Makanisa ya Kikristo ya Mungu
[084]
Hivi Hamjui?
(Toleo La 1.5 20020731-20110326)
Kifungu kisemacho “hivi hamjui au hamfahamu” kimetumika mara 15 kwenye
Agano Jipya. Jarida hili linatathmini maana yake na kilichomgusa mwandishi na
kuona kuwa ni muhimu kijulikane na waumini wa Kanisa la kwanza.
Christian Churches of God
PO
Box 369, WODEN ACT 2606,
AUSTRALIA
E-mail: secretary@ccg.org
(Hatimiliki ©
2002, 2011 Dave Treat, ed. Wade Cox)
(rev. 2011)
(tr. 2015)
Masomo
haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa
kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na
tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia.
Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala
yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni katika
tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Hivi Hamjui?
Paulo alitumia usemi
wa “hivi hamjui ya kuwa” mata kumi na tatu kwenye nyaraka zake kwa makanisa ya
Warumi na Wakorintho. Alikuwa anaonyesha kushangazwa kwake kwa alichoshangaa
kugundua kuwa alikuwa analazimika kuwafundisha tena mafundisho ya msingi ambayo
alidhani kwamba walikuwa wanayajua vizuri sana. Ni mafundisho yapi basi haya na
yanaweza kutuathirije sisi leo? Kama tujuavyo kuwa Mungu habadiliki, yatupasa
tufikiri mambo ambayo Paulo alikuwa anayataja na jinsi yanavyofanana na siku
zetu sisi za leo. Hebu na tuzipitie aya zenye maneno haya ili tujue kile
alichokuwa anajaribu kukisema Paulo.
Aya ya kwanza
yenye maneno haya ni Warumi 6:3 inayosema:
Warumi 6:3 Hamfahamu ya kuwa sisi sote
tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?
Tumeweza kuona
kwenye dhana muhimu ambayo kwamba usemi huu umetokana kwao ili kuweka maana
yake. Warumi 6:1-13 inasema:
Warumi 6:1-2 Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi
ili neema izidi kuwa nyingi? 2 Hasha! Sisi tulioifia
dhambi tutaishije tena katika dhambi?
Kumbuka kuwa ni Paulo ndiye asemaye hapa. Tunawezaje kuwa wafu katika
dhambi na huku tukiwa tunaishi kwa wakati huohuo? Ni kama dhambi inaishi ndani
yetu ama la. Haiwezekani kabisa kuwa ni mtu wa namna mbili zote.
Warumi 6:3-13 Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? 4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima. 5 Kwa maana kama mlivyounganika naye katika mfano wa mauti yake, kadhalika mtaunganika kwa mfano wa kufufuka kwake; 6 mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena; 7 kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi. 8 Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; 9 tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. 10 Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. 11 Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu. 12 Basi, dhambi isitawale ndani ya miili yenu ipatikanayo na mauti, hata mkazitii tamaa zake; 13 wala msiendelee kuvitoa viungo vyenu kuwa silaha za dhuluma kwa dhambi; bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama walio hai baada ya kufa, na viungo vyenu kwa Mungu kuwa silaha za haki.
Kitabu cha
tafsiri kijulikanacho kama Matthew Henrey’s Commentary kwenye aya ya 3 inasemaon:
Ubatizo hufundisha umuhimu wa mfu katika dhambi, na kwa huo tukazikwa
kutokana na mambo yote machafu na yasiyompendeza Mungu na kutoyafuatilia tena
mambo machafu na kuanza kutembea na Mungu kwenye upya wa uzima. Maprofesa waovu
na watenda dhambi yawezekana kuwa walikuwa na ishara za nje za kufa dhambini,
na za kuzaliwa upya kwenye haki na utakatifu, bali hawakuweza kamwe kupita
kutoka kwenye familia ya Shetani hadi kwwenye ile ya Mungu. Asili ya dhana au
wazo liitwalo mtu wa kale, ni kwa kuwa lilitoholewa kutokana na baba yetu wa
kwanza, Adamu, na mtu huyo wa kale alisulibiwa pamoja na Kristo, kwa kila
muumini wa kweli, kwa neema iliyotolewa pale mtini. Imedhoofishwa na katika hali
ya kufa, kwayo, ila angali anajitahidi kupambana bado awe mzima, na hata
ikiwezekana ashinde. Lakini mwili wote wa dhambi, kwa vyovyote vile hauzipendi
sheria za Mungu, basi unapasa kuondolewa, ili kwamba muumini asifanyike tena
kuwa mtumwa wa dhambi, ila aishi katika Mungu, na kumtumikia kwa furaha.
Kumbuka rejea
yake kwa ukweli kwamba mwili wa dhambi kwa namna yoyote ile si sehemu ya sheria
takatifu na wala hauipendi. Katika siku za Paulo vuguvugu la imani ya Wanostiki
lilikuwepo na lilikuwa imara. Moja ya mafundisho makuu ya imani ya Wanostiki
lilikuwa ni kwamba torati ya Mungu haifai na kama mtu akiishika anakuwa wa
mwilini zaidi. Ili kupambisha juu nia yao ya kutamani na kupenda mali za
kidunia, basi inampasa mtu ajitenge kabisa na torati. Hili ni jambo moja ambalo
Paulo analifanya hapa anaposema, “Tufanye dhambi ili
neema iongezeke?” Neema pekee bila torati ilikuwa ndiyo mtazamo na imani
ya Kinostiki na Kiantinomia na waliyaingiza mafundisho haya au kuyapenyeza
kwenye kanisa la kwanza na Paulo alikuwa anayapinga mafundisho haya.
Hatuwezi kujitosa
kwenye tama za dunia na kutenda upotoe na tukadhani kuwa tumefunikwa na neema
ya Mungu. Tunatenda dhambi sote na kupungukiwa na utukufu wa Mungu, ila hii
haitupi leseni ya kutenda dhambi, kama wanavyomini Wanostiki wahafidhina.
Tufanyapo dhambi yatupasa kuomba msamaha na kuenndelea mbele. Hatuendelei
kwenye dhambi hiyohiyo kwa jinsi ya mwenendo na matendo yetu. Tumebatizwa kwa mauti
ya Kristo. Mtu wa kale haishi tena. Sisi tu kiumbe kipya na tunapaswa kuhakikisha
kuwa matendo yetu na nia zetu ni vitu vipya pia. Habari njema ni kwamba nasi tumebatizwa pia kwenye
maisha yake. Kama tutavumilia na kuishinda dhambi kutupeleka mbali na ukamilifu
maishani mwetu, basi tutaurithi uzima wa milele au Aionian ambao Mungu
ametuahidi. [nano hili limetafsiriwa kwa Kiingereza kama “eternal” au “milele” kwenye
mifano yote kwenye lugha ya Kiyunani.]
Warumi 6:16 Hamjui ya kuwa kwake yeye
ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii, mmekuwa watumwa
wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti, au kwamba ni
utumishi wa utii uletao haki.
Ili kuielewa aya
hii vizuri yatupasa kuziangalia aya zinazoizunguka. Aya za 15-19 kwenye Biblia ni
Msingi unaosomeka kwenye lugha ya Kiingereza:
Warumi 6:15-19 Ni nini basi? Tufanye dhambi kwa
sababu hatuwi chini ya sheria bali chini ya neema? Hasha! 16 Hamjui
ya kuwa kwake yeye ambaye mnajitoa nafsi zenu kuwa watumwa wake katika kumtii,
mmekuwa watumwa wake yule mnayemtii, kwamba ni utumishi wa dhambi uletao mauti,
au kwamba ni utumishi wa utii uletao haki. 17 Lakini
Mungu na ashukuriwe, kwa maana mlikuwa watumwa wa dhambi, lakini mliitii kwa
mioyo yenu ile namna ya elimu ambayo mliwekwa chini yake; 18 na
mlipokwisha kuwekwa huru mbali na dhambi, mkawa watumwa wa haki. 19 Nasema kwa jinsi ya kibinadamu kwa sababu ya udhaifu wa
miili yenu. Kwa kuwa kama mlivyovitoa viungo vyenu vitumiwe na uchafu na uasi
mpate kuasi, vivyo hivyo sasa vitoeni viungo vyenu vitumiwe na haki mpate
kutakaswa.
Tena tunaona
kutajwa kwa imani ya Kinostiki kwamba neema imechukua mahala pa sheria na
sheria imetanguka. Mtume Paulo anaonyesha
ukweli kwamba kwa kuwa tupo kwenye kipindi cha neema, haituondoi sisi kutoka
kwenye majukumu yetu au wajibu wetu wa kuishika sheria kama ananyoonyesha
kwenye aya ya 15.
Wengi wetu tuliona
kilichotokea wakati Kanisa la Mungu kwenye karne ya 20 liliamua kuwa
hawakupaswa wala kuhitajika kuzishika sheria. Kanisa lile lilitapikwa kutoka
kwenye kinywa cha Mungu, lilitawanyikiambali na viongozi wake waliuawa kipindi
cha majuma 40 tu baada ya kutangaza tangazo hili la wazi.
Hatuwi chini ya
sheria wakati tunapokuwa tukizitii tu. Wengi hujaribu kudai kwamba Paulo
aliitangua torati kwa kupitia maandiko yake haya. Wengi wa “Wakristo” mamboleo
wanamtaja yeye wakati wanapotoa hoja zao kupinga ushikaji wa sheria za torati.
Ni kama tu Paulo alikuwa mwendawazimu, vinginevyo asingeweza kabisa kusema kabisa
kuwa torati imetanguka na haina umuhimu tena, kwa kuwa kama tuonavyo kwenye aya
zinazofuatia, anapingana moja kwa moja na wazo hilo.
Warumi 7:12 Basi torati ni takatifu, na
ile amri ni takatifu, na ya haki, na njema.
Tuliona kwenye aya
ya 15 ya sura ya 6 kuwa Paulo anatuambia tusiendelee na dhambi. Dhambi ni nini?
Ni kitendo cha kutangua au kuvunja sheria za torati. Kama hatuzivunji sheria
basi tunatenda dhambi na kwa hiyo hatuyafuati mafundisho ya Paulo au ya Kristo yaliyosema:
Matthew 5:17 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au
manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.
Watu wanaojaribu
kuyatumia maandiko ya Paulo ili kuhalalisha msimamo wao wa Kiantinomia au hali
ya kutoshika sheria, wanafanya hivyo kwa uvunjifu wao wenyewe. Mtume Petro
aliandika kwenye 2Petro 3:15-18:
2Petro 3:15-18 Nanyi
uhesabuni uvumilivu wa Bwana wetu kuwa ni wokovu, kama vile na ndugu yetu
mpenzi Paulo alivyowaandikia kwa hekima aliyopewa; 16 vile
vile kama katika nyaraka zake zote pia, akitoa humo habari za mambo hayo;
katika nyaraka hizo yamo mambo ambayo ni vigumu kuelewa nayo; na mambo hayo
watu wasio na elimu, wasio imara, huyapotoa, kama vile wayapotoavyo na maandiko
mengine, kwa uvunjifu wao wenyewe. 17 Basi, wapenzi
mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao
wahalifu mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu. 18 Lakini,
kueni katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu
una yeye sasa na hata milele.
Paulo anakuwa ni mmoja
wa watu walionukuliwa sana kati ya watu na mitume waliowahi kuishi hapa duniani.
Warumi 7:1 Ndugu zangu, hamjui (maana
nasema na hao waijuao sheria) ya kuwa torati humtawala mtu wakati anapokuwa yu
hai?
Huu ni mkanusho wa
moja kwa moja unaokusudia kupinga imani ya Kiantinomia na ukengeufu wake, hali
na mafundisho yaliyokuwa yametapakaa nyakati za Paulo. Paulo anaendelea mbele
kwa kusema kwenye aya za 2-25:
Warumi 7:2-6 Kwa maana mwanamke aliye na
mume amefungwa na sheria kwa yule mume wakati anapokuwa yu hai; bali akifa yule
mume, amefunguliwa ile sheria ya mume. 3 Basi
wakati awapo hai mumewe, kama akiwa na mume mwingine huitwa mzinzi. Ila mumewe
akifa, amekuwa huru, hafungwi na sheria hiyo, hata yeye si mzinzi, ajapoolewa
na mume mwingine. 4 Kadhalika, ndugu
zangu, ninyi pia mmeifia torati, kwa njia ya mwili wa Kristo, mpate kuwa mali
ya mwingine, yeye aliyefufuka katika wafu, kusudi tumzalie Mungu matunda. 5 Kwa maana tulipokuwa katika hali ya mwili, tamaa za
dhambi, zilizokuwako kwa sababu ya torati, zilitenda kazi katika viungo vyetu
hata mkaizalia mauti mazao. 6 Bali sasa
tumefunguliwa katika torati, tumeifia hali ile iliyotupinga, ili sisi tupate
kutumika katika hali mpya ya roho, si katika hali ya zamani, ya andiko.
Hii ni hatua ya
kweli na halisi. Sisi tupo chini sheria ya roho, na sio ya waraka. Kristo
aliongeza uweza wa kiroho kwenye torati ambao haukuwahi kuwepo hapo zamani.
Warumi 7:7-13 Tusemeje, basi? Torati ni
dhambi? Hasha! Walakini singalitambua dhambi ila kwa sheria; kwa kuwa
singalijua kutamani, kama torati isingalisema, Usitamani. 8 Lakini
dhambi ilipata nafasi kwa ile amri, ikafanya ndani yangu kila namna ya
kutamani. Kwa maana dhambi bila sheria imekufa. 9 Nami
nalikuwa hai hapo kwanza bila sheria; ila ilipokuja ile amri, dhambi ilihuika,
nami nikafa. 10 Nikaona ile amri iletayo uzima ya kuwa
kwangu mimi ilileta mauti. 11 Kwa maana dhambi,
kwa kupata nafasi kwa ile amri, ilinidanganya, na kwa hiyo ikaniua. 12 Basi torati ni takatifu, na ile amri ni takatifu, na ya
haki, na njema. 13 Basi je! Ile iliyo njema ilikuwa mauti
kwangu mimi? Hasha! Bali dhambi, ili ionekane kuwa ni dhambi hasa, ilifanya
mauti ndani yangu kwa njia ya ile njema, kusudi kwa ile amri dhambi izidi kuwa
mbaya mno.
Haya ni maelezo
mazuri sana yanayotoa mwelekeo mzuri tulionao kuhusu dhambi na matendo yake.
Hata kwenye makanisa ya Mungu, dhambi haichukuliwi kuwa ni kitu kiovu kama
inavyostahili. Mambo haya hayatushitui tena sisi kabisa. Ni mambo
yanayokubalika kabisa kwenye jamii zetu kutoa au kuharibu mimba za vichanga na
kuwa na familia za watu wa jinsia moja. Hali hii ya kuvumilia matendo ya dhambi
inaziharibu jamii zetu na haitaweza kuvumiliwa milele. Basi na tusikutwe tukiwa
na msimamo dhaifu au kuonea aibu dhambi. Itatupeleka upotevuni na kutuangamiza.
Warumi 7:14-25 Kwa maana
twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini,
nimeuzwa chini ya dhambi. 15 Maana sijui
nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo
ninalolitenda. 16 Lakini kama nikilitenda lile
nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema. 17 Basi
sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani
yangu 18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu,
yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali
kutenda lililo jema sipati. 19 Kwa maana lile jema
nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi
nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 21 Basi nimeona sheria hii, ya kuwa kwangu mimi nitakaye
kutenda lililo jema, lipo lililo baya. 22 Kwa
maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani, 23 lakini
katika viungo vyangu naona sheria iliyo mbali, inapiga vita na ile sheria ya
akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya dhambi iliyo katika viungo
vyangu. 24 Ole wangu, maskini mimi! Ni nani
atakayeniokoa na mwili huu wa mauti? 25 Namshukuru Mungu,
kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Basi, kama ni hivyo, mimi mwenyewe kwa akili zangu
naitumikia sheria ya Mungu, bali kwa mwili wangu sheria ya dhambi.
Watu wengi, wanapobanwa
sana, wanakubaliana na angalau amri sita, bali wanazichukulia nne za kwanza
kuwa zinahusu tu mahusiano yetu na Mungu, jambo ambalo ni kosa. Paulo anasema kuwa
sheria ni takatifu na kamilifu.
Sheria ndiyo kitu
kinachoainisha au kuonyesha dhambi na hiki ndicho anachomaana Paulo. Asingeweza
kuijua dhambi kama isingekuwa torati. Anataka kuzitii sheria, ila hata hivyi
anatendadhambi kwakuwa mwili ni dhaifu. Ila kama asemavyo Paulo, hahukumiwi na
adhabu ya mauti kwa kuwa anatamani kushika sheria moyoni mwake. Ni dhambi ndiyo
ikaayo ndani yetu ambayo sasa inatupeleka kwenye hukumu ya mauti. Kristo
amezifisha dhambi. Sote tunatenda dhambi, na kama isingekuwa kujitoa sadaka kwa
Kristo, basi tungeupokea mshahara wa dhambi, ambao ni mauti. Kristo ametu0okoa
kutoka kwenye hukumu hii kwa njia ya kujitoa kwake sadaka. Sasa tuko chini ya sheria ya roho na sio
chini ya waraka. Kuwa kwetu chini ya roho ya sheria hakunaanishi kuwa hatuzitii
sheria. Bali inamaanisha tu kwamba sheria sasa zimeandikwa mioyoni mwetu. Hatuzitii
tena ssheria kwa kuwa tunazo tu bali, kwa kuwa tunazihitaji. Nia za mioyo yetu
zimehuishwa upya kwa njia ya Roho Mtakatifu.
1Wakorintho 3:16 Hamjui
ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani
yenu?
Hebu na tuwe na
mtazamo mzuri kwenye taswira kamili kwa kusoma 1Wakorintho 3:1-19 inayosema:
1Wakorintho 3:1-2 Lakini,
ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni,
bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo.
2 Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa
mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi,
Kanisa la Mungu
katika karne ya 20 lilishindwa kutulisha nyama. Hatukuwa tayari
kuila hadi sasa. Haikuwa hivyo hadi katika michache ya mwisho ambapo wengi wetu
tuligundua kuwa tulipaswa kujibidiisha kuutunza wokovu sisi wenyewe; na kwamba
hatuingia kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu kwa njia ya kujishikilia kingo za
makoti ya wahubiri. Tangu tulipogundua hilo na tukaanza kusoma kwa bidii na
makini, Mungu ametupa nyama nyingi sana inayohitajika na kuendelea kutufungua
macho yetu kwenye kweli zaidi na zaidi.
1Wakorintho 3:3-4
3 kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya
mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya
mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? 4 Maana
hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je!
Ninyi si wanadamu?
1Wakorintho 3:5-19
Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na
kila mtu kama Bwana alivyompa. 6 Mimi nilipanda, Apolo
akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. 7 Hivyo,
apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. 8 Basi
yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu
yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe. 9 Maana
sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la
Mungu. 10 Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa,
mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine
anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. 11 Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka,
isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. 12 Lakini
kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au
miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri.13
Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule
moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. 14
Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. 15 Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe
ataokolewa; lakini ni kama kwa moto. 16 Hamjui ya kuwa
ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu? 17 Kama mtu akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamharibu
mtu huyo. Kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, ambalo ndilo ninyi. 18 Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye
hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye
hekima. 19 Maana hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za
Mungu. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao.
Sisi tu hekalu la
Mungu na roho wake anakaa ndani yetu. Yatupasa kuwa waangalifu sana jinsi
tujengavyo kwenye msingi uliowekwa na Mitume. Yatupasa kupambanua kati ya kweli
na uwongo na kuhakikisha kuwa hatupotoshwi kwa mafundisho ya uwongo. Wajenzi ni
watu waliopewa wajibu au jukumu la kufundisha na kuwaongoza watu wa Mungu. Wajenzi
wanapaswa kuogopa kutumia vifaa vya ujenzi visivyofaa kwa kuwa vinaweza
kuudhoofisha mfumo mzima wa ujenzi. Ili kuwa na jingo imara, inapasa msingi
wake wapasa uwe imara na mgumu na kisha kila tabaka na awamu inayoendelea kujengwa
kutoka hapo na kuendelea mbele yapasa ijengwe kwa malighafi nzuri. Vifaa vya
ujenzi ni mafundisho ya kanisa, Mungu atatupima kwa kigezi cha uelewa wetu na
kwa njia ya utii na uaminifu wetu kwenye mafundisho tunayofundisha na
kujifunza. Mafundisho yote ya uwongo yataangamizwa ni wajibu wetu kama Wakristo
kuhakikisha kabisa kuwa hatuliachilii au kuliruhusu hekalu linajisike kwa mafundisho
ya uwongo na mapotofu.
1Wakorintho 5:6 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba
chachu kidogo hulichachusha donge zima?
Kwenye 1Wakorintho 5:1-13 tunasoma:
1Wakorintho 5:1-13 Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako
hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye. 2 Nanyi
mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo
aliyetenda jambo hilo. 3 Kwa maana kweli,
nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha
kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo. 4 Katika
jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja
na uweza wa Bwana wetu Yesu; 5 kumtolea Shetani mtu
huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu. 6 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo
hulichachusha donge zima? 7 Basi, jisafisheni,
mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa
chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo; 8 basi na tuifanye karamu, si kwa chachu ya kale, wala kwa
chachu ya uovu na ubaya, bali kwa yasiyochachika, ndio weupe wa moyo na kweli. 9 Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane
na wazinzi. 10 Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa
dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang'anyi, au na wenye kuabudu
sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia. 11 Lakini,
mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa
ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au
mnyang'anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye. 12 Maana
yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani? 13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni
yule mbaya miongoni mwenu.
Mwili wa Kristo,
watu wanaounda kanisa, wana wajibu wa kuhakikisha kuwa linafundisha vizuri.
Iwapo sisi, kama mwili wa Kristo, tukimuachia mshirika yeyote, wakiwemo
watumishi wahubiri wetu, kuenenda kwa makusudi kabisa kinyume na maagizo ya
torati ya Mungu nasi tusifanye chochote, basi tutakuwa hatuyaishii mafundisho
haya wala watuwajibiki kwa mujibu wa tulivyoagizwa na kuamriwa. Tumeagizwa sio
tu kwa kundi, bali ni kwa kila mtu binafsi yake pia, agizo la kumuondoa mtu
huyo kutoka kundini. Mwenendo wa dhambi ni sawa na saratani. Itaenea kwenye
mwili mzima kama haitaondolewa. Yapasa kuondolewa ili kunusuru uhai na sehemu ya
mwili iliyobakia.
Dhambi ni kama chachu. Inatakiwa kuwa na kiasi kidogo tu cha chachu ili kuchachusha donge zima. Tunaiondoa chachu ya dhambi mahali tulipo ili kulilinda kutaniko lote, bali pia ili mtu aondolewe ni budi ayaone au kuambiwa makosa yake na atubu. Kama hataamua kutubu ndipo ataachwa ili ahukumiwe kwenye ufufuo wa pili wa wafu. Kama kwa namna nyingine, akiamua kutubu, ndipo atarejeshwa kundini na kuwa na sehemu kwenye ufufuo wa kwanza wa wafu pe of leaven. It only takes a small amount of leaven.
Kwenye 1Wakorintho 6:2-3 tunasoma:
1Wakorintho
6:2-3 Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu
utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? 3 Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana
mambo ya maisha haya?
Aya hii imepotoshwa
kwa kutafsiriwa visivyo kwa wengine kumaanisha kwamba tutawahukumu malaika
wote. Ni dhana potofu na uwongo kwa sisi kudhania kwamba tutawahukumu malaika
waliobakia watiifu kwa Mungu. Malaika wanaotajwa hapa ni wale walioasi. Wakristo
wa kweli wanakwenda kupewa wajibu wa kuuhukumu ulimwengu na malaika waasi kwa
ajili ya matendo yao. Hatutapewa mamlaka kabisa ya kuwahukumu malaika watiifu
ambao wanatuangalia na kutulinda sisi na maisha yetu yote.
Ni nni basi
kilikuwa ni jambo la muhimu kumpelekea Paulo aandike hivi? Tunaona hilo kwenye
1Wakorintho 6:1-8.
1Wakorintho 6:1-8 Je! Mtu wa
kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki,
wala si mbele ya watakatifu? 2 Au hamjui ya kwamba
watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je!
Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? 3 Hamjui
ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya? 4 Basi, mkiwa na mahali panapohukumiwa mambo ya maisha
haya, mwawaweka kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika kanisa? 5 Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo, kwamba
kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima, awezaye kukata maneno ya ndugu zake?
6 Bali mwashitakiana, ndugu kwa ndugu, tena mbele yao
wasioamini. 7 Basi imekuwa upungufu kwenu kabisa kwamba
mnashitakiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali kudhulumiwa? Maana si afadhali
kunyang'anywa mali zenu? 8 Bali kinyume cha hayo
ninyi wenyewe mwadhulumu watu na kunyang'anya mali zao; naam, hata za ndugu
zenu.
Wapendwa waumini
kwenye kanisa la Korintho walikuwa wanakwenda au kupelekana kwenye mahakama za
wamataifa badala ya kuyapeleka mambo yao mbele za mkutano wa kanisa ili
yafanyiwe maamuzi au kusuluhishwa. Alichukisudia kuwaambia Paulo ni kwamba,
watakatifu wanakwenda kuuhukumu ulimwengu na watawahukumu pia malaika walioasi
kutokana na matendo yao. Yatupasa tuweze kuhukumu kati ya mema na mabaya
kuanzia mambo ya ulimwengu huu tuliopo. Wapendwa waumini wa Korintho kwa hakika
hawakufanya hukumu ya haki kwa kuzitendea kazi kanuni zilizo kwenye sheria ya
Mungu na kwa hiyo, wapendwa waliamua kwenda kwenye mahakama za kidunia.
Jambo lingine
lipasalo kulijua hapa ni kwamba uongozi wa kanisa unawajibu kuhakikisha kuwa
hukumu zao ni za haki na takatifu. Mojawapo ya matatizo makubwa yaliyolikkumba
kanisa la Mungu kwenye karne ya ishirini lilikuwa ni kutoweza kutoa hukumu za
haki. Sisi kama Wakristo tunawajibu wa kusimamia haki na utakatifu. Tusiruhusu
dhuluma au hukumu isiyo ya haki kufanyika kanisani, vinginevyo itawafanya
waaminio waamue watoke kanisani na kwenda kutafuta hukumu za haki nje ya
kanisa. Yanasemaje basi kwa mashirika ya kidini yanayojiita kuwa ni Kanisa la
Mungu na huku waumini wake hawapati haki ndani ya kanisa? Yatupasa kujikite
sana kwenye kuielewa torati au sheria na kanuni za Mungu ili tuweze kutoa huku
za haki na ni wajibu wa kila Mkristo kusoma na kuzielewa kanuni hizi na kuweza
kutoa hukumu kwa haki na halali.
1Wakorintho 6:9 Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu?
Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu,
wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,
Tunaposoma 1Wakorintho
6:9-14 tunapata uelewa mzuri wa kile kinachosemwa hapa.
1Wakorintho 6:9-14 Au hamjui ya kuwa
wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi
ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala
walawiti, 10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi,
wala watukanaji, wala wanyang'anyi. 11 Na baadhi yenu
mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini
mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu
wetu. 12 Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si
vyote vifaavyo; vitu vyote ni halali kwangu, lakini mimi sitatiwa chini ya
uwezo wa kitu cho chote. 13 Vyakula ni kwa
tumbo, na tumbo ni kwa vyakula; lakini Mungu atavitowesha vyote viwili, tumbo
na vyakula. Lakini mwili si kwa zinaa, bali ni kwa Bwana, naye Bwana ni kwa
mwili. 14 Naye Mungu alimfufua Bwana, na tena
atatufufua sisi kwa uweza wake.
Hapa tunaona
namna ya mienendo itakayotufanya kuwa kwenye hukumu walio kwenye ufufuo wa pili
wa wafu. Tumeoshwa na kusafishwa kwa dhabihu ya Kristo, lakini hatuwezi
kuenenda kwa namna walivyoenenda watu hawa. Kama anavyoonyosha Paulo kuwa wengi
wetu tuliyatenda mambo haya kabla hatujaitwa na kubatizwa, bali sasa
tumeachananayo na kuenenda kwa mwenendo tofauti. Hatuyatendi tena mambo haya.
Sisi ni viumbe wapya kwa kupitia Roho wa Mungu.
Kwenye aya ya 12
inaonekana kuwa Paulo anasema kuwa vitu vyote vimetakaswa na kuhalalishwa kwa
yeye kuvifanya. Hili ndilo suala lenyewe? Tumekwishaona tayari kwamba sheria za
Mungu zingali zinatakiwa bado kuheshimiwa na tumeagizwa kama Wakristo kuzitii
hizo sheria za torati .
Sisi sote tunahali
ya kufanya maamuzi kuhusu mambo ya kutenda tunayoyataka. Hii haimaanishi kuwa
ni haki na ni vizuri kwetu. Kama Wakristo yatupasa kuchagua kuhusu mwenendo
wetu na ni juu yetu kuchagua mema au mabaya; uzima au mauti.
1Wakorintho 6:15 Au hamjui ya kuwa yeye
aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa
mwili mmoja.
Ni kama miili
yetu ilivyo hekalu la Mungu, ndipo mwili wa Kristo, ambalo ni mtu mmojammoja
wanaounda kanisa, nao ni aina ya upanuzi wa hekalu. Kila mmoja ni mashirika au sehemu ya mwili mzima.
Aya ya 16 hadi 18:
1Wakorintho 6:16-18 Au hamjui ya kuwa yeye
aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa
mwili mmoja. 17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho
moja naye. 18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo
mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya
mwili wake mwenyewe.
Anachokisema Paulo
hapa ni kina tafsiri ya maana mbili. Tukiwa tunatakiwa kuepuka uzinzi wa
kimwili, yatupasa pia kujiepusha na zinaa ya kiroho. Mwanamke kahaba ni mfano
wa dini ya uwongo. Wale walioungana kwenye dini hii ya uwongo hufanyika kuwa
wamoja nayo. Kama tukiungqanishwa kwenye dini ya uwongo, basi hatuwezi kuungana
kwenye arusi tukawa ni bibi arusi wa bwana arusi, Yesu Kristo. Tumeambiwa
kuujaribu mwili ambao ni kanisa. Yatupasa kukusanyika pamoja na kushiriki ibada
kwenye mwili wa Kristo. Tumeagizwa kujua pale ulipo na ni nani wao na namna
pekee tutayoweza kuijua ni kwa mafundisho yao. Ni kama alivyosema Kristo Mathayo
7:16: “utawatambua kwa matendo yao”. Yatupasa kuwa na msingi mzuri kwenye mafundisho
ya kweli na kanuni za Mungu ili kuuendeleza mwili huu.
Aya ya 19 inasema:
1Wakorintho 6:19 15 Je! Hamjui ya kuwa miili yenu ni
viungo vya Kristo? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya
kahaba? Hasha!
Paulo anasisitiza
kuwa miili yet uni hekalu la Mungu na Roho wa Mungu anakaa ndani yetu. Anafanya
neno la nyongeza kwa kusema kuwa wala si mali yetu sisi wenyewe. Kwenye aya ya 20
tunasoma:
1Wakorintho 6:20 15 maana
mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.
Tumenunuliwa kwa
gharama. Bei hiyo ilikuwa ni uhai wa Kristo. Alimlipia kila mmoja wetu kwa damu
yake. Sisi sasa tu watu wa Mungu. Mwili wetu si wetu wenyewe, ili tumtukuze
bwana wetu, Mungu Baba, kwa miili yetu. Tunamtukuza kwa kujiepusha na tama za mwili na matendo ya kidunia na
kuzitii sheria zake. Tunayashika yaliyomema na ya haki na kukataa maovu na
upotoe wa dunia hii. Mungu anasema watu wake ni watu muhimu wa aina yake. Kama
tukifanana na kuendana na watu wengine wa dunia na hakuna anayeona kuwa sisi tu
watu wa tofauti, ndipo basi hatuna tofauti yoyote na huenda yatupasa kutathmini
maisha yetu ili kuona kuwa tunaishi sawasawa na mujibu wa neno halisi na la kweli
la Mungu. Njia ya Mungu ni tofauti sana na ya dunia hivyo ingeweza kuwa dhahiri
sana kuwa sisi tu watofauti. Yatupasa kujitahidi kila siku kuwa ni watu wa
tofauti na wa aina yake. Kwa kweli, kama tunakiiadhimisha siku ya Mwezi Mpya
kwa kuitakatifuza na kudhani kuwa tunaweza kuishika torati ya Mungu,
tutaonekana kuwa ni watu wa aina ya kipekee. Na ukweli wa mambo, hata
tutaonekana ni wa pekee aina yake hata kwenye Makanisa mengi ya Mungu.
1Wakorintho 9:24 Je! Hamjui, ya kuwa
wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni
mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.
Kwenye uwanja wa
michezo, riadha inagharimu juhudi ya takriban asilimia 110% ili kushinda
shindano. Paulo anatuonya sisi kupiga mbio ili tuweze kupokea zawadi au tuzo.
Ni tuzo gani basi anayoisema Paulo hapa? Hebu na tutazame kwenye 1Wakorintho
9:25-27 na tuone anachikisema Paulo.
1Wakorintho 9:25-27 Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote;
basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji
isiyoharibika. 26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si
kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa; 27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe,
nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa.
Taji tunayoishindania
na kuikazia mbio haiharibiki ambayo watapewa Wakristo wa kweli ataporudi
Kristo. Paulo anasema kuwa anautesa mwili wake. Paulo alipigana vita endelevu,
kama sisi, dhidi ya mambo ya kimwili ya mwanadamu na dhambi. Ni wale
wanaovumilia hata mwisho ndio wataipokea taji. Ni watendaji wa neno na sio
wasikiaji watakaohesabiwa haki.
Taji hii si ya
kudumu kama baadhi ya wenye imani ya “mtu aokokapo mara moja huendelea milele”
wanavyotutaka sisi tuamini. Paulo anasema kwenye aya ya 27 kwamba aliutaabisha
mwili wake ili uyatii mambo ambayo yeye hangeweza kuyashinda/ kama hatutakuwa
makini na kujibidiisha ili kushinda na kufanana zaidi na viongozi wetu na kaka
yetu mkubwa Yesu Kristo, hatutaipokea taji, Paulo anachoongelea hapa.
Tutajikuta wenyewe tukiwa kwenye ufufuo
wa 2 wa wafu. Kumbuka kuwa ni ufufuo wa 2 wa wafu. Wengi
wamejaribu kutushawishi huko nyuma kuwa kama hatukuishi kama ushirika wa
kipekee tutakataliwa kwenye ufufuo wa 3 ambako tutalelelewa,
tukionyeshwa jinsi kila mmoja alivyofanya matendo mema na kisha kutupwa kwenye
ziwaa la moto. Namna bora tunayoabudu ni neema kubwa sana kulik0o hivyo. Soma
jarida la Mafundisho Potofu ya Ufufuo wa Tatu (Na. 166) ili
kupata habari kwa kina zaidi kuhusu jambo hili.
2Wakorintho 13:5 Jijaribuni
wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui
wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa.
Hebu na tutazame
aya hii kwa kina tena uelewa mzuri wa kile anachokisema Paulo hapa. Tutaona kwenye
2Wakorintho 13:1-14.
2Wakorintho 13:1-9. Hii
ndiyo mara ya tatu ya mimi kuja kwenu. Kwa vinywa vya mashahidi wawili au
watatu kila neno litathibitishwa. 2 Nimetangulia
kuwaambia; na, kama vile nilipokuwapo mara ya pili, vivyo hivyo sasa
nisipokuwapo, nawaambia wazi wao waliotenda dhambi tangu hapo, na wengine wote,
ya kwamba, nikija, sitahurumia; 3 kwa kuwa mnatafuta
dalili ya Kristo, asemaye ndani yangu, ambaye si dhaifu kwenu, bali ana uweza
ndani yenu. 4 Maana, alisulibiwa katika udhaifu,
lakini anaishi kwa nguvu za Mungu. Maana sisi nasi tu dhaifu katika yeye;
lakini tutaishi pamoja naye kwa uweza wa Mungu ulio kwenu. 5 Jijaribuni
wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui
wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa. 6 Lakini natumaini kama mtajua ya kuwa sisi hatukukataliwa. 7 Nasi twamwomba Mungu, msifanye lo lote lililo baya; si
kwamba sisi tuonekane tumekubaliwa, lakini ninyi mfanye lile lililo jema,
tujapokuwa sisi tu kama waliokataliwa. 8 Maana
hatuwezi kutenda neno lo lote kinyume cha kweli, bali kwa ajili ya kweli. 9 Maana twafurahi, iwapo sisi tu dhaifu, nanyi mmekuwa
hodari. Tena twaomba hili nalo, kutimilika kwenu.
Ili sisi tuwe na nguvu
yatupasa tuweze kujisimamia wenyewe. Kanisa kwa takriban miaka 40 iliyopita au
limekuwa linachunga idadi kubwa ya wafuasi na sio mahiri wa kutafakari. Na hii
ndiyo sababu iliyowapelekea watu wengi kuwafuta viongozi wa kanisa kwenye
ukengeufu. Paulo anatoa mfano wa huduma na ilimaanisha haikuonekana wala
kujulikana.
2Wakorintho 13:10–14
Kwa sababu hiyo, naandika haya nisipokuwapo, ili, nikiwapo, nisiutumie ukali
kwa kadiri ya uwezo ule niliopewa na Bwana, kwa kujenga wala si kwa kubomoa. 11 Hatimaye, ndugu, kwaherini; mtimilike, mfarijike, nieni
mamoja, mkae katika amani; na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi. 12 Salimianeni kwa busu takatifu. 13 Watakatifu
wote wawasalimu. 14 Neema ya Bwana Yesu Kristo, na
pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote.
Paulo anaashiria
kuwa aliwahi kuwaambia jambo hili waumini wa kanisa la Korintho mara mbili
kabla ya kipindi hiki. Inaonekana kuwa kanisa la korintho lilikuwa gumu kidogo
au vivu kuelewa. Paulo anarudia tena hapa kukanusha na kukemea mafundisho ya
Kinostiki yaliayokuwa wanaenezwa siku hizo. Wanostiki walikuwa hawamwamini
Mungu, kwa namna waliyokuwa wanamchukulia Kristo, kuwa aliishi kama mwanadamu
halisi. Kiumbe ni muovu kwa mtazamo wao kwa hiyo kimsingyo kimsingi
isingewezekana kwa Mungu mtakatifu kuishhi ndani ya mtendadhambi. Paulo alikuwa
anajaribu tu kuonyesha ukweli kwamba Kristo anaishi ndani yetu, kinyume na
mawazo yaliyokuwa yakifundishwa siku zile. Tumepewa agizo na wajibu wa
kujitathimini wenyewe. Tunafanya hivyo kwa kuzitathimini njia zetu na matendo
yetu kwa kulinganisha na mneno ya Biblia. Kama mafundisho yetu na imani yetu
haifanani na Maandiko Matakatifu, basi tutakuwa sio wafuasi wa Kristo. “Maandiko
Matakatifu” yaliyoko hapa yanatokana na yafsiri ya Biblia King James Version. Inajitahidi
kuelezea vizuri sana kuwezesha kuipata maana halisi kusudiwa ya maandiko
matakatifu. Tunapaswa kuitafuta kweli kwa bidii sana ili tuipate. Si kazi rahisi
ila tumeagizwa kufanya hivyo. Ni kama asemavyo Mtume, “Yeye asemaye anamjua
Mungu na asizishike amri zake yeye ni mwongo”. Yatupasa kujua bila shaka kwamba
amri hizo ni.
1Wathesaloniake 5:21
jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema;
Yatupasa
kuyajaribu mafundisho tunayoyasikia ili kuona kama ni ya kweli au sivyo.
Yatupasa pia kujichunguza wenyewe ili kuona kama matendo na mwenendo wetu
vinaendana sawa na mafundisho yetu. Hii ni muhimu sana hasahasa kwenye majira ya maadhimisho ya Pasaka. Paulo
alisema kwamba tumaini lake ni kwamba Wakorintho walikuwa hawana mashaka kuwa
wao ni wa Kristo. Namna pekee tunayoweza kuifanya hivyo ni iwapo kama tutakuwa
tunajisomea kwa bidii ili kuthibitisha mafundisho yetu. Yatupasa kuwekeza hela zetu
mahali ilipo midomo yetu.
Kwa kuhitimisha,
tunaona kuwa Paulo hakuwa amependezwa kabisa na tabia au mwenendo wa waumini wa
makanisa ya Warumi na Wakorintho.
Wapendwa ndugu
zangu, sisi tu mwili wa Kristo. Roho wa Mungu anakaa ndani yetu. Tunamtii na
kumcha Mungu kwa kuwa tunampenda, na sio kwa kuwa tumehesabiwa haki kwa
kuishika sheria yake. Hebu na tujifunze kutokana na makosa na mapungufu
yaliyoonekana kwenye makanisa ya Warumi na Wakorintho. Hebu na tukimbie mbio za
mashindano haya ili tushinde, na tusiwekwe tu kwenye nafasi ya pili au ya tatu.
Hebu na tuendelee kujisomea na kujifunza kama Waberoya, ili tuejitwike majukumu
yetu kama washirika wa mwili wa Kristo. Endelea kuendeleza uelewa wa kina wa
Biblia na wa kanuni na sheria au torati ya Mungu ili asiwepo mtu wa kutuambia
“Hivi Hamjui?”