Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[038A]
Ishara za Mbinguni:
Sehemu ya I
(Toleo La 1.5 20080503-20131204)
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki © 2008, 2013 Wade Cox)
(tr. 2014)
Masomo haya yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu
bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja
na tangazo la hati miliki ni lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa
mpokeaji kutoa au kuchangia kwa nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza
kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka
maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote
katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Ishara za Mbinguni: Sehemu ya I
Watu wengi
watakuwa makini kujua kwamba tumeweka kipindi cha Siku za Mwisho na ujio wa Masihi
kwa miaka zaidi ya 21 ya Yubile 120 ya mwisho, kilichofunika Mizunguko mitatu
ya Sabato iliyoanzia katika mwaka wa kumi na tisa, ambao ulikuwa ni mwaka wa
kwanza wa Mzunguko wa Tano wa Sabato wa Yubile ya 120. Maandalizi ya mzunguko
Utakaso na Marejesho ya Sayari hii ulianzia kwenye vita ile.
Tumeshughulika na
kuelezea kuhusu Vita vya Mwisho na umuhimu wake kwa Masihi kuwa kwake hapa
kuyatiisha mataifa ya Dunia kwa mujibu sawa na ilivyotabiriwa. Kipindi cha
mwaka wa Saba cha kuyatiisha mataifa ya dunia ni lazima kiishie mapema kabla ya
mwanzo wa Mwaka wa Yubile kuanzia Siku ya Upatanisho ya mwaka 2026 na kuishia
mwaka 2027 na kuanza kwa Yubile Mpya ya Yubile zote tangu ile ya Ezra na
Nehemia itakayokuwa katika mwakaa 2028 (soma majarida ya Usomaji wa Torati Ulivyofanywa na Ezra na Nehemia
(Na. 250) na Kuanguka kwa Yeriko (Na. 142)).
Kwa hiyo ni wazi
kabisa kwamba Kristo atakuwa amekwisha kuja hapa, mapema kabisa kabla ya mwaka 2019
na huenda ni mapema kabisa kabla ya mwaka 2018 kwa ajili ya kuhitajika kwa
mavuno makuu mnamo mwaka 2025.
Tunajua kwa ukweli
kwamba Biblia inatuambia kuwa Mashahidi wawili watasimama huko Yerusalemu na
kuhudumu kwa kpindi cha siku 1260 na kisha watauawa na kulazwa mitaani kwa siku
tatu na hatimaye watafufuliwa (soma jarida la Mashahidi (pamoja na Mashahidi Wawili) (Na. 135)). Hii inamaana kwamba whishoni mwake kabisa
hawa Mashahidi watakuwepo hapa duniani wakati wa maadhimisho ya Pasaka mwaka
2015. Tunatarajia pia kushuhudia wongofu wa Yuda na masalia ya Lawi mapema
kabla ya Masihi kuanza kuyatiisha mataifa ya dunia.
Tunajua kwamba
Vita vya Mwisho vimekwishaanza tayari tangu kipindi cha kushambuliwa kwa nchi
ya Afghanistan na Iraq, kama tulivyoelezea huko nyuma kabla kwenye jarida la Miaka Thelathini ya Mwisho: Pambano la Mwishp (Na.
219). Kwenye kanda zilizorekodiwa imeelezewa
kwa wazi sana kwamba vita hivi vilianza mwaka 2001. Kipindi cha utimilifu wa
Mataifa kiliishia mwaka 1996 (soma jarida la Kuanguka kwa Misri (Na. 36)). Miaka Thelathini ya Mwisho ilianzia mwaka 1997.
Mchakato huu ulionyeshwa kwa ishara ya tukio la kupatwa kwa mwezi. Kulikuwa na
na matukio makuu ya kupatwa kwa mwezi wakati wa Pasaka na Sikukuu ya Vibanda
kwenye maadhimisho ya mwaka 1996. Kishea huu mwaka wa 1997 kulikuwa na upatwaji
mdogo wa mwezi wakati wa Pasaka na kupatwa kamili kwa mwezi kulitokea wakati wa
maadhimisho ya Sikukuu ya Vibanda. Mwaka 1997, kulikuwapo pia upatwaji kamili
wa jua katika siku ya 1 ya mwezi wa Abibu au Nisani na upatwaji nusu wa jua
ulitokea siku ya 1 ya mwezi Tishri. Matukio haya ya mfululizo ya kupatwa kwa
jua na mwezi hayakutokea kwa bahati mbaya. Yanauhusiani pia na Kalenda ya
Hekaluni kwa mujibu wa muunganisho wa wala hayaendani na Kalenda ya Hilleli ya
Wababeloni (soma pia jarida la Ubadilishaji wa Kalenda ya Mungu katika Yuda (Na. 195B)). Kuna mzunguko kamili wa nyakati kati ya
miaka ya 1997 na 2015. Mizunguko iliyo kwenye kipindi hiki yanaonekana au
kuoneshwa kwa ishara za matukio haya ya kupatwa mwezi na jua. Kipindi hiki chenye
mzunguko na kipindi kingine kilichofuatia kitaonekana namna na umuhimu wake
sana kwenye historia ya ulimwengu. Kipindi kinaqchofuatia kwenye miaka kumi na
miwili ya kuelekea Yubile ya kurudi kwa mataifa. Hiki ni cha ukamilishaji wa
Tukio la Pili la Kutoka lililoandikwa kwenye Isaya sura ya 66.
Mapepo wnyewe, na
ibada zao za jua, wameuweka mwaka 2012 kuwa ni kama mwaka wa mwisho wa imani
yao na mamlaka yao, na Mzunguko Mpya unaanza toka mwaka huu. Tunajua kwamba
mfumo wao utapaswa uishe kwa ajili ya ujio wa Mashahidi, wakiwa na shahidi mkuu
Eliya, anayeonekana kuwa Atarejesha Mambo
Yote ambavyo maana yake pamoja na mabo mengine, kwamba atakuja kurejesha
kwa watu umuhimu wa kuzishika sheria zilizo kwenye Torati ambazo Shetani
amezivunja na kuzihalifu wakati wa kufungwa kwa Bustani mwanzoni mwa Yubile ya
Kwanza, Yubile 120 zilizopita. Mnamo mwaka 3974 KK.
Mwaka 2012 ni
Mwaka wa Sabato wa mzunguko wa hamsini. Katika mwaka huo Torati ya Mungu itasomwa
kwa mara nyingine tena kwa mara ya tatu kabla ya kutolewa kwa hukumu dhidi ya
mfumo na utaratibu huu uliopo leo.
Vita
vimekwishaanza tayari na mfumo wa Munyama unazidi kupata nguvu tena ka tena na huku
ukichukua mamlaka ya kiutawala wa Kidola chini ya kile wanachikiita kuwa ni Agizo au Utaratibu Mpya wa Ulimwengu. Mfumo
huu unendelea hata sasa chini ya Shetani amoja na wafuasi wake hapa Duniani
tangu mwaka 2012 wakati Torati ya Mungu iliposomwa na kutafsiriwa na kuenekezwa
kwa Mara ya tatu. Nabii wa Uwongo pamoja na Mpingakristo wataendelea kuendeleza
harakati zao tangu sasa hadi atakaporudi Masihi ulimwenguni.
Haya ni masomo
mawili tofauti kutoka kwenye Maandiko Matakatifu ambayo yamesababisha nadharia
fulani ya kukisia na yanaweza kutupatia mwanga kwa masuala ya kama kwenye
nyakati.
Nabii Yoeli
anasema, "Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla haijaja hiyo
siku ya Bwana iliyo kuu na itishayo." (Yoeli 2:31)
Injili ya Mathayo
inamnukuu Kristo akisema, "Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua
litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na
nguvu za mbinguni zitatikisika; ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu
mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana
wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi."
(Mathayo 24:29-30)
Kwahiyo tunaweza
kudhania na kuamini kwamba kutakuwa na tukio la kiastronomia ambalo litapelekea
kutokea maafa au kuharibika kukubwa kwenye mchakato wa mizunguko.
Kuna dhana kuhusu
vipindi vya mizunguko ambavyo vipindi vine vya mizunguko ya nyakati za kupatwa
kwa mwezi, na kuelekea chini hadi kwa kinachoitwa tetradi, kutokea. Kwa kweli, itatokea mara sita kwenye karne ya
ishirini na moja. Kinachomaanisha hapa, kwa vyovyote vile, ni kwamba wakati ule
tu ambapo ni kwa bahati mbaya ikatokea wakati wa Siku Takatifu au Sikukuu za
Mungu ambapo tunatarajia mlolongo wa mfuatano wa matukio ya kinabii kujitokeza
unaomhusu Masihi na nabii hizi za Kibiblia kwenye miaka ya 2014 hadi 2015, na
wakati wake muhimu mwaka 2015, kama tutakavyijionea hapo chini. Mnamo mwaka
2034, tarehe 3 Aprili kutakuwa na mkingo wa kipindi cha Pasaka na kupatwa kwa
mwezi nusu kutatokea tarehe 28 Septemba 2034. Mwaka huu ni Mwaka wa Kwanza na
Usomaji wa kwanza wa Torati kwenye kipindi hiki kinachotarajiwa kuwa ni cha
Milenia mpya.
Matukio haya ya
kupatwa jua na mwezi yataonekana kutokea kwenye Mwandamo wa Mwezi wa Mwaka wa
Kwanza na katika Mwandamo wa Mwezi na katika Mwandamo wa tatu wa Mwezi unaofuatiwa
na Pentekoste na wakati wa Pasaka mwishoni mwa maadhimisho ya Pasaka katika
Siku ya Kwanza ya maadhimisho ya Mikate Isiyo na Chachu kwa kufuata Kalenda ya
Hekaluni.
Baadhi ya wale
walioshiriki na kuamini dhana hizi wamejaribu kuunganisha kwa kuzilinganisha na
kalenda ya Hilleli na utaratibu wake ili kuzifanya ziendane na vipindi vya
Pasaka kwa mwaka mmoja lakini wakikosa maana muhimu za siku zilizohusishwa.
Makala moja kati ya hizo liliandikwa na Joe Kovacs kwenye gazeti latolewalo
kila siku maarufu kama World Net Daily la Aprili 30, 2008.
http://worldnetdaily.com/index.php?fa=PAGE.view&pageId=63076.
Usipokuwa unazijua
tofauti iliyopo kati ya utaratibu wa Hekalu la Zamani na ile ya Kalenda ya
Hilleli ya Wayahudi hatutaweza kufikia kujua maana kamili na kuyana madhanio au
fikra kuhusu mambo mengine. Ni kama yalivyo mambo mengine yote ya kiroho
hatuyajui hadi pale tunapoyafanya yale tuliyofunuliwa na Mungu. Mche na kumtii
Mungu kwanza, na ndipo atayathibitisha
mawazo yetu.
Kipindi cha
mwisho cha mwandamano wa matukio haya ya kupatwa kwa jua na mwezi yaliyotokea
kilikuwa na umuhimu na maana sana kwa Wayahudi katika Israeli na kimepelekea vita
vya mwaka 1967 na kuiunganisha Yerusalemu kutoka mwaka huo, ikijumuishwa Pasaka
ya mwaka 1968. Hii ilikuwa ni miaka 9.5 kabla ya Yubile iliyofuatia kwenye siku
ya Upatanisho ya mwaka 1977. Ulikuwa ni mwaka wa sita wa Mzunguko wa miaka ya
Sabato, na Yerusalemu ulikuwa mikononi mwa Waisraeli ambao ulikuwa ni mwaka wa
Sabato, ambao ni mzunguko mmoja kabla ya Usomwaji wa Torati. Kwa hakika, Yuda
hawakuzishika Sabato au Usomaji wa Torati lakini hii haikuenenda sawa na ni
kinyume na na Marejesho na watafanya sawasawa na wanavyotakiwa kufanya kwenye
kipindi hiki chote cha matukio yote. Upatwaji wa Mwezi mara zote unakuwa
mwekundu kwa wale wanaotaka kufanya rangi zaidi.
Maana ya tetradi yamekuwa
yakionyehwa kama ilivyoripotiwa kwenye makala. Ni tetradi hiyohiyo ya mwezi wa
rangi damu iliyotokea baada ya Israeli kufanyika kuwa taifa mwaka 1948 na
ilitokea mnamo Siku za Kwanza za mwezi wa Kwanza na wa Saba ya miaka ya 1949 na
1950.
Mwaka 2015, upatwaji
kamili wa mwezi ulitokea pia katika Mwaka Mpya, mnamo tarehe 20 Machi 2015 na
upatwaji kamili wa jua kufanyika tarehe 4 Aprili 2015, ambayo ni siku baada ya
Siku Takatifu ya Kwanza ya mwanzo wa Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu.
Kuna upatwaji wa
sehemu ya jua utakaotokea Siku ya Baragumu ambayo itakuwa ni Jumapili ya tarehe
13 Septemba 2015. Jumapili ya tarehe 27 Septemba, Siku ya Takatifu ya Kwanza ya
Sikukuu ya Vibanda, kutakuwa na Upatwaji kamili wa Jua.
Inaumuhimu wake
sana pia kwamba hakukuwa na tetradi za kiastronomia kwemye miaka ya 1600 hadi
karne ya ishirini. Tetradi za miaka ya 1500
hazikutokea wakati wa Sikukuu yeyote ya Kalenda Takatifu. Mungu alitoa ishara kwenye
Marejesho.
Tofauti iliyopo
kati ya Kalenda ya Zamani ya Hekaluni na Kalenda ya Hilleli ina maana na umuhimu
wake katika kupambanua mambo haya kwa mtazamo wa kweli. Kalenda haifanyi hivyo.
Wale wanaoifuata kalenda ile kwenye Makanisa ya Mungu hawaelewi kabisa.
Wakristo wa mrengo
wa Utrinitariani wamechanganyika katika kupokea kwao. Hitimisho lake liko wazi.
Ishara za Mbinguni zinaendana na kile ambacho Mitume wanachosema, mwandamano wa
mfululizo wote wa maukio na matendo. Ni kwa mujibu wa Kalenda ya Zamani ya
Hekaluni na hawa Watrinitariani wanaozishika kwa kuziadhimisha Sikukuu za
Kipagani watapata mtihani wao wa kwanza wa kutofautisha na kuondoa utaratibu
wao mbaya na wa uwongo na imani yao. Tangu hapo na kuendelea kwa kweli inapata
joto. Watateseka wakati wa Mashahidi kwa ajili ya uasi wao na hatimaye
watawaua, lakini kwa wakati huu kila kitu kitakoma na watalazimika kutii ama
vinginevyo watakufa.
Ripoti ya Kovacs
kuhusu mawazo au dhana ya Blitz yangezewa kusaidia sana iwapo kama yeye na
mwenzake Blitz wangekuwa wameelewa maana ya na umuhimu wa Lakenda ya Zamani ya
Hekalu na kile kilichotokea kwa kipindi chote hicho. Ukosoaji wao unaweza kuwa
una mapungufu kuelezea. Mengineyo mengi kama ya Hal Lindsay aliyafafanua pasipo
hata kusoma makala yenyewe.
Nukuu kutoka
kwenye maneno ya Kristo ilisema: "Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku
wala saa." (Mathayo 25:13) imetumika kusema kuwa hatuwezi kujua au kuamua
ni wakati upi atakaorudi Kristo. Pia anasema, "Walakini habari ya siku ile
na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba
peke yake." (Mathayo 24:36). Mungu yupo kwenye mchakato wa kuwaambia wao
sasa.
Madai kwamba hizi
sikukuu ziliwekwa kwa maana ya kuziadhimisha tu ni ya uwongo. Kipindi cha mpito
cha kutoonekana Mwezi kinaamua mwanzo wa miezi na mpangilio wa siku za
kuadhimisha sikukuu na vigezo hivi vyenye mashiko na maana vinatuama kwenye
nyakati za kutoonekana kwa mwezi vya miezi wa Kwanza na wa Saba. Hukumu ni
lazima itawapata wale wote wanaozifuata kalenda za uwongo na potofu na ni
pamoja na wale wanaoifuata Kalenda ya Hilleli pia.
Imeandikwa kuwa
Mungu hafanyi jambo lake lolote mpaka awaonye watu wake kwa kupitia watumishi
wake, manabii anaowafunulia kwanza mapema kabla yake.
Tumeelezewa
kuhusu mchakato na mfuatano wa matukio ya manabii kwa miaka mingi sana na tutaendelea
kufanya hivyo.
Wanawali wenye
busara wanaendelea kujiandaa na Kanisa la Mungu linaaonya Mataifa kwamba Kristo
anakuja na wenye kuuzingiraji mji (walinzi wanakuja kutoka nchi ya mbali (Jeremia
4:15)).
Jedwali la ratiba ya kutokea kwa Upatwaji wa jua na mwezi limechorwa hapo
chini. Inayofuatia ni Kalenda ya Kale ya Hekaluni kama ilivyoandaliwa na
kuchapishwa na Kanisa la CCG na kisha Kalenda ya Hilleli, ambayo inaonyesha matatizo
yaliyoko na sababu iliyowapelekea wawe na habari nusu nusu.
Ishara za
Mbinguni zitalazimika kuonekana zaidi kuliko matukio haya ya kupatwa kwa mwezi
na jua na yataamulia na mengine na ni mambo yaliyo na maelezo zaidi nay a kina
zaidi.
|
Aina
ya Kupatwa |
Eneo la
Kizoni |
Tarehe |
Nambari za Idadi ya Sarosia |
|
2014 |
Jumla ya Upatwaji wa Mwezi |
25Li15 |
2014-4-15 |
L122 |
|
Kupatwa
kwa Jua kila Mwaka |
8Ta51 |
2014-4-29 |
S148 |
||
Jumla ya Upatwaji wa Mwezi |
15Ar05 |
2014-10-8 |
L127 |
||
Upatwaji wa Sehemu ya Jua |
0Sc24 |
2014-10-23 |
S153 |
||
2015 |
Jumla
ya Upatwaji |
29Pi27 |
2015-3-20 |
S120 |
|
Jumla
ya Upatwaji |
14Li24 |
2015-4-4 |
L132 |
||
Upatwaji wa Sehemu ya Jua |
20Vi10 |
2015-9-13 |
S125 |
||
Jumla ya Upatwaji wa Mwezi |
4Ar40 |
2015-9-27 |
L137 |
||
CCG |
|
Hilleli |
Mwandamo wa Mwezi Mpya 2014 Yerusalemu 30/3/14 Uliadhimishwa tarehe 31/3/14 |
|
|
Mlo wa Meza ya
Bwana |
13 Aprili 2014 |
|
Maadhimisho ya Pasaka |
14 Aprili 14 – 20 Aprili 14 |
15 Aprili – 21 Aprili |
Maadhimisho ya Pentekoste |
8 Juni 14 |
3/4 Juni |
Siku ya Baragumu |
24 Septemba 14 |
25/26 Septemba |
Iku ya Upatanisho |
3 Octoba 14 |
4 Octoba |
Sikukuu ya Vibanda |
8 Octoba 14 – 15 Octoba 14 |
9-16 Octoba |
Mwandamo wa Mwezi Mpya 2015 20 Machi 15 |
|
|
Mlo wa Meza ya
Bwana |
2 Aprili 2015 |
|
Maadhimisho ya Pasaka |
3 Aprili 15 – 9 Aprili 15 |
4 Aprili 15 – 10 Aprili |
Maadhimisho ya Pentekoste |
24 Mei 15 |
24 Mei |
Siku ya Baragumu |
13 Septemba 15 |
14/15 Septemba |
Iku ya Upatanisho |
22 Septemba 15 |
23 Septemba |
Sikukuu ya Vibanda |
27 Septemba 15 – 4 Octoba 15 |
28 Septemba – 5 Octoba |
q