Makanisa Ya Kikristo Ya Mungu
[CB018]
Naomi
na Ruthu
(Toleo La 2.0
20020216-20070202)
Kitabu cha Ruthu ni hadithi ya kupendeza sana inayohusika na ujasiri,
unyenyekevu, upendo na urafiki katikati ya wanawake wawili. Tutajionea pia kwamba
kutoka kwenye hadithi hii kwamba kuna masomo au mafundisho muhimu na maelekezo
kwa Wakristo.
Christian
Churches of God
E-mail: secretary@ccg.org
(Hati Miliki ©
2002, 2007 Christian Churches of God, ed. Wade
Cox)
Masomo haya
yanaweza kunukuliwa na kuwapa watu bure ikiwa tu kama yatanukuliwa kikamilifu
bila kubadilisha au kufuta maneno. Jina la mchapishaji na anuani yake pamoja na tangazo la hati miliki ni
lazima iwekwe pia. Hakuna malipo atakayotakiwa mpokeaji kutoa au kuchangia kwa
nakala yoyote atakayo pewa. Nukuu fupi zaweza kuwekwa toka kokote ikiwa zitafaa
kukithi haja ya lugha lakini bila kukiuka maadili ya sheria ya hati miliki.
Masomo haya pia yanapatikana Ulimwenguni kote katika tovuti yetu ya:
http://www.logon.org na http://www.ccg.org
Naomi na Ruthu
Tunasoma kwamba Naomi na Ruthu kwenye Kitabu cha Ruthu.
Hadithi hii imetokana kipindi ambacho viongozi wa Israeli walikuwa wanaitwa
Waamuzi. Kipindi hiki kilikuwa ni kabla ya kile cha wafalme na hakukuwa na
wafalme wowote. Naomi alikuwa
ni mwanamke wa Kiisraeli wa kabila la Yuda. Ruthi alikuwa ni mwanamke kijana
kutoka Moabu. Alikuwa ni Mmataifa (ambaye ni wakutoka taifa linguine) na mgeni
miongoni mwa Waisraeli. Habari hii ni muhimu kwenye historia ya Israeli na kwa
Mpango wa Mungu.
Akiw na mume wake na watoto wake wawili wa kiume,
Naomi aliondoka nyumbatni kwake huko Yudea na wakenda kuishi huko Moabu.
Familia ilikwenda huko ili kutafuta maisha mazuri kwa kuwa kulikuwa na njaa
kali huko Bethelehemu ambalo walikuwa wanaishi hpo kabla (Ruthu 1:1-2). Wakati
wana wa Israeli walipokuwa wanamtii Mungu Mmoja Wapekee na wa Kweli
walibarikiwa. Lakini wakati walipoiabudu miungu mingine (ya uwongo) waliadhibiwa.
Wakati mwingine Mungu aliyaachilia majeshi ya maadui yawashambulie hadi
kuwashinda na kuwaibia mazao yao. Wakati mwingine walikosa mvua kabisa ya
kuwezesha kukuza mazao wao (Walawi 25). Kwa hiyo, hadithi hii ilikuwa ni wakati
ambao watu hawakuwa na hali iliyosawa kwa Mungu.
Wamoabu walikuwa ni maadui hapo zamani na
Waisraeli na kulikuwa na vita vya mara kwa mara katikati yao. Lakini kwa
kipindi hiki Israeli walikuwa katika amani na hawa Wamoabu. Hawa Wamoabu
walikuwa ni wa uzao wa Lutu ambaye alikuwa ni mpwa wake Ibrahimu (Mwanzo
19:30-38). Kwa hiyo kulikuwa na uhusiano wa karibu na wa kindugu kati ya watu hawa
wawili. Hata hivyo, hawakuwa wanamuabudu Mungu mmoja na wala hwakuwa kwenye
imani au dini moja.
Mume wa Naomi aliitwa jina lake Elimeleki
na watoto wke wakiume walikuwa ni Maloni na Kilioni.
Wakati akiwa huko Moabu, mume wake Naomi alifariki na waoto wake wa kiume
wakakua na kuwaoa wnawake wa Kimoabu. Majina yao walikuwa ni Orpa na Ruthu (Ruthu 1:3-4). Israeli walifundishwa kuwa
wasiwaoane na watu wa makabila ya kipagani ya Wamataifa wanaoishi karibu nao
wakiwazunguka wowote, lakini wanawake wa Kimoabi waliruhusiwa kuwaoa (Kumbukumbu
la Torati 7:1-3). Hii ilitokana na kwamba wakati Israeli walipojichanganya na
makabila mengine, walijikut wanaabudu miungu mingine ya kipagani ya nchi
nyingine. Hata hivyo, hakun mwanaume wa Kimoabi aliyeruhusiwa au kujumuishwa kwenye
mkutano wa Mungu. Sababu ya hili inaweza kuonekana kwenye Kumbukumbu la Torati
23:3-4.
Miaka kumi baada ya kufariki kwa mume wake Naomi
alikabiliwa na kipindi cha huzuni kubwa. Wanawe wote wawili kina Maloni na Kilioni
walifariki pia (Ruthu 1:5). Kulikuwa na uwezekano mkubwa wa kuwa kulikuwa na
mlipuko wa ugonjwa kwenye familia yake na Mungu aliruhusu wanaume hawa wafariki
ili wasiweze kuendeleza maambukizo ya ugonjwa huu kwa vizazi vijavyo. Huko
mbeleni kwenye hadithi hii tutajionea kwamba siku za mbeleni watu wawili muhimu
kwenye mstari wa kiuzao wa Yuda watazaliwa na Ruthu. Hata hivyo, hakuna mtoto
aliyezaliwa na yeyote kati ya watoto hawa wa Naomi kabla ya kufariki kwao.
Wakati akiwa huko Moabu, Naomi hakuwa anaabudu miungu
migeni ya Wamoabu. Alibakia kuwa mwaminifu kwenye imani yake mwenyewe. Kwa
kipindi kirefu na kwa kupitia mfano wake mzuri, Naomi aliweza kuwafundisha
wakamwanaze kuhusu imani yake. Kwa kuishika kwake Torati na amri ningine za
Mungu na kwa kujiepusha kwake kuiabudu miungu ya kigeni ya nchi za mataifa,
Naomi alikuwa ni shuhuda wa Mungu wa Pekee na wa Kweli. Hakujali kuwa wa
tofauti na ni kama tulivyo sisi tulio kwenye Kanisa la Mungu leo.
Wakati Naomi alipogundua kwamba ile njaa kali
iliyoikumba Yudea imekwisha, aliamua kurudi nyumbani. Alitaka kuwa pamoja na
watu wake mwenyewe waliokuwa wanaabudu na kumuamini imani sawa kama
aliyokuwanayo yeye. Pia kwa kuwa familia yake yote ilikuwa imekufa kwa hiyo
hakukuwa na sababu kwa yeye kuendelea kukaa zaidi huko Moabu. Naomi alikuwa
bado ana uhusiano wa kifamilia huko nyumbani kwake. Mabinti zake wote wawili
ambao walikuwa pia ni wakamwanae waliamua kufuatananaye anaporudi nyumbani kwake
ingawaje Naomi alijaribu sana kuongeanao juu ya uamuzi wao huo. Alifanikiwa
kumshawishi Orpa lakini Ruthu hakushawishika bado kuendelea kubakia huko Moabu
(Ruthu 1:6-15).
Ruthu aliweka nadhiri na ahadi ya kwenda pamoja na
Naomi na kumkubali Mungu wake na imani yake na jinsi ya kuishi au mtindo wa
maisha yake (Ruthu 1:16-18). Hii inamaanisha kwamba alikuwa ameandaliwa kurudi
naye nyumbani kwa watu wake na kuachana na miungu yake na imani zao. Hiki siyo
kitu rahisi kufanya. Ilimaanisha kwamba angeenda mbali na wazazi wake, kaka
zake na dada zake, marafiki zake na mahali alipokulia na kulelewa.
Wakristo watuwazima wanatarajiwa kufanya hivi
wanapofikia kumjua Mungu Mmoa, Wapekee na Wakweli na Torati yake. Kama watu
wazima inatupasa kutubu na kubatizwa katika Mwili wa Kristo, ambao ni Kanisa
(Ufalme) wa Mungu. Baada ya kubatizwa haitupasi kurudi nyuma kwa kuyarudia
maisha ya dhambi. Inatupasa kujaribu iwezekanavyo kuitii Torati ya Mungu na
kuendelea kukua tena na tena katika imani (Warumi 6:1-6; Wakolosai 3:3-10).
Ruthu alikuwa ameongoka kikwelikweli. Mungu
alimfanya kufikia kuujua na kuuelewa ukweli kupitia Roho wake Mtakatifu kama
anavyotufanyia hata sisi leo. Lakini Orpa aliamua kuwa kitendo cha kuondoka na
kwenda mbali na nyumbani kwake na kuanza kuishi maisha mapya kingekuwa ni
kitendo kigumu kidogo (Ruthu 1:15). Alichagua kuishi pamoja na watu wake
mwenyewe na kuendelea kuiabudu miungu ya Wamoabu. Ni sawa tu kama ilivyo kwa
Wakristo wanafurahia kumtii Mungu kwa kipindi kifupi, lakini wanapokwazwa na
kitu fulani au mtu fulani wanapenda kufanya hivyo, ndipo wanaamua kurudi nyuma
na kuzigeukia njia zao za kale za maisha yao ya zamani (soma Luka 9:62). Mungu
na Kristo hawawatumii watu wa namna hiyo kuwasaidia kwenye Ufalme.
Ndipo Naomi na Ruthu walikwenda
Bethlehemu na watu wote walifurahia sana kuwaona. Naomi alikuwa amebadilika
sana kiasi kwamba marafiki zake hawakuweza kumtambua kwa mara moja. Alionekana
na haiba ya uzee na mwenye huzuni na alikuwa amedhoofika na mwenye mnyong’onyeo
mkubwa kwa kuwapoteza watoto wake wakiume na mume wake. Pia alikuwa maskini
sana aliyeonekana hohehahe. Lakini marafiki zake wallimtia moyo na wakamwambia
kwamba mambo yatakuwa sawa na mazuri tu sasa na kwamba sasa alikuwa nyumbani.
Hata kwa mambo haya yote, Naomi alipata mateso na masumbufu wakati alipokuwa
huko Moabu hakusimama wala kuacha kumuabudu Mungu wala kuiacha imani yake (Ruthu
1:19-22).
Wengi wetu tutapitia mateso
ya namna kama haya katika maisha yetu. Wakati mwingine wale tuwapendao wataumwa
au kupatwa na magonjwa na kufa na inatufanya tuhuzunike sana. Tunaweza kupatwa
na hasira kirahisi na kumchukia Mungu katika vipindi kama hivi na kukata tama
kwa kupungukiwa na imani na kurudi nyumbani kama alivyofanya Orpa. Lakini kama
tutamtumaini Mungu, ndipo tutapata nguvu zaidi na zaidi kutokana na majaribu
yetu. Inatupasa kuishikilia imani na inatupasa kusaidiana kwenye nyati zote
ngumu. Kila mtu anahitaji kutiwa moyo kwa wakati na namna fulani.
Wote wawili, yaani Naomi na Ruthu walikuwa maskini
kwa kuwa walikuwa hawana waume zao wa kuwahudumia. Kwa hiyo iliwapasa kutafuta
jinsi ya kujitafutia mahitaji yao wenyewe, hususan chakula cha kutosha kwa
ajili ya kukitumia wakati huo huo na kwa siku zilizofuatia mbeleni. Wote wawili
walikuwa ni wanawake mahiri na werevu na walikuwa na uwezo wa kujihudumia wao
wenyewe. Mara moja tu wakaiona njia ya kufanya hilo.
Kuvpura au kuvuna masazo ya mazao au nafaka kilikuwa
ni kitu cha kawaida kufanywa na watu maskini katika Israeli. Na haikuwa wizi
kufanya hivyo. Kwa mujibu wa Torati, iliagiza kwamba kitu chochote nyua baada
ya kuvuna mashambani, kwenye shamba la mizabibu au bustanini kilibakizwa kwa
ajili ya kukikusanya na kuvunwa na watu maskini (Walawi 19:9-10). Wajane na wageni waliruhusiwa pia
kuvuna. Ni namna ambayo jamii ilikuwa inawahudumia watu maskini. Mungu pia
anawatarajia walio matajiri na wenyevingi miongoni mwetu kuwagawia watu maskini.
Ruthu alijitoa kwenda kuvuna mavuno kwa minajiri
hii kipindi cha majira ya baridi akikusudia apate chakula kwa ajili ya Naomi
nay eye mwenyewe. Kwa msaada na neema ya Mungu Ruthu alikwenda kuvuna masalio
ya mazao kwenye shamba la Boazi ambaye alikuwa ni ndugu wa marehemu mumewe
Naomi. Boazi alikuwa hajaoa na mtu tajiri sana na mwenye kuamini Mungu Mmoja,
wa Pekee na wa Kweli. Alinuia kumfanya Ruthu awe salama wakati anapokuwa
anavuna masalia ya mazao shambani mwake. Na pia alimpenda na kumzimia sana
Ruthu visivyo kawaida (Ruthu 2:1-16).
Ruthu alifanya kazi kwa bidii na weledi mkubwa na
akarudisha nyumbani chakula kingi sana. Naomi alipendezwa na akamshauri Ruthu kubakia
na kuendelea kuvuna masalia ya mazao ya shambani mwa Boazi na kwamba asiende
kwenye shamba lolote linguine. Ruthu akamkubalia na akabakia mle hadi mwishoni
mwa mavuno ya shayiri na ngano (Ruthu 2:17-23).
Sikukuu za Mungu zinaitwa mavuno pia. Mavuno ya shayiri ni mavuno ya kwanza,
yanayovunwa sambamba na majira ya Pasaka na Mikate Isiyotiwa Chachu. Mavuno ya
ngano yanakuwa wakati wa Pentekoste. Mavuno ya mwisho ni mavuno ya mwisho,
yanayofanyika majira ya Sikukuu ya Kukusanya au ya Vibanda. Tutajifunza zaidi
kuhusu hilo kwenye jarida la Siku Takatifu za Mungu (Na. CB22).
Ni kama vile Ruthu alivyoendelea kuvuna masalio ya
mazao hadi mwishoni mwa mavuno, ndivyo pia Wakristo wanapaswa kubakia kwenye
Kanisa la Mungu hadi mwishoni mwa mavuno ya Kanisa. Mara tu baada ya kubatizwa
kwetu na kuingizwa kwenye Kanisa la Mungu inatupasa kusema hapa na kufanya kazi
hadi kazi itakapofikia mwisho na Kristo kurudi. Hatupaswi kuzigeukia njia za dunia
za mataifa.
Ni jambo linalopendeza kujua kawa ni mmiliki wa
mashamba yaliyoandaliwa udongo na kisha kupanda mbegu na kuimwagilia. Lakini
wavunaji waliruhusiwa kushiriki kwenye uvunaji mavuno pasipo hata kufanya
maandalizi yoyote y kazi. Kazi hizi zote za maandalizi ya udongo, kupanda mbegu
na kuvuna mazao kunafanana na kitendo cha kulihubiri Neno la Mungu.
Mfano wa mpanzi ulio kwenye Mathayo 13:3-9 unaelezea
jambo hili. Hapa Neno la Mungu inaliita “mbegu”. Kristo ndiye anayeuandaa
udongo (sisi) kwa hiyo mbegu (Neno la Mungu) liweze kukua maishani mwetu. Hii
inajitokeza kwa kipindi kirefu na zaidi sana karibu ianze kipindi ambacho hata
hatujaijua. Sio kila mtu anaweza kulielewa Neno la Mungu kwa wakati huu. Mungu
amewachagua watu wachache na kumpa Kristo ili wamsaidie kuliandaa Kanisa kwa
ajili ya Ufalme wa Mungu. Kristo anafanya kazi kwa maelekezo au mwongozo wa wa
Mungu, na sisi tunafanya kazi chini ya maongozi na maelekezo ya Kristo.
Kwa hiyo, hebu na tuendelee na hadithi ya Naomi na
tujionee kuwa Mungu alikuwa anafanya kazi kwa mujibu sawa na mpango kwenye
maisha yake. Pia alijua mengi kuhusu Torati kwa ajili ya kuwalinda wanawake na
familia zao. Alimwambia Ruthu amfanye Boazi kujua kwamba alikuwa anataka kuolewa
naye. Hii ilihitaji ujasiri mkubwa kwa Ruthu kukifanya kwa kuwa alikuwa ni Mtu
wa Mataifa na aliye najisi kwa mujibu wa itikadi ya Waisraeli. Alihesabiwa kuwa
duni kuliko hata mtumishi wa Boazi. Lakini ilikuwa ni haki yak echini ya Torati
kudai ndoa na ulinzi kutoka kwenye familia ya marehemu mume wake.
Ruthu alimpenda na kumheshimu Naomi na alikuwa
tayari kumsikiliza mwanamke huyu mtu mzima. Kwa hiyo, kwa maelekezo ya Naomi,
chaguo lililokuwa moyoni mwake na aliyemuangukia alikuwa ni Boazi na ndiye
ambaye alikwenda kwake kwa kujivuta kimnyato na kulala miguuni mwake. Kisha
akaomba kwamba Boazi ndiye atakaye “mfunua vazi lake” na aipeleke juu. Boazi
alijua maana ya tendo hilo na alifurahi kuona kuwa Ruthu alimpenda na kumchagua
yeye nay eye pia alimpenda. Jambo hili halikuwa dhambi. Jambo hili lingekuwa geni
sana kama wanawake wangefanya hivyo leo, lakini ilikuwa ni sesturi ya wakati
ule (Ruthu 3:1-10).
Inamaanisha tu kwamba Ruthu alikuwa anamuomba Boazi
amchukue na kumuweka kwenye himaya yake ya ulinzi ili afanye kazi zake akiwa ni
ndugu wa karibu san chini ya Sheria za Kilawi za Kuendeleza ukoo (Ruthu
3:1-18). Alitaka aolewe nay eye ili aendeleze kumzalia mtoto ambaye hatimaye
angekuwa ni wa uzao wa marehemu mume wake. Hii ingemuhakikishia pia kwamba yeye
pamoja na Naomi wangeweza kuwa na sehemu yao kwenye urithi kwenye kabila la
Yuda.
Boazi alikuwa na furaha nyingi kuwafanyia hili
wanawake hawa. Alikuwa ni ndugu na alikuwa na haki na wajibu wa kisheria
kuwasaidia. Alikuwa hajaoa na tajiri sana, lakini alikuwepo ndugu mwingine wa
karibu wa Elimeleki ambaye alikuwa na haki ya kwanza ya kudai kumuoa Ruthu kwa
mujibu wa Torati. Kwa hiyo jambo hili lilipaswa kushughulikiwa na lipate
ufmbuzi wake kwanza (Ruthu 3:11-18).
Kwenye jamii zetu leo, mwanamke yuko huru kuolewa
tena iwapo kama mume wake atafariki, na ataolewa kwa yeyote ampendaye. Lakini
kwenye Israeli ya kale mwanamke aliolewa kwenye kabila la mume wake. Hii
inamaana kuwa falimi ya mume wake ilibeba jukumu la kumtunza kwa kipindi chote
ambacho atabakia kwenye familia ile. Siku hizo familia ziliishi na kufanya kazi
pamoja na kugawana kila walichokuwa nacho. Wanawake hawakwenda mbali nje ya
nyumbani kwao ili kutafuta au kufanya kazi huko.
Baba alikuwa ni kichwa cha familia. Hii ilikuwa ni
pmoja na jukumu la kungalia au kulinda mali pamoja na wanawake walio ndani ya familia.
Pia kama mtu yeyote kwenye familia akifa pasipo kuacha mrithi, Torati iliagiza
ndugu wa marehemu huyo amuoe mjane aliyefiliwa na huyo mume. Mtoto wa kwanza
anyezaliwa kwenye ndoa hiyo ndiye anakuwa mrithi halali wa Yule mwanaume
aliyefariki. Hii iliruhusiwa kwa lengo la kuhakikisha kwamba jina lake
lisishaulike katika Israeli. Ni jinsi pia ambayo familia zilitumia katika
kuwatunza wanawake wajane (Kumbukumbu la Torati 25:5-9).
Naomi alikuwa na familia yenye rslimali huko
Bethlehemu, ambayo kwayo alitaka kuidai. Kwa hiyo mwanaume ambaye angemuoa
Ruthu alipaswa kumkomboa (kumnunua kwa kurudisha kidaiwacho) urithi wa familia
ya Naomi. Boazi alisema kuwa angeweza kufanya hivyo, lakini jambo la kwanza
alimualika ndugu wa karibu sana ili afanye yampasayo kwanza kwenye familia ya
Naomi. Kipindi hiki kil mtu alimjua na kumpenda Ruthu. Waliona jinsi alivyomhudumia
mkamwanae na alivyofanya kazi kwa bidii, na kwamba aliamini na kuabudu sawasawa
na walivyokuwa wao wote.
Boazi akaongea na yule ndugu mwingine kuhusu hali
ilivyokuwa na kwamba mtu yule alikuwa amemaanisha kununua ardhi. Boazi
akamwambia kuwa kitendo cha kuinunua ardhi kinamaanisha ia kwamba atatakiwa
amuoe Ruthu ili amzalie mrithi na atakaye liendeleza jina la Elimeleki, lakini hakuwa
tayari kufanya hivyo. Alivua kiatu chake kitendo kilichoashiria kwamba hakupenda
kufanya kazi hiyo kwa ajili ya familia ya Elimeleki (Ruthu 4:1-10). Kitendo cha
kuvua kiatu kilikuwa ni kama kuweka mkataba ulio kinyume kabisa leo.
Ndipo, Boazi na Ruthu waliweza kuoana. Wakazaa
mtoto aliyeitwa Obedi. Naomi alimfurahia sana mjukuu wake huyu. Na marafiki
zake wakaungana naye kufurahi na wakamwambis kuwa jina lake litakuwa kuu na la
kutukuka katika Israeli. Na ndivyo alivyokwa Obedi, kwamba alikuwa ndiye babu
yake mfalme Daudi (Ruthu 4:11-22). Pia kuhusu vizazi ishirini na nane baada ya
Daudi, Yesu Kristo alizaliwa katika mstari wa uzao wa Yuda (Mathayo 1:7).
Yumenena kuhusu mambo yaleyale ambayo Wakristo
wanaweza kujifunza kutoka kwenye hadithi hii na kuna mambo mengine mengi
tutakayoweza kujifunza baadae huko mbele. Israeli walikuwa ni wateule wake
Mungu. Lakini inawezekana kwa kwa Wamataifa (ambao ni wale wanaotokana na taifa
linguine lisilo la Israeli) na kufanyika kuwa Israeli wa kiroho. Hii
inawezekana tunapogeuka kutokana kwenye ibada za kuiabudu miungu mingine na
tunapoanza kumuabudu Mungu wa Pekee na wa Kweli na kuzishika Sheria zake.
Tunauona mfano huu kwenye hdithi ya Ruthu, ambaye alikuwa
tayari kuziachilia mbali imani zake za kipagani na kuondoka nyumbani kwake,
kuwaacha marafiki zake na kuanza kuchukua njia mpya ya uzima pamoja na Naomi. Alijitoa
kikamilifu kabisa kumtumikia Mungu wa Pekee na wa Kweli. Sisi sote tunapaswa
kuhiyari kufanya hivyo wakati tunapobatizwa na kuitwa kuingia kwenye Kanisa
lake Mungu.
Kwa kujifunza zaidi na kwa kina kuhusu yaliyjiri
kwenye Kitabu cha Ruthu soma jarida la Ruthu (Na. 27).
q