara, BWANA, kwa mikono yako. 18 BWANA atatawala milele na milele. 19 Kwa maana, farasi za Farao na magari yake na wapanga farasi wake waliingia ndani ya bahari, BWANA akayarudisha maji ya bahari juu yao; bali wana wa Israeli walikwenda katika nchi kavu katikati ya bahari.

 

Israeli waliokolewa, na kwa tendo hili alipanda mbegu kwenye Urithi wa Mlima wa Yahova. Yakobo kama Israeli hutawala kutoka katika mlima wa Mungu (tazama Kum. 32:8). Yakobo kama Israeli (maana yake ni “yeye atakayetawala kama Mungu) aliwekwa na Yahova katika patakatifu pake, ambako mikono yake imeanzisha. Kwa namna hii sisi tunafanyika kuwa ni warithi wa pamoja na Yahova, na kama warithi, tunapata urithi wake kama elohim tuliopewa uweza huu bure kama wateule wa Eloah Baba yetu (tazama Rum. 8:17; Gal. 3:29; Tit. 3:7; Ebr. 1:14; 6:17; 11:9; Yak. 2:5; 1Pet. 3:7; pia tazama Mal. 2:10; Ebr. 2:11). Sisi tu wana wa Mungu pamoja na Jeshi la malaika wa  Mungu (tazama Ayu. 1:6; 2:1) na sote tumetakasika na Baba (Mal. 2:10) na kufanyika kuwa na mwanzo mmoja na Masihi (Ebr. 2:11) na kufanyika kuwa mwana wa Mungu katika uweza kutoka katika ufufuo wake kutoka kwa wafu (Rum. 1:4).

 

Lakini watu walinung’unikia kukombolewa kwao.

 

Kutoka 15:20-27 inasema: Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza. 21 Miriamu akawaitikia, Mwimbieni BWANA, kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewtupa baharini. 22 Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji. 23 Walipofika mahali palipoitwa Mara hawakupata kuyanywa yale maji ya Mara, kwa kuwa yalikuwa machungu; kwa ajili ya hayo, jina lake likaitwa Mara. 24 Ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, Tunywe nini? 25 Naye akamlilia BWANA; BWANA akamwonyesha mti, naye akautia katika hayo maji, maji yakawa matamu. Basi akawawekea amri na huku huko, akawaonja huko; 26 akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya BWANA, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa mimi ndimi BWANA nikuponyaye. 27 Wakafikilia Elimu, palipokuwa na chemchemi kumi na mbili, na mitende sabini; wakapanga hapo karibu na maji.

 

Israeli walipata kupona kutoka katika maovu yao, na walianzishwa na wale kumi na mbili, na sabini, ambaye angweza kumwagilia maji na kuwalinda chini ya Masihi, kama walivyofanya huko Elimu [tazama majarida ya Musa na Miungu ya Misri (Na.105) na Pentekoste ya Sinai (Na.115)]

 

Lakini Mungu kwanza aliwakemea kwa chakula kingi sana kiasi cha kushindwa kukiyeyusha kwenye matumbo yao.

 

Kutoka 16:9-12 inasema: Musa akamwambia Haruni, Haya, sema na mkutano wote wa wana wa Israeli, Njoni karibu mbele ya BWANA; kwa kuwa yeye ameyasikia manung’uniko yetu. 10 Ilikuwa Haruni aliponena na huo mkutano wote wa wana wa Israeli, wakaangalia upande wa bara, na tazama, utukufu wa BWANA ukaonekana katika hilo wingu. 11 BWANA akanena na Musa, akinena, 12 Nimeyasikia manung’uniko ya wana wa Israeli, haya! Sema nao, ukinena, Wakati wa jioni mtakula nyama, na wakati wa asubuhi mtashiba mkate; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.

 

Bwana akawalisha manna jangwani kwa kipindi cha miaka arobaini. Wale wote waliokataa urithi wa Mungu walikufa. Kule kuwalisha jangwani kulikuwa ni kivuli cha yale yanayokwenda kutokea, kama ilivyoelekezwa kwa kanisa, kama wateule, na na Roho Mtakatifu kama alivyokuwa ni kiini kwa kipindi cha Yubile arobaini. Hatuwezi kumuona Mungu kwa hali zetu tulizonazo sasa, vinginevyo tutakufa hakika. Hakuna mtu aliyewahi kumuona, au hatakayeweza kumuona kamwe kabisa. Yeye pekee hawezi kufa, aishiye na kukaa ndani yake ni nuru siyosogeleka (1Tim. 6:16).

 

Tunatakiwa kuitunza kama ukumbusho hadi Masihi atakapokuja.

 

Kutoka 16:32-36 inasema: Musa akasema, Hili ni neno BWANA aliloliamuru, Pishi moja ya kitu hicho na kiwekwe kwa ajili ya vizazi vyenu; ili kwamba wao wapate kukiona kile chakula nilichowalisha ninyi barani, hapo nilipowaleta kutoka nchi ya Misri. 33 Basi Musa akamwambia Haruni, Twaa kopo, ukatie pishi moja ya hiyo Mara ndani yake, uiweke mbele ya BWANA, ilindwe kwa ajili ya vizazi vyenu. 34 Kama vile BWANA alivyomwagiza Musandivyo Haruni alivyoiweka hapo mbele ya Ushahidi, ili ilindwe. 35 Na wana wa Israeli walikula Mana muda wa miaka arobaini, hata walipofikilia nchi iliyo na watu, wakala ile Mana, hata walipofikilia mipakani mwa nchi ya Kanaani. 36 Hiyo omeri ni sehemu ya kumi ya efa.

 

Mungu aliachilia mbali masharti ili kwamba sisi tuweze tuzirithi ahadi zake na ili tuweze kuwa ni hazina ya tofauti ya namna yake kwake.

 

Kutoka 19:1-25 inasema: Mwezi wa tatu baada ya kutoka Waisraeli katika nchi ya Misri, siku iyo hiyo wakafika jangwa la Sinai. 2 Nao walipokuwa wameondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, wakatua katika lile jangwa; Israeli wakapiga kambi huko wakiukabili mlima. 3 Musa akapanda kwa Mungu, na BWANA akamwita toka mlima ule, akisema, Utawaambia nyumba ya Yakobo, na kuwaarifu wana wa Israeli, maneno haya. 4 Mmeona jinsi niivyowatenda Wamisri, na jinsi nilivyowachukua ninyi juu ya mbawa za tai, nikawaleta ninyi kwangu mimi. 5 Sasa basi ikiwa mtaitii sauti yangu kweli kweli, na kulishika agano langu, hapo ndipo myakapokuwa tunu kwangu kuliko makabila yote ya watu; maana dunia yote pia ni mali yangu, 6 nanyi mtakuwa kwangu ufalme wa makuhani, na taifa takatifu. Hayo ndiyo maneno utakayowaambia wana wa Israeli. 7 Musa akaenda akawaita wazee wa watu, akawafunulia maneno haya yote, BWANA aliyokuwa amemwagiza. 8 Watu wote wakaitika pamoja wakisema, Hayo yote aliyoyasema BWANA tutayatenda. Naye Musa akamwambia BWANA maneno ya hao watu. 9 BWANA akamwambia Musa, Tazama, mimi naja kwako katika wingu zito ili watu hawa wasikie nitakaposema nawe, nao wapate kukuamini wewe nawe hata milele. Musa akamwambia BWANA hayo maneno ya watu. 10 BWANA akamwambia Musa, Enenda kwa watu hawa, ukawatakase leo na kesho, wakazifue nguo zao, 11 wawe tayari kwa siku ya tatu; maana siku ya tatu BWANA atashuka katika mlima wa Sinai machoni pa watu hawa wote. 12 Nawe utawawekea mipaka watu hawa pande zote, ukisema, Jihadharini, msipande mlima huu, wala msiuguse, hata mapambizo yake; kila mtu atakaye ugusa mlima huu, bila shaka atauawa. 13 Mkono wa mtu awaye yote usiguse mtu huyo, ila hakika yake atapigwa kwa mawe, au kupigwa kwa mkuki; kwamba ni mnyama au kwamba ni mwanadamu, hataishi. Hapo panda itakapotoa sauti kwa kufuliza ndipo watakapoukaribia mlima. 14 Musa akatelemka mlimani akawaendea watu akawatakasa, nao wakafua nguo zao. 15 Akawaambia watu; Mwe tayari siku ya tatu msimkaribie mwanamke. 16 Ikawa siku ya tatu, wakati wa asubuhi, palikuwa na ngurumo na umeme, na wingu zito juu ya mlima, na sauti ya baragumu iliyolia sana. Watu wote wakiokuwa kituoni wakatetemeka. 17 Musa akawatoa hao watu katika kituo, akawaleta ili waonane na Mungu; wakasimama pande za chini za kile kilima. 18 Mlima wa Sinai wote pia ukatoa moshi, kwa sababu BWANA alishuka katika moto; na ule moshi wake ukapanda juu kama moshi wa tanuu, mlima wote ukatetemeka sana. 19 Na hapo sauti ya baragumu ilipozidi kulia sana, Musa akanena, naye Mungu akamwitikia kwa sauti. 20 BWANA akaushukia mlima, juu ya kilele cha mlima; BWANA akamwita Musa aende hata kilele cha mlima; Musa akapanda juu. 21 Ndipo BWANA akamwambia Musa, Shuka chini, uwaonye watu wasije wakapasua njia waje kwa BWANA kutazama, kisha wengi miongoni mwao wakaangamia. 22 Makuhani nao, wamkaribiao BWANA, na wajitakase, BWANA asije akawafurikia. 23 Musa akamwambia BWANA, Watu hawa hawawezi kuukaribia mlima wa Sinai; kwa kuwa wewe ulituusia, ukisema, Wekeni mipaka kandokando ya mlima, na kuutenga. 24 BWANA akamwambia, Nenda, ushuke wewe; nawe utakwea, wewe, na Haruni pamoja nawe; lakini wale makuhani na watu wasipenye kumkaribia BWANA, asije yeye akawafurikia juu yao. 25 Basi Musa akawatelemkia hao watu na kuwaambia hayo.

 

Mungu alitoa sheria zake kwa kupitia Malaika Mkuu, (Malaika wa Shauri Kuu wa Septuagint, yaaani LXX). Kwa njia hii, kwa kupitia mwombezi aliye kati yetu, Mungu aliutoa utaratibu wa sheria akampa Musa, na mwamba wake wa kiroho alikuwa ni Kristo (1Kor. 10:4).

 

Kutoka 20:1-17 inasema: Mungu akanena maneno haya yote akasema, 2 Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.

 

[I] 3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.

 

[II] 4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu ya mbinguni, wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usikisujudie wala kukitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.

 

[III] 7 Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.

 

IIV] 8 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. 9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; 10 lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. 11 Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.

 

[V] 12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.

 

[VI] 13 Usiue.

 

[VII] 14 Usizini.

 

[VIII] 15 Usiibe.

 

[IX] 16 Usimshuhudie jirani yako uongo.

 

[X] 17 Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako.

 

Mgawanyo wa sheria hizi kwenye Amri Kuu, umetolewa hatimaye kwenye Kumbu kumbu la Torati. Muundo unnajieleza kwa uwazi sana, kwenye hizi amri nne za kwanza zinazohusika na upendo wa Mungu, na hizi sita zinazofuatia zinahusiana na upendo wa kila mtu na mwenzake. Hii kwa hiyo inahusika na watu wa kawaida (tazama pia kwenye jarida la Pendo na Muundo wa Sheria [200]. Amri ya Tano inaunganisha sehemu mbili kwa pamoja na kuzifanya ziwe na uhusiano kama wa kifamilia.

 

Wajibu wetu kwanza ni kwa Mungu, na hatimaye ni kwa ndugu zetu wapendwa. Wajibu wetu ni kujitahidi tufae na tukubalike na Mungu aliye Hai wa walio hai na sio wa waliokufa.

 

Mathayo 22:29-46 inasema: Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu. 30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala kuolewa, bali huwa kama malaika mbinguni. 31 Tena kwa habari ya kiyama ya wafu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema, 32 Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. 33 Na makukutano waliposikia, walishangaa, kwa mafunzo yake. 34 Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja. 35 Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu; 36 Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? 37 Akamwambia, Mpende Bwana, Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. 38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza. 39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. 40 Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii. 41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu akawauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo? 42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi. 43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema, 44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako? 45 Basi Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe? 46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena.

 

Ni kwa jinsi gani basi Daudi alimwita Bwana na elohim? (Zab. 45:6-7; Ebr. 1:8-9).

 

Bwana alikuwa ni elohim wa Israeli ambaye alinena na manabii na mababa wa imani. Yeye ndiye alikuwa ni yule Malaika wa Yahova akiwaongoza Israeli kama kichwa chao (Zek. 12:8).

 

Sehemu ya kwanza ya sheria inahusiana na upendo kwa Mungu. Hii inatakiwa ifanyike kwa moyo wote na akili na roho. Sehemu ya pili inahusu kumpenda jirani yako, kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Kwa hiyo basi, kama hatutawapenda jirani yetu tunayemuona, ni kwa namna gani tunaweza kumpenda Mungu tusiyemuona?

 

1Yohana 4:20-21 inasema: Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo, kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. 21 Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, apenda na ndugu yake.

 

muundo wa Amri Kuu ya Kwanza huandaa msingi wa Amri Kuu ya Pili, na amri hizi mbili zinategemea na torati na manabii. Hivyo basi, amri kumi za Mungu ni pea ndogo ya zile mbili, na nyingine zote zilizobakia ni pea ndogo ya zile kumi nyine. Amri Kuu ya Kwanza inahusiana na zile nne za kwanza kati ya zile amri kumi.

 

Mungu anashughulika na huu muundo, kwa maana halisi ya kuwa kwake yeye kuwa ni kiini cha uumbaji na wokovu. Yeye hutoa uzima wa milele kwa ye yote ampendaye, kwa utaratibu aliouweka.

 

Amri ya kwanza inatengaza muunganiko wa Mungu na ubora wake.

 

Kutoka 20:1-3 inasema: Mungu akanena maneno haya yote akasema, 2 Mimi ni BWANA, Mungu wako, niliyekutoa katika nchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. 3 Usiwe na miungu mingine ila mimi.

 

Amri ya pili inashughulika na kufuru ya ibada za sanamu na matendo ya kuabudu vitu vinavyoonekana. Mungu anataka watu wamwabudu yeye peke yake na kwa roho na kweli.

 

Inasema hivi: [II] 4 Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu ya mbinguni, wala kilicho majini chini ya dunia. 5 Usikisujudie wala kukitumikia; kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao, 6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu.

 

Amri hii inatuelekeza sisi jinsi ya kuabudu na kile kinachopaswa kuabudiwa. Hatupaswi kujifanyia mfano wa kitu cho chote kwa ajili ya kukipigia magoti, au kukiabudu, au kukifantia maombi. Hii inamaana ya kitu cho chote kama inavyosema: kwa hiyo, msalaba, au nembo ya kitu cho chote, hata kwa vile vinavyodaiwa kuwa vinawakilisha hali fulani ya uwepo wa Mungu au mwakilishi wa Mungu, au Mungu mwenyewe na aina nyingine fulani sio Kristo na wanaoitwa kuwa ni watakatifu waliokufa zamani, ambao kwayo ni Kristo tu ndiye alifufuka.

 

Amri ya tatu imewekwa kwa lengo la kulinda uweza wa jina la Mungu, na shughuli zinazohusiana na kutumika kwa jina lake, kama vile zile za utoaji wa hukumu, au utoaji wa huduma au ya kimaongozi. Shughuli zote ni kwa nguvu zake na uweza wake na mamlaka yake.

 

Inaendelea katika [III] 7 Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako, maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure.

 

Amri ya nne imewekwa ili kuhakikisha kwamba muundo wake wote umefungamanishwa na mtiririko wa Sheria zake, ndani ya kalenda na utaratibu wake. Amri ya nne haielekezi kwenye adhimisho la siku ya Sabato tu, bali inaelekeza utaratibu wa hiyo Sabato, na sheria yote mzima na muundo na utaratibu wake.

 

Inaendelea katika [IV] 8 Ikumbuke siku ya Sabato uitakase. 9 Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; 10 lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. 11 Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.

 

Kwa hiyo, uanzishwaji wa kalenda kwa utaratibu mwingine wowote au msingi ni tendo la kufuru, na uvunjaji wa Sheria na ni ashirio la kuabudu Mungu meingine wa uongo.

 

Mungu ameziweka Sabato na Miandamo ya Mwezi Mpya na Sabato za kila mwaka na Sikukuu. Hakuna utaratibu wowote uliokubalika au kuruhusiwa zaidi ya ule aliouanzisha na akaupa baraka zake. Utaratibu bandia wa maadhimisho ya ibada za Jumapili, na maadhimisho ya Christmas na Easter, ni utaratibu wa mfumo wa Kipagani unaoendana sambamba na Mungu wa Utatu. Ni uvunjaji wa amri zote nne zilizopo kwenye fungu la Amri Kuu ya Kwanza na ni uvunjaji wa sheria na amri zote [tazama majarida ya Chimbuko la Christmas na Easter [235]; Fundicho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya 1 Bustani ya Edeni [246] na Fundisho la Chanzo cha Dhambi Sehemu ya 2 Uzao wa Adamu [248]. Hakuna mfumo wala muundo ulioruhusiwa zaidi ya ule alioufanya na kuuweka Mwenyezi Mungu.

 

Mambo mengi zasa yaliyo kwenye Ukristo wa leo yametuama kwenye mtazamo unaodhania tu kwamba amri za Mungu zimekoma wakti wake na hazina maana au umuhimu tena. Hii inakinzana na hali ya kudharau kukubwa kwa muundu wa sheria na amri hizi za manabii na ujumbe wa Kristo na wa Mitume wake. Kuna utofauti katika Sheria za Mungu kati ya Sheria inayotuama katika Amri Kuu Mbili (na Amri Kumi ambazo zinaziendeleza) kwa upande mmoja na sheria za utoaji wa sadaka unaanzisha kile kinachoitwa Sheria Kuu za muhimu, ambazo zimeanzisha sehemu ya utaratibu wa Hekalu kwa upande mwingine. Sehemu kubwa ya Ukristo mambo leo unachanganya mambo haya na kimakosa sana huifungamanisha Kalenda na mambo mengine makubwa na sheria pamoja na sadaka, katika kujaribu kudharau sheria za Mungu na kuzigeuza na mfumo wa kipagani wa ibaza za Jua na wa Imani za Siri na Fumbo za kidini. Tofauti hizi zimeelezewa kwenye jarida la Tofauti ya Sheria [096] na pia imepimwa katika utaratibu wa majarida ya amri za binafsi zao wenyewe.

 

q